Back Index Next

Katika kipindi cha kubakia hapo, wageni hawa huendelea kupata kila aina ya makaribisho yasiyokuwa na mipaka ya kisheria. Kutokana na hali kama hii mara ghafla mume huyu humkuta

mkewe amekwishaanzisha uhusiano wa kimapenzi na mmoja wa marafiki zake hao. Hapa ndipo mume huyu huzusha ugomvi na mkewe na kuwasha moto wa volkano dhidi yake, pamoja na ukweli ulio wazi kwamba, yeye ndiyo sababu iliyoleta huzuni hii kubwa na msiba ndani ya nyumba yao. Mume huyu anasahau kwamba, yeye ndiye aliyekuwa kiongozi na muandalizi wa njia ya mkewe kulifikia giza hili na dhambi hii kubwa.

Baada ya tatizo kama hili baina ya mke na mume, hapo hujitokeza moja katika mambo mawili. Ama mume huyu aendelee kubaki na mkewe huyu muovu katika hali ya maisha ya dhiki yatakayokuwa yakiumiza roho yake na kuiadhibu nafsi yake, na kutokuaminiana tena na mkewe. Au pengine aende mahakamani ili akapate kufungua madai dhidi ya mkewe na kudai fursa ya kutoa talaka. Na mara nyingi talaka ndiyo uamuzi ambao mume huuchagua ili atatue tatizo hili. Lakini uamuzi huu unakuja baada ya kutokea fedheha, aibu na unyonge mkubwa katika familia hii. Na mwisho huu mbaya huleta matokeo ya kusikitisha, kwani familia hii hubomoka na maisha mazuri ya ndoa ya wawili hawa huvunjika.

Zaidi ya hapo msiba mkubwa hubaki kwa watoto ambao huwa bado wanahitajia kuwa na mama yao. Kuishi mbali na mama, watoto hawa hukosa huruma na upole wa mama yao, pia hukosa malezi mazuri na mwelekeo mwema. Hapo ndipo mahali ambapo hujitokeza fundo la moyo kwa watoto hawa na kujihisi kuwa na upungufu katika jamii wanayoishi. Watoto hawa hubadilika taratibu katika tabia zao na hatimaye hutokea wakajiunga katika magenge au makundi yenye mielekeo mibaya na kujikuta wamo miongoni mwa wezi na majambazi.[24]

Mengi ya matukio ya aina hii yamekuwa yakitokea katika nchi zisizo za Kiislamu. Katika moja ya makala zake, gazeti la Kisovieti liitwalo Pravda liliandika kama ifuatavyo: “Asilimia themanini ya makosa ya uvunjaji sheria yafanywayo na vijana wenye umri wa kukaribia balehe (miaka kumi mpaka kumi na tano) yanatokana na kuvunjika kwa familia.”Pia likaendelea kueleza gazeti hilo kwamba: “Katika kila matatizo tisa yanayohusu ndoa, moja katika matatizo hayo, matokeo yake huwa mume na mke kupeana talaka.” Pravda likaendelea kutoa sababu za matatizo hayo kwa kusema: “Sababu za msingi zinazochangia kuleta hali hii, ni kuharibika kwa mwenendo wa jamii kutokana na ulevi wa kupindukia.[25]

Sasa basi, ukweli uliopo ni kwamba matokeo ya yote haya yanakuja kutokana na uovu unaosababishwa na kutokujisitiri wanawake kama sheria inavyowataka. Uislamu kwa upande wake haukuharamisha bila mantiki mavazi yasiyowafunika wanawake kwa mujibu wa sheria, isipokuwa ni kwa lengo la kuzuwia maovu haya, na pia haukufaradhisha vazi la Hijabu kwa mwanamke isipokuwa ni kwa nia ya kumuepusha mwanamke asifikwe na maovu haya na mengine mfano wa haya. Kwa hiyo Uislamu unawalazimisha wanawake kuvaa Hijabu ambalo ndilo vazi rasimi kisheria ili kuzuia kuzuka kwa maovu kama yalivyotangulia kuelezwa.

Magazeti na vyombo vingine vya khabari kila mara vinatuarifu habari mbali mbali zinazohusu matatizo ya ndoa na khiyana zinazofanyika baina ya mke na mume, na hali hii husababisha watu kupeana talaka na pengine ikasababisha kutokea mauaji. Kila unapofanyika uchunguzi, sababu za msingi zinarudi kwenye upuuzaji wa Hijabu kwa ile maana yake halisi iliyokusudiwa na Uislamu. Ni mara nyingi tunasoma magazetini au kusikia redioni kwamba mtu kamuacha mkewe na wanawe kwa ajili ya msichana asiye na Hijabu ambaye kakutana naye ofisini au katika mabustani ya mapumziko na au mahali pengine. Au ni mara ngapi tumesikia na pengine kuona mke anamuacha mume wake ili tu akaolewe na kijana aliyekutana naye sinema au pwani wakati wa kuogelea? Kuna gazeti moja liliandika kama ifuatavyo: “Mtu mmoja alimuua rafiki yake ili amchukue mkewe ambaye alikuwa akijidhihirisha wazi mbele ya bwana huyo bila Hijabu wala aibu. Gazeti liliendelea kueleza kwamba, kuna mwanamke mwingine ambaye yeye alimuua mumewe kwa msaada wa huyo mpenzi wake na kisha wakamkatakata viungo vyake na kuvitupa ndani ya mfereji wa maji machafu.

 Bibi huyu alifanya madhambi haya ili tu aolewe na huyo bwana mpya.”Pia kulitolewa habari na gazeti moja la Kiarabu ambalo liliandika tukio moja miongoni mwa matukio yanayosababisha ndoa za watu kuvunjika, hasa mijini ndiko kwenye matukio mengi ya aina hii. Tukio hilo kwa hakika lilikuwa la kuhuzunisha sana, na cha kuhuzunisha zaidi ni kwa kuwa lilitokea katika moja ya nchi za Kiislamu, lau lingekuwa limetokea katika nchi za magharbi, hali hii ingekuwa ni mahala

pake kwa kuwa nchi hizo ndiyo vituo vya kila aina ya maovu, kama vile zinaa na uchafu mwingineo. Lakini ni vipi leo mambo haya yanatokea hata katika nchi takatifu za Kiislamu ambazo hapo kabla zilikuwa zimetakasika kutokana na uchafu huo?

Hapana shaka, hayo ni matokeo ya wanawake kuuwacha utamaduni wao wa Kiislamu katika suala la mavazi, pia mienendo ya Waislamu imebadilika na wameshawishika na utamaduni mbaya wa kimagharibi. Kutokana na kupotea kwa Waislamu na kuacha mwelekeo na utamaduni wao, sasa hivi imekuwa kazi ngumu kuyaepuka maovu na balaa hizi isipokuwa njia pekee ni kurudia utamaduni wetu kama alivyotuamrisha Mwenyezi Mungu na Mtume wake (s.a.w.w).

Ewe msomaji mpendwa, hebu kaa tayari nikusimulie hicho kisa ili ujionee mwenyewe umuhimu wa Hijabu kwa maana yake kamili na pia ubaya wa kuacha Hijabu: “Naam, wanamichezo wa nchi fulani walitoa mwaliko wa kimichezo kwa mmoja wa wanamichezo mashuhuri wa nchi fulani. Kwa bahati nzuri mwanamichezo mualikwa aliukubali mualiko huo na kufanya safari kuelekea huko akifuatana na mkewe ambaye hakuwa amevaa Hijabu, na kwa sura binti huyo alikuwa kaumbika.

Walipofika uwanja wa ndege wa nchi aliyoalikwa mwanamichezo huyu na mkewe, kwa pamoja walilakiwa na wenyeji wao ambao nao ni wanamichezo. Mwanamichezo huyu mgeni alisalimiana na wenyeji wake kisha akamtambulisha mkewe kwa wenyeji hao nao wakampa mikono mkewe huyu, kitendo ambacho Uislamu umekiharamisha. Wanamichezo hawa wenyeji walionyesha furaha kubwa sana na tabasamu kwa mke wa rafiki yao kiasi kwamba mmoja wao alimtamani mke wa mgeni wao na akafikiria lau angemuoa yeye.

 Isitoshe alifikiria pia njia za kumuwezesha kutimiza azma yake hiyo. Mwisho wa yote alitumia kila ujanja na mbinu za kishetani za kumhadaa bibi yule na akapata fursa ya kukaa naye faragha. Hapo alimuuliza thamani ya mahari aliyopewa alipoolewa na mumewe, na bila kusita mwanamke yule alitaja thamani ile, k.m. dinari alfu moja. Bwana yule aliendelea kusema; ‘Mimi nitakupa dinari elfu tatu kwa sababu uzuri wako unastahiki hivyo, siyo thamani aliyokupa mumeo ni ndogo mno na kwa kweli amekudhulumu.’ Kisha akamuuliza mumeo ana kazi gani afanyayo zaidi ya michezo? Yule mama akajibu; ‘Mume wangu ni karani katika wizara fulani.’ Bwana yule aligutuka na kusema ‘Aah!!! Hii ni dhuluma kubwa uliyofanyiwa, hivi kweli pamoja na uzuri wote ulionao unakuwa mke wa karani?

Haiwezekani kabisa, wewe thamani yako ni kubwa mno. Napenda kukufahamisha kwamba, mimi ni mhandisi na ninayo shahada ya udaktari na nimemaliza Chuo Kikuu, nataka kukuoa lakini kwanza mumeo huyu akuache.’ Na mwisho yule bwana alimuhadaa mke wa rafiki yao na wakaafikiana afanye kila hila adai talaka toka kwa mumewe naye atamuowa. Yote haya wakati

yanafanyika masikini mume yule hana habari anandelea na michezo.

Ziyara hiyo ilipokwisha bwana yule na mkewe wakarudi nyumbani kwao. Baada ya safari yao bwana huyu akaanza kuona mabadiliko ya tabia ndani ya nyumba yake. Tabia ya mkewe ikawa si nzuri tena, wakati hapo zamani alikuwa akiliona tabasamu la mkewe ambalo lilikuwa likimsahaulisha taabu ya kutwa nzima kazini, leo ni kinyume chake. Baadaye alimuuliza mkewe sababu ya mabadiliko haya. Mke akajibu, ‘Wewe umenidanganya.’ Mume akasema, ‘Nimekudanganya nini?’ Mke akasema, ‘Umenioa kwa mahari ndogo ambayo mimi sikustahiki, yuko mtu ambaye anaweza kunioa kwa mahari inayonistahiki na sasa nipe talaka yangu.’ Mume huyu akili zilimruka baada ya kusikia majibu ya mkewe. Alipigwa na butwaa la majonzi ambalo yeye ndiye aliyeliandaa siku aliposafiri na mkewe asiye na sitara na kumtambulisha kwa watu wasio maharimu wake.

Hata hivyo bwana huyu alijaribu kumpa rai mkewe abadili uamuzi wake, lakini jitihada zake zilishindikana na baadaye akamwacha mkewe kwa uchungu mkubwa hali akiwa bado anampenda. Na yule bibi baada tu ya kuachwa, alisafiri hadi kwa yule bwana aliyemuhadaa akiwa na ushahidi wa talaka mkononi ili akatimize lengo lake la kuolewa upya.”

Fikiria ewe msomaji, hili ni tukio katika matukio mengi yanayoharibu ndoa za watu. Hebu tafuta sababu yake, hutapata isipokuwa ni kwa sababu bibi yule alikuwa hakusitiriwa Kiislamu, na lau angekuwa kavaa Hijabu inayositiri maungo yake na uzuri wake, je bibi huyu angetumbukia katika mtego huu? Je, mume huyu naye angeingia katika machungu ya kumwacha mkewe hali ya kuwa bado anampenda kutokana tu uovu aliouandaa mwenyewe kwa kumwacha mkewe bila ya kuwa na sitara ya Kiislamu?   Lakini taabu hii na machungu haya aliyataka mwenyewe kwa kutomlea mkewe ndani ya malezi ya Kiislamu. Na haya ndiyo malipo ya mtu anayekwenda kinyume na

kanuni za Ki-Islamu na hukmu za Qur-an.

Wakati huo huo tunajiuliza, hivi kweli mke huyu baada ya kuachwa na yule mume wa kwanza, je ndoa ile kwa huyu mume wa pili ilidumu? Jawabu la swali hili linasema kuwa: “Mara nyingi ndoa za aina hi huwa hazidumu isipokuwa chache tu miongoni mwa hizo, kwa sababu mume wa aina hii huwa hamuowi mwanamke kwa lengo la kujenga maisha ya ndoa kwa maana ya mke na mume, bali huwa anaowa ili tu atosheleze matamanio yake ya kijinsiya na kuyashibisha matamanio yake ya kinyama. Matokeo yake ni kwamba bibi yule aliachwa na kurudi kwenye mji wao hali ya kuwa ni mwenye huzuni na majonzi tele. Alipata hasara ya kumpoteza mumewe wa kwanza ambaye alikuwa akiishi naye kwa kila aina ya mapenzi na huruma. Ewe msomaji mpendwa, hili ni tukio moja tu kati ya maelfu ya matukio ya hiyana za ndoa za watu. Lakini hebu fanya uchunguzi juu ya sababu zinazosababisha hali hii. Huwezi kupata sababu isipokuwa ni ile tabia ya wanawake kujidhihirisha na kuyaacha wazi maungo yao. Lau mwanamke yule angelikuwa na Hijabu, akausitiri uzuri wake ipasavyo, hivi kweli angenaswa katika mtego huu? Na je, lau yule mume angejikuta ameanguka ndani ya machungu yale ambayo kwa hakika yeye mwenyewe ndiye aliyeyaandaa? Hapana shaka kwamba haya ndiyo malipo ya mtu yeyote anayekwenda kinyume na kanuni za Uislamu na hukmu za Qur’an.

NAFASI YA SINEMA NA PICHA ZA VIDEO KATIKA UHARIBIFU WA JAMII

Sinema na picha za video zinachangia kwa kiwango kikubwa katika kuharibu mwelekeo sahihi na wa kweli kwa vijana kutokana na kuonesha filamu zinazohusu mambo ambayo ni ya siri baina ya mke na mume. Isitoshe sinema hizi huonesha maumbile ya sehemu hizi mbili za siri wazi wazi kiasi kwamba, hupanda mbegu mbaya kifikra kati ya wasichana na wavulana. Si hivyo tu bali sinema hizi zinawaondolea vijana wetu aibu machoni mwao na kuwapokonya imani, kisha kuwaingiza kwenye matendo maovu na machafu ambayo yanawafanya wasahau utamaduni wao wa Kiislamu na kuwafanya waige wanayoyaona humo.

Ni mara nyingi sinema na picha za video zimekuwa zikitumiwa kupotosha jamii zetu, kwa kuonesha miili iliyo uchi ya wanawake. Wacheza sinema huthubutu kudhihiri mbele ya watazamaji kwa kitendo ambacho kwa kweli ni aibu na ni fedheha kwa mwanadamu kukitenda hadharani, na hiyo ni tabia ya kinyama kabisa. Kwa hali hiyo basi, sinema zinatangaza uchafu huu wazi wazi na kuupigia kampeni huu kama kwamba ni kitendo kizuri. Mwenyezi Mungu anajua sana idadi ya maovu haya na matukio yanayotokea kutokana na jamii zetu kuendelea kuoneshwa filamu hizi chafu. Katika kuonesha madhara ya filamu hizi, kuna kijana mmoja wa kiume alikwenda kuangalia filamu zinazohusu mapenzi kati ya mume na mke. Baada ya kuangalia onesho hilo ambalo liliyateka mawazo yake na alirudi nyumbani kwao haraka sana. Alipofika tu alimkamata dada yake aliyekuwa kalala na kumtenda kitendo kichafu huku akiigiza namna ya kitendo hicho kama alivyoona katika filamu. Kitendo hiki kilisababisha maumivu makali kwa nduguye huyu aliyekuwa mdogo kwa umri, maumivu ambayo baadaye yalisababisha kifo cha msichana huyu.[26]

Bila shaka ndugu msomaji kwa mfano huu mmoja tu, unaona ni jinsi gani sinema zimekuwa ni nyenzo kubwa ya kueneza uchafu ndani ya jamii zetu. Kwa hiyo basi, sinema hizi ni vituo vikubwa wanavyovitumia wakoloni wa magharibi katika kuwavua Hijabu mabinti zetu na hatimaye kuwasukumiza kwenye shimo la maovu. Vile vile vituo wanavyotumia kugeuza vijana wetu kuwa watumwa wa matamanio yanayohusu mambo ya jinsiya na kuwafanya kuwa wasomi wa maraha na upuuzi huo. Sasa hivi imefikia mahali ambapo vijana wetu hakuna wanachokiwaza isipokuwa starehe tu, hawafikirii tena suala la maendeleo au utalaamu wa aina mbali mbali.

Hizi ni siasa za mataifa hayo makubwa, na lengo lao ni kuona vijana wetu na mataifa yetu hayajikwamui kiuchumi wala kisiasa, ili maendeleo ya viwanda, uchumi na elimu viendelee kuwa chini ya milki yao. Kamwe hawataridhika mpaka watuone sisi Waislammu tunabakia katika unyonge na udhalili, tukiendelea kuwategemea wao kwa kila mambo makubwa na hata madogo, na wao waendelee kuwa watawala wetu. Kwa hakika wametunyooshea panga zao mbele ya nyuso zetu na wametufanya kuwa ni vinyago vyao na wanatuchezea na kututumia namna wapendavyo.

Mpaka hapa mimi nauona umuhimu wa kuelekeza tena usemi wangu kwa Waislamu wote wanaohisi wajibu na jukumu katika dini. Mimi nawaambia kwamba, “Zipigeni vita sana sana hizi sinema za X[27] na wawakemee watu wasiziangalie. Si hivyo tu bali wanapaswa kuwatahadharisha watu, kwani kujiingiza katika mambo hayo licha ya kuwa ni kumuasi Mwenyezi Mungu, bali hali hii inatumikia maslahi ya maadui wa Uislamu na kuharibu mwenendo wa vijana wa Kiislamu kwa kutumia kigezo cha utaalamu na maendeleo.

MADHARA YA KUCHANGANYIKA WANAUME NA WANAWAKE

Mchanganyiko unaokusudiwa hapa ni ule wa kukaa pamoja wanaume na wanawake wakawa wanatazamana ana kwa ana bila kuwepo kizuizi baina yao kitakacho tenganisha pande mbili hizi.

Kutokana na maumbile ya wanaadamu yalivyo, sheria ya Kiislamu haikubaliani na kitendo hiki cha kuchanganyika wanawake na wanaume, na hapana shaka kwamba Mwenyezi Mungu anachukizwa na jambo hili. Kwa nini basi jambo hili liwe baya? 1. Ni kuvunja moja katika sheria za Kiislamu (Hijabu) na ni kukaribisha maovu katika jamii.

2. Jambo hili huandaa na kurahisisha njia za kupatikana mahusiano ya kijinsiya baina ya pande mbili hizi kinyume na utaratibu uliowekwa kisheria.

3. Jambo hili huwa ndiyo chanzo na sababu ya kuharibu familia na kuzitenganisha na ni kivutio kikubwa cha maovu ndani ya jamii.

4. Jambo hili linasababisha misiba na majonzi, pia linaleta uharibifu mkubwa kati ya pande mbili husika. Kwa hiyo mchanganyiko kati ya wanaume na wanawake ni kirusi chenye maradhi hatari yanayotishia usalama na mwenendo wa familia, kiasi kwamba tunaweza kuyafananisha na maradhi ya kansa ambayo mgonjwa huwa hapati nafuu isipokuwa kwa kuikata shemu iliyopatwa na ugonjwa huo na kukiondoa kiini cha ugonjwa. Katika nchi au jamii zilizoruhusu mchanganyiko

huu, hapana shaka kwamba zimechangia sehemu kubwa ya ongezeko la maovu na kufikia idadi inayotisha hasa katika mashule na vyuo vikuu ambako wasichana na wavulana wanachangaywa pamoja utadhani ni viumbe wenye jinsiya moja.

Matokeo ya mchanganyiko huu ni kugeuka kwa mashule haya na vyuo hivi kuwa vituo vya mafunzo ya uhuni na mambo machafu ambapo lengo lake lilikuwa ni kupafanya kuwa mahali pa

kujifunza elimu. Yote haya yanakuja kwa sababu ya kukosekana kwa sitara au kizuwizi cha kuzitenganisha jinsiya hizi mbili. Katika ripoti moja iliyotolewa na Jaji mmoja wa Kimarekani anasema: “Asilimia 45% ya wasichana wanaosoma katika shule za mchanganyiko hupoteza bikra zao kabla ya kutoka shuleni, na asilimia hii huzidi kadri wasichana wanavyoendelea katika masomo ya juu.”Huko Uingereza wasichana wamekuwa wakiandaliwa kutembea na vidonge vya kuzuwiya mimba, na kwamba asilimia 80% ya wasichana hutembea na vidonge hivyo katika mikoba yao. Hii ni dalili ya wazi inayotuonesha kwamba, wasichana hao huwa wako tayari wakati wowote ule kutenda kitendo kichafu kwa kuwa kinga wanayo. Wasichana hawa wanayafanya haya kukwepa matokeo mazito yanayoweza kuwakuta ndani ya uchafu huo wanaoutenda.28 Lakini je hivi kweli ni sahihi kumuacha msichana akawa katika mazingira kama haya ndani ya jamii hasa ya Kiislamu?

Baada ya maelezo haya bila shaka ina dhihiri wazi hekima kubwa iliyomo katika Uislamu katika kupiga marufuku michanganyiko baina ya wanaume na wanawake. Hapana shaka kabisa kwamba, Uislamu lengo lake ni kutaka kuiepusha jamii kutokana na hatari tulizozitaja hapo kabla. Ndiyo maana umeharamisha mchanganyiko kati ya wanaume na wanawake katika sehemu zote, kama vile mashuleni, vyuoni, katika sehemu za sherehe, na kwa ujumla popote katika jamii mchanganyiko kati ya wanaume na wanawake hauruhusiwi.

Yote haya makusudio ni kuihifadhi jamii kutokana na maovu yanayozaliwa na michanganyiko. Na ama hali ya mikusanyiko ya wanaume na wanawake tunayoiona katika msimu wa Hija na katika maeneo matakatifu na pia ndani ya kumbi za Huseiniyyah, mikusanyiko kama hiyo haikuharamishwa hasa kwa kuwa wanawake wanaohudhuria ndani ya maeneo hayo huwa wako katika hali ya kujisitri kama sheria inavyowataka wajisitri.

UISLAMU SIYO DINI YA NADHARIA.

Mara nyingi tunasoma katika baadhi ya magazeti kwamba, baadhi ya watu waliohadaika na wasiojuwa chochote kuhusu Uislamu, eti wanajaribu kutoa fikra zao katika kukosoa baadhi ya kanuni za sheria ya Kiislamu. Miongoni mwa kanuni ambazo wamekuwa wakijaribu kuzikosoa kwa kutumia kalamu zao ni hili vazi la Hijabu. Waandikapo husema; “Mimi sioni umuhimu wa Hijabu, kwani Hijabu katika maoni yangu sio lazima kwa kuwa inarudisha nyuma maendeleo.”Au hupata wakasema kuwa; “Kuna ubaya gani wanaume na wanawake kuchanganyika pamoja?”Na mengine mengi wanasema lakini kifupi ni hayo. Sisi tunawajibika kuwaambia watu hawa na wengine mfano wa hao kwamba; “Ninyi ni kina nani? Ninyi ni kina nani hasa mpaka mnathubutu kutoa maoni yenu dhidi ya desturi na mila ya Mbinguni? Na mna utukufu gani mbele ya maamuzi ya Mwenyezi Mungu na sheria nzima ya Kiislamu? Na je Uislamu ni dini ya fikra za kinadharia mpaka mumediriki kuusemea kwamba mimi naona kadhaa, au mtazamo wangu katika sheria ya Kiislamu naona hivi au vile.? Kisha nawauliza hawa wanaosema maneno haya; “Je, ninyi kweli ni Waislamu? Ikiwa wao ni Waislamu wanawajibika kuwa watiifu katika maamrisho ya Mwenyezi Mungu na makatazo yake, pia washikamane na sheria za Kiislamu ambazo miongoni mwake ni Hijabu. Na kama ninyi siyo aislamu basi, hamna haki ya kuingilia mambo ya Kiilamu, ala hamna haki ya kutoa maoni yenu potofu mbele ya Umma wa Kiilamu.

Mpaka hapa ndugu msomaji nashangazwa na ujeuri wa watu hawa dhidi ya Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Na ni kwa misingi gani viumbe hawa dhaifu wamejasirika na kufikia kiasi cha kukosoa hukmu na kanuni za Mwenyezi Mungu? Je wanasahau kwamba Mwenyezi Mungu anasema katika Suratul Maidah katika Aya tatu mfululizo: “Na wale wasiyohukumu ( kwa sheria) aliyoiteremsha Mwenyezi Mungu basi watu hao ni makafiri, madhalimu, mafasiki.[28]

Watu hawa mbele ya Mwenyezi Mungu watabeba mzigo mzito kwa makosa yao ya kuhamasisha watu kuvunja amri za Mwenyezi Mungu na kutenda machafu yaliyo katazwa. Malipo (adhabu) yao pia ni mazito kutokana na maneno yao hayo, kwa adhabu kali watakayoadhibiwa kutokana na wao kuunga mkono maasi na kuyatia nguvu yatendwe.

Back Index Next