rudi nyuma Yaliyomo endelea

1332.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema katika kuzungumzia faida za utoaji wa Zaka, katika Kafi na Wasail, Mlango 1, Hadith 9 :

“Bila shaka Zaka imefaradhishwa kwa ajili ya kuwajaribu (mtihani) matajiri na wenye mali na kuwatimizia mahitaji ya wenye shida na kwa yakini, iwapo watu wangalikuwa wakitoa Zaka ipasavyo, basi kusingalikuwapo na Waislamu masikini na wenye shida na wala kusingalikuwa na mmoja kumtegemea mwingine na wala kusingalikuwapo na wenye kuwa na njaa au wasiokuwa na nguo. Lakini taabu na shida zote walionazo masikini ni kutokana na wenye mali na utajiri kutotimiza wajibu wao wa kutoa Zaka na Sadaka. Hivyo Allah swt humtenga mbali na neeema na baraka Zake yule ambaye hatimizi wajibu wake huo. Nami naapa kwa kiapo cha Allah swt ambaye ameumba viumbe vyote na anawapatia riziki zao, kuwa hakuna kinachopotea katika mali katika nchi kavu au majini isipokuwa ile isiyotolewa  Zaka.

Faida ya tatu, Nafsi yetu inatoharishwa kwa udhalilisho wa ugonjwa sugu wa ubakhili na hivyo inatubidi sisi lazima tuutibu ugonjwa huu unaoangamiza na kutumaliza.

1333.  Hivyo Amesema Allah swt katika Qur'an Tukufu, Surah al-Tawba, Ayah 103 :

“Chukua Sadaka katika mali yao, uwasafishe na kuwatakasa kwa ajili ya hizo (Sadaka zao na kuwataja kwa vizuri (mbele yangu) na uwaombee dua. Kwa hakika kuwaombea kwako kutawapa utulivu, na Allah swt ndiye asikiaye na ajuaye.”

1334.  Vile vile Amesema Allah swt katika Qur'an Tukufu, Surah

al – Hashri, 59,  Ayah 9:

“Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda waliohamia kwao, wala hawaoni choyo katika vifua vyao kwa waliyopewa (Wahajiri), bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji.  Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.”

1335.  Amesema Allah swt katika Qur'an Tukufu, Surah al –Baqarah, Ayah 28 :

“Allah swt huongezea katika Sadaka”

1336.  Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu, Surah al – Sabaa, 34, Ayah 39 :

‘Chochote kile mtakachokitoa (katika njia yake), basi Atawalipeni (humu humu duniani) malipo yake, Naye ni Mbora wa wanao ruzuku.’

1337.  Amesema Allah swt katika Qur'an Tukufu, Surah al –Rum, 30,  Ayah 39 :

‘Na mnachokitoa kwa riba ili kiongezeke katika mali ya watu, basi hakiongezeki mbele ya Allah swt . Lakini mnachokitoa kwa Zaka kwa kutaka radhi ya Allah swt, basi hao ndio watakaozidishiwa.’

1338.  Amesema Bi. Fatimah az-Zahra a.s. bintie Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika hotuba aliyoitoa kuzungumzia Fadak katika Bihar al-Anwaar, J.8, Uk 109 :

“Kwa ajili ya kujitakasa na dhambi la Shirk, Allah swt ametufaradhishia kuikamilisha imani yetu (yaani mtu yeyote anayetaka kujitakasisha na unajisi basi inambidi kuleta imani kwa moyo wake kamilifu), na Sala inamwepusha na magonjwa ya kiburi na kujifakharisha, na Zaka inamwepusha mtu kwa magonjwa ya ubahili ili mwanadamu awe mkarimu na mpenda kutoa kwa ajili ya mema ili atakasike) na hii pia ndiyo sababu kuu katika kujiongezea riziki .”

1339.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib  a.s. ameripotiwa akisema katika

  Al-Kafi:

“Yeyote yule anayetumia kutoka mali yake katika njia ya kheri, basi Allah swt anamlipa mema humu duniani na kumwongezea katika malipo yake.”

1340.  Vile vile ameripotiwa akisema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib  a.s.  katika Wasa’il as-Shiah : Mlango Sadaka, Hadith 19, J.6, Uk. 259 :

“Tafuteni riziki yenu kwa kutoa Sadaka.”

1341.   Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripotiwa katika Kitab ‘Uddatud-Da’i kuwa  alimwuliza mtoto wake :

“Je nyumbani kuna kiasi gani kwa ajili ya matumizi?”

Naye alimjibu :

“Zipo Dinar arobaini tu.” 

Imam a.s. alimwambia

“Dinar zote hizo zigawe Sadaka.”

Kwa hayo mtoto wake alimwambia Imam a.s.

“Ewe Baba ! Mbali na Dinar hizi arobaini, hatutabakia na akiba yoyote.”

Imam a.s. alimwambia :

“Nakuambia kuwa zitoe Dinar zote Sadaka kwani ni Allah swt tu ndiye atakayetuongezea kwa hayo. Je wewe hauelwei kuwa kila kitu kina ufunguo wake ? Na ufunguo wa riziki ni Sadaka ( kutolea

mema ).”

Kwa hayo, mtoto wake aliyekuwa akiitwa Muhammad, alizitoa Sadaka Dinar hizo na hazikupita siku kumi, Imam a.s. alitumiwa Dinar elfu nne.

Hapo Imam a.s. alimwambia mwanae :

“Ewe Mwanangu ! Sisi tulitoa Dinar arobaini tu na Allah swt ametupa Dinar elfu nne badala yake.”

1342.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib  a.s. amesema katika Nahjul Balagha kuwa :

“Mtu anapokuwa masikini au mwenye shida basi fanyeni biashara pamoja na Allah swt kwa kutoa Sadaka.”

1343.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema :

“Zakat-i-Fitrah inakamilisha saumu za mwezi Mtukufu wa Ramadhani.”

1344.  Amesema Allah swt katika Qur'an Tukufu, Surah al – Tawbah,  9, Ayah 60 :

“Wa kupewa Sadaka ni mafakiri, na masikini, na wanaozitumikia, na wa kutiwa nguvu nyoyo zao, na katika kukomboa watumwa, nawenye madeni, na katika Njia ya Allah swt , na wasafiri. Huu ni wajibu uliofaradhiwa na Allah swt . Na Allah swt ni Mwenye kujua Mwenye hikima.”

1345.  Vitu saba vina Zaka Sunnah :

Mali ambayo mtu anataka kuitumia katika kufanyia biashara

Mfano mchele, dengu, dengu iliyoparazwa. Lakini mbogamboga kama vile biringanya, matango, matikimaji, maboga hayana Zaka.

Vitu vilivyotengezwa vya kuvaa na mawe kama almasi n.k.

Iwapo mtu atakuwa na mali aliyoizika au aliyoificha ambayo hawezi kuitumia basi kwa misingi ya uwezo inambidi kutoa Zaka ya mwaka mmoja.

Iwapo mtu atauza sehemu ya mali kiasi fulani kabla ya kuisha kwa mwaka kwa misingi ya kukwepa kulipa Zaka, basi itambidi uanzapo mwaka mpya, alipie Zaka sehemu hiyo aliyokuwa ameuza kwa ajili ya kukwepa Zaka yake.

Mtu anayepokea malipo kutokana na kukodisha majumba, maduka, mashamba, mabustani au hamaam (mabafu yanayotoza malipo kwa kutumia ).

KHUMS

1346. Allah swt anavyotuelezea katika Qur'an Tukufu, Surah al-Anfaal, 8, Ayah 41 :

NA JUENI ya kwamba ngawira mnayoipata, basi khums (sehemu moja katika tano) ni kwa ajili ya Allah swt na Mtume, na jamaa, na mayatima, na masikini, na wasafiri, ikiwa nyinyi mmemuamini Allah swt na tuliyoteremsha kwa mja wetu(Muhammad) siku ya kipambanuo (katika Vita vya Badr), siku ( Waislamu na Makafiri ) yalipokutana majeshi mawili. Na Allah swt ni Muweza wa kila kitu.

1347.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, katika Man la yahdhurul Faqih, J.2, uk.41

“Kwa kuwa Allah swt ametuharamishia Zaka sisi Ahlul-Bayt a.s.hivyo ametuwekea Khums kwa ajili yetu na hivyo Sadaka pia ni haram kwetu na zawadi imeruhusiwa kwa ajili yetu.”

1348.  Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema, katika Usuli Kafi, J. 1, Uk.545 :

“Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kununulia chochote kutoka kifungu ambacho Khums haijalipwa na hadi pale wasipoifikisha kwa wanaostahiki kwetu.”

1349.  Vile vile Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema, katika Al-Kafi, J.1, Uk. 546 :

“Siku ya Qiyamah wakati ule utakuwa mgumu kabisa pale wanaostahiki Khums watakapotokezea kudai haki zao kutoka wale wasioilipa.”

1350. Miongoni mwa marafiki tajiri mmoja kutokea Uajemi alimwandikia barua Al-Imam ‘Ali ar-Ridha a.s. na alimwomba Imam a.s. ruhusa ya kuitumia ile mali ambayo khums haijatolewa. Basi Imam a.s. alimwandikia majibu kama ifuatavyo : Imenakiliwa kutoka Al-Wafi, Al-Kafi na Tahdhib

“Bila shaka Allah swt ni Wasi’ na Mkarimu na amechukua dhamana ya kumlipa thawabu na malipo mema yule mtu ambaye atatekeleza hukumu zake na ameweka adhabu kwa yeyote atakayekwenda kinyume ya hayo. Bila shaka mali iliyo halali kwa ajili ya mtu ni ile ambayo Allah swt ameihalalisha na kwa hakika Khums ni dharura yetu na ni hukumu  ya Dini yetu na ni njia ya kujipatia kipato kwa jili ya riziki sisi na wenzetu na imewekwa kwa ajili ya kulinda hishima zetu dhidi ya wapinzani wetu. Hivyo kamwe musiache kutoa na kulipa Khums. Na kila inapowezekana kusijikoseshe Du’a zetu na kwa hakika kwa kutoa Khums kunazidisha riziki yenu na  kutoharisha na ni hazina kubwa kwa ajili ya Siku ile ambayo kutakuwa na taabu tupu na mateso (Siku ya Qiyamah). Na kwa hakika Mwislamu sahihi ni  yule ambaye amemwahidi Allah swt kwa ahadi na ‘ibada, basi atimize kwa ukamilifu. Na iwapo atakubali kwa mdomo tu ilhali moyoni anakataa na kupinga basi atambue kuwa yeye si Mwislamu.

1351.  Imeripotiwa kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib  a.s. katika Al-Kafi J.5, Uk. 144  kuwa :

“Iwapo mimi nitapenda kumpatia kitu rafiki yangu basi mimi nitampa zawadi kwani ninaipenda zaidi kuliko Sadaka.”

1352.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib  a.s. kwa muda wa siku saba hakupata mgeni nyumbani kwake basi alisema huku akilia :

“Nasikitika mno na ninakhofu kuwa isije Allah swt akaniondolea rehema na baraka zake.”

1353.  Amesema Allah swt katika Qur'an Tukufu  Surah al- Ma’arij,70, Ayah 24 – 25 :

Na ambao katika mali yao iko haki maalumu.

Na mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba…

1354.  Al Imam Musa bin Ja’afer a.s. amepokelewa riwaya kuwa  :

“Katika ukoo wa Bani Israil kulikuwa na mtu mwema ambaye alikuwa na mke aliye mwema pia. Siku moja aliota ndoto ambamo aliambiwa kuwa Allah swt amempangia kiasi fulani cha umri wake ambapo nusu ya umri huo utapita katika raha na mustarehe wakati nusu ya umri uliobakia utapita katika shida na dhiki na umasikini.

Hivyo Allah swt amekupa fursa wewe kuchagua iwapo utapenda kupitisha umri wako wa nusu ya awali ya raha na mustarehe na baadaye dhiki na umasikini ? Hivyo chagua mojawapo. Kwa hayo mtu huyo alijibu kuwa : ‘Mimi ninaye mke wangu aliye mwema na hushirikiana naye katika maswala yote, hivyo nitapenda kupewa muda wa kuweza kuongea naye kabla sijatoa uamuzi wa chaguo langu.’

Mke wake alimshauri mumewe kuukubalia umri ule wenye neema uwe ndio wa kuanzia kwani: ‘Inawezekana Allah swt anataka kututeremshia neema na baraka zake hivyo tukaongoka.’

Hivyo usiku uliofuatia, bwana huyo aliulizwa jibu alilolifikia katika uamuzi wake. Naye akajibu : ‘Mimi ninataka kuupitisha nusu ya umri wangu katika neema, raha na mustarehe.’ Kwa hayo akajibiwa kuwa hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa mujibu wa chaguo lake.

Kuanzia hapo yeye alijaaliwa kila aina ya raha na akawa tajiri mkubwa mwenye mali na milki nyingi.

Katika kutajirika huku, mke wake akamwambia, ‘Ewe Bwanangu! Usiwasahau kuwasaidia na kukidhi haja za majamaa zetu na mafukara na masikini na uwe na uhusiano mwema pamoja nao. Na uwazawadie watu fulani fulani wakiwemo majirani na marafiki, zawadi mbalimbali.’

Mtu huyo alizingatia na kutekeleza ushauri uliokuwa umetolewa na mke wake. Na hivyo alifungua milango ya kugawa mali yake katika masuala hayo hadi ulipofika wakati wa kuisha kwa nusu ya umri wake wa awali.

Kuisha huku kwa nusu ya kwanza ya umri wake, aliota ndoto tena ambamo aliambiwa kuwa : ‘Kwa kutokana na uwema wako wa kuwasaidia wenye shida na dhiki imekuwa kipaumbele kwako, basi Allah swt amekubadilishia sehemu hii ya pili kuwa katika raha na mustarehe kama ilivyo sasa.’”

1355. Wakati wa mavuno kwa kiwango kile ambacho bado Zaka haijapigiwa hisabu, inagawiwa kwa kuchota mkono moja kwa wapita njia kama vile alivyosema Allah swt katika Qur'an Tukufu, Surah al –Al-An-‘Aam 6, Ayah 141 :

Na Yeye ndiye aliye ziumba bustani zenye kutambaa juu ya chanja, na zisiyo tambaa, na mitende, na mimea yenye matunda mbali mbali, na mizaituni na mikomamanga inayo fanana. Kileni matunda yake inapo zaa, na toeni haki yake siku ya kuvunwa kwake. Wala msitumie kwa fujo. Hakika Yeye hawapendi watumiayo kwa fujo.

1356.  Yaani kuwakopa Waislamu ambao wanashida ya kukopa deni ili kukidhi masuala yao. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, katika Al-Kafi:

“Katika mlango wa Jannat kumeandikwa ‘Yapo mema kumi kwa mtoa Sadaka na mema kumi na nane kwa mkopeshaji madeni.’”

1357.  Vile vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, katika  Al-Wafi :

“Wakati Mumin mmoja anapomkopesha Mumin mwenzake deni kwa ajili ya kutaka ridhaa ya Allah swt , basi Allah swt anamhisabia deni hilo katika Sadaka hadi kuja kulipwa kwake.”

1358.  Vile vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripotiwa akisema kuwa :

“Kwa kupuuzia ‘Ma’un’ (mambo ya nyumbani ) ambayo Allah swt ameahidi katika Qur'an Tukufu adhabu, basi si Zaka inayozungumziwa, bali ni kuwasaidia kwa kuwakopa wale wenye shida na wenye shida wanapokuja kuazima vitu vya nyumbani, basi inabidi  kuwa azima vitu vya nyumbani.”

1359.  Abu Basir amemwambia Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa

“Majirani zetu wanapokuja kuazima vyombo au vitu vingine vya nyumbani, na tunapo waazima basi huvunja vunja na kuviharibu vitu vyetu na hivyo sisi tunalazimika kuwakatalia kwa misingi hiyo, sasa je kuwakatalia huku ni dhambi ?”

1360.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimjibu :

“Iwapo watu hao wanatabia kama hiyo, basi si dhambi kuwanyima.”

1361. Inabidi kuwapa muda au kuwasamehe madeni wale ambao hawana uwezo wa kuyalipa madeni hayo. Na kuhusiana na swala hili Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema :

“Iwapo mtu anataka asidhalilishwe Siku ambayo hakuna mwingine wa kuwaokoa isipokuwa Allah swt , basi inambidi awape muda wa kulipa madeni wadaiwa wake au kuwasamehe madeni yao.”

1362.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema :

“Yeyote yule atakayempa muda wa kulipa madeni ambaye hana uwezo wa kulipa ( basi kwa ajili yake ) thawabu zake mbele ya Allah swt  ni sawa na thawabu za kutoa Sadaka kila siku kwa kiasi hicho hadi atakapolipwa.”

1363.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliambiwa kuwa :

“Abdur Rahmaan bin Sababah anamdai deni marehemu mmoja, nasi twamwambia yeye kuwa amsamehe lakini yeye anakataa kata kata kumsamehe deni lake.”

1364.  Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akasema :

“Ole wake, je haelewi kuwa iwapo atamsamehe marehemu deni lake basi Allah swt atamlipa Dirham kumi kwa kila Dirham yake moja. Na iwapo hatamsamehe basi atalipwa Dirham moja kwa Dirham yake moja.”

1365.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, Al-Kafi, J.2,Uk. 204 :

“Mtu yeyote atakayemsaidia Mumin kwa mavazi wakati wa baridi au joto basi Allah swt atamjaalia mavazi ya Jannat (Peponi au Paradiso ) na atampunguzia shida kali wakati wa kutoa roho yake (wakati anapokufa ) na atampanulia kaburi lake na Siku ya Qiyamah atakapotoka nje ya kaburi lake atakuwa akitoka katika hali ya furaha kwa kuonana na Malaika.”

1366.  Vile vile Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema, Al-Kafi, J.2, Uk.205:

“Iwapo Mwislamu yeyote atamsaidia mtu asiye na mavazi kwa mavazi au aliye na dhiki ya mali, akasaidiwa ( nyumba,mali n.k ) basi Allah swt anamwekea Malaika elfu saba hadi Siku ya Qiyama kwa ajili ya kumwombea maghfirah kwa kila dhambi lake.”

1367.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, katika Al-Wafi, al-Kafi na kunakiliwa pia katikaTahdhiib :

“Baada ya kufariki kwa mtu, huongoka  kwa mambo matatu

RIBA

1368.  Dhambi la riba ni miongoni mwa Madhambi Makuu.

1369.  Kwa mujibu wa Qur’an tukufu, kuchukua riba ni dhambi ambalo linasababisha adhabu kali kabisa kutoka kwa Allah swt.  Adhabu za kuchukua na kutoza riba ni kali kabisa kuliko madhambi mengine. Kama ilivyoelezwa katika Surah Aali Imran, 3, : 130 - 131:

‘Enyi Mlioamini! Msile riba, mkizidisha mara dufu kwa mara dufu; na mcheni Allah ili muweze kuwa na ufanisi’

‘Na ogopeni moto wa Jahannam ambao umetayarishiwa makafiri.’

1370.  Allah swt anatuambia katika Qur'an Tukufu, Surah al Baqarah, 2, Ayah 275 :

‘Wale wanaokula riba, hawasimami ila kama anavyosimama yule ambaye Shaitani kamzuga kwa kumsawaa; na haya ni kwa sababu wamesema, ‘biashara ni kama riba’, Allah ameihalalisha biashara na kaiharamisha riba.  N a aliyefikiwa na mauidha kutoka kwa Mola wake, kishaakajizuia, basi yamekwisha mthibitikia yale (mali) aliyoipata; na hukumu yake iko kwa Allah. Lakini wanaorejea (kula riba) basi hao ndio watu wa Motoni, humo watakaa milele.’

1371. Ayah hiyo inatuthibitishia kuwa wale wanaochukua riba watabakia kwa milele katika Jahannam (Motoni) na kamwe hakutakuwa na uwokovu kwa ajili yao. Allamah Muhammad Husain Tabatabai (a.r.) katika Tafsiri ya Al-Mizan , anasema:

“Adhabu aliyoiweka Allah swt kwa ajili ya mla riba ni kali kabisa kwani hakuna mahala pengine palipozungumzwa kwa ajili ya wale wavunjao kutoka Furu-i-Diin. Kosa lingine ni lile la kulea urafiki pamoja na maadui wa Islam. Athari za riba zipodhahiri na bayana kwetu sote. Kukusanya na kuficha mali ndiko kunako ongezea tofauti kati ya  tabaka la masikini na tajiri. Umasikini ni ugonjwa ambao unamdhalilisha na kumshusha hadhi mgonjwa wake, unateketeza uthamini wake na kuharibu maadili yake. Na haya yanaelekeza katika mutenda maovu, uizi, ubakaji na mauaji. Walanguzi ndio watu wanaowajibika kwa kuteketea kwa usawa wa kijamii, ambao wamejilimbikizia mali kupita kiasi kwamba haiwafikii wanao hitaji na wenye dharura. Kwa kuvunjika kikamilifu kwa mshikamano wa kijamii unaweza kuzua na kukuza vita vya wenyewe kwa wenyewe au vita vya ndani na kuendelea hadi kuzuka kwa vita vya dunia ambavyo hatima yake itakuwa ni mauaji na maangamizo. Katika ulimwengu wa sasa ikiwa na silaha za kisasa za teknolojia ya hali ya juu na ya maafa makubwa katika nuklia na kemikali, vita vinapozuka si kwamba vinaleta mauaji ya wanaadamu tu bali humgeuza yeye kuwa ni picha tu, mgonjwa na asiye na uwezo wowote na ameharibika kimwili kwa vizazi na vizazi vijavyo.

1372.  Katika kitabu ‘Islam and World Peace’ imeandikwa:

“Islam inasema kuwa mapato ya mtu yatokane na kiwango cha juhudi na kazi iliyofanyika.” Kwa sababu  uwekezaji wenyewe haufanyi kazi wala jitihada ya aina yoyote ile. Hivyo, mali ya matajiri haitakiwi kamwe kuongezeka kwa kutokana na riba.”

1373.  Mtume Muhammad s.a.w.w. anasema katika Hadith moja, katika Wasa’il al-Shiah  :

“Ibada inayo sehemu sabini. Na muhimu kabisa ni mtu kujipatia kipato chake kilicho halali.”

1374. Vile vile Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema, katika Muhajjatul Baidha :

“Mfanyabiashara mwaminifu atahesabiwa pamoja na Mitume a.s. Siku ya Qiyama. Uso wake utakuwa uking’ara kama mbalamwezi.”

1375.  Qur’an Tukufu inarejea kutuambia katika Qur'an Tukufu, Surah al-Baqarah, 2 Ayah  275 :

‘‘Na aliyefikiwa na mauidha kutoka kwa Mola wake, kishaakajizuia, basi yamekwisha mthibitikia yale (mali) aliyoipata; na hukumu yake iko kwa Allah. Lakini wanaorejea (kula riba) basi hao ndio watu wa Motoni, humo watakaa milele.’

1376.  Ayah ya hapo juu ya Qur’an inaendelea Qur'an Tukufu, Surah al-Baqarah, 2 Ayah 276 :

‘Allah huyafutia (baraka mali ya ) riba: na huyatiabaraka (mali yanayotolewa) sadaqa . Na Allah hampendi kila kafiri (na) afanyaye dhambi.’

1377.  Qur’an Takatifu inatuambia Surah al-Baqarah, 2, Ayah 278  :

‘Enyi Mlioamini ! Mcheni Allah, na acheni yaliyobakia katika riba, ikiwa mmeamini.’

1378.  Ushahidi wa imani ya mtu katika utiifu wa Hukumu za Allah swt, ayah hiyo hiyo inaendelea : Qur'an Tukufu, Al-Baqarah, 2,

        Ayah 279

‘Na kama hamtafanya hivyo, basi fahamuni mtakuwa na vita na Allah na Mtume Wake….’

1379. ‘Na mkiwa mmetubu, basi matapata rasilimali zenu; msidhulumu wala msidhulumiane.’

1380. Vile vile Mtume Muhammad s.a.w.w. amezungumzi katika hotuba yake huko Makkah :

“Muelewe kuwa riba iliyokuwa imekusanywa katika zama za ujahiliyya sasa imesamehewa kabisa. Kwanza kabisa mimi binafsi nina wasameheni ile riba ( iliyopo shingoni mwenu) ya (mjombangu) '‘Abbas ibn Abdul Muttalib."

1381.  Imeripotiwa kutoka Al-Imam Ja’afer as-Sadiq a.s. kuwa, katika

     Al-Kafi:

“Kuchukua Dirham (au pesa moja) kama riba ni vibaya sana machoni mwa Allah swt kuliko kuingiliana na mwanamke aliyeharamishwa kwako.”

1382.  Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Wasa’il al-Shiah :

“Mtume Muhammad s.a.w.w. amemlaani vikali yule ambaye anayekubali riba, anayelipa riba, aneyeinunua riba, anayeiuza riba, yule anayeandika mikataba ya riba na yule anayekuwa shahidi wa mikataba hiyo.”

1383.  Ibn Baqir anaripoti kuwa  Al-Imam Ja’afer as-Sadiq a.s. alijulishwa kuhusu mtu mmoja aliyekuwa akitoza na kupokea riba kama ndiyo halali kama vile ilivyo halali maziwa ya mama. Kwa hayo, alisema Al-Imam Ja’afer as-Sadiq a.s. katika 

        Al-Kafi :

“Iwapo Allah swt atanipa uwezo mimi juu ya mtu huyu, basi nitamkata kichwa.”

1384.  Sama’a anasema kuwa yeye alimwuliza Al-Imam Ja’afer as-Sadiq a.s. je ni kwa nini Allah swt ametaja kuharamishwa kwa riba mahala pengi katika Qur’an.

Al-Imam Ja’afer as-Sadiq a.s. alimjibu, Wasa’il al-Shiah :

‘Ili kwamba watu wasiache tendo la kutoa misaada (kama vile kutoa mikopo bila ya riba).”

1385.  Amesema al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika Wasa’il al-Shiah :

“Shughuli mbaya kabisa ni ile ambayo inahusisha riba.”

1386.  Zurarah anasema kuwa yeye alimwuliza Al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. kuhusu  Ayah ya Qur’an isemayo  katika Qur'an Tukufu, Surah Al-Baqarah,2, Ayah 276:

‘‘Allah huyafutia (baraka mali ya ) riba: na huyatia baraka (mali yanayotolewa) sadaqa .’

1387.  Na akaongezea kusema :

“Lakini mimi ninaona kuwa mali na utajiri wa watoza riba inaendelea kuongezeka tu kila siku.”

1388.  Amesema Al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. katika Wasa’il al-Shiah :

“Loh ! hasara inawezekana kuwa kubwa sana ? Kwa merejeo ya Dirham moja yeye anaipoteza Dini yake.  Na iwapo yeye atafanya Tawba humu duniani basi kutafikia mwisho kwa mali aliyoichuma humu duniani kwa njia iliyo haramu na hivyo kuwa fukara.”

1389.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema, katika  Mustadrakul Wasa'il :

“Yule anayechukua riba basi Allah swt atalijazatumbo tumbo lake kwa moto kiasi hicho hicho. Iwapo yeye amechuma zaidi kwa kutokana na mapato ya riba, basi Allah swt hatakubalia matendo yake mema. Hadi kwamba kiasi cha punje moja kama kitabakia ambacho kimepatikana kwa njia ya riba. Allah swt pamoja na Malaika Wake wataendelea kumlaani huyu mtu.”

1390.  Vile vile Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema :

“Usiku wa Mi’raj Mimi niliwaona baadhi ya watu waliokuwa wakijaribu kusimama lakini hawakuweza kufanikiwa kwa sababu ya matumbo yao makubwa, niliuliza, ‘Ewe Jibraili ! Je ni watu gani hawa ?’

1391.  Jibraili alijibu :

“Hawa ndio wale waliokuwa wakichukua riba. Sasa wao wanaweza kusimama tu kama wale waliokamatwa na Mashetani.”

1392.  Mtume Muhammad s.a.w.w. aliendelea,

“Na hapo nikawaona wao wakikusanywa katika njia za wafuasi wa Firauni. Kwa kuona uchungu wa joto la Moto mkali, wao walipiga kelele : ‘Ewe Allah swt ! Je Qiyama itakuwa lini ?’

(Hivyo imekuwa dhahiri kuwa Moto unaozungumziwa katika riwaya hii ni adhabu katika Barzakh ).

1393.  Imepokelewa kutoka kwa Mtume Muhammad s.a.w.w. akisema, katika Mustadrakul Wasa'il :

“Wakati zinaa na riba vitakapokuwa ni vitu vya kawaida katika mji wowote basi Allah swt huwapa ruhusa Malaika kuwaangamiza wakazi wake.”

1394.  Ipo riwaya nyingine isemayo kuwa Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema, katika  Mustadrakul Wasa'il  kuwa :

“Utakapofika wakati Ummah wangu utaanza kutoza na kupokea riba, basi mitikisiko na mitetemeko ya ardhi yatakuwa yakitokea mara kwa mara.”

1395.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema, Wasa’il al-Shiah  :

“Iwapo mtu atazini pamoja na mama yake katika Al-Ka’aba tukufu, basi dhambi hili litakuwa hafifu mara sabini kuliko tendo la kutoza na kupokea riba.”

1396.  Amesema al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. katika Wasa’il al-Shiah :

“Katika macho ya Allah swt, kuchukua Dirham moja ya riba ni mbaya kabisa hata kuliko matendo thelathini ya kuzini pamoja na maharimu wake yaani baba kuzini pamoja na binti yake.”

USAMEHEVU

1397.  Kwa upande mmoja Uislamu unawasisitiza Waislamu kutafuta nyenzo za kujipatia mahitajio yao ya kila siku katika maisha yao kwa njia zifuatazo:

1398.  Ibada ni za aina saba, na mojawapo ni kule kujitafutia mahitaji ya kila siku kwa njia zilizo halalishwa katika Dini. [75]

1399.  Yeyote yule aliye na maji pamoja na ardhi katika uwezo wake, na wala halimi katika ardhi hiyo, na iwapo atakumbwa na hali ya kukosa chakula cha kujilisha yeye pamoja na familia yake, basi atambue wazi kuwa huyo amekosa baraka za Allah swt. [76]  

1400.  Moja ya matendo yaliyo bora kabisa ni kilimo kwani mkulima anajishughulisha katika kilimo na upandaji wa mazao ambayo yanawafaidisha wote bila ya kuchagua iwapo huyu ni mwema au mwovu. [77]  

1401.  Yeyote yule asiyejitafutia mahitaji yake ya maisha basi kamwe hatakuwa na maisha ya mbeleni kwani atateketea.

1402.  Na yeyote yule anayejitahidi kwa bidii kubwa kwa kujipatia mahitaji kwa ajili ya familia yake basi huyo ni sawa na yule ambaye anapigana vita vya Jihad. [78] 

1403. Kwa upande wa pili, Islam inaamini kuwa iwapo mtu atakuwanavyo mali na milki, kilimo na viwanda, utajiri na starehe lakini bila ya Taqwa ya Allah swt  kama vile imani juu ya Allah swt na Mitume a.s, Imani juu ya siku ya Qiyama, thawabu, na adhabu na bila ya kuwa na tabia njema na kuuthamini ubinadamu kama vile msamaha, ushirikiano katika mambo mema, moyo wa utoaji, kuonea huruma n.k. basi kamwe haviwezi kumpatia maendeleo.

1404.   Allah swt anatuambia katika Qur’an Tukufu Surah Al A’S’R,

           103 : Ayah 1-3

1405.   Imam Hussein a.s. amenakiliwa akisema:

“Kama kwa kweli kuna milki ya mali ya mtu humu duniani, basi hiyo ni  kuwa na tabia njema. Iwapo watu wote watakufa, basi kifo jema kabisa mbele ya Allah swt ni kule kujitolea mhanga katika njia ya Allah swt.”

1406.   Usamehevu upo wa aina mbili:

·   Sisi tunamsamehe mtu pale tunajikuta kuwa hatuna uwezo wa kulipiza kisasi. Kwa hakika aina hii ya usamehevu unatokana na subira na kuvumilia na kamwe si kusamehe. Kwa maneno mengine, ni aina mojawapo ya kutoweza kujisaidia na udhaifu.

·   Sisi tunamsamehe mtu ingawaje tunao uwezo wa kulipiza kisasi. Aina hii ya usamehevu ndio unaofundishwa na Islam pamoja viongozi wetu.

1407.  Amesema Al-Imam Ali as. :

“Mtu anayestahiki kusemehe wengine ni yule ambaye ni mwenye uwezo mkuu  zaidi katika kuwaadhibu wengine.”[79]

1408.  Katika wusia wake wakati akiongea na Harith Hamdani, Al- Imam Ali a.s. alisema:

“Tuliza ghadhabu zako na kumsamehe mtu aliyekukosea wakati wewe ukiwa na uwezo au cheo chako.” [80]

“Wakati wewe utakapomzidi nguvu adui yako, basi zingatia kumsamehe ikiwa ndiyo shukurani ya kupata uwezo huo.” [81]

1409.  Amesema al-Imam as- Sadique a.s.

“Kuwasamehe wengine wakati mtu yupo katika madaraka ni sambamba na tabia na desturi za Mitume a.s pamoja waja wema.” [82] 

1410.  Baadhi ya Ayah za Qur’an tukufu zizungumziazo maudhui haya:

Qur'an Tukufu, Sura  Al- A’araf  (7) Ayah ya 199,

Uchukulie kusamehe na kuamrisha mema na kujiepusha na majaheli[83]

Vile vile Allah swt anatuambia katika Qur'an Tukufu, Sura A’araf ( 7 ) Ayah ya 200,

‘Na iwapo wasiwasi wa Shaitani utakusumbua basi jikinge kwa Allah, Yeye ndiye Asikiaye na Ajuaye yote.’

1411.  Qur'an Tukufu, Sura  Aali ‘Imran  (  3 )  Ayah  134

‘Wale wanaotumia wakiwa katika hali nzuri na dhiki na ambao huzuia ghadhabu zao na kusamehe (makosa ya) watu ; kwani Allah huwapenda wafanyao mema.‘  [84]

rudi nyuma Yaliyomo endelea