rudi nyuma Yaliyomo endelea

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.

Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo

Na ambao anahifadhi tupu zao.

Isipokuwa kwa wake zao, au iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi –

Lakini wanaotaka kinyume ya haya, basi hao ndio wanaoruka mipaka.

Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,

Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,

Na ambao wanazihifadhi sala zao.

Hao ndio watakao hishimiwa Jannat.

244.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, katika Al-Kafi:

“Katika mlango wa Jannat kumeandikwa ‘Yapo mema kumi kwa mtoa Sadaka na mema kumi na nane kwa mkopeshaji madeni.”

Sifa nne za watu wa Jannat

245.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. :

“Yeyote yule atakayekuwa na sifa nne basi Allah swt ataliandika jina lake miongoni mwa watu wa Jannat :

246.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema :

“Mumin masikini na mafukara ndio watakaokuwa wa kwanza kuingia  Jannat kwa miaka arobaini kabla ya Mumin matajiri kuingia Jannat.

(Nitawapeni mfano. Ni sawa na meli mbili zinazopita katika vituo vya ukaguzi wa maofisa wa forodha. Naye baada ya ukaguzi anaona kuwa meli moja haina chochote, ipo tupu, hivyo ataiachilia ipite na kuendelea na safari yake. Na pale anapoikagua meli ya pili, anakuta kuwa imejaa shehena na hivyo huisimamisha na kuanza uchambuzi na ukaguzi.)

247.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliulizwa kuhusu Ayah ya

    Qur'an Tukufu : Surah al-Waqiah, 56, Ayah ya  10 , 11 , 12

Na wa mbele watakuwa mbele

Hao ndio watakao karibishwa

Katika Bustani zenye neema

248.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema :

“Jibrail a.s. kaniambia: ‘Inamaanisha Al Imam 'Ali ibn Abi Talib  a.s. na Mashi’ah. Wao ndio watakao kuwa wa kwanza kabisa kukaribia Jannat , wakiwa wamemkurubia Allah swt , Aliye Mkuu, kwa heshima mahususi waliyojaaliwa.’”

249.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema :

“Je itakuwaje pale ambapo wewe utakuwa umesimama mbele ya Jahannam, na Daraja (Siraat) litakapowekwa, na watu watakapoambiwa: ‘Vukeni Daraja ( Siraat ) hili.’

Na wewe utauambia moto wa Jahannam ‘ Huyu ni kwa ajili yangu, na huyu ni ka ajili yako !’

Hapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib  a.s. alijibu :

“Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. , je ni nani hao watakaokuwa pamoja nami ?”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamjibu :

“Hao ni Mashi’ah wako, watakuwa pamoja nawe popote pale uwapo.”

Amepokewa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akisema :

“Haki ipo pamoja na Al Imam 'Ali ibn Abi Talib  a.s.  na Al Imam 'Ali ibn Abi Talib  a.s. yupo pamoja na haki.”

JAHANNAM

250.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuhusu adhabu katika daraja la tatu

la Jahannam  ( iitwayo Saqar) ni kama ifuatavyo :

“Humo yako Mateso makali mno, inapopumua wakazi wake huungua kuwa majivu kwa kutokana na joto lake, lakini hawatakufa. Nyama yao itaunganikana tena ……… Humo pia kuna kisima kiitwacho Saqar ambayo ni kwa ajili ya wale wajivunao, wakandamizaji na wadhalimu, na walioasi na ambapo mateso yatakuwa makubwa zaidi.

Iwapo hii ndiyo itakuwa hali ya daraja la nne la Jahannam  sasa hebu fikiria hali itakayokuwa katika daraja la tano, sita na saba.

Tumwombe Allah swt atuepushe na Jahannam  !  Amin.

251. Al Imam Musa al-Kadhim a.s. amesema :

“Muelewe waziwazi kuwa hakuna atakayeishi katika Jahannam  kwa milele isipokuwa kafiri, Munafiki na watendao madhambi na uasi. Ama kwa watu wataomaliza kutimiza kipindi cha adhabu zao, watatolewa huru kutoka Jahannam.”

252.  Qur’an Tukufu Surah ya Al-Balad, 90, Ayah ya 19-20 

zisemazo :

Lakini waliokanusha Aya Zetu, hao ndio watu wa upande wa shari. Moto uliofungiwa (kila upande) utakuwa juu yao.

253.  Qur’ani Tukufu  Surah al-Humazah, 104, Ayah 5 – 9 :

Hasha! Bila shaka atavurumizwa katika (Moto unaoitwa) Hutama.  Na ni jambo gani litakalokujulisha (hata ukajua) ni nini ( Huo Moto unaoitwa ) Hutama ? Ni Moto wa Allah swt uliowashwa (kwa ukali barabara). Ambao unapanda nyoyoni. Hakika huo (Moto) watafungiwa (wewemo ndani yake ). Kwa magogo marefu marefu

254.  Qur’ani Tukufu  Surah al-Mursalat, 77: Ayah ya 32:

"Hakika (Moto huo) hutoa macheche yaliyo kama majumba."

Milango ya Jahannam

255.  Mlango wa kwanza

256.  Mlango wa pili

257.  Mlango wa tatu

258.  Mlango wa nne

259.  Mlango wa tano

260.  Mlango wa sita

261.  Mlango wa saba

262.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amenakiliwa katika

uk.145, J.1 ya al-Zamakhshari’s Rabee’ al-Abrar akiwa amemwuliza Malaika Jibrail a.s.,

“Je ni kwa nini mimi kamwe sijamwona Malaika Mikaili a.s. akicheka au kutabasamu?”

Malaika Jibraili a.s. alimjibu:

“Mikaili kamwe hakucheka wala kutabasamu kuanzia pale Jahannam  ilipoumbwa. ” 

263.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema,

“Katika safari yangu ya usiku wa (‘Israa), mimi nilisikia sauti kubwa mno, hivyo nilimwuliza Malaika Jibrail a.s., ‘Je sauti hii kubwa ni ya nini, Ewe Jibraili ?’

Naye alinijibu,

‘Ni jiwe lililotupwa kutokea juu kuangukia ndani mwa Jahannam , na imekuwa ikianguka kwa muda wa vipindi sabini vya baridi, na sasa ndipo ilipofika chini.”

264.  Abu ‘Asim ‘Ubayd ibn ‘Umayr ibn Qatadah al-Laythi, Hakimu wa

 Makkah (aliyeariki 68 A.H.), amesema,

“Jahannam  hupumua mara moja kwa sababu yake Malaika na Mitume a.s. yote hutetemeka, kiasi kwamba hata Mtume Ibrahim a.s. hupiga magoti na kusema, “Ewe Mola wangu ! Nakuomba uniokoe!”

265.  Abu Sa’eed al-Khudri amenakiliwa akisema,

“Iwapo milima itapigwa kwa rungu mara moja inayotumiwa na Malaika wa Jahannam , basi itavunjika vipande vipande na kuwa vumbi.”

266.  Tawoos ibn Keesan al-Khawlani amenakiliwa akisema,

“Wakati Jahannam ilipoumbwa, Malaika walishtushwa mno, na wakati nyie wanaadamu mulipoumbwa, basi walitulia.”

267.  Al-Hasan ibn Yasar al-Basir amesema,

“Kwa kiapo cha Allah swt! Hakuna hata mja mmoja wa Allah swt anayeweza kustahimili joto la Jahannam ! Tumeambiwa iwapo mtu atasimama Mashariki na Jahannam  ikawa upande wa magharibi na ikafunuliwa kidogo tu, basi bongo ya mtu huyo aliye Mashariki itachemka. Iwapo kama kiasi cha ndoo moja ya usaha wa Jahannam  ukimwagwa juu ya ardhi hii ya dunia, basi hakuna hata kiumbe kimoja kingalibakia hai.”

268.  Abu Zar al-Ghaffari, Allah swt amwie radhi, alikuwa akisema,

“Waambieni wale ambao hupenda kulimbikiza utajiri wao kuwa watachomwa nayo juu ya paji la uso wao, pembeni mwao, na migongoni mwao hadi watakapokuwa wamejaa kwa mioto.”

269. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema, kama vile tuambiwavyo katika uk.243, J.8, ya Bihar al-Anwar,

“Hakuna Mja wa Allah swt mwenye utajiri au mali na hataki kulipa Zaka isipokuwa kwamba atachomwa kwa vipande hivyo vya mapesa vitakavyokuwa vimepashwa moto katika moto wa Jahannam na kwamba watatumbukizwa katika adhabu hizo kuanzia juu ya vipaji vyao vya nyuso zao na migongo yao hadi pale Allah swt atakapokuwa amemaliza kupokea mahisabu na adhabu za waja wake Siku ya Qiyamah, muda ambao ni wa maelfu ya miaka kwa mujibu wa mahisabu yetu. Hapo ndipo watakapotumwa ama kuingia Jannat   au  Jahannam  .”

270.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema :

“Italetwa mbele yake, naye atachukizwa nayo; na itakapoletwa karibu yake, itauchoma uso wake na kifuvu kitadondoka. Iwapo ataweza kunywa hata kidogo kutokamo, basi matumbo yake yatakatika vipandevipande na kutokezea sehemu za nyuma ya kutokezea haja kubwa.”

271.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ameripotiwa akisema,

“Sala za mtu anayekunywa pombe hazikubaliwi kwa siku arobaini; na iwapo atakufa huku pombe ikiwamo tumboni mwake, basi Allah swt atamlazimisha anywe sadiid, maji yatokayo kwenye sehemu za uchi wa malaya ambayo yatakusanywa katika birika huko Jahannam  na kupewa watu hawa, na kwayo matumbo na ngozi zao zitachomwa.”

272.  Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. anavyotupatia picha ya

Jahannam, tumwombe Allah swt asitutumbukize humo :

‘Janga kubwa kwa mtu ni kule kutumbukia katika Jahannam ; yeye atajihisi kuwa anachemshwa mzimamzima, na ataona mateso yake yasiyona mwisho, na kiumbe fulani kinakoroma na kupumua, viumbe vyote vilivyo humo hukosa raha na kamwe hawapati fursa ya kupumzika, na kamwe hawatapata kupumzika kutokana na adhabu zake au mauti ya uhakika. Yeye hasinzii hata kidogo wala hakutakuwa na mapumziko katiko mateso yake : Kutakuwa na maumivu yakudumu kiasi ambacho tunamwomba Allah swt atunusuru na kutusaidia .’  ( Hotuba  83 ).

273.  ‘Kwa hakika ni mahala pabaya kabisa kuliko sehemu yoyote ile,

mahala ambapo mikono ya wakazi wake yanakuwa yamefungwa shingoni mwao, na vichwa vyao vimefungwa na miguu yao kwa minyororo na mavazi yao yametengenezwa kwa  lami. Mashati yao yametengenezwa kwa moto wakati ambapo adhabu zao za moto usiozimika kamwe hazitakwisha kamwe mahala ambapo mlango wake utakuwa umejazwa watu, katika moto mkali kabisa kiasi kwamba sauti zao zinasikitisha na kutisha, na miale ya moto ikipaa na kufikia kila sehemu na wala hakuna kujitoa kutoka humo na wala hakuna muda utakaokwisha,na wala haina mwisho wake kwa wale wanaoteketezwa na kuchomwa humo.’   ( Hotuba 109 ).

274. ‘Joto lake ni kali mno, kufikia chini kwake ni mbali mno, sakafu

 yake ni chuma, vinywaji vyake ni usaha.’   (Hotuba 120 ).

275.  ‘Siku ya Qiyamah, madhalimu wote wataletwa bila ya kuwapo na mtu yoyote wa kuwasaidia au kuwatetea, na hivyo watatumbukizwa katika moto wa Jahannam na humo atasagwasagwa kama vile machine za kusaga zifanyavyo, hadi hapo atakapojigonga kichwa katika sakafu ya chini kabisa.’ ( Hotuba 164 )

276. ‘Iwapo Malik (msimamizi wa Jahannam) atakuwa mkali, husababisha sehemu yake moja kuminyana na sehemu zingine, anapogombeza, milango yake huruka juu na chini (hutema kama volkeno). (Hotuba 183 )

277.  Ayah 23 ya Surah al-Fajr, 89 na katika Ayah zinginezo pia :

Basi Siku hiyo italetwa Jahannam. Siku hiyo mwanadamu atakumbuka, lakini kukumbuka huko kutamfaa nini ?

278.  Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa, 4,  Ayah 140 :

Naye amekwisha kuteremshieni katika Kitabu hiki ya kwamba mnaposikia Aya za Allah swt zinakanushwa na zinafanyiwa kejeli, basi msikae pamoja nao, mpaka waingie katika mazungumzo mengine. Hivyo mtakuwa nanyi mfano wao hao. Hakika Allah swt atawakusanya wanafiki na makafiri wote pamoja katika Jahannam.

279.  Vile vile Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Surah

al-Nisaa, 4 ,  Ayah 145 :

Hakika wanafiki watakuwa katika tabaka ya chini kabisa Jahannam, wala hutompata yeyote wa kuwanusuru.

280.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Nisaa, 4,

  Ayah 55 :

Basi wapo miongoni mwao walioamini, na wapo walioyakataa. Na Jahannam yatosha kuwa ni moto wa kuwateketeza.

281.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Jinn, 72,

 Ayah 23 :

….. Na wenye kumuasi Allah swt na Mtume wake, basi hakika hao watapata Moto wa Jahannam wadumu humo milele.

282.  Allah swt antuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa, 4 ,

Ayah 115 :

Na anayempinga Mtume baada ya kudhihirikia uwongofu, na akafuata njia isiyokuwa ya Waumini, tutamuelekeza aliko elekea, na tutamwingiza katika Jahannam. Na hayo ni marejeo maovu.

283.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Kahaf, 18,

 Ayah 106 :

Hiyo Jahannam ni malipo yao kwa walivyokufuru na wakafanyia kejeli Ishara zangu na Mitume wangu.

284. Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu,Sura al-‘A’raf, 7, 

Ayah 179 :

Na tumeiumbia Jahannam majini wengi na watu. Wana nyoyo, lakini hawafahamu kwazo. Na wana macho, lakini hawaoni kwayo. Na wana masikio, lakini hawasikii kwayo. Hao ni nyama howa, bali wao ni wapotofu zaidi. Hao ndio walio ghafilika.

285.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-‘A’raf,

7, Ayah 18 :

Akasema : Toka humo, nawe umekwisha fedheheka, umekwisha fukuzwa. Hapana shaka atakaye kufuata miongoni mwao, basi nitaijaza Jahannam kwa nyinyi nyote.

286.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura az-Zumar,

39,  Ayah 32 :

BASI NI NANI dhalimu mkubwa kuliko yule aliyemsingizia uwongo Allah swt na kuikanusha kweli imfikiapo ?  Je! Siyo katika Jahannam makazi ya hao makafiri?

 

287.  Na vile vile  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu ,

Sura al-A’raf, 7, Ayah 36 :

Na wale watakaokanusha Ishara zetu na wakazifanyia kiburi, hao ni watu wa Motoni; humo watadumu.

288.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Hud, 11,

  Ayah 113 :

Wala msiwategemee wanao dhulumu, usije ukakuguseni Moto. Wala nyinyi hamna walinzi badala ya Allah swt, wala tena hamtasaidiwa.

289.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Surah

al-Maidah,5,  Ayah 2 :

…. Na saidianeni katika wema na ucha Mungu. Wala msisaidiane katika dhambi na uadui….

290.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Jathiyah,

 45,  Ayah  24 :

Na walisema:Hapana ila huu uhai wetu a duniani – twafa na twaishi, na hapana kinacho tuhiliki isipokuwa dahar. Laini wao hawana ilimu ya hayo, ila wao wanadahani tu.

291.  Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. anasema Safari ndefu lakini

matayarisho ya safari ni madogo. Tukiwa watumwa wa dunia basi tutatumbukia Jahannam .

292.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema katika Mizanul

Hikmah kuwa :

“Mapenzi ya dunia ndiyo chanzo chote cha kila aina ya madhambi.”

293. Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al- ‘Asra’, 17,

Ayah 18 :

Anayetaka yapitayo upesiupesi, tutafanya haraka kumletea hapa hapa tunayoyataka kwa tumtakaye. Kisha tumemwekea Jahannam ; ataingia humo hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa na kufurushwa.

294.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Tawbah,

9,  Ayah  34 – 35 :

Enyi mlioamini! Hakika wengi katika makuhani na wamonaki wanakula mali za watu kwa batili na wanazuilia Njia za Allah swt. Na wanaokusanya dhahabu na fedha, wala hawazitumii katika Njia ya Allah swt. Wabashirie khabari ya adhabu iliyochungu.

Siku (mali yao) yatakapotiwa moto katika moto wa Jahannam , na kwa hayo vikachomwa vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo yao, “Haya ndiyo (yale mali) mliojilimbikia nafsi zenu, basi onjeni (adhabu ya ) yale mliyokuwa mkikusanya.”

(Imeelezwa katika riwaya kuwa neno lililotumika katika Ayah hii kanz inamaanisha mali yoyote ile ambamo zaka haijatolewa).

295.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Anfal, 8,

  Ayah  15 – 16:

Enyi Mlioamini! Mkikutana na waliokufuru vitani msiwageuzie mgongo.

Na atakayewageuzia mgongo wake siku hiyo – isipokuwa kwa mbinu za vita au kuungana na kikosi – basi atakuwa amestahiki ghadhabu ya Allah swt . Na pahala pake ni Jahannam, na huo ni mwisho muovu.

296.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Maida,

 5,  Ayah 32 :

Kwa sababu ya hayo tuliwaandikia Wana wa Israili ya kwamba aliye muuwa mtu bila ya yeye kuuwa, au kufanya uchafuzi katika nchi, basi ni kama amewauwa watu wote. Na mwenye kumuokoa mtu na mauti ni kama amewaokoa watu wote. Na hakika wakiwajia Mitume wetu na hoja zilizo wazi. Kisha wengi katika wao baada ya haya wakawa waharibifu katika nchi.

297.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa,4,

 Ayah 93 :

Na mwenye kumuuwa Mumiin kwa kukusudia, basi malipo yake ni Jahannam humo atadumu, na Allah swt amemkasirikia, na amemlaani, na amemuandalia adhabu kubwa.

298.  Qur’ani Tukufu , Sura al-Ali Imran, 3, Ayah 21 :

Hakika wanaozikataa Ishara za Allah swt , na wakawauwa Manabii pasipo haki, na wakawauwa watu waamrishao Haki wabashirie adhabu kali.

299.  Watu wa Jannatwatawauliza watu wa Jahannam kile

kilichowaingiza Jahannam. Nao watawajibu kuwa wao hawakuwa miongoni mwa waliokuwa wakisali. Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Muddathir, 74,  Ayah 39 – 46 :

Isipokuwa watu wa kuliani.

Hao watakuwa katika mabustani, wawe wanaulizana

Khabari za wakosefu:

Ni nini kilichokupelekeni Motoni (Saqar) ?

Waseme : Hatukuwa miongoni waliokuwa wakisali.

Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.

Na tulikuwa tukizama pamoja na waliozama katika maovu.

Na tulikuwa tukiikanusha Siku ya malipo.

300.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu,Surah

 al-Fussilat,41, Ayah 7 :

Ambao hawatoi Zaka na wanaikataa akhera.

301.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Nisaa, 4,  

Ayah  10 :

Hakika wanaokula mali ya mayatima kwa dhuluma, hapana shaka yoyote wanakula matumoni mwao moto, na watingia Motoni.

302. Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al- Baqarah,

2, Ayah 275 :

Wale walao riba hawasimami ila kama anavyosimama aliyezugwa na Shaitani kwa kumgusa. Hayo ni kwa kuwa wamesema: Biashara ni kama riba. Lakini Allah swt ameihalalisha biashara na ameiharamisha riba. Basi aliyefikiwa na mawaidha kutoka kwa Mola wake Mlezi,, kisha akajizuia, basi yake ni yaliyokwisha pita, na mambo yake yako kwa Allah swt. Na wenye kurudia basi hao ndio watu wa Motoni, humo watadumu.

Allah swt huiondolea baraka riba, na huzibariki sadaka…

303.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Ibrahim,

14,  Ayah 28 – 29 :

Hebu hukuwaona wale waliobadilisha neema ya Allah swt kwa kukufuru, na wakawafikisha watu wao kwenye nyumba ya maangamizo ?

Nayo ni Jahannam ! Wataingia.  Maovu yaliyoje makazi hayo !

304. Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Surah

al-Mutaffifiin, 83, Ayah 1 – 10 :

Ole wao hao wapunjao!

Ambao wanapojipimia kwa watu hudai watimiziwe.

Na wao wanapowapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa

Katika Siku iliyo kuu,

Siku watapomsimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote ?

Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

Unajua nini Sijjin ?

Kitabu kilichoandikwa.

305. Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Humaza,

104,  Ayah 1 – 5.

Ole wake kila safihi, msengenyaji !

Aliyekusanya mali na kuyahisabu.

Anadhanim kuwa mali yake yatambakisha milele !

Hasha! Atavurumishwa katika Hutama

Na nani atakujuvya ni nini Hutama ?

Moto wa Allah swt uliowashwa.

Ambao unapanda nyoyoni.

Hakika huo utafungiwa nao

Kwenye nguzo zilionyooshwa.

306.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Surah

al-Mumin, 23, Ayah 43 :

Hapana umma uwezao kutanguliza ajali yake wala kuikawiza.

307.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Asra’,

17,  Ayah 27 :

Kwa hakika wabadhirifu ni ndugu wa Masheitani. Na Shaitani ni mwenye kumkufuru Mola wake Mlezi.

308.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Zukhruf,

43,  Ayah 74 :

Kwa hakika wakosefu watakaa katika adhabu ya Jahannam

Hawatapumzishwa nayo na humo watakata tamaa.

309.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Nisaa,

   4,  Ayah 14 :

Na anayemuasi Allah swt na Mtume wake, na akaipindukia mipaka yake, (Allah swt ) atamtia Motoni adumu humo, na atapata adhabu ya kudhalilisha.

310.  Allah swt amewaamrisha Malaika kuwa:

Mtu anaponuia kutenda jambo jema wamwamdikie thawabu. Na anapoanza kutembea katika kulifanya tendo jema basi hapo pia anaongezewa thawabu nyingi na pale anapolianza kutenda tendo jema basi huongezewa zaidi ya hayo na anapomaliza kulitenda tendo jema basi hapo analipwa thawabu nyingi mno zisizo na  hisabu.

Lakini mtu anaponuia kutenda dhambi basi hapo haandikiwi adhabu, na anajitoa kwenda kutenda dhambi napo pia haandikiwi kwa sababu inawezekana akarudia njiani na anapolianza tendo ovu pia kuna uwezekano wa kutolikamilisha na kwa masikitiko makubwa, anapolikamilisha basi kwa huruma zake Allah swt, huandikiwa dhambi moja tu.

T A W B A

311.  Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Al-Mahajjat-ul-Baydha:

“Majonzi makubwa ya watu wa Jahannam ni kuahirisha kwao Tawba”

312.  Amesema al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika,

Was’il al-Shiah, J.16, Uk.74:

“Yeyote yule anayefanya Tawba ni sawa na yule mtu ambaye hana mzigo wowote wa madhambi ya aina yoyote ile.”

313.  Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Qurar-ul-

Hikam, Uk. 240:

“Wapo waahirishaji ambao huahirisha kufanya Tawba hadi hapo mauti inapowafikia.”

314.   Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwambia

Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s., katika Bihar al- Anwar, J. 77, Uk. 63:

“Ewe ‘Ali ! Amebarikiwa yule ambaye anatazwa na Allah swt wakati pale anapolia kwa ajili ya kutaka msamaha wa madhambi ambayo hakuna mwingine ajuaye illa Allah swt tu.”

(Baadhi ya Ahadith zinasisitiza kuwa haimpasi mtu kuwaambia watu wengine juu ya madhambi yake mwenyewe. Hivyo inambidi aungame madhambi yake kwa Allah swt tu na wala si kwa mtu mwingine.)

315.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Bihar al- Anwa , J. 3, Uuk. 314:

“Katika kila sehemu ya tatu ya usiku na usiku wa kuamkia Ijumaa kuanzia usiku uingiapo( hadi alfajiri) Allah swt huwauma Malaika mbinguni ili kuita: ‘Je yupo mwenye kuomba ili nimtimizie ombi lake ?’ Je yupo yeyote mwenye kufanya tawba ili nimrejee ? Je yupo aombaye msamaha ili nimsamehe ?’ “

Tanbihi: Katika utamaduni wa Kiislamu, tunafundishwa kuwa kulala katika usiku wa kuamkia Ijumaa kunaitwa usingizi wa masikitiko ; kwa sababu Siku ya Qiyama watu watakuwa wakisikitika mno kwa kulala usiku hizo.

316.  Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s.katika,  Bihar al-

Anwar, J. 92, Uk. 216:

“Fungeni milango ya madhambi kwa kumwomba Allah swt , na mufungue milango ya utiifuu kwa kusema Bismillah-ir-Rahmaan-ir-Rahiim.”

KULINDA HESHIMA YA WAUMINI

317.   Amesema al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika, 

Bihar al- Anwar , J. 74, Uk. 301:

“Ni faradhi kwa kila Mwislamu kusitiri na kuzificha aibu sabini (70) za Mwislamu mwenzake (ili kulinda heshima yake).”

(Makosa na kasoro zake zote zishughulikiwe kibinafsi na wala zisienezwe na kutangazwa kwa watu wengine).

318.    Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Bihar

al- Anwar, J. 74, Uk. 165:

“Kubali msamaha akuombao Nduguyo Mwislamu na kama hakufanya hivyo, jaribu kumvumbulia hivyo.”

319.    Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, 

Mustadrak Al-Was’il al-Shiah’il-ush-Shiah,   J. 12, Uk. 305 na 14155:

“Hali mbaya kabisa ya uhaini ni kutoboa habari zilizo siri.”

320.    Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Ghurar-

ul-Hikam, Uk. 322:

“Kumuonya kwako aliyetenda makosa miongoni mwa au mbele ya  watu ni kumdhalilisha.” (Inakubidi uongee naye katika faragha).”

321.   Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s.katika, Al-kafi,

J. 2, Uk. 192:

“Katika matendo yote aypendayo Allah swt, ni kule kumletea furaha Mwislamu kwa mfano : kumshibisha, kumwondolea majonzi yake, au kumlipia madeni yake.”

M A T E N D O  M E M A

322.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Bihar al- Anwar , J. 76, Uk. 43:

“Kwa kufanya usuluhisho na amani miongoni mwa watu wawili (kwa kulinganisha) ni borai kuliko ibada za sala na saumu zake mwenyewe.”

323.    Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Nahjul-

Balagha, Uk. 511 , Semi No. 248;

“Iwapo mtu atakufikia wewe kwa mema, basi inakubidi uhakikishe kuwa fikira zake zinabakia kweli.”

324.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

  Bihar al- Anwar , J. 96, Uk. 119:

“Yeyote yule awaongozaye watu kwa taqwa (atalipwa) sawa na yale ayatendayo (aliyeongozwa) hayo matendo mema..”

325.   Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s.katika, Al-Khisal

cha Saduq, Uk. 323:

“Yapo matendo sita ambayo Mwislamu Momiin anaweza kufaidika nayo hata baada ya kufariki kwake:

·     Kumwacha nyuma mtoto atakaye mwombea maghfira,

·     Kuacha Mus.-hafu sharifu ambao watu watakuwa wakisoma,

·     Kuchimba kisima cha maji kitakachokuwa kikiwafaidisha watu,

·     Mti alioupanda yeye,

·     Sadaka aliiyoitoa katika kusababisha maji yakatirika vyema,

·     Ahadith na Sunnah nzuri atakazokuwa ameacha nyuma yake na zikifuatwa na watu.

326.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.katika,

Bihar al- Anwar, J. 76, Uk. 126:

“Iwapo isingalikuwa vigumu kwa Ummah wangu basi ningalikuwa nimewaamrisha kupiga miswaki kwa kila Sala.”

DHULUMA NA UONEVU

327.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Thawab-ul-A’amaal, Uk. 309:

“Siku ya Qiyama, mwitaji ataita:’ Je wako wapi wadhalimu na wasaidizi wao na wale wote waliowatengenezea wino au waliowatengenezea na kuwakazia mifuko yao au waliowapatia wino kwa ajili ya kalamu zao ? Kwa hivyo, wakusanye watu wote hawa pamoja nao !’ “

328.    Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Nahjul-

Balagha, Uk. 347:

“Kwa kiapo cha Allah swt, Iwapo nitapewa umiliki wa nchi sana pamoja na yale yote yaliyomo chini ya mbingu zilizo waz  ili nimuasi Allah swt kwa kiasi cha mimi kunyofoa punje moja ya shairi kutoka kwa sisimizi, basi mimi kamwe sitafanya hivyo.”

329.   Amesema Al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika,

Al-Kafi, J. 2, Uk. 330:

“Zipo aina tatu za dhuluma: moja, ni ile ambayo Allah swt anasamehe, pili, ile ambayo Allah swt haisamehe, na tatu ni ile ambayo Allah swt haipuuzii.

Hivyo, dhuluma ambayo Allah swt haisamehe ni ukafiri dhidi ya Allah swt. Na dhambi ambalo Allah swt anaisamehe ni kile mtu anachojifanyia dhidi yake mwenyewe na Allah swt. Lakini dhambi ambalo Allah swt haipuuzii ni ile ambayo inavunja haki za watu. “

rudi nyuma Yaliyomo endelea