rudi nyuma Yaliyomo endelea

Kwa hayo Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. alinijibu:

“Kwa hakika wewe umeniuliza swala kubwa sana, ingawaje umeniuliza kwa kifupi sana. Kwa kiapo cha Allah swt mimi ninakujibu kuhusu dini yangu na dini ya mababu zangu kupitia huyo tunavyomwabudu Allah swt. Nayo ni:

‘Kwa kukiri imani yetu kuwa hakuna Allah swt mwingine isipokuwa ni Allah swt, na kwamba Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w. ni Mtume wa Allah swt, na kusadiki kuwa chochote kile kilichomteremkia yeye (Qur'an Tukufu) ni kutoka kwa Allah swt, na kuwa na mapenzi (yetu) ya wapenzi wetu na watiifu kwetu (Ahlul Bayt a.s.) na kuwachukia maadui wetu, kujisalimisha kwa njia yetu, na kumsuburi Al Qaim a.s. (Imam wa kumi na mbili ambaye atadhihiri pale itakapotokea amri ya Allah swt), na kutaka (kudumisha yale yaliyofaradhishwa na mambo yaliyo halalishwa) na kwa kuwa mcha Allah swt halisi (kwa kujiepusha na yale yote ambayo ni haramu).

984.     Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema, Yaumul-Khalas, Uk. 269:

“Atakapo dhihiri Al Qaim a.s., basi mikono yake itakuwa juu ya vichwa vya waumini, naye atawapa maendeleo ya kiakili na kukamilisha subira yao na kile wanacho kiangalia mbele. Baada ya hapo Allah swt ataongezea nuru yao macho na uwezo mkubwa wa kusikiliza ili kwamba kamwe kusitokezee vizuizi baina yao na Al Qaim a.s. pale atakapo amua kuongea nao, na watakapomsikiliza, wataweza kumwona ilhali atakuwa mahala pake.”

985.     Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., amesema  Bihar al-Anwaar,

J. 52, Uk. 391:

“Wakati wa Al Qaim a.s. muumin atakaye kuwa mashariki ataweza kumwona muumin mwenzake aliye magharibi, na vivyo hivyo muumin aliye magharibi ataweza kumwona muumini aliye mashariki.

Tanbih.

Ndugu msomaji ! Kwa hakika sasa hivi tunayo ala za mawasiliano mbalimbali kama vile Satellite, Television yafuatayo ambayo yanaweza kuwa yenye manufaa makubwa kwetu ili kuwaza kuangalia vyema na kuelewa hiyo riwaya vitu ambavyo havikuwapo wakati maneno matukufu ya riwaya hiyo yalipokuwa yakisemwa.

986.     Al Imam Muhammad al-Baquir a.s., amesema Bihar al-Anwaar, J. 53, Uk. 7:

“Huyu Al Imam Mahdi Sahibuz-Zamaan a.s. atakuwapo mahala ambapo ni karibu na Al Ka’aba Tukufu baina ya nguzo na nafasi ya kusimamia ya Mtume Ibahim a.s. na atatoa mwito, atakapo kuwa akisema:

‘Enyi watu wangu hasa ambao Allah swt amewawekeni kwa kuwatayarisha nyinyi kwa ya furaha ya kudhihiri kwangu juu ya ardhi hii ! Njooni kwangu kwa utiifu. Na kwa hakika kauli hii itawafikia wale wote watakapokuwa nafasi wanaposalia na hata kama watakuwa vitandani wakiwa mashariki ya ardhi au magharibi yake. Na watamsikiliza kwa mwito wake huo mmoja tu ambayo yatafikia kila sikio la kila mtu, nao watajitayarisha kwa ajili ya kuja kwake. Kwa hakika haitawachukua muda wowote isipokuwa pumzi tu kiasi kidogo kukusanyika hapo baina ya mlingoti na nafasi ya kusimama ya Mtume Mtume Ibahim a.s., wakimwitikia Al Imam Mahdi Sahibuz-Zamaan a.s.’”

987.     Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimwambia mfuasi wake aliyekuwa halisi, Mufadhdhal, mambo fulani kutokea kisa cha Al Imam Muhammad al-Mahdi Sahibuz-Zamaan a.s. na kudhihiri kwake,

“Ewe Mufadhdhal ! Waambie wafuasi wetu habari za Al-Mahdi ili wasiwe na shaka katika Dini yao.”

Bihar-ul-Anwaar, J. 53, Uk. 6.

988.     Al Imam Mahdi Sahibuz-Zamaan a.s., amesema Kamal-ud-Din, Uk. 445:

“Mimi ni Al Mahdi na mimi ni yule ambaye bado nipo hai na ambaye nitaijaza ulimwengu kwa haki na uadilifu kama vile ilivyojazwa kwa maovu na dhuluma.

Kwa hakika ardhi haitabakia bila ya kuwa na mbashiri, na watu kamwe hawataisha bila ya kuwa na kiongozi. Na hii ni amana na hivyo msiwaambie wote wale Waislam wenzenu isipokuwa wawe ni watu wa Allah swt (wawe katika haki).”

989.     Al Imam Mahdi Sahibuz-Zamaan a.s. amesema, Kamal-ud-Din, Uk. 484:

“Kwa mambo yanayotokea kwa Waislam, murejee katika riwaya zetu, ( yaani Wanazuoni au Ma’ulamaa), kwa sababu wao ndio wawakilishi wangu kwenu na mimi ni Hujjatullah juu yao.”

990.     Al Imam Mahdi Sahibuz-Zamaan a.s. alimwandikia barua Sheikh Al Mufid, Bihar al-Anwaar, J. 53, Uk. 175:

“Sisi tunaelewa hali yako na mazingara yako na hakuna jambo lolote lako lililojificha kwetu sisi.”

991.     Al Imam Mahdi Sahibuz-Zamaan a.s. alimwandikia barua Sheikh Al Mufid, Bihar al-Anwaar, J. 53, Uk. 175:

“Si kwamba sisi hatukujali wewe au tumekusahau, kwa sababu kama ingekuwa hivyo, matatizo na balaa zingekuwa zimekuondokea wewe na maadui wako wangekuwa wameisha kumaliza. Hivyo, muogope Allah swt na uwe mtiifu kwake, asifiwe Allah Jalli Jalalahu.”

Dua :

Tunamwomba Allah swt aharakishe kudhihiri kwa Imam wetu wa kumi na mbili Al Imam Mahdi Sahibuz-Zamaan a.s. ili aweze kudumisha usawa, ukweli, na haki katika ulimwengu mzima.  Amina.

UMMA WA WAISLAM KATIKA ZAMA ZA MWISHO.

992.         Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w., amesema Waqayi-ul-Ayyam, Uk. 439:

“Kutakuja zama kutakuja wakati katika zama miongoni mwa watu kuwa:

Wao hawatawaheshimu Wanazuoni wao (yaani Maulamaa) ila kwa mavazi yao mazuri;

wao hawatasikiliza Qur'an Tukufu ila kwa sauti ya kuvutia;

Na wao hawatamwabudu Allah swt isipokuwa katika mwezi wa Ramadhani tu;

 wanawake wao hawatakuwa na aibu,

maskini miongoni mwao hawatakuwa na subira, na

matajiri wao hawatakuwa wakarimu, kwani wao hawataridhirika kwa kidogo na wala hawatakinai kwa wingi.

Wao hawatashiba kwa kingi, wao watafanya kila jitihada kwa ajili ya matumbo yao;

 dini yao itakuwa ni mapesa (mali na utajiri); na

 wake zao ndio watakuwa Qiblah zao (tunapoelekea kusali huko Al-Ka’abah tukufu); na

majumba yao ndio itakuwa Misikiti yao;

wao watakimbia kutoka Maulamaa wao kama vile kondoo anavyo kimbia kutoka kwa mbwa mwitu.

Hapo watapokuwa kama hivyo (basi Allah swt atawatumbukiza katika mambo matatu). 

Atawaondolea baraka katika mali zao.

Watatawaliwa na mtawala dhalimu.

Watakufa (kutoka humu duniani) wakiwa hawana imani iliyo halisi.”

993.         Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w. amesema, Bihar al-Anwaar, J. 23, Uk. 22:

“Utafika wakati katika umma wangu kwamba :

watawala wao watakuwa wakatili na wadhalimu,

Maulamaa na Wanazuoni wao watakuwa waroho wa mali na utajiri na watakuwa na imani kidogo,

waumini wao watakuwa ni wanafiki,

wafanya biashara wao watakuwa wakijishughulisha kwa kutoa na kupokea riba na kuficha maovu na kasoro ya vitu wanavyonunua na kuuza na

wanawake wao watakuwa wamejihusisha mno na mambo ya kujirembesha ya dunia. 

Hivyo, wakati huo,

mwovu kuliko wote miongoni mwao ndio watakaokuwa wakiwaongoza wao, na

wema miongoni mwao watakuwa wakiwaita watu lakini hakuna mtu atakaye wajibu.”

994.         Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w., amesema Al-Ithna-'Asheriyyah, Uk. 202:

“Utafika wakati katika Umma wangu ambapo wao watakuwa wakipenda vitu vitano na kuvisahau vitu vitano:

Wao watakuwa wakiipenda dunia na kuipuuzia Akhera.

Wao watapenda mali na kusahau hesabu ya siku ya Qiyamah

Waume zao watawapenda wanawake waovu na kuwasahau Hur al-‘Ayn

Wao watapenda majumba na watayasahau makaburi yao.

Wao watajipenda wenyewe kupita kiasi na kumsahau muumba wao.

Kwa hakika watu kama hawa hawanipendi mimi na mimi pia siwapendi wao.”

UMRI WETU TUUTUMIE VYEMA.

995.         Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w. alimwambia Abu Dhar, Bihar al-Anwaar, J. 77, Uk. 77:

“Ewe Aba Dhar ! Faidi vitu vitano kabla ya vitu vitano:

Ujana kabla ya uzee,

Siha yako kabla ya magonjwa,

Utajiri wako kabla ya umaskini,

Ufaragha wako kabla hujawa mashughuli, na

 maisha yako kabla ya kifo chako.”

996.     Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., amesema Ghurar-ul-Hikam, 

Uk. 257:

“Itakapofika siku ya Qiyamah,  kikundi cha watu kitasimama na kuja kubisha hodi katika mlango wa Jannat. Nao wataulizwa ni nani wao, nao watajibu: Sisi ni watu wa subira na kwa hayo wataulizwa ni kitu gani walichokifanyia subira, nao watajibu sisi tumefanya subira kwa ajili ya Allah swt dhidi ya kumwasi Allah swt. Kwa hivyo Allah swt atasema kuwa hao ni wasema ukweli na atawaruhusu waingie Jannat. Kwani Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu:

Sura Az-Zumar, 39, Ayah 10:

‘Sema: Enyi waja wangu mlio amini ! Mcheni Mola wenu Mlezi. Wale wafanyao wema katika dunia hii watapata wema. Na ardhi ya Allah swt  ni kunjufu. Hakika wenye subira watapewa ujira wao bila ya hisabu.’”

997.     Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., amesema Ghurar-ul-Hikam, Uk. 206:

“Aliye na furaha ni yule ambaye hana matamanio na matarajio makubwa katika maisha yake na anafaidi kila fursa anayoipata.”

DINI NA KUSOMEA MAMBO YAKE.

998.         Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w. amesema, Bihar al-Anwaar, J. 1, Uk. 176:

“Ole wake yule Mwislam ambaye habakizi siku moja katika juma zima kwa ajili ya kujifunza masuala ya dini yake na wala kujaribu kufanya uchunguzi na utafiti wa dini yake.”

999.         Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w., amesema Al-Muhajjat-ul-Baidha, J. 1, Uk. 15:

“Yeyote yule anayesomea dini ya Allah swt, basi kwa hakika ana uwezo mkubwa wa kuondoa matatizo yake na kumpatia yeye riziki kutokea mahala ambapo yeye alikuwa hata hajaweza kuwazia.”

1000.   Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema Bihar al-Anwaar,

J. 1, Uk. 214:

“(Vijana wa Kish’ia lazima wawe na program au utaratibu wa kujifunza masuala ya dini). Mimi ninapomwona kijana wa Kishi’a ambaye hana program au utaratibu kama huu basi mimi nitamfundisha somo.”

1001.   Al Imam Muhammad al-Baquir a.s., amesema Bihar al-Anwaar, J. 2, Uk. 29:

“Wajulishe wafuasi wetu kuwa kwa hakika bila shaka wao watakuwa miongoni mwa wale watakao okoka siku ya Qiyamah kwa masharti iwapo wao watakuwa watimizaji wa yale wanayo amrishwa.”

1002.         Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema, Bihar al-Anwaar, J. 2, Uk. 153:

“Yeyote yule kutokea Ummah wangu atakaye hifdhi ( kariri ) hadithi arobaini ambazo zinahitajiwa na watu katika maisha yao ya kidini (kwa ajili ya Tabligh na muongozo), basi Allah swt atamwinua akiwa hakimu kutoka waliokufa Siku ya Qiyamah.”

UPOLE NA MATOKEO YAKE MAZURI

1003.         Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ,Bihar al-Anwaar, J. 71, Uk. 373:

“Kwa hakika mja anaweza kujipatia daraja la yule anayefunga saumu katika nyakati za mchana na anayesali usiku kucha, kwa tabia zake nzuri za upole.”

1004.   Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alimwambia mtoto wake Al Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. ,Bihar al-Anwaar, J. 78,

Uk. 111:

“Ewe Mwanangu !

Hakuna utajiri uliona thamani kuliko akili na

hakuna umasikini uliosawa na ujahili;

hakuna ugaidi ulio mbaya kabisa kama kiburi,na

hakuna maisha yenye raha kuliko kuwa mpole.”

1005.   Al Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema, Khisal-i-Sadduq, Uk. 29:

“Kwa hakika, bora ya bora zote ni tabia njema.”

1006.   Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema, Bihar al-Anwaar,

J. 71, Uk. 394:

“Tabia njema ipo katika njia tatu:

Kujiepusha na vitu vilivyo haramishwa,

kutafuta yale yaliyo halalishwa, na

kutendea haki wana nyumba wake.”

1007.   Al Imam Zaynul 'Abediin a.s., amesema Khisal-i-Sadduq, Uk. 317:

“Kauli njema huongezea mali, utajiri, na riziki, na huahirisha ajali, na hutengeneza mapenzi miongoni mwa wenye nyumba, na humfanya mtu akaingia Jannat.”

1008.   Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, Al-Kafi, J. 2, Uk. 103:

“Yapo mambo matatu ambayo yeyote yule atakayezifikisha kwa Allah swt, basi Allah swt atamfaradhishia Jannat kwa ajili yake:

Kutoa mchango katika umaskini,

desturi nzuri pamoja na watu wote, na

 kujitendea haki nafsi yake.”

1009.         Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w.amesema, Al-Kafi, J. 2, Uk, 100:

“Kwa mambo ambayo umma wangu utajipatia Jannat ni hasa kwa mema yote, na desturi nzuri.”

ATHARI MBAYA ZA HASIRA NA TABIA MBAYA.

1010.            Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w.amesema, Al-Kafi, J. 2, Uk. 302:

“Hasira inaiharibu imani kama vile siki(huwa chachu) inavyoharibu asali.”

1011.   Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, Al-Kafi, J. 2, Uk. 303:

“Ghadhabu ni ufunguo wa kila aina ya shari.”

1012.   Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amenakili kutoka kwa mzazi wake a.s. ambaye amenakili kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ambaye Amesema kuwa, Bihar al-Anwaar, J. 75, Uk. 27:

“Mtu mmoja alimwijia Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w. ili afundishwe tendo ambalo litaondoa kizuizi baina yake na Jannat.

Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w. alimwambia:

Usiwe mkali;

usiwaombe watu vitu,

watakie watu kile ujitakiacho wewe mwenyewe.”

1013.   Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, Al-Kafi, J. 2, Uk. 303:

“Yeyote yule anayezuia ghadhabu zake, basi Allah swt atazificha siri zake.”

1014.   Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema  Al-Kafi, J. 2, Uk. 303:

“Ghadhabu ni kitu kinacho teketeza moyo wa hakimu; kwani yeyote yule asiyeweza kudhibiti vyema ghadhabu yake basi kamwe hawezi kuitumia busara yake.”

KUOMBA TAWBA YA Allah swt.

1015.   Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., amesema Bihar al-Anwaar, J. 6, Uk. 22 :

“Mjipake manukato ya Istighfar ili hata tone na mabaki ya madhambi yenu yasiwadhalilishe nyie.”  

1016.   Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alimfundisha mtu mmoja kwa kumwomba Allah swt dua kwa kumwambia, Bihar al-Anwaar,

J. 94, Uk. 242 :

“Sifa zote ni za Allah swt kwa kila neema; na mimi ninamwomba kila la kheri na kila la wema; na naomba Allah swt aniepushe na kila aina ya shari; na ninamwomba Allah swt msamaha kwa madhambi yote.”

1017.   Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa, Khisal-i-Sadduq, Uk. 317:

“Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w. aliulizwa kuwa bora wa waja ni nani, naye alijibu:    Wao ni:

1018.   Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., amesema Makarim-ul-Akhlaq, Uk. 313:

“Anapozidisha muumin Mwislam kwa kuomba Istighfar ya Allah swt, basi rikodi ya matendo yake mema yataongezeka na yatakuwa yaking’ara.”

SALAA YA JAMA’A.

1019.         Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.,amesema Bihar al-Anwaar, J. 88, Uk. 4:

“Allah swt huheshimu sana yule mja anayesali sala kwa Jama’a na baada yake anapoomba kitu chochote basi Allah swt lazima humtimizia.”

1020.   Al Imam Musa al-Kadhim a.s., amesema Bihar al-Anwaar,

J. 88, Uk. 4 na Wasa'il ush-Shi'ah, J. 8, Uk. 290:

“Fadhila za sala ya Jama’a kwa sala ya mtu anayesali peke yake ni kila raka’a moja katika Jama’a ni bora kuliko raka’a elfu moja (1000) zinazosaliwa na mtu peke yake.”

1021.         Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., amesema Mustadrak-ul-Wasa'il, J. 6, Uk. 446:

“Sala moja ya mtu katika Jama’a ni bora kuliko sala za miaka arobaini anazosali akiwa nyumbani kwake (peke yake).”

1022.         Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w.amesema, Bihar al-Anwaar, J. 88, Uk. 6:

“Safu ya mistari katika sala ya Jama’a inayosaliwa juu ya ardhi ni sawa na safu za Malaika huko mbinguni; na Raka’a moja inayosaliwa katika Jama’a ni sawa na Raka’a ishirini na nne na kila raka’a moja inayosaliwa na wapenzi wa Allah swt kuliko sala za miaka arobaini. Hivyo, siku ya Qiyamah ambayo ni siku ya uadilifu wakati Allah swt atakapo wakutanisha wanaadamu wote kuanzia mwanzoni hadi mwisho, basi hakutabakia na muumin yeyote ambaye amesali sala ya Jama’a, kwamba Allah swt atampunguzia shida zake za siku ya Qiyamah na ataambiwa aingie Jannat.”

1023.         Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w. siku moja aliijiwa na Kipofu mmoja ambaye alisema, At-Tahdhib, J. 3, Uk. 266:

“Kulikuwa hakuna mtu yeyote wa kumchukua Msikitini ili aweze kushiriki katika sala ya Jama’a pamoja na Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w. pale aliposikia Adhana ikitolewa.

Hapo Mtume Muhammad  Mustafa s.a.w.w. alimwambia:

“Funga kamba kutoka nyumbani kwako hadi Msikitini na ushiriki katika sala ya Jama’a.”

1024.   Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema, Bihar al-Anwaar, J. 88, Uk. 11:

“Mtu yeyote ambaye anaiacha sala ya Jama’a bila ya kuwa na Udhuri inayokubalika bali bila sababu yoyote, kwa misingi ya kutotaka kushiriki katika mkusanyiko wa Waislam, basi atakuwa hana Sala yoyote.”

1025.   Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s., amesema Bihar al-Anwaar, J. 88, Uk. 12:

“Kwa hakika sala ya Jama’a imefaradhishwa ili kuwepo imani halisi katika umoja, katika Islam, na katika kumwabudu Allah swt kiwazi wazina ambayo imedhihirishwa kuwa bayana, kwa sababu, ili iweze kuwadhihirikia watu wa mashariki na wa magharibi (wa dunia hii).

Hivyo ukweli na asili wa Uislam utadhihirika na kujulikana na makafiri na mapagani kabla ya Uislam utakuwa ni kama kiza mbele ya nuru, kiza ambacho hatimaye kinapotea.

Vile vile sala ya Jama’a husababisha watu kutambuana na kuelewana na inawezekana wengine wakawa mashahidi kuhusu wengineo kuhusu Uislam wao, ambamo kuna uwezekano na vile vile kushirikiana katika mambo mema na ya kumfurahisha Allah swt mambo ambayo yanawazuia wasimuasi Allah swt kupita kiasi.”

NEEMA NNE ZA ALLAH swt

1026.   Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Amesema kuwa kila asubuhi, kila Mwislamu anatakiwa azikumbuke neema nne za Allah swt.  Hofu yangu ni kwamba asipozikumbuka, kuna hatari ya kuzipoteza neema hizo:

·   Namshukuru Allah swt ambaye amenisaidia kumtambua Yeye na hakuuacha moyo wangu gizani.

·   Namshukuru Allah swt ambaye ameniweka pamoja na wafuasi wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.

·   Namshukuru Allah swt ambaye ameiweka riziki yangu kwake Yeye na si mikononi  mwa watu.

·   Namshukuru Allah swt ambaye amezifunika dhambi zangu na aibu zangu na hakunidhalilisha mbele ya watu.

1027.  Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.,Nur al-Absaar

Shablanji.

“Mwovu wa watu ni yule anayewawekea pingamizi na anakuwa mkali kwa watu wake wa nyumbani.”

1028.   Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu :

“Enyi mlioamini! Ingieni katika hukumu za Uislamu zote, wala msifuate vyayo za Shaytani;  kwa hakika yeye kwenu ni adui dhahiri.”

SIFA ZA KUPENDEZA ZA MWANAMKE

1029.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., amesema Wasa'il

ush-Shi'ah,Vo. 20, Uk.172

“Malipo ya mwanamke mcha Allah swt kwa kumpa mume wake bilauri moja ya maji ni zaidi ya kufanya ibada mwaka mzima ambamo mchana anafunga saumu na usiku zake anakesha katika kufanya ibada.”

1030.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., amesema Al-Kafi, J.5,

Uk. 508:

“Ni kwa mwanamke kujiweka msafi kabisa kwa kujipaka manukato bora kabisa na kuvaa mapambo ambayo yatamfanya yeye amvutie bwana wake na ajiweke tayari kwa ajili ya bwana wake usiku na mchana.” [74]

1031. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., amesema Nahjul Balagha,

Msemo 494:

“Jihadi ya mwanamke (vita katika njia ya Allah swt ) ni kuwa na uhusiano mwema na kuwa mshiriki wa bwana wake.”

1032. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., amesema Usuli kafi, J. 5,

Uk. 327

“Iwapo ningetaka kukusanya mema yote ya dunia hii na Aakhera kwa ajili ya Mumin basi mimi ningeziweka kwa ajili ya

moyo mnyenyekevu,

 ulimi wenye shukurani na isemayo mema,

mwili ufanyao subira wakati wa shida na dhiki.

(Kwa ajili ya mwanamme Mimi ningempa) Mke mcha-Allah swt ili anapouona uso wake anajawa na furaha na yeye (mwanamke) anaihifadhi na kulinda mali yake, pale bwana wake anapokuwa hayupo.”

1033. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., amesema Bihar al-Anwaar, J.103, Uk. 252

“Amelaaniwa! Amelaaniwa kabisa mwanamke yule ambaye anautonesha moyo wa mume wake na kumfanya akasirike.

Lakini amebahatika kabisa mwanamke yule ambaye anamheshimu bwana wake wala hamghadhabishi na huwa mtiifu kwa bwana wake.”

1034.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema Bihar al-Anwaar,

J.103, Uk. 235

“Bora ya mwanamke ni yule anayezaa, mvutiaji kimapenzi, mtunza siri zenu, na mcha-Allah swt. Na humtii bwana wake na hupendwa na Jama’a na ndugu zake. Pale anapokuwa pamoja na bwana wake, anamwonyesha urembo na mavazi yake ambayo kwa hakika huyaficha kwa ajili ya wanaume wengine isipokuwa mume wake tu.

Kwa hakika huwa msikivu na mnyenyekevu kwa mazungumzo yake na huzitii amri zake. Pale anapokuwa faragha anavaa vizuri kabisa na kutimiza mahitaji ya bwana wake kutoka kwake. Daima huwa anakuwa amevaa vizuri na kujirembesha kwa ajili ya bwana wake tu na kamwe huwa si mtu aliyejisahau kwa ajili ya bwana wake            ( hujiweka tayari kwa ajili ya bwana wake.).”

1035. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., amesema Bihar al-Anwaar,

J.104, Uk. 98:

“Kutokea kwa furaha ya mwanamme Mwislamu ni kwamba

ana mke mcha-Allah swt na

nyumba kubwa ya kukidhi wananyumba,

 usafiri mzuri na

watoto wema.”

1036.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema

“Vita vya Jihad kwa ajili ya mwanamke ni kuwa na uhusiano na kuwa mwema kwa mume wake na haki za mwanamme kwa mke wake ni zaidi ya haki za wote juu yake.”

1037.  Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu Surah Al-Baqara, 2,

Ayah ya 231:

Na mtakapo wapa wanawake talaka, nao wakafikia kumaliza eda yao,  basi warejeeni kwa wema au waachilieni kwa wema. Wala msiwarejee kwa kuwadhuru mkafanya uadui. Na atakayefanya hivyo, amejidhulumu nafsi yake. Wala msizichukulie Aya za Allah swt kwa maskhara. Na kumbukeni neema ya Allah swt juu yenu, na aliyo kuteremshieni katika Kitabu na hikima anachokuonyeni kwacho. Na mcheni Allah swt , na jueni kwamba hakika Allah swt ni Mjuzi wa kila kitu.

1038. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., amesema Wasa'il ush-Shi'ah,

J.22, uk.9:

“Muoe na wala msitoe talaqa kwa sababu ‘Arshi Ilahi hutetemeka kwa talaka.”

1039.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., amesema  Al-Kafi, J. 6, Uk. 54

“Allah swt hufurahishwa mno kwa nyumba ile ambamo harusi huwapo na hughadhabishwa kwa nyumba ile ambamo huwa na talaka. Na hakuna kinachomkerehesha Allah swt kama talaka.”

SEMI ZA IMAM ALI IBN ABI TALIB a.s.

UADILIFU.

1040.  Taji la mfalme ni uadilifu wake mwenyewe.

1041.  Utatawala iwapo nawe utakuwa mwadilifu.

1042.  Uadilifu huangamiza ulafi , uroho na tamaa.

1043. Ngome ya Utukufu (ya Allah swt) huikinga nchi yenye mtawala mwadilifu.

SHURUTISHO NA SHARI

1044.  Kulazimisha/Kushurutisha kunaifanya akili iwe kipofu.

1045.  Shari kunamfanya mtu awe mwoga wa uadilifu (ataiongopea)

1046.  Uchokozi ni hatua ya kukaribia maangamizi.

1047.  Kinachodhulumu haki ni kule kusaidia vilivyo batilifu.

1048.  Udhalimu kwa mwenye dhiki ni dhuluma kubwa kuliko zote zile.

1049.  Allah swt huharakisha kuanguka kwa wachokozi.

1050.  Ushidi wa mshari ni kushindwa kwa nafsi yake.

1051.             Kustarehe humu duniani kwa fidia ya akhera ni kujidhulumu nafsi yako.

1052.             Kuwakandamiza yatima na wajane kunaleta magonjwa na kupotea kwa ne’ema.

ULIMI NA USEMI:

1053.  Mtu amehifadhika chini ya ulimi wake.

1054.  Ulimi mtamu/mzuri hupata marafiki wengi.

1055. Ulimi wako utasema kile kilichozoeshwa. (Kwa hivyo jihadhari kabla ya kusema).

1056.   Akili ni busara. Akili ya mpumbavu ipo chini ya ulimi  wake(anasema kabla ya kufikiri).

1057.  Ulimi ni mkalimani wa akili.

1058.  Ulimi wa mtu ni uzani wake mwenyewe.

1059.  Ulimi unaathari za kuchoma zaidi ya mkuki.

1060.  Usemi wa kweli ni ulimi mtukufu.

1061.  Jihadhari na ulimi, kwani ni sawa na mshale unaoweza kufyatuka  kutoka upinde.

1062.   Mtu bila kusema (ulimi useme mema na kukataza mabaya) ni ama sanamu au mnyama.

1063. Ulimi  wa mwenye busara ipo akilini mwake (huongea na akili yake na hufikiria zaidi na kusema kwa uchache kwani ni yenye manufaa).

1064.  Kuujaribu (kucheki) ulimi ni afadhali kuliko kulitazama tumbo.

1065.  Yeyote yule asiye uhifadhi ulimi wake basi ataujutia mbeleni.

UKIMYA NA KUSEMA.

1066.   Kila vile busara ya mtu iongezekavyo ndivyo vivyo hivyo maneno yake hupunguavyo.

1067.  Ukimya ni majibu ya maswali mengi sana.

1068.  Ukimya ni jibu bora kabisa kwa mpumbavu.

1069.  Mazungumzo bora ni yale yaliyo mafupi na yenye manufaa.

1070.  Bora ya misemo ni ile iliyochujwa na kuhakikishwa.

1071.  Ukae kimya ili ukae salama.

1072.  Kusema kupita kiasi kunamdharaulisha mtu.

1073.  Urefu wa mazungumzo huidhoofisha hotuba.

1074.   Hotuba ni kama dawa; kiasi kidogo kinaponya na kwa kuzidi kiasi kunaweza kumwua mgonjwa.

1075. Usimpuuzie yule asemaye bali wewe uyatilie maanani yale ayasemayo.

1076.  Kusema kidogo ndivyo kukosolwa kidogo.

KIFO (MAUTI).

1077.  Watu wako wamelala hali wako hai na huwa macho baada tu ya kufa.

1078. kujielekeza kwa mabaki ya matamanio ya mtu ndiko kujiuwa  haraka.

1079.  Ufe kabla ya kifo kukuijia.

1080.  Mauti inaidhihaki tamaa.

1081.   Mauti ni kutenganisha toka kitakachoisha na kuelekea kule pasipokwisha.

1082. Kuikumbuka mauti kila mara kutampunguzia mtu tamaa za duniani.

1083.  Wale watembeao juu ya ardhi siku moja watazikwamo.

1084.  Tamaa hukuongoza katika njia ya upotofu.

1085.  Wakati hatuna matumaini huwa hatuhuzuniki.

1086.  Kufadhaika huwa pamoja na tamaa.

1087.  Kinachoipatia madhara na hasara dini ni tamaa.

1088.  Waroho ni watumwa wa matilabayao.

1089.  Kutokuwa na mategemeo kunaituliza na kuipumzisha roho.

1090.  Uroho huuangamiza uadilifu

1091.    Ubinadamu ni wa aina mbili; wale wenye matamanio matupu na   wale watakao kuja kuwa wasioridhika.

1092.  Tamaa huingamiza hadhi ya mtu bila ya kuongezeka kwa bahati   yake.

1093.  Hata kama wakiwa uchi na wenye njaa, hao walioridhika huwa ni  wenye furaha.

1094.  Kuridhika ni hazina isiyo na kifani.

1095.  Kuridhika ni hadhi na heshima isiyodidimia milele.

1096.  Mwenye kuridhika tu ndiye aishiee kwa amani na usalama.

USTAHIMILIVU, UVUMILIVU NA UTULIVU.

1097. Kutokuwa na saburi ya akili ni yenye madhara kuliko ustahimilivu.

1098.  Chifu ya sababu ya Islam ni utulivu kwa Allah swt

1099.  Ustahimilivu ni matunda ya Imani.

1100.  Ujue kuwa utulivu ni hatua ya awali katika dini halisi na uaminifu ni mwili

1101.  Kwa ustahimilivu, bahati mbaya huwa sivyo tena bahati mbaya.

1102. Ule uwezo wa uvumilivu wa ghadhabu (hasira) ni bora kuliko kuchukua kisasi.

MALI (UTAJIRI).

1103.  Mapenzi ya mali inachochea tamaa na kuharibu wema.

1104.  Usia unawafariji warithi

1105.  Mali ni chanzo cha hamaki.

1106.  Bora ya akiba ni pale ambapo kazi zinatawanywa vyema.

1107. Fedha haimnufaishi mwenye kuwa nayo hadi hapo anapotengana nayo.

AKILI NA UPUMBAVU.

1108.  Uadui ni kazi ya wapumbavu.

1109.  Dhana ya mwenye akili ni mafumbo.

1110. Kwa kumtii Allah swt ni sawa kwa hisa ya akili na hekima ya mtu.

1111.  Kupigana vita dhidi ya matakwa yake mtu ni jihad kubwa kabisa.

1112.  Sababu ya busara na akili ni kukubalia ujinga wake mwenyewe.

1113.  Mwerevu hulenga pale na thabiti.

1114.  Mpumbavu hulenga pale penye mali.

1115.  Dhana ya mtu inategemea akili yake ilivyo.

1116. Dhana ya mwenye busara na hekima ni sahihi kabisa kuliko  kithibitisho cha mpumbavu

1117. Kwa kujitenganisha na vitu vya muda na kujiweka tayari kwa maisha ya kudumu ndiko kunako busara na hekima hisa kubwa.

1118.   Mtu huyo ni mwenye busara ambaye matendo yake yanathibitisha  yaliyoyasema.

1119. Mtu mwenye busara hasemi ila pale penye dharura au penye sababu.

rudi nyuma Yaliyomo endelea