rudi nyuma Yaliyomo endelea

33.   Amesema Al-Imam Zayn Al-Abedin a.s. , Al-Kafi, J. 2,

Uk.81:

“Yeyote yule atendaye matendo yake kwa mujibu wa vile alivyoamrisha Allah swt, ni miongoni mwa watu bora.”

34.   Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s., Al-Kafi, J.2,

Uk. 124:

“Yeyote yule aliye na mapenzi ya Allah swt,anachukia kwa ajili yake Allah swt, na anatoa msaada kwa ajili ya Allah swt, basi huyo ni miongoni mwa wale ambao Imani yao imekamilika.”

35.   Amesema Al-Imam Al-Hasaan Al-Askari, Imam wa Kumi

na Moja, a.s. , Bihar al-Anwaar, J.17, Uk. 218:

“Hakuna sifa zaidi ya hizi mbili: Kuwa na Imani kwa Allah swt na kuwa mwenye manufaa kwa Waislamu.”

TAQWA NA UMUHIMU WAKE KWA WAISLAMU

36.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. , Bihar

al- Anwar, J. 71, Uk. 373:

 “Miongoni mwa kitu kilicho muhimu kabisa kwa kuwafikisha watu hadi kufikia Peponi ni taqwa na tabia njema.”

37.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. , Bihar

al- Anwar , J.77, Uk. 130:

 “Wakati wa kutoa uamuzi wa kitu, fikiria matokeo yake. Iwapo ni nzuri kwako wewe kuendelea na maendeleo, fuata hivyo, lakini iwapo inakupotosha, uiachilie mbali …..”.

38.   Aliulizwa Al-Imam As - Sadique a.s. kuhusu maana ya

Taqwa, na alijibu , Safinat ul-Bihar, J.2, Uk.678:

“Allah swt hakukosi mahala pale alipokuamrisha wewe uwepo, na hakuoni pale ambapo amekuharamishia wewe kuwepo.”

39.  Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., Mustadrak

Al-Wasa’il-ush-Shi’h, J.8, Uk.466 no. 10027:

 “Onyesha heshima zako kwa ajili ya Allah swt kama vile utakavyoonyesha heshima zako mbele ya mtu mwema miongoni mwa ukoo wako.”

40.   Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam ‘Ali ibn

Abi Talib a.s. , Ghura-ul-Hikam, Uk. 321:

“Kwa mtu kuinamisha macho yake kutamwia kama kizuizi dhidi ya matamanio (shahwa) yake.”

41.   Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib

a.s. amewaambia wana wake Al Imam Hassan ibn Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. na Al Imam Hussein ibn Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. wakati ‘Abdur Rahman ibn Muljim (Allah amla’ani) alipokuwa amempiga dharuba ya upanga kichwani mwake, katka Nahjul Balagha, Barua no. 47:

“Ninawasihini nyote mumwogope Allah swt na nyinyi wala musiwe na uchu wa starehe za dunia hii hata kama itawakimbilia nyinyi. Wala musikisikitikie kitu chochote cha dunia hii ambacho mumekikosa. Semeni ukweli na mutende (kwa kutumai) malipo. Muwe adui wa mdhalimu na msaidizi wa mdhulumiwa.”

42.   Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam ‘Ali ibn

Abi Talib a.s. , Nahjul Balagha, Barua no. 31:

“Ninawauusieni kumwogopa Allah swt, Ewe mwana wangu, kubakia katika Amri Zake, kuujaza moyo wako kwa ukumbusho Wake na kubakia katika kumtegemea Yeye tu. Hakuna Hakuna ushikamano unaotegemewa kuwa madhubuti baina yako na Allah isipokuwa wewe iwapo utaishikilia menyewe.

43.   Abi Osama Amesema kuwa alimsikia Al Imam Ja'afer as-

Sadiq a.s.  akisema, Al-Kafi, J.2, Uk. 77

“Muwe nakhofu za Allah, taqwa, ijtihadi, kusema ukweli, uaminifu katika amana, tabia njema na ujirani mwema. Muwaite wengine kwenu (kwa tabia zenu njema), wala si kwa maneno tu. Muwe watu wenye kupendeza na kamwe musiwe watu wa kutuaibisha. Ninawausieni murefushe rukuu’ na sujuda zenu.  Kwani kila mmoja wenu anaporefusha rukuu’ na sujuda basi Shaytani hulia nyuma yenu kwa kusea ‘ Ole wako ! yeye ametii; amesujudu na mimi nilikataa.”

44.   Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein bin Al Imam ‘Ali

ibn Abi Talib a.s.  Amesema, Bihar al- Anwar , J.69, Uk. 277:

 “Kwa hakika marafiki wa Allah hawatakuwa na khofu yoyote juu yao wala hawatakuwa watu wenye kuhuzunika) iwapo watadumisha yaliyofaradhishwa na Allah swt, wakafuata Sunnah za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.wakajiepusha na yale yaliyoharamishwa na Allah swt, wakawa wacha Allah swt wema katika kile walichonacho katika utajiri na wadhifa wa humu duniani, wakajitahidi kujitafutia kile kilicho halali, wakaamua kutojifakharisha wala kutojilimbikia katika mali na utajiri isipokuwa katika kutoa misaada na kutoa malipo ya kulipa yaliyofaradhishwa kwake. Basi kwa hakika hao ndio waliobarikiwa katika mapato yao na watalipwa mema kwa yale waliyoyatanguliza huko Aakhera.”

45.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ,

Mustadrak al-Wasa’il, J. 12, Uk. 89:

 “Kwa hakika Wana wa Adam wapo sawa na meno ya kitana kuanzia zama za Mtume Adam a.s. hadi leo, na wala hakuna utukufu wa Mwarabu juu ya asiye Mwarabu, wala Mwekundu juu ya Mweusi isipokuwa kwa Taqwa.”

46.   Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s., Al-Kafi, J. 2, Uk.

76:

“Kwa hakika, tendo dogo kabisa lifanywalo pamoja na Taqwa ni bora kabisa kuliko tendo kubwa (au matendo mengi) lifanywalo bila Taqwa.”

K U O M B A  D U A

47.   Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s., Al-Kafi J. 2,

Uk.493:

“Dua yoyote inayoombwa kwa Allah swt, inakuwa imezuiwa na mbingu hadi hapo iwe imeshirikishwa na Salawat i.e. kumsaliwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.pamoja na Ahlil Bayt a.s.”

48.   Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. Al-Kafi J.2,

Uk.491:

“Muminiin waombao Dua zao hazikukubaliwa humu duniani watatmani kuwa dua zao hata moja zisingelikubaliwa pale watakapoonyeshwa hapo Aakhera, mema kupita kiasi ya thawabu (akipewa yeye kwa kutokujibiwa Dua zake na kwa mateso na shida alizozipata akiwa humu duniani).”

49.    Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam ‘Ali ibn

Abi Talib a.s. Bihar al- Anwar , J.93, Uk. 295:

“Tendo lipendwalo sana mbele ya Allah swt humu duniani ni Dua na ibada iliyo bora kabisa mbele Yake ni unyenyekevu na ucha-Allah swt.”

50.    Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam ‘Ali ibn

Abi Talib a.s. Al-Khisal cha Sadduq, Uk. 302:

“Milango ya Peponi ipo wazi kwa nyakati tano: wakati mvua inyeshapo;  wakati wa Vita vitukufu; wakati wito wa Sala utolewapo (wanapotoa Adhaan) ; wakati wa kusoma Qur’an Tukufu wakati ambapo jua linazama  na linachomoza alfajiri.”

51.    Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam ‘Ali ibn

Abi Talib a.s. Bihar al- Anwar , J.93, Uk. 343:

“Mujiweke tayari kuomba Dua katika nyakati tano: Wakati usomwapwo Qur’an; Wakati utolewapwo Aadhaan; Wakati unaponyesha mvua; Wakati wa kwenda kupigana katika vita vitakatifu kwa ajili ya kuwa shahidi; Wakati madhulumu anapoomba dua, kwa sababu yeye hana kizuizi cha aina yoyote chini ya  mbingu.”

52.    Amesema Al Imam Hussain ibn ‘Ali bin Abi Talib a.s. ,

katika Dua-i-‘Arafah:

“Ewe Mola Wangu ! Wewe U karibu kabisa wa kuombwa; Na mwepesi wa kujibu;  na Wewe Mkarimu wa kutoa;  na unamtosheleza umpaye; unamsikia vyema akuulizae; Ewe Uliye Rahmaan wa dunia na Aakhera na Mremehevu kote !”

53.    Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam ‘Ali ibn

Abi Talib a.s. , Nahjul Balagha, Msemo 135:

“Anayejaaliwa vitu vinne hanyimwi vinne: Anayejaaliwa kuomba Dua hanyimwi kukubalika kwake; anayejaaliwa kufanya Tawbahanyimwi kukubalika kwake; anayejaaliwa kuomba msamaha  hanyimwi kusamehewa kwake; anayejaaliwa kutoa shukuurani zake hanyimwi kuongezewa kwake.”

54.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. Bihar al- Anwar ,

J. 78, Uk. 216:

“Siku ya Qiyama, Allah swt atazihesabu Dua zote alizokuwa akiziomba Mja wake na kuuzibadilisha katika matendo mema na kwa hayo atawapandisha daraja katika Jannat (Peponi).”

55.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. At- Tahdhib, J. 4,

Uk. 112:

“Ponyesheni magonjwa yenu kwa kutoa Sadaka[51] na mujiepushe na balaa za kila aina kwa Dua”

56.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. Wasail-ush-Shi’ah 

J. 7, Uk. 60:

“Mwombe Allah swt maombi yako na daima uwe ukisisitiza katika kumwomba kwani Allah swt mwenyewe anapenda mno kubakia kwa kumsisitiza miongoni mwa waja wake Muminiin.”

57.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. Al-Kafi, J. 2, Uk.

467:

“Ninakuusieni muombe Dua’, kwa sababu hamtaweza kumkaribia Allah swt kwa vinginevyo kama hivyo.”

58.    Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam ‘Ali ibn

Abi Talib a.s. Ghurar-ul-Hikam, Uk. 185:

“Inawezekana kuwa wewe umemwomba Allah swt Dua ya kitu fulani ambacho yeye hakukujaalia kwa sababu yeye anataka kukupa kitu kilicho bora zaidi ya kile ulichokuwa umekiomba, hapo mbeleni(unatakiwa kufanya subira - mtarjum).”

AHLUL BAYT a.s.

59.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. , Bihar

al- Anwar , J.27, Uk. 113:

 “Mfano wa Ahlul-Bayt yangu kwa Ummah wangu ni sawa na Safina ya Mtume Nuh a.s. Wote wale watakaoipanda ndani yake basi wameokolewa na wote wale waupingao, basi wamezama na kupotea ……….”

60.    Amesema Al-Imam Muhammad al-Baqir a.s., Imam wa

tano, Bihar al- Anwar , J. 2, Uk. 144 :

“Ahadith zetu (za Alhul Bayt) zinahuisha nyoyo.”

61.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. , Bihar

al- Anwar , J.38, Uk. 199:

 “Muhuishe mikutano na mikusanyiko yenu kwa makumbusho ya Ali ibn Abi Talib a.s.”

62.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. , Ikmal-ud-

    Din, J. 1, Uk.253: na yenye maana yakaribiayo katika Yanabi-ul-

Muwaddah, uk. 117:

 Ipo riwaya kupitia Jabir-il-Ju’fi iliyopokelewa kutoka Jabir-ibn-Abdillah isemayo: Mimi nilisema: Ewe Mtume wa Allah swt, sisi tunamwelewa Allah swt na Mtume wake s.a.w.w. Sasa jee hawa ‘Ulul-Amr ni wakina nani ambao utiifu wao umefardhishwa sawa na wako ?

Hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.. alisema:

“Ewe Ja’abir ! Wao ni, baada yangu, Makhalifa wangu na Ai’mmah wa Waisilamu; wa kwanza miongoni mwao ni Ali ibn Abi Talib a.s.; atafuatia (Imam) Hassan, na (Imam) Husayn; atafuatia Ali ibn il Husayn; atafuatia Muhammad ibn Ali; ajulikanaye katika Tawrati kama Baqir, ambaye utakutana naye, Ewe Ja’abir ! Pale utakapomtembelea, umpe salaam zangu. Baada yake Musa ibn Ja’afar; atafuatia Ali ibn Musa, atafuatia Muhammad ibn Ali; atafuatia Ali ibn Muhammad, atafuatia Hassan ibn Ali; na baada yake (atakuja) Al-Qaim, ambaye jina lake ni sawa na jina langu. Yeye ndiye atakaye kuwa Mamlaka Ya Allah swt juu ya ardhi hii na Aliyebakia miongoni mwa Waja wake. Yeye ndiye mwana wa (Al-Imam) Hassan ibn Ali ( al-‘Askari). Huyu ndiye shakhsiyyah ambaye Allah swt atafungua Dhikiri zake Mashariki na Magharibi na huyu ndiye Shakhsiyyah ambaye atakuwa ghaibu kwa wafuasi na wapenzi wake ambavyo hakuna nyoyo zozote zile zinazoweza kukubali isipokuwa nyoyo za wale tu ambao Allah swt ameshakwishakuzijaribu kwa ajili ya Imani.”

Ja’abir alisema: “Mimi nilimwuliza ‘Ewe Mtume wa Allah swt ! Je wafuasi wake watafaidika naye wakati akiwa ghaibu ? Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.. alijibu: ‘Naam. Kwa kiapo cha Yule aliyenichagua kuwa Mtume, wao watafaidika kwa nuru yake na watafaidika kwa ibada akiwa ghaibu kama vile kufaidika kwa watu kutokana na (nuru ya ) jua hata pale linapofunikwa kwa mawingu…….’”

63.    Amesema Malik ibn Anas kuhusu mema ya Imam

As-Sadique a.s. , Bihar al- Anwar  J. 47. Uk. 28:

“Hakuna macho yaliyowahi kuona, hakuna masikio yaliyokwisha kusikia, na wala hakuna moyo uliyokwisha  shtushwa kwamba kunaweza kuwapo na mtu yeyote aliye bora zaidi kuliko (Imam) Ja’afar as- Sadique  (a.s.) katika Taqwa, elimu, ibada na Ucha-Allah swt.”

64.    Amesema Al Imam Hussain ibn ‘Ali bin Abi Talib a.s.,

Al-Irshaad, Uk. 204:

“Kwa roho yangu, hakuna Imam isipokuwa ni Hakimu kwa Kitabu, anaimarisha uadilifu, anaamini katika Dini ya Ukweli, na anajizuia nafsi yake pamoja na njia ya Allah swt.”

MAPENZI YA AHLUL-BAYT a.s.

65.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. , Al-Jami’-

ul-Saghir, J. 1 Uk. 14:

“Wafunzeni watoto wenu vitu vitatu: Mapenzi ya Mtume wenu, Mapenzi ya Ahlul-Bayt, usomaji wa Qur’an.”

66.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s., Bihar al- Anwar ,

J. 74, uk. 354:

“Mtu yeyote ambaye hawezi kutufanyia wema wowote sisi Ahlul-Bayt basi wawafanyie mema wafuasi wetu walio wema; na yeyote yule asiyeweza kutuzuru, basi wanaweza kuwazuru wafuasi wetu walio wema ambavyo thawabu za kutuzuru sisi zitaandikiwa yeye.”

67.     Amesema al-Imam Muhammad al-Baqir a.s., Al-Kafi, J.1,

Uk. 187:

“Kwa kile kilicho bora kabisa kwa mja kumkaribia  Allah swt ni utiifu kwake Allah swt, utiifu kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.. na utiifu kwa ulil Amr.”

Aliendelea kusema:

“Mapenzi yetu (ya Ahlul-Bayt) ni Imani na chuki dhidi yetu ni kufr.”

68.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. Bihar al- Anwar ,

J.27, Uk.91:

“Kwa hakika zipo daraja za ibada, lakini mapenzi yetu , Ahlul-Bayt, ni ibada iliyo bora kabisa.”

SIFA NA TABIA ZINAZOKUBALIKA

69.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Al-Kafi,

J.2, Uk.235:

 “Je niwatambulisheni Mu’miin ni nani? Muumin ni yule ambaye waumini wengine wanamwamini kwa nyoyo zao na mali pia. Je niwatambulisheni Mwislamu ni nani ? Mwislamu ni yule ambaye Waislamu wengine wanakuwa wamehifadhika kwa ulimi na mikono yake….. Ni haramu kwa Mumiin kumfanyia ubaya mumin mwenzake, au kumwacha katika hali ya shida, au kumsengenya au kumkataa kwa ghafla.”

70.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. Usul-i-Kafi, J.2,

Uk. 374: 

“Haimpasi Mwislamu kuhudhuria au kushiriki katika mikutano au mikusanyiko ambapo Sharia za Allah swt zinavunjwa na kwamba yeye (huyo Mwislamu) hana uwezo wa kuyazuia hayo.”

71.   Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. Khisal  cha

Sadduq, J. 1, Uk. 88:

“Yeyote yule kwa tabia yake husema  ukweli, basi matendo yake yametakasika; Na allah swt humwongezea riziki yule aliye na nia njema; na yeyote yule awatendeaye mema familia yake, Allah swt humwongezea umri mrefu.”

72.   Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Ali ibn Abi Talib

 a.s., Safinat ul-Bihaar, J.1, Uk.599:

“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.. alijiwa na mtu mmoja aliyeomba kufundishwa tendo kwayo ataweza kupendwa na Allah swt pamoja na watu, utajiri wake utaongezeka, mwili wake utakuwa na siha nzuri, umri wake utaongezeka na atainuliwa Siku ya Qiyama pamoja na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w..

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.. alimjibu: ‘Hizi ndizo njia sita zinazohitaji sifa sita:

Iwapo wataka Allah swt akupende, lazima umwogope na ujiepushe na madhambi,Iwapo wataka watu wakupende, lazima uwe mkarimu kwao na ukatae walichonacho mikononi mwao, Iwapo wataka Allah swt akuongezee utajiri wako, hunabudi kutoa malipo yaliyofaradhishwa kwako i.e. Zaka, Khums, na zinginezo.

Iwapo wataka Allah swt aupatie mwili wako afya njema, basi uwe ukitoa sadaqa kila mara iwezekanavyo, Iwapo wataka Allah swt aurefushe umri wako, basi uwe ukiwajali maJama’a zako,

Iwapo wataka Allah swt akuinue pamoja nami Siku ya Qiyama, basi ni lazima urefushe sujuda zako mbele ya Allah swt, aliye Pekee na Mmiliki.”

73.   Amesema Al-Imam Ar-Ridhaa a.s. Imam wa Nane,

‘Uyun-ul-Akhbaar ur-Ridhaa, J.1, Uk.256:

“Mumin hawezi kuwa mumin kamili hadi hapo atakapokuwa na mambo matatu: Sunna za Allah swt, Sunna za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w..  na Sunna za Imam a.s. wake. Ama Sunna za Allah swt ni kuzificha siri zake; kama vile Allah swt anavyosema katika Sura Al-Jinn, 72, Ayah 26 & 27.

 Yeye ndiye mwenye kujua ya siri, wala hamdhihirishii yeyote siri yake,

Usipo kuwa Mtume wake aliye mridhia. Naye huyo humwekea walinzi mbele yake na nyumba yake.

 Na ama Sunnah za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.ni kule kupatana na kuelewana na watu, wakati ambapo Allah swt alimtuma Mtume wake kuwapenda  watu na Amesema: ‘Uzoee usamehevu na uwafundishe mema na ujiondoe kutoka majaheli

Ama kuhusu Sunnah za Imam a.s. (kuwa imara na) mwenye subira katika siku nzuri na siku mbaya na nzito, ambavyo Allah swt anatuambia katika Sura Al-Baqara, 2, Ayah 177.

Sio wema kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi. Bali wema ni wa anaye muamini Allah  swt na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii, na anawapa mali, kwa kupenda kwake, Jama’a na mayatima na masikini na wasafiri, na akawa anashika Sala, na akatoa Zaka, na wanao timiza ahadi yao wanapo ahidi, na wanao vumilia katika shida na dhara na wakati wa vita; hao ndio walio sadikisha, na hao ndio wajilindao.

74.    Amesema Al Imam Muhammad al-Taqi a.s. (al-Jawad

Imam wa Tisa),  Muntah al-‘Amal, Uk.229:

“Mumin anahitaji mambo matatu: mafanikio yatokayo kwa Allah swt, mwenye kujipa mawaidha, kukubaliwa na yule ampaye nasiha.”

75.   Al Imam Hussein ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s. Imam wa Nne,

aliulizwa  “Ewe mwana wa Mtume ! Huanzaje siku  yako ?”  Na Imam a.s. alijibu, Bihar al- Anwar, J.76, Uk. 15:

“Mimi huanza siku yangu huku nikitakiwa kutimiza mambo manane (8): Allah swt ananitaka nitimize yaliyafaradhiwa juu yangu; Na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.. ananitaka nitimize yale yaliyo Sunna yake; Familia yangu inanitaka mimi niwatimizie mahitaji yao kama chakula n.k.; Nafsi yangu inanitaka niitimizie matamanio yangu; Shaytani aninitaka mimi nitende madhambi; Malaika wawili wanaonihifadhi wananitaka mimi nitende matendo kwa moyo halisi, Malaika wa Mauti anataka roho yangu na Kaburi inautaka mwili wangu. Basi mimi ndivyo nilivyo baina ya mzunguko wa matakwa hayo.”

76.    Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. , Bihar al- Anwar ,

J. 67 Uk.305:

“Kwa hakika kila kitu kinashawishiwa na Mumin kwa sababu Dini ya Allah swt inamfanya yeye awe ni mtu mwenye nguvu, na wala yeye kamwe hashawishiwi na kitu chochote kile, na kwa hakika hii ndiyo dalili ya kila Mumin.”

WAFUASI HALISI WA AHLUL-BAYT a.s. NA SIFA ZAO

77.    Al Imam Muhammad al Baqir a.s. alimwambia, Ja’bir,

Al-Kafi, j. 2, Uk. 74:

“Je inatosheleza kwa mtu kujiita Shia na mfuasi wetu ati kwa kudhihirisha mapenzi yetu, Ahlul Bayt ? Kamwe sivyo hivyo !, Kwa kiapo cha Allah swt, huyo mtu kamwe hawezi kuwa mfuasi wetu isipokuwa yule ambaye amejawa khofu ya Allah swt na kumtii ipasavyo. Ewe Ja’abir! Wafuasi wetu hawawezi kutambuliwa isipokuwa kwa sifa zifuatazo watakazokuwanazo kama unyenyekevu, kujitolea; uadilifu; kumsifu Allah kupita kiasi; kufunga saumu na kusali; kuuwatii wazazi; kuwasaidia masikini, wenye shida, wenye madeni, na mayatima wanaoishi karibu naye; kusema ukweli; kusoma Qur’an; kuuzuia ulimi kusema chochote kuhusu watu isipokuwa kwa mapenzi; na kuwa mwaminifu kwa maJama’a kwa maswala yote …….”

78.    Amesema Sulayman Ibn Mahran kuwa

Yeye alimtembelea Imam Ja’afer as-Sadique a.s. wakati ambapo baadhi ya wafuasi (Mashiah) walikuwa karibu naye na alimsikia Imam a.s. akiwaambia, Al-Amali, cha Saduq, Uk. 142:

“(Mujiheshimu) muwe kama vito vya thamani kwa ajili yetu na wala kamwe musiwe wenye kutuaibisha sisi. Waambieni watu kuhusu mema, na muizuie ndimi zenu zisizungumze mneno maovu na mambo yasiyo na maana.”

79.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s., Al-Kafi J. 2,

Uk. 56:

“Kwa hakika, sisi huwapenda wale walio na busara, wenye kuelewa, wenye elimu, wenye kufanya subira, waaminifu na wenye imani. Kwa hakika Allah swt aliwajaaliwa Mitume a.s. kwa tabia njema. Kwa hivyo yeyote yule aliye na sifa hizo basi amshukuru Allah swt, lakini yule ambaye hana hayo basi amlilie Allah swt, Aliye Mkuu na Mwenye uwezo, na amwombe hayo. “Ja’abir kwa unyenyekevu alimwuliza Imam a.s. ndiyo yapi hayo”, na Imam a.s. alimjibu: “Nayo ni: Ucha-Allah swt, kutosheka, subira, kushukuru, kuvumilia, tabia njema, furaha, hima, bidii, shauku, mkarimu, mkweli na mwaminifu katika amana.”

80.   Amesema Al-Imam Muhammad al-Baquir a.s., Al-Kafi,

J. 2, uk.75:

“Yeyote yule anamtii Allah swt basi ni mpenzi wetu, na yeyote yule asiyemtii Allah swt basi ni adui wetu (sisi Ahlul-Bayt)…..”

MADHAMBI NA ATHARI ZAKE

81.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. , Bihar

    al- Anwar, J. 77, Uk. 79 na Mustadrak Al-Wasail, J.11, Uk. 330:

 “Msitazame udogo wa dhambi, lakini muangalie mliyemuasi (Allah swt).”

82.    Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam ‘Ali ibn

Abi Talib a.s. Bihar al- Anwar, J. 70, Uk.18:

“Iwapo mtu anapenda kujiona vile alivyo mbele ya Allah swt, basi ajitathmini kwa madhambi na maasi yake mbele ya Allah swt; basi kwa kipimo hicho ndivyo alivyo huyo mtu mbele ya Allah swt.”

83.    Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. aliwauliza watu ni kwa nini

wanamwudhi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Basi mmoja wa watu alimwuliza Imam a.s. vipi, naye Imam a.s. aliwaambia, Usul-i-Kafi , J.1, Uk. 219 :

“Je hamujui kuwa matendo yenu yapoyanajulishwa kwa Mtume Mtukufu s.a.w.w. na pale aanapoona madhambi dhidi ya Allah swt miongoni mwao, basi husikitishwa mno. Kwa hivyo musimuudhi Mtume wa Allah swt na badala yake munatakiwa kumfurahisha (kwa kutenda mema).”

84.    Amesema Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. Ghurur al-

Hikam, Uk. 235:

“Kukosa kusamehe ni kasoro moja kubwa kabisa na kuwa mwepesi katika kulipiza kisasi ni miongoni mwa madhambi makubwa kabisa.”

85.   Kutokea Asbaghi bin Nabatah kutokea kwa Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. Amesema, Al-Khisal,cha as-Sadduq, J. 2, Uk. 360:

“Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.. kuwa Allah swt anapoikasirikia Ummah na kama hakuiadhibu basi bei za vitu vitapanda juu sana yaani maisha yatakuwa ghali, maisha yao yatakuwa mafupi, biashara zao hazitaingiza  faida, mazao yao hayatukuwa mengi, mito yao haitakuwa imejaa maji, watanyimwa mvua (itapungua), na watatawaliwa na waovu miongoni mwao.”

(Yaani Hadithhiyo juu inatubainishia kuwa iwapo kutakuwa na jumuiya ambayo imejitumbukiza katika madhambi basi wanabashiriwa kupatwa na mambo saba hayo yaliyotajwa.)

86.   Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. Amesema kuwa amekuta

katika kitabu cha Al-Amir al-Muminiin Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. akisema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.Amesema, Safinat –ul-Bihar, J. 2, Uk.630:

“Wakati zinaa  itakapokithiri katika jumuiya basi idadi za mauti za ghafla zitakithiri; na patakapokuwa na uovu basi Allah swt atawatumbukiza katika maisha ya ghali na hasara. Wakati watu watakapoacha kulipa zaka , basi ardhi itazinyakua baraka zake kutokea mazao, matunda, madini na vitu vyote kama hivyo. Wakati watakapotenda bila haki kwa mujibu wa Shariah, basi itakuwa sawa na kumsaidia dhalimu na ugaidi. Na watakapozikiuka ahadi zao, basi Allah swt atawafanya maadui wao kuwasaliti na kuwakandamiza. Wakati watakapoacha uhusiano pamoja na ndugu na Jama’a zao, basi yote yale wayamilikiayo yatakwenda mikononi mwa waovu. Na wakati watakapojiepusha na kutoa nasiha ya mambo mema na kuyakataza maovu na kama hawatawafuata waliochaguliwa Ahl-ul-Bayt a.s., basi Allah swt atawasalitisha kwa walio wenye shari miongoni mwao na katika hali hii, wataomba duaa lakini hazitakubalika.”

87.    Amesema Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s., Bihar al- Anwar

, J .70, Uk. 55:

“Machozi hayaishi illa kwa nyoyo kuwa ngumu, na nyoyo haziwi ngumu illa kukithiri kwa madhambi.”

88.    Allah swt alimwambia Mtume Dawud a.s.: Ithna-

Ashariyyah, Uk. 59:

“Ewe Dawud ! Wabashirie habari njema wale watendao madhambi kuhusu msamaha wangu, ambayo inajumuisha kila kitu kilichopo humu duniani, ili wasikate tamaa ya msamaha wangu; na waonye wale watendao mema kwa adhabu zangu ili wasije wakajifanyia ufakhari kwa utii wao, kwani ufakhari ni dhambi mbaya kabisa.”

ELIMU NA THAMANI YAKE

89.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., Bihar

al- Anwar , J. 2, Uk. 25:

“Waalimu pamoja na wanafunzi wanashirikiana katika kuulipwa mema wakati watu wengine hawabahatiki..”

90.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., Bihar

al- Anwar , J. 2, Uk. 121:

“Yeyote yule aienezaye Din kwa watu bila ya yeye mwenyewe kuwa na ilimu ya kutosha, basi anaidhuru Din zaidi kuliko vile anavyoitumikia.”

 

91.   Amesema Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. , Nahjul Balagha,

semi No. 482:

“Thamani ya kila kitu ni katika ubora wake.”

Yaani thamani ya mtu ni katika ilimu yake. Cheo na utukuzo wake utakuwa katika kiwango cha ilimu aliyonayo. Macho yetu hayaangali sura, urefu ukubwa wa mwili wa mtu bali humthamini kwa kufuatana na kiwango cha ilimu aliyonayo. Hivyo inatubidi sisi sote tujitahidi katika kutafuta na kuipata ilimu kwa kiasi tuwezacho.

92.  Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika

Bihar al- Anwar, J. 2, Uk.36:

“Elimu ni amana ya Allah swt juu ya ardhi hii na wanazuoni ndio wenye amana hii. Hivyo yeyote yule atebdaye kwa mujibu wa ilimu yake, basi kwa hakika ameiwakilisha amana vile ipasavyo …”

93.    Al-Imam Muhammad Baqir a.s. amesema:, Bihar al- Anwar ,

J. 78, uk. 189:

“Jitafutieni ilimu kwa sababu kujifunza ni matendo mema na kusoma kwenyewe ni ‘ibada.”

94.    Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.Amesema:, Bihar al- Anwar

, J. 1, Uk. 179:

“Mtu ambaye anatafuta ilimu, ni sawa na mpiganaji vita katika njia ya Allah swt.”

 

95.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s.katika Bihar al-

Anwar , J. 2, Uk. 92:

“Uichunge sana ilimu yako na utazame ni kwa nani unaitoa.”

96.     Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s.katika, Al-Kafi,

J.1, Uk.36:

“Muitafute ilimu na kuipamba kwa subira na ukuu ; na uwe mnyenyekevu kwa yule ambaye anaitafuta ilimu kutoka kwako”

97.    Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s.katika, Al-Kafi,

J. 1, Uk. 35:

“Yeyote yule ajifunzae ilimu na kutenda vilivyo, na kuifundisha kwa ajili ya Allah swt, basi Malaika watatmukuza mbinguni .”

98.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Bihar al- Anwar , J.1, Uk. 204:

“Wema wa duniani humu pamoja na Aakhera ni pamoja na ilimu.”

ILIMU NA FADHILA ZA KUJIFUNZA

99.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika, 

Bihar al- Anwar , J. 1, Uk. 184:

 “Yeyote yule atafutaye ilimu ni sawa na mtu anayefunga saumu mchana na akikesha macho usiku kucha akifanya ibada. Iwapo atajifunza ilimu kwa sehemu fulani, basi itakuwa kwake ni afadhali kabisa hata kuliko kuwa na dhahabu ya ukubwa wa mlima Abu Qubais na ambayo itagawiwa sadaqa katika njia ya Allah swt.”

100.   Al-Imam Zaynul ‘Aabediin a.s. Amesema katika, Usul-i

-Kafi, J. 1, Uk. 35:

“Iwapo watu wangalikuwa wakitambua kile kilichopo ndani ya kutafuta ilimu, basi wao wangaliitafuta hata kama itawabidi kusafiri na hata kuhatarisha maisha yao katika kuipata.”

101.  Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. Amesema, Qurar-ul-Hikam,

Uk. 348:

“Kutafuta ilimu haitawezakana wakati mwili unastareheshwa.” (yaani mtu hataki kutaabika)

 

102.   Amesema Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s.katika, Bihar al-

Anwar, J. 2, Uk.152:

“Hifadhini maandiko  na vitabu vyenu kwa sababu hautapita muda mutakapovihitaji.”

103.    Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. Amesema katika, Al-Kafi,

J. 1, Uk. 30:

“Kwa hakika, kukamilika kwa Din ni kule kuitafuta ilimu na kuitekeleza ipasavyo, na muelewe waziwazi kuwa kutafuta ilimu ni faradhi zaidi kwenu nyinyi kuliko kutafuta mali na utajiri.”

104.  Amesema al-Imam al-Hassan ibn Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. katika, Bihar al- Anwar, J. 78, Uk. 111:

“Wafundisheni watu wengine ilimu muliyonayo na mujaribu kujifunza ilimu waliyonayo wengineo.”

105.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

 Bihar al- Anwar , J. 1, Uk.167:

 “Fadhila za ilimu zinapendwa zaidi na Allah swt hata kuliko fadhila za ibada.”

ILIMU NA FADHILA ZA  KUIFUNDISHA

106.   Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Ithna-Ahariyyah, Uk. 11:

 “Mtu yeyote aliyekuwa na ilimu kuhusu swala fulani na akaificha pale atkapoulizwa basi Allah swt  atamkasirikia kwa ghadhabu za moto.”

(yaani mtu anapokuwa na habari ambazo zitamsaidia mtu aliyepatwa na shida na ikaweza kumsaidia kuimarisha hali yake, badala ya kumsaidia yeye akaificha, basi hapo kwa hakika ametenda dhambi kubwa.)

107.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

 Bihar al- Anwar, J. 92, Uk. 19:

 “Qur’an Tukufu ni chuo kikuu ; hivyo jielimisheni kiasi muwezavyo kutokea chuo hiki.”

108.    Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika,

Sunnahn-i-ibn-Majah, J. 1, Uk.88:

“Kwa hakika, kile kitakachoendelea kumfikia mtu hata baada ya kufa kwake, miongoni mwa matendo yake mema ni : ilimu ambayo yeye amewafundisha na kuieneza  kwa wengineo, mtoto mwema aliyemwacha, kuacha Qur’an Tukufu ikapatikana.”

rudi nyuma Yaliyomo endelea