rudi nyuma Yaliyomo endelea

109.   Amesema al-Imam Ali ar-Ridha a.s. katika,  Ma’anil

Akhbaar, Uk. 180  na‘Uyun-il-Akhbaar –ir- Ridha, J. 1, Uk. 207:

“Rehema za Allah swt ziwe juu ya yule ambaye anazihuisha amri zetu.”

Na halikuwapo mtu akamwuliza Imam a.s. ni vipi wanaweza kuhuisha amri zao, na Imam a.s. alimjibu:

“Anaweza akijifunza ilimu zetu na akawafundisha watu. Kwa hakika, iwapo watu wangelikuwa wamezijua faida na mema ya semi zetu, basi kwa hakika wangalitufuata sisi.”

ELIMU – HEKIMA – MA’ARIFA.

110.  Elimu ni fidia kwa juhudi za akili.

111.  Wema ni sababu kuu ya elimu.

112.  Kumwogopa Allah swt ni matokeo ya elimu.

113.  Jumla ya utukufu wote, ni elimu au ma’arifa.

114.  Yeyote afundishaye herusi moja, amenifunganisha nae

        minyororo.

115.  Elimu iliyo bora ni ile inayomfaa mwenye kuwa nayo.

116.  Elimu ni hazina na maisha.

117.  Unyenyekevu ni matokeo ya elimu na ma’arifa.

118.  Mtu mwenye elimu yu hai hata kama amekufa.

119.  Dini ni ghala na elimu ni mwongozo wa kuifikia ghala.

120.  Ili kupata ufanisi itikia elimu na kupuuzia ujahiliya.

121. Wengi wanaelezea ma’arifa, lakini ni wachache waiingizayo akilini mwao.

122. Bakhshishi iliyo kamili ya Allah swt ni ile maisha iliyotegemea elimu na hekima.

123.  Wapumbavu wengi mno wanawafanya wasomi kuwa wachache.

124. Aliyeelimika anamwelewa vyema mjinga kwani yeye binafsi alikuwa mjinga awali.

125. Na mtu aliye jahili hataweza kumwelewa mtu aliyeelimika kwani hajaelimika mwenyewe.

126.  Wana elimu wanaishi katika kiwiliwili kilichokufa cha ujahili.

127.  Ma’arifa huuwa ujahili.

128.  Elimu ndiyo iipatiayo maisha Roho.

129.  Ma’arifa chache (ya Allah swt) huharibu mwenendo wa mtu.

130.  Hakuna chochote kile pasi na nuru  ya kweli tu itakayokutakasisha.

131.  Kuwaheshimu waliosoma ni kumheshimu Allah swt.

132.  Ma’arifa ni chanzo cha khofu ya Allah swt    (--inaletwa na )

133. Kile kikomazacho ma’arifa ni matendo kwa kutumia hekima na ma’arifa hayo.

134.  Kufundisha ndiko kujifunza.

UMUHIMU WA MAARIFA

135.    Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alielekea Msikitini na huko akakuta makundi mawili ya Waislamu. Kikundi cha kwanza kilikuwa kikijifunza ilimu ya Dini, na kikundi cha pili kilikuwa kinafanya ‘ibada.

Kwa kuona hayo Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. :

“Vikundi vyote viko katika kheri, ama hawa wanamwomba Allah swt  na hawa wanajifundisha na kuwafundisha wengine wasio na ilimu, kwa hakika hawa ndio bora, nimetumwa kwa watu ili kuwafundisha.”

Kisha akakaa pamoja nao.

136.   Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“Ewe Kumail ! Hakuna harakati zozote utakazozifanya, ila unahitaji kuwa na maarifa.”

137.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“ Kukosa macho ni jambo jepesi kuliko kukosa mwanga (maarifa)”.

138.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

”Usizungumzie usilolifahamu”.

139.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema  :

“ Elimu ni msingi wa kila heri”.

140.  Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. :

“ Katika hadith inayotokana na mababa zake, toka kwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ambae ameipokea toka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.

 “Watu wengine walio na thamani (qimmah) kwa watu ni wale walio na elimu nyingi kati yao, na wale wenye thamani duni kati yao ni wale wachache wao wa elimu”.

KUTAFUTA ELIMU.

141.  Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. :

“Kutafuta elimu ni faradhi (lazima) kwa kila Mwislamu Mwanamme na Mwislamu Mwanamke”

142.  Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. :

“ Kujitolea nafsi yake mtu kwa ajili ya kutafuta elimu, mfano wake ni kama anaepigana vita kwa ajili ya Allah  swt.”

143.    Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.

“Watu ni aina mbili; Aalimu (mwenye elimu) na mwenye kujifundisha, ama watu wengine ni upumbavu na wapumbavu mahala pao ni motoni”.

144.  Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. :

“Kuwa mwenye elimu au mwenye kujifundisha elimu, jiepushe kuwa mwenye kupumbazika na kuona ladha ( ya kutojihangaisha kutafuta elimu.)

145.  Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.

“ Sikupenda kumwona kijana, kijana kati yenu ila amekuwa kati ya moja ya hali mbili;

Ima awe mwenye elimu au

mwenye kutafuta elimu, na kama hakufanya hivyo basi amepoteza nafasi yake, na aliye poteza nafsi yake amefanya dhambi na anayefanya dhambi ndio amekaa motoni.”

AKILI.

146.  Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema

“ Hakika heri yote hupatikana kwa akili”.

147.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“ Akili ni jahazi ya elimu.”

148.  Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“ Hakugawa Allah swt kwa waja wake kitu kilicho bora kuliko akili, usingizi wa mwenye akili ni bora kuliko kukesha kwa mtu mjinga, kufuturu (kutofunga) kwa mtu mwenye akili ni bora kuliko Saumu ya mtu mjinga, na kutosafiri kwa mtu mwenye akili ni bora kuliko safari ya mtu mjinga”.

149.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema  

“ Ubinadamu wa mtu hutokana na akili yake.”

150.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.:Kumwambia mtoto wake Al Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. :

“Ewe Mwanangu! Hakika ya utajiri ni utajiri wa akili na ufakiri mkubwa ni kuwa mtu mpumbavu.”

151.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“Akili ndio mjumbe wa haki.”

152.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“ Rafiki wa kila mtu ni akili yake, na adui ni ujinga wake”.

153.  Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“ Mwenye kutekeleza (vitendo) kutokana na kile anachojua, Allah swt humrithisha (humjalia) elimu ambayo haijui.”

154.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema  :

“ Akili ni kitu cha maumbile,  huzidi kwa elimu na majaribio.”

155.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“ Asiejaribu mambo hudanganyika.”

156.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema  :

“ Na majaribio ya muda mrefu ni nyongeza ya akili.”

157.  Al Imam Musa al-Kadhim a.s. amesema :

“ Ewe Hisham! Hakika kwa Allah  swt juu ya watu kuna dalili (burhani) mbili: Dalili ya wazi, na dalili ya ndani. Na ama ile ya wazi ni Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. , Manabii na Maimamu a.s. na ama ya ndani ni akili.”

158.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema

“Mwenye kuwa nayo akili, amekuwa na  dini.”

159.  Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“ Mwenye kuijua nafsi yake, hakika amemjua Allah swt.”

160.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“ Huzijua mtu aibu za nafsi yake, ni maarifa yenye kunufaisha zaidi.”

161.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“ Na akili ni ngao (ngome) ya majaribu.”

162.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema

“ Na kila ujuzi unahitaji majaribio.”

163.  Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Kutafuta elimu ni bora kuliko kufanya ibada. Amesema Allah swt,

Hakika wanaomwogopa Allah swt miongoni mwa waja wake ni wanachuoni.

164.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema  

“ Hakuna zaka iliyo bora katika elimu kuliko kuifanyia kazi.”

165.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.  amesema:

“ Mweney kuwa na yakini (uhakika wa Jambo) hufanya amali (kazi) hali ya kuwa yeye ni mwenye kupigania Jihadi.”

166.  Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Lau (mtihani wa Allah  swt) husubiri, na asiyefahamu hakanushi.”

167.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“Hasubiri mtu yeyote katika uchungu wa haki ila yule anae kuwa na yakini (uhakika) wa matokeo yake.”

168.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema  :

“ Hakuna kitu chochote kile ila kina upeo wake,”

akaulizwa” Ni nini upeo wa Yaqini (kuwa na uhakika)?. Akasema “Usiogope kitu chochote.”

169.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“ Kutoa majabali kutoka mahali pake ni rahisi kuliko kuutoa moyo kutoka katika chochote.”

170.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema  :

“ Haisafiki kazi mpaka isihi (iwe sahihi) elimu.”

171.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“ Mwanachuoni katika zama zake, hayamhujumu matatizo.”

172.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema  :

“ Aliye kamilika kiakili hayawi mazito kwake matatizo.”

173.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.  amesema:

“Akili iliyokamilika, ndiyo yenye kuvunja mabaya.”

174.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema  :

“ Lengo la elimu ni kufanya kazi vizuri”.

MAELEZO 1.

Katika nadharia za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na Mawasii wake, elimu ni kitu bora kuliko kitu kingine chochote kile, kiasi kwamba jambo hili limeweza kuwastajaabisha watu wengi kutokana na hadithi nyingi zilizo pokewa zinazo sifa ubora wa elimu, hadithi kadhaa zimesikiwa toka kwenye ulimi wake Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na Maimamu a.s.  Lakini je! Mshangao huo utabaki mpaka lini? Mshangao mbele ya uhakika wa mambo yalivyo hausaidii kitu. Je hatuamini kwamba maendeleo ya Dunia na Akhera hupatikana kwa elimu?. Jibu liko wazi kwamba kwa elimu hupatikana na maendeleo. Kwahiyo tunajionea wazi kuwa thamani ya elimu iko juu sana.

MAELEZO 2.

Mwanadamu hutokea akajifunza elimu, lakini elimu yake ikawa ni upuuzi mtupu na balaa kwa watu, kutokana na kule kuvuka mpaka kwake na kuitumia elimu yake isivyo ndivyo na kinyume cha mtu mwenye akili, matokeo ya mtu wa ina hii ni kugundua mambo ambayo hayana faida yoyote kwa wengine, elimu kama hii humpoteza yeye mwenyewe na ummah pia katika dunia na akhera, hatimaye mtu huyu hugunduwa utengenezaji wa pombe na mabomu.

175.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema  :

“ Inamtosha mtu kuwa mjinga kwa kutokuzijua aibu zake.”

176.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.  amesema:

“Enyi watu! Hakuna heri katika dini isiyo na mafunzo ndani yake.”

177.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“ Mfanya ibada bila ya mafunzo ni kama punda mwenye kuzunguka, anazunguka na wala hachoki.’’

178.  Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema  :

“Mwenye kueneza elimu basi anao ujira mfano wa mwenye kutekeleza kwa hiyo (kutokana na elimu hiyo).”

179.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.  amesema:

“ Upingeni ujinga kwa elimu.”

180.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema  :

“Katika kuwasifu waja wa Allah swt: Nawakasimamisha masikio yao (kwakusikiliza ) elimu yenye manufaa kwao.”

181.  Al Imam Musa al-Kadhim a.s. amesema:

“ Nimekuta elimu ya watu iko katika mambo manne:

Kwanza kati ya hayo manne ni kumjua Mola wako,

Pili kujuwa alicho kiumba,

Tatu kujuwa anacho taka kwako,

Nne kujuwa chenye kukutoa katika dini yako.”

182.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema  :

“Lau ningeijiwa na kijana miongoni mwa vijana wa ki-Shi’a hajifunzi (elimu ya dini) ninge mtia adabu.”

183.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.amesema  :

“ Rafiki wa kila mtu ni akili yake na adui wake ni ule ujinga wake.”

184.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“ Mwenye akili ni kufikiri ataona (kuona muongozo)

185.  Al Imam Musa al-Kadhim a.s.  amesema:

“ Kila kitu kina dalili, dalili ya mwenye akili ni kufikiri na dalili ya kufikiri ni kunyamaza.”

186.  Mtume Mtukufu Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema :

“Kufikiri kwa muda wa saa moja ni bora kuliko ibada ya mwaka.”

187.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“ Kufikiri ni kioo kilicho safi.”

188.  Al Imam Hassan al-'Askari a.s.  amesema:

“Haikuwa ibada kwa uwingi wa kufunga na kusali, hakika ya ibada ni kufikiri (na kuzingatia) kuhusu Allah swt.”

189. Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.  amesema:

“Elimu ndio kichwa cha kila heri na ujinga ndio kichwa cha kila shari.”

190. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.  amesema  :

“ Ujinga ni Umauti.”

UJAHILI:

191.    Hakuna maumivu ya kupita zaidi ya ujahili.

192.  Watu ni adui kwa kile walichobakianacho jahili.

193.  Fadhila za jahili ni sawa na bustani juu ya chungu cha kinyesi.

194.  Wasi-wasi ni matokeo ya ujinga.

195. Nia kuu ya busara ni kule mtu kukubali na kukiri ujinga wake (iwapo anao).

196. Ni mtu mpumbavu kabisa iwapo atapuuzia umuhimu wake (atajidharau, kujidhalilisha)

197.  Mjinga ni mwenye hasara hata kama akiwa katika hali gani ile.

198.  Ujinga uliodhalilishwa (wa ujinga) ni kule kumtii mwanamke.

UTUKUFU NA UMUHIMU WA WANAZUONI

199.  Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika, 

    Bihar al- Anwar , J. 2, Uk. 49:

 “Yapo makundi mawili ya Ummah wangu kwamba wanapokuwa wachaAllah swt, Ummah wangu utakuwa sahihi na wakati watakapokuwa wameingiliwa na ufisadi, basi Ummah wangu utageuka kuwa waovu.”

 Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliulizwa kuhusu waliokuwa wakimaanishwa. Alijibu :   “Wanazuoni wa Din na watawala.”

200.  Amesema Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika, Bihar

al- Anwar , J. 1, Uk. 222:

“Utakapokuwa umekutana na Mwanazuoni basi uwe mwenye kutaka kujua mengi kuliko kujifanya msemaji zaidi, na ujifunze namna ya kusikiliza na namna ya kuzungumza vyema, na wala usimkatize kauli yake yoyote atakayokuwa akizungumza.”

201.  Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika Ithna-

Ashariyyah, Uk. 245:

“Ewe ‘Ali ibn Abi Talib  ! Malaika Jibraili alitaka alitamani kuwa mwanadamu kwa sababu saba zifuatazo:

1.  Sala za Jama’a

2.  Uhusiano pamoja na wanazuoni

3.  Kudumisha amani miongoni mwa watu wawili

4.  Kuwahurumia na kuwahishimu mayatima

5.  Kuwatembelea na kuwajua hali wagonjwa,

6.  Kuhudhuria na kushiriki katika mazishi

7. Kuwagawia maji mahujjaji

Kwa hivyo nyinyi pia muwe watu wa kuzipenda na kuvitekeleza vitu hivyo.”

202.  Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. Amesema katika, Nahjul

Balagha, Semi No. 265:

“Iwapo matamshi ya watu wenye busara yatakuwa katika malengo yao, basi huwa kama matibabu, lakini yanapokuwa siyo sahihi basi ni sawa na ugonjwa.”

203.  Amesema al-Imam Hassan al ‘Askari a.s. katika, Al-

Ihtijaj, J. 2, Uk. 155:

“Maulamaa wa Kishia’h ni walinzi wa mishikamano ya Islam.  Kwa hivyo, yeyote yule katika wafuasi wetu anayechukua jukumu hili basi ni bora kuliko kupigana vita dhidi ya Waroma (kwa sababu huyu analinda mishikamano ya imani zetu).

204.  Amesema al-Imam ‘Ali ar-Ridha a.s. katika, Bihar al-

Anwar , J. 2, Uk. 5:

“Jihadharini kuwa hakimu wa kidini wa kweli ambaye anapatia watu mema na huruma, na kuwahifadhi dhidi ya maadui wao, kuwazidishia neema za Peponi  na kuwapatia ridhaa za Allah swt kwa ajili yao (kwa kupitia hidaya).”

205.  Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Bihar al-

Anwar , J.2, Uk. 43:

“ ….  Malipo kwa Mwanazuoni ni zaidi kuliko malipo ya mtu afungaye saumu nyakati za mchana na kusali nyakati za usiku na akipigana vita vya jihadi kwa ajili ya Allah swt. Na, wakati mwanazuoni anapokufa, basi kutatokezea pengo katika Islam ambalo haliwezi kuzibwa illa kwa aina yake tu.”

206.  Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Nahjul

Balagha,semi No. 147:

“Ewe Kumayil ! Wale wanaojilimbikizia utajiri na mali ni watu waliokwisha kufa hata kama watakuwa bado hai, wakati maulamaa (wanazuoni) wenye elimu watabakia hadi hapo dunia itakapokuwa ikibakia. Hata kama watakuwa lakini mafunzo na mifano yao itabakia mioyoni mwa watu.”

207.  Amesema al-Imam Husayn a.s. katika, Tuhaful ‘Uqul,

Uk. 172:

“ ….. Kwa hakika, njia ya masuala ya Waislamu na hukumu za Shariah zipo katika mikono ya Wanazuoni wakiAllah swt ambao ndio wenye amana za Allah swt katika mambo ayatakayo na yale asiyoyataka …”

KUWA MAKINI KUHUSU AKHERA

208.  Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Bihar al- Anwar, J. 1, Uk. 203,

“Wafuasi wa Mtume Isa a.s. walimwuliza ni watu gani wawafanye marafiki wao, naye a.s. aliwajibu: “Pamoja na wale ambao wanapokuwa nanyi humkumbusha Allah swt, mazungumzo yao hukuzidishieni ilimu na matendo yao huwavutieni ninyi kutenda matendo mema kwa ajili ya Aakhera.”

209.  Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Qurar-ul-

Hikam, Uk. 335:

“Kusiwepo na shughuli ya aina yoyote ile ambayo itakuzuia kutenda matendo kwa ajili ya Aakhira, kwa hivyo, muda wa kufanya hivyo upo mdogo sana.”

210.  Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema katika, Qurar-ul-

Hikam, Uk. 274:

“Yeyote yule atakayeiuza Aakhera yake kwa maisha ya humu duniani, basi kwa hakika amepoteza yote kwa pamoja.”

211.  Al-Imam ‘Ali ibn Muhammad al-Hadi a.s. Amesema

katika, Bihar al- Anwar, J. 78, Uk. 370:

“Kumbuka pale utakapokuwa kitandani ambapo mauti imekukalia kichwani na huku umezungukwa na ndugu na maJama’a zako, na hapo hakuna mganga anayeweza kukuepusha na kifo hicho wala hakuna rafiki anayeweza kukusaidia.”

JANNAT.

212.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema,

“Kila mtu katika Jannat atahudumiwa kwa vitu vizuri vya Jannat kiasi kwamba hata atakapopata wageni kwa malaki na malaki lakini hakutapungua chochote… neema nyingi tele…”

213.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alijibu :

“Allah swt ni mwadilifu. Iwapo matendo mema ya mwanamme yatakuwa zaidi ya mwanamke, basi mwanamme atapewa fursa kwanza kufanya chaguo na uamuzi iwapo anapendelea kuishi na mke wake au hapana. Na vivyo hivyo iwapo matendo mema ya mwanamke yatakuwa zaidi basi naye atapewa chaguo kama hili yaani iwapo atapenda kuishi na mume wake au hapana. Iwapo mwanamke huyo hatamchagua bwanake awe mume wake hapo Jannat, basi huyo mwanamme aliyekuwa mume wake humu duniani hatakuwa mume wake huko Jannat .”

214. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alisema kuwa Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu Sura-i-Yasin,36, Ayah ya 78

‘Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake – akasema: “Nani atakaihuisha mifupa na hali imesagika ?”

215.  Katika Milango yote 8 ya Jannat kumeandikwa :

Hakuna mungu mwingine isipokuwa Allah swt tu; Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Wake; Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ni mja  (Walii) Wake halisi,

216.  Mlango wa kwanza

Katika mlango wa kwanza wa Jannat kumeandikwa :

Zipo njia mbalimbali za kujipatia kila kitu, na njia za kujipatia riziki ni nnne :

217.  Mlango wa pili

Zipo njia mbalimbali za kujipatia kila kitu, na njia za kujipatia furaha katika maisha ya Aakhera ni nne :

·   Kuonyesha huruma kwa mayatima,

·   kuwawia wema wajane,

·   kuwasaidia wacha-mungu katika kufanikisha malengo yao na

·   kuwaangalia na na kuwasaidia masikini na wasiojiweza.

218.  Mlango wa tatu

Zipo njia mbalimbali za kujipatia kila kitu, na na njia za kujipatia siha njema katika maisha haya mafupi ni nne :

·   Kuongea kwa uchache,

·   kulala kidogo,

·   kutembea kidogo na

·   kula kidogo.

219.  Mlango wa nne

·   Yeyote yule amwaminiaye Allah swt na siku ya Qiyamah basi lazime awe mkarimu kwa wageni wake;

·   Yeyote yule amwaminiaye Allah swt na siku ya Qiyamah basi lazime awe mkarimu kwa jirani zake;

·   Yeyote yule amwaminiaye Allah swt na siku ya Qiyamah basi lazime awe mkarimu kwa wazazi wake;

·   Yeyote yule amwaminiaye Allah swt na siku ya Qiyamah basi lazime awe ni mwenye kusema mema au anyamaze kimya.

220.  Mlango wa tano

221.  Mlango wa sita

222.  Mlango wa saba

·   Moyo halisi unapatikana kwa mema manne:

·   Kuwatembelea wagonjwa,

·   kutembea nyuma ya jeneza,

·   kununua sanda kwa ajili ya maiti na

·   kulipa madeni.

223.  Mlango wa nane

·   Yeyote yule anayetaka kuingia katika milango hii basi lazima awe na sifa nne zifuatazo :

·   Ukarimu,

·   adabu njema,

·   moyo wa kujitolea na

·   kujiepusha katika kuwadhuru waja wa mungu.

224. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. ananakiliwa riwaya na Muhammad ibn Qays katika ukurasa wa 115 wa kitabu

         Al-Mahasin:

“Siku moja Shaitani alimwona Mtume Nuh a.s. akisali, basi Shaitani alimwonea wivu Mtume Nuh a.s. na hakuweza kujizuia, akasema. “Ewe Nuh ! Allah swt aliyetukuka, Mkuu, amejenga mwenyewe Bustani ya Eden , akapanda miti na kutiririsha mito ndani mwake. Na kisha akaangalia mandhari hayo na kusema, “Kwa hakika waumini na waongofu ndio washindi ! La, Kwa Utukufu wangu ! Mtu mwenye utovu wa adabu (mwenye madhambi) kamwe hataingia kuishi humu.’”

225.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alisema,

“Mitume yote imekatazwa kuingia Jannat kabla yangu, na mataifa yote yamekatazwa kuingia humo kabla ya waumini watufuatao sisi, sisi Ahlul Bayt a.s., kuingia ndani mwake.”

226.  Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amenakiliwa akisema, uk.139, J.8

ya Bihar al-Anwar, akisema, 

“Jannat  inayo milango sabini na moja ya kuingilia : Ahlul Bayt a.s. yangu na wafuasi wao wataingilia milango sabini, wakati ambapo watu wengine wataingilia mlango uliobakia.”

Taqwa

227.  Qur’ani Tukufu , Sura  al-Maryam ,19 , Ayah 63 :

Hiyo ndiyo Jannat tutayowarithisha katika waja wetu walio kuwa wachamungu.

228.  Vile vile twaambiwa katika Qur’ani Tukufu , Sura  al-Hujurat ,

49, Ayah 13 :

Enyi watu ! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumekujaalieni kuwa na mataifa na makabila ili mjuane. Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu kwa  Allah swt ni  huyo aliye mchamungu zaidi katika nyinyi….

229.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Maidah,

5, Ayah 85 :

Basi Allah swt atawalipa, kwa yale waliyoyasema, Bustani zipitazo mito katika yake; humo watadumu. Na haya ndiyo malipo ya wafanyao wema.

230.  Allah swt anasema katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Tawbah,

9, Ayah 111:

Hakika Allah swt amenunua kwa Waumini nafsi zao na mali zao kwa kuwa wao watapata Jannat. Wanapigana katika Njia ya Allah swt – wanauwa na wanauawa. Hii ni ahadi aliyojilazimisha kwa Haki katika Taurati na Injili na  Qur'an. Na nani atimizae ahadi kuliko Allah swt ? Basi furahini kwa biashara yenu mliyo fanya naye. Na huko ndiko kufuzu kukubwa.

231.  Allah swt anasema katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Naziat,79,

 Ayah 40 – 41 :

Na ama yule anayeogopa kusimamishwa mbele ya Allah swt Mlezi, na akijizuilia nafsi yake na matamanio,

Basi huyo, Jannat itakuwa ndiyo makaazi yake !

232. Allah swt atuambia katika Qur’ani Tukufu, Surah

al-Waqia,56,Ayah 10–13 :

Na wa mbele watakuwa mbele. 

Hao ndio watakao karibishwa

Katika Bustani zenye neema.

233.  Qur’ani Tukufu , Sura al-Dahar, 76, Ayah 12 :

Na atawajaza Bustani za Jannat na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.

234. Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Ra’d, 13,

Ayah 24 :

Hao ndio watu wa Jannat, watadumu humo, kuwa ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.(Wakiwaambia) Assalamu ‘Alaikum ! amani iwe juu yenu, kwa sababu ya mlivyo subiri! Basi ni mema mno  malipo ya Nyumba ya Akhera.

235.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa, 4,

 Ayah 13 :

Na anayemtii Allah swt na Mtume wake, Yeye atamtia katika Jannat zipitazo mito kati yake, wadumu humo. Na huko ndiko kufuzu kukubwa.

236.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Safaat,

37, Ayah 39 – 43 :

Wala hamlipwi ila hayo hayo mliyokuwa mkiyafanya.

Isipokuwa waja wa Allah swt  walio khitariwa.

Hao ndio watakaopata riziki maalumu,

Matunda, nao watahishimiwa.

237.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Maidah,

5, Ayah 119 :

Allah swt atasema: Hii ndiyo Siku ambayo wasemao kweli utawafaa ukweli wao. Wao watapata Bustani zipitazo mito kati yake. Humo watadumu milele. Allah swt amewawia radhi, nao wawe radhi naye. Huku ndiko kufuzu kukubwa.

238.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura Ta-Ha, 20,

 Ayah 75– 76 :

Na atakayemjia naye ni Muumini aliye tenda mema, basi hao ndio wenye vyeo vya juu.

Bustani za milele zipitazo mito kati yake,wadumu humo. Na hayo ni malipo ya mwenye kujitakasa.

239.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura Ali Imran,

 3,   Ayah 133-136 :

Na yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi, na Jannat ambayo upana wake ni mbingu na ardhi, iliyowekwa tayari kwa wachamungu,

Ambao hutoa wanapokuwa na wasaa na wanapokuwa na dhiki, na wanajizuia ghadhabu, na wasamehevu kwa watu; na Allah swt huwapenda wafanyao wema;

Na ambao pindiwafanyapo uchafu au wakijidhulumu nafsi zao humkumbuka Allah swt na wakamwomba msamaha kwa dhambi zao – na nani anayefuta dhambi isipokuwa Allah swt ? – na wala hawapendelei na waliyo yafanya na hali wanajua.

Hao malipo yao ni msamaha kwa Mola wao Mlezi, na Bustani zipitazo mito kati yake. Humo watadumu, na mwema mno ujira wa watendao.

240.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Rahman,

55,  Ayah 46 :

Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Allah swt atapata Jannat (Bustani) mbili

241.  Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. amesema katika Majma’ul Bayan :

“Mtu yeyote ambaye anajua na kutambua wazi kuwa mimi nifanyapo jema au baya, basi Allah swt yupo anashuhudia matendo yangu haya, basi mtu kama huyu daima atakachokuwa akikifanya basi atakuwa mwangalifu mno katika matendo yake na atajiambia kuwa lau nitafanya kazi hii njema basi Allah swt atalipa mema kadha na kadha na lau nitafanya maasi na madhambi, basi Allah swt ataniandikia adhabu kadha wa kadha. Kwa hivyo watu kama hawa wamewekewa Bustani mbili katika Jannat.”

242.  Qur’ani Tukufu , Sura al-Mujadilah, 58, Ayah 21 :

Allah swt ameandika : Hapana shaka Mimi na Mtume wangu tutashinda. Hakika Allah swt ni Mwenye nguvu, mwenye kushinda.

Tawallah maana yake ni kuwa rafiki wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na Ahl al-Bayt a.s. na

Tabarrah inamaana ya kujiepusha na kujiweka mbali na kutokuwa na uhusiano wowote pamoja na wale maadui wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. pamoja Ahl al-Bayt a.s.

243.  Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Ma’arij,

70,  Ayah 22 -34 :

Isipokuwa wanaosali,

Ambao wanadumisha Sala zao,

Na ambao katika mali yao iko haki maalumu

Kwa mwenye kuomba na anayejizuilia kuomba;

Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,

rudi nyuma Yaliyomo endelea