rudi nyuma Yaliyomo endelea

440. Daraja moja lingine la uwongo ni kule kula kiapo cha uwongo,

kutoa ushahidi wa kiuwongo au kuficha ushahidi katika Mahakama ya Shariah.  Hakuna shaka kuwa  haya ndiyo uwongo ambazo zimo katika Madhambi Makuu. Insha Allah yote hayo yatazungumzwa kiundani ili kueleweka vyema.

441.  Amesema al-Imam Zayn-al-‘Aabediin a.s. katika Al-Kafi:

“Jiepusheni na uwongo, ama iwe ndogo au kubwa, au iwe katika hali ya masikitiko au huzuni au katika mzaha.”

442.  Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Al-Kafi :

“Mtu yeyote hawezi kamwe kuionja Imani yake hadi hapo ajiepushe na uwongo, haidhuru kama itakuwa katika huzuni au mzaha.”

443.  Imeripotiwa kutoka Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema

katika  Wasa’il al-Shiah :

“Hakuna wema katika uwongo hata kama itakuwa katika hali ya huzuni au furaha. Wala hautakiwi kutoa ahadi za uwongo kwa watoto wako, ahadi  ambazo hauna nia ya kuzitimiza. Kwa hakika uwongo unampotosha mtu kutenda madhambi makubwa makubwa ambayo hatimayake humtumbukiza mtu katika Moto wa Jahannam.”

444.  Mtume Muhammad s.a.w.w. alipokuwa akimwusia Abu Dhar

al-Ghaffari,alimwambia :

“Ewe Abu Dhar ! Mtu yeyote atakayejihifadhi dhidi ya uharamisho sehemu zake za siri na ulimi wake, basi ataingia Peponi.  Mtu yeyote atakayetamka uwongo katika mzaha basi uwongo huo katika mzaha utampeleka hadi Jahannam !”

“Ewe Aba Dhar ! Ole wake yule mtu ambaye anapozungumza huzungumza kwa uwongo ili aweze kuwachekesha watu.  Vile vile ole wake ! Ole Wake !  Ewe Abu Dhar ! Yule ambaye atakayekaa kimya ataongoka. Hivyo kukaa kimya kwako ni faradhi kuliko kunasibisha uwongo na kusitoke kamwe uwongo hata kiasi kidogo kutoka kinywani mwako.”

445.  Bwana Abu Dhar anasema:

“Je tawba ya mwenye kusema uwongo kwa kujua hivyo,

itakuwaje ?”

446.  Mtume Muhammad s.a.w.w. alisema  katika Wasa’il al-Shiah ::

“Kufanya Isteghfar na kusali sala tano kwa kutimiza masharti yake ndiyo yanayoweza kuyaosha madhambi hayo."

447.  Vile vile Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema katika  Jihad :

“Laana ya Allah swt inamwia msema uwongo hata kama atasema katika  mzaha”

448. Vile vile Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema, katika Al-Khisal :

“Mimi ninachukua dhamana ya kumpatia nyumba katika daraja iliyo ya juu kabisa katika Jannat kwa ajili ya mtu yeyote ambaye anajiepusha na ugomvi na vita halafu hata kama yeye atakuwa katika haki. Na nitampatia nyumba mtu yeyote yule katika daraja iliyo ya kati ambaye anajiepusha kusema uwongo hata kama atakuwa katika mzaha. Na vile vile nitampatia nyumba katika bustani za Jannat kwa mtu yeyote yule mwenye tabia njema.”

449.  Imepokelewa riwaya kutoka  Safinatul Bihar, j.2, uk. 473

 kuwa Asma’ binti ‘Umays anasema,  :

“Usiku wa kwanza wa ‘Aisha, Mtume Muhammad s.a.w.w. alinipa chombo kimoja cha  mazima akisema ‘wape wanawake wanywe’ 

450.  Wanawake wakasema :

“Sisi hatuna njaa’ Mtume Muhammad s.a.w.w. kwa kuyasikia hayo alisema :’Njaa pamoja na Uwongo musivichanganye kwa pamoja !”

451.  Asma’ akauliza :

“Iwapo sisi tutakuwa tukitamani au tukitaka kitu na tukasema kuwa hatukitaki au hatukitamani, basi jee huo ni uwongo ?”

452.  Basi Mtume Muhammad s.a.w.w. alimjibu :

“Naam ! Bila shaka kila aina ya uwongo unaandikwa kiasi kwamba hata uwongo mdogo mdogo pia huitwa uwongo.”

453.  Ipo riwaya moja kutoka kitabu Bihar al- Anwar , j. 16, mlango wa

 hishima ya ndugu mu’miin …, uk. 241 ipo riwaya ifuatayo :

Siku moja al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. alikuwa ameketi pamoja na mwanae Isma’il, na akaja mfuasi wake mmoja akatoa salaam na akaketi pamoja nao. Wakati Imam a.s. alipoondoka kuelekea nyumbani mwake, basi na yule mtu pia akaondoka kumfuata Imam a.s. hadi kizingitini mwa nyumba ya Imam a.s.  Imam a.s. hapo hapo aliagana nae na kuingia nyumbani mwake, mwana wa Imam a.s., Isma’il alimwuliza babake ni kwa nini hakumkaribisha mtu huyo kuingia nyumbani mwao kama desturi njema ?  Imam  Ja'afar as- Sadique a.s. alimwambia kuwa haikuwa munasibu kwa mtu yule kuingia ndani, kwani mimi binafsi sikuwa nataka huyo mtu aje ndani na wala sikutaka Allah swt anihesabu miongoni mwa watu ambao wanasema nini mdomoni na wanavyo nini moyoni mwao !”

454.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema kuwa uwongo Mkuu upo

     katika makundi matatu :

·   Kumwita mtu kwa jina mbali na jina la mzazi wa kweli.

·   Kusema ndoto za uwongo ambazo hakuziota,

·   Au aseme kile ambacho mimi (Mtume Muhammad s.a.w.w.) sikusema..

455.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema katika  Bihar al- Anwar,

 j.15, uk. 42 kuwa :

“Uwongo ulio ovu kabisa ni kunakili kwa riwaya zilizo za uwongo.”

456.  Siku moja al-Imam Husayn ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwapo

katika baraza la Mua’wiyah na hapo mtu mmoja akaanza kutamka maneno yenye kashfa dhidi ya al-Imam Husayn ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s..

457.  Al-Imam Husayn ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s. alimjibu :

“Ewe ‘Umar ibn ‘Uthman ! Tabia yako ina upumbavu ambao wewe hauwezi kuuelewa. Mfano wako ni kama ule wa mbu ambaye akijiona mkubwa aliukalia mtende na wakati wa kutaka kuruka, aliuambia mtende : ‘jizatiti kwa umadhubuti, kwani niko naruka kwa ajili ya kuteremka !’  Kwa hayo mti  ukamjibu : ‘Mimi wala sijui ni kutoka wakati gani umenikalia juu, sasa hebu niambie kuondoka kwako kutaniangusha ?!”

458.  Tuelewapo kuwa jambo lililopo ni uwongo basi na kulisikiliza pia

ni haram. Kama vile kuandika na kusomwa kwa uwongo umeharamishwa basi na kunakili uwongo pia umeharamishwa.  Kwa hakika Qur'an Tukufu  imekuwa ikiwalaumu Mayahudi na Makafiri kwa kupeleka habari za uwongo za huku kupeleka  huko na za huko kuleta huku. Qur'an Tukufu  inatuambia :

‘ Enyi wasikilizaji wa maneno ya uwongo….’

459.  As-Shayk Sadduq (a.r.) ameinakili riwaya ifuatayo kutoka kwa

al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. kuwa al-Imam a.s. aliulizwa  :

“Je inaruhusiwa kusikiliza uwongo wa waongo kwa makini ?”

460. Amesema al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. katika  kumjibu (Kitab-i-’itiqadat):

“Hapana ! Iwapo mtu anamsikiliza kwa hamu na basi huwa anafanya ibada kwa mujibu wake.  Iwapo msemaji anamwamini Allah swt  basi msikilizaji atafanya ibada ya Allah swt .  Na iwapo msemaji anafuata maneno ya Shaitani basi msikilizaji atafanya ibada ya Shaitani.”

461. Allah swt anatuambia katika Qur'an Tukufu, Surah Haj, 22,

Ayah 30 :

“Mjiepusheni na maneno ya upuuzi”

462. Allah swt anatuambia katika Qur'an Tukufu, Surah Furqan, 25,

Ayah 72

‘Na wale ambao hawashuhudii shahada za uwongo…’

463.  Popote pale ambapo kutakuwa na hatari ya maisha, mali au

heshima ya mtu na kama kwa kusema uwongo kutamwondolea hatari hizo basi kunaruhusiwa kusema uwongo katika sura hizo. Hatari hizo ama ziwe kwa ajili yake mwenyewe au kwa ajili ya mtu mwingine. Hata hivyo imeruhusiwa kula kiapo cha uwongo kwa ajili ya kunusuru hayo. Katika baadhi ya nyakati, ni faradhi kusema na kula kiapo cha uwongo katika kuyanusuru maisha ya mtu, mfano,  iwapo dhalimu atataka kumwua Mwislamu, ataka kumpiga na kumdhuru Mwislamu, au anataka kumdhalilisha na kumkashifu, anataka kumdhulumu na kumnyang’anya mali yake au anataka kumfunga mahabusu. Sasa iwapo huyo mdhalimu akikuomba anwani ya Mwislamu huyo, basi ni faradhi kwako kutompatia anwani yake, halafu hata kama itakubidi useme uwongo na ule kiapo cha kiuwongo kuwa wewe haujui chochote.

464.  Sheikh Ansari anawanakili Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. na

al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. katika Makasib  kuwa Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema , Wasa’il al-Shiah ,Kitab al-Iman, j. 3, mlango na. 12:

"Mnaweza kula kiapo cha uwongo lakini mumnusuru ndugu yenu Mwislamu asiuawe kibure !”

465.  Ismail Ibn Sa’ad ambaye Hadith yake ni sahihi anasema katika

Wasa’il al-Shiah , Kitabul Iman, j. 3, nambari 12 :

“Mimi nilimwuliza Al-Imam ‘Ali  ar-Ridha  a.s. kuhusu mtu ambaye amekula kiapo cha uwongo mbele ya mfalme kwa ajili ya kutaka kuinusuru mali yake.”

466.  Al-Imam ‘Ali  ar-Ridha  a.s. alimjibu :

“Hakuna shida yoyote.”

467.  Mwandishi anasema kuwa yeye alimwuliza tena Al-Imam

‘Ali  ar-Ridha  a.s. :

“Je inaruhusiwa kwa mtu kula kiapo cha uwongo kwa ajili ya kunusuru mali ya Mwislamu mwenzake kama vile alivyokula kiapo cha uwongo kwa ajili ya mali yake mwenyewe?”

468.  Al-Imam ‘Ali  ar-Ridha  a.s. alimjibu:

“Naam ! Inaruhusiwa.”

469.  Al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s.  anasema katika  Faqiyyah :

“Iwapo itambidi Mwislamu kula kiapo cha uwongo kwa ajili ya kumnusuru Mwislamu mwenzake pamoja na mali yake isichukuliwe na mdhalimu au mwizi, basi hakuna shida ndani ya kula kiapo cha uwongo na si hayo tu, bali hatatakiwa kulipa kaffara ya kula kiapo cha uwongo na badala yake atapewa malipo mema kabisa pamoja na thawabu nyingi mno kutoka kwa Allah swt.”

470.  Vile vile iwapo ataweza kuvumilia hasara basi ni Sunnah

kuvumilia na hivyo asiseme uwongo.  Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Nahjul-Balagha,  kuwa :

“Ni alama ya Imani kuwa mtu aseme ukweli tu hata katika wakati wa kupatwa hasara na asiseme uwongo kwa ajili ya kupata faida.”

471.  Al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. amesema katika Wasa’il al-Shiah,

Kitab Haj :

“Mazungumzo yapo aina tatu :”

·   Ukweli

·   Uwongo

·   Kuwasuluhisha  watu

472.  Kuna mtu aliuliza :”Mimi niwe fidia kwako ! Je kuwasuluhisha

 watu ni kitu gani ?

473.  Al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s.  alimjibu :

“Wewe umsikie mtu mmoja akimzungumza mtu mwingine na ukamwambia mtu mwingine kuwa fulani bin fulani alikuwa akikuzungumza vyema kabisa (ambapo kwa hakika ni kinyume chake kabisa) ”

474.  Vile vile iwapo bibi na bwana wamekwisha tengana na umefika

wakati wa talaqa basi inambidi mtu azungumze hata uwongo ilimradi aweze kuwasuluhisha, na kwa hakika hili ndilo litakuwa jambo jema kabisa.

475.  Mtu anaweza kumwendea mume na kumwambia kuwa “Loh ! Mke

wako kwa kweli anasikitika mno kwa kuachana kwani anakupenda kupita kiasi na hivyo hataweza kuvumilia kuachana kwenu na anaweza kuugua.”

476.  Na vivyo hivyo amwendee bibi na kumtengenezea mambo kama

hayo ya uwongo ili kusafishwe mazingira na kuleta usuluhisho na  muungano baina ya bibi na bwana.

477.  Imepokelewa kutoka kwa Mtume Muhammad s.a.w.w. akiwa

amesema :

“Hakuna tendo lililo bora kabisa baada ya kutimiza yaliyo faradhishwa kama vile kuwasuluhisha watu !  Hii ni kheri ambayo inayoeneza kheri  duniani kote.”

478. Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema kuwa Mtume

Muhammad s.a.w.w. alisema wakati wa usia, katika Wasa’il al-Shiah , Kitab Hajj, mlango 141:

“Ewe Ali ! Bila shaka Allah swt anapendelea uwongo katika kusuluhisha na hapendezewi ukweli katika kuzua ufisadi na

magomvi !”

479.  Vile vile Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema :

“Kusuluhisha miongoni mwa watu, kufikiria usulihisho na kuepusha magomvi ni bora kuliko sala na saumu.”

480.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema :

“Hakuna uwongo kwa mtu anayesuluhisha.”

481.  Amesema al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. :

482.  Mtume Muhammad s.a.w.w. anasema :

“Zipo nafasi tatu ambapo uwongo unapendeza: kudanganya katika vita, ahadi aitoayo mume kwa mke wake na kuwapatanisha watu.”

483. Ama kuhusiana na ahadi ya mume kwa mke wake, Islam

inapendelea kuwaona wakiishi kwa raha na mustarehe na waishi kwa kupendana. Hivyo kumwambia mke wako uwongo wa kumtimizia jambo fulani, kama unao uwezo basi vyema kabisa, lakini kama hana uwezo, basi anaweza kumpa ahadi ya uwongo ili kuepukana na ugomvi na kumuudhi mke wake.

Kwa mfano, wewe hauna uwezo wa kumtimizia ombi fulani la mke wako, kama kwa mfano anataka nyumba, lakini wewe kwa kutokuwa na uwezo huo, utamdanganya kuwa nitakujengea au kukununulia ili kumridhisha mke wako. Sote tunajua kuwa ukaidi wa mwanamke ni ukaidi mkubwa kabisa  na vile vile Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema kuwa “mwanamke ni kama mfupa wa ubavu, upo umepinda, hivyo usijaribu kuunyosha, utavunjika” hivyo tutumie mbinu kama hizi kwa nia njema ili kutuliza mambo nyumbani.

484. Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Al-Kafi

(ikizungumzia thawabu za Allah swt na juu ya adhabu na matumaini ya kusamehewa) :

“Jiepusheni na kusema uwongo ! Pale mtu anapotarajia kupata  kitu basi anataka akipate tu hicho kitu (basi huwa tayari kufanya kazi yoyote ili aipate) na vile vile mtu anapokiogopa kitu chochote kile, basi hujiweka mbali nacho.”

485.  Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Nahjul-Balagha, :

“Mtu yeyote anayefikiria kuwa yeye anamtegemea Allah swt  lakini matendo yake hayaonyeshi hivyo basi kwa kiapo cha Allah swt aliye Mkuu, mtu huyo ni mwongo.  Ingawaje mtu anapokitegemea kitu basi mwenendo wake hudhihirisha hivyo.  Lakini itawezekanaje yeye amtegemee Allah swt ambapo matendo yake hayadhihiri hivyo ? (mtu kama huyu kwa hakika si miongoni mwa wale wamtegemeao Allah swt  basi anajidanganya mwenyewe).  Vile vile mtu anapokiogopa kitu chochote basi matendo yake yatadhihirisha hali hiyo yaani ataamua kukikimbia kitu hicho. Lakini mtu anapodai kuwa anamwogopa Allah swt na kwa nini sasa hakimbii mbali na madhambi ?”

486.  Al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s.  amesema katika Misbah

As-Shari’ah :

“Wakati musemapo Allahu Akbar basi muelewe kile kilicho baina ya mbingu za juu na ardhi, vyote ni vidogo mbele ya Allah swt na kwa undani wa moyoni mwenu muelewe kwa sababu Allah swt anapoona kuwa kuna mja wake ambaye hasemi Allahu Akbar kutokea undani mwa moyo wake, basi Allah swt (humwambia) ‘Ewe mwongo ! Wewe unataka kunidanganya basi kwa kiapo cha heshima na Utukufu Wangu basi mimi nitakuepusha na dhikr yangu !’”

487. Mtu anaposema kuwa :”Mimi ninayo furaha kuwa Mtume Muhammad s.a.w.w. ni Mtume wangu  na Qur'an Tukufu  ni kitabu Kitakatifu na kuwa Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. ni Imamu wangu. Na vyote hivyo vipo kwa ajili ya kuniongoza.” 

Ingawaje anatamka kwa mdomo lakini kimatendo utaona kuwa Shaitani na matamanio yake ya nafsi ndio viongozi wake !  Na huvifuata hivyo !  Utaona kuwa yeye havitilii maanani mafunzo na hidaya ya Qur'an Tukufu . Na vile vile hatilii maanani maamrisho na mafunzo yaliyotolewa na Maimamu a.s.  Kwa hivyo mtu kama huyu  ni mwongo.

488.  Wakati mtu anapofanya dua na akasema “(Ewe Mola wangu !)

Mimi ninapoziangalia madhambi yangu basi hulia na ninapoangalia ukarimu wako ninajawa na matumaini kuwa Wewe utanisamehea.”

Kwa hakika utaona kuwa tunatamka hivyo lakini hatujali madhambi na hata anapotambua kuwa jambo fulani ni dhambi, basi hulitenda bila ya woga wowote ule !  Uso wake haushtuki hata punje kidogo wakati wa kutenda dhambi !  Basi hujitoa katika ukarimu na rehema za Allah swt !  Je mtu kama huyu anapoyatamka maneno kama hayo yalivyo katika dua, anasema ukweli ? Je uwongo wake si upo wazi !?

489. Vile vile mtu anapotamka “Mimi ninalia kwa kutokwa nafsi yangu

na ninalilia maswala ya kaburini na ninalilia khofu ya Qiyama”

ingawaje ni dhahiri kuwa hakuna anachokililia kitu kama hicho Huo ni uwongo wake kwani matendo yake hayaonyeshi kama kweli anayo khofu kama hiyo moyoni mwake.  Al-Imam Zaynul ‘Aabediin a.s. amesema katika Dua-i-Abu Hamza Thumali : “Ewe Allah swt !  Labda Wewe umenipata katika ngazi za waongo na kwa hivyo (umeniondolea mtazamo wako wa kirehema) na umeniacha katika hali niliyonayo.”  Yaani mimi nimekuwa nikiyatimiza matamanio ya nafsi yangu na wala sijui nitaangukia katika maangamizo yapi.

490. Mfano wa kuwaambia uwongo Maimamu a.s. ni kama vile

tunavyosema katika Ziyarat :

“Enyi Aimma Ma’asumiin a.s.! Mimi nimezikubali kauli zenu na ninayafuata hukumu (na maamrisho) zenu na mimi ni mwenye kuwatiini.” 

Sasa iwapo mtu atazisikia kauli na maamrisho ya Maimamu a.s. na asizifuate na badala yake akazifuata matamanio na maamrisho ya nfsi yake basi bila shaka mtu kama huyu ni Shaitani ! Basi inadhihirika waziwazi kuwa huyo ni mwongo kwa Maimamu a.s. !

491. Vile vile mfano mwingine wa kusema uwongo upo unapatikana

katika Ziyarat, wakati tusemapo :

“Enyi Aimma watoharifu ! Mtu yeyote aliye na amani pamoja nanyi basi mimi pia nitakuwa na amani pamoja naye na yeyote yule atakayepigana vita pamoja nanyi au kuwapinga basi nami nitakuwa na vita naye na nitampinga vile vile  !”

492. Kwa hakika hivyo ndivyo tunavyodai, lakini matendo yetu ni kwamba tunao urafiki mzuri wa kidugu pamoja na maadui wa

Islam ! Na badala yake sisi tunafanya uadui pamoja na wapenzi na wafuasi wa Aimma a.s.. Wakati anaposema

“Enyi Maasumiina.s. ! Mimi ninawaacha wale wanaokukhilafu nyinyi.” 

Lakini kwa hakika haya haytekelezwi kimatendo Sasa jee mtu kama huyu si mwongo mbele ya Maimamu a.s. ?

493.  Hivyo sisi tunaweza kusema kuwa muumin hawasemi uwongo

mfano kuwa kila Mumiin anakuwa na khofu ya Allah swt  kama vile tunavyoambiwa katika Qur'an Tukufu  : ‘Kama nyinyi ni mumiin wa kweli basi muwe mukiniogopa Mimi tu’ (Surah Aali-Imran, 3, Ayah ya 175).  

Na vivyo hivyo Mumiin wote ndio wanaomtegemea Allah swt tu na bila shaka wote wanakuwa na khofu ya Allah swt  na matumaini yao pia yanakuwa na ngazi mbalimbali na kamwe haiwezekani zinalingana na za Aimma a.s.

494.  Dua-i Abu Hamza Thumali :

“Ewe Allah swt ! Mimi madhambi niliyoyatenda si kwamba nikukupinga wewe na wala sikutenda madhambi hayo kuwa nikichukulia hukumu zako ati ni za kawaida na wala sikutenda madhambi kwa kufikiria kuwa adhabu zako ni ndogo bali  nimetenda kwa kutokana na kasoro zangu za kinafsi na ujeuri wangu..”

495.  Du’a :

“Ewe Allah swt ! Nakuomba unipatie yakini ya kweli kwayo ambayo mimi niweze kutii amri zako kikamilifu.” 

496.  Inapatikana katika riwaya kuwa “Mtu anapokitaka kitu basi kwa

kufanya jitihada, anakipata tu.”

497.  Qur'an Tukufu  katika Surah at-Tawbah, 9, Ayah ya 119 :

‘Muwe pamoja na Wasemao ukweli.’  Katika Ayah hii Allah swt anatuambia kuhusu ‘Sadiqiin’ ambao ndio Ahlul Bait a.s. ya Mtume Muhammad s.a.w.w.’

KUSEMA UONGO[53]

498.  Anas Ibn Maliki Khisal-i-Sadduq, Uk. 321:

Anaelezea kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema “Chukueni mambo sita kutoka kwangu, na mimi nakubalia, na kutoa dhamana (Ya wewe kuingizwa Jannat)

 1. Usiseme uongo 

  2.Unapo toa ahadi, usivunje

 3. Unapo pewa amana na wengine, basi uwemuaminifu

 4. Tazama chini ( usitende dhambi ).

 5. Chunga heshima yako

 6. Idhibiti mikono yako na ulimi wako.

499.    Amesema Imam Al Hassan  al-‘Askari a.s,Bihar

al-Anwaar, J. 72, Uk.263:

“Iwapo maovu yote yatawekwa katika nyunba moja, basi ufunguo

( wa milango yake ) itakuwa ni uongo.”

500.   Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin a.s. Tuhaful-'Uqul,

 Uk. 201:

“Jiepusheni na kusema uongo hata kama ni uongo mgogo au mkubwa, kama kwa wadilifu au unasema kwa kdhihaki, kwasababu mtu anapo  sema uongo mdogo basi anaweza kudiriki kusema uongo mkubwa pia. 

501.   Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Bihar al-Anwaar, J. 75,

Uk. 196:

Wakati mmoja Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. aliulizwa kuhusu umbali baina ya ukweli na uongo naye akiwa akionyesha umbali huo baina ya macho yake na maskio yake kwa vidole vinne katika kutoa jibu hilo, “Kile majo yako yanayooonani ukweli na mengi na yale yanayo sikilizwa na maskio yako ni sehemu kubwa ni uongo.”

502.   Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir a.s., Al-Kafi,

J. 2, Uk. 339:

“Kwa hakika Allah swt ameyawekea maufuli maovu fulani, na ufunguo wake Allah swt ameweka katika pombe, lakinimaovu yatokanayo na kusema uongo ni zaidi hata kuliko pombe yenyewe.”

503.   Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s., Bihar al-Anwaar,

J. 78, Uk. 347:

“Muwe wasema ukweli na mujiepushe na usemaji uongo.”

504.  Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir a.s., Al-Kafi,

J. 2, Uk. 339:

“Kwa hakika Allah swt ameya wekea maufuli maovu fulani, na ufunguo wake Allah swt ameweka katika pombe, lakinimaovu yatokanayo na kusema uongo ni zaidi hata kuliko pombe yenyewe.”

505.  Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. Bihar al-Anwaar,

J. 78, Uk. 347:

“Muwe wa sema ukweli na mujiepushe na usemaji uongo.”

MARAFIKI NA URAFIKI.

506.            Mtume Muhammad  s.a.w.w. Amesema, Bihar

al-Anwaar, J. 74, Uk. 192:

“Mtu anaathirika kwa imani ya marafiki zake.  Kwa hivyo, muwe waangalifu kabisa katika urafiki wenu pamoja nao.[54]

507.     Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Amesema: Bihar

al-Anwaar, J. 76, Uk. 267:

“Uwe rafiki wa yule ambaye atakuwa ndio heshima yako, si wewe uwe heshima yake. (Ufanye urafiki na wale walio juu yako ili wewe uweze kupata maendeleo kutokana na urafiki huo).

508.     Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. Amesema, Bihar

al-Anwaar, J. 74 Uk. 282:

“Ndugu yangu mpenzi ni yule (anayenitambulisha) makosa na kasoro zangu.

509.     Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Amesema, Khisal-i-

Sadduq, J. 1, Uk. 88.:

“Kwa hakika kuna marafiki wa aina tatu kwa ajili ya Muislam:

1. Rafiki anayesema mimi niko pamoja nawe iwapo upo hai au umekufa: Na hili ndio matendo yake.

2. Rafiki anayesema mimi nipo rafiki wako hadi ukingoni mwa kaburi na nitakuacha:hawa ni watoto wake.

3. Rafiki anayesema mimi nitakuwa nawe hadi pale utakapo kufa:hii ni mali ambayo ataiacha humu duniani kwa warithi wake baada ya kifo chake.

Tanbih

Kutokana na riwaya hii, na kama hizi sisi tunaelewa kuwa kitu ambacho kitakuwa pamoja na huyo mtu aliye kufa na kuaga dunia hii katika siku ya Qiyamah imani na matendo yake mema. Na suala hili limezungumziwa katika ahadithi nyingi sana za Kiislam na vile vile katika ayah za Qur’an tukufu, kwa mfano:

510.  Allah swt anatuambia katika Qur’an Sura Ar-Raa;d, 13, ayah

 ya 29.

Wale walio amini na wakatenda mema watakuwa na raha na marejeo mazuri.

511. Allah swt anatuambia katika Qur’an Sura Al-Kahf,18, ayah 30.

Hakika wale walio amini na wakatenda mema – hakika Sisi hatupotezi ujira wa anaye tenda mema.

512. Allah swt anatuambia katika Qur’an tukufu Sura Al-Kahf, 18, ayah ya 107.

Hakika wale walio amini na wakatenda mema mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi.

513.  Allah swt anatuambia katika Qur’an tukufu Sura Maryam,19, ayah ya 96.”

Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi.

514.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. , Bihar

al-Anwaar, J. 74 Uk. 187:

“Muwe waangalifu katika kutafuta marafiki wa kweli na mujaribu kuwafanyia majaribio, kwa sababu wao watakuwa ndio msaada wenu pale mnapokuwa katika hali nzuri na watetezi wenu pale mtapokuwa katika shida na matatizo.”

515.         Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin a.s. , Bihar al-Anwaar, J. 78, Uk. 141:

“Kukutana pamoja na wacha Mungut kunawaleteeni mema.”

516.     Al Imam Zaynul 'Abediin a.s. Amesema, Bihar al-

Anwaar, J. 78, Uk. 151:

“Jitahadharisheni na urafiki wa watendao madhambi, na kuwasaidia madhalimu.”

MARAFIKI WASIO WEMA

517.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Al-Usul-i- Kafi,

J. 2, Uk. 379:

“Anayetafuta uhusiano na marafiki wa wale wanao wadhalilisha wapenzi wa Allah swt basi watambue kuwa wao wamemuasi Allah swt.”

518.     Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. Amesema, Wasa'il ush-Shi'ah, J. 16, UK. 146:

“Mnapojulishwa kuhusu marafiki zenu wanapotenda maovu, nendeni mumwambie:

Ewe fulani bin fulani ! Ama acha kutenda madhambi au ukae mbali nasi:

Na hapo utengane naye hadi atakapo acha kutenda maovu.

519.     Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili kutoka baba

yake Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. ambaye Amesema kuwa baba yake Al Imam Hussein ibn Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. Amesema , Al-Kaf ,  J. 2, Uk. 641:

“Ewe mwanangu ! Jichunge na makundi matano na kamwe usifanye urafiki nao, wala usiongee nao na wala usifanye urafiki pamoja nao.

Kwa hayo Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. alimuuliza baba yake

Je ni makundi gani hayo matano. Imam a.s. alimujibu:

Jitahadharishe na wala usifanye urafiki pamoja na yule msema uongo kwa sababu yeye ni kama mazua mazua anaye kufanyia vitu vya mbali vikawa karibu, na anakifanya kiwe mbali kile ambacho kiko karibu nawe.

Jihadhari na usifanye uhusiano pamoja na mtu ambaye hana tabia njema, kwa sababu atakuuza kwa thamani kwa tonge moja au hata chini ya hiyo.

Jihadhari na wala usifanye uhusiano na bahili kwa sababu yeye atakunyima kutoka mali yake pale wewe utakapo hitaji hasa.

Jihadhari na usifanye urafiki pamoja na mpumbavu, kwa sababu yeye atataka kukufaidisha wewe lakini kwa uhakika anakudhuru zaidi.

Jihadhari na usifanye uhusiano pamoja na yule ambaye hawajali ndugu na maJama’a zake, kwa sababu mimi nimemona mtu kama huyo akilaaniwa katika kitabu cha Allah swt (yaani Qur'an Tukufu) katika sehemu tatu.

Nayo ni:

Sura Al Baqarah, 2, Ayah ya 27; 

Wanao vunja ahadi ya Allah  swt baada ya kwisha ifunga, na wakayakata aliyo amrisha Allah  swt kuungwa, na wakafanya uharibifu katika nchi; hao ndio wenye Khasara.

Sura Al-Raa’d,  13, ayah ya 25

Na wale wano vunja ahadi ya Allah  swt baada ya kuzifunga, na wanakata aliy amrisha Allah  swt yaungwe, na wanafanya fisadi katika nchi: Hao ndio watakao pata laana, na watapata Nyumba mbaya.

Sura Muh'ammad, 47, ayah 22

Basi yanayo tarajiwa kwenu mkitawala ndio mfisidi katika nchi na mwatupe Jama’a zenu ?

520.            Amesema Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s., Mustadrak-ul-

Wasa'il, J. 12, Uk. 197:

“Ewe Kumail ! sema kile kilichopo katika hali yoyote ile. Uwe marafiki pamoja na wacha Allah swt na jiepushe na watendao maovu, jiweke mbali na wanafiki na usiwe pamoja na wadanganyifu na wahalifu na wahaini.”

KUWAHUDUMIA WATU

521.            Amesema Mtume Muhammad  s.a.w.w. , Shahab-ul-

Akhbar, Uk. 194:

“Yeyote yule atakaye mpuuzia ndugu yake Muislam mwenzake matatizo na shida za dunia hizi, basi Allah swt atampunguzia shida na matatizo yake huko Akhera.”

522.            Amesema Al Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s., Bihar

al-Anwaar, J. 7, Uk. 318:

“Kwa hakika, maombi ya shida za watu zinazokuijia wewe ni miongoni mwa neema na baraka za Allah swt juu yako.  Hivyo usisikitike kwa sababu ya neema na baraka hizi.”

523.            Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., Bihar al-Anwaar,

 J. 74, Uk.166:

“Popote pale utakapoona ndugu yako Muislam ana shida, jaribu kuangalia kama utaweza kumusaidia. (Usimpuuze mpaka akutamkie shida zake.)”

524.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa amenakili

kutoka mababu zake a.s. ambao wamemnakili Mtume Muhammad  s.a.w.w. akisema, Bihar al-Anwaar, J. 74, Uk. 382:

“Yeyote yule anayemlisha muumin aliye na njaa akashiba basi Allah swt atamlisha mpaka ashibe kutoka matunda ya Jannah;

Na yeyote yule atakaye mvisha nguo yule aliye na shida za nguo, Allah swt atamvisha nguo zilizofumwa na za hariri, na

yeyote yule atakaye mumalizia kiu muumin basi Allah swt atamjaalia kinywaji kilichopigwa lakiri;

Na yeyote atakaye msaidia muumin kupunguza shida yake, basi Allah swt atamweka chini ya Arshi yake siku ya Qiyama siku ambayo hakutakuwa na kivuli chochote isipokuwa kivuli cha Arshi yake.”

525.         Mtume Muhammad  s.a.w.w. Amesema, Al-Kafi, J. 2, Uk. 164:

“Watu wanamtegemea Allah swt kwa ajili ya riziki, kwa hiyo mpenzi miongoni mwa watu kwake Allah swt ni yule ambaye anawasaidia wale watu wanaomtegemea Allah swt na kuwafanya watu wa familia ya nyumbani wakawa na furaha.”

526.            Amesema Mtume Muhammad  s.a.w.w., Al-Kafi, J. 2, 

Uk. 199:

“Yeyote yule atakaye wasaidia Waislam ndugu zake wakati wa shida, Allah swt atamwondolea shida na matatizo sabini na tatu, moja ambayo ni ambayo iko humu duniani na sabini na mbili zingine zitakazo kuwa wakati wa shida kubwa, ambapo watu watakuwa mashughuli katika mambo yao ya binafsi (katika Akhera).”

KUTOA MIKOPO

527.            Amesema Mtume Muhammad  s.a.w.w., Bihar al-Anwaar,

J. 76, Uk. 369:

“Yeyote yule anayeijiwa na ndugu yake Muislam kwa ajili ya kukopa na kama yeye hampi mkopo, basi Allah swt atamharamishia kuingia Jannat siku ambayo waja mema watakuwa wakilipwa na kufidiwa.”

rudi nyuma Yaliyomo endelea