Imani, misingi na mafundisho yote ya Ukristo ni kazi ya Paulo ambayo aliifanya kwa shabaha ya kuungwa mkono na kukubalika kwa wafuasi wapya miongoni mwa ambao hawakuwa Wayahudi wa zama zake. Kwa kuingiza na kuchanganya imani za kipagani katika mafundisho ya Yesu, Paulo alipata mafanikio makubwa mno katika kazi yake lakini kwa kufanya hivi aliharibu na kuivunjilia mbali imani ya kuamini Mwenyezi Mungu mmoja asiye kuwa na mshirika. Kwa kufanya hivi Paulo alifanikiwa kuyapotosha kabisa mafundisho yote ya Yesu na badala yake akaanzisha maradhi mabaya na yaliyoenea kwa haraka aliyotatoa katika upagani - ambapo imani hizi bado tunazo mpaka leo katika ukristo. Ni hapa kwenye kiini na kitovu cha mafundisho ya Yesu palipotoshwa na hii ndio sababu kuu ya tofauti za msingi kati ya Uislamu na Ukristo.
Inafurahisha kuona kwamba "imani na misingi ya Ukristo" ambayo Quran inaikubali inaweza pia kuthibitishwa kwa urahisi kabisa, kuwa ni sehemu ya mafundisho ya wanafunzi wa mwanzo kabisa wa Bwana Yesu, ambapo imani na misingi ambayo Quran inaikataa inaweza kuthibitishwa kuwa ni maongezo (nyongeza) yaliyoongezwa na viongozi wa juu wa kanisa au Paulo. Waliyaongeza haya kwa sababu walipendezwa na falsafa na mifumo ya dini za Wapagani wa Kigiriki na wa Kirumi".[15]