rudi nyuma Yaliyomo endelea

Ufafanuzi:

Aina ya tatu ya dhuluma ni ile ambayo mtu hukiuka na kuvunja haki za watu. Njia saheli ya kutaka kusamehewa ni kwanza kumridhisha yule ambaye haki zake zimekiukwa na kuvunjwa. Iwapo mtu huyo atamsamehe yule aliyemvunjia haki zake, basi hapo dhuluma hiyo itageuka kuwa dhuluma dhidi yake binafsi. Na hapo ndipo ataweza kuwa mstahiki wa kuomba msamaha wa Allah swt.

330.   Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. Amesema katika, Tasnif

Ghurarul Hikam, J. 2, Uk.36 :

“Dhuluma husababisha miguu kupotoka, inaondoa baraka na kuangamiza umma au taifa.”

331.   Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. Amesema katika, Nahjul-

Balagha, Barua  na 53:

“Hakuna kitu kinachovutia na kuharakisha kuondolewa kwa neema za Allah swt spokuwa kuendekea kwa dhuluma, kwa sababu Allah swt anazisikiliza dua za madhulumu na huwa yuko tahadhari pamoja na madhalimu.”

HAKI ZA WAISLAMU WENZAKO

332.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Bihar al- Anwar , J. 75, Uk. 150 :

“Yeyote yule anayemhuzunisha Mwislamu mwenzake basi kamwe hawezi kumfidia hata kama atamlipa dunia nzima kwani haitatosha (ispokuwa iwapo atatubu na kumfurahisha Mwislamu huyo).”

333.   Al-Imam Musa al-Kadhim a.s. Amesema katika, Bihar

al- Anwar, J. 2, Uk. 75:

“Moja ya faradhi miongoni mwenu  kuelekea Mwislamu mwenzenu ni kutokumficha kitu chochote ambacho kinaweza kumfaidisha humu duniani au Aakhera.”

334.    Al-Imam Al-Hassan Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.

Amesema katika,

“Watendee watu vile utakavyopenda wewe kutendewa.”

335.  Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Ghurarul-

Hikam, Uk.181:

“Alla swt humrehemu mtu ambaye anahuisha yaliyo haki na kuangamiza na kuteketeza yale yaliyo batili, au hukanusha dhuluma na kuimarisha uadilifu.”

336.   Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s.katika, Tuhfatul-

Uqul, Uk. 277:

“Tabia hizi nne ni kutokea tabia za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.. : haki, ukarimu, subira na kuvumilia katika shida, na kusimamia haki ya Mumiin.”

337.  Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Nahjul-

Balagha, Barua  na 53 :

“Kwa hakika ni watu wa kawaida ndio walio nguzo za Din, nguvu ya Waislamu na hifadhi dhidi ya maadui.  Hivyo mwelekeo wako daima uwe kuelekea wao na uwanynyekee.”

338.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s.katika, Al-Kafi,

J. 2, Uk. 170:

“Allah swt haabudiwi zaidi ya thamani kuliko kutimiza haki ya Mumiin.”

339.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Bihar al- Anwar, J. 67, Uk. 72:

“Yeyote yule anayemuudhi Mumiin, basi ameniudhi mimi.”

340.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Mustadrak al-Was’il, J. 17, Uk. 89:

“Yeyote yule atakayemdhulumu Muumin mali yak pasi na hakie, basi Allah swt ataendelea kumghadhibikia na wala hatazikubalia matendo yake mema atakayokuwa akiyatenda; na hakuna hata mema moja itakayoandikwa katika hisabu zake nzuri hadi hapo yeye atakapofanya tawba na kuirudisha hiyo mali kwa mwenyewe.”

SALAAM -- KUSALIMIANA

341.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

  Bihar al- Anwar , J. 76, Uk. 4:

“Pale munapokutana miongoni mwenu basi muwe wa kwanza kwa kutoa salaam na kukumbatiana; na munapoachana, muagane kwa kuombeana maghfirah.”

342.  Al-Imam Hussein ibn Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.

Amesema katika, Bihar al- Anwar, J. 78, Uk. 120:

“Thawabu sabini (70) ni kwa ajili ya yule ambaye anaanza kutoa salaam na thawabu moja ni kwa ajili ya yule anayeijibu hiyo salaam.”

( Wakati watu wawili wanapoonana, mtanguliaji katika kutoa salaam hupata thawabu zaidi ).

343.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. Amesema katika, Bihar

al-Anwaar, J. 69, Uk. 393:

“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliwakusanya watoto wa ‘Abdul Muttalib na kuwaambia:  Enyi watoto wa Abdul Muttalib ! muwe waanzilishi wa salaamu, mujali Jama’a zenu, musali sala za usiku wakati watu wengine wanapokuwa wamelala, walisheni vyakula watu, na muongee maneno mazuri na hayo kwa hakika mutaingia Peponi kwa amani.”

344.   Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. Amesema, Wasa'il ush-

Shi'ah, J. 12, Uk. 55:

“Yeyote yule anayekuwa ni muanzilishi wa kutoa salaamu basi atakuwa ni mpenzi sana wa Allah swt pamoja na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.”.

KUTENDA MEMA NA KUZUIA KUTENDA MABAYA.

345.    Allah swt anatuambia katika Qur’an Sura Al Imran,

  3, ayah 104.

 Na uwe kutokana na nyinyi umma unao lingania kheri na unao amrisha mema na unakataza maovu. Na hao ndio walio fanikiwa.

346.     Amesema Mtume Mtukufu s.a.w.w., Bihar al-Anwaar, 

J. 100, Uk. 92.

“Itakapofika wakati katika umma wangu ambapo Waislam watakuwa wakitekenya wengine wafuate mema na wajizuie na mabaya, basi kwa hakika watakuwa wametangaza vita dhidi ya Allah swt.”

347.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema,  Bihar al Anwaar, 

J. 100, Uk. 94.

“Yeyote yule anayeacha kukataza wengine wasifanye maovu kwa maneno na kwa matendo (ni tofauti na kuona maovu yakitendeka) basi huyo ni maiti inayotembea miongoni mwa walio hai.”

348.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.

Mustadrak Al-Wasa'il-ush-Shi’ah, J. 11, Uk. 278:

“Kumzuia Muislam asitende matendo maovu ni sawa na Allah swt kumlipa thawabu za Hija 70 zilizokubaliwa…”

349.   Alisema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Nahjul Balagha,

Uk. 392 Barua no. 31:

“Ambizeni miongoni mwenu kutenda mamea; basi mtakuwa miongoni mwa watendao mame.  Muwazuie wengine wasitende maovu kwa maneno yenu, na mujiepushe, na uwezo wenu wote, na yeyote yule anayetenda hivyo.  Mumtumikie Allah swt kama ni wajibu wenu; na angalieni kusiwepo na mulaumiaji au lawama yoyote itakayoweza kuwazuia nyie katika kutekeleza maswala ya Allah swt.  Jitupeni jitumbukizeni katika hatari kwa ajili ya kunusuru ukweli popote pale itakapo hitajika.” 

350.   Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. Amesema, Al-Kafi,

J. 5, Uk.56:

“Kwa hakika kuwaambia watu yaliyoyakweli na kuwazuia kwa yale yaliyo potofu ndiyo sirah ya Mitume a.s. na waja wema. Kwa hakika ni jambo moja kubwa (wajib) kutokana na hiyo mambo mengine mengi yaliyo faradhishwa yanaweza kubakia, Ummah zingigine zinawea kunusurika, maelewano ni halali, dhuluma imekatazwa, na hakikaamani itajaa juu ya ardhi

 hii …”

351.    Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Ghurar-ul-

Hikam,Uk. 236:

“Uimara wa dini ni kule kuamrisha yaliyo mema na kukatza yale  yaliyo maovu, na kubakia katika mipaka ya Allah swt.”

352.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Wasa'il

    ush-Shi'ah, J. 16, uk. 135

“Yeyote anayeona maovu au mabaya yanatendeka basi ayazuie kwa matendo yake, kama ana uwezo huo, bila shaka; kama hawezi kufanya hivyo, basi azuie kwa ulimi wake, na kama hawezi kufanya hivyo pia basi anaweza kulaani kimomoyo.”

353.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ,

At-Tahdhib, J. 6, Uk. 181:

“Yeyote yule katika ‘Umma wangu anayechukua jukumu nakumamrisha mema na kukataza maovu na anaye jihusisha katika ucha-Allah swt,wataishi kwa raha na mustarehe na watakapo acha kufanya hivyo, basi baraka na neema za Allah swt zitaondolewa kwao.”

354.    Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.,  Nahjul

Balagha, Barua No. 47, Uk. 422:  

“Akiwambia Al Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. na Al Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. wakati Ibn Muljam (Laana za Allah swt zile juu yake) alipompiga dharuba kali katika Masjid Kufa…”Muogopeni Allah swt (Na akasema tena)Muogopeni Allah swt katika mambo ya Jihad, (Jitihada za vita vitakatifu), kwa misaada ya mali, maisha na mazungumzo yenu katika njia ya Allah swt…”

Msiache kuamrisha mema na kukataza maovu isije hawa waovuwakachukua nafasi juu yenu, na baadaye(Katika hali hiyo)mtakapo Sali basi salah zenu hazita kubaliwa…

355.    Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Mustadrak

    Al-Wasa'il-ush-Shiah, J. 12, Uk. 185:

“Kuamrisha mambo memani jambo mmoja jema kabisamiongoni mwa watu.”

356.   Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Bihar al-Anwaar,

J. 100, Uk. 89:

 “Matendo mema yote kwa ujumla, ikiwemu Jitihada za vita vitakatifu vya Jihad katika njia ya Allah swt, kwa kulinganisha na kuamrisha mema na kukataza maubaya, ni sawa na kyasi kidogo cha mate ya kilinganishwa na bahari yenye kina kirefu.”

357.   Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir a.s., Al-Kafi

J. 5, Uk. 56:

“Allah swt alimteremshia Wahyi Mtume Shua’ib a.s

“Mimi nitawaadhibu watu wako kiasi cha laki moja na kati yao arobaini elfu ni waovu na elfu sitini ni katika watendao wema.”

Mtume Shua’ib a.s aliulizia hawa waovu wanastahili adhaabu lakini hawa watendao wema je akasema kwa hayo Allah swt alimterenshia wahi tena” Wao(walio wema)wamehusiana na watendao dhambi na hawa kuwa wakali hawa kughadhabishwa kwasabasbuadhabu na khofu zangu. 

358.   Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., Wasa'il

ush-Shi'ah, J. 16, Uk. 120:

 “Wambieni wenzenu wa tende wemana wajizui na ubaya kwani hamutambui kuwa kwakuamrisha mema kamwe haikaribishi mauti wala kukatisha riziki.

359.   Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Mustadrak-ul-

Wasa'il, J. 12, Uk.181:

 “Ole wale  watu ambao hawaisaidi Dini ya Allah swt kwa kuamrisha mema na kwa kutaza maovu.

ULIMI NA MAOVU YAKE.

360.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., Bihar

al-Anwaar, J. 71, Uk.286:

 “Matokeo yatokanayo na ulimi ni mabaya kabisa (yaliyo sabasishwa nayo) kuliko dharuba ya upanga mkali.

361.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Bihar

al-Anwaar  J. 71 Uk.277:

“Miongoni mwa mambo yote, ulimi unastahilikuwekwa katika mahabusukwakipindi kirefu zaidi kuliko kitu kinginechochote. (Kwasababu madhambi yetu mengi yana tokana nayo, kama vile kuwasuta watu, kusema uongo, kuzua mambo, kuwadhihaki wengine, na vile vile kuwa tuhumu watu wengi, n.k)

362.   Amesema Al Imam Amiril Momineen a.s. Ghurar-ul-

Hikam Uk. 228:

“Fikirieni na mupime kabla hamja ongea ili kwamba muweze kujizuia dhidi ya ( kutenda ) makosa.”

363.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Waqayi-

ul-Ayyam, Uk. 297:

“Maangamizo ya mtu yako katika mambo matatu “Tumbo lake, matamaniyo yake, na ulimi yake.”

364.  Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. Bihar al-

Anwaar, J. 78, Uk.178 :

 “Hakuna mtu yeyote aliye salimika kutokana na ulimi wake hadi hapo yeye atakapo udhibiti ulimi wake.” 

KUSENGENYA NA KUTAFUTA KOSA.

365.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Al-Usul-

i- Kafi, J. 2, Uk. 57:

“Uzushi unafanya kazi dhidi ya Imani ya Mwislamu, Mumim kwa haraka zaidi kuliko ugonjwa wa Ukoma unavyo enea mwilini.”

366.    Amesema Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Ghurar-ul-Hikam

Uk. 307:

“Msikilizaji wa kile kinacho sengenywa ni sawa na yeye ndiomsengenyaji.”

367.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Bihar al-

Anwaar, J. 75,  Uk. 261:

“Kuacha tabia ya kusengenya ina thamani kubwa sana mbele ya Allah swt kuliko kusali sala yenye raka’h elfu kumi zilizo sunnah.

368.  Amesema ‘Abdul Mu’min-il-Ansari. Bihar al- Anwar ,

J. 75 , Uk. 262:

“Kuwa wakati moja yeye alikuwa mbele ya Imam Abil HassanMusa Ibn Jaffer a.s ambapo Abdillahi Jaffer alikuwa akitokezea na Abdul Mu’min alitoa tabasamu mbele yake. Na hapo Imam a.s alimuuliza Abdul Mu’min iwapo alimpenda Abdillahi Jaffer na alipomjibu Imam kuwa yeye hakumpenda (‘Abdillah ) isipokuwa yeye alikuwa ni Imam wa saba. Hapo Imam a.s alimwambia yeye ni ndugu yako, ni Mu’min na Mu’min moja ni ndugu wa Mu’min mwingine hata kama wazazi wake ni watu tofauti. Hivyo amelaaniwa yule anayemtuhumu ndugu yake wakiislamu, analaaniwa yule anayemgeuka ndugu yake Mwislamu, analaaniwa yule asiyempa muongozo mwema ndugu yake Mwislamu, na analaaniwa yule ambaye anamsengenya Mwislamu mwenzake.”

369.   Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Amesema, Tara'if-ul-

Hikam, Uk. 182:

“Mwovu miongoni mwa watu ni yule ambaye anatafuta kasoro za watu wengine wakati akiziacha kasoro zake.”

370.   Al Imam Musa al-Kadhim a.s. Amesema, Bihar

al-Anwaar, J. 74, Uk.232:

“Amelaaniwa mtu yule ambaye anawasengenya ndugu zake wengine (Waislamu wenzake).”

UHARAMISHO WA KUSEMA UWONGO [52]

371.  Allah swt anatuambia katika Qur’an Tukufu, Surah An-Nahl,16,

Ayah ya 105,

Wanaozua uwongo hawana imani

372.  Vile vile Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema :

“Mtu mwovu kabisa ni yule ambaye ni msema uwongo.”

373.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema :

“Allah swt humlaani mwongo hata kama atasema ukweli”

374.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema:

“Jitahadharisheni, Mimi ninawaambieni dhambi Kuu kabisa katika Madhambi Makuu :

375.  Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema :

“Ugonjwa wa kusema uwongo ndio ugonjwa mbaya kabisa.”

376.  Vile vile Imam Hasan al-‘Askari amesema katika Mustadrad al-Wasa'il,Kitabu Hajj, mlango wa 12:

“Maovu yote yamefungwa katika chumba kimoja kwa kufuli, na uwongo ndio ufunguo wake.”

377.  Amesema al-Imam Musa ibn Ja'afar a.s. :

“Mtu mwenye busara kamwe hawezi kusema uwongo hata kwa matamanio yake mwenyewe.”

378.  Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema :

“Itakuwa vyema kwa Waislamu iwapo hawatafanya urafiki na udugu pamoja na Mwongo.”

379.  Amesema al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika  Al-Kafi, j.2:

“Uwongo unateketeza misingi ya Imani.”

380.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema  katika  Al-Mustadrak al-Wasail :

“Mumin anaposema uwongo bila ya shida yoyote,basi Malaika elfu sabini humlaani !!”

“Na hutoka harufu mbaya kabisa kutokea moyoni mwake, harufu hiyo hufika hadi ‘arsh .”

“Na Allah swt humwandikia kwa dhambi hilo moja, madhambi sabini ya zinaa na zinaa zenyewe si zinaa za kawaida bali zinaa pamoja na mama yake .”

381.  Riwaya moja inasema :

‘Uwongo ni mbaya zaidi kuliko ulevi.’

382.  Allah swt anatuambia katika Qur’an Tukufu, Surah

An-Nahl,16, Ayah ya 105,

Wanaozua uwongo hawana imani.

383.  Vile vile Allah swt anatuambia katika Qur'an Tukufu, Surah

Az-Zumar ,39, Ayah ya 3,

..Bila shaka Allah hamuwongozi aliye mwongo, aliye kafiri.

384. Kwa mujibu wa Ayah za Qur'an Tukufu  tunaambiwa kuwa

 mwongo ni mstahiki wa adhabu za Allah swt  na Allah swt huwa daima ameghadhabikia. Kama vile tuonavyo katika Ayah zifuatazo :

Surah Aali-Imran, 3,  Ayah ya 61

‘.. Tutake laana ya Allah swt iwashukie waongo.’

385.  Surah An-Nuur ,24 , Ayah ya 7 :

‘… Laana ya Allah iwe juu yake iwapo ni miongoni mwa waongo.’

386.  Allah swt anatuambia katika Qur'an Tukufu, Surah Baqarah, 2,

Ayah ya 197,  kuwa : ‘Na katika Hajj hairuhusiwi maneno machafu wala ufusuka.’  Katika Ayah hii takatifu neno ‘fisq’ inamaanisha uwongo kwa mfano katika Qur'an Tukufu, Surah Al-Hujurat , 49, Ayah ya 6, tunaona kuwa uwongo unaitwa kuwa ni ‘ufasiki’. Ayah yenyewe inasema :

Enyi mlioamini ! Iwapo mtaijiwa na mwongo na habari yoyote basi msikubalie tu bali mufanye upelelezi….. 

387. Tumepewa hukumu ya kujiepusha na kuabudu masanamu na kutosema uwongo na inasemwa kuwa : ‘Basi mjiepusheni na uchafu (wa mfano wa masanamu) na jiepusheni na maneno ya uwongo.’    Qur'an Tukufu, Surah Al-Haj, 22, Ayah 30,Hapa  qauli dhur  au laghwu  inamaanisha uwongo.

388.  Katika riwaya dhambi linaitwa Ithm  au Dhambkwa Mfano amesema al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. :

Uwongo yote kwa yote ni ithm na dhamb.

389.  Mwongo huwa ni mustahiki wa laana na ghadhabu za Allah swt

na  mfano wa kauli isemwayo katika Qur'an Tukufu Surah An-Nuur, 24 , Ayah 7,  isemayo :

… Laana ya Allah iwe juu yake iwapo ni miongoni mwa waongo.

390.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema katika Mustadrak al-Wasail  kuwa

“Jiepusheni na uwongo kwani uwongo huufanya uso wenu kuwa mweusi.”

391. Amesema al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika Usuli Kafi, Kitabul Iman wal-Kufr, mlango wa uwongo :

“Bila shaka Allah swt ametengenezea kufuli  kila dhambi na ufungua wa kufuli hizo ni ulevi ambapo uwongo ni mbaya hata kuliko ulevi.”

392. Iwapo ulevi unaangamiza akili na fahamu lakini uwongo si kwamba unaangamiza akili na fahamu lakini unamfanya mtu akose adabu na heshima kiasi kwamba yeye huwa tayari kwa jambo lolote la kishetani. Iwapo mlevi atakapokuwa amelewa, huwa hana uwezo wa kuiharibu jamii kwani anakuwa hana fahamu wala habari zake mwenyewe lakini mwongo akiwa katika fahamu zake timamu huweza kuiharibu na kuiteketeza jamii nzima kwa hila na uwongo wake. Na hivyo kuleta hasara kubwa sana kwa jamii nzima.

393.  Zipo riwaya zisemazo kuwa Siku ya Qiyama midomo ya wasema uwongo itakuwa ikinuka harufu mbaya kabisa !.

394.  Harufu mbaya iliyozungumzwa hapo juu, itakuwa mbaya kabisa kiasi kwamba hata Malaika Siku ya Qiyama watachukizwa kumkaribia huyo mwongo anayenuka harufu mbaya. Lakini si Siku ya Qiyama tu, bali hata humu duniani pia wanaisikia harufu mbaya ikitoka vinywani mwa wasema uwongo. Ipo Hadith ya Mtume Muhammad s.a.w.w. isemayo :

“Wakati mja wa Allah swt anaposema uwongo, basi hutokwa na harufu mbaya kabisa kutoka mdomo wake kiasi kwamba hata Malaika pia wanajiweka naye mbali.”   (Mustadrak al-Wasail.)

395. Allah swt  humlaani msema uwongo kama vile Aya ya Mubahila inavyoelezea Qur'an Tukufu, Surah An-Nuur, 24, Ayah ya 7

kama ilivyokwishaelezwa kuwa inadhihirisha waziwazi.

‘… Laana ya Allah iwe juu yake iwapo ni miongoni mwa waongo.’

396.  Imepokelewa riwaya kuwa harufu mbaya inayotoka midomo ya mwongo huifikia mbingu.

397.  Imepokelewa riwaya kuwa Malaika walio karibu ya Allah swt pia humlaani msema uwongo.

398. Amesema al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika Al-Kafi : “Uwongo ni kiangamizacho Imani.”

399. Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Al-Kafi :

“Mtu yeyote hataweza kuionja imani hadi hapo atakapoiacha uwongo, ama uwongo huo uwe wa kikweli au kimzaha.”

ndivyo inavyopatikana kwa mujibu wa riwaya,.

400. Ipo katika Hadith moja ya Mtume Muhammad s.a.w.w. isemayo :

“Kwa mtazamo wa heshima na kiadabu, mtu aliye chini kabisa ni yule msema uwongo.”

401. Imeripotiwa kuwa uwongo ni ufunguo wa kufuli ambayo imepigwa katika nyumba iliyofungwiwa maovu yote.

402.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema katika Mustadrak al-Wasail kuwa : “Jiepusheni na uwongo kwani hiyo ni mojawapo ya aina za ufiski, na vyote hivi viwili ni vitu vya Jahannam.”

403.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema katika Al-Mustadrak al-Wasail kuwa : “Zipo alama tatu za mnafiki : kusema uwongo, kufanya khiana na kugeuka ahadi alizozitoa.”

404.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema katika Al-Mustadrak al-Wasail  :

“Ushauri wa mwongo hauna umuhimu wowote.”

405.  Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Al-Mustadrak al-Wasail:

“Na ugonjwa wa uwongo, ni ugonjwa mbaya kabisa wa kiroho.”

406. Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema : “Bila shaka Ibilisi hujipaka wanja, huvaa uchawi vidoleni na hutumia vyombo vya kuvutia hewa  puani. Ama wanja wake kufanya ni visingizio na uvivu, ama uchawi wake vidoleni ni uwongo na chombo cha kuvutia puani ni takabari na ghururi !”

407.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema katika Al-Mustadrak al-Wasail :

“Mapato maovu kabisa  ya  mwanadamu, ni uwongo.”

408. Imeripotiwa katika Al-Mustadrak al-Wasail kuwa Mtume Muhammad s.a.w.w. alijiwa na mtu mmoja aliyeuliza :

“Ewe Mtume Muhammad s.a.w.w. Je ni matendo yapi hasa yanawafanya watu waingine Motoni (Jahannam) ?”

409.  Mtume Muhammad s.a.w.w. alimjibu :

“Uwongo ! Iwapo mtu atasema uwongo, basi atakuwa amejiingiza katika dhambi la uasherati, na hivyo amekufuru, na anayekufuru ataingia Motoni (Jahannam).”

410.  Amesema al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. katika  Wasa’il

al-Shiah :

“Kwa hakika mtu ambaye anapindukia kusema uwongo huadhibiwa adhabu ya kumuasi Allah swt ambavyo mojawapo ni ugonjwa wa usahaulivu !” Na hivyo ndivyo ilivyo kuwa mtu husema uwongo na mara husahau kama yeye alikuwa amesema uwongo na hatimaye uwongo wake hukamatwa na hivyo kudhalilika, na katika kujaribu kujitetea na kujihifadhi inambidi azungumze uwongo mmoja baada ya mwingine na hivyo huingia katika machachari ya kutaka kuilinda uwongo wa kwanza. Lakini hatambui kuwa kila asemavyo uwongo mmoja baada ya mwingine, anaendelea kujidhalilisha tu.” 

Yaani mara nyingi tunajaribu kuinusuru uwongo mmoja kwa uwongo hata mia, bila hata ya kuona aibu, na hii ndiyo laana ya Allah swt kwa msema uwongo. Hapa roho na akili yake vinamkataza, lakini wasiwasi wa Shaitani unamburuta tu katika kusema uwongo baada ya uwongo kwani yeye anakuwa yu mfungwa wa Shaitani.

411. Msema uwongo huadhibiwa kwa adhabu mahususi. Mheshimiwa Rawandi katika kitabu chake  Da’awat anaandika Hadith moja ndefu ya Mtume Muhammad s.a.w.w. katika maudhui haya ambayo inazungumzia vile alivyokuwa akisimulia Mtume Muhammad s.a.w.w. kile alichokiona katika Me’raj, kuwa :

“Nilimkuta mtu mmoja amelazwa juu ya tumbo lake na yupo mtu mwingine ambaye amesimama juu ya kichwa chake na ambaye anayo nyundo ya misumariambayo anakaa akimpiga yule mtu aliyelazwa na kumjeruhi. Uso wake unajeruhiwa kiasi cha kubomokabomoka kabisa katika vipande vipande ! Nyundo inapoinuliwa juu mtu huyo huwa salama na punde inapoteremka chini hujeruhiwa hivyo hivyo na hivyo ilivyo adhabu zake.”

Kwa hayo  Mtume Muhammad s.a.w.w. anasema kuwa :

“Mimi niliuliza ni sababu gani ya kuadhibiwa hivi ?” 

Alijibiwa :

“Huyu ni yule mtu ambaye alipokuwa akitoka nyumbani kwake, alikuwa akisema uwongo kiasi kwamba watu wa duniani walikuwa wakipata hasara kubwa kutoka na uwongo wake. Basi adhabu hii atabakia nayo hadi Qiyama.”

412. Mwongo hukosa sala za usiku wa manane (salatul Layl) na baraka zote zipatikanazo kwa sala hii huzikosa na baraka mojawapo ya sala hii ni kupatikana na kuongezeka kwa riziki. Bwana Sharif, anamnakili Al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. akiwa amesema, katika Bihar al- Anwar : “Mtu anaposema uwongo hukosa baraka ya kusali sala za usiku wa manane na kama atakosa baraka za sala hiyo basi na baraka za riziki pia hukosekana !”

413. Allah swt Anasema katika Qur'an Tukufu,  Sura Az-Zumr, 39, Ayah 3 :

..Bila shaka Allah hamuwongozi aliye mwongo, aliye kafiri.

414.  Mtume ‘Isa ibn Maryam a.s. amesema , katika Al-Kafi: “Mtu ambaye anakithiri kwa uwongo basi ubanadamu wake humwondokea.” Na kwa hayo huwa ana uhusiano na watu kwani na watu wenyewe huwa hawana moyo nae.”

415.  Uwongo ni ukhabithi na uchafu mkubwa.

416.  Uwongo upo mbali na imani bali tuseme kuwa ni kinyume ya imani.

 

417.  Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema, katika Al-Mustadrak al-Wasail : “Kila kutakavyozidi kusemwa kwa uwongo, basi ndivyo vivyo hivyo imani ya mtu itakwenda ikipungua !”

418.  Mwongo ndiye mwenye madhambi mengi kuliko wote.

419.  Katika Al-Mustadrak al-Wasail  ipo Hadith ya Mtume Muhammad s.a.w.w. inayosema :

“Mojawapo ya dhambi kuu niya mtu mwenye mazungumzo na uwongo wa mtu kupindukia kiasi.”

420.  Mwongo hujiteketeza kwa uwongo wake

421. Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Al-Mustadrak al-Wasail 

“Jiepusheni na uwongo hata kama mtaona ufanisi ndani yake, lakini kwa hakika huo si ufanisi bali ni maangamizo ndani yake.”

422.  Mwongo hastahiki kuwa ndugu na rafiki wa watu

423.  Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Wasa’il al-Shiah :

“Inambidi kila Mwislamu asiufanye uhusiano na kiudugu na urafiki pamoja na msema uwongo aliyekithiri !”  

424.  Akaendelea Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. kusema :

“Kwani rafiki wake mwongo pia huchukuliwa kuwa ni mwongo ! Kiasi kwamba hata kama atasema ukweli wowote, ukweli huo hautasadikiwa kuwa ni ukweli.”

425.  Allah swt hawaongozi wafujaji na waongo

426.  Allah swt anatuambia katika Qur'an Tukufu,  Sura Al-Mumin, 40, Ayah ya 28,  kuwa

‘Kwa hakika Allah hamwongozi yule ambaye amepindukia mipaka na mwongo.’ Hivyo inamaanisha kuwa msema uwongo na mfujaji huwa wako mbali na haki na uhakika.

427.  Mwongo huonekana kuwa ni binadamu, lakini sivyo

428.  Ipo riwaya katika kitabu kiitwacho ‘Uyunil Akhbar ar-Ridhaa a.s.:

“Kwa hakika mwongo huonekana kuwa ni binadamu lakini katika hali ya Barzakh hana uso wa kibinadamu. Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema akiwa anamwelezea Bi.Fatimah az-Zahra a.s. tukio la Mi’raj,: “Usiku wa Mi’raj mimi nilimwona mwanamke mmoja ambaye kichwa chake kilikuwa kikifanana na kichwa cha nguruwe na mwili mzima uliobakia ulikuwa kama wa punda. Sababu ya hayo ni kuwa yeye alikuwa na tabia ya fitina na alikuwa akisema uwongo.”

429.  Allah swt anatuambia katika Qur'an Tukufu, Sura An-Nahl,16, Ayah 116 na 117 :

Na msiseme kwa sababu ya uwongo usemao midomo yenu, hili ni halali na hili ni haramu ili msije mkamzulia uwongo Allah. Hakika wale  wanaomzulia uwongo Allah , hawatafanikiwa.

430. ‘(Duniani) Kuna faida kidogo tu lakini (Aakhera) watapata adhabu kali ziumizazo.’

431.  Amesema al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. katika Al-Kafi:

“Msituzulie hata uwongo mmoja kwani kama hivi uwongo utakutoweni nje ya Dini bora kama ya Islam.”  Yaani kwa kuwazulia Maimamu a.s. uwongo hata moja kunatokomeza Nuru ya Imani kutoka moyoni mwa waongo. Iwapo uwongo kama huu utazuliwa kwa Maimamu a.s. katika hali ya saumu, basi saumu inabatilika papo hapo.

432.  Ni jambo la kawaida kwetu sisi kusema :

“Allah swt yupo shahidi kuwa kile nikisemacho ni sahihi au Allah swt anajua kuwa kile nikisemacho ni kweli mtupu.”

433.  Amesema al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. katika Al-Kafi:

“ ‘Mtu yeyote atakayesema kuwa Allah swt anajua’ wakati Allah swt anajua asili (yaani kinyume na achojidai huyo mtu kwa kutenda kinyume) basi ‘arsh-i-Ilahi inatetemeka kwa kuona Ukuu wa Allah swt.”

434. Vile vile Amesema al-Imam Ja'afar as- Sadique a.s. katika 

Wasa’il al-Shiah ,Kitabul Iman, mlango na.5 :

“Iwapo mtu atasema kuwa ‘Allah swt anajua wakati kwamba ni mwongo’ basi Allah swt anamwambia ‘je ewe haukumpata mwingine wa kumdanganya isipokuwa mimi tu? Ambaye unamzulia uwongo ?”

435. Kwa mujibu wa riwaya zinginezo, inasema kuwa wakati mtu

anapomfanya shahidi Allah swt katika uwongo anaouzua, basi Allah swt humwambia :

“Je haujampata mdhaifu mwingine yeyote kuwa shahidi wako katika uwongo na uzushi wako huo isipokuwa umenipata mimi tu ?”

436.  Amesema al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika Kashaful Hujjat :

“Kamwe musinakili Ahadith kutoka mtu ambaye hategemewi kuwa sahihi amasivyo wewe utakuwa umesema uwongo mkubwa kabisa.na mwongo ni mtu aliyedhalilika mbele ya Allah swt na viumbe vyake.”

437. Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Nahjul-

Balagha, alimpa nasiha Harith Hamdani kwa barua aliyokuwa amemwandikia:

“Usiwe ukiwaambia watu yale yote uliyoyasikia, kwani kunatosheleza katika kusema uwongo.”

438.  Mtume Muhammad s.a.w.w.  amesema, katika Wasa’il

al-Shiah  :

“Mtu yeyote atakachoninasabia kile ambacho sijakisema, basi makao yake yatakuwa ni Jahannam (Motoni) tu.”

438. Bwana Nuuri katika kitabu chake Darus-Salaam anaandika

kuwa bwana mmoja aliyeelimika na mwenye matendo, kwa ajili ya kukisanifu kitabu maqame’ alimwendea Bwana Muhammad ‘Ali huko Karmanshah na kusema :

“Mimi nimeota usingizini kuwa ninaiparua nyama ya al-Imam Husayn ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s., sasa je nini utabiri wa ndoto hii ?”

439.  Bwana  Muhammad ‘Ali aliinamisha kichwa chake na kufikiria,

baada ya punde  akasema : “Bila shaka wewe ni khatibu wa kusoma Majlis na kusoma masaibu.”  Huyo Bwana akajibu : “Naam !”   Akamwambia :

“Ama shughuli hii uiache au usome kwa kutoa maudhui yako kutokea vitabu vinavyoaminiwa na kutegemewa kwa usahihi.”

Imeandikwa katika kitabu Shifaus-Suduur kuwa siku moja Shekhe mmoja alikuwa akisoma waadhi mbele ya Ayatullah al-Haj Muhammad Ibrahim Kalbasi. Sheikh huyo alikuwa akionyesha kuwa al-Imam Husayn ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s. alisema “Ya Zainab! Ya Zainab !”  kwa kuyasikia hayo Ayatullah Kalbasi akasema kwa sauti ya kupaaza : “Allah swt auvunje uso wako ! Al-Imam Husayn ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s. hakusema mara mbili, badala yake alisema mara moja tu !”

rudi nyuma Yaliyomo endelea