rudi nyuma Yaliyomo endelea

1120. Kila mtu aliye mwenye busara na hekima huwa yuko masikitikoni.

1121.  Mwenye busara ni mwenye faida hata kama akiwa katika hali gani ile.

1122.  Kujihusisha na wapumbavu  ni kuitesa Roho.

1123.  Mpumbavu yupo peke yake hata kama akiwa katika jamii.

1124. Kutoka kupata hekima (matakwa yake) hayawezi kufidiwa na fedha.

1125.  Hakuna ugojwa ulio mbaya kabisa kuliko kutokwa kwa hekima.

UWEMA NA MATENDO MEMA.

1126.  Kwa uwema mtu anaweza kumteka mtu aliye huru.

1127.  Wema haufi kamwe.

1128.  Kazi iliyo bora zote ni kujijumuisha pamoja na walio wema.

1129.  Kuwa mwema kwa mema ni uwema na hii ndiyo fahamu ya mtu ya hali ya juu.

1130.  Thamani ya mtu inategemea uzani wa uadilifu wake.

1131.  Angukia ndani kwa wema na uangukie nje kwa matakwa.

TAMAA

1132. Mapenzi ya mali (utajiri) yanachochea tamaa na kuupoteza uwema.

1133.  Tamaa haielewi mipaka yake.

1134.  Kuwa na imani ya Allah swt ni jitihada iliyo bora kabisa.

1135. Tamaa iliyo kuuu kabisa ya wanyama ni kule kushibisha tumbo lao wenyewe.

1136. Tamaa iliyo kuu ya wanyama porini kule kuwanyanyasa wengineo.

1137.  Tamaa kuu ya mwanamke ni kuivutia dunia kwake na kuchochea fujo humo.

1138. Jitihada kuu kabisa ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.humu duniani ni kuiongoza dunia.

1139.  Tamaa yako iwe ni ile kwa ajili ya akhera na hapo utajirekebisha.

1140.  Thamani ya mtu inategemea utukufu wa jitihada zake.

1141.  Ukuu na ufahari wa mtu unategemea utukufu wa jitihada zake na wala sio pale penye kuozapo mifupa ya mababu zetu.

REHEHMA NA MSAMAHA:

1142.  Kusamehe ni taji la ukubwa na fahari.

1143.  Rehema inaitukuza nguvu.

1144. Itakuwa ni vyema iwapo rehema itashirikishwa pamoja na ukubwa.

1145. Itakuwa ni adhabu kubwa itakayotolewa mbali na kuombwa   msamaha.

1146.  Unyenyekevu inatangaza ukubwa.

1147.  Unyenyekevu ni matunda ya elimu na hekima.

1148. Unyenyekevu bila ya kutazama panapostahili ni sawa na huna uwezo.

1149.  Majivuno huangamiza na kumharibia sifa mtu.

1150.  Kwa kuwa na majivuno au kiburi ni sawa na kuipa akili sumu.

1151.  Kiburi hukandamiza mwenendo wa maendeleo.

1152.  Majivuno huua na kuudhalilisha ukubwa.

1153.  Unyenyekevu ni sawa na wavu uliotandwa kwa ukubwa.

1154.            Kujivuna na kule kujideka ni matokeo ya wale wenye akili kasoro.

ULIMWENGU:

1155.  Ulimwengu huu ni sawa na daraja ituvushayo kwenda akhera.

1156.  Dunia hii ni sawa na duka la maovu.

1157.  Mapenzi ya dunia ni chanzo (mizizi) cha matatizo na maovu yote.

1158.  Ufahari wa wapumbavu na walio wajinga ni mapenzi ya dunia.

1159.  Dunia ni chungu mno zaidi kuliko ule utamu wake ulio nao.

1160.  Kuipatia dunia hii talaka ni sawa na kupanga harusi na Akhera.

1161.  Dunia hii ni sumu na wale wailao sumu ni majahili.

1162. Uishi kwa kiwiliwili chako humu duniani na uifanyishe kazi nafsi(imani) yako kwa ajili ya akhera.

WATU

1163. Watu ni zaidi ya vile walivyokuwa awali na huishi zaidi ya walivyokuwa wakiishi mababu zao.

1164. Mtu aliye jasiri kuliko wengine ,atulizaye matamanio yake (subira).

1165.  Itakuwa ni jambo la upuuzi iwapo nafsi itakuwa imedhoofika hali mwili wa mtu bado ana siha nzuri na iliyo njema.

1166.  Yule aijuaye na kuelewa ubinadamu huchagua upweke.

1167.  Yule ampandae Allah swt hupigana na aibu za watu.

1168.  Yeyote yule asiyejifikiria na kujithamini mwenyewe basi amepotoka.

MATAKWA YA SUBIRA

1169. Hekima iliyo kuu kabisa ni kule kupingana na matakwa na matamanio ya mtu.

1170.  Atakuwa ni mtu mwenye furaha kuu iwapo ataishinda nafsi yake mwenyewe.

1171.  Adui wa kupindukia wa mtu ni yale matakwa yake.

1172.  Vita vilivyo bora kuliko vyote ni vile vita dhidi ya nafsi ya mtu.

1173. Ulafi wa sehemu zetu za siri ndizo nyavu zilizo tegwa na Shaytani.

MADHAMBI.

1174. Kuishi kwako hapa (mbali na utukufu) na dhambi lisiloweza  kusamehewa.

1175. Usiogopeshwe na chochote kile isipokuwa madhambi yako mwenyewe.

1176.  Madhambi yanaharibu ibada ya Allah swt.

1177.  Uharibifu ni matunda ya madhambi.

1178.  Madhambi yanampotezea mtu utukufu wake.

1179.  Kujiepusha na madhambi ni afadhali kuliko kutenda mema .

1180.  Kutenda madhambi ni ugonjwa na dawa yake ni kujiepusha nayo na kufanya tawaba

MAFUNZO YA TAHADHARI.

1181.  Kila mtazamo wako wa fahamu ni fundisho kwako

1182.  Walio kufa wamewachia mafunzo kwa ajili ya walio hai.

1183. Nijia walizozipitia wale waliokufa na waliotutangulia ni zenye kutufunza na kututahadharisha sisi tuzifuatazo.

1184.  Uhakika wa mambo ni mkufunzi wa kutosha kabisa.

1185.  Umri mkubwa ni mkufunzi aliye bora kabisa .

SHAURI

1186.  Kutoa onyo la upole katika umati wa watu ni jambo lililo bure.

1187. Mtoa mashauri asiye na uwema ni sawa na vile upinde  unavyokuwa bila uzi.

1188.  Mshauri aliye bora kuliko wengine ni yule akuelezeaye makosa na dosari zako.

UAMINIFU,UADILIFU

1189.  Ulimi mtukufu ni ule ulio adilifu.

1190. Kwa kutimiza ahadi ni mfano ulio bora kabisa wa uaminifu na uadilfu.

1191. Ukweli ina maana ya kwamba ulinganifu wa matamko kwa mujibu ya maamrisho ya Allah swt  atakavyo.

UDANGANYIFU NA KHIANA

1192.  Urafiki haupo kamwe katika uongo.

1193.  Kwa kubadilisha maana halisi ya jambo kuna haribu asili yake.

1194.  Kusema uongo kunaharibu habari.

1195.  Kusema uongo panapostahili,kutamlindia heshima za mtu.

1196.  Kusema uongo na unafiki kunadhalilisha nidhamu na heshima ya mtu.

UKIASI NA UFUJAJI.

1197.  Aliyebarikiwa ni yule ambaye anaelewaye vyema thamani yake na asiyevuka mipaka.

1198.  Kwa kupima kiasi ni nusu ya hifadhi.

1199.  Ufujaji unapotea kabla ya njaa.

1200.  Ufujaji unapoteza uwema na sadaka.

1201.  Tamaa ya mali kunaharibu ukiasi alionao mtu.

1202.  Kiasi kwa uangalifu kinabakia zaidi ya kile kilicho fujwa.

1203.  Hakuna ufahari katika ufujaji.

1204.  Kupima kiasi ni njia ya usalama na ya amani.

UWEMA ( HISANI )

1205.  Heshima na ukukuzi hauwezi kamwe kulinganiswa na ubaya,sio yenye wema.

1206.  Mwenendo wa mtu ni diraja ya akili yake.

1207.  Urithi ulio bora kabisa ni uungwana wa mtu.

1208.  Hakuna chochote kile chenye thamani dhidi ya uungwana.

KUWAHESHIMU WAZAZI

1209.  Kuwatazama wazazi ni fardhi iliyo kuu kabisa.

1210. Kuwatunza na kuwastahi wazazi wako (kuwalea) na malezi ya watoto wako, ndiyo yatakayo kulea wewe na kukustahi.

PUPA

1211.  Hakuna ushindi uliopo katika pupa.

1212.  Lawama huwa ni daima kwa yeyote aendeleae kwa pupa

HUSUDA

1213.  Husuda humwibia mtu raha zake.

1214.  Silaha ya husuda ni malalamiko na mapingamizi.

1215.  Husuda huitafuna uwema kama vile moto iharibuavyo mbao.

KAZI

1216.  Matendo ndiyo matokeo ya nia.

1217. Uwemwaminifu katika kazi zako, kwami majaribio ya Allah swt  yako macho sana juu yako.

1218.  Siku ya mwisho ni siku ya Qiyamah na wala si siku ya kufanya kazi.

1219.  Shauku ya uaminifu ni uharibifu mambo mema.

1220.  Upande ulio mgumu wa tendo, ni kuhifadhi utukufu wa jambo.

1221.  Bila ya uaminifu , kazi zote hazitakuwa na thamani yeyote ile.

1222. Itakuwa ni wema iwapo mambo mema yawe rafiki yako na matilaba, adui yako.

1223.  Elimu kiasi kidogo huharibu mienendo na tabia.

1224.  Kazi nyingi zenye tamaa, zitaharibu zingine zote.

1225. Hakuna aheshimiwaye zaidi kuliko wengine ila ni yule mwenye kufanya ibada.

1226.  Hakuna usalama ulio bora kuliko ibada .

1227.  Kumtii Allah swt ni sehemu ya busara ya mtu.

1228.  Ibadi ni pahala palipobora pa kujihifadhia.

1229.  Ibada ni mahala palipo bora pa kujihifadia.

1230.  Kujionesha au kujidai kunaharibu na pia kuighasi ibada.

KUFANYA GHIBA.

1231.  Hakuna uwema au uamnifu katika kufanya ghiba.

1232.   Yeyote yule asikilizaye ghiba basi ndiye mfanya ghiba mwenyewe.

1233.   Yeyote yule awasemae wengineo kwako, ndivyo vivyo hivyo ujue wazi wazi kuwa ndivyo akusemaye wewe kwa wengineo.

KUCHEKA

1234. Kucheka kwa wastani (bila kutoa sauti) ni mcheko ulio bora kuliko vyote.

1235.  Kucheka kwa kupita kiasi kutamharibia mtu heshima yake.

1236.  Kucheka kwa kupita kiasi kunaiuwa bongo.

SIFA

1237.  Majivuno yanadhihaki sifa na pia kuiharibu.

1238.  Uwema na ukarimu kunavuna sifa njema.

1239.  Yeyote yule akusifuaye ndiye akuuae.

MISEMO.

1240.  Utakatifu huambatana na busara.

1241.  Kutoridhika  kwa mtu kutamfutia utulivu.

1242. Saumu ya akili ni kuiepusha kutoka matamanio yote yaliyo maovu.

1243.  Uoga ni kutokana na moyo uliodhoofika na usio na uimara.

1244.  Vitu vinavyotuharibu sisi ni karibu tu tutakavyo ungana navyo.

1245.  Kufuatilia mateso na matatizo yamkabiliayo mtu, yanadhihirisha ukubwa wake na ustahimilivu na uwema wake.

1246.  Yeyote asemaye maneno na misemo ya wale wenye busara, basi ndivyo anavyojivisha utukufu wao.

1247.  Maisha marefu hukutana na matatizo mengi.

1248.  Ardhi ni msafishaji bora.

1249.  Makabiliano ndiyo yanayomsaidia sana mtu.

1250.  Ukweli na mabishano ndiyo yaliyo bora kabisa.

1251.  Mtu ajigambaye basi ndiye ajidhalilishaye yeye nafsi yake.

1252.  Mtu mwenye mafanikio bora kabisa.

1253.  Yeyote yule mwenye kuhofu ndiye abakiaye salama.

1254. Tajiri hasemwi kwa kuongezeka kwa uwema na kuiendeleza subira.

1255.  Uso wenye mcheko (mcheshi) huuepusha kutoka moto wa uadui.

1256.   Kwa kukatalia zawadi ndiko kunamaanisha kutokuwa na shukrani.

1257. Hakuna chochote mbali na kule kufanya Tawbah ila ni kujipunguzia ule mwenendo unaofutilia.

1258.   Usiligeuze tumbo lako likawa ni kaburi la wanyama.

1259.   Ugonjwa ni moja wapo ya aina mbili za kifungo.

1260.   Kuzuzuliwa kwa ghadhabu ni dhambi pia.

1261.  Ndugu huongezea na kufurahikia furaha zetu na hutuondolea na kutuponya yale maumivu tuliyonayo.

1262.  Ubongo (akili) huwa ni mfano wa ghala (stoo) ambayo ilifungwa kabisa na maswali tu ndio zifunguazo kutoka humo.

1263.  Hata kama pazia itaondolewa mbele yangu ,basi hakuna chochote kile kitachoongezeka katika imani yangu.

1264.   Pale Allah swt ampendeleapo Mja wake yeyote,Yeye humshugulisha katika mapenzi yake.

1265.  Nywele za kijivu huelezea kuwa ni hatua ya kuikaribia mauti

BAADHI YA DUA’ ZA IMAM ALI (A.S.)

1265.  Ewe Allah swt,mbariki yule ambaye hazina yake kuu ni imani na silaha zake ni machozi.

1266.  Ewe Allah swt, wewe ni mkuu kabisa kwa kumwangamiza yule  ambaye umeshakwisha kumtukuza hapo awali.

1267.  Sala ni silaha ya mumini.

1268.   Je kuna yeyote yule ambaye anaelewa vyema uwezo wa Allah swt na tena asimwogope Allah  swt?

1269.  Je kuna yeyote akuelewaye vile wewe ulivyo na tena asiwe na khofu yako?

1270. Ewe Allah swt, ngozi hii yangu hafifu, haitaweza kustahimili moto mkali wa Jahannam.

1271. Mishale yote hailengi penye kuheshimiwa na kwa kupatwa na shida na majaribio.

1272. Ewe muumba ,wewe upo pekee mwenye kuheshimiwa na mwenye kudumu daima milele na umelazimishia viumbe vyako kwa kifo na kwa kupatwa na shida na majaribio.

1273.   Ewe muumba, nisamehee madhambi yangu pasipo mimi kujua kwangu .

1274.   Ewe mola , unisamehe madhambi yangu yale ambayo yanayoweza kuniteremshia juu yangu laana na adhabu na ghadhabu zako.

1275.  Ewe mola wangu, nisamehee madhambi yangu yale yanayoweza kuwa sababu ya kuharibu na kuzighasi zile baraka zako zilizo juu yangu.

1276.  Ewe mola, nisamehe madhambi yangu ambayo ndiyo yanayozuia na kuzipoteza ibada zangu kabla ya kukufikia wewe.

1277. Ewe mola wangu, nisamehee madhambi yangu yale ambayo inanikatiza mimi katika imani yangu.

1278. Ewe mola, mimi nakukaribia wewe kupitia kwa kukukumbuka  wewe .

1279. Ewe mola, mimi nakuomba wewe uniweke furaha na niwe nimeridhika na yale  wewe uliyonijaalia maishani mwangu na katika bahati yangu  (kwa ajili yangu).

1280. Ewe mola wewe ni mwepesi  sana wa kubariki na kurehemu, msamehe yule ambaye hana chochote ila ni ibada na sala zako tu. 

1281. Ewe Allah swt !, Je wewe utauachilia Moto uzikumbe nyuso ambazo ziko zimeangukia mbele yako kwa unyenyekevu?

1282.   Ewe Allah  swt, zipatie nguvu mikono na miguu katika kutekeleza wajibu na huduma katika kazi zako.

1283.   Na uzipatie nguvu mbavu zangu ili nipate hali ya kukufikia wewe.

DUA.

1284.  Al Imam Muhammad al-Baquir a.s., Bihar al-Anwaar, J. 91, Uk.6:

“Ewe Mola wetu sisi kwa hamu kubwa utujaalie haki, Serikali ya Kiislam, (ambayo kwa hakika ipo uadilifu serikali ya Al Imam Mahdi Sahibuz-Zamaan a.s., tunamwomba Allah swt atuharakishie kudhihiri kwake). Kwa kupitia hii serikali takatifu, uihamasishe na kuipenda Islam na wafuasi wake ambao na papo hapo kuwadhalilisha unafiki na wanafiki.  Na, katika kipindi hicho utuweke sisi miongoni mwa wale watu wanaowaita wengine katika utiifu wako na kuwaongoza katika njia yako utukufu; na, utujaalie heshima na ukuu katika dunia hii na Akhera.

Aamin Ya Rabbal ‘Alamiin.

 

1285.  Kuna aina nne ya watu:

1286.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amebainisha kuwa:

“Mimi nimetumwa kuja kukamilisha maadili.

1287.  Imenakiliwa kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Moyo ulio msafi- halisi ni ule  ambamo hakuna chochote kile isipokuwa Allah swt  tu”

1288.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambamo twaambiwa:

“Imani ya mtu haitokamilika hadi hapo mimi niwe mpenzi wake kuliko hata baba, mama, watoto wake, mali yake na hata kuliko maisha yake.”

1289.  Allah swt abatuambia katika Qur’an Tukufu, Surah Qaaf, 50, Ayah 33:

“Na anayemuogopa ( Allah swt Mwingi wa kurehemu, na hali ya kuwa humuoni na akaja kwa moyo ulioelekea ( kwa Allah swt).” (50:33)

1290. Qur’an Tukufu, Surah Attaghaabun, 64, Ayah 11,  inatuambia:

“ Haufiki msiba wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na mwenye anayemwamini Allah swt huuongoza moyo wake. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu”

1291.  Amesema Allah swt katika Qur’an Tukufu, Surah Ar-Raa’d, 13, Ayah 28:

“Sikiliza: Kwa kumkumbuka Allah swt nyoyo hutulia.”

1292.  Na vile vile mwishoni mwa Surah al-Fajr, 89, Ayah 28 twaabiwa

“Ewe nafsi yenye kutua”!

“Rudi kwa Mola wako, hali ya utaridhika, na umemridhisha.”

1293.  Allah wt amesema katika Qur'an,Surah, Hajj , 22 , Ayah 32:

Ndio hivyo! Na anayetukuza ibada za Allah swt, anayeziheshimu alama za (dini ya ) Allah swt, basi hili ni jambo la katika utawala wa nyoyo.

1294.  Qur’an Tukufu, Surah Al Hajj, 22, Ayah 54:

“Na ili walio pewa ilimu wajue kuwa hayo ni Haki itokayo kwa Mola wako Mlezi na waiamini, na ili zinyenyekee kwake nyoyo zao. Na hakika Allah swt ndiye anaye waongoa wenye kuamini kwenye Njia iliyo nyooka.”

1295. Allah wt amesema katika Qur'an, Surah, Ash-Shams, 91,   Ayah 9-10:

“Bila shaka amefaulu aliyeyeitakasa (nafsi yake) na bila shaka amejihasiri aliyeiviza (nafsi yake)”  Qur’an Tukufu Tukufu inatuelezea:

Qur’an Tukufu, Surah Al Qiyamah, 75, Ayah 1 – 2:

“Naapa kwa siku ya Qiyamah. Tena naapa kwa nafsi inayojilaumu; (kuwa mtafufuliwa na mtalipwa)”.

1296.  Twaambiwa katika Qur’an Tukufu Surah, Ash-Shams, 91,   Ayah 8:

“ Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake” 

1297.       Qur’an Tukufu, Surah Al Baqara, 2, Ayah 283,  inazungumzia kulipa kwa amana:

“Na atakaeficha basi hakika moyo moyo wake ni wenye kuingia dhambini.”

1298.  Anaelezea Allah swt katika Qur’an Tukufu, Surah Al Kahf, 18, Ayah 28:

“Wala usiwatii wale ambao tumezighafilisha nyoyo zao wakafuata matamanio yao yakawa yamepita mpaka.”

1299.  Allah swt katika Quran: :

“Na watakaokuwa na uzani khafifu, basi hao ndio waliozitia hasarani nafsi zao kwa sababu ya kuzifanyia ujeuri Aya zetu.”

1300.  Amesema Allah swt katika Qur’an Tukufu, Surah Al Hajj, 22, Ayah 46:

“Kwa hakika macho hayapofuki, lakini nyonyo ambazo zimo vifuani ndizo zinapofuka.

1301.  Amesema Allah swt katika Qur’an Tukufu, Surah Al Baqara, 2, Ayah 10:

“Nyoyoni mwao mna maradhi, na Allah swt amewazidishia maradhi.”

1302.   Allah swt anatuambia katika Qur’an Tukufu, Surah Al I’mran, 3, Ayah 7:

“Wale ambao nyoyoni mwao mna upotofu wanafuata zile zinazobabaisha kwa kutaka kuwaharibu watu kutaka na kujua hakika yake vipi........”

1303.  Amesema Allah swt katika Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 13:

“Kwa sababu ya kuvunja agano lao tuliwalaani, na tukazifanya nyoyo zao kuwa ngumu. Wanayabadilisha maneno kutoka pahala pake, na wamesahau sehemu ya yale waliyo kumbushwa. Na huachi kuvumbua khiana kutokana nao, isipo kuwa wachache na miongoni mwao. Basi wasamehe na waache. Hakika Allah swt hawapenda wafanyao wema.”

1304.  Amesema Allah swt katika Qur’an Tukufu, Surah, Al H’adiid, 57, Ayah 16:

“Je! Wakati haujafika bado kwa walio amini zikanyenyekea nyoyo zao kwa kumkumbuka Allah swt na haki iliyo teremka? Wala wasiwe kama walio pewa Kitabu kabla yao, muda wao ukawa mrefu, kwa  Kwa hivyo nyoyo zao zikiwa ngumu, na wengi wao wakawa wapotovu.”

1305.  Amesema Allah swt katika Qur’an Tukufu, Surah At Tawba, 9, Ayah 45:

“Nyoyo zao zina shaka; kwa hivyo wanasitasita kwa ajili ya shaka yao.”

1306.      Amesema Allah swt katika Qur’an Tukufu, Surah Al Mut'ffifiin, 83, Ayah 14:

“Sivyo hivyo! Bali yametia juu ya nyoyo zao (maovu) waliokuwa wakiyachuma.”

1307.  Twaambiwa katika hadith Tukufu kuwa:

“Mtu mwenye furaha kuu katika siku ya Qiyama ni yule atakaye yaona maneno aliyokuwa akiyatamka ‘naomba msamaha wa Allah swt’ chini ya kila dhambi alilolitenda. Kwa hivyo inambidi kila Mwislam miongoni wetu apige msasa kila ovu alilolitenda ama sivyo, Allah swt azitowazo onyo zake za upole zitabadilika na kuwa ghadhabu kubwa sana.

1308.  Qur’an Tukufu, Surah Yusuf, 12, Ayah 53  kuhusu Mtume Yussuf a.s., inazungumziwa Nafsi :

“Nami sijitoi Nafsi yangu; kwa hakika (kila) Nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu”

Amesema Allah swt katika Qur’an Tukufu, Yusuf, 12, Ayah 53: 

“Nami sijitoi Nafsi yangu; kwa hakika (kila) Nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu”

1309.  Amesema al-Imam Muhammad al-Baquir a.s. : Al-Kafi, j. 2,

       uk.330

“Zipo aina tatu za dhuluma:

ZAKA

1310.  Allah swt katika Qur'an Tukufu, Surah al –Tawbah, Ayah

34 – 35 :

Siku (mali yao) yatakapotiwa moto katika moto wa Jahannam , na kwa hayo vikachomwa vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo yao, “Haya ndiyo (yale mali) mliojilimbikia nafsi zenu, basi onjeni (adhabu ya ) yale mliyokuwa mkikusanya.

1311.  Amesema Allah swt katika Qur'an Tukufu, Surah Ali-Imran, 3 , Ayah 180 :

Wala wasione wale ambao wanafanya ubakhili katika yale aliyowapa Allah swt katika fadhila Zake kuwa ni bora kwao. La ni vibaya kwao. Watafungwa kongwa za yale waliyoyafanyia ubakhili – Siku ya Qiyamah.

1312.  Imeandikwa katika Minhaj-us-Sadiqiin kuwa imeelezwa katika Hadith kuwa :

‘Yeyote yule aliyebarikiwa na Allah swt kwa mali na utajiri, lakini kwa sababu za ubakhili wake hakutoa Zaka na malipo mengine yaliyofaradhishwa kwake, basi Siku ya Qiyamah mali hiyo itatokezea kwake katika sura ya nyoka, ambaye atakuwa mwenye sumu kali kwani hatakuwa na unywele wowote juu ya kichwa chake na atakuwa na alama mbili za rangi nyeusi chini ya macho yake na hii ndiyo dalili ya kutambulisha kuwa nyoka huyo ni mkali sana na hatari kabisa. Basi nyoka huyo atajiviringisha shingoni mwa mtu huyo kama mnyororo. Katika hali ya kumsuta, nyoka huyo atasema: ‘Mimi ni mali yako ile ambayo wewe ulikuwa ukijivuna na kujifakharisha duniani.’

1313.  Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema katika Wasail-as Shiah, mlango 3, J.6, Uk. 11:

“Mtu yeyote ambaye hatatoa na kulipa Zaka ya mali yake basi Siku ya Qiyamah Allah swt atamwadhibu kwa miale ya mioto katika sura ya nyoka wakubwa ambao watakuwa wakinyofoa na kula nyama yake hadi hapo hisabu yake itakapokwisha.”

1314.  Vile vile Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema katika Tafsir Minhaj as-Sadiqiin kuwa :

“Iwapo mtu aliye na mali na utajiri atakapoijiwa na ndugu au jamaa yake kwa ajili kuomba msaada kutokea mali na utajiri huo alionao, na yeye kwa sababu ya ubakhili wake akimnyima, basi Allah swt atamtoa nyoka mkubwa kabisa kutokea mioto ya Jahannam ambaye huizungusha ulimi wake mdomoni ili kwamba mtu huyo amwijie ili aweze kujiviringa shingoni mwake kama mnyororo mzito.”

1315.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema katika Wasa’il as-Shiah, Zakat,mlango 3, Hadith 1, J.6, Uk. 11 na Al-Kafi :

“Mtu yeyote anayemiliki dhahabu na fedha na asipotoa Zaka yake iliyofaradhishwa (au Khums, kama vile inavyoelezwa katika Tafsir al-Qummi), basi Allah swt atamfunga kifungo katika mahala pa upweke na atamwekea nyoka mkubwa kabisa ambaye atakuwa amedondosha nywele zake kwa sababu ya sumu kali aliyonayo, na wakati nyoka huyo atakapotaka kumshika basi mtu huyo atakuwa akijarbu sana kukimbia lakini atkaposhindwa hatimaye na atakapotambua kuwa hataweza kujiokoa basi atamnyooshea mikono yake mbele ya nyoka huyo. Lakini nyoka huyo atazitafuna mikono hiyo kama vile anavyotafunwa mtoto mdogo wa ngamia na atajiviringisha shingoni mwake kama mnyororo. Na hapo Allah swt anatuambia kuwa ‘Yeyote yule anayemiliki mifugo, ng’ombe na ngamia na siyetoa Zaka ya mali yake, basi Allah swt Siku ya Qiyamah atamfunga kifungo cha upweke na kila mnyama atamwuma na kila mnyama mwenye meno makali atampasua na yeyote yule ambaye hatoi Zaka kutokea mitende, mizabibu na mazao yake ya kilimo, basi huyo siku ya Qiyamah basi atafungwa shingoni mwake kwa mnyororo wenye urefu wa takriban magorofa saba.”

1316.  Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema katika Wasa’il as-Shiah Mlango 3, J.6, Uk.11 :

“Allah swt amefaradhisha Zaka pamoja na Sala. Ameamrisha kutekeleza Sala na kutoa Zaka hivyo iwapo mtu atasali bila ya kutoa Zaka, basi atakuwa hakukamilisha Sala.”

1317. Vile vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. Wasa’il as-Shiah, Zakat,mlango 3, Hadith 13, J.6, Uk. 11: amesema kuwa :

“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliingia katika Masjid an-Nabawi, na aliwataja watu watano kwa majina yao na akasema kuwa inukeni na mtoke humu Msikitini na wala msisali kwani nyinyi hamutoi Zaka.

(Wasiolipa Zaka wamefukuzwa kutoka Msikitini !)

1318. Vile vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema katika Wasa’il as-Shiah, ZAKAT,mlango 3, Hadith 24, J.6, Uk 14 :

“Mtu yeyote asiyelipa Zaka ya mali yake basi yeye wakati wa mauti yake atataka kurudishwa humu duniani ili aweze kutoa na kulipa Zaka, kama vile Allah swt anatuambia: ‘Ewe Allah swt nirudishe tena ili nikafanye mema niliyokuwa nimeyaacha !’ Yaani wakati wa kifo chake atasema kuwa arudishwe humu duniani ili akaitumie mali aliyoilimbikiza katika njia njema, lakini atajibiwa kuwa kamwe haitawezekana hivyo kurudi kwake.”

1319. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameelezea tafsir ya Ayah isemayo kuwa : ‘Allah swt atawaonyesha matendo yao katika hali ya kusikitisha mno kuwa wao hawatatoka nje ya Jahannam’ kama ifuatavyo katika Wasa’il as-Shiah,mlango 5, Hadith 5, J.6, Uk 21 :

“Mtu yule ambaye anakusanya na kulimbikiza mali yake na anafanya ubakhili katika kuitumia katika mambo mema na kwa kutoa zaka n.k., basi anapokufa huku amewaachia mali hiyo wale ambao watatumia mali hiyo katika utiifu wa Allah swt au kwa kutenda madhambi, basi iwapo itatumiwa katika utiifu wa Allah swt basi atakuwa mtu wa kujivuna na iwapo itatumiwa katika maasi na madhambi basi itamdhalilisha.”

1320. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema, Wasa’il as-Shiah,mlango 5, Hadith 5, J.6, Uk21 :

“Hakuna kitu kinachokimaliza Islam kama Ubakhili na njia ya Ubakhili ni sawa na njia ya sisimizi ambayo haionekani na yenyewe ipo kama Shirk ambayo inayo aina nyingi.”

1321. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib  a.s. amesema katika Safinat al-Bihar, J.1 Uk. 155 :

“Watu watakapokataa kutoa Zaka, basi baraka itakuwa imeondolewa kutoka ardhini kwa kutoa mazao na matunda kutoka mashamba yao,na madini.”

1322.  Vile vile Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema katika Wasa’il as-Shiah, Mlango 1, Hadith  13 :

“Muwatibu wagonjwa wenu kwa kutoa Sadaka na mutokomeze balaa, maafa kwa Du’a na muhifadhi mali zenu kwa kutoa Zaka.”

1323.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema Wasa’il as-Shiah,mlango 5, Hadith 10, J.6, Uk23 :

“Allah swt anazo mahala pengi humu ardhini ambazo huitwa ‘kilipiza  kisasi’ hivyo Allah swt anapomjaalia mtu mali na utajiri, na huyo mtu haitumii kwa kutoa malipo aliyofaradhishiwa, basi huwekewa nafasi mahala hapo. Mali ambayo anakusanya kwa mbinu zake zote,inapomtoka na anaiachia wengine.”

1324. Zipo riwaya nyingi ambazo zinazumngumzia kukufurishwa kwa mtu asiyetoa Zaka kwa sababu za ubakhili wake. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.amesema katika Wasa’il as-Shiah,mlango 4, Hadith 2, J.6, Uk 18 :

“Bila shaka Allah swt amewawekea hisa mafukara na wenye shida katika mali za matajiri ambayo imefaradhishwa. Faradhi ambayo inapotimizwa inakuwa ni yenye kuwafakharisha matajiri hao na ni kwa sababu ya kutoa huko Zaka kunakoharamisha kumwagwa damu yao na wanaolipa zaka wanaitwa Waislamu.”

1325. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, Wasa’il as-Shiah,, J.6, Uk 18 :

“Mtu yeyote yule ambaye hatatoa Zaka hata lau kwa kiasi cha Qirat (1.20 Dinar yaani punje nne za Shayiri) basi huyo si Mumin wala si Mwislamu na watu kama hawa ndivyo alivyoelezea Allah swt  kuwa watakuwa wakitaka warudishwe humu duniani ili watekeleze

mema.”

1326.  Vile vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameeleza katika Wasa’il as-Shiah,, J.6, Uk 18:

“Mtu yeyote yule ambaye hatatoa Zaka hata kwa kiasi cha Qirat moja (sawa na punje nne za Shayiri) basi huyo atakuwa  bila imani na kufa kwa mauti ya Myahudi au Mnasara.”

1327.  Amesema vile vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. katika Wasa’il as-Shiah, Zakat, mlango 3, Hadith 1, J.6, Uk. 19 na  Kafi :

“Allah swt ameruhusu kumwagwa damu ya watu wa aina mbili ambapo hukumu hii itatekelezwa pale atakapodhihiri Al-Imam Muhammad Mahdi, Sahibuz-Zamaan, a.s. na hivyo mmoja miongoni mwa watu hao wawili ni yule anayefanya zinaa ilhali anayo mke wake hivyo atauawa kwa kupigwa mawe hadi kufa kwake na wa pili ni yule asiyetoa Zaka, huyo atakatwa kichwa.”

1328.  Vile vile amesema, katika Wasa’il as-Shiah,mlango 5, Hadith 8, J.6, Uk 20 :

“Mali haipotei katika majangwa na Baharini isipokuwa ile isiyolipiwa Zaka na atakapodhihiri Al-Imam Muhammad Mahdi, Sahibuz-Zamaan, a.s. basi wale wote wasiolipa Zaka watasakwa na kukamtwa na watakatwa shingo zao.”

1329. Amesema Allah swt katika Quran: Surah al –Fussilat, 41, Ayah

6–8 : 

“Ole wao wanaomshirikisha, ambao hawatoi Zaka na wanaikataa Aakhera.” 

1330. Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. , katika  Al-mustadrak:

“Kwa kiapo cha Allah swt ambaye anayo roho ya Mtume Wake katika kudura yake, kuwa hakuna mtu anayemfanyia khiana Allah swt isipokuwa Mushrikina kama hawa ambao hawatoi Zaka kutoka mali zao.”

1331. Vile vile Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwambia Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s., katika Al-Khisal, Uk. 450, Mlango Kumi :

“Ya Ali ! Katika Ummah wangu wapo makafiri wa makundi kumi :

Mfitini na mchonganishi

Mchawi

Dayyuth yaani mwanamme yule ambaye anajua kuwa mke wake anazini lakini hajali bali anapuuzia,

Mwanamme yule ambaye anauroho wa kiharamu wa kutafuta wanawake mbalimbal kwa kulawiti,

Anayewalawiti wanyama 

Anayezini pamoja na wale walioharamishwa kwake yaani ambao ni mahram kwake,

Anayechochea na kuzidisha moto wa fitina na chuki miongoni mwa watu, 

Anayewasaidia makafiri kihali na mali kupigana dhidi ya Waislamu,

Asiyetoa Zaka

Asiye Hijji ilhali ana uwezo kamili na kutimiza masharti yake na akifa katika hali hiyo.”

rudi nyuma Yaliyomo endelea