rudi nyuma Yaliyomo endelea

528.            Amesema Mtume Muhammad  s.a.w.w., Bihar al-Anwaar,

J. 76, Uk. 367:

“Yeyote yule anayetakiwa na ndugu yake Muislam kwa kukopeshwa na kama yeye hamkopeshi mkopo, Allah swt atamzuia kuingia Jannat siku ambayo waja wema watakuwa wakilipwa mema yao.”

KUWASAIDIA WENYE SHIDA

529.            Amesema Mtume Muhammad s.a.w.w., Tuhaful-'Uqul, Uk.34:

“Waulizeni maswali walio elimika, muongee pamoja na wale wenye hekima, na mujihusishe pamoja na masikini.”

530.            Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., Ghurar-ul-Hikam

J. 4, Uk. 190:

“Sababu mojawapo ya kuteketea na kupotea kwa mali na utajiri wa mtu ni kule kutowajali na kutowasaidia wale wenye shida.”

531.            Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., Al-Hayat, Volume

 2, Uk. 51:

“Mtume Muhammad s.a.w.w. amemnakili Allah swt kwa kuameambiwa usiku wa Mi’raj: Ewe Ahamad! Mapenzi yangu ni kule kuwapenda masikini. Wafanye masikini wawe karibu nawe na uwaweke karibu nawe ili mimi niweze kukufikia wewe………..”

532.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. :

“Yeyote yule anayemmalizia muumin njaa yake kiasi kwamba akaridhika kikamilifu, basi hakuna binadamu yeyote miongoni mwetu au miongoni mwa Malaika wanaojua kiasi cha thawabu yake siku ya Qiyamah isipokuwa Allah swt mmiliki wa Malimwengu yote. Na aliongezea: Kumlisha Muislam aliye na njaa ni njia moja kubwa sana ya kuomba Tawba( usamehevu).”

 Baada ya hapo alisoma ayah ya Qur'an Tukufu Sura Al-Balad, 90,

 ayah 14 – 16.

Au kumlisha siku ya njaa

Yatima aliye Jama’a,

Au masikini aliye vumbini.

ZAWADI NA KUWAFURAHISHA MUUMIN

533.            Mtume Muhammad  s.a.w.w. Amesema, Al-Ithna-'Asheriyyah,

Uk. 223:

“Wakati sadaka inapotolewa na mtu kutoka mikononi mwake, basi hiyo sadaka inasema:

Mimi nilikuwa kitu cha kwisha, lakini wewe umenipa maisha;

Mimi nilikuwa sina thamani sasa wewe umenifanya niwe na thamani kubwa;

mimi nilikuwa ni adui nawe umenifanya mie kuwa rafiki;

Wewe ulikuwa daima ukinilinda na kunihifadhi lakini sasa mimi nitakulinda na kukuhifadhi hadi siku ya Qiyamah.”

534.            Amesema Al Imam Musa al-Kadhim a.s., Bihar al-Anwaar,

J. 74 Uk. 314:

“Yeyote yule atakaye mfurahisha Muumin, basi kwa hakika kwanza kabisa amemfurahisha Allah swt, na pili amemfurahisha Mtume Muhammad s.a.w.w. na tatu ametufurahisha sisi Ahlul Bayt a.s. ”

535.            Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., Nahjul Balagha

  Uk. 533, Msemo. 328:

“Allah swt ameweka mahitaji ya wale wasio na uwezo katika mali ya matajiri. Kwa hivyo atakapokuwa mtu asiye na uwezo akabakia katika hali ya njaa basi ni kwa sababu matajiri wamemnyima haki yake.”

536.     Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. Amesema, Bihar al-Anwaar,

J. 75, Uk. 314:

“Kwa kiapo cha Allah swt ! Yeyote yule anayeizuia mali yake isiwasaidie Mumin wenye shida basi siku ya Qiyamah kamwe hawataonja chakula cha Jannat wala Kinywaji kilichopigwa Lakiri.”

SADAKA NA MISAADA

537.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa :

“Sadaka inalipia madeni na inaongezea katika barakah.”

538.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa :

“ Sadaka inamwepusha mtu na ajali mbaya.”

539.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa:

“Mtu yeyote yule aliye mja wa Allah swt akiwa Mumin akatoa Sadaka, basi Allah swt baada ya kifo chake huyo mtu huwaweka vyema na kuwasaidia wananyumba yake katika hali njema.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akaendelea kusema :

“Faida ya kutoa Sadaka ni kwamba inamsaidia kulipia madeni na viile vile kuongezea katika baraka.”

540.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Kusaidia na kutoa sadaka vyote hivyo vinaondoa umasikini na hurefusha umri wa mtu. Na yule anayetoa huweza kuepukana na aina sabini za ajali mbaya.

541. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika kuelezea tafsiri ya aya, ya Qur'an Tukufu, Sura Al-Layl, 92 , Ayah ya 5 na 6 :

Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali

Ama mwenye kutoa na akamcha Mungu.

Ndipo amesema kuwa;

Allah swt ndivyo anavyo walipa wale watendao mema, kwa mema yao mara kumi, au hata mara laki moja na hata zaidi ya hapo.

Na vile vile amesema kuwa: anayetoa katika njia ya Allah swt basi Allah swt humjaalia kila aina ya tawfiqi katika kazi hiyo ya khairi.”

542. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amemnakili Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa

“Mtu yeyote yule ambaye anamwamimi Allah swt kuwa atamlipa na atamwongezea zaidi ya kile anacho kitoa basi huyo mtu kwa moyo mkunjufu na bila aina ya ubakhili wowote atatoa sadaka na misaada kwa wingi kabisa.”

543. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amemnakili Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa

“Siku ya Qiyama ardhi itakuwa imepata moto kupita kiasi na mumin watakuwa katika kivuli na kivuli hicho itakuwa ni kile alicho kuwa akitoa Sadaka.”

544. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akisema kuwa:

“Enyi watu! Toeni sadaka bila shaka sadaka inaongezea katika mali yenu, na hivyo mtoe sadaka na Allah swt atawarehemu.”

545.  Al Imam Musa al-Kadhim a.s. amesema kuwa:

“ Toeni sadaka mjipatie riziki.”

546.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“ Toeni sadaka mjiongezee riziki yenu. Bila shaka anayeamini kuwa Allah swt hulipa mambo yote. Basi yeye huwapa sadaka masikini kwa kupita kiasi. Allah swt humjaalia riziki kwa njia mbalimbali kwa  kile huyu mtu akitoacho katika mali yake.”

547.  Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akisema kuwa :

“Kuwa na akida ya Tawhid ni nusu ya sehemu ya dini, enyi watu!  Toeni Sadaka ili mpate riziki zaidi”.

548. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s.  ametoa riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa :

 “Kuwa mali halisi ya mtu ni ile ambayo yeye ametolea sadaka.”

549.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:

“Toeni Sadaka asubuhi na mapema ili balaa zisiwafikieni katika siku nzima.”

550. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa:

“Sadaka ni kinga dhidi ya moto wa Jahannam .”

551. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema:

“ Enyi watu muwatibu wagonjwa wenu kwa kutoa Sadaka.”

552. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. katika Nahjul Balagha amesema kuwa:

“Mnapoona riziki yenu inapungua na kuwa finyo basi muwe mkitoa sadaka ndivyo mtakuwa mkifanya biashara na Allah swt.”

553.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“ Imani ya muumini inakuwa na sifa nne za lazima,

·  Awe na tabia njema,

·  Awe mkarimu na mwepesi wa kutoa

·  Asizungumze zaidi ya yale yanayo takikana (hazungumzi mambo ovyo ovyo)

·  Hutumia kile kiasi kinacho takiwa ,siyo mfujaji ( anaotoa katika njia ya Allah swt ).

554.  Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa:

“Iwapo mimi nitakwenda Hijja moja basi afadhali niwafanye huru watumwa kumi, lakini iwapo mimi nitajichukulia jukumu la kuwalisha familia ya Waislamu ambao wanashida ya chakula na ambao wanaishi kwa njaa nikawamalizia shida zao, nikawavalisha nguo wale ambao hawana nguo, na nikawarudishia heshima yao miongoni mwa watu, basi mimi ninaona jambo hili ni afadhali na bora zaidi kuliko hata kwenda kuhiji Hijja sabini.”

555.  Al Imam Musa al-Kadhim a.s. aliijiwa na mtu mmoja

na aliyeuliza,

“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Mimi ninazo pesa na utajiri je ni jambo gani afadhali nitoe sadaka au nimnunue mtumwa na kumfanya huru?”

 556.  Kwa hayo Al Imam Musa al-Kadhim a.s.  alimjibu kuwa:

“Kuwa mimi ninaonelea kuwa kutoa Sadaka ni afadhali zaidi.”

557.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza Maimuna binti Harun, Je Kijakazi wako amekuwaje? Akasema Maimuna kwa hayo alimjibu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., ‘Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Mimi nimemfanya huru.’

 Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwambia “Iwapo kama wewe ungelichukua jukumu la kumlisha, kumtunza, kumsaidia na kumwonea huruma basi ingekuwa afadhali zaidi.”

 

558.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Muwatibu wagonjwa wenu kwa Sadaka, na muzuie maafa kwa kuomba dua na kutoa sadaka muongezee riziki zenu zipanuke, na kwamba Sadaka inawaepusheni na mitego ya mashetani sabini.”

559.  Siku moja walikuja wagonjwa wakilalamikia magonjwa yao mbele ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., naye akawaambia;

“Nendeni mtoe Sadaka kwa ajili ya magonjwa yenu na mtapona, iwapo mtu atatoa Sadaka kwa kile akitumiacho kwa  siku dharura wake, basi Allah swt huahirisha hata kifo chake na vile vile humwepusha na ajali mbaya.”

560.  Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. aliulizwa na Sahaba mmoja  :

“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Mimi watoto wangu wawili wamefariki na amebakia mtoto wangu mdogo.”

Kwa hayo Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. kamwambia:

“Basi toa Sadaka kwa niaba ya mtoto wako huyo.”

 Na siku moja Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. alipomtembelea huyo mtu akamwambia,

“Mwambie mtoto wako huyo atoe Sadaka kwa mkono wake walau kiasi kidogo chochote kile au hata kama kitakuwa ni kipande kidogo tu. Utambue wazi kuwa kiasi chochote kile hata kikiwa kiasi gani kama kitatolewa kwa roho safi  basi mbele ya Allah huwa ni kipenzi, kwani Allah swt ameelezea kuwa:

Qur’an Tukufu, Surah Az-Zilzalah,99, Ayah7 - 8

Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona !

Na anaye tenda chembe ya uovu atauona !

561. Vile viel Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. alimwelezea kuwa:

“Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah Al-Balad,90, Ayah11 - 16

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani ?

Kumkomboa mtumwa;

Au kumlisha siku ya njaa

Yatima aliye jamaa,

Au masikini aliye vumbini

“Hivyo ewe Sahabi  uelewe kuwa Allah swt anaelewa wazi wazi kuwa si watu wote wenye uwezo wa kuwanunua na wenye kufanya huru watumwa hivyo yeye ameweka thawabu hizo hizo kwa wale watakao toa Sadaka au watakao walisha yatima na masikini.”

562.  Al Imam Musa al-Kadhim a.s.alijiwa mtu mmoja mbele yake na kuelezea habari za mtoto wake, na kwa hayo Al Imam akamjibu :

“Toa Sadaka kwa niaba yake.”

Na mtu huyo akajibu kuwa

“Sasa mtoto wake amekuwa na umri  yaani amekuwa kijana.”

Basi Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alimwambia kuwa

“Mtoto wako atoe Sadaka kwa mkono wake, hata kama itakuwa ni kipande cha mkate, na hapo ndipo Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alisema riwayah ya Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. kuwa:

“Katika Israil alikuwa mtu mmoja aliyekuwa akimpenda mno mtoto wake, na akaona katika ndoto yake anaanmbiwa kuwa, mtoto wako huyo umpendaye mno atakufa usiku wa ndoa yake. Kulipowadia usiku wa arusi baba mzazi wa mtoto huyo, usiku kucha akawa katika wasiwasi na hakupata usingizi na kamwe hakupata raha usiku huo.

Na kulipo pambazuka asubuhi na mtoto alipotoka chumbani mwake akiwa hai basi baba yeke alimwuliza

 ‘Ewe mwanangu! Je katika usiku huu wako wa kuamukia leo umefanya mema yoyote?’

 Kwa  hayo mtoto akajibu

“Ewe baba yangu! hakuna jambo la maana sana lililotendeka, bali alitokezea masikini mmoja akaja mlangoni kuomba chakula, alikuwa na njaa na kile chakula walichokuwa wameniwekea, mimi nikampa chakula chote huyo mtu aliyekuja kuomba.’

 Kwa hayo baba yake akasema

“Kwa sababu hii tu ndiyo Allah swt amekuondoshea balaa kubwa iliyokuwa ikupate wewe usiku huo.”

563.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa:

“Kwa kutoa Sadaka kwa mkono wako mwenyewe basi unajiepusha na ajali mbaya, unajiepusha na balaa na maafa sabini na mitego ya mashetani sabini na ambamo kila shetani yuko anakwambia ‘ewe fulani!  Usitoe Sadaka kamwe.”

564.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Mgonjwa atoe Sadaka kwa mkono wake mwenyewe na anayempa amwambie amwombee dua”.

565. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika hadith zake amesema kuwa:

“Mkono uliye juu yaani mtoaji ni afahali kuliko mkono ule ulio chini yake, yaani mpokeaji.”

566.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:

“Kuna aina tatu ya mikono wa

·   kwanza ni mkono ule wa Allah swt  ambao uko juu kabisa na kwa hakika neema zote ni za Allah swt,

·   mkono wa pili ni ule mkono wa yule mtu anaye toa, ambaye anatoa katika njia ya Allah swt na

·   mkono wa tatu ni wa yule anaye pokea ambao mkono uliochini wa yule anayetoa. Kwa hivyo enyi watu chochote kile kinachobakia miongoni mwenu mtoe katika njia ya Allah swt  na musikalifishe nafisi zenu”.

567.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.  amesema kuwa:

“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa amemfanyia usia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.; Ewe Ali! Ninakufanyia usia wa mambo mema machache na uyakumbuke vyema.

Ewe Allah swt umsaidie Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Baada ya hapo wakati akifanya usia, Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alisema: Ama kuhusiana na sadaka tafadhali usiwe na mnunguniko wowote. Utoe kiasi kwamba mpaka uhisi kwamba wewe umefuja mali yako, lakini utambue wazi kuwa hiyo sio ufujaji bali hiyo umetoa katika njia ya Allah swt.”

568. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa kuna riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa

“Toeni Sadaka, angalau hata kwa sa’  ya tende, na kama sa’ moja hiyo hamnayo basi mtoe tende kwa kiganja kimoja na hata kama hivyo haitawezekana basi mtoe tende kiasi chochote kile na kama hivyo haitawezekana basi mtoe angalau kokwa moja ya tende, na kama hivyo pia haitawezekana basi yule masikini aliyekuja kuwaomba mumwambie maneno mazuri na matamu na maneno matakatifu katika kumwelezea kuwa hakuna chochote, na hayo pia ni sadaka.

Kwa sababu isitokee Siku ya Qiyama kwamba Allah swt atakapo kuuliza hesabu ya neema alizokujaalia akakuambia

‘Ewe mja! Mimi nilikupa mambo chungu nzima, sasa hebu angalia nafsini mwako je kwa kutumia neema hizo wewe umejiandalia nini?’

Na hapo wewe utaangalia sehemu zote nne za dunia na utajawa na masikitiko, na utakuta hakuna jambo lolote lile litakalo kuokoa dhidi ya adhabu za Allah swt.”

569.  Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa:

“Mtoe tende kiasi fulani kwani itawaokoa na moto wa Jahannam , mpanue riziki zenu na mteremshiwe riziki nyingi kwa kutoa Sadaka na kupitia dua mziondoe balaa na shida zenu.”

Mkumbuke kuwa kwa kutoa Sadaka hamtapungukiwa katika mali yenu. Na miongoni mwa jamaa zenu wanapokuwa na shida muwasaidiapo hiyo siyoSadaka bali hiyo ni wajibu wenu.”

570.  Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa:

“Kulikuwa na mja mmoja aliyekuwa akifanya ibada ya Allah swt kwa umri wake wa miaka  themanini.

Siku moja alimwona mwanamuke mmoja mzuri aliyekuwa akipendeza naye akawa ameingia katika mtego wake.  Yeye alitimiza matamanio yake visivyo halali na mara akatokezea Malakul mauti (malaika anayetoa roho). Ulimi wake ulifunga kuongea na jasho lilianza kumtoka na kutokwa kwa roho na mara hapo alipita masikini akiomba.

Basi mtu huyu ambaye alikuwa katika hali ya kukata roho alimwambia yule masikini kwa ishara kuwa mahala fulani kuna mkate hivyo auchukue hivyo aweze kula huyo masikini, na masikini huyo alivyoelekezwa akauchukua mkate akaondoka zake.

Kwa hiyo ikatokea kwamba Allah swt aliibatilisha ibada zake za miaka themanini kwa sababu ya kuzini na ikatokea kwamba Allah swt akamsamehe madhambi yake yote kwa sababu ya kutoa Sadaka kwa moyo mkunjufu.”

571.  Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s.  amesema kuwa;

“ Katika zama za Bani Israil kuliwahi kutokea baa la njaa ambao uliendelea kwa muda wa miaka mingi. 

Katika wakati huo ikatokezea kwamba bibi kizee mmoja akiwa amekabwa na njaa hali ya juu alikuwa ameketi akiwa na kipande kidogo cha mkate huku akitaka kukila kipande hicho, mara akasikia mlangoni sauti ikisema ya masikini aliyekuwa amekuja kuomba:

‘Ewe mja wa Allah swt! Mimi nakufa kwa njaa naomba unisaidie, bibi kizee huyo akajiambia kwa hakika Sadaka ndiyo wakati huu muafaka wa kutoa, na kile alichokuwa akila akakitoa haraka akampa huyo aliyekuwa akiomba.

Bibi kizee huyo alikuwa na mtoto mmoja aliyekuwa amekwenda porini na ghafla kule alishambuliwa na mnyama. Kwa kusikia sauti ya mtoto wake huyo bibi kizee ikimwita, alikimbia kumfukuza mnyama huyo na kwa muujiza wa Allah swt  ni kwamba,  Allah swt alimtuma Malaika Jibrail a.s kwenda kumwokoa mtoto huyo katika mdomo na mabano ya mnyama wa huyo muuwaji, na Malaika Jibraili a.s. akamwambia ‘Ewe bibi kizee ! Je umefurahi sasa? Kwa kile ulichokitoa sadaka basi Allah swt naye amekulipa mema yake.”

572.  Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:

“ Mfanye mema katika hali ya shida na ufakiri, na wema huo ni Sadaka.

Toeni Sadaka kama itakuwa ni kiasi gani kwa udogo wake. Mnaweza kutoa kiasi cha tende mkajiokoa na  Jahannam. Kwa hakika udogo huo siyo hoja na Allah swt ataulea udogo huo kama kwamba nyie mnavyo walea watoto wadogo wanaonyonya maziwa, na siku ya Qiyama wakati mema yenu hayo  ( mliyokuwa mkisema ni madogo) yatakapoletwa mbele yenu mtaona kuwa ni sawasawa na ukubwa wa milima mikubwa sana.”

573. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameseama kuwa Allah swt anasema kuwa :

“Hakuna kitu kingine mbali na Sadaka ambacho mtu anaweza kumpatia mtu mwingine kidhahiri, na kwa hakika mimi ndiye wakili wake musitahiki, na mimi ninayepokea kwa mikono Sadaka hiyo halafu hata ikiwa kama ni tende kidogo haidhuru mimi ndiye ninaitunza, kama vile mwanadamu anavyowatunza watoto wake.

Siku ya Qiyama huyo mtoa Sadaka atastaajabishwa mno kwa Sadaka zake ndogo alizokuwa akitoa zimekuwa kubwa kama milima ya Uhud, milima mikubwa sana.”

574. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa: 

“Toeni Sadaka asubuhi na mapema kwa sababu kunaondoa balaa kwa siku nzima.”

575.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Kwa kutoa Sadaka asubuhi na mapema basi mtoa Sadaka huepukana na kila aina ya matatizo na mabaya yote kwa siku nzima.”

576.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Toeni Sadaka asubuhi, na kwa mapenzi kabisa, mwenyewe kutoa Sadaka amebahatika. Basi humwomba Allah swt amani kutokana na balaa zote zilizoko ardhini na mbinguni, na kwa hakika Allah swt humjaalia hivyo kwa sababu ya kutoa Sadaka.” 

577. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anaelezea kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwusia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa:

“Ewe Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.! Sadaka huondoa balaa ambazo lazima zitatokezea, na kwa kutenda mema pamoja na ndugu na majamaa kunarefusha umri.

Ya Ali! Iwapo jamaa na ndugu ni watu wenye shida, basi kuwapa Sadaka  hao haitakuwa ni Sadaka.

Ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.! Kusema maneno bila vitendo ni ya bure hayana maana, na Sadaka  bila kuwa na nia nayo haiwi Sadaka.”

578. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa: Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza mtu mmoja

“Je leo umefunga Saumu?”

Mtu huyo alijibu

“La hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.”

 Tena Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza:

“Je leo umeshawahi kumtembelea aliye mgonjwa?”

 Naye akajibu:

“Hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.  aliendelea kumwuliza naye aliendelea kumjibu hapana hakufanya hivyo.

579. Mwishoni Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliendelea kumwuliza:

“Je umemlisha masikini yeyote?”

 Naye akajibu: “Hapana Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.!” 

Na hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipomwambia huyo mtu :

“Nenda kwa wananyumba wako, nenda ukawatendee  na uwe nao kwa  mema na uwawie wema, basi hayo ndiyo yatakuwa Sadaka  yako kwao.”

580.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambaye ameseama:

“kwa baraka za Sadaka Allah swt humwondolea mwenye kutoa Sadaka balaa sabini, ambamo kuna magonjwa, madhara yatokanayo na moto, kuzama maji, kufunikwa na majumba mpaka kufa na atamwepusha ili asiwehuke au asiwe mwehu.”

581.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa: 

“Ili kutaka kuepukana na shari za madhalimu basi toeni Sadaka.”

582.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anaelezea kuwa: Siku moja Myaudi mmoja likuwa akienda kukata miti porini na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwangalia na kuwaambia Ma-Sahaba wake :

 “Myahudi huyu leo ataumwa na nyoka na kifo chake kitasababishwa na sumu ya nyoka. Myahudi huyo kama kawaida yake alikata kuni na alijitwisha kichwani mwake na akarud akiwa salama.

Na tena Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipomwona Myahudi huyo akamwambia ateremshe mzigo wa kuni huo na auweke chini. Na Myahudi akafanya hivyo alivyoambiwa, na katika mzigo huo wa kuni wakaona kuna nyoka mweusi mwenye sumu kali sana huku akiuma kuni.

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza Myahudi yule,’Je wewe leo umefanya jambo gani?’

 Myaudi huyo akasema: Mimi nimekata kuni na kuzifunga tu, lakini wakati nilivyokuwa nikirudi nilibakiwa na vipande viwili vya mkate na kipande kimoja mimi nikala na kipande kimoja nikampa masikini Sadaka.

 Hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema kwa kiapo cha Allah swt ni kwa sababu ya Sadaka  ndiko balaa hii imekuondokea, kwa hakika Sadaka humwepusha mtu na ajali mbaya.”

583.  Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. siku moja alikuwa pamoja na Ma-sahabawake katika Masjid Nabawi, na upande mmoja wa ukuta ukaanguka chini. Kulikuwa na mtu mmoja hapo ambaye aliponea chupu chupu tu, kulianguka kizingiti kizito karibu na muguu wake. Lakini yeye bahati nzuri hakupata udhuru wowote.

Hapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. aliwaambia Ma-sahaba wake, hebu mwulizeni huyu mtu leo amefanya matendo gani? Na wakati alipoulizwa huyo mtu akasema:

“Mimi nilipotoka nyumbani mwangu leo nilikuwa na kokwa chache za  tende. Na kukatokezea na masikini mmoja akaniomba basi mimi nikampa kama Sadaka .

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. akajibu

“Basi kwa sababu hiyo tu leo, Allah swt amekuepusha na balaa hii ambayo ingekumaliza.”

584. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. siku mmoja alimwambia Sahabi wake 

    Mayassari kuwa:

“Ewe Mayassari je wajua kuwa wewe umeisha fikiwa na mauti mara nyingi, lakini Allah swt amekuongezea umri wako zaidi kwa sababu ya wewe kuwa mkarimu na kuwajali jamaa na ndugu zako umewawia wema ndio maanake umri wako umezidi.”

585.  Al Imam Hasan al-'Askary a.s. anasema kuwa:

“ Wakati mmoja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akiwa pamoja na wenzake walikuwa safari na wenzake hao walikuwa na mali nyingi sana. Na njiani wakapata habari kuwa wako majambazi wanaowapora matajiri mali zao. Kwa kusikia hayo hao matajiri walianza kutetemeka na wakaingiwa na hofu na wakaanza kumwuuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. je tufanyeje sasa?

Na kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akawajibu:

‘Mkabidhini mali yenu yule ambaye ataweza kuifadhi mali yenu, na kwa kweli ataitunza sana na baada la kupungua hata itazidi pia, sio hayo tu na pale mutakapokuingiwa na shida ya mali yenu basi yeye kila siku atawarudishia pamoja na nyongeza yake. ‘

Kwa kusikia hayo hao wenzake aliokuwa nao katika safari wakamwuliza :

“Je ni nani huyo?”

 Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akawajibu:

“Yeye ni miliki wa malimwengu zote Allah swt.”

 Basi hao wenzake wakamwuliza je tunaweza kumkabidhi vipi mali zetu hizi? Hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akawaambia: Toeni Sadaka  muwape wale wanaostahiki. Kwa kusikia hayo wakauliza ewe mjukuu wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Hapa tulipo tutawatoa wapi hawa masikini na mafakiri tutawatafuta wapi? Basi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. aliwajibu: munuie kuwa  sehemu moja ya mali yenu mtatoa Sadaka basi na msiwe na wasiwasi Allah swt atailinda mali yenu yote.

“Wale waliokuwa naye pamoja safarini walinuia hivyo kama vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alivyowaambi,a na Imam a.s. akawaambia sasa nyie mko katika amani ya Allah swt, na wakiwa wanaendelea na safari majambazi hao walikumbana nao na kwa kudura za Allah swt wao wakawapita salama usalimini bila ya kudhurika na kusumbuliwa, hadi wakafika mwisho wa safari yao.

Waliopofika tu mwisho wa safari yao wao wakatoa sehemu moja walizokuwa wamenuia kama Sadaka na sehemu iliyo bakia walifanyia biashara yao, na Allah swt akawajaalia baraka kiasi kwamba wakapata faida hata zaidi ya mara kumi.” 

586.  Siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alikuwa Mina pamoja na Ma-sahaba wake wakila zabibu. Mara akatokezea mtu mmoja na  akaomba. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kwa mkono wake akachukua fungu moja la zabibu akampa basi huyo akakataa kupokea, akisema “mimi sitaki zabibu hizi bali ninataka pesa tasilimu kama zipo ndio nichukue”.

Basi kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia “Allah swt atakuzidishia” na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. hakumpa chochote, baada ya muda si muda huyo mwombaji tena akarudi kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. na akamwambia Imam a.s. “Nipe zile zabibu ulizokuwa ukitaka kunipa.” Na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia Allah swt atakutafutia njia yake, pamoja na hayo Imam a.s. hakumpa chochote.

Wakati bado wakiwa wamekaa akatokezea mtu mwingine kuja kuomba, na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alitoa mbegu tatu tu za zabibu akampa huyo mwombaji. Mwombaji huyo alianza kumshukuru Allah swt kwa kumjaalia riziki hiyo na akaonyesha shukurani kwa ujumla. Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alichota mikono ya zabibu miwili akampa na hapo tena huyo mwombaji akaendelea kumshukuru Allah swt zaidi na zaidi. Kwa kusikia hayo tena Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia mtumwa wake kama tuna pesa zozote zile tulizo nazo kwetu mpe huyo. Na huyo mfanyakazi wa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kwa amri yake alimpa Dirham Ishirini alizokuwa nazo. Mwombaji akiwa anachukua Dirham akasema: ‘Ewe Allah swt! Nakushukuru mno sana na hakuna mwingine wa kushirkishwa nawe. Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. nguo aliyokuwa amejifunika akampa huyo mwombaji na huyo mwombaji baada ya kuivaa na kujifunika na hiyo nguo akamshukuru Allah swt ambaye amemjaalia nguo ya kujifunika. ‘Ewe Aba ‘Abdillah! Allah swt akulipe kila la heri. Na baada ya kusema hayo akaondoka zake. Kwa kuona haya Ma-sahaba wakamwambia Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa kila alivyoendelea yeye kumsifu Allah swt ndivyo wewe ulivyoendelea kumpa na kama asinge omba kwa kutaja jina la Al Imam a.s. lazima angeendelea kumpa chochote zaidi ya hayo.”

587.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“ Mimi nilinunua ardhi pamoja na mtu mmoja. Mtu huyo huyo alikuwa ni mnujumi, kwa hiyo yeye kila alipokuwa akipiga mahesabu yake na elimu ya nyota yake aliyokuwa nayo alikuwa akiangalia saa nzuri ndipo alipokuwa akienda shambani mwake, nami bila kujali kama saa mbaya nilikuwa nikienda shambani mwangu, na sisi tulipokuwa tayari basi ardhi au sehemu yangu ikawa na faida zaidi kuliko sehemu yake.

Kwa hivyo yeye bila kusita katika  hali ya kustaajabisha aliniambia mimi sijawahi kuona kama hivi. Mimi kila saa zilizokuwa nzuri nilikuwa nikija shambani mwangu. Na wewe bila kujali saa nzuri au mbaya ulikuwa ukija kwenye shamba lako. Sasa itakuwaje mimi nipate hasara au kasoro?

 Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu ngoja nikwambie hadithi moja ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliyesema kuwa:

‘Mtu yeyote anayetaka Allah swt amwepushe na maovu na mabaya ya siku nzima basi yeye aianze siku yake kwa kutoa Sadaka, na yeyote anayetaka ajiepushe na balaa na maovu ya usiku basi yeye usiku unapoingia atoe Sadaka na ujue kwamba mimi daima ninapotoka nyumbani mwangu huwa ninatoa Sadaka. Kwa hivyo kufanya biashara na Allah swt hivi afadhali zaidi kuliko elimu yako ya nyota na kupiga ramli.”

 

588.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema :

“Mtoe Sadaka  usiku kwa sababu huiondoa ghadhabu ya Allah swt, husamehe madhambi mazito, na hukusababishia hesabu zako siku ya Qiyamah zikaenda vizuri. Kutoa Sadaka  katika siku kunaiongezea mali yako na kuilinda na kunaufanya umri wako uwe mrefu.”

589.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“ Kwa kutoa Sadaka  yaani kunapokucha kunayeyusha madhambi kama vile chumvi inavyoyeyuka katika maji. Na kunapotolewa Sadaka usiku basi kunaondoa ghadhabu za Allah swt.”

590. Ibn ‘Abbas amesema kuwa: Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu, Sura Al-Baqarah,2, Ayah 274  

rudi nyuma Yaliyomo endelea