UTETEZI WA SHERIA
Muhtasari nne juu ya
Sheria mbali mbali binafsi
Za kiislamu
Kimeandikwa
na:
Allamah
Sayyid Saeed Akhtar Rizvi
Kimetafsiriwa na:
Dr.
Mohamed S. Kanju
Kimechapishwa na:
BILAL MUSLIM
MISSION OF TANZANIA
P.O.Box 20033
Dar es Salaam
Tanzania
www.al-islam.org and ebooked by www.ShiaLibrary.com and www.islamkutuphanesi.com . May Allah be pleased with all. |
Haki ya kunakili imehifadhiwa na:
ã
Bilal Muslim Mission of Tanzania
ISBN 9987
620 26 4
Toleo la Kwanza:
2001, Nakala: 2000
Kimetolewa na kuchapishwa
na:
BILAL MUSLIM
MISSION OF TANZANIA
S.L.P. 20033
DAR-ES-SALAAM
TANZANIA
YALIYOMO
1.
Dibaji 4
2.
Historia Fupi Ya Mwandishi Wa Kitabu Hiki 5
3.
Utangulizi 11
4.
Muhtasari juu ya Sheria za ndoa uliwasilishwa
mbele ya Tume ya
Serikali ya Kenya juu ya
Sheria za ndoa n.k 17
6.
Muhtasari juu ya Sheria za mirathi
uliwakilishwa
mbele ya Tume ya
Serikali ya Kenya juu ya
Sheria za ndoa n.k 28
7.
Muhtasari juu ya Waraka wa Tanzania juu ya
Sheria ya ndoa
inayofanana sawa kwa wote Imechapishwa
katika Standard (DSM)
Jumatatu, 8 Desemba 1969 42
8.
Muhtasari juu ya Hijabu na Mirathi
uliwasilishwa kwa Mheshimiwa Al-Haj
Sheikh Ali Hassan Mwinyi 56
9.
Barua ya Wizara ya Elimu Juu ya Hijabu 64
10.
Mahkama ya Kadhi: Baadhi ya Mapendekezo
Imechapishwa
katika The Democrat (DSM) 17-23, Aug,
1999 65
DIBAJI
Tunamshukuru
Allãh (s.w.t.) na kwa baraka za Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na Ahlul~Bayt (a.s.)
kwa kutujaalia kuweza kufanikisha juhudi zetu hizi katika kuchapisha kitabu
hiki juu ya sheria za ki-Islamu.
Kitabu hiki kilochopo mikononi mwako
ni tafsiri ya kitabu cha kiingereza kiitwacho In Defense of Islamic Laws kilicho
andikwa na Allamah Al-Haj Sayyid Saeed Akhtar Rizvi, Muasisi na Mhubiri Mkuu wa
Mission hii.Kitabu hiki kimekua maarufu katika ulimwengu wa ki-Islamu.Watu
wengi kutoka Afrika ya Mashriki wametuomba kukitafasiri katika lugha ya
kiswahili.
Tunamshukuru Dr, Mohammad Salehe
Kanju kwa kukitafsiri kitabu hiki katika lugha ya kiswahili.
Kwa manufaa ya wasomaji wetu
tumeongeza makala juu ya Mahakama ya
Kadhi ambayo ilitayarishwa na Mwandishi baada ya kitabu cha asili ya
kiingereza kuchapishwa.
Mission inatoa shukurani zake za
dhati kwa Bwana Mahmood Khimji ambaye kwa juhudi zake kitabu hiki kinawafikia
wasomaji wetu mikononi na Sayyid Murtaza Rizvi kukipanga vizuri katika kompyuta
na wale wote wanaotuunga mkono kwa njia moja au nyingine kwa kufanikisha
kuchapishwa kitabu hiki, Tunamuomba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) awalipe malipo mema
hapo Duniani na baadaye huko, Akhera.
Wamaa Tawfeeqi
Illah Billah
BILAL MUSLIM MISSION OF TANZANIA
HISTORIA FUPI YA
MTUNZI WA KITABU
HIKI
ALLAMAH SAYYID
SAEED AKHTAR RIZVI
Hujjatul Islam Wal Muslimin Allamah Al-Haj Sayyid
Saeed Akhtari Rizvi, alizaliwa katika Familia ya Maulamaa mwezi Mosi Rajab 1345
A.H. (5th Januari 1927 M.) katika mji wa Ushri Khurd, Wilaya ya Siwan, Bihar,
India. Mazazi wake Marehemu Ustadul Ulamaa Sayedul Hukama Maulana Al-Haj Sayyid
Abdul Hassan Rizvi (radhi za Mwenyezi Mungu Zimshukie) alikuwa Mmoja wa
Maulamaa wakubwa wa India.
Allamah
Rizvi alianza masomo yake katika mji wa Gopalpur makazi ya jadi yake na
kuendelea huko Patna na Banaras. Alifaulu Shahada ya juu katika mtihani wa
lugha za Kiarabu, Kiajemi na Kiurdu kutoka (Chuo Kikuu cha) Allahabad Board,
U.P., na akafanikiwa kupata Shahada ya juu zaidi ya elimu ya dini -
"Fakhru 'L-Afadhil" kutoka chuo cha Jami'ul 'Uloom Jawadia, Banaras.
Kuanzia ujana wake, alikuwa akijishughulisha
kikamilifu katika jamii, elimu na kuinua dini ya Jumuiya. Katika mwaka wa 1948,
alichukuwa nafasi ya baba yake kama Imamu wa Jumuiya huko Hallaur katika wilaya
ya Basti, U.P. na akaendelea na nafasi hiyo hadi mwaka wa 1951. Kuanzia 1952 -
1959 alifanya kazi kama Mwalimu wa Urdu na Kiajemi katika shule ya Sekondari ya
juu ya Husainganj (huko) Husainganj, Siwani.
Muda wa
miaka yote hii alitumia likizo zake na wakati wake katika shughuli za Jumuiya
kama kuendeleza shughuli za Anjumani Wazifa-e-Sadat-wa Momineen na
Anjuma-e-Tarraqi-e-Urdu.
Katika
Mwezi Desemba 1959, alikwenda Tanzania (wakati huo ikijulikana kama Tanganyika)
ambako alihudumia kama Imam wa Jumuiya huko Lindi (1959-1962) Arusha
(1963-1964) na Dar es Salaam (1965-1969).
Baada
ya juma moja tu kuwasili kwake Afrika, alianza kujifunza lugha ya Kiswahili na
kuangalia hali ya nchi kwa mtazamo wa kubalighisha Uislamu wa kweli miongoni
mwa jamii ya wazawa (wa asili). Katika
nyakati hizo kulikuwa hakuna Shia-Ithna-asheri hata mmoja mwenye asili ya
Kiafrika katika bara lote. Katika mwaka wa 1962 alitayarisha mpango kwa
ajili ya tablighi na akaupeleka kwa sekritariati ya Halmashauri Kuu ya Khoja
Shia Ithnaasheri wakati huo ikiwa Arusha. Katika mwaka wa 1963 mpango huu
ulijadiliwa kwa urefu. Katika hatua hiyo haukuweza kutekelezwa kama
ilivyoshauriwa, lakini mwelekezo wa taratibu uliwekwa katika utekelezaji.
Katika mwaka 1964 Sekritariati ilitayarisha taarifa (memorandum) iliyotegemea
juu ya msingi wa taratibu yake ambayo iliwekwa katika agenda ya mkutano wa tatu
wa mwisho wa mwaka wa muungano wa Jamati za Khoja Shia Ithna-asheri za Afrika
(Federation of Khoja Shia Ithna-Asheri Jamaats of Africa) uliofanyika Tanga.
Hivyo Bilal Muslim Mission ilizaliwa.
Kuanzia
siku hiyo, Allamah Rizvi alitumia muda wake katika shughuli za Tabligh. Katika
mwaka 1963 Bilal Muslim Mission of Tanzania ilisajiliwa. Wakati kazi
ilipoongezeka, Marehemu Ayatullah Al-Uzma Sayyid Muhsin Al-Hakeem (Najaf, Iraq)
aliamuru Halmashauri Kuu ya Khoja Shia Ithna-asheri ya Afrika kumtoa katika
majukumu ya Jamaat, na kuanzia hapo gharama zote za Allamah Sayyid Rizvi
zilichukuliwa na marehemu Ayatullah Al-Uzma Sayyid Muhsin Al-Hakeem na baada
yake zikachukuliwa na marehemu Ayatullah Al-Uzma Sayyid Abul Qasim Al-Khu'i.
Kwa
juhudi zake katika Mission hii makumi ya maelfu ya Waafrika wamekubali imani ya
Shia pole pole kupitia mafundisho, maandishi na masomo kwa njia ya Posta, sasa
Jumuiya ya Shia imestawi nchini Guyana chini ya Bwana Lateef Ali ambaye amefanikiwa
kueneza ujumbe mpaka Trinidad na Tobago.
Mission
ina kituo kwa ajili ya kufundishia Mubalighina mjini Dar es Salaam ambacho vile
vile kina Bweni lenye nafasi. Kuna shule za chekechea, Msingi, Secondary na
Madrasah ya Qur’ãn na Misikiti. Kwa nyongeza, Mission inaendesha masomo aina
nne kwa njia ya Posta ambayo kwayo mwanga wa Ushia umefika mbali kwa marefu na
mapana. Mission imechapisha vitabu zaidi ya miamoja na ishirini kwa Kiingereza
na Kiswahili, sehemu kubwa ikiwa ni ya vitabu vya Allamah Rizvi au tarjuma yao.
Kuna
Bilal Muslim Mission nchini Kenya (imeanzishwa sawia na Misheni ya Tanzania)
Burundi, Malagasy na Msumbiji. Yakitiwa moyo na Bilal Muslim Mission of
Tanzania, Mashirika yenye majina kama haya yameanzishwa nchini
Seneghal,Naijeria,Ghana,Sweden na Marikani.
Katika
mwaka wa 1978 alirudi na kukaa nchini India ambako alianza kuandika tarjuma ya
Kiingereza ya Tafsir al-Mizan cha Marehemu Allamah Sayyid Muhammad Husayn
at-Tabataba'i. Juzuu kumi za tarjuma hii zimekwisha chapishwa na World
Organization For Islamic Service (WOFIS)
Tehran Iran.
Mwezi
Desemba 1980, alikwenda London kwa mualiko wa (Shirika la) Imam Sahebuz Zaman Trust. Kule London alikua
pamoja na marehemu Hujjatul Islam Al-Mujahid Sayyid Mhadi al-Hakeem katika
kuanzisha World Ahlul-Bayt (A.S.) Islamic League (WABIL) ni mmoja wa wadhamini
watatu wa Shirika hili. Alikuwa Mkurugenzi wa Kamati ya maandalizi ambayo
ilirasimu katiba ya WABIL na ilipanga mkutano wake wa kwanza wa katiba. Mkutano
huu ulifanyika mwezi Augosti 1983 ambao kwayo wajumbe 80 kutoka nchi 30
walishiriki. Katika mkutano huo alichaguliwa kuwa mkurugenzi mkuu (wa shirika
hilo).
Alirudi
Tanzania mwaka 1986 kuendeleza shughuli za Bilal Muslim Mission of Tanzania na
sasa hugawanya wakati wake kati ya Tanzania, India, na Canada.
Mwaka
wa 1991 Ilianzishawa Ahlul~Bayt (A.S.) World Assembly (ABWA) Tehran,Iran na
Allamah Rizvi alichguliwa mmoja wa wana kamati ya Halmashuri kuu na mjuube. Na
vile vile ni Muasis na Mwenye Kiti wa Ahlul~Bayt (A.S.) Assembly of Tanzania.
Mwaka wa 1993 ameanzisha Bilal Charitable trust of
India,Gopalpur. Hadi sasa zaidi ya Misikiti 25 na Hussaeinia zimejengwa na
zaidi ya nyumba 30 za kuishi kwa watu ambao hawana makazi na vile vile shule za
chekechea, Msingi, Secondary na teknolojia zimeanzishwa na Tasisi hii.
Allamah
Rizvi ameanzisha Madrasa nyingi za Kidini na kufungua Markazi za Tablighi
katika sehemu mbalimbali ulimwenguni, kati ya sehemu hizo ni India, Marekani,
Uingereza, Canada, na nchi za Kiafrika.
Kufikia
sasa ameandika vitabu 124 (78 kwa Kiingereza, 29 kwa Kiurdu, 11 kwa Kiarabu na
6 kwa Kiswahili) ambavyo 91 vimekwisha chapishwa na 6 vinachapishwa.Kwa muda
huu, anajishughulisha katika kuandika vitabu 3 vya Kiingereza, Kiarabu na
Kiurdu. Baadhi ya vitabu vyake vimetafsiriwa kwa lugha za Ki-Japan
Ki-Indonesia, Ki-Thai, Ki-Burma, Ki-Urdu, Ki-Hindi, Ki-Gurjati, Ki-Sindhi,
Ki-Ajemi, Ki-Swahili, Ki-Hausa, Ki-Shona, Ki-Taliani, Ki-Faransa Ki-Swidish
Ki-Bosni Ki-Arabi Ki-Holanzi.
Vile vile
amefanya kazi na baadhi ya Maulama wa Qum kuweka vizuri na kusahihisha
Adh-Dhariah fi Tasanif As-shia, Kitabu kikubwa cha habari za vitabu na
watungaji wake kilichoandikwa na marehemu Ayatullah Agha Buzrg at-Tehrani.
Amepewa
Ijazat (Mamlaka) na Ma-Ayatullah wakongwe kumi na Tisa wa Najaf (Iraq) na Qum
(Iran) kwa simulizi ya hadithi (riwayah) kwa mambo ya hukumu kwa Shariah na
vile vile kushughulikia suala lolote ambalo kwalo ruhusa ya Mujtahid ni muhimu.
Ni
mtaalam wa lugha. Huandika, huzungumza na kutoa mihadhara kwa Ki-Urdu,
Ki-Arabu, Ki-Ingereza, Ki-Swahili na Ki-Ajemi. Vile vile anayo elimu (ya
maandishi) ya Ki-Hindi na Ki-Gujarati. Mbali na ukubwa na upana (wa eneo)
anaoshughulikia, na ziara za mara kwa mara ndani ya Afrika Mashariki, amezuru
kama nchi 45 za Asia, Afrika, Ulaya na Marekani.
ORODHA YA BAADHI ZA VITABU
VYA
ALLAMAH RIZVI
Kwa Kiingereza
1 Islam
2. Need of Religion
3.
God : An Islamic
Perspective
4. Justice of God
5. Prophethood
6.
Imamate
7.
Qur’an and Hadith
8. Day of Judgement
9.
What a Muslim Should
Know & Believe
10.
The Return of Al-Mahd
11. Elements of Islamic
Studies
12. Fast
13.
Family
Life of Islam
14.
Charter
of Rights
15.
Hijab
16.
Muhammad (S.A.W.) is the
Last Prophet
17.
The Holy Prophet
18.
Four California Lectures
19.
Taqiya
20.
Inner Voice
21.
Rulings On Morden Problems
22.
Islamic Laws
23.
In Defence of Islamic Laws
24.
Wahhabis’ Fitna Exposed
25.
On To The Right Path
26.
Pork
27.
Slavery
28.
Sects of Islam
29.
Shi’ite Sects
30. Your Questions Answered 1
31. Your Questions Answered 2
32. Your Questions Answered 3
33. Your Questions Answered 4
34. Your Questions Answered 5
35. Your Questions Answered 6
36. Your Questions Answered 7
37.
Your
Questions Answered 8
38.
A
Few Questions Answered
39. Fadak
40. The Ideal Islamic Government
41. Meaning & Origin of Shiism
42. The Quran Its Protection from
Alteration
43. Prophecies About the Holy
Prophet of Islam in Hindu
Christian & Jewish Scriptures
44.
Some
East African Ithna-
Asheri Jamaats
45.
The
Khoja Shia Ithna-Asheri
Community in East Africa
46.
A
Correspondence Between a
Christian and a Muslim
47.
Selected
Articals Vol 1
48.
Selected
Articals Vol 2
UTANGULIZI
Katika mwaka wa
1964, Bunge la Tanganyika lilipitisha Sheria ya “ki-Islamu” (Taarifa
mpya) ambayo ilimpa uwezo Waziri anayehusika na mambo ya Sheria kutengeneza na
kutangaza Taarifa ya Sheria ya ki-Islamu baada ya kushauriana na
Wasomi wa sheria katika madhehebu za ki-Islamu. Kwa mujibu wa Gazeti la Standard Tanzania
(13/ 7/67) liliandika : “Inafahamika kwamba Tanganyika ni nchi ya
kwanza kupata kutekeleza zoezi la kupanga kanuni ya sheria ya ki-Islamu katika
mfumo wa sheria iliamriwa halali. Taarifa hizi zitasaidia sana Mahakama
ambazo hutegemea juu ya vitabu vya kiada”.
Khoja shia
Ithna-asheri territorial council of Tanzania (Jumuiya ya Khoja shia Ithana-sheri) walilichukulia
uzito suala hili. Bwana Mohamed G.
Dhirani, aliyekuwa wakati huo Rais wa Baraza ya Jumuiya iliyotajwa,
alinichukuwa mpaka kwenye Ofisi za Mwanasheria Mkuu, ambako nilimkuta wakili
mkuu wa mradi huo. Alikuwa ni mwislamu
wa Zanzibar. Alinishauri niandike kwa
Kiingereza, sheria zote za Shi’a zihusikanazo na masuala haya kwa matumizi ya
Ofisi yake. Hivyo niiandika “sheria
za ki-Islamu zinazohusika na ndoa, kuvunjika kwa ndoa, makubaliano ya ndoa,
wosia, mirathi na waqf”. Bwana
Fida Hussein Abdallah Hameer, aliyekuwa Katibu wa Baraza wakati huo
alitayarisha Sekretariati kwa ajili ya kusaidia.
Miwishowe
makaratasi (yenye taarifa) yalimfikia Bwana Bashir Rahim, aliyekuwa mrasimu wa
Bunge Muandamizi ambaye alikamilisha sura nne za ndoa (kama inavyokubalika na madhehebu
makubwa matatu ya Sheria ya Uislamu - Shafii,Hanafi na Shi’a). Ilichapishwa chini ya mamlaka ya bwana Rashid
Kawawa, aliyekuwa wakati huo makamu wa
rais wa Tanzania, ambaye alikuwa anapasika vile vile na Idara ya Sheria. Ilitokea kama sheria ndogo zilizotungwa chini
ya Taarifa rasmi mpya ya Sheria ya ki-Islamu (Na. 56 ya 1964) (Katika) Nyongeza
ya Gazeti (La Serikali Na. 34 la 27 Juni 1967).
Ilieleweka zile sura zilizobakia zinazohusu utunzaji wa watoto na talaka
nk. zitachapishwa mwishoni mwa mwaka, na
kisha hapo Sheria zitaanza kutekelezwa.
Sasa mandhari
inahamia Kenya. Serikali ya Kenya wakati
huo iliunda Tume juu ya sheria za ndoa,
talaka na mirathi, chini ya uwenyekiti wa Mheshimiwa Jaji Spry wa Mahakama Kuu
ya Kenya. Tume ilitakiwa itoe mapendekezo kwa ajili ya sheria mpya
yenye uwezo mkubwa na kwa kadiri itakavyoweza kutumika kama sheria inayofanana
ya ndoa, na talaka itumikayo kwa watu wote nchini Kenya. Ambayo itakuwa badala
ya Sheria iliyopo juu ya suala lihusianalo na
Sheria ya mila, Sheria ya “ki-Islamu”, (haswa ya kwetu) Sheria
ya Baniani na Sheria za Bunge
zinazohusika na kutayarisha rasimu ya Shria mpya; ikitoa kipaumbele mahususi
kwa hadhi ya wanawake kuhusiana na ndoa na talaka katika jamii huru ya
kidemokrasia.
Nilikwenda
Mombasa Julai 1967 kwa mintaarafu fulani mingine na wahusika wa Supreme Council (Halmashauri Kuu
ya Shia Ithna-asheri) walinichukuwa nikaonane na wakili
ambaye alikuwa bingwa katika sheria binafsi za Uislamu. Kwa kuelezewa matukio ya Tanzania, aliniomba
nimplekee nakala ya Sheria za “Ki-Islamu” ambayo nimeiandika kwa
ajili ya Tanzania. Nami niliahidi hivyo.
Kabla ya
hii, niliandika majibu kwa maswali ya
Tume ambayo yalipelekwa kabla kwenye Tume.
Kurudi Dar es
Salaam, nilikusanya taarifa ya Sheria za “Ki-Islamu” zilizotajwa (karibu
karatasi ndefu mia moja, kurasa zilizopigwa mashine kwa karibu karibu) zikiwa
zimerudufiwa, na kutumwa Halmashauri Kuu ya Khoja Shia Ithna-asheri.
Katika juma la
tatu la Augusti 1967, niliitwa haraka Mombasa
ambako tume ilikuwa ikae kwa ajili ya kusikiliza kuanzia 21/8/1967. Niliandika muhtasari (au taarifa) kwa ajili ya
kuwasilisha mbele ya tume, ambayo ilikamilishwa baada ya majadiliano na maofisa
wakuu watendaji (wa Halmashauri Kuu).
Muhtasari ule uliwasilishwa kwenye tume na kisha ukachapishwa katika “The
Light” ya Julai – Augusti 1967. (Marehemu) Haji Mohamedali Meghji, Rais
wa Halmashauri Kuu ya Khoja Shia Ithna-asheri aliandika barua iliyoambatanishwa ya maelezo (ya ziada)
dondoo ambayo imechapishwa marudufu kabla ya muhtasari wa kwanza.
Mheshimiwa Jaji
Spry alisikika akiwaambia wenzake baadae kwamba “watu hawa walijua kuhusu
walichokuwa wakiongea”.
Muhtasari
mwingine juu ya Sheria ya Mirathi ambao ulioandikwa na mimi, ulitumwa kwenye
tume na kuchapishwa katika “The Light” ya Januari – Aprili
1968. Ni Muhtasari wa pili katika
mkusanyo huu.
KURUDI
TANZANIA:
Wakati matukio
hayo hapo juu yalipokuwa yanafanyika nichini Kenya, ghafla Serikali ya Tanzania
ilisimamisha zoezi la upangaji wa Kanuni (wa Sheria ya “ki-Islamu”).
Tume ya Kenya
iliwasilisha taarifa yake na mapendekezo wakati Fulani katika mwaka wa 1969. Tarehe 10/9/69 Serikali ya Tanzania
ilichapisha waraka (White Paper) No. 1 wa 1969 uliosema kwamba inataka kutunga
Sheria ya Ndoa iliyo sawasawa (kwa wote),
na ikatoa maelezo ya masharti iliyoyataka yawekwe kwenye Sheria
iliyokusudiwa.
Pamoja na kuchapishwa
kwa waraka, Serikali ilikaribisha maoni na mapendekezo kutoka kwenye Jumuiya na
watu binafsi. Wakristo, Mabaniani na
Maismailiya walichapisha maoni yao katika magazeti. Niliwafuata Bakwata kwa madhumuni haya;
walikataa kwa mkato kabisa kuingilia mpango wa Serikali. Nilikuwa sina njia nyingine bali kuandika kwa
niaba ya Shi’a Ithna-sheri tu. Maoni
yalikuwa ya ukweli na pengine kifungu cha mwisho kilikuwa kikali kidogo. Nilipeleka mswada kwa Bwana Anverali M.
Rajpar, aliyekuwa wakati huo Rais wa Khoja Shia Ithna-sheri Territorial Council
of Tanzania, aliniambia niendelee na niuchapishe kwenye Gazeti la Standard kwa
niaba ya Tanzania Council. Ilitokea
katika Standard (Dar es Salaam) tarehe 8 Desemba 1969 (Jumatatu) na
baadaye dondoo zake zilichapishwa katika “The Light” ya Desemba 1969. (Mswada) huu hutokea kama muhtasari wa tatu
katika kijitabu hiki.
Wakati wa miezi
ya baadaye, Halmashauri Kuu (Supreme Council) ilinitumia taarifa mbili za tume
ya Kenya, nilishagazwa kuona kwamba karibu mapendekezo mengi ya waraka wa
Tanzania yaliondolewa kutoka kwenye mapendekezo ya Tume ya Kenya.
Wakati naandika
muswada wa Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971, katika mwanga wa waraka wa Serikali na
maoni niliyopokea, Bwana Bashir Rahim, aliyekuwa wakati huo msawidi mkuu wa
Bunge, alijaribu kwa uwezo wake kuingiza masharti ya Sheria za “ki-Islamu”. Kabla ya kukamilisha muswada huo,
ulionyehswa kwa wanachuoni wa kila dini na madhehebu, na mabadiliko fulani
yalifanywa kwa kutegemea juu ya ushauri wao.
HALI
ILIYOPO SASA:
Serikali ya
Tanzania sasa inataka kutunga Sheria ya Mirathi iliyo sawa kwa wote; ambayo
itawapa wanawake kigawanyo sawa na kile cha wanaume. Wakati wanachuo wa “ki-islamu” (sio Bakwata)
walipotoa kauli zao dhidi ya sheria
hiyo, aliyekuwa wakati huo Rais (wa Jamhuri ya Tanzania) Mheshimiwa Al – Haji
Ali Hasani Mwinyi aliwahakikishia kwamba rai haikuwa kubadilisha sheria ya “ki-Islamu”,
bali kuweka haki ya mirathi kwa wanawake wale ambao hawana haki kama hizo
kabisa – bali wao wenyewe wanachukuliwa kama bidhaa za mirathi.
Wakati huo huo
katika mwaka wa 1990, mashirika mabalimbali ya “ki-Islamu” (Mbali na Bakwata)
yalianza kufanya kampeni kwa
ajili ya washichana wa “ki-Islamu” kuruhusiwa kuvaa Hijab mashuleni. Wawakilishi wao walikutana mara nyingi, na
kutegemea juu ya majadiliano yao, niliandika Muhtasari juu ya Hijab na mirathi,
ambao hatimaye uliwasilishwa kwa Rais Al-Haj Ali Hassan Mwinyi. (Muhtasari huo) umewekwa katika kijitabu hiki
kama Muhtasari wa nne. Inafurahisha
kuona kwamba Rais alitamka katika hotuba ya hadhara tarehe 10/8/1995 kwamba
wasichana wa “ki-Islamu” sasa wanaruhusiwa kuvaa Hijab mashuleni; na Kaimu
Kamishina wa Elimu alitoa mwongozo kwenye suala hili kwa taasisi za Elimu,
ambao barua yake halisi yaweza kuonekana
katika ukurasa ufuatao, na tarjuma yake ya kiingereza imetolewa mwiso wa
kitabu hiki.
Bilal Muslim
Mission of Tanzania inaona kwamba muhtasari hizi zina hoja zilizo wazi
kuthibitisha kwamba Sheira za “ki-Islamu” zilizoanzia kutokana na
hekima ya Mungu haziwezi kubadilishwa, na kwamba Sheria ya “ki-Islamu” ni mfumo
pekee ambao huweza kutoa haki na uhuru katika jamii.
Ni kwa sababu hii
kwamba Misheni hii imeamua kuchapisha Muhtasari nne pamoja katika kijitabu
hiki. Nawashukuru kwa ari hii, na kuomba
kwa Allah Subhanahu wa Ta’ala kuwapa tawfiq zaidi, na akifanye kitabu hiki
kuwa njia ya mwongozo kwa Waislamu na
kwa wasio Waislamu hali kadhalika.
31st October
1998
1
Dondoo kutoka
barua iliyoambatanishwa : Muhtasari
ufuatao uliandikwa na Maulana Sayyid Saeed Akhtar Rizvi kwa ajili ya kuwasilisha mbele ya tume juu ya
Sheria za Ndoa, talaka na
Mirathi, iliyowekwa na Serikali ya Kenya chini ya uweneyekiti wa Mheshimiwa
Jaji Spry wa Mahakama Kuu ya Kenya.
Masharti ya Rejea
kwa ajili ya Tume ni:-
“Kufikiria Sheria
iliyopo ihusikananyo na Ndoa, Talaka na mambo yahusianayo na hayo;” “Kutoa
mapendekezo kwa ajili ya Sheria mpya itoayo uwanja mpana na, kwa kadiri
itakavyoweza kutekelezwa sheria ya Ndoa sawa kwa watu wote, na talaka itumikayo
kwa watu wote nchini Kenya, ambayo itachukuwa nafasi ya sheria iliyopo juu ya
suala lihusianalo na Sheria ya mila,
Sheria ya ki-Islamu, Sheria ya ki-baniani na
amri zinazohusika za Bunge na kutayarisha muswada wa Sheria mpya.”
“kutoa kipaumbele
mahususi kwa hadhi za wanawake kaitka kuhusiana
na ndoa na talaka katika jamii huru ya kidemokrasia”.
Tume ilituma
maswali mapema kwa pande zote zinazohusika, na Halmashauri Kuu (Supreme
Council) ikapeleka majibu yao
(yalioandikwa na Maulana Sayyid Saeed Akhtar
Rizvi) kwenye Tume kabla.
Tume ilikaa kwa
ajili ya kusikiliza mjini Mombasa kuanzia tarehe 21 Augasti 1967. Ujumbe wetu ulitokea mbele ya tume tarehe 22
Augasti. Pamoja na Muhtasari, taarifa
iliyobeba mambo mengi ya shria za ki-Islamu na mkusanyo wa hotuba juu ya
Usul-Din “Islam” zote zikiwa zimeandikwa na kukusanywa na Maulana Sayyid Saeed Akhtar Rizvi,
ziliwasilishwa mbele ya Tume.
Ni wazi kwamba
juhudi ya Maulana katika suala hili imestahiki kusifiwa mno, na sisiti kukiri
kwamba uwasilishaji ufuatao usingelifanikiwa bila muongozo na msaada wake.
Wajumbe wa
msafara walikuwa, Maulana Sayyid Saeed Akhtar Rizvi,Mulla Asgherali M. M.
Jaffer (Hon. Gen.Secretary – Mh. Katibu Mkuu),Bw. Hassan A. M. Jaffer (Mh.
Mhazina Mkuu) Maulana Sheikh Maqbool
Hussain (Mombasa) Bw. Bashir H. Pira na mimi mwenyewe.
Mh. Katibu Mkuu
wa Halmashauri Kuu ya Khoja Shia Ithna-asheri Mulla Asgheri M. M. Jaffer
aliwasilisha kama msomaji wa Shia Ithna-asheri, na alisoma wasilisho mbele ya
Tume.Vile vile alijibu maswali yaliyoulizwa na Tume, na kufafanua nukta mbali
mbali zinazohusika na Ndoa, Talaka n.k. kwa mujibu wa madhehebu ya Shia.
MOHAMEDALI MEGHJI:
Rais, Shia Ithna-ashri-Halmashauri Kuu (ya Khoja)
P. O. Box 1085, Mombasa.
*****
1.Kwa niaba ya
Jumuiya ya shia Ithna-asheri ya Kenya, tunachukuwa fursa hii ya kufanya
uwasilishaji huu kwa ajili ya kufikiriwa na Tume.
2.Katika
uwasilishaji huu, tunakomea maelezo yetu kwenye Sheria za dini zilizofungana na
Ndoa, Talaka, wosia na mirathi ya Madhehebu ya ki-Islamu ya Shia Ithna-asheri.
3.Inafahamika
kwamba matatizo ya kijamii aina mbalimbali yatokeayo kwa kutmia vibaya au
tafsiri potofu za mila, desturi au sheria za dini katika utekelezaji wa jumla,
hutoa sababu kwa uwajibikaji wa makini kwa Serikali, na Serikali katika hamu
yake kuwapatia watu wake ustawi katika suala hilo inakabiliwa na jukumu ngumu la Serikali la kutokomeza maovu ya kijamii. Juhudi yoyote katika muelekeo huu yafaa kuungwa
mkono na hustahiki ushirikiano wote.
Lakini tunahisi kwamba wazo la kutunga Sheria ya wote kuchukua mahali pa
Sheria ya ki-Islamu iliyopo sasa sio sahihi.
Hata desturi za
kimila (zisizo na mamlaka ya kidini) ni ngumu kubadilisha. Hii
huwa hatari mno zaidi katika suala kama la Sheria ya ki-Islamu ambayo ni sehemu muhimu
ya dini yetu, ambayo haikomei kwenye
ibada tu. Sheria hizi haziwezi kuvunjwa
bila ya kupata hisia ya hatia na dhambi.
Kwa hiyo,
tunahisi kwamba njia nzuri “itakuwa kuacha mamia ya maua kuchanua.” Umoja wa Kitaifa hauhitaji kwamba raia
wote yawapasa kuwa na lahaja inayofanana
au imani ya dini inayofanana. Hivyo kwa
nini inafikiriwa kwamba ni muhimu kuwa na Sheria ya Ndoa inayofanana na talaka
ya kutumika kwa watu wote wa Kenya.
4.Sheria zetu za
Shia Ithna-asheri hazikutegemezwa juu ya “Rai” (maoni) au “Qiyas”
(anolojia). Zimetegemea kabisa
juu ya Qur’an Tukufu na Hadith za
Mtukufu Mtume na Maimamu wetu Kumi na Mbili.
Kwa vile tume
inahusika na mambo ya Ndoa na Mirathi, lazima
tuonyeshe kwamba kanuni za msingi na mambo mengi namna kwa namna ya mirathi yanaelezwa katika Qur’an
Tukufu. Kusema kweli, maudhui hii
imeshughulikiwa zaidi kwa ukamilifu katika Kitabu Kitukufu. Hali kadhalika, kanuni za msingi za ndoa na
talaka zimetegemezwa juu ya Qur’an Tukufu.
Mambo ambayo
hayako wazi katika Qur’an Tukufu yanaelezwa katika Hadithi kama ilivyotajwa
hapo juu.
Wanachuoni wetu
ambao wanaitwa MUJTAHID hawatoi hukumu yoyote kwa maoni yao, analojia (Qiyas)
au (kwa) ijimai. Hakuna mamlaka kama
hayo yaliyotolewa kwa yeyote katika Sheria ya madhehebu yetu. Wanaweza kutofautiana katika kutafsiri Hadith
fulani zinazohusu baadhi ya mambo madogo, lakini hata hivyo tofauti hiyo ni
tofauti katika tafsir, sio ya maoni.
Madhehebu ya Shia
Ithna-ashri hufuata katika mambo yote ya dini hukumu za Mujtahid mkubwa wa
zama. Anachukuliwa kuwa yeye ni mwakilishi wa Imamu wetu wa Kumi
na Mbili na ni mtu wa mwisho juu ya mambo
yote ya dini. Kwake yeye amekabidhiwa katika masuala fulani, mamlaka za
ulezi wa watoto, ulinzi katika ndoa na talaka, utekelezaji wa Wosia na mali ya
marehemu na mambo kama hayo.
5.Sheria ya
ki-Islamu ya madhehebu ya Shia Ithna-asheri ni chombokilichofumwa vizuri.
Hatuwezi kubadilisha au kurekebisha, moja au mbili ya mambo yake bila kuharibu
ufumaji wote.
[1] Hukumu za Ndoa na Talaka zinabeba uzito
wa moja kwa moja juu ya uhalali au vinginevyo wa mtoto; juu ya wema au dhambi
ya pamoja ya mwanaume na mwanamke; katika haki ya wao wenyewe kwa wenyewe ya
mirathi na ile ya mtoto; mbali na kutokana na jamii na shida za kisheria.
[2] Katika sheria za ki-Islamu mtu hawezi
kutumia kitu chochote kilichopatikana kiharamu (kwa maana ya kidini) amma kwa
kilimwengu au kwa madhumuni ya kidini.
Kwa hiyo, kama mabadiliko yanafanywa katika sheria za mirathi na mtu
fulani anapewa zaidi kuliko mgao wake kwa mujibu wa Qur’an Tukufu, maisha yake
yote yatakuwa duni. Maisha yake ya kila siku yatakuwa ni orodha
ndefu ya kuchupa mipaka, Sala zake, Hija, chakula na mavazi vitakuwa haramu katika
maana ya kidini.
Hivyo ni wazi
kwamba mfumo wa Sheria ya ndoa, talaka na mirathi hauwezi kubadilishwa;
vinginevyo hii itaanzisha muingilio wa moja kwa moja katika dini yetu.
6.Kuhusu hamu
ya Tume “Kutoa kipaumbele kwa hadhi ya wanawake katika kuhusiana na Ndoa na
Talaka katika jamii huru ya kidemokrasia”.
Tunataka kuwakilisha kama
ifuatavyo:-
(a) katika sheira ya madhehebu yetu mwanamke
anazo haki hizo upendeleo na ulinzi wa salama tangia Karne ya Kumi na nne,
nyingi ya hizo hazikufikiriwa katika Jamii zisizo za ki-Islamu mpaka Karne
iliyopita na baadhi ya hizo ziko mbele ya inayoitwa zama ya kisasa.
(b) Uislamu kwa mujibu wa madhehebu ya Shia,
umempa mwanamke haki ya kufanya mkataba yeye mwenyewe katika Ndoa kama ni mtu
mzima na makanifu.
(c)
Uislamu umempa mwanamke kitambulisho cha
kujitegemea. Mwanamke wa ki-Islamu anamiliki mali yake
mwenyewe hata baada ya kuolewa, na mume hawezi kuingilia.
(d) Mwanamke anaweza kumfungulia mume wake
mashtaka, anawezakutoa ushahidi dhidi yake.
Anarithi kutoka kwa mume kwa haki na mwanaume kutoka kwa mwanamke.
Haki hii, ya wote
pamoja ya mirathi (kurithiana) ilitolewa wakati hakuna jamii kamwe ilifikiria
kuhusu haki hii.
7.Mgao wa
mwanamke kwa kawaida ni, nusu ya ule (mgao) wa mwanaume. Lakini hii ni mantiki
kabisa. Uislamu umemfanya mwanaume kuwa
na jukumu la kutunza familia. Hakuna
mzigo kama huo uliowekwa juu ya mwanamke. Hata mke tajiri anahusika kupata matunzo yake
kutoka kwa mume wake ingawa anaweza kuwa
ni maskini. Kwa vile matunzo ya familia
ni jukumu la mwanaume, amepewa mgao marudufu karibu katika mirathi yote.
Vile vile, mwanamke hupata
mahari ambayo hutoka kwa mume kwenda kwa
mke. Kwa hiyo uwiyano wa mgao uliowekwa
katika Qur’an Tukufu ni wa haki zaidi.
8.Sheria ya
Uislamu ihusianayo na Wosia haimruhusu mtu kuusia zaidi ya thuluthi moja ya
mali yake kamili. Hivyo hali ya kifedha
ya wale watakao kuwa warithi siku zote inalindwa na mbali ya kutwaliwa kokote
isivyo haki na yeyote. Usalama huu bado
unakosekana katika jamii nyingi ambazo huruhusu mtu kutoa mali yote kwa mgeni
haswa.
9.Sasa tunakuja
kwenye baadhi ya mambo ya Ndoa:-
(a)MITALA :
Jamii ya Waafrika ilikuwa, na kwa kiwango fulanini jamii ya
kimitala. Uislamu vilevile huruhusu
mitala. Umeruhusu wake wanne kwa wakati
mmoja na imeamuru usawa katika
kuwahudumia wake wote.
(b)Yapasa
ikumbukwe kwamba mitala sio kitu cha lazima wala sio kitu kinachotetewa. Ni ruhusa tu pamoja na ukomo Fulani na
masharti. Na katika baadhi ya mazingira
ruhusa hii imethibitisha manufaa mazuri mno.
Kwa mfano, kama
mke ana ugonjwa sugu au ni mgumba au kwa sababu nyingine fulani haiwezekani kwa
wawili hao kuishi kama mume na mke.
Suluhisho litolewalo na jamii fulani ni kumtaliki mke na kuoa mwingine. Lakini je, hii ni haki? Je, ni wema au uadilifu kumfukuza mwanamke
katika hali ya uzee au katika umri wake wakati kutoka kwenye nyumba yake, kwa
sababu ame kuwa mgonjwa siku zote au
ametokea kuwa mgumba? Uislamu hupinga ukatili huo kwa kuruhusu mitala.
10.(a) TALAKA: Hakuna haja kusisitiza kwamba katika
hali fulani talaka ndio suluhisho pekee lililobakia kwa wawili hao (mume na
mke). Manufaa ya mfumo wa talaka yanaweza kuonekana kutokana na ukweli kwamba
hata Baniani na Wakristo wengi wamelazimika kwa nguvu ya moja kwa moja isio
epukika kutnga sheria za talaka.
(b) Ni lazima
tuonyeshe kwenye wakati wa mwanzo kwamba madhehebu ya Shia-Ithanaseri ya
ki-Islamu imeweka kanuani ngumu zilizotegemea juu ya Qura’n Tukufu na Hadithi,
kuhusiana na talaka.
(c) Talaka
imetangazwa na Mtukufu Mtume kuwa ni kitu kilichotwezwa katika halali zote.
(d) Qur’an Tukufu
imeweka mfumo wa usuluhisho wakati wowote kukiwa kuna kutokuelewana kati ya
mume na mke.
(e) MASHARTI YA TALAKA: Talaka inaruhusiwa
mradi tu inatamkwa mbele ya watu wawili mashahidi. “Adil” (watu wamuelekeo thabiti) ambao
husikiliza maeneno na kuelewa asili au chanzo cha talaka. Talaka lazima itamkwe katika utaratibu
uliothibitishwa,
Zaidi ni lazima vile vile kwamba mume awe mtu
mzima, mwenye akili timamu na
mwenye kuelewa vizuri atendaye kwa utashi wa uhuru wake mwenyewe,
na sio katika mshituko wa hasira au kutishwa.
Nakwamba lazima awe na nia ya dhahiri ya kuvunja ndoa.
Kwa kadiri
mwanamke anavyohusika,yeye wakati wa Talaka lazima awe katika hali ya tohara na
kwamba talaka haiwezi kutamkwa hata wakati wa tohara ambao kwamba mume
amekutana naye kimwili.
Kama moja ya
masharti yaliyotajwa hapo juu yakivunjwa
Talaka itakuwa batili na kutenguka.
(f) Talaka tatu
haziwezi kutolewa kwa wakati mmoja. Kama
mtu atasema kwamba anatoa talaka tatu,
hata moja haitakuwa halali.
(g) Katika hali
nyingi, talaka inaweza kutenguliwa, na mume ana lazimika kumtunza mke
aliyetalikiwa wakati wa kipindi cha “Iddat” (kwa kawaida ni miezi mitatu)
katika nyumba yake; vinginevyo ahiari kutoka (mwenyewe).
(h) Wakati wa
kipindi kilichotajwa cha “IDDAT” mume
anayo haki ya kutengua talaka kwa maneno au kitendo na kutakuwa hakuna
haja ya taratibu zozote.
Kanuni hizi ngumu
zimekuwa siku zote zikitekelezwa na madhehebu yetu. Shukurani kwa Shariat yetu, talaka katika
madhehebu ya Shia-Ithanasheri ziko mara chache sana.
11.HAKI YA MWANAMKE KUHUSIANA NA UVUNJANI WA NDOA: Mwanamke hakupewa haki ya kumpa talaka mume wake. Sababu
yeneyewe sio ngumu sana kuelewa.
Familia ni msingi wa jamii ya binadamu na kwa vile kila jamii huhitaji
mamlaka ya mwisho kuiweka katika mpango ulioandaliwa vizuri. Familia lazima
vile vile ipate kiongozi mkuu. Sheria ya
ki-Islamu imetoa nafasi hiyo kwa mume,
na mume amepewa haki ya kutoa talaka.
Lakini mke ana haki ya kudai talaka katika
hali nyingi: Km:
(1) Anaweza
akaomba Khula ambayo inaweza kukubalika juu yake na mume;
(2) Anaweza
kumuomba Mujtahidi kumpa talaka katika hali ambako mume ametoweka, au akapuuza
kumtunza.
(3) Katika
hali ya mume yakuwa mwenda wazimu, imma imetokea kabla au baada ya ndoa, ana
haki ya kuifuta ndoa bila haja yoyote ya kupeleka kesi kwa Mujtahid.
(4) Na anaweza kuibatisha Ndoa baada ya
kuipeleka kesi kwa Mujtahid, kama mume ni hanithi.
12.Katika
uwasilishaji wetu, tulionyesha mapema kwamba sheria sawa kwa wote katika jamii
ya kilimwengu kama hii ya Kenya haina umuhimu kwa umoja wa kitaifa. Sasa tunaomba kuwasilisha kwamba kuishi
pamoja, kwa amani na urafiki miongoni mwa watu walioambatanishwa kwenye imani
za dini mbalimbali na sheria kunaweza kupatikana tu kama uhuru utatolewa kwao
kutekeleza sheria kama hizi, na kutenda
kimujibu (kama itakikanavyo).
Haitakuwa nje ya
sehemu (ya maudhui) kutaja hapa kwamba
Uislamu una seti ya theolojia inayojumuisha mambo yote ya maisha. Na kwamba amri zake na maelekezo hayakomei
kwenye ibada za sala za kila siku na maombi pekee. Ni mfumo wa maisha ambao hutoa huduma ya
mipangilio namna namna kwa jaamii, ndoa, maadili, na hali kadhalika uendeshaji
wa biashara katika maisha ya kibinadamu.
Pengine itakuwa
ni kitu cha kuvutia kwamba hivi karibuni Tanzania imechapisha “Taarifa ya
sheria ya ki-Islamu. “ Huu ni utungaji mdogo wa Sheria chini ya “Taarifa mpya
ya shria ya ki-Islamu” (No. 56 ya 1964).
Nyongeza ya Gazeti (la Srikali)
No. 34 ya 27 Juni, 1967 yahusika. Hatua hii iliyokuja wakati mzuri katika
Tanzania imethibitisha kwamba nchi yoyote inayopigania uhuru wa kuabudu na
utekelezaji wa dini inaweza kwa usalama kuweka sheria mbali mbali kuhusiana na
Ndoa, Talaka, Mirathi au mambo yoyote kama hayo. Vile vile huonyesha kwamba hatua kama hiyo
inatekelezeka. Tunaweza kuongeza kwamba
vile vile hudokeza kwamba mpangilio kama huo unasaidia kwenye kuelewa vizuri na
uhusiano katika nchi ambako mazingira ya
maridhia yanatakiwa yafanyike, na
tunaweka mikononi mwa tume kupendekeza hatua kama hiyo nchini Kenya.
13.Kujaribu
kuweka mpaka kati ya Qur’an Tukufu na Sheria ya ki-Islamu kamwe hakuwezi
kufikirika. Jaribio lolote la kuvuruga
au katika maneno ya masharti ya rejea ya Tume, “Kubadilisha Sheria ya
ki-Islamu” kutakuwa hakukubaliki. Kama
ilivyoelezwa hapo juu, sheria ya ki-Islamu imetegemezwa juu ya Qur’an Tukufu
na kubadilisha Sheria ya Kiislamu ni
sawa sawa na kubadilisha Qur’an Tukufu.
14.Tumewasilisha maswali yaliyotumwa na Tume yakiwa
yamekamilishwa ipasavyo sambamba pamoja na mpangilio wa sheria ya ki-Islamu
(katika Kiingereza) kwa mujibu wa Sheria ya Madhehebu ya Shia kuhusiana na
Ndoa, uvunjaji wa Ndoa, Wosia, Mirathi, Makubaliano na Wakf; na tutafurahi
kujibu maswali yoyote yajitokezayo kutoka humo na kuwasilisha ufafanuzi
utakiwao.
MOMBASA, 22 AGOSTI 1967.
2
MUHTASARI
JUU YA SHERIA ZA MIRATHI:*
ANGALIA: Tuna furaha kufunga pamoja
na huu muhtasari uliowasilishwa kwenye tume juu ya sheria ya mirathi
iliyoteuliwa hivi karibuni na Serikali ya Kenya. Masharti ya rejea yakiwa, kufirikiria sheria zilizopo sasa
zinazohusu ndoa, talaka na mambo yanayohusika pamoja na hayo na kupendekeza
Sheria inayofanana ya kutumika kwa watu wote wa Kenya ikitoa kipaumbela kwenye
hadhi ya wanawake kuhusiana na ndoa na talaka katika jamii huru ya kidemokrasia.
Sekritariati hii
ina wiwa na Maulana Sayyid Saeed Akhtar Rizvi mwanachuo mkazi wa Dar es
Salaam, Muasisi na Mhubiri Mkuu, wa Bilal Muslim Mission of Tanzania kwa juhudi
zake kubwa katika kuandaa muhtasari huu.
Vile vile tuna viwa na Mulla Hussein A. Rahim M. B. E. wa Zanzibar, kwa
muongozo wake wenye thamani.
Tunaomba Allah (
S.A.W.) kwamba awalipe kwa wingi hapa duniani na kesho akhera.
ASGHARALI M. M. JAFFAR,
Mh. Katibu Mkuu,
Halmashauri Kuu K. S.
Ithna-Asheri
P. O. Box 1085, MOMBASA
*****
1. Kwa niaba ya
Jumuiya ya Shia Ithna-Asheri ya Kenya tunaomba ruhusa ya kutoa uwasilishaji huu
kw aajili ya kufikiriwa na Tume.
2. Maelezo yetu
yanakomea kwenye Sheria za dini zinazohusika na wosia na Mirathi kwa mujibu wa
madhehebu ya ki-Islamu ya Shia
Ithna-Asheri, isipokuwa ambako palipokuwa na maana kutoa maoni ya madhehebu
nyingine ili kuifanya nukta yetu kuwa wazi.
3. Tayari
tumewasilisha maswali yaliyotumwa na Tume yakiwa yamekamilishwa ipasavyo pamoja
na mpangilio wa sheria za ki-Islamu (kwa Kiingerza) kwa mujibu wa Sheria ya
Madhehebu ya ki-Islamu ya Shia Ithna-Asheri ihusianayo na Mirathi na Wosia
miongoni mwa mambo mengine. Katika wasilisho hili tutajitahidi kueleza
kanuni za msingi chini ya hukumu hizo.
4. Tunaelewa
kwamba tume hii itatoa kipaumbele kwenye hadhi ya wanawake. Tunajasiri kutumaini kwamba Sheria ya
ki-Islamu inayotajwa kwa mujibu wa madhehebu ya Shia, itakuwa ya msaada mkubwa
kwa Tume katika kazi yake juu ya suala hili.
Haitakuwa nje ya
sehemu (ya maudhui) kutaja kwamba mila ya ki-Arabu ya zamani ilikuwa na lengo
moja la msingi katika mtizamo, yaani, uzuiaji wa kudumu wa mali katika familia.
Pamoja na lengo hili katika mtizamo, urithi ulikomea kwa ndugu wa kiume pekee
tu, na hata miongoni mwao ni kwa wale tu ambao walikuwa na uwezo wa kubeba
silaha.
Hatukusudii
kushughulika sana juu ya nukta hii; itoshe tu kusema kwamba tabia kama hii,
zaidi au kidogo ilikuwepo katika jamii zote katika wakati huo na imebakia
katika jamii nyingi mpaka sasa. Uislamu
ulitoa kwa kudhihirisha uwekaji wa sheria ya haki ya kurithi kwa wale ambao
walienguliwa na taasisi za zamani. Moja
ya matokeo ya faida ya sheria mpya ya Mungu ilikuwa kunyanyua hadhi ya wanawake
katika mizani ya ustaarabu, kwa kunyanyua uchumi wao na nafasi ya kijamii, na
kuwapa wajane, mama, mabinti na dada na ndugu wengine wa kike haki ya kurithi.
5. Moyo huu
umehifadhiwa katika Sheria ya madhehebu ya Shia ambayo, kwa kunukuu maneno ya
mwanachuoni mkubwa Sayyed Amir Ali, “Ni ya wepesi mkubwa mno na haihusishi mjadala
wowote kuhusiana na haki za ndugu wa kiume na wa kike - “Asabah na Zav-il-Arham”.
Kisha aliendelea kusema kwamba “Tofauti kubwa, kusema kweli, kati ya Shia na
Sheria ya mirathi ya Sunni iko katika suala la jinsia ya Kuumeni. Shia wanakataa kwa kupinga itikadi ya Taasib au jinsia ya Kuumeni; hatimaye
uhusiano wa Kuumeni wa jinsia ya kiume, au inayoitwa “Asbah Sahihi” katika
fikihi ya Sunni (Sheria ya Sunni), hawana upendeleo maalum wala hawafadilishwi
kwenye kuunganisha mahusiano na marehemu kupitia wanawake. Kwa mfano, Shia
wanaona ni kinyume cha uadilifu kuwatoa watoto wa binti kwa kupendela kizazi
cha mbali cha kaka, kwa msingi wa kubunia kwa kuwa kwao kuungana na marehemu
kupitia mahusiano ya kuumeni. (Mohameden
Law, by Ameer Ali Vo. 2; P. 128).
Kwa mfano:
(a) Kama Muislamu
Sunni akifa akiacha nyuma yake binti wa binti yake pamoja na mtoto wa kiume wa
kaka yake, mtoto wa kiume wa kaka yake atachukuwa urithi wote kama ASABAH
(ndugu wa kuumeni wa jinsia ya kiume).
Kwakumuondoa mjukuu mwenyewe wa marehemu. Chini ya Sheria ya Shia Inthna-Asheri, mjukuu
wa kike (anayezaliwa na binti yake) wa marehemu, kama mtoto kwa nasaba,
huchukuwa mali yote kwa kumuondoa mtoto wa kiume wa kaka yake.
(b) Kama Muislamu
Sunni akifa, akiacha nyuma binti na kaka, binti huchukuwa mgao ulioainishwa,
yaani moja kwa mbili za mwanaume na inayobakia huenda kwa kaka kama Asabah.
Chini ya Sheria ya Shia Ithna-Asheri, huchukuwa mali yote, nusu kama kiainisho
cha mgao wake, na nusu nyingine kwa itikadi ya kurudisha.
6. Kanuni zinazoongoza
zinaweza kuelezwa kwa ufupi katika maneno yafuatayo:-
(a) Mrithi mwenye
uhusiano wa karibu na marehemu hurithi kwa kumfadhilisha zaidi kuliko yule
mwenye kufungamana naye kwa mbali;
(b) Yeyote yule
anayehusiana na marehemu kupitia mtu yeyote harithi wakati mtu yule anaishi;
(c) Kaka na dada
wa kuzaliwa mama mmoja, baba mmoja wanapendelewa kuliko kaka na dada wa
kinasaba; lakini kaka na dada wa tumbo mmoja watarithi pamoja nao.
(d) Wakati uhusiano ni sawa, mwanamume kwa
kawaida hupata marudufu ya mgao wa mwanamke, isipokuwa katika hali ya warithi
wanaohusiana kwa mama ambao kwa ujumla hugawanya urithi miongoni mwao kwa sawa
sawa bila tofauti ya jinsia.
Inaweza ikaulizwa
kwa nini mgao wa mwanamke, kwa kawaida ni nusu ya ule wa mwanaume? Kusema kweli, ni yenye mantiki kabisa.
Uislamu umemfanya mwanaume kuwajibika kwa ajili ya matunzo ya familia. Hakuna mzigo kama huo uliowekwa juu ya
mwanamke. Hata mke tajiri anapasika
kupata matunzo yake kutoka kwa mume wake ingawa anaweza akawa masikini. Kwa vile anatakiwa kubeba gharama zote,
amepewa mgao marudufu karibu katika kila mirthi. Vile vile mwanamke hupata mahari ambayo
hutoka kwa mwanaume kwenda kwa mwanamke.
Hivyo uwiyano wa migao uliowekwa na Qur’an Tukufu ni wa haki zaidi.
7. MAKUNDI NA TABAKA ZA WARITHI:
Katika Shriat za
Shia Ithna-Ahsri, warithi wamegawanywa katika makundi mawili, yaani, wale ambao
hurithi kwa haki ya “Nasab” (nasaba); na wale ambao wanarithi kwa haki ya ‘Sabab’
ambao kwamba muhimu ni wa ndoa (kuoana).
Makundi yote hurithi kwa pamoja.
Kundi la kwanza
yaani mahusiano ambayo yanapasika kurithi kwa sababu ya unasaba limegawanyika
katika tabaka tatu:-
(a) Tabaka la Kwanza:
(i) Wazazi na (ii) Watoto (au katika kukosekana
kwao, wajukuu-wowote kwenda chini-yaani: kilembwe, kitukuu na kuendelea).
(b)
Tabaka
la Pili:
Kama hakuna
mrithi kabisa katika tabaka la kwanza, basi wazazi na dhuria wa wazazi wa
marehemu watarithi: Ina maana:
(i) Babu zake marehemu (wowote kwenda juu).
(ii) Kaka na Dada
(au katika kukosekana kwao-dhuria wa kaka na dada).
(c) Tabaka
la Tatu:
Kama hakuna
mrithi aliyepo si katika tabaka la kwanza au la pili, basi dhuria wa mababu
(wowote kwenda juu) watarithi. Ina
maana: ndugu wa upande wa kiume na
upande wa kike wa marehemu, ami, wajomba na shangazi wa marehemu (au
katika kukosekana kwao, basi watoto wao
kwenda chini).
Kama ilivyoelezwa
hapo juu mume au mke au wakeze marehemu watarithi pamoja na tabaka zote hizi.
8. Dhul – Fardh na Dhul Qarabat:
Ni muhimu kutaja
kwamba, chini ya sheria ya Shia, warithi katika kundi au tabaka lolote
watakalokuwa wamegawanywa katika mafungu matatu, kuhusiana na haki ambayo
wanapasika wao kushiriki katika mirathi:-
(1) DHUL-FARDH: wale ambao wana haki kwenye
mgao ulioainishwa katika mirathi ni hawa:
(a) Mama
(b) Mume
(c) Mjane au
Wajane
(d) Mtu au watu
wanaohusiana kwa mama yuleyule tu.
(2) DHUL-QARABAT: Wale ambao huchukuwa
urithi kwa sababu ya uhusiano wao na marehemu, lakini ambao mgao wao hushuka na
kupanda kwa kutegemea idadi ya warithi na mazingira. Hawa ni:-
(a) Mtoto au
watoto wa kiume
(b) Kaka kamili
au katika kutokuwepo kwao ndugu kwa upande wa baba (mama mbali mbali)
(c) Mababu
(d) Ami na
Shangazi
(e) Wajomba na
mama wadogo.
(3) DHUL – FARDH WAL-QARABAT; Hawa ni
warithi ambao wakati mwingine hurithi kwa sababu ya uhusiano wao na wakati
mwingine hutegemea migao yao iliyopangwa; hawa ni:
(a) Baba ambaye hurithi mgao uliopangwa kama
kuna mtoto wa marehemu; na huchukuwa kwa uhusiano kama hakuna mtoto wa
marehemu.
(b) Binti au Mabinti ambao hupata mgao wao
uliopangwa bila kuwepo baba wa marehemu au kaka yake au kaka zao wenyewe; na
wanachukua kwa ushusiano wakati wakiwa pamoja na yeyote kati yao.
(c) Dada kamili
au dadaze au katika kutokuwepo kwao, dada wa nasaba au dadaze, ambao hupata
mgao uliopangwa wakati bila kuwepo babu au kaka, kakaze wa daraja moja kama wao
wenyewe, na huchukuwa kwa uhusiano wakati wakiwa pamoja na yeyote kati yao.
Angalia : Wakati kukiwa na mrithi
mmoja tu, imma Dhul-Fardh au Dhul-Qarabat, au mwenye kupasika kwa sababu ya
uhusiano maalum wa Sabab (kuoana-ndoa), mrithi kama huyo huchukuwa mirathi
yote. Kwa mfano, binti pekee huchukua
mgao wake uliopangwa, yaani, nusu moja na iliyobakia huenda kwake kwa
kurudisha. Mtoto wa kiume pekee huchukua
mali yote kwa haki ya Qarabat, hakuna mgao ulioainishwa uliowekwa kwake kwa
Sheria. Wakati marehemu ni mwanamke na
hakuacha nyuma yake jamaa anayehusiana na yeye isipokuwa mume, ambaye anahusika
na kurithi kwa sababau ya ndoa, anachukuwa urithi wote kwanza kama mgao wake
ulioainishwa, na uliobakia kwa kurudisha.
9. MIGAO: Kwa kadiri migao inavyohusika iko sita kwa idadi, yaani:-
(1)
Nusu
moja (2) Moja ya nne (3) Moja ya Nane
(4) Moja ya tatu
(5) Mbili ya tatu (6) Moja ya sita.
(1)
NUSU
MOJA : Wafuatao wanapasika kwenye nusu moja ya urithi:
(a)
Mume wakati mke hakuacha mtoto;
(b)
Binti wakati hakuna mtoto wa kiume;
(c)
Dada kamili kwa kukosekana warithi wengine
ambao wametajwa mapema;
(d)
Dada wa nasaba wakati hakuna kaka na dada
kamili.
(2)
MOJA
YA NNE : Wafuatao
wanahusika kwenye moja ya nne:
(a)
Mume, wakati kuna nasaba ya dhuria ya mke;
(b)
Mke, wakati hakuna nasaba ya dhuria ya mume;
(3)
MOJA
YA NANE : Hii huchukuliwa na mjane au wajane wakati kuna
nasaba ya dhuria ya mume.
(4)
MOJA
YA TATU : Wafuatato wanapasika kwenye moja ya tatu:-
(a)
Mama, wakati hakuna nasaba ya dhuria ya
marehemu, wala hakuacha kaka wawili, au dada wanne au kaka mmoja na dada
wawili.
(b)
Kaka na dada tumbo moja, wakati wakiwa wawili
au zaidi katika idadi.
(5)
MBILI
YA TATU : Wafuatao wanapasika kwenye mbili ya tatu:
(a)
Mabinti wawili au zaidi, wakati hakuna mtoto
wa kiume;
(b)
Dada kamili wawili au zaidi wakati hakuna
kaka kamili au hakuna kakaze (baba mmoja mama mabali mbali).
(6) MOJA YA SITA : Moja ya Sita inachukuliwa na wafuatao:
(a)
Wote baba na mama wakati marehemu ameacha
nasaba ya dhuria.
(b)
Mama, wakati wanakuwepo pamoja naye kaka
wawili au zaidi wa damu kamili au kaka mmoja na dada wawili au dada wanne wa
damu kamili (au kwa baba yule tu, baba yule akiwa yupo).
(c)
Kaka mmoja au dada wa tumbo moja.
10. MGAWANYO WA MALI: Wakati kuna mmoja
tu wa warithi waliotajwa hapo juu akiwa
mwanaume au mwanamke hupata mali yote.
Kama ni Dhul-Qarabat, huipata kwa sababu ya uhusiano; kama ni
Dhul-Fardh, kwanza anapata mgao wake uliopangwa, na kisha mabaki anapewa yeye
kama kurudisha (Radd).
Kama wako warithi
wawili au zaidi, itagawanywa katika utaratibu ufuatao: Kwanza mume; au mke au
wake watachukuwa mgao wao; kisha ndugu
Dhul – Fardh watapata mgao wao; kisha mabaki yatagawanywa miongoni mwa warithi Dhul-Qarabat.
Mfano: Kutoa mfano wa utaratibu
wetu, ngoja nichukulie kwamba mtu anakufa anamuacha baba yake, mama,
mke, watoto wanne wa kiume, mabinti watano, wajukuu watatu, babu, kaka watatu
na shangazi wawili.
Kwa vile ameacha
wazazi na watoto wakiume na mabinti, ambao wanahusika na tabaka la kwanza la
warithi, babu na kaka (ambaowanahusika na tabaka la pili) na mashangazi (ambao
wanahusika na tabaka la tatu) wataondolewa kwenye urithi.
Hali kadhalika,
wajukuu wataondolewa kwa sababu ya kuwepo watoto, juu ya msingi wa karibu
kuwaondoa wa mbali zaidi.
Mfumo huu wa
kuondoa hutuacha na warithi wafuatao: mke, Baba, Mama, Watoto wanne wa kiume na
mabinti watano.
Mke atapata 1/8
ya mali kwa sababu marehemu ameacha watoto; Baba na Mama wote watapata kila
mmoja, moja ya sita 1/6.
Kigawanyo cha
kawaida cha 8 na 6 itakuwa 24. Hivyo mali itagawanywa katika migao 24 – ambapo
kutoka hiyo mke atapata 3 (yaani 1/8), baba 4 (yaani 1/6) na mama vile vile 4
(yaani 1/6). Itaonekana kuwa baba ameshughulikiwa hapa kama Dhul – Fardhi, sio
kama dhul – Qarabat, kwa sababu ya
watoto wa marehemu, na mama kupata mgao pungufu (yaani 1/6 badala ya 1/3) kwa
sababu ya mantiki hiyo hiyo.
Vyovyote vile,
baada ya kupunguza 3 + 4 + 4 (yaani 11/24) tumebakiwa na migao 13. Hii itagawanywa miongoni mwa watoto, mtoto wa
kiume akipata marudufu ya mgao wa binti.
Ina maana kwamba – kila mmoja wa watoto wanne wa kiume atachukuwa migao
miwili (kufanya 8) na kila mmoja wa mabinti atapata mgao mmoja (kufanya
5). Hivyo migao yote imekwisha.
11. DHUL-FARDH LAZIMA WAPATE MGAO WAO
ULIOPANGWA:
Katika mfano wa
hapo juu, migao imelingana na mahitaji ya manfungu ya mirathi. Lakini kuna weza kuwa na hali wakati migao
iliyopangwa yaweza kuzidi kigawanyo cha kawaida cha migao. Kwa mfano, kama
mwanamke ataacha mume nyuma yake mabinti wawili na mama, migao yao kwa kuhusiana
itakuwa moja ya nne, mbili ya tatu na moja ya sita. Kigawanyo cha kawaida 3, 4, na 6 ni 12,
ambacho huwakilisha migao ambayo kwayo mali itagawanywa – 3 ikiwa mgao wa mume,
8 wa mabinti na 2 wa mama. Lakini 3 + 8
+ 2 hufanya 13, sio 12.
Masunni hugawa
mali kwenye migao 13, na kuleta upungufu kwa wote. Lakini miongoni mwa Shia, Mama na mume, wao
wakiwa ni dhul-Fardh, lazima wapate mgao wao kamili, yaani 3 + 2. Na mabaki yaani 7/12 yatagawanywa sawa sawa
miongoni mwa mabinti, kwa sababu watoto vile vile ni miongoni mwa Dhul-Qarabat.
Hivyo wakati
wowote kunapokuwa na upungufu katika migao iliyopangwa, huangukia juu ya Dhul –
Qarabat, ambao migao yao hupasika na kupanda na kushuka, sio juu ya Dhul-
Fardh.
12. IMAM : Mrithi wa Marehemu asiye na mrithi:
Kama hakuna
mrithi katika tabaka yoyote na makundi yaliyotajwa hapo juu, Imam atakuwa
mrithi wake. Kwa vile Imamu wetu yuko
kwenye ghaibu kwa wakati huu, Mujtahid atapokea mali ile kwa niaba ya Imamu na
ataitumia katika utangazaji wa imani na unyanyuaji wa dini ya Jumuiya ya Shia
kwa kupendelea zaidi katika eneo lile lile alilokuwa akiishi marehemu.
Mtu ambaye hana
mrithi isipokuwa Imamu, ameruhusiwa katika Sheria ya Shia kutoa kwa wosia mali
yake yote ili mradi utoaji huo ni kwa ajili ya faida ya Shia Ithna-asheri
masikini, Ithna - asheri mayatima au Ithna-Asheri wasafiri mafukara tu.
13. KUONDOA KUTOKA MIRATHI :
Hakuna mwandishi wa wosia mwenye haki yoyote ya kumzuiya yeyote katika warithi wake kutokana na haki
yake ya mgao wa mirathi. Hata kama
anafanya wosia kuhusu suala hili, utakuwa umetenguka na batili katika
sheria. Lakini mrithi atazuiwa kutoka
kwenye mirathi kama akitokea kuwa sio Mwislamu au kwa makusudi na kwa dhulma
amemuua marehemu ambaye kwamba mali yake angerithi.
14. HATI ZA WOSIA :
Ufanyaji wa wosia
unatambuliwa na kuhimizwa na Sheria ya Ki-Islamu. Wosia unaweza ukawa wa mdomo
au katika maandishi. Mwandishi wa Wosia ameruhusiwa kurithisha mpaka theluthi
moja ya mali yake halisi. Kurithisha kokote
kunakozidi theluthi moja ni batili, vinginevyo mpaka ikubaliwe na warithi. Mpangilio ya hukumu juu ya suala hili
unatolewa katika kitabu kilicho andamana “ISALAMIC LAW-Sheria za Ki-Islamu” na
sio muhimu kueleza kwa kinaganaga hapa.
15. ULIPAJI WA MADENI NA GHARAMA KUTOKA KWENYE
MALI:
Inaweza
kuonyeshwa hapa kwamba katika hali zote, madeni ya halali yampasayo marehemu
pamoja na gharama fulani fulani lazima yapewe umuhimu wa kwanza katika ulipaji
wa urithi na migao ya warithi.
Neno “Deni”,
Maana yake madeni ya kawaida ailiyoyaingia mwenyewe au kwa niaba ya marehemu na
hujumuisha vile vile madeni ya kidini kama Zakat
(kodi ya maskini) Khumus (hutolewa
moja ya tano) Kaffara (malipo ya
kosa au fidia), Nazar (nadhiri) nk., na neno “gharama” hujumuisha wajibu wa
kupeleka wakili kwa gharama za mali ya marehemu, kutekeleza Hija Makka kama
ilikuwa wajibu juu ya marehemu na haikutekelezwa na yeye wakati wa uhai
wake. Gharama za mazishi vile vile
zinatakiwa kupewa umuhimu wakulipwa.
Baada ya kulipa
madeni yaliyotajwa na gharama na urithi ulioelekezwa na wosia wa marehemu kufikia mwisho wa
theluthi moja ya mali halisi, mabaki yatagawanywa miongoni mwa warithi.
16. Katika
kuhitimisha, tungependa kurudia tuliyoyasema mapema mbele ya Tume juu ya Sheria
ya mambo ya Ndoa. Tunahisi kwamba wazo
la kutunga Sheria ya wote kuchukua mahali
pa Sheria ya ki-Islamu iliyopo sasa sio makosa tu bali ni kufuru kwa
mtizamo wetu wa kidini. Itakuwa ni sawa
sawa na kuweka dini inayofanana juu ya wote ambapo litakuwa ni wazo lisilo na
maana. Sheria za ki – Islamu ni sehemu
ya dini yetu. Sheria hizi haziwezi kubadilishwa au kuvunjwa bila kupata hisia
ya hatia na dhambi.
17. Hukumu
zinazohusu mirathi zimewekwa kwa usahihi wa juu mno na Qur’an Tukufu na
zinaelezewa kiukamilifu kwa uwazi katika Hadithi za Mtukufu Mtume na Maimamu
kumi na mbili na hakuna shaka hata kidogo kwamba hukumu hizi ni kwa mujibu wa
kanuni pana ya undugu wa mtu ambao Uislamu unataka kuanzisha.
18. Sheria ya
ki-Islamu ya madhehebu ya Shia Ithna-Asheri ni kitu kilichofumwa vizuri. Hatuwezi kubadilisha au kurekebisha moja au
mambo yake mawili bila kuharibu ufumaji mzima.
Kwa mfano, katika Sheria ya Ki-Islamu mtu hawezi kutumia kitu chochote
kilichopatikana kiharamu (katika maana ya kidini) amma kwa kidunia au kwa
madhumuni ya kidini. Kama kwa mfano
mabadiliko yanafanywa katika sheria ya mirathi, mtu fulani kwa maana hiyo
kikawaida atapata zaidi kuliko haki ya mgao aliogawiwa na Qur’an Tukufu na pato
hili la haramu litafanya maisha yake yote kuwa duni. Maisha yake ya kila siku yatakuwa ni orodha
ndefu ya kuchupa mipaka; Sala zake, Hija yake, hata chakula chake na mavazi
vitakuwa haramu, katika maana ya dini.
Hivyo hawezi kutegemea amani katika maisha ya kesho akhera.
3
MUHTASARI JUU YA WARAKA WA TANZANIA
JUU YA SHERIA YA NDOA INAYOFANANA
(SAWA) KWA WOTE*
ANGALIA: Muhtasari huu kwa
kutoepukika imeunganisha baadhi ya ibara kutoka kwenye Muhtasari uliowasilishwa
kwenye Tume ya Serikali ya Kenya.
*****
Kwa niaba ya
Jumuiya ya Shia Ithna-Asheri ya Tanzania, tunachukuwa fursa hii ya kuwaslisha
maoni yafuatayo kwa mapendekezo ya Serikali juu ya shria inayofanana kwa wote
ya Ndoa (Waraka wa Serikali Na. 1 wa mwaka 1969).
Madhumuni
yaliyodaiwa na mapendekezo haya ni kuondoa hali iliyopo ambayo kwayo “Sheria
zilizopo hazitambui Ndoa zote zilizofungwa chini ya Sheria tofauti kama
zinazolingana sawa”.
Lakini je, ni
lazima kwa madhumuni haya kutunga sheria ya ndoa inayofanana kwa wote? Je, suala hili haliwezi kufikiwa kirahisi kwa
kuleta pamoja Ndoa zote chini ya mamlaka ya kisheria ya mahakama moja chini ya
rejesta moja?
Katika mwaka wa
1964 “Taarifa mpya ya Sheria za ki-Islamu” ilipitishwa inayosema kwamba hukumu
za sheria za ki-Islamu za Ndoa ziwekwe katika mpango ulio wazi. Sheria ndogo chini ya amri hiyo ilichapishwa
kama nyongeza ya Gazeti Na. 34 la 27 Juni 1967.
Hii ndio ilikuwa iwe ni awamu ya kwanza.
Tunashangaa kwa
nini sera hii haikuweza kuendelezwa, au
angalau kupanuliwa kujumlisha tofauti za sheria za ndoa za kimila hali
kadhalika na za ki-Baniani na za Kikiristo.
Sheria hizi zingeweza kupangiwa kanuni na kuwekwa chini ya mamlaka ya
kisheria ya Mahakama moja.
Hapo, na hapo tu,
sura yenye mambo mengi ingeweza kuongezwa kushughulikia migongano ya sheria;
(ni) baadhi ya mifano ambayo kwamba imetolewa katika Waraka wa Serikali.
Tunatambua kwamba
matatizo mabalimbali ya jamii yanayojitokeza ya matumizi mabaya au tafsiri
potofu za sheria za kimila au zakidini kwa ujumla hutoa sabau kwa Serikali
kuhusika kwa makini. Serikali katika
juhudi za kuwapatia watu wake ustawi katika suala hilo, inakabiliwa na jukumu la kutokomeza maovu ya kijamii.
Juhudi yoyote
katika muelekeo huu yafaa kuungwa mkono na kustahiki ushirikiano wote. Lakini tunahisi kwamba wazo la kutunga Sheria
ya wote kuchukuwa mahali pa taarifa mpya ya shria ya Ki-Islamu sio sahihi.
Hata desturi
zakimila (zisizo na mamlaka ya ki-Mungu) ni ngumu kubadilisha. Hii huwa hatari mno zaidi katika suala la
sheria ya ki-Islamu ambayo ni sehemu muhimu ya dini yetu. Sheria hizi haziwezi kuvunjwa bila kupata
hisia ya hatia na dhambi.
Kwa hiyo tunahisi
kwamba njia nzuri ingelikuwa “kuacha
mamia ya maua kuchanua.” Umoja wa kitaifa hauhitaji kwamba raia wote
lazima wawe na lahaja inayofanana au imani ya dini inayofanana. Hivyo kwa nini inafikiriwa kwamba ni muhimu kuwa na Sheria ya Ndoa na Talaka
inayofanana ya kutumika kwa watu wote wa Tanzania?
Sheria zetu za
Shia Ithna-Asheri hazikutegemezwa juu ya “Ra’i (maoni) au “Qiyas”
(analojia). Zimetegemezwa kabisa juu ya
Qur’an Tukufu na Hdithi za Mtukufu Mtume na Maimamu wetu Kumi na Mbili.
Kwa vile waraka
unahusika na mambo ya Ndoa, lazima tuonyeshe kwamba kanuni zetu za msingi za
Ndoa na Talaka zimetegemezwa juu ya Qur’an
Tukufu. Mambo ambayo hayako wazi
katika Qur’an yanaelezwa katika Hadithi.
Wanachuoni wetu
ambao wanaitwa MUJTAHID hawatoi hukumu yoyote kwa maoni yao, analojia
(Qiyas) au (kwa) ijimai. Hakuna mamlaka
kama hayo yaliyotolewa kw ayoyote katika sheria ya madhehebu yetu. Wanaweza
kutofautiana katika kutafsiri Hadithi fulani zinazohusu baadhi ya mambo
madogo, lakini hata hivyo tofauti hiyo ni tofauti katika tafsir, sio ya maoni.
Shia Ithan-Asheri
hufuata katika mambo yote ya dini hukumu za Mujtahid mkubwa wa zama. Anachukuliwa kuwa yeye ni muwakilishi wa
Imamu wetu wa kumi na mbili na ni mtu (mwanachuoni) wa mwisho juu ya mambo yote
ya kidini.
Kwake yeye
mumewekwa ndani yake masuala fulani, uwezo wa ulezi wa watoto, ndoa na talaka,
utekelezaji wa wosia na mali ya marehemu na mambo kama hayo.
Sheria ya
ki-Islamu ya madhehebu ya Shia Ithna-Asheri ni chombo kilichofumwa vizuri. Hatuwezi kubadilisha au kurekebisha moja au
mbili ya mambo yake bila kuharibu ufumaji wote.
Kwa mfano, hukumu
za ndoa na talaka zinabeba uzito wa moja kwa moja juu ya uhalali wa mtoto; juu
ya dhambi ya pamoja ya mwanaume na mwanamke katika haki ya wao kwa wao wenyewe
ya mirathi na ile ya mtoto. Mbali na mambo mengine ya jamii na matatizo halai.
Katika sheria ya
ki-Islamu mtu hawezi kutumia kitu chochote kilichopatikana kiharamu (kwa maana
ya kidini) amma kwa kidunia au kwa madhumuni ya kidini. Kwa hiyo, kama mabadiliko yanafanywa katika
sheria za mirathi, kwa mfano, mtu fulani anapewa zaidi kuliko haki ya mgao wake kwa mujibu wa Qur’an Tukufu
maisha yake yote yatakuwa duni. Maisha
yake ya kila siku yatakuwa ni orodha ndefu ya kuchupa mipaka, Sala zake, Hija,
chakula na mavazi vitakuwa haramu katika maana ya dini.
Hivyo ni wazi
kwamba mfumo wa Sheria ya ndoa, talaka na mirathi hauwezi kubadilishwa. Vinginevyo hii itaanzisha muingilio wa moja
kwa moja katika dini yetu.
Kuhusu haki ya
mwanamke katika sheria ya ki-Islamu tunataka kuwakilisha kwamba:
Katika sheria ya
madhehebu yetu mwanamke anazo haki hizo, upendeleo na ulinzi kwa muda wa Karne
Kumi na Nne zilizopita, nyingi ya hizo hazikufikiriwa katika jamii zisizo za
ki-Islamu mpaka kwenye Karne iliyopita na baadhi ya hizo mbele ya inayoitwa
zama ya kisasa.
Uislamu kwa
mujibu wa madhehebu ya Shia umempa mwanamke haki ya kufanya mkataba yeye
mwenyewe katika ndoa kama ni mtu mzima na makanifu.
Uislamu umempa
Mwanamke kitambulisho cha kujitengemea.
Mwanamke wa ki-Islamu anamiliki mali yake mwenyewe hata baada ya
kuolewa, na mume hawezi kuiingilia.
Mwanamke anaweza
kumfungulia mume wake mashitaka, anaweza kutoa ushahidi dhidi yake. Anarithi kutoka kwa mume kwa haki na mwanaume
kutoka kwa mwanamke. Haki hii ya wote
pamoja ya mirathi (kurithiana) ilitolewa wakati hakuna jamii kamwe ilifikiria
kuhusu haki hii.
Mgao wa mwanamke
kwa kawaida ni nusu ya ule (mgao) wa mwanaume.
Lakini hii ni mantiki kabisa.
Uislamu umemfanya mwanaume kuwa na jukumu la kutunza familia. Hakuna mzigo kama huo uliowekwa juu ya
mwanamke.
Hata mke tajiri
anahusika kupata matunzo yake kutoka kwa mume wake ingawa anaweza kuwa ni
masikini. Kwa vile matunzo ya familia ni
jukumu la mwanaume, amepewa ngao marudufu karibu katika mirathi yote.
Mwanamke hupata
Mahr (sio bei ya kuziba pengo ambalo ni geni kwenye fikira za Ki-Islam) ambayo
hutoka kwa mwanaume kwenda kwa mwanamke.
Uwiyano wa mgao uliowekwa katika Qura’an Tukufu kwa hiyo ni wa haki zaidi.
Sheria ya Uislamu
ihusikanayo na Wosia hairuhusu mtu kuusia zaidi ya thuluthi moja ya mali yake
kamili. Hivyo hali ya kifedha ya wale
watakaokuwa warithi (pamoja) na mke siku zote inalindwa na kutwaliwa isivyo
haki na yeyote. Usalama huo bado unakosekana katika jamii nyingi ambazo
huruhusu mtu kutoa mali yake yote hata
kwa mgeni.
Sasa tukija
kwenye waraka wa Serikali wenyewe, kuna pendekezo moja ambalo katika mfumo wake uliopo, hukata ndani kabisa kwenye
mzizi wa dini zote. Ni ule ushauri wa
kwamba, “kama mwanaume ana kaa na mke kinyumba kwa muda wa zaidi ya miaka
miwili basi atachukuliwa kwamba amemoa mwanamke huyo, na kama wamepata watoto,
(basi) watoto hao watachukuliwa kuwa watoto halali wa mume na mke huyo.”
Kama nia ni kutoa
usalama kwa mke halisi ambaye Ndoa yake haikusajiliwa au ambaye Cheti chake cha
Ndoa kilipotea, neno kinyumba halileti maana.
Itapaswa
libadilishwe kwa (maneno), “Kuishi pamoja kama mume na mke katika mazingira ya
kifamilia, mradi inawezekana kwa wao kuoana na mmoja wao akadai ndoa ambayo
haikukataliwa na mwingine; au katika hali ya kifo cha mmojawapo, kwa kawaida
inajulikana kwamba walikuwa wameoana na haithibitishwi kwamba hakukuwa na ndoa
kabisa.”
Vile vile,
tulitaja mapema, katika Uislamu mke hana wajibu wa kumtunza mume. Hivyo, makusudio ya Waraka kumfanya mke
apasike kumtunza mume wake inakwenda kinyume kabisa na mamrisho ya Qur’an
Tukufu.
Kwa vile mjadala
unaendelea juu ya suala la mitala, ni muhimu kuthibitisha tena kwamba
tumeridhishwa vya kutosha na hali yenye kutaka kwa hakika umuhimu wa mitala
katika hali nyingi. Jamii ya ki-Afrika, kama Waraka kwa usahihi
unavyothibitisha, ni jamii ya ki-Mitala.
Uislamu unakubaliana nao. Lakini
Uislamu umeweka mpaka kwa wake wanne kwa wakati mmoja na umeamrisha, kwa
taratibu makhsusi, usawa katika huduma na haki ya wake wote kama waraka
unavyotaka iwe.
Inapasa ikumbukwe
kwamba mitala sio kitu cha lazima wala hakitetewi. Ni ruhusa tu yenye mipaka fulani na
mashariti. Na katika baadhi ya mazingira
ruhusa hii imeonyesha kuwa yenye manufaa mno.
Kwa mfano: kama
mke ana ugonjwa sugu, au mgumba au kwa sababu nyingine fulani haiwezekani kwa
wawili hawo kuishi kama mume na mke.
Suluhisho litolewalo na jamii fulani ni kumtaliki mke na kuoa mwingine. Lakini, je ni haki? Je, ni wema au uadilifu kumfukuza mwanamke
katika hali ya uzee, katika umri wake wa kati kutoka kwenye nyumba yake, kwa
sababu amekuwa mgonjwa siku zote au ametokea kuwa mgumba?.
Uislamu hupinga
ukatili huo kwa kuruhusu mitala.
Hii ni mbali
kabisa na utafiti wa kitakwimu kwamba wanawake wanawazidi wanaume katika
Tanzania, wanawake 100 kwa wanaume 95; au katika ile misiba fulani kama vita,
wanaume hukumbana na kifo zaidi kuliko wanawake. Kama mitala hairuhusiwi na jamii,
italazimisha aslimia tano ya wanawake nchini kujiingiza katika ukahaba.
Tunafikiri kiasi
hiki kitatosha kuonyesha hekima ya Waraka wa Serikali katika kutambua mitala
kama halali na desturi yenye “manufaa”.
Lakini, katika mfumo wake wa sasa, Waraka hautakidhi madhumuni
yanayohitajiwa. Je, itatokea nini kama
pamoja na hali kuruhusu ndoa ya pili, mke wa kwanza akakataa kwa “hiari na kwa
uhuru kukubali kuigeuza ndoa ya mke mmoja”
kuwa ya mitala? Je;
haitamlazimisha mwanaume kuwa “kwenye hali ambapo amma amtaliki mke wake wa
kwanza au akae kinyumba (isvyo halali) na mke mwingine”, pamoja na athari zake zote zisizofaa
zisizoepukika?.
Njia nzuri ni
kumtaka mwanaume aende kwenye baraza (au mahakama) iliyopendekezwa ya ndoa au
kamati ya jumuiya yake na kuwathibitishia haja zake. Kama wakikubali, kukataa kwa mke wa kwanza
hakupasi kufikiriwa kabisa.
Tunachukulia
kwamba, kwa vile hakuna suala la kubadilisha asili ya ndoa katika ndoa ya Mwislamu, Mwislamu hatahitaji
idhini ya mke wa kwanza (au wake) kabla
ya kuoa mke mwingine.
TALAKA: Hakuna haja ya
kusisitiza kwamba katika hali fulani talaka ndio suluhisho pekee lililobaki kwa
wanandoa. Manufaa ya mfumo wa talaka
yanaweza kuonekana kutokana na ukweli kwamba hata mabaniani na wakristo
wamelazimika kwa nguvu ya moja kwa moja isiyoepukika kutunga sheria za talaka. Waraka umetambua hoja hii. Vile vile lazima ikumbukwe kwamba Uislamu,
wakati ambapo unakubali hoja hii katika hali fulani, umetamka kwamba ni “Sheria
halali yenye kuchukiza mno”. (makuruhu),
itumikayo tu katika hali zilizo ngumu mno.
Qur’an Tukufu imeweka
chombo cha usuluhisho na jumuiya nyingi za ki-Islamu zina kamati kama
hizo. Kwa bahati mbaya baadhi ya pande
fulani hawakupendelea kabisa mfumo huu muhimu.
Matumizi haya mabaya ya uhalali wa talaka lazima yaachwe na jaribio la
waraka kudhibiti hali hii linakaribishwa sana.
Masharti ya Talaka: Lazima tuonyeshe katika mwanzo kwamba madhehebu ya Shia Ithan-asheri ya
Sheria ya ki-Islamu imeweka kanuni ngumu zilizotegemezwa juu ya Qur’an Tukufu
na Hadithi kuhusiana na talaka. Talaka
inaruhusiwa mradi tu inatamkwa mbele ya watu wawili mashahidi “Adil” (watu
waliothibitishwa uaminifu wao) ambao husikia maneno na kuelewa chanzo cha
talaka. Talaka lazima itamkwe katika
utaratibu uliothibitishwa.
Zaidi, ni lazima
vile vile kwamba mume awe mtu mzima, mwenye akili timamu na mwenye kuelewa
vizuri, atendaye kwa utashi wa uhuru wake mwenyewe na sio katika mshituko wa
hasira au kutishwa, na kwamba lazima awe na nia ya dhahiri ya kuvunja ndoa.
Kwa kadiri
mwanamke anavyohusika, yeye wakati wa talaka lazima awe katika hali ya tohara
na kwamba talaka haiwezi kutamkwa hata wakati wa tohara ambao kwamba mume
amekutana naye kimwili.
Kama moja ya
mashariti yaliyotajwa hapo juu yakivunjwa, talaka itakuwa batili na kutenguka.
Sheria ya
ki-Islam haimpi mwanamke haki ya kutoa talaka, maoni yoyote kwamba mwanamke
apasa kupewa haki ya kumtaliki mumewe yatakuwa ni kuingilia maadili ya dini,
ambayo waraka umekariri kusema, sio nia ya Serikali.
Familia ni msingi
wa jamii, na kama ilivyo kila jamii, huhitaji mamlaka ya mwisho kuhifadhi
nidhamu na ustawi wa jamaa (wa familia).
Uislamu umetoa nafasi hiyo kwa mume ambaye amepewa haki ya kutoa talaka.
Lakini mwanamke
wa ki-Islamu anapasika kutoa maombi ya kuvunja ndoa au kuibadilisha yeye
mwenyewe katika mazingira yafuatayo:-
·
Anaweza kuomba (Khula) ambayo yaweza
kukubaliwa juu yake na mume.
·
Anaweza kumuomba Mujtahid (ambaye ni Kadhi
katika Sheriat za Shia Ithna – Asheri) kumpa talaka kama mume maetoweka, au
anakataa kumtunza.
·
Anaweza kuifuta ndoa kama mume ni mwenda
wazimu au akawa mwenda wazimu baada ya ndoa.
·
Na anaweza kuibatilisha ndoa (baada ya kupeleka suala lake kwa Mujtahid) kama
mume ni hanithi.
Itakuwa muhimu,
wakati wa kuandika hati ya rasimu, kutambua talaka iliyotolewa na Mujtahid na
ubatilisho wa ndoa kwa kadiri ambavyo ndoa za Shia Ithna-Asheri zinavyohusika.
Hukumu
zilizotajwa hapo juu zinauhusiano juu ya masharti ya waraka kuhusiana na mume
aliyetoweka. Kutoa talaka kwa Mujtahid
(au hakimu katika suala la wasio kuwa Shia Ithna – Asheri au wasiokuwa
Waislamu) ni sahihisho bora zaidi kuliko kudhania kwamba mume kafa (kwa
madhumuni ya ndoa yake) na kudhani anaishi (kwa madhumuni mengine, pamoja na
ndoa nyingine kama ipo yoyote) wakati mmoja na huo huo!
Kwa vile Waraka
kwa usahihi hutambua talaka iliyotolewa na mume mwislamu kama mwisho (wa ndoa),
na kuitaka mahakama kusajili talaka hiyo bila uchunguzi wowote zaidi, tunataka
kusisitiza kwamba talaka kama hiyo iwe inafanya kazi kuanzia tarehe ya kutamkwa
kwa utaratibu wa talaka na mume, na sio tarehe ya kusajiliwa.
Waraka humtaka
Mwislamu akusudiaye kutoa taarifa ya kusudio lake siku 21 kabla kwa “Sheikh
aliyeruhusiwa na Waziri kufungisha Ndoa.”
(Waraka) umepuuza
ukweli kwamba Mvulana wa ki-Islamu na msichana wanaweza kufunga Ndoa wao
wenyewe bila kuwa na haja ya “kumwita Sheikh na kumuomba afungishe ndoa”. Tuna hakika sio nia ya Serikali kutengeneza
Sheria mpya ya Uislamu ambayo ingelianzisha wachungaji kama wa Kikristo. Basi nini hii maana ya kutajwa Sheikh
aliyeruhusiwa na Waziri? Ni wazi kwamba
wazo hili linakwenda kinyume kabisa na Uislamu.
Vile vile
tunashindwa kuona haja yoyote kwa ajili ya pendekezo hili la taarifa ya siku
21. Tuchukulie msichana kutoka Kigoma na
mvulana kutoka Pangani (wote wanaishi Dar es Salaam). Wakamjulisha Sheikh wa Jumuiya yao mjini Dar
es Salaam kwamba wanataka kuoana. Sheikh
yule hatarajiwi kuchapisha au kutangaza kusudio la ndoa katika magazeti au
radio. Basi, vipi ataweza kujua kama
kuna kikwazo chochote cha halali dhidi ya ndoa ile?
Na hata hivyo,
hakutakuwa hata ndoa moja kama hiyo ya kusudio la kiharamu katika ndoa elfu
moja. Tunafikiri, ni bora kuiondoa
sheria hii na kuibadilisha na nyingine kwa maana kwamba kama itakuja kufahamika
hata baada ya kuona kwamba wasingeweza kuona kihalali, ndoa
itakuwa batili na kutenguka kuanzia mwanzo.
Kwa kadiri
usajili wa Ndoa na Talaka unavyohusika, katika Jumuiya yetu rejesta za ndoa
zimekuwepo kwa zaidi ya miaka 125 na tunatoa vyeti kwa wanandoa.
Lakini lazima
tusisistize kwa nguvu sana kwamba uhalali wa ndoa au talaka hauwezi kufanywa
kwa kupasishwa na usajili. Yaweza
ikafanywa kuwa ni kosa kwa zile ambazo hazikusajiliwa; lakini isije ikaathiri
uhalali wa ndoa au talaka.
Hivyo hivyo,
katika hali nyingine pia, kama ndoa ni sahihi kwa mujibu wa dini, isije
ikachukuliwa kuwa ni batili kama inapingana na masharti yoyote yaliyowekwa na
waraka. Vinginevyo, itakuwa ni
uingiliaji wa moja kwa moja katika dini.
Madhumuni ya
muhtasari huu ni kuidhihirishia Serikali kwamba utungaji wa sheria lazima
ufanye juhudi ya kuhifadhi sheria za dini za Jumuiya mbalimbali zinazoishi
chini ya bendera moja, hususani wakati
sheria hizo zikiwa ni zenye athari nyingi juu ya misingi hiyo kama ndoa na
maisha ya kifamilia.
Kama
tulivyoonyesha mapema, katika Uislamu Sheria na dini havitenganishwi, kwa vile sheria
zetu zimeanzia kutoka kwenye Qur’an Tukufu ni wazi kwamba kama sheria yoyote
inatungwa ambayo imma hupingana na maamrisho ya Qu’ran au Hadithi; kwa kawaida
itasababisha vurugu kubwa katika akili
za Umma wa ki-Islamu na kwa hiyo Jumuiya yote ya Uislamu itakuwa katika
usumbufu.
Mwishoni,
tunapenda kufanya muhtasari wa maoni yetu kwa ifuatavyo:
Tunahitaji kwamba
badala ya kutunga Sheria inayofanana kwa wote, “Amri ya Taarifa mpya ya Sheria
za “ki-Islamu” lazima ziwe katika matumizi kwa ajili ya Waislamu na uandikwe
muswada wa Sheria ndogo chini ya Amri hiyo, uchapishwe na ifanywe itumike kwa
mapema iwezekanvyo.
Kwa kadiri
mapendekezo ya Waraka yanavyohusika tunakubali kabisa kwamba “Ndoa lazima iwe
muungano wa hiari” (ibara ya 6 ya waraka maelezo ya Kiingerza) kwamba wanandoa
wasije wakawa ndani ya hadhi iliyokatazwa ya undugu au unasaba (ibara ya 9);
kwamba yeyote kati ya mume au mke anweza kumiliki mali yake mwenyewe.” (ibara
ya 19); kwamba mke awe na uwezo wa kutoa
ushahidi dhidi ya mumewe (ibara ya 21); kwamba kuwe na masharti ya talaka “kama
ndoa imevunjika kabisa” na kwamba “Talaka zisishughulikiwe juu juu (ibara ya
24); na kwamba kuwe na mabaraza ya usuluhisho” na “utambulisho kamili upewe
mabaraza kama hayo ambayo yapo katika Jumuiya mbali mbali kabla ya sheria hii
mpya unayokusudiwa” (ibara 25).
Tunakubaliana na
mapendekezo yafuatayo pamoja na masharti na sifa fulani:-
Umri wa chini wa
miaka 15 na 18 kwa wasichana na wavulana mtawalia (ibara ya 7) na usajili wa
ndoa (ibara ya 17), na wa talaka (ibara ya 27) ni mambo mazuri tunakubaliana
nayo ilimradi, kuvunja au kukiukwa kwao hakufanyi ndoa au talaka batili na
kutenguka.
Matamshi ya
Mwislamu ya Utaratibu (formula) ya talaka yanatambuliwa na Waraka kama ushahidi
wa kuvunjika kabisa kwa ndoa na mahakama inapaswa “kutoa cheti cha kuvunja
ndoa”.
Tunakubali
pendekezo hili, ilimradi cheti kinachosemwa kinaanzia nyuma kuanzia tarehe ya
kutamkwa kwa utaratibu wa talaka na mume.
Tuko katika
maafikiano kamili na pendekezo kuruhusu Ndoa ya mke mmoja kubadilishwa kuwa ya
mitala. Lakini hatufikirii kuwa ni
busara kusisistiza juu ya idhini ya mke wa kwanza (ibara ya 12). Mume anapaswa kuwa na haki ya kwenda kwenye
baraza la Ndoa lililopendekezwa na uamuzi wao utakuwa wa mwisho.
Vile vile,
tunaona kwamba Ndoa ya Mwislamu ikiwa yenye uwezekano wa mitala, mume wa
ki-Islamu hatatawaliwa na sharti hili.
Tunafikiri kwamba
pendekezo la kudhania mume (aliyetoweka kwa muda wa miaka 5) kama aliyekufa sio
la busara. Njia nzuri ni kumruhusu
Hakimu (au Mujtahid) kutoa talaka kama mazingira yatahitajia hivyo.
Haki ya mwanamke
kudai talaka au kuvunja au kutengua ndoa lazima ikomee kwenye mazingira
yaliyotajwa mapema katika muhtasaari huu.
Utungaji wowote wa sheria uendao
kupita mpaka huo, utakuwa ni uingiliaji wa moja kwa moja katika dini yetu.
Tunakataa kwa
nguvu pendekezo kwamba kukaa kinyumba na mwanamke kwa muda wowote (mpaka wa
miaka 2 ni wa kiholela kabisa) huwafanya hao wawili mume na mke kihalali. Vinginevyo mpaka utamkaji unabadilishwa kama,
ilivyopendekezwa katika ibara ya 11 ya muhtasari huu, pendekezo hili haliwezi
kukubaliwa.
Tunakataa kabisa
pendekezo la kumfanya mke kuwajibika kumtunza mume wake (ibara ya 19).
Tunafikiri kwamba
pendekezo la kutaka taarifa ya siku 21 halina maana kabisa, na kuunganisha
katika hali ya Waislamu pamoja na usemi “taarifa itapelekwa kwa Sheikh, ambaye
ameruhusiwa na Waziri kufungisha ndoa” huhitaji kuangaliwa kwa tahadhari sana,
kwani huonyesha kuanzishwa kwa sheria mpya ya uchungaji ambao ni kinyume kabisa
na misingi ya Ki – Islamu. Kwa hiyo
hatuwezi kukubaliana nalo.
4
MUHTASARI JUU YA HIJABU NA MIRATHI*
Mheshimiwa Rais,
1. Kwa niaba ya
Jumuiya na mashirika mbali mbali ya ki-Islamu, tunachukua fursa ya kufanya
wasilisho hili kwa ajili yako wewe Mheshimiwa kulifikiria kwa huruma.
2. Kaika
wasilisho hili tunakomea wenyewe kwenye masuala mawili ambayo yalikuwa yakikera
akili zetu kwa muda mrefu. Nayo ni: Hijabu kwa ajili ya wasichana wa ki-Islamu
katika taasisi za elimu na Sheria za ki-Islamu zinazohusu Wosia na Mirathi.
3.
Mheshimiwa: Sisi wote ni raia wa nchi
huru, na tumejipa katiba ambayo, pamoja na mambo mengine kuhakikisha uhuru wa
kuabudu, dini, muungano na kuzungumuza.
Hususan tanarejea kwenye Ibara 18 (1), 19 (1) (2) na 20 (1) ya Katiba
ambazo ni kama ifuatavyo:-
18 (1) Bila chuki kueleza shria za nchi, kila mtu anao
Uhuru wa kutoa maoni na kuzungumza, na kutaka, kupokea, kugawa au kusambaza
habari na maoni kupitia chombo chochote cha habari bila kujali mipaka ya
kitaifa, na vile vile ana haki kutokana na kuingiliwa mawasiliano yake.
19 (1) Kila mtu
ana haki ya Uhuru wa mawazo au dhamira, itikadi au imani, na hiari katika mambo
ya dini, pamoja na uhuru wa kubadili dini au imani yake.
19 (2) Bila chuki
kwenye sheria zinazohusika za Jamhuri ya Muungano, taluma ya dini, ibada na
utangazaji wa dini utakuwa huru na jambo la binafsi la mtu binafsi, na mambo na
uendeshaji wa vyombo vya Dini hautakuwa sehemu ya shughuli za mamlaka ya Dola.
20 (1) Kila mtu ana haki ya kupewa uhuru, kutegemea
Sheria za nchi, kukusanyika kwa uhuru na kwa amani, kuunganika na kushirikiana
na watu wengine, kutoa maoni hadharani, na muhimu zaidi kuunda au kujiuunga na
mashirika au vyama (vikundi) vilivyoundwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au
kuendeleza itikadi zake au masilahi yoyote mengine.
4. Allah (SWT) amesema katika Qur’an Tukufu
neno lake la
mwisho:
“Na sikuwaumba
majini na watu isipokuwa kwamba wanitumikie mimi”. (Sura 51, aya 56) Waislamu
wote kuanzia mwanzo kabisa wanakubali kwamba neno “li ya budun” ambalo linatokana na (neno) “Ibadah” na linatafsiriwa hapa kama “tumikia”, maana yake
unyenyekevu kamili.
Mheshimiwa:
Hakuna awezaye kufahamu zaidi kuliko busara zako nzuri kwamba “Ibadah” katika Uislamu sio kawaida ya
baadhi ya ibada zenye kutekelezwa katika nyakati au siku makhususi. Huzunguka maisha yote ya Mwislamu. Uislamu maana yake kujisalimisha kwenye
majaaliwa ya Allah (SWT) na wakati tunapoahidi kufanya hivyo tunaitwa Waislamu
(ili) kutuongoza katika maisha yetu ya kidunia, na kutusaidia kufika karibu
Yake katika maisha ya kesho akhera Allah (SWT) ametuma kwetu kupitia kwa Mtume
Wake wa mwisho (s.a.w.) mfumo wa sheria wenye mambo mengi unaojumuisha mambo
yote ya maisha … ya nyumbani, ya kijamii ya kifedha, ya kimaadili na ya kiroho.
5. Mheshimiwa
unajua vizuri sana kwamba Qur’an Tukufu haikushughulikia suala lolote la sheria
kwa ufafanuzi zaidi (na uanagalifu) na katika namna ya utaratibu kwama sheria
ya ndoa, wosia, mirathi na mambo mengine yanayohusika nayo, pamoja na adabu ya
mavazi kwa wanawake.
6. HIJAB:
Ni lazima iwekwe wazi kuanzia
mwanzo kwamba hukumu zinazoelekeza
Wanawake kuvaa katika namna ambayo hufunika mwili wote na kuhifadhi muruwa wao
zimetajwa kwa wazi katika Qur’an Tukufu.
Ni urithi wa kawaida kwa Waislamu wote na haukukomea kwenye madhehebu au
Jumuiya fulani. Vile vile, sio mila ya
kitamaduni, ni sheria ya lazima ya Mungu, na haiwezi kuachwa bila kupata hisia
ya dhambi na hatia.
7. Kuna aya si
chini ya tisa katika sura mbali mbali za Qur’an Tukufu zinazofafanua hukumu ya
Hijab. Kwa ruhusa yako Mheshimiwa tunanukuu mbili ya hizo hapa chini:-
“Nasema (Ewe Mtume) kuwaambia waumini wanawake
wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao, wala wasidhihirishe viungo vyao
isipokuwa vinavyodhihirika; na waangushe shungi zao mpaka vifuani mwao, na wasionyeshe
mapambo yao ila kwa waume zao, au baba zao,
au baba za waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao, au kaka
zao, au wana wa kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawake wenzi wao, au wale iliyowamiliki mikono yao
ya kuume, au watumishi wanaume wasio na matamanio ya kijinsia au watoto wadogo
ambao hawajapata elimu ya siri za wanawake; wala wasipige miguu yao ili
yajulikane wanayoyaficha katika mapambo yao; na tubieni nyote kwa Allah; enyi
waumini, ili mpate kufudhu (kesho akhera)”. (Sura 24 Aya 31).
‘Ewe Mtume’.
Waambie wake zako, na binti zako na wanawake wa waumini wateremshe chini
“Jilbab” zao, ili kwamba wapate kuhishimiwa ….” (Sura 33, Aya 59).
(Jilbab = Joho
Kubwa kuliko shela na fupi kuliko kashida, ambayo hufunika kichwa na kifua cha
mwanamke).
8. Kwa
kutegemea juu ya aya hizi na aya
nyingine za Qur’an Tukufu na Hadithi sahihi za Mtukufu Mtume (SAW) Wanachuoni
wa ki-Islamu, bila utengano wowote wa hitilafu, wameamuru kwamba:-
(a) Wanawake wa
ki-Islamu lazima wafunike mwili mzima wakati wanapotoka majumba yao. Uso tu (lakini sio kichwa na nywele ) na
viganja vya mikono vinaweza kuwa wazi.
(b) Kuna hukumu
maalum nz za shuruti za mavazi kwa ajili ya Sala na Hajj.
(c) Nguo isiwe
yenye kubana kuonyesha mikunjo kunjo ya mwili, wala nyepesi, (na kuonekana)
kuyashinda madhumuni ya vazi (kama ilivyokusudia).
(d) Wanawake
hawapaswi kuvaa vazi ambalo kwa ujumla hutumiwa na wanaume, wala wanaume kuvaa
za wanawake.
9. Mheshimiwa!
Wizara ya Elimu katika nchi yetu imechagua sare kwa ajili ya wasichana wa shule
za msingi, ambayo ni mfano wa vazi la kimagharibi. Tunashangaa kwa nini uamuzi kama huo
ulichukuliwa. Blauzi na sketi sio vazi
la ki-Afrika, wala si la kikristo au la ki-Islamu. Kwa nini mtindo huo ni mtakatifu mno kiasi
kwamba hauwezi kubadilishwa? Ingelikuwa
vizuri zaidi kuwa na hamu yetu yakitaifa badala yake kuamuru (kuvaa) gauni refu
na bui bui. Kwa vile ni vazi
linalovaliwa na mamilioni ya wanawake wa ki-Afrika. Je, si wakati muafaka kwamba wenyewe
tunaondokana na tabia kwamba yote yale yanayokuja kutoka nchi za Ulaya
(Magharibi) ni mazuri kwetu, ambapo maadili yetu wenyewe ni ya “kishenzi”?
10. Kwa mtazamo
wa ukweli hapo juu, kwa unyenyekevu Mheshimiwa tunaomba uielekeze Wizara ya
Elimu kuagiza (uvaaji) wa sare kama hizo kwa wasichana wa shule zenye kufunika
vichwa vyao na mwili mzima, kuacha wazi nyuso na viganja. Inaweza kurahisishwa
kwa kuvaa: skafu, gauni, suruali na
soksi.
Tunaamini kwamba
itakuwa ni sare yenye heshima zaidi, na itaruhusu hata wasichana kushiriki katika
riadha na michezo kwa uhuru bila hofu ya kuonekana aibu yoyote.
11. Mheshimiwa:
Kama kwa sababu
yoyote ni vigumu kuanzisha sare hizi kwa wasichana wote, basi wasichana wa ki-Islamu waruhusiwe nchi nzima
kuvaa sare hizo bila pingamizi au kizuizi chochote, kwa vile ni sheria ya dini
yao na sio kikabila au mila ya kitamaduni.
12. Kabla
hatujaendea masuala mengine, tungependa kwa huruma zako Mheshimiwa kutoa
taarifa kwako kwamba wasichana wa ki-Islamu wanaoishi Uingereza na Ufaransa
wamepata haki yao ya kuvaa Hijab mashuleni, ingawa ilichukuwa hatua za
kimahakama (na katika suala la Ufaransa, uingiliaji kati ya Tume ya haki za
binadamu ya Uingereza) kuipata haki
hiyo. Karibu na nyumbani nchini
Kenya,mwaka huu (1990) msichana Mwislamu wa ki-Afrika alishinda kesi mahakamani
dhidi ya mamlaka za shule wakati zilipokataa kumruhusu kuingia shule na Hijab.
Gazeti rasmi la KANU (liitwalo) the Kenya times (Nairobi) liliandika tahariri
tarehe 2/2/1990 ambayo kwayo pamoja na mambo mengine liliandika:
“ Kwa nchi ya
Kidemokrasia kama hii yetu, ambako uhuru wa kuabudu kwa dini zote umehifadhiwa
katika Katiba, ni vigumu kuamini kwamba baadhi ya watu wanaona ni sawa
kuwanyima wengine uhuru huu”.
“Dini, kama
tujuavyo, ni jambo lililo karibu sana na mioyo ya baadhi ya watu kuwanyima
uhuru wa kuelezea hisia zao wakati wowote wanapotaka kufanya hivyo ni kuwa
dhidi ya juhudi zote katika kujenga
jamii yenye amani na upendo”.
“Chukuwa Uislamu
kwa mfano, ni mfumo kamili wa maisha.
Kumtaka mfuasi yeyote muaminifu wa dini hii kuacha baadhi ya mambo ya
maisha haya, hakika ni kumuambia akatae yale yalioandikwa katika Qur’an
Tukufu. Na sisi ni nani, katika wadhifa
wowote ule uwao tunaoundesha, kuingilia maisha ya ndani ya watu wengine na dini
zao? Suala la msichana huyu wa ki –
Islamu kuambiwa afunue kichwa chake
wakati akiwa katika eneo la Shule halipaswi
kutokea. Hali kadhalika kuwanyima
watoto haki yao ya elimu kwa sababu wanavaa vilemba si ya kuvumiliwa.”
13. SHERIA YA KIISLAMU YA MIRATHI:
Tumepata kuelewa
kwamba Serikali inakusudia kufanya mabadiliko katika sheria ya ki-Islamu ya
mirathi. Tulikerwa mno na habari hizi:
Kama tulivyo wasilisha mapema, Qur’an Tukufu imeweka kwa usahihi na
uwazi mno zaidi hukumu zinazohusiana na mirathi, kwa ufafanuzi kabisa ikitoa
kwa warithi mbali mbali migao yao katika mali ya Mwislamu marehemu. Sheria ya ki-Islamu ni chombo kilichofumwa
vizuri. Hatuwezi kubadilisha au
kurekebisha moja au mbili ya mambo yake bila kuharibu ufumaji wote. Kwa mfano, katika sheria ya ki-Islamu mtu
hawezi kutumia kitu kilichopatikana kiharamu (katika maana ya dini), amma kwa
kidunia au kwa madhumuni ya kidini. Kwa
hiyo kama madiliko yanafanywa katika Sheria ya mirathi, kwa maana hiyo mtu
fulani kwa kawaida atapata zaidi kuliko mgao wake (ule ambao amegaiwa na Qur’an Tukufu). Pato hilo la haramu litafanya maisha yake
yote kuwa duni. Maisha yake ya kila siku
yatakuwa ni orodha ndefu ya madhambi na
kuchupa mipaka. Sala zake zitakuwa
batili; Hija yake itakuwa batili na kutenguka; hata chakula chake na mavazi
vitakuwa haramu katika maana ya
dini. Mtu kama huyo kamwe hawezi
kutarajia amani katika maisha ya kesho akhera.
14. Hatujui ni
nini maana halisi ya zoezo hili. Kwa
hiyo hatuwezi kusema zaidi kwa sasa.
Lakini tunarudia kusema kwamba sheria hizi zimeegemezwa juu ya Qur’an
Tukufu na haiwezekani kuweka mpaka baina ya Sheria hizi na Qur’an Tukufu. Jambo lolote la kubadilisha migawanyo ya ki –
Qur’an itakuwa sawa na kubadilisha Qur’an Tukufu .
15. Hata hivyo,
katika mintaarafu hii, tungetaka kuvuta nadhari yako Mheshimiwa kwenye Amri ya
Taarifa mpya ya Sheria ya ki-Islamu ya Serikali ya Tanzania (Na. 56 ya 1964),
ambayo chini yake, kazi ilianzishwa ya kupanga kanuni za Sheria za ki-Islamu,
ikitoa utambulisho halisi kwa madhehebu.
Sura nne zinazo husika na Ndoa, Ulinzi wa watoto n.k. zilichapishwa pia
kama sheria ndogo chini ya sheria hiyo katika nyongeza ya Gazeti Na 34 la 27 Juni 1967. Ilikuwa ni hatua ambayo ilifurahisha Umma
wote wa Ki-Islamu wa nchi hii. Kwa bahati mbaya mpango ule uliachwa. Bado, kama mpango ule utahuishwa, ambao kwayo
hukumu za kila Madhehebu zinatambuliwa kama Sheria zitumikazo kwenye Jumuiya
hiyo, na sheria hizo zikapangiwa kanuni katika juzuu moja kwa
rejea za urahisi kwa Mahakama za Sheria, itakuwa hatua ya kusifia sana ambayo
kwamba Umma wote wa Waislamu wa Tanzania watakuwa siku zote na shukurani kwako
wewe Mheshimiwa.
MAHAKAMA YA KADHI:
BAADHI YA MAPENDEKEZO*
Waislamu nchini kwa muda mrefu wamekuwa wakidai kuwepo na Mahakama ya Kadhi katika Tanzania itakayoangalia na kushughulikia mambo maalum ambayo yanajumuishwa zaidi na Sharia za Kiislamu kuliko Sheria za Mahakama za kawaida.
Ukweli kwamba tayari ipo Mahakama ya Biashara (Uchumi), ni uthibitisho tosha kwamba mambo maalum (ya aina moja) yanahitaji kushughulikiwa na Mahakama maalum ambayo vitabu vya Sheria vya kawaida huyafafanua kwa nadra (uchache).
Hata hivyo, tayari inakubalika kimsingi kwamba hakuna utata katika suala hili, kwani Rais Benjamin Mkapa ameshasema atayashughulikia matatizo yote yanayowakera Waislamu na kuhakikisha kuwa Waislamu wote nchini hawajisikii kunyanyaswa kwa vile sera ya Chama tawala (Serikali) ni Usawa miongoni mwa Wananchi wake, bila kujali jinsia, rangi (Utaifa), au Dini.
Kwa mantiki hii, mapendekezo kadhaa yanatolewa kuisaidia Mahakama ya Kadhi iweze kufanya kazi zake kwa ufanisi na kupatikana madaraka kamili ya kisheria ya Mahakama ya Kadhi.
Ili Mahakama iweze kupata hadhi yake, haya ni mapendekezo ambayo yangeweza kusaidia kufikia lengo hilo.
Mswada unalenga kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi katika kila Wilaya ya Tanzania, ili kuangalia mambo yote yahusianayo na Sharia ya Kiislamu katika masuala ya Ndoa, talaka, haki ya kulea watoto, mgawanyo wa mali, Urithi n.k. pale ambapo wahusika wa utata huo ni Waislamu, waliooana kwa mujibu wa sharia na desturi ya ndoa za Kiislamu.
Ukweli ni kwamba makusudio ya mswada huu ni mazuri, lakini upo uwezekano mkubwa kwamba kutokana na ukosefu wa Kitabu makhususi cha Sheria za Kiislamu, Makadhi katika wilaya mbali mbali wakifikia kwenye uamuzi wa kesi zinazofanana, wanaweza wakatoa hukumu zinazopingana.
Hivyo, upo umuhimu wa kukiandaa kitabu makhsusi kitakachotumika kama Mwongozo wa Makadhi ili kuiepuka migongano.
Hapo zamani mwaka 1964, Bunge la Tanganyika kwa wakati huo lilipitisha “Sharia ya Kiislamu (Sheria ndogo)” iliyompa madaraka Waziri aliyehusika na mambo ya Sheria kuandaa na kuchapisha kipengele cha Sharia ya Kiislamu baada ya kushauriana na wanachuoni wa Sharia za Madh-hebu za Kiislamu.
Katibu Mkuu wa Bunge wakati huo, alikamilisha kuandika Mswada wa ndoa wenye sehemu 4 (kama ulivyokubaliwa na wanachuoni wa Sharia za Kiislamu kutoka Madh-hebu matatu Kiislamu Shafi’i, Hanafi na Shia).
Mswada huu
uliotolewa kama Sharia ndogo chini ya kifungu kidogo cha Sharia ya Kiislamu (Na:
56 ya mwaka 1964) ikiwa ni sehemu ndogo ya Gazeti
la Serikali na Na: 34 la tarehe 27, Juni, 1967.
Ilifahamika kuwa sehemu zilizosalia, kuhusiana na kuwalea watoto na talaka n.k. zingechapishwa mapema. Lakini zoezi hili lilisitishwa na badala yake serikali ilitunga sheria ya ‘Ndoa’ kupitia Mswada wa Ndoa wa mwaka 1971.
Hata hivyo, kanuni ya Sheria ya Ki-Islamu 1964 bado haijafutwa na bado ni sehemu ya Kitabu cha Bunge. Na kwa sababu sasa serikali inakusudia kuanzisha Mahakama za Makadhi katika kila Wilaya, ni wakati muafaka wa kufufua tena mswada wa sheria ya Kiislamu ya mwaka 1964 ili ufanyiwe kazi na kazi hii ianzie pale ilipoachiwa.
Jambo muhimu hapa ni kuepusha uwezekano wa Makadhi kutoa hukumu zitakazoleta utata. Vinginevyo, mzigo wa kazi za Mahakama Kuu utaongezeka kwa kuwa rufani kutoka Mahakama za Makadhi zitajazana kwenye Mahakama ya Rufaa.
Madhehebu za Makadhi wa Wilaya:
Kwa vile Waislamu wengi wa Tanzania ni wafuasi wa Madhehebu ya Shafii ni vizuri makadhi wa Wilaya watokane na Madhehebu ya Shafii.
Lakini iwapo wahusika au mhusika wa mgogoro ni wa Madhehebu isiyo ya Shafii, inapendekezwa kuwa Kadhi wa Wilaya asaidiwe na wanachuoni wa madh-hab inayohusika.
Hii itafuta uwezekano wa kutolewa hukumu isiyo sawa na itawapa imani ya kutendewa haki wahusika au mhusika. Wasaidizi wa Kadhi wa Wilaya waliotajwa hapo juu itabidi watayarishwe katika kila Wilaya na wanaweza kuangaliwa upya (kuteuliwa) muda baada ya muda.
Iwapo mapendekezo mawili muhimu yaliyotajwa hapo juu katika makala haya yatakubalika na kufanyiwa kazi, itakwenda hatua kubwa kuwatendea haki na usawa Waislamu wote nchini.
* Uliwasilishwa
mbele ya Tume ya Serekali ya Kenya juu ya Sheria za Ndoa, Talaka na Mirathi;
kwa niaba ya Khoja Shia Ithna – asheri (Supreme Council of Africa, Mombasa)
22/8/1967
* Uliwakilishwa
mbele ya Tume ya Serikali ya Kenya juu ya Sheria za Ndoa, Talaka na Mirathi:
kwa niaba ya Khoja Shia Ithna-Asheri Supreme Council of Afrika Mombasa, 1967.
* Imechapishwa katika Standard (Dar es Salaam)
Jumatatu, 1969 kwa niaba ya Khoja Shia
Ithna-Asheri Territorial Council of Tanzania.
* Uliwasilishwa kwa Mheshimiwa Al-Haj Sheikh Ali Hassan Mwinyi, Rais wa Muungano wa
Jamhuri ya Tanzania, kwa niaba ya wawakilishi wa Mashirika (Taasisi) mbali
mbali ya Ki-Islamu ya Dar es Salaam mwaka 1990
* Imechapishwa katika The Democrat (Dar es Salaam) Aug 17-23,1999.