Usahihi wa Historia Uislamu na Waislamu

Kimeandikwa na : Sayed Ali Asgher Razwy


YALIYOMO

Kuhusu Mwandishi. 2

Utangulizi . 4

Jografia ya Arabuni. 12

Ikolojia (uhusiano wa viumbe na mazingira) ya Arabia. 17

Arabia kabla ya Uislamu...19

Hali ya Ustawi wa Jamii ..24

Hali ya dini katika Arabia ya kabla ya Uislamu..26

Elimu miongoni mwa Waarabu kabla ya Uislamu.28

Hashim kabla ya kuzaliwa Uislamu ..32

Kuzaliwa kwa Muhammad na miaka ya mwanzo ya uhai wake...36

 

Ndoa ya Muhammad Mustafa na Khadij a ...40

Kuzaliwa kwa Ali Ibn Abi Talib....42

Kabla tu ya Tangazo la Ujumbe wake..46

Kuzaliwa kwa Uislamu..48

Waliosilimu mwanzoni na mateso kutoka kwa wapagani...60

Hijra mbili za Waislamu kwenda Abyssinia ( A.D.D. 615 - 616 )...73

Hamza aukubali Uislamu - A.D. 615...76

Kusilimu kwa Umar- A.D. 616 ...79

Kususiwa kiuchumi na kijamii kwa Bani Hashim.84

Vifo vya Khadija na Abu Talib - 616A.D...94

Safari ya Muhammad kwenda Taif..99

Maeneo Mapya ya Uislamu..103

Hajira (Kuhama)...105

Mwaka wa kwanza wa Hijiria .112

Vita vya Kiislamu ....124

Mwaka wa pili wa Hijiria.126

Vita vya Badr ....128

 

 

Ndoa ya Fatima Zahra na Ali Ibn Abi Talib..137Vita vya Uhud .. 141

Kuzaliwa kwa Hasan na Husein ...157

Vita vya Khandaq.160

Waislamu na Wayahudi..168

Mkataba wa Hudaybiyya.171

Ushindi wa Khaybar....183

Vita vya Mu'utah..197

Mapambano ya Dhat es - Salasil.205

Kutekwa kwa Makka..208

Vita vya Hunain.226

Vita vya Tabuk...238

Kutangazwa kwa Surat Bara'ah (At- Taubah)..242

Msafara wa mwisho....249

Hija ya Muago...251

Jeshi la Usamah.268

Abu Bakr kama Kiongozi katika Swala.277

Wosia Usioandikwa wa Mtume wa Allah (s.a.w.)..282

Wake zake Muhammad (s.a.w.) Mtume wa Allah (s.w.t)..288

Kifo cha Muhammad (s.a.w.) Mtume wa Allah 295.295

 

 

Hisia za Familia na za masahaba wa Muhammad Mustafa (s.a.w.)

Juu ya kofo chake....306

Kifo cha Muhammad Mustafa (s.a.w.) na Umma wake...308Muhammad Mustafa (s.a.w) na Urithi wake..309

Nadharia ya Kisunni juu ya Serikali .319

Kugombea madaraka (1).327

Kugombea madaraka (2).334

Kugombea madaraka (3).337

Kugombea madaraka (4).346

Tahakiki ya Saqifah....352

Saqifah na mantiki ya Historia ...364

Saad Ibn Ubadah, Ansari - Mgombea wa Ukhalifa..387

Abu Bakr; Khalifa wa kwanza wa Waislamu.389

Matukio Muhimu ya Ukhalifa wa Abu Bakr..392

Demokrasia na Waislamu..414

Umar bin al-Khattab, Khalifa a pili wa Waislamu.419

Uthmani Khalifa wa Tatu wa Waislam .. 455

 

 

Ali Ibn Talib, Khalifa wanne wa Waislam.506Utangulizi wa Vita.529

Vita vya Basra (Vita vya ngamia)..540

Kubadilisha Makao Makuu kutoka

Madina kwenda Kufa..569

Ufufukaji wa Bani Umayyah .579

Vita vya Siffin. 600

Kuuawa kwa Ali ..628

Baadhi ya yaliyoakisi katika Ukhalifa wa Ali..634

Sera ya Ali (a.s.), ya Ndani na ya Nje ...636

Ali (a.s) kama Mjumbe wa Amani ..648

Ali na mifano bora ya Uhuru na Fursa... 658

Orodha ya "Watu wa kwanza" katika Uislamu...663

"Mgawanyo wa lazima" wa Uislamu..667

Mihanga ya Muhammad kwa ajili ya Uislamu...672

Kushindwa kukubwa kwa Abu Bakr na Umar ...675

Ni nani aliyeandika historia ya Uislamu na vipi?..682
 

 


 

The .HTML version of this book is taken from
www.al-islam.org and ebooked by www.ShiaLibrary.com and www.islamkutuphanesi.com . May Allah be pleased with all.


 

Kimetarjumiwa na : Al-Akh Ramadhan Kanju Shemahimbo

P. O. Box 19701 Dar-es-Salaam

©Haki ya kunakili imehifadhiwa na: AL-ITRAH FOUNDATION

ISBN: 9987-427-20-0

Kimeandikwa na: Sayed Ali Asgher Razwy

Kimetarjumiwa na: Ramadhani Kanju Shemahimbo

P.O. Box 19701, Dar es Salaam/Tanzania.

Kimehaririwa na: Dr. M. S. Kanju

na Ustadh Abdallah Mohamed

Email: mokanju2000@yahoo.com

P. O. Box 19701, Dar-es-Salaam, Tanzania

Simu: +255 22 2110640

Kupangwa katika Kompyuta na: Ukhti Pili Rajab.

Toleo la kwanza: Novemba 2005 Nakala:1000

Kimetolewa na kuchapishwa na: AFItrah Foundation

PO Box 19701, Daressalaam, Tanzania Simu: +255 22 2110640 Fax: +255 22 2113107 Email: info@alitrah.org Website: www.alitrah.org

NENO LA MCHAPISHAJI USAHIHI WA HISTORIA YA UISLAMU

Hii ni historia ya vuguvugu la Uislamu ambalo lilianzishwa na Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) mnamo mwaka 610 A.D. huko Makka, na kuendelea alipohamia Madina mpaka alipofarika. Inahusisha kipindi cha miaka tisini kuanzia 570 A.D. wakati yeye Muhammad alipozaliwa huko Makka, hadi mwaka 661 wakati mrithi wake, Ali ibn Abi Talib, alipouawa huko mjini Kufah.

Historia zisizo na idadi zimeandikwa huko nyuma na zitaandikwa wakati ujao. Maendeleo ya kuvutia ya Uislamu katika nyanja ya ulinganiaji katika nyakati zetu wenyewe; kufufu-ka upya kwa mataifa ya Kiislamu baada ya karne nyingi za usingizi mzito; kujidukiza kwa mafuta kama wakala mpya katika siasa za kidunia katika karne hii; bali juu ya yote na hivi karibuni kabisa, yale mafanikio ya Mapinduzi ya Kiislamu ndani ya Iran, yote haya yanakuwa, kote Mashariki na Magharibi, kama vichocheo vya shauku mpya katika Uislamu. Mapinduzi ndani ya Iran yamechokonoa mlipuko wa dunia nzima wa mvuto katika Uislamu, na vitabu vingi vipya vinaandikwa juu ya somo hilo - na wote, Waislamu na wasiokuwa Waislamu.

Hili tena ni jaribio letu kubwa la kutoa kitabu kikubwa kinachohusu historia ya Uislamu na waislamu kwa luhga ya Kiswahili. Tumekiona kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wa maendeleo makubwa ya elimu katika nyanja zote, ambapo uwon-go, ngano za kale na upotoshaji wa historia ni mambo ambayo hayana nafasi tena katika akili za watu.

Kutokana na ukweli huo, Taasisi yetu ya 'Al-Itrah Foundation' imeona ikitoe kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili, kwa madhumuni yake yale yale ya kuwahudumia Waislamu, hususan wazungumzaji wa Kiswahili.

Tunamshukuru ndugu yetu, Al-Akh Ramadhani Kanju Shemahimbo kwa kukubali jukumu hili la kukifanyia tarjuma kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa kwa kitabu hiki.

Ni matumaini yetu kwamba kitabu hiki kitakuwa ni mwanga kwa wasomaji wetu na kuzidisha upeo wao wa elimu katika dini.

Mchapishaji: Al-Itrah Foundation S. L. P. 19701 Dar-es-Salaam.

 

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

KUHUSU MWANDISHI

Sayyed Ali Asghar Razwy (1925-1996)

Marehemu Seyyid Ali Asghar Razwy anakumbukwa sana kama mwanachuoni wa Kiislamu mwenye maneno mazuri, ambaye haiba yake njema na moyo wa uchangamfu vililmpendezesha kwa wote waliokuwa na bahati nzuri ya kukutana naye. Wakati wote wale waliozungumza naye waliondoka wakiwa wameathirika sana kifikra, wakiwa wame-jifunza kitu kutoka kwa mtaalamu huyu mwenye mvuto.

Seyyid Ali Asghar alizaliwa huko Simla, India mnamo mwaka 1925. Baba yake, Agha Seyyid Muhammad Shah alikuwa amehamia hapo zamani kutoka Baluchistan. Agha Seyyid Muhammad Shah alikuwa, yeye mwenyewe ni Aalim, aliyepata elimu yake huko Najaf na Qum, na alikuwa ndiye mwakilishi wa Marehemu Ayatullah Seyyid Abul Hassan Al-Isfahani (R.A.).

Seyyid Ali Asghar Razwy alijiunga katika utumishi wa serikali ya India mara baada ya kuhitimu Shahada ya B.A. Hons kutoka Chuo Kikuu cha Kashmir. Baadaye alishiriki kikamilifu katika vuguvugu la kuunda Pakistani na mwishowe akahamia Pakistani ambako alijiunga na Idara ya mambo ya nje.

Mnamo mwaka 1950, alikwenda Washington D.C. kama mjumbe wa ujumbe wa Kibalozi wa Pakistani. Mnamo mwaka 1954, alihamishiwa Kabul na mwaka mmoja baadaye Seyyid Ali Asghar akahamia Canada na halafu Marekani mnamo mwaka 1960 ambako alifanya kazi na shirika moja la kibiashara.

Akiwa mfanyakazi wa huduma za kijamii, alijiunga na The Muslim World League na kwa miaka mingi akawa ni chimbuko la uongozi kwa iliyokuwa jumuiya changa ya Kishia katika Marekani ya Kaskazini. Anayo sifa ya kipekee ya kuwa mzungumzaji wa kwanza, katika Marekani ya Kaskazini, kuhutubia jamaa ya waumini kwa Kiingereza.

Miongoni mwa kazi zake za maandishi za awali ni wasifu - The Biograpy of Seyyidati Khadijatul-Kubra na Salman Far si. Seyyid Ali Asghar pia aliandika idadi ya vijitabu na majarida ya kidini juu ya mada mbalimbali. Muswada huu wenye sifa daima, A Restatement of The History of Islam and Muslims ulikubaliwa kuchapishwa (kama kitabu) na Mulla Asgharali M. M. Jaffer, aliyekuwa Raisi wa The World Federation mnamo Julai, mwaka 1996.

2

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kwa kuchapishwa kwa kitabu hiki, ambacho Marehemu alikifanyia kazi kwa kipindi cha miongo ya miaka, miezi minane tu baada ya kifo chake cha kuhuzunisha, mnamo Septemba, 15, mwaka 1996 kwenye hospitali ya Calvalry huko New York, yeye ameacha urithi wa kudumu wa maarifa na elimu yake na hivyo kujihakikishia mwenyewe thawab-l 'jari - thawabu zenye kuendelea

Wasomaji wanaombwa kusoma Surat al-Fatiha kwa ajili ya kumbukumbu yake.

3

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

UTANGULIZI

HII NI HISTORIA MPYA YA UISLAMU. Ni historia ya vuguvugu la Uislamu ambalo lilianzishwa na Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) mnamo mwaka 610 A.D. huko Makka, na ulikamilishwa kwa msaada wa binamu yake, mshiriki na mshikamakamu wake, Ali ibn Abi Talib, mnamo mwaka 632 A.D. hapo Madina. Inahusisha kipindi cha miaka tisini kuanzia 570 A.D. wakati yeye Muhammad alipozaliwa huko Makka, hadi mwaka 661 wakati mrithi wake, Ali ibn Abi Talib, alipouawa huko mjini Kufah.

Historia zisizo na idadi zimeandikwa huko nyuma na zitaandikwa wakati ujao. Maendeleo ya kuvutia ya Uislamu katika nyanja ya ulinganiaji katika nyakati zetu wenyewe; kufufu-ka upya kwa mataifa ya Kiislamu baada ya karne nyingi za usingizi mzito; kujidukiza kwa mafuta kama wakala mpya katika siasa za kidunia katika karne hii; bali juu ya yote na hivi karibuni kabisa, yale mafanikio ya Mapinduzi ya Kiislamu ndani ya Iran, yote Haya yanakuwa, kote Mashariki na Magharibi, kama vichocheo vya shauku mpya katika Uislamu. Mapinduzi ndani ya Iran yamechokonoa mlipuko wa dunia nzima wa mvuto katika Uislamu, na vitabu vingi vipya vinaandikwa juu ya somo hilo - na wote, Waislamu na wasiokuwa Waislamu.

Siku hizi wakati viongozi wa dunia ya Kikristo wanapofanya kazi kimyakimya ili kufanik-isha ndoto ya siku nyingi ya imani ya umoja wa Kikristo, Waislamu wengi pia wanaangalia nyuma kwa hamu kubwa kwenye lile taifa bora wakati Uislamu ulipokuwa mfumo wa mawazo ya aina moja. Uislam, hata hivyo, ulikuwa mfumo wa mawazo ya aina moja tu wakati wa uhai wa Mtume wake, Muhammad aliyebarikiwa. Mara tu alipofariki, ufa wa kwanza ulijitokeza katika ile "nguzo imara" ya Uislamu. Wafuasi wake - Waislamu -walikingamizwa kwenye makundi mawili. Katika kingamizo hili, wengi wa maswahaba zake walikuwa upande mmoja na watu wa nyumbani kwake kwa upande mwingine. Wakati watu wa nyumbani kwake wakiwa wameshughulishwa na mazishi yake, baadhi ya maswahaba zake walishughulika katika "kuchagua" kiongozi mpya wa kumrithi Mtume.

Katika ule mwanya kati ya kifo na mazishi yake, hili kundi la mwisho (la maswahaba) lil-ijikusanya katika banda la Saqifah hapo Madina, na likamchagua mmoja kati yao wenyewe kama mkuu mpya wa umma wa Waislamu. Wao, kisha wakawakabili watu wa ile familia iliyoondokewa kwa jambo lililokwisha fanywa na kuthibitishwa. Mkabiliano huu, kwa bahati mbaya sana, ukawa Sura ya kudumu ya historia ya Waislamu.

Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t,), Rehma na amani juu yake na juu ya Ahlul-Bayt wake, alitokana na ukoo wa Bani Hashim. Baada ya kifo chake mwaka632 A.D., binamu

4

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

yake, mkwe wake na mrithi mstahiki wake, Ali ibn Abi Talib, alimfuatia yeye kama mkuu mpya wa Bani Hashim. Wengi wa maswahaba wa Muhammad, Mtume wa Uislamu, walikuwa wamelea uadui wa siri juu yake. Hawakuweza kumuonyesha uadui wao wakati wa uhai wake Mtume lakini mara walipokuwa na amri juu ya serikali yake hapo Madina, walikuwa wameazimia, kutoiachia, kwa kukosea kwa namna yoyote ile, iangukie kwenye mikono ya Ali ibn Abi Talib. Watu wa nyumba ya Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) hivyo walizuiwa, kwa nguvu kubwa ya wanadamu, sio tu kwenye urithi wa moja kwa moja bali pia kwenye nafasi zote za mamlaka na madaraka katika serikali za wafuasi wake zilizofuatia.

Marafiki, wafuasi na wanaounga mkono nyumba ya Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.w.t.) wamekuwa kihistoria wakiitwa Shia; na marafiki, wafuasi na wanaowaunga mkono maswahaba, yaani, lile kundi lililofanikiwa kutwaa madaraka hapo Madina, limekuwa likiitwa Sunni. Nitayatofautisha pia makundi haya mawili kwa majina haya.

M. Shibli, mwanahistoria mashuhuri wa Kihindi wa Uislamu, anasema kwamba takriban historia zote za Uislamu zimeandikwa na wanahistoria wa Sunni. Kauli hii inamaanisha kwamba wanazuoni wa Shia hawakuandika historia yoyote ya Uislamu. Kwa nini hawakuandika? Hawakuandika historia kwa sababu ya wazi. Makhalifa wote, masultani na wafalme, wote walikuwa Sunni. Aliyekuwa Shia hakuweza kuchapisha ufafanuzi wa historia ya Kiislamu ambao ulikuwa unatofautiana na ule ufafanuzi wa kiserikali, na hakuwa na haja ya kuendeleza kile alichoamini kuwa ni upotoshaji wa ukweli. Yeye, kwa hiyo, aliamua kutoandika historia yoyote kabisa.

Kwa namna hii, yalikuwa ni yale "maelezo" ya kiserikali ya historia ya siku za mwanzo za Uislamu ambayo yalipata kuenea na yakapata kukubalika. Lilikuwa ni jambo la kimantiki kabisa la kufanya kwa serikali za karne za mwanzoni za Uislamu kuingiza kwenye mzun-guko, ile hekaya tu, ambayo ilikuwa inakubaliana na itikadi ya kundi lao. Ilikuwa pia na mantiki kabisa kwa wafuasi wa sera za serikali hizo tunazozizungumzia, kutii itikadi hiyo. Na katika kutii itikadi hiyo ya kundi, kama walihisi kwamba ni muhimu kufunika ukweli, au kwa kiwango chochote, kufunika ule upande mwingine wa Hadith hiyo, ilikuwa na mantiki kabisa kufanya hivyo.

Hakuna jambo lolote la ajabu, la kushangaza au kushitusha katika mwenendo wa wanahistoria wa Sunni. Kitu chenye mantiki kabisa kwao kukifanya kilikuwa, na bado ni, kutetea uhalali wa matukio ambayo yalitukia ndani ya Saqifah, ambamo baadhi ya maswahaba, katika shambulizi la kuwahi kabla ya wengine, walitwaa serikali ya Muhammad, kiongozi wa Arabia.

Kile ambacho hata hivyo ni cha kushangaza na cha kushitusha, ni kwamba wanahistoria wa kimagharibi, yaani, wale Mustashriq, wamemeza, kama jambo la kweli kabisa, kila

5

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ambalo wanahistoria wa "baraza" la Kiislamu limewachotea wao kama "ukweli." Hawa Mustashriq wanadhaniwa kwamba hawana upendeleo, sio wafuasi, na wasiohusika kwa jazba kwa hali yoyote ile. Matokeo ya mashindano fulani katika zama za kale za Uislamu, kwa njia moja au nyingine, yasingeweza kuleta tofauti yoyote kwao. Na bado, vitabu vya wengi wao vinaonyesha, sio ukweli bali ufafanuzi na propaganda za kundi lililokuwa madarakani. Kwa maana hii, kazi zao ni uigaji wa vile vitabu "vilivyotiwa msukumo" na kile Wakomunisti wanachokiita "jamii inayotawala" ya Waislamu.

Vitabu vya Mustashriq vinaweza kuwa na maana ya kisayansi tu kama watachukua ushau-ri wa mwanahistoria mashuhuri wa Hispania ya Kiislamu, Dr. J. A. Conde. Yeye anasema: "Namna ya msiba unaojiingiza wenyewe kwenye mambo ya wanadamu unaweza kuelekea kudai kwamba katika uhusiano wa matukio ya kihistoria, yale yenye umuhimu wa hali ya juu kabisa, yashuke kuvifikia vizazi vijavyo kupitia kwenye njia zinazotiliwa mashaka kwa haki kabisa, za simulizi zilizoandikwa na makundi yanayoshinda. Mabadiliko ya falme, mapinduzi ya maana kabisa na kuangushwa kwa falme maarufu za kiukoo yote hay a yanaelekea kuwajibika na kasoro hii.

Ilikuwa ni kutokana na Warumi kwamba historia ya kujitwalia kwao wenyewe iliandikwa; simulizi za upinzani wao na vita vya umwagaji damu dhidi ya wa-Carthaginia zimetufikia sisi kutoka kwao wenyewe; au kama waandishi wa Kigiriki nao pia wamelijadili suala hili, watu hawa walikuwa ni walipa kodi na wategemezi wa Roma, wala hawakuzificha zile sifa zisizostahili zilizokusudiwa kuunga mkono fadhila yake. Scipio kwa hiyo anaonekana kwetu kama mtu anayevutia sana kati ya mashujaa, lakini je, sio kwamba kwa kiasi fulani hivi, ni kwa sababu historia ya maisha yake ni kazi ya mashabiki na wasifiaji wake?

Ni kweli kwamba yule Hannibal mwenye daraja kubwa na maarufu hawezi kuonekana vinginevyo zaidi ya mashuhuri na kwenye heshima hata katika masimulizi ya maadui zake wabAya kabisa, lakini kama ile chuki isiyotulizika na sera za uchokozi za Roma zisingeamuru kuteketezwa kwa zile kumbukumbu za kisaliti (za wa-Carthaginia), jenerali huyu maarufu bila shaka angetokezea kwetu kwa sifa inay-otofautiana sana na ile iliyowasilishwa na yule mshenzi katili, aliye elezewa na Livy na kukubaliwa na wasomaji wake kama ndio taswira ya Hannibal.

Kwa hiyo utambuzi thabiti na wa haki unatukataza sisi kutosheka wenyewe na ushahidi wa upande mmoja tu. Hii inahitaji kwamba tulinganishe mahusiano ya makundi yote kwa uadilifu makini, na inatutaka sisi kuyaonyesha bila ya lengo jingine zaidi ya lile la kuugundua ukweli."

(History of the Dominion of the Arabs in Spain - kilichotafsiriwa kutoka kwenye ki-Hispania na Mrs. J. Foster, Juz. I, uk. 1)

 

6

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Haiwezi kupingika kwamba Mustashriq wengi wametoa michango isiyofaa kabisa kwenye uchunguzi, elimu na ufahamu wa Uislamu. Ni kutokana tu na jitihada zao kwamba hazina nyingi zisizo na thamani, za historia, fani na fasihi za Kiislamu zimeokolewa kutokana na kusahaulika, na zimekuwa zimehifadhiwa. Inawezekana kabisa kwamba hazina nyingi kama hizo zingeweza kupotea daima kama isingekuwa kwa juhudi zao za kuziokoa. Miongoni mwao kuna watu ambao wana ufahamu wa kushangaza wa kina wa mafunzo ya Kiislamu, na ambao elimu zao ni za ki-ensaiklopidia kwa upana. Wamesoma na kupata viwango vikubwa vya maelezo, na kisha wameyafupisha, wakayapanga na kuyahariri kati-ka uchambuzi wa kistadi na wa ukosoaji. Wengine wao wamejitolea maisha yao na mali zao kwenye uchunguzi wa Uislamu, na k wao wao ulimwengu wa Kiislamu una deni kubwa la shukurani.

Lakini licha ya mapenzi na hamu ya elimu, na kujifunga kwenye ukweli kwa wanafunzi wa Magharibi, inaonekana kwamba wakati wengi wao wanapoufafanua Uislamu, historia yake na sheria zake, jambo fulani huenda kombo. Ni vigumu kuamini lakini ni kweli kwamba baadhi yao wanaonyesha kushindwa kwa ajabu kupenyeza kwenye mwonekano wa kawaida na usiobadilika wa matukio kwenye mambo na nguvu, na ukweli ulio dhahiri ambavyo wakati mwingine vimefichwa kwa makusudi. Na baadhi yao wanashindwa hata kuona yaliyo dhahiri.

Nimenukuu hapo juu utaratibu wa kuandika historia ya kisa yansi na isiyo na upendeleo kama ulivyoelezwa na Dr. J. A. Conde, ambaye yeye mwenyewe ni Mustashriq maarufu sana. Kanuni hii, yaani ile ya, hakuna ubigwa wa hukumu na maamuzi katika historia, inat-ulia katika akili ya kwaida, na hauna kitu cha ajabu juu yake. Na bado, wengi wa Mustashriq wameyakubali, kwa wepesi wa kusadiki ambao ni wa kipumbavu, yale maelezo ya matukio yaliyotokea punde tu kufuatia kifo cha Muhammad (s.a.w.), kama yalivy-otolewa na lile kundi lililofanikiwa katika kujitwalia lenyewe utawala wake (Muhammad s.a.w.).

Mfano wa dhahiri wa uzuzu huo, na msingi wa kutotambua wa hawa Mustashriq, kuhusu suala hili, ni kule kukubaliwa na wao, kama "ukweli" wa kihistoria wa ile taarifa ya uwon-go kwamba Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) alifariki bila ya kumteua mtu yeyote kama mrithi wake, na kwamba aliliacha suala la kumtafuta kiongozi wa umma wa Waislamu kwenye hiari ya wafuasi wake wenyewe.

Hakuna Mustashriq aliyesita na kufikiria, kwa kiasi ninavyotambua mimi, ili kuchunguza kama hili ni kweli au kama ni lenye uwezekano wa kuwa kweli kwamba Muhammad ali-watelekeza Waislamu bila ya kiongozi, na ikawabidi kumpata kiongozi katika mfumo usio na mipaka na unaoruhusu kila mbinu, wa kikatili, huru kwa wote na kushindana kwa ajili ya madaraka. Ili kuepukana na kazi ngumu ya kutafuta ukweli, Mustashriq wamekubaliana tu na wanahistoria wa Sunni kwamba Muhammad, Mtume wa Uislamu, hakuwa na chaguo

7

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

au upendeleo katika suala la urithi wake mwenyewe; na lolote lililotokea ndani ya Saqifah kwa hiyo, lilikuwa ni sawa na halali, na pia lilikuwa kwa faida kubwa ya umma wa Waislamu.

Huu muegemeo wa uungaji mkono Saqifah wa Mustashriq umewaingiza kwenye njia ya upofu ambamo hawawezi kupata majibu ya maswali ya msingi katika historia ya Uislamu, na wanajikuta wenyewe wamenasa, kama walivyonasa wanahistoria wa Sunni, kwenye nyavu za ukweli wenye mashaka na hitilafu nyingi.

Wanahistoria wengi wa Sunni na wengi miongoni mwa Mustashriq wamefanya majaribio ya makusudi ya kuipunguza nafasi iliyochukuliwa na Ali ibn Abi Talib katika historia ya Uislamu. Wao, bila shaka, wanastahiki kwenye maoni na dhana zao hata kama hizi hazikuthibitishwa na ukweli. Katika uwasilishaji wangu, nimejitahidi kuweka mkazo juu ya ukweli. Kwa kufanya hivyo, imekuwa ni matumaini yangu kwamba ukweli wenyewe utachukua nafasi kama "muamuzi." Kwa vile ukweli ni "muamuzi" asiyekuwa na upendeleo, anaweza kutegemewa kurudisha uwiano kwenye uchambuzi wa nafasi zili-zochukuliwa na wahusika wakuu katika historia ya Uislamu mchanga. Nimeuchagua (ukweli) na nimeutunga pamoja, kama lulu, kwenye "mkufu", ili kwamba wingi wa ukweli huo uweze kuonekana mahali pamoja.

Historia haina mahakama ya juu inayotoa fatwa; inao waandika tarikh tu, wenye kuweza kukosea. Na bado, historia inaweza kupata mahakama yake ya juu yenyewe au mahakama isiyopendelea, kwenye mantiki ya ukweli.

Ninayo sababu nyingine na ya mawazo yakinifu ya kutegemea juu ya ukweli. Kwa kuandi-ka Hadith ya siku za mwanzoni za Uislamu, vipo vyanzo vikuu vitatu, navyo ni, Qur'an Tukufu (kitabu cha Uislamu kilichoteremshwa); Hadithi (kumbukumbu za matendo na maneno matukufu ya Muhammad, kama yalivyosimuliwa kwa sanad ya watoa habari au wasimulizi); na matukio kama yalivyoandikwa na wanahistoria wa Kiarabu. Kati ya vitatu hivi, kile cha kwanza, yaani, Qur'an, inakubaliwa na Waislamu wote kuwa ni takatifu kiasili. Kama mwislamu anapinga maandiko ya Qur'an, papo hapo anakuwa kafiri. Lakini wakati ambapo maandikoko ya Qur'an, kwa kadiri Waislamu wanavyohusika, Hayakuvunjwa, Aya zake ni zenye kupatwa mara kwa mara na hitilafu na wakati mwingine (na) tafsiri zinazopingana, na hakuna kitu kama makubaliano ambamo, au ambayo tafsiri zake ni sawasawa. Hadithi vilevile zinapatwa na kikwazo; nyingi sana kati ya hizo ni za bandia ingawa kuna baadhi ambazo zinakubaliwa na wote, Sunni na Shia kuwa ni sahihi. Nimejaribu kwa hiyo, kuwa mchaguzi katika kuzidondoa zile Aya tu za Qur'an na zile Hadithi (maneno ya Mtume) zenye maelezo ambayo tofauti kati ya Sunni na Shia ni ndogo sana. Lakini ukweli wa kihistoria ni eneo ambamo hakuna nafasi kubwa ya mfarakano. Nimefanya udondozi wa mara kwa mara sana, kutoka kote, kwa wanahistoria wa zamani na wa kisasa, katika kitabu hiki, mara nyingi juu ya suala au tukio hilohilo. Nimefanya

8

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hivyo ili kuwasilisha kwa msomaji zaidi ya hoja moja ya maoni au tafsiri zaidi ya moja ya matukio yenye umuhimu zaidi. Tukio hilohilo likiangaliwa kwa mitazamo tofauti huonekana tofauti kwa watazamaji mbalimbali na kwa hiyo, ni yenye kupatwa na tafsiri mbali mbali. Ni katika matumaini kwamba msomaji atashiriki katika maoni Haya ambayo nimejaribu, kwenye matukio mengi, kuacha zaidi ya mwanahistoria mmoja kuelezea kisa hicho hicho. "Wacha wataalamu waifanye kazi hiyo," umekuwa ndio wito wangu katika kutafsiri upya mambo muhimu ya historia ya Uislamu.

Sababu nyingine ya kwa nini nimewasilisha ushahidi wa wanahistoria kwa kiwango kikub-wa hivyo, ni kutegemeza tasnifu yangu na ushahidi, kiasi kwamba msomaji, kama akipen-da, aweze kurejea kwenye vyanzo ambavyo anaweza kuviona kama ni vya kuaminika kabisa.

Imesemekana kwamba kujasiri, kama kulivyo, katika kuchunguza yale yasiyojulikana, kupita kiasi, ni kutilia shaka yanayojulikana. Mengi ya yale yanayoitwa "mambo yanay-ofahamika" katika historia ya Uislam mchanga, ni dhana hasa za uchamungu au hata matakwa ya uchamungu ambayo kutokana na kung'ang'ania kurudiwa rudiwa na mlolon-go mrefu wa vizazi vya Waislamu, yamepata "mng'ao kama sio hadhi ya "masharti ya imani". Nilipozihoji baadhi ya dhana za Waislamu nyingi ambazo zinatambulika kama "ukweli" wa kihistoria, niligundua kwamba haziwezi kuhimili uchunguzi makini wa uchambuzi wa kukosoa. Msomaji mwenyewe anaweza kwa hiyo, kuamua kama atazishik-ilia hizo au atakubali ukweli ambao baadhi yake atauona ni mchungu sana na mkali. Kuna wale watu ambao huwa wanauogopa ukweli. Ukweli unatishia njozi zao, visa vyao wanavyopendelea, na dhana zao. Hivi (vilivyotajwa) vya mwisho, kutokana na ufananaji (wa mawazo) wa siku nyingi, vimezoeleka sana kwao kiasi kwamba wanahisi ni salama na vinatosha kuishi navyo bila ya "udukizi" wa ukweli. Wanalinganisha ukweli na "ukosefu wa usalama."

Hata hivyo, ukweli pekee ndio unaoweza kuwaletea wao usalama wa kweli. Ukweli ni laz-ima utetewe kwa gharama yoyoye ile, na watu wote, lakini hususan na wanahistoria. Ukweli lazima ukubaliwe hata kama unamuumiza rafiki na kumnufaisha adui. Uaminifu wa kwanza wa mwanahistoria lazima uwe ni ukweli, na lolote lile liwalo lazima lisimpo-toshe katika kuutafuta huo ukweli.

Vita vya mawazo na mgongano wa maoni unakuwa wa kuvutia sana pale ambapo mwenge wa uchunguzi unapogeuziwa mbali kutoka kwenye dhana za kifalsafa na itikadi dhahania za kisiasa kwenda kwenye tabia na mienendo ya (watu) shaksia ambayo ilifanya kazi muhimu katika matukio ambayo tunayachunguza. Historia huchimbuka kwenye uhai na uumbaji wa mhusika; inakuwa yenye kutikisika pamoja na watu wa kusawarika ambao "hufanya" matukio au kuyashughulikia au kuyapinga. (Wanaipamba) wanaiwekeza historia pamoja na elementi za "maslahi ya wanadamu", na mguso wa mfululizo wa mambo.

9

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Vyovyote vile historia iwavyo - ajali au vifo visivyozuilika, au shinikizo la hali ya maa-muzi ya kiuchumi, au vitendo vya viongozi wenye nguvu, au matokeo ya nguvu ambazo hakuna anayezijua, au matumaini ya pamoja ya watu - vyovyote historia iwavyo, Waarabu wenyewe wanaiona na kuitafsiri historia yao wenyewe zaidi kwa kigezo cha utendaji binafsi, kuliko kitu kingine chochote. Na wanaweza wakawa sahihi. Hata hivyo, kama ilivyo katika kila jitihada, historia inatengenezwa na wale wanaotenda. Inategemea, katika mwingiliano wake, sio wa nguvu zisizoeleweka bali wa wanadamu. Migongano ya historia sio ya kati ya dhahania za falsafa, uchumi au elimujamii, bali kati ya wanadamu. Imesemekana kwamba hata katika nyakati zake za kisosholojia, historia haiwezi kupuuza kipengele cha shaksia ya mwanadamu. Historia ya miaka 23 ya awali ya kazi ya Uislamu ambayo inajumuisha ujumbe wote wa Muhammad kama Mtume wa Allah (s.w.t.) imeten-genezwa kwa sehemu kubwa, karibu na yeye mwenyewe, na vitendo vya mshirika wake, Ali ibn Abi Talib.

Huu ndio ushahidi wa historia. Lakini ni ushahidi ambao wanahistoria wengi kwa kawai-da wamejaribu kuuficha. Ni kwenye ushahidi huu ambako nimejaribu kuvuta mazingatio ya wasomaji wa kitabu hiki.

Lakini licha ya kwenda upande kwa wakati uliopita na wakati wa sasa kwa uandishi wa historia wa kimagharibi juu ya Uislamu, kuna matumaini mapya kwamba wanahistoria wa wakati ujao watafanya marekebisho kwa ajili ya yaliyoachwa na mapungufu ya wanahistoria wa zamani. Wanachotakiwa kufanya tu ni kutokuwa na upendeleo, na kutokuyakubali kibubusa yale maelezo na maamuzi ambayo yamekuwa ni istiari iliyochakaa ya historia ya Uislamu, bali kuugundua upya ukweli wao wenyewe kupitia ulinganisho na uchunguzi wa ushahidi.

Katika utangulizi wa Cambridge History of Islamu, Juz. I, kilichochapishwa na University Press, Cambridge (1970), P.M. Holt anaandika hivi:

"Uchunguzi wa historia ya Uislamu sasa unapanuka, uhakika mwingi wa dhahiri wa uandishi wa zamani wa historia wa kimagharibi (mara nyingi unaoonyesha utetezi na maelezo ya wanahistoria wa mapokezi wa Waislamu) umepotea, na ni polepole kupitia utafiti wa kina ambapo ufahamu wa kweli zaidi wa mambo ya zamani unaweza kupatikana."

Uhakika wa uandishi wa zamani wa historia wa Kimagharibi unaoakisi utetezi na tafsiri ya wanahistoria wa mapokezi wa Waislamu haujapotea bado lakini natutegemee kwamba utapotea, na ufahamu wa kweli zaidi wa mambo ya zamani utapatikana kadiri siku zinavyokwenda.

Jitihada ya kuitafsiri historia ya Uislamu, hususan ile historia ya karne yake ya kwanza, ni kama kuingia kwenye eneo lililotegwa mabomu; kuchemka kwake na migogoro, lawama

10

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kali na ubishani, na mtu anaweza kulisogelea tu kwa tahadhari sana. Hata hivyo, tafsiri inabakia ya msingi kwa kuielewa historia. Bila ya tafsiri, historia inakuwa ni rundo la habari zisizoratibiwa na ni orodha ya matukio "yaliyokufa" na tarehe zisizo na uhusiano na kila mojawapo. Bado haya matukio "yaliyokufa" yanajirudisha nyuma kwenye maisha wakati athari zinapohusishwa na sababu, na uunganishaji wa mambo unapoanzishwa. Jambo linalohusiana na mambo mengine linakuwa na maana ya kihistoria; katika kuliten-ga kwake, linaweza kuwa halina maana kabisa.

Hata Nadharia ya Einstein ni kule kuielewa dunia sio kama mfululizo wa matukio bali kama mahusiano.

Kama ilivyoelezwa hapo juu, kuna vitabu vingi kupita kiasi juu ya Uislamu lakini vingi ya hivyo ni tafsiri zilizokaririwa za kisa cha kuzaliwa na kukua kwake, na uzoefu wake wa kidini, kama kilivyokabidhiwa kwa waandishi wake na wanahistoria wa baraza wa serikali ambayo ilizaliwa pale Saqifah, na serikali zake zilizofuatia - zile serikali za Damascus na Baghdad. Kisa hicho, hata hivyo, kina upande mwingine pia.

Kanuni ya sheria ya zamani ya Kirumi ilikuwa ni audi alteram partem - (katika mgogoro wowote ule, sikiliza na ule upande mwingine); au audiatur et alter a pars - (acha na ule upande mwingine usikilizwe). Tendo la pamoja la wanadamu - ambalo linaitwa siasa -limejaa misiba mingi, yenye kuvunja moyo ambayo imeyaharibu maisha ya kila mtu duni-ani. Mingi ingeweza kuepukwa kama sheria hii ingetiiwa na wote.

Utaratibu huu kwamba katika mgogoro wowote ule, pande zote katika suala hilo zina-paswa kusikilizwa - umefanywa ni kifungu madhubuti katika mifumo ya sheria ya mataifa mengi, lakini zaidi hasa katika ile ya Marekani na Ulaya Magharibi. Thomas Jefferson alikuwa akifafanua tu utaratibu huu, ambao bila ya huo hapawezi kuwepo na haki yoyote, wakati alipotamka kwa mshangao: "Tafadhalini sana, natusikilize kila upande kwa uhuru kabisa." Wanafunzi wa Uislam, wa Kimarekani na wa Ulaya, katika masuala mengi, wamesikia tu upande mmoja wa Hadith; kitabu hiki ni jitihada ya kuwasilisha ule upande mwingine. Ni pamoja na dhamira hii kwamba nikitoe kwa ajili ya uamuzi wa wasomaji wenyewe.

Kutoka kwenye woga unaonywea kwenye ukweli mpya; Kutoka kwenye uzembe ambao unaridhika na nusu-ukweli; Kutoka kwenye kiburi kinachodhani kinajua ukweli wote; Ewe Mungu wa Ukweli utuokoe!

11

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

JOGRAFIA YA ARABUNI

Ni makubaliano ya wanahistoria kuanza historia ya eneo kwa jografia yake. Wanafanya hivyo kwanza kwa sababu tamthiliya ya historia inaonyeshwa kwenye "uwanja" wa pazia lake la ki-jografia; na halafu tena kwa sababu ya kipengele kinachojulikana katika siasa za kijografia kama "utambuaji wa jografia". Imesemekana kwamba sio desturi nyingi nyingine zinaungana kuunda athari ambazo zikitendekea kupitia vizazi vinavyofuatana, hutengeneza tabia ya watu na dola, na tabia huchukua sehemu muhimu katika kuunda historia yao.

Peninsula (rasi) ya Arabia ndio chanzo cha Uislamu. Uislamu "umezaliwa" ndani yake humo, na "ukakua" ndani yake, na ulikuwa tayari "umekomaa" ulipotoka ndani yake.

Ilikuwa katika miji ya Kiarabu ya Makka na Madina ambamo utambulisho wa Uislamu fasaha ulikuzwa, na Uislamu kwa kweli "ulitengemaa." Ufahamu wa jografia ya Arabia, kwa hiyo ni muhimu sana kwa ajili ya kuelewa mkondo wa historia yake.

Ufuatao ni mukhtasari wa jografia ya peninsula ya Arabia: Arabia, kama eneo lolote jingine, ina namna ya mandhari inayonyoosha na kuwabadili wale wanaoishi ndani yake na wanaopita humo. Ni ardhi kavu, nzito isiyokalika, na iko au ilikuwa, mpaka kupatikana kwa mafuta, ni kikwazo cha kudumu cha uhai kwa umahiri wa mwanadamu.

Uhai wake humo ulitegemea uwezo wake wa kukubaliana nayo.

Kinyume na fikra za watu wengi, Arabia sio kwamba yote ni nyika ya mchanga. Ina sehemu kubwa tofauti katika umbo juu ya usawa wake wa ardhi, sehemu zake muhimu zikiwa ni mchanga wenye joto kali, milima yenye rangi ya urujuari, mabonde membamba yaliyo katikati, vilele vyake vya ajabu vinavyochoma kwenye anga ya shaba, mawe yenye kupukutika, nyanda ngumu, maumbile ya kushtusha ya miamba ya ki-jiometria na yenye umbo la pia, vichuguu vya mchanga vinavyohamahama daima na chemchemi na mazingi-ra ya maziwa, vijito na bustani.

Ingawa karibu sehemu kubwa ya usawa wa ardhi ya jangwani ni wazi na kame, Arabia ina sehemu nyingi ambazo zinaonekana vizuri kwenye mwanga wa picha. Zina mandhari nzuri za ajabu zenye mahadhi nzuri, zenye kutawala mawazo zenye kupumbaza na kuhadaa - uzuri wa mchanga laini, ambao kama mawimbi ya bahari, daima uko unatembea. Uzuri huu unafi-fia haraka zaidi kuliko uzuri wa nakshi za mti usio na maua na wenye manyoya kwenye ukungu, na hata zaidi ya theluji iliyodondoka mara. Mawimbi ya mchanga yamerefuka kufikia upeo wa macho na zaidi, katika dunia ya ukimya na utupu. Jua linaweka mabaka

12

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

yenye mwanga mkali juu ya mchanga, na upepo unafanya michoro ya kisanii ndani yake na kuifuta punde kidogo baadae. Hivyo upepo wakati wote unaumba, unaharibu na kuumba tena mandhari. Na mandhari haya, katika tash'bihi zake zisizo na ukomo yamezaliwa kutia nuru na kutoonekana katika hewa ya jangwani, na kuyeyuka bila kutambuliwa, Sura ya nchi inakuwa ikibadilika na kupata daima Sura mpya nyingi za ajabu, na inakuwa ikisogea bila kutabirika toka sehemu moja kwenda nyingine. Mchanga unaweza kurundikwa kuwa chuguu kubwa linaloweza kufikia zaidi ya mita 150 juu ya msingi wa mwamba. Kutegemea mwelekeo na nguvu ya upepo, vichuguu hivyo huchukua namna nyingi za maumbo kama mwezi muandamo wa sherehe au migongo mirefu iliyosambamba au mkusanyiko mkubwa wa milima kama piramidi ambayo inaweza kuitwa milima ya mchanga.

Ikiwa kama jangwa hilo linazo Sura nyingi, pia inazo hali nyingi, na nyingi zao hazitabiri-ki. Kitambo kimoja inaweza kuwa ya udanganyifu unaofaa na utulivu lakini kitambo kidogo tu kinachofuatia, inaweza kuwa na ghasia mbaya, rahisi kubadilika, yenye kuogofya na kutoaminika kama bahari iliyochafuka. Misafara mizima ya watu ngamia na farasi, inase-mekana kupotea ndani yake, imemezwa, kama kwamba na michanga katili yenye njaa.

Katika dhoruba ya mchanga ambayo inaweza kudumu kwa masiku kidogo, jua mwezi, nyota, kontua za Sura ya nchi na peo za macho vimefutiliwa mbali, na safu za mchanga zenye hasira zinazunguka ovyo ovyo, na kutoa vivuli vya kisanii (surreal) juu ya usawa wa jangwa linaloghadhibika. Katika kiangazi, jua la wima linatoa tufani ya joto ambayo huchoma ardhi kama iliyochomwa na mwenge wa moto, jangwa linakuwa lenye mgawanyiko wa element mbili - joto na mchanga. Wakati mwingine wimbi la vumbi lina-fuatiwa na manyunyu yenye baridi na upepo yanayoonyesha "pinde mbili" za mvua -upinde mkubwa ukiwa na mdogo zaidi kati yake. Hivyo kitisho na uzuri vyote vinapatana kwenye mzunguko wa maisha ya jangwani.

Lakini kuanzia upande mmoja hadi mwingine na daima, hilo jangwa linabakia kutengwa, kimya, baya, lisilostaarabika la kutisha na kuogofya; na linabakia limefunikwa katika hofu yake kuu na upweke. Baadhi ya watu wanaamini kwamba hili jangwa lenye mkanganyiko lina "muujiza" wake ambao kwa kina sana huwagusa watu. Ni kwa kuegemea kwenye pazia hili kwamba, Mwarabu - mtoto wa jangwa - alifikia kilele cha maisha yake.

Arabia ndio peninsula (rasi) kubwa duniani lakini Waarabu wenyewe wanaiita Jazirat-ul-Arab (kisiwa cha Arabia), ambayo kwa namna nyingine ndicho. Ikipakana upande wa Mashariki na Ghuba ya Uajemi, Kusini na bahari ya Arabia, na upande wa kaskazini na "bahari kuu ya mchanga" ya jangwa la Syria. Ki-umbo, Arabia ni ya pembe nne yenye eneo la maili mraba milioni 1.2. Pwani ya Bahari nyekundu kutoka Ghuba ya Aghaba upande wa kaskazini mpaka Bab-el-Mendeb upande wa Kusini, ina urefu wa maili 1,200; na kutoka Bab-el-Mendeb upande wa Magharibi hadi Ras-el-Hadd upande wa Mashariki ni karibu urefu huohuo.

13

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kwa Sura, Arabia ni uwanda wa juu, mkubwa unaonyanyuka taratibu kutoka Mashariki kwenda Magharibi.

Mbali na Yemem na mabonde yaliyotawanyika katika safu za milima ya Magharibi nchi yote ni ya mchanga na mawe, na kavu na iliyochakaa.

Ifuatayo ni migawanyiko ya Kisiasa ya peninsula ya Arabia (1992)

1. Falme ya Saudia.

2. Jamhuri ya Yemen

3. Usultani wa Oman

4. Umoja wa Falme za Kiarabu

5. Qatar

6. Bahrain

7. Kuwait.

Yafuatayo ni maelezo mafupi ya kila moja ya maeneo haya saba ya kisiasa:

1. Falme ya Saudia

Hii Falme ya Saudia inachukua maili za mraba 850,000 za peninsula ya Arabia. Idadi ya watu wake inakisiwa kuwa milioni kumi, na mji wake mkuu ni Riyadh.

Majimbo yake ya "Pwani" ni Hijaz na Asir kwenye bahari ya Red Sea. Uwanda mfinyu wa Pwani ya Tihama unakwenda sambamba na bahari nyekundu (Red Sea).

Miji pacha ya Makka na Madina iko mwenye jimbo la Hijaz. Hijaz kwa hiyo, ndio nchi takatifu ya Uislamu. Hesabu ya watu wa Hijaz inakadiriwa kuwa milioni mbili, na eneo lake ni maili mraba 135,000. Miji mikuu na miji ya kawaida ya Hijazi ni Jeddah, bandari ya Makka, na sehemu kuu ya kibiashara ya nchi hiyo; Yanbu, Bandari ya Madina; Ta-if, kituo cha mlimani kilichoko Kusini Mashariki ya Makka, na mji mkuu wa kiangazi wa falme hiyo; Khaybar, Tabuk na Tayma. Huu "Mpango kabambe" wa Uislamu ulikamilishiwa Hijaz, na historia ya kuzaliwa na kukua kwake kumefungamana bila kutengeka na jimbo hili kunakolifanya kitovu cha ulimwengu wa Kiislamu.

Asir ndio ukanda wenye rutuba kiasi wa nyanda za Pwani na milima upande wa Kusini Magharibi, Kaskazini mwa Yemen, wenye vilele vinavyonyanyuka kufikia futi 10,000, na mvua za kutosha kufanya kilimo cha matuta ya mkingamo. Kile kituo maarufu cha mlimani cha Abha na makazi muhimu ya kilimo ya Jizan yako Asir. Jizan ndio bandari ya Asir.

14

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Najd ni nyanda za juu za katikati ya Arabia yenye muinuko wa wastani wa futi 3,000. Hali inayotawala ya topografia (mandhari) yake ni ule mfumo wa milima uitwao Tuwayq. Riyadh, mji mkuu wa falme hii, upo Najd. Chemchemi za Buraydah na Hayil ziko sehemu ya Kaskazini ya Najd.

Al-Hasa au jimbo la Mashariki liko kwenye Ghuba ya Uajemi. Mafuta yote na gesi ya falme hii zipatikana katika jimbo hili. Linazo pia zile chemchemi maarufu za Hofuf na Qatif. Vituo vya kibiashara vinavyoongoza jimboni humu ni Al-Khobar na mji wa bandari wa Dammam. Miji mingine maarufu ni Dhahran na Ras Tanura.

Ruba'-al-Khali (upande wa wazi) ulioko Kusini ndio bonge kubwa la mchanga duniani linaloendelea, na linachukuwa eneo la maili mraba 250,000. Kwa Waarabu linajulikana tu kama "Ar-Ramal" (michanga). Kwa jumla ni jangwa lisilo na uhai, na ni moja kati ya sehemu ambazo ni pweke mno na kame za dunia. An-Nufud kaskazini mwa peninsula hii ndio jangwa kuu la pili katika Arabia. Lina eneo la maili mraba 30,000.

2. Jamhuri ya Yemen

Jamhuri ya Yemen iko Kusini na Kusini Magharibi ya peninsula ya Arabia, na idadi ya watu ya milioni kumi na moja na eneo la maili mraba 190,000. Ndio eneo pekee la peninsula hii linalopata mvua za monsuni, na kuifanya sehemu yenye rutba sana na yenye watu wengi. Mlima mrefu sana wa Arabia, an-Nabi Shu'aib, uko Yemen na unafikia urefu wa futi 12,350. Sana'a ndio makao makuu na mji mkubwa zaidi katika nchi hii. Upo katika muinuko wa futi 7200, na unafahamika kwa hali yake ya hewa ya kiafya nzuri. Aden ndio mji mkuu wa kibiashara. Al-Mocha, Al-Huhaydah, Ta'izz na Mukalla ni miji mingine mikuu. Sayun na Shibam ni miji ambayo ni maarufu kwa magorofa yake marefu.

3.   Falme ya Oman

Falme ya Oman inachukua pembe ya Kusini Mashariki ya peninsula ya Arabia na ina majimbo ya Oman na Dhafar. Ina idadi ya watu milioni moja na eneo la maili mraba 90,000. Muscat ndio makao makuu na Matrak ndio mji mkubwa zaidi.

4.Umoja wa Famle za Kiarabu (Imarati)

Jamhuri ya Falme za kiarabu inaudwa na nchi saba:

Abu Dhabi, Dubai, Ajman, Sharjah, Fujaira, Ras-el-Khaimah, na Ummul-Qawain. Zina jumla ya maili mraba 32,000 na idadi ya watu 500,000. Makao makuu ya umoja huo ni Abu Dhabi ambayo pia ndio kubwa zaidi na mji maarufu zaidi wa falme hizo.

15

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

5. Dola ya Qatar

Qatar ina eneo la maili mraba 4,250 na idadi ya watu 200,000. Makao makuu yake ni Doha. Qatar ina idadi ndogo zaidi ya watu katika dola yote ya Kiarabu.

6. Dola ya Bahrain

Bahrain ni mkusanyiko wa visiwa 30, vyenye eneo la maili mraba 240 kwa jumla, na idadi ya watu 300,000. Manama, mji mkuu wa dola hii, upo kwenye kisiwa cha Bahrain, na Muharraq ndio mji mkuu wa pili katika mkusanyiko huu wa visiwa.

7. Dola ya Kuwait

Kuwait ina maili mraba 6,200 kwa eneo na inayo idadi ya watu milioni 1.5. mji wa Kuwait ndio makao makuu.

Hali ya nchi

Ingawa Tropik ya Kansa inapita katikati ya peninsula ya Arabia, nchi hiyo sio ya joto jingi. Kiangazi chake ni kirefu na chenye joto jingi, chenye halijoto linalopanda hadi kufikia nyuzi joto 130 Farenhaiti katika sehemu nyingi. Vipupwe vyake ni vifupi na vyenye baridi. Mvua ni haba, zenye wastani wa inchi nne kwa mwaka. Pembe yake ya Kusini-Magharibi; hatahivyo, hupata mvua kubwa kiasi, kwa kadiri ya inchi ishirini.

Uotaji wa Mimea

Uotaji mimea kwa jumla umetawanyika sana kutokana na kukosekana mvua na kwa sababu ya kuwepo chumvi nyingi kwenye udongo. Miti halisi ni adimu sana na vichaka ni vya kawaida. Mimea yote imebidi ijitohoe yenyewe ili kukubaliana na hali ya kuwepo jangwa.

Mtende huota kila penye maji. Ndio mti maarufu unaopandwa sana katika peninsula yote. Matunda ya tende ndio zao kuu la Waarabu wengi, na mti wake unatoa mbao yenye thamani na mazao mengineyo. Miti aina ya Tamarisk na Acacia pia inapatikana katika sehemu nyingi za nchi hii.

Nafaka

Nafaka kuu za Arabia ni ngano, shairi, mahindi na ulezi. Kahawa inalimwa Yemen; na pamba kwa viwango tofauti huko Yemen na Oman. Matunda ya maembe yamelimwa kwa mafanikio katika Oasisi za jimbo la Al-Hasa la Saudi Arabia, na minazi inakua huko Oman. Misitu kama iliyopo Saudi Arabia, ni vikundi vichache vya miti ya mirende (junipers) katika nyanda za juu za Yemen.

16

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

IKOLOJIA (UHUSIANO WA VIUMBE NA MAZINGIRA) YA ARABIA

Sehemu muhimu ya Ikolojia ya peninsula ya Arabia ni maji.

Kuwepo au kutokuwepo kwake kumeiunda historia yake kwa kiwango kikubwa. Wakazi walivutiwa na eneo la Makka huko Hijazi kwa kuwepo kwa chemchemi iliyogunduliwa na Hajra, mke wa Nabii Ibrahim (a.s.) mama yake Ismail (a.s.) na aliiita kwa jina la "Zamzam".

Kwa kuhakikishiwa kupatikana kwa maji yake mazuri kwa misimu yote, waliujenga mji wa Makka kuizunguka hiyo chemchemi. Eneo la maji la jimbo hili linahusisha visima, mabubujiko na mibubujiko ya kasi. Eneo lote halina mito na vijito mbali na ule Hajat wenye urefu wa maili sitini ulioko Jamhuri ya Yemen. Lakini hata hiki sio kijito cha kudu-mu; kinakuwa kijito tu wakati mvua nyingi zinaponyesha kwenye bonde lake.

Kipengele kipya na chenye sehemu nyingi zenye umuhimu mkubwa katika siasa ya uchu-mi ni kuwepo kwa hazina kubwa ya mafuta katika peninsula ya Arabia. Mnamo 1900 peninsula yote ilikuwa na watu wachache, na ilikuwa kame, iliyokumbwa na umasikini na iliyotengwa.

Ilikuwa ni moja ya majimbo machache ulimwenguni takriban iliyokuwa haijaguswa na athari za Magharibi. Ndipo yalipokuja mafuta na kila kitu kikabadilika. Saudi Arabia ili-uza shehena yake ya kwanza mwaka 1923, na kisima chake cha kwanza cha mafuta kilichimbwa mwaka 1938. Ndani ya miaka michache, mapato ya mwaka kutokana na mafuta yalivuka dola milioni moja. Falme hiyo ilivuka kiwango cha dola bilioni moja mwaka 1970; dola bilioni 100 mwaka 1980.

Maisha ndani ya Saudi Arabia na katika ghuba ya Uajemi yalibadilishwa na athari za uta-jiri mpya mali za kustaajabisha, maendeleo ya haraka ya kiuchumi, kuwasili kwa wafanyakazi wa kigeni, ushawishi wa kimataifa pengine kimsingi zaidi kuliko maisha yamebadilika penginepo popote kwa wakati wowote katika uzoefu wa mwanadamu.

Utajiri wa mafuta unabadilisha Sura ya nchi katika sehemu nyingi za Saudi Arabia na nchi za Ki-sheikh za ghuba. Umefanya iwezekane kupata tekinologia ya kisasa ya kuvuta maji kutoka kwenye vina vikuu au kubadili maji ya bahari kwa kuyaondoa chumvi, na kuifanya ardhi kame kuwa ya kilimo kwa kutumia umwagiliaji. Kuigeuza ardhi kuwa ya kilimo pia kunabadilisha hali ya takwimu ya idadi ya watu, vifo na maradhi (demografia) ya peninsula hii. Makabila ya kuhamahama yanapata mizizi katika makazi ya kudumu popote

17

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

upatikanaji wa maji unapokuwa wa hakika. Mbinu za kisasa zaidi zinatumika katika kujaribu kudhibiti mwondoko wa mchanga na kuondoa hali mbaya ya mazingira.

Myama maarufu sana huko Arabia alikuwa ni ngamia. Ngamia wa kiarabu ni yule wa aina ya nundu moja, mbali na yule wa Asia ya kati mwenye nundu mbili (Bactrian). Huyu mwenye nundu moja (Dromedary) ana kwato bapa, pana zenye wayo nene yenye vidole ambazo hazizami kwenye mchanga, na anaweza kusafiri masafa marefu jangwani. Maziwa ya ngamia yalifanya sehemu muhimu ya mlo wa Waarabu wa jangwani, na manyoya yake waliyatumia kutengenezea mahema yao.

Ngamia, kwa hiyo, alikuwa na umuhimu wa lazima kwa uhai katika jangwa.

Lakini cha kushangaza na kustaajabisha, ngamia takriban ametoweka kutoka Saudi Arabia na nchi zote za Ki-sheikh za Ghuba ya Uajemi. William J. Polk anaandika kwenye kitabu chake, "Passing Brave" kilichochapishwa na Alfred A. Knopf, New York, mwaka 1973, hivi:

"Punde kabla ya kifo chake mwaka 1960, yule mchunguzi mkuu wa Kiingereza juu ya majangwa, St. John Philby, alibashiri kuwa ndani ya miaka thelathini, Arabia itakuwa haina ngamia. Alichekwa wakati huo, lakini leo inaonyesha ubashiri wake ungekuwa mkubwa mno. Ngamia na mtegemezi wake, yule mhamajihamaji, takriban wametoweka kutoka Arabia. Hivyo enzi hiyo iliyoanza karibu miaka 3,000 iliyopita pamoja na ufugaji wa ngamia, inaisha. Ngamia amefanya jukumu muhimu katika kuibuka kwa ustaarabu."

Magari makubwa ya dizeli, magari moshi na ndege za Jeti vimechukua nafasi ya ngamia na misafara yake imekuwa "haifai" katika Arabia.

18

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ARABIA KABLA YA UISLAMU

Katika kuandika historia ya Uislamu, ni kawaida kuanza na ukaguzi wa hali ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na ya kidini ya Arabia kabla tu ya tangazo la Muhammad (s.a.w.) la ujumbe wake kama Mtume wa Allah (s.w.t.)

Ndio mapatano ya pili ya wanahistoria (ya kwanza likiwa ni kutoa maelezo ya ki-jogografia ya eneo hilo). Nitazingatia mapatano haya, na nitachambua kwa ufupi, hali ya kijumla katika Arabia katika mwisho wa karne ya sita na mwanzo wa karne ya saba A.D.

Hali ya Kisiasa katika Arabia.

Sura inayoonekana sana ya maisha ya kisiasa ya Arabia kabla ya Uislamu ilikuwa ni kutokuwepo kabisa kwa mfumo wa kisiasa katika muundo wowote ule. Ukiiondoa Yemen iliyoko Kusini Magharibi, hakuna sehemu ya peninsula ya Arabia iliyokuwa na serikali kwa wakati wowote ule, na Waarabu kamwe hawakutambua mamlaka yoyote ile mbali na mamlaka ya machifu wao wa makabila yao. Haya mamlaka ya machifu wa kikabila hata hivyo, yaliegama, kwa namna nyingi, juu ya tabia na nafasi zao, na yalikuwa ya uungwana kuliko kisiasa.

Mwanafunzi wa kisasa wa historia anaona mshangao kwamba Waarabu wameishi, kizazi baada ya kizazi, karne baada ya karne, bila ya serikali ya aina yoyote ile. Kwa vile hapakuwa na serikali, hapakuwa na sheria na utulivu. Kanuni pekee ya nchi ilikuwa ni hali ya uhalifu. Kama inavyotokea, inapofanyika jinai, upande uliodhuriwa ulichukua hatua mikononi mwao, na ukajabiru kupitisha 'hukumu' kwa yule mwovu. Mtindo huu ulis-ababisha mara nyingi matendo ya ukatili wa kuogofya.

Kama Waarabu walifanya kiasi kidogo cha kujizuia, haikuwa ni kwa sababu ya wepesi wa hisia alizokuwa nazo juu ya maswali ya kweli na batili lakini ni kwa sababu ya kuhofia kuchochea visasi na mauaji ya kurithi kisasi. Mauaji ya kisasi cha kurithi yalimaliza vizazi vizima vya Waarabu. Kwa vile hakukuwepo na vitu kama polisi, mahakama au majaji, ulinzi pekee mtu alioweza kuupata kutokana na maadui zake, ulikuwa katika kabila lake mwenyewe.

Kabila lilikuwa na jukumu la kulinda watu wake hata kama walitenda maovu. Ukabila au 'asabiyya' (moyo wa kiukoo) ulichukua nafasi ya kwanza kabla ya maadili. Kabila lililoshindwa kulinda watu wake kutokana na maadui zao lilijihatarisha kwenye kebehi, kashfa na dharau. Maadili, kwa kweli hayakuingia kwenye picha mahali popote pale. Kwa vile Arabia haikuwa na serikali; na kwa vile waarabu walikuwa na utawala huria kwa

19

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

silika yao, walifungana katika mapigano yasiyokwisha. Vita ilikuwa ni desturi ya kudumu ya jamii ya kiarabu. Jangwa liliweza kuchukua idadi ndogo tu ya watu, na hali ya vita vya kikabila ilidumisha uthibiti mkali juu ya ongezeko la watu. Lakini Waarabu wenyewe hawakuiona vita katika mwanga huu. Kwao wao, vita vilikuwa burudani au kiasi mchezo wa hatari, au aina ya tamthiliya ya kikabila, iliyofanywa na wenye weledi (ubingwa), kwa mujibu wa mfumo wa kanuni za zamani na ushujaa, ambapo "watazamaji" walishangilia.

Amani ya kudumu haikuwa na mvuto kwao na vita vilitoa fursa ya kukwepa kazi ngumu na kutokubadilika kwa mwenendo wa maisha katika jangwa. Wao kwa hiyo walichochea msisimko wa mapambano ya silaha. Vita viliwapa fursa ya kuonyesha vipaji vyao katika kutupa mishale, ufundi wa kurusha panga na upandaji wa farasi, na pia, katika vita, wangeweza kujipatia sifa kwa ushujaa wao na wakati huohuo kuleta fahari na heshima kwa makabila yao. Kwa mara nyingi, Waarabu walipigana ili kupigana tu, ama iwepo au isiwepo sababu ya kuchochea vita.

Anasema G.E.Grunebaum:

"Katika karne ya kabla ya kuja Uislamu makabila yalitawanya nguvu zao zote katika vita vya kuviziana, wote dhidi ya wote."

(Classical Islam - A History 600-1258-1970)

Yale makabila ya wahamaji yalizunguka kwenye peninsula yote na kupora misafara na makazi madogomadogo. Misafara mingi na vijiji vilinunua kinga ya mashambulizi Haya kwa kulipa kiwango maalum cha fedha kwa watekanyara wa wahamaji.

Ni muhimu kuzingatia ule ukweli katika usiku wa kuzaliwa Uislamu hakukuwa na serikali katika ngazi yoyote katika Arabia, na ukweli huu unawezakuwa umeathiri kuinukia kwa Uislamu wenyewe. Ukosekanaji mzima wa serikali, hata katika hali ya kuanzishwa tu, ni kitu kisichokuwa cha kawaida kabisa kwamba kimeonwa na kutolewa maoni na mus-tashirik wengi, miongoni mwao ni:

D.S. Margoliouth:

"Arabia ingebakia ya kipagani angekuwapo mtu katika Makka ambaye angeweza kutoa pigo; ambaye angeweza kutenda. Lakini wengi wao, kama walivyokuwa wabaya wa Moham med, hapakuwa na mmoja wao aliyekuwa na ujasiri wa namna hii; na (kama ilivyoonekana) hapakuwepo na mahakimu kwa ujumla ambao kwao angeweza kushitakiwa."

(Mohammed and the Rise of Islam, 1971).

20

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Naye Maxime Rodinson asema:

"Mauaji ya halaiki yalibeba adhabu kubwa kwa mujibu wa sheria zisizoandikwa za jangwani. Katika utendaji waarabu huru walikuwa hawakufungwa na kanuni ya sheria zake kwa msaada wa jeshi la polisi. Ulinzi pekee wa maisha ya mtu ni ile hakika iliyowekwa na mila na desturi, ambayo ingenunuliwa kwa gharama kubwa. damu kwa damu na uhai kwa uhai. Kisasi cha kurithi, tha 'r, kwa kiarabu, ni moja ya misin-gi ya jamii ya kibedui."

(Mohammed, 1971) Asema Herbert J. Muller:

"Katika Arabia ya Mohammed hakukuwa na dola kulikuwa tu na makabila huru yaliyotangaa na miji. Huyu Mtume (s.a.w.) aliunda dola yake mwenyewe, na aliipa sheria tukufu iliyoandikwa na Allah (s.w.t.)"

(The Loom of History, 1958)

Watu wa Arabia walitokana na makundi mawili, wenye maskani na wahamiaji. Hijazi na Arabia ya Kusini ilitapakaa miji mingi midogo na mikubwa michache. Nchi yote iliy-obakia illikuwa na watu waliotapakaa wakitokana na Mabedui. Walikuwa nyuma katika dhana ya uraia na siasa lakini pia walikuwa ni chanzo cha wasiwasi na hofu kwa wale wenye maskani. Waliishi kama maharamia wa jangwani, na walikuwa na sifa mbaya kwa ubinafsi wao usiozuilika na vurugu zao za upambanuzi wa kikabila.

Yale makabila maarufu zaidi yalitumia kiwango maalum cha mamlaka katika maeneo yao husika. Katika Makka kabila lenye nguvu lilikuwa la Quraishi, katika Yathrib, makabila yenye nguvu yalikuwa ni yale makabila ya Kiarabu ya Aus na Khazraji, na makabila ya kiyahudi ya Nadhir, Qaynuqa'a na Quraydha. Maquraishi wa Makka walijiona wenye we ni bora kuliko Mabedui lakini hawa Mabedui walikuwa na dharau tu juu ya hawa watu wa mjini ambao kwao wao walikuwa ni "Taifa la wauza maduka tu".

Waarabu wote walikuwa na sifa mbaya kwa namna fulani ya tabia kama vile majivuno, kiburi na majisifu, ulipizaji kisasi na kupenda kwingi uporaji. Kiburi chao kilihusika kwa namna fulani na kushindwa kwao kuanzisha dola yao wenyewe. Walikosa nidhamu ya kisi-asa, na mpaka kuja kwa Uislamu, hawakutambua mamlaka yoyote kama ni yenye umuhimu mkubwa katika Arabia.

Walitambua mamlaka ya mtu aliyewaongoza kwenye uvamizi lakini angeweza kulaz-imisha utii wao ikiwa tu walikuwa na uhakika wa kupata mgao mzuri wa ngawira, na mamlaka yake yaliisha mara tu shughuli hiyo ilipokwisha.

21

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hali ya kiuchumi

Kiuchumi, Wayahudi ndio waliokuwa viongozi wa Arabia. Walikuwa ndio wenye ardhi nzuri yenye kulimika katika Hijazi, na walikuwa wakulima wazuri zaidi nchini humo. Walikuwa pia ndio wawekezaji wa vile viwanda vilivyokuwepo katika Arabia wakati huo, na walikamata ukiritimba wa utengenezaji wa zana za kivita.

Utumwa ulikuwa ni asisi ya kiuchumi ya Waarabu. Watumwa wa kiume na wa kike wali-uzwa na kununuliwa kama wanyama, na waliunda tabaka la waliokandamizwa zaidi katika jamii ya kiarabu.

Tabaka lenye nguvu zaidi, la waarabu, liliundwa na mabepari na wakopeshaji fedha. Viwango vya riba walivyotoza kwenye mikopo vilikuwa vikubwa mno, na viliundwa maalum kuwafanya matajiri zaidi na zaidi, na wale wakopaji kuwa masikini zaidi.

Vituo maarufu zaidi vya mjini katika Arabia vilikuwa Makka na Yathrib, vyote katika Hijazi. Wakazi wa Makka zaidi walikuwa ni wafanyabiashara, wachuuzi na wakopeshaji wa fedha.

Misafara yao ilisafiri wakati wa kiangazi kwenda Syria na wakati wa kipupwe kwenda Yemen. Walisafiri pia kwenda Bahrain upande wa Mashariki na Iraq upande wa Kaskazini Mashariki. Misafara ya biashara ilikuwa msingi wa uchumi wa Makka, na kuiendesha kwake kulihitaji ujuzi, uzoefu na uwezo.

R.V.C. Bodley asema:

"Kuwasili na kuondoka kwa misafara kulikuwa ni matukio muhimu katika maisha ya watu wa Makka. Karibu kila mmoja ndani ya Makka alikuwa na namna ya kitega uchumi katika ile mali ya maelfu ya ngamia, mamia ya watu, farasi na punda walioon-doka na ngozi za wanyama, zabibu kavu na minara ya fedha na kurudi na mafuta, manukato na bidhaa mbalimbali kutoka Syria, Misri na Fursi (Persia), na viungo na dhahabu kutoka upande wa Kusini."

(The Messenger, 1946, Uk. 31)

Huko Yathrib, Waarabu waliendesha maisha yao kwa kilimo na Wayahudi waliendesha maisha yao kama wafanyabiashara na wanaviwanda. Lakini Wayahudi hawakuwa wafanyabiashara tu na viwanda; miongoni mwao pia walikuwepo wakulima wengi, na wameileta ardhi nyingi mbovu kwenye kulimika. Kiuchumi, kijamii na kisiasa, Hijazi ilikuwa ndio sehemu mashuhuri zaidi katika Arabia mwanzoni mwa karne ya saba.

22

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Francesco Gabrielli anasema:

"Katika mkesha wa Uislamu, watu wenye kujishughulisha mno na walioendelea wa Arabia waliishi katika mji wa Maquraish. Wakati wa himaya za Arabu ya Kusini za Petra na Palmyra ulikuwa umepita kwa muda kiasi katika historia ya Arabia. Sasa hali ya baadae ilikuwa inaandaliwa hapo katika Hijazi."

(The Arabs - A Compact History-1963)

Waarabu na Wayahudi wote walikula riba. Wengi miongoni mwao walikuwa wala riba wajuzi; waliishi kwa riba waliyotoza kwenye mikopo yao.

E.A.Belyaev anaeleza:

"Riba ilitumika sana Makka, kwani ili kushiriki katika msafara wenye faida, watu wa Makka wengi waliokuwa na kipato cha wastani walikimbilia kwa wala riba; mbali na riba kubwa, angeweza kutegemea kupata faida baada ya kurudi salama kwa msafara. Wafanyabiashara matajiri zaidi walikuwa wachuuzi na wala riba.

Wakopeshaji fedha kwa kawaida walichukua dinari kwa dinari, dirham kwa dirham, kwa maneno mengine, asilimia mia moja ya riba. Katika Qur'an 3:125, Allah (s.w.t.) akiwaambia waumini, alisema: 'Msile riba mara mbili maradufu.' Hii ingeweza kumaanisha kwamba riba ya asilimia mia mbili au hata mia nne ilidaiwa.

Nyavu za riba ya Makka hazikuwakamata wakazi wenzao tu na wa makabila yao bali pia watu wa makabila ya Ki-Bedui ya Hijazi walioshugulika katika biashara ya Makka. Kama katika Athens ya zamani "njia kuu za kukandamiza uhuru wa watu zilikuwa ni pesa."

(Arabs, Islamu and the Arab Caliphate in Early Middle Ages, 1969)

23

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

HALI YA USTAWI WA JAMII

Arabia ilikuwa ni jamii iliyoshikiliwa na wanaume. Wanawake hawakuwa na hadhi ya aina yoyote zaidi ya kuwa bidhaa za ngono. Idadi ya wanawake mtu anayoweza kuoa haikukadiriwa. Mwanaume alipokufa, mwanae 'alirithi' wake zake wote isipokuwa mama yake mzazi tu.Tabia ya kikatili ya Waarabu ilikuwa ni kuwazika watoto wao wa kike wachanga wakiwa hai. Hata kama Mwarabu hakutaka kumzika binti yake akiwa hai, alikuwa bado lazima adumishe mila hii ya 'heshima' kwa vile hana uwezo wa kuhimili shinikizo la jamii.

Ulevi ullikuwa ni mazoea mabaya ya kawaida ya Waarabu. Ulevi wao ulifuatana na uchezaji kamari wao. Walikuwa walevi waliokithri na wacheza kamari waliokubuhu. Mahusiano ya jinsia zao yalikuwa yamelegea sana. Wanawake wengi waliuza mapenzi kupata maisha yao kwa vile kulikuwa na kidogo sana kingine ambacho wangeweza kufanya. Wanawake hawa walipeperusha bendera kwenye nyumba zao na waliitwa "mabibi wa bendera" Dhaat-ur-rayyat).

Sayyid Qutb wa Misri katika kitabu chake, Milestone kilichochapishwa na International Islamuic Federation of student organizations, Salimiah, Kuwait mnamo 1978 (uk; 48,49), amemnukuu yule mpokezi wa Hadithi mashuhuri, Imam Bukhari, juu ya desturi ya ndoa katika Arabia kabla ya Uislamu kama ifuatavyo:

"Shihab (az-Suhri) amesema: 'Urwah b. az-Zubayt alimfahamisha yeye kwamba Aisha, mke wa Mtume (s.a.w.) alimjulisha kwamba ndoa wakati wa Ujahilia zilikuwa za aina nne:

1.        Moja ilikuwa ni ndoa ya watu kama ilivyo hivi sasa, ambapo mtu anamfungia uchumba mtoto wa kulea au binti yake kwa mtu mwingine, na huyu mwingine anatoa mahari kwa binti kisha anamuoa.

2.        Aina nyingine ilikuwa pale ambapo mtu alimwambia mkewe akiwa ametakasika kutokana na hedhi, 'Nenda kwa N. (yaani fulani) na muombe kufanya ngono naye;' kisha mumewe anakaa mbali naye na hamgusi kabisa mpaka iwe wazi kwamba ana mimba kutoka kwa mwanaume mwingine aliyefanya naye ngono.

Inapodhihirika kwamba anayo mimba, mumewe anafanya naye ngono kama akipen-da. Anafanya hivyo kwa sababu tu ya kutaka kupata mtoto mwenye daraja (mwema). Aina hii ya ndoa ilijulikana kama nikah al-Istibda (ndoa ya kutafuta ngono).

24

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

3.  Aina nyingine ilikuwa pale ambapo kikundi cha wanaume chini ya kumi (raht) walipomtembelea mwanamke huyo huyo na wote wakawa wamefanya ngono naye. Kama alipata ujauzito na kuzaa mtoto, wakati mausiku kadhaa yalipopita baada ya kumzaa, aliwaita wote, na hakuna mmoja wao angeweza kukataa. Walipofika wote mbele yake, huwaambia 'Ninyi' mnajua matokeo ya matendo yenu; nimezaa mtoto na ni mwanao wewe, akimtaja anayemtaka kwa jina lake. Mtoto wake anaambatanishwa kwa mwanaume huyo, naye hangeweza kukataa.

4.  Aina ya nne ni wakati ambapo wanaume wengi wanapomuendea mwanamke mmoja mara kwa mara, na haepukani na yoyote anayemjia. Wanawake hawa ni malaya (baghaya). Walitumia kuweka mabango milangoni kwao kama ishara. Yeyote aliye-wataka wao aliwaingilia.

Kama mmoja wao alishika mimba na akazaa mtoto, walijikusanya (wanaume) wote kwake na kumuita mtaalamu wa utambuzi wa Sura (physiognomist). Kisha wal-imuambatanisha mtoto huyo kwa mwanaume ambaye wamemfikiria ndio baba, na mtoto alibakia ameambatanishwa kwake na aliitwa mwanae, hakuna pingamizi lolote kwa mwenendo huu lililoweza kufanyika.

Alipokuja Muhammad (s.a.w.w) kuhubiri haki alivunja aina zote za ndoa za ujahilia isipokuwa ile watu wanayotumia leo.

25

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

HALI YA DINI KATIKA ARABIA YA KABLA YA UISLAMU

Kipindi katika historia ya Arabia kilichotangulia kuzaliwa kwa Uislamu kinajulikana kama Wakati wa Ujahilia. Kuamua kutokana na zile imani na matendo ya wapagani wa Kiarabu, inaonekana kwamba lilikuwa ndio jina linalostahili. Waarabu walikuwa wafuasi wa "dini" mbalimbali ambazo zinaweza kupangwa katika makundi yafuatayo:

1. Waabudu-Masanamu au Washirikina

Waarabu wengi walikuwa wakiabudu masanamu. Waliabudu masanamu mengi na kila kabila lilikuwa na lakwao sanamu au masanamu na miungu yao. Al-Kaaba huko Makka, ambayo kutokana na Hadith, ilijengwa na Nabii Ibrahim (a.s) na mwanae, Ismail (a.s) na wao waliitoa Wakfu kwa ibada za Mungu Mmoja, wameigeuza kuwa hekalu la mapagani na dini zote, likihifadhi masanamu 360 ya mawe na miti.

2.   Walahidi (Atheists)

Kundi hili lilikuwa limeundwa na wayakinifu nao waliamini kwamba dunia ilikuwa ya milele.

3. Wazandiki

Waliathiriwa na imani ya Kiajemi ya upili katika desturi. Waliamini kwamba kuna miungu wawili wanaoziwakilisha zile nguvu pacha za wema na uovu au mwanga na giza, na wote wamefungwa katika vita isiokwisha ya ukubwa.

4.Wa-Sabai

Waliabudu nyota

5. Wayahudi

Warumi walipoibomoa Jerusalem mwaka 70 A.D. na kuwatoa Wayahudi nje ya Palestana na Syria, wengi wao walipata makazi mapya huko Hijazi Arabia. Chini ya athari zao, waarabu wengi pia walikujageuka kuwa kwenye dini ya uyahudi. Vituo vyao vyenye nguvu vilikuwa katika miji ya Yathrib, Khaybar, Fadak na Ummu-ul-Qura.

26

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

6. Wakristo

Warumi waliwageuza kabila la Ghassan la Arabia ya Kaskazini kuwa wakristo. Baadhi ya koo za Ghassan zilihamia na kufanya makazi huko Hijazi. Huko Kusini, kulikuwa na wakristo wengi ndani ya Yemen ambapo imani hii ililetwa mwanzoni na wavamizi wa Ethiopia. Kituo chao chenye nguvu kilikuwa mji wa Najran.

7.Waamini Mungu Mmoja

Kulikuwa na kikundi kidogo cha waaminio Mungu mmoja kilichokuwepo Arabia katika usiku wa kuchomoza Uislamu. Wanachama wake hawakuabu-dia masanamu, na walikuwa wafuasi wa Nabii Ibrahimu (a.s). Watu wa famil-ia ya Muhammad (s.a.w.), Mtume wa baadae, na Ali bin Abi Twalib, Khalifa wa baadae, na watu wengi zaidi wa ukoo wao - Bani Hashim - walikuwa kwenye kundi hili.

27

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ELIMU MIONGONI MWA WAARABU KABLA YA UISLAMU

Miongoni mwa Waarabu walikuweko watu wachache sana walioweza kusoma na kuandi-ka. Wengi wao hawakuwa na shauku sana ya kujifunza fani hizi. Baadhi ya wanahistoria wana maoni kwamba elimu ya watu ya wakati ule takriban ilikuwa ya simulizi tu. Wayahudi na Wakristo walikuwa ndio watunzaji wa elimu kama hiyo ambayo Arabia ilikuwa nayo.

Elimu ya taaluma kubwa kamilifu ya wapagani wa Kiarabu ilikuwa ni ushairi wao. Walidai kwamba Mungu alijaalia Ubora usiokifani, wa kichwa, juu ya Wagiriki (ushahidi wake ni sayansi na falsafa yao); wa mikono, juu ya Wachina (ushahidi wake ni ufundista-di wao); na wa ulimi kwa Waarabu (ushahidi wake ni ufasaha wao). Fahari yao kubwa, nyakati zote kabla na baada ya Uislamu, ilikuwa ni ule ufasaha wao katika ushairi. Umuhimu wa mashairi unatathminiwa kama ifuatavyo:

Amesema D.S. Margoliouth:

"Katika Arabia ya kuhamahama, washairi walikuwa sehemu ya zana za kivita kwa kabila lao; walitetea kabila lao, na kuponda yale makabila ya maadui kwa kutumia nguvu iliyopaswa hasa kufanya kazi kiajabu, lakini ambayo kwa kweli ilitokana na kutunga vifungu mahiri vya namna ambayo ingeweza kuvutia uhakiki, na hivyo ingeweza kuenea na kukumbukwa sana.

(Mohammad na Kuchomoza Uislamu, 1931) E.A. Belyaev naye asema:

"Taarifa nyingi juu ya hali ya uchumi, utawala wa jamii na mengi ya Waarabu katika karne ya tano na ya sita A.D., zinatokana na mashairi ya kale au kabla ya Uislamu, yanayojulikana kwa 'uaminifu wa kipicha' kwa Sura zote za maisha ya kikabila ya Arabia na mazingira yake. Wataalam kwa hiyo, wanaukubali ushairi huu kama 'muhimu sana na chanzo cha kuaminika kwa kuelezea Waarabu na desturi zao katika kipindi hiki."

(Arabs, Islam and the Arab Caliphate in the Early Middle Ages, 1969)

28

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mashairi ya Kiarabu yalikuwa na utajiri katika ufasaha na matumizi ya tamathali za usemi katika mazungumzo au maandishi, lakini yalikuwa na ukomo wa masafa, na yalikuwa na upungufu wa maana. Maneno yaliyomo yaweza kuwa ya kuvutia lakini yalikuwa chapwa! Kazi bora za mashairi yao takribani hufuatia kabisa utaratibu uleule wa fikira na mawazo. Hata hivyo yalikuwa ni kioo cha uaminifu katika maisha ya zamani ya uarabuni. Vile vile katika kuchimbua sanaa ya ushairi, washairi wa kiarabu kwa hadhari walikuwa wakien-deleza moja ya sanaa kubwa za binadamu - lugha ya Kiarabu.

Utungaji mkubwa wa mapagani wa Kiarabu ni ule ulioitwa "Golden Odes", mkusanyiko wa mashairi saba, yakidhaniwa ya ubora usiopitwa, yenye nguvu na ufasaha. Yalitundikwa ndani ya Al-Kaaba kama changamoto kwa yeyote mwenye kutamani kuyapita au kulin-gana nayo. Sir William Muir anaandika kuhusu mashairi Haya kama ifuatavyo:

"Mashairi saba yaliyotundikwa yalikuwa hai kuanzia hata kipindi kilichomtangulia Muhammad, kielelezo cha kushangaza cha ufasaha usio hila. Uzuri wa lugha na utajiri wa kuenea haraka wa matumizi ya tamathali za usemi katika mazungumzo na maandishi unakubaliwa na wasomaji wa ulaya, lakini somo la mshairi liliwekewa ukomo, na yale yasiyo ya kawaida yalikengeukwa.

Haiba ya kimada wake, baka la kuonewa wivu lililowekwa na dalili za karibuni za kambi yake, na upweke wa makazi yake (huyu kimada) yaliyotelekezwa, ukarimu na ushujaa (wa mwenye kimada), heshima isiyo na upinzani wa kabila lake, sifa nzuri za ngamia wake - hizi zilikuwa ndio mada ambazo, pamoja na tofauti ndogo katika uten-daji, na bila hila yoyote ya njama au Hadith, zilitawala ndoto za Mwarabu - na baad-hi ya hizo ziliongeza mafuta kwenye mazoea mabaya ya kudumu ya watu, makuu, uhasidi, kisasi na majivuno."

(The life of Mohammed, 1877)

Pamoja na kutokeza kwa Uislamu, msisitizo ulihamishwa kwa muda, kutoka ushairi kwen-da nathari na ushairi ukapoteza nafasi yake ya ukubwa na hadhi kama vile "Malikia" wa sanaa za Arabuni. "Utungaji" mkubwa wa Uislamu ulikuwa ni Qura'n Tukufu, Kitabu cha Uislamu na kilikuwa katika nathari. Waislamu huamini kwamba Qur'an "iliandikwa" Mbingnii kabla ya kuteremshwa kwa Muhammad, Mjumbe wa Mungu.

Wanaamini kwamba kipaji cha mwanadamu kamwe hakiwezi kutoa kitu chochote amba-cho kinaweza kulingana na mtindo wake au yaliyomo ndani yake. Kwa vizazi kumi na tano vilivyopita, imekuwa kwao mtindo wa maandishi, filosofia, theologia, sheria, metafisikia na mawazo ya kimafumbo.

29

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Jaribio limefanyika katika kurasa zilizopita kufafanua hali ya kawaida ya Arabia na aina ya maisha ya Waarabu kabla ya Uislamu. "Taaswira" hii ni halisi kama ilivyochorwa kutoka kwenye "nyaraka" za Waarabu wenyewe wa kabla ya Uislamu.

Tukiamua kutokana na Taaswira hii, inaonyesha kwamba Arabia kabla ya Uislamu ilikuwa haina vistawishi vya kijamii au historia ya kina, na Waarabu waliishi katika taflisi ya maadili na utumwa wa kiroho. Maisha kwao yalikuwa hayana maana, lengo na mwelekeo. Moyo wa ubinaadamu ulikuwa kwenye minyororo, na ulikuwa ukisubiri, kama ilivyokuwa, ishara ya kufanya jitihada kubwa mno, ya kujinasua na kuwa huru.

Ishara hiyo ilitolewa mwaka 610 A.D. na Muhammad, mwana wa Abdillah, katika mji wa Makka, alipotangaza ujumbe wake wa Utume, na akaanzisha harakati iliyoitwa Uslamu katika kazi yake ya kuzunguka dunia.

Uislamu ulikuwa ndio neema kubwa kwa mwanadamu daima uliwaweka huru wanaume na wanawake, kupitia utu kwa Muumba wao, kutokana na utumwa katika udhahiri wowote. Muhammad, Mtume (s.a.w.) wa Allah. (s.w.t.) alikuwa ndio mkombozi mkuu wa wanadamu. Yeye alimnasua mwanadamu kutoka kwenye "Mashimo ya Maisha"

Peninsula ya Arabia ki-jiogorafia ilikuwa pembezoni na kisiasa, eneo lisilojulikana mpaka mwanzoni mwa karne ya saba A.D. Ni wakati huo ambapo Muhammad (s.a.w.) alipoiwe-ka kwenye ramani ya kisiasa ya dunia kwa kuifanya uwanja wa matukio ya maana sana ya historia.

Kabla ya Uislamu, Waarabu walishika nafasi ya pembeni tu katika historia ya Mashariki ya kati, na wangebaki daima taifa la watu wanaodhani kila kitu kina roho, na wachunga kondoo kama Muhammad (s.a.w.) asigewapatia kiini na kichocheo kilichoyaunganisha makabila yao ya kihamajihamaji yaliyokuwa yametawanyika, kwa nguvu yenye kujiende-sha, yenye lengo maalum. Alitengeneza "taifa" kutoka kwenye bonge lenye mashimoshi-mo lisilokuwa na umbo la msingi. Aliwapamba Waarabu na nguvu mpya, udhanifu na kipaji cha ubunifu, na walibadili mwelekeo wa historia.

Alianzisha elimu ya viumbe na mazingira ya akili na falsafa mpya kabisa, na kazi yake ili-weka kipindi cha waziwazi kaitka historia ya ulimwengu; na ilikuwa ni mwisho wa enzi moja na mwanzo wa nyigine.

Akiandika kuhusu njiapanda hii katika historia, Francesco Gabrieli anasema katika kitabu chake, The Arabs - A Compact History, (1963):

"Ndivyo ilivyokoma dibaji ya kipagani katika historia ya watu wa Arabia. Yeyote anayeilinganisha na yaliyofuata, yaliyowapa Waarabu nafasi ya msingi katika jukwaa

30

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

la dunia, na kutia msukumo mawazo makubwa na kazi kubwa, sio tu kwa mtu asiye wa kawaida aliyeibuka kutoka miongoni mwao, bali kwa tabaka la wasomi wote, ambalo kwa vizazi vingi lilikusanyika na kutangaza neno lake, (mtu) hawezi ila kutambua mruko wa majaaliwa ya watu hawa unavyoanza hapa. mpaka hapo utarat-ibu wa maisha yake, ya udhaifu na yaliotawanyika, yalipata umoja, kituo cha kusuku-ma mbele, lengo na yote Haya chini ya ishara ya imani ya dini.

Hakuna upendo wa ajabu wa mambo ya kale unaoweza kutufanya tushindwe kutambua kwamba bila ya Muhammad (s.a.w.) na Uislamu, yumkini huenda wangebakia bila akili kama mimea kwa karne nyingi humo jangwani, wakijiangamiza wenyewe katika utoaji damu wa vita zao zenye kuleta madhara kwa pande zote, wakiwaangalia Byzantium, Ctesiphon na hata Axum kama mianga mikubwa ya kujulisha habari za ustaarabu iliyoko nje kabisa ya uwezo wao."

31

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

HASHIM - KABLA YA KUZALIWA UISLAMU

Katika karne ya tano (A.D). mtu aliyeitwa Qusay, alizaliwa katika kabila la Quraish. Alipatia heshima kubwa na umaarufu kwa kabila lake kwa ajili ya hekima zake. Aliijenga upya Al-Kaaba iliyokuwa katika hali ya kukatisha tamaa, na aliwaamuru Waarabu kujen-ga nyumba zao kuizunguka. Alijenga pia "ukumbi wa mji" wa Makka, wa kwanza katika Arabia. Viongozi wa koo mbalimbali walikusanyika katika ukumbi huu kutafakari juu ya maswala yao ya kijamii, kibiashara, kiutamaduni na kisiasa. Qusay aliunda sheria juu ya kugawa chakula na maji kwa Mahujaji waliokuja Makka, na aliwashawishi Waarabu kuli-pa kodi kwa ajili ya msaada wa huduma zao.

Edward Gibbon anasema:

"Qusay, aliyezaliwa takriban A.D. 400, ni babu yake mkubwa Abdul-Muttalib, na hivyo wa tano katika kizazi cha kupanda toka Muhammad, alipata mamlaka makub-wa huko Makka.

(The decline and Fall of the Roman Empire)

Qusay alifariki mwaka 480 A.D., na mwanae, Abd Manaf, alitwaa madaraka ya kazi zake. Na yeye pia alijipatia sifa kutokana na uwezo wake. Alitambulika kwa ukarimu wake na maamuzi yake mazuri. Alifuatiwa na mwanae Hashim. Ni huyu Hashim aliyeupa ukoo wake jina lake uliokuja kuwa maarufu katika historia kama Bani Hashim. Hashim alikuwa ni mtu wa namna ya pekee. Alikuwa ni yeye aliyewafanya Maquraishi kuwa wafanyabi-ashara na wakawa wafanyabiashara bora. Alikuwa ndiye mtu wa kwanza kuanzisha zile safari mbili za misafara ya Maquraish, ya kiangazi na kipupwe, na wa kwanza kuandaa tharid (mchuzi) kwa Waarabu. Lakini kwake yeye, Waarabu wangeweza kubakia wachun-ga kondoo daima.

Uongozi wa uongofu na wema na ukarimu zilikuwa ni mbili tu kati ya sifa nyingi ambazo Muhammad, nabii wa baadaye, "alizorithi" toka kwa mababu zake. Hashim alioa mwanamke wa Yathrib na kutokana naye alipata mtoto wa kiume - Abdul-Muttalib. Kwa wakati upasao, Abdul Muttalib alikuwa amrithi baba yake kama mkuu wa ukoo wa Hashim.

32

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Edward Gibbon:

"Huyu babu yake Muhammad (Abdul Muttalib), na nasaba yake ya jadi, wanaonekana katika kumbukumbu za kigeni na za ndani kama mabwana (wafalme) wa nchi yao; lakini walitawala, kama Percales huko Athens, au Medics huko Florence, kwa maoni ya hekima zao na msimamo; athari zao ziligawanyika pamoja na urithi wao. Kabila la Kuraish, kwa udanganyifu au nguvu (sic), walijipatia usi-mamizi wa Al-Kaaba; ile ofisi ya kikasisi iliyoendelezwa kupitia mishuko minne ya nasaba hadi kwa babu yake Muhammad; na ukoo wa Hashim, kutoka pale alipochipukia, lilikuwa ndio liliheshimiwa sana na tukufu kwenye macho ya nchi yao.

Mshuko wa Muhammad kutoka kwa Ismail ulikuwa ni hadhi ya taifa au hekaya (sic), lakini kama hatua za mwanzo za jadi hii ni za giza na mashaka (sic), angeweza kutoa vizazi vingi vya uungwana (usharifu) safi na halisi; alichipukia kutoka kwenye kabi-la ya Quraish na ukoo wa Hashim ulio maarufu sana wa Waarabu, mabwana wa Makka, wasimamizi warithi wa Al-Kaaba.

(The Decline and Fall of the Roman Empire)

Hashim alikuwa na ndugu yake mdogo alikuwa akiitwa Al-Muttalib, mtoto wa Abd Manafi. Kwa kipindi, alikuwa ndiye mkuu wa ukoo huo, na alipofariki mpawe - Abdul Muttalib - mtoto wa Hashim, alimfuatia yeye kama mkuu mpya wa ukoo huo. Abdul Muttalib alidhihirisha sifa zote zilizoyafanya majina ya baba na babu yake kuwa makub-wa na maarufu.

Kama ilivyoonekana kabla, mji wa Makka kama Arabia yote, ulikuwa hauna serikali wala mtawala, lakini ulimilikiwa na kabila la Quraish. Quraish ilitokana na koo kumi na mbili, na Banu Hashim ulikuwa mmoja wao. Kwa kupinga uharibifu wa tabia wa nyakati; watu wa ukoo wa Banu Hashim, walikumbuka, nusu karne kabla ya kuzaliwa Muhammad, kufanya juhudi za kujaribu kuzuia kuanguka kwa maadili ya Waarabu na kuimarisha hali ya kijamii, kiuchumi na ukuzi wa akili ya nchi hiyo. Wao, kwa hiyo, walibuni au kuunda 'shirikisho la wenye maadili.' Malengo makuu ya shirikisho yalikuwa kuzuia vita kutokana na kugawanyika na kuwalinda wanyonge na wasio na ulinzi kutoka kwa maadui.

Hawa Banu Hashim vilevile walijishughulisha katika ustawi wa uchumi wa Waarabu na walianzisha mfumo wa biashara na nchi majirani kwa kutuma misafara kwenda Syria wakati wa kiangazi na Yemen wakati wa kipupwe, kama ilivyoelezwa kabla. Misafara iliondoka Makka ikiwa imebebeshwa bidhaa kama matunda ya tende, lijamu na hatamu za farasi na ngamia, mablanketi yaliyotengenezwa kwa sufi au manyoya ya ngamia; manuka-to na mimea yenye kunukia uzuri, viungo, ubani, pembe na ngozi za wanyama wa jang-

33

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wani, na farasi wa ukoo safu. Walirudi na nguo, mafuta ya zeituni, silaha, kahawa, matun-da na nafaka.

Yote haya, shirikisho la wenye maadili na biashara ya misafara yalikuwa, bila ya ubishi, ni zawadi kubwa ya Bani Hashim kwa Waarabu. Lakini zawadi kubwa mno sio tu kwa Waarabu, bali kwa dunia nzima, ilikuwa iwe ni yule mtoto aliyekuwa aitwe Muhammad mwana wa Abdullah ibn Abdul Muttalib na Amina binti Wahab, alikuwa aje kuwa mfadhili mkuu, sio tu kwa Waarabu bali kwa wanadamu wote. Moj a ya matukio maarufu lilitokea wakati wa waj ibu wa Abdul Muttalib kama msimamizi wa Al-Kaaba, lilikuwa ni uvamizi wa Makka toka kwa jeshi la Ki-habeshi likiongozwa na yule jemadari wa Kikristo, Abraha. Hilo jaribio la kuiteka Makka lilishindwa kama ilivyoelezwa katika Aya ya Qur'an Tukufu ifuatayo:

Usahihi-2.jpg

"...Na akawapelekea juu yao, ndege makundi makundi, wakawatupia mawe ya udongo mkavu. Na akawafanya kama majani yaliyotafunwa tafunwa." (Sura ya 105: 3-5 )

Kawa vile wavamizi walikuja na tembo(ndovu), ule mwaka wa kampeini yao ulikuja kuju-likana kama "Mwaka wa Tembo". Huu mwaka wa Tembo uko sawia na mwaka 570 A.D. ambao pia umetokea kuwa ndio mwaka wa kuzaliwa Muhammad, nabii wa wakati ujao. Lile jeshi la uvamizi liliondoka Makka, na masharti ya makubaliano ya kusimamisha vita yakajadiliwa, kwa niaba ya mji wa Makka, na Abdul Muttalib.

Sir John Glubb:

"Mnamo mwaka 570 A.D. Abraha, kaimu mfalme wa Kikristo wa Uhabeshi wa huko Yemen aliingia Makka. Makuraish walikuwa waoga sana au wanyonge mno wa kulipinga jeshi hilo la Kihabeshi na Abdul Muttalib, akiongoza ujumbe, alitoka kwen-da kujadiliana na Abraha.

(The Great Arab Conquest, 1963)

Mmoja wa binamu wa mbali wa Hashim, alikuwa ni Abd Shams. Umayya fulani aliyedai kuwa ni mtoto wake, alimwonea wivu Abdul Muttalib juu ya mamlaka na hadhi yake kubwa. Wakati mmoja, alifanya jaribio la kumnyang'anya uwezo na mamlaka yake lakini alishindwa. Kushindwa huko kulimkereketa sana moyoni mwake. Aliweka chuki dhidi ya Abdul Muttalib na watoto wake, na akairithisha kwa wanae mwenyewe na wajukuu zake waliokuja kujulikana kama Bani Umayya.

34

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Lakini kulikuwa na kitu zaidi ya wivu wa kikabila katika uadui wa Bani Umayya kwa Bani Hashim. Koo hizi mbili zilikuwa na tofauti kati yao katika tabia na mwenendo, na katika mtazamo wao na mwelekeo kwenye maisha, kama matukio yalivyokuwa yaje kubainisha mara, wakati Bani Umayya walipoongoza genge katika kuupinga Uislamu.

Bani Hashim walikusudia kuwa ngao ya Uislamu. Allah (s.w.t.) mwenyewe aliwachangua wao kwa ajili ya kusudio hili tukufu. Ibn Khaldun, mwanahistoria mashuhuri na mwana-elimujamii, anaandika katika kitabu chake kiitwacho Muqaddimah (Dibaji) kwamba Mitume wote wa haki lazima wapate kuungwa mkono na kundi fulani lenye nguvu. Msaada huu, anasema, ni muhimu, kwa sababu unasimama kama kinga ambayo inawalin-da wao dhidi ya maadui zao na inawapa wao kiwango cha ulinzi, bila hicho hawawezi kutekeleza ujumbe wao Mtukufu.

Katika suala la Muhammad, Mtume wa Uislamu, hawa Bani Hashim walifanya hilo "kundi lenye nguvu" lililomlinda yeye kutokana na nia mbaya ya Bani Umayya, wakampatia usalama na wakamuwezesha kutekeleza ujumbe wake Mtukufu. Abdul Muttalib alikuwa na watoto wa kiume kumi. Wanne wao walikuwa maarufu katika historia. Hawa walikuwa: -

1. Abdullah, baba yake Muhammad

2. Abu Talib, baba yake Ali

3. Hamza, yule shahidi -shujaa wa vita vya Uhud.

4. Abbas, mhenga wa Makhalifa wa Bani Abbas wa Baghdad.

Abdullah na Abu Talib walikuwa watoto wa mama mmoja ambapo hawa watoto wengine nane wa Abdul Muttalib walizaliwa na wake zake wengine.

35

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

KUZALIWA KWA MUHAMMAD NA MIAKA YA MWANZO YA UHAI WAKE

Abdullah alikuwa ndiye mtoto kipenzi cha Abdul Muttalib.

Alipokuwa na umri wa miaka kumi na saba, alimuoa Amina, bibi wa uzao bora wa Yathrib, mji ulioko Kaskazini ya Makka. Hakuwa hata hivyo, amekadiriwa kuishi muda mrefu, na akafa miezi saba tu baada ya ndoa yake.

Muhammad, Mtume wa Mungu wa wakati ujao, alikuwa bado mimbani. Sheikh Muhammad el-Khidhri Buck, profesa wa historia ya Kiislamu, chuo kikuu cha Misri, Cairo, anasema katika kitabu chake, Nur-ul-Yaqin fi-sirat Sayyid al-Murasalin (1953) hivi:

"Yeye (Muhammad Ibn Abdullah) alizaliwa katika nyumba ya ami yake, Abu Talib, katika "mtaa wa Bani Hashim" huko Makka, tarehe 12 Rabil-awal ya ule Mwaka wa Tembo, tarehe ambayo inaoana na tarehe 8 Juni 570. Mkunga wake alikuwa ni mama yake Abdur Rahmani Ibn Auf. Mama yake, Amina, alituma habari za uzazi huu wa kheri kwa babu yake, Abdul Muttalib, ambaye alikuja, akamchukuwa mikononi mwake, na akampa jina hili la Muhammad."

Mgao wa Muhammad katika urithi wake ulikuwa ni mtumwa mmoja wa kike, Ummu Ayman; ngamia watano na kondoo kumi. Huu ni ushahidi kwamba Mitume wanaweza kurithi mali, na kama wanaweza kurithi mali toka kwa wazazi wao, wanaweza pia kurithisha mali kwa watoto wao wenyewe. Kuwa mitume hakuwabatilishii wao katika kupokea urithi wao wenyewe wala hakuwabatilishii watoto wao kupokea wa kwao. Kauli hii inaweza kuonekana kama isiyofuata mantiki katika muktadha huu lakini sio. Muhammad, Mtume wa Uislamu, alitoa kwa mwanae, Fatima kama zawadi, shamba la Fadak.

Lakini alipofariki; Abu Bakr, aliyekuwa Khalifa, na Umar, Mshauri wake, walilikamata shamba hilo kwa kisingizio kwamba Mitume hawarithishi mali yoyote kwa watoto wao wenyewe, na mali yeyote wanayomiliki, inahusika baada ya kifo chao, sio kwa watoto wao, bali kwa umma wao. Ni faini kali ambayo mtu anapaswa kulipa katika Uislamu kwa kuwa tu mtoto au binti wa Mtume wake. Mtu mwingine yoyote katika umma huu anayo haki ya kurithi utajiri au mali ya baba yake lakini sio binti wa Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.)!

Ilikuwa ni desturi miongoni mwa Maquraish kuwapeleka watoto wao jangwani kupitisha miaka yao ya mwanzo katika hali ya hewa ambayo ilikuwa ni yenye kutia afya kuliko ile ya Makka. Watoto walijenga miili yenye nguvu zaidi katika maeneo ya wazi na hewa safi

36

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ya jangwani kuliko ambavyo wangekuwa katika hewa ya mjini yenye kusonga na kukirihi.

Kulikuwa na sababu nyingine moja zaidi ya kwanini Waarabu wa koo bora waliwapeleka watoto wao kuishi jangwani. Walikuwa wanasisitiza ufasaha katika kuongea na walikuwa "washabiki" wakubwa wa maneno. Walivutiwa na lugha ya Kiarabu, maneno yake, maana zao na tofauti ndogo ndogo katika maana zao; na walijivunia sana katika ufasaha wao binafsi. Kwa kweli, matabaka ya juu katika Makka walipata mamlaka yao juu ya uwezo wao wa balagha. Makka ilikuwa ndio sehemu ya makutano ya misafara mingi na Kiarabu chake kilikuwa kimechafuliwa na kuwa "Kiarabu pijini" (chenye maneno mchanganyiko).

Waarabu wa koo bora hawakutaka watoto wao kujifunza na kuongea kiarabu pijini cha Makka; waliwataka wazungumze tu lugha safi na isiyochanganywa ya jangwani. Wao, kwa hiyo, waliwapeleka watoto wao mbali na Makka ili kuwakinga kutokana na athari zote haribifu kama hizi katika miaka yao ya awali ya maisha yao.

Amina alimtoa mwanae, Muhammad, kwa Halima, mwanamke wa kabila la Banu Asad, aliyekuwa akiishi Mashariki ya Makka, kwa ajili ya malezi. Mtoto mchanga huyu, Muhammad aliishi miaka yake minne ya kwanza ya maisha yake huko jangwani na mama mnyonyeshaji wake. Wakati fulani katika mwaka wake wa tano wa maisha yake, mama huyu anasemekana alimrudhisha kwa mama yake huko Makka.

Muhammad alikuwa na umri wa miaka sita wakati Amina, mama yake, alipofariki. Alichukuliwa baadae na Abdul Muttalib, babu yake, mpaka nyumbani kwake. Lakini miaka miwili tu ilipita wakati Abdul Muttalib naye alipofariki.

Kabla tu ya kifo chake, Abdul Muttalib aliwaita watoto wake wote pamoja, na akawaam-bia kwamba anaacha "urithi" namna mbili kwao; mmoja ulikuwa uongozi wa ukoo wa Bani Hashim, na mwingine ulikuwa ni Muhammad Ibn Abdullah, mpwa wao, yatima wa miaka nane. Kisha akawauliza ni nani miongoni mwao alitaka uwezo wake na mamlaka kama kiongozi wa kabila hilo, na ninani miongoni mwao atachukuwa dhima ya kijana huyo ambaye amepoteza shauku kubwa ya kufanywa kiongozi wa kabila lakini hata mmoja hakujitolea kuchukua dhima juu ya Muhammad.

Kama Abdul Muttalib alivyolitazama kusanyiko hilo na kutafakari maisha ya baadaye ya kijana huyo, Muhammad, ukimya wa wasiwasi ukatanda mahali hapo. Lakini haukuchukua muda mrefu. Abu Talib, mmoja wa watoto wake, alijitokeza mbele na akase-ma kwamba alimtaka yule mwana wa marehemu kaka yake, Abdullah, na kwamba hakuwa na haja yoyote ya mamlaka na madaraka.

37

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Tamko hili la wazi la Abu Talib lilikamilisha suala hilo kwa Abdul Muttalib. Aliamua kum-fanya Abu Talib sio tu mlezi wa Muhammad bali pia mlezi wa ukoo wa Bani Hashim.

Abdul Muttalib alitangaza, alipokaribaia kufariki, kwamba mwanae, Abu Talib, atamfuatia yeye kama kiongozi mpya wa Bani Hashim, na kwamba atakuwa pia mlezi wa Muhammad. Kisha akaliamuru kusanyiko hilo kumtambua Abu Talib kama kiongozi mpya wa Bani Hashim. Wao wakakubaliana, na akawaruhusu kuondoka.

Historia ilithibitisha uamuzi wa Abdul Muttalib. Mwanae na mirthi wake, Abu Talib, alitekeleza kazi zote kwa heshima sana.

Sir John Glubb:

"Katika mwaka wa 578 Abdul Muttalib alifariki. Kabla ya kifo chake, alimkabidhisha mwanawe, Abu Talib, kumuangalia Muhammad. Abdullah, baba yake Muhammad, alikuwa ndugu wa Abu Talib kwa baba na mama yao. Watoto wengine wa Abdul Muttalib ni dhahiri walitokana na wake wengine tofauti.

(The life and Times of Muhammad, 1970)

Abu Talib na mkewe walifurahi sana na kumpokea Muhammad kwenye familia yao. Hawakumchukua nyumbani kwao tu, bali mioyoni mwao pia, na walimpenda zaidi ya walivyowapenda watoto wao wenyewe.

Abu Talib alikuwa ni mtu mwenye hadhi kubwa na mwenye kuheshimika. Wakati wa wajibu wake kama kiongozi wa Bani Hashim alibeba vyeo vya "Bwana wa Quraish," na "Kiongozi wa bonde". Kama watu wengine wa kabila lake alikuwa pia ni mfanyabiashara, na misafara yake ilisafiri kwenda na kurudi hadi Syria na Yemen.

Katika kila msimu, misafara ya Abu Talib iliondoka Makka kwenda vituo mbalimbali. Mara chache, yeye mwenyewe aliandamana na msafara kusimamia mauzo na ununuzi wa bidhaa katika masoko ya kigeni. Muhammad akiwa bado mdogo anasemekana kasafiri naye kwenda Syria pamoja na msafara mmojawapo alipokuwa na miaka kumi na miwili.

Mapema katika maisha, Muhammad, nabii wa baadae alijenga sifa ya ukweli, uaminifu na maamuzi yenye busara. Kwa vile hakukuwa na mabenki siku zile, alikuja kuwa "benki" ya watu wa Makka. Walileta fedha zao, mapambo ya vito, na vitu vinginevyo vya thamani kwake kwa uhifadhi wa salama, na wakati wowote walipotaka kurudishiwa kitu chochote, aliwarudishia. Walimuita yeye al-Amin (Mwaminifu) na as-Sadiq (Mkweli).

38

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir William Muir:

"Kwa kujaaliwa na akili safi adilifu na tamaa dhaifu, mkimya na mwenye mazinga-tio, yeye (Muhammad) aliishi zaidi kiupweke, na tafakari ya moyoni mwake ilimpa-tia shughuli kwa masaa ya mapumziko yaliyotumiwa na watu wenye tabia duni katika michezo ya kikatili na ufisadi. Tabia njema na muelekeo wa heshima wa kijana huyu asiyejionyesha vilimletea kukubalika kwa wananchi wenzie; na alipata lile jina, kwa kuafikiana kwa jumla, la Al-Amin, 'mwaminifu.' Hivyo aliheshimiwa na kutukuzwa, Muhammad aliishi maisha ya utulivu na ya kitawa katika familia ya Abu Talib."

(The life of Muhammad 1887, uk 20)

Wakati Muhammad alipokuwa na umri wa miaka ishirini, ilizuka vita miongoni mwa Maquraish, kabila lake, na kabila la Hawazin. Ingawa alikuwapo katika kampeni za vita hii, hakushiriki kwenye nafasi yoyote katika mapigano. Hakuua au kujeruhi mtu yoyote, hivyo kuonyesha katika kipindi hiki cha mwanzo cha maisha yake, kuchukia kwake umwa-gaji wa damu. Anasemekana, hata hivyo, kuwahi kuokota mishale kutoka uwanjani, na kuitoa kwa ami zake ambao walikuwa wanapigana.

Miaka michache baadae, Muhammad aliingizwa kama mwanachama wa lile Shirikisho la Wenye Maadili. Kama ilivyotajwa mapema, hili Shirikisho limejiapia lenyewe kuwalinda wayonge, kuwapinga madhalimu na waonevu, kukomesha unyonyaji wa namna yoyote ile.

Ikumbukwe kwamba ulikuwa ni ukoo wa Bani Hashim, ambao Muhammad nabii wa baadae alitokana nao, ambao ndio ulioanzisha lile Shirikisho la Wenye Maadili. Lilikuwa ni jambo lililotukia tu! Hakuna njia ya kujibu swali hili. Lakini kwa taratibu zao za kisi-asa, Bani Hashim walikwishatangaza vita juu ya udhalimu na dhulma. Waliweka wazi kwamba hawatakula njama na wenye nguvu dhidi ya wanyonge; wala hawangeridhia katika unyonyaji wa maskini kwa Maquraishi wa Makka.

Sio miaka mingi baadae, Muhammad alikuwa aanzishe utaratibu wa ujenzi upya wa jamii ya wanadamu, sehemu ya uchumi ambayo itatambua wazi uharibifu wa unyonyaji. Angezichukua zile "fursa" za Maquraishi na "haki " zao za kunyonya maskini na wanyonge, kutoka kwao.

Montgomery Watt:

"Lile Shirikisho la Wenye Maadili linaelekea kuchukua sehemu muhimu sana katika maisha ya Makka, na kwa sehemu kubwa kuelekezwa kwa watu na sera ambazo baadae Muhammad alijikuta anapingana nazo. Hususan ukoo wake wa Bani Hashim ulikuja kuwa na wajibu mkubwa katika Shirikisho la Wenye Maadili."

(Muhammad, Prophet and Statesman, 1961)

39

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

NDOA YA MUHAMMAD MUSTAFA NA KHADIJA

Khadija, binti ya Khuwaylid, alikuwa mkazi wa Makka. Naye pia alikuwa wa kabila la Quraishi. Aliheshimiwa sana na watu wa Makka kwa sababu ya tabia yake ya mfano na uwezo wake wa kupanga. Kama vile watu wa Makka walivyomuita Muhammad 'Sadiq' na 'Amin', walimuita Khadija 'Tahira', yenye maana ya "Aliye safi." Alikuwa akijulikana pia miongoni mwa Waarabu kama 'Malkia wa Wafanya biashara.' Wakati wote misafara ilipoondoka Makka au kurudi Makka, waliona kwamba mzigo wake ulikuwa mkubwa kwa ujazo kuliko mizigo yote ya wafanyabiashara wa Makka ikichanganya pamoja.

Muhammad alipokuwa na umri wa miaka 25, ami yake na mlezi wake, Abu Talib, alimshauri Khadija, na kuelewa kwake kwa kimya, kwamba amchague yeye kama wakala wake katika mmoja wa misafara yake, uliokuwa uondoke kwenda Syria punde tu, mara.

Khadija kwa kweli alikuwa akihitaji wakala kwa wakati ule hasa. Alikubali kumchagua Muhammad kama wakala wake. Alichukua madaraka ya bidhaa za Khadija, na msafara ukatoka kwenda Syria. Mtumwa wa Khadija, Maisara, pia alifuatana naye na akamsaidia kama msaidizi wake.

Safari hii ya kibiashara kwenda Syria ilifanikiwa kupita matarajio, na Khadija alivutiwa sana na uwezo wa wakala wake na uaminifu wake kiasi kwamba aliamua kumpa madaraka ya shughuli zote za biashara zijazo baadae. Safari hii pia ilithibitisha kuwa mwanzo wa ndoa yao.

Edward Gibbon:

"Nyumbani au ugenini, kwenye amani au vita, Abu Talib, ami yake Muhammad aliye-heshimiwa sana kuliko ami zake wengine, alikuwa ndiye kiongozi na mlezi wa ujana wake; katika mwaka wake wa 25 aliingia kwenye huduma za Khadija, mjane aliyekuwa tajiri na mwadilifu wa Makka, ambaye mara tu alimtunza uaminifu wake kwa zawadi ya uchumba na mali.

Makubaliano ya ndoa, katika mfumo rahisi wa kizamani, yanaonyesha kupendana kwa Muhammad na Khadija; yanamuelezea yeye Muhammad kama mtu hodari zaidi wa kabila la Quraish; na anatamka mahari ya wakia kumi na mbili za dhahabu na ngamia ishirini, ambayo ilitolewa kwa ufadhili wa ami yake.

(Decline and Fall of the Roman Empire) 40

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abu Talib alisoma khutba ya ndoa ya Muhammad na Khadija, na hotuba yake au waadhi unathibitisha bila shaka yoyote kwamba alikuwa akiabudu Mungu mmoja.

Alianza hotuba yake katika mfumo wa "Kiislam" kwa kutoa sifa na shukrani kwa Allah (s.w.t.) kwa rehma zake na baraka zisizoidadi na neema, na alimalizia kwa kumuomba Rehma na neema Zake juu ya maharusi wapya hao.

Ndoa ya Muhammad na Khadija ilifanikiwa sana. Imebarikiwa na furaha kuu isiyo na kifani kwa wote, mume na mke. Khadija alijitolea maisha yake kwenye huduma kwa mumewe na Uislamu. Alitumia utajiri wake mkubwa wote kwa kuimarisha Uislamu, na katika ustawi wa Waislamu.

Khadija alikuwa na hisia za ujumbe kama zile zile alizokuwa nazo Muhammad, na alikuwa na shauku kama aliyokuwa nayo ya kuona Uislamu unaushinda upagani. Kwa shauku yake ya kuuona ushindi wa Uislamu, aliongeza uwajibikaji na uwezo. Alimuondoa mumewe katika ulazima wa kutafuta maisha, na hivyo kumuwezesha kutoa muda wake wote katika ulazima wa kutafuta kujiandaa kwa kazi kubwa iliyokuwa imelala mbele yake.

Huu ndio mchango wa maana sana alioutoa kwenye kazi ya mumewe kama Mtume wa Mungu. Alikuwa ndio egemeo ambalo Muhammad alilihitaji katika miaka yote ya maan-dalizi kwa ajili ya Utume.

Ndoa ya Muhammad na Khadija ilibarikiwa pia na kuzaliwa kwa binti yao, Fatima Zahra. Ingawa neema ambazo Mungu amewajaalia juu yao zilikuwa nyingi, hapakuwa na yoyote waliyoithamini zaidi ya binti yao, Fatima Zahra. Alikuwa ni mboni ya macho ya baba yake, na "Bibi wa Peponi" wa baadae. Baba na Mama walitoa kwa wingi mno mapenzi yao juu yake, na alileta matumaini ndani ya nyumba yao.

41

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

KUZALIWA KWA ALI IBN ABI TALIB

Ali alizaliwa tarehe 13 Rajab ya mwaka wa thelathini wa Tembo (A.D. 600). Binamu yake, Muhammad, alikuwa ana miaka thelathini wakti huo. Wazazi wa Ali walikuwa ni Abu Talib Ibn Abdul Muttalib, na Fatima, binti Asad, wote wa ukoo wa Bani Hashim.

Ali alizaliwa ndani ya Al-Kaaba huko Makka.Yule mwanahistoria maarufu, Masud, Herodotus wa Waarabu anaandika kwenye ukurasa wa 76 wa juzuu ya 2 ya kitabu chake, Murujudh-Dhahab kwamba moja ya ubora ambao Ali alikuwa nao ulikuwa kwamba alizaliwa ndani ya Nyumba ya Allah (s.w.t.) Baadhi ya mabingwa wengine ambao wathibitisha kuzaliwa kwa Ali ndani ya Al-Kaaba, ni :-

1.   Muhammad Ibn Talha Shafii katika Matalibul-usul uk 11.

2.  Hakim katikaMustadrak, uk. 483, Juz. 111.

3.  Al- Umari katika Sharh Ainia uk. 15.

4.  Halabi katika Sira, uk. 165, Juz. 1.

5.   Sibt Ibnul- Jauzi katika Tadhkira Khawaisil Umma, uk.7.

6.   Ibn Sabagh Malik katika Fusuulul Muhimma uk. 14

7.   Muhammad Ibn Yusuf Shafi'i katika KifAyatut-Talib uk. 261.

8.   Shablanji katika Nurul Absar, uk. 76.

9.    Ibn Zahra katika Ghiyathul Ikhtisar, uk.97.

10.   Edvi katika Nafahatul Qudsia uk. 41.

Miongoni mwa wanahistoria wa kisasa, Abbas Mahmud al-Akkad wa Misri anaandika katika kitabu chake Al-Abqariyat ul-Imam Ali, (Cairo, 1970) kwamba Ali Ibn Abi Talib alizaliwa ndani ya Al-Kaaba.

Mwanahistoria mwingine wa sasa, Mahmud Said at-Tantawi, wa Supreme council of Islamic Affairs (Baraza la juu la Mashauri ya Kiislamu), Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, anaandika katika ukurasa wa 186 wa kitabu chake kiitwacho Min Fadha-il al-Ashrat al-Mubashirina bil-Janna, kilichochapishwa mwaka 1976 na Matab'a al-Ahram at-Tijariyya, Cairo, Misri hivi:-

"Rehma za Allah (s.w.t.) ziwe juu ya Ali Ibn Abi Talib. Alizaliwa ndani ya Al-Kaaba. Alishuhudia kuchipuka kwa Uislamu; alishuhudia Da'wa ya Muhammad na alikuwa ni shahidi wa Wahyi (kushuka kwa Qur'an al-Majid). Mara moja tu aliukubali Uislamu ingawa alikuwa bado mtoto, na alipigana maisha yake yote ili kwamba Neno la Mungu liwe juu kabisa."

42

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mshairi wa Kiarabu alitunga ubeti ufuatao juu ya kuzaliwa kwa Ali:

Yeye (Ali) ndiye yule ambaye ile Nyumba ya Allah (s.w.t.),

iligeuzwa kuwa wodi ya wazazi;

Na yeye ndiye aliyeyatupa masanamu nje ya Nyumba hiyo; Ali alikuwa mtoto wa kwanza na wa mwisho,

daima kuzaliwa ndani ya Al-Kaaba.

Ilikuwa ni desturi ya Waarabu kwamba wakati mtoto anapozaliwa, aliwekwa chini ya miguu ya sanamu au masanamu ya ukoo huo, hivyo kuashiria "kumkabidhi" kwa huyo mungu wa kipagani. Watoto wote wa Kiarabu "walitolewa" kwa masanamu isipokuwa Ali Ibn Abu Talib. Wakati watoto wengine wa Kiarabu walipozaliwa, mmoja wa waabudu sanamu alikuja kuwasalimia na kuwabeba mikononi mwake.

Lakini Ali alipozaliwa, Muhammad, mjumbe wa baadae wa Allah (s.w.t.) alikuja kwenye eneo la Al-Kaaba kumsalimia. Alimbeba mtoto huyo mikononi mwake, na kumtoa kwenye kumtumikia Allah (s.w.t.) Mtume huyu wa baadae lazima awe alikwishajua kwamba yule mtoto aliyekuwa mikononi mwake siku moja atakujakuwa adui asiyeshindika wa wanaoabudu masanamu wote na washirikina na wa miungu yao na miungu ya kike. Wakati Ali alipokua, aling'oa uabudu masanamu na ushirikina kutoka Arabia kwa upanga wake.

Kuzaliwa ndani ya Al-Kaaba kulikuwa ni moja kati ya sifa nyingi ambazo Mungu amez-ijaalia juu ya Ali. Sifa nyingine aliyokuwa nayo ni kwamba kamwe hakuabudu masanamu. Hii nayo inamfanya awe wa kipekee kwa vile Waarabu wote waliabudu masanamu kwa miaka na miaka kabla ya kukana uabudu masanamu na kuukubali Uislamu. Ni kwa sababu hii ambapo anaitwa, "Karama llahu waj-hahu" ("Ambaye Allah (s.w.t.) ameutukuza uso wake.")

Uso wake ulitukuzwa hasa na Allah (s.w.t.) kwani ulikuwa ndio uso pekee katika maswa-haba ambao kamwe haukuinama mbele ya Sanamu lolote.

Ali alikuwa ndiye mtoto mdogo kabisa katika familia hiyo. Kati ya kaka zake watatu, Talib na Aqil, walikuwa wakubwa kwa miaka kumi zaidi yake.

Kuzaliwa kwa Ali kuliujaza moyo wa nabii wa baadaye furaha isiyo kifani. Mtoto huyu alikuwa ni mtu mmoja "maalum" kwake yeye. Ingawaje Muhammad alikuwa na binamu wengi wengine na walikuwa na watoto wao mwenyewe, na Ali mwenyewe alikuwa na kaka zake wakubwa watatu; lakini hakuonyesha mvuto wowote juu ya yeyote kati yao. Ali, na Ali peke yake ndiye alikuwa kitovu cha mvuto wake na mapenzi.

43

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wakati Ali alipokuwa na miaka mitano, Muhammad alimchukua kama mtoto wake wa kupanga, na kuanzia hapo tena hawakutengana tena daima. Kuna Hadith kwamba wakati mmoja kulitokea njaa huko Makka, na maeneo yanayoizunguka, na Abu Talib, akiwa kati-ka dhiki kubwa wakati huo, alikuwa akiona ugumu kutunza kundi kubwa la watu. Ilimjia Muhammad kwamba alipashwa kujaribu kupunguza baadhi ya uzito wa majukumu ya ami yake, na alishawishika kwa hiyo, kumchukua Ali.

Ni kweli kwamba Muhammad alimchukuwa Ali lakini sio kwa sababu iliyoelezwa hapo juu. Katika nafasi ya kwanza kabisa, Abu Talib hakuwa kwenye hali ya dhiki kubwa kiasi kwamba hakuweza kumlisha mtoto wa miaka mitano; alikuwa ni mtu mwenye hadhi na uwezo, na misafara yake ilikwenda na kurudi kati ya Hijaz na Syria au kati ya Hijaz na Yemen. Katika nafasi ya pili, kulisha mtoto wa miaka mitano kungekuwa vigumu kuleta tofauti yoyote kwa mtu ambaye alilisha hata wageni kama wangekuwa na njaa.

Muhammad na Khadija walimchukua Ali baada ya kufa kwa watoto wao wenyewe wa kiume. Ali kwa hiyo aliziba uwazi katika maisha yao. Lakini Muhammad, Mtume wa baadae, pia alikuwa na sababu nyingine ya kumchukua Ali. Alimchagua Ali kumlea, kumuelimisha na kumuandaa kwa ajili ya takdir kubwa iliyokuwa ikimngojea katika nyakati zijazo.

Dr. Taha Hussein wa Mirsi anasema kwamba Mtume wa Allah (s.w.t.) mwenyewe alikuwa kiongozi wa Ali, mwalimu na mwelekezaji, na hii ni sifa moja nyingine zaidi ambayo anayo Ali, na ambayo hakuna mwingine yeyote anayeshirikiana naye kwayo.

Kuhusu Uislamu imesemekana kwamba kati ya dini zote za dunia, ni hii moja pekee iliyokuwa katika mwanga wa historia, na hakuna sehemu ya Hadith yake iliyoko gizani.

Bernard Lewis asema:

"Katika insha juu ya Muhammad na chanzo cha Uislamu, Ernest Renan anazungumzia kwamba, tofauti na dini zingine ambazo zilianzishwa kwa usirisiri, Uislamu ulizaliwa katika mwanga kamili wa historia. "Mizizi yake iko kwenye usawa wa ardhi, na maisha ya Mwanzilishi wake yanafahamika vema kwetu sisi kama ya wale waleta mabadiliko wa karne ya kumi na sita .

(The Arabs in History, 1960) G. E. Von Grunebaum:

"Uislamu unaweka tamasha la maendeleo ya dini ya ulimwengu katika mwanga wa historia."

(Uislamu, 1969)

44

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kadhalika, inaweza kusemwa kwamba kati ya marafiki na Masahaba wote wa Muhammad, Mtume wa Uislamu, Ali ndiye pekee aliyekua katika mwanga kamili wa historia. Hakuna sehemu ya maisha yake, ama katika uchanga wake, utoto wake, uvulana wake ujana wake, uanaume wake au kupevuka, ambayo imefichikana kutoka kwenye mwangaza wa historia. Alikuwa ndio kivutio kikuu cha macho yote tangu kuzaliwa kwake mpaka kufa kwake. Kwa upande mwingine maswahaba waliobakia wa Mtume (s.a.w.) wanakuja kwenye mvuto wa nadhari ya mwanafunzi wa historia baada tu walivyokubali Uislamu, na kidogo, kama kipo, kinajulikana mpaka kufikia hapo.

Ali alijaaliwa kuwa mkono wa kuume wa Uislamu, na ngao na kingio la Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) Takdira au maajaliwa yake yalikuwa kiungo kisichotenganishwa na takdira ya Uislamu, na maisha ya Mtume wake. Alikuwepo katika kila hali ya mambo katika historia ya harakati hii mpya, na alishika nafasi ya kuwa nyota ndani yake. Ilikuwa, kwa dharura, ni nafasi ambayo yeye pekee ndiye angeweza kuishika. Aliakisi "taswira" ya Muhammad. Kitabu cha Allah (s.w.t.) chenyewe kimemuita "nafsi" au mwandani (nafsi ya pili) ya Muhammad katika Aya ya 61 ya Sura ya tatu, na alionyesha jina lake maarufu toka upande mmoja hadi mwengine, wa historia.

Katika miaka ijayo, muundo wa ufanyaji kazi pamoja wa Muhammad na Ali - amir na mfuasi - utakuja kuweka "Ufalme wa Mbingnii" katika ramani ya dunia.

45

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

KABLA TU YA TANGAZO LA UJUMBE WAKE

Licha ya ukweli kwamba Arabia ilikuwa ni shimo la uovu na ngome ya ibada ya masamu na ushirikina, Muhammad mwenyewe hakuwa kamwe amechafuliwa na inda au dhambi yoyote, na kamwe hakuinama mbele ya sanamu lolote. Hata kabla hajatangaza kwamba amekuja kusimamisha ufalme wa Mbingnii hapa duniani, tabia yake na mwenendo wake mwenyewe vilikuwa ni kiakisi (picha) cha Qur'an Tukufu. Hata wakosoaji wake hawakuweza kuonyesha tofauti kati ya tabia yake na maagizo ya Qur'an wakati wowote, kabla na baada ya Tangazo.

Baada ya Tangazo la ujumbe wake kama Mtume wa Mungu, aliziweka mila na desturi za kipagani chini ya amri ya kupigwa marufuku, lakini hakuna ushahidi kwamba kabla ya kufanya hivyo, yeye mwenyewe aliwahi kutenda jambo la kipagani, au hasa tendo lolote lenye kukinzana na Qur'an.

Inaonekana kwamba, Qur'an, kitabu cha Mungu kilikuwa kimegandamizwa kwenye moyo wa Muhammad tokea mwanzo, na pia inaonyesha kwamba "alihubiri" Uislamu hata kabla ya kubaathiwa, bali tu kupitia matendo yake na sio kwa maneno. Matendo yake yalikuwa fasaha sawa kama ilivyokuwa hotuba zake, na yaliutangazia ulimwengu ni vipi alivyokuwa mtu wa adabu. Hata hivyo walikuwa ni wale mapagani waliomwitaAmin (mwaminifu) na Sadiq (mkweli), na walikuwa ni watu haohao ambao, katika miaka ya baadae, walimsum-bua, wakamuwinda, wakamfukuza, na kuweka na kutangaza malipo juu ya kupatikana kichwa chake.

Pamoja na kupotoka na ukorofi, kama mapagani wa Kiarabu walivyokuwa, bado walivu-tiwa na ukweli; hata ukiwa kwa adui. Bado kupendezewa kwao na ukweli wa Muhammad hakukuwazuia kutafuta kumuangamiza aliposhutumu ibada yao ya masanamu na ushirikina wao. Walishikwa na kiu juu ya damu yake tangu pale alipowaita kwenye Uislamu lakini hawakujiuliza kuhusu kuwa kwake mkweli. Juu ya hoja hii hapawezi kuwepo na ushahidi wa kuaminika kabisa hasa zaidi ya wao.

Wenyeji wa Makka walipendezewa sio tu na uadilifu wa Muhammad, bali pia na maamuzi yake. Wakati mmoja, Maquraish walikuwa wanajenga upya Al-Kaaba, na katika ukuta mmoja wapo walikuwa waweke lile Jiwe Jeusi. Mtu alikuwa alilete lile Jiwe Jeusi kwenye eneo la ujenzi, alinyanyue kutoka ardhini, na aliweke katika sehemu yake juu ya ukuta huo. Ni nani alikuwa alifanye hili?

46

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kila ukoo uliidai heshima hiyo iwe juu yao wenyewe, lakini zile koo nyingine hazikuwa tayari kumkubalia yeyote katika jambo hili. Kutokubaliana huku kulisababisha maneno makali, na wakaidi wakatishia kuamua kwa upanga, ni nani angeweka lile Jiwe Jeusi mahali pake katika ule ukuta.

Wakati ule, mzee mmoja wa Kiarabu akaingilia kati, na akashauri kwamba badala ya kupi-gana na kuuana, wakuu wa koo zile wangepaswa wasubiri na kuona ni nani atakuwa mtu wa kwanza kuingia katika maeneo ya Al-Kaaba asubuhi itakayofuatia, na kisha kulikabid-hi suala hilo kwake kulitolea hukumu.

Ulikuwa ni ushauri wa busara, na wale wakuu wakaukubali kwa busara. Asubuhi iliyofu-ata ule mlango wa Al-Kaaba ulipofunguliwa, walimuona Muhammad akiingia kupitia hapo. Wote walifurahi kwamba alikuwa ni yeye, na wakakubali wote kurufaisha mgogoro wao kwake, na kukubali uamuzi wake.

Muhammad aliagizia kipande cha nguo kiletwe, na kitandazwe pale chini. Kisha yeye akaliweka lile Jiwe juu yake, na akamwambia kila chifu kunyanyua moja ya pembe zake na kulibeba mpaka chini ya ule ukuta wa Al-Kaaba. Ilipokwisha fanywa hivyo, yeye mwenyewe alilinyanyua lile Jiwe na kuliweka kwenye nafasi yake.

Uamuzi wa Muhammad ulimridhisha kila mmoja. Kwa hekima zake, ameziokoa zile nyuso na ameepusha umwagaji wa damu. Tukio hili pia lilithibitisha kwamba nyakati za migogoro, Waarabu waliheshimu maoni yake. Alikuwa kiongozi wa watu mwenye kipaji.

47

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

KUZALIWA KWA UISLAMU

Tangazo la Muhammad la Ujumbe wake

Wakati Muhammad alipokuwa na umri wa miaka 40, aliamriwa na Allah (s.w.t.) kupitia Malaika Wake Jibril, kutangaza Upweke Wake Allah (s.w.t.) kwa waabudu masanamu na washirikina wa dunia nzima, na kutoa ujumbe wa amani kwa wanadamu waliokaa kivita. Kwa mwitiko wa amri hii ya Mbingnii, Muhammad alianzisha programu nzito sana iit-wayo Uislamu ambayo ilikuwa ibadili mwisho wa mwanadamu daima.

Kabla ya Mwito huo kumjia wa kutangaza Upweke wa Muumba, Muhammad alikuwa na tabia ya kutumia muda wake mwingi katika taamuli na tafakari. Ili kujikinga na kuingili-wa kati na wasiwasi usio na lazima, alikwenda mara kwa mara kwenye pango la mlimani liitwalo Hira, maili tatu kaskazini-Mashariki ya Makka, na kutumia zile siku nyingi za kiangazi pale.

Alikuwa huko Hira pale siku moja yule Malaika Mkuu Jibril alipotokea mbele yake, na kumletea zile habari njema kwamba Mungu amemchagua yeye kuwa Mtume Wake wa Mwisho kwa ulimwengu, na ameweka juu yake jukumu la kuwaongoza wanadamu kuto-ka kwenye msukosuko wa dhambi, makosa na ujinga, kwenda kwenye mwanga wa uon-gofu, Haki na Ujuzi. Jibril kisha akamwambia Muhammad "soma" Aya zifuatazo:

"Soma kwa jina la Mola Wako Aliyeumba. Amemuumba mwanadamu katika pande la damu! Soma, na Mola Wako ni Mtukufu mno. Ambaye Amemfunza

(kuandika) kwa kalamu.

Amemfunza mwanadamu Me asilolijua.

Aya hizi tano zilikuwa ndio wahyi wa mwanzoni kabisa, na zilikuja kwa Muhammad katika "Usiku wa Cheo" au "Usiku Uliobarikiwa" ndani ya mwezi wa Ramadhani (mwezi wa tisa wa kalenda ya Kiislam) wa mwaka wa 40 wa Tembo. Zipo mwanzoni mwa Sura ya 96 ya Qur'an Tukufu. Jina la Sura hiyo ni Iqra'a (soma) au 'Alaq (Pande la damu Iililoganda).

Huu Usiku wa Cheo au Usiku Uliobarikiwa hutokea, kwa mujibu wa Hadith, wakati wa kumi la mwisho la mwezi wa Ramadhani, na inaweza ikawa mwezi 21, 23,25, au 27 ya mwezi huo.

Katika maelezo yao husika ya mapokezi ya Muhammad ya Wahyi wa Kwanza, Waislamu wa Sunni na Shia hawakubaliani. Kwa mujibu wa Hadith za Sunni, kule kutokea kwa Jibril

48

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kulimshutukiza Muhammad, na alipomwambia Soma, Muhammad alisema, "Siwezi kusoma." Hili lilitokea mara tatu, na kila mara Muhammad alipotamka kutojua kusoma kwake, Malaika huyo alimbana kwa nguvu kwenye kifua chake. Mwishowe, aliweza kurudia Aya hizo tano ambapo Malaika huyo alimwachia na akatoweka.

Pale Malaika Mkuu Jibril alipotoweka, Muhammad, ambaye sasa alikuwa 'amefanywa" Mtume wa Allah (s.w.t.) alishuka kutoka kwenye majabali hayo ya Hira, na akaenda nyum-bani kwake katika hali ya hofu kubwa. Alikuwa anatetemeka kwa baridi, na alipoingia nyumbani kwake, alimuomba mke wake, Khadija, amfunike na blanketi ambavyo alifanya. Alipopata nafuu sawasawa kutokana na mshituko huo, alimwelezea mke wake ile Hadith ya mkutano wake wa ajabu na Malaika Mkuu Jibril ndani ya pango la Hira.

Maelezo ya Hadith ya Sunni juu ya tukio hili yametolewa katika makala iliyoandikwa na Sheikh Ahmad Zaki Hammad, Ph.D, yenye kichwa cha habari Be hopeful, iliyochapishwa kwenye jarida la kila mwezi, Islamic Horizons la Jamii ya Kiislam ya Amerika Kaskazini, Plainfield, Indiana, la Mei-Juni 1987, kama ifuatavyo:

"Mtume (s.a.w.) katika hatua za mwanzo huko Makka, alihofia kwamba ile hali ya Wahyi ilikuwa ni mguso wa uovu uliokuwa ukimuwinda, ukimchezea kiakili, kutibua utulivu wake na amani ya mawazo. Alihofia kwamba huenda moja ya majini limemgusa. Alilieleza hili kwa Khadija. Hofu yake ilizidi kufikia kiasi kwamba - na tafadhali usishangazwe na Hadith sahihi ndani ya Bukhari - Mtume (s.a.w.) alitamani kuua nafsi yake kuliko kuguswa na uovu, kuchezewa, kupotoshwa, au kuchafuliwa."

Lakini kulingana na maelezo ya Waislamu wa Shia, Muhammad Mustafa, kinyume na kushutushwa au kuhofishwa na kutokea kwa Jibril, alimkaribisha kama aliyekuwa akim-tarajia. Jibril alimletea zile habari njema kwamba Allah (s.w.t.) amemchagua yeye kuwa Mtume Wake wa mwisho kwa wanadamu na akampongeza kwa kuteuliwa kuwa mpokea-ji wa heshima kubwa kuliko zote kwa mwanadamu katika dunia hii.

Muhammad hakusita katika kuupokea ujumbe wa Utume wala hakuwa na ugumu wowote katika kurudia zile Aya za Wahyi wa mwanzo. Alizisoma au kuzirudia bila ya taabu yoy-ote, mwenyewe. Jibril, kwa kweli, hakuwa mgeni kwake, na alijua pia kwamba sababu ya kuwepo kwake mwenyewe ilikuwa ni kutekeleza ujumbe uliowekwa juu yake na Allah (s.w.t.) kama Mtume Wake. Alikuwa "mwenye kuuelewa ujumbe" hata kabla ya kufika kwa Jibril. Yeye Jibril alimpa tu ishara ya kuanza.

Waislamu wa Shia pia wanasema kwamba kitu kimoja ambacho Jibril hakuwa akifanye, kilikuwa ni kutumia nguvu za kimwili juu ya Muhammad kusoma. Kama alifanya, itakuwa kwa kweli ni mtindo wa ajabu wa kumpa Muhammad huo uwezo wa kusoma - kwa kum-minya au kumkaba. Wanasisitiza zaidi kwamba Muhammad Mustafa hakuazimia kujiuwa

49

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

katika wakati wowote wa maisha yake, sio hata katika nyakati za huzuni sana; na kwam-ba haijawahi kumjia kwamba angeweza kamwe kuguswa na "uovu" au kwamba angeweza "kupotoshwa" au "kuchafuliwa."

Hata hivyo, Muhammad alihisi wasiwasi juu ya ukubwa wa jukumu lililo mbele yake. Alitambua kwamba katika utekelezaji wa kazi yake, atakuja kukabiliwa na upinzani mkub-wa, mgumu, na uliodhamiriwa wa mapagani wa dunia nzima. Ile hali ya wasiwasi wake ilikuwa karibu kudhihirika. Alikuwa, kwa hiyo, kwenye hali ya uzito wa mawazo alipoon-doka pale pangoni kurudi nyumbani. Na alimuomba Khadija kumfunika ndani ya blanketi wakati akikaa chini kumuelezea yale matukio ya kule Hira.

Khadija alipoisikia Hadith aliyomwambia Muhammad, alimliwaza na kumpa moyo kwa kusema, "Ewe mwana wa ami yangu, kuwa mwenye furaha nzuri, Allah (s.w.t.) amekuch-agua we we kuwa Mtume Wake. Wewe siku zote ni mpole kwa majirani zako, mwenye msaada kwa jamaa zako, mkarimu kwa mayatima, wajane na masikini, na mwenye upen-do kwa wageni. Allah (s.w.t.) kamwe hatakuacha wewe peke yako."

Inawezekana kwamba Muhammad alizidiwa kwa muda kidogo na mawazo juu ya uwa-jibikaji wake kwa Allah (s.w.t.) katika kuubeba mzigo mzito wa jukumu lake jipya, lakini pale aliposikia maneno ya kuliwaza ya Khadija, mara moja alijisikia zile fadhaa zote ndani yake zikipungua. Alimtuliza na kumpa moyo kwamba pamoja na Mkono wa Allah (s.w.t.) juu ya bega lake, atasimama sawia na majukumu yake na ataweza kushinda vikwazo vyote. Baada ya kipindi kifupi, Jibril alitokea tena mbele ya Muhammad wakati alipokuwa ndani ya pango la Hira, na akawasilisha kwake wahyi wa pili:

"Ewe uliyejifunika (shuka). Simama na uonye. Na Mola wako mtukuze. (Sura ya 74; Aya ya 1-3)

Hii amri kutoka Mbinguni ya "simama na uonye" ilikuwa ni ishara kwa Muhammad (aliye-funikwa na shuka) kuanza kazi yake. Jibril alimweleza yeye kazi zake mpya ya kwanza kabisa ilikuwa ni kuangamiza ibada ya miungu ya uongo, na kusimamisha beramu ya Tawhid - imani ya Upweke wa Muumba - ulimwenguni; na alikuwa awaite wanadamu kwenye dini ya Haki - Uislamu. Uislamu maana yake ni kunyenyekea kwa Allah (s.w.t.) na kumkubali Muhammad kama mja na Mtume Wake.

Jioni ile Muhammad alirudi nyumbani mwenye fahamu na dhamira juu ya kazi yake mpya kwamba alikuwa anapaswa kuutangaza Uislamu, na kwamba alikuwa aanzie kutoka nyumbani kwake mwenyewe - kwa kuutangaza kwa mkewe.

50

Usahihi-3.jpg

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad alimweleza Khadija juu ya kutembelewa kwa mara ya pili na Jibril, na wajibu uliowekwa juu yake na Allah (s.w.t.) wa kumwita yeye Khadija kwenye Uislamu. Kwa Khadija, historia na ukamilifu wa uadilifu wa mume wake vilikuwa ni uthibitisho usiopingika kwamba alikuwa ni mjumbe wa ki-ungu, na aliukubali Uislamu bila kusita. Kwa kweli, kati yake na Uislamu, kulikuwa na "uhusiano wa kiitikadi" fulani uliokuwepo kabla. Kwa hiyo, wakati Muhammad Mustafa alipoleta Uislamu kwake, Khadija "aliutam-bua" mara moja, na akaufuata kwa matumaini. Aliamini kwamba Muumba ni Mmoja, na kwamba Muhammad alikuwa ni Mtume Wake, naye akatamka:

"Nashuhudia kwamba hakuna mungu ila Allah (s.w.t.); na ninashuhudia kwamba Muhammad ni mtumwa na Mtume Wake."

Muhammad; huyu Mtume mpya wa Mungu, alijishindia mfuasi wake wa kwanza - Khadija - mke wake. Alikuwa ndiye wa kwanza, wa kwanza kabisa kuthibitisha imani yake katika Tawhid (Upweke wa Muumba), na alikuwa ndiye wa kwanza kabisa kumkubali Muhammad kama Mtume wa Allah (s.w.t.) kwa wanadamu wote. Alikuwa ndio Mwislamu mwanamke wa kwanza.

Muhammad "aliutambulisha" Uislamu kwa Khadija. Alimuelezea maana yake, na aka-muingiza kwenye Uislamu.

Heshima ya kuwa mtu wa kwanza katika ulimwengu mzima kushuhudia Upweke wa Allah (s.w.t.) na kuukubali utume wa Muhammad, ni ya Khadija kwa wakati wote.

F.E. Peters anasema:

"Yeye (Khadija) alikuwa wa kwanza kuukubali ukweli wake wa wahyi wake (Muhammad), mwislamu wa kwanza baada ya Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Alimtia moyo na kumsaidia Muhammad wakati wa miaka migumu ya mwanzo ya mahubiri yake ya hadhara, na katika miaka ishirini na tano ya ndoa yao hakuoa mke mwingine. Ndoa yao ilikuwa, kwa kiwango chochote cha akili cha kuamua, ni uwiano wa mapenzi na vilevile ubia wa ushirikiano.

(Allah (s.w.t.) 's Commonwealth, New York)

Kama ilivyoonyeshwa kabla, Ali Ibn Abi Talib, alikuwa akiishi wakati huu na walezi wake, Muhammad na Khadija. Wale vijana wawili wa Muhammad na Khadija - Qasim na Abdullah walikwisha kufa katika uchanga wao. Baada ya kifo chao, walimchukua Ali kama mtoto wao. Ali alikuwa na umri wa miaka mitano alipokuja nyumbani kwao, na alikuwa na miaka kumi pale Muhammad alipofanywa Mtume wa Allah (s.w.t.) Muhammad na Khadija walimlea na kumsomesha. Katika miaka iliyofuatia, alijionyesha

51

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mwenyewe kuwa ni "matokeo" bora sana ya malezi na elimu ile Muhammad na Khadija waliyompa.

Sir William Muir:

'Mara tu baada ya kuijenga upya Al-Kaaba, Muhammad alijiliwaza mwenyewe kwa kupotea kwa mwanae mdogo Qasim kwa kumchukua Ali, mtoto wa rafiki yake na mlezi wake aliyetangulia, Abu Talib. Ali, wakati huu akiwa sio zaidi ya miaka mitano au sita ya umri, alibaki daima baadaye na Muhammad, na walionyeshana upendo wa baba na mwana.'

(The life of Muhammad, London, 1877)

Kwa kuwa Ali alikuwa mmoja wa familia ya Mtume (s.a.w.) mwenyewe, alikuwa bila ya kukwepa, wa kwanza miongoni mwa wanaume kuupokea ujumbe wa Uislamu. Alishuhudia kwamba Mungu ni Mmoja, na kwamba Muhammad alikuwa Mtume Wake. Na alikuwa na shauku ya kusimama nyuma ya Muhammad Mustafa kuswali. Kwa vile Muhammad hakuonekana kamwe kwenye Swala isipokuwa pale Ali alipokuwa pamoja naye.

Mvulana huyu pia alihifadhi Aya za Qur'an Tukufu kila pale ziliposhushwa kwa Muhammad. Kwa namna hii, alikua hasa na Qur'an. Kwa kweli, Ali na Qur'an "vilikua" pamoja kama "mapacha" ndani ya nyumba ya Muhammad Mustafa na Khadija-tul-Kubra. Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.w.t.) alikwishapata mwislamu wa kike wa kwanza kwa Khadija, na mwislamu wa kwanza wa kiume kwa Ali Ibn Abi Talib.

Muhammad Ibn Is'haq anatuambia:

"Ali alikuwa ndiye mwislamu wa kwanza kumwamini Mtume wa Allah (s.w.t.) kuswali naye na kuuamini ujumbe wake mtukufu, alipokuwa ni mvulana wa miaka kumi. Mungu alimpendelea kwa vile alilelewa katika uangalizi wa Mtume (s.a.w.) kabla Uislamu kuanza."

(The life of the Messenger of God)

Muhammad Husein Haykal naye asema:

"Hivyo basi Ali alikuwa ndio kijana wa kwanza kuingia Uislamu. Alifuatiwa na Zayd ibn Harithah, mtumwa wake Muhammad. Uislamu ulibakia umefungiwa ndani ya kuta nne za nyumba moja. mbali na Muhammad mwenyewe, wafuasi wa dini mpya walikuwa ni mkewe, binamu yake, na mtumwa wake."

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

52

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Marmaduke Pickhtalls:

"Wa mwanzo kati ya wafuasi wake (Muhammad) alikuwa ni mke wake, Khadija; wa pili binamu yake wa kwanza Ali, ambaye alimtwaa (kumlea); wa tatu mtumishi wake Zaid, aliyekuwa mtumwa hapo awali."

(Introduction to the Translation of Holy Qur 'an, Lahore, Pakistan, 1975)

Shahidi wa tatu kuukubali Uislamu, alikuwa Zayd ibn Harithah, huria wa Muhammad, na mtu wa nyumba yake.

Tor Andre:

"Zayd alikuwa mmoja wa watu wa mwanzo kuukubali Uislamu, kwa kweli alikuwa wa tatu, baada ya Khadija na Ali."

(Muhammad, the Man and his Faith, 1960)

Ali ibn Abi Talib alikuwa ndio mwanaume wa kwanza kukubali Uislamu, na kutangulia kwake hakuna shaka yoyote. Allama Muhammad Iqbal, yule mshairi-mwanafalsafa wa Indo-Pakistan, anamwita yeye, sio wa kwanza, bali "mwislamu wa mwanzo kabisa."

Ibn Ishaq:

"Kutoka kwa Yahya ibn al-Ash'ath ibn Qays al-Kindi kutoka kwa baba yake, kutoka kwa babu yake Afiif: Al-Abbas ibn Abdul Muttalib alikuwa rafiki yangu aliyekuwa akienda mara kwa mara Yemen kununua manukato na kuyauza wakati wa maonyesho. Nilikuwa pamoja naye huko Mina, alikuja mtu katika ujana wa maisha yake na akatekeleza kanuni zote za wudhu 'u na kisha akasimama na kuswali. Kisha akatoka mwanamke akachukua wudhu 'u na akasimama na kuswali. Kisha akatoka kijana anayekaribia utu uzima, akachukua wudhu 'u, kisha akasimama na akasali kando yake.

Nilipomuuliza Al-Abbas ni nini kilikuwa kinaendelea, akasema kwamba alikuwa ni mpwa wake Muhammad Ibn Abdullah Ibn Abdul Muttalib, anayedai kwamba Allah (s.w.t.) amemtuma kama Mtume; yule mwingine ni mtoto wa ndugu yangu, Ali Ibn Abi Talib, ambaye amemfuata katika dini yake; yule wa tatu ni mke wake, Khadija binti ya Khuwaylid ambaye pia anamfuata katika dini yake. Afiif alisema baada ya kuwa amekuwa mwislamu na Uislamu ukiwa umejengeka imara moyoni mwake, 'Laiti mimi ningekuwa wa nne!'

(The Life of the Messenger of God)

53

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Shahidi wa nne aliyeukubali Uislamu, ni Abu Bakr, mfanyibiashara wa Makka.

Hapo mwanzoni, Muhammad alihubiri Uislamu kwa siri kwa hofu ya kuamsha uhasama wa waabudu masanamu. Aliwaita tu wale watu kwenye Uislamu ambao alijuana nao yeye binafsi. Inasemekana kwamba kwa juhudi za Abu Bakr, huyu mwislamu wa nne, watu wengine wachache wa Makka pia waliukubali Uislamu. Miongoni mwao walikuwa Uthman bin Affan, Khalifa wa baadae wa Waislamu; Talha, Zubayr, Abdur Rahman bin Auf, Saad bin Abi Waqqas, na Ubaidullah ibn al-Jarrah.

Kwa muda mrefu Waislamu walikuwa wachache kwa idadi na hawakuthubutu kuendesha Swala zao hadharani. Mmoja wa wafuasi wa mwanzo wa Uislamu alikuwa ni Arqam bin Abi al-Arqam, kijana wa ukoo wa Makhzuum. Alikuwa tajiri na akiishi katika nyumba yenye nafasi kubwa katika bonde la Safa. Waislamu walikusanyika kwenye nyumba yake kuswali Swala zao za jamaa. Miaka mitatu ikapita kwa namna hii. Kisha katika mwaka wa nne, Muhammad aliamriwa na Allah (s.w.t.) kuwaita jamaa zake mwenyewe kwenye Uislamu waziwazi.

Usahihi-4.jpg

"Na waonye jamaa zako wa karibu." Sura ya 26; Aya ya 214)

Jamaa zake Muhammad walihusisha watu wote wa Bani Hashim na Bani al-Muttalib. Alimuamuru binamu yake mdogo, Ali, kuwaita wakubwa wao wote kwenye dhifa - watu arobaini.

Wakati wageni wote walipokuwa wamekusanyika kwenye ukumbi katika nyumba ya Abu Talib, na wameshiriki katika mlo wao, Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) akasimama kuongea nao. Mmoja wa wageni hao alikuwa ni Abu Lahab, ami yake Mtume (s.a.w.) kwa upande wa baba yake. Alikuwa amesikia minong'ono ya nini mpwa wake alichokuwa akifanya hapo Makka kwa siri, na yumkini akahisi sababu ya kwa nini amewaalika Bani Hashim kwenye karamu. Mtume (s.a.w.) alikuwa ameanza tu kuongea pale aliposimama; kifidhuli akamkatiza, na yeye mwenyewe akahutubia ule mkusanyiko, akisema:

"Ami zangu, kaka zangu na binamu zangu! Msimsikilize huyu "msaliti," na msiitupe dini ya mababu zenu kama akiwaiteni kutwaa dini mpya. Kama mtafanya hivyo, basi kum-bukeni kwamba mtaamsha ghadhabu za Waarabu wote dhidi yenu. Hamna nguvu za kupi-gana dhidi yao wote. Kwanza kabisa, sisi ni wachache mno. Kwa hiyo, ni kwa faida yenu kuwa imara katika dini yenu ya jadi."

54

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abu Lahab, kwa hotuba yake, alifanikiwa kuzua mtafaruku na vurugu kwenye mkutano huo hivyo kwamba kila mtu alisimama na kuzunguka na kusukumana. Kisha wakaanza kuondoka, na mara ukumbi ukawa mtupu.

Muhammad, jaribio lake la kwanza la kugeuza kabila lake mwenyewe likashindwa. Lakini bila kuhangaishwa na kizuizi hiki cha kwanza, alimuamuru binamu yake, Ali, kuwaalika wageni walewale kwa mara ya pili.

Siku chache baadae wageni wale wakaja, na walipokwisha kula chakula cha jioni, Muhammad alisimama na kuzungumza nao kama ifuatavyo:

"Ninamshukuru Allah (s.w.t.) kwa rehma zake. Namhimidi Allah (s.w.t.) na ninaom-ba mwongozo wake. Ninamuamini Yeye na ninaweka dhamana yangu Kwake. Ninashuhudia kwamba hakuna mungu ila Allah (s.w.t.); Hana mshirika; na mimi ni Mtume Wake. Allah (s.w.t.) ameniamuru mimi niwaiteni ninyi kwenye dini Yake kwa kusema: "Waonye jamaa zako wa karibu'. Mimi, kwa hiyo, ninawaonya, na kuwatak-eni ninyi mkiri kwamba hakuna mungu ila Allah (s.w.t.) na kwamba mimi ni Mtume Wake.

"Enyi wana wa Abdul Muttalib! hakuna yeyote aliyewahi kuja kwenu kabla na kitu chochote bora kuliko kile nilichokuleteeni mimi. Kwa kukikubali kwenu, mambo yenu yatahakikishwa hapa duniani na kesho Akhera. Ni nani kati yenu atanisaidia katika kutekeleza kazi hii muhimu? Nani miongoni mwenu atasaidiana pamoja nami katika kutekeleza kazi hii nzito? Nani ataitikia mwito wangu? Ambaye atakuwa khalifa wangu, makamu wangu na waziri wangu?"

Walikuwepo wageni arobaini katika ukumbi huo. Muhammad alisita kidogo kuacha uzito wa maneno yake uingie kwenye mawazo yao lakini hakuna mtu kati yao aliyejibu. Mwishowe kimya kilipokuwa kizito mno, kijana Ali akasimama na kusema kwamba atam-saidia Mtume wa Allah (s.w.t.); angeshiriki katika uzito wa kazi yake; na angekuwa Khalifa wake, makamu na waziri wake. Lakini Muhammad alimuashiria akae chini, na akasema: "Subiri! Pengine mtu mzima kuliko wewe ataitika mwito wangu."

Muhammad alirudia mwaliko wake lakini bado hakuna hata mmoja aliyeelekea kushtuka, na alikaribishwa tu na kimya chenye wasiwasi. Kwa mara nyingine tena, Ali akajitolea msaada wake lakini Mtume (s.a.w.) bado akitaka kwamba mtu mzima wa ukoo wake angeweza kukubali mwaliko wake, na akamuomba Ali asubiri. Yeye tena akatoa ombi hilo kwa ukoo wake kwa mara ya tatu kufikiria mwaliko wake, na yakatokea yaleyale. Hakuna mtu katika mkutano ule aliyeonyesha shauku. Alilichunguza lile kundi na kumtupia macho kila mmoja kati yao lakini hakuna aliyetikisika. Baada ya muda mrefu akauona mwili pekee wa Ali akinyanyuka kwenye mkutano ule wa watu wakimya, kujitolea msaada wake kwake. Safari hii Muhammad alikubali kujitolea kwa Ali. Alimvuta karibu, akamkumbat-

55

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ia kifuani kwake, na akauambia mkutano: "Huyu ni waziri wangu, mrithi wangu na Khalifa wangu. Msikilizeni na mtii amri zake."

Edward Gibbon:

"Miaka mitatu ilitumika kimya kimya katika ubadilishaji wa watu kumi na nne waliobadili dini, matunda ya awali ya ujumbe wake Muhammad; Lakini katika mwaka wa nne alirudia tena kazi yake ya utume, na kwa kuazimia kuwapa familia yake ule mwanga wa haki tukufu, alitayarisha karamu ya kuwakaribisha wageni arobaini wa kizazi cha Hashim. 'Marafiki na ndugu zangu,' Muhammad aliuambia mkusanyiko huo, 'Ninakupeni ninyi, na ni mimi pekee ninayeweza kuwapeni, zawa-di iliyo bora sana, hazina za dunia hii na ijayo. Allah (s.w.t.)ameniamuru niwaiteni kwenye utumishi Wake. Nani miongoni mwenu atanisaidia katika kazi hii? Ni nani kati yenu atakayekuwa mwenzangu na waziri wangu?'

Hakuna jibu lililorudishwa, mpaka kimya cha kushangaza na mashaka, na aibu baada ya muda mrefu ilivunjwa na ujasiri wa haraka wa Ali, kijana aliyekuwa katika mwaka wa kumi na nne wa umri wake. 'Ewe Mtume' alisema, 'Mimi ndimi. Yeyote atakayes-imama dhidi yako, nitayang'oa meno yake, nitayapasua macho yake, nitavunja miguu yake, nitararua tumbo lake. Ewe Mtume, mimi nitakuwa waziri wako juu yao.' Muhammad alikubali ahadi yake kwa furaha, na Abu Talib kwa kejeli sana alishauri-wa kuheshimu hadhi ya juu ya mwanae."

(Decline and Fall of the Roman Empire) Washington Irving:

Enyi wana wa Abd al-Muttalib,' aliita Muhammad kwa shauku, 'kwenu ninyi, kati ya watu wote, Allah (s.w.t.) ametoa zawadi hizi zenye thamani kubwa. Kwa Jina Lake ninakupeni neema za dunia hii, na furaha ya milele ya Akhera. Nani kati yenu atashirikiana nami katika uzito wa ahadi yangu? Nani atakuwa ndugu yangu, msaidizi wangu na waziri wangu?'Wote walibakia kimya; wengine wakistaajabu; wengine wakitabasamu kwa mshangao na dhihaka.

Mwishowe Ali, akianza kwa ghera ya ujana, alijitolea binafsi kumtumikia Mtume ingawa kwa wastani akitambua ujana wake na udhaifu wake wa kimwili. Muhammad akatupa mikono yake kumzunguka kijana huyu mkarimu, na kumkumbatia kifuani mwake. 'Muoneni ndugu yangu, waziri wangu, khalifa wangu' aliguta, 'Wote msikie maneno yake, na mumtii.' ".

(The Life of Muhammad)

56

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir Richard Burton:

"Baada ya muda mrefu wa kutafakari, kwa kuchochewa na hasira za ushupavu wa kipumbavu wa Wayahudi, ushirikina wa Wasyria na Wakristo wa Kiarabu, na kule kuabudu masanamu kunakochukiza kwa watu wasioamini wa nchi yake, mwenye shauku pia - na ni moyo gani mkuu usiokuwa na shauku? - Yeye (Muhammad) alid-hamiria kurekebisha maovu yale ambayo yalisaidia wahyi kudharaulika kwa wasomi na wenye madhara kwa washenzi. Alijitambulisha kama aliyejaaliwa katika ujumla wa jamaa zake na wenzake katika ukoo. Hatua hiyo ilishindwa, isipokuwa kwamba ilimpatia mtu aliyesilimu mwenye thamani ya askari wa farasi elfu moja ambaye ni Ali, mwana wa Abu Talib."

(The Jew the Gypsy and El Islamu, San Francisco, 1898)

Ali amejitolea huduma zake kwa Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) na Mtume (s.a.w.) alimkubali. Kwa watu wazima wa kabila hilo, tabia ya Ali ingeweza kuonekana ya pupa na yenye kushupaa lakini mara alithibitisha kwamba alikuwa na ujasiri na uvumilivu wa kutimiza, mkubwa zaidi kuliko waliokuwa nao wengine, ushujaa huo hata kuota. Mtume wa Allah (s.w.t.) kwa upande wake, aliupokea msaada huo sio tu na muonekano wa shukrani na furaha bali pia alitamka kwamba Ali alikuwa, kutoka muda ule, Khalifa wake.

Tamko la Muhammad lilikuwa la wazi na lisilo na mashaka. Ni upuuzi kubishana, kama watu wengine wanavyofanya, kwamba ukhalifa wa Ali kwa Muhammad, ulikomea kwenye kabila la Bani Hashim. Lakini Muhammad mwenyewe hakuuwekea mipaka ukhalifa wa Ali kwa Bani-Hashim. Ali alikuwa Khalifa wake kwa Waislamu wote na kwa wakati wote.

Ile karamu ambayo Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) alimtangaza Ali kama mrithi wake, ni maarufu katika historia kwa jina la karamu ya Dhul- 'Ashiir - "karamu ya jamaa wa karibu." Jina hili limetoka kwenye Qur'an tukufu yenyewe (Sura ya 26; Aya ya 214). Ajabu, Sir William Muir ameliita tukio hili la kihistoria "lisiyothibitishwa." Lakini ni nini "kisichothibitishwa" au kisicho yamkini kiasi hicho kuhusiana na hilo? Kuna kitu kinaweza kuwa na mantiki zaidi kwa Mtume wa Allah (s.a.w.) kuliko kuanza kazi yake ya kuhubiri Uislamu nyumbani kwake mwenyewe, na watu wa familia yake mwenyewe na ukoo wake mwenyewe, hasa baada ya kuamriwa kwa dhati na Allah (s.w.t.) kuwaonya jamaa zake wa karibu?

Ile karamu ya Dhul- 'Ashiir ambayo Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) alimteua Ali ibn Abi Talib, kama mrithi wake, ni tukio la kihistoria, na usahihi wake umethibitishwa, mion-goni mwa wengine, na wanahistoria wa Kiarabu wafuatao:

57

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

1. Tabari, Tarikh, juz. 2, uk. 217

2. Kamil ibn Athir, Tarikh, juz. 2, uk. 22

3. Abul Fida, Tarikh, juz.1, uk.116

Sir William Muir:

"Binamu yake (Muhammad), Ali, sasa akiwa na umri wa miaka 13 au 14, tayari ali-toa dalili za hekima na uamuzi ambao ulimbainisha yeye katika maisha ya baadae. Ingawa alikuwa ana juhudi isiyoshindika, alikosa nguvu ya msukumo ambayo ingem-fanya kuwa mhubiri wa Uislamu mwenye kufaa sana. Alikua tangu utotoni katika dini ya Muhammad, na uhusiano wake wa mapema uliimarisha misimamo ya miaka ya ukubwani."

(The Life of Muhammad, London, 1877)

Tunayo mashaka mengi sana kuhusu kauli ya Sir William Muir kwamba Ali "alikosa nguvu ya msukumo ambayo ingemfanya yeye kuwa mhubiri wa kufaa sana wa Uislamu." Ali hakukosa nguvu wala kitu kingine chochote. Katika upeo wa migogoro yote ya Uislamu, alichaguliwa kutekeleza yale majukumu ya hatari kabisa, na kila wakati aliya-timiza.

Kama mhubiri, vilevile Ali alikuwa bila kifani. Hakukuwa na yeyote kati ya maswahaba wote wa Mtume (s.a.w.) aliyekuwa mhubiri mwenye nguvu kuliko yeye. Alizitangaza rasmi zile Aya 40 za mwanzo za Surat Bara'a (Tawba), ile Sura ya tisa ya Qur'an Tukufu, kwa mapagani huko Makka, kama mhubiri wa kwanza wa Uislamu, na kama mtu anayemuwakilisha Mtume wa Allah (s.a.w.) binafsi. Na alikuwa ni Ali aliyeyaingiza mak-abila yote ya Yemen katika Uislamu.

Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) , alimlelea Ali kama mtoto wake mwenyewe, na kama Ali alikosa chochote, yeye Mtume (s.a.w.) angekijua. Alimtangaza Ali kuwa waziri wake, mrithi wake na Khalifa wake katika wakati ambao hakuna ambaye angeweza kubashiri ile hali ya baadae ya Uislamu. Hii inaonyesha tu uhakika usio na kikomo ambao Mtume wa Uislamu aliokuwa nao juu ya mvulana huyu wa miaka kumi na minne.

Ali aliashiria matarajio na matumaini ya Uislamu. Katika mapinduzi makubwa ambayo Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliyaanzisha pale kwenye karamu ya Dhul- 'Ashiira, alihamasisha ule uwezo, udhanifu, na ari na juhudi za ujana; Ali alikuwa mfano wa yote haya.

Mambo mawili yalitokea pale kwenye Karamu. Moja lilikuwa kwamba Mtume (s.a.w.) ali-utoa nje Uislamu kwenye uwazi. Uislamu haukuwa tena harakati ya "siri"; ulikuwa

58

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"umeibuka." Kwenye karamu ya jamaa zake wa karibu, Muhammad alikuwa "amejiingiza katika jambo" na sasa hakungeweza kuwa na kugeuka nyuma. Wakati ulikuwa umek-wishafika wa kuutoa ujumbe wa Uislamu nje ya ukoo wake mwenyewe, kwanza kwa Maquraishi wa Makka, kisha kwa Waarabu wote, na hatimae, kwa dunia yote iliyobakia. Jingine lilikuwa kwamba alimpata Ali ambaye alikuwa ndiye mfano halisi wa shauku, kuji-tolea na ushupavu, na alikuwa na thamani kubwa zaidi kuliko askari wa farasi elfu moja.

Imeelezwa kwamba siku kadhaa baada ya ile karamu ya Dhul- 'Ashiira ya pili, Muhammad alipanda kile kilima cha Safa karibu na Al-Kaaba, na akaita: "Enyi wana wa Fihr, Enyi wana wa Lui, Enyi wana wa Adi, na Quraishi wote waliobakia! Njooni hapa, na munisik-ilize. Nina kitu muhimu sana cha kuwaambieni ninyi."

Wengi wa watu wale wa Makka waliosikia sauti yake, walikuja kumsikiliza. Akiwahutubia, alisema: "Mtaniamini kama ingekuwa niwaambie kwamba kuna jeshi lime-jificha nyuma ya vilima vile, na lilikuwa likiwatazameni ili kuwashambulieni mara tu litakapowaona tu hamkujilinda?" Walisema wangemuamini kwa sababu hawajamsikia akisema uongo.

"Kama hivyo ndivyo," alisema Muhammad, "basi sikilizeni hili kwa makini. Mola wa Mbingu na Ardhi ameniamuru mimi kuwaonyeni ninyi juu ya wakati wa kuogopesha sana unaokuja. Lakini kama mtakuwa wasikivu, mtaweza kujiokoa wenyewe na laana ya milele..." Alikuwa amefikia hapo tu wakati Abu Lahab, ambaye alikuwepo miongoni mwa wasikilizaji hao, alipomuingilia kati tena kwa kusema: "Kifo juu yako! Umepoteza muda wetu kutuambia hili tu? Hatutaki kukusikia. Usituite tena."

Kuanzia hapo Abu Lahab akafanya ni mazoea ya kumfuata Mtume (s.a.w.) kila alipokwen-da. Kama alianza kusoma Qur'an au kusema kitu kingine, yeye Abu Lahab alimkatiza au alianza kumsumbua. Chuki ya Abu Lahab kwa Muhammad na Uislamu aliichangia na mkewe, Ummu Jameel. Wote walikuwa wenye kulaaniwa na Allah (s.w.t.) ndani ya Qur'an Tukufu (Sura ya 111).

59

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

WALIOSILIMU MWANZONI NA MATESO KUTOKA KWA WAPAGANI

Ingawa Abu Lahabi mara nyingi alifanikiwa katika kuyatawanyisha yale makundi yaliyokusanyika kusikiliza waadhi za Mtume, habari hata hivyo zilienea Makka kuhusu mawaidha hayo. Baadhi ya watu walizungumza kuhusu ujumbe wa Uislamu. Wale wenye fikra miongoni mwao waliuliza hili swali: "Ni dini gani hii ambayo Muhammad anatuitia sisi?" Swali hili lilionyesha udadisi kwa upande wao kuhusu huu ujumbe wa Uislamu, na wachache miongoni mwao walitaka kujua zaidi juu yake.

Katika siku zilizofuata, Muhammad alifanya majaribio mengi ya kuwahubiria watu wa Makka. Abu Lahab na mshirika wake, Abu Jahal, walifanya kila walichoweza kuihujumu kazi yake lakini hawakuweza kumkengeusha kutoka kwenye shabaha yake.

Muhammad, rehma na amani ziwe juu yake na kizazi chake, alitambua kwamba kazi yake haitakuwa rahisi. Alijua kwamba atakumbana na vikwazo vingi, na kwamba atakuwa apambane na upinzani mkali na wa kudumu wa waabudu masanamu. Lakini alitegemea rehma za Mungu kumuwezesha kuushinda upinzani.

Ulikuwa ni ujumbe wa ajabu ambao Muhammad alileta kwa Waarabu, na ulikuwa wa kipekee. Hakuna hata mtu mmoja aliyewahi kusikia kitu kama hicho kabla. Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) aliwaambia Waarabu wasiabudu kundi la vitu visivyo na uhai vilivyotengenezwa kwa mawe au magogo (miti) ambavyo wameviunda wenyewe, na ambavyo havikuwa na uwezo wa ama kuwapa wao chochote au kuchukua chochote kutoka kwao. Badala yake, aliwaambia, wanapaswa kutoa utii wao kwa Allah (s.w.t.) Mola wa ulimwengu wote. Aliwaambia pia kwamba katika macho Yake, katika macho ya Muumba wao, wote walikuwa sawa, na kama watakuwa Waislamu, watakuwa wote ni ndugu wa kila mmoja wao.

Muhammad pia alipenda kuirekebisha jamii ya Kiarabu. Hii sheria mpya ambayo ameiwe-ka mbele kwa ajili ya madhumuni Haya, ilifanya Imani badala ya damu, kuwa kiungo maalum cha jamii hiyo. Lakini Waarabu hao wamezaliwa katika mfumo wa mila na des-turi za kipagani; waliamini katika msingi wa miundo ya kikabila na udugu. Kwao wao "damu" ilikuwa tu ni kigezo cha mpangilio wa kijamii. Katika mawazo yao, kama dini ingeruhusiwa kuchukua nafasi ya damu katika mgawanyo huu, ingeweza kuvuruga muun-do wote wa jamii ya Kiarabu.

Muhammad pia aliwataka wale Waarabu matajiri kugawana utajiri wao na masikini na wale wenye kipato cha chini. Wale masikini, alisema, walikuwa na haki ya kupokea fungu

60

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

lao kutoka kwenye mali ya matajiri. Ugawanaji huo, aliendelea kusema, utahakikisha ugawaji wa haki wa mali katika jamii.

Wengi wa Waarabu matajiri walikuwa wakopesha-fedha; ama hasa, walikuwa "wala riba wakubwa." Wamekuwa matajiri kwa kukopesha fedha kwa watu masikini kwa viwango vikubwa sana vya riba. Wale masikini hawakuweza kamwe kulipa madeni yao, na kwa hiyo wakanasa katika utumwa wa kiuchumi milele. Kugawana mali yao ya haramu na watu walewale waliokuwa wakiwanyonya, ilikuwa kwao ni sawa na "kufuru." Kwa kuwapen-dekezea kwamba wagawane mali yao na masikini, Muhammad alichezea kiota cha nyigu!

Kwa Waarabu, yote haya yalikuwa mambo mapya na yasiyojulikana; kwa kweli yalikuwa ya kimapinduzi. Kwa kuhubiri mambo ya kimapinduzi kama haya, Muhammad ali-wakasirisha wale wenye madaraka tangu zamani. Waliokasirika sana miongoni mwao ni ule ukoo wa Umayya wa Maquraish. Watu wake ndio waliokuwa wala-riba wanaoongoza na mabepari wa Makka, na walikuwa ndio makuhani wakuu wa hekalu la wapagani. Ndani ya Muhammad na huo ujumbe wa Uislamu, waliona tishio kwenye utaratibu wao wa kijamii ambao uliegama kwenye heshima na nguvu.

Wao, kwa hiyo, waliamua kudumisha hali kama ilivyo. Katika miaka iliyokuja, walikuwa waunde kikosi cha vita visivyotulizika dhidi ya Uislamu, na upinzani wa kufa baada ya mapambano na Muhammad.

Lakini walikuwepo pia watu wachache walioona mvuto wenye nguvu katika yale mawazo mapya ambayo Muhammad alikuwa anayaanzisha, kwa ujumla yakiitwa Uislamu. Kwa kweli, waliyaona ni yasiyokanika, na kwamba waliyakubali.

Miongoni mwa waliosilimu mwanzo kwenye Uislamu walikuwa Yasir; mke wake, Sumayya; na mtoto wao wa kiume, Ammar. Walikuwa ndio ukoo wa kwanza ambao watu wake wote waliukubali Uislamu sawia, hivyo kuwa Familia ya Kiislam ya Kwanza.

Uislamu ulikuwa na mvuto maalum kwa matabaka ya waliokandamizwa hapo Makka. Pale watu wa matabaka haya walipokuwa Waislamu, walitambua pia kwamba kama wapagani, walidharauliwa na kutengwa na tabaka la juu la wenye kujali tabaka na wenye kujali utaifa wa hali ya juu wa Makka lakini Uislamu uliwapa kujiheshimu kupya. Kama Waislamu waliona fahari mpya ndani yao wenyewe.

Wengi wa waliosilimu mwanzo walikuwa "masikini na wanyonge." Lakini walikuwepo Waislamu wachache matajiri pia kama Hudhayfa bin Utba na Arqam bin Abil-Arqam. Na wale watu wote ambao Abu Bakr aliwaleta kwenye Uislamu - Uthman, Talha, Zubayr, Abdur Rahman ibn Auf, Saad ibn Abi Waqqas na Abu Ubaidah ibn al-Jarrah - walikuwa pia ni matajiri na wenye nguvu. Walikuwa ni watu wa koo mbalimbali za Kiquraish.

61

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Tunaweza kuchukulia kwamba pale mwanzoni, lile tabaka la juu la wapagani wa Makka lilishuhudia zile juhudi za Uislamu za kutaka kupata kutambuliwa zaidi kwa burudani kuliko kwa kero, bila ya kuzungumzia zile chuki na mpagao uliowashika baadae kidogo. Lakini jinsi harakati hii mpya ilivyoanza kushika kasi, walihisi kwamba yale mawazo ambayo Muhammad alikuwa akiyatangaza, yalikuwa kwa kweli ni "hatari," na hayakuwa na chochote cha kichekesho juu yake. Walihoji kwamba mababu zao wameabudu masana-mu kwa vizazi visivyo na idadi, kwa hiyo ibada ya masanamu ilikuwa ni sawa; na hawakuweza kumruhusu Muhammad kucheza na mtindo wao wa ibada.

Lakini Muhammad hakuridhika tu kukanusha ibada ya masanamu. Ya hatari zaidi na ya kutisha kwa Bani Umayya wenye-uchu wa mali ilikuwa ni mawazo yake ya haki za kiuchumi na jamii yaliyotishia kuangusha ngome yao ya heshima; muundo wa zamani wa madaraka na kundi la watu wenye madaraka; na taasisi zote za zamani zilizopitwa na wakati. Waliweka wazi, kwa hiyo, kwamba heshima ilikuwa ni kitu ambacho hawatakiacha - kwa gharama yoyote ile - iwe jahannam au maji marefu.

Lakini wazo moja ambalo lile tabaka la juu lililojichagua lenyewe la Quraish, lililoliona la kufedhehesha zaidi, lilikuwa ni ile "dhana" iliyopangwa na Muhammad, kwamba wale watu wa matabaka ya waliokandamizwa, waliodharauliwa, walionyonywa, wengi wao wakiwa watumwa wao, ambao sasa wamesilimu, wamekuwa wanaolingana - walinganao na Maquraish wakubwa na wenye nguvu! Dhana yao kuu ya maisha ilikuwa ni majigam-bo na makuu, na usawa na watumwa wao wenyewe, walio achwa-huru na watumishi, ulikuwa kwao hauwaziki kabisa. Walikuwa wamejawa na ghiliba ya "ubora" wao binafsi kuliko wanadamu wote.

Kwa kutangaza rasmi hii kanuni ya "kinyume" ya usawa - usawa wa bwana na mtumwa, tajiri na masikini; na Mwarabu na asiyekuwa Mwarabu; kwa kukana madai ya ubora wa ukoo, na kufundisha kwamba mbele ya Allah (s.w.t.) hali ya muumini ilikuwa ya juu sana kuliko hali ya wasioamini wote katika dunia, Muhammad alitenda "uhaini" dhidi ya Maquraish!

Maquraish waliabudu masanamu mengi sana, na utaifa ilikuwa mojawapo.

Lakini kujivunia utaifa hakuthaminiwi katika Uislamu. Kwa mujibu wa Qur'an Tukufu, watu wote wametokana na Adam, na Adam alikuwa ni udongo. Ibilisi (Shetani) alilaaniwa kabisa kwa sababu alihoji ubora wa kile alichodhania kuwa asili yake ni ya juu kama kinyume na alichokiona kuwa uchini sana wa asili ya mwanadamu. "Mwanadamu," alise-ma, "ameumbwa kwa udongo ambapo mimi nimeumbwa kutokana na moto." Hisia kama hizi za utenganishaji ambazo huja pia kwa wanadamu hasa kwa nia ya kudai hadhi bora ya damu katika utu wao, zimekataliwa na Uislamu kwa nguvu kabisa. Uislamu umeangusha chini umaarufu wa utaifa, rangi na heshima, na umewakataza Waislamu

62

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kuwagawa watu katika makundi kwa misingi ya damu na/au ujirani wa kijografia au hadhi maalum ambazo wanaweza kuzidai juu yao wenyewe.

Machoni mwa Qur'an, mtu aliye bora sana ni yule muttaqi - yaani, mtu ambaye anampen-da na kumtii Allah (s.w.t.) wakati wote. Katika Uislamu, kipimo pekee cha ubora wa mtu, ni mapenzi yake kwa Muumba. Mitihani mingine yote ya maisha binafsi haina maana yoy-ote.

Lakini kama ilivyoelezwa hapo juu, Maquraish hawakuwa katika hali ya kupokea mawa-zo haya. Pengine walikuwa kiufahamu hawawezi kuyazingatia haya. Waliyaona kama ni kufuru ya daraja, na kwa hiyo, yasiyoweza kuvumilika kabisa. Ulikuwa ni wakati huo basi pale walipoamua sio tu kumpinga Muhammad, Mtume wa Uislamu, bali pia kuangamiza huo "uasi" ulioitwa Uislamu wenyewe kabla haujaota mizizi na kuwa wenye kuji-tosheleza.Walisukumwa na Kiburi - majivuno yanayojijaza yenyewe kuzidi kipimo cha mwanadamu - na kwa tamaa ya madaraka kufanya uamuzi kama huo dhidi ya Muhammad na Uislamu.

Wakiwa na uamuzo huu, Maquraish walitangaza nia yao ya kupigana katika kulinda masanamu yao na miungu yao na vilevile katika ulinzi wa mfumo wao wa kiuchumi na kijamii.

Makka ilikuwa katika hali ya kivita!

Maquraish walifungua mapambano dhidi ya Uislamu kwa kuwabughudhi na kuwatesa Waislamu. Mwanzoni, mateso yaliishia kwenye kuzomea na kebehi na matusi. Lakini kiasi muda ulivyoendelea mbele, makafiri hao walitoka kwenye ukali wa maneno kwenda kwenye ukali wa matendo. Walijizuia kuumiza majeraha ya mwili juu ya Muhammad mwenyewe kwa hofu ya kuchochea visasi; lakini hawakuwa na kusita katika kuwaumiza Waislamu, askari wa kawaida. Kwa muda mrefu, walikuwa ni hawa askari wa kawaida waliobeba sehemu kubwa ya ghadhabu za Maquraish.

Ibn Ishaq:

"Kisha Maquraish wakawachochea watu dhidi ya maswahaba wa Mtume (s.a.w.) ambao wamekuwa Waislamu. Kila kabila liliwashambulia Waislamu miongoni mwao, wakiwapiga na kuwashawishi kutoka kwenye dini yao. Mungu alimkinga Mtume wake kutokana nao kupitia ami yake (Abu Talib), ambaye, alipoona kile Maquraish walichokuwa wakikifanya, aliwaita Bani Hashim na Bani Muttalib kusi-mama naye katika kumkinga Mtume. Hili walikubaliana kulifanya, isipokuwa Abu Lahab."

(The Life of the Messenger of God)

63

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Baadhi ya waathirika wa mateso:

Bilal, yule aliyekuwa mtumwa wa Kihabeshi wa Umayya bin Khalaf. Umayya na makafiri wengine walimtesa katika mwanga mkali wa jua la moto sana la Makka, na wakamtesa kupita kiasi cha uvumilivu wa binadamu. Lakini aliimarishwa na asili ya nguvu za ndani na ujasiri ambavyo kamwe havikumvunja moyo. Kumpenda Allah (s.w.t.) na mapenzi kwa Mtume Wake vilimuwezesha kuyavumilia mateso kwa furaha. Abu Bakr akamnunua kuto-ka kwa bwana wake na akamwacha huru. Mtume (s.a.w.) alipohamia Madina, alimteua Bilal kuwa Muadhini wa kwanza wa Uislamu. Sauti yake kubwa yenye kuvuma ilisikika kwenye anga la Madina kwa ukelele wa Allah-u-Akbar (Mungu ni Mkubwa).

Katika miaka ya baadae, wakati utekaji wa peninsula ulipokamilika, Mtume wa Allah (s.w.t.) alimchagua Bilal kuwa katibu wake wa hazina.

Khabab ibn el-Arat. alikuwa ni kijana wa miaka ishirini aliposilimu. Alikuwa mtegemezi wa Banu Zuhra. Maquraish walimtesa siku baada ya siku. Alihama pamoja na Mtume (s.a.w.) kwenda Madina.

Suhaib bin Sinan, alikuwa ametekwa na kuuzwa kama mtumwa na Wagiriki. Alipokuja kuwa mwislamu, Maquraish walimpiga kikatili sana lakini hawakuweza kuitingisha imani yake.

Abu Fukaiha, alikuwa mtumwa wa Safwan bin Umayya. Alisilimu katika wakati mmoja na Bilal. Kama Bilal, aliburuzwa pia na bwana wake katika mchanga wa moto akiwa ame-fungwa kamba miguuni mwake. Abu Bakr alimnunua na kumpa uhuru. Alihamia Madina na Mtume (s.a.w.) lakini akafa kabla ya vita vya Badr.

Lubina, alikuwa mtumwa wa kike wa Mumil bin Habib. Amin Dawidar anaandika katika kitabu chake, Pictures From the Life of the Prophet (Cairo, Egypt, 1968), kwamba Umar bin al-Khattab, khalifa wa baadae wa Waislamu, alimtesa, na kila alipopumzika, alisema: "Sikuacha kukupiga kwa sababu ya huruma. Nimesimama kwa sababu nimechoka." Alirudia kumpiga baada ya kupumzika. Abu Bakr alimnunua na akamuacha huru.

Zunayra, alikuwa mtumwa mwingine wa kike. Alipotangaza imani yake katika Uislamu, Umar ibn al-Khattab, na Abu Jahl, walipokezana katika kumtesa mpaka akawa kipofu. Amin Dawidar anaeleza kwamba miaka mingi baaadae alirudia kuona tena, na Maquraish wakakuhusisha kupona huku na "uchawi" wa Muhammad. Abu Bakr akamnunua na kumwacha huru.

Nahdiyya na Ummu Unays walikuwa ni watumwa wengine wawili wa kike ambao walikuja kuwa Waislamu. Mabwana zao waliwatesa kwa kuukubali Uislamu. Abu Bakr aliwanunua na akawapa uhuru wao.

64

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Walikuwepo Waislamu wengine ambao hawakuwa watumwa bali walikuwa "masikini na wanyonge." Wao pia walipata mateso. Miongoni mwao walikuwa ni Ammar ibn Yasir na wazazi wake. Mtu mwingine wa kundi hili alikuwa ni Abdullah ibn Masud, kijana wa Kiislam. Alitambulikana miongoni mwa maswahaba wa Mtume (s.a.w.) kwa elimu yake na maarifa, na alikuwa mmoja wa mahafidh (wa Qur'an kwa kichwa) wa mwanzoni katika Uislamu, kila Aya mpya ilipoteremshwa, aliisikia kutoka kwa Mtume (s.a.w.) na akaikariri.

Imeelezwa kwamba wakati Surat Rahman (Sura ya 55) iliposhuka, Mtume wa Allah (s.w.t.) aliwauliza maswahaba zake, ni nani miongoni mwao angekwenda kwenye Al-Kaaba na kuisoma mbele ya makafiri. Masahaba wengine walirudi nyuma lakini Abdullah ibn Masud akajitolea kwenda. Alikwenda kwenye Al-Kaaba na akaisoma Sura hiyo mpya kwa sauti kubwa. Baada ya Mtume (s.a.w.) mwenyewe, Abdullah ibn Masoud alikuwa ndiye mtu wa kwanza kusoma Qur'an ndani ya Al-Kaaba mbele ya kundi lenye uhasama la makafiri. Hawa makafiri walimponda mara kwa mara lakini hawakuweza kumtishia kuwa kimya.

Ibn Ishaq anasema:

"Yahya ibn Urwa ibn al-Zubayr aliniambia, kama kutoka kwa baba yake kwamba mtu wa kwanza kusoma Qur'an kwa sauti hapo Makka, baada ya Mtume (s.a.w.) mwenyewe alikuwa ni Abdullah ibn Masud."

(The Life of the Messenger of God)

Mwanachama mwingine wa kundi hili alikuwa Abu Dharr al-Ghiffari. Alikuwa wa kabi-la la Ghiffar ambalo liliishi maisha yao kwa unyang'anyi. Kutoka kwa wasafiri alisikia kwamba ametokea Mtume (s.a.w.) hapo Makka ambaye amewashauri Waarabu kutupilia mbali ibada ya masanamu, na kumuabudu Allah (s.w.t.) peke yake, kutosema chochote ila kweli tupu, na kutowazika mabinti zao wakiwa hai. Alijihisi kwamba amevutiwa sana na Mtume huyu, na akasafiri kwenda Makka kuthibitisha ukweli wa taarifa alizozisikia kuhusu yeye.

Huko Makka alikuwa mgeni. Alikwisha kusikia kwamba Muhammad amekwishajifanyia maadui wengi mwenyewe kwa kuhubiri kinyume na ushirikina wa Kiarabu. Yeye, kwa hiyo, alisita kumuuliza mtu yeyote kumhusu Muhammad. Aliitumia siku nzima kwenye kivuli cha Al-Kaaba kuangalia wapita njia. Wakati wa jioni, Ali ibn Abi Talib alibahatika kupita hapo alipokuwa. Ali aligundua kwamba Abu Dharr alikuwa mgeni pale mjini, na akamkaribisha nyumbani kwake kwa ajili ya chakula cha jioni.

Abu Dharr akaukubali mwaliko huo, na baadae alimwelezea Ali juu ya madhumuni ya kutembelea kwake Makka. Ali, kwa kweli, alifurahi sana kumuelekeza mgeni wake mbele

65

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ya bwana wake, Muhammad Mustafa. Abu Dharr alijifunza kutoka kwa Mtume wa Allah (s.w.t.) maana ya ujumbe wa Uislamu. Aliona vyote, Mtume (s.a.w.) na ujumbe wake havikataliki. Alivutiwa na ile nguvu ya mvuto ya Uislamu. Baada ya kusilimu, kitu cha kwanza kabisa ambacho alitaka kufanya ni kuwakataa katakata makafiri. Alikwenda kwenye Al-Kaaba na kusema kwa sauti kubwa:

"Hapana mungu ila Allah (s.w.t.), na Muhammad ni Mtume Wake."

Kama ilivyotarajiwa, makafiri hao wakamvamia, na wakaanza kumuangushia vipigo juu yake. Kutoka kwenye ghasia hizi aliokolewa na Abbas ibn Abdul Muttalib, ami yake Mtume. Aliwaambia wale watu wa Makka kwamba Abu Dharr alikuwa wa kabila la Ghiffar ambao eneo lao limelala kutagaa zile njia za misafara kwenda kaskazini, na kama watamfanyia madhara yoyote, watu wa kabila lake watazuia upitaji wa misafara yao ya biashara kwenda Syria.

Abu Dharr al-Ghiffari ni mmoja wa watu maarufu kwenye historia ya Uislamu. Alikuwa ndiye mtu asiyekuwa na woga kabisa na asiyeogopa kusema kweli miongoni mwa maswa-haba wote wa Muhammad Mustafa ambaye wakati mmoja alisema "Mbingu haijawahi kutandaza mwamvuli wake juu ya mtu yeyote aliyekuwa mkweli kuliko Abu Dharr."

Woga wa vurugu za Maquraishi haukuzizuia nyoyo hizi za kishujaa na adilifu kuukubali Uislamu, na kila mmoja wao aliacha alama juu yake kwa kujitolea mhanga kwake.

Pia mtu mashuhuri miongoni mwa Waislamu wa awali alikuwa ni Mas'ab ibn Umayr, binamu ya baba yake Muhammad. Miaka mingi baadae, katika Kiapo cha Kwanza cha Akaba, wananchi wa Yathrib walimuomba Mtume (s.a.w.) kuwarudisha pamoja nao mwal-imu wa Qur'an, na bahati ikaangukia juu yake. Hii ilimfanya awe mtumishi wa kwanza katika Uislamu. Alikuwa pia ndiye mshika bendera wa jeshi la Waislamu katika vita vya Uhud lakini akauawa kwenye mapigano.

Kama jamaa wa familia ya Makka alikubali Uislamu, alitenganishwa nao kwa wakati wote, bila ya matumaini yoyote juu yake ya kurejesheana uhusiano. Watu wa Makkah wengi wal-iuona Uislamu kama "nguvu yenye kutenganisha" iliyokuwa ikivunja familia zao, na baad-hi yao walidhani kwamba walipaswa kuzuia "utenganishaji" huu usienee. Lakini mbali na tishio la kutumia nguvu kukomesha harakati hii mpya, hawakuweza kufikiria kitu kingine chochote ambacho kingeweza kuonekana chenye matokeo mazuri zaidi katika kusi-mamisha maendeleo yake. Walifikiria pia kwamba kama hawatafanya haraka na kwa uthabiti wa kutosha, haikuelekea kutowezekana kwamba kila nyumba hapo Makka kuwa uwanja wa vita ambamo wahusika wakuu wa ile imani ya zamani na hii mpya wangejiin-giza kwenye mapambano ya umwagaji damu mkubwa dhidi ya kila mmoja wao.

66

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Walikuwepo baadhi ya wengine miongoni mwa wapagani waliodhania kwamba Muhammad alishawishiwa na lengo la kukataa mtindo wao wa jadi wa ibada na masana-mu yao. Wote waliweka vichwa vyao pamoja na wakajaribu kufikiria juu ya ufumbuzi usio wa kawaida wa tatizo hilo. Baada ya mjadala mrefu, waliamua kumtuma Utba, mmoja wa wakuu wa Maquraish, kuonana na Muhammad, na kujaribu kumshawishi kuacha kazi yake hiyo. Utba alijulikana kwa uwezo wake wa kushawishi.

Alimwendea Mtume wa Allah (s.a.w.) na akasema: "Ewe Muhammad! Usipande mbegu ya mfarakano na kutoelewana miongoni mwa Waarabu, na usiilaani miungu ya kiume na ya kike, mababu zetu waliyoabudu kwa karne nyingi, na tunaiabudia leo. Kama nia yako katika kufanya hivyo ni kuwa kiongozi wa kisiasa, tuko tayari kukukubali kama mkuu wa Makka. Kama unataka mali, ni kiasi cha kusema tu, na tutakupatia kila tutakachoweza. Na kama umwenye kutaka kuoa katika ukoo bora, wewe utaje tu, nasi tutaandaa hilo kwa ajili yako."

Muhammad aliyasikia yote aliyoyasema Utba lakini badala ya kuonyesha tamaa yoyote ya cheo au mali au urembo, alisoma mbele yake Surat Sajda, (Sura ya 32 ya Qur'an), ule wahyi mpya kabisa kutoka Mbinguni. Kusoma kulipokwisha, Utba alirudi kwa Maquraish na kuwashauri wamwache Muhammad na wasimuingilie tena. Aliwaambia pia kwamba kama Muhammad akishindwa katika kazi yake, basi wao (Maquraish) hawatapoteza cho-chote; lakini kama atafanikiwa katika hilo, basi watashiriki katika mamlaka yake yote na utukufu.

Lakini Maquraish hawakuukubali ushauri wa Utba wa kujizuia katika kumshughulikia Muhammad na wafuasi wake. Waliendelea kuwatesa Waislamu kama mwanzoni na wakabaki kufikiria juu ya mkunjo mpya utakaoleta matokeo bora katika kusimamisha maendeleo ya Uislamu kuliko ukatili wao wote ulivyokwishafanya mpaka hapo.

Muhammad alilindwa na ami na mlezi wake, Abu Talib. Kwa wakati wote Abu Talib alipokuwa hai, wapagani hao hawakuweza kumsumbua mpwa wake. Iliwajia baadhi yao kwamba wangepaswa pengine kumshawishi Abu Talib mwenyewe, kutotilia maanani ulinzi wake juu ya Muhammad kwa niaba ya mshikamano wa kikabila. Kwanza, mshika-mano wa kabila ulikuwa ni kitu chenye umuhimu zaidi kulichukulia kwa purukushani hata na Abu Talib, licha ya mapenzi yake yote kwa mpwawe.

Maquraish waliamua kutuma ujumbe, unaotokana na watu mashuhuri wa kabila hilo, kwa Abu Talib. Ujumbe huo ulimwendea, na ukamsihi kwa niaba ya mshikamano wa kikabila wa Maquraish kupuuza ulinzi wake kwa Muhammad ambaye alikuwa "anauvuruga" vibaya sana.

67

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abu Talib, kwa kweli, hakuwa na nia ya kupuuza ulinzi wake kwa Muhammad. Bali aliwaridhisha wale wajumbe wa Maquraish kwa maelezo ya kiuchamungu na maneno yenye kutuliza, na wakarudi majumbani kwao "mikono mitupu."

Wajumbe hao pia waligundua kwamba wamerudi nyumbani kutoka kwenye "kufukuza-zimwi;" lakini hawakushituliwa na kushindwa kwao, na wakati fulani baadae, walifanya jaribio jingine la kuvunja "ushirikiano" wa Abu Talib na Muhammad. Ujumbe mpya ukaenda kumuona Abu Talib, na safari hii, wajumbe wake walichukua pamoja nao kijana mmoja mwenye sura nzuri, Ammarra ibn Walid, ambaye walimtoa kwa Abu Talib kama "mwana" kama angewapa wao Muhammad.

Abu Talib atakuwa ameucheka sana huu mwanzo wa jambo hili la Maquraish. Hivi kweli waliamini kwamba angewapa mwanae mwenyewe wamuue, na kwamba angelea mmoja wa watoto wao kama mwanae hasa? Jambo lenyewe lilikuwa la kipumbavu. Lakini kwa mara nyingine tena, Abu Talib aliishughulikia hali hiyo kwa desturi yake ya maarifa na upole, na wakarudi.

Hili jaribio la pili la Maquraish la kumbembeleza Abu Talib kumtoa Muhammad, pia lil-ishindwa. Pale maana ya kushindwa huku ilipozama akilini mwao, walitambua kwamba majaribio ya amani ya kulitatua tatizo hili yote Hayakuzaa matunda. Waliamua kujaribu kitu chenye matokeo ya haraka zaidi.

Kwa ajili ya maudhi tu na kuvunja moyo, watunga-sera wa Maquraish walichukuwa msimamo mgumu na wakatuma ujumbe wao wa tatu na wa mwisho kwa Abu Talib. Jukumu lake lilikuwa ni kumshurtisha kumsalimisha Muhammad kwao. Viongozi wa ujumbe huo waliwasilisha kauli ya mwisho kwa Abu Talib: ama alikuwa amsalimishe Muhammad kwao, vinginevyo atakabiliana na matokeo ya kukataa kwake kufanya hivyo.

Abu Talib alikuwa mtu mwenye moyo wa furaha na tabia ya uchangamfu, lakini ilikuwa siku nzito katika maisha yake. Maquraish hao, alijua, hawakuwa wakiganganya. Kwa hiyo alimwita Muhammad na kumjulisha juu ya madhumuni ya uwakilishi wa Maquraishi, na kisha akaongeza : "Oh maisha ya ami yako! Usinitwishe mzigo juu yangu ambao nitauona ni zaidi ya nguvu zangu kuubeba."

Muhammad akajibu: "Ewe ami yangu! Kama Maquraishi wataliweka jua kwenye mkono wangu wa kulia na mwezi kwenye mkono wa kushoto, mimi sitaacha kutangaza Upweke wa Allah (s.w.t.) katika kutekeleza wajibu huu, ama nitafanikiwa na Uislamu utaenea; au, kama nitashindwa, nitachakaa katika jaribio hilo."

Abu Talib hakuwa mtu wa kumshawishi Muhammad asihubiri Uislamu. Bali alikuwa anajaribu ushupavu wake. Jibu la wazi la Muhammad lilimvutia na kumridhisha kwamba

68

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hatasita, na akasema: "Nenda mwanangu, na fanya chochote unachotaka. Hakuna atakayethubutu kukufanyia madhara yoyote." Sir William Muir:

". lakini wazo la kutelekezwa na mlinzi wake mpole (Abu Talib) lilimlemea Muhammad. Alibubujikwa na machozi, na akageuka ili kuondoka. Ndipo Abu Talib akaita kwa sauti kubwa: "Mtoto wa ndugu yangu! Rudi." Hivyo akarudi. Na Abu Talib akasema: "Nenda kwa amani, mpwa wangu, na sema lolote unalotaka. Kwani Wallah, kwa namna yoyote ile, sitakuacha kamwe."

(The Life of Muhammad, 1877) Muhammad Husein Haykal:

"Abu Talib akasema: "Endelea, mpwa wangu, na sema utakalo. Wallah. ninaapa kamwe sitakusaliti kwa maadui zako."

Abu Talib aliwasilisha uamuzi wake kwa Bani Hashim na Bani al-Muttalib na akaongea nao kuhusu mpwa wake kwa mvuto mkubwa sana na kuzingatia kwa undani utukufu wa cheo cha Muhammad. Aliwataka wote kumlinda Muhammad dhidi ya Maquraishi. Wote waliahidi kufanya hivyo isipokuwa Abu Lahab aliyetam-ka wazi uadui wake kwake na kujitoa kwake kwenda kambi ya upinzani.

"...Maquraish waliwasababishia maswahaba wa Muhammad kila aina ya madhara ambayo kutokana nayo aliokolewa tu kupitia ulinzi wa Abu Talib, Bani Hashim, na Bani al-Muttalib."

(The Life of Muhammad)

Kukwamishwa na kuzuiwa kwa kurudiwa rudiwa kwa namna hii na Abu Talib, uvumilivu wa waabadu masanamu ulifikia mahali pa kuvunjika. Baada ya kushindwa kwa ubalozi wao wa mara ya tatu kwa Abu Talib, waliamua kutupia ukatishwaji tamaa wote na hasira walizoficha mioyoni juu ya wale Waislamu wasiokuwa na ulinzi. Walitumaini kuivunja ile dini mpya kwa vitisho na ukatili.

Waathirika wa kwanza wa msuguano na ushari wa wapagani walikuwa ni wale Waislamu wasiokuwa na ushirikishwaji wa kikabila hapo Makka. Yasir na mke wake, Sumayya, na mtoto wao, Ammar, hawakuwa na ushirikishwaji wa kikabila. Hapo Makka walikuwa ni "wageni" na hapakuwa na wa kuwalinda. Wote watatu waliteswa kikatili sana na Abu Jahl na makafiri wengine. Sumayya, mkewe Yasir, alikufa wakati akiwa anateswa. Yeye kwa hiyo akawa Shahidi wa Kwanza katika Uislamu. Baadae kidogo, mumewe, Yasir, aliteswa pia hadi kufa, naye akawa Shahidi wa Pili katika Uislamu.

69

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Maquraishi walichafua mikono yao kwa damu isiyokuwa na hatia! Katika orodha ya mashahidi, Sumayya na mume wake Yasir, wanashika nafasi miongoni mwa wale wa juu kabisa.Waliuawa bila ya sababu yoyote mbali na kumcha kwao Mungu na mapenzi yao kwa Uislamu na Muhammad Mustafa. Wale Waislamu waliouawa kwenye vita vya Badr na Uhud, walikuwa na jeshi la kuwalinda na kuwasaidia. Lakini Yasir na mke wake hawakuwa na mtu yoyote wa kuwalinda; hawakuwa wameshika silaha yoyote, na walikuwa ndio wasiokuwa na ulinzi kabisa kati ya mashahidi wote wa Kiislamu. Kwa kuji-tolea mhanga maisha yao, walidhihirisha ukweli wa Uislamu, na walitia nguvu katika muundo wake. Waliifanya desturi ya muhanga na kufa kishahidi kuwa sehemu muhimu ya maadili ya Uislamu.

Bilal, Khabab ibn el-Arat, Suhaib Rumi, na Waislamu wengine masikini na wasio na ulinzi walifanywa wasimame kwenye jua kali, na wakapigwa viboko na makafiri. Walinyimwa chakula na maji kwa matumaini matupu kwamba njaa na kiu vitawalazimisha kumtupa Muhammad na Uislamu.

Pale Maquraish walipomuona Muhammad peke yake, waliichukua fursa hiyo kumuudhi yeye. Wao kwa kweli walipenda kumuua lakini walilazimika kuizuia tamaa hii. Kama wangemuua, wangesababisha kisasi au hata vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Wakati mmoja, Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliingia kwenye Al-Kaaba kusoma Qur'an Tukufu. Alikuwa anasoma Qur'an wakati ghafla alipozungukwa na waabudu sana-mu. Walimsongasonga, na wangeweza kumfanyia madhara makubwa lakini walishindwa kwa kuingiliwa kati na Harith ibn Abi Hala, mpwa na mtoto wa kulea wa Khadija, aliye-bahatika kutokea kwenye tukio hilo wakati huohuo. Alijitosa kwenye ghasia hiyo kumuokoa Mtume wa Allah (s.a.w.) kutokana na vurugu hizo za washirikina wa Makka.

Harith ibn Abi Hala aliwapiga mateke na kupigana kwa ngumi zake. Inawezekana kabisa, yeye pia alikuwa amebeba upanga kama Waarabu wote walivyofanya lakini hakutaka kuu-toa, na kusababisha umwagaji damu ndani ya maeneo ya Al-Kaaba. Lakini katika tafrani hiyo, mmoja wa waabudu masanamu hao aliuchomoa upanga wake, na kumchoma kwa kurudiarudia. Alianguka kwenye dimbwi la damu yake mwenyewe, na akafa kwa majeraha mengi katika kifua chake, mabega na paji la uso. Alikuwa Mwislamu wa kwanza kuawa ndani ya maeneo ya Al-Kaaba. Harith alikuwa kijana wa miaka kumi na saba, na aliyafanya maisha yake kuwa dhabihu kwa ajili ya Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.). Alikuwa ndiye muathirika kijana mdogo wa vurugu zenye kuzunguka na kuongezeka za makafiri. Alijipatia taji la kufa kishahidi na kuwa Shahidi wa tatu katika Uislamu. Kifo chake, mapema sana katika uhai wake, kilimfanya Mtume (s.a.w.) kuwa mwenye huzuni sana.

Wanahistoria wa Kiarabu wako kimya kuhusu suala hili lakini mapigano mabaya zaidi laz-ima yawe yalitokea ndani ya Makka kati ya Waislamu na waabudu masanamu katika miaka

70

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ya kabla ya kuhama kwa Mtume (s.a.w.) kwenda Madina. Abu Talib alimlinda mpwa wake wakati wote alipokuwa hai. Baada ya kifo chake, wajibu huu ulirithiwa na mwanae, Ali.

Ali alikuwa bado ni kijana wakati alipojiteua mwenyewe kuwa mlinzi wa Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.). Baada ya mauaji yale, ndani ya Al-Kaaba, ya Harith ibn Abi Hala, Ali alifuatana na bwana wake wakati wowote alipotoka nje ya nyumba yake, na alisi-mama kati yake na maadui zake. Kama mtu mshari alimwendea Muhammad kwa kumkamia, Ali mara moja alimpa changamoto, na akapambana naye.

D.S.Margoliouth:

"Wale watu ambao kuingia kwao katika Uislamu kulikaribishwa sana walikuwa watu wenye nguvu za kimwili, na upiganaji mwingi wa dhati lazima uwe ulitokea hapo Makka kabla ya Hijra; vinginevyo ile hali ya kuwa tayari ambayo kwayo Waislam baada ya Hijra waliweza kuonyesha kutokana na idadi yao ya mashujaa waliojaribi-wa, ingekuwa isiyoelezeka. Shujaa aliyejaribiwa lazima awe amejaribiwa mahali fulani; na hakuna mapigano ya nje yaliyotajwa au ambayo angalau ni jambo la doke-zo kwa wakati huu."

(Muhammad and the Rise of Islamu, London, 1931)

Hakukuwa na mapigano ya nje hapo Makka kabla ya Hijra ya Mtume (s.a.w.) kwenda Madina, lakini kulikuwa na mapigano mengi sana mitaani na kwenye sehemu za wazi za mji huo. Ilikuwa ni katika "viwanja vya vita" hivi ambavyo Ali, yule simba kijana, alimopata umahiri wote huu wa kivita. Haya "mapigano" hapo Makka yalikuwa ni "mazoezi ya mwisho" ya dhima aliyotakiwa kuchukua miaka michache baadae huko Madina katika mapambano ya silaha kati ya Uislamu na upagani. Ilikuwa pia katika siku hizi za mwanzoni, kabla ya Hijra ya Mtume (s.a.w.) kwenda Madina, ambayo Ali alikuwa "msitari wa kwanza wa ulinzi wa Uislamu." Kwa kweli, alikuwa pia, kwa wakati huohuo, msitari wa pili na wa mwisho wa ulinzi wa Uislamu. Hili yeye, na yeye peke yake, lilikuwa lidumu kwa maisha yake yote yaliyobakia.

Maquraish waliitesa miili ya Waislamu wasiokuwa na ulinzi huko Makka kwa matumaini kwamba watawalazimisha kuuacha Uislamu, lakini walishindwa. Hakuna hata mmoja kati ya hawa Waislamu "masikini na wanyonge" aliyeukana Uislamu kamwe. Mazingira mabaya yanaweza kushirikiana kumvunja hata yule mtu mwenye nguvu sana, na kwa Waislamu, mazingira hayo hayakuweza kuwa mabaya zaidi. Lakini mazingira yale hayakuweza kuwavunja. Uislamu uliwaweka pamoja.

Kwa hawa Waislamu "masikini na wanyonge", Uislamu ulikuwa ni desturi "inayotia nguvu". Umeyavuta maisha pamoja kwa ajili yao; umeyawekea maana ndani yake,

71

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

umeyaendesha malengo kupitia humo, na umeweka upeo pande zote. Wao, kwa hiyo, walitupilia mbali usalama, starehe na anasa za maisha; na baadhi miongoni mwao kama Sumayya na mume wake, Yasir, waliyapuuzilia mbali maisha yenyewe; lakini walithibitisha Imani yao. Walikufa lakini hawakuafikiana na Upotofu.

Allah (s.w.t.) awe radhi na nafsi hizi za kishujaa na tukufu na azirehemu. Imani na uadili-fu wao vilikuwa, kama Maquraishi walivyogundua, visivyoshindika kwa kiasi kama isivyoshindika imani na uadilifu wa bwana na kiongozi wao, Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.w.t.) Walikuwa ni almasi ambazo Muhammad alizipata kwenye mawe ya dunia. Walikuwa wachache kwa idadi lakini wasio na bei kwa tathmini; ya kuweza kuelezeka, sio kwa wingi bali kwa ubora tu, na ubora huo ulikuwa adhimu sana.

72

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hijra mbili za Waislamu kwenda Abyssinia (A.D.D 615-616)

Muhammad Mustafa (rehma na amani juu yake na Ahlul-Bait wake), alishirikiana katika huzuni zote na madhara ya wafuasi wake walioteswa kwa kuamini kwamba "Mungu ni Mmoja", lakini hakuwa na njia ya kuwalinda. Pale vurugu za washirikina dhidi ya Waislamu zilipokuwa hazionyeshi dalili yoyote ya kutoshadidi, aliwashauri waondoke Makka na kutafuta hifadhi huko Abyssinia (Ethiopia) ambayo wakati huo ikitawaliwa na mfalme wa Kikristo, anayefahamika sana kuwa ni mtu muadilifu na mcha-Mungu.

Kwa kuitikia ushauri huu, kikundi cha Waislamu, chenye wanaume kumi na mmoja na wanawake wanne, kiliondoka Makka na kwenda Abyssinia. Kikundi hicho kilimhusisha Uthman bin Affan, khalifa wa baadae wa Waislamu; mke wake, Ruqayya; na Zubayr bin al-Awwam, binamu yake Mtume. Mtukufu Mtume (s.a.w.) alimteua Uthman bin Mazun, mmoja wa maswahaba wake wakuu, kama kiongozi wa kikundi hiki.

Ibn Ishaq:

"Wakati Mtume (s.a.w.) alipoyaona madhara ya maswahaba wake na kwamba ingawa ameweza kuyaepuka kutokana na kusimama na Allah (s.w.t.) na ami yake, Abu Talib, hakuweza kuwalinda, aliwaambia: 'Kama mngekwenda Abyssinia (ingekuwa bora kwenu), kwani huyo mfalme (huko) hatavumilia dhulma na ni nchi ya kirafiki, mpaka wakati huo ambapo Allah (s.w.t.) atakapowatoeni kwenye dhiki yenu.' Hapo maswahaba wake wakaenda Abyssinia, wakiogopa kuasi na kukimbilia kwa Allah (s.w.t.) pamoja na dini yao. Hii ilikuwa Hijra ya kwanza katika Uislamu.

(The Life of the Messenger of God) Hijra ya kwanza ilifanyika katika mwaka wa tano wa tangazo la Uislamu - 615. A.D.

Mfalme wa Abyssinia aliwakaribisha wakimbizi hao wa Kiislam kutoka Makka kwenye falme yake. Aliwapatia hifadhi, na walifurahia amani, usalama na uhuru wa kuabudu chini ya himaya yake. Kama mwaka mmoja baadae, Waislamu hao huko Abyssinia walisikia minong'ono kwamba Maquraishi huko Makka wameupokea Uislamu. Kama ilikuwa kweli basi hakukuwa na sababu ya wao kuishi uhamishoni. Walikuwa na hamu ya nyumbani, na waliamua kurudi Makka.

Lakini walipowasili Makka, waligundua kwamba sio tu kwamba ile minong'ono waliy-oisikia ilikuwa ya uongo, bali pia kwamba Maquraishi wameongeza mateso ya Waislamu.

73

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wao, kwa hiyo, wakaondoka Makka kwa mara nyingine. Waislamu wengine wengi pia walifuatana nao. Kundi hili jipya lilikuwa na wanaume 83 na wanawake 18. Muhammad Mustafa akamteua binamu yake wa kwanza, Jafar ibn Abi Talib, kaka yake mkubwa Ali, kama kiongozi wa kikundi hiki.

Hajra hii ya pili ya Waislamu kwenda Abyssinia, ilitokea katika mwaka wa sita wa kutangazwa Uslamu, unawafikiana na mwaka wa 616. A.D.

Hijra hii ya Waislamu kwenda Abyssinia, na kupokewa kwao katika baraza la kirafiki la nchi ile, kuliwaogofya Maquraishi. Waliichukulia hofu ile kwamba Waislamu wanaweza kuongezeka nguvu, au kupata washirika wapya, na kisha, siku yoyote, wanaweza kurudi Makka kushindana nao. Ili kubadili mwelekeo wa tishio hili linalowezekana, kama walivy-oliona, waliamua kutuma ujumbe kwenye baraza la mfalme wa Abyssinia kumshawishi kuwahamishia (kwa kuwakabidhi) Waislamu hao Makka.

Wakimbizi hao wa Kiislamu ambao walitarajia kuachwa katika amani, walishangazwa na kuwasili, katika mji mkuu wa Abyssinia, kwa ujumbe kutoka Makka, ukiongozwa na Amr bin Al-Aas. Amr alileta zawadi nono kwa ajili ya mfalme na watumishi wake ili kujipen-dekeza kwao.

Pale mfalme alipokutana na wajumbe wa Maquraishi, Amr alisema kwamba Waislamu wale walioko Abyssinia hawakuwa wakimbizi kutokana na mateso bali walikuwa watoro wa haki na sheria, na akamuomba kuwahamishia Makka. Mfalme, hata hivyo, akataka kusikia upande wa pili wa Hadith pia kabla ya kutoa uamuzi, na akamwita Jafar ibn Abi Talib kwenye baraza kujibu mashtaka yale dhidi ya Waislamu.

Jafar alitoa utetezi kabambe kabisa. Ufuatao ni mukhtasari wa hotuba yake ndani ya baraza la Abyssinia katika kujibu maswali yaliyotolewa na yule mfalme wa Kikristo.

"Ewe Mfalme! Tulikuwa tu watu wajinga na tuliishi kama wanyama wa porini. Wale wenye nguvu kati yetu waliishi kwa kuwinda wanyonge. Hatukutii sheria yoyote na hatukukubali mamlaka yoyote mbali na ile nguvu ya kinyama. Tuliabudu masanamu yaliyotengenezwa kwa mawe au magogo ya miti, na hatukujua chochote cha heshima ya utu. Na kisha Allah (s.w.t.) kwa Rehma Zake, akatutumia Mtume Wake ambaye alikuwa mwenyewe ni mmoja wetu. Tulijua juu ya ukweli wake na uaminifu wake. Tabia yake ilikuwa nzuri sana, na alikuwa wa ukoo-bora sana wa Waarabu. Alituita sisi kwenye ibada ya Mungu Mmoja, na akatukataza kuabudu masanamu. Alitusihi tuseme kweli, na kuwatetea wanyonge, maskini, watu wa chini, wajane na mayatima. Alituamuru tuwaheshimu wanawake, na kutowakashifu kamwe. Tulimtii na kufuata mafundisho yake. Watu wengi katika nchi yetu ni washirikina bado, na walichukia kusilimu kwetu kwenye hiyo dini mpya ambayo inaitwa Uislam. Walianza

74

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kututesa sisi na ilikuwa ili kuepukana na mateso kutoka kwao kwamba tulitafuta na kupata hifadhi katika himaya yako."

Wakati Jafar alipomaliza hotuba yake, mfalme alimuomba asome baadhi ya Aya zili-zoshushwa kwa Mtume wa Waislamu. Jafar akasoma Aya chache kutoka kwenye Surat Maryam, Sura ya 19 ya Qur'an Tukufu. Mfalme aliposikia Aya hizi, alisema kwamba asili yake Aya hizo, ilikuwa ni sawasawa na ile ya Injili. Ndipo basi akatamka kwamba amerid-hika na ukweli wake, na akaongeza, kwenye huzuni kubwa ya Amr bin Al-Aas, kwamba Waislamu wale wako huru kuishi kwenye himaya yake kwa kiasi cha muda wowote wau-takao.

Lakini Amr bin Al-Aas alijishauri mwenyewe juu ya mkakati mpya, ambao, aliamini, ungeshambulia vile vigezo dhidi ya Jafar. Siku iliyofuata, kwa hiyo, alirudi kwenye baraza hilo na alimwambia mfalme kuwa yeye mfalme alipaswa kupuuza madai ya ulinzi wake kwa Waislamu hao kwa sababu waliikana jinsia-asili tukufu ya Kristo, na wao wakadai kwamba alikuwa ni binadamu kama watu wengine.

Alipoulizwa na mfalme juu ya suala hili, Jafar alisema: "Ufahamu wetu juu ya Yesu ni kama ule wa Allah (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.), yaani, Yesu ni mja wa Allah (s.w.t.) Mtume Wake, Roho Wake, na Amri Yake iliyotolewa kwa Maryam, yule bikra maasuma."

Mfalme akasema: “Yesu yu kama vile tu ulivyomuelezea alivyo, na si kingine zaidi ya hayo." Kisha akizungumza na wale Waislamu, akasema: "Nendeni majumbani kwenu na mkaishi kwa amani. Sitawatoa kamwe kwa maadui zenu." Alikataa kuwahamisha wale Waislamu, akarudisha zile zawadi ambazo Amr bin Al-Aas alizileta, na akaufukuza ule ujumbe wake.

Washington Irving

"Miongoni mwa wale waliokimbilia Abyssinia, alikuwemo Jafar, mtoto wa Abi Talib, ambaye ni nduguye Ali, hivyo ni binamu wa Muhammad. Alikuwa ni mtu wa ufasa-ha wenye mvuto na umbo la kupendeza mno. Alisimama na kujitokeza mbele ya mfalme wa Abyssinia, na akazifasili imani za Kiislamu kwa ghera na uwezo.

Mfalme ambaye alikuwa Mkristo wa Nestoria, aliziona imani hizi zenye kufanana sana kwa namna nyingi na zile za madhehebu yake na zenye kupingana sana na zile za ibada nzito ya masanamu ya Maquraishi, kwamba mbali sana na kuwakabidhi wale wakimbizi, aliwachukua zaidi mahsusi kwenye upendeleo na ulinzi, na kuzirudisha kwa Amr bin Al-Aas na Abdullah, zile zawadi walizozileta, na kuwatoa kutoka kwenye baraza lake.

(Life of Mohammed)

75

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Waislamu walikaa miaka mingi huko Abyssinia na waliishi kwa amani. Miaka kumi na tatu baadae - katika mwaka wa 7 A.H. (A.D. 628) - walirejea, sio kwenda Makka bali Madina. Kuwasili kwao kulifuatana na kutekwa kwa Khaibar na Waislamu.

Jafar ibn Abi Talib alikuwa ndio kiongozi wa Waislamu wote waliokuwa wamehamia Abyssinia katika mwaka wa 615 na 616. Anaonekana kama ndio alikuwa mtu pekee wa ukoo wa Bani Hashim kuondoka kwenda Abyssinia pamoja na wale wakimbizi wengine. Watu wengine wote wa Bani Hashim walibakia Makka.

Montegomery Watt:

"Mbali na watu wawili wa pekee Waislamu wote wa mwanzo waliobakia Makka (na hawakwenda Abyssinia) walitokana na kikundi cha koo tano, kikiongozwa na ukoo wa Muhammad wa Bani Hashim. Kikundi hiki kinaelekea kuwa ni namna ya Umoja wa Waadilifu ulioundwa upya. Kwa hiyo ndio kiini cha upinzani kwa wale wafanya biashara wakubwa pamoja na tabia yao ya ukirikimba."

(Muhammad, Prophet and Statesman, 1961)

76

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

HAMZA AUKUBALI UISLAMU - A.D. 615

Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) ingawa yuko salama chini ya ulinzi wa ami yake, Abu Talib, hakusalimika na bughudha za washirikina. Wakati wowote walipopata mwanya wa kumuudhi, hawakuupoteza. Wakati mmoja Abu Jahal alimkuta akiwa peke yake, na akatumia lugha ya kishenzi na ya kuchukiza sana juu yake Muhammad. Jioni hiyo hiyo wakati ami yake, Hamza ibn Abdul Muttalib alivyorudi nyumbani kutoka safari ya mawin-doni, mtumwa wake wa kike alimuelezea kile kisa cha fedhuli isiyo na sababu ya Abu Jahal kwa Muhammad na ustahimilifu wa Muhammad, ambao yeye alikuwa shahidi.

Hamza alikuwa mpiganaji, mwindaji na mwanamichezo, na alikuwa hana habari sana na mambo ya kila siku ya mjini hapo. Lakini tabia ya Abu Jahal kwa mpwa wake ilimpan-disha sana hasira kiasi kwamba alichukua upinde wake, na akaingia kwenye mkutano wa Maquraish ambamo yeye Abu Jahal alikuwemo akiwachambulia wenzie matukio ya siku ile.

Hamza akampiga kichwani mwake na upinde wake, na kumsababishia atokwe na damu, na akasema: "Na mimi pia nimekuwa Mwislamu."

Huu ulikuwa ni mtihani kwa Abu Jahal lakini aliona kwamba kimya kilikuwa ni sehemu bora ya ujasiri, na hakugombana na Hamza, pia akawazuia rafiki zake ambao walitaka kusimama kumtetea.

Betty Kelen:

"Ami yake Muhammad, Hamza, mtu wa umri wake mwenyewe, alisifika kuwa mwenye nguvu sana na uwezo kati ya Maquraish, shujaa wao katika vita na michezo. Alitumia muda wake mwingi kwa kuwinda vilimani. Siku moja alipokuwa anarudi kutoka kwenye msako na uta wake ukinin'ginia kwenye bega lake, mtumwa wake wa kike alimweleza jinsi Abu Jahal alivyomrundikia matusi mpwa wake.

Hamza alijikuta mwisho kabisa wa uvumilivu wote. Alimpenda Muhammad, ingawa alikuwa hamuelewi (japo kwa makosa, sio kweli). Alikimbilia Msikitini, ambako alimuona Abu Jahal akiwa amekaa miongoni mwa marafiki zake. Akanyanyua uta wake mzito na akampiga nao pigo kubwa sana kichwani mwake. "Utamtukana tena nitakapojiunga na dini yake?" alipiga kelele, akinyoosha misuli yake mikubwa mbele ya Maquraish.

Hamza akawa Mwislamu, na hili lilitia nguvu kwenye imani hiyo. Baadhi ya Maquraish walikuwa waangalifu zaidi juu ya kumwita Muhammad mshairi.

(Muhammad, the Messenger of God, 1975) 11

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hamza akawa mwislamu mcha-mungu na shujaa wa Uislamu. Alikuwa ndiye askari-mwenza wa mpwawe mwingine, Ali, na ilikuwa ni wao wote waliowauwa wengi wa vion-gozi wa Maquraish katika vita vya Badr, vilivyokuwa vipiganwe miaka michache baadae.

Katika vita vya Uhud, Hamza alimuua mshika-bendera wa pili wa wapagani, na pale wali-poshambulia mstari wa Waislamu, alijItosa kati yao. Alikuwa akipasua njia yake kupitia kwenye safu zao pale alipopigwa na mkuki uliotupwa na Wahshi, mtumwa wa kihabeshi. Wahshi alipangwa kwa ajili ya kazi hii hasa, na Hindu, mke wa Abu Sufyan na mama yake Muawiya; na muabudu sanamu mwingine wa Makka. Hamza alianguka chini na akafa mara moja.

Baada ya kusambaratika kwa Waislamu siku ile, Hindu na wanawake wengine makatili kutoka Makka, walikatakata viungo vya miili ya Waislamu waliouawa. Alipasua tumbo la Hamza, akalin'goa ini lake, na akalitafuna. Alimkata pia pua yake, masikio, mikono na miguu, akavitunga kama "mkufu," na kuingia Makka ameuvaa kama tuzo la vita.

Muhammad Mustafa alisikitishwa sana na kifo na kukatwakatwa kwa mwili wa muumini hodari wa Uislamu kama Hamza. Alitoa majina ya "Simba wa Mungu", na "Kiongozi wa Mashahidi" juu yake.

Hamza aliukubali Uislamu katika mwaka wa tano wa kutangazwa Uislamu.

78

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

KUSILIMU KWA UMAR - A.D. 616

Tukio maarufu la mwaka wa sita wa Tangazo la Uislamu lilikuwa ni kusilimu kwa Umar bin Khatab, khalifa wa baadae wa Waislamu. Alikuwa mmoja wa maadui wakali sana wa Uislamu na Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) na alikuwa mtesaji mkubwa wa Waislamu. Yule mwanahistoria wa kisasa wa Kimisri, Amin Dawidar, anasema kwamba chuki ya Umar kwa Uislamu, na uhasama wake kwa Muhammad, vilifanana tu na chuki na uhasama kwavyo wa ami (mjomba) wake wa upande wa kikeni, Abu Jahl.

Inasemekana kwamba siku moja kwa maudhi tu, Umar alikusudia kumuua Muhammad, na hivyo kuuzima mwale wenyewe wa Uislamu. Aliondoka nyumbani kwake akiwa na nia hii.

Kama ilivyokwisha elezwa, Waislamu kwa wakati huu (siku za mwisho za mwaka wa sita) walikuwa bado wanajikusanya katika nyumba ya Arqam bin Abi Arqam kuswali Swala zao za jamaa. Walikuwa wanaanza kujikusanya wakati mmoja wao, akitazama nje ya dirisha, akamwona Umar akija kuelekea nyumbani hapo na upanga uliochomolewa. Katika hali ya wasiwasi kiasi, aliwaambia wale watu wengine wa jamaa ile kile alichokiona. Labda, na wao pia walikuwa na wasiwasi. Lakini Hamza, ambaye pia alikuwemo ndani ya nyumba hiyo ya Arqam, aliwatuliza, na akasema kwamba kama Umar alikuwa anakuja na nia nzuri, basi ilikuwa ni sawa sawa; lakini kama sivyo, basi yeye Hamza atamchoma kwa upanga wake Umar mwenyewe. Lakini ilitokea kwamba Umar alikuja kwa nia ya kusilimu, na akafanya hivyo.

Hadithi inaelezwa kwamba Umar alikuwa anakwenda kuelekea Dar-ul-Arqam kwa nia ya kumuua Muhammad wakati mpita njia alipomsimamisha, na kumjulisha yeye kwamba dada yake mwenyewe na mumewe wamekuwa Waislamu, na akamshauri kuiweka nyumba yake mwenyewe sawa kabla ya kuanza mpango mwingine wowote mkubwa wa kubuni-wa tu.

Muhammad Husein Haykal:

"Umar alikwenda pale (Dar-ul-Arqam) - kwenye nyumba ya Arqam, akiwa amekusu-dia kumuua Muhammad na hivyo kuwaondolea Maquraish mzigo, na kusimamisha upya heshima ya ile miungu ambayo Muhammad aliipinga. Akiwa njiani kuelekea Makka alikutana na Nu'aym ibn Abdullah. Baada ya kujua nia ya Umar, Nu'aym akasema, "Wallahi umejidanganya mwenyewe, ewe Umar! Unadhani Bani Abd Manaf watakuacha utembee ukiwa hai pindi utakapokuwa umemuua mtoto wao Muhammad? Kwa nini usirudi nyumbani kwako mwenyewe na angalau

ukakuweka sawa?"

(T he Life of Muhammad)

79

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Umar alikasirika kusikia kwamba dada yake na mumewe wamekuwa Waislamu. Mara moja akabadili njia kutoka ile ya kwenda kwenye nyumba ya Arqam na kuchukua ya kwenda nyumbani kwa dada yake kuchunguza madai yale. Kwa majibu ya maswali yake, dada yake alimpa jibu makinifu lakini la ukwepaji.

Ibn Ishaq:

"Umar alifika kwenye mlango (wa nyumba ya dada yake) wakati Khabbab (sahaba wa Mtume) alikuwa akisoma chini ya uongozi wake ile Sura ya Taha na pia "Jua litakapokunjwa" (81:1). Washirikina walikuwa wakikiita kisomo hiki "takataka". Umar alipoingia, dada yake aliona kwamba alikusudia madhara na akaficha zile karatasi ambazo walikuwa wakisoma. Khabbab akatorokea ndani ya nyumba. Umar akauliza ni upuuzi gani aliokuwa akisikia, ambapo dada yake akamjibu kwamba yalikuwa ni mazungumzo tu kati yao..."

(The Life of the Messenger of God)

Umar alihamaki kwa kile alichoamini kuwa ni uongo, na akampiga dada yake usoni. Pigo hilo lilisababisha mdomo wake kutokwa na damu. Alikuwa ampige tena lakini kule kuona damu kulimfanya asite. Ghafla alionekana kupunguza ukali, na kisha kwa sauti iliyobadi-lika akamuomba amuonyeshe kile alichokuwa akisoma. Alimhisi amebadilika lakini akase-ma: "Wewe ni muabudu masanamu mchafu, na siwezi kukuruhusu kugusa Neno la Allah (s.w.t.)"

Umar mara moja aliondoka zake, akaoga, akarudi nyumbani kwa dada yake, akasoma yale maandishi ya Qur'an, na kisha akaenda kwenye nyumba ya Arqam ambako alisilimu rasmi.

Sir William Muir anasema kwamba kusilimu kwa Umar kulitokea mwishoni mwa mwaka wa sita wa ujumbe wa Mtume. Anaongezea tanbihi ifuatayo chini ya kurasa:

"Kusilimu kwa Umar kulitokea ndani ya Dhil-Hajj, mwezi wa mwisho wa mwaka. Waumini wanasemekana sasa kufikia kwa jumla watu 40 wanaume na wanawake; au kwa hesabu zingine, wanaume 45 na wanawake kumi na moja."

(The Life of Muhammad, 1877, uk. 95)

80

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Umar alikuwa na miaka kama 35 wakati aliposilimu.

Muhammad Husein Haykal:

"Kwa wakati ule, (aliposilimu) Umar ibn al Khattab alikuwa mtu mzima wa miaka thelathini na tano kwa umri."

(The Life of Muhammad)

Waislamu wengi wanadai kwamba kwa kusilimu kwa Umar, Uislamu ulipata nguvu mpya, na Waislamu walikuwa sasa wametiwa moyo kuwapinga wapagani. Waliweza sasa, kulingana na madai haya, kutoka nje ya sehemu zao za kujifichia, na kuswali waziwazi kwenye maeneo ya Al-Kaaba, ama hasa, alikuwa ni Umar mwenyewe aliyewatoa kwenye sehemu zao za kujifichia, na hawakuwa sasa wakimuogopa Abu Jahl au mtu mwingine yeyote.

Muhammad Husein Haykal:

"Waislamu waliorudi kutoka Abyssinia walifanya hivyo kwa sababu mbili. Kwanza, Umar ibn al Khattab alisilimu mara tu baada ya Hajira yao. Pamoja naye, alileta kwenye kambi ya Waislamu ukakamavu , dhamiri, na msimamo ule ule wa kikabila ambao alikuwa akipiga nao Waislamu kabla. Hakuficha kamwe kusilimu kwake wala kamwe hakuwakwepa wale wapinzani wa Kiquraishi. Badala yake, alitangaza kusilimu kwake hadharani na aliwapinga Maquraishi wazi wazi.

Hakuridhika na kujificha kwa Waislamu wenyewe, mienendo yao ya siri kutoka upande mmoja wa Makka hadi mwingine, na kusimamisha kwao Swala kwenye umbali wenye usalama kutokana na mashambulizi yoyote ya Maquraishi. Umar alian-za kupigana na Maquraishi mara tu alipoingia kwenye imani ya Uislamu, daima akishinikiza njia yake karibu na Al-Kaaba, na akasimamisha Swala yake pale pamoja na Waislamu wowote walioamua kujiunga naye."

(The Life of Muhammad)

Lakini madai haya ya ajabu yanapata nguvu ndogo katika ushahidi. Na kama ushahidi huo una maana yoyote, unaelekea kupingana na madai yenyewe.

Madai mengine ni ya ubadhilifu sana. Kwa mfano, yule mwanahistoria wa Kimisri, Amin Dawidar, anasema ndani ya kitabu chake, Pictures From the Life of the Messenger of God kwamba kusilimu kwa Umar kulikuwa ni pigo la kifo kwa Maquraishi.

Kilichotokea hasa ni kwamba kusilimu kwa Umar kulioana na wimbi jipya na ambalo halijawahi kutokea, la hofu kuu lililotojikeza juu ya Waislamu. Ambapo kabla ya kusilimu kwake ni Waislamu wale tu walioathirika na mateso ambao hawakuwa na wakuwalinda,

81

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

sasa hakuna mwislamu, sio hata Muhammad Mustafa mwenyewe, aliyekuwa salama kutokana na nia mbaya za washirikina.

Muhammad Husyn Haykal:

"Huko uhamishoni kwao (nchini Abyssinia) walisikia kwamba kwa kusilimu Umar Maquraishi wamesimamisha mateso yao juu Muhammad na wafuasi wake. Kwa mujibu wa Hadith moja baadhi yao walirudi Makka, kwa mujibu wa nyingine, waliru-di wote. Walipofika Makka waligundua kwamba Maquraishi wamerudia mateso ya Waislamu kwa chuki zaidi na nguvu mpya. Kwa kushindwa kuhimili, baadhi yao walirudi Abyssinia wakati wengine waliingia Makka chini ya ulinzi wa kiza cha usiku na wakajificha kabisa."

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Lakini hii haikuwa ndio basi. Mengine mengi yalikuwa bado yatokee. Sasa Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) hakuweza walau kuishi Makka. Kwa kweli, zaidi kido-go ya wiki ilikuwa imepita tangu kusilimu kwa Umar, wakati Muhammad na watu wote wa familia na ukoo wake, walikuwa waondoke Makka, na waende uhamishoni. Kwa hiyo, ile dhana kwamba kusilimu kwa Umar kuliwafanya Waislamu kuacha tahadhari zao na mkao wa kiulinzi, na kutowaogopa makafiri, moja kwa moja hailingani na mambo.

S. Margoliouth:

"...hatuna kumbukumbu yoyote ya tukio lolote ambalo juu yake Umar alionyesha ujasiri mkubwa wa kuonekana, ingawa mifano mingi inapatikana juu ya ukatili wake na hamu ya kuua; katika vita vya Hunain alikimbia, na kwenye tukio jingine aliokole-wa maisha yake kwa utu wema wa adui."

(Muhammad and the Rise of Islam, 1931)

Profesa Margoliouth amefanya marejeo kwenye lile tukio ambapo adui mwenye utu mwema alinusuru maisha ya Umar. Atakuwa lazima anarejea ile vita ya Handaki au kule kuzingirwa kwa Madina (627 A.D). Katika vita vile, Ali ibn Abi Talib alimuua yule jemadari wa Makka, Amr ibn Abd Wudd, ambapo maaskari-wenza wake walikimbia kwa haraka kuvuka lile Handaki. Walipokuwa wakikimbia, Umar alijaribu kumpita mmoja wao. Shujaa huyu aliyekuwa akirudi nyuma, alikwisha wahi kusikia kwamba Ali kamwe alikuwa hamuandami adui anayekimbia.

Yeye, kwa hiyo, alitambua kwamba yoyote huyo anayemfukuzia basi, hawezi kuwa ni Ali. Kwa upekuzi tu, aliibia kutazama nyuma na akagundua kwamba alikuwa ni Umar aliyekuwa akimjia kwa vitisho. Alipomuona Umar, mara moja aligeuza hatamu za farasi wake kumkabili, na hili lilimfanya Umar asimame. Shujaa huyu aliyemjua Umar,

82

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

akamwambia: "Kama mama yangu asingenifanya niapie kwamba kamwe sitamuua Quraishi, ungekuwa maiti sasa hivi. Mshukuru yeye (mama), na usisahau kwamba nimeyasalimisha maisha yako."

Ifahamike kwamba Hamza alisilimu mwaka mmoja kabla Umar hajawa mwislamu, na ameadhimisha kusilimu kwake kwa kumshambulia Abu Jahl, ami (mjomba) wa kikeni wa Umar, kwa upinde wake. Mtu hawezi kumtegemea Umar kuigiza mfano wa Hamza kwa kumshambulia ami yake mwenyewe, lakini hakuna kumbukumbu yoyote kwamba alishambulia muabudu sanamu mwingine yoyote kwa kuonyesha fidhuli kwa Mtume wa Allah (s.a.w.). Zaidi ya hayo, pale Hamza alipokubali Uislamu na akaitoa damu pua ya Abu Jahl, Umar mwenyewe alikuwa muabudu sanamu.

Ilikuwa ni wajibu wake, kwa jina la "mshikamano wa kikabila," kushindana na Hamza, na kulinda heshima ya kaka wa mama yake. Hata hivyo, kwa mujibu wa madai mengi yaliyosambaa, alikuwa ndiye mtu shupavu sana, anayetisha sana, mwenye hasira kali, na mkaidi sana hapo Makka. Na ni nani isipokuwa Umar angeweza kuthubutu kumtia chang-amoto Hamza? Lakini changamoto hiyo haikutokea kamwe.

83

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kususiwa kiuchumi na kijamii kwa Bani Hashim

Mwaka wa sita wa Tangazo ulikuwa unakaribia. Wapagani walikuwa tayari wamemaliza miaka mitatu kupiga kampeni dhidi ya Uislamu. Wamezalisha uchungu mwingi na uhasama dhidi ya Waislamu katika miaka hii mitatu, lakini walikuwa na kidogo sana, kama kilikuwapo chochote, cha kuonyesha kwa ajili ya juhudi zao. Walitumia kila silaha dhidi ya Waislamu kuanzia vivutio mpaka ushawishi, hadi matusi mpaka kebehi, na dhihaka mpaka vitisho vya kutumia nguvu na utumiaji hasa wa nguvu zenyewe, lakini bila mafanikio. Ile nguvu ya imani ya Waislamu iliwakanganya.

Kutofaulu kwao kwa mara kwa mara kuliwalazimu Maquraish kutathimini upya ile hali ana kwa ana, Muhammad na Uislamu, na baadhi yao walijaribu kuliangalia tatizo lao kwa namna nyingine mpya. Katika kutafuta kwao ufumbuzi wa tatizo hili linalichusha, alianza taratibu kuwapambanukia juu yao kwamba adui yao hakuwa kile kikundi cha wale Waislamu wasio na mizizi na waliokumbwa na umasikini walioko pale Makka. Adui wa kweli - adui wa waabudu masanamu na washirikina - walimtambua alikuwa ni Abu Talib! Hata hivyo alikuwa ni Abu Talib aliyekuwa akimlinda Muhammad na Uislamu kwa uaminifu na msimamo thabiti. Waislamu, kwa upande mwingine, hawakuwa na uwezo wa kumlinda Muhammad. Kwa kweli, walikuwa wao wenyewe katika haja kubwa ya ulinzi. Mafanikio haya katika "kumtambua adui" yalikuwa na uzito wa udhihirisho kwa viongozi wa Maquraishi katika harakati zao dhidi ya Uislamu, na yamewawezesha kupanga mkakati mpya.

Abd-al-Rahman 'Azzam:

"Mwishowe, ule utawala wa wachache wa pale Makka uliamua kwa wasiwasi mkub-wa kuchukua hatua dhidi ya Abu Talib. Kwa mawazo yao, yeye ndiye aliyekuwa mlinzi hasa wa kufuru hii, ingawa bado alikuwa ni mtetezi wa kuheshimika wa mila za Makka na hajasilimu kwenye dini ya Muhammad (sic - japo sio kweli). Walikubaliana kumpelekea masharti ya mwisho...

(The Eternal Message of Muhammad, London, 1964)

Huko nyuma, Maquraish walikwishawahi kufanya majaribio ya "kumtenga" Muhammad kutoka kwenye ukoo wake, na walitegemea kwamba wangeweza ama kumchombeza au kumhadaa Abu Talib katika kutotilia maanani msaada wake na ulinzi kwa mpwa wake na Uislamu. Kama wangemtenganisha Muhammad na ukoo wake, walitumaini, wangeweza kutatua hilo tatizo gumu na sumbuvu kwa njia rahisi ya "kumfilisi" yeye.

84

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Lakini Abu Talib hakuwaacha Maquraishi "kumtenga" Muhammad. Sio tu yeye mwenyewe aliyekuwa akimlinda mpwa wake, alikusanya pia ukoo wote wa Bani Hashim nyuma yake. Huu ukoo wa Bani Hashim ulikuwa imara katika msaada wake kwa Muhammad, na wakuu wa Maquraish walijikuta wanyonge mbele yake.

Baada ya mashauriano marefu na mjadala, Maquraishi walikubali kwamba "ukaidi" wa Bani Hashim ulihitaji hatua madhubuti, na waliamua kumtenga na kumfukuza sio tu Muhammad bali walinzi wake wote pia, yaani, ule ukoo wa Bani Hashim wote.

Ilitarajiwa kwamba jaribio lolote la kuwafukuza Bani Hashim lingepelekea kwenye kingamizo la vikundi hapo Makka. Kila mmoja hapo Makka angekuwa ajitangaze mwenyewe kuwapendelea au kuwapinga Bani Hashim. Lakini mara ikaja kuwa dhahiri kwamba katika mkabala huu, Bani Hashim watakuta Arabia yote imejipanga dhidi yao.

Muhammad Husein Haykal:

"Ni kama haiwezekani kwa sisi kufikiria nguvu na kiasi cha jitihada ambazo Maquraishi walitumia katika mapambano dhidi ya Muhammad, au uvumilivu wake katika miaka mingi mirefu ya mapambano hayo. Maquraishi walimtishia Muhammad na jamaa zake, hususan ami zake. walimdhihaki yeye na ujumbe wake, na walimtusi yeye vilevile na wafuasi wake. Waliwaagiza washairi wake kumtukana yeye kwa uho-dari wao makini sana na kuelekeza utani wao mkali dhidi ya mahubiri yake. Walimpa madhara na maumivu kwenye nafsi yake na kwenye nafsi za wafuasi wake.

Walimuahidi hongo za pesa, za hadhi ya kifalme na mamlaka, za vyote vile vinavy-omridhisha mtu aliye mgumu kabisa wa kuridhisha miongoni mwa watu. Hawakuwafukuza tu na kuwatawanya wafuasi wake kutoka kwenye nchi yao wenyewe, bali waliwadhuru katika uchuuzi na biashara zao wakati ikiwafukarisha. Ilimtahadharisha yeye na wafuasi wake kwamba vita pamoja na masaibu yake inge-waangukia juu yao. Mambo yote yaliposhindikana, walianza msusio juu yao uliopangwa kuwaua kwa njaa."

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Siku chache kabla ya mwanzo wa mwaka wa 7, wakuu wa koo mbali mbali za Quraishi walikutana katika kikao kizito cha faragha ndani ya "baraza la mji" la Makka, na pale, kwa makubaliano, walirasimu na kutia sahihi waraka unaotamka kwamba ila tu, kama huo ukoo wa Bani Hashim utamkabidhi Muhammad kwao, utafanyiwa mgomo wa kiuchumi na kijamii. Wakajiapiza wenyewe kutonunua chochote, wala kuuza chochote, kwa watu wa ukoo wa Bani Hashim, na waliweka marufuku kuoana kati yao na wao.

85

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mkataba huu ulipelekwa kwenye makabila mengine kwa ajili ya kuidhinishwa. Walipokwishaidhinisha, ukatundikwa kwa taadhima kwenye ukuta wa Al-Kaaba. Kuidhinishwa kwa mkataba huo kulikuwa ni kitendo cha uchokozi!

Abu Talib aliweza kuona dhahiri kwamba mfumo wa wasiwasi ulikuwa unaelekea kwa Bani Hashim. Hali ya Makka imekuwa ya mlipuko kiasi kwamba ukoo wa Bani Hashim ulijikuta kwenye hatari kubwa. Abu Talib alitambua kwamba haitakuwa busara kuishi kati-ka mji, wakati wowote adui anaweza kuzichoma moto nyumba zao. Kwa maslahi ya usala-ma wa ukoo huo, yeye, kwa hiyo, akaamua kuondoka Makka, na kutafuta usalama wa ukoo huo katika bonde karibu ya Makka ambalo baadae lilikuja kujulikana kama Sh'ib Abu Talib. Bonde hilo lilikuwa na namna ya ulinzi wa asili, na lilikuwa kwa hali yoyote lenye usalama wa kuishi kuliko kuishi kwenye nyumba zao mjini hapo ambazo zilikuwa sio sala-ma kwa mashambulizi.

Katika siku ya kwanza ya mwaka wa 7 wa Tangazo la Uislamu, kwa hiyo, zile koo mbili za Bani Hashim na Bani al-Muttalib ziliondoka Makka na zikachukua makao kwenye bonde. Koo hizo zilikuwa katika hali ya kuzingirwa (karantini). Ilikuwa iwe karantini ndefu!

Muhammad Husein Haykal:

"Ule mkataba ambao koo za Quraishi ziliuingia wa kumgomea Muhammad na kuwazingira Waislamu uliendelea kutekelezwa kwa miaka mitatu mfululizo."

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Marmaduke Pickthall:

"Kwa miaka mitatu, Mtume (s.a.w.) alikuwa amefungiwa pamoja na jamaa zake wote katika ngome yao ambayo ilikuwa katika moja ya mabonde linalokwenda hadi Makka."

(Introduction to the Translation of Holly Qur 'an,1975)

Hadithi ya karantini ya Bani Hashim ni mlango wa kusisimua katika utenzi wa Kiislam, na umesimuliwa na kila mwanahistoria wa somo hilo, miongoni mwao:

Sir William Muir:

"...Maquraishi walifanya muungano dhidi ya Bani Hashim - kwamba hawatawaoa wanawake zao, wala kuwaoza wanawake kwao; kwamba hawatauza chochote kwao, wala kununua kitu chochote kutoka kwao; na kwamba kuhusiana nao kwa aina yoyote ile kukome.

86

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Amri ya kupigwa marufuku huko iliwekwa kwa maandishi kwa uangalifu, na yaka-fungwa kwa mihuri mitatu. Pale wote walipojifunga wenyewe kwenye mkataba huo, kumbukumbu hiyo ikatundikwa kwenye ukuta wa Al-Kaaba, na hivyo kibali cha kidi-ni kikatolewa kwenye mahitaji yake.

Bani Hashim hawakuweza kuhimili mwelekeo wa maoni ya umma ambayo yamepa-ta nguvu kali hivyo dhidi yao, na yenye wasiwasi kwamba yanaweza kuwa ni utan-gulizi tu wa mashambulizi ya wazi, au wa mapigo ya gizani ambayo bado ni mabaya zaidi, walijitenga kwenye nafasi ya mji iliyojitenga inayojulikana kama Sh'ib Abi Talib. Imeundwa na moja ya mabonde mikatiko ya milima, ambamo yale mawe yanayochomoza ya Abu Qubais yamelemea kwenye viunga vya Mashariki ya Makka. Iliingiliwa kwenye upande wa mji kwa njia ya chini yenye lango, kwa njia hiyo ngamia alipita kwa taabu. Kwenye pande nyingine zote ilitengwa na mji kwa maja-bali na majengo.

Katika usiku wa kwanza wa mwezi wa kwanza wa mwaka wa saba wa ujumbe wa Muhammad, hawa Bani Hashim, pamoja na Mtume (s.a.w.) na familia yake, walijitenga kwenye kambi ya Abu Talib; na pamoja nao kilifuata pia kizazi cha Al-Muttalib, ndugu yake Hashim. Amri ya utenganisho ilitumiliwa kwa ukali kabisa. Hawa Bani Hashim mara wakajikuta wamekatwa kwenye njia yao ya kupatia nafaka na mahitaji yao mengine ya maisha; na uhaba mkubwa ukajitokeza kwa sababu hiyo ... akiba hiyo ya Bani Hashim isiyotosheleza iliyojalizwa tena kwa majaribio ya nadra na ya siri, iliwaweka kwenye upungufu na dhiki. Raia waliweza kusikia uliaji wa watoto wanaoteseka kwa njaa ndani ya bonde hilo ... miongoni mwa ndugu wa kundi hili lililotengwa, walipatikana waliojaribu, mbali na vitisho vya Maquraishi, kupitisha mara kwa mara mahitaji kwa hila wakati wa usiku, kwenye kambi ya Abu Talib. Hakim, mjukuu wa Khuwalid, alikuwa, japo jaribio lenyewe wakati mwingine lilikuwa hatari, akibeba mahitaji kumpelekea shangazi yake Khadija.

(The Life of Muhammad, London, 1877)

Mwanzoni mwa karantini hiyo, Ali alikuwa na umri wa miaka 16, na alibebeshwa kazi ngumu na ya hatari ya kuwapatia chakula ukoo mzima. Alitekeleza kazi hii kwa kuhatar-isha sana maisha yake na alileta maji na nafaka wakati wowote alipopata chochote kile. Kwa mfuko mmoja wa ngozi ya mbuzi wa maji, ilimbidi alipie kipande kimoja cha dha-habu, na alijiona mwenye bahati kama alifanikiwa kuufikisha kule kwenye bonde. Juhudi zake, hata hivyo, zilileta nafuu ya kiasi tu kwenye kabila hilo lililozingirwa.

Abu Talib mwenyewe hakuwa akilala usiku. Kwake yeye usalama wa kimwili wa mpwa wake ulipewa umuhimu wa kwanza kuliko kitu kingine chochote. Wakati Muhammad ali-poshikwa na usingizi, Abu Talib alimuamsha na kumwambia alale katika kitanda cha

87

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mmojawapo kati ya wanawe wanne, na alimuamuru mwanae kulala kwenye kitanda cha Muhammad. Baadae kidogo, atamuamsha mpwa wake tena, na kumwambia aende kwenye kitanda cha mwanae mwingine.

Aliutumia usiku wote katika kumhamisha Muhammad kutoka kwenye kitanda kimoja na kumuweka kwenye kingine. Hakudanganyika juu ya maadui zake; walikuwa wang'ang'an-ifu, wadanganyifu, mafisadi na wasiosamehe. Yeye, kwa hiyo, hakuwatweza. Kama mmoja wao angenyemelea ndani ya bonde hilo kwa nia ya kumuua Muhammad, yumkini kabisa, angemuua mmoja wa watoto wa Abu Talib. Yeye Abu Talib na mkewe daima walikuwa tayari kuwatoa mhanga watoto wao kwa ajili ya Muhammad.

Kulikuwa na nyakati ambapo Ali, licha ya ujasiri na uwezo wake mkubwa, alishindwa kupata mahitaji yoyote, na watoto (na watu wazima pia) waliishi kwa njaa. Lakini kuishi kwa njaa na kiu kulikuwa ni kawaida ndani ya bonde hilo. Wakati maji yakiwepo, akina mama walichemsha majani makavu ndani yake ili kuwaliwaza watoto wao wanaolia. Kilio cha watoto wenye njaa kiliweza kusikika nje ya bonde hilo, na Abu Jahl na Bani Umayya walikipokea kwa kicheko cha dhihaka. Walichekelea "ushindi" wao wa kuwafanya watoto wa Bani Hashim kulilia maji na chakula.

Zawadi ya thamani sana kwa hizi koo zilizotengwa katika miaka hii mitatu, ilikuwa ni maji. Maji yalikuwa ni zawadi ya maisha, na koo mbili hizi ziliyapokea kutoka kwa Khadija. Yeye alimpa Ali vile vipande vya dhahabu ambavyo alinunulia maji. Masikitiko yake juu ya wale waliomzunguka yalijionyesha kwa njia nyingi. Aliswali na kuomba rehma za Allah (s.w.t.) juu ya waliotengwa. Swala ilikuwa ndio "mkakati" wake wa kushughulikia shida. Ilikuwa, alivyouona, ni mkakati rahisi lakini wenye nguvu.

Mara chache, wale marafiki wachache ambao Bani Hashim walikuwa nao huko Makka, walijaribu kuingiza chakula kwa magendo ndani ya bonde hilo, lakini kama hao mapagani walikikamata, walikichukua.

Mmoja wa marafiki wa Bani Hashim aliyekuwako Makka alikuwa ni Hisham ibn Amr al-Aamiri. Aliwaletea chakula na maji kila mara kiasi alivyoweza. Muda aliouchagua wa kupeleka hayo mahitaji kwenye bonde hilo, ulikuwa ni masaa machache kabla ya kucha; lakini hatimae Maquraishi walimkamata, na walitishia kumuua kama angeng'ang'nia kule-ta ngamia wake waliosheheni bondeni hapo kwa ajili ya Bani Hashim. Rafiki mwingine wa siri wa Bani Hashim alikuwa ni Hakim ibn Hizam, mpwawe Khadija. Yeye na mtumwa wake walibeba chakula na maji kumpelekea Khadija ambayo mara moja aliyatoa kwa watoto.

Abul Bukhtari alikuwa mmoja wa marafiki wa Hakim. Yeye pia alileta mahitaji ya lazima kwa Bani Hashim. Usiku mmoja yeye na Hakim walikuwa wamepanda ngamia kwenda

88

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

huko kwenye bonde wakati waliposhitukizwa na Abu Jahl. Aliwaambia kwamba atawanyang'anya zile bidhaa na ngamia. Mwanzoni, Abul Bukhtari akajaribu kuelewana naye kwa maneno lakini hakutaka kusikiliza kitu chochote. Alizuia ile njia ya kwendea kwenye bonde na akakataa kuwapisha wapite.

Abul Bukhtari alijaribu kulazimisha kumpita Abu Jahl, na hili lilisababisha ugomvi mkali wa ngumi kati yao. Mizozo kama hii ilizuka mara kwa mara karibu na bonde hilo lakini wale marafiki wachache ambao ukoo wa Bani Hashim waliokuwa nao hapo mjini, hawakuvunjika moyo, na walifanya kila kitu walichoweza kuwaletea msaada.

Hisham bin Amr al-Aamiri, Hakim bin Hizam, na Abul Bukhtari, hawakuwa Waislamu lakini hawakutaka kuona mtoto yeyote au hata mtumwa wa Bani Hashim akifa kwa njaa, na wakahatarisha maisha yao wenyewe mara kwa mara katika kuleta chakula na maji kwenye Sh'ib Abu Talib. Walikuwa vilevile wakifurahia kulipia madeni ya huduma za msaada kama hizo kwa miaka mitatu, na chote walichokitafuta kama malipo yao kilikuwa ni usalama wa zile koo zilizotengwa.

Haina budi ionyeshwe hapa kwamba ile chuki na hasira ya Bani Umayya ya Quraishi ilielekezwa sio dhidi ya Waislamu bali dhidi ya ukoo wa Bani Hashim. Nia yao ilikuwa ni kuuangamiza Uislamu. Lakini hawangeweza kuangamiza Uislamu bila ya kumuua Muhammad. Walifanya idadi kubwa ya majaribio ya kumuua lakini walishindwa kwa sababu hawakuweza kumfikia. Alikuwa salama na shwari katika "ngome" ambayo Abu Talib na Bani Hashim wameijenga kwa ajili yake.

Bani Umayya waliwalenga kwa usawa kabisa Bani Hashim kama wahusika wa kushindwa kwao kote na kukatishwa tamaa katika vita vyao juu ya Uislamu, na kamwe hawakuipu-uza ili kuwashinda katika mapambano yao marefu na magumu dhidi yake.

Na kwa Waislamu ambao hawakutokana na ukoo wa Bani Hashim, walikuwepo wengi, na wote walikuweko Makka. Hawakwenda Sh'ib Abu Talib pamoja na Bani Hashim. Wengine miongoni mwao wanasemekana walikuwa matajiri, wenye uwezo na mashuhuri, na wote walidai kwamba walikuwa wakimpenda Mtume wao; lakini cha kushangaza, hakuna hata mmoja wao aliyekuja kumuona sembuse kumletea msaada wowote, wakati wa miaka mitatu ya karantini. Walifurahia starehe na usalama wa majumbani mwao hapo mjini kwa miaka mitatu wakati Mtume wao, Muhammad Mustafa, akiishi kwenye ncha ya upanga, akizungukwa na maadui wenye kiu na damu yake, na katika hali ya wasiwasi kamili akiwa hajui kamwe ni matata gani mchana au usiku unaokuja utamletea yeye na kwa ukoo wake.

Karantini hii ya Bani Hashim iliondolewa miaka mitatu baadae, mwaka wa A.D. 619, na ukoo huo ukarudi mjini. Miaka kumi imepita tangu Muhammad, rehma na amani ziwe juu yake na Ahlul-Bait wake, alipotangaza kwa mara ya kwanza ujumbe wake. Mgomo wa

89

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Maquraishi umeshindwa kuzaa matokeo yaliyotarajiwa. Watu wa Bani Hashim walikuwa majasiri, na murua wao ulikuwa juu. Ilikuwa haiwaziki kwao vilevile, hapo mwishoni mwa karantini, kama ilivyokuwa hapo mwanzoni, kumtoa Muhammad, mpendwa wao, kwa maadui wake.

Bani Hashim na Bani Al-Muttalib walirejea majumbani kwao huko Makka baada ya miaka mitatu. Muda wote wa miaka hii mitatu, utajiri wote wa Khadija na Abu Talib ulikwisha. Walikuwa waanze, kama ilivyokuwa, mwanzo mpya katika maisha, kwa kuweka matofali yao kwenye nafasi zao - moja moja.

Kama wakuu wa Maquraishi waliiondoa karantini, haikuwa kwa sababu kulikuwa na "mabadiliko ya moyo" yoyote kwa upande wao. Waliiacha karantini hiyo kwa sababu kulikuwa na nguvu nyingine zilizokuwa zikifanya kazi dhidi yake. Yafuatayo ni maelezo yaliyotolewa katika chanzo cha mapema sana kinachopatikana hadi leo, ‘Wasifu wa Mtukufu Mtume wa Uislamu' cha Muhammad ibn Ishaq, cha matukio yaliyofikia kilele katika kurudi Makka kwa koo za Bani Hashim na Bani al-Muttalib kutoka Sh'ib Abu Talib, baada ya miaka mitatu.

Kutanguka kwa mgomo

"Bani Hashim na Bani al-Muttalib walikuwa katika bonde (maficho ya mlimani) la Sh'ib kwa vile Maquraishi waliweka ahadi ya kuwatenganisha. Kisha baadhi ya watu wa kabila la Quraishi lenyewe walichukua hatua za kuutangua mgomo huo dhidi yao. Hakuna aliyehangaika sana na hili kuliko Hisham ibn Amr ... kwa sababu ya kwam-ba alikuwa mtoto wa ndugu ya Nadla bin Hashim bin Abd Manafi kwa mama yake na alihusiana kwa karibu sana na Bani Hashim. Aliheshimiwa sana na watu wake. Nimesikia kwamba wakati koo hizi mbili zilipokuwa kwenye bonde lao, alikuwa akipeleka ngamia aliyesheheni chakula usiku na kisha, alipokuwa amemfikisha kwenye mlango wa njia, alimuondolea hatamu yake, akampiga kwa kishindo ubavu-ni, na akamfanya akimbie ndani ya uchochoro wa njia inayoelekea kwao. Atafanya vivyo hivyo safari nyingine, akiwaletea nguo.

Akaenda kwa Zubayr bin Abu Umayya bin Al-Mughira ambaye mama yake alikuwa ni Atika binti ya Abdul Muttalib na akasema: 'Unaridhika kula chakula na maji na kuvaa nguo wakati ukijua hali ya ami zako wa kikeni? Hawawezi kununua au kuuza au kuchanganya damu. Wallahi kama wangekuwa ami za Abu'l-Hakam bin Hisham (Abu Jahl), na ukamtaka afanye alivyokutaka wewe ufanye, asingelikubali hilo kamwe.' Yeye (Zubayr) akasema, 'Unanishangaza wewe Hisham, mimi nitafanya nini? Nipo mtu mmoja tu. Wallahi, kama ningekuwa na mtu mwingine wa kuniunga mkono mimi, ningeutangua mapema sana.' Akasema, 'Nimepata mtu - mimi mwenyewe.' 'Tafuta mwingine,' akasema. Hivyo Hisham akaenda kwa Al-Mutim bin

90

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Adiy na akasema, 'unaridhika kwamba koo mbili za Bani Abd Manafi ziangamie huku ukiona ukiwaafiki kuwafuata Maquraishi? Utaona kwamba hivi karibuni watak-ufanyia vivyo hivyo na wewe.' Mutim akatoa jibu kama lile la Zibayr na akataka mtu wa nne.

Hivyo Hisham akaenda kwa Abu'l Bukhtari bin Hisham ambaye alitaka mtu wa tano, na kisha kwa Zama'a bin Al-Aswad bin Al-Muttalib, ambaye aliomba mtu wa sita, na akamkumbusha udugu na wajibu wao. Aliuliza endapo wengine walikuwa tayari kushirikiana kwenye kazi hii. Akampa majina ya wale wengine. Wakakubaliana wote kukutana usiku karibu na Hujun, juu ya Makka, na walipokutana, walijifunga kulichukulia swala la ile hati hadi wamepata utanguzi wake.

Siku iliyofuata, wakati watu walipokusanyika pamoja, Zubayr alivaa joho, akazungu-ka Al-Kaaba mara saba; kisha akaja mbele na kusema: 'Enyi watu wa Makka, hivi sisi tule na kujivisha wenyewe wakati Banu Hashim wanaangamia, wakiwa hawawezi kununua wala kuuza? Wallahi sintapumzika hadi pale hati hii ya mgomo muovu itakapopasuliwa!

Abu Jahal akapaza sauti: 'Unajidanganya. Haitapasuliwa.'

Zama'a akasema: "Wewe ni muongo mkubwa; hatukuipenda hati hii hata pale mwan-zo iliporasimiwa na kutiwa saini."Abu'l Bukhtari akasema, 'Zama'a anasema kweli. Hatukuridhika na hati hii ilipokuwa inaandikwa, na haturidhiki nayo sasa hivi.'

Al-Mutim akaongeza: "Wote mnasema kweli, na yeyote anayesema vinginevyo, huyo ni muongo. Tunamuomba Allah ashuhudie kwamba tunajitoa kwenye wazo zima na kile kilichoandikwa kwenye hati hiyo." Hisham akaongea kwa maana hiyo hiyo, na akawaunga mkono marafiki zake.

Kisha Al-Mutim akaiendea ile hati na kuichana vipande vipande. Aligundua kwamba wadudu walikwisha itafuna isipokuwa yale maneno, "Kwa Jina lako Ewe Allah (s.w.t.)" Hii ni kanuni iliyozoeleka ya Maquraishi ya kuanzia maandishi yao. Mwandishi wa hati hii alikuwa ni Mansur bin Ikrima."

Mutim ibn Adiy akachana ile hati ya fedheha ya Maquraishi katika vipande vipande. Vile vipande vikapeperushwa na upepo, na hakuna sazo lililoachwa. Ni kitendo kilichohitaji msimamo na ujasiri - msimamo kwamba Bani Hashim walikuwa waathirika wa udhalimu, ukatili na majuto, wasio na hatia; na ujasiri kuwakaidi Maquraishi. Kitendo chake imara kilikuwa ni ishara kwamba ile karantini ya Bani Hashim imekwisha, na kwamba watu wake sasa wanaweza kurejea mjini. Mutim mwenyewe na wapiganaji vijana wa ukoo wake walikwenda kwa vipando vyao wakiwa katika mavazi kamili ya kivita, kwenye bonde hilo

91

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

na kumsindikiza Muhammad Mustafa na watu wote wa koo mbili za Bani Hashim na Bani al-Muttalib, kurudi Makka na majumbani kwao.

Dr. Muhammad Hamidullah anaandika kwenye ukurasa wa 10 wa kitabu chake, Introduction to Uislamu, kilichochapishwa na International Islamuic Federation of Student Organizations, Salimiah, Kuwait (1977):

Baada ya miaka mitatu, watu wanne au watano wasiokuwa Waislamu, wenye ubinaadamu zaidi kuliko wote waliobakia na wanaotokana na koo tofauti, walitangaza bayana shutuma zao za ule mgomo wa kiuonevu.

Dr. Hamidullah amedhania kwamba kushindwa kwa mgomo huu ni matokeo ya ubi-nadamu wa "watu wanne au watano wasiokuwa Waislamu." Walikuwa, anasema, 'wenye ubinadamu zaidi kuliko wengine waliobaki.' Ana haki. Lakini walikuwa na ubinadamu zaidi hata ya waleWaislamu waliokuwa wakiishi Makka?

Kwa mshangao, cha ajabu, jibu la swali hili lenye kughasi ni la kukubali. Hata hivyo, mbali na hawa mashujaa watano - wasiokuwa Waislamu, wote - ubinadamu haukumsukuma mtu mwingine yeyote hapo Makka - asiyekuwa mwislamu au mwislamu - kuwakaidi Maquraishi na kutenda katika ulinzi wa Bani Hashim.

Kuna swali jingine moja, yaani, kwa nini Zubayr alijiona yuko yeye peke yake?

Wakati Hisham alipolijulisha kwa mara ya kwanza hili suala la kutangua huu Mkataba wa washirikina wa kuwagomea hawa Bani Hashim, kwa rafiki yake Zubayr, na akamsuta kwa kutokuwa na hisia juu ya mateso ya Bani Hashim, na kwa kushindwa kwake kushughuli-ka kuyamaliza mateso yale, Zubayr akasema, "Unanishangaza ewe Hisham, mimi nifanye nini? Mimi ni mtu mmoja pekee. Wallahi, kama ningekuwa na mtu mwingine wa kuniun-ga mkono, ningeutangua mapema tu."

Jibu la Zubayr ni la fumbo. Kwa nini alijiona yuko peke yake? Kwa nini asijaribu kuorod-hesha uungaji mkono wa Waislamu ambao walikuwa wengi hapo Makka? Kwa mujibu wa wanahistoria, baadhi ya Waislamu hapo Makka walikuwa ni watu wenye hadhi na wenye mali, na walikuwa na ushawishi wa kutosha kwa washirikina. Lakini kwa sababu za kisirisiri, haikuwajia ama kwa Zubayr mwenyewe au kwa rafiki yake yoyote, kuwaku-sanya Waislamu hawa kwenye kundi moja - "timu" - ambalo lilimaliza huu mgomo kwa Bani Hashim.

Zubayr na rafiki zake walifanikiwa katika juhudi zao za kuwarudisha Bani Hashim hapo mjini. Lakini kwa kitendo chao hiki, wamedhihirisha kwamba wale Waislamu ambao walikuwa wanaishi Makka, hawakuwa "wenye lazima" kwa Muhammad au kwa Uislamu.

92

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ni mojawapo ya ukweli mkubwa kabisa unaofanana na uongo katika historia ya Uislamu kwamba ule mkono uliofikia na kuchana vipande vipande, ule mkataba wa washirikina wa kuutenga na kuuhamisha ule ukoo wa Bani Hashim, ulitokana, sio kwa "mu'min" bali kwa "asiyeamini" Mutim ibn Adiy! Sio Mutim wala yeyote kati ya marafiki zake wanne, yaani, Hisham ibn Amr, Zubayr ibn Abu Umayya, Abu'l Bukhtari ibn Hisham, na Zama'a ibn Al-Aswad, aliyekuwa mwislamu. Lakini wote watano walikuwa mashujaa wenye maadili, na hawakuridhia katika dhulma iliyokuwa ikifanywa kwa Bani Hashim. Hawakutulia mpaka waliporejesha haki ndani ya Makka.

Kusema kweli, hawa mashujaa watano hawakuwa Waislamu. Lakini wao na wao wenyewe tu walikuwa na ujasiri na busara ya kutetea kanuni ambayo ni ya Kiislam, yaani, ile Kanuni ya Haki. Walitetea haki, na kitendo chao cha kishujaa, kiliwaletea sifa njema ya kudumu katika kisa kirefu cha historia ya Uislamu.

Waislamu, kwa upande mwingine, sio tu hawakushughulika; hawakuupinga walau, ule ubeuzi na uonevu wa Maquraishi katika kuwafukuza Bani Hashim kutoka Makka. Walidumisha, kwa miaka mitatu, upweke wenye hadhari na ukimya usioaminika. Matendo yao, inavyoonekana, yalitawaliwa na busara. Kwa hiyo, yote yale waliyofanya, ilikuwa ni kupitisha muda, na kuangalia mwelekeo wa matukio, kama watazamaji wasiojali.

93

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Vifo vya Khadija na Abu Talib

Shukrani kwa uungwana na ujasiri wa wale mashujaa watano wa Makka, kwa vile watu wa ukoo wa Bani Hashim wamewewza sasa kuishi majumbani mwao tena. Lakini walikuwa hata hawajaweza kupata nafuu vizuri kutokana na uchovu wa kuishi kwenye maficho ya mlimani kwa miaka mitatu, wakati Khadija, yule mke, rafiki na sahaba wa Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.w.t.), na yule mfadhili wa Uislamu na Waislamu, alipougua na kufa. Maisha yake yote aliishi katikati ya starehe na wingi wa anasa lakini miaka ile mitatu ya uhamishoni ilikuwa ni wakati wa ugumu uliozidi kiasi kwake ambao bila ya kuk-wepa ulimuua.

Kama ilivyoonyeshwa kabla, Khadija alikuwa ndiye mwanamke wa kwanza hasa katika dunia nzima kutamka kwamba Mungu ni Mmoja, na Muhammad alikuwa ni Mtume Wake kwa wanadamu wote. Heshima na sifa ya kuwa Muumini wa Kwanza katika dunia nzima ni yake milele. Alijitolea raha zake, mali yake, na nyumba yake kwa ajili ya Uislamu; na sasa itaonekana kama amejitoa mhanga maisha yake pia. Bila ya shaka, kama angeishi katika nyumba yake yenye nafasi na anasa hapo Makka, akiwa amezungukwa na watu-mishi wake wa kike, angeweza kuishi kwa miaka mingi zaidi. Lakini alipendelea kusima-ma na mume wake na ukoo wake, na kushiriki machungu ya maisha pamoja nao. Katika wakati wa karantini, ilimbidi avumilie sio tu makali ya njaa na kiu bali pia na vipeo vya juu vya joto katika kiangazi na baridi wakati wa kipupwe, na bado hakuna aliyesikia kamwe neno la kulalamika kutoka kwake, na kamwe hakupoteza utulivu wake. Kama nyakati zilikuwa nzuri au mbaya, ama alikuwa na kitu kwa wingi au alikuwa hana cho-chote, daima alikuwa mwenye furaha hata kule uhamishoni. Kukoseshwa na ugumu kamwe havikuuchukiza moyo wake. Ulikuwa ni moyo wake uliokuwa chanzo cha nguvu isiyoshindika, faraja na ujasiri kwa mume wake katika nyakati unyonge uliokithiri za maisha yake.

Katika ile miaka ya karantini, Khadija alitumia mali yake nyingi sana kwa kununulia mahi-taji muhimu ya maisha kama maji, chakula na nguo kwa ajili ya ukoo huo na mumewe. Aliporudi kwenye nyumba yake, senti yake ya mwisho ilikuwa imekwenda; na alipokufa, hamkuwa na pesa ya kutosha humo ndani ya nyumba ya kununulia sanda. Shuka la mumewe lilitumika kama sanda yake, na alizikwa ndani yake.

Muhammad Mustafa kamwe hakuoa mke mwingine wakati Khadija alivyokuwa hai, na kama asingekufa, inawezekana kabisa kwamba asingeoa mwanamke mwingine yeyote.

94

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Edward Gibbon

"Katika miaka 24 ya ndoa yao, mumewe Khadija aliyekuwa kijana alijinyima haki ya kuoa wake wengi, na fahari au upendo wa mke huyu mwenye kuheshimika ulikuwa bado haujafedheheshwa na jamii ya upinzani. Baada ya kifo chake, Mtume (s.a.w.) alimuweka katika cheo cha wanawake wanne wema, pamoja na dada yake Musa, mama yake Isa (Yesu), na Fatima, mpendwa bora wa mabinti zake.

(The Decline and Fall of the Roman Empire) Sir John Glubb

"Khadija alikuwa mfuasi wa kwanza wa Muhammad. Kutoka wakati wa mwito wake wa kwanza, mpaka kifo chake miaka tisa baadae, Khadija hakuyumba kamwe. Wakati wowote Mtume (s.a.w.) alipokabiliana na dhihaka au hitilafu, alikuwa na uhakika, pale atakaporudi nyumbani jioni, wa kumpata mliwazaji mcheshi na mwenye upendo. Alikuwa tayari wakati wote kwa akili yake timamu kuhifadhi ujasiri wake na kumpunguzia mzigo wa hofu zake."

(The Life and Times of Muhammad, New York, 1970)

Ibn Ishaq, yule mwandishi wa wasifu wa Mtume, anasema kwamba kulipokuwa na kuanza tena kushuka kwa Wahyi baada ya kusimama kwake kufuatia kushuka kwa awali, Khadija alipokea Heshima Tukufu na salamu ya amani kutoka kwa Allah (s.w.t.) Ujumbe huo ulifik-ishwa kwa Muhammad na Jibril, naye alipoufikisha kwa Khadija, akasema Khadija: "Allah (s.w.t.) ni Amani (as-Salam), na kutoka Kwake ni Amani tupu, na amani iwe juu ya Jibril."

Muhammad Mustafa daima alimkumbuka Khadija kwa mapenzi, upendo na shukurani. Wakati wa maradhi yake mafupi, alikesha usiku mzima akimuuguza, kumliwaza na kumuombea. Alimwambia kwamba Allah (s.w.t.) amemjengea kasiri la lulu ndani ya Pepo. Kifo chake kiliujaza moyo wake huzuni nzito.

Khadija alikufa mwezi 10 ya Ramadhani ya mwaka wa kumi wa Tangazo la Uislamu. Alizikwa huko Hujun juu ya Makka. Baada ya mazishi, Mtume (s.a.w.) mwenyewe alisawazisha udongo wa kaburi lake.

Mwezi mmoja baada ya kifo cha Khadija, Mtume (s.a.w.) alipata mshituko mwingine katika kifo cha Abu Talib, ami yake na mlezi wake. Abu Talib alikuwa ndio ngao ya Uislamu tangu kuanzishwa kwake. Vifo vya marafiki hawa wawili, Khadija na Abu Talib, vilikuwa ndio mshituko mkubwa na huzuni ambavyo ilimbidi avivumilie katika miaka hamsini ya maisha yake. Aliuita ule mwaka wa vifo vyao "Mwaka wa Huzuni."

95

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ule mwaka wa 619 uligeuka kuwa mwaka wa huzuni kwa Muhammad Mustafa kwa maana zaidi ya moja. Kifo cha mpenzi wa mtu kwa kawaida ni chanzo cha huzuni. Lakini kwa upande wake yeye, vifo vya hawa marafiki wawili havikuwa tukio la kinafsi tu. Mara tu, alifahamishwa maana ya vifo vyao kwa mfululizo wa matukio yasiyofungamana.

Ibn Ishaq

Khadija na Abu Talib walikufa mwaka mmoja, na kwa kifo chake Khadija matatizo yalifuatia haraka nyuma ya kila mtu, kwani alikuwa mtoaji msaada mkubwa kwake katika Uislamu, na alikuwa akimwelezea matatizo yake. Kwa kifo cha Abu Talib, alipoteza nguvu na tegemeo katika maisha yake binafsi na ulinzi na kinga dhidi ya kabila lake. Abu Talib alikufa miaka mitatu kabla ya yeye (Muhammad) kuhamia Madina, na ilikuwa hapo ambapo kwamba Maquraishi walimshughulikia kwa njia ya maonevu ambayo wasingeweza kuthubutu kuifuata katika uhai wa ami yake. Baradhuli mdogo kwa kweli alimtupia vumbi kichwani mwake.

Hisham kutoka kwa baba yake, Urwa, aliniambia kwamba Mtume (s.a.w.) aliingia ndani ya nyumba yake, na alikuwa amesema, "Maquraishi kamwe hawakunitendea hivi wakati Abu Talib alipokuwa hai."

(The Life of the Messenger of God) Washington Irving

"Muhammad mara akatambua kupotelewa alikokupata katika kifo cha Abu Talib ambaye alikuwa sio tu ndugu mpendwa, bali mlinzi imara na mwenye madaraka, kutokana na umaarufu wake hapo Makka. Kwa kufa kwake hapakuwa na mtu yeyote wa kusimamisha na kukinza uhasama wa Abu Sufyan na Abu Jahl."

Bahati ya Muhammad ikawa inakuwa mbaya na mbaya zaidi katika mahali pake pa asili. Khadija, mfadhili wake wa awali, yule sahaba mwaminifu wa faragha yake na upweke, yule muumini mwenye shauku kwenye mafundisho yake, alikuwa amekufa; vilevile na Abu Talib, wakati fulani aliyekuwa mhifadhi mwaminifu na madhubuti. Akinyimwa uzoefu wa ulinzi wa Abu Talib, Muhammad amekuwa kwa namna fulani, aliyetengwa na jamii hapo Makka, akilazimika kujificha na kubakia kuwa mzigo juu ya ukarimu wa wale ambao mafundisho yake mwenyewe yamewaingiza kwenye mateso (sic-japo kwa makosa). Kama manufaa ya dunia yangekuwa ndio lengo lake, yamepatikana vipi?

(Life of Muhammad)

Katika kusema kwamba Muhammad aligeuka kuwa "mzigo juu ya ukarimu wa wale ambao mafundisho yake mwenyewe yamewaingiza kwenye mateso," yule mwanahis-toria aliyetajwa hapo juu, ameelezea dhana ambayo kwamba hatuwezi kukubaliana nayo. Muhammad kamwe hakuwa mzigo kwa mtu yeyote kwa wakati wowote. Watu

96

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wa ukoo wake, hawa Bani Hashim, waliona kama ni upendeleo na heshima kumkinga na kumlinda yeye dhidi ya maadui zake.

Sir William Muir:

"Kujitolea ambako Abu Talib alijitokeza yeye binafsi na familia yake kwa ajili ya mpwa wake, ambapo bado alikuwa haamini ujumbe wake (sic. - hii sio kweli), kulithibitisha tabia yake kama ya utukufu wa kipekee na asiye na choyo. Kunatoa kwa wakati huo huo uthibitisho mzito wa uaminifu wa Muhammad. Abu Talib asingeweza kufanya hivyo kama mdanganyifu anayejipendeza; na alikuwa na uwezo wa kutosha kufanya uchunguzi."

Wakati mkuu wa familia alipoona maisha yanadhoofika, aliwaita ndugu zake, wana wa Abd al-Muttalib, kuzunguka kitinda chake, akamuweka mpwa wake mikononi mwao kumlinda; na, akapokelewa dhamana hiyo, akafa kwa amani, na akazikwa sio mbali sana na kaburi la Khadija. Muhammad alimlilia kwa uchungu sana ami yake; na sio bila sababu. Kwa miaka arobaini amekuwa ni rafiki yake mwaminifu - nguzo ya utotoni mwake, mlezi wa ujana wake, na katika maisha ya baadae, aliyemtegemea kwa ulinzi. Kutokuamini kwake hasa (sic - hii sio kweli) kulifanya athari zake kuwa na nguvu zaidi. Kwa kiasi cha muda alipokuwa hai, Muhammad hakuwa na haja ya kuogopa vurugu au mashambulizi. Lakini hapakuwa na mkono (mtu) wenye nguvu sasa ya kumlinda kutokana na maadui zake. Khadija wa pili anaweza kupatikana, lakini sio Abu Talib wa pili.

(The Life of Muhammad, London, 1877) Sir John Glubb:

"Mtume (s.a.w.) alifanya juhudi kubwa sana kumshawishi Abu Talib kurudia ile sha-hada ya imani ya Kiislam, lakini alilala kimya bila ya kujibu, mpaka alipokufa (sic. hii sio kweli). Abu Talib kwetu sisi anaelekea kuwa mtu wa kuvutia. Msema kweli, mwaminifu na mwenye huruma, alivumilia mashaka mengi, hasara na hitilafu ili kumlinda mpwa wake, ingawa hakuwa akiamini mafundisho yake (sic. - hii sio kweli). Huchukuliwa kama shujaa na Waislamu, kwani alikufa katika ukafiri (sic. -hii sio kweli). Hata hivyo, kama isingekuwa kwa ujasiri imara ambao kwawo alisi-mama nao kwa mpwa wake, Uislamu ungekufa katika chimbuko lake.

(The Life and Times of Muhammad, New York, 1970)

Nimewanukuu hapo juu Sir William Muir na Sir John Glubb neno kwa neno. Wamepiga vijembe kwamba Abu Talib alikufa katika ukafiri. Kama watapewa changamoto ya kutoa rejea ya maelezo hayo, watamtaja Bukhari. Bukhari anasema kwamba Abu Talib

97

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

alipokuwa kwenye kitanda chake cha umauti, Mtume (s.a.w.) alimsisitiza awe mwislamu lakini akasema kwamba kufanya hivyo kutamfedhehesha kwa marafiki zake wa kiquraishi.

Waandishi wa "Hadith" hii walisahau kitu kimoja. Abu Talib alikuwa anakufa, na akijua kwamba hatawaona "marafiki" zake Maquraishi tena. Alijua kwamba anakwenda mbele kwa Muumba wake. Kwa muda kama huu asingelijali sana juu ya Quraishi. Shauku yake wakati wote ilikuwa ni kupata radhi za Allah (s.w.t.) na alithibitisha kwa matendo yake zaidi kuliko ambavyo mtu mwingine yeyote angeweza kuthibitisha kwa maneno yake, kwamba imani yake katika Tawhid ya Allah (s.w.t.) na katika ujumbe wa Muhammad kama Mtume Wake, ilikuwa kama jiwe na haitikisiki.

Abu Talib alikuwa mu'min mwenye moyo wa bidii katika Uislamu. Kujiambatanisha kwake kwenye Uislamu kunadhihirishwa na msimamo wake na mantiki ya mambo.

Hakuna mtu anayeweza kumpenda Muhammad na uabudu masanamu kwa wakati mmoja; mapenzi mawili hayo yote yanajitenga. Na hakuna mtu anayeweza kumpenda Muhammad na bado auchukie Uislamu. Upendo kwa Muhammad na chuki kwa Uislamu haviwezi kuwa pamoja. Mwenye kumpenda Muhammad, ni lazima, bila kukwepa, aupende Uislamu. Wala hawezi mtu akamchukia Muhammad na akaupenda Uislamu. Dhana kama hiyo itakuwa kichekesho kikubwa sana.

Kama kuna kitu kimoja chochote kisicho na shaka yoyote ile katika historia ya Uislamu, ni mapenzi ya Abu Talib kwa Muhammad. Kama ilivyoonyeshwa kabla, Abu Talib na mkewe, Fatima bint Asad, walimpenda Muhammad zaidi ya walivyowapenda watoto wao wenyewe. Wote mume na mke walikuwa tayari daima kuwatoa watoto wao muhanga kwa ajili ya Muhammad. Mapenzi kama hayo yangeweza tu kuwa na kiini kimoja tu, kile cha imani juu ya Muhammad na Uislamu. Mkewe Abu Talib, Fatima bint Asad, yule mama wa kunyonya wa Muhammad, alikuwa ndiye mwanamke wa pili kuingia Uislamu, wa kwan-za akiwa ni Khadija.

Abu Talib alikuwa na fahari kwamba Allah (s.w.t.) amemchagua Muhammad, mwana wa kaka yake, Abdullah, katika viumbe wote, kuwa Mtume Wake wa Mwisho kwa wanadamu. Muhammad alikuwa ni kipenzi mkubwa na fahari kuu ya ami yake, Abu Talib.

Vitendo vitukufu vya Abu Talib ni sehemu muhimu sana katika Hadith ya Uislamu. Hakuna Hadith ya Uislamu ambayo ama itakuwa imekamilika au kuwa ya kweli kama haikuingiza maelezo ya jukumu lake kama mlinzi wa Muhammad na ngao ya Uislamu. Matendo yake ndio uthibitisho fasaha wa imani yake juu ya Allah (s.w.t.) na Mtume Wake. Allah (s.w.t.) awarehemu waja wake watiifu, Khadija; Abu Talib na mke wake, Fatima binti Asad. Wote watatu walikuwa ndio "vyombo" ambavyo kwavyo Ameuimarisha Uislamu, na kuuwezesha kuwepo.

98

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Safari ya Muhammad kwenda Taif

Zaidi ya miaka kumi imepita tangu muhammad, rehma na amani juu yake na Ahlul-Bait wake, alipoanza kutangaza Uislamu. Mafanikio yake katika miaka hii kumi yamekuwa kidogo ni ya wastani, yakiishia kama ilivyokuwa, kwenye kusilimisha chini ya watu 170 wake kwa waume hapo Makka. Lakini baada ya kifo cha mke wake, Khadija, na ami yake, Abu Talib, ilionekana kwamba Maquraishi wangemnyang'anya hata yale mafanikio mado-go kutoka mikononi mwake. Makka ilithibitika kuwa isiyokalika kwa Waislamu na iliji-tokeza kwa Mtume (s.a.w.) kwamba alipaswa, pengine kujaribu kuilingania hii imani mpya kwenye mji mwingine. Mji wa karibu sana ulikuwa ni Taif, maili 70 upande wa Kusini-Mashariki ya Makka, na alikwenda huko mwishoni mwa mwaka 619. Alifuatana pamoja na Zayd bin Haritha.

Akiwa huko Taif, Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) aliwatembelea wakuu watatu wa makabila ya wenyeji wa hapo, na akawalingania waache uabudu masanamu wao mbaya, na kukubali Tawhid ya Allah (s.w.t.) kukana heshima zilizoundwa na watu za jamii yote, na kuamini katika usawa na udugu wa watu wote.

Wale wakuu wa Taif walikuwa watu wa majivuno na kiburi, na hawakutaka hata kumsik-iliza Muhammad. Walimkaribisha kwa dhihaka na kebehi na wakamshakizia wale watu wazembe na mabaradhuri wa mji huo. Walimshambulia yeye na Zayd kwa kuwatupia madongo na mawe. Akiwa amejeruhiwa na kufunikwa na damu, Muhammad aliyum-bayumba kutoka nje ya Taif. Mara alipofika nje ya kuta za mji, karibu azirai lakini mkuli-ma wa bustani mmoja alimchukua nyumbani kwake, akamfunga majeraha yake, na akamwacha apumzike na kurudisha nguvu, mpaka alipojisikia mwenye nguvu za kutosha kuanza tena safari yake kuvuka nchi ngumu kati ya Taif na Makka.

Lakini Muhammad alipowasili kwenye viunga vya Makka, alihisi kwamba hangeweza kuingia tena kwenye mji wake wa asili sasa kwa vile ami yake, Abu Talib, hakuwepo pale kumlinda. Uhasama wa wapagani juu yake umefikia kiwango cha hatari. Alitambua kwamba kama ataingia Makka, anaweza kuuawa. Muhammad hakuweza kuingia mji wake wa nyumbani, na hapakuwa na sehemu nyingine ya kwenda. Je, angefanya nini?

Katika hali hii mbaya, Muhammad alituma habari kwa mabwana wakubwa watatu wa hapo mjini akiwaomba kila mmoja wao amchukue chini ya ulinzi wake. Wawili wao walikataa lakini yuke wa tatu - yule muungwana Mutim ibm Adiy - aliijibu ile ishara yake ya wasi-wasi. Alikuwa ni Mutim yuleyule, ambaye hapo mwanzoni, aliwaasi wale wakubwa wa Maquraishi kwa kuchanachana ule mkataba wa kuwagomea Bani Hashim, na alizirudisha

99

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

zile koo mbili za Bani Hashim na Bani al-Muttalib kutoka Sh'ib Abu Talib kuja mjini. Mutim aliamuru wanae, wapwa zake na vijana wengine wa ukoo wake kuvaa mavazi yao ya kivita. Kisha yeye akatoka, katika mavazi maridadi na kamili ya kivita, akiwa mbele yao, kwenda nje ya mji. Alimleta Muhammad Mustafa pamoja naye, kwanza kwenye mae-neo ya Al-Kaaba ambako Muhammad alifanya ile mizunguko saba ya desturi, na kisha akamsindikiza nyumbani kwake.

Abd-al-Rahman 'Azzam:

"Hakuna hata mmoja kati ya machifu wa Makka ambao Muhammad aliomba kwao ulinzi kwa ajili ya kuingia kwa salama hapo mjini aliyeweza kumtolea msaada; laki-ni chifu mmoja muungwana wa kipagani, al-Mutim ibn Adiy, alimchukua chini ya ulinzi wake na kumrudisha nyumbani. Hivyo ndivyo Muhammad alivyoingia tena Makka - akilindwa na mshirikina!"

(The Eternal Message of Muhammad, chapa ya New English Library, London, 1964) Sir John Glubb:

"Huko Taif Mtume (s.a.w.) alipigwa mawe na kufukuzwa. Akiogopa kurudi Makka sasa kwa vile hakufaidi tena ulinzi wa Abu Talib, alituma ujumbe kwa baadhi ya waabudu masanamu wakuu, akiwaomba ulinzi wao. Wawili walikataa lakini hatimae Mutim ibn Adiy, mkuu wa ukoo wa Nufal wa Quraishi, alikubali kumlinda. Asubuhi iliyofuata, yeye, wanae na wapwa zake walitoka na silaha kamili kwenda kwenye uwanja wa hadhara wa Al-Kaaba, na kutangaza kwamba Muhammad alikuwa chini ya ulinzi wao. Ulinzi huu wa Mutim ibn Adiy ulimuwezesha Mtume (s.a.w.) kurudi Makka.

(The Life and Times of Muhammad, New York, 1970)

Maombi ya Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.w.t.) wakati wa kurudi kwake kutoka Taif, kwa Mutim ibn Adiy, asiyekuwa mwislamu kuomba ulinzi wake, yanaleta tena, swali baya sana, katika namna iliyolenga sana, kwenye msimamo na tabia ya Waislamu. Kwa nini Mtume (s.a.w.) hakumuomba yeyote kati yao kumchukua kwenye ulinzi wake ingawaje baadhi yao walisemekana kuwa matajiri na maarufu, na wengine wao wali-tangazwa kuwa ndio tishio la wapagani? Kwa nini ikawa kwamba Mtume (s.a.w.) alitafu-ta ulinzi wa asiyekuwa mwislamu lakini hakujidhalilisha japo kwa kuwajulisha hao Waislamu kwamba alitaka kuingia tena Makka na alikuwa akihitaji ulinzi?

Au swali jingine! Kwa nini hao Waislamu wenyewe hawakwenda kwenye lango la mji na kumsindikiza Mtume wao nyumbani kwake? Hapa walikuwa na fursa nzuri ya kumuonye-sha yeye kwamba wanastahili kuaminiwa naye hata kama aliwaona hawafai. Lakini wali-

100

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ikosa fursa hiyo. Hawakufanya kitu chochote ambacho kingeweza kuonyesha kwamba wana shauku yoyote juu ya usalama wake binafsi.

Arabia ya kipagani, hata hivyo, haikukosa sehemu yake ya uungwana na ushujaa. Sifa hizi zilionyeshwa na Mutim ibn Adiy, Abul Bukhtari na wengine wachache. Walikuwa ndio mashujaa wa Arabia, na ilikuwa ni uungwana wao ulioifanya nchi yao kuwa maarufu katika karne za baadae. Arabia ya kipagani kamwe haikutoa watu waungwana zaidi kuliko hawa. Hata Waislamu wanapaswa kutambua deni lao la shukurani kwao. Hata hivyo ilikuwa ni wao walioweza kuwapa changamoto Maquraishi katika baadhi ya nyakati ngumu sana za maisha ya Mtume wa Uislamu. Kwa kufanya hivyo, walishinikizwa tu na mawazo yao binafsi ya uungwana. Walichukulia kuwa ni wajibu wao kuwalinda wale wasio na ulinzi.

Kushindwa kule kwa Taif kulikuwa ni kwa kuvunja moyo sana kwa Mtume, na alijua kwamba bila ule uingiliaji kati wa kishujaa wa Mutim ibn Adiy, asingeweza kabisa kuin-gia Makka. Kwa mtazamaji wa kawaida inaweza kuonekana kwamba Mtume (s.a.w.) ali-fikia kilele cha uvumilivu wa kibinadamu na subira. Maendeleo ya Uislamu yamesimama, na mtazamo wa baadae haukuweza kuonekana wazi zaidi.

Lakini je, Muhammad alikubali kukata tamaa mbele ya kushindwa kwa mfululizo na mbele ya makabiliano makali na washirikina? Ingekuwa ni kawaida tu kama angekubali. Lakini hakukubali. Hakukatia tamaa kamwe rehma za Allah (s.w.t.) zisizo na mpaka. Alijua kwamba anafanya kazi ya Allah (s.w.t.) na hakuwa na shaka yoyote kwamba ange-muongoza kumtoa kwenye giza la ukosaji matumaini na msaada kwenda mahali pa ushin-di na baraka.

Ilikuwa ni katika moja ya nyakati za kiza kikuu na huzuni kubwa za maisha yake ambapo Muhammad, Mtume wa Uislamu, alinyanyuliwa na Allah (s.w.t.) kwenda mbingu ya juu kabisa, huenda ni katika kutambua kukataa kwake kukubali kushindwa na kutokuwa imara katika mpangilio wa kazi. Allah (s.w.t.) alimtunuku Mtume wake na Isra' na Mi'raj. Isra' ni ile safari yake ya usiku kutoka "Msikiti mtukufu" kwenda "Msikiti wa Mbali" (Masjid al-Aqsa); na Mi'raj ni kule kupanda kwenda Mbingnii. Isra' na Mi'raj ziliashiria matukio makubwa na ya kihistoria ambayo tayari yalikuwa yametawala mawazoni, ingawa kwa wakati huo hapakuwa na uwezo wa kuyatambua.

Maana ya kimuujiza ya Mi'raj inahusika kwenye juhudi za kudumu za nafsi binafsi dhidi ya maovu. Ina vipingamizi vyake na madhaifu yake. Lakini kama ina ukweli kwake yenyewe, na kweli katika Imani juu ya Allah (s.w.t.), Yeye ataipa ushindi dhidi ya maovu. Hadithi ya Mi'raj, kwa hiyo, ni mwanzo unaofaa kwenye safari ya nafsi ya mwanadamu katika maisha. Hatua ya kwanza juu ya safari hii ni ya kuchukuliwa kupitia mwenendo wa utashi - hisia ya wajibu binafsi kwa ajili ya ustawi wa wanadamu wenzie, utumishi kwa

101

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Allah (s.w.t.), kupitia kutumikia viumbe Vyake, na utambuzi wa kuwepo Kwake nasi nyakati zote.

Isra' imetajwa katika Aya ya kwanza ya Sura ya 17 ya Qur'an Tukufu kama ifuatavyo:

Ametakasika aliyemchukua mja wake usiku mmoja kutoka Msikiti Mtukufu mpaka Msikiti wa mbali, ambao tumevibariki vilivyouzunguka, ili tumuonyeshe baadhi ya Ishara zetu. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia na Mwenye kuona.

Isra' na Mi'raj zilitokea katika usiku wa tarehe 27 ya Rajab (mwezi wa saba wa kalenda ya Kiislam) wa mwaka wa kumi na mbili wa Tangazo la Uislamu, yaani, mwaka mmoja kabla ya Hijira ya Mtume (s.a.w.) kutoka Makka kwenda Madina.

102

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Maeneo Mapya ya Uislamu

Yathrib ulikuwa ni mji kwenye chemchem karibu maili 250 kaskazini ya Makka. Mnamo mwaka wa 620 A.D., watu sita wa Yathrib walitembelea Makka kwa ajili ya Hija. Kukutana kwao kwa bahati na Muhammad kulisababisha kuingia kwao kwenye Uislamu. Walimwambia yeye kuwa waliiacha Yathrib katika hali ya kutokota na kwamba inaweza kulipuka wakati wowote kwenye vita. Lakini walionyesha matumaini kwamba Allah (s.w.t.) atairudisha amani kwenye mji wao kupitia kwa Mtume Wake. Waliahidi pia kuru-di Makka na kukutana naye mwaka unaofuata.

Huu ulikuwa ndio mwanzo wa Uislamu huko Yathrib.

Wakati hawa Waislamu wapya sita waliporejea Yathrib, waliongea na jamaa zao na marafi-ki kuhusu Uislamu, na wakawaona wanaridhia, hata kuwa na shauku ya kusikiliza. Mwaka mmoja baadae, wakati msimu wa hija ulipofika, wenyeji kumi na wawili wa Yathrib, pamoja na wale sita wa mwanzo, walitembelea Makka. Miongoni mwao walikuwemo wanawake wawili pia. Walikutana na Mtume wa Allah (s.w.t.) huko Aghaba. Aliwaelezea juu ya Shuruti za Imani katika Uislamu, na wote wakaukubali Uislamu. Wakati huo huo, walimpa pia kiapo chao cha utii. Hiki kinaitwa Kiapo cha Kwanza cha Aghaba.

Waislamu hawa walimhakikishia kwa dhati Mtume wa Allah (s.w.t.) kwamba:

Hawatamshirikisha Allah (s.w.t.) kamwe na yeyote, hawatamuabudu yeyote isipokuwa Allah (s.w.t.); hawatanyang'anya na kuiba kamwe; hawatawaua kamwe watoto wao wachanga wa kike; hawatawatukana watu wengine kamwe; hawatawakashifu tena wanawake; watakuwa sahihi na safi daima; watamtii Allah (s.w.t.) na Mtume Wake; na watakuwa waaminifu kwake wakati wote.

Hawa waumini wapya walimuomba Mtume (s.a.w.) kuwapa mwalimu wa kwenda naye Yathrib kuwafundisha Qur'an na maadili ya Uislamu. Alimtuma Mas'ab ibn Umayr, mmoja wa ami zake (Mas'ab alikuwa binamu ya baba yake), pamoja na kikundi hicho kwenda kuutangaza Uislamu huko Yathrib. Ujumbe wa Mas'ab ulifanikiwa, na familia nyingi huko Yathrib ziliukubali Uislamu.

Hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Muhammad kuchagua mtumishi. Profesa Margliouth anasema kwamba Mas'ab ibn Umayr alikuwa chaguo la kwanza la mtumishi katika Uislamu.

103

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kiapo cha pili cha Aghaba

Mwaka 622 A.D., wenyeji wa Yathrib sabini na watano walikuja Makka katika msimu wa hija. Mtume (s.a.w.) alikutana nao mahali palepale huko Aghaba ambako alikutana na lile kundi la watu kumi na wawili mwaka uliopita. Watu hawa 75 waume kwa wake pia wal-iukubali Uislamu. Walimpa kiapo chao cha utii, na wakamkaribisha Yathrib.

Ami yake Mtume, Abbas ibn Abdul Muttalib, alikuwa pamoja naye safari hii. Anasemekana kwamba aliwaambia wale "wenyeji" kutoka Yathrib kuwa: "Muhammad anatukuzwa sana na watu wake mwenyewe. Kama mtaweza kusimama naye kwa heri na shari, mchukueni mwende naye Yathrib; la sivyo, basi liacheni suala zima."

Mmoja wa viongozi wa watu wa Yathrib alikuwa ni Bira'a ibn Ma'ruur. Alisema: "Tulipokuwa watoto, wanasesere wetu tuliokuwa tukiwapenda sana walikuwa ni panga na mikuki." Mkuu mwingine, Abul Haithum, alimkatisha, na akasema: "Ewe Mjumbe wa Allah (s.w.t.)! Kitatokea nini wakati Uislamu utakapokuwa mkubwa na wenye nguvu? Hapo tena wewe utaondoka Yathrib na kurejea Makka?"

Muhammad Mustafa akatabasamu na kusema: "La hasha. damu yenu ni damu yangu na damu yangu ni damu yenu. Tokea siku ya leo ninyi ni wangu na mimi ni wenu, na sitaten-gana nanyi kamwe."

Waislamu wale wa Yathrib waliridhika na uhakikisho waliopewa na Muhammad Mustafa, na wakarudi Yathrib kuueneza Uislamu miongoni mwa jamaa zao. Uislamu ukaanza kupa-ta maendeleo imara huko Yathrib. Ilipoonekana kwamba imani hii mpya imepata mahali pa usalama katika mji ule, Mtume (s.a.w.) aliwashauri wale waathirika wa mateso pale Makka kuhamia pale. Kwa kufuata ushauri wake, Waislamu wakaanza kuondoka Makka, katika vikundi vidogo vidogo, na kuanza makazi katika majumba yao mapya hapo Yathrib.

Kile Kiapo cha Pili cha Aghaba ni tukio muhimu katika historia ya Uislamu. Kilikuwa ndio nanga ambayo juu yake kile chombo dhaifu kilikuja kupumzika mwishoe, baada ya kurushwa huku na kule kwa miaka kumi na tatu katika bahari zisizodhibitika za upagani ndani ya Arabia.

104

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hajira (Kuhama)

Wakati wengi wa Waislamu walipoondoka Makkah na kufanya makazi huko Yathrib, ilionekana kwa waabudu masanamu kwamba kama Uislamu utapata mizizi katika ile Nchi ya CHEMCHEM iliyopo kaskzini mwao, na ukaweza kujitegemea, itakujaleta tishio kwenye maslahi yao ya kibiashara huko Syria. Waliuona Uislamu kama "hatari kubwa" mpya inayonyanyua kichwa chake huko kaskazini. Kwa hiyo, waliitisha mkutano katika ukumbi wao wa jiji ambamo walifikiria njia yenye kufaa zaidi ya kuivuruga mapema hii "hatari kubwa". Baada ya majadiliano kiasi, walikubaliana, kwa pamoja, kwamba njia ya pekee ya kuizuia hii hatari kubwa mpya, ni kwa kumuua mwanzilishi wake - Muhammad mwenyewe - akiwa angali bado yupo Makka. Uamuzi huu ukazua maswali mengine machache kama vile ni nani atakayemuua, vipi, lini na wapi. Wakayajadili zaidi maswali haya, wakafikiria uwezekano wa namna nyingi, na hatimae wakaamua, kwa pamoja tena, kwamba mpiganaji mmoja kutoka kila ukoo wa kila kabila linaloishi Makka na viunga vyake, atachaguliwa; wote watashambulia nyumba ya Muhammad kwa wakati mmoja, na watamuua, kabla tu ya alfajiri ya siku inayofuatia. Tendo lililofanywa kwa pamoja kama hilo, waliamini, "lingewakwamisha" Bani Hashim ambao hawangeweza kuwa na uwezo wa kupigana dhidi ya koo zote hizo kwa wakati mmoja kwa kulipiza kisasi cha kuuawa kwa Muhammad.

Mtume, hata hivyo, alikuwa tayari kukutana na dharura kama hii. Kwa kuarifiwa wakati wa mpango wa Maquraishi wa kumuua, na mtu aliyesilimu kwa siri. Alimwita binamu yake mpendwa, Ali ibn Abi Talib, akamfahamisha ule mpango wa Maquraishi, na wa kwake mpango wa kuwazidi maarifa. Mpango wake ulikuwa ni kumuweka Ali kwenye kitanda chake yeye mwenyewe, na kisha kutoroka nje ya nyumba hiyo wakati wowote wenye fursa. Hao Maquraishi, kwa kumuona Ali akiwa amefunikwa na shuka, watadhania kwamba Muhammad alikuwa amelala, alimueleza. Alimuomba Ali pia kurudisha dhamana zote za wapagani kwa wenyewe, na kisha kuondoka Makka na kumkuta yeye huko Yathrib. Ali alielewa kila kitu, na Mtume (s.a.w.) akamdhamini kwenye ulinzi wa Allah (s.w.t.)

Muhammad Husein Haykal

Wale vijana ambao Maquraishi waliwaandaa kwa ajili ya kutekeleza mauaji ya Muhammad walikuwa wamezingira nyumba yake wakati wa usiku ili asije akatoro-ka. Katika huo usiku wa Hajira, Muhammad alitoa siri ya mpango wake kwa Ali ibn Abi Talib na akamuomba ajifunike shuka la kijani la Mtume, na alale kwenye kitanda cha Mtume. Alimuomba tena akae hapo Makka mpaka atakapokuwa amerudisha vitu vyote vya thamani vilivyokuwa vimewekwa kwa Muhammad, kwa wenyewe.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

105

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Marmaduke Pickthall:

"Wauaji walikuwa mbele ya nyumba yake (Muhammad). Alitoa shuka lake kwa Ali, akimtaka alale kwenye kitanda hicho ili kwamba yeyote atakayekuwa anatazama ndani angefikiria kwamba Muhammad amelala pale.

(Introduction to the Translation of Holy Qur'an, Lahore, 1975)

Washirikina waliizunguka nyumba ya Muhammad. Walichungulia ndani wakaona mtu aliyelala amefunikwa na blanketi, na wakaridhika kwamba "windo" lao liko salama. Ule wasaa wa fursa kwa ajili ya Mtume (s.a.w.) kutoroka ulifika muda baada ya usiku wa man-ane wakati ambapo wale askari wa doria wamesinzia. Alitembea kimya kimya na kuwapi-ta na kutoka nje ya maeneo ya nyumba yake.

Wale askari wa doria wa kipagani walikutwa wamejisahau, na Mtume wa Allah (s.w.t.) ali-fanikiwa katika kuukwepa kwa hila uchunguzi wao!

Ali alilala kwenye kitanda cha Mtume (s.a.w.) usiku mzima. Kabla tu ya mapambazuko, wale wauaji wa kipagani wenye kuhifadhi vichwa vya maadui, walivamia ndani ya nyumba panga zikiwa zimechomolewa kwenda kumuua Mtume. Lakini mshangao wao na mfad-haiko havikuwa na mipaka pale walipotambua kwamba alikuwa ni Ali na sio Muhammad ambaye alikuwa amelala pale kitandani. Wakamkamata Ali kwa kumhoji na pengine kwa kumtesa. Lakini mkuu wa wale askari wa doria akawaambia kwamba Muhammad hawezi kuwa amekwenda mbali sana, na kwamba wanaweza bado kumkamata kama hawatapoteza muda wao wenye thamani katika kumhoji Ali, hapo ndipo wakamuachia. Tukio hili linait-wa katika historia ya Kiislam Hajira au Kuhama.

M. Shibli, mwanahistoria ya Kiislam mashuhuri wa Kihindi, anaandika katika wasifa juu ya Mtume wa Allah (s.a.w.):

"Wapagani wa Makka walimchukia Muhammad, na bado walimuamini. Yeyote aliyekuwa na vitu vya thamani, alivileta na kuvihifadhi kwake. Alikuwa ndiye "mwenye-benki" wao. Alitambua juu ya mpango wa Maquraishi wa kumuua yeye. Kwa hiyo, yeye, akamwita Ali na akasema: "Allah (s.w.t.) ameniamuru mimi kwenda Yathrib. Wewe utalala kwenye kitanda changu na kesho urudishe amana za watu wa Makka kwa wenyewe." Hii ilikuwa ni hali yenye kuleta maafa na yenye hatari mbaya sana. Ali pia alijua kwamba Quraishi wamekusudia kumuua Mtume wa Allah (s.a.w.) usiku ule, na kwamba kulala kwenye kitanda chake ni kulala katika meno ya kifo. Lakini ni lini ambapo Ali alikiogopa kifo? Yule shujaa wa Khaibar akalala kwenye meno ya kifo usingizi mzito ambao hajawahi kuulala maishani mwake mwote.

(Life of the Apostle of God, Azamgarh, India, 1976)

106

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mtume (s.a.w.) hakuwa na muda wa kumwelezea Ali kwa kinaganaga ni amana ngapi alikuwa nazo na zilikuwa zikadhiwe kwa nani. Ilitosha kwake yeye kumwambia Ali arud-ishe amana zote kwa (wapagani) wenye mali zao, na yeye (Ali) akafanya hivyo. Ilikuwa kama vile tu kwenye karamu ya Dhul-Ashiira wakati kile ambacho Mtume (s.a.w.) alikuwa afanye, kilikuwa ni kumwambia tu Ali awakaribishe kwenye chakula watu wazima wote wa ukoo wa Bani Hashim. Hakukuwa na maelekezo ya kina yaliyokuwa lazima. Ali bila ya kufikiri alielewa nini bwana wake alichokitegemea kutoka kwake. Kule kukabidhiwa kurudisha zile amana za watu wa Makka kwao, ni ushahidi tosha kwamba Ali alikuwa msiri na "mwandishi binafsi" wa Mtume wa Uislamu hata kabla ya kule Kuhama kwenda Yathrib.

Ikiwa Hajira inasisitiza uaminifu wa Ali usio na mjadala kwa bwana wake, Muhammad, inaonyesha pia ujasiri wake wa ajabu. Wale askari wa doria wa maadui wangeweza kumuua ama kwa kuamini kwamba alikuwa ni Muhammad, au katika kugundua kwamba siye, kwa kuvunjika moyo tu. Alilijua hili vizuri sana, lakini kwake yeye hakuna hatari iliyokuwa kubwa sana kama angeweza kuokoa maisha ya Mtume wa Allah (s.a.w.) . Ilikuwa ni kujitolea huku na ujasiri huu kuliko mpatia ushindi yeye wa sifa nyingi za Qur'an Tukufu. Qur'an imetoa sifa kwenye uaminifu wake na ujasiri wake alioonyesha katika usiku ule wa majaaliwa wa Hajira (Kuhama) kama ifuatavyo:

Usahihi-5.jpg

"Na katika watu yupo ambaye huiuza nafsi yake kwa kutaka radhi za Allah. Allah ni mpole kwa waja wake."(Sura ya 2; Aya ya 207)

Razi, yule mfasiri maarufu wa Qur'an, anasema ndani ya Tafsir Kabir yake (juz. 2,uk. 189) kwamba Aya hii ilishuka hasa kwa kutambua kazi kubwa na tukufu ya Ali katika usiku wa Hijiria alipomuwezesha Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) kuondoka Makka. Kwa sababu ya Ali, aliweza kuondoka kwa usalama.

Katika usiku ule wa kihistoria, ilifanyika shughuli ya kibiashara ya ajabu na ya kimuujiza, ya kwanza na ya mwisho ya aina yake katika historia nzima ya Maumbile. Yalikuwa ni mapatano ya kuuza-na-kununua kati ya Allah (s.w.t.) na mmoja wa waja Wake. Mja aliyehusika hapa ni Ali ibn Abi Talib.

Katika usiku mkimya na usio na mbaramwezi, Allah (s.w.t.) alikuja kwenye "soko" kama "Mteja." Alikuja kununua bidhaa maalum. Mja Wake, Ali, alikuja kwenye "soko" kama "mfanyabiashara." Shughuli yake: kuuza ile bidhaa ambayo Allah (s.w.t.) alikuwa anaitafuta. Hiyo "bidhaa" ilikuwa ni roho yake, maisha yake!

Allah (s.w.t.) huyo "Mteja" aliangalia sana sifa ya "bidhaa" hiyo, na akaiona ni bora sana. Yeye, kwa hiyo, aliamua kuinunua papo hapo. Alilipa "thamani" yake kwa huyo

107

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"mfanyabiashara," na bidhaa ikabadilishanwa, sawasawa kama kwenye mapatano ya biashara nyingineyo ile. Kutokea muda ule, ile "bidhaa" - maisha ya Ali - ikakoma kuwa yake, na ikawa mali pekee ya Allah (s.w.t.) Yale mapatano ya kuuza na kununua kati ya Bwana na mtumwa kwa hiyo yakakamilika, kwa ridhaa kamili ya pande zote.

Walikuwepo "mashahidi" pia wa mapatano haya. Walikuwa ni Malaika na nyota - wengi mno - wakiangalia kutoka kwenye "majumba yao ya kisanii" ya mbinguni. Walitazama kwa kimya cha mshangao na kimya cha uvutiwaji vile Ali alivyouza maisha yake kwa Allah (s.w.t.) Qur'an Tukufu ikawa ndio "msemaji" wao kwa watu wa dunia hii, na ikaandika kile wao - hao mashahidi - walichokiona katika usiku ule wa kukumbukwa.

"Kumbukumbu" ya mapatano haya, kama ilivyohifadhiwa na Qur'an, tunayo hivi sasa, na ni ya kudumu na isiyoweza kuharibiwa. Itadumu kwenye dunia hii kwa muda ambao wale Malaika na zile nyota - "wale mashahidi" wa mapatano hayo - watakavyodumu huko Mbinguni!

Ali aliuza ile "bidhaa" kwa Allah (s.w.t.) Sasa akiwa ameondokana na ule "wasiwasi" kwa ajili ya usalama wa ile "bidhaa," angeweza kulala, na akaenda kulala - kwenye kitanda cha Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.). Katika Usiku ule wa Majaaliwa, alilala fofofo. Wakati wa alfajiri, alipoamka, au kwa usahihi zaidi, alipoamshwa na sauti kubwa na mgongano wa mikuki na panga za wale wauaji wenye kuhifadhi vichwa vya maadui, waliotumwa na Maquraishi, kumuua Muhammad, alikwishapata uzima!

Katika waja Wake wote, Allah (s.w.t.) alimchagua Ali kutekeleza Mpango Wake. Mpango ule ulikuwa ni kumlinda Mtume Wake, kutokana na maadui zake. Hawa maadui walik-wishaandaa mpango kwa ajili ya kuangamiza Uislamu. Waliamini kwamba kama wange-muua Muhammad, Uislamu ungeangamia. Wao, kwa hiyo, wakapanga na kula njama za kumuua Muhammad. Bali hawakujua kwamba Allah (s.w.t.) alikuwa na mpango wake mwenyewe - Mpango-Tibuzi (wenye kutibua) - tayari kwa ajili ya tukio hili.Ulikuwa ni Mpango-Tibuzi wa Allah (s.w.t.) ambao ulikuwa uje kuwakwamisha Maquraishi kwa kuokoa maisha ya Mtume Wake. Rejea ya Qur'an kwenye Mpango-Tibuzi wa Allah (s.w.t.) inapatikana kwenye Aya ifuatayo:

Usahihi-6.jpg

"Na makafiri walipanga mipango na Allah akapamnga mipango, na Allah ndiye mbora wa wenye kupanga." (Qur'an; 3: 54

108

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali ibn Abi Talib alikuwa ndiye "kiungo muhimu" katika Mpango-Tibuzi wa Allah (s.w.t.) Jukumu la Ali lilihakikisha mafanikio ya Hajira (Kuhama) ya Muhammad, na mafanikio hayo ya Hijira peke yake yalifanya kuanzishwa kwa dola ya kisiasa ya Madina kuwezekana. Kama Hajira ingeshindwa, hiyo Dola ya Madina kamwe isingekuja kuwepo. Hiyo Dola ya Madina ndio lilkuwa chombo cha kimaada cha Utawala wa Mbinguni wa mwanzo na wa mwisho Duniani. Allah (s.w.t.) alimfanya mja Wake, Ali ibn Abi Talib, kuwa chombo ambacho kupitia hicho Aliuweka ule Utawala katika dunia hii.

Wakati Muhammad alipokuwa ametoka nje ya mzingo wa nyumba yake, alikwenda kwenye nyumba ya Abu Bakr, na akamwambia kwamba Allah (s.w.t.) amemuamuru kuon-doka Makka usiku uleule. Kwa vile hawakuwa na muda wa kusita, waliuondoka mji mara moja, na wakaenda kwenye pango linaloitwa Thaur Kusini ya Makka. Walilifikia pango hilo na wakaingia kukiwa bado kuna giza.

Walikuwa wamejificha ndani ya pango hilo wakati, masaa machache baadae, wale wauaji walipotokea pia katika ufukuzaji wao. Kwa mujibu wa Hadith, buibui alitanda utando kwenye mlango wa pango, na ndege alitaga yai hapo mlangoni. Wale wauaji walihoji kwamba kama mtu yeyote angeingia ndani ya pango, ule utando na yai vingevunjika, laki-ni kwa vile vyote ni vizima, hakuna aliyeingia humo. Hivyo kwa kuridhika kwamba wale watoro hawakuwa ndani ya pango lile, waliacha msako wao na wakarudi Makka.

Wakati wale wauaji wakiwa wanajadili ile hoja ya kama waingie au wasiingie kule pango-ni kuwakamata hao watoro ambao wanaweza kuwa wamejificha ndani yake, Abu Bakr alishikwa na hofu, na akamwambia Mtume: "Sisi tupo wawili tu na maadui zetu ni wengi sana. Tuna nafasi gani ya kuokoa maisha yetu kama wataingia hapa pangoni?" Mtume (s.a.w.) akasema: "Hapana. Hatupo wawili. Yupo Wa Tatu pamoja nasi, naye ni Allah (s.w.t.)" Tukio hili limetajwa ndani ya Qur'an Tukufu kama ifuatavyo:

Usahihi-7.jpg

"Na Allah ali mnu suru Mtume Wake walipomtoa waliokufuru. Na walipokuwa pangoni, alimwambia sahibu yake: "usihuzunike. Hakika Allah yuko pamoja nasi." Na Allah akamteremshia utulivu juu yake (Mtume)." (Sura ya 9; Ay a ya 40)

Mtume (s.a.w.) pamoja na Abu Bakr walikaa kwa siku tatu ndani ya pango hilo. Huko Makka, kwa wakati huu, shauku ya kumkamata Mtume (s.a.w.) imepungua. Katika siku ya

109

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

nne, Abdullah, mtoto wa Abu Bakr, alikuja na ngamia wawili kwa ajili ya kupanda wao. Abu Bakr alimtoa mmoja wa ngamia hao kwa Mtume (s.a.w.) lakini akakataa kumpokea kama zawadi, na akalipa bei yake kabla ya kumpanda. Yeye na Abu Bakr ndipo wakapan-da ngamia hawa, na wakiiambaa Makka kuelekea kaskazini na Mashariki, walisafiri kuelekea Yathrib upande wa kaskazini.

Muhammad ibn Ishaq:

"Pale Abu Bakr alipoleta wale ngamia wawili kwa Mtume, alimtoa yule mbora zaidi kwake na akamuomba ampande. Lakini Mtume (s.a.w.) alikataa kumpanda mnyama ambae hakuwa wake binafsi, na wakati Abu Bakr alipotaka kumpa ngamia huyo, ali-taka kujua alichokuwa amelipa kumnunua, na akamnunua kutoka kwake."

(Life of the Messenger of God)

Wasafiri hawa wawili wakatembea umbali kati ya Makka na Yathrib kwa siku tisa, na siku ya kumi wakafika Quba, mahali palipo maili mbili Kusini ya Yathrib ambapo walikaa kati-ka nyumba ya Kulthum bin Hind, kama wageni wake. Mtume (s.a.w.) aliamua kusubiri kuwasili kwa Ali kutoka Makka kabla ya kuingia Yathrib. Katika wakati huo, alijenga msingi wa Msikiti hapo Quba. Lilikuwa ni jengo lisilokamilika ambalo kwisha kwake kunasemekana kulichukua siku kumi na nne.

Mtume wa Allah (s.a.w.) alifika Quba siku ya Jumatatu. Siku ya Alhamisi Ali naye akawasili. Alikuwa amekwisha rudisha fedha na vito, nyaraka na vitu vingine vya thamani vya watu wa Makka kwao wenyewe. Bwana wake alifurahi sana kumuona yeye, na akamshukuru Allah (s.w.t.) Ambaye alimtoa salama kwenye mji wa Makka.

Muhammad ibn Ishaq:

"Ali alibakia Makka kwa siku tatu, usiku na mchana mpaka akawa amerudisha zile amana ambazo Mtume (s.a.w.) alikuwa amezishikilia. Hili lilipokwisha kutendeka, alijiunga na Mtume, na akakaa naye katika nyumba ya Kulthum."

(The Life of the Messenger of God)

S. Margoliouth:

"Siku ya Jumatatu tarehe 8 ya mwezi wa Rabi ul Awwal wa mwaka wa 1 H.A., kulin-gana na Septemba 20 ya mwaka 622 A.D, Mtume (s.a.w.) alifika Quba, hivi sasa ikiwa ni mahali pakubwa kwa bustani na miti ya matunda. Ukarimu ulitolewa na mfuasi mmoja mtu mzima, Kulthum ibn Hind, jina la ambaye "mafanikio" ya utumwa wake yalielekea kwa Mtume (s.a.w.) kuwa ya ishara njema (Isabah, iii, 1138). Ulikubalika, ingawa kwa mapokezi ya wageni nyumba ya mfuasi mwingine ilionekana kuwa yenye kufaa zaidi. Hapo Quba, Mtume (s.a.w.) aliamua kubaki

110

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mpaka Ali atakapojiunga naye ambapo ilitokea siku ya Alhamisi; pamoja naye alikuwepo Suhaib ibn Sinan, ambaye alilazimishwa kukabidhi akiba zake kwa Maquraishi. Siku ya Ijumaa, Mtume (s.a.w.) alisafiri kutoka Quba kuelekea Yathrib, na anasemekana alifanya ibada ndani ya Wadi Ra'unah.

(Muhammad and the Rise of Islam, London, 1931)

Njia ilikuwa imejipanga kundi kubwa lenye furaha la watu wa Yathrib waliokuwa wamevaa mavazi yao ya sikukuu. Wanawake na watoto walikuwa wakiimba nyimbo za makaribisho kutoka kwenye mapaa ya nyumba zao. Yalikuwa ni mandhari ambayo ni vigu-mu sana kuweza kuwa yamebuniwa katika njozi. Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) lazima awe alivutiwa sana na mapokezi ya namna ile.

Kila mkazi (wa Kiarabu) wa Yathrib alikuwa na shauku ya kuwa mwenyeji wa Mtume wa Uislamu ambaye alikuwa anaingia mjini kwake kama mgeni. Lakini kwa kutokutaka kumkatisha tamaa hata yule mkazi mnyonge zaidi, alishusha hatamu za yule ngamia-jike, na akatangaza kwamba angekaa popote pale atakaposimama. Yule ngamia-jike akatembea polepole kupita nyumba nyingi, na kisha akasimama mbele ya nyumba ya Abu Ayyub, baadae akawa ndiye mwenyeji mwenye fahari wa Mtume wa Allah (s.a.w.), Abu Ayyub alikuwa mwenyeji maarufu wa Yathrib, na alitokana na ukoo wa Bani Najjar. Wote Amina, mama yake Mtume, na mama wa babu yake, Abdul Muttalib, walitokana na ukoo huu.

111

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mwaka wa Kwanza wa Hijiria

Kulingana na uchunguzi wa marehemu Mahmud Pasha al-Falaki wa Misri, siku ambapo Muhammad Mustafa, Mjumbe wa Allah (s.a.w.) , aliyofika Quba ilikuwa ni Jumatatu, tare-he 8 ya mwezi wa Rabi ul Awwal wa mwaka wa 13 wa Tangazo la Utume, tarehe ambayo inafikiana na tarehe 20, Septemba 622 A.D.

Katika Ijumaa iliyofuata, 12 Rabi ul Awwal (Septemba, 24), Mtume wa Allah (s.a.w.) aliondoka Quba, na akaingia Yathrib. Alifikia kwenye nyumba ya Abu Ayyub, kama ilivy-oelezwa tayari.

Ujenzi wa Msikiti hapo Yathrib

Tendo la kwanza la Muhammad Mustafa, Allah (s.w.t.) ampe amani yeye na Ahlu-Bait wake, wakati alipofika Yathrib, lilikuwa ni kujenga Msikiti wa kumuabudia Allah (s.w.t.) ndani yake. Mbele ya nyumba ya Abu Ayyub palikuwa na eneo la wazi mali ya mAyatima wawili. Mtume (s.a.w.) aliwaita wao na walezi wao, na akawaambia kwamba alikuwa anataka kununua ardhi ile. Wakamwambia kwamba wangefurahi sana kuifanya ardhi ile zawadi kwake. Lakini alikataa kuipokea kama zawadi, na akasisitiza kuilipia kwa bei yake. Hatimae walikubali kupokea malipo kwa ajili ya ardhi yao. Malipo yakafanywa na uchim-baji wa kiwanja ukaanza mara moja.

Akielezea sababu kwa nini Mtume (s.a.w.) hakuipokea ile ardhi kama zawadi, M. Abul Kalam Azad anasema katika kitabu chake, Rasul-e- Rahmat (Mtume wa Rehma), (Lahore, Pakistan, 1970):

Mtukufu Mtume (s.a.w.) hakutaka kuchukua wajibu wa mtu yeyote. Ni nani anayeweza kudai kuwa muaminifu zaidi kwake kuliko Abu Bakr? Na yeye mwenyewe alisema kwamba anamshukuru sana Abu Bakr kwa msaada wake wa utu na mali kuliko mtu mwingine yeyote. Na tena, pale Abu Bakr alipotaka kumpa zawadi ya ngamia kwenye usiku wa kuon-doka Makka kwenda Yathrib, yeye hakuikubali mpaka alipokuwa amemlipa Abu Bakr bei yake. Vivyo hivyo, huko Yathrib, alipotaka kununua ardhi kwa ajili ya kujenga Msikiti juu yake, wamiliki wake waliitoa kwake kama zawadi. Lakini alikataa kuipokea kama zawadi. Ardhi hiyo ilichukuliwa tu pale wamiliki wake walipokubali kupokea bei yake kutoka kwake ambayo aliilipa.

Huu Msikiti wa Yathrib ulikuwa ndio bora sana katika urahisi wa dhana na usanii muun-do. Vifaa vilivyotumika katika ujenzi wake vilikuwa ni matofali yasiyochomwa na mota kwa ajili ya kuta, na makuti ya mtende yaliyozuiliwa na magongo ya minazi. Shubaka la

112

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Msikiti huo lilielekea upande wa Jerusalem upande wa kaskazini. Kila moja kati ya pande zile nyingine tatu ulitobolewa na lango. Sakafu ya Msikiti haikuwa na matandiko hapo mwanzoni, hata angalau mikeka iliyochakaa. Vibanda viwili pia vilijengwa kwenye ukuta wa nje, kimoja cha Sauda binti ya Zama'a; na kingine kwa ajili ya Aishah, binti ya Abu Bakr, wale wakeze wawili Mtume (s.a.w.) kwa wakati huo.

Vibanda vipya vilijengwa kwa ajili ya wake wapya kama walivyoingia katika miaka ya baadae. Ilikuwa ni mara ya kwanza ambapo Waislamu walifanya kazi kama timu moja katika mradi wa jamii. Katika miaka iliyofuatia, timu hii ilikuwa ijenge jengo kubwa la Kiislam.

Kwa kuhamasishwa na kuwepo kwa Mtume wa Allah (s.a.w.), kila mmoja wa Masahaba alikuwa anachuana ili kuwashinda wengine. Miongoni mwa Masahaba hao alikuwa ni Ammar ibn Yasir, ambaye, kwa mujibu wa Ibn Ishaq, alikuwa ndiye mtu wa kwanza katika Uislamu kujenga Msikiti. Ibn Ishaq hakutaja bayana ni Msikiti upi ambao Ammar ali-jenga. Lakini Dr. Taha Husain wa Misri anasema kwamba Ammar alijenga Msikiti huko Makka kwenyewe na aliswali ndani yake, nyuma kabisa kabla hajahamia Yathrib.

Wakati Msikiti ulipokuwa unajengwa, lilitokea tukio ambalo Ibn Ishaq ameliandika kama ifuatavyo:

"Ammar b. Yasir aliingia ndani wakati wakiwa wamemzidishia mzigo wa matofali, akisema, "Wananiua. Wananitwisha mimi mizigo wasiyoweza kuibeba wao wenyewe." Ummu Salma, mkewe Mtume (s.a.w.) akasema: "Nilimuona Mtume (s.a.w.) akipitisha mkono wake kwenye nywele zake (Ammar) - kwani alikuwa ni mwenye nywele zenye mawimbi - na akasema, "Wapi, ibn Sumayya! Sio hao watakaokuua wewe, bali ni kundi la watu waovu."

(Ubashiri huu unasemekana ulikuja kutimizwa wakati Ammar alipouawa huko Siffin - Suhayli, ii, uk. 3)

Ali alitunga shairi la rajaza siku hiyo (Msikiti ulipokuwa unajengwa):

Yupo mmoja anayejitahidi usiku na mchana Kutujengea sisi Msikiti wa tofali na ufinyanzi Na mtu anayekimbia mavumbi mbali.

Ammar alilikariri na kuanza kulighani.

Alipolishikilia sana, mmoja wa Masahaba wa Mtume (s.a.w.) alidhani ni yeye aliyeleng-wa ndani yake, kwa mujibu wa kile Ziyad b. Abdullah el-Bakkai alivyoniambia mimi kutoka kwa Ibn Ishaq. Huyu wa baadae (ibn Ishaq) kwa kweli alimtaja mtu mwenyewe.

113

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Alisema: "Nimesikia ulichokuwa ukisema kwa muda mrefu, Ewe Ibn Sumayya, na Wallahi nafikiri, nitakupiga kwenye pua!" Sasa alikuwa na fimbo mkononi mwake, na Mtume (s.a.w.) alikasirika sana na akasema: "Kuna nini kati yao na Ammar? Anawakaribisha wao Peponi ambapo wao wanamkaribisha motoni. Ammar ana thamani kwangu kama uso wangu mwenyewe. Kama mtu atakuwa na tabia namna hii hatasamehewa, hivyo muepuke."

Sufyan b. Uyana ametaja kutoka kwa Zakariya kutoka kwa al-Shabi kwamba mtu wa kwanza kujenga Msikiti alikuwa ni Ammar bin Yasir.

(Suhayli anasema: Ibn Ishaq alimtaja mtu huyo, lakini Ibn Hisham alipendelea asi-fanye hivyo, kama kutomtaja mmoja wa maswahaba wa Mtume (s.a.w.) katika mazin-gira yanayoaibisha. Kwa hiyo haitakuwa haki kamwe kutafuta kumjua. Abu Dharr anasema: Ibn Ishaq alimtaja mtu huyo na akasema,: "Mtu huyu alikuwa ni Uthman b. Affan." Wahariri wa Cairo wanasema kwamba katika ile Mawahib al-Laduniya, al-Qastalani, (kafa A.D. 1517), amesema kwamba mtu huyo anasemekana kuwa alikuwa ni Uthman b. Mazun. Huyu mwandishi wa mwisho anaweza kupuuzwa kwa usalama katika nukta hii.)"

Katika eneo la ujenzi wa Msikiti huo, mtu anaweza kushuhudia vituko vyenye kuumiza sana katika Hadith ya siku za mwanzo za Uislamu - Muhammad Mustafa, Mjumbe wa Allah (s.a.w.) akiondoa vumbi, kwa mikono yake mwenyewe, kutoka kwenye kichwa na uso wa Ammar ibn Yasir. Hakumpendelea sahaba mwingine yoyote kwa dalili za mguso, upendo na huruma.

Wakati Mtume wa Allah (s.a.w.) alipowalaumu maswahaba zake kwa kumwingilia Ammar, na akasema kwamba yeye (Ammar) alikuwa anawakaribisha peponi ambapo wao walikuwa wanamkaribisha motoni, yeye (Mtume) alikuwa, yumkini kabisa, anafasiri ile Aya ya 41 ya Sura ya 40 (Sura-tul-Mu'min) iliyoko ndani ya Qur'an ambayo inasomeka kama ifuatavyo:

"Na enyi watu wangu! Kwa nini mimi nakuiteni kwenye uokovu, nanyi mnaniita kwenye moto?"

Akitoa maelezo juu ya Aya hii, Abdullah Yusuf Ali, yule mfasiri wa Qur'an Tukufu anasema:

"Inaweza kuonekana ni ajabu kwa mujibu wa sheria za dunia hii kwamba angekuwa anawatafutia wao wema, ambapo wao wanamtafutia maangamio yake; lakini huo ni upeo wa Imani."

114

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Yule sahaba aliyezozana na Ammar ibn Yasir wakati Msikiti wa Yathrib ulipokuwa unaj engwa, hakuwa mwingine zaidi ya Uthman bin Affan, mmoja wa makhalifa wa baadae wa Waislamu. Alichukizwa na kufanya kazi kwenye vumbi na matope, na kufanya nguo zake kuingia tope. Wakati Mtume wa Allah (s.w.t.) alipomuonyesha kutoridhika kwake, ilibidi anyamaze kimya lakini tukio hilo lilimkereketa moyoni mwake, na hakulisahau kamwe. Miaka mingi baadae alipokuwa khalifa, na kuwa na mamlaka mikononi mwake, aliwaamuru watumwa wake kumuangusha chini Ammar ibn Yasir na kumpiga - mtu ambaye alikuwa na thamani kwa Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.w.t.) kama uso wake (Mtume) mwenyewe.

Madai kwamba hakuwa Uthman bin Affan bali alikuwa ni Uthman bin Mazun au mtu mwingine yoyote yule, ambaye, kwa kumtisha Ammar ibn Yasir, aliamsha hasira za Mtume wa Allah (s.w.t.), ni jaribio tu la kujionyesha kwa wanahistoria "wanaojipen-dekeza" wa nyakati zilizofuata baadae.

Kwa wakati huu, Ammar ibn Yasir tayari alikwishapata sifa bora nne ambazo lazima ziwe zimemfanya yeye kuwa husuda wa maswahaba wengine wote wa Muhammad, Mjumbe wa Allah (s.a.w.). Sifa hizo zilikuwa ni:

1.  Alitokana na familia ya kwanza ya Kiislam.

2.  Alikuwa mtoto wa Mashahidi wa Kwanza na wa Pili wa Uislamu. Mama yake, Sumayya, alikuwa wa kwanza, na baba yake, Yasir, alikuwa shahidi wa pili katika Uislamu. Ilikuwa ni heshima ambayo haikupatwa na sahaba mwingine yoyote wa Muhammad Mustafa.

3.   Alikuwa ndio mjenzi wa Msikiti wa kwanza.

4.   Alikuwa ni kipenzi cha Muhammad Mustafa, Mjumbe wa Allah (s.a.w.) . Allah (s.w.t.) awape rehemu Ammar ibn Yasir na wazazi wake.

Adhana na Swala

Ilikuwa ni amri kwa Waislamu kuswali mara tano kwa siku. Walipaswa kusimamisha shughuli za kazi zao za siku, na kutekeleza wajibu huu. Lakini hapakuwa na njia ya kuwatahadharisha kwamba wakati umefika kwa ajili ya kuswali.

Kwa mujibu wa Hadith za Sunni, sahaba mmoja alimshauri Mtume (s.a.w.) kwamba lingepulizwa tarumbeta au kengele ingegongwa kuwatahadharisha Waislamu kabla ya wakati wa kila Swala. Mtume (s.a.w.) hakukubali ushauri huu, kama alivyosema kwamba hakutaka kuchukua desturi za Kiyahudi au Kikristo.

115

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abdillah bin Ziyad alikuwa mwenyeji wa Yathrib. Alikuja kumuona Mtume, na akasema kwamba alipokuwa nusu-macho au nusu-usingizini, mtu alitokea mbele yake na kumwambia kwamba sauti ya mwanadamu ingetumika kuwaita waumini kwenye Swala; na pia alimfundisha hiyo Adhana (mwito wa Swala), na namna ya kuisoma.

Wanahistoria wa Sunni wanasema kwamba wazo hilo lilikubalika kwa Mtume, na akalichukua papo hapo. Yeye ndipo akamwita Bilal, akamfundisha jinsi ya kuwaita Waislamu kwenye Swala; na akamchagua kuwa Muadhini wa kwanza wa Uislamu.

Hadithi hizi hazifuatwi na Waislamu wa Shia. Wao wanasema kwamba kama vile Qur'an Tukufu ilivyoshushwa kwa Muhammad Mustafa, na Adhana ilikuwa vivyo hivyo.

Wanatetea kwa dhati kwamba ile namna ya kuwaita waumini kwenye Swala haingeweza kuachwa kwenye ndoto au ruya za Mwarabu fulani. Wanaendelea kusema kwamba kama Mtume (s.a.w.) ameweza kuwafundisha Waislamu jinsi ya kuchukua udhuu, na ni vipi, lini na nini cha kusema katika kila Swala, angeweza pia kuwafundisha jinsi na wakati gani wa kuwatahadharisha wengine kabla ya wakati wa kila Swala.

Kwa muj ibu wa Hadith za Shia, yule Malaika aliyemfundisha Mtume wa Allah (s .w.t.) j insi ya kuchukua udhuu kujiandaa kwa Swala, na jinsi ya kuswali, pia alimfundisha namna ya kuwaita wengine kwenye Swala.

Yathrib yawa Madina

Hili jina "Yathrib" mara likawa halifai. Watu wakaanza kuuita mji huo "Madina-tun-Nabi," - Mji wa Mtume. Kiasi muda ulivyopita, matumizi yakafanya ufupisho wa jina hili utwaliwe kirahisi kama "Madina" - "Mji," na hivyo ndivyo jina la mji wa Mtume wa Uislamu lilivyobakia tangu hapo.

Makundi ndani ya Madina

Wakati Mtume (s.a.w.) na wale wahamiaji kutoka Makka walipofika Yathrib (sasa Madina), waliyakuta makabila matatu ya Kiyahudi, yaani, Quainuqa, Nadhir na Quraydha, na makabila mawili ya Kiarabu, yaani, Aus na Khazraj, yakiishi kwenye mji huo.

E.A.Belyaev:

"Idadi ya watu wa asili ya Madina ilijumlisha makabila yake matatu ya Kiyahudi, Quainuqa, Qurayza na Nadhir; na ya makabila mawili ya Kiarabu, Aus na Khazraj.

(Arabs, Islam and the Arab Caliphate in the Early Middle Ages. 1969)

116

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hao Wayahudi walikuwa wakulima, wachuuzi, wafanyabiashara, wakopesha-fedha, wami-liki-ardhi na wenye viwanda. Wamekuwa matajiri kupitia matumizi ya riba na walitawala ukiritimba wa viwanda vya zana za vita katika Arabia.

Haya makabila mawili ya Kiarabu ya Madina, Aus na Khazraj, yaliishi kwa kilimo. Kabla ya kuwasili kwa Mtume, walikuwa wamefungana kwenye vita dhidi yao wenyewe vilivy-odumu kwa zaidi ya vizazi vitano. Walipigana vita vyao vya mwisho miaka minne tu iliy-opita, yaani, mnamo 618 A.D., na iliwaacha wachovu sana na walegevu.

Walikuwepo pia Wakristo wachache wanaoishi Madina. Hawakukubaliana na Mtume wa Uislamu kwa sababu aliikana ile imani ya Utatu, na akahubiri Tawhiid ya Muumba.

Kundi la nne ndani ya Madina lilikuwa lichomoze baadae kidogo, likiundwa na "wanafi-ki" au "waliokosa imani." Wakati wa ujumbe wa Mtume (s.a.w.) huko Makka, walikuwepo Waislamu wengi ambao walikuwa wafiche imani yao ya kweli kwa kuhofia mateso. Hapo Madina, hali iligeuka. Watu hawa (wanafiki) walikuwa Waislamu jina; usoni wali-tangaza Uislamu lakini hawakuwa wakweli. Walikuwa chanzo cha nguvu isiyodhihirika ya uchochezi, hujuma na uasi.

Mkataba au Katiba ya Madina

Raia wa Yathrib walimtambua Muhammad kama mtawala wao, na akawapa "Mkataba wa Uraia" ambao unaaminika kuwa ndio waraka wa kwanza ulioandikwa katika Uislamu (mbali na Qur'an). Mkataba wa asili kama ulivyohifadhiwa na Ibn Ishaq, una masharti arobaini na saba (47). Yafuatavyo ni yale ambayo ni muhimu zaidi kati ya hayo:

*   Migogoro yote kati ya pande zozote mbili ndani ya Yathrib itapelekwa kwa Muhammad kwa uamuzi wake juu yake.

*  Waislamu na Wayahudi watakuwa na haki sawa.

*    Kila kundi ndani ya Yathrib litafuata imani yao, na hakuna kundi lolote litakaloingilia katika mambo ya kundi jingine lolote.

*    Katika tukio la shambulio lolote la nje juu ya Yathrib, makundi yote, yaani, Waislamu na Wayahudi, yataulinda mji.

*    Makundi yote yatajiepusha na kumwaga damu ndani ya mji.

*   Waislamu hawatakwenda vitani dhidi ya Waislamu wengine kwa faida ya wasiokuwa Waislamu.

117

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

R.V.C. Bodley:

"Muhammad alitengeneza mkataba na Wayahudi ambamo, miongoni mwa mambo mengine, iliainishwa kwamba Wayahudi na Waislamu wasaidiane pamoja katika mambo yote yanayohusu mji huo. Walikuwa wawe washirika dhidi ya maadui wote wa kawaida, na hili bila ya wajibu wa pande mbili kwa Uislamu au Uyahudi. Sharti muhimu la mkataba huu linasomeka kama ifuatavyo: Wayahudi wanaojiunga wenyewe kwenye umoja wetu watakuwa na haki sawa na watu wetu wenyewe kwenye msaada wetu na madaraka yetu mazuri. Wale Wayahudi wa matawi tofauti wanaoishi Yathrib wataunda pamoja na Waislamu dola moja ya pamoja. Watafuata dini yao kwa uhuru kama Waislamu. Watumishi na washirika wa Wayahudi watanu-faika kwa usalama na uhuru huo huo.

(The Messenger, the Life of Muhammad, New York, 1946)

Muhajirina na Ansari

Muhammad alibadili majina ya makundi yale mawili ya Waislamu ambao sasa walikuwa wanaishi Madina. Aliwaita wale wakimbizi kutoka Makka "Muhajirin" (Wahamiaji); na akawaita wale wenyeji wa Yathrib ambao waliwakaribisha wao, "Ansar" (Wasaidizi). Makundi haya mawili yalijulikana kwa majina haya daima baadae.

Hali ya kiuchumi hapo Madina

Utajiri wa Madina ulikuwa karibu wote umekusanyika katika mikono ya Mayahudi. Hao Waarabu (sasa Ma-ansari) waliishi kwenye umasikini na dhiki ya kudumu. Sababu moja ya kwa nini walikuwa masikini sugu, ilikuwa ni viwango vikubwa vya riba walivyokuwa wakilipa kwa Mayahudi kwenye mikopo yao.

D.S. Margoliouth:

"Ingawa tunasikia majina ya mmoja au wawili wa matajiri wa Yathrib, wengi wao wanaonekana walikuwa masikini. Hapo Yathrib wakati wa Mtume, kulikuwa na vazi moja tu la harusi; mapambo yalikuwa yakiazimwa kutoka kwa Wayahudi. Umasikini huu ulikuwa hasa ukikuzwa na ukopeshaji-pesa wa Kiyahudi."

(Muhammad and the Rise of Islam, Londln, 1931)

Lakini kama Maansari walikuwa masikini, Muhajirin walikuwa masikini zaidi. Katika kukimbia kutoka Makka, waliacha kila kitu walichokuwa wakikimiliki, na walipokuja Yathrib kutafuta hifadhi, walikuwa hawana kitu. Kwa kifupi, hali yao iligeuka kuwa ya

118

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kukatisha tamaa. Walikuwa wafanye kitu ili wapate kuishi. Lakini kwa vile hawakujua kitu kuhusu kilimo, cha maana walichoweza kufanya kilikuwa ni kufanya kazi kama vibarua wasio na ujuzi katika mashamba na bustani za Wayahudi na Ansari.

D.S. Margoliouth:

"Ilikuwa mwanzoni imepangwa kuwa wale Wakimbizi wawasaidie Wasaidizi (Ansar) katika kazi zao za nje; lakini kwa kutokujua chochote cha utunzaji wa mitende, wali-weza tu kufanya zile kazi za kitumishi zaidi; hivyo wengine hasa walikata kuni na kuchota maji; wengine waliajiriwa kwenye kunywesha mitende, wakibeba mifuko ya ngozi migongoni mwao; na Ali, angalau wakati mmoja, alipokea tende kumi na sita kwa kujaza ndoo na maji, na kuzimwaga juu ya udongo kwa ajili ya kutengeneza matofali kwa kiwango cha tende moja kwa ndoo moja; ambacho kwa shida kilimpa-tia mlo aliokula pamoja na Mtume."

(Muhammad and the Rise of Islam, London, 1931)

Kuwafungamanisha Muhajirina kwenye maisha ya kiuchumi ya Madina, lilikuwa ni tatizo gumu sana, na lilielemea ubunifu wote wa Mtume. Hakutaka mtu yoyote wa jamii ya Kiislamu, sana sana wale Muhajirina, awe mzigo kwa mtu mwingine yeyote, na alifanya kila lile aliloweza kufanya kupunguza utegemezi wao juu ya Ansari.

Udugu wa Muhajirina na Ansari

Moja ya shughuli za mwanzo za Mtume (s.a.w.) za kuwajenga upya wale Muhajirina wasio na makazi pale Madina, na kuwafungamanisha katika maisha ya kiuchumi na kijamii ya mji huo, ilikuwa ni kuwafanya wawe "ndugu" wa Ansari. Miezi michache baada ya kuwasili kwake hapo Madina, aliwaambia Muhajirina na Ansari kwamba walipaswa kuishi kama "ndugu" wa kila mmoja wao, na akawaunganisha wawili wawili kama ifuatavyo:

Muhajir                                  ndugu ya                                 Ansari

Ammar ibn Yasir                            "                                     Hudhayfa al-Yamani

Abu Bakr Siddiq                             "                                     Kharja bin Zayd

Umar bin Khattab                           "                                     Utba bin Malik

Uthman bin Affan                           "                                     Aus bin Thabit

Abu Dharr al-Ghiffari                     "                                     Al-Mundhir b. Amr

Mas'ab ibn Umayr                          "                                     Abu Ayyub

Abu Ubaidah Aamer al-Jarrah          "                                     Saad ibn Maadh

Zubayr ibn al-Awwam                     "                                     Salama bin Waqsh

Abdul Rahman bin Auf                   "                                     Saad ibn Rabi

Talha ibn Ubaidullah                       "                                     Ka'ab ibn Malik

119

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali ibn Abi Talib pekee ndiye aliyeachwa bila ya "ndugu." Alikuwa anastaajabu kwa nini wakati Mtume wa Allah (s.a.w.) alimshikilia mikononi mwake na akamwambia: "Wewe ni ndugu yangu katika dunia hii na katika akhera."

Muhammad ibn Ishaq:

"Mtume (s.a.w.) mwenyewe alimshika Ali mkononi na kusema: "Huyu ni ndugu yangu." Hivyo Mtume wa Allah (s.a.w.) Bwana wa waliotumwa, na kiongozi wa Wacha-Mungu, Mtume wa Mola wa mbingu na ardhi, asiye na mshirika wala asiyelingana na yoyote, na Ali ibn Abi Talib wakawa ndugu."

(The Life of the Messenger of God) Edward Gibbon:

"Baada ya safari ya hatari na ya haraka kandoni mwa mwambao wa bahari, Muhammad alisimama hapo Kuba, maili mbili kutoka mjini, na akafanya kuingia kwake kwa uwazi ndani ya Madina siku kumi na sita baada ya kukimbia kwake toka Makka. Wafuasi wake shupavu sana walikusanyika kumzunguka yeye; na walio sawa, ingawa sifa mbali mbali za Waislamu zilitambulikana kwa majina ya Muhajirina na Ansari, wakimbizi wa Makka na wasaidizi wa Madina.

Kufutilia mbali mbegu za wivu, Muhammad kwa hekima na busara akawaunganisha wawili wawili wale wafuasi wake wakuu kwa haki na wajibu wa udugu; ambapo Ali alijikuta binafsi bila mwenza, na Mtume (s.a.w.) kwa upendo mwingi akatamka kwamba yeye atakuwa sahiba na ndugu wa yule kijana mtukufu.

.(The Decline and Fall of the Roman Empire) Muhammad Husein Haykal:

"Wazo la kwanza kumjia yeye (Muhammad) lilikuwa lile la kupanga upya safu za Waislamu ili kuunganisha umoja wao na kufuta kila uwezekano wa kuibuka tena kwa mgawanyiko na uhasama. Kwa kulitambua lengo hili, aliwataka Waislamu kusuhu-biana wao kwa wao kwa ajili ya Allah (s.w.t.) na kujifunga wenyewe wawili wawili. Alieleza jinsi yeye na Ali ibn Abi Talib walivyokuwa ndugu..."

(The Life of Muhammad, 1935)

Muhammad, Allah (s.w.t.) ampe rehma na Ahlul-Bait wake, aliwafanya Muhajirina na Ansari kuwa "ndugu" wa kila mmoja wao. Lakini Ali, kama yeye mwenyewe, alikuwa Muhajir (mhamiaji), na bado yeye (Muhammad) alimchagua yeye kuwa ndugu yake. Kwa kufanya hivyo, alikuwa akibainisha kile cheo cha kipekee na hadhi maalum ya Ali katika

120

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Uislamu. Ali, ingawa bado kijana, tayari alikuwa amemzidi kwa cheo kila mtu katika kutu-mikia Uislamu bidii ya wajibu kwa Allah (s.w.t.) na Mtume Wake. Alikipata cheo hiki kikubwa kwa kutumia uwezo wake na tabia.

Hii haikuwa, hata hivyo, mara ya kwanza ambapo Mtume wa Allah (s.a.w.) alimtangaza Ali kuwa ndugu yake. Mapema, wakati akiwa bado yuko Makka, aliwafanya maswahaba zake wakuu kuwa "ndugu" wa kila mmoja. Jozi hizo za "udugu" zilikuwa za Abu Bakr na Umar; Uthman bin Affan na Abdur Rahman bin Auf; Talha na Zubair; Hamza na Zayd bin Haritha; na Muhammad Mustafa ibn Abdullah na Ali ibn Abi Talib.

Imam Nuurdin Ali ibn Ibrahim al-Shafi'i amemnukuu Mtume wa Allah (s.a.w.) katika kitabu chake Siirat Halabia (juz. 2, uk.120) alisema: "Ali ni ndugu yangu katika dunia hii na vile vile katika dunia ya Akhera."

Makadirio ya wajibu wa Muhajirina na wa Ansari

Hawa Muhajirina walikwisha poteza mali walizokuwa nazo huko Makka, na wote waliin-gia Madina wakiwa mikono mitupu. Walitokana na vikundi vya wilaya mbili. Kikundi kimoja kilikuwa ni cha wale watu waliokuwa wachuuzi na wafanyabiashara kitaaluma, na walikuwa matajiri sana. Walipokwenda Madina, waliingia kwenye biashara, wakafanikiwa kwayo, na wakawa matajiri tena.

Kundi jingine lilitokana na "watawa" wa Kiislam. Walikuwa masikini huko Makka, na walipohamia Madina, bado walichagua kuwa masikini. Walibeua utajiri wa kidunia, na hawakuchukua mamlaka ya kiuchumi mikononi mwao wakati wowote ule.Wawakilishi wa kundi hili walikuwa watu kama Abu Dharr al-Ghiffari; Ammar ibn Yasir na Miqdad ibn al-Aswad. Allah (s.w.t.) aliwasifia katika Kitabu Chake kama ifuatavyo:

Usahihi-8.jpg

"(Sehemu yake) wapewe mafakiri Muhajirina waliotolewa majumbani mwao na mali yao kwa ajili ya kutafuta fadhila kutoka kwa Allah na radhi zake, na wanamsaidia Allah na Mtume Wake. Hao kwa hakika ndio wakweli." (Sura ya 59 Aya ya 8)

Maansari waliwafanyia wema mhajirina kutoka Makka kuliko vile ndugu za hawa Muhajir wenyewe ambavyo wangeweza kuwafanyia. Waliwaweka katika nyumba zao wenyewe, wakawapa vifaa vya matumizi ya nyumbani; wakawafanya washirika katika kilimo, au wakawapa nusu ya ardhi yao. Wale Ansari waliokuwa kwenye biashara, wakawafanya

121

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hawa Muhajir washirika katika biashara. Historia haiwezi kuonyesha ukarimu unaolingana na wa hawa Ansari. Walikuwa ni "wenyeji" sio tu kwa wale Muhajirina wasiokuwa na makazi na mafukara peke yake bali pia na kwa Uislamu wenyewe, uliong'olewa Makka, ukaota mizizi mipya hapo Madina, ukachipua na mara ukawa na uwezo.

Hawa Ansari walikuwa wa lazima kwa ajili ya kudumu kihakika kwa Uislamu. Wapi ungekuwa Uislamu uwe, na wapi wangekuwepo Muhajirina kama Ansari wasingewapa hifadhi? Wakati uhasama na waabudu masanamu ulipoanza, walikuwa ni Ansari, na wala sio Muhajirina, waliochukua sehemu kubwa ya mapigano. Bila ya msaada mkubwa na imara ambao waliutoa kwa Mtume, vile vita vya Waislamu visingepiganwa, mbali na ushindi uliopatikana. Walikuwa pia wapokeaji wa sifa na utambulikanaji wa Mbingnii, kama tunavyosoma kwenye Aya ya Qur'an Tukufu ifuatayo:

Usahihi-9.jpg

"Lakini wale ambao, kabla yao, walikuwa na makazi (huko Madina) na walikuwa wameami-ni, wakaonyesha mapenzi yao kwa wale waliohamia kwao, wala hawaoni choyo vifuani mwao kwa vile walivyopewa (Muhajirina), bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushiwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa." (Sura ya 59; Aya ya 9).

Hawa Muhajirin, mwanzoni, hawakuwa na jinsi ya kuwalipa hao Ansari kwa ukarimu na wema wao. Lakini je waliwahi kutoa shukurani zao? Inaonekana kwamba ukiwaondoa Muhajirin wawili, hakuna aliyeshukuru. Hawa wawili wa kuwaondoa walikuwa ni Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) na Ali, mshika makamu wake. Walikiri deni lao la shukurani kwa Ansari kwa maneno na vitendo pia, na kamwe hawakuipoteza nafasi ya kufanya hivyo. Hata hivyo, wote Muhammad na Ali, kama walezi pekee wa maadili ya Uislamu, walitambua kwamba Uislamu umepata mahali pa usalama hapo Madina pamoja na Ansari. Hawa Ansari kwa hiyo, walishika nafasi maalum katika mioyo yao.

Muhajirin waliobakia, yaani, wale matajiri miongoni mwao, hawakushiriki katika wasi-wasi wa Muhammad na Ali kwa ajili ya Ansari. Wakati madaraka yalipoingia mikononi mwao, waliwasukuma wale Ansari nyuma, na wakawashusha wahusike na dhima ndogo ndogo tu. Mwanzoni, waliwapuuza kabisa Ansari. Lakini kupuuzwa hakukuwa kubaya sana kulinganishwa na kile kilichokuwa kiwafike katika nyakati za baadae.

122

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

(Kati ya kipindi kilichoshughulikiwa na Sira na kuhaririwa kwa kitabu chenyewe inatishia misiba mikubwa miwili ya Karbala, wakati Husein na wafuasi wake walipouawa katika mwaka wa 61 H.A., na kilio cha Madina mnamo mwaka 63 H.A. wakati Ansari kama elfu kumi wakiwemo maswahaba wa Mtume (s.a.w.) wasiopungua themanini walipouawa. Imenukuliwa katika - Introduction to the biography of the Prophet by Ibn Ishaq).

Muhajirin waliwaghilibu watetezi wa wapagani wa Makka - Banu Umayya - juu yao. Banu Umayya walikuwa maadui wakubwa wa Ansari. Kama ukarimu wa Ansari kwa Muhajirin hauna kifani katika historia, utomvu wa shukurani wa hawa Muhajirin kwa wahisani wao pia hauna kifani. Wakati Muhajirina walipokuja Madina, Maansari ndio waliokuwa mabwana wa Madina. Ilikuwa tu ni kwa uungwana wa Ansari kwamba Muhajirin waliweza kuingia na kuishi Madina. Lakini mara tu Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) na rafiki na mlezi wa Ansari, alipokufa, wakakoma kuwa mabwana nyumbani kwao wenyewe. Kifo chake kilikuwa ndio ishara ya mgeuko wa ghafla katika ustawi wao.

123

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Vita vya Kiislamu

Muhammad Mustafa, Mtume Wa Allah (s.a.w.) ilibidi apigane mfululizo wa vita katika kuutetea Uislamu kutoka kwenye makazi yake mapya hapo Madina. Vile vita ambavyo aliongoza jeshi la Kiislam yeye mwenyewe, vinaitwa "Ghaz'wa" na ile misafara ambayo aliyotuma kutoka Madina chini ya amri ya mmojawapo wa maswahaba wake, inaitwa "Sariyya".

Kwa kukisia, Mtume (s.a.w.) alizindua kampeni za kijeshi 80 katika ile miaka kumi tangu kuhama kwake mwaka 622 A.D. mpaka kufa kwake mwaka 632 A.D. Baadhi ya kampeni hizi hazikuwa chochote zaidi ya ujumbe wa upelelezi. Idadi iliyohusika ndani yake ilikuwa ndogo sana, na hasa walichokifanya kilikuwa ni kuangalia mienendo ya koo au kabila fulani. Zingine zilikuwa ni misafara ya ki-tablighi. Nyingine nyingi zilikuwa ni za mik-waruzano midogodogo tu. Bado nyingine zilikuwa ni za udadisi tu kwa sababu ya tukio maalum lililohusiana nazo. Nitatoa maelezo ya juu juu ya kampeni hizo ndogo, na nitawe-ka msisitizo hasa kwenye yale mapambano makubwa ya Uislamu.

Hapo nyuma kabisa kabla ya Uislamu, Wagiriki na Warumi waligundua kwamba vita vinaweza kubadili hatma za mataifa. Miongoni mwa kampeni za Mtume, kuna vita vitano ambavyo vinaweza kusemekana kwamba vimebadili hatma za mataifa. Navyo ni vita vya Badr, Uhud, Khandaq, Khaybar na Hunayn.

Vita hivi vilikuwa haviepukiki. Maquraishi wa Makka waliamini kwamba kama Waarabu wote wataukubali Uislamu, itakuwa na maana kwao (Maquraishi) ya kupoteza mapato yote ya Hijja, na kupotea kwa heshima waliyokuwa nayo kama walezi wa masanamu. Mafanikio ya Uislamu waliyabashiri kwa usawa kabisa kama pigo la kifo cha heshima. Ilikuwa ni hofu hii, hofu ya kupoteza mamlaka ya kiuchumi na kisiasa na hadhi ambayo iliharakisha vita kati yao na Waislamu.

Tangu kule kuhama kwa Waislamu toka Makka, hali ya kivita isiyopingika ilijitokeza kati yao na Maquraishi. Katika siku za mwanzoni hapo Madina, Waislamu hawakuthubutu kusogeza silaha zao wakati wowote. Askari wa doria waliwekwa mjini kote kila usiku kuwatahadharisha wakazi endapo adui atafanya shambulizi la ghafla. Mtume (s.a.w.) hakuweza kulala usiku akihofia mashambulizi wakati wowote. Ilikuwa ni katika mazingi-ra kama Haya ambapo ilikuwa achukue hatua za maksudi kwa ajili ya usalama wa Madina. Kama mkuu wa dola inayoondokea, usalama wa dola hiyo ulikuwa ndio wajibu wake wa kwanza.

124

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kwa manufaa ya usalama, Waislamu iliwabidi kutupia macho nyendo za adui, marafiki zake adui na wasaidizi wao.

Mtume (s.a.w.) alituma msafara wa kwanza mnamo mwezi wa tisa wa mwaka wa kwanza wa Hijiria, chini ya uongozi wa ami yake, Hamza ibn Abdul Muttalib. Muhajirina thelathi-ni walishiriki ndani yake. Makusudio yao yalikuwa ni kuzuia msafara wa kibiashara wa Maquraishi. Lakini kabila moja, lenye urafiki kwa pande zote, likasuluhisha kati yao. Hapakuwa na mapigano, na msafara ule ukarudi Madina.

Katika mwezi uliofuatia, Mtume (s.a.w.) aliwatuma Muhajirina sitini chini ya uongozi wa binamu yake, Ubaida ibn al-Harith, kwenda Raghib, karibu na Red Sea (bahari nyekundu). Walikabiliana na msafara wa Maquraishi. Pande zote mbili zilirushiana mishale michache lakini hapakuwa na majeruhi. Wafanyibiashara wawili wa Makka waliuacha msafara wao, wakaja upande wa Waislamu, wakasilimu, na wakafuatana na msafara ule wakati ulipore-jea Madina.

Ubaida ibn al-Harith anasemekana alirusha mshale kwa adui. Ulikuwa ndio mshale wa kwanza kurushwa kwa ajili ya Uislamu.

Sir William Muir:

"Ubaida anajulikana katika Hadith kama ni yeye ambaye katika tukio hili, "alirusha mshale wa kwanza kwa ajili ya Uislamu."

(The Life of Mohammed, London, 1877)

Hapakuwa na kampeni nyingine za kivita katika muda uliobakia wa mwaka wa kwanza wa Hijiria.

125

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mwaka wa pili wa Hijiria

Msafara wa kwanza ambao Muhammad Mustafa aliuongoza yeye mwenyewe, ulikuwa ni ile Ghaz'wa (kampeni) ya Waddan. Alimteua Saad ibn Ubadah kama gavana wa Madina, na akachukua kikundi cha wafuasi wake kwenda Waddan, kijiji kati ya Madina na Makka. Msafara wa Maquraishi ulielezewa kwamba ulisimama pale. Lakini msafara huo uliondo-ka Waddan kabla ya kuwasili kwa Waislamu. Wao, kwa hiyo, walipumzika kwa siku chache na kisha wakarudi Madina.

Mnamo mwezi wa saba (Rajab) wa mwaka wa pili wa Hijiria, yaani, miezi kumi na tano baada ya kuhamia Makka, Mtume (s.a.w.) alituma watu saba chini ya uongozi wa binamu yake Abdullah ibn Jahash, kwenda Nakhla, oasis iliyoko Kusini, ambako walikuwa wachunguze mienendo ya msafara fulani wa Maquraishi.

Huko Nakhla, Abdullah aliuona msafara mdogo wa Maquraishi uliokuwa ukirejea Makka. Wenye msafara huo walikuwa ni Amr bin al-Hadhrami, Uthman bin Abdullah bin al-Mughira, na kaka yake, Naufal, na Hakam bin Kaisan. Abdullah akawashambulia na kuka-mata mizigo yao. Amr bin al-Hadhrami aliuawa; Uthman na Hakam wakatekwa; na Naufal akafanikiwa katika kutoroka.

Msafara huu unachukuliwa kwamba ni muhimu kwa sababu ilikuwa ni mara ya kwanza ambapo palikuwa na mapambano kati ya Waislamu na wapagani. Ilikuwa pia ni mara ya kwanza ambapo palikuwa na umwagaji wa damu kati yao, na Waislamu walikamata ngawira kutoka kwao.

Abdullah bin Jahash na kundi lake wakarudi Madina pamoja na wafungwa wao na ngawira za vita. Kati ya wafungwa wawili hao, Hakam bin Kaisan alisilimu na akaishi Madina. Uthman bin Abdullah alikombolewa na ndugu zake, na akaenda Makka.

Kubadilishwa kwa Qibla - February 11, A.D. 624.

Katika miezi kumi na sita ya kwanza baada ya Hajira, Qibla cha Waislamu kwa ajili ya Swala kilikuwa Jerusalem (walielekea Jerusalem wakati walipokuwa wakiswali). Kisha Mtume wa Allah (s.a.w.) akapokea wahy (ufunuo) ukimuamuru kubadilisha sehemu ya mwelekeo kutoka Jerusalem upande wa kaskazini kwenda Makka upande wa Kusini.

Dr. Montgomery Watt na John Christopher wametoa "sababu" zao juu ya kubadilika kwa muelekeo wa Qibla. Wanasema kwamba, hapo mwanzoni. Mtume (s.a.w.) alitegemea kwamba kuelekea Jerusalem wakati wa kuswali, kungefanya nyoyo za Wayahudi wa Yathrib kumnyenyekea yeye, na wangemkubali kama Mjumbe wa Allah (s.a.w.). Lakini

126

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

aligundua, wanaendelea kusema kwamba, ingawa alielekea Jerusalem, wakati alipokuwa akiswali, wale Wayahudi walibakia wenye kushuku ukweli na uaminifu wake. Kisha wanaongeza kwamba baada ya miezi kumi na sita, Mtume (s.a.w.) alikata tamaa ya kuwaingiza Wayahudi wale kwenye Uislamu.

Kwa mujibu wa Dr. Montgomery Watt na John Christopher na baadhi ya mustashirki wa Magharibi, mara Mtume (s.a.w.) alipopoteza matumaini ya kuwapata wale Wayahudi kwenye Uislamu, aliondoa shauku juu yao, na akaamua kuweka dhamira yake kwa Waarabu. Huku kubadilika kwa Qibla, wanadai, kulikuwa ni tendo la hisia za kuwaridhisha Waarabu.

Hatujui kama Wayahudi hawa walikasirika ama kama Waarabu hawa walifurahishwa na kubadilika kwa Qibla. Sisi, kwa kweli, wala hatujui ni Waarabu wa wapi, kwa mujibu wa Dr.Watt, ambao Mtume (s.a.w.) alikuwa anajaribu kuwafurahisha - ni Waarabu wa Madina ama Waarabu wa Makka!

Waarabu wa Madina walikuwa wameukubali Uislamu na walimtii Mtume. Kwao wao kitu muhimu kilikuwa ni kumtii yeye Mtume (s.a.w.) kwa vile alikuwa ndiye mfasili wa ujumbe wa Allah (s.w.t) kwa wanadamu. Walielekea Makka walipokuwa wanaswali na hawakuuliza maswali yoyote ya kwa nini Qibla kilibadilishwa.

Waarabu wa Makka walikuwa bado ni waabudu masanamu. Na wao pia walisikia habari za kubadilika kwa Qibla kutoka Jerusalem kwenda Makka. Lakini hakuna ushahidi wowote kwamba mmoja wao yeyote, kwa kuridhishwa na kufurahishwa na mabadiliko haya, alikuja Madina na kujitolea kuwa mwislamu. Walibakia walivyokuwa, ama Qibla kilikuwa Jerusalem au Makka, kwao haikuonyesha tofauti yoyote.

Maelezo ya Waislamu ni rahisi na yenye mantiki; Allah (s.w.t.) amemuamuru mja Wake, Muhammad, kubadili Qibla, na alitii. Hii amri ya kubadili Qibla ilitolewa ndani ya Aya ya 44 ya Sura ya pili ya Qur'an Tukufu.

Katika mwezi wa Shaban (mwezi wa nane), mwaka wa pili wa Hijiria, kufunga katika mwezi wa Ramadhani (mwezi wa tisa) kulifanywa ni amri ya lazima kwa Waislamu. Wao, kwa hiyo, walifunga katika mwezi uliofuata (yaani, mwezi wa Ramadhani). Mwisho wa mwezi wa kufunga, walitakiwa kutoa Zaka-ul-Fitr, Zaka maalum.

Katika mwaka huo huo, kodi nyingine, Zaka-ul-Mal, iliwekwa juu ya Waislamu. Kodi hii inakadiriwa katika kiwango cha asilimia 2.5 ya mali ya mwislamu. Katika nyakati za Mtume, kodi hii ilikuwa ikilipwa kwenye Bayt-ul-Mal au hazina ya umma, na ilitumika katika ustawi wa masikini na watu wagonjwa katika jamii. Lakini kama hakuna Bayt-ul-Mal, Waislamu lazima wailipe kwa masikini wanaostahiki, wajane, mayatima na wale watu katika jamii ambao hawana uwezo wa kujikimu wenyewe

127

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Vita vya Badr

Vita vya kuvunja moyo kati ya Maquraishi na Waislamu vingeshadidisha kwenye uhasama wa dhahiri wakati wowote. Abu Jahl alikuwa mmoja wa "wachuuzi" katika Makka ambaye aliyeendeleza vita-visivyokoma vya kisirisiri dhidi ya Muhammad Mustafa na wafuasi wake. Ushari wake wa kiuzalendo uliiweka Makka katika hali ya wasiwasi wa kudumu.

V.C.Bodley:

"Wazimu wa Abu Jahl juu ya Muhammad ulibakia katika kiwango cha kuchemka. Aliweka vikundi vya mashambulizi daima kwenye hali ya kuendelea kushambulia, vikishambulia makundi yoyote ya Waislamu yaliyo pembeni ambayo yangeweza kushambuliwa kwa ghafla. Alifanya uvamizi kwenye vitongoji vya Madina na kuharibu mazao na bustani. Alimfanya Muhammad aone kwamba hisia zake hazi-jabadilika, kwamba makusudio yake bado ni ya kimauaji."

(The Messenger, the Life of Mohammed, New York. 1946)

Mapema mwezi March, 624, habari zilipokelewa Madina kwamba msafara wa Maquraishi ulikuwa ukirejea Makka kutoka Syria. Msafara huo haukuwa umebeba bidhaa tu bali pia na silaha. Ilikadiriwa kuwa msafara huo ulitengeneza faida ya dinari 50,000 (vipande vya dhahabu). Silaha hizo na utajiri mpya uliopatikana vilikuwa vitumike, kwa mujibu wa habari hizohizo, kuandaa jeshi la kupigana dhidi ya Waislamu. Msafara huo uliongozwa na Abu Sufyan, mkuu wa ukoo wa Banu Umayya.

Muhammad Mustafa aliamua kuuzuia msafara huo wa Makka. Alimteua Abu Lababa kama gavana wa Madina, na akaondoka mjini hapo na kikosi cha watu 313. Kati ya hawa, 80 walikuwa Muhajir, na 233 walikuwa Ansari. Mwisho wa safari yao ulikuwa ni Badr, kijiji Kusini-Magharibi ya Madina ambako wakitegemea kukutana na huo msafara wa Makka.

Waislamu hawakulijua hilo bado kwamba hawangeuona kamwe msafara wa Maquraishi, na kwamba watakuwa, badala yake, wawe kwenye mapambano, kwenye uwanja wa vita, na jeshi la Maquraishi.

Wakati huohuo, wapelelezi wa Makka walimjulisha Abu Sufyan kwamba kundi la Waislamu limeondoka Madina, na lilikuwa likienda kwa haraka kuelekea kwenye msafara wake. Mara tu alivyosikia hivyo, aliiacha ile njia ya msafara ya kawaida, akauongoza ule

128

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

msafara wake kuelekea Magharibi kwenye pwani ya bahari ya Red Sea, na kisha akageukia upande wa Kusini kuelekea Makka, vile vile alituma ujumbe Makka kuomba msaada. Mjini Makka Abu Jahl alikuwa tayari akishughulika kuchochea ghadhabu za watu dhidi ya Waislamu, kufuatia tukio la Nakhla.

Aliitikia kwa shauku sana mwito wa Abu Sufyan, na akakiongoza nje ya Makka kikosi cha wapiganaji 1000 chenye wapanda farasi 100, dhidi ya Waislamu. Msururu wa ngamia 700 ulibeba vifaa kwa ajili ya vita na mahitaji mengineyo. Askari wa miguu walivaa ngao na deraya.

Muhammad Mustafa hakujua kwamba jeshi limeondoka Makka na lilikuwa likisonga mbele kuelekea Madina kuulinda msafara wa Maquraishi, na kuwapa changamoto Waislamu. Wakati Mtume (s.a.w.) alipowasili kwenye maeneo ya Badr, alimtuma Ali kuchunguza nchi iliyozunguka pale. Katika visima vya Badr, Ali aliwashitukiza baadhi ya wabeba maji. Katika majibu kwa maswali yake, walimwambia kwamba walikuwa wan-abeba maji kwa ajili ya jeshi ambalo lilikuja kutoka Makka, na ambalo lilipiga kambi upande wa pili wa vile vilima vya karibu.

Ali aliwapeleka wale wabeba maji mbele ya Mtume wa Uislamu. Kutoka kwao alijua kwamba ule msafara wa Maquraishi tayari ulikuwa umekwisha toroka, na kwamba Waislamu wale, katika muda ule ule, walikabiliwa na jeshi la Makka.

Sir William Muir:

"Katika kufika kwenye maeneo karibu na Badr, Muhammad alimtuma Ali, pamoja na wengine wachache, kuchunguza ile ardhi iliyoinuka juu ya chemchemu. Hapo wali-washitukiza wabeba-maji watatu wa maadui, wakiwa karibu na kujaza mifuko yao ya ngozi ya kondoo. Mmoja akatorokea kwa Maquraishi; na wale wengine wawili wakakamatwa na kupelekwa kwenye jeshi la Waislamu. Kutoka kwao Muhammad alitambua ukaribu wa adui zake. Walikuwepo watu 950; mara tatu zaidi ya idadi ya watu wa jeshi la Waislamu. Walikuwa wamepanda juu ya ngamia 700 na farasi 100, hawa wapanda farasi wakiwa wamefunikwa na ngao za chuma.

(The Life of Muhammad, London, 1877)

Taarifa hii muhimu ya kuhusu maadui ilipokelewa kupitia Ali ibn Abi Talib. Kitendo chake, kwa upande mmoja, kiliwatahadharisha Waislamu; na kwa upande mwingine, kili-wapora maadui ile fursa ya kuwashitukiza. Waislamu walikuwa tayari kuwakabili. Hata hivyo, kuwepo kwa adui hai, mshari na mwenye kutisha, badala ya msafara tajiri, ndani ya umbali wa jirani sana, kulibadilisha kabisa hali kamili kwa Waislamu, na iliwabi-di wafanye tathmini mpya ya hatari na uwezekano wa mkabiliano naye. Hawakuwa wame-

129

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

jiandaa vema, na walikuwa na farasi wawili tu na ngamia 70 pamoja nao.Wengine wao walikuwa na panga lakini hawakuwa na ngao na wengine walikuwa na ngao bali hawakuwa na panga. Mtume (s.a.w.) ambaye alivitambua vikwazo hivi vya dhahiri, aliitisha baraza la vita, na akalifikisha suala hili mbele ya maswahaba zake kwa tafakari na uamuzi.

Mtu wa kwanza aliyesimama na kuzungumza juu ya wakati huu mgumu, alikuwa ni Miqdad. Alizungumza hisia na mawazo ya Muhajirina aliposema: "Ewe Mtume wa Allah, fanya kile ambacho Allah (s.w.t.) amekuamuru kufanya. Tuko pamoja nawe, sasa na wakati wote; na hatutakuambia kile Wana wa Israeli walichomwambia Musa: 'Wewe na Mungu wako mwende mkapigane dhidi ya adui; na sisi, tutabaki hapa, na kukaa hapa.' Hapana, hatutawaiga wale Wana wa Israeli. Tutakufuata wewe na kuzitii amri zako."

Muhammad alitoa baraka zake kwa Miqdad. Lakini Miqdad alikuwa ni Muhajir, na Muhammad alikuwa na shauku ya kujua ni nini Ansari watafanya. Yeye aliona kwamba wale Ansari wangepigana katika kuilinda Madina yenyewe lakini wasingependa kupigana nje ya mji wao. Akihisi shauku yake, Saad ibn Muadh, mmoja wa viongozi wa Ansari, alisimama na kusema: "Tumeshuhudia kwamba wewe ni Mjumbe wa Allah. Tumekupa kiapo chetu cha kukutii wewe. Popote utakapokwenda, tutakwenda pamoja nawe. Kama kutakuwa na kuonyeshana dhamira na washirikina, tutasimama imara katika kukuunga mkono kwetu. Kwa vita na kwa amani, tutakuwa daima waaminifu kwako."

Matamshi Haya yenye msimamo wa wazi ya kuunga mkono ya kiongozi wa Ansari, yalimridhisha Mtume, na akaomba baraka za Allah (s.w.t.) juu yao wote. Yeye alijua kwamba sio vita vya Badr wala vita vyovyote vile vingeweza kupiganwa bila ya msaada wa Ansari. Hawa Ansari walikuwa, kwa hakika, wa muhimu sana kwa ajili ya mafanikio katika mapambano kati ya Uislamu na upagani, kama ilivyoonyeshwa kabla.

Kwa namna halisi na kwa kiasi, Waislamu walikuwa kwenye upungufu lakini kasoro hizi zilifutwa na hamasa zao. Walikuwa na imani na uongozi wa kimajaaliwa wa Muhammad. Na walikuwa wameungana. Muungano na umoja wao wa dhamira vilikuwa viwe chanzo cha nguvu kubwa kwao katika mapambano yajayo na jeshi la Makka.

Kwa kuhakikishiwa msaada wa Ansari, Muhammad Mustafa alichukua uamuzi wa kukubali changamoto ya Maquraishi. Yeye na askari wa kawaida wa jeshi la Madina wanaelekea kutambua wazi kwamba matokeo ya mapambano na adui siku itakayofuata, yatakuwa yamezidi katika athari zake.

130

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir William Muir:

"Muhammad alikuwa anayafahamu kabisa mazingira hayo magumu. Majaaliwa ya Uislamu yalitegemea juu ya matokeo ya mapambano yanayokuja."

(The Life of Mohammed, London, 1877)

Mtume (s.a.w.) aliwaamuru Waislamu kukita mahema yao juu ya ardhi ya pale waliposimama. Lakini kijana mmoja wa Ansari alionyesha faida za kuchagua sehemu nyingine ya kupiga kambi ambapo ardhi ilikuwa juu zaidi na imara, na pia alipendekeza kwamba Waislamu wachukue milki ya visima vyote vya Badr. Mapendekezo yake yalikubalika moja kwa moja.

S. Margoliouth:

"Hubab mtoto wa al-Mundhir, mdogo kwa Mtume (s.a.w.) kwa miaka ishirini, baada ya kuhakikisha kwamba walikuwa kwenye vita vya kawaida, na kule kuwa na ujuzi maalum wa vile visima vilivyoko jirani, alimshauri Mtume (s.a.w.) kukaa mbele ya vyote isipokuwa kimoja, ambacho katika mzunguko wake wangefanya hifadhi, ili kuwa na ugawaji wa maji wa kuaminika kwa ajili ya vikosi hivyo; kule kuwa na nguvu hii ya asili yenye thamani baadae kutasaidia. Mtume (s.a.w.) aliyakubali mapendekezo yake na akaliweka jeshi lake chini ya usimamizi wa Hubab.

(Mohammed and the Rise of Islam, London, 1931)

Matukio mara yakadhihirisha kwamba mapendekezo ya Hubab yalikuwa mazuri sana, na kukubaliwa kwake na Mtume (s.a.w.) kuliwapa Waislamu faida kubwa ya kimbinu juu ya maadui.

Vita hivi vya Badr vilipiganwa katika mwaka wa pili wa Hijiria, kwenye tarehe 17 ya mwezi wa Ramadhani, mwezi wa tisa wa kalenda ya Kiislam (March 15, A.D.624). Lile jeshi la Makka lilitoka nje ya kambi yao mapema asubuhi kukutana na Waislamu. Majeshi haya maw-ili yakajipanga katika mpango wa kivita. Mtume (s.a.w.) akachukua upinde mkononi mwake na akatembea kati ya mistari iliyopanga safu za Waislamu. Tendo lake la mwisho kabla ya vita kuanza, lillikuwa ni kumuomba Allah (s.w.t.) kutoa ushindi kwa waja Wake wanyenyekevu.

Vita vikaanza katika desturi ya Kiarabu ya taratibu za vita ambamo shujaa wa upande mmoja alipanda au kutoka nje ya msitari, na kuwapa changamoto mashujaa wa adui kukutana naye katika pambano la mtu mmoja mmoja.

Hii ilimpa fursa ya kujipatia sifa binafsi kwa kuonyesha ujasiri wake mwenyewe, nguvu zake na ujuzi katika upanda farasi. Majeshi hayo mawili yalifanya kama namna ya kibwa-gizo kwa ajili ya mapambano kati ya mashujaa wachache wanaojigamba. Baada ya Haya

131

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mapambano ya awali, ilikuwa ni desturi kwa majeshi hayo mawili kushambuliana, na kuin-gia kwenye mapigano ya mkono kwa mkono.

Kutoka upande wa Makka, wapiganaji watatu, Utba mtoto wa Rabia; Shaiba, kaka yake; na Walid, mtoto wake; walitoka kwenye nafasi ya wazi kati ya majeshi hayo mawili, na wakawapa changamoto Waislamu. Changamoto yao ilichukuliwa na Hamza, ami yake Muhammad na Ali; Ubaida ibn al-Harith, binamu yake Muhammad na Ali; na Ali ibn Abi Talib.

Walid ibn Utba alikuwa mmoja wa wapiganaji wakali sana wa Makka. Ali alijikuta akika-biliana naye. Walikuwa ndio jozi ya vijana zaidi, na walikuwa wa kwanza kuingia kwenye kupigana. Zile jozi zingine mbili zikapumzika, kuwaangalia wale wapiganaji vijana waw-ili wakipambana. Vijana hawa wawili walitupiana mapigo machache, na kisha Ali akapiga pigo lake ambalo lilimuua Walid.

Mara baada ya Walid kuuawa, wale wapiganaji wengine nao wakashambuliana. Hamza akamuua Utba. Lakini Ubaida alijeruhiwa vibaya sana na Shaiba. Wakati Ali alipomuona Ubaida anaanguka chini, alimshambulia Shaiba, na akamuua pia. Kwa maadui zao wawili kufa, na hakuna mtu uwanjani, Ali na Hamza walimbeba Ubaida kumrudisha kwenye safu za Waislamu ambako alikufa kwa sababu ya majeraha yake. Alikuwa mwislamu wa kwanza kuuawa kwenye uwanja wa mapambano.

Sir William Muir:

"Ndugu hawa wawili, Shaiba na Utba, na Walid, mtoto wa Utba, walisonga mbele kwenye nafasi kati ya majeshi hayo, na wakawataka shari mashujaa watatu kutoka kwenye jeshi la Muhammad kupambana nao mmoja mmoja. Muhammad aki-wageukia jamaa zake, akasema: "Enyi wana wa Hashim! Amkeni na mpigane, kwa mujibu wa haki yenu." Ndipo Hamza, Ubaida na Ali, wale ami na binamuze Mtume, wakatoka mbele.

Hamza alivaa unyoya wa mbuni kifuani mwake, na nyoya jeupe lilitambulisha kofia ya vita ya Ali. Kisha Utba akamwita mwanae, Walid, "Simama na upigane." Hivyo Walid alitoka mbele na Ali akatoka dhidi yake. Walikuwa ndio vijana zaidi ya hao sita. Mapambano yalikuwa mafupi; Walid alianguka akiwa amejeruhiwa vibaya kwa upanga wa Ali.

(The Life of Mohammed, London, 1877) Sir John Glubb:

"Machifu watatu wa Makka, Utba, Shaiba na Walid, mtoto wa Utba, walijitokeza mbele ya msitari wa Maquraishi na kuwataka vita Waislamu watatu kukutana nao

132

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

katika pambano la mmoja mmoja. Muhammad akiwageukia Muhajir aliita: "Enyi Bani Hashim, simameni na mpigane." Watu watatu wakiwa wamefunikwa na ngao za chuma walitoka kwenye safu za Waislamu. Walikuwa ni Hamza, ami yake Mtume; Ali ibn Abi Talib, binamu yake, na mfuasi wa kwanza wa kiume; na Ubaida ibn Harith.

Ile jozi ya vijana zaidi ilishambuliana mwanzo, Ali akitoka mbele kukutana na Walid. Baada ya muda kidogo wa kucheza na panga, Walid aliangushwa na upanga wa adui yake mwislamu. Kisha Hamza akamshambulia Utba na akamkata na kumuangusha chini. Ubaida ibn Harith, shujaa wa tatu wa Kiislam, alipata jeraha baya sana kutoka kwa Shaiba. Ali na Hamza haraka sana wakamuua Shaiba, wakimbeba Utba kwenda kufia kwenye safu za Waislamu.

(The Great Arab Conquests, 1963)

Badr ilikuwa ndiyo pambano la kwanza, katika uwanja wa vita, kati ya Uislamu na Wapagani. Ilianzishwa upande wa Uislamu, na Ali ibn Abi Talib, simba kijana, na ushindi wake ulikuwa ni ishara ya mafanikio ya Uislamu. Vita nyingine zote za Kiislam zilifuata mkondo huohuo; Ali alikuwa ndiye mshindi katika kila moja yao.

Maquraishi walituma mashujaa watatu dhidi ya Waislamu, na wote watatu waliuawa. Abu Jahl, kwa hiyo, hakuwa na shauku ya kuchukua majaribio zaidi na Ali na Hamza, na akaa-muru majeshi yake kusonga mbele. Watu wa Makka waliwashambulia Waislamu lakini hawakuweza kuvunja mipangilio yao. Walishambulia tena na tena lakini safu za Waislamu zilibakia imara chini ya ukamanda wa Ali na Hamza.

Watu wa Makka walikuwa wakijikusanya kwa ajili ya mashambulizi mapya wakati Muhammad alipowaashiria Waislamu kusonga mbele. Ali na Hamza waliongoza mapam-bano ya kujibu shambulizi, na wote walileta mauji na fadhaa kwenye kundi kubwa la safu za adui. Wengi wa viongozi na maafisa wa Makka waliuawa, miongoni mwao Abu Jahl mwenyewe. Baada ya kifo chake, waabudu-masanamu hao hawakuweza kujikusanya, na walianza kurudi nyuma. Waislamu walishikilia fursa yao, na kule kurudi nyuma kwa watu wa Makka mara kukawa ni msambaratiko. Uislamu umepata ushindi wake wa kwanza na wa muhimu sana!

S. Margoliouth:

"Kwa hakika inaonekana kwamba kushinda kwa pambano hili muhimu kulikuwa katika kustahili kukubwa kwa ushujaa wa Ali na Hamza. Mtukufu Mtume (s.a.w.) anasemekana kutoa sifa maalum kwa ujasiri wa Simak ibn Kharashah; Sahl ibn Hunaif; al-Harith ibn al-Simmah; na Kais ibn al-Rabi; wote wakiwa ni watu wa Madina.

(Mohammed and the Rise of Islam, London, 1931) 133

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Tor Andre:

"Kufikia mchana vita vilikuwa vimekwisha. Watu arobaini na tisa wa adui walikuwa wameanguka na Ali aliuwa watu ishirini na wawili, ama peke yake au pamoja na msaada wa wengine. Idadi kama hiyo hiyo walitekwa. Waumini walipoteza watu kumi na wanne katika uwanja wa mapambano."

(Mohammad, the Man and his Faith, 1960)

Kama ilivyoonyeshwa hapo juu, Badr ndio vita muhimu sana katika historia nzima ya Uislamu, na moja kati ya zile maarufu katika historia ya ulimwengu. Ushindi ulihakikisha kuwepo kwa Uislamu, na uhai wa dhahiri wa jumuiya ya Waislamu ya Madina ambayo mpaka sasa imetokea, kwa vyovyote, kuwa ya hatari.

A.Nicholson:

"Lakini umuhimu wa mafanikio ya Muhammad (katika vita vya Badr) hayawezi kupimwa kwa uharibifu wa vitu aliousababisha (juu ya wapagani wa Makka). Tukitazama mambo ya maana sana yaliyohusika, ni lazima tukubali kwamba Badr, kama masafa marefu, ni moja ya vita vikubwa na vya kukumbukwa sana katika historia yote.

(A Literary History of the Arabs, 1969)

Ali ibn Abi Talib na vita vya Badr

Msanifu wa Ushindi wa Waislamu huko Badr, bila ya shaka yoyote, alikuwa ni Ali ibn Abi Talib. M. Shibili, yule mwanahistoria wa Kihindi aliyeandika vitabu vya kutegemewa vya wasifu kwa Ki-Urdu vya Umar bin Khattab na vya Mtume wa Uislamu, anasema katika kitabu chake Life of the Apostle, kwamba shujaa wa vita vya Badr ni Ali ibn Abi Talib.

F.E.Peters:

"Badr ilikuwa ni ushindi kwa Waislamu, kwa jumla kama ilivyokuwa haikutegeme-wa; Waislamu walipoteza watu kumi na wanne na Maquraishi watu 50 hadi 70, pamoja na kiongozi wao, Abu Jahl. Ulikuwa ni ushindi mkubwa sana wa kisaikolojia na kulikuwa na wingi wa ngawira kwa ajili ya wale Muhajir waliodhikika kiuchumi. Hili halikuwa shambulio la hivihivi tu, hata hivyo. Lilipambanisha Waislamu dhidi ya wasio-Waislamu katika Vita Tukufu (Jihad), na akina baba dhidi ya watoto wao katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Majeruhi wa Maquraishi walikuwa wengi mno, na kwa vile wengi wao walitokana miongoni mwa machifu wao, uongozi hapo Makka ulidhoofishwa kabisa daima.

(Allah s Commonwealth, 1973) 134

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Uongozi wa washirikana wa Makka kwa hakika ulidhoofishwa daima hapo Badr. Shujaa aliyehusika na hili alikuwa ni Ali. Yeye peke yake aliwauwa watu wa Makka 22, na kumi na wawili wao wakiwa ni wale watu maarufu wa ukoo wa Bani Umayya. Jeshi la Waislamu lililobakia liliuwa wapagani wengine 27.

Miongoni mwa ngawira za vita vya Badr ulikuwepo upanga ambao ulikuwa uje kuwa ndio upanga maarufu kabisa katika historia nzima ya Uislamu. Jina lake lilikuwa ni Dhul-Fiqar.

Washington Irving:

"Miongoni mwa ngawira za vita vya Badr ulikuwa ni upanga maarufu wenye hali ya kupendeza uitwao Dhul-Fiqar. Muhammad daima baadae aliushika akiwa vitani, na mkwe wake, Ali aliurithi baada ya kifo chake."

(The Life of Muhammad)

Abdullah Yusuf Ali, yule mtarjuma na mfasiri wa Qur'an Tukufu, anasema kwamba vile vita vya Badr vinaitwa Furqan katika elimu ya Kiislam, kwa sababu ilikuwa jaribio la kwanza la nguvu kwa njia ya vita, katika Uislamu, kati ya nguvu za wema na uovu. Furqan ina maana ya kibainishi kati ya ukweli na uongo; uamuzi kati ya nguvu za Imani na Ukafiri. Vita vya Badr vinaitwa kwa jina hili.

Wafungwa wa kivita

Waislamu walikamata wafungwa wa kivita hamsini. Waliletwa mbele ya Mtume (s.a.w.) ambaye alikuwa aamue wafanyiwe nini. Alishauriana na maswahaba zake katika jambo hilo. Umar allimshauri awauwe wote, lakini Abu Bakr akamshauri kuwaachia huru kwa fidia. Mtume (s.a.w.) akaukubali ushauri wa Abu Bakr.

Kwa vile hapakuwa na nyumba ya kizuizi hapo Madina, Mtume (s.a.w.) aliwagawanya wale wafungwa miongoni mwa familia za Waislamu. Familia hizi ziliwatendea wafungwa wao kama vile walikuwa wageni. Baadhi yao walilisha chakula chao wenyewe kwa "wageni" wao na wenyewe wakakaa na njaa. Kwa kweli waliwafedhehesha wafungwa wao kwa mashaka yao juu ya ustawi wao.

Wale wafungwa matajiri waliachiliwa kwa fidia. Wale wafungwa ambao hawakuweza kulipa fidia lakini waliweza kusoma na kuandika, walitakiwa kuzifundisha sanaa hizo kwa watoto wa Kiislam, na walipofanya hivyo, pia na wao waliachiliwa. Wale wafungwa waliokuwa mafukara sana, waliachiliwa bila ya fidia yoyote.

Matokeo ya vita vya Badr

Ushindi wa Badr uliwapa Waislamu heshima kubwa sana. Lile tishio kwa usalama wa Madina liligeuzwa, na Muhammad Mustafa aliweza sasa kuweka misingi ya Ufalme wa kwanza na wa mwisho wa Mbingnii hapa Duniani.

135

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

S. Margoliouth:

'Hakuna tukio katika historia ya Uislamu lililokuwa na umuhimu zaidi kuliko vita hii (ya Badr); Qur'an inaviita sawa kabisa - Siku ya Ukombozi, siku ambayo kabla yake Waislamu walikuwa wanyonge, baada yake wakawa wenye nguvu. Utajiri, umaaru-fu, heshima, mamlaka, vyote vilipatikana au kwa hali yoyote vililetwa karibu na hiyo - Siku ya Ukombozi."

(Mohammed and the Rise of Islam, London, 1931)

Tokeo moja la kusikitikia la vita vya Badr, hata hivyo, lilikuwa kwamba ushindi wa Uislamu uliwasha mioto mipya na mikali zaidi ya chuki na uhasama katika vifua vya Banu Umayya dhidi ya Muhammad Mustafa na Ali ibn Abi Talib. Chuki zao na wivu juu ya Bani Hashim ilidumu vizazi vingi. Lakini baada ya vita vya Badr, uhasama wao ulielekezwa kwa Ali na kwa watoto wa Muhammad Mustafa.

Kama kwa Waislamu, Ali alikuwa ndio alama ya ushindi wa Uislamu, kwa Banu Umayya, alikuwa ni alama ya kuangamia kwa ushirikina wao na heshima zao. Kwa hiyo, wao, vizazi vyao vilivyofuata, na marafiki zao na wanao waunga mkono, kamwe hawakumsamehe Ali kwa jukumu alilotekeleza hapo nyuma, wakati na baada ya vita vya Badr. Chuki yao inaeleweka. Alikuwa ni Ali, na ni Ali peke yake ambaye alishambulia, sio tu pale Badr, bali katika kila pambano, kwa mashambulizi makubwa, ile nguvu iliyolingana sawa na kumakinika ya upagani, na akaiangamiza.

136

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ndoa ya Fatima Zahra na Ali ibn Abi Talib

Allah swt. aliwapa ushindi Waislamu katika vita vya badr katika mwaka wa 2 wa Hijiria. Miezi miwili baada ya vita hivyo, Fatima Zahra, binti yake Muhammad Mustafa, na Ali, mwana wa Abi Talib walifunga ndoa.

Fatima Zahra alikuwa na miaka mitano tu wakati mama yake - Khadija (R.a.), alipofariki, na kuanzia hapo na kuendelea, baba yake, Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) alichukua wajibu wa kazi za mama pia kwa ajili yake. Kifo cha mama yake kilileta pengo katika maisha yake lakini baba yake alilijaza kwa upendo na huruma.

Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliweka uangalifu wa hali ya juu kwenye elimu na malezi ya binti yake. Kama alikuwa ndiye mfano bora kwa watu wote, binti yake alikuwa awe mfano bora kwa wanawake wote, na alikuwa hivyo. Alimfanya yeye kuwa mfano bora wa uwanauke katika Uislamu. Alikuwa ni mfano halisi wa ibada na utii kwa Muumba, na alikuwa ni mfano halisi wa usafi wa ki-ungu na utakatifu. Katika tabia na hulka, alikuwa na mfanano unaovutia sana kwa baba yake. Fatima, binti huyu, alikuwa ni picha ya Muhammad, baba yake.

Kwa kufanya utii na ibada kwa Allah (s.w.t.) Fatima Zahra alipanda kufikia cheo kikubwa mbele ya Allah (s.w.t.) kama ilivyoshuhudiwa na Qur'an Tukufu. Allah (s.w.t.) alimpa utukufu mkubwa sana juu yake, na Mtume wa Uislamu (s.a.w.), kwa upande wake, alim-wonyesha kiwango cha heshima ya juu sana, moja ambayo hakuionyesha kwa mwanaume au mwanamke mwingine yeyote yule katika wakati wowote wa maisha yake.

Wakati Fatima alipokuwa, maswahaba wawili wazee - wa kwanza na kisha baadae mwingine - walimuomba baba yake wamchumbie. Lakini aligeukia pembeni kwa kuchukia, na akasema:

"Hili suala la ndoa ya Fatima, binti yangu, liko mikononi mwa Allah (s.w.t.) Mwenyewe, na Yeye pekee ndiye atamchagulia yeye mchumba".

Allah (s.w.t.) alifanya uchaguzi Wake kama ipasavyo. Alimchagua mja Wake, Ali ibn Abi Talib, kuwa ndiye mchumba wa binti ya mja Wake mpendwa mno, Muhammad Mustafa. Alipenda kuwaona Fatima binti Muhammad na Ali ibn Abi Talib wakioana.

Miezi miwili baada ya vita vya Badr, yaani, katika mwezi wa Dhilqa'da (mwezi wa 11) wa mwaka wa 2 H.A., Ali alikwenda kwa Muhammad Mustafa, na akasema: "Ewe Mtume wa Allah, umenilea mimi kama mwanao mwenyewe. Ulinijaza na zawadi zako, ukarimu wako na wema wako. Ninawiwa nawe kila kitu katika maisha yangu. Sasa ninaomba wema mmoja zaidi kutoka kwako."

137

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mtume (s.a.w.) alielewa nini Ali alichokuwa akijaribu kukisema. Uso wake ulichangamka kwa tabasamu pana, na alimtaka Ali asubiri kwa muda kidogo mpaka apate majibu ya binti yake.

Aliingia ndani, akamwambia Fatima kwamba Ali alikuwa anaomba uchumba kwake, na akamuuliza ni lipi jibu lake. Akabakia kimya. Yeye Muhammad akatafsiri kimya chake kama idhini yake, akarudi kwa Ali, akamjulisha kwamba ombi lake limekubaliwa, na akamwambia afanye matayarisho ya harusi.

Katika siku ya mwisho ya Dhilqa'ada, Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) ali-wakaribisha Muhajirina na Ansari, kuhudhuri karamu, katika tukio la kuolewa kwa binti yake. Alikuwa ndiye mwenyeji wao. Wakati wageni wote walipofika, na wakawa wamek-wishakaa, alichukua, kwa mara nyingine tena, idhini ya kisheria ya binti yake kwa ajili ya ndoa na Ali ibn Abi Talib.

Muhammad Mustafa alimtukuza Allah (s.w.t.) na akamshukuru Yeye kwa ajili ya rehema Zake zote. Yeye kisha akasoma hotuba ya ndoa; akawatangaza Ali na Fatima kama mume na mke, na akaomba baraka za Allah (s.w.t.) ziwe juu yao wote. Wageni wote wakam-pongeza Mtume (s.a.w.) kwa tukio hili lenye baraka tele. Baada ya sherehe hii, wageni wale walikula karamu ya nyama ya kondoo, mkate, maji ya tende na maziwa.

Siku chache baadae, yaani, katika Dhil-Hajj (mwezi wa 12 wa kalenda ya Kiislam), Fatima Zahra ilibidi aiage nyumba yake ya kuzaliwa ili aweze kwenda kwenye nyumba ya mumewe. Baba yake alimsaidia katika kumpakia kwenye ngamia-jike wake (Muhammad). Madina ilivuma kwa sauti za Allah-u-Akbar. Salman Muajemi alishikilia hatamu za ngamia-jike huyo, na akatembea mbele yake, huku akisoma Qur'an Tukufu. Mtume wa Allah (s.a.w.) alitembea upande mmoja wa ngamia-jike huyo, na Hamza, Simba wa Mungu, upande mwingine.

Vijana wote wapanda farasi wa Bani Hashim walipanda kama wasindikizaji wa Bibi-harusi huyo, pamoja na panga zinazomeremeta zikiwa zimenyanyuliwa juu kabisa. Nyuma yao walikuwa ni wanawake Muhajira na Ansari, na nyuma yao hawa wakaja Muhajirina na Ansari wenyewe. Walikuwa wakisoma qaswida kutoka kwenye Qur'an Tukufu kumtukuza Allah (s.w.t.) Usomaji huo wa qaswida uliwekwa vituo vya mara kwa mara na mrindimo wa sauti za Allah -u-Akbar.

Maandamano haya ya kitukufu yaliuzunguuka Msikiti Mkubwa wa Madina, na kisha yakaishia kwenye ukomo wake - nyumba ya Bwana-harusi - Ali ibn Abi Talib. Muhammad Mustafa akamsaidia binti yake kushuka toka kwenye ngamia-jike. Akamshika mkono wake, na kwa ishara akauweka kwenye mkono wa mumewe, na kisha, akisimama kwenye kizingiti cha nyumba hiyo, akasoma du'a ifuatayo:

138

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Ewe Allah (s.w.t.)! Ninawaweka Ali na Fatima, waja wako wanyenyekevu, kwenye ulinzi wako. Uwe Wewe ndio Mlinzi wao. Wabariki hawa. Kuwa radhi nao, na uwape neema zako zisizo na mipaka, huruma, na fadhila Zako bora juu yao. Uifanye ndoa yao kuwa yenye matunda, na uwafanye wote imara katika upendo Wako, na ibada Zako."

Ilikuwa kwa kweli ni siku ya furaha katika maisha ya Muhammad Mustafa. Lakini ni vipi ambavyo angependa kwamba mke we mpendwa, Khadija, angekuwa pamoja naye ili wote kwa pamoja wakashuhudia ndoa ya binti yao.

Siku chache baadae, Mtume wa Allah (s.a.w.) alikwenda kwa binti yake, na akamuuliza kama alimuonaje mume wake. Binti akasema kwamba alimuona ni mwenza bora katika kufanya ibada na utii kwa Allah (s.w.t.) Baadae, alimuuliza Ali alimuona vipi mke wake, na akasema alimuona ni mwenza bora katika kumuabudu Muumba. Nyakati nzuri kabisa za maisha kwa wote mume na mke zilikuwa zile walipokuwa wamekwenda Mbele ya Mola wao, na wakazama katika kumuabudu Yeye.

Kati ya Ali na Fatima Zahrah, kulikuwa na utambulisho kamili wa manufaa. Wote walilele-wa na kufundishwa na Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) na Khadija-tul-Kubra. Wote kwa hiyo, walikuwa na ukamilifu wa wazazi wao. Wote waliweka ibada kwa Allah (s.w.t.) mbele ya kitu kingine chochote kile. Hapakuwepo na nafasi kabisa ya kutoelewana kati yao. Mawazo yao, maneno na matendo yao, yote "yalizoeshwa" na Qur'an Tukufu. Ndoa yao kwa hiyo, ilikuwa timilifu tu na ya furaha tu kama ile ndoa ya Muhammad na Khadija ilivyokuwa.

Kama ilivyoelezwa kabla, furaha kuu ya Fatima ilikuwa ni kuwa na subira juu ya Allah (s.w.t.) Alitumia muda wake mwingi katika Swala. Furaha yake kuu ya pili ilikuwa ni kutekeleza wajibu wake kwa familia yake. Allah (s.w.t.) aliridhia kumpa watoto wanne -kwanza wavulana wawili na kisha wasichana wawili. Alisaga nafaka katika kinu alichope-wa na baba yake kama sehemu ya mahari yake, na akawaokea mikate. Kusaga nafaka siku hadi siku kulisababisha malengelenge kutoka kwenye mikono yake lakini hakulalamika kamwe kwa mume wake au kwa baba yake juu ya malengelenge hayo, na alifanya kazi zake za nyumbani kwa furaha kabisa.

Hizi kazi za nyumbani zingeweza kuwa kama za kushurutisha sana kwa Fatima Zaharah lakini alipata furaha na nguvu katika kumkumbuka Allah (s.w.t.) Kitabu cha Allah (s.w.t.) kilikuwa ndio rafiki yake wa kudumu. Alisahau uchovu wa kazi vile alivyokuwa akisoma vifungu kutoka kwenye kitabu hicho. Na alipowalaza watoto wake katika kitanda chao, alisoma tena baadhi ya vifungu kutoka kwenye kitabu hicho hicho kama "nyimbo za kibembelezo" kwa ajili yao. Walikua huku wakiisikia Qur'an Tukufu toka utotoni mwao. Aliligandisha Neno la Allah (s.w.t.) juu ya mioyo yao michanga. Kwa kupitia

139

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"mfyonzo" kama huu, Qur'an na watoto wa Fatima Zahrah vikawa havitenganishiki kwa wakati wote.

Katika mwaka huo huo, yaani, mwaka wa 2 H.A., Sala za hadhara kwenye sikukuu mbili kwa ajili ya Waislamu, yaani, Idd-el-Fitr na Idd-el-Udh-ha., zilifanywa kuwa sunnah (zenye kustahili) juu yao.

140

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Vita vya Uhud

Hivi vita vya uhud vilikuwa ni kisasi dhidi ya Waislamu kufuatia vile vita vya Badr. Baadhi ya watu mashuhuri wa Quraishi kama vile Abu Jahl, Utbah, Shaiba, Walild, Umayya bin Khalaf, na Hanzala bin Abu Sufyan, waliuawa kwenye vita vya Badr. Baada ya kifo cha Abu Jahl, uongozi wa watu wa Makka ulipitia kwa mwenza wake, Abu Sufyan, ambaye alikuwa mkuu wa ukoo wa Banu Umayya. Kulikuwa na huzuni nzito hapo Makka kwa kupotea kwa wakuu wengi lakini Abu Sufyan alizikataza zile familia zilizofiwa kulia na kuomboleza kuondokewa kwao. Machozi, alijua, yangeweza kusafisha uovu kutoka nyoy-oni. Lakini muda na machozi, alidai, havitaachiliwa kuponya majeraha yaliyoupata utawala wa kikabila wa Makka huko Badr. Yeye mwenyewe alikula kiapo kwamba atajie-pusha na kila anasa mpaka awe amewatendea Waislamu kama walivyomtendea. Yeye na wakuu wengine wa Maquraishi waliutumia mwaka mzima wa shughuli za msisimko ambamo waliandaa na kufundisha jeshi jipya.

Mwaka mmoja baada ya vita vya Badr, lile jeshi jipya la waabudu-masanamu wa Makka lilikuwa tayari kusimama uwanjani dhidi ya Waislamu. Mnamo Machi 625 Abu Sufyan aliondoka Makka akiongoza wapiganaji elfu tatu waliozoeshwa. Wengi wao walikuwa askari wa miguu lakini walisaidiwa na kikosi chenye nguvu cha wapanda farasi. Pia wakiandamana na jeshi hilo, walikuwa ni kundi la wanawake wenye kupenda vita. Kazi yao ilikuwa ni kuendeleza "vita vya kimawazo" dhidi ya Waislamu kwa kusoma mashairi na kuimba nyimbo za mapenzi ili kuhimiza ujasiri na shauku-ya-kupigana ya askari hao. Walijua kwamba hakuna kilichohofisha kwa Waarabu kiasi hicho kama dhihaka za wanawake kwa waoga, na vile vile walijua kwamba hakuna chenye kufaa zaidi kuwageuza kuwa wapiganaji wasiojali kabisa, kama ahadi ya mapenzi ya kimwili. Majikedume haya yalikuwa ni pamoja na wake za Abu Sufyan na Amr bin Al-As, na dada zake Khalid bin Walid.

D.S. Margoliouth:

"Abu Sufyan anaonekana kufanya juhudi zake zote, na, kama badala ya muziki wa kijeshi, alisababisha ama kuruhusu jeshi hilo kufuatiwa na kundi la wanawake, ambao, kwa kutishia na kuahidi, walikuwa waweke ujasiri wa vikosi hivyo kwenye kiwango sahihi; kwani hakuna chochote alichohofia aliyekimbia kutoka kwenye uwanja wa mapambano, zaidi kuliko kushutumiwa na wanawake wa kwao. Wanawake wa Kikuraishi walifanya kazi ya kipekee yenye uhakika. Mke wa Abu Sufyan alitoa ushauri kwamba mwili wa mama yake Muhammad ufukulliwe na kuwekwa kama mateka; lakini Maquraishi waliukataa ushauri huu (ambao kwamba uwezekano wake kwa kweli ulikuwa na mashaka) kwa kuhofia visasi."

(Muhammad and the Rise of Islam, 1931) 141

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kana kwamba vile vidokezo vya mapenzi vilivyotolewa na wale wanawake wa Kikuraishi havikutosheleza, Abu Sufyan aliweka kampeni yake kwenye "utakatifu wa kidini" vilevile. Kuondoa mashaka kabisa katika akili ya mtu yoyote kwamba alikuwa kwenye vita tukufu dhidi ya Waislamu, alimuweka Hubal, lile sanamu ambalo ukoo wa Banu Umayya walili-abudu kama mungu wao mkuu, juu ya ngamia, na akalibeba kwenda nalo ndani ya vita. Kazi ha Hubal ilikuwa ni kuzidisha hamasa ya waabudu-masanamu kwa kuwepo kwake kwenye uwanja wa vita.

Mapenzi ya kijinsia na dini vilikuwa ndio vitu viwili vipya vilivyoandaliwa na Maquraishi katika vita vyao dhidi ya Muhammad na Uislamu.

Betty Kelen:

"Katika kiti chenye mwamvuli (mgongoni mwa tembo) alipanda Hubal, kwenye mapumziko kutoka kwenye Al-Kaaba. Abu Sufyan alikuwa ameshikilia kabisa kwamba mbali kabisa na mawazo ya kisasi na njia za misafara, alikuwa ameingia kwenye vita vya jihad."

(Muhammad, the Messenger of God, 1975)

Muhammad Mustafa, Mtume wa Uislamu, pia alizisikia habari za uvamizi wa Madina unaokaribia kutoka kwa watu wa Makka, na yeye pia aliwaamuru wafuasi wake kujiandaa kwa ulinzi. Waislamu mia saba walikuwa tayari kumfuata kwenye vita.

Mtume (s.a.w.) aliliweka jeshi lake kwa mlima wa Uhud kuwa nyuma yake hivyo kwamba lilisimama kuelekea Madina. Wakati jeshi la watu wa Makka lilipokuja, lilichukua nafasi yake mbele ya Waislamu hivyo kwamba lilikuwa limesimama kati yao na Madina ambayo ilikuwa nyuma yao.

Sir William Muir:

"Abu Sufyan, kama kiongozi wa upagani, aliliteta jeshi la Makka; na wakielekea Uhud, akaliongoza mbele ya Muhammad. Bendera ilikuwa imeshikwa na Talha mtoto wa Abdal Uzza. Vikosi vya upande wa kulia viliongozwa na Khalid; na vya kushoto na Ikrima mtoto Abu Jahl. Amr bin Al-As alikuwa juu ya farasi wa Kiquraishi."

(The Life of Muhammad, 1877)

Sir John Glubb:

"Waislamu walisonga mbele na watu 700 dhidi ya wapiganaji 3000 kutoka Makka. Zaidi ya hayo, wakati Waislamu waliweza kukusanya nguvu ya watu mia moja tu wenye deraya, na bila ya farasi, Maquraishi na washirika wao walikuwa na watu 700 wenye deraya na wapanda farasi 200.

142

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wakitaka kuziba nyuma yao kutokana na idadi yao ndogo, Waislamu walijipanga chini ya mlima Uhud. Upande wao wa kulia na nyuma vilifunikwa na milima, lakini upande wao wa kushoto ulikuwa kwenye uwanja wa wazi na kwa hiyo uliachwa kwenye shambulizi la askari wa farasi wa adui. Kujihami dhidi ya hili, Muhammad aliweka wapiga mishale hamsini kwenye upande huu, pamoja na amri ya kutoiacha nafasi yao kwa hali yoyote ile, ambapo kutokea hapo wanaweza kuulinda upande wa kushoto wa Waislamu kutokana na farasi wa Maquraishi.

Watu wa Makka waliweka safu yao kuwaelekea Waislamu kwa namna ambayo Waislamu, migongo yao ikielekea Uhud, walikuwa wakitazama kuelekea Madina, ambapo safu ya Maquraishi iliwakabili na Madina ikiwa nyuma yao, hapo wakiwa kati ya Waislamu na mji huo.

Maquraishi walikuwa wamekuja na wanawake wachache, wakiwa wamepanda kati-ka vitanda vya kubebwa na ngamia. Hawa sasa, wakati safu mbili hizo zilipokuwa zinasogeleana, waliendelea kuamsha shauku ya watu wa Makka, wakipiga vijingoma, wakisoma mashairi ya kivita na kushusha nywele zao ndefu."

(The Great Arab Conquests)

Vita vya Uhud vilianza kama vile tu vita vya Badr vilivyoanza, kwa mpiganaji wa Makka kuchomoza kutoka kwenye safu zao na kuwapa changamoto Waislamu kwa mapambano ya mtu mmoja mmoja.

Sir William Muir:

"Akipepea bendera ya Kikuraishi, Talha, yule mshika-bendera wa jeshi la Makka, alisonga mbele, na kuwapa changamoto maadui kwenye pambano la mtu mmoja mmoja. Ali alitoka mbele, na, akimvamia, kwa pigo moja la upanga wake alimuan-gusha chini. Muhammad, ambaye aliliangalia kwa makini pambano hilo la haraka, aliguta kwa mshangao, kwa sauti kubwa: "Allah-u-Akbar!" na mguto huo, ukirudiwa, ulipaa kwa sauti kubwa mno kutoka kwenye jeshi zima la Waislamu."

(The Life of Muhammad, London, 1877)

Muhammad Husein Haykal:

"Talha ibn Abu Talha, mshika bendera wa Makka, alichomoka mbele akiwataka Waislamu kupambana naye. Ali ibn Abu Talib alitoka mbele kupigana naye. Pambano hilo lilikwisha mara wakati Ali alipompiga adui yake dhoruba moja kali sana. Kwa furaha kuu, Mtume (s.a.w.) na Waislamu walipiga ukelele mkubwa, "Allah-u-Akbar."

(The Life of Muhammad, 1935, Cairo)

143

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

R.V.C.Bodley:

"Watu wa Makka, wakisaidiwa kwa ukarimu sana na wanawake ambao walileta vigo-ma vyao, walirusha matusi kwa Waislamu. Haya yalipokelewa na Hind, mke wa Abu Sufyan, ambaye aliongoza vipokeo vya shangwe alipokuwa akicheza kulizunguka lile sanamu lililokuwa limekaa juu ya ngamia.

Talha, yule mshika-bendera wa wapagani wa Kiquraishi, alikuwa ndiye mtoa chang-amoto wa kwanza wa watu wa Makka. Vile alipotoka kwenye safu za Abu Sufyan, Ali alitoka kwenye safu za Muhammad. Watu wawili hawa wakakutana katikati ya 'ardhi isiyo na mwenyewe.' Bila ya maneno au madoido ya kutangulia, pambano likaanza. Talha kamwe hakupata nafasi. Jambia la Ali liliwaka katika lile jua la asubuhi na kich-wa cha mshika-bendera huyo kiliruka kutoka kwenye mabega yake na kikabingirika kwenye mchanga.

'Allah-u-Akbar! aliguta Muhammad. 'Allah-u-Akbar!' 'Allah-u-Akbar!' ilirudiwa kutoka kwa Waislamu waliokuwa wakiangalia kwa shauku."

(The Messenger, the Life of Muhammad, New York, 1946)

Sir John Glubb:

"Zile safu mbili zilisogea kutoka kila upande. Talha ibn Abdul Uzza, wa Abdul Dar, akiungua kwa chuki juu ya dhihaka za Abu Sufyan, na akiwa amebeba bendera ya Maquraishi, alitoka nje mbele ya safu na akatoa changamoto kwa mwislamu yoyote kwenye pambano la mtu mmoja mmoja. Ali alichepuka mbele na akamuua kwa pigo moja la upanga wake, huku bendera ya Maquraishi ikidondoka chini. Kutoka kwenye safu za Waislamu ikatoka sauti kubwa, "Allah-u-Akbar, Mungu ni Mkuu."

(The Life and Times of Muhammad)

Hili ni moja ya maonyesho ya kuvutia katika historia ya Uislamu. Muhammad, Mjumbe wa Allah (s.w.t.) alikuwa akimwangalia binamu yake, Ali, akipambana, na alisisimuliwa na ushindi wake wa haraka. Wakati lile pigo zito la upanga wa Ali lilipomuua jenerali wa wapagani, Muhammad alipiga ukelele Allah-u-Akbar, na ukelele huo wa kivita ulifuatish-wa na jeshi zima la Uislamu.

Pigo la Ali lisilozuilika limesababisha bendera ya watu wa Makka, ile nembo ya uabudu masanamu na ushirikina, kuanguka chini kwenye vumbi. Alishinda raundi ya kwanza kwa Uislamu, na alikuwa ametoa pigo la kifo kwenye hamasa ya Maquraishi.

144

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wakati Ali aliporudi kwenye safu zake, ndugu yake Talha, Uthman ibn Abu Talha, alifanya jaribio la kuipata tena ile bendera ya Makka. Lakini Hamza akatoka kwenye safu za Waislamu, na akamuua.

Muhammad Husein Haykal:

"Wakati Ali alipomuua yule mshika-bendera wa Makka, Talha ibn Abu Talha, ilinyanyuliwa mara moja tena na Uthman ibn Abu Talha. Na pale Uthman alipoanguka mikononi mwa Hamza, ilinyanyuliwa tena na Abu Sa'd ibn Abu Talha. Mara alipoinyanyua ile bendera ya Makka aliwakemea Waislamu: "Mnajidai kwamba mashahidi wenu wako peponi na wetu wako motoni? Wallahi, mnadanganya! Kama mmoja wenu kwa ukweli anaamini habari kama hiyo, naaje hapa mbele apigane na mimi." Changamoto yake ilimvuta Ali ambaye alimuua papo hapo. Hawa Banu Abd al Dar waliendelea kuishika bendera ya Makka mpaka wakapoteza watu tisa."

(The Life of Muhammad)

Ali, simba kijana, peke yake aliuwa washika bendera nane wa waabudu-masanamu wa Makka. Ibn Athir, yule mwanahistoria wa Kiarabu, anaandika katika Tarikh Kamil: "Mtu aliyewaua washika-bendera wa wapagani alikuwa ni Ali." Baada ya kifo cha mshika-bendera wake wa tisa, Abu Sufyan aliliamuru jeshi lake kusonga na kushambulia mipango ya Waislamu. Wakati Mtume (s.a.w.) alipoliona jeshi likisogea, yeye pia aliwatahadharisha Waislamu. Alishika upanga kwenye mkono wake, na akautoa kwa yeyote ambaye angeweza kuuletea heshima. Baadhi ya waliokuwa na matumaini walitokeza mbele yake kuuchukua lakini akawanyima.

Muhammad Ibn Ishaq :

"Mtume (s.a.w.) alivaa makoti mawili ya deraya katika siku ya vita vya Uhud, na alichukua upanga na akaupunga akisema: "Ni nani atauchukua upanga huu na haki yake?" (yaani, kuutumia kama ipasavyo na unavyostahili kutumiwa). Baadhi ya watu walisimama ili kuuchukua lakini aliuzuilia kuwapa mpaka Abu Dujana Simak bin Kharasha, ndugu yake B. Saida, aliposimama na kuuchukua.

Umar alisimama kuuchukua, akisema: "Nitauchukua pamoja na haki yake," lakini Mtume (s.a.w.) aligeukia pembeni na alikokuwa na akaupunga mara ya pili akitumia maneno yale yale. Kisha Zubayr bin al-Awwam akasimama naye pia akakataliwa, na wawili hawa wakawa wamefedheheka sana."

(The Life of the Messenger of God)

145

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mtume (s.a.w.) alimpa upanga huo Abu Dujana, mmoja wa Ansari. Aliuchukua na akautu-mia kama ulivyostahili kutumiwa. Alithibitisha ile imani bwana wake aliyokuwa amemuwekea. Wale wanawake wa Makka walikuwa wamekaa kitako juu ya ngamia wao na walikuwa wakiangalia lile tendo la haraka. Jeshi lao liliposonga mbele kushambulia Waislamu, na wao pia waliingia kazini. Walianza kuwachochea wapiganaji wao kuwaua Waislamu. Waliimba nyimbo ambazo zilikuwa zimejaa ukaribisho na dharau - ukaribisho kwa mashujaa wao na dharau kwa wale waoga. Kwa muziki wao na ushairi wao wenye ushawishi wa hali ya juu, waliwachochea watoto hao wa jangwani wenye pupa kwenye ghadhabu za kupigana.

Betty Kelen:

"Vikiwa vimejengwa juu kabisa ya ngamia wengi vilikuwa ni vibanda vidogo, au machela, ambamo walipanda kikosi cha wanawake waliofunzwa vyema na Hind kuimba tenzi za kivita ambazo zitawaweka wanaume wao katika msisimko au ghadhabu na kupinga woga.

Vita viliungwa. Hind na wanawake wenzie walisonga mbele pamoja na majeshi, wak-itawanyika uwanjani kwa karibu sana kiasi walivyoweza kuthubutu kuwafikia wale wanaume wanaopigana, huku wakipiga vigoma vyao kwa mpigo mkali na wakike-mea:

"Mabinti wa Nyota ya Asubuhi inayong'ara, Wakiwaangalieni kutoka kwenye vitanda vyenye hariri ni sisi, Wacharazeni! Katika mikono yetu tutawakumbatia; Kimbieni, na kamwe tena hatutawashikeni."

(Muhammad, the Messenger of God)

Muhammad Husein Haykal:

"Hapo kabla wanawake wa Kiislam (huko Arabuni) walikuwa wakijionyesha sio tu kwa waume zao bali kwa wanaume wengine wowote waliowataka. Walikuwa waki-toka nje kwenye sehemu za wazi mmoja mmoja au katika vikundi na kukutana na wanaume na vijana bila ya kizuizi au hisia ya aibu. Waliangaliana kwa hisia kali na vidhihirisho vya mapenzi na tamaa. Hili lilifanyika kwa ukweli wa wazi na ukosefu wa aibu kwamba Hindi, mke wa Abu Sufyan, hakuwa na haya yoyote juu ya kuimba katika wakati wa hadhara na wa hatari kama Siku ya Uhud.

"Songeni mbele nasi tutawapiga pambaja nyie! Songeni mbele na sisi tutatandaza mabusati kwa ajili yenu! Geuzeni migongo yenu nasi tutawaepuka ninyi! Geuzeni migongo yenu nasi kamwe hatutawajieni ninyi."

146

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Miongoni mwa idadi ya makabila, uzinzi haukuonekana kamwe kama ni kosa kubwa. Kucheza kimapenzi na kufanya urafiki na mwanamke vilikuwa ni matendo ya kawai-da. Mbali na cheo maarufu cha Abu Sufyan na jamii yake, wana tarikh wanasimulia, kuhusu mke wake, Hadith nyingi mno za mapenzi na hisia kali na wanaume wengine bila ya kuweka doa lolote juu ya heshima yake".

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Watu wa Makka walijiandaa vema na walikuwa wengi zaidi kuliko Waislamu. Zaidi ya hayo, kuwepo katika uwanja wa vita, kwa mungu wao, Hubal, na wanawake wao, ulikuwa ni uhakikisho kwamba hamasa yao haitalegea, hususan, baada ya hawa wanawake kuwa wameingiza kwenye mapambano, kisaidizi kipya na cha kuhatarisha cha kishawishi.

Lakini licha ya manufaa haya ya dhahiri na yasiyo dhahiri, hawa watu wa Makka walikuwa wakifanya maendeleo, kidogo, kama yalikuwepo. Kwa kweli, hapo mwanzoni, vita vilielekea kwenda dhidi yao.

D.S.Margoliouth:

"Inaelekea pia kwamba katika kuanza mambo yalikuwa yakienda kama vile Mtume (s.a.w.) alivyodhania. Wale mashujaa wa Badr, Ali na Hamza, walisababisha vifo bila kizuizi kama hapo kabla; ujasiri wa Kiquraishi ulilazimika kukutana na mashujaa hawa katika mwandamano wa mapambano ya mtu mmoja mmoja, ambamo mashujaa wao wenyewe waliuawa, na kuangushwa kwao kulieneza mfadhaiko na hofu."

(Muhammad and the Rise of Uislamu, London, 1931)

Shambulizi la Ali, Hamza na Abu Dujana lilieneza hofu na fadhaa katika safu za Makka, na wakaanza kuyumba. Waislamu wakaendeleza fursa yao.

Sir John Glubb:

"Ali ibn Abi Talib aliendelea bila hofu kwenye safu za adui - ilikuwa ni Badr tena; Waislamu walikuwa wasioshindika."

(The Great Arab Conquest, 1963)

Ali alizivunja safu za Maquraishi, na alikuwa tayari yuko ndani kabisa ya safu zao. Wakishindwa kuhimili shambulizi lake, walianza kuachia uwanja. Akiwa hayuko mbali naye, ami yake, Hamza, alikuwa akishughulika kukata njia yake kati ya kundi kubwa la maadui. Kati yao, walikuwa wakilisaga jeshi la Maquraishi.

147

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ilikuwa ni katika wakati huu ambapo matukio mawili yalitokea ambayo yalisababisha mpinduko katika mafanikio ya Waislamu, na ambayo yaliwanyang'anya ushindi kutoka mikononi mwao. La kwanza lake likiwa ni kifo cha Hamza.

Hinda, mke wa Abu Sufyan, alikuwa amekuja kutoka Makka na mtu mmoja, Wahshi, mtumwa wa Kihabeshi, kuja kumuua Hamza, na alikuwa amemuahidi kumpa sio tu uhuru wake bali pia na dhahabu nyingi, madini ya fedha na hariri katika kufanikiwa kwake. Alikuwa anafahamika kwa ustadi wake katika kutumia silaha ya "taifa lake", mkuki.

Wahshi alijificha nyuma ya jiwe akingojea wasaa wa fursa, na mara ukatokea. Pale tu Hamza alipomuua muabudu-sanamu mmoja, na akamrukia mwingine, Wahshi akasimama, akachukua shabaha kali, na akairusha ile silaha ya kombora ambayo kwayo hapakuwa na kinga dhidi yake. Mkuki huo ukampata Hamza kwenye kinena. Alianguka chini na akafa karibu mara moja.

Tukio jingine lilihusisha sehemu kuu ya jeshi la Madina. Kutetereka na kuchanganyikiwa kwa jeshi la Makka kulikuwa kunaonekana wazi kabisa kwa muda huu, na Waislamu walichukulia kwamba tayari wamekwishapata ushindi. Kwa shauku kubwa ya kutokosa fursa ya kumpora adui, walisahau nidhamu yao. Hila hii iligunduliwa na wale wapiga mishale waliokuwa wamewekwa na Mtume (s.a.w.) pale katika kijinjia muhimu cha mlimani. Wao pia walidhania kwamba adui alikuwa amekwisha shindwa, na alikuwa anakimbia. Walifikiri kwamba kama wenzao kule kwenye uwanja wa vita watakamata mizigo ya adui, basi wao wenyewe watapoteza sehemu yao ya ngawira. Hofu hii iliwachochea wao kushuka kule chini bondeni dhidi ya amri halisi ya Mtume. Kapteni wao, Abdullah ibn Jubayr, aliwasihi wasiache kile kijinjia lakini hawakumsikiliza, na wakaenea ndani ya bonde. Tamaa yao ya ngawira iliwanyima Waislamu ushindi katika vita vya Uhud!

Sasa, jenerali mmoja wa Makka, Khalid bin al-Walid, akagundua kwamba kile kijinjia muhimu upande wa kushoto wa jeshi la Madina hakikuwa na ulinzi. Yeye haraka sana akaichukua fursa hiyo kuwashambulia askari doria wachache waliokuwa bado wapo pale kwenye kinjia kile, kwa wapanda farasi wake. Wale doria walipigana kishujaa lakini wote pamoja na Abdullah ibn Jubayr, walizidiwa nguvu, na wakauawa. Mara moja Khalid akakiteka kinjia kile, akalishambulia lile jeshi la Madina kwa kutokea nyuma.

Lile jeshi la Madina lilikuwa linashughulika kukusanya ngawira, bila kuelewa kabisa kitu kingine chochote kile. Ghafla, lilishitukizwa na shambulio la lile jeshi la farasi la Makka nyuma yao. Abu Sufyan pia aliigundua hila ya Khalid, na ule mkanganyiko wa Waislamu. Alikusanya upya vikosi vyake, akarudi kwenye uwanja wa mapambano na kuanzisha mashambulizi ya mbele juu yao. Sasa wakajikuta wameshikwa katika mashambulizi ya mbele na nyuma ya maadui, na wakahofu. Ilikuwa sasa ni zamu yao kushindwa. Walianza

148

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kukimbia lakini bila kujua ni upande gani wa kukimbilia, na kila mmoja alikimbia na njia yake.

Mshangao haukuishia kwa askari wa kawaida wa jeshi la Waislamu tu; ulikuwa ni wa jumla. Baadhi ya maswahaba wakuu wa Mtume (s.a.w.) walikumbwa pamoja na wengine kabla ya shambulizi la adui. Miongoni mwa waliokimbia walikuwa wote Abu Bakr na Umar. Inasimuliwa na Anas bin Nadhr, ami yake Anas bin Malik, kwamba Abu Bakr alisema katika nyakati za baadae kwamba pale Waislamu walipokimbia kutoka kwenye vita vya Uhud, na wakamuacha Mtume wa Allah (s.a.w.) yeye alikuwa wa kwanza kurudi kwake. Umar mara nyingi alisema kwamba wakati Waislamu waliposhindwa huko Uhud, alikimbia na kupanda kwenye kilima (Tarikh Tabari, juz. IV, uk. 96). Baadhi ya maswahaba waliweza kufika Madina na wengine walitafuta hifadhi kwenye mapango na makorongo ya mlima.

Uthman bin Affan, khalifa wa tatu wa Waislamu baadae, hakushiriki katika vita vya Badr lakini alikuwepo Uhud. Hata hivyo, aliiona milio ya migongano ya panga na mikuki imezi-di kiasi kidogo katika ujasiri wake, na alikuwa miongoni mwa wakimbizi wa mwanzo. Sheikh Muhammad Khidhri Buck anasema katika kitabu chake cha wasifu wa Mtume (s.a.w.) kwamba Uthman alikuwa mtu mwenye aibu sana, na kwamba ingawa alikimbia kutoka kwenye uwanja wa vita, hakuingia Madina. Kuwa na aibu kwake kulimzuia kufanya hivyo.

Pale Waislamu walipokuwa wanakimbia kupita alipokuwapo Mtume, alijaribu kuwazuia lakini hakuna hata mmoja aliyejaribu kumsikiliza. Katika muda mfupi mambo yali-wageukia, na ushindi ukakwapuliwa kutoka mikononi mwao. Ilikuwa ni gharama iliyokuwa wailipe kutokana na kukosa utii kwa Mtume wao, na kwa shauku ya wasiwasi juu ya kukusanya ngawira.

Ufuatao ni ushuhuda wa Qur'an Tukufu juu ya mwenendo wa Waislamu katika vita vya Uhud

Usahihi-10.jpg

"Tazama! Mlikuwa mnapanda juu ya mlima, Bila ya kutupa jicho la pembeni kumuangalia yeyote yule, Na Mtume akiwa nyuma yenu anawaiteni mrudi. Hapo Allah akawapeni dhiki baada ya dhiki kwa njia ya kukulipisheni, kuwafundisha msisikitikie ngawira iliyowakoseni, na kwa (madhara) yaliyokufikeni. Kwani Allah ni Mwenye kujua yote mnayoyafanya." (Sura 3: Aya ya 153)

149

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mtume (s.a.w.) alikuwa amempa bendera ya Uislamu ami yake, Masaab ibn Umayr, kati-ka vita vya Uhud. Aliuawa na adui, na ile bendera ya Uislamu ikaanguka chini. Wakati Ali alipoona ile bendera inaanguka chini, alikurupuka mbele, akaisimamisha, na akainyanyua juu mara nyingine tena.

Washington Irving:

"Hamza alichomwa na mkuki wa Wahshi, yule mtumwa wa Kihabeshi, aliyekuwa ameahidiwa uhuru wake kama angemuua Hamza. Musaab ibn Umayr, pia, aliyekuwa amebeba bendera ya Muhammad, aliangushwa chini, lakini Ali aliikamata ile bendera tukufu, na akainyanyua juu sana katikati ya wimbi la vita.

Kwa vile Musaab alifanana sana na Mtume (s.a.w.) mwenyewe, ukelele ulitolewa na adui kwamba Muhammad ameuawa. Maquraishi walitiwa moyo na hamasa maradu-fu kwa kusikia sauti hiyo; Waislamu wakakimbia kwa kukata tamaa, wakiwa wame-wabeba pamoja nao Abu Bakr na Umar, ambao walikuwa wamejeruhiwa."

(The Life of Muhammad) Muhammad Husein Haykal:

"Wale waliodhania kwamba Muhammad alikuwa amekufa, ikiwa ni pamoja na Abu Bakr na Umar, walikwenda kuelekea mlimani na wakakaa chini. Wakati Anas ibn al-Nadr alipouliza ni kwa nini wanakata tamaa mapema hivyo, na akaambiwa kwamba Mtume wa Allah (s.a.w.) alikuwa ameuawa, akajibu kwa ukali: "Na mtajifanyia nini nyie wenyewe na maisha yenu baada ya Muhammad kufa? Simameni, na mfe kama alivyokufa yeye." Akageuka, akashambulia dhidi ya adui, na alipigana kwa ushujaa sana (mpaka akauawa)."

(The Life of Muhammad, 1935, Cairo)

Waislamu wengi walikuwa wamekimbia kutoka kwenye uwanja wa vita lakini Ali alikuwa bado anapigana. Alikuwa amebeba bendera ya Uislamu kwenye mkono mmoja, na upanga katika ule mwingine. Yeye pia aliusikia ule ukelele "Muhammad amekufa." Lakini ulim-fanya kutojali sana juu ya maisha yake mwenyewe.

Mtume, hata hivyo, alikuwa kwenye sehemu nyingine ya uwanja wa mapambano. Alikuwa amejeruhiwa, na kichwa chake na uso ulikuwa unatoka damu. Waislamu wachache, zaidi hasa Ansari, walikuwa wakimlinda. Lilikuwa ni kundi hili dogo, na kelele zao za kivita ndivyo vilivyovuta nadhari ya Ali. Alipasua njia yake katikati ya mistari ya adui na akawafikia wapiganaji wenzie. Walikuwa wamesimama kumzunguka Mtume, na wakion-gozwa na Abu Dujana, walikuwa wakifanya kila walichoweza kumkinga Muhammad

150

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kutokana na silaha za makombora za adui. Ali alisisimka kumwona bwana wake akiwa hai bado lakini hakuwa na muda wa kuswalimiana. Wale waabudu-sanamu walikuwa wamean-za upya mashambulizi yao, na sasa ilikuwa ni Ali ambaye alipaswa kuwapiga kuwarudisha nyuma. Walishambulia kwa marudio lakini aliwakwamisha kila mara.

Muhammad Husein Haykal:

".. wakati mtu mmoja alipokemea kwamba Muhammad ameuawa, vurugu zilichukua madaraka kamili, hamasa ya Waislamu ilishuka chini na wapiganaji wa Kiislamu walipigana kwa mtawanyiko na bila ya lengo. Vurugu hizi zilihusika na kumuua kwao Husayl ibn Jabir Abu Hudhayfah kwa makosa, kwani kila mtu alitafuta kuokoa maisha yake mwenyewe kwa kukimbia isipokuwa watu kama Ali ibn Abi Talib ambaye Allah (s.w.t.) alimuongoza na kumlinda."

(The Life of Muhammad, 1935, Cairo)

Katika vita vya Uhud, wengi wa maswahaba waliotangazwa kuwa majasiri sana na waaminifu, waliwageuzia migongo maadui, na wakakimbilia kujificha. Lakini walikuwe-po wachache ambao hawakukimbia. Mmoja wao alikuwa ni Ummu Ammarra Ansariyya, bibi kutoka Madina. Alikuwa muumini asiyekuwa na hofu, na Waislamu wote wanaweza kwa haki kabisa kujivunia ujasiri wake. Alitambulikana kwa ujuzi wake kama daktari na muuguzi, na alikuja Uhud pamoja na jeshi la Madina.

Mwanzoni mwa vita hivyo, Ummu Ammarra Ansariya alileta maji kwa ajili ya wapiganaji hao au aliwahudumia kama walikuwa wamejeruhiwa. Lakini Waislamu waliposhindwa na wakakimbia kutoka kwenye uwanja wa vita, wajibu wake ulibadilika kutoka ule wa muuguzi kuwa wa mpiganaji. Wakati mmoja maadui walileta watupa mishale ili kumrushia mishale Mtume. Ummu Ammarra alichukua ngao kubwa na akaishikilia mbele yake kumlinda kutokana na yale makombora yanayoruka.

Muda mfupi baadae, watu wa Makka wakashambulia kwa panga na mikuki ambapo Ummu Ammarra alitupa ile ngao, na akawashambulia kwa upanga. Muabudu-sanamu mmoja akaja kwa hatari karibu sana na Mtume (s.a.w.) lakini Ummu Ammarra akaja mbele yake, na wakati yule muabudu-sanamu alipotupa dhoruba, pigo hilo liliangukia begani mwake. Ingawa Ummu Ammarra alikuwa amejeruhiwa, hakuingiwa na hofu, na kwa dhamiri kabisa akasimama kati ya Mtume (s.a.w.) na maadui zake, akiwadharau wao na kutoogopa kifo.

Wakati huo kulikuwa na utulivu wa muda katika mapigano. Kwa kuchukua fursa hiyo, Ali alimtoa Mtume (s.a.w.) kutoka kwenye ile sehemu ya hatari mpaka kwenye pango ambako angeweza kupata mapumziko kidogo, na ambako majeraha yake yangeweza kufungwa.

151

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

D.S.Margoliouth:

"Yule shujaa Ali pamoja na (baadhi) watu wengine majasiri walipomuona (Mtume) walimbanisha faraghani kwenye pango ambako angeweza kuuguzwa."

(Muhammad and the Rise of Islam)

Fatmah Zahra, binti ya Mtume, alikuja kutoka mjini pamoja na kikundi cha wanawake wa Kiislam aliposikia habari za kushindwa kwa Waislamu. Ali alileta maji katika mbonyeo wa ngao yake, na Fatmah Zahra akaiosha damu kutoka kwenye uso wa baba yake, na akam-funga majeraha yake.

Wajibu wa wale Wanawake wa Makka

Kufukuzwa kwa Waislamu kutoka kwenye uwanja wa vita kulikuwa ni mwaliko kwa wale wanawake kutoka Makka kutafuta na kupata kutosheleza hamu yao ya kuua juu ya miili ya wale mashahidi. Walikata pua zao, masikio, mikono na miguu, na waliwapasua matumbo yao, wakatoa viungo, na wakavifanya mikufu kama mashada ya ushindi wa vita.

Muhammad ibn Ishaq:

"Saleh bin Kaysan aliniambia kwamba Hind, binti ya Utba, na wale wanawake aliokuwa nao, waliwakatakata maswahaba wa Mtume (s.a.w.) waliokufa. Waliwakata masikio yao na puazao na Hind akatengeneza kutokana navyo bangili za miguuni na skafu na akatoa bangili (zake mwenyewe) na skafu na vidani kwa Wahshi, yule mtumwa wa Jubayr bin Mutim. Alikata ini la Hamza na akalitafuna, lakini hakuweza kulimeza na akalitupilia mbali.

Al-Hubab bin Zabban, kaka yake B. Harith bin Abdu Manat, ambaye wakati huo alikuwa ndiye mkuu wa vile vikosi vya watu weusi, alipita karibu na Abu Sufyan alipokuwa anaichoma pembe ya mdomo wa Hamza kwa ncha ya mkuki wake, akise-ma: "Onja hiyo, wewe muasi." Hulays aliguta kwa mshangao, "Oh! Banu Kinana, hivi huyu ndiye mkuu wa Maquraishi anayefanya hivyo kwa binamu yake aliyekufa kama mnavyoona?"

(The Life of the Messenger of God)

Waislamu Sabini na tano waliuawa kwenye vita vya Uhud, na miili ya wengi wao ilikat-wakatwa na Hinda na wale wanawake makatili wengine kutoka Makka.

Chuki juu ya Muhammad, Ali na Hamza ilikuwa ni moto ambao ulimmeza Hinda. Ingawa Hamza peke yake alikuwa ndio muathirika wa uchu wa ula-binadamu wa Hinda katika vita

152

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

vya Uhud, Muhammad na Ali hawangetegemea kutendewa kwa tofauti yoyote kutoka kwake kama wangeangukia mikononi mwake. Aliirithisha chuki yake juu ya Muhammad na Ali kwa wanae na wajukuu zake, na vizazi vitakavyofuatia.

Kuondoka kwa Jeshi la Makka.

Baada ya mshituko wa kwanza wa kushindwa ulipopita, baadhi ya Waislamu walirudi kwenye uwanja wa mapambano. Abu Bakr na Umar walikuwa miongoni mwao. Wao pia waliingia kule kwenye pango ambako Ali alimpeleka Mtume.

Kwa wakati huu, Abu Sufyan ambaye alikuwa tayari kurudi Makka, anaelezwa kuwa alikuja karibu na lile pango. Akiwa amesimama chini ya vile vilima, alibishana kidogo na Umar.

Sir John Glubb:

"...Maquraishi wangeweza kuupanda Mlima Uhud kwa gharama ya majeruhi wachache na kuweza kumuua Mtume wa Allah (s.a.w.) na kile kikundi kidogo cha wafuasi waliojitoa ambao walibakia pamoja naye. Pale Abu Sufyan alipomuuliza Umar ibn al-Khatab kama Muhammad alikuwa amekufa, alimjibu, "Hapana, Wallahi, anakusikia unavyoongea." Lakini haikumjia Abu Sufyan kuchukua fursa hiyo ya uvunjaji hatari wa usalama.

Ukatili wa kinyama wa mauaji hay a (katika vita vya Uhud) unafafanua kwa mara nyingine tena ile tofauti ya kipekee kati ya mapigano rahisi na mara nyingi ushujaa ya Waarabu na unyama wa uadui baina ya koo mbili. Abu Sufyan anazungumza kwa maelewano na Umar ibn al-Khatab kwenye uwanja wa vita wa Uhud, kwani hakuna kati yao aliyeua ndugu wa mwenzie. Lakini mke wa Abu Sufyan, Hinda, binti ya Utba ibn Rabia, anaikatakata maiti ya Hamza, aliyemuua baba yake."

(The Life and Times of Muhammad)

Maquraishi walidhania wamemaliza kazi yao. Walikuwa wamewashinda Waislamu na wameokoa heshima yao. Hivyo wenyewe wakiwa wameridhika, waliondoka kwenye uwanja wa vita na wakaelekea kwenye mji wao wa nyumbani upande wa Kusini. Lakini Mtume, akiwa bado hana uhakika na nia zao, alimtuma Ali kwenda kuwaangalia kwa mbali na kumpa taarifa za mienendo yao.

Ali alirudi na kukmfahamisha Mtume (s.a.w.) kwamba Maquraishi wameshaipita Madina, na walikuwa wakienda kuelekea Makka. Hii ilimhakikishia Mtume. Waislamu ndipo wakashuka kutoka mlimani, wakawaswalia maiti wao, na wakawazika.

153

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali na Vita vya Uhud

Katika vita vya Uhud, Ali alimuua mshika-bendera wa kwanza wa jeshi la wapagani. Wakati mshika-bendera huyo alipoanguka chini, na bendera pia ilianguka chini pamoja naye. Ali kwa hiyo aliiangusha nembo ya upagani.

Baadae, vita vilipokuwa vinachachamaa, wapagani walimuua Musaab ibn Umayr, mshika-bendera wa jeshi la Waislamu. Musaab alianguka chini, na bendera pia ikaanguka pamoja naye. Lakini muda uliofuata tu, Ali akatokea; aliinyanyua ile bendera iliyoanguka kutoka ardhini, na akaikunjua kwa mara nyingine. Alikuwa kwa hiyo sawasawa kama ishara ya kuangamia kwa uabudu-sanamu na ushirikina kama alivyokuwa ishara ya kunyanyuka na kuzaliwa-upya kwa Uislamu. Hapo Uhud, rafiki na adui wote waliona kwa macho yao yale matendo ya ajabu ya ushujaa na ujasiri wa Ali, na kujitolea kwake kwa bwana wake, Muhammad, Mtume wa Allah (saw) Ali alipigana vile vita vya Uhud kwa ule upanga mashuhuri, Dhu'l-Fiqar.

Muhammad ibn Ishaq:

"Upanga wa Mtume (s.a.w.) ulikuwa unaitwa Dhu 'l-Fiqar. Muhadithin mmoja alinieleza kwamba Abu Najih alisema, 'Mtu mmoja aliguta katika vita vya Uhud:

'Hakuna upanga ila Dhu 'l-Fiqar Na hakuna shujaa kama Ali. "

(The Life of the Messenger of God)

Katika mikono ya Ali, Dhu'l-Fiqar ulikuwa ni radi iliyoshambulia na kuumaliza upagani, uabudu masanamu na ushirikina. Lakini kwa Uislamu, ulikuwa ndio mletaji wa matumai-ni, nguvu mpya, maisha mapya, na heshima, utukufu na ushindi. Akielezea juu ya matukio ya Uhud, kufuatia kutimuliwa kwa Waislamu wakati Mtume (s.a.w.) alipokuwa amesham-buliwa na maadui zake, M. Shibli, yule mwanahistoria wa Kihindi, anasema:

Ilikuwa ni wakati mbaya sana katika historia ya Uislamu. Waabudu-masanamu wal-imshambulia Mtume wa Allah (s.a.w.) kama miungu ya ghadhabu ya hadithini lakini kila mara walizuiwa kwa ncha ya Dhu'l-Fiqar.

Shibli anaendelea kusema kwamba hao waabudu-masanamu walikuja kama "mawingu meusi na ya kutisha, tayari kuwapasukia Waislamu." Kama Ali asingeyapunguza nguvu mashambulizi ya watu wa Makka, basi kupasuka kwa wingu huku kungeikumba Madina, na Uislamu ungesombwa katika mafuriko ya uabudu-masanamu. Kama Ali pia angeshind-wa katika wajibu wake kama wengine wengi walivyoshindwa, waabudu-masanamu hawa wangemuua Mtume wa Allah (s.a.w.) na wangeuzima mwanga wa Uislamu. Lakini Ali na

154

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Waislamu wengine wachache, wakiwa ni pamoja na Abu Dujana na Ummu Ammarra Ansariyya, walilizuia balaa hili. Katika vita hivi vya kuhuzunisha, Waislamu 75 waliuawa. Kati yao wanne walikuwa ni Muhajir, na waliobakia walikuwa ni Ansari.

Mashahidi wa Uhud

Tukio la kusikitisha sana kati ya matukio ya vita vya Uhud lilikuwa ni kifo cha Hamza na kuharibiwa kwa mwili wake. Baada ya kuondoka kwa watu wa Makka, Mtume (s.a.w.) alikwenda kuona maiti ya ami yake.

Masikio na pua vilikuwa vimekatwa; tumbo limepasuliwa, na viungo vyake vilikuwa vimeondolewa. Alijawa na huzuni kwa kuuona mwili ule wa shahidi katika hali ile, na akaamuru ufunikwe.

Hinda, mke wa Abu Sufyan, na mama yake Mu'awiyyah, anaitwa "mla-ini" katika historia ya Uislamu. Ibn Ishaq anasema kwamba alilitafuna ini la Hamza lakini hakuweza kulimeza. Lakini Ibn Abdul Birr anasema katika kitabu chake, Al-Isti 'aab, kwamba kwa kweli alitengeneza moto katika uwanja wa vita hivyo, akalichoma ini la Hamza kwenye moto huo, na akalila!

Wakati Mtume (s.a.w.) aliporudi Madina, alivisikia vilio vya huzuni vya watu wa zile familia zilizoondokewa. Ndugu na jamaa wa mashahidi wa Uhud walikuwa wanawaom-boleza watu wao waliokufa.

Alimaka kwa mshangao: "Wapi! Hakuna hata mtu wa kuomboleza kifo cha ami yangu, Hamza." Viongozi wa Ansari kusikia kauli hii, wakaenda majumbani kwao, na wakawaa-muru wanawake zao kwenda kwenye nyumba ya Mtume, na kuomboleza kifo cha ami yake.

Wakati huo kundi la wanawake wa Madina likakusanyika katika nyumba ya Muhammad, na wote walikililia kifo cha huzuni cha Hamza, shujaa wa Uislamu.Mtume (s.a.w.) akaom-ba baraka za Allah (s.w.t.) juu yao wote. Baada ya hapo ikawa ni desturi hapo Madina kwamba wakati wo wote mtu yoyote akifa, waombolezaji wake walianza vilio vyao kwa nyimbo za maombolezo ya Hamza.

Watu wa Madina walianza kwanza kumuombeleza Hamza kisha wakawaombolezea watu wao wenyewe waliokufa.

155

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad Ibn Ishaq:

"Mtume (s.a.w.) alipita kwenye makazi ya Banu Abdul Ashal na Zafar na akawasikia wakilia kwa ajili ya wafu wao. Macho yake yalijawa na machozi na akasema: "Lakini hakuna wanawake wanaolia kwa ajili ya Hamza." Wakati Sa'd bin Mu'adh na Usayd bin Hudayr waliporudi majumbani kwao, waliwaamuru wanawake zao kujitayarisha na kwenda kulia kwa ajili ya ami yake Mtume (s.a.w.)

(The Life of the Messenger of God)

Mbali na Hamza, Muhajirina wengine watatu walipata taji la kufa kishahidi katika vita vya Uhud. Walikuwa ni Abdullah ibn Jahash, binamu yake Mtume; Masaab ibn Umayr, ami yake Mtume; na Shams ibn Uthman. Hasara kwa Ma-Ansari ilikuwa kubwa sana. Waliacha maiti sabini na moja hapo uwanjani, na wengine wengi waliojeruhiwa. Allah (s.w.t.) awape rehema hao wote.

Vita vya Uhud vilikuwa ni wakati wa majira ya upinzani wa kipagani kwa Uislamu. Ingawa walikuwa washindi kwenye vita, Maquraishi hawakuweza kufuatilia na kufaidi ushindi wao, na mafanikio yao yalibadhirika mara tu.

156

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kuzaliwa kwa Hasan na Husein

Mnamo tarehe 15 ya mwezi wa Ramadhani ya mwaka wa 3 H.A. (Machi, 625), Allah (s.w.t.) aliridhia kumbariki binti ya Mtume Wake, Muhammad, kwa kuzaa mtoto wake wa kwanza. Muhammad Mustafa alikuja akionyesha furaha; alimchukua mtoto mchanga huyo mikononi mwake, akambusu, akamsomea adhana kwenye sikio lake la kulia, na iqamah kwenye sikio lake la kushoto; na akamwita Hasan.

Mwaka mmoja baadae, yaani, mnamo tarehe 3 Shaaban ya mwaka wa 4 H.A. (Februari, 626), Allah (s.w.t.) aliridhia kumpa binti ya Mtume Wake, mwanae wa pili. Mtume (s.a.w.) akaja, mwenye tabasamu na furaha, akamchukua mtoto huyo mikononi mwake, akambusu, akamsomea adhana kwenye sikio lake la kulia, na iqamah kwenye sikio lake la kushoto, na akamwita Husein.

Kuzaliwa kwa kila mmoja wa mabwana hawa kulikuwa ni tukio la kufurahia kwa Muhammad. Aliwachukulia kama miongoni mwa baraka kubwa za Allah (s.w.t.) na akamshukuru Yeye kwa ajili yao. Katika kuzaliwa kwa kila mmoja wao, Waislamu walim-iminika kwenye ule Msikiti Mkubwa na kumpongeza yeye. Aliwapokea kwa tabasamu na shukurani, na akashirikiana furaha yake pamoja nao.

Hapakuwa kamwe na siku ambayo Mtume (s.a.w.) hakutembelea nyumba ya binti yake kuwaona watoto wake. Alipendelea kuwaona wao wakitabasamu, hivyo aliwachekesha na kuwarusharusha; Aliwakumbatia na kuwadekeza, na alichukulia kila hatua yao na kila neno kama shani.

Wakati mabwana hawa wawili walipokua kidogo, na wakawa wanaweza kutembea hapa na pale, mara nyingi sana walitoka nje ya nyumba yao kuingia Msikitini. Kama babu yao alikuwa katikati ya hotuba, aliacha mara moja, akateremka kutoka kwenye mimbari, akawachukua mikononi mwake, akawabeba na kurudi nao, akawakalisha karibu naye mwenyewe juu ya mimbari, na kisha akaendelea na hotuba yake. Kama alikuwa anaongoza Swala ya jamaa, na alikuwa kwenye sijdah, watoto hawa wote, mara kwa mara, walipan-da juu ya shingo na mgongo wake. Alipendelea kurefusha sijdah hiyo kuliko kuwavuruga, na kunyanyuka kutoka kwenye sajdah pale tu waliposhuka kutoka kwenye shingo au mgongo wake kwa hiari yao. Kama alitoka nje ya nyumba yake au Msikitini, walipanda mabegani mwake. Watu wa Madina waliwaita "Wapandaji wa Mabega ya Mtume wa Allah (s.a.w.)," walikuwa wamemganda sana yeye kuliko walivyowaganda wazazi wao wenyewe.

157

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad, Mtume wa Uislamu, kamwe hakuwa na furaha zaidi kuliko alipokuwa na Hasan na Husein. Walikuwa ni matunda ya macho yake, na furaha ya moyo wake, na kati-ka kuwa pamoja nao peke yao yeye alipata burudani ya kweli na kamilifu. Alicheza pamo-ja nao mchezo wa kujificha na kutafutana, na kama walikuwa wanacheza na watoto wengine, alikaa karibu nao kiasi tu cha kusikia uzuri wa sauti ya kicheko chao. Kwa ajili yao, aliweza kuacha hata mambo muhimu ya nchi. Walipotabasamu, alisahau usumbufu na wasiwasi wote wa nchi na serikali. Alipenda kusoma kila ujumbe ambao walimwandikia katika tabasamu zao za kimalaika.

Mwanzoni, Mtume wa Allah (s.a.w.) alimlea binti yake mwenyewe, Fatima Zahrah, ambaye alimwita Bibi wa Peponi. Sasa alichukua wajibu wa kuwalea watoto wake wawili - Hasan na Husein - ambao aliwaita Mabwana wa Vijana wa Peponi. Kwake yeye elimu yao ilikuwa ni jambo lenye umuhimu mkubwa, na yeye mwenyewe alishughulikia kila jambo ndani yake. Lengo lake lilikuwa wazi: aliwataka wao kuwa mazao bora kabisa ya Uislamu, na walikuwa hivyo. Aliijenga tabia yake mwenyewe kwenye tabia zao, na akawafanya kuwa mfano kwa umma wake ambao ulikuwa uigize mpaka mwisho wa wakati wenyewe.

Ali na Fatmah Zahrah pia walikuwa na mabinti wawili - Zainab na Ummu Kulthum. Walipokua, waliolewa na binamu zao - watoto wa Jafar ibn Abi Talib, yule Shahidi mwenye Mbawa (Tayaar) wa Uislamu. Zainab aliolewa na Abdullah ibn Jafar, na Ummu Kulthum aliolewa na Muhammad ibn Jafar.

Hasan, Husain, Zainab na Ummu Kulthum, watoto wote wanne walistareheshwa na babu yao, Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) na siku za furaha sana katika maisha yao wote watano ni zile walizokuwa pamoja.

Kifo cha Fatima binti Asad, Mama yake Ali ibn Abi Talib

Katika mwaka wa 4 A.H (626 A.D.) Fatima binti Asad, mjane wa Abu Talib na mama yake Ali, alifariki hapo Madina. Alimlea Muhammad, Mtume (s.a.w.) wa baadae, kama mwanae mwenyewe, naye Muhammad alimwita yeye mama yake. Alikuwa ndiye mwanamke wa pili katika Arabia kuukubali Uislamu, wa kwanza akiwa ni Khadija, mke wa Mtume.

Muhammad alimkosa mama yake mapema sana maishani lakini mara akapata mama wa pili kwa Fatima binti Asad. Yeye, kwa hiyo, hakukosa mapenzi na upendo ambavyo ni mama peke yake anayeweza kuvitoa. Wakati mama yake wa kunyonya alipofariki, alihud-huria mazishi, na akasema: "Allah (s.w.t.) airehemu roho yako tukufu. Ulikuwa kwangu mimi kama mama yangu mwenyewe. Ulinilisha mimi wakati wewe mwenyewe ukikaa na njaa. Lengo lako katika kufanya hivyo lilikuwa ni kumridhisha Allah (s.w.t.) kwa maten-do yako." Alitoa shuka lake mwenyewe kwa ajili ya sanda yake, na alizikwa nalo. Alikuwa

158

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mara kwa mara akisema, "Nilikuwa yatima na akanifanya mimi ni mwanae. Alikuwa ndiye mtu mpole sana kwangu baada ya Abu Talib."

Kaburi lilipochimbwa tayari, Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliliingia; alilala ndani yake, na akasema: "Ewe Allah! Uhai na mauti viko mikononi Mwako. Wewe peke yako ndiye hutakufa kamwe. Mrehemu mama yangu, Fatima binti Asad, na umpe jumba kubwa huko Peponi. Wewe ni Mwingi wa Rehema."

Wakati Fatima binti Asad alipozikwa, Muhammad Mustafa alirudia Allah-u-Akbar mara arobaini, na akaomba: "Ewe Allah! Muweke kwenye Nuru, na ujaze moyo wake na Nuru."

Muhammad Mustafa alikuwa ndiye Mtekelezaji wa hati ya wosia ya Fatima binti Asad.

Fatima binti Asad alikuwa ni mwanamke wa kipekee sana kwa vile watoto wawili kati ya watoto aliowakuza, Muhammad, na Ali, walitokea kuwa watu wa kipekee katika historia ya Uislamu. Nyumbani kwake ndipo chimbuko halisi la Uislamu. Wote Muhammad, Mtume (s.a.w.) wa baadae wa Uislamu, na Ali, shujaa wa baadae wa Uislamu, walizaliwa katika nyumba yake, na walikulia ndani yake. Wote walikuwa "Matunda" ya elimu yake.

Fatima binti Asad pia ni mama yake Jafar, yule shujaa wa vita vya Muutah, na Shahidi mwenye Mbawa (Tayaar) wa Uislamu. Hili jina la mumewe, Abu Talib, linajitokeza kwenye historia kama mfadhili mkubwa sana wa Uislamu, lakini nafasi yake Fatima katika Uislamu si ya umuhimu wa chini kuliko ya mumewe. Anachangia sifa hiyo pamoja naye ya kumlea na kumsomesha Muhammad, Mtume (s.a.w.) wa baadae wa Allah (s.w.t.) Kama mumewe alimlinda Muhammad kutokana na maadui zake huko nje, yeye Fatima alimpa upendo, faraja na usalama huko nyumbani. Ilikuwa ni ndani ya nyumba yake ambamo Muhammad alipata usalama wa kihisia na ukaribu wa hisia wa familia.

Kama Khadija alikuwa ndiye mwanamke wa kwanza mwislamu na mfadhili mkubwa sana (mwanamke) wa Uislamu, Fatima binti Asad alikuwa mwanamke wa pili mwislamu, na mfadhili wa pili (mwanamke) mkubwa sana wa Uislamu. Allah (s.w.t.) awawie radhi waja Wake, Khadija na Fatima binti Asad, na Awarehemu hao.

159

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Vita vya Khandaq

Baada ya vita vya Uhud, Abu Sufyan na wale viongozi wengine wa wapagani waligundua kwamba walipigana vita visivyo na uamuzi, na kwamba ushindi wao haukuwazalia matun-da yoyote. Uislamu ulikuwa, kwa kweli, umeimarika kutoka kinyume chake pale Uhud, na katika muda mfupi wa kustaajabisha, umerejesha mamlaka yake hapo Madina na maeneo yanayoizunguka.

Wapagani waliuona Uislamu ni tishio kwenye usalama wao wa kiuchumi na mamlaka ya kisiasa katika Arabia, na hawangeweza kamwe kukubaliana na kuwepo kwake. Walijua kwamba kama wangeweza kumuua Muhammad, maslahi yao yangepata ulinzi, na mamlaka yao juu ya wengine yangedumishwa katika Arabia. Wakiwa na lengo hili waliamua kushusha shambulizi la mwisho na la kuvunja nguvu juu ya Madina na kuangamiza Waislamu wote.

Montgomery

Lengo la mkakati la watu wa Makka halikuwa ni chochote pungufu zaidi ya kuiangamiza jamii ya Waislamu kama hivyo, au - kile kinacholingana na jambo hilo hilo - kumuondoa Muhammad kutoka kwenye nafasi yake ya mamlaka.

(Muhammad, Prophet and Statesman)

Wakisukumwa na lengo hili, na kwa nguvu ya shauku ya kufanya fidia kwa ajili ya kushindwa kwa siku zilizopita, hawa viongozi wa Makka walianza maandalizi kwa ajili ya vita vya juhudi zote; vita ambavyo vitakuwa ni mwisho wa vita nyingine zote kwa kuuteketeza kabisa Uislamu!

Ndani ya miaka miwili Maquraishi waliunda jeshi la mapambano la wapiganaji elfu kumi. Hili lilikuwa ndio jeshi kubwa kabisa lililowahi kukusanywa na Waarabu mpaka wakati huo. Pamoja na shangwe kubwa na kujiamini, jeshi hili la kutisha liliondoka Makka mwezi wa Februari, 627A.D. kwenda kuiteka Madina na kufutilia mbali Uislamu.

Muhammad Husein Haykal

Wakati habari za uhamasishaji huu mkubwa mno zilipomfikia Muhammad na Waislamu huko Madina, ziliwatia wote wasiwasi. Uhamasishaji wa Arabia yote dhidi yao uliingiza hofu ndani ya mioyo yao kwani walikuwa wanakabiliwa na matarajio sio tu ya kushindwa bali kuteketezwa kabisa. Uzito halisi wa hali hiyo ulikuwa dhahiri katika ukweli kwamba lile jeshi ambalo makabila ya Kiarabu sasa walikuwa wameliunda lilikuwa limezidi katika idadi na zana, kitu chochote ambacho Peninsula hiyo imewahi kushuhudia kabla.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

160

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mtume (s.a.w.) aliitisha mkutano wa dharura wa maswahaba wake wakuu kushauriana nao katika suala la kuulinda mji. Kitu kimoja kilikuwa wazi. Waislamu walikuwa wachache sana kwa idadi na wadhaifu sana katika zana kwamba walikuwa hawawezi kukutana na lile jeshi linalovamia kwenye ardhi ya wazi. Madina ilikuwa ilindwe kutoka ndani yake. Lakini vipi? Vipi askari wa ulinzi wachache wa Waislamu wataweza kulizuia jeshi la Makka kutokana na kuivamia na kuizagaa Madina ambayo ingekuwa imejaa idadi ya watu wasio-fuzu, lilikuwa ndio swali katika akili ya kila mtu.

Mmoja wa marafiki wa karibu wa Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) alikuwa ni Salman yule Muajemi. Alizaliwa na kukulia huko Uajemi (Iran) lakini aliishi kwa miaka mingi huko Syria na Palestina, na alikuwa na uzoefu wa vita na operesheni za kuzingira za wote, Waajemi na Warumi. Madina ilikuwa na ulinzi wa asili au uliotengenezwa na watu katika pande tatu lakini ilikuwa wazi katika upande mmoja, yaani, ule upande wa kaskazi-ni. Salman alimwambia Mtume (s.a.w.) kwamba kama handaki lingechimbwa katika upande wa kaskazini, mji ule pengine ungeweza kulindwa kwa mafanikio.

Wazo hili, ingawa ni geni na lisilo la kawaida katika Arabia, lilimvutia Mtume. Akalikubali na kuwaamuru Waislamu kulichimba handaki hilo.

Muhammad Husein Haykal

Salman al-Farsi, aliyejua vizuri zaidi juu ya mbinu za vita kuliko ilivyokuwa kawaida hapo katika Peninsula. Alishauri kuchimbwa kwa handaki kavu kuzunguka Madina na kuimarisha kwa majengo yaliyomo ndani yake. Waislamu waliharakisha kutekeleza ushauri huo. Handaki lilichimbwa na Mtume - rehema na amani za Allah (s.w.t.) ziwe juu yake - alifanya kazi kwa mikono yake sambamba na maswahaba zake kutoa uchafu, kuwatia moyo wale Waislamu wanaofanya kazi, na kumshawishi kila mtu kuongeza juhudi zake.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Kwa kuwa lile jeshi la Makka lilijulikana kwamba linasogelea Madina kwa haraka, hapakuwa na muda wa kupoteza, na Waislamu walifanya kazi kwa harakati kubwa - kwa kupokezana. Ndani ya siku sita handaki hilo likawa limechimbwa, mapema tu kuwazuia wavamizi kuuchukua mji kwa uvamizi.

Kikosi cha wapanda farasi wa Makka kilikuja kama kimbunga lakini ghafla kikazuiwa, katika kasi yake, na handaki hilo. Wapanda farasi hao waliwasimamisha farasi wao kwenye ukingo wake. Mkakati wao mkuu ulikuwa ni kuiteka kwa nguvu Madina kwa masaa machache lakini sasa ilionekana kwao kwamba hawawezi kufanya hivyo. Hapa kulikuwa na handaki, kikwazo kipya ambacho hawakuweza kukipita. Limeingia vipi kwenye mkakati wao? Waliduwazwa kabisa na handaki hilo.

161

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hatimae, na baada ya majadiliano marefu, makamanda wa Makka waliamua kuizingira Madina, na kuwalazimisha Waislamu kuswalimu amri, kwa msuguano (kuwadhoofisha). Walifunga njia zote za kutoka nje ya Madina, na kuwazunguka Waislamu. Madina ilikuwa katika hali ya kuzingirwa!

Ingawa alikuwa ni Abu Sufyan ambaye aliongoza kampeni hiyo nzima, na alikuwa ndiye mkurugenzi wake wa utendaji, hakuwa mtu mpiganaji yeye mwenyewe. Mpiganaji wa jeshi lake alikuwa ni Amr ibn Abd Wudd, mkali zaidi kati ya wapiganaji wa wapagani wa Arabia. Matumaini ya Abu Sufyan ya ushindi wa haraka na wenye uamuzi juu ya Waislamu yalikuwa juu yake huyu. M. Shibli, yule mwanahistoria wa kihindi, na Abbas Mahmud Al-Akkad, yule mwanahistoria wa Misri, wanasema kwamba Amr ibn Abd Wudd alihesabiwa, na Waarabu wa wakati huo, kuwa zaidi ya usawa na askari wa farasi elfu moja.

Amr ibn Abd Wudd hakuwa akipendezewa na vita tulivu au mzingiro (karantini). Alitweta kwa kutaka vitendo. Wakati siku chache zilipokuwa zimepita, na hakuna chochote kili-chotokea, alipoteza subira, na akaamua kuiteka Madina kwa vitendo vyake mwenyewe. Siku moja, akiranda kuzunguka Madina kwa kuvizia, yeye pamoja na mashujaa wengine watatu wa Makka waligundua sehemu yenye mawemawe ambapo lile handaki halikuwa pana sana. Waliwatia chonjo farasi wao kutoka kwenye sehemu hiyo, na wakafanikiwa katika kulivuka lile handaki!

Sasa Amr alikuwa ndani ya mzingo wa Madina. Kwa ujasiri kabisa akasonga mbele kwenye kambi ya Waislamu, na kuwapa changamoto mashujaa wa Kiislam kutoka na kupi-gana dhidi yake katika desturi ya jadi ya Kiarabu ya mapambano ya watu wawili wawili.

Changamoto ya kwanza ya Amr ilipita bila kujibiwa kwa hiyo akairudia lakini bado haku-pata jibu. Hiyo ndiyo fahari kuu ya jina lake kwamba hakuna yeyote katika kambi ya Waislamu aliyethubutu kukabiliana naye katika kupimana nguvu. Kama waabudu masana-mu waliyaona kwake matumaini ya ushindi, Waislamu waliona katika changamoto yake hukumu ya kifo chao.

Amr ibn Abd Wudd alitoa changamoto yake yenye dharau kwa mara ya tatu na akawadhi-haki Waislamu wakati huo huo kwa woga wao.

Kwa Amr lazima itakuwa imeelekea kwamba Waislamu walikuwa wameishiwa na nguvu kwa woga, ambavyo wengi wao, kwa kweli, walikuwa hivyo. Qur'an Tukufu pia imecho-ra picha ya hali ya Waislamu katika kuzingirwa Madina katika Aya zifatazo:

162

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usahihi-11.jpg

"Tazama! Walikujieni kutoka juu yenu, na kutoka chini yenu, na tazama; macho yalipofifia, na nyoyo zikapanda kooni, nanyi mkamdhania Allah dhana mbalimbali." (Sura ya 33; Aya ya 10)

Usahihi-12.jpg

"Tazama! Na kundi moja kati yao likasema: 'Enyi watu wa Yathrib! Hamuwezi kuhimili (shambulizi). Hivyo rudini' na kundi jingine kati yao likaomba ruhusa kwa Mtume (s.a.w.) likisema: 'Hakika nyumba zetu ni tupu na wazi' Wala hazikuwa wazi; hawakutaka chochote ila kukimbia tu." (Sura ya 33; Aya ya 13)

Amr ibn Abd Wudd pia alionyesha mshangao kwamba wale Waislamu hawakuwa wakionyesha shauku yoyote ya kuingia peponi ambako alikuwa tayari kuwapeleka.

Ni kweli kwamba wengi wa Waislamu walikuwa wamekumbwa na hofu lakini alikuwepo mmoja kati yao ambaye hakuwa hivyo. Alikuwa, kwa kweli, amejitolea kuikubali chang-amoto ya kwanza kabisa ya Amr lakini Mtume (s.a.w.) alimzuia, akitegemea kwamba mtu mwingine yeyote angependa kumkabili Amr. Lakini aliweza kuona kwamba hakuna hata mmoja aliyethubutu kunyoosheana panga naye.

Huyu kijana mdogo aliyekuwa tayari kuipokea changamoto ya Amr hakuwa mwingine yoyote mbali na Ali ibn Abi Talib, yule shujaa wa Uislamu. Pale Amr alipotupa changamoto yake ya tatu, na hapakuwa na mtu aliyemjibu, Ali alisimama na kuomba ruhusa ya Mtume (s.a.w.) ya kutoka na kupigana dhidi yake.

Mtume wa Uislamu hakuwa na budi tena sasa ila kumruhusu binamu yake, Ali, yule Simba wa Uislamu, kwenda na kunyamazisha zile dhihaka na kejeli za Amr Ibn Abd Wudd.

Ali alivaa lile vazi la vita la Mtume wa Uislamu. Mtume (s.a.w.) mwenyewe akaning'inizia Dhu'l-Fiqar (upanga wake) pembeni mwake, na kumuombea kwa ajili ya ushindi wake, akisema: "Ewe Allah! Ulimwita kwenye huduma yako, Ubaida ibn al-Harith, ile siku ambayo vita vya Badr vilipopiganwa, na Hamza ibn Abdul-Muttalib, siku ambayo vita vya Uhud vilipopiganwa. Sasa ni Ali pekee aliyebakia nami. Kuwa Wewe Mlinzi wake, mpatie yeye ushindi, na mrudishe salama kwangu."

163

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wakati Mtume (s.a.w.) alipomwona Ali akienda kuelekea kwa adui yake, alisema: "Yeye ndiye tashihisi wa Imani yote ambaye anakwenda kupambana na tashihisi ya Ukafiri wote."

Muda mchache baadae, Ali alikuwa amesimama mbele ya Amr. Mashujaa wawili hawa wakatambulishana, na wakapimana. Ali alikuwa na seti ya kanuni ambazo alizitumia katika hali zote ama za vita au za amani. Kwenye vita vya handaki, Waislamu na wapagani waliona maonyesho ya matumizi ya kanuni hizo. Wakati wowote alipokabiliana na adui, alimpa hiari ya kuchagua kati mambo matatu. Nayo yalikuwa ni:

1.  Ali aliutambulisha rasmi Uislamu kwa adui yake. Alimualika kuacha uabudu-sanamu na kuukubali Uislamu. Mwaliko huu ulimfanya Ali muba-ligh wa Uislamu katika uwanja wa vita wenyewe.

2.  Kama adui huyo hakuukubali mwaliko wa Ali wa kuukubali Uislamu, alimshauri yeye kujiondoa kutoka kwenye vita, na asipigane dhidi ya Allah (s.w.t.) na Mtume wake. Kupigana dhidi yao, alimuonya, kutamletea tu laana ya milele juu yake katika dunia zote mbili.

3. Kama adui huyo hakukubali chaguo hili la pili pia, na akakataa kujiondoa kwenye vita, basi Ali alimkaribisha kutupa dhoruba ya kwanza. Ali mwenyewe kamwe hakuwa wa kwanza kushambulia adui.

Amr ibn Abd Wudd alidharau hata kufikiria lile chaguo la kwanza na la pili lakini akakubali hili la tatu, na akapiga dhoruba kubwa kwa upanga wake mkubwa sana ambao ulikata kupita kwenye ngao, kofia ya chuma na kilemba cha Ali, na kufanya jeraha kubwa sana kwenye paji lake la uso. Damu iliruka kutoka kwenye jeraha hilo katika mchirizi lakini Ali hakuvunjika moyo. Alipata nguvu, na kisha akatupa pigo la kujibu kwa upanga ule maarufu Dhu'l-Fiqar, na ukampasua yule mpiganaji wa kutisha wa Arabia katika vipande viwili!

Wakati Amr alipouawa, wale mashujaa watatu katika msafara wake waligeuka na kuwatia chonjo farasi wao kukimbia. Ali akawaacha wakimbie. Ilikuwa ni moja ya kanuni zake kutomfukuza adui anayekimbia. Yeyote yule aliyetaka kuokoa maisha yake, Ali alimwacha ayaokoe.

Kifo cha Amr ibn Abd Wudd kilivunja mgongo wa mashambulizi ya Makka dhidi ya Uislamu, na kuvunja hamasa yao. Nguvu za asili pia zilitangaza vita dhidi yao. Joto lilishu-ka kufikia kiwango cha kuganda, na wingu la vumbi lilinyanyuka ambalo lilivuma kwenye nyuso zao. Wakiwa wamekata tamaa na kuvunjika moyo, wale jamaa wa makabila wenye kigeugeu walianza kuwaacha marafiki zao wa Makka, kwanza mmoja mmoja na wawili

164

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wawili na watatu watatu, na kisha kwa makumi na ishirini ishirini, na baadae kidogo, kwa mamia. Ule muungano ukaanza kutoweka polepole kwa uwazi kabisa. Abu Sufyan alilaz-imika kuacha kuzingira, na akatoa ishara kwa jeshi lake kurudi nyuma kutoka Madina. Jeshi lake lilitawanyika, na kampeni yake ilikuwa imeshindwa vibaya. Madina ilikuwa imeokolewa.

Kushindwa kwa mzingiro (karantini) wa Madina kwa waabudu-masanamu wa Makka lilikuwa ni tukio muhimu sana katika historia ya Arabia. Ilimaanisha kwamba watakuwa hawawezi kamwe kuandaa uvamizi mwingine wa Madina. Baada ya vile vita vya handa-ki, uamuzi ukahama, hatimae na kwa dhahiri kabisa, kutoka kwa waabudu-sanamu wa Makka kwenda kwa Waislamu wa Madina.

Madina na Uislamu viliokolewa na wazo na shujaa. Wazo lilikuwa ni lile handaki ambalo liliwazuia askari wa farasi wa Makka. Ilikuwa ni fikra mpya kabisa katika vita vya Uarabuni, na Waarabu hawakuwa na uzoefu nayo. Bila ya hilo handaki, wale watu elfu kumi wa kabila la majambazi wangeweza kuivamia na kuizagaa Madina, na wangemuua kila mtu humo. Heshima ya kuiokoa Madina-tun-Nabi, mji wa Mtume, na makao makuu ya Uislamu, inakwenda kwa Salman yule Muajemi, na kwa bwana wake, Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Huyu wa kwanza alianzisha wazo jipya katika kanuni za kijeshi; na huyu mwingine alionekana tayari ni mwenye kulisikiliza, na papo hapo akalitekeleza.

Kila mmoja hapo Madina alidai kuwa ni rafiki au sahaba wa Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) Mji huo ulikuwa na fungu lake wenyewe la watu wenye kutafuta umaarufu. Lakini walikuwepo wachache, kwa kweli wachache sana, watu ambao Muhammad mwenyewe amewakiri kama marafiki zake. Salman, yule Muajemi alihusika kwenye kundi hili teule, ule mzunguko wa ndani kabisa wa marafiki wa Mtume wa Allah (s.a.w.)

Salman alikuwa mtu wa kimo kirefu sana na nguvu za kimwili nyingi mno. Wakati handaki lilipokuwa linachimbwa, alifanya kazi kama ya watu sita wengine. Hili lilimshawishi mmoja wa Muhajirina kutangaza kwamba Salman alikuwa mmoja wao, yaani alikuwa Muhajirina. Lakini alipingwa mara moja na Ansari ambao mmoja wao alisema kwamba Salman alikuwa ni Ansari na sio Muhajir. Makundi mawili hayo yalikuwa bado yanabishana wakati Mtume (s.a.w.) alipowasili hapo kwenye tukio. Yeye pia aliyasikia madai ya pande zote mbili na ali-furahishwa nayo. Lakini aliyakatisha mabishano hayo kwa kutoa "fatwa" yake binafsi. Alisema kwamba Salman hakuwa Muhajir wala Ansari bali alikuwa ni mtu wa nyumba yake mwenyewe - ni Ahlul-Bayt - mtu wa nyumba ya Muhammad Mustafa mwenyewe!

Yule mwanahistoria wa Kiarabu, Ibn Athir, amemnukuu Mtume (s.a.w.) ndani ya kitabu chake, Tarikh Kamil, juz. 2, uk.122, kwamba alisema: "Salman ni mmoja wetu. Yeye ni mtu wa Nyumba yetu." Hii ndio heshima kubwa kabisa ambayo kamwe haijawahi kutole-wa kwa sahaba wake yeyote na Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.)

165

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Salman alikuwa ni mkristo aliyekuwa akiishi huko Ammuria-Asia Ndogo, wakati ali-posikia kwa mara ya kwanza habari zisizokuwa na yakini za kutokea kwa Mtume (s.a.w.) huko Hijazi. Ili kuhakikisha habari hizi, alikuja Madina. Wakati alipouangalia kwa mara ya kwanza uso wa Mtume, aliguta kwa mshangao: "Huu hauwezi kuwa uso wa mtu ambaye amewahi kamwe kusema uongo," na papo hapo akasilimu.

Uislamu ulimkubali Salman kama vile yeye "alivyoukubali" Uislamu. Uislamu ukawa ni kiunganisho cha hisia zake, naye akawa ni sehemu yake ya "mtiririko wa damu." Huko Madina, safari moja mgeni mmoja akamuuliza yeye jina la baba yake. Jibu lake lilikuwa ni: "Uislamu! Jina la baba yangu ni Uislamu. Mimi ni Salman mtoto wa Uislamu." Salman "alichanganyika" kwenye Uislamu kwelikweli kiasi kwamba alikuwa hatofautishiki nao.

Tishio kwenye usalama wa Madina, hata hivyo, halikwisha kwa kuchimbwa kwa hilo han-daki. Madini ilikuwa bado sio salama. Kwenye sehemu ambayo lile handaki lilikuwa jem-bamba, yule jenerali wa jeshi la Makka na mashujaa wengine watatu, waliweza kuruka juu yake na kwenda (kwa farasi) kwenye kambi ya Waislamu. Kama walifanikiwa kuanzisha daraja ya kuvukia juu ya handaki hilo, jeshi la farasi lote la Makka na askari wa miguu, na maharamia wasiotabirika wangeweza kuingia mjini humo na kuuteka. Lakini Ali aliwazuia na kuwashinda kabisa. Hivyo werevu wa Salman, busara za Muhammad na upanga wa Ali vilithubutu kuwa ulinzi bora wa Uislamu dhidi ya muungano wa kutisha wa washirikina katika historia ya Uarabuni.

Ilikuwa ni desturi katika vita za Kiarabu kumpora adui aliyeshindwa silaha zake, mavazi ya chuma - deraya na farasi wake. Katika kuizingira Madina, Amr alikuwa amevaa deraya nzuri sana katika Arabuni yote. Ali alimuua lakini hakugusa kitu chochote ambacho kilikuwa mali yake, kwa mshangao mkubwa sana wa Umar ibn al-Khattab. Baadae, wakati dada yake Amr alipokuja kwenye maiti yake kumlilia kifo chake, yeye pia alishangaa kugundua kwamba silaha zake na mavazi viko salama. Alipoambiwa kwamba alikuwa ni Ali aliyemuua, alitunga beti kadhaa za kumsifia yeye (Ali). Beti hizi zimenakiliwa na yule mwanahistoria wa Misri, Abbas Mahmud Al-Akkad, katika kitabu chake, Al-Abqariyyat Imam Ali (kipaji cha Imam Ali), na zinaweza kutarjumiwa kijuujuu kama ifuatavyo:

"Kama mtu mwingine mbali na Ali angemuua Amr, Ningehuzunikia kifo chake maisha yangu yote. Lakini mtu aliyemuua yeye ni shujaa na hana kifani. Baba yake pia alikuwa ni muungwana."

Akitoa maelezo juu ya mistari hii, Abbas Mahmud Al-Akkad anasema kwamba kabila halikuchukulia kuwa ni fedheha kama mmojawapo wa mashujaa wao aliuawa na Ali. Ali alikuwa ndiye jasiri zaidi na muungwana zaidi kwa maadui, na pia alikuwa asiyeshindika. Baada ya kushindwa kwa kule kuizingira Madina, yale makabila yote kati ya Madina na

166

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Bahari Nyekundu na kati ya Madina na Yammama kwa upande wa Mashariki, yaliweka saini mikataba ya amani na Mtume wa Uislamu.

Katika mwaka huo huo, yaani mwaka wa 5 H.A. (627 A.D.), Hajj (kwenda kuhiji Makka) ilifanywa ni lazima kwa wale Waislamu wote waliokuwa na hali nzuri ya kifedha na walio na afya njema.

167

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Waislamu na Wayahudi

Mnamo mwaka wa 70 A.D. Yule jenerali wa Kirumi, Titus, aliiteka Jerusalem na akakome-sha utawala wa Kiyahudi wa Palestina. Kufuatia utekaji nyara wa Warumi, Wayahudi wengi waliondoka kwenye nchi yao na wakatangatanga kwenye nchi nyingine. Baadhi ya makabila ya Kiyahudi yalivuka jangwa la Syria na kuingia kwenye peninsula ya Arabia ambako waliweka makazi yao huko Hijazi. Baada ya kupita muda walijenga makoloni mengi huko Madina na kati ya Madina na Syria. Wanasemekana pia kwamba waliwabadili Waarabu wengi na kuwaingiza kwenye Ujuda (dini ya Wayahudi).

Mwanzoni mwa karne ya saba A.D., kulikuwa na makabila matatu ya Kiyahudi yaliyokuwa yanaishi Madina (Yathrib). Haya yalikuwa ni Banu Qainuka'a, Banu Nadhir na Banu Qurayza. Makabila yote matatu yalikuwa matajiri na yenye nguvu, na pia, yalikuwa yamestaarabika zaidi kuliko hao Waarabu. Wakati ambapo Waarabu walikuwa wote ni wakulima, hawa Wayahudi walikuwa wawekezaji mali wa viwanda, biashara na uchuuzi katika Arabia, na walisimamia maisha ya kiuchumi ya Madina (Yathrib). Yale makabila mawili ya Kiarabu - Aus na Khazraj - walikuwa wamejawa na madeni kwa Wayahudi daima.

Mbali na Madina, vituo vizito vya Wayahudi katika Hijazi vilikuwa Khaibar, Fadak na Wadi-ul-Qura. Ardhi katika mabonde haya ilikuwa ndio yenye rutuba zaidi katika Arabia yote, na wakulima wake wa Kiyahudi walikuwa ndio wakulima wazuri zaidi katika nchi hiyo.

Kule kuhama kwa Muhammad, Mtume wa Uislamu, kutoka Makka kwenda Madina (wakati huo Yathrib) kulimkutanisha na Wayahudi kwa mara ya kwanza. Hapo mwanzoni walikuwa na urafiki naye. Aliwapa ule mkataba maarufu wa Madina, na wakamtambua yeye kama mtawala wa mji wao, na wakakubali kufuata uamuzi wake katika migogoro yote. Walikubali pia kuulinda mji huo katika kitendo cha kuvamiwa na adui.

Lakini, kwa bahati mbaya, urafiki huu haukudumu kwa muda mrefu. Mara moja ikaonekana wazi kwamba hao Wayahudi walitoa urafiki wao kwa Muhammad kwa masha-ka mengi. Kwa maslahi yao binafsi, walipaswa kutekeleza wajibu wao wa makubaliano kwa uaminifu lakini hawakufanya hivyo. Kwa mabadiliko haya katika tabia zao, kulikuwa na sababu nyingi, miongoni mwao zikiwa:

1. Wakati Muhammad alipowasili Madina, alirekebisha maisha ya Waarabu au yeyote yule aliyeingia Uislamu. Aliwafundisha wao kuwa na msimamo

168

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wa kadiri na wastani katika kila jambo na akawafundisha thamani ya nid-hamu katika maisha. Waliacha kunywa pombe na kucheza na kamari vyote ambavyo vilikuwa ndio vyanzo vya kuharibikiwa kwao huko nyuma; na waliacha kuchukua mikopo kwa viwango vya juu vya riba kutoka kwa Wayahudi. Pale Waarabu walipoacha kuchukua mikopo na kuitolea riba juu yake, chanzo kikubwa cha mapato kwa Wayahudi ghafla kikakauka, na walilikasirikia sana hili. Waliweza kuona sasa kwamba nguvu yao katika maisha ya kiuchumi ya Madina ilikuwa inaanza kulegea.

2.   Wayahudi pia walitambua kwamba Uislamu ulikuwa ni adui wa mfumo wao wa unyonyaji, na mfumo wa kibepari. Walianza kuuona Uislamu kama ni tishio kwa maslahi yao ya kiuchumi.

3.    Makuhani wa Kiyahudi walimchukia Muhammad kama vile walivyom-chukia wakopesha fedha. Alikuwa amewaonyesha Wayahudi jinsi makuhani wao walivyofuata tafsiri potovu ya maandiko yao, na jinsi walivyochafua vitabu vyao. Makuhani hao, kwa upande wao, walijaribu kuwashawishi waumini wao kwamba Muhammad hakuwa na elimu ya maandiko yao, na walijaribu kuwaonyesha wao "makosa" katika Qur'an

Wayahudi hao pia waliamini kuwa walikuwa salama tu mradi yale makabila mawili ya Madina, Aus na Khazraj, yalikuwa yanapigana yenyewe kwa yenyewe. Amani kati ya Aus na Khazraj, walidhania, italeta tishio kwa maisha yao katika Arabia. Kwa sababu hii, walikuwa daima wakichochea ugomvi kati yao.

Kati ya makabila matatu ya Kiyahudi ya Madina, hawa Banu Qainuka na Banu Nadhir yalikuwa tayari yamefukuzwa baada ya vita vya Badr na Uhud kwa mfuatano wake, na walikuwa wameondoka na mizigo yao, na makundi ya wanyama, na wamefanya makazi huko Khaibar.

Hili kabila la tatu na la mwisho la Wayahudi wa Madina lilikuwa la Banu Qurayza. Kwa mujibu wa masharti ya ule Mkataba wa Madina, ilikuwa ni wajibu wao kuchukua sehemu muhimu katika kuulinda mji huo wakati wa kule kuzingirwa kwa mwaka 627 A.D. Lakini sio tu hawakutoa mtu yeyote au vifaa wakati wa mzingiro bali walikamatwa wakila njama na maadui kuwekea mzingo maangamizi ya Waislamu. Baadhi ya Wayahudi pia walisham-bulia nyumba moja ambayo ndani yake wanawake wengi wa Kiislam na watoto walichukua hifadhi kama ilivyodhaniwa kuwa ni sehemu yenye usalama kwao kuliko kwenye nyumba zao wenyewe. Kama Amr ibn Abd Wudd angeushinda upinzani wa Waislamu, hawa Wayahudi wangewashambulia kwa nyuma. Katikati ya wapagani wa Makka na Wayahudi wa Madina, Waislamu wangeuawa kwa halaiki. Ilikuwa ni kuwepo kwa akili ya Muhammad na kujasiri kwa Ali ambako kulizuia maafa kama haya..

169

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

R.V.C.Bodley

Wale Wayahudi mwanzoni hawakuelekea kulisikiliza pendekezo la Abu Sufyan (la kuwashambulia Waislamu kutokea nyuma), lakini baada ya muda walielewana na wakakubali kuwasaliti Waislamu pale muda utakapoelekea kuwa muafaka.

(The Messenger - the Life of Muhammad)

Tabia ya Wayahudi wakati ule wa mzingiro wa Madina ilikuwa ni uhaini mkubwa dhidi ya Nchi. Kwa hiyo, wakati lile jeshi la muungano lilipovunjika na ile hatari ya Madina ikawa imezuiwa, Waislamu wakaguezia macho yao kwao.

Wale Wayahudi wakajifungia kwenya ngome zao na Waislamu wakawazingira. Lakini siku kadhaa baadae, walimuomba Mtume (s.a.w.) kuondoa mzingiro ule, na wakakubali kupele-ka mgogoro huo kwenye usuluhishi.

Mtume (s.a.w.) aliwaruhusu wale Wayahudi kuchagua msuluhishi wao wenyewe. Hapa walifanya kosa lililowagharimu sana. Wangemchagua Muhammad mwenyewe - aliye mfano halisi wa msamaha - awe hakimu wao. Kama wangefanya hivyo, angeweza kuwaruhusu waondoke Madina na mizigo na wanyama wao, na kadhia hiyo ingefikia mwisho.

Lakini Wayahudi wale hawakumchagua Muhammad kama hakimu wao. Badala yake, wal-imchagua Sa'ad ibn Muadh, kiongozi wa washirika wao wa awali, wale Aus. Sa'ad alikuwa ni mtu asiyejali kabisa maisha yake mwenyewe na ya wengine vilevile.

Sa'ad alipata jeraha baya sana wakati wa vita vya Handaki, na kwa kweli alikufa baada ya kutoa hukumu juu ya majaaliwa ya wale Wayahudi. Aliutaja uhaini kwamba ni kosa lisilosameheka, na hukumu yake ilikuwa kali. Aliitekeleza Taurati, lile andiko la Wayahudi, na akawahukumu wanaume wote kifo, na wanawake na watoto kuwa watumwa. Hukumu yake ilitekelezwa papo hapo.

Wale Wayahudi wa kabila la Qurayza waliuawa kwenye majira ya kuchipua ya mwaka wa 627 A.D. Kutoka tarehe hii, Wayahudi wakakoma kuwa nguvu hai katika maisha ya kiuchumi na kisiasa ya Madina.

170

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mkataba wa Hudaybiyya

Kwa mujibu wa Hadith za Kiislam, ile Al-Kaaba ya Makka ilijengwa na Mitume Ibrahim na mwanae, Ismail. Waliitoa Waqfu kama kituo cha kiroho cha dunia ya waabudu Mungu mmoj a. Na sasa Al-Kaaba ilikuwa ndio "Qibla " cha Waislamu ambacho ina maana kwamba walikuwa wageukie kukielekea wakati wanaposali Swala zao. Lakini walezi wa hiyo Al-Kaaba walikuwa ni wale waabudu masanamu wa Makka, na walikuwa wakiitumia kama hekalu la kitaifa la ushirikina, wakiweka ndani yake masanamu 360 ya makabila yao.

Kwa desturi za kijadi za Kiarabu, kila mmoja alikuwa huru kuitembelea hiyo Al-Kaaba -bila ya silaha. Pia, kwa desturi za jadi, mapigano ya aina yoyote yalikatazwa wakati wa miezi minne mitukufu ya mwaka. Moja ya miezi hii ulikuwa ni Dhilqa'ada, mwezi wa 11 wa kalenda ya Kiislamu.

Waislamu walitamani kuona ilikuwa ni nini kwao, ile Nyumba ya Allah (s.w.t.) Kwa hiyo, katika Dhilqa 'ada ya mwaka wa sita wa Hijiria, Mtume wao alitaarifu kwamba atatembe-lea Makka kufanya Umra au Hija Ndogo - bila ya kuwa na silaha lakini akiwa na wafuasi wake. Kwa dhamira hii, aliondoka Madina mwishoni mwa Februari 628 A.D., pamoja na idadi ya wafuasi wake 1,400. Walichukua ngamia na wanyama wengine kwa ajili ya kafara lakini hawakuwa na silaha yoyote isipokuwa panga zao.

Wakati msafara huu wa mahujaji ulipofika kwenye viunga vya Makka, Mtume (s.a.w.) ali-julishwa kwamba wale waabudu-sanamu hawatamruhusu yeye kuuingia mji huo, na kwamba, watatumia nguvu kumzuia asifanye hivyo. Taarifa hii ilisababisha wasiwasi mkubwa miongoni mwa Waislamu. Walisimama karibu na kisima mahali panapoitwa Hudaybiyya kaskazini ya Makka. Mtume (s.a.w.) alituma ujumbe kwa Maquraishi kwamba alitaka afanye tu ile mizunguko ya kidesturi saba, ya Al-Kaaba, kutoa kafara wanyama wao, na kisha warudi Madina na wafuasi wake. Maquraishi hawakukubali. Ujumbe mwin-gi tena ulitumwa lakini Maquraishi walisema kwamba hawatawaruhusu Waislamu kuingia Makka.

Hatimae, Mtume (s.a.w.) alimuamuru Umar ibn al-Khattab kwenda Makka kuwaelezea wale waabudu-masanamu madhumuni ya safari ile ya Waislamu, kuwahakikishia wao kwamba Waislamu hawakuwa na nia ya kupigana dhidi ya mtu yoyote yule, na kuwapa ahadi kwamba baada ya kufanya taratibu (ibada) za Umra wataondoka Makka mara moja na watarudi Madina.

Lakini Umar alikataa kwenda. Alisema hakuna mtu huko Makka wa kumlinda yeye. Alishauri, hata hivyo, kwamba Mtume (s.a.w.) angemtuma Uthman bin Affan na ujumbe wake kwenda Makka kwa vile wale waabudu masanamu hawatamfanyia madhara yoyote.

171

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir William Muir

Mjumbe wa kwanza kutoka kambi ya Waislamu kwenda Makka, mtu aliyesilimu kutoka kabila la Bani Khuzaa, Maquraishi walimkamata na kumfanyia ukatili; wakamtia kilema ngamia wa Mtume (s.a.w.) ambaye alikuwa amempanda, na hata kumtishia maisha yake. Lakini hasira sasa zilikuwa zimetulia zaidi, na Muhammad alitaka Umar aende Makka kama balozi wake. Umar alijipa udhuru mwenyewe kwa sababu ya uadui binafsi wa Maquraishi juu yake; alikuwa, zaidi ya hayo, hana ndugu wenye uwezo hapo mjini ambao wangeweza kumkinga kutokana na hatari; na alielekeza kwa Uthman kama mjumbe anayefaa zaidi.

(The Life of Muhammad, 1877) S. Margoliouth.

Wakati huu ilikusudiwa kutuma mwakilishi kwenda Makka, lakini ule utambuzi kwamba wengi wa Waislamu walikuwa na madoa ya damu ya Makka, uliwafanya wale mashujaa wa Uislamu wasiwe tayari kuhatarisha maisha yao kwenye safari hii fupi; hata Umar, ambaye kwa kawaida alikuwa tayari kabisa na upanga wake, alirudi nyuma. Hatimae mkwewe Mtume, Uthman bin Affan, ambaye alichagua kumuuguza mkewe badala ya kupigana huko Badr, alitumwa kama mjumbe anayekubalika humo...

(Muhammad and the Rise of Islam, 1931)

Ni ajabu kabisa kwamba Umar hakuwa tayari kuhatarisha maisha yake kwa kutembelea Makka. Hapakuwa na hatari yoyote iliyohusika juu yake kwa sababu hakuwa mmojawapo wa wale Waislamu ambao "walitiwa doa na damu ya Makka." Kwa vile Umar hakuua mtu yeyote wa Makka, atakuwa ni mtu anayekubalika kwa hawa waabudu masanamu kwa nyakati zote. Kukataa kwake kutii amri ya Mtume wa Allah (s.a.w.) kwa hiyo, hakuelewe-ki.

Umar hakwenda Makka. Hata hivyo, alilitatua tatizo hilo kwa kumtoa mshika nafasi yake, Uthman bin Affan. Badala yake, kwa hiyo, Uthman alitumwa Makka kufanya mazungum-zo na Maquraishi. Kama Umar mwenyewe, Uthman pia hakuwa na doa la damu ya pagani yeyote.

Waabudu masanamu hao walimkaribisha Uthman na wakamwambia yeye kwamba alikuwa huru kufanya hiyo Umra. Lakini alisema kwamba yeye peke yake hataweza kufanya Umra, na kwamba walikuwa wamruhusu Mtume (s.a.w.) na Waislamu wote waliokuwa pamoja naye, kuingia mjini humo. Hili halikukubaliwa na Maquraishi, na ilielezwa kwamba walimkamata yeye. Ilinong'onwa pia kwamba walimuua.

172

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wakati tetesi la kuuawa kwa Uthman zilipomfikia Mtume, alikitafsiri kitendo hicho cha Maquraishi kama makataa (kauli ya mwisho), na akawataka Waislamu kutoa upya kiapo chao cha utii kwake. Waislamu wote wakatoa kiapo chao cha utii kwa Mtume wa Allah (s.a.w.) bila kujali matukio yanayoweza kutokea baada ya hapo.

Kiapo hiki kinaitwa "Kiapo cha Ridhwan" au "Mkataba wa Uaminifu," na wale Waislamu waliokitoa, wanaitwa "Masahaba wa chini ya mti," kwa sababu Mtume (s.a.w.) alisimama chini ya mti walipokuwa wakipita kwa safu mbele yake wakitoa upya kiapo chao cha utii kwake. Idadi yao imetajwa kuwa 1,400.

Uamuzi huu wa Waislamu wa kujasiri matokeo unaonekana kuwaweka Maquraishi katika hali ya akili ya kutosha, kwa vile walivyotambua kwamba ukaidi wao unaweza kus-ababisha umwagaji damu usio wa lazima. Uthman, ilitokea kwamba, hakuwa ameuawa kama ilivyotetwa bali alikuwa amekamatwa tu, na sasa wakamuachilia - kitendo kinacho onyesha mabadiliko katika msimamo wao. Pia kuonyesha mabadiliko haya kulikuwa ni ule uchaguzi wao mtu mmoja, Suhayl bin Amr, ambaye walimtuma kwenye kambi ya Waislamu kukamilisha mkataba na Mtume wa Uislamu. Suhayl alikuwa ni mtu aliyeju-likana kama mpatanishi hodari lakini hakuwa madhubuti.

Suhayl aliwasili Hudaybiyya na kufungua majadiliano na Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) Baada ya mazungumzo marefu na mjadala wenye kuchosha walifanikiwa katika kufikia mkataba, ambao masharti yake muhimu sana yalikuwa kama yafuatayo:

1. Muhammad na wafuasi wake watarudi Madina bila ya kutekeleza Umra (Hija Ndogo) ya mwaka ule.

2.  Kutakuwa na amani kati ya Waislamu na Maquraishi kwa kipindi cha miaka kumi kutoka tarehe ya kusaini mkataba huo.

3. Kama mtu yeyote wa Makka ataukubali Uislamu na kutafuta hifadhi kwa Waislamu huko Madina, watamrejesha Makka. Lakini kama mwislamu, aliyekimbia kutoka Madina, akitafuta hifadhi kwa wapagani wa Makka, hawatamrejesha.

4. Makabila yote ya Arabia yatakuwa huru kuingia kwenye mahusiano ya mkataba na kundi lolote - Waislamu ama Maquraishi.

5. Waislamu watatembelea Makka kufanya hijja katika mwaka unaofuata lakini hawatakaa katika mji huo kwa zaidi ya siku tatu, na silaha pekee ambazo wataruhusiwa kuja nazo, zitakuwa ni panga zao ndani ya ala zao.

173

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mkataba huu unaitwa Mkataba wa Hudaybiyya. Ndio nyaraka ya kisiasa maarufu sana katika historia ya Uislamu. Katibu aliyechaguliwa kuandika masharti yake alikuwa ni Ali ibn Abi Talib.

Wakati Mkataba wa Hudaybiyya ulipokuwa unaandikwa, lilitokea tukio ambalo linatoa kiangaza kinachofichua juu ya tabia za baadhi ya waongozaji waliohusika katika kurasimu masharti yake.

Akitoa imla kwa Ali, Mtume (s.a.w.) alisema: "Andika, Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu." Suhayl, yule mjumbe wa Makka, mara moja akatoa pingamizi, na akasema, "Usiandike hivyo. Badala yake, andika, 'Kwa Jina Lako Ewe Allah'" Mtume (s.a.w.) akakubaliana na madai haya.

Mtume (s.a.w.) tena akamwambia Ali aandike: "Huu ni mkataba wa amani kati ya

Muhammad, Mtume wa Allah na Maquraishi.." Suhayl tena akapinga, na akasema:

"Kama tumekukubali wewe kama mjumbe wa Allah kwa nini tuwe tunapigana dhidi yako? Kwa hiyo, usiandike hayo maneno, 'Mtume wa Allah' na andika jina lako mwenyewe tu na jina la baba yako."

Mtume (s.a.w.) alikuwa ameridhia kukubaliana na dai hili pia lakini Ali alikuwa amek-wisha andika tayari maneno haya, "Muhammad ni Mtume wa Allah." na alikataa kuyafu-ta. Alimwambia bwana wake: "Hiki cheo cha juu kimewekwa juu yako na Allah (s.w.t.) Mwenyewe, na sitayafuta kamwe haya maneno 'Mtume wa Allah (s.a.w.) .' kwa mkono wangu." Kwa sababu hiyo, Mtume (s.a.w.) akaichukua ile kalamu mkononi mwake mwenyewe, na akayafuta yale maneno ambayo yalikuwa ni yenye kuchukiza kwa wale waabudu masanamu.

Huu Mkataba wa Hudaybiyya ulisainiwa katika nakala mbili, moja kwa kila upande. R.V.C.Bodley

Ile karatasi ya awali ya Mkataba wa Hudaybiyya ilibakia na Muhammad ambapo nakala yake ilikabidhiwa kwa Suhayl kwa uhifadhi wa salama katika hifadhi ya nyaraka ya Makka.

(The Messenger - the Life of Muhammad, 1946)

Huko Makka viongozi wa Maquraishi waliukaribisha ule Mkataba wa Hudaybiyya kama ushindi wa werevu wao. Walichukulia kwamba Muhammad ameshindwa ujanja na kwam-ba mkataba huo ulikuwa ni sawa na, hata kama sio tangazo rasmi la, "kusalimu amri." Maquraishi walifurahia sana juu ya kile walichofikiria ni kusalimu amri kwa adui lakini matukio yalikuwa mara tu yaonyeshe kwamba walikuwa wamekosea. Mbali kabisa na

174

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kuwa ni kusalimu amri, ule Mkataba wa Hudaybiyya ulikuwa ni mmojawapo kati ya ushin-di mkubwa sana wa Uislamu.

Miongoni mwa wafuasi wa Mtume, hata hivyo, ule Mkataba wa Hudaybiyya ulikuwa uzae hisia zenye mzozo mkali sana. Kwa namna ya kipekee. Kama vile walivyokuwa wale wapagani wa Makka, wale "wazalendo wapofu" katika kambi ya Waislamu pia waliulin-ganisha na "kusalimu amri." Waliongozwa na Umar ibn al-Khattab. Aliyaona masharti yake ni "yenye kufedhehesha," na alikuwa amesikitishwa sana nayo kiasi kwamba alimgeukia Abu Bakr kwa majibu ya maswali yake, na mahojiano yafuatayo yalifanyika kati yao:

Umar: Hivi yeye (Muhammad) ni Mtume au sio Mtume wa Allah? Abu Bakr: Ndio. Yeye ni Mtume wa Allah. Umar: Sisi ni Waislamu au sio Waislamu? Abu Bakr: Ndio. Sisi ni Waislamu.

Umar: Kama sisi ni Waislamu, basi ni kwa nini tunasalimu amri kwa wapagani katika jambo linalohusu imani yetu?

Abu Bakr: Yeye ni Mtume wa Allah. na wewe usiingilie katika jambo hili.

Ufidhuli wa Umar ulishadidi kwa kiwango cha juu baada ya kuaswa na Abu Bakr, na akaenda kumuona Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Baadae alisema: "Nilikwenda mbele ya Mtume, na nikamuuliza: 'Wewe sio Mtume wa Allah?' akanijibu, 'Ndio, mimi ndimi.' Nikauliza tena: 'Sisi Waislamu hatuko sahihi, na wale washirikina hawako kwenye makosa?' Akajibu, 'Ndio, hivyo ndivyo.' Niliuliza zaidi: 'Basi ni kwa nini tunaonyesha unyonge zaidi kwao? Hata hivyo sisi tunalo jeshi. Kwa nini tunafanya amani nao?' Akasema: 'Mimi ni Mtume wa Allah (s.w.t.) na ninafanya kile tu Anachoniamrisha kufanya."

Lakini inaonekana Umar hakuridhika hata na majibu ya Mtume (s.a.w.) mwenyewe kwa maswali yake. Yale masharti ya Mkataba wa Hudaybiyya yamesababisha wasiwasi mkubwa katika akili yake, hivyo alisema: "Nilirudia rudia kumuuliza Mtume (s.a.w.) kuhusu yale masharti ya mkataba huu, na sijawahi kamwe kuongea naye kwa namna hii."

Sir John Glubb.

Wengi wa Waislamu walivunjwa moyo na matokeo ya Hudaybiyya, wakiwa walitara-jia uingiaji kwa ushindi ndani ya Makka. Umar ibn al-Khattab, kama kawaida, alita-

175

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mka hasira zake, 'Huyu siye Mtume wa Allah, na sisi sio Waislamu na wao sio washirikina?' alitaka kujua kwa hasira kutoka kwa Abu Bakr mpole na mwaminifu. 'Kwa nini tusipigane nao; kwa nini tuafikiane hivyo?'

(The Great Arab Conquests)

Tor Andre

Umar aligeukia kwa taharuki kwa Abu Bakr na viongozi wengine waliokuwa karibu na Mtume (s.a.w.) kuhakikisha kama kweli walidhamiria kuridhia fedheha hii (ingawa sio kweli). Alitamka baadae kwamba kamwe kabla ya hapo hajawahi kuwa na mashaka kuhusu ukweli wa Muhammad, na kama angepata angalau watu mia moja wenye mawazo kama hayo, angejiuzulu kwenye umma wa Kiislam.

(Muhammad - the Man and his Faith)

Maxime Rodinson

Umar na baadhi ya wengine walikasirikia lile wazo la kufanya maafikiano na hawa wapagani. Huyu khalifa wa baadae alikuja kumlaumu Mtume. Alitamka baadae kwamba kama angekuwa na watu mia moja upande wake, angejitoa. Lakini Muhammad alikuwa hatingishiki.

(Muhammad, kilichotafsirwa na Anne Carter)

R.V.C.Bodley

Wengi wa wale mahujaji, na Umar hasa, waliaibika sana kwamba Muhammad ame-wakubalia Maquraishi katika karibu kila jambo. Ilionekana ni ajabu kwao kwamba, baada ya kuletwa umbali wote huu na kiongozi wao ambaye hakuwa na woga wa kumuandama adui ambaye alimshinda yeye, wasimamishwe nje ya lengo lao. Ilielekea kushangaza zaidi kwamba amejishusha mwenyewe mbele ya yule mjumbe wa Makka kwa kiasi cha ama kumwita Mola wake kwa jina Lake halali wala kutumia cheo chake mwenyewe, kwa sababu tu yule kafiri amedai hivyo. Umar alifikia kiasi cha kuuliza: "Wewe kweli ni Mtume wa Allah?" Umar alikwenda kuona ni nini Waislamu wengine walichohisi. Aliwakuta wao katika hali hiyo hiyo ya mawazo kama aliyokuwa nayo. Kwa mara ya kwanza tangu Uislamu uanze, kulikuwa na dalili za uasi.

(The Messenger - The Life of Muhammad)

Umar alitamka baadae kwamba tangu aliposilimu, hajawahi kuwa na mashaka kama hayo juu ya ukweli wa Muhammad kama aliyokuwa nayo ile siku Mkataba wa Hudaybiyya uli-posainiwa.

176

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hii ina maana kwamba Umar alikuwa akisumbuliwa na mashaka ya mara kwa mara kuhusu ukweli wa Muhammad na ujumbe wake wa Utume. Yumkini alikuwa akiyazuia kila wakati yalipojitokeza. Lakini kwenye kigezo cha kuthibitisha uasili wake cha Mkataba wa Hudaybiyya, mashaka yake sugu yaliibuka kwa nguvu kali mno kiasi kwamba hakuweza kuyazima. Akitawaliwa na mashaka yake, yeye kwa kweli alifikiria kuuacha udugu wa Kiislamu wenyewe lakini hakuweza kumpata mtu yoyote kwenye kambi hiyo ambaye angeweza kumsaidia kumuunga mkono katika "ujasiri" wake.

Mwelekeo wa mapokezi ya Sunni umekuwa kwamba katika kuonyesha ufedhuli na dharau kwa Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (rehma na amani juu yake na Ahlul-Bait wake), Umar alichochewa na mapenzi yake kwa Uislamu. Kwa mujibu wao, aliupenda sana Uislamu kiasi kwamba "alijisahau." Mwanzoni, alikataa kutii amri ya Mtume (s.a.w.) ya kupeleka ujumbe kwa Maquraishi huko Makka. Kukataa kule, yumkini, kulichochewa na mapenzi hayo hayo.

Wale watu wanaohusisha unafiki wa Umar na mapenzi yake kwa Uislamu, kwa kweli, wanamaanisha kwamba yeye aliupenda Uislamu zaidi kuliko Muhammad, Mtume wa Uislamu mwenyewe alivyoupenda! Pia, kwa tabia yake, alikuwa anamaanisha kwamba Mtume wa Allah (s.a.w.) alikuwa anakosea katika kutafuta amani na Maquraishi lakini yeye mwenyewe alikuwa sahihi, na kwamba ilikuwa ni wajibu wake "kumsahihisha" yeye Muhammad Mustafa.

Kama siku moja hivi kabla, Umar alitoa kiapo cha "kumtii Mtume wa Allah (s.a.w.)" katika hali yoyote ile, kwenye amani na kwenye vita, kwenye neema na kwenye dhiki. Ilikuwa pengine ni kiapo hiki kilichomsukuma kujionyesha yeye binafsi kuwa ni "mfuasi" bora zaidi (wa Uislamu) kuliko "mfalme" mwenyewe (Mtume)!

Kama ni sadfa kwamba wote, Maquraishi wa Makka, na Umar na wafuasi wake katika kambi ya Waislamu, walisoma, "kusalimu amri" kwa Waislamu, katika Mkataba ule wa Hudaybiyya, basi kweli ilikuwa ni ajabu. Lakini kama vitisho vya kijeshi vya Umar vingeishia kwenye kuonyeshana nguvu na Maquraishi, basi mtu anaweza kukisia ni sehe-mu gani angeishughulikia ndani yake, akimpima kutokana na "kumbu kumbu ya matendo" yake mwenyewe, ya kabla na baada.

Akiandika juu ya huu Mkataba wa Hudaybiyya, Lt. Jenerali, Sir John Glubb anasema katika kitabu chake, "The Life and Times of Muhammad":

Madukuduku yaliyovumiliwa na Waislamu pale Hudaybiyya yanadhihirishwa na namna ambavyo zile siku za wasiwasi zilivyobakia zimeganda kwenye kumbukumbu zao. Miaka mingi baadae, wakati majeshi ya Waislamu yalipokuwa tayari yamejenga himaya kubwa, wakati marafiki wakongwe wakizungumzia zile siku za mwanzoni,

177

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

heshima kubwa kabisa ilionyeshwa daima kwa wale watu ambao walipigana kule Badr na kwa wale waliokula kiapo pale Hudaybiyya - ile migogoro miwili mizito ya mwanzo wa Uislamu.

(The Life and Times of Mohammed)

Hapakuwa na yeyote miongoni mwa maswahaba wote wa Muhammad Mustafa ambaye alikuwa na mwenendo wa kiheshima, kote katika vita vya Badr na pale Hudaybiyya, na kwa kweli, katika nyakati zote za hatari katika historia ya Kiislamu, kama Ali ibn Abi Talib. Huko nyuma, alijitokeza mwenyewe kuwa wa kwanza katika vita; huko Hudaybiyya kila mmoja aliona kwamba alikuwa pia wa kwanza katika amani. Amedhihirisha mara nyingi katika vita kwamba alikuwa na imani kamili juu ya Muhammad na ujumbe wake, na sasa alikuwa anadhihirisha katika amani kwamba hakuna chochote ambacho kinaweza kamwe kutingisha imani yake juu ya bwana wake.

Baada ya kuondoka kwa wale wajumbe wa Makka, Mtume (s.a.w.) aliwaamuru Waislamu kunyoa vichwa vyao na kuchinja wanyama wao kama kafara, kama kanuni za Umra. Lakini alishtuka kuona kwamba wengi wao walikuwa katika hali ya uasi na hawakutaka kutii amri zake.

Kilichotokea hasa ni kwamba, Umar alimdharau hadharani Mtume wa Allah (s.a.w.) na kwa mfano wake huo, amewatia moyo wafuasi wake pia kufanya vivyo hivyo. Mtume (s.a.w.) aliingia kwenye hema lake, na akamwambia mkewe kwamba Waislamu walikuwa wanakaidi amri zake. Mkewe akasema kwamba kama angewapuuza hao, na akatekeleza kazi hiyo yeye binafsi, watamfuatisha yeye.

S. Margoliouth

Waislamu walinuna kimya wakati walipoambiwa na Muhammad wanyoe vichwa vyao na kutoa makafara yao. Mwishowe (kwa ushauri wa mkewe, Ummu Salamah), alitekeleza wajibu huo yeye binafsi, na wafuasi wake wakafanya vivyo hivyo.

(Muhammad and the Rise of Uislamu)

Kazi yake ilipokamilika, Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliondoka Hudaybiyya na wale mahujaji, ili kurudi Madina. Alikuwa bado katika safari ya siku saba kutoka Madina, wakati wahy ufuatao ulipokuja kutoka Mbinguni:

178

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hakika tumekupa ushindi wa dhahiri (Sura ya 48; Aya ya 1)

Ulikuwa ni ule Mkataba wa Hudaybiyya ambao huu wahy mpya umeuita "Ushindi wa dhahiri." Amin Dawidar, yule mwanahistoria wa Kimisri, ameandika katika kitabu chake Pictures From the Life of the Prophet (Cairo, 1968 uk.465) kwamba wakati Mtume wa Allah (s.a.w.) alipotangaza rasmi huu wahy mpya unaoitwa "Ushindi," Umar ibn al-Khattab alikuja kumuona, na akauliza: "Huu ndio unaouita Ushindi wa Dhahiri?" "Ndio," akasema Mtume wa Allah (s.a.w.) "kwa Yule Ambaye mikononi Mwake yamo maisha yangu, huu ni Ushindi wa Dhahiri."

Mkataba wa Hudaybiyya ulikuwa kweli ni "Ushindi wa Dhahiri" kama maendeleo ya mfu-lulizo wa matukio ya historia yalivyokuwa yaonyeshe, licha ya ajizi juu yake ya Waislamu wengi katika kambi ya Mtume.

Muhammad Mustafa alikuwa ni Mtume wa amani. Kama angeruhusu mashinikizo ya wale "wazalendo wapofu" katika kambi yake kutumia mbinu za mabavu, ujumbe wake wote ungekuwa hatarini, na vizazi vya wakati ujao vingemshitaki rasmi kwa kupenda kwake "ugomvi." Lakini alikataa mashinikizo ya kuvutiwa kwenye usuluhishi wa silaha, na badala yake, alivutiwa na usuluhishi wa amani, na akapata matokeo ambayo hakuna ushindi wa kijeshi ambao ungeweza kuyapata.

Mkataba ya Hudaybiyya ulikuwa ni matunda ya ustadi wa utawala wa majaaliwa na kipa-ji cha kisiasa cha hali ya juu sana. Ulileta manufaa makubwa sana kwa Uislamu. Miongoni mwao:

1. Maquraishi wa Makka walimkubali Muhammad kuwa ni sawa na wao. Kabla ya hapo walimuona kama muasi na mkimbizi wa kisasi chao.

2. Kwa kuuweka saini mkataba huo, Maquraishi walitoa utambuzi wa kimya wa ile Dola ya Kiislam ya Madina inayochipukia.

3. Wale Waislamu waliokuweko Makka, walificha imani yao mbele ya waabudu masanamu kwa hofu ya mate so kutoka kwao. Lakini baada ya Mkataba wa Hudaybiyya, walianza kutekeleza Uislamu hadharani.

4. Hadi mwaka wa 6 A.H. Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) alikuwa amefungwa katika mapambano yasiyokwisha na wapagani wa Kiarabu na Wayahudi, na hapakuwa na fursa kwa ajili yao ya kuuona Uislamu katika

179

Usahihi-13.jpg

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

matendo. Baada ya Mkataba wa Hudaybiyya waliweza "kuutathmini" Uislamu kwa mara ya kwanza. "Tathmini" hii ilisababisha kusilimu kwa wengi wao, na Uislamu ukaanza kuenea kwa kasi sana. Mkataba wa Hudaybiyya ulifungua milango ya kubadilisha-dini.

5. Makabila mengi ya Kiarabu, ingawa bado wapagani, yalitaka kuingia mikataba ya uhusiano na Waislamu lakini yalijihisi kuzuiwa na upinzani wa Maquraishi. Sasa yaliachiwa uhuru wa kufanya ushirikiano na Waislamu.

6. Mkataba wa Hudaybiyya ni jibu zuri sana kwa wale wakosoaji wanaodai kwamba Uislamu ulienea kwa ncha ya upanga. Hakuna uthibitisho bora zaidi kuliko Mkataba wa ukataaji huu wa vita kwa Muhammad, kama chombo cha sera, na cha mapenzi yake halali ya amani. Wapagani wa Kiarabu walivutiwa sana na propaganda za Maquraishi kwamba Muhammad alitamani sana vita. Sasa waliweza kuona kwa macho yao wenyewe kwamba Muhammad alirudi Madina bila hata ya "kulipiza," ingawa alikuwa na jeshi pamoja naye, na ingawa aliwahi kuwashinda hao Maquraishi mara mbili - mnamo mwaka 624 na 627.

Huu Mkataba wa Hudaybiyya pia unaonyesha chuki ya Qur'an juu ya vita. Kabla ya mkataba, Waislamu walikuwa wamekwisha kushinda zile vita mbili za kihistoria za Badr na Ahzab (Handaki). Kama wangeshindwa katika yoyote kati ya hizo, Uislamu ungetowe-ka kabisa daima kutoka kwenye uso wa dunia. Ushindi katika vita vyote hivi viwili uli-hakikisha uhai wa kivitendo wa Uislamu. Machoni mwa Qur'an, miongoni mwa kampeni zote za Muhammad, ule Mkataba wa Hudaybiyya pekee ndio ulikuwa "Ushindi wa Dhahiri".

Mkataba wa Hudaybiyya ulikuwa ndio utangulizi wa kwenye ushindi wa Uislamu dhidi ya nguvu za upagani, ushirikina, uabudu masanamu, ujinga, dhulma na unyonyaji. Umar ibn al-Khattab alileta kiburi kwenye sharti la tatu la Mkataba huo kwa vile lilikuwa halikubaliani; lakini ilikuwa, kwa usahihi kabisa, ni sharti hili hasa lililowaweka Maquraishi kwenye kujihami mara moja tu, na walikuja kwa kuomba kwa Mtume (s.a.w.) alibatilishe.

Miezi kumi na nane baada ya kusainiwa kwa Mkataba wa Hudaybiyya, Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliingia Makka, kama mshindi, na alifuatana na waumini elfu kumi. Kutekwa kwa Makka kulikuwa ni matokeo ya moja kwa moja ya Mkataba huu. Kwa sababu ya matokeo haya, wanahistoria wengi wameuita kwa usahihi kabisa huu Mkataba wa Hudaybiyya kama ubingwa wa ustadi wa utawala wa Muhammad.

180

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Marmaduke Pichthall.

Kulikuwa na mfazaiko miongoni mwa Waislamu juu ya masharti haya (ya Mkataba wa Hudaybiyya). Waliulizana wenyewe kwa wenyewe: 'Uko wapi huo ushindi ambao tuliahidiwa?' Ilikuwa ni wakati wa safari ya kurudi kutoka al-Hudaybiyya ambapo ile Sura inayoitwa ushindi iliteremshwa. Makubaliano haya (ya kusitisha vita) yalithibitika, kwa kweli, kuwa ndio ushindi mkubwa ambao Waislamu mpaka hapo walikuwa wameupata. Vita vilikuwa ni kipingamizi kati yao na waabudu masanamu, lakini sasa marafiki walikutana na kuongea pamoja, na dini hii mpya ikae-nea kwa haraka sana. Katika miaka miwili iliyopita kati ya kusainiwa kwa makubaliano hayo na kuanguka kwa Makka, idadi ya waliosilimu ilikuwa kubwa zaidi kuliko jumla ya idadi ya wote waliokuwa wamesilimu hapo kabla. Mtume (s.a.w.) alisafiri kwenda al-Hudaybiyya na watu 1400. Miaka miwili baadae, wakati watu wa Makka walipoyavunja makubaliano hayo, alikwenda dhidi yao pamoja na jeshi la watu 10,000.

Introduction to the translation of Holy Qur 'an, 1975)

Kanuni mbili muhimu za Kiislamu zinaweza kuonekana katika utekelezaji wake ndani ya Mkataba wa Hudaybiyya, yaani:

1. Vita lazima iepukwe kwa gharama yoyote ile, labda ikiwa haizuiliki kabisa. Ufumbuzi wa matatizo yote lazima utafutwe na kupatikana kwa njia za amani, kwa kweli bila kuzihatarisha kanuni za Kiislamu. Kwa wapagani na Waislamu wengi, ilionekana kwamba Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) , ametoa "mamlaka kamili" kwa Suhayl, yule mjumbe wa Makka, kwa hiyo kwamba yeye (Suhayl), kwa namna fulani, alitamka masharti yake mwenyewe. Licha ya kujitokeza kama huko, Mtume (s.a.w.) aliyakubali masharti yale. Bila shaka, hapakuwa na hatari kwenye kanuni yoyote. Ilikuwa haiwaziki kwamba Mtume wa Uislamu atapingana na kanuni yoyote ya Kiislamu.

2. Mtume wa Allah (s.a.w.) . hana lazima ya kukubali kushindwa (kwa kus-tahi) na maoni au matakwa ya wafuasi wake, au ya watu kwa jumla. Idadi kubwa sana ya maswahaba zake Muhammad walikuwa hawakubaliani na kutiwa saini kwa Mkataba wa Hudaybiyya. Lakini alipuuza upinzani wao, na akaendelea na kuusaini. Yeye, kwa kweli , wala hakutafuta hata ushauri wa hata mmoja wao katika suala hilo. Kutoka mwanzo mpaka mwisho, aliongozwa, sio na matakwa ya "watu" au matakwa ya "wingi" wa watu bali na amri za Allah (s.w.t.) zilizohifadhiwa katika Kitabu Chake, makhsusi kwenye Aya ifuatayo:

181

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usahihi-14.jpg

Na wahukumu baina yao kwa aliyoyateremsha Allah, wala usifuate matamanio yao. Nawe tahadhari nao wasije kukufitini ukaacha baadhi ya aliyokuteremshia Allah. Na wakigeuka, basi jua kwamba hakika Allah anataka kuwasibu kwa baadhi ya dhambi zao. Na hakika wengi wa watu ni wapotofu. (Sura ya 5; Aya ya 49)

182

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ushindi wa Khaybar

Khaybar ni mji ulioko maili 90 kaskazini ya Madina, ndani ya harra au eneo la volkano, lililo na maji mengi na chemchemu zinazotoka kwenye mawe yake meusi ya msingi ya volkano. Lina mfumo mzuri wa umwagiliaji na linatoa mavuno mengi ya tende na nafaka.

Nyuma kabisa kabla ya wakati wa Mtume wa Uislamu, bonde la Khaybar na mabonde mengine upande wa kaskazini na Kusini, yalikuwa chini ya ukoloni wa Wayahudi. Kama ilivyooneshwa kabla, Wayahudi hawa hawakuwa tu ndio wakulima wazuri wa nchi hiyo, walikuwa pia ni wenye kuongoza katika viwanda na biashara, na walimiliki ukiritimba wa viwanda vya silaha.

Katika nyakati za Mtume, viwanda vizuri vya zana za vita katika Arabia vilikuwa vyote vipo Khaybar. Wale Wayahudi ambao walifukuzwa kutoka Madina, walikuwa pia wameweka makazi huko Khaybar, na walikuwa wanatambulika kwa ustadi wao katika ufuaji-chuma.

Betty Kelen

Hawa Qaynuka walifukuzwa kutoka Madina. Aghalabu walikuwa ni wafuachuma, wakiwa wamejifunza ile sanaa ya kufua deraya bora na zenye kumeremeta, panga zenye umbo la mwezi na helimeti za kuzuia jua ambazo zilifaharisha vita humo jang-wani. Walitengeneza dereya nzuri za shaba nyeusi, zilizofuliwa na kung'arishwa, pamoja na helmeti za kufanana, na panga zinazomeremeta ambazo makato yake makali yanaweza kuifanya hewa kuvuma kwa mlio.

(Muhammad - the Messengeer of God)

Wayahudi wa Khaybar pia walisikia habari kuhusu huo Mkataba wa Hudaybiyya na masharti yake. Kama vile tu Maquraishi wa Makka na Umar bin al-Khattab na baadhi ya "wapenda vita" wengine miongoni mwa Waislamu kule Madina walivyoutafsiri huo mkataba kama "kusalimu amri" kwa Waislamu, ndivyo hivyo pia walivyouona wale Wayahudi wa Khaybar kama ni dalili ya mwanzo ya kuanguka kwa mamlaka ya Nchi ya Madina. Wakitegemea hii nadharia ya "kuanguka," walianza kuyashawishi yale makabila ya Waarabu kati ya Khaybar na Madina kuwashambulia Waislamu. Moja ya makabila haya lilikuwa lile la Ghatafan, marafiki wa Wayahudi wa Khaybar.

Walianza kupeleka misafara yao ya mashambulizi kule kwenye mbuga za malisho karibu na Madina. Moja ya malisho haya yalikuwa ni ya Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Katika safari moja, mtoto wa Abu Dharr al-Ghiffari alikuwa anachunga ngamia wa Mtume (s.a.w.)

183

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wakati hawa Ghatafan waliposhambulia. Wakamuua, na kumteka mama yake ambaye alikuwa pamoja naye, na wakaliswaga pamoja nao lile kundi la ngamia. Waislamu, hata hivyo, waliweza, wakati ule ule tu, kuwakuta wale majambazi na kumuokoa mke wa Abu Dharr al-Ghiffari.

Muhammad aliamua kukomesha uchokozi huu usio na sababu. Alifikiria kwamba hau-takuwa uangalifu kungoja mpaka hao Wayahudi na washirika wao waweke mzingiro mwingine hapo Madina, na kwamba ingekuwa vizuri kuwawahi mapema. Yeye, kwa hiyo, aliwaamuru Waislamu kujikusanya na kuelekea Khaybar.

Mnamo Septemba 628 Mtume (s.a.w.) aliondoka Madina na askari 1600. Baadhi ya wanawake wa Kiislam pia waliandamana na jeshi hilo kwenda kufanya kazi kama wauguzi na kutoa huduma ya kwanza kwa wale walioumia na wagonjwa

Khaybar ilikuwa na ngome nane. Imara zaidi na mashuhuri zaidi ya zote ilikuwa ni ile ngome ya al-Qamus. Kapteni wa askari walinzi wake alikuwa ni shujaa maarufu aliyekuwa akiitwa Mehrab. Alikuwa na, chini ya uongozi wake, wale wapiganaji wazuri wa Khaybar, na walikuwa ni askari waliokuwa na silaha bora wa wakati huo katika Arabia yote.

Muhammad Husein Haykal

Vile vita vya Khaybar vilikuwa moja ya vita kubwa. Idadi kubwa ya Wayahudi waliokuwa wakiishi Khaybar walikuwa ndio wenye nguvu zaidi, matajiri zaidi, na waliojiandaa vizuri zaidi kwa vita kati ya watu wote wa Arabia.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Waislamu, hata hivyo, waliweza kuzikamata ngome zote za Khaybar isipokuwa al-Qamus ambayo ilithibiti kuhimili mashambulizi. Muhammad alimpeleka Abu Bakr katika wakati mmoja, na Umar katika wakati mwingine, na wapiganaji waliochaguliwa, kujaribu uteka-ji wa al-Qamus. Wote walifanya hilo jaribio na wote walishindwa. Baadhi ya Makapteni wengine walijaribu pia kuiteka ngome hiyo lakini wao pia walishindwa. Huku kushindwa kwa marudio rudio kulianza kuhujumu ile hamasa ya jeshi hilo.

Muhammad alitambua kwamba jambo la kutia shauku lazima lifanyike ili kurudisha ile hamasa ya Waislamu inayonywea, na iwe mara moja. Na wakati jaribio jingine zaidi la kuiteka al-Qamus lilipoharibika pia, akili yake ilipata uamuzi, na akatangaza: "Kesho nita-toa bendera ya Uislamu kwa shujaa ambaye anampenda Allah (s.w.t.) na Mtume Wake, na ambaye Allah (s.w.t.) na Mtume Wake wanampenda yeye. Ni mtu anayemshambulia adui lakini hakimbii, na yeye ataiteka Khaybar."

Masahaba walijua kwamba utabiri wa Mtume wa Allah (s.a.w.) utatokea kuwa kweli, na

184

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwamba Khaybar itatekwa katika siku inayofuata. Kila mmoja wao, kwa hiyo, aligeuka kuwa mgombea wa sifa na heshima ya kuiteka Khaybar. Wengi wao walikaa macho usiku mzima kwa tamaa ya kuwa "mpendwa wa Allah (s.w.t.) na Mtume Wake," na kuwa shujaa atakayeiteka Khaybar.

Asubuhi iliyofuata, maswahaba walijikusanya mbele ya hema la Mtume. Kila mmoja wao alikuwa amejipamba katika mavazi ya kijeshi, na alikuwa akichuana na wengine katika kuonekana mwenye kuvutia zaidi.

Wakati huo, Mtume wa Allah (s.a.w.) akatoka nje ya hema lake, na ule umati mkubwa ukaanza kuonyesha dalili za kutotulia. Kila sahaba alijaribu kujionyesha zaidi kuliko wengine kwa matumaini ya kuonwa na jicho la bwana. Lakini huyo bwana hakuonekana kumtambua yeyote kati yao ila alitoa swali moja tu: "Yuko wapi Ali?"

Ali wakati huu alikuwa kwenye hema lake (akiwa anumwa na macho na yamevimba). Alijua kwamba, kama alikuwa yeye ndiye "mpendwa wa Allah (s.w.t.) na Mtume Wake," basi ni yeye, na si mwingine yeyote yule, atakayeiteka ile ngome ya al-Qamus. Mtume (s.a.w.) aliagiza aitwe.

Ali alipokuja, Mtume (s.a.w.)(akamtemea mate machoni na yakapona) kisha yeye kwa taadhima kabisa akaiweka bendera ya Uislamu mikononi mwake. Alimuombea baraka za Allah (s.w.t.) ziwe juu yake, na akaomba kwa ajili ya ushindi, na akamuaga na kumtakia kila la kheri. Huyu kijana shujaa ndipo akasonga mbele na kuelekea kwenye ile ngome ngumu katika Arabia yote ambako wale mashujaa wakubwa wa wapiganaji wa Kiebrania walikuwa wanamngojea yeye. Alipigana dhidi yao wote, akawashinda wote, na akaisimi-ka ile bendera ya Kiislam kwenye mnara mkuu wa ngome hiyo.

Wakati yule mshindi aliporudi kule kambini, Mtume wa Allah (s.a.w.). alimpokea kwa tabasamu nyingi, mabusu na pambaja nyingi, na akamuomba Allah (s.w.t.) kuweka fadhi-la Zake njema juu ya simba Wake.

Ibn Ishaq

Burayda b. Sufyan b. Farwa al-Aslami alinisimulia kutoka kwa baba yake Sufyan b. Amr b. Al-Akwa: Mtume (s.a.w.) alimtuma Abu Bakr pamoja na bendera yake dhidi ya moja kati ya ngome za Khaybar. Alipigana lakini alirudi akiwa amepoteza watu na hakuichukua. Kesho yake alimtuma Umar na mambo yale yale yakatokea. Mtume (s.a.w.) akasema: "Kesho nitampa bendera mtu ambaye anampenda Allah (s.w.t.) na Mtume Wake. Allah (s.w.t.) ataiteka kwa hali yoyote ile. Yeye si mwenye kukimbia." Siku iliyofuatia akaitoa bendera kwa Ali.

(The life of the Messenger of God) 185

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Edward Gibbon

Kaskazini-Mashariki ya Madina, ule mji wa zamani na wa kitajiri wa Khaybar ulikuwa ndio makao ya mamlaka ya Wayahudi katika Arabia: eneo hilo, sehemu yenye rutuba humo jangwani, ilikuwa imejaa mashamba makubwa na ng'ombe, na ikilindwa na ngome nane, baadhi ya hizo zilikuwa zikisifiwa kuwa na nguvu zisizoshindika. Majeshi ya Muhammad yalikuwa ya wapanda farasi 200 na askari wa miguu 1400: katika ule mfuatano wa mizingiro (karantini) nane ya mara kwa mara na michungu, walikuwa kwenye hatari na uchovu, na njaa; na wale majasiri wakubwa kabisa walilikatia tamaa tukio hilo. Mtume (s.a.w.) alihuisha imani yao na moyo kwa mfano wa Ali, ambaye kwake alitoa jina la Simba wa Mungu, labda tunaweza kuamini kwamba shujaa wa Kiyunani wa kimo kikubwa sana alipasuliwa kwenye kifua kwa upanga wake usiozui-lika; lakini hatuwezi kusifia ile staha ya mapenzi, inayomuonyesha yeye kwamba alil-ing'oa kutoka kwenye bawaba zake lile lango la ngome na kuishika na kuitumia ile ngao nzito sana kwenye mkono wake wa kushoto (sic - japo kwa makosa).

(The decline and Fall of the Roman Empire) Washington Irving

Mji wa Khaybar ulikuwa umelindwa sana kwa maboma ya mbele, na ngome yake, Al-Qamus, iliyojengwa kwenye mwamba wa mporomoko, ilichukuliwa kuwa isiy-oingilika. Kuzingira mji huu kulikuwa ndio kazi muhimu sana ambayo Waislamu walikuwa bado hawajaifanya. Pale Muhammad alipoziona kuta zake imara na za kutisha, na ngome yake iliyojengwa kwa mawe, anasemekana aliomba msaada wa Allah (s.w.t.) katika kuiteka.

Kuizingira ile ngome kulichukua muda kiasi, na kukaushughulisha ujuzi na uvu-milivu wa Muhammad na vikosi vyake, kwani bado walikuwa na uzoefu mdogo katika mashambulizi ya sehemu zilizojengewa ngome. Muhammad aliongoza masham-bulizi yeye mwenyewe; wale wazingiraji walijilinda kwa mahandaki, na wakaja na magogo ya kuvunjia ili kuyapiga kwenye kuta hizo; upenyo baada ya muda uli-patikana, lakini kwa siku kadhaa jaribio la kuingia lilizuiwa kwa nguvu sana. Abu Bakr kwa wakati mmoja aliongoza mashambulizi, akiwa ameshika bendera ya Mtume; lakini, baada ya kupigana kwa ujasiri mkubwa, alilazimika kukimbia. Shambulizi lililofuata liliongozwa na Umar ibn al-Khattab, aliyepigana mpaka mwisho wa siku bila mafanikio yoyote ya maana.

Shambulizi la tatu liliongozwa na Ali, ambaye Muhammad alimpa upanga wake mwenyewe, unaoitwa Dhu 'l-Fiqar, au Mwenye Makali. Katika kuikabidhi mikononi mwake ile bendera tukufu, alimtangaza yeye kama "mtu aliyempenda Allah (s.w.t.) na Mtume Wake; na ambaye Allah (s.w.t.) na Mtume Wake wanampenda yeye; mtu ambaye alikuwa hajui woga, wala ambaye kamwe hajageuka nyuma mbele ya adui."

186

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Na hapa ingekuwa vizuri kutoa maelezo ya Hadith juu ya hali na tabia ya Ali. Alikuwa mwenye urefu wa kati, lakini mwenye afya na pande la mtu, na mwenye nguvu nyingi mno. Alikuwa na Sura ya tabasamu, mwekundu mno, mwenye ndevu nyingi. Alitambulikana kuwa mwenye tabia maridhawa, akili ya busara, na ari ya dini, na kutokana na moyo wake wa kijasiri, alipewa jina la Simba wa Mungu.

Waandishi wa Kiarabu wanaandika kwa kuutia chumvi nyingi ya upendo ule ujasiri wa Khaybar, wa huyu shujaa wao kipenzi. Alikuwa amefunikwa, wanasema, na fulana nyekundu, ambayo juu yake imefungwa deraya ya chuma. Akikwea na wafuasi wake juu ya rundo kubwa la mawe mbele ya ule upenyo, aliisimika ile bendera juu yake, akidhamiria kutorudi nyuma mpaka ile ngome iwe imechukuliwa. Wale Wayahudi walishambulia mbele ghafla kuwasukuma chini wale washambuliaji. Katika mapigano yaliyotokea, Ali alipigana mkono kwa mkono na yule kamanda wa Kiyahudi, Al-Harith, ambaye alimuua. Ndugu wa huyu aliyeuawa alisonga mbele kuja kulipa kisasi cha kifo chake. Alikuwa wa kimo kirefu; akiwa na deraya maradufu, vilemba viwili, aliyefunga helmeti ya kinga, ambayo mbele yake inameremeta almasi kubwa. Alikuwa na panga zilizofungwa kuning'inia pande zote mbili, na alikuwa anatikisa mkuki wenye ncha tatu, kama chusa cha ncha tatu. Wapiganaji hawa wakapimana kwa macho, na wakakabiliana kwa majigambo ya mtindo wa kiMashariki. "Mimi" akasema yule Myahudi, "ni Merhab, niliye na silaha sehemu zote, na mkali katika mapambano." " Na mimi ni Ali, ambaye mama yake, wakati wa kuzaliwa kwake, alimpa jina la Al-Haidarr (simba mwenye nguvu)."

Waandishi wa Kiislam wanafanya kazi fupi juu ya huyu shujaa wa Kiyahudi. Alimsonga Ali kwa mkuki wake wenye ncha tatu, lakini ulipanguliwa kwa ustadi sana, na kabla hajaweza kujiweka sawa mwenyewe, pigo kutoka kwenye upanga, Dhu'l-Fiqar lilipasua na kugawa ngao yake, likapita kwenye ile helmeti ya kinga, kupita vile vilemba viwili, na kwenye fuvu sugu, na kupasua kichwa chake mpaka kwenye meno yake. Lile umbo lake refu lilianguka kama gogo mpaka chini ardhini.

Wayahudi sasa wakarudi ndani ya ngome, na shambulizi kubwa likafanyika. Katika joto la harakati hizo ngao ya Ali ilidondoka kutoka mkononi mwake, ikiuacha mwili wake wazi; akivuta ghafla lango, hata hivyo, kutoka kwenye bawaba zake, alilitumia kama ngao katika sehemu ya mapambano iliyokuwa imebakia.

Abu Rafii, mtumishi wa Muhammad, alitoa ushuhuda wa jambo hili: "Mimi baadae," yeye anasema, "nilichunguza lango hili nikiwa pamoja na watu saba na sisi wote wanane tulijaribu bila mafanikio kulitumia hilo."

187

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

(Tendo hili gumu la kishujaa na la ajabu limeandikwa na yule mwanahistoria Abul Fida. "Abu Rafii," anahoji Gibbons, "alikuwa shahidi wa kuona kwa macho; lakini ni nani atakuwa shahidi wa Abu Rafii?" Tunaungana na mwanahistoria huyu maarufu katika shaka yake lakini kama tutahoji kwa hadhari sana uthibitisho wa shahidi wa macho, historia itakuwa nini?)

(The Life of Muhammad)

Sir William Muir

Wayahudi walikusanyika kumzunguka chifu wao Kinana na wakajipanga wenyewe mbele ya ile ngome Al-Qamus, wakiwa wameazimia juu ya mapambano ya mwisho kabisa. Baada ya majaribio yasiyo na mafanikio ya kuwaondoa, Muhammad alipan-ga shambulizi la mwisho. "Nitaiweka ile bendera," alisema - ile bendera kubwa nyeusi - "kwenye mikono ya yule anayempenda Allah (s.w.t.) na Mtume Wake , na ambaye anapendwa nao Allah (s.w.t.) na Mtume Wake; yeye atapata ushindi." Asubuhi iliyofuata ile bendera iliwekwa mikononi mwa Ali, na vikosi vikasonga mbele. Wakati huo, mpiganaji mmoja akatoka mbele kutoka kwenye msitari wa Wayahudi, na akatoa changamoto kwa maadui zake kwenye pambano la mmoja mmoja: "Mimi ni Merhab," alipiga ukelele, "Kama Khaybar yote inavyojua, mpiganaji aliyejawa na silaha, wakati vita inapopamba moto." Ndipo Ali akasonga mbele akisema: "Mimi ni yule ambaye mama yangu aliniita Simba; kama simba wa mvumo wa msituni. Ninawapima maadui zangu katika kipimo cha mapandikizi ya watu."

Wale wapiganaji wakaanza kupigana, na Ali akakipasua kichwa cha Mirhab vipande viwili. Ile safu ya Waislamu sasa ikafanya shambulizi la mwisho kabisa, na, baada ya mapigano makali, wakamrudisha nyuma yule adui. Katika vita hii, Ali alifanya mambo makubwa ya ajabu ya kishujaa. Akiwa amepoteza ngao yake, alikamata linta ya mlango, ambayo aliishika na kuitumia kwa mafankio sana badala yake. Hadithi, katika mwenedo wake mpana, imeibadilisha hii ngao ya papo kwa hapo kuwa mhim-ili mkubwa sana, na kumkuza shujaa huyu kuwa Samson wa pili. Ushindi huo ulikuwa wa wazi, kwani Wayahudi walipoteza watu 93; ambapo kwa Waislamu ni watu 19 tu waliouawa katika vita yote nzima.

(The Life of Muhammad. London, 1877) R.V.C.Bodley

Yeye (Muhammad) alianza vita (vya Khaybar) kwa kupunguza moja moja zile ngome ndogo ndogo. Hili lilipokamilika, alisonga mbele dhidi ya Al-Qamus, ile ngome kuu ya Khaybar. Ilikuwa ni sehemu inayoonekana kutisha na kuta zake ngumu zilizojeng-wa na mwamba wa asili. Njia zote zilikuwa zimelindwa sana, na karibu ya ngome hiyo palikuwa na walinzi walioandaliwa vyema na walio na mahitaji ya kutosha. Vita vya kuzingira havikuwa vimezoeleka kwa hawa wahamahamaji waliozoea uvamizi wa jangwani. Hata hivyo, Muhammad alikuwa na idadi ya zana za uzingira-

188

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ji wa papo kwa hapo zilizokuwa zimewekwa pamoja hapo mahali. Zilizokuwa za nguvu sana kati ya hizo ni magogo ya kuvunjia ya mitende ambayo, hatimae, yali-fanya upenyo mdogo katika hizo kuta.

Ndani ya hizi, Abu Bakr alifanya shambulizi la kishujaa, lakini alirudishwa nyuma. Kisha Umar akajaribu, lakini alipofikia mdomo wa ule mpenyo, ilimbidi arudi nyuma, akiwa amepoteza wengi wa watu wake. Mwishowe, Ali alijitokeza mbele ya ule ukuta, akiwa amebeba ile bendera nyeusi. Alivyokuwa anashambulia, alikariri: "Mimi ni Ali yule Simba; na kama simba anayenguruma msituni, ninawapima maadui zangu kwa kipimo cha mapandikizi ya watu."

Ali hakuwa pandikizi la mtu, lakini alifidia upungufu wake wa urefu kwa upana wake mkubwa na nguvu zake nyingi sana. Leo alikuwa anaogopesha ndani ya koti lisilo na mikono refu jekukudu ambalo juu yake amevaa deraya yake ya kifua na ya mgongo. Kichwani mwake iling'ara helmeti yenye njumu iliyopambwa kwa fedha. Kwenye mkono wake wa kulia alipunga upanga wa Muhammad mwenyewe, Dhu 'l-Fiqar, ambao aliukabidhiwa pamoja na ile bendera nyeusi.

Tena na tena askari wakongwe walimkurupukia Ali. Tena na tena walipepesuka kuto-ka kwake na mikono au vichwa vikiwa vimekatwa. Mwishowe, yule shujaa wa Wayunani wote, mtu aliyeitwa Merhab, aliyewapita uwezo askari wote, alijitokeza mwenyewe mbele ya Ali. Alikuwa amevaa deraya maradufu, na kuzunguka helimeti yake kilikuwa ni kilemba kinene kilichoshikiliwa na almasi kubwa. Alikuwa ame-fungwa mkanda wa dhahabu ambao ulining'inia panga mbili. Hakuzitumia panga hizi, hata hivyo, na aliua kushoto na kulia kwa mkuki wake mrefu wenye ncha tatu. Kwa muda kidogo pambano lilisimama na wapiganaji waliegemea kwenye silaha zao wakiangalia pambano. Merhab, kama Goliath wa Gath, na kamwe hajawahi kushind-wa. Ukubwa wake peke yake ulitishia maadui kabla hawajafika karibu naye. Mkuki wake wenye chembe uliwavunja moyo wale washika panga wastadi.

Mirhab alianza kushambulia kwanza, akimkusudia Ali kwa mkuki wake wenye vyembe vitatu. Kwa muda kidogo, Ali, akiwa hana mazoea na aina hii ya silaha, alizidiwa kidogo. Kisha akajiweka imara na akshindana kwa silaha na huyu Myunani. Kutishia na kupangua kuliupeperusha ule mkuki hewani. Kabla Merhab hajaweza kuchomoa moja ya panga zake, upanga wa Ali ulikwisha pasua kichwa chake kupitia helimet na kilemba chake hivyo kikaangukia pande zote za mabega yake.Wale Wayahudi, kumuona shujaa wao amekufa, wakakimbilia mjini. Muhammad akatoa ishara ya shambulio la jumla. Waislamu wakasonga mbele. Ali aliongoza mashambu-lizi hayo. Alikuwa amepoteza ngao yake wakati wa pambano na, kupata badala yake, aling'oa mlango kutoka kwenye bawaba zake, ambao aliunyanyua mbele yake.

(The Messenger - the Life of Muhammad, 1946) 189

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad Husein Haykal

Wakitambua kwamba hii ndio kambi yao ya mwisho katika Arabia, wale Wayahudi walipigana sana. Jinsi siku zilivyokwenda, Mtume (s.a.w.) alimtuma Abu Bakr pamo-ja na kikosi na bendera kwenye ngome ya Na 'im; lakini hakuweza kuishinda mbali na mapigano makali. Mtume (s.a.w.) tena akamtuma Umar bin al-Khattab katika siku iliyofuatia, lakini hakupata mafanikio yoyote bora zaidi ya Abu Bakr. Katika siku ya tatu, Mtume (s.a.w.) alimwita Ali ibn Abi Talib, na, akimtakia kheri, alimuamuru kuivamia ile ngome. Ali aliongoza majeshi yake na akapigana kijasiri sana. Katika mapambano hayo, alipoteza ngao yake na, akijilinda mwenyewe kwa lango alilolika-mata, aliendelea kupigana mpaka ile ngome ikavamiwa na vikosi vyake. Lango hilo hilo lilitumiwa na Ali kama daraja ndogo ya kuwawezesha wapiganaji wa Waislamu kuziingia zile nyumba zilizokuwa ndani ya ile ngome.

(The Life of Muhammad, Cairo,1935)

Matokeo ya Ushindi wa Khaybar

Ushindi wa Khaybar ni tukio muhimu katika historia ya Uislamu kwani ndio mwanzo wa Dola ya Kiislam na Milki. Mwanahistoria wa Kihindi, M. Shibli, anasema katika kitabu chake cha wasifa wa Mtume:

Khaybar ilikuwa ndio vita ya kwanza ambamo wasiokuwa Waislamu walifanywa raia wa Nchi ya Kiislam. Ilikuwa ndio mara ya kwanza kwamba kanuni za serikali katika Uislamu zilifafanuliwa na kutumika. Kwa hiyo, Khaybar ndio vita vya kwanza vya mafanikio ya Uislamu.

Hapo Khaybar, Dola ya Kiislamu changa ilipata raia wapya na maeneo mapya. Ulikuwa ni mwanzo, sio tu wa hiyo Dola la Kiislamu bali pia wa upanukaji wake. Kama ushindi wa Khaybar ndio mwanzo wa Dola ya Kiislam, basi Ali ibn Abi Talib, mtekaji wake, ndiye msanifu wake mkuu.

Kabla ya ushindi wa Khaybar, Waislamu walikuwa masikini sana au nusu-masikini. Khaybar mara ghafla ikawafanya kuwa matajiri. Imam Bukhari amemnukuu Abdullah bin Umar bin al-Khattab akisema: "Tulikuwa na njaa wakati wote mpaka kwenye ushindi wa Khaybar." Na mwandishi huyo huyo amemnukuu Aishah, mke wa Mtume, akisema: "Haikuwa mpaka wakati wa ushindi wa Khaybar ambapo niliweza kula tende mpaka kuridhika moyo wangu."

Muhajirina hapo Madina hawakuwa na njia ya kutengenezea maisha na kwa hiyo hawakuwa na kipato cha uhakika. Waliweza kuishi tu hivi hivi mpaka wakati wa ushindi

190

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wa Khaybar. Mara tu Khaybar ilipokuwa imetekwa, kulikuwa na mabadiliko ya ghafla katika mali zao.

Montgomery Watt

Mpaka ilipotekwa Khaybar mapato ya jamii ya Kiislamu yalikuwa ya wasiwasi, na wale Muhajirina waliishi kwa kiasi fulani kutokana na misaada au ukarimu wa Maansari.

(Muhammad, Prophet and Statesman)

Khaybar ilionyesha tofauti kwa jamii ya Waislamu kati ya umasikini mkubwa sana na ulimbikizaji mali.

S. Margoliouth

Wakati Waislamu walipokuja kugawana ngawira zao waligundua kwamba ule ushindi wa Khaybar ulizidi kila faida nyingine ambayo Allah (s.w.t.) alitunuku juu ya Mtume wao.

(Mohammed and the Rise of Uislamu, 1931)

Ule ushindi wa Khaybar ulitunukia faida zisizo na mpaka kwa Waislamu; baadhi ya hizo zilikuwa:

1. Kiasi kikubwa cha dhahabu na fedha ambacho Wayahudi walikuwa wamekilimbikiza kwa vizazi vingi.

2. Maghala mazuri kabisa yenye silaha mpya kabisa za nyakati hizo kama panga, mikuki, marungu, ngao, deraya, pinde na mishale.

3. Makundi makubwa ya farasi, ngamia na ng'ombe, na makundi ya kondoo na mbuzi.

4.  Ardhi nzuri inayolimika yenye viunga vya mitende.

Sir John Glubb

Watu wa Khaybar, kama wale wa Madina, waliishi kwa kilimo, hasa cha mitende. Hata leo hii, makabila hayo yana methali isemayo, "Kupeleka tende Khaybar," ambayo ina maana kama ile ile ya usemi wetu, "Kupeleka makaa ya mawe Newcastle." Khaybar ilisemekana kuwa ndio oasis tajiri kabisa huko Hijazi.

(The Life and Times of Mohammed) 191

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Baada ya kushindwa Wayahudi huko Khaybar, Mtume (s.a.w.) ilimbidi afanye baadhi ya mipango mipya kwa ajili ya utawala wa yale maeneo mapya waliyoshinda.

S. Margoliouth

Sasa Muhammad alijishauri juu ya mpango ambao ulikuwa desturi ya kawaida inay-ojulikana ya Uislamu. Kuwaua au kuwafukuza wale wakazi wachapakazi wa Khaybar isingekuwa busara nzuri, kwani isingefaa kwamba Waislamu, ambao watakuwa wakati wote wakitakiwa jeshini, wakaishi mbali sana na Madina. Aidha, ujuzi wao kama wakulima hautalingana na ule wa wamiliki wa awali wa ardhi hiyo. Hivyo alia-mua kuwaacha wale Wayahudi katika kazi yao kwa malipo ya nusu ya mazao yao, yakikadiriwa na Abdullah mtoto wa Rawahah kuwa kama mizigo 200,000 ya tende.

(Mohammed and the Rise of Islam, 1931)

Pigo moja la nguvu la upanga wa Ali lilisuluhisha matatizo ya kiuchumi ya jamii ya Waislamu, na kuweka ukomo kwenye umasikini wake daima. Aliweka pia ukomo kwenye utegemezi wa Waislamu juu ya hali ya kigeugeu na nyepesi kubadilika, kuwalisha, mara atakapoitoa ile ardhi ya Khaybar yenye rutuba kwao.

Bado kuna maana nyingine ambamo hivi vita vya Khaybar vilikuwa vya umuhimu mkub-wa sio tu kwa Waislamu wa wakati wa Mtume (s.a.w.) bali pia kwa vizazi vya baadae. Ilikuwa ni kuondoka, kwa mara ya kwanza, kutoka kwenye desturi ya jadi ya vita vya Kiarabu. Mtindo wa Kiarabu wa mapigano ulikuwa mara nyingi ni wa kiungwana lakini mara nyingi sana ulikuwa usio na ufanisi. Waarabu walijua kidogo kuliko chochote juu ya mikakati, na kile walichojua wao kuhusu mbinu za kivita ni kupiga-na-kukimbia. Waliweka matumaini yao ya ushindi katika uwezo wao wa kuwakamata waathirika wao kwa kustukiza.

Kwa karne nyingi, wamepigana dhidi ya kila mmoja wao, na kwa kawaida walifuata mtindo ule ule wa asili wa kupiga-na-kukimbia, bila mabadiliko katika mbinu. Tumeona jinsi handaki lilivyozuia jeshi la wapiganaji elfu kumi, na kulisimamisha kabisa kwenye kuizin-gira Madina mnamo mwaka 627A.D. Wale majemedari wakubwa wa waabudu- masana-mu kama Khalid bin Walid na Ikrama bin Abu Jahl walikanganywa na lile handaki, na wakawa hawana msaada wowote mbele yake.

Yote hii ilikuwa ibadilike baada ya Khaybar. Ali ibn Abi Talib aliwafundisha Waislamu ustadi wa kuweka mzingiro, na kuteka sehemu zilizojengewa ngome. Aliwafundisha jinsi ya kupanga mikakati ya vita, na jinsi ya kupigana vita vilivyoandaliwa rasmi na vyenye uamuzi kama jeshi lenye nidhamu. Hapo Khaybar, Ali aliuweka ufunguo wa ushindi wa dunia nzima mikononi mwa Waislamu.

192

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Shamba la Fadak

Fadak ilikuwa ni makazi mengine ya Wayahudi karibu na Khaybar. Watu wa Fadak kwa hiari yao walituma wawakilishi wao kwa Mtume (s.a.w.) wakiahidi kujadiliana masharti ya kujisalimisha. Aliikubali ahadi yao ya kujisalimisha, na akawapa haki ya kukaa kwenye ardhi yao kama raia wa Dola ya Kiislam. Fadak ilipatikana kwa namna hii bila ya nguvu yoyote ile kwa upande wa jeshi la Waislamu. kwa hiyo, ilichukuliwa, kama mali binafsi ya Mtume (s.a.w.) .

Muhammad Husein Haykal

Utajiri wa Khaybar ulikuwa ugawanywe miongoni mwa watu wote wa jeshi la Waislamu kwa mujibu wa sheria kwa sababu walipigana ili kuupata. Utajiri wa Fadak, kwa upande mwingine, uliangukia kwa Muhammad, kwa vile hakuna mwis-lamu na hakukuwa na mapigano yoyote yaliyohusika katika kuupata kwake.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Katika siku za mwanzo za historia ya Uislamu, Waislamu, walipokuwa bado wapo Makka, walikuwa masikini sana, na hawakuwa na njia yoyote ya kupatia maisha. Khadija, mke wa Mtume, aliwalisha na kuwapa makazi wengi wao. Alitumia utajiri wake wote juu yao hivyo kwamba alipokufa, hapakuwa na chochote ambacho angeweza kumuachia binti yake, Fatima Zahrah. Sasa wakati shamba la Fadak lilipochukuliwa na Mtume, yeye Mtume (s.a.w.) aliamua kulifanya zawadi kwa binti yake kama fidia kwa mihanga mikub-wa aliyofanya mama yake kwa Uislamu. Yeye, kwa hiyo, alilitoa lile shamba la Fadak kwa binti yake, na likawa mali yake.

Wale Mayahudi wa Wadi-ul-Qura na Tayma, oasis nyingine katika Hijazi, pia walikubali kujisalimisha kwa Mtume (s.a.w.) kwa masharti yale yale ya Khaybar na Fadak, na wakaishi kwenye ardhi zao.

Jafar ibn Abi Talib

Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) alikuwa bado yuko Khaybar wakati binamu yake, Jafar ibn Abi Talib, aliporudi kutoka Abyssinia baada ya kukosekana kwa karibu miaka kumi na nne. Wakati Jafar alipotambua huko Madina kwamba bwana wake alikuwa yuko Khaybar, alielekea huko mara moja. Kwa kutukiza, kuwasili kwake huko Khaybar, kulioana na kutekwa kwa ile ngome ya Al-Qamus na kaka yake, Ali. Muhammad alimpen-da Jafar kama mwanae mwenyewe. Alitupa mikono yake kumkumbatia na akasema: "Sikijui kinachonifanya niwe na furaha zaidi; huu ushindi wa Khaybar au kurudi kwa Jafar."

193

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad Husein Haykal

Muhammad alikuwa na faraha sana kwa kuungana tena na Jafar kiasi kwamba alise-ma hakuweza kueleza ni lipi lilikuwa kubwa zaidi: ushindi juu ya Khaybar au kuungana tena na Jafar.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Umrah au Hijja Ndogo - A.D.629 (8 H.A.)

Mwaka mmoja baada ya Mkataba wa Hudaybiyyah, Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) alikwenda Makka kufanya hijja. Alifuatana na Waislamu elfu mbili. Kulingana na mashar-ti ya Mkataba huo, wale washirikina waliihama Makka kwa siku tatu. Waislamu waliuin-gia mji kutokea upande wa kaskazini, na hawakuwahi kumuona mtu yoyote wa Makka. Mtume wa Allah (s.a.w.) alimpanda ngamia-jike wake, al-Qas 'wa. Rafiki yake, Abdullah ibn Rawaha, alishikilia hatamu zake alipokuwa akiingia maeneo ya Al-Kaaba. Alikuwa anasoma Aya za ile Sura inayoitwa, Ushindi, kutoka kwenye Qur'an. Waislamu wengine walikuwa wakiitikia kwa kurudia "Tuko chini ya amri Yako, Ewe Allah (s.w.t.)! Tuko chini ya amri Yako, Ewe Allah (s.w.t.)!

Wakati Waislamu wote walipokuwa wamekusanyika ndani ya uwanja wa Al-Kaaba, Bilal alipanda juu ya jengo hilo na kupiga Adhana (mwito wa Waislamu kwenye Swala) - ya kwanza kabisa katika Nyumba ya Allah (s.w.t.) na watu elfu mbili wakaitika kwenye wito wake.

Washirikina walikuwa wakishuhudia mandhari hii kutoka kwenye vilele vya vilima vinavyozunguka lile bonde la Makka. Hawajawahi kuona nidhamu ya namna hiyo hapo kabla, wakati Waislamu wa uzao-bora walipokuwa wakitii bila ukaidi, wito wa mtumwa wa zamani wala hawajaona udhihirisho wa usawa na umoja. Lile kundi kubwa la Waislamu lilisogea kama mwili mmoja, na Maquraishi waliweza kuona kwa macho yao wenyewe kwamba ulikuwa ni mwili ambamo mlikuwa hamna utofautishaji kati ya matajiri na masikini, mabwana na watwana, weusi na weupe, na Waarabu na wasiokuwa Waarabu. Maquraishi pia waliweza kuona kwamba ule udugu, usawa na umoja wa watu ambao Uislamu ulikuwa unauendeleza haukuwa dhana ya kinadharia bali ulikuwa ni kweli tupu. Ilikuwa ni mandhari ya kuvutia sana na haingeweza kushindwa kugusa nyoyo hata za wale waabudu sanamu sugu kabisa.

Ule mwenendo wa Waislamu ulikuwa wa namna yake. Walikuwa na shauku sana ya kutok-ufanya kitu chochote kile ambacho kimekatazwa, na walikuwa na moyo wa kufanya kitu kimoja tu - kutii amri za Allah (s.w.t.)

Na bado udhihirishaji huu ndani ya Al-Kaaba wa nidhamu wa Waislamu, ulikuwa usio-fanyiwa mazoezi, uliojitokeza wenyewe kabisa. Si kwa chochote katika dunia hii ambacho

194

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mwarabu alikuwa na mzio (allergic) sana kuliko kwenye nidhamu; lakini alibadilishwa, ndani ya miaka michache, kwa muujiza wa Uislamu. Ule "mguso" wa Uislamu umem-fanya kuwa kiigizo cha nidhamu miongoni mwa mataifa ya dunia.

M. Shibli, yule mwana historia wa Kihindi, anaandika ndani ya kitabu chake Sira-tun-Nabi (Maisha ya Mtume), juz.1,uk.504, chapa ya 11 (1976), kilichochapishwa na Maarif Printing Press, Azamgarh, U.P., India, kwamba mwishoni mwa siku tatu, wakuu wa Maquraishi walimwendea Ali ibn Abi Talib, na wakamwambia: "Tafadhali mfahamishe Muhammad kwamba ule muda uliopangwa umepita na yeye na wafuasi wake, kwa hiyo, waondoke hapa Makka." Ali alitoa ujumbe huo kwa Mtume. Naye Mtume (s.a.w.) mara moja akatekeleza, na akawaamuru Waislamu kuondoka Makka ambapo waliondoka hapo na wakaanza safari yao ndefu kuelekea nyumbani.

Waislamu walifanya ile Umrah, na kisha wakarudi majumbani kwao huko Madina. Ilikuwa ni katika wakati huu ambapo Khalid ibn al-Walid na Amr bin Al-Aas walipoamua kusil-imu. Walikwenda Madina, wakasilimu na kujiunga na safu za Muhajirina. Wote hawa wal-ijaaliwa kuwa maarufu katika siku za baadae kama majenerali wa Abu Bakr na Umar ibn al-Khattab kwa mfuatano.

Barua za Mtume (s.a.w.) kwa Watawala wa Nchi Jirani

Mnamo Augasti 629, Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliandika barua kwa watawala wa nchi jirani akiwaita kwenye Uislamu.

E.Von Grunebaum

Mnamo mwaka 629, Muhammad alituma barua kwa watawala sita - mfalme wa Uajemi, mfalme wa Byzantine, Najashi wa Abyssinia, gavana wa Misri, mtoto wa mfalme wa Bani-Ghassan, na chifu wa Bani Hanifa huko Kusini-Mashariki ya Arabia, akiwalingania kwenye Uislamu.

(Classical Uislamu - A History 600 - 1258)

Muhammad alikuwa Mtume wa Allah (s.w.t.), sio tu kwa Waarabu bali kwa dunia nzima.

Ulikuwa ni wajibu wake kufikisha ujumbe wa mwisho wa Allah (s.w.t.) kwa wanadamu,

na alifanya hivyo. Profesa Margoliouth, hata hivyo, anazichukulia barua hizi kama mwan-

zo wa uchokozi na utekaji nyara. Anasema:

Karibu na wakati wa vita vya Khaybar, yeye (Muhammad) alitangaza mpango wake wa kuuteka ulimwengu kwa kutuma barua kwa watawala ambao umaarufu wao amekwisha usikia.

(Mohammed and the Rise of Islam, 1931)

Ni kweli kwamba ule mpango wa Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) ulikuwa ni mmoja wa "kuiteka-dunia," bali sio kwa nguvu ya silaha. Makusudio yake yalikuwa ni kuziteka

195

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

akili na nyoyo za wanaume na wanawake, ambayo Uislamu uliyafanya katika wakati wake, na bado unayafanya hadi leo.

Katika kuzituma barua hizi, Mtume (s.a.w.) alishawishiwa na shauku yake kwamba watu wote waishi katika utii wa amri na sheria za Allah (s.w.t.). Utii kwenye hizo amri na sheria peke yake ndio unaoweza kuhakikishia amani, furaha na ustawi wa mwanadamu katika dunia hii, na wokovu wake huko Akhera.

196

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

VITA VYA MU'UTAH

Mnamo mwaka 629, lile kabila la Kiarabu la kikristo la Banu Ghassan lilikuwa likitawali-wa na Shorhail, mtoto wa mfalme ambaye alikuwa ni mtwana wa mfalme wa Byzantine. Alikuwa mmoja wa wale watawala ambao walipokea barua kutoka kwa Muhammad Mustafa akiwataka kuingia Uislamu. Katika siku hizo alikuwa na baraza huko Muutah, mji uliokuwa Mashariki ya Bahari ya Chumvi. Wakati mwakilishi wa Mtume, Harith bin Umayr, alipowasili kwenye baraza lake akiwa na barua yake, aliamuru kuuawa kwake.

Kuuawa kwa Harith bin Umayr kilikuwa ni kitendo cha kikatili kisichosababishwa na uchokozi, na mauaji ya balozi yanachukuliwa kama kosa lisilosameheka katika mataifa mengi. Mtume (s.a.w.) aliamua kuchukua hatua ya kuadhibu. Aliandaa jeshi la watu 3000, na akalituma chini ya ukamanda wa rafiki yake na muachwa huru, Zayd bin Haritha, kwen-da Muutah, kudai fidia. Wakati huo huo, alifanya mkusanyiko wa ukamanda na madaraka. Kama akifa Zayd, amri ya jeshi hilo ilikuwa iende kwa Jafar ibn Abi Talib. Kama na yeye ikibidi auawe, basi jenerali wa tatu ilikuwa awe Abdullah ibn Rawaha.

Wakati Shorhail aliposikia kwamba kuna jeshi linaloelekea kwenye makao yake makuu kutoka Madina, yeye pia aliwakusanya watu wake, na mara akawa tayari kukutana nalo. Alipanga vikosi vyake upande wa Kusini, nje ya kuta za Muutah. Viliundwa na askari wal-inzi wa Kirumi wa Muutah, na makundi ya askari wa kikabila yaliyokusanywa wakati huo huo. Pale Waislamu walipowasili na kuitathmini hali halisi, walitambua kwamba yatakuwa ni mapigano yasiyolingana kwa jinsi walivyozidiwa idadi na maadui.

Viongozi wa Waislamu wakafanya baraza la kivita. Zayd bin Haritha akapendekeza kwamba watume mjumbe mara moja kwa Mtume (s.a.w.) kumuarifu yeye juu ya kutolingana katika nguvu za majeshi hayo mawili, na kumuomba atume askari wa nyongeza. Lakini Abdullah bin Rawaha akampinga, na akasema kwamba uamuzi wa kupigana au kutopigana haukuwa juu ya idadi yao, na kama wamezidiwa idadi na maadui, haikuwa na muhimu kwao. "Tunapigana ili kupata shahada ya kufa kishahidi, na sio heshima ya ushindi, na hii ni fursa yetu; tusiikose hii," alisema. Abdullah bin Rawaha aliushinda mjadala kwa hoja zake zenye nguvu, na Waislamu wakasonga mbele kukutana na maadui. Katika pambano la mwanzo kabisa la silaha, Zayd ibn Haritha, yule jenerali wa kwanza wa Waislamu, akauawa.

Betty Kelen

Zayd alibeba bendera ya Mtume (s.a.w.) na akauawa mara moja kabisa, Mwislamu wa kwanza kufa kwa ajili ya dini katika ardhi ya ugenini.

(Mohammed, Messenger of God) 197

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kisha kamandi ya jeshi ikaenda kwa Jafar ibn Abi Talib, kaka yake mkubwa Ali. Alipigana kishujaa na kwa muda mrefu, akiwaua maadui wengi kiasi kwamba miili yao ilijipanga kama kamba ya kuni kumzunguka yeye. Lakini baadae askari wa Kirumi alitambaa kuto-ka nyuma, bila ya kuonekana, na akampiga kwa upanga wake kwenye mkono wake wa kulia, na akaukata kabisa. Jafar hakuiachia bendera ianguke chini, na alizidi kumbana adui. Baadae kidogo, Mrumi mwingine akaja kutokea nyuma, na kwa pigo la upanga wake, akaukata mkono wa kushoto pia. Shujaa huyu, akiwa bado hajakata tamaa, aliishikilia bendera chini ya kidevu chake, na akaendelea kusonga mbele. Lakini kuondoka mikono yote miwili, hakuweza kujilinda mwenyewe, na katika muda mchache, Mrumi wa tatu alimso-gelea, na akamuua kwa rungu lake kichwani mwake. Baada ya kifo cha Jafar, Abdullah bin Rawaha alichukua uongozi wa jeshi hilo, naye pia alianguka akipigana dhidi ya upinzani mkali.

Washington Irving

Miongoni mwa ujumbe tofauti ambao Muhammad ameutuma nje ya mipaka ya Arabia kuwavuta watoto wa kifalme wa jirani kuingia kwenye Uislamu, ulikuwa ni mmoja kwa gavana wa Basra, soko kuu ndani ya mipaka ya Syria. Mwakilishi wake aliuawa huko Muutah na Mwarabu wa kabila la kikristo la Ghassan, na mtoto wa Shorhail, aliyekuwa gavana, aliyetawala Muutah kwa jina la Heraclius.

Muhammad alituma jeshi la watu 3000 dhidi ya mji huu wenye hatia. Ilikuwa ni safari ya maana sana, kama ambavyo ingeweza, kwa mara ya kwanza, kuleta silaha za Uislamu kupambana na zile za Himaya ya Kirumi. Ukamanda ulikabidhiwa kwa Zaid,mtumwa wake aliyemuacha huru. Baadhi ya maafisa waliochaguliwa waliun-ganishwa naye. Mmojawapo alikuwa binamu yake Muhammad, Jafar, huyo huyo ambaye, kwa ufasaha wake, alithibitisha uhalali wa mafundisho ya Uislamu mbele ya mfalme wa Abyssinia, na akamshinda yule balozi wa Kiquraishi. Alikuwa katika ujana wake sasa, na akitambulika kwa ujasiri na uzuri wake wa kidume.

(The Life of Mohammed)

Wakati Jafar alipokuwa anamshambulia adui, aliimba wimbo. Sir William Muir ametoa tafsiri ifuatayo ya wimbo wake huo:

Peponi! Oh Peponi! Mahali pazuri kiasi gani pa kupumzikia! Maji yake ni ya baridi pale, na kivuli kizuri.

Roma, Roma! Saa yako ya majonzi inakaribia. Wakati nitakapopambana naye, nita-mtupa chini ardhini.

198

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Pale Jafar alipouawa, mwili wake uliletwa kambini. Abdullah bin Umar bin al-Khattab, ambaye alikuwa pamoja na jeshi hilo, anasema kwamba aliyahesabu majeraha kwenye mwili wa shujaa huyu, na akayakuta zaidi ya hamsini, na yote yalikuwa mbele. Jafar alithubutu upanga na mkuki hata baada ya kupoteza mikono yake, lakini hakukwepa.

Wakati majenerali wote watatu waliochaguliwa na Mtume (s.a.w.) walipokuwa wameuawa, Waislamu waliachwa bila kiongozi kwa muda. Kisha Khalid bin al-Walid ambaye alikuwa akipigana kwenye safu, akaikamata ile bendera, na akamudu kuwaku-sanya wale Waislamu. Usiku majeshi yale yaliacha mapigano, na hii ilimpa fursa ya kupanga upya watu wake. Anasemekana kupigana vita vya kujihami katika siku iliyofuata lakini akitambua kwamba ilikuwa vigumu kupata ushindi, aliamuru kurudi nyuma kutoka Muutah, na akafanikiwa kufikisha mabaki ya lile jeshi Madina.

Pale wapiganaji hao walipoingia Madina, walipata "mapokezi" ambayo lazima yali-wafanya wao kusahau yale "mapokezi" ambayo Warumi waliwapa huko Muutah. Walikaribishwa na makundi yanayowazomea ambayo yaliwatupia mavumbi nyusoni mwao na takataka vichwani mwao, na kuwasuta wao kwa kumkimbia adui badala ya kufa kama wanaume kama sio kama mashujaa. Hatimae, Mtume (s.a.w.) mwenyewe alilazimi-ka kuingilia kati kwa niaba yao kuwaokoa kutokana na kuvunjiwa heshima na maudhi.

Sir Willam Muir

Safu za Waislamu tayari zilikuwa zimevunjika; na wale Warumi wakiwa katika ufukuzaji kamili walifanya maangamizi makubwa sana miongoni mwa wale wakim-bizi. Hivyo, tofauti kabisa, katika kitabu cha Wackidi. Baadhi ya maelezo yanadai kwamba Khalid alilikusanya jeshi, na ama aliigeuza siku dhidi ya Warumi, ama ali-ifanya kuwa vita isiyo na mshindi. Lakini mbali na kwamba kifupi cha maelezo yote ni ushahidi wa kutosha wa kinyume chake, mapokezi ya hilo jeshi wakati wa kurudi kwao Madina, yanakubaliana na uamuzi mmoja tu, yaani, kushindwa kabisa, kunakofedhehesha na kusikorekebishika.

(The Life of Mohammed, London, 1861)

Sir John Glubb

Katika vita vya Muutah, Jafar ibn Abu Talib, kaka yake Ali, aliichukua ile bendera kutoka kwa Zaid anayekufa na akainyanyua juu mara nyingine tena. Maadui wakam-zonga huyu shujaa Jafar, ambaye mara tu aligubikwa na majeraha. Hadithi inaelezea kwamba wakati mikono yake yote ilipokatwa ikiwa bado imeng'ang'ania ile bendera, bado alisimama imara, akiishikilia bendera hiyo kati ya vigutu vyake, mpaka askari wa ki-Byzantine alivyompiga pigo lililomsababishia kifo.

199

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wakati wale Waislamu walioshindwa walipokaribia Madina, Mtume (s.a.w.) na watu wa pale mjini walitoka kuwalaki. Wale raia wakaanza kuwatupia uchafu wale askari wenye huzuni, wakiwapigia mayowe, "Nyie wakimbizi, mmeikimbia njia ya Allah (s.w.t.)!" Lakini Muhammad, kwa ule upole wa ubaba ambao alijua jinsi ya kuutumia vizuri, aliingilia kati kwa niaba yao.

Asubuhi iliyofuata huko Msikitini, Mtume (s.a.w.) alitangaza kwamba ameona, kati-ka ruiya, wale mashahidi wa Muutah huko peponi, wakiegemea katika makochi, lakini Jafar alikuwepo pale katika umbo la Malaika mwenye mbawa mbili, zilizotapakaa ile damu ya kifo cha ushahidi kwenye manyoya yao. Ilikuwa ni kwa matokeo ya ruiya hii kwamba shahidi huyu tangu hapo akijulikana kama Jafar Mwenye Kuruka, Jafar at-Tayyar.

(The Great Arab Conquests)

Betty Kelen

Pale lile jeshi lilipokuja likielekea nyumbani, yeye (Muhammad) alitoka kwenda kuwalaki, mtoto wa Jaafer akiwa juu ya mgongo wa farasi mbele yake. Kulikuwa ni kurudi nyumbani kunakohuzunisha kwa hawa watu ambao walirudi kutoka vitani wakiwa hai, wakimfuata Khalid, ambapo ndugu zake Mtume (s.a.w.) mwenyewe na maswahaba wapendwa wakiwa wameanguka. Watu wa Madina waliokota michanga na uchafu humo njiani kulirushia lile jeshi linalorudi, wakipiga makelele, "Waoga! Wakimbizi! Mumemkimbia Allah (s.w.t.)"

(Muhammad, the Messenger of God)

Baadhi ya wanahistoria wa Kiislamu wamefanya juhudi kubwa "kuthibitisha" kwamba Muutah ulikuwa ni ushindi wa Waislamu ambapo haukuwa. Haieleweki ni kwa nini kushindwa kunachukuliwa na wao kama ushindi. Hili jaribio la kuthibitisha kwamba Waislamu walishinda vita hiyo, kunaweza kuwa kumechochewa na shauku yao ya kuwatambulisha askari wa Waislamu kama wasioshindika. Lakini watauzima ukweli hivi hivi tu kuthibitisha kwamba Waislamu walikuwa hawashindiki. Hata hivyo, Waislamu wal-ishindwa katika vita vya Uhud!

Abul Kalam Azad, yule mwandishi wa Kihindi wa wasifa wa Mtume, anasema kwamba Waislamu walilazimisha kushindwa kwa kipigo kwa Warumi wa Muutah. Anahakiki yale mapokezi ambayo wenyeji wa Madina waliwapa wale "washindi" pale waliporudi nyumbani, lakini anayahusisha na "kutokujua" kwao, na anasema kwamba walipokea taarifa za uongo za matokeo ya vita hivyo.

200

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Lakini kama wenyeji hao walipokea taarifa za uongo, basi ni ajabu kwamba hakuna hata mmoja kati ya hao wapiganaji aliyejaribu kuwasahihisha. Hakuna hata mmoja kati yao, kwa mfano, aliyewaambia wenyeji hao kwamba: "Hii ndio namna yenu ya kuwapokea mashujaa wa Uislamu, kwa uchafu na takataka? Mnawalipa watetezi wa hii dini kwa kuwazomea na kuwakashifu?" Bali hawakuuliza swali lolote la namna hiyo.

Hata kama wenyeji wa Madina walipotoshwa kwamba Waislamu walishindwa huko Muutah, kama Azad anavyodai, basi ingewachukua muda kiasi gani kuweza kugundua huo ukweli? Katika nafasi ya kwanza, hao wapiganaji wenyewe hawakupinga pale wenyeji walipowafunika na takataka, kama ilivyokwisha onekana. Katika nafasi ya pili, baadhi yao walitahayari kabisa kutoka nje ya nyumba zao. Hawakutaka kuonekana hadharani kwa hofu ya kulaumiwa au hata kufanyiwa ukatili na wenyeji hao kwa woga wa kinyonge waliouonyesha mbele ya jeshi. Shauku yao kubwa ilikuwa ni kujificha wenyewe kwa kila mtu mwingine.

D. S.Margoliouth

Wale waliosalia kwenye mapigano Haya ya maafa makubwa ya (Muutah) walilakiwa na Waislamu kama watoro, na wengine walikuwa hata waoga wa kutokeza hadharani kwa kiasi cha muda. Watu wa Madina walikuwa wavumilivu kiasi hicho katika miaka yao nane ya hali ya vita.

(Mohammed and the Rise of Uislamu, 1931) Muhammad Husein Haykal

Mara tu Khalid na lile jeshi walipofika Madina, Muhammad na Waislamu walitoka kwenda kuwalaki, Muhammad akimbeba mkononi mwake, Abdullah, mtoto wa Jafar, kamanda wa pili wa jeshi la Waislamu. Baada ya kuzijua hizo habari, watu hao walirusha mavumbi kwenye nyuso za askari wa Kiislam na kuwashutuma kwa kukimbia mbele ya macho ya adui na kuiacha njia ya Allah (s.w.t.) Mtume wa Allah (s.a.w.) alihojiana na watu hao kwamba wale wapiganaji hawakukimbia bali wali-jiondoa tu ili, kwa mapenzi ya Allah (s.w.t.) kuja kushambulia tena. Mbali na uthibitisho huu kwa upande wa Muhammad wa lile jeshi la Waislamu, watu hao hawakuwa tayari kuwasamehe kujitoa kwao na kurudi. Salamah ibn Hisham, mmo-jawapo katika msafara huu, hakwenda ama Msikitini kuswali wala kujionyesha hadharani kwa kuepuka kuadhibiwa kutokana na kukimbia kutoka kwenye njia ya Allah (s.w.t.) Isingekuwa ule ukweli kwamba watu hawa hawa, hasa Khalid ibn al-Walid, walijipatia sifa kubwa katika vita dhidi ya adui huyo huyo, heshima yao ingebakia daima yenye madoa.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

201

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Ushahidi" mwingine ambao Abul Kalam Azad ameupata wa huo "ushindi" wa Waislamu huko Muutah, ni kwamba hao Warumi hawakuwafukuza. Anasema kwamba kama hao Warumi wangeshinda hiyo vita vya Muutah, wangewafukuza hao Waislamu mpaka kwenye milango ya Madina yenyewe, na zaidi ya hapo.

Lakini hao Warumi wangeweza kuwa na sababu nyingine ya kutowafukuza hao Waislamu. Mojawapo ilikuwa kwamba kwa jeshi lao la farasi, wasingeweza kuwa na ujanja humo jangwani. Kwao jangwa lilikuwa kama bahari, na sio wao wala Wayunani waliokuwa na "meli" yoyote ya "kusafiria" ndani yake. Cha maana walichoweza kufanya, kilikuwa ni kutekeleza shughuli zao "ufukweni" kama "majeshi ya nchi kavu" ambayo wao, kwa kweli, ndiyo waliyokuwa, na katika kizuizi kilichoamuliwa kimkakati na ki-ustadi wa mbinu dhidi ya taifa la "Pwani" kama hao Waarabu.

Kama Waarabu walikimbilia jangwani mbele ya adui mkakamavu, usalama wao ulipata uhakiuka. Hakuwa tu ameandaliwa kupenya hilo jangwa. Matatizo ya lojistiki (mpangilio wa ugavi na usafirishaji wa watu na vitu) peke yake ya kuwashambulia kwenye asili yao wenyewe kulivunja nguvu ile mioyo yenye ujasiri mkubwa ya siku zile. Jangwa lilikuwa ndio "ngome" ambayo iliwalinda Waarabu kutokana na shauku za watekaji wote wa nyakati zilizopita, na kuwahakikishia uhuru wao na kujitegemea.

Sir John Glubb

Msingi wa operesheni zote za vita za mwanzoni, dhidi ya Uajemi na dhidi ya Syria kwa namna moja, ni kwamba wale Waajemi na Wabyzantium hawakuweza kutembea ndani ya jangwa, wakiwa wamepanda farasi. Waislamu walikuwa kama majeshi ya baharini, wakivinjari karibu na ufukweni ndani ya meli zao, ambapo Waajemi na Wabyzantium kwa kufanana waliweza kushika nafasi juu ya ufukwe tu (yaani, sehe-mu iliyolimwa) wasiweze kushuka "baharini" na kumshambulia adui ndani ya asili yake mwenyewe ya jangwa. Hali kadhalika hao Waarabu, kama vile wale maharamia wa Norway au Wadenishi walioshambulia Uingereza, walikuwa mwanzoni wanao-gopa kusogea ndani ya nchi mbali na "meli" zao. Wakishambulia maeneo yaliyokuwa "ufukweni" mwa hilo jangwa, waliharakisha kurudi kwenye asili yao wakati hatari ilipowatishia.

(The Great Arab Conquests, 1963)

202

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Joel Carmichael

Kuna kufanana kwa ajabu kati ya mkakati wa Mabedui na ule wa majeshi ya bahari-ni ya kisasa. Ikiangaliwa kutoka mahali pafaapo kuangalia mambo ya wahamaji hamaji, hilo jangwa, ambalo waliloweza kulitumia vizuri, lilikuwa kama bahari kubwa ambayo ndani yake walimiliki vile vyombo vilivyokuwepo. Mabedui wali-weza kulitumia kwa ugavi wa vifaa na mawasiliano - na kama kimbilio wanaposhind-wa. Waliweza kutokeza kutokea ndani yake kabisa wakati wowote walipopenda na kuchurupuka kurudi tena kwa hiari yao. Hii iliwapa usogeaji mkubwa sana na uimara, alimradi walikuwa wanasonga dhidi ya jamii zenye maskani.

(Shaping of the Arabs, 1967)

Vita hivyo vilipiganwa nje kidogo tu ya Muutah. Kama Waarabu wangewashinda Warumi na kuwafukuza, basi walifanya nini na mji huo ambao uliangukia miguuni kwao? Kama watekaji, iliwabidi waumiliki. Lakini hakuna mwanahistoria aliyedai kwamba Waislamu waliingia mji wa Muutah na wakaumiliki.

Waarabu walivuma kwa kupenda kwao ngawira. Huu ni ukweli unaojulikana kwa kila mwanafunzi wa historia yao, na wanahistoria kama Abul Kalam Azad hawawezi kutokuu-jua. Mwanahistoria huyu huyu anasema kwamba idadi ya Warumi na washirika wao ambao waliopigana hapo Muutah ilikuwa ni elfu mbili. Kama Waislamu waliwashinda hao Warumi, basi walipaswa wawe wameteka maelfu wa Warumi, na iliwabidi warudi Madina wakilemewa na nyara na hazina za Muutah. Lakini hawakufanya hivyo. Kumbukumbu za kihistoria ziko kimya juu ya jambo hili. Hakuna utajo wa ngawira yoyote au wafungwa wowote wa kivita katika maelezo ya hivyo vita vya Muutah. Ukimya huu ni ushahidi unao-jieleza wazi kwamba hao Waislamu hawakuwa ndio washindi. Kwa kweli, walijiona wao wenyewe ni wenye bahati kuweza kuwa wameondoka wakiwa hai kutoka kwenye uwanja wa vita.

Muhammad Husein Haykal

Baada ya vita vya Muutah, jeshi la Waislamu likiongozwa na Khalid ibn al-Walid, lilirudi Madina sio walioshinda wala walioshindwa, lakini wakifurahia kabisa kuweza kurudi.

(The Life of Muhammad,Cairo, 1935)

203

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Tunawapenda wale Waislamu ambao walijijua kwamba walionyesha woga katika vita vya Muutah, na waliuonea haya. Lakini walikuwepo Waislamu wengine, baadhi yao maswaha-ba wa Mtume, ambao walikimbia kutoka vitani, sio mara moja, bali mara nyingi, na hawakuwa na haya juu ya utendaji wao. Mtu anaweza akapendezewa nao kwa kujikausha kwao hata hivyo. Kuokoa maisha yao wenyewe ya thamani, waliweza kukimbia kutoka kwenye medani ya vita, na kisha kuirudia wakati mizani ilipoinamia upande wa Waislamu. Vita vya Muutah vilikuwa ni kushindwa kwa Waislamu. Na kwa Warumi, haikuwa cho-chote zaidi ya mikwaruzo midogo ya mpaka. Waliwasukuma Waarabu kuwarudisha jang-wani, na kwao wao tukio hilo lilifungwa.

204

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mapambano ya Dhat es-Salasil

Vita vya Muutah vilipiganwa mwezi wa Septemba 629. Katika mwezi uliofuata, Mtume (s.a.w.) alipokea taarifa kwamba watu wa kabila la Qadha'a walikuwa wakijikusanya huko kaskazini mwa Wadi-ul-Qura kwa nia ya kuvamia Madina. Haya yalikuwa ni matokeo ya moja kwa moja ya kule kushindwa kwa Waislamu kule Muutah. Makabila ya kipagani yaliamini kwamba uwezo wa Waislamu ulivunjika kule Muutah, na kwamba kama watashambulia Madina, hawakudhani wangekutana na upinzani wowote.

Ilimbidi Mtume (s.a.w.) kuchukua hatua-kinzani kuvuruga matembezi ya kikabila kuingia Madina. Yeye, kwa hiyo, alituma jeshi la askari mia tatu chini ya ukamanda wa Amr bin Al-Aas, kuwachunguza wale wa-Qadha'a katika nchi yao wenyewe, na kuwatawanya, ikibidi kuwa lazima.

Amr aliondoka Madina, na kusimama kaskazini mwa Wadi-ul-Qura, karibu na chem-chemii iliyokuwa ikiitwa Dhat es-Salasil. Alishtuka kuona makundi ya watu wa makabila wenye silaha wakizurura ndani ya hilo bonde na akatuma mjumbe kwa Mtume (s.a.w.) akimuomba askari wa ziada. Mtume (s.a.w.) mara moja alitekeleza, na akatuma watu wengine mia mbili chini ya ukamanda wa Abu Ubaidah ibn al-Jarrah. Kundi hili la pili walikuemo Abu Bakr na Umar.

Wakati Abu Ubaidah alipofika kwenye kambi ya Amr bin Al-Aas, alionyesha kwamba angetaka kuchukua uongozi wa vikosi vyote vya ziada. Lakini majibu ya Amr kwa pen-dekezo hili yalikuwa ni hapana yenye mkazo. Alifanya ieleweke wazi kwa Abu Ubaidah kwamba yeye (Amr) alikuwa ndiye kamanda mkuu wa vikosi vyote, cha kwake mwenyewe na vile vya ziada vile vile, ambavyo huyu wa baadae (Abu Ubaidah) alivyole-ta, watu mia tano wote.

Wakati wa usiku kulikuwa na kushuka kwa ghafla kwa hali ya joto, na hali ya hewa ikawa ya baridi isiyo ya kawaida. Wale askari wa farasi wakawasha mioto midogo midogo kwa ajili ya joto, na wakakaa kuizunguka. Amr, hata hivyo, aliwaamuru kuizima mioto hiyo. Wote wakatii isipokuwa Abu Bakr na Umar. Amr akarudia kutoa amri yake. Lakini bado wakabakia kimya ambapo Amr akatishia kuwatupa wote kwenye moto huo kama wataen-delea kutomtii yeye. Umar akamgeukia Abu Bakr na kumlalamikia juu ya tabia isiyo na adabu na ya ghafla ya Amr. Abu Bakr akamwambia kwamba Amr aliuelewa ujanja wa vita vizuri zaidi kuliko wao wanavyo zielewa, na kwa hiyo walipaswa kumtii. Ndipo wao wakauzima huo moto.

Katika siku iliyofuata kulikuwa na mapigano yasiyo na utaratibu lakini wale watu wa makabila walipigana bila mpango au nidhamu na walitawanywa mara moja. Waislamu walita-

205

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ka kuwafukuza kwenye vilima na mabonde lakini Amr aliwakataza kufanya hivyo. Watu hao wa makabila waliacha mizigo yao na Waislamu wakaikusanya. Waliteka vile vile ngamia wengi na kondoo, na kisha wakarudi Madina.

Wakati wa vita hiyo, na katika safari ya kurejea, Amr bin Al-Aas aliongoza vikosi vyake katika Swala. Kwa hiyo aliwadhihirishia kwamba alikuwa ni kiongozi wao katika nyanja zote - kivita na kidini. Abu Ubaidah, Abu Bakr na Umar, wote watatu, walipokea amri kutoka kwake, na waliswali Swala zao nyuma yake.

Pale msafara huo uliporudi Madina, Umar alilalamika kwa Mtume (s.a.w.) kuhusu ile tabia yake isiyo ya heshima na ya uonevu ambayo mkuu wake wa kikosi, Amr bin Al-Aas, aliy-omtendea yeye na Abu Bakr huko Dhat es-Salasil. Ilikuwa ni desturi ya Mtume (s.a.w.) kuwahoji Makapteni wake waliporudi kutoka kwenye msafara. Walikuwa wampe taarifa pana yenye kueleweka juu ya mwenendo wa vita hivyo.

Amr alikuwa tayari kutetea vitendo vyake. Alimwambia Mtume (s.a.w.) kwamba Waislamu walikuwa wachache sana, na ile mioto mikubwa ingeweza kufichua ukosefu wao wa idadi kubwa kwa maadui. Ilikuwa ni kwa maslahi ya usalama wao wenyewe, alise-ma, kwamba aliwaamuru wao kuizima. Aliendelea kusema zaidi kwamba ile sababu ya kwa nini aliwakataza watu wake kuwafukuza wale maadui ilikuwa kwamba hao maadui walikuwa kwenye nchi yao wenyewe, na wangeweza kujikusanya kirahisi na kuwasham-bulia wao. Hao Waislamu, alifafanua, walikuwa wakipigana kwenye nchi wasiyoizoea, na walikuwa, kwa hiyo, katika hali ngumu. Mtume (s.a.w.) aliridhika na maelezo ya Amr, na akayakataa malalamiko ya Umar.

Sir William Muir

Kule kurudishwa nyuma kwa majeshi yake kutoka Muutah kuliathiri vibaya ile hadhi kubwa ya Muhammad miongoni mwa makabila ya mpakani mwa Syria. Kulikuwa na minong'ono kwamba yale makabila ya kibedui ya maeneo yale yalikuwa yameku-sanya jeshi kubwa, na walikuwa hata wakitishia shambulio la ghafla juu ya Madina. Amr, yule mwislamu mpya, aliwekwa kwa hiyo kuwa kiongozi wa watu mia tatu pamoja na farasi thelathini, pamoja na maagizo ya kuyakomesha yale makabila yenye uadui na kuwashawishi wale aliowaona ni wepesi kukubali, na kushambulia mara kwa mara ule mpaka wa Syria.

Baada ya mwendo wa siku kumi aliweka kambi kwenye chemchemi karibu na mipa-ka ya Syria. Pale aliona kwamba maadui walikuwa wamekusanyika kwa idadi kubwa, na kwamba aliweza kutafuta msaada kidogo kutoka kwenye makabila ya kienyeji. Alisimama na kutuma mjumbe kwa ajili ya majeshi ya nyongeza. Muhammad mara moja akajibu, na akatuma watu mia mbili, ambao miongoni mwao walikuwemo Abu Bakr na Umar, chini ya uongozi wa Abu Ubaidah. Katika kujiunga na Amr, Abu Ubaidah alitaka achukue uongozi wa jeshi lote, au

206

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

angalau abakie kuwa kiongozi juu ya kikosi chake mwenyewe; lakini Amr, akitoa ahadi ya uamuzi na uimara ambao ulimtambulisha katika siku za baadae, alisisitiza katika kushika uongozi mzima. Abu Ubaidah, mtu mwenye tabia ya upole na mwenye kushawishika kirahisi, akashindwa. "Kama unakataa kukubali mamlaka yangu," alisema, "sina shauri bali kukutii wewe; kwani Mtume (s.a.w.) aliniagiza kabisa nisiruhusu mabishano, wala mgawanyiko wowote wa uongozi." Amr akajibu kwa sharti: "Mimi ni mkuu wako. Umeleta tu nyongeza kwenye jeshi langu." "Naiwe hivyo," alisema Abu Ubaidah. Amr kisha akaanza kuongoza vile vikosi vilivyoun-gana, na akaongoza Swala; kwani hapo mwanzoni utendaji wa kiroho katika Uislamu uliunganishwa na ule wa kisiasa na kijeshi.

(The Life of Mohammed, London, 1877) Muhammad Husein Haykal

Wiki chache baada ya kurudi kwa Khalid, Mtume (s.a.w.) alitafuta kufidia zile pengo katika heshima ya Waislamu katika sehemu za kaskazini za peninsula hiyo ambazo yale mapambano yaliyotangulia na wale Byzantium yalizosababisha. Yeye, kwa hiyo, alimwagiza Amr ibn al-Al-Aas kuwaamsha Waarabu watembee kuelekea al-Sham. Alimchagua Amr kwa kazi hii kwa sababu mama yake yeye huyu alitokana na mojawapo ya hayo makabila ya kaskazini, na alitegemea kwamba Amr ataweza kutu-mia kiungo hiki kurahisisha kazi yake. Wakati alipowasili kwenye chemchem iliyokuwa ikiitwa al-Salasil, katika nchi ya Judham, akihofia kwamba maadui wanaweza kumkuta, alituma ujumbe kwa Mtume (s.a.w.) akiomba askari wa ziada. Mtume (s.a.w.) alimtuma Abu Ubaidah ibn al Jarrah akiongoza kundi la Muhajirina

ambalo walikuwemo Abu Bakr na Umar...

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Amr bin Al-Aas alikuwa mwislamu mpya. Lakini mara alipokuwa mwislamu, alinyanyukia haraka sana kutoka askari wa kawaida mpaka jenerali katika jeshi la Madina. Ni dhahiri kabisa, alikuwa amejaaliwa na uwezo usiokuwa na kifani kote, kama jenerali na kama mtawala. Mtume, kwa hiyo, aliwaweka watu ambao walikuwa wakubwa kwa miaka mingi kuliko yeye, na ambao waliingia Uislamu muda mrefu zaidi kabla yake, chini ya uongozi wake.

Abu Ubaidah na Abu Bakr walikwisha kuwa Waislamu miaka ishirini kabla ya Amr, na hivyo wao waliwakilisha "shaba" ambapo Amr bin Al-Aas alikuwa "kajiwe" tu katika imani kwa wakati huu. Na bado Mtume (s.a.w.) alimuamuru Abu Ubaidah kutumika chini ya Amr.

Hii inathibitisha tu kwamba ilipofika wakati wa Mtume (s.a.w.) kuchagua mtu kushika uongozi katika shughuli fulani, alitilia maanani, sio umri wake, bali uwezo wake - uwezo wa kupata matokeo!

207

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kutekwa kwa Makka

Maquraishi walishindwa kutumia ushindi wao wenyewe juu ya Waislamu katika vita vya Uhud, lakini hawa Waislamu waliposhindwa katika vita vya Muutah na Wakristo, wali-jaribu kutumia ule ushindi wa Wakristo, na kurudisha ile hali ya kabla y a Hudaybiyya katika Arabia. Kushindwa kwa Waislamu kule Muutah kulichukua nafasi kubwa katika matukio yaliyotangulia kuanguka kwa Makka mnamo mwaka 630.

Muhammad Husein Haykal

Tunaweza kukumbuka kwamba mara tu Khalid na lile jeshi waliporudi Madina bila ya uthibitisho wa ushindi (katika vita vya Muutah), waliitwa wakimbizi. Askari wengi na makamanda walijihisi kuabika sana kiasi kwamba walikaa majumbani ili wasionekane na kudhalilishwa hadharani. Vile vita vya Muutah viliwapa Maquraishi ile picha kwamba Waislamu na nguvu zao sasa wameangamizwa na kwamba, hadhi yao na hofu ambavyo hapo kabla waliviingiza kwa wengine vyote vimetoweka. Hii iliwafanya Maquraishi kuegemea kwa nguvu sana kwenye hali zilivyokuwepo kabla ya Mkataba wa Hudaybiyya. Walidhani sasa wangeweza kuanzisha vita ambavyo dhidi yake Waislamu walikuwa hawawezi kujihami wenyewe, bila kuzungumzia juu ya kujibu mashambulizi au kulipiza kisasi.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Kulingana na makubaliano ya ule Mkataba wa Hudaybiyya, yale makabila ya Waarabu yalikuwa huru kuingia kwenye mahusiano ya mkataba ama na Waislamu au hao Maquraishi. Kwa kuchukua fursa ya mapatano haya, lile kabila la Banu Khuza'a waliandi-ka mkataba wa urafiki na Mtume wa Uislamu, na kabila lingine - Banu Bakr - wakawa washirika wa Maquraishi. Uhasama ulidumu baina ya haya makabila mawili tangu nyakati za kabla ya Uislamu lakini sasa yote yalipaswa yafuate masharti ya ule Mkataba wa Hudaybiyya, na kuepuka kushambuliana.

Lakini miezi kumi na nane baada ya huo Mkataba wa Hudaybiyya kutiwa saini, kundi la wapiganaji la Banu Bakr ghafla likawashambulia Banu Khuza'a majumbani mwao wakati wa usiku. Wakati wa shambulio hili unatolewa kama ni mwishoni mwa Rajab ya mwaka wa 8 A.H. (Novemba 629). Banu Khuza'a hawakufanya chochote kuchochea shambulio hili. Walichukua hifadhi katika maeneo ya Al-Kaaba lakini maadui zao waliwafuatilia hata hapo, na wakawaua baadhi yao. Wengine waliokoa maisha yao kwa kutafuta ulinzi wa Budail bin Waraka na rafiki yake, Rafa'a, katika nyumba zao, hapo Makka.

208

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad Husein Haykal

Ule Mkataba wa Hudaybiyya uliandika kwamba mtu yoyote asiye wa Makka akitaka kujiunga na kambi ya Muhammad au ile ya Maquraishi anaweza kufanya hivyo bila ya kipingamizi. Kwa msingi wa kipengele hiki, lile kabila la Khuza'a lilijiunga na safu ya Muhammad, na lile la Banu Bakr likajiunga na Maquraishi. Kati ya Banu Khuza'a na Banu Bakr idadi ya migogoro ya zamani ambayo ilikuwa haijasuluhishwa ilibidi isimamishwe kwa sababu ya mipango mipya. Pamoja na Maquraishi kuamini kwamba (baada ya vita vya Muutah) uwezo wa Waislamu umevunjika, Banu al Dil, ukoo mmoja wa Banu Bakr, walidhani kwamba muda umefika wa kilipiza kisasi chao dhidi ya Khuza'a.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Banu Bakr wasingeweza kuwashambulia Khuza'a bila ya kula njama na kutiwa moyo kama sio kuungwa mkono kwa uwazi na Maquraishi. Tabari, yule mwanahistoria, anase-ma kwamba Ikrima bin Abu Jahl, Safwan bin Umayya na Suhayl bin Amr, wote watu mashuhuri wa Quraishi, walijibadili wenyewe na kupigana kwenye upande wa Banu Bakr dhidi ya Khuza'a. Kati ya hawa watatu, huyu wa mwisho kutajwa ndiye mweka saini mkuu wa Maquraishi kwenye Mkataba wa Hudaybiyya.

Maxime Rodinson

Katika Rajabu ya mwaka wa 8 (Novemba 629), katika mfululizo wa kisasi cha kurithi baina ya koo ambacho kilikuwa kikiendelea kwa miongo kadhaa, baadhi ya wale waliotaharuki sana katika Maquraishi kule nyuma yao, walishambulia kikundi cha kabila la Khuza'a, washirika wa Muhammad, sio mbali sana kutoka Makka. Mtu mmoja aliuawa na waliobakia waliumizwa vibaya na kulazimishwa kukimbilia ndani ya eneo tukufu la Makka. Wakifuatiliwa hata huko walichukua hifadhi kwenye nyumba mbili za kirafiki. Kwa aibu sana hawa Banu Bakr waliweka mzingiro kwenye nyumba hizo. Kwa jumla watu ishirini wa Khuza'a waliuliwa.

(Mohammed, kilichotafsiriwa na Anne Carter)

Mmoja wa wakuu wa Khuza'a, Amr bin Salim, alikwenda Madina na kumsihi Mtume (s.a.w.) kuingilia kati. Mtume alishituka kusikia habari hizo za ufisadi. Kama mshirika wa hao Khuza'a, alipaswa kuwalinda kutokana na maadui zao. Lakini kabla ya kufikiria hatua za kijeshi, alijaribu kutumia njia za amani ili kupata marekebisho na haki. Alituma mjumbe kwa Maquraishi, na akashauri kwamba:

209

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

* Wale wateja wa Maquraishi, yaani, Banu Bakr, au Maquraishi wenyewe walipe fidia ya damu kwa Banu Khuza'a, au;

*  Maquraishi wabatilishe ulinzi wao wa Banu Bakr, au;

* Watangaze ule Mkataba wa Hudaybiyya kuwa umefutwa.

Zarqani anasema kwamba mtu aliyewajibia Maquraishi alikuwa ni Qurtaba bin Umar. Alimwambia mjumbe wa Mtume (s.a.w.) kwamba lile la mwisho tu kati ya masharti yale matatu ndio lililokuwa linakubalika kwao. Kwa maneno mengine, Maquraishi wal-imwambia kwamba ule Mkataba wa Hudaybiyya pamoja na makubaliano yake ya miaka kumi ya kusimamisha vita, tayari ni "kanuni isiyo na nguvu" kiasi wao walivyohusika.

Wale wakaidi wa Maquraishi walikuwa wepesi kuukana ule Mkataba wa Hudaybiyya laki-ni haraka sana wale viongozi wao wakweli zaidi na makinifu walitambua kwamba lile jibu walilopeleka Madina lilikuwa ni kosa la kijinga kwani lilitamkwa, sio kwa busara na heki-ma, bali kwa ufedhuli na ujinga. Na pale walipofikiria juu ya matokeo gani ya kitendo chao yatakayokuwa, waliamua kuchukua hatua haraka sana kuzuia maafa. Lakini vipi? Baada ya mjadiala wa kusisimua, walikubaliana kwamba Abu Sufyan aende Madina, na ajaribu kumshawishi Mtume (s.a.w.) kurudia upya ule Mkataba wa Hudaybiyya.

Wakati Abu Sufyan alipowasili Madina, alikwenda kwanza kumuona binti yake, Ummu Habiba - mmoja wa wake zake Mtume. Alipokuwa anataka kukaa juu ya zulia, binti yake akalivuta kutoka chini yake, na akasema: "Wewe ni muabudu masanamu usiye na tohara, na siwezi kukuruhusu kukalia zulia la Mtume wa Allah (s.a.w.)" Alimfanya kama mtu aliyetengwa na jamii, asiyegusika. Akishtushwa na mapokezi kama hayo, alimuacha na kuondoka na akaenda Msikitini akitegemea kumuona Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Lakini Mtume (s.a.w.) hakumpa fursa ya kuonana naye. Baadae aliomba msaada wa Abu Bakr, Umar na Ali lakini wote walimwambia kwamba hawawezi kumuombea yeye kwa Mtume, na akarudi Makka mikono mitupu.

Maquraishi waliuvunja ule mkataba, na wajumbe wa Khuza'a walikuwa bado wapo Madina, wakidai haki. Kama Mtume (s.a.w.) angesamehe lile kosa la Maquraishi, angeiabisha vibaya sana heshima yake machoni mwa Waarabu wote. Asingeweza kukubali hili litokee. Hatimae, Mtume (s.a.w.) aliamua kuiteka Makka, na aliwaamuru Waislamu wakusanyike.

Jeshi hilo la Uislamu liliondoka Madina mnamo mwezi kumi ya Ramadhini ya mwaka wa 8 H.A. (1 Feb.630). Habari kwamba kuna jeshi lililokuwa linaelekea upande wa Kusini, zilienea haraka sana humo jangwani, na hata zikafika Makka kwenyewe. Wale watu wa ukoo wa Bani Hashim ambao walikuwa bado wako Makka, wakaamua, baada ya kusikia habari hizi, kuondoka hapo mjini na kukutana na hilo jeshi linalokuja. Miongoni mwao

210

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

walikuwa ni Abbas bin Abdul Muttalib, yule ami yake Mtume; Aqiil bin Abi Talib, na Abu Sufyan bin al-Harith bin Abdul Muttalib, binamu zake. Walijiunga na jeshi hilo la Uislamu, na wakaingia tena Makka pamoja nalo.

Mnamo mchana wa mwezi 19 Ramadhan, jeshi hilo liliwasili Merr ad-Dharan kaskazini ya Makka, na likasimama hapo ili kuupitisha usiku huo. Usiku Mtume (s.a.w.) aliwaamuru wapi-ganaji wake kuwasha mioto midogo midogo, na uwanda wote ukamulikwa na maelfu ya mioto.

Abu Sufyan na Hakim bin Hizam walikuwa wameondoka pia Makka kwenda kuchunguza zile taarifa za uvamizi wa Waislamu. Wakielekea kaskazini kwenye njia iendayo Madina, wao pia waliwasili Merr ad-Dharan, na walipigwa na butwaa kuona mioto midogodogo isiyo na idadi ikiwaka ndani ya bonde hilo. Walipotambua kwamba wako kwenye kambi ya Waislamu, walipata taabu sana wasijue chakufanya kujiokoa wao wenyewe au mji wao.

Abbas bin Abdul Muttalib pia alikuwa na wasiwasi mkubwa juu ya usalama wa watu wa Makka. Alihofia kwamba kama watatoa upinzani, watauawa kwa wingi. Alikuwa amem-panda yule farasi mweupe wa Mtume (s.a.w.) kupita mle kambini, ambapo katika mpaka wake wa Kusini, alikumbana ghafla na Abu Sufyan na Hakim bin Hizam. Aliwaambia kwamba wanaweza kuona ile idadi ya Waislamu, na kwamba Maquraishi hawakuwa na uwezo wa kushindana nao. Abu Sufyan alimuuliza ni nini yeye angepaswa kufanya . Abbas akamwambia afuate nyuma yake juu ya farasi wake mwenyewe, na kwamba atampeleka kwa Mtume, na atajaribu kupata hati ya usalama kwa ajili yake. Hakim bin Hizam akaru-di Makka kwenda kuelezea juu ya kile alichokiona na kusikia. Abbas na Abu Sufyan wali-wapanda farasi wao kuingia kwenye kambi ya Waislamu wakati huo huo, walipita karibu na hema la Umar, naye Umar akataka kujua ni akina nani hao wageni wawili.

Pale Umar alipomtambua Abu Sufyan, alisisimka, na akamwambia: "Ewe adui wa Allah (s.w.t.) hatimae uko kwenye mamlaka yangu, na sasa nitakuua." Lakini Abbas akamwambia kwamba yeye (Abu Sufyan) yuko chini ya ulinzi wake. Pale pale Umar alikimbia kwenda kumuona Mtume (s.a.w.) na kumuomba ruhusa yake ili amuue (Abu Sufyan). Lakini Mtume (s.a.w.) alimwambia tu Abbas amlete asubuhi itakayofuata.

Mapema sana asubuhi iliyofuata, Abbas, Abu Sufyan na Umar, wote watatu walitokea mbele ya hema la Mtume. Umar alikuwa na hamu ya kumuua Abu Sufyan lakini Mtume (s.a.w.) alimzuia, na akamualika Abu Sufyan kusilimu. Abu Sufyan hakuwa na moyo sana wa kuukubali Uislamu lakini Abbas alimwambia kama hakusilimu, basi Umar atamuua, na hatarudi kamwe Makka. Akikabiliwa na tishio la kifo, Abu Sufyan aliitamka Shahada ambayo ilimwingiza rasmi kwenye jamii ya Waislamu.

Abbas pia alimuomba Mtume (s.a.w.) kumpa Abu Sufyan upendeleo fulani ambao angeulinganisha na "heshima maalum." Mtume (s.a.w.) akasema wale watu wote wa

211

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Makka watakaoingia kwenye nyumba ya Abu Sufyan, au watakaokaa kwenye nyumba zao wenyewe, au watakaoingia kwenye maeneo ya Al-Kaaba, watakuwa salama kutokana na madhara yote. Abu Sufyan alijivuna sana kwamba Mtume (s.a.w.) ameitangaza nyumba yake kuwa kimbilio la waabudu masanamu wa Makka. Marafiki zake wa baadae na wapenzi wanaringia ile "heshima maalum" yake mpaka leo.

Ilikuwa ni Ijumaa, Ramadhan 20, 8 A.H. (Feb.11, 630) pale jeshi la Waislamu lilipovunja kambi pale Merr ad-Dharan, na kuelekea Makka. Abbas na Abu Sufyan walisimama juu ya ukingo wa kilima kuangalia vile vikosi vikipita mbele yao. Huyu Abu Sufyan alivutiwa sana na utaratibu huo, na nidhamu, ile idadi na moyo wa mshikamano wa mipangilio, na akamwambia Abbas:

"Mpwa wako kwa hakika amepata ufalme mkubwa na mamlaka makubwa." Abbas akamkaripia: "Ole wako! Huu ni Utume na sio ufalme." Abu Sufyan alikuwa hajawahi kuona mandhari ya kutisha kama hii hapo kabla, na kwa hisia zake za kipagani, na uono wake wenye kikomo kabisa, aliweza kuitafsiri tu katika istilahi za mamlaka yakinifu. Lakini alitambua kwamba mchezo wake na waabudu masanamu umekwisha hatimae, na kitu muhimu sasa kilikuwa ni kuokoa maisha yake na yao.

Abu Sufyan aliharakisha kurudi Makka, na akiingia kwenye maeneo ya Al-Kaaba, alike-mea kwa sauti kubwa: "Enyi watu wa Makka! Muhammad amewasili pamoja na jeshi lake, na hamna uwezo wa kumpinga yeye. Wale miongoni mwenu watakaoingia nyumbani kwangu, watakuwa salama kutokana na madhara yote, na sasa ni kusalimu amri kwenu tu bila ya masharti kutakakoweza kuwaokoeni na mauaji ya halaiki."

Mke wa Abu Sufyan, Hinda, aliusikia mwito wake huo. Alishikwa na hasira kali, akatoka kwa kasi nje ya nyumba yake, akamshika kwenye ndevu zake, na akapiga may owe: "Enyi watu wa Makka! Muueni huyu mpumbavu asiye na bahati. Ana upungufu wa akili. Muondoeni yeye na mlinde mji wenu kutokana na adui yenu."

Lakini ni nani anayeweza kuilinda Makka na vipi? Sasa hivi, Abu Sufyan alikuwa amezungukwa na raia wengine wa Makka, na mmoja wao akamuuliza: "Nyumba yako inaweza kuchukua watu wachache tu. Ni vipi watu wengi watakavyopata kimbilio ndani yake?" Akasema: "Wale wote watakaokaa ndani ya nyumba zao au watakaoingia kwenye viwanja vya Al-Kaaba, watakuwa pia salama." Amri hii ilikuwa na maana kwamba kile ambacho waabudu masanamu hao wanachoweza kufanya kuokoa maisha yao, kilikuwa ni kubaki ndani ya nyumba zao, na kuepuka kushindana na wale wavamizi.

Washington Irving

Muhammad aliandaa msafara wa siri wa kuishtukiza Makka. Njia zote zinazoelekea Makka zilifungwa kuzui taarifa zozote za harakati zake kubebwa na kupelekwa

212

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Makka. Lakini miongoni mwa wakimbizi kutoka Makka, alikuwepo mtu mmoja, Hatib, ambaye familia yake ilibakia nyuma, na walikuwa bila kiunganisho au marafi-ki wa kuweza kujali juu ya ustawi wao. Hatib sasa alifikiria kupata msaada kwa ajili yao miongoni mwa Maquraishi, kwa kuisaliti mipango ya Muhammad. Yeye kwa hiyo, aliandika barua inayofichua lile jambo kubwa lililokusudiwa, na akaitoa mikononi mwa mwanamke anayeimba, ambaye alijitolea kuipeleka Makka. Mwanamke huyo alikuwa tayari njiani wakati Muhammad alipofahamishwa juu ya usaliti huo. Ali na watu wengine watano, wenye vipando vizuri, walitumwa kum-fukuzia huyo mjumbe. Walimkuta mara moja, lakini wakampekua mwili mzima bila mafanikio. Wengi wao wangejiachia huo upekuzi na kurudi lakini Ali alikuwa na hakika kwamba Mtume wa Allah (s.a.w.) asingeweza kukosea wala kupewa taarifa za uongo. Akichomoa upanga wake, aliapia kumuua huyo mjumbe labda barua ikitole-wa. Tishio hilo lilileta athari. Aliitoa barua hiyo kutoka kati ya nywele zake.

Hatib, katika kulaumiwa kwa usaliti wake, aliukubali; lakini alikiri shauku ya kupata msaada kwa ajili ya familia yake masikini, na uhakika wake kwamba barua ile isingekuwa na madhara, na isiyo na mafanikio dhidi ya malengo ya Mtume wa Allah

(s.a.w.).

Umar alizikataa sababu hizo na angemkata kichwa chake; lakini Muhammad, akikumbuka kwamba Hatib alipigana kishujaa katika kuitetea dini katika vita vya Badr, alimsamehe.

Muhammad, ambaye alikuwa hajui ni upinzani gani atakaokutana nao, alifanya ugawaji wa uangalifu wa vikosi vyake alipokuwa akikaribia Makka. Wakati kikosi kikubwa kilisonga mbele moja kwa moja, vikosi imara vilisonga juu ya vilima kwenye pande zote. Kwa Ali ambaye aliongoza kikosi kikubwa cha wapanda farasi, alikabidhiwa ile bendera tukufu, ambayo ilikuwa aisimike juu ya Mlima Hadjun, na kuibakisha hapo mpaka Mtume (s.a.w.) atakapoungana naye. Amri dhahiri zilitolewa kwa majenerali wote kuwa wenye subira, na kwa namna yoyote ile wasiwe wa kwan-za kushambulia.

(The Life of Muhammad)

Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliingia Makka tokea upande wa kaskazini. Usamah, mtoto wa rafiki yake na shahidi wa Muutah, Zayd bin Haritha, alikuwa amepanda nyuma ya farasi pamoja naye. Kichwa cha Muhammad kilikuwa kimeinamishwa chini, na alikuwa akisoma ile Sura kutoka ndani ya Qur'an iitwayo "Ushindi"

Ali alibeba ile bendera ya Uislamu alivyokuwa juu ya farasi mbele ya kile kikosi cha wapanda farasi. Mtume (s.a.w.) alimuamuru Zubayr bin al-Awwam kuingia mjini hapo kutokea upande wa Magharibi, na Khalid bin al-Walid kutokea upande wa Kusini. Alitoa amri kali kwa jeshi lake wasimuue mtu yoyote isipokuwa katika kujihami. Alitamani siku

213

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

nyingi kuyaharibu yale masanamu ndani ya Al-Kaaba lakini alitaka kufanya hivyo bila ya umwagaji damu wowote. Amri zake zilikuwa wazi na dhahiri; hata hivyo, Khalid aliuwa watu wa Makka 28 kwenye lango la Kusini la mji huo. Alisema kwamba alikutana na upin-zani.

Sir John Glubb

Utwaaji wa Waislamu, wa Makka ulikuwa kwa kweli si wa kumwaga damu. Yule mwenye harara, Khalid bin al-Walid aliua watu wachache kwenye lango la Kusini na alikaripiwa vikali na Muhammad kwa kufanya hivyo.

(The Great Arab Conquests)

Miaka nane kabla Muhammad aliondoka Makka kama mkimbizi pamoja na kunadiwa kichwa chake, na sasa alikuwa anaingia mji huo huo kama mtekaji wake. Tabia yake, hata hivyo, haikuashiria kiburi au hata kushangilia sana bali shukrani na unyenyekevu -shukrani kwa Allah (s.w.t.) kwa neema zake katika kuweka mafanikio juu ya Mtumwa wake mnyenyekevu, na unyenyekevu katika kuzingatia kiburi cha fahari za kidunia, na kufifia kwa vitu vyote vya kibinadamu.

Mtume (s.a.w.) aliingia na ngamia wake ndani ya viwanja vya Al-Kaaba, akashuka kwenye ngamia wake, akamwita binamu yake, Ali ibn Abi Talib, na wote wakingia ndani ya Al-Kaaba, wakizitambua zile Amri Tukufu kwa wale Mitume, Ibrahim na Ismail:

Usahihi-15.jpg

"...na tuliagana na Ibrahim na Ismail kwamba itakaseni Nyumba Yangu ..." (Sura y a 2; Aya ya 125)

Mtume (s.a.w.) pamoja na Ali waliikuta ile Nyumba ya Allah (s.w.t.), (Al-Kaaba) katika hali ya unajisi; ilikuwa imegeuzwa kuwa hekalu la masanamu 360, na ilibidi itakaswe. Mtume (s.a.w.) aliangusha chini kila sanamu huku akisoma Aya ifuatayo kutoka kwenye Qur'an:

Usahihi-16.jpg

"Ukweli umefika, na uongo umetoweka. Hakika ya uongo(kwa asili yake) lazima utoweke."

(Sura ya 17; Aya ya 81)

Sanamu kubwa sana ndani ya hekalu hilo lilikuwa ni lile la Hubal, mungu wa kifamilia wa ukoo wa Banu Umayya. Abu Sufyan alikwenda nalo juu ya ngamia kwenye vita vya Uhud

214

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kuwatia moyo wale wapiganaji kwa kuwepo kwake. Hubal aliwekwa juu ya kiegemeo kirefu, na Mtume (s.a.w.) hakuweza kumfikia. Yeye, kwa hiyo, alimwamuru Ali kupanda juu ya mabega yake, na kuliangusha chini. Katika kutii ile amri ya Kitume, ilimbidi Ali kusimama juu ya mabega ya Mtume; alilenga pigo kwenye yule mungu mkuu wa waabudu masanamu, na akamvunja vipande vipande. Kwa pigo lile kubwa, Ali aliweka mwisho wa kudumu kwa uabudu masanamu ndani ya ile Al-Kaaba! Al-Kaaba, Nyumba ya Allah (s.w.t.) ikawa imetakaswa!

Abul Kalam Azad

Baadhi ya masanamu yalikuwa yamewekwa juu ya viegemeo virefu na Mtume (s.a.w.) hakuweza kuyakuta. Alimuamuru Ali kupanda juu ya mabega yake na kuyaangusha chini. Ali akapanda juu ya mabega ya Mtume, na akayaangusha chini yale masanamu. Yeye kwa hiyo aliondoa uchafu wa uabudu masanamu kutoka kwenye Al-Kaaba kwa zama zote.

(The Messenger of Mercy, Lahore, Pakistan, 1970)

Wakati masanamu yote yalipokuwa yameharibiwa, taswira zote zilikuwa zimefutwa, na dalili zote zilizobakia za ushirikina zilikuwa zimefutiliwa mbali kabisa. Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) alimtuma Bilal kupiga Adhana. Bilal alipiga Adhana na bonde la Makka likavuma kwa ile takbir yake yenye nguvu na ya kuvutia. Mtume (s.a.w.) ndipo akafanya mizunguko saba ya Al-Kaaba, na akaswali Swala ya kutoa shukruni kwa Muumba wake.

Wakati huo huo, Maquraishi walikuwa wamekusanyika katika baraza ya Al-Kaaba wakim-subiri Mtume. Walitegemea kwamba angeonana nao kabla ya kutoa fatwa juu ya hatima yao.

Hapo Mtume (s.a.w.) alitokea kwenye kizingiti cha Al-Kaaba. Alilitazama lile kundi la watu lililokuwa mbele yake na akawahutubia kama ifuatavyo:

"Hakuna mungu ila Allah (s.w.t.) Yeye ni Mmoja na Mpweke kabisa, na Yeye hana washirika. Sifa zote na shukrani ni Kwake. Yeye ametimiza ahadi Yake. Amemsaidia mja wake kupata ushindi, na Ameyatawanya makundi ya maadui zake.

'Enyi watu! Nisikilizeni! Kiburi chote, majisifu, majivuno, na madai yote ya damu ya Nyakati za Ujahiliya yako chini ya miguu yangu leo.

'Enyi Maquraishi! Allah (s.w.t.) amevunja kiburi cha Zama za Ujahilia, na Yeye ame-vunja majivuno ya ukabila. Watu wote ni wana wa Adam, na Adam alikuwa ni ukafi tu udongo."

215

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mtume (s.a.w.) kisha akasoma Aya ifuatayo kutoka kwenye Qur'an:

Usahihi-17.jpg

"Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumeku jaalieni kuwa ni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika aliye mbora zaidi kati yenu mbele ya Allah ni yule mcha-mungu zaidi miongoni mwenu. Hakika Allah ni Mwenye kujua, Mwenye habari." (Sura ya 49; Aya ya 13)

Aya hii ndio waraka wa usawa na udugu wa watu wote katika Uislamu. Hapawezi kuwa na tofauti yoyote kati ya watu kwa misingi ya ukabila, rangi, utaifa, ukoo wala utajiri. Bali wakati ambapo Uislamu unavunja tofauti za aina nyingine zote, unatetea sifa yake ya kipekee, na hiyo ni sifa ya imani na tabia.

Muhammad ndipo akawauliza swali Maquraishi: "Mnafikiri nitawafanya nini sasa?" Wakasema: "Wewe ni ndugu mkarimu, na mtoto wa ndugu mkarimu. Tunategemea wema na msamaha tu kutoka kwako." Akasema: "Nitawaambia kile Yusufu alichowaambia ndugu zake, 'hakuna lawama juu yenu leo.' (Qur'an. Sura ya 12 Aya ya 92). Ondokeni sasa, nyote ni waachwa huru wangu."

Mtume (s.a.w.) alitangaza msamaha wa jumla hapo Makka. Msamaha huo uliwafikia na makafiri pia. Alilikataza jeshi lake kuteka nyara za mji huo au kuzuia kitu chochote kili-chokuwa mali ya Maquraishi. Hao Maquraishi hawakuacha kukamilisha kitu chochote kuzingira uharibifu wake, na uharibifu wa Uislamu; lakini katika saa yake ya ushindi alisamehe makosa yao yote na uhalifu wao.

Maquraishi, hapo mwanzoni, walikuwa hawasadiki. Hawakuweza kuamini masikio yao wenyewe. Vipi Muhammad anaweza kuzuia vishawishi vya kuwaua wote, baada ya yote yale ambayo wamemtendea kwa zaidi ya miongo miwili, na hasa sasa hivi ambapo alikuwa ana mamlaka makubwa kiasi hicho mikononi mwake? Kule kutokupenda kwake Muhammad kutumia madaraka yake kulikuwa ni kitu ambacho kabisa kilizipita akili-tam-buzi za washirikina wa Makka. Muda mwingi ulipita kabla ya maana ya dhamira ya Muhammad kuingia akilini mwao, na ule msamaha ukaanza kuonekana wenye kuwezekana na wa kweli kwao.

Nia ya Muhammad, Mtume wa Amani, ilikuwa ni kuiteka Makka bila ya umwagaji wa damu, na katika hili alifanikiwa. Ilikuwa ni hapa ambapo alijidhihirisha mwenyewe, kwa maneno ya Qur'an Tukufu "...rehma kwa wanadamu wote." Historia haiwezi kutoa

216

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mfano wa uvumilivu kama huo. Sio kwamba wapagani hawakuangamizwa tu; sio tu kwamba hawakuwa walipe fidia yoyote kwa makosa yao ya wakati uliopita; hawakuingili-wa katika umiliki wa zile nyumba ambazo Muhajiriin waliziacha hapo Makka, na ambazo walizikalia.

Kutoka pale kwenye al-Al-Kaaba, Mtume (s.a.w.) alikwenda kwenye Mlima Safa, na watu wa Makka walikuja kumthibitisha kama mkuu wao katika hali zake mbili - kama Mtume wa Allah (s.w.t.) na kama mtawala wao wa kidunia. Watu wote walitoa kiapo cha uamini-fu kwa Muhammad kwa kuweka mikono yao juu ya mkono wake. Baadae ikaja zamu ya wanawake kutoa hicho kiapo cha uaminifu. Lakini hakutaka kugusa mkono wa mwanamke yeyote ambaye hakuwa mke wake,. Yeye, kwa hiyo, alimtuma Umar ibn al-Khattab kupokea hicho kiapo cha wanawake kwa niaba yake.

Sir John Glubb

Mtume (s.a.w.) kisha akamtuma Umar ibn al-Khattab kupokea hivyo viapo vya wanawake.

(The Great Arab Conquests)

Wakati kula viapo kulipokwisha, Mtume wa Allah (s.a.w.) alijishughulisha na yale masu-ala mapya ya kisiasa na kiutawala yaliyotokana na ule ushindi wa Makka.

Ile Hadith nzito ya kuvutia ambayo ilianza mnamo Februari 12, mwaka 610, katika pango la Hira, ilifikia kileleni mnamo Februari 11, mwaka 630, katika baraza ya Al-Kaaba. Ilikuwa ni siku ya hisia, ahadi na sherehe, na siku kubwa katika historia, yenye umuhimu na uashiriaji. Ile hamu iliyoelekea kutokuwa na matumaini mwaka 620 kule Taif, imekuwa jambo kamilifu mwaka 630 hapo Makka.

Maquraishi waliendeleza mapambano marefu na makali dhidi ya Uislamu kwa miaka ishirini lakini wengi miongoni mwao sasa waliweza kuona kwamba yale masanamu ambayo waliyaabudu kama miungu yao, yalikuwa ni vitu bure kabisa. Wao, kwa hiyo, wal-iukubali Uislamu. Miongoni mwao, kulikuwemo na aina zote za watu waliosilimu: wachache ambao waliridhika kwamba Muhammad alikuwa ndiye Mtume wa kweli wa Allah (s.w.t.) na walimkubali yeye kama hivyo. Lakini kulikuwa na wengine wengi ambao waliukubali Uislamu kwa sababu walikuwa na kidogo sana cha kuchagua kutokana nacho. Walitambua kwamba ilikuwa hakuna sababu ya kupingana na kundi la wengi, na vile vile waliona kwamba hayakuwa maafikiano mabaya hata hivyo kujitangaza kuwa Waislamu, na walifanya hivyo, kwa mashaka gani, lilikuwa ni swali la kujibiwa na hali yenyewe ya baadae.

Watu wote wa ukoo wa Banu Umayya, pamoja na Hinda, mke wa Abu Sufyan, yule mla watu wa Uhud, pia "waliukubali" Uislamu.

217

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hapa mtu anaweza kuweka kituo kutafakari juu ya "kuukubali" Uislamu kwa Banu Umayya. Mtu anaweza kujisalimisha kwa adui kwa sababu ya hofu, na hofu pia inaweza kuufunga mdomo wake. Hofu inaweza kufanya mambo mengi lakini kuna kitu kimoja hai-wezi kukifanya - haiwezi kubadilisha chuki kuwa upendo. Kwa miaka ishirini, Banu Umayya wameongoza upinzani wa mapagani kwa Uislamu. Walifanya vita vya kiuchumi, kisiasa, kijeshi na kisaikolojia dhidi ya Mtume Wake, na dhidi ya wafuasi wake. Sasa kufikiria kwamba onyesho moja la nguvu za kijeshi lililoonyeshwa na Muhammad "lili-waridhisha" wao kwamba yeye alikuwa ni Mtume wa kweli wa Allah (s.w.t.) litakuwa ni vigumu kulitegemea kutoka kwenye asili ya mwanadamu. Hilo onyesho moja la uwezo la Waislamu halikubadili ile chuki, kinyongo na uchungu wa Banu Umayya kuwa upendo na haiba, hususan katika wakati ambao Uislamu umewanyima wao sio tu yale masanamu waliokuwa wakiyaabudu kama miungu yao bali pia umewanyima hadhi yao, fursa, uluwa na mamlaka. Walikuwa, kwa hiyo, na hali ile ile ya mawazo ambayo kila taifa linaloshind-wa linakuwa nayo. Mioyo yao ilikuwa imejaa chuki, kinyongo na hisia za kulipa kisasi dhidi ya walezi wa Uislamu.

Hawa Bani Umayya waliukubali Uislamu kwa kujirejea katika kuogopa sana kuvunjika kwa juhudi zote za upagani hapo Makka. Juhudi zao za kuokoa kale yao, na mapambano ili kudumisha uhusiano wao na upagani kama wapagani yameshindwa lakini pengine wangeweza kufanya kitu hicho hicho kama Waislamu. Mabingwa wa hayo masanamu, kwa hiyo, waliingia kwenye safu za waumini wakijifanya kama ni Waislamu. Hili lili-wafanya wao kuwa hatari zaidi kuliko hapo kabla wakati upinzani wao kwa Uislamu ulipokuwa dhahiri. Wakati huu, hata hivyo, walikwenda "kichinichini" wakivuta muda kusubiri fursa ya kujitokeza watakapouvunja Uislamu, kama ikiwezekana; la sivyo, basi watazibadili sifa-bainifu zake zinazoutambulisha, na wangerudisha desturi nyingi za Zama za Ujahilia kiasi iwezekanavyo.

Bani Umayya hawakuweza kuuharibu Uislamu wakati wa uhai wa Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) kwa sababu alichukua tahadhari zenye nguvu dhidi ya kuzuka tena kwa upagani. Alikuwa macho wakati wote, na hawakuweza kutoa mshitukizo wa ghafla kwake. Yeye pia alichukua tahadhari ya kutowapa nafasi yoyote ya madaraka ambayo wangeweza kuitumia kama msingi wao wa kujiongezea wenyewe.

Baadhi ya wanahistoria wamedai kwamba Mtume (s.a.w.) alikuwa na shauku ya kuwain-giza Bani Umayya katika utumishi wa Uislamu kwa vile walikuwa na ujuzi mwingi adimu na vipaji. Von Grunebaum, kwa mfano, anaandika hivi:

Muhammad kwa upande wake alihitaji uzoefu wa tabaka la watawala wa Makka; upanuzi wa umma na zaidi ya yote mfumo wake wa asili usingeweza kuendeshwa bila ya msaada wa wale watu wa mji huo.

(Classical Islam - A History 600-1258,1970)

218

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hili ni moja ya yale madai ambayo hayawezi kuthibitika mbele ya uchunguzi makini. Hakuna ushahidi kama Mtume (s.a.w.) aliwahi kamwe kuweka "uzoefu" wa Bani Umayya kwenye kazi yoyote. Lisilo na maana kama hilo hilo ni lile dai kwamba upanuzi wa umma na mfumo wake wa asili usingeweza kuendeshwa bila wao. Kama hao Bani Umayya walikuwa na uwezo huo wanaohusishwa nao, kwa nini hawakuutumia katika vita vyao beuzi dhidi ya Muhammad na Uislamu, na kwa nini walishindwa? Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliunda na kuimarisha ile Dola ya Kiislamu kwenye meno ya upinzani wa Bani Umayya. Hiyo Dola ya Kiislamu isingeweza kuishi pamoja kwa amani na utawala wa wachache wa kipagani uliokuwa ukiongozwa na Bani Umayya, na ilimbidi auangamize. Hakuwa amevutiwa na huo "uzoefu" wao kabla au baada ya kuukubali Uislamu, na hakumchagua yeyote kati yao kama jenerali au kama mtawala au hakimu au chochote kile. Hii sehemu ya sera yake juu yao haingeweza kuwa wazi zaidi.

Baadhi ya wanahistoria wa ki-Sunni wameeleza kwamba Mtume (s.a.w.) alimteua Mu'awiyyah, mtoto wa Abu Sufyan na Hinda, kuwa "mwandishi" wake wa kuandika Aya za Qur'an. Mu'awiyyah anaweza kuwa ameandika baadhi ya Aya za Qur'an lakini haina maana kwamba hazingeweza kuandikwa bila yeye. Wapo waandishi wengi wanaopatikana kwa Mtume. Kwanza kabisa, wakati Mu'awiyyah alipoingia Uislamu, nyingi ya Aya za Qur'an zilikuwa tayari zimekwisha teremshwa, na kulikuwa na kidogo, kama kilikuwepo, kwa yeye kuandika. Katika nafasi ya pili, alikuwa ni mmoja tu kati ya waandishi wengi. Kama kuandika Aya za Qur'an ni "sifa" kwake, basi anashirikiana pamoja na wanakili wengine wengi. Hata hivyo, Abdullah bin Saad bin Abi Sarh, yule ndugu wa kunyonya wa Uthman bin Affan pia alikuwa mwandishi. Alizibadilisha Aya za Qur'an alipokuwa anaziandika. Mtume (s.a.w.) alimtangaza yeye kama kafiri. Alikuwa auwawe lakini aliokolewa na Uthman. Mtume (s.a.w.) alimfukuza kutoka Madina.

Ujuzi wa Mu'awiyyah kama mwandishi, kwa hiyo, haukuwa mmoja ambao ulikuwa na upungufu katika baraza la Madina. Wanahistoria wamehifadhi majina 29 ya waandishi wa Mtume.

Hata hivyo, yale maelezo ya Von Grunebaum yaliyonukuliwa hapo juu, yanaweza, kwa kweli, kuwa sahihi, kama yakifanyiwa marekebisho kidogo kusomeka kwamba haikuwa Mtume (s.a.w.) wa Uislamu bali ni Abu Bakr na Umar waliohitaji uzoefu na ubingwa wa Bani Umayya, walikuwa ni wote hao ambao hawakuweza kuiongoza hiyo dola mpya bila ya msaada wao. Hao Bani Umayya walikuwa wa muhimu sana kwa Abu Bakr na Umar. Hadithi ya kufufuka kwa Bani Umayya wakati wa ukhalifa wa Abu Bakr na Umar inaelezewa kwenye mlango mwingine.

Mtume (s.a.w.) hata hivyo, alijaribu kuwaridhisha kwa vitulizo kwa matumaini kwamba wangevua uadui wao kwa Uislamu, na siku moja, wao wenyewe au watoto wao wangekuwa Waislamu waaminifu. Lakini juhudi zake hazikuzaa matunda. Hakuna ali-

219

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

chowafanyia wao, ambacho kamwe kililainisha nyoyo zao kuelekea kwenye Uislamu. Kamwe hawakupata akili ya utambulisho na Uislamu au kuutii. Walikuwa kihisia, kiasili na kiitikadi hawawezi kukubaliana nao. Kwa kushindwa tu kufikia malengo yao kwa upan-ga, ndipo walipouona ulazima na kukubali amri ya amani. Lakini kwao wao, ni njia tu ime-badilika, sio mwisho.

Hiyo siku Abu Sufyan; mke wake Hinda, mtoto wao Mu'awiyyah, na watu wengine wa ukoo wa Umayya walipoukubali Uislamu, Farasi mnafiki wa ushirikina pia aliingia kwenye ngome ya Uislamu. Ali ibn Abi Talib, yule mwana falsafa wa Uislamu, alitoa mukhtasari wa asili ya uingiaji kwenye Uislamu wa Bani Umayya kama ifuatavyo:

"Bani Umayya hawakuwa Waislamu wa kweli, walijisalimisha tu, kwenye nguvu kuu -iliyowazidi"

Katika kutoa fatwa hii juu ya kusilimu kwa Bani Umayya na kuwa Waislamu, Ali alikuwa anafasili Aya ifuatayo kutoka kwenye Kitabu cha Allah (s.w.t.):

Usahihi-18.jpg

Mabedui wanasema: 'Tumeamini'. Sema (uwaambie) "Ninyi bado hamjaamini, bali semeni, 'Tumesilimu', kwani imani haijaingia katika nyoyo zenu." (Sura ya 49; Aya ya 14)

Mtume (s.a.w.) wa Uislamu alitumia majuma mawili hapo Makka kuwaelimisha wale watu wapya wa Makka walioingia katika Uislamu, na katika kuanzisha serikali ya mji ule. Alikuwa amekwisha "twahirisha" ile Al-Kaaba, na Waislamu sasa walikuwa wanaumiliki huo mji ambao ulikuwa ndio kitovu cha kijamii, kisiasa, kiutamaduni, kibiashara na kidi-ni cha Arabia. Makabila yote ya Kiarabu sasa yaliyatambua mamlaka ya serikali yake kama yenye umuhimu mkubwa.

Mtume (s.a.w.) aliimarisha yale maeneo mapya yaliyopatikana kati ya Makka na Madina na sehemu zilizo karibu ya Makka. Ndipo yeye akaanza kazi ya kuitengeneza upya ile jamii ya Ki-Arabu. Huko nyuma, Waarabu walikuwa na uzoefu wa miundo ya asili ya uka-bila na ukoo tu katika mfumo wao wa kijamii lakini sasa wamekuwa "taifa" (umma) chini ya uongozi wake. Uwajibikaji wao kama Waislamu, haukuangalia asili ya rangi zao, ushirikishwaji wa kikabila, uhusiano wa kitaifa au kilugha au hata mipaka ya kijografia. Uwajibikaji wa Waislamu ulivuka vikwazo vyote vya asili na tofauti zilizowekwa na binadamu. Walipaswa kutoa uaminifu wao mpya kwenye Jumuiya ya Waumini ambayo ilimkiri Allah (s.w.t.) kwamba ni Mmoja, na Muhammad kama Mtume Wake.

220

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Makabila mengi karibu ya Makka yalikuwa bado ni wapagani, na Mtume (s.a.w.) alitaka kuwalingania kwenye Uislamu. Pia, yalikuwepo makabila mengine ambayo yalikuwa yameupokea Uislamu lakini yalikuwa bado Hayajalipa Zaka zao kwenye Hazina ya Umma, na alitaka awakumbushe kulipa madeni yao yale. Yeye, kwa hiyo, alituma wajumbe wakakusanye Zaka katika pande mbalimbali, pamoja na maagizo maalum juu ya kazi zao, wajibu na madaraka yao.

Mmoja wa hawa wakusanyaji wa Zaka alikuwa ni Khalid bin al-Walid. Mtume (s.a.w.) alimtuma kwa kabila la Banu Jadhima kukusanya Zaka zilizokuwa hazijalipwa lakini alivuka mipaka ya madaraka yake, na akaitia doa mikono yake kwa damu ya Waislamu wasio na hatia!

Muhammad ibn Ishaq

Msafara wa Khalid baada ya kutekwa Makka, kwa Bani Jadhima wa Kinana, na msa-fara wa Ali kusahihisha makosa ya Khalid.

Hakim aliniambia kwamba Mtume (s.a.w.) alimwita Ali na akamwambia aende kwa hawa watu na kuliangalia suala lao, na kukomesha vile vitendo vya zama za upagani. Hivyo Ali alikwenda kwao pamoja na fedha ambazo Mtume (s.a.w.) alizituma na akalipa fidia ya damu na akafidia hasara zao za kifedha. Wakati damu na mali vyote vilipokuwa vimekwisha kulipiwa bado alikuwa na pesa zilizobakia. Aliuliza kama kuna fidia yoyote ambayo ilikuwa haijalipiwa bado na waliposema hakuna, aliwapa zile pesa zilizobakia kwa niaba ya Mtume. Kisha alirudi na kutoa taarifa kwa Mtume (s.a.w.) alichokuwa amekifanya naye akamsifu. Kisha Mtume (s.a.w.) akasimama na akielekea Qibla, akanyanyua mikono yake juu, na akasema: Ewe Allah (s.w.t.)! Mimi sina hatia mbele Yako kwa aliyoyafanya Khalid. Haya ameyafanya mara tatu.

Khalid na Abdur Rahman ibn Auf walijibizana kwa maneno makali kuhusu jambo hili. Huyu Abdur Rahman akamwambia Khalid: "Umefanya kitendo cha kipagani katika Uislamu." Khalid akasema kwamba alikuwa amelipiza tu kisasi cha baba yake Abdur Rahman. Yeye akamjibu kwamba ni muongo kwa sababu yeye Abdur Rahman mwenyewe alimuua yule muuaji wa baba yake, lakini Khalid alilipiza kisasi cha ami yake hivyo kwamba kulikuwa na hisia mbaya kati yao.

Katika kuyasikia haya Mtume (s.a.w.) akamwambia Khalid: "Waache maswahaba wangu, kwani Wallahi kama ungekuwa na mlima wa dhahabu na ukautumia katika njia ya Allah (s.w.t.) usingeweza kukaribia sifa njema za maswahaba wangu."

(The Life of the Prophet)

221

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Washington Irving

Akiwa kwenye ujumbe maalum (akiwa njiani kuelekea Tehama) Khalid bin Walid ilimbidi apitie kwenye nchi ya kabila la Jadhima. Alikuwa na watu 350 pamoja naye na alikuwa amefuatana na Abdur Rahman, mmoja wa waliosilimu mapema sana. Maagizo yake kutoka kwa Mtume (s.a.w.) yalikuwa ni kuhubiri amani na mapenzi, kufundisha dini, na kujiepusha na vurugu, vinginevyo labda wakishambuliwa.

Sehemu kubwa ya hilo kabila la Jadhima walikuwa wameingia kwenye Uislamu lakini baadhi yao walikuwa bado ni wa dini ya Sabean. Katika wakati uliopita kabila hili lili-pora na kumuua ami yake Khalid, pia na baba wa Abdur Rahman, walipokuwa wakire-jea kutoka Arabia ya shangwe. Wakiogopa kwamba Khalid na jeshi lake wanaweza kulipiza kisasi kwa matendo yale mabaya, walijiandaa na silaha katika kuwasogelea kwao. Khalid kwa siri alifurahia katika kuwaona wakija (juu ya vipando vyao) kuwala-ki katika mpango huu wa kivita. Akiwasalimia kwa sauti ya haraka haraka, aliwauliza kama walikuwa Waislamu au makafiri. Walijibu kwa mkazo wa sauti ya kugugumia, "Waislamu." " Kwa nini basi mnakuja kutulaki mkiwa na silaha mkononi?" "Kwa sababu tunao maadui miongoni mwa makabila ambao wanaweza kutushambulia sisi kwa ghafla," walisema. Khalid kwa ukali kabisa aliwaamuru kushuka chini na kuweka silaha zao pembeni. Baadhi yao walikubali. Na mara moja walikamatwa na kufungwa kamba; wale waliobakia wakakimbia. Akichukulia kukimbia kwao kama kukiri makosa yao, aliwaandama kwa mauaji makubwa; akaiharibu nchi hiyo, na katika kuchemka kwa raghba yake aliwaua hata baadhi ya wale wafungwa.

Muhammad, wakati aliposikia juu ya hiki kitendo kiovu na cha kikatili, alinyanyua mikono yake juu mbinguni, na akamuomba Allah (s.w.t.) Ashuhudie kwamba yeye hakuwa na hatia juu ya hilo. Khalid wakati alipolaumiwa nalo wakati aliporudi, hakuwa na jibu akahamishia lawama zote kwa Abdur Rahman, lakini Muhammad akakataa kwa hasira tuhuma zozote dhidi ya mmoja wa wafuasi wake wa awali na mashuhuri. Yule Ali mkarimu alitumwa mara moja kwenda kurudisha kwa watu wa Judham kile ambacho Khalid alikinyang'anya kutoka kwao, na kufanya fidia ya kifedha kwa ndugu wa wale waliouawa.

Ilikuwa ni kazi inayoendana na tabia ya Ali, na aliitekeleza kwa uaminifu. Akiulizia juu ya hasara na mateso ya kila mtu mmoja, alimlipa mpaka akaridhika kabisa. Wakati kila hasara ilipokuwa imefidiwa, na damu yote kulipiwa, aligawanya zile pesa zili-zobakia miongoni mwa watu, akifurahisha kila moyo kwa ukarimu wake. Hivyo Ali alizipokea shukurani na sifa za Mtume, lakini huyu mlipiza kisasi Khalid alilaumiwa na hata wale aliofikiria kuwafurahisha. "Tazama" alimwambia Abdur Rahman, "Nimelipiza kisasi cha kifo cha baba yako." "Badala yake sema," huyu mwingine alimjibu kwa hasira, "umelipiza kifo cha ami yako. Umeifedhehesha dini kwa kitendo kinachomstahili muabudu sanamu."

(The Life of Muhammad)

222

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir John Glubb

Baada ya kuikalia Makka, wajumbe walitumwa kwa yale makabila yanayoizunguka kuwasisitiza wao wAyaharibu masanamu yao ya kienyeji na madhabahu ya kipagani. Kikundi kimoja kama hicho kiliongozwa na Khalid bin Walid, yule mshindi wa Uhud. Khalid alikuwa ni mpiganaji mwenye mafanikio makubwa lakini mtu mkaidi, mwenye vurugu na mwenye kiu ya damu. Alitumwa kwa Bani Jadhima, ukoo wa Banu Kinana, katika ukanda wa Pwani Kusini-Magharibi ya Makka.

Kwa majonzi yaliyoingiliana wakati mmoja, hawa Bani Jadhima walikuwa wamemuua ami yake Khalid miaka mingi kabla, wakati alipokuwa anarudi kutoka kwenye safari ya kibiashara ya Yemen. Mtume, ambaye yumkini alikuwa hajui kwamba Khalid ana ugomvi binafsi na wale watu aliotumwa kuwasilimisha, alimwambia aepuke umwagaji damu. Wakati alipowakuta. Bani Jadhima, Khalid ali-waambia waweke silaha zao chini kwani vita ilikuwa imekwisha na kila mmoja sasa ameukubali Uislamu. Wakati walipokuwa wamefanya hivyo, hata hivyo, yeye ghafla alikamata idadi kadhaa ya watu hao, akawafunga mikono yao nyuma ya migongo yao, na akatoa amri kwamba wakatwe vichwa vyao, kama kisasi kwa ajili ya kuuawa kwa ami yake.

Mpanda farasi mmoja wa Kiarabu aliyekuwa pamoja na jeshi la Khalid, baadaye alieleza jinsi kijana mmoja wa Bani Jadhima, mikono yake ikiwa imefungwa, alivy-omuomba yeye amruhusu kuongea na wanawake kadhaa waliokuwa wamesimama mbali kidogo. Yule mwislamu alikubali na akamuongoza yule mfungwa kuelekea kwa wale wanawake. "Kwa heri, Hubaisha," yule kijana alimwambia msichana mmoja miongoni mwao, " maisha yangu yako mwishoni sasa." Lakini msichana alip-iga kelele, "Hapana, hapana, maisha yako yarefushwe kwa miaka mingi ijayo." Yule mfungwa aliongozwa kurudishwa na mara moja akakatwa kichwa chake. Alipokuwa anaanguka, yule msichana alitoka kwenye lile kundi la wanawake na akamkimbilia. Akimuinamia, alimgubika na mabusu mengi, akikataa kumuachia mpaka walipomuua na yeye pia.

Mtume (s.a.w.) kwa kweli alishitushwa pale aliposikia juu ya kitendo cha Khalid. Akiwa amesimama kwenye uwanja wa Al-Kaaba, alinyanyua mikono yake juu ya kichwa chake na akakemea kwa sauti: " Ewe Allah! Mimi sina hatia mbele Yako kwa kile Khalid alichokifanya." Ali alitumwa mara moja pamoja na fungu kubwa la pesa kulipa fidia ya damu kwa ajili ya wale wote waliokuwa wameuawa, na fidia ya ukarimu kwa ajili ya hasara yoyote ya mali.

(The Life and Times of Muhammad, 1970, uk.320)

223

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad Husein Haykal

Muhammad alikaa Makka kwa siku kumi na tano wakati ambapo alisimamia mambo ya mji huo na akawaelekeza watu wake kwenye Uislamu. Katika kipindi hiki, alitu-ma wajumbe kuwalingania watu kwa amani kwenye Uislamu na kuharibu masanamu bila ya kumwaga damu yoyote. Khalid ibn al-Walid alitumwa huko Nakhlah kumharibu al-Uzza, mungu wa kike wa Banu Shayban. Kazi yake ilipokamilika, ibn al-Walid aliendelea kuelekea Jadhimah. Kule, hata hivyo, watu walikamata silaha wakati wa kukaribia kwake. Khalid aliwaambia waweke silaha zao chini kwani watu wote walikuwa wameukubali Uislamu. Mmoja wa wale watu wa kabila la Jadhima aliwaambia watu wake: "Ole wenu, Banu Jadhima! Ninyi hamjui kwamba huyu ni Khalid? Wallah hakuna kinachowangojeni ninyi mara mtakapokuwa mmeweka chini silaha zenu isipokuwa utekwaji, na mara mtakapokuwa mateka, msitegemee chochote bali kifo." Baadhi ya watu wake wakajibu: "Unatafuta kutufanya sisi wote tuuawe? Wewe hujui kwamba watu wengi wameingia kwenye Uislamu, kwamba vita vimek-wisha, na kwamba usalama umerudishwa tena?" Wale walioshikilia wazo hili walien-delea kuongea na watu wa kabila lao mpaka wakasalimisha silaha zao. Papo hapo, ibn al-Walid akaamuru wafungwe kamba, na akawauwa baadhi yao. Wakati alipozisikia habari hizi, Mtume (s.a.w.) alinyanyua mikono yake kuelekea juu mbinguni na akaomba: "Ewe Allah! Ninakishutumu kile Khalid ibn al-Walid alichokifanya."

Mtume (s.a.w.) alimpa pesa Ali ibn Abi Talib na akamtuma kwenda kuchunguza mambo ya kabila hili, na kumtahadharisha kupuuza desturi zote za kabla ya Uislamu. Alipofika, Ali alilipa fidia ya damu ya waathirika wote na akafidia wenye mali zao kwa kuharibiwa kwao.

Kabla ya kuondoka, alizitoa zile pesa zote ambazo Mtume (s.a.w.) alimpa kwa kabila hilo kiasi tu kwamba kama kulikuweko na hasara zozote zile ambazo zingeweza kukosa kuonekana kwa wakati ule.

(The Life of Muhammad, Cairo,1935)

Ule ujumbe wa kidiplomasia ambao Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) alio-ufanya kwa kabila la Jadhima, kupitia kwa Ali, ulikuwa wa muhimu kabisa, Khalid alikuwa ameua watu ambao hawakuwa ni Waislamu tu bali pia walikuwa hawana hatia ya kosa lolote. Kukosa kufanya marekebisho ya maovu yake kungeweza kuwapatia Waislamu sifa sio tu kwa ukatili usio na maana na matumizi mabaya tele ya madaraka, bali pia kwa usaliti. Wapagani na wale Waarabu ambao wangeweza kuitwa Waislamu, katika tarehe hizi za mwanzo, kwa heshima tu, wangeweza, bila kukwepa, kuunganisha vitendo viovu vya Khalid na Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Ilikuwepo hata hatari kwamba wataweza kuukana Uislamu na kurudi tena kwenye uabudu masanamu, kwa kumchukia Khalid tu. Mtume, kwa hiyo, aliingia ndani ya Al-Kaaba, na mara tatu akakikana hadharani kitendo cha Khalid, na akaiomba Mbingu iwe ni Shahidi kwamba hakuwa na lawama juu ya hilo.

224

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hawa Bani Jadhima waliachwa wamekongolewa na kuvunjwa kabisa na Khalid. Mtume (s.a.w.) alitaka sio kuwafariji tu na kuwajenga upya, bali pia kurudisha imani na mapenzi yao. Ilikuwa ni kazi ngumu na yenye kuhitaji uangalifu sana, na alimchagua Ali kuitekeleza. Khalid alikuwa ameharibu picha ya Uislamu, na Mtume (s.a.w.) alijua kwam-ba hakuna yoyote miongoni mwa maswahaba wake isipokuwa Ali aliyekuwa na uwezo wa kuirudishia mng'ao wake halisi.

Ali alithibitisha mara nyingine tena kwamba bwana wake asingeweza kumchagua mtu yeyote bora kuliko yeye kwa kazi hii nyeti, na alidhihirisha mara nyingine tena kwamba alikuwa wa kwanza katika vita, na alikuwa pia ni wa kwanza katika amani. Aliwashangaza na kuwavutia sana Bani Jadhima kwa uadilifu wake, ukarimu wake, wema wake, na kuji-husisha kwake juu ya furaha yao na ustawi wao.

Kwa ubora wake wa kuhutubia, Ali alizikamata tena nyoyo za Bani Jadhima kwa ajili ya bwana wake, Muhammad Mustafa, na kwa Uislamu. Huu ulikuwa ni wajibu ambao ulikuwa "unaafikiana" na yeye kuutimiza. Aliupenda wajibu huu zaidi kuliko mtu mwingine yeyote. Alipenda kufunga vidonda vya kisaikolojia vya watu wengine, na alipenda kuleta furaha na faraja kwenye mioyo iliyo na majonzi. Alijaaliwa na kila kipawa maalum kutekeleza wajibu kama huu.

225

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Vita vya Hunain

Kule kutekwa kwa Makka kulichochea uingiaji kwa wingi wa Waarabu kwenye Uislamu katika sehemu nyingi za nchi hiyo. Lakini yalikuwepo baadhi ya makabila yaliyokuwa yakiishi Mashariki na Kusini-Mashariki ya Makka ambayo hayakutaka kuacha uabudu masanamu. Walitishiwa na maendeleo ya haraka ya Uislamu, na walifikiria kwamba kama utaendelea kuenea kwa kasi hiyo hiyo, watazungukwa na Waislamu hivi karibuni, na watakuwa wametengwa na makabila mengine ya wapagani.Viongozi wao waliwaza kwamba haitakuwa busara kuwaacha Waislamu waunganishe mafanikio yao ya hivi karibuni na kuwa na nguvu sana. Wao, kwa hiyo, waliamua kuchukua hatua mara moja kwa kuwashambulia Waislamu huko Makka na kuwaagamiza. Makabila makubwa miongoni mwao yalikuwa ni Thaqiif, Hawazin, Bani Sa 'ad na Banu Jashm, wote wapiganaji wakali, wenye wivu na uhuru wao na wenye fahari na mila zao za kivita. Walikuwa wamefahamu kwamba Makka imesalimu amri kwa Muhammad bila ya kufanya shambulio lolote lakini walihusisha kule kushindwa kwa watu wa Makka kukataa kuswalimu amri kwake na tabia yao ya kike. Na kwa upande wao wenyewe, walikuwa na imani kwamba walikuwa na uwezo zaidi katika uwanja wa mapambano kuliko wapiganaji wa Kiislam au wapiganaji wo wote wengine.

Mwishoni mwa Januari 630, Mtume (s.a.w.) alipokea taarifa kwamba kabila la Thaqiif na Hawazin walikuwa wameondoka kwenye kituo chao cha nyumbani, na walikuwa wanakwenda kuelekea Makka. Wakati habari hizi zilipothibitishwa, yeye pia aliagiza uku-sanyikaji wa jumla ndani ya ule mji uliotekwa hivi karibuni.

Mtume (s.a.w.) hakutaka Makka igeuke uwanja wa mapambano.Yeye, kwa hiyo, haraka sana akaondoka Makka mnamo Januari 26,630 akiongoza wapiganaji 12,000, kwenda kukutana na adui. Kutoka kwenye jeshi hili, watu elfu kumi walikuwa wanatoka Madina, na wale wengine elfu mbili walikuwa ni askari wapya kutoka watu wa Makka waliosilimu hivi karibuni.

Jeshi hili jipya lilikuwa ndio jeshi kubwa sana liliwahi kukusanywa katika Arabia mpaka wakati ule. Wakati mipangilio yake mbali mbali ilipokuwa inatoka nje ya lango la mji, katika mavazi maridadi ya kivita, Abu Bakr aliyekuwa anaangalia, alivutiwa sana, na akatam-ka ghafla: "Hatuwezi kushindwa safari hii kwa sababu ya kukosa wingi." Lakini mapema sana akathibitika kwamba amekosea. Waislamu walishindwa mwanzoni ingawa walikuwa mara tatu ya wingi wa adui. Qur'an yenyewe ilitaka tahadhari ya Waislamu, kwa uwazi hasa, kwamba wingi peke yake haukuwa hakikisho kwamba watakuwa washindi.

226

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir William Muir

Majuma manne yalikuwa yamepita tu tangu yeye (Muhammad) alipokuwa ametoka Madina, wakati aliposonga mbele kutoka Makka akiongoza vikosi vyake vyote, viki-wa vimetuna sasa, kwa kuongezeka kwa kikosi cha kuongeza nguvu kutoka Makka, kwenye idadi kubwa ya watu 12,000. Safwan, kwa maombi yake, alimpatia yeye suti mia moja za deraya na kibanda kizima cha silaha kamili na ngamia wengi kiasi. Ule mpango wa askari wa makabila, kila moja likiwa na bendera inayopepea mbele yake, ulikuwa wa kushangaza sana kiasi kwamba Abu Bakr alianza ghafla, wakati vile vikosi vilivyopangwa vilipopita, kwa ugutaji huu wa ghafla: "Leo hii hatutashindwa kwa sababu ya uchache wa idadi yetu."

(Life of Muhammad, London, 1861)

Wakati ile safu ya kwanza iliyokuwa na kikosi cha Waislamu, kikiongozwa na Khalid ibn al-Walid, kilipoingia kwenye bonde la Hunain upande wa Kusini-Mashariki ya Makka, adui tayari alikuwa amelala kwenye mavizio, tayari kukipokea kwa silaha zake za makombora. Mwanya ulikuwa mfinyu sana, njia ilikuwa mbaya sana, na Waislamu walikuwa wanasonga mbele dhahiri kwa kutotambua kuwepo kwa adui. Ilikuwa kabla tu ya mawio wakati kwa ghafla tu, Hawazin walipoanzisha shambulizi lao.

Fumanizi hili lilikuwa halikutegemewa kabisa na shambulizi la adui lilikuwa la haraka sana kiasi kwamba Waislamu hawakuweza kulihimili. Kikosi hicho, kilichoundwa na watu wa kabila la Banu Sulaym, kilivunjika na kikakimbia. Sehemu kubwa ya jeshi hilo ilikuwa nyuma kidogo tu. Safu ya Khalid ilipata pigo usoni mwake, na likatia hofu ndani ya watu wake hivyo kwamba wao pia waligeuzia migongo yao kwa adui. Na wakaanza kukimbia. Mara kila mtu katika jeshi hilo alikuwa anakimbia, na haikuchukua muda kabla Muhammad hajaachwa peke yake pamoja na wafuasi wake waaminifu wachache karibu yake.

Watu waliokuwa wakiongozwa na Khalid ndio wa kwanza kukimbia mbele ya maadui wanaoshambulia, na walifuatiwa na wale Umayya wa Makka waliosilimu hivi karibuni na marafiki zao na wafuasi wao. Nyuma yao walikuwa raia wa Madina. Waislamu wengi wal-iuawa katika kukimbia huko, na wengine wengi walijeruhiwa. Mtume (s.a.w.) aliwaita wale watoro lakini hakuna hata mtu mmoja aliyemsikiliza.

Jeshi la Waislamu lilikuwa katika msambaratiko wa kukimbia bila mpango na adui waki-wa kwenye kasi kali ya kuwafukuza. Mtume, kwa kweli, hakuondoka kwenye nafasi yake, na alisimama imara kama jiwe. Watu nane walikuwa bado wako naye, wote wakitazama kioja cha kukimbia kwa jeshi lao. Walikuwa ni:

227

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

1. Ali ibn Abi Talib

2. Abbas ibn Abdul Muttalib

3. Fadhil ibn Abbas

4. Abu Sufyan ibn al-Harith ibn Abdul Muttalib

5. Rabi'a, kaka yake Abu Sufyan ibn al-Harith

6. Abdullah ibn Masood

7. Usamah ibn Zayd ibn Haritha

8. Ayman ibn Ubaid

Kati ya hawa nane, watano wa mwanzo walikuwa ni wa ukoo wa Banu Hashim. Walikuwa ni ami zake na binamu zake Mtume.

Mtume (s.a.w.) alimwomba ami yake, Abbas ibn Abdul Muttalib, kuwaita wale Waislamu waliokuwa wanakimbia. Abbas alikuwa na sauti yenye nguvu sana, na akaguta: "Enyi Muhajirina na Enyi Ansari! Enyi washindi wa Badr na enyi watu wa Mti wa Kiapo! Mnakwenda wapi? Mtume wa Allah (s.a.w.) yuko hapa. Rudini kwake." Sauti ya Abbas ilivuma katika lile bonde finyu na karibu kila mtu aliisikia, na ilionekana kuwa na matokeo katika kusimamisha kukimbia kwa Waislamu.

Ansari walikuwa wa kwanza kusimama, na kurudi kwenye vita. Wakitiwa moyo na mfano wao, wengine pia walipata nguvu tena. Mara wakaweza kujikusanya tena. Mapambano makali yalitokea. Mwanzoni, matokeo yalionekana kutokuwa na uhakika lakini baadae Waislamu walianza kuwabana maadui. Mara tu waliporudisha hamasa zao, wakafanya mashambulizi. Adui bado alipigana kijasiri lakini wakazuiwa katika usogeaji wao na ile adadi kubwa ya wanawake na watoto aliokuja nao. Waislamu walizidi kusonga mbele na baadae ilikuwa ni Mabedui ambao walikuwa wanakimbia pande zote.

Sir William Muir ameielezea Hadith ya kushindwa na kupata nguvu tena kwa Waislamu katika vita vya Hunain kwa kirefu kiasi. Anaandika katika kitabu chake, The Life of Muhammad, (London, 1877) hivi:

Mapema sana wakati wa asubuhi, ambapo alfajiri ilikuwa bado ya rangi ya kijivu, na anga ikiwa imetanda mawingu, jeshi la Muhammad lilikuwa kwenye mwendo. Akiwa amevaa mavazi kamili ya kivita, kama kwenye siku ya Uhud, alipanda juu ya farasi wake mweupe, Duldul, nyuma ya vikosi vyake.

Kikosi kilichoundwa na Banu Sulaim na kikiongozwa na Khalid, walikuwa wakipan-da kwa msururu taratibu juu ya njia ya mlimani ya mteremko na nyembamba, wakati ghafla Hawazin walipochupa kutoka kwenye mavizio yao, na wakawashambulia kwa kasi. Wakibumbuazwa na uvamizi huu wa ghafla, Banu Sulaim walikatika na kurudi nyuma. Mshituko huu ulipita kutoka safu hadi safu. Wakikerwa na utusitusi wa saa

228

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hizo, na wembamba na mikunjokunjo ya njia, hofu ikalishika jeshi lote; wote waligeuka na wakakimbia. Jinsi kikosi kwa kikosi walivyoharakisha kumpita yeye, Muhammad alikemea: "Mnakwenda wapi? Mtume wa Allah (s.w.t.) yuko hapa! Rudini! Rudini! - lakini maneno yake hayakuwa na athari yoyote, isipokuwa kikun-di cha marafiki na wafuasi waliojitolea walijikusanya karibu naye.

Kiwewe kiliongezeka, kundi la ngamia lilisukumana bila mpango mmoja dhidi ya mwingine; ilikuwa kelele tupu na ghasia, na sauti ya Muhammad ilipotea katikati ya mshindo huo. Mwishoe, walipoona zile safu za vikosi vya Madina vikiondoka katika kukimbia kwa pamoja, alimuambia ami yake, Abbas, aliyekuwa ameshikilia farasi wake, kuita kwa sauti kubwa: "Enyi watu wa Madina! Enyi wa Mti wa Kiapo! Enyi watu wa Surat Baqra !" Abbas alikuwa na sauti yenye nguvu sana, na alipoguta maneno haya tena na tena kwa sauti yake yote, yalisikika mbali na karibu. Mara moja yakagusa hisia katika nyoyo za watu wa Madina. Walizuiwa katika kukimbia kwao, na wakaharakisha kwa Muhammad, wakipiga kelele, "Ya Labeik! Sisi tuko hapa kwa mwito wako!" Watu mia moja kati ya hawa wafuasi watiifu, walijinasua kwa taabu kutoka kwenye wale ngamia waliokuwa wameziba ile njia finyu, wakajitupa juu ya adui aliyekuwa anasonga mbele na kusimamisha maendeleo yake. Lilipopata nafuu kutokana na shinikizo, lile jeshi lilipata nguvu polepole, na likarudi kwenye vita. Mapambano yalikuwa makali; na matokeo, kutoka na ubaya wa asili wa ardhi na kishindo cha Mabedui wakali, yalibakia kwa muda kiasi ya mashaka. Muhammad ali-panda kwenye kilima na akaangalia yale mapambano. Akitiwa nguvu na yale mand-hari, alianza kuguta kwa sauti kubwa; "Sasa ndio tanuru limepata moto: Mimi ni yule Mtume asiyesema uongo. Mimi ni kizazi cha Abdul Muttalib."

Kisha akimuagiza Abbas kumuokotea ukofi wa changarawe, aliutupa kuelekea kwa maadui, akisema, "Maangamizi yawakamate hao!" Walikuwa kwa kweli tayari wamekwishayumba. Uimara wa kikosi cha Madina, na shauku ya wale waliobakia wakati pale walipoitwa tena, ulikuwa umepata ushindi. Adui alikimbia, na ushindi ulikuwa kamili. Wengi waliuawa na kwa nguvu sana Waislamu waliendeleza mashambulizi, kiasi kwamba waliuwa miongoni mwa waliobakia, baadhi ya watoto wadogo - ukatili ambao Muhammad alikuwa ameukataza kabisa.

Betty Kelen

Waislamu waliweka kambi mbali na Bonde la Hunain na wakati wa alfajiri wakam-sogelea adui kupitia kwenye njia nyembamba. Mtoto wa Umar anaelezea kile kili-chotokea baadae:

"Tuliteremka kupitia kwenye korongo kavu la mto, pana na lenye mteremko tukishu-ka polepole katika mwanga hafifu wa asubuhi; lakini adui alikuwa pale kabla yetu na alikuwa amejificha katika vinjia vidogo, njia za pembeni na sehemu finyu. Walikuwa

229

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

katika jeshi, wakiwa na silaha kamili wakijua hasa ni nini cha kufanya, na Wallahi, tulikuwa na hofu wakati tuliposhuka na ghafla Hawazin walitushukia kama mtu mmoja!

Mabedui walishambulia kwa mawe, majabali, mishale, mikuki na panga. Kile kikosi cha Muhammad, chini ya jenerali Khalid, kilivunjika, ngamia wakasukumana na kugongana, wakilia kwa mikwaruzo na kusongamanisha miguu yao mirefu.

Yeye Muhammad aliona miongoni mwa wale watu wanaokimbia, wafuasi wake wapya kutoka Makka, na aliwaita wao kama mmoja wao wenyewe: 'Mnakwenda wapi enyi watu? Rudini! Njoni kwangu! Mimi ni Mtume wa Allah (s.w.t.) Mimi ni Muhammad, mtoto wa Abdullah!'

Sio hata mmoja aliyesikiliza, na kwa nini wasikilize? Alikuwepo mpiganaji wa Hawazin akiwafukuza akiwa juu ya ngamia wa rangi ya damu ya mzee, bendera yake ikipepea kutoka kwenye mkuki mrefu, na kila wakati alipoutumbukiza ubapa wa mkuki ule, ulichomoza upande mwingine wa kifua cha mtu. Sauti ya Mtume (s.a.w.) ilizama kwenye makelele ya watu, na milio ya ngamia. Alimuambia ami yake Abbas, mtu mwenye mapafu makubwa, kuchukua huo mwito, 'Enyi marafiki, ukumbukeni ule mti wa mkangazi...' Na Ali, akiwa kimya kabisa lakini katika mapambano kama jinni mkali, alirukaruka kiushindi karibu yake, akipigania kufika nyuma ya farasi wa yule kiongozi wa Hawazin na kumlemaza.

(Muhammad, Messenger of God) Muhammad Husein Haykal

Waislamu walifika Hunain wakati wa jioni na wakaweka kambi kwenye mlango wa bonde hilo mpaka alfajiri. Wakati wa alfajiri siku iliyofuata jeshi hilo lilianza kuon-doka, na Muhammad, akiwa amempanda farasi wake mweupe, alikuwa nyuma wakati Khalid ibn al-Walid, akiongoza kikundi cha askari kutoka Banu Sulaym, alikuwemo kwenye kikosi hicho.

Wakati Waislamu walipokuwa wanapita kwenye korongo la Hunain, Malik ibn Awf aliamuru jeshi lake kushambulia katika giza kabla ya alfajiri, kwanza kwa mishale na kisha kwa shambulizi la jumla. Safu za Waislamu zikavunjika na waliingiwa na hofu. Baadhi yao walikimbia kutoka nje ya korongo hilo haraka sana kama walivyoweza katika kutafuta usalama. Akishuhudia kile kilichowakuta Waislamu, Abu Sufyan hakuhisi kutokuwa na furaha hata ndogo kwa kushindwa maadui zake wa awali ambao mpaka sasa walikuwa wakisherehekea ushindi wao juu ya Makka. Alisema, "Waislamu hawatadhibitiwa mpaka wawe wametupwa ndani ya bahari."

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

230

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Makabila ya kipagani yalishindwa lakini yaliweza kujikusanya tena, na yanasemekana kuweza kurudi nyuma kwa mpango mzuri kutoka kwenye bonde la Hunain.

D.S.Margoliouth

Jenerali Malik, mtoto wa Auf, anasemekana kukusanya wapanda farasi wake wa kutosha kufanya waweze kusimama imara mpaka watu dhaifu wa kundi lao wawe wamekingwa, na kisha waweze kuwafikisha kwenye usalama kwenye kilima ambapo wanaweza kupata njia yao ya kwenda Taif. Pale ni dhahiri baadhi ya wanawake waliokolewa, ingawa wengine waliangukia kwenye mikono ya Waislamu. Khalid mtoto wa al-Walid, ambaye ukatili wake tayari ulikwishapata karipio kutoka kwa Mtume, alipata jingine kwa kufikiri kwamba ni kazi yake kuwaua hawa majikedume; kitendo ambacho kilikuwa kinyume kabisa na dhana za Mtume (s.a.w.) za ushujaa.

Kama vile tu alivyoona ni muhimu kuwakaripia wengine ambao walifikiria ni wajibu wao kuwaua watoto wa makafiri. "Ni nini kilicho bora chenu," aliuliza, "kama sio watoto wa makafiri?"

Mafanikio ya muhimu sana yalipatikana, na ubashiri wa Mtume (s.a.w.) ulithibitika kuwa thabiti katika wakati ambapo kinyume chake kingeweza kuwa na matokeo mabaya; kwani Abu Sufyan angeweza kuwa na uwezo wa kutumia fursa ya janga, ingawa lisiwe lenye nguvu sana, kuweza kusababisha jingine.

(Muhammad and the Rise of Islam, London, 1931)

Hunain ilikuwa ni vita iliyoongozwa binafsi na Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) mwenyewe. Vita vilianza na kushindwa kwa Waislamu, na walikimbia njia ya kila upande ili kuokoa maisha yao wenyewe, bila kutambua kabisa kuwepo, katika uwanja wa mapambano, kwa Mtume (s.a.w.) wao. Mwishoni, hata hivyo, walikuwa washindi, shukrani kwa ujasiri na ushupavu wa Mtume (s.a.w.) mwenyewe na wachache kati ya jamaa zake.

M. Shibli, mwanahistoria wa Kihindi, anaandika katika kitabu chake cha wasifu wa Mtume:

Badala ya ushindi (wa Waislamu) mtu anaweza kuona kushindwa kwao (katika vita vya Hunain). Mtume (s.a.w.) alitazama pote na hakuona mtu yeyote pamoja naye isipokuwa wachache wa marafiki zake. Abu Qatada, sahaba mmoja, ambaye alikuwe-po huko Hunain, anasema kwamba wakati jeshi lilipokuwa linakimbia, alimuona Umar ibn al-Khattab, na akamuuliza: "Ni hali gani ya mambo ya Waislamu?" Yeye akasema: "Hayo ni Mapenzi ya Allah (s.w.t.)"

(The Life of the Prophet {Siraatun-Nabi, juz. 1, uk. 535-536}, 1976, Azamgarh, India).

231

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir William Muir

Kinyume kilichopatikana mwanzoni mwa siku hiyo, kilihusishwa na Mtume (s.a.w.) na matumaini ya kujiona ambayo kwayo waumini walitegemea juu ya jeshi lao kubwa. Mafanikio ya baadae sawasawa yalipachikwa kwenye msaada wa wa jeshi lisiloonekana ambalo lilipigana dhidi ya adui yao. Shambulio hilo limegusiwa hivi kwenye Qur'an:"

Hakika Allah amewasaidieni kwenye medani za vita nyingi: na katika siku ya Hunain, wakati kwa kweli mlifurahia katika wingi wa jeshi lenu. Lakini idadi yao kubwa kwa namna yoyote ile haikukunufaisheni ninyi: ardhi ilikuwa finyu sana kwenu pamoja na upana wake wote. Kisha mligeuza migongo yenu na mkakimbia."

(The Life of Muhammad, London, 1877, uk.143)

"Majeshi yasiyoonekena" ambayo yaliwasaidia Waislamu, ina maana, katika muktadha huu, nguvu ya hali ya juu. Mwanzoni mwa vita hivyo, walishindwa na kufukuzwa. Lakini walitiwa moyo na mfano wa Mtume (s.a.w.) mwenyewe ambaye ujasiri wake uliwarud-ishia hamasa yao, na walimpiga adui kwa ari na nguvu mpya.

Vita vya Uhud vilianza kwa ushindi wa Waislamu na viliishia na kushindwa kwao; vita vya Hunain vilianza na kushindwa kwao na vikaishia na ushindi wao. Kulikuwa na mauaji makubwa kwa Waislamu wakati wa mwanzo ambayo yalisababishwa na hofu yao wenyewe na kukosa ushupavu.

Muhammad Husein Haykal

Ushindi haukupatikana kirahisi. Waislamu walilipa gharama kubwa sana. Wangeweza kuimudu kwa gharama ndogo kama wasingerudi nyuma hapo mwanzoni na kus-ababisha kauli ya dhihaka ya Abu Sufyan kwamba watakuwa watupwe baharini. Ingawa vitabu vya msingi wa rejea havikuorodhesha wale wote waliouawa katika vita hivyo, vimetaja kwamba makabila mawili ya Kiislam yalikuwa karibu yote yameangamizwa kabisa, na kwamba Mtume (s.a.w.) aliendesha Swala ya jeneza kwa ajili yao. Kufidia sehemu ya hii hasara kubwa ya maisha ya watu, ni yale mamlaka yasiyo na shaka ushindi uliyoyaleta kwa Waislamu. Zaidi ya hayo, ushindi ulileta mateka na ngawira zaidi kwa ajili yao kuliko walivyowahi kuona hapo kabla.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935) Ali na vita vya Hunain

Shujaa wa vita vya Hunain alikuwa ni Ali ibn Abi Talib kama vile alivyokuwa shujaa wa vita vyote vilivyotangulia. Katika wakati ambapo maswahaba wote walikimbia kutoka kwenye medani ya vita, na watu wanane tu walikuwa wamebaki na Mtume, alikuwa ni Ali

232

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

aliyesimama kati yake na adui, na akamkinga yeye. Makabila yalishambulia kwa kurudia lakini aliyarudisha nyuma kila wakati sawa na alivyokwisha kufanya huko Uhud. Kwa wakati fulani, ilikuwa ni Uhud tena.

Mwishowe, Ali alifanikiwa katika kuugeuza mwelekeo wa vita hivyo. Kwanza alimsababisha Uthman bin Abdullah, mmoja wa viongozi wa adui, kuanguka kutoka kwenye ngamia wake, kuyumba, na kuuawa; na baadae, alimuua, katika pambano la mkono kwa mkono, Abu Jerdel, kiongozi wa Hawazin. Wakati majenerali hawa wawili walipokuwa wameuawa, adui alivunjika moyo, akashindwa vita.

M.Shibli

Banu Malik wa kabila la Thakiifwalipigana kwa ujasiri wa makusudi lakini pale kiongozi wao, Uthman ibn Abdullah, alipouawa, walianza kuyumba...

(The Life of the Prophet, Azamgarh, India, 1976)

Abu Sufyan, mkuu wa Bani Umayya, alikuweko kwenye kambi ya Waislamu, kama ilivy-oelezwa hapo juu. Ingawa alikwisha "kuukubali" Uislamu, alivutiwa na kusisimka kuona kule kukimbia kwa Waislamu, na akawa na matumaini kwamba watatupwa baharini. Wakati Hikda bin Umayya, "Mwislam" mwingine wa ukoo wa Bani Umayya, alipoona ukimbiaji wa Waislamu, pale mwanzoni mwa vita, alitamka: "Hatimae uchawi wa Muhammad umevunjika." Wote lazima watakuwa wamebuni, katika fikra zao, picha za kumrudisha Hubal, mungu wao wa jadi, kwenye kiti chake ndani ya Al-Kaaba.

Abu Sufyan na watu wengine wa ukoo wake, hawakuweza kuficha furaha zao wakati kwao wao ilionekana kana kwamba Waislamu walikuwa wameshindwa na watu wa makabila ya wapagani. Lakini furaha yao ilidhihirika kuwa ya kudumu kwa muda mfupi sana. Baadae kidogo kulikuwa na mabadiliko katika matokeo ya vita hivyo, na kisha ilikuwa ni hawa wapagani ambao mwishowe na kwa uwazi kabisa walioshindwa. Kinyume hiki lazima kiwe kilisababisha kijicho kikubwa sana kwa Abu Sufyan na jamaa wa ukoo wake vile walivyopoteza matumaini ya mwisho, mazuri kabisa waliyokuwa nayo ya kufufua "Zama za Ujahilia."

Jamaa wa kabila walikuwa wameacha mizigo yao yote na maelfu ya wanyama wao. Mtume (s.a.w.) aliamuru mizigo hiyo ikusanywe, wanyama hao wakusanywe na kupelek-wa Jirana, sehemu ya katikati baina ya Taif na Makka, na iwekwe hapo kusubiri kuwasili kwake yeye mwenyewe. Kwa wakati huo, aliamua kuiteka Taif ambayo bado iliendelea kubaki kama ngome ya mwisho ya makafiri, na akaamuru sehemu kubwa ya jeshi kutem-bea kuelekea kwenye mji huo. Wale watoro toka kwenye vita ile pia walikuwa wamepata hifadhi kwenye ngome ya Taif.

233

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Akiwa njiani kuelekea Taif, Mtume (s.a.w.) alipita kikundi kidogo cha watu waliokuwa wamesimama karibu na mwili wa mwanamke aliyeuawa. Katika kuuliza, aligundua kwamba aliuawa na Khalid bin al-Walid.

Muhammad ibn Ishaq

Mmoja wa maswahaba alituambia kwamba Mtume (s.a.w.) siku ile (mara baada ya vita vya Hunain) alipita karibu na mwanamke ambaye alikuwa amemuawa na Khalid bin al-Walid ambapo watu walikuwa wamekusanyika karibu yake. Wakati aliposikia yaliyotokea, alituma ujumbe kwa Khalid na kumkataza kuua mtoto, mwanamke au mtumwa aliyekodiwa.

(The Life of the Messenger of God)

Mtume (s.a.w.) alizingira Taif lakini haikufanikiwa na ikaachwa. Taif, hata hivyo, ilisalimu amri kwa hiari majuma kadhaa baadae.

Kutoka Taif, Mtume (s.a.w.) alikwenda Jirana kugawanya ngawira za vita ambazo ziliku-sanywa katika uwanja wa Hunain. Sehemu aliyompa Abu Sufyan na wanae, wakuu wa ukoo wa Bani Umayya, ilikuwa kubwa zaidi kuliko sehemu aliyompa mtu mwingine yoy-ote katika kambi ya Uislamu. Bani Umayya hawakuweza kuamini kwamba walikuwa na bahati nzuri kama hiyo. Abu Sufyan, ambae alikuwa na sababu nzuri ya kutarajia kidogo kuliko chochote, baada ya "utendaji" wake katika vita vya Hunain, aliguswa sana na ukarimu wa Mtume, na akaongea naye kwa shauku: "Wewe umkarimu katika vita sio chini ya ulivyo mkarimu kwenye amani."

Mustashriq wengine wamemaanisha kwamba ile sehemu ambayo Mtume (s.a.w.) aliyotoa kwa Abu Sufyan na wanae, ilikuwa kwa kweli ni hongo la kuwabakisha wawe Waislamu, na kwamba hapakuwa na njia nyingine yoyote ambayo angeweza kupatia utii wao. Wao wanasema zaidi kwamba Mtume (s.a.w.) kamwe hakusita kuwahonga waabudu masanamu kama alidhani kwamba wangeuza imani zao kwake kwa kubadilishana na ngamia, kondoo, na vipambo vidogodogo na vitu vizuri vyenye thamani ndogo.

Sisi hatukubaliani nao. Baada ya kutekwa Makka, Abu Sufyan, wanae na watu wengine wa ukoo wa Bani Umayya, walikuwa chini ya huruma ya Muhammad. Angeweza kuwaangamiza wote, na waabudu masanamu wote wa Arabia wasingeweza kufanya lolote kuwaokoa. Haikuwa lazima kwake kuwahonga wao au mtu mwingine yeyote katika kuukubali Uislamu. Kusilimu kwao kulikuwa na thamani ndogo kwa Uislamu vyovyote vile. Katika kutoa zawadi juu ya Abu Sufyan na wanae, Mtume (s.a.w.) wa Uislamu alikuwa akidhihirisha tu chaguo lake kutoka kwenye ulipizaji wa kisasi. Kwa Waarabu, itakumbukwa, ulipizaji wa kisasi ulikuwa ni tabia yao mbaya. Alijaribu kumaliza uadui wao kwa Uislamu kwa upole wake na ukarimu. Zawadi hizo zilikuwa ni ishara ya mfano

234

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wa mwelekeo huu tu.

Abu Sufyan, watoto wake na watu wengine wa Bani Umayya - wapokeaji wa zawadi hizo, waliitwa, daima baadae Muallafa Qulubuhum - wale wenye kuimarishwa nyoyo zao. Mtume (s.a.w.) aliwapa maadui zake sehemu kubwa kutoka kwenye ngawira kwa ajili tu ya Taliif al-Qulub - kuimarisha nyoyo zao.

Dr. Muhammad Hamidullah anasema katika kitabu chake, Introduction to Islam, uk. 80, (1977):

Wale ambao nyoyo zao ni za kuimarishwa ni wa namna nyingi. Faqihi mkuu, Abu Ya'la al-Farra, anaonyesha: "Na kwa wale ambao nyoyo zao ni za kuimarishwa, wapo wa aina nne:

1.   Wale ambao nyoyo zao ni za kupatanishwa kwa kuja kwao kwenye msaada wa Waislamu;

2.   Wale ambao nyoyo zao ni za kuimarishwa ili kwamba wajiepushe na kufanya madhara kwa Waislamu;

3.    Wale wanaovutiwa kwenye Uislamu;

4.   Wale ambao kwa kuwatumia wao kuingia kwenye Uislamu kunakuwa na uwezekano kwa watu wa makabila yao.

Ni halali kunufaisha kila moja ya makundi haya ya 'wale ambao nyoyo zao ni za kuimarishwa' wawe Waislamu au washirikina." Abu Sufyan na ukoo wake walikuwa ni wa kundi lile la pili; nyoyo zao "zilikuwa ziimarishwe ili kwamba wataweza kujie-pusha kutokana na kufanya madhara kwa Waislamu."

Maansari na ngawira za Hunain

Baadhi ya vijana wa Ansari walikuwa hawakuridhika na kile walichokiona kuwa ni ugawaji "usio haki" wa ngawira za vita. Wachache miongoni mwao walinung'unika kwamba wakati ulipofika wa kugawa ngawira, Mtume (s.a.w.) alifanya "upendeleo" kwa Maquraishi. Wakati Mtume (s.a.w.) alipolisikia hili, aliamuru Ansari waku-sanyike katika hema, na akawahutubia hivi:

"Ni nini hiki ninachokisikia kutoka kwenu, Enyi Ansari, kuhusu ugawaji wa ngawira? Mmefadhaika kwa sababu nimetoa sehemu kubwa ya ngawira kwa watu wa Makka kuliko niliyowapeni ninyi? Lakini hebu niambieni hili: hivi sio kweli kwamba mli-abudu masanamu na Allah (s.w.t.) akawapeni mwongozo kupitia kwangu mimi? Hivi sio kweli kwamba mlitenganishwa na ugomvi wa wenyewe kwa wenyewe na Allah

235

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

(s.w.t.) akawaunganisha kupitia kwangu mimi? Sio kweli kwamba mlikuwa masikini na Allah (s.w.t.) akawafanyeni matajiri kupitia kwangu mimi?"

Katika kujibu kila swali, Ansari walisema: "Ndio, hivyo ndivyo ilivyo, na ni neema ya Allah (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.)."

Lakini maswali haya yalikuwa ni balagha tu - maswali yasiyohitaji majibu - na Mtume wa Allah (s.a.w.) mwenyewe aliyajibu.

Sir William Muir

"...Lakini nyie mngeweza kujibu (na mkajibu kwa dhati, kwani ningehakikisha hilo mimi mwenyewe) - ulikuja Madina ukiwa umekanwa kama mlaghai, na tukashuhu-dia ukweli wako; ulikuja kama mkimbizi asiye na msaada na tukakusaidia wewe; mtu aliyetengwa na jamii, nasi tukakupa hifadhi, ukiwa fukara, nasi tukakufariji wewe. Kwa nini mnachanganyikiwa akilini kwa sababu mambo ya maisha Haya, kwa hili nilitafuta kuelekeza nyoyo za watu hawa (Maquraishi wa Makka) kwenye Uislamu, ambapo ninyi tayari mko imara kwenye imani zenu? Hamridhiki ninyi kwamba wengine wapate hayo makundi ya mifugo na hao ngamia, ambapo ninyi mnamchukua Mtume wa Allah (s.w.t.) kurudi naye majumbani kwenu? Hapana, mimi sitawaacheni ninyi milele. Kama wanadamu wote wangekwenda njia moja, na watu wa Madina njia nyingine, hakika, ningekwenda ile njia ya watu wa Madina. Mola awe mwema juu yao, na awabariki wao, na watoto wao na watoto wa watoto wao milele."

(The Life of Muhammad, London, 1861)

Wakati Ansari waliposikia maneno haya, waligubikwa na machozi, na wakapaza sauti: "Waache wengine wachukue hao kondoo, ng'ombe na hao ngamia waondoke nao. Tunachokitaka sisi ni Muhammad, na sio kitu kingine chochote."

Ansari walipatwa pia na hofu kwamba Mtume (s.a.w.) angeweza kuamua kuishi hapo Makka, na kupafanya makao yake makuu. Lakini aliwahakikishia kwamba yeye kamwe hatawaacha wao au Madina, na kwamba yeye na wao hawatenganishiki milele.

Kutoka Jirana, Waislamu walirudi Makka ambako Mtume (s.a.w.) alifanya ile mizu guko saba ya Al-Kaaba, na akatekeleza ibada za Hijja Ndogo (Umra).

Vita vya Hunain vilikuwa ndio "limbuko" la mwisho la Arabia ya upagani. Wakati Waislamu walipopata ushindi, pazia hatimae likaanguka kwenye dibaji ya ushenzi na upagani, ya mfululizo wa matukio ya historia ya Arabuni. Lakini wapagani au kwa usahihi zaidi, watetezi wa siri wa upagani wa Kiarabu walikuwa bado wapigane mapigano, ya jeshi linalorudi nyuma, na askari, marefu na magumu, dhidi ya Uislamu.

236

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hapo Makka, Mtume (s.a.w.) alitoa maelekezo ya mwisho kwenye mambo yanayohusu uongozi na sera. Kabla ya kuondoka Makka kwenda Madina, alimteua Akib bin Usayd kama gavana wa mji huo. Huu ulikuwa ndio uteuzi wa kwanza wa kudumu wa kiserikali katika Uislamu. Yeye pia aliutangaza mji wa Makka kuwa makao makuu ya kidini ya Kiislam.

Baada ya kumaliza mwezi mzima wenye matukio mengi hapo Makka na viungani mwake, Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) na jeshi lake, walirudi Madina.

D. S. Margoliouth

Kwa kuipa himaya ya Kiislam makao makuu ya kidini, yasiyotumika wakati wowote kama makao makuu ya kisiasa, mwanzilishi aliyapatia makao hayo nguzo ambayo imelinda uendeleaji wa mfumo huo katikati ya misukosuko mikali kabisa.

Kutembelea Makka ambako kuliandamana na mabadiliko mengi sana kulisimamish-wa kwa Mtume (s.a.w.) kupitia kwenye taratibu za hijja ndogo. Baadae, Akib, mtoto wa Usaid, aliteuliwa kuwa gavana wa Makka kwa mshahara wa dirham moja kwa siku; huu ulikuwa ni uteuzi wa kwanza wa kudumu wa kiserikali kufanywa katika Uislamu; huko Khaibar, mji mwingine pekee wa muhimu ambao Waislamu walikuwa wameuteka, serikali ya (wenyeji wa) hapo ilibaki. Mbali na gavana, kiongozi wa kiro-ho aliachwa hapo, Mu'adh mtoto wa Jabal, mwenyeji wa Madina, ambaye katika uho-dari wake wa kufundisha hiyo dini mpya, Mtume (s.a.w.) alikuwa na imani nao. Mtume (s.a.w.) alirudi Madina pamoja na jeshi la Waislamu baada ya kutokuwepo kwa zaidi ya mwezi.

(Muhammad and the Rise of Islam, London, 1931)

237

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

VITA VYA TABUK

Vita vya Muutah ambavyo Waislamu walishindwa, vilipiganwa mnamo Septemba mwaka 629. Kushindwa kwao kulitafsiriwa katika jamii nyingi kama ni ishara ya kuanguka katika mamlaka ya Dola mpya ya Kiislamu. Maharamia wa Kiarabu lazima watakuwa wame-ona inatia hamu kushambulia Madina baada ya kuanguka huku kwa kubuniwa. Lakini katika kiangazi cha mwaka 630, minong'ono ilikuwa ikizunguka hapo Madina kwamba hayakuwa yale makabila ya Arabia ya kaskazini bali ni vikosi vya Kirumi ambavyo vilikuwa vinajikusanya katika mpaka wa Syria kwa ajili ya uvamizi wa Hijazi.

Muhammad, Mtume (s.a.w.) wa Uislalmu, aliamua kuchukua hatua za tahadhari kwa ajili ya ulinzi wa Madina, na akawaamuru wafuasi wake kujiandaa na mapambano marefu upande wa kaskazini.

Ilikuwa ni mwezi wa Septemba, na hali ya hewa ya Hijazi mwaka ule ilikuwa ni ya joto kupita kiasi. Zaidi ya hayo, ukame mrefu ulitishia jimbo hilo na hali ya nusu njaa. Majibu ya Waislamu, kwa hiyo, yalikuwa yamepooza sana. Hawakupenda kuondoka majumbani mwao kwa wakati kama huu.

Sir John Glubb

Mnamo Septemba au Oktoba 630, Mtume wa Allah (s.a.w.) alitoa amri ya kujiandaa kwa msafara wa kwenye mpaka wa Byzantium. Hali ya hewa ya Hijazi ilikuwa bado ni ya joto kali sana, maji na malisho yalikuwa adimu, na mizunguko ya jeshi kubwa kama hilo ingekuwa ni migumu sana. Huenda kumbukumbu za maafa ya Muutah zili-wakosesha watu wengi nia ya kupambana na Byzantium tena.

(The Life and Times of Muhammad)

Washirikina hapo Madina waliichukua fursa hii kupandikiza mfarakano katika vichwa vya waumini wapya katika Uislamu. Sio kwamba hawakushiriki tu katika vita bali pia wali-jaribu kuwageuza wengine mawazo kutofanya hivyo. Katika jaribio la kudhoofisha nia na makusudi ya Waislamu, walianza kueneza habari za wavumishaji wa mambo ya kutisha kwamba maadui safari hii hawakuwa wale askari wa kikabila wa kuchukuliwa kwa nguvu, masikini, wenye zana duni, wasiojiamini na wajinga waliopigana bila mpango na bila nid-hamu bali ni Warumi ambao walikuwa ndio dola iliyoendelea sana na yenye nguvu sana duniani, na ambao, kwa kweli, watawateketeza Waislamu.

238

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hata hivyo, Waislamu wengi waliitika kwenye mwito wa Mtume, na wakachukua silaha kuilinda dini. Wakati ilipochukuliwa idadi ya vichwa, walipatikana watu 30,000 walioji-tolea. Lilikuwa ndio jeshi kubwa sana lililowahi kukusanywa katika Arabia hadi hapo.

Mtume (s.a.w.) alimteua Ali ibn Abi Talib kama kaimu wake hapo Madina wakati wa kutokuwepo kwake yeye mwenyewe. Alimchagua Ali kuwa kaimu wake kwa sababu zifu-atazo:

Alitaka kuonyesha kwa dunia yote kwamba alimuona Ali kuwa mwenye sifa zinazostahili zaidi kuliko mtu mwingine yoyote za kuwa mtawala wa Waislamu wote, na kuwa mkuu wa Umma wa Kiislamu. Yeye, kwa hiyo, alimchagua kama mwakilishi wake katika makao yake makuu.

Wapiganaji wote walikuwa wanakwenda na msafara huo, wakiiacha Madina bila vikosi vyovyote. Kama litatokea shambulizi lolote juu ya mji huo kutoka kwa waporaji wa mak-abila ya kihamaji, Ali anaweza kutegemewa katika kuishughulikia hali hiyo kwa kutumia ushujaa na uwezo wake.

Wanafiki wengi walibaki nyuma hapo Madina, na wengine wengi walilikimbia jeshi na kurudi mjini. Walikuwa ni tishio linalowezekana kwa usalama wa makao makuu ya Uislamu. Mtume, kwa hiyo, alichagua mtu wa kutawala mahala pake ambaye alikuwa na uwezo wa kuikinga Madina dhidi ya shambulizi lolote la wapagani, ama kwa uchokozi kutoka nje au kupitia uchochezi wa ndani.

Kwa upande wa wanafiki hapakuwa na kitu kisichokubalika zaidi kuliko kumuona Ali kwenye mamlaka juu yao. Wakati jeshi lilipoondoka Madina, walianza kunong'ona kwamba Mtume (s.a.w.) alimuacha Ali hapo Madina kwa sababu alitaka kumuepuka. Ali alid-halilishwa kusikia kwamba bwana wake amemuona kama "mzigo." Yeye, kwa hiyo, upesi sana akalikimbilia lile jeshi na akalikuta hapo Jurf. Mtume (s.a.w.) alishangaa kumuona yeye lakini wakati Ali alipoeleza ni kwa nini alikuja, yeye Mtume (s.a.w.) alisema:

"Watu hawa ni waongo. Nilikuwacha Madina kuniwakilisha mimi kwa kutokuwepo kwangu. Huridhiki wewe kuwa kwangu kama Harun alivyokuwa kwa Musa isipokuwa kwamba hakutakuwa na Mtume baada yangu."

Washington Irving

Wengi wamefahamu kutokana na hayo yaliyoelezwa kwamba Muhammad alimkusu-dia Ali kama khalifa au mshikamakamu wake; kuwa ndio maana ya neno la Kiarabu lililotumika kuonyesha uhusiano wa Haruni kwa Musa.

(The Life of Muhammad)

239

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali aliridhika kwa ule uhakika ambao Mtume (s.a.w.) alimpa, na akarudi Madina kuchukua dhima ya kazi yake kama khalifa.

Wakati Mtume (s.a.w.) alipokutana na kuzungumza na Ali katika kambi yake huko Jurf, baadhi ya maswahaba wake walikuwa pamoja naye. Mmoja wao alikuwa ni Saad bin Abi Waqqas, mshindi wa baadae wa vita vya Qadsiyya dhidi ya Waajemi. Alisimulia kwa Waislamu wengine kwamba ilikuwa ni mbele yake ambapo kwamba Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) alipomwambia Ali kwamba yeye (Ali) alikuwa kwake Muhammad ni kama vile alivyokuwa Harun kwa Musa, isipokuwa kwamba yeye Ali hakuwa Mtume. Baada ya matembezi magumu jeshi hilo lilifika kwenye mpaka wa Syria, na likasimama kwenye kitongoji kiitwacho Tabuk lakini Mtume (s.a.w.) hakuweza kuona dalili zozote za jeshi la Warumi au jeshi lingine lolote au adui. Mpaka huo ulikuwa na amani na ukimya. Habari alizozisikia huko Madina kuhusu uvamizi unaoweza kufanywa karibuni na Warumi, zilikuwa za uongo.

Amani na utulivu kwenye mpaka wa Syria ni uthibitisho mwingine kwamba Warumi waliviona vita vya Muutah kama si kingine chochote zaidi ya uvamizi wa kikundi cha Waarabu wa jangwani. Kama Muutah ingekuwa ni vita kubwa mno hivyo kama baadhi ya wanahistoria wa Kiislam wanavyodai ilikuwa, Warumi wangedumisha ngome yao kwenye mpaka huo. Lakini hawakudumisha hata doria seuze ngome!

Mtume wa Allah (s.a.w.) kisha akatafakari juu ya hatua inayofuatia ya kuchukuliwa hapo

Tabuk.

Washington Irving

Akiitisha baraza la vita, yeye (Muhammad) alitoa swali la ama waendelee mbele au la (kutoka Tabuk). Kwa hili Umar akajibu kimkato: "Kama unao wahy kutoka kwa Allah (s.w.t.) wa kuendelea mbele, fanya hivyo." "Kama ningekuwa na wahy kutoka kwa Allah (s.w.t.) wa kuendelea mbele," alijibu Muhammad, "nisingetaka ushauri wenu."

(The Life of Muhammad)

Mwishowe, Mtume (s.a.w.) aliamua kutokuendelea kwenda Syria bali kurudi Madina. Jeshi hilo lilikaa siku kumi hapo Tabuk. Ingawa halikuingia kwenye shughuli yoyote, kuwepo kwake pale mpakani kulikuwa na matokeo ya kufaa. Makabila mengi ya kaskazi-ni ya kibedui yaliingia Uislamu. Dauma-tul-Jandal, sehemu ya kimkakati kati ya Madina na Syria, ilipatikana kama eneo jipya.

240

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Punde tu kabla ya jeshi hilo kuondoka Tabuk, watawa wa nyumba kubwa ya utawa ya Mtakatifu Catherine katika bonde la Sinai, walikuja kumuona Mtume. Alikutana nao kwa mazungumzo, na akawapa mkataba ambao unalingana na Mkataba wa Madina ambao ali-wapa Mayahudi. Masharti yake makuu yalikuwa :

1.  Waislamu watayalinda makanisa na nyumba za watawa za Wakristo. Hawatavunja mali yoyote ya kanisa wala kujenga misikiti au kujenga nyumba kwa ajili ya Waislamu.

2. Mali zote za kanisa (za Wakristo) zitasamehewa kutokana na kodi yoyote ile.

3. Hakuna mtu yoyote mwenye mamlaka ya kikanisa atakayelazimishwa na Waislamu kuacha kazi yake.

4. Hakuna Mkristo atakayelazimishwa na Waislamu kusilimu na kuwa mwis-lamu.

5. Kama mwanamke wa kikristo ataolewa na mwislamu, atakuwa na uhuru kamili wa kufuata dini yake mwenye we.

Jeshi lilipata nguvu tena kutokana na kazi ngumu na uchovu wa ile safari ndefu, na Mtume (s.a.w.) alilipa ishara ya kurudi nyumbani. Aliwasili Madina baada ya kutokuwepo hapo kwa mwezi mmoja.

241

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kutangazwa kwa Surat Bara'ah ( At-Taubah)

Wakati msimu wa hijja ya mwaka wa 9 H.A. ulipowadia, Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) alikuwa na idadi kubwa ya kazi zilizombana ambazo zilihitaji uangalizi wake wa haraka kiasi kwamba alikuwa hawezi kuondoka Madina. Yeye, kwa hiyo, alimtuma Abu Bakr kwenda Makka kama kiongozi wa kundi la mahujaji mia tatu kwenda kuongoza ibada za Hijja.

Lilikuwa ni jukumu la uongozi halisi, mbele ya watu, la kwanza kabisa la Abu Bakr. Abu Bakr na mahujaji hao waliondoka Madina. Siku moja baada ya kuondoka kwao. Mtume (s.a.w.) alipokea kutoka Mbingnii wahy mpya uitwao Bara'a (At-Taubah) - Sura ya tisa ya Qur'an, na aliamriwa kwa dhati kabisa kuitangaza huko Makka ama yeye mwenyewe binafsi au kutoa mamlaka ya kufanya hivyo kwa mtu kutoka kwenye familia yake mwenyewe, lakini sio kwa mtu mwingine yeyote.

Kulingana na amri hii ya Mbingnii, Muhammad Mustafa alimwita binamu yake, Ali ibn Abi Talib, akampa kipando chake apande, na akamuamuru kupeleka ule wahy mpya Makka, na kuutangaza huko katika mkusanyiko wa mahujaji - Waislamu na mapagani.

Muhammad ibn Ishaq

Wakati At-Taubah iliposhuka kwa Mtume (s.a.w.) baada ya kuwa alikwishamtuma Abu Bakr kusimamia hijja, mtu mmoja alionyesha nia kwamba angeipeleka kwa Abu Bakr. Lakini akasema: "Hakuna mtu atakayeitangaza kutoka kwangu bali mtu wa nyumba yangu mwenyewe." Ndipo akamwita Ali na akasema: "Chukua sehemu hii kutoka mwanzo wa At-Taubah, na uitangaze kwa watu siku ya kafara wakati watakapokusanyika huko Mina."

(The Life of the Messenger of God) Washington Irving

Muhammad alimtuma Abu Bakr kama mkuu wa mahujaji kwenda Makka, yeye mwenyewe akiwa ameshikwa sana na shughuli za jamii na za nyumbani kiasi cha kumfanya asiweze kukosekana Madina.

Sio muda mrefu sana baadae Muhammad akamwita mkwe wake na Sahaba mtiifu,

242

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali, na akimpandisha juu ya ngamia mwepesi sana kati ya ngamia wake, alimhimiza kufanya haraka kwa kasi yote kwenda Makka, huko akatangaze mbele ya umati wa mahujaji waliokusanyika kutoka sehemu zote, Sura muhimu ya Qur'an, aliyoipokea hivi punde kutoka mbingnii.

Ali alitekeleza kazi yake kwa moyo na usahihi wake uliozoeleka. Aliufikia huo mji mtukufu kileleni mwa tamasha hilo kubwa la kidini. Alisimama mbele ya umati mkubwa uliokusanyika kwenye kilima cha Al-Akaba, na akajitangaza yeye mwenyewe kama mjumbe kutoka kwa Mtume, akiwa amebeba wahy muhimu. Kisha yeye akasoma ile Sura ambayo yeye alikuwa mbebaji, ambayo ndani yake ile dini ya upanga (sic) ilitangazwa katika ugumu wake wote.

Wakati Abu Bakr na Ali waliporudi Madina, huyu Abu Bakr alionyesha mshangao na kutoridhika kwake kwamba hakufanywa kuwa mtangazaji wa wahy muhimu kama huo, kama ulivyoonyesha kuunganishwa na kazi yake ya awali, lakini alitulizwa kwa uhakikisho kwamba wahy mpya wote lazima utangazwe na Mtume (s.a.w.) mwenyewe, au na mtu kutoka kwenye familia yake wa karibu.

(The Life of Muhammad)

Sir William Muir

Kuelekea mwishoni mwa hijja, katika sikukuu ya kuchinja (kafara), pale mahali pa kutupia mawe karibu na Mina, Ali aliusomea kwa sauti ule umati mkubwa uliokusanyika karibu yake katika ile njia nyembamba, ile amri ya mbingnii.

Alipokuwa amemaliza kusoma kifungu hiki, Ali aliendelea: "Nimeamriwa kuwatangazieni kwamba hakuna asiyeamini atakayeingia peponi. Hakuna muabudu sanamu atakayefanya hijja baada ya mwaka huu; na hakuna mtu yoyote atakayefanya mzunguko wa Nyumba Tukufu akiwa uchi. Yeyote yule aliye na mkataba na Mtume, utaheshimiwa mpaka ukomo wake. Miezi minne imeruhusiwa kwa kila kabila kurudi kwenye nchi zao kwa usalama. Baada ya hapo wajibu wa Mtume (s.a.w.) unakoma."

Mkusanyiko mkubwa wa mahujaji ulisikiliza kwa utulivu mpaka Ali alipomaliza. Kisha wakatawanyika na kuondoka kila mtu kwenda nyumbani kwake, kutangaza kwa makabila yote ya peninsula nzima hii amri kali ambayo wameisikia kutoka kwenye midomo ya Ali.

(The Life of Muhammad, London, 1877)

Muhammad Husein Haykal

... Baada ya (Ali) kumaliza kisomo chake cha Qur'an, aliendelea kwa maneno yake mwenyewe: "Enyi watu, hakuna asiyeamini atakayeingia Peponi; hakuna mshirikina

243

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

atakayefanya hijja baada ya mwaka huu; na hakuna mtu aliyeko uchi atakayeruhusi-wa kuizunguka Al-Kaaba. Yeyote aliyeingia mkataba na Mtume wa Allah - rehema na amani ziwe juu yake - atatimiziwa mkataba wake mpaka kipindi chake kitakapokwisha." Ali alitangaza haya maagizo manne kwa wale watu na kisha akampa kila mtu miezi minne ya amani ya kawaida na msamaha ambayo ndani yake mtu yoyote anaweza kurudi nyumbani kwa usalama. Kuanzi wakati ule na kuendelea, hakuna muabudu sanamu aliyefanya hijja na hakuna mtu aliye uchi aliyefanya mizunguko ya Al-Kaaba. Kuanzia siku ile na kuendelea, Dola ya Kiislam ilianzishwa.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Ali ibn Abi Talib "alizisoma tena zile Aya za Allah (s.w.t.)" huko Mina, akimuwakilisha Mtume wa Allah (s.a.w.). Hii lazima iwekwe akilini na msomaji kwamba "kusoma Aya za Allah (s.w.t.)" ni kitendo chenye madaraka makubwa. Ni kitendo, kwa kweli, muhimu sana kiasi kwamba Allah (s.w.t.) Mwenyewe alikitwaa. Tunasoma katika Qur'an:

Hizi ni Aya za Allah. Tunakusomeeni kwa haki, Hakika wewe ni miongoni mwa Mitume.

(Sura ya 2; Aya ya 252)

Haya tunayokusomea ni katika Aya na ukumbusho wenye hekima. (Sura ya 3; Aya ya 58) Hizi ni Aya za Allah. Tunakusomea kwa haki; Na Allah hapend i kuwadhulumu walimwengu. (Sura ya 3; Aya ya 108)

Kulingana na Aya hizi, Allah (s.w.t.) Mwenyewe Alizisoma Aya Zake kwa Muhammad, Mtume Wake, na baadae (mara alipokwisha kuzisikia) akazisoma kwa wanadamu wote. Kusoma Aya za Allah (s.w.t.) kulikuwa ni moja kati ya kazi zake muhimu. Umuhimu wa kazi hii unaakisiwa na Aya zifuatazo za Qur'an Tukufu:

Usahihi-19.jpg

Ewe Mola wapelekee miongoni mwao Mtume, anayetokana nao wenyewe. Atakayewasomea Aya Zako na awafundishe Kitabu na Hekima na awatakase; hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hekima. (Sura ya 2; Aya ya 129)

244

Usahihi-20.jpgUsahihi-21.jpg

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usahihi-22.jpg

Kama tulivyotuma Mtume kwenu, anayetokana na ninyi, anayekusomeeni Aya Zetu na kuku-takaseni, na kukufudisheni Kitabu na Hekima, na kukufundisheni yale mliyokuwa hamyajui.

(Sura ya 2; Aya ya 151)

Usahihi-23.jpg

Hakika Allah aliwafanyia wema mkubwa Waumini, pale alipowapelekea Mtume aliyetoka miongoni mwao wenyewe, Aliyewasomea Aya Zake na kuwatakasa, na kuwafundisha Kitabu na Hekima, ambapo kabla ya hapo walikuwa katika upotovu uliowazi. (Sura ya 3; Aya ya 164)

Usahihi-24.jpg

Yeye ndiye aliyempeleka kwa watu wasiojua kusoma, Mtume anayetoka miongoni mwao, awasomee Aya Zake na awatakase, na awafundishe Kitabu na hekima, ingawa kabla ya hapo, alikuwa katika upotovu ulio dhahiri. (Sura ya 62; Aya ya 2)

Kulingana na Aya hizi, Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) alikuwa na kazi za kufanya zifuatazo:

1. Kusomea watu Aya za Allah (s.w.t.);

2. Kuwafundisha maandiko na hekima;

3. kuwatakasa;

4. Kuwafundisha katika elimu mpya.

Ya kwanza kutajwa katika kazi za utume ni, "kusoma Aya za Allah (s.w.t.)" Ni muhimu sana kwamba inachukua utangulizi juu ya kazi nyingine zote za Mtume.

245

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kusoma Aya za Allah (s.w.t.) kumetajwa pia pekee pekee katika Qur'an katika Aya zifu-atazo:

Usahihi-25.jpg

Hivyo tumekutuma kwenye umati ambao wamekwisha kupita kabla yao umati zingine, ili uwasomee haya tunayokufunulia kwa njia ya wahy. .. (Sura ya 13; Aya ya 30)

Usahihi-26.jpg

Ama mimi nimeamrishwa nimuabudu Allah, Mlezi wa mji huu, ...-na niisome Qur'an: na mwenye kuongoka, basi ameongoka kwa faida ya nafsi yake mwenyewe, na mwenye kupotea, basi sema: "Hakika mimi ni miongoni mwa waonyaji." (Sura ya 27; Aya ya 91 - 92)

Usahihi-27.jpg

...Hakika Allah amekuteremshieni ukumbusho, Mtume, anayekusomeeni Aya za Allah zina-zobainisha, Ili kuwatoa walioamini na wakatenda mema kutoka kwenye Giza, na kuwapele-ka kwenye Nuru... (Suraya 65; Ayaya 10-11)

Pia kuna onyo lifuatalo katika Qur'an Tukufu:

Usahihi-28.jpg

...Hakika wale waliozikanusha Aya za Allah, watakuwa na adhabu kali (katika Akhera). Na Allah ni Mwenye Nguvu na Mwenye kulipiza kisasi. (Sura ya 3; Aya ya 4)

Ilikuwa ni kazi hii - Kusoma Aya za Allah (s.w.t.) - ambayo Ali ibn Abi Talib alitakiwa aitekeleze.

246

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kama ilivyoelezwa hapo juu, katika Dhil-Hija ya mwaka wa 9 H.A., Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.), alikuwa na shughuli sana hivyo kutoweza kwenda Makka kutekeleza Hija, na kutangaza ile Surah ya Bara'a iliyoshuka karibuni. Kwa hiyo, kwa amri dhahiri ya Allah (s.w.t.), ilimbidi achague mtu mwingine wa kutekeleza kazi hii. Mtu aliyechaguliwa alikuwa ni Ali ibn Abi Talib.

Mnamo mwaka wa 8 H.A. (A.D. 630) wakati wa kutekwa Makka, Ali na bwana wake, Muhammad Mustafa waliitakasa Nyumba ya Allah (s.w.t.) (Al-Kaaba) kutokana na masanamu ya Waarabu. Ali aliyavunja masanamu yale vipande vipande, na akavitupa vipande hivyo nje ya Al-Kaaba. Mnamo mwaka wa 9 H.A. (A.D.631), aliitakasa Al-Kaaba kutokana na waabudu masanamu wenyewe kwa kuwatangazia kwamba hawataruhusiwa tena kamwe kuingia katika maeneo yake matukufu.

Msimu wa hija wa mwaka wa 9 H.A, ulikuwa ndio mkusanyiko wa mwisho wa waabudu masanamu wa Arabia katika maeneo ya Al-Kaaba au hapo Makka.

Allah (s.w.t.) alimchagua Ali ibn Abi Talib kuirudisha Nyumba Yake (Al-Kaaba) kwenye hali yake ya utakaso wake wa asili, na akatuma Agizo maalum kwa Muhammad Mustafa, Mtume Wake, kufanya kusudi Lake lieleweke kwake (Ali). Ali, mtumwa wa Allah (s.w.t.) aliirudisha ile Nyumba Tukufu na Iliyobarikiwa kwenye hali ileile ambayo Mtume Ibrahim na Ismail (A.S) waliyoiacha nayo karne nyingi nyuma.

Katika kutangaza hapo Mina katika mwaka wa 9 H.A., ile Sera ya Dola ya serikali ya Kiislam, Ali alikuwa ndiye "Chombo" cha Allah (s.w.t.), kama vile katika mwaka wa 7 H.A., alivyokuwa "Mkono" wa Allah (s.w.t.) ambao uliiteka Khaybar kwa ajili ya Uislamu, na akaweka msingi wa Ufalme wa Mbinguni juu ya Ardhi. Kisa cha ushukaji na utangazaji wa Sura ya Bara'a (Sura ya 9 ya Qur'an Tukufu), kinadhihirisha kwamba:

1. Ali ibn Abi Talib ni mtu wa familia ya Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliyebarikiwa.

2. Kazi za Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) zinaweza kufanywa, katika kutokuwepo kwake, na Ali tu, na sio na mtu mwingine yoyote.

3. Mwakilishi au mshikamakamu wa Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) anaweza kuchaguliwa na Allah (s.w.t.) Mwenyewe au na Mtume Wake, lakini sio na umma wa Kiislam.

4. Ali ndiye mtu mwenye sifa stahilifu zaidi za kumuwakilisha Mtume wa Allah (s.a.w.) na hakuna mtu mwingine mwenye sifa bora zaidi kuliko

yeye.

247

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

5. Kazi muhimu zaidi ya Mkuu wa Dola ya Kiislamu ni kutangaza Amri za Allah (s.w.t.) katika dunia hii. Ingawa Abu Bakr alikuwapo mahali hapo huko Makka, hakuruhusiwa kutangaza Amri za Allah (s.w.t.); bali Ali ibn Abi Talib ndiye aliyezitangaza.

Marmaduke Pickthall

Ingawa Makka ilikuwa imekwishatekwa na watu wake sasa walikuwa ni Waislamu, ile amri rasmi ya hija ilikuwa imebadilishwa; wapagani wa Kiarabu wakiifanya katika namna yao na Waislamu kwa namna yao. Ilikuwa ni baada tu ya msafara wa mahu-jaji ulipokuwa umeondoka Al-Madina katika mwaka wa tisa wa Hijiria, wakati Uislamu ulikuwa umetawala huko Arabia ya Kaskazini, ambapo lile Tangazo la Tauba, kama linavyoitwa, lilipoteremshwa. Mtume (s.a.w.) alituma nakala yake kwa Abu Bakr, kiongozi wa hija, pamoja na maagizo kwamba Ali alikuwa ndiye alisome Tangazo hilo kwenye mkusanyiko wa watu uliokuwako huko Makka. Madhumuni yake yalikuwa kwamba baada ya mwaka ule Waislamu tu, ndio wafanye hija, nafasi zikiwa zimetolewa tu kwa waabudu masanamu kama wale ambao walikuwa na mkataba na Waislamu na hawajawahi kuvunja mkataba wao wala hawa-jawahi kumsaidia yeyote aliyekuwa dhidi yao (Waislamu). Hao walikuwa watumie fursa ya mkataba wao kwa muda ule, lakini mkataba wao utakapokwisha watakuwa kama waabudu-masanamu wengine. Tangazo lile linaweka mwisho wa uabudu masanamu katika Arabia.

(Introduction to the Translation of Holy Qur 'an, Lahore, Pakistan, 1975)

Yalikuwa ni mapenzi yake Allah (s.w.t.) kwamba mja Wake mpendwa, Ali ibn Abi Talib, aweze, kwa kusoma Tangazo Lake, kukomesha uabudu masanamu katika Arabia daima.

248

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Msafara wa Mwisho

Baada ya kutekwa kwa Makka makabila mengi ya kipagani yalikuja kuwa Waislamu kwa hiari, ambapo kuna mengine ambayo yaliingia Uislamu wakati Mtume (s.a.w.) alipotuma mubaligh wake kwao kuwaelekeza kwenye kanuni na matendo ya dini. Mmoja wa muba-ligh wake alikuwa ni Ali ibn Abi Talib. Bwana wake alimtuma kwenda Yemen katika mwaka wa 10 H.A. kuyaalika makabila ya Yemen kwenye Uislamu.

Ingawa ule msafara wa mwisho ambao Mtume (s.a.w.) aliuandaa ulikuwa ni ule ambao ulikuwa utumwe kwenda kwenye mpaka na Syria chini ya uongozi wa Usama bin Zayd bin Haritha, haukuondoka kamwe Madina katika wakati wa uhai wake. Kwa hiyo, ule msafara wa Ramadhani ya mwaka wa 10 H.A. ambao aliutuma Yemen chini ya uongozi wa Ali, ulikuwa ndio wa mwisho ambao hasa uliondoka Madina alipokuwa bado yuko hai.

Ali aliwasili Yemen pamoja na wapanda farasi wake katikati ya kipupwe, na aliwalingania watu wa kabila la Madhhaj kuukubali Uislamu, lakini walimjibu kwa mfululizo wa mishale na mawe ambapo na yeye aliviashiria vikosi vyake vifanye mashambulizi. Waliwashambulia wale watu wa kabila na kuwashinda lakini hawakuwafukuza kwa sababu ujumbe wa Ali ulikuwa wa amani na sio wa vita. Amri zake kwa vikosi vyake zilikuwa ni kupigana tu katika kujihami wenyewe.

Madhhaj waliomba amani ambayo Ali bila kusita aliwapatia, na akatoa mwaliko wake upya kwao kuukubali Uislamu. Safari hii wao na pia kabila la Hamdan waliitikia mwito wake, na wakasilimu. Ujumbe wa Ali ulifanikiwa. Yemen yote wakawa Waislamu kwa kupitia juhudi zake. Alitekeleza ujumbe wake, kama kawaida, kwa ustadi mzuri sana na kujiamini, na akadhihirisha kwamba alikuwa ndiye mubaligh wa Uislamu kwa uwezo hal-isi.

M. Shibli

Kikundi chenye nguvu sana na chenye uwezo huko Yemen kilikuwa kiliundwa na jamaa wa kabila la Hamdan. Mwishoni mwa mwaka wa 8 H.A., Mtume (s.a.w.) alimtuma Khalid bin Walid kuwalingania kwenye Uislamu. Khalid alikaa miezi sita mion-goni mwao akihubiri Uislamu lakini hakuweza kupata wafuasi wapya wowote, na ujumbe wake ulishindwa. Alikuwa ni jenerali na mtekaji lakini sio mhubiri na mubaligh. Mwishowe Mtume (s.a.w.) alimwita arudi Madina, na badala yake, akamtuma Ali ibn Abi Talib.

Ali aliwakusanya watu wa kabila la Hamdan katika bonde, akasoma mbele yao ule ujumbe wa Mtume wa Allah (s.a.w.) na akawafikishia Uislamu. Safari hii waliitika -kwa kuukubali Uislamu. Kabila zima, wote wakawa Waislamu.

249

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali alituma taarifa juu ya matokeo ya ujumbe wake kwa Mtume (s.a.w.) huko Madina. Wakati Mtume (s.a.w.) alipoisoma taarifa hiyo, alimshukuru Allah (s.w.t.) kwa Rehema Zake, na akinyanyua macho yake kuelekea juu Mbinguni, akaomba baraka juu ya kabila la Hamdan. Hili alilifanya mara mbili.

(Sira-tun-Nabi, Juz.11, (Toleo la 10) 1974, Chapa ya Ma'arif Printing Press, Azamgarh, India).

Katika miaka kumi ya mwisho ya maisha yake, Mtume (s.a.w.) wa Uislamu aliandaa mis-afara themanini ambayo iliondoka Madina kwa shughuli mbalimbali - mingine ya kivita na mingine ya amani. Msafara wa Ali kwenda Yemen ni wa manufaa maalum kwa sababu ulikuwa ni wa mwisho wa yote. Hakuna msafara mwingine ulioondoka Madina katika uhai wa Mtume.

Mwaka wa 10 H.A. (631A.D.) unaitwa 'Mwaka wa Wajumbe'. Makabila mengi ya Kiarabu yalituma wajumbe huko Madina kwa kuukubali Uislamu, na kumpa Muhammad Mustafa kiapo chao cha utii kama mtawala wao wa kidunia.

Katika mwaka wa kwanza wa Hijiria (A.D. 622) Madina ilikuwa na hadhi ya Serikali ya Jiji lakini kwa miaka kumi ilikuwa imechipuka kuwa makao makuu ya Serikali ya "Taifa". Peninsula yote ilikuwa imekubali mamlaka yake ya kiroho na kidunia. Muhammad Mustafa, (Rehema Allah (s.w.t.) ziwe juu yake na juu ya kizazi chake), alikuwa amesi-mamisha amani ya ndani katika nchi nzima, na alikuwa amechukua hatua zenye nguvu kulinda maslahi ya "Kitaifa" ya umma wa Kiislamu. Hakukuwa na tishio kwenye usalama wa Dola ya Kiislamu kutokana na uvamizi wowote wa nje.

Wayahudi na Wakristo walilkuwa wanalipa kodi au ushuru (Jizya). Walikuwa wanafaidika na haki zote za uraia wa Dola ya Kiislamu, na walikuwa wakifaidi uhuru kamili wa kidi-ni. Waarabu, wengi wao sasa wakiwa wamesilimu na kuwa Waislamu, walikuwa katika mkesha wa ufufukaji wa "Kitaifa" wenye nguvu. Kulikuwa na chache tu ya neema zisizo na idadi ambazo Uislamu ulizileta kwenye peninsula ya Arabia.

250

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hija ya Muago

Katika Dhil-Qaddah, (mwezi wa 11 wa kalenda ya Kiislam) ya mwaka wa 10 H.A., Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) alitangaza kwamba atatembelea Makka kufanya Hija. Habari hizo zikaenea nchi nzima na idadi kubwa ya Waislamu ilikusanyika Madina ili kuongozana naye kwenda Makka. Idadi yao inakadiriwa kuwa zaidi ya 100,000. Kabla ya kuondoka kwake, alimteua Abu Dujana Ansari kama gavana wa Madina wakati wa kutokuwepo kwake. Mnamo mwezi 25 Dhil- Qaddah, aliondoka Madina, akifuatana na wake zake wote.

Waislamu waliangalia kila hatua, kila tendo, na kila ishara ya Mtume (s.a.w.) kwenye safari hii, na kila kitu ambacho alikifanya, likawa ni mfano wa wakati wote, wa kuigwa na Waislamu wote.

Maxime Rodinson

Baada ya kuanguka kwa Makka, Muhammad alifanya (kwa mara ya pili tangu kuhama kwake) ibada ya Umra, ibada ya maandamano kuzunguka Al-Kaaba, na zile safari kati ya Safa na Marwa (utengano wa yadi 400). Lakini hakushiriki katika Hija... Anaweza kuwa alikuwa na wazo la kuirudisha kwenye upagani hiyo Hija. Baada ya kuiteka Makka, katika Dhil-Hijja iliyofuata, Attab, gavana ambaye Muhammad alikuwa amemuweka hapo Makka, aliendesha hiyo ibada; Waislamu na mapagani wote walishiriki. Mwaka uliofuatia, Dhil-Hijja ya mwaka wa 9 (March-April 631), Muhammad bado alibaki nyuma na kutojiunga na Hija. Alikuwa bado hajakamilisha mafundisho yake juu ya kila jambo moja moja la hija na alikuwa hayuko radhi kufanya ibada hiyo pamoja na mapagani. Alimtuma Abu Bakr kwenda kuongoza ibada hizo. Alikutwa humo njiani na Ali, ambaye alikuwa mbebaji wa wahy mpya kabisa kutoka juu ambao ilikuwa ni kazi yake kuona unatekelezwa. Wapagani kwa kawaida walikuwa wasishiriki tena baada ya hapo katika hija. Katika kumalizika kwa muda wa makubaliano matakatifu ya miezi minne, wote ambao walikuwa bado hawajasilimu au kufanya mapatano maalum na Muhammad, watachukuliwa kama maadui. Huu ndio ulikuwa mwaka wa mwisho kwa mapagani kuruhusiwa kujiunga na hija.

Mwaka mmoja baadae, katika Dhul-Hijja ya mwaka wa 10 (Machi 632) Mtume (s.a.w.) alitangaza kwamba ataongoza mwenyewe ibada hiyo, kwa sababu sasa hekalu na sehemu takatifu zote zimetakaswa na kuwepo kokote kwa upagani. Aliwasili Makka mnamo 5 Dhil- Hajji (3 Machi). Mnamo mwezi 8 Dhil-Hijja, ibada zilianza. Macho yote yalimtazama Mtume (s.a.w.) kwa sababu mwenendo wake wakati wa ibada hizo utakuwa ni sheria.

(Muhammad)

251

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Siku ya mwezi 9 Dhil-Hajj ya mwaka wa 10 H.A., Mtume (s.a.w.) alitoa hotuba ya kihis-toria katika bonde la Arafat ambayo ndani yake alitoa mukhtasari wa mambo muhimu katika mafundisho yake. Mtume (s.a.w.) kwanza alimshukuru Allah (s.w.t.) kwa neema na rehema zake zisizo na idadi, na kisha akasema:

"Enyi Waislamu! Nisikilizeni kwa makini. Hii inaweza kuwa safari yangu ya mwisho yakuwa pamoja nanyi, na ninaweza nisiwe hai kufanya hija nyingine.

Allah (s.w.t.) ni Mmoja na Yeye hana washirika. Msimshirikishe mtu yeyote au kitu chochote pamoja Naye. Muabuduni Yeye, muogopeni Yeye, mtiini na mumpende Yeye. Msizikose Swala zenu za wajibu. Tekelezeni kikamilifu ule mwezi wa mfungo. Toeni Zaka kwa desturi yake, na tembeleeni Nyumba ya Allah (s.w.t.) wakati wowote mtakapoweza.

Kumbukeni kwamba kila mmoja wenu anawajibika kwa Allah (s.w.t.) kwa kila kitu mnachofanya katika dunia hii, na hivi karibuni tu mtajikuta wenyewe mbele Yake.

Ninazifuta desturi zote, matendo na mila za Wakati wa Ujahilia. Ninakataa haki ya kulipiza kisasi kwa ajili ya damu ya binamu yangu, Ibn Rabi'a; na ninakataa riba kwenye mikopo iliyotolewa na ami yangu, Abbas ibn Abdul-Muttalib.

Ninawalinganieni wote kuonyesha heshima kwa utu, maisha na mali ya kila mmoja wenu kwa namna ileile kama mnavyoonyesha heshima kwa utukufu wa siku hii. Waumini wote ni ndugu kwa kila mmoja wao. Kama kitu ni mali ya mmoja wao, ni haramu kwa wengine kukichukua bila ya ruhusa yake.

Kuweni waaminifu katika maneno na vitendo vyenu, na kuweni waaminifu kwa kila mmoja wenu, na bakini mmeungana wakati wote.

Mnazo haki kuhusu wanawake; hivyo pia mnao wajibu juu yao. Watunzeni kwa mapenzi, upole, heshima na upendo.

Watumwa mlionao wao pia waliumbwa na Allah (s.w.t.). Msiwe wakali kwao. Kama wakikosea, wasameheni. Wapeni wale kile mnachokula ninyi na wapeni wavae namna ileile ya nguo mnazovaa nyie.

Watu wa familia yangu ni kama ile nyota ya kaskazini. Watawaongoza kwenye uon-gofu wale wote watakaowatii na kuwafuata wao. Ninawaachieni miongoni mwenu urithi wa vitu viwili - Kitabu cha Allah (s.w.t.) (Qur'an) na watu wa nyumba yangu. Vyote vinakamilishana na havitenganishiki. Kama mtavinyenyekea vyote hivi ham-tapotea kamwe.

252

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Na kumbukeni kwamba mimi ndiye wa mwisho wa Mitume wa Allah (s.w.t.) kwa wanadamu. Baada yangu mimi hakutakuwa na Mtume mwingine au mitume wa Allah

(s.w.t.)"

Muhammad Mustafa alimalizia hotuba yake kwa du'a nyingine fupi ya shukurani kwa Muumba wake, na akamuomba Yeye awe Shahidi kwamba ametekeleza kazi yake, ame-timiza wajibu wake, na amefikisha ujumbe wa Uislamu kwa watu wake.

Hotuba hii, kama hutuba nyingine zote za Mtume, inafahamika kwa uwazi wake na maar-ifa yake ya kawaida ya kiutendaji. Alifupisha ndani yake mafundisho yake ili yagande kwenye nyoyo na akili za wasikilizaji wake kwa wakati wote.

Mtume (s.a.w.) alikuwa ameonyesha kwa Waislamu jinsi ya kutekeleza taratibu za Hija, na alikuwa amefagilia mbali mabaki ya upagani.

Katika hotuba yake, Mtume (s.a.w.) pia alidokeza kwamba alikuwa pengine hana muda mrefu wa kuishi. Ilikuwa ni karibu na wakati huu ambapo ile Sura ya 110 ya Qur'an Tukufu inayoitwa "Msaada" (Suratun-Nasr), ilipoteremshwa, na ambayo inasomeka kama ifutavyo:

"Itakapokuja nusura ya Allah, na ushindi, Na ukawaona watu wanaingia katika dini ya Allah kwa makundi,

Zitukuze sifa za Mola wako, na umuombe msamaha; hakika Yeye ndiye mwenye kupokea toba. "

Imam Bukhari anasimulia kwamba wakati Sura hii iliposhuka, Umar ibn al-Khattab alimuuliza Abdullah ibn Abbas kama angeweza kumuelimisha yeye juu ya maana yake. Ibn Abbas akasema: "Aya hizi zina maana kwamba wakati wa Mtume (s.a.w.) wa kututo-ka sisi unakaribia."

Wanahistoria wengi wa siku za baadae wa Mashariki na Magharibi wamedai kwamba kifo cha Mtume (s.a.w.) kilikuwa cha ghafla na kisichokuwa kimetegemewa. Lakini kifo chake hakikuwa cha ghafla wala kisichotegemewa. Kwa kweli, alikuwa wa kwanza yeye mwenyewe kuzungumza juu ya jambo hilo, na wakati ile Sura inayoitwa "Msaada" (Nasr) ilipoteremshwa, mashaka madogo sana yalikuwa yamebaki katika akili za maswa-haba wakuu kwamba kazi yake ya kidunia ilikuwa inafikia mwisho. Taarifa za kifo ziko kwenye Aya ya tatu ambamo alilinganiwa "kuomba msamaha Wake," na watu wenye utambuzi walikuwa wepesi kuupata ujumbe huo.

253

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Marmaduke Pickthall

Ilikuwa ni wakati wa hija ya mwisho ambapo ile Sura inayoitwa an-Nasr ilipoteremshwa, ambayo yeye (Muhammad) aliipokea kama tangazo la kifo kina-chokaribia.

(Introduction to the translation of the Holy Qur 'an, Lahore, Pakistan, 1975)

254

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kutawazwa kwa Ali ibn Abi Talib kama Mtawala

wa Baadae wa Waislamu, na kama Kiongozi

wa Umma wa Kiislam

Hija ya mwisho ilikuwa imekwisha, na Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) na lile kundi kubwa la wafuasi wake, walikuwa sasa wako tayari kurudi majumbani kwao. Alitoa ishara na ile misafara ya mahujaji ikaanza kuondoka Makka.

Katika kipande kifupi upande wa kaskazini ya Makka, kuna bonde linaloitwa Khumm, na huko Khumm kulikuwa na kisima au bwawa la maji (Ghadiir). Khumm ipo katika maku-tano ya njia nyingi. Wakati Mtume (s.a.w.) alipowasili katika ujirani wa Ghadiir, alipokea ujumbe mpya - wahy unaofuata kutoka Mbinguni:

Usahihi-29.jpg

Ewe Mtume! Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako. Na kama hutafanya hivyo, basi utakuwa kama hujafikisha ujumbe Wake wowote. Na Allah atakulinda na watu. Hakika Allah hawaongoi watu makafiri. (Sura ya 5; Aya ya 67)

Agizo la Mbinguni lilikuwa mara chache, kama ilikuwa, ni yenye kuamrisha hivyo, kama ilivyo kwenye Aya hii, na ilihusishwa, dhahiri kabisa, kwenye jambo lenye umuhimu sana ambalo Mtume (s.a.w.) ilimbidi ajieleze mwenyewe - hapo hapo. Yeye, kwa hiyo, aliamu-ru mwenyewe msafara wake usimame, na aliirudisha misafara yote ambayo ilikuwa imek-wenda ama mbele au imekwenda pande zingine tofauti tofauti. Yeye mwenyewe alisubiri mpaka msafara wa mwisho ambao ulikuwa umeondoka Makka, pia umewasili jirani na kisiwa cha Khumm.

Mahujaji walikuwa wakagawanyike hapo Khumm kwenye misafara yao tofauti na walikuwa wakatawanyike, kila mmoja akielekea aendako. Mtume (s.a.w.) alikuwa na tangazo muhimu sana la kutangaza kabla ya kutawanyika kwa mahujaji, na alikuwa na shauku sana kwamba idadi kubwa kabisa ya Waislamu walisikie kutoka kwake.

"Mimbari" ilitengenezwa kwa haraka bila vifaa maalum kwa matandiko ya ngamia, na Mtume (s.a.w.) akapanda juu yake ili kwamba kila mtu kwenye ule mkusanyiko mkubwa aweze kumuona yeye kwa macho yake mwenyewe. Binamu yake, Ali, alikuwa amesima-

255

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ma karibu yake.

Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) alikuwa sasa yuko tayari kutoa lile tanga-zo la kihistoria katika kutimiza lile agizo tukufu lililonukuliwa hapo juu. Alimshukuru Allah (s.w.t.) kwa ile Neema kubwa ya Uislamu, na kwa Rehema Zake na Wema Wake, na kisha akauliza swali hili kwa Waislamu:

"Je, ninayo haki au sina haki kubwa zaidi juu ya nafsi zenu kuliko ninyi wenyewe mliyonayo juu yake?"

Waislamu wakajibu kwa sauti moja: "Mtume wa Allah anayo haki kubwa juu ya nafsi zetu kuliko sisi wenyewe tuliyonayo juu yake (hiyo nafsi)." "Kama hivyo ndivyo," alisema, "basi ninao ujumbe muhimu sana wa kufikisha kwenu," na akauelewesha ujumbe huo kama ifuatavyo:

"Enyi Waislamu! Mimi ni binadamu kama ninyi, na ninaweza kuitwa hivi karibuni mbele ya Mola wangu. Urithi wangu wa thamani sana kwenu ni Kitabu cha Allah (s.w.t.) na watu wa Nyumbani kwangu, kama nilivyowaambieni kabla. Sasa sikilizeni hili kwa makini kwamba mimi ni Bwana (Maula) wenu ninyi wote - wa Waumini wote. Wale wanaume na wanawake wote wanaonikubali mimi kama Bwana wao, ninawataka wamkubali (hapa aliushika mkono wa Ali na akaunyanyua juu zaidi ya kichwa chake) Ali pia kama Bwana (Maula) wao. Ali ni Bwana wa wale wanaume na wanawake wote ambao mimi na Bwana wao."

Alipokwisha kuutoa ujumbe huu, Muhammad Mustafa alinyanyua mikono yake kuelekea juu mbinguni, na akasema:

"Ewe Allah sw! Kuwa Rafiki wa yule ambaye ni rafiki wa Ali, na kuwa ni Adui wa yule ambaye ni adui yake. Msaidie yule anayemsaidia Ali, na umtelekeze yule anayemtelekeza yeye Ali."

Uliopita ni mukhtasari wa yale ambayo Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliyoyase-ma hapo Khumm. Maneno halisi na muktadha wa hotuba yake yamehifadhiwa katika kile kitabu maarufu Taudih-ed-Dala'il kilichoandikwa na profesa mkubwa wa Kisunni, Allamah Shahab-ud-Diin Ahmed. Ufuatao ni ufupisho wa hotuba hiyo kama ilivyoandik-wa katika Taudih-ed-Dalai ’l:

Ninatoa sifa na shukurani kwa Allah (s.w.t.) kwa neema Zake zote. Nashuhudia kwamba hapana Mola ila Allah (s.w.t.) na Yeye ni Mmoja, Mwenye Nguvu zote, Mkamilifu. Wote tunamtegemea Yeye. Yeye hana mke, hana mtoto, hana washirika. Mimi ni mmoja wa waja Wake lakini Yeye amenichagua mimi kama Mtume Wake

256

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwa ajili ya uongofu kwa wanadamu. Enyi watu! muogopeni Yeye katika nyakati zote na kamwe msimuasi Yeye. Msipigane ila kwa ajili ya Uislamu, na kumbukeni kwam-ba elimu ya Allah (s.w.t.) imekizunguka kila kitu.

Enyi Waislamu! tahadharini kwamba wakati nitakapokuwa nimeondoka, watatokea watu ambao watahusisha Hadith za uongo kwangu mimi na watakuwepo watu wengine watakaoziamini hizo. Lakini ninaomba ulinzi wa Allah (s.w.t.) kwamba nisi-je kamwe kusema kitu chochote bali Ukweli na kuwaiteni kwenye lolote ila kile Yeye alichoteremsha kwangu. Wale wanaovuka mipaka katika jambo hili, watapata adhabu.

Kufikia hapa sahaba mmoja, Ibada ibn Samit, alisimama na akauliza: "Ewe Mtume wa Allah (s.w.t.)! wakati huo utakapofika, ni nani tutakaye muangalia kwa ajili ya mwongo-zo?"

Mtume wa Allah (s.w.t.) alijibu kama ifuatavyo:

"Muwafuate na kuwatii 'Watu wa Nyumba yangu' (Ahlul-Bait)." Wao ndio warithi wa elimu yangu ya kinabii na utume. Watawaokoeni kutokana na upotovu, na watawaongozeni kwenye uongofu. Watawalinganieni kwenye Kitabu (Qur'an Tukufu) na Sunnah yangu. Wafuateni hao kwa sababu hawana shaka kamwe juu ya jambo lolote. Imani yao juu ya Allah (s.w.t.) haiyumbi. Wao ndio wale walioongozwa sawasawa; wao ndio wale Maimamu, na ni wao peke yao wanaoweza kuwaokoeni kutokana na ukafiri, uasi na uzushi.

Allah (s.w.t.) amekuamuruni kuwapenda Ahlul-Bait wangu. Utii kwao umefanywa ni lazima juu yenu (Qur'an Tukufu: Sura ya 42; Aya ya 23). Wao ndio wale walio-takaswa (Qur'an Tukufu Sura ya 33; Aya ya 33). Ndio wale waliopewa uadilifu na ubora ambao hakuna mtu mwingine yoyote aliyenao. Wao ndio Wateule wa Allah (s.w.t.) Mwenyewe.

Sasa nimeamriwa na Allah (s.w.t.) kutoa tangazo hili:

Hapa aliushika mkono wa Ali, akaunyanyua juu kabisa, na akasema: "Fahamuni ninyi wote, yeyote yule ambaye mimi ni Maula (Bwana) wake, Ali ni Maula (Bwana) wake. Ewe Allah! Kuwa Rafiki wa yule ambaye ni rafiki wa Ali, na kuwa Adui kwa yule ambaye ni adui wa Ali. Ewe Allah! Msaidie yule anayemsaidia Ali, na mtelekeze yule anayemtelekeza Ali."

Hotuba ilikwisha. Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.w.t.) alikuwa kiutaratibu na kirasmi amekwisha kumtangaza Ali ibn Abi Talib kuwa Mkuu wa Waislamu wote, na

257

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

amemteua kama kiongozi wa Dola na Serikali ya Kiislamu.

Mara tu baada ya kutolewa tangazo hili, Aya nyingine, Aya ya mwisho ya Qur'an Tukufu, iliteremshwa kwa Muhammad. Inasomeka kama ifuatavyo:

Usahihi-30.jpg

Leo hii nimekukamilishieni dini yenu, na Nimekutimizieni Neema Yangu, na Nimekuchagulieni Uislamu kuwa dini yenu. (Sura ya 5; Aya ya 3)

Ilikuwa ni siku ya 18 ya mwezi wa 12 wa mwaka wa 10 wa kalenda ya Kiislam (Machi 21, 632) wakati Aya ya mwisho ya Ufunuo ilipoteremshwa duniani hapa. Wahy ulikuwa umeanza mwaka 610 A.D., katika pango la Hira huko Makka, na ulifikishwa mwisho mwaka 632 A.D., katika bonde la Khumm kwa tangazo kwamba Ali ibn Abi Talib atakuwa ndiye Mtekelezaji Mkuu, baada ya Muhammad mwenyewe, wa Serikali ya Madina na Dola ya Kiislamu.

Ibn Hajar Asqalani anaandika katika Isaba kwamba baada ya kutoa tangazo hili, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliweka kilemba juu ya kichwa cha Ali ibn Abi Talib, na hivyo kukamil-isha kutawazwa kwake.

Masahaba wote walimpongeza Ali katika tukio hili tukufu wakati Mtume wa Allah (s.a.w.) mwenyewe alipomtawaza yeye na kumtangaza kama mshikamakamu na mrithi wake. Miongoni mwa wale ambao walimpongeza walikuwa Umar bin al-Khattab na wake za Mtume.

Hasan bin Thabit Ansari alikuwa ndiye mshairi wa baraza la Mtume, na alitungia mashairi matukio yote muhimu. Kutawazwa kwa Ali kulikuwa ni moja kati ya matukio ya kihisto-ria sana ambayo yalikitia changamoto kipawa chake cha ushairi. Alitunga wimbo wa sifa ambao aliutoa kwa heshima ya Ali.

Ifuatayo ni tarjuma ya haraka haraka ya beti zake:

Katika siku ya Ghadir Khumm, Mtume (s.a.w.) na Waislamu aliwaita, na nilimsikia wakati yeye aliposema:

"Ni nani Mola wenu, na ni nani Bwana wenu?" Wote wakasema: "Allah (s.w.t.)

ndiye Mola wetu, na wewe ndiye Bwana wetu, na hakuna yeyote kati yetu

anayeweza kukukaidi wewe."

Hivyo alimuomba Ali asimame. Wakati Ali aliposimama, aliushika mkono wake,

na akasema:

"Nakuchagua wewe kama kiongozi baada yangu. Kwa hiyo, yeyote yule ambaye

258

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Bwana wake ni mimi,

Ali ni Bwana wake pia. Kwa hiyo, nyote nyie muwe marafiki zake wa kweli na

wafuasi wake."

Mtume (s.a.w.) kisha akaomba, akisema: "Ewe Allah! kuwa Rafiki kwa wale

ambao ni marafiki wa Ali;

na kuwa Adui wa wale ambao ni maadui zake."

Mshairi mwingine ambaye alitunga mashairi katika tukio la kutawazwa kwa Ali, alikuwa ni Qays ibn Ubada Ansari. Alisema:

Wakati maadui walipoasi dhidi yetu, nilisema kwamba Mpaji wetu, Allah (s.w.t.) anatutosha sisi, na Ndiye Mlinzi bora tunayeweza kuwa naye.

Ali ni Bwana wetu na ni bwana wa waumini wote. Hili linathibitishwa na Qur'an Tukufu na ni hivyo tangu ile siku Mtume wa Allah (s.a.w.) aliposema: "Yeyote yule ambaye Bwana wake ni mimi, Ali ni Bwana wake pia" Hili kwa hakika lilikuwa ni tukio la kufahamika sana.

Chochote kile Mtume wa Allah (s.a.w.) alichokisema siku ile, ni mwisho; ndio neno la mwisho, na hakuna kabisa nafasi ya hoja yoyote ndani yake.

Kwa mshangao na kutosadikika, hata mtu kama Amr bin Al-Aas "alitiwa moyo" kutoa shairi kwa heshima ya Ali hapo Ghadir Khumm. Ifuatayo ni mistari miwili ya utunzi wake:

Pigo la upanga wa Ali ni kama kile kiapo cha utii ambacho kila mmoja ali-kichukua ile siku ya Ghadir, na ambacho kilimfanya kila mtu kusalimu amri mwenyewe mbele ya mamlaka yake (mapya).

Kama hizo Aya mbili za Qur'an zinazohusu kutawazwa kwa Ali, zitasomwa katika utarat-ibu wa mpango wake, na katika fuo lake la kihistoria, maana zao zitakuwa wazi. Nitazinukuu mara nyingine tena katika uchambuzi mfupi; na kwa wepesi wa rejea, nitazi-ita Aya ya kwanza na ya pili.

{1}. Ewe Mtume! Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako.

Na kama hutafanya hivyo, basi utakuwa kama hujafikisha ujumbe Wake wowote. Na Allah atakulinda na watu. Hakika Allah hawaongoi makafiri.

{2} Leo hii Nimekukamilishieni dini yenu na Nimekutimizieni neema Yangu, na Nimekuchagulieni Uislamu kuwa dini yenu.

Kutawazwa kwa Ali kulitokea ndani ya mfumo wa Aya hizi mbili za Qur'an. Kutawazwa kwake kulikuwa ni jambo lenye mkazo kiasi kwamba Muhammad Mustafa, Mpokezi wa

259

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wahy, aliamriwa, katika Aya ya kwanza, kusimamisha chochote alichokuwa anakifanya, na ashuhulishwe kwanza na hilo. Yeye, kwa hiyo, aliwaamuru mahujaji wote wakusanyike katika bonde la Khumm, na akawaambia kwamba Ali atawatawala wao kama mrithi wake katika Ufalme wa Mbinguni katika Ardhi.

Mara tu Mtume (s.a.w.) alipokwisha kufanya hivyo, kisha hii Aya ya pili ilishushwa kama ishara ya idhini ya Mbinguni ya kitendo chake. Kutangazwa kwa Ali kama mrithi wake kulikuwa ndio ukamilisho na kilele cha kazi ya maisha ya Muhammad. Kwa tangazo hili, kazi yake kama Mtume wa Allah (s.a.w.) ilikamilika. Alikuwa amemtangaza Ali kuwa mrithi wake kwenye matukio mengi wakati uliopita lakini pale Ghadir-Khumm, alimtawaza rasmi kama Kiongozi wa Umma wa Kiislamu wa baadae.

Kati ya Aya hizi mbili za Qur'an-moja yenye nguvu sana katika kudai kitendo na ile nyingine ikiwa dhahiri mno katika kuthibitisha kwake usimikwaji wa Ali kama mrithi wa Mtume (s.a.w.) - na kauli ya Mtume: "Ali ni Bwana wa wale wanaume na wanawake wote ambao mimi ni Bwana wao," kuna uwiano wa kimantiki na wa dhahiri.

Walaghai wengine wamejadili bila msingi hili neno Maula kama lilivyotumiwa na Mtume (s.a.w.) wakati aliposema: "Ali ni maula wa wale wanaume na wanawake ambao mimi ni maula wao. Wanakubali kwamba kauli hiyo ni halisi lakini wanalitafsiri neno maula sio kama "Bwana" bali ni kama "rafiki." Lakini hii haikuwa ndio dhimiri ya Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Hivi aliirudisha ile misafara yote na kuwaamuru wakusanyike katika lile bonde la Khum lisilo na kivuli kwa ajili tu ya kuwaambia kwamba Ali ni rafiki yao? Je, ilichukuliwa na maswahaba wakati ule kwamba Ali hakuwa rafiki yao, na Mtume (s.a.w.) ikambidi awahakikishie wao kwamba yeye (Ali) kwa kweli alikuwa ni rafiki yao?

Wale watu wanaolitafsiri hili neno maula kama "rafiki," labda wanasahau kwamba Mtume (s.a.w.) alilitumia kwa kujihusisha yeye mwenyewe kabla hajalitumia kumhusu Ali, na hili linaweza kuruhusu tu tafsiri moja sahihi, ndio kusema, kama Muhammad, Mtume, ndiye Bwana wa Waislamu wote, Ali pia ni Bwana wao.

Walaghai hao pia wanasahau kwamba kabla ya kumtangaza Ali kama mrithi wake na mkuu wa Waislamu wote, Mtume (s.a.w.) alikwisha kuwauliza swali lifuatalo:

"Ninayo au sinayo haki kubwa zaidi juu ya nafsi zenu kuliko mliyonayo ninyi wenyewe juu yenu?"

Jibu la Waislamu kwa swali hili lilikuwa ni "ndio" isiyo na kifani. Swali hili lilikuwa ni la utangulizi wa tangazo la Mtume (s.a.w.) kwamba Ali alikuwa ndiye mrithi wake. Hilo swali na hilo tangazo vilikuwa ni sehemu ya muktadha huo huo, na kama vikisomwa pamoja, havitaacha shaka yoyote akilini mwa msomaji kwamba hili neno maula maana yake ni "Bwana" na sio "rafiki."

260

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wengi wa wafasiri wa Ki-Sunni wamekubali kwamba ile amri ya Allah (s.w.t.) kwa Mtume Wake katika ile Aya ya kwanza inafungamana hasa na tangazo kwamba Ali ndiye Mkuu wa Waislamu wote. Baadhi ya wafasiri hawa ni:

Wahidi katika Asbab-un-Nuzuula

Suyuti katika Tafsir Durr al-Manthur

Ibn Kathir

Imam Ahmad bin Hanbal

Abu Ishaq Nishapuri

Ghazali katika Sirrul-Alamiin

Tabari katika Tarikh-ar-Rusul wal-Muluuk

Sheikh Abdul Haq Muhaddith wa Delhi, India

Hapa ni lazima pia ielezwe kwamba kabla ya kushushwa kwa Aya hiyo ya kwanza (5:67), amri zote zinazohusika na Shari 'ah (mfumo wa kanuni na taratibu za dini ya Kiislam), kama vile Sala za kila siku, Funga, Zaka, Hajj (kwenda Hija Makka), na Jihad - kwa haki-ka zile sheria zote kwa maisha ya mtu binafsi, kijamii, kiuchumi na kisiasa za Waislamu, zilikuwa tayari zimekwisha kutolewa kwa Muhammad. Alikuwa amekwisha zifikisha, na Waislamu walikuwa wakizifanyia kazi, na zimekuwa sehemu muhimu za maisha yao. Alikuwa amekwisha kutambulisha na kutekeleza kila sheria.

Kitu pekee ambacho Mtume (s.a.w.) alikuwa bado hajakifanya hadi kufikia wakati huo, kilikuwa ni kumtambulisha rasmi kwa umma wake, mrithi wake mwenyewe. Umma huo ulikuwa unayo haki ya kujua ni nani atakayekuwa mtawala wake baada ya kifo chake (yeye Mtume). Hiki ndicho alichokifanya wakati alipoamriwa "kufikisha ujumbe." Hii amri ya Allah (s.w.t.) ilikuwa na nguvu sana, na Mtume (s.a.w.) hakuweza kuahirisha utekelezaji wake kwa muda mwingine.

Lakini mara tu baada ya Mtume (s.a.w.) kutekeleza ile amri ya mbingnii, kwa uwazi kamili na kwa uamuzi wa mwisho kabisa, ile Aya ya pili (5:3) iliteremshwa, na iliweka muhuri wa uthibitisho juu ya kitendo chake.

Kwa usimikwaji rasmi wa Ali ibn Abi Talib kama mrithi wa Muhammad na kama kiongozi wa Waislamu wote, imeandikwa katika Aya za mwisho zilizoteremshwa kwenye Kitabu cha Allah (s.w.t.).

Aya ya mwisho ya Kitabu cha Allah (s.w.t.) ilishushwa na iliandikwa mnamo Machi 21, 632, kama ilivyoelezwa kabla, na mlango wa Wahy ukafungwa milele. Siku themanini baadae, yaani, mnamo Juni 8, 632, Muhammad Mustafa aliagana na umma wake, na akaenda mbele ya Mola wake. Hakuna kumbukumbu kwamba aliupa umma wake amri

261

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mpya zozote au makatazo (Awamir au Nahawi), ya mafundisho au ya vitendo, katika muda wa hizi siku 80. Uislamu ulitangazwa kuwa umekamilika na kutimia mara tu baada ya Mtume Wake kumteua Ali ibn Abi Talib kuwa mrithi wake.

Allah (s.w.t.) awazidishie waja Wake, Muhammad na Ali, na watu wa familia zao, Fadhila Zake, na Neema na Baraka Zake.

Muhammad Mustafa angeweza sasa kuangalia nyuma kwa kuridhika juu ya kazi yake, na angeweza kuangalia mbele kwenye wakati ujao kwa matumaini mapya, kwa kujiamini na furaha. Kwa kumuweka Ali kama mrithi wake, aliuona uendeleaji wa ile kazi ambayo kwayo alitumika bila kujizuia kwa miaka 23, na ambayo ilikuwa imejaa vitisho na hatari nyingi. Kazi yake imehitaji mihanga isiyo na idadi kwa upande wake. Sasa ilionekana kwake kwamba zile suluba zake zote na ile mihanga mwishowe imezaa matunda, kwa vile alijua kwamba Ali atakiendesha chombo cha Uislamu kule kiendako kwa ustadi uleule kama yeye mwenyewe alivyofanya.

Muhammad hakumchagua Ali kuwa mrithi wake kwa sababu tu kwamba alikuwa binamu yake, mkwewe, na sahaba wake mpendwa; wala hakumchagua kwa sababu ya sifa binafsi zake yeye Ali. Muhammad alikuwa na kidogo sana cha kufanya na uchaguzi wake. Mpangilio wa muda wa kushuka kwa Aya hizi mbili za mwisho za Qur'an Tukufu (5:67 na 5:3), na matukio yaliyopita wakati wa muda baina ya wahy hizi mbili, na uwiano wao, vinamuongoza mfuatiliaji kwenye hatima moja tu, yaani, uchaguzi wa Ali kama mrithi wa Mtume (s.a.w.) wa Uislamu, ulifanyika Mbinguni. Allah (s.w.t.) Mwenyewe aliyemchagua Ali. Allah (s.w.t.) asingeweza kuchagua wa tatu au wa pili. Angeweza kuchagua tu yule msafi sana, mbora, wa kipekee kabisa, kama alivyokuwa Ali. Ali alikuwa ndio alama na kielelezo dhahiri cha Ukweli wa Uislamu, na alikuwa ndiye shahidi wa kwanza wa Ukweli wa Mtume (s.a.w.) wa Uislamu. Allah (s.w.t.) awabariki wao wote na familia zao.

Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) alitumia kila nafasi kutaka uangalifu wa Waislamu kwenye daraja tukufu ya Ali. Katika moja ya Hadithi zake mashuhuri (kauli, simulizi), alisema kwamba uhusiano wake na Ali ulikuwa ni sawa na ule wa watangulizi wake wa kinabii - Musa na Harun - pamoja na tofauti tu kwamba Ali hakuwa ni Mtume.

Hadithi hii ilisimuliwa na Saad bin Abi Waqqas, na imeandikwa na Imam Muslim katika Sahihi yake kama ifuatavyo:

Amir bin Sa'd bin Abi Waqqas amesimulia kutoka kwa baba yake kwamba Mtume wa Allah (s.w.t.) (amani iwe juu yake) akimwambia Ali alisema: "Unayo daraja ileile katika uhusiano na mimi kama Harun aliyokuwa nayo kwa Musa lakini pamoja (na tofauti hii ya wazi) kwamba hakuna nabii baada yangu." Sa'd akasema: "Nilikuwa na hamu kubwa ya kuisikia moja kwa moja kutoka kwa Sa'd, hivyo nilikutana naye na

262

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

nikamweleza kile ambacho Amir (mwanae) alikuwa amenisimulia, ndipo akasema: "Ndio, niliisikia." Mimi nikasema: "Uliisikia wewe mwenyewe?" Hapo akaweka vidole vyake juu ya masikio yake na akasema: "Ndio, na kama sivyo, basi masikio yangu yote nayazibe kabisa."

Sa'd bin Abi Waqqas amesimulia kwamba Mtume wa Allah (s.w.t.) (amani iwe juu yake) alimuacha Ali ibn Abi Talib nyuma yake alipokuwa anakwenda Tabuk, ambapo yeye (Ali) alisema: "Ewe Mtume wa Allah, unaniacha mimi hapa pamoja na wanawake na wato-to?" Hapo Mtume (s.a.w.) akasema: "Huridhiki wewe kuwa kwangu mimi kama alivyokuwa Harun kwa Musa bali kwa tofauti kwamba hakutakuwa na nabii baada yangu mimi?"

Hadithi hii imesimuliwa kutoka kwa Shu'ba kwa sanadi ileile ya wapokezi. Amir bin Sa'd bin Abi Waqqas amesimulia kutoka kwa baba yake kwamba Mu'awiyyah bin Abu Sufyan alimteua Sa'd kama gavana na akasema: "Ni nini kinachokuzuia kumtukana Abu Turab (Ali)?" Akasema: "Ni kwa sababu ya mambo matatu ambayo nilimsikia Mtume wa Allah (s.w.t.) akiyasema juu yake ambayo kwayo sintamtukana yeye, na kama ingekuwa nipate hata moja tu ya yale mambo matatu, lingekuwa na thamani sana kwangu kuliko ngamia wekundu. Nilimsikia Mtume wa Allah (s.w.t.) akisema kuhusu Ali pale alipomuacha yeye (huko Madina) wakati alipokuwa anakwenda kwenye msafara (Tabuk). Ali alimwambia: "Ewe Mtume wa Allah (s.w.t.) hivi unaniacha mimi hapa na wanawake na watoto.?" Hapo Mtume wa Allah (s.w.t.) akamwambia: 'Hivi huridhiki wewe kuwa kwangu mimi kama Haroun alivyokuwa kwa Musa bali pamoja na tofauti kwamba hakuna utume baada yangu?' Na mimi pia nilimsikia akisema ile Siku ya Khaibar: 'Nitampa bendera hii mtu ambaye anampenda Allah (s.w.t.) na Mtume Wake, na ambaye Allah (s.w.t.) na Mtume Wake wanampendwa.' Yeye (msimuliaji) akasema: Tulikuwa tunaisubiri kwa hamu sana wakati yeye (Mtume) aliposema: 'Mwiteni Ali.' Alikuja na macho yake yalikuwa yanawasha. Alimuweka mate kwenye macho yake na akampa ile bendera, na Allah (s.w.t.) akampa ushindi..

Safari ya tatu ilikuwa ni wakati Aya ifuatayo iliposhuka: "...Tuwaite watoto wetu na watoto wenu..."

Mtume wa Allah (s.a.w.) alimwita Ali, Fatima, Hasan na Husein na akasema: "...EweAllah! Hawa ndio watu wafamiliayangu..."

Hadithi ya Mtume (s.a.w.) ambamo amesema kwamba Ali alikuwa kwake kama Harun alivyokuwa kwa Musa, inakubaliana na Aya za Qur'an Tukufu zifuatazo:

(Musa aliomba):

"Ewe Mola wangu! Nikunjulie kifua changu;

263

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Niwepesishie kazi yangu;

Na uniondolee vifundo kwenye ulimi wangu;

Wapate kuyaelewa maneno yangu;

Na unipe waziri katika familia yangu;

Harun, ndugu yangu,

Kwake yeye uniongezee nguvu zangu,

Na umshirikishe katika kazi yangu:

Ili tukutukuze sana;

Na tukukumbuke sana;

Hakika Wewe unatuona sisi."

(Allah (s.w.t.)) Akasema:

Usahihi-31.jpg

"Hakika umekubaliwa maombi yako, Ewe Musa!" Na hakika tulikwisha kukufanyia hisani juu yako mara nyingine kabla. (Sura ya 20; Ay a ya 25 hadi 37)

Nabii Musa (a.s.) alimuomba Allah (s.w.t.) ampatie Waziri kutoka kwenye familia yake mwenyewe. Hakutaka waziri kutoka miongoni mwa maswahaba na marafiki zake. Aliomba kwamba Harun, ndugu yake, awe ndiye Waziri wake, na angekuwa ni chanzo cha nguvu kwake.

Allah (s.w.t.) alijibu du'a ya Mtume Wake Musa, akampa ndugu yake, Harun, kama waziri wake, na akamfanya kuwa chanzo cha nguvu kwake.

Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Mwisho wa Allah, pia alichagua waziri wake kutoka kwenye familia yake mwenyewe. Chaguo lake lilikuwa ni Ali, ndugu yake. Ali aliongeza nguvu zake, na alishiriki kwenye kazi yake pamoja naye, kama vile ambavyo aliahidi kufanya, miaka mingi iliyopita, katika karamu ya Dhu ’l- 'Ashiira huko Makka katika mku-sanyiko wa wazee wa koo za Bani Hashim na Bani Muttalib.

Usahihi-32.jpg

(Kabla ya hapa) Na hakika tulimpa Musa Kitabu na tukamweka pamoja naye, nduguye Haroun, kuwa waziri. (Sura ya 25; Ay a ya 35)

Allah (s.w.t.) Mwenyewe alimchagua Harun kuwa Waziri. Haukuwa umma (watu) wake Musa ambao walimchagulia Waziri wake.

264

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usahihi-33.jpg

Tulimuahidi Musa masiku thelathini, na tukayatimiza kwa kumi zaidi: Hivyo ikatimia ahadi ya Mola wake, masiku arobaini. Na Musa akamwambia ndugu yake Harun (kabla ya kuon-doka): Shika mahala pangu miongoni mwa watu wangu; ufanye haki na wala usifuate njia ya waharibifu. (Sura ya 7; Aya ya 142)

Musa alimweka ndugu yake, Harun, kwenye madaraka juu ya umma (watu) wake, na haku-uacha (huo umma) bila ya kiongozi ingawa alikuwa anaondoka kwa siku arobaini tu.

Muhammad Mustafa (rehma na amani ziwe juu yake na kizazi chake) hakukengeuka kwenye mwenendo huu wa manabii na mitume wa Allah (s.w.t.) Yeye pia hakuwaacha Waislamu bila ya kiongozi, na alimchagua ndugu yake, Ali, kama kiongozi na mtawala wao baada yake.

Musa aliomba:

Usahihi-34.jpg

"Ewe Mola wangu! Nisamehe mimi na ndugu yangu! Na utuingize katika Rehema Yako! Kwani Wewe ni Mwenye kurehemu kuliko wote wenye kurehemu. (Sura ya 7; Aya ya 151)

Musa hakujiombea yeye peke yake tu; alimuombea ndugu yake Harun pia. Muhammad Mustafa pia aliombea wote, yeye mwenyewe na ndugu yake, Ali. Aliomba rehema za Allah (s.w.t.) juu yao wote na familia zao.

Usahihi-35.jpg

Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Harun. Amani iwe juu ya Musa na Haroun. Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema. Hakika wawili hao ni katika waja walioami-ni. (Sura y a 37; Ay a ya 114, 120, 121, 122)

265

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Allah (s.w.t.) aliweka Rehema Zake juu ya Musa na Harun, na aliweka Rehema Zake juu ya Muhammad na Ali, waja Wake walioamini. Wote wanne walitenda haki, na Allah (s.w.t.) akawalipa wao, na akashusha amani na salamu kwao.

Ingawa Harun alichaguliwa ki-mungu kuwa mrithi na msikamakamu wa Musa, alikufa katika uhai wake (Musa), hivyo kusababisha kuchaguliwa kwa kiongozi mpya. Kiongozi mpya alikuwa ni Yush'a bin Nun (Joshua). Kama Harun, yeye pia, aliteuliwa ki-mungu kuwa mshikamakamu wa Musa, na umma haukuwa na lolote la kufanya katika kuchaguliwa kwake.

Baada ya kifo cha Musa, mshikamakamu wake, Yush'a bin Nun, aliwaongoza Bani-Israil kwenye ushindi.

Vigezo vya hekima katika suala la kuchagua na kuweka kiongozi wa umma wa Kiislam, baada ya kifo cha Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.w.t.) vinaweza kuonekana wazi katika Aya za Qur'an zilizonukuliwa hapo juu. Ali alikuwa ndiye chaguo la Mbinguni. Chote alichokuwa afanye Muhammad, ni kule kutoa lile tangazo rasmi kwamba Ali atakuwa ndio kiongozi wa Waislamu baada ya kifo chake yeye mwenyewe. Ilikuwa ni kutoa Tangazo hili ambako aliwaamuru Waislamu kukusanyika kwenye bonde la Khumm.

Mwislamu wa kisasa anaweza kuchukulia kwamba hili Tangazo la kihistoria lililotolewa na Mtume, lazima lingefuatiliwa na sherehe ya kimataifa miongoni mwa Waislamu. Inaonekana kuwa ni ajabu kusema kwamba haikuwa hivyo. Walikuwepo Waislamu waliokuwa na furaha lakini walikuwepo wengine wengi ambao hawakufurahia. Hawa wengine waliwazia mategemeo mengine, na walijali tamaa nyingine, na mategemeo na tamaa zao havikubadilisha mwelekeo wa tangazo la Mtume (s.a.w.) pale Ghadir-Khumm. Tangazo lake, la wazi kabisa na lisilo na mashaka, ilivuruga matumaini na tamaa zao.

Lakini hawakuvunjika moyo. Walitunga jambo jingine. Walianza kunon'gona kwenye masikio ya Waarabu kwamba uteuzi wa Ali kama Mkuu wa Waislamu wote kulikuwa ni kitendo kilichochochewa na tamaa ya Mtume (s.a.w.) ya kuhodhi mamlaka ya kisiasa katika familia yake mwenyewe - katika ukoo wa Bani Hashim - na kuwaondoa wengine wote, na kwamba haikuwa na uhusiano wowote na Wahy. Walitegemea kwamba ikiwa "hoja" yao itawavutia Waarabu, basi watakuwa na uwezo wa kuwaingiza kwenye kugombania madaraka ambamo wao wenyewe wanaweza wakawa wa juu. Tokea muda huo, Kwa hiyo, walianza kufanya kazi ya kujipangia mkakati mpya wa kupambana na hali hiyo mpya.

Walikuwa ni akina nani watu hawa? Hawakuainishwa kwa majina yao lakini kuwepo kwao na uwezo wao katika fitna vinaonekana katika ile Aya ya kwanza (5:67). Mtume, ni dhahiri, alikuwa anasita kuchukua hatua, akiwa anajua upinzani mkubwa wa Waarabu wengi kwenye kuchaguliwa kwa Ali kama kiongozi wa baadae wa Dola ya Kiislam. Lakini

266

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

alihakikishiwa kwamba Allah (s.w.t.) atamlinda kutokana nao hao; kwamba akushinde kusitasita kwake, na autangaze ushika-makamu wa Ali ibn Abi Talib.

Kupinga lile Tangazo la kihistoria pale Ghadir-Khumm kulikuwa ni kumpinga mwenyewe. Upinzani juu yake, mpaka wakati wa Tangazo lile, hata hivyo, ulikuwa umejificha na kuto-jionyesha; lakini muda si mrefu ulikuwa utokeze kichwa chake cha husuda katika wakati wa uhai wake yeye mwenyewe. Suala hili limeshughulikiwa katika Sura ya 39.

Kule kuteuliwa, na Muhammad Mustafa, pale Ghadir-Khumm, kwa Ali ibn Abi Talib kama mrithi wake, kumesimuliwa na maswahaba wake wafuatao:

Khuzayma bin Thabit

Sahl bin Sa'ad

Adiy bin Hatim

Aqba bin Aamir

Abu Ayyub Ansari

Abul-Haithum bin Taihan

Abdullah bin Thabit

Abu Ya'la Ansari

Nu'man bin Ajlan Ansari

Thabit bin Wadee'a Ansari

Abu Fadhala Ansari

Abdur Rahman bin Abd Rabb

Junaida bin Janada

Zayd bin Arqam

Zayd bin Sherheel

Jabir bin Abdullah

Abdullah bin Abbas

Abu Said al-Khudri

Abu Dharr al-Ghiffari

Salman el-Farsi

Jubayr bin Mutim

Hudhayfa bin Yaman

Hudhayfa bin Usayd

Miongoni mwa wanahistoria ambao wameandika matukio ya Ghadir-Khumm ni Athiir-ud-Diin ndani ya kitabu chake Usudul-Ghaba; Halabi katika kitabu chake Siira-tul-Halabiyya; na Ibn Hajar katika kitabu chake al-Sawa 'iq-al-Muhriqa.

Wapokezi wa Hadith waliotaja matukio ya Ghadir-Khumm ni akina Muslim, Nasai, Tirmidhi, Ibn Majah; Ahmad Hanbal na Hakim.

267

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Jeshi la Usamah

Zayd bin Haritha alikuwa ni mtumwa aliyeachwa huru na rafiki wa Muhammad Mustafa. Aliuawa katika vita vya Muutah mnamo A.D.629 ambavyo aliongoza Waislamu dhidi ya Warumi. Waislamu walishindwa katika vita hivyo, na walikimbilia Hijazi.

Mtume (s.a.w.) wa Uislamu alitaka kufutilia mbali ile kumbukumbu ya kushindwa kule lakini alikuwa akisubiria muda unaofaa kwa kufanya hivyo. Tangu wakati ule Mtume, rehema na amani juu yake na Ahlul-Bait wake, alipohamia Yathrib (Madina) mnamo mwaka 622, alifanya kazi kwa bidii sana. Alikuwa amebeba mzigo wa majukumu ambayo hata shirika la mashirika ya watu lingeona kwamba ni mazito zaidi mno. Tangu ile Hijja ya Muago mnamo Machi 632, alifanya kazi takriban bila kupumzika. Kazi ngumu mfululizo na ugumu maishani mwote vilichukua hesabu yake, na akaugua. Maradhi haya yalikuwa yawe ya kufisha. Ingawa alijisikia udhaifu hata kabla maradhi hayajaanza, hakuuruhusu udhaifu huo kuingilia kati kazi zake kama Mtume wa Allah (s.a.w.). na kama kiongozi mkuu wa Waislamu.

Ule "wakati unaofaa" uliosubiriwa kwa muda mrefu unaelekea kuwa umewadia mwishoni. Mtume (s.a.w.) aliandaa na kuanzisha jeshi jipya kufanya uvamizi wa mpaka wa Syria. Hadhi ya Uislamu ilikuwa imevunjwa katika vita vya Muutah, na wakati ulikuwa umefika wa kuirudisha upya. Kuongoza jeshi hilo, Mtume (s.a.w.) alimchagua Usamah, kijana wa miaka 18, mtoto wa Zayd bin Haritha, shahidi wa Muutah. Wote baba na mwana walikuwa vipenzi wakubwa wa Mtume. Lakini hakuwafanya kuwa majenerali kwa ajili ya upen-deleo; aliwafanya majenerali kwa sababu walifuzu kwa uwezo wao wa kusimamia watu wengine, na kuwaongoza kwenye vita.

Mnamo mwezi 18 Safar ya mwaka 11 A.H., Muhammad Mustafa aliweka bendera ya Uislamu mikononi mwa Usamah, akamweleza kwa kifupi malengo ya pambano hilo, na akampa maelekezo juu ya jinsi atakavyoliendesha. Kisha ndipo akawaamuru maswahaba wake wote, isipokuwa Ali na watu wengine wa Bani Hashim, kupiga ripoti kikazi kwa Usamah, na kuwajibika chini yake. Masahaba hawa walijumuisha watu wazima, watu matajiri sana, na watu wenye nguvu sana wa Maquraishi kama vile Abu Bakr, Umar, Abdur Rahman bin Auf, Abu Ubaida ibn al-Jarrah, Sa'ad bin Waqqas, Talha, Zubayr, Khalid bin Walid, na wengine wengi. Mtume (s.a.w.) alimuamuru Usamah kuondoka haraka mbele ya maswahaba hao na jeshi kuelekea kwenye kituo chake.

268

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir William Muir

Katika siku ya Jumatano iliyofuata, Muhammad alishikwa na maumivu ya kichwa makali na homa; lakini yalipita. Asubuhi iliyofuata alijikuta amepona kabisa kuweza kufunga kwa mkono wake mwenyewe kwenye mlingoti wa bendera, ile bendera kwa ajili ya jeshi. Aliikabidhi kwa Usamah pamoja na maneno haya: 'Pigana chini ya bendera hii kwa jina la Allah (s.w.t.) na kwa njia Yake. Hivyo utawashinda na kuwaua wale watu ambao hawamuamini Allah (s.w.t.)' Kisha kambi ikawekwa hapo Jurf; na kundi lote la wapiganaji, bila ya kumuondoa hata Abu Bakr na Umar, waliitwa kuji-unga nayo.

(The Life of Muhammad, London, 1877)

Muhammad Husein Haykal

Waislamu hawakukaa kwa muda mrefu hapo Madina kufuatia kurudi kwao kutoka kwenye Hija ya Muago huko Makka. Mtume (s.a.w.) aliamuru mara moja ukusanya-ji wa jeshi kubwa na akaliamrisha kwenda al-Sham. Alituma pamoja na jeshi hilo idadi ya wazee wa Kiislam, wale Muhajirina wa mwanzo, miongoni mwao ambamo Abu Bakr na Umar walikuwemo. Alitoa uongozi wa jeshi hilo kwa Usamah ibn Ziyad ibn Haritha,

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Mtume (s.a.w.) alilitaka jeshi hilo kuondoka Madina mara moja. Lakini ni ajabu kwamba jeshi hilo halikuonyesha shauku ya kumuitika yeye. Badala ya utii, Mtume (s.a.w.) aliku-tana na upinzani - kutoka kwa baadhi ya maswahaba wake! Tokea wakati huo na kuende-lea, Mtume (s.a.w.) ilimbidi apambane na matatizo mawili; moja lilikuwa ni kuvuka katika maradhi yake na jingine ni kushinda ule upinzani wa jeshi lake. Zile siku chache za mwisho za maisha yake hapa duniani zilitawaliwa na pambano hili lenye ncha-mbili.

Wale watu wakubwa wa Ki-Quraishi walichukia sana kule kunyanyuliwa kwa mvulana wa miaka 18 juu yao wote, na kwamba pia, mtoto, sio wa nasaba bora ya Quraishi, bali wa mtu aliyekuwa mtumwa kabla! Kwa hiyo, badala ya kuripoti kwake kikazi, wengi miongoni mwao wakaanza kutoroka na kuchelewesha muda kwa makusudi. Wengine miongoni mwao walikuwa hawakuridhika kabisa na uchaguzi wa Usamah kama jenerali wao kiasi kwamba walionyesha waziwazi kutoridhika kwao.

R.V.C. Bodley

...Wakongwe hawakulipenda lile wazo la kuwashambulia wale Warumi ambao walikuwa bado wanaogofya na mvulana, ambaye alikuwa na uzoefu mdogo wa kivi-ta, kama kiongozi wao. Muhammad alikuwa, hata hivyo, hashitushwi na malalamiko hayo. Alikuwa anaanzisha kigezo, kilichotazamwa tangu hapo miongoni mwa

269

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Waislamu, kwamba umri na hadhi katika jamii hakusababishi kufanya majenerali wazuri. Alikuwa akijenga ndani yao ujumbe wa demokrasia ambao walikuwa wau-peleke duniani kote. Bila ya kujadili ule uteuzi alimuita Usamah Msikitini na kumk-abidhi bendera ya Uislamu pamoja na kumnasihi namna ya kuiletea heshima.

(The Messenger, New York. 1946)

Kuteuliwa kwa Usamah kama jenerali hakukuwa, hata hivyo, ndio sababu pekee ya kwa nini baadhi ya maswahaba hawakupenda kwenda Syria. Kulikuwa na baadhi ya sababu nyingine pia za kwa nini waliamini ilikuwa ni muhimu sana kwao kubakia Madina, bila kutilia maanani amri za Mtume wa Allah (s.a.w.) Usamah alimuuliza Mtume (s.a.w.) kama haingekuwa bora kuahirisha ule uvamizi wa Syria mpaka atakapopona homa yake. Lakini Mtume (s.a.w.) alisema: "La. Nakutaka wewe uondoke muda huu huu."

Usamah alikwenda kwenye kambi yake huko Jurf lakini wachache wa maswahaba waliku-ja kuripoti kwa ajili ya kazi. Walijua kwamba ugonjwa wa Mtume (s.a.w.) umeleta "wasi-wasi" juu ya Umma (jamii), na waliona kwamba ni "hatari" kuondoka Madina kwa wakati kama huu ingawa waliona ni "salama" kudharau amri zake. Waliweka ile kanuni ya dha-habu ya "Usalama Kwanza" mbele ya amri za Mtume wa Allah (s.a.w.)

Mtume (s.a.w.) alikuwa na homa na maumivu makali ya kichwa lakini alimudu kwenda Msikitini, na kuhutubia ule mkusanyiko pale ambao ulijumuisha wengi wa waliochelewa nyuma, hivi:

"Enyi Waarabu! Mmekuwa wanyonge kwa sababu nimemteua Usamah kama jenerali wenu, na mnaleta maswali kama anazo sifa za kuwaongozeni ninyi kwenye vita. Ninajua ninyi ni watu wale wale mlioleta swali hili hili kuhusu baba yake. Wallahi, Usamah ana sifa za kuwa jenerali wenu kama vile baba yake alivyokuwa na sifa za kuwa jenerali. Sasa tiini amri zake na muende."

Betty Kelen

Mara baada ya ile Hijja ya Muago, pamoja na nia yake kuongezeka kasi zaidi kuelekea kaskazini kana kwamba katika kumfikisha mwisho, Muhammad aliandaa jeshi jipya la kupigana ugenini kwenda Syria, akimuweka mtoto wa Zayd, Usamah, kuliongoza - dhidi ya ushauri wa baadhi ya majenerali wake, kwa vile Usamah alikuwa na miaka ishirini tu. Muhammad aliwaambia kwa ukali, 'Mnamkemea yeye kama mlivyomkemea baba yake, lakini yeye anastahili zaidi uongozi kama baba yake alivyokuwa.'

Hakutaka tena kupoteza muda kutetea utendaji wake. Aliiweka bendera yake kwenye mikono ya Usamah na akamtuma kwenda kwenye uwanja wa kukusanyikia, lakini

270

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mabishano yale yaliendelea kumchoma moyo hata hivyo.

(Muhammad, Messenger of God)

Wakati wowote Mtume (s.a.w.) alipopata nafuu kidogo kutokana na homa na kichwa chake, aliwauliza wale waliokuwepo kama jeshi la Usamah limeondoka kwenda Syria. Aliendelea kuwahimiza, 'Pelekeni jeshi la Usamah mara moja.'

Wapiganaji wa kawaida wa jeshi hilo waliitika amri za Mtume, na wakapiga ripoti kikazi kwa mkuu wa kikosi huko Jurflakini wengi wa maswahaba wakubwa hawakufanya hivyo. Wengine miongoni mwao walisita humo mjini; wengine, chini ya msukumo wa Mtume (s.a.w.) kwa muda wote, walikwenda Jurf lakini wakarudi. Walibaki wakisafiri kati ya kambi na mjini. Wengine wao walikuja mjini kuchukua vitu ambavyo vilikuwa vinakosekana kwenye zana, na wengine walitaka kusikia habari. Bado wengine walirudi "kujulia hali ya afya ya Mtume." Walikuwepo pia wale maswahaba ambao hawakwenda Jurf kabisa. Walibakia pale mjini kwa sababu ya "mapenzi" yao kwa Mtume (s.a.w.) kwa vile walikuwa hawakuwa na ule "moyo" wa kumuacha yeye katika wakati ambapo anaumwa vibaya sana.

Lakini haya malalamiko ya "mapenzi" na "wasiwasi" kwa ajili ya ustawi wake hayakumpendeza Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Kigezo cha kuthibitisha mapenzi yao kwake kilikuwa ni utii wao kwenye amri zake. Aliwaamuru kuondoka kwenda Syria lakini hawakwenda. Walimuasi yeye wakati wa siku zake za mwisho wa maisha yake.

Betty Kelen

Maradhi yake Mtume (s.a.w.) yalizidi, lakini alijaribu kuyatupilia mbali kwa ajili ya Usama, kwani vile habari za ugonjwa wa Muhammad zilivyoenea kote, huyu kijana alikuwa akipata muda mgumu kukusanya vikosi vyake. Watu wengine waliokuwa wamejiunga naye, walikuwa wakirejea Madina, na kwa uhakika hakuna waliokuwa wanabakia.

(Muhammad, Messenger of God)

Mwishowe, lisilopingika likatokea. Muhammad, Mtume (s.a.w.) wa mwisho wa Allah (s.a.w.) katika dunia hii, akafa. Juhudi yake ya kuwatoa maswahaba zake nje ya Madina, zikafika mwisho, pamoja na muonekano wa "ushindi" kwa maswahaba. Hawakupiga ripoti kikazi kwa Usamah na jeshi halikwenda kwenye pambano - wakati wa maisha yake!

Kwa Waislamu, kila amri ya Muhammad ni amri ya Allah (s.w.t.) Mwenyewe kwa sababu yeye ndiye Mfasiri wa amri hizo, wa Mapenzi na Makusudio ya Allah (s.w.t.) Uasi kwa Muhammad ni uasi kwa Allah (s.w.t.) Mwenyewe. Kwa hiyo, wale watu waliomuasi yeye

271

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

(Muhammad) walipata ghadhabu za Allah (s.w.t.)

Vita vya Muutah vilipiganwa mnamo mwaka 629 A.D., na kuishia kwenye kushindwa kwa Waislamu. Mtume (s.a.w.) alitaka kufuta lile doa la kushindwa. Lakini haikuwa mpaka miaka mitatu baadae - mnamo mwaka 632 A.D. - ambapo alimuamuru Usamah kuvamia mpaka wa Syria katika ufidiaji wa yale maafa ya Muutah.

Upangiliaji wa muda wa msafara wa Usamah unazua msongamano wa maswali. Kwa nini Mtume (s.a.w.) asitume msafara wake wa kuadhibu huko Syria katika muda wowote wakati ile miaka mitatu ya kati? Kwa nini alichagua muda kabla tu ya kifo chake mwenyewe kuutuma msafara huo? Kwa nini, ghafla tu, ilikuja kuwa muhimu sana juu yake kuwatuma maswahaba wake na wapiganaji nje ya Madina?

Kama ilivyoonyeshwa kabla, baada ya ile Hijja ya Muago, afya ya Mtume (s.a.w.) ilianza kuonyesha dalili za mfadhaiko. Miezi miwili baadae, hali yake ilizidi kuwa mbaya zaidi, na siku kadhaa baadae, akafa.

Pia, kama ilivyoonyeshwa kabla, Mtume (s.a.w.) aliwaambia Waislamu katika zaidi ya tukio moja kwamba hakuwa na muda mrefu zaidi wa kuishi katika dunia hii. Tabari, yule mwanahistoria, amemnukuu Abdullah ibn Abbas akisema: (kama miezi miwili baada ya ile Hija ya Muago) "Mtume wa Allah (s.w.t.) alituambia kwamba huenda angekufa ndani ya muda wa mwezi mmoja." (Ta 'rikh Tabari, juz.2, uk. 435).

Pia imesimuliwa kwamba usiku mmoja Mtume (s.a.w.) alikwenda kwenye uwanja wa makaburi ya Al-Baqi, akifuatana na mtu wa nyumbani. Baada ya kuwaombea wafu, alimwambia huyo mwenzie: "Wao (wale wafu) wako kwenye hali nzuri kuliko wale ambao wako hai. Hivi punde maovu mapya mengi sana yatatokea, na kila moja litakuwa lenye kuogofya na kutisha sana kuliko lile lililolitangulia."

Kwa upande mmoja Mtume wa Allah (s.a.w.) alikuwa akitabiri kifo chake mwenyewe, na alikuwa pia akitabiri kutokea kwa maovu mapya na kuzuka kwa vurugu mpya; na kwa upande mwingine akiwashawishi Masahaba zake kuondoka Madina na kwenda Syria!

Kuzingatia kukaribia kwa kifo chake yeye mwenyewe, ni lipi la muhimu sana kwa Mtume (s.a.w.) kufanya: kutafuta kulipiza kisasi kwa ajili ya kifo cha rafiki yake ambaye aliuawa miaka mitatu iliyopita kwenye mpaka wa mbali au kulinda Nchi ya Madina na umma wa Kiislam kutokana na hatari ambazo, alisema, zilikuwa zijitokeze karibuni?

Jibu la wazi kwa swali hili ni kwamba kama kisasi cha kifo cha Zayd kingeweza kusubiri kwa miaka mitatu, kingeweza kusubiri zaidi kidogo, na kwamba usalama wa Nchi na ule wa umma, ulikuwa ni wa muhimu zaidi sana kuliko kitu chochote kingine. Kwa hiyo,

272

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mtume (s.a.w.) alipashwa kulipanga jeshi hilo ndani ya, na kuizunguka Madina, badala ya kulituma nje ya nchi.

Lakini inaonekana kwamba Mtume (s.a.w.) mwenyewe hakuweza kukubaliana na tathmi-ni hiyo. Hakukiona chochote chenye umuhimu zaidi kuliko kutuma maswahaba zake kwenda Syria nje ya Arabia yenyewe. Alipogundua kwamba wanapuuza amri zake, akawalaani. Shahristani, yule mwanahistoria, ameandika katika kitabu chake, Kitab al-Milal wan-Nihal (uk.8): "Mtume wa Allah (s.a.w.) alisema: 'Jeshi la Usama lazima lion-doke mara moja. Allah (s.w.t.) awalaani wale watu ambao hawaendi pamoja naye.'"

Ilikuwa ni mara yake ya kwanza katika uhai wake ambapo Muhammad Mustafa, Mtume (s.a.w.) wa Rehma na aliye Rehma kwa ulimwengu wote, alipomlaani mtu yoyote. Kabla ya hili, alikuwa hajawahi kamwe kumlaani mtu yoyote - sio hata wale maadui zake wenye msimamo mkali kabisa kama Abu Jahl na Abu Sufyan. Hakuwalaani watu wa Taif pale walipompiga mawe na kumfukuza nje ya mji wao. Pia, huko nyuma, kama mtu yeyote alikuwa hawezi kwenda vitani, hakumlazimisha kwenda, na alimwacha abakie nyumbani. Lakini katika suala la jeshi la Usamah, hakutaka kusikia sababu zozote au visingizio kuto-ka kwa mtu yeyote kwa kushindwa kwake kwenda na jeshi hilo. Amri yake kwa maswahaba zake ilikuwa ni isiyobadilika, isiyoyumba na yenye mkazo.

Katika dakika za mwisho za maisha yake, mtu hupenda kwamba ndugu zake wote na marafiki wawe karibu naye. Anapenda na kutegemea kwamba baada ya kifo chake, watashiriki katika mazishi yake; watamuombea, na watailiwaza familia yake. Lakini kinyume na kanuni zote za mwenendo huu katika wakati kama huu, Muhammad Mustafa alikuwa akifanya kila aliloliweza kuwaondoa maswahaba na marafiki zake kutoka Madina. Hakumtaka yeyote kati yao kubaki pamoja naye. Waislamu wa Sunni wanadai kwamba Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Uislamu, hakuchagua mrithi wake mwenyewe, na alili-acha suala la kuchagua kiongozi wa Umma kwa maswahaba zake. Kama wako sahihi katika madai yao, basi ile amri ya Mtume (s.a.w.) kwa maswahaba kuondoka Madina na kwenda Syria, kunaleta tatizo lenye ugumu sana kwao.

Ni dhahiri kwamba Mtume (s.a.w.) alikuwa afariki. Yeye mwenyewe amesema hivyo mara kwa mara. Muda ulikuwa umewadia, kwa hiyo, kwa maswahaba zake kukusanya vichwa vyao pamoja na kutafuta sehemu mpya ya mamlaka. Lakini Mtume (s.a.w.) alikuwa ana-sisitiza kwamba waende mamia ya maili mbali na yeye - na kutoka Madina. Kama aliwata-ka wao kuchagua au kuteua mrithi wake kupitia "ushauri wao wa makubaliano," angeweza yeye kuwaamuru wao kuondoka Madina? Tena, yeye mwenyewe aliuonya umma kwamba ulikuwa unatishiwa na hatari mpya kubwa kubwa. Asingeweza kwa hiyo, kuwataka maswahaba zake kubakia Madina, na kuukinga umma kutokana na hatari hizo kubwa? Hata hivyo, ni nani angeukinga umma wa Muhammad kutokana na hatari hizo kama sio maswahaba zake wenyewe?

273

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kwa vile Mtume (s.a.w.) alijua kwamba atakufa, asingetayarisha kamwe na kuandaa jeshi la Usamah. Badala yake, angependekeza kwa maswahaba zake kwamba wanapashwa kutengeneza mkakati, kwa ushauri wa makubaliano, kuzuia yale maovu mapya na hatari ambazo tayari zimetishia kwenye upeo wa macho ya Madina.

Lakini Muhammad Mustafa hakufanya hivi. Yeye, kwa kweli, alifanya kinyume chake tu. Aliwaamuru maswahaba zake kutoka nje ya Madina, na kamwe hajawahi kuwa na mkato kwao hivyo kama alivyokuwa safari hii. Je, inaweza kuwa na maana kwamba walikuwa ni maswahaba wenyewe ambao aliwaona kama watunzi wa maovu na hatari mpya zinazo-tishia umma wake?

Kwa kweli, usalama na wokovu wa Waislamu ulilala kwenye utii wao usio na kuuliza kwenye amri za Mtume (s.a.w.) wao. Pale walipomuasi yeye, waliufungua mlango wa maovu yote, vurugu na hatari.

Katika mazingira yalimotokea matukio ya wakati huo, inaonekana kwamba Muhammad Mustafa alikuwa na sababu muhimu sana za kuchelewesha jeshi la Usamah mpaka dakika za mwisho. Alikwisha kutangaza wazi, kwa usahihi kabisa na kwa kurudia rudia kwamba Ali ibn Abi Talib atakujakuwa mrithi wake. Lakini alikuwa pia anatambua kuwepo kwa hisia za kichinichini za upinzani wa maswahaba zake kwa Ali.

Mtume (s.a.w.) pia alijua kwamba kile kikundi kilichokuwa kinampinga Ali, kilikuwa na nguvu sana na chenye hadhari sana. Kwa hiyo, aliwaza kwamba kama wakati wa kifo chake, watu wa kikundi hiki kinachozungumziwa, watakuwa nje ya Madina, yeye (Ali) atamrithi bila ya kadhia yoyote. Lengo hasa la Mtume, katika kuandaa jeshi la Usamah, kwa hiyo, lilikuwa ni kuwatuma wale watu mbali kutoka Madina, ambao wangempa Ali changamoto katika kupanda kwake kwenye kiti cha ukhalifa. Alitegemea kwamba katika kutokuwepo kwa maswahaba hapo Madina, Ali angekipanda kiti, na watakaporudi, wangemkuta yeye imara kabisa katika usimamizi wa serikali.

Jeshi la Usamah, kwa hiyo, lilikuwa ni utangulizi wa kuhamisha madaraka kutoka kwa Muhammad kwenda kwa mrithi wake, Ali ibn Abi Talib.

Lakini maswahaba hawakuwa waondoke Madina. Kule kubakia Madina, walimpinga Mtume (s.a.w.) mwenyewe, na pia walizipuuza laana zake. Walijua kwamba kama Ali mara atakapopanda kwenye hicho kiti, basi wao (maswahaba) watakuwa wamefungiwa nje ya "makasri ya madaraka" daima dumu, na walikuwa, kwa sababu hii, wazuie kupanda kwa Ali kwenye kiti hicho kwa gharama zote. Hawakuwa na nia ya kufungiwa nje ya "makasri ya madaraka"

Mambo yafuatayo yawekwe akilini na msomaji kwa ajili ya kutathmini upya kwa tukio

274

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwenye mfululizo wa matukio ya jeshi la Usamah:

1. Vita vya Muutah vilipiganwa mnamo A.D.629. Wakati wa kiangazi cha mwaka A.D.632, mpaka wa Syria ulikuwa tulivu na shwari, na hapakuwa na tishio lolote, la kweli au la kuhisiwa, la uvamizi wa Madina kutokea kaskazini. Kwa kweli, hakukuwa hata na tetesi la shambulizi juu ya Madina au Hijazi kutoka kwa yeyote yule. Na bado, Muhammad Mustafa alikuwa akionyesha shauku kubwa ya kupeleka jeshi lake huko Syria.

2.   Jeshi la Usamah liliandaliwa, inavyoonekana, ili kurudisha hamasa ya Waislamu baada ya kushindwa kwao katika vita vya Muutah, na kuwaadhibu wale watu waliomuua baba yake, Zayd bin Haritha. Mtume (s.a.w.) alimtwisha Usamah kazi ya kulipiza kisasi kutoka kwa wauaji wa baba yake. Sasa Ja'afar bin Abi Talib, Shahidi mwenye Mbawa (at-Tair) wa Uislamu, na kaka mkubwa wa Ali, naye pia aliuawa kwenye vita hivyo hivyo. Lakini Mtume (s.a.w.) hakumtuma Ali au mtu mwingine yoyote wa ukoo wa Bani Hashim pamoja na jeshi hilo. Aliwabakisha wao wote pamo-ja naye hapo Madina.

3.   Mbali na maradhi yake makali, Mtume (s.a.w.) alikuwa akilihimiza jeshi hilo kwenda Syria. Yeye kwa hasira aliutupilia mbali ule wasiwasi uliotangazwa wa baadhi ya Masahaba zake juu ya hali yake, na akawaamuru kwenda pamoja na Usamah mara moja.

4.   Usamah bin Zayd bin Haritha alikuwa ndio mkuu wa jeshi wa wale maswahaba wa Mtume (s.a.w.) ambao walikuwa wazee wa kutosha kuwa babu zake kama vile Abu Bakr, Umar, Uthman, Abu Ubaidah bin al-Jarrah, Abdur Rahman bin Auf, na wengine wengi. Mtume (s.a.w.) kwa hiyo alikuwa akiikazia kanuni, kabla tu ya kifo chake, kwamba Waislamu wasiwe wa kumfikiria mtu kustahili uongozi kwa sababu tu alikuwa mtu mzima.

5.   Kama mtu mwenye sifa zinazostahili anakuwepo wa kuwa kiongozi, basi mtu asiye na sifa hizo asimuondoe mahali pake. Masahaba walitoa vipingamizi kwenye uongozi wa Usamah juu ya msingi huu. Mtume (s.a.w.) alikubali kwamba yule tu mwenye sifa zinazostahili ndiye anayepaswa kupewa madaraka makubwa. Lakini alisisitiza kwamba Usamah alikuwa anastahili zaidi kuliko wale watu wote walioamriwa kuwa chini yake, licha ya ujana wake mdogo.

6.   Waislamu wa Sunni wanasema kwamba Mtume (s.a.w.) "alishauriana" na maswahaba zake, na hili liliifanya serikali yake kuwa ya "kidemokrasia." Ni kweli kwamba "alishauriana" nao mara chache katika masuala madogo lakini yeye mwenyewe ali-fanya maamuzi bila kuwahusisha wao. Pale Hudaybiyah, Umar bin al-Khattab alion-

275

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

goza upinzani kwake alipokuwa akijadili masharti ya amani pamoja na wapagani. Alipuuza upinzani wake, akaendelea na kusaini mkataba nao. Baadae, mafaqihi wa Sunni walieleza kwamba Mtume (s.a.w.) alipuuza upingaji wa Umar kwa sababu alikuwa (yeye Mtume) akitenda chini ya amri ya Mbinguni. Wako sahihi. Lakini kuteuliwa kwa Usamah kama mkuu wa jeshi hakukuwa na uhusiano wowote na amri za Mbinguni na Mtume (s.a.w.) alikuwa huru kutangua amri zake wakati anapokabili-wa na upinzani kutoka kwa maswahaba. Bali alikataa hata kuzungumza nao juu ya suala hilo seuze "kutaka ushauri" wao juu ya suala hilo.

7.  Amri za Mtume (s.a.w.) kwa maswahaba zake kuwa jeshini chini ya Usamah, na kuon-doka Madina kwenda Syria, zilikuwa wazi sana. Lakini hawakuondoka Madina, na akafa. Wao, kwa hiyo, waliijua dhamiri yao ambayo ilikuwa ni kuwepo kimwili hasa pale Madina wakati wa kifo chake.

8.   Masahaba wale wa Mtume (s.a.w.) ambao aliwaamuru kupiga ripoti kikazi kwa Usamah - mkuu wao - walikuwa wakimdharau wakati alikuwa bado yu hai. Ikiwa waliweza kutojali amri zake na matakwa yake katika uhai wake, wanaweza kama kawaida, kutojali amri na matakwa yake katika suala la mrithi wake baada ya kifo chake. Waliweka tamaa na maslahi yao binafsi mbele ya amri na matakwa ya Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) aliyebarikiwa.

276

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abu Bakr kama kiongozi katika Swala

Wanahistoria wa Sunni wanadai kwamba wakati Muhammad Mustafa alipokuwa hawezi kuhudhuria kwenye Swala za jamaa kwa sababu ya maradhi yake, alimuamuru Abu Bakr kuongoza Swala za jamaa, na wanalitanguliza hili kama "ushahidi" kwamba alimtaka yeye Abu Bakr kuwa ndio mrithi wake.

Kuna matoleo mbalimbali ya Hadith hii yaliyopo hadi sasa. Kwa mujibu wa mojawapo, Bilali alikuja kumuuliza Mtume (s.a.w.) kama ataongoza Swala, naye akasema: "La, mwambie Abu Bakr aongoze Swala."

Kuna toleo la pili ambamo wakati wa Swala, Mtume (s.a.w.) alimuuliza mtu mmoja, Abdullah bin Zama'a alikokuwa Abu Bakr. Ibn Zama'a alitoka nje kwenda kumwita Abu Bakr lakini hakumpata. Bali alimpata Umar, na akamwambia aongoze Swala. Lakini pale Umar alipotamka takbir (Allah-u-Akbar), Mtume (s.a.w.) alimsikia, naye akasema: "Hapana! Hapana! Allah (s.w.t.) na waumini wanakataa hiyo. Mwambie Abu Bakr aongoze Swala hiyo."

Kufuatana na Hadith ya tatu, Mtume (s.a.w.) aliwauliza wale waliokuwa karibu naye kama wakati wa Swala ulikuwa umekwishafika. Wakasema umefika, ndipo akawataka wamwambie Abu Bakr aongoze hiyo Swala ya jamaa. Lakini mkewe, Aisha, akasema kwamba baba yake alikuwa mtu mwenye huruma sana, na kama ataona nafasi yake (Mtume) pale Msikitini iko wazi, yeye (Abu Bakr) atalia sana, na hakuna atakayeweza kusikia sauti yake. Lakini Mtume (s.a.w.) alisisitiza kwamba Abu Bakr asimame kama kiongozi wa Swala.

Zipo Hadith nyingine pia kama hizi katika vitabu vya historia na maudhui yao zote ni kwamba Abu Bakr aliongoza jamaa katika Swala wakati wa siku za mwisho za Mtume (s.a.w.) duniani hapa.

Muhammad ibn Ishaq

Ibn Shihab alisema, Abdullah ibn Abu Bakr bin Abdur Rahman bin al-Harith bin Hisham aliniambia kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abdullah bin Zama'a bin al-Aswad bin al-Muttalib bin Asad kwamba wakati Mtume (s.a.w.) alipokuwa mgonjwa sana na mimi pamoja na idadi fulani ya Waislamu tulikuwa pamoja naye, Bilali alimwita kwa ajili ya Sala, na akatuambia kuwa tumuamuru mtu maarufu aongoze hiyo Swala. Hivyo nilitoka nje na hapo alikuwepo Umar na watu, Abu Bakr hakuwe-

277

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

po pale. Nilimwambia Umar asimame na kuongoza Swala, alifanya hivyo, na alipose-ma Allah-u-Akbar, Mtume (s.a.w.) akasikia sauti yake, kwani alikuwa na sauti yenye nguvu sana, na akauliza alikokuwa Abu Bakr, akisema mara mbili zaidi, "Allah (s.w.t.) na Waislamu wanakataa hiyo," Kwa hiyo nikatumwa kwa Abu Bakr na aliku-ja baada ya Umar amekwisha maliza Swala ile naye akaongoza. Umar akaniuliza ni nini nilichokifanya hasa, akisema, "Pale uliponiambia niongoze Swala, nilidhani kwamba Mtume (s.a.w.) amekupa amri kwa jambo hilo; lakini kwa hilo nisingeweza kufanya hivyo." Nilijibu kwamba hakunituma kufanya hivyo, bali pale nilipokuwa sikuweza kumpata Abu Bakr nilidhani kwamba yeye (Umar) alikuwa anastahili zaidi ya wale waliokuwepo kuongoza Swala.

(The Life of the Messenger of God)

Yaliyopita ni maelezo ya mwanzoni kabisa yaliyopo hadi sasa ya Hadith kwamba Abu Bakr aliongoza Swala. Msimulizi wake alikuwa ni Abdullah bin Zama'a. Yeye mwenyewe anasema kwamba Mtume (s.a.w.) alimtuma yeye kumwambia mtu maarufu ambayo ina maana mtu yoyote, aongoze Swala, na hakumtaja makhsusi Abu Bakr. Hata baadae, wakati Mtume (s.a.w.) alipomkataza Umar kuongoza Swala, hakumuamuru Abu Bakr kuchukua nafasi yake. Aliuliza tu alikokuwa Abu Bakr.

Abdullah bin Zama'a alidhani kwamba Umar alikuwa ndiye "mwenye kustahili zaidi" kuongoza Swala lakini Mtume wa Allah (s.a.w.) hakukubaliana naye.

Sir William Muir

Imesimuliwa kwamba katika tukio moja Abu Bakr alitokea kutokuwepo wakati adhana ya Swala ilipopigwa na Bilali, na kwamba Umar akiwa amepokea, kama alivyoamini kimakosa, amri ya Muhammad kuongoza katika nafasi yake, alisimama pale Msikitini, na katika sauti yake nzito akaanzisha Takbir, "Mungu ni Mkubwa!" kwa matayarisho ya Swala. Muhammad akisikia hili kwa bahati tu kutoka nyumbani kwake, alikemea kwa kutumia nguvu, "Hapana! Hapana! Allah (s.w.t.) na kundi zima la waumini wanakataza hilo! Si mwingine bali Abu Bakr! Asiongoze Swala mtu mwingine bali yeye tu."

(The Life of Muhammad, London. 1877)

Kama ilivyoelezwa hapo juu, kwa mujibu wa wanahistoria wa Sunni, lengo la Mtume (s.a.w.) katika kumuamuru Abu Bakr kuongoza Swala lilikuwa ni "kumtangaza" yeye kama mrithi wake.

Inawezekana kabisa kwamba Abu Bakr aliongoza Waislamu katika Swala katika wakati wa uhai wa Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Ambacho, hata hivyo, kisichoelewaka ni kama alifanya hivyo kwa amri ya Mtume, au, angalau kwa idhini yake ya kimyakimya. Dai la kwamba Abu Bakr aliongoza Swala kwa amri ya Mtume (s.a.w.) linaleta maswali kwa

278

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

sababu alikuwa afisa mdogo katika jeshi la Usamah, na Mtume (s.a.w.) alikuwa amemua-muru yeye kuondoka Madina na kupiga ripoti kwa Mkuu wake wa Kikosi huko Jurf ambavyo, inavyoonekana, kamwe hakufanya hivyo.

Hata kama ikichukuliwa kwamba Mtume (s.a.w.) alimuamuru Abu Bakr kusimama kama Imamu (kiongozi wa Swala), bado haieleweki kama ni vipi ilikuwa ni "kuidhinishwa" kwa ugombea wake wa urithi. Hata hivyo, Abu Bakr mwenyewe, Umar bin al-Khattab, na Abu Ubaidah ibn al-Jarrah, wote watatu walikwisha tumika chini ya Amr bin Al-As katika vita vya Dhat es-Salasil, na waliswali Swala zao nyuma yake kwa majuma mengi tu. Amr bin Al-Aas aliliweka wazi kwao wote watatu kwamba yeye alikuwa ndiye bosi wao sio tu katika jeshi bali pia kama kiongozi katika ibada za kidini.

Kama ilivyokwisha kuelezwa, Waislamu wa Sunni wanashikilia kwamba Mtume (s.a.w.) alimchagua Abu Bakr kuongoza Swala ya jamaa kabla tu ya kufa kwake kwa sababu alim-taka yeye awe ndiye khalifa wake.

Ibn Hajar Makki, mwanahistoria wa Sunni, anasema katika kitabu chake, Tathiir al-Janan (uk.40):

"Abu Bakr aliwaongoza Waislamu katika Swala (kwa amri ya Mtume). Hii, kwa hiyo, ni ijma (makubaliano) ya wanazuoni wote kwamba ukhalifa wake ulikuwa kwa agizo la Mtume."

Lakini Masunni haohao pia wanalichukulia wazo la kwamba kuwaongoza Waislamu wengine kwenye Swala hakutunukii heshima yoyote juu ya muongozaji mwenyewe, na kwamba sio lazima kwa mtu kuwa na "sifa stahilivu" kusimama kama Imamu (kiongozi wa Swala). Kwa kuhusiana na hili, wananukuu "Hadith" ifuatayo ya Mtume wa Uislamu (s.a.w.) iliyosimuliwa na Abu Hurayra:

"Swala ni wajibu wa lazima juu yenu, na unaweza kuiswali nyuma ya mwislamu yoyote hata kama ni fasiq (hata kama anatenda madhambi makubwa)."

Kwa mujibu wa "Hadith" hii mtu fasiq (mtenda madhambi) anastahili vilevile kuwa Imam wa Swala kama mtakatifu; katika suala la kusimama kama Imam, mwenye dhambi na mtakatifu wanakuwa na usawa!

John Alden Williams

Na kuwasikiliza na kuwatii Maimam na Ma-Amirul-Mu'minin (ni lazima) - Yeyote yule aliyeupata Ukhalifa, ama awe mchaji au fisadi, ama watu walikubaliana naye na wanamfurahia au kama aliwashambulia kwa upanga mpaka akawa Khalifa na akait-

279

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wa "Amirul-Mu'minin." Kwenda kwenye vita tukufu (jihad) kunafaa pamoja na mchaji au kamanda fisadi mpaka siku ya Qiyamah; mtu hamuachi yeye. Ugawaji wa ngawira za vita na kutoa adhabu zilizoagizwa na Sheria ni kwa Maimam. Haiwi kwa mtu yeyote kuwashutumu au kushindana nao. Kukabidhi pesa za Zaka kwao (kwa ajili ya ugawaji) inaruhusiwa na inafaa; yeyote anayewalipa wao atakuwa ametimiza wajibu wake iwe huyo Imam alikuwa mcha-mungu au fasiq. Swala ya mkusanyiko nyuma ya Imam na wale anaowaongoza ni halali na kamili; rakaa zote. Yeyote atakayezirudia ni mzushi, anayeitelekeza Hadith na kupinga Sunnah. Hakuna lazima kabisa katika Swala yake ya Ijumaa, kama haamini kuswali na Maimam, wawe wowote wale, wazuri au wabaya; iliyo Sunnah ni kuswali rakaa mbili nao na kulichukulia jambo hilo kuwa limekwisha. Katika hilo usiache shaka yoyote katika kifua chako.

(Some Essential Hanbali Doctrines from a Credal Statement in Themes of Islamic Civilization, p.31, 1971)

Kwa mujibu wa fatwa ya Hanbali iliyonukuliwa hapo juu, yeyote na kila mtu anaweza kuwaongoza Waislamu katika Swala. Abu Hurayra na Abu Sufyan wanazo sifa zinazostahili sana kuweza kuwa viongozi wa Swala kama Abu Bakr.

Dhana hii iliundwa na vizazi vya baadae vya Waislamu. Mtu mmoja ambaye hakuishiriki pamoja nao, alikuwa ni Muhammad Mustafa, Mfasiri wa Ujumbe wa Mwisho wa Allah kwa wanadamu. Alimuona Umar bin al-Khattab kuwa "hana sifa zinazostahili" kuongoza Waislamu kwenye Swala, na akamkataza kufanya hivyo.

Waislamu wa Shia wanaichukulia kama ilivyokuwa ni ya uongo, ile "Hadith" ambayo Abu Hurayra ameihusisha kwa Mtume wa Uislamu (s.a.w.) kwamba ni halali kuswali nyuma ya mtu yoyote, hata aliye fasiq. Wao wanasema kwamba Imam (kiongozi wa Swala) lazima awe:

Ni Mwislamu

Mwanaume

Mtu mzima

Mwenye akili timamu

Mkweli (Muadilifu)

Mjuzi Mtu mwenye heshima nzuri, yaani, mtu anayefahamika kuwa na tabia nzuri.

Hadithi ya kwamba Abu Bakr aliwaongoza Waislamu katika Swala katika uhai wa Mtume, ama ni ya kweli au ya uongo. Kama ni ya kweli, basi ina maana kwamba alitekeleza wajibu

280

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ambao kwa kulingana na Abu Hurayra na mafaqihi na wanachuoni wa Ki-Sunni, mtu yey-ote na kila mtu mwingine alikuwa na sifa zinazostahili kufanya, na haikumfanya yeye kuwa "maalum" kwa namna yoyote ile; kama ni ya uongo, basi ina maana kwamba hakuongoza mkutano wowote kabisa wa Sala wakati Mtume (s.a.w.) alipokuwa bado yu hai.

Lakini kama Hadith hii ni ya kweli, basi pia ina maana kwamba Swala yoyote inayoswali-wa nyuma ya Umar ibn al-Khattab, ni halali. Mtume (s.a.w.) alisema kwamba Allah (s.w.t.) Mwenyewe hakutaka Umar kusimama kama kiongozi wa Swala. Kung'ang'ania kwa Umar juu ya kuwaongoza Waislamu katika Swala, kabla au baada ya kifo cha Mtume, kusingeweza pengine kuzifanya Swala zile kuwa zisizokubalika zaidi kwa Allah (s.w.t.)!

281

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wosia Usioandikwa wa Mtume wa Allah (s.a.w.w)

Uislamu ulikuwa ndio sababu kamili ya kuwepo kwa Muhammad Mustafa, Mtume mtuku-fu wa Allah (s.a.w.w). Alitumwa duniani hapa kuja kueneza Uislamu. Ili kusambaza ujumbe wa Uislamu, ilimbidi kupambana dhidi ya vipingamizi vigumu lakini alivishinda. Aliufanya Uislamu uweze kuwepo kwa kutumia makafara makubwa ambayo aliyatoa kwa ajili yake. Mfumo wa Uislamu na utaratibu wa manufaa yake vilikuwa kwake ni kama bus-tani ambayo ameikuza kwa damu ya wapenzi wake mwenyewe.

Ni nini kinachoweza kuwa na mantiki zaidi kuliko kufikiria kwamba Muhammad angeta-ka kuchukua hatua ambazo zingeweza kuhakikisha usalama na uhai wa Uislamu kwa wakati wote? Ni nini kingekuwa cha kawaida zaidi kwake kuliko kutaka kwamba kuona Uislamu unakuwa haudhuriki? Yeye, kwa hiyo, alifikiria juu ya kulinda maslahi ya baadae ya Uislamu, kwa kadiri ilivyokuwa kwenye mamlaka yake kufanya hivyo, kwa kuandika mirathi na wosia wake.

Hivi mwislamu anaweza kufikiria kwamba Muhammad Mustafa angeweza kupuuza wajibu muhimu kama wa kuandika mirathi kwa ajili ya umma wake? Mirathi, wosia wa Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.w) wenye kueleza kwa uwazi, utaratibu na uamuzi wake wa mwisho, amri zake kuhusiana na uhamishaji wa mamlaka kwa mrithi wake, lilikuwa ni jambo la lazima kabisa la uimarishaji wa Uislamu. Kwa hiyo, kabla tu ya kifo chake, aliwaamuru wale maswahaba waliokuwa karibu yake kumletea kalamu, karatasi na wino ili aweze kuamuru hati kwa ajili ya umma ambayo itaulinda kutokana na kupotea, na itauzuia kutokana na kugawanyika.

Lilikuwa ni ombi la maana sana la mtu aliyekuwa kwenye kitanda chake cha mauti, na ambaye angeweza kufa wakati wo wote.

Lakini alikutana na ukaidi!

Lilikuwepo kundi la maswahaba wake ambalo halikumtaka yeye aandike wosia wake. Imam Bukhari anaandika katika juzuu ya 1 ya Sahih yake: Umar akasema, 'Mtume wa Allah (s.a.w.w) amezidiwa na maumivu. Hatuhitaji wosia wowote. Tayari tunacho Kitabu cha Allah (s.w.t.) na kinatutosha Kitabu cha Allah.' (uk.25)

Bukhari ameandika tukio hilo hilo katika Juz.11 ya Sahih yake katika maneno yafuatayo:

282

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Mtume wa Allah (s.w.t.) akasema: 'Nileteeni kipande cha karatasi. Nitawaandikieni kitu juu yake ambacho kitawazuieni kutokana na kupotea.' Lakini wale watu waliokuwepo pale, wakaanza kubishana miongoni mwao wenyewe. Baadhi yao wakasema kwamba Mtume wa Allah (s.w.t.) alikuwa anaweweseka." (uk. 121)

Hapa Bukhari amejaribu kuficha kutambulikana kwa Umar nyuma ya pazia la maneno baadhi yao.

Lakini Sheikh Shihab-ud-Din Khaffaji, mwanahistoria wa ki-Sunni, amekosa aibu katika suala hili, na anasema:

"Umar akasema: 'Mtume wa Allah anaropoka.'"

(Nasim-ur-Riyadh, Juz. 1V, uk. 278)

Kwa mwislamu kusingizia kwamba Mtume wa Mwisho wa Allah (s.a.w.w) na Adhimu sana alikuwa "anaweweseka" ilikuwa ni kauli ya uovu kabisa na ya kizembe. Inawezekana kweli kwamba Mletaji na Mfasiri wa Ujumbe wa Mwisho wa Allah (s.a.w.w) kwa wanadamu, angeweza kuwa "mzungumzaji wa kuweweseka?" Na tena, ni kipi kili-chokuwa hakina maana au bila mantiki au la kulaumika katika ombi lake la kumuacha aandike wosia wake?

Maoni ya Umar yasiyo na sababu yalisababisha mabishano miongoni mwa wale maswa-haba ambao walikuwepo pale chumbani kwa Mtume. Wachache kati yao walisema kwamba walipaswa kumtii Bwana wao, na kumletea kalamu, karatasi na wino. Lakini wale wengine ambao walikuwa wengi, walimuunga mkono Umar na wakamnyima vile vifaa vya kuandikia. Mabishano yakawa makali sana kiasi kwamba ilimbidi Mtume (s.a.w.) kuwaamuru watoke chumbani kwake, na wamuache peke yake.

Bukhari anaandika zaidi katika Sahih yake:

"Wakati Mtume (s.a.w.) maradhi yake yalipochukua hatua mbaya, alisema, 'Nileteeni karatasi ili niweze kuwaandikieni wosia ambao utakuzuieni kutokana na kupotea baada ya kifo changu.' Umar bin al-Khattab akasema, 'Hapana. Haya ni mazungum-zo yasiyokuwa na maana. Kitabu cha Allah (s.w.t.) kinatutosha' Mtu mwingine akasema: 'Ni lazima tulete karatasi,' mpaka kukawa na mabishano, na Mtume (s.a.w.) akasema: 'Ondokeni hapa.'"

Kumdharau Mtume wa Allah (s.a.w.w) kwa Umar kumekingamiza msafara wa Mtume (s.a.w.) kwenye makundi mawili. Ilikuwa dhahiri kutoka wakati huu kwamba utengano uli-inua kichwa chake katika umma wa Kiislamu.

283

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Yumkini ilikuwa mara ya mwisho ambapo Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.w) na Mtawala wa Waislamu, alieleza haja yoyote mbele ya maswahaba zake. Lakini walimdha-rau. Alishituka lakini pengine hakushangazwa na ukaidi wao. Haikuwa ni mara ya kwan-za kumfanyia ukaidi yeye. Jeshi la Usamah liliwafichua.

Sir William Muir

Wakati huu, akimtambua Umar, na watu wengine maarufu mle chumbani, yeye Muhammad alisema kwa sauti: 'Nileteeni hapa wino na karatasi, ili niweze kuwaandikieni maandishi yatakayokuzuieni msipotee daima.' Umar akasema, 'Anaweweseka huyo. Kwani Qur'an haitutoshi sisi?'

(The Life of Muhammad, London, 1877)

Muhammad Husein Haykal

Akiwa bado yuko kwenye mashambulizi makali ya homa, na amezungukwa na wageni, Muhammad aliomba kwamba aletewa kalamu na wino na karatasi. Alisema kwamba angetoa imla ya kitu kwa faida ya wafuasi wake, akiwahakikishia wao kwamba kama watashikamana nacho, hawatapotea kamwe. Baadhi ya watu waliokuwepo walifikiri kwamba kwa vile Mtume - Rehema na amani ziwe juu yake - alikuwa mgonjwa sana na kwa vile Waislamu tayari walikuwa wanayo Qur'an, hakuna maandishi zaidi yaliyokuwa na lazima. Imesimuliwa kwamba wazo hilo lilikuwa ni la Umar. Watu waliokuwepo pale wakahitilafiana miongoni mwao wenyewe, wengine wakitaka kuleta vifaa vya kuandikia na kuandika kile Mtume (s.a.w.) atakacho amuru, na wengine wakidhani kwamba maandishi yoyote ya ziada mbali na yale ya Kitabu cha Allah (s.w.t.) yatakuwa yamezidi kiasi. Muhammad akawaambia waondoke, akisema, 'Msigombane mbele yangu.' Ibn Abbas alihofia kwamba Muhammad anaweza kupoteza kitu muhimu kama hawakumletea vile vifaa vya kuandikia lakini Umar alisimama imara kwenye uamuzi wake ambao aliuege-meza juu ya maneno ya Allah (s.w.t.) Mwenyewe ndani ya Kitabu Chake: "Ndani ya Kitabu, Hatukuacha kitu chochote."

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Katika makala yenye kichwa cha Iqbal and Islamic Polity, iliyochapishwa katika toleo la mwezi wa April 1964 la gazeti la kila mwezi la Muslim News International, la Karachi, Pakistani, mwandishi, Jamilud-Din Ahmad anasema:

"...Swali linalozikabili nchi za Kiislamu ni, kama sheria ya Kiislamu ina uwezo wa mabadiliko - swali ambalo litahitaji juhudi kubwa za kisomi na lina uhakika wa kujibiwa kwa kukubali; alimradi ulimwengu wa Kiislamu ukabiliane nalo katika msi-mamo wa Umar - akili ya kwanza ya ukosoaji na huru katika Uislamu, ambaye, kati-

284

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ka dakika za mwisho za Mtume, alikuwa na moyo kuthubutu kutamka maneno haya ya ajabu: 'Kinatutosha Kitabu cha Allah (s.w.t.)'"

Mwandishi aliyetajwa hapo juu inavyoonekana anajivunia sana "moyo wa kijasiri" wa Umar.

Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.w) alikuwa kwenye kitanda cha mauti yake, na huen-da hakuwa na masaa mengi ya kuishi. Ilikuwa ni wakati huu ambapo Umar alichagua kuonyesha moyo wake wa kijasiri. Pale Hudaybiyya, Muhammad Mustafa alimtuma kupeleka ujumbe kwa Maquraishi huko Makka lakini alikataa kwenda kwa kutoa dharura kwamba kwa vile hakuna hata mtu mmoja katika mji ule wa kumlinda yeye, wangemuua. Pia wakati Mkataba wa Hudaybiyya ulipotiwa saini, Umar aliongozwa, na "mapenzi" yake juu ya Uislamu kumkaidi Mtume wa Allah (s.a.w.w) na sasa wakati Mtume (s.a.w.) alipokuwa anakufa, "mapenzi" yale yale yakajithibitisha kwa mara nyingine tena, na yakamlazimisha yeye kumzuia Mtume (s.a.w.) kuamuru maandishi yoyote ambayo "yangedhoofisha mamlaka ya Kitabu cha Allah (s.w.t.)!"

Kama Umar alichochewa kumkaidi Muhammad Mustafa kwa sababu hii, basi ina maana yeye Umar aliamini kwamba Muhammad alikuwa ayape changamoto mamlaka ya Qur'an. Lakini Umar alijuaje kwamba Muhammad angeyapa changamoto mamlaka ya Qur'an? Kama Mtume (s.a.w.) angekuwa ameamuru kuandikwa kwa wosia ule, maneno yake machache ya mwanzo yangeonyesha, bila ya shaka yoyote, kama alikuwa, kwa maneno ya Umar, "anaweweseka" na alikuwa "anaropoka"

Labda haikuingia akilini mwa Jamilud-Din Ahmad kwamba Umar alikuwa anapambanisha akili yake ya "ukosoaji na yenye kujitegemea" dhidi ya Qur'an Tukufu ambayo inasema: Imeagizwa, mmoja wenu anapofikiwa na mauti, Kama akiacha mali, afanye wosia kwa wazazi wake na jamaa zake, kwa namna nzuri inayopendeza. Ni wajibu haya kwa wacha-mungu. (Sura ya 2; Ay a ya 180)

Lakini inawezekana kwamba Umar alichochewa kutomtii Mtume (s.a.w.) sio kwa woga wake kwamba Mtume, katika dakika zake za mwisho za maisha yake, angetangua kazi aliyoifanya katika uhai wake, kwa kupuuza mamlaka ya Qur'an; bali kwa dhana yake kwamba yeye Mtume (s.a.w.) angeweka kwa maandishi kile alichokisema mapema kule Ghadir-Khum mbele ya mkusanyiko wa mahujaji, akimteua Ali ibn Abi Talib kama mrithi wake. Umar alikuwa amzuie bila kujali gharama. Wosia uliobeba muhuri na saini ya Mtume, unaomtaja Ali kama mkuu wa baadae wa Dola la Kiislam utakuwa ni hati ambayo itauweka ukhalifa mbali na wagombea wengine wote wa ukhalifa huo. Mtume (s.a.w.) alifahamu fika kuhusu nia za maswahaba wake wakuu kuhusiana na urithi wa Ali kama kiongozi mkuu wa utawala wa Kiislamu. Vile alivyoendelea kuwa mnyonge wa dhahiri, waliendelea kuonekana kuwa washupavu zaidi katika kumkaidi yeye. Jeshi la

285

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usamah bado lilikuwa limening'iniza moto. Katika kuchukia kabisa, Mtume (s.a.w.) aliomba laana ya Allah (s.w.t.) juu ya wale watu ambao hawakupiga ripoti kikazi kwa Usamah lakini hawakusogea. Na walikuwa hawakushituka kabisa wakati walipowaambia watoke nje ya chumba chake.

Mwislamu wa siku hizi anaweza kuona ni jambo la ajabu sana kwamba sahaba yeyote wa Mtume wa Uislamu anaweza kuhusisha amri zake na "kuweweseka." Lakini upo ulingan-isho wa ki-Qur'an kwa tabia kama hiyo. Inaonekana kwamba wale maswahaba wa Muhammad, Mtume wa Waarabu, waliosema kwamba alikuwa "anaweweseka," walikuwa na watangulizi wao wenyewe katika ndugu zake Yusuf, Mtume wa Bani-Israil. Ndugu zake Yusuf walisema kwamba Yakoub, baba yao ambaye pia alikuwa Mtume, alikuwa "anaweweseka." Walidhani kwamba wao ndio walikuwa "watanashati" ambapo yeye hakuwa. Qur'an imewanukuu kama ifuatavyo:

Usahihi-36.jpg

Pale waliposema: "Hakika Yusufu na nduguye wanapendwa sana na baba yetu kuliko sisi: Hali sisi ni kikundi chenye nguvu! Hakika baba yetu yumo katika upotofu wa dhahiri. (kich-wani mwake) Muueni Yusufu au mtupeni nchi ya mbali (isiyojulikana), Ili uso wa baba yenu ukueleekeeni ninyi. (na kutakuwa na muda wa kutosha) Na baada ya haya mtakuwa watu wema. (Sura ya 12; Aya ya 8 na 9)

Maoni ya Mtarjuma - (wa Kiingereza)

Wale ndugu kumi sio tu waliwaonea wivu na kuwachukia ndugu zao wadogo Yusufu na Bin-yamin (Benjamin). Walimdharau na kumfedhehesha baba yao kama mjinga asiye na akili - katika upungufu wake wa akili kutokana na uzee. Kwa kweli Yakoub alikuwa na busara ya kuona kwamba watoto wake wadogo na wasio na makosa wal-itaka ulinzi na kufahamu umashuhuri wa kiroho wa Yusufu. Lakini busara yake, kwao ilikuwa ni upumbavu au wenda wazimu au upunguani, kwa sababu iligusa mapenzi-binafsi yao, kama ukweli mara nyingi unavyofanya. Na walitegemea mabavu ya idadi yao - ndugu kumi vibonge dhidi ya mzee Yakoub, kijana Yusufu, na mtoto Bin-yamin.

(A. Yusufu Ali)

286

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kuelezea mstari wa mwisho wa Aya ya pili, iliyonukuliwa hapo juu, mfasiri anaendelea kusema kwamba:

Wao (ndugu zake Yusufu) wanasema kwa kejeli, "Kwanza tumuondoe Yusufu. Itakuwa ni muda wa kutosha kisha tujifanye kuwa 'wema' kama yeye, au tutubie uovu wetu baada ya kuwa tumepata manufaa yake yote katika vitu vya kimaada."

Hapa mwanafunzi wa historia anaweza akauliza swali: Kwa nini Muhammad asiamuru kuandikwa wosia wake baadae, baada ya kushindwa kwake kwa awali; kwa kweli, zilikuwepo nyakati ambapo maswahaba walikusanyika tena kumuona yeye, na angeweza kuwasomea wosia wake wakati huo.

Tunaweza kuchukulia kwamba Muhammad angeweza kuamuru kuandikwa wosia wake katika muda wa baadae lakini ni nini kilichokuwepo cha kumzuia Umar na wafuasi wake kudai kwamba uliamriwa katika hali ya "kuweweseka" na ulikuwa "wa kipuuzi," na ulikuwa, kwa hiyo, usiokubalika kwa umma. Muhammad alikuwa hajasikia chochote kibaya zaidi tangu zama za Abu Jahl, na alikuwa hana hamu ya kulisikia tena, hususan akiwa yuko kwenye kitanda cha mauti yake. Yeye, kwa hiyo, aliliacha kabisa jambo hilo.

Hila ya Umar ingefanya kazi hata kama Muhammad angeamuru kuandikwa kwa wosia wake. Kuiongeza ufanisi tabia ya Umar, watetezi wake wanasema kwamba dini ilikuwa imekamilishwa na kutimilishwa, na wosia, kwa hiyo, haukuwa na lazima. Ni kweli kwamba dini ilikuwa imekamilika na kutimia lakini haikuwa na maana kwamba na umma ulikuwa timilifu, na kwamba ungeweza kuachana na mwongozo kwa vile haukuwa kwenye hatari yoyote ya kukengeuka kutoka kwenye njia ya Haki. Umma ungeweza kupo-toka kutoka kwenye unyofu, na umefanya hivyo. Vita vyote vya wenyewe kwa wenyewe, mifarakano na utengano katika Uislamu, vilisababishwa na upotofu.

Kwa umma kuthibitisha kwamba wosia kama ule haukuwa lazima, ni kujitwalia madaraka makubwa sana wenyewe. Ulipaswa kuliacha jambo hili kwenye uamuzi wa mtu ambaye Allah (s.w.t.) amemchagua kuwa Mtume Wake kwa wanadamu. Yeye peke yake ndiye ali-jua kama wosia ulikuwa na lazima au la. Ni haki gani waliyonayo umma ya kuzuia uhuru wa kutenda wa Mwakilishi wa Allah (s.a.w.) kwenye dunia hii?

Ukaidi wa Umar kwa Muhammad, ambapo Muhammad alikuwa tayari yuko kwenye mlan-go wa mauti, ni moja kati ya matukio ya kutisha sana katika historia ya Uislamu, na haku-na kiwango cha upendezeshaji cha wanahistoria kinachoweza kuliondoa kijanja. Tukio hilo hilo lilikuwa pia ndio utangulizi wa makabiliano yaliyopatikana baina ya maswahaba na watu wa nyumba yake Mtume.

287

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wake zake Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.w.t)

MKE WA KWANZA WA MUHAMMAD ALIKUWA NI KHADIJA. Walioana huko Makka na wakaishi kwa robo karne ya mapenzi na furaha pamoja - mpaka kifo chake. Wakati Khadija alipokuwa hai, Muhammad hakuoa mwanamke mwingine.

Baada ya kifo cha Khadija, Muhammad akaoa wanawake wengi wengine lakini hakuna mmoja kati yao ambaye angeweza kamwe kuchukua nafasi ile ile katika moyo wake kama aliyokuwa nayo Khadija. Wakati alipokufa, ile furaha yake kamili, ya maisha ya ndoa, pia iliondoka pamoja naye. Mpaka mwisho wa maisha yake, alikumbuka mengi juu yake, na akamkumbuka kwa mapenzi, upendo na shukrani.

Mwanamke wa kwanza Muhammad aliyemuoa baada ya kifo cha Khadija, alikuwa ni Sawdah binti Zama'a, mjane ambaye mumewe alikufa huko Abyssinia.

Mke wa tatu wa Mtume (s.a.w.) alikuwa ni Aisha, binti ya Abu Bakr. inasemekana kaole-wa huko Makka lakini alikwenda nyumbani kwa mumewe huko Madina.

Mtume (s.a.w.) mara nyingi alijaribu kupata mahusiano mema na ukoo au kabila kwa kuoa mmoja wa wanawake zake. Kumuoa kwake Ummu Habiba binti ya Abu Sufyan, na Safiya binti ya Akhtab, kulikuwa ni ndoa kama hizo.

Mmoja wa wake za Mtume (s.a.w.) alikuwa ni Hafsa binti ya Umar ibn al-Khattab. Mumewe aliuawa katika vita vya Badri, na baba yake alikuwa na shauku ya mume mpya kwa ajili yake. Alimposesha kwa marafiki zake wa moyoni, kwanza kwa Uthman bin Affan, na kisha kwa Abu Bakr. Wote walisikitikia kukosa uwezo kwao wa kumuoa.

Umar alidhalilika kwa kule kukataliwa kwa binti yake hata na marafiki zake mwenyewe, na akalalamika kwa Mtume (s.a.w.) kuhusu hilo. Mtume, ili kutuliza uchungu wa moyo wa Umar, akasema kwamba madhali hakuna mtu mwingine aliyemtaka binti yake, yeye atam-chukua harimu yake mwenyewe.

Ukimuacha Khadija, wake wengine wote wa Mtume (s.a.w.) walibakia bila mtoto. Gavana wa Misri alikuwa amemtumia mtumwa wa kike Mkibti aliyeitwa Maria. Aliingia kwenye harimu yake, na akamzalia mtoto wa kiume ambaye alimwita Ibrahim.

Kuzaliwa kwa mtoto wa kiume kulimpa Maria umuhimu wa kipekee, kwenye maudhi

288

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

makubwa na uchungu wa mioyo wa wake wenzie. Mtume (s.a.w.) alitoa mapenzi makub-wa juu ya kijana mdogo huyo, na alitumia masaa mengi pamoja naye, akimbeba mikononi mwake. Lakini kwa bahati mbaya, kijana huyo hakuishi muda mrefu, na akafa katika mwaka ule wa kuzaliwa kwake.

D. S. Margoliouth

Miaka yake (Muhammad) ya mwisho ilichangamshwa na kwa muda kwa kuzaliwa kwa mtoto wa kiume na kimada/suria wake (sic - hili sio kweli) wa ki-Kibti - Maria, ambaye alimkubali kama ni wake, na ambaye alimwita kwa jina la muasisi wa kud-haniwa (sic - japo si kweli) wa dini yake, Ibrahim. Kimada/suria huyo (sic) akiwa ni chanzo cha wivu mkali wa wake zake wengi wasiokuwa na watoto, tukio hili la bahati liliwasababishia uchungu wa moyo mkali sana; ambao kwa kweli ulipunguzwa kwa haraka na kifo cha mtoto huyo (ambaye aliishi kwa miezi kumi na moja tu).

(Muhammad and the Rise of Islam, London, 1931) Muhammad Husein Haykal

Kwa kuzaa mtoto, hadhi ya Maria ilipanda katika taadhima ya Muhammad; yeye sasa alimuona kama mke huru, hasa, anayefurahia nafasi yenye fadhila kubwa.

Ilikuwa ni kawaida kwamba mabadiliko haya yangechochea sio wivu kidogo mion-goni mwa wake zake wengine waliokuwa wagumba. Ilikuwa ni kawaida pia kwamba heshima na upendo wa Mtume (s.a.w.) kwa mtoto huyo aliyezaliwa na mama yake viliongezea wivu huo. Zaidi ya hayo, Muhammad kwa ukarimu kabisa alimzawadia Salma, mke wa Abu Rafi, kwa jukumu lake kama mkunga. Alisherehekea uzazi huo kwa kutoa kipima cha nafaka kwa mafukara wote wa Madina. Alimkabidhi huyu mtoto aliyezaliwa hivi karibuni kwenye malezi ya Ummu Sayf, mama wa kunyonye-sha, ambaye alikuwa akimiliki mbuzi saba, ambao maziwa yake alikuwa Ayaweke kwenye haki ya matumizi ya huyu mtoto mchanga. Kila siku Muhammad alitembe-lea nyumba ya Maria ili akaone ule uso mwangavu wa mwanae na kujihakikishia yeye mwenyewe maendeleo ya afya ya mtoto huyo na ukuaji wake. Yote hii ili-chochea wivu mkali miongoni mwa wake zake wagumba. Swali lilikuwa, ni kwa muda mrefu kiasi gani wake zake hawa wangekuwa na uwezo wa kuvumilia mateso Haya ya kila siku.

Siku moja, pamoja na tabia za fahari ya mababa wapya, Mtume (s.a.w.) aliingia chumbani kwa Aisha pamoja na yule mtoto mikononi mwake, ili amuonyeshe kwa Aisha. Alimuonyesha yeye kufanana kwake kukubwa na mwanae. Aisha akamtazama yule mtoto na akasema kwamba hakuona kufanana kokote kule. Wakati Mtume

289

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

(s.a.w.) aliposema jinsi mtoto anavyokua, Aisha akajibu kwa chukichuki kwamba mtoto yeyote akipewa kiwango cha maziwa kama alichokuwa anapewa yeye angekua na ukubwa tu na mwenye nguvu kama yeye. Kwa kweli, kuzaliwa kwa Ibrahim kulileta maumivu mengi sana kwa wake za Mtume (s.a.w.) kiasi kwamba wengine wao wangekwenda kwa majibu makali zaidi ya haya na sawa na haya. Ilifikia kiasi kwamba Wahy wenyewe ulilazimika kutamka shutuma maalum. Bila shaka, jambo zima liliacha chapa katika maisha ya Mtume (s.a.w.) na vilevile katika historia ya Uislamu

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Wakati mmoja, Hafsa anasemekana kuwa "alimshitukiza" mumewe akiwa na Maria, na akaieleza "siri" hii kwa Aisha. Wake wengine wa Mtume (s.a.w.) waliisikia habari hii kuto-ka kwa Aisha. Kulikuwa na umbeya mwingi na uropokaji kuhusu tukio hili. Hatimae, Qur'an Tukufu ilibidi iingilie kati kwa karipio kwa mabibi wawili hao katika Aya ifuatayo:

Usahihi-37.jpg

"Kama ninyi wawili hamkutubia kwa Allah, basi nyoyo zenu zimekwisha kuelekea huko; laki-ni kama mtasaidiana dhidi yake (Mtume), hakika Allah ndiye mlinzi wake,na Jibrilu, na wau-mini wema na zaidi ya hayo, Malaika pia watamsaidia." (Sura ya 66; Aya ya 4)

Maelezo ya Mfasiri

"Nyumba ya Mtume (s.a.w.) haikuwa sawa na nyumba zingine. Wake bora wa Mtume (s.a.w.) walitegemewa kuwa na tabia njema ya hali ya juu na ukimya kuliko wanawake wa kawaida, kwani walikuwa na kazi ya hali ya juu ya kutekeleza. Lakini walikuwa binadamu hata hivyo, na walikuwa wenye kupatwa na udhaifu wa jinsia yao, na wakati mwingine walishindwa."

"Ujinga wa Aisha wakati mmoja ulisababisha matatizo magumu sana: akili ya Mtukufu Mtume (s.a.w.) ilipata uchungu sana, na aliacha ujamaa na wake zake kwa muda fulani. Binti ya Umar, Hafsa, alikuwa pia wakati mwingine mwepesi wa kutu-mia vibaya nafasi yake, na pale wawili hawa walipoungana katika ushauri wa kisiri, na kuzungumzia mambo na kupeana siri, walisababisha huzuni kubwa kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w)."

(A.Yusufu Ali)

Wengi wa wafasiri na watarjuma wa Qur'an wamelitafsiri neno la Kiarabu Saghat linalo-tokea kwenye Aya ya 4 ya Sura ya 66, iliyonukuliwa hapo juu, kama "kuelekea." Tarjuma yao inasomeka kama ifuatavyo:

290

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mioyo yenu imekwisha kuelekea.

Kuelekea kwenye nini? "Mioyo yenu imekwisha kuelekea," ni tafsiri isiyo na maana kati-ka muktadha huu. Tafsiri sahihi ya neno Saghat ni "imepotoka," M. Abul Ala Mauduudi ametoa tafsiri sahihi ya Aya hii ambayo ni kama ifuatavyo:

"Kama nyie (wanawake) wote mtatubia kwa Allah, (ni bora kwenu), kwani mioyo yenu imepotoka kutoka kwenye njia ya haki, na kama mtasaidiana dhidi ya Mtume, basi mjue kwamba Allah ndiye Mlinzi wake, na baada Yake ni Jibril na waumini wema na Malaika ndio wenzake na walinzi wake..."

(Tafhiim-ul-Qur'an, Juz. 6, Lahore, Pakistani, tarjuma ya Kiingereza ya Muhammad Akbar Muradpuri na Abdul Aziz Kamal, chapa ya pili, Mei 1987)

Wakati Hafsa "alipomshitukiza" Muhammad akiwa pamoja na Maria, alipaswa ati kutoa ahadi kwa Hafsa kwamba yeye hatakutana Maria tena. Hili, kwa kweli, limekatazwa. Mke mmoja hakuwa na haki kuzuia uhuru wa mumewe kukutana na wake zake wengine. Jaribio kama hilo kwa upande wa mke mmoja lingekuwa kinyume sio tu na sheria za Kiislamu bali pia na desturi za Arabia, wakati wote, kabla na baada ya Uislamu.

Sir William Muir

Katika suala la Zainabu, Muhammad (s.a.w.) alitoa ujumbe kutoka Mbinguni ambao ulikataza ahadi yake ya kutengana na Maria, ukamkemea Hafsa na Aisha kwa ukaidi wao, na ukadokezea juu uwezekano wa wake zake wote kuachwa kwa mwenendo wa uasi sana kwake mwenyewe. Kisha akajiondoa kwenye ujamaa nao, na kwa mwezi mzima akaishi peke yake pamoja na Maria. Umar na Abu Bakr walifedheheka sana kwa kutengwa kwa mabinti zao kwa ajili ya kimada duni (ingawa sio kweli) na wakahuzunikia umbeya wa mwenendo mzima.

(The Life of Muhammad, London, 1877)

Kutoka kwenye hayo yaliyotangulia inaweza kuonekana kwamba maisha ya nyumbani ya Mtume (s.a.w.), baada ya kifo cha Khadija, hayakuonyesha ufasaha wowote. Wengi wa wake zake walikuwa ni wanawake wenye wivu, na "ajali" ya kwanza ya wivu wao ilikuwa ni amani ya nyumba yake.

D. S. Margoliouth

Kukaa kwa wake katika harimu ya Mtume (s.a.w.) kulikuwa kufupi, kutokana na kutostahili kwa tabia; katika moja au zaidi ya masuala, wale wageni walifundishwa na wale wake za Mtume (s.a.w.) wenye wivu kanuni ambazo, walipozitamka bila

291

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kujua maana, zilimfanya Mtume (s.a.w.) kuwafukuza papo hapo. Mmoja alifukuzwa kwa kutangaza katika kufa kwa yule mtoto mchanga Ibrahim kwamba baba yake angekuwa ni Mtume, asingeweza kufa - matumizi ya ajabu ya uwezo wa fikira..

(Muhammad and the Rise of Islam, London, 1931)

Ilikuwa ni mazoea ya Mtume (s.a.w.), mara kwa mara, kuondoka nyumbani kwake usiku na kwenda kutembelea makaburi ya Baqii kuwaombea marehemu waliozikwa pale. Kabla tu ya maradhi yake ya mwisho, aliyatembelea makaburi hayo mara nyingine tena, labda kwa mara ya mwisho, na akakaa hapo na kuwaombea marehemu hao mpaka usiku wa manane. Baadhi ya wanahistoria wanasema kwamba ilikuwa ni katika safari hii kwamba alipatwa na homa ya baridi, na ilikuwa ndio mwanzo wa maradhi yake makali. Aisha anasemekana kumfuata katika moja ya safari hizi.

D. S. Margoliouth

Wakati wa usiku wa manane, inavyosemekana, Mtume (s.a.w.) alikwenda kwenye uwanja wa makaburi unaoitwa al-Baqii, na akaomba msamaha kwa ajili ya wale marehemu waliozikwa pale. Hili kwa hakika alilifanya hapo kabla; Aisha safari moja alimfuata yeye kama mpelelezi alipotoka wakati wa usiku, kwa kumdhania yeye kwamba amedhamiria mapenzi fulani; lakini alikokuwa akienda, aligundua, ilikuwa ni makaburini. (kutoka Musnad ya Imam Ahmad Hanbal, juz. Iv, uk. 221).

(Muhammad and the Rise of Islam, London, 1931)

Wanawake aliowaoa Mtume (s.a.w.) baada ya kifo cha Khadija, walikuwa tofauti sana na yeye (Khadija) kwa tabia na mwenendo. Khadija alikuwa amempa mumewe msaada thabiti na usio na mbwembwe katika uenezaji wa Uislamu, na alijitolea muhanga utajiri wake wote mkubwa kwa ajili ya lengo hilo. Kujitolea muhanga kwake kulimshusha mpaka kwenye hali ya ufukara lakini hakulalamika kwa mumewe kuhusu kukosa kitu chochote. Ndoa yake ilikuwa na utajiri katika baraka za upendo na urafiki wa mumewe, na katika furaha isiyo na kikomo.

Muhammad Mustafa mwenyewe aliishi maisha ya kawaida kabisa. Hata pale alipokuwa ndio mtawala wa Arabia nzima, alikuwa bado ni mwenye kujihini kama alivyokuwa huko Makka kabla ya kuhama kwake kwenda Madina. Aisha mwenyewe anasema hana kum-bukumbu kama mumewe aliwahi kula chakula cha ridhaa ya moyo wake mara mbili kwa siku moja.

Wakati ngawira za vita au mapato ya dola yalipokuja, Mtume (s.a.w.) aliyagawanya mion-goni mwa Waislamu. Wake zake waligundua kwamba hata wale wanawake masikini kabisa hapo Madina walikuwa kwa hivyo wakawa matajiri lakini sio wao. Ilijitokeza kwao

292

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwamba hawakupaswa wakoseshwe ukarimu mkubwa wa mume wao. Hata hivyo, wao hawakuzoea kuishi maisha ya kujihini kiasi hicho kama alivyokuwa yeye. Walilijadili suala hili miongoni mwao wao wenyewe, na wote wakakubaliana kwamba walipaswa kupata sehemu katika vile vitu vizuri na halali - sawa na wale wanawake wengine wa Madina.

Wake za Mtume, kwa hiyo, wakawasilisha madai yao kwake. Walikuwa na kauli moja katika kudai posho kubwa ya kujikimu kutoka kwake. Wawili wao, yaani, Aisha na Hafsa, wal-isimama kama "wazungumzaji" wao. Walipokuwa wakisisitiza madai yao kwake, Abu Bakr na Umar wakaja kumuona Mtume (s.a.w.) kwa shughuli fulani za kibinafsi au za

umma.

Mtume (s.a.w.) alikaa kimya, akiwa amezungukwa na wake zake. Pale Abu Bakr na Umar walipogundua yale yanayopikwa, walikasirika sana, na wakawalaumu kwa ukali kabisa mabinti zao kwa kudai pesa zaidi kutoka kwa mume wao.

Muhammad Husein Haykal

Abu Bakr alimuinukia binti yake Aisha na kumvuta nywele zake na vivyo hivyo Umar akamfanyia binti yake, Hafsa. Wote Abu Bakr na Umar wakawaambia binti zao: "Mnathubutu kumuomba Mtume wa Allah (s.a.w.) kile ambacho hawezi kumudu kukitoa?" Wao wakajibu: "Hapana, Wallahi hatumuombi yeye kitu kama hicho."

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Hatimae jambo hilo lilikomeshwa pale iliposhushwa Aya mpya kwa sababu hii, na ambayo inasomeka kama ifuatavyo:

Usahihi-38.jpg

Ewe Mtume! Waambie wake zako: "Ikiwa mnataka maisha ya dunia hii na mapambo yake, basi njooni, nitakulipeni kitokea nyumba, na kukuacheni kwa njia nzuri. Na ikiwa mnampenda Allah na Mtume Wake, na nyumba ya Akhera, Basi Allah amewaandalia wafanyao mema, miongoni mwenu, malipo makubwa. (Sura ya 33; Aya ya 28 na 29)

293

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Maelezo ya Mfasiri:-

Nafasi ya wake za Mtume (s.a.w.) haikuwa sawa na ile ya wake wa kawaida. Walikuwa na kazi na wajibu maalum... wake wote katika nafasi yao ya juu walipaswa kufanya kazi na kusaidia kama akina-mama wa umma. Yao hayakuwa ni maisha ya kutulia, kama yale ya masuria, ama kwa anasa zao wenyewe au anasa za mume wao. Wanaambiwa hapa kwamba walikuwa na sehemu katika Kaya Tukufu (ya Mtume) kama walipenda starehe na mapambo ya dunia tu. Kama hali ilikuwa ni hiyo, wangeweza kuachwa na kukimiwa vya kutosha, na zaidi.

(A.Yusufu Ali)

Qur'an Tukufu iliwapa nafasi wake za Mtume, yaani, ama walikuwa wamchague Allah (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.), na kuishi maisha ya kujinyima na kujitoa muhanga; au wangeweza kuchagua anasa, starehe na mapambo ya dunia hii ambavyo kwa suala hilo ingewalazimu kuachana na mume wao daima. Fursa hiyo ilikuwa ya dhahiri, na wake hao walikuwa na uhuru wa kuchagua.

Aisha, Hafsa na mabibi wengine saba walilitafakari jambo hilo, na kisha wakaamua kusamehe burudani na starehe za dunia hii, na kubaki katika nyumba ya Mtume (s.a.w.) kama wake zake.

Wakati Muhammad Mustafa (rehema na amani juu yake na Ahlul-Bait wake) alipokufa mwaka 632, alikuwa na wake tisa katika harimu yake. Aisha aliishi kwa nusu karne baada yake, na mke aliyeishi zaidi ya wake wengine wa Mtume, alikuwa ni Maimuna. Yeye, ilivyokuwa, alikuwa ndiye mwanamke wa mwisho aliyemuoa.

294

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kifo cha Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.w.t.)

MALENGO YA MAISHA YA MUHAMMAD MUSTAFA (s.a.w.), kama Mtume wa Mwisho wa Allah (s.w.t.) katika dunia hii yalikuwa:

•   Kuangamiza ibada ya masanamu na ushirikina;

•   Kutangaza rasmi Tauhidi ya Muumba;

•   Kufikisha Ujumbe wa Muumba kwa wanadamu;

•   Kukamilisha mfumo wa dini na sheria;

•   Kutakasa nafsi za wanaume na wanawake;

•   Kukomesha dhulma, uovu na ujinga;

•   Kuanzisha mfumo wa amani pamoja na haki;

•   Kuunda chombo katika namna ya hali ya kisiasa kwa ajili ya utambuzi wa malengo hayo yote yaliyopita, na chombo ambacho kitadumisha mwendo wa kazi yake.

Ndani ya ile miaka 23 ya kazi yake kama Mtume wa Allah, Muhammad (s.a.w.) alikuwa amefanikisha malengo yote Haya, na kisha ilianza kuonekana kama ilivyo kwa wanadamu wengine wote, yeye pia ilimbidui aondoke kwenye dunia hii. Kama ilivyoelezwa hapo kabla, alipokea taarifa hii kwa mara ya kwanza pale Suratun-Nasr (msaada), Sura ya 110 ya Qur'an Tukufu, iliyonukuliwa mapema katika kitabu hiki, iliposhushwa kwake.

Muhammad Mustafa alitumia maisha yake yote katika Swala na ucha-mungu lakini baada ya kuteremshwa kwa Nasr kuzama kwake katika kumuabudu Muumba wake kukawa kukubwa zaidi kuliko hapo kabla, katika kujiandaa kukutana Naye.

Mtume (s.a.w.) mwenyewe alidokeza, angalau katika matukio haya mawili kwamba kifo chake hakikuwa mbali sana naye:

1. Katika hotuba yake ya Hij a ya Muago pale Arafat siku ya Ijumaa, mwezi 9 Dhil-Hajj, mwaka wa 10 H.A., alisema: "Labda, hii ndio Hija yangu ya

295

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mwisho." Katika kumalizia hotuba yake, aliuliza swali kwa mahujaji, yaani, "Mtakapoulizwa na Mola wenu kuhusu kazi yangu, majibu yenu yatakuwa yapi?" Mahujaji wakajibu kwa sauti moja: "Ulifikisha ujumbe wa Allah (s.w.t.) kwetu, na ulitimiza wajibu wako." Alipolisikia jibu hili, alitazama kuelekea Mbinguni, na akasema: "Ewe Allah! kuwa shahidi kwamba nimetekeleza wajibu wangu."

2. Wakati wa "kutawazwa" kwa Ali ibn Abi Talib pale Ghadir-Khumm, mnamo mwezi 18 Dhil-Hajj, 10 H.A., Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.a.w.w) alizungumzia tena kifo chake kilichokuwa kinakaribia kwa kusema: "Mimi pia ni mwanadamu, na ninaweza kuitwa mbele ya Mola wangu wakati wowote."

Makumi ya maelfu ya Waislamu waliyasikia matangazo haya ya Mtume wao (s.a.w.), na wote walijua kwamba hatakuwa nao kwa muda mrefu zaidi. Yeye mwenyewe alijua kwamba alikuwa amekamilisha kazi yake ambayo Mola wake alimkabidhi, na alikuwa, kwa hiyo, na shauku ya kukutana Naye.

Mtume (s.a.w.) alitumia nyakati zake za kila usiku pamoja na wake zake mbalimbali kwa zamu. Mnamo mwezi 19 Safar ya mwaka wa 11 H.A., ilikuwa ni zamu yake kulala kwenye chumba cha Aisha. Usiku, alitembelea viwanja vya makaburi vya Baqii akiwa pamoja na mtumishi wake, Abu Muwayhiba, ambaye baadae alisimulia kwamba:

"Mtume (s.a.w.) alisimama katikati ya makaburi na akayahutubia kwa maneno yafu-atayo: 'Amani iwe juu yenu ninyi mlioko kwenye makaburi haya. Mumebarikiwa katika hali yenu ya sasa ambamo mmejitokeza kutokea kwenye hali ambamo watu wanaishi katika dunia. Mashambulizi ya kuangamiza yanashuka moja baada ya jingine kama mawimbi ya giza, kila moja bay a zaidi ya yale yaliyotangulia.'"

Muhammad Husein Haykal anasema kwamba yale maradhi "makali" ya Mtume (s.a.w.) yalianza asubuhi iliyofuatia ule usiku ambao alitembelea uwanja wa makaburi, yaani, mnamo mwezi 20 Safar. Yeye anaendelea kusema:

Ilikuwa ni hapo kwamba watu waliingiwa na wasiwasi na lile jeshi la Usamah halikuondoka. Kweli, ile Hadith ya Abu Muwayhibah inatiliwa shaka na wanahisto-ria wengi ambao wanaamini kwamba maradhi ya Muhammad (s.a.w.) yasingeweza kuwa ndio sababu pekee ambayo ilizuia hilo jeshi kutoondoka kwenda al-Sham, kwamba sababu nyingine ilikuwa ni kule kutoridhika kwa wengi, pamoja na idadi ya Muhajirina wakubwa na Ansari, kuhusiana na uongozi wa jeshi hilo.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

296

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Tukio lifuatalo linaelekea kuwa limetokea asubuhi ya mwezi 20 ya Safar:

Sir William Muir

Usiku mmoja Mtume (s.a.w.) alitembelea kwenye viwanja vya makaburi nje ya viun-ga vya mji. Huko alichukua muda mrefu akiwa amezama katika tafakari na kuwaombea marehemu. Wakati wa asubuhi, akipita kwenye mlango wa Aisha, ambaye alikuwa anaugua kutokana na maumivu makali ya kichwa, alimsikia aki-lalamika (kupiga kite): kichwa changu! oh, kichwa changu! Akaingi ndani na akase-ma: "Hapana, Aisha, kwa hakika mimi ndio ningekuwa na haja ya kulia - kichwa changu kichwa changu!" Kisha kwa mwelekeo wa upole: "Lakini usingependa wewe kuchukuliwa wakati nikiwa bado hai; ili niweze kukuswalia wewe, na kukusetiri wewe, Aisha, katika sanda yako, hivyo nikupeleke wewe kaburini?"

"Hilo litokee kwa mwingine," alimaka Aisha, "na sio kwangu mimi!" kimzaha akaongeza: "Ah, hilo ndilo unalolitaka wewe! Hakika, naweza kukuota wewe, baada ya kwisha kunifanyia yote haya na kunizika mimi, unarudi moja kwa moja nyumbani kwangu, na kutumia jioni hiyo hiyo kwa kucheza mahali pangu na mke mwingine!"

Mtume (s.a.w.) akatabasamu kwa mzaha wa Aisha, lakini maradhi yalizidi kumsonga kwa nguvu kuweza kutoa jibu katika mwelekeo huo huo.

(The Life of Muhammad, London, 1877) Betty Kelen

Yeye (Mtume) aliomba usiku kucha (kwenye makaburi ya Baqii) na akarudi nyumbani kwake, akiingia kwenye nyumba ya Aisha, ambaye alikuwa anaumwa na kichwa, na alipomuona Mtume (s.a.w.) alikunja uso wake na akasema, "Oh! kichwa changu!"

"Hapana, Aisha," alisema Mtume (s.a.w.), "ni oh! kichwa changu mimi!" Akaketi chini kwa nguvu, kichwa chake kikimgonga, maumivu yakibana viungo vyake muhimu, sasa akasema: "Hivi inakuhuzunisha kujifikiria wewe mwenyewe kufa kabla yangu, ili kwamba niweze kukusetiri kwenye sanda na kukuzika wewe?"

Alikuwa anaonekana kama mgonjwa wa kufa, lakini Aisha, ambaye aliamini kwamba alikuwa kwa hali yoyote ile amefika mwisho wa njia yake ya ndoa za kidiploma-sia, alimpa jibu la kisirani: "Hapana. Kwa sababu naweza pia kufikiria kuja kwako wewe moja kwa moja kutoka makaburini kusherehekea usiku wa harusi."

(Muhammad, The Messenger of God)

297

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad Husein Haykal

Asubuhi iliyofuata, Muhammad (s.a.w.) alimkuta Aisha, mke wake, akilalamikia maumivu ya kichwa, na akiwa ameshikilia kichwa chake kati ya mikono miwili, huku akiugulia, "oh! kichwa changu!" Yeye mwenyewe akiwa na maumvu ya kichwa, Muhammad (s.a.w.) alijibu, "Lakini hasa, Ewe Aisha, ni kichwa changu mimi!" Hata hivyo, maumivu hayakuwa makali sana kiasi cha kumlaza kitandani, kumzuia kazi zake za kila siku, au kumzuia yeye kuongea na wake zake na hata kutaniana nao. Aisha alivyoendelea kulalamika kuhusu kichwa chake, Muhammad (s.a.w.) alimwambia: "Haitakuwa vibaya hata hivyo, Ewe Aisha, kama ingekuwa ufe kabla yangu mimi. Kwani nitaweza hapo kukuswalia na kuhudhuria mazishi yako." Lakini hili liliamsha tu harara za Aisha mwenye ujana, ambaye alijibu: "Wacha hayo yawe majaaliwa mema ya mtu mwingine na sio mimi. Kama hilo litanitokea mimi, utakuwa una wake zako wengine utakaokuwa pamoja nao."

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Mtume (s.a.w.) hakutoa jibu lolote kwa dhihaka ya Aisha, na akaegemea kwenye ukuta. Pale maumivu yalipopungua, alinyanyuka na akawatembelea wake zake wengine kama alivyokuwa akifanya siku zote. Siku ya mwezi 24 Safar, alikuwa kwenye nyumba ya mke wake, Maimuna, alipopata shambulizi la ghafla la maumivu makali ya kichwa na homa. Inasemekana kwamba aliwaita wake zake wote na akawaomba wamhudumie kwenye chumba cha Aisha. Walikubali kufanya hivyo.

Mtume (s.a.w.) alikuwa amechoka sana kiasi cha kushindwa kutembea mwenyewe. Kwa hiyo, Ali alimsaidia kwa upande mmoja, na Abbas, ami yake, upande mwingine, na wal-imsindikiza kutoka kwenye chumba cha Maimuna kwenda kwenye chumba cha Aisha. Alikaa kwenye chumba cha Aisha mpaka kifo chake siku chache baadae.

Lakini licha ya homa na udhaifu wake, Mtume (s.a.w.) alikwenda Msikitini kila mara alipoweza, na akawaongoza Waislamu kwenye Swala. Siku ya mwezi 26 Safar, anase-mekana kujisikia vizuri kidogo, na alikwenda Msikitini akisaidiwa na Ali na Abbas. Aliongoza Swala ya zuhr, na baada ya Swala, akaongea na mkusanyiko wa waumini.

Hii ilikuwa ndio hotuba ya mwisho ya Mtume wa Uislamu, na ndani yake alitoa dokezo moja zaidi lililifichikana la kifo chake kilichokuwa kinakaribia. Wanahistoria wa Sunni wanasema kwamba Abu Bakr ambaye alikuwepo katika hadhara hiyo, alielewa kile Mtume (s.a.w.) alichokisema, na akaanza kulia kwani alikuwa na moyo wa huruma sana. Mtume (s.a.w.) alimwona akilia na akajaribu kumliwaza, na kisha akigeukia ule mkusanyiko, akasema:

298

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Namshukuru sana Abu Bakr zaidi kuliko mtu mwingine yoyote kwa msaada wake wa hali na mali, na kwa usuhuba wake. Kama katika umma huu, ingekuwa kamwe nichague mtu kama rafiki, ningeweza kumchagua yeye. Lakini sio lazima kwa sababu udugu wa Kiislamu ni kifungu imara zaidi kuliko kingine, na kinatutosha sisi sote. Na kumbukeni kwamba milango yote inayofungukia Msikitini, lazima ifungwe isipokuwa mlango wa nyumba ya Abu Bakr."

Mtume (s.a.w.) aliwaonya Waislamu wasije wakarudia kwenye kuabudu masanamu, na kukumbuka kwamba wao walikuwa wenye kumuabudu Mungu Mmoja, na akaongeza:

"Kitu kimoja ambacho kamwe msije mkakifanya, ni kuabudu kaburi langu. Yale mataifa ya siku zilizopita ambayo yaliabudu makaburi ya mitume yao, walipatwa na ghadhabu ya Mola, na waliangamizwa. Jihadharini, msije mkawafuata wao."

Mapema siku hiyo ilitolewa taarifa kwa Mtume (s.a.w.) kwamba Ma-Ansari walikuwa na huzuni kubwa sana kwa sababu ya maradhi yake. Ulikuwa, kwahiyo wakati muafaka wa kuwaambia Muhajirina kuhusu Ma-Ansari na huduma yao kubwa kwa Uislamu. Akasema:

"Msije mkasahau hata mara moja kile walichokufanyieni Ansari. Wamekupeni makazi na hifadhi. Walichangia nyumba zao na mkate wao pamoja nanyi. Ingawa hawakuwa matajiri, walitanguliza mahitaji yenu mbele kuliko yao. Wao ni 'wakfia' wangu kwenu. Watu wengine wataongezeka kwa idadi lakini wao watapungua tu. Yote yaliyokuwa wajibu kwa Ansari, wameyatimiza kwa uaminifu kabisa, na sasa ni zamu yenu kutimiza wajibu wenu kwao."

Ansari pia walikuwepo mle ndani ya Msikiti, na walikuwa wakijaribu kuzuia vilio vyao vya kikweukweu. Akiongea nao, Mtume (s.a.w.) akasema:

"Enyi Ansari! Baada ya kifo changu mtakabiliwa na huzuni nyingi na matatizo."

Wakamuuliza: "Ewe Mtume wa Allah! una ushauri gani kwetu? Itatupasa tufanyeje zitakapofika hizo nyakati ngumu?"

Yeye akasema: "Msiache ustahimilivu wenu, na wekeni imani zenu kwa Allah (s.w.t.) wakati wote."

Ule msafara wa kijeshi wa kwenda Syria bado ulikuwa umesimama. Mtume (s.a.w.) ali-washutumu maswahaba zake kwa kutojali maadili kwao katika kupiga ripoti kikazi kwa jenerali wao, na akawaamuru kwa mara nyingine kuondoka hapo mjini papo hapo. Alikatisha kuongea kwa muda kidogo, na kisha akaomba laana ya Allah (s.w.t.) juu ya watu wale wote watakaodharau amri yake ya kwenda Syria.

299

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hotuba yake ikaisha. Mtume (s.a.w.) alishuka kwenye mimbari na kurudi chumbani kwake. Alijihisi kuzimia kutokana na ile juhudi ya kuongea, na hakwenda pale Msikitini tena. Ilikuwa ndio mara ya mwisho kuonekana hadharani.

Sehemu ya kwanza ya hotuba yake ambayo inahusiana na Abu Bakr, inaelekea ni ya uongo, na inaonekana kuwa imeongezwa. Kama ilivyokwisha kuonyeshwa, Abu Bakr alikuwa chini ya amri ya kujiunga na jeshi la Usamah lakini inawezekana kwamba Mtume (s.a.w.) alipuuza kushindwa kwake kuripoti kikazi. Mtume (s.a.w.) anaweza pia kuwa ali-tambua mchango wake wa mali kwa Uislamu. Aliwakomboa watumwa wengi huko Makka, na alitoa mali yake yote kuandaa msafara wa Tabuk.

Hadithi ya kwamba Mtume (s.a.w.) aliamuru milango yote iliyokuwa ndani ya Msikiti ifungwe isipokuwa mlango wa chumba cha Abu Bakr, ni Hadith ya kubuni ya dhahiri pia. Abu Bakr aliishi katika kitongoji cha Madina kilichokuwa kikiitwa Sunh. Hakuwa akiishi hapo mjini, na hakuwa na chumba ambacho mlango wake ulifungukia Msikitini.

Mtume (s.a.w.) pia alisema katika hotuba yake kwamba kama ingekuwa amchague mtu yoyote kuwa rafiki, angemchagua Abu Bakr.

Kama hotuba hii vile ilivyosimuliwa, ni sahihi, basi ina maana kwamba Mtume (s.a.w.) ali-tangaza hadharani kwamba hakutaka kumfanya Abu Bakr kuwa rafiki. Kama kauli yake itafafanuliwa, itasomeka hivi: "Kama ingekuwa nichague rafiki, ningemchagua Abu Bakr. Lakini sitamchagua. Sisi wote ni wahusika wa udugu wa Kiislam wa ulimwengu mzima, na hilo linatutosha sisi sote."

Hata hivyo, kulikuwepo na nini cha kumzuia Muhammad Mustafa kumchagua Abu Bakr kama rafiki? Hakuna! Malaika Mkuu Jibril hakuja kutoka mbinguni kumwambia asimch-ague Abu Bakr kama rafiki, wala hakuwepo yeyote duniani hapa aliyetishia kumfanyia madhara yoyote kama angemchagua yeye (Abu Bakr) kuwa rafiki.

Kwa vile huku kulikuwa ni kuonekana kwa mara ya mwisho hadharani kwa Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.a.w.w) na kwa vile, kwa mujibu ya madai ya Sunni, alimpen-da sana Abu Bakr, alipaswa kuitumia nafasi hii, sio tu kwa kumtangaza yeye kama rafiki bali pia na kumtangaza yeye kama khalifa (mrithi) wake. Kama angefanya hivyo, angeweza mtu yoyote kumpinga? Lakini kwa sababu moja au nyingi za ajabu, hakufanya hili wala lile. (Muhammad hakumchagua Abu Bakr kama rafiki wala hakumfanya yeye kuwa mrithi wake). "Mapenzi" yake kwa Abu Bakr yalipaswa kupata maelezo, lakini hayakupata; "kukosekana" kwa ajabu sana kwa upande wake katika wakati muhimu kabisa.

300

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Tarehe 27 ya Safar, Mtume (s.a.w.) alijihisi mnyonge sana kuweza kusimama na kuswali. Wanahistoria wa Sunni wanasema kwamba ilikuwa ni kuanzia tarehe hii kwamba alimua-muru Abu Bakr kuongoza Waislamu katika Sala. Yeye mwenyewe, wanasema, alibakia amekaa na akafanya vitendo vya Swala.

Bukhari, mkusanyaji wa Hadithi (maneno ya Mtume), anasimulia tukio lifuatalo katika Sahih yake:

"Mnamo mwezi 28 Safar, Abbas ibn Abdul Muttalib alikuja kumuona Ali, na akase ma: 'Wallahi, Muhammad karibuni atakufa. Ninaweza kulijua hilo kutokana na kuonekana kwa nyuso za watoto wa Abdul Muttalib wanapotaka kufa. Mimi, kwa hiyo, nashauri kwamba uzungumze naye na umuulize yeye kuhusu suala la urithi (ushikamakamu) wake.' Lakini Ali akasema: 'Hapana. Sio katika hali aliyonayo sasa hivi. Mimi sipendi kulileta suala hilo."

Wanahistoria wa Kishia wanaikataa kabisa "Hadith" hii. Wao wanasema kwamba Mtume (s.a.w.) alikuwa ametangaza, sio mara moja, bali mara nyingi tu kwamba Ali alikuwa ndiye mrithi wake na mtawala wa Waislamu wote. Kama Waarabu hawakuwa wamkubali kama bwana wao hata baada ya matangazo mengi, tangazo moja zaidi lingekuwa vigumu kuweza kufanya mabadiliko. Mtume, kwa kweli, alifanya jaribio la kuandika wosia wake pale alipoitisha kalamu, karatasi na wino lakini alikutana na dharau. Na Ali hakutaka mtu yoyote aonyeshe "moyo wake wa kujasiri" kwa kukemea kwamba Mtume wa Allah (s.a.w.w) alikuwa "akiropoka." Kusikia hiyo kauli ya tusi kungeweza tu kuharakisha kifo cha bwana wake kutokana na mshituko.

Kama Hadith hii ni ya kweli, inaelekeza tu kwenye upendo wa Ali kwa bwana wake, na kupenda kusaidia kwake kumkinga kutokana na kila mshituko.

Waislamu wa Kishia pia wanasema kwamba Abbas mwenyewe angeweza kulichukua suala hilo la kujadili na Mtume (s.a.w.) ambaye alikuwa ni mpwa wake. Mtume (s.a.w.) alikuwa mchangamfu, na mwenye kuweza kufikiwa hata na wageni. Kulikuweko na nini, kwa hiyo, kwa Abbas, cha kuwa na mashaka nacho?

Masahaba waliweza kuona kwamba Mtume (s.a.w.) hatapona kutokana na homa yake na maumivu ya kichwa. Mara alipokuwa amezuiliwa kwenye kitanda cha mauti yake, wengi wao walijihisi kwamba walikuwa "salama" kama wangeacha kumtii yeye. Kwa hiyo, lolote alilofanya katika kuwashinikiza wao katika kwenda Syria, wao hawakwenda, na msafara wa Usamah kamwe haukutimizwa - katika uhai wake!

Wakati wa mchana, Muhammad Mustafa alimwita Ali, na akamwambia: "Kwangu mimi ni mwisho wa safari. Nitakapokufa, wewe uoshe mwili wangu, uuvishe sanda, na uushushe

301

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kaburini. Ninadaiwa pesa na watu fulani na fulani, miongoni mwao Myahudi mmoja alin-ipa mkopo wa kutayarishia jeshi la Usamah. Lipa madeni haya kwao wote pamoja na huyo Myahudi." Kisha akaivua pete aliyokuwa amevaa, akampa Ali, na akamuomba aivae ambapo aliivaa. Na pia alimpa yeye (Ali) upanga wake, mkuki, deraya na silaha nyingine-zo.

Jumatatu, Rabi al-Awwal 1, 11 H.A.

Jumatatu, mwezi 1 Rabi al-Awwal ya 11Hijiria ilikuwa ndio siku ya mwisho ya Muhammad ibn Abdullah (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.w.t.) katika dunia hii. Kulikuwa na nyakati ambapo alijisikia nafuu kidogo lakini wakati mwingine, alikuwa dhahiri kwenye maumivu makali. Aisha, mke wake, anasimulia ifuatavyo:

"Jinsi siku ilivyosogea kuelekea mchana, Fatima Zahra, binti yake Mtume wa Allah (s.a.w.w) alikuja kumuona Mtume. Alimkaribisha na kumwambia akae kandoni mwake. Kisha akamwambia kitu ambacho sikuweza kusikia lakini alianza kulia. Alipoyaona machozi ya binti yake, alimwambia kitu kingine ambacho pia sikuweza kusikia lakini yeye alianza kutabasamu. Yeye alifanana sana na baba yake katika mwenendo, tabia na Sura."

Muda baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.), Aisha alimuuliza Fatima ni kitu gani ambacho baba yake alimwambia yeye ambacho kwanza kilimfanya alie na kisha kikamfanya atabasamu.

Fatima akasema: "Kwanza baba yangu aliniambia kwamba alikuwa anakaribia kufa. Nilipolisikia hili, nilianza kulia. Kisha akanijulisha kwamba mimi ndio nitakayekuwa wa kwanza kabisa kukutana naye huko mbinguni, nalo pia, ni hivi karibuni tu. Nilipolisikia hili, nilifurahi sana, na nikatabasamu."

Washington Irving

Mtoto pekee wa Muhammad aliyekuwa amebakia, Fatima, mke wa Ali, alikuja sasa kumuona yeye Muhammad. Aisha alizoea kusema kwamba hajawahi kumuona mtu yoyote anayefanana na Mtume (s.a.w.) zaidi katika uzuri wa moyo kama huyu binti yake. Alimshuhulikia siku zote kwa upendo wa heshima. Alipokuja kwake, alizoea kusimama, kumfuata, kumshika mkono na kuubusu, na humkalisha kwenye sehemu yake mwenyewe Mtume. Kukutana kwao katika safari hii kunasimuliwa hivyo na Aisha, katika Hadith zilizohifadhiwa na Abulfida.

"Karibu mwanangu," alisema Mtume, na akamfanya akae karibu naye. Kisha akanong'ona kitu fulani katika sikio lake, ambacho kwacho alilia. Katika kutambua huzuni yake, alinong'ona kitu kingine zaidi, na sura yake ikan'gara kwa furaha.

302

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Hii ina maana gani?" nilimuuliza Fatima. "Mtume (s.a.w.) anakuheshimu wewe kwa dalili ya mategemeo ambayo hajayaonyesha juu ya yeyote kati ya wake zake." "Siwezi kutoa siri ya Mtume wa Allah (s.a.w.w)" alijibu Fatima. Hata hivyo, baada ya kifo chake, alisema kwamba kwanza alimtangazia kifo chake kilichokuwa kinakaribia; lakini alipomwona yeye analia alimtuliza kwa kumhakikishia kwamba angemfuata baada ya muda mfupi na kuwa Malkia wa peponi."

(The Life of Muhammad)

Kuelekea mchana ule Mtume (s.a.w.) alikuwa na hali ya kutotulia. Aliulowesha uso wake mara kwa mara kwa maji baridi kutoka kwenye gudulia lililokuwa karibu yake. Alipomuona katika maumivu kama hayo, Fatima alilia: "Oh mateso ya baba yangu!" Mtume (s.a.w.) alijaribu tena kumliwaza, na akasema: "Baada ya siku hii ya leo, baba yako hatakuwepo kwenye mateso tena." Na akaongeza: "Wakati nikifa, sema, "Sisi wote ni wa Allah na Kwake ndio marejeo yetu."

Sasa, kupumua kwake kukawa sio kwa kawaida, na alisikika akinong'ona kitu. Ibn Saad anasema katika Tabaqaat yake kwamba Mtume (s.a.w.) alikuwa akisema: "Ninachokitafuta sasa ni kuwa pamoja na Allah (s.w.t.)" Haya yalikuwa ndio maneno yake ya mwisho.

Muhammad (s.a.w.) alisikika akiyarudia maneno haya mara tatu, na kisha akanyamaza kimya - daima! Muhammad, Mtume wa Mwisho wa Allah (s.a.w.w) kwenye dunia hii, akafariki.

Aisha anasema: "Niliweka mto chini ya kichwa chake, na nikafunika kichwa chake na shuka. Kisha nikasimama pamoja na wanawake wengine, na wote tukaanza kulia, tukipi-ga vifua na vichwa vyetu, na kujipiga makofi kwenye nyuso zetu."

Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.w.t.) alifariki siku ya Jumatatu ya kwanza ya Rabi al-Awwal ya mwaka wa kumi na moja Hijiria wakati wa mchana. Alikuwa ameishi kwa miaka 63 iliyopungua siku nane tu.

Wanahistoria wa Ki-Sunni wanasema kwamba Mtume (s.a.w.) alifariki, sio kwenye tarehe mosi bali mnamo tarehe 12 Rabi al-Awwal. Waislamu wa Shia wanasema kwamba alifariki, sio kwenye mwezi mosi ya Rabi al-Awwal bali siku moja mapema zaidi, yaani mwezi 28 Safar.

Makubaliano ya wanahistoria wa kisasa wa Magharibi, ni kwamba, Mtume (s.a.w.) alifariki mnamo tarehe 8 Juni, 632. Tarehe nane ya Juni, kwa bahati, pia ndio siku ya kuzaliwa kwake.

303

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mazishi ya Mtume (s.a.w.)

Mwili wa Mtume wa Uislamu (s.a.w.w.) ulioshwa siku ya Jumanne. Ni watu sita tu waliokuwapo kwenye huduma hii ya mazishi. Nao walikuwa ni:

Ali ibn Abi Talib

Abbas ibn Abdul Muttalib

Fadhl ibn Abbas

Qathm ibn Abbas

Usamah ibn Zayd bin Haritha

Aus bin Khuli Ansari

Usamah, mkuu wa jeshi la kwenda Syria, alikuwa yuko Jurf, akiwa bado anawangojea maswahaba. Baadhi yao walimpelekea habari kwamba Mtume (s.a.w.) alikuwa anafariki, na kwamba angepaswa arudi Madina. Alirudi, na muda kidogo baadae, bwana wake aka-fariki.

Ali aliuosha mwili wa Mtume (s.a.w.) wakati Usamah akiwa anammwagia maji. Wakati mwili ulipokwaisha kuoshwa, Ali aliufunika na sanda, na akauswalia. Kisha yeye akatoka nje, na akawaambia Waislamu waliokuwa ndani ya Msikiti, waende chumbani na kuswali Swala ya maiti. Bani Hashim walikuwa wa kwanza kumswalia, na kisha Muhajirina na Ansari wakatekeleza wajibu huu.

Hapo Madina, palikuwa na wachimba-kaburi wawili. Walikuwa ni Abu Ubaida bin al-Jarrah na Abu Talha Zayd bin Sahl. Waliitwa wote lakini ni huyu wa mwisho tu ndiye aliyepatikana. Alikuja na akalichimba kaburi. Ali aliingia mle kaburini ili kulisawazisha vizuri. Kisha akaunyanyua mwili kutoka pale chini, na akauteremsha taratibu ndani ya kaburi, akisaidiwa na ami yake na binamu zake. Kaburi kisha likafunikwa kwa udongo, na Ali akanyunyizia maji juu yake.

Wakati Ali na watu wengine wa Bani Hashim walipokuwa wanashuhulika na mazishi ya Mtume wa Uislamu (s.a.w.), Abu Bakr, Umar, Abu Ubaidah bin al-Jarrah, na wengineo, walikuwa wanashughulika huko Saqifah wakicheza bahati na sibu ya madai ya ukhalifa. Abu Bakr, ilivyotokea, alikuwa ndiye mgombea aliyeshinda. Alipokuwa amepokea viapo vya utii vya Ansari hapo Saqifah, yeye na marafiki zake walirudi kwenye Msikiti wa Mtume (s.a.w.w.). Ndipo akapanda kwenye minmbari ya Mtume (s.a.w.) kupokea viapo kama hivyo kutoka kwa watu wengine. Siku ya Jumatatu jioni, na kutwa nzima ya Jumanne, watu walikuwa wanakuja Msikitini kuchukua kiapo cha utii kwake. Kuchukua kiapo kulikwisha baadae sana usiku wa Jumanne, na ilikuwa ni Jumatano tu ambapo huyu khalifa mpya alipopata muda wa kugeuzia mawazo yake kwa bwana wake aliyekwisha fariki, na kufanya Swala ya maiti kaburini pake.

304

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.a.w.) kiongozi wa Waislamu wote, na Rehma kuu ya wanadamu, hakupata mazishi ya kitaifa. Kiasi kidogo tu cha watu - ndugu zake wa karibu - walimfanyia mazishi. Wengi wa wale waliodai kwamba walikuwa ni maswahaba na rafiki zake, walimtelekeza wakati wa saa yake ya kufa. Kutokuwepo kwao kwenye mazishi yake kulikuwa ndio kuvurugika kukubwa kabisa kwa mipango kwenye mazishi yake.

Ibn Saad anasema katika Tabaqaat yake kwamba Ali ibn Abi Talib aliyalipa madeni yote ya Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Uislamu. Alimtuma mpiga-mbiu mjini kote Madina, na wakati wa msimu wa Hijja, alituma mpiga-mbiu huko Makka, kutangaza kwamba yeye Ali angelipa madeni yote ya Muhammad (s.a.w.), na kwamba yeyote ambaye alikuwa na madai, aende kwake kulipwa. Aliwalipa wadai bila ya kuwauliza maswali yoyote na bila ya kutaka uthibitisho kwamba Muhammad (s.a.w.) alikuwa anadaiwa na wao kitu cho-chote, na hili alikuwa akilifanya mpaka mwisho wa siku zake.

305

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hisia za Familia na za Masahaba wa

Muhammad Mustafa (s.a.w.)

juu ya Kifo chake

WATU WA FAMILIA YA MUHAMMAD MUSTAFA (s.a.w.) walikuwa wamesongwa na wimbi kubwa la huzuni kwa kifo chake. Binti yake, Fatima Zahrah, alikuwa ndiye "Nuru ya macho yake." Lakini sasa macho yale yalikuwa yamefumbwa daima; yasingeweza kum-salimia yeye na watoto wake tena. Wala asingeweza kusikia kutoka midomoni mwake ile sauti ya upendo na upole ikimkaribisha nyumbani; walinyamazishwa daima. Kwake yeye alikuwa ni baba, ni "mama," Malaika mlezi, na Rehma ya Allah (s.w.t.) juu ya ardhi. Kwake yeye, alikuwa ndio kitovu cha uhai wenyewe.

Kwa Muhammad (s.a.w.), binti yake, Fatima, na familia yake, walikuwa ndio mfano hal-isi wa mapenzi yake yote, upendo wake, shangwe zake na furaha zake. Alimradi wakati alipokuwa hai, alimtendea kwa heshima kubwa mno, na alimuonyesha tofauti ambayo inastahili tu kwa Malkia. Lakini kwake yeye, alikuwa ni zaidi kabisa kuliko malkia. Kati ya watu wote aliowajua yeye Mtume (s.a.w.) yeye (Fatima) alikuwa wa kwanza na wa mbele kabisa katika moyo wake.

Sasa Fatima alikuwa na haja moja tu - kukutana na baba yake huko mbinguni. Aliitambua haja hii mapema - majuma kumi tu baada ya kifo chake. Kifo chake (Fatima) kilimuacha mume wake na watoto wake kuvumilia sio moja bali huzuni mbili.

Hasan na Husein (a.s) walikuwa ni wajukuu wa Muhammad Mustafa (s.a.w.). Walikuwa ni vipenzi vyake. Walikaa mapajani mwake wakati alipokuwa yuko Msikitini au nyumbani, na walipanda mabegani mwake alipokuwa akitembea nje. Mapaja yake yalikuwa ndio "pepo" yao, na mabega yake yalikuwa ndio "vipando" vyao. Sasa ile "pepo" na "vipando" vilikuwa vimewapotea daima. Macho yao, yakiwa na utando wa machozi, yalimsaka bila mafanikio, babu yao mpendwa kila mahali. Mimbari yake na baraza ya Msikiti wake vilikuwa sasa viko tupu, na kuta zake nzio zenyewe zilionekana kuwa katika maombole-zo. Msikiti wake ulikuwa kama koa ambamo lulu yake imekwisha toka. Vilio vya maom-boleza na malalamiko ya watoto hawa wadogo wawili vilirudi kutoka kwenye kuta za Msikiti wake katika mwangwi wenye majonzi.

Watoto wote wawili waliingiliwa na hisia ngeni, zisizoeleweka na za wasiwasi, na wal-ishikwa na hofu zisizo yakini na zisizotajika. Walikuwa ni wadogo sana kuweza kupam-banua hisia hizi au kuelewa hofu hizi; lakini hata hivyo walihisi hiyo hisia mpya ya kukosa usalama ambayo iliwasumbua wao wote. Kwa mara ya kwanza katika miaka michache

306

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

waliyoishi, waliwindwa na hali isiyo na usalama. Babu yao alikuwa, kwao wao, ni dalili na ishara ya usalama, na sasa alikuwa ameondoka.

Kwa Ali, kifo cha Muhammad (s.a.w.) kilikuwa ni msiba mkubwa katika maisha. Dunia yake ilikuwa imemzunguka Muhammad (s.a.w.) tangu alipozaliwa. Muhammad (s.a.w.w) alikuwa ndio kitovu na mzingo wa dunia yake. Kutoka kwenye dunia ile, Muhammad alikuwa ametoweka, na sasa Ali hakujua namna atakavyoishughulikia. Alijihisi kama ame-funguliwa kutoka kwenye minyororo yake, na maisha ghafla yalionekana kupoteza sababu yake ya kuwepo, kwa ajili yake yeye.

Ali alikuwa ndio roho ya Uislamu. Tabia yake ilikuwa adhimu sana na haiba yake ilikuwa haiwezi kulinganishikika. Lakini alikuwa ametegemea juu ya Muhammad (s.a.w.) awe kama kichocheo cha roho na haiba yake kukua. Alikuwa na kila sifa ya uwezekano ambao ulimfanya yeye kuwa wa muhimu sana kwa Uislamu lakini zimechukua ustadi wa ajabu wa Muhammad (s.a.w.) kuzifanya zijulikane.

Na sasa wakati akiwa na umri wa miaka 32, wakati akiwa kwenye ujana wa maisha yake, wakati akiwa kwenye ufanisi wa nguvu zake, na wakati akiwa angeweza kutoa zaidi kwa Uislamu na kwa dunia yote, zaidi kuliko alivyokwishatoa, Muhammad (s.a.w.) akafariki. Kifo cha Muhammad (s.a.w.) kilikuwa ni kipingamizi kwa Ali ambacho hakuweza kukom-boka kutokana nacho kwa maisha yake yote yaliyobakia.

Hisia za Fatima Zahrah, Hasan, Husein na Ali (a.s), kwa kifo cha Muhammad (s.a.w.) zilikuwa za kawaida na za kutibika. Wote watano waliunda jamii ya familia, iliyoungan-ishwa katika mapenzi yao, na utii wao kwa Allah (s.w.t.), Muhammad (s.a.w.) alikuwa ndio "mhimili" wa jamii hii ndogo. Kwa kifo chake, "jamii" hii ilivunjika, ikiwaacha watu wengine wa familia hiyo wakiwa wamekanganyikiwa kabisa. Labda hawakujua kwa wakati ule, ingawa walikuwa waje kujua punde tu, kwamba kifo cha Muhammad (s.a.w.) kimeashiria tu mlolongo mzima wa mishtuko na huzuni mpya kwao. Tokea hapo na kuen-delea, walikuwa wawe kwenye hali ya "kuzingirwa" na huzuni. Kila siku mpya ilikuwa ilete mshituko mpya, na huzuni mpya. Lakini kwa kupitia msukosuko huu wa majanga na misiba, imani yao katika rehema za Allah (s.w.t.) na katika ushindi bora wa haki na ukweli, ulibakia imara kama jiwe, na ya kudumu. Matumaini yao ya kupata radhi za Allah (s.w.t.) yalizidi kuongezeka nguvu zaidi daima kwa kila wimbi jipya la mshituko na huzuni.

Ili kuhimili mshituko wa kifo cha Muhammad (s.a.w.), watu wa familia yake walitafuta na kupata msaada kutoka kwenye kile Chanzo Kimoja ambacho hakishindwi kamwe - Rehma za Allah (s.w.t.) zisizo na mipaka.

307

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kifo cha Muhammad Mustafa (s.a.w.) na Umma wake

Waislamu waliwajibika kwa Muhammad (s.a.w.) kwa kiapo cha namna mbili; kwanza katika wadhifa wake kama Mtume wa Allah (s.w.t.); na pili katika wadhifa wake kama Mtawala wa Arabia. Hakuna ambaye angeweza kuzuia uwajibikaji na utiifu kwake katika wadhifa wowote ule, na akabakia kuwa bado ni mwislamu.

Katika mwenendo wake kama Mtume wa Allah (s.w.t.) Muhammad (s.a.w.) amewapatia wokovu kutoka kwenye fedheha ya kuabudu masanamu, na alikuwa amewafundisha kumuabudu Mungu Mmoja; na katika mwenendo wake kama Mtawala wa Arabia, alikuwa amewaletea ukombozi kutokana na machafuko ya kisiasa na vita vya maangamizi. Alikuwa amewapa sheria na taratibu. Alikuwa pia amewapa ukombozi kutokana na maadili ya vurugu, umasikini wa kiuchumi na utamaduni usiofaa. Alikuwa amewafanya kuwa matajiri na waliostaarabika, na alikuwa amewafanya kuwa taifa kubwa. Kwa kifupi, alikuwa ndio mfadhili wao mkubwa kabisa. Cha mwisho kabisa ambacho wangeweza kumfanyia kilikuwa ni kumpatia utii na upendo wao. Utii na upendo kwa Muhammad (s.a.w.) ulikuwa uwe ndio kigezo cha imani ya Waislamu katika kazi yake - katika Uislamu!

Walikuwepo wale Waislamu, wengi wao wakitokana na watu wa kawaida, ambao walimpa Muhammad (s.a.w.) upendo wao na hakuna ambaye angeweza kukataa kwamba upendo wao ulikuwa ni halisi. Wakati alipofariki, walipatwa na majonzi; walivunjika mioyo, na kwao wao ule Msikiti, mji na dunia yote ilionekana iliyotelekezwa.

Lakini hisia za maswahaba wakubwa wa Muhammad (s.a.w.) kwenye kifo chake, zilikuwa tofauti. Wakati Muhammad (s.a.w.) alipofariki, maswahaba wake wakuu hawakushtushwa na kifo chake. Kama kifo chake kiliwahuzunisha, wao hawakuonyesha kuhuzunika kokote. Kitu kimoja ambacho hawakukifanya, kilikuwa ni kutokutoa rambirambi zao kwa ile familia iliyoondokewa. Hakuna hata mmoja miongoni mwao aliyekuja na kuwaambia: "Enyi watu wa Nyumba ya Muhammad, tunachangia pamoja nanyi huzuni yenu kwa kifo chake. Kifo chake ni pengo sio kwenu tu bali kwetu sisi sote."

Katika wakati ambapo huruma inatarajiwa hata kutoka kwa wageni, kwa kweli, hata kwa maadui, haisadikiki lakini ni kweli kwamba Masahaba wa Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.w.t.) waliinyima familia yake mwenyewe. Waliiacha familia yake kuomboleza kifo chake yenyewe.

308

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad Mustafa (s.a.w.) na Urithi Wake

KAMA KIONGOZI, MUHAMMAD (s.a.w.) ALIKUWA KATIKA TABAKA LA WALE MASHUHURI KABISA - katika dunia nzima. Alijaaliwa na uwelewa wa kustaajabisha, uwezo wa kuona mbali na kipaji cha siasa. Katika miaka yake kumi ya mwisho ya uhai wake, alitakiwa afanye maamuzi muhimu sana katika historia ya Uislamu. Maamuzi yale yaliwagusa sio Waislamu tu au Waarabu bali wanadamu wote. Alikuwa pia anatambua kwamba vitendo vyake na maamuzi yake vingegusa vitendo na maamuzi ya kila kizazi cha Waislamu mpaka mwisho wa wakati wenyewe.

Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.w.t.) kwa hiyo, hakufanya uamuzi wowote, haid-huru uwe wa kawaida kiasi gani, kwa msingi wa kusudi maalum; wala kufanya maamuzi kwa utaratibu wa "kubahatisha." Maamuzi yake yote yalikuwa ni ya kujaaliwa. Yalikuwa ni vigezo kwa umma wa Kiislam (taifa au jamii) kwa wakati wote. Ilikuwa ni pamoja na ujuzi na ufahamu huu kwamba alisema au kutenda kitu chochote na kila kitu.

Muhammad (s.a.w.) alifanikiwa, baada ya mapambano marefu na ya kikatili dhidi ya waabudu masanamu na washirikina wa Arabuni, katika kuanzisha Ufalme wa Mbinguni Duniani ili umma wake uweze kuja kuishi kwa amani na usalama, kupendwa na kuonewa wivu na wanadamu waliobakia. Ufalme wa Mbinguni Duniani ulikuwa ndio kazi ya maisha ya Muhammad (s.a.w.). Alijua kwamba yeye ni binadamu, na atakuja kufa siku moja, lakini kazi yake, kama ilivyounganishwa kwenye huo "Ufalme" ingeishi. Alijua kwamba baada ya kifo chake, mtu mwingine tena angeendeleza ile kazi aliyoianzisha yeye. Alijua pia kwamba umakamu (urithi wa kazi yake) uliopangwa vizuri ndio nanga ya utulivu. Alijua yote haya na mengi zaidi ya haya. Hakuna mwislamu ambaye angeweza kamwe kuthubutu kudhania kwamba Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.w.t.) hakuyajua yote haya vizuri zaidi kuliko mtu mwingine yeyote.

Urithi wa Muhammad (s.a.w.) ulikuwa pia ni jambo la kunong'onwa sana miongoni mwa Waislamu wengi. Swali moja ambalo lilitawala sana katika akili za wengi wao, hususan baada ya kutekwa Makka, lilikuwa, ni nani atakayemrithi yeye kama Mkuu mpya wa Dola ya Madina, baada ya kufa kwake.

Swali hili linatoa nafasi kwa jibu moja tu, yaani, mwislamu bora zaidi! Mrithi wa Muhammad (s.a.w.) anapaswa kuwa, sio mtu wa daraja la pili, bali tunda bora kabisa la Uislamu; mtu ambaye Uislamu wenyewe utamkubali kwa fahari kama "chombo cha kipaji."

"Chombo cha kipaji" kama hicho kilikuwa ni Ali ibn Abi Talib, Muhammad (s.a.w.) "alim-

309

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

gundua" yeye mapema maishani; alimuandaa na alimteua yeye kama mrithi wake, hivyo kuhakikisha ukabidhi wa mamlaka wa amani na utaratibu. Alikuwa na hamu kubwa sana ya kuzuia kushindania madaraka miongoni mwa maswahaba wake baada ya kifo chake yeye mwenyewe.

Lakini, kwa bahati mbaya, mpango huu haukufanikiwa, na urithishaji, baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.) haukuwa wa amani na wa utaratibu. Kulikuwa na kushindania madaraka kukali miongoni mwa maswahaba zake ambamo baadhi ya wagombea wapya wa madaraka walifanikiwa katika kukamata Dola ya Madina. Kufanikiwa kwao kuliashiria mwisho wa ghafla wa Utawala wa Mbinguni Duniani, na kuliashiria, wakati huohuo, kuzaliwa kwa Dola ya Kiislam - Dola iliyoongozwa na watu ambao walikuwa Waislamu. Utawala wa Mbinguni Duniani au Dola ya Kiislam haikudumu muda mrefu baada ya kifo cha Mtume. Kifo cha Taifa la Kiislamu, likiwa bado katika uchanga wake, kinaweza kuamsha udadisi wa mwanafunzi wa historia. Anaweza kushangaa ni kwa nini liliishi kwa muda mfupi kiasi hicho, na jinsi ilivyowezekana kwa hawa wagombea wapya kupindua mpango uliofanywa na Mtume (s.a.w.) mwenyewe kwa ajili ya ukabidhianaji wa amani na utaratibu wa madaraka, na kulazimisha kukubalika kwa mpango wao wenyewe juu ya umma wa Waislamu.

Lifuatalo ni jaribio la kujibu swali hili

Wagombea wapya wa madaraka hawakuunga mkono ule mpango uliofanywa na Mtume (s.a.w.) wa kukabidhi madaraka. Wao na wafuasi wao walikuwa na ajizi nyingi za kuuhusu, na walikuwa wamekusudia kukamata Dola ya Madina wao wenyewe. Kwa ajili hii, walikuwa wamekwishapanga mkakati wa hali ya juu na walikuwa wameingia katika kazi ya kuutekeleza hata kabla ya kifo cha Mtume (s.a.w.).

Hila kuu katika mkakati wa hawa wagombea wa madaraka ulikuwa ni kueneza ile taarifa ya uongo kwamba si Kitabu cha Allah (s.w.t.) kilichoelezea maoni yoyote juu ya jambo la uongozi wa umma wa Waislamu, wala Mtume wa Allah (s.a.w.w). kuchagua mtu yeyote kama mrithi wake. Waliwaza kwamba kama Waislamu wakiamini dai kama hilo kuwa la kweli, basi watachukulia kwamba Mtume (s.a.w.) aliiacha kazi ya kutafuta kiongozi wa baadae wa serikali yake kwa umma wenyewe, na katika umma huo, kwa kweli, kila mtu alikuwa huru kuingia kwenye orodha na kunyakua madaraka mwenyewe, kama angeweza.

Dr. Hamid-ud-Din:

"Qur'an Tukufu haikutaja kitu chochote kuhusu namna ya kuchagua khalifa. Hadithi za kutegemewa za Mtume (s.a.w.) nazo pia ziko kimya kuhusiana na hili. Kutokana na hili, mtu anaweza kuchukua uamuzi kwamba Shari 'ah (Sheria Tukufu) imeliacha jambo hili kwenye mapendekezo ya Umma wenyewe ili uweze kuchagua viongozi wao kulingana na mahitaji yao wenyewe, na kulingana na hali itakayokuwepo wakati

310

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

huo."

(History of Islam by Dr. Hamid-ud-Din, M.A.{Honors}, Punjab; M.A.{Delhi};

PH.D.[Harvard University, U.S.A.}, Published by Ferozesons Limited,

Publishers,Karachi,Pakistan,page 188, 4thedition, 4th printing, 1971)

Hila hii ilipata mafanikio ya kushangaza, na ina maisha marefu ya kustaajabisha. Ilitumika wakati huo na inatumika siku hizi.Huko nyuma ilikuwa ikitumika huko Mashariki tu; sasa inatumika kote Mashariki na Magharibi. Wachache huko Mashariki na hakuna yeyote huko Magharibi walioshindana nayo. Mafanikio yake yanathibitishwa na ushahidi wa wanahis-toria wafuatao:

Marshall G.S. Hodgson:

"Qur'an haikutoa, kwa mfano hasa, mambo ya kisiasa yanayoweza kutokea kwa kifo cha Mtume (s.a.w.)"

(The Venture of Islam, Vol1, 1974)

Dr. Muhamed Hamidullah:

"Ukweli kwamba zimekuwepo tofauti za maoni, katika kifo cha Mtume (s.a.w.), unaonyesha kwamba hakuacha maelekezo ya wazi na sahihi kuhusu kurithiwa kwake."

(Introduction to Islam, Kuwait, 1977)

Francesco Gabrieli:

"Muhammad (s.a.w.) alifariki, baada ya kuugua kwa muda mfupi, mnamo tarehe 8 Juni, 632. Hakuweka au hakuweza kuweka ushahidi wa kisiasa na hakumteua mtu aliyekuwa anastahili sana kumrithi yeye."

(The Arabs, A Compact History, New York, 1963)

G. E. Von Grunebaum:

"Mtume (s.a.w.) alifariki mnamo tarehe 8 Juni, 632. Hakufanya maandalizi kwa ajili ya mtu atakayemrithi."

(Classical Islam - A History 600 - 1258) John B. Christopher:

"Tatizo la haraka sana lililoikabili Jumuiya changa ya Madola ya Kiislamu lilikuwa ni urithi kwenye uongozi wa umma pale Muhammad (s.a.w.) alipofariki; tatizo hili lilikutwa na kuanzishwa kwa ukhalifa.

311

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kwa sababu Muhammad (s.a.w.) hakufanya maandalizi kwa ajili ya mtu atakayem-rithi, ile jumuiya ya Kiislam iliyoathirika ikageukia nyuma kwenye vigezo vya kika-bila vya kuchagua Sheikh mpya mara tu baada ya Mtume (s.a.w.) alipofariki."

(The Islamic Tradition, Introduction, New York)

Bernard Lewis:

"Katika asili zake, ile taasisi kubwa ya Kiislam ya ukhalifa ilikuwa ni ushitukizaji wa ghafla. Kifo cha Mtume (s.a.w.), bila ya urithishaji uliopangwa, kilihimiza mgogoro kwenye jumuiya changa ya Kiislamu."

(The Legacy of Islam - Politics and War - 1974)

George Stewart:

"Kuipitia upya historia, mtu anasita na kushangaa ni vipi ukhalifa umetokea kuwepo. Muhammad (s.a.w.) hakuacha usia wowote; hakumteua mtu yoyote kufuata katika nyayo zake, hakukaimu kwa yeyote mamlaka ya kiroho, na hakutoa funguo za Utawala wa Mbinguni kwa mtu ambaye ni Mtume..."

(George Stewart katika makala yake, Is the Caliph a Pope? iliyochapishwa katika kitabu, The Traditional Near East, kilichohaririwa na Stewart Robinson, na kuchapishwa na Prentice-Hall, Inc., N.J., 1966)

Robert Frost wakati fulani alisema: "Nadharia, kama ukiishikilia kwa nguvu ya kutosha na kwa muda mrefu wa kutosha, inapata kuthaminiwa kama kanuni ya imani." Maelezo haya yanaweza kubadilishwa kidogo yasomeke kama ifuatavyo: "Uongo, kama ukiushikilia kwa nguvu ya kutosha na kwa muda mrefu wa kutosha, unapata kuthaminiwa kama kanuni ya imani."

Wingi usio na idadi, wa wanahistoria wa Uislamu, wamedai kwamba Mtume (s.a.w.) hakumtaja bay ana mtu yeyote kama kiongozi wa baadae wa Dola ya Madina baada ya kifo chake yeye mwenyewe. Kwao wao, na kwa wengine wengi, dai hili limekuwa ni kanuni ya imani sasa.

Lakini sio kwa Waislamu wa Shia. Wao wanatetea kwamba Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.w.t.) alitangaza kwa kurudiarudia na kwa msimamo ulio wazi kabisa kwamba Ali alikuwa ndio mshikamakamu wake na kiongozi wa Waislamu wote.

Muhammad (s.a.w.) alionyesha uelekeo kwa ajili ya umma wake, na aliwaonya wao wasiukengeuke baada ya kifo chake. Lakini umma ulikengeuka hata hivyo, na

312

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ukengeukaji huu umewafikisha, kwa kujua au kwa kutojua, kwenye kufufua mila ya kipagani.

Baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.), baadhi ya maswahaba walikusanyika kwenye ukumbi wa nje ya Madina uliokuwa ukiitwa Saqifah, na wakamchagua Abu Bakr kama kiongozi wa Waislamu. Hapakuwa na kigezo katika Uislamu kwa ajili ya uch-aguzi kama huo, lakini kilikuwepo kigezo kwa ajili hiyo katika asasi za kisiasa za nyakati kabla ya Uislamu.

Wanahistoria watatu wa wakati mmoja wa Pakistani wanaandika katika historia zao

History of the Islamic Caliphate kama ifuatavyo:

"Baada ya kifo cha Muhammad (s.a.w.), tatizo muhimu na gumu sana ambalo Waislamu ilibidi wakabiliane nalo, lilikuwa lile la kuchagua khalifa. Qur'an iko kimya juu ya jambo hili, na Mtume (s.a.w.) pia hakusema lolote juu yake. Katika nyakati za kabla ya Uislamu, desturi ya Waarabu ilikuwa ni kuchagua wakuu wao kwa wingi wa kura. (Kwa kushindwa kupata kigezo kingine) kanuni hiyo hiyo ilifu-atwa katika kumchagua Abu Bakr."

(History of the Islamic Caliphate (Urdu), Lahore, Pakistan. Professor M. Iqbal, M.A., L.L.B.; Dr. Peer Muhammad Hasan, M. S., Ph. D.; Professor M. Ikram Butt, M.S.)

Kwa mujibu wa wanahistoria hao watatu waliotajwa hapo juu, kazi muhimu kabisa mbele ya Waislamu wakati wa kifo cha Mtume (s.a.w.) ilikuwa ni kutafuta kiongozi, kwa vile Mtume (s.a.w.) aliwaacha bila kiongozi. Kukosekana kwa kigezo katika Uislamu wenyewe kwa ajili ya kutafutia kiongozi, walilazimika kuchukua mila ya kipagani, na wakamchagua Abu Bakr kama kiongozi wao mpya.

Mtindo huu wa kutafuta kiongozi kwa ajili ya Waislamu ulikuwa haukubaliani na busara za Uislamu. Ulikuwa, kwa hiyo, ni upotofu, kama ilivyokwisha tajwa. Upotofu huu umezingatiwa na Mustashirki wengi; miongoni mwao ni:

R. A. Nicholson:

"Kwamba Muhammad (s.a.w.) hakuacha mtoto wa kiume ilikuwa labda haikuwa na maana zaidi kuliko kupuuza kwake au kukataa kuteua mrithi. Waarabu walikuwa ni wageni na mtiririko wa kurithiana katika mamlaka ya kifalme, ambapo wazo hilo lilikuwa halijaingia bado la mtawala mkazi mwenye haki ya ki-Mungu katika famil-ia ya Mtume (s.a.w.). Ilikuwa inakubaliana kwa kinaganaga na mazoea ya Waarabu kwamba jamii ya Waislamu ichague kiongozi wake yenyewe, kama vile katika siku za upagani kabila lilichagua kiongozi wake lenyewe. "

(A Literary History of the Arabs)

313

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Profesa Nicholson anasema kwamba: "Waarabu walikuwa ni wageni na mtiririko wa kurithiana katika mamlaka ya kifalme. Anaweza akawa sawa. Waarabu, hata hivyo, walikuwa hawana uzoefu na vitu vingine vingi kama vile imani katika Tauhidi ya Allah (s.w.t.) na walikuwa na uzoefu mkubwa na masanamu yao ya mawe na miti; waliambatana nayo kwa ushupavu, na wengi wao wakafa kwa ajili yao."

Hata hivyo, ule "ugeni" wa Waarabu kwenye mtiririko wa kurithiana katika mamlaka ya kifalme haukudumu kwa muda mrefu; ulidhihirisha kuwepo kwa muda mfupi sana. Kwa kweli, huo "ugeni" wao ulidumu kwa chini ya miaka thelathini (kutoka 632 hadi 661). Baada ya ile miaka thelathini ya ugeni na kanuni ya mtiririko wa kurithiana wa mamlaka ya kifalme, wakaja kuwa na ujuzi sana nayo, na ujuzi wao mpya umedumu mpaka kufika kwenye nyakati zetu wenyewe.

Kwa kuwa "wageni" na utaratibu wa mtiririko wa kurithiana wa mamlaka ya kifalme, Waarabu walikuwa wanapapasa gizani, ambapo ghafla wakajikwaa kwenye mfano kutoka kwenye zama zao wenyewe za kabla ya Uislamu, kutoka kwenye siku zile walipokuwa waabudu masanamu, na wakaudaka. Walisisimka kwamba walikuwa wamepata "wokovu."

Francesco Gabrieli:

"Kwa kuchaguliwa kwa Abu Bakr kanuni ilianzishwa kwamba Ukhalifa au Uimam (Uimam katika suala hili ni kisawe cha khalifa) ulikuwa ubakie kwenye lile kabila la Makka la Quraishi ambalo Muhammad alitokana nalo. Lakini wakati huohuo mwe-nendo wa uwezo wa uchaguzi wa nafasi hiyo uliidhinishwa, kama ule wa bwana au kwa kukataa madai ya kurithiana ya familia ya Mtume (s.a.w.) (Ahlul Bait) inay-owakilishwa na Ali."

(The Arabs, A Compact History, 1963)

Francesco Gabrieli anasema kwamba: "kwa kuchaguliwa kwa Abu Bakr, utaratibu ulianzishwa kwamba Ukhalifa utabakia katika lile kabila la Makka la Quraishi. Lakini hasemi ni nani aliyeanzisha "utarattibu" huu. Je, anayo idhini ya Qur'an au Hadith za Mtume (s.a.w.) za kuiunga mkono? Haina. Kwa kweli, ulikuwa ni "utaratibu" wenye kusu-di maalum uliotekelezwa na wale watu ambao walitaka kujitwalia Ukhalifa au Uimamu kwa wao wenyewe. Waliuona "utaratibu" huu ni wenye kufaa sana kwa sababu uliwaweze-sha wao kuikamata serikali ya Muhammad (s.a.w.w), na kuing'ag'ania wakati wakiwazuia watoto wake kutokana nayo. Lakini kivitendo kama ulivyo "utaratibu" huu, unayo idhini yake, sio ndani ya Qur'an bali katika "jamii ya kipagani," kama ilivyoonyeshwa na mwanahistoria huyu mwenyewe."

314

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Bernard Lewis:

"Mgogoro wa kwanza katika Uislamu ulikuja wakati wa kifo cha Mtume (s.a.w.) mwaka 632. Muhammad (s.a.w.w) hajawahi kudai kuwa zaidi ya mwanadamu anayekufa - tofauti sana juu ya wengine kwa sababu alikuwa Mtume wa Allah na mwenye kuleta neno la Allah (s.w.t.) bali mwenyewe sio kama Mungu wala asiyeku-fa. Alikuwa, hata hivyo, hakuacha maagizo ya wazi juu ya nani alikuwa amrithi yeye kama kiongozi wa Jumuiya ya Kiislamu na mtawala wa Dola changa ya Kiislamu, na Waislamu walikuwa na ujuzi wa kisiasa mdogo sana wa Arabia ya kabla ya Uislamu wa kuwaongoza wao. Baada ya mabishano kiasi na kipindi kifupi cha mvutano wa hatari, walikubaliana kumteua Abu Bakr, mmoja wa waliosilimu mwanzoni kabisa na mwenye kuheshimiwa sana, kama khalifa, naibu, wa Mtume (s.a.w.) - hivyo kuunda, takriban bila ya kutegemea, ile taasisi kubwa ya kihistoria ya Ukhalifa.

(The Assassins, 1968)

Kama ilivyoelezwa mapema, ile taarifa ya uongo kwamba Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.a.w.w) hakuacha maagizo yoyote juu ya ni nani alikuwa amrithi kama kiongozi wa Jumuiya ya Kiislam, imekuwa ni Kanuni ya Imani kwa wengi wa wanahistoria, wa zamani na wa sasa, Waislamu na wasiokuwa Waislamu. Mtu labda anaweza kuwapuuza hao wanahistoria wa Kisunni kwa kung'ang'ania kwenye "kanuni ya imani" hii lakini ni ajabu kwamba wanazuoni wa safu kama hiyo na sifa kama Nicholson na Bernard Lewis hawakufanya chochote zaidi katika vitabu vyao juu ya Uislamu kuliko kuandika tena mtin-do usiobadilika wa historia ambao "ulirithishwa" kwao na wanahistoria wa mabaraza ya Damascus na Baghdad ya karne za mbeleni. Bernard Lewis, hata hivyo, amekiri, kama Nicholson na Gabrieli, kwamba wale Waislamu ambao walimchagua Abu Bakr kama khalifa wao, walikuwa na ujuzi wa kisiasa mdogo sana wa Arabia ya kabla ya Uislamu wa kuwaongoza

Bernard Lewis anaendelea kusema kwamba ile taasisi kubwa ya kihistoria ya Ukhalifa ilizaliwa "takriban bila ya kutegemewa."

Taasisi muhimu sana ya kisiasa ya Uislamu - Ukhalifa - ilizaliwa kwa hiyo "takriban bila ya kutegemewa!"

315

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

George Stewart:

"Cheo cha Ukhalifa kilikuja kuwepo sio kwa mpango wa makusudi au katika busara ya kuganga yajayo, bali takriban kutokana na kama ajali... Ukhalifa uliumbwa kutokana na ajali za ghasia za zama hizo ambazo zilifanya uzaliwe."

(The Traditional Near East, 1966) Akiandika kuhusu jamii ya Kiarabu ya kabla ya Uislamu, Profesa John Esposito, anasema:

"Kikundi cha familia kadhaa zinazohusiana kilitengeneza ukoo. Mkusanyiko wa koo kadha uliunda kabila. Makabila yaliongozwa na chifu (shaykh) ambaye alichaguliwa kwa makubaliano ya watu wa sawa na yeye - yaani, wakuu wa koo au familia zina-zoongoza."

(Islam - the Straight Path, 1991, uk. 5)

Katika kitabu hicho hicho (na mlango huo huo), Profesa Esposito anaendelea kusema -

katika ukurasa wa 16:

"..Jamii iliyoegemea kwenye ushirikishwaji wa kikabila na sheria na desturi ya kika-bila iliyotungwa na watu ilibadilishwa kuwa jamii iliyounganishwa kidini (umma wa Kiislamu) uliotawaliwa na sheria ya Allah (s.w.t.)"

(Abu Bakr alichaguliwa na kuwa mkuu (sheikh) kwa "makubaliano ya mamwinyi - yaani wakuu wa koo au familia zinazoongoza." Ilikuwa ni ile "sheria na desturi ya kikabila iliyotungwa na watu" iliyompa mamlaka. Kitu kimoja ambacho hakikutekelezwa katika kuch-aguliwa kwake, ni "sheria ya Allah (s.w.t.)")

Wanahistoria wote waliotajwa hapo juu wanakubaliana katika kueleza kwamba:

1.  Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w.), hakutoa maagizo yoyote kwa umma wake kuhusiani na mwenendo wa serikali ya baadae ya Kiislam, na hakumteua mtu yoyote kuwa kiongozi wake baada ya kifo chake yeye mwenyewe. Katika suala la ushikamakamu, hakuwa na msimamo wa wazi wa sera.

2.  Wakati Muhammad alipokufa, Waislamu walilazimika watafute kiongozi mpya wa jumuiya hiyo. Kwa kukosa muongozo na kigezo, hawakuwa na chaguo bali kurudia nyuma kwenye taasisi na desturi za kisiasa za Zama za Ujahilia ili kupata kiongozi, na Abu Bakr akawa ndio chaguo lao.

316

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kama wanahistoria hawa wako sawa, basi ni kosa baya kupita kiasi kwa upande wa Qur'an Tukufu na Mfasiri na Mtangazaji wake, Muhammad (s.a.w.), kuacha kuwaelimisha Waislamu katika jambo la kuchagua viongozi wao.

Lakini halikuwepo na lisingeweza kuwepo kosa baya kupita kiasi kama hilo kwa upande wa ama Qur'an au Muhammad (s.a.w.). Qur'an imeeleza, kwa maneno ya wazi na makali, ni zipi sifa za kiongozi aliyeteuliwa na Allah (s.w.t.) na Muhammad (s.a.w.) aliuambia umma, kwa maneno ya kufahamika kirahisi na makali, ni nani mwenye sifa hizo. (Suala hili limeshughulikiwa katika mlango mwingine).

Wakati huu, hata hivyo, Abu Bakr alichaguliwa kuwa khalifa wa Waislamu. Amri ya Allah (s.w.t.) haikutekelezwa katika kuchaguliwa kwake. Kuchaguliwa kwake, kwa hiyo, kunazua maswali ya msingi, kama:

1.   Matakwa ya Allah (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.) hayakuonekana popote katika uchaguzi wa Abu Bakr. Kwa vile alichaguliwa na baadhi ya maswahaba wa Mtume (s.a.w.), alikuwa ni mwakilishi wao au mwakilishi wa Waislamu. Mtume (s.a.w.) peke yake angechagua mrithi wake, na hakumchagua Abu Bakr. Je, bado Abu Bakr anaweza kuitwa mrithi wa Mtume wa Allah?

2.  Wajibu mkubwa katika mfumo wa jamii yoyote unatekelezwa na serikali au hasa, na kiongozi wa serikali hiyo. Qur'an inashikilia kwamba yenyewe ni pana na haikuacha kitu chochote cha muhimu. Lakini mashabiki wa Abu Bakr wanasema kwamba Qur'an haikuwaambia Waislamu namna ya kumpata kiongozi wa serikali yao. Kama wako sawa, sasa basi, je, tunaweza kudai mbele ya wasiokuwa Waislamu kwamba Qur'an ni mkusanyiko wa sheria ulio kamili na sahihi, na haikusahau jambo lolote muhimu la maisha ya mwanadamu kulifikiria?

3.  Kama Muhammad Mustafa (s.a.w.) mwenyewe hakuwaongoza Waislamu katika nadharia na utendaji wa serikali, basi, je, tunaweza kudai mbele ya wasiokuwa Waislamu kwamba yeye ni mfano bora kwa wanadamu wote katika kila kitu?

4.  Hivi mafundisho ya Muhammad (s.a.w.) yalikuwa pungufu na yasiyotosheleza kiasi hicho kwamba mara tu baada ya alipokufa, wafuasi wake walilazimika kutekeleza desturi, vigezo na mila za kipagani? Na kwa kuwa walifanya hivyo, je, hakuacha mwenendo wake kuwa wakutiliwa mashaka?

Ukweli ni kwamba Qur'an Tukufu ni kanuni pana na timilifu ya maisha. Lakini watakaopata uongofu ndani yake, ni wale tu watakaoutafuta. Hakuna ushahidi kwamba uongofu kutoka kwenye Qur'an ulitafutwa katika uchaguzi wa Abu Bakr. "Utaratibu"

317

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

uliotekelezwa katika uchaguzi wake ulitolewa kutoka kwenye uzoefu wa kisiasa wa Arabia ya kipagani. Uongozi wake uliegemea kwenye desturi iliyochimbuliwa kwenye mamlaka ya kikabila ya kabla ya Uislamu.

Kama vile Qur'an ilivyo kanuni timilifu ya maisha, Muhammad Mustafa (s.a.w.), Mletaji na Mfasiri wake, ndiye mfano bora kwa wanadamu. Alijua kwamba alikuwa anapaswa kutii sheria zilezile za uhai na umauti kama walivyokuwa binadamu wengine. Alikuwa pia amejaaliwa na hisia za historia, na alijua ni nini kilitokea wakati viongozi wakubwa walipofariki. Kitu kimoja ambacho asingeweza kukifanya, ni kuwaacha watu wake kuwa wapinzani kwa mara nyingine tena kama walivyokuwa katika Zama za Ujahiliya. Kitu kimoja ambacho kisingeweza, na hakikuweza kumtoka kwenye uangalifu wake, kilikuwa ni taratibu ya urithi katika Ufalme wa Mbingnii Duniani.

Abu Bakr alichaguliwa katika ukumbi wa Saqifah kama kiongozi wa serikali ya Waislamu kwa msaada wa Umar bin al-Khattab. Kwa hiyo, serikali yake, na vilevile serikali za warithi wake wawili - Umar na Uthman - wote watatu, walikuwa ni "matokeo" ya Saqifah. Nitazitaja serikali zao kama serikali za Saqifah ili kuzitofautisha na serikali ya Ali ibn Abi Talib ambayo haikuwa matokeo ya Saqifah. Serikali ya Ali ilikuwa ni ule Ufalme wa Mbinguni Duniani (uliorudishwa).

318

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Nadharia ya Kisunni juu ya Serikali

Wale waislamu wanaotangaza kwamba wanafuata sunnah (kauli na vitendo) ya Muhammad Mustafa (s.a.w.) Mtume wa Uislamu, na maswahaba zake, wanaitwa Ahl-us-Sunnah wal-Jama'at au Sunni. Wao pia wanajiita wenyewe Waislamu "wenye imani hal-isi", na wanafanya idadi kubwa ya Waislamu duniani.

Waislamu wa Sunni wanaamini kwamba Mtume wa Uislamu (s.a.w.) hakumteua mtu yey-ote kama mrithi wake, na yeye (yamkini) alichukulia kwamba baada ya kifo chake, Waislamu watajitafutia kiongozi wao wenyewe. Wanaendelea kusema kwamba Mtume (s.a.w.) wala hakuwaeleza wafuasi wake ni jinsi gani wangepaswa kuchagua viongozi wao wa baadae au ni sifa gani ambazo viongozi hao lazima wawe nazo. Hivyo, kwa kukosa vyote, kigezo na mwongozo katika jambo la kutafuta viongozi wao, maswahaba hao hawakuwa na chaguo bali kuchukua njia ya ufaraguzi (yaani, nje ya kanuni za Uislamu).

Lakini ufaraguzi sio busara, kama ilivyotarajiwa, ilitokea kuwa njia potovu hasa ya kuta-futia viongozi wa umma wa Kiislam. Katika mfano mmoja maswahaba walimpata kiongozi kupitia kilichochukuliwa kama uchaguzi. Katika mfano mwingine, yule aliyeko madarakani wa kwanza (ambaye alichaguliwa), akateua na kumuweka mrithi wake mwenyewe. Katika mfano wa tatu, yule mwenye madaraka wa pili (ambaye aliteuliwa), akateua kamati ya watu sita na akawapa jukumu la kuchagua mmoja kati yao wenyewe kama kiongozi wa baadae wa umma wa Kiislam.

Huyu kiongozi wa tatu, aliyechaguliwa hivyo, aliuawa katikati ya vurugu na machafuko, na umma ukaachwa bila kiongozi. Masahaba hapo wakageukia kwenye familia ya Mtume wao (s.a.w.), na wakamuomba mmoja wa watu wake kuchukua uongozi wa serikali ya Waislamu, na kwa sababu hiyo kuuokoa kutokana na kuvunjika na kuvurugika.

Huyu mwenye madaraka wa nne alikuwa bado anawatawala Waislamu wakati mgombea mwingine wa uongozi alipoibukia huko Syria. Aliipuuza ile shera ya uchaguzi, akapinga mamlaka halali ya Waislamu kwa kutekeleza utaratibu wa mabavu, na akafanikiwa katika kuikamata serikali. Kitendo chake kilifanya idadi ya "taratibu" za kutafuta viongozi wa umma wa Kiislam kuwa nne, ndio kusema.

1. Uchaguzi

Abu Bakr alichaguliwa kuwa khalifa (mrithi wa Mtume) kwa wingi wa kura ndani ya Saqifah. (Ali ibn Abi Talib, wa nne kwenye mamlaka, alichaguliwa pia kuwa khalifa kwa wingi wa Muhajirina na Ansari waliokuwepo Madina wakati wa kifo cha khalifa wa tatu)

319

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

2. Uteuzi

Umar aliteuliwa na Abu Bakr kama mrithi wake.

3. Uteuzi wa matajiri wenye mamlaka

Uthman alichaguliwa kuwa khalifa na kamati ya watu sita iliyoteuliwa na Umar.

4. Kukamatwa kwa serikali kwa mabavu yasio na aibu

Muawiya bin Abu Sufyan aliikamata serikali ya Waislamu kwa nguvu za kijeshi.

Waislamu wa Sunni wanaziona hizi "taratibu" zote nne kama ni za halali na zenye nguvu. Kwa mwenendo huu, mifano "halali" minne tofauti ya kutafuta kiongozi wa umma wa Kiislam ikaja kuwepo.

Hapa hakuna budi ielezwe kwamba ingawa Waislamu wa Sunni wameupa kila mmoja wa mifano hii minne tofauti ya kutafutia viongozi kwa ajili ya umma "hadhi" ya "kanuni", hakuna hata mmoja kati yao uliopatikana kutoka kwenye Kitabu cha Allah (s.w.t.) (Qur'an), au kwenye Kitabu cha Mtume (Hadith). Yote ilipatikana kutoka kwenye kadhia zilizotokea baada ya kifo cha Mtume wa Uislamu (s.a.w.).

Katika historia ya nchi yoyote ile, utengenezaji wa katiba ndio hatua ya kwanza kuelekea kwenye ujenzi wa taifa. Hiyo katiba ndio sheria-mama ya nchi. Ndio mfumo wa msingi wa mamlaka ya umma. Inaonyesha na kufafanua wajibu, kazi na madaraka ya serikali. Maamuzi yote makubwa yanayogusa maslahi ya taifa yanafanywa kwa kuzingatia kanuni zake. Chochote kinachokubaliana nayo, kinachukuliwa kwamba ni halali na chenye nguvu; ambacho hakikubaliani, kinaachwa kama kisicho cha kikatiba.

H. A. R. Gibb:

"Sheria inaitangulia nchi, kote kimantiki na katika misingi ya wakati; na nchi inakuwepo kwa madhumuni mamoja tu ya kuilinda na kuitekeleza sheria."

(Law in the Middle East)

Nadharia ya Sunni juu ya serikali inasumbuliwa na kioja kilichojengwa ndani kwa ndani. Kama taratibu, sera na vitendo vya viongozi wa kisiasa vinapaswa kufuata kanuni za katiba; lakini hawafanyi hivyo. Badala yake, ni katiba inayofuata matukio yatokanayo na maamuzi na vitendo vya viongozi wa kisiasa. Kwa maneno mengine, sio katiba inayoen-desha serikali; badala yake ni serikali, yaani, ni viongozi wa kisiasa wanaoongoza serikali ndio ambao "wanaiendesha" hiyo katiba.

320

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kwa kweli, hakuna kitu kama nadharia ya Sunni juu ya serikali. Wakati wowote tukio jipya lilipotokea, mafaqihi wa Kisunni walitengeneza "nadharia" au "kanuni" mpya ili kuipa mantiki. Kwa njia hii wameingiza nadharia yao ya serikali yenye tabia ya kigeugeu na wa kuendana na matukio ambayo kwa kweli ni ya ajabu kabisa.

Nadharia na utendaji wa serikali ya Kisunni imechunguzwa na kuchambuliwa na wanafun-zi wengi wa maendeleo ya kisiasa ya Kiislamu, wote, wa zamani na wa sasa, Waislamu na wasiokuwa Waislamu.

Mwandishi wa Sharh-Mawaqif, mwandishi wa jadi wa Kiarabu, anaamini kwamba vitu vinavyohitajika kwa mgombea wa uongozi, ni uwezo wake wa kutwaa na kushikilia madaraka. Anasema:

"Anapokufa Imam na mtu mwenye sifa muhimu anakidai cheo hicho (bila ya kiapo cha utii, yaani Bay 'a kuchukuliwa kwake, na bila kuteuliwa kwake kurithi), madai yake ya ukhalifa yatakubalika, alimradi tu mamlaka yake yanadhibiti watu; na ni dhahiri hali itakuwa ni hiyohiyo wakati huyo khalifa mpya akitokea kuwa mbumbum-bu au muovu. Na hali kadhalika ikiwa khalifa kwa njia hii amejiimarisha kwa nguvu kubwa na baadae anashindwa na mtu mwingine, yule khalifa aliyeshindwa ataon-doshwa madarakani na yule mshindi atatambuliwa kama Imam au Khalifa."

Mchambuzi mwingine wa nyakati za jadi, Taftazani, ana maoni kwamba kiongozi anaweza kuwa dhalimu au anaweza kuwa mwovu; anakuwa hata hivyo ni mtawala halali wa Waislamu. Anaandika katika kitabu chake, Sharh-Agha 'id-Nasafi hivi:

"Imam hana haki ya kuondolewa madarakani kwa sababu ya kuwa kwake mkukan-damizaji na asiyemcha Mungu."

Stewart Robinson amemnukuu Imam Ghazzali, katika kitabu chake, The Traditional Near East, kwamba anasema:

"Sultani mfanya-maovu na mkatili ni lazima atiiwe."

Wachambuzi wa kisasa wa maoni ya kisiasa ya Kiislam pia wameona kutokuwiana katika nadharia ya Sunni ya serikali. Ufuatao ni ushahidi wa wachache wao:

H. A. R. Gibb:

"Nadharia ya Kisunni juu ya serikali ilikuwa, kwa kweli, ni kuongeza ufanisi historia ya jamii. Bila ya vigezo, hakuna nadharia, na mfumo wote wa kuvutia wa tafsiri ya vyanzo vyake, ni utetezi tu baada ya matukio (post eventum?), wa vigezo ambavyo

vimeidhinishwa kwa ijma."

(Studies on the Civilization if Islam, 1962)

321

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Bernard Lewis:

Hitilafu hii kati ya nadharia na vitendo - kati ya maagizo ya kiungwana ya sheria na mambo ya kikatili ya serikali - imewasababisha baadhi ya wanazuoni kuukataa mfumo mzima wa kisiasa na kikatiba wa mafaqih wa jadi wa Kiislam kuwa ni muun-do wa kinadharia na wa bandia, kwa ulivyohusiana kidogo sana na ukweli kama haki za raia zilivyohifadhiwa sana katika katiba za udikteta wa kisasa. Ulinganishaji umetiwa chumvi sana na sio wa haki. Mafaqih wakubwa wa zama za kati za Uislamu hawakuwa wapumbavu wala wapotoshaji - wala wasiojua ukweli, wala wakaidi wa kuulinda huo ukweli. Kinyume chake, walisikitishwa na wasiwasi mkubwa wa kidi-ni, uliotokea hasa kutokana na kutambua kwao lile pengo kati ya mafundisho mema ya Uislamu na zile desturi za mataifa ya Kiislam. Tatizo la waandishi wa kifaqih juu ya serikali lilikuwa zito kuliko lile lililoletwa na tabia ya mtawala mmoja au mwingine. Lilihusu mwelekeo uliochukuliwa na jamii ya Kiislamu kwa jumla tangu siku zile za Mtume (s.a.w.) - mwelekeo ambao umeiongoza jamii hiyo mbali sana kutoka kwenye mambo ya kimaadili na kisiasa ya Uislamu uliobashiriwa. Bado kutil-ia shaka uhalali wa mfumo wa serikali ambao chini yake Waislamu waliishi, kulikuwa ni kupinga imani ya asili ya umma wa Kiislam, hali ambayo haikubaliki kwa ulamaa wa Kisunni, ambao ufafanuzi wao hasa wa imani ya asili unaegemea kwenye vigezo na utendaji wa jamii (ya Kiislamu). Faqih alilazimika kwa hiyo, kwa kiwango fulani, kutetea utaratibu uliopo, ili kuthibitisha imani na mfumo wa Sunni dhidi ya madai kwamba wamepotoka na wamewaingiza Waislamu kwenye hali ya dhambi."

(The chapter on Politics and War published in the volume, Legacy of Islam, 1974)

G. E. Von Grunebaum:

"Katika kuwasilisha wajibu wa khalifa, mtu anahisi juhudi za mashaka za mwandishi za kulinganisha ile kazi kamilifu na mambo duni ya kipindi chake. Sheria imeweka kanuni zisizobadilishika, bila kufikiria kuongezeka kwa kukosa uwezo kwa mtawala wa Waumini katika kutekeleza hata zile kazi zake za wastani kabisa. Hivyo nadharia inalazimika kukubaliana, na kuenea kwa dhana ya uchaguzi kuingiza uchaguzi wa mpiga kura mmoja mwenye mpaka - kwa maneno mengine, kuidhinisha ile hali hal-isi ambamo khalifa anachaguliwa na mtangulizi wake au kiongozi wa kijeshi anayetokea kuwa katika madaraka. Hata uwezekano wa wingi wa viongozi wa jamii itabidi ukubaliwe. Na katika zama zingine na ustaarabu mwingine, nadharia ya mam-laka inakuja kuwa silaha katika kupigania mamlaka."

(Islam, London, 1969)

322

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

John Alden Williams:

"Kauli wakilishi ya namna wanasheria wa Kiislam wa mwishoni mwa kipindi cha kati walivyoyaona matatizo ya madaraka na uongozi wa Kiislam inaonyeshwa na mtu wa Syria wa wakati mmoja na Ibn Taymiya (na ambaye Hanbal kwa kawaida hawakukubaliana naye). Ibn Jama'a (kafa 1333) ambaye alikuwa mmoja wa watu-mishi wakubwa wa utawala wa kidini wa Mamluki, na Qadhi Mkuu wa Cairo kwa mara mbili. Ingawa alikuwa mfuasi wa Shafi'i, kama al-Mawardi, ni maoni ya Ibn Jama'a yanayokubaliana na yale ya Ahmad ibn Hanbal katika maelezo ya kiimani yanayopatikana kwenye mfumo wa imani: Imam aliyeko madarakani atiiwe bila kujali ni vipi ameingia madarakani pale. Katika mgongano kati ya umoja na haki, umoja wa umma lazima uwe na kipaumbele. Kwa nyongeza, yeyote atakayeshika madaraka yenye nguvu katika sehemu yoyote ile lazima atambuliwe na Imamu, kama hana namna yoyote ya kumuondoa. Kwa kifupi, watawala lazima wachukuliwe kana kwamba walikuwa safi, kama wako hivyo au la; haja ya Jamii kulindwa kutokana na makosa iliihitajia. Yalikuwa ni maoni ya kimantiki lakini Ibn Taymiya alihisi kwamba ilikuwa muflisi kimaadili."

(From Imam and Legality. From Emancipated Judgment in the Governance of Muslims. Cha Ibn

Jama'a (d. 1333 A.D.),Al- Ahkam fi Tadbir Ahl al-Islam).

Uimamu uko wa namna mbili: ule wa uchaguzi, na ule wa kunyang'anya. Uimamu wa kuchaguliwa unathibitishwa kwa njia mbili, na Uimamu wa kunyang'anya, kwa njia ya tatu. Njia ya kwanza katika Uimamu wa kuchaguliwa ni kwa kiapo cha wale wenye mamlaka kufungua na kufunga. Njia ya pili ni kwa Imamu kuchaguliwa kama mrithi na yule aliyekuwa mbele yake.

Na kwa njia ya tatu, kukubalika kwa mnyang'anyi kunafanywa halali, inatekelezwa kwa kumshinda mwenye kutumia nguvu halisi, na kama hakuna Imamu kwa wakati huo, na mtu akajiweka mwenyewe ambaye vinginevyo hana sifa ya cheo hicho, na anawashinda watu kwa nguvu zake na kwa majeshi yake bila uchaguzi wowote au kuteuliwa kwenye urithi, basi kukubalika kwake ni halali na mtu analazimika kumtii yeye, ili umoja wa Waislamu uhakikishwe na wanaongea kwa sauti moja. Haina tofauti kama ni mbumbumbu au ni dhalimu, kwa mujibu wa maoni yaliyo sahihi kabisa, na kisha mwingini anainukia na kumshinda yule wa kwanza kwa nguvu zake na majeshi, na yule wa kwanza anaondoswa madarakani, kisha yule wa pili anakuwa ndiye Imamu, kwa ajili, kama tulivyosema, ya ustawi wa Waislamu na umoja wao wa kujieleza. Kwa sababu hii, mtoto wa Umar alisema katika vita vya Harra: "Tuko pamoja na yule mwenye kushinda" (uk. 91).

Kwa kweli, Umma ulikabidhi mambo yake kwa Khalifa, na ulimuomba yeye awe mtawala kamili kabisa. Mbali na swali la kama hii kwa kawaida sio mikingamo -

323

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

maelezo yanayopingana yenyewe, hapakuwa na chombo cha uhakika cha kumchagu-lia yeye au kuhakikisha urithishaji wa amani wa mamlaka yake, na aghalabu au hata kwa desturi watu waliingia kwenye mamlaka kwa njia za kikatili, ambazo zimekatali-wa na sheria. Ulikuwa ni ukweli wa kuhuzunisha kwamba katika mataifa mengi, isipokuwa yale machache kama ufalme wa ukhalifa wa Uthmaniah (Ottoman Empire) na wa Mongolia ambao walifanikiwa katika kuanzisha kanuni ya kurithiana, "hakuna kitu chochote kilichomfaa mtu kwa ajili ya madaraka kama silika za kijinai."

(Themes of Islamic Civilization, 1971, University of California Press, Berkeley)

Mafaqih na wana fikra wa Sunni walikuwa na uwezo wa kufanya marekebisho na maafikiano yasiyokwisha. Walikuwa tayari kuwakubali kama watawala halali, sio tu wale madhalimu na wanyang'anyi wa Kiislamu bali pia hata wasiokuwa Waislamu.

Bernard Lewis:

"Mengi yameandikwa kuhusu Vita vya Kidini juu ya Ulaya. Kidogo hasa kimeandik-wa kuhusu matokeo ya hivi na mapambano mengine yanayofanana na hayo katika nchi za Kiislamu. Kwa mara ya kwanza tangu mwanzo, Waislamu walilazimika kwa kushindwa kijeshi kuachia maeneo makubwa ya nchi ya zamani ya Kiislamu kwa watawala wa Kikristo, na kuacha idadi kubwa ya Waislamu chini ya utawala wa Kikristo. Mambo yote yalikubalika kwa utulivu wa ajabu. Kote Magharibi na Mashariki, watawala wa Kiislamu walikuwa tayari kujihusisha na majirani zao wapya, na hata ikibidi kufanya ushirikiano nao dhidi ya ndugu zao Waislamu - kama wajibu wa Sheria Tukufu - ya kunyenyekea kwa madhalimu, kulikuwa rahisi kuipan-ua hoja hiyo ya kuwahusisha wasiokuwa waumini.'Ambaye madaraka yake yameshinda lazima atiiwe,' alimradi tu kwamba anawaruhusu Waislamu kutekeleza dini yao na kuitii Sheria Tukufu. Eneo la mtawala kama huyo linaweza kuwa pia kuchukuliwa kama sehemu ya Nyumba ya Uislamu."

(Politics and War, kwenye kitabu, Legacy of Islam).

Kifupi na kiini cha uchambuzi huo uliopita ni kwamba nadharia ya Sunni ya kiserikali inaruhusu utaratibu mmoja tu, yaani, mabavu ya kikatili. Takriban mafaqih na wana fikra wote wa Sunni wametoa baraka zao kwenye "utaratibu" huu. Kama utaratibu, mabavu ya kikatili yamekuwa ndio kawaida pekee ya nadharia ya Sunni ya kiserikali tangu Mu'awiyah atwae ukhalifa mnamo A.D. 661. Ina maana kwamba kama mtu anaweza kuhuisha, katika Ufalme wa Mbingnii katika ardhi, sehemu yoyote, ile sheria ya zamani inayojulikana kama "Mwenye Nguvu Mpishe," basi ndiye mtawala wa haki wa umma wa Kiislam. Serikali haina nadharia ya muundo au chombo zaidi ya mabavu ya kidhalimu. Amri za Allah (s.w.t.) zilizohifadhiwa ndani ya Qur'an Tukufu, matakwa, vigezo na amri

324

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

za Mtume Wake (s.a.w.w), na mfumo mzima wa maadili, vyote havifai. Haishangazi sana labda, msimamo huu wa mafaqih wa Sunni unaendelea kuwepo katika nyakati hizi za kisasa. Baraza la Ukhalifa likikutana huko Cairo, Misri, mnamo 1926, lili-weka utaratibu kwamba mwislamu anaweza kihalali kuwa khalifa kama atazatiti madai yake kwa ushindi, hata kama hatatimiza lolote kati ya masharti mengine yanayotakiwa na wanasheria (mafaqih).

Katika uchambuzi wake uliotolewa hapo juu, Dr. Williams amemnukuu Abdullah mtoto wa Umar bin al-Khattab (khalifa wa pili) akisema kwamba yeye (Abdullah) yupo pamoja na mwenye kushinda yoyote yule atakayekuwa. Huyu Abdullah alijulikana kwa uchamungu wake na moyo wa dini na ujuzi. Alitumia au alijaribu kutumia muda wake mwingi akiwa pamoja na Mtume (s.a.w.) kiasi alivyoweza, na kama yeye Abdullah akisema lolote, lilikuwa (na bado) linachukuliwa kama jambo la kuaminika katika mfumo mzima wa Sunni. Inashangaza kwamba hakufikiria kwamba katika mgogoro wowote kati ya watu wawili tofauti au vikundi viwili, suala la haki na batili halikuwa na uhusiano wowote. Kitu cha muhimu pekee kilikuwa ni kushinda. Kwa mujibu wake yeye, yoyote anayeshinda, anayo haki. Kama jambazi anafanikiwa katika kuwaua washindani wake wote na akawa ndiye mshindi wa dhahiri katika kugombania madaraka, basi mantiki ya mafanikio itamfanya yeye kuwa ndio mtu bora kwa nafasi hiyo muhimu na ya juu kabisa katika ulimwengu wa Kiislamu. Anachotakiwa kufanya kuthibitisha kwamba yeye ndiye mgombea mwenye sifa zinazostahili kabisa kwa kiti cha ukhalifa, ni kudhihirisha kwamba anaweza kukitwaa kwa mabavu ya kikatili, na kama atafanya hivyo, kitakuwa ni chake - hakuna sifa katika Uislamu kama mabavu ya kikatili!

Mafaqih, wana-fikra na wachambuzi wa kisiasa wa Sunni wameonyesha msimamo wa kushangaza katika ufafanuzi wao, katika kutetea ile kanuni ya kwamba utii lazima utolewe kwa yeyote aliye na mamlaka mikononi mwake. Hii labda ndio sababu kwa nini utii wa kimyakimya kwa mtawala umekuwepo, kwa maneno ya Elie Kedourie, "desturi ya kisiasa ya kutawala katika Uislamu," na sababu ya kwa nini heshima ya ziada ya Waislamu ime-tolewa kwa ajili ya jambo lililokwisha fanywa na kuhitimishwa; — "mwenendo wake usio na makosa kwenye historia ya Uislamu."

Waislamu wa Shia wanaipuuza nadharia ya Sunni juu ya serikali kwa kukosa kwake muafaka wa kimaadili na kukosa kwake msimamo. Wanasema kwamba kanuni lazima iwe ima ni sahihi au ima lazima itakuwa ya makosa, na kigezo pekee cha kuthibitishia uasili wake kama ni wa kweli au wa uongo ni Qur'an Tukufu. Waislamu wa dunia nzima wanaweza kwa kukubaliana kabisa kuifanya kuwa sheria lakini kama inapingana na Qur'an, haiwezi kuwa ya Kiislamu. Chanzo cha makubaliano ya kimaadili katika Uislamu ni Qur'an, na sio "wingi."

325

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Waislamu wa Shia pia wanasema kwamba lazima pawepo na msimamo katika utekeleza-ji wa Sheria au kanuni. Lakini kama haipo, na "sheria" mpya au "kanuni" mpya inabidi itu-mike kutosheleza kila hali mpya, basi itakuwa isiitwe sera, bali manufaa. Kama ilivy-oelezwa hapo juu, msimamo pekee katika nadharia ya Sunni ya serikali inapatikana kukubaliwa kusiko na sifa, na mafaqih na wanazuoni wa Sunni, kwa "kanuni" kwamba nguvu ndio usuluhishi wa dunia hii, na Waislamu, kwa hiyo, lazima waisujudie (kama hes-hima). Hata Imam Ghazali anasema kwamba "kanuni" hii lazima iungwe mkono kwa sababu ni amri kwa Waislamu ya Qur'an Tukufu yenyewe.

Imam Ghazali ni mmoja wa watu wenye heshima kubwa katika ulimwengu wa Kiislam. Anaonekana kwa ujumla kama mwana-theologia mkubwa sana wa Uislamu wa Sunni. Wanazuoni wa Kisunni wamefika mbali kiasi cha kudai kwamba kama mtu yeyote angeweza kuwa Mtume baada ya Muhammad Mustafa (s.a.w.), angekuwa Ghazali. Na bado, aliwashauri Waislamu kuridhia kimyakimya kwenye mamlaka ya mtu mmoja ya dik-teta au kiongozi wa kijeshi kwa sababu (alisema kwamba) wajibu wao wa kutii mamlaka yaliyopo umeegemea kwenye kitabu cha Qur'an chenyewe: "Mtiini Allah, Mtume Wake na wale wenye mamlaka juu yenu." Inashangaza kwamba mtu kama Imam Ghazali hakuweza kufanya chochote ila kuidhinisha tafsiri isiyo na asili kabisa ya Aya hii.

Qur'an Tukufu, kwa bahati, ni ngeni kwa nadharia zote hizi za serikali na kanuni za vyama vya kisiasa zilizogunduliwa, zilizoelezwa kwa ufasaha na kuwekwa katika mpango wa wazi na wengi wa Waislamu, na hii kwa sababu rahisi, yaani, inayo nadharia yake yenyewe ya serikali na falsafa yake yenyewe ya kisiasa. Haina, kwa hiyo, haja yoyote na nadharia ngeni au falsafa ya serikali.

Falsafa ya kisiasa ya Qur'an imeshughulikiwa katika mlango mwingine katika kitabu hiki.

326

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kugombea Madaraka - 1

Waislamu wa Sunni wanadai kwamba maswahaba wote wa Muhammad Mustafa Mtume wa Allah (s.a.w.) aliyebarikiwa, walikuwa ni mifano ya mwendo wa kuigwa, na kwamba hawakuguswa na uroho wa pesa, tamaa ya madaraka wala malengo yoyote ya kidunia. Wanasema pia kwamba maswahaba wote walipendana wenyewe na kwamba mahusiano yao hayakuchafuliwa na ubeuzi wala husuda.

Hilo, kwa bahati mbaya, liko mbali na ukweli wenyewe ulivyo. Tungependa iwe hivyo lakini ushahidi wa historia hauungi mkono dhana kama hiyo, na mambo ya kikatili yanauchanilia mbali uongo na ufasaha wa usemaji wa wapenzi wa maswahaba waliotu-rithisha sisi. Mpenzi wao mwenye msimamo mkali kabisa hawezi kukataa kwamba kugombea madaraka miongoni mwao kuliibuka hata kabla ya mwili wa Mtume (s.a.w.) haujafanyiwa mazishi. Ushahidi wa historia, kwa hiyo, ungetufanyia uwezekano wa kufanya uchambuzi wenye ukweli zaidi wa tabia ya maswahaba wa Mtume (s.a.w.), na nafasi zao mbalimbali katika historia ya Kiislamu.

Ingekuwa, kwa kweli, ni vigumu kibinadamu kwa maswahaba wote wa Mtume (s.a.w.) kufanana kwa kila hali. Hakuna watu wawili wanaoonyesha mwenendo wa tabia unao-fanana kwenye matukio na mazingira ya nje yao. Kuukubali Uislamu, na usahaba wa Mtume wake (s.a.w.) hakukulazimisha kutakasika silika za kila Mwarabu. Walikuwa ni kundi lililochanganyika. Baada ya kusilimu, baadhi yao walifikia viwango vya juu; wengine walibakia palepale walipokuwa.

Ugumu wa kutathmini nafasi ya sahaba wa Mtume (s.a.w.) umeambatana na upotovu wa tafsiri yake. Kulingana na fasiri moja, mwislamu yeyote aliyemuona Mtume wa Uislamu, alikuwa ni sahaba wake. Waislamu wengi sana walimwona katika miaka 23 ya ujumbe wake kama Mtume wa Allah, na wote hao, kwa hiyo, walikuwa "maswahaba" zake. Lakini Waislamu wa Shia hawaikubali tafsiri hii. Wanasema kwamba cheo cha sahaba kilikuwa ni kitu ambacho Muhammad (s.a.w.) pekee aliweza kukitoa kwa mtu fulani. Kama hakufanya hivyo, basi haikuwa kwa wengine kudai heshima hii.

Waislamu wa Sunni wananukuu "Hadith" ya Mtume (s.a.w.) ambayo anadaiwa kwamba alisema: "Masahaba wangu wote ni kama nyota. Yeyote mtakayetafuta uongofu kwake, mtaupata." Anasemekana pia kwamba alisema: "Masahaba wangu wote ni wema, wenye haki na wakweli."

Kama Hadith hizi ni sahihi, na maswahaba wote wa Mtume (s.a.w.) ni kweli wao ni "nyota," basi kwa ajabu sana, kwa kushangaza sana, moja ya nyota zenyewe; kwa kweli, moja ya nyota yenye kung'ara sana katika kundi zima la nyota la maswahaba, ilionyesha mashaka makubwa juu yao. Nyota husika yenyewe ni Umar ibn al-Khattab, khalifa wa pili wa Waislamu. Sio alionyesha tu kwamba hakukubaliana na Hadith hizi mbili na nyingine

327

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

zinazofanana nazo; bali alizikataa pia. Wakati wa ukhalifa wake mwenyewe, aliwaamuru hao maswahaba wa Mtume (s.a.w.) - hao nyota - kubakia Madina au wasiondoke Madina bila ruksa yake. Yeye kwa hiyo alizuia uhuru wao wa kutembea, na walilichukia sharti hili. Lakini alichukuwa madhila ya kuwaeleza kwamba alikuwa anafanya hivyo kwa maslahi yao wenyewe!

Kuhusu suala hili, Dr. Taha Husein anaandika katika kitabu chake, Al-Fitnatul-Kubra (Mageuzi Makubwa), kilichochapishwa mwaka 1959 na Dar-ul-Ma'arif, Cairo, Misri: Umar alikuwa na sera kuhusiana na Muhajirina wakubwa na Ansari. Walikuwa mion-goni mwa watu wa awali kabisa kuukubali Uislamu, na waliheshimiwa sana na Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Wakati wa uhai wake, aliwaweka wengi wao katika uon-gozi wa mambo muhimu. Umar pia alishauriana nao katika mambo ya maslahi ya jamii, na yeye pia aliwafanya wengi wao kuwa maswahaba na washauri wake. Hata hivyo, alihofia fitna juu yao, na pia alihofia fitna kutoka kwao. Kwa hiyo, aliwazuia hapo Madina, na hawakuweza kutoka nje ya Madina bila ya ruksa yake. Hakuwaruhusu kwenda kwenye zile nchi zilizotekwa isipokuwa pale tu alipowaamu-ru kwenda. Alihofia kwamba watu katika nchi zile "wangewatukuza" wao (kwa sababu ya hadhi yao kama maswahaba wa Mtume (s.a.w.)), na akahofia kwamba hili litaongoza hao (maswahaba) kwenye vishawishi. Aliyaogopa pia matokeo ya "kutukuzwa" huku kwa maswahaba, kwa ajili ya serikali. Hapana shaka kwamba kuzuiwa huku kulichukiwa na wengi wa maswahaba hao, hususan na wale Muhajirina miongoni mwao.

Itakuwa vema tu kama tutaichunguza kwa kuikosoa hii sera ya Umar kuhusiana na kundi hili mashuhuri miongoni mwa maswahaba. Wakati alipowaamuru kubakia Madina, labda alikuwa sawa katika sera yake. Kwa nini tusiviite vitu kwa majina yao halisi? Au, bora zaidi, kwa nini tusiifasiri ile sababu iliyomshawishi Umar kuwazuia maswahaba hapo Madina, kwa istilahi za kisasa? Umar aliogopa kwamba hao maswahaba, kama watakwenda huko kwenye majimbo, wataweza kunywea kwenye vishawishi vya kutumia uwezo na hadhi zao!

Kama matukio yaliyofuata baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.) yatatazamwa katika mazingi-ra yake ya kibinadamu, itatoa kinga ya kuhimili mshituko kwa wale wanaotegemea maswahaba kuwa Malaika, lakini wawaone ni wamoja, watu wa kawaida. Kama wengi wa maswahaba walijionyesha wenyewe kama watu wanaoendeshwa na tamaa na maslahi binafsi baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.), ilikuwa ni kwa sababu wakati wa uhai wake hawakuwa na matumaini wala fursa ya kuwatambua wao. Lakini mara tu baada ya kufari-ki kwake,walijihisi kwamba walikuwa huru kuandama malengo yao wenyewe katika maisha.

Mtazamo wa kimapokezi wa Sunni kwenye ukadiriaji wa nafasi ya maswahaba umekuwa kile Thomas Fleming alichokiita "mtazamo wa mng'aro wa dhahabu." Mtazamo huu unamwelezea kila mmoja wa maswahaba kama muungano wa shujaa-mtakatifu na mwenye kipaji. Lakini uelezaji huu sio wa kweli kwa maisha, na kwa sababu sio wa kweli,

328

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

unawatoa kwenye kitovu cha kuonekana vizuri. Maoni yenye ukweli zaidi yangekuwa kwamba hao maswahaba walikuwa binadamu kama watu wengine wote, na kwamba wao pia wangeweza kunywea kwenye vishawishi vya kunufaika na fursa au mamlaka yaliyoko mikononi mwao.

Lord Action, mwanahistoria maarufu wa Uingereza, na mwenyewe akiwa mfuasi wa Katoliki, wakati mmoja alitoa onyo lifuatalo kwa wale watu ambao walitoa visingizio kwa ajili ya matendo maovu kupindukia ya Mapapa wa Ufufuko Mpya wa Kanisa Katoliki:

"Siwezi kukubali sheria zenu za kanisa kwamba tuwahukumu Papa na Mfalme tofau-ti na watu wengine, kwa ufidhuli wa upendeleo kwamba hawakufanya kosa lolote...madaraka yanaelekeza kwenye maovu, na mamlaka kamili hupotosha kikamilifu.. Hakuna uasi mbaya kuliko ule ambao ofisi inamtakasa mbebaji wake."

Qur'an Tukufu imetoa sifa nzito kwa wale Waislamu waliothibitisha wao wenyewe kus-tahiki usahaba wa Muhammad (s.a.w.). Lakini pia imewaonyesha wale wale miongoni mwao ambao hawakustahili usahaba huo. Aya nyingi zilishuka katika kuwakosoa kwao.

Sifa za maswahaba wengi wa Mtume (s.a.w.) zilichafuliwa na husuda. Kinyongo chao kwa kuchaguliwa kwa Usamah bin Zayd bin Haritha kama Kamanda Mkuu wa msafara wa Syria, kilikuwa ni udhihirisho wa wazi wa husuda hii. Katika miaka ya baadae, chuki hiyo hiyo ilisababisha kuuawa kwa khalifa mmoja, na ikasababisha maasi dhidi ya mwingine.Si wengi miongoni mwa maswahaba waliofanya jitihada za makusudi kuzuia chuki zao kwa maslahi makubwa ya Uislamu, na ya umma wa Mtume (s.a.w.).

Migogoro ya maswahaba ina muda mrefu tangu iingie kwenye historia. Iwezekane, kwa hiyo, kwa mwislamu wa kisasa kuamka juu ya misimamo ya jazba ya kizamani, na waan-galie kwa makini ule "utendaji wa zamani" wa wao wote. Inaweza ikawa vigumu lakini inawezekana kufanya hivyo ikiwa madhumuni ya kujitolea kwake sio watu bali ni ukweli tu. Kilicho muhimu hata hivyo, ni kuelewa na sio hisia!

Muhammad Mustafa (s.a.w.), alikwisha "mtawaza" rasmi Ali ibn Abi Talib kama mrithi wake huko Ghadir- Khum, na alikwisha mtangaza kama kiongozi wa baadae wa Waislamu wote. Walikuwepo maswahaba wachache waliokuwa wanatambua kwamba vitendo vya Mtume (s.a.w.) vilikuwa havina shaka. Waliamini kwamba vitendo vyake vyote vilikuwa ni msukumo kutoka mbingnii, na kwamba havikuchochewa na ukabila wowote. Walijua kwamba ikiwa amemnyanyua Ali kama Kiongozi Mkuu wa Dola ya Kiislamu, ilikuwa ni kwa sababu Ali alikuwa na sifa zote muhimu kwa ajili ya madaraka kama hayo.

Lakini kulikuwa na kikundi kingine cha maswahaba ambacho kiliamini kwamba Mtume (s.a.w.) hakuwa huru kabisa kutokana na hisia za asabiyya (mshikamano wa kikabila; aina ya utaifa wa kikabila; "kabila langu, liwe sawa au na makosa;" mapenzi ya moyo wa ukoo). Waliyahusisha matangazo na kauli zake zinazoonyesha ubora wa Ali, kwenye asabiyya yake. Utawala wa Ali haukukubalika kwao. Walijiona wao wenyewe ni wenye

329

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

sifa nzuri tu kuweza kuongoza Dola changa ya Madina kama Ali, na walitambua kwamba ili kuiendesha hasa, walipaswa kuchukua hatua kabla muda haujapita sana.

Kulikuwa na njia moja tu kwa watu wa kundi hili ya kufanikisha lengo lao, nayo ilikuwa ni kuiteka Dola ya Madina katika muda muafaka. Wakiwa na shabaha hii mawazoni mwao, walianza kutangaza imani yao wenyewe, yaani, kwamba Utume na ukhalifa havipaswi kuchanganyika katika nyumba hiyo hiyo. Hakukuwa na njia yoyote ya wao kuuondoa Utume kwenye nyumba ya Muhammad (s.a.w.) bali labda ilikuwa inawezekana kuuondoa ukhalifa humo.

Waliamua kujaribu. Kampeni hiyo ilifunguliwa na Umar bin al-Khattab. Yeye alikuwa ndiye kiongozi wa kikundi hicho kilichotaka kuteka serikali. Kwenye kumbukumbu yapo mahojiano mafupi aliyowahi kufanya, wakati wa utawala wake, na Abdullah ibn Abbas, ambamo alisema kwamba kwa vile Mtume (s.a.w.) alikuwa ni wa ukoo wa Bani Hashim, "Waarabu" hawakupenda lile wazo la kwamba na khalifa pia awe ni mtu wa ukoo huo huo. Mahojiano hayo yalikwenda kama ifuatavyo:

Umar: Ninaelewa kwamba Waarabu walikuwa hawakutaka kwamba ninyi (Bani Hashim) muwe ndio viongozi wao.

Abdullah ibn Abbas: Kwa nini?

Umar: Kwa sababu hawakulipenda lile jambo la kwamba mamlaka yote ya kiroho na kidunia yawe ni haki ya pekee ya Bani Hashim kwa wakati wote.

Abbas Mahmoud Al-Akkad, mwanahistoria wa kisasa wa Misri, anasema katika kitabu chake, 'Abqariyyat al-Imam Ali, kilichochapishwa Cairo mnamo mwaka 1970:

Umar aliielezea sababu katika kauli ifuatayo, kwa nini baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.), Ali hakuweza kuwa mrithi wake:

"Maquraishi walichagua khalifa kutokana na hiari yao wenyewe. Hawakuwa tayari kuona kwamba Utume na Ukhalifa vyote viwe ni mali ya Bani Hashim."

Maquraishi hawa ambao walisukumwa na tamaa yao ya kutwaa serikali ya Muhammad (s.a.w.), waliunda mpango uliofanywa kwa uangalifu sana, kwa ajili ya azma hii, wasiache chochote cha kuhatarisha.

Bukhari, Abu Daud na Tirmidhi (wakusanyaji wa Hadith) wamemnukuu Abdullah Ibn Umar bin al-Khattab akisema:

Katika wakati wa Mtume (s.a.w.) tulikuwa tumezoea kusema kwamba watu bora katika umma ni Abu Bakr, Umar na Uthman."

(The Virtues of the Ten Companions - cha Mahmud Said Tantawi wa The Council of

Islamic Affairs, Cairo, Egypt, 1976) John Alden Williams

330

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Ahmad bin Hanbal amesema: "Wabora wa umma huu - baada ya Mtume (s.a.w.) -ni Abu Bakr al-Siddiq, kisha Umar ibn al-Khattab, kisha Uthman ibn Affan. Tunatoa upendeleo kwa wale watatu (juu ya Ali) kama maswahaba wa Mtume (s.a.w.) walivy-owapendelea. Hawahitilafiani katika hilo. Kisha baada ya wale watatu wanakuja wale Wapiga Kura Watano (Ashab as-Shura) walioteuliwa na Umar alipokuwa anafariki: Ali ibn Abi Talib, Zubayr, Talha, Abd al-Rahman ibn Auf, na Sa'd ibn Abi Waqqas. Wote hao walifaa kwa ukhalifa, na kila mmoja wao alikuwa Imam. Katika hili tunakwenda kwa mujibu wa Hadith ya mtoto wa Umar:

Wakati Mtume wa Allah alipokuwa hai - rehma juu yake na amani - na maswahaba zake wakiwa bado wapo, tulikuwa tukiwahesabu kwanza Abu Bakr, kisha Umar, kisha Uthman, na kisha tukanyamaza kimya."

(Baadhi ya Mafundisho Muhimu ya Hanbali kutoka kwenye Maelezo ya Kanuni za Imani).

(Themes of Islamic Civilization, 1971)

Maelezo ya Abdullah ibn Umar ni uthibitisho kwamba njama za kumnyanyua Abu Bakr, Umar, na Uthman juu ya Ali, zilianzishwa wakati wa uhai wa Mtume (s.a.w.) mwenyewe, kwa matarajio, na matayarisho kwa ajili ya nyakati za mbele. Maquraishi walikwisha kua-mua kabla ni nani watakuwa viongozi wa umma baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.), na kwa mpangilio gani.

Wakati Mtume wa Allah (s.a.w.w) alipofariki, Abu Bakr hakuwepo Madina; alikuwa nyumbani kwake huko Sunh, kitongoji cha Madina. Lakini Umar alikuwepo kwenye tukio hilo. Alichomoa upanga wake na akaanza kupiga kelele:

"Wanafiki wanasema kwamba Mtume wa Allah (s.a.w.w) amekufa. Lakini hakufa. Yuko hai. Amekwenda, kama Musa alivyokwenda, kumuona Mola Wake, na atarudi baada ya siku arobaini. Kama mtu yeyote atasema kwamba amekufa, nitamuua." Waislamu wengi waliingiwa na wasiwasi walipomsikia Umar akijitapa kwa hasira. Kwa kupunga upanga wake, na kwa kutishia kuua, alifanikiwa katika kuwanyamazisha watu. Baadhi yao walifikiri kwamba anaweza akawa anasema kweli, na Mtume (s.a.w.) anaweza akawa hakufariki. Baadhi ya wengine walianza kunong'onezana na kujiuliza kama Mtume (s.a.w.) alikuwa amefariki kweli. Lakini wakati huo Abu Bakr aliwasili pale Msikitini na akasoma Aya ifuatayo ya Qur'an Tukufu mbele ya umati wa Waislamu:

Usahihi-39.jpg

"Hakuwa Muhammad ila ni Mtume tu. Wamekwishapita kabla yake Mitume. Je, akifa au akauawa ndio mtageuka mrudie ya nyuma? Na atakayerudi nyuma huyo hatamdhuru kitu Allah. Na Allah atawalipa wanaomshukuru."(SW« 3; Aya ya 144)

331

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Waislamu walipoisikia Aya hii, waliridhika kwamba Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w.), alikuwa tayari amekwishafariki, na haukubakia wasiwasi wowote juu ya hilo kwenye akili ya mtu yoyote.

Kama ilivyoonyeshwa kabla, Umar hakumwacha Muhammad Mustafa (s.a.w.) aandike mirathi na wosia wake wa mwisho akihofia kwamba atamtaja Ali kama mrithi wake. Kisha Mtume (s.a.w.) akafariki. Lakini katika ule muda kati ya kufa kwa Mtume (s.a.w.) na kuwasili kwa Abu Bakr, Umar alikuwa bado ana hofu wasije wale Waislamu waliokuwe-po pale Msikitini, wakamtambua Ali kama kiongozi wao. Ili kuwahi kuvuruga uwezekano huu, alichomoa upanga wake, na akaanza kupiga makelele kwamba Muhammad (s.a.w.) hakufa bali alikuwa hai ili isijetokea kwa mtu yeyote kwamba kiongozi mpya wa umma anapaswa kuchaguliwa. Umar alikuwa anamaanisha kwa njia hii kwamba wakati Mtume (s.a.w.) akiwa bado yuko hai, ni nani atahitaji mrithi; baada ya kuwa warithi wote walikuwa ni kwa ajili ya wafu na sio kwa waliohai! Wanasiasa wengi, wakati wote kabla na tangu ya Umar, wameficha taarifa za kifo cha mfalme au mkuu wa nchi kwa wananchi mpaka mrithi wake awe amekwisha chaguliwa.

Kifo cha Mtume (s.a.w.) kilikuwa ni kweli. Lakini Umar angemuua mtu kama angeueleza ukweli huo? Angemuua mtu kwa kusema ukweli? Hivi ni dhambi mtu kusema kwamba mtu aliyekufa amekufa, na adhabu ya kusema hivyo ilikuwa ni kifo?

Kuwathibitishia Waislamu kwamba Muhammad (s.a.w.) alikuwa hajafariki, Umar akaleta mfano kama wa Musa. Lakini mfano huo uliingiwa na dosari ya dhahiri. Bani Israil wal-imwona Musa akiondoka sehemu waliyokuwa mpaka alipopotea machoni mwao. Lakini mwili wa Muhammad Mustafa (s.a.w.) ulikuwa umelala chumbani kwake, na haukuondo-ka machoni mwa mtu yeyote. Waislamu, pamoja na Umar mwenyewe, waliweza kuuona, na kuugusa, na kuuhisi kwamba ni wa baridi na usio na uhai.

Mwandishi wa Kihindi wa wasifa wa Umar, M. Shibli, na wengineo wanasema kwamba yeye (Umar) alikuwa akitishia kuwauwa Waislamu kwa kutokana na mapenzi yake juu ya Muhammad (s.a.w.). Alikuwa, wanavyosema, katika hali ya mshituko. Na alikuwa anashindwa kushikamana na ukweli! Umar alikuwa kati ya miaka ya hamsini wakati Mtume (s.a.w.) alipofariki.

Je, inawezekana kwamba hajawahi kumuona mtu yoyote akifariki, na alikuwa hajui kufa kuna maana gani?

Ukweli unaotisha ni kwamba Umar alikuwa akijifanya tu. Kujifaragua kwake kulikuwa ni pazia la nia yake halisi. Kusisitiza kwake kwamba Muhammad (s.a.w.) alikuwa hajafa, kulikuwa ni moja kati ya mfululizo wa mbinu kuficha mahali maalum pa mamlaka na uon-gozi kwenye macho ya watu. Wakati fulani alikuwa tayari kumuua mtu yeyote kwa kuse-

332

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ma kwamba Mtume (s.a.w.) amekufa lakini muda mfupi unaofuatia tu, pale Abu Bakr alipotokea, na kusoma Aya kutoka kwenye Qur'an, akawa mbadilikaji wa mara moja kwenye wazo la kwamba yeye Mtume (s.a.w.) alikuwa ni binadamu, anaweza kufa, na amekufa kweli. Alikiri pia kutokujua kwake Qur'an, na akasema kwamba imeonekana kwake kama ni mara ya kwanza kuisikia ile Aya ambayo Abu Bakr alimsomea yeye na Waislamu wengine ndani ya Msikiti.

Kuwasili kwa Abu Bakr kulimtuliza Umar, na akili zake zote zikamrudia kabisa. Kisha akakimbilia, pamoja na Abu Bakr, kwenda Saqifah, kutoa madai ya ukhalifa, na kuuteka kabla ya Maansari kuweza kuuteka. Mazishi ya mwili wa Mtume (s.a.w.) yalikuwa ni kitu wanachoweza kuwaachia watu wa familia yake mwenyewe.

Njama za Umar za kuthibitisha kwamba Muhammad Mustafa (s.a.w.) alikuwa hai, zilivun-jika ghafla. Alikuwa na uwezo, hatimae, wa kuweza kukubaliana na ukweli! Kanuni ya sheria ya zamani ya Kirumi ni kwamba suppressio veri ni sawa na suggestio falsi. Hii ina maana kwamba kuficha ukweli ni sawa na kueneza uongo!

Mwanzoni, katika mlango huu, nilinukuu kifungu kutoka kwenye kitabu, Al-Fitnatul-Kubra au mageuzi makubwa, cha Dr. Talha Husein, kuhusu kizuizi kilichowekwa na Umar bin al-Khattab, khalifa wa pili wa Waislamu, juu ya uhuru wa kutembea wa Muhajirina.

Umar aliwakataza Muhajirina kuondoka Madina bila ya idhini yake. Lakini walikuwa ni akina nani hawa Muhajirina ambao walikatazwa kuondoka Madina? Muhajirina wote walikuwa wameondoka Madina - ukiwaacha wawili tu, yaani, Uthman bin Affan na Ali ibn Abi Talib!

Kwa vile Uthman alikuwa na uwezo mdogo wa utekaji au uongozi, angeweza kuwa amekaa Madina kwa hiari yake, Umar, kwa hiyo, ilimbidi aitekeleze sheria hii kwa ajili ya Ali pekee.

Umar hakuweza kutamka wazi kwamba kati ya Muhajirina wote, Ali peke yake haruhusi-wi kuondoka Madina. Ni kwa sababu gani Umar angeweza kumkataza Ali kuondoka Madina? Inavyoonekana hakuna. Yeye, kwa hiyo, ilimbidi atumie istilahi ya jumla ya "Muhajirina" kuzuia uhuru wa Ali wa kutembea.

Hata hivyo, alikuwa ni Ali, kama akiwa yeyote, ambaye asingeshawishika kutumia sauti yake juu ya jeshi, kama hicho ndicho Umar alichokuwa akikiogopa.

333

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kugombea Madaraka - 2

Mkutano wa Ansari ndani ya Saqifah

Mnamo A.D.622, ansari walimkaribisha muhammad (s.a.w.w.), mtume wa Allah (s.a.w.w) aliyebarikiwa, huko Madina, na walimkubali kama kiongozi wao wa kiroho na kidunia. Waislamu wengine wa Makka, yaani Muhajirina, pia walihamia Madina, na Ansari wakawakaribisha kwa mikono miwili. Walishirikiana nao majumba yao na chakula chao. Katika nyakati nyingi, waliwanyima watoto wao wenyewe chakula ambacho walikitoa kwa Muhajirina wenye njaa.

Muhammad (s.a.w.) aliifanya Madina kuwa makao makuu ya Uislamu, na kwa wakati huo, mji huo ukaanza kuchukua sifa bainifu za dola. Jinsi muda ulivyoendelea, ule mji mdogo dola ulikua na kuwa serikali imara yenye vyanzo vyake vya mapato, hazina yake, jeshi, mfumo wa sheria na utawala na vyombo vya kidiplomasia.

Ilikuwa haikwepeki kwamba itakuja kutokea kwa Ansari (na Waislamu wengine) kwamba siku itafika ambapo Muhammad (s.a.w.), mwanzilishi wa Dola ya Madina, atakuja kuwaa-ga na atakuja kuiaga dunia hii. Uwezekano huu uliwakabili pamoja na maswali mapya au hasa magumu kama vile:

1.  Kifo cha Muhammad Mustafa (s.a.w.) kitakuwa na athari gani kwa Dola changa ya Madina na kwa umma wa Kiislam?

2.  Ni nani atakayemrithi Muhammad (s.a.w.) kama kiongozi mpya wa Dola ya Madina wakati atakapofariki?

3.  Ni ipi itakayokuwa hali ya Ansari baada ya kifo cha Muhammad (s.a.w.)? Huyo kiongozi mpya atakuwa maridhawa tu na muadilifu kama alivyo

yeye?

4.  Hivi Ansari wataendelea kuwa mabwana katika nchi yao wenyewe - Madina -baada ya kifo cha Muhammad (s.a.w.)?

Ansari walikuwa wamesikia ile hotuba ya Mtume. wa Allah (s.a.w.w) pale Ghadir-Khum akimteua Ali kama mrithi wake, na waliuunga mkono kwa moyo wote utaratibu huu. Lakini pia waliuhisi ule mkondo wa kichinichini wa uadui wa Muhajirina kwa Ali, na hawakuwa na hakika kama urithi wake utakuwa salama au kama utafanyika kamwe. Ilikuwa ni dhahiri kabisa kwao kwamba kulikuwa na upinzani mkubwa, miongoni mwa Muhajirina, juu ya urithi wake, na kwamba, miongoni mwao, alikuwa yu peke yake. Mara

334

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

tu Ansari walipoupata ukweli huu, walianza kujishughulikia wao wenyewe. Ilikuwa ni kwa sababu hii ndipo wakajikusanya ndani ya Saqifah.

Mtu anaweza akakipuuza kitendo hiki cha Ansari hata kama mtu hatakisifu kwa sababu wazo kubwa sana katika akili zao, kufuatia kifo cha bwana wao, Muhammad (s.a.w.), lilikuwa ni la kujilinda. Ingawa walipaswa kuahirisha mkusanyiko wao wa kisiasa mpaka baada ya mazishi ya mwili wa bwana wao, kwa wakati huo ilijitokeza kwao kwamba walipaswa kushughulika mara moja, vinginevyo watakuwa wamechelewa sana.

Kama ilivyoelezwa kabla, Ansari walikuwa wametoa hifadhi kwa Uislamu katika wakati ambapo hali yake ilikuwa nyonge sana. Kwa ajili ya Uislamu, wamewafanya Waarabu wote kuwa maadui zao. Kwa ajili ya Uislamu, wamejidharaulisha mbele ya Arabia yote. Katika kila vita ya Kiislam, walijitoa wenyewe kwa heshima kabisa. Wengi wa vijana wao wameuawa kwenye vita hivi. (Katika vita vya Uhud, Waislamu 75 waliuawa; kati yao wanne walikuwa Muhajirina, na waliobakia wote walikuwa Ansari). Walionyesha mapen-zi yao kwa Uislamu na utii wao kwa Mtume (s.a.w.) katika kila sehemu.

Ansari walijua kwamba Ukhalifa ulikuwa ni haki ya Ali lakini walijua pia kuhusu "azimio" la Waarabu la kuuondoa ukhalifa nje ya nyumba ya Mtume (s.a.w.). Tafsiri yao juu ya "azimio" hili lilikuwa kwamba Muhajirina hawatamuachia Ali akifikie kiti cha ukhalifa.

Lakini kama sio Ali, basi ni nani mwingine atakayekuwa mrithi wa Muhammad (s.a.w.)? Jibu pekee la wazi kwa swali hili lilikuwa: Ni Muhajirina mwingine. Lakini Muhajirina yeyote mwingine mbali na Ali alikuwa hakubaliki kwao - kwa Maansari. Wao, kwa hiyo, waliamua kuweka mgombea wao wa uongozi wa umma. Hata hivyo, ilikuwa ni msaada wao, uliokuwa sababu, na sio msaada wa Muhajirina, ambao uliofanya Uislamu kuwepo.

Wasiwasi wa Ansari ni wenye kueleweka vizuri sana. Kwao wao, matarajio ya Dola ya Madina kuangukia kwenye mikono ya Bani Umayya, maadui wa jadi wa Allah (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.), ambao sasa wamekuwa Waislamu, yalikuwa ya kuchukiza sana. Wao (Ansari) walikuwa wamewaua wengi wao katika vita vya Kiislam. Kama Dola ya Madina ambayo iliimarika kwa msaada wao, ikawa kamwe imetekwa na watoto wa wale wapagani ambao wao Ansari waliwaua, watawatendea vipi hao Ansari, lilikuwa ndio swali lisilotamkika lililo ndani ya moyo wa kila Ansari. Matukio yalithibitisha kwamba hofu yao haikuzalika kutokana na ndoto yoyote ile.

Bani Umayya walipigana kwa chuki sana dhidi ya Uislamu na Mtume Wake. Wakati Mtume (s.a.w.) alipoiteka Makka, wao "walisilimu" kwa sababu hakukuwa na chochote cha kufanya tena. Kama ilivyoelezwa kabla, Mtume (s.a.w.) hakuwapa kamwe nafasi yoyote ya madaraka ingawa aliwapa sehemu kubwa kutoka kwenye ngawira ya vita ya Hunayn. Kwa upande wake yeye, ilikuwa ni kitendo cha ishara ya mapatano lakini

335

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

haikupunguza uadui wao kwa Uislamu.

Lakini Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.w.t.) hakuwa amekufa kwa muda mrefu wakati Abu Bakr alipowainua hawa maadui wa jadi wa Uislamu, na maadui wa kiukoo wa Mtume wake (s.a.w.), kwenye vyeo vikubwa ndani ya jeshi. Alimfanya Yazid, mtoto wa Abu Sufyan, kuwa jenerali katika jeshi lake. Wakati Syria ilipotekwa, Umar ambaye alim-rithi Abu Bakr kama khalifa, alimfanya huyo Yazid kuwa gavana wa kwanza huko. Yazid alikufa miaka michache baadae ambapo Umar akamfanya mdogo wake, Mu'awiyyah, kuwa gavana mpya wa Syria. Kana kwamba alikuwa hajafanya ya kutosha kwa Bani Umayya, Umar, akiwa kwenye kitanda cha mauti yake, aliitengeneza hali katika namna ambayo ilihakikisha urithi wa Uthman, Bani Umayya mwingine. Katika ukhalifa wa Uthman, watu wa ukoo wake, Bani Umayya, walikuwa wakitawala kila jimbo katika himaya hiyo na walikuwa wakiongoza kila idara katika jeshi.

Ansari walihofia pia kwamba kama Muhajirina wataitwaa Dola ya Madina, basi wao (Muhajirina) wataidhalilisha misaada yao Ansari kwa Uislamu, na watawashusha kutekeleza wajibu, kama utakuwepo wowote, mdogo sana ndani ya Uislamu.

Kwa kujaaliwa na ujuzi wa kubashiri hali ya mambo kama walivyokuwa, Ansari walifanya uchambuzi sahihi na wa kweli wa hali hiyo. Mkusanyiko wao pale Saqifah ulikuwa moja kwa moja ni wa asili ya kujilinda. Ulichochewa na hisia tu za kupona. Lakini kwa bahati mbaya, waling'ang'ania husuda yao wenyewe. Husuda yao ilisababisha malengo yao yasi-fanikiwe. Tabaka zao za kikabila - Aus na Khazraji - zilitiliana shaka, na ilikuwa ni shaka hii ambayo iliwafichua kwa Muhajirina.

Kama ilivyokwisha kuelezwa, kitendo kile cha Ansari cha kukusanyika pale Saqifah kinaleta wasiwasi, lakini hisia yao ilikuwa na maana. Matukio ya baadae yalithibitisha vyakulitosha kwamba walikuwa sahihi na walikuwa na sababu ya kuhoji nia za Muhajirina juu yao. Miongoni mwa Muhajirina, mlinzi pekee wa maslahi yao alikuwa ni Ali ibn Abi Talib. Lakini pale Maquraishi walipofanikiwa katika kumpinga asiingie madarakani, wal-ifanikiwa pia katika kuwateremsha hadhi hao Ansari mpaka kwenye hali ya watu wa kawaida tu.

Muhammad (s.a.w.) alipokufa, na urithi wa Ali kuzuiwa, Ansari walikoma kuwa mabwana nyumbani kwao wenyewe - Madina!

336

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kugombea Madaraka - 3

Saqifah Banu Sa'ida

Bukhari amemnukuu Umar bin al-Khattab akisema:

"Wakati yeye (Mtume (s.a.w.) alipofariki, Maansari walitupinga sisi. Walijikusanya ndani ya Saqifah Banu Sa'ida. Ali, Zubayr na marafiki zao pia walitupinga."

Ni nini hicho ambacho Umar na marafiki zake walichokuwa wakikifanya, na ambacho Maansari walikipinga?

Wakati Mtume (s.a.w.) alipofariki, Maansari, siku zote wakiwa wepesi kuhisi mikondo ya kichinichini ya kisiasa, na wenye hofu na tamaa na dhamira za Muhajirina, walijikusanya katika ukumbi nje ya Madina unaoitwa Saqifah, na walimwambia Saad ibn Ubada, kion-gozi wao, kile walichokijua juu ya mipango ya Muhajirina. Saad alikuwa mgonjwa na akamwambia mwanae, Qays, kwamba yeye alikuwa hakujihisi kuwa na nguvu za kutosha kuhutubia huo mkutano, na kwamba atamweleza alichotaka kukisema, na yeye Qays akakirudie kwa waliohudhuria.

Saad akaongea na mwanae, naye akafikisha maana yake kwa Ansari.

Hotuba ya Saad

"Enyi kundi la Ansari! Mnao umuhimu katika Uislamu ambao hakuna mtu anayeweza kuukataa, na hili peke yake linakufanyeni ninyi kuwa kitu maalum katika Arabia yote. Mtume wa Allah (s.a.w) alihubiri Uislamu miongoni mwa watu wake mwenyewe kwa miaka 13 na ni wachache wao tu walioukubali ujumbe wake. Walikuwa wanyonge sana kiasi kwamba walikuwa hawana uwezo wa kumlinda yeye au kutetea Uislamu. Allah (s.w.t.) katika baraka Zake alipendelea kuweka heshima ya kumlinda Muhammad (s.a.w.) juu yenu. Alikuchagueni ninyi mbali na watu wengine kutoa hifadhi kwa Mtume Wake na Waislamu wengine kutoka Makka. Aliridhia kuuimarisha Uislamu kupitia kwenu ili kwamba mpigane na maadui wa dini Yake. Mmemlinda Mtume Wake kutokana na maadui zake mpaka ujumbe wa Uislamu ukaenea katika Arabia yote. Kupitia panga zenu ameiteka Arabia kwa ajili ya Uislamu, na ilikuwa ni kwa kupitia panga zenu kwamba wapagani wote walishindwa. Kisha wakati ukafika ambapo Mtume wa Allah (s.a.w) aliiaga dunia hii; alikuwa radhi juu yenu alipokuwa akienda mbele za Mola wake. Kwa hiyo, baada ya kifo chake, ni haki yenu kuitawala Arabia."

337

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ansari walionyesha makubaliano ya pamoja na Saad, na wakaongeza kwamba kwa maoni yao, hapakuwepo na mtu aliyestahili zaidi yake kuwa mtawala wa Waislamu wote.

Ilikuwa ni wakati huu ambapo Abu Bakr, Umar na Abu Ubaidah ibn al-Jarrah, waliwasili ndani ya Saqifah. Pale Ansari walipowaona, mmoja wao - Thabit bin Qays - akasimama na kuwaambia kama ifuatavyo:

"Sisi ni waja wa Mungu, na ni wanusuru wa Mtume Wake (s.a.w.). Na ninyi, wakim-bizi kutoka Makka, ni watu wachache tu. Lakini tunajua kwamba mnataka kuiteka Dola ya Madina, na mnataka kutuondoa sisi humo."

(Tabari na Ibn Athir)

Hii ni kauli yenye kufichua. Ina maana kwamba Muhajirina walikuwa wanapanga mipan-go ya kupora mamlaka, na ule mkusanyiko wa Ansari mle Saqifah ulikuwa ni jibu tu la mwanzo wa jambo lao.

Wakati Thabit bin Qays alipofanya ufichuzi huu, hakuna hata mmoja kati ya Muhajirina hawa watatu aliyempinga. Umar anasema kwamba pale Thabit bin Qays alipokaa chini, yeye alisimama na kuongea kitu kinachofaa. "Nilikuwa nimeandaa hotuba nzuri sana niki-tarajia tu jambo kama hili," alisema. (Tarikh-ul- Khulafa).

Huku ni kukubali kwa Umar mwenyewe kwamba alikuwa amefanya maandalizi yaliy-ochanganuliwa kabla kukabiliana na dharura yoyote ile. Lakini Abu Bakr alimzuia, na yeye mwenyewe akasimama kuwahutubia Ansari.

Alisema:

"Hakuna shaka kwamba Allah (s.w.t.) alimtuma Muhammad (s.a.w.) na Imani ya kweli na nuru ya dini Yake. Yeye (Muhammad) kwa hiyo, aliwaita watu kwenye dini ya Allah (s.w.t.) Tulikuwa wa kwanza kuitikia wito wake. Tulikuwa wa kwanza kuukubali Uislamu. Yeyote aliyesilimu baada yetu sisi, alifuata kutangulia kwetu. Zaidi ya hayo, sisi tuna uhusiano na Mtume wa Allah (s.a.w.w), na sisi ndio wenye sharafu kubwa zaidi ya Waarabu wote kwa damu na nchi. Hakuna kabila lisilotambua mamlaka ya Maquraishi, na nyie, Maansari, ndio mliotoa hifadhi na mliosaidia. Nyinyi ni ndugu zetu katika imani. Tunawapenda na kuwathamini ninyi kuliko watu wengine. Lakini viongozi lazima wawe wanatoka kwa Maquraishi. Sisi tutakuwa ndio watawala na nyie mtakuwa mawaziri. Msione wivu juu yetu. Mmetusaidia sisi huko nyuma, na sasa hampaswi kuwa wa kwanza kutupinga sisi. Ninawaombeni mtoe viapo vyenu vya utii kwa mmoja wa hawa watu wawili, Umar au Abu Ubaidah. Nimewateua wote wawili kwa sababu hii; wote wanastahili heshima hii, na wote wana sifa zinazafaa kwa cheo cha Amir."

338

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad Husein Haikal:

"Umar na Abu Bakr walikuja kwenye uwanja wa Saqifah. Wakifuatiwa na idadi ya Muhajirina, walikalia viti vyao katika mkutano huo. Mara, mzungumzaji akasimama na kuwahutubia Ansari kama ifuatavyo: "Sifa zote na shukrani ni zake Allah (s.w.t.) Sisi ni Ansari, yaani Wasaidizi wa Allah (s.w.t.) na sisi ni jeshi la Uislamu. Ninyi, Muhajirina, ni watu wachache tu katika jeshi hilo. Hata hivyo, mnajaribu kutun-yang'anya sisi haki yetu ya uongozi."

Kwa kweli, kwa Ansari, lilikuwa ni lalamiko la siku nyingi, hata katika wakati wa uhai wa Mtume (s.a.w.). Sasa pale Umar alipolisikia tena, alichukia sana, na alikuwa tayari kulikomesha kwa upanga kama ikibidi kuwa lazima. Lakini Abu Bakr alimzuia na akamuomba kuwa muungwana. Yeye kisha akawageukia Ansari na akasema: "Enyi Ansari! Tunayo jadi na kizazi kitukufu sana. Sisi ndio tunaoheshimiwa sana na kutukuzwa mno na vilevile ndio tulio wengi sana katika kundi lolote ndani ya Arabia. Zaidi ya hayo, sisi ndio ndugu wa damu wa karibu sana wa Mtume (s.a.w.). Qur'an yenyewe imetoa upendeleo kwetu sisi. Kwani ni Allah (s.w.t.) Mwenyewe - Yeye ashukuriwe na atukuzwe - Ambaye amesema, Wa kwanza kabisa walikuwa ni Muhajirina, kisha Ansari, na kisha wale waliowafuata hay a makundi mawili katika wema na uadilifu. Sisi ndio wa kwanza kuhama kwa ajili ya Allah (s.w.t.) na ninyi ni Ansari, yaani, Wenye kunusuru. Hata hivyo, ninyi ni ndugu zetu katika imani, wen-zetu katika vita, na wanusuru wetu dhidi ya maadui. Yote mazuri mliyodai juu yenu ni ya kweli, kwani ninyi ndio wabora zaidi wa wanadamu. Lakini Waarabu hawataukubali uongozi wa kabila lolote isipokuwa la Quraishi. Kwa hiyo, sisi tutakuwa ndio viongozi, na nyie mtakuwa mawaziri wetu." Kufikia hapa Ansari mmoja akasimama na akasema: "Kila uamuzi utategemea juu yetu sisi. Na uamuzi wetu sisi ni kwamba mnaweza kuwa na kiongozi wenu; sisi tutakuwa na wa kwetu." Lakini Abu Bakr akasema kwamba kiongozi wa Waislamu lazima atokane na Quraish, na mawaziri kutokana na Ansari. Kufikia hapa aliishika mikono ya Umar na Abu Ubaidah na akasema: "Yeyote kati ya hawa watu wawili anazo sifa za kuwa kiongozi wa Waislamu. Chagueni mmoja kati yao."

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Lakini Umar alisimama na akasema kwa kupinga: "Ewe Abu Bakr, sio sahihi kwa mtu yeyote kupewa nafasi ya kwanza juu yako we we kwa sababu we we ndio mbora wetu sisi sote.Wewe ulikuwa 'sahaba wa kwenye pango,' na wewe ndiye 'wa pili katika wawili.' Na kuna yeyote aliyesahau kwamba Mtume (s.a.w.) alikuamuru kuongoza Swala wakati alipokuwa mgonjwa? Kwa hiyo, wewe ndiye mtu anayestahili zaidi kuwa mrithi wake."

339

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ansari mwingine alisimama kuwajibu Abu Bakr na Umar, na akasema: "Tunatambua kutangulia kwenu katika Uislamu na sifa zenu nyingine, na tunawapenda pia. Lakini tunao wasiwasi kwamba baada yako, watu wengine wataitwaa serikali, na hawatakuwa wema na waadilifu kwetu. Kwa hiyo, tunashauri kwamba wawepo watawala wawili, mmoja Muhajir na mwingine Ansari (huu ulikuwa ufichuaji mbaya wa kwanza upande wa Ansari wa udhaifu wao wenyewe). Kama huyo Muhajir akifariki, nafasi yake ichukuliwe na Muhajir, na kama huyo Ansari akifariki, nafasi yake ichukuliwe na Ansari mwingine. Kama mkiukubali mpango huu, tutakupeni kiapo chetu cha utii. Huu ndio utaratibu mzuri ambao unaweza kufanywa kwa sababu kama Quraishi anakuwa ndio kiongozi pekee wa dola, Ansari wataishi kwa hofu, na kama Ansari anakuwa Khalifa, Maquraishi wangeishi kwa hofu."

Abu Bakr akazungumza kujibu hivi:

"Allah (s.w.t.) alimtuma Muhammad (s.a.w.) na Kitabu Chake kwa wanadamu. Wakati huo kila mmoja alikuwa akiabudu masanamu. Muhammad alipowaambia wayabomoe masana-mu hayo, wao walilichukia hilo. Hawakutaka kuyatelekeza. Kwa hiyo, Allah (s.w.t.) akawachagua Muhajirina kushuhudia Utume wa Muhammad (s.a.w.). Waarabu waliobakia waliwatukana na kuwatesa Muhajirin, lakini walikuwa imara katika msaada wao kwake. Walikuwa wa kwanza kumuabudu Allah (s.w.t.) na walikuwa wa kwanza kumtii Mtume Wake. Wana uhusiano naye, na wao ni ndugu zake. Kwa hiyo, wao peke yao wanastahili kuwa warithi wake, na hakuna mtu atakayewapinga katika hili isipokuwa madhalimu.

Nanyi, Enyi Ansari! Ni watu ambao ubora wenu haukanushiki. Hakuna mtu anayeweza kuishinda nafasi yenu ya juu katika Uislamu. Allah (s.w.t.) aliwafanyeni ninyi kuwa wanusuru wa dini Yake na Mtume Wake. Na ilikuwa ni kuelekea kwenu ambako alihamia. Kwa hiyo, cheo chenu katika Uislamu ni cha juu kabisa baada ya Muhajirin. Tunakupendeni na kukutukuzeni ninyi. Lakini inastahili tu kwamba vion-gozi watoke kwa Muhajirin na mawaziri kutoka kwa Ansari. Chochote tukachoki-fanya, tutakifanya kwa kushauriana nanyi."

Mzungumzaji aliyefuatia alikuwa ni Hubab ibn al-Mundhir wa Madina. Alisema:

"Enyi kundi la Ansari! Watu hawa (Muhajirin) wapo chini ya ulinzi wenu. Hawana mamlaka yoyote ya kuwapinga ninyi. Macho ya Waarabu wote yanakutazameni ninyi, na mnao utanguliaji ule ule katika Uislamu kama walionao. Wallah wao (Muhajirin) kamwe hawakuthubutu kumuabudu Allah (s.w.t.) hadharani mpaka mlipowapa hifadhi katika mji wenu. Hakuna mahali ambapo Swala iliswaliwa wazi-wazi isipokuwa kwenye mji wenu. Waabudu masanamu na washirikina hawakushind-wa ila kwa panga zenu. Kwa hiyo, uongozi ni haki yenu na wala sio yao. Lakini kama hawatakubaliana na hili, basi pawepo na viongozi wawili, mmoja kutoka kila kimoja kati ya vikundi hivi viwili."

340

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Umar alijibu hotuba ya Hubab ibn al-Mundhir kwa kusema: "Haiwezekani kwamba pawepo na wafalme wawili katika falme moja. Waarabu hawataukubali utawala wa mtu yeyote ambaye si wa kabila la Quraishi kwa vile Mtume wa Allah (s.w.t.) mwenyewe alikuwa mtu wa kabila hilo. Khalifa wa Waislamu kwa hiyo, lazima awe ni mtu wa kabila lile lile kama Mtume mwenyewe. Ule ukweli kwamba yeye alikuwa ni Quraish unakamilisha kabisa hoja yote. Sisi ni Maquraishi, na hakuna mtu yeyote atakayeweza kubishana nasi katika wajibu wetu wa uongozi."

Hubab ibn al-Mundhir akasema tena:

"Enyi Ansari! Msimsikilize mtu huyu na wenzie. Ukhalifa ni haki yenu. Uchukueni. Kama hawakubaliani na haki hii, wafukuzeni ndani ya mji wenu. Kisha mnachagua kiongozi kutoka miongoni mwenu wenyewe. Kile mlichokipata kwa panga zenu, msikitoe hicho kwa watu hawa, na kama mtu yoyote ananipinga mimi hivi sasa, nita-mnyamazisha kwa upanga wangu."

Abu Ubaidah ibn al-Jarrah ndipo akasimama, na akasema:

"Enyi kundi la Ansari! Mlikuwa wa kwanza kumsaidia Mtume wa Allah, na kutoa hifadhi kwa dini yake. Je, mtakuwa ninyi wa kwanza sasa kusababisha msambaratiko katika dini ile?"

Mzungumzaji aliyefuatia alikuwa ni Ansari mwingine, ambaye ni Bashir bin Saad. Alijua kwamba Ansari walikuwa wamedhamiria kumchagua Saad ibn Ubada kama kiongozi wa umma wa Kiislam. Alikuwa na chuki na Saad na hakupenda kumuona yeye akiwa mtawala wa Arabia. Kwa hiyo, alichokisema ndani ya Saqifah kili-chochewa, sio na mapenzi na Abu Bakr au wale Muhajirin bali na chuki yake juu ya Saad. Alisema:

"Enyi kundi la Ansari! Bila shaka tuna kipaumbele katika Uislamu, na katika vita vya Kiislam. Lakini kwa vile ni hivyo, tusilazimike kuwa wabinafsi. Nia yetu iwe tu ni kutafuta radhi za Allah (s.w.t.) na kumtii Mtume Wake (s.a.w.). Huduma zetu kwa Uislamu zilikuwa ni kwa ajili ya Allah (s.w.t.) na sio kwa ajili ya manufaa ya dunia, na Yeye atakulipeni kwa ajili hiyo. Kwa hiyo, tusijaribu kuwekeza juu ya huduma hizo sasa. Mtume wa Allah (s.a.w) alitokana na kabila la Quraishi; kwa hiyo, ni haki kwamba warithi wake wawe pia wanatokana na kabila hilohilo. Wanastahili kuwa warithi wake. Ukhalifa ni haki yao na sio yetu, na tusiwapinge katika jambo hili. Kwa hiyo, muogopeni Allah (s.w.t.) na msijaribu kuchukua kisichokuwa chenu."

Hotuba hii ya Bashir bin Saad ilimtia hamasa Abu Bakr ya kusimama mara nyingine tena na kusema:

"Kama nilivyosema kabla, viongozi wawe wanatokana na Quraishi. Kwa hiyo, Enyi Ansari! msisababishe mgawanyiko miongoni mwa Waislamu. Ni ushauri wangu

341

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwenu kwamba mtoe kiapo cha utii kwa mmoja kati ya watu wawili hawa walioko hapa, Umar na Abu Ubaidah bin al-Jarrah. Wote wawili ni Maquraishi wanaostahili."

Lakini Umar akamwingilia kati akisema, "Inawezekanaje kwamba mtu mwingine yeyote apokee kiapo cha utii wakati wewe upo miongoni mwetu. Wewe ndiye mtu mzima zaidi katika Quraishi, na umetumia muda mwingi zaidi pamoja na Mtume (s.a.w.) kuliko yeyote kati yetu. Kwa hiyo, mtu yeyote asijiweke mwenyewe mbele yako. Nyoosha mkono wako ili nikupe kiapo changu cha utii." Umar aliushika mkono wa Abu Bakr, na akauweka mkono wake juu yake kama ishara ya kiapo. Alikuwa, kwa kitendo hiki, amemthibitisha Abu Bakr kama khalifa. Abu Ubaidah bin al-Jarrah na Bashir bin Saad Ansari pia wakatokea mbele, wakaweka mikono yao juu ya mkono wa Abu Bakr, kiapo chao kwake.

Bashir bin Saad Ansari alikuwa akionyesha shauku sana katika kutoa kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Hubab ibn al-Mundhir aliyekuwa anamtazama, akasema kwa sauti kubwa:

"Ewe Bashir! Wewe ni msaliti kwa watu wako mwenyewe. Tunajua ni kwa nini uliru-ka mbele kuchukua kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Wewe unamchukia Saad ibn Ubadah, wewe haini mnyonge. Ni jinsi gani unavyochukia kumuona yeye akiwa Amir wa Waislamu."

Ilikuwa ni katika wakati huu wa maamuzi ya hatma ambapo wengi wa watu wa mak-abila ya Kibedui ambao waliishi kati ya Madina na Makka walijitokeza uwanjani. Walikuwa na uadui na Ansari, na walikuwa wameingia hapo mjini waliposikia habari za kifo cha Mtume wa Allah (s.a.w.w) Walipong'amua kile kinachopikwa pale Madina, walijitawanya karibu na Saqifah. Kutokeza kwao kwa ghafla kuliongeza nguvu nyingi sana kwenye hamasa ya Abu Bakr na Umar; na kwa wakati huo huo, kulitia mawimbi juu ya uhakika wa Ansari. Watu hawa wa makabila walikuwa wote wana silaha. Kwa kutokea kwao, nguvu ya ushawishi katika ule mjadala mrefu kati ya Muhajirin na Ansari, ikaenda kwa Muhajirin.

G .E . Von Grunebaum:

"Katika kipindi cha vurugu Ansari hatimae walishawishika kutong'ang'ania juu ya urithi kwenda kwa mmoja wa watu wao wenyewe wala juu ya watawala wawili wa Sahaba na Msaidizi, na kwa kiasi fulani chini ya shinikizo kutoka kwa Mabedui ambao walikuwa wanamiminika kuingia ndani ya mji huo, walikubali kufanya heshi-ma kwa Abu Bakr."

(Classical Islam - A History 600 - 1258)

342

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Umar alisema baadae kwamba mpaka walipotokea wale watu wa makabila, alikuwa na mashaka makubwa kuhusu matokeo ya ule mjadala na Ansari. Kutokea kwao katika muda muafaka, na matumizi yao ya shinikizo juu ya Ansari, kulihakikisha makubaliano ya hawa Ansari katika kufika kwa Abu Bakr kwenye kiti.

Hila ya Bashir ilishinda. Aliihujumu ile nia ya - kupigana ya Ansari. Malalamiko ya Saad ibn Ubada na Hubab ibn al-Mundhir hayakuwa na mafanikio yoyote. Wakati Umar, Abu Ubaidah na Bashir walipotoa kiapo cha utii kwa Abu Bakr, wengine wote walifuata kama kondoo. Ansari walikuwa wameshindwa mapambano!

Ufumbuzi wa mafanikio ya Abu Bakr katika kuchaguliwa khalifa hapo Saqifah ulikuwa ni ule uadui wa pamoja wa yale makabila mawili ya Madina ya Aus na Khazraj. Yote yalikuwa yamepigana "Vita vya Miaka Mia Moja" vya wenyewe kwa wenyewe, na walikuwa wamesimamisha uhasama wao kwa sababu tu ya kuchoka kwao kimwili.

G .E . Von Grunebaum:

"Hawa Aus na Khazraj walikuwa hali ya kuendelea katika vita vya msituni dhidi yao kwa vizazi na vizazi. Ugomvi wao ulifikia kwenye kilele cha kumwaga damu mnamo mwaka 617 katika "Vita vya Bu'ath," ambavyo baada yake wahusika wakuu walicho-ka sana kiasi kwamba ilififia mpaka kwenye mapatano ya kusimamisha vita, yaki-ingiliwa tu na vitendo vya kisasi vya mara kwa mara.

(Classical Islam - A History 600 - 1258)

Vita vya mwisho vikubwa kati ya Aus na Khazraj vilikuwa vimepiganwa miaka minne tu kabla ya kutokea kwa Mtume (s.a.w.) hapo Madina kama Mpatanishi. Mara tu wote walipomkubali yeye kama kiongozi wao, walikubaliana pia kuridhia kwenye maamuzi yake katika migogoro yao yote, na walifanya makubaliano ya kusitisha mapambano kwenye vita vyao visivyokwisha. Lakini mara tu yule Mpatanishi na hakimu alipokufa, chuki zao za zamani, hofu na wasiwasi viliwaka moto tena. Pale viongozi wa Aus walipoona kwamba Khazraj walikuwa wamemtoa Saad ibn Ubada - Mkhazraji - kama mgombea wa ukhalifa, walifikiria kwamba kama atachaguliwa kuwa khalifa, basi wao -Aus - watashushwa mpaka kwenye hadhi ya utwana kwa wakati wote. Maslahi yao, waliona, yatalindwa vema kama kiongozi wa umma angekuwa ni Muhajir kutoka Makka badala ya Khazraj wa Madina. Wao kwa hiyo, wakaharakisha kumhakikishia Abu Bakr kwamba walikuwa watiifu kwake kabla Khazraj hawajaweza kumtangaza Saad ibn Ubadah kama mkuu mpya wa Madina. Ilikuwa kwa hiyo ni Aus wa Madina ambao walikuwa hasa wamesaidia katika kupatikana kwa mafanikio ya Abu Bakr katika kuchaguliwa kwake kama khalifa. Vipengele vingine, kama vile usaliti wa Bashir bin Saad, mwenyewe akiwa Khazraj, kwa kabila lake mwenyewe, la Khazraj; na uingiliaji wa watu wa kabila la Kibedui katika wakati mgumu, pia vilichangia mafanikio ya Abu Bakr.

343

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Maxime Rodinson:

"Watu wa Madina, hususan wale wa kabila la Khazraj, walihisi kwamba Wahamiaji wa Kiquraishi ambao walikuwa wamekuja pamoja na Muhammad (s.a.w.) ambao walikuwa siku zote wakiwaonea wivu, sasa watajaribu kudai uongozi juu yao wenyewe. Mtume (s.a.w.) alikuwa amekufa. Hapakuwa na sababu tena ya kuendelea kuwatii hawa wageni. Waliitisha mkutano katika ukumbi wa moja kati ya koo zao -Banu Sa 'ida, kuzungumzia njia bora ya kulinda maslahi yao. Walichoshauri kufanya kilikuwa ni kuchagua mmoja wa watu wao maarufu, Sa'd ibn Ubadah, kama Kiongozi mpya wa Madina.

Abi Bakr alikuwa katika nyumba ya Muhammad (s.a.w.), alidokezwa juu ya hili na akakimbilia kwenye sehemu hiyo pamoja na wanasiasa wenzie, Umar na Abu Ubaidah. Waliungana humo njiani na kiongozi mwingine wa kabila jingine la Madina, la Aus, mahasimu wa Khazraj. Jambo la mwisho kabisa walilotaka lilikuwa ni kuona madaraka yakiwa kwenye mikono ya Khazraj. Mitaani humo msisimko ulikuwa unaenea kwa watu wa makabila mengine ya Madina, ambao walikuwa hawana tamaa ya kushika nafasi ya ukibaraka katika mchezo wowote wa madaraka ambao ulikuwa karibu uanze. Usiku ulipoingia, kila mtu alikuwa amesahau ule mwili (wa Mtume (s.a.w.)) uliokuwa bado umelala katika kibanda kidogo cha Aishah (ingawa - la kibanda - si sahihi).

Majadiliano yaliyoendelea kwa mwanga wa tochi na taa za mafuta, yalikuwa marefu, makali na yenye rabsha. Mtu mmoja wa Madina alishauri kwamba wangechaguliwa viongozi wawili, mmoja Quraishi na mmoja wa Madina. Watu wengi walitambua kwamba hiyo itakuwa ni njia ya kukaribisha ugomvi na balaa juu ya jamii. Kila mmoja alikuwa anapiga kelele kwa wakati mmoja; wangeweza hata kufikia kupi-gana."

(Muhammad, tafsiri ya Ann Carter, 1971)

Walifikia kupigana. Saad ibn Ubadah alimkamata Umar kwenye ndevu zake. Umar ali-tishia kumuua yeye kama angeng'oa unywele mmoja toka kwenye ndevu zake. Umar akamwambia Hubab ibn al-Mundhir: "Allah akuuwe wewe," naye huyu akamwambia: "Allah akuuwe wewe."

Hubab ibn al-Mundhir alifanya juhudi kubwa kuokoa hali hiyo. Alipojaribu kuwazuia Ansari kutoa kiapo cha utii kwa Abu Bakr, kundi moja likamvamia, likampokonya upan-ga wake, na likamsogeza pembeni. Walikuwa ni Mabedui wanaowaunga mkono Muhajirin. Hubab alikosa upanga wake lakini bado alizipiga nyuso za wakazi wa Madina ambao walikuwa wakitoa kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Aliwalaani na kusema: "Enyi Ansari! Naweza kuona kwa macho yangu mwenyewe kwamba watoto wenu wanaomba chakula kwenye milango ya nyumba za hawa watu wa Makka lakini badala ya kupata chakula wanapigwa kwenye meno na watu hawa, na wanafukuzwa."

344

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abu Bakr akamuuliza Hubab: "Unawazia hofu kama hizo kutoka kwangu mimi?" Akasema: "La. Sio kutoka kwako bali kutoka kwa wale watakaokuja baada yako." Akijaribu kumhakikishia, Abu Bakr akasema: "Kama hilo likitokea, mnaweza wakati wote kukana kiapo chenu kwa makhalifa wenu." Yeye kwa uchungu akajibu kwa ukali sana: "Itakuwa tumekwisha kuchelewa sana wakati huo, na haitasaidia chochote."

Ulikuwa ni mkutano huu wa fujo, wa kiajabu ajabu na usio na mpangilio, wa ndani ya ukumbi wa Saqifah ambao ulimchagua Abu Bakr kama khalifa. Ansari hawakuridhika sana na kuchaguliwa kwake. Wao kwa hali yoyote ile, hawakuteua mtu anayestahiki-sana. Umar kwa ustadi sana aliliweka kando suala la sifa-stahilifu, na kamwe hakuliruhusu liibuke ndani ya mjadala huo. Suala la sifa za mgombea lilifunikwa chini ya wingu la ufasaha wa kukwepa kwepa.

Saad ibn Ubadah, kiongozi wa Khazraj, na "mshindi wa pili" ndani ya Saqifah ambamo mbinu-zote-zinakubaliwa na huru kwa watu wote, alikuwa mmoja wa wale watu ambao walikataa kula kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Alimwambia Abu Bakr: "Ewe Abu Bakr! Kama nisingekuwa kwenye hali hii ya kutokujiweza kwa sababu ya maradhi yanayonid-hoofisha, ningekurudisheni Makka wewe na marafiki zako, kwa ndugu zenu wenyewe." Saad kisha akawaomba marafiki zake wamtoe nje ya Saqifah. Kwa muda fulani Abu Bakr hakumuingilia yeye, na kisha siku moja akamtumia ujumbe akimtaka aje kutoa kiapo cha utii. Saad akakataa. Umar akamshinikiza Abu Bakr achukue kiapo chake kwa nguvu. Lakini Bashir bin Saad Ansari akaingilia kati kwa kusema: "Saad akiwa amekwisha kataa, kamwe hatokupeni kiapo chake cha utii. Kama mkimlazimisha yeye, inaweza kusababisha umwagaji wa damu, na watu wa Khazraj wote watasimama pamoja naye dhidi yako. Kwa maoni yangu mimi, haitakuwa busara kulazimisha jambo hili. Yeye, hata hivyo, ni mtu mmoja tu, na akiachwa alivyo, hawezi kufanya madhara yoyote kwa namna yoyote ile."

Wale watu wote waliokuwepo kwenye lile baraza la khalifa, waliyaunga mkono maoni ya Bashir, na Saad aliachwa kwa amani. Alipona maradhi yake, na miaka mitatu baadae, aka-hama kwenda Syria.

Maandishi ya hotuba zilizotolewa pale Saqifah, na maelezo juu ya matukio yaliyotokea pale, yamechukuliwa kutoka kwenye vitabu vifuatavyo:

1.  Tarikh - Tabari

2.  Tarikh al-Kamil - Ibn Athir

3. Kitab-al-Imama was-Siyasa - Ibn Qutayba Dinwari

4.  Siraat-ul-Halabiyya - Halaby

345

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kugombea Madaraka 4

Wakati Abu Bakr alipokubaliwa kuwa khalifa pale saqifah, yeye, Umar bin al-Khattab na Abu Ubaidah bin al-Jarrah walirudi kwenye Msikiti wa Mtume (s.a.w.). Ndani ya Msikiti mlikuwa na watu wengi, miongoni mwao, watu wa ukoo wa Bani Umayya; Saad bin Abi Waqqas; Abdur Rahman bin Auf; na baadhi ya Muhajirina wengine.

Alipowaona wamekutana faragha kwenye kundi moja. Umar alisema kwa sauti: "Abu Bakr amechaguliwa kuwa khalifa wa Waislamu. Sasa nyie wote hapa mpeni kiapo cha utii. Ansari, Abu Ubaidah na mimi tayari tumekwisha fanya hivyo."

Bani Umayya waliokuwepo mle ndani ya Msikiti walikuwa wa kwanza kuitika mwito wa Umar, na kuchukua kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Saad ibn Abi Waqqas, Abdur Rahman bin Auf na wengineo waliwafuatia hao, na wakachukua kiapo cha utii kwa Abu Bakr.

Takriban "mamwinyi" wote walichukua kiapo cha utii kwa Abu Bakr siku ya Jumatatu. Wale "watu wa kawaida" hawakujua kuhusu kuchaguliwa kwa Abu Bakr bado. Walikuja pale Msikitini siku ya Jumanne. Kutwa nzima walikuwa wakija na kuingia na kutoka nje ya Msikiti, na Abu Bakr alikuwa akishughulika kupokea viapo vyao vya utii kwake. Ilikuwa tu siku ya Jumatano ambapo hatimae alikuwa huru kushughulikia mambo mengine.

Wakati huohuo, muda wote wa kinyang'anyiro kikali cha madaraka ndani ya Saqifah, na baadae, Ali ibn Abi Talib na watu Bani Hashim, walikuwa wakishughulikia mazishi ya Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.). Pale Mtume alipokuwa amekwishafanyiwa mazishi, Ali na Bani Hashim walirudi majumbani kwao.

Watu wengi hapo Madina walikuwa wamekwisha kuchukua kiapo cha utii kwa Abu Bakr lakini walikuwepo wengine ambao walikuwa bado. Muhimu sana miongoni mwao wote alikuwa ni Ali ibn Abi Talib, kiongozi mpya wa ukoo wa Bani Hashim. Khalifa mpya na washauri wake waliamini kwamba ilikuwa ni muhimu sana kwamba Ali achukue kiapo cha utii sawa na watu wengine. Wao, kwa hiyo, walituma aitwe kutoka nyumbani kwake lakini alikataa kuja. Kukataa kwake kulimkasirisha Umar. Mapema kidogo, alikuwa mtu mwenye kuathiri uteuzi, lakini sasa amekuwa Mtendaji Mkuu wa serikali mpya ya Saqifah. Yeye, kwa hiyo, alikwenda pamoja na wasindikizaji wenye silaha kutekeleza amri za serikali, na akatishia kuichoma nyumba ya binti ya Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w.), kama Ali asingekuja kwenye baraza kuchukua kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Mtu mmoja alikumbusha kwamba nyumba ile ilikuwa ni mali ya binti ya Mtume (s.a.w.), hivyo Umar angewezaje kuichoma. Lakini Umar akasema haidhuru kama nyumba hiyo ilikuwa ni ya mtoto wa Mtume (s.a.w.). Kilichokuwa na umuhimu hasa, alisisitiza, ni kiapo cha utii

346

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ambacho Ali alipaswa akichukue. Edward Gibbon:

"Bani Hashim peke yao walikataa kiapo cha utii (kwa Abu Bakr); na kiongozi wao (Ali), katika nyumba yake mwenyewe, alidumisha zaidi ya miezi sita (ingawa sio kweli), kimya kizito na cha upweke, bila ya kupatiliza vitisho vya Umar, ambaye ali-jaribu kuyachoma kwa moto makazi ya binti ya Mtume (s.a.w.)."

(The Decline and Fall of the Roman Empire)

Hata mtu kama Shibli, mwandishi wa wasifu wa Umar, na mmoja wa washabiki wake wakubwa sana, amelazimika kukubali kwamba "Umar alikuwa mtu mwenye hasira mbaya sana, na haishangazi kabisa kama alifanya jaribio la kuchoma moto nyumba ya binti ya Mtume (s.a.w.)." - (Al-Faruuq)

Uzuri ulioje, utamu ulioje, na ujasiri ulioje wa Umar kujaribu kuchoma nyumba ya Fatima Zahra! Siku tatu baada ya kifo cha Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Mwisho wa Allah (s.a.w.w) kwa wanadamu, Umar alifika mlangoni mwa nyumba ya Fatima Zahra. Kundi lingine la wachomaji moto mali wa maksudi lilikuwa pamoja naye, na alidai kiapo cha utii cha Ali kwa Abu Bakr.

Uonyeshaji huu wa "ushujaa" lazima utakuwa "umemfurahisha" sana Allah (s.w.t.) hasa, pale mtu anapokumbuka kwamba mbali na Ali na Fatima, walikuwemo pia ndani ya nyumba yao, watoto wao wadogo wanne - wajukuu wa Muhammad Mustafa (s.a.w.). Walipishana kwa umri kutoka miaka miwili hadi nane. Watoto hao lazima watakuwa "wal-isisimka" kusikia sauti ya Umar. Kwao wao, lazima alikuwa kama mfano wa "Santa Claus," (Baba Chrismas) - Santa Claus huyo wa jangwani, akiwa amesimama mlangoni mwa nyumba yao akiwa na "zawadi" ya moto kwa ajili yao. "Zawadi" yake, huenda atakuwa amewaeleza, ilikuwa na nguvu ya kubadili zile kuta za kijivu zisizovutia za nyumba yao ndogo kuwa ndimi za moto zinazoruka na kualika alika zenye rangi nyingi.

Kipi tena angewafanyia hao ili "kuwaliwaza" na "kuwafariji" baada ya kifo cha babu yao, Muhammad (s.a.w.), ambaye alikuwa akiwapenda sana? Hivi wamekwishawahi kamwe kuona kioja cha "fataki" yenye kumeremeta kupita kiasi kama hicho anachoweza kuwaonyesha punde hivi tu kama baba yao, Ali ibn Abi Talib, hakuchukua kiapo cha utii kwa Abu Bakr?

Kwa wakati huu, Zubayr ibn al-Awam alikuwa pia pamoja na Ali. Mke wake alikuwa mmoja wa mabinti wa Abu Bakr lakini mama yake yeye alikuwa ni Safiyah bint Abdul Muttalib, shangazi yake Muhammad (s.a.w.) na Ali. Yeye, kwa hiyo, alidai kwamba na

347

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

yeye pia alikuwa mtu wa ukoo wa Bani Hashim. Umar alimuamuru kuchukua kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Lakini alikataa na kutishia kutumia upanga wake kama atasumbuliwa sana. Umar aliwakemea vibaraka wake wanyakue upanga wake. Walifanikiwa katika kumzidi nguvu. Alinyang'anywa silaha, na akapelekwa kwenye baraza la baba-mkwe wake. Ilikuwa ni katika hali hii kwamba alitoa kiapo chake cha utii kwake.

Umar alijaribu kupata nguvu kwa vitisho, kufoka - kwa kiburi, na udanganyifu. Zamani, mtu alikuwa anaweza kutaja udanganyifu wake lakini sasa ilikuwa haiwezekani kufanya hivyo. Pamoja na Zubayr kumalizwa hivyo, Umar aligeuzia mazingatio yake kwa Ali, na alipelekwa kule kwenye baraza. Humo ndani ya baraza, Umar alirudia dai lake la kiapo lakini Ali akasema:

"Mimi ni mtumwa wa Allah (s.w.t.) na ni ndugu yake Muhammad, Mtume Wake. Mtumwa wa Allah (s.w.t.) hawezi kuwa mtumwa wa mtu mwingine yeyote. Kama mmefanikiwa katika kuiteka serikali ya Muhammad (s.a.w.) kwa sababu ninyi, kama ulivyosema, ninyi mpo karibu zaidi kwake kuliko Ansari, basi mimi ni mdogo wake, na ni nani miongoni mwenu ambaye anaweza kudai kuwa karibu naye zaidi kuliko mimi? Waislamu wote wanapaswa kunipa mimi viapo vyao, na sio mtu mwingine yeyote. Mnainyang'anya familia ya marehemu bwana wenu haki yao. Mliwashawishi Ansari kwa hoja kwamba Mtume wa Allah (s.a.w.w) alikuwa ni mmoja wenu, na hakuwa mmoja wao, na waliuachia ukhalifa kwenu. Sasa naitumia hoja hiyo hiyo -hoja yenu - ambayo mliitumia dhidi ya Ansari. Sisi ndio warithi wa Mtume wa Allah (s.a.w.w) katika uhai wake na baada ya kifo chake. Kama mnauamini ujumbe wake, na kama mmeukubali Uislamu kwa uaminifu, basi msizichukue kwa nguvu haki zetu."

Umar alimjibu hivi:

"Wewe ni mtumwa wa Allah (s.w.t.) lakini sio ndugu yake Mtume Wake (s.a.w.). Kwa hali yoyote, itakubidi utoe kiapo cha utii kwa Abu Bakr, na hatutakuachia hapa mpaka umefanya hivyo."

Ali akasema:

"Ewe Umar! Kama unatetea suala la Abu Bakr kwa shauku kubwa namna hiyo, hilo linaeleweka. Leo unamfanya mfalme ili kwamba kesho akufanye wewe kuwa mfalme. Mimi sitafanya kile unachonitaka nifanye, na sitampa kiapo changu."

Abu Ubaidah ibn al-Jarrah alikuwa mwanachama wa "kundi la watu watatu" (troika), na kwa hiyo, alikuwa wakili mkali wa serikali ya Saqifah. Yeye pia alifanya jaribio la kumshawishi Ali kuitambua ile serikali mpya, na kuchukua kiapo cha utii kwa kiongozi wake. Alisema:

"Ewe binamu ya Mtume (s.a.w.)! wewe ni mdogo kuliko watu hawa. Wao ni wakub-

348

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wa sana kuliko wewe na wanao uzoefu mkubwa kuliko ulionao wewe. Inakubidi uchukue kiapo cha utii kwa Abu Bakr sasa hivi, na kisha, siku isiyo na jina, zamu yako inaweza kuja pia. Unastahili kuwa kiongozi wa Waislamu kwa sababu ya utan-guliaji wako kwenye Uislamu, ushujaa wako, ujuzi wako, elimu yako, na utumishi wako kwenye Uislamu. Na kisha wewe ni mkwe wa Mtume wetu."

Ali alimjibu kama ifuatavyo:

"Enyi Muhajirin! Msiyatoe madaraka na mamlaka ya Mtume wa Allah (s.a.w.w) nje ya nyumba yake kwenda kwenye majumba yenu. Wallahi, urithi wa Muhammad (s.a.w.) ni haki yetu sisi. Yeye mwenyewe alitoa tamko hili, na sio mara moja bali mara nyingi tu. Hivi yupo mtu kati yenu ambaye ana ujuzi mzuri na uelewa wa Qur'an kuliko nilionao mimi? Yupo yeyote miongoni mwenu ambaye anayo elimu nzuri ya vitendo na Hadith za Mtume wa Allah (s.a.w.w) kuliko niliyonayo mimi? Yupo yeyote kati yenu ambaye anaweza kuiendesha serikali yake vyema kuliko mimi niwezavyo? Kama yupo, mtajeni, na mimi nitamstahi yeye. Lakini hayupo. Ni mimi tu niwezaye kutoa amani ya kweli, ustawi na haki ya kweli kwa Waislamu wote. Kwa hiyo msiangukie kwenye vishawishi vyenu, na msiweke tamaa na mapenzi yenu wenyewe mbele ya amri za Allah (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.). Na kama mkifanya hivyo, mtapotoka kwenye Haki, na mtaangukia kwenye Upotovu."

Bashir bin Saad, yule yule aliyekuwa Ansari wa kwanza kuchukua kiapo cha utii kwa Abu Bakr ndani ya Saqifah, alikatisha hotuba ya Ali, na akasema:

"Ewe Ali! Kama ungetuambia hayo kabla, sisi tusingekuwa tumempa kiapo cha utii mtu yeyote badala yako wewe."

Ali akamwambia:

"Wewe ulikuwa huyajui yote haya? Unachojaribu kushauri ni kwamba kama vile wote nyie mlivyomtelekeza Mtume wa Allah (s.a.w.w) mara tu alipofariki, mimi pia ningemtelekeza, na mimi pia ningeingia Saqifah kugombea ukhalifa pamoja nanyi? Hili nisingeweza kulifanya. Kufanya hivyo kusingestahili kabisa kwangu mimi. Nisingeweza kumtoroka Mtume wa Allah (s.a.w) katika kufa kwake kama nisivyomtoroka wakati wa uhai wake."

Baada ya maelezo haya, Ali alitoka kwenye baraza ya Abu Bakr iliyokuwa imeendeshwa kwenye Msikiti wa Mtume (s.a.w.). Hizo ndizo zilikuwa mbinu za kuchaguliwa kwa Abu Bakr kama khalifa wa Waislamu - mfululizo wa ufaraguzi wa kuwa tayari kufanya lolote, na mara nyingi wenye misukosuko. Wakati wa kuchukua viapo kwa faragha ndani ya Saqifah, na vile vya hadhara ndani ya

349

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Msikiti wa Mtume (s.a.w.), kulipokamilika, Abu Bakr, khalifa mpya, akatoa hotuba yake ya uzinduzi. Baada ya kumshukuru Allah (s.w.t.) na kumtukuza, alisema:

"Enyi Waislamu! wale kati yenu waliokuwa wakimwabudu Muhammad, basi nawa-jue kwamba amekufa; lakini wale kati yenu waliokuwa wakimwabudu Allah (s.w.t.) nawajue kwamba Yeye yuko Hai, na hatakufa kamwe.

Enyi Waislamu! Ingawa mmenichagua mimi kama kiongozi wenu, mimi sio mbora sana miongoni mwenu. Kama mtu mwingine angechukua dhima ya mzigo huu ambao mmenitwisha mimi, ingekuwa bora sana kwangu. Kama mnanitegemea niwatawale kama vile tu Mtume wa Allah (s.a.w) alivyofanya, basi lazima niwaambie kwamba hiyo haiwezekani. Mtume (s.a.w.) alipokea Wahy kutoka Mbingnii, na alikuwa asiyetekosea (maasum) ambapo mimi ni mtu wa kawaida tu. Mimi sio bora kuliko ninyi. Kwa hiyo, kama mkiniona ninakwenda katika njia iliyonyooka, nifuateni; lakini kama mnaniona nikiikengeuka, nishutumuni. Kama nikifanya sawa, niungeni mkono; kama nikifanya makosa, nisahihisheni. Nitiini mimi pale tu nitakapokuwa ninamtii Allah (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.). Lakini kama mkiniona ninawakiuka wao, nanyi pia mniepuke.

Mnayo Qur'an pamoja nanyi, na imekamilika. Mtume wa Allah (s.a.w) amekuonyesheni kwa maagizo na kwa mifano pia namna ya kujiweka nyie wenyewe katika maisha haya. Mwenye nguvu zaidi miongoni mwenu ni yule anayemuogopa Allah (s.w.t.) Mdhaifu sana miongoni mwenu mbele ya macho yangu ni yule mwenye-dhambi. Taifa linaloacha jihadi, linapoteza hadhi yake. Salini Swala zenu kwa wakati makhsusi, na msizikose. Allah (s.w.t.) awe na huruma juu yenu, na Akusameheni ninyi wote."

Hotuba ya khalifa mpya ilikuwa ni ya maelezo ya malalamiko-binafsi kweli, porojo lisilo na dhamira maalum, isiyotia moyo au umaizi. Kauli ya mwanzo, hata hivyo, ilikuwa na maana. Aliwaambia Waarabu kwamba kama walikuwa wakimuabudu Muhammad (s.a.w.), amekufa! Hivi kuna Waarabu wowote waliomuabudu Muhammad? Kwa miaka 23, Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.a.w) aliyebarikiwa, alikuwa akilifundisha somo la Tauhid (Mungu mmoja) liingie kwenye vichwa vya Waarabu. Ikiwa baada ya juhudi kubwa namna hiyo, walianza kumuabudu yeye badala ya kumuabudu Allah (s.w.t.) basi kazi yake yote kama Mtume, lazima iamuliwe kwamba ilishindwa kabisa.

Lakini ujumbe wa Muhammad (s.a.w.) haukuwa kazi bure. Waislamu walimuabudu Allah (s.w.t.) na hawakumuabudu Muhammad. Wao, kwa hakika, walirudia mara nyingi kwa siku kwamba Muhammad alikuwa ni mtumwa wa Allah (s.w.t.) na Abu Bakr alilijua hili. Hivyo ni kwa nini aliona umuhimu kuwaambia kwamba kama walikuwa wakimuabudu Muhammad, amekufa?

350

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kauli ya Abu Bakr ilikuwa ni hila ya ujanja. Muhammad (s.a.w.) ndio kwanza amefariki, na ilikuwa ni kawaida kwa Waislamu kuwa na huruma kwa watu wa familia yake kwa kuondokewa kwao kukubwa. Lakini Abu Bakr alikuwa na hofu na huruma hii. Aliiona ni ya hatari kwa usalama wake binafsi juu ya ufalme. Kipindi cha maombolezo rasmi kingeweza kuwa cha hatari pia kwake. Yeye, kwa hiyo, alilinganisha maombolezo juu ya kifo cha Muhammad (s.a.w.) na "kumuabudu" Muhammad (s.a.w.), na ni nini kinachoweza kuwa cha kulaumika katika Uislamu kama "kumuabudu" Muhammad - mwanadamu -badala ya kumuabudu Allah (s.w.t.)!

Abu Bakr, kwa njia hii, aligeuza azma ya umma wa Kiislamu mbali na huruma yoyote ambayo ungeweza kuihisi kwa familia inayohuzunika ya Muhammad (s.a.w.).

Waarabu hawakuabudu kitu chochote vizuri zaidi kuliko vipande vya mawe au miti; Muhammad (s.a.w.) aliwafanya wawe wanaomuabudu Allah (s.w.t.) - Muumba mmoja na Mola wa Ulimwengu. Waarabu walikuwa ni wachunga kondoo au maharamia; Muhammad (s.a.w.) akawafanya wafalme na washindi. Waarabu walikuwa washenzi na wajinga; Muhammad (s.a.w) akawafanya taifa lililostaarabika zaidi duniani. Alikuwa ni mfadhili mkubwa sio tu kwa Waarabu wa wakati wake mwenyewe bali kwa wanadamu wote kwa wakati wote. Mtu kama huyo alipofariki, Waarabu, Waislamu, ambao walikuwa wafaidika-ji wa kazi yake kwao, walipaswa kupondwa na huzuni. Lakini cha kushangaza, kushtusha na kisichopingika, hawakuwa hivyo! Ingawa walikuwa wamepoteza baraka kubwa sana ambayo Allah (s.w.t.) alishusha kwao - kupitia Mpendwa Wake Mwenyewe, Muhammad - hawakuonyesha hisia zozote za hasara hata kidogo.

Haikujitokeza kwa umma wa Kiislamu kwamba Muhammad (s.a.w.) alikuwa ni mwon-gozaji wake, na kiongozi wake sio tu katika maisha bali hata katika kifo, alipaswa kupata mazishi ya kitaifa, na palipaswa kuwa na kipindi cha maombolezo rasmi kwa ajili yake.

Umma wa Kiislamu ni dhahiri uliona kwamba kuomboleza kwa ajili ya kifo cha Muhammad (s.a.w.), na kumfanyia mazishi, zilikuwa ni kazi ambazo ni vema kuachiwa kwa watu wa familia yake mwenyewe. Watu wa familia yake waliomboleza kwa ajili yake, na walimfanyia mazishi.

351

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Tahakiki ya Saqifah

Muhammad ibn Ishaq, mwandishi wa wasifa wa Mtume wa Uislamu, anaandika katika Siirah yake - (Maisha ya Mtume wa Allah):

Umar alisema: "Na tazama! wao Ansari walikuwa wanajaribu kutuondoa sisi kutoka kwenye asili yetu na kupora mamlaka kutoka kwetu. Alipomaliza (Ansari mmoja) hotuba yake, nilitaka kuzungumza, kwani nilikuwa nimeandaa hotuba kichwani mwangu ambayo ilinifurahisha sana. Nilitaka kuitoa mbele ya Abu Bakr na nilikuwa ninajaribu kulainisha makali yake fulani; lakini Abu Bakr akasema, 'Taratibu Umar,' Sikutaka nimuudhi na kwa hiyo akazungumza yeye. Alikuwa ni mtu mwenye maari-fa na heshima kubwa kuliko mimi, na Wallahi, hakuacha hata neno moja ambalo nilikuwa nimelifikiri na aliisema kwa namna yake isiyo na kifani, vizuri zaidi kuliko ambavyo ningeweza kufanya mimi.

Yeye (Abu Bakr) alisema: 'Mazuri yote mliyoyasema juu yenu wenyewe (Ansari) yanastahiki. Lakini Waarabu watayakubali tu mamlaka yaliyo katika kabila la Quraishi, wao wakiwa ndio wabora wa Waarabu kwa damu na nchi. Nawapeni mmoja kati ya watu wawili hawa: mkubalini yule mnayempenda.' Baada ya kuyasema hayo aliukamata mkono wangu na ule wa Abu Ubaidah ibn al-Jarrah ..."

Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w.w), hakuwa amekufa kwa zaidi ya saa moja bado, pale Abu Bakr alipofufua ule ufidhuli wa Nyakati za Ujahilia kwa kudai mbele ya Ansari kwamba Quraishi, kabila ambalo yeye anatokana nalo, lilikuwa "zuri" kuliko au "bora" kwao Ansari "kwa damu na nchi!"

Abu Bakr alijuaje kuhusu "ubora" huu wa Quraishi? Qur'an na Mletaji wake, Muhammad (s.a.w.), hawajasema kamwe kwamba kabila la Quraishi lilikuwa na "ubora" kwa yeyote yule au kwamba lina ubora wowote kamwe. Kwa kweli, lilikuwa ni kabila la Quraishi ambao walikuwa ndio wasiokata tamaa kati ya waabudu masanamu wote wa Arabia. Waliyashikilia masanamu yao na walipigana na Muhammad (s.a.w.) na Uislamu, kwa hasira za kinyama, kwa zaidi ya miaka ishirini. Ansari, kwa upande mwingine, waliukubali Uislamu kwa hiari na bila ya kusita.

"Ubora" wa Quraishi ambao Abu Bakr alitambia hapo Saqifah, mbele ya Ansari, ulikuwa ni dhamira ya kabla ya Uislamu ambayo aliifufua ili kutia nguvu madai yake ya ukhalifa.

Siku chache tu kabla, Umar alizuia kalamu, karatasi na wino kwa Muhammad (s.a.w.) wakati yeye (Muhammad) alipokuwa kwenye kitanda chake cha umauti, na alitaka kuandi-ka wosia wake. Wosia, Umar alisema, haukuwa na haja kwa sababu "kinatutosha Kitabu cha Allah." Lakini kule Saqifah, yeye na Abu Bakr walikisahau Kitabu hicho, ambacho kwa mujibu wake hicho, ubora unazingatiwa sio kwa damu na nchi bali kwa ucha-mungu. Katika Kitabu hicho, hiki ndicho tunachokisoma:

352

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usahihi-40.jpg

Hakika aliye mbora kati yenu mbele ya Allah ni yule mcha-mungu zaidi kati yenu. (Sura ya 49, Aya ya 13)

Mbele ya Allah (s.w.t.) wabora ni wale watu tu ambao wana tabia njema, ambao wanamuo-gopa Allah (s.w.t.) na wanaompenda. Lakini kitu kimoja ambacho Abu Bakr na Umar hawakukitangaza mle Saqifah ni Kitabu cha Allah (s.w.t.). Kabla ya kuingia Saqifah, walikuwa wamesahau kwamba mwili wa Mtume wa Allah (s.a.w) ulikuwa unasubiri maziko; na baada ya kuingia, wakasahau Kitabu cha Allah (s.w.t.) - "sadfa" ya kushangaza ya usahaulifu!

Dr. Muhammad Hamidullah:

"Qur'an imekataa ubora wowote kutokana na lugha, rangi au mifano yoyote ya asili isiyoepukika, na inatambua ubora pekee wa watu ulioegemea kwenye ucha-mungu."

(Introduction to Islam, Kuwait, 1971)

Madai ya Abu Bakr juu ya ubora wa Quraishi kwa misingi ya damu na nchi, yalikuwa ni dalili ya kwanza ya kuzuka tena kwa upagani katika Uislamu!

Sir John Glubb:

"Juu ya matukio yaliyofuatia kifo cha Mtume wa Uislamu:

Hii ghasia kali ilikuwa wala haijakwisha pale mtu alipoharakishia kwa Abu Bakr kumjulisha kwamba watu wa Madina walikuwa wanakusanyika kwenye ukumbi wa wageni wa ukoo wa Bani Sa'idah, wakishauriana kumchagua Saad ibn Ubadah, kion-gozi wa kabila la Khazraj, kama mrithi wao kwa Mtume (s.a.w.)."

Muhammad alikuwa hajafa kwa zaidi ya saa moja kabla ugombea madaraka kutishia kuuingiza Uislamu kwenye makundi ya uadui. Abu Bakr mpole na mkimya, Umar ibn al-Khattab mkali waliondoka kwa haraka kwenda kukabiliana na changamoto hiyo mpya. Walifuatana na yule mwerevu na mpole Abu Ubaidah, mmoja wa wafuasi wa awali, ambaye tutasikia mengi zaidi juu yake baadae.

Miaka kumi kabla, Maansari walimkaribisha Mtume (s.a.w.) yule aliyeteseka, kwenye

353

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

majumba yao na wakawa wamempa ulinzi, lakini Muhammad (s.a.w.) kidogokidogo aliku-ja kupata umaarufu na nguvu, na alikuwa amezungukwa na ndugu zake mwenyewe wa Quraishi (hii si kweli). Watu wa Madina, badala ya kuwa walinzi wa Waislamu, walijiku-ta kwenye nafasi ya chini kabisa kwenye mji wao wenyewe. Shutuma zilizimwa wakati wa uhai wa Mtume (s.a.w.), lakini alikuwa hata hajafa pale makabila ya Aus na Khazraj yalipoamua kuutupilia mbali utawala wa Quraishi. "Wao wawe na kiongozi wao wenyewe," walipiga makelele watu wa Madina. "Na kuhusu sisi, tutakuwa na kiongozi kutokana na sisi wenyewe." Kwa mara nyingine tena, Abu Bakr, mtu dhaifu mwenye umbo dogo wa miaka sitini mwenye kuinama kidogo, alikabiliwa na tukio la ghasia za kusisimua. Alilikabili kwa utulivu wa dhahiri. "Enyi watu wa Madina," alisema, "Mazuri yote ambayo mmeyasema juu yenu, yanastahili. Lakini Waarabu hawatakubali kiongozi ila atokanaye na Quraishi."

"Hapana! Hapana! Hiyo sio kweli! Kiongozi kutoka kwetu na mwingine kutoka kwenu." Ukumbi ulijaa makelele, jambo hilo lilibaki kwenye mashaka,uhasama ulizi-di tu kuongezeka.

"Hivyo sivyo," alijibu Abu Bakr kwa uimara. "Sisi ndio wabora wa Waarabu. Hapa ninawapeni fursa ya kuchagua watu wawili hawa; mchagueni yule mtakayempa kiapo chenu cha utii," na akawanyooshea mkono maswahiba wake wawili, Umar na Abu Ubaidah, wote Maquraishi.

(The Great Arab Conquest, 1967)

Sir John Glubb amefanya rejea kwenye "ghasia kali" iliyofuatia mara tu baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.). Ni kweli kwamba kulikuwa na vurugu na ghasia nyingi. Lakini sehemu yake kubwa ilianzishwa na umuhimu wa hali halisi. Mara tu Abu Bakr alipowasili kwenye tukio, alimhakikishia kila mtu kwamba Mtume (s.a.w.) alikuwa amefariki na vurugu ikafikia mwisho. Vurugu ilidumishwa kwa kiasi ilivyokuwa inahitajika lakini sasa ilikuwa haihitajiki tena.

Ansari walikuwa wanayaangalia matukio hayo. Ilionekana kwao kwamba kukataa kwa Muhajirina kuandamana na jeshi la Usamah kwenda Syria; kukataa kwao kutoa kalamu, karatasi na wino kwa Mtume (s.a.w.) wakati alipokuwa kwenye kitanda chake cha umauti na akiwa alitaka kuandika wosia wake; na sasa kukataa kifo chake, kote kulikuwa ni sehemu ya mkakati mkubwa wa kuutoa ukhalifa nje ya nyumba yake. Waliridhika pia kwamba Muhajirina walikuwa wakimpuuza Mtume (s.a.w.) wakati wa uhai wake, hawakukubali kamwe Ali achukue nafasi yake kwenye utawala. Wao, kwa hiyo, waliamua kuchagua kiongozi wao wenyewe.

Lakini Ansari walizidiwa ujanja na Muhajirina. Ansari hawakuwa na mfumo wa ujasusi unaowafanyia kazi, lakini Muhajirina walikuwa nao. Yule mtu aliyemjulisha Abu Bakr na Umar kile Ansari walichokuwa wakikifanya, alikuwa mwenyewe ni Aus wa Madina.

354

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kama ilivyokwisha elezwa tayari, alitoa sauti kali kwa Khazraj.

Kwa kweli mpelelezi huyu alikutana na Umar na akamjulisha juu ya ule mkutano wa Ansari kule Saqifah. Abu Bakr alikuwa ndani ya chumba cha Mtume (s.a.w.). Umar alimwita nje. Alitoka nje na wote wawili wakatoka mbio kuelekea Saqifah. Walimchukua pia Abu Ubaidah pamoja nao. Waliunda "kamati ya watu watatu" ya wenye athari juu ya uchaguzi wa kiongozi.

Ansari mle Saqifah hawakuwa wakila njama dhidi ya Abu Bakr au Umar au dhidi ya mtu yeyote yule. Walikuwa wakijadili jambo lililogusa Uislamu na Waislamu wote. Kuwasili kwa hii "kamati ya watu watatu" katika mkutano wao, kuliwashitusha Khazraj lakini kukawafurahisha Aus. Hawa Aus sasa walipata matumaini ya kuwakwamisha maadui zao - Khazraj - kwa msaada wa hii "kamati ya watu watatu."

Sir John Glubb anasema kwamba Abu Bakr na Umar "walitoka kwa haraka kukabiliana na changamoto hii mpya." Inakuwaje kwamba Abu Bakr na Umar wao tu ndio walikuwa wak-abiliane na changamoto ambayo ilikuwa "inatishia" sio wao tu, bali umma mzima wa Kiislam? Ni nani aliyewapa mamlaka ya kukabiliana na "changamoto" hii? Hata hivyo, kwa wakati huu, wao walikuwa ni kama mtu mwingine yoyote wa jamii hiyo. Na vipi hawakumuamini mtu mwingine kwenye "faragha" yao kana kwamba walikuwa kwenye kazi maalum ya siri?

Mwanahistoria huyu anasema tena kwamba watu wa Madina walijikuta kwenye nafasi ya chini kabisa katika mji wao wenyewe wa nyumbani. Hiyo ni kweli lakini haikutokea wakati wa uhai wa Mtume (s.a.w.). Yeye aliwafanya Ansari kana kwamba walikuwa wafalme, na walikuwa na nafasi ya kwanza moyoni mwake. Lakini mara tu alipofariki, kila kitu kikabadilika upande wao, na walikoma kuwa mabwana katika majumba yao wenyewe.

Muhammad Husein Haykal:

"Ni ya kukasirisha kwa kiasi gani zaidi ambako mandari hii fupi lazima imekuwa kwa Muhammad (s.a.w.) ambapo kwa wakati huo huo alikuwa akabiliane na mambo yenye umuhimu mkubwa sana kama jeshi la Usamah lililokwisha hamasishwa na hatma ya Ansari inayotishiwa na pia ya umma wa Waarabu uliounganishwa pamoja hivi karibuni na dini ya Kiislam?"

(The Life of Muhammad)

Sehemu yenye msisitizo ya swali hili ni siri kubwa mno. Inaelekea kwamba kulikuwa na utambulisho wa tishio hilo. Wote, Mtume (s.a.w.) mwenyewe na marafiki zake Ansari, walikuwa na wasiwasi wa kutokea kwa uovu fulani ambao ulining'inia kama wingu juu yao. Lakini ni nani anayeweza kuwatishia Ansari na kwa sababu gani?

355

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Katika mfuatano wa matukio hayo, ilikuwa wazi kuona kwamba watu pekee wanaoweza kuwatishia Ansari walikuwa ni wale wageni wao wenyewe wa zamani kutoka Makka -Muhajirina. Hakuna wengine mbali na Muhajirina, katika peninsula yote ya Arabia, aliyekuwa katika hali ya kutoa tishio kwenye usalama wa Ansari.

Aus na Khazraj walikuwa na chuki na kushukiana wenyewe kwa wenyewe. Walikuwa, kwa hiyo, rahisi kuhujumiwa na maadui zao. Na kwa vile viongozi wao walikuwa wanau-tambua unyonge huu miongoni mwa watu wao, walikuwa wako katika kujihami mle Saqifah. Na pale mmoja wa viongozi wao alipowaambia Muhajirina: "Tutachagua viongozi wawili - mmoja kutoka kwetu na mmoja kutoka kwenu," ilikuwa ni dhahiri kwamba alikuwa anazungumza kwa hali ya unyonge, sio umadhubuti. Kwa kule kupendekeza utawala wa pamoja, Ansari walikuwa wamefichua udhaifu wao wenyewe kwa wapinzani wao.

Clausewitz aliandika kwamba nchi inaweza kupuguzwa nguvu na athari za ugomvi wa ndani. Na chama pia kinaweza kupunguzwa nguvu na athari kama hizo hizo. Kimsingi ilikuwa ni athari hizo za ugomvi wa ndani ndizo zilizowashinda Ansari. Wao walikuwa wamechukua hatua potovu mbaya sana. Saad ibn Ubadah alikuwa amewatahadharisha kwamba walikuwa wanadhihirisha unyonge wao wenyewe kwa wapinzani wao lakini madhara yaliyotendeka hayawezi kubadilishwa hasa kwa vile Aus waliamini kwamba Muhajirina watakuwa waadilifu zaidi kwao kuliko Saad ibn Ubadah wa Khazraj.

Katika mjadala huo wa kusisimua, mkali na mrefu humo Saqifah, Abu Bakr aliwaambia Ansari, miongoni mwa mambo mengine, kwamba Waarabu hawatamkubali kiongozi ambaye hatokani na Quraishi. Lakini angeweza kuwa karibu sana na ukweli kama angekuwa amesema kwamba kiongozi asiyetokana na Quraishi hatakubalika kwake yeye binafsi, kwa Umar na kwa Muhajirin wengine wachache. Hata hivyo, yeye alijuaje kwamba Waarabu hawatakubali uongozi wa asiyekuwa Quraishi? Je, hayo makabila ya Waarabu yalituma ujumbe kwake kumueleza kwamba hawatamtambua Ansari yeyote kama kiongozi? Abu Bakr aliwajumuisha Waarabu wote kwa Muhajirina wachache ambao walitaka kujitwalia madaraka wenyewe.

John Alden William:

"Machimbuko ya Ukhalifa - Uimamu yamekuwa ni maswali yenye wasiwasi sana katika historia ya Kiislamu. Kundi lenye watu wengi, la Sunni, limeacha nyaraka zinazoelekea kuashiria kwamba ukhalifa ulikuja kuwepo kwa ghafla, na kama jibu kwa kifo cha Mtume (s.a.w.) mwaka 632. Alimradi Mtume (s.a.w.) alipokuwa hai, alikuwa ndio kiongozi safi - mwenye kuingilika, mpole, mwenye upendo wa ubaba, mpiganaji na hakimu, na "daima muadilifu" kwa watu wake. Sasa amekufa bila kutarajiwa. Wakiwa wanakabiliwa na pengo hili, na bila mrithi juu yake (sic), umma

356

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ulianza kugawanyika kwenye makundi ya makabila yake. Kwa hatua za haraka, Abu Bakr na Umar, walifanikiwa kufanya mmoja wao wenyewe kukubaliwa na wote kama mtawala. Maelezo ya kina ya matukio ya Umar, katika zamu yake alipokuwa mtawala, ni kama yafuatayo:

"Ninakaribia kuwaambieni kitu ambacho Allah (s.w.t.) amependa kwamba niweze kukisema. Yeyote yule anayekielewa na kukitii, naakichukue pamoja naye popote anapokwenda. Nimesikia kuwa mtu mmoja amesema kwamba, " kama Umar angek-ufa, ningemkaribisha fulani (yaani Ali) - (Mhariri). Mtu yeyote asijidanganye mwenyewe kwa kusema kwamba kule kukubaliwa kwa Abu Bakr kulikuwa ni jambo ambalo halikufikiriwa kwanza, ambalo (wakati huo) lilikuwa limeidhinishwa. Kwa hakika ilikuwa hivyo, lakini Allah (s.w.t.) aliepusha uovu wake. Hakuna yeyote mion-goni mwenu ambaye kwake watu watajitiisha wenyewe kama walivyofanya kwa Abu Bakr. Yeyote atakayemkubali mtu kama mtawala bila kushauriana na Waislamu, ukubalikanaji kama huo hauna uhalali kwa yeyote kati yao ... (wote) wapo katika hatari ya kuuawa. Kilichotokea ni kwamba pale Allah (s.w.t.) alipomchukua Mtume Wake, Ansari (watu wa Madina) walitupinga na wakakusanyika pamoja na wakuu wao katika ukumbi (wa Saqifah) wa Banu Saidah, na Ali na Zubayr na marafiki zao wakajiondoa kutoka kwetu (kuandaa mwili wa Mtume (s.a.w) kwa ajili ya mazishi -Mhariri) ambapo Muhajirina (wahamiaji kutoka Makka) walijikusanya kwa Abu Bakr.

Nilimuambia Abu Bakr kwamba ili tubadili tuende kwa ndugu zetu Ansari kwenye ukumbi wa Bani Saidah. Katikati yao alikuwepo (kiongozi wao) Sa'ad Ibn Ubadah ambaye alikuwa mgonjwa. Mzungumzaji wao ndipo akaendelea: Sisi ni wenye kum-nusuru Allah na ni kikosi cha jeshi la Uislamu. Ninyi, Enyi Muhajirina ni katika familia yetu na kikundi cha watu wenu walikuja kufanya makazi.

Na tazama! Walikuwa wanajaribu kutukata kutoka kwenye asili yetu (katika kabila ya Mtume - Mhariri) na kutupokonya mamlaka. Nilitaka kuzungumza, lakini Abu Bakr akasema, taratibu, Umar. Sikutaka ni muudhi, hivyo alizungumza kwa namna yake isiyo na kifan, vizuri zaidi kuliko ambavyo ningefanya mimi. Alisema. 'Mazuri yote mliyoyasema kuhusu ninyi wenyewe yanastahiki. Lakini Waarabu watAyatambua mamlaka katika makabila hili tu la Quraishi, wao wakiwa ndio Waarabu bora zaidi kwa damu na nchi.

Ninakupeni mmoja kati ya watu wawili hawa: mkubalini yule mumpendaye'. Baada ya kusema hayo aliukamata mkono wangu na ule wa Abu Ubaidah Ibn al-Jarrah (ambaye alifuatana nasi)."

(Themes of Islamic civilization 1971)

357

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kwa hatua za haraka, Dr. Williams anasema, Abu Bakr na Umar, walifanikiwa katika kupa-ta mmoja wao kukubalika kama mtawala. Kwa kweli kwa hatua za haraka Abu Bakr na Umar walifanikiwa katika kuwafanya wote wawili kukubalika kama watawala. Hatua zao za haraka pia zilihakikisha kwamba Ali (na Ansar) watawekwa nje ya baraza la siri la utawala. Humo Saqifa, madaraka na mamlaka yaliingia kwenye mikono yao, na hapo yalikuwa yadumu. Hata baada ya kufa kwao, watawala wa baadaye walikuwa wawe ni watu walioandaliwa tu na wao wenyewe. Huu ulikuwa ndio ustadi mkubwa wao mkakati wa mkuu. "Hatua za haraka" zilizaa malipo ya mwisho mazuri ya kushangaza juu yao!

Wazo muhimu la hotuba za Abu Bakr ndani ya Saqifah lilikuwani ubabaishaji. Ilikuwa pia ni moja ya siri za mafanikio yake. Ingawa alikuwa mgombea wa ukhalifa na alikuwa mwanachama wa upinzani kwa Ansari, alijitokeza kwao kama asiyetaka, asiye mfuasi, mtu wa tatu. Kama angeingia Saqifah kama mgombea au kama msemaji wa muhajirina, upinzani wa Ansari ungekuwa mgumu. Lakini aliwaambia:

"Ninakupeni mmoja kati ya watu wawili hawa - Umar na Abu Ubaydah. Mkubalini mmojawapo kama kiongozi wenu.."

Abu Bakr aliwasifu Ansari na akatambua utumishi wao mkubwa kwa Uislamu lakini juu ya yote, kwa kufanikiwa kujifanya kuwa huru na asiyependelea, alifanikiwa katika kuwapoza. Kuhusu Muhajirina alisema kwamba walikuwa na nafasi ya kwanza katika kuukubali Uislamu, na kwamba walikuwa wa kabila la Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Ansari, kwa kweli, hawangeweza kuyakataa madai haya. Aliendelea kuliimarisha suala la Muhajirina kwa kunukuu mbele yao Hadith ya Mtume (s.a.w.) ambayo ndani yake anadai-wa kusema:

"Viongozi watakuwa kutokana na Quraishi."

Kama nipe nikupe ya kumtambua yeye kama Amir (khalifa), Abu Bakr alipendekeza kuwafanya Ansari kwua mawaziri wake. lakini pendekezo hili lilikuwa ni kitulizo tu kwa Ansari. Kamwe hawakuwa mawaziri au washauri au chochote katika Serikali ya Saqifah. Katika kuyaeleza kwa mukhtasari matukio ya Saqifah, Umar alilalamika kwamba Ansari walikuwa "wanajaribu kuwaondoa kutoka kwenye asili zao."

Ni asili zipi hizo ambazo Ansari walikwua wakijaribu kumuondoa Umar, na kwa namna gani? Kauli hii haina usahihi. Katika ukweli wa mambo, hivi haikuwa ni Umar ambaye aliyekuwa akijaribu kuwaondoa Ansari kutoka kwenye asili zao?

Kila mara, ilionekana kwamba Umar alipotewa na kumbukumbu. Kulikuwa na nyakati ambapo alisahau amri za Allah (s.w.t.) kama zilivyoshuka kwenye Qur'an Tukufu. Kama yeye mwenyewe alivyokiri; na kulikwa pia na wakati ambapo alisahau matamko na maele-zo ya Mtume wa Allah (s.a.w). Hivyo inaonekana kwamba yeye hakuwa na kumbukum-

358

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

bu ya matukio mawili katika uhai wa Mtume (s.a.w.), moja likihusiana na ule Mkataba wa Pili wa Aghaba (A.D. 622), na hilo jingine likihusiana na vita vya Hunayn (A.D. 630), na yote yalihusiana na Ansari.

Katika Mkataba wa Pili wa Aghaba, Abul Haitham wa Yathrib (Madina ya baadae), alimuuliza Muhammad Mustafa (s.a.w.) swali lifuatalo:

"Ewe Mtume wa Allah! Kitakuja kutokea nini wakati Uislamu utakapokuwa imara;

je utaondoka tena Yathrib na kurejea Makka, na kuifanya ndio Makao yako Makuu?"

"Kamwe," ndio lilikuwa jibu la dhahiri la Mtume wa Allah (s.a.w). kwa Abul Haithum na wenziwe. "kuanzia siku hii ya leo, damu yenu ni damu yangu, na damu yangu ni damu yenu. Kamwe sitawaacheni ninyi, na ninyi na mimi tutakuwa hatuten-ganishiki," aliwahakikishia.

Wakati ulifika ambapo Uislamu ulikuwa imara na hai na Muhammad Mustafa (s.a.w.) alikumbuka ahadi yake kwa Ansari. Aliifanya Madina - mji wao - makao makuu ya Uislamu. Muhammad (s.a.w.) hakuwahi kamwe kuwaambia Muhajirina kwamba damu yake ni damu yao au damu yao ni damu yake. Ilikuwa, kwa hiyo, ni Umar aliyekuwa aki-jaribu kuwakata Ansari kutoka kwenye asili zao, na sio vinginevyo. Kadhia ya pili ilitokea mara tu baada ya vita vya Hunain. Mtume (s.a.w.) aliwaamuru Ansari kukusanyika katika hema huko Jirana, na walipokusanyika, aliwahutubia kama ifuatavyo:

"...Mimi sitawaacheni ninyi kamwe. Kama wanadamu wote wakienda upande mmoja, na watu wa Madina wakaenda upande mwingine, mimi nitakwenda njia waliyokwenda watu wa Madina Allah (s.w.t.) aliridhie juu yao, na awabariki, na watoto wao na watoto wa watoto wao daima."

Muhammad-Mtume wa Allah (s.a.w) aliwambia Ansari kwamba yeye angekwenda njia yao hata kama dunia yote iliyobakia wakienda njia nyingine. Katika kuwapinga na kuwashinda hawa Ansari, mtu anaweza kuona ni njia ipi waliyokwenda Muhajirina. Muhammad (s.a.w.) na Ansari walikuwa wamechagua upande mmoja wa kusafiria. Lakini mle Saqifah, Muhajirina walichagua upande uliopotoka juu yao wenyewe!

Umar pia alikamata "Mamlaka" ambayo, alisema, Ansari walikuwa wakijaribu "Kutunyang'anya." Kauli hii tena inakosa Mashiko. Ni "mamlaka" gani ambayo Umar alikuwa akiyazungumzia juu yake? Na ni " mamlaka" gani aliyokuwa nayo hata hivyo? Ni nani aliyempa hayo mamlaka ambayo Ansari walikuwa wakijaribu kuyapora kutoka kwake? Na kwa nini aliingia Saqifah? Hivi hakuingia pale kupora mamlaka kutoka kwa Ansari?

Ule mkutano ndani yaukumbi wa Saqifah ulikuwa na jambo moja tu katika " ajenda" yake, nalo lilikuwa ni "mamlaka." Ilikuwa ni Abu Bakr na Umar waliofanikiwa katika kuyashika mamlaka yale. Mara yalipokuwa mikononi mwake, Umar angeweza kuwa mkosoaji na angeweza kumudu kuwakemea Ansari kwa kujaribu kwao kumuondoa kutoka kwenye

359

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"asili" yake, na kwa kujaribu kupora "mamlaka" kutoka kwake.

Kama ilivyoelezwa kabla, wakati Mtume (s.a.w.) alipofariki, Abu Bakr hakuwepo pale Msikitini. Alikuwa yuko Sunh, mbali kidogo kutoka Madina. Kutokuwepo kwake kulim-tia Umar kwenye fadhaa kubwa. Alipunga upanga hewani na kutishia kumuua yeyote ambaye angesema kwamba Mtume amefariki. Hii hali ya karibu-kupagawa ilisababishwa na hofu wasije wale Waislamu mle Msikitini wakampa Bay 'ah (kiapo cha utii) Ali ibn Abi Talib, na wakamtambua yeye kama mtawala wao. Lakini akiwa hajui ni wakati gani Abu Bakr atatokea, yeye alimgeukia Abu Ubaidah, na akamwambia: "Ewe Abu Ubaidah! Nyoosha mkono wako, na nitakupa kiapo changu cha utii ili uweze kuwa Amir wa Waislamu. Nimemsikia Mtume wa Allah (s.w.t.) akisema kwamba wewe ndiye Amiin (mwaminifu) wa Umma huu."

Lakini Abu Ubaidah akakataa kupokea kiapo cha Umar, na akamuonya akisema:

"Maajabu gani ya dunia hii, Ewe Umar, uweze kunipa mimi Ukahalifa ambapo mtu kama Abu Bakr yupo miongoni mwetu? Umesahau kwamba yeye ndiye "Sidiq" na ni wa pili kati ya wawili wakati wote kwa pamoja walipokuwa ndani ya pango."

Jibu la Abu Ubaida lilimucha Umar hana la kusema. Yeye akaonekana "mwenye kupa-gawa" tena, akitishia kumuua yeyote ambaye angesema kwamba Mtume alikuwa amefariki, na akabakia katika hali hiyo mpaka Abu Bakr alipokuja. Abu Bakr alipokuja, yeye (Umar) mara moja akapona " mpangao " wake.

Baadae kidogo, ile "kamati ya watu watatu" ya Abu Bakr, Umar na Abu Ubaidah ilitum-bukia ndani ya Saqifah. Humo Abu Bakr aliwashawishi Ansar kutoa kiapo chao cha utii kwa Abu Ubaidah au kwa Umar. Katika muda chini ya saa moja, Abu Ubaidah ibn al-Jarrah, mchimba kaburi wa Madina, alikuwa amekwishapokea pendekezo la kuwa mtawala wa Arabia mara mbili - kwanza kutoka kwa Umar na kisha kutoka kwa Abu Bakr. Yeye lazima iwe alikuwa mtu wa kusifika sana kuweza kupendekezwa, sio na mtu mmoja tu, bali na wenye athari juu ya uchaguzi wawili!

Kwa kweli, mbali na ukweli kwamba alikuwa ni mfuasi wa awali wa Uislamu, Abu Ubaidah hakuwa na kingine chochote cha kuonyesha. Kuhusu yeye, yule mwanahistoria wa Kiingereza, Sir William Muir, anaandika katika kitabu chake The life of Muhammad hivi:

"Hapakuwa na chochote katika yaliyotangulia ya Abu Ubaidah cha kukubaliana na madai ya ukhalifa. Alitajwa hivi hivi tu na Abu Bakr kwa kuwa kwake Quraishi mwingine pekee aliyekuwepo."

Sir William Muir yu sahihi katika kuonyesha kwamba hakuna chochote katika yaliyotangulia ya Abu Ubaidah cha kuweza kukubaliana na madai ya Ukhalifa. Lakini basi, kulikuwa na kitu gani katika yaliyotangulia ya Umar mwenyewe cha kukubaliana na madai

360

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kama hayo? Ni lini na wapi alipojidhihirisha yeye mwenyewe katika kuutumikia Uislamu, ama kwenye medani ya vita au kwenye baraza?

Hapa mwanahistoria huyu anaonyesha mshangao kwamba Abu Bakr angeweza kupen-dekeza ukhalifa kwa Abu Ubaidah, mtu asiyekuwa na chochote katika habari zake zilizo-pita. Lakini huenda hakutambua kwamba katika hali iliyoko kwenye uchunguzi, suala la mambo yaliyopita ya mgombea wa ukhalfia, halikuwa na uhusiano wowote. Hawa wenye sauti katika uchaguzi wangependekeza ukhalifa kwa mtu yeyote miongoni mwa Muhajirina alimradi tu kwamba mtu huyo hakuwa ni Ali ibn Abi Talib au mtu mwingine wa ukoo wa Muhammad Mustafa Mtume wa Allah (s.a.w.).

Sir, William Muir anasema kwamba Abu Bakr alimtaja Abu Ubaidah kwa sababu tu ndiye alikwua Quraishi pekee aliyekuwepo. Hapa tena amesema kweli. Haina budi, hata hivyo, ikubmukwe akilini kwamba Abu Bakr na Umar walikuwa wamehusika na kazi muhimu sana ya kuteua Kiongozi Mkuu wa Ufalme wa Mbingnii juu ya Ardhi. Mtu anaweza kuuliza kama wangeweza kuwa wabahatishaji kama walivyokuwa. Na ni nini kingetokea kama badala ya Abu Ubaidah, Quraishi mwingine, Abu Sufyan - angekuwepo pale? Hivi Abu Bakr angependekeza ukhalifa kwake? Kweli kabisa, angeweza. Hata hivyo Abu Sufyan hakuwa mtu wa kabila la Quraishi tu bali pia alikuwa mmoja wa wakuu ambapo sio Abu Ubaidah wala Umar wala hata yeye mwenyewe walikuwa wakuu.

Umar na Abu Bakr walikuwa wakizunguka wakipendekeza utawala wa Arabia kwa mtu wa "kustahiki" lakini je utawala huu ulikuwa ni mali ya mtu ambao wangeweza kuuweka juu ya mtu yeyote waliyetokea kumpenda? Kama ulikuwa, basi ni nani aliyewapa? Hata hivyo, wao hawakuurithi. Kama haikuwa hivyo, basi walikuwa na haki gani kuutoa kwa mtu yeyote? Walikuwa wakizunguuka kupendekeza kitu ambacho sio chao. Kama hawakuja kukimiliki kwa njia za haki, kisheria, kwa njia iliyokubaliwa na Allah (s.w.t.), basi walikuwa wanamiliki kitu ambacho ni wazi kabisa wamekipora.

Kugombea uongozi, baada ya kifo cha Muhammad (s.a.w.) kulikuwa wazi tu kwa watu wa kabila la Quraishi, na sio kwa mwislamu mwingine yeyote. Abu Bakr, Umar na Abu Ubaidah - ile "kamati ya watu watatu" walitengeneza kanuni za ugombea huo, na kanuni hizo zilikuwa zenye kubadilika. Sasa Bani Hashim walikuwa pia ni ukoo wa Kiquraishi, na wao pia walikuwa watolewe katika ugombea madaraka. Lakini vipi? Hili lilileta tatizo kwa kamati ya watu watatu. Kamati hii iliweza kuliepuka tatizo hilo kwa werevu ambao ni muhimu kuswalia katika jangwa. Ilitangaza kwa ukweli kwamba ukoo wa Bani Hashim ulitoa Mtume kwa ajili ya Waarabu - heshima kubwa sana juu yao na kwamba walipaswa kuridhika nayo; na kuhusu warithi wake, haitakuwa kwa maslahi ya Umma kama Bani Hashim watawatoa wao pia; kwa hiyo, koo mbali na Bani Hashim zingepaswa kuwatoa wao.

Koo hizo zingekuwa zipi, ilikuwa ni juu ya "kamati ya watu watatu" kuamua. Zile koo ambazo hawa watu wa " kamati ya watu watatu" wenyewe wanazotoka, zitakuwa, bila

361

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

shaka ndio za kwanza.

Hivyo kile kilichothubutu kuwa chombo chenye thamani sana kwa kabila la Quraishi, yaani kuwemo kwa Muhammad (s.a.w.) Mtume, ndani yake kulithibitika kuwa ni "Madaraka" makubwa mno kwa ukoo wa Bani Hashim. Hawa Bani Hashim "waliondole-wa" kwenye kushiriki katika kugombea mamlaka kwa sababu tu Muhammad alitokana na wao!

Umar alifanya mgeuko wa nyuzi 180 humo Saqifah. Kabla ya kuingia Saqifah, alikuwa akitoa ubashiri kwamba kama ile familia iliyotoa mtume, ingekuwa pia itoe mrithi wake, "Waarabu" wataasi dhidi yao. Lakini alipokabiliana na Ansari mle Saqifah, alitabiri kwamba "Waarabu" hawatakubali uongozi wa mtu kama hakuwa wa kabila ambalo Mtume mwenyewe anatokana nalo. Yeye na Abu Bakr waliweka madai ya ukhalifa kwa misingi ya kwamba wao wote walikuwa watu wa kabila moja na Muhammad (s.a.w.) ambapo wao Ansari hawakuwa.

Al-Marehemu Maulana Abu Ala Maududi wa Pakistani ametoa sifa za juu sana kupin-dukia, juu ya Maquraishi. Anasema kwamba watu wa kabila la Quraishi ni watu wenye vipaji na uwezo wa kipekee, na walitoa viongozi wote wa Waislamu. Kuyafanya madai yake yasadikike, amenukuu maelezo yenye kudai ubora wao, ambayo anasema, yalitolewa na Mtume (s.a.w.) na Ali ibn Abi Talib.

Lakini inawezekana kabisa kwamba Ansari wangeweza kutoa viongozi wakuu kama hao hao, au kwa kweli hata wakubwa zaidi kuliko Maquraishi waliotoa. Lakini "kamati ya mtu watatu" waliwapigia turufu kuwazuia wasiingie mle Saqifah na umma wa Kiislam haukuweza kufaidika na ustadi wao wa uongozi.

Usahihi wa maelezo yanayowasifia Maquraishi ambayo Maududi ameyahusisha kwa Ali, yanatia wasiwasi. Ali angepata machache sana ya kusifia katika Quraishi. Alikuwa hajafikia hata umri wa miaka kumi na nne walipofanya jaribio la kwanza la kumzuia Muhammad (s.a.w.). Ali alikabiliana na upinzani wao. Upanga wake siku zote ulikuwa uki-tiririka damu yao ya kipagani au ya watetezi wa upagani. Yeye na wao walikuwa katika makabiliano ya kudumu maisha kati yao.

Waislamu wa Shia wanapingana na kanuni ya uchaguzi wa kiongozi kwa misingi ya kujit-walia au "kutangulia" tu. Kwa mujibu wao, mapendekezo, yanayodhibiti katika kuchagua kiongozi lazima yasiwe ni uhusiano wake na Quraishi au umri wake, bali tabia yake, uadil-ifu wake, uwezo na uzoefu. Tabia inakuja ya kwanza. Jinsi gani kiongozi wa Waislamu anavyofanya aeleweke mwenyewe kwenye maisha - sio tu kwa jukumu hili au lile, sio kwa muda huo, bali kwa kudumu na kwa upeo wa ufahamu.

362

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Uchaguzi wa kiongozi unahitaji uchunguzi wa hali ya juu unaofikia mbali zaidi ya tabia za kimaadili. Hata hivyo, uongozi wa Waislamu (ukhalifa) sio zawadi katika mashindano ya maadili. Kiongozi (khalifa) lazima awe mtu, sio tu mwenye tabia njema na uadilifu bali pia mwenye uwezo wa dhahiri na uzoefu mkubwa. Kwa maneno mengine, uteuzi wa mgombea bora, - bora katika kila hali ya istilahi hiyo; wa juu katika uadilifu binafsi bali pia mtu mwenye uwezo ambao umeonyeshwa, kuthibitishwa - sio mara moja au mbili bali kwa mara nyingi lazima iwe ndio kanuni. Na kwa kweli lazima awe na ile sifa ya ziada bali ya lazima na tena adimu iitwayo taqwa.

Hao wateuzi; kama kipo chombo kama hicho, wanao wajibu juu ya uchanguzi wa makini na kamilifu wa sifa zote za ustahilifu, na maelezo binafsi ya siku za nyuma ya mtu ambaye ataweza kuwa mgombea wa nafasi hiyo ya juu sana katika Uislamu. Lazima wapime uwezo wake, maamuzi, uhuru na muonekano wa utulivu wake kwa masharti ya kama ndiye mtu ambaye wanaweza kwa makini sana kumuidhinisha kama anayeweza kuwa khalifa.

Kama tulivyokwishaona, tabia na uwezo wa mgombea au wagombea wa ukhalifa haviku-jadiliwa mle Saqifah. Yalikuwa ni mambo "yasiyohusika". ufasaha wa Muhajiri na Ansari ulizalisha swali moja tu, yaani, je, kiongozi wa Waislamu, awe Muhajirin au Ansari?

Ansari walikubali kushindwa mle Saqifah walipokabiliwa na werevu wa wapinzani wao, Muhajirina, kwamba ukahifa wa umma wa Kiislam ulikuwa ni "haki" pekee ya Quraishi kwa sababu Muhammad (s.a.w.) mwenyewe alikuwa ni Quraishi!

363

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

SAQIFAH NA MANTIKI YA HISTORIA

Katika utangulizi wa kitabu hiki, nilimtahadharisha msomaji juu ya tabia na wepesi wa Mustashriq wengi, kukubali, bila kuangalia undani wake, mengi ya maelezo ya uongo na madai ya uongo ambayo yaliingizwa kwenye mzunguko, zamani sana, na wale wanahis-toria ambao walikuwa kwenye "orodha ya malipo" ya Serikali ya Damascus na Baghdad - zote zikiwa warithi wa Serikali ya Saqifah. Kwa mfano kuna makubaliano miongoni mwao kwamba Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.) hakuchagua mrithi wake mwenyewe wala hakuwaambia Waislamuu namna wanavyopaswa kuchagua viongozi wao kwa ajili ya Serikali ambayo aliianzisha, na alifariki akiacha kila kitu, dhahiri kabisa, kwenye mashauri yao na hiari zao.

Baadhi ya mifano ya kukubali kusiko na udadisi kwa Mustashriq juu ya dai hili, ilitoka katika Sura ya 45. Ufuatao ni mfano mwingine zaidi.

"Muhamamd alifariki hapo Madina mnamo tarehe 8, Juni, 632, bila ya kuacha maagizo kwa ajili ya Serikali ya baadae ya jamii ya Waislamu."

Habari hii inatokea kwenye makala yenye kichwa cha habari Caliphate, kwenye ukurasa wa 643, juzuu ya 4, chapa ya 14 ya 1973 ya Encyclopedia Britannica. Ni kipande cha propaganda cha dhahiri lakini hiyo Encyclopedia Britannica, kile kienezaji kikuu cha elimu, kimeikubali. Ni taarifa ya uongo ya kihistoria yenye kugawa mno katika Uislamu, lakini cha ajabu, inapita bila kupingwa, karne baada ya karne.

Hawa Mustashirki wanaweza wasilete pingamizi kwenye huu uongozi wa muda mrefu unaokubalika kwenye mila na desturi, lakini hata hivyo unazua maswali fulani ya msingi. Maswali hayo ambayo yanahusiana na maadili ya Uislamu na falsafa ya kisiasa ya Muhamamd Mtume wa Allah (s.a.w.) yameorodheshwa hapo chini. Yote yanasimama kwenye dhana ya kwamba Muhamamd (s.a.w.) haku...(rudia haku.J hakuteua mrithi wake mwenyewe wala hakutoa maagizo yoyote kwa maswahaba zake kwa ajili ya serikali ya baadae ya umma wa Kiislam. Kwa hiyo, wakati alipofariki, Umma wake ulijikuta wenyewe katika hali ya mfadhaiko mkubwa kabisa.

1. Je, Muhammad (s.a.w.) Mtume wa Allah (s.w.t.) na Muasisi wa Serikali ya Madina, alijiona binafsi ni mwenye uwezo wa kuchagua mrithi wake mwenyewe au la?

364

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

2.    Kipi kingefaa, ni sababu za kubuni juu ya kushindwa kwa Muhammad (s.a.w.) kuteua mrithi wake mwenyewe?

3.    Kwa vile Muhamamd (s.a.w.) hakuteua mrithi wake mwenyewe, je, aliik-abidhi jamii ya Waislamu jukumu hilo la kuchagua au kuteua kiongozi wao wenyewe?

4.    Kwa vile jamii ya Kiislamu ilikosa mwongozo juu ya kuteua kiongozi, je maswahaba wa Muhamamad, kwa ridhaa yao ya pamoja, na kabla ya kuweka kiongozi (au hata baada ya kuweka kiongozi) waliandaa orodha ya masharti au miongozo ambayo wao waliishika (baadaye)?

5.  Upi ulikuwa msimamo na mwenendo wa maswahaba wakubwa wa Muhamamd (s.a.w.) juu ya uongozi wa jamii ya Waislamu baada ya kifo chake?

6.  Upi ulikuwa mwenendo (Sunnah) wa Muhamamd (s.a.w.) kuhusiana na uteuzi na uwekaji wa watumishi?

7.   Ni ipi Fatwa ya Qur'an juu ya mwenendo (sunnah) wa Muhamamd

8.    Muhamamd (s.a.w) alifanya nini hasa kuhusu kurithiwa kwake?

9.     Ni nini hasa kilichotokea baada ya kifo cha Muhammad (s.a.w)?

10.  Je, swala la urithi lina umuhimu gani katika historia kwa jumla? Jaribio limefanyika katika kujibu maswali haya kama ifuatavyo:

Swali la 1

Je, Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w.), na muasisi wa Serikali ya Madina, aliona binaf-si yeye ni mwenye uwezo wa kuchagua mrithi wake mwenyewe au la?

Jibu

Hakuna hata mtu mmoja ambaye angefikiria, kati ya Waislamu wote, kwamba Muhamamd hakuwa na uwezo na kumuweka mrithi wake mwenyewe. Mwislamu hawezi kudhania kwamba Mtume (s.a.w.w) alikosa uwezo wa kuteua mrithi kwa ajili yake mwenyewe.

Waarabu walikuwa ni kizazi chenye sifa mbaya ya kiburi, cha wajinga, wenye ghasia na wasio na sheria. Muhamamd (s.a.w.) alizieneza sheria za Allah (s.w.t.) miongoni mwao, na

365

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

akawalazimisha kuziheshimu na kuzitii sheria hizo. Aliunda taasisi ya kisiasa iliyoitwa Dola au Serikali ya Madina. Katika Dola hiyo, madaraka yake yalikuwa hayana mpaka. Aliwachagua watumishi wake wote, wa kiraia na kijeshi. Aliweza kumuweka mtumishi au kumfukuza, bila kufuata msingi maalum, na bila ya kutoa sababu zozote kwa mtu yeyote kwa kufanya hivyo.

Mwelekeo wa tabia (sunnah) ya Muhammad (s.a.w.) ilikuwa thabiti na ya kudumu daima. Alikuwa kwa kweli, ni mwaminifu kiasi kwamba alikuwa takriban ni "mwenye kutabiri-ka." Waislamu wote walijua kwamba angeteua na kuweka watu wenye uwezo katika nafasi zote muhimu, na pia walijua kwamba angefanya hivyo bila kushauriana nao. Wala haku-toa mamlaka kwa maswahaba wake wo wote ya kuweka watumishi. Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w.). pekee ndiye alikuwa na uwezo wa kuteua na kuweka mrithi wake mwenyewe, na hakuna yeyote ambaye angemfanyia hivyo badala yake.

Swali la 2

Kipi kingefaa, ni sababu za kubuni juu ya kushindwa kwa Muhamamad (s.a.w.) kuteua mrithi wake mwenyewe?

Jibu

Kama Muhammad (s.a.w.) angekufa bila ya kuchagua mrithi na atakayemfuata baada yake, anajiweka kwenye lawama ya kutotekeleza wajibu. Yeyote anayedai kwamba yeye hakuchagua mrithi wake, anashauri kwamba alikiacha chombo dhaifu cha Uislamu kwenye bahari iliyochafuka bila ya dira, bila ya usukani, bila ya nanga na bila ya Nahodha, na kukiacha kabisa kwenye huruma ya upepo na mawimbi. Ni kudhania kwamba hakuwa mwangalifu wa maslahi muhimu kabisa ya umma wa Kiislamu na kwamba alikuwa amezembea kwenye ustawi wa vizazi vya Waislamu, vitakavyokuja baadae. "Uzembe" kama huo kwa upande wake ungeweza kuwa na sababu tatu zinazowezekana, yaani:

a) Watu wote wa Umma wa Kiislamu wamekuwa wenye ufahamu mkubwa, wenye heki-ma, wacha-mungu na wenye kumpenda Allah (s.w.t.) na kila mmoja wao alikuwa amepa-ta elimu kamili ya tafsiri ya Qur'an. Vile vile kila mmoja alikuwa analingana, katika kila hali na kila mtu mwingine. Ilikuwa haiwezekani kwa shetani kumshawishi au kumpoteza yeyote kati yao. Kwa hiyo, Muhammad (s.a.w.) angeweza kuacha wajibu wa kuteua na kuchagua mrithi wake kwenye fursa ya kubahatisha. Angeweza kufarijika kwa kudhani kwamba yeyote yule atakayefanywa kiongozi wa jamii hiyo kwa mkondo wa matukio, atakuwa ni mtu sahihi, na Serikali ya Madina na jumuiya ya waumini vyote vingeweza kuwekwa chini ya uangalizi wake.

Lakini hivyo sivyo ilivyokuwa na isingeweza kuwa hivyo. Haiwezekani hata kwa watu wawili kulingana katika uwezo, tabia na desturi. Muhammad (s.a.w.) alijua kwamba

366

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Waarabu wote waliokubali Uislamu, sio lazima kuwa walikuwa wote ni Waislamu waaminifu. Miongoni mwao, ilikuwemo idadi kubwa ya "wanafiki" au "Waislamu wachache." Kuwepo kwao pale Madina kunashuhudiwa na Qur'an yenyewe. Waliukubali Uislamu kwa nje tu bali moyoni walikuwa wapagani. Walikuwa ndio maadui wa Muhamamd, wa Uislamu, na wa Dola aliyokuwa ameianzisha. Walifanya "safu ya tano" ya upagani hapo Madina, tayari kutumia fursa ya kwanza ya kuudhoofisha Uislamu. Kama Muhammad (s.a.w.) angekuwa aiache Dola hii mpya bila ya kiongozi, kwa kweli angeiwe-ka mkononi mwa hawa wahujumu wa kiitikadi, silaha zenyewe hasa ambazo kwazo watauangamizia.

Muhammad aliyajua yote haya, na alifariki, sio ghafla, bali baada ya maradhi ya muda mrefu, yeye alikuwa na muda wa kutosha kushughulikia mambo muhimu ya Dola, lenye umuhimu zaidi likiwa ni uteuzi wa usimamishaji wa mrithi wake mwenyewe. Kitu kimo-ja ambacho asingeweza kukifanya, kilikuwa ni kuitelekeza serikali yake, ambayo ilikuwa ni Ufalme wa Mbinguni Duniani, kwenye uangalizi wa mpenda fursa asiyejulikana au mpenda vituko mwenye majigambo.

b) Muhammad (s.a.w.) hakuupenda hasa Uislamu. Alitiwa shauku tu na malengo yake binafsi. Alitaka kuiweka peninsula yote ya Arabia chini ya mamlaka yake, na Uislamu ulikuwa ndio njia ya ambayo alifanikiwa nayo katika kufanya hivyo. Lakini mara alipo-timiza lengo lake hakujali kwamba baada ya kufa kwake, ile serikali ambayo ameianzisha, ilikuwa imara au ilichanguka. Hakujali kama, baada ya kifo chake, Waarabu walibakia waaminifu kwa Uislamu ama walirejea kwenye uabudu masanamu na ushenzi.

Ni nini kitakachokuwa cha kipumbavu zaidi kuliko kudhania kwamba Muhammad (s.a.w.) hakuupenda Uislamu? Akiwa Makka, alivumilia mateso, njaa, kiu, kunyimwa, ufidhuli na uhamisho, yote hayo kwa ajili ya Uislamu. Wakati alipokuwa Madina alitakiwa kutoa mihanga mikubwa zaidi kwa ajili ya Uislamu. Wawili wa ami zake, binamu zake watatu, watoto wa kufikia wawili na ndugu mmoja wa kunyonya, na marafiki wengi waliuawa katika kuutetea Uislamu. Kwa wakati upasao, akawa mkuu wa Madina lakini hakuna cho-chote kilichobadilisha mtindo wa maisha yake. Watu wengi wa jumuiya hiyo mpya walikuwa mafukara, naye aliwalisha. Aliwalisha chakula chake yeye mwenyewe kiasi kwamba mara nyingi, yeye na wanawe walilazimika kukaa na njaa. Hii iliendelea mwaka baada ya mwaka. Alifanya makafara yote haya na mengine yasiyo na idadi kwa ajili tu ya kuufanya Uislamu uweze kuwepo na uwe na nguvu.

Hapo Makka, Maquraishi walimuahidi Muhammad madaraka, utajiri na vivutio kama angeiacha kazi yake kama Mtume wa Uislamu. Lakini alivipiga mateke vyote hivyo. Katika kuvipiga mateke hivyo, alikuwa akiipiga mateke "tamaa." Labda haikumjia kwamba kulikuwa na kitu kama tamaa. Kiini hasa cha kazi yake kwa ajili ya Uislamu kilikuwa ni mapenzi yake tu juu yake. Mapenzi haya yalimchukua kutoka mwanzo hadi mwisho.

367

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Alikuwa na "tamaa" moja tu katika maisha, nayo ilikuwa ni kuona Uislamu unakuwa ni wa kudumu. Aliitimiza "tamaa" hiyo kwani tunajua kwamba Uislamu ni wakudumu milele.

C) Muhammad (s.a.w.) hakuteua mrithi wake kwa sababu alikuwa anaogopa upinzani.

Muhammad (s.a.w.) alikuwa haijui kabisa hofu. Aliushinda upagani katika wakati ambapo yeye alikuwa peke yake katika dunia nzima, na kwamba dunia yote ilikuwa imejaa uhasama dhidi yake. Upagani ulitumia nguvu zake zote ili kumvunja lakini ulishindwa. Yeye aliuvunja. Kwa kutumia ujasiri wake binafsi, alipata ushindi juu ya dunia nzima. Katika mawili kati ya mapambano ya Uislamu, Waislamu walishindwa, na walikimbia kutoka kwenye medani ya vita. Lakini yeye alisimama imara na hakukimbia, na kwa kweli, alikuwa ni kiungo cha kukusanyikia watoro wa vita. Utulivu wake wa akili ulihuisha ule ushupavu wa Waislamu, na wakarudi vitani.

Baada ya vita ya Hunain, Arabia yote ilikuwa chini ya miguu ya Muhammad (s.a.w.), na hakuna kabila au muungano wa makabila ambao uliweza kushindana na nguvu zake. Nguvu zake, ndani ya peninsula, zilikuwa kubwa. Suala la yeye kuogopa upinzani wa mtu yoyote, kwa hiyo haliji.

Swali la 3

Kwa vile Muhammad (s.a.w.w.) hakuteua mrithi wake mwenyewe, je, aliikabidhi jamii ya Waislamu jukumu hilo la kuteua na kuchagua kiongozi wao wenyewe?

Jibu

Kuteua Mtendaji Mkuu wa umma wa waumini lilikuwa ni jambo muhimu. Muhammad (s.a.w.) alitambua umuhimu wake. Lakini kwa sababu zisizojulikana, alijizuia kumteua. Sababu pekee inayowezekana kwamba hakumteua inaweza kuwa kwamba aliuachia umma jukumu hilo.

Lakini si Abu Bakr na Umar wala wanahistoria wa baadae wa Sunni, ambao wametoa dai hili kamwe. Hawajadai, kwa mfano, kwamba Muhammad Mustafa (s.a.w.) alisema: "Enyi Waislamu! Sipendi nijichagulie mrithi wangu mwenyewe,"

au "Siwezi kujichagulia mrithi wangu mwenyewe,"

au

"Sina uwezo wa kuchagua mrithi wangu mwenyewe. Kwa vile sina uwezo huo, ninakuachieni ninyi wajibu huo. Nitakapofariki, mnateua na kuchagua kiongozi wenu wenyewe."

Hakuna hata mtu mmoja aliyejaribu kuhusisha kauli kama hiyo kwa Muhammad Mustafa (s.a.w.). Muhammad Mustafa (s.a.w.) hakuwapa maswahaba zake mamlaka ya kuteua hata

368

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mtumishi mdogo seuze kwa kiongozi mkuu wa baadae wa Dola ya Kiislamu! Swali la 4

Kwa vile jamii ya Kiislamu ilikosa mwongozo juu ya kuteua kiongozi, je, maswahaba wa Muhammad (s.a.w.), kwa ridhaa yao ya pamoja, na kabla ya kuweka kiongozi (au hata baada ya kuchagua kiongozi) waliandaa orodha ya masharti au mwongozo ambao wal-iushika (baadae)?

Jibu

Masahaba wa Muhammad (s.a.w.) hawakuandaa, katika wakati wowote, mfumo wa masharti wa kuwaongoza katika kuchagua kiongozi. Katika jambo hili, walishika kanuni ya kuangalia manufaa yao. Kwanza waliteua kiongozi, na kisha wakaunda "masharti" au "kanuni" kwa ajili ya uchaguzi wake. Waislamu "walichagua" wale makhalifa wa kwanza "walioongoka" wanne. Uteuzi wa kila mmoja wao ulisababisha kugunduliwa kwa "masharti" mapya au "kanuni" mpya. Hizi "kanuni" nne ziliunganishwa ipasavyo katika fikra za kisiasa za Waislamu.

Lakini mara khalifa mpya akaingia madarakani huko Syria. Kuibuka kwake kulisababisha kugunduliwa kwa "kanuni" mpya ijulikanayo kama " mwenye nguvu mpishe." "Kanuni" hii ilizifanya zile "kanuni" nne za kwanza kuwa zisizotumika tena. Kutoka wakati huu, ukhalifa ukawa uwe ni tuzo ya mgombea aliyeweza kutumia nguvu ya kinyama kwa ukatili zaidi kuliko wapinzani wake. "Kanuni" hii imepata ukubalikanaji wa kimataifa miongoni mwa Waislamu katika historia yao yote ndefu .

Swali la 5

Upi ulikuwa msimamo na mwenendo wa maswahaba wakubwa wa Muhammad (s.a.w.) juu ya uongozi wa jamii yaWaislamu baada ya kifo chake?

Jibu

Waislamu wa Sunni wanasema kwamba Abu Bakr na Umar ndio walikuwa maswahaba wakuu wa Muhammad Mustafa (s.a.w.). Walikuwa ni wote hao, maswahaba wakuu, ambao walitwaa Dola ya Madina katika wakati ambapo Ali na watu wote wa Bani Hashim walikuwa wakishughulika na mazishi yake.

Mara tu Mtume (s.a.w.) alipofariki, maswahaba zake wakubwa walikusanyika katika Ukumbi wa Saqifah kudai uongozi wa umma. Uongozi huu, kwa maoni yao, ulikuwa ni muhimu sana kiasi kwamba hawakuweza kutulia hata kumzika bwana na mfadhili wao aliyefariki. Kushindania madaraka kwa wazi kuliibuka kwa dakika chache tu za kifo cha

369

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mtume (s.a.w.). Zamakhshari, mmoja wa wanazuoni na wanahistoria wa kuaminika wa Sunni, anaandika kuhusiana na hili, hivi:

"Yalikuwa ni makubaliano ya maswahaba wote kwamba baada ya kifo cha Mtume ili-wabidi wateue mrithi wake mara moja. Waliamini kwamba kufanya hivyo ilikuwa ni muhimu zaidi kuliko hata kushughulikia mazishi ya bwana wao. Ulikuwa ni umuhimu huu ambao ulimchochea Abu Bakr na Umar kuhutubia ule mkusanyiko wa Waislamu. Abu Bakr alisema: 'Enyi watu! hebu nisikilizeni. Wale kati yenu waliokuwa wakimuabudu Muhammad, nawajue ya kwamba amekufa; lakini wale waliokuwa wakimuabudu Allah, nawajue kwamba Yuko hai, na kamwe hatakufa. Kwa vile Muhammad amekufa, inawabidi sasa muamue ni nani atakayekuwa kion-gozi wenu wa baadae.' Wakasema: 'Umesema kweli; ni lazima tuwe na kiongozi mpya.' Sisi Sunni na Mu'tazili, tunaamini kwamba umma wa Waislamu ni lazima kwa wakati wote usikae bila ya kiongozi. Mantiki peke yake inaamuru hivi. Pia, Mtume wa Allah (s.a.w). alitekeleza sheria, na alitangaza rasmi amri kuhusu kuulin-da Uislamu, na ulinzi wa Madina na ulinzi wa Arabia. Baada ya kifo chake, anapaswa awepo mtu wa kutekeleza sheria zake, na kutekeleza amri zake."

Kutokana na ushahidi huu uliopita, ni dhahiri kwamba maswahaba wa Mtume (s.a.w.) walitambua ilivyokuwa muhimu kwa umma kupata kiongozi. Walijua kwamba kama hapakuwa na mtu wa kutekeleza sheria na amri alizozitangaza, umma wake ungeangukia kwenye vurugu.

Hali hiyo imejawa na kejeli. Masahaba waliridhika kwamba ilikuwa ni muhimu sana kwa umma wa Waislamu kuwa na mtendaji mkuu lakini kulikuwa na mtu mmoja ambaye hakuamini kwamba ilikuwa muhimu, naye alikuwa ni Muhammad (s.a.w.)! Ingawaje kama angeamini hivyo, angeupatia umma huo mtendaji mkuu. Alikuwa ndiye mtu pekee ambaye haikujitokeza kwake kwamba palipaswa kuwa na mtu wa kutekeleza zile sheria na amri ambazo yeye mwenyewe alikuwa amezitangaza rasmi.

Hao maswahaba wakubwa hawakuhudhuria mazishi yake. Kwao wao, kilichokuwa na umuhimu zaidi kuliko kuhudhuria mazishi ya bwana wao, kilikuwa ni kupata kiongozi mpya. Tatizo hili lilikuwa gumu sana lakini "walilitatua" kwa kumchagua mmoja kati yao, yaani, Abu Bakr, kama kiongozi mpya wa Waislamu.

Miaka miwili baadae, Abu Bakr alikuwa amelala akifariki. Juu ya kitanda chake cha mauti, alimteua Umar kuwa mrithi wake, na kiongozi wa Waislamu. Katika kumteua Umar kama mrithi wake, hakujua tu kwamba alikuwa anatekeleza wajibu wake muhimu sana bali ali-tambua kwamba kama hakufanya hivyo, atakuwa mwenye kuulizwa mbele za Allah kwa kushindwa kwake kufanya hivyo.

370

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Asmah, mke wa Abu Bakr, anasema kwamba wakati mume wake alipokuwa kwenye kitanda chake cha mauti, Talha alikuja kumuona, naye akasema: 'Ewe Abu Bakr! umem-fanya Umar kuwa amir wa Waislamu, na unajua kabisa kwamba alikuwa dhalimu mno wakati ulipokuwa khalifa. Bali sasa kwa vile atakuwa na uhuru wa kufanya atakalo, sijui ni vipi atakavyowaonea Waislamu. Baada ya muda mfupi utafariki, na utajikuta mwenyewe mbele ya Allah (s.w.t.) Katika muda huo utatakiwa kumueleza Yeye juu ya matendo yako. Je, umeandaa tayari majibu yako?' Abu Bakr akakaa juu ya kitanda hicho, na akasema: 'Ewe Talha! je, unajaribu kunitisha mimi? Sasa sikiliza, kwamba pale nitakapokutana na Mola wangu, nitasema kwamba nilimchagua mtu aliye bora kama amir wa umma wa Waislamu.'

Abu Bakr aliongeza kwamba elimu na uzoefu wake juu umma ya Umar vilimthibitishia yeye kwamba hakuna mtu katika wa Waislamu ambaye angeweza kuubeba uzito wa ukhal-ifa vizuri zaidi kama ambavyo yeye (Umar) angeweza. Alikuwa, kwa hiyo, na imani kwamba majibu yake yatamridhisha Allah (s.w.t.)

Abu Bakr alijua kwamba atakuja kujitetea mwenyewe katika Mahakama ya Allah (s.w.t.) kwa kumteua Umar kama mtawala wa Waislamu. Aliridhika kwamba asingeweza kumch-agua mtu mwingine bora zaidi kuliko Umar kuwa mrithi wake. Na wasiwasi wa Talha juu ya kuwajibika kwa Abu Bakr mbele Allah, unaonyesha tu uangalifu wake kuhusu wajibu wake wa "kuamrisha wengine kufanya mema na kukataza maovu."

Kejeli tena! Masahaba wote walikuwa waabudu-masanamu kabla ya Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w.), aliyebarikiwa, hajawasilimisha kwenye Uislamu. Sasa, wao kama Waislamu wa dhati, walikuwa wanatambua kwamba walikuwa ni wenye kuwajibika kwa Allah (s.w.t.) kuhusu wajibu wao wa kuchagua mrithi wake. Lakini cha ajabu, na cha kushangaza, alikuwepo mtu mmoja ambaye ni dhahiri hakuwa na ufahamu kwamba, siku moja, yeye pia atakuja kusimama katika Mahakama ya Allah (s.w.t.), na kuulizwa kuhusu wajibu wake wa kuchagua mrithi wake. Yeye alikuwa ni Muhammad (s.a.w.), Mtume Wake Mwenyewe Allah (s.w.t.)! Waislamu wanaamini kwamba Abu Bakr alikuwa tayari kutetea kitendo chake cha kuchagua mrithi wake, kwa majibu ambayo alijua, yatamridhisha Allah (s.w.t.) Je, wanaamini pia kwamba Muhammad, Mtume wao, alikuwa tayari kutetea kushindwa kwake kuteua mrithi wake mwenyewe, kwa majibu ambayo Allah (s.w.t.) atapata kuridhika nayo?

Baada ya kifo cha Abu Bakr, mrithi wake, Umar ibn al-Khattab, alitawala kama khalifa kwa miaka kumi. Katika miaka ya mwisho ya uhai wake, alionekana mara kwa mara akiwa katika lindi la mawazo. Kila alipoulizwa na marafiki zake, kama alikuwa akifikiria juu ya nini, alisema: "Sijui nifanye nini kwa umma wa Muhammad, na jinsi ya kuteua amir atakayeuongoza baada ya kufa kwangu."

371

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ni wazi kwamba Umar aliona kuteua mrithi wake lilikuwa ni jambo la umuhimu mkubwa sana kwa jinsi alivyotumia muda wake mwingi na akili kwenye suala hilo.

Wasiwasi wa Umar kuhusu uongozi wa umma baada ya kifo chake mwenyewe, ulichangi-wa na Aisha, mjane wa Mtume (s.a.w.). Tabari, mwanahistoria huyu, anasimulia yafuatayo kuhusiana na hili:

"Wakati Umar alipokuwa anafariki, alimtuma mwanae kwa Aisha kuomba ruksa ya kuzik-wa karibu na Mtume na Abu Bakr. Aisha akasema: 'Kwa furaha kubwa,' kisha akaongeza: 'Nitolee Salam zangu kwa baba yako, na mwambie kwamba asije akawaacha Waislamu bila ya kiongozi vinginevyo kutakuwa na vurugu baada ya kifo chake.'"

Aisha alionyesha wasiwasi mkubwa sana juu ya ustawi wa Waislamu kama vile tu ambavyo angepaswa kufanya. Wakati Umar alipokuwa anafariki, alimshauri asiuache umma bila ya kiongozi, ama sivyo, alionya, ghasia zitafuatia kifo chake. Inashangaza kwamba Aisha hakuwahi kumshauri mume wake mwenyewe kuteua kiongozi kwa ajili ya Waislamu, na hakumuonya kwamba ghasia zitafuatia kifo chake kama angewaacha bila ya kiongozi.

Lakiini Aisha, binti ya Abu Bakr, alikuwa na sababu nzuri tu ya kuwa na "makini" na mume wake, na hakulileta kwenye mjadala pamoja naye, suala la uteuzi wa mrithi, wakati wowote.

Swali la 6

Upi ulikuwa mwenendo (sunnah) wa Muhammad (s.a.w.) kuhusiana na uteuzi na uwekaji wa watumishi?

Jibu

Katika miaka kumi ya mwisho ya maisha yake, Muhammad (s.a.w.) aliandaa misafara ya kijeshi zaidi ya themanini. Aliwatuma wengi wao chini ya amri ya kiongozi fulani; mingine aliiongoza yeye binafsi.

Wakati wowote Muhammad (s.a.w.) alipotuma msafara nje, aliteua mmoja wa maswahaba zake kama kapteni wake. Aliwaamuru wale wapiganaji wa kawaida kumtii yeye, na akam-fanya huyo kapteni kuwajibika kwake yeye mwenyewe Mtume. Pale msafara uliporudi Madina, alimhoji yule kapteni ili kupata taarifa. Haikuwahi kutokea kwamba aliwaambia watu wa msafara au kikosi cha upelelezi kwamba walipaswa kuchagua au kuteua kapteni wao wenyewe.

Katika kadhia ambapo Muhammad (s.a.w.) alipokuwa akiongoza mwenyewe msafara nje ya Madina, aliteua gavana wa mji huo, na akamfanya mwenye mamlaka ya kusimamia she-ria na maagizo wakati wa kutokuwepo kwake yeye mwenyewe. Hakuwahi kuwaambia raia

372

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwamba katika kipindi ambacho hatakuwepo, ilikuwa ni wajibu wao kujichagulia au kuji-teulia gavana wao wenyewe.

Katika mwaka 630 ambapo Muhammad (s.a.w.) aliiteka Makka, na kuijumuisha kwenye ile Dola mpya, aliteua mtawala kwa ajili ya mji ule, na alifanya hivyo bila ya kushauriana ama na watu wa Makka au na maswahaba zake mwenyewe.

Montgomery Watt:

"Kiasi cha madaraka ya utawala wa Muhammad katika miaka yake miwili au mitatu ya mwisho kinadhihirishwa na uteuzi wake wa "wakala" kusimama badala yake katika maeneo mbalimbali, na kwa hakika na suala zima la uteuzi wa nafasi za utawala. Tokea mwanzoni Muhammad aliteua watu kufanya shughuli mbalimbali ambazo yeye alihusika nazo. Hivyo aliteua makamanda wa misafara ambapo yeye hakuwepo binafsi. Uteuzi mwingine wa kawaida tangu nyakati za awali kabisa ulikuwa ni ule wa Kaimu hapo Madina wakati Muhammad alipokuwa hayupo hapo mjini."

(Muhammad at Madina, 1966) Maxime Rodinson:

"Yeye (Mtume) ama aliteua kiongozi au alichukua mamlaka mwenyewe. Anaelekea kuwa alikuwa na kipaji cha kijeshi kama alichokuwa nacho kwenye mikakati ya kisi-asa. Alikabidhi baadhi ya shughuli zake kwa watu ambao walikuwa kama mawakala wake binafsi. Wakati wowote, kwa mfano, alipoondoka Madina, alikuwa akiacha mwakilishi nyuma yake.

(Muhammad, kilichotafsiriwa na Anne Carter, 1971)

Hiyo ilikuwa ndio sera na mwenendo wa Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w.), katika kuteua na kuweka watumishi wake, na kamwe haukuwa na ukengeukaji ndani yake kwa wakati wowote.

Swali la 7

Ni ipi Fatwa ya Qur'an juu ya mwenendo (sunnah) wa Muhammad (s.a.w.)?

Jibu

Kwa mujibu wa Qur'an, vitendo vya Muhammad ni vitendo vya Allah (s.w.t.) Mwenyewe. Msomaji mwislamu anatakiwa atafakari juu ya maana ya Aya zifuatazo za Qur'an Tukufu:

373

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usahihi-41.jpg

Wakati ulipotupa (ukufi wa mchanga), Sio wewe uliyetupa, bali ni Allah Aliyetupa...(Sura ya 8; Aya ya 17)

Usahihi-42.jpg

Bila shaka wanaofungamana nawe,kwa hakika wanafungamana na Allah;Mkono wa Allah uko juu ya mikono yao:basi anayevunja ahadi yake, anavunja kwa kuidhulumu nafsi yake, na anayetekeleza alimuahidi Allah,Allah atamlipa ujira mkubwa. (Sura ya 48; Aya ya 10)

Waislamu wote wanaamini kwamba chochote alichokisema au kukitenda Muhammad (s.a.w.), kilikuwa ni wahyi kutoka Mbinguni. Kwa maneno mengine, alikuwa ni chombo ambacho amri za Mbinguni zilitekelezwa kupitia kwake.

Kama ilivyoelezwa kabla, Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w) hakuchangia pamoja na mtu yeyote yule mwingine mamlaka yake ya kuteua gavana kwa ajili ya mji, au jemadari kwa ajili ya msafara wa kijeshi. Yeye na yeye peke yake aliyatekeleza tokea mwanzo hadi mwisho. La muhimu zaidi kuliko uteuzi wa gavana au jemadari, ilikuwa ni uteuzi wa mrithi wake mwenyewe, na mkuu wa baadae wa umma wa Waislamu. Hakukuwa na sababu ya kuigeuka sera na mwenendo wake mwenyewe, na kuuacha umma wake wote bila ya kiongozi. Tabia yake ilikuwa yenye msimamo thabiti, na ufuatao ni ushahidi wa Qur'an Tukufu:

Usahihi-43.jpg

"Hutapata mabadiliko katika mtindo wa Allah (wa utendaji), hutapata mageuko katika mwendo wa Allah (wa utendaji). Sura ya 35; Aya ya 43)

Huo (ulikuwa) ndio mwendo wa Allah (ulithubutu) uliokwisha pita zamani:

Usahihi-44.jpg

Wala hutapata mabadiliko katika mwendo wa Allah (uliothubutu). (Sura ya 48; Aya ya 23)

374

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hakukuwa na mabadiliko katika mwenendo wa Mtume wa Allah (s.a.w.w). Hakuwatelekeza Waislamu ili waje kuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji. Alimteua binamu yake Ali ibn Abi Talib, kuwa mrithi wake, na kiongozi mkuu wa baadae wa umma wa Waislamu. Alimtambulisha Ali kwa umma huo kama mtawala wa baadae, katika Karamu ya Dhu ’l- 'Ashiira, mara tu baada ya tangazo la kwanza, hadharani la ujumbe wake kama Mtume wa Mwisho na Mkuu kabisa wa Allah (s.w.t.) ulimwenguni.

Swali la 8

Muhammad (s.a.w.) alifanya nini hasa kuhusu kurithiwa kwake?

Jibu

Muhammad aliunda Dola mpya - Dola ya Kiislamu. Katika kuunda Dola hiyo ya Kiislamu, lengo lake lilikuwa ni kuanzisha Ufalme wa Mbinguni Duniani. Hili alilifanya kwa msaada na ushirikiano wa binamu yake, Ali ibn Abi Talib. Alimchagua Ali miongoni mwa maswahaba zake wote, kumfuatia yeye, kama mkuu wa Dola ya Kiislam, na kama Mtawala wa Waislamu wote.

Kumteua Ali kama mrithi wake, Muhammad hakusubiri mpaka alipokuwa ameiunda hasa hiyo Dola ya Kiislam, na kuiimarisha kama ufalme wa mbinguni na duniani. Alimtangaza Ali kuwa mrithi wake katika wakati ambapo Dola hiyo haijawa na uhai wo wote. Alimtangaza Ali kuwa mrithi wake katika wakati uleule alipotangaza kwamba Allah (s.w.t.) amemtuma yeye kama Mtume Wake wa Mwisho kwa wanadamu.

Muhammad (s.a.w.) alimtaja Ali ibn Abi Talib kama mrithi wake kwenye Karamu ya Dhu ’l- 'Ashiira huko Makka wakati yeye Ali akiwa na umri wa miaka kumi na tatu tu; na alitumia muda wa uhai wake wote kumuandaa yeye kwa ajili majukumu mazito yaliyokuwa mbele yake.

Miaka ishirini baadae, katika bonde kubwa la Khum, karibu na Ghadiir, Muhammad (s.a.w.) alifanya matengenezo ya mwisho katika kazi yake aliualika umma wake, kwenye mkusanyiko mkubwa, kukutana na mkuu wao wa baadae. Kwa kufanya hivyo, alifuata amri ya Mbinguni iliyohifadhiwa katika Aya ya 70 ya Sura ya tano ya Qur'an Tukufu; na alitimiza wajibu wake juu ya umma wake. Umma wake ulikuwa na haki ya kujua ni nani atakaye uongoza baada ya kifo chake (yeye Muhammad).

Muhammad Mustafa (s.a.w.) hakumteua Ali kuwa mrithi wake kwa kufafanua au kutafsiri tu sheria za Kiislam. Alimteua Ali kuwa mrithi wake kwa kuzitenda na kuzitekeleza she-ria hizo. Kwa maneno mengine, alimteua Ali kuongoza serikali ya Kiislam.

Kama kuna sheria, lazima awepo mtu wa kuidumisha - katika dola ya mji wa Madina -

375

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kama kwingineko. Kitendo pekee cha kupitisha sheria hakina maana yoyote. Yenyewe peke yake, sheria haiwezi kuhakikisha usalama, ustawi na furaha ya mwanadamu. Baada ya sheria kupitishwa, ni muhimu pia kuunda nguvu ya utendaji, ya kuitekeleza. Kama sheria haiwezi kudumishwa, haiwi ni chochote zaidi ya kipande cha karatasi. Kama serikali inakosa mamlaka ya utendaji, haiwezi hata kuitwa ni serikali. Kwa hiyo, pale Uislamu ulipopitisha sheria, uliunda pia mamlaka ya utendaji.

Katika wakati wa Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w.), sheria hazikuwa zikifafanuliwa na kutangazwa rasmi tu; zilidumishwa na kutekelezwa pia. Yeye alizidumisha na kuzitekeleza.

Muhammad (s.a.w.) alimteua Ali kudumisha sheria za Kiislamu, na kutekeleza amri za Allah kama zilivyoshushwa kwake ndani ya Qur'an. Alimteua Ali kushika mamlaka ya utendaji juu ya Waislamu, baada ya kifo chake yeye mwenyewe.

Swali la 9

Ni nini hasa kilichotokea baada ya kifo cha Muhammad (s.a.w.)?

Jibu

Baada ya kifo cha Muhammad Mustafa, aliyebarikiwa, Ansari walijikusanya katika banda la Saqifah ili kuchagua kiongozi. Abu Bakr, Umar na Abu Ubaidah - Muhajirina hawa watatu - waliwatembelea. Waliwaambia hao Ansari kwamba kwa vile Muhammad (s.a.w.) hakuteua mrithi wake, iliwabidi wachagua mtu wa kujaza nafasi hiyo. Kitendo chao, walisema, hakikuwa tu ni halali bali pia kilikuwa ni muhimu sana, ikiwa ni kwa kuuokoa umma kutokana na vurugu na ghasia.

Hawa Muhajirina watatu waliingia kwenye majadiliano makali na Ansari mle Saqifah. Mada ya mjadala huo ilikuwa: ' Je, mrithi wa Muhammad (s.a.w.) na mtawala wa Waislamu awe ni Muhajir (wa Makka) au Ansari (wa Madina).' Wasemaji wakali waliijadili mada hii vya kuchosha.

Ingawa kulikuwa na mambo mengine muhimu ambayo hayakuwa kwa jumla yasiyohusi-ka kwenye mjadala huo, kama vile matakwa ya Allah (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.), sifa zilizohitajika kwa mgombea au wagombea kwenye nafasi iliyowazi ya mtawala wa Arabia, na maslahi ya Uislamu na umma wa Waislamu, hayo hayakujadiliwa. Masuala haya hayakuwemo kwenye "ajenda" za mkutano huo mle Saqifah. Wasemaji hao, kwa hiyo, hawakutoka nje ya mada yao.

Hatimaye, kwa ustadi, uvumilivu na kwa maarifa, hawa Muhajirina watatu walilisuluhisha kwa mapatano tatizo hili, au, kiasi, walitunga "papo kwa papo" ufumbuzi wake.

376

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Francesco Gabrieli:

"Katika lile baraza la vurugu lililofanyika kwenye makao makuu ya Banu Sa'idah hapo Madina, Umar, takriban kama kwa kushitukiza, alimuweka Abu Bakr kama khalifa au mrithi wa Mjumbe wa Allah. Kama matukio mengi na asasi nyingi, ukhal-ifa ulizaliwa katika ufaraguzi.

(The Arabs - A Compact History, 1963)

Ukhalifa au uongozi wa umma wa Waislamu ndio taasisi muhimu sana ya kisiasa katika Uislamu wote.

Kwa kweli, kuweko hasa kwa Uislamu kunategemea juu ya khalifa au kiongozi wa umma. Kwa hiyo, haisadikiki kwamba uliachwa si kwenye ubora wowote bali ufaraguzi! Itakuwa haishangazi kwamba ulimwengu wa Kiislamu umekuwa mara kwa mara umefunikizwa kwenye damu juu ya suala la urithi na uongozi.

Vita, mapambano ya wenyewe kwa wenyewe, mapinduzi, migogoro, uchochezi na ghasia zimekuwa haziepukiki wakati umma ulipochagua ufaraguzi mle Saqifah, badala ya kielele-zo cha ki-ungu na "mpango" wa majaaliwa wa Muhammad Mustafa (s.a.w.), kwa ajili ya upokezanaji wa utaratibu mzuri na wa amani wa mamlaka kutoka kwake mwenyewe kwenda kwa mrithi wake.

Watetezi wa Saqifah wanasema kwamba kitendo cha Umar kilichochewa na shauku yake ya kuzuia uongozi wa umma kutokana na kuwa daima mali ya familia moja - hasa, famil-ia ya Muhammad Mustafa (s.a.w.). Wanasema kwamba ukiritimba kama huo wa mamlaka ungeweza kuwa ni "janga" kwa Uislamu. Hoja hii ambayo ni ngumu kueleweka, ya wanahistoria wa Sunni imekuwa ni kipokeo cha kawaida na kisichoeleweka cha siku-za-baadae kinachoimba maangamizi. Lakini hakuna hata mmoja kati yao ambaye amewahi kueleza ni kivipi.

Kama baada ya kifo cha Muhammad (s.a.w.) utawala wa Waislamu ungegeuka kuwa "mali" ya familia yake mwenyewe, hivi Waarabu wangeukana Uislamu, na kurudi kwenye uabudu masanamu? Au Waajemi na/au Warumi wangeivamia na kuiteka Arabia na kuwaangamiza Waislamu wote?

Katika mawazo ya Abu Bakr na Umar, kulikuwa na njia moja tu ya "kuuokoa" umma wa Muhammad (s.a.w.) kutokana na "janga," na hiyo ilikuwa ni kwa kuikataa familia yake kwenye uchaguzi, na kwa kujitwalia serikali yake wao wenyewe!

Umar alikuwa na shauku kwamba ukhalifa usije ukawa ni wa kurithiana katika ukoo

377

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mmoja wowote ule, na kwamba unapaswa kubaki ukizunguka miongoni mwa Waislamu ili kwamba "kila kijana wa Kiarabu aweze kuwa na bahati ya kuwa khalifa." Hata hivyo, licha ya ndoto na tahadhari juu ya mambo ya baadae ya Umar, ukhalifa ulikuja kuwa wa kurithi-ana ndani ya miaka kumi na sita ya baada ya kifo chake mwenyewe.

Lakini ulikuwa wa kurithiana siyo katika familia ya Muhammad (s.a.w.) bali katika famil-ia ya maadui zake wakuu - wale watetezi wa upagani wa Makka - wale watoto wa Abu Sufyan na Hinda. Hivyo ndoto za Umar hazikuendelea zaidi ya miaka kumi na sita labda kama lilikuwa ni lengo lake kwamba ukhalifa uje kuwa wa kurithiana katika nyumba ya Abu Sufyan. Kama ilikuwa hivyo, basi lazima ikubalike kwamba yeye alikuwa ni mtu wa ajabu kweli kutokana na ndoto zake.

Abu Bakr na Umar walifanikisha muujiza wa ufaraguzi mle Saqifah.

Akizungumzia juu ya machafuko kufuatia kifo cha Muhammad (s.a.w.), na akitoa sababu zake za kwa nini binamu yake, Ali, alikataliwa katika kugombea ukhalifa, Sir John Glubb anaandika hivi:

"Waarabu hawakuwa tayari kamwe kutoa heshima kwenye fahari, daraja, au fursa za kurithiana au vyeo.

(The Great Arab Conquests, 1963)

Uchambuzi huu, wa mwanahistoria huyu, wa tabia ya Kiarabu, unakwenda kinyume na ushahidi wa historia. Watawala wa kale wa Uturuki (Seljukes), Mamluki, na watawala wa Uthmainia (Ottoman Turks) waliwatawala Waarabu kwa karne nyingi. Waarabu waliwatii kama kondoo. Wao, kwa kweli, waliukubali ule usemi usio na uthibitisho wa kwamba Waturuki wawe wanaamrisha, na wao Waarabu wawe ni wenye kutii.

Hakuna yeyote anayeweza kusema ni kwa muda mrefu kiasi gani zaidi huo utawala wa Kituruki juu ya ardhi za Waarabu ungechukua kama Waingereza na Wafaransa wasingeusi-mamisha.

Katika kusalimu amri kwao kwa jumla na kwa kinyonge kwa Waturuki, Waarabu walikuwa wakitoa heshima kabisa kwenye "fahari, daraja au fursa za kurithiana au vyeo." Kwa karne nyingi Waturuki walizitawala nchi za Kiarabu kwa ukali, na hakuna aliyewahi kusikia manung'uniko japo madogo sana ya upinzani kutoka kwa Waarabu.

Kwa hakika, Waarabu hawana tofauti na watu wengine ikiwa ni pamoja na Waingereza, ambao na mwanahistoria huyu mwenyewe anatokana nao. Kama wengine wanatoa heshima kwenye fahari, daraja, au fursa na vyeo, Waarabu nao wanatoa heshima kwavyo. Haieleweki ni kwa nini Sir John Glubb ana shauku ya kufanya mambo ya kutukuzwa sana

378

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwa Waarabu!

Mwandishi huyo huyo anaendelea kusema:

"(Utawala wa) Kurithiana hakukukubaliwa na Waarabu kama msingi wa kufaa wa kupokezana mamlaka. Katika uteuzi wa wakuu wa kawaida, mgombea aliyefaa zaidi, wa familia inayotawala kwa kawaida ndiye aliyechaguliwa. Katika uteuzi wa khalifa, chaguo la kawaida kabisa, na lile ambalo katika nadharia ndilo lilifanywa katika kadhia za wale wanne wa kwanza, lilikuwa ni lile la kiongozi wa Kiislam anayefaa zaidi.

Kwa vitendo ugumu wa kuteua mgombea safi na hatari inayojitokeza ya vita vya wenyewe kwa wenyewe mara nyingi ulisababisha matumizi ya haki ya kurithi kwa mtoto wa kwanza katika falme za Kiislamu za baadae.

Waarabu, hata hivyo, kamwe hawakuutwaa ule utaratibu wa urithi wa moja kwa moja wa mtoto mkubwa."

(The Great Arab Conquests, 1963)

Mwanahistoria huyu, inavyoelekea, kwa mara nyingine tena, yuko kinyume na mambo. Pale anaposema kwamba kurithiana kamwe hakukukubaliwa na Waarabu kama msingi unaofaa wa kupokezana mamlaka, anapaswa kuweka wazi, kwamba Waarabu anaowazungumzia, walitokana na kizazi cha wakati wa Mtume (s.a.w.) mwenyewe, na sio na wale waliokuja baada yake. Ndani ya miaka thelethini ya kifo cha Mtume (s.a.w.), Waarabu hao hao walikuwa wakinyenyekea kwa miguuni kwa yule khalifa wa Syria, na waliukubali urithianaji kama msingi unaofaa wa kupokezana mamlaka bila haya. Sio kwamba walimkubali tu Yazid, mtoto wa Mu'awiyah, kama khalifa wao halali, bali kwa miaka 600 iliyofuatia, yaani, mpaka kukomeshwa kwa ukhalifa wenyewe mnamo mwaka 1258, hawakuwahi kuuliza swali kuhusu haki ya mtoto wa khalifa kumrithi baba yake.

Geoffrey Lewis:

"Kwa khalifa wa tano, yule mwenye nguvu sana Mu 'awiyah (661 -680), cheo hicho (ukhalifa) kilikuwa ni cha kurithiana kiukoo. Utawala wake wa Bani Umayya ulichukuliwa nafasi yake na ule wa Bani Abbas mnamo mwaka 750."

(Turkey, 1965)

Dr. Hamid-ud-Din:

" Kuanzia wakati wa Mu'awiyah, kiti cha ukhalifa kilikuwa ni haki ya kurithiwa ya Bani Umayya. Kila khalifa alimteua mwanae au ndugu mwingine yoyote kama mrithi wake, na Waislamu kwa unyenyekevu kabisa walimkubali kama khalifa wao, nao

379

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hawakuuliza maswali."

(History of Islam, 1971, uk. 364 kilichotolewa na Ferozsons Ltd,

Karachi na Lahore, Pakistan).

Waarabu pekee ambao hawakukubali urithianaji wa kiukoo kama msingi wa kupokezana mamlaka, walikuwa ni maswahaba wa Muhammad (s.a.w.) mwenyewe. Sababu yao ya kutokubali urithianaji kama msingi wa kupokezana mamlaka, ilikuwa ni mtazamo wa heki-ma. Kama wangekubali urithianaji wa kiukoo kama msingi wa kupokezana mamlaka, basi kungekuwa hakuna njia ya wao kuwa makhalifa.

Katika nadharia ya Shia juu ya serikali, urithianaji wa kiukoo hauchukuliwi kama msingi wa kupokezana mamlaka. Kwa mujibu wa nadharia ya Shia, haki ya kuchagua mrithi wake mwenyewe, ilihusika pekee kwa Muhammad Mustafa (s.a.w.), na sio kwa maswahaba zake; na yeye alimchagua Ali. Na hakumchagua Ali kwa sababu ya udugu, bali kwa sababu ilikuwa ni amri ya Allah (s.w.t.) kwake yeye kufanya hivyo.

Pale Waarabu walipokataa kukubali kule kuteuliwa na Muhammad Mustafa (s.a.w.) kwa Ali ibn Abi Talib kama mrithi wake, hawakuwa kwa hakika wakitetea "kanuni." Kukataa kwao kulikuwa ni mwanzo tu wa kuondoa kituo maalum cha madaraka na mamlaka kuto-ka kwenye nyumba ya Muhammad (s.a.w.). Mara tu "kanuni" ilipotimiza lengo lao, wao -Waarabu - walikuwa wa kwanza kuitelekeza.

Laura Veccia Vaglieri:

"Kuelekea mwishoni mwa utawala wake, Mu'awiyah, akitumia ustadi wake wote wa kidiplomasia, alimudu kuwashawishi wale watu mashuhuri wa himaya hiyo kumtam-bua mwanae Yazid kama mrithi kwenye utawala, bila kuigusa ile kanuni kwamba hes-hima kuu lazima itolewe katika muda wa kurithi. Kwa njia hii alipata muafaka. Kinadharia, hiari ya wachaguzi iliheshimiwa, kwa vile ilikubalika kwamba wanaweza kumkataa yule mrithi aliyeteuliwa na mkuu anayetawala (kwa kweli, ni watu mashuhuri wanne au watano tu waliokataa kuridhia ombi la Mu'awiyah), lakini kwa hali halisi hii ilidokeza kufutwa kwa mfumo wa uchaguzi, ambao ulikuwa ndio chan-zo cha matatizo mengi huko nyuma, na ilianzisha urithianaji wa kiukoo.

Mageuzi ya Mu'awiyah yalifuatwa na makhalifa wote waliokuja baada yake, na yali-wawezesha Bani Umayya kushikilia madaraka kwa miaka 90, na Bani Abbas kwa karne tano."

(Cambridge History of Islam, 1970)

Mu'awiyah alipuuza ile "kanuni" ya uchaguzi ambayo haikuwa ni chochote zaidi ya kichekesho hata hivyo.

Hata hivyo, katika shughuli yote hii iliyopinda ya "kuchagua" au "kupendekeza" au

380

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"kuteua" mtawala wa Waislamu, kulikuwa na "kanuni" mmoja iliyokuwa ikifanya kazi. ilikuwa ni ile "kanuni" ya kuwaondoa watu wa familia ya Muhammad Mustafa Mtume wa Allah (s.a.w.) aliyebarikiwa, kutoka kwenye mahali maalum pa madaraka na mamlaka. Saqifah, kwa kweli, ilikuwa ni vuguvugu ya nguzo imara, iliyounganishwa na kuchanganyika ya maswahaba wakubwa na wasaidizi wao ya kuwaondoa Bani Hashim kutoka kwenye serikali ya Kiislam. Kama ungekuwepo msimamo thabiti wowote ama kati-ka matendo ya makhalifa watatu wa kwanza, au, mwingine wa maswahaba, au wa Bani Umayya na Bani Abbas, ulikuwa ni katika kuitumia "kanuni" hii. Katika jambo hili, yalikuwepo makubaliano miongoni mwao wote. Ilikuwa ndio asili na kiungo muhimu cha sera yao wote iliyopangwa na kuratibiwa. Hata kwa zile falme ambazo zilikuwa zifuatie za Bani Umayya na Bani Abbas, ishara za Saqifah zilikuwa na nguvu, dhahiri na bayana. Walifuata masharti, kwa uaminifu, takriban kwa ushabiki uliokithiri ya "sera" iliyoundwa kwenye ukumbi wa Saqifah. Kiini cha sera ile kilikuwa ni uadui wa wazi kwa Ali ibn Abi Talib, binamu wa kwanza wa Muhammad (s.a.w.), na kwa Bani Hashim, ukoo wa Muhammad (s.a.w.).

Swali la 10

Je, suala la urithi lina umuhimu gani katika historia kwa jumla?

Jibu

Suala la kurithisha au kuhamisha madaraka kutoka kwa mwenye cheo mmoja kwenda kwa mwingine, limekuwa moja ya matatizo magumu na yenye mzozo ya historia ya mwanadamu. Katika kadhia nyingi, tatizo hili limetatuliwa katika juhudi ambamo mbinu zote zinakubalika, na madaraka yamekuwa ni tunzo la yule aliyekatili zaidi kati ya wag-ombea. Ukweli kwamba taifa lina serikali ya kikatiba, hakuihakikishii kwamba itakingika kutokana na ugombaniaji wa madaraka. Ugombeaji wa Stalin na Trotsky baada ya kifo cha Lenin mnamo 1924, na kuuawa kwa Beria baada ya kifo cha Stalin mnamo 1953, ni miwili kati ya mifano mingi kutoka kwenye historia ya sasa.

Kwenye matukio yasiyo na idadi ndani ya historia, suala la urithi limechokonoa vita vya wenyewe kwa wenyewe ambamo wanaume na wanawake wasio na idadi wameangamia. Wengi wetu tunaweza kushawishika kujigamba kwamba tumepitia zama hizo za kikatili ambamo maelfu ya wanaume na wanawake waliuawa kabla suala la ni nani atakayekuwa mtawala halijafumbuliwa. Lakini hakuna sababu ya kutojali. Kugombea madaraka kunaweza kuibuka mahali popote wakati wowote bila kukwepa tu baadae kama ilivy-otokea huko nyuma. Harakati za kichini chini huenda zinatokota wakati wote lakini kwa hakika zinakuja kuchemka wakati kiongozi wa nchi atakapofariki.

Geoffrey Blainey:

"Uchunguzi wa sababu zinazofanana kwenye vita nyingi za karne ya kumi na nane unaonyesha ishara moja ya wazi. Kifo cha mfalme kilikuwa mara nyingi ndio dalili ya vita. Kiungo kinawakilishwa kwenye majina maarufu yaliyotolewa kwenye vita

381

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

nne muhimu. Kwa namna hii kulikuwa na Vita ya urithi wa Hispania, na vita ya urithi wa Uholanzi, na zilifuatiwa na vya urithi wa Australia na kisha wa Bavaria Majina yao kiushawishi yanamaanisha kwamba suala la nani afuatie kwenye kiti kilichokuwa wazi lilikuwa ndio chanzo kikuu cha vita hizo.

Vita hizi nne za urithi hazikuwa ndio vita pekee ambazo zilitanguliwa na kushawishi-wa na kifo cha mtawala. Mnamo mwaka 1700, watawala wa Saxony, Denmark na Urusi waliingia vitani dhidi ya Sweden ambayo mtawala wake kijana, Charles X11, hajakaa muda mrefu kwenye madaraka. Katika mwaka wa 1741 vikosi vya Sweden vilivamia Urusi, ambayo mfalme wake wa kabla ya mapinduzi, alikuwa na umri wa mwaka mmoja. Mnamo 1786 kifo cha Frederick Mkuu wa Prussia aliandaa njia ya mapambano ya Austri-Russia dhidi ya Uturuki katika mwaka uliofuata. Na mnamo Machi, 1792 kifo cha Mfalme Leopold II huko Vienna kilikuwa ni moja ya matukio yaliyoashiria Tangazo la Ufaransa la vita dhidi ya Austria katika mwezi uliofuatia.

Katika vita zote nane za karne ya kumi na nane ziliashiriwa na kushawishiwa na kifo cha mfalme; na vita hizo zilianzisha nyingi ya vita kubwa za karne hiyo. Wala vita hivyo vya kukesha na mgonjwa anayekaribia kufa havikukoma kabisa baada ya 1800. Hivyo vita mbili kati ya Prussia na Denmark zilitanguliwa na vifo vya wafalme wa Kidenishi, vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Marekani vilifuatia kifo cha raisi mnamo 1861, Vita Vikuu vya Kwanza vilitanguliwa na kuuawa kwa mrithi wa Austria."

(The Causes of War, 1973)

Kugombea madaraka ni tabia ya kudumu ya historia ya mwanadamu. Huko nyuma, kwa mara nyingi kifo cha mfalme kilikuwa ni ishara ya maasi katika nchi yake mwenyewe. Kama alikuwa ameikamata nchi pamoja kwa uongozi madhubuti, kifo chake kilichukuli-wa kama ni fursa ya kuishambulia serikali kuu, na kudai uhuru wa jimbo lenye upinzani. Mara nyingine, kifo cha mfalme kilikuwa ni kukaribisha majirani wenye tamaa kuivamia nchi yake kwa matumaini kwamba huyo kiongozi mpya, kwa kukosa uzoefu, hatakuwa na uwezo wa kutoa upinzani wenye nguvu kwao, na watajitwalia nchi mpya wenyewe.

Historia ya tawala za Kiislamu imeloweshwa katika damu za Waislamu. Huko nyuma, wakati wowote mfalme au sultani alipofariki, wanae na ndugu zake walirukiana makooni kuchinjana. Wakati mwingine wadogo na hata watoto wachanga hawakuachwa kama walikuwa kwenye nasaba ya moja kwa moja kutoka kwa mtawala, na kwa hiyo, walikuwa wenye uwezekano wakuwa vyanzo vya matatizo. Wakati wa kifo cha mtawala, kuenea kwa vita na migogoro ya wenyewe kwa wenyewe, na maasi katika majimbo, vilionekana kuwa ni kawaida.

Wanahistoria wengi wa kisasa ambao wamesoma nadharia ya kisiasa ya Uislamu na uwezekano wake, na wamejaribu kuanisha sababu na athari, wameihusisha migogoro ya

382

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ndani ya Uislamu na vita vya "kushindwa" kwa Muhammad Mustafa (s.a.w.) kuteua mrithi wake mwenyewe. Kuna dokezo lililofichwa au mifano yenye shaka katika vitabu vyao kwamba "alihusika" nazo. Lakini baadhi ya mifano mingine haikufichika au kuwa na shaka kiasi hicho.

Edward Jurji:

"Hali ya kivita, iliyokuwepo kati ya Mtume na ndugu zake, ilifikia kikomo katika ushindi kamili wa majeshi ya Kiislam uliofikishwa kileleni na kuingia kwa ushindi kwa Muhammad katika mji alimozaliwa kwa kubomoa kumbukumbu za uabudu masanamu. Ingawa kazi yake ilibakia ya Kiutume, Muhammad alikuwa ameongeza kuja kutumia upanga wa kiongozi wa kijeshi na kusimamia mambo ya dola ya kisi-asa yenye hima, akitambua wajibu wa dola hiyo katika historia. Kifo chake kilipo-tokea tarehe 8 Juni, 632, alirithisha kwa wafuasi wake urithi wa dini-na-siasa daima ulioelemewa na kusumbuliwa kwa karne nyingi na jukumu la kupata khalifa (mrithi) anayekubalika kujaza nafasi ya juu kabisa katika Uislamu. Ukhalifa (urithi) kama jambo, lililokuzwa na kimya cha kuchosha cha Mtume juu ya suala la ni nani angem-fuatia, lilikuwa ni mzizi wa uovu mwingi, na balaa la ndani kubwa la Uislamu, chan-zo cha mipasuko na mifarakano, na urithi wa kuhuzunisha wa machozi na damu."

(The Great Religions of the Modern World, 1953)

Kwa mujibu wa mwanahistoria huyu, kilikuwa ni "kimya kinachochosha cha Mtume (s.a.w.) juu ya suala la, ni nani angemfuatia yeye, ambalo lilikuwa "mzizi wa uovu mwingi, balaa kubwa ya ndani ya Uislamu, chanzo cha mipasuko na mifarakano, na urithi wa kuhuzunisha wa machozi na damu."

Hivi huu ndio "urithi" ambao Muhammad (s.a.w.) aliouachia umma wake? Ikiwa Waislamu wa sasa wanaamini kile kioja cha Saqifah kwamba hakuteua mrithi wake mwenyewe, basi watakubaliana na uamuzi wa mwanahistoria huyu. Lakini kama watakubaliana na uamuzi huu, itawabidi wapingane na Qur'an Tukufu ambayo imemuita Muhammad ni "rehma kwa ulimwengu mzima."

Sir John Glubb:

"Mtume alifariki bila ya kuacha maagizo yoyote kuhusiana na mrithi. Ilipofahamika tu kwamba amefariki, watu wa Madina walikusanyika pamoja na wakaamua kuch-agua mkuu wao wenyewe. Upinzani wa wadai wa ukhalifa ulisababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Waislamu visivyokwisha, ambavyo labda vingeweza kuepukwa kama Muhammad angeweka sheria kwa ajili ya urithi (ushika makamu)."

(A Short History of the Arab Peoples, 1969)

383

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kama Waislamu wa sasa, baada ya kusoma fatwa hii ya mwanahistoria, bado wanashikil-ia kwamba Mtume wao hakuchagua mrithi wake mwenyewe, basi lazima wakiri kwamba vile vita vyote vya umwagaji damu vya wenyewe kwa wenyewe vya historia yao, vilikuwa ni "zawadi" yao kutoka kwake - kutoka kwake yeye ambaye alikuwa ndiye mfano wa rehema. Je, vita, hususan vya wenyewe kwa wenyewe, ni laana au ni baraka? Kama ni laana - na hakuna laana kubwa katika dunia kuliko vita - hivi wataamini kwamba Mtume wao alikuwa ndiye mletaji kwao Uislamu - wa amani?

Kwa kweli, moja ya malengo ya Muhammad (s.a.w.), kama Mtume wa Allah (s.a.w.w), lilikuwa ni kufuta vita, na kurudisha amani ya kweli ulimwenguni. Vita ndio laana kubwa kabisa, na amani ni moja ya baraka kuu za Allah (s.w.t.) Yeye alikuwa ni Mtume wa Amani. Kwa kweli, harakati aliyoianzisha, yenyewe iliitwa Amani au Uislamu. Kama Mwislam anaamini kwamba Muhammad alikuwa mchocheaji wa vita na umwagaji damu, atakoma kuwa mwislamu.

Sasa chaguo mbele ya mwislamu ni rahisi: ama anaamini kwamba Muhammad

haku..(narudia) hakuteua mrithi wake mwenyewe, au anaamini kwamba alifanya hivyo.

Kama anaamini kwamba Muhammad (s.a.w.) hakuteua, basi itamaanisha kwamba alileta huzuni na misiba yote iliyopita na ya baadae juu ya umma wa Waislamu. Imani kama hiyo itakuwa, kwa kweli, ni "ukosoaji" wa kimya kimya wa mwislamu, kumkosoa Muhammad kwa "kosa la kutofanya vizuri" kazi yake. Lakini ajiulize yeye mwenyewe kama anaweza "kumkosoa" yule Mtume wa Mwisho na Mkuu kabisa wa Allah (s.w.t.) na bado akawa ni mwislamu!

Kama mwislamu wa wakati huu anaamini kwamba Muhammad (s.a.w.) aliteua mrithi wake mwenyewe, basi lazima akiri kwamba ule mkutano uliofanyika pale Saqifah ulikuwa "hauna mamlaka" kwa sababu ulifanywa kwa ukaidi wa amri za Allah (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.). Maovu yote, mabalaa ya ndani ya Uislamu, mipasuko na mifarakano, ule urithi wa huzuni wa damu na machozi, na vita vya wenyewe kwa wenyewe visivyo na kikomo vya Waislamu, vilikuwa na chanzo chao mle Saqifah.

Uislamu umetoa uhuru wa chaguo kwa Waislamu wote. Kwa upande mmoja wanao uamuzi wa majaaliwa wa Muhammad (s.a.w.); na kwa upande mwingine, kuna ule uamuzi uliofanywa kwenye ukumbi wa Saqifah. Wanaweza kuchagua wowote wanaoutaka.

Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.a.w.w) na mfasiri wa Qur'an, alikuwa ndiye mwenye ujuzi zaidi kati ya wanadamu. Sio tu kwamba alikuwa na ujuzi wa historia, na ujuzi wa sababu za kuibuka, kupungua nguvu na kuanguka kwa mataifa, alikuwa pia na ujuzi na ufahamu wa asili ya mwanadamu. Mikondo ya historia yote ilikuwa yenye kuju-likana kwake. Kwa sababu alikuwa amejaaliwa na ujuzi kama huo, hakuliacha suala la urithi kwenye nafasi ya kubahatisha. Alikuwa ameanza utekelezaji wa ratiba ya kujenga upya jamii ya wanadamu, na alikuwa ameanzisha Ufalme wa Mbingnii juu ya Ardhi. Na

384

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

alijua kwamba hataishi milele.

Muhammad (s.a.w.) alijua kwamba atakufa lakini ujumbe wake utaishi. Ujumbe wake uli-hitajia kuendelezwa. Kuendelezwa kulikuwa ni muhimu sana kwa mafanikio ya ujumbe wake, na chochote kilikuwa kisiukatishe, sio hata kifo chake mwenyewe. Kwa hiyo ili kutoa mwendelezo kwenye kazi yake, alimchagua Ali ambaye ingawa bado mdogo kwa miaka, alikuwa ndio mfano halisi wa sifa zote za uongozi katika Uislamu. Muhammad (s.a.w.) alitoa tamko la majaaliwa katika karamu ya Dhu ’l- 'Ashiira kwamba Ali alikuwa ni waziri wake, mshikamakamu na mrithi wake. Lakini pia alikuwa amefanya uchunguzi wa maisha na uchambuzi yakinifu wa tabia na uwezo wa Ali, na akammwona yeye ni asiyelin-ganishika.

Ali alikuwa wa namna ya kipekee. Alikuwa ni mtu mwenye-uwezo zaidi katika Uislamu!

Hata kama hakuna ushahidi wa kihistoria unaoweza kupatikana kwamba Muhammad (s.a.w.) aliteua mrithi wake mwenyewe, bado inawezekana kufanya tafsiri chache kutoka kwenye tabia na mwenendo wake. Alikuwa mwangalifu, mwenye hadhari na makini wa iti-faki katika maisha ya ndani na ya nje. Busara, kuona mbali na upangaji makini uliainisha kazi yake. Madai ya kwamba hakuuambia umma wake ni nani atakayeuongoza katika vita na amani, na ni nani atakayeuelekeza katika dharura nyingine za maisha, ni kinyume kabisa na tabia yake.

Muhammad (s.a.w.) alikuwa ndiye mwalimu wa Waislamu. Aliwafundisha kila walichok-ijua. Juu ya elimu ya Uislamu, hakuwaficha chochote kile. Kudai kwamba aliwaficha taar-ifa yenye muhimu sana kwao, yaani, jina la mtu ambaye atashika usukani wa chombo cha Uislamu, baada ya kifo chake yeye mwenyewe, kunashindana na kanuni zote za maarifa ya kawaida na mantiki.

Itakumbukwa kwamba wakati Muhammad Mustafa (s.a.w.) alipokuwa yuko Makka, wakazi wa Makka walileta fedha na vitu vyao vya thamani kwake kwa ajili ya kuvihifad-hi - kabla na baada alipoanza kuutangaza Uislamu kwa sababu walimuamini. Uaminifu na ukweli wake vilikuwa havina shaka yoyote.

Katika mwaka 622 A.D. Muhammad Mustafa (s.a.w.) alihama kutoka Makka na kwenda Madina. Kabla ya kuondoka Makka, alimfanya Ali mwenye-mamlaka kwa ajili ya kurud-isha amana zote kwa wenyewe (wapagani) - wenyewe wale wale waliokuwa na uchu wa kumuua yeye kwa kutangaza Uislamu. Lakini amana ni kitu kitakatifu, na lazima kiheshimiwe na kila mtu, hususan na Mtume wa Allah!

"Amana zinaweza kuelezewa au kutekelezwa. Amana za kuelezwa ni zile ambapo mali imekabidhiwa au kazi inatolewa na mtu kwa mtu mwingine anayemwamini, kuitekeleza ama mara moja au katika dharura nyinginezo maalum, kama vile kifo.

385

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Amana za kutekelezwa zinatokea kwenye madaraka, au nafasi, au fursa; kwa mfano, mfalme anashika falme yake kwa dhamana kutoka kwa Allah kwa ajili ya watu wake."

(A. Yusuf Ali, Mtarjumu na Mfasiri wa Qur 'an Tukufu).

Baada ya kuondoka kwa Muhammad kutoka Makka, Ali alirudisha amana zote kwa wenyewe.

Lakini kwa Muhammad (s.a.w.) hakukuwa na "amana" kubwa zaidi kuliko Uislamu. Allah (s.w.t.) aliweka juu yake wajibu wa kufikisha amana hii kwa wanadamu wote. Kwa hiyo, kabla ya kifo chake, ilimlazimu kumfanya mtu kuwa na dhamana ya kusimamia "amana" hii.

Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Uislamu, alimfanya Ali mwenye-mamlaka ya kusimamia "amana" hii; na kwa usemi wake wa kisiasa - Serikali ya Madina.

Dhamana bora ya usalama wa Dola ambayo Muhammad (s.a.w.) alikuwa ameianzisha, ilikuwa ni katika kuwafahamisha Waislamu ni nani atakayekuwa kiongozi wao baada ya kifo chake yeye mwenyewe. Usalama wa Dola hiyo utakuwa, kwa kweli, umehatarishwa vibaya kama angeshindwa kuwajulisha wafuasi wake ni nani atakayemfuatia yeye kama Mtendaji Mkuu.

Hakuna mwislamu ambaye angethubutu kudhania kwamba Muhammad Mtume wa Allah (s.a.w.), angesema au kufanya kitu chochote chenye madhara kwenye maslahi ya Uislamu. Wala ambaye angethubutu kudhania kwamba Muhammad (s.a.w.) angesema au kufanya kitu kisicho na mantiki.

Kuchukulia kwamba Muhammad (s.a.w.) hakuteua mrithi wake mwenyewe, na hakum-tambulisha kwa umma wa Waislamu, hakuungwi mkono ama na ukweli au na mantiki. Ukweli na mantiki viko upande wake - kudumu na bila ukwepaji. Ilikuwa ni katika ule ukumbi wa Saqifah ambamo mantiki ya historia ilikwenda kombo.

386

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Saad Ibn Ubadah, Ansari - mgombea wa Ukhalifa

Saad ibn Ubadah alikuwa ndio kiongozi wa kabila la Khazraj la Madina. Hawa Khazraj na Aus, makabila mawili ya Ansari, walikuwa wamejipatia sifa kwa utumishi wao kwenye Uislamu. Utumishi wao ulitambuliwa hata na Abu Bakr pale alipokuwa akibishana na kushindana nao mle Saqifah.

Katika vita vya Uislamu, Ansari walikuwa wakati wowote wako msitari wa mbele. Walipigana dhidi ya nguvu mkusanyiko wa waabudu masanamu wote wa Arabia. Abu Qatadam, Ansari mmoja, alidai, na kweli kwamba hakuna kabila katika Arabia yote lililo-toa wahanga wengi kwa ajili ya Uislamu kuliko Ansari. Ansari wengi waliuawa katika kutetea Uislamu kuliko watu wa kabila lolote lile jingine.

Kulikuwa na wakati ambapo Uislamu ulikuwa "hauna makazi." Hakuna kabila lililotoa hifadhi na ukarimu kwa Uislamu na kwa Mtume wake isipokuwa Ansari. Walimkaribisha Muhammad (s.a.w.) kuwa mgeni wao, na walimfanya kuwa mfalme wa mji wao - Yathrib (Madina).

Ulikuwa ni mji wa Ansari ambao ulipata heshima ya sifa ya kuwa makazi na makao makuu ya Uislamu. Ilikuwa ni katika mji wao ambamo Muhammad, Mtume wa Allah (s.a.w.w). alijenga "jengo" kubwa la Ufalme wa kwanza na wa mwisho wa Mbinguni juu ya Ardhi.

Mnamo A.D. 623 (2 Hijiria), Muhammad (s.a.w.) aliongoza msafara kwenda Waddan, na alimteua Saad ibn Ubadah kuwa gavana wa Madina wakati wa kutokuwepo kwake yeye mwenyewe. Saad, kwa hiyo, alikuwa ndio gavana wa kwanza wa Madina.

Katika vita vya Uhud, Mtume wa Allah (s.a.w.w). alitoa bendera ya Khazraj kwa Saad. Katika vita hivyo hivyo, Waislamu walishindwa. Ukiacha maswahaba 14, kila mtu mwingine alikimbia kutoka kwenye uwanja wa vita. Saad alikuwa mmoja wa hao mashu-jaa 14 waliopigana dhidi ya adui, na kumlinda Mtume (s.a.w.)

Katika msafara wa Mustaliq na katika kuzingirwa Madina (vita vya Khandaq), Saad alishi-ka bendera ya Ansari.

Kwenye mwaka wa 6 Hijiria Mtume alikwenda kwenye msafara na alimteua Saad kuwa

387

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

gavana wa Madina wakati wa kutokuwepo kwake.

Ansari walikuwa na viongozi wawili, Saad ibn Ubadah na Saad ibn Mua'dh. Saad ibn Mua'dh alifariki kutokana na jeraha alilolipata katika vita vya Khandaq. Baada ya kifo chake, Saad ibn Ubadah alikuwa ndio kiongozi pekee wa Ansari.

Humo Saqifah, Ansari walimwambia Saad kwamba alikuwa ndio mtu mwenye kufaa sana kuwa khalifa, na walitangaza kumuunga mkono kwao katika ugombea wake. Saad alikuwa maarufu kwa ukarimu wake. Wakati mwingine alikaribisha wageni wengi kiasi cha 80. Yoyote yule - rafiki au mgeni, aliweza kutegemea ukarimu wake.

Saad alikataa kutoa kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Miaka mitatu baadae, aliondoka Madina, kwenda Syria na akaweka maskani huko. Alikuwa yuko Syria wakati alipopigwa na mshale uliotupwa na mtu asiyejulikana, na kwa hiyo alikufa katika mazingira yanayotatan-isha.

Saad ibn Ubadah alikuwa Ansari wa kwanza na wa mwisho aliyewahi kuwa mgombea wa ukhalifa. Yeye hakuwahi kuwa khalifa. Mle Saqifah, mlango wa ukhalifa ulifungwa nyu-soni mwa Ansari, na waliwekwa nje kwa wakati wote, milele.

388

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abu Bakr, Khalifa wa kwanza wa Waislamu

Abu Bakr alikuwa ni mwana wa Abu Qahafa, na aliishi kama mfanyabiashara hapo Makka. Yeye alisilimu baada ya Khadija, Ali ibn Abi Talib, na Zayd bin Haritha.

Inasemekana kwamba Abu Bakr alitoa mali nyingi katika kumsaidia Muhammad (s.a.w.) kuliko mtu mwingine yeyote. Hapo Makka, aliwaacha huru watumwa wengi lakini haku-na ushahidi kwamba alitoa msaada wowote kwa Muhammad (s.a.w.). Muhammad, kwa kweli, hakutaka msaada wowote kutoka kwa Abu Bakr au kutoka kwa mtu yoyote yule, bali wakati mmoja hapo Makka, ukoo wake, Bani Hashim, ulikuwa katika hali ya kuzin-girwa kwa miaka mitatu, na ulikuwa katika dhiki kubwa. Hakuna ushahidi wowote kwamba Abu Bakr alifanya jaribio lolote la kuiondoa hiyo dhiki ya ukoo huo uliokuwa umezin-girwa lakini upo ushahidi kwamba baadhi ya makafiri waliwaletea mahitaji muhimu, na walifanya hivyo kwa hatari kubwa mno juu maisha yao wenyewe.

Wakati Muhammad (s.a.w.) alipokuwa tayari kuhama kutoka Makka kwenda Yathrib, Abu Bakr alimpa ngamia. Lakini Muhammad alikataa kumpanda ngamia huyo bila kumlipia gharama yake. Kwanza alilipa gharama ya ngamia kwa Abu Bakr, kisha ndipo akampan-da. Abu Bakr aliandamana na Muhammad (s.a.w.) katika safari hiyo, na alikuwa naye mle pangoni.

Binti ya Abu Bakr, Aisha, aliolewa na Muhammad (s.a.w.) na alikuwa mmoja wa wake zake wengi hapo Madina.

Dr. Montgomery Watt anaandika katika makala yake juu ya Abu Bakr katika Encyclopedia Britannica, juz. 1, uk. 54 (1973) kama ifuatavyo:

"Kabla ya Hijira (kuhama kwa Muhammad kutoka Makka kwenda Madina, A.D.622), yeye (Abu Bakr) alionekana wazi kama mtu wa pili kwa Muhammad kwa uchumba wa Muhammad kwa binti yake Aisha na kwa Abu Bakr kuwa sahaba wa Muhammad kwenye ile safari ya kwenda Madina."

Kwa mujibu wa makala hii, hizi basi ndio zilikuwa sifa mbili muhimu za Abu Bakr za kuwa wa "pili" kwa Muhammad, yaani, (1) binti yake aliolewa na Muhammad, na (2) alisafiri pamoja na Muhammad kutoka Makka kwenda Madina!

389

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hivi wakuu wa nchi na viongozi wa mataifa wanachaguliwa kwa misingi ya sifa kama hizi? Kama ndivyo wanavyochaguliwa, basi Abu Bakr alikuwa na washindani sio chini ya kumi na sita kwenye kiti cha Arabia. Kulikuwa na takriban wanaume kumi na sita ambao mabinti zao waliolewa na Muhammad (s.a.w.w.) kwa nyakati tofauti; mmoja wao alikuwa ni Abu Sufyan mwenyewe, na wawili wao walikuwa Mayahudi.

Hoja ya pili katika makala hii haina "nguvu" zaidi kuliko ile ya kwanza. Kulingana na hoja hii, Abu Bakr alikuja kuwa mkuu wa dola ya Madina kwa sababu wakati mmoja alisafiri pamoja na Muhammad kutoka mji mmoja kwenda mwingine - zoezi la ajabu la kikweli katika "mantiki ya kisayansi."

Hapo Makka, Mtume (s.a.w.) alimfanya Abu Bakr kuwa "ndugu" wa Umar ibn al-Khattab; huko Madina, alimfanya "ndugu" wa Kharja bin Zayd.

Katika kuzingirwa kwa Khaybar, Abu Bakr alipewa bendera, na aliongoza vikosi kwenda kuiteka hiyo ngome lakini bila mafanikio.

Katika msafara wa Dhat es-Salasil, Muhammad Mustafa (s.a.w.) alimtuma Abu Bakr pamoja na wapiganaji wa kawaidi wengine 200 chini ya ukamanda wa Abu Ubaidah bin al-Jarrah kwenda kuongezea nguvu vikosi vya Amr bin Al-Aas. Huyu Amr alichukua uon-gozi wa vikosi vyote. Abu Bakr kwa hiyo, alitumikia mabwana wawili katika msafara mmoja - kwanza Abu Ubaidah na kisha Amr bin Al-Aas.

Vilikuwepo vita na misafara mingi ya Uislamu lakini hakuna ushahidi kwamba Abu Bakr alijipatia sifa kamwe katika mojawapo ya hizo. Katika msafara wa Syria, Mtume wa Allah alimweka Abu Bakr chini ya uongozi wa Usamah bin Zayd bin Haritha.

Mtume (s.a.w.) hakuwahi kumteua Abu Bakr kwenye nafasi yoyote ya madaraka na mam-laka, kiraia au kijeshi. Safari moja alimtuma Makka kama kiongozi wa kikundi cha mahu-jaji kwenda kuendesha ibada za Hijja. Lakini baada ya kuondoka kwa Abu Bakr, Mtume (s.a.w.) alimtuma Ali ibn Abi Talib kutangaza huko Makka, ile Sura ya tisa ya Qur'an Tukufu (Surat al-Bara'ah au at-Tauba), ujumbe mpya ulioshuka kutoka Mbingnii. Abu Bakr hakuruhusiwa kuisoma. Ali ndiye aliyeisoma.

Sifa nyingine pekee ya Abu Bakr ilikuwa kwamba kabla tu ya kifo cha Mtume (s.a.w.), yeye aliongoza Swala ya jamaa.

Montgomery Watt:

"Tokea 622 hadi 632 yeye (Abu Bakr) alikuwa mshauri mkuu wa Muhammad, lakini hakuwa na shughuli maarufu ya umma isipokuwa kwamba alisimamia msafara wa mahujaji kwenda Makka mwaka 631, na aliongoza Swala za jamaa huko Madina wakati wa maradhi ya mwisho ya Muhammad.

(Encyclopedia Britanicca, Juz, 1. uk.54, 1973)

390

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Baadhi ya waandishi wanadai kwamba Abu Bakr alitokana na "familia ya kwanza ya Kiislamu." Labda, ina maana kwamba watu wote wa familia walisilimu kabla ya watu wote wa familia yoyote nyingine kusilimu. Lakini kama mtoto na baba wa mtu ni watu wa familia yake, basi dai lake haliwezi kuwa chochote ila la uongo. Mtoto wa Abu Bakr, Abdur Rahman, alipigana dhidi ya Mtume wa Uislamu katika vita vya Badr. Inasemekana kwamba aliposhambulia Waislamu, Abu Bakr mwenyewe alitaka kumshambulia katika pambano la watu wawili tu, lakini hakuruhusiwa kufanya hivyo na Mtume (s.a.w.).

Baba yake Abu Bakr, Abu Qahafa, aliishi Makka. Hakusilimu mpaka Makka iliposalimu amri kwa Mtume (s.a.w.) mnamo A.D. 630. Abu Bakr mwenyewe anasemekana kwamba alimleta mbele ya Mtume, na ilikuwa ni hapo tena ambapo alisilimu. Familia ambayo watu wake wote walikuwa wamesilimu kabla ya familia nyingine yoyote, ilikuwani familia ya Yasir. Yasir, mke wake, na mtoto wao, Ammar, wote watatu walisilimu kwa wakati mmoja, na walikuwa miongoni mwa Waislamu wa mwanzoni.

Wakati Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.a.w.w) alipofariki, Abu Bakr (na Umar) hawakuhudhuria mazishi yake. Walikwenda kwanza kwenye ukumbi wa Saqifah, na kisha kwenye Msikiti Mkuu, kupata na kuhesabu kura zao. Wakati huohuo, Muhammad (s.a.w.) alikuwa amekwisha kuzikwa.

Wakati Abu Bakr alipochukua madaraka ya serikali, hakuwaruhusu Waislamu kuadhimisha kipindi cha maombolezo kwenye kifo cha Mtume wao. Hapakuwa na wala mazishi ya kitaifa kwa ajili ya Muhammad Mustafa (s.a.w.), Mtume wa Mwisho na Mkuu, wa Allah (s.w.t.) Duniani; wala hakukuwa na maombolezo rasmi au yasiyo rasmi juu ya kuondoka kwake. Ilionekana kana kwamba kifo chake na mazishi yake yalikuwa ni mambo yasiyo na muhimu kabisa katika mioyo ya maswahaba zake mwenyewe.

391

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Matukio Muhimu ya Ukhalifa wa Abu Bakr

Vita vya Kwanza vya wenyewe kwa wenyewe katika Uislamu.

Mara tu baada ya taarifa za kifo cha Muhammad Mustafa zilipoenea nje ya viunga vya Madina, mitume wa uongo walitokea katika sehemu nyingi za nchi. Waliojulikana zaidi miongoni mwao walikuwa ni Musailama huko Yamama; Tulaiha Asadi huko Najd; Laqait bin Malik huko Oman; na Aswad Ansi huko Yemen. Baadhi yao walitaka serikali ya Madina kushirikiana madaraka nao, na baadhi ya wengine walitaka "kujitawala" katika maeneo yao. Abu Bakr alituma vikosi vyake dhidi yao ambavyo viliwazimisha.

Msafara wa Usamah.

Kama ilivyoelezwa mapema, Mtume (s.a.w.) alikuwa ameandaa, akiwa kwenye kitanda chake cha mauti, jeshi jipya la kushambulia Syria. Alikuwa amemteua Usamah, kijana wa miaka 18, kama kiongozi wa jeshi hili, na aliwaweka maswahaba zake wote chini ya amri yake huyo. Maagizo yake kwa jeshi hili yalikuwa ni waondoke Madina haraka. Lakini maswahaba hawakutaka kuondoka Madina, na hawakuondoka - mpaka Mtume (s.a.w.) akafariki.

Lakini baada ya kifo cha Mtume, wakati Abu Bakr alipohisi usalama kwenye kiti chake cha madaraka, alionyesha uharaka mkubwa sana katika kutuma jeshi la Usamah kwenda Syria. Alisema kwamba kitu kimoja ambacho asingeweza kukifanya ni kutangua amri ya bwana wake aliyefariki.

Abu Bakr alitembea na jeshi la Usamah kwa mwendo kidogo kujipatia "sifa" mwenyewe binafsi. Alipofikiria kwamba amejipatia sifa za kutosha, alimuomba yule Jenerali ruksa ya kurudi mjini. Alimuomba pia Jenerali huyo amruhusu Umar kubaki pamoja naye (Abu Bakr) hapo Madina kwa vile atahitaji ushauri wake katika kuiendesha serikali.

Usamah aliyakubalia maombi yote na Abu Bakr na Umar wakarudi Madina.

Kwa urefu, Usamah aliondoka Madina na akatembea kuelekea kaskazini mbele ya jeshi lake bila Abu Bakr na Umar. Lakini jeshi lake lilikuwa limepoteza uchangamfu wake. Yeye sasa labda hakujua la kufanya, na alirudi Madina baada ya kutokuwepo kwa miezi miwili.

392

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir John Glubb:

"Mnamo Septemba 632, baada ya miezi miwili ya kutokuwepo, Usamah alirejea Madina na kondoo na ngamia waliotekwa nyara, ingawa ni maelezo machache juu ya oparesheni yake yaliyotufikia. Inaonekana kwamba alishambulia makabila ya Kibedui badala ya vikosi vya Byzantine."

(The Great Arab Conquests, 1963)

Usamah bin Zayd bin Haritha, kipenzi cha Muhammad (s.a.w.), na Jenerali wa msafara wa kwenda Syria, anaonekana kupotea mara moja kwenye historia; ni kidogo sana kina-chosikika kuhusu yeye baada ya kurudi kutoka kwenye msafara wake. Anaweza kuwa ameshiriki katika kampeni za Abu Bakr na Umar katika viwango vya chini.

Malik ibn Nuweira na mauwaji ya Kabila lake.

Ibn Khalikan, yule mwanahistoria, anasema kwamba Malik ibn Nuweira alikuwa ni mtu mwenye hadhi kubwa katika Arabia. Alikuwa ni mpanda farasi maarufu, shujaa wa ukoo, mshairi maarufu, na rafiki yake Muhammad Mustafa (s.a.w.).

Ibn Hajar Asqalani anasema katika kitabu chake cha wasifa wa maswahaba kwamba wakati Malik aliposilimu, Mtume (s.a.w.) alimteua kama Mkusanya Mapato wa kabila lake la Banu Yirbo. Alikusanya Zaka kutoka kwenye kabila lake, na akazipeleka Madina. Lakini aliposikia habari za kifo cha Mtume (s.a.w.), aliacha kukusanya Zaka hizo, na akawaam-bia watu wake kwamba kabla ya kupeleka makusanyo yoyote Madina, alitaka kujua hiyo serikali mpya katika mji huo imekaaje.

Malik hakulipa Zaka kwa serikali hiyo mpya huko Madina, na Abu Bakr akatuma jeshi la kuadhibu chini ya uongozi wa Khalid bin al-Walid kuonyesha madaraka yake, na kukusanya ile Zaka iliyoshindikana kulipwa.

Khalid alikuwa na mazungumzo mafupi na Malik, na huyu Malik alijua kwamba atauawa. Baadhi ya wanahistoria wanasema kwamba Khalid alimpenda mke wa Malik, na akaamu-ru kuuawa kwake. Malik alimgeukia mke wake, na akasema: "Wewe ndiye utakayesababisha kifo juu yangu mimi." Lakini Khalid alilikataa hili na kusema: "Hapana, umekuwa murtad, na urtad wako ndio unaosababisha kifo chako." Ingawa Malik alilalami-ka kwamba alikuwa ni Mwislam, Khalid hakumsikiliza, na Malik akauawa.

Abu Qatada Ansari alikuwa ni sahaba wa Mtume (s.a.w.). Alikuja na Khalid kutoka Madina. Alishitushwa sana na kuuawa kwa Malik na Khalid kiasi kwamba alirudi mara moja Madina, na akamwambia Abu Bakr kwamba hatatumika chini ya kamanda ambaye ameua mwislamu.

393

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Baada ya kumuua Malik ibn Nuwaira, Khalid "akamuoa" mjane wake. Huko Madina, Umar alikuwa ameshituka sana kiasi kwamba alidai, kutoka kwa Abu Bakr, ufukuzwaji wa mara moja wa Khalid. Alisema kwamba Khalid alipaswa kushitakiwa kwa makosa yote mawili, ya mauwaji na zinaa. Kwa mujibu wa sheria za Kiislam, Khalid alikuwa apigwe mawe mpaka afe. Lakini Abu Bakr alimtetea Khalid, na akasema kwamba alifanya tu "kosa la maamuzi."

Watu wa kabila la Bani Yirbu walikuwa wameishikilia Zaka lakini mbali na hilo walikuwa ni Waislamu katika kila hali ya neno hilo. Abu Qatada mwenyewe alishuhudia kwamba ali-isikia Adhana katika kijiji cha Malik, na aliwaona jamaa wa kabila lake wakiswali Sala za jamaa. Hata hivyo, Khalid aliamuru vikosi vyake kuwaangamiza.

Tabari anaandika katika Taarikh yake kwamba pale Khalid na vikosi vyake walipoingia kwenye nchi ya Bani Yirbu, waliwaambia watu wa kabila hilo: "Sisi ni Waislamu." Wao wakasema: "Na sisi pia ni Waislamu." Watu wa Khalid wakauliza: "Kama ninyi ni Waislamu, kwa nini mmebeba silaha? Hakuna vita kati yetu. Wekeni silaha zenu chini ili sisi wote tuweze kuswali."

Watu wa kabila hili wakaweka chini silaha zao, lakini mara tu walipokwisha kufanya hivyo, wapiganaji wa Khalid wakawakamata, wakawafunga, na wakawaacha watetemeke kwenye usiku ule wa baridi. Asubuhi iliyofuata, wote waliuawa. Kisha Khalid akazipora nyumba zao, akawateka wanawake zao na watoto, na wakawapeleka Madina kama wafungwa wa kivita.

Sir John Glubb

"Abu Bakr alimtuma Khalid bin Walid kwenda Najid pamoja na watu 4000. Koo nyingi za Bani Tamim, ziliharakisha kumtembelea Khalid lakini tawi la Bani Yirbu la kabila hilo, chini ya mkuu wao, Malik ibn Nuwaira, lilibaki nyuma. Malik alikuwa ni chifu mwenye heshima maalum, mpiganaji, aliyejulikana kwa ukarimu wake na mshairi maarufu. Ujasiri, ukarimu na ushairi zilikuwa ndio sifa tatu zilizopendwa sana miongoni mwa Waarabu. Kwa kutokupenda kujidhalilisha mwenyewe kwa kum-nyenyekea Khalid, aliwaamuru wafuasi wake kutawanyika na yeye mwenyewe inavyoonekana akaenda upande wa pili wa jangwa peke yake pamoja na familia yake. Abu Bakr alikuwa ametoa maagizo kwamba mtihani utakaotumika kwa waasi wanaoshukiwa ulikuwa kwamba watakiwe kurudia utaratibu wa shahada ya Kiislam na kwamba waitikie kwenye wito wa Swala. Khalid, hata hivyo, alipendelea njia za shari zaidi na akatuma vikundi vya wapanda farasi kuwazunguka wale watoro na kupora mali zao. Kikundi kimoja kama hicho kilimkamata Malik ibn Nuwaira na familia yake na wakawaleta kwa Khalid, ingawa walitamka kwa dhati kwamba walikuwa ni Waislamu. Watu wa Madina ambao walikuwa pamoja na jeshi hilo walipinga kwa nguvu sana dhidi ya ukatili wa Khalid, lakini bila mafanikio.

394

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wafungwa hao waliwekwa chini ya ulinzi lakini, wakati wa usiku, Malik ibn Nuwaira na wafuasi wake waliuawa kikatili. Ndani ya masaa 24 Khalid alikuwa amemuoa mjane wa mwathirika wake.

Malik ibn Nuwaira aliuawa wakati akishuhudia kwamba ni mu'min. Kwa hakika ndoa ya Khalid na mrembo Laila ilizusha wasiwasi kwamba Malik aliuawa pamoja na kusudi la kumfanya apatikane kwa mtekaji.

Wale watu wa Madina, ambao walikuwa tayari wamepinga vitendo vya kikatili vya Khalid, walikuja juu kwa hasira kwa kifo cha Malik. Mtu mmoja, Abu Qatada, rafiki wa zamani na sahaba wa Mtume, aliharakishia Madina kulalamika kwa Abu Bakr, ambaye alimwita Khalid kujibu shutuma hizo. Umar ibn al-Khattab alimshinikiza khalifa kumnyang'anya Khalid ukamanda wake. Khalid akirejea Madina, alidai kwamba hakuamuru kuuawa kwa Malik, bali kwamba maagizo yake kwa walinzi wake yalikuwa hayakueleweka. Mweye hekima Abu Bakr, chochote ambacho angek-ifikiria juu ya maadili ya wakili wake, alikuwa anatambua umahiri wake. 'sitaurud-isha kwenye ala upanga ambao Allah ameuchomoa kwa ajili ya utumishi Wake,' ali-tamka kwa mshangao. Visingizio vya Khalid vikakubalika."

(The Great Arab Conquests, 1963, uk.112)

Wale jamaa wa kikabila wa Banu Yirbu walitamka kwamba Allah ni Mmoja, na Muhammad ni Mjumbe Wake, na waliswali Swala zao kama kawaida. Waliukubali pia ule utaratibu wa kulipa Zaka, na walikuwa wakiilipa kwa Mtume (s.a.w.). Lakini wakasi-mamisha malipo ya Zaka kwa serikali ya Abu Bakr ndipo akasema kwamba wamekuwa murtadi, na akatangaza vita juu yao.

Wakiwa wanafuata masharti rasmi, wanahistoria wa Sunni wamewaweka kundi moja wale jamaa wote wa kikabila ambao walizuia kodi zao kwa serikali ya Saqifah kama "murtad." Hivi walikuwa ni murtad kweli?

Mafaqihi wa Kiislam wameifafanua "murtadi" kama ukanusho wa Uislamu. Lakini kushindwa kuswali au kufunga wakati wa Ramadhani au kwenda kuhiji Makka au kutoa Zaka, sio ukanusho wa Uislamu. Mtu ambaye hatekelezi wajibu wa lazima uliowekwa juu yake na Uislamu lakini anatamka kwamba ni mwislamu, hawezi kuitwa murtad. Kama mtu angekuwa awe murtadi kwa kukosa Swala au funga au kutoa Zaka, basi Waislamu wengi wa kila kizazi wangekuwa waitwe murtadi. Lakini hawakuitwa hivyo.

Hakuna Aya ndani ya Qur'an inayoitaka serikali ya Kiislamu kuwaua wale Waislamu ambao hawatoi Zaka. Hakuna Hadith ya Mtume wa Uislamu (s.a.w.) inayoeleza kwamba adhabu ya kukataa kutoa Zaka ni kifo.

395

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mbali na kutowaua Waislamu kwa kushindwa kwao kutoa Zaka, Mtume (s.a.w.) kwa kweli alitoa msamaha wa kulipa kodi (Zakat), angalau katika kadhia moja. Hiki ndicho mwanahistoria wa Sunni wa wakati huu, Dr. Muhammad Hamidullah, anachoandika katika kitabu chake, Introduction to Islam, (Kuwait, 1977):

"... ujumbe kutoka Taif ulikuja Madina ukiahidi kujisalimisha (kusilimu). Lakini uliomba kusamehewa kwenye Swala, kodi na utumishi wa kijeshi... Mtume aliridhia kuruhusu msamaha kwenye malipo ya kodi na utoaji wa utumishi wa kijeshi... kiten-do hiki cha Mtume kinaonyesha kwamba tahafifu inaweza kutolewa kwa wafuasi wapya..."

Hapa ulikuwepo mfano wa jambo lililowahi kutokea. Mtume (s.a.w.) alitoa msamaha kwa wakazi wa Taif kwenye malipo ya kodi. Lakini Abu Bakr hakufuata ule mfano wa kiutume uliotangulia; aliamua kufanya mfano wake mwenyewe; watu wote wa kabila la Malik ibn Nuwaira walikuwa wauawe, na wanawake na watoto kufanywa wafungwa wa kivita.

Mbali na Qur'an na Hadithi, Waislamu wa Sunni pia wanayakubali mamlaka ya "makubaliano" (ijma). Kwa kweli, makubaliano katika fiqihi ya Sunni ni kanuni muhimu sana kiasi kwamba yanakadiriwa kama ni kitu takriban kisicho na makosa. Kulikuwa na makubaliano ya Waislamu wote pamoja na Umar mwenyewe katika kupinga uamuzi wa Abu Bakr wa kupigana dhidi ya wale Waislamu ambao hawakulipa kodi zao. Lakini Abu Bakr aliyapuuza makubaliano yao na akasema kwamba kama makabila yangezuia hata kile kipande cha kamba ambacho walifungia ndama, katika sehemu ya Zaka, angepigana dhidi yao, na angekichukua kutoka kwao. Maagizo yake kwa vikosi vyake yalikuwa dhahiri: Waangamizeni wale watu wote ambao hawalipi Zaka.

Vikosi vya Abu Bakr vilitekeleza maagizo yake. Waliwafanyia wale Waislamu wa makabila vitisho visivyosemeka, na kufanya vitendo vya ukatili mkubwa juu yao kwa kuzuia Zaka.

Hivyo vinavyoitwa "vita vya murtad" vilivyopiganwa katika ukhalifa wa Abu Bakr, vilikuwa kwa kweli ni vita vya wenyewe kwa wenyewe - vya kwanza katika Uislamu. Vita hivi vilipiganwa na Waislamu dhidi ya Waislamu - kisa cha vita hivyo kwa upande wao kikiwa ni kukataa kwa baadhi ya makabila kulipa Zaka kwenye serikali ya Abu Bakr.

Abu Bakr alianza utawala wake na vita ya wenyewe kwa wenyewe lakini akaiita ni vita ya murtad. Pale vita vya wenyewe kwa wenyewe vilipopewa jina vita vya murtad, viligeuka kuwa vya "kuheshimika" na "vitukufu," na ikawa ni wajibu kwa Waislamu wote kushiriki ndani yake.

396

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Katika shauku yao ya kumtetea Khalid, Waislamu wengi kwa utulivu kabisa wanadai kwamba baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.), Malik na kabila lake waliritad, na adhabu iliyoagizwa katika Uislamu kwa ajili ya murtad ni kifo. Kama sababu yao ya kumtetea Khalid ni kwamba alikuwa sahaba wa Mtume (s.a.w.), basi Malik alikuwa pia ni sahaba wa Mtume (s.a.w.). Usahaba wa Mtume, kwa hiyo, hauwezi kuwa ndio sababu yao ya kumtetea Khalid. Lazima iwepo sababu nyingine au ziwepo sababu zingine. Kwa kweli walimtetea Khalid kwa sababu alikuwa ni chombo cha sera ya serikali ya Saqifah. Malik aligongana na serikali ya Saqifah alipozuia kuipa kodi. Mbali na hili, yeye na jamaa wa kabila lake walikuwa ni Waislamu wa vitendo. Lakini kwa sababu ya "kuvunja miiko yake" kwao, walilipa malipo ya adhabu yanayotisha - waliangamizwa!

Mbele ya kuzongwa na ushahidi dhidi ya Khalid, Abu Bakr alilazimika kumkosoa yeye lakini kama bwana mwenye shukrani, alimtetea na akaupachika uhalifu wake kwenye "kosa la maamuzi." Kama zawadi kwa kitendo chake cha ujasiri wake wa harakaharaka, alimpachika jina la "upanga wa Allah," na mwaka mmoja baadae, wakati peninsula yote ilipokuwa chini ya mamlaka yake, yeye (Abu Bakr) alimteua Khalid kama kamanda mkuu wa majeshi yake huko Syria.

Hatia kama uzinzi na mauaji ya halaiki ya Waislamu hazikuweza kusamehewa tu kama "makosa ya maamuzi" madogo tu bali zingeweza kwa kweli kuzawadiwa kama watendaji wake wangetoa uungaji mkono wao wa kupita kiasi kwa serikali ya Saqifah.

Hilo hitimisho la "kosa la maamuzi" umeonekana kuwa ni ugunduzi muafaka kwa Waislamu wengi. Uliwawezesha kuidhinisha kila jinai, na kumlinda kila mhalifu. Katika miaka iliyofuatia, walificha baadhi ya vitendo vya kutisha mno na matendo mabaya kupita kiasi, katika historia ya Kiislam kwa maelezo kwamba yalikuwa ni "makosa ya utenda-ji" tu.

Hapa mtu anaweza kuona jambo la kuvutia katika matumizi ya unafiki huu ujulikanao sana. Katika ukhalifa wa Abu Bakr, wale Waislamu wote waliozuia Zaka, walishutumiwa naye na wanahistoria wa Sunni kama "murtadi," na waliuawa. Lakini (wanahistoria hao hao ) katika ukhalifa wa Ali ibn Abi Talib, wale watu wote waliofanya uasi dhidi ya mamlaka yaliyowekwa kihalali, na ambao walisababisha vifo vya makumi ya maelfu ya Waislamu, walitolewa kwenye lawama na kuondolewa tuhuma kwa sababu walifanya "kosa la maamuzi" tu, na "walitubia."

Hili "kosa la utendaji" lilikuwa ni blanketi pana ajabu!

Kama ilivyoelezwa hapo juu, Abu Bakr aliuanzisha ukhalifa wake kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe. Lakini aliweza kuigeuza kama vita vya murtad, na kwa kudhamiria, ali-fanikiwa kuugandamiza upinzani wote juu yake mwenyewe.

397

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ushindi mwingine wa Abu Bakr

Mtume wa Allah (s.a.w.w) alimteua mtu mmoja, Ziad bin Labiid kama gavana wa Hadhramaut na Kinda. Wakati alipokufa, mtu mmoja, Ash'ath bin Qays aliamsha maasi dhidi ya serikali ya Madina ambayo sasa ilikuwa ikiongozwa na Abu Bakr. Abu Bakr alim-tuma jenerali wake, Ikrima bin Jahl, kurudisha mamlaka yake huko Kusini mwa Arabia. Ikrima alimshinda Ash'ath, akamteka na akampeleka kama mfungwa huko Madina. Ash'ath aliomba msamaha. Abu Bakr sio tu alimsamehe yeye bali pia alimuoza dada yake kwake.

Huko Bahrain, makabila ya Banu Bakr na Banu Abdul-Qays yalikuwa yamekataa kulipa kodi. Hatua za kuwaadhibu zilichukuliwa dhidi yao, na walilazimishwa kulipa kodi zao.

Vita hivi vinajulikana kwa jina la kijenasi (la kubatiza), la vita vya "Ridda" (yaani, vita dhidi ya murtad ili kuficha ukweli wenyewe wa mambo).

Abu Bakr alimaliza mwaka mzima kupigana dhidi ya Ahl-er-Ridda - watu walioritadi na mitume wa uongo. Mwishoni mwa mwaka wote hao walikuwa wametiishwa, na mamlaka yake yakaimarika katika nchi hiyo. Hata hivyo, katika mwisho wenye mafanikio wa vita hivi, hakutaka vikosi vyake kukaa bure; alivituma kwenda kuvamia nchi jirani za Syria na Uajemi.

John Alden Williams

"Wakati Abu Bakr alipomalizana na suala la wale walioritadi, aliona vema kuvituma vikosi vyake dhidi ya Syria. Kwa kulitekeleza hili, aliwaandikia watu wa Makka, al-Taif, al-Yaman, na Waarabu wote huko Najdi na Hijazi kuwaita kwenye vita vya jiha-di na kuamsha tamaa zao juu yake na katika ngawira inayoweza kupatikana kutoka kwa Wagiriki (Byzantines). Kwa sababu hiyo, watu ukichanganya na wale ambao walisukumwa na uroho na vile vile wale waliokuwa na matumaini ya ujira wa mbing-nii, walikwenda kwa wingi huko Madina. Imesimuliwa kutoka kwa al-Waqidi kwam-ba Abu Bakr alimpeleka Amr ibn al-Aas Palestina; Shurahbil ibn Hasana na Yazid ibn Abu Sufyan huko Damascus."

(Themes of Islamic Civilization, 1971)

Mapambano dhidi ya Syria na Uajemi yalianzishwa na Abu Bakr lakini alikufa kabla hajaweza kuyamalizia. Yalifikishwa kwenye mwisho wenye mafanikio na mrithi wake, Umar ibn al-Khattab.

Kukamatwa kwa Shamba la Fadak na Abu Bakr

Fadak lilikuwa ni moja ya mashamba aliyoyapata Mtume wa Uislamu baada ya ushindi wa

398

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Khaybar kwenye mwaka wa 7 Hijiria. Lakini kwa vile vikosi vyake havikulazimika kulip-igania, na lilitolewa kwake kwa hiari, lilichukuliwa kwamba ni mali ya Allah (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.).

Kama ilivyoonyeshwa kabla, Mtume wa Allah (s.w.t.) aliifanya Fadak kuwa zawadi kwa binti yake, kwa upande mmoja ikiwa kama fidia kwa mihanga mingi mama yake, Khadija, aliyoitoa kwa ajili ya Uislamu.

Abu Bakr alipoikamata serikali ya Waislamu, moja ya vitendo vyake ilikuwa ni kuchukua umiliki wa nguvu wa Fadak. Aliwafukuza wapangaji wa Fatima Zahra kutoka shambani kwake, na pia alimnyang'anya mali ambayo baba yake alimpa hapo Madina penyewe. Wakati Fatima alipolalamika dhidi ya kukamatwa huku, Abu Bakr alimjibu kwa "Hadith" ya baba yake. Alisema kwamba alikuwa amemsikia Mtume wa Allah akisema kwamba Mitume hawana warithi wowote, na utajiri kama huo, mali au vitu wanavyokuwa navyo wakati wa uhai wao, baada ya kufa kwao vinakuwa sio mali ya watoto wao, bali ya umma.

Fatima akasema kwamba Fadak sio mirathi ya baba yake; ilikuwa ni zawadi. Alinena kwa dhati kwamba Fadak ilikuwa ni mali binafsi ya Mtume wa Allah, na ilikuwa kama mali binafsi ambayo alimpa yeye Fatima.

Abu Bakr akauliza kama kulikuwa na mashahidi wowote.

Hii ilikuwa ni ajabu kweli. Ni miaka minne tu imepita baada ya ushindi wa Khaybar. Abu Bakr sio tu alikuwepo wakati wa kuizingira bali pia alifanya jaribio lisilofanikiwa la kuite-ka hiyo ngome. Alikuwa ameona kwa macho yake kile ambacho Mtume (s.a.w.) alikifanya na Fadak. Sasa miaka minne baadae, alikuwa akijifanya kama hana anachokijua. Kulingana na Bukhari, yule mkusanyaji wa Hadith, mahojiano yafuatayo yalitokea kati ya mdai na mtetezi.

Fatima: Ewe Abu Bakr, kama baba yako atafariki, nani atakayekuwa mrithi wake? Abu Bakr: Ni mimi, ambaye ni mwanae.

Fatima: Ni nani mrithi wa baba yangu mimi? Abu Bakr: Ni wewe, binti yake.

Fatima: Kama mimi ndiye mrithi wake, basi kwa nini uliikamata Fadak?

Abu Bakr: Nimemsikia Mtume wa Allah (s.w.t.) akisema: "Sisi ni kundi la Mitume, na hatuna warithi wowote wa kurithi mali zetu. Mali yoyote tuliyonayo, inakuwa ni mali ya umma pale tunapofariki."

Fatima: Lakini baba yangu aliiweka Fadak juu yangu mimi kama zawadi wakati wa uhai

399

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wake, na ilikuwa mikononi mwangu miaka yote hii.

Abu Bakr: Unao mashahidi wowote?

Fatima: Ali na Ummu Ayman ndio mashahidi wangu.

Abu Bakr: Ushahidi wa mwanaume mmoja na mwanamke mmoja hautoshi. Lazima wawepo ama wanaume wawili au mwanaume mmoja na wanawake wawili. Lakini kwa vile sio hivyo, kesi hii imefutwa.

Masikio ambayo Fatima alikuwa akiongea nayo, hayakuwa tayari kusikiliza hoja yoyote au sababu. Mashahidi hao wasingeleta tofauti yoyote kwa wale ambao walikuwa wamea-mua kutoshawishika. Kundi linaloshitakiwa lilikuwa na hoja moja yenye kuthubutu kabisa kwa upande wao! Ilikuwa ni hoja ambayo ilikuwa na nguvu ya kuzima hoja nyingine yoyote, na iliweza.

Kutilia nguvu utekelezaji wake katika kukamata lile shamba la Fadak, Abu Bakr alinukuu "Hadith" ya Mtume wa Allah (s.w.t.) Lakini ni ajabu kwamba yeye peke yake aliisikia "Hadith" hii. Na ni ajabu kama hiyo kwamba Muhammad hakuwaambia watu wa familia yake kwamba hawatarithi mali yake baada ya kifo chake kwa sababu alikuwa Mtume wa Allah, bali alizunguka akinong'oneza "Hadith" kwenye masikio ya watu wa nje.

Abu Bakr ndiye mtu pekee katika umma wa Muhammad (s.a.w.) aliyeisimulia "Hadith" hii na ambaye aliyeiweka kinyume na mamlaka ya Qur'an Tukufu. Fatwa ya Qur'an ni kama ifuatavyo:

Usahihi-45.jpg

"Wanaume wanayo sehemu katika wanayoyaacha wazazi na jamaa wa karibu, na wanawake wanayo sehemu katika waliyoyaacha wazazi na jamaa wa karibu; ikiwa mali hiyo ni kidogo au nyingi - hizi ni sehemu zilizofaridhiwa. (Sura ya 4; Aya ya 7)

Na kila mmoja tumemwekea warithi katika waliyoyaacha wazazi wawili na jamaa wa karibu. Na kwa wale pia ambao mikono yenu ya kulia imewaahidi, wapeni fungu lao.

Usahihi-46.jpg

Hakika Allah ni Shahidi wa kila kitu.(Sura ya 4; Aya ya 33)

400

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kwa mujibu wa Aya hizi, Allah (s.w.t.) amewapa watoto haki ya kurithi mali iliyoachwa na wazazi wao. Kuna Aya nyingine ambayo inayonyima haki hiyo kwa watoto wa mitume wa Allah (s.w.t.) hususan, kwa binti wa Muhammad (s.a.w.)?

Hata kama ikichukuliwa kwamba "Hadith" hiyo iliyonukuliwa na Abu Bakr sio ya uongo, na warithi wa Mitume hawawezi kurithi mali zao, basi "sheria" hii ilipaswa kutumika kwa watoto wa Mitume wote, na sio tu kwa binti ya Muhammad. Lakini kwa mujibu wa Qur'an, Mitume waliopita walikuwa na warithi wao, na warithi wale walirithi mali iliyoachwa na Mitume wao - baba zao.

Usahihi-47.jpg

"Na Suleiman alikuwa mrithi wa Daudi." (Sura y a 27; Ay a ya 16)

Maelezo ya Mfasiri kwenye Aya hii:

Hoja hapa ni kwamba Sulaiman sio tu kwamba alirithi ufalme wa baba yake bali na umaizi wake wa kiroho na cheo cha utume, ambacho sio lazima kiende kutoka kwa baba kwenda kwa mtoto.

(A. Yusuf Ali)

Kwa kiasi chochote, haikuwa ni lazima kwa Fatumah Zahra kuleta mashahidi. Yeye tayari alikuwa akiimiliki Fadak. Umiliki wake wa Fadak ulitegemea kwenye agizo lenye uzito au idhini yenye muwazo yakinifu ya Muhammad Mustafa (s.a.w.) kama Mtume wa Allah (s.w.t.) na mkuu wa Waislamu wote, na haiwezi kupingwa kisheria. Mzigo wa uthibitisho kwamba umiliki wa Fatima wa shamba hilo sio wa haki, ulikuwa juu ya Abu Bakr.

Jambo la muhimu ni kwamba mahakama itengwe na wenye mamlaka, na wenye mamlaka wasije wakaiingilia mahakama. Lakini katika suala la Fadak. Abu Bakr ambaye alikuwa ndiye anayelalamikiwa, alikuwa yeye mwenyewe ndiye hakimu, na mzee wa baraza la mahakama, na hukumu yake lazima ilikwenda dhidi ya mlalamikaji kama ambavyo inge-fanya katika mahakama isiyorasmi au chemba ya kidhalimu.

Kukamatwa kwa Fadak kilikuwa ni kitendo cha udhalimu mkubwa mno. Si muda mrefu baada ya Fadak, Abu Bakr alikabiliwa na matatizo mengi mapya na magumu. Ili kuyatat-ua hayo, aliweka vigezo viwili. Kimoja kilikuwa ni uteuzi wa maswahaba kama mahakimu. Kwa nafasi hizi, alichagua watu waliokuwa wakitambulika kwa ujuzi wao na uamuzi mzuri. Kama angekuwa muadilifu, alipaswa kulipeleka suala la Fadak kwa mmoja wa mahakimu wake kwa ajili ya hukumu badala ya kuchukuwa hatua za upande mmoja katika kulikamata.

401

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kigezo cha pili kilikuwa ni kushauriana na maswahaba. Kama Abu Bakr alikuwa na tatizo gumu, alikaa Msikitini, akawaita maswahaba wakubwa, na akaliweka tatizo hilo mbele yao. Baada ya kujadiliana, walilifumbua tatizo hilo. Kama Abu Bakr angekuwa muadilifu, angepaswa kuwaomba wao watoe uamuzi wao wenye haki juu ya Fadak. Lakini hakufanya hivyo.

Hii "Hadith" aliyoinukuu Abu Bakr kama "sababu" yake ya kuchukua umiliki wa Fadak, ilikuwa kwa kweli ni muundo wa kisheria wenye kusudi maalum ulioundwa kukidhi hali ambayo ilitishia kuhatarisha nafasi yake. Ulikuwa ni "utaratibu" uliobuniwa kwa mara ya kwanza na ya mwisho. Mara mgogoro huo ulipopita, utaratibu huo ulizikwa, usije kufukuliwa tena kamwe.

Katika makabiliano yake ya kisheria na serikali ya Saqifah, juu ya kukamatwa kwa Fadak, Fatima Zahra hakutegemea haki hata kidogo. Kifo cha baba yake, bila shaka, kilikuwa ndio mshituko mkubwa na huzuni kuu juu yake yeye. Lakini baadhi ya maswahaba zake Mtume (s.a.w.) hawakufikiri kwamba huzuni yake ilikuwa kubwa vya kutosha, na walitafuta kufanya wa kwao "mchango" juu yake. Ilikuwa ni pale alipokuwa katikati tu ya maom-bolezo juu ya baba yake ambapo Abu Bakr alipomfukuza meneja wake wa shamba kutoka Fadak, na mawakala wake wakachukua umiliki wake.

Muda mrefu baada ya mlalamikaji na watetezi katika suala la shamba la Fadak wakiwa wameiaga dunia, Umar ibn Abdul Aziz, khalifa wa Bani Umayya, akalirudisha kwa warithi wa Fatima Zahra. Alikuwa mwadilifu na mcha-mungu, na alitambua kwamba ule ukamat-waji wa Fadak ulikuwa ni kitendo cha kikorofi na unyang'anyi wa dhahiri.

Kitendo cha serikali ya Saqifah katika kuikamata Fadak hakikuhusika hata kidogo na she-ria au tafsiri yake.Viongozi wake walishawishiwa na lengo moja, yaani, kuwakosesha watoto wa Muhammad Mustafa (s.a.w.) uwezo wao wa maisha. Sadaka ilikuwa ni hara-mu juu yao, na hawawezi kuipokea. Rasilimali iliyokuwa ikiwapatia, waliinyang'anywa, na haki yao ya urithi ilikuwa haitambuliwi.

Kujitenga kwa Ali na maisha ya kawaida

Baada ya mapinduzi Haya, Ali alitumia muda wake mwingi zaidi nyumbani ambako aliji-husisha mwenyewe na kazi ya kuzikusanya Aya za Qur'an, na kuzipanga katika kufuata utaratibu wa miaka na matukio. Alikuwa kwa hiyo anadhihirisha kwamba kazi yake ilikuwa ni kutumikia Uislamu licha ya mazingira yasiyofungamana nayo.Mara nyingi ali-dondoa, mbele ya marafiki zake, zile Hadith za Mtume (s.a.w.) kwamba watu wa Nyumba yake na Qur'an ndio vilikuwa "mirathi" yake kwa umma wa Waislamu, na kwamba vyote hivyo havitenganishiki kimoja kutoka kingine

402

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hakuna hata mmoja kati ya maswahaba aliyekuwa na ujuzi bora zaidi kuliko Ali wa kuzikusanya Aya za Qur'an. Alikuwa mmoja kati ya maswahaba wachache wa Mtume (s.a.w.) walioijua Qur'an kwa moyo.

Kwa bahati mbaya, Umar ibn al-Khattab alitumia miaka kumi na nne akijaribu kuhifadhi Sura ya pili ya Qur'an (Al-Baqarah), lakini hakuweza.

Kukusanya Aya zote za Qur'an zilizotawanyika, katika mpangilio ule ule ambamo zilishu-ka, ilikuwa ni kazi ambayo ingeweza kufanywa na mtu mahsusi aliyedarisishwa na Muhammad Mustafa (s.a.w.) mwenyewe. Mtu kama huyo alikuwa ni Ali. Alikaa muda mwingi naye kuliko mtu mwingine yoyote yule. Alikuwa, kwa maneno halisi, amekua na Qur'an. Yeye mwenyewe alisema kwamba haikuwepo Aya yoyote katika Qur'an, juu yake ambayo alikuwa hajui ni lini ilishuka, wapi ilishushwa, na kwa nini ilishushwa. Alikuwa anajua wakati, mahali na tukio la kushuka kwa kila Aya ya Qur'an Tukufu.

Ali aliimaliza hiyo kazi aliyojipa mwenyewe. Lakini bahati mbaya kwa Uislamu, kundi lililokuwa madarakani, kwa kufuata sera zao, halikutaka kuitambua kazi yake. Hakuna kitu ambacho kilikuwa hakitakiwi na kundi hilo kuliko kutambua utumishi wa Ali kwa Uislamu. Halikuwa kwa hiyo, "limeukubali" mkusanyo wa Ali wa Aya za Qur'an Tukufu.

Katika siku zilizofuatia mara tu baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.), watu wengi walikuja kumuona Ali, na baadhi yao walimshauri kutwaa kwa nguvu kilichokuwa chake kihalali. Miongoni mwa watu hawa walikuwepo marafiki wa kweli wachache, na pia walikuwepo wafuata maslahi binafsi wengi wasiokuwa na maadili. Wote walimuahidi kumuunga mkono. Hawa wa kundi la mwisho, kwa kweli, waliahidi uumungaji mkono wao kwa sababu zilizofichika. Walitarajia kuchochea vita katika Uislamu na kunufaika katika mashindano ya kikatili ya Waislamu.

Mara tu baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.), ami yake, Abbas ibn Abdul Muttalib, alimwen-dea Ali, na akasema: "Nyoosha mkono wako, nami nitakupa kiapo changu cha utii. Kitendo changu hiki cha kuonyesha hisia kitakuwa na athari kubwa ya kisaikologia juu ya Waislamu. Watasema kwamba ami yake Mtume ametoa kiapo chake cha utii kwa Ali; nasi pia, kwa hiyo, tumpe yeye kiapo chetu."

Abbas, kwa kweli, alikuwa mmoja wa hao marafiki wa kweli wachache. Katika kundi jingine la "watakia heri" wa Ali alikuwa ni Abu Sufyan, kiongozi wa Bani Umayya, adui wa milele wa Muhammad (s.a.w.), alama ya upinzani wa kipagani na chuki kwa Uislamu. Katika matukio yaliyofuatia kifo cha Mtume (s.a.w.), aliiona fursa yake ya kuuangamiza Uislamu, na aliitumia. Alikuja kwa Ali na akasema: "Inafedhehesha mno kuona watu wa koo duni kabisa za Quraishi zikipora haki yako, na kuikamata serikali ambayo ni yako. Chote unachotakiwa kufanya ili kuichukua kutoka kwao, ni kunipa mimi ishara, nami

403

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

nitaijaza mitaa ya Madina kwa askari wa chini na wa farasi, waliotayari kufa kwa amri yako."

Binadamu gani angeweza kuikataa ahadi hii? Na Ali alikuwa na nini cha kupoteza sasa hata hivyo? Ambacho angepoteza, alikwisha kipoteza. Lakini basi ni nani katika umma wa Waislamu aliyeupenda Uislamu kama yeye alivyoupenda? Yeye kamwe hakuruhusu vishawishi au uchokozi kumfanya yeye afanye kitu chochote ambacho kingezuia maslahi makubwa zaidi ya Uislamu na Waislamu. Uislamu ulikuwa bado ni mafanikio hafifu yenye uwezekano kabisa wa kuharibiwa na kupotoshwa na nguvu ndani na nje ya Madina lakini kwa Ali ulikuwa na mlinzi ambaye hakuruhusu hilo litokee.

Kama Ali alikuwa ndiye "hakimu bora katika Uislamu," alikuwa pia ni hakimu mzuri wa watu. Jibu lake kwa Abu Sufyan, liliundwa kama swali, lilikuwa bainishi. "Tangu lini umekuwa mtakia heri wa Uislamu?" aliuliza Ali. Lilikuwa ni swali la kiufasaha tu, na kwalo tu aliibeua ahadi ya Abu Sufyan kwa dharau ambayo ilistahili, na akamtolea sauti ya mfyonzo (squelch).

Kwa jibu hili, Ali alidhihirisha kwa mara nyingine tena kwamba yeye na yeye peke yake ndiye aliyekuwa mlezi wa kweli hasa wa Uislamu. Katika wakati huu wa kuamua hatima yake, aliyaacha maslahi na matamanio yake binafsi lakini aliuokoa Uislamu kutokana na kuangamia.

Ulikuwa ni wakati muhimu sana katika historia ya Uislamu mchanga. Maasi dhidi ya serikali ya Abu Bakr yalikuwa yakitokea ghafla kote nchini. Kama Ali angezikubali ahadi za ami yake, Abbas ibn Abdul Muttalib, na za Abu Sufyan, angeweza kufanikiwa kuika-mata serikali ya Madina. Lakini mafanikio yake yangekuja kwa gharama tu, kwa Uislamu, ya vita vya wenyewe kwa wenyewe hapo Madina ambapo palikuwa ndio kiini cha dola ya Uislamu na jamii.Vita ndani ya Madina kwa hali ya mambo yalivyo ingeweza kusi-mamisha ghafla kazi ya Uislamu.

Ali aliushinda mtihani huu kama alivyoishinda mingine mingi maishani mwake. Hakushawishika na matamanio.

Jamii ya Cincinnati iliyoundwa mwishoni mwa Mapinduzi ya Marekani na maafisa walio-tumikia pamoja na Washington, kwa muda mrefu imedumisha uhusiano na vizazi vya maafisa wa Kifaransa waliotumikia upigania haki wa Marekani. Tafsiri ya Kiingereza ya wito wa Jamii hiyo ni: "Aliachia kila kitu ili kuliokoa taifa."

Huenda kwa kufaa zaidi ungekuwa wito uliotungwa kwa ajili ya Ali ibn Abi Talib ambao ungesomeka hivi:

404

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Aliachilia kila kitu ili kuuokoa Uislamu."

Kifo cha Fatima Zahra

Ali alikuwa amepata mishituko mibaya miwili katika siku moja; wa kwanza ulikuwa ni kifo cha rafiki na mfadhili wake, Muhammad (s.a.w.), Mtume wa Allah (s.w.t.). Kifo cha Mtume kiliweka mwisho mgumu kwenye furaha na ustawi wa Ali na familia yake katika dunia hii. Wa pili ni kunyang'anywa haki yake ya urithi. Masahaba waliutoa ukhalifa nje ya nyumba yake, wameujitwalia wao wenyewe.

Ali alikuwa akijaribu kupata ahueni kutoka kwenye mishtuko hii miwili pale ulipokuja mshtuko wa tatu, wenye kuumiza tu kama ile miwili ya kwanza. Takriban siku sabini na tano au tisini na tano baada ya kifo cha Mtume wa Allah (s.w.t.) binti yake mpendwa, na mkewe Ali - Fatima Zahra - naye pia akafariki. Ali alijawa na huzuni kwa kifo chake. Fatima Zahra alizikwa usiku, kulingana na maombi yake mwenyewe. Ni watu wa familia yake tu waliofahamu juu ya kuzikwa kwake na mahali ya kuzikwa kwake. Watu wa Madina hawakujua ni lini na wapi alipozikwa.

Baada ya kifo cha baba yake, Fatima Zahra hakutamani kitu kingine zaidi kuliko kuungan-ishwa naye huko Mbinguni. Kifo chake Fatima kiliharakishwa, ama kusababishwa, na mfululizo wa mishituko ambayo ilikuja kama mawimbi, moja baada ya jingine, kufuatia kifo cha baba yake. Wengi wa maswahaba wa baba yake hawakuhudhuria mazishi ya baba yake; kwenye mazishi yake yeye walitengwa kwa makusudi. Alikutana na baba yake huko Mbinguni, na aliipata ile furaha ambayo ilimuepuka tangu kifo chake (baba yake), kwa mara nyingine tena.

Ali alikuwa na umri wa miaka 32 tu pale Mtume wa Allah (s.w.t.) na binti yake walipofari-ki. Lakini baada ya kufa kwao, ule muda aliokuwa amebakiwa nao, ulikuwa kama zama zisizofahamika za miaka ambamo alijaribu kufifiliza huzuni zake katika ibada za Allah (s.w.t.) na utumishi kwenye Uislamu. Licha ya tofauti zake na kutokukubaliana na watawala wa nyakati hizo, kamwe hakuchukua sera ya mkinzani. Alikuwa yuko tayari daima kuwatumikia Waislamu. Kila kitu alichowahi kusema au kufanya, kilikadiriwa kuimarisha Uislamu au kunufaisha Waislamu. Ali alidhihirisha tena na tena kwamba upen-do wake na chuki zake, urafiki wake na uadui wake, vilikuwa kwa ajili ya Allah (s.w.t.) na kwa Allah pekee. Msimamo wake juu ya watu ulikuwa siku zote hauna upendeleo. Upendo na chuki zake zilikuwa vivyo hivyo hazina upendeleo. Yeye alipenda na alichukia - kwa ajili tu ya Allah (s.w.t.). Aliwapenda wale waliompenda Allah (s.w.t.) na aliwachukia wale waliomwasi Allah (s.w.t.)

Sera za Abu Bakr

Abu Bakr na Umar walifahamu kwamba Waarabu walikuwa na tamaa mbili: kupenda upo-

405

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

raji na ulipizaji kisasi. Walizitumia tamaa zote hizi kwa ustadi. Waliwapa Waarabu kionjo cha uporaji kwa kuwashutumu wale Waislamu kama murtadi wale ambao walizuia malipo ya kodi kwa serikali yao. Mara tu Waislamu hawa walipoitwa murtadi, ilikuwa halali kuwaua, kupora nyumba zao, na kuwafanya wanawake na watoto wao kuwa watumwa.

Lakini ukomeshaji wa "murtadi" ulikuwa ni jambo dogo na la kienyeji. Ili kutatua matati-zo yao muda-mrefu, Abu Bakr na Umar walipata kwa bahati, mpango thabiti zaidi wa utekelezaji. Hawakuwaacha wale washindi wa mikwaruzano na vita vya murtadi kurejea Madina. Badala yake, waliwaamuru kwenda mpaka kwenye mipaka ya Syria na Uajemi, na kuzivamia nchi hizo kwa wakati mmoja. Uamuzi huu ulikuwa matokeo ya kipaji cha kisiasa kama ambavyo matukio yalikuwa yaonyeshe baadae kidogo.

Noldeke:

"Ilikuwa kwa ni sera nzuri ya kuyageuza yale makabila ya porini yaliyoshindwa kabla, kuelekea kwenye lengo lililo nje ambamo wanaweza kukidhi ashiki yao ya ngawira kwa kiwango kikubwa, kudumisha hisia zao za kivita na kujiimarisha wao wenyewe katika kujiambatanisha kwao na ile dini mpya."

(From the Sketches from Eastern History)

Noldeke angekuwa sahihi zaidi kama angerekebisha maelezo yake yakasomeka kwamba yale makabila "yangejiimarisha yenyewe katika kujiambatanisha kwao na serikali mpya ya Saqifah," badala ya "dini mpya." dini haiimarishwi kwa kuua watu wenginena kwa kupora nyumba zao na miji yao. Lakini makabila yale kwa hakika yaliimarika katika kujiambatanisha kwao na serikali ya Saqifah ambayo iliwapa fursa nzuri sana za "kukidhi ashiki yao ya ngawira kwa kiwango kikubwa."

Geoffrey Blainey:

"Profesa Quincy Wright, ambaye alikamilisha huko Chicago mnamo 1942, uchunguzi wa kivita wenye malengo, alihitimisha kwamba sababu kubwa na ya mara kwa mara ya vita vya kimataifa ilikuwa ni tabia ya uchokozi "kujiingiza kwenye vita vya nje kama mbinu ya kukwepea matatizo ya ndani." Hoja ya Wright ina nguvu zaidi katika toleo la sasa la Encyclopedia Britannica, ambayo aliiandikia makala juu ya vyanzo vya vita: alikuwa na shaka kama udikteta wa ki-imla unaweza kuwepo bila ya kudhi-haki au kushambulia msingiziwa wa nje.

(The Causes of War, New York, 1973)

406

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir Basil H. Liddell Hart:

"Madikteta hufanya vita kwenye nchi zingine kama njia ya kukwepea mazingatio ya kwenye hali za ndani na kuruhusu kutoridhika kujitokeza wazi.

(Why Don t We Learn From History? 1971)

Pale majeshi ya Waislamu yaliposhambulia vituo vya ulinzi kwenye mipaka ya falme za Warumi na Waajemi, kutoridhika kwao kulijitokeza wazi."

Profesa James M. Buchanan:

"Lazima tujihadhari na mizimu ya Orwell '1984,' wakati maadui wa nje wanapoten-genezwa, wa kweli au wa kubuni, kwa lengo la kupata msaada wa kuungwa mkono kwa serikali ya taifa."

(Imenukuliwa na Leonard Silk katika New York Times, Oktoba 24, 1986)

Mwanahistoria wa kisasa wa Pakistani, Dr. Hamid-ud-Din, anasema kwamba Abu Bakr alikuwa na sababu nzito sana ya kushambulia Uajemi na Roma. Katika Ta'arikh yake anaandika hivi:

"Waarabu walikuwa wameungana chini ya bendera ya Uislamu, na Waajemi wali-waona kama hatari ya kudumu. Makabila ya Kikristo ya Waarabu wa Iraqi mara kwa mara yaliwachochea Waajemi dhidi ya Waarabu Waislamu. (Iraqi siku hizo ilikuwa sehemu ya Falme ya Uajemi). Lakini Waajemi walikuwa hawawezi kuwasikiliza Waarabu hao kwa sababu ya vita vyao vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vilikuwa vimeiharibu nchi yao. Hata hivyo, Abu Bakr alikuwa hana shaka kwamba kama amani ya ndani itarejea huko Uajemi, basi Waajemi hao watawashambulia Waarabu. Alikuwa kwa hiyo, wakati wote mwenye tahadhari, na hakuufumbia macho kamwe ule utaratibu wa "usalama kwanza." Mikwaruzano ilikuwa imekwisha anza kati ya wahamaji wa Iraqi na kabila la Waislamu la Waiil. Mathanna bin al-Haritha, chifu wa Waiil, alikwenda Madina na kutaka ruksa kutoka kwa Abu Bakr ya kushambulia Iraqi. Khalid bin al-Walid alikuwa hivi karibuni yuko huru kutokana na vita dhidi ya murtadi huko Arabia ya Kati ambavyo alikuwa amevikomesha kwa mafanikio makubwa. Abu Bakr alimteua kama msaidizi wa Mathanna."

(History of Islam, cha Hamid-ud-Din, Ph.D. [Harvard University],

Lahore, Pakistani, 1971)

407

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abu Bakr, inavyoonekana, alikuwa na sababu nzito za kuwashambulia Warumi. Dr. Hamid-ud -Din anaandika zaidi katika Ta 'arikh yake:

"Kama vile walivyokuwa Waajemi, Warumi pia walikuwa wanaihofia ile serikali ya Waarabu iliyoimarishwa hivi karibuni. Waliiona kama tishio kwao. Kulikuwa, kwa hiyo, wakati wote hatari ya shambulizi kutoka kwao juu ya Madina. Abu Bakr hakuwa kamwe asiyelizingatia tishio hili. Kwa hiyo, alituma afisa mmoja, mtu mmoja Khalid bin Said, akiongoza kikundi cha wapiganaji, kwa uchunguzi na upelelezi wa mpaka wa Roma. Inaonekana kwamba huyu Khalid "alichochewa" katika kuwashambulia Warumi."

Majenerali wa Abu Bakr "waliituliza" Arabia, wakakusanya Zaka kutoka kwa makabila ambayo hayakuwa yamelipa mapema, na wakati kulipokuwa hakuna kilichobaki cha wao kufanya nyumbani, walifanya safari fupi za majaribio ndani ya nchi za Uajemi na Byzantine (Roma). Mafanikio madogo madogo yalifuatiwa na ushindi mkubwa. Mtiririko imara wa dhahabu, na fedha, wa wanawake na watumwa, ulianza kumiminika kuingia Madina. Muhajirina na Ansari wakasahau mijadala yao ya haki na batili. Walisahau pia husuda za wao kwa wao na kutuhumiana. Vile vita vya Uajemi na Syria viliimarisha ile serikali ya Saqifah hapo Madina.

Malengo ya vita vya Abu Bakr na Umar

1.  Kuwanyamazisha wakosoaji wa serikali ya Saqifah, na kukomesha usaili wa aina zote.

2.  Kuwasadikisha Waislamu kwamba zile sera za serikali ya Saqifah zili-tokana na moyo halisi wa kidini.

3.  Kuwapa Waarabu fursa ya kuridhisha ashiki zao za uporaji. Makisio yalikuwa kwamba mara tu hao Waarabu watakapoonja raha za ushindi na uporaji, watakuwa na muda mchache au mwelekeo wa kurafakari masuala ya wema, uadilifu au falsafa. Matamanio yao binafsi yatatangulia juu ya kila kitu kinginecho.

4.  Kuhakikisha usalama wa serikali ya Saqifah kwa hali yoyote ile. Viongozi wake walitegemea kwamba katika mchanganyiko wa vita na ushindi, Waarabu wataisahau kidogo kidogo ile familia ya Mtume wao, na hili litakuwa ndio ushindi wao wa kweli.

Kuwapa fursa maadui wa familia ya Muhammad Mustafa (s.a.w.) ya kupanda kwenye nafasi za juu ili kwamba waweze kushikiza muundo wa madaraka wa Saqifah.

408

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ingawa Ali hajawahi kukabilana na Abu Bakr na Umar, walikuona kuwepo kwake kama "tishio" kwa usalama wao. Kujiweka wao wenyewe "salama" waliamini kwamba wali-paswa kutafuta kituo kipya cha madaraka. Hiki walikikuta tayari katika familia ya Abu Sufyan na Bani Umayya wengine wa Makka, na wakaghushi muungano nao.

Sir John Glubb:

"Makamanda wa safu watatu (wa Abu Bakr katika vita vya Syria) walikuwa ni Amr bin Al-Aas, Shurahbil bin Hasana, na Yazeed bin Abu Sufyan (baba yake, mzee Abu Sufyan, mshindi wa Uhud, na mpinzani wa siku nyingi wa Muhammad), alikuwa kwa wakati huo alikuwa ameachwa kwa kupewa ugavana huko Yemen."

(The Great Arab Conquests. 1963)

Serikali ya Saqifah ilimteua Abu Sufyan kuwa gavana wake huko Yemen, na mtoto wake mkubwa, Yazid, kuwa jenerali wake katika vita vya Syria. Mdogo wake Yazid, Mu'awiyah, aliteuliwa kama afisa wa jeshi, na alifuatana naye kwenda Syria.

Uwezekano mpya uliundwa kwa ajili ya wale Bani Umayya wote ambao nuSura wachun-gulie kaburi, na kutoka kwenye maisha yao yote ya shida wakati wa Muhammad Mustafa (s.a.w.), ghafla waliruka kwenye nafasi za juu katika wakati wa Abu Bakr.

Abu Bakr na Umar walidhihirisha mabadiliko yenye nguvu sana ya mwelekeo kwa Bani Umayya katika kipindi chao chote cha utawala wao. Wamefanya hivyo labda kwa ajili ya kuhakikisha mamlaka ya kikundi na umoja. Abu Bakr, inaonekana, alivutiwa sana na Abu Sufyan na wanawe. M. Shibli, yule mwanahistoria, amesimulia tukio lifuatalo katika kitabu chake Life of the Prophet, hivi:

Machoni kwa Muhammad, tajiri na masikini, bwana na mtumwa, mweupe na mweusi, walikuwa wote ni sawa. Salman, Shuaib na Bilal, wote watatu waliwahi kuwa watumwa wakati fulani lakini machoni pake, hawakuwa kwa namna yoyote ile duni kwa wakuu wa Quraishi.

Siku moja Salman na Bilal walikuwa wakienda mahali wakati walipokutana na Abu Sufyan na Abu Bakr. Salman au Bilal (mmoja kati yao) akasema: "Kwa nini ncha ya upan-ga haikuiona shingo ya huyu adui wa Allah bado?"

Abu Bakr alishituka sana kusikia kauli hii, na akasema: "Unathubutuje kutumia lugha kama hiyo kwa bwana wa Maquraishi?" Kisha yeye mara moja akaenda kumuona Mtume na akamlalamikia kuhusu kile alichokuwa amekisikia. Lakini Mtume akasema: "Nategemea kwamba hukuwakasirisha Salman na Bilal. Kama umewakasirisha, basi umemkasirisha Allah."

409

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abu Bakr alirudi kwa Salman na Bilal, na akawauliza: "Je, mmenikasirikia?" Wao wakasema: "Hapana, Allah (s.w.t.) Akusamehe."

(Life of the Prophet, Juz. 11; Azamgarh, India, 1974)

Dr. Hamid-ud-Din:

"Muhammad alipofariki, Abu Bakr akawa khalifa. Abu Bakr alikuwa akiielewa sana ile hadhi ya juu ya Bani Umayya, na alikuwa akiizingatia sana heshima na sifa yao. Alimteua Yazid, mtoto wa Abu Sufyan, kuwa jenerali wa jeshi. Kwa wakati huu, Bani Umayya walifanya matendo makubwa sana kwa ajili ya Uislamu mpaka watu wakasahau uhasama wao wa zamani kwa Uislamu. Wakati Damascus iliposhindwa, Umar bin al-Khattab (ambaye alimrithi Abu Bakr kama khalifa) alimteua Yazid bin Abu Sufyan gavana wake. Wakati Yazid alipokufa, yeye (Umar) alimteua Mu'awiyah (mdogo wake Yazid), kama gavana mpya wa Damascus."

(History of Islam, Lahore, Pakistan, 1971)

Katika tathimi hii, mwanahistoria huyu amechomeka maelezo yake binafsi kabisa. Ni matendo gani makubwa waliyoyafanya Bani Umayya "kwa ajili ya Uislamu" wakati wa ukhalifa wa Abu Bakr au hata wa Umar? Hao Bani Umayya walifanya matendo makubwa, yaani, waliteka nchi mpya, lakini baadae sana, na sio kwa ajili ya Uislamu bali kwa ajili yao wenyewe. Na wakuwa ni watu gani hao ambao walisahau uhasama wa zamani wa Bani Umayya kwa Uislamu? Watu waliokuwa wa kwanza kusahau uhasama wa Bani Umayya kwa Uislamu hawakuwa ni wengine zaidi kuliko Abu Bakr na Umar wenyewe!

Ushirikiano wa Abu Bakr na Umar pamoja na familia ya Abu Sufyan na familia ya Umayya dhidi ya familia ya Muhammad na Bani Hashim ulikuwa ni wa kudumu na usiovunjika. Kama warithi wa kiroho na "zana" za sera za Abu Bakr na Umar, hawa Bani Umayya walitumikia kipindi cha "kujifunza" ambacho mwisho wake walikuwa tayari kudai na kupokea zawadi yao. Zawadi yao ilikuwa ni ile serikali ya Saqifah yenyewe!

Hii ndio Hadith ya kupanda kwa Bani Umayya kwenye madaraka. Ilikuwa ni katika namna hii ambayo kwa maneno ya Gibbon, "mabingwa wa uabudu masanamu wakawa ndio vion-gozi wakuu wa dini na himaya yake (Muhammad)," - moja ya mguso kamili wa kihisto-ria wa kejeli.

Kuugua na kufa kwa Abu Bakr

Mnamo mwaka wa 13 A.H. (A.D.634) Abu Bakr alishikwa na maradhi, na alipohisi kwam-ba atakufa, alijishauri juu ya kuteua mrithi wake mwenyewe. Akamwita mwandishi wake, Uthman bin Affan, kuandika wosia wake. Pale Uthman alipofika, alikaa juu ya kitanda chake, na akaanza kumtolea imla kama ifuatavyo:

410

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehma na Mwenye kurehemu. Mimi, Abu Bakr, mrithi wa Mtume wa Allah..."

Abu Bakr alikuwa amefikia kiasi hiki tu pale alipopatwa na kipindi cha kuzimia na akapoteza fahamu. Alipokuwa bado amezimia, Uthman, mwandishi wake, yeye mwenyewe akaongeza maneno haya:

"Namteua Umar kama mrithi wangu na mtawala wenu."

Pale Abu Bakr alipopata fahamu, alimtaka Uthman amsomee kile alichokuwa amek-wishaandika, naye akasoma:

"Mimi, Abu Bakr, mrithi wa Mtume wa Allah, namteua Umar kama mrithi wangu na mtawala wenu."

Abu Bakr alipoyasikia haya, alimfurahia sana Uthman. Akampa baraka zake, na kisha akaendelea na imla yake iliyokuwa imebakia.

(Tabari - Taarikh, Juz.4, uk. 52)

Uthman hakuwa na njia ya kujua kama Abu Bakr atapata fahamu tena na kukamilisha imla ya wasia wake. Kwa upande wake yeye Uthman alikuwa tayari ameghushi hati, na yeye pamoja na baadhi ya wengine walikuwa wailazimishe juu ya umma - umma wa Muhammad - kama wosia na hati ya wasia wake huo wa mwisho!

Ingawa Abu Bakr alikuwa na vipindi vingi vya kuzimia wakati alipokuwa akitoa imla ya wasia wake, Umar hakukemea kwamba yeye (Abu Bakr) alikuwa anaweweseka na alikuwa akiropoka. Alikuwa ni Umar yule yule ambaye alikataa kumruhusu Mtume (s.a.w.) kutoa imla ya wosia wake ingawa yeye Mtume hakuzimia, na hakupoteza fahamu wakati wowote.

Umar aliushika wasia wa Abu Bakr mkononi mwake, na akapita akizunguka kuwataka watu kutii kile khalifa wa Mtume alichokuwa ameandika ndani yake.

Kuchaguliwa kwa Abu Bakr na demokrasia

Wanahistoria wengi wanadai kwamba kuchaguliwa kwa Abu Bakr kulisimamiwa na kanuni za kidemokrasia. Lakini madai kama hayo hayawezi kupatikana kwa misingi ifu-atayo:

1. Wakati Muhammad Mustafa (s.a.w.) alipofariki, wengi wa Waarabu walikuwa wamekwisha silimu. Kwa mujibu wa kanuni za demokrasia, wote walipaswa kushiriki katika uchaguzi wa kiongozi wao. Lakini kama haikuwezekana

411

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kufanya hivyo, basi wakuu wa makabila yote walipaswa kutakiwa ushauri juu ya jambo hilo. Lakini kama hili nalo lingekuwa haliwezekani, basi mrithi wa Mtume angechaguliwa ndani ya Msikiti wake, katika mkusanyiko wa Muhajirina na Ansari wote waliokuwepo hapo Madina. Hili, kwa hakika kabisa, lilikuwa linawezekana.

Lakini hakuna hata moja kati ya njia hizi iliyotwaliwa. Kilichotokea hasa ni kwamba baadhi ya watu wa yale makabila mawili ya Ansari, yaani, Aus na Khazraj, walikusanyika ndani ya Saqifah kumchagua kiongozi wao wenyewe. Wapelelezi wa Abu Bakr na Umar waliwajulisha wao kuhusu huo mkutano wa Ansari, na wakaenda waukikimbia. Wakiwa njiani humo wakamchukua Abu Ubaida bin Jarrah pamoja nao.

2.  Abu Bakr na Umar wanapigiwa debe kama mabingwa wakubwa wa demokrasia. Kama wangekuwa, walipaswa kuwaambia wale Ansari kuvunja ule mkutano wao mle Saqifah, na kisha kukusanyika upya ndani ya ule Msikiti Mkuu kuchagua kiongozi mbele ya Muhajirina na Ansari wote. Lakini hawakufanya hivyo.

Abu Bakr na Umar, katika hotuba zao mle Saqifah, walitambua utumishi wa Ansari kwa Uislamu, lakini wakaongeza: "Serikali ambayo mna shauku ya kuitwaa, iliundwa na Muhammad (s.a.w.). Sasa kwa vile amefariki, inapaswa iwe mikononi mwa warithi wake, na sio kwenu ninyi. Sisi ndio warithi wake. Sisi ni Maquraishi sawa na alivyokuwa yeye."

Katika demokrasia, sheria ya msingi ni kwamba mgombea wa nafasi anaingia kwenye uchaguzi kwa uzito wa sifa zake binafsi. Ni lazima awe na sifa na uwezo, uzoefu na uadilifu n.k. Yeye hadai kwamba anagombea nafasi na ana-paswa kuchaguliwa kwa sababu anahusiana na kiongozi wa zamani wa dola. Na bado Abu Bakr aliwaambia wale Ansari kwamba alikuwa na haki zaidi kwenye uongozi kuliko wao waliyokuwa nayo kwa sababu alikuwa karibu sana na Mtume (s.a.w.) kuliko walivyokuwa wao.

3. Katika suala la kumteua Umar kama mrithi wake, Abu Bakr hakujifanya kutekeleza kile kichekesho cha uchaguzi, alizidisha na bila kufuata msingi maalum akamtangaza Umar kama khalifa anayefuata.

Waislamu wa Sunni wanadai kwamba Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) hakuteua mrithi wake mwenyewe, na aliacha (uamuzi wa) kurithiwa kwake juu ya umma. Lakini Abu Bakr alichagua mrithi wake mwenyewe, na kwa kufanya hivyo, aliikiuka sunnah ya Mtume (s.a.w.). Kama ilikuwa ni sunnah

412

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ya Mtume (s.a.w.) kutoteua mrithi wake mwenyewe, basi Abu Bakr alipuuza kwa kuteua mrithi wake mwenyewe. Alipuuza pia, wakati huo huo, desturi ya demokrasia.

Abu Bakr hakuwa peke yake katika kuikana demokrasia kwa matendo yake. Yule mtu ambaye anahusika sana na kuchaguliwa kwake (huyo Abubakr), yaani Umar, mwenyewe aliikataa. Aliwaonya Waislamu wasije wakajaribu kutafuta kiongozi kupitia uchaguzi tena, na akasema kwamba Allah (s.w.t.) aliwaokoa wao kutokana na athari za madhara makubwa za mtindo wa namna hii wa kutafuta kiongozi katika suala la Abu Bakr.

Abu Bakr alifariki mnamo Agosti ya mwaka 634, na alizikwa kando ya Mtume wa Uislamu (s.a.w.w) katika kaburi lake.

413

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Demokrasia na Waislamu

Waislamu wa kisasa wanaamini na kudai kwamba serikali katika Uislamu ni ya kidemokrasia katika mwenendo. Serikali inayoendeshwa na Waislamu inaweza kuwa ya kidemokrasia katika mwenendo lakini serikali ya Kiislam sio ya kidemokrasia.

Hadi mwisho wa Vita vya Dunia vya Kwanza, Waislamu waliishi kila mahali chini ya utawala wa wafalme na masultani. Waliwaita wafalme na masultani wao Dhwillullah (kivuli cha Allah), na walifurahia sana kuishi kwenye kivuli hicho (kana kwamba Allah ana kivuli), ijapokuwa, ukiondoa wachache tu, wafalme na masultani hao walikuwa ndio mad-halimu wakubwa, madikteta na wenye mabavu wabaya zaidi wa watawala. Walitumia madaraka kamili juu ya wananchi wao, na waliweza kumuua yoyote yule aliyewakasirisha.

Baada ya Vita vya Kwanza vya Dunia, madaraka ya wafalme na masultani yalianza kufi-fia. Katika utambuzi unaobadilika wa karne ya ishirini, wafalme na masultani hao wakawa "wa kizamani," na Waislamu wakafanya ugunduzi kwamba demokrasia ilikuwa ni ya Kiislam. Wakaanza kuimba sifa za demokrasia, na wengi wao wakawa "wafuasi" wake. "Kubadilika" kwao kuingia kwenye demokrasia kuna maana kwamba katika zile karne kumi na nne za historia yake, Uislamu ulikuwa "sio wa kidemokrasia," na ni muda tu baada ya 1919 tangu pale ulipokuwa "wa kidemokrasia."

Wale Waislamu wanaodai kwamba demokrasia ni Uislamu, wanasema kwamba, baada ya kifo cha Mtume wa Allah (s.w.t.) maswahaba zake walianzisha ile al-Khilafat ar-Rashida (Ukhalifa ulioongoka), na ulikuwa ndio mfano bora wa serikali ya kidemokrasia.

Al-Khalifat ar-Rashida ilidumu kwa miaka thelathini tu. Baada ya ile miaka thelathini, ile demokrasia ya Kiislam ilibadiliwa na ufalme wa kidikteta. Ule mfumo wa serikali ulioit-wa "demokrasia ya Kiislam" ulikomea hapo. Demokrasia ya Kiislam ikadhihirika kuwa ni bidhaa inayoharibika haraka sana. Ilidumu, takriban, chini ya miaka thelathini - wala sio hata kwa kizazi kizima!

Demokrasia ya Kiislam ilikufa bila kudaiwa (kimyakimya), bila kuombolezwa na bila kuimbwa. Ni nani aliyeiuwa? Je, ni wapagani? Ni waabudu masanamu? Wanafiki? Wachawi? Wayahudi? Au Wakristo? Hapana. Ni Waislamu wenyewe ndio walioiuwa. Na walikuwa ni Waislamu gani hao walioiuwa demokrasia ya Kiislam? Hawakuwa wale Waislamu wa karne za baadae. Walitokana wote na kizazi (generation) cha wakati wa Muhammad Mustafa (s.a.w.) mwenyewe, na wote walikuwa ni "maswahaba" zake. Kama programu ya Uislamu inaingiza uanzishwaji wa demokrasia kama muundo mzuri wa serikali kwa ajili ya Waislamu, basi itakuwa hali gani kwa wale wahujumu walioiharibu katika utoto wake? Demokrasia ya Kiislam ilianzishwa na maswahaba wa Mtume (s.a.w.)

414

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

lakini wale watu waliyoiharibu, walikuwa pia ni maswahaba zake. Wakati kundi moja la maswahaba, likiongozwa na Abu Bakr na Umar, lilianzisha desturi ya demokrasia ya Kiislam (kama inavyodaiwa na Waislamu wa Sunni), kundi jingine la maswahaba, likiongozwa na Mu'awiyah ibn Abu Sufyan na Amr bin Al-Aas, liliivunja. Kundi la tatu la maswahaba, likiongozwa na Abdullah ibn Umar bin al-Khattab na Abu Hurayra, lilishuhu-dia mapambano kati ya demokrasia ya Kiislam na wachimbia kaburi (walioiua) wake. Walikuwa watazamaji wakimya wa mapambano ya kifo cha demokrasia ya Kiislam. Pale kulipokuwa hakuna shaka iliyobaki kwamba Mu'awiyah ndiye "mshindi," wao, wakiwa wameyaona mambo kama yalivyokuwa na wayakinifu, walitangaza kwamba walikuwa pamoja naye - pamoja na Mu'awiyah - muangamizaji wa demokrasia ya Kiislam!

Faris Glubb:

"Serikali ya Kiislam ilikuwa imebomolewa kabisa katika sehemu kuu ya Ulimwengu wa Kiislam kwa kutwaliwa kwa madaraka na Mu'awiyah mwaka wa 40 Hijiria. Mu'awiyah alivunja Ufalme wa Allah ulioanzishwa na Mtume na akaubadilisha na ufalme wa kidunia. Alibadili ukhalifa wa haki na wa kidemokrasia kwa ufalme wa kidhalimu wa kurithiana..

(Makala yenye kichwa cha habari "The islamic Ideal of Ethical Government, " iliyochapishwa kwenye Muslim News International, London, Machi 1963)

Abu Bakr, Umar, Mu'awiyah, Amr bin Al-Aas, Abdullah bin Umar bin al-Khattab, na Abu Hurayra, wote walikuwa maswahaba wa Mtume wa Uislamu. Abu Bakr na Umar walianzisha demokrasia ya Kiislam; na Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas wakaivunja. Je, ina maana kwamba wajenzi na wavunjaji - makundi yote - yako sawa, na demokrasia na ufalme wa kidikteta vyote ni vya "Kiislam?"

Tunaweza kisimamisha hukumu, kwa muda huu, juu ya demokrasia ya "Kiislam" lakini mafaqihi na wanazuoni wa Sunni wa wakati huu hawako tayari kuongeza kwamba heshi-ma ufalme kama pia kuwa ni "Kiislam." Kulingana na wao, hakuna kitu kama ufalme wa Kiislam. Wanakubaliana kwa pamoja katika kuutangaza ufalme kuwa "sio Kiislam."

G.H. Jansen:

"Hali halisi ya kisiasa ya dola ya Kiislam au taratibu kwa kawaida ni ya manufaa makubwa. Alipojishughulisha na kazi ya utendaji ya kuandaa katiba mpya kwa ajili y a Pakistani ambay o ' itakuwa katika ulingano na mafundisho na historia y a Uislamu,' (Rais) Ayub Khan aliwataka wataalam wake kuchunguza historia ya Kiislam na katiba za nchi nyingine za Kiislam. Mambo mawili yalijitokeza wazi kutoka kwenye uchunguzi huu: Hapakuwa na nafasi ya ufalme katika Uislamu, na urithi hauwezi kuwa katika msingi wa kurithiana kiukoo. Umma wote kwa jumla lazima uwe na haki ya kuchagua kiongozi wao na haki ya kumuondoa. (Hii ina maana kwamba falme zote

415

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

za Kiislam, na kujisingizia kwao kwa kidini, zilikuwa sio za Kiislam kabisa). Katika misingi hii miwili kwa kweli yapo makubaliano miongoni mwa waboreshaji wetu wa kisiasa, lakini katika kila hali nyingine ya sera ya Kiislam zipo tofauti za maana na za msisitizo.

(Militant Islam, New York)

Ikhwaan al-Muslimiin (Udugu wa Kiislam) wa Misri, imezishutumu tawala zote za kijeshi (udikteta) vile vile kama sio za Kiislam.

G.H. Jansen:

"Hawa Ikhwaan al-Muslimin wametilia mkazo kwamba hakuna serikali iliyoanzish-wa kwa nguvu inayoweza kukubalika, kwa sababu mashauriano (shura'a) ni lazima kulingana na Sura ya 42 Aya ya 35 ya Qur'an. Kwa hiyo tawala za kijeshi zilizotokana na mapinduzi sio za Kiislam."

(Militant Islam, New York)

Ni makubaliano kwa hiyo, ya wanazuoni wa Sunni wa Pakistani na wasemaji wa Sunni wa Ikhwaan al-Muslimin wa Misri, kwamba ufalme na tawala za kijeshi zote sio za Kiislam.

Lakini ni makubaliano ya siku za baadaye. Mafaqihi na wanazuoni wa Sunni wa nyakati za zamani wasingeidhinisha wazo hili. Makubaliano yao yalikuwa tofauti kabisa na haya. Walitetea uwezo wa juu kabisa wa ukatili, kama ilivyoonyeshwa kabla.

Na hivi huu msemo "sio Kiislam" sio tasifida (neno la staha badala ya lenyewe) ya "upa-gani"? kama ndivyo, na ikiwa kwa mujibu wa mafaqihi wa Sunni wa Pakistani, ufalme ni taasisi ya kipagani, basi ni nini fatwa yao juu ya hao wafalme wenyewe. Wanaweza wafalme kuendesha serikali isiyo ya Kiislam, na bado wakawa ni Waislamu wa kweli? Na ni ipi fatwa yao juu ya yule mtu ambaye kwanza alijitwalia ile Khilafa ar-Rashida katika mapinduzi, na kisha akaibadilisha na kuwa ufalme, yaani, Mu'awiyah bin Abu Sufyan? Alikuwa akijigamba mara kwa mara kwamba yeye alikuwa ndiye wa kwanza wa wafalme wa Waarabu.

Maoni ya mafaqihi wa Sunni wa Pakistani na yale maoni ya Ikhwaan al-Muslimin kule Misri juu ya mwenendo wa ufalme na tawala za kijeshi, yanafanana na ya Muhammad Asad, mwanachuoni wa kisasa, wa Sunni wa Ulaya. Anaandika katika kitabu chake, State and Government in Islam (1980):

".. Na tuwe wazi katika akili zetu juu ya jambo moja angalau: haijakuwepo

kamwe dola ya kweli ya Kiislam baada ya wakati wa Mtume na ukhalifa wa Madina ulioongozwa na warithi wa mara tu wa Mtume, wale Khulafau Rashidiin wanne, Abu

416

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Bakr, Umar, Uthman na Ali."

Kwa mujibu wa maamuzi hayo yaliyopita, Dola ya Kiislam ilikoma kuwa ya Kiislam mara tu Mu'awiyah alipoitwaa.

Lakini Mu'awiyah alifika mbali zaidi ya kuibadilisha ile Khilafa ar-Rashida kuwa isiyo ya Kiislam, yaani, ufalme wa kipagani. Aliupitisha ufalme kama "urithi" wake kwa umma wa Waislamu. Umma wa Waislamu kwa hiyo, umetawaliwa kwa karne zote hizi, na wafalme, na unatawaliwa na wao hata leo hii katika miaka ya 1990 - katika nchi kama Saudi Arabia, Jordan na Morocco.

Lakini, hata hivyo, Mu'awiyah huyu huyu, kwa Waislamu wa Sunni, bado ni "sahaba na mwandishi" wa Mtume (s.a.w.), na, ooh! ndio, "Mwenyezi Mungu amuwiye radhi" (kwa kubadili ukhalifa wa Kiislam kuwa ufalme wa kipagani).

Labda ni zoezi la kuvutia kuwaza kama wanazuoni wa Sunni wanaweza kuyaona makosa katika hoja zao wenyewe, na hitilafu za wazi katika makubaliano yao wenyewe. Kama wanaweza, basi itapendeza kuona jinsi watakavyozirazinisha (kuzitazama kimamtiki)

Waislamu wengi wanaangalia nyuma kwa shauku sana kwenye zama zile za miaka the-lathini ya ile Khulafa ur-Rashidun (makhalifa walioongoka) kama "zama za ustawi" za Uislamu. Kwa kweli, hazikuwa za ustawi hivyo kama wanavyoziona wao, au, vizuri zaidi, zilikuwa za ustawi kwa wale Waislamu ambao walilimbikiza viwango vikubwa vya dha-habu juu yao katika ile miaka ya "ustawi".

Walikuwapo wanne tu wa hawa makhalifa "waongofu". Watatu kati yao walikutana na vifo vya kikatili, wawili katikati ya vita vya wenyewe kwa wenyewe. Mmoja wao, yaani, Abu Bakr, ambaye hakuuawa, na ambaye alikufa kifo cha kawaida, alikuwa khalifa kwa miaka miwili tu.

G.H. Jansen:

"Hata hivyo chanzo kingine cha mfano wa kisheria ni zile sunna za Khalifa al-Rashidun, wale 'makhalifa waongofu,' wale watawala wanne waliomfuatia Muhammad. Walikuwa ni Abu Bakr, Umar, Uthman na Ali, na vipindi vyao vinne vilidumu kuanzia 632 hadi 661 A.D. Huu muda mfupi wa miaka ishirini na tisa unazingatiwa, kupitia kwenye ukungu unaovunga kwa makusudi, wa wakati, kama 'zama za ustawi' wa Uislamu. Kwa nini zifikiriwe hivyo kunajadilika, kwani ufupi wake ulikuwa kwa sababu ya hao makhalifa wanne, wawili waliuawa na mmoja alikatwa na maadui zake, nyumbani kwake, wakati alipokuwa anasoma Qur'an. Migawanyiko yote ambayo ilikera Uislamu na ulimwengu wa Kiarabu tangu hapo, ilizaliwa wakati wa zile zama za 'ustawi'.

417

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Zilikuwa kwa hakika ni zama za kupendeza, kipindi ambapo Waislamu Waarabu waliteka sehemu yote kubwa inayopanuka kuanzia Tripolitania upande wa Magharibi mpaka kwenye mipaka ya India upande wa Mashariki. Kwa hiyo, zile 'sunnah' za kile hawa watawala wanne adhimu lakini wenye mikosi walichokisema na kukifanya zil-iongezwa kwenye mkusanyiko unaokua wa sheria za Kiislam.

(Militant Islam, New York)

Wanahistoria wawili wa kisasa wa Pakistani, Profesa Sayyed Abdul Qadir na Profesa Muhammad Shuja-ud-Diin, wamemnukuu Abul Kalam Azad katika kitabu chao, History of Islam (Lahore, Pakistan) katika mlango wenye kichwa "The Meaning of Khilafat" -Maana ya Ukhilafat - kama ifuatavyo:

"Inapaswa kuwepo serikali kwa ajili ya uongozi, ustawi na furaha ya mwanadamu ambayo itauokoa ulimwengu kutoka kwenye ukatili, udhalimu ukandamizwaji na unyonyaji; na ambayo itarudisha amani na usalama kwa wote ili iwezekane kutangaza Sheria ya Allah (s.w.t.) juu ya ardhi hii, kwa sababu hiyo kuigeuza iwe pepo."

Ilikuwepo serikali kama hiyo - ile iliyoanzishwa na Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) (rehema na amani juu yake na kizazi chake), pale Madina - ambayo ilikuwa inaigeuza dunia hii kuwa pepo kwa kutangaza Sheria ya Allah (s.w.t.) juu yake. Lakini muda wa serikali hiyo ulikatishwa na kifo chake (s.a.w.). Baada ya kifo chake, watu wapya walitwaa mamlaka ya serikali yake. Lakini malengo yao, sera na programu zao hazikuwa ni sawa na zake, na wao, kwa hiyo, walibadili mwenendo wa serikali yake.

Serikali ya Muhammad (s.a.w.) ilikuwa ndio Ufalme wa Mbinguni juu ya Ardhi, lakini baada ya kifo chake, iligeuka kuwa serikali ya "Ki-Aristotle".

418

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Umar bin al-Khattab, Khalifa wa Pili wa Waislamu

Katika Nyakati za Ujahilia, Umar aliishi kama dalali. Shibli, mwandishi wa wasifa wake, anasema kwamba katika ujana wake alichunga ngamia.

Kabla ya kusilimu, Umar alikuwa mmoja kati ya maadui wenye msimamo mkali sana, wa Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.)

Pale Muhammad (s.a.w.) alipotangaza ujumbe wake, watu wengi walimkubali yeye kama ni Mtume wa Allah (s.w.t.) Umar alimtambua kama Mtume wa Allah (s.w.t.) baada ya miaka sita.

Wanahistoria wengine wanadai kwamba Umar alikuwa mtu wa kutisha sana, na aliposil-imu, wale waabudu masanamu walishikwa na hofu juu ya maisha yao. Lakini hili ni suala la uongo unaojitokeza unaopingana na ukweli unaotisha. Wakati Umar aliposilimu, waabudu masanamu walibakia pale walipokuwa, na hakuna kilichobadilika kwao; lakini alikuwa ni Muhammad aliyelazimika kuondoka nyumbani kwake, na ikambidi atafute hifadhi katika korongo linalohuzunisha. Aliishi kwa miaka mitatu katika korongo hilo, na katika miaka hiyo mitatu ya uhamishoni, maisha yake yalikuwa kwenye hatari mbaya sana kila mchana na kila usiku. Katika kipindi chote hiki cha siku zaidi ya 1000, Umar, kama Waislamu wengine wengi hapo Makka, alikuwa ni mtazamaji mkimya wa mateso ya bwana wake. Hakufanya jaribio lolote la kumaliza mateso hayo.

Muhammad Mustafa (s.a.w.) alianzisha udugu kati ya Waislamu, kote - hapo Makka na kule Madina. Hapo Makka, alimfanye Umar kuwa "ndugu" wa Abu Bakr, na kule Madina, alimfanya yeye kuwa "ndugu" wa Utban bin Malik. Kwa kuwa ndugu yake yeye mwenyewe, Muhammad alimchagua Ali ibn Abi Talib katika miji yote miwili.

Katika mwaka wa 3 A.H., binti yake Umar, Hafsa, aliolewa na Mtume (s.a.w.).

Umar alikuwa ni mmoja wa watoro wa vita vya Uhud (Baladhuri). Yeye mwenyewe alisema baadaye kuwa: "Pale Waislamu waliposhindwa kule Uhud, nilikimbia kuelekea mlimani."

(Suyuti katika al-Durr al-Manthur).

Katika kuizingira Khaybar, Umar alifanya jaribio la kuiteka ile ngome lakini alishindwa. Umar alikuwa mmoja wa watoro wa vita vya Hunain. Abu Qatada, sahaba wa Mtume (s.a.w.) anasema: "Huko Hunain wakati Waislamu walipokuwa wakikimbia, nami pia nilikimbia, na nilimuona Umar pamoja na wengine." (Bukhari na Kitabul-Maghazi).

419

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Katika mwaka wa 8 A.H. Mtume (s.a.w.) alimtuma Umar kama mpiganaji wa kawaida pamoja na wengineo kwenda kupiga ripoti kikazi kwa Amr bin Al-Aas, kamanda wao, katika vita vya Dhat es-Salasil.

Mnamo mwaka wa 11 A.H. Mtume wa Allah (s.w.t.) alitayarisha ule msafara wa Syria na akamteua Usamah bin Zayd bin Haritha kama kamanda mkuu wake. Alimuamuru Umar kutumikia kama mpiganaji wa kawaida kwenye msafara huo.

Ingawa Umar aliishi miaka kumi na nane akiwa pamoja na Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah (s.w.t.) yeye Mtume (s.a.w.) hakuwahi kumchagua kwenye nafasi yoyote ya mamlaka - ya kiraia au kijeshi.

Wakati Mtume wa Allah (s.w.t.) alipokuwa kwenye kitanda chake cha mauti, aliwataka maswahaba wamletee kalamu, karatasi na wino ili aweze kutamka wasia wake lakini Umar alimpuuza. Hakumuacha Mtume (s.a.w.) atamke wasia na mirathi yake.

Umar hakuwepo kwenye mazishi ya Mtume wa Uislamu. Alikuwa akizozana na Ansari katika banda la Saqifah wakati mwili wa Mtume (s.a.w.) ulipokuwa unazikwa. Umar alikuwa ndio mtengeneza ukhalifa wa Abu Bakr. Katika ukhalifa wa Abu Bakr, Umar alikuwa ndiye mshauri wake mkuu.

Bani Umayya walikuwa ndio mabingwa wa jadi wa uabudu masanamu na maadui wakub-wa wa Muhammad na ukoo wake, Bani Hashim. Muhammad (s.a.w.) alikuwa ameyavun-ja madaraka yao lakini Umar akayafufua. Sehemu kuu ya sera zake, kama mkuu wa serikali ya Saqifah, ilikuwa ni kuwarejesha Bani Umayya. Aliitoa Syria kwao kama "ada" yao (anayolipa mtu kwa kupewa himaya), na akawafanya wao kuwa ukoo wa kwanza katika himaya hiyo.

Mwanafunzi wa kisasa wa historia anaweza kukuta madai yaliyofanywa kwa niaba ya maswahaba wa Mtume (s.a.w.) kama yaliyotiwa chuku na yenye kukanganya. Anaweza kugundua ndani yake mgongano wa dhana zenye kupendwa, na ukweli wa kihistoria. Lakini kama atapenda kufanya tathimi ya hali halisi ya tabia walizofanya katika uhai wa Mtume (s.a.w.), hakuna njia bora ya kufanya hivyo mbali na kuyapa kisogo maneno ya kuonyesha nderemo na balagha, na kuweka mazingatio kwenye ukweli na ukweli pekee.

Matukio makuu ya ukhalifa wa Umar

Wakati Umar alipochukua madaraka ya ukhalifa, majeshi ya Waislamu yalikuwa yanapi-gana dhidi ya Wafursi huko Iraq na Warumi huko Syria. Jeshi lililokuwa Syria lilikuwa chini ya uongozi wa Khalid bin al-Walid, yule jenerali kipenzi cha Abu Bakr. Kitendo cha kwanza cha Umar kama khalifa kilikuwa ni kumfukuza kwenye ukuu wake wote, na kum-

420

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

teua Abu Ubaidah bin al-Jarrah kama kamanda mkuu wa majeshi ya Waislamu yaliyokuwa Syria.

Shibli anasema kwamba Umar alikuwa, kwa muda mrefu, na chuki ya siri juu ya Khalid kwa sababu ya maovu yake mabaya kupindukia. Umar kweli alimfukuza Khalid kwa sababu ya maovu yake mabaya mno lakini inaonekana kwamba chuki binafsi pia ilikuwa ikifanya kazi. Alikuwa na wivu juu ya umaarufu na kupendwa kwa Khalid. Kama alichukia kuvuka mipaka kwa Khalid, alipaswa kumshitaki rasmi, na angeagiza uchunguzi kamili wa uhalifu wake katika kumuua Malik ibn Nuweira na katika kumtwaa bila haki mjane wake. Kama Khalid angethibitika kuwa na hatia, basi Umar angepaswa kutoa hukumu juu yake kwa mujibu wa sheria ya Kiislam. Lakini hakukuwa na mashitaka wala uchunguzi. Khalid alifukuzwa papo hapo na alikufa katika umasikini na mashaka mnamo mwaka 21A.H.

Ukhalifa wa Umar ni mashuhuri sana kwa utekaji wake mwingi. Majenerali wake walite-ka Iraq, Iran, Azerbaijan, Kirman, Seistan, Khurasan, Syria, Jordan, Palestina na Misri, na akaziunganisha zote na kwenye himaya ya Waislamu. Wote huu ulikuwa ni ushindi wa kudumu. Warumi waliipoteza Syria, Palestina na Misri daima; na huko Uajemi, ule ufalme wa Sassani ukakoma kuwepo.

Miongoni mwa matukio mengine ya ukhalifa wa Umar, lilikuwemo lile la kuzuka kwa tauni huko Syria mnamo mwaka 18 A.H., na njaa huko Hijazi katika mwaka huo huo. Kati ya hayo, ile tauni na njaa viliua zaidi ya watu 25,000 (Suyuti na Abul Fida).

Uongozi wa kiraia na kijeshi na sera

Kwa vile himaya ilikwisha kuwa kubwa kwa pande zote, Umar alilazimika kuanzisha mfumo wa uongozi. Lakini Waarabu walikuwa hawana uzoefu wowote wa uongozi. Umar, kwa hiyo, aliuacha ule muundo wa uongozi wa Kifursi na Kirumi katika majimbo yaliy-otekwa bila kuugusa. Watumishi wa Kifursi na Kirumi walizifanya zile kazi za siku hadi siku kama mwanzoni.

Umar alianzisha kambi za makazi ya wanajeshi nyingi huko Iraq, Syria na Misri. Kwa vile aliwataka Waarabu kuwa tabaka halisi la wapiganaji na watawala, hakuwaruhusu kununua ardhi na kufanya makazi au kuwa wakulima katika zile nchi zilizotekwa.

Kukadiria mapato ya ardhi, Umar tena ilibidi aiachie ile mifumo ya Wafursi na Warumi. Lakini huko Iraq ilionekana ni muhimu kukagua ardhi inayolimika na kukadiria kodi zake. Waarabu hawakujua chochote kabisa juu ya ukadiriaji wa mapato ya ardhi. Kulikuwepo hata hivyo, na upekee mmoja kwa Uthman bin Hunaif wa Madina, Alikuwa ni mtu mwenye uwezo mkubwa kama mtaalam wa mapato. Ingawa ilikuwa ni sera ya Umar kutowaajiri wenyeji wa Madina (Ansari) kwenye nafasi zozote muhimu, katika suala hili

421

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hasa hakuwa na ujanja, na alimteua Uthman bin Hunaif kama kamishna wa maendeleo ya ardhi huko Iraq. Qadhi Yusuf anasema kwamba Uthman bin Hunaif alikuwa ni bingwa katika Arabia yote katika utozaji kodi, ukadiriaji wa mapato ya ardhi na urutubishaji wa ardhi (Kitabul-Kharaj na Siyar-ul-Ansar).

Muda chini ya mwaka mmoja, Uthman bin Hunaif alikuwa amemaliza kazi ya kuchukua vipimo vya jimbo lote jipya, na ya kufanya makadirio kwa ajili ya ukusanyaji wa mapato ya ardhi. Kwa hiyo alikuwa kamishna wa fedha wa kwanza wa Iraqi, na hivi, mmoja wa Ansari wachache wa kushika nafasi yoyote ya mamlaka katika ukhalifa wa Abu Bakr na wa Umar na Uthman bin Affan.

Walato Syria, Jordan na Palestina zilipotekwa, Umar alimteua Yazid bin Abu Sufyan kuwa gavana wa Syria; Shurahbil bin Hasan gavana wa Jordan, na Amr bin Al-As kuwa gavana wa Palestina. Abu Ubaidah bin al-Jarrah aliteuliwa kuwa gavana wa mji wa Damascus. Pale Amr bin Al-Aas alipoiteka Misri, Umar akamfanya yeye kuwa ndio gavana wake.

Yazid bin Abu Sufyan, gavana wa Syria, alikufa katika ile tauni ya mwaka wa 18 A.H. Wakati Umar aliposikia habari za kifo chake, alikwenda kumuona Abu Sufyan na kutoa rambirambi zake kwake. Lakini Abu Sufyan aliyakatisha masikitiko ya Umar, na aka-muuliza, "Ni nani utakeyemteua gavana wa Syria mahali pa marehemu mwanangu,Yazid?" Umar akasema: "Bila shaka, ni ndugu yake, Mu'awiyah." Abu Sufyan maramoja hiyo akasahau huzuni ya kifo cha mwanawe, na akafurahia kunyanyuliwa kwa Mu'awiyah, mwanae wa pili, kuwa gavana. Umar akamteua Mu'awiyah kuwa gavana mpya wa Syria. Wakati Abu Ubaidah alipokufa, Umar akaiweka Damascus pia chini ya mamlaka ya Mu'awiyah. Aliuweka mshahara wake katika vipande 60,000 vya dhahabu kwa mwaka (Ist 'ab, Juzuu ya I).

Baada ya kumfukuza Khalid bin al-Walid kama kamanda mkuu wa vile vikosi vilivyokuwa Syria, Umar alikuwa amemteua yeye, kwa muda, kuwa gavana wa wilaya ya Kinnisirin lakini akamfukuza tena kwa kudaiwa kwake kuwa na "majivuno."

Saad bin Abi Waqqas, yule mshindi wa vita vya Qadsiyyah vilivyopiganwa dhidi ya Wafursi, alikuwa ni gavana wa Umar wa Iraq. Naye pia alifukuzwa mnamo mwaka wa 21 A.H.

Amr bin Al-As alikuwa gavana wa Umar wa Misri. Umar hakumfukuza yeye lakini alipun-guza madaraka yake kwa kumteua Abdullah bin Saad bin Abi Sarah kama "mlinzi" juu yake katika masuala yake ya kihazina.

Umar alikuwa msimamizi mshurutishaji sana kwa majenerali wake na magavana wote. Alikuwa mwepesi wa kutega masikio yake kwenye malalamiko yoyote dhidi yao, na

422

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

alikuwa mwepesi zaidi wa kuwafukuza - isipokuwa mtu mmoja pekee - Mu'awiyah! Alikuwa daima ni mpole kwa watoto wa Abu Sufyan na ukoo wa Bani Umayya.

Mu'awiyah, mtoto wa Abu Sufyan na Hinda, gavana wa Syria, aliishi Damascus katika ufahari wa kifalme, akizungukwa na watu wanaovutia. Ulikuwa ni mtindo wa maisha ambao Umar hakuuvumilia kwa gavana mwingine yoyote. Lakini Mu'awiyah, kwake yeye, alikuwa "maalum," na sheria zilizotumika kwa wengine, hazikutumika kwake.

Tabari amesimulia tukio lifuatalo katika juzuu ya V1 ya Taarikh yake. Umar alikuwa Damascus na Mu'awiyah alikuwa akimtembelea kila siku - asubuhi na jioni - akiwa amepambwa na mavazi ya kifalme, pamoja na farasi waliotandikwa vizuri sana na walinzi. Wakati Umar alipozungumzia, kwa ukali kiasi, juu ya tamasha lake hilo, yeye alisema kwamba Syria ilikuwa imejaa wapelelezi wa Kirumi, na ilikuwa ni muhimu kuwafutia kwa ule "utukufu" wa Uislamu. Tamasha lake hilo, alisema, lilikuwa ni nembo ya nje tu ya utukufu huo - utukufu ule wa Uislamu.

Lakini Umar hakuridhika, na akasema: "Huu ni mtego uliowekwa na mtu mwenye hila na ujanja."

Mu'awiyah akajibu: "Basi nitafanya chochote utakachosema, Ewe Amiru'l-Mu'minin." Umar akasema: "Kama nikikataza kitu chochote, unanichanganya na kunikanganya na maneno. Ninakosa kujua la kufanya."

Hapa Umar anaweza kuonekana "asiye na uwezo" kabisa mbele ya mfuasi wake mwenyewe. Anaweza kumsamehe Mu'awiyah kitu chochote na kila kitu. Yeye, kwa kweli, alionekana akiwabembeleza Abu Sufyan na wanawe kwa kujishaua. Mara alipowaweka kwenye usukani wa mambo, waliimarisha nafasi yao, na ikawa haiwezekani kuwang'oa. Ilikuwa ni kwa namna hii kwamba Bani Umayya wapenda dunia, wanyang'anyi, mabeberu, na wanyonyaji kiuchumi walilazimishwa kwa nguvu juu ya Waislamu. Kulelewa kwa wema kwa Bani Umayya, inaonekana, kulikuwa ni moja ya kawaida katika usawazishaji wa sera wa Saqifah.

Tafakari kiasi juu ya ushindi wa Waarabu

Majenerali wa Umar walivamia Uajemi, Syria, na Misri. Warithi wake katika ufalme wa Bani Umayya waliusogeza ushindi huo mbali kiasi cha Ufaransa ya Kusini kwa upande wa Magharibi, na mipaka ya Magharibi ya China na bonde la Indus kwa upande wa Mashariki. Wanafunzi wa historia wameonyesha mshangao katika kasi na ukubwa wa uvamizi huo wa Waarabu katika karne za sita/saba. Waliupata ushindi wote huo ndani ya miaka 100 - kwa hakika ni moja ya mifululizo ya ushindi inayofahamika sana katika historia ya dunia.

423

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Karne nyingi baadae, msako unaendelea wa jibu la swali hili: Waarabu hawa walishindaje kiasi hiki na kwa haraka hivyo? Sababu nyingi zimetolewa na wanahistoria juu ya mafanikio ya vikosi vya Waarabu, miongoni mwao: vita vya wenyewe kwa wenyewe na vurugu huko Uajemi, vita kati ya Uajemi na Roma ambavyo vilichukua miaka 26, na ambavyo viliziacha himaya zote mbili zikiwa zimechakaa kabisa, kupindukia na kuangu-ka; kutoridhika kwa raia wa Roma huko Syria na Misri ambao waliwakaribisha hao Waarabu kama wakombozi, na hasara kwa Roma ya "himaya" ya kutoungwa mkono nyumbani; utegemezi wa wote Waajemi na Warumi juu ya mamluki na askari wa kuandik-ishwa waliokosa hamasa; mateso kwa misingi ya dini ya vikundi vinavyopingana, na kanuni za imani za wote Wafursi na Warumi; na mzigo mkubwa wa kodi ambao zile jamii za kigeni zilizotawaliwa na Uajemi na Roma, na wakulima wadogo wa himaya zote mbili, waliolazimika kuubeba. Vile vile, Wafursi na Warumi walikuwa wamekwazwa na mizigo mizito, na walikosa usogevu. Waarabu hawa, kwa upande mwingine, walikuwa na wepesi mkubwa wa kutembea. Waliweza kushambulia waliposhabahia, na kisha wakarudi jang-wani juu ya ngamia wao wepesi sehemu ambako askari wa farasi wa adui wasingeweza kuingia kwani walikuwa hawana msaada wa lojistiki (ugavi wa usafirishaji wa watu na vifaa).

Katika mapambano yao, Waarabu walikuwa kila wakati wamezidiwa idadi na maadui zao lakini hiki hakikuwa kikwazo muhimu kwao. Historia imesheheni na mifano ya majeshi madogo ya waliojitolea wanaopambana na kushinda majeshi makubwa ya kuandikishwa.

Lakini Waislamu wenyewe, hawazitilii maanani, nyingi ya sababu hizi kwa mafanikio yao. Kufuatana na wengi wao, siri ya mafanikio yao ilikuwa katika uchamungu na ghera ya kidini ya wapiganaji wa Waislamu. Nguvu ya msukumo nyuma ya ushindi wa Waarabu kwenye karne ya saba, wanavyosema, ilitokana na Uislamu, na kila Mwarabu aliyeondo-ka kwenye peninsula hiyo kwenda kushambulia Fertile Crescent (eneo la umbo la mwezi mwandamo lenye rutuba lililoanzia Mashariki ya Mediteranian mpaka Ghuba ya Uajemi), alikuwa Mujahid au mpiganaji wa jihadi tukufu, anayepigana kwa utukufu wa Allah (s.w.t.)

Madai haya, hata hivyo, yana sehemu tu ya ukweli. Bila shaka yoyote walikuwepo wale Waislamu waliopenda kueneza mwanga wa Uislamu duniani lakini vilevile walikuwapo wengine, nao ndio waliokuwa wengi mno, waliopigana kwa ajili ya zawadi za mali ambazo mapambano hayo yalielekea kuwaletea. Walikuwa wamejenga tamaa ya kidunia ya dhahiri ya madaraka na utajiri.

Joel Carmichael:

"Vichocheo vilivyowatoa Mabedui nje ya peninsula vilikuwa ni njaa ya kimwili na uroho, matokeo ya asili ya mazingira ya dhiki huko na ya fursa zisizo na mwisho kwa ajili ya utajirishaji zilizotolewa na jamii zilizoendelea walizozishinda. Hivyo, ingawa

424

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

walikuwepo bila shaka watu wengine vilevile ambao "waliua kwa ajili ya akhera," wengi wa watu hawa wa makabila kwa kweli "waliua kwa tamaa ya dunia."

Vipengele vinavyohusu dunia nyingine vya mafundisho ya Muhammad vilikuwa vimepotezwa umaarufu kabisa wakati wa mapambano na ile ngawira ya ajabu ambayo ingeweza kupatikana: Hivyo Quraishi mmoja maarufu, ambaye alionekana kuwa mchamungu sana kwamba alikuw mmoja wa wale watu kumi ambao Muhammad aliweza kutoa tamko lake binafsi wakati wa uhai wake kwamba watain-gia peponi kwa sababu ya ghera yao Uislamu, alicha nyuma yake mali ambayo thamani yake halisi inaelekea ilikuwa kati ya dirham milioni 35 na 52; alikuwa na nyumba kuni na moja hapo Madina peke yake, na vilevile nyingine huko Basra, Kufa, Fustat na Alexandria. Mwingine wa hao wachamungu kumi walioahidiwa pepo na Muhammad mwenyewe alimiliki ardhi na majengo kwa kiwango cha dirham milioni 30; wakati wa kifo chake mtumishi wake alikuwa na zaidi ya dirham milioni mbili taslim.

Mara utaratibu huu utakapoangaliwa kwa maono, inadhihirika wazi kabisa ni ya kipumbavu kiasi gani dhana hii asili, ya zamani, ya upanuzi wa Waarabu kama ni vuguvugu la kiuchamungu kupindukia lililoamshwa na raghba binafsi ya kidini ya Muhammad.

. inaelekea kutokuwa na shaka kwamba kitu cha mwisho Waislamu wa

Kiarabu walichokuwa wakifikiria kilikuwa ni kumbadilisha mtu yoyote. Zaidi hasa, uchamungu ambao ulikuwa uwe ndio ishara ya Uislamu wa baadae, angalau katika baadhi ya dalili zake, ulikuwa mgeni kabisa watekaji wa awali wa Kiarabu.

Imeonyeshwa kwamba, ile nguvu ya msukumo nyuma ya mapambano ya Waislamu wa Kiarabu haikuwa ya kidini hata kidogo, bali ni shauku ya kihamaji iliyoota mizizi kwenye hali ya millennia, ya peninsula ya Arabia. Watu kama Khalid na Amr bin Al-Aas, kwa mfano, walikuwa dhahiri sio wachamungu au wenye miujiza; matamanio yao yalikuwa ya kuhisika kabisa.

Kule kugeuka kwa ghafla kwa tabaka la juu la Makka kwenda upande wa Waislamu ni mfano unaojieleza wa kule kuingia kwa haraka na kusikokwepeka kwa dalili za kidunia kwenye shughuli za awali kabisa za Umma, ambazo ingawa zimeundwa kwa misingi ya dini, zilijieleza kiufasaha katika misingi ya siasa.

(The Shaping of the Arabs, New York, 1967)

Ni kweli kwamba dini ndiyo iliyokuwa jambo lililowatoa Waislamu nje ya Arabia; lakini mara ilipokwisha kufanya hivyo, haikuchukua nafasi yoyote ile muhimu katika yale

425

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mapambano yaliyofuatia. Nafasi yake ilikuwa ni ya kuchochea katika kuzuka kwa Waarabu. Kama dini na uchamungu vilikuwa ndio chanzo cha mafanikio ya Waislamu katika mapambano yao, basi ni vipi mtu ataelezea mafanikio ya yale mataifa ambayo hayakuwa Waislamu? Mataifa hayo, mengine yalikuwa maadui wa Uislamu hata hivyo yalikuwa, kwa wakati mmoja, washindi kwa kiwango ambacho kililingana, na wakati mwingine kilizidi, ule ushindi wa Waislamu. Mapambano ya Waarabu yalikuwa yanashangaza kwa ukubwa wake lakini hayakuwa, kwa hali yoyote ile, ya kipekee.

Takriban miaka elfu moja kabla ya kuanzishwa kwa Uislamu, Alexander (the Great) kijana Mmasedonia, iliteka, ndani ya miaka kumi, nchi zote kuanzia peninsula ya Balkan mpaka kwenye mipaka ya China, na kutoka Libya mpaka Punjab huko India. Alikuwa ni mshirik-ina. Kila alipokwenda, aliabudu miungu ya huko. Alimuabudu Zeus huko Ugiriki, Ammon-Re huko Libya; Marduk huko Babeli; na Ahura huko Persepolis. Vita vyake havikuchochewa na dini yoyote. Kwa kweli, dini haikujitokeza mahali popote katika mapambano yake. Kama angekuwa afe na umri wa miaka 32, angekuwa amekwishaiteka dunia yote iliyobakia.

Baada ya Wagiriki wa zamani, Warumi walikuwa ndio watekaji wakuu na watawala. Walijenga moja kati ya himaya kubwa sana yenye nguvu katika historia, na moja ambayo ilidumu kwa muda mrefu zaidi kuliko nyingine yoyote kabla na baada. Kama Wagiriki kabla yao, na wao pia walikuwa wakiabudu masanamu, ingawa ile Himaya ya Roma Mashariki ilibadilishwa kwenye Ukristo mapema kwenye karne ya tano A.D.

Katika karne ya kumi na tano, Wamongolia wakiongozwa na Genghiz Khan, waliitingisha dunia yote. Walikuwa ndio maadui wabaya zaid ambao Uislamu uliwahi kukutana nao. Bara Asia lote lilikuwa chini yao, na walifikia chupuchupu ya kuufuta kabisa Uislamu kwenye bara hilo. Mapambano yao yalikuwa ya haraka na hata ya kiwango kikubwa zaidi kuliko mapambano ya Waarabu. Katika muda wa miaka hamsini, walikuwa wameiteka China yote, Russia yote, Asia ya Kati na ya Magharibi yote, na walikuwa wamepenyeza ndani ya Ulaya hadi Hungary. Ambapo Waislamu katika mwendo wao mapambano, wal-ishindwa huko Tours upande wa Magharibi, na huko Constantinople kwa upande wa Mashariki, Wamongolia walikuwa wakati wote ni washindi kila mahali. Walijitoa kutoka Ulaya ya Kati kwa sababu tu ya kifo, huko Karakorum mbali, cha Khan wao Mkuu.

Wamongolia walikuwa hawana dini yoyote kabisa. Ni nini kilichowaingiza kwenye kazi ya kuiteka dunia? Kwa hakika sio ghera ya kidini au kiuchamungu.

Katika karne ya 16, Washindi wa Wakastile (Castilian Conquistadores) waliiweka Hispania katika safu ya mbele ya mataifa ya ulimwengu. Wachache wao tu waliondoka kwenye Pwani ya Hispania, na wakaiteka dunia yote mpya. Waliyaweka mabara mawili chini ya miguu ya mfalme wa Hispania. Ni kweli kwamba walichochewa na ghera ya kidi-

426

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ni ingawa hawakuwa na uchamungu mwingi - lakini ilikuwa ni ghera ya Kikatoliki. Ghera yao haikuwa kinyume sana na ya Kiislam kama ilivyokuwa ya kuupinga-Uislamu. Kabla tu ya kugundua na kuziteka nchi za Marekani, walikuwa wamewashinda Waislamu wa Granada mnamo mwaka 1492, wamewafukuza kutoka Hispania, na walikuwa wamefutil-ia mbali kila mabaki ya utamaduni wa Kiislam kutoka kwenye ghuba ya Iberia (Hispania na Ureno ya zamani)

Katika karne ya 17, Wadachi walikwea kwenye kilele cha heshima. Hadithi ya kipindi hicho muhimu cha historia inasomeka kama kisa cha matendo makubwa na ya kishujaa. Nyumbani walikuwa wamefungiwa kwenye mapambano makali dhidi ya maadui wawili -Wahispania na bahari, na waliwashinda wote. Walikuwa wamewafukuza Wahispania kutoka Uholanzi, na walikuwa wameitawala ile Bahari ya Kaskazini yenye dhoruba na ghasia.

Wakiwa tayari wamewashinda maadui wawili hawa, Wadachi walitafuta nchi mpya za kuteka. Ile elimumwendo ya vita dhidi ya Hispania na Bahari ya Kaskazini, iliwapa kasi ya ushindi na mafanikio ambayo yaliwachukua duniani kote. Katika kuzidi nguvu, Wadachi waliizunguka dunia, wakiteka na kuanzisha makoloni na kujenga.

Wadachi hawakuwa mabaharia na wanamaji wazuri tu; walikuwa pia wafanya biashara wazuri na waanzilishi wa makoloni. Walijenga viwanda huko India, na walianzisha makoloni huko Amerika ya Kaskazini na ya Kusini, na Afrika ya Kusini. Koloni lao la Afrika ya Kusini likawa moja ya yale yaliyofanikiwa sana katika historia ya makazi na uanzishaji wa makoloni katika dunia nzima.

Wadachi walikuwa pia ni wajenzi wa falme vilevile. Maili elfu kumi na mbili kutoka nyumbani, waliiteka East Indies ambayo ilikuwa tajiri zaidi ya falme zote za Kipindi cha Ubeberu, na waliishikilia kwa miaka 350.

Hata hivyo, katika Zama za Ustawi wa sanaa na fasihi (Golden Age), karne ya 17, Wadachi walikuwa wachache sana kiidadi. Lakini juu ya uchache waliokuwa nao, ubora wao ulikuwa mzuri sana. Hawakuacha uchache wao kutia mawimbi juu ya kile ambacho wangeweza kukifanikisha, na kuthibitisha kwa namna hii kwamba hakuna uhusiano kati ya idadi kubwa na mafanikio

Ni kumbukumbu ya ajabu ya mafanikio kwa taifa dogo kama hilo la Wadachi. Walithibitisha pia kwamba hakuna uhusiano, wa lazima, kati ya dini na mafanikio. Karne nyingi kabla ya mwanzo wa umashuhuri wao, Wadachi walikuwa ni Wakristo wachamungu lakini ilikuwa ni katika karne ya 17 tu ambapo kupanda kwa butwaa na kuchanganyikiwa kwao kulipoanza.

427

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Katika karne ya 19, Waingereza walijindia himaya yao ambayo juu yake kamwe jua halikutua. Huko Amerika ya Kaskazini, waliitawala nusu ya kaskazini ya bara hilo; Huko Afrika, himaya yao ilipanuka kuanzia Alexandria upande wa kaskazini hadi Cape Town upande wa Kusini; na huko Asia ya Kusini, waliteka kuanzia Kabul hadi Rangoon. Waliitamalaki Australia na New Zealand. Walianzisha Amani ya Kiingereza juu ya eneo lote hili kubwa, robo ya dunia.

Katika karne ya 18 pale Waingereza walipokuwa wanajenga himaya yao, walikuwa na watu 35,000 tu wenye silaha, na 7,500 kati yao walikuwa wakishughulika katika kuituliza Ireland.

Wakati Jeshi la Wanamaji lilipoishikilia Himaya ya Uingereza pamoja, meli yao ya kibi-ashara iliunda himaya nyingine - himaya isiyoonekana. Ilikuwa ni ile himaya yao ya biashara ambayo ilijumuisha nyingi ya zile nchi ambazo zilikuwa nje ya eneo la mamlaka yake ya kisiasa.

Katika wakati mmoja, pale mamlaka ya Uingereza yalipokuwa kwenye kilele chake, haku-na nchi duniani iliyoweza kuwashinda wao juu ya ardhi au juu ya bahari.

Kwa mfuatano, pamoja na upanuzi wa madaraka yao ya kisiasa na umaarufu wao wa kib-iashara, Waingereza pia walianzisha mamlaka yao ya kiutamaduni duniani. Walieneza lugha ya Kiingereza karibu dunia nzima ili iwe inazungumzwa au inaeleweka katika nchi nyingi za dunia.

Waingereza waliyatimiza yote haya na mengine mengi lakini sio kwa sababu ya uchamungu wao na ghera ya kidini. Walivutiwa katika dini kiuvuguvugu tu. Hawakuiteka hata inchi moja ya ardhi ya kigeni kwa ajili ya Kristo au Biblia; waliteka tu kwa ajili ya Uingereza, na kujenga Himaya ya Kiingereza.

Mfumo wa zamani wa ufalme wa Uingereza, Ufaransa, na Uholanzi uliishika dunia kikamilifu kwa karibuni karne mbili. Mataifa ya Kiislam kila mahali yalikuwa chini ya miguu ya mamlaka haya. Lakini katika matokeo ya Vita Kuu za Dunia, mbili, himaya zao zilianguka. Kutoka kwenye masalia ya himaya zao iliibuka idadi kubwa ya mataifa mapya. Moja ya mataifa haya mapya ilikuwa ni Taifa la Kizayuni la Israel.

Mnamo tarehe 14 Mei, 1948, Waingereza waliachilia dhamana yao ya madaraka juu ya Palestina, na walowezi wa Kiyahudi wa nchi hiyo wakatangaza kuzaliwa kwa Taifa la Israel. Katika siku iliyofuatia (Mei 15) nchi tano za Kiarabu zikaivamia Israel kwa nia ya dhahiri ya "kuisukuma Israel baharini." Lakini hawakuweza kuisukuma Israel baharini. Israel iliwashinda wote, na ikawabidi wanyamaze kimya.

428

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Tangu hapo, vimekuwapo vita vingine kati ya Waarabu na Israel. Ilikuwepo moja mwaka 1956 na nyingine mwaka 1967. Katika vita vyote hivyo, Israel iliwashinda Waarabu, na ikateka eneo kubwa kutoka kwao pamoja na Jerusalem ya Zamani.

Mnamo Augosti 1969, sehemu ya Msikiti wa Al-Aqsa huko Jerusalem ilishika moto. Ulikuwa ni uchomaji moto wa makusudi. Waislamu wote - Waarabu na wasiokuwa Waarabu vilevile - walikasirishwa na ufisadi huu. Mawimbi ya mshituko wa tukio hili yal-izifikia pembe za mbali sana za ulimwengu wa Kiislam, miisho yake miwili ambayo iko mbalimbali kwa maili 10,000 - kutoka Indonesia upande wa Mashariki hadi Mauritania upande wa Magharibi. Mataifa ya Kiislam yalifanya mkutano huko Rabat Morocco kufikiria hatua za kuirudisha Jerusalem kutoka Israel. Lakini kile walichokifanya, ni kupi-tisha maazimio na kuishutumu Israel. Israel yenye jeuri ilijasiri na kuudharau ulimwengu wa Waislamu mkubwa na uliosambaa, lakini wenyewe ukakosa ujasiri na busara ya kuka-bili changamoto hiyo.

Mnamo Oktoba 1973, Misri iliishambulia Israel kwenye Yom Kippur (siku ya toba ya Wayahudi) wakati Wayahudi walipokuwa wanajishuhulisha na ibada zao. Wayahudi hao walikutwa hawakujiandaa lakini walipata fahamu tena baada ya kushitukizwa huko, na mara moja wakajibu mashambulizi. Walitembea kupita kwenye jangwa la Sinai, wakavu-ka Suez, wakaanzisha kituo cha uvamizi kwenye ukingo wa Magharibi wa mfereji huo -maili 60 kutoka Cairo, na wakakizingira Kikosi cha Tatu cha Jeshi la Misri!

Lilikuwa ni shinikizo la Amerika juu ya Israel ambalo lilikiokoa kile Kikosi cha Tatu cha Jeshi la Misri. Lakini cha kushangaza, Misri ilidai kwamba kitendo kile cha kijeshi dhidi ya Israel kilikuwa ni "ushindi" kwake. Vita na "ushindi," serikali ya Misri ilisema, vimerudisha hamasa na heshima binafsi ya Misri ingawa ilikuwa ni Umoja wa Mataifa na Marekani ambazo katika hili, kama katika matukio ya awali, zimewaokoa kutokana na maafa.

Mnamo Juni 1982 Israel iliivamia Lebanon. Ikawafukuza wapiganaji wa msituni wa Kipalestina kutoka nchini humo huku dunia yote ya Kiarabu ikiangalia kwa kimya cha kuvunjika moyo - pandikizi kweli kweli lisilojiweza kama lilikuwepo kamwe.

Katika vita vyote hivi kitu kimoja ambacho Waarabu hawakukikosa ni uwezo wa kiuchu-mi. Walikuwa nao mwingi kuliko nchi nyingine yoyote katika Dunia ya Tatu. Na kuhusu watumishi, Waarabu waliwazidi idadi Waisraeli kwa zaidi ya 50 kwa 1. Hata hivyo, hawa-jawahi kabla ya hapo kukabilana na ukweli wenye mashaka wa mchanganyiko wa utajiri na ukosefu wa uwezo; wingi wa mali na umuflisi wa hamasa; umuhimu wa mkakati na fed-heha, kama wanavyofanya katika makabiliano yao na Israeli. Inaweza kusemwa pia kwamba nchi nyingine za Kiarabu, kwa mfano, Jordan, zinafurahia "uhuru" wao tu kwa "heshima" ya Israeli.

429

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kwa hiyo inaonekana kwamba dini, yoyote ile, ya kipagani, ya kuamini kila kitu hata miti na mawe vina roho (animistic), Kikristo au ya Kiislam, ilikuwa na kidogo sana, kama kilikuwepo chochote, cha kuhusika na mapambano ya kijeshi ya nchi.

Jambo linalojirudia katika historia ya ulimwengu ni kwamba katika wakati wowote maalum, taifa lolote moja, ni kubwa, kijeshi, kisiasa, na kwa mara nyingi, na kitaalamu vilevile. Kwa muda huo au katika kipindi maalum cha historia, haizuiliki na haishindiki.

Ile miaka mia moja kutoka 632 hadi 732 ilikuwa ndio karne ya Waarabu. Walikuwa wakub-wa, walikuwa washindi, walikuwa hawazuiliki na walikuwa hawashindiki - katika karne ile. Uislamu uliwaunganisha na ukawapa akili ya mwelekeo, lengo na nguvu ya msukumo. Bila ya Uislamu, hali yao ya baadae ingekuwa isiyo na umuhimu na isiyo na faida tu kama vile hali yao ya zamani ilivyokuwa. Lakini hakuna uhusiano kati ya mapambano yao kwa upande mmoja, na uchamungu na shauku ya kidini kwa upande mwingine.

Siku za Mwisho za Umar bin al-Khattab

Mmoja wa marafiki wa Umar alikuwa ni mtu fulani Mughira bin Shaaba, Umar alikuwa amemteua kama gavana, kwanza wa Basra, na baadae wa Kufa.

Mtumwa wa Mughira alikuwa na malalamiko fulani dhidi yake. Alimuomba Umar aingilie kati, na katika kukataa kwake Umar, alimshambulia, na akamjeruhi vibaya. Mganga akaitwa. Akampa Umar dawa ya kunywa lakini yote ikatoka kwenye lile jer-aha lililokuwa na upenyo katika kitovu chake. Yule mganga alipoligundua hili, alimwambia Umar kwamba hakukuwa na matumaini ya kupona kwake, na akamshau-ri kutoa wasia wake wa mwisho kwani ni muda mdogo tu uliokuwa umebakia juu yake katika dunia hii.

Habari zikaenea haraka sana kwamba khalifa alikuwa amejeruhiwa vibaya, na habari hizo zikasababisha ghasia kubwa humo mjini. Masahaba wengi wakaenda kwa Umar kuulizia afya yake. Baadhi yao wakashauri kwamba amteue mtu kama mrithi wake. Umar akasema:

"Kama nitamteua mtu kuwa kama mrithi wangu, hakutakuwa na kasoro yoyote katika hilo kwa vile Abi Bakr aliniteua mimi kama mrithi wake, na alikuwa ni mbora kuliko mimi. Lakini kama sitateua mtu yoyote kama mrithi wangu, hakutakuwa na kasoro yoyote katika hilo pia kwani Mtume wa Allah hakuteua mrithi wake mwenyewe, na alikuwa ni mbora kuliko sisi wote (Abu Bakr na Umar)."

Aisha pia alimtumia Umar habari akimhimiza kuchagua mtu kama khalifa kabla ya kifo chake mwenyewe, vinginevyo, alionya, "vurugu na fujo vinaweza kuenea katika nchi."

430

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Umar akamwambia mjumbe wa Aisha akamwambie kama ifuatavyo: "Nimelifikiria jambo hili, na nimeamua kuteua watu sita kama wajumbe wa kamati ya uchaguzi, na kuwatwisha wao na kazi ya kuchagua mmoja kutoka miongoni mwao wenyewe kama khalifa. Watu hao sita ni: Ali, Uthman, Abdur Rahman bin Auf, Talha, Zubair na Saad bin Abi Waqqas. Mtume wa Allah alikuwa ameridhika nao wote sita wakati alipoiaga dunia hii, na kila mmoja wao anazo sifa za kuwa khalifa wa Waislamu."

Umar ndipo akawaita watu wote sita wa kamati ya uchaguzi nyumbani kwake kuwaelezea wao ni nini walikuwa wafanye. Walipofika, alizungumza nao kama ifuatavyo:

"Enyi kundi la Muhajirina! Hakika, Mtume wa Allah alikufa, na aliridhika na nyie wote sita. Nimeamua, kwa hiyo, kuufanya (uchaguzi wa khalifa) ni suala la mashau-riano miongoni mwenu, ili kwamba muweze kuchagua mmoja miongoni mwenu wenyewe kama khalifa. Kama watano kati yenu wakikubaliana juu ya mtu mmoja, na yuko mmoja anayepingana na hao watano, muuweni. Kama wanne wakiwa upande mmoja na wawili upande mwingine, wauweni hao wawili. Na kama watatu wako upande mmoja na watatu upande mwingine, basi Abdur Rahman ibn Auf atakuwa na kura makata, na khalifa atachaguliwa kutoka kwenye kundi lake. Katika hali hiyo, wauweni wale watatu walioko upande unaopinga. Mnaweza, kama mkitaka, kuwakaribisha baadhi ya watu wakubwa wa Kiansari kama watazamaji bali khalifa lazima awe mmoja wenu ninyi Muhajirina, na wala sio mmoja wao. Hawana hisa katika ukhalifa. Na uchaguzi wenu wa khalifa mpya lazima ufanyike ndani ya siku tatu."

(Tariikh Tabari)

Umar alimuamuru mwanae, Abdullah, pia kuhudhuria mikutano ya ile kamati ya uchaguzi mpya iliyoundwa, ingawa sio kama mgombea wa ukhalifa, na akamwambia: "Kama wajumbe wa kamati hii wasipokubaliana miongoni mwao, wewe utawaunga mkono wale walio wengi. Kama kuna mfungamano wa watatu katika kila upande, basi wewe utaunga mkono lile kundi la Abdur Rahman bin Auf."

Sir John Glubb:

"Umar aliagiza kiwango cha juu cha siku tatu kwa ajili ya majadiliano yao (ile kamati ya uchaguzi). Mwishoni mwa kipindi hicho, lazima watake wasitake kwa pamoja wamchague khalifa. Kama ikitokea uamuzi kutokuwa wa pamoja, yule mgombea wa walio wengi alikuwa apitishwe, na wajumbe walio wachache wakiuawa wote mara moja."

(The Great Arab Conquests, 1967)

431

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Pale Umar aliporidhika kwamba amefanya wajibu wake katika suala la kurithiwa kwake, aliwauliza baadhi ya wale watu waliokuwa karibu yake, ni nani kati ya wale wateuliwa sita, wao wangependa kumuona kama khalifa wao mpya. Mmoja wa waliokuwepo akam-taja Zubair. Umar akasema: "Utamfanya kuwa khalifa wako mtu ambaye ni mu'min anapokuwa amefurahi, na kafir anapokuwa amekasirika?" Mtu mwingine alimtaja Talha. Umar akasema: "Utamfanya kuwa khalifa wako mtu ambaye ameweka rehani zawadi ya Mtume wa Allah (s.w.t.) kwa mwanamke wa Kiyahudi?" Mtu wa tatu akamtaja Ali. Umar akasema: "Kama mkimfanya huyo kuwa khalifa wenu, hatakuacheni mpotee kutoka kwenye haki lakini ninajua kwamba hamtamchagua."

Walid bin Aghaba, kaka wa kambo wa Uthman, alikuwepo pia kwenye mkusanyiko huo. Aliposikia maoni ya Umar juu ya wagombea, alitamka kwa mshangao: "Ninamjua atakayekuwa khalifa afuataye." Umar ambaye alikuwa amelala, alikaa wima juu ya kitan-da, na akauliza, je ni nani. Walid akasema "Uthman."

Umar alimuamuru Abu Talha Ansari kuwaongoza Waislamu kwenye Swala kwa kipindi chote ambacho khalifa mpya atakuwa hajachaguliwa, na pia kuwaangalia wale wajumbe wa kamati ya uchaguzi wakati wa majadiliano yao. Alimpa pia watu hamsini wenye sila-ha wa kumuwezesha kutekeleza wajibu wake. Watu hawa walikuwa wawe, inapobidi, kama machakari (watekelezaji wa hukumu ya kifo). - Tarikh Kamil.

Kwenye siku iliyofuatia, Umar aliwaita wale wajumbe wa kamati ya uchaguzi tena, na pale walipofika akasema: "Kwa hiyo kila mmoja wenu anapenda awe ndiye khalifa baada yangu mimi?" Kila mmoja akawa kimya. Umar akalirudia swali lake ambapo Zubair akasema: "Na kuna kosa gani katika hilo? Ulikuwa khalifa na ukaumudu. Kwa nini sisi tusiweze?" Umar ndipo akauliza: "Nikuambieni kitu kuhusu kila mmoja wenu?" Zubair akajibu: "Endelea, Haya tuambie." Umar akatoa maoni juu yao kama ifuatavyo:

"Saad bin Abi Waqqas ni mtupa mishake mzuri lakini ni kiburi, na ukhalifa uko nje ya uwezo wake. Talha ni fidhuli, mroho na mwenye majivuno. Abdur Rahman anapenda sana starehe na anasa; kama atakuwa khalifa, wake zake wataendesha serikali. Zubair ni mu'min anapokuwa kwenye hali ya furaha lakini ni kafiri anapokasirika. Ali anastahili kuwa ndio mtawala wa Waislamu katika kila hali lakini ana tamaa sana ya makuu."

Kisha Umar ndipo akamgeukia Uthman, na akasema:

"Niamini mimi. Ni kama ninaona kwa macho yangu mwenyewe kwamba Maquraishi wamekuvika mkufu huu (ukhalifa) shingoni mwako, na umewaghilibisha ili wakubalike, Bani Umayya na Banu Abi Muayt (familia ya Uthman) juu ya Waislamu, na umewapa uta-jiri wote wa umma. Kisha mbwa mwitu wa Waarabu wakaja, na wakakuua. Wallahi, kama (Maquraishi) watafanya, kwa hakika wewe utafanya; na kama ukifanya, wao (Waarabu) kwa kweli watafanya." Yaani, (Kama Maquraishi watamfanya Uthman khalifa wao, yeye

432

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

atatoa madaraka na mamlaka yote kwa Bani Umayya; na atakapofanya hivyo, Waarabu watakuja kumuua).

Umar aliwaambia wale wajumbe wa kamati ya uchaguzi kwamba Mtume wa Allah (s.w.t.) alikuwa "ameridhishwa" nao wakati alipoiaga dunia. Lakini je, Mtume (s.a.w.) alikuwa ameridhishwa na hawa watu sita tu? Je, alikuwa amekasirishwa na Muhajirina na Ansari wote waliobakia? Kama hakuwa, basi kwa nini Umar aliwatenga wote kutoka kwenye hiyo kamati yake ya uchaguzi? Hakuwapa wale Muhajirina na Ansari waliobakia haki hata ya kutoa maoni sembuse haki ya kuchagua mtawala wao.

Ingawa Umar aliteua Maquraishi sita kama wachaguzi kwa sababu kama alivyosema, Mtume (s.a.w.) alikuwa ameridhika nao, yeye mwenyewe hakuona chochote kwao cha kusifika. Aliwaona wenye kiburi, mafedhuli, waroho, wenye majivuno, wanyanyasaji, wenye hamaki, wala rushwa na wapenda makuu.

Kama, katika uchaguzi wa Abu Bakr, utaratibu ulikubalika kwamba ni haki ya umma wa Waislamu kuteua au kuchagua watawala wao, basi ni vipi wale maswahaba maarufu wa Mtume (s.a.w.), na Aisha, mjane wake, wakamsisitizia Umar kuteua mrithi wake mwenyewe?

Hivi hawakujua kwamba mtawala alikuwa achaguliwe na umma? Lakini Umar, badala ya kuikataa au kuikiri hii haki ya umma, akasema kwamba kama angechagua mtu kuwa khalifa, angekuwa anafuata kigezo cha Abu Bakr; na kama asingechagua, basi angekuwa ana-fuata kigezo cha Mtume (s.a.w.) mwenyewe. Kiutekelezaji, hata hivyo, hakufata ama kigezo cha Abu Bakr wala cha Mtume (s.a.w.). Alitaja majina ya watu sita kama wajumbe wa kamati ya uchaguzi, na akawafanya wenye wajibu wa kumchagua khalifa kutokana na wao wenyewe - bila ya kujali maoni au matilaba ya umma wa Waislamu.

Ni kweli kwamba Umar hakutaja mtu yoyote kama mrithi wake lakini kamati yake ya uchaguzi, kwa kweli, ilikuwa ndio uteuzi wenyewe. Uundwaji wake ulihakikisha kuchaguli-wa tu kwa mgombea wa Umar mwenyewe. Sharti lake la kwanza lilikuwa kwamba yule mgombea atakayepata wingi wa kura, atakuwa ndio khalifa. Hapakuwa na njia kwa Ali ya kupata wingi wa kura hizo. Abdur Rahman bin Auf alikuwa mume wa dada wa kambo wa Uthman. (Bibi huyu alikuwa binti ya mama yake Uthman na mume wake wa pili). Saad bin Abi Waqqas alikuwa ndiye binamu wa kwanza wa Abdur Rahman, na alikuwa chini ya ushawishi wake. "Mshikamano wa kikabila" au "uzalendo povu wa kikabila" ulikuwa na nguvu sana miongoni mwa Waarabu.

Talha alikuwa wa ukoo wa Abu Bakr, na alikuwa amemuoa mmoja wa binti zake (dada yake Aisha). Kwa hiyo, ilikuwa haifikiriki kwamba yoyote kati yao atampigia kura Ali. Hivyo, Ali alikuwa aziondoe kura nne hata kabla ya kuanza mazungumzo. Kile alichoweza

433

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kukifanya kilikuwa ni kutumaini kwamba anaweza kuipata kura ya Zubair. Kwa hali yoy-ote, Abdur Rahman bin Auf - yule mwenye nguvu katika uchaguzi aliyeteuliwa binafsi, alikuwa na kura ya veto). Kama msiri wa Umar, ilikuwa haikwepeki kwamba atatoa kura yake na uungaji mkono wake kwa kipenzi cha Umar tu, na kaka wa mke wake mwenye we - Uthman.

Sasa wale wachache katika ile kamati ya uchaguzi walikuwa na moja kati ya nafasi mbili ambazo zilikuwa wazi mbele yao, yaani, ama kuridhia na uteuzi wa yule mwenye nguvu katika uchaguzi na kumkubali Uthman kama khalifa au kujipitishia wenyewe hukumu ya kifo!

Hudhaifa, ambaye ni sahaba, anasimulia kwamba wakati fulani kabla jaribio halijafanywa juu ya maisha yake, maswahaba wachache wakikuwa wamemuuliza Umar, ni nani atakayemrithi yeye kama khalifa, naye akawaambia, ni Uthman. (Kanz-ul-Umma na Tarikh-Ahmad).

Mwandishi wa kitabu Riyadh-un-Nadhra anaandika katika muktadha huo huo kama ifu-atavyo: "Katika msimu wa Hijja mtu mmoja alimuuliza Umar ni nani atakayekuwa khalifa wa Waislamu baada yake, naye akasema, ni Uthman bin Affan."

Umar hakutamani sana kitu kingine kama kumteua Uthman kuwa mrithi wake lakini kwa sababu alizozijua yeye mwenyewe tu, hakutaka kufanya hivyo wazi wazi. Wakati huo huo, hakuwaruhusu Waislamu kutekeleza hiari zao katika suala la kuchagua mtawala wao. Wangeachiwa wao wenyewe, wasingemchagua kipenzi chake, na alilijua hili. Yeye, kwa hiyo, aliunda mtindo wa kuupa umma kiongozi wake. Mtindo huu mpya, ulijisokota katika changamano yenye kutatiza, ulihakikisha kuchaguliwa kwa Uthman.

Umar alikuwa amekusanya ile Kamati ya Uchaguzi ili kufanya ghilba tu!

Huenda ingeokoa manufaa ya umma vizuri zaidi kama Umar angemteua wazi wazi Uthman kama mrithi wake badala ya kuunda jopo la wateuzi kwa ajili ya lengo hili. Uteuzi wa moja kwa moja na wa wazi ungezizuia vita za wenyewe kwa wenyewe katika Uislamu. Jopo lake la wateuzi limethibisha kuwa kichocheo cha vile vita vya Basra, Siffin na Nahrwan. Alifikia lengo lake kwa wakati huo lakini kwa gharama tu ya uadilifu wa Uislamu hapo baadae.

Abdullah ibn Abbas ibn Abdul-Muttalib alikuwa ndio binamu wa kwanza wa Muhammad Mustafa (s.a.w.) na Ali ibn Abi Talib. Aliposikia kwamba Umar alikuwa ametoa mamlaka maalum kwa Abdur Rahman bin Auf katika lile jopo la wateuzi, alimwambia Ali:

434

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Ukhalifa umetupotea kwa mara nyingine. Mtu huyu (Umar) anataka Uthman awe ndiye khalifa mpya. Ninajua watauondoa ukhalifa kwenye nyumba ya Muhammad."

Ali alitoa maelezo yafuatayo:

"Ninakubaliana na unachokisema. Nalifahamu fika jambo hili. Hata hivyo, nitahud-huria mikutano hiyo ya Shura (kamati ya uteuzi), na Waislamu wataona kwa macho yao wenyewe ule mgongano kati ya maneno ya Umar na matendo yake. Kwa kuliwe-ka jina langu katika kamati yake ya uteuzi, ameitambua, angalau, haki yangu ya kuwa khalifa ambapo huko nyuma, alipita huku akisema kwamba utume na ukhalifa havipaswi kuchanganyika katika nyumba moja hiyo hiyo."

Abdullah ibn Abbas amejuaje kwamba Umar alitaka Uthman awe ndiye khalifa? Kama ilivyoelezwa kabla, ilikuwa ni dhahiri kutokana na katiba ya ile kamati ya uchaguzi. Kutupia jicho kwenye hadidu za rejea zake kulitosha kumkinahisha mtu yoyote kwamba matokeo ya kutafuta kwake yalikuwa yamekwisha kuamuliwa. Hadidu za rejea hizo zili-tangaza, kwa sauti kubwa na kwa uwazi kabisa, kwamba ukhalifa utakuwa ni tunzo kwa Uthman na Bani Umayya. Kwa hiyo, baada ya kutangazwa na Umar kule kuundwa kwa ile kamati ya uteuzi, kama Ali alikuwa bado anayo shauku yoyote iliyobakia juu ya ukhalifa, na malengo yake yaliyotangazwa, ilikuwa ni ya kitaalam kabisa na ya kinadharia, na kama yeye mwenyewe alivyosema, kushiriki kwake kwenye mikutano yake hakutafanya lolote zaidi ya kuonyesha hitilafu za msingi ndani yake.

Hizi ni zama za demokrasia. Watu wanawachagua viongozi wao. Uchaguzi unafanyika kuanzia ngazi za chini hadi za juu za maisha ya jamii; toka wenyeviti wa kamati za shule na vikundi vya kuchangisha pesa hadi wakuu wa serikali na nchi. Lakini haijawahi kutokea kwamba wale wagombea wa nafasi ambao wanashindwa kwenye uchaguzi na wapinzani wao, wanahukumiwa kifo. Wale wagombea wanaoshindwa, wanakuwa viongozi wa upin-zani, na kuwepo kwa upinzani wenye nguvu kunaonekana ni lazima kwa ajili ya kuwepo kwa demokrasia yenyewe. Kama upinzani utauawa, basi demokrasia inakuwa imekufa, na nchi inakuwa ya kiimla.

Amri ya Umar ya kuwauwa wale wachache katika kamati yake ya uteuzi haina mfano katika historia ya mwanadamu. Aliamuru kuuawa kwa wale maswahaba wote wa Muhammad Mustafa (s.a.w.), ambao, kama wagombea wa ukhalifa, watapata kura chache kuliko idadi ya upinzani wao, ingawaje alijua kwamba ilikuwa ni kazi ya wengine kutoa au kuzuia kura zao. Kwa maneno mengine, alihukumu kwambani "kosa" kupata kura chache zaidi ya mpinzani wake mtu, na adhabu yake ni kifo!

Huu ulikuwa ni uamuzi wa mwisho wa mtu ambaye hapo nyuma alisema: "Kitabu cha Allah kinatutosha." Hivi kweli alikiamini alichokisema? Hivi alikisoma Kitabu hicho? Je,

435

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

alipata kibali katika kitabu hicho cha hii amri yake ya kuua mgombea wa nafasi fulani kwa sababu alipata kura chache kuliko mpinzani wake?

Hapa ni lazima ibainike kwamba hakuna hata mmoja kati ya Muhajirina sita hawa aliye-peleka maombi kwa Umar ya kuwa mjumbe wa kamati yake ya uteuzi. Kitendo chake cha kuwachagua kilikuwa cha kidhalimu kabisa. Kisha yeye akaweka juu yao jukumu la kuch-agua khalifa kwa masharti kwamba kama mmoja wao yoyote hatakubaliana na wengi, atapoteza maisha yake.

Ni dhahiri kabisa Umar alichagua ile "dawa" ya kidikteta ya kuondoa haki ya kutofautiana kutoka kwa Waislamu.

Kwa karne nyingi, Waislamu wa Sunni wameongea kwa shauku kubwa kile wanachokiita "uadilifu wa Umar." Je, amri yake ya kuua mtu au watu wa kamati yake wanaotofautiana ni mfano wa "uadilifu" huo? Hivi huo ndio mfano wa uadilifu ambao kwa fahari kabisa wanauunga mkono kwa mataifa ya dunia?

Umar alikufa siku ya Jumamosi ya mwisho ya Dhil-Hajj (mwezi wa mwisho wa kalenda ya Kiislam) ya mwaka wa 23 H.A. (A.D.644), na alizikwa karibu na Mtume (s.a.w.) na Abu Bakr.

Wajumbe wa Kamati ya Uteuzi

Umar, akiwa kwenye kitanda cha umauti wake, aliwateua Muhajirina sita kuwa wajumbe wa jopo ambalo lilikuwa lichague mmoja kati yao wenyewe kama khalifa wa baadae wa Waislamu. Hao walikuwa ni Ali bin Abi Talib, Uthman, Talha, Zubayr, Abdur Rahman bin Auf na Saad bin Abi Waqqas. Ukimuacha Ali, wajumbe wengine wote wa jopo hilo walikuwa mapepari, au hasa, mabepari mamboleo. Walipokuja kutoka Makka, walikuwa masikini na wasio na makazi lakini katika kipindi cha miaka kumi na mbili, yaani, tangu kifo cha Muhammad Mustafa (s.a.w.) mwaka 632 hadi kifo cha Umar mwaka 644, kila mmoja wao, isipokuwa Ali, amekuwa tajiri kama Croesus. Katikati ya tarehe hizi mbili, walikuwa wamekusanya utajiri mwingi, na wamekuwa matajiri wakubwa wa nyakati zao. Ali hakuwa na sifa za uanachama wa "klabu" hii ya kipekee lakini Umar alimwingiza vivyo hivyo. Mbali na ukweli kwamba Ali aliishi kama mkulima wa bustani ambapo wanachama wenzie wengine watano waliishi kwa mapato ya ardhi zao na maeneo yao ya makazi, kulikuwepo na mwanya mwingine, usiovukika zaidi, ambao ulimtenga yeye kutoka walikokuwa wao. Katika tabia, haiba, mwenendo, mwelekeo, falsafa na mtazamo wa maisha, Ali na hao waliobaki kati yao, walikuwa ni kinyume kabisa.

Katika mlango wa huko nyuma, ilionyeshwa kwamba ule ubeti maarufu wa Keats, "Uzuri ni Ukweli na Ukweli ni Mzuri," unaweza kubadilishwa usomeke kama "Uwezo wa

436

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kiuchumi ni uwezo wa kisiasa na uwezo wa kisiasa ni uwezo wa kiuchumi." Mamlaka ya kiuchumi na mamlaka ya kisiasa yanakubaliana. Karl Marx alisema: "Tabaka lolote la kijamii lililo na uwezo wa kiuchumi, pia linao uwezo wa kisiasa na kijamii." Na George Wald, profesa wa Biologia katika Chuo Kikuu cha Harvard, alisema katika hotuba huko Tokyo mwaka 1974 kwamba: "Utajiri binafsi na uwezo binafsi wa kisiasa vinabadilis-hana."

Hapawezi kuwa na shaka kwamba uwezo wa kiuchumi ni ubao wa kuchupia wa uwezo wa kisiasa. Hili limekuwa ni mwelekeo unaokubalika katika historia yote.

Rais Abraham Lincoln aliifafanua demokrasia kama ni Serikali ya watu, iliyowekwa na watu, kwa ajili ya watu.

Katika uchaguzi wa rais wa Marekani wa mwaka 1984 wakati rais Ronald Reagan alipoch-aguliwa tena, Warusi walikejeli:

"Serikali ya Marekani ni ya mamilionea, iliyowekwa na mamilionea, kwa ajili ya mamilionea."

Wajumbe wote wa kamati ya uteuzi ya Umar walikuwa ni mamilionea - isipokuwa Ali ibn Abi Talib! Ifuatayo ni taswira iliyoachwa na wanahistoria ya wajumbe wa Kamati ya Uteuzi ya Umar:

D.S. Margoliouth:

"Uthman mwana wa Affan, mdogo kwa Mtume kwa miaka sita, alikuwa mfanyabi-ashara wa nguo; alishughulika pia kama mkopeshaji pesa, akitoa chambele kwenye biashara ambazo alikuwa apate nusu ya faida (Ibn Sa'd, iii, 111), na katika masuala ya fedha alionyesha ukali wa ajabu (Waqidi W. 231). Dada yake alikuwa mwuuza kofia za kike, aliyeolewa na kinyozi (Isabah, i, 714). Hakuwa mtu wa kupigana, kama historia yake ya baadae ilivyothibitisha, kwani alikwepa uwanja wa mapam-bano mmoja, akakimbia kwenye mwingine, na aliuawa kikasisi, akisoma Qur'an." Ibn Sa'd anasema katika Tabaqat yake kuhusu Uthman: "Alipokufa, aliacha dirham milioni 35, dinari 150,000, ngamia 3000 na farasi wengi. Alijijengea mwenyewe kasri huko Madina kwa marumaru na mbao za mvule. Alikuwa na watumwa 1000."

(Muhammad and the Rise of Islam, London, 1931) E.A. Belyaev:

"Katika ujana wake, kabla ya kuanza Uislam, Uthman alikuwa ni tajiri sana na alipa-ta pesa nyingi kutokana na biashara za riba zilizokuwa na faida sana. Tamaa ya kipa-

437

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

to na kipawa cha biashara cha Uthman vilipata eneo kamili alipokuwa khalifa. Alijijengea mwenyewe nyumba ya mawe huko Madina yenye milango ya mbao za thamani kubwa na akajipatia mali isiyohamishika kwenye mji huo, pamoja na mabus-tani na vyanzo vya maji. Alikuwa na mapato makubwa kutokana na mashamba yake ya matunda huko Wadi-ul-Qura, Hunain na sehemu nyinginezo, yaliyokadiriwa kuwa na thamani ya dinari 100,000, mbali na makundi makubwa ya farasi na ngamia walioko kwenye mashamba haya.

Siku alipokufa Uthman, hazina yake binafsi ilikutwa na dinari 150,000 na dirham milioni moja. Akitunisha utajiri wake kwa gharama ya hazina ya Waislam, Uthman pia aliwapa baadhi ya masahaba wa karibu wa Muhammad uhuru wa kuitumia hazina hiyo, akijaribu kuhalalisha vitendo vyake haramu kwa kuwahusisha hawa Waislam wakongwe wa kuaminika sana na uharibifu wake mwenyewe wa mali. Hawa "masahaba" walimsifu kwa vifijo khalifa Uthman kwa ukarimu wake na roho nzuri, bila shaka kwa sababu zao madhubuti za manufaa binafsi.

Zubeir ibn al-Awwam, kwa mfano, mmoja wa wanaofahamika sana miongoni mwao, alijenga majumba makubwa yenye vyumba vingi vya kupangisha kwa bei nafuu huko Kufa, Basra, Fustat na Alexandria. Mali yake ilikadiriwa kuwa na thamani ya dinari 50,000, kwa nyongeza yake ambayo alimiliki farasi 1,000 na watumwa 1,000.

"Sahaba" mwingine, Talha ibn Ubaidullah, alijenga nyumba kubwa ya vyumba vingi ya kupangisha huko Kufa na akajipatia mashamba huko Iraq ambayo yaliingiza dinari 1000 kila siku; alijenga pia jumba la kifahari la matofali na mbao za thamani hapo Madina.

Abdur Rahman ibn Auf, ambaye pia ni "sahaba" mashuhuri, pia alijijengea makazi ya kitajiri yenye nafasi kubwa; mazizi yake yalikuwa na farasi 100 na malisho ya ngamia 1000 na kondoo 10,000, na robo ya urithi aliouacha baada ya kifo chake ulikadiriwa kuwa na thamani ya dinari 84,000.

Tamaa kama hiyo ya utajiri ilikuwa imeenea sana miongoni mwa masahaba wa Mtume na msafara wa Uthman..

(Arabs, Islam and the Arab Caliphate in the Early Middle Ages,

New York, 1969)

Bernard Lewis:

"Sa'd ibn Abi Waqqas alijenga nyumba yake huko Al-Aqiq. Aliifanya ndefu na yenye nafasi, na akaweka baraza kuzunguuka sehemu ya juu. Sa'id ibn al-Musayyib alise-

438

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ma kwamba wakati Zayd ibn Thabit alipokufa, aliacha vipande vya dhahabu na fedha ambavyo vilivunjwa kwa shoka, kwa nyongeza ya mali na mashamba yenye thamani ya dinari 100,000."

(Islam in History, New York, 1973)

Dr. Taha Husain wa Misri anaandika katika kitabu chake, al-Fitna-tul-Kubra (mageuzi makubwa) kilichochapishwa na Dar-ul-Ma'arif, Cairo, 1959, uk, 47:

"Wakati Uthman alipokuwa khalifa, hakuondoa tu kile kizuizi kilichokuwa kimewek-wa na Umar juu ya masahaba kwenda kwenye nchi nyingine, bali pia aliwapa zawa-di kubwa kutoka kwenye hazina ya umma. Alimpa Zubeir dirham 600,000 katika siku moja, na akampa Talha dirham 100,000 katika siku moja na kuwawezesha kununua ardhi, mali na watumwa kwenye nchi nyingine."

Abdur Rahman bin Auf alikuwa mhusika kwenye mzingo wa ndani wa marafiki wa Uthman. Kuhusu yeye Sir William Muir anaandika hivi:

"Abd al-Rahman, ambapo baada ya miaka alikuwa na mazoea ya mlo wa gharama juu ya mkate mzuri na kila aina ya nyama, alikuwa akilia alipokuwa akiangalia meza yake iliyoandaliwa kifahari na akifikiria mlo wa dhiki wa Mtume."

(The Life of Muhammad, London 1877)

Mapenzi aliyokuwa nayo Abdur Rahman kwa bwana wake aliyekwishafariki, Muhammad (s.a.w.w.), yalikuwa ya kuhuzunisha sana. Wake zake na wakeze wadogo walitayarisha mapochopocho ya aina nyingi na utamu mwingi kwa ajili yake. Wakati alipoketi kula, kumbukumbu zilimjia za nyakati ngumu za Mtume (s.a.w.w.). "Alimkumbuka" sana na "alizikumbuka" nyakati zile, na alitokwa na machozi mengi mno, na kisha akala kwa pupa kila kitu pale mezani.

Sir William Muir anahitimisha maoni yake juu ya masahaba wa Mtume wa Allah swt. kama ifuatavyo:

"Katika kufuatilia kumbukumbu za kihistoria za "masahaba" na wafuasi wa mwanzo wa Muhammad, mambo machache yanaonyesha kwa nguvu sana mtazamo wa Uislam kama, kwanza, idadi ya wake zao na wake wadogo na ule urahisi wa talaka; na, kinachofuata, ni ule utajiri mwingi walioulimbikiza; tofauti muhimu sana na zile siku za mwanzo za Ukristo."

(The Life of Muhammad, London, 1877) 439

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sir William Muir amefanya uonevu mkubwa, kwanza kabisa, kwa kuwachanganya pamo-ja masahaba wote ambapo kulikuwa na makundi mawili tofauti kati yao. Kundi la kwanza ambalo ndani yake mna masahaba walio wengi, ndilo moja ambalo amelifafanua kwa usahihi kabisa ndani ya kitabu chake, lakini pia kulikuwepo na jingine kundi, ingawa dogo sana, na hakulijali kabisa.

Pili, Sir William Muir ameihusisha tamaa ya kutotosheka na mali ya masahaba na "mtazamo wa Uislam," na huu hasa ni uonevu mkubwa kabisa. Hii tamaa ya mali ya masahaba, au hasa, tamaa ya wengi wa masahaba wa Mtume (s.a.w.w.), inaonyesha, sio mtazamo wa Uslamu, bali hisia dhidi ya mtazamo huo. Ugonjwa mkubwa wa kuthamini mali na pesa unakwenda kinyume na mtazamo na busara za Uislamu. Qur'an mewakemea vikali wale watu wanaolimbikiza dhahabu na fedha

Kama mtu anataka kuuona mtazamo wa kweli hasa wa Uislamu, ataupata, sio katika viten-do vya matajiri wa majuzijuzi wa Madina, bali katika maisha, tabia na matendo ya masahaba wa Mtume (s.a.w.w.) kama vile Ali ibn Abi Talib, Salman Farsi, Abu Dharr al-Ghiffari, Ammar ibnYasir, Uwais Qarni na Bilal. Mutashirki watabadilisha tathmini yao juu ya mtazamo wa Uislam ikiwa kama watautafakari katika maisha ya kawaida, halisi na yaliyotakasika ya masahaba hawa wa kundi hili la mwisho.

Ifahamike kwamba wale wajumbe wa kamati ya uteuzi walikuwa wote ni watu wa Makka. Hapakuwa na mtu wa Madina miongoni mwao.Umar aliwaacha nje kwa uangalifu sana. Wakati alipokuwa akiwaelezea wajumbe wa kamati nini walichotakiwa wafanye, aliwaam-bia hivi: "Enyi kundi la Muhajirina." Aliwaambia kwamba khalifa awe ni mmoja wao, na kwamba watu wa Madina hawakuwa na haki katika ukhalifa. Masahaba wengine wal-imshinikiza Umar kuteua mrithi wake mwenyewe. Alitaja watu kadhaa ambao waliokuwa wamekufa, na akasema kwamba kama yeyote kati yao angekuwa hai, angemteua yeye kama mrithi wake.

Dr. Taha Husain:

"Mtume wa Uislam alikuwa amefariki, sio masiku bali masaa machache wakati Uislam ulipokabiliwa na mgogoro wake wa kwanza - katika suala la kurithiwa kwake. Ansari waliwaambia Muhajirina: 'kiongozi mmoja kutoka kwetu na mmoja kutoka kwenu.' Lakini Abu Bakr hakukubaliana na hili, na alinukuu Hadith ya Mtume ifuatayo: 'Watawala watatokana na Makuraish.' Kisha akawaambia Ansari: 'Sisi tutakuwa watawala na ninyi mtakuwa mawaziri.' Ansari waliukubali mpango huu (isipokuwa Saad ibn Ubada).

Hivi ndivyo utawala wa kikabila wa Uislam ulivyozaliwa. Haki yake ya kutawala ilibaki kwenye udugu na Muhammad. Mamlaka yote yaliwekwa kwa Makuraish. Maansari walikuwa washauri. Kila Mwislam anayo haki ya kutoa ushauri. Makuraish

440

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

walikuwa watawale, na Ansari na Waislam wengine walikuwa watoe ushauri lakini sio kutawala.

Wakati Umar alipokuwa anakufa, aliulizwa kuhusu mrithi wake, na akasema: 'Kama Abu Ubaida bin al-Jarrah angekuwa hai, ningemfanya kuwa khalifa. Kama Khalid bin al-Walid angekuwa hai, ningemteua kuwa amir wa Waislam. Na kama Salim, huria wa Abu Hudhaifa, angekuwa anaishi leo hii, basi ningemchagua kama mtawala wenu.' Huyu Salim alikuwa ni mtumwa aliyekuja kutoka Istakhar huko Uajemi. Alikombolewa, na akawa 'mawali' huria wa Abu Hudhaifa Alifahamika sana kwa uchamungu wake. Waislam wengi walimfuata katika masuala ya dini hata katika nyakati za Mtume. Wakati mwingine aliwaongoza Waislam kwenye swala vilevile. Aliuawa katika vita vya Riddah (dhidi ya walioritadi) wakati wa ukhalifa wa Abu Bakr. Alikuwa mtu mtiifu na mchamungu."

(Al-Fitna-tul-Kubra kilichochapishwa na Dar-ul-Ma'arif, Cairo, 1959)

Ilikuwa ni bahati mbaya sana kwa umma kwamba Salim alikuwa amekufa vinginevyo Umar angemfanya kuwa ndiye mrithi wake, na angeweza kuwa khalifa mzuri. Kwa vyovy-ote vile, Umar aliiangusha chini ile "Hadith" ya Mtume ambayo Abu Bakr aliinukuu mbele ya Ansari mle Saqifah ambayo kulingana nayo hakuna yoyote ila Makuraish, waliokuwa na haki ya kuwa watawala. Hapa Umar, "kuhani" mkuu wa taasisi ya Sunni, alikuwa yuko tayari, radhi na mwenye shauku ya kumfanya Salim kuwa khalifa wa Waislam, ambaye alikuwa:

(a) sio Mquraishi

(b) sio Mwarabu

(c)  'asiyekuwa huru', huria, mtu aliyekombolewa na Mwarabu, na ambaye alikuwa chini ya ulinzi wake.

Umar "alithibitisha" pale kwenye kitanda chake cha umauti kwamba ile "Hadith" ya "uhu-siano wa Quraishi" ambayo kwayo Muhajirina walidai "ubora" wao juu ya Ansari mle Saqifah, ilikuwa ya uwongo, na "alithibitisha" kwamba ili kuwa khalifa wa Waislam, haikuwa lazima kuwa Kuraish hata hivyo.

Umar aliweza kumfikiria mtu aliyewahi kuwa mtumwa ambaye alikuwa hatambuliki kwa lolote isipokuwa uchamungu wake, kwa ajili ya nafasi muhimu kabisa katika Uislam lakini hakuweza kumfikiria Ansari kwa nafasi hiyo, hata kama alikuwa amejitambulisha mwenyewe katika vita na katika amani. Hao Ansari, kwa kweli, hawakuweza kuziba hata nafasi zilizokuwa na umuhimu mdogo. Katika kitabu chake, Al-Faruuq, M. Shibli, yule mwanahistoria wa Kihindi, amechapisha orodha ya majina ya maafisa wa kiraia na wa kijeshi wa wakati wake Umar. Ikiwa na mtu mmoja pekee (Uthman bin Hunaif), orodha yote imetokana na majina ya watu ambao walikuwa ni maarufu kwa uadui wao kwa Ali,

441

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwa Bani Hashim, na kwa Ansari.

Hawa Ansari walikuwa ni watu wale wale ambao, wakati mmoja, waliwahi kutoa hifadhi kwa Umar kwenye mji wao. Walimpa chakula, mavazi na makazi wakati alipokuwa hana hata kimoja kati ya vitu hivi. Sasa alikuwa ndio anawalipa? Tabia ya Umar kwa Ansari ina tofauti kubwa na tabia ya Muhammad, Mtume wa wa Allah swt. kwao. Yeye aliwapenda Ansari. Aliwateua wengi wao kama magavana wa Madina, na aliwafanya wengi wao kuwa makamanda wa misafara mbali mbali. Katika tukio moja alisema kwamba ingekuwa bora awe nao (Ansari) kuliko kuwa na watu wengine wowote. Pia aliwaona wao kuwa wenye uwezo na sifa za kuwatawala hao Muhajirina.

Montgomery Watt:

"Maoni ya Muhammad kuhusu Sa'd bin Mu'adh wakati alipokuwa anataka kuamua kesi ya Banu Qurayza, "Simama kwa niaba ya bwana wako (Sayyid)," yanaweza kuchukuliwa kuthibitisha maoni kwamba Ansari walikuwa na uwezo wa kutawala juu ya Makuraishi, na Hadith hiyo ilipindishwa kwa njia nyingi ili kuondoa maana hii.

(Muhammad at Madina, Oxford, 1966)

Mtume wa Allah swt. alimwita Sa'd Kiongozi wa Kuraish. Sa'd ni dhahiri alikuwa na uwezo wa kuwatawala Makuraish, na kwa nini asiwe nao? Hata hivyo ni nini kilikuwepo katika "sifa" za Makuraish ambacho Ansari hawakuwa nacho? Hakuna. Lakini Ansari walipoteza uwezo wao wa kuwatawala Makuraishi mara tu baada ya Muhammad (s.a.w.w.), bwana wao, alipofariki. Wakati wa ukhalifa wa Abu Bakr na Umar, ilikuwa ni "kuondolewa staha" kuwa Ansari kushika nafasi yoyote muhimu katika serikali.

Laula Veccia Baglieri:

"Akiwa amelala karibu ya kufa, Umar alikuwa na wasiwasi kuhusu kurithiwa na aka-teua kamati ya watu sita, wote Makuraish, ambao kazi yao iwe ni kuchagua mmoja katika idadi yao hiyo kuwa khalifa. Wenyeji wa Madina hawakuwa na nafasi tena katika uchaguzi wa mkuu wa dola.

(Cambridge History of Islam, Cambridge, 1970)

Mbali na kutokuwa na nafasi katika uchaguzi wa mkuu wa dola, bila ya kuzungumzia wao wenyewe kuwa mkuu wa dola, wenyeji wa Madina, hawakushiriki katika kila kitu. Wangeweza kutoa "ushauri" kwa Abu Bakr na Umar. Humo Saqifah, Abu Bakr na Umar waliwaambia wao kwamba watashauriana nao (Ansari) katika mambo yote.

Wachache, kama wapo, wanaweza kupinga ile tafsiri ya kawaida ya jambo hili lenye

442

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kusikitisha kwamba lile jambo moja la muhimu sana na la msingi kabisa katika mwaka wa kwanza wa Hijiria, yaani, ule msaada wa Ansari, limekuwa ni jambo lililopuuzwa lenye kuvutia sana.

Yale matamshi yenye kubashiri janga ya Hubab ibn al-Mandhir katika zile ghasia za Saqifah yalithibitisha tu kuwa ni ya kweli. Aliionyesha ile hofu kwamba watoto wa Ansari watakuja kuomba chakula katika milango ya nyumba za Muhajirina, na hawatakuja kupa-ta chochote. Mabaya zaidi yatakuja kuwafikia katika nyakati za Yazid bin Muawiyyah.

Ansari walipigana katika mapambano yote ya Abu Bakr na Umar lakini kama wapiganaji wengine tu na kamwe sio kama majemedari. Ule utajiri mpya uliokuwa ukija kwa mafu-riko kuingia Madina baada ya kutekwa kwa Uajemi na (eneo la) Mwezi Mwandamo lenye Rutuba, pia unaokekana kuwapitia mbali isipokuwa wachache, ambao walishirikiana kisal-iti na serikali ya Saqifah. Miongoni mwa hao walikuwa ni wale wapelelezi wawili kutoka kwenye kabila la Aus ambao walitoa habari juu ya Khazraj kwa Abu Bakr na Umar. Wengine walikuwa ni Muhammad bin Maslama, Bashir bin Saad, na Zayd bin Thabit. Walionyesha ari kubwa katika kutoa kiapo cha utii kwa Abu Bakr mle Saqifah.

Zayd bin Thabit alikuwa amejisabilia mno kwa Uthman, na kwa sababu hii, alipokea zawa-di nyingi na tunzo kutoka hazina. Alikuwa mtoto wa wazazi masikini lakini katika ukhal-ifa wa Uthman, akawa mmoja wa watu matajiri hapo Madina.

Watumishi wawili wa hazina ya umma hapo Madina na huko Kufa ambao walikuwa wameteuliwa na Abu Bakr, walizitupa funguo za hazina hizo zilizokuwa chini yao, mbele ya Uthman, kwa malalamiko dhidi ya uporaji wa pesa za umma wa yeye mwenyewe Uthman na mmoja wa magavana wake. Uthman alizitoa funguo zote kwa Zayd bin Thabit. Zayd bin Thabit alikuwa pia ni mwenyekiti wa kamati iliyoteuliwa na Uthman kukusanya Aya za Qur'an, na kuzichapisha katika juzuu moja, kama ilivyoelezwa kabla.

Zayd bin Thabit alikuwa mmoja wa Ansari wachache walioshiriki katika mafanikio katika nyakati za Umar na Uthman. Alikuwa pia mmoja wa Ansari wachache ambao hawakushiri-ki katika vita vya Ali huko Basra, Siffin na Nahrwan. Wengi wa Ansari walipigana upande wa Ali dhidi ya maadui zake katika vita hizi.

Tafsiri zifuatazo zinaweza kufanywa kutoka kwenye mipango ya Umar ya kutafuta khalifa:

1. Sio lazima kwa khalifa wa Waislam kuwa Kuraish. Hata mtumwa aliyekombolewa kama Salim anaweza kuwa khalifa wao. Ile "Hadith" kwamba viongozi lazima wawe ni watu wa kabila la Kuraish, ilikuwa ime-buniwa na ilihusishwa kwa Mtume (s.a.w.w.) kwenye tukio maalum, na

443

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwa lengo maalum; ilifanya kazi mle Saqifah, na iliwazuia Ansari

2.  Khalifa aliyepo madarakani anaweza kiimla tu kuifinya haki ya na mam-laka ya kuchagua khalifa mpya kwa watu watano au sita bila ya kuhusisha Umma wa Waislam. Umma wa Waislam unaweza kupuuzwa kirahisi.

3.  Ndani ya kamati ya uteuzi, kama mtu hakubaliani na walio wengi, anas-tahili kifo, hata kama ni rafiki ya Mtume wa Uislam (s.a.w.w.); hata kama alipigana vita ya Badr; na hata kama ni "Sahaba wa kwenye Mti." Hakuna cha kumuokoa.

4.  Umma wa Waislam unaweza kuachwa bila kiongozi kwa muda wa siku tatu. Sio lazima kuchagua khalifa mara tu baada ya kifo cha khalifa aliyekuwa madarakani. Khalifa alichaguliwa mara tu baada ya kifo lakini kabla ya mazishi ya Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), kwa msingi kwamba umma wa Waislam haupaswi kukaa bila ya kiongozi hata kwa muda mdogo. Umar kwa hiyo akaweka mfano mpya, yaani, kuwezekana kwen-da na hali halisi katika matumizi ya "taratibu" za kisiasa.

5.  Vile vikwazo na kasoro za tabia ambazo Umar aliziona kwa wajumbe wa kamati ya uteuzi, kama vile tamaa, hasira, kiburi, majivuno, uroho, upen-deleo wa kidugu na shauku, n.k., sio kizuizi kwa ukhalifa. Mtu anaweza kuwa kiburi, mwenye majivuno, mnyanyasaji na mroho; bado anaweza kuwa khalifa wa Waislam. Khalifa halazimiki kuwa na tabia nzuri sana na uwezo.

Fatwa ya Mu'awiyyah juu Kamati ya Uteuzi ya Umar

Ibn Abd Rabbih anaandika katika kitabu chake maarufu, Iqd-ul-Farid (Mkufu wa kipekee), Juz. 11, ukurasa wa 203, kwamba miaka mingi baada ya Mu'awiyyah kuwa amejizatiti bara bara kwenye mamlaka, na akawa ameimarisha nafasi yake kama khalifa wa Waislam, ali-toa, siku moja, swali lifuatalo kwa mmoja wa watumishi wake wa baraza:

Mu 'awiyyah: Wewe ni mtu mwenye hekima, mjuzi na mwenye elimu. Ningependa kujua ni nini hasa kwa maoni yako, kilikuwa chanzo cha vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Uislam.

Mtumishi: Ni kuuawa kwa Uthman.

Mu 'awiyyah: Hapana.

Mtumishi: Kupanda kwa Ali kwenye madaraka.

444

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mu 'awiyyah: Hapana.

Mtumishi: Basi nitamuomba Amirul'Mu'minina anielimishe juu ya suala hili.

Mu 'awiyyah: Sawa, nitakuambia ni nini kilichokuwa chanzo cha vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Waislam. Migogoro yote na vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Waislam kiini chake kilikuwa kwenye kamati ya uteuzi ambayo Umar aliiteua kuchagua khalifa.

Mu'awiyyah alikuwa sahihi. Hizi mbegu za vita vya wenyewe kwa wenyewe ndani ya Uislam zilipandikizwa siku ile Umar alipochagua wajumbe wa kamati yake ya uteuzi. Badala ya mgombea mmoja wa ukhalifa, alifanya wagombea sita. Kama uamuzi wake wa kuteua mrithi wake ungekuwa wa moja kwa moja na wazi kama ule wa Abu Bakr ulivyokuwa, Uislam ungeepushwa na hii hali ya kiwewe na ya kutisha ya vita vya wenyewe kwa wenyewe mapema katika kazi yake. Wale Waislam waliopigana na kuuana wenyewe katika vita hivi, hawakutokana na watu wa nyakati za baadae sana; walitokana na kizazi cha wakati wa Mtume (s.a.w.w.) mwenyewe.

Vita vya wenyewe kwa wenyewe vilianza katika Uislam katika wakati ambao kanuni zake zilipaswa kuwa bado ni safi. Lakini ule mfumo wa uchaguzi ulioundwa na Umar ulikuwa na makabiliano yaliyojengeka ndani kwa ndani, na uliuchukua Uislam kupita kwenye mgawanyiko mkubwa. Sera yake ilithibitisha kuwa isiyo na manufaa, na mtindo wake wa kuwapa Waislam kiongozi kupita kwenye jopo la wateuzi ulitokea kuwa moja ya misiba mikubwa ya historia ya Uislam.

Umar na Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah swt.

Umar alisilimu mwishoni mwa mwaka wa sita wa Mwito. Miaka saba baadae, alihama pamoja na Waislam wengine kwenda Madina. Huko Madina, hawa wahamiaji (Muhajirina) walifanya mwanzo mpya katika maisha.

Hapo Madina, kulikuwa na nyakati ambapo Umar alikuwa amkumbushe Muhammad (s.a.w.w.) kwamba kwake yeye (Umar), yeye (Muhammad) alikuwa atarajie mtu ambaye ana hifadhi kubwamoyo wa ujasiri. Kama hakukubaliana naye (Muhammad), hakuwa na woga kabisa katika kuonyesha kutokukubaliana kwake. Hivyo, miongoni mwa masahaba wote, yeye (Umar) pekee alikuwa na moyo wa ujasiri wa kuonyesha hasira na dharau yake kwake (Muhammad) pale Hudaybiyya wakati yeye Muhammad alipoweka sahihi mkataba wa amani na Makuraish.

Kulikuwa na nyakati nyingine ambapo Umar aliiona ni "kazi" yake isiyopendeza "kusahi-hisha" "makosa" ya Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt. Yafuatayo ni matukio ambamo Umar alijitokeza kama mkosoaji wa matendo ya Muhammad (s.a.w.w.), Mtume

445

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wa Uislam.

Wakati Abdallah bin Ubayy alipokufa, Mtume (s.a.w.w.) alihudhuria mazishi yake, na aka-muomba Allah swt. amsamehe na kushusha rehema juu ya nafsi yake. Umar alijaribu kumshawishi asimfanyie hivyo kwa kueleza kwamba Ibn Ubayy alikuwa Munafiq.

Ni kweli kwamba Abdallah bin Ubayy alikuwa mnafiki. Lakini unafiki wake haukuwa siri kwa mtu yoyote hapo Madina. Kila mtu alijua kwamba ni mnafiki. Katika usiku wa vita vya Uhud, alikiondoa kikosi chake cha wapiganaji 300 kutoka kwenye jeshi kwa kisingizio kinachodhaniwa kuwa Waislam hawakukubali mpango wake wa vita hivyo.

Katika vita hivyo, Waislam walishindwa. Lakini walishindwa sio kwa sababu ya kuasi kwa Ibn Ubayy bali kwa sababu ya uroho wao wenyewe na utovu wa nidhamu. Kujiondoa kwa vikosi vya Ibn Ubayy hakukuathiri matokeo ya vita kwa njia yoyote ile.

Kwa vile Ibn Ubayy alichukua nafasi ya kujitenganisha katika mgogoro, Waislam walikuwa na tahadhari wakati wote juu ya nini angekifanya. Hakuweza, kwa hiyo, kuwashitukiza. Alikuwa mnafiki anayejulikana na wa "dhahiri".

Wa hatari zaidi kwa Uislam walikuwa wale wanafiki ambao walikuwa "wamefichika" machoni mwa Waislam. Waumini wa kweli waliwaona kama ni Waislam waaminifu na wakawaamini. Uaminifu huu wa Waislam juu yao uliifanya jamii ya Waislam na Dola ya Madina visiwe na uswalama sana kwa kuhujumiwa na wao. Qur'an Tukufu inashuhudia kuwepo hapo Madina, kwa idadi kubwa, ya hawa wanafiki, na imewakemea tena na tena. Walikuwa ni wao - hawa wanafiki waliojificha - na sio Abdallah bin Ubayy na wafuasi wake - ambao walikuwa chanzo halisi cha hatari kwa usalama wa Uislam.

Mtoto wa Abdallah bin Ubayy alikuwa ni mu'min wa kweli. Alijitolea kumuua baba yake. Lakini Muhammad (s.a.w.w.), mletaji wa rehma, hakumruhusu. Na wakati Ibn Ubayy alipokufa, Muhammad Mustafa alimsamehe makosa yake yote, mengi yake ambayo, alijua, yalikuwa ni matokeo ya kukata tamaa. Kabla ya Mtume (s.a.w.w.) kufika toka Makka, yeye Ibn Ubayy alitarajia kuwa mfalme wa Madina.

Kusamehe na kusahau ilikuwa ni sifa ya ukarimu wa Muhammad (s.a.w.w.). Mwanzoni, alikuwa ameonyesha ukarimu kama huo kwa waabudu masanamu wa Makka wakati alipouteka mji huo, na akatoa msamaha kwao wote. Ilikuwa, kwa hiyo, kabisa, ni "katika hulka" kwa yeye kusimamia taratibu za mazishi kwa Ibn Ubayy, kuona kwamba amezik-wa kikamilifu, na kuiombea nafsi yake, na kutoa rambirambi kwa mwanawe, licha ya upin-zani wa Umar.

Mwishoni mwa mwaka 630, Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt. alipata msiba

446

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

binafsi. Mwanawe, Ibrahim, kutoka kwa mke wake wa Kimisri, Maria yule Mkibti, alifari-ki akiwa na umri wa miezi 11 (wengine wanasema miezi 16). Muhammad (s.a.w.w.) alikuwa akimpenda sana huyo. Alihuzunika sana kwa kifo chake, na hakuweza kuyazuia machozi yake. Umar alijitolea kumtaka uangalifu yeye (Muhammad) juu ya "ukosefu wa adabu" wa kutoa machozi wakati wa kifo cha mwanawe.

Kama Umar alikuwa na haki katika jitihada zake za kumzuia Mtume wa Allah swt. katika kusikitika pamoja na wale watu wenye ukiwa wa familia ya Abdallah bin Ubayy, na katika kuomba rehma za Allah swt. juu ya nafsi yake (Ibn Ubayy); au kama alikuwa na haki ya kumzuia kulia wakati wa kifo cha mwanawe mwenyewe, basi lazima isemwe kwamba Uislam ni dini "inayo dhalilisha" sana ambayo inawanyima Waislam hata "haki" ya kusamehe maadui zao, na inawazuia uhuru wa uonyeshaji wa hisia zisizo na madhara kama huruma na huzuni. Lakini hivyi sivyo ilivyo. Uislam sio wa "kidhalilishaji." Kwa kweli ni wenye utu zaidi kati ya dini zote, na unawahimiza wafuasi wake kuwa wasamehevu, wapole, wastahifu na wenye kufikiria wengine; na unawaamrisha wasiwe ni wenye visasi kamwe. Ulipizaji kisasi ulionekana kama ni sifa au tabia ya kipagani. Uislam pia unawaamrisha Waislam, katika Aya zifuatazo za Qur'an Tukufu, kulipa wema juu ya ovu:

Usahihi-48.jpg

Na wanaouondoa uovu kwa wema (Sura ya 13; Aya ya 22)

Usahihi-49.jpg

Zuia maovu kwa kutenda yale yaliyo mema zaidi. (Sura ya 23; Aya ya 96)

Usahihi-50.jpg

Wala wema na uovu haviwezi kuwa sawa. Zuieni (maovu) kwa yaliyo mema: Hapo yule ambaye baina yako na yeye ulikuwepo uadui, atakuwa kama rafiki na mwandani. (Sura ya 41; Aya ya 34)

Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), mfasiri wa Qur'an Tukufu, alionyesha mfano wa utekelezaji wa amri hizi mbili za Mbinguni kwenye kifo cha Abdallah ibn Ubayy.

Katika kiangazi cha mwaka wa 632 A.D., Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt.,

447

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

alilala kwenye kitanda chake cha umauti ndani ya nyumba yake hapo Madina. Jambo lake la mwisho alilolitaka lilikuwa ni kutimiza amri iliyoko ndani ya Kitabu cha Allah swt., ya kuandika wasia na mirathi. Lakini Umar hakuliunga mkono wazo hili. Kwa maoni yake yeye, kuandika wasia halikuwa ni jambo sahihi kwa Mtume wa Uislam kulifanya. Kule Hudaybiyya, alimpinga Mtume lakini alishindwa katika upinzani wake; safari hii, hata hivyo, hakuwa na nia ya kushindwa. Alimpinga Mtume anayekufa, na alipata mafanikio mazuri sana katika upinzani wake. Ule wasia Mtume aliotaka kuandika, haukuandikwa kamwe.

Kama Umar alikuwa na haki katika jitihada zake za kuzuia uhuru wa kutenda wa Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah, basi ina maana kwamba Muhammad alikuwa na "makosa." Na kama yeye Muhammad alikuwa na "makosa," basi ina maana kwamba Qur'an Tukufu ilikuwa nayo ina "makosa" kwa sababu ilidai kwamba:

"Wala yeye (Muhammad) hasemi (lolote) cha matamanio yake.Hayakuwa haya ila ni wahyi alioteremshiwa."(Sura ya 53; Aya ya 3 na 4)

Kama Umar alikuwa sawa, basi Muhammad (s.a.w.w.) na Qur'an walikuwa "wamekosea." Hili ndio jawabu pekee ambalo uelekeo wa hoja kama hii unaloweza kuelekeza. Ni juu ya Waislam sasa kuamua kama hii ndio "mantiki" anayovutia kwao, na kwa hiyo, inakubali-ka kwao.

Wakati Muhammad Mustafa alipofariki katika mwaka wa A.D.632, warithi wake - Abu Bakr na Umar- hawakuchelewa kulitwaa shamba la Fadak kutoka kwa binti yake. Umar alikuwa mtu mwangalifu sana, na alikuwa labda amechochewa na moyo wake wa ujasiri "kurekebisha kosa" ambalo Muhammad (s.a.w.w.) alilifanya katika kutoa shamba la Fadak kwa binti yake mnamo mwaka wa 628 A.D.

Umar alikuwa, kwa makusudio na malengo yote, amejichagua mwenyewe kama "mdhibiti" wa maneno na matendo ya Muhammad wakati yeye mwenyewe, Muhammad (s.a.w.w.), alipokuwa bado yu hai. Kama alitangua amri zake (Muhammad) baada ya kifo chake, kuhusiana na kurithiwa kwake au na shamba la Fadak, hakuna kitu cha ajabu kuhusu hilo. Kama alikuwa na aibu katika jambo hili, basi alizitupa nje mara tu Muhammad alipokufa.

Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt., alionyesha haja yake, akiwa kwenye kitanda chake cha mauti, ya kuandika wasia wake, na kama ilivyoonyeshwa kabla, Umar alimzuia kwa kupiga kelele kwamba Kitabu cha Allah swt. kilikuwa kinatosha kwa umma wa Waislam, na kwamba haukuhitaji maandishi mengine yoyote kutoka kwake yeye.

Umar, inaonekana, kwa kweli aliamini kile alichokisema, yaani, wasia au maandishi yoyote mengine ya Mtume yalikuwa ni ziada kwani Qur'an ilikuwa na majibu ya mwisho kwa

448

Usahihi-51.jpg

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

maswali yote. Na kama kulikuwa na mashaka yoyote yaliyokuwa yamebaki katika kichwa cha mtu yeyote juu ya jambo hili, aliyaondoa pale alipokuja kuwa khalifa.

Muhammad aliishi katika mioyo ya masahaba na marafiki zake. Baada ya kifo chake, wal-itaka kuhifadhi kumbukumbu zao zote za maisha yake. Kumbukumbu hizi zilikuwa za namna mbili - maneno yake na matendo yake. Zote mbili kwa pamoja ziliunda Sunnah yake (mwenendo). Kila kitu alichosema, na kikanukuliwa na sahaba, kinaitwa Hadith au 'sunnah'.

Lakini Umar hakutaka masahaba wahifadhi kumbukumbu yoyote ile ya maneno na matendo ya Mtume. Yeye, ni dhahiri, alikuwa na mashaka mengi juu ya manufaa, kwa umma wa Kiislam, wa kumbukumbu hizi. Kwa hiyo, yeye akawakataza masahaba kunukuu simulizi za Mtume kwa mazungumzo au maandishi. Kwa maneno mengine, alizipiga marufuku Hadith za Mtume (s.a.w.w).

Ufuatao ni uthibitisho wa wanahistoria wa kisasa wawili juu ya kizuizi cha Umar juu ya Hadith:

Muhammad Husein Haykal:

"Umar ibn al-Khattab, wakati mmoja alijaribu kushughulikia tatizo la kuziweka Hadith kwenye maandishi. Masahaba wa Mtume alioshauriana nao walimtia moyo, lakini hakuwa na uhakika wa sawasawa kama aendelee. Siku moja alipata uamuzi na akatangaza: "Nilitaka Hadith za Mtume ziandikwe, lakini ninahofia kwamba Kitabu cha Allah kitaingiliwa. Hivyo sitaliruhusu hili litokee." Yeye, kwa hiyo, akabadili mawazo yake na akawaagiza Waislam katika majimbo yote: "Yeyote aliye na nyara-ka yenye Hadith ya Mtume, ataiteketeza." Hadith, kwa hiyo, zikaendelea kusimuliwa kwa mdomo na hazikukusanywa na kuandikwa mpaka wakati wa al-Mamun.

(The Life of Muhammad, Cairo, 1935)

Dr. Muhammad Hamidullah:

"Abu Dhahabi anasimulia: Khalifa Abu Bakr alikusanya kitabu, ambacho ndani yake mlikuwa na Hadith za Mtume 500, na akakikabidhi kwa binti yake Aisha. Asubuhi iliyofuata, alikichukua tena kutoka kwake na akakiharibu, akisema: "Niliandika nili-chokuwa ninakielewa; inawezekana hata hivyo kwamba panaweza kuwa na vitu ndani yake ambavyo havikubaliani kimaandishi na kile ambacho Mtume alikuwa amekisema."

Na kuhusu Umar, tunajifunza kutokana na chanzo cha Ma'amur ibn Rashid, kwamba kataka ukhalifa wake, Umar wakati mmoja alitaka ushauri kutoka kwa masahaba wa Mtume juu ya suala la kuzikusanya na kuziandika Hadith. Kila mtu aliliunga mkono wazo hilo. Hata hivyo, Umar aliendelea kusita na kumuomba Allah kwa mwezi

449

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mzima ili kupata mwongozo na ujulisho. Mwishowe, aliamua kutoifanya kazi hiyo, na akasema: "Watu wa mwanzoni walipuuza Vitabu Vitukufu na wakamakinika tu kwenye mwenendo wa mitume; Sitaki kuweka uwezekano wa kuchanganya kati ya Qur'an Tukufu na Hadith za Mtume."

(Introduction to Islam, Kuwait, uk. 34 -35, 1977)

Mmoja wa masahaba ambaye Waislam wa Sunni wanamuona kama mmoja wa mabingwa wa Hadith, alikuwa ni Abu Hurayra. Alikuwa daima yuko tayari kunukuu Hadith. Hapakuwa na wakati kamwe ambapo kumbukumbu haikumjia juu ya jambo alilokuwa amemsikia Mtume (s.a.w.w.) akilisema au jambo ambalo alimuona yeye akilifanya. Safari moja Umar alimuuliza:

"Ewe Abu Hurayra! Hebu niambie. Hivi Mtume wa Allah alikuwa hana la kufanya hapa duniani ila kunong'oneza Hadith masikioni mwako?"

Umar ndipo akamuamuru Abu Hurayra asiwe anasimulia Hadith tena.

Abu Hurayra alikuwa mtu wa makundi na mbwambwaji sana. Pale Umar alipomnyima uhuru wa kusimulia Hadith, alijihisi amefutikwa. Lakini alikuwa mtu mvumilivu, na alisubiri kimya kimya wakati atakapokuwa ameondolewa kifungo. Fursa yake ilikuja wakati Umar alipofariki, na alirudi, kwa usongo sana, kwenye kazi ya kusimulia Hadith. Leo hii, vitabu vya Hadith, vilivyoandikwa na wakusanyaji wa Sunni, vimefurika Hadith zilizosimuliwa na yeye.

Ingekuwa vizuri labda kukisia juu ya uamuzi wa Umar wa kuzipiga marufuku Hadith za Mtume (s.a.w.w.). Hivi aliamini kwamba marufuku hayo yatadumu kuliko ukhalifa wake mwenyewe? Hakuna jinsi ya kujua jibu la swali hili. Lakini hakuwa na maana ya marufuku hayo kuwa na nguvu tu wakati wa uhai wake; atakuwa amemaanisha tu yawe ni ya kudumu milele. Kama hivyo ndivyo, basi hivi alitaka kuwanyima Waislam kumbukumbu za miongozo na vigezo vya Mtume wao milele?

Muhammad Husein Haykal anasema katika kifungu kilichonukuliwa hapo juu kutoka kwenye kitabu chake kwamba Umar "alichukua hatua kwa kujaaliwa ya Allah" kuziweka Hadith za Mtume (s.a.w.w.) chini ya marufuku. Hii ina maana kwamba mamlaka ya Umar ya kuzuia Hadith, yalikuwa yamedokezwa kwenye huko kujaaliwa ambako yeye ndiye mpokeaji, na hakusita kukutekeleza. Katika kutekeleza mamlaka yake ya "majaaliwa" ali-ipuuza hata ijma ya masahaba. Ijma, kwa kawaida, ni kanuni muhimu sana katika fiqhi ya Sunni. Lakini Umar alikuwa na haki katika kuipuuza. Hata hivyo ijma ya wenye kuweza kukosea, binadamu wenye mwanzo wa kilimwengu hawawezi kamwe kuchukua nafasi ya mamlaka ya "majaaliwa" ya Umar.

450

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Lakini sheria ya Umar ya kuzuia Hadith inaacha swali moja muhimu sana, yaani, je, inawezekana kuuelewa na kuutekeleza Uislam hasa, na kuzitia amri za Allah swt., zilizomo ndani ya Qur'an Tukufu, bila ya kizijua na kuzielewa Hadith, kauli, hotuba, amri, makata-zo, vigezo mifano na maelezo ya Muhammad Mustafa (s.a.w.w.)? Ilikuwa, kwa mfano, iki-wezekana kwa masahaba kujua, kwa kusoma Qur'an tu, jinsi ya kuzisali Swala tano za kisheria kama Muhammad mwenyewe asingewafundisha? Au, wangeweza kujua ni kiasi gani cha Zaka cha kulipa, lini kilipwe na ni nani apewe kama wangekuwa hawakumuona Mtume mwenyewe akiilipa?

Bila ya Hadith, Waislam wasingeweza kamwe kuelewa itikadi ya Uislam wala wasingezin-gatia utekelezekaji wake. Kuhusu suala hili, yule mwanazuoni, mtarjuma na mfafanuzi wa Qur'an, mzaliwa wa Austria, wa siku hizi, Muhammad Asad, anaandika katika kitabu chake, Islam at The Crossroads, kama ifuatavyo:

Sunnah ya Mtume ni, (kwa hiyo) inayofuata baada ya Qur'an, chanzo cha pili cha sheria ya Kiislam ya mwenendo wa kijamii na kibinafsi. Kwa kweli ni lazima tuione Sunnah kama ndio ufafanuzi halali wa mafundisho ya Qur'an na njia pekee ya kuepu-ka kutofautiana kuhusu fasiri yake na utohozi kwenye matumizi ya kivitendo. Aya nyingi za Qur'an zina maana za kiistiari na zinaweza kueleweka kwa namna tofauti isipokuwa kama ungekuwepo utaratibu wa wazi wa fasiri. Na vipo, zaidi ya hayo, vipengee vingi vya umuhimu wa kiutendaji ambavyo havikuelezwa wazi na Qur'an.

Kusudi lililoenea kwenye Kitabu Kitukufu, ili kuwa na hakika, linalingana mwote; lakini kufasiri kutoka humo mwelekeo halisi ambao tunapaswa kuuchukua sio jambo rahisi, katika kila mas'ala. Alimradi tunaamini kwamba Kitabu hiki ni neno la Allah, lililo kamili katika muundo na lengo, uamuzi pekee wa kimantiki na kwamba kamwe hakikulengwa kutumika bila kutegemea mwongozo binafsi wa Mtume ambao umeju-muishwa katika mfumo wa Sunnah. (uk. 117-118)

Maneno ya Mtume na vitendo vyake vilikuwa ni fasiri ya kinaganaga na utekelezaji wa kanuni za Kitabu cha Allah swt. Kitabu hicho, kwa kurudia rudia na kwa kusisitizia, kime-wataka Waislam kumtii yeye, Muhammad, na kumfuata, kama katika Aya zifuatazo:

Usahihi-52.jpg

"Sema: Ikiwa ninyi mnampenda Allah, basi nifuateni mimi: Allah atakupendeni na kukufu-tieni madhambi yenu; kwani Allah ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu." (Suraya3:Ayaya31)

451

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usahihi-53.jpg

"Hakika Allah amewafanyia wema mkubwa Waunini pale alipowaletea Mtume kutoka mion-goni mwao anayewasomea Aya Zake, na anawatakasa, na anawafunza Kitabu na Hekima, ambapo kabla ya hapo walikuwa katika upotovu ulio wazi."(Sura ya 3: Aya ya 164)

Usahihi-54.jpg

"Hiyo ni mipaka ya Allah. Na anayemtii Allah na Mtume wake, Yeye Atamwingiza katika pepo inayopita mito chini yake, wakae humo daima. Na huko ndiko kufuzu kukubwa."(Sura ya 4: Aya ya 13)

Usahihi-55.jpg

"Enyi mlioamini! Mtiini Allah, na mtiini Mtume, na wenye mamlaka miongoni mwenu. Na kama mkikhitilafiana katika jambo kati yenu, basi lirudisheni kwa Allah na Mtume wake.." (Sura ya 4: Aya ya 59)

Usahihi-56.jpg

"Na hatukutuma Mtume yoyote ila atiiwe, kwa idhini ya Allah." (Sura ya 4: Aya ya 64)

Usahihi-57.jpg

"Lakini hapana! Naapa kwa Allah! Hawataamini, Mpaka wakufanye wewe ndiye muamuzi katika yale wanayokhitilafiana. Kisha wasione uzito katika nyoyo zao juu ya hukumu utay-otoa, bali wanyenyekee kabisa."(Sura ya 4: Aya ya 65)

452

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usahihi-58.jpg

"Mwenye kumtii Mtume, basi amemtii Allah.."(Sura ya 4: Aya ya 80)

Usahihi-59.jpg

"Na mtiini Allah na Mtume Wake ikiwa ninyi ni waumini."(Sura ya 8: Aya ya 1)

Usahihi-60.jpg

"Na wenye kumtii Allah na Mtume Wake, na wakamuogopa Allah na wakamcha,basi hao ndio wenye kufuzu."(Sura ya 24: Aya ya 52)

Usahihi-61.jpg

"Hakika ninyi mnayo ruwaza (kigezo) njema kwa Mtume wa Allah, kwa yule anayemtaraji Allah na siku ya mwisho, na akamkumbuka Allah kwa wingi sana." (Sura ya 33: Aya ya 21)

Usahihi-62.jpg

"Enyi mlioamini! Mtiini Allah na mtiini Mtume, Wala msiviharibu vitendo vyenu."(Sura ya

47: Aya ya 33)

Usahihi-63.jpg

"Na anachokupeni Mtume, basi kichukueni, na anachokukatazeni, basi jiepusheni nacho. Na mcheni Allah."(Sura ya 59: Aya ya 7)

Kutokana na Aya zilizotangulia, ni wazi kwamba kukataza Hadith kwa Umar kulikuwa katika njia ya mgongano wa ana kwa ana na amri za Qur'an Tukufu. Qur'an kama Neno dhahiri la Allah, na Hadith kama neno dhahiri la Mtume Wake wa Mwisho, vinaunda kitu kizima kimoja, kila kimoja kikifafanua, kikitia nguvu na kikitia nuru kile kingine. Mafaqih wa Sunni labda hawakutaka kugombana na Umar lakini walitambua kwamba hapakuwa na njia kwa wao kuachana na Hadith, na bado wakajiita wenyewe ni Waislam, na kwamba

453

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kizuizi chake (juu ya Hadith) kusingeweza kuishi pamoja na Uislam. Wao, kwa hiyo, kwa uangalifu sana wakachukua tahadhari juu ya suala hilo. "Wacha Hadith za Mtume wetu ziwe huru kutokana vizuizi," yalikuwa ndio makubaliano yao ya kimya kimya hata kama uelekezaji upya wa fikra ulikuwa mchungu kwa baadhi yao, na waliamua kujishughulisha wenyewe kwenye kazi muhimu sana ya kukusanya, kupanga kwa utaratibu na kuhifadhi, kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya vizazi vya baadae, zile kumbukumbu za maneno na matendo ya Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), Mwelekezaji na Kiongozi wao katika dunia hii na katika dunia ijayo.

454

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Uthman, Khalifa wa Tatu wa Waislam.

Kabla tu ya kifo chake, Umar alimwitaAbu Talha Ansari, na akawaambia:

"Allah ameupa heshima Uislam kupitia kwenu (Ansari), na sasa uchukue watu wako hamsini wenye silaha kuwaangalia wale wajumbe wa kamati ya uteuzi, na usiwaachie wakatawanyika bila ya kuchagua khalifa jambo ambalo ni lazima walifanye ndani ya siku tatu."

Wateuzi walianza mazungamzo yao katika nyumba ya Miswar bin Makhrama - mpwawe Abdur Rahman bin Auf. Abu Talha Ansari alianza mkesha wake wa ulinzi wa siku tatu. Amr bin Al-Aas na Mughira bin Shaaba, pia walitokeza kwenye mlango wa nyumba ya Miswar, wakiwa na shauku ya kushiriki katika utendaji wa kamati hiyo lakini wapiga mishale wa Abu Talha hawakuwaruhusu kuingia ndani.

Kwa sababu ya yale "madaraka maalum" aliyokuwa amempa Umar, Abdur Rahman bin Auf alijiona mwenyewe kama mtu muhimu wa kamati ya uteuzi. Katika kuipima hali, alielewa kwamba hakuna hata mmoja kati ya wale wajumbe wengine watano aliyekuwa tayari kuondoa jina lake kutoka kwenye ugombea huo, na kila mmoja wao alidhamiria kuendeleza dai lake kwa nguvu sana. Yeye, kwa hiyo, taratibu alijenga mkakati wake mwenyewe, na kisha akaiambia ile kamati kwamba yeye ataliondoa jina lake kutoka kwenye orodha ya wagombea kama itamruhusu, badala yake, kuwa kama mwenyekiti na mratibu wa mikutano yake.

Wajumbe wengine walikubali lakini Alialisita kumpa Abdur Rahman madaraka zaidi. Pale wajumbe wengine waliposisitiza kwamba yeye pia akubali, akamwambia:

"Nitakukubali kama mwenyekiti wa kamati ya uteuzi kama utakula kiapo kwamba hutakuwa mtumwa wa tamaa zako mwenyewe binafsi, na kwamba uamuzi wako utachukuliwa tu kwa ajili ya kupata radhi za Allah na Mtume Wake."

Abdur Rahman bila ya kusita akala kiapo cha kufanya hivyo, na hivyo akawa mwenyekiti wa kamati hiyo. Kwa kuuzulu ugombea wake, alipata uwezo zaidi ya wale wajumbe wengine, na akajitupa kwenye jukumu la "mwenye sauti katika uchaguzi."

Abdur Rahman aliitisha mfululizo wa mikutano pamoja na wagombea wengine katika jaribio la kupata ufumbuzi wa kufaa wa tatizo hilo lakini juhudi zake hazikuzaa matunda yoyote. Maamuzi ya wagombea wengine katika zile siku mbili za kwanza pia yaliishia

455

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

katika mkwamo.

Katika siku ya tatu na ya mwisho, Abdur Rahman alimtembelea kila mjumbe wa kamati nyumbani kwake mwenyewe. Katika mikutano hii ya faragha, alimuuliza kila mgombea, ni nani angependa kumuona kama khalifa kama yeye mwenyewe hakuchaguliwa. Jibu lilikuwa ni Uthman au Ali. Hii ilimaanisha kwamba chaguo limepunguzwa kwa hawa watu wawili, mmoja wao atakuwa awe ndio khalifa, lakini ni yupi hasa?

Usiku ule, Abdur Rahman, mwenye sauti katika uchaguzi, alikwenda kwa rafiki yake mkuu, Amr bin Al-Aas, akamuelezea mashaka yake, na akaongeza:

"Nimekanganyikiwa sana katika jambo hili kiasi kwamba sijapata mapumziko yoyote kwa siku tatu. Leo ndio siku ya mwisho, na bado sijapata jawabu la tatizo letu. Kinachonitia wasiwasi mimi ni ile hofu isijekuwa Ali akawa ndio khalifa. Na kabla ya Umar kufariki, nilitambua kutokana na namna yake na mwelekeo kwamba na yeye pia alizongwa na hofu kama hiyo hiyo."

Amr bin Al-Aas alikuwa mahiri zaidi kuliko Abdur Rahman au mtu mwingine yoyote yule katika aina ya mchezo kama huo ambao Abdur Rahman alikuwa akijaribu kuucheza. Akasema: "Najua hatua itakayo mshinda na kumzuia Ali." Kisha yeye akamuelezea Abdur Rahman hatua hiyo. Naye akalipokea wazo hilo zuri na akajisikia mwenye furaha na kuji-amini kwamba atamzuia Ali kuweza kuwa khalifa.

Asubuhi iliyofuatia, Waislam walikusanyika ndani ya Msikiti wa Mtume (s.a.w.w.). Ilikuwa ni siku ya maana sana maishani mwao ambapo wataweza kujua ni nani atakayekuwa mtawala wao wa baadae. Wakati huu, yule mwenye sauti katika uchaguzi na wajumbe wengine wa kamati ya uteuzi pia walifika na wakaketi kwenye nafasi zao. Baada ya kimya kifupi, yule mwenye sauti akasimama. Alitoa taarifa ya madhumuni ya kuku-sanyika huko, akasisitiza umuhimu wake, na akawataka Waislam kuzingatia uamuzi wa kamati ya uteuzi ambayo Umar aliiteua.

Hali ya hewa iliingiwa na wasiwasi, na kila mtu akawa ameamka, tayari kana kwamba atasema dakika yoyote. Abdur Rahman bin Auf, yule mwenye sauti katika uchaguzi, alimgeukia Ali, akaushika mkono wake, na akamuuliza swali lifuatalo:

"Kama tukikupa wewe kushika serikali ya Waislam, na tukakupa mamlaka juu ya mambo yao, je, utaahidi kwa dhati kwenda kwa mujibu wa Kitabu cha Allah, Sunnah ya Mtume Wake, na mienendo ya Abu Bakr na Umar?"

(Hili sharti la kutenda kwa mujibu wa mienendo ya Abu Bakr na Umar lilikuwa haliku-tamkwa na Umar mwenyewe. Lilikuwa ndio ile "hatua" ambayo Amr bin Al-Aas aliipen-dekeza kwa Abdur Rahman bin Auf. Alijua kwamba Ali hataikubali.)

456

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali alimjibu yule mwenye sauti katika uchaguzi kama ifuatavyo:

"Nitatenda kwa mujibu wa Kitabu cha Allah, na Sunna ya Mtume Wake. Na kuhusu kufuata mienendo ya Abu Bakr na Umar, nina uamuzi wangu mwenyewe, na nitautu-mia huo."

Ali alijua kile ambacho kitatokea tu baada ya hilo.

Huyu mwenye sauti katika uchaguzi akauachia mkono wake. Yeye kisha akamgeukia Uthman, na akarudia swali lile lile kwake. Uthman mara moja akakubali. Hapo yule mwenye sauti katika uchaguzi mwenyewe akawa wa kwanza kumpa kiapo cha utii. Alimpongeza kwa kuwa khalifa mpya, na akawaashiria na wengine kutoa viapo vyao vya utii kwake.

Khalifa akawa amechaguliwa. Khalifa mpya wa Waislam alikuwa ni Uthman bin Affan.

Ali aliuachia ukhalifa ukaponyoka kutoka mkononi mwake lakini hakukubaliana na utarat-ibu huo. Hakuwaona Abu Bakr na Umar kama warithi halali wa Muhammad (s.a.w.w.), na alikataa kuwafuata katika jambo lolote lile.

R.V.C. Bodley:

"Wale washauri sita walioteuliwa na Umar walikutana mara tu baada ya mazishi kumalizika. Ukhalifa kwanza ulipendekezwa kwa Ali kwa masharti kwamba atawale kwa mujibu wa Qur'an, Sunnah ya Muhammad, na taratibu zilizowekwa na Abu Bakr na Umar. Ali aliyakubali yale masharti mawili ya kwanza, na akakataa hilo la tatu. Pendekezo hilo kwa hiyo, likaondolewa na Uthman akafuatwa kwa masharti hayo hayo. Akiwa sio mwaminifu kuliko Ali, aliyakubali hayo bila ya kusita."

(The Messenger - the Life of Mhammad, New York, 1946)

Abdur Rahman alijua kwamba hakuna hata mmoja kati ya masahaba aliyekuwa na elimu zaidi ya Kitabu cha Allah swt., au ambaye alikuwa ameshikamana sana na Mtume Wake (s.a.w.w.) kuliko Ali. Lakini pale alipoitaja Qur'an na Sunnah ya Mtume, katika pendekezo lake la ukhalifa kwa wagombea, alikuwa "akijipendekeza." Kutamka kwake kwamba Ali atende kwa kulingana na amri za Qur'an na afuate Sunnah ya Muhammad, kulikuwa kwa kimbinu badala ya kibusara; kwa kuremba zaidi kuliko kawaida. Nia yake hasa ilikuwa ni katika kujifunga kwa Ali katika kufuata mienendo ya Abu Bakr na Umar, wote ambao walifanya iwezekane kwake na kwa wengine wengi kuwa matajiri na wenye uwezo mkubwa.

457

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ubepari, lile "sanamu lenye sura mbaya sana" la Nyakati za Ujahilia, na masanamu mengine ambayo Makuraish waliyaabudu hapo Makka, yalikuwa yamezikwa na Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt. Lakini baada ya kifo chake, lile sanamu la kibepari likafufuka, na lilikuwa "limerudishiwa nafasi yake" hapo Madina. Mfumo wa kibepari haraka sana ukaota mizizi katika jamii ya Kiislam, na walizama sana kiasi kwamba ikawa haiwezekani kuwang'oa. Baada ya kifo cha Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), huo mfumo wa kibepari uliendelea kupata nguvu zaidi na zaidi.

Wajumbe wote wa jopo lililoteuliwa na Umar kuchagua khalifa, walikuwa mabepari isipokuwa Ali. Walijua kwamba kama Ali angeishika serikali, angeliuua mfumo wa kibepari; angewalazimisha hao mabepari kutapika mali yote ya haramu waliyokuwa tayari wameibugia kilafi, na angehuisha ule urahisi na usafi halisi wa jamii ya Kiislam kama vile ulivyokuwa wakati wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt. Yule mwenye sauti katika uchaguzi na wale waliotajirika hivi karibuni hawakuwa na hamu ya kurudi kwenye siku zile za ukosefu wa anasa na kujinyima.

Lakini hata kama Umar hakutaka kumfanya Uthman kuwa mrithi wake, na hata kama hakuwa na upendeleo kwa mgombea yoyote, na hata kama kungekuwa hakuna njama kati ya Abdur Rahman, mwenye sauti katika uchaguzi, na Amr bin Al-Aas, Ali bado asingeweza kuwa khalifa. Kitu kimoja wajumbe wote wa kamati ya uteuzi, na Waislam wengine wengi ambao waliunda ule utawala wa kikabaila wa Waarabu walichokiogopa zaidi, kilikuwa ni kuona mtu mkali, imara na mwenye nguvu kama Ali katika nafasi ya uongozi wa mambo yao. Walijua vile vile kwamba Ali, asiye na kuyumba binafsi katika masuala ya kanuni, atakuwa mgumu kwao, na kwamba ataushurutisha umma wote kuishi kwa utii juu ya amri za Qur'an.

Lakini mtindo wa Uthman, tabia na utendaji, kwa upande mwingine, vimekuwa thabiti daima katika kuwa vya kawaida mno kiasi kwamba vingeweza kutegemewa katika kutunuku ukadiri juu ya ukhalifa. Ukadiri wake ulikuwa uwe ni uhakikisho kwamba hataingilia haki na ridhaa za wachaguzi. Kulinda maslahi yao, kwa hiyo, kulikuwa ni muhimu zaidi kwao kuliko kulinda maslahi ya Uislam.

Sifa njema za mgombea wa nafasi muhimu kabisa katika Uislam hazikuonekana popote katika fikira za yule mwenye sauti katika uchaguzi. Ukweli ni kwamba maslahi ya Uislam au sifa za mgombea yalikuwa ni mambo yaliyokuwa na umuhimu mdogo sana katika mah-esabu yake. Uamuzi wake ulitawaliwa, sio na maslahi ya Uislam, bali na nia yake katika kuendeleza hali ilivyo. Mvutano ndani ya kamati ya uteuzi, kwa hiyo, ulikuwa ni pamoja na pambano la kupimana nguvu kati ya mfumo wa kibepari na wenye kupenda usawa wa kijamii na kiuchumi wa Kiislam. Ali alifanya kila alichoweza kukifanya ili kulinda upen-da usawa lakini uwezekano ulikuwa kinyume kabisa na yeye.

458

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kuchaguliwa kwa Uthman kama khalifa kulikuwa ni ushindi kwa ubepari. Umar alikuwa ameutunga mpango wa "Shura" (kamati ya uteuzi), na alikuwa amemkabidhi Abdur Rahman bin Auf jukumu la kuutekeleza. Huyu, kama mwenyekiti wa kamati hiyo, aliki-fanya kama ni kigezo cha sharti kwamba mgombea wa ukhalifa atatii sio tu Kitabu cha Allah na kufuata Sunnah ya Mtume Wake, bali pia, afuate taratibu za Abu Bakr na Umar. Kwa hiyo aliyaweka matendo ya Abu Bakr na Umar kama ni sawa na Qur'an na Sunnah ya Mtume Wake.

Ali alikataa kuyalinganisha matendo ya Abu Bakr na Umar na Kitabu cha Allah swt. na Sunnah ya Mtume Wake (s.a.w.w.). Alikataa kuwafuata watu wenye kukosea ambao walikuwa ndio viongozi wa kisiasa wa wakati wake akijua kwamba kukataa kwake kutamgharimu kukosa utawala wa dola ya Waislam. Alidharau kiti hicho cha utawala kwa sababu bei aliyokuwa anatakiwa alipie, ilikuwa ililkuwa inapingana na Ukweli na Haki. Alitamka hadharani kwamba mienendo ya Abu Bakr na Umar haikubali. Kama mienendo yao ilikuwa haikubaliki kwake, basi ukhalifa wao pia lazima utakuwa haukukubalika kwake. Huu ni ushahidi unaothibitisha kwamba hakutoa kiapo cha utii kwao. Lakini kama Sunni wanasisitiza kwamba Abu Bakr na Umar walipokea kiapo cha utii kutoka kwake, basi watakuwa wamekichukua kutoka kwake kwa ncha ya upanga.

Ali angeweza kutamka, kama alivyofanya Uthman, kwamba alikuwa anAyakubali mashar-ti ya yule mwenye sauti katika uchaguzi, na baada ya kuchukua hatamu za uongozi mkononi mwake, angeweza kuyakataa, tena, kama Uthman alivyofanya. Wanasiasa wengi wanaona maneno matupu na usaliti ni jambo la kawaida na linalotambulika katika ujuzi wa uongozi. Lakini Ali hakuona hivyo. Kwake yeye penye nia hapakuwa na njia. Kwake yeye hizo njia pia zilikuwa ziwe za kuheshimiwa tu na za haki kama zile nia zenyewe.

Upingaji wa Ali

Ali alimwambia yule mwenye sauti katika uchaguzi:

"Sio mara ya kwanza ambapo ninyi mmewanyima warithi na watoto wa Muhammad, Mtume wa Allah swt., haki zao kwa usaliti. Kwa hili mtawajibika mbele ya Allah swt. Lakini kwangu mimi, ni vyema kuweka imani yangu kwa Allah Ambaye pekee ndie Mkweli, Mwadilifu na Mwenye kurehemu."

Yule mwenye sauti katika uchaguzi alifanya majaribio katika kujipendezesha kwa ajili ya jukumu lake kwa namna ile ile kama Abu Ubaidah bin al-Jarrah alivyofanya baada ya kuchaguliwa kwa Abu Bakr pale Saqifah lakini haikuchukua muda kabla hajajilaani mwenyewe kwa ulaghai wa kisheria na undumilakuwili katika jambo ambalo juu yake hali ya baadae ya Uislam wenyewe ulikuwa ukitegemea.

459

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abdur Rahman bin Auf, mume wa dada yake Uthman, aliishi kiasi cha kutosha kuona matunda ya kazi yake ya kuwa mwenye sauti katika uchaguzi. Aliiona rushwa ikienea kati-ka mtego wake kama pweza katika dola ya Waislam, na "alishitushwa" sana na upendeleo wa kindugu katika ajira na kutokufaa kwa khalifa aliyekuwa amemchagua kiasi kwamba alitamka kwamba hataongea naye (kulikuwa hakuna chochote kingine cha kufanya tena). Wakati fulani baadae, alipokuwa karibu ya kufa, Uthman alikuja kumuona lakini hakuzipokea salamu zake na akageuzia uso wake kuelekea ukutani. Alikufa katika hali hii, bila ya kujibizana neno na khalifa.

Dr. Taha Husain wa Misri anasema katika kitabu chake, al-Fitna-tul-Kubra kwamba Abdur Rahman bin Auf alikufa mwenye aibu tele na majuto kwa kile alichokuwa ameki-fanya kama mwenyekiti wa kamati ya uteuzi ya Umar.

Kupinga kwa Ammar bin Yasir

Ammar bin Yasir, sahaba na kipenzi cha Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), alimshutumu Abdur Rahman na mashoga zake, akisema:

"Mmepora haki za familia ya Mtume wenu, sio mara moja bali kwa kurudia rudia, na mmeziweka hizo juu ya watu ambao hawastahili kabisa."

Pongezi za Abu Sufyan kwa Uthman

Uthman alipokuwa khalifa, furaha ya Bani Umayya haikuwa na mpaka. Maisha kwao, wal-ijua, yatakuwa mazuri na ya kupendeza kuanzia hapo, na ilikuwa hivyo. Kiongozi wao, Abu Sufyan, sasa akiwa na umri wa miaka 90 na kipovu, alikuja kumpongeza khalifa mpya, na akampa ushauri ufuatao:

"Ni baada ya muda mrefu ambapo ukhalifa umekuja kwetu. Sasa upigeni kama mpira, na uutmie huo katika kuwaimarisha Banu Umayya. Haya madaraka mapya uliyonayo mikononi mwako, ni kila kitu. Ndio ukweli pekee. Hakuna kitu kingine ambacho ni cha kweli au muhimu. Pepo na moto si lolote si chochote."

"Ushauri" wa Abu Sufyan kwa Uthman ulikuwa ndio kigezo cha msukumo wa Bani Umayya kwenye Uislam, na kilikuwa kibaki bila ya kubadilishwa kwa karne yote ya umi-liki wao wa kisiasa isipokuwa katika miaka mitatu na nusu ya u khalifa wa Umar bin Abdul Aziz (R).

Kuchaguliwa kwa Uthman kama khalifa kwa mara nyingine tena kumekazia ule ukweli wa methali isemeyo kwamba pale kwenye pesa, pana nguvu.

(Charles E. Hurwitz ni mshirika wa uvamizi ambaye ananunua makampuni ya Kimarekani

460

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

na kisha anazikongoa mali zake ili kulipia deni la utwaaji wake. Anatawala himaya ya kifedha yenye thamani inayokisiwa kuwa $8.5 billion mnamo 1990. Yeye wakati mmoja alitoa $60 milion kutoka kwenye mfuko wa pensheni wa wafanyakazi wa kiwanda. Kuhusu wale wafanyakazi waliovunjika moyo, aliwakumbusha "ukweli wa maisha." Alisema: "Ipo Hadith ndogo kuhusu Utawala wa Dhahabu. Wale ambao wanayo dhahabu, ndio wanao tawala.")

Uwiano wa mamlaka ya kiuchumi na mamlaka ya kisiasa ni wa wazi sana kuweza kuhita-ji ufafanuzi au mkazo wowote. Umar aliwachagua watu matajiri sana katika Arabia yote kama wateuzi wa khalifa. Mteuzi pekee ambaye hakuwa tajiri, alikuwa ni Ali. Umar haku-taka Ali kuwa khalifa lakini hakuweza kupata sababu yoyote yenye kuelekea kuwa ya kweli ya kumuondoa Ali kutoka kwenye kamati yake ya uteuzi. Kumuondoa Ali kungeweza kufanya chuki juu ya, na uadui kwa familia na ukoo wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) kuwa ya dhahiri zaidi.

Umar aliishi na ugonjwa wa hofu isije ikawa Ali kuwa ndio amekuwa khalifa wa Waislam. Wakati mmoja iliarifiwa kwake kwamba mtu mmoja alisema kwamba baada ya kifo chake (Umar), atamtambua Ali kama khalifa. Hili lilimuogopesha sana Umar, na mara moja akawaonya Waislam dhidi ya kufanya hivyo.

John Alden Williams

(Umar alisema) "Karibu nitawaelezeni jambo ambalo Allah amependa kwamba niliseme. Ye yote yule anayelielewa na kulisikiliza, naalichukue popote anapokwen-da. Nimesikia kwamba mtu mmoja amesema, 'Kama Umar angekufa, nitamtukuza fulani' (yaani, Ali )."

(Themes of Islamic Civilization, uk. 61, 1971)

Kabla tu ya kifo chake, Umar alikuwa amemwita Abdur Rahman bin Auf chumbani kwake kwa ajili ya kikao cha faragha. Haijulikani walizungumza juu ya kitu gani kwa sababu Umar anasemekana kudai kiapo kutoka kwa Abdur Rahman kwamba ataliweka suala la mambo yaliyoongelewa kuwa ni siri kubwa ambayo Abdur Rahman alifanya.

Akimtaka Rais Nixon ajiuzulu kwenye uraisi, kufuatia uchunguzi wa Watergate huko Washington D.C., Seneta James L. Buckley (Republican) wa New York, alisema mnamo tarehe 19 Machi, 1974 kwamba:

"Mwenendo wa utawala wakati wote unaakisi na kuonyesha mwenendo wa kiongozi wake, na wasaidizi wa kiongozi huyo na mawakala wake hufanya kile wanachohisi na kuamini kwamba anawataka wao wakifanye."

Wasaidizi na mawakala wa Umar walifanya hasa kile "walichohisi" na kuamini aliwataka

461

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wao wakifanye. Miaka kadhaa kabla, Uthman bin Affan aliijaza nafasi ya katibu binafsi wa Abu Bakr. Alikuwa akiandika wasia na mirathi ya Abu Bakr wakati yeye akiwa kwenye kitanda cha mauti yake. Abu Bakr alikuwa ameanza tu kutoa imla, na Uthman alikuwa ameandika tu maneno, "Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehma, Mwenye kurehemu. Mimi,

Abu Bakr, mrithi wa Muhammad, Mtume wa Allah .." pale alipopoteza fahamu.

Lakini kabla hajarudiwa na fahamu, Uthman mwenyewe aliongeza maneno haya: "....

Ninamteua Umar kama mrithi wangu na mtawala wenu," na hivyo kuimalizia sentensi hiyo.

Uthman "alihisi" na kujua hasa kile ambacho Abu Bakr angemtaka yeye afanye. Aliendelea na akakifanya. Kitendo chake kilipata uthibisho wa Abu Bakr pale alipopata fahamu.

Abdur Rahman bin Auf "alihisi" na alijua kile ambacho Umar alimtaka yeye akifanye, na alikifanya. Akiwa amejaaliwa na utambuzi kama alivyokuwa, aliweza kusoma dalili zote katika mkondo wa sera za Umar!

Uthman bin Affan, Khalifa wa Tatu wa Waislam, 644 - 656

Uthman bin Affan alitokana na ukoo wa Umayya. Anasemekana kuukubali Uislam kupitia juhudi za Abu Bakr, na alikuwa mmoja wa wafuasi wa awali. Alikuwa mmoja wa watu matajiri wa Makka.

Uthman hakushiriki katika vita vya Badr, na alibakia Madina.

Uthman alikuwepo kwenye vita vya Uhud lakini alikimbia kuokoa maisha yake wakati Waislam waliposhindwa. Baadhi ya watoro walirudi Madina lakini sio Uthman. Sheikh Muhammad el-Khidhri Buck wa Misri anaandika katika kitabu chake, Nuur al-Yaqiin fi Siirat Sayyed al-Mursaliin (Cairo, uk.138, 1953) kwamba Uthman alikuwa na haya sana ambazo zilimzuia kuingia Madina.

Wakati wa majadiliano ya Hudaybiyya, Mtume (s.a.w.w.) alimtuma Uthman kama mjumbe wake kwa Makuraish huko Makka. Sababu ya kumtuma kwake, ilikuwa kwamba Umar alikataa kwenda, na alimlenga yeye kama mjumbe bora kwa shughuli hiyo, akijua kwamba yeye (Uthman) alikuwa ni kipenzi cha Abu Sufyan, na kwa hiyo, angekuwa salama kutokana na madhara yoyote. Uchaguzi wake haukuwa na uhusiano wowote na kufaa kwake kwa kazi hiyo.

Uthman anasemekana kuchukua nafasi kubwa katika kuandaa msafara wa kwenda Tabuk. Hapo Madina, anasemekana kwamba alinunua kisima na akakikabidhi kwa jumuiya. Wakati wa ukhalifa wake, Uthman alikusanya Aya za Qur'an na kuzipanga kama toleo

462

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

rasmi la ujumbe wa mwisho wa Allah kwa wanadamu. Kulikuwepo na nakala nyingine zilizokuwepo hadi wakati huo lakini alizikusanya na kuzichoma moto.

Watangulizi wa Uthman katika serikali ya Saqifah walikuwa ni Abu Bakr na Umar. Ingawa Abu Bakr na Umar hawakufanikisha kitu chochote cha kusifika hasa wakati wa uhai wa Muhammad (s.a.w.w.), baada ya kifo chake walijionyesha wenyewe kwamba walikuwa watu wenye uwezo wa ajabu sana. Lakini Uthman, kwa upande mwingine, alikuwa mtu wa udhaifu wa kuvutia sana, wakati wote kabla na baada ya kupanda kwenye madaraka ya watangulizi wake wawili. Mbali na kutoa michango ya kifedha kwenye baadhi ya juhudi za jumuiya, hakufanya kamwe kitu chochote cha kumtofautisha na watu wa kawaida.

Uthman alikuwa tayari amekwishastaafu, akiwa na umri wa miaka 72, wakati alipokuwa khalifa. Lakini kwa upande wake yeye, kustaafu hakukuwa ni kikwazo. Kulikuwa, kwa kweli, ni moja ya rasilimali zake chache.

Wale wateuzi walikuwa wakigumia chini ya nidhamu kali iliyokuwa imewekwa juu yao na Umar; alikatiza mwingi wa uhuru wao. Sasa kwa vile amekufa, hawakuwa na nia ya kuru-dia kwenye siku zile za mfadhaiko, na walitaka kufaidi uhuru wao. Wao, kwa hiyo, walich-agua khalifa dhaifu na mwenye umri mkubwa ambaye nguvu yake juu ya serikali, walijua itakuwa dhaifu siku zote.

Kuchaguliwa kwa Uthman kama khalifa, lilikuwa ni jibu lisiloepukika dhidi ya ugumu wa kufuata sheria wa nyakati za Umar.

Uthman alisimulia Hadith 146 za Mtume wa Uislam (s.a.w.w.).

Ndoa za Uthman

Wakati mmoja kulikuwa na wasichana watatu wakiishi kwenye kaya ya Khadija. Majina yao yalikuwa ni Zainab, Ruqayya na Umm Kulthum. Zainab aliyekuwa mkubwa kati ya hao watatu, alikuwa ameolewa na mtu mmoja Abul-'As ibn ar-Rabi wa Makka. Mtu huyu alipigana dhidi ya Mtume (s.a.w.w.) katika vita vya Badr, na alitekwa na Waislam. Ili kufidia uhuru wake, mke wake alituma kwa Mtume (s.a.w.w.), mkufu ambao wakati mmoja ulikuwa mali ya Khadija, na alikuwa amempa yeye kama zawadi wakati wa harusi yake. Abul-'As aliachiwa huru; akarudi Makka, na akampeleka Zainab Madina kama alivyoahidi kufanya. Zainab, hata hivyo, alifariki mara tu baada ya kuwasili Madina. Baadae, Abul-'As pia akaenda Madina, akasilimu, na akaishi pamoja na Waislam.

Wale wasichana wengine wawili, Ruqayya na Umm Kulthum, waliolewa na Utba na Utaiba, watoto wa Abu Lahab na Umm Jamiil. Umm Jamiil alikuwa dada yake Abu Sufyan, kiongozi wa ukoo wa Umayya. Abu Sufyan, kwa hiyo, alikuwa ni mjomba wao

463

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Utba na Utaiba.

Haijulikani kwa kiwango chochote cha uhakika hawa wasichana watatu walikuwa ni akina nani. Wengi wa wanahistoria wa Sunni wanadai kwamba walikuwa ni mabinti wa Muhammad na Khadija. Kwa mujibu wa wanahistoria wengine, walikuwa ni mabinti wa Khadija kwa ndoa yake ya mwanzoni.

Waislam wa Shi'a wanakataa. Wanasema kwamba Zainab, Ruqayya na Umm Kulthum hawakuwa mabinti wa Muhammad na Khadija; kwa kweli, wala hawakuwa mabinti wa Khadija kwa ndoa yoyote ya mwanzo; walikuwa mabinti wa dada (mjane) yake Khadija. Dada yake Khadija pia alifariki, na katika kufariki kwake, yeye (Khadija) aliwachukua wasichana hao watatu nyumbani kwake mwenyewe na akawalea kama watoto wake mwenyewe.

Kwa mujibu wa Waislam wa Shi'ah, Muhammad na Khadija walikuwa na watoto watatu na sio sita. Wawili wa kwanza wao - Qasim na Tayyib au Tahir - walikuwa wavulana, na wote walifariki katika utoto wao. Wa tatu na mtoto wa mwisho alikuwa msichana - Fatima Zahrah. Yeye alikuwa ndiye mtoto wao pekee ambaye hakufariki katika uchanga wake.

Hawa wasichana, Zainab, Ruqayya na Umm Kulthum - hawangeweza kuwa mabinti wa Mtume wa Uislam. Kama wangekuwa, asingeweza kuwaozesha kwa waabudu masanamu ambao waume za wote watatu walikuwa. Ni kweli kwamba wasichana wote watatu wali-olewa zamani kabla ya kuchomoza Uislam. Lakini bado hakuvunja amri zozote za Qur'an katika wakati wowote - kabla na baada ya alipofanywa kuwa Mtume wa Allah swt. Na Qur'an iko wazi juu ya makatazo ya ndoa ya mwanamke wa Kiislam kwa pagani.

Ukatazaji wa ndoa ya mwanamke Muislam na mshirikina unatokea kwenye Aya zifuata-zo za Qur'an Tukufu:

Usahihi-64.jpg

"Msiwaoze (mabinti zenu) kwa makafiri."(Sura ya 2: Aya 221)

Usahihi-65.jpg

"Wanawake hao (walioamini) sio halali kwa makafiri, wala hao makafiri hawahalalikii wanawake hao." (Sura ya 60: Aya ya 10)

Kuna Aya nyingine katika Qur'an ambazo, bila kurejelea mahsusi kwenye ndoa,

464

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

zinafanya ugumu kwa Muislam kuozesha binti au mabinti kwa muabudu sanamu. Baadhi ya hizo ni:

Usahihi-66.jpg

"Basi laana ya Allah ipo juu ya makafiri."(Sura ya 2: Aya ya 89)

Usahihi-67.jpg

"Hakika Allah ni adui wa makafiri."(Sura ya 2: Aya ya 98)

"Enyi mlioamini! Hakika washirikina ni najisi."(Sura ya 9: Aya ya 28)

Hivi anaweza Muislam, hata kama ni wa "kiasi kidogo" au Muislam wa "takwimu" (Muislam jina tu), kuamini kwamba Muhammad (s.a.w.w.), Mletaji na Mfasiri wa Qur'an Tukufu, angeweza kuwaozesha binti zake kwa watu wale ambao Allah swt. amewalaani; ambao ni maadui Zake; na ambao ni najisi?

Kwa mu'min, Aya za Qur'an zilizotajwa hapo juu, ni ushahidi usiokanushika kwamba Zainab, Ruqayya na Umm Kulthum, wote watatu wakiwa wameolewa, wakati mmoja, kwa waabudu masanamu watatu huko Makka, walikuwa sio mabinti wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) na Khadija.

Ikumbukwe pia kwamba Mtume (s.a.w.w.) ambaye alikuwa mpenzi sana wa watoto, hakusema lolote kamwe kuhusu Zainab, Ruqayya na Umm Kulthum. Wazazi wanatoa mapenzi sawa kwa watoto wao wote, na hawafanyi ubaguzi wowote kati yao. Lakini alikuwa akitoa sifa za juu kabisa juu ya binti yake, Fatima Zahrah. Kuamua kulingana na Hadith, wala hakuwa na habari kwamba wanawake watatu wanaoitwa Zainab, Ruqayya na Umm Kulthum walikuwa wanaishi.

Ruqayya na Umm Kulthum walikuwa bado wanaishi na waume zao wakati wahyi mpya, Sura ya 111 ya Qur'an, iliposhuka kutoka Mbinguni. Katika Sura hii Abu Lahabi na mke wake, Umm Jamiil, wakwe za Ruqayya na Umm Kulthum, walilaaniwa kwa upotovu wao.

Wahyi huu mpya uliamsha ghadhabu za wawili hawa wazee, na waliwaamuru vijana wao kuwataliki wake zao, na kuwarudisha nyumbani kwa Khadija. Vijana hao waliwatii wazazi

465

Usahihi-68.jpg

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wao, wakawataliki wake zao nao (hao wake) wakarudi nyumbani kwa Khadija. Muda fulani baadae, Ruqayya aliolewa na Uthman bin Affan. Alifariki mnamo mwaka A.D. 624. Baada ya kifo chake, dada yake, Umm Kulthum, aliolewa pia na Uthman. Alifariki miaka michache baadae.

Ile miaka ya huko Makka, baada ya kutangazwa kwa Uislam, na ile miaka ya awali huko Madina, ilikuwa ya majaribu kwa hatari nyingi juu ya Muhammad (s.a.w.w.). Kila siku ilileta changamoto mpya kwake. Aliyaweka maisha yake kwenye mkondo wa moto mara tu alipotoka nje ya nyumba yake. Na bado Ruqayya na Umm Kulthum hawatajwi kamwe wakitoa huduma kwa baba yao. Kwa upande mwingine, Fatima Zahrah alimsaidia baba yake katika dharura mbali mbali, kote Makka na Madina. Ruqayya na Umm Kulthum wote walikuwa wakubwa kuliko Fatima kwa miaka mingi, na walipaswa kumtia moyo na kum-fariji baba yao wakati wowote alipokuwa ameonewa na waabudu masanamu hapo Makka au alipokuwa amejeruhiwa katika vita huko Madina lakini kamwe hawakufanya hivyo.

Wanahistoria wa Sunni wamempa Uthman cheo cha Dhun-Nuurayn ambacho kina maana ya "mmiliki wa nuru mbili," kwa sababu aliwaoa, kulingana na wao, mabinti wawili wa Mtume (s.a.w.w.), heshima ambayo hakuipata hata Abu Bakr na Umar!

Uthman alikuja kuwa mwenye kumiliki nuru mbili baada ya kuwaoa Ruqayya na Umm Kulthum. Lakini wasichana wote hawa wawili walikuwa wameolewa na waabudu masanamu, yaani, Utba na Utaib, watoto wa Abu Lahabi, kabla ya kuolewa na Uthman. Kwa hiyo, kila mmoja wa hawa watoto wawili wa Abu Lahabi walipaswa kuitwa Dhun-Nuur -mwenye kumiliki nuru moja. Kila mmoja wao, Utba na Utaib, alikuwa mmiliki nuru moja ambayo aliirithisha kwa Uthman, hivyo kumfanya yeye kuwa mmiliki wa nuru mbili. Hata hivyo, nuru hizo zilibakia hivyo hivyo; ni umiliki tu ndio uliobadilika!

Matukio Makuu ya Ukhalifa wa Uthman

Mnamo A.D.645, kulikuwepo na maasi katika majimbo ya Azerbaijan na Armenia, na yal-izimishwa.

Mwaka 647, Mu'awiyah bin Abu Sufyan, gavana wa Uthman huko Syria, aliivamia Asia Ndogo na akaiteka Ammuria.

Mnamo mwaka 648, Abdallah bin Saad bin Abi Sarh, gavana wa Uthman huko Misri, ali-iteka Tripoli huko Libya.

Hawa wote Mu'awiyah na Abdallah bin Saad bin Abi Sahr walijenga manowari na wakayashinda majeshi ya majini ya Byzantine upande wa Mediterranian ya Mashariki.

466

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mnamo mwaka 649 manowari za Muawiyyah ziliteka Cyprus.

Mnamo mwaka 651 majemedari wa Uthman waliteka Hirat huko Afghanistan.

Mnamo mwaka 652, nakala rasmi ya kwanza ya Qur'an Tukufu ilitengenezwa hapo

Madina, na nakala zake zikasambazwa kwenye majimbo yote.

Mnamo mwaka 652-54, Abdallah bin Aamir, gavana wa Uthman wa Basra, alimtuma

jemedari wake, Abdur Rahman bin Samira upande wa mashariki, ambako aliteka Balkh

huko Khurasani, na Kabul na Ghazni huko Afghanistani. Ushindi huu mpya uliifanya

himaya ya Waislam yenye kupakana na bara kubwa la Pakistani ya Kihindi.

Upendeleo na ukabila katika Ukhalifa wa Uthman

Uthman aliwapenda watu wa ukoo wake, Bani Umayya, kwa kiwango ambapo mapenzi yake yaligeuka kuwa ni maradhi. Bani Umayya walikuwa ndio maadui wakubwa wa Uislam, na walipigana dhidi ya Mtume wake kwa zaidi ya miongo miwili. Sasa ghafla, Uthman aliwafanya ni mabwana wa himaya ya Waislam. Yeye mwenyewe akawa kibara-ka wao, na wakachukua hatamu za serikali mikononi mwao wenyewe. Watawala wa kweli wa himaya hiyo, katika ukhalifa wa Uthman, walikuwa ni Marwan (binamu na mkwewe Uthman) na Hakam bin Abul-Al-Aas (ami yake Uthman na baba yake Marwan).

Uthman alifungua milango ya hazina ya umma kwa ndugu zake. Aliwapa zawadi nono, maeneo makubwa na vyeo vya juu. Kisha, kana kwamba hajawafanyia vya kutosha, akawakataza wenyeji wa Madina kuchunga ngamia na ng'ombe wao kwenye malisho karibu na mji. Malisho haya yalikuwa yamefanywa wakfu na Mtume (s.a.w.w.) lakini kwa mujibu wa sheria mpya za Uthman, wanyama wanaoweza kuchungwa humo ni wale tu waliokuwa ama wake yeye au wa Bani Umayya. Mtume (s.a.w.w.) alikuwa amewaambia Waislam kwamba ile ardhi yote iliyokuwa inanyweshwa kwa mvua, ilikuwa ni mali ya umma wote, na kwa hiyo, wanyama wa watu wote wanaweza kuchungwa humo. Alikuwa amewaambia kwamba ardhi hizi haziwezi kutwaliwa na mtu yoyote kwa matumizi binaf-si kama ilivyokuwa imefanyika Nyakati za Ujahilia.

Qur'an Tukufu imeelezea Hadith ya Nabii Saleh katika sura yake ya saba (Al-A'raaf). Kwa mujibu wa Hadith hii, watu wenye viburi na majivuno wa nyakati za Nabii Saleh, wali-wazuia watu wanyonge na dhaifu na ng'ombe wao njia ya kufikia kwenye chemchemi za maji. Ilikuwa ni kwa kuingilia kati kwa Saleh tu ambako kulikowafanya waweze kupata maji kutoka kwenye chemchemi hizo. Kama maji vile, na malisho pia yalichukuliwa kama zawadi ya bure ya Allah swt. Kwa viumbe wake lakini wale wenye kiburi waliwanyima viumbe hao. Kile kilichokuwa kimefanya na matajiri na wenye uwezo wa wakati wa Thamuud, yalikuwa yakifanywa hapo Madina na matajiri na wenye uwezo wa mji huo -Bani Umayya. Waliunda kikundi chenye mawazo kama hayo, na kukamata ngazi zote za mamlaka.

467

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Serikali hapo Madina ikageuka kuwa fungamano la kurugenzi ya mabinamu, mashemeji na ndugu wengine wa Uthman. Waislam wengine hawakuwa na haki ndani yake. Watu muhimu ndani ya "kurugenzi" hiyo walikuwa:

Hakam bin Abul Al-Aas

Hakam alikuwa ami yake Uthman. Huko Makka, alikuwa mmoja wa majirani wa Muhammad (s.a.w.w.), na mmoja wa wachokozi wake. Alikidhihaki Kitabu cha Allah swt., na alimfanyia mzaha Mtume Wake.

Mnamo mwaka 630 Mtume (s.a.w.w.) aliiteka Makka ambapo Hakam, mwanawe Marwan na Bani Umayya wengine wengi "waliukubali" Uislam. Lakini Hakam na mwanawe hawakuweza kamwe kuusHind uadui wao kwa Uislam na Mtume wake. Walipoweza kuud-huru Uislam, walifanya hivyo. Hatimaye, Mtume (s.a.w.w.) akawafukuza kutoka Madina. Wakati alipofariki, na Abu Bakr alipokuwa khalifa, Uthman alimuomba kumruhusu ami yake na mkwewe kurudi Madina lakini alikataa. Wakati Umar alipokuwa khalifa, Uthman alimbembeleza awaruhusu wawili hawa waliotengwa na jamii kurudi Madina lakini yeye pia alikataa. Ndipo Uthman akawa khalifa, na yeye, kwa kweli, hakupoteza muda wowote katika kuwarudisha Madina, na kutoa heshima kubwa sana juu yao.

Yaquubi, mwanahistoria huyu, anasema kwamba wakati Hakam alipoingia Madina, alikuwa amevaa matambara machafu kama omba omba lakini alipotoka kwenye kasiri la Uthman, alikuwa amevaa hariri za thamani sana na zilizotariziwa. Uthman alimteua Hakam kama mkusanyaji wa Zaka kutoka kwenye kabila la Banu Qaza'a. Baladhuri, mwanahistoria, anasema kwamba Hakam alikusanya dirham 300,000, na alipozileta kwa khalifa, yeye akamrudishia ziwe zake na azitumie.

Yaquubi amemnukuu mtu fulani anayeitwa Abdur Rahman ibn Yasir katika Historia yake kama ifuatavyo:

Kazi ya afisa ilikuwa ni kukusanya kodi kutoka kwa wafanya biashara wa masoko ya Madina. Jioni moja niligundua kwamba Uthman, khalifa, alimjia, na akamtaka yeye amlipe Hakam pesa zote alizokuwa amekusanya siku ile. Ilikuwa ni kawaida ya Uthman kutoa zawadi kutoka kwenye hazina ya umma kwa watu wa familia yake. Mkusanya kodi huyo alijaribu kumdanganya Uthman na akasema kwamba ataziwa-muhurisha atakapokuwa amekusanya zote zilizokuwa bado kulipwa. Lakini Uthman akamwambia: "Wewe ni mtunza hazina wangu, fanya kile ninachokuambia ufanye." Yule mkusanyaji akajibu kwa ukali kwamba yeye ndiye mtunza hazina sio wa Uthman wala wa ndugu zake bali wa Waislam tu. Asubuhi iliyofuata, afisa huyo alikuja Msikitini, na akihutubia mkusanyiko, akasema: "Enyi Waislam! Uthman anasema kwamba mimi ni mtunza hazina wake. Mimi sio. Mimi ni mtunza hazina wa Waislam. Sitaki kuwa mtunza hazina wake." Kisha akazitupa zile funguo za hazina

468

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mbele ya Uthman, na akatoka nje. Uthman akaziokota zile funguo, na akazitoa kwa Zayd bin Thabit.

Marwan bin al-Hakam

Marwan alikuwa ni mtoto wa Hakam na ni binamu wa karibu wa Uthman. Alikuwa amemuoa binti ya Uthman, Umm Aban.

Marwan alikuwa "waziri mkuu" wa Uthman. Aligawanya zawadi kutoka kwenye hazina ya umma kwa yeyote aliyemtaka, na alizigawa nafasi za mamlaka katika serikali kwa washabiki wake. Na pia aliuweka mhuri wa khalifa kwenye milki yake na aliufanyia matu-mizi holela na mabaya. Uthman alikuwa mikononi mwake, na alitekeleza ushauri wake kiupovu.

Baada ya mapigano yenye mafanikio ndani ya Afrika, mmoja wa majemedari wa Uthman alimpelekea ngawira za vita yeye huko Madina. Ngawira hii ilikisiwa kuwa ya vipande nusu milioni vya dhahabu. Uthman alivitoa vyote kwa Marwan.

Baladhuri, yule mwanahistoria, amemnukuu Abdallah bin Zubeir kama ifuatavyo:

"Katika mwaka wa 27 Hijiria, Uthman alitutuma kwenye mpaka huko Afrika. Kaka yake wa kunyonya, Abdallah bin Saad bin Abi Sarh, alikuwa ndiye mkuu wa jeshi hilo. Aliteka viwango vikubwa vya ngawira; akaweka nne ya tano yake kwa ajili ya jeshi hilo, na akapeleka moja ya tano yake kwa Uthman huko Madina. Uthman akaitoa yote kumpa Marwan."

Katika safari nyingine, Uthman alimpa mkwe wake dirham milioni nne kutoka kwenye hazina ya umma. Alilifanya shamba la Fadak pia kuwa zawadi kwake. Marwan alikuwa ajionyeshe mwenyewe kama mfanya kazi hodari katika ukhalifa wa Uthman, na alionye-sha tabia ya kiunyonya damu ya upokonyaji.

Harith bin al-Hakam

Harith, mdogo wake Marwan, alikuwa amemuoa binti wa pili wa Uthman. Alipokea zawadi ya dirham 300,000 kutoka hazina. Baladhuri anasema kwamba wakati mmoja ngamia fulani walipelekwa kwa khalifa kama sehemu ya Zakat, na aliwatoa wote kwa Harith.

Abdallah bin Khalid

Abdallah bin Khalid alikuwa mkwe we mwingine wa Uthman. Wakati alipompa binti yake, alimuamuru Abdallah bin Aamir, gavana wa Basra, kumpa yeye (Abdallah bin Khalid) dirham 600,000 kutoka kwenye hazina ya umma.

469

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Walid bin Aqaba

Walid alikuwa mtoto wa Aqaba bin Abi Mu'ait. Aqaba alikuwa mume wa kwanza au wa pili wa mama yake Uthman. Huko Makka, alikuwa pia ni jirani ya Muhammad, na kama Umm Jamiil, yeye pia alikusanya takataka na kuzitupa mlangoni kwake Muhammad (s.a.w.w.). Alipigana dhidi ya Mtume (s.a.w.w.) huko Badr, akatekwa, na kwa amri yake, akauawa.

Walid na kaka zake - ndugu wa kuzaliwa nao Uthman - walimuhurimu wakati Makka ilipotekwa.

Safari moja, Mtume (s.a.w.w.) alimtuma Walid kwa kabila la Banu Mustalaq kwenda kuku-sanya kodi. Aliondoka Madina lakini mara akarudi na kumwambia Mtume (s.a.w.w.) kwamba hao Banu Mustalaq wameukana Uislam, na wamekataa kulipa kodi zao.

Mtume (s.a.w.w.) alishangazwa kuyasikia haya. Lakini kabla hajalichunguza suala hilo, viongozi wa Banu Mustalaq wenyewe waliwamuhuri Madina kuja kulipa kodi zao. Walimhakikishia Mtume (s.a.w.w.) kwamba wao walikuwa ni Waislam wa kweli. Walid hakuwa amewatembelea kamwe.

Ilikuwa ni baada ya tukio hili ambapo Aya ifuatayo ilishushwa kwa Mtume wa Allah swt:

Usahihi-69.jpg

"Enyi mlioamini! Kama akikujieni fasiq (mtu mwovu) na habari yoyote ile, ichunguzeni kwanza, msije mkawadhuru watubila ya kujua, na baadaye mkaja kujuta kwa mliyoyaten-da."(Sura ya 49: Aya ya 6)

Kilikuwa ni Kitabu Cha Allah swt. Kilichomwita Walid fasiq, na alikuja kujulikana kwa jina hili daima baadae.

Umar bin al-Khattab alikuwa amemwambia Uthman kwamba kama atakuwa khalifa, amteue Saad bin Abi Waqqas kuwa gavana wa Kufa. Uthman akawa khalifa, na akamteua Saad kuwa gavana wa Kufa kama alivyokuwa ametaka Umar. Lakini ndani ya mwaka mmoja, Uthman akamfukuza Saad na akamteua Walid katika nafasi yake kama gavana mpya.

Mara tu Walid alipojikuta mwenyewe katika milki ya jimbo hilo tajiri, akawa mlevi, wa vyote, madaraka na mvinyo. Alikuwa mlevi wa kutupwa. Alikuwa amelewa hata

470

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

alipowaongoza Waislam kwenye Swala. Asubuhi moja, aliingia Msikitini akiwa katika hali ya ulevi. Aliongoza Swala, na akatapika katika qibla cha Msikiti. Habari za ulevi wake zikawa zinazidi mno kwamba hata Uthman akashindwa kuzifumbia macho, na akalazimi-ka kumwita arudi Madina. Badala yake, Uthman alimteua Said bin Al-Aas kama gavana mpya wa Kufa.

Said bin Al-Aas

Baba yake Said, adui kichaa wa Mtume wa Allah swt., aliuawa katika vita vya Badr. Baada ya kifo chake, Uthman alimtwaa mwanawe, na akamkuza humo nyumbani mwake mwenyewe. Katika mwaka wa 30 Hijiria, Uthman alimfukuza Walid na akamteua Said kuwa gavana mpya wa Kufa. Alimpa pia zawadi ya dirham 100,000 kutoka kwenye hazi-na ya dola.

Kama watu wengine wa ukoo wake, Said pia alizichukulia hazina za umma kama utajiri wake binafsi, na akazitumia kama alivyotaka. Kama mtu yoyote alilalamika, alimnya-mazisha kwa mamlaka yake ya "kipolisi". Aliweza kumfanya mtu yeyote apigwe na ali-weza kufanya nyumba ya mtu yeyote ichomwe moto.

Magavana walikuwa wakilipora kila jimbo katika himaya hiyo. Walielekea kuwa baraka za kimya kimya kama sio uhimizaji wa dhahiri wa khalifa. Bila ya kukwepa, wasiwasi ulian-za kuchemka na kuunguza pole pole. Uthman aliambiwa kwamba siku moja utakuja kutokea mlipuko. Akishitushwa na kutoridhika kunakozidi kukua na kuongezeka kwa malalamiko, aliitisha mkutano wa magavana wake wote. Walikuja, wakampa ushauri wa juujuu, kasha wakatawanyika. Said bin Al-Aas alikuwa pia miongoni mwao. Lakini baada ya mkutano ule aliporudi Kufa, wakazi wa mji ule walimzuia karibu na Qadsiyya, na wakamwambia kwamba hawatamruhusu kuingia Kufa. Hakuweza kuingia Kufa, na akaru-di Madina. Katika nafasi yake, Uthman akamteua Abu Musa al-Ashari kama gavana mpya.

Abdallah bin Saad bin Abi Sarh

Huyu Abdallah alikuwa ni ndugu wa kunyonya wa Uthman. Baba yake, Saad bin Abi Sarh, alikuwa mmoja wa munafiqiin wa Madina.

Abdallah, wakati mmoja, alikuwa mmoja wa waandishi wa Mtume (s.a.w.w.). Wakati Mtume alipomtakia Aya yoyote ya Qur'an, aliigeuza kwa kubadili alama zake za kuto-fautisha matamshi au herufi au maneno. Mara akakamatwa na Mtume (s.a.w.w.) akam-fukuza kutoka Madina. Akaukana Uislam, na akaenda Makka, na akaanza kueneza habari kwamba Muhammad (s.a.w.w.) mwenyewe ndiye aliyeziunda zile Aya za Qur'an, na akadai kwamba ni wahyi kutoka Mbinguni.

471

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wakati Makka ilipotekwa, Mtume (s.a.w.w.) aliamuru kwamba Abdallah auawe kama kafir hata kama akiwa ndani ya Al-Kaaba yenyewe. Lakini Uthman alimudu kumficha ndani ya nyumba yake mwenyewe. Baadae, wakati hali iliporudi kuwa ya kawaida, alimleta mbele ya Mtume (s.a.w.w.) na akasema kwamba alikuwa anaomba msamaha na pia alikuwa anataka kutoa kiapo cha utii. Lakini Mtume hakutoa mkono wake, na akakaa kimya cha kulazimisha kwa muda kiasi cha kutosha. Uthman alimuombaomba sana yeye amsamehe Abdallah. Hatimae, akamsamehe. Lakini mara tu Uthman na Abdallah walipotoka machoni kwa Mtume, aliwageukia wale waliokuwa karibu naye, na akasema: "Nilikuwa kimya kwa muda mrefu kiasi kile nikitegemea kwamba mmoja wenu angemuua yule." Baladhuri anaandika ndani ya kitabu chake, Ansab-ul-Ashraf (uk. 358):

"Mtume akasema: 'Hivi hakuwepo mtu yoyote kati yenu ambaye angeweza kumuua mbwa huyu kabla hajapata msamaha?"

Umar bin al-Khattab akajibu: 'Ewe Mtume wa Allah, kama ungetuashiria sisi, tunge-muua.' Mtume (s.a.w.w.) akasema: 'Nisingeweza kuwaashirieni. Kufanya hivyo kusingenistahili mimi."

Pale Uthman alipokuwa khalifa, alimteua Abdallah kuwa gavana wa Misri. Kwa kuteuli-wa kwake, utawala wa kidhalimu na unyonyaji ulianza huko Misri. Neema ya Misri ikageuka kuwa matatizo; ustawi ukageuka kuwa dhiki. Kila mmoja alimchukia huyo gavana mpya. Na huyu gavana akawa na mgongano na Muhammad ibn Hudhaifa.

Baba yake Muhammad, Hudhaifa, alikuwa mmoja wa wafuasi wa awali kabisa wa Uislam. Alikufariki akiwa anapigana kwenye vita vya Yarmuk. Wakati wa kifo chake, Uthman alichukua dhima ya Muhammad, mwanawe mdogo, na akamlea. Alipokua, aliomba ruksa ya kwenda kwenye vita vya kigeni. Uthman alimruhusu kuandamana na Abdallah bin Saad kwenda Misri kama mmoja wa washauri wake.

Muhammad bin Hudhaifa alikuwa muadilifu na mchamungu sana, na alitumia muda wake mwingi sana katika ibada. Wakati rushwa na ufisadi vilipoinua vilipozidi katika utawala, alimuonya Abdallah, na akamhimiza kurudisha serikali nzuri. Lakini Abdallah hakuusikia maonyo hayo mazuri. Hata hivyo, Muhammad aling'ang'nia juhudi zake za kumrekebisha. Abdallah, hata hivyo, alionekana kuwa na, kama Marwan, dalili za upotovu katika tabia yake, na alifurahia kufanya yale tu ambayo amekatazwa kuyafanya.

Hatimae, Muhammad akapoteza matumaini. Kutoka muonyaji wa kirafiki na mwenye huruma, aligeuka na kuwa mkosoaji aliyezinduka na mkali - kwanza wa Abdallah bin Saad, na baadae wa Uthman mwenyewe kwa kumchagua kama gavana wa Misri mtu kafiri ambaye kuuawa kwake kuliamrishwa na Mtume wa Allah swt. mwenyewe.

472

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Watu wa Misri walimpenda Muhammad bin Hudhaifa kwa uaminifu wake na ujasiri wake katika kumkosoa huyu gavana mpotofu, na walimsaidia. Abdallah alimwandikia Uthman kwamba huyu kijana aliyemlea (yeye Uthman), alikuwa anaeneza uchochezi wa maasi dhidi ya serikali, na kwamba kama hakutafanyika lolote la kumzuia, hali itamshinda kuid-hibiti.

Uthman hakujua la kufanya. Ilionekana kwake kama angeweza kuyanyamazisha malalamiko ya Muhammad kwa vipande vya dhahabu na vya fedha. Yeye, kwa hiyo, alimpelekea dirham 30,000 na vipande vingi vya vitambaa venye thamani kubwa kama zawadi. Mwanzo wa mchezo huu, bahati mbaya kwa Uthman, ulimgeukia mwenyewe. Muhammad alizileta zile pesa na vitambaa ndani ya Msikiti mkuu, akavirundika vyote chini mbele ya Waislam, na akasema:

"Enyi Waislam! Mnaona kile ambacho Uthman anajaribu kukifanya? Anajaribu kuin-unua Imani yangu. Ametuma sarafu hizi na vitu hivi kwangu kama hongo."(Tarikh Kamil: Kamil ibn Athiir, juz.3; uk.135)

Uthman aliandika barua nyingi sana za kutuliza kwa Muhammad, na akamkumbusha kwamba alikuwa na deni la shukrani kwake. Lakini Muhammad alizipuuza, na wasiwasi juu ya Abdallah bin Saad uliendelea kukusanya kasi.

Viongozi wa Waislam wa Misri waliitisha mkutano ambao ndani yake waliamua kutuma ujumbe kwenda Madina kadai kutoka kwa Uthman kufukuzwa kwa Abdallah bin Saad.

Baada ya kuondoka kwa ujumbe wa Misri, nafasi ya Abdallah ikawa kama hailindiki. Kwa kuogopa mapinduzi, yeye pia aliondoka Misri kwenda Madina, upande, kwa kujitetea mwenyewe mbele ya baraza la khalifa. Katika kutokuwepo kwake, Muhammad ibn Hudhaifa alishika madaraka ya serikali.

Wakati Abdallah alipofika Elath, alisikia kwamba kasiri la Uthman limezingirwa, na kwamba amewekwa kizuizini humo ndani yake. Alionelea kwamba isingekuwa salama kwa yeye kwenda Madina, na akaamua kurudi Misri. Lakini hapo mpakani, alijulishwa kwamba Muhammad ibn Hudhaifa ameagiza kwamba azuiliwe, na asiruhusiwe kuingia tena Misri. Papo hapo, akaenda Palestina akisubiri mambo yatakavyojiri huko Madina. Kwa wakati huo, Uthman aliuawa huko Madina, na pale Abdallah aliposikia habari hizo, aliondoka Palestina na akaenda Damascus kuishi huko chini ya ulinzi wa Mu'awiyyah.

473

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Magavana Wapya wa Majimbo Kufa

Katika mwaka wa kwanza wa ukhalifa wa Uthman, Saad bin Abi Waqqas alikuwa ndio gavana wa Kufa. Kisha Uthman akamfukuza, na akamteua kaka yake wa karibu, Walid bin Aqaba, kama gavana mpya wa Kufa.

Basra

Umar alikuwa amemteua Abu Musa al-Ashari kama gavana wa Basra. Uthman akamfukuza, na akamteua binamu yake mwenyewe, Abdallah bin Aamir, kama gavana mpya.

Syria

Umar alikuwa amemteua Muawiyyah bin Abu Sufyan kama gavana wake wa Syria. Uthman alimthibitisha kama gavana wake katika jimbo lile.

Misri

Amr bin Al-Aas aliiteka Misri, na Umar alikuwa amemteua yeye kama gavana wa jimbo hilo. Uthman alimfukuza, na badala yake, alimteua ndugu yake mwenyewe wa kunyonya, Abdallah bin Saad bin Abi Sarh. Mtu huyu alikuwa ni kafiri, na Mtume (s.a.w.w.) aliamu-ru kuuawa kwake lakini aliisimamisha hukumu hiyo wakati Uthman alipomuombea msamaha. Hivyo Uthman kwanza aliokoa maisha ya kafiri na kasha akamfanya gavana juu ya Waislam.

Wanahistoria wa Kisasa na Ukhalifa wa Uthman

Yafuatayo ni maelezo ya baadhi ya wanahistoria wa kisasa juu ya rushwa, ufisadi, upen-deleo wa kindugu na matumizi mabaya ya madaraka katika wakati wa Uthman, khalifa wa tatu wa Waislam.

E.A. Belyaev:

"Uporaji usio na kivicho wa hazina ya Waislam, ulipata malalamiko kutoka kwa wale masahaba wachache wa Mtume waliodhani kwamba mapato yote yalikuwa mali ya Waislam na lazima yagawiwe sawa sawa kati yao. Mashuhuri kabisa wa hawa wap-inzani wa tofauti za utajiri alikuwa ni Abu Dharr al-Ghiffari. Katika wakati wa uteka-ji nyara, 'sahaba' mtu mzima huyu ambaye, kwa mujibu wa Hadith, Muhammad alimuweka kama mfano kwa Waislam wengine, alikuwa amekwenda Syria ambako alimuadhiri hadharani gavana na viongozi wa vita kwa kujitwalia ngawira na ushuru

474

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ambavyo kwa maoni yake yeye vilikuwa 'mali ya Allah,' inayowahusu Waislam wote. (uk.143).

Muawiyyah akamuomba khalifa kumuondoa huyu mchochezi hatari, ambaye alikuwa anaongezeka kuwa maarufu miongoni mwa watu wa kawaida, kutoka Syria. Akiwa ameitwa na Uthman, Abu Dharr alifanya makazi hapo Madina, lakini, katika kugun-dua pale kwamba khalifa alikuwa ametoa zawadi nono kutoka kwenye hazina ya Waislam kwa mpwa wake (ingawa sio kweli) na mkwe wake, Marwan ibn al-Hakam, wakati ambapo akitoa dirham 300,000 kutoka mahali hapo hapo kwa mpwa wake mwingine, Harith ibn al-Hakam, na dirham 100,000 kwa mtu mmoja aitwaye Zaid ibn Thabit, alianza kumshutumu kwa ukali, akiwaahidi wote wanne, kwa msingi wa Qur'an Tukufu, adhabu kwenye moto wa Jahannam.

Akifuatilia shutuma zake, huyu mtetezi wa haki za watu asiye suluhishika na asiye-hongeka (Abu Dharr) alitamka kwamba watu matajiri wanaongezea utajiri wao kwa kuwanyang'anya masikini. Khalifa aliamuru "mkorofi" huyu afukuziwe kwenye sehemu mbali na makazi ya watu, ambako alifariki kutokana na umasikini uliokithiri, akimuacha mjane wake bila hata uwezo wa kulipia mazishi yake ya wastani.

Wakati wa utawala wa Uthman, ndugu zake, watu wa utawala wa kikabila unaoshik-ilia utumwa, wa Makka, walijitwalia nafasi za kiserikali na wakamiliki mashamba kwenye nchi zilizotekwa. Mapokezi ya kihistoria yanatoa wajibu wenye madhara hasa kwa mpwa na mkwe wa khalifa, Marwan, ambaye, kwa kunufaika na udhaifu wa baba mkwe wake, alichukua madaraka halisi ya serikali ya Madina na akafumbia macho kwa kila namna matendo ya kidhalimu ya ndugu zake wenye uchu, na wanyang'anyi. Hawa ndugu wa khalifa, watu wa ukoo wa Umayya, walikuwa wame-teuliwa na Uthman kama magavana na viongozi wa vita; wao walijitwalia zile ardhi zilizochukuliwa kama mali ya jumuiya ya Waislam.

Ukamataji wa ardhi kama huo, pamoja na unyang'anyi, usaliti na vurugu zilizofany-wa na watawala hawa, zilisababisha kuongezeka kwa manung'uniko, yaliyoonyesh-wa kwa nguvu sana na wale marafiki zake Umar ambao walikuwa wameondolewa kwenye nafasi zao zenye umashuhuri na maslahi. Kukerwa kwao kuliyashirikisha makabila ya Kiarabu (hususan ya Iraki) ambayo maslahi yao ya mali yalipungua kutokana na ubadhilifu wa kidhalimu wa hazina ya dola mikononi mwa wateuliwa wa Uthman.

Khalifa Uthman mwenyewe aliweka mfano wa matumizi mabaya ya mapato ya serikali kwa manufaa ya familia yake binafsi; wakati binti yake alipoolewa na Abdallah ibn Khalid, kwa mfano, Uthman aliwapa dirham 600.000 kutoka kwenye bait-ul-mal ya Basra, ambapo wakati Abdallah ibn Sarh alipotuma qanatir 3,000

475

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

(sawa na ratili 300,000) za dhahabu kutoka Afika, aliamuru dhahabu hiyo itolewe kwa familia ya al-Hakam (uk.144).

(Arabs, Islam & the Arab Caliphate in the Early Middle

Ages, New York, 1969)

Sir John Glubb:

"Mnamo mwaka 646 Uthman alimteua kaka yake wa mama mmoja, Walid ibn Uqba, kuwa gavana wa Kufa. Baba yake, Uqba, alikuwa amechukuliwa mateka huko Badr alipokuwa akipigana upande wa Makuraish na alikuwa amehukumiwa kifo na Mtume mwenyewe. Kwa kilio chake cha uchungu, "Ni nani atakayeangalia watoto wangu wadogo?" Muhammad alimjibu kwa mkato, "moto wa jahannam." Huyu gavana mpya wa Kufa alikuwa ni mmoja wa wale watoto wadogo ambao Mtume wa Allah swt. mwenyewe aliwapangia kwenda motoni. Walid pia alikuwa na sifa ya ulevi. Lawama juu ya uteuzi wa Uthman ilikuwa inazidi kuwa kubwa. Ndugu yake wa kun-yonya, Ibn Abi Sarh, alikuwa amefanywa kuwa gavana wa Misri, ingawa Mtume

alikuwa amemtaja kuwa mwenye kustahili kifo kwa sababu ya ukafiri...(uk. 290-

291)"

Katika mfumo wa utawala wa Kiislam dola haikuwa utaratibu usiohusika na mtu maalum bali (katika nadharia angalau) ni chombo kilichochaguliwa na Allah swt. Hakuna ghiliba yoyote anayoweza kumhalalisha mtu anayependelea maslahi ya kidunia ya ndugu zake kwenye kazi ya Allah swt. Mwenyewe.

Kufuru za dhahiri za wengi wa wateuliwa wa Uthman, na ule ukweli kwamba wao ama baba zao walikuwa wapinzani wakali sana wa Mtume, kuliwachukiza wale Waislam wengi, wachamungu waaminifu huko Makka na Madina. Masahaba walikuwa bado ni wengi wa wastani, bila ya kuwataja wale watu ambao walipigana kule Badr na Uhud, au wale waliokula kiapo cha chini ya Mti kati ya mikono ya Mtume wa Allah swt. huko Hudaibiyya. Wote hawa sasa waliona mfumo wa utawala wa Kiislam ukitawaliwa na maadui wa Mtume, ambao hali kadhalika walifaidi zile fadhila za kidunia ambazo zilikuwa ni tuzo ya wale waumini waaminifu. (uk. 297).

Mfano wa kile Waislam halisi walichokihisi kuhusu zama za Uthman unatolewa na suala la Abu Dharr. Bwana huyu alikuwa mfuasi wa awali kabisa na aliishi maisha yake kama walii halisi. Yeye sasa, kwanza akiwa Damascus na kasha Madina, alian-za kutoa mahubiri yanayoshutumu ukatishaji tama wa nyakati hizo. Huko Syria, huko Iraq, na hata huko Madina, wale Waislam viongozi waliishi kwenye makasiri ya marumaru, wakiwa wamezungukwa na watumwa na mahawara, wakiwa wamevaa mavazi ya anasa na kujifurahisha kwa vyakula vya gharama.

476

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hapawezi kuwa na shaka kabisa kwamba Abu Dharr alikuwa na haki katika madai yake kwamba utajiri na anasa yote hii vinadhoofisha yale maadili ya Kiarabu ya zamani ya ustahimilivu na uangalifu wa matumizi. Lakini watawala wa himaya hiyo walidai kwamba maneno yake yalikuwa yakiwachochea watu kuasi, na Uthman akaa-muru kufukuziwa kwake kwenye oasisi iliyojitenga peke yake huko Arabia ya Kati. Huko, miaka miwili baadae, alifariki kwa dhiki, na heshima yake mara moja ikatukuzwa kama ile ya walii.

(The Great Arab Conquests, London, 1963)

Uthman na marafiki wa Muhammad, Mtume wa Allah swt.

Ikiwa Uthman hakuweza kuonyesha mapenzi makubwa ya kutosha kwa Maadui wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) na Uislam kama vile Hakam, Marwan, Walid, na Abdallah bin Saad bin Abi Sahr, vile vile hakuweza kutumia uhasama mwingi juu ya waumini wa kweli, wenye kumpenda Allah swt. na marafikiwaaminifu wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) kama Abu Dharr el-Ghiffari, Ammar ibn Yasir na Abdallah ibn Masud. Hadith yao italiweka suala hili wazi.

Abu Dharr el-Ghiffari

Ilifikishwa habari kwa Uthman kwamba Abu Dharr al-Ghiffari alizungumza mbele ya Waislam ndani ya Msikiti kama ifuatavyo:

"Mimi ni Abu Dharr el-Ghiffari, sahaba wa Muhammad, Mtume wa Mwisho wa Allah swt. Allah alimnyanyua Adam, Nuh na kizazi cha Ibrahim na Imran juu zaidi ya walimwengu wote. Muhammad amerithi urithi wa mitume wote hawa. Anajumuisha katika utu wake sifa zao, tabia na mafanikio yote. Na mrithi wa Muhammad ni Ali ibn Abi Talib. Enyi Waislam, ambao leo mmekangany ikiwa, ikiwa baada ya kifo cha Mtume wenu, mngelimuweka yeye (Ali) mbele ya wengine, kama Allah swt. alivyomuweka mbele ya wengine, na kama mngewarudisha nyuma wale watu ambao Allah swt. aliwarudisha nyuma, na kama mngeliyaacha mamlaka na madaraka katika sehemu yake ya amuhuri, yaani, katika nyumba ya Mtume wenu, basi mngezipata baraka za Allah swt. Asingekuwapo hata mtu mmoja masikini au fukara. Wala watu wawili wowote wale wasingehitilafiana katika tafsiri ya ujumbe wa Allah swt. na kila mmoja angetekeleza wajibu wake Kwake, na kwa watu wote katika jumuiya, kama ilivyofanyika wakati wa uhai wa Mtume Wake mwenyewe. Mngeukuta muongozo na elimu katika chanzo chake amuhuria, yaani, katika nyumba ya Muhammad (s.a.w.w.). Lakini mliyaachia mamlaka na madaraka ya nyumba ya Mtume wenu yakaporwa, na sasa mnaipata adhabu."

Waleta habari hawa (wachochezi) pia walimweleza Uthman kwamba Abu Dharr alikuwa

477

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

akiwatahadharisha Waislam kwenye upotofu wake (Uthman) wa kutoka kwenye mwenen-do wa Mtume (s.a.w.w.) na pia kwenye mwenendo wa Abu Bakr na Umar.

Uthman alimuamuru Abu Dharr kuondoka Madina, na kwenda Syria na kuishi huko. Huko Syria, Mu'awiyah alikuwa ameizatiti nafasi yake, na akawa amepandikiza mfumo wa maisha ya kidunia badala ya ule wa Kiislam. Abu Dharr alishuhudia uovu na vitendo vya kinyume na Uislam katika baraza la Syria. Aligundua kwamba dhahabu na fedha ya jimbo hilo ilikuwa ikifujwa hapo Damascus katika anasa za wakubwa wakati ambapo Waislam walikuwa wanakaa na njaa. Mu'awiyah mara moja akatambua kwamba Abu Dharr alikuwa hadhibitiki hapo Damascus kuliko alivyokuwa hadhibitiki huko Madina. Abu Dharr alizisoma zile Aya za Qur'an ambamo ndani yake wenye kuhodhi mali wameshutumiwa. Alikuwa mkosoaji wa wazi na alisema kweli bila kujali madhara ya ukweli huo kwake. Mu'awiyah, alikuwa amejijengea kasri mwenyewe binafsi. Abu Dharr akamwambia:

"Kama ulijenga kasri hili kutoka kwenye mfuko ambao ni mali ya Waislam, basi ume-saliti imani; na kama umelijenga kwa mali yako binafsi, basi umekuwa na hatia ya ubadhilifu na majivuno."

Abu Dharr alimwambi Mu'awiyah na wakubwa wa Syria kwamba watakuja kuwekwa alamahuko motoni kwa dhahabu na fedha ambazo walikuwa wamezihodhi. Mwishowe subira ya Mu'awiyah ikafikia kiwango cha kuvunjika na akamuandikia Uthman hivi:

"Ninahofia kwamba Abu Dharr anaweza akawachochea watu kwenye maasi. Ikiwa hutaki maasi katika nchi hii, basi ungemrudisha yeye Madina mara moja."

Uthman alikubali. Mu'awiyah alimpakia Abu Dharr kwenye ngamia bila ya kiti cha mwamvuli, na alimuamuru yale mwendesha ngamia kusafiri bila kupumzika hadi Madina. Abu Dharr aliwasili Madina nusu maiti kwa majeraha, uchovu na uchi.

Lakini hata katika hali hii, Abu Dharr hakuweza kuridhia uongo, udhalimu, unyonyaji na kutokutii kwenye amri za Allah swt. Kupenda kweli na haki vilichoma kifuani mwake kama muali wa moto. Kama suala lolote la ubadhilifu lilifika machoni mwake, alilishutu-mu, na aliwakemea waliolitenda hilo hadharani. Mwishowe Uthman hakuweza kuvumilia tena. Alimwita Abu Dharr kwenye baraza yake na majadiliano yafuatayo yakatokea baina yao:

Uthman: Ndiyo

Abu Dharr: Je, utanihamishia Kufa?

Uthman: Hapana.

478

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abu Dharr: Je, utanipeleka Basra?

Uthman: Hapana.

Abu Dharr: Ni wapi tena basi utakakonihamishia?

Uthman: Ni sehemu gani hasa unayoichukia sana?

Abu Dharr: Rabza.

Uthman: Huko ndiko nitakako kupeleka we we.

Uthman alitimiza ahadi yake, na akamhamishia Abu Dharr al-Ghiffari kwenda Rabza. Na alitoa amri pia kwamba asionekane mtu yoyote wa kuzungumza naye au wa kuongozana naye. Lakini Ali alikuja kumuona, na kuzungumza na kutembea naye. Pamoja na Ali, walikuwepo wanawe mwenyewe, watoto wa Aqiil ibn Abi Talib, na mpwa wake, Abdallah ibn Jafar.

Lilikuwa ni tukio la kuhuzunisha sana. Ali alikuwa anatengana na rafiki mwandani, na rafi-ki na mpendwa wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.). Moyo wake binafsi ulijawa na majonzi, lakini alijaribu kumliwaza rafiki yake kwa maneno haya yafuatayo:

"Ewe Abu Dharr, ulikuwa umewakasirikia watu hawa kwa sababu walikengeuka kutoka kwenye njia iliyoonyeshwa na Allah swt. Kwa hiyo, Allah swt. mwenyewe atakufidia. Wanakuogopa wewe kwa sababu wanafikiria kwamba utawanyima dha-habu na fedha yao. Lakini kama ungekuwa pia ni kama wao, wangekuwa marafiki zako."

Kisha Husain, yule mjukuu mdogo wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) akageuza macho yake yenye kulenga lenga machozi kumtazama yule mpendwa wa babu yake, ambaye sasa anakwenda uhamishoni, na akasema:

"Ewe ami yangu, Allah swt. ataubadili sawa wakati kama huu. Maadui zako 'wameyaokoa' maslahi yao ya kidunia kutoka kwako lakini wewe umeiokoa Akhera yako kutoka kwao. Walichokiokoa wao hakina thamani kabisa lakini ulichokiokoa wewe, ni kitu ambacho kitadumu milele."

Ali na marafiki zake walitembea kimya kimya pamoja na Abu Dharr, na wakati wa kuten-gana ulipofika, Abu Dharr akasema:

"Enyi watu wa Nyumba ya Muhammad! Mwenyezi Mungu akubarikini. Kila ninapowaoneni ninyi, kumbukumbu ya hunijia ya rafiki yangu mpendwa, Muhammad, Mtume na kipenzi cha Allah swt."

479

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abu Dharr, mke wake na mtumwa wake, walihamishiwa Rabza ndani ya jangwa, na baada ya muda fulani, akafariki huko. Mkewe na mtumwa wake wakamfunika uso wake, na wakauelekeza Al-Kaaba, na kasha wakakaa kando ya njia wasijue la kufanya. Wakati huo huo, wakawaona wapanda farasi wakija kutokea upande wa Iraq. Wapanda farasi hawa walikuwa ni Abdallah ibn Mas'ud, rafiki wa siku nyingi wa Mtume (s.a.w.w.) na wasafiri wengine.Walikuwa wakienda Madina. Walipomuona mjane wa Abu Dharr, walisimama na kumuuliza yeye alikuwa ni nani na alikuwa anafanya nini kwenye sehemu ile isiyokaliwa na watu.

Yule mtumwa wa Abu Dharr akawaambia kama wao walikuwa ni kina nani, na akawafa-hamisha kwamba mwili wa Abu Dharr ulikuwa umelala bila ya kuzikwa kwani ardhi ilikuwa ya mwamba na walikuwa hawana uwezo wa kuchimba kaburi.

Abdallah ibn Mas'ud alitokwa na machozi na akaomboleza kile kifo cha rafiki yake mwenyewe, na rafiki ya Mtume wa Allah swt. Abdallah ibn Mas'ud na marafiki zake wakaichimba kaburi, wakatayarisha mazishi mepesi, na wakamsalia, na wakamzika bwana Abu Dharr al-Ghiffari.

Muhammad ibn Ishaq:

"Burayda b. Sufyan al-Aslami kutoka kwa Muhammad b. Al-Kaaba al-Qurazi kuto-ka kwa Abdallah ibn Mas'ud aliniambia kwamba wakati Uthman alipomhamisha Abu Dharr kwenda Rabza, na wakati wa ajali yake ulipofika, hapakuwa na mtu yoyote pamoja naye isipokuwa mke wake na mtumwa. Aliwaagiza kuja kuuosha mwili wake na kuuvisha sanda, na wamlaze juu ya njia, na kuueleza msafara wa kwanza utakao-pita kwamba yeye ni nani, na wawaombe msaada wa kumzika. Alipofariki wakayafanya hay a. Abdallah ibn Masud aliwamuhuri pamoja na watu fulani wengine kutokea Iraq wakienda hijja wakati walipoliona lile jeneza pembeni mwa njia. Yule mtumwa akasimama na akasema, "Huyu ni Abu Dharr, rafiki yake Mtume. Tusaidieni kumzika."

Abdallah ibn Mas'ud aliangua kilio kwa sauti kubwa na akasema: "Mtume alisema kweli; umetembea peke yako, na ukafa peke yako, na utakuja kufufuliwa peke yako."

Kisha yeye na marafiki zake wakashuka kutoka kwenye ngamia zao na wakamzika, na akawaelezea habari zake na kile alichokisema Mtume walipokuwa njiani kwenda Tabuk."

(The Life of Muhammad) Dr. Taha Husain:

"Abu Dharr alikuwa mmoja wa wafuasi wa mwanzoni kabisa kwenye Uislam, na alikuwa mmoja wa wale ambao walipendwa na kusifiwa na Mtume mwenyewe.

480

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mtume alikuwa akisema: "Mbingu ya samawati haijawahi kuning'iniza kivuli chake juu ya mtu ambaye alikuwa mkweli kuliko Abu Dharr."

Abu Dharr aligundua kwamba Uthman alitoa pesa nyingi sana kwa Marwan bin al-Hakam; na alitoa kwa ndugu yake, Harith bin al-Hakam dirham 300,000; na alimpa Zayd bin Thabit Ansari dirham 100,000. Abu Dharr aliyashutumu yote haya, na akawaambia wale wenye kuhodhi ni jinsi gani watakavyochomwa kwenye moto wa jahannam. Alisoma ile Aya ya Qur'an: Wabashirie adhabu chungu wale wanaohod-hi dhahabu na fedha na wala hawazitumii katika njia ya Allah (9:34).

Marwan bin al-Hakam alimjulisha Uthman kile alichokuwa akikisoma Abu Dharr. Uthman alimtuma mtumwa wake kwa Abu Dharr ili kumkataza yeye kuisoma Aya hiyo ya Qur'an inayohusika. Abu Dharr akasema: "Je, Uthman ananikataza mimi kusoma Kitabu cha Allah, na kusahau amri Zake? Kama inanibidi kuchagua kati ya radhi za Allah na radhi za Uthman, kwa hakika nitachakua hizo radhi za Allah."

Abu Dharr hakubadili msimamo katika shutuma zake kwa wale wanaolimbikiza mali, na alitoa mwito kwa Waislam wasiwe wafujaji wa mali.

(al-Fitna-tul-Kubra, kilichochapishwa Cairo 1959 uk. 163)

Abu Dharr alipambana na ile madhehebu ya kisiasa inayojitangaza. Katika Uislam, sauti yake ilikuwa ya kwanza iliyosimama kupinga dhidi ya ukiritimba wa kidini na kisiasa, na unyonyaji wa kiuchumi, na sauti yake ilikuwa ndio ya kwanza pia kusimama katika ulinzi dhidi ya "ukandamizwaji" wa Uislam. Sauti yake ilikabwa lakini mawazo yake hayakuwezekana kuyazima. Aliyatoa mawazo yake kutoka kwenye Qur'an Tukufu. Jaribio lolote la kuzima mawazo yake ni jaribio la kuizima Qur'an Tukufu.

Sauti ya Abu Dharr ilikuwa ni sauti ya Dhamira ya Uislam, na jukwaa lake lilikuwa ni Haki za Watu. Mwenyezi Mungu ambariki milele yote.

Ammar ibn Yasir

Ammar ibn Yasir naye alikuwa mmoja kati ya wafuasi wa mwanzoni kabisa katika Uislam. Kama ilivyoelezwa mapema, mama yake na baba waliteswa mpaka kufa na wapagani hapo Makka. Walikuwa ndio (waliokufa) mashahidi wa kwanza na wa pili wa Uislam, na hii ndio heshima ambayo hakuna hata mmoja katika Uislam wote anayeweza kushirikiana nao. Kama Abu Dharr al-Ghiffari, Ammar alikuwa naye mmoja kati ya wapendwa wa Muhammad, Mtume wa Allah swt. ambaye wakati mmoja alisema:

481

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Ammar ndio mfano halisi wa Imani yote"

Kama vile Abu Dharr al-Ghiffari na wengine wachache, Ammar pia hakupendwa sana na mawakala wa mamlaka ya kiuchumi na kisiasa wa wakati wake, na mapambano ya ana kwa ana kati yake na wao yalikuwa hayaepukiki.

Dr. Taha Husain:

"Ammar alihama kwanza kwenda Abyssinia, na kisha kwenda Madina. Yeye alikuwa Mwislam wa kwanza kujenga Msikiti. Aliujenga hapo Makka penyewe, na aliswali ndani yake. Na alijenga, pamoja na wengine, ule Msikiti wa Mtume (hapo Madina). Wakati Waislam wengine walibeba tofali moja kwa wakati, yeye alibeba mbili. Na vilevile alichimba, pamoja na wenzie wengine, lile handaki wakati wa kuzingirwa kwa Madina. Alifunikwa na mavumbi. Mtume wa Allah swt. mwenyewe alimuondoa mavumbi kutoka kwenye kichwa na uso wake.

Wakati Ammar alipozisikia habari za kifo cha Abu Dharr al-Ghiffari, aliomboleza kwa ajili yake. Uthman aliyatafsiri maombolezo yake (kwa ajili ya Abu Dharr) kama ni lawama kwake yeye mwenyewe. Alikasirika sana, na akamuamuru na yeye pia kuondoka Madina, na kwenda Rabza (uhamishoni). Pale Ammar alipokuwa tayari kuondoka Madina, Bani Makhzuum ambao yeye alikuwa mtegemezi kwao, wakasirishwa sana. Ali pia alichukia. Alikwenda kumuona Uthman, akamlaumu kwa kumhamisha Abu Dharr, na akamwambia asifanye kama hivyo tena kwa Ammar. Uthman akamwambia: "Wewe huna tofauti na Ammar, na wewe pia unastahili kufukuzwa toka Madina." Ali akamjibu: "Endelea, na fanya hivyo." Kisha Muhajirina wengine waliingilia kati na kumwambia Uthman kwamba hawezi kumhamisha kila mtu ambaye alitokea kumchukia.

Wakati mmoja, Uthman alikuwa amechukua kipande cha kito kutoka hazina kwa ajili ya familia yake mwenyewe. Miongoni mwa wale watu waliokipinga kitendo hiki, alikuwa ni Ammar ibn Yasir. Uthman alishikwa na ghadhabu. "Unathubutu vipi kuni-hoji mimi?" alifoka kwa sauti kubwa. Kisha akawaamuru watumwa wake wamka-mate. Wakamkamata, na Uthman akampiga kikatili mpaka akapoteza fahamu. Alitolewa pale Msikitini katika hali hiyo mpaka kwenye nyumba ya Umm Salma, mjane wa Mtume. Ammar alikosa fahamu kwa kutwa nzima iliyobaki. Wakati alipopata fahamu mwishowe, alinyanyuka, akachukua udhuu, akasali swala zake, na akasema: "Al-Hamdulillah, yaani, Namshukuru Allah, Sio mara ya kwanza kwamba mimi nimeteswa kwa kusema kweli." (safari ya kwanza ambapo Ammar aliteswa kwa kuunga mkono ukweli wa Uislam, alikuwa yuko Makka. Katika siku zile, Abu Jahl alikuwa ndiye aliyekuwa akimtesa)

482

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Katika wakati mwingine, masahaba fulani wa Mtume walitunga barua ya ushauri kwa Uthman, na walimuomba Ammar kuiwasilisha kwake. Wakati Ammar alipoiwasilisha ile barua kwa Uthman, alishikwa na hasira tena. Kwa mara nyingine tena, aliwaamu-ru watumwa wake kumuangusha chini. Walimuangusha chini na Uthman akampiga mateke kwenye kinena, na akampiga mpaka akazimia."

(al-Fitna-tul-Kubra, kilichopigwa chapa Cairo mwaka 1959) Abdallah ibn Mas'ud

Abdallah ibn Mas'ud alikuwa mmoja wa masahaba wakuu wa Mtume (s.a.w.w.). Kama ilivyoonyeshwa kabla, alikuwa ndiye mtu wa kwanza kusoma Qur'an ndani ya Al-Kaaba mbele ya viongozi wa Makuraish, nao walimpiga kwa kufanya hivyo. Alikuwa ni mmoja kati ya watu wenye ujuzi mkubwa kabisa hapo Madina. Alitumia muda wake mwingi akiwa pamoja na Mtume (s.a.w.w.), na alikuwa na uzoefu zaidi na vitendo na mifano yake kuliko wengi wa masahaba wengine. Ilikuwa ni kwa sababu hii kwamba Umar alimuom-ba awe anakuwa naye wakati wote. Kulikuwa na nyakati nyingi ambapo Umar alikuwa hajui jinsi Mtume alivyowahi kutatua tatizo au alivyochukua uamuzi katika suala fulani. Katika nyakati kama hizo, alimuona Abdallah ibn Masud na aliamua kutokana na ushauri wake. Katika miaka yake ya baadaye, Umar alikuja kumteua yeye kama mtunza hazina wa Kufa.

Dr. Taha Husain:

'Abdallah ibn Mas'ud alikuwa ndio mtunza hazina wa Kufa wakati Saad bin Waqqas alipokuwa ndio gavana wa mji huo. Uthman alimfukuza Saad, na akamfanya Walid bin Aqaba kuwa gavana mpya. Walid alichukua mkopo kutoka kwenye hazina. Pale wakati uliopangwa ulipopita, na mkopo huo ukiwa bado haujarudishwa, Ibn Mas'ud alimuomba yeye kuulipa mkopo huo. Alimjulisha Uthman kuhusu hilo. Uthman akamwandikia: "Wewe ni mtunza hazina wangu. Usiudai ule mkopo kutoka kwa Walid." Ibn Mas'ud alilikasirikia hili. Alitupilia mbali zile funguo za hazina, na akabakia nyumbani.

Kutokea wakati ule, Abdallah ibn Mas'ud akawa mkosoaji wa sera za hazina na siasa za Uthman. Walid akamwandikia Uthman kuhusu yeye, naye Uthman akamwagizia Walid kumpeleka Ibn Mas'ud Madina.

Ibn Mas'ud aliwasili Madina, na akaenda Msikitini. Wakati alipoingia mle Msikitini, Uthman alikuwa anasoma hotuba. Pale Uthman alipomuona yeye akiingia mle Msikitini, alisema: "Mtu muovu na mbaya anakuja mbele yenu." Ibn Mas'ud akase-ma: "Hivyo sivyo. Mimi ni sahaba na rafiki wa Mtume wa Allah. Nilipigana huko Badr, na mimi ni sahaba wa kwenye Mti." Aisha pia alisikia akiwa chumbani kwake

483

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kile Uthman alichokuwa amesema, naye akaguta akisema: "Hiyo ndiyo aina ya lugha unayotumia kwa sahaba wa Mtume wa Allah?"

Uthman alimuamuru Abdallah Ibn Mas'ud kutoka nje ya Msikiti wa Mtume. Watumwa zake Uthman walimtupa nje ya Msikiti, na kumuangusha chini huku wakimvunja mbavu zake.

Ali alisimama kumlaumu Uthman, na alisema: "Umemuumiza rafiki ya Mtume kwa sababu tu ya taarifa kutoka kwa Walid. Wewe unajua kwamba Walid ni muongo." Yeye kisha akambeba Ibn Mas'ud kwenda naye nyumbani kwake.

Lakini Uthman hakutosheka na kile alichokuwa amekifanya. Baada ya kuvunja mbavu za Abdallah ibn Mas'ud, alisimamisha malipo yake ya pensheni, na akamzuia kuondoka Madina. Ibn Mas'ud alitamani kwenda Syria na kushirika katika mapam-bano lakini Uthman alikariri kile alichowahi kusikia Marwan akisema: "Amezusha matatizo ya kutosha hapo Kufa; usimuachie akafanya kama hayo tena huko Syria."(uk.160)

(al-Fitna-tul-Kubra, kilichopigwa chapa huko Cairo mwaka 1959)

Kama ilivyoelezewa kabla, Abdallah ibn Mas'ud alikuwa amefanya ukusanyaji wake mwenyewe wa Aya za Qur'an, na alikuwa amezipanga katika kufuata utaratibu wa miaka na matukio. Lakini Uthman alikuwa amemteua kipenzi chake, Zayd bin Thabit, kukusanya na kuzipanga Aya za Qur'an. Hakuwa "ameutambua" ule ukusanyaji wa Ibn Mas'ud, na alimuamuru kukabidhi hiyo nakala yake. Abdallah Ibn Mas'ud akakataa kufanya hivyo ndipo watumwa wa Uthman walipoivamia nyumba yake, na kwa kutumia mabavu wakaikamata ile nakala ya Qur'an kutoka kwake. Nakala hii ilichomwa moto kwa amri ya Uthman.

Uthman alitumia mamlaka ya dola katika kushughulika na watu kama Abu Dharr al-Ghiffari, Ammar ibn Yasir na Abdallah ibn Mas'ud kwa sababu walikataa kukubaliana na taratibu zao. Wote watatu iliwabidi walipie fidia juu ya kukataa huku lakini walizilipa kwa moyo mkunjufu kabisa.

Uthman, hata hivyo, alikuwa pia akivurugana na baadhi ya wale watu ambao hawakuwa wenye kujishughulisha sana na mambo kama taratibu. Miongoni mwao walikuwamo Abdur Rahman bin Auf na Amr bin Al-Aas. Wote hawa walikuwa wanahusika moja kwa moja na upandaji wake kwenye cheo hicho.

Uthman na wale 'wenye athari katika uchaguzi'

484

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Uthman alipaswa kuwa mwenye shukurani kwa watu wawili hawa waliomfanya yeye kuwa khalifa wa Waislam. Lakini kama alikuwa ni mwenye shukurani kwao, hakuonyesha hivyo. Badala ya kuonyesha shukurani kwao, alivunja imani kidhalimu tu na mmoja wao, na akamfanya yule mwingine kuwa adui asiyekuwa na huruma juu yake mwenyewe.

Abdur Rahman bin Auf

Wakati Waislam walipopoteza kabisa matumaini kwamba Uthman atarekebisha mwenen-do au njia zake, wakageukia, katika kuvunjika moyo, kwa Abdur Rahman ibn Auf; wakamwambia kwamba hakuna chochote katika Dar-ul-Islam kilichokuwa sawa, kila kitu kilikuwa kinakwenda ovyo ovyo tu, na majukumu juu ya dola hii yalikuwa yote ni yake kwa vile ilikuwa ni yeye aliyemfanya Uthman kuwa khalifa.

Abdur Rahman alikubali kwamba alichokuwa amekifanya ni makosa, na akaongeza:

"Mimi sikutegemea hali ya kufedhehesha kama hii kutoka kwa Uthman. Ametusikitisha. Na sasa Allah swt. awe ni Shahidi kwamba sitazungumza naye tena."

Kukataa kwa Abdur Rahman kuzungumza na Uthman hakukuweza kuondoa madhara ambayo yaliyokuwa yamefanyika wala kubadili chochote kwa mtu yeyote. Lakini alishik-ilia "msimamo" wake na hakuzungumza na Uthman tena ili kumuonyesha jinsi alivy-ochukizwa na vitendo vyake (Uthman).

Amr bin Al-Aas

Amr bin Al-Aas aliipiga Misri kwa maamuzi yake mwenyewe. Baada ya kuitwaa, aliteuli-wa na Umar kuwa gavana wa Misri. Wakati mmoja kabla ya kifo chake mwenyewe, Umar alikuwa amemtuma Abdallah bin Saad bin Abi Sarh, ndugu wa kunyonya wa Uthman, kwenda Misri kushirikiana mamlaka ya kifedha na Amr bin Al-Aas.

Wakati Umar alipokufa na Uthman akawa khalifa, Abdallah bin Saad alimuandikia kumueleza kwamba Amr bin Al-Aas alikuwa anachezea hazina ya umma. Na Uthman mara moja akamfukuza Amr, na akamfanya Abdallah kuwa gavana mpya na amiri jeshi mkuu wa jeshi lililokuwa Misri.

Baada ya kufukuzwa kwa Amr, mfalme wa Byzantine alituma kundi la wapiganaji amba-lo lilifanikiwa kuiteka Alexandria mnamo A.D. 646. Abdallah bin Saad hakuweza kulilin-da jimbo hilo, na Uthman akalazimika kumrejesha Amr kama gavana na kamanda mkuu. Amr akayashinda maj eshi ya Byzantine, na akaikalia tena Alexandria. Lakini mara tu Misri ilipokuwa haina tena vikosi vya Byzantine, Uthman akamfukuza tena Amr, na akaweka mamlaka yote ya Misri kwa kaka yake wa kunyonya.

485

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Misri ilikuwa ndio kipenzi cha kwanza cha Amr bin Al-Aas. Tamaa yake kubwa maishani ilikuwa ni kutawala Misri. Sasa akiwa amenyimwa, sio tu matunda ya kazi yake bali pia na utambulikanaji kwa utumishi wake, alirejea Madina, mwenye uchungu mkali, mwenye hasira na mtu aliyevunjika moyo. Kwa vile pale Madina alikuwa hana chochote cha kufanya, alijushughulisha mwenye we na adhabu kwa, na kupanga njama dhidi ya, yule mwanzilishi wa uvunjikaji moyo wake - Uthman. Wakati huyu Uthman alipouawa na waasi, yeye alijisifu waziwazi hivi:

"Mimi ndio Abu Abdallah. Ninapoamua kufanya jambo, hakuna kitu kinachoweza kunizuia mimi."

Sir John Glubb:

"Amr ibn al-Al-Aas, mtekaji wa Misri kwa mara mbili, ambaye alifukuzwa na Uthman ili kumpendelea ndugu yake wa kunyonya, alikuwa akihangaika kueneza chuki hapo Madina."

(The Great Arab Conquests, uk.299, 1963)

"Amr ibn al-Al-Aas, mtekaji wa Misri mara mbili, alikuwa akiishi Madina tangu kufukuzwa kwake na Uthman, na alikuwa miongoni mwa wakosoaji wakali kabisa wa huyu khalifa mtu mzima."

(The Great Arab Conquests, uk.324, 1963)

Amr ibn al-Al-Aas alikuwa na mapambano mengi makali na Uthman ndani ya Msikiti Mkuu na katika kasri la huyu Uthman. Katika moja kati ya mapambano hayo, alimtaka aombe msamaha hadharani (Atubie) kwa tabia yake isiyo na hakika katika mambo ya kiserikali.

Sir John Glubb:

"Amr ibn al-Al-Aas, wakati alipotakiwa ushauri (na Uthman), alimjibu kikatili, 'Wewe umeutiisha umma wote kwa Bani Umayya. Wewe umepotoka, na watu vivyo hivyo wamepotoka. Ama ufanye uamuzi wa kuwa muadilifu au uiache kazi hii."

(The Great Arab Conquests, uk.300, 1967)

Amr ibn al-Al-Aas alimshutumu na kumlaani Uthman hadharani, na hakumuacha hata baba yake. Cha kushangaza ni kwamba, haukimjia kamwe kutumia mamlaka yale yale ya dola dhidi yake ambayo aliyatumia dhidi ya Abu Dharr al-Ghiffari, Ammar ibn Yasir na Abdallah ibn Mas'ud. Alikuwa na makabiliano, sio moja, bali ni mengi, na Amr ibn al-Al-Aas, na bado, hakuwahi kumtishia kumhamisha kwenda Rabza, na hakuwahi kuwaamuru watumwa wake kumtoa nje ya Msikiti au kwenye kasri yake, na kumvunja mbavu zake.

486

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Huenda Uthman aliona, kama mtu mwangalifu kiasi alivyokuwa yeye, kwamba masham-bulizi ya maneno ambayo Amr ibn al-Al-Aas alimfanyia yeye hayakuvunja mfupa wowote hata hivyo katika mwili wake na, kwa hiyo, haikuwa lazima kumuadhibu yeye. Zaidi ya hayo, walitofautiana lakini wanatofautiana ndani ya desturi za "shirika la watu maalum" pekee ambamo wote wawili walihusika. Lakini Abu Dharr al-Ghiffari, Ammar ibn Yasir na Abdallah ibn Mas'ud, walikuwa "sio wanachama." Kwa hiyo, sheria zile zile hazikutumi-ka kwao wao ambazo zinatumika kwa "mwanachama" kama Amr ibn Al-Aas.

Sababu za kuuliwa kwa Uthman

Uthman alikuwa ni khalifa kwa miaka kumi na miwili. Ule mfumo wa madaraka aliourithi kutoka kwa Umar, ulifanya kazi vizuri kiasi kwa nusu ya kwanza ya utawala wake. Ilikuwepo amani kwa ajili yake na kwa ajili ya Waislam. Lakini katika nusu ya pili, manung'uniko yalianza kuongezeka dhidi yake, na yaliendelea kuongezeka mpaka kufikia hatua ya kuwaka moto mnamo A.D. 656 wakati kundi la watu walioghadhibika na kukasirika lilipomuua yeye ndani na kasri lake mwenyewe huko Madina.

Watu walikuwa na sababu halali za kutokuridhika kwao. Walijua kwamba viwango visivyo na idadi vya dhahabu na fedha vilikuwa vikiingia kwenye hazina kutoka majimboni lakini hawakuviona kabisa. Vyote vilipotelea kwenye makasha binafsi ya watu wa tabaka la watawala. Hili tabaka la watawala liliundwa pekee na watu wa ukoo wa Bani Umayya -ukoo ambao Uthman mwenyewe anatokana nao. Bani Umayya, chini ya Uthman, walifikia utajiri ambao hawakuutegemea japo ndotoni na kiwango cha juu kabisa cha matumizi mabaya ya madaraka. Waislam walichukia kiburi chao, majivuno na maringo yao, na ushenzi wao na mikogo yao yenye kuhamakisha ya utajiri na madaraka.

Uthman aliwafukuza magavana na makamanda wote waliokuwa wameteuliwa na Abu Bakr na Umar, na badala yao, aliwateua wale watu ambao "hati za utambulisho" pekee zilikuwa kwamba wao ni Bani Umayya. Watu huko majimboni waligumia chini ya visigi-no vya hawa magavana na makamanda wapya. Walevi wa madaraka kama walivyokuwa, maovu yao na kiburi chao hakikuwa na mipaka. Walijiona wao wenyewe kwamba wako juu na nje kabisa na upeo wa mkono wa sheria. Malengo binafsi ya Bani Umayya yalichukua kipaumbele juu ya malengo ya umma, na "haki" yao ya unyang'anyi, ilikuwa na amri juu ya haki za umma wa Kiislam. Umma uliwajua wao kama wabinafsi wasiom-cha mungu na wanyonyaji wa kupindukia ambao walitwaa umiliki wa zana halisi ya Uislam - ile serikali ya Madina. Majimbo, kwa hiyo, yakajawa na manung'uniko na maasi.

Walezi wa awali wa Bani Umayya walikuwa ni Abu Bakr na Umar. Ilikuwa ni wote wawili hawa ambao, kama ilivyokuwa, walifungua kizibo cha chupa, lakini sasa ilionekana kwa umma kwamba hapakuwa na njia ya kumpenyeza jini kurudi tena ndani ya chupa. Uthman naye aliibadili mizania ya mgawanyo wa kisiasa kwa kuwatenganisha maveterani wawili wa vita kama Abdur Rahman bin Auf na Amr bin Al-Aas. Aliwasababishia uhasama Bani

487

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ghiffari na washirika wao kwa kumhamisha Abu Dharr kwenda Rabza ambako baadae ali-fia huko. Aliwachonganisha Banu Makhzuum na washirika wao kwa kumpiga kikatili Ammar bin Yasir, na aliwafanya Bani Hudhail na Bani Zuhra kuwa maadui zake kwa kum-fanya Abdallah ibn Mas'ud kupigwa na watumwa wake.

Uthman alikuwa salama alimuradi alihamisha au aliwapiga marafiki za Mtume wa Allah swt., kama Abu Dharr al-Ghiffari, Ammar bin Yasir, na Abdallah bin Mas'ud. Hawakutokana na makabila yenye nguvu na Uthman hakuwa na chochote cha kuhofia kutoka kwao. Lakini tena akamfukuza Amr bin Al-Aas, gavana wa Misri. Kwa kufanya hivyo, aliandika hukumu yake mwenyewe ya maafa. Amr bin Al-Aas alimchakuria kiota cha manyigu juu yake. Uthman alionekana kuwa shauku ya kujipatia maadui wapya. Askari "aliyeandikishwa" upya kwenye safu za maadui zake alikuwa ni Aisha, mjane wa Mtume (s.a.w.w.). Katika nyakati za baba yake na Umar, Aisha alitunzwa kama malkia. Lakini Uthman hakuonyesha uhusiano kama huo kwake kama walivyofanya. Yeye alipun-guza hata pensheni yake, na hivyo akamuamsha ghadhabu zake. Yeye Aisha alimwita Na'athal (Myahudi wa Madina), na aliwachochea watu wazi wazi dhidi yake akisema: "Huyu Na'athal amerudia tena kwenye upagani. Muueni huyu, eh! Allah swt. Amuuwe huyu."

R.V.C. Bodley:

"Uthman hakuwahi kuwa mtu aliyejitokeza sana wakati Muhammad alipokuwa yuko hai. Leo alionyesha kwamba hakuwa na zile sifa za wale waliomtangulia. Aliyumbishwa kirahisi na hakuwa na haya katika kubadilisha viongozi wa kijeshi na magavana kwa kuweka vipenzi wake, bila ya kujali uwezo wao. Vilevile alifanya lile kosa la kumchukiza Aisha.

Dharau yenyewe ilikuwa ni ndogo, lakini ya namna yakuweza kuamsha hisia zote za Aisha za kulipiza kisasi. Uthman aliipunguza pensheni yake ikawa ya kiwango kilek-ile cha wale wajane wengine!

Aisha alikuwa akijidhania yeye mwenyewe siku zote kama kipenzi cha Muhammad. Wakati wa utawala wa baba yake na wa Umar, alikuwa amechukuliwa katika hali kama ile ile ya wakati mumewe alipokuwa hai. Lakini kwa kufariki kwa watetezi wake hawa wawili, alijua kwamba ilihitajia uhodari wake wote kulinda nafasi yake. Pale, kwa hiyo, Uthman alipofanya shambulizi lake la kichini chini, Aisha aliamua kwamba huyu hakuwa mrithi anayestahili wa mume wake. Alipokwisha kulimaliza hilo, kile kilichokuwa kimebakia sasa kilikuwa ni kutafuta njia nzuri ya kumuondoa adui. Sababu au njia zilizotumika hazikuwa na maana juu ya hali hiyo. Pale Aisha alipotaka jambo lifanywe, basi lilitekelezwa bila kujali maadili. Katika suala hili Uthman alimpa Aisha kila aina ya msaada.

(The Messenger - The Life of Muhammad, New York, 1946) 488

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Madina, wakati fulani iliyokuwa alama ya uchamungu na ushikiliaji maadili, ilikuwa ime-badilika. Mji wa Mtume (s.a.w.w.) umegeuka, baada ya kifo chake, kuwa ni alama ya maovu ambayo vita vya kigeni na ukabaila usiozuiliwa vinAyaleta baadaye. Lazima isije ikachukuliwa kwamba Waislam wa Madina walikubaliana na mikengeuko yote hii na kupotoka kutoka kwenye Uislam wa amuhuri. Hawakukubaliana. Lakini hawakuwa na uwezo wa kusimamisha yale matumizi mabaya ya madaraka ndani ya serikali hiyo. Walipinga lakini malalamiko yao hayakusikilizwa hata kidogo. Sauti za akina Abu Dharr al-Ghiffari, Ammar ibn Yasir na Abdallah ibn Mas'ud zilizosimama kupinga dhidi ya wimbi la kuthamini mali lilivyokuwa linatishia kuumeza Uislam, zilinyamazishwa kwa nguvu za kinyama. Wakijikuta wamekwama, masahaba waliokuwepo Madina, mwaka 654 walianzisha kampeni ya kuandika barua kwa Waislam wa kwenye majimbo, wakiwaomba wafanye uwakilishi kwa khalifa dhidi ya maovu ya Marwan na magavana wa majimbo, na kumuomba yeye awauzulu hao.

Wale Waislam wa majimboni, wenyewe wakiwa waathirika wa dhulma na vitisho, na wakiwa hawajui la kufanya, waliamua, baada ya kuandikiana barua kadhaa na masahaba hao, kutuma ujumbe kwenda Madina kuwamuhurisha manung'uniko yao kwa khalifa, na kumuomba yeye kuirekebisha hali hiyo. Uthman alijua kuhusu zile barua ambazo masahaba walikuwa wamezituma kwenye majimbo. Lakini badala ya kuchukua hatua za kunusu-ru, alifanya kitendo cha kuvunja heshima. Tabari, mwanahistoria huyu, anasema kwamba Uthman alimuandikia Muawiyyah, gavana wake wa Syria, kama ifuatavyo:

"Watu wa Madina wamerudia tena kwenye ukafiri; wamevunja kiapo cha utii kwangu. Sasa hivi wanakusudia uhaini. Wewe, kwa hiyo, nitumie haraka sana hapa Madina, wale wapiganaji wakali kabisa wa Syria, juu ya wanyama wenye kasi." (Tarikh Tabari, juz. 111.)

Lakini Muawiyyah hakuwa na nia ya kumfanyia msaada Uthman. Tabari anaendelea kuse-

ma:

"Pale Muawiyyah alipoipokea barua ya Uthman, aliamua kuangalia hali kama ilivyo, na alipendelea kutopingana na masahaba wa Mtume wazi wazi kwa sababu alijua kwamba walikuwa wameungana wote katika upinzani wao kwa Uthman."

Muawiyyah alikuwa akiiangalia hali jinsi gani inavyoweza kuingia mikononi mwake. Hakuwa ni mtu ambaye anaweza kuzuiwa na aibu za kimaadili kuwapinga hao masahaba wa Mtume (s.a.w.w.). Alikuwa na uwezo lakini hakuwa tayari tu kumsaidia Uthman.

Abul Fida, mwanahistoria huyu, anasema kwamba mnamo mwaka 656 ujumbe wa watu 700 ulikuja Madina kutokea Misri, na wajumbe wa namna kama hiyo pia walikuja kutoka Kufa na Basra. Walikuja wakitaka marekebisho ya utawala wa kirasimu na usimamizi wa kibadhirifu wa fedha za umma, kuanzia Madina na kwenye majimbo yote. Kama Uthman angelikutana nao, akawasikiliza malalamiko yao, na kama angewahakikishia tu kwamba

489

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

yuko katika kukubaliana nao, wangeweza kuridhika, na wangeweza kurudi majumbani kwao. Lakini kwa bahati mbaya, yeye hakufanya hivyo.

Ujumbe wa Misri ambao ulikuwa umeweka kambi kwenye viunga vya Madina, ulituma mjumbe pamoja na barua kwa Uthman, wakimuomba wakutane naye. Katika barua hiyo walikuwa wamemuomba amuondoe kaka yake wa kunyonya, Abdallah bin Saad bin Abi Sarh, kutoka kwenye nafasi yake kama gavana wa Misri, na kuanzisha mabadiliko fulani ya kiutawala. Lakini badala ya kuyafikiria maombi yao, Uthman aliwaamuru watumwa wake kuutoa nje ule ujumbe wa Misri.

Wamisri hao ndipo wakaingia mjini, na waliwaambia wale watu wengine kile Uthman ali-chokifanya. Wale wajumbe wa Kufa na Basra walikuwa tayari wako Madina, na wakatam-ka kuwaunga mkono kwao Wamisri. Makundi yote matatu ya uwakilishi yaliweka kambi katika sehemu ambayo wanaiona kasri ya khalifa. Katika Ijumaa iliyofuata, Uthman alion-goza Swala ya jamaa, na akaisoma khutba. Asingeweza kuwa hovyo zaidi na asiye na busara hivyo. Akiwa amesimama kwenye minmbari, na akiongea na wale wawakilishi kutoka Misri na Iraq, alisema:

"Mtume wa Allah swt. alikwisha tabiri kwamba wafitini, siku moja watakuja kwenye mji wake kuvuruga amani ya mji huo. Aliwalaani wote hao, na sasa mnaona mna-chokifanya." Ile hadhara ilionyesha kukasirishwa na matamshi haya, na kukawa na ghasia kubwa mle msikitini. Mtu mmoja akamrushia jiwe Uthman ambalo lilimpata usoni; akaanguka kutoka kwenye minmbari, na akabebwa kutolewa mle msikitini na kupelekwa kwenye kasri yake.

Baada ya tukio hili, Uthman alikuwa kwenye hali ya kuzingirwa ndani ya kasri yake. Lakini alikuwa akiweza kwenda msikitini, na bado alikuwa anaziongoza Swala. Siku chache baadae, hata hivyo, Wamisri na Wairaqi walimkataza kuingia mle msikitini labda kama angewasikiliza kile walichokuwa wakiseme, na walimteua mtu mmoja aitwaye Ghafiki, mjumbe wa uwakilishi kutoka Misri, kuwaongoza katika Swala.

Katika wasiwasi wake, Uthman alitafuta msaada wa Ali katika kuwatawanya wazingi-raji hao. Ali akamwambia:

"Malalamiko yao ni ya halali, na madai yao yana mantiki. Hawatatawanyika tu eti kwa sababu ninawaomba watawanyike. Wao watatawanyika tu kama utawapa ahadi yako ya kukubali madai yao." Uthman akasema:

"Ninakupa wewe mamlaka ya kujadiliana nao. Yoyote yanayoweza kuwa masharti yako ya makubaliano nao, mimi nitayakubali."

490

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali alikutana na viongozi wa ujumbe wa Misri na akazungumza nao. Walikubali kurudi Misri kama Uthman angemrudisha ndugu yake wa kunyonya, maarufu Abdallah bin Saad, na kama, badala yake, amteuwe Muhammad ibn Abu Bakr kama gavana mpya. Ali alimwambia Uthman kile ambacho angepaswa kukifanya kama alitaka Wamisri hao waon-doke Madina.

Uthman alikubali kumteua Muhammad ibn Abi Bakr kama gavana mpya wa Misri. Hili liliwaridhisha Wamisri. Muhammad ibn Abu Bakr aliondoka Madina kwenda Misri kusi-mamia kazi zake mpya, na wengi wa Wamisri hao walifuatana naye. Uthman aliweza kwa mara nyingine tena kuingia Msikitini na kuwaongoza Waislam katika Swala. Kadhia hiyo, inavyoonekana, ilifungwa.

Lakini kwa bahati mbaya haikufungwa. Mtu nafsi ya Uthman, Marwan, aliifufua tena, kama ndondocha. Aliposikia kwamba Wamisri wameondoka Madina pamoja na gavana wa chaguo lao wenyewe, alimpa Uthman ushauri ufuatao:

"Baadhi ya Wamisri wameondoka Madina lakini wale waliokuja kutoka kwenye majimbo mengine, bado wangali wapo hapa. Watu wa mfano wa Wamisri watawahimiza na wao pia kutoa madai magumu. Ili kulizuia hili lisije likatokea, ni lazima utoe hotuba ndani ya msikiti ukisema "Wamisri walikuwa wamesikia uvumi tu nchini mwao. Walipokuja Madina, waligundua kwamba yale yote waliyokuwa wameyasikia, hayakuwa chochote ila ni uongo tu. Waliridhika na wakarudi majum-bani kwao. Sasa na ninyi wengine pia mnapaswa kuondoka Madina, na kurudi majumbani kwenu."

Uthman hakutaka kusema uongo usio na haya kama huo lakini Marwan alikuwa na uwezo wa kumfanya yeye afanye lolote. Baada ya kusita kwa muda kidogo, alikubali. Akaongoza Swala, na baada ya hotuba akasema:

"Enyi Waislam! Wamisri walikuwa wamesikia habari za upotofu kuhusu khalifa wao, na walikuja Madina kuzithibitisha. Hapa waligundua kwamba yale yote waliyokuwa wameyasikia, yalikuwa yote ni uongo. Wao, kwa hiyo, waliridhika na wamerudi Misri. Sasa na ninyi wengine pia mnapaswa kurudi majumbani kwenu."

(Ta'arikh Tabari, Juz. 111)

Maneno haya yalipotoka tu kinywani mwa Uthman vurumai likazuka mle Msikitini. Kila mmoja akaanza kumpigia mayowe: "Uthman, tubia! Uthman tubia! Unaongopa. Muogope Allah. Unasema uongo ndani ya Nyumba ya Allah swt. Mwenyewe, na katika mimbari ya Mtume Wake."

491

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Uthman alipatwa na hofu, na kwa kutokujua afanye nini, ilimbidi "kutubia." Alimuomba Allah swt. amsamehe dhambi yake, na kisha akaenda nyumbani.

Ali alishangazwa kupita kiasi na kugeuka kwa Uthman, na kukosa haya kwake katika kutoa maelezo ya uongo ndani ya Msikiti. Hata hivyo, alimtembelea mzee huyu tena na akamkemea kwa kile alichokuwa amekifanya. Uthman alimuomba yeye kuingilia kati tena, ya yeye na Waislam kwa niaba yake.

Ali alimwambia kwamba yeye (Uthman) angeweza bado, kama angetaka, kuipata imani na heshima ya Waislam kama angeyakubali makosa yake, na kama kwa unyofu kabisa angeyaombea msamaha. Yeye pia alimuonya kwamba kama hatafanya hivyo, basi wale wageni waliokuwa wamo mle mjini, wanaweza wakamuweka kizuizini katika kasri lake, na kama wakifanya hivyo, basi yeye Ali anaweza kushindwa kuwasuluhisha.

Uthman, katika hali ya taadibu, alimhakikishia Ali kwamba yeye kwa hakika atafanya kama alivyomshauri. Ali naye, kwa upande wake, akawahakikishia wale Wairaqi, Wamisri na Waislam wengine kwamba khalifa atayakubali madai yao yote, na akawakumbusha kwamba wao pia walikuwa na wajibu, kama vile kumheshimu yeye (khalifa), kumtii na kumsaidia yeye.

Katika siku iliyofuatia, Uthman aliingia ndani ya Msikiti, akayakiri makosa yake, akaom-ba msamaha na baraka kutoka kwa Allah swt. akidhamiria kutokurudia makosa hayo, na akaahidi kuchukua hatua za haraka juu ya madai ya Waislam ya mabadiliko ndani ya serikali.

Ile hadhira ilihuzunishwa sana na kutubia kwa khalifa huyu mtu mzima, na kwa uhakik-isho wake, na machozi mengi yalimwagika kwa pande zote kama ishara ya "mabadiliko ya Moyo." Ilionyesha kana kwamba yale machozi yalikuwa yamesafisha chuki zote, kinyon-go na uchungu wa wote waliohusika.

Kwa juhudi za Ali, suluhisho, inavyoonekana, lilipatikana, na lilikuwa ni muujiza. Lakini kama ilivyotokea, ulikuwa ni muujiza uliodumu kwa muda mfupi sana.

Uthman aliondoka pale Msikitini pamoja na maazimio mengi ya kiuchamungu. Lakini alipoingia kwenye kasri yake, alimkuta Marwan, mpangaji sera wake mkuu, akimsubiria ampatie ushauri mpya. Lakini kabla hajaweza kusema lolote, mkewe Uthman, Naila, ambaye pia alikuwepo, alimzuia yeye, na mabishano yafuatayo yalitokea baina yao:

Naila: Tafadhali, wewe sasa ufunge mdomo wako baada ya madhara yote ambayo umekwisha yafanya. Kama hukufanya hivyo, bila shaka utasababisha kuangamia kwa mzee huyu -Uthman. Wewe kwa upotovu wako, unamsukumizia kwenye ukingo wa shimo la kifo.

492

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Marwan: Wewe ni nani kuingilia kwenye mambo haya? Umesahau kwamba wewe ni binti ya mtu ambaye hakujua hata namna ya kuchukua udhu kwa ajili ya Swala?

Naila: Wewe ni muongo uliyekamilika kabisa. Kabla ya kumtaja baba yangu, ulipaswa kukumbuka kwamba wewe na baba yako ni watu mliolaaniwa na Allah swt. na Mtume Wake (s.a.w.w.). Kama nisingekuwa ninajizuia kwa sababu ya huyu mzee (Uthman), ningelikufundisha adabu.

Kisha Naila akamgeukia mumewe, na akamwambia:

"Usimsikilize mtu mjinga na fedhuli huyu. Yeye ni nani? Ni nani anayemjali? Kama unataka usalama wako mwenyewe, basi tekeleza ushauri wa Ali. Wewe huoni ni sifa na umaarufu kiasi gani alionao miongoni mwa Waislam?"

Huu ulikuwa ni ushauri wa busara kabisa ambao Uthman aliwahi kuupata kamwe kutoka kwa ndugu yoyote wa familia yake mwenyewe lakini hakuukubali. Naila ndipo akaondoka mbele ya mume wake. Mara tu alipokuwa ametoweka machoni pao, Marwan akamwambia Uthman:

"Umefanya kosa kubwa sana mle Msikitini kwa kukubali makosa yako, na kwa 'kutubia' hadharani. Kukubali madhambi yako kumeyatoa makundi kutoka kule Msikitini na kuyaleta langoni mwa nyumba yako. Wapo hapa tu kwa sababu wameuona udhaifu wako. Kama ungelikuwa 'imara' juu yao, wasingethubutu kuja hapa. Njia pekee ya kuwashughulikia hawa, na kuwaonyesha madaraka na mamlaka yako, ni kuwa 'imara'juu yao."

Kundi la Waislam, lilikuwa kwa kweli limekusanyika nje ya kasri la khalifa. Lakini lilikuwa ni kundi la amani. Waislam wengi kutoka nje na ndani ya mji walikuwa wameku-sanyika wakitegemea kusikia matangazo yoyote muhimu kuhusiana na yale mabadiliko ya sera na utawala. Uthman alipaswa atoke kwenda kuwapokea. Lakini hakutoka. Badala yake, alimpa Marwan ruhusa yake kwenda kuonana nao ili kuwavutia wao hao kwa "uimara." Wake.

Wazo la Marwan la kuwa imara kwa Waislam lilikuwa ni kutumia nguvu, lugha ya matusi na vitisho. Pamoja na yale mamlaka mapya ya "kufanya apendavyo" kutoka kwa Uthman, alitoka nje, na akilikabili lile kundi ambalo lilikuwa la amani na la kirafiki, alisema:

"Kwa nini mmekusanyika hapa? Madhumuni yenu ni nini? Je, mmekuja kutusham-bulia au kutuibia au kutupora sisi hapa? Kama hivyo ndivyo, basi sikilizeni hili kwa makini. Ninyi hamtafanikiwa. Hamuwezi kutupokonya madaraka na mamlaka kutoka mikononi mwetu. Hatutatishiwa na ninyi au na mtu mwingine yoyote yule. Sasa ondokeni hapa. Allah swt. awalaani ninyi."

493

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Safari hii Uthman na Marwan walikuwa wamevuka mahali ambapo walikuwa hawawezi kurudi nyuma tena!

Waislam walipigwa na butwaa kwa mshituko na chukizo kwa ufidhuli wa mkwe wake Uthman. Lakini hawakukaa kufanya mzaha naye. Badala yake, walikwenda kuonana na Ali na kumuelezea yeye maana halisi ya "hotuba" ya Marwan.

Ali alishikwa na mshangao kusikia hadithi hii. Hivi kulikuwa kuna kitu chochote ambacho angeweza kukifanya ili kuzuia huo unyumbulikaji wa hali? Alilitafakari swali hilo, na kisha akamwendea Uthman na kumwambia:

"Hivi huu ndio ukarimu ulioutoa kwa ndugu zako Waislam? Kama umekosa kabisa busara mbele zao, ulipaswa, angalau, kuhofia ghadhabu ya Allah swt. Katika shauku yako ya kumlinda kafiri na muongo, umeipoteza hofu hiyo pia, na sasa unaweza kuse-ma uongo hadharani na Msikitini, na unaweza kuvunja viapo vyenye taadhima bila ya kufumba jicho. Umemruhusu Marwan akuelekezee wewe kokote anakotaka. Kumbuka, atakuingiza kwenye shimo la udhalimu kama hajafanya hivyo tayari, na wewe hutaweza kujinasua mwenyewe kamwe humo. Sasa sitajaribu kutafakari kati yako na Waislam. Sitakuwa na haja na mambo yako. Hii ni safari yangu ya mwisho kukutembelea. Wewe fanya unavyotaka. Lakini kama bado utanihitaji mimi, basi kwanza itakubidi uachane na Marwan. Mimi nitajitenga nawe muda utakapokuwa Marwan anasimama kati yako na mimi."

Ali aliondoka kwenye kasri la Uthman kwa dhamira ya kutorudi tena hapo. Wakati Naila, mke wake Uthman, alipomuona anaondoka, alifadhaika sana. Matukio yamethibitisha kwamba yeye alikuwa na uamuzi mzuri kuliko wengi wa wale waliokuwa karibu na Uthman. Ingawa ushauri wake haukukubaliwa, alikuwa bado na shauku ya kuokoa kila ambacho angeweza, na akamwambia mume wake:

"Ni mara ngapi nimekuambia uachane na Marwan. Yeye ni laana, mzigo juu yako. Unajua kwamba ni mtu muflisi wa sifa nzuri, ni muflisi wa maadili, na ni muflisi wa busara. Hali ni ya hatari sana, na inazidi kuwa mbaya zaidi. Umepoteza imani yako kwa kusaliti uaminifu wa Waislam. Sasa kama kuna mtu yeyote ambaye bado anaweza kukuokoa wewe, mtu huyo ni Ali. Kama yeye huyo hatakusaidia, basi wewe umepotea."

Uthman kama alivyokuwa amevurugwa na tukio hili, alitambua kwamba kile mke wake alichokuwa amemwambia yeye, kilikuwa ndio ukweli wa hali ya juu kabisa. Yeye, kwa hiyo, alituma mjumbe kwenda kumuomba Ali aje. Lakini Ali alikataa kwenda ambapo Uthman aliamua kwenda yeye mwenyewe kumuona Ali. Ili asionwe na mtu yeyote, basi alikwenda wakati wa usiku. Mbele ya Ali, khalifa huyu mzee aliielezea hali nzima ya

494

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kutoweza kujisaidia mwenyewe, na akaomba radhi juu ya makosa yake mengi, na akamhakikishia kwamba atakuwa, huko baadae, akishika ahadi yake, ikiwa yeye Ali atap-atanisha kati yake (Uthman) na Waislam. Ali, hata hivyo, akasema:

"Unasimama kwenye mimbari ya Mtume wa Allah swt., na kusema maneno ya uongo. Unawapa Waislam kiapo chako cha ahadi yako ya kuingia kwenye haki, na kisha unaivunja. Sasa kila mtu ameona jinsi unavyoheshimu ahadi zako. Kama Waislam wanataka kukuona wewe na kuzungumza nawe, Marwan anawatukana na kuwalaani. Unanitegemeaje mimi nikuamini wewe sasa hivi ukiwa na rekodi kama uliyonayo? Sikubali wajibu wowote juu ya matendo yako yoyote. Njia zipo, na uamauzi ni wako. Epukana na Marwan. Kama huwezi kufanya hivyo, basi usitegemee chochote kutoka kwangu. Ukiwa na Marwan karibu yako, na kama mshauri wako mkuu, hakuna chochote ninachoweza kukufanyia hata hivyo."

Uthman alimpenda sana mkwe wake kiasi cha kushindwa kutengana naye. Masharti ya Ali kwa hiyo, yalikuwa kwake hayakubaliki, na akarudi nyumbani. (Ali hakuwa akimwambia Uthman kwamba amhamishe Marwan kutoka Madina kama Mtume wa Allah swt. alivyokuwa amefanya; yeye alikuwa akimwambia tu kwamba huyu asiwe anampotosha.)

Wakati Marwan alipokuwa anapambana na Waislam hapo Madina, Uthman alikuwa anaandika barua kwa magavana wake wote akiwataka watume vikosi vyao Madina ili aweze "kuwatia adabu" wale "waasi." Matumaini yake makubwa yalikuwa kwa Mu'awiyah, na kwake yeye aliandika barua nyingi, akimsisitiza alete wapiganaji huko Madina au awatume pamoja na maafisa wake waaminifu. Lakini sio Mu'awiyah wala yey-ote mwingine kati ya magavana wake aliyeitikia ishara zake za wasiwasi.

Siku moja mtu mmoja alimwona Uthman nje ya kasri lake, na akatoa maneno: "Jinsi gani ninavyotamani kwamba ningeweza kukuburuza wewe na wale walio karibu yako kwenye takataka." Uthman akasema kwamba wale walio karibu naye, hawakuwa wengineo mbali na masahaba wa Mtume wa Allah swt. Alijibu kwa ukali kwamba hao "masahaba" lazima wawe Hakam, Marwan, Walid bin Aqaba, Said bin Al-Aas, Abdallah bin Saad bin Abi Sahr, na waliobaki wa kundi hilo. Uthman akanong'ona: "Ngoja hilo jeshi lije, na ndipo nitakuadhibu wewe."

Lakini jeshi hilo halikuja kamwe. Mu'awiyah alikawia na kuwaza kwamba kama kulikuwa na vurugu huko Madina, atatumia hila ndani yake, na kama ikiwezekana, ataondoka na ukhalifa wenyewe.

Wakati mambo haya yalipokuwa yanatokea huko Madina, habari mbaya zilikuja kutoka kaskazini. Muhammad ibn Abu Bakr, gavana mteule wa Misri, alikuwa amewasili huko

495

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Elath kwenye mkono wa Bahari Nyekundu unaoitwa Ghuba ya Aqaba, na alikuwa anakaribia kuingia Misri. Alikuwa ameweka kambi hapo Elath wakati watu fulani wa msa-fara wake walipomuona mpanda ngamia mpweke akija kutoka Madina. Wakamsimamisha ili kumsaili, na walipoona majibu yake ni ya kukwepa, walimpekua. Ukaguzi mrefu wa mwili wake na mizigo ulizaa barua iliyokuwa imefichwa katika kijibomba cha risasi chini ya mfuko wake wa vikorokoro. Barua ilikuwa imeandikwa kwa Abdallah bin Saad bin Abi Sarh, gavana wa Misri, na ilikuwa na muhuri wa khalifa mweyewe. Waliileta ile barua na mbeba barua mbele ya Muhammad ibn Abi Bakr. Yeye akauvunja ule muhuri, na alishtush-wa kusoma ujumbe ufuatao:

"Wakati Muhammad ibn Abi Bakr na watu wa kundi lake watakapowasili hapo Misri, wakamate, na uwauwe wote, na uendelee na kazi zako kama gavana wa Misri."

(Kama ilivyoelezwa kabla, Abdallah bin Saad ibn Abi Sarh hakuwepo huko Misri kwa wakati huu; alikuwa yuko Palestina.)

Mwanzoni Muhammad hakuweza kuyaamini macho yake mwenyewe. Uthman anawezaje kumuagiza gavana wake amuue yeye na wenziwe? Aliisoma na kuisoma tena na tena barua ile mpaka maana yake ilipoanza kuzama akilini mwake.

Muhammad aliamua kurudi Madina. Huko Madina, aliingia ndani ya Msikiti wa Mtume (s.a.w.w.), na akaiweka ile barua mbele ya masahaba kwa ajili ya uchunguzi makini. Baadhi yao na watu wa kundi la Muhammad, walikwenda kwa Uthman, kumuonyesha ile barua, na mabishano haya yakatokea kati yao:

Masahaba: Je, wewe uliandika barua hii?

Uthman: Hapana.

Masahaba: Ni muhuri wa nani huu juu ya barua hii?

Uthman: Ni wangu.

Masahaba: Huu ni mwandiko wa nani? Uthman: Ni wa mwandishi (katibu) wangu. Masahaba: Huyu mpeleka barua hii ni mtumwa wa nani? Uthman: Ni wangu

496

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Masahaba: Ni nani aliyemtuma kwenda Misri?

Uthman: Mimi sijui.

Masahaba: Muhuri juu ya barua ni wako; mwandiko ni wa mwandishi wako; mtumwa kenda Misri. Kama yote haya huyatambui kiasi hicho, basi itakuwa kote, kwa manufaa yako wewe, kwamba aliyeibeba ni wako, na kisha hujui ni nani aliyemtuma huko, na kwa manufaa ya umma wa Waislam, kwamba ujiuzulu kwenye ukhalifa. Acha mtu mwingine, mwangalifu na mwenye kufaa kwa kazi hiyo, asimamie serikali ya Waislam.

Uthman:           Ukhalifa ni joho ambalo Allah swt. amenipa mimi, nami siwezi kulivua

kwa hali yoyote ile. Ninachoweza kukifanya, hata hivyo, ni 'kutubia.'

Masahaba: Kutubia kwako hakuwezi kutughilibu sisi tena. Tayari umekwisha kutubia mara nyingi. Wewe, kwa hiyo, ondoka na utoe nafasi kwa mtu mwingine bora zaidi yako kwa kazi hii kubwa ya Ukhalifa. Unasema kwamba humjui aliyetuma barua hii. Kama unasema kweli, basi haiwezi kuwa mtu mwingine yeyote mbali na mkwe wako ambaye ndiye mwandishi wako. Yeye aliiandika na kuituma barua hiyo. Yeye ndiye mhalifu halisi ambaye alikuwa achukuwe maisha ya Waislam wengi wasio na hatia. Sasa kama wewe ni mkweli, basi mkabidhi yeye kwetu sisi ili tuweze kumchunguza yeye, na tuthibitishe haki.

Uthman:          Siwezi kumkabidhi Marwan kwenu ninyi.

Masahaba: Sisi basi tunaelewa kwamba wewe ni mshiriki katika jinai hiyo, na wewe pia ulitaka Waislam wasio na hatia wauawe katika kuwasili kwao huko Misri kwa sababu tu kwamba wewe na Marwan hamuwapendi watu hao.

Masahaba hao ndipo wakaenda Msikitini kuwaeleza wale Wairaqi na Wamisri matokeo ya mazungumzo yao pamoja na khalifa. Wamisri, pale pale, wakaizingira kasri ya Uthman. Wajumbe waliokuja kutoka Kufa na Basra nao pia wakapigilia mahema yao kuizunguka ile kasri ya khalifa, na wakatangaza kwamba yeye atakuwa mfungwa wao mpaka atakapomtoa Marwan kwao kwa ajili ya kushtakiwa na kuhukumiwa. Wakati wa karantini hiyo, maji ya kunywa yakaisha ndani ya kasri. Uthman aliomba kwa baadhi ya masahaba kuletewa maji lakini waliyapuuza maombi yake. Mwishowe, alituma ujumbe kwa Ali, nay eye Ali akatuma maji na walinzi wenye silaha. Walinzi hao iliwabidi kuingia kwa nguvu ndani ya kasri kufikisha kimiminika hiki chenye kuleta na chenye kuokoa uhai.

Uthman bado alikuwa na matumaini kwamba mmoja wa magavana wake, hususan Mu'awiyah, angetuma vikosi vyake ambavyo vitateketeza kabisa waasi hawa wakaaidi na

497

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wenye kujiamini mno. Waasi wenyewe, kwa wakati huo, walikuwa wakikaza kitanzi chao kwenye shingo yake.

Mauaji ya Uthman

Matukio madogo madogo mengi yalitokea wakati wa kuzingirwa kwa kasri la Uthman. Kulikuwa na nyakati ambapo aliona kwa macho yake mwenyewe baadhi ya masahaba wakuu wa Mtume miongoni mwa wazingiraji wakiwasisitiza wao kuweka mkazo wao juu ya wale waliozingirwa.

Siku moja ilitokea kwa Ibn Ayyadh fulani, mmoja wa masahaba wa Mtume (s.a.w.w.) kusuluhisha kati ya wazingiraji na wale waliozingirwa katika jaribio la kurudisha amani hapo Madina. Alikuja kwenye lango la kasri na kumwita Uthman kwa jina lake. Uthman alichungulia kwenye dirisha lililokuwa juu, na akauitikia mwito. Ibn Ayyadh alimuomba ajiuzulu na hivyo kumaliza ile hali ya vurugu ndani ya mji, na pia kuwaokoa Waislam kutokana na uwezekano wa umwagaji damu. Alikuwa hajamaliza maombi yake bado wakati mmoja wa watupa mishale wa Uthman alipomuua kwa mshale.

Ukelele wa kuonyesha uchungu ulitoka kwa wazingiraji. Walimuomba Uthman amsalim-ishe huyo muuaji kwao lakini akasema:

"Nitawezaje kusalimisha wasaidizi na walinzi wangu mwenyewe kwenu ili muwaue? Haiwezekani kamwe."

Jibu la Uthman lilikuwa na athari za cheche kwenye baruti kavu. Lile kundi lilisonga mbele kutaka kuingia ndani ya kasri lile na kumkamata yule muuaji wa Ibn Ayyadh. Marwan, Said bin Al-Aas, Mughira bin Khins, na mamluki wa Uthman walijaribu kuilin-da ile kasri kutoka kwa ndani, na kuwarudisha wale wazingiraji. Hawa wazingiraji wal-ishambulia na malango mengine pia lakini wakakuta walinzi kila kwenye lango mojawapo.

Wakati mapambano haya yakiendelea kwenye malango ya kasri la Uthman, Ansari mmoja, bwana fulani Amr bin Hazm, aliwaita wale wazingiraji kwenye nyumba yake ambayo ilikuwa inapakana na nyumba ya Uthman. Waliingia nyumbani kwake, wakapanda juu, na kutokea huko juu wakashukia kwenye nyumba ya Uthman na panga zikiwa zimechomole-wa. Palikuwa na mapigano madogo na wale mamluki ambao baadhi yao waliuawa lakini wale wa Bani Umayya wote - Marwan, Said bin Al-Aas na Mughira bin Khins miongoni mwao - walifanikiwa kutoroka kupitia mlango wa siri. Marwan anasemekana kuwa ali-jeruhiwa lakini akapona baadae. Katika ghasia hizo mtu mmoja akamuua Uthman. Mke wake, Naila, anasemekana kunyanyua mkono wake kumlinda kutokana na upanga, na vidole vyake vilifyekwa katika jaribio hilo.

498

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Uthman aliuawa ndani ya kasri lake, akiwa ametelekezwa na Bani Umayya. Miaka kumi na mbili baada ya kuchaguliwa au kuteuliwa kwake kama khalifa. Ukhalifa wake ukawa shaghala baghala; watumishi wake wakaangamizwa; matumaini yake yakaingia shaka, msimamo na uwezo vikapinduliwa.

Uthman alikuwa na umri wa miaka 84 wakati wa kifo chake. Alikuwa ameibomoa ile nyumba iliyojengwa kwa harubu nyingi na Abu Bakr, Umar na Abdur Rahman ibn Auf. Alishindwa kuonyesha kwa kusadikisha hasa sifa za uongozi, uwezo na msukumo muhimu kwa khalifa. Alikuwa amekwishaangukia kwenye uzulufu na alikuwa amepoteza njia yake.

Uthman alibakia kuwa mfungwa kwenye kasri yake kwa muda wa siku 49. Alimsihi sana Mu'awiyah aje Madina na ayaokoe maisha yake. Lakini Mu'awiya hakuwa na "jibu" kwa maombi yake - kimyaaa! Kwa kukisia kutokana na kimya chake cha makusudi, inaonekana kwamba Mu'awiyah hakuwa akimjali hata kidogo Uthman. Inashangaza kwamba wapenzi wengi wa Uthman wanamlaumu Ali kwa "kutokuyaokoa" maisha ya Uthman ingawaje yeye Ali hakuwa na njia yoyote ya kufanya hivyo; lakini wanafumbia macho kutojali kwa Mu'awiyah juu yake (Uthman) ingawa alikuwa na kila namna ya uwezo wa kumuokoa. Kikosi kidogo cha jeshi lake, kama angelikipeleka Madina, kingeweza kuwashinda au kuwaua wale waasi wote lakini hakufanya hivyo!

Amr bin Al-Aas alikuwa ni mmoja wa masahaba wa Mtume (s.a.w.w.). Uthman alim-fukuza mara mbili akiwa kama gavana wa Misri. Hakumsamehe kamwe Uthman kwa kumfukuza kwake; alikuwa na usongo juu yake. Inawezekana kabisa kwamba alikuwa ni yeye aliyepanga mauaji ya Uthman, na hakufanya angalau jitijada japo kidogo ya kuficha dhamira yake. Lakini alikuwa amejawa na hila na ujanja, na aliweza kukwepa ukosoaji wa historia.

Mawakala wengine wawili - wachochezi katika mauaji ya Uthman walikuwa ni Talha na Zubeir. Waliuwasha moto wa ghadhabu na chuki za umma dhidi ya Uthman kama vile alivyofanya Amr bin Al-Aas. Wote hao waliamini, kama vile Amr bin Al-Aas na Mu'awiyah walivyoamini, kwamba hawakuwa na chochote cha kupoteza katika kuvunji-ka kwa sheria na amani, na kuna takriban kila kitu cha kupatikana. Wote walikuwa ni nyongeza kwenye uhalifu dhidi ya Uthman ama kwa ushiriki wa moja kwa moja au kwa kuridhia na kutojali kwao.

Wakati Uthman alipouawa, Madina ilikuwa imejaa wanawake na wanaume mashuhuri kabisa. Miongoni mwao walikuwepo wajane wa Mtume (s.a.w.w.) isipokuwa Aisha ambaye alikuwa yuko Makka; Saad bin Abi Waqqas, Abdallah bin Umar bin al-Khattab; Muhajirina na Ansari; wakongwe wa vita vya Badr na Uhud; na wengi wa wale masahaba ambao walikula kiapo cha Mti kule Hudaibiyya. Lakini wote isipokuwa Ali tu, hakuna hata mmoja kati yao, aliyeonyesha shauku japo kidogo tu ya kuokoa maisha ya khalifa.

499

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hakuna asichokifanya Ali kumuokoa Uthman lakini sio yeye au mtu mwingine yeyote ambaye angeweza kumuokoa mtu ambaye alikuwa ameamua kujiangamiza mwenyewe. Marwan alizuia juhudi zake zote Ali, za kugeuza kule kuteketea kwa ukhalifa, na akak-wamisha majaribio yake yote ya kusuluhisha kati ya khalifa na Waislam.Yeye Marwan alisimama kama kikwazo kigumu kisichoshindika kati yao. Uthman hakusikiliza ama zile nasaha za mke wake mwenyewe, Naila, wala maonyo na ushauri wa Ali, bali alishikilia kuchokoza balaa. Kwake yeye, kupayuka kwa Marwan kulikuwa ni sawa na ufunuo wenyewe, na kwake yeye peke yake, Uthman alitoa uaminifu wake wa kwanza.

Miongoni mwa wafuasi wake, Uthman aliweza kuwategemea watu wawili tu - Marwan na Saad bin Al-Aas - wote hao wakiwa ni wale waliolaaniwa na Mtume wa Allah swt. Mafaqih na wana-theologia wa Sunni wanaweka umuhimu mkubwa kwenye utaratibu wa makubaliano. Hapa kulikuwepo na makubaliano ya Masahaba wa Mtume (s.a.w.w) katika kuzuia uungaji mkono wao kwa Uthman, na katika kumpinga yeye. Walijizuia msaada wao kwake, na walimpinga yeye takriban wote kwa pamoja. Walimtelekeza, auwawe, kwa maneno ya Umar, na "mbwa mwitu wa Waarabu." Nani alikuwa sahihi na nani alikuwa amekosea? Ni swali la mafaqih na wanatheologia wa Sunni kulijibu.

Matokeo ya kuuawa kwa Uthman

Wakati Ali alipopanda kwenye kiti cha ukhalifa, aliwakuta watu wa Madina wamegawanyika makundi mawili. Moja ya makundi haya lilikuwa likipiga makelele kuta-ka kulipiza kisasi kwa ajili ya damu ya Uthman. Na lile kundi jingine liliamini kwamba Uthman amelipa fidia tu kwa ajili ya vitendo vyake visivyo na busara, na suala la kutaka kisasi kwa ajili ya damu yake, kwa hiyo, halikuwa na lazima. Vyovyote vile ambavyo Ali angefanya, ilikuwa haiepukiki kwamba moja ya makundi haya litafanya uasi dhidi ya madaraka yake.

Serikali hii mpya ilikuwa inayumba sana na Ali alikuwa anajitahidi kuiimarisha wakati moja ya haya makundi mawili lilipoanza kumlazimisha awaadhibu wauaji wa Uthman. Akawaambia:

"Si kama sitambui ile haja ya kuwaadhibu wauaji wa Uthman. Lakini je, tunayo nguvu ya kufanya hivyo? Kwa wakati huu, ni wao ndio wenye nguvu. Wanaweza kutuamuru sisi; na sisi hatuwezi kuwaamuru wao. Kama wakitaka, wanaweza kutudhuru, na sisi hatuwezi kuwafanyia madhara yoyote. Je mnaweza kupen-dekeza njia yoyote ambayo tunaweza kuwashinda au kuwazuia wao?"

Madina, kwa wakati huu kwa kweli, ilikuwa kwenye mikono ya lile kundi ambalo lilimpin-ga Uthman - wale waasi. Ni amri yao iliyokuwa inatembea hapo Madina, na hakuna mtu aliyethubutu kuwapinga. Ikiwa Ali ataamua kuweka adhabu juu yao, ilikuwa inawezekana kabisa kwamba wangempinga kwa nguvu ya silaha. Walikuwa wanazitambua nguvu zao

500

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wenyewe, na udhaifu wa serikali ya Madina. Kama kile kikundi cha kwanza, yaani wanao-taka kulipiza kisasi kingegundua udhaifu wowote kwa wale waasi, basi kingewapinga wao wakati ule wa kuzingirwa kwa kasri la Uthman. Lakini hakikufanya hivyo. Wakati wa karantini, viongzi wake walijificha. Lakini mara tu Ali alipochaguliwa khalifa, wakaji-tokeza, na wakaanza kudai hatua kutoka kwake, ya kuwakamata wale waasi waliokuwa wamemuua Uthman.

Viongozi wa kile kikundi cha kwanza waliamua kumpinga Ali. Ulikuwa ni ushauri wa Aisha, ambaye alikuwa ni mmoja wao, na ambaye tayari alikuwa Makka, kwamba lazima waishambulie Madina kwa sababa muuaji au wauaji wa Uthman wote walikuwepo pale. Lakini Talha na Zubeir, wale viongozi wengine wawili, ambao walikuwa wamemwambia Ali kwamba walikuwa wanakwenda Makka kufanya Umra (hijja ndogo), hawakukubaliana naye, na wakasema:

"Ewe umm-ul-mu'min! Sahau Madina. Jeshi letu haliwezi kupigana dhidi ya waasi walioko pale. Inatupasa sisi, kwa hiyo, twende zetu Basra."

(Tabari, Historia, juz.111)

Aisha, Talha, na Zubeir, viongozi wa kile kikundi cha kwanza, walikuwa na jeshi; walikuwa na silaha na walikuwa na pesa, na bado walikwepa kushambulia Madina kwa sababu walikosa nguvu ya kuwashinda waasi hao. Kama hawakuweza kupigana na waasi hao ingawa walikuwa na jeshi, angewezaje Ali, ambaye hakuwa na jeshi, kupigana dhidi yao?

Kama Aisha, Talha na Zubeir kweli walitaka kulipa kisasi, walipaswa kushambulia Madina badala ya kwenda mamia ya maili kuvuka jangwa hadi Basra. Lakini waliweza kuona kwamba waasi hao walikuwa wengi tu kiasi cha kutoweza kuwaadhibu. Watu wa Madina, wa Misri, wa Kufa, na wa Basra, walikuwa wote wamehusika na kifo cha Uthman, moja kwa moja au kwa namna nyingine.Walikuwepo wale masahaba ambao waliandika barua kwa viongozi wa waasi, na kuwakaribisha Madina, na kuna wale Muhajirina na Ansari waliojitolea uungaji mkono wao kwao (hao waasi). Bila kuwaunga mkono kwao kwa kimya kimya, waasi hawa wasingeweza kamwe kuthubutu kumuua khalifa aliyekuwa madarakani kwenye nyumba yake mwenyewe.

Kulikuwako na nji mbili za kuwaadhibu hao wauaji wa Uthman. Moja ilikuwa ni kumuua kila mtu aliyeshiriki, moja kwa moja au kwa namna nyingine, katika mauaji yake bila ya kujali alikuwa ni nani - Muhajir, Ansari, Mmisri au Muiraqi. Hii ni wazi kabisa ilikuwa haiwezekani. Lakini kama ingewezekana, basi Dola lisingeua maelfu ya watu kwa kisasi cha kuuawa kwa mtu mmoja tu.

Njia nyingine ilikuwa ni kuyachunguza mauaji, na kumpata mhalifu au wahalifu haswa,

501

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kuwashitaki, na katika kuthibitika kwa jinai, kumuua au kuwaua wote. Ali alikuwa tayari kabisa kutwaa mwelekeo huu lakini kwanza ilimbidi arudishe amani na utulivu katika nchi baada ya vurugu (za kiutawala) na ghasia zilizokuwa zimedumu miezi mingi. Kifo cha Uthman hakikuwa ni matokeo ya ushari wowote wa ghafla ambao aliufanya. Majadiliano ya siku nyingi na marefu yalikwisha kuutangulia uhalifu wenyewe. Aliuawa baada ya kushindwa kwa majadiliano yote hayo. Wajumbe walikuja kumuona kutoka miji ya mbali, na kumweleza juu ya maovu ya kupindukia ya magavana wake. Aliahidi kureke-bisha hali hiyo lakini alishindwa kutekeleza ahadi yake.

Pale ujumbe huo ulipomkumbusha juu ya ahadi yake ya kumfukuza mmoja wa magavana wake, yeye akasema:

"Mnanishauri kwamba niwafukuze wale miongoni mwa magavana wangu ambao inaelekea hamuwapendi, na kwamba nichague watu mnaowapenda ninyi kuendesha serikali. Kama ingekuwa nitende kulingana na matakwa yenu, nitakuwa mtu nisiye na hadhi, na ninyi mtakuwa mnakamata mamlaka yote ya serikali na sio mimi."

(Tarikh Kamil - Ibn Athir, Juz. 111, uk.86)

Wale wajumbe walighadhibishwa na majibu ya Uthman, na wakasema:

"Wewe huna uwezo wa kuyaweka sawa yale makosa ya serikali yako. Kwa hiyo, ni lazima ujiuzulu kwenye ukhalifa. Kama hufanyi hivyo, basi tutalazimika kuchukua hatua kali zaidi."

Uthman akasema:

"Ninyi mnatishia kuniua mimi? Kama hivyo ndivyo, basi ni jinai gani juu ya agizo ambalo kwalo mtaniuwa mimi? Katika Uislam, kuuawa ndio adhabu juu yangu:

(a) Kuua mtu asiye na hatia;

(b) Ukafiri;

(c) Ubakaji wa mwanamke safi.

Mimi sijatenda lolote kati ya jinai hizi. Ni kwa msingi gani mwingine tena ninyi mnataka kuniuwa mimi?"

Majibu ya wajumbe hao yalikuwa kama ifuatavyo:

"Kwa wale watu wanaofanya ufisadi juu ya ardhi, au wanaopora haki za watu wengine, adhabu iliyoagizwa ndani ya Kitabu cha Allah ni kuuawa. Kwa ukorofi kabisa umetumia vibaya mamlaka ya serikali. Umemfukuza kutoka Madina sahaba wa Mtume wa Allah anayeheshimiwa sana, na vikaragosi wako wamewapiga marafi-

502

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ki zake wengine. Umeulazimisha umma kuwakubali walevi na makafiri kuwa vion-gozi wao. Wewe na magavana wako mmewatishia na kuwadhulumu Waislam, na mmewapora haki zao. Mmeyafanya yote haya na zaidi. Licha ya hayo, kama utajiuzu-lu kwa hiari yako, hatutakuingilia, na tutakuacha kwenye amani."

Lakini Uthman hakutaka kujiuzulu kwa sababu, alisema kwamba, ukhalifa ni "joho" ambalo alikuwa amepewa na Allah swt., na hawezi akalivua.

Allah anaweza kwa kweli, kumpa joho la ukhalifa yoyote ampendaye. Lakini joho la ukhalifa ambalo Uthman alikuwa amelivaa, hakulipewa na Yeye Allah swt., bali alilipewa na Abdur Rahman bin Auf!

Majadiliano haya yanaweka bayana kwamba watu walichukua hatua ya mwisho kabisa, pale tu kila kitu kingine kiliposhindwa. Waliridhika kwamba kuuawa kwa Uthman ni halali kabisa. Kuridhika kwao kulitiwa nguvu zaidi kwa maneno na vitendo vya watu wakubwa kama Aisha, Talha, Zubeir na Amr bin Al-Aas ambao kila mmoja wao ameagiza kifo juu yake, wazi wazi ama kwa mzunguko.

Uthman na "Abdallah ibn Saba"

Ukhalifa wa Uthman umewabwagia Waislam serikali iliyodhoofika sana, na mingi ya mivurugiko ya kiuchumi, kisiasa na kijamii iliyojitokeza kutokana nayo, ilikutana na mwitiko wa mashaka na wakati mwingine wa kinyume. Mivurugiko hiyo hatimaye ilis-ababisha kifo cha khalifa mwenyewe.

Wanahistoria wengi wa Sunni wanaona vigumu kukubali kwamba Uthman alijiletea maangamizi yeye mwenyewe. Wanayo shauku mno ya "kueleza" au kutumia hekima kuonyesha ni kwa nini mambo yalikwenda kombo katika ukhalifa wake. Lakini kwa njia gani? Shauku yao iliwaelekeza kwenye kubuni mtu wa ajabu na kisirani ambaye walimwi-ta "Abdallah ibn Saba"

Uundwaji wa Abdallah ibn Saba "ulifumbua" matatizo mengi sana ya wanahistoria wa Kisunni. Alifanya uhamishaji wa hatia uwe wenye kuwezekana kwao. Kwa mujibu wa waliomuunda, yeye alikuwa ni Myahudi kutoka Yemen aliyekuwa ameingia kwenye Uislam, akahamia Madina, na kisha akapita akizunguka kueneza mafundisho ya uongo na ya uasi, na kueneza manung'uniko na chuki dhidi ya Uthman. Alikuwa, kama wanavyodai, anahusika na huzuni zote na mabalaa, na hatimaye na kifo chenyewe cha Uthman!

Abdallah ibn Saba, inavyoonekana, mara akawa ndiye mtu mwenye nguvu zaidi katika Dar-ul-lslam yote. Na baadae, ilikuwa ni yeye aliyempindua khalifa kutoka kwenye madaraka yake na kuitupa serikali yote ya Waislam kwenye vurugu.

Alichokuwa akikifanya Abdallah ibn Saba, kilikuwa ni uhaini mkubwa. Hivi kulikuwa na kitu rahisi cha kufanya kwa Marwan kuliko kumkamata yeye na kumuua kwa uhaini wake,

503

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kama alikuwa yuko Madina? Au, je, kulikuwa ni kitu chochote rahisi zaidi kwa gavana wa jimbo au hata afisa wa ngazi ya chini, kuliko kumkamata yeye na kuzima maisha yake, kama angekuwa katika mojawapo ya majimbo? Hakuna. Lakini kwa sababu za ajabu, ali-tamba toka mji hadi mji na kutoka jimbo hadi jimbo, akimkosoa khalifa, na hakuna hata mtu mmoja aliyemgusa. Inavyoonekana, yeye aliishi maisha ya kichawi basi!

Inashangaza kwamba Uthman ameweza kumfukuza sahaba wa cheo cha juu wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) kama Abu Dharr al-Ghiffari kwenda Rabza (Abu Dharr ali-fia huko Rabza); aliweza kumpiga Ammar ibn Yasir mpaka kuzimia, na aliweza kuvunja mbavu za Abdallah ibn Mas'ud, wote hawa masahaba mashuhuri wa Muhammad; na bado aliweza kuwapa uhuru Amr bin Al-Aas na "Abdallah ibn Saba" wa kuwachochea Waislam dhidi yake yeye mwenyewe kwa makemeo na matusi yanayochoma.

Wakati Uthman alipouawa, "Abdallah ibn Saba" huenda aliona alikuwa amekamilisha kazi yake na "akaingia mitini." Lakini miezi michache tu baadae, "akaibuka tena" katika mke-sha wa vita vya Basra (vita ya Ngamia). Ilikuwa ni yeye, waundaji wake wanavyodai, ambaye alihusika vita hivyo vya kusikitisha. Hata hivyo, wakati, au mara baada ya vita hivyo, akatoweka tena, na safari hii alitoweka milele. Kwa hakika ni ajabu sana kwamba ameweza kutokomea bila ya kuacha alama na dalili nyuma yake. Kitendo chake cha kutoweka kilikuwa kikamilifu sana kana kwamba hakuwahi "kuwepo".

Kwa kweli, huo "umuhimu" uliosababisha kubuniwa kwa Abdallah ibn Saba, ulikuwa umekoma kuwepo. Waundaji wake, kwa hiyo, wakamzika. Lakini hadi leo hii, anafufuli-wa mara kwa mara pale wanahistoria wa Sunni wanapotaka "kuelezea" habari zisizokuba-lika za kipindi kile cha historia.

Dr. Taha Husain, mwanahistoria wa kisasa wa Misri, ameutangua ubuniwaji wa Abdallah ibn Saba katika kitabu chake kiitwacho, al-Fitna-tul-Kubra. Ameonyesha kwamba Tabari ndiye mwanahistoria wa kwanza ambaye aliandika kuhusu Abdallah ibn Saba. Alimsikia kutoka kwa Umar bin Saif. Abdallah bin Saba alizaliwa kichwani mwa Umar bin Saif. Lakini katika vyanzo vingine kabla ya Tabari, Abdallah bin Saba hakutajwa mahali popote. Hii ni ajabu kwa sababu "mhusika" mashuhuri kama Abdallah ibn Saba aliyeivuruga jamii ya Waislam katika zama za Uthman, awe hakupata kutambuliwa kokote kutoka kwa wanahistoria wa kabla ya Tabari.

Dr. Taha Husain anaendelea kuleta swali kwamba hata kama ikichukuliwa kwamba Abdallah ibn Saba alikuwa akieneza mafundisho ya uongo na ya uasi, hivi ni yeye ambaye "alimshawishi" Uthman kumteua mtu kama Marwan kama waziri wake mkuu? Muhajirina na Ansari walikasirishwa na kunyanyuliwa kwa Marwan kwani machoni mwao alikuwa ni mtu wa kuepukwa sana kama ukoma. Na hivi Uthman alikuwa akitekeleza ushauri na mwongozo wa Abdallah ibn Saba pale alipowafukuza magavana wa majimbo wale waliokuwa wameteuliwa na Umar bin al-Khattab, na akachagua ndugu zake mwenyewe badala yao? Hili lilikuwa ni moja ya malalamiko huko majimboni.

504

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hadith ya Abdallah ibn Saba ni mbinu ya kuficha makosa ya mtu. Lakini mbinu hiyo haikuwa yenye nguvu zaidi!

Ikiwa kwa upande mmoja, watetezi wa Uthman wameanzisha mtu wa kubuniwa kama Abdallah ibn Saba ili kufunika makosa na utawala mbaya wake Uthman, kwa upande mwingine wameamua kukataa ukweli wa mambo ya kihistoria. Katika mengi ya maandishi juu ya historia ya kale ya Uislam, yanayoonekana katika miaka ya karibuni, watetezi wa Uthman wamefikia kiasi cha kukataa kwamba alifukuza gavana yoyote kati ya wale walio-teuliwa na Abu Bakr au Umar au kwamba kuna kitu chochote cha kulaumika ndani yake kama alifanya hivyo, au, kwamba alifanya kosa lolote jingine.

Ni kazi na haki kabisa ya mabingwa watetezi wa Uthman kama wanataka kuendelea kuishi na uongo na udanganyifu au kwa usahihi zaidi kwa kujidanganya wenyewe. Lakini ukweli mchungu unaouma hautatoweka tu hivi hivi ati kwa sababu tu mtu havipendi. Hiki ndio kile yule mwanahistoria wa sasa, wa Kimisri, Dr. Taha Husain, anachokiandika juu ya suala hili katika kitabu chake al-Fitna-tul-Kubra:

"Tusiwafuate wale watu ambao wanaukataa ukweli wa habari zilizotufikia kuhusu migogoro na migongano ya masahaba wa Muhammad, Mtume wa Allah, na vurugu ambazo zilitokea kwa wakati huo huo. Kama tukifanya hivyo, tutakuwa kwa kweli, tunaukataa msingi mzima wa historia ya Uislam, kuanzia pale Mtume alipotangaza ujumbe wake. Wale watu waliosimulia kutokukubaliana kwa masahaba, na wakasimulia na mageuzi ya kisiasa ya wakati huo, ni wale wale waliohadithia harakati za mwanzoni, mapambano na ushindi, na maisha (Sira) ya Mtume na ukhal-ifa (wa Abu Bakr na Umar). Katika suala hili, hatuna uhuru wa kuteua na kuchagua. Hatuwezi kuchukua yale tunayoyataka tu na kuyakana yale tusiyoyapenda. Hatuwezi tukaziita baadhi ya Hadith ni za kweli na nyingine ni za uongo.

"Kitu kimoja ambacho juu yake hakina shaka ni kwamba Waislam waligawanyika katika suala la Uthman, na mgawanyiko wao uliishia katika kifo chake, na ndio kamwe hawakuwa wameunganishwa tena tangu hapo.

"Lakini migawanyiko ile na kutokuelewana kule kulikuwa na sababu zake. Ni kweli kwamba Waislam walimuua Uthman lakini hawakufanya hivyo bila ya vyanzo au sababu."

(al-Fitna-tul-Kubra, kilichochapishwa Cairo mwaka 1959)

505

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali ibn Abi Talib, Khalifa wa nne wa Waislamu

Ali alitokana na ukoo wa Bani Hashim, ukoo mashuhuri sana katika Arabia yote; na kati-ka Bani Hashim, alitokana na familia maarufu sana - familia ya Abdul Muttalib. Huyu Abdul Muttalib alikuwa na watoto wa kiume kumi. Wawili wao walikuwa ni Abdallah, baba yake Muhammad Mustafa, na Abu Talib, baba yake Ali. Abdallah na Abu Talib walikuwa ni watoto wa mama mmoja ambapo hao ndugu zao wengine walizaliwa na wake wengine wawili wa baba yao.

Mama yake Ali, Fatima, pia alitokana na ukoo wa Hashim. Alikuwa binti ya Asad, mtoto wa Hashim. Asad na Abdul Muttalib walikuwa ni ndugu. Alikuwa kwa hiyo, ndiye dada binamu wa kwanza wa Abdallah na Abu Talib.

Mama yake Ali, Fatima binti Asad, alikuwa ni mwanamke wa pili katika Arabia yote kuukubali Uislam, wa kwanza akiwa ni Khadija.

Fatima binti Asad alikuwa ndiye mama wa kunyonya wa Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah swt. Alimlea kama mwanawe mwenyewe, na kwa kweli alimpenda kuliko hata watoto wake mwenyewe, na yeye Mtume, alikuwa akimwita yeye, mama yake.

Baba yake Ali, Abu Talib, alikuwa ndiye Mtetezi wa Uislam, na alikuwa ndiye Mlinzi na Mlezi wa Muhammad. Aliuunga mkono Uislam na Muhammad kama kawaida, na alikuwa hana hofu mbele ya upinzani na vitisho kutoka kwa wapagani.

Akiwa Makka na Madina, kote Muhammad Mustafa alitangaza kwamba Ali alikuwa ni ndugu yake katika dunia hii na katika ile ya Akhera.

Ali alikuwa ndiye mshindi wa vita vya Badr. Na pia aliwauwa nusu ya idadi ya watu wa Makka wote waliokuwa wameuawa katika vita hivyo.

Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah swt. alimuoza binti yake wa pekee, Fatima Zahra kwa Ali. Mwenyezi Mungu aliibariki ndoa hii na watoto. Watoto wale walikuwa ni waja wachamungu kwelikweli. Furaha yao kuu maishani mwao ilikuwa ni kuwa na subira juu ya Mola wao.

Katika vita vya Uhud, Waislam wengi walikimbia kutoka kwenye uwanja wa mapambano. Mmoja ambaye hakukimbia alikuwa ni Ali. Aliyaokoa maisha ya bwana wake,

506

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad, siku hiyo.

Katika kuzingirwa kwa Madina, Ali alimuua Amr ibn Abd Wudd, na hapo akaiokoa Madina kutokana na kuvamiwa, na watu wake kutokana na kuuawa kwa halaiki.

Ali aliiteka Khaybar. Kwa ushindi wa Khaybar, ukawa ni dola lenye eneo. Hadi ushindi wa Khaybar, Uislam ulikuwa ni dola ya mji, iliyoishia kwenye kuta za Madina. Ali alikuwa ndiye mwandishi aliyeandika ule Mkataba wa Hudaybiyya.

Wakati Makka iliposalimu amri kwa Mtume (s.a.w.w.), Ali alipanda mabegani mwa Mtume na akavunja yale masanamu yaliyokuwa ndani ya Al-Kaaba. Yeye na bwana wake, Muhammad, wakaitakasa Nyumba ya Allah kwa nyakati zote kwa kuondoa alama za uabudu masanamu na ushirikina kutoka ndani yake. Kwa namna hii, Ali alishirikiana na Muhammad, Mtume wa Allah swt. kuanzia mwanzo hadi mwisho, katika kuunda mfumo wa Ufalme wa Mbinguni juu ya Ardhi.

Katika vita vya Hunain, Waislam walikimbia kwa mara nyingine tena. Ali akajiweka katikati ya Mtume na wapiganaji wa kipagani waliotaka kumuua. Alipigana dhidi yao mpaka Waislam walipokusanyika.

Mnamo Oktoba mwaka 630 (9 A.H.) Mtume aliongoza msafara wa kwenda Tabuk, na akamchagua Ali kuwa mwakilishi wake hapo Madina.

Miongoni mwa masahaba wote wa Mtume (s.a.w.w.), Ali alikuwa ndiye mjuzi zaidi. Alikuwa na ujuzi kamili wa Qur'an na tafsiri yake. Alikuwa mbora wa mahakimu wote, na alikuwa ndiye msemaji mwenye ufasaha wa lugha zaidi wa Waarabu.

Kabla tu ya kifo chake, Mtume alitayarisha na kuandaa jeshi la kwenda Syria, na akamteua Usama bin Zayd bin Haritha, kuwa kiongozi wake. Ukimuacha Ali peke yake, aliwaamu-ru Muhajirina wote kutumika chini ya Usama. Ali alikuwa abakie na Mtume hapo Madina.

Katika kuutetea Uislam, ilikuwa ni familia ya Ali ambayo ndiyo iliyojitoa mhanga zaidi. Ubaidullah ibn al-Harith ambaye aliuawa kwenye vita vya Badr, na alikuwa shahidi wa kwanza wa Kiislam katika medani ya vita, alikuwa ni binamu yake wa kwanza. Mas'ab ibn Umayr na Hamza waliuawa katika vita vya Uhud, na wote wawili walikuwa ni ami zake. Jafar Tayyar ambaye aliuawa kwenye vita vya Muutah alikuwa ni kaka yake mkubwa.

Wakati Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) alipofariki, Ali aliandaa mazishi yake, na akamzi-ka. Alikuwa anajua ni nini masahaba wengine walichokuwa wakikifanya wakati yeye akishughulika na kazi hizi lakini hakuruhusu kitu chochote kumvuruga mawazo.

507

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Alitanguliza wajibu wake mbele, kabla ya maslahi yake, na kanuni zake mbele ya siasa.

Edward Gibbon:

"Kuzaliwa, muungano, tabia ya Ali, vilivyomnyanyua yeye juu ya watu wake wote, kunaweza kuthibitisha haki yake kwenye nafasi ya uongozi iliyowazi ya Arabia. Mwana wa Abu Talib alikuwa, katika haki yake mwenyewe, ndiye mkuu wa familia ya Hashim, na mrithi wa ufalme au mlezi wa mji na hekalu la Makka. Nuru ya utume ilikuwa imekwishazimika; lakini mumewe Fatima angeweza kutegemea urithi na baraka za baba yake; Waarabu walikuwa aghalabu wakivumilia utawala wa kike; na wale wajukuu wawili wa Mtume walikuwa mara kwa mara wakibembelezwa kwenye mapaja yake, na kuonyeshwa kwenye mimbari yake, kama matumaini ya zama zake, na Mabwana wa Vijana wa Peponi.

Waumini wa kweli wa mwanzoni wangetamani kutembea mbele yao katika dunia hii na hiyo ijayo; na kama wengine wangekuwa hali ya tabia ya hatari na ngumu sana, ghera na uadilifu wa Ali havikuzidiwa kamwe na mbadili dini yeyote wa hivi kari-buni. Aliunganisha sifa za mshairi, mpiganaji, na walii: hekima zake bado ziko hai katika mkusanyiko wa Hadith za kimaadili na kidini; na kila adui, katika mapambano ya ulimi au ya upanga, alitulizwa na ufasaha na ujasiri wake. Tangu dakika za mwan-zo za ujumbe wake mpaka kwenye ibada za mwisho za mazishi yake, Mtume hakuachwa kamwe na rafiki mkubwa, ambaye alifurahia sana kumwita ndugu yake, mshika makamu wake, na Harun Mwaminifu wa Musa wa pili. Mwana wa Abu Talib alikuja kulaumiwa baadae kwa kupuuza kulinda maslahi yake kwa tamko lenye uzito tu la haki yake, ambalo lingenyamazisha mashindano yote, na akaidhinisha urithi wake kwa maagizo ya Mbinguni. Lakini shujaa huyu asiyekuwa na wasiwasi alijiami-ni mwenyewe: wivu wa himaya, na pengine hofu ya upinzani, vingeweza kuahirisha uamuzi wa Muhammad; na kitanda cha kuugulia kilikuwa kimezingirwa na mwerevu Aisha, binti ya Abu Bakr.

Madai ya urithi na ari kubwa ya Ali vilikuwa ni chukizo kwa tabaka la juu la watu wazima, wenye shauku ya kutawazwa na kutwaa tena fimbo ya enzi kwa uchaguzi huru na wa mara kwa mara; Makuraish hawakuweza kamwe kukubaliana na fahari ya kupindukia ya kizazi cha Hashim."

(The Decline and Fall of the Roman Empire)

Maelezo mafupi hayo ya wasifa, yaliyopita ni sahihi kwa jumla lakini kauli nyingine zinahitaji mabadiliko kidogo. Gibbon amekosea katika kueleza kwamba Ali hakulinda maslahi yake kwa tamko lenye uzito la Mtume. Mtume alikuwa ametoa matamko kama hayo, sio mara moja bali ni mara nyingi sana kama ilivyoelezwa kabla.

508

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mwanahistoria huyu amezungumzia pia juu ya "hofu ya upinzani" ya Mtume. Mtume (s.a.w.w.) hakuwa na hofu juu ya mtu yeyote. Alikuwa amewashinda maadui wenye kuo-gopesha zaidi kuliko wale ambao upinzani wao ungeweza "kumtishia" yeye katika saa yake ushindi.

Gibbon anaendelea kuzungumzia juu ya "uchaguzi huru na wa mara kwa mara." Hilo taba-ka la juu la watu wazima lilikuwa na shauku ya kutawazwa na kutwaa tena fimbo ya enzi lakini kwa ajili yao tu, na sio kwa uchaguzi huru na wa mara kwa mara. Upandaji wa Abu Bakr kwenye madaraka ulikuwa ni "ufaraguzi," na Umar alikuwa ndiye "mwenye sauti ya uchaguzi" katika suala lake. Pale Abu Bakr alipokuwa anafariki, alimteua Umar kama mrithi wake kwa amri. Kwa kufanya hivyo, alitupilia mbali upuuzi wa uchaguzi. Umar, kabla ya kifo chake, aliunda jopo la wateuzi sita, na aliizuilia nafasi ya khalifa iwe ndani yake. Hakuna mtu yeyote nje ya jopo hili anayeweza kuchagukiwa kama khalifa.

Uchaguzi pekee ambao ulikuwa huru kweli ni ule wa Ali ibn Abi Talib. Alichaguliwa katika uchaguzi huru wa kwanza na wa mwisho daima katika historia yote ya Uislam.

Mwishowe, Gibbon anasema kwamba Makuraish hawakuweza kukubaliana na fahari ya kupindukia ya kizazi cha Hashim. Ni sawa. Lakini Makuraish hao hao ambao hawakuweza kupatanishwa na fahari ya kupindukia ya kizazi cha Hashim, walikuwa na shauku ya kukubaliana na fahari ya kupindukia ya kizazi cha waabudu masanamu wa zamani na wala-riba wa Makka. Katika hamu yao ya kutaka kupatanishwa nao hawa, Makuraish ambao walikuwa wamechukua fimbo ya enzi hapo kabla, sasa wakaiweka juu yao.

Kurejeshwa Ufalme wa Mbinguni juu ya Ardhi - (Ukhalifa wa Ali ibn Abi Talib)

Baada ya kuuawa kwa Uthman, woga na hofu viliwaingia masahaba wa Mtume (s.a.w.w.). Wajumbe wa kamati ya uteuzi ya Umar walikimbilia kwenye usalama wa kutojulikana kwao. Mauti ya Uthman yametia hofu katika nyoyo zao. Nchi nzima ilikuwa imejawa na fadhaa, na hakuna hata mtu mmoja, haidhuru angekuwa jasiri na mwenye shauku kiasi gani, ambaye alikuwa tayari kutia shingo yake kwenye kitanzi kwa kulikubali jukumu la kuiendesha serikali. Ilikuwa ni dhima iliyojaa hatari kubwa na mbaya sana.

Lakini ilikuwa ni lazima jambo lifanyike. Chombo cha Uislamu hakingeweza kuachwa kuelea ovyo kwa muda mrefu, na mkono imara ilibidi upatikane wa kukiendesha bila ya kuyumba.

Miaka kumi na mbili ya utawala mbovu imewaamsha Waislam katika usingizi wao mrefu na kuridhika kwao. Sasa wametambua kwamba uongozi wa umma ulipaswa kuwa katika mikono ya mtu ambaye angeweka maslahi ya umma mbele ya maslahi ya familia yake mwenyewe. Kwa hiyo, mara tu baada ya Uthman alipokufa, macho yote yalimgeukia Ali. Masahaba wa Mtume hawakuweza kufikiria juu ya mtu mwingine yeyote ambaye alikuwa

509

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

na uwezo na ujasiri wa kukomesha rushwa katika serikali na vurugu katika nchi, na kudu-misha amani, na sheria na utaratibu kwenye Dar-ul-Islam - Nchi ya Kiislam ambayo ilikuwa imeharibiwa na migogoro ya kiuchumi na kijamii, na ilikuwa imekubwa na mfu-atano wa haraka haraka wa viwewe.

Muhajirina na Ansari mashuhuri wote, kwa hiyo, walikusanyika kwenye Msikiti wa Mtume (s.a.w.w.), na wakakubaliana, katika mkutano wa siri, kumwomba Ali kuchukua madaraka ya serikali na kuliongoza jahazi la taifa kwenye usalama. Ujumbe kwa hiyo ulimwendea kwa Ali, na kumwomba akubali jukumu hili.

Tabari anasema katika Tarikh yake kwamba Muhajirina na Ansari karibu wamsonge Ali. Walimwambia kwamba umma ulikuwa hauna msimamizi, na serikali ilikuwa haina kion-gozi, na kwamba yeye, Ali, pekee alikuwa ndio mtu mwenye sifa stahilifu kabisa za kui-jaza nafasi hiyo, sio tu kwa sababu ya ukaribu wake na Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah swt., bali pia kwa sababu ya sifa zake binafsi na utumishi wake kwa Uislam.

Ilikuwa ni mara ya kwanza tangu kufa kwa Mtume wa Allah swt ambapo ilionekana kwa mtu yoyote hapo Madina kwamba kulikuwa na kitu kama "sifa" za kuwa khalifa. Huko nyuma suala la sifa lilifutikwa kila mara kiongozi mpya alipokuwa apatikane. Umar alim-fanya Abu Bakr kuwa khalifa kwa sababu yeye alikuwa ndio mtu mzima zaidi katika masa-haba wote. Abu Bakr alililipia fadhila tendo la urafiki la Umar kwa kumchagua yeye kama mrithi wake. Uthman alichaguliwa kuwa khalifa kwa sababu alikuwa tajiri na mdhaifu.

Ali, hata hivyo, hakulikubali pendekezo la masahaba hao, na akasema kwamba alipende-lea kuwa mshauri zaidi kuliko kuwa khalifa.

Lakini masahaba hao pia hawakukubali kukataa kwa Ali, na wakasema:

"Hakuna mtu aliyetoa utumishi wa kutambulika kwa Uislam, wala hakuna mtu aliyeko karibu zaidi na Muhammad kuliko wewe. Tunakuona wewe kama mtu mwenye kustahiki zaidi kati ya watu wote kuwa Khalifa wetu."

(Tarikh Kamil, Juz.111, uk.99, Ibn Athir) Ali bado hakukubali, na masahaba bado wakachagiza, na wakasema:

"Tunakusihi kwa jina la Allah swt ukubali huu ukhalifa. Kwani wewe huioni hali ya umma? Je, huzioni hatari mpya zikizuka kila mahali katika nchi za Kiislam? Nani atazisimamisha kama sio wewe?"

(Tarikh Kamil, Juz.111, uk.99, Ibn Athir)

510

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Lakini Ali ni wazi alikuwa ametulia kwenye wazo la kukubali ukhalifa. Haukuwa ni utulivu wa kawaida bali ulikuwa ni matokeo ya fikra za muda mrefu na za busara.

Huko nyuma, wakati mmoja, "tamaa" ilimgharimu Ali kiti cha utawala wa Arabia. Umar alizungumzia kwamba angemchagua Ali kama mtawala wa Waislam kama yeye Ali asingekuwa na "tama" sana. Umar alizungumza kana kwamba tamaa ni kitu cha kushutu-miwa. Kauli yake vilevile ilimaanisha kwamba yeye mwenyewe na baadhi ya wengine wamekuwa makhalifa bila ya tamaa yoyote ile. Huenda ukhalifa ulikuwa ni kitu ambacho kimelazimishwa juu yao zaidi ya kupenda kwao; na hawakuwa na nafasi ila kukubali mzigo wa dhima hiyo!

Kwa vile Umar na Abu Bakr hawakuwa na tamaa, wote hao, na Abu Ubaidah ibn al-Jarrah, wote watatu, lazima wawe ama wamesukumwa na kuburuzwa kwenda kwenye banda la Saqifah!

Kupokea kwa Ali kwa maombi ya masahaba kukubali huo ukhalifa, kungeashiria kwamba alikuwa, hatimaye, ameagana na tama. Huko nyuma, alikuwa kamwe hajapoteza fursa ya kuvuta nadhari ya umma kwenye ubora wa haki zake binafsi, na kwenye haki ya suala lake. Aliamini kwamba ilikuwa ni haki yake ya asli kuwa mrithi wa kwanza wa Mtume wa Allah. Haki hii haikuwa ni kitu ambacho watu wengine wangeweza "kumpa" yeye, ingawa waliweza kuiondoa kutoka kwake, na waliiondoa.

Jambo muhimu katika sera ya serikali ya Saqifa, kama ilivyoonyeshwa kabla, ilikuwa ni kumpinga Ali na Bani Hashim kwenye ukhalifa. Katika hili washika cheo wake wawili wa kwanza walifanikiwa. Mshika cheo wa tatu, hata hivyo, aliuawa katikati ya mvurugiko wa sheria na utaratibu, na hakupata muda wa kuteua mrithi wake mwenyewe. Lakini kama angeishi, angeweza, bila shaka yoyote, kumchagua mkwe wake, Marwan, au binamu yake, Mu'awiyah, kuwa mrithi wake.

Ali alikiukwa katika mara tatu mfululizo huko nyuma. Lakini sasa, baada ya kifo cha Uthman, Waislam walihisi kwamba walikuwa, kwa mara ya kwanza, huru hasa kuteua au kuchagua khalifa kwa ajili yao wenyewe, na chaguo lao kwa hafasi hiyo lilikuwa ni Ali. Kugongana kwa matukio hatimaye, kumeleta ule ukhalifa uilokuwa ukitafutwa kwa muda mrefu, karibu yake. Lakini kwa mshangao wa kila mmoja, Ali hakuonyesha shauku yoyote ya kuukamata. Kwa nini?

Kwa kweli, shauku ya Ali ya kuwa khalifa haikuchochewa na tamaa kama Umar alivyokuwa amedai ingawa hata hivyo hakuna kosa lolote katika kuwa na tamaa. Ali alita-ka kuwa khalifa kwa sababu alijua kwamba yeye na yeye peke yake ndiye aliyekuwa na uwezo wa kukiongoza chombo cha Uislam katika mkondo uleule ambao Mtume wa Allah swt. ameupangilia kwa ajili yake. Watu wengine, yeye alijua, waliukosa uwezo huu.

511

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Taasisi ya ukhalifa ambayo ilikuwa ni urithi wa Muhammad, Mtume wa Allah swt., na ambayo kwa hiyo, ilipaswa kuwa ishara ya unyofu na mamlaka ya kiroho ya Uislam kwa dunia yote, imekuwa, badala yake, katika muda wa robo tatu karne tangu kifo chake, ni ishara ya anasa isiyofifishwa na ubeberu wa dhahiri. Mabadiliko makubwa yamejitokeza katika mtindo wa maisha wa Waislam. Badala ya kuigiza maisha halisi na ya kimaadili ya Muhammad (s.a.w.w.), wengi wao waliiga mitindo ya maisha ya kigeni. Kilichowasukuma wao sasa, hakikuwa ni maadili ya Kiislam bali ni tamaa ya kuwa matajiri na wenye mamlaka kwa gharama yoyote ile. Ule urahisi wa asili na kule kupenda usawa kwa enzi za Mtume wa Uislam, hakukubakia tena. Ubora wa maisha ya umma kwa dhahiri kabisa ulikuwa umeshuka.

Ali aliyajua yote haya vizuri zaidi kuliko mtu mwingine yeyote. Alikuwa akiyapima mapi-go ya moyo ya umma wa Waislam, na alikuwa amefuatilia maendeleo yake au kukosa maendeleo kwake katika pande zote.

Ali pia alijua kwamba ukhalifa haukua tena kitu ambacho mtu anaweza kukichukua na "mazuri na matatizo yake." Mazuri yote yalikuwa yametoweka; na yote yaliyokuwa yame-bakia, yalikuwa ni yale matatizo yake. Kuukubali ukhalifa sasa kutakuwa na maana tu ya kujitwika matatizo hayo.

Mwaka 656 ukhalifa ulikuwa urithi wa fujo na kasoro.

Ali aliona kwamba kama ataukubali ukhalifa, kutakuwa na njia mbili za wazi mbele yake, na itambidi atwae mojawapo. Njia moja itakuwa ni kufuata mkondo wa matukio; kuridhia katika kushuka kwa jumla kwa maadili; kufumbia macho ufisadi na tamaa ya mali ya mag-avana wa majimbo; kuruhusu urasimu katika kunyonya na kukandamiza umma; na kuvu-milia vitendo visivyo vya Kiislam na vya upagani mamboleo vya waungwana wapya. Lakini njia kama hiyo ni kinyume na Uislam, na kwa hiyo, ilikuwa ni ya kinyume zaidi kwake.

Njia ya pili kwa Ali, ilikuwa ni kukubali upinzani wa dunia nzima ambao lazima utajipan-ga wenyewe dhidi yake, na kupigana nao bila kujali matokeo yake madhali ulikuwa unavunja amri za Allah swt. Kama atafanya hivyo, atakuwa anamuigiza tu rafiki na bwana wake wa zamani, Muhammad (s.a.w.w.). Huyu pia aliipinga dunia yote na alipigana dhidi yake bila ya kujali matokeo yake pale alipotangaza ujumbe wake kwa mara ya kwanza. Ali alijua kwamba ikiwa ataukubali ukhalifa, lile tabaka jipya la waungwana wa Kiarabu lita-mpinga, na utawala wake utaanza na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Vita vya wenyewe kwa wenyewe sio mwanzo wenye ndege njema lakini ni ipi njia nyingine mbadala kwake?

Chaguo lililokuwa mbele ya Ali halikuwa kati ya kushinda vita vya wenyewe kwa wenyewe, kama ilikuwepo moja, wala sio kupigana kamwe; badala yake lilikuwa, kati ya

512

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ni lipi lililokuwa sawa na lipi ni makosa; kati ya ukweli na uongo; kati ya kushika kanuni na kufuata siasa-halisi. Alitaka kujenga upya miundombinu ya jamii ya Kiislam au hasa kurudisha ile miundombinu kama vile tu ilivyokuwa wakati wa Mtume wa Allah swt. laki-ni alitambua kwamba angeweza kufanya hivyo tu katika meno ya upinzani uliodhamiriwa hasa kutoka kwa Makuraish.

Ali aliyapima yote haya, na kisha bila kutaka kuanza ukhalifa wake kwa vita ya wenyewe kwa wenyewe, akalikataa ombi la masahaba la kuwa khalifa wa Waislam.

Mwandishi wa kitabu cha Kitabul-ul-Imama was-Siyassa anatoa maelezo yafuatayo ya matukio haya:

Wakati ujumbe wa Muhajirina na Ansari ulipomwendea Ali na kumwomba kuukubali ukhalifa, yeye alikataa. Ujumbe huo ukarudi Msikitini na ukatoa taarifa ya kushind-wa kwake kwa masahaba waliokuwa wapo hapo. Lakini hao masahaba wakasema, "Wakati habari za kifo cha Uthman zitakapofika kwenye sehemu nyingine za himaya hii, hakuna atakayesita kuuliza kama khalifa mpya amechaguliwa au la, na vurugu ambayo sasa ipo kwenye mipaka ya Madina tu, itaenea kwenye majimbo yote. Kuna njia moja tu ya kudhibiti uhalifu usienee, na hiyo ni kumlazimisha Ali kuwa khalifa. Kwa hiyo, rudini kwake, na sisitizeni juu ya kuchukua kwake madaraka ya serikali, na msirejee mpaka awe amekubali kufanya hivyo. Kwa njia hii, habari za kifo cha Uthman na kupanda kwa Ali kwenye kiti cha mamlaka, zitasafiri pamoja kwenda kwenye kila sehemu ya Dar-ul-Islam, na hali itabakia shwari chini ya udhibiti."

Ujumbe huo ulirudi kwenda kumuona Ali, na safari hii, wajumbe wake walivuka mipaka ya ushawishi wa kawaida. Walisema kwamba umma wa Waislam uko kwenye shida kubwa, na ikiwa yeye hataunasua, atawajibika mbele ya Allah swt. na Mtume Wake kwa ajili hiyo. Je, ataucha umma wa Muhammad kwenye hiyo shida kubwa, waliuliza. Kidokezi hiki kipya cha kufaa kilielekea kufanya kazi. Lakini akiwa mwenye kutambua huo upinzani mkubwa kwake wa Makuraish, Ali alikuwa bado anasitasita kulikubali pendekezo hilo. Yeye, kwa hiyo, aliweka kukubali kwake kwa masharti yake mwenyewe, na akauambia ujumbe huo:

"Ninao ujuzi na ufahamu kamili wa Kitabu cha Allah swt., na sunna na mwendo wa Mtume Wake. Katika kuutawala umma wa Waislam, nitatanguliza amri na makatazo yao mbele ya kitu chochote kingine. Sitaonyesha kuyumba katika jambo hili. Nitachukua madaraka ya serikali ikiwa tu sharti hili litakubalika kwenu. Kama ndi-vyo, na Waislam wapo tayari kuchukua kiapo cha utii kwangu, basi waambieni waku-sanyike ndani ya Msikiti wa Mtume." Ujumbe huo ulikuwa tayari kukubali masharti yoyote, na tayari kabisa ukakubali kushika masharti ya Ali.

(Kitab-ul-Imama was-Siyassa)

513

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Baada ya kifo cha Umar, msiri wake, Abdur Rahman bin Auf, alipendekeza ukhalifa kwa Ali kwa sharti kwamba atatoa kiapo cha kufuata sera na taratibu za Abu Bakr na Umar. Ali alikataa kutoa kiapo chochote, na akalikaidi pendekezo lililotolewa na Abdur Rahman bin Auf. Sasa ukhalifa ule ule ulikuwa unapendekezwa kwake kwa mara nyingine tena lakini bila ya masharti yoyote. Kwa kweli, ilikuwa ni yeye Ali ambaye alikuwa anaweka mashar-ti juu ya kukubali kwake pendekezo la kufanywa khalifa na umma wa Waislam.

Ali aliwaambia masahaba kwamba yeye hataridhia uamuzi wao; badala yake, wao wata-lazimika kuridhia uamuzi wake ikiwa watashikilia juu ya kuchukua kwake madaraka ya serikali. Na aliongeza kwamba wao - Waislam - wampe yeye utii usio na maswali - wakati wa amani na wa vita. Wao wakakubali. Kukubali kwao kulikuwa ni ushindi wa maadili. Umma wa Waislam ulikuwa, hatimaye, umesalimu amri kwenye maadili ya Ali!

Umma wa Muhammad, Mtume wa Allah aliyebarikiwa, katika kutafuta usalama na wokovu, walikuwa "wamemwita" Ali ibn Abi Talib kuugeuza ule mwelekeo wa kwenye vurugu na machafuko ndani ya Dar-ul-Islam. Tabari, mwanahistoria huyu, anasema kwamba Ali alipewa "mwito" huo siku ya Alhamisi. Raia wa Madina walikuwa na furaha sana kwa mafanikio yao ya "kumwita" yeye, na walisema kwamba wataswali Swala yao ya Ijumaa pamoja na khalifa wao mpya.

"Kwa nini isiwe aliyembora zaidi?" lilikuwa ndio swali akilini mwa umma wa Waislam pale "walipomwita" Ali kama khalifa wa Uislam. Wakati hatimae walipokuwa huru kuch-agua, wakachagua, kwa silka na bila kukwepa, yule mbora zaidi. Vilevile, wakati umma wa Waislam ulipokuwa unashikilia kwamba Ali achukue cheo cha juu kabisa katika Uislam, ulikuwa, bila kujijua, unasukumizia mbali wale "walafi wa marupurupu" ambao walikuwa wameitapakaa Dar-ul-Islam.

Siku ya Ijumaa, mwezi 18 ya Dhil-Hajj, mwaka wa 35H.A. (Juni 17, 656) Ali ibn Abi Talib aliingia kwenye Msikiti wa Mtume hapo Madina, na alielekea kwenye mimbari kupitia katikati ya kundi la Waislam. Kundi hilo lilikaa katika hali ya kungojea, mikondo ya msisimko ikilimulika kundi hilo, na lilielekea kunyanyuka kwa mtingishiko. Ilikuwepo takriban hali ya mtukuto wa dhahiri na ubadilikaji upya katika mwelekeo wa "kitaifa" wa Waislam.

Ali alishikilia upinde mkononi mwake, na akaegemea kwenye mimbari vile Waislam walipoanza kutoa kiapo cha utii kwake. Kati yake na wao, ulikuwa ni "mkataba wa wazi uliofikiwa waziwazi," na hapakuwa na lolote la siri kuuhusu. Wengi wa Muhajirina na Ansari waliokuwa wapo Madina walimpa kiapo chao cha utii.

514

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ibn Hajar Makki ameandika katika kitabu chake maarufu cha al-Sawa 'iq al-Muhriqah:

"Wale wakongwe wa vita vya Badr wakasema (kumwambia Ali): 'Hakuna mtu anayestahili ukhalifa zaidi yako wewe. Nyoosha mkono wako ili tuweze kukupa wewe kiapo chetu cha utii.' Na hapo wakatoa kiapo cha utii wao kwake."

Ilikuwa ni kwa mara ya kwanza na ya mwisho katika historia ya Uislam, ambapo mtawala hakuwekwa kwa kulazimisha juu ya Waislam. Walichagua mtawala wao wenyewe, na chaguo lao lilikuwa la hiari. Haikutumika ama nguvu, wala tishio la kutumia nguvu, wala shinikizo ama mahongo, wala ulaghai wa maneno katika kuchaguliwa kwake. Hapakuwa na mpagao wa kutwaa madaraka. Kila mmoja alikuwa huru kutoa au kukataa na kiapo chake. Ali mwenyewe alikuwa akipokea viapo takriban bila kufikiri, kama alivyokuwa amezama kwenye njozi juu ya nyakati za bwana wake, Muhammad (s.a.w.w), alipokuwa akipokea kiapo cha Makuraish mara tu baada ya kutekwa kwa Makka mnamo mwaka 630.

Edward Gibbon:

"Vurugu ya makelele ya siku tano ilitulizwa kwa kutawazwa kwa Ali; kukataa kwake kungechochea mauji ya jumla. Katika hali hii ya kuhuzunisha yeye aliimarisha heshi-ma inayostahili ya kiongozi wa Bani Hashim; alitamka kwamba bora angetumikia kuliko kutawala; alikaripia ukaidi wa wageni; na akataka ridhaa rasmi kama sio ya hiari ya wakuu wa taifa."

(The Decline and Fall of the Roman Empire)

Talha na Zubeir walikuwa ndio wa kwanza wa masahaba wa Mtume (s.a.w.w.) kuchukua kiapo cha utii kwa khalifa mpya. Muhajirina na Ansari ndio waliofuatia. Wakafuatiwa na watu wa kawaida. Wa kwanza ambaye hakuwa sahaba kuchukua kiapo cha utii kwa Ali alikuwa ni Malik ibn Ashtar, askari wa upanga mashuhuri zaidi wa Arabia. Hudhaifa ibn Al-Yamani alikuwa ni mmoja wa masahaba maarufu wa Mtume (s.a.w.w.). Alikuwa akiishi huko Kufa na alikuwa amezuiwa kitandani na maradhi ya muda mrefu. Alipozisikia habari za kupanda kwa Ali kwenye kiti cha utawala, aliomba apelekwe kwenye msikiti mkuu wa Kufa. Wakati Waislam walipokusanyika kwa ajili ya Swala, ali-panda kwenye mimbari na akasoma khutba. Alimshukuru Allah swt. kwa baraka Zake, na akaomba rehema Zake Allah swt. ziwe juu ya Mtume Wake, Muhammad (s.a.w.w.), na juu ya kizazi chake, na akasema:

"Enyi Waislam! Nimepokea habari kwamba huko Madina, Ali ibn Abi Talib amechaguliwa kuwa mrithi wa Mtume wa Allah swt. Mimi ninawasihi mtoe kiapo chenu cha utii kwake kwa sababu yeye yuko pamoja na Haki na Haki iko pamoja na yeye, na baada ya Mtume mwenyewe, yeye ndiye mbora wa wale wote walioumbwa au watakaoumbwa kamwe."

515

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hudhaifa ndipo kwa njia ya ishara akaweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto, na akasema: "Ewe Allah! Kuwa Wewe Shahidi kwamba nimechukua kiapo cha utii kwa Ali, khalifa wangu mpya. Zikubali shukurani zangu kwamba Wewe umenipa muda wa kutosha mpaka kumuona yeye akiwa mtawala wa umma wa Muhammad, Mtume Wako."

Hudhaifa alirudishwa nyumbani kwake, na siku chache baadae akafariki. Alikuwa mmoja wa marafiki waaminifu na wapendwa sana wa Muhammad Mustafa.

Ansari, kwa jumla, walikuwa wameonyesha shauku kubwa sana katika kumleta Ali kwenye mamlaka lakini miongoni mwao walikuwepo watu wengine ambao walivizuia viapo vyao vya utii kwake. Hawa walikuwa ni:

Zayd bin Thabit

Hassan bin Thabit

Kaab bin Malik

Abu Said Khudri

Muhammad bin Maslama

Nu'man bin Bashir

Rafa' bin Khudaij

Maslama bin Mukhalid

Kaab bin'Arja

Miongoni mwa watu wa Makka, masahaba wafuatao hawakutoa kiapo chao cha utii kwa Ali:

Abdallah bin Umar bin al-Khattab

Saad bin Abi Waqqas

Mughira bin Shaaba

Abdallah bin Salam

Qadama bin Ma'azun

Suhaib bin Sinan

Wahban bin Saifi

Usama bin Zayd bin Haritha

Wakati nadhari ya Ali ilipokuwa imeelekezwa kwa wale watu ambao walikuwa hawakumpa kiapo chao cha utii, alisema kwamba utii sio kitu ambacho kinaweza kupatikana kwa nguvu. Ili kueleweka vema alisema, utii ni lazima uwe wa hiari. Baadae, ilifikishwa taarifa kwake kwamba watu hao hao walikuwa wakitoroka kimya kimya kuon-doka Madina. Ali hakufanya jaribio lolote la kuwazuia. Alisema kwamba chini ya utawala wake, kila mtu alikuwa na uhuru wa kukaa Madina au kuondoka, na kwamba yeye binaf-si hatamlazimisha mtu yeyote kukaa au kuondoka. Wapinzani wake wa kisiasa wote waliondoka Madina, na wengi wao walikwenda Syria au Makka.

516

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

(Miezi michache baadae, vita ya Basra au vita vya Ngamia vilipiganwa. Abdallah bin Umar bin al-Khattab na Saad bin Abi Waqqas walitoa tamko la kutokuwa upande wowote katika vita hivyo. Kwao kulikuwa ni kutokuwa na upande wowote kwa hiari juu ya masu-ala ya haki na upotofu ingawa walijua ni nani alikuwa haki na nani alikuwa muovu. Wengine wao pia walidai kuwa walikuwa "hawafungamani" na upande wowote, lakini walikuwa "hawafungamani" kwa faida ya maadui wa Ali).

Yaqubi, mwanahistoria huyu, anasema kwamba baada ya kutawazwa huko, Sa'sa'a ibn Sauhan 'Abidi, aliyekuwa sahaba, alimwambia Ali:

"Wallahi, umeleta heshima na utukufu kwenye ukhalifa. Ukhalifa haukuleta heshima na utukufu kwako wewe. Umeunyanyua kwa kuukubali; wala haukukunyanyua wewe. Wewe hukuuhitaji, bali wenyewe ulikuhitaji wewe."

Mwanahistoria mwingine, Khattib Baghdadi, amemnukuu Imam Ahmad bin Hanbal akise-ma:

"Ukhalifa haukuwa pambo kwa Ali; yeye ndiye alikuwa pambo kwa ukhalifa."

Imam Ahmad bin Hanbal aliuweka ukweli wote kwa kifupi. Ali alikuwa kwa hakika ndiye pambo na utukufu wa ukhalifa.

Wakati huo, Muadhini akaleta adhana kwa ajili ya Swala ya Ijumaa. Ali, khalifa mpya, akaongoza jamaa hiyo. Baada ya Swala, alitoa hotuba ya uzinduzi. Alianza mazungumzo yake kwa kumtukuza Allah swt., na kwa kumshukuru Yeye kwa neema na baraka Zake nyingi zisizo na idadi mojawapo ikiwa ni kwamba Ameirudisha haki ya Ali kwake. Alimtakia rehema na amani za Allah, juu ya Muhammad Mustafa na watu wa Nyumbani kwake, na kisha akasema:

"Enyi Waislam! Mmenipa mimi kiapo chenu cha utii, na ninajua kwamba hamku-fanya hivyo bila ya busara ya kutosha. Hata hivyo, malengo yenu na malengo yangu katika kazi zilizoko mbele yetu, sio lazima ziwe zinafanana. Ninataka kuwahama-sisha kwa ajili ya utii na ibada kwa Allah swt; lakini wengi miongoni mwenu wanategemea kwamba nitawapa mali nyingi au vyeo vikubwa katika serikali. Hiki ni kitu ambacho hakitatokea.

"Kumbukeni kwamba kuna njia mbili za maisha; ya haki na ya upotovu. Wengine wenu watatwaa ile njia ya haki na wengine ile ya upotofu. Mnao uhuru wa kuchagua. Lakini kama mtaona kwamba kundi kubwa limefuata ile njia ya upotofu, msifad-haishwe au kushangazwa nalo. Imekuwa kama hivyo mara nyingi, na dunia imejaa ukweli ambao kuaminika kwake ni kwa mashaka. Lakini haki na uadilifu vitashinda mwishoni hata kama ni katika muda maalum vitaonekana kuwa katika hali ya kujiha-mi.

517

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Kwa kweli, pale Allah swt. alipomtuma Muhammad kama Mtume Wake kwa ulimwengu huu, hapakuwa na hata mtu mmoja katika Arabia yote aliyekuwa akijua chochote kuhusu uongofu na unyoofu. Aliwatoa Waarabu katika giza la dhambi na uovu mpaka wakaiona nuru ya uongofu, na wakaipata njia ya kwenye wokovu wa milele. Nilikuwa pembeni mwake tangu mwanzo wa kazi yake mpaka mwisho wake, na nilipigana dhidi ya kumuasi Allah maisha yangu yote. Sikuhisi kamwe uchovu wa mapambano hayo wala sikuogofyeshwa na upinzani wa walezi na mabingwa wa utaratibu wa kabla ya Uislam, hata kama ulikuwa wa kutisha kiasi gani.

"Enyi Waislam! Ninawasihi mnisaidie katika ratiba yangu ya kujenga upya. Allah ni Shahidi wa kauli yangu kwamba shabaha yangu kuu ni kurudisha haki katika Dar-ul-Islam (dola ya Kiislam), kama vile tu ilivyokuwa ni matilaba yake kwamba mimi nifanye hivyo. Sitapumzika mpaka niwe nimeuangamiza udhalimu. Sikilizeni hili kwa makini: Sitavuka mipaka ya Kitabu cha Allah kwa kitu chochote. Sitakuwa na upendeleo kwa yeyote yule awaye. Machoni mwangu, ninyi wote mnalingana. Nitazieneza Sheria za Allah ambazo zimehifadhiwa ndani ya Kitabu Chake, na nitafanya hivyo kwa kuzingatia vigezo tu vya Mtume Wake, Muhammad, aliyebariki-wa.

"Kazi yangu leo hii ni ile ile kama ilivyokuwa katika nyakati za Mtume wa Allah, Muhammad; rehema na amani ziwe juu yake na kizazi chake, na ni kuanzisha au kusi-mamisha upya Ufalme wa Allah swt. katika dunia hii."

Kwa maneno haya, Ali alionyesha sera za serikali yake. Alifafanua malengo yake, na akaelezea namna ya jinsi atakavyoyafanikisha. Alilenga katika kuirudisha upya ile ofisi kuu kabisa katika Uislam, na alizieleza kwa mukhtasari zile taratibu za falsafa yake ya kisi-asa.

Watu wenye utambuzi waliweza kuhisi kwamba serikali ya Ali ingekuwa tofauti kabisa na zile serikali zilizopita, sio tu katika mtindo, sura na nguvu, bali pia katika sifa bainifu, msingi na falsafa. Walihisi kwamba kutakuwepo na tofauti ya ukamilifu na ubora kati ya serikali hizo. Walijua kwamba atahakiki mmomonyoko na uharibifu wa viwango vya maadili binafsi na ya jamii. Kupanda kwake madarakani, kwa hiyo, hakukupendelewa na walezi wa mfumo wa kijamii ambao mategemeo yake yalikuwa upendeleo na nguvu, na kutokujali maadili na ukiukaji wa kanuni.

Kwa mshangao kabisa, ilionekana kana kwamba historia ilikuwa inataka kujirudia yenyewe. Huko Makka, Muhammad Mustafa alikabiliwa na walezi wa mfumo wa jamii ambao ulitegemea upendeleo, nguvu na unyonyaji. Alipojaribu kuubadili mfumo ule, wasi-mamizi wake walimpinga. Upinzani wao ulisababisha mapambano ya silaha. Sasa Ali alikabiliwa na mfumo uleule, na jaribio lake la kuubadili, lilikuwa pia liishie kwenye mapam-

518

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

bano ya silaha na wasimamizi wake.

Kwa upande mwingine, kupanda madarakani kwa Ali kulipokewa sana na kwenye tabaka jingine la watu - lile litokanalo na masikini, mafukara, wasiojiweza, wasio na nguvu, walionyonywa, na wale waliokuwa wanaishi kwa woga na hofu kuu. Watu wa tabaka hili walijua, kana kwamba kwa silika, kwamba Ali atawapatia uhuru kutokana na hofu na umasikini. Walijua vile vile kwamba akipewa nafasi, Ali ataufanyia kazi uhusiano wote wa jamii ya Waislam, na ataubadilisha. Mahadhi, mwendo na mwelekeo wa hotuba zake vili-washa mishumaa ya nuru ya matumaini mapya na kanuni fulani za maisha ndani ya nyoyo zao, na waliweza kutabiri kwamba ataweza kuhuisha ule urithi wa kisiasa wa Muhammad, Mtume wa Allah swt. katika serikali yake.

Hali ya Umma wakati wa Kuingia Madarakani kwa Ali

Wakati Ali alipochukua mamlaka ya serikali mikononi mwake, alikabiliwa na hali ya kutisha sana. Nchi yote ilikuwa inasisimka kwa uchochezi, na maadui zake walitapakaa kila mahali kama mavu. Wanahistoria wawili wa kisasa wa Pakistani, Profesa Sayed Abdul Qadir na Profesa Muhammad Shuja-ud-Din, wametoa mukhtasari wa hali ya Dar-ul-Islam katika mwaka 656 kama ifuatavyo:

Waislam hawakuwa tena wameungana. Walikuwa wamegawanyika katika kambi nyingi. Waislam wengi waliweka maslahi yao binafsi mbele ya maslahi ya jumla ya umma.

Mapambano ya hivi karibuni yameleta mikononi mwa Waislam ule utajiri mkubwa wa himaya mbili tajiri sana za dunia - ya Uajemi na ile ya Roma. Kila mmoja wao alitaka sehemu kutoka kwenye mafanikio haya, na walijaribu kunyakua kila kile mtu alichoweza. Katika utafutaji huo wa kikatili wa pesa, Waislam wengi waliweka pembeni mifano bora ya Kiislam kana kwamba ilikuwa isiyopasika.

Ingawa Talha na Zubeir, wawili wa masahaba wenye nguvu sana, walikuwa wa kwanza kutoa kiapo cha utii kwa Ali, walikuwa wa kwanza pia kukikana. Kwa kuvunja kiapo chao, waliusukuma umma kwenye vita vya wenyewe kwa wenye we.

Mu'awiyah alikuwa gavana wa Uthman huko Syria. Ule uasi wa Talha na Zubeir dhidi ya mamlaka halali huko Madina, ulimtia moyo yeye wa kuukaidi. Ali alimtaka yeye atoe kiapo chake cha utii kwake lakini alikataa, na badala yake, alidai kutoka kwa Ali, zichukuliwe hatua dhidi ya wauaji wa Uthman. Mu'awiyah alikuwa na mapenzi kidogo sana na Uthman lakini alikuwa na mapenzi makubwa sana ya kuongezea matatizo ya Ali. Alitegemea kwamba Ali atajaribu kuwaadhibu wale watu wote ambao walikuwa wameasi dhidi ya Uthman, nao wangempinga yeye, na upinzani wao ungesababisha vita vya

519

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wenyewe kwa wenyewe. Vita vya wenyewe kwa wenyewe hapo Madina, yeye aliwaza moyoni, vingefanya iwezekane kwa yeye kuukamata ukhalifa.

Lakini Ali hakunasa katika mtego wake, na alimwambia Mu'awiyah: "Kwanza nipe kiapo chako cha utii, na uniache nirudishe amani katika dola. Mara hali itakaporudia kwenye kawaida, ndipo sisi wote, tutakapowafikisha wauaji wa Uthman mashtakani, na haki itatawala."

Lakini Mu'awiyah hakuwa na nia ya kutoa kiapo cha utii kwa Ali. Yeye, kwa hiyo, alishik-ilia juu ya kukamatwa na kuuawa kwa wauaji wa Uthman.

Wakitoa maoni yao juu ya majibu ya Mu'awiyah kwa Ali, maprofesa hawa wawili wanaen-delea kusema kwamba:

"Kwa maoni yetu sisi, Ali alikuwa na haki kabisa. Maslahi ya watu binafsi, hata kama yangekuwa na umuhimu kiasi gani, hayawezi kutolewa muhanga kwa maslahi ya 'Taifa.' Hata kuwepo na misiba mikubwa kiasi gani ya mtu mashuhuri sana, umoja wa nchi lazima ulindwe kwa gharama zote. Maslahi ya 'Taifa' bado yanabakia kuwa ni muhimu, na hayawezi kutolewa muhanga kwa ajili ya maslahi ya mtu binafsi. Kuhakikisha usalama wa dola ya Kiislam ni wajibu wa kwanza wa kiongozi wa umma wa Waislam. Ikiwa kama Ali angefuata ushauri wa Mu'awiyah, vita vingezu-ka katika kila sehemu ya dola. Lakini maadui wa Ali hawakushiriki katika kujishuhul-isha kwake juu ya amani, na msimamo wao ulisababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe miongoni mwa Waislam. Kama Talha, Zubeir na Mu'awiyah wangekuwa na ukweli wowote, wangeyaweka chini maslahi yao wenyewe mbele ya maslahi ya Uislam, na Waislam wasingemwaga damu ya kila mmoja wao."

(History of Islam, Part 1)

Yaliyoelezwa hapo ni makadirio sahihi ya ghasia za kisiasa katika Bunge la Uislam wakati Ali alipochukua madaraka ya serikali. Wanahistoria wengine wengi pia wameyachambua matukio yaliyotokea kabla ya vile vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Waislam. Wamejaribu kuonyesha sababu zake lakini wengi wao, inavyoelekea, wameacha jambo muhimu sana, au kama hawakuliacha, basi wamejaribu kulificha.

Kuporomoka kwa bunge la Saqifah kulikuwa na uhakika wa kufuatiwa na ghasia nyingi, kubwa. Lakini jambo ambalo wanahistoria hawa walikuwa hawako tayari kulikubali ni kwamba vile vikwazo vikali vilivyochipukia katika wakati wa ukhalifa wa Ali, vilipandik-izwa katika nyakati za (viongozi) waliomtangulia. Maasi yaliyotokea ghafla katika wakati wake, yote yalipata mizizi wakati wa huko nyuma. Sir John Glubb, mwanahistoria wa kisasa, anaandika katika kuhusu ukhalifa wa Uthman bin Abdul Aziz kama ifuatavyo:

520

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Utawala wa Umar bin Abdul Aziz, ulikuwa umesafika kabisa kutokana na maasi na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, lakini bado inaweza kujengwa hoja kwamba ilikuwa ni katika wakati wake ambapo mbegu zilipandwa, za yale mapinduzi ambayo yalikuwa yaangushe kabisa himaya hiyo. Hili halikuwa lenye kushangaza bali hasa lilikubaliana na maendeleo ya kawaida ya kisiasa. Kwani imekuwa ikitokea mara kwa mara kwamba nchi imebakia shwari katika vipindi vya utawala wa kidhalimu na kidikteta lakini kwamba uasi ulitokea ghafla mara tu utawala wa haki na huru zaidi ulipokuwa umeanzishwa. Hivyo ule ukhalifa mwema wa Umar bin Abdul Aziz ulianzisha vuguvugu ambalo lilikuwa liongozee kwenye kuiangamiza familia yake."

(The Empire of the Arabs, uk.175, 1963)

Sir John Glubb ametoa tafsiri sahihi na potovu pia katika kifungu kilichoelezwa hapo juu. Yuko sahihi katika kueleza kwamba "imetokea mara nyingi kwamba nchi imebakia shwari katika vipindi vya utawala wa kidhalimu na kidikteta lakini maasi yakatokea ghafla mara tu baada ya utawala wa haki na huru zaidi ulipoanzishwa." Falme ya Waarabu ilikuwa shwari katika vipindi vya utawala wa kidhalimu na kidikteta vya serikali ya Saqifah lakini uasi uliibuka ghafla mara baada ya ule utawala wa haki na huru wa Ali ulipokuwa umeanzishwa.

Lakini hatuwezi kukubaliana na mwanahistoria huyu pale anapodai kwamba ilikuwa ni katika wakati wa Umar ibn Abdul Aziz ambapo "mbegu zilipandwa, za yale mapinduzi ambayo yaliangamiza kabisa ufalme wa Bani Umayya." Mbegu kama hizo hazikupandwa wakati wa Umar ibn Abdul Aziz bali zilipandwa na watangulizi wake na warithi wake pia.

Wala hatuwezi kukubaliana na madai ya mwanahistoria huyu kwamba "ukhalifa mwema wa Umar ibn Abdul Aziz ulianzisha vuguvugu ambalo lilikuwa lisababishe kuangamia kwa familia yake." Ukweli wenyewe ni kinyume chake. Yumkini kabisa kwamba mwenendo wa kitakatifu wa Umar ibn Abdul Aziz ulitoa ucheleweshaji kwa muda kwa Bani Umayya, na kwamba, bila ya yeye, wao wangeweza kuangamia mapema zaidi kuliko pale walipoangamia.

Umar ibn Abdul Aziz hastahili kwenye mtindo usiobadilika wa Bani Umayya. Alikuwa mchamungu na mpenzi wa Mungu sana na wao walikuwa wasiomjua Mungu kiasi kwamba hawakuweza kupatana. Walimuua kwa kutumia sumu.

Dr. Hamid-ud-Din:

"Hapakuwa na mapambano makubwa wala nchi yoyote mpya iliyotekwa wakati wa ukhalifa wa Umar ibn Abdul Aziz. Na bado ukhalifa wake ulikuwa maarufu sana katika historia ya Uislam kwa sababu ya mabadiliko aliyoyaanzisha. Alihuisha democra-sia halisi ya Kiislam mienendo ya Khulafa-i-Rashida (makhalifa walioongoka).

521

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kuanzia wakati wa Mu'awiyah, ukhalifa uligeuka kuwa ni serikali binafsi ya khalifa. Yale maovu yote ambayo ni sehemu ya serikali za kidikteta na kidhalimu, yaliingia kwenye ukhalifa. Watu walikuwa wamepoteza uhuru wao. Baytul-Mal (hazina ya umma) imekuwa ni mfuko binafsi wa mtawala. Hakuna chochote kilichotumika kuondoa dhiki za maskini, na yote ilitumika kwenye fahari na starehe za tabaka la watawala. Umar ibn Abdul Aziz alikusudia kukomesha vitendo hivi. Kitu cha kwan-za alichokifanya, kilikuwa ni kukamata yale mashamba makubwa ambayo wafanyabiashara wa Bani Umayya walijitwalia wao wenyewe.

Njia nyingi zisizokuwa za haki na za haramu zilitumika kulita mapato zaidi kwenye hazina ya umma. Kwa mfano, wale Dhimmiy (wasiokuwa Waislam wanoishi chini ya ulinzi wa Dola ya Kiislam)), ambao walikuja kuukubali Uislam, walilazimishwa kuli-pa jizya (kodi ya kichwa). Kwa mujibu wa sheria ya Qur'an, ni wale raia wasiokuwa Waislam tu wa Dola ya Kiislam, waliopaswa kulipa jizya. Umar ibn Abdul Aziz ali-tuma maagizo kwa magavana wote katika majimbo kwamba endapo Dhimmiy yoy-ote atasilimu, basi asidaiwe jizya. Aliikomesha tabia hii, na mamia ya maelfu ya Dhimmiy wakawa Waislam baada ya kuenezwa kwa agizo hili.

Mu'awiyah alikuwa ameanza desturi ya kumlaani Ali ibn Abi Talib hadharani.Yeye mwenyewe na magavana wake na watendaji wa dola walitumia takriban lugha isiyo na kiasi na ya matusi kutoka juu ya mimbari za misikiti juu ya Ali. Baada ya Mu'awiyah, warithi wake waliiendeleza tabia hii. Lakini Umar ibn Abdul Aziz aliikomesha. Aliwaamuru magavana wake kusoma Aya za Qur'an kutoka juu ya mimbari badala ya kumlaani Ali.

Mabadiliko haya hayakupendelewa na kundi la wale wenye mamlaka la Bani Umayya, na mapenzi ya khalifa ya kufuata sheria na haki hayakumfanya apendwe sana pamoja nayo. Wafanyibiashara wa Bani Umayya waliamini kwamba kama angetawala himaya hiyo kwa muda mrefu wa kiasi chochote kile, basi watakuja kupoteza mamlaka yao na marupurupu yao. Wao, kwa hiyo, walibuni njama, na wakamlisha sumu katika chakula chake. Alikufa kutokana na athari za sumu hii mnamo mwezi wa Rajab wa mwaka 101 H.A. (720 A.D.)

(History of Islam, kilichochapishwa na Ferozsons Ltd, Karachi na Lahore,

Pakistan, uk.324, 331-3,1971).

Ilikuwa haikwepeki kwamba mtu kama Umar ibn Abdul Aziz angekuwa shahidi. Yeye ni mmoja wa Waislam waliokufa kishahidi. Mwenyezi Mungu aihurumie roho yake njema.

Ali alikabilana na mabishano ya mawanda makubwa mno. Lakini hayakumtisha. Kwa moyo safi na akili yenye msimamo juu ya Mapenzi ya Allah, swt., aliianza kazi ya kurud-isha amani na utawala wa Allah kwenye dola ya Uislam. Kuchukua kiapo kwa Ali

522

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hakukuwahi kumalizika wakati uasi ulipoibuka pande zote kumzunguka yeye. Kama aliushughulikia mmojawapo, mwingine ulichomoza kichwa chake. Hivyo ile miaka michache ya utawala wake ilitumika katika kuizima. Baadhi ya wakosoaji wake walisin-gizia kwamba maasi hayo yalikuwa ni matokeo ya "ujinga" wake.

Maasi ya wakati wa utawala wa Ali hayakusababishwa na ujinga wake. Kama ilivy-oonyeshwa hapo juu, yaliota mizizi huko nyuma. Mtu mwingine yoyote angeweza kuka-biliwa na wimbi hilo hilo la matatizo, na inaelekea kabisa kwamba angeshindwa kupam-bana nayo.

Kwa hali hiyo, Ali aliendesha utawala wa nchi, na pia alijaribu kuyazuia maasi hayo kama ilivyokuwa wajibu wake. Alilishinda kundi moja la maasi huko Basra, na angeweza kul-ishinda lile jingine huko Siffin kama kundi hilo lisingechukua kimbilio kwenye usaliti. Hata katika nyakati hizi za ghasia, alitekeleza mabadiliko muhimu ya kiuchumi na kijamii.

Ingawa sababu za maasi zilitokea kabla ya ukhalifa wa Ali mwenyewe, chache kati ya hizo zinaweza kuelezwa zaidi kama ifuatavyo kwa uelewa mzuri zaidi wa matukio yaliyotokea baadae.

1.    Sera ya Ali ilikuwa ni ya ki-Qur'an halisi. Hakuwa aafikiane na maadili na tarat-ibu za Kiislam kwa ajili ya kung'ang'ania tu kwenye madaraka na mamlaka. Kama angekuwa ametwaa sera za kisiasa hasa pia, angeweza kufanikiwa vizuri sana lakini kufanya hivyo kungebadili mwelekeo wa serikali yake kutoka ile ya Kiislam na kuwa ya "kikabila."

Ahmad Hasan Zayyat wa Misri, anasema ndani ya kitabu chake, Adab al-Araby (uk. 174) hivi:

"Ali hakuyumba kabisa katika masuala ya dini, na hakuujua udanganyifu katika mambo ya kidunia. Ilikuwa ni utukufu huu wa tabia yake ambao Mu'awiyah aliutu-mia kwa manufaa yake."

2.  Ali hakujaribu kuwaridhisha matajiri na wenye nguvu dhidi ya masikini na wany-onge. Yeye siku zote aliyaweka maslahi ya masikini na wanyonge mbele ya maslahi ya tabaka la waungwana wa Kiarabu. Tabaka hili la waungwana wa Kiarabu lililichukia hili, na lilimuonyesha kuchukia kwao.

Alipokuwa akigawanya mapato ya hazina ya umma, Ali hakutofautisha kati ya mabwana na watwana, matajiri na masikini, na Waarabu na wasiokuwa Waarabu. Machoni mwake, wote walikuwa sawa. Mamwinyi wa Kiarabu walilalamika dhidi utendewaji wa namna hii lakini yeye aliyapuuza malalamiko yao. Mara malalamiko yao yalilipukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe.

523

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

3. Mara tu baada ya Ali kuchukua madaraka ya serikali, aliwauzulu magavana na watendaji wote waliokuwa wameteuliwa na Uthman. Lakini wengi wao hawakuwa na nia ya kuachia nafasi zao.

Kufukuzwa kwa Magavana wa Uthman

Wakati Ali alipochukua madaraka ya serikali, magavana na wakusanya kodi wa Uthman walikuwa wakkipora nchi bila ya hofu ya kuhojiwa na serikali kuu. Kitendo cha kwanza cha Ali kilikuwa ni kutoa amri ya kufukuzwa kwao.

Mughira bin Shaaba alikuwa mmoja wa masahaba wa Mtume (s.a.w.w.). Umar alikuwa amemteua kuwa gavana wa Kufa lakini Uthman alimfukuza. Yeye alikuwa hajachukua kiapo cha utii kwa Ali lakini alimshauri dhidi ya kufanya mabadiliko yoyote ya mazito katika sera na watumishi. Alisema kwamba kama magavana walioteuliwa na Uthman hawakutambua mamlaka yake yeye (Ali) kama khalifa.basi asiwaondoe kwenye kazi zao. Alimtahadharisha Ali kwamba kama atawafukuza, kabla ya kuimarisha madaraka yake mwenyewe, wataasi dhidi ya mamlaka yake.

Binamu wa kwanza wa Ali, Abdallah ibn Abbas, pia alimpa ushauri ambao, kimsingi, ulikuwa sawa na ule wa Mughira. Busara, alisema, inaamuru uangalifu kwa wakati huu.

Lakini ushauri kama huo ulikuwa haukubaliki kwa Ali. Yeye aliamini kwamba ni mwenye kuwajibika kwa Allah swt. kwa matendo yake yote, na asingeweza, kwa hiyo, kuruhusu watu wasiofaa na madhalimu kutawala juu ya Waislam. Yeye, kwa kweli, alijiona yeye mwenyewe mwenye kuwajibika kwa Allah swt., sio tu kwa matendo yake binafsi, bali pia kwa matendo ya magavana wake. Yeye kwa hiyo, aliweka imani yake kwa Allah swt., aki-jua kwamba alikuwa anafanya jambo la sawasawa, na akakataa kubatilisha maagizo yake.

Colonel Osborne:

"Ali alishauriwa na baadhi ya washauri wake kuahirisha kuwafukuza wale magavana waovu waliokuwa wameteuliwa kabla mpaka yeye mwenyewe atakapokuwa salama dhidi ya maadui zake wote. Ngome ya Uislam hii, shujaa asiye na woga wala fedhe-ha alikataa kuwa na hatia ya unafiki wowote au kukubaliana na dhulma. Hii tabia yake ya kiungwana isiyoyumba ilimgharimu dola na maisha yake. Yeye kamwe hathamini kitu chochote juu ya haki na ukweli.

Watu wengine wanadhani kwamba kama Ali asingewafukuza magavana wa Uthman, asingewachochea katika kumpinga yeye. Lakini wazo kama hilo limeegemea kwenye ushamba. Magavana hao wa Uthman wangempinga Ali bila ya kujali ni nini alichok-ifanya. Walikuwa ni maadui zake wa tangu zamani.

524

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Zifuatazo ni baadhi ya sababu za kwa nini Ali aliwafukuza magavana wa Uthman:

1.  Makusudio ya Ali yalikuwa ni kurudisha ile serikali ya Muhammad Mustafa, na kutekeleza mfumo wa Kiislam. Ili kufanya hivi, ilimbidi "kusafisha" ile serikali aliyokuwa ameirithi, kwa kuondoa kutoka humo lile kundi la walafi la Bani Umayya. Badala yao, ilikuwa ateuwe watu wachamungu ambao waliamini kwam-ba wanawajibika kwa Allah swt. kwa yote yale ambayo wameyatenda.

2.  Waislam walikuwa wamemuomba Uthman awaondoe magavana wake wenye majivuno na ubinafsi, na kuteuwa watu wachamungu badala yao. Lakini ali-wageuzia sikio la uziwi kwenye maombi yao ambapo walichukua hatua zingine kulazimisha kubadilishwa kwa magavana. Kama Ali angepitisha muda kwenye suala hili, wangeipindua serikali yake kama vile walivyoipindua ile serikali ya mtangulizi wake.

3.   Kama Ali asingewafukuza magavana wa Uthman, angejifanya mwenyewe awe mwenye kubanwa na kosa la "kuwa na hatia kwa ushirikiano."

4.   Mu'awiyah hakuwa ametosheka na kutawala Syria peke yake; alitaka kutawala dola yote ya Waislam kama khalifa wake. Alipogundua kwamba Uthman alikuwa amejifanyia maadui wengi sana yeye mwenyewe binafsi, alijaribu kutumia fursa ya hali hiyo. Alimshauri Uthman kwamba angeondoka Madina na aende naye (Mu'awiyah) Syria, ambako, alimhakikishia yeye, kwamba atakuwa salama ambapo katika makao makuu yake mwenyewe, alimtahadharisha, kuwa angeweza kuuawa. Mu'awiyah alikuwa na sababu nzuri sana za kujaribu kum-chukua Uthman kwenda naye Damascus, Uthman angekuwa "khalifa asiyekuwa na madaraka." Mu'awiyah angemnyang'anya mamlaka yake yote na kuyachukua mikononi mwake mwenyewe, na kwa hiyo, angekuwa khalifa asiyepingika katika uhai wake Uthman mwenyewe, na halali kisheria baada ya kifo chake Uthman. Lakini Uthman hakwenda Syria, na mkakati wa Mu'awiyah haukufanya kazi. Lakini wakati Uthman alipouawa, Mu'awiyah alianzisha kampeni yake dhidi ya Ali akitafuta kulipiza kisasi kwa ajili ya damu yake. Ali hakuwa na fursa japo ndogo ya uchaguzi katika jambo hilo ila kumfukuza Mu'awiyah.

5.     Uthman alikuwa ameteua magavana, sio kwa sababu walikuwa na uwezo wowote ule au kwa kuwa walipenda kuwatumikia Waislam. Aliwateua kwa sababu tu walikuwa na udugu naye. Ali aliuona uchaguzi huu kama ni kuingilia kati juu ya haki za wale watu ambao walikuwa wanafaa kwa uwezo wao, uchamungu, na utumiishi kwa Uislam, kutawala Waislam. Yeye, kwa hiyo, akawaondoa hao.

525

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

6. Uthman alikuwa amewateua watu wa familia yake mwenyewe kama magavana wa majimbo. Magavana wake walikuwa na watu na vifaa muhimu kwa vita. Uthman alikuwa amezingirwa, chini ya ulinzi ndani ya kasri lake kwa muda wa siku 49. Alituma maombi mengi sana kwao ili waje kumuokoa lakini hawakuja, na akauawa. Ikiwa kama magavana hawa wameweza kumtelekeza mfadhili wao wenyewe kwa urahisi namna hiyo, ni vipi Ali angeweza kuwategemea wao katika kuhitajika sana kumtii yeye? Yeye kwa hiyo, aliamua kutokuwa chini ya miguu yao.

Mtu mmoja kwa jina la Abu Tufail Kinani, mkazi wa Madina, wakati mmoja alikwenda Damascus kumuona Mu'awiyah. Walipokutana, mabishano yafuatayo yalitokea kati yao:

Mu 'awiyah: Ulikuwa wapi wewe wakati Uthman alipouawa?

Kinani:          Nilikuwa niko Madina.

Mu 'awiyah:   Je, ulifanya chochote ili kuokoa maisha yake kutokana na maadui zake?

Kinani:         Hapana.

Mu 'awiyah: Kwa nini hukufanya? Ulijua kwamba ilikuwa ni wajibu wako kufanya kila linalowezekana ili kumuokoa yeye.

Kinani: Ninadhani ilikuwa iwe hivyo. Lakini chochote kile kilichokuzuia wewe kujaribu kuokoa maisha yake, pia kilinizuia na mimi kujaribu kuokoa maisha yake.

Magavana Wapya

Katika mwezi wa Muharram wa mwaka wa 36 H.A., Ali aliwateua magavana wafuatao:

1. Qays ibn Saad Ansari, gavana wa Misri.

Qays aliweza kuingia Misri bila ya upinzani na kuchukua mamlaka ya serikali. Huko Misri, aliwakuta Waislam wamegawanyika katika makundi matatu. Moja lilikuwa likiund-wa na wafuasi wake mwenyewe; la pili la wapinzani wake, yaani, wafuasi wa Uthman; na kundi la tatu lilikuwa halijakata shauri katika utiifu wao. Qays aliamua kujishughulisha na haya makundi mawili ya mwisho, lakini kutoa uangalifu wa moyo wake wote kwenye utawala wa nchi.

Qays, kwa muonekano wa dhahiri, alikuwa ndiye mtu wa kuvutia sana hapo Madina.

526

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Alikuwa mrefu, mkali na mwenye nguvu kimaumbile; na alikuwa ni mashuhuri kwa elimu yake, uchamungu na ufasaha. Alikuwa pia ni mtu wa ufahamu na uonambali mkubwa, na alikuwa halingani kabisa na watu kama akina Mu'awiyah, Amr bin Al-Aas na Mughira bin Shaaba katika maarifa na akili. Lakini kama bwana mkubwa wake mwenyewe, Ali, yeye pia hakuamini kwamba penye nia pana njia. Falsafa yake ya maisha ilikuwa ikitawaliwa na ile kanuni kwamba sera ya kisiasa lazima itegemee mafundisho ya Qur'an.

2.  Uthman bin Hunaif, gavana wa Basra.

Uthman aliweza pia kuingia Basra na kuchukua madaraka ya serikali. Yeye pia aliwakuta Waislam huko Basra wamegawanyika katika makundi matatu kama Qays alivyokuta huko Misri, na yeye pia alitwaa sera kama ile aliyokuwa ametumia Qays huko Misri.

Uthman bin Hunaif alitokana na familia mashuhuri ya Ansari. Alikuwa ni rafiki wa karibu wa Mtume (s.a.w.w.). Wakati wa ukhalifa wa Umar, alikuwa ndiye kamishna wa fedha wa Iraq.

3.  Ammara bin Shihab Ansari, gavana-mteule wa Kufa.

Ammara aliondoka Madina kwenda kushika kazi yake huko Kufa. Lakini pale alipofika Zabala, kituo cha njiani kwenye njia iendayo Iraq, alikutana na mtu mmoja, Talha bin Khuwaylid Asadi, akitokea Kufa. Alimshauri Ammara kurejea Madina, ama vinginevyo, alisema, atakwenda kuuawa huko Kufa. Papo hapo, Ammara hakwenda Kufa, na akarudi Madina.

4.   Sahl bin Hunaif Ansari, gavana-mteule wa Syria.

Sahl aliondoka Madina. Kabla hajaukuta mpaka wa Syria, alikutana na kundi la askari wapanda farasi. Walimuuliza yeye ni nani na alikuwa akienda wapi. Aliwaambia kuwa yeye ndiye gavana mpya wa Syria. Wao wakasema walikuwa ni watu wa Syria na kwamba hawamkubali mtu yoyote kama mtawala wao isipokuwa Mu'awiyah. Waliongeza pia kwamba kama angeendelea kwenda mbele zaidi angeuawa. Hapo, Sahl hakuingia Syria, na akarudi Madina.

Sahl alikuwa ni ndugu yake Uthman bin Hunaif. Yeye pia alikuwa ni sahaba wa Mtume (s.a.w.w.), na alikuwa amepigana katika vita vyake vyote, akijipatia sifa ndani yake kwa ujasiri wake.

5. Ubaidullah ibn Abbas, gavana wa Yemen.

Ubaidullah alikuwa ni binamu wa kwanza wa Muhammad na Ali. Aliingia Yemen bila ya

527

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

upinzani wowote na akachukua madaraka ya serikali. Yayla bin Umayya ambaye alikuwa gavana wa Uthman huko Yemen, alikuwa ameondoka kabla ya kufika kwake, na alikuwa amechukua hazina ya umma na kuondoka nayo.

6. Qathm ibn Abbas, gavana-mteule wa Makka.

Qathm alikuwa mdogo wake Ubaidullah. Anasemekana alikuwa amechukua kufanana kunakovutia sana na Mtume. Alikuwa bado yuko Madina wakati Makka ilipogeuka kuwa kituo cha upinzani kwa Ali. Yeye kwa hiyo, ilimbidi asubiri mpaka hali iliporudia kwenye kawaida huko Makka. Baada ya kifo cha Ali, aliondoka Arabia, akaenda Samarkand iliyoko Asia ya Kati, na akafa huko.

Miezi michache baada ya kupanda kwake kwenye mamlaka, ilimbidi Ali aondoke Madina kwenda Basra kukabiliana na changamoto ya waasi, na alimteua Sahl bin Hunaif Ansari kuwa gavana wa makao makuu katika kutokuwepo kwake yeye mwenyewe.

Baada ya vita ya Basra, Ali alimteua Abdallah ibn Abbas kama gavana mpya wa mji ule. Abdallah alikuwa ni "mwanafunzi wa kuchukua kazi" ya bwana wake, Ali, na alipata umaarufu mkubwa kwa elimu yake. Alikuwa ni mmoja wa mabingwa wa mwanzo kabisa katika tafsiri ya Qur'an Tukufu. Alikufa huko Taif akiwa na umri wa miaka 70.

528

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Utangulizi wa Vita

Kama ilivyoonyeshwa hapo kabla, magavana wa Ali walikuwa hawakuweza kuingia Syria na Kufa kwa sababu ya upinzani wa magavana wa Uthman kwake yeye. Lakini Syria na Kufa havikuwa ndio vituo pekee vya uchochezi wa maasi. Matatizo yalikuwa yanapikwa kwa ajili ya Ali ndani ya Madina yenyewe yakitishia usalama wa dola. Yeye kwa hiyo, alilazimika kuahirisha kuchukua hatua juu ya matatizo yanayoibuka kutokana na uchochezi wa maasi katika majimbo ya mbali kwa muda fulani.

Kama ilivyoonyeshwa hapo kabla, wakati Ali aliposimikwa kwenye cheo kama khalifa wa Waislam, watu wawili wenye nguvu sana hapo Madina, yaani, Talha na Zubeir, walikuwa wa kwanza kutoa kiapo cha utii kwake. Wote wawili, kama wengine wengi, wamekuwa matajiri sana katika utawala wa wale makhalifa watatu wa kabla ya Ali. Waliendelea kupa-ta utajiri zaidi na zaidi, na sasa, kwa kupanda kwa Ali madarakani, walitaka pia kuwa magavana wa yale majimbo yenye utajiri ya Basra na Kufa. Walipokuwa wanatoa kiapo cha utii kwa Ali, walikuwa sirini wakitumainia kwamba kama nipe nikupe, Ali angewateua kama magavana. Lakini Ali aliwateua watu wengine kama magavana, na hakuwapa wao kitu chochote. Hili liliwatoa matumaini. Ingawa walivunjika mioyo, hawakufikiria sana juu ya kukatishwa tamaa kwao, na wakiwa watu wenye ubwana, waliamua kujishughulikia wao wenyewe.

Talha na Zubeir walibuni mbinu ya kumghilibu Ali. Walimwendea kwake, na wakamjul-isha kwamba wanakwenda Makka kufanya umra (hijja ndogo). Mara tu mabwana wakub-wa wawili hawa walipokuwa Makka, walivunja kiapo chao cha utii kwa Ali. Walitamka kwamba walikuwa wametoa kiapo chao kwa mashaka mengi akilini mwao. Kwa wakati huu, Aisha, binti ya Abu Bakr, na mmoja wa wajane wa Mtume, alikuwa pia yuko Makka. Alikuwa amefanya Hijja lakini hakuwa amerudi Madina pale aliposikia kwamba Ali amekuwa khalifa, na alitangaza kwamba atalipiza kisasi kwa ajili ya kifo cha Uthman. Talha na Zubeir walimwendea nyumbani kwake huko Makka. Walimpa maelezo juu ya yale matukio ya Madina. Kile alichokisikia kutoka kwao, kilimtia nguvu katika azma yake ya kuwa mtetezi wa Uthman. Kwa Talha na Zubeir alikuwa amepata waungaji mkono wenye shauku kubwa katika "shughuli" yake. Hili lilifanya ule "utawala wa watu watatu" wa Aisha, Talha na Zubeir, uliopangwa kwa makabilano na Ali, mrithi wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), na kiongozi wa haki wa Waislam. "Kiungo muhimu" cha huu utawala wa watu watatu kilikuwa ni chuki juu ya Ali.

Utambulisho wa kila mmoja wa "watawala" hawa umetolewa hapa chini ili kumwezesha msomaji kuuelewa mfuatano wa yale matukio ambayo yalisababisha kutokea kwa vita vya

529

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

pili vya wenyewe kwa wenyewe katika Uislam. Talha bin Ubaidullah

Baba yake Talha, Ubaidullah na baba yake Abu Bakr, Abu Qahafa, walikuwa ni ndugu. Mama yake Talha alikuwa ni binti ya Hadhrami, na baba yake, Ubaidullah, alikuwa ni mume wake wa pili. Kwa muda mfupi, alikuwa pia mke wa Abu Sufyan, baba yake Mu'awiyah lakini alikuwa amemtaliki.

Talha alimuoa Umm Kulthum, binti ya Abu Bakr, na hili lilimfanya kuwa shemeji yake Aisha. Pale Abu Bakr alipomteua Umar kuwa mrithi wake, Talha alipinga kwa nguvu sana, na alimvuta nadhari yake juu ya kiburi cha khalifa-mteule huyo. Baadaye, wakati Umar mwenyewe alipokuwa anafariki, alimfanya Talha kuwa mjumbe wa kamati yake ya uteuzi.

Talha alivunja kiapo chake cha utii kwa Ali kwa sababu huyu Ali hakumfanya kuwa gavana wa Basra. Huenda alikuwa na sababu hizo hizo kwa upinzani wake, hapo mapema, kwa Uthman, ambaye pia hakumchagua kuwa gavana. Baladhuri, mwanahistoria wa Kiarabu, anasema katika kitabu chake, Ansab-ul-Ashraf juz. 1, uk. 113:

"Miongoni mwa masahaba wa Mtume wa Allah, walikuwepo wachache waliomke-mea Uthman kwa ukali sana kama alivyofanya Talha."

Pale kasri la Uthman lilipozingirwa na waasi, alikuwa ni Talha ambaye aliwazuia watumwa wake (Uthman) kuingiza maji ndani yake. Usiku, alilirushia mishale lile kasri lakini Uthman alikuwa analijua hilo. Tabari, yule mwanahistoria, anasema katika Tarikh yake, juz.111, uk. 411:

"Uthman mara nyingi alikuwa akiomba: 'Ewe Allah! Nakuomba uniokoe na madhara ambayo Talha anaweza kunifanyia. Yeye ndiye ambaye amewachochea watu dhidi yangu, na ndio yeye aliyesababisha nyumba yangu kuzingirwa."

Chuki ya Talha kwa Uthman lazima ilikuwa imezidi mno. Hakuweza kumsamehe kupoto-ka kwake hata baada ya kufa kwake. Aliamuru jeneza la Uthman na wabeba jeneza wake wapigwe mawe. Uthman hakuweza hata kuzikwa kwenye uwanja wa makaburi ya Waislam; ilibidi azikwe kwenye makaburi ya Wayahudi.

Zubeir bin Awwam

Mama yake Zubeir alikuwa ni Safiya, binti ya Abdul Muttalib bin Hashim. Kwa hiyo mama yake alikuwa ni shangazi yake Muhammad (s.a.w.w.) na Ali.

530

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Zubeir pia alikuwa amemuoa mmoja wa mabinti wa Abu Bakr, na hii ilimfanya kuwa she-meji yake Aisha. Kama Talha, yeye pia alimpinga mkwe wake dhidi ya uteuzi wa Umar kama khalifa. Na wakati Umar alipokuwa anafariki, alimfanya Zubeir pia kuwa mjumbe wa kamati yake ya uteuzi.

Ibn Saad anasema katika Tabaqaat yake kwamba Zubeir alikuwa pia ni tajiri sana kama Talha.

Zubeir alishiriki tamaa ya Talha ya dhahabu na uchu juu ya madaraka ya kisiasa. Alikuwa akitegemea kwamba Ali angemtendea kwa namna ile ile kama Uthman alivyowatendea binamu zake wawili, yaani kwa kumfanya yeye kuwa gavana. Hata hivyo, alikuwa ni bina-mu yake Ali.

Lakini Ali hakumtendea binamu yake, Zubeir, kama Uthman alivyowatendea binamu zake. Kulipokuwa hakukubakia mashaka yoyote akilini mwa Zubeir kwamba Ali hatamchagua yeye kuwa gavana, alivunja kiapo chake cha utii kwake, na akasimama katika maasi dhidi yake.

Zubeir alichangia chuki yake na Talha kwa Uthman, na mara kwa mara aliwasukumiza wale waasi wamuue Uthman. Ibn Qutayba, mwanahistoria wa Kiarabu, anasema kwamba siku chache baada ya Ali kupanda madarakani, Talha na Zubeir walikuja kumuona Ali, na mabishano yafuatayo yakatokea kati yao:

Talha/Zubeir: Hivi unajua ni kwa nini tulichukua kiapo cha utii kwako?

Ali:                 Mlichukua kiapo cha utii kwa sababu zile zile kama Waislam wengine -

kunitii mimi.

Talha/Zubeir: Hapana. Tulichukua kiapo hicho kwa matumaini kwamba utalipiza kiten-do chetu hicho kwa kutupa sisi fungu katika serikali. Hata hivyo, ilikuwa ni kwa msaada wetu sisi ndipo ukawa khalifa.

Ali:                Ninaweza nikawatakeni ushauri katika masuala ya serikali lakini hakuna

kitu kama "fungu" kwa ajili yenu katika serikali.

Talha na Zubeir waliaibika sana kwa kukataa kwa Ali kugawana madaraka pamoja nao, na yafuatayo yalikuwa ndio maoni yao juu ya matokeo ya kukutana naye:

Talha: Hapo Madina, walikuwepo wajumbe watatu wa kamati ya uteuzi. Kati yao, mmoja (Saad bin Abi Waqqas) alikataa na kiapo chake cha utii kwa Ali lakini

531

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Zubeir na mimi tulimpa yeye viapo vyetu. Wote sisi ndio tuliofanya iwezekane yeye kuwa khalifa lakini amesahau mapema sana kile tulichomfanyia yeye.

Zubeir: Tuliiandaa orodha ya makosa ya kijinga ya Uthman, na tulimlaumu yeye, yote kwa ajili ya Ali. Wakati wa ghasia hii, Ali alikuwa amekaa nyumbani kwake. Kisha, kwa msaada wetu sisi akawa khalifa. Lakini mara tu alipokuwa khalifa, akasahau huduma zetu, na akatoa vyeo vya zawadi vyote kwa watu wengine.

Madhumuni ya maoni haya yaliletwa kwenye nadhari ya Ali. Yeye alimwita Abdallah ibn Abbas, na akamtaka ushauri wake juu ya jambo hili. Ibn Qutayba anaandika katika kitabu chake Kitab-ul-Imama wa-Siyassa, kwamba Abdallah ibn Abbas alisema: "Ni maoni yangu kwamba ungemteua Talha kuwa gavana wa Basra, na Zubeir kuwa gavana wa Kufa. Hii itawaridhisha wao na kuwanyamazisha."

Ali alisita na kuwaza juu ya ushauri wa binamu yake, na kisha akasema:

"Hapana. Sidhani kama ninaweza kukubaliana na wewe katika hoja hii. Ninawajua wote vizuri sana. Kama nitawafanya kuwa magavana, basi udhalimu, uonevu na uny-onyaji vitaachiliwa huko Basra na Kufa, na kilio cha wale wanaoonewa kitagubikwa tena. Kama ningekuwa niteue watu kama Talha na Zubeir kama magavana, basi ita-nipasa nimvumilie Mu'awiyah pia kubakia kama gavana wa Syria."

Ibn Qutayba anaendele kuandika zaidi:

Amr bin Al-Aas, Talha na Zubeir walikuwa wa kwanza kumshutumu Uthman. Walikuwa ndio wa kwanza kuwachochea watu wazi wazi kumuua Uthman. Talha na Zubeir walikuwa wa kwanza kuchukua kiapo cha utii kwa Ali, na wote hawa walikuwa ndio wa kwanza kuvunja ahadi yao ya uaminifu."

Tangu pale Umar alipowateua kuwa wajumbe wa kamati ya uteuzi, Talha na Zubeir walikuwa wameweka tamaa ya kuja kuwa khalifa. Lakini Abdur Rahman bin Auf akam-fanya Uthman kuwa khalifa badala ya yeyote kati yao.

Fursa ya pili ya kuweza kuwa khalifa ilikuja mara tu baada ya kifo cha Uthman. Lakini safari hii, walihisi kwamba Waislam walikuwa hawawataki wao. Walitambua kwamba kwa lolote lile watakalofanya, Waislam hawatawakubali. Kila mmoja hapo Madina alikuwa ameona kwa macho yake mwenyewe mwenendo wao juu ya Uthman wakati wa kuzingir-wa kwa kasiri lake.

Talha na Zubeir vile vile walifahamu kwamba haikuwa ni Ali aliyekuwa akiwakumbakum-ba wengine ili kupanda juu (cheo cha ukhalifa) bali walikuwa ni Waislam waliokuwa

532

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"wanakumbakumba" kumuweka yeye hapo. Kuchaguliwa kwa Ali kama khalifa kulikuwa ni kwa hiari, na upingaji wowote ule uliokuwepo kwa ajili hiyo, ulitoka kwake mwenyewe. Talha na Zubeir pia walijua kwamba kama wangekataa na kiapo chao cha utii kwake, wata-jidhihirisha wenyewe wazi wazi mno. Kwa kutotaka hili kutokea, walichukua kiapo cha utii kwa Ali.

Walipoona ukhalifa uko nje ya uwezo wao, Talha na Zubeir walitupia macho Basra na Kufa kama zawadi ya kujifariji kwao. Walitegemea kwamba Ali hatapuuza hadhi yao kati-ka umma, na kama wajumbe wa kamati ya uteuzi ya Umar. Vile vile wao walisadiki kwamba Ali hataacha kutilia maanani heshima na ushawishi wao kwa watu wa Basra na Kufa. Lakini Ali hakuvutiwa na hadhi zao na ushawishi, na hakuwapa wao Basra na Kufa.

Talha na Zubeir walitambua kwamba Madina imethibitisha kuwa ubao mbovu hasa wa kuchupia wao kwa ajili ya malengo yao. Wao, kwa hiyo, waliamua kwenda Makka, na kujaribu bahati yao huko. Ali hakufanya jaribio lolote la kuwazuia wao. Talha na Zubeir waliondoka Madina na uhaini mioyoni mwao.

Kama Ali angewateua Talha na Zubeir kuwa magavana wa Basra na Kufa, wangeimarisha nafasi zao katika majimbo yao husika, na kisha wangekana kiapo chao kwa serikali kuu. Umma sasa ungejikuta wenyewe unatawaliwa na watawala wanne wanaojitegemea na wenye uadui - Talha huko Basra; Zubeir huko Kufa; Mu'awiyah huko Syria; na Ali huko Hijazi. Katika kuzuka kwa vita ya wenyewe kwa wenyewe isiyozuilika miongoni mwao, Dola ya Kiislam angevunjikia kwenye vurugu na kuwa "serikali" ya makabila ya Kiarabu kwa mara nyingine kama ilivyokuwa katika Nyakati za Ujahilia.

Ilikuwa ni busara na kipaji cha Ali ambavyo viliiokoa Dar-ul-Islam (Dola ya Kiislam), kutokana na maangamizi hayo ya kuhuzunisha.

Ni ukweli unaofahamika vema kwamba maamuzi na sera za kiserikali, katika masuala mengi, yanaamuliwa na mashinikizo ya makundi ya maslahi maalum. Talha na Zubeir, na wafuasi wao waliunda kundi kama hilo. Walitia shinikizo lakini lilipokutana na upinzani, waliingia vitani.

Aisha binti Abu Bakr

Aisha alikuwa binti ya Abu Bakr, khalifa wa kwanza wa Waislam. Alizaliwa miaka minne baada ya Mtume wa Uislam kutangaza ujumbe wake, na alikuwa na umri wa miaka tisa wakati alipoolewa naye. Alikuwa ni mke wake wa tatu. Kwa vile alibaki bila kuwa na mtoto, alimtwaa Abdallah bin Zubeir, mtoto wa dada yake, kama mwanawe mwenyewe. Ilikuwa ni kwa mazingira haya ndipo akaitwa Umm Abdallah, mama yake Abdallah.

533

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Aisha alikuwepo katika vita ya Uhud. Bukhari anasema kwa idhini ya Anas kwamba alimuona Aisha na Umm Salama wakileta maji kwenye mifuko ya ngozi, na kuyatoa kwa wapiganaji waliojeruhiwa ili wanywe. Aisha alimchukia sana Ali. Alimchukia sana kiasi kwamba hakuweza hata kumtaja jina lake. Bukhari amesimulia tukio lifuatalo:

Aisha anasema kwamba pale hali ya Mtume wa Allah swt. ilipokuwa mbaya, aliom-ba ruhusa ya wake zake wengine ili atumie muda wake wote chumbani kwangu kwani alitaka mimi nimuuguze. Siku ile alikuwa katika chumba cha Maimuna. Kwa vile alikuwa dhaifu sana, ilibidi afanye kusaidiwa na watu wawili waliomtoa kutoka kwenye chumba cha Maimuna kumleta chumbani kwangu. Mmoja wa watu hao wawili alikuwa ni Abdallah ibn Abbas.

Maelezo ya Aisha ya Hadith hii yalifikishwa kwa Abdallah ibn Abbas, na yeye akasema kwamba yule mtu mwingine aliyekuwa amemsaidia Mtume wakati alipokuwa anatoka kwenye chumba cha Maimuna, alikuwa ni Ali.

Wanahistoria wamejaribu kutafuta sababu za kwa nini Aisha alimchukia Ali. Moja ya sababu inasemekana kuwa ni lile tukio la ifk, yaani, "ule uwongo." Kadhia hiyo ilitokea katika mwaka wa sita wa Hijiria. Wakati jeshi la Madina lilipokuwa linarudi kutoka kwenye msafara wa kwa Banu Mustaliq, Aisha ambaye alikuwa amefuatana na Mtume, kwa kughafilika aliachwa nyuma. Alikuja kutokea baadae akiwa na muongoza ngamia. Kadhia hii ilisababisha uropokaji fulani miongoni mwa watu, na kusababisha sana ugonjwa wa moyo kwa Mtume (s.a.w.w.). Anasemekana kutafuta maoni ya Usama bin Zayd bin Haritha na Ali ibn Abi Talib katika suala hili. Usama, inavyoelezwa, alimwambia Mtume kwamba Aisha alikuwa hana hatia kabisa lakini Ali anasemekana kwamba alisema kumwambia Mtume kwamba haikuwa lazima kwake kuvumulia maudhi kama hayo kwa sababu angeweza wakati wote kupata wanawake wengine wa kuwaoa.

Aisha pia alidai kwamba Ali alimpiga mtumishi wake wa kike katika jaribio la kumtaka aeleze ule "ukweli."

Mtume alishikwa na fadhaa bila kujua ni upi ukweli wa jambo hilo wakati wahyi mpya uli-poshuka kutoka mbinguni ambao ulimwondolea Aisha tuhuma za hatia zote au lawama. Kutokuwa na hatia kwake kulikubalika na tukio hilo lisilopendeza inavyoonekana lika-fungwa kabisa.

Ingawa kadhia hii ilikuwa na mwisho wa kufurahisha kwa Aisha, hakumsamehe kamwe Ali kwa ule "ushauri" wenye kudaiwa kwamba yeye alimpa mumewe, yaani, kwamba alikuwa amemwambia wanawake wengine walikuwa wanapatikana kwa ajili yake wakati wote, na kwamba hakupaswa kuhuzunika sana juu ya tukio hilo.

534

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ikiwa kama Ali alitoa ushauri kama huo kamwe kwa Mtume, basi hakuwa amefanya cho-chote zaidi ya kufafanua ile Aya ya tano ya sura ya 66 ya Qur'an (Surat Tahriim) kama ifu-atavyo:

Kama akikupeni talaka, bila shaka Mola wake atampa badala yenu, wake wengine

walio bora kuliko ninyi... (at-Tahriim, 66:5)

Kwa mujibu wa Aya hii ya Qur'an, walikuwepo wanawake ambao walikuwa wabora zaidi kuliko wake za Mtume, na Allah angeweza kuwatoa kwake yeye.

Hadith ya kwamba Ali alimpiga mtumishi wa Aisha, haikubaliani na hulka yake. Alikuwa ndio muungwana kabisa wa watu, na hata katika uwanja wa mapambano, hakutaka kuwa wa kwanza kumshambulia adui yake. Alimtaka adui yake amshambulie yeye kwanza. Ni pale tu adui alipokuwa amepiga dhoruba ndipo Ali alipojihisi kuwa huru kujitetea mwenyewe. Haiwaziki kwamba angeweza kumpiga msichana asiyejiweza. Wakati jeshi liliposonga mbele, Aisha aliachwa nyuma, alikuwa peke yake kabisa, na mtumishi wake hakuwa pamoja naye. Ni vipi angeweza kujua kilichotokea kama hakuwa na bimkubwa wake? Hata kama mtu angetishia kumuua, bado asingeweza kueleza chochote.

Sir William Muir, mwanahistoria wa Kiingereza, ameonyesha kwamba msimuliaji wa Hadith hii alikuwa ni Aisha mwenyewe, na hii, yeye anasema, "inafanya ushahidi wake kuwa wa kutiliwa shaka."

Lakini Aisha hakulihitaji tukio la ifk ili kumchukia Ali. Chuki yake kwa Ali ilikwenda kwenye nyakati za kabla - mbali na tukio hili. Alikuwa na wivu juu ya Khadija, na binti yake, na watoto wa binti yake. Muhammad alikuwa akiwadekeza na kuwakumbatia watoto wa binti ya Khadija wakati wote, na Aisha angeweza kufikiria kwamba kama angekuwa na watoto wowote, yeye Muhammad angewapenda kama alivyokuwa akiwapenda binti na wajukuu wa Khadija, lakini hakuwa na hata mmoja.

Kuwa na wivu kwa binti na wajukuu wa Khadija kungeweza kuwa ni kawaida na asilia kwa Aisha. Lakini kilichokuwa sio cha kawaida na asilia, hususa kwa mke wa Mtume wa Allah swt., kilikuwa ni kuruhusu wivu wake kuwa usiotawalika na tena tamaa isiyowiana.

Aisha mwenyewe kila mara alikuwa akisema kwamba ingawa hakumwona kamwe Khadija, alikuwa anamuonea wivu sana kuliko alivyokuwa kwa wake wenzie wengine. Sababu moja ya wivu wake ilikuwa kwamba mume wake alikuwa kila wakati akimkum-buka Khadija kwa mapenzi halisi na shukrani. Katika wakati mmoja, alikuwa akimtukuza na kumsifia Khadija pale Aisha alipopoteza subira, na akasema kwa hasira: "Kwa nini unazungumza juu ya huyo mwanamke mzee wakati wote? Kwani Allah hakukupa wake wazuri zaidi kuliko yeye?"

535

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Asilani!" alijibu Mtume. "Allah kamwe hajanipa mimi mke bora kuliko Khadija. Yeye aliniamini mimi wakati ambapo wengine walinipinga mimi. Yeye alinisaidia mimi wakati nilipokuwa sina mtu yoyote wa kunisaidia. Yeye alikuwa wa kwanza kuukubali Uislam ambapo kila mmoja mwingieo ni muabudu sanamu. Na Allah alinibariki mimi na watoto kupitia kwake, na kupitia kwake peke yake." (Bukhari na Siyar-us-Sahabiyyat)

Lakini Aisha hakuweza kuzima au kuficha chuki yake kwa Khadija, binti yake na wajukuu zake. Hata kifo cha Khadija na Fatima havikuweza kumshawishi yeye kusahau chuki yake ya tangu kale. Alimchukia Ali na wajukuu wa Khadija.

Ilikuwa haizuiliki kwamba Aisha angezozana na Uthman. Mara moja Uthman alipokuwa anatumia lugha chafu na ya matusi, kutoka kwenye mimbari, kwa ajili ya Abdallah ibn Masoud, rafika ya Mtume wa Allah, na yeye alijitokeza kwa ajili ya kumlinda yeye. Kulikuwa na nyakati zingine ambapo alikuwa amejaribu kupunguza majivuno ya Uthman. Mlango wa chumba chake ulifungukia Msikitini, na mara kwa mara aliweka kwenye saka-fu yake jozi ya viatu na shati ambavyo vilikuwa vya Mtume, akatoa kichwa chake nje, na akimweleza Uthman wakati alipokuwa juu ya mimbari, alisema:

"Kabla ya vitu hivi, ambavyo ni vya Mtume wako, havijakusanyikiwa na vumbi lolote juu yake, umekwishabadilisha amri zake, Hadith zake, sunnah zake, na umek-wisha kuiharibu dini yake."

Aisha alikuwa tayari amekwishatia mashaka kwamba Uthman "amempuuza" yeye. Kisha amepunguza mshahara wake. Hili lilimfanya aghadhibike. Hili pamoja na maudhi mengine madogo madogo lilimfanya awe adui mkali wa Uthman. Abbas Mahmud Al-Akkad wa Misri anasema katika kitabu chake, Abqarriyat al-Imam Ali (Cairo, 1970), kwamba Aisha alikuwa amempa Uthman jina la "Na'thal". Huyu Na'thal alikuwa mzee mmoja wa Kiyahudi hapo Madina. Inasemekana kwamba ndevu za Uthman zilikuwa na namna fulani ya kufanana na ndevu zake. Aisha, katika nyakati za hasira, aliwachochea watu wazi wazi dhidi ya Uthman, na alisema: "Muueni huyu Na'thal. Amekuwa kafir." Umar Faroukh anaandika katika ukurasa wa 190 wa kitabu chake, The History of the Arabic Thought Till the Days of Ibn Khaldoun, kilichochapishwa mwaka 1983, na Dar-ul-'Ilm lil-Malaiin, Beirut, Lebanon:

Imesimuliwa kwamba Aisha alikuwa na desturi ya kusema: "Muueni huyu Na'thal (Uthman bin Afan); amekuwa kafir."

Kuzingirwa kwa kasri la Uthman kulikuwa kumekwishaanza wakati Aisha alipoondoka Madina kwenda Makka kufanya Hijja. Marwan alimuomba abakie Madina lakini hakum-sikiliza, na akauondoka mji. Katika kipindi cha kutokuwepo kwake Madina, Uthman ali-uawa.

536

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Huko Makka, Aisha alikuwa na shauku sana ya kusikia habari za mambo yaliyokuwa yana-tokea huko Madina. Baada ya Hijja, alifungasha mizigo yake ili kurudi Madina. Kabla ya kuondoka Makka, hata hivyo, alifahamishwa kwamba mtu anayeitwa Akhdhar, alikuwa amewasili kutoka Madina. Alimwita na kumuuliza kilichokuwa kinatokea huko Madina, naye akasema:

"Uthman amewaua wale waasi na ameurudisha mji chini ya udhibiti." Aisha alishitushwa kusikia taarifa hii, na akasema:

"Hivi Uthman amewaua wale watu ambao wamekuja Madina kulalamika dhidi ya udhalimu, na kudai haki? Wallahi, sisi hatufurahishwi na hili."

(Tarikh Tabari, Juz. 111, uk. 468)

Lakini katika siku iliyofuata, msafiri mwingine alikuja kutoka Madina, na alimwambia Aisha kwamba wale waasi wamemuua Uthman, na kwamba Akhdhar alikuwa amempa taarifa za uongo. Aisha akasema:

"Mwenyezi Mungu aweke umbali kati ya Rehema Zake na Uthman. Lolote ambalo limetokea, Uthman alilisababisha mwenyewe juu yake. Allah hamdhulumu yeyote."

Wakati habari za kifo cha Uthman zilipothibitishwa, Aisha aliamua kuondoka Makka mara moja. Kuwepo kwake Madina, yeye aliamini, kulikuwa ni muhimu sana kabla ya uchaguzi wa khalifa mpya. Aliondoka Makka lakini alikuwa bado hajafika mbali wakati alipokutana na msafiri mwingine, Ubaid bin Abi Salma, akija kutoka Madina. Aisha alimuuliza ni nini kilichokuwa kimetokea huko Madina kabla yeye hajaondoka. Yeye akasema:

"Uthman ameuawa, na watu wa Madina wametoa kiapo chao cha utii kwa Ali ibn Abi

Talib"

Kupanda kwa Ali kwenye cheo cha ukhalifa, hakukuwa aina ya taarifa ambazo Aisha alikuwa tayari kuzisikia. Lakini akitegemea kwamba alikuwa hajazisikia habari hizo sawa-sawa, aliuliza: "Umesema kwamba watu wa Madina wametoa kiapo chao cha utii kwa Ali?" Ubaid akajibu: "Ndio, wametoa. Na ni nani tena aliyekuwepo hapo ambaye wangeweza kumpa kiapo chao cha utii kwake?" Aisha akaguna:

"Oh! kiasi gani ninavyotamani ardhi ingepasuka au mbingu kuangukia juu ya ardhi kama Ali amekuwa khalifa. Sasa siwezi kwenda Madina. Nitarudi Makka."

(Tarikh Kamil, Juz. 111, uk. 105)

537

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Aisha alimuamuru muongoza ngamia wake kurudi Makka, na akasema:

"Uthman aliuawa wakati akiwa hana hatia. Wallahi, sasa nitalipiza kisasi kwa ajili ya damu yake."

Kauli ya Aisha ilimshangaza Ubaid bin Abi Salma, na yeye akauliza:

"Ewe mama wa waumini! Utalipiza kisasi kwa kifo cha Uthman? Lakini kwani hakuwa ni yule mtu uliyemwita 'Na'thal,' na wewe hukuwa yule mwanamke uliyewashawishi Waislam kumuua yeye kwa sababu, kama ulivyosema, alikuwa ameguka kuwa kafir?"

Aisha akajibu:

"Ndio, ni kweli kwamba nilimwita Uthman kwa jina hilo, na watu wengine pia wal-imwita kwa jina hilo hilo. Ni kweli pia kwamba nilisema kuwa amepotoka, na kwamba alipaswa kusahihishwa. Lakini ninachokisema sasa ni kweli zaidi kuliko nili-chokisema kabla, na ninachokisema sasa ni kwamba Uthman alikuwa ametubia kabla ya kifo chake. Kwa hiyo, wakati alipouawa alikuwa hana hatia, na nitalipiza kisasi kwa ajili ya damu yake."

Aisha alijuaje kama Uthman alikuwa ametubia? Mpaka anaondoka Madina, alikuwa bado hajatubia, Hata baada ya kumaliza Hijja, na akawa tayari kurudi Madina, alikuwa bado hajatubia, vinginevyo asingeonyesha kuridhika katika kuuawa kwake. Lakini aliposikia habari kwamba Ali amekuwa khalifa, yeye ghafla akafanya ugunduzi kwamba Uthman alikuwa ametubia, na alikuwa hana hatia. Alitangaza kwamba yeye ni mtetezi wa Uthman, na kwamba yeye ataanzisha mapambano ya kulipiza kisasi kwa ajili ya damu yake.

Wakati huo Marwan ambaye alikuwa ameondoka Madina wakati wa kupanda kwa Ali kwenye ukhalifa, pia alikuwa amewasili Makka. Alikwenda kwa Aisha na akampa maele-zo fasaha ya kuuawa kwa Uthman ambayo yanasemekana yalimsikitisha sana, na kumfik-isha karibu ya kulia machozi.

Aisha alianzisha kampeni yenye pande mbili; ilimbidi athibitishe (1) "kutokuwa na hatia" kwa Uthman, na (2) "hatia" ya Ali.

Wasafiri walizichukua habari za kampeni ya Aisha hadi Madina. Talha na Zubeir wali-sisimka sana kusikia habari hizo. Waliona dalili ya matumaini juu yao katika kampeni yake. Walimwandikia barua Aisha, na wakampa baraka zao, wakampenda kwa uamuzi na shughuli yake; wakamtia moyo na kumhimiza kuimarisha propaganda yake dhidi ya Ali. Baadae kidogo wao wenyewe walikuwa waende Makka "kufanya umra."

538

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Aisha, chini ya mwongozo wa Marwan, alianza kukusanya msaada. Mtu wa kwanza kuitikia mwito wake, alikuwa ni Abdallah bin Aamir al-Hadhrami, gavana wa Uthman huko Makka. Pamoja naye alimchukua pia Said bin Al-Aas, Walid bin Aqaba na Bani Umayya wengine waliokuwako Makka, kwenye "kambi" ya Aisha. Wakati huo huo, Talha na Zubeir pia waliwasili kutoka Madina, na waliunda ushirikiano na Aisha na Marwan -ushirikiano dhidi ya Ali bin Abi Talib. Sasa wengi wa wale wadhamini wa kichinichini wa mauaji ya Uthman walikuwa wapo Makka. Kwa vile kulikuwa na umoja wa nia na kufanana kwa malengo miongoni mwao, uundaji wa ushirikiano haukuleta matatizo yoy-ote.

Nia iliyodhaniwa ya ushirikiano huu ilikuwa ni kutafuta kulipiza kisasi kwa ajili ya damu ya Uthman, na washirika hao walikubaliana kwamba hapakuwa na njia nzuri ya kukipata kisasi hicho kuliko kuukamata ukhalifa wenyewe. Lakini nyuma ya pazia la kutafuta kulipiza kisasi, ulijificha uchu wa madaraka, na hofu za watu, na kijicho na ulipizaji kisasi usio na huruma wa mwanamke.

539

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Vita vya Basra (vita vya Ngamia)

Vita vya Pili vya Wenyewe kwa wenyewe katika Uislam

Waislam walikuwa wamepigana vita moja ya wenyewe kwa wenyewe wakati wa ukhalifa wa Abu Bakr, khalifa wa kwanza. Ndani ya kizazi hicho hicho, wao sasa walikabiliwa na tishio kali la kupigana nyingine. Vita vya kwanza cya wenyewe kwa wenyewe vilipiganwa na serikali dhidi ya baadhi ya raia zake wapinzani; vita hivi vya pili vilipiganwa na raia wapinzani dhidi ya serikali yao.

Maprofesa Sayyed Abdul Qadir na Muhammad Shuja-ud-Din, wameandika katika kitabu chao cha History of Islam (historia ya Uislam) Sehemu ya 1 (Lahore, Pakistan) kama ifu-atavyo:

Aisha alikuwa anarudi Madina kutoka Makka baada ya Hijja pale aliposikia habari za kuuawa kwa Uthman, na kupanda kwa Ali kwenye cheo cha ukhalifa ndipo akaamua kutokwenda Madina, na kurudi Makka. Talha na Zubeir pia waliwasili Makka. Gavana wa Uthman hapo Makka alikuwa ni Abdallah bin Aamir Hadhrami. Marwan na jamaa wengine wa Bani Umayya walikuwa wakiishi kama wageni wake. Wote hao walifanya mkutano na kukubaliana kwamba watalipiza kisasi kwa ajili ya damu ya Uthman. Waliunda jeshi hapo Makka la wapiganaji 3000, na wakaamua, baada ya majadiliano kiasi, kutembea kwenda Basra. Waliishikilia Basra, wakaikamata hazina, na waliwaua Waislam 600 ambao waliwashuku kuwa wanawapinga, na wakaeneza hofu katika mji huo.

Kutafuta kulipiza kisasi kwa ajili ya damu ya Uthman kulikuwa ni kisingizio kwa ajili ya vita. Kilikuwa ni kificho sio tu kwa ajili ya malengo ya viongozi wa maasi bali pia kwa ajili ya madhambi yao. Hapakuwa na njia ya wao kuficha nia zao, malengo na maazimio yao na vile vile ushiriki wao katika mauaji ya Uthman ila kwa kudai kwamba wao walikuwa ni watetezi wake. Kitu kimoja ambacho kilikuwa wazi kwa kila mtu ni kwamba kama Ali angeweza kuimarisha serikali yake, moja ya mambo ya kwanza kabisa ambayo angeyafanya, lingekuwa ni kuazisha uchunguzi kwenye mauaji ya Uthman, na ilikuwa haikwepeki kwamba kesi ya mashitaka ya jinai ingeelekea kwa viongozi wa maasi wenyewe. Jukumu walilokuwa wamechukua wakati wa kuzingirwa kwa Uthman, lilikuwa halifichiki kwa mtu yoyote. Mashahidi walioshuhudia, wote walikuwepo hapo Madina na wangethibitisha chini ya kiapo, kile walichokuwa wamekiona.

Kwa wale viongozi wa maasi kwa hiyo, kulikuwa na njia moja ya kumzuia Ali na haki yake isiyobadilika wala kuzuilika, na hiyo ilikuwa ni kuanzisha kelele ya kisasi kabla hajaweza kuviweka vyombo vya sheria katika hali ya utendaji. Hili ndilo hasa wao walilo-lifanya. Wengine miongoni mwao pia walikiri kwamba walichokuwa wanakifanya,

540

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kilikuwa ni kulipia madhambi yao, na kulikuwa hakuna njia bora ya kulipia madhambi kuliko "kuosha damu kwa damu." Walikuwa wameua khalifa mmoja, na sasa walikuwa wamuuwe mwingine. Hii ndio ilikuwa njia pekee, wao walijadili, ya wao kupata "wokovu."

Hakuna anayejua ni kwa haki gani Aisha, Talha na Zubeir walikuwa wanatafuta kulipiza kisasi kwa ajili ya damu ya Uthman. Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa na uhusiano na Uthman. Kila mmoja wao alitokana na ukoo tofauti. Ndugu wa karibu wa Uthman walikuwa ni mjane wake, Naila, na watoto wake wa kiume na wakike, na wao walikuwa hawatafuti kulipiza kisasi chochote kutoka kwa mtu yoyote. Ilikuwa ni baada ya tu ya kuuliwa kwake ambapo Uthman alipata watetezi wa kujiteua wenyewe wa jinsia zote, waliokuwa tayari na wenye shauku ya "kumlinda" yeye!

Aisha hakuweza kumuona Ali kwenye cheo cha ukhalifa. Chuki yake juu ya Ali ilikuwa inazidi nguvu. Kama mtu mwingine mbali na Ali angekuwa khalifa, asingeweza kuanzisha hili tukio la hatari lenye misiba mbele yake ambalo ndani yake makumi ya maelfu ya Waislam waliuawa. Wakati ambapo, kisa cha ugomvi halisi kwa upande wake kilikuwa ni chuki yake isiyofifia juu ya Ali, alipata pia sababu nyingine ya kushinikiza mapambano hayo dhidi yake kwa nguvu zaidi. Kama ikibidi afanikiwe katika kumuondoa Ali kutoka kwenye kitovu cha madaraka, yeye alikuwa amfanye mpwa na mwanawe wa kumlea, Abdallah bin Zubeir, kuwa ndiye khalifa mpya.

Watatu kati ya magavana wa Uthman ambao walikuwa wamefukuzwa na Ali ni Abdallah bin Aamir Hadhrami wa Makka; Ya'la bin Umayya wa Yemen; na Abdallah bin Aamir bin Kurayz wa Basra. Baada ya kufukuzwa kwao, huyu wa kwanza aliishi Makka, na hawa wawili wengine pia walikuja wakaishi Makka. Waliichukua hazina pamoja nao. Wakazi wengine wa Makka pia walitoa michango mikubwa kwenye masanduku ya fedha ya waasi. Kwa njia hii, hawa waasi walipata fedha muhimu ya kutosha kuimarisha vita vyao.

Viongozi wa waasi walifanya mkutano nyumbani kwa Abdallah bin Aamir Hadhrami, aliyekuwa gavana wa Makka hapo awali, kuamua ni nini walichokuwa wafanye.

Uvamizi wa Madina, na safari ya kwenda Syria, yalifikiriwa lakini yakaonekana hayawezekani kwa sababu mbali mbali. Mwishowe, Abdallah bin Aamir bin Kurayz, aliyekuwa gavana wa Basra hapo awali, alishauri kwamba wangekwenda Basra. Ushauri huu ulimvutia kila mtu, na ulikubaliwa na wote. Talha aliupokea kwa hamu sana, na akase-ma kwamba familia nyingi za ukoo wake zilikuwa zinaishi Basra, na kwamba anaweza kutegemea msaada wao.

Wale viongozi wa maasi ndipo wakapanga mkakati wao: kwanza wataishika Basra; waki-wa na Basra kama kituo chao, wataweza kuikalia Kufa ambako Zubeir alikuwa na wafuasi

541

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wengi. Wakiwa na Basra na Kufa mikononi mwao, wao walivyoona, itawezekana kwa wao kumtenga Ali huko Hijazi, na kuvamia maeneo yake; na kumsHind, na kuupora ukhalifa kutoka kwake.

Nia ya waasi hawa iliyotangazwa ilikuwa ni kuwaua wale watu ambao walimuua Uthman. Wale watu waliomuua Uthman, wote walikuwa wako Madina, lakini wale watetezi wake wa kujiteua walikuwa wakisonga mbele kuelekea Basra - maili 800 kwa upande wa mashariki, ndani ya Iraq!

Talha na Zubeir walimuomba Abdallah ibn Umar bin al-Khattab kuandamana nao kwenda Basra lakini yeye alikataa kwenda.

Aisha alimhimiza Hafsa binti Umar bin al-Khattab na wajane wengine wa Mtume waliokuwa bado wapo Makka baada ya Hijja, kwenda naye Basra, na kushiriki katika vita dhidi ya khalifa. Wote walikataa isipokuwa Hafsa. Yeye alikuwa tayari kwenda na Aisha lakini kaka yake, Abdallah bin Umar, alimkataza kufanya hivyo.

Umm Salma alikuwa mmoja wa wajane wa Mtume (s.a.w.w.). Aisha alimtumia barua huko Madina akimualika kushiriki katika kampeni yake. Umm Salma alimjibu kama ifuatavyo:

"Ewe Aisha! Umesahau kwamba Mtume wa Allah alikuamuru ubakie nyumbani na sio kuvuka mipaka iliyowekwa na Dini yetu? Jihadi ya wanawake iko katika kujizuia. Macho yao yasiwe makakamavu, na sauti zao zisiwe kubwa. Unadhani kwamba kama Mtume wa Allah alikuwa akukute we we ukifukuzana na ngamia katika jangwa, angependezewa? Kama ningekuwa nimuasi mume wangu, nisingeweza kamwe kumkabili tena. Kwa hiyo, muogope Allah nyakati zote. Itakuwa ni kwa faida yako mwenyewe kubakia nyumbani, na sio kwenda na kuingia kwenye mambo ya hatari."

Aisha alidai kwamba alikuwa anakwenda kwenye ujumbe wa amani. Kama alikuwa, basi ulikuwa ni ujumbe wa amani wa ajabu sana kuliko yote. Alisindikizwa kwenda Basra na wapiganaji 3000, wakiwa na silaha tele za hatari hatari, na wakiwa na kiu ya damu ya Waislam wasio na hatia!

Hatimae maandalizi yote yalikamilika, na jeshi la Aisha, Talha na Zubeir, liliondoka Makka, kwa kishindo kikubwa cha nderemo, kuelekea kwenye mafikio yao ya mbali -Basra.

Wakati lile jeshi la Makka lilipokuwa linatembea kuelekea mashariki, mtu mmoja alizusha swali la ni nani atakayekuwa khalifa endapo utapatikana ushindi dhidi ya Ali. Mtoto wa Talha akasema kwamba baba yake atakuwa ndio khalifa lakini mtoto wa Zubeir akampin-ga kwa kudai kwamba ni baba yake pekee atakayekuwa khalifa.

542

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mabishano makali yalianza ambayo yangesababisha kurushiana ngumi kati ya vijana waw-ili hao wakati Aisha alipowasili kwenye tukio hilo. Aliingilia kati baina yao, na mashabiki wao, na akalifutilia mbali swali hilo linalokera kwa vile lilikuwa si la wakati muafaka.

Ingawa Aisha alilizima lile swali la uongozi kwa wakati ule, aliagiza hata hivyo kwamba mpwa wake, Abdallah bin Zubeir ataliongoza jeshi hilo katika Swala. Hukumu hii ilikuwa na umuhimu maalum katika mazingira ya nyakati. Katika kadhia moja, wakati wa marad-hi ya mwisho ya Mtume, baba yake Aisha, Abu Bakr, aliwaongoza Waislam fulani kwenye Swala. Lile jambo la kwamba aliwaongoza katika Swala, lilitumika, mara baada ya kifo cha Mtume, kama "hoja" kwa upendeleo wake (Abu Bakr) na "sifa" ya kuwa khalifa.

Aisha alimpenda mpwa wake, Abdallah bin Zubeir, zaidi kuliko mama yake mwenyewe alivyompenda, na alidhamiria kumfanya khalifa afuataye. Juu ya kusisitiza kwake, hata Zubeir ilimbidi kusimama nyuma ya mwanawe mwenyewe kutekeleza swala zake. Kama Aisha alivyoona, kwa kuzingatia kigezo cha baba yake mwenyewe, hakuna yeyote katika lile jeshi waasi atakayeweza kudai kwamba alikuwa na "sifa" kama zile zile za kuwa khalifa kama mpwa wake alizokuwa nazo kwa vile yeye ndiye peke yake aliyekuwa amelion-goza hilo jeshi katika Swala.

Suala la uongozi lilikuwa linamsumbua Said bin Al-Aas pia. Alilizungumza na Talha na Zubeir na majibizano yafuatayo yalitokea kati yao:

Said: Kama mtashinda vita dhidi ya Ali, nani atakuwa khalifa afuataye? Talha: Yeyote atakayechaguliwa na Waislam, ndiye atakayekuwa khalifa wao.

Said: Wakati mlipoondoka Makka, mlidai kwamba nia yenu ya kupigana vita dhidi ya Ali, ilikuwa ni kulipiza kisasi kwa ajili ya damu ya Uthman. Kama malengo yenu haya-jabalika, basi mnapaswa kumfanya mmoja wa watoto wake kuwa khalifa mpya, na wote wapo hapa pamoja nasi katika jeshi hili.

Talha: Hivi unadhani tutawapita Muhajirina wakubwa na kumfanya mmoja wa vijana wako asiye na ujuzi kuwa khalifa wetu? Kamwe.

Said ndipo akaelewa kwamba mazungumzo ya kulipiza kisasi kwa ajili ya damu ya Uthman yalikuwa ni hila tu, na lengo halisi la wale "watawala watatu" lilikuwa ni kun-yakua madaraka kwa ajili yao wao wenyewe.

Mgeni mashuhuri kwenye kambi ya waasi alikuwa ni Mughira bin Shaaba. Alizungumza na Aisha na Marwan, na akawashauri kuacha mpango wao wa kuivamia Basra. Alimwambia Marwan:

543

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

" ..Kama unakwenda Basra kuwatafuta wauaji wa Uthman, basi sharti utambue

kwamba wako hapa kwenye kambi yako mwenyewe na sio Basra. Ndio makamanda wa jeshi lako. Walimuua Uthman kwa sababu kila mmoja wao alitaka awe ndiye khalifa. Lakini wakashindwa, na baada ya kushindwa kwao, wakaibuni hii hadithi ya kutafuta kulipiza kisasi."

Lakini Aisha na Marwan hawakuwa na nia ya kuuacha mpango wao mkubwa wa mapam-bano. Hawakuukubali ushauri wa Mughira, ndipo yeye, Said bin Al-Aas, Abdallah bin Khalid na wengine wachache wakajitoa wenyewe kutoka kwenye jeshi la waasi, na wakaenda Ta'if.

Lile jeshi la waasi lilianza tena matembezi yake kuelekea Basra lakini tukio lisilokuwa la kawaida lililifanya lisimame mara nyingine tena.

Wakati Aisha alipokuwa anapita kwenye kisima fulani kwenye kijiji kilichokuwa kwenye njia kuu, mbwa koko fulani walimzunguka ngamia wake, na wakaanza kumbwakia Aisha kwa ukali sana. Aisha alitoa kichwa chake kutoka kwenye machela iliyofunikwa, na aka-muuliza mtoto wa Talha kama alikuwa analijua jina la kile kijiji walichokuwa wanakipita. Yeye akasema walikuwa wanapita kwenye kitongoji kinachoitwa Haw-ab.

Pale Aisha alipolisikia lile jina la Haw-ab aliingiwa na hali ya fadhaa. Alimuamuru mwon-goza ngamia wake kumkalisha huyo ngamia, na akasema kwamba ilimbidi kurudi Madina haraka sana badala ya kuendelea japo kidogo tu kuelekea Basra.

Kubadilisha kwa ghafla kwa mwelekeo wa safari kwa Aisha, kulimzangaza mtoto wa Talha, na akamuuliza ni kwa nini hakuweza kwenda Basra. Yeye Aisha akasema kwamba kumbukumbu imemjia ya utabiri wa Mtume (s.a.w.w.) na akamweleza ilivyokuwa kwa maneno yafuatayo:

"Yeye, Mtume siku moja alikuwa na wake zake, na akiongea nao alisema: 'siku itafi-ka ambapo mbwa wa Haw-ab watakuja kumbwekea mmoja wenu, na hiyo itakuwa siku ambapo atakuwa kwenye upotovu wa wazi.' Kisha yeye akanigeukia mimi, na akasema: 'angalia ewe mwanamke mwekundu! Usije ukawa ndiye mke yule.' Na hivi sasa ninaweza kusikia na kuona kwamba mbwa wa Haw-ab wananibwekea mimi. Kwa hiyo, ni mimi niliyeko kwenye upotovu wa dhahiri."

Lakini mtoto wa Talha hakuvutika, na akasema:

"Ewe mama wa waumini! Usiwajali mbwa hao wanaobweka. Tunayo mambo muhimu sana ya kufanya. Kwa hiyo, natusonge mbele kuelekea kwenye mafikio yanayotupungia mkono kutoka upande wa mashariki."

544

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Lakini Aisha alionekana kuwa amedhamiria kurudi Madina. Akishtushwa na kusisitiza kwake juu ya kurudi Madina, mtoto wa Talha alimwita Abdallah bin Zubeir akitegemea kwamba ataweza kumshawishi dhidi ya kulitelekeza lile jeshi la waasi.

Abdallah bin Zubeir alifika kwenye eneo la tukio na yeye pia akayasikia maelezo ya Aisha. Lakini ilimbidi amzuie kwa gharama yoyote ile. Kama alikuwa alitelekeze lile jeshi la waasi, juhudi zote za viongozi wa maasi za kutwaa madaraka, zitavunjika papo hapo. Zaidi ya hayo, watakuwa hawana mahali pa kwenda. Yeye, kwa hiyo, akamwambia shangazi yake kwamba kile kijiji ambacho mbwa wake walikuwa wamembwekea, na wakawa wamemtingisha wazi wazi, hakikuwa Haw-ab; kilikuwa ni kijiji kingine kisichoeleweka vizuri. Aisha, hata hivyo, hakuridhika, na akatamka kwamba hatakwenda Basra.

Abdallah bin Zubeir sasa ilimlazimu kuchukua hatua za mwisho kabisa kumhakikishia shangazi yake kwamba katika kwenda Basra, hakuwa akipotoka, na kwamba kubweka kwa mambwa fulani kusimlegeze moyo. Kisha akala kiapo kwamba jeshi lile lilikuwa limeiacha Haw-ab mbali sana huko nyuma. Yeye vile vile aliwakusanya Waarabu hamsini-wa jangwani, akawaleta mbele ya Aisha, na wote wakaapia kwamba Haw-ab kwa uhakika ilikuwa mbali sana kutoka pale alipokuwa yeye.

Wanahistoria wa Kiarabu wanasema kwamba ule "ushahidi" ambao Abdallah aliutoa mbele ya Aisha, ulikuwa ndio kosa la kwanza la kusema uongo baada ya kiapo, katika Uislam.

Tabari, mkuu wa wanahistoria wa Kiarabu, pia amelisimulia tukio hili. Anaongeza kwamba kupitia juhudi za mwanawe wa kumlea, Abdallah bin Zubeir, na "mashahidi" wake hamsini, Aisha mwishowe aliridhika kwamba wale mbwa wanaombwekea hawakuwa wa Haw-ab hata hivyo, bali wa kijiji kingine. Alilitupilia mbali tukio hilo kama bahati mbaya. Dhamira yake mbaya ilikuwa "imetulizwa," na alikuwa tayari kukaa kwenye kipando kuelekea Basra.

Kwa wakati huu, Ali alikuwa anashughulishwa na kutathmini hali halisi. Katika maadui zake wote, alijua kwamba Mu'awiyah, gavana wa Syria, alikuwa ndiye aliyekuwa hatari zaidi, na alihisi kwamba alipaswa kuzingatia kumshughulikia yeye kwanza. Lakini tena akasikia kwamba Talha na Zubeir ambao hapo mapema waliondoka Madina kwenda Makka "kutekeleza umra," wamekivunja kiapo chao cha utii kwake, na kwamba wao na Aisha, ambaye alikuwa tayari yuko Makka, wamenyanyua bendera ya uasi dhidi yake. Ililetwa habari kwake pia kwamba viongozi hao watatu walikuwa tayari wanasonga mbele pamoja na jeshi lililoandaliwa vema kuelekea kwenye mji muhimu wa Basra ndani ya Iraq kwa nia ya kuuteka.

Aisha alikuwa kamwe hajafanya siri ya uadui wake kwa Ali lakini yeye Ali hakufikiria

545

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kamwe kwamba atafikia kiasi cha kufanya vita dhidi yake. Kwake yeye, ushirikiano wa Talha, Zubeir na Mu'awiyah ulikuwa ukielekea kuwezekana lakini ushirikiano wa Talha, Zubeir na Aisha haukuelekea kamwe. Lakini alikuwa huyu hapa, pamoja na washirika wake, wakiwa ni tishio la moja kwa moja kwenye usalama wa Dola ya Kiislam kuliko Mu'awiyah mwenyewe.

Ali alilazimika kusimamisha kila kitu ili kukabiliana na upinzani wa Aisha, Talha na Zubeir. Alilalamikia uchokozi wao usio na maana na usio wa wakati muafaka, na alijaribu kuwashawishi kuacha kusababisha umwagaji wa damu ya Waislam ambao ulikuwa hauk-wepeki kama wangeasi dhidi ya mamlaka halali. Alituma barua kwa Aisha ambayo mad-humuni yake yalikuwa kama ifuatavyo:

"Kwa jina la Allah ambaye ni Mwingi wa Rehma na Mwingi wa Kurehemu. Umeondoka nyumbani kwako kwa uvunjaji wa moja kwa moja wa amri za Allah na Mtume Wake, na sasa unapanda mbegu za vita vya wenyewe kwa wenyewe miongo-ni mwa Waislam. Hebu sita japo kwa muda kidogo na ufikirie kuhusu hili: Wewe unahusika nini na majeshi na vita? Je, ni kazi yako wewe kupigana? Na unapigana dhidi ya nani? Dhidi ya Waislam? Nafasi yako wewe iko nyumbani kwako. Allah amekuamrisha wewe kubakia nyumbani kwako. Kwa hiyo, muogope Yeye, na usimuasi Yeye, na urudi mara moja kwenda Madina."

Aisha aliipokea barua ya Ali lakini maombi yake hayakuwa na athari yoyote juu yake yeye, na wala hakuijibu kabisa.

Ali alituma barua kama hizo hizo kwa Talha na Zubeir na wao pia hawakumjibu. Ali alita-mbua kwamba wale viongozi wa waasi walikuwa wamedhamiria kabisa kumwaga damu ya Waislam. Akitamani kuwazuia wasifanye hivyo, aliamua kuwaingilia kati. Lakini angeweza tu kulizuia jeshi lao kwa jeshi lake mwenyewe, naye alikuwa hana jeshi!

Khalifa huyu mpya ilimbidi aandae jeshi kama ilikuwa alizuie jeshi la waasi lisifike na kuikalia Basra. Aliingia Msikitini, akawafahamisha Waislam kile waasi walichopanga kuk-ifanya, akawaelezea juu ya haja ya kuwa na jeshi la kukabiliana na changamoto yao na ali-wataka wao kujitokeza kama askari wa kujitolea.

Ali alishitushwa na mwitiko alioupata kwa maombi yake. Hakuna mtu aliyejitolea kupigana dhidi ya waasi hao. Alirudia maombi yake, na majibu yalikuwa ni yale yale. Baada ya kila Swala, Ali aliusihi mkusanyiko wa waumini kusimama katika kutetea serikali iliyoanzishwa kihalali. Aliwakumbusha kwamba alikuwa amechukua uongozi wa serikali yao juu ya msisitizo wao wenyewe. Aliwakumbusha pia kwamba alifanya ridhaa yake mwenyewe ya ukhalifa kwa kutegemea juu ya ahadi yao ya kumtii yeye - katika amani na katika vita. Waislam, inavyoonekana, walikuwa wamesahau ahadi yao. Ali alijihisi alikuwa amekwamishwa kabisa.

546

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Baada ya siku chache, hata hivyo, mtu mmoja alisimama mle Msikitini na akamwambia Ali kwamba yeye atamtii amri zake. Baadhi ya wengine, wenye kujali kama yeye, walifu-ata mfano wake. Mara Ali akawa na uwezo wa kukusanya pamoja kikosi kidogo cha wapi-ganaji wa kujitolea 700 waliokuwa tayari kumtii yeye.

Sir Johb Glubb:

"Mara tu Ali aliposikia kwamba Zubeir, Talha na Aisha wameondoka Makka, aliamua kuwafuata, lakini alipata ugumu sana katika kuandaa kikosi kwa ajili ya madhumuni hayo. Miezi mitatu tu kabla, Masahaba na watu wa Madina walikuwa wamemuomba awe khalifa. Sasa ni wachache tu walioweza kumsaidia yeye ingawa Zubeir na Talha wanaoonekana wazi kutokuwa na maadili walikuwa wamekusanya watu 3000 kuto-ka Makka na makabila ya jirani."

Mnamo Oktoba mwaka 656, miezi minne baada ya kuuawa kwa Uthman, Ali alitoka kumfuata Zubeir na Talha. Alikuwa na watu 700 tu pamoja naye. Akiwa mnyonge sana kuendelea, alipiga kambi kwenye kisima cha jangwani mahali paitwapo Najid.

(The Great Arab Conquests, uk. 318, 1967)

Kabla ya kuondoka Madina, Ali alimwita Umm Salma, mmoja wa wajane wa Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt., na akamuaga. Umm Salma akamwambia:

"Kwa jina Allah, ninakuweka kwenye ulinzi Wake. Kwa Uwezo na Utukufu Wake, wewe pekee ndio uko pamoja na haki, na maadui zako wote wapo kwenye batili. Kama isingekuwa amri ya Allah kwa wake za Mtume Wake kubakia nyumbani, ningefuatana nawe katika mapambano hay a."

Umm Salma alikuwa na mtoto kutokana na ndoa yake ya kwanza, akamkabidhi kwa Ali, na akasema:

"Ndiye mwanangu pekee. Yeye ndio kitu cha thamani kabisa nilichonacho katika dunia hii. Ninamkabidhi kwako. Atajitoa muhanga, kama ikibidi, maisha yake kwa ajili yako."

Ali alivutiwa sana na kitendo cha Umm Salma. Alimshukuru yeye, na akachukua likizo ya kuvunja moyo kutoka kwake asijue kama atakuja kurudi tena Madina kamwe. Mtoto wake Umm Salma aliandamana naye kwenda Iraq.

Ali alimteua Sahl ibn Hunaif Ansari kuwa gavana wa Madina wakati wa kutokuwepo kwake, na alimtuma Qathm ibn Abbas kwenda Makka kwenda kuchukua mamlaka ya mji ule kama gavana wa mji. Kitu cha mwisho ambacho alikifanya Ali hapo Madina, kilikuwa ni kutembelea kaburi la

547

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad Musrafa (s.a.w.w.), na la Fatima Zahra - baba na bintiye. Muhammad alikuwa kiongozi wake, mfadhili na rafiki yake, na Fatima alikuwa ni mke wake. Aliwaaga wote hao kwa moyo uliojaa huzuni na macho yaliyojaa machozi.

Katika kuwasili kwake huko Iraq, Ali na kikosi chake kidogo walipiga kambi mahali panapoitwa Dhi-Qaar. Abdallah ibn Abbas, binamu yake, anasimulia kuwasili hapo kam-bini, kwa rafiki mpya, kama ifuatavyo:

"Tulikuwa tupo Dhil-Qaar wakati mchana mmoja, tulipomuona mtu mmoja anakuja kuelekea kambini kwetu. Alikuwa mzee sana, na mdhaifu sana. Vitu pekee alivyokuwa navyo ni kifuko kidogo cha chakula cha akiba na mfuko wa maji wa ngozi ya mbuzi. Wakati huu akaingia kambini, na akaomba kukutana na Ali. Alipoletwa mbele ya Ali, akajitambulisha mwenyewe kama Uways Qarni kutoka Yemen. Mara tu tulipolisikia jina lake, tulijua kwamba ni yule rafiki na mpendwa aliyekuwa hajawahi kuonekana, wa bwana wetu, Muhammad, Mtume wa Allah swt. Alimuomba Ali anyooshe mkono wake ambapo akaunyoosha. Kisha naye akauweka mkono wake juu ya mkono wa Ali, na akatoa kiapo cha utii kwake."

Ali alimsalimia yule rafiki na kipenzi cha bwana wake, Muhammad, kwa uchangamfu kama vile ambavyo Mtume mwenyewe angefanya, kama angekuwa yupo pale mwenyewe.

Mheshimiwa Uwais aliingizwa ipasavyo katika jeshi la Madina. Kwa Ali, kuwasili kwa Uwais Qarni katika kambi hiyo kulikuwa ni kijaliza adimu kwenye mpangilio wa matukio ya baadae ya kikatili na ya kisirani ya uchochezi, uhaini, usaliti na maasi, ambayo yameitawala Dola ya Kiislam. Kwa kitambo kidogo, alisahau ya wakati ule na akazama kwenye njozi za nyakati zilizopita; nyakati za bwana wake, Muhammad (s.a.w.w.). Zile zilikuwa hasa "nyakati njema za kale;" zile zilikuwa ndio nyakati bora kweli. Ni vipi ali-tamani angeweza kurudi kwenye nyakati zile ambapo, kama msaidizi mkuu wa Muhammad, alikuwa ameulinda Uislam na umma wake yeye kutokana na waabudu masanamu. Sasa katika kijalizo cha kushtusha, umma ule umepinga mamlaka yake, na ukaonekana kuwa na kiu na damu yake. Alizinduliwa kutoka kwenye mawazo yake ya zama nzuri na za kuvutia na wakati uliopo wa kutisha na uliotengeka.

Hatua za awali za Ali za kuepukana na vita, alizozifanya kutoka Madina, zilikuwa zimeshindwa lakini alikuwa na shauku kubwa ya kuzuia vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Waislam. Kwa hiyo, mara tu baada ya wapiganaji wake walipokuwa wamepiga kambi, alianzisha kampeni yake ya kuleta amani, na akafanya mfululizo wa ishara mpya za kidiplomasia kwa viongozi wa maasi ili waje kujadiliana masharti ya amani pamoja naye kuliko kuombea usuluhishi wa silaha. Aliwatuma baadhi ya wale masahaba maarufu wa Mtume kwenda kuwasihi Ayesha, Talha na Zubeir wasiivunje amani lakini bila mafanikio.

548

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Edward Gibbon:

"Maisha ya Swala na tafakuri hayakupoozesha juhudi za kivita za Ali; lakini katika umri wa utu uzima, baada ya uzoefu wa muda mrefu wa wanadamu, bado aliisaliti katika tabia yake, ile pupa na kutokuwa na hadhari kwa ujana. Katika siku za mwan-zo za utawala wake, aliacha kujipatia ama kwa zawadi au pingu, vile viapo vyenye mashaka vya Talha na Zubeir, wakuu wa Kiarabu wawili wenye nguvu sana. Walitoroka kutoka Madina kwenda Makka, na kutokea hapo kwenda Basra; wakasi-mamisha bendera ya uasi; na wakaichukua kwa nguvu serikali ya Iraq, au Assyria ambayo waliitaka bure kama zawadi kwa ajili ya utumishi wao. Barakoa ya uzalendo inaruhusiwa kufunika ukiukaji wa utaratibu wa dhahiri kabisa; na maadui, labda wale wauaji, wa Uthman, sasa walidai kisasi kwa ajili ya damu yake. Walifuatana katika msafara wao na Aisha, mjane wa Mtume, aliyehifadhi mpaka saa ya mwisho ya maisha yake chuki isiyo na huruma dhidi ya mume na watoto wa Fatima.

(The Decline and Fall of the Roman Empire)

Katika kuacha kupokea ama kwa zawadi au pingu, kiapo cha wasiwasi cha Talha na Zubeir, Ali alikuwa hasaliti pupa na kutokuwa na hadhari kwa ujana, kama Gibbon anavy-odai. Ali alikuwa anajua kwamba Talha na Zubeir wana udanganyifu mioyoni mwao. Kuwapa wao zawadi kutakuwa ni hongo tu, na Ali alikuwa sio mtu wa kumpa hongo mtu yoyote kwa ajili ya kitu chochote.

Huko Madina, Abdallah ibn Abbas alikuwa amemshauri Ali kumteua Talha na Zubeir kuwa magavana wa Basra na Kufa. Kubashiri kutokana na tabia zao na muelekeo wao wa baadae, kuwateua Talha na Zubeir kuwa magavana, kungekuwa ni kosa baya sana kwa upande wa Ali. Kama angefanya hivyo, angelazimika kupigana, sio dhidi ya mmoja bali Mu'awiyah watatu!

Na kuhusu pingu, Ali sio mtu wa kumkamata mtu yoyote kwa kosa lililofikiriwa lakini hal-ijatendwa bado. Wakati Talha na Zubeir walipokuja kwake na kumuomba ruhusa ya kwenda Makka kutekeleza umra, aliwaruhusu waende lakini akawaambia kwamba hawakuwa wakienda Makka kwa ajili ya kutekeleza hijja.

Kama ilivyoonyeshwa hapo juu, Ali aliweza kukusanya hapo Madina, sio zaidi ya wapi-ganaji mia saba. Kwa kikosi kidogo kiasi hicho, asingeweza kukabiliana na changamoto ya waasi. Yeye, kwa hiyo, alimtuma Muhammad bin Jaafar na Muhammad ibn Abu Bakr kwenda Kufa kuleta wapiganaji wa kuongezea nguvu kutoka huko. Gavana wa Kufa kwa wakati huu alikuwa ni Abu Musa al-Ashari, naye aliwapinga hao. Wakati uimarishaji ulipochelewa kuja, Ali alimtuma kwanza Abdallah ibn Abbas na Malik ibn Ashtar, na kisha Imam Hasan na Ammar ibn Yasir kwenda Kufa, kuandikisha askari.

549

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Imam Hasan aliupuuza upinzani wa Abu Musa, akaingia kwenye Msikiti mkubwa, akawahutubia Waislam wa Kufa kwa hotuba ambayo ndani yake aliwakumbusha ni nini ilikuwa kazi na wajibu wao kwa Allah swt., na Mtume Wake (s.a.w.w.).

Kuwasili kwa Hasan - kipenzi cha Muhammad - hapo Kufa, kulisababisha msisimko. Hotuba yake ilikuwa haijakwisha bado pale watu walipoanza kupiga makelele: tunakutii, tupo kwa ajili yako.

Wakati huo huo, Malik ibn Ashtar aliingia kwenye kasri ya gavana. Aliwafukuza watu-mishi wa Abu Musa na akalikamata lile jengo. Abu Musa alitoroka kutoka Kufa usiku, na akatafuta hifadhi kwa Mu'awiyah huko Damascus.

Imam Hasan, Ammar bin Yasir, Abdallah ibn Abbas na Malik ibn Ashtar walirudi Dhi-Qaar wakiwa na wapiganaji 12,000 wa Kufa pamoja nao.

Gavana wa Ali huko Basra alikuwa ni Uthman bin Hunaif Ansari, sahaba wa Mtume yule yule ambaye Umar alikuwa amemteua kama Kamishna wa Fedha wa Iraq.

Aliposikia kwamba jeshi la Aisha, Talha na Zubeir lilikuwa kwenye vitongoji vya Basra, alimtuma mmoja wa marafiki wa Ali - Abul Aswad ad-Du'ali - kwenda kuwaona na kujua sababu za kwa nini walikuja. Abul Aswad alimwendea Aisha, na mabishano yafuatayo yakatokea baina yao:

Abul Aswad: Ewe mama wa waumini, lengo lako ni nini katika kuja Basra pamoja na jeshi?

Aisha:                 Nimekuja kulipiza kisasi kwa ajili ya mauaji ya Uthman ambaye aliuawa katika

nyumba yake mwenyewe ingawa alikuwa hakutenda dhambi yoyote.

Abul Aswad; Yeyote ambaye atakuwa amemuua Uthman, hayupo Basra.

Aisha:                  Ndio, ninajua. Lakini kupata kulipiza kisasi, ninahitaji ushirikiano na msaada

wa watu wa Basra.

Abul Aswad: Ninatumaini hujasahau bado kwamba Mtume wa Allah swt. alikuwa amekuamuru wewe kubakia nyumbani. Kwa hali yoyote, sio kazi yako kujiingiza kwenye siasa na vita. Haifai kabisa kwa mjane wa Mtume kuondoka nyumbani kwake, na kupigana dhidi ya Waislam.

Aisha:            Hivi atathubutu Muislam yoyote kupigana dhidi yangu mimi?

Aisha aliamini kwamba kama atakwenda kwenye uwanja wa vita mbele ya jeshi lake,

550

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wapiganaji wa maadui wenyeji, katika kumuona akiwakabili wao, watakuja ama upande wake, au wataiacha vita hiyo, na kumtelekeza bwana wao.

Abul Aswad halafu yake akaenda kuwaona Talha na Zubeir, na akawauliza nia yao ilikuwa nini katika kuja Basra katika mpango wa kijeshi.

Talha/Zubeir: Tunataka kisasi kwa Ali kwa ajili ya mauaji ya Uthman.

Abul Aswad: Ali hakumuua Uthman wala hakuwa na ushiriki wowote katika mauaji yake, na hilo mnalijua.

Talha/Zubeir: Kama hakushiriki, kwa nini anawalinda hao wauaji?

Abul Aswad: Ina maana kwamba mmevunja kiapo cha utii ambacho mlimpa Ali?

Talha/Zubeir: Kiapo hicho kilichukuliwa kutoka kwetu kwa ncha ya upanga. kwa hiyo kilikuwa ni batili.

Abul Aswad aliweza kuona kwamba wale viongozi wa waasi walikuwa wameshikilia vita, na kwamba mazungumzo ya ziada pamoja nao yalikuwa hayana maana. Yeye kwa hiyo, akarudi Basra, na akamweleza Uthman ibn Hunaif kile ambacho Aisha, Talha na Zubeir walikuwa wamemwambia.

Viongozi wa maasi hawakuficha nia zao lakini Uthman ibn Hunaif hakuwa na jeshi lenye nguvu, na alijua kwamba asingeweza kuulinda mji dhidi yao. Kwa hiyo, walipotokea kwenye milango la mji, alifanya majadiliano pamoja nao. Pande mbili hizo zilikubaliana kwamba mpaka atakapofika Ali, waasi hao hawatafanya kitu chochote cha kuvuga mpango uliopo, na Uthman ibn Hunaif ataendelea kufanya kazi kama gavana wa Basra.

Lakini hazikupita hata siku mbili wakati viongozi wa maasi walipoyavunja makubaliano ya kusitisha vita. Jeshi lao liliushambulia mji wakati wa usiku, na wakauvamia kwa nguvu, na mara lilipokaribia kuta zake, lilionekana kupagawa. Wapiganaji walizagaa ndani ya mji na wakaua Waislam 600, ikiwa ni pamoja na 40 ndani ya Msikiti Mkuu wenyewe.

Talha na Zubeir walipenya kwenye nyumba ya gavana ambamo walimkamata Uthman ibn Hunaif, na wakawaua wale waliojaribu kumlinda yeye. Walitaka kumuua yeye pia lakini yeye aliwaambia kwamba kama watamuua yeye, basi kaka yake, Sahl ibn Hunaif, ambaye alikuwa gavana wa Madina, angewaua ndugu zao wote waliokuwa wanaishi katika mji ule, katika kulipiza kisasi. Wao, kwa hiyo, walilazimika kuichunga hamu yao ya kumuua yule rafiki wa kuheshimika wa Muhammad (s.a.w.w.). Lakini walimpiga, wakamng'oa nywele zote katika kichwa chake, nyusi zake, na ndevu zake, na wakamfukuza kutoka Basra.

551

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Aliweza hata hivyo, kuifikia kambi ya bwana wake, na akapepesuka mbele yake, mahutu-ti kama anayekufa!

Ali alisikitika sana kumuona Uthman ibn Hunaif katika hali ambayo Talha na Zubeir waliyomtoa nayo. Hakuweza kumtambua yeye. Alijaribu kumfariji huyo rafiki wa zamani wa Muhammad Mustafa kwa machozi yake.

Jeshi la waasi sasa lilikuwa limeushika mji wa Basra. Lilikuwa limefanikiwa katika kufanikisha lengo lake la kwanza. Viongozi wake waliwafukuza marafiki wote na wafuasi wa Uthman ibn Hunaif kutoka mjini hapo kama hawakuwaua.

Ali hakuwa na chaguo sasa bali kuamuru jeshi lake kusonga mbele kwenda Basra. Wakiwa wamesimama hapo Zawiya, kaskazini ya Basra, alituma barua kwa mara nyingine tena kwa kila kiongozi wa waasi akishauri kwamba pande zote zisuluhishe kutofautiana kwao kwa majadiliano badala ya kupigana dhidi ya mwingine na kuuana wenyewe.

Viongozi wa waasi hawakuwa na tamaa ya kuzijibu barua za Ali. Bila kumuachia masha-ka yoyote akilini mwake kwamba wameitupa amani kama zana ya sera yao, waliamua kuk-abiliana naye nje ya ngome za mji.

Sir John Glubb:

"Jeshi la khalifa lilipokuwa linakaribia Basra, wale waasi walitoka kuja kukabiliana nalo, wakiongozwa na Zubeir na Talha. Basra yote haikuwa nao. Bani Bakr, kabila ambalo wakati fulani liliongozwa na yule shujaa Muthana, lilijiunga na jeshi la Ali. Bani Tamiim waliamua kutopendelea upande wowote. Jeshi la Ali sasa likawa na nguvu kidogo. Katika siku za Ujahilia, wanawake waliokuwa wamepanda kwenye machela juu ya ngamia, mara kwa mara walifuatana na makabila yao kwenye vita, kuwatia moyo wapiganaji. Aisha, "Umm-ul-Mu'minin," aliandamana na jeshi la waasi katika kiti chake cha ngamia."

(The Great Arab Conquests, uk. 320, 1967)

Wakati majeshi mawili hayo yalipokabiliana, Ali alitoka kwenye safu yake na akamwita Talha na Zubeir kuja kupambana naye. Dr. Taha Husein wa Misri anasema kwamba majemedari wote walitoka kwenye safu zao wakiwa katika mavazi kamili ya kivita kiasi kwamba sehemu za miili yao zilizoweza kuonekana, ni macho yao tu. Pale Aisha alipowaona wao wakienda, aliogopeshwa na kile ambacho kingeweza kutokea kama wangekutana na Ali katika vita. Lakini alijulishwa kwamba Ali alikuwa hana silaha, na hakuwa, kwa kweli, amevaa hata deraya, na akawa ameondolewa shaka. Ali aliwauliza kwa nini wamevunja kiapo cha utii ambacho walikuwa wamempa yeye kwa hiari zao, na kwa nini walitaka kupigana dhidi yake.

552

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wakimjibu, Talha na Zubeir walikariri ule msururu wa shutuma za zamani kwamba alikuwa anawalinda wauaji wa Uthman, na kwamba walikuwa wakiitafuta haki kwa ajili ya kifo cha Uthman. Ali aliwaambia kwamba wao walijua vizuri sana tu, kwamba yeye hakuhusika kabisa na kifo cha Uthman au na wauaji wake. Kisha yeye akaongeza: "Kwa vile hamtaki kusikiliza hoja, ninashauri kwamba tujaribu kidokezi kipya ili kuamua mgogoro huu. Mtakumbuka kwamba bwana wetu, Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt, wakati mmoja aliitisha Mubahila (kulaaniana) pamoja na Wakristo wa Najran. Hebu natuige mfano wake, na tusimamishe Mubahila, na kuomba kama ifuatavyo:

"Ewe Mola wa Viumbe wote! Tunaomba Huruma Zako. Wewe Unafahamu yote ninayohisi au ninayofikiri au ninayoyafanya. Hakuna kinachofichikana mbele ya macho Yako. Kama nimeshiriki, wazi wazi au kwa kificho, katika mauaji ya Uthman, au kama nimewasaidia wale watu ambao wamemuua Uthman, au kama nilifurahia kwa siri wakati alipouawa, onyesha chuki Yako kwangu. Bali kama sina hatia ya kosa lote la ushiriki wa njama katika mauaji ya Uthman, basi onyesha chuki Yako kwa wale wote wanaodai kwamba mimi ni mshiriki katika uhalifu dhidi ya Uthman."

Talha na Zubeir hawakuukubali mwaliko wa Ali kusimamisha Mubahila, na wakatamka wazi: "Hatukuoni wewe kama unastahili ukhalifa, na sisi kwa hali yoyote hatuna upungu-fu zaidi wa sifa au kutokustahili zaidi kuwa khalifa kuliko wewe ulivyo." (Tarikh Tabari, juz.111, uk. 519).

Kitu kimoja Talha na Zubeir walichokifanya, kilikuwa ni kuacha kile kisingizio cha kulip-iza kisasi kwa ajili ya kifo cha Uthman; walikuwa wapigane dhidi ya Ali ili waweze kuwa makhalifa.

Jaribio jingine la kuokoa amani lilikuwa limeshindikana lakini Ali bado hakutaka kuona Waislam wakiwauwa Waislam. Yeye, kwa hiyo, alimwita Zubeir ambaye hata hivyo alikuwa ni binamu yake, kwenye kikao cha faragha, na akamkumbusha juu ya zile siku ambapo wao wote walikuwa wapiganaji-wenza, na walipigana dhidi ya maadui wa dini chini ya bendera ya Mtume wa Allah. Je hazikuwa, alimuuliza Zubeir, siku za shani, na sasa, yeye, Zubeir, binamu yake, alikuwa anataka kupigana dhidi yake; ilikuwa inawezekana vipi; ni vipi Zubeir atapigana dhidi yake yeye, binamu yake mwenyewe?

Ali pia alimkumbusha Zubeir kuhusu utabiri wa Mtume (s.a.w.w.). "Unaukumbuka ule wakati," alimuuliza Zubeir, "ambapo Mtume wa Allah swt, alikwambia wewe, mbele yangu, kwamba siku moja utakuja kupigana dhidi yangu, na kwamba utakuwa umepotoka kwa kufanya hivyo?" "Oh ndio," alitamka ghafla Zubeir, "ninakumbuka aliyokuwa ameyasema Mtume. Lakini nilikuwa nimeusahau utabiri huo, na sasa sitapigana dhidi yako." Kumbukumbu pia ilimjia Zubeir ya utabiri mwingine wa Mtume wa Allah swt. ambaye alisema kwamba rafiki yake mwandani, Ammar ibn Yasir, atakuja kuuawa na

553

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kundi la watu waovu. Sasa Zubeir ghafla alitambua kwamba Ammar alikuwa kwenye jeshi la Ali.

Zubeir aligeuza hatamu za farasi wake na akarudi kwenye safu zake mwenyewe, uso wake ukionyesha ishara za mgogoro wa ndani na mfadhaiko mkubwa. Katika kujibu maswali ya shauku ya Aisha na ya mwanawe mwenye tamaa na mgomvi, alisema kwamba Ali amemkumbusha yeye juu ya utabiri wa Mtume wa Allah swt. mwenyewe, na yeye, kwa kutambua kwamba yuko kwenye upotofu, alikuwa amempa Ali kiapo kingine cha kutokupigana dhidi yake. Mwanawe mwenye shari akasema kwamba sababu hasa ya kuji-toa kwake kwenye vita ilikuwa sio ule utabiri wa Mtume bali ni kumuogopa Ali.

Zubeir alipandwa na hasira kwa kashfa hii. Alisema kwamba alikwisha kuapa kutokupigana dhidi ya Ali, na akaongeza kwamba chaguo lililokuwa mbele yake lilikuwa wazi: ama ajiaibishe miongoni mwa Waarabu kwa kukimbia kwenye vita kama muoga, au ajiimarishe mwenyewe kukabiliana na laana, na aliona kwamba kujiaibisha kama muoga ndio kwepe-si katika maovu hayo mawili.

Zubeir aliondoka kwenye uwanja wa vita, inavyoelekea, kwa nia ya kurudi Madina. Alikuwa amesafiri maili chache tu wakati alipogundua kwamba alikuwa akifuatwa kwa siri na mtu mgeni kwake. Mgeni huyu alikuwa ni mtu wa Basra, mtu aitwaye Amr bin Jarmuz. Ingawa Zubeir alishtuka kwa wasiwasi, aliendelea kwenda mpaka alipofikia kiji-ji. Hapo alishuka ili aoge, aswali na kupumzika. Lakini alikuwa amefika mwisho wa safari yake. Pale alipokuwa anaswali, Amr bin Jarmuz alimshambulia na kumuua.

Zubeir alikuwa ameondolewa kwenye hesabu lakini Talha na Aisha walidhamiria kupigana hata bila yeye. Ali, hata hivyo, bado alisita kupigana, na akaamua kufanya jaribio moja jingine la kuiokoa amani. Alimtuma kijana mmoja, aitwaye Muslim ibn Abdallah ambaye alifahamika kwa uchamungu wake, pamoja na nakala ya Qur'an, kwenda kumuomba adui kuuweka mgogoro huo kwenye Hukmu ya Allah, na kusisitiza amani kwa ajili ya utukufu wa damu ya Waislam.

Akiwa amesimama mbele ya kundi la maadui kwa karibu kiasi, Muslim ibn Abdallah akai-funua ile Qur'an, na akasema: "Nitasoma kifungu kutoka kwenye Kitabu cha Allah ili mjue ni zipi amri na Makatazo Yake." Hotuba yake, hata hivyo, ilikatishwa na watupa mishale wa adui ambao waliirushia mishale ile nakala ya Qur'an aliyokuwa anaisoma. Wakati alipokuwa anajaribu kuikinga ile nakala ya Qur'an, mmoja wa watumwa wa Aisha alim-nyemelea, akamshambulia na kumuua.

Mwili wa Muslim ibn Abdallah uliletwa mbele ya Ali, na ukawekwa chini. Ali alikuwa anaomboleza kifo chake wakati mwili mwingine, wa mmoja wa wapiganaji wake ambaye alikuwa amepigwa na kuuawa kwa mishale na lile jeshi la Basra, ulipoletwa mbele yake.

554

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Alijaribu kuiondoa mishale hiyo kutoka kwenye maiti hiyo lakini alikuwa hajaondoa mishale mingi pale miili zaidi ya wapiganaji wake, iliyotobolewa na mishale, ilipowasili na ikapangwa mbele yake katika muonekano wa wazi kwa majeshi yote mawili. Waasi walikuwa wanachukua mazoezi ya kutupa mishale kwenye jeshi la Ali.

Tabari anasema katika Tarikh yake (juz. 111, uk. 522) kwamba wakati Ali alipoiona miili hii mbele yake, yeye alisema: "Sasa ni halali kupigana dhidi yao."

Kisha Ali aliinua mikono yake kuelekea juu mbinguni, na kisha akaomba:

"Ewe Mola Wangu! Kuwa Shahidi kwamba sikubakisha kufanya kitu chochote kuhi-fadhi amani miongoni mwa Waislam. Sasa hakuna hiari iliobakia kwangu bali ni kuliruhusu jeshi langu kujihami lenyewe kutokana na mashambulizi wasiyoya-chokoza. Sisi ni waja Wako wanyenyekevu. Tujaalie Neema na Huruma juu yetu. Tupatie sisi ushindi dhidi ya adui bali kama ni mapenzi Yako kumpa yeye, basi tupatie sisi taji la kifo cha kishahidi."

Ali alimaliza maombi yake, na kisha akivigeukia vikosi vyake, akavihutubia kama ifu-atavyo kabla tu ya kuvipa ishara ya kupigana:

"Enyi Waislam! Msiwe wa kwanza kumshambulia adui; mwacheni adui awe wa kwanza kuwashambulieni ninyi. Mara atakaposhambulia, basi itabidi mjihami wenyewe. Kama Allah akiwapeni ushindi juu ya maadui zenu, basi kumbukeni kwamba na wao pia ni Waislam. Kwa hiyo, msiwauwe wale waliojeruhiwa miongoni mwao. Kama watakimbia kutoka kwenye medani ya vita, msiwaandame, na muwaache waokoe maisha yao. Kama mtakamata mateka, msije mkawaua. Msiwakatekate wale waliokufa, na msiwanyang'anye deraya zao au silaha au vitu vingine vya thamani ambavyo mnaweza kuvikuta kwenye miili yao. Msiipore kambi yao, na msiwaudhi wanawake zao hata kama watatumia lugha mbaya na yenye matusi dhidi yenu au viongozi wenu. Lakini juu ya mambo yote, msiwe wasahaulifu, wakati wowote, juu wa uwepo wa Muumba wenu katika maisha yenu. Mpo machoni pake kila wakati."

Majeshi mawili hayo ndipo yakashambuliana. Waasi walikuwa tayari wamekwisha mpoteza Zubeir, mmoja majemedari wao wawili, kwa kuondoka. Jemedari mwingine, Talha, alikuwa pia alitegemewa kukutana na majaaliwa kama ya Zubeir. Abul Fida, mwanahistoria huyu, anasema kwamba Marwan alimuomba mtumwa wake amfunike ili asiweze kuonekena. Wakati yule mtumwa alipomfunika, alipachika mshale kwenye uta wake, akaulenga kwa Talha, na akamwambia mtumwa wake:

"Nilimuona mtu huyu (Talha) wakati wa zile siku ambazo Uthman alikuwa amezin-

555

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

girwa ndani ya nyumba yake. Alikuwa akiwachochea na kuwahimiza lile kundi kuin-gia ndani ya nyumba, na kumuua Uthman. Lakini leo anataka kulipiza kisasi kwa ajili ya damu yake. Inasikitisha eeh! Yeye alimpenda Uthman kweli kweli. Hapa, nitampa yeye zawadi kwa ajili ya mapenzi yale. Anastahili sana zawadi. Hata hivyo, mapenzi kama yale yasipite bila ya kuzawadiwa."

Marwan akauachia mshale ule. Ilikuwa ni pigo la kufisha ambalo lilimpata Talha kwenye paja, naye akachopea kwenda kwenye kifo chake nyuma ya jeshi lake.

Ibn Saad:

"Katika vita vya Ngamia, Talha alikuwa juu ya farasi wake karibu na Aisha wakati Marwan alipomrushia mshale ambao ulimchoma mguu wake. Kisha Marwan akase-ma: "Wallahi, sasa sitakuwa na kumtafuta yule mtu ambaye alimuua Uthman."

(Tabaqat, juz.111, uk. 223) Hakim:

"Ibrahim ibn Muhammad ibn Talha alisema kwamba Marwa bin al-Hakam alimuua babu yake (Talha) kwa mshale katika vita vya Ngamia."

(Mustadrak)

Sir John Glubb:

"Zubeir alikuwa binamu wa kwanza wa Mtume. Mama yake alikuwa ni dada wa baba yake Muhammad. Zubeir na Ali walikuwa wamefahamiana na kufanya kazi pamoja maisha yao yote. Wakati wao sasa walipokutana kati ya safu za majeshi yao husika, Ali alimuuliza Zubeir kama alikuwa analikumbuka hili na ule wakati walipokuwa wote ni wadogo, na pale walipokuwa wote wamejawa na hisia kali za ghera ya kidi-ni na upendo binafsi kwa Muhammad; jinsi Mtume wa Allah alivyosema hili na Ali na Zubeir wakasema lile. Ni nyakati nzuri kiasi gani, siku zile zilikuwa. Zubeir alilaz-imika kutoa machozi na akaapia kwamba hatampinga Ali kamwe kwa kutumia nguvu. Ali alikuwa na sifa ya kuwa mzungumzaji mwenye ushawishi.

Mapigano yalipoanza, Zubeir, kufuatana na kiapo chake, alijitoa kwenye uwanja wa mapambano. Akitembea katika bonde la jangwa, mbali kidogo kutoka kwenye uwanja wa vita, alikabiliwa na kuuawa na mtu aliyekuwa amechelewa nyuma yake. Kwa njia hii isiyo na maana na ya kufedhehesha ndivyo akafa mmoja wa mashujaa wakub-wa wa awali wa Uislam. Wakati huo huo, Talha alikuwa amejeruhiwa kwa mshale na alirudishwa Basra ambako alikufa muda mfupi baadae."

(The Great Arab Conquests, uk. 320, 1967)

556

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Zubeir na Talha walikufa kwa sababu zenye wasiwasi. Inaelekea kwamba walikuwa wanatambua kwamba kile walichokuwa wanakwenda kupigania sio chao, na ilikuwa sio haki. Wote wawili walikuwa miongoni mwa mashujaa maarufu wa siku za mwanzo za Uislam lakini katika vita vya Basra, ushujaa wao uliwatupa mkono. Hawakuonyesha ushu-jaa, na walikufa kama kondoo. Maelezo pekee juu ya hili yanaweza kuwa kwamba hamasa yao ilivunjika, na walishindwa hata kabla vita havijaanza. Kwao kulikuwa ni kushindwa kwa maadili.

Kwa kweli, Talha na Zubeir walikuwa wameingia kwenye kipingamizi kikubwa. Wakati mmoja, walikuwa na shauku sana ya kumuondoa Uthman. Walifanya uamuzi na wakashindwa. Baada ya kifo cha Uthman, kukaa kwa muda hapo Madina, kwa kweli kungekuwa ni hatari sana kwao. Hawakuipata njia ya kujitoa kwenye kipingamizi hicho ila kwa kupiga kelele kwamba walikuwa wanatafuta kulipiza kisasi kwa ajili ya kifo cha Uthman. Kuwakamata wauaji wa Uthman ilikuwa ni kazi ya utawala uliowekwa kihalali ambao ulikuwepo wakati huo, na ambao ulikuwa umetangaza kwamba utalichunguza suala hilo. Lakini hicho ndio ambacho hasa Talha na Zubeir walichokuwa wakikiogopa. Hawakutaka uchunguzi wowote ule. Fursa yao pekee ya kuokoa shingo zao ilikuwa ni kui-weka dola kwenye ghasia, na kuliacha kwenye ghasia. Katika jaribio hili walifanikiwa. "Walifanikiwa" kwa maana ya kwamba hawakumruhusu Ali kuchunguza kifo cha Uthman, na badala yake, walimlazimisha kushughulika na uasi wao.

Inashangaza kwamba Talha na Zubeir, wafuasi wa mwanzoni kabisa wa Uislam na walivyokuwa masahaba wa Mtume (s.a.w.w.), wameweza kuvunja kiapo chao cha dhati bila kutegemewa kama walivyofanya. Kama kweli waliamini kwamba Ali alikuwa ame-husika katika mauaji ya Uthman, walipaswa kusema hivyo ndani ya Msikiti wa Mtume (s.a.w.w.), mbele ya mkusanyiko wa Muhajirina na Ansari wote badala ya kuchukua kiapo cha utii kwake. Lakini hawakufanya hivyo, na wakachukua kiapo cha utii. Alimradi walikuwa na matumaini kwamba Ali atawateua kuwa magavana, basi walinyamaza kimya. Lakini mara tu walipopoteza matumaini hayo, wakavunja kiapo chao, na wakasimama katika maasi. Uasi ulikuwa ndio njia pekee ambamo wangeweza kumzuia Ali kuchunguza kifo cha Uthman.

Kama Talha na Zubeir wangekuwa wakweli katika kutafuta kisasi kwa ajili ya kuuawa kwa Uthman, kuna kitu kimoja tu ambacho wangeweza kukifanya. Wangemwambia Ali kwamba watampangia muda wa mwisho kwa ajili ya kufanya uchunguzi wake juu ya kifo cha Uthman, na alipaswa kuwatia mbaroni hao wahalifu kabla ya muda huo kwisha. Lakini hawakupanga muda kama huo; badala yake, walianzisha uasi kwa kisingizio cha kutafuta kulipiza kisasi kwa mauaji ya Uthman.

Wanahistoria wengine wanasema kwamba Ali alisikitikia vifo vya Talha na Zubeir. Ikiwa kama alifanya hivyo, kumbukumbu lazima ingemjia ya mwanzo wa heshima na mwisho

557

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wa fedheha wa mashujaa hawa wawili wa Uislam wa asili. Talha na Zubeir walilipa ghara-ma kubwa kwa ajili ya tamaa yao potofu, na kama usemi wa kisasa wa Kiarabu unavyose-ma, wao "wamepaliwa na kukata tamaa kwao wenyewe."

Pamoja na Talha na Zubeir kuondoshwa kwa namna hii, yule ngamia ambae Aisha alikuwa amempanda, ilikuwa ndio sehemu ya kupatia moyo kwa lile jeshi la Basra. Wapiganaji wa Aisha walipigana kwa nguvu sana na kwa ujasiri wa makusudi kabisa, na wakajifanya wao wenyewe kuwa ngome hai karibu na ngamia wake. Mpiganaji mmoja alishikilia hatamu zake mkononi mwake.

Kapteni mashuhuri wa Ali, Malik ibn Ashtar, alimkata mkono wake kwenye kiwiko. Mara moja, mpiganaji mwingine akachukua nafasi ya yule wa kwanza, na akazishika hatamu za ngamia huyo mkononi mwake. Malik ibn Ashtar akamkata mkono wake pia. Bingwa wa tatu akaingia, na yeye pia akapoteza mkono wake. Hii iliendelea mpaka ile mikono iliyokatwa ikapangwa rundo mbele ya ngamia huyo.

Pande zote kuzunguka ngamia wa Aisha, watu walikuwa wakishambuliana, na walikuwa wanakufa. Aisha akiwa amekaa kwenye machela yake juu ya ngamia huyo, alikuwa aki-wasisitiza wapiganaji wake kumlinda yeye, na kushambulia na kumuua adui ambaye alimuua khalifa wao Uthman, asiyekuwa na hatia. Kila mara waliposikia sauti yake, wali-pata moyo wa kufanya juhudi kubwa zaidi. Walikuwa wakirusha dhoruba mbaya kwa maadui sio tu kwa ajili ya kumlinda Umm-ul-muminin bali pia kulipiza kisasi kwa kifo cha Uthman.

Malik alikuwa bado akiendelea na kamchezo kake ka kukata mikono ya wale watu wote walioshikilia hatamu za ngamia wa Aisha. Wakati huu akamuona Abdallah ibn Zubeir, yule mshari wa jeshi la Makka, na kipenzi cha Aisha, akiupunga upanga wake. Alikuwa ndio "chanzo cha nguvu" cha vita vya Basra ambamo maelfu ya Waislam waliuawa. Kama isingekuwa uchochezi wake, vita vya Basra visingepiganwa kamwe.

Malik akasahau ngamia wa Aisha, na akamrukia kwa ukali kabisa Abdallah ibn Zubeir, akamuangusha chini ardhini. Alipokuwa anamnyooshea upanga kwenye shingo yake, kilio cha uchungu kilimtoka Aisha ambaye alidhania kwamba Malik atamuua mpwa wake. Kwa hofu kubwa, alipiga mayowe: "Oh muokoeni Abdallah ama sivyo Malik atamuua."

Lakini ni nani ambaye alikuweko kwenye jeshi la waasi ambaye angeweza kumuokoa mpwawe Aisha kutoka kwa Malik? Kila aliyefika karibu ili kumuokoa, aliuawa yeye mwenyewe. Alipousikia ukulele wa Aisha wenye uchungu, alimwambia Abdallah: "Ninashawishika kukumaliza kwa upanga wangu lakini nakuachia maisha yako kwa sababu ya udugu wako na Mtume wa Allah swt."

558

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Malik aliyastahi maisha ya Abdallah zaidi kwa dharau kuliko kwa huruma. Abdallah akasi-mama kutoka kwenye mavumbi, na kama alivyokuwa ametishiwa na kukoswakoswa huku na kifo, upesi sana akajiweka mbali na upeo wa upanga wa Malik, kwa nia ya kutokuka-matwa na yeye tena.

Malik akarudi kwenye mchezo wa kukata mikono ya waasi. Lakini hawakuvunjwa moyo na hofu ya kupoteza mikono yao kwake. Aisha alikuwa akiwahimiza kwa vile alivyokuwa akiendelea kupiga makelele: "Mbarikiwe, wanangu! Ni fahari kwenu kwa kumlinda mama yenu kijasiri namna hiyo."

Hatimaye Malik akachoka kukata mikono ya watu, na akaamua kuumaliza mchezo huo ambao umedumu kwa muda mrefu sana. Alikita miguu yake kwenye miili ya wale maiti, akalenga pigo la upanga wake usiokwepeka, na akamuua ngamia wa Aisha.

Ngamia huyo alianguka akiwa amechafuliwa kila upande na damu yake, na machela ya Aisha ikaanguka chini pamoja na ngamia huyo. Lakini Aisha hakuumia. Ali upesi sana akamtuma kaka yake Aisha, Muhammad ibn Abu Bakr, na Amar ibn Yasir, kwenda kuwe-ka ile machela chini, na akamwambia amsindikize dada yake kwenda kwenye nyumba ya mjane wa muungwana mmoja wa Basra.

Ngamia wa Aisha alikuwa ndio nembo ya kuonekana wazi ambayo kwayo jeshi la Basra lilikuwa likipigania. Pale alipouawa, ile "nembo" ikatoweka. Ghafla lile jeshi la Basra likawa halina chochote cha kupigania, na likaanza kuvujika - wazi wazi. Kila mmoja ndani yake akaanza kukimbilia kila upande. Katika kukimbia kwao, wapiganaji hao walimsahau hata Aisha ambaye walikuwa wakipigana kwa ajili yake kwa ujasiri kabisa muda mchache tu hapo nyuma. Mara kukawa hakuna kilichobakia katika medani ya vita isipokuwa maiti na majeruhi. Kwa vile Ali alilikataza jeshi lake kuwafukuza watoro, wengi wa waasi wali-weza kutoroka, na vita ikawa imekwisha kabisa.

Ali alitangaza tena yale maagizo aliyokuwa ameyatoa kabla ya vita kwamba wale waliok-ufa wasiibiwe au kukatwakatwa; kambi ya adui isiporwe; na wale wapiganaji waliosalimu amri wasiuawe. Alishikilia kwamba jeshi lake yeye mwenyewe lazima lionyesha mfano wa uungwana, uvumilivu, staha na uaminifu kama maadili ya msingi yanayojenga mfumo wa kijeshi wa Kiislam halisi.

Sir John Glubb:

"Vita vya Ngamia vilipiganwa mnamo Desemba mwaka 656. Mara tu baada ya adui kujitoa, Ali alitoa maagizo kwamba kusiwe na ufukuziaji na kwamba mauaji yakome mara moja.

559

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wakati Ali alipoingia Basra, alifanya jitihada ya kusuluhisha pande zote. Lile jeshi lililoshindwa lilitendewa ustahimilivu. Ali alisisitiza kwamba yaliyopita yawe yamepita, kwani alikuwa wa hulka ya upole na ustahimilivu, pengine ya ukimya tu na alitaka kuiunganisha himaya kuliko kulipiza kisasi yeye mwenyewe juu ya maadui zake."

(The Great Arab Conquests, uk. 322, 1963)

Ali alikuwa mstahimilivu, na alitaka kuiunganisha himaya na umma (watu) wa bwana wake, Muhammad (s.a.w.w.); lakini hakuwa "mkimya" kama Sir John Glubb anavyodha-nia. Sababu ya kutowaadhibu waasi ni kwamba alikuwa anachukia umwagaji damu kwa jumla, na hasa ule wa ndani ya Waislam.

Aliepuka pia kuuangamiza ule mji wa maasi wa Basra kwa sababu hiyo hiyo, yaani, imani yake juu ya utukufu wa damu ya Waislam. Kwa bahati, hakuna mtu mwingine miongoni mwa watu wa wakati ule aliyeshirikiana naye katika imani hii. Hawakuchukizwa kama yeye kuhusu kumwaga damu ya Waislam; waliimwaga, na kwa mbubujiko mwingi.

Aisha alimtetea kwa Ali mpwa wake na mwanawe wa kupanga, Abdallah ibn Zubeir, na akamuomba amsamehe. Ali akasema: "Msamaha kwa Abdallah bin Zubeir peke yake? Msamaha upo kwa kila mtu."

Ali alimuachia, sio tu Abdallah ibn Zubeir bali pia maadui wa kupita kiasi kama vile Marwan bin al-Hakam, Walid bin Aqaba, Abdallah bin Aamir, na Bani Umayya wote.

Hakuna popote katika historia ya ulimwengu ambapo mshindi amewatendea maadui zake aliowashinda kwa ustahimilivu kama Ali, kabla au tangu hapo. Katika kutoa msamaha kwa waasi, alikuwa, kwa mara nyingine tena, akimuiga rafiki na bwana wake wa zamani, Muhammad, Mtume wa Allah aliyebarikiwa, ambaye pia aliwasamehe washirikina wa Makka, miongoni mwao wakiwemo maadui zake wabaya, wakati alipouteka mji ule. Ali alifuata nyayo za Muhammad (s.a.w.w.), na aliishi katika kuiga maisha yake matakatifu.

Siku chache baadae, Aisha alikuwa tayari kusafiri. Kutokana na maombi yake, Ali alimpeleka Makka. Kaka yake, Muhammad, alikwenda pamoja naye. Huko Makka, alifanya Umra, na kisha akaenda Madina.

Aisha anayo sifa ya kuwa mwenye ujuzi sana katika masuala ya dini, na alikuwa pia ni muhadittha, yaani msimuliaji wa Hadith za Mtume (s.a.w.w.). Akiwa na elimu kiasi hicho, hivi inawezekana kwamba alikuwa hajui kuwa yeye hakuwa na haki ya kulipiza kisasi kwa ajili ya damu ya Uthman? Kulipiza kisasi ni kazi ya upande uliokosewa, na kutoa adhabu kwa mhalifu/wahalifu ni wajibu wa serikali. Aisha hakuwa ama na udugu na Uthman kwa namna yoyote ile wala yeye hakuwa mwakilishi wa serikali ya Waislam. Lakini hata hivyo

560

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

aliipinga serikali halali kwa kisingizio cha kisasi, na akalazimisha idadi kubwa ya Waislam katika mlipuko wa vita. Shauku yake ya vita iliwafanya maelfu ya watoto kuwa mayatima, na maelfu ya wanawake kuwa wajane.

Mwanamke fulani, aitwaye Umm Aufa al-Abdiyya, wakati mmoja alimuuliza Aisha: "Ewe Ummul-muminin, nini maoni yako juu ya mwanamke anayemuua mwanawe mwenyewe?" Aisha akasema kwamba mwanamke kama huyo atatupwa kwenye moto wa jahannam. Umm Aufa akaendelea kuuliza: "Litamfika lipi mwanamke aliyeua zaidi ya watoto 20,000 wake mwenyewe katika wakati mmoja na mahali pamoja?" Aisha alikasirishwa na kijem-be hicho, na akamkemea Umm Aufa atoweke. (Iqd-ul-Farid, juz. 111, uk. 108).

Watu wengine wa familia yake Aisha mwenyewe walitamani Aisha asingeongoza majeshi na kupigana vita. Safari moja, alituma mtumishi kwa mpwa wake, Ibn Abil-Atiiq, akimuomba ampelekee yeye Aisha farasi wake ili ampande. Wakati mpwa wake alipom-pokea yule mtumishi, alimwambia mtumishi huyo:

"Mwambie Ummul-muminin kwamba Wallahi, hatujaosha bado yale madoa ya damu iliyomwagika katika vita vya ngamia. Je, anataka aanzishe vita vya farasi sasa?"

(Baladhuri katika Ansab al-Ashraf, juz.1, uk. 431)

Kauli ya Ibn Abil Atiiq ilisababishwa na utani. Lakini mnamo mwaka 669 siku ilifika hasa ambapo Aisha alipanda farasi katika "mapambano" mengine. Wakati jeneza la Imam Hasan (a.s.) lilipoletwa kwenye kaburi la babu yake, Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), kwa ajili ya mazishi, Marwan ibn al-Hakam na watu wengine wa Bani Umayya walitokea kwenye tukio hilo, katika mavazi ya kivita. Walikwenda kuwazuia Bani Hashim kumzika Imam Hasan kando ya babu yake. Bani Umayya hao hawakuwa wenyewe tu; Aisha, Ummul-muminin, alikuja nao, akiwa amepanda juu ya farasi!

Aisha atakuwa ameshindwa katika vita vya Basra lakini "alishinda" yale "mapambano" ya Madina. Hasan hakuweza kuzikwa pamoja na babu yake kwa sababu ya upinzani wake yeye na Bani Umayya, na akazikwa kwenye uwanja wa makaburi wa Jannat-ul-Baqi.

Hakuna njia ya kutumia busara katika majukumu ambayo Aisha, Talha na Zubeir waliy-achukua baada ya kifo cha Uthman. Ule ukweli kwamba walikuwa watu maarufu katika historia ya Waislam, haubadilishi au kuathiri yale majukumu waliyochukua. Kosa haliwi na shutuma nyepesi eti kwa sababu limetendwa na mtu maarufu. Kosa ni kosa tu bila kujali ni nani aliyelitenda.

Wake za Mtume walikuwa wakitegemewa hasa kuwa waangalifu katika kila kitu wali-chokisema au kukifanya. Hata hivyo, walitakiwa wawe mifano mbele ya umma namna ya

561

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mwenendo na adabu. Kupotoka kutoka kwenye ubora kunaweza kupuuzwa katika wake za watu wa kawaida lakini sio kwao wao. Ikiwahutubia wao, Qur'an inasema: "Enyi wake wa Mtume! Atakayefanya maovu dhahiri miongoni mwenu, atazidishiwa adhabu mara mbili. Na hayo ni rahisi kwa Mwenyezi Mungu." (Al-Ahzab, 33:30)

Wanahistoria wengine wamejaribu kupunguza nguvu ya kiwewe cha matukio haya kwa kizazi kijacho, kwa kudai kwamba vitendo vya wale "Masahaba wa vita vya Ngamia" vilikuwa ni "makosa ya maamuzi" madogodogo tu. Makumi ya maelfu ya Waislam walik-ufa katika vita vya Basra bila ya sababu yoyote mbali na makosa madogodogo ya maamuzi kwa upande wa "Masahaba wa Jamal!"

Marerejeo yalikwishafanywa kwenye mlango wa huko nyuma, kwa "Abdallah ibn Saba" wa miujiza na wa kubuniwa, ambaye alikuwa, kwa mujibu wa wanahistoria wengi wa Sunni, ndiye "kichocheo" halisi katika kuuawa kwa Uthman. Wanahistoria hao hao waliona ni lazima kueleza matukio mengine yanayotatanisha na yenye wasiwasi kwa "kumrejeleza" yeye. Huenda huu ndio mfano uliopo hadi sasa wa mapema sana katika historia ya urejelezaji.

Kwa mujibu wa wanahistoria hawa, Abdallah bin Saba na wafuasi wake waliiona amani kama adui yao asiyeshindika. Walisadiki kabisa kwamba kama mazungumzo ya Ali juu ya amani yatafanikiwa, basi wao watakuwa ndio maiti wake wa kwanza. Kwa hiyo, dhamana pekee waliyoweza kuona kwa ajili ya usalama wao, ilikuwa ni kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe ya Waislam.

Ilikuwa ni pamoja na ufahamu huo, wanavyosema wanahistoria wa Sunni, ambapo Abdallah bin Saba na kundi lake, wakashambulia wakati wa usiku, yale majeshi mawili, kwa wakati mmoja kwa mpigo. Katika giza, pande zote zisingeweza kuwaona au kuwatambua wakala halisi wa uchochezi, na kila upande uliridhika kwamba upande mwingine ndio ulioanza vita hivyo.

Ubuniwaji wa Abdallah ibn Saba ulilazimishwa na haja ya uwazaji yakinifu kwa ajili ya geresha ya dondoo zinazosumbua katika historia. Ni ubunifu wa kistadi kweli hasa lakini kwa bahati mbaya kwa wagereshaji wa historia, na kwa wale watetezi wa wale "Masahaba wa Jamal," Abdallah ibn Saba hayajibu maswali yote juu ya tabia zao. Kwa mfano, je, hivi alikuwa ni Abdallah ibn Saba ambaye alivunja makubaliano ya kusitisha mapigano na Uthman ibn Hunaif, na ambaye alishambulia Basra wakati wa usiku, akaiteka, akaikama-ta hazina ya mji huo, na akawauwa Waislam zaidi ya 600 katika mji huo? Na je, alikuwa ni Abdallah ibn Saba ambaye alitishia kumuua Uthman ibn Hunaif, akamfanyia ukatili, akamtoa kwenye nyumba yake na akamhamisha kutoka Basra?

Na inakuwaje kwamba wakati Ali alipomtuma Abdallah ibn Muslim pamoja na nakala ya Qur'an Tukufu kwenda kuwaonya wale waasi kwamba watastahili ghadhabu ya Allah swt.

562

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ikiwa watachagua vita kuliko amani, wakakipiga mishale kile Kitabu, na wakamuua yeye (Abdallah ibn Muslim, yule mbebaji wa Qur'an)? Hivi alikuwa ni Abdallah ibn Saba ndiye aliyemuua huyu?

Na alikuwa ni nani ambaye alikuwa anachukua mazoezi ya kurusha mishale kwenye jeshi la Ali? Wapiga mishale katika jeshi la waasi walikuwa wamewaua zaidi ya vijana ishirini kabla yeye hajawaruhusu kupigana. Hivi wapiga mishale hawa walikuwa wakiwaua wapi-ganaji wa Ali bila ya kujua Aisha, Talha na Zubeir? Kama walijua, je, "watawala watatu" hawa walifanya chochote kuwazuia?

Aisha aliishi kwa miaka mingi baada ya vita ya Basra lakini hakumtaja kamwe Abdallah ibn Saba na jukumu lake la kama mchochezi wa vita. Yeye mara kwa mara alikuwa akise-ma kwamba alitamani kama angekuwa amekufa zamani kabla ya vita vile ambamo ndani yake maelfu mengi ya Waislam waliuawa. Kama Abdallah ibn Saba angekuwa ni mtu aliyeko kwenye historia, yeye Aisha angemlaani kwa ule umwagaji damu katika vita vya Basra. Abdallah ibn Saba alibuniwa muda mrefu sana baada ya vita vya Basra, na kifo cha Aisha.

Kama Abdallah ibn Saba angekuwa ni mtu hasa katika historia, angeweza kuwa katikati kabisa ya matukio na habari za nyakati hizo, baada ya kufanya jukumu "maarufu" kama hilo katika historia ya mwanzoni ya Uislam. Je, hakuwepo kwenye vita vya Siffin na Nahrwan? Hakuchochea yeye vita hivyo viwili pia baada ya kuwa alipata mafanikio kiasi hicho huko Basra? Na je, Mu'awiyah na Ma-Khariji pia hawakuwa waathirika wa njama zake? Ni nini hasa kilitokea, kama ni ubaya, kwa mtu mashuhuri katika historia ya Waislam kama huyu?

Abdallah ibn Saba alikuwa mtu wa usanisi na wa kusudi maalum. Alitengenezwa maalum na wapenzi na washabiki wa watu fulani maarufu katika historia ya mwanzoni mwa Waislam. Nia yao ilikuwa ni kulinda heshima, na pia, kama ikiwezekana, kuficha utambu-lisho wa watu hawa. Watu hawa walikuwa kwa kweli wanahusika, kwanza na mauaji ya Uthman, khalifa wa tatu, na tena, kwa kuzuka kwa Vita vya Pili vya Wenyewe kwa wenyewe katika Uislam - vita vya Basra au vita vya Ngamia. Walitegemea kwamba heshima ya watu hao wanaohusika itakuwa swalama kwenye maamuzi ya historia kama wangeweza kulazimisha kukubalika kwa lawama ya matukio haya juu ya Abdallah ibn Saba.

Abdallah ibn Saba, inavyoelekea, alikuwa mtu mashuhuri sana katika historia ya Waislam. Alifanikiwa, kwanza, katika kuwaburuza kwenda Basra, viongozi wasiotaka kama vile Aisha, na majenerali "wapenda amani" kama vile Talha na Zubeir, Abdallah ibn Zubeir, na Marwan, na jeshi lao lote, njia nzima kuvuka jangwa kubwa la Arabia, na kisha, katika kuwachombeza wao kuanza mashambulizi juu ya jeshi la Ali. Waislam hawakuwa na shauku tu ya kumtii yeye; walikuwa pia na shauku ya kufa kwa ajili yake, na wengi walik-

563

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ufa, katika vita vya Basra. Lazima atakuwa alikuwa ni mtu mwenye haiba kubwa. Mtu hawezi kuacha kupenda ujasiri wake na nguvu zake za kushangaza.

Lakini licha ya haiba yake yote, na uwezo na umahiri wake, Abdallah ibn Saba anaonekana alikuwa ni mtu mwenye haya. Hii inathibitishwa na ule ukweli kwamba alikuwa na "mzio" wa kutangazwa. Mara tu baada ya ile vita ya Basra, alitumbukia kwenye giza, na haku-tokeza tena kamwe. Labda alikufa akiwa amesahaulika na bila kuombolezwa. Inawezekana vile vile kwamba wale "wakunga" waliokuwepo wakati wa kuzaliwa kwake, walikuwepo pia kwenye "mazishi" yake, na walikuwa wakidhania kwamba kazi yake ilikuwa imekamilika, na kwamba wangeweza kumzika, wasije kumfukua tena kamwe.

Vita vya Basra au vita vya Ngamia ni mmoja wa misiba mikubwa sana katika historia ya Uislam. Ilipiga pigo la mwisho kwenye umoja wa umma wa Waislam, na Uislam kamwe haukupona kutokana na kiwewe chake. Wanahistoria wengi wa Kiislam wanasimulia kisa cha vita vya Basra lakini wakati wakifanya hivyo wanajaribu kupunguza makali (kwa kutosisitiza) ya baadhi ya mambo muhimu, na wanajaribu kumbabaisha msomaji. Sababu yao ya kufanya hivyo ni kwamba wale viongozi wa maasi katika vita vya Basra walikuwa ni "masahaba" wa Mtume (s.a.w.w.), na kwa hiyo, ni lazima watolewe kwenye hatia yoy-ote ile au uhalifu. Hata hivyo, "hadhi yao maalum," wanasema, inawapa haki ya kutende-wa hivyo.

Lakini uaminifu wa mwanahistoria lazima uwe kwenye ukweli, na sio kwa watu, hata kama ni "Masahaba" wa Mtume. Kazi ya mwanahistoria ni kuelezea mambo. Anaweza akayachanganua mambo, akayatafsiri, na akatoa majumuisho yanayohitimishwa kwayo lakini ni lazima asiyachezee. Lazima amuwezeshe msomaji kujiamulia mwenyewe sifa za sahaba wa Mtume kwa msingi wa "ushahidi wa nyendo" zake badala ya kujaribu kuweka pazia la maneno ya ujanja ili kuficha madutu kwenye uso wake. Kushindwa kwa mwanahistoria kufanya hivi kuna maana kwamba anaficha Ukweli, kitu ambacho ni sawa na kutangaza Uwongo!

Kama vita vya Basra visingepiganwa, basi vita vya Siffin na Nahrwan pia visingepiganwa. Mbegu za mfarakano katika Uislam zilipandwa na zikachipua katika vita vya Basra. Kama Aisha, Talha na Zubeir wasingepinga utawala halali wa Waislam, milango ya utengano katika Uislam isingefunguliwa kamwe.

Viongozi wa maasi walikuwa watendaji huria. Uchaguzi wao ulipatikana kutokana na mchanganyiko wao binafsi wa tamaa, chuki, hatia na kijicho. Haikuwa ni uadilifu uliowa-chochea wao bali ni maudhi, maslahi binafsi na uchu wa madaraka vilivyojionyesha kama uungwana. Ushari wao ulidhihirika kuwa na matokeo ya kinyume sio tu kwa Waislam bali pia kwa wao wenyewe.

564

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hivi wanahistoria wa Kiislam walisita na kutafakari ni nini kingeweza kutokea kama hawa "watawala watatu" wa Basra wangekuwa washindi katika vita vyao dhidi ya Ali? Mambo mawili yangeweza kutokea katika tukio la kushinda kwao, yaani, (1) kwa kuchemkwa na hasira kama walivyokuwa, wangeweza kufanya hapo Basra katika mwaka 656 A.D. kile ambacho Yazid mtoto wa Mu'awiyah alikifanya katika mwaka wa 680 A.D. huko Karbala, yaani, wangewaua ovyo watu wote wa familia ya Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt.; na (2) baada ya ushindi wao dhidi ya Ali, wangemkabili Mu'awiyah bin Abu Sufyan, gavana wa Syria, katika mfungamano mpya wa majeshi.

Katika mfungamano huu mpya, Aisha, Talha na Zubeir wangekuwa kwenye upande mmoja, na Mu'awiyah na Amr bin al-Al-Aas upande mwingine. Ulimwengu wa Kiislam ungegawanyika katika kambi mbili hizi hasimu, na katika mapambano yatakayofuata ya mamlaka ya jeshi moja juu ya jingine, pande mbili hizo zingeangamizana.

Lazima izingatiwe na msomaji kwamba hakuna mmoja kati ya wapinzani hawa katika hii nadharia mpya ya mlinganyo, ambaye alikuwa "amekwazwa" kama alivyokuwa Ali, na ubinadamu wake na kujizuia, na pia kwa chuki yake kubwa kwenye umwagaji wa damu. Kwa hiyo, vita kati yao ingekuwa ya kishenzi na kikatili sana, na isiyodhibitiwa na "vizuizi" vyovyote vile kwa ajili ya utukufu wa damu ya Waislam. Ulimwengu wa Waislam ungekuwa umefunikizwa kwenye damu ukiacha pengo kubwa la madaraka. Kwenye pengo hili angeingia mfalme wa Byzantium (Roma) na jeshi lake, na wangeizima nuru ya Uislam!

Hawa "watawala watatu" kwa makusudi na kwa kutojali, walichokoza vita ambavyo vingeweza kuongezeka na kuwa balaa kubwa kwa umma wa Waislam. Kutokana na balaa hili linalowezekana, ilikuwa ni ufundi, busara, ubinadamu na weledi wa Ali katika utawala ambao uliokoa umma wa Muhammad. Mwenyezi Mungu amrehemu yeye na watu wengine wote wa Ahlul-Bayt Muhammad (s.a.w.w).

Inadaiwa pia na wanahistoria wengine kwamba "Masahaba wa Jamal" waliyajutia yale waliyoyafanya, na walikuwa "wametubia" kwa unyofu kabisa; kwa hiyo, hawana hatia kabisa. Inawezekana kabisa kwamba wale Masahaba wa Jamal walihitaji utakasaji -utaratibu wa "kutubia" - kuwatakasa na hisia zao za hatia. Lakini hakuna ushahidi wa "kutubia" kwao ambao umetufikia sisi. Ali alikuwa ametoa ukombozi kwao, sio mara moja bali kwa kurudiarudia, na walikuwa wameukataa.

Kama Masahaba wa Jamal walitubia, basi ni juu ya Allah (swt) pekee kukubali kutubia kwao. Allah (swt.) ataikubali toba yao kama walikuwa waaminifu. Lakini kukubaliwa na Allah swt. kwa toba yao hakutajulikana kwetu sisi mpaka Siku ya Qiyammah. Kazi ya mwanahistoria, kama ilivyoelezwa mapema, ni kutenga tu Ukweli kutoka kwenye rundo la Uwongo ambamo utakuwa umefichwa humo, na kisha kuueleza, kwa uwazi na usahihi.

565

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Atatafsiri mambo lakini ni lazima asiyafiche au kuyazusha au kuyageuza kwa hofu yasi-jikuwa yanaonyesha picha isiyofaa ya watu anaowapendelea katika historia ya Uislam.

Baada ya vita hivyo, Ali aliwaswalia wafu wa majeshi yote mawili, na akawaagiza watu wake kuwazika maiti wote waliokuwa wamelala kwenye uwanja wa vita. Maagizo yake kwao yalikuwa ni kuonyesha heshima kwa wale Waislam waliokufa wakiwa ama ni marafiki au maadui. Ilikuwa ni pale tu maiti wote walipokuwa wamekwishazikwa, ambapo aliweza kurudisha akili yake kwenye masuala mengine.

Ali anaingia Basra

Mwanahistoria Mas'ud, "Herodotus wa Waarabu," (Herodotus ni jina la mwanahistoria wa kwanza huko Ugiriki aliyepewa cheo cha - Baba wa historia, hivyo Mas'ud ni baba wa historia wa Waarabu), ameongeza mwishoni mwa kitabu chake, The Golden Meadows, mukhtasari ufuatao wa mwenendo wa jeshi la Ali lilipokuwa linaingia Basra. Ni kiangazio pia juu ya mfumo wake wa kijeshi, na nafasi ya Ansari ndani yake.

Mtu mmoja maarufu wa Basra aliniambia kwamba wakati lile jeshi lenye ushindi lilipokuwa linakaribia kwenye lango kuu la mji, alipanda juu ya ngome za ulinzi ili alione, na hiki ndicho alichokiona:

Kulikuwa na vikosi vingi vya askari wa farasi na askari wa miguu katika jeshi la Madina ingawa jeshi lenyewe lilikuwa ni dogo mno. Akitembea mbele ya kikosi cha wapanda farasi, kile cha kwanza ambacho kiliingia Basra, alikuwa ni mpanda farasi mmoja mtu mzima. Upanga ulikuwa unaning'inia ubavuni mwake, na alikuwa ame-beba bendera ya kile kikosi alichokuwa anaongoza. Niliulizia kwa watu wa karibu yangu yeye alikuwa ni nani na wao wakaniambia alikuwa ni Abu Ayub Ansari, yule rafiki na wakati mmoja aliyekuwa mwenyeji huko Madina, wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt. Kikosi chake cha wapanda farasi 1,000 kiliundwa na wapiganaji wa Ansari.

Nyuma yao, alikuwepo mpanda farasi mwingine. Alikuwa amevaa kilemba cha man-jano iliyofifia na joho jeupe. Alikuwa amebeba upinde kwenye bega lake la kulia, na bendera ya kikosi chake kwenye mkono wake wa kushoto. Yeye pia alikuwa mbele ya wapanda farasi 1,000, na wao pia walikuwa Ansari. Yeye alikuwa, nilivyogundua, ni Khuzaima ibn Thabit Ansari.

Afisa wa tatu alikuwa amepanda farasi wa rangi ya hudhurungi mwenye nguvu sana. Alikuwa amevaa kilemba cheupe, akiwa ameshika upanga na upinde, na akiongoza kikosi cha wapanda farasi 1,000. Huyu alikuwa ni Abu Qatada ibn Rabi'i Ansari.

Afisa wa nne alikuwa amepanda farasi wa vita mzuri mweupe. Mavazi yake yalikuwa meupe na kilemba chake kilikuwa cheusi. Alionekana kuwa mtu wa hadhi kubwa na

566

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

maarufu, na alipandikiza heshima na unyenyekevu miongoni mwa waangaliaji wote. Alikuwa mzee sana lakini alikuwa na ukakamavu wa kijeshi. Alikuwa akisoma Qur'an huku akiwa amepanda farasi kuelekea mjini. Upanga ulining'inia ubavuni mwake, na upinde ukining'inia kutoka kwenye bega lake la kulia. Nyuma yake walikuwapo wapanda farasi 1,000. Walikuwa zaidi ni watu wazima, na wote walibe-ba mikuki mirefu mikononi mwao. Nilipouliza yule alikuwa ni nani, niliambiwa kwamba alikuwa ni Ammar ibn Yasir, rafiki na mpendwa wa Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) na Ali ibn Abi Talib. Wakifuata nyuma yake, walikuwa ni Muhajirina na Ansari wote, na wengi wao walikuwa ni askari wakongwe wa Badr.

Jicho langu lilikamatwa baadae na mtu mwenye umbile zuri sana. Alikuwa amepanda farasi jasiri mwenye rangi mchanganyiko. Vazi lake lilikuwa jeupe na kilemba chake kilikuwa ni cheusi. Huyu alikuwa ni Abdallah ibn Abbas, binamu wa kwanza wa Muhammad Mustafa na Ali ibn Abi Talib. Pamoja naye walikuwa ni kaka zake na wapwa zake.

Mpaka wakati huu, takriban jeshi lote la farasi lilikuwa limeingia Basra, na niliona kwamba vikosi viwili vya mwisho vilikuwa vinakaribia lango la jiji. Sasa, cha kwanza chao kilifika. Mbele yake alikuwepo mpanda farasi mwenye umbo imara. Alikuwa katika mavazi kamili ya kivita, na alitia hofu ndani ya nyoyo za wale wote waliomuona yeye. Alikuwa amebeba bendera nyeusi kwenye mkono wake wa kulia, na mkuki kwenye mkono wa kushoto. Alionekana kama ndiye mshika bendera wa hilo jeshi ama afisa mwingine wa ngazi ya juu. Dhana yangu ilikuwa kweli. Alikuwa ni Malik ibn Ashtar, Mnadhimu Mkuu wa jeshi la Madina, na mtumia upanga hodari ambaye Arabia imewahi kutoa kamwe. Hakuna mshindani ambaye alikabiliana naye, aliyemkwepa kamwe. Aliongoza wapiganaji elfu nne wa wote wapanda farasi na wale wa miguu.

Mtu wa mwisho kupita katika uchunguzi alikuwa ni mpanda farasi aliyekuwa mwenye kung'aa kama jua. Katika upande wake wa kulia na wa kushoto kulikuwa na vijana wawili, kila mmoja aking'aa kama mwezi kamili. Wote watatu walikuwa wamevaa mazazi meusi. Wale farasi wenye fahari na wanaorukaruka waliokuwa wamewapanda, walikuwa weusi pia. Kijana mwingine akiwa amebeba mkuki, alikuwa juu ya farasi mbele yao. Yule mtu aliyekuwa katikati, niligundua, alikuwa ndiye jemadari mkuu wa jeshi hili - Ali ibn Abi Talib. Wale vijana wawili upande wake wa kulia na kushoto, walikuwa wanawe, Hasan na Husein - matunda ya macho ya Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt. Yule kijana aliyekuwa mbele yao , alikuwa pia ni mwanawe, Muhammad ibn Hanafiyyah.

Nyuma yao, kulikuwa na vikundi kadhaa vyingine vya watu wenye silaha. Wao walikuwa wakileta ulinzi wa nyuma ya jeshi hilo. Miongoni mwao walikuwemo watoto wa Jaafar Tayyar, watoto wa Aqiil ibn Abi Talib, na vijana wengine wa Bani Hashim. Walikuwa ndiyo wapanda farasi wa mwisho kuingia Basra.

567

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali alishuka kutoka kwenye farasi wake pale kwenye lango la Msikiti Mkuu wa Basra. Aliingia ndani ya Msikiti huo, akaswali, na akamshukuru Allah swt., kwa Neema Zake, na kwa zawadi ya ushindi. Raia wa Basra walikuwa wamejikusanya kwenye uwanja wa Msikiti wakisubiri kuwasili kwa Ali. Sasa alitoka mle Msikitini ili kuwahutubia. Aliwalaumu kwa tabia yao ya kutojali, wakati wote wa mapambano, na akawaambia:

"Mlikuwa wafuasi wa mnyama. Aliponguruma mlimtii; pale alipouawa, wote mlikimbia, na mkatawanyika."

Kisha Ali akachukua kiapo cha utii kutoka kwa raia wa Basra. Aliwashauri kumtii Allah na Mtume Wake wakati wote, na kamwe wasiwe tena kama kondoo wenye bumbuazi.

Kutoka pale Msikitini, Ali alikwenda kwenye hazina. Hazina hiyo ilikuwa imeporwa. Aliamuru mali yote iliyokuwa imeibiwa irudishwe kwenye hazina mara moja. Alipoitembelea hazina hiyo kwa mara ya pili baadae kidogo, aliona vipande vya dhahabu na fedha vimelundikwa rundo hapo chini. Alivitazama vilima hivi vidogo vya dhahabu na fedha, na akasema: "Jaribuni kumshawishi mtu mwingine." Kisha yeye akamuagiza yule mtunza hazina kugawanya kila kitu kwenye vile vikosi. Mtunza hazina aligawa kila kitu, na hakuna kilichobakia kwenye hazina hiyo.

Kwa sababu fulani za kisirisiri, Ali na Maansari walikuwa wanaelewana tangu mwanzo. Na kwa sababu za kisiri kama hizo tu, Ansari hawakuweza kuelewana na Makuraish. Kulikuwa na uchangamfu kidogo sana, kama ulikuwepo kamwe, kati ya Makuraish na Ansari. Haikuwa mpaka Ali alipokuja kuwa khalifa ambapo Ansari waliweza, kwa mara ya kwanza tangu kifo cha rafiki yao, Muhammad (s.a.w.w.), kuwa na nafasi ya maana katika serikali ya Waislam. Ali aliwateua kwenye vyeo vya juu kabisa ndani ya dola - vyote kama majemadari katika jeshi na kama magavana katika majimbo. Katika nyanja zote, Ansari walijidhihirisha wenyewe kwa uwezo wao na uadilifu wao.

Ali alifuta ile sifa ya "kijimbo" ya ukhalifa kwa "kuondoa Uquraishi" katika utawala wakati aliporudisha haki za Ansari kwao. Katika serikali yake, mtu hakuwa awe Quraish Iili kupanda katika cheo cha juu. Mtu yeyote - ama alikuwa Quraishi au la - aliweza kupanda kwenye cheo cha juu wakati wa ukhalifa wa Ali, kama angeweza kuwasilisha "vitambulisho" viwili - sifa na uwezo.

568

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kubadilisha Makao Makuu kutoka Madina kwenda Kufa

Mnamo Rajab ya mwaka 36 h.a. (january 657) Ali aliamua kuhamisha makao makuu ya serikali yake kutoka Madina huko Hijazi kwenda al-Kufa huko Iraq. Wakati amani na utulivu vilipokuwa vimerudishwa hapo Basra, alimteua Abdallah ibn Abbas kama gavana wake mpya, na kisha akaondoka kuelekea Kufa ambayo ilikuwa kuanzia hapo, ndio makao makuu ya Uislam.

Mnamo mwezi 12 Rajab mwaka 36 H.A., Ali aliwasili katika milango ya Kufa. Waungwana mashuhuri wa mji huo wakatoka kuja kumlaki na kumpongeza kwa ushindi wake. Akiingia mjini hapo, Ali kwanza alikwenda kwenye Msikiti Mkuu, akaswali Swala ya shukrani kwa Allah swt. kwa ushindi huo, na kisha akatoa hotuba ambayo ndani yake aliwashukuru watu wa Kufa kwa kumuunga mkono kwao, na akawasifu kwa utendaji wao kwa kijasiri katika vita vya Basra.

Waungwana wa mji wa Basra walimuomba Ali akae kwenye kasri ya gavana lakini yeye hakukubali. Badala yake, akachagua nyumba ya hali ya kawaida kwa ajili ya makazi yake.

Wanahistoria wamejaribu kutafuta sababu za kwa nini Ali alibadilisha makao makuu kutoka Madina kwenda Kufa. Maprofesa Sayed Abdul Qadir na Muhammad Shuja-ud-Din wanaandika katika kitabu chao, The History of Islam, (historia ya Uislam, kilichochapish-wa Lahore, Pakistan):

"Miezi saba baada ya kuchukua madaraka ya serikali, Ali aliifanya Kufa kuwa makao makuu yake mapya. Zifuatazo zilikuwa ni baadhi ya sababu zilizochochea mabadiliko haya:

1.    Vile vita vya Basra au vita vya Ngamia vilipiganwa na kushinda kwa msaada wa watu wa Kufa. Ali alifanya Kufa kuwa makao yake, kiasi fulani kwa kutambua utumishi wao huu.

2.    Ali alikuwa na shauku ya kuiokoa Madina kutokana na maafa ya ugomvi wa wenyewe kwa wenyewe kama ule ulioishia kwa kuuawa kwa Uthman. Yeye hakupenda Madina kugeuka eneo la matukio ya machafuko ya kisiasa kwa wakati wowote, na alitaka kuuokoa mji wa Mtume kutokana na kuharibiwa au kunajisiwa katika vita vinavyowezekana hapo baadae.

3.   Kufa ilikuwa kwenye nafasi ya katikati zaidi katika dola hiyo. Urahisi wa

569

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kiutawala wa maeneo hayo makubwa na yanayosambaa ulihitajia mabadiliko haya.

4. Ilikuwa ni rahisi kwa Ali kufuatilia nyendo za Mu'awiyah kutoka Kufa kuliko kutoka Madina."

(The History of Islam)

Kh. Muhammad Latif Ansari wa Pakistani, mwanahistoria wa siku hizi, ameonyesha katika kitabu chake, History of Islam, kwamba kama vile tu Abu Jahl na Abu Sufyan walivy-ohusika na kuhama kwa Muhammad kutoka Makka kwenda Madina, ndivyo mwanawe, Mu'awiyah, alivyohusika na kuhama kwa Ali kutoka Madina kwenda Kufa. Yeye anasema kwamba vita vya wenyewe kwa wenyewe vilikuwa vimekwishaanza lakini maeneo ya mapigano yalikuwa mbali sana kutoka Madina. Ali, kwa hiyo, alibadili makao hayo kwa sababu za mkakati, na hii inaunga mkono madai yake kwamba ilikuwa ni uasi wa Mu'awiyah, gavana wa Syria, uliohusika na uhamaji wake (Ali) kutoka Hijazi kwenda Iraq.

Kwa kweli, zilikuwepo sababu yakinifu na za udhanifu kwa nini Ali alibadilisha makao makuu. Baadhi ya hizo ni hizi:

(1). Wakati Ali aliposhika kiti cha ukhalifa, vituo muhimu vya mijini vya dola hiyo vilikuwa ni Damascus huko Syria, Makka na Madina huko Hijazi, na Basra na Kufa huko Iraq.

Damascus ilikuwa imeshikiliwa na Mu'awiyah, na ilikuwa, kwa hiyo, kitovu cha upinzani kwa Ali. Kati ya hiyo miji mingine minne, Makka, mwanzoni, ilikuwa mikononi mwa viongozi wa maasi - Aisha, Talha na Zubeir. Wakiwa Makka, walianzisha jeshi la watu wa kujitolea lenye wapiganaji 3,000. Waliondoka Makka pamoja na jeshi lao kuelekea Basra, na wakaukalia mji huo. Wengi wa wale watu wa Makka ambao hawakwenda Basra pamoja na jeshi hilo la waasi, walilipatia msaada wao wa nyenzo. Kwa sababu hiyo Ali akaiondoa Makka.

Madina ilikuwa na sifa ambayo sio nzuri hata kidogo. Kama ilivyoelezwa kabla, wakati Uthman alipouawa, Madina ilikuwa chini ya miguu ya waasi. Muhajirina na Ansari walitambua kwamba hapakuwa na mtu katika Dola ya Kiislam wa kuweza kuuokoa mji huo kutokana na kuporwa, watu kutokana na kuangamizwa, na serikali kutokana na kuanguka, isipokuwa Ali. Wao kwa hiyo, walimsihi kuchukua mamlaka ya serikali.

Ali aliwaambia Muhajirina na Ansari kwamba atalikubali pendekezo lao endapo watampa kiapo cha kutii amri zake mwote katika amani na katika vita. Walimpa kiapo

570

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

chao cha kumtii yeye, na akalikubali pendekezo lao.

Lakini ni siku chache tu zilikuwa zimepita wakati uasi ulipoibua kichwa chake huko Makka dhidi ya mamlaka ya makao makuu. Ali aliingia Msikitini, na kuwataka Muhajirin na Ansari kusimama katika kuilinda serikali kuu. Jibu lao pekee lilikuwa ni ukimya. Ali akawakumbusha kile kiapo ambacho walikuwa wamempa cha kumtii yeye na bado tu hawakuvutika. Kuwasihi kwake kote na makumbusho yote yalielekea kuan-gukia kwenye masikio ya uziwi.

Ilikuwa ni baada ya majuma mengi ya makumbusho na juhudi kubwa ndipo Ali akaweza kuorodhesha msaada wa watu mia saba waliojitolea hapo Madina. Hiki ndio kiasi Madina ilichoweza kumfanyia. Aliondoka Madina na watu hawa waliojitolea -na asirudi tena.

Basra, mji wa nne, ulikuwa umekubali mamlaka ya Ali, na yeye alikuwa amemteua Uthman ibn Hunaif Ansari kuwa gavana wake mpya. Lakini kabla ya Ali kuwasili Iraq, ule "utawala wa watu watatu" wa Aisha, Talha na Zubeir ulikuwa tayari umekwishaite-ka Basra. Uthman ibn Hunaif kwa shida tu aliweza kutoroka kutoka Basra akiwa hai.

Sasa "chaguo" la Ali lilipunguzwa na kuwa la mji mmoja tu - Kufa. Ali alimtuma Imam Hasan na Ammar ibn Yasir kwenda Kufa kumletea msaada wa kumuongezea yeye nguvu. Kufa ilituma wapiganaji 12,000 kwenda Basra, na walikuwa ni wapiganaji hawa ambao waliopigana katika vita vya Ngamia, na wakaushinda ule "utawala wa watu watatu" wa Aisha, Talha na Zubeir.

Makka, Madina na Basra zimemuacha Ali bila kufahamu fika kuhusu kile ambacho wangeweza kufanya katika dharura. Lakini raia wa Kufa walikuwa wamemtumia msaada katika wakati muhimu sana katika muda wake. Aliweza kuona wazi kwamba kama kuna vita na Mu'awiyah, alikuwa na jeshi la Kufa tu la kutegemea. Ilikuwa, kwa hiyo, ndio mantiki ya matukio yaliyoshawishi uamuzi wa Ali wa kuifanya Kufa makao makuu ya dola.

Watu wa Madina, inavyoonekana, walikuwa na vuguvugu la upendeleo wa matukio yanayotokea karibu yao. Wakati Ali alipotangaza kwamba atayahamisha makao makuu ya serikali kwenda Kufa, hakuna mtu miongoni mwao aliyelalamika dhidi ya uamuzi huu. Hawakuonyesha hisia kwa mabadiliko ya maana kubwa kama haya kana kwamba wasingejali kama mji wao unakuwa makao makuu ya Uislam au la!

(2). Madina ndio chimbuko la utamaduni na ustaarabu wa Kiislam. Mfano halisi wa maisha ya Kiislam uliweza kuonekana katika hali yake bora hapo Madina tu. Vita na

571

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mapambano ya kigeni vilikuwa vimeleta watu wa tamaduni nyingi tofauti katika milki ya Kiislam. Kama Madina ingekuwa pia ibakie kama makao makuu ya kisiasa na kiutawala ya dola hiyo, kama ilivyokuwa makao ya kiroho, basi watu wageni, na tamaduni zao ngeni na asili zisizo za Kiislam, wangeweza kuja kuishi ndani yake. Wenyewe wangeleta maadili, mila, tabia, desturi na ufuasi wa dini zao pamoja nao. Kwa kufanya hivyo, wangeweza ama kuumiliki ule utamaduni halisi wa Kiislam au wangeupunguza nguvu. Kwa vyovyote vile, Uislam halisi ungewekwa wazi nyakati zote kwenye athari za kigeni.

Joel Carmichael:

"Uislam uligongana na dhana kubwa sana za kiweledi za Kikristo, zilizojaa fikra za Greece na Roma. Mawazo ya Kikristo yaliingiza sio tu dhana nzima ya Kiyunani, bali pia na mawazo ya kawaida huko Uajemi na kwingineko katika Mashariki kongwe. Kwa sababu hiyo namna mbalimbali za mila na mawazo, ugumu muhumu wa mawazo na desturi, wote takriban ukiwa umekwisha meng'enywa (kurahisishwa) na Ukristo, ulipandikizwa kwa jumla kwenye ulimwengu mpya wa Kiislam."

(The Shaping of the Arabs, New York, uk. 194, 1967)

Lakini Ali alihamisha kitovu cha kisiasa cha Kiislam kutoka Madina, na kwa hiyo akauokoa mtindo wa maisha wa Kiislam katika chimbuko lake hasa. Aliiokoa Makka na Madina kutokana na umililikiwaji wa kiutamaduni wa Wakristo, Wayahudi, Wagiriki, Warumi na Majusi. Alizidumisha sifa za miji hii miwili kama zilivyokuwa wakati wa Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt., mwenyewe.

(3). Katika masuala mengi, makao makuu ya taifa pia yanakuwa makao makuu ya tabia mbaya, madhambi, uhali fu na maovu mengine. Babylon, Roma ya zamani na Byzantium (Istanbul), miji mikuu ya madola makubwa, ilikuwa pia sehemu za starehe za nyakati zao. Wanaume na wanawake wa mataifa yaliyotekwa wanatembelea miji hii mikubwa ya kifalme, na wanakuja pamoja na tabia zao mbaya. Ukuaji usiodhibitiwa, kujazana, na kutokujulikana kwa kutandawaa kwa vituo vya miji mikubwa huzaa maovu ya kila aina. Miji mikuu mingi ya kisasa inastahili kuchukua nafasi ya pili kwa Babylon na Roma kongwe.

Madina ilikuwa ndio kiini cha mafundisho ya Qur'an, na pia ilikuwa na kaburi la Muhammad, Mtume wa Allah swt., ndani yake. Muhammad alikuwa ndiye mfasiri wa Ujumbe wa Mwisho wa Allah swt. kwa wanadamu, na kazi yake ilikuwa ni kuwalika wanadamu kuishi maisha safi, ya kiungwana na sahihi. Uislamu ulikuwa ndio mjenzi wa tabia, uwezo wa hali ya juu, na hapakuwa na mfano bora wa maisha sahihi na yaliy-otakaswa kuliko maisha ya Mletaji wake. Kama Madina ingekuwa kama miji mikuu mingine ya kifalme ya hapo nyuma, basi mwaliko wa Uislamu kwa wanadamu waliobakia

572

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ungekuwa ni uvyosi (dhihaka). Ali ali uokoa utukufu wa Madina, na maadili ya kijamii ya ratiba ya kitabligh ya Kiislamu kwa kutenganisha vituo vya kiroho (au kidini) na vituo vya kisiasa vya dola.

Ali kwa kweli alikuwa ni mtu wa kiubashiri katika mawazo yake. Aliiokoa Madina kutokana na kugeuka kuwa mfano halisi wa Damascus au Baghdad au Cordova. Maonyesho makubwa ya ustaarabu yaliendelea kwa kasi sana huko Syria yakiendelezwa na kuzidishwa na himaya iliyokuwa ikipanuka kwa kasi. Utajiri wa zile nchi zilizotekwa ulimiminikia Damascus (na baadae, huko Baghdad na miji mingine). Pamoja na utajiri, kilikuja kiambatani chake - anasa - na tamaa ya tabaka linalotawala kutaka kukuza na kulea "sanaa." Wasichana waimbaji na wachezaji walikuja kwenye vituo vya miji mikub-wa ya dola ya Waarabu kwa mmiminiko imara.

Wale wasomaji wanaotaka kuona mukhtasari wa tabia wa wakati wa ustawi wa himaya za Bani Umayya na Bani Abbas, wanaweza kufanya hivyo kwenye vitabu vingi sana, mion-goni mwavyo ni zile juzuu ishirini za Kitab al-Aghani cha Abul-Faraj Isfahani, au katika kitabu kingine kiitwacho The Ring of the Dove cha Imam Hazm wa Hispania, wote waki-wa vioo vya kuaminika vya nyakati zao.

A. J. Arberry:

"Dola hiyo iliendelea kuongezeka katika utajiri, jinsi biashara ilivyokwenda mbali zaidi; utajiri ulijikusanya mikononi mwa wale wachache walioushika, ambao walipenda utajiri ambao ungewashangaza wahenga wao wa Kibedui. Makasiri mazuri sana na yenye samani za kifahari - majumba yaliyopangwa yaliupamba mji mkuu Baghdad na vituo vya majimbo, Bokhara, Samarkand, Balkh, Shiraz, Damascus, Aleppo, Jerusalem, Cairo, Tripoli, Tunis, Fez, Palermo, Cordova. Maisha ya fahari na anasa (dolce vita) ya utawala wa makabaila mbaya unaopen-dezeshwa yanatoa taaswira kwa mng'aro kabisa, kama yalivyokuwa maisha huko Andalusia katika mkesha wa utekaji wa Uingereza wa Norman, katika The Ring of the Dove, kitabu cha muongozo chenye changamano sana juu ya mapenzi ya shu-jaa wa ukoo bora na mwanamke tajiri (aliyeolewa) kilichotungwa na mwanathe-ologia mashuhuri, Ibn Hazim. Wavulana watumwa na wasichana waimbaji, hudu-ma zinazofanya maisha kuwa bora ambazo zilikuwa hazijulikani kwa Waarabu wa kale, ziliwapatia wanaume wa Kiislamu starehe mpya na washairi wakawapatia msamiati mpya. Mvinyo ulikatazwa kwa Waumini na katazo la wazi la Kitabu Kitukufu; lakini watawala wa Kiislamu walijiingiza kikamilifu, na mamanju wao walishindana kutukuza sifa za pombe (binti zabibu).

(Aspects of Islamic Civilization, uk. 15, 1967)

Ni lazima isidhaniwe, hata hivyo, kwamba ni ile miji ya mbali tu kama vile Cordova na Baghdad iliyochafuliwa na tabia mbaya za anasa na utajiri. Makka na Madina zenyewe

573

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hazikuwa salama kutokana na vivutio vyao. Ella Marmura:

"Ushairi wa mada ya mapenzi ulipata ufafanuzi katika namna mbili tofauti. Moja ilikuwa ya kupendeza, yenye kufurahisha na ya kistaarabu, na hii ilimea katika miji ya Makka na Madina. Yote ilikuwa ni miji ya neema lakini iliyonyang'anywa mam-laka ya kisiasa. Wengi wa vijana makabaila wa Kiislamu ambao hawakuwa wamein-gizwa kwenye ofisi za umma, walifuja utajiri wao katika kutafuta starehe. Shule za uimbaji zilichipukia na kiasi cha ushairi wa hisia za mapenzi kilipangwa katika muzi-ki. Kiongozi wa shule hii ya ushairi alikuwa ni Umar ibn Abi Rabiah (kafa mwaka 720), kabaila wa Makka. Namna ya pili ya ghazal - ushawishi wa ngono kwa wanawake ilistawi zaidi miongoni mwa Mabedui, ikielezea nguvu ya hisia na iki-fafanua uchungu wote na kutokuwa na matumaini ya mapenzi ya kusikitisha.

("Arabic Literature: a Living Heritage, " iliyochapishwa katika kitabu, Introduction to Islamic Civilization, kilichohaririwa na R. M. Savory, New York, 1976)

Philip K. Hitti:

"Kusalimu amri kwa Makka kulimaanisha kukubali kwake Uislamu. Mmoja baada ya mmoja Makuraishi walihamia kwenye makao makuu mapya (Madina) kushiriki katika kuitangaza dini mpya na kuanza kazi mpya. Nafasi za juu kabisa ndani ya serikali na jeshi zilikuwa wazi kwa ajili yao. Makuraish wengi walishiriki katika mapambano ambayo katika kipindi cha imani halisi, hususan chini ya Umar ibn al-Khattab, yalis-ababisha kutekwa ile Ghuba yenye Rutuba, Uajemi na Misri. Baadae wengine wali-tumikia kama magavana wa majimbo katika milki iliyopatikana karibuni. Maisha hapo Makka kisha yakajengeka katika mikondo miwili tofauti, mmoja wa sham-rashamra na mwingine wa uchamungu.

Baada ya ushindi, ngawira, ushuru na kodi vilipata njia kwa wingi ndani ya mji; zikawa ni chanzo kipya cha mapato. Hii ilifidia sana hasara ya misafara ya biashara. Hijja, bila shaka, iliendelea; kwa kweli iliongezeka. Mwanzoni ikiwa kituo cha biashara, Makka sasa iligeuka kuwa kituo cha starehe. Watu wake waliopata utajiri hivi karibuni walileta wanawake maharimu wa Kiislamu, wacheza ngoma na waim-baji, wanaume kwa wanawake, na dhana mpya za ni nini kinachofanya maisha mazuri. Waliishi maisha ya kifahari katika majumba yenye mabustani na mazingira ambayo mfano wake, Makka haijawahi kamwe kuuona kabla ya hapo. (uk.21-22).

Wakati huohuo, maisha huko Madina, kama huko Makka, yalikuwa yanaendelea katika uelekeo tofauti, uelekeo wa hali ya kidunia. Hata hivyo, mtirirko wa dhahabu kuto-ka majimboni katika namna ya kodi ya kichwa na kodi ya ardhi ulimiminikia Madina

574

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwanza. Kiwango kilichokuwa kinafurika kwenye hazina ya umma kilikuwa kikub-wa mno. Katika kutafuta kuungwa mkono na lile tabaka jipya la wanaotafuta starehe, Madina ilikuwa, juu ya mpinzani wake kwa upande wa kusini, na manufaa ya mwinuko mkubwa (kutoka usawa wa bahari), ugavi wa maji mzuri zaidi, na bustani zenye maeneo makubwa zaidi. Viongozi wastaafu wa serikali, watumishi wa serikali na jeshi, walileta watumwa na hawara zao, waimbaji wao, wachezaji na wanamuziki, waume kwa wanawake - na kuanzisha hali ya mazingira ambayo haijawahi kuonekana hapo kabla ndani ya Mji Mtukufu huo. (uk.55)"

(Capital Cities of Arab Islam, 1973)

Hivyo ndivyo ilivyokuwa Madina hata baada ya hadhi yake ilipokuwa "imepunguzwa," na ikawa imefanywa kuwa mji wa jimbo. Lakini ikiwa kama ingebakia kuwa makao makuu ya kisiasa na kibiashara ya dola hiyo ya Waislamu, ingekuwa, bila ya shaka, pia ndio makao makuu yao ya "burudani", yakivuta sifa zote za Kibohemia za nyakati zao, katika kutafuta furaha za hisia.

(4). Qur'an Tukufu, Kitabu cha Allah swt., kilishushwa katika Kiarabu safi kabisa. Makka na Madina zilikuwa ndio chimbuko la Kiarabu cha Qur'an. Watu wanaozungumza lugha za kigeni na wanaoishi katika yale makao makuu ya wateka-ji wao, waliichafua lugha yao (lugha ya watekaji). Kama Madina ingebakia kuwa mji wa kifalme, kile Kiarabu cha Qur'an kingeweza, bila kuepukika, kupatwa na athari nyingi za kigeni. Maarifa ya Qur'an na ufafanuzi wake, na msamiati wake, hayakuweko katika mpango wowote katika karne ya kwanza ya Hijiria. Lakini ilikuwa ni muhimu kwa ajili ya kueleweka kwa Qur'an kwa kizazi cha wakati huo na vizazi vitavyofuata kwamba ile lugha ya Makka na Madina ibakie kama ilivyokuwa wakati wa Mtume (s.a.w.w.) ili kwamba maneno hayo ya Kiarabu yasi-je yakapata maana tofauti na zile zilizokuwa zikitumika katika wakati wake.

Lugha zote zinazoishi zinabadilika, na maneno yanabadilika maana zake. Kama kiumbehai chochote kinachoishi, maneno pia yanazali wa na vilevile yanakufa. Na kama kiumbehai kingine chochote kinachoishi, yanao uwezekano wa kuathiriwa na athari za kigeni na za kutoka nje. Mfano wake mzuri ni kule "kutohoa" Kiingereza cha kisasa. Kiarabu pia kingeweza "kutoholewa" lakini kiliokolewa kutokana na majaliwa haya na Ali ambaye alibadili muelekeo wa shughuli za wageni mbali na Madina. Yeye, kwa hiyo, ndiye mfadhili wa kwanza na mkuu sana wa lugha ya Kiarabu na sayansi za Qur'an.

(5). Watawala wa Bani Umayya wa Damascus waliishi kwa kuigiza wafalme wa Byzantium na Uajemi. Walikuwa wamejikusanyia wenyewe vifaa vyote vya anasa na ufuska ambavyo mamlaka yao yaliweza kuwatengenezea. Ule wepesi wa asili na usawa wa Uislamu vilikuwa vimetoweka kutoka Syria kama viliwahi kuwepo kamwe hapo mwanzoni. Ali, hata hivyo, alitaka kuwasilisha kwa ulimwengu mzima picha

575

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ileile ya Uislamu ambao Muhammad Mustafa aliiwasilisha kwa Waarabu huko Makkaa na Madina. Lakini ilikuwa ni picha ambayo majirani wa Syria na wengi wa Wasiryia wenyewe hawajawahi kuiona kamwe. Kwa kweli, katika miaka iliyofuatia, watawala wao walikuwa wawaonyeshe wao picha, sio ya Uislamu, bali picha dhidi ya Uislamu.

John Alden Williams:

"Wafalme wa Kiajemi wote, kutoka Ardashir mtoto wa Papak hadi Yazdagird, wali-jitenga binafsi na wajumbe wao kwa pazia.

Safari moja nilimuuliza (yule mwanamuziki maarufu wa baraza) Ishaq ibn Ibrahim al-Mawsili: Je, wafalme wa Amawi walijionyesha kwa wajumbe wao na waimbaji?" Yeye akajibu, "Mu'awiyah na Marwan 1, Abd al-Malik, Walid 1, Suleiman, Hisham na Marwan II, walitenganishwa na wajumbe wao kwa pazia, hivyo kwamba hakuna mjumbe aliyeona kile alichokuwa akikifanya khalifa, kama alitekwa na muziki huo, au alitingisha mabega yake, au alicheza, au alitupa nguo zake, hivyo hakuna isipokuwa watumwa wake maalum ndio waliomuona. Na kwa makhalifa wa Amawi waliobakia, hawakuwa na aibu ya kucheza au kuvua nguo zao na kuonyesha nyuchi zao mbele ya wajumbe na waimbaji wao. Lakini kwa hilo, hakuna kati yao aliyekuwa kama Yazid ibn Abd al-Malik na Walid ibn Yazid kwa kutokuwa na haya na lugha chafu mbele ya wajumbe wao, na kuvua nguo zao, bila ya kujali walichokuwa wanakifanya." (uk. 81)

(Life at the Cali ph 's Court: kutoka kwenye Kitabu al-Taj, Cairo, 1914, uk. 5. Kisichokuwa na jina: kati ya 847 - 861 A.D. - Themes of Islamic Civilization, Berkeley, 1971)

Pale Ali alipofanya Kufa kuwa makao yake makuu, marafiki na maadui waliona kwa macho yao wenyewe ule Uislamu wa Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt. Waliona kwamba mtawala halali wa Waislamu alifanya kazi kwa mikono yake mwenyewe katika mashamba na mabustani, na alijikimu yeye mwenyewe na familia yake kutokana na malipo aliyoyatokea jasho yeye mwenyewe. Waliona kwamba aliishi kwa mkate wa shairi mkavu lakini kila mtu mwingine katika milki yake alikuwa anakula vizuri. Waliona kwamba shati lake mwenyewe lilikuwa limefunikwa na viraka, raia zake walikuwa wakivaa vizuri. Waliona pia kwamba hakuwa na kasri la marumaru bali aliishi kwenye kibanda cha matope, na kwamba hapakuwa na askari wa zamu au doria mlangoni mwa nyamba yake, na kwamba alikuwa anafikiwa na kila mtu katika kila saa ya mchana au usiku.

(6). Kwa maslahi ya usalama wa Makka na Madina, Ali alitaka kuzifanya zisiwa maarufu kisiasa ili zisiweze kuvuta nadhari zisizohitajika. Mamlaka ya Mbinguni Duniani ambao Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) alikuwa ameuanzisha, ulikoma, baada ya kifo chake, kuwa wa "mbinguni," na ulikuwa umegeuka kuwa serikali bandia ya Kigiriki au Kiajemi. Chini ya hali hiyo ya mabadiliko, hadhi na sifa ya utukufu ya miji hiyo

576

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

pacha Makka na Madina zilikuwa siku zote katika hatari kubwa. Akizitabiri nyakati za mbele, Ali aliweka miji yote miwili nje ya mzunguko wa matukio ya kisiasa. Mwanawe mdogo, Husein, pia alikuwa na shauku hiyo hiyo ya kulinda utukufu wa mji wa babu yake. Yeye pia aliyaona mawingu ya mvua yakijikusanya kwenye upeo wa macho, na yeye pia aliondoka Makka, katika muda muafaka tu, kuondoa nadhari ya serikali mbali nayo.

Baada ya mauaji ya Karbala mnamo mwaka 680, ilikuwa ni ile miji mitukufu ya Kiislamu - Madina na Makka - iliyovuta akili ya Yazid, mtoto wa Mu'awiyah. Alimtuma jemedari wake, Muslim bin Aqaba, kwenda Madina pamoja na jeshi la Syria ambalo liliuwa raia 10,000 kwa ukatili. Waliokufa wali jumuisha masahaba wengi wa Mtume (s.a.w.w.). Madina ilitupwa kwenye ridhaa ya jeshi la wavamizi. Msikiti Mkuu wa Mtume (s.a.w.w.) uligeuzwa kuwa zizi la wapanda farasi wa Syria. Wale wachache ambao walikuwa hawakuawa, iliwabidi wachukue kiapo cha utii kwa Yazid. Muslim bin Aqaba aliwaambia kwamba Yazid alikuwa ndio bwana wa maisha yao, na angeweza kuwauza kwenye utumwa, kama angetaka kufanya hivyo.

Alfred Guillaume:

"Kati ya kipindi kilichohusika na Sir a na kuhaririwa kwa kitabu chenyewe inaji-tokeza ile misiba miwili ya Karbala, pale Husein na wafuasi wake walipouawa mnamo mwaka 61 H.A., na kule kutekwa nyara kwa Madina mnamo mwaka 63 H.A. wakati Ansari elfu kumi wakiwemo masahaba sio chini ya themanini wa Mtume walipouawa.

(The Life of Muhammad, uk. xxvii, 1967)

Muslim bin Aqaba aliiacha Madina ikiungua taratibu na kuwa mabaki na kisha akaelekea Makka. Lakini alikufa kabla hajafika aendako, na uongozi wa vikosi vyake ukaenda kwa afisa mwingine wa Yazid, aitwaye Ibn Namir.

Huko Makka, Abdallah ibn Zubeir alikuwa amejitangaza mwenyewe kuwa khalifa. Ibn Namir aliushambulia mji huo kutoka kwenye vilima vinavyouzunguka na akaichoma Al-Kaaba. Lakini alikuwa hajaukamata mji huo bado wakati Yazid alipokufa huko Damascus. Mara baada ya hapo, ibn Namir akaacha kuuzingira na akaondoka kwenda Syria.

Lakini kile ambacho Makka na Abdallah ibn Zubeir walichokipata ilikuwa ni nafuu ya muda tu. Wakati Abdul Malik bin Marwan alipokuja kuwa khalifa, Makka kwa mara nyingine tena ikageuka uwanja wa vita. Jemedari wake, Hajjaj bin Yusuf aliizingira Makka, akaishambulia, na akabomoa sehemu ya Al-Kaaba. Abdallah bin Zubeir alichachamaa na kushikilia kwa miezi saba. Aliuawa katika maeneo ya Al-Kaaba, na mji ukasalimu amri kwa watekaji.

577

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Philip K. Hitti:

"Katika mwaka 683 jeshi la Syria lilitumwa na Yazid dhidi ya mdai ukhalifa, Abdallah bin Zubeir. Muasi huyo alitafuta kimbilio kwenye ardhi isiyodhuriwa ya nyumba tukufu lakini hatahivyo alishambuliwa na Al-Kaaba ikashika moto. Lile Jiwe Jeusi lilikatika vipande vitatu. Nyumba ya Allah, kwa maneno ya mwanahistoria mashuhuri, al-Tabari, "ilionekana kama kifua kilichochanika cha mwanamke mwenye huzuni."

(Capital Cities of Islam, 1973)

Ali alitafuta, kwa kubadilisha makao makuu, kuziokoa Makka na Madina kutokana na maangamizi ambayo yaliikumba licha ya juhudi zake za kinyume chake. Lakini basi ni nani mwingine katika ulimwengu wote wa Waislamu aliyeshiriki katika kuhusika kwake yeye na wanawe katika heshima na usalama wa miji hii miwili? Pale Husein ibn Ali alipo-hisi kwamba hatari inaisogelea miji hiyo, yeye aliondoka haraka sana, na watu wote wa familia yake, kuelekea Iraq, ambako alijua, alikuwa na makutano na kifo. Lakini Abdallah bin Zubeir hakusita katika kukaribisha unajisi na uharibifu kwenye miji hiyo, na mauaji ya halaiki juu ya wakazi wake.

Ulimwengu wa Kiislamu bado unapaswa kukubali deni lake la shukurani kwa Ali kwa busara zake, busara zake na ubinadamu. Alivilinda vyanzo vya Uislamu katika uhai wake, na Alichukua hatua kwa ajili ya ulinzi wavyo baada ya kufa kwake. Hakuna njia nyingine yoyote ambayo angeweza kuiokoa Hijazi kutokana na kupatwa na mivurugiko hiyo, gha-sia na kiwewe vilivyosababishwa na siasa na vita, isipokuwa kwa kuhamisha makao makuu kutoka Madina kwenda Kufa.

Wakati Ali alipobadilisha makao ya dola hiyo, Mu'awiyah alidhani kwamba alikuwa, hati-maye, amemkamata Ali akifanya jambo ambalo linaweza kuhojiwa, na alimwandikia kwamba yeye Ali alikuwa "ameutelekeza" mji wa Mtume - kitendo ambacho ni cha "kulaumika" sana kiasi kwamba hakiwezi kusameheka.

Miaka minne tu baadae, Mu'awiyah mwenyewe akawa ndiye mtawala wa juu kabisa wa dola ya Waislamu, na hapakuwa na mtu yoyote anayeweza kumuuliza juu ya kitendo chake chochote. Ikiwa kama alikuwa na mapenzi sana na mji wa Mtume kama alivyojifanya kuonyesha katika barua yake kwa Ali, angeweza kuufanya kuwa makao yake makuu. Lakini hakufanya hivyo wala hata mmoja kati wa warithi wake, wala hawakufanya hivyo makhalifa wa utawala wa Bani Abbasi.

578

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ufufukaji wa Bani Umayyah

Bani Umayya walikuwa ni Ukoo mmojawapo wa Makuraishi Wa Makkah. Kama ilivy-oelezwa kabla, walikuwa ni maadui wa jadi wa Bani Hashim - ukoo mwingine wa Makuraish. Wakati Muhammad, mtu wa ukoo wa Bani Hashim - alipotangaza kwamba alikuwa ni Mtume wa Allah swt., na akawataka Waarabu kutelekeza uabudu masanamu wao, na kuamini katika Mungu Mmoja, Bani Umayya walimpinga, na walipigana dhidi yake kwa miaka ishirini.

Lakini walishindwa. Mapambano yao ya muda mrefu na makali dhidi ya Muhammad na Uislamu yalifikia mwisho wenye kufedhehesha mnamo mwaka 630A.D., wakati alipoite-ka Makka. Walilazimika kukubali kushindwa, na "wakaukubali" Uislamu.

Ushindi wa Uislamu, hata hivyo, uliwasha mioto mipya ya chuki katika nyoyo za Bani Umayya dhidi ya walezi wake - Muhammad na Ali, kama ilivyoonyeshwa katika mlango mmoja uliopita. Walikuwa waangalifu vya kutosha katika kuficha chuki yao kwa Muhammad lakini hawakujaribu kuficha chuki yao juu ya Ali. Alikuwa ni Ali aliyeharibu sio tu zile nembo zenye kuonekana za dini ya Bani Umayya bali pia alileta kifo kwenye heshima zao. Lakini mara wakaonyesha kwamba wanaweza kuwa chini lakini walikuwa hawajatoka nje. Wao, kwa hiyo, walivuta subira kwa miaka thelathini - hadi mwaka 661A.D. - wakati walipokuwa, hatimaye, na uwezo wa kuikamata ile zawadi iliyotafutwa kwa muda mrefu - ukhalifa wa Waislamu. Bani Umayya walikuwa ndio maadui wabaya sana kati ya maadui wote wa Uislamu. Kufanikiwa kwao kukamata ukhalifa wa Waislamu, kwa hiyo, kumeleta mshangao mkubwa miongoni mwa wanahistoria. Yafuatayo ni maoni ya baadhi yao juu ya ukweli huu wenye mashaka kuaminika katika historia ya Waislamu.

Edward Gibbon:

"Wale watesaji wa Muhammad walipora urithi wa watoto wake; na mabingwa wa uabudu masanamu wakawa ndio viongozi wakuu katika dini na dola yake. Upinzani wa Abu Sufyan ulikuwa mkali na sugu; kusilimu kwake kulikuwa kwa kuchelewa na kusiko na ari; imani yake mpya ilitiwa nguvu na haja na manufaa; alitumikia, alipi-gana, huenda aliamini; na madhambi ya nyakati za ujahilia yalifidiwa na sifa za hivi karibuni za familia ya Umayya. Mu'awiyah, mtoto wa Abu Sufyan, na yule katili Hind, alikwezwa mwanzoni mwa ujana wake kwa cheo au jina la mwandishi wa Mtume; uamuzi wa Umar ulimkabidhi serikali ya Syria; na alilitawala jimbo hilo kwa zaidi ya miaka arobaini, ama katika cheo cha chini au cha juu. Kazi iliyotukuzwa ya kuwatafuta wauaji wa Uthman ilikuwa ndio kichwa na kisingizio cha tamaa yake.

(The Decline and Fall of the Roman Empire)

579

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

E. A. Freeman:

"Ukhalifa ungeweza labda kutolewa kwa mwenye kustahili sana katika waumini; ungeweza labda kuwa wa kurithiana katika familia ya Mtume; lakini Muhammad asingeweza kamwe kudhania kwamba utakujakuwa ni wa kurithiana katika ukoo wa maadui zake wabaya kabisa."

(History of the Saracens)

R. A. Nicholson:

"Wakati wale makabaila wa Makka walipoukubali Uislamu, walisalimu amri tu kwa kisichokwepeka. Walikuwa sasa wapate fursa ya kujilipizia kisasi wenyewe. Uthman bin Afan, ambaye alimrithi Umar kama khalifa, alitoka kwenye ukoo mashuhuri wa Makka, Bani Umayya au kizazi cha Umayya, ambao ulikuwa siku zote ukiongoza katika upinzani kwa Muhammad, ingawa Uthman mwenyewe alikuwa miongoni mwa masahaba wa mwanzoni wa Mtume. Yeye alikuwa mchamungu, mtu mzima mwenye nia njema - zana nyepesi mikononi mwa ndugu zake wenye tamaa. Mara moja wao walipanda kwenye vile vyeo vyote vyenye faida na maarufu na wakaishi maisha ya anasa, ambapo mara kwa mara tabia zao mbovu zilisababisha kuzuka kwa swali la endapo hawa wafuasi wa dakika za mwisho hawakuwa bado wapagani nyoy-oni mwao.

Sababu nyingine zilichangia kuchochea manung'uninko ya jumla. Ukuaji wa haraka wa anasa na vitendo vya kifisadi katika miji mitakatifu na vilevile kwenye makazi mapya ulikuwa ni chukizo kwa Waislamu wachamungu. Wale Waislamu wabora wa kweli, Masahaba wa Mtume, wakiongozwa na Ali, Talha na Zubeir walijitahidi kuuchimba ule uungwana wa kiadui ambao uliwatishia kuwaangamiza. Kikundi kili-chojitenga kijeshi kilikuwa tayari kwa uasi dhidi ya kiburi na uroho wa Bani Umayya. Maasi yalizuka ghafla, na mwishowe, khalifa huyu mzee, aliuawa ndani ya nyumba yake mwenyewe.

(A Literary History of the Arabs, uk. 190, 1969)

Nicholson amekosea katika kueleza kwamba Ali, Talha na Zubeir walijitahidi kuwachim-ba Bani Umayya ambao waliwatishia kuwaangamiza. Ali hakujitahidi kuwadhoofisha Bani Umayya ingawa Talha na Zubeir walijitahidi kumchimba Uthman, na walifanikiwa katika juhudi zao. Kwa upande wao, Bani Umayya walimtishia Ali - lakini hawakuwatishia Talha na Zubeir - kwa maangamizo. Kwa kweli, Talha, Zubeir na Aisha walipigana vita vya Basra (vita vya Ngamia) dhidi ya Ali, kwa msaada wa Bani Umayya.

580

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Philip K. Hitti:

"Kati ya makhalifa wanane (wa Bani Umayya) katika kipindi cha 715 - 750 ni waw-ili tu ndio waliostahili ule urithi ulioanzishwa na Mu'awiyah na kutajirishwa na Abd-al-Malik na al-Walid. Hao sita waliobakia, watatu wao wakiwa ni watoto wa mama zao watumwa, walikuwa hawana uwezo, wengine wakiwa mafasidi kama sio wapoto-fu. Yule mrithi-ndugu wa al-Walid alikuwa anapendelea sana ulevi, uwindaji, na kusikiliza nyimbo na muziki kuliko kuendesha shughuli za dola. Mtoto wake alimpi-ta baba yake. Alitumia muda mwingi katika nyumba zake za starehe huko jangwani, ambako mabaki yake bado yanaonekana, kuliko hapo makao makuu.

Anasemekana kujiingiza katika kuogelea katika dimbwi la pombe na kugugumia kiasi cha kutosha kushusha kina chake. Zaidi ya mwasherati asiyerekebishika, khalifa huyu wakati mmoja alitenda jambo la kufuru isiyokuwa ya kawaida; kuifanya shabaha nakala ya Qur'an kwa ajili ya mishale ya upinde wake. Bila shaka, kule kukua kwa haraka kwa utajiri, wingi wa watumwa na mahawara, kuongezeka kwa nyenzo kwa ajili ya kujiingiza kwenye starehe, na tabia nyingine mbaya za ustaarabu wa kitajiri wa mjini - dhidi yake ambazo watoto hao wa jangwani walikuwa hawakujengeka kwa kiwango chochote cha kutoathirika - walikuwa wameanza kudhoofisha nguvu ya Uarabu."

(Capital Cities of Arab Islam, uk. 78-79, 1973)

Arnold J. Toynbee:

"Moja ya mambo ya kejeli kubwa ya historia yote ni yale maangamizi ya ile nyumba ambayo Muhammad aliijenga. Muhammad alikuwa na muanguko mkubwa. Mtume huyu asiyefanikiwa alishindwa kwenye shauku ya kufanikiwa kama mtawala mwele-di na mwenye mikakati. Lakini, katika kutafuta na kupata mafanikio ya kidunia huko Madina, Muhammad, bila kujua, alikuwa akiwafanyia kazi washindi wake huko Makka. Pale ilipokuja kwenye mashindano ya Siasa halisi (ya hali na mali), wafalme wa biashara wa Makka walikuwa na uwezo zaidi ya mwenzao wa mjini, mgeni wa biashara, na wenye uwezo zaidi sana kuliko binamu na mkwe wake Muhammad, hodari lakini asiye na uwezo, Ali.

Baada ya Muhammad kufanikiwa kukata njia ya msafara wa biashara wa Makka kwenda Syria, watu wa Makka walisalimu amri kwa masharti nafuu ambayo huyu mkimbizi wa Makka mwenye hisia za huruma, aliyowapa wao; lakini katika utii wa nje kwa Muhammad na Uislamu, Bani Umayya walificha ndimi zao mashavuni mwao. Hawakuwa na dhamira ya kuondoshwa madarakani kwa muda mrefu. Sasa kwa vile wameshindwa kwanza kuuzuia Uislamu na kisha kuurudisha nyuma, njia nyingine pekee kwao ilikuwa ni kuukubali harakaharaka baada ya kuukamata kwa

581

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hila ya kusilimu kwa maneno tu. Walisubiri wakati mzuri mpaka kwa Ali wakampa-ta mtu wao wa kumwonea na kwa Mu'awiyah wakapata mtu wa bahati yao.

Mu'awiyah alikuwa ni mmoja wa mabwana wakubwa kabisa, wanaojulikana kwenye historia, wa aina ya mtawala mjanja, mwenye subira. Analingana na Augustus, Philip wa Macedon, Liu Pang, na Cavour. Maskini Ali alizidiwa ujanja kabisa na yeye. Ndani ya kipindi cha miaka ishirini na tisa ya kifo cha Muhammad, ile ambayo Muhammad alikuwa ameianzisha, na ambayo warithi wake wameipanua kwa haraka sana na kuwa himaya kubwa, ikageuka kuwa ngawira isiyo na ubishani ya Mu'awiyah mwana wa Hindi: yule Malikia wa biashara, kigogo wa Makka ambaye alikuwa adui mkubwa sana wa Muhammad. Tofauti na Muhammad, Mu'awiyah alianzisha ufalme - Utawala wa Umayya - ambao ulidumu kwa miaka 90 na ukaitawala dunia kutoka Multan na Tashqand hadi Aden, na kutoka Aden hadi Gibralter na Narbonne.

Mu'awiyah na warithi wake, wakiwa wapagani wasiotubia katika yote bali majina tu (isipokuwa kwa Muislamu halisi mmoja tu, Khalifa Umar II), walifikia uamuzi wa kuupinga Uislamu kwa kujiingiza katika karaha mbaya sana katika ustaarabu. Walikuwa walevi wa pombe, na walipamba makasiri yao kwa nakshi na michoro ya rangi katika mtindo wa Kiyunani ambao ulikuwa umeenea huko Syria kwa miaka 1000 iliyopita. Walifurahia katika kuvunja miiko ya Kiislamu katika taswira ya miun-do ya maisha. Waliajiri wasanii wa Kikristo ambao walikuwa mahodari katika nyan-ja hii; na hawakupendezewa na taswira za wanyama na wanaume. Maagizo yao waliyoyapendelea sana yalikuwa ni picha za wanawake - bora zaidi wakiwa uchi, au angalau uchi mpaka kwenye kiuno.

Waliwezaje hawa Bani Umayya kusalimika na utovu wa heshima na kufuru hii kwa muda mrefu hivi hadi miaka 90? Wakati Jezebel na Ahab walipopinga ibada ya imani halisi ya Yahwah, adhabu inayostahili ilitolewa kwa haraka sana. Hivyo, ni vipi hawa Bani Umayya walimudu kuendelea hivyo vizuri sana kuliko Utawala wa Umar? Mtu anaweza asiwapende au kuwasifia Bani Umayya, lakini werevu wao unadai heshima zetu za kusita, na hawezi kujizuia kushukuru utaratibu wa kisanii wa kufanya mambo ambao wao wameturithisha sisi."

(East to West - A Journey Round the World, 1958. uk.214-5 - The Shocking Umayyads)

Toynbee anaweza kudai kwamba ni mwanahistoria mashuhuri lakini madai hayo hayalaz-imishi kufanya maoni yake, ambayo ameyaeleza kifahari sana, katika dondoo iliyopita, ama kuwa ni sahihi au hata yenye akili. Kwa kujitia kumdhihaki Muhammad (s.a.w.w.) na Ali, anasaliti tu dosari katika jicho lake mwenyewe, bainifu sana la Wamisionari wa Kiingereza wa karne ya 19 katika makoloni. Maoni yake yako zaidi kwenye aina ya tahaki-

582

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ki ndefu yenye lawama na matusi au mabishano, isiyokosa mguso wa rasharasha za kebe-hi, kuliko mchanganuo wowote wa mambo wenye shabaha na ukosoaji.

Yale maneno ya mwanzoni yanavutia sana. Toynbee anasema "moja ya kejeli kubwa ya historia yote ni yale maangamizi ya nyumba ambayo Muhammad alikuwa ameijenga. Muhammad alikuwa na muanguko mkubwa." "Kejeli" hiyo lazima iwe ilikuwa na sababu lakini Toynbee hasemi sababu hizo zilikuwa zipi. Anatilia maanani zile athari tu.

Toynbee ni matokeo ya ule utamaduni wa kisasa wa Magharibi, wa kuthamini mali, wa kubadili asili ya mambo, na Waislamu wanaweza kutogundua kutoweza kwake kuyaelewa maadili ya kijamii ya Uislamu. Mafanikio ya Uislamu yalikuwa yametaarifiwa katika dhana ya kimapokezi (dhana ya Nabii Ibrahim) ya kafara. Muhammad na Ali walitoa mhanga sio tu utajiri wao wa mali bali pia walitoa mhanga uhai wa wengi wenye thamani kwa ajili ya kuufanya Uislamu kuweza kuwepo. Wakati, baada ya vifo vyao, Uislamu ulipohitaji makafara mapya, watoto wao walikuwa tayari kuyatoa. Wajukuu wa Muhammad (s.a.w.w.) na watoto wa Ali walitoa muhanga maisha yao huko Karbala kwa ajili ya mifano ambayo wote walikuwa wamejitahidi kuifanya isisahaulike milele.

Makafara yaliyotolewa na Muhammad, Ali na watoto wao, ndio ushindi na heshima ya Uislamu lakini Toynbee anayalinganisha na "kejeli."

Muhammad hakuwa na "muanguko" - mkubwa ama mdogo - ingawaje Toynbee angeta-ka kwamba angekuwa na muanguko.

Toynbee alimwita Muhammad Mustafa "Mtume asiyefanikiwa" ambaye "alishindwa kwenye shauku yake ya kufanikiwa kama mtawala mweledi." Alikuwa vipi "asiyefanikiwa"? Wajibu wake ulikuwa ni kufikisha ujumbe wa mwisho wa Allah swt. kwa wanadamu, na aliufikisha, na ulikubaliwa katika sehemu zote za peninsula ya Arabia ndani ya wakati wa uhai wake. Wala hakushindwa kwenye shauku yake ya kuwa mtawala mweledi. Yeye alikuwa mtawala mweledi. Ujumbe wake ulikuwa mpana, na moja ya kazi zake kama mjumbe wa Allah swt. ilikuwa ni kuwaelimisha Waislamu katika utaratibu wa mfumo wa kisiasa. Hili alilifanya huko Madina.

Muhammad (s.a.w.w.) hakuwa katika "mashindano" na wapagani au watetezi wa siri wa upagani wa Makka. Yeye alikuja ulimwenguni hapa kueneza sheria za Utawala wa Mbinguni, na sio "kushindana" na mtu yeyote, mwisho wa wote kabisa, na wala riba wa Makka na waabudu masanamu. Kusingizia kwamba alikuwa akishindana na Bani Umayya ni maoni ya kipuuzi kabisa kuliko yote ya Toynbee.

Waabudu masanamu wa Makka hawakuwa "wenye uwezo zaidi" ama kwa Muhammad au kwa Ali, naye Ali hakuwa "dhaifu," na hakuwa "amezidiwa ujanja" na Mu'awiyah.

583

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Toynbee hana uwezo wa "kuwahukumu" wao kwa mtazamo wa maadili ya kijamii ya Kiislamu. "Siasa halisi" yake (ya kujali hali, mali na mazingira) isingeweza kuwa na man-ufaa yoyote kwa Muhammad na Ali. Tafsiri zake zinaonekana wazi zimeathiriwa na uta-maduni wake - wa kutafuta maslahi, utamaduni wa kidunia wa Magharibi ya kisasa. Hana utambuzi wa utamaduni wa Qur'an, na Qur'an inabeua "siasa halisi."

Muhammad na Ali walikuwa wanaidhihirishia dunia kwamba katika siasa, kama katika dini, malengo hayathibitishi uhalali wa matendo. Katika Uislamu matendo yenyewe yanakuwa ndio malengo. Matendo ambayo maadui zao - Bani Umayya - waliyoyafanya ili kufikia malengo yao, yalikuwa na uhakikisho uliojengeka ndani yake wa "mafanikio". Lakini Muhammad na Ali hawakuamua mafanikio au kushindwa kwa vipimo hivyohivyo kama Bani Umayya walivyofanya au kama Toynbee anavyofanya. Kwa Muhammad na Ali, mafanikio yalikuwa ni kupata radhi za Allah swt. tu, na kushindwa kulikuwa ni upotezaji wa radhi hizo tu. Kwa kuamua kwa kipimo hiki, wote hao walikuwa wamefaniki-wa sana. Mwenyezi Mungu awape rehma wao na watoto wao daima na milele.

Toynbee anaendelea kusema kwamba Bani Umayya hawakuwa na dhamira ya kuondosh-wa kutoka kwenye madaraka kwa muda mrefu. Hivi hizo dhamira za Bani Umayya zilikuwa na maana yoyote mwaka 63O A.D., wakati Muhammad Mustafa alipoiteka Makka? Alikuwa ameteketeza ushirikina wao na mamlaka ya kiuchumi na kisiasa, na Ali alikuwa amevunja nguvu yao ya kijeshi. Walimuangukia miguuni kwake, na wangebakia wameanguka daima kama Abu Bakr na Umar wasingewanyanyua, na wasingewarudishia madaraka ya kiuchumi na kisiasa. Ghafla, kilichokuwa kikionekana hakiwezekani chini ya Muhammad, kilionekana kutarajiwa chini ya Abu Bakr na Umar. Walikuwa ni hao wote walioifanya dola ya Waislamu kuwa "ngawira isiyo na ubishani ya Mu'awiyah mtoto wa Hindi."

Mapenzi, heshima na shukurani ambayo Toynbee "hawezi kujizuia" kuzitoa kwa Bani Umayya, zinaeleweka vizuri sana. Yeye ni mwenzao kifalsafa. Wote wanaunganishwa pamoja katika uadui wao unaofanana kwa Uislamu na kwa walezi wake, Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) na Ali.

"Hukmu" ya Toynbee juu ya Muhammad na Ali ni mfano wa kuigwa wa upuuzi mkubwa ambao wanazuoni maarufu wanaweza kuuzusha.

Hitti na Toynbee wote wamevuta taswira ya baadhi ya makhalifa - warithi wa Mtume wa Uislamu - ile ambayo Banu Umayya wameitoa. Ukweli kwamba umma wa Waislamu ulilundikiwa makhalifa kama hao, kwa kweli ni "moja ya kejeli kubwa ya historia yote." Lakini kejeli hiyo ina maelezo yoyote? Inayo, ndio. Kitabu hiki ni jaribio la kuielezea kejeli hiyo.

584

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Bani Umayyah walifaidi umaarufu kiasi hapo Makka kama walezi wa hekalu la masana-mu na kama matajiri wala-riba wakubwa. Wakati Muhammad alipoiteka Makka, alikome-sha uabudu masanamu wao na ula-riba wao, na wakapoteza umaarufu.

Lakini kupoteza umaarufu huko hakukudumu kwa muda mrefu. Kulidumu tu kuanzia kule kutekwa kwa Makka na Muhammad mnamo Februari 630 hadi kwenye kifo chake mnamo Juni 632. Wakati tu "jua" la Utume lilipozama kwenye macheweo, ile "nyota" ya Bani Umayya ikachomoza juu yake.

Haitakuwa sahihi kuonyesha ufufukaji wa Bani Umayya kuanzia tarehe ambayo Uthman alikuwa khalifa wala hata pia kuanzia tarehe Mu'awiyah alipoutwaa ukhalifa bali kuanzia tarehe 8 Juni, 632, tarehe ya kifo cha Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), Mtume wa Uislamu.

Ni uhusiano gani kati ya kifo cha Muhammad (s.a.w.w.) na ufufukaji wa Bani Umayya? Kama ilivyoonyeshwa hapo juu, Muhammad alihusika na kupoteza umaarufu kwa Bani Umayya. Lakini mara tu alipofariki, waliruka kutoka kwenye ukosa umaarufu, ingawa sio kwa uwezo wao wenyewe. Abu Bakr na Umar, wale watawala wapya wa serikali aliyoiun-da Muhammad (s.a.w.w.), waliwainua Bani Umayya kutoka kwenye ukosa umaarufu na kutoeleweka kwao, na wakawaweka kama nguvu katika mandhari ya kisiasa ya Uislamu.

Bani Umayya waliinuka na uamuzi mzito - kulipiza kisasi kutoka kwa Muhammad na Ali na/au watoto wao.

Kukubali Uislamu kwa Bani Umayya, baada ya kushindwa kwao kuuangamiza, kulikuwa ni ushahidi tu wa uthabiti wao. Walitambua kwamba mashambulizi yao ya kutokea mbele ya Uislamu yalikuwa yote yameshindwa, na kwamba walipaswa kujaribu kitu ambacho sio cha kawaida. Walifanya hivyo. Mkakati wao mpya ulikuwa ni kuingia kwenye safu za waumini, wakijifanya kama ni Waislamu; kuyaangalia matukio kutoka ndani, na kisha kuushambulia Uislamu pale wakati muafaka utakapojitokeza wenyewe, kama ilivyoelezwa kwenye mlango wa huko nyuma.

Wakati muafaka ulikuja baada ya kifo cha Muhammad (s.a.w.w.).

Taarifa ilikuwa imekwishapatikana ya ahadi ya Abu Sufyan, kiongozi wa ukoo wa Bani Umayya, kwa Ali, ya kujaza mitaa yote ya Madina na askari wa miguu na wa farasi, waki-wa tayari na radhi kufa kwa amri yake Ali, kama ataipinga serikali ya Saqifah.

Abu Sufyan alikuwa amerusha pigo la hatari sana kwa Uislamu lakini alikosa shabaha kwa mara nyingine tena. Alikuwa amejaribu kujipendekeza kwa Ali, mlezi wa Uislamu, lakini alishindwa. Ali alikuwa macho kama siku zote. Lakini Abu Sufyan hakuhangaishwa na kushindwa kwake. Ilijitokeza kwake kwamba kama angejaribu kujipendekeza kwa vion-gozi wa serikali ya Saqifah, angewakuta ni wenye kuvutika zaidi kuliko Ali. Aliwaendea

585

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

na kweli walikuwa hivyo!

Wakati wa ukhalifa wa walezi wao, Abu Bakr na Umar, Bani Umayya walizizatiti nafasi zao kimya kimya. Hawakujaribu kuvuruga mambo na kuleta misukosuko. Wakati ulikuwa haujafika bado wa wao kufanya jaribio la kuvamia uwanja wa Uislamu. Wao, kwa hiyo, walikaa pembeni. Lakini Uthman alipokuja kuwa khalifa, walihisi kwamba wakati ulikuwa umefika wa wao kutupilia mbali tahadhari yao na uvumilivu wao, na wakaivamia dola hiyo kama tai, tayari kwa kumeza kila kitu. Uthman akawafukuza magavana wote wa majimbo waliokuwa wameteuliwa na Abu Bakr na Umar, na akazijaza nafasi hizo na watu wa famil-ia yake mwenyewe na ukoo wake. Yeye pia aliwapa Bani Umayya zile ardhi zenye rutuba nyingi na malisho kama mali yao binafsi, na akawapa zawadi dhahabu yote na fedha iliyokuwa ndani ya hazina ya umma.

Mnamo mwaka 656 Ali alichukua madaraka ya serikali mikononi mwake. Aliwafukuza magavana wote waliokuwa wakiipora nchi, na aliwaagiza Bani Umayya kurudisha kwenye dola ile ardhi yote, ada za himaya, maeneo na malisho ambayo walikuwa wamejitwalia kinyume cha sheria.

Lakini Bani Umayya hawakuwa na nia ya kuachia kitu chochote. Walisema wazi kwamba watang'ang'ania, kwa muda mrefu iwezekanavyo, kwenye nafasi zao za tangu huko nyuma, marupurupu yao na fursa zao, na kama Ali bado anazitaka, itambidi azichukue kwa nguvu ya silaha.

Ali alilijua hilo kwamba atakutana na upinzani mkubwa kama angejaribu kugawanya mali kwa usawa. Lakini aliuweka wajibu wake kwa Allah swt. na umma wa Waislamu mbele ya matakwa au kinyongo cha wale wa tabaka la juu katika Dar-ul-Islam. Hakuwa na uchaguzi katika suala hilo, na ilimbidi abomoe ngome za upendeleo bila kujali matokeo yake. Katika suala hili, hapakuwa na nafasi kabisa ya masikilizano.

Rais Jimmy Carter:

"Hii sio kazi ya mtu mwenye moyo dhaifu. Itakutana na upinzani mkali kutoka kwa wale ambao sasa wanafaidi upendeleo maalum, wale wanaopendelea kufanya mambo gizani, au wale ambao maeneo ya milki zao yanatishiwa."

(Why Not the Best? Uk. 148, 1975)

Kutangaza nguvu kulikuwa hakukwepeki

Talha na Zubeir walikuwa nje ya mahesabu ya kivita, na makabiliano mapya ya Ali yalikuwa ni pamoja na wale maadui wa zamani - Bani Umayya - wale wahujumu wa itika-di ya Kiislamu. Makabiliano haya yalikuwa ni uthibitisho wa mafanikio ya Umar katika kuwakingamiza Waarabu kati ya maadui wengi na marafiki wachache wa Nyumba ya

586

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Muhammad, Mtume wa Allah swt.

Upinzani wa Bani Umayya kwa Ali ulikuwa ni udhihirishaji wa hisia za upagani dhidi ya Uislamu. Kwa muda mrefu, chuki ya Bani Umayya dhidi ya Uislamu na Banu Hashim ilikuwa ikiungua polepole kama makaa ya moto lakini kwa kuingia kwa Ali kwenye kiti cha ukhalifa, ikageuka kuwa ndimi za moto unaonguruma, unaotishia kuunguza, kwa maneno ya Toynbee, "ile nyumba ambayo Muhammad aliijenga."

Baada ya vita vya Basra, (vita vya Jamal), watu wote wa ukoo wa Bani Umayya walikuwa wamejikusanya nyuma ya Mu'awiyah, gavana wa Syria. Alikuwa ndio kiongozi wao, na alikuwa ndiye kiongozi wa hisia za kipagani dhidi ya Uislamu. Katika vita vyake dhidi ya Ali, alisaidiwa na kutenda jinai hiyo na Amr bin Al-Aas. Amr alikuwa sio Bani Umayya lakini kufanana kwa shauku zao kulichochea mfungamano wake na Mu'awiyah.

Ufuatao ni utangulizi mfupi wa historia ya Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas. Itamfahamisha msomaji kiini hasa cha upinzani wao kwa Ali.

Mu'awiyah bin Abu Sufyan

Mu'awiyah alikuwa mtoto wa Hind na Abu Sufyan. Abu Sufyan alikuwa mume wa tatu wa Hind. Mwanamke huyu alikuwa mmoja wa maadui wachungu sana wa Uislamu, Mtume wake na familia yake. Katika vita vya Badr, baba yake, Utba, aliuawa na Hamza. Mwanawe mkubwa, Hanzala; kaka yake, Walid; na ami yake, Shaiba; waliuawa na Ali. Kwa sababu hii, aliweka nadhiri kwamba atakuja kunywa damu yao (M. Shibli katika Sirat-un-Nabi, juz. I, uk. 370, chapa ya 4, 1976, Azamgarh, India). Katika vita vya Uhud, Hind alipasua tumbo la Hamza, akatoa ini lake, na akalitafuna, na kuanzia hapo akawa "maarufu" katika historia kama "mla maini."

Kama Mu'awiyah alikuwa mwana wa Hindi, yule mla maini wa Uhud, alikuwa pia baba yake Yazid, yule muuaji katili wa Karbala, aliyefungulia hofu kuu na kumuua mjukuu wa kiume mdogo na vitukuu vya Muhammad (s.a.w.w.). Mmoja wa masahaba wa Mtume waliochukua kiapo cha utii kwa Yazid alikuwa ni Abdallah bin Umar ibn al-Khattab. Alikuwa ni mtazamaji wa "nje ya ulingo" wa mauaji hapo Karbala, ndani yake ambayo kurasa za historia ya Uislamu zilichafuliwa na damu takatifu zaidi kabisa katika viumbe wote.

Yazid alijikweza kwa nasaba ndefu "yenye kutambulika" ya uhasama kwa Banu Hashim -Walezi wa Uislamu.

Wakati Mtume alipoiteka Makka mwaka 630, Abu Sufyan, Hind, watoto wao, Yazid na Mu'awiyah, na watu wengine wa ukoo wa Bani Umayya, wakasilimu. Jalal-ud-Din Suyuti

587

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ameandika katika ukurasa wa 135 wa kitabu chake, Tarikh-ul-Khulafai (Historia ya Makhalifa):

"Mu'awiyah alisilimu pamoja na baba yake, Abu Sufyan ile siku ilipotekwa Makka. Walikuwepo katika vita vya Hunayn, na walikuwa miongoni mwa muallafatul-qulub.”

Baadhi ya wanahistoria wanasema kwamba baada ya kutekwa Makka, Mtume (s.a.w.w.) alimteua Mu'awiyah kama mmoja wa waandishi wake. Kama mwandishi, kazi yake, pengine ilikuwa ni kuandika barua za Mtume (s.a.w.w.).

Huko Makka na Madina, kote, Mtume (s.a.w.w.) alimfanya kila Muislamu kuwa ndugu wa Muislamu mwingine. Yeye kwa hiyo, alimpa Mu'awiyah naye pia "ndugu."

Muhammad ibn Ishaq:

"Mtume alifanya udugu kati ya Mu'awiyah bin Abu Sufyan na al-Hutat. Mtume ali-fanya hivyo kati ya baadhi ya masahaba wake, kwa mfano, kati ya Abu Bakr na Umar; Uthman na Abdur Rahman bin Auf; Talha bin Ubaydullah na Zubeir bin Awwam; Abu Dharr al-Ghiffari na al-Miqdad bin Amr al-Bahrani; na Mu'awiyah bin Abu Sufyan na al-Hutat bin Yazid al-Mujashi'i. Al-Hutat alikufa mbele ya Mu'awiyah wakati wa ukhalifa wake na kwa sababu ya udugu wake, Mu'awiyah alichukua kile alichokiacha kama mrithi wake. Al-Farazadaq alimwambia Mu'awiyah:

"Baba yako na ami yangu, ewe Mu'awiyah, waliacha urithi,

ili kwamba mrithi wake apate kuurithi.

Lakini inakuwaje wewe kuibugia mali ya Hutat

wakati mali ngumu ya Harb ilikuwa inayeyuka mkononi mwako?"

(The Life of the Messenger of God)

Kama ilivyoonyeshwa kabla, Abu Bakr alikuwa amemteua Yazid bin Abu Sufyan kama mmoja wa majemedari wake katika mapambano ya Syria. Syria ilitekwa baada ya kifo cha Abu Bakr - katika ukhalifa wa Umar. Alimteua Yazid kuwa gavana wa kwanza wa Syria. Mwaka 639 hata hivyo, tauni ilizuka huko Syria na Palestina, na ikaua maelfu ya watu, miongoni mwao ni Yazid bin Abu Sufyan na Abu Ubaidah bin al-Jarrah. Kwenye nafasi ya Yazid, Umar alimteua mdogo wake na Yazid, Mu'awiyah, kama gavana mpya.

Sir John Glubb:

"Kulikuwa na balaa la njaa huko Hijazi mwaka 639. Zaidi ya njaa hiyo, huo mwaka wa 639 ulishuhudia kuzuka kwa tauni huko Syria na Palestina. Waarabu wengi walik-

588

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ufa, mpaka idadi kubwa wakakimbilia jangwani kutoka kwenye ile miji iliyokuwa imetapakaa tauni. Kabla ya hili uhamiaji kwenye jangwa ungeweza kukamilishwa, hata hivyo, mkuu wa majeshi, Abu Ubaidah, alishambuliwa na kufa. Alizikwa katika bonde la Jordan. Yazid bin Abu Sufyan, ambaye alikuwa ameshiriki kikamilifu kama kamanda wa safu katika mapambano yote ya Syria alikuwa muathirika pia.

Yule khalifa asiyechoka aliamua kutembelea Syria mwenyewe ili kupanga upya utawala baada ya kupotea kwa viongozi wengi sana. Kwa kweli tauni hiyo ilikuwa mbaya sana miongoni mwa Waarabu, ambao 25,000 kati yao wanasemekana waliku-fa, kiasi kwamba ilihofiwa kwamba Wabyzantium wangeweza kutumia fursa hiyo kujaribu utekaji mpya wa Syria.

Katika nafasi ya Abu Ubaidah na Yazid ibn Abu Sufyan, Mu'awiyah ibn Abu Sufyan

aliteuliwa kuwa gavana wa Syria."

(The Great Arab Conquests, uk.214, 1967)

Mu'wiyah alikuwa gavana wa Umar huko Syria katika kipindi kilichokuwa kimebakia cha ukhalifa wake. Wakati Uthman alipomrithi Umar kama khalifa, yeye pia alimthibitisha Mu'awiyah kama gavana wake. Mu'awiyah alitwaa uvumilivu wa kidini kuhusiana na Ukristo ndani ya Syria, na kwa uangalifu na ustadi sana akawalea watu wa Syria, kiasi kwamba akawa maarufu sana kwao.

Franceso Gabrieli:

"Mtoto wa Abu Sufyan alikuwa tayari amewekwa na Umar katika serikali ya Syria, kazi ambayo alikuwa ameshiriki chini ya amri za kaka yake mkubwa, Yazid. Miaka ishirini ya utawala wa busara ulimpatia mapenzi ya wageni wa Kiarabu waliokuwa wamejikita pale."

(The Arabs, A Compact History, uk. 74, 1963)

Mu'awiyah aliifanya Syria kuwa isiyoshindika, na alijifanya yeye mwenyewe kuwa asiyeweza kudhurika wakati wa ukhalifa wa walezi wake, Umar na Uthman.

E. A. Belyaev:

"Alipokuwa bado ni gavana tu wa Syria, Mu'awiyah aliunda himaya kubwa ya mali kwa ajili yake mwenyewe, ndugu zake, na wafuasi wapiganaji wake, akawa kabaila mkubwa kwa utwaaji wa kiasi kikubwa wa ardhi. Khalifa huyu wa Bani Umayya alikaa juu ya misingi imara ya kiuchumi na alikuwa na majeshi maaminifu zaidi kuliko wapinzani wake wa kisiasa. Alikuwa amegeuka kuwa gavana wa kudumu mwenye nguvu sana wa Syria tajiri na iliyostaarabika mapema sana katika siku za Umar, na baada ya kuwa amemaliza zaidi ya miaka ishirini katika nafasi hii muhimu,

589

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

akawa kiongozi aliyejiandaa upya, wa utawala wa kikabila wa Kiarabu katika Syria."

(Arabs, Islam and the Arab Caliphate in the Early Middle Ages, 1969)

Ilikuwa ni kwa namna hii kwamba Mu'awiyah, mwanasiasa asiye na kifani, wa Waarabu, alivyoibuka kutoka kwenye mabaki ya juhudi zilizoshindwa kufufua zama za upagani, kugeuka, kwanza kuwa adui mkubwa wa Ali ibn Abi Talib, mrithi wa Mtume (s.a.w.w.), na kisha kuwa ndiye mrithi yeye mwenyewe binafsi!

Mu'awiyah alikuwa mtu wa uzushi mwingi.Aliubadili ukhalifa kuwa ufalme, na akajigam-ba wazi wazi: "Mimi ndio wa kwanza wa wafalme wa Kiarabu." Ufalme, kwa kweli unakuwa ni wa kurithiana, na ilibidi uwe ni wa kurithiana katika ukoo wake. Yeye, kwa hiyo, alimfanya mwanawe Yazid kuwa mrithi wake. Hata wale Waislamu ambao mwan-zoni walipuuza au kufumbia macho maovu yake, walishtuka wakati aliposhusha kishindo hiki kwa ajili ya familia yake.

Uteuzi wa Mu'awiyah wa mwanawe Yazid, kuwa kama khalifa, ulikuwa ni uvunjaji wa dhahiri wa kiapo alichokuwa amekitoa kwa Hasan ibn Ali cha kutomteua mwanawe kama mrithi wake mwenyewe. Lakini Mu'awiyah hakuwa mtu wa kuzuiwa na kiapo chochote au kanuni ya maadili. Maadili mikononi mwake yaligeuka kuwa majeruhi wa kwanza.

Mu'awiyah hata hivyo, alikuwa anatambua kwamba Waislamu hawatamkubali kwa hiari Yazid kama khalifa wao. Yeye, kwa hiyo, aliunyamazisha upinzani kwa dhahabu na fedha au kwa hadaa na vitisho. Lakini kama silaha hizi zilishindwa, basi alitumia silaha ngumu kutambulika, ya siri na yenye uwezo wa kumuepushia hatari - sumu. Alikuwa ni "muasisi" katika historia ya Kiislamu, katika fani ya kunyamazisha wakosoaji na maadui zake daima kwa njia ya sumu. Akitarajia upinzani kutoka kwa Hasan kwenye urirhi wa Yazid, alipan-ga kifo chake. Mwanahistoria Mas'ud, anaandika hivi:

"Mu'awiyah alituma ujumbe kwa Jo'dah bint Ash'ath, mke wa Hasan, kwamba kama ataweza kumuua mume wake, yeye atamlipa dirham 100,000, na atamuozesha mwanawe Yazid kwake yeye."

Mu'awiyah aliamsha shauku kwa Jo'dah ya kuwa malkia, na alipompelekea yeye sumu hiyo, kama ilivyopangwa kati yao, akaitoa kwa mumewe, na akafariki kutokana nayo. Mu'awiyah alimzawadia kwa kumpa dirham 100,000, lakini alijitoa kwenye ahadi yake ya kumuozesha kwa Yazid kwa kusema: "Ninampenda mwanangu."

Abdur Rahman bin Khalid bin al-Walid, gavana wa zamani wa Hims (Emassa) alikuwa pia ameuawa kwa njia kama hiyo hiyo. Wakati mmoja Mu'awiyah alitembelea Hims; akaingia Msikitini, na akiihutubia jamaa, akasema:

590

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

" Nimekuwa mzee sana sasa na siko mbali sana na kifo. Mimi, kwa hiyo, nataka kuteua mtu kama mtawala wenu."

Mu'awiyah alikuwa akitegemea kwa siri kwamba ili kumfurahisha yeye, watu wa Hims wangependekeza jina la Yazid kama khalifa atakayefuatia. Lakini hakuna hata mmoja aliyemtaka huyo Yazid aliyeharibika tabia, kama khalifa. Kwa upande mwingine, watu hao walimheshimu sana Abdur Rahman bin Khalid bin al-Walid, na wakapendekeza jina lake kuwa khalifa wa baadae wa Waislamu. Mu'awiyah alificha kutoridhika kwake na akarudi Damascus. Umaarufu wa Abdur Rahman ulimtisha, na akaanza kumtazama kama mpin-zani mwenye uwezekano wa kiti hicho. Yeye kwa hiyo, aliamua kufanya kitu cha kufanya kiti hicho kuwa "salama" kwa ajili ya mwanawe Yazid.

Wakati fulani baadae, Abdur Rahman aliugua, na akawa mgonjwa wa kitandani. Mu'awiyah alimshawishi mganga wa Abdur Rahman kuchanganya sumu katika dawa yake na kuitoa kwake. Katika kufanikiwa kwake, alimuahidi kumpa (huyo mganga), kama zawadi, mapato ya Hims kwa mwaka mmoja mzima. Mganga huyo akakubali, na akampa Abdur Rahman ile "dawa" aliyokuwa ameichanganya. Ilifanya kazi yake na ikamuua. (Isti'aab, juz.II, uk. 401).

Baada ya kifo cha Uthman, Waislamu wengi walimkubali Ali kama mkuu mpya wa dola ya Waislamu. Lakini walikuwepo wengine wengi ambao hawakumkubali, na Mu'awiyah, kwa kweli, alikuwa mmoja wao.

Ahmad ibn Daud Dinawari, mwanahistoria wa Kiarabu, anaandika hivi:

"Ulimwengu wa Kiislamu ulimtambua Ali kama mtawala mkuu wa Uislamu lakini Mu'awiyah na Bani Umayya waliobakia, ambao walikuwa wameifanya Syria ni ngome yao, hawakumkubali."

Ali alituma mjumbe kwa Mu'awiyah kumtaka kiapo chake. Lakini badala ya kumjibu, Mu'awiyah alimweka kizuizini yule mjumbe kwenye baraza lake, na akamwalika Amr bin Al-Aas kutoka Palestina kwa "mashauriano." Alinuia kuorodhesha msaada wake (Amr).

Amr bin Al-Aas

Amr bin Al-Aas alikuwa akiishi Palestina kwa wakati huu, na alikuwa akiyaangalia mand-hari ya kisiasa. Yeye alisisimka kupokea mwaliko kutoka kwa Mu'awiyah, na aliruka kuikamata fursa hii. Lakini msaada wake, alimwambia Mu'awiyah, ulikuwa na bei, na ilikuwa ni Misri.

Kwa Mu'awiyah bei hiyo ilionekana kuwa ya juu sana lakini baada ya kusita kidogo alikubali kuilipa kwa kubadilishana na ushsuri na utendaji wa Amr katika vita ambavyo

591

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

alikuwa avifanye dhidi ya Ali, mrithi wa Mtume wa Allah swt., na mtawala wa Waislamu wote. Mu'awiyah alikuwa amteue Amr bin Al-Aas kuwa gavana wake huko Misri kama ikibidi huyu Amr atafanikiwa kuitwaa kutoka kwa Ali. Amr bin Al-Aas alitegemewa kuchukua nafasi muhimu, ikiwa kama ni mwenye kisirani, katika historia ya Uislamu. Alikuwa ni mtu mwenye uwezo wa ajabu . Uwezo wake unathibitishwa na nafasi za juu alizozishika wakati wa ukhalifa wa Abu Bakr na Umar. Kulikuwa na kashfa katika kuzali-wa kwake; alizaliwa katika nyumba ya " kahaba" huko Makka.

Edward Gibbon:

"Kuzaliwa kwa Amr wakati mmoja kulikuwa kwa aibu na maarufu sana; mama yake, kahaba mwenye sifa mbaya, alishindwa kuamua miongoni mwa Makuraish watano; lakini ushahidi wa kufanana ulimuamulia mtoto huyo kuwa wa Al-Aas, aliyekuwa mtu mzima zaidi kati ya wapenzi wake."

(The Decline and Fall of the Roman Empire)

Washington Irving:

"Mmoja wa washambuliaji wa kuogopesha wa Muhammad alikuwa ni kijana aitwaye Amr; alikuwa ni mtoto wa kahaba wa matajiri hapo Makka, anayeelekea kuwa ameshinda katika kuwapumbaza macho Phrynes na Aspasias wa Greece, na ame-hesabu baadhi ya malodi wa nchi hiyo miongoni mwa wapenzi wake. Wakati alipomzaa mtoto huyu, aliwataja baadhi ya wale wa kabila la Kuraish waliokuwa na madai sawa kwenye ubaba. Kitoto hicho kilitangazwa kuwa chenye kufanana zaidi na Al-Aas, aliyekuwa mtu mzima zaidi kati ya wapenzi wake, ambapo kwa nyongeza ya jina lake la Amr, alipata jina la Ibn al-Al-Aas, mtoto wa Al-Aas."

Ulimwengu umetunuku zawadi zake bora kabisa juu ya mtoto huyu mwenye kipaji, kana kwamba kwa kufidia dosari ya kuzaliwa kwake. Ingawa mdogo, alikuwa tayari ni mmoja wa washairi maarufu sana wa Arabia. Alimshambulia Muhammad kwa mashairi mafupi ya vipokeo yenye istihizai na vichekesho.

(The Life of Muhammad) R. V. C. Bodley:

"Kulikuwa na Amr ibn al-Al-Aas, mtoto wa kahaba mmoja mrembo sana wa Makka. Wakubwa wote wa Makka walikuwa ni marafiki zake, kwa hiyo yeyote, kuanzia Abu Sufyani kwenda chini, angeweza kuwa ndiye baba yake Amr. Kwa kadiri mtu yeyote ambavyo angeweza kuwa na hakika, angeweza kujiita mwenyewe Amr ibn Abi Lahab au ibn al-Abbas au ibn yoyote yule miongoni mwa wakubwa wa juu kumi wa Kiquraishi."

(The Messenger, New York, uk. 73, 1949)

592

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Makuraishi wakati mmoja walimtuma Amr kama balozi wao kwenye baraza la Abyssinia kudai kurudishwa kwa wakimbizi wa Kiislamu kutoka Makka ambao walitafuta hifadhi huko. Ujumbe wake, bila kutegemea, ulishindwa.

Mnamo mwaka 629 Amr aliukubali Uislamu. Baada ya kusilimu kwake, Mtume alimtuma yeye, kwa mara chache, kama kapteni wa misafara iliyoshambulia makabila ya wapagani. Msafara muhimu sana ambao aliuongoza wakati wa uhai wa Mtume, ni wa mashambulizi ya Dhatus-Swalasil ambamo aliongoza kundi la watu 500, miongoni mwao akiwemo Abu Bakr, Umar bin al-Khattab na Abu Ubaidah ibn al-Jarrah. Msafara huu, kwa bahati uli-fanikiwa.

Amr alikuwa gavana wa Umar huko Misri. Lakini wakati Uthman alipokuja kuwa khalifa, alimfukuza, na yeye akarudi Madina akijikaza kwa mfundo. Alikuwa ni "mtaalamu" kamili katika kubuni njama, katika kupandikiza mifaraka na katika kueneza chuki. Alizitumia taaluma hizi dhidi ya Uthman, na akafanya shambulizi la kumpaka matope na uchongezi dhidi yake. Alijigamba wazi wazi kwamba amewachochea hata wale wachunga kondoo wa huko mlimani kumuua Uthman, na kujigamba kwake hakukuwa ni kupayuka ovyo. Uthman alikuwa amemwingiza kwenye mateso ya kisiasa lakini hakuwa na nia ya kuteseka katika ukimya milele wakati alikuwa anaweza kumuwaza yeye (Uthman) akimd-hihaki huko Madina, na aliweza kuwaona (mawazoni) wapenzi wake Uthman wakipiga makelele ya furaha huko Misri - jimbo ambalo yeye Amr alikuwa ameliongeza kwenye himaya. Aliazimia kuchukua hatua yeye mwenyewe.

Kupoteza madaraka ni moja ya matukio machungu sana ambayo yanaweza daima kumte-sa mtu. Sio tu anakoseshwa uwezo wa kupanga matukio bali pia wa kuonekana kwa ishara na nishani za cheo.

Talha na Zubeir hawajawahi kupanga matukio. Walifanya jaribio la kutwaa ukhalifa kwa nguvu lakini walishindwa. Jaribio hilo halikuwagharimu maisha yao tu bali pia na sifa zao. Amr bin Al-Aas, kwa upande mwingine, alikuwa hasa amepanga matukio, na yaliyo maarufu vilevile. Lakini ghafla, Uthman akamfanya yeye kuwa duni. Tokea muda huo, yeye alijawa na kutaka kulipiza kisasi, na "alishughulika" kwa bidii na bila kuchoka, kumuangamiza muanzilishi wa kuvunjika moyo kwake - Uthman - khalifa aliyekuwa madarakani.

Punde tu Madina ilikuwa tayari kulipuka. Amr alikuwa amejijengea, katika siku za nyuma, kasri moja huko Palestina. Kabla tu ya mlipuko huo, alitoroka Madina, na akaenda kuishi kwenye kasri lake. Kisha akakaa kuangalia jinsi juhudi zake zitakavyoweza kuzaa matun-da. Aliposikia kwamba Uthman ameuawa, alisisimka sana, na akafurahia waziwazi juu ya "kufanikiwa" kwake.

593

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Uwezo na kuona mbali kwa Amr kulikuwa hakuna shaka yoyote. Kwa kuondoka Madina katika wakati muafaka, na kwa "kuishi maisha ya kijijini" huko Palestina, alijiokoa mwenyewe sio kutokana na shitaka tu, wakati wa uhai wake mwenyewe, la kupanga maua-ji ya Uthman, lakini pia kutokana na shitaka la maandishi ya historia.

Jambo moja ambalo Amr alilifahamu lilikuwa kwamba asingeweza kujipendekeza kwa Ali. Waliwakilisha mitindo miwili isiyopatana, na falsafa mbili zisizopatana. Lakini alijua kwamba ushirikiano na Mu'awiyah ulikuwa unawezekana. Wote walikuwa wabinafsi wenye akili sana. Wote walishiriki katika mauaji ya Uthman, mmoja kwa kuwachochea watu kumuua, na mwingine kwa kuzuia kwa makusudi misaada yote juu yake. Sasa wote walikuwa na shauku ya kuvuna matunda ya mafanikio yao.

Kwa hiyo, Amr bin Al-Aas na Mu'awiyah bin Abu Sufyan - wale mabingwa wawili wa njama, wa majungu, wa utata na ukweli wa mashaka, wa ulaghai na udanganyifu, wa mafumbo (kutoeleweka) kwa makusudi na umakini katika lengo - wakabuni ushirikiano, wa kuwa nguzo na kutegemeana wenyewe kwa wenyewe dhidi ya Ali ibn Abi Talib. Ushirikiano wao uliegemea, sio kwenye itikadi bali katika kutathmini maslahi yao ya pamoja. Wakati Mu'awiyah alipompa Amr ile nafasi muhimu katika kampeni yake ya mfumo wa madaraka kama mpanga mikakati mkuu wa kisiasa, yeye (Amr) hakuikubali mpaka malipo ya uhakika haraka yalipopatikana juu yake. Malipo hayo yalikuwa ni Misri.

Kwa kuchukulia kidokezi kutoka kwenye "utawala wa watu watatu" wa Basra, Amr alimshauri Mu'awiyah kuanzisha kampeni ya propaganda dhidi ya Ali akimshutumu kwa mauwaji ya Uthman. Mu'awiyah mara moja akutekeleza ushauri huo, na akafungulia vita baridi dhidi ya Ali.

Katika Msikiti mkuu wa Damascus, bendera ya Bani Umayya ilikunjuliwa kila siku baada ya Swala ya mchana. Kulikuwa na vitu viwili vikivyokuwa vimening'inia kwenye bendera hiyo. Kimoja kilikuwa ni shati lililokuwa na madoa ya damu ambalo Uthman anadaiwa kuwa alikuwa amelivaa wakati anauawa, na kingine kilikuwa ni vidole vya Naila, mke wake, vilivyokuwa vimekatwa. Watu wa Syria walitembea kuizunguka bendera hii, wakil-ia, na kupiga makelele na kumlaani Ali, watu wa familia yake, na Bani Hashim, na kuapia kwamba watamalizia kisasi chao juu ya wauaji wa Uthman. Maprofesa Sayed Abdul Qadir na Muhammad Shuja-ud-Din wameandika katika kitabu chao, History of Islam kwamba huu ulikuwa ni mwanzo wa desturi iitwayo "tabarrii."

Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas waliichochea Syria kwenye mpagao, kiasi kwamba kila Msyria alikuwa ameingiwa na wazimu dhidi ya Ali, na akawa na kiu na damu yake. Baada ya miezi mitatu, mjumbe wa Ali alirudi Kufa kumtaarifu yeye kushindwa kwa ujumbe wake huko Damascus.

594

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mu'awiyah alikuwa amechagua vita dhidi ya Ali. Lakini Ali hakutaka vita. Alikuwa na shauku kubwa ya kuepuka vita. Hakuna kitu kilichokuwa kinachukiza sana kwake kama kuona Waislamu wanauana wenyewe kwa wenyewe.

Akitarajia kinyume cha matumaini, lakini bila kutaka kubakisha juhudi yoyote ile, Ali alimuandikia barua Mu'awiyah. Katika barua yake, hakujaribu kumkumbusha Mu'awiyah kwamba Mtume wa Allah swt. mwenyewe alikuwa amemteua yeye Ali kama mtawala wa Waislamu wote. Kwa Mu'awiyah, yeye Ali alijua, hoja hii haitakuwa na uzito sana. Badala yake, alichukua mwelekeo mwingine wa hoja ambao ulikuwa na uwezekano wa kuwa na "mvuto" kwake. Madhumuni ya barua yake yalikuwa kama ifuatavyo:

"Nakuomba umtii Allah na Mtume Wake, na ujiepushe na kufanya kitu chochote kinyume na maslahi ya Waislamu. Wewe unajua kwamba watu wale wale ambao wal-itoa kiapo chao cha utii kwa Abu Bakr na Umar, sasa wamenipa mimi kiapo chao cha utii. Hakuna nafasi ya ubishani juu ya suala hili. Wewe unajua kwamba Muhajirina na Ansari waliwachagua makhalifa waliotangulia, na sasa wamenichagua mimi. Waislamu wengine pia wamenipa kiapo chao cha utii. Wewe pia, kwa hiyo, unapaswa kunipa mimi kiapo chako cha utii. Umeeneza fitna na uongo mwingi kwa kisingizio cha kisasi cha damu ya Uthman ambapo unatambua vema kabisa ni nani aliyeimwa-ga damu hiyo. Baada ya kutoa kiapo cha utii kwangu mimi, wewe wasilisha kesi ya kuuawa kwa Uthman, nami nitaihukumu kwa kuzingatia Kitabu cha Allah swt. na vigezo vya Mtume Wake, ili kwamba ukweli na uongo viweze kujitenga."

Lakini Mu'awiyaha hakutaka kuacha tamaa zake. Aliamini kwamba kitu kimoja kina-choweza kumkwamisha katika kufanikisha tamaa zake, kilikuwa ni amani. Yeye, kwa hiyo, alijionyesha mwenyewe kama tu "mwenye mzio" wa vita kama wale wa "utawala wa watu watatu" wa Basra walivyofanya kabla yake. Alikuwa na jibu moja tu kwenye maombi ya Ali juu ya amani, nalo lilikuwa ni vita.

Kwa mtazamo wa Mu'awiyah, kelele za kisasi kwa kifo cha Uthman, ilikuwa ni uvumbuzi mzuri sana wa kupigana dhidi ya Ali. Alilia machozi mengi sana ya mamba (ya ghilba) kwa ajili ya damu ya Uthman lakini kwa tabia yake yeye mwenyewe, wakati wote wa kabla na baada ya kuuawa kwa Uthman, alithibitisha kwamba hakumjali kabisa Uthman. Aliandaa jeshi la wapiganaji 80,000 wa kupigana dhidi ya Ali lakini hakutuma angalau watu wachache kwenda Madini kuuvunja mzingiro wa kasri la Uthman, na kuokoa maisha yake!

Uthman angeweza kuliwazika kwa kujua kwamba siku ingefika ambapo wakosoaji wake watageuka kuwa wapenzi wake, na maadui zake kuja kuwa watetezi wake - baada ya kifo chake. Alikuwa na wakosoaji wengi sana hapo Madina, miongoni mwao wakiwa ni Aisha, Talha na Zubeir lakini mkali sana kuliko wote, kama ilivyoelezwa kabla, alikuwa ni Amr bin Al-Aas. Huyu kwa kweli, anaweza kuwa ndiye mpangaji mwenyewe hasa wa mauaji

595

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ya Uthman.

Lakini kwa ugeuzaji wa mambo usio wa kawaida, yeye - Amr bin Al-Aas - yule mshiri-ka wa Mu'awiyah - sasa alikuwa anatembea, mbele ya jeshi la Syria, kudai "haki" juu ya kifo cha Uthman, kati ya watu wote - kutoka kwa Ali!

Kama Talha na Zubeir - watangulizi wake maarufu katika kazi ya kutafuta kisasi - Amr bin Al-Aas naye pia ni somo la kuvutia katika kugeuza tabia upinduaji wa uhusikanaji na dhihaka. Alikuwa ni mtu mgumu, kitendawili na kigeugeu anayedharau majaribio katika uchambuzi, upambanuzi na uainishaji wa mwenendo.

Moja ya malengo ya Mu'awiyah ya kuanzisha vita vya wasiwasi dhidi ya Ali lilikuwa ni kumlazimisha yeye kutwaa sera ya ukomeshaji wa kikatili juu ya wale watu wote waliokuwa wamekuja Madina kutoka majimboni kumuona Uthman. Sera kama hiyo inge-muingiza Ali katika utatanishi wa mapigano yasiyo na mwisho. Lakini Ali hakutwaa sera ya ukomeshaji. Alitwaa sera ya ushawishi, kwa masikitiko makubwa sana ya Mu'awiyah. Mpango wa Mu'awiyah haukufanya kazi.

Mu'awiyah alidai kutoka kwa Ali, kama wale "watawala watatu" wa Basra walivyofanya, kukabidhiwa kwake watu wasio na idadi ambao yeye alidai, walishiriki moja kwa moja au kwa kificho, katika mauaji ya Uthman. Madai haya yanazua maswali ya msingi kama vile:

1.   Hivi gavana wa jimbo la nchi anayo haki ya kudai kutoka kwenye serikali kuu iliyowekwa kisheria kwamba imkabidhi yeye watuhumiwa wa kesi ya mauaji, hata kama mauji hayo hayakutokea kwenye jimbo lake husika? Na je, anayo haki ya kuitishia hiyo serikali kuu kwamba kama haikutekeleza madai yake, yeye ataanzisha vita dhidi yake?

2. Mu'awiyah hakuwa ama mrithi wala ndugu wa karibu wa Uthman; alikuwa ni jamaa wa mbali tu. Kuna mfano wowote katika historia ya mahakama ya nchi yoyote ile ambamo, sio yule ndugu wa karibu, bali jamaa wa mbali anayedai kutoka serikali kuu kwamba imkabidhi mamia au maelfu ya wale watu ambao anawashuku kuwa washiriki katika mauaji? Je, anaweza kuchukua sheria mikononi mwake mwenyewe? Serikali kuu ya nchi inaweza kuruhusu raia zake kuchukua sheria mikononi mwao wenyewe? Kama inaweza, kuna chochote kitakachobakia katika madaraka yake, na kutasalia chochote katika sheria na taratibu?

3.  Mu'awiyah aliandikiana barua nyingi na Ali. Katika mojawapo aliandika: "Tutawawinda wauaji wa Uthman katika kila pembe ya dunia, na tutamuua kila

596

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mmoja wao. Hatutapumzika katika kazi hii mpaka, ama tunawaua wote au tunakufa sisi wenyewe." Azimio la kupendeza kwelikweli! Lakini wakati Mu'awiyah alipoku-ja kuwa khalifa, alilitekeleza azimio lake mwenyewe?

Baada ya kujiuzulu kwa Hasan bin Ali katika ukhalifa mwaka 661 A.D., Mu'awiyah akawa mkuu wa dola ya Waislamu. Wauaji wote halisi au wa kushukiwa walikuwa wanaishi katika himaya yake. Je, alimkamata yoyote kati yao, ukiachiliambali kumuua yoyote kati yao? Je, alijitahidi japo kiasi cha kuanzisha uchunguzi rasmi katika mauji ya Uthman? Hakufanya hivyo. Shauku yake ilikuwa ni kuukamata ukhalifa. Mara alipofanikiwa na hilo, akamsahau Uthman!

Ukweli ni kwamba Mu'awiyah kwa kweli alitaka Uthman auawe. Yalikuwa ni matumaini yake kwamba kutakuwa na ghasia baada ya kifo cha Uthman, na ataweza kufanya hila ndani yake msukumo wake wa kutwaa madaraka. Pale alipodai kutoka kwa Ali kukabidhi-wa wale "wauaji" wa Uthman, alikuwa anajua kwamba walikuwa wametawanyika katika Hijazi, Iraqi na Misri, na kwamba ilikuwa ni vigumu kuwakusanya pamoja. Lakini ukichukulia kwamba ilikuwa inawezekana kuwakamata, bado haikuwa ni rahisi kuwaua wote. Lakini kama ingewezekana kuwaua wote, bado ingekuwa sio haki kuwaua wote kwa sababu ya kuuawa kwa mtu mmoja.

Kutafuta na kulipiza kisasi kwa ajili ya mauaji, ni haki ya mrithi/warithi wa muathirika, na ni wajibu wa serikali kutekeleza haki. Mu'awiyah alikuwa sio mrithi wa Uthman wala alikuwa sio kiongozi wa serikali ya Waislamu. Alikuwa si zaidi ya mrithi kuliko Aisha, Talha na Zubeir walivyokuwa. Shauku yake na yao ilikuwa ni katika kuukamata ukhalifa tu.

Kama Mu'awiyah hakuweza kushughulika katika wakati muafaka kuokoa maisha ya Uthman, alikuwa bado anayo nafasi ya kuthibitisha kwamba alikuwa ni mlipiza kisasi wa kweli wa kifo chake. Wakati walipiza kisasi wengine watatu, yaani, Aisha, Talha na Zubeir walimpinga Ali, Mu'awiyah angekwenda kwenye msaada wao. Hata hivyo, wote wanne walikuwa wametiwa msukumo na nia hiyohiyo. Mauaji ya Uthman yameamsha kiu ya damu kwao wote. Kufanana kwa lengo kulipaswa kuunda uhusiano mzito baina yao. Lakini sababu yoyote ile iliyomzuia Mu'awiyah kwenda Madina kuokoa maisha ya Uthman, pia ilimzuia kwenda Basra kuwaongeza nguvu washirika wake wa "kiroho".

Madai ya kwamba Mu'awiyah hakuwa na haja yoyote na Uthman, akiwa hai au amekufa, yanatiwa nguvu zaidi na majibu yake ya swali aliloulizwa na binti ya Uthman. Wakati alipokuwa khalifa, alitembelea Madina. Hapo Madina, aliitembelea familia ya Uthman ambaye binti yake, aitwaye Aisha, alimuuliza yeye, kwa kukusudia hasa, kama alikuwa bado anakumbuka chochote kuhusu tangazo lake alilokuwa akilirudia mara kwa mara kwamba alikuwa anatafuta kulipiza kisasi kwa ajili ya kifo cha baba yake.

597

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mu'awiyah alimjibu binti huyo kama ifuatavyo:

"Nimefanikiwa katika kurudisha amani katika nchi baada ya matatizo mengi, na wewe unapaswa sasa kufurahi kwamba unaitwa binti ya khalifa mmoja na mpwa wa khalifa mwingine. Lakini kama kwa ajli yako, ningekuwa mwenye kuwakamata na kuwaua wale wauaji wa baba yako, basi amani ile ingetoweka kwa mara nyingine tena. Ikiwa itatoweka, basi ninaweza kupoteza yale madaraka ambayo nimeyapata baada ya jitihada ngumu kama hizo; na kama hilo likitokea, basi wewe utashushwa kwenye hali ya mwanamke wa kawaida."

(Iqd-ul-Farid)

Mu'awiyah, myakinifu, alikuwa na uwezo mkubwa mno na wa kushangaza wa kutumia lugha ya utatanishi!

Kwa Mu'awiyah, kufikia malengo yake, njia zote zilikuwa ni nzuri. Hapakuwa na kitu ambacho yeye hakuweza kukifanya ili kuwa khalifa wa Waislamu. Aliweza kwa kweli, kwenda mbali zaidi kiasi cha kuweza kuwa mtwana wa mamlaka yasiyokuwa ya Kiislamu kupigana dhidi ya mrithi halali wa Mtume wa Allah swt., na mtawala wa Waislamu wote. Kwa kufanya hivyo, alikuwa anaunga mkono sera ambayo ilijitokeza kwenye mizizi hasa ya Uislamu.

Sir John Glubb:

"Ili kuweza kuwa huru kumkabili mpinzani wake (Ali), Mu'awiyah alikuwa amekamilisha makubaliano ya kusitisha vita na Byzantium ambamo alikubali kulipa ushuru wa mwaka kwa Mfalme."

(The Great Arab Conquests, uk. 338, 1967) D. M. Dunlop:

"Kabla Mu'awiyah hajafanikiwa kwenye Ukhalifa, wakati baada ya Siffin alibakia kwenye makabiliano na Ali, alijiimarisha mwenyewe katika mpaka wake wa kaskazi-ni kwa makubaliano ya kusitisha vita na Byzantium, kwa masharti ambayo kwamba alikubali kulipa ushuru ambao ulikuwa unatambulika, kwa Mfalme Constans II, na mnamo mwaka 678 kuelekea mwishoni mwa Ukhalifa wake, baada ya kushindwa kwa uvamizi mkubwa wa Waarabu juu ya Constantinople katika vile vinavyoitwa Vita vya Miaka Saba na shambulio la Mardaites katika mpaka wake wa kaskazini, Mu'awiyah akalipa tena ushuru kwa Mfalme, wakati huu akiwa Constantine IV. Katika tarehe za baadaye majeshi ya Byzantium yaliivamia Syria na wakaitwaa tena Antiokia na Aleppo."

(Arab Civilization to A.D. 1500, 1971) 598

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Hiki "cheo" kipya ambacho Mu'awiyah alikipata kama mtwana wa mfalme wa Byzantium, kilimpa uhuru wa kupigana vita dhidi ya Ali ibn Abi Talib, mrithi wa Muhammad, Mtume wa Allah swt. Alipigana dhidi ya Kiongozi wa Waumini, dhidi ya wakongwe wa Badr, dhidi ya masahaba wa ule Mti wa Kiapo, na dhidi ya Muhajirin na Ansar akiwa amelind-wa na Wakristo wa Himaya ya Roma Mashariki!

Lakini kwa Mu'awiyah, kuwa mwenye "kigeugeu," dau halikuwa lazima liwe la ukubwa kama taji na ufalme. Aliweza kuwa kigeugeu katika mambo yenye umuhimu mdogo pia. Alikuwa kwa mfano, na hisia za kupenda sana pesa, na aliamini kwamba katika kuichuma, ugumu mwingi mno "uliopitwa na wakati" katika matumizi ya kanuni za Kiislam haukuwa wa lazima hasa. Jambo muhimu kwake lilikuwa ni kutengeneza pesa. Ibn Ishaq, mwan-dishi wa wasifu wa Mtume (s.a.w.w.), amekwisha kunukuliwa tayari juu suala la kukamat-wa na Mu'awiyah kwa mali ya al-Hutat bin Yazid al-Mujashi'i, "kaka" yake, wakati wa kifo chake. "Udugu" huu ulifanya kazi wote kwa manufaa yake Mu'awiyah. Ili kujaza mifuko yake, aliweza hata kuuza masanamu. Mu'awiyah, mrithi wa Abu Bakr, Umar na Uthman, na khalifa wa Waislamu, aliweza kuwa mchuuzi wa masanamu kama alitegemea kwamba angeweza kupata faida katika shughuli hiyo.

Sir John Glubb:

"Sicily ilivamiwa zaidi ya mara moja na kundi la manowari za Waarabu wakati wa utawala wa Mu'awiyah. Hadith ya udaku inasimulia kwamba safari moja wavamizi walibeba 'masanamu' ya dhahabu na fedha, yaliyotapakaa lulu. Huenda pengine ina maana ya mabadiliko ya fikira za Waarabu kwamba huyu khalifa badala ya kuangamiza kabisa machukizo kama hayo, aliyapeleka India, ambako alidhania kwamba mauzo yao yatampatia bei kubwa."

(The Great Arab Conquests, uk. 355, 1967)

Uuzaji wa masanamu wa Mu'awiyah bin Abu Sufyan ulikuwa ni uibukaji wa wazi wa marudio ya uovu wa Bani Umayya. Vitendo vyake vilichochewa na juu ya misingi, sio ya manufaa yaliyoonyeshwa (ya Kiislamu), bali ya yaliyozoeleka (ya kipagani), ambayo yalikuwa ni sifa bainifu za jina na nasaba ya Bani Umayya. Yeye alikuwa, inavyoelekea, akitafuta, labda kwa kujificha, ule "Ujinga Uliopotea" wa nasaba yake. Yeye aliurudisha na kuupamba ule Ujahiliya wa kabla ya Uislamu. Upinzani wake kwa Ali, kwa hiyo, haukuwa tu au hata kimsingi wa kimaumbile tu; ulikuwa wa udhanifu. Uislamu kama nguvu ya kimaadili, ulipambana na tishio baya sana kutoka kwa Mu'awiyah na kwa Bani Umayya.

599

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Vita vya Siffin

Kumgeuza mawazo Mu'awiyah asipigane vita dhidi ya waislamu, Ali alitumia zile hoja zote ambazo alikuwa amezitumia, hapo kabla, katika nasaha zake kwa Aisha, Talha na Zubeir kwa lengo hilo hilo, na matokeo katika masuala yote yalikuwa ni yale yale. Katika mawazo ya maadui zake wote, amani ingeweza tu kuchanganya yale matatizo magumu tayari ya Dar-ul-Islam. Wao waliona dawa moja tu kwa ajili ya matatizo hayo, nayo ilikuwa ni vita.

Safari hii, hata hivyo, Ali alikabiliwa na adui aliyekuwa na hila nyingi zaidi, mjanja, mwenye kudhuru kwa siri na hatari zaidi kuliko ule "utawala wa watu watatu" wa Aisha, Talha na Zubeir ulivyowahi kuwa. Kwa kweli, alikuwa staidi sana kiasi kwamba katika kulinganisha, Talha na Zubeir walikuwa ni washamba kweli kweli wa kisiasa.

Huko Basra, kile kikundi cha waasi kilikuwa ni muungano wa maslahi yanayotofautiana, na wanachama wake waliunganishwa pamoja tu na chuki yao ya pamoja juu ya Ali. Ulikosa umoja wa lengo. Aisha alikuwa anapigana ili kumpandisha mpwa wake, Abdallah bin Zubeir, kwenye kiti cha ukhalifa. Lakini Talha na Zubeir walikuwa wasimkubalie katika suala hili; wao wenyewe walikuwa ni wagombea wa zawadi hiyo. Kwa hiyo muungano wao ulikuwa sio kabisa ule wa 'utawala wa watu watatu' wa mmoja kwa wote na wote kwa mmoja ambao wafuasi wao wangependa uwe.

Ule utawala wa watu watatu wa Basra ulitiwa mikosi na kuchechemezwa na wale washau-ri wake waliogawanyika lakini Mu'awiyah hakuwa hivyo. Alitafuta ushauri wa Amr bin Al-Aas na wengineo lakini yeye mwenyewe ndiye aliyefanya maamuzi yote.

Ali alikuwa bado anatafuta umoja. Umoja wa umma wa Muhammad ulikuwa unatishiwa na mifadhaiko na kero, na yeye alikuwa anajitahidi kuulinda na kuuhifadhi. Lakini kwa bahati mbaya, maadui zake hawakushiriki naye katika shauku hii. Hamu yao pekee ilikuwa ni kuuchanilia mbali umoja wa umma, na walifanikiwa katika kuuchana.

Wakati wa majira ya kuchipua (spring) ya mwaka 657, Mu'awiyah aliondoka Damascus pamoja na jeshi lake kwenda kupigana vita huko Iraqi. Aliuvuka mpaka na kusimama kwenye kijiji kiitwacho Siffin - kwenye ukingo wa mto Euphrates. Kitendo chake cha kwanza kilikuwa ni kuumiliki ule mwambao.

Kusikia taarifa za kusonga mbele kwa jeshi la Syria, Ali alimteua Aqaba ibn Amr Ansari kama gavana wa Kufa, akamwita Abdallah ibn Abbas kutoka Basra aje kuongozana naye, na akaondoka Kufa pamoja na jeshi lake kwenda Siffin mnamo April 657. "Wakongwe Sabini wa vita vya Badr na Masahaba 250 wa Mti wa Kiapo walitembea chini ya bendera

600

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

yake pamoja na jeshi hilo kwenye kingo za mto Euphrates kuelekea Siffin." (Mustadrak, juz. III).

Walipowasili Siffin, jeshi la Ali lilikuta njia yake ya kufikia mwambaoni imezuiwa na kikosi kizito cha majeshi ya Syria. Ali alimtuma Sa'sa' ibn Sauhan, sahaba wa Mtume, kwenda kwa Mu'awiyah, kumtaka awaondoe wapiga mishale wake kutoka pale mtoni, na kuruhusu uhuru wa kufikia maji, kwa kila mtu. Mu'awiyah, bila shaka, alikataa kufanya hivyo ndipo Ali alipoviamuru vikosi vyake kuchukua ule mwambao kwa nguvu. Vikosi vyake viliwafukuza Wasyria, na wakautwaa ule mwambao. Sasa kukawa na fadhaa na hofu ndani ya kambi ya Mu'awiyah. Alibuni mzuka wa kifo ndani ya jangwa kwa kiu. Lakini Amr bin Al-Aas alimhakikishia kwamba Ali kamwe hatamnyima maji mtu yoyote.

Watu wa Syria walikuwa hawana njia ya kuyafikia maji. Majemadari wa Ali walikuwa na mawazo kwamba watamrudishia Mu'awiyah sarafu yake mwenyewe (kulipiza kile ali-chokifanya). Hapakuwa na kitu rahisi zaidi kwao kuliko kuliacha lile jeshi lote la Syria kufa kwa kiu. Lakini Ali kwa uunngwana kabisa akawalaumu kwa kutaka kwao kuigiza mfano ambao wao wenyewe waliushutumu, na akatangaza hivi:

"Mto huu ni wa Mwenyezi Mungu. Hakuna kizuizi juu ya maji kwa mtu yeyote yule, na yeyote anayeyataka, anaweza kuyachukua."

Mikwaruzano midogo midogo ilianza wakati wa Dhil-Hajj 36 H.A., Mei 657. (Dhil-Hajj ndio mwezi wa mwisho wa kalenda ya Kiislamu) na iliendelea hapa na pale kwa majuma machache yaliyofuatia. Kwa kuingia kwa Muharram (mwezi wa kwanza wa mwaka wa Kiislamu), mapigano yakasimamishwa kwa mwezi mmoja. Wakati wa mwezi huu wa kusi-tisha mapigano (Muharram), Ali alianzisha upya kutafuta kwake amani lakini juhudi zake za kutatua matatizo hayo kwa majadiliano, au kupata ufumbuzi ambao utaondoa mapigano miongoni mwa Waislamu, hazikufanikiwa kwa sababu nyepesi tu kwamba mshindani wake, Mu'awiyah, hakuiona amani kama ndio uchaguzi unaofaa. Alikataa maridhiano kwa sababu yalikuwa hayachukuani na maslahi yake.

Ali angeweza kufanywa asiye na matarajio mema na undumilakuwili, misiba na matukio machungu - bado yeye alikuwa tayari kuamini, licha ya mifano yote, katika matazamio ya amani, na alikuwa tayari kuyafanyia kazi.

Pale siku ya mwisho ya Muharram ilipopita, na mwezi wa Safar ukaanza, Ali alimtuma Merthid ibn Harith kupeleka ujumbe kwa watu wa Syria. Alisimama mbele ya jeshi la Syria, na akausoma ujumbe huo kama ifuatavyo:

"Enyi watu wa Syria! Ali, yule Kiongozi wa Waumini, anakufahamisheni ninyi kwamba aliwapeni kila nafasi ya kuthibitisha ukweli na kujiridhisha ninyi wenyewe.

601

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Alikualikeni ninyi kufuata Kitabu cha Allah swt., lakini hamkusikiliza hata kidogo. Sasa hakuna jingine zaidi analoweza kuwaambia. Allah hawapendi wale wanaoisali-ti Haki."

(Tarikh Tabari, juz. IV, uk. 6)

Wakati majeshi hayo mawili yalipokabiliana, Ali alitoa maagizo yafuatayo kwa vikosi vyake kama ambavyo alifanya kabla ya vita vya Basra (vita vya Ngamia):

"Enyi Waislamu! Subirini adui yenu aanzishe uhasama, na mjitetee wenyewe pale atakapokushambulieni. Kama mtu yeyote kati ya maadui anataka kuikimbia vita na kuokoa maisha yake, mwacheni afanye hivyo. Ikiwa Allah atakupeni ushindi, msi-ipore kambi ya adui; msiikatekate miili ya waliokufa wala kuwanyang'anya deraya na silaha zao, na msiwasumbue wanawake zao. Juu ya mambo yote, mkumbukeni Allah nyakati zote."

Ali aliyahamisha na kuyapanga upya majeshi yake. Alitoa uongozi wa vikosi vya upande wa kulia kwa Abdallah ibn Abbas, vile vya upande wa kushoto kwa Malik ibn Ashtar, ambapo yeye mwenyewe aliongoza pale katikati. Pamoja naye walikuwepo masahaba na marafiki za Muhammad, (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt., miongoni mwao Ammar ibn Yasir. Wakati huu, majeshi ya Syria yakashambulia, na Ali akayaashiria majeshi yake kuwafukuza,

Vita vya Siffin vikawa vimeanza.

Ammar ibn Yasir alikuwa na umri zaidi ya miaka 70 kwa wakati huo lakini moto wa imani juu ya Allah swt., na mapenzi kwa Mtume Wake, Muhammad (s.a.w.w.), ulichoma kwa ukali sana kifuani mwake, na alipigana kama vijana wadogo. Kuongezea kwenye mguso wa kuvutia wa mapambano hayo, alibeba silaha zilezile ambazo kwazo alikuwa amepi-gana, miaka mingi ya nyuma, akiwa pamoja na Muhammad Mustafa, dhidi ya washirikina wa Makka huko Badr.

Adui aliyekutana naye Ammar hapo Siffin alikuwa amejigeuza kama Muislamu lakini hakuweza kumhadaa yeye Ammar. Macho yenye kupenyeza ya Ammar yaliutambua ule uso uliokuwa nyuma ya barakoa. Lazima atakuwa amefurahishwa sana kukutana na adui yule wa siku nyingi, baada ya kupita kwa miaka mingi, katika pambano jipya. Kwake yeye vile vita vya Siffin vilikuwa vyenye kuleta kumbukumbu ya vita vya Badr. Kwa mara nyingine tena alikuwa anapigana, upande wa Muhammad na mshika-makamu wake, Ali, dhidi ya maadui zao. Alivyokuwa akiwapiga watu wa Syria, alibakia akisema:

"Tunapigana dhidi yenu leo juu ya tafsiri ya Qur'an kama vile tu wakati wa Mtume wetu, tulipigana dhidi yenu juu ya kushushwa kwake."

602

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Imam Ahmad bin Hanbal katika Musnad yake, na Hakim katika Mustadrak yake, wames-imulia kwa idhini ya Abu Said al-Khudri, sahaba wa Mtume (s.a.w.w.) kwamba Mtume wa Allah alimwambia Ali:

"Ewe Ali! Kama vile ninavyopigana dhidi ya waabudu masanamu juu ya kushushwa kwa Qur'an, siku moja utapigana juu ya tafsiri yake."

Ammar alisita kwa muda mchache kuzungumza na wapiganaji wenzie, na akawaambia:

"Rafiki zangu! Mshambulieni adui. Hakuna muda wa kukawia na kusita. Milango ya Peponi iko wazi kabisa leo hii lakini kuruhusiwa kuingia, mnapaswa kuthubutu panga na mikuki ya maadui hawa wa Allah na Mtume Wake. Washambulieni. Vunjeni panga zao, mikuki yao, na mafuvu yao, nanyi mtaiingia milango ya pepo na baraka za milele, na huko, mtakuwa pamoja na Muhammad, Kipenzi cha Allah swt. Mwenyewe."

Ammar mwenyewe aliongoza mashambulizi, na mara tu alikuwa yuko ndani kabisa ya safu za Wasyria. Katikati ya mapambano, alijisikia kuwa na kiu, alizidiwa na joto. Alirudi kwenye safu zake kutuliza kiu yake, na akawaomba wenzie kumletea maji. Ilitokea tu kwamba kwa muda ule, hawakuweza kupata maji popote pale, lakini mmoja wao alipata maziwa, na akamletea yeye kikombe kimoja.

Pale Ammar alipokiona kikombe cha maziwa mbele yake, alihisi mtukuto wa kusisimua mwilini mwake. Midomo yake ikajikunja katika tabasamu pana, naye akaguta kwa mshangao: Allah-u-Akbar (Mola ni Mkubwa). Mtume wa Allah swt., alizungumza kweli tupu." Waliokuwa wamesimama pembeni wakamwomba aeleze maana ya mshangao wake, na yeye akasema:

"Mtume wa Allah aliniambia mimi kwamba chakula changu cha mwisho katika dunia hii kitakujakuwa ni maziwa. Sasa ninajua kwamba wakati wa mimi kukutana naye umekwishafika. Nilikuwa nikiusubiri wakati huu kwa muda mrefu sana, kwa hamu kubwa. Hatimaye, huu hapa. Al-Hamdu lillah."

Ammar bin Yasir alibadilika kwa mapenzi kwa Allah swt., na mapenzi kwa Mtume Wake, Muhammad (s.a.w.w.). Akayanywa yale maziwa, akapanda juu ya farasi wake, na kisha akatumbukia kwenye safu za Wasyria. Ghafla, akamuona Amr bin Al-Aas akiwa katikati yao, na akapiga kelele:

"Laana iwe juu yako, Ewe mtumishi wa Mu'awiyah! Uliiuza dini yako kwa kubadil-ishana na Misri. Umesahau utabiri wa Mtume wa Allah aliposema kwamba kikundi cha watu waovu kitakuja kuniua mimi? Sikiliza na tazama tena. Wewe hunitambui

603

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mimi? Mimi ni Ammar, Ammar bin Yasir, rafiki wa Muhammad Mustafa."

Amr, bila shaka alikuwa ameyapima machaguo yote, na alikuwa ameamua kupendelea Misri. Lakini alinyamaza kimya, akijua kwamba kufunua kinywa chake kutakuwa ni kukubali kosa lake, na chochote atakachokuwa amekisema, atajifichua mwenyewe tu.

Ammar alikuwa anachukua kipando cha mara ya mwisho katika dunia hii. Baadae kidogo tu alikuwa aingie Peponi ambako rafiki na kipenzi chake, Muhammad (s.a.w.w.) alikuwa akimsubiri yeye, tayari kwa kumkaribisha na kumpangusa mavumbi ya Siffin kutoka kwenye nywele zake zenye mawimbi na uso wake mng'aavu kama vile miaka mingi ya nyuma, alivyokuwa amempangusa mavumbi ya Handaki la Madina kutoka kwenye nywele zake zenye mawimbi na uso wake mng'aavu.

Akishambulia kushoto na kulia, Ammar alisonga mbele, akiwa hana habari kabisa juu ya hatari zote juu yake. Kichwa chake na uso viligandamana na damu na vumbi kiasi kwamba hakuweza kutambulika. Kwa wakati ule, mpiganaji mmoja wa Syria, akilenga shabaha kali sana, alimrushia mkuki ambao ulimpata kwenye moyo wake, na akaanguka kutoka kwenye farasi. Katika kile kitendo cha kuanguka kutoka kwenye farasi, alibadilishana maisha yake kwa Taji la Shahidi na akalivaa kichwani mwake. Akiwa amevaa taji hili adhimu lenye kung'aa, Ammar bin Yasir alijiunga pamoja na wenye Uzima wa Milele huko Peponi, wakiongozwa na rafiki yake, Muhammad Mustafa (s.a.w.w.). Kipenzi cha Allah swt.

Mashujaa hodari wawili wa Syria walikuja kumuona Mu'awiyah. Kila mmoja wao alidai kwamba yeye ndiye aliyerusha ule mkuki ambao umemuua Ammar, na kila mmoja alikuwa ni mgombea wa zawadi kwa ajili ya "tendo" lake la kishujaa. Amr bin Al-Aas alikuwa pamoja na Mu'awiyah, na akawauliza: "Kwa nini nyie wote mna shauku ya kurukia kwenye moto wa jahannam?"

Wanahistoria na wasimulizi wa Hadith wameuandika huu utabiri maarufu wa Mtume wa Allah swt. kwamba Ammar bin Yasir atakuja kuuawa na watu wapotofu.

Sir John Glubb:

"Pale Waislamu wa mwanzoni huko Madina walipotishiwa na Makuraish, ambao waliwarudisha nyuma kwa kuchimba handaki, Ammar ibn Yasir alikuwa akipepesu-ka na mzigo wa udongo. Mtume mwenyewe alikuwa amemuona na akaja kumsaidia, akampokea mzigo wake na akakipangusa vumbi kichwa chake na nguo zake. Kwa moyo huu wa upole wa kiuzazi ambao ulikuwa ni mojawapo ya sababu za utii wa wafuasi wake, yeye akasema, "Masikini Ammar! Watu makatili na madhalimu watakuwa hakika ndio kifo chako wewe." Inaelekea kuwa yamkini tamko hili lilitole-

604

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wa kwa utani, akiwalaumu wafuasi wake kwa kumchosha mfuasi huyu mwenye kuji-tolea. Lakini sentenso hii ilikumbukwa kama utabiri.

Sasa katika siku ya pili ya vita vya Siffin, Ammar aliuawa akipigana kwa ajili ya Ali na akikemea kwa sauti, "Ewe Pepo, uko karibu kwa kiasi gani?" Hiyo ndio ilikuwa heshima kubwa iliyozingatiwa na majeshi yote mawili kwa kumbukumbu ya Mtume kwamba kifo cha Ammar kiliingiza hamasa kiasi kikubwa katika jeshi la Ali kama kilivyodukiza unyong'onyevu katika lile la Mu'awiyah. Kwani maana ya utabiri huo ilikuwa kwamba wale watu waliomuua Ammar watakuwa wanapigana katika njia ya uovu."

(The Great Arab Conquests, London, uk. 326, 1963)

Sir John Glubb amekosea katika kupendekeza kwamba Mtume (s.a.w.w.) alitoa tamko hilo "kiutani." Mtume alikuwa hatanii. Hapakuwa na muda kwa ajili ya utani. Alikuwa makini kabisa wakati alipomwambia Ammar kwamba watu makatili na madhalimu watakuja kumuua yeye (Ammar).

Kifo cha Ammar kilikuwa na athari nzito sana kwa marafiki na maadui, na kilichochea mgongano katika mawazo. Wairaqi sasa wakapigana kwa raghba mpya wakiwa wamesadi-ki kuwa walikuwa wanapigana kwa ajili ya Haki. Wakati huohuo, watu wa Syria wakawa wamesambaratika kwa mashaka. Wengi wao waliacha kupigana, miongoni mwao ni Amr bin Al-Aas mwenyewe. Mwanawe, Abdallah, akamwambia:

"Leo hii tumemuua mtu ambaye kutoka usoni mwake Mtume wa Allah mwenyewe aliondoa mavumbi, na alikuwa amemwambia yeye kwamba kundi la watu waovu litakuja kumuua."

Amr bin Al-Aas aliinukuu ile Hadith ya Mtume (s.a.w.w) mbele ya Mu'awiyah, na akase-ma: "Sasa ni dhahiri kwamba sisi ndio wale watu ambao wako kwenye makosa."

Mu'awiyah alimtaka Amr anyamaze kimya, na asiwafanye wengine wakaisikia hiyo Hadith ya Mtume, na akaongezea kwamba Ammar kwa hakika aliuawa na Ali ambaye alimleta kwenye vita hivyo.

Mmoja wa masahaba ambaye alikuwepo katika msafara wa Mu'awiyah, kwa tahadhari alitoa maoni juu ya matamshi ya Mu'awiyah kwamba kama Ali alimuua Ammar kwa sababu alikuwa amekuja kwenye vita hivyo pamoja naye, basi bila ya shaka yoyote ile, Muhammad alimuua Hamza kwa sababu alimchukua pamoja naye kwenye vita.

Pale Ali aliposikia kwamba Ammar alikuwa ameuawa kwenye mapambano, aliisoma ile Aya ya 156 ya Sura ya pili ya Qur'an Tukufu kama ifuatavyo:

"Sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake ndio marejeo yetu."

605

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kifo cha Ammar kilikuwa ni mshituko mkubwa sana kwa Ali. Walikuwa marafiki tangu zile siku Ammar na wazazi wake walipokuwa wakiteswa na Makuraish kwa kuukubali Uislamu, na rafiki yao, Muhammad (s.a.w.w.) alipowaliwaza. Lakini Muhammad mwenyewe alikuwa, kwa siku nyingi, ametengana nao. Sasa Ammar pia aliiondoka dunia hii, akimuacha Ali peke yake. Ali alizongwa na huzuni na hisia mbaya ya "upweke."

Ali na marafiki zake waliswali Swala ya jeneza kwa ajili ya Ammar ibn Yasir, rafiki wa Allah swt., sahaba wa Muhammad (s.a.w.w.), na Shahidi wa Siffin, na wakamzika.

Kama vile tu marafiki zake wawili, Muhammad na Ali, Ammar alikuwa pia amepigana na Makuraishi maisha yake yote. Mapema, Makuraishi walikuwa wamewaua wazazi wake, na sasa wamemuua yeye mwenyewe. Kila Yasir mmoja kati ya watatu hao alipata taji la Shahada.

Huzuni ya Ali kwa kifo cha Yasir ililingana na furaha ya Mu'awiyah. Huyu Mu'awiyah mara kwa mara alisema kwamba Ammar alikuwa ni mmoja kati ya mikono miwili ya Ali (mkono mwingine ukiwa ni Malik ibn Ashtar), na alijigamba kwamba alikuwa ameukata mkono ule.

Yalipoanza tena mapigano, watoto wawili wa Hudhaifa ibn al-Yaman, Said na Safwan, waliuawa katika mapambano na vikosi vya Syria. Ilikuwa ni dua ya mwisho ya baba yao kwamba watakuja kufa wakipigana kwa ajili ya Ali.

Siku nyingi zikapita katika mapigano yasiyo na utaratibu. Ilikuwa ni katika mapigano haya madogo madogo ambamo Ali alipata hasara kubwa mbili kwa vifo vya masahaba wawili wa Mtume (s.a.w.w.). Mmoja wao alikuwa ni Khuzaima ibn Thabit Ansari (yule ambaye ushahidi wake mmoja ulikuwa ni sawa na ushahidi wa watu wawili wengine); na Uways Qarni. Huyu wa mwisho, kama ilivyoelezwa mapema, aliwasili kutoka Yemen, na alikuwa amekutana na Ali kwa mara ya kwanza katika usiku wa kuamkia vita vya Basra. Tamaa ya maisha yote ya Khuzaima na Uways Qarni ilikuwa ni kupata hadhi ya shahada katika Uislamu. Waliipata katika vita vya Siffin.

Vifo vya Khuzaima na Uways Qarni vilimkera sana Ali kiasi kwamba alituma ujumbe kwa Mu'awiyah atoke kuja kupigana yeye mwenyewe binafsi, na hivyo kuokoa maisha ya maelfu ya Waislamu waliokuwa wakifa pande zote. Mu'awiyah, bila shaka, hakuukubali mwaliko huo. Ilikuwa ni dhahiri kuona kwamba kujikoga kisiasa na ushujaa havikua lazi-ma sana viote kwenye mti mmoja.

Watu walikuwa wanakufa kwa idadi kubwa lakini hakukuwa na matokeo ya hakika ya kuonyesha. Ali aliuona huu ukosefu wa maendeleo kuwa yenye kuleta madhara kwenye hamasa ya vikosi vyake, na akaamua kurekebisha hali hiyo. Jioni ile alimwita Abdallah ibn

606

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abbas ambaye alikuwa ndiye mshauri wake mkuu, na Malik ibn Ashtar ambaye alikuwa ndiye Mnadhimu Mkuu wake, kwenye kikao. Wote kwa pamoja walitengeneza mkakati mpya wa kuvifikisha vita kwenye hatma yenye mafanikio.

Katika siku iliyofuatia, Ali na Malik walikuwa wawashambulie maadui kwa wakati mmoja, mmoja kutoka kuliana mwingine kutoka kushoto. Wakiweka uratibu kamili, msawazisho na umakini, walikuwa wamuweke adui katika mashambulizi ya mbele na nyuma kwa wakati mmoja, na kisha kuelekea kwenye kitovu chake, Malik alikuwa aon-goze mashambulizi ambayo yatamlazimisha adui kusalimu amri.

Baada ya Swala ya usiku, Ali alihutubia vikosi vyake kama ifuatavyo:

"Enyi Waislamu! Kesho mtalazimika kupigana vita vya maamuzi, kushinda au kushindwa. Kwa hiyo, tumieni usiku huu katika ibada kwa Muumba wenu. Tafuteni rehema Zake, na muombeni ili Yeye akupeni uimara na ushindi. Na kesho mthibitishieni kila mtu kwamba ninyi ni watetezi wa Haki na Kweli."

(Tarikh Kamil, ibn Athir, Juz. III, uk.151) Vita vya Lailatul-Harir

Asubuhi iliyofuata, Ali na Malik walipanda farasi zao, na wakaenda mbele ya majeshi ya Syria wakichunguza mpangilio wao. Walifanya mabadiliko kidogo katika mpango wao wa mapambano, na kisha, kwa ishara kutoka kwa Ali, Malik akashambulia upande wa kushoto wa adui.

Majeshi ya Syria yalikuwa na wingi wa idadi kuliko Malik, na makamanda wao walijaribu kuutumia vizuri. Kila aliposhambulia, wao walitawanyika lakini kwa namna fulani wali-weza kujikusanya tena. Malik alipigana kutwa nzima. Kwa kawaida, majeshi hayo mawili yalisimamisha mapigano baada ya jua kuzama, na kurudi kambini kwa ajili ya Swala na mapumziko lakini siku ile Malik alikataa kurudi. Vile vile hakuwaruhusu Wasyria kurudi kambini kwao, na akawabakisha kwenye uwanja wa mapambano.

Baada ya mapumziko mafupi kwa ajili ya Swala zake, Malik akaanzisha shambulio lake la ghafla juu ya jeshi la Syria. Safari hii mashambulizi yake yalikuwa ya harara sana kiasi kwamba Wasyria waliswagwa mbele yake kama kondoo. Baada ya Swala ya usiku, Ali pia alirejea kwenye uwanja wa mapambano, na akaushambulia ule upande wa kulia wa Wasyria. Katikati yao, walianza kulisaga jeshi la Syria. Waliua maelfu ya wapiganaji wa Syria na kueneza woga na hofu katika safu zao. Mikoromo na may owe ya Wasyria walio-jeruhiwa na wanaokufa, milio ya vyuma vya silaha, migongano ya vyuma, upanga wa Malik wenye ncha mbili ukichana ngao za Wasyria, na ukelele wake wa kivita wa Allah-

607

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

u-Akbar, vililijaza lile anga la usiku la jangwani.

Malik alikuwa hodari na jabari kupita kiasi. Alionekana kwa hakika, mbele ya maadui, kuwa ndiye Kipaji hasa wa Ushindi. Alikuwa ni chombo maalum na cha hatari mikononi mwa Majaaliwa. Kila alipopita, ushindi ulishambulia pamoja naye.

Edward Gibbon:

"Katika pambano hili la umwagaji damu mwingi yule khalifa halali alionyesha mwe-nendo wa hali ya juu wa ushujaa na ubinadamu. Vikosi vyake viliamriwa kusubiri shambulio la mwanzo la adui, kuwaacha ndugu zao wanaokimbia, na kuheshimu miili ya wafu, na usafi wa mateka wa kike. Alipendekeza kwa wingi sana kuokoa damu ya Waislamu kwa kutumia mtindo wa mapigano ya watu wawili wawili tu; lakini mpin-zani wake mwenye kugwayagwaya kwa woga aliikataa changamoto hiyo kama huku-mu ya kifo kisichokwepeka. Safu za majeshi ya Syria zilivunjwa na shambulizi la shujaa aliyekuwa amepanda farasi mwenye rangi mbili, na akautumia kwa nguvu zisi-zozuilika, upanga wake mzito na wenye ncha mbili. Kila mara alipomchoma muasi, alikemea Allah-u-Akbar, 'Mwenyezi Mungu ni Mshindi!' na katika zile ghasia za vita vya usiku alisikika akiurudia mara mia nne ule mguto mkubwa sana wa mshangao.

(The Decline and Fall of the Roman Empire)

Shujaa aliyezivunja safu za Wasyria alikuwa ni Malik. Lakini tayari alikuwa amewaua wengi wao - wale askari wa kawaida wa Syria - kiasi kwamba alikuwa amekwishaanza kuwapuuza. Alitafuta mawindo ya ngazi ya juu zaidi. Katika vita vya Basra, alimaliza mapigano kwa kumuua yule ngamia aliyekuwa amembeba Aisha mgongoni mwake. Dhamira yake sasa ilikuwa ni kumuua au kumteka Mu'awiyah, na hivyo kukomesha vita vya Siffin. Kwa silika za mwindaji, kwa hiyo, alianza kusogea kuelekea kwenye windo lake.

Malik alimpanda farasi wake kupita kwenye madimbwi ya damu na matuta marefu ya maiti wa Syria, bila kuzuilika, bila ya huruma na labda bila kukwepeka. Kila aliyejaribu kupigana naye au kumzuia njia, alikatwa vipande.

Mu'awiyah sasa aliweza kuona kwa macho yake mwenyewe kwamba wakati umetimia. Alichokuwa anakiona kikimkaribia yeye, hakikuwa ni Malik, yule Mnadhimu Mkuu wa Ali, bali Malaika wa Kifo. Ile ardhi ngumu chini ya miguu yake ilionekana kwake kugeu-ka kuwa mchanga-didimizi. Walinzi wake, ingawa wa kuchaguliwa kwa ujasiri wao, nguvu na utii kwake na nyumba yake, walikuwa hawana uwezo mbele ya Malik. Hawakuweza kumzuia kusonga mbele kuelekea kwenye mawindo yake bali walifanya kitu cha ubora wa pili - waliweka tayari farasi wenye nguvu kwa ajili yake (Mu'awiyah) kupanda na kutoro-

608

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ka kutoka kwenye uwanja wa vita kwa kufichwa na giza la usiku.

Katika hali hii ya hatari ya kutisha, Mu'awiyah alimgeukia Amr bin Al-Aas, na akasema:

"Kuna matumaini yoyote kwamba tunaweza bado kuokoa maisha yetu au uwanda huu wa upweke ndio umepangiwa kuwa eneo la makaburi yetu? Na hivi, wewe bado unaitaka Misri? Kama unaitaka, basi fikiria mara moja juu ya mkakati wa kumzuia Malik ama sivyo sisi sote pamoja na wewe, tutauawa katika muda mchache ujao."

Matumaini ya uhai yalikuwa yenye nguvu sana kwa Amr bin Al-Aas. Aliweza kukabiliana na hali yoyote ile, na alikuwa, kwa hakika, tayari na mkakati kwa ajili ya muda huu muafa-ka. Mkakati wa Amr ulikuwa ukwapue sio tu yale mawindo bali hata ushindi wenyewe kutoka kwenye mkono wa Malik!

Vita alivyokuwa akipigana Malik, ni maarufu sana katika historia kama "Vita vya Layla-tul-Harir." vilikuwa ndio upeo wa mapambano makali katika uwanda wa Siffin katika kingo za mto Euphrates. Vilikuwa pia ndio kilele cha juu kabisa cha shughuli za kisiasa na kijeshi za wote, Ali na Malik, kama matukio yalivyokuwa yaonyeshe punde tu.

Tangu Ali alipokuwa ametaka kiapo cha utii kutoka kwa Mu'awiyah, yeye Mu'awiyah ali-fungulia vita vya kifalsafa dhidi yake. Moja ya silaha alizotumia katika mapambano yake ya kifalsafa dhidi ya Ali ilikuwa ni dhahabu au kishawishi cha dhahabu. Mama yake, Hind, alikuwa ametumia jinsia kama silaha yake katika mapambano dhidi ya Uislamu katika vita vya Uhud. Kwa silaha ya dhahabu, Mu'awiyah alifanikiwa kuwatongoza wengi wa maafisa wa ngazi ya juu katika lile jeshi la Iraq, na alipunguza ari yao ya kupigana. Alikuwa hakuwajaza tu na dhahabu na fedha bali alikuwa pia amewaahidi kuwateua wao kama magavana wa majimbo na kuwa makamanda katika jeshi lake kama watamsaliti Ali katika wakati ule muhimu ndani ya mapambano hayo.

Ule wakati muhimu ukawa umewadia. Mapigo makubwa sana ya Malik yalikuwa yame-watupa Wasyria kwenye vurugu isiyo na matumaini. Matarajio yao pekee kwa ajili ya usalama wao yalikuwa ni katika lile giza la usiku ambalo litawaficha ama lingeweza kuwa-ficha kwenye macho ya Malik.

Malik ambaye alijiwazia kwamba alikuwa amefikia mahali pa kumuua au kumteka Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas, bila kujua kwamba wote wawili walikuwa na silaha ya siri ambayo itaokoa maisha yao na kumkanganya yeye. Silaha ya siri ya Mu'awiyah ilikuwa tayari inafanya kazi kimya kimya na kudhuru kwa siri lakini kwa kufaa sana. Ilikuwa ni mbegu ya uhaini aliyokuwa ameipanda kwenye jeshi la Iraq. Mbegu hiyo ghafla ikachipua kwenye vita vya Layla-tul-Harir!

609

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Malik alikuwa bado analitwanga lile jeshi la Syria vibaya sana pale Amr bin Al-Aas alipowaamuru wapiganaji wake kuning'iniza nakala za Qur'an kwenye ncha za mikuki yao kama ishara ya kutaka kwao kuurejesha mgogoro huo kwenye Hukmu ya Allah inay-opatikana ndani yake.

Wale maofisa ndani ya jeshi la Iraq ambao walikuwa wamenunuliwa na Mu'awiyah, na ambao walikuwa tayari kutekeleza wajibu wao, walikuwa wakisubiri ishara. Mara tu walipoziona nakala za Qur'an juu ya mikuki, waliweka panga zao kwenye ala zao na wakaacha kupigana, kwa mshangao mkubwa na fadhaa kwa Ali, Ibn Abbas, na wale wachache kati ya maafisa wao waaminifu. Papo hapo, Abdallah Ibn Abbas akaziona zile nakala za Qur'an zilizotundikwa, na akaelewa ni nini kilichokuwa kinaendelea. Kauli yake fupi ilikuwa:

"Vita vimekwisha; usaliti umekwishaanza."

Na hivyo ikawa. Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas walikuwa wameomba suluhisho la silaha, na walikuwa wameshindwa. Wao sasa wakakata rufaa kwenye usaliti, na kama matukio yalivyokuwa yaonyeshe punde, walikuwa wafanikiwe! Mtu wa kwanza katika jeshi la Iraq kuacha kupigana alikuwa ni Ash'ath bin Qays, yule yule ambaye binti yake Jo'dah, atakuwa aje kumuua Hasan bin Ali kwa sumu miaka kadhaa baadaye. Alikuwa ndiye kion-gozi wa wasaliti katika jeshi la Iraq. Alikuja kumuona Ali na akamwambia:

"Watu wa Syria hawataki kuona umwagaji zaidi wa damu miongoni mwa Waislamu. Wanataka Kitabu cha Allah kiamue kati yao na sisi. Sisi kwa hiyo, hatuwezi kupigana dhidi yao tena."

Viongozi wa yale makabila mengine ambao walikuwa katika mapatano pamoja na Mu'awiyah, wakaacha kupigana kwa kumuigiza Ash'ath bin Qays.

Watu wa makabila wakafuata mfano wa viongozi wao, na wao wakaacha kupigana pia. Kwa hiyo mapigano yakafikia kusimama kwa kweli kwenye pande nyingi muhimu. Kikosi kimoja tu - kile kilichoongozwa na Malik - kilibakia uwanjani kikipigana na kuwaumiza watu wa Syria.

Haikujitokeza kwa wale wasaliti ndani ya jeshi la Iraq kwamba kama Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas walikuwa na heshima yoyote juu ya Qur'an, wangewataka wao kulifanya Neno la Allah kuwa msuluhishi katika mgogoro wao kabla au hata wakati wa mapambano laki-ni hawakufanya hivyo. Waliikumbuka Qur'an pale tu kushindwa na kuangamizwa kwa jeshi la Syria kulipojitokeza mbele yao juu ya upeo wa macho.

Ash'ath bin Qays ghafla akashikwa na mapenzi juu ya maisha ya Waislamu. Alikamata

610

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

nakala ya Qur'an, akasimama akiliangalia jeshi lake, na akapiga kelele:

"Enyi Waislamu! Mlazimisheni Ali kukubali suluhisho la Kitabu cha Allah, na hapo hapo kusimamisha huu umwagaji wa damu."

Umwagaji wa damu ya Waislamu ulimshitua pale tu Ali alipokuwa kwenye nafasi ya kushinda vita hivyo. Ushindi wa Ali, yeye alijua, hautabadilisha kitu chochote kwa ajili yake. Lakini kwa tukio la kushindwa kwa Ali, alikuwa amehakikishiwa zawadi nono kuto-ka kwa Mu'awiyah. "Shauku" yake ya kutaka kuokoa maisha ya Waislamu kwa hiyo, ilikuwa inaeleweka.

Wakati huu, Ali alikuwa amezungukwa na viongozi wa makabila ndani ya jeshi lake, na walianza kumsihi aache kupigana dhidi ya watu wa Syria, ambao, wao walisema, kwa wakati ule hasa, walikuwa wanamuomba yeye, kwa jina la Kitabu cha Allah swt., kusimamisha kuuawa kwa Waislamu. Ali aliwaonya kwamba walikuwa wanalaghaiwa na adui, na akawasihi kushikilia fursa yao ya kwenye ushindi. Yeye aliwaambia pia kwamba yale maombi kwa jina la Kitabu cha Allah (swt.) hayakuwa ni chochote bali ni hila ya kuwanyang'anya wao matunda yao ya ushindi, na kuepuka kwao kushindwa na kifo.

Lakini dhahabu na fedha za Mu'awiyah zilionekana kuwa ni hoja yenye nguvu sana kuliko kitu chochote ambacho Ali alichoweza kusema. Wasaliti hao mara wakawa mafidhuli; wal-imuomba Ali amrudishe Malik kutoka kwenye uwanja wa vita, na kutangaza kusimamish-wa kwa mapigano mara moja. Ali alisita lakini alitambua kwamba hakuwa na nafasi ya kutosha katika kukabiliwa na maasi yanayokaribia ndani ya jeshi lake mwenyewe, na aka-tuma mjumbe kwa Malik kumuondoa kwenye mstari wa mbele. Malik alikuwa ame-jishughulisha sana na kuyasaga mabaki ya jeshi la Syria kiasi kwamba alikuwa hata haja-gundua kwamba jeshi lake mwenyewe lilikuwa halipigani tena. Yeye, kwa hiyo, alimwambia yule mjumbe kwamba haukuwa muda wa yeye kuondoka kwenye uwanja wa vita, na kuacha kazi yake ikiwa haijakamilika.

Malik alikuwa karibu sana agundue kwamba upanga wake mzito na wenye ncha mbili ambao ulikuwa umeua idadi kubwa ya jeshi la Syria, utakuwa hauna nguvu dhidi ya sila-ha mpya iliyobuniwa na Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas - silaha ya usaliti!

Pale mashushushu na mamluki wa Mu'awiyah katika kambi ya Ali waliposikia majibu ya Malik, walimwambia kwamba kama yeye hatarudi kutoka kwenye uwanja wa vita mara moja, wao watamkamata Ali, na kumkabidhi mikononi mwa Mu'awiyah. Safari hii Ali ili-bidi atume ishara ya huzuni kwa Malik ambaye aliambiwa kwamba ikiwa hatarudi kambi-ni kwake wakati ule ule, hatakuja kumuona tena bwana wake.

Malik alisaga meno kwa hasira kwani alikuwa anaona sasa mawindo yake yakimponyoka kutoka mikononi mwake. Aliingia pale kambini kwa ghadhabu kubwa, akiwa na uchu wa

611

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kuwauwa wale wasaliti lakini akaihisi ile hatari kwa bwana wake ambaye alikuwa katikati yao, na wote walikuwa wameweka mikono yao kwenye mipini ya panga zao. Wakati alipowalaumu kwa ukali juu ya upumbavu na udanganyifu wao, walimsogelea kwa kumkamia na panga zao zikiwa zimechomolewa. Lakini Ali alisimama katikati yao, na akawambia wale wasaliti:

"Mnaweza kuacha kupigana dhidi ya adui yenu lakini angalau msimuue rafiki yenu wenyewe mkubwa mno."

Ali hakupenda Mu'awiyah ayaone mapigano ya ndani katika kambi yake mwenyewe. Vita vya Siffin vilikuwa vimekwisha. Pale ambapo nguvu ya Mu'awiyah ilishindwa, hila na ujanja vilifanikiwa. Ushindi ulitoka mikononi mwa Ali kwa hila, na tokea hapo alikuwa awe kwenye hali ya kujihami katika vita visivyo na mafanikio dhidi ya Mu'awiyah. Kule kusimamisha mapigano kuliashiria mwanzo wa kuanguka kwake kisiasa.

Baada ya kukoma kwa uhasama, ilikubaliwa kwamba vile vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Waislamu virejeshwe kwenye usuluhishi, na maamuzi ya wasuluhishaji yakubaliwe na pande zote mbili. Ilielezwa wazi katika haya majadiliano ya awali kwamba hao wasuluhishi watafanya maamuzi yao tu "kwa mtazamo wa Kitabu cha Allah swt." Mu'awiyah alimteua Amr bin Al-Aas kama msuluhishi anayewakilisha upande wake; na wale waasi ndani ya jeshi la Ali wakapendekeza jina la Abu Musa al-Ash'ary kuiwakilisha Iraq.

Abu Musa alikuwa ni mtu aliyechanganya upumbavu na utii wenye shaka kwa Ali. Alikuwa punde aonyeshe sifa zote, moja ya kichwa chake, na nyigine ya moyo wake, katika kukabilana kwake na Amr bin Al-Aas ambaye alikuwa halingani naye kwa kitu cho-chote, jambo la mwisho kabisa ni katika werevu wa diplomasia na majadiliano.

Ali kwa silika alimkataa Abu Musa ambaye alimuona siku zote kuwa mwenye maudhi. Chaguo lake yeye mwenyewe lilikuwa ni Abdallah ibn Abbas au Malik ibn Ashtar. Lakini wote hao hawakukubalika sio kwa Mu'awiyah ama kwa mashushushu wake ndani ya jeshi la Iraq kama Ash'ath bin Qays na wengineo. Walisema kwamba walitaka mtu "asiye na upendeleo" na "asiye mfuasi" kama vile Abu Musa alivyokuwa lakini Abdallah ibn Abbas na Malik Ibn Ashtar hawakuwa hivyo. Ali akawauliza: "Kama hivyo ndivyo, basi kwa nini hamumkatai Amr bin Al-Aas ambaye si mwenye kukosa upendeleo au kukosa ufuasi?" Wakamjibu kwamba wao wanahusika na mambo ya upande wao tu, na sio mambo ya wengine.

Ali aliyakataa mashinikizo ya wasaliti hao lakini walikuwa wote wakijinenepesha juu ya dhahabu ya Mu'awiyah ambayo hawakuwa tayari kuipoteza kwa gharama yoyote ile. Ilikuwa, kwa kweli, imepangwa kabla kwamba Abu Musa ataiwakilisha Iraq. Hatimaye,

612

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wasaliti hawa wakafanikiwa katika kumbambika huyu mjinga Abu Musa juu ya bwana wao kama "mwakilishi" wake.

Pale makubaliano ya kuacha mapigano yalipokuwa yanarasimiwa, tukio fulani lilitokea ambalo lilikumbusha Hudaybiyya. Huyo mwandishi aliandika maneno: "Haya ni makubaliano kati ya Ali ibn Abi Talib, Kiongozi wa Waumini, na Mu'awiyah bin Abu

Sufyan.." Amr bin Al-Aas, mwakilishi wa Mu'awiyah, alikataa na akasema: "Futa

maneno 'Kiongozi wa Waumini.' Kama tungekuwa tumemkubali Ali kama Kiongozi wa Waumini, tusingekuwa tunapigana dhidi yake." Papo hapo Ali akasema: "Mtume (s.a.w.w.) alisema kweli pale alipobashiri tukio hili hasa. Wakati mkataba wa Hudaybiyyah ulipokuwa unaandikwa, na nikawa nimeandika maneno, 'Huu ni mkataba kati ya

Muhammad, Mtume wa Allah, na.' waabudu masanamu wakanikatiza, na wakase-

ma kwamba kama wangekuwa wamemkubali Muhammad kama Mtume wa Allah, wasingekuwa wanapigana dhidi yake, na walisisitiza juu ya kufutwa kwa maneno 'Mtume wa Allah,' kutoka kwenye maandishi ya Mkataba."

Huko Hudaybiyyah, Muhammad (s.a.w.w.) alifuta yale maneno "Mtume wa Allah" kutoka kwenye mswada wa mkataba; hapo Siffin, Ali, akifuata nyayo za Muhammad, aliruhusu maneno "Kiongozi wa Waumini" kufutwa kwenye mswada wa mkataba. Makubaliano ya kuacha mapigano yalisainiwa ipasavyo na kushuhudiwa na pande zote, na nakala zilibadil-ishanwa kwa kuhifadhiwa katika hifadhi ya nyaraka.

Masharti ya kuacha mapigano yalikuwa:

1.  Wasuluhishi wote watatawaliwa na sheria kwamba maamuzi yao yatafikiwa kwa mtazamo wa Kitabu cha Allah swt. Kama watashindwa kuamua jambo lolote kwa msin-gi huu, basi watachukua uamuzi wao kulingana na mifano na Hadith za Mtume wa Allah swt.

2.  Uamuzi wa wasuluhishi, kama umeegemea juu ya Kitabu cha Allah swt., utazipasa pande zote.

3. Wasuluhishi watachunguza sababu zote zilizosababisha kifo cha Uthman, na vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Waislamu (kushauri hatua za marekebisho kwa ajili ya baa-daye).

4.  Wasuluhishi watatangaza maamuzi yao ndani ya miezi sita kutoka tarehe ya kuacha mapigano.

5.   Wanaopigana vita watafuata kanuni ya kusitisha mapigano. Watawalinda wasuluhishi ambao watakuwa na uhuru kamili wa kutembea katika nchi yote.

6.   Wasuluhishi watakutana mahali fulani katika mpaka kati ya Iraq na Syria.

613

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kifungu muhimu kabisa katika mkataba huu kilikuwa ni kwamba wasuluhishi watakifanya Kitabu cha Allah swt. kama kiongozi chao, na kwamba hawatatawaliwa na tamaa na uchu wao.

Vita vya Siffin vilikuwa vimekwisha rasmi lakini Malik ibn Ashtar, sasa "dragoni wa Arabia aliyetiwa mnyororo," kwa ushupavu kabisa akakataa kushuhudia hati hiyo ya makubaliano. Yeye aliiona kama ni hati ya fedheha na udhalimu.

R. A. Nicholson:

"Vita kubwa ilipiganwa hapo Siffin, kijiji kwenye kingo za Mto Euphrates. Ali takrib-an alikuwa amepata ushindi wakati Mu'awiyah alipomfikiria hila. Aliamuru majeshi yake kuweka Qur'an kwenye ncha za mikuki yao na kukemea, "Kitabu cha Allah hiki hapa: Wacha kituamulie!" Mbinu hii dhaifu ilifanikiwa. Ndani ya jeshi la Ali mlikuwa na waumini wenye msimamo mkali kwao wao ambao hili pendekezo la kusuluhish-wa kwa Qur'an liliwavutia kwa nguvu isiyozuilika. Wao sasa wakaruka kwa kukamia, wakitishia kumsaliti kiongozi wao, labda kama atawasilisha kusudi lake kwenye Kitabu cha Allah. Bure kabisa Ali alipingana na waasi hao, na kuwaonya wao juu ya hila ambayo walikuwa wanamsukumia yeye ndani yake, nalo hili pia katika muda ambao ulikuwa waukumbatie. Hakuwa na uchaguzi bali kukubali na kumtoa kama msuluhishi wake, mtu mwenye utii wa mashaka, Abu Musa as-Shari, mmoja wa masahaba wazee sana wa Mtume waliokuwa hai. Mu'awiyah, kwa upande wake alimtaja Amr bin Al-Aas, ambaye ustadi wake ulikuwa umechochea hila ya uamuzi."

(A Literary History af the Arabs, uk. 192, 1969)

Wasuluhishi hao wawili, Abu Musa na Amr bin Al-Aas, walitangaza kwamba watakuja kukutana, miezi sita baadaye, huko Adhruh, kutoa hukumu yao katika mgogoro huo kati ya pande hizo mbili. Ali na Mu'awiyah ndipo wakarudi kutoka Siffin kungojea uamuzi wa wasuluhishi hao.

Wakati Ali aliporudi Kufa, aliingia kazini kuiunda upya serikali, lakini, kwa bahati mbaya, alilazimika kuahirisha mipango yake kwa sababu ya kuzuka kwa maasi mapya katika jeshi lake.

Wakati wa vita vya Siffin, Mu'awiyah alikuwa amepandikiza mbegu za uhaini ndani ya jeshi la Iraq, kama ilivyoelezwa kabla. Hili alilifanya kwa kutoa zawadi za dhahabu na fedha, na kwa kutoa ahadi za kutoa ardhi, mali binafsi, na vyeo vya kiraia na kijeshi vya ngazi ya juu kwa wale watu mashuhuri katika jeshi la Ali, kwa malipo ya msaada wao kwake. "Uwekezaji" wake ulileta faida kubwa sana kwake. Wale wapokeaji wa zawadi zake walikuwa wamemlazimisha Ali kusimamisha mapigano, na kukubali usuluhishi, na

614

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwa njia hii, yeye Mu'awiyah alikuwa amefanikiwa katika kukwepa janga na kifo hapo Siffin. Wao sasa walikaa kwa matarajio, wakisubiri utekelezwaji, na Mu'awiyah, wa ahadi zake.

Lakini Mu'awiyah aliporudi Damascus, alihisi kwamba sasa angeweza kumudu kuachana na huduma za wengi wa wateja wake ndani ya jeshi la Ali. Yeye, kwa hiyo, akawaambia kwamba hakuwa amewaahidi kitu chochote.

Wale wateja wakatambua kwamba walikuwa wamelaghaiwa na Mu'awiyah. Kwa huzuni kubwa na kukata tamaa, walimgeukia Ali, na wakamtaka yeye ayakatae makubaliano ya kuacha vita, na kurudia kupigana tena dhidi ya Mu'awiyah. Lakini Ali alikataa kufanya hivi, na akasema kwamba ilimbidi asubiri na kuona kama uamuzi wa wasuluhishi utakuwa unaendana na amri za Qur'an Tukufu au la kabla ya kuchukua hatua nyingine yoyote.

Lakini wale waliokuwa wateja wa Mu'awiyah hawakutaka kusubiri. Walimshinikiza Ali kupigana, na pale alipokuwa hakukubali, wao na wafuasi wao walitoka kwenye jeshi lake kwa pamoja, na wakavunja kiapo chao cha utii kwake. Walikuwepo watu 12,000 hawa waliokana kiapo chao cha utii kwa Ali baada ya vita vya Siffin. Hawa wanaitwa Khawarij, na walijikusanya katika sehemu inayoitwa Harura ambapo kutokea hapo walianza kupora nchi iliyozunguka hapo, na kuwaua watu wasiokuwa na hatia, na kwa kweli, kila mtu ambaye alikataa maoni yao juu ya serikali na siasa.

Ali alijaribu kuwashawishi hawa Khawarij kurejea Kufa, na kutoa mbele yake zile hoja zao za kutokukubaliana naye. Aliyajibu maswali yao na pingamizi zao vya kuridhisha sana, na baadhi yao, wakiwa wameridhika kwamba alikuwa yu sahihi, walirudisha kiapo chao cha utii kwake lakini wengine wengi hawakufanya hivyo. Sasa wakadai kwamba kwa kukubali kuurejesha mgogoro wake na Mu'awiyah kwenye kusuluhishwa na binadamu wanaoweza kufanya makosa, badala ya Kitabu cha Allah swt., Ali alikuwa amegeuka kuwa "kafir," na kwamba "kutubia" kwake pekee ndiko kutamletea yeye wokovu.

Ali alivumilia ujeuri na ufidhuli wa Khawarij kwa matumaini kwamba watatambua kosa lao lakini hili liliwafanya kuwa wajeuri na mafidhuli zaidi. Sasa, viongozi wao wakaamua kuondoka Kufa, na kuweka makao yao makuu katika sehemu nyingine. Walichagua kijiji kinachoitwa Nahrwan kwa ajili ya lengo hili, na wakawaamuru Khawarij wote kukusanyi-ka pale. Kutokea Nahrwan, Khawarij wakaeneza hofu katika nchi. Walitenda maovu mapya mabaya zaidi ili kuficha hatia yao, aibu na majuto yao. Walipita wakiwaua watu bila ya kuchagua, bila kuwaacha hata wanawake na watoto. Kisha habari zikaja kwamba walikuwa wanapanga kuishambulia Kufa yenyewe.

Ilimbidi Ali kuchukua hatua mara moja kuzuia uhalifu na vurugu za Khawarij, na alikwen-da mwenye mpaka Nahrwan kukutana na viongozi wao. Aliwaambia kwamba kulikuwa na

615

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hati ya usalama kwa wale wote miongoni mwao ambao wataiacha kambi yao, wakarudi majumbani kwao, na wakaishi kwa amani na majirani zao. Wengi wao walitambua kwam-ba hawakuwa na sababu ya kupigana dhidi ya Ali, na waliondoka Nahrwan ili kurudi majumbani kwao. Lakini kiini cha watu 4,000 wasiokata tamaa walibakia wakaidi katika madai yao kwamba Ali alikuwa lazima "atubie" kabla ya kuweza kumkubali kama kion-gozi wa Waislamu. Wao, kisha wakapaza ukelele wa shime ya vita "Hapana hukmu ila ya Allah," na wakashambulia vikosi vya Ali. Ingawa walishambulia kwa kujisahau bila kujali, hawakuleta madhara makubwa kwenye vikosi vya Ali. Pale huyu Ali alipojibu mashambulizi, Khawarij walishindwa; wengi wao waliuawa, na ni wachache tu waliotoro-ka kutoka kwenye uwanja wa mapambano.

Ingawa Khawarij waliitwaa kama wito ile Aya ya Qur'an ya "Hapana hukmu ila ya Allah," hawakuwa ama na nia wala uwezo wa kuweka Mamlaka ya Mbinguni katika dunia hii. Walitaka tu madaraka juu yao wenyewe. Walikuwa ni mchanganyiko wa mlipuko wa ugaidi, siasa na ushabiki wa kidini uliopindukia (ulokole). Kama ikibidi wakafanikiwa, watakuwa tu wamerudisha ubinafsi wa kikabila wa Waarabu wa kabla ya Uislamu. Hadi leo, wanabakia kiajabu ajabu wasiochanganyika katika historia ya umma wa Waislamu.

Dr. Hamid-ud-Din:

"Kharij waliwazuia watu kujiandikisha katika jeshi la Ali. Na kama mtu yeyote alipingana na imani zao, walimuua papo hapo. Kwa njia hii, Waislamu wengi waliuawa. Ali alituma mjumbe kwenda kuwashauri waachane na kufanya uhalifu dhidi ya watu wasio na hatia lakini wakamuua na yeye pia.

Kambi ya Kharij ilikuwa ipo Nahrwan. Ali pia aliongoza jeshi lake kwenda Nahrwan. Aliwataka Khawarij kuwatoa wale watu waliowauwa Waislamu wasio na hatia kwa ajili ya kushtakiwa na kuhukumiwa. Lakini walipiga kelele kwa sauti moja kwamba wao wote ndio waliowaua, na kwamba waliona kuwauwa watu kama hao (wale Waislamu ambao walikuwa hawachangii imani yao) kama ni wajibu wa heshima kuu. Ali kwa mara nyingine tena aliwaonyesha makosa yao, na akawasihi warejee majumbani kwao lakini majibu yao yakawa ni kinyume.

Mwishowe, Ali alimtuma Abu Ayub Ansari pamoja na bendera ya Uislamu katikati ya majeshi hayo mawili yanayopingana. Abu Ayub akaikunjua ile bendera, na akatangaza kwamba yoyote yule kutoka kwenye kambi ya Khawarij atakayekuja chini ya bendera hiyo, atakuwa yuko salama.

Khawarij wengi kwa kutambua makosa yao, walikuja chini ya bendera hiyo iliyokuwa imesimamishwa na Abu Ayub. Lakini wapiganaji wao 4,000 wakakataa kuiacha kambi yao. Walikuwa wamedhamiria kupigana dhidi ya Ali. Wakapiga

616

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kelele, "Hakuna hukmu ila ya Allah," na kisha wakalishambulia jeshi la Ali. Walipigana kwa ushupavu wa mashabiki lakini wakazingirwa na kushindwa, na kari-buni wote wakafa.

(History of Islam, Lahore, Pakistan, uk. 202, 1971)

Ule ukelele wa shime ya vita wa Khawarij, "Hakuna hukmu ila ya Allah," ulikuwa ni ujan-ja wa vitimbi tu, ulioundwa ili kuchukua madaraka ya kisiasa mikononi mwao, na kumny-ima kila mtu mwingine yoyote.

Kwa wakati huo, Amr bin Al-Aas na Abu Musa al-Ashari, wale wasuluhishi wawili, walikuwa wamemaliza majadiliano yao ya siri, na walikuwa wako tayari kutoa tangazo. Wote walikuwa wamekubaliana kwaamba ilikuwa ni kwa maslahi ya Dar-ul-Islam kwamba Ali na Mu'awiyah wote wajiuzulu au waondolewe, na umma wa Waislamu wajichag-ulie kiongozi mpya wao wenyewe.

Wasuluhishi hao na waandamizi wao walikutana huko Adhruh. Watu mia nne wa kila upande pia waliwasili katika eneo la tukio, kwa mujibu wa makubaliano ya kuacha mapigano. Ujumbe wa Syria ulikuwa ukiongozwa na Abul Awar Salmi, na ule wa Iraq uliongozwa na Abdallah ibn Abbas na Shuayh ibn Hani.

Watu wengine wengi pia walikuja Adhruh kusikiliza hukumu ya wasuluhishi juu ya majaaliwa ya Dar-ul-Islam. Miongoni mwao alikuwa ni Abdallah ibn Umar, Abdallah ibn Zubeir, Abdur Rahman bin Abu Bakr, Saad bin Abi Waqqas, na Mughira bin Shaaba.

Amr bin Al-Aas alimwambia Abu Musa kwamba yeye alikuwa anamheshimu sana kwa vile yeye Abu Musa hakuwa tu sahaba wa Mtume wa Allah swt., bali pia alikuwa ni mwanazuoni mkubwa, na kwa sababu hii, alimstahi yeye katika kila kitu, na pia kwa sababu hii, yeye Abu Musa anapaswa kuwa wa kwanza kutoa tangazo hilo la uamuzi wao wa pamoja, ambao yeye Amr atauthibitisha baadae.

Abdallah ibn Abbas alimuonya Abu Musa kwamba Amr angeweza kumzidi maarifa na kumpita ujanja, na akamshauri kwamba amwache Amr awe wa kwanza kutoa tangazo hilo. Lakini Abu Musa hakuusikiliza ushauri huu wa busara, na akasema:

"Jambo lenyewe ni thabiti na hakuna nafasi ndani yake kwa Amr bin Al-Aas kufanya ujanja au kushinda."

Abu Musa alikuwa amejisahau, ameleweshwa na kule kuonyeshwa "heshima" kulikofany-wa na Amr bin Al-Aas kwake. Yeye ndipo akapanda kwenye mimbari kutoa hilo tangazo la kihistoria, na akasema:

"Enyi Waislamu! Huzuni nyingi na taabu zimeuadhibu umma wa Muhammad kwa vita vya Ali na Mu'awiyah. Kwa hiyo, sisi wote tumeamua kuwaondoa wote wawili, na tumekubaliana kwamba haki ya kuchagua khalifa mpya itolewe kwa umma wa

617

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Waislamu wenyewe - kwenu ninyi nyote."

Ule ujumbe wa Iraq uliaibika sana kusikia tangazo hili lakini ukaamua, hata hivyo, kusik-iliza yule msuluhishi mwingine atasema nini. Abu Musa akaketi chini baada ya tangazo lake, na kisha Amr bin Al-Aas akasimama ili kutoa tangazo lake. Yeye akasema:

"Enyi Waislamu! Nyie wote mmesikia kile alichokisema Abu Musa kuhusu kuon-dolewa kwa Ali. Amemuuzulu Ali kama khalifa. Ninaunga mkono uamuzi wake, na ninatangaza kwamba Ali ameuzuliwa kwenye ukhalifa. Na katika nafasi ya Ali, ninamteua Mu'awiyah kama khalifa wenu mpya.."

Abu Musa alikuwa bado hajamalizia maelezo yake wakati yalipozuka makelele ya hasira. Abu Musa alilalamika kwa kuchanganyikiwa na kwa hasira: "Muongo! Sijasema hayo mimi. Wewe ni muongo usiye na haya kabisa. Wewe ni mbwa aliyebebeshwa mzigo wa vitabu na ambaye anatweta na kutoa ulimi wake anapokuwa chini ya mzigo huo." Amr ali-weza kuimudu hali hiyo, na akazirudisha sifa hizo kwa kusema: "Wewe ni punda ambaye amebebeshwa vitabu, na ambaye anatoa mlio mkali chini ya mzigo mzito."

Huyu "mbwa" na huyu "punda" walizungumza kwa sauti kali, walikemea na kutazamana kwa vitisho kwa muda mchache, na kisha wakashambuliana vikali sana. Walitwangana na kupigana, na "walibweka" na "kulia kipunda" katikati ya zogo mpaka wakawa wamep-welewa na sauti. Kulikuwa na vicheko pia, ingawa dhidi ya Abu Musa pekee.

Baada ya miezi sita ya majadiliano ya faragha, "mlo" pekee ambao wasuluhishi hao - Amr bin Al-Aas na Abu Musa walikuwa wameuandaa kwa ajili ya "ujenzi wa maadili" wa mamia ya Waislamu ambao walikuwa wametoka kwa makundi kwenda Adhruh kwa ajili ya "karamu" hiyo, ulikuwa ni "muziki" ambao ulitolewa na yule wa kwanza wao kwa "kubweka" na yule wa pili kwa "kulia kipunda."

"Onyesho" lilikuwa, hatimaye, limekwisha, na Waislamu ambao walikuwa wameku-ja kutoka sehemu za mbali, waliondoka Adhruh ili kurejea majumbani kwao.

Abu Musa aligundua kwamba amekuwa kichekesho cha Waarabu wote, na akakimbilia Yemen kwenda kuficha aibu yake. Yeye alikuwa ni mtu mwenye uhodari wa wastani lakini kugongana kwa matukio kulikuwa kumemuweka yeye katika hali ambamo huenda ali-fikiria kwamba alikuwa anatawala hatima ya umma wa Waislamu. Majivuno yake yalikuwa yanapigana na busara, na majivuno yakashinda. Kazi aliyotakiwa aishike ilikuwa ni kubwa sana kwa mtu aliyekwamishwa na ukosefu wa uwezo kama alivyokuwa yeye, na aliiharibu. Alikuwa ni mmoja wa wasiri wa Umar bin al-Khattab ambaye alikuwa amem-teua kuwa gavana, kwanza wa Basra na kisha wa Kufa.

618

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Lile tishio kwa Mu'awiyah lilikuwa limepita kudumu, na katika juhudi zake za kuukama-ta ukhalifa, uamuzi sasa umepitia kwake. Madai yake ya ukhalifa yalitegemea juu ya ile hukumu ambayo Amr bin Al-Aas, yule "mwenye sauti katika uchaguzi" aliyoitoa pale Adhruh.

Hukumu ya Amr ilikuwa ni ujanja wa kiinimacho cha kisiasa ambacho kingemsisimua Machiavelli; lakini kwa watu wa Syria, ilikuwa na mamlaka ya kibali kutoka mbinguni kwenyewe, na ilikuwa, kwa hivyo, isiobadilika.

R. A. Nicholson:

"Ni desturi ya fikira za Kiarabu za kimaadili kwamba huu udanganyifu wenye maam-risho ulitukuzwa na wafuasi wa Mu'awiyah kama ushindi wa kidiplomasia ambao ulimpa yeye kisingizio kinachofaa kwa utwaaji wa cheo cha khalifa."

(A Literary History of the Arabs, uk. 192-193, 1969)

Usuluhishi uligeuka kuwa kichekesho na hasara tupu. Uamuzi wake, kwa hali yoyote, ulikuwa wa kupita uwezo wa kisheria. Hakuna mtu hata mmoja aliyewapa hao wasuluhishi mamlaka ya kutoa hukumu juu ya ukhalifa au kuuzulu au kuteua khalifa. Wafuasi wa Mu'awiyah walikuwa wanatafuta kulipiza kisasi kwa ajili ya kuuawa kwa Uthman. Mu'awiyah alikuwa amewashawishi kwamba Ali alikuwa anahusika na kifo cha Uthman, na ilikuwa ni kwa sababu hii kwamba walipigana hapo Siffin. Hawakupigana vita dhidi ya Ali ili kumtawalisha Mu'awiyah.

Lakini wasuluhishi hao hawakuchunguza machimbuko ya vita vya wenyewe kwa wenyewe. Walizungumzia tu kuhusu ukhalifa ingawa haukuwa ndio suala lenye mgogoro. Kazi yao pekee ilikuwa ni kutafuta ni nani aliyemuua Uthman, na ikiwa kama Mu'awiyah alikuwa anayo haki ya kulipiza kisasi juu ya uhalifu huo.

Abu Musa alitoa hukumu yake ya "Mungu mtu" kwa "kumuuzulu" Mu'awiyah. Uenguliwaji wa Mu'awiyah ulikuwa na maana gani hata hivyo? Na Abu Musa alimuengua yeye kutoka kwenye kitu gani? Mu'awiyah hakuwa khalifa, wala hakukuwa na mtu aliyependekeza jina lake kwenye ukhalifa. Kwa upande mwingine, Ali alikuwa ndiye khalifa halali wa Waislamu. Alichaguliwa kwa makubaliano ya Muhajirin na Ansar, na sehemu zote za himaya hiyo, pamoja na kujitenga kwa Syria pekee, zilikuwa zimemtambua yeye kama kiongozi wao.

Kama wasuluhishi, au hasa, kama wenye sauti, Amr bin Al-Aas na Abu Musa walikuwa wamejiingiza kwenye majadiliano marefu juu ya siasa na vita, na labda kwenye hali ya baadaye ya umma wa Waislamu lakini kitu kimoja walichokuwa hawakukifanya kilikuwa ni kuiangalia Qur'an Tukufu. Waliiweka Qur'an nje ya majadiliano yao huko Adhruh kama

619

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

vile tu, miaka mingi nyuma, watangulizi wao katika kuwa na sauti katika uchaguzi, walivyoiweka Qur'an nje ya majadiliano yao katika banda la Saqifah huko Madina.

Kwa "utukizi" wa ajabu, wenye sauti ya uchaguzi wote wa Waarabu, ama ndani ya Saqifah au katika Kamati ya Uchaguzi ya Abdur Rahman bin Auf, au huko Adhruh, walijidhihirisha wenyewe "wenye mzio" na Qur'an Tukufu. Au, ilikuwa ni kinyume chake - Qur'an Tukufu ikijionyesha yenyewe kuwa "yenye mzio" na wenye sauti katika uchaguzi? Wenye sauti ya uchaguzi waliiweka Qur'an nje ya mashauriano yao au Qur'an yenyewe ilikaa nje yao - njia zote, ilikuwa kwa kweli moja ya "utukizi" wa ajabu katika historia ya Waislamu. Kwa sababu za kisirisiri, wenye sauti katika uchaguzi wote kwa upande mmoja, na Qur'an Tukufu kwa upande mwingine, vilibakia vimetengana kwa mbali sana, kimoja hadi kingine.

Amr bin Al-Aas na Abu Musa walipaswa kuifanya Qur'an kuwa mwongozo wao katika usuluhishi. Walikuwa na wajibu wa kuunda maamuzi yao katika mtazamo wa sheria za Kitabu cha Allah swt. Amri za Allah swt katika hali hii ndio mkato wa wazi.

Usahihi-70.jpg

"Enyi mlioamini! Mtiini Mwenyezi Mungu, na mtiini Mtume na Wenye mamlaka miongoni mwenu. Kama mkikhitlafiana katika jambo lolote, basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na siku ya Mwisho: hilo ni bora zaidi na lenye mwisho mzuri zaidi." (Sura ya 4; Aya ya 59)

Wasuluhishi hawa, inavyoonekana, walisahau vyote; amri za Allah zote zilizotajwa katika Aya hiyo iliyopita, na wajibu wao wenyewe. Lakini Qur'an haikuwasahau wao, na ikaonyesha kile walichokifanya au walichoshindwa kufanya katika Aya inayofuata:

Usahihi-71.jpg

"Wanaitwa kwenye Kitabu cha Mwenyezingu, ili kiwahukumu (katika migogoro yao) kisha kundi moja kati yao hukataa, nao wamegeuka."(Sura ya 3; Aya ya 23)

Amr bin Al-Aas na Abu Musa - wale wasuluhishi walijifanya kuwa lile kundi lililokigeu-ka Kitabu cha Allah swt. Walikuwa wamependelea kuongozwa na matamanio yao binafsi, na kwa sababu hii, waliivuta hukumu ya Qur'an juu yao wenyewe:

620

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usahihi-72.jpg

"Na watakaoshindwa kuhukumu kwa yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu; basi hao ndio waasi."(Sura ya 5; Ay a ya 47)

Katika vita vya Siffin, majeshi ya Iraq na Syria yalikabiliana kwa siku 110. Yalikuwepo mapambano 90 kati yao ambamo ndani yake Wairaqi 25,000 na Wasyria 45,000 wali-uawa.Vita hivi vya kutisha vilikuwa ni matunda ya tamaa na uchu wa madaraka wa Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas. Mu'awiyah alikuwa ndiye gavana wa Syria, na alikuwa haoni karaha sana kwa kitu chochote kuliko kile cha kuipoteza nafasi hiyo. Amr bin Al-Aas alikuwa ni gavana wa Misri lakini alikuwa amefukuzwa na Uthman, na alikuwa na hamu sana ya kukipata tena cheo chake cha zamani. Kubakia au kurudia vyeo vyao, wote walikuwa tayari kufanya kitu chochote na kulipa gharama yoyote Ukweli na Haki havikuwa na maana yoyote kwao. Waliweza kuigharikisha Dar-ul-Islam kwa uongo, na kwa damu ya Waislamu ili kufanikisha nia na matamanio yao.

Wale "wakubwa watatu" wa Basra (Masahaba wa vita vya Ngamia), na Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas waliimaizi fursa yao kubwa kwenye kifo cha Uthman, na wakaikamata. Kisasi kwa ajili ya damu yake kilikuwa ni ubao mwembamba ambao uligawa maadili yao kwenye uchu wao wa dhahiri wa madaraka. Uthman - aliyekufa alikuwa na thamani sana kwao kuliko Uthman - alivyokuwa hai. Kwa hiyo, wao walimpa msaada wote walioweza - ili afe. Lakini mara tu alipokufa, ikawa halali, kwa kweli, ilikuwa ni wajibu, juu yao kufanya mauaji ya halaiki kwa jina la kulipiza kisasi kwa kuuawa kwake.

Vita vya Basra na vya Siffin vilikuwa ndio mauaji ya halaiki ya Waislamu yaliyoshurutish-wa na mantiki ya "Siasa ya hali na mali."

Toynbee anasema kwamba Muhammad na Ali walikuwa hawalingani na wachuuzi mafa-hari wa Makka (Bani Umayya) katika siasa za hali na mali. Kwa maana fulani, anaweza kuwa sahihi. Muhammad na Ali walisita kuua hata muabudu masanamu, bila kuzungumzia kuua Mwislam. Hawakuweza kuua mtu yeyote kwa ajili ya madaraka ya kilimwengu. Walikuwa, kwa hiyo, wamekwazwa katika "mashindano" yao na Bani Umayya.

621

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kifo cha Malik ibn Ashtar na kupokonywa kwa Misri

Gavana wa Ali huko Misri alikuwa ni Muhammad bin Abu bakr. Mnamo mwaka 658 (38 H.A.) Mu'awiyah alimtuma Amr bin Al-Aas pamoja na jeshi la wapiganaji 6,000 kuiteka Misri kwa ajili yake. Muhammad alimuomba Ali kumtumia msaada wa kuihami Misri. Ali alitambua kwamba mtu pekee atakayeweza kuiokoa Misri kutoka kwenye makucha ya Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas, alikuwa ni Malik bin Ashtar. Yeye, kwa hiyo, alimtuma Malik kama gavana mpya wa Misri, na akamwita Muhammad ibn Abu Bakr kurudi Kufa.

Lakini Malik wala Muhammad hawakuweza kamwe kuvifikia vituo vyao. Malik aliondo-ka Kufa kwenda kuchukua madaraka ya Misri. Lakini mashushushu wa Mu'awiyah, waki-wa wamejifanya kama wamiliki wa nyumba za kulala wageni kijijini, walikuwa wakisubiri kumpokea yeye kwenye mpaka. Walimtilia sumu kwenye kinywaji chake, na akafa kutokana na athari zake (Abul Fida).

Malik alikuwa ni mshindani asiyeshindika wa Mu'awiyah.

Yule shushushu aliyekuwa amemtilia Malik sumu, mara moja akatoa taarifa ya "mafanikio" yake kwa Mu'awiyah, na yeye Mu'awiyah hakuweza kuamini bahati yake nzuri. Katika kilele cha furaha, alisema kwa mshangao: "Leo Ali amepoteza mkono wake wa pili." Kwa kumuua Ammar bin Yasir katika vita vya Siffin, Mu'awiyah alikuwa ameukata mkono mmoja wa Ali; na sasa kwa kumuua Malik, amekata mkono wake mwingine pia. Baada ya kifo cha Malik, Ali alikuwa amepoteza mikono yote miwili. Mu'awiyah alikuwa ameukata mkono wa Ali kwa msaada wa silaha yake ya siri lakini yenye nguvu sana - sumu!

Sumu "iliwayeyusha" washindani wa Mu'awiyah wasioshindika, na kumuondolea yeye hofu kudumu.

Francesco Gabrieli:

"Katika miaka ile Amr bin Al-Aas iliiteka upya Misri kwa ajili ya Bani Umayya, akimuengua kwa njia ya sumu, Malik al-Ashtar ambaye Ali alikuwa amemtuma kwenda huko kama gavana.

(The Arabs, A Compact History, uk. 69, 1963)

Kwa Ali, kifo cha Malik kilikuwa ni pigo lenye kuyumbisha. Kama angekuwepo kamwe mtu mmoja katika Arabia ambaye alikuwa ni jeshi la mtu mmoja, alikuwa ni Malik. Kuwepo kwake kulichochea kujiamini katika jeshi lake mwenyewe, na jina lake lilitia hofu

622

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

katika mioyo ya maadui. Waarabu hawakutoa kwamwe mshika upanga mwenye kuogope-sha zaidi yake. Kwa kutumia ujasiri na uwezo, alijisogeza mwenyewe mpaka kwenye upeo wa ubingwa. Ni moja ya misiba katika historia ya Waislamu kwamba kazi yake ilikatwa ghafla katika ujana wa maisha yake. Alikuwa jasiri, shupavu, mwenye akili, muungwana na muumini. Walikuwepo watu wengi, ambao mpaka kifo cha Ammar ibn Yasir, walikuwa hawajajiamulia kama wapigane au wasipigane upande wa Ali. Ilikuwa ni baada tu ya kutimia kwa utabiri wa Mtume wa Allah swt. kwamba Ammar atakuja kuuawa na watu waovu, ambapo waliporidhika kwamba haki na kweli iko upande wa Ali. Lakini Maliki hakuwa kamwe na matatizo kama hayo. Yeye alijua Ali na Ukweli walikuwa hawatengan-ishiki, na alikuwa thabiti kabisa katika utii na uungaji mkono kwake.

Wanahistoria wengine wamesingizia kwamba Malik alikuwa mmoja wa wale watu waliokuwa wamehusika katika kifo cha Uthman. Ni kweli kwamba Malik alikuja Madina kutokea Kufa pamoja ujumbe wa watu lakini hakuwa amekuja kumuua Uthman. Alikuja kumuomba tu Uthman kumuondoa gavana muovu na asiye na maadili. Yeye alikuwa ndiye mtu wa fahari kabisa ndani ya Arabia, na kitu kimoja ambacho asingeweza kukifanya ni kuua mzee wa miaka 84. Malik, kwa hakika, wala hakuingia kwenye kasiri la Uthman kwa wakati wowote ule. Kama angekuwa ameingia, Naila (mkewe Uthman) angezitoa habari hizi wakati Ali alipokuwa anawahoji mashahidi wa uhalifu huo; na Marwan angetangaza habari hizo za kuingia huko kwa dunia nzima. Lakini hakufanya hivyo kamwe.

Dai la kwamba Malik alikuwa mmoja wa wauaji wa Uthman, lilibuniwa na Mu'awiyah. Alikuwa anatoa mawazo mapya nyakati zote. Katika vita vya Siffin, pale alipomwona Malik akiwaendea kwa nguvu walinzi wake, aliguta kwa woga na hofu: "Ooh niokoeni kutokana na Malik; yeye ndiye aliyemuua Uthman." Mu'awiyah alijua kabisa kwamba Malik hakumuua Uthman lakini alijua pia kwamba wale watu wa Syria walimpenda sana Uthman na wangemvamia muuaji wa Uthman kama majini, endapo wangempata. Kwa kumwita Malik muuaji wa Uthman, alitumaini kwamba angewazindua watu wa Syria kufanya juhudi kubwa mno kuzuia mashambulizi yake, na hivyo kuokoa maisha yake mwenyewe. Wanahistoria wa Damascus wenye kujipendekeza walikichukua kilio hicho kutoka kwa Mu'awiyah, na tangu hapo, uongo huo umekuwa ukipita kutoka kizazi hadi kizazi.

Ni moja ya kejeli za historia ya Waislamu kwamba ingawa Aisha, Talha na Zubeir waliwa-chochea wazi wazi watu kumuua Uthman, hawakuwa wametuhumiwa kamwe katika baraza lake. Na ni nini kilichomzuia Mu'awiyah mwenyewe kwenda Madina kuokoa maisha yake Uthman? Hakuna! Lakini hakufanya hivyo kamwe. Alizuia msaada wake kwa makusudi, na kumuacha Uthman afe. Lakini baada ya kifo chake, alifanya ushirikiano, kwa kubadilishana na Misri, na Amr bin Al-Aas, ili "kutafuta kulipiza kisasi kwa kifo cha Uthman." Kama ilivyoelezwa kabla, Amr alikuwa mmoja wa maadui wasiosuluhishika kabisa wa Uthman, na huenda alikuwa ndiye muuaji hasa!

623

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mpangilio wa mambo ulibadilika baada ya kifo cha Uthman. Kwanza Aisha, Talha na Zubeir, na kisha Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas walisimama kama wahusika wakuu wa Uthman kutafuta kulipiza kisasi kwa ajili ya damu yake. Shauku zozote mbalimbali na mara nyingi za utusitusi za wale wanaume na wanawake waliozunguka maiti ya Uthman, ni dhahiri kwamba usalama wake haukuwa hofu yao walau hata kidogo. Huu ni ukweli ambao hauwezi kukanushika lakini pia ni ukwali ambao wanahistoria wa Sunni hawapen-di kuufichua. Inafariji zaidi sana na ni rahisi sana kwao kudai kwamba Muhammad ibn Abu Bakr au Malik ibn Ashtar walihusika katika mauaji ya Uthman kuliko kukubali kwamba Aisha, Talha, Zubeir, Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas, wote walishiriki katika msiba huu wa kutisha wa kifo cha khalifa huyu mzee.

Malik ibn Ashtar alifariki wakati Ali akiwa anamhitaji sana, na hapakuwa na mtu ambaye angeweza kuchukua nafasi yake. Mshituko wa Ali, wa kifo cha marafiki kama Ammar ibn Yasir na Malik ibn Ashtar, ulikuwa wa kuumiza sana lakini alihimilishwa na Imani yake. Aliuona kila mshituko mpya, kila huzuni mpya, na kila msiba mpya, mtihani juu ya imani yake, na ilibakia imara. Imani yake katika rehema za Muumba wake ilikuwa kubwa mno kuliko kitu chochote ambacho kingeweza kumfika, na hakukubali kukata tamaa hata kidogo.

Malik alikuwa ni mtu wa namna ya kipekee kweli kweli. Alikuwa mjuzi wa vita kikamil-ifu, aliyejitoa, mwenye kuheshimika, na mwenye uhodari kwa kiwango cha juu kabisa na mwenye kujiamini. Alikuwa ni mfalme miongoni mwa watu.

Mtu mashuhuri zaidi kuliko yeye katika upekee wake wa ujasiri na wa dhahiri, na wepesi na ufuatiliaji wa adui unaojulikana sana, hauonekani popote katika historia ya Arabuni. Propaganda imefanya majina wa watu wengine kujulikana zaidi kuliko yeye lakini bado anabakia kutolinganishika. Alikuwa ndiye 'Asiye Kifani' wa Uislamu.

Huenda haiwezekani kumpa Malik ibn Ashtar heshima iliyokubwa zaidi kuliko ile aliyope-wa na bwana wake mwenyewe, Ali Ibn Abi Talib. Katika vita vya Layla-tul-Harir, Ali ali-weka mikono yake juu ya mabega ya Malik, na akasema:

"Umenitumikia mimi kwa heshima na utii ule ule ambao mimi nilimtumikia bwana wangu, Muhammad, Mtume wa Allah aliyebarikiwa."

Kupokonywa Misri

Amr bin Al-Aas aliingia Misri bila upinzani wowote, na pindi alipokabiliana na Muhammad ibn Abu Bakr, alimshinda kwa urahisi sana. Muhammad alikuwa hana jeshi, na alijaribu kupigana akiwa na wapiganaji wachache tu. Watu wa Syria walimkamata, na wakamtesa mpaka akafa. Amr akaikalia Misri, na ikawa sehemu ya milki za Mu'awiyah.

624

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali alimpenda Muhammad ibn Abu Bakr kama mwanawe mwenyewe. Kifo chake kilikuwa ni mshituko mwingine mbaya mno uliombidi kustahimilia. Aliswali kwa ajili yake na akamuombea rehema na baraka za Allah juu ya nafsi yake tukufu.

Mnamo mwaka wa 659 Mu'awiyah aliongeza vita vyake vya kero dhidi ya Ali, na akatu-ma vikosi kwenda Jazirah na Hijazi kutishia watu, na kuwavunja hamasa zao. Sera yake mwanzoni ilikuwa ni kuwatia cheche za hofu na kuacha moto ufanye yaliyobakia lakini manahodha wake mara wakaigeuza kuwa taswira yenye kubadilika ya vurugu na kifo. Huko Jazirah, Nu'man bin Bashir aliishambulia Ainat-Tamar akiwa na watu 2,000; Sufyan bin Auf aliishambulia Anbar na Madaen akiwa na wapiganaji 6,000; Abdallah bin Masadah Fizari aliishambulia Tima pamoja na kundi la maharamia 1,700; na Zahhak bin Qays na wafuasi wake wakauangamiza mji wa Waqsa. Waliwaua wale wanaume wote, wanawake na watoto ambao waliwashuku kuwa na urafiki kwa Ali, na wakaipora hazina ya umma popote walipoiona.

Dr. Hamid-ud-Din:

"Kule kuipata Misri kuliimarisha mikono ya Mu'awiyah kupita kiasi. Kisha yeye aka-tuma vikosi vya jeshi lake ndani ya Hijazi, Jazirah na Iraq. Walipita wakipora, kueneza hofu na kuua. Mu'awiyah alishambulia kingo za Tigris yeye mwenyewe binafsi, na akaitwaa hazina ya umma huko Jazirah."

(History of I slam, Lahore, Pakistan, uk. 204, 1971)

Mu'awiyah na majenerali wake walikuwa wametwaa sera ya kufanya vita vya mara kwa mara dhidi ya mrithi wa Mtume wa Uislamu na kiongozi wa Waislamu wote. Kwao wao, vita vya mara kwa mara vilimaanisha vita visivyo vya kawaida; vitendo vichache vya kawaida vya kijeshi, na hofu isiyo na kikomo. Waliitumbukiza Dar-ul-Islam kwenye kiwewe ambacho haijaweza kutokana nacho kamwe.

Katika mwaka 660, Mu'awiyah alimtuma Bisr bin Artat pamoja na wapiganaji 3000 kwenda Hijazi na Yemen katika ghasia za uporaji, kubomoa, kuunguza na kuua. Huko Yemen, Bisr aliuwa kwa mikono yake mwenyewe, vichanga mapacha wa Ubaidullah ibn Abbas ambaye alikuwa gavana wa jimbo hilo. Wakati aliporudi Syria, akiwa amevimbiwa damu isiyo na hatia, makumi ya maelfu ya Waislamu yalikuwa yameuawa.

Mmoja wa magavana wa Ali katika wilaya ya mpakani, alikuwa ni Kumayl ibn Ziyad. Aliomba ruksa ya bwana wake ya kuivamia Syria. Uvamizi kama huo ndani ya Syria, yeye alisema, utamlazimisha Mu'awiyah kusimamisha mashambulizi yake ndani ya Hijazi na Iraq. Lakini maombi yake yalipata majibu bainifu kutoka kwa Ali ambaye alimuandikia hivi:

625

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Sikutegemea kabisa wewe kupendekeza kwamba tushambulie miji na vijiji vya Syria. Ni kweli kwamba watu wa Syria ni maadui zetu lakini pia wao ni binadamu, na zaidi ya hayo, wao ni Waislamu. Kama tutatuma vikosi vya mashambulizi ndani ya Syria, inawezekana kabisa kwamba waathirika wa vitendo vyetu vya hatua za kuadhibu hawatakuwa wale Wasyria majambazi ambao wanasumbua mipaka yetu bali ni makundi ya raia wa Syria - watu ambao sio wapiganaji. Hivi itakuwa ni sawa na haki, kwa hiyo, kuwapora na kuwaua kwa makosa ambayo wao hawakuyatenda? La hasha. Hawatapata adhabu kwa makosa ya viongozi wao. Kitu cha maana kwetu sisi kufanya, kwa hiyo, ni kuimarisha ulinzi wetu wenyewe dhidi ya adui, na kum-fukuza kabla hajaweza kufanya madhara yoyote kwa watu wetu."

Ile mantiki inayotawala ya "taswira" ya kulipiza hofu kwa hofu haikumvutia Ali; yeye ali-iona kimsingi ni yenye kupotosha.

Ingawa Ali aliwafukuza wale wavamizi kutoka kwenye milki zake, sheria na amani ilikuwa imevunjika. Wasyria walianza kuusumbua ule mpaka kwa marudio yanayoongeze-ka. Bisr bin Artat aliishinda ile ngome ndogo inayolinda ule mji wa mkakati wa Anbar na akaukalia. Kisha yeye akawaua kwa upanga makundi yote kama ilivyokuwa kawaida yake

yeye.

Ali aliwaita watu wa Iraq kusimama katika kulinda makazi yao dhidi ya Wasyria lakini akawaona si wenye kuonyesha hisia. Wakati wa kipupwe walisema kulikuwa na baridi sana kuweza kwenda kwenye mapambano, na wakati wa kiangazi walisema kulikuwa kuna joto sana. Viongozi wengi wa Iraqi walikuwa bado wanamfanyia kazi Mu'awiyah kwa malipo ya zawadi na ahadi zake, na walieneza chuki katika nchi. Mu'awiyah pia alifanya bidii ya kudhoofisha utii kwa Ali wa jeshi la Iraqi. Kwake yeye, mgogoro haukuishia kwenye utendaji wa majeshi, bali uliendelezwa nyuma ya mpaka na mawakala na mashabi-ki wake, kwa uchochezi na hujuma, na kwa propaganda na kutia kasumba.

Kwa vile kulikuwa hakuna hatua za adhabu dhidi yao, wale majambazi wa Syria walitiwa moyo wa kujipenyeza ndani na ndani zaidi ya Iraq.

Ali alifanya majaribio mengi ya kuwatoa Wairaqi kwenye ulegevu na unyong'onyevu wao lakini walijifanya kana kwamba yale mashambulizi ya Wasyria yalikuwa hayawaumizi wao. Tabia yao ya kutojitokeza ilimkera sana yeye kiasi kwamba aliwaambia kwamba kama hawatatii maagizo yake, na kuchukua silaha ili kulinda mipaka yao, atawaacha hapo Kufa, na pamoja na wafuasi wachache aliokuwa nao bado, atakwenda kujaribu kumsi-mamisha adui, bila ya kujali matokeo.

Tishio hili lilionekana kufanya kazi. Wairaqi ghafla wakatambua kwamba kama Ali atawaacha, watakuwa wamebakia bila kiongozi. Wao, kwa hiyo, wakamhakikishia yeye

626

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kwamba watamtii - katika amani na katika vita. Ali mara moja akaanza kazi ya kuliandaa upya jeshi, na kuhamasisha vikosi vipya. Alimuita Abdallah ibn Abbas kutoka Basra, na akawaamuru viongozi wengine na vikosi vyao kukusanyika katika kambi ya Nukhayla karibu ya Kufa.

Ali alijitosa kazini kufidia muda ambao ulikuwa tayari umepotea kutokana na uchelewaji wa mwanzoni wa Wairaqi katika kutii maagizo yake. Lakini huu mkurupuko mpya wa nguvu uliwashitua maadui zake, na wakatumbukia kwenye njama ya kumuwahi kumvuru-gia mipango yake mapema.

Ali alikuwa amekamilisha matayarisho yake kwa ajili ya kuivamia Syria lakini pale alipokuwa anatoa maelekezo ya mwisho katika mpango wake wa ugavi wa usafirishaji wa watu na mizigo vitani, akauawa katika Msikiti Mkuu wa Kufa wakati wa mawio ya Ramadhani 19 ya mwaka wa 40 H.A. (27 Januari, 661).

627

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kuuawa kwa Ali

Kuanzia kwenye nusu ya pili ya mwaka 658, Mu'awiyah, gavana wa Syria, alikuwa akien-deleza kwa makini vurugu dhidi ya miliki za Ali. Uvamizi wake mwingine ulifika Ain-at-Tamar na Anbar, maili 170 tu kaskazini ya Kufa. Watu wa Kufa walikuwa hawapendi kupi-gana na watu wa Syria kiasi kwamba Ali aliona vigumu kuchukua hatua za kuadhibu zenye kufaa. Mu'awiyah binafsi aliongoza shambulizi kukatiza Jazirah kutoka Raqqa hakdi Mosul, na hakukutana na upinzani wowote mahali popote pake. Mwishowe, Ali alitangaza ndani ya msikiti wa Kufa kwamba yeye ataondoka mjini hapo pamoja na wafuasi wake waaminifu wachache katika jaribio la kusimamisha uvamizi wa Syria dhidi ya Iraqi, hata kama itagharimu maisha yake. kitishio hiki kiliwaamsha raia wa Kufa kwenye tishio la kuachwa bila kiongozi kama Ali atakuwa auawe wakati akipigana dhidi ya Wasyria. Walichokozwa na kuchukua hatua na walianza kuhamasishana kwa ajili ya ulinzi.

Vita vya Siffin vilikuwa ni jaribio la kwanza la nguvu kati ya Ali na Mu'awiyah. Kimapambano, vita hivyo vilikuwa ni ushindi wa karibu kwa Ali, lakini kisiasa, viligeuka kuwa mvutano. Baada ya muda fulani ilionekana kwamba Ali angeishinda changamoto ya Mu'awiyah. Lakini mara tu Ali akauawa ndani ya Msikiti wa Kufa, na lile jaribio la pili la nguvu halikutokea kamwe.

Kwa mujibu wa maelezo ya kihistoria ambayo baadhi yao ni yenye kukubalika kabisa, Makhariji watatu walikutana hapo Kufa (wengine wanasema ni huko Makka) kubuni njama. Kila mmoja wao alijitolea kuwaua kila mmoja kati ya viongozi watatu mashuhuri katika Dar-ul-Islam - Ali, Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas. Kwa kuwauwa hao, inadaiwa, walitumainia kukomesha vita vya wenyewe kwa wenyewe ndani ya Uislamu, na kurudisha amani kwa umma wa Waislamu.

Mmoja wa wala-njama hao watatu alikuwa ni mtu mmoja aitwaye Abdur Rahman bin Muljim (La 'natullah Alayhi.). Alikaa huko Kufa ili kumuua Ali, na wale wengine wawili-wakaenda Syria na Misri kumuua Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas. Mipango ya mauaji hayo ambayo yangetokea ya Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas, kwa mujibu wa Hadith zilizoko kwenye mzunguko, ilikwenda kombo, na wao walikamatwa na wakauawa.

Makhariji walikuwa wameshindwa pale Nahrwan, na wengi wao walikufa katika mapam-bano lakini wachache walikuwa wametoroka. Abdur Rahman bin Muljim (L.A.) alikuwa ni mmojawapo wa wale waliokuwa wametoroka. Alijawa na tamaa ya kumuua Ali, na alikuwa anaitafuta fursa hiyo ya kufanya hivyo. Kwa kutukizia, alikutana na mwanamke wa Kikhariji, aitwaye Qattama, ambaye baba yake na kaka zake waliuawa pia huko Nahrwan, na yeye pia alikuwa amelea chuki isiyokwisha juu ya Ali.

628

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Abdur Rahman akatokea kumpenda Qattama, na akamposa. Mwanamke huyo akamwambia kwamba thamani ya mahari yake ilikuwa ni kichwa cha Ali ibn Abi Talib. Hii ilimuimarisha tu Abdur Rahman katika azma yake. Alimuahidi mpenzi wake mwezi kama angeuomba, lakini yeye akasema kwamba hakuna chochote ambacho kingemvutia yeye kama asingeweza kukipata kichwa cha Ali ibn Abi Talib!

Abdur Rahman bin Muljim (L.A.) aliitengeneza kwa uangalifu mipango yake ya kumuua Ali. Makhariji wengine waaminifu wachache walijitolea huduma zao kwake, na kwa pamoja walikariri mazoezi ya mauaji hayo. Abdur Rahman bin Muljim (L.A.) alichukua tahadhari moja zaidi - aliuloweka upanga wake kwenye sumu kali, na akiacha inywee kwenye upanga huo kwa siku tatu.

Asubuhi ya mwezi 19 Ramadhani ya mwaka wa 40 H.A., Ali alikuja kwenye Msikiti Mkuu wa Kufa, na akaadhini (mwito wa Swala). Yeye akachukua nafasi yake kwenye mihirabu, na baada ya muda waumini wakaanza kuwasili. Walisimama nyuma yake katika safu zili-zofuatana, na Swala ikaanza. Waliosimama katika safu ya mbele, pamoja na waumini wengine, walikuwa ni Abdur Rahman ibn Muljim na wale alioungana nao (L.A.). Walikuwa wakiangalia nyendo za Ali. Katika mikunjo ya majoho yao, walikuwa wamebe-ba panga zilizokuwa zimeng'arishwa kwa mng'ao wa hali ya juu, na zilizokuwa zimelowekwa kwenye sumu.

Mara tu pale Ali alipogusa ardhi kwa paji lake la uso kwa ajili ya sajdah, Abdur Rahman bin Muljim (L.A.) alichomoka kwenye safu yake, na akanyemelea kwenye mimbari. Na mara tu Ali aliponyanyua kichwa chake kutoka ardhini, ibn Muljim (L.A.) akampiga dho-ruba mbaya sana kwenye paji lake la uso kwa nguvu kubwa sana kiasi kwamba likapasu-ka.

Damu ilitoka kutoka kwenye paji la uso la Ali katika michirizi kadhaa, na yeye akaguta kwa mshangao:

"Kwa jina la Mola wa al-Al-Kaaba, mimi nimefuzu!"

Watu waliokuwa kwenye jamaa ile walitambua kile kilichokuwa kimetokea, na mara tu walipohitimisha Swala hiyo, wakamzunguka. Wanawe, Hasan na Husein, wakambeba hadi nyumbani kwake. Mganga akaja, na akajaribu kulifunga lile jeraha la kutisha lakini hakuweza kuzuia kule kuvuja kwa damu. Dhoruba hiyo ya upanga ilikuwa mbaya sana kwa vyovyote vile, lakini ile sumu kutoka kwenye bapa lake ilikuwa pia ikienea kwa hara-ka sana katika mwili wake. Wanahistoria wa Kiarabu wanasema kwamba ilikuwa ni mara ya pili ambapo Ali alijeruhiwa katika paji la uso, mara ya kwanza ikiwa ni pale, katika vita vya Handaki vilivyopiganwa mwaka wa 627, upanga wa Amr bin Abd Wudd ulipasua kupita kwenye ngao na helmeti yake, na ukapiga kwenye hilo paji la uso. Paji lake la uso

629

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

lilikuwa bado lina kovu lililoachwa na upanga wa Amr.

Haya ndio maelezo yaliyoachwa na wanahistoria wa Kiarabu juu ya kuuawa kwa Ali, na yamekubalika kuwa ni ya kweli na makundi makubwa ya Waislamu walio wengi. Ingawa maelezo haya yana idhini ya "makubaliano" (ijma) ya wanahistoria wengi nyuma yake, ukweli wake, hata hivyo, una mashaka kwa misingi ya "ushahidi wa kimazingira." Kuna "migongano" mingi sana ndani yake.

Hakuna mtu anayetilia shaka ule ukweli kwamba alikuwa ni ibn Muljim aliyemuua Ali. Lakini je, lilikuwa ni wazo lake mwenyewe binafsi la kumuua yeye? Inawezekana kabisa kwamba wazo hilo lilipandikizwa akilini mwake na mtu mwingine ambaye alitumia mbinu zisizoelezeka ili kufanya hivyo. Ibn Muljim (L.A.) hakujua kwamba alikuwa ni mtumwa wa mtu, na aliendelea mbele na akamuua Ali.

Kwa wakati huu hakuna mtu katika Dar-ul-Islam aliyevutiwa sana na kuuawa kwa Ali kuliko Mu'awiyah. Mpango wa kumuua Ali, ustadi ulioonyeshwa katika utekelezaji wake, na mafanikio yake, vinaonyesha mguso wa werevu kamili na kiwango cha juu sana cha utaalam ambavyo vilikuwa ni sifa bainifu za Mu'awiyah pekee, ambapo ibn Muljim alikuwa si chochote zaidi ya boga. Mu'awiyah alitumia "ustadi" huo huo katika kuondoa kutoka kwenye mazingira, vitisho vya kweli au vya kudhaniwa, kwenye usalama na madaraka yake mwenyewe, katika matukio mengine mengi ya nyakati za baadae, pamoja na matokeo kama hayo hayo.

Wapelelezi wa Mu'awiyah walimwambia kwamba Ali alikuwa anafanya maandalizi kwa ajili ya kuishambulia Syria. Katika vita vya Siffin, Mu'awiyah alikuwa hakukubali busara aliyotendewa na Ali. Safari hii, kwa hiyo, Ali alikuwa ameamua kutopigana vita vya kusi-tasita bali vya haraka haraka ambavyo vingekomesha maasi ya Mu'awiyah, na ambavyo vingerudisha amani kwenye himaya ya Waislamu yenye kujihami. Mu'awiyay pia alijua kwamba Ali alikuwa, safari hii, na vyote, uwezo na uamuzi wa kuufikisha mgogoro huo kwenye hatma ya haraka na ya mafanikio. Tegemeo lake pekee, kwa ajili ya usalama wake hapo baadae, kwa hiyo, kama huko nyuma, lilikuwa kwenye msaada ambao angeweza kuupata kutoka kwa "marafiki" zake wa siku nyingi na wa kuaminika - usaliti na njama. Yeye kwa hiyo, akawahamasisha hao, na wao hawakumvunja matumaini.

Mu'awiyah alikifanya kile kitendo cha mauaji ya Ali kionekane ni cha papo hapo na cha kusadikika kwa kujifanya yeye mwenyewe na shoga yake, Amr bin Al-Aas, kuwa "waathirika" wenye uwezekano na waliokusudiwa wa njama na imani iliyopindukia ya wapinzani wa aina yoyote ya serikali wa Kikhariji. Wote wawili "walikwepa" kuuawa kwa "mkupuo wa bahati njema" isiyo ya kawaida. Mmoja wao "alishikwa na maradhi" katika siku ile ambayo alikuwa "auawe," na hakwenda Msikitini; mwingine hakuugua, lakini ali-ingia ndani ya Msikiti akiwa amevaa deraya yake chini ya joho lake. Yeye "alishambuli-

630

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wa" na "muuaji" wake lakini "aliokolewa" na deraya yake. "Kuugua" kungekuwa ni kiten-do kisichokuwa cha hadhari, na kingewafichua "waathirika" wote. Kwa namna hii, "ugonjwa" na "deraya" viliwaokoa wote Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas kutoka kwenye majambia ya "wauaji" wao wa Kikhariji.

Lakini Ali hakuwa na "bahati" sana. Hakuugua, na hakuvaa deraya yake wakati alipoingia Msikitini. Humo ndani ya Msikiti, Ibn Muljim alikuwa akimsubiri pamoja na upanga uli-olowekwa kwenye sumu. Pindi Ali aliponyanyuka kutoka kwenye sajdah, alimpiga kwenye paji lake la uso, na akalitia ufa. Dhoruba hiyo ilionekana ya kufisha.

Wengi wa wanahistoria wa Kiarabu waliandika historia ambazo zilikuwa "zimepandik-izwa" na Mu'awiyah na wafuasi wake. Yeye kwa kweli alikuwa huru kuingiza maelezo yoyote katika historia zile. Kwa hiyo, yeye alimudu kujiokoa yeye binafsi na Amr bin Al-Aas kutokana na mashtaka rasmi ya maandishi ya historia, na alikuwa ni ibn Muljim pekee aliyeingia kwenye vitabu vya historia kama mhalifu wa kweli na wa peke yake wa kosa hilo.

Kwa utukizi, mauaji ya Ali yalifanyika katika mkesha wa uvamizi wake wa Syria. Ingawa wapinzani wa aina yoyote ya serikali wa Kikhariji walikuwa wamelenga majambia yao kwa viongozi wote watatu mashuhuri wa kisiasa wa ulimwengu wa Kiislamu, yaani, Ali, Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas, kwa utukizi, hawa wawili wa mwisho waliyakwepa majaribio hayo juu ya maisha yao, na Ali peke yake ndiye aliyeuawa.

Kwa utukizi mwingine tena, hawa wawili waliokwepa, yaani, Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas, walikuwa ni marafiki mwandani wa kila mmoja wao, na wote wawili walikuwa -utukizi tena - maadui wa kudumu milele wa huyu wa tatu, yaani, Ali, ambaye alikuwa ndie mmoja pekee aliyeuawa.

Kuna utukizi mwingi sana wa ajabu ambao uliokoa maisha ya Mu'awiyah na Amr bin Al-Aas lakini ukachukua uhai wa Ali.

Ali alitumia muda uliokuwa umebakia kwake katika Swala na uchaji; katika kusoma imla ya wasia wake; katika kutoa maagizo kwa wanawe, mawaziri na makamanda kuhusu mwe-nendo wa serikali; na katika kuwasihi wote wasije kamwe wakawasahau wazee, wag-onjwa, masikini, wajane na mayatima kwa wakati wowote ule.

Ali alitangaza kwamba mwanawe mkubwa, Hasan, atamrithi yeye kama kiongozi wa Mamlaka ya dini na ya dunia, na kama mtawala wa Waislamu wote.

Ingawa Ali alikuwa akizinduka taratibu kutokana na kuporeza damu na nguvu ya sumu, akili yake timamu ilikuwa elekevu na safi mpaka dakiki ya mwisho. Kwa wale watu wote

631

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

waliokuja kumuona yeye, alisema kwamba walipaswa kutambua, kwa wakati wote, juu ya kuwepo kwa Muumba wao katika maisha yao, kumpenda Yeye, na kutumikia Viumbe Vyake.

Ile sumu ilikuwa imefanya kazi yake, na asubuhi ya mwezi 21 Ramadhani ya mwaka wa 40 H.A., Ali ibn Abi Talib aliiaga dunia hii kwenda mbele za Muumba wake ambaye alikuwa akimpenda na kumtumikia maisha yake yote. Alikuwa "amelewa mapenzi ya Mungu." Shauku yake kubwa sana katika maisha ilikuwa ni kuwa na subira juu ya Muumba wake, kila wakati wa uhai wake, na aliifanikisha, na hii ndio maana ya ule mguto wake wa mshangao pale katika mihirabu ya msikiti pindi alipoihisi ile ncha ya upanga kwenye paji la uso wake: "Kwa Jina la Mola wa al-Al-Kaaba, mimi nimefuzu."

Hasan na Husein waliosha mwili wa baba yao, wakaufunika kwenye sanda, wakaswali Swala ya jeneza kwa ajili ya mwili huo, na kisha wakauzika kimya kimya wakati wa usiku huko Najaf Ashraf, kwenye umbali kidogo kutoka Kufa. Hakuna alama zozote zilizowek-wa kwenye kaburi hilo, na eneo la kaburi likafanywa siri, kama ilivyotakiwa na Ali mwenyewe.

Ali, mtu mwema sana wa Uislamu, shujaa, bingwa wa kuongoza shughuli za kiserikali, mwanafalsafa na shahidi, aliiaga dunia hii, na dunia haikuweza kupata mtu wa fahari kama yeye milele yote.

Wengi miongoni mwa Waislamu walikuwa ni waombolezaji wa kifo cha Ali lakini hakuna aliyemuomboleza yeye kwa majonzi sana kuliko ma-Dhimmi (Wayahudi, Wakristo, na Mamajusi). Wao walivunjika mioyo kabisa. Na pale wagonjwa, wasiokuwa na uwezo, walemavu, na mayatima na wajane katika dola hiyo waliposikia kwamba amefariki, wali-hisi kwamba dunia yao ilikuwa imeanguka. Yeye alikuwa ni baba kwao wote. Alikuwa amewashika wote mkononi. Aliwajumuisha wote katika Swala zake. Wengi miongoni mwao hawakuwa wakijua mpaka baada ya kifo chake kwamba alikuwa ni yeye aliyekuwa akiwalisha na kuwatunza. Yeye alikuwa amewashikilia wanadamu wote mkononi mwake.

Wakati ambapo Ali alikuwa akipatikana wakati wote kwa masikini na wanyonge, shauku na hofu yake kubwa yeye mwenyewe ilikuwa ni endapo mmoja wao akawa yeye hawezi kumfikia. Ilikuwa ni kwenye utawala wake tu ambapo ma-Dhimmi (wasiokuwa Waislamu), wasio na nguvu na wasio na ulinzi walipata usalama kamili. Hakuna hata mtu mmoja aliyeweza kuwatishia au kuwanyonya. Kwa kifo chake, usalama wao ulikuwa ume-toweka daima!

Ni kauli ya kweli kabisa kwamba matumizi ya madaraka hayawezi kuchanganyika na ufasihi wa wema, kwani mara tu mtu anapotwaa madaraka ya mambo ya umma, yale mafundisho mepesi ya maadili ambayo ndani yake inawezekana kabisa, kwa bahati,

632

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kuweza kuendesha maisha binafsi, mara yanafumba vya kutisha kwa kiasi kwamba yanazuia tofauti zote za wazi kati ya haki na batili. Ukweli huu, hata hivyo, unalo kinzano lake lenyewe pekee - ndani ya Ali. Alitetea kanuni, katika maisha ya kijamii kama katika maisha binafsi, bila ya kujali gharama. Yeye siku zote aliweka jambo la sawa mbele ya jambo la werevu, bila ya kujali gharama. Chanzo cha kanuni hizo ambazo ziliongoza maisha yake ya binafsi na ya kijamii, kilikuwa ni Al-Qur'an al-Majid kama ilivyokuwa pia chanzo cha falsafa yake ya kisiasa.

Ali alikuwa na wakosoaji na maadui wengi lakini hawakuweza kuonyesha hata mfano mmoja ambapo alipotoka kutoka kwenye kanuni yoyote. Hawawezi kuonyesha mgongano wowote kati ya fikra na maneno yake kwa upande mmoja, au kati ya maneno yake na vitendo kwa upande mwingine. Kwa kawaida alikuwa na msimamo katika fikra, maneno na vitendo.

Ali alionyesha ushindi mkubwa kabisa wa tabia na itikadi. Alikuwa ni mkusanyiko wa nadra wa mapenzi juu ya Allah, bidii ya kazi, nguvu iliyoimarishwa na upendo, mpachano wa mpangilio, na uadilifu madhubuti. Urithi wake mkubwa sana kwa ulimwengu wa Kiislamu utabakia daima kuwa ni tabia yake adhimu.

633

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Baadhi ya yaliyoakisi katika Ukhalifa wa Ali

Wakati mnamo mwaka 656 waislamu walipomkubali Ali kama khalifa wao, na wakampa yeye kiapo chao cha utii, madaraka ya kidini na kidunia yalichanganywa pamoja ndani ya mtu mmoja. Hivyo wao "waliidhinisha" mkataba ambao ulikuwa umetengenezwa, mape-ma mwanzoni mwa mwaka 632, na Mtume wa Allah swt., mwenyewe kwa ajili ya kurithi-wa kwake.

Hakuna amri katika Uislamu, kubwa au ndogo, ya nadharia au rasmi, ambayo imeachwa kwenye haja au matakwa au kura za watu. Chombo muhimu sana cha kisiasa katika Uislamu ni ukhalifa. Ni muhimu kwa sababu kuwepo kwa umma wa Waislamu na uhai wa Uislamu ulikitegemea. Itakuwa kwa hiyo, haifikiriki kwamba kitaweza kuachwa kwenye haja au matakwa au kura za makundi ya mitaani.

Sheria katika Uislamu ni neon sio mapenzi ya mwanadamu bali ya Allah swt. Baada ya kifo cha Muhammad (s.a.w.w.), Ali hakuwa na mamlaka yoyote ya kisiasa laki-ni alikuwa bado ni mrithi wake. Kama alikuwa nayo ama hakuwa na mamlaka mikononi mwake, utii ulilazimu kwake kama mrithi wa Mtume wa Uislamu. Kitu pekee kilichobadi-lika, baada ya kuchaguliwa kwa Ali, kilikuwa kwamba wale watu ambao walizuia kiapo chao cha utii kwake huko nyuma, sasa walimpa yeye, kwa hiari.

Katika wale Waislamu ambao walichukua kiapo cha utii kwa Ali, kulikuwa na makundi mawili. Makundi yote yalichukua kiapo cha utii kwake lakini kwa sababu tofauti. Kundi la kwanza lilimjua yeye kuwa kiongozi wa Utawala wa Mbinguni juu ya Ardhi; kundi la pili lilimtambua tu kama Mtendaji Mkuu wa serikali ya Waislamu. Lile kundi la kwanza lilijua kwamba Muhammad (s.a.w.w.) mwenyewe alimuweka yeye kama kiongozi wa umma wa Kiislamu, na lilijua kwamba hairuhusiwi kuchukua kiapo cha utii kwa mtu mwingine yeyote. Kundi la pili, hata hivyo, lingeweza kutoa kiapo chao cha utii kwa yey-ote ambaye angeweza kufanikiwa katika kutwaa madaraka.

Muhammad (s.a.w.w.) hakuwa mwalimu tu na kiongozi wa maadili mema bali alikuwa pia ni mwasisi wa zama mpya duniani kwa wanadamu wote. Alifungua milango ya zama mpya, akaingiza kwenye historia nguvu mpya iitwayo Uislamu, akafungulia katika ulimwengu mzima elimumwendo mpya ambayo itaweza, na inaweza, na itageuza maisha ya mwanadamu na kubadili mahusiano wa binadamu. Alikuwa ni "mtangulizi" wa wale wanaume na wanawake wote wanaotafuta wokovu wa wanadamu wote.

Lengo la msingi la Muhammad lilikuwa ni kuanzisha Mamlaka ya Mbinguni juu ya Ardhi, yaani, Serikali ya Kiislamu. Aliwafundisha wanadamu somo la Tawhiid (mafundisho ya

634

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Upweke wa Muumba), na aliwaalika kukubali Ukuu Wake. Alieneza sheria za Allah swt., akazitilia nguvu, na akaunda jamii ambayo sifa bainifu yake ilikuwa ni usafi. Katika jamii hiyo kulikuwa na utawala wa haki, elimu na uongofu, na alifuta unyonyaji, dhulma, ujin-ga na ushirikana kutoka ndani yake. Uislamu, dini pekee yenye kuamini Mungu Mmoja ambayo inawakilisha mfumo kamili wa kijamii-kiuchumi na kisiasa, kiasili ni yenye uhasama kwa serikali zote za kiimla, hususan zile ambazo zinatwaa maadili yasiyopatana na yanachukiza kwenye mfumo wa maadili wa Kiislamu.

Kuanzishwa kwa Mamlaka ya Mbinguni juu ya Ardhi ilikuwa ni sehemu ya kwanza ya ujumbe wa Muhammad. Sehemu ya pili ya ujumbe wake ilikuwa ni kuhakikisha kuende-lea kwake. Yeye hakuuanzisha "Ufalme" kwa ajili ya kipindi cha uhai wake tu bali kwa wakati wote, na sio kwa Waarabu tu bali kwa wanadamu wote. Yeye, kwa hiyo, alimteua kama mrithi wake, mtu ambaye yeye alijua kwamba ataendeleza kazi yake. Mtu kama huyo alikuwa ni Ali ibn Abi Talib, kama ilivyoelezwa kabla.

635

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Sera ya Ali (a.s.), ya Ndani na ya Nje

Sera ya Ndani

Moja ya malengo muhimu ya uislamu lilikuwa ni kuwazuia wale wenye nguvu kuwaonea wanyonge, na kukomesha unyonyaji katika miundo yake yote. Wakati Ali alipochukua mamlaka ya ukhalifa, aliwafukuza magavana waliokuwa wameteuliwa na Uthman. Aliambiwa kwamba isingefaa kufanya hivyo, na kwamba alipaswa kuimarisha nafasi yake kwanza kabla ya kuwafukuza hao. Lakini majibu yake kwa ushauri huo yalikuwa:

"Enyi Waislamu! Hivi mnapenda nifanye ushirikiano na ukatili, dhulma, usaliti na udanganyifu? Mnataka kwamba niwe msaidizi katika unyonyaji wa umma wa Muhammad? Wallahi mimi sitafanya hivyo kamwe mradi yale maumbo ya mviringo ya mbinguni yanavutana kila moja. Mimi nitazinyang'anya kutoka mikononi mwa mporaji zile haki za wanyonge, na nitazirudisha kwa wenyewe."

Kigezo cha msingi cha kulinganisha mifumo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa, kinapaswa kiwe, sio kigezo cha dola moja juu ya jingine na ubeberu bali kigezo cha ubinadamu, yaani, kipimo ambacho ndani yake kila mfumo una uwezo wa kweli wa kupunguza, kuzuia, na kufuta, kiasi ikavyowezekana, miundo mbali mbali ya unyonyaji wa watu. Ali alikuwa ndiye adui asiye na huruma kabisa wa unyonyaji katika miundo yake yote, na aliufuta kutoka kwenye milki zake wakati wa ukhalifa wake. Mpangilio wa kijamii, yeye aliamini, ulikuwepo tu kwa ajili ya kumtumikia binadamu na kwa ulinzi wa heshima yake.

Muhammad Mustafa (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt., alikuwa ameziangusha heshima zote zilizoundwa na wanadamu lakini baada ya kifo chake, zote zilirudi tena. Ali alitangaza kwamba alikuwa azibomoe heshima zile tena. Abu Ishaq Madaini, yule mwanahistoria, anaandika kama ifuatavyo, kuhusiana na hili:

"Baadhi ya masahaba wa Mtume walimwambia Ali kwamba wakati wa kugawa mali ya hazina ya umma kwa Waislamu, alipaswa kutoa sehemu kubwa kwa waungwana wa Kiarabu kuliko wale Waarabu wa kawaida; na alipaswa kutoa sehemu kubwa kwa Waarabu kuliko kwa wasiokuwa Waarabi. Walidokeza kwamba kufanya hivyo kutakuwa ni kwa maslahi yake yeye mwenyewe, na waliivuta nadhari yake kwenye mfano wa Mu'awiyah ambaye alikuwa amepata urafiki na watu wengi matajiri na wenye uwezo kwa njia ya 'ukarimu' wake.

Ali akawaambia: 'Hivi ninyi mnanitaka mimi nisiwe mkweli na mwenye kufanya haki kwa masikini na wanyonge wa Waarabu na wasiokuwa Waarabu? Kufanya hivyo

636

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kunaweza kuwa siasa nzuri sana lakini sio maadili mema. Kama ningekuwa nifuate ushauri wenu, ningekuwa, kwa kweli, ninawaigiza mapagani. Hivyo ndivyo mnavy-onitaka mimi nifanye? Kile chenye muhimu kwangu mimi, ni radhi za Allah, na sio radhi za waungwana wa Kiarabu. Kama ningekuwa ninagawa mali yangu mwenyewe kwa Waislamu, nisingeweza kufanya ubaguzi dhidi ya wale wasiokuwa Waarabu na watumwa. Lakini mali ambayo ninaigawa kwao sasa sio yangu; ni yao wenyewe. Nitawezaje kuonyesha ubaguzi? Nitawezaje kumnyima mtu mgao wake kwa sababu tu yeye sio Mwarabu, na niitoe kwa mtu mwingine ati kwa sababu ni Mwarabu? Hili sintalifanya abadan."

Sio Makuraish tu na mabwanyenye wa Kiarabu ambao hawakupata kutendewa upendeleo kutoka kwa Ali zaidi ya wale wasiokuwa Makuraish na wasiokuwa Waarabu katika ugawa-ji wa hazina ya umma, bali watu wa familia yake yeye mwenyewe walipata kidogo zaidi ya mtu yeyote katika utawala wake. Mmoja wao alikuwa ni kaka yake mkubwa, Aqiil. Aliuona ujira wake kuwa ni mdogo kiasi kwamba hakuweza kukidhi maisha nao, na akaondoka Kufa na akaenda Syria ambako aliishi kwa fahari na anasa kwenye baraza la Mu'awiyah. Ali mara kwa mara aliwaonya Waislamu juu ya hatari ya kupingana na maadili, na ya kuharibu thamani zao kwa kuthamini pesa na mali.

Wakati Ali alipopanda kwenye kiti cha ukhalifa, alijifunga kukomesha tabaka la kiuchumi la Waarabu, na mfumo wao wa kibepari uliokuwa kinyume na Uislamu. Katika kipindi cha miaka minne ya utawala wake, yeye alikuwa ametimiza wajibu wake. Ule mfumo wa kitabaka wa Waislamu na mfumo wao wenyewe mpya wa kibepari, yote ilikuwa imetowe-ka kwenye utawala wake. Wale 'makuhani wakuu' wote wa uchumi wa mfumo wa kitabaka wa Waarabu, na ubepari mamboleo wao, walitafuta hifadhi huko Damascus. Kama Waislamu wote ni sawa, basi usawa wao ulipaswa kuwa ni kitu cha dhahiri lakini haikuwa hivyo. Ali aliufanya uwe dhahiri. Na kama Uislamu unajivunia wenyewe kwa mshikamano wake na haki, basi haki hiyo ilipaswa kuwa ni kitu cha kuonekana lakini hakikuwa. Ali ali-ifanya ionekane. Aliufanya usawa kuwa dhahiri na haki kuonekana.

Kutoka kwa maofisa wake mwenyewe, Ali alidai na kulazimisha uaminifu binafsi na wa mali, wa hali ya juu kabisa. Alitoa tahadhari kwa kila mtu kwamba hata ile ofisi yenye nguvu sana ndani ya serikali haiwezi kutumika kama hifadhi kwa ajili ya wahalifu wala fursa zake za halali kutumika katika kuzuia ushahidi wa utendaji maovu.

Ni sababu kuu zipi, za vitendo na sera za Ali? Inaonekana kwamba kila jambo katika maisha yake lilitawaliwa na taqwa (woga wa kufanya jambo ambalo litamchukiza Allah swt.). Alizingatia wazo lile tu, alisema neno lile tu, na alifanya tendo lile tu ambalo alifa-hamu, kwamba litampatia radhi za Allah swt. Kila wazo lake, kila neno lake, na kila tendo lake, lilijaribiwa juu ya kigezo asili cha taqwa. Uhai wake wote ulizunguka kwenye swali moja, yaani, nitafikiri juu ya nini au nitasema nini au nitafanya nini ambacho kitampen-

637

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

deza Muumba wangu?

Kwa wadanganyifu wa nyakati zote, malengo yametimiza uhalali wa njia. Kwao wao, njia zote, nzuri au mbaya, ni halali, kama wataweza kufikia malengo fulani. Lakini kama Ali alikuwa atumie njia fulani kufikia lengo, ilikuwa iwe na uthibitisho wa Qur'an Tukufu. Katika matukio mbalimbali, zile zinazoitwa busara na hekima za kidunia zimeamuru mweleko fulani wa utendaji. Lakini kama mwelekeo huo wa utendaji ulikuwa unapingana na Qur'an Tukufu, Ali aliudharau, na alifanya hivyo bila ya kujali kabisa matokeo.

Sera hii ilimfanya Ali atabirike sana na kukosa usalama. Inasemekana kwamba kama mtu anao uwezo wa kutabiri, kisha mtu ana kiasi fulani cha udhibiti wa hali au wa mtu, na udhibiti una maana ya uwezo. Maadui wa Ali walijua hasa kile ambacho angefanya kile ambacho asingefanya katika hali inayotakiwa. Huku kujulikana kabla, kwa vitendo na hisia zake, kuliwapa fursa juu yake, na walikuwa tayari daima kuitumia fursa hiyo. Walichukua pia fursa ya hali ya juu sana ya uadilifu na ujasiri wake.

Moja ya sifa zinazotambulika za serikali ya Ali ilikuwa ni "uwazi" na umakini wake. Kama kulikuwa kamwe na serikali ambayo ilikuwa "wazi," basi ilikuwa ni serikali yake. Alikuwa na mashaka na usiri, na aliamini tu katika "mikataba ya wazi iliyofikiwa kwa uwazi." Mu'awiyah mwenyewe alijivunia kwamba msingi wa "mafanikio" yake binafsi ulikuwa kwenye usiri wake, na alichukulia "kushindwa" kwa Ali kwenye ukweli kwamba yeye Ali hakuwaficha raia zake kitu chochote.

Kutokana na maoni ya werevu, Mu'awiyah alikuwa sahihi. Aliwaacha watu wakikisia juu ya kila hatua zake ambapo kwa upande wa Ali, kubahatisha hakukuwa na lazima. Katika kushughulika na Ali, maadui zake waliweza kutotumia minong'ono ya aina zote. Kwake yeye, usiri uliashiria ujanja, na kama kitu chochote kilikuwa cha kijanja, kilikuwa hakikubaliki kwake. Tangu siku ya kwanza aliipiga marufuku imani ya kupeleleza na usiri katika utawala wake. Wakati rafiki yake mmoja alipomuuliza Ali ni kwa nini amekubali kuchukua madaraka ya serikali pamoja na wingi wa matatizo yake, yeye alisema kwamba alifanya hivyo ili kurudisha Mamlaka ya Mbinguni juu ya Ardhi, akijua kwamba hakuna mwingine yeyote katika Dar-ul-Islam ambaye alikuwa na uwezo huo. Baada ya vita vya Siffin, Ali alisema katika moja ya du'a zake:

"Ewe Allah! Wewe unatambua vema kwamba mapambano tuliyofanya, hayakuwa ni kwa ajili ya kupata mamlaka ya kisiasa, wala kwa ajili ya kupata nchi wala mali za kidunia; bali, ni nia yangu kutekeleza zile kanuni zenye kung'ara za dini Yako tukufu, na kurekebisha mwenendo wa mambo katika ardhi Yako, ili kwamba waja Wako wanyonge waweze kuishi kwenye amani, na sheria Zako ambazo zilikuwa haz-itimizwi, ziweze kusimamishwa na kutekelezwa kwa mara nyingine kama zilivyokuwa wakati wa Mtume na rafiki Yako, Muhammad."

638

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali hakuweza kuficha dharau na chuki yake kwa wale Waarabu ambao, wakiwa kama "wapenzi wakubwa wa marupurupu" wamekuwa matajiri sana na wenye uwezo. Yeye na wao "walichukiana". Kwa upande mwingine, alivutiwa bila kuzuilika kwa masikini na wanyonge. Hao walikuwa ni marafiki zake. Miongoni mwa matajiri na wenye uwezo, Abu Sufyan na Mughira bin Shaaba, walifanya majaribio ya kupima kujipendekeza kwake laki-ni yeye alikuwa ameyapuuza, na alikuwa ameweka umbali usiovukika kati yake m wenye we na wao.

Ali aliugeuza ukhalifa wake kuwa "shule" ambayo ndani yake aliufudisha au kuuelimisha upya umma wa Waislamu. Alikabiliwa na kazi kubwa ya kuelimisha upya, lakini ali-itekeleza kwa mfumo uliokamilika na kwa sifa bainifu ya kipawa. Alikuwa ni "chuo kikuu cha mtu mmoja" ndani ya Uislamu. "mtaala" wake katika "chuo kikuu" chake uliweka msisitizo mkubwa katika ujenzi wa tabia ya Waislamu. Aliupata "mpango makini" wa ujenzi wa tabia ndani ya Kitabu cha Allah swt., na alipata "mifano" juu yake katika maisha ya Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt. Katika "chuo kikuu" hicho, aliufasiri ule "mpango makini" na ile "mifano" kwa ajili ya ujenzi wa maadili na elimu ya "wanafunzi" wake - umma wa Waislamu.

Ali alikuwa bingwa wa ule mtazamo ambao uliwaunganisha wanadamu katika utii kwa Muumba wao. Alikuwa bingwa wa mtazamo wa Muumba wetu juu ya haki, ukweli, ubora na amani. Bidii yake kuu ya maisha yake ilikuwa ni kurudisha haki kamili kwenye Dola ya Kiislamu. Katika utafutaji huu, alifanikiwa vizuri sana.

Sera ya Nje ya Ali (a.s.)

Wakosoaji wa Ali mara kwa mara wanaonyesha kwamba yeye hakushambulia nchi nyingine kama watangulizi na warithi wake walivyofanya, na hakusukuma mipaka ya dola ya Kiislamu upande wowote.

Ali alikuwa khalifa kwa miaka minne, na miaka ile ilikuwa mifupi kwa maasi na vita vya wenyewe kwa wenyewe, na wakati wake wote ulitumika katika juhudi za kurudisha amani kwenye dola ya Kiislamu.

Lakini kama kusingekuwa na maasi na vita vya wenyewe kwa wenyewe, na kama utawala wa Ali nyumbani ungekuwa na amani na utulivu, je, angeanzisha uvamizi na mapigano ya nchi za jirani? Hakuna njia ya kujibu swali hili, lakini kuamua kutokana na tabia yake na mwenendo wake, inaonyesha kutoelekea kabisa kwamba angefanya hivyo. Inaonyesha kabisa kutowezekana kwamba angejitafutia "sifa" yeye mwenyewe au kwa Uislamu kwa kuvamia na kuteka nchi nyingine. Kutafuta "sifa" kama hiyo ni kinyume na hulka yake.

Msingi wa kuielewa sera ya Ali nyumbani na nje, umo katika ukweli kwamba yeye

639

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

alikuwa ndiye wasii na mrithi halali wa Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt., na Mtume wa amani. Muhammad alikuwa ni Mtume wa Allah swt., kwa wanadamu. Alikuwa ndio tashihisi ya sifa bora za tabia na hulka. Ndani ya maisha yake, kuna mfano kamili kabisa kwa Waislamu wote kuigiza, na utaratibu wake kwa ajili ya ustawi, furaha na wokovu wa mwanadamu, ndio ulio mpana zaidi.

Unabii na Utume ndio heshima kubwa kabisa mwanadamu anazoweza kupata katika dunia hii. Kuwa Nabii au Mtume maana yake ni kuchaguliwa na Allah swt. Mtu kwa hakika laz-ima awe amejaaliwa na tabia ya kipekee kuweza kuchaguliwa na Muumba Mwenyewe kutoka kwenye kundi kubwa la wanadamu ili kuwa Mtume Wake kwa wanadamu.

Mtu wa namna hiyo alikuwa ni Muhammad (s.a.w.w.). Aliteuliwa na Allah swt. kuwa chombo Chake katika utekelezaji wa mpango na utaratibu Wake kwa ajili ya dunia hii. Aliitoa jamii ya mwanadamu kutoka kwenye utumwa wa kimaadili na kiroho, na kuiweka mbali na ujinga, hofu na upweke ambao ulikuwa umeizonga. Allah swt., alikuwa ametuma mitume wengine wengi kabla yake lakini yeye alichaguliwa wa mwisho wao wote, na ujumbe aliouleta, haukutawaliwa na mipaka ya wakati au mahali; ulikuwa ni wa wakati wote, na ujumbe wake muhimu ulikuwa ni falsafa ya kilimwengu.

Muhammad alikuwa kwa hakika amejaaliwa na tabia ya kipekee kabisa ya kichwa, mkono na moyo. Mojawapo kati ya ubora huu unaweza ingeweza kirahisi tu kumfanya mtu mashuhuri kabisa katika historia. Lakini katika hatua hii, tutaangalia tu moja ya sifa zake nyingi - sifa ya rehma. Yeye alikuwa ni mfano wa rehma. Qur'an Tukufu imemuita Muhammad "rehma kwa viumbe wote."

"Hatukukutuma wewe, ila uwe ni rehma kwa walimwengu wote."(Sura ya 21; Aya ya 107)

Sifa hii ya rehma juu ya Muhammad (s.a.w.w.) kama Mtume wa Allah swt., haiendani na uchokozi na tamaa ya mapambano. Vita na umwagaji damu haviwezi kuwa mahali pamo-ja na rehma.

Ujumbe ambao Muhammad aliuleta kutoka Mbinguni, na ambao aliueneza katika ardhi, unaitwa Uislamu, na Uislamu maana yake ni "amani na uswalama." Uislamu ni dini ya amani. Mtu anayeukubali Uislamu huitwa Muislamu, yaani, aliyefanya amani. Muhammad mwenyewe alimwelezea Muislamu kama ni mtu ambaye ulimi na mikono yake, raia wengine watulivu wako swalama navyo.

Moja ya maneno ya msingi katika istilahi za Kiislamu ni Iman ambalo lina maana "kanuni za amani," na huyo mtu mwenye Imani huitwa Mu 'min yenye maana kwamba "mtu

640

Usahihi-73.jpg

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

anayeshika kanuni za amani." Muhammad (s.a.w.w.) ambaye alileta ujumbe wa mwisho wa Allah swt. kwenye dunia hii, anaitwa al-Rasul al-Amin, yaani, "Mtume wa Imani." Makka, mji, ambao yeye aliutoa ujumbe huu, inaitwa al-Baladul-Amin, yaani, "Mji wa Amani." Makka, kwa hiyo, ni sehemu takatifu, na yeyote anayeingia humo, anakuwa swalama kutokana na madhara.

Jina la mama yake Muhammad (s.a.w.w.) ni lenye maana ya "amani." Na jina la baba yake ni Abdallah ambalo lina maana ya "mtumwa wa Allah." Kama mtumwa wa Allah swt., anamtii Allah swt., na haingilii haki za wengine - watumwa wengine wa Allah swt. Amina na Abdallah walimleta Mtume wa Imani hapa duniani kukomesha umwagaji wa damu na kueneza neema ya amani juu ya ardhi.

Jina la mama mlezi wa Muhammad Mustafa lilikuwa ni Umm Ayman lenye maana ya "mama wa Majaaliwa." Malaika aliyeleta ujumbe huo wa Mbinguni kwa Muhammad, anaitwa al-Ruuh-ul-Amin yaani, "Roho wa Imani." Mrithi wake anaitwa Amir al-Mu'minin yaani, "kiongozi wa waumini wenye amani." Kwa hiyo, tangu mwanzo mpaka mwisho, Uislamu ni amani na usalama.

Neno lingine la msingi katika istilahi za Kiislamu ni Jihad. Kuna ukungu mwingi katika mzunguko wa neno hili kwamba si rahisi kuonekana liko kwa maana gani. Katika mizun-guko isiyo ya Kiislamu, Jihad ya Uislamu inalinganishwa na uchokozi wenye nia mbaya ambavyo sivyo. Ukweli hasa, Jihad maana yake ni juhudi au mapambano. Moja ya aina ya Jihad inayotukuzwa sana iliyolazimishwa juu ya Muislamu ni kupambana dhidi ya ujinga na dhulma, na kuzishinda tamaa zake mtu mwenyewe na silika duni. Uislamu umevitam-bua vita kama ni sheria lakini umewaruhusu wafuasi wake kupigana tu:

(a) ama katika kujihami,

(b) au, kwa kutoa adhabu kwa uvunjaji wa amani, pia inayoitwa Qisas kwa lugha ya Kiarabu ambayo ina maana ya "hatua-kinzani." Qisas kinaruhusiwa tu katika kuzima uchokozi. Uislamu hauruhusu Waislamu kufanya vita kwa sababa yoyote ya tatu.

Huko Makka, Muhammad (s.a.w.w.) aliwasilisha kwa Waarabu utaratibu wa kidini, wenye maadili, ujenzi upya wa unyofu na wa kijamii. Baada ya kuhamia Madina, aliongeza kise-hemu cha uchumi na cha kisiasa ndani yake. Ilimchukua miaka kumi na tano huko Makka kufanya kazi ya kuweka msingi wa Uislamu, na ilimchukua miaka mingine kumi hapo Madina ya kujenga na kukamilisha "jengo" lake. Miaka hii 23 ilikuwa ndio miaka muhimu sana katika kazi ya Uislamu kama mfumo wa ulimwengu.

Wakati Muhammad alipoanza kutekeleza mpango wake, alikabiliwa mara tu na bila kuk-wepa na changamoto nyingi. Kwa kawaida, Uislamu ulimtengeneza Ali ibn Abi Talib kama

641

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

jibu la changamoto hizo. Miaka hiyo 23 ya ujumbe wa Muhammad kama Mtume wa Allah swt., ilikuwa ni milolongo mirefu ya migogoro - yote ya kivita na ya amani - na Ali ali-ishinda yote kabisa.

Ali alikuwa ndio wasii na mrithi wa Muhammad (s.a.w.w.). Wakati yeye alipoanza kutekeleza mpango wa Muhammad Mustafa, yeye pia alikabiliana na changamoto nyingi. Robo ya karne ilikuwa imepita tangu kufa kwa bwana wake, Muhammad (s.a.w.w.), na tangu hapo Waislamu wengi wakaanza kuabudu nguvu za kiuchumi na kisiasa kama "masanamu" yao mapya. Uvunjaji wa masanamu haukuwa jambo lolote geni kwa Ali. Miaka mingi hapo kabla, yeye na bwana wake, Muhammad, waliyavunja masanamu ya Makuraish ndani ya Al-Kaaba. Sasa ametakiwa kwa mara nyingine tena kuyavunja "masanamu" mapya ya Waarabu. Lakini alitambua kwamba mabingwa wa hayo "masanamu" mapya wangesimama katika kuyatetea kama vile tu mabingwa wa yale masanamu ya zamani walivyowahi kusimama kuyatetea katika nyakati za Muhammad (s.a.w.w.).

Uislamu ulikuwa ni vuguvugu la kimapinduzi kwa maana ya kwamba ulikuwa ni mwisho wenye mkazo wa zama za kale zisizokubali mabadiliko, yaani, zama za kishirikina, na mwanzo wa zama mpya na zwnye nguvu, yaani, zama za kuamini mungu mmoja. Malengo yake yametangazwa ndani ya Qur'an Tukufu, na Mtume wake alikuwa amepewa dhima ya kazi maalum, kama tunavyosoma katika Aya ifuatayo:

Usahihi-74.jpg

"Kama tulivyompeleka kwenu Mtume kutoka miongoni mwenu, anakusomeeni Aya zetu, na kukutakaseni, na kukufundisheni Kitabu na hekima, na kukufundisheni yale mliyokuwa

ya 2; Aya ya 151)

Malengo haya, bila shaka, nia ya muhimu sana kwamba yamerudiwa rudiwa, kwa ajili ya msisitizo, katika matukio mengine matatu. Yanatokea ndani ya Aya za Qur'an zifuatazo:

1.  Sura ya 2; Aya ya 129

2.  Sura ya 3; Aya ya 164

3.  Sura ya 62; Aya 2

Malengo ya serikali ya Ali yalikuwa sawasawa na yale malengo ya Qur'an. Sera yake, kwa hiyo, ilikuwa:

1. kuzisimulia Aya za Allah swt. (mbele ya Waislamu);

2. kuwatakasa (hao Waislamu);

642

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

3. kuwafundisha (hao Waislamu) katika Kitabu na hekima;

4. kuwafundisha (hao Waislamu) katika elimu mpya.

Kama ilivyoelezwa hapo juu, pale Ali alipojaribu kuitekeleza sera hii, alikutana na upin-zani, lakini sio kutoka kwa wapagani. Cha kushangaza sana, alipata upinzani kutoka kwa Waislamu. Waislamu wenyewe, na sio wapagani, walimuwekea vipingamizi katika utekelezaji wa mipango yake, na katika kufanikisha malengo yake.

Malengo yaliyotangazwa ndani ya Qur'an kwa ajili ya umma wa Waislamu hayajumuishi utekaji wa nchi nyigine kwa nguvu za kijeshi. Wale wakosoaji wa Ali wanaosikitika kwam-ba yeye hakuongeza maeneo mapya kwenye ramani ya Uislamu, watasikitikia pia kile kimya kilicholingana cha Qur'an juu ya suala la kupanua utawala wa Kiislamu kwa kupi-tia vita na uvamizi. Kwa kweli, kuamua kwa maandishi yake, Qur'an inaonekana kutokuwa na upendeleo na vituko vya kijeshi vya aina yoyote ile.

Wengi wa viongozi wa kisiasa na kijeshi wa dunia wanakubaliana na raisi Charles de Gaulle pale aliposema: "Upanga ndio mhimili wa dunia," yenye maana kwamba dunia inauzunguka upanga. Ufaransa ya zama za kati iliita dhana hii "fort mayne" - mkono wenye nguvu, yaani, yeyote yule aliyekuwa na mkono wenye nguvu, basi hutawala.

Viongozi wengi pia wanakubaliana na falsafa ya kisiasa iliyotolewa kimuhtasari katika maneno ya hekima kwamba kwenye mapenzi na vitani lolote lile ni sawa. Katika ufukuzi-aji wa tamaa zao, waliona kuwa ni sawasawa kabisa kufanya vita juu ya mataifa mengine, kuwauwa watu wao, na kuwafanya watumwa wanawake na watoto wao. Ikiwa kama baad-hi ya viongozi hawa wameilowesha dunia kwenye damu, na wameharibu miji na ustaarabu, walitangazwa kwa shangwe kama mashujaa wakubwa na ni watu wenye vipaji vikubwa vya kijeshi wa historia. Hata hivyo, ushujaa na vipaji vyao vimemthibitisha tu Gibbon kwamba yu sahihi pale aliposema kwamba:

"Historia ni nini ila usajili wa maovu, upumbavu na misiba ya wanadamu."

Je, Uislamu pia unalinganisha mpango wake na uchu wa kuteka mataifa mengine ya kigeni? Kama inafanya hivyo, basi una tofauti gani na mipango ya kuiteka dunia ya viongozi wa kijeshi kama vile Alexander the Great, Julius Ceaser, Attila the Hun, Genghis Khan, Hulago Khan, Tamerlane, Napoleon na Hitler wote ambao wametembea na wale "madada wa ushindi - mauaji, utekaji nyara, moto, maangamizi, vifungo, wizi na uporaji? Vita vyote vinafanana katika mambo kama matatu: vifo, maangamizi na uporaji. Kurasa za historia zimetiwa madoa kwa damu ya watu wanyonge na wale wasio na hatia iliyomwag-wa na wenye nguvu na makatili.

643

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kama Waislamu pia walitia madoa kurasa za historia kwa damu, je, huo ni uthibitisho wa ukweli au hata wa umashuhuri wa Uislamu? Wanaweza Waislamu wakajivunia katika vita vya uvamizi wasivyochokozwa, na utekaji? Kama watajivunia, watajikuta wenyewe wakipingana na Kitabu cha Allah ambacho kinasema:

Usahihi-75.jpg

"Bila shaka imekwisha kufikieni Nuru kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na Kitabu kina-chobainisha - kwa (kitabu) hicho Mwenyezi Mungu huwaongoza wote wenye kutafuta radhi Zake katika njia za amani na swalama, na huwatoa katika giza na kuwapeleka kwenye nuru, kwa idhini Yake - na kuwaongoza kwenye njia iliyonyooka." (Sura ya 5; Aya ya 15 - 16.)

Waislamu wengi wanashikwa na pumbazo kwa zile "fahari za kijeshi" za karne ya 632-732 za historia yao. Rais Lincoln aliziweka "fahari" za kijeshi katika mtazamo sahihi kwani fahari inang'arisha pale aliposema:

"Fahari ya kijeshi ni ule upindemvua unaovutia ambao unaibukia kwenye umwagika-ji wa damu."

Damu ya nani? Ile Damu ya wanyonge, wasiotenda makosa, na mara nyingi, wasio na hatia!

Rais Truman wakati mmoja aliita vita "uzushi mbaya wa mwanadamu." Kuna uzushi wowote mbaya kuliko vita? Ni uzushi gani mbali na vita wenye uwezo wa kuua watu kwa kiwango kikubwa, na kuwafanya watoto kuwa mayatima na wanawake kuwa wajane? Ni uzushi gani mwingine wa mwanadamu wenye uwezo wa kushusha miji kuwa vifusi na majivu, na kuzalisha chuki isiyokoma na uhasama miongoni mwa mataifa?

Ukweli ni kwamba Uislamu na vita havichanganyiki. Uislamu ni neema ya Allah swt. Kwa kweli, ndio neema kubwa kabisa ya Allah juu ya ardhi. Jina lake lina maana ya amani; na amani na uswalama ni neema ambapo kupigana na umwagaji wa damu ni laana. Vita na utekaji wa Waarabu havikudhihaki pamoja na utaratibu wa Uislamu. Vingi kati ya vita hivi vilichochewa na haja au manufaa ya kisiasa, au kwa tamaa tupu ya mapambano. Wengi wa Waarabu waliotoka nje ya Arabia, baada ya kifo cha Mtume, hawakuwa mubalighina wa Uislamu. Walikuwa ni watekaji wa wazi wazi. Wengi wao walikosa elimu ya Uislamu, na hawakuwa na shauku ya kuueneza Uislamu. Wengi wao walizaliwa na kulelewa katika

644

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

desturi za kipagani, na walikuwa wakipigana dhidi ya Waislamu miaka miwili au mitatu tu ya nyuma.

G. E. Grunebaum:

"Muhammad mwenyewe alikuwa anatambua kabisa kwamba wale Mabedui walikuwa wamefanikiwa kushawishika kwa juu juu tu. "Waarabu (yaani, Mabedui) wanasema, tumeamini (amanna). Sema (uwaambie): Hamjaamini. Lakini semeni: Tumesilimu (aslamna). Kwani imani bado haijaingia mioyoni mwenu." (Qur'an 49:14).

(Classical Islam - A History 600 - 1258,uk. 51, 1970)

Ingawa hapo mwanzoni, Waarabu walipelekwa nje ya peninsula ya Arabuni kwa sababu za kisiasa, kama ilivyoelezwa hapo juu, mara tu walipata sababu zao binafsi za kudumisha kasi ya utekaji nchi. Nguvu iliyowasukuma kwa upande wao ilikuwa ni kupenda ngawira. Waarabu walikuwa wasioshindika katika vita kama walikuwa na uhakika wa kupata ngawira. Mbali na hili, hakuna kitu kingine kilichowavutia hata kidogo. Kama walikuwa hawana matumaini ya ngawira, hawakuwa na shauku ya kupigana. Mwelekeo wa Waislamu wa Madina juu ya Uthman wakati wa siku za mwisho za maisha yake, unaifanya hoja hii kuwa ya wazi kabisa. Walikuwa ni Waislamu wale wale ambao waliyarudisha nyuma mashambulizi ya wapagani. Lakini sasa ndani ya mji wao, mkuu wa dola yao alikuwa amezingirwa ndani ya kasri yake mwenyewe. Wazingiraji walikuwa mamia machache ya wageni, wasiokuwa na mizizi hapo mjini, na wasiokuwa na msaada wa jeshi lolote lenye silaha. Mzingiro ulichukua muda wa siku 49, na uliondolewa pale tu Uthman alipouawa.

Lakini Waislamu wa Madina hawakuzinduka na kuchukua hatua. Kwa nini? Hawakuzinduka kuchukua hatua za kumlinda khalifa wao kwa sababu hawakuwa na matumaini ya kupata ngawira.

Kupenda uporaji kwa Waarabu kulikuwa ni mazoea ya tangu zamani. Ni kupenda huku ambako ndiko kulikohusika na balaa la Uhud. Wapenda ngawira waliondoka kwenye ile njia ya mkakati, katika kuyaasi maagizo ya Mtume, na kwa kufanya hivyo, wakaubadili ushindi kuwa kushindwa. Qur'an pia imetoa ushahidi juu ya upendeleo huu wa Waarabu ndani ya Aya ya 152 - 153 za sura yake ya tatu - al-Imran.

M. Shibli:

"Tatizo gumu sana lilikuwa ni kupenda uporaji kwa Waarabu. Ilikuwa ni kupenda huku ambako ndiko kulikotawala vita vyao vingi. Katika nyakati za upagani, mapen-zi ya ngawira yalikuwa ni ugonjwa kwao. Lakini walipokuja kuwa Waislamu, mapen-

645

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

zi ya ngawira hayakupungua kwao."

Inasimuliwa kwamba safari moja, Mtume wa Allah swt. aliwatuma baadhi ya masahaba zake kwenye kabila fulani kwa ajili ya kuchukua hatua za kiadhabu. Viongozi wa kabila hilo husika walikuja kuwaomba Waislamu kama wanaweza kujadiliana masharti ya amani pamoja nao. Jemadari wa kundi la masahaba akasema kwamba amani inakubalika kabisa kwake kama watasilimu. Kabila hilo likasilimu kwa hiyo masahaba wakarudi Madina. Lakini walikuwa hawana furaha kabisa juu ya matokeo haya, na wakamlaumu jemadari wao kwa kuwanyima fursa ya kujipatia wenyewe ngawira. Hawakuridhika tu na kule kumlaumu yeye, bali pia, katika kuwasili Madina, walilalamika kwa Mtume dhidi ya jemedari wao. Lakini Mtume aliunga mkono uamuzi wa jemedari huyo, na akasema kwamba Allah swt. atamlipa kwa kuokoa maisha ya watu wengi.

(Life of the Prophet, Juz. II, 1976, Azamgarh, India).

Masahaba hawa wa Mtume walikuwa ndio Waislamu wa "mfano." Walipaswa wawe "wanyoofu." Ingekuwa na mantika kabisa kuchukulia kwamba wao walikuwa ni marafiki binafsi wa Mtume wa Allah swt., wasingekuwa wamechanganyikiwa na tamaa ya utajiri. Au, kama, kwa wakati mmoja, walikuwa wamechanganyikiwa na tamaa kama hiyo, ingeleta mantiki kuchukulia kwamba urafiki wake kwao ulirekebisha tabia yao kwa kiwan-go fulani kwamba yale mapenzi ya ngawira hayakuwa ule ugonjwa tena kwao ambao wali-wahi kuwa nao mwanzoni. Lakini walizithibitisha dhana hizi kuwa za uongo. Walikuwa ni hawa masahaba "wachamungu" na "watiifu" ambao walikuwa na hamu ya kupora kabila moja. Lakini kabila hilo husika liliukubali Uislamu kwa wakati muafaka, na hivyo wakayaepuka manyakuzi yao.

Mapenzi ya uporaji ya Waarabu wa kawaida (wasiokuwa masahaba, wananchi wa kawaida), ndiyo hayakuzuilika kabisa.

Sir John Glubb:

"Wakati Mabedui ndio waliounda sehemu kubwa ya yale majeshi ya Waarabu ambayo ndiyo yaliteka Uajemi na Byzantium kwa ajili ya dini hiyo, ile silika ya uporaji ilikuwa imejengeka isivyong'oleka katika hali yao."

(The Great Arab Conquests, uk. 313,1967)

Kupenda uporaji ilikuwa ni silika ya Waarabu. Ali alitaka kubadili, au, angalau, kuichujua silika hii, na akajaribu. Lakini jaribio hilo lilifanikiwa kwa kiasi tu, na gharama yake ilikuwa ya juu sana.

646

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wakati wote katika na baada ya vita vya Basra (vita vya Ngamia), Ali alikuwa amevikataza vikosi vyake kupora kambi ya adui na mji wa Basra. Yalikuwa ni masikitiko makubwa sana kwao. Wao, hata hivyo, hawakuwa na nia ya kusameha matunda ya kazi yao kirahisi hivyo. Waliamini kwamba mji wa Basra ulikuwa ni zawadi yao kama watekaji, na kwamba wao walikuwa na haki ya kumfanya adui yao kuwa mfungwa. Pale walipokataliwa haki hii na Ali, walitishia kutotii amri zake.

Ilikuwa ni hali ya hatari kwa Ali. Alipaswa kuzima maasi ya vikosi vyake. Alifanikiwa kulifanya hili pale alipotoa swali lifuatalo kwa wale waasi wenye uwezo sana: "Ni nani kati yenu atakayemchukua Aisha kama mgao wake wa wafungwa wa vita?"

Swali hili lilikuwa halijajitokeza kwamwe kwa waasi hao, na likawaacha wamekan-ganyikiwa na bila la kusema. Vipi Muislamu atamfanya Aisha, mjane wa Mtume wake, kuwa mfungwa, na bado akabakia kuwa Muislamu? Ndipo wao wakaridhia kukubaliana na maagizo ya Ali - hakuna kupora na hakuna wafungwa!

Hata hivyo, kukosekana kwa fursa ya kuipora Basra, kuliendelea kuchoma mioyo ya wengi wa wapiganaji wa Ali, na pia wao walichukia vizuizi alivyokuwa ameviweka juu yao. Kuchukia kwao kulitokota pole pole mpaka kulipokuja kulipuka katika vita vya Siffin. Kulikuwa ni kuchukia huku ambako kulitumiwa kiustadi sana na Mu'awiyah kulikotokea ghafla kama maasi, na Ali alilazimika kusimamisha mapambano ambayo takriban alikuwa ameshinda.

647

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali (a.s.) kama Mjumbe wa Amani

Ali kama msaidizi mkuu wa Uislamu na mlinzi na ngao ya Muhammad (s.a.w.w.), ni maudhui pana na ngumu. Bali Ali kama Mjumbe wa Amani ni maudhui pana vivyo hivyo na ngumu vivyo hivyo. Ni watu wachache, kama walikuwepo, waliopenda amani zaidi ya, au waliochukia vita kuliko Ali.

Wanafunzi wa historia wanajua kwamba maombi kwa ajili ya amani, haki na uadilifu, yanafanywa tu na wale watu ambao ni wanyonge na ambao wako katika hali ya kujihami. Hakuna sababu kwa wale wenye nguvu na wenye shari kutoa maombi kwa ajili ya amani. Alexander the Great, Julius Ceaser, Genghis Khan, Tamerlane na watekaji wengine wakuu katika historia hawakufanya maombi yoyote kwa ajili ya amani kwa yale mataifa waliyoy-ashinda. Ikiwa Louis XIV na Napoleon waliwasihi kamwe maadui zao juu ya amani, ilikuwa ni pale tu majeshi yao yalipoanza kurudishwa nyuma. Katika nyakati zetu, haikuwa ni Hitler aliyekuwa akiomba amani kwa mtu yoyote; yalikuwa ni yale mataifa aliyokuwa ameyateka yaliyokuwa yakiomba amani kwa ajili ya ubinadamu.

Kama kuna mpangilio wowote katika historia ambao ni wenye msimamo, ni ule wa kwamba wenye nguvu, waliolewa madaraka, wanapuuza kabisa; na wanyonge wanatafuta au wanajaribu kutafuta kimbilio kwenye maadili muhimu na misingi ya kimaadili.

Katika kanuni hii ya kawaida na ya kilimwengu, ipo hata hivyo, tofauti moja, nayo hiyo ni kwa Ali ibn Abi Talib. Hata pale alipokuwa na nguvu na maadui zake walipokuwa wanyonge, aliomba kutoka kwao amani kwa ajili ya ubinadamu, na aliwaomba wao kujiepusha na umwagaji damu. Hata pale alipokuwa mshindi, aliwatendea maadui zake aliowashinda kana kwamba wao watamuunga mkono kwa kuacha vita. Kama adui alilemewa, na alitaka kuokoa maisha yake, alichopaswa kufanya kilikuwa ni kumuomba tu Ali kuokoa maisha yake, na yeye Ali aliyaokoa maisha ya adui huyo.

Na alifanya hivyo bila ya kutanguliza masharti yoyote. Maadui zake walilijua hili kupitia uzoefu wa siku nyingi, na waliitumia kila fursa ya utambuzi huu. Wengi miongoni mwa watu walikwepa adhabu ya kifo kwa njia hii, kwa ajili ya uhaini na uasi.

Kama ilivyoonyeshwa kabla, Ali kwa desturi alikuwa na msimamo katika kutetea kanuni. Kwa desturi hii, ilimbidi alipe gharama kubwa sana. Lakini je, kulikuwa na njia nyingine? Kwake yeye kulikuwa hakuna. Kama angekuwa, kwa wakati wowote ule, katika kipindi chake, amepingana na kanuni, basi asingekuwa na tofauti na watawala wengine. Hao watawala na viongozi wengine wanatoa heshima za waziwazi kwenye mifano na utaratibu

648

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wao binafsi lakini katika utekelezaji wanaonyesha mapenzi yao tu kwenye siasa ya hali na mali; kwenye falsafa ya siasa bila maadili; na wanaweka maslahi yao binafsi mbele ya kitu kingine chochote.

Kama Ali angepuuza kanuni kwa ajili ya sera, basi serikali yake ingekoma kuwa ni Mamlaka ya Mbinguni juu ya Ardhi. Hili hakuweza kuliruhusu. Yeye alikuwa ameuhuisha Mamlaka ya Mbinguni juu ya Ardhi ambao ulianzishwa kwanza na Muhammad (s.a.w.w.). Wote hawa walitambua kwamba "Mamlaka" hayo yalikuwa ni muundo nyeti na wenye kuweza kuvunjika, na kwamba ulikuwa unatishiwa kutoka pande zote na nguvu zenye uadui - zote, za dhahiri na za siri. Walijua pia kwamba kama wangepingana na kanuni, basi "Mamlaka" hayo yangeanguka kutokea humo. Kufanya hivyo, kwa hiyo, kulikuwa hakuwaziki kwao wao. Wao hawakupingana na kanuni, na kama ilibidi walipe gharama kubwa kwa ajili ya kuitetea, walilipa kwa furaha kabisa.

Ali alikuwa anashughulikia baa la maadili linaloletwa na vita. Yeye aliamini kwamba vita na maandalizi ya vita, vilikuwa haviendani na afya na ustawi wa jamii ya wanadamu. Kuvishinda vita (kwa maana ya kuvizuia), kwa hiyo, kulikuwa ndio mshughuliko wake mkubwa.

Kwake Ali, hakukuwa na jema lolote katika vita. Yeye bila kuyumba alizitumia na kuzitil-ia nguvu amri za Qur'an kwenye siasa na vita. Kama angeweza kupata ushindi kwa njia yenye utata, alipendelea kusamehe ushindi bali hakutafuta kimbilio kwenye udanganyifu. Taratibu zake mwenyewe na utu wake vilikuwa, kwake yeye, vina umuhimu mkubwa zaidi kuliko ushindi katika vita.

Kama ilivyokwisha kuonyeshwa mapema kwenye mlango uliotangulia huko nyuma, katika nyakati za Mtume, kila wakati Ali alipokutana na adui katika pambano, alimpa mambo matatu ya kuchagua. Haya yalikuwa:

1. Kubali Uislamu; au,

2.  Usipigane dhidi ya Muhammad ambaye ni Mtume wa Allah, na ujitoe katika vita hivi;

3.  Kama machaguo hayo mawili ya awali hayakubaliki kwako, basi wewe kuwa wa kwanza kunishambulia mimi.

Wakati wa ukhalifa wake yeye mwenyewe, Ali alilazimika kupigana dhidi ya wale Waislamu ambao walisimama katika uasi dhidi ya serikali kuu. Aliwaomba wamalize migogoro kupitia majadiliano badala ya kupigana. Kupigana, kwake yeye kulikuwa ndio chaguo la mwisho, na lenye kuchukiza sana. Lakini kama mtu yoyote alimpinga yeye, basi huyo mpinzani ilibidi awe wa kwanza kumshambulia yeye Ali. Yeye kamwe hakuwa wa kwanza kumshambulia adui yake. Alisisitiza kupigana pambano la kujihami tu.

649

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Katika mapambano ya Mtume, kabla ya mapigano ya jumla ya vikosi, mabingwa wa kila upande walipigana wawili wawili kama vile wale wapiganaji wa kimaonyesho wa Kirumi. Katika vita vya Uhud, bingwa kutoka kwenye jeshi la Makka alitoka kwenye safu zao na kuwapa changamoto Waislamu. Ali alitoka kwenda kupambana naye. Muda kidogo baadae, Ali alikuwa amemshinda mpinzani wake, na alikuwa ameweka goti lake kifuani mwake ili kumpa pigo la kifo. Katika muda huo, kama kitendo chake cha mwisho cha ujasiri, yule bingwa aliyeanguka akamtemea Ali mate.

Kingekuwa ni kitendo cha kawaida kabisa na cha kibinadamu kwa upande wa Ali kuutum-bukiza upanga wake kwenye moyo wa mkosaji wake, ambaye, sasa akiwa ameshindwa, amevunja kanuni za desturi ya uungwana wa kipagani - kosa lisilosameheka katika Arabia.

Lakini Ali alifanya kinyume chake kabisa. Alinyanyuka kutoka kwenye kifua cha adui yake, akauweka upanga wake kwenye ala yake, na akarudi kwenye safu zake mwenyewe.

Majeshi yote yalikuwa yakiangalia mfululizo wa matukio haya, na wote walishangaa lakini hakuna aliyeshangazwa zaidi kuliko yule adui ambaye alikuwa ameshindwa wakati uleule, na hakuweza kuamini kwamba alikuwa salama. Ni nini ilikuwa maana ya kitendo hiki cha ajabu, alijiuliza kwa mshangao; hivi Ali hatamuua kwa ufidhuli wake huu?

Yule shujaa wa Makka alinyanyuka pale chini, alimkimbilia Ali, na akamuuliza ni kwa nini hakumuua yeye. Ali akasema:

"Kitendo chako cha kijinga kilinifanya mimi nikasirike. Sasa kama ingekuwa nikuue wewe, ningeridhika dhidi ya dhara binafsi. Lakini mimi sitafuti kuridhika dhidi ya madhara binafsi. Sipendi kumuua mtu yeyote kwa sababu binafsi yoyote ile."

Yule pagani alipoyasikia majibu ya Ali, mshangao wake ukawa mkubwa zaidi kuliko mwanzo. Lakini alielewa kwamba Ali alikuwa anapigana kwa ajili ya mfano bora. Jibu la Ali lilitimiza kile ambacho upanga wake haukukitimiza; lilivunja kule kutoamini kwa adui yake, na yule adui akasilimu.

Tendo hili moja lilielezea falsafa ya Ali ya maisha. Alidhihirisha wazi kwamba chuki yake, kama vile tu upendo wake, ilikuwa haiathiriwi na hisia. Hakuchukia au kupenda kwa ajili yake binafsi; alichukia au kupenda kwa ajili ya Allah swt. tu. Kama alipigana, ilikuwa ni kwa kutaka radhi za Allah tu; na kama alifanya amani, ilikuwa pia kwa kutafuta radhi za Allah swt. Sababu yake kamili ilikuwa ni kupata radhi za Allah swt.

Kama Ali alidharau kuua kwa sababu ya kanuni yake, alidharau pia kuua kwa sababu ya ubinadamu wake. Ilikuwa ni kwa ubinadamu wake kwamba mtu hatari na mdanganyifu kama Amr bin Al-Aas alikuwa na deni la uhai wake katika vita vya Siffin. Abbas Mahmud

650

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Al-Akkad wa Misri anaandika katika kitabu chake, 'Abqariyyat Imam Ali (Cairo,1970): Ushujaa na uadilifu wa Ali havikumruhusu kutumia fursa ya hali ambamo alimkuta adui yake katika hali ngumu na bila msaada. (Katika vita vya Siffin) Amr bin Al-Aas ghafla ali-tambua katika pambano kwamba alikuwa akikabilana na Ali, na akaanguka chini kuan-gukia uso wake. Mtu mwingine yoyote angeweza kumuua, na hivyo kuondosha chanzo cha matatizo ya kila wakati lakini Ali aligeuza uso wake pembeni kwa kukirihika, na haku-jishughulisha naye.

Katika vita vya Siffin, Ali mara nyingi alipigana kwa kujigeuza (ili asitambulike). Yeye kwa hiyo alikuwa amejigeuza wakati Amr bin Al-Aas alipokabiliana naye lakini muda kidogo baadae akamtambua. Katika kumtambua, yeye hakupoteza fahamu za akili yake. Aliangukia uso wake na akafunua matako yake, akijua fika jinsi ambavyo Ali angeipokea hila hii. (Ali alikuwa anatabirika!)

Ali alirudi nyuma kutoka kwenye kioja hiki cha kinyaa. Afisa mdogo katika jeshi lake Ali akaguta: "Huyu ni Amr bin Al-Aas. Usimwache akatoroka. Muue huyo." Lakini Ali aliepu-ka kumuua Amr bin Al-Aas kwa vile alivyokuwa amelala katika hali ile ya kinyonge.

Vita vya mwisho ambavyo Ali ilibidi apigane, vilikuwa ni vita vya Nahrwan, vilivyopigan-wa mwaka wa 658. Katika vita vile, mpiganaji wa kikharij alijikuta akiwa chini ya ncha ya upanga wa Ali. Akitegemea kukatwa katika vipande viwili, alinywea kwa hofu, na upanga wake na ngao vikamdondoka kutoka mikononi mwake. Lakini kwa wakati ule, alis-hangazwa kumuona Ali akirudisha mkono wake, kugeuza hatamu za farasi wake kutoka alikokuwa yeye, na kupambana na mtu mwingine kabisa. Bila kuamini macho yake mwenyewe, alikemea: "Ewe Ali! Hivi ndio hutaniua mimi?" Ali akamjibu "Hapana." Yule Kharij akauliza, "kwa nini? itamaanisha adui mmoja kupungua kwa ajili yako."

Kisha mahojiano yafuatayo yakatokea baina yao:

Ali:          Siwezi kukuua wewe sasa hivi kwa sababu umepoteza upanga wako na

ngao yako, na huna chochote cha kuweza kujilinda nacho.

Khariji: Ninafahamu, na hiki ndio kile nilichokisikia tu kwamba wewe humuui adui asiyekuwa na silaha. Lakini nimesikia pia jambo jingine, na ningeta-ka kujua kama ni kweli.

Ali:          Ni nini hicho ulichokisikia na ambacho unataka kukithibitisha sasa hivi?

Khariji: Nimesikia kwamba hukatai ombi hata la adui kama sio la kupita kiasi. Kama hili ni kweli, basi ningekuomba unipe upanga wako sasa kwa vile nimepoteza wa kwangu.

651

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ombi hilo halikuwa la busara sana, hasa ukichukulia wakati wake na mahali pake lakini Ali hakusita. Alikamata makali ya upanga, na akampa yule adui yake kwenye mpini. Adui huyo akauchukua, akajihakikishia yeye mwenyewe kwamba Ali alikuwa hana upanga, na akauliza:

Khariji: Sasa hivi huna silaha Ali. Hebu niambie ni nani atakayekuokoa kutokana nami sasa?

Ali:         Allah. Allah ataniokoa mimi. Imani yangu iko Kwake, na wala sio kwenye

huo upanga au ngao.

Jibu la Ali lilimshangaza yule Khariji asiyekata tamaa kwa mara nyingine tena, lakini pia lilimshinda, na akasema kwa mshangao:

"Umenishinda, Ewe mtu wa ajabu! Kuanzia sasa hivi, mimi nitakuwa mtumishi wako. Nitapigana upande wako dhidi ya maadui zako, na nitawaua hao."

Pendekezo la Khariji huyu lilipaswa kumfurahisha Ali, naye alipaswa kumkaribisha yeye kwenye safu zake mwenyewe, lakini akasema:

"Usipigane kwa ajili yangu wala dhidi yangu. Pigana tu kwa ajili ya Haki na Ukweli. Kama unaamini kwamba Haki na Ukweli viko upande wangu, basi kwa hali yoyote ile, pigana upande wangu."

Mkono wa Ali ulikuwa ndio silaha yenye nguvu zaidi sana katika ghala la Uislamu. Katika kila tukio, ulifungua lango la ushindi ambapo kila mkono mwingineo ulishindwa kufanya hivyo. Mkono wake pia ulikuwa "ufunguo" wa amani, na amani haiwezi kupata mtetezi mkubwa zaidi kuliko yeye mahali popote. Lakini kama ilivyoelezwa hapo juu, yeye alikuwa mtetezi wa amani kutoka kwenye nafasi ya nguvu, na sio kutoka moja ya unyonge. Kazi yake ilikuwa ni umbile la amani yenyewe.

Ali alikuwa hajengi ufalme. Yeye kwa hiyo, hakushughulika kama mjenga ufalme. Mjenga ufalme lazima awe mchokozi, mvamizi. Yeye lazima azishinde nchi nyingine na anapaswa aangushe falme zingine ambazo katika mabaki yake atajenga ufalme wa kwake mwenyewe. Ali hakuwa na malengo kama hayo. Kwa hiyo, yeye hakuvamia nchi yoyote. Nia yake yeye ilikuwa ni kurudisha kasi ya kazi ambayo bwana wake, Muhammad, Mtume wa Allah swt. alikuwa ameianzisha. Hili alifanikiwa kulifanya katika ile miaka michache ya ukhalifa wake.

Ali aliishi maisha halisi kabisa katika maana sahihi ya istilahi yenyewe. Vazi lake liliten-genezwa kutokana na kitambaa duni kabisa lenye viraka chungu nzima juu yake. Chakula

652

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

chake kilikuwa ni magamba makavu ya mkate wa shairi uliyochacha ambayo ilimbidi ayaloweke kwenye maji ili yaweze kulika. Mara chache, yeye alikula tende kiasi. Alikuwa akijinyima sana chakula, na mara kwa mara akiwaambia Waarabu wasile sana, na hasa, wasile sana nyama. ("Enyi Waarabu! Msiyafanye matumbo yenu kuwa makaburi ya wanyama.")

Hapo Madina, Ali aliyafanya maisha yake kama ya kibarua. Wakati alipokuwa mtawala wa Waislamu, mtindo wake wa maisha haukubadilika. Bado aliishi kama kibarua. Aliwatawala Waislamu kwa "ushirikiano" wa kazi. Kwa namna fulani, serikali yake ilikuwa ndio "Serikali ya Leba" (ya wafanyakazi) ya kwanza katika historia, na pia ndio ya mwisho, kwani hakuwa mfanyakazi wa kukaa kwenye "kiti chenye mikono" bali kwa hakika alifanya kazi kwenye mashamba na mabustani kwa ajili ya ufanisi.

Ali mara kwa mara alitoa heshima kubwa kwenye mazungumzo yake na kibarua, mfanyakazi na fundi stadi. Walikuwa ni "marafiki wa Allah," na je, mtu angefanya vizuri zaidi kuliko kuwalea hao - marafiki wa Allah? Yeye aliwalea, na alivutiwa nao kisilika. Kinyume chake, na inaweza kuonekana ni ajabu, yeye hakuweza kamwe, katika wakati wowote wa maisha yake, kufanya urafiki na matajiri. Kutokea mwanzo, ulikuwepo mfarakano usiofumbulika kati yake na wao. Alikuwa mbali sana na "makabaila" na "wak-wasi," na "mabepari" wa siku zile kama pembe moja ya dunia ilivyo kutoka kwenye nyingine. Ali alikuwa akijihisi vibaya sana juu yao.

Ali alitoa heshima kwa kazi za mikono kwa mfano wake yeye mwenyewe. Alitengeneza nguo zake binafsi na viatu vyake yeye mwenyewe, alikamua mbuzi wake mwenyewe, ali-chota maji kutoka kwenye visima, na kutwisha na kuwatua mizigo ngamia wa misafara. Wakati alipokuwa Madina, alipata riziki yake kama mtunza bustani wa mkulima wa kiyahudi. Aliyanywesha mashamba yake. Alikifanya kibarua kuwa na heshima, na vibarua kujivunia kuitwa hivyo. Falme yake ilikuwa ni nchi ya ukarimu wa kijamii na "pepo ya vibarua" ya uhakika kiasi ambacho dunia haijawahi kuona kabla au baada.

Ingawa ile miaka minne ya utawala wa Ali ilitingishwa na maasi na vita vya wenyewe kwa wenyewe, hapakuwa na hata mtu mmoja katika milki zake aliyepatwa na njaa kwamwe. Sio kwamba hapakuwa na njaa tu bali pia hapakuwa na kupanda kwa gharama za maisha. Kila mmoja alikuwa na chakula kingi na matumizi ya kumtosha. Huko Kufa, mayatima, wajane, vikongwe, na wagonjwa wote hawakuwa na wasiwasi juu ya chakula na makazi; Ali aliwaondolea matatizo yao yote. Katika majimbo, magavana wake walikuwa wawal-ishe masikini na wenye njaa kabla hawajaweza kujilisha wao wenyewe.

Kwa mayatima, Ali alionyesha mapenzi na upendo mwingi sana mpaka ikasemekana kwamba alikuwa anawadekeza. Alizikusanya lawalawa zote, asali na mapochopocho mengine aliyoweza kupata, na akawalisha kwayo hawa. Ali alikuwa mmoja wa wahisani,

653

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wanahuruma wakubwa walioishi kamwe. Hapo Kufa, alikuwa ametoa makazi kwa mkoma mmoja katika sehemu nje ya mji. Alimtembelea kila siku, akamuosha na kumfunga vidon-da vyake, akamlisha kwa mikono yake mwenyewe kwa vile alikuwa hana mikono, akam-laza kitandani, na kisha akarudi mjini. Ali hakuwa mpiganaji-mwema tu wa Uislamu, na mjumbe wake wa amani; alikuwa pia ndiye mlezi wa kwanza wa elimu katika umma wa Waislamu. Mahmoud Said al-Tantawi wa Misri anaandika katika kitabu chake cha Masahaba Kumi wa Muhammad, kilichochapishwa Cairo katika mwaka 1976:

"Ali alisimama katika kilele cha utukufu katika matawi yote ya elimu. Alikuwa ndiye mtu mwenye elimu zaidi kabisa katika sheria za Kiislamu. Alikuwa ndiye bingwa mkubwa kabisa katika elimu ya Qur'an. Alikuwa na uelewa sahihi zaidi wa malengo, na ufahamu kamili zaidi wa maana ya Qur'an kuliko mtu mwingine yeyote. Alidumisha usafi wa Kiarabu kama lugha, na akaweka sheria zake za kisarufi (nahau). Alikuwa ndiye fasaha zaidi wa waongeaji wote, na alipozungumza aligusa kila moyo kwa kiasi ambacho hakuna kitu kingine katu kilichoweza kufanya hivyo. Watu waliosikia hotuba zake, mara nyingi walilia kama watoto wadogo.

Ustadi huu ungekuwa sio wa kawaida kabisa kama ungepatikana kwa mtu mwingine yeyote. Lakini sio wa ajabu kwa Ali kwa sababu alipaswa kuwa kama hivi. Hata hivyo, alikuwa ni Mtume wa Allah swt. mwenyewe aliyemkuza, na akamuelimisha yeye. Ali alikuwa wa kipekee kwa maana ya kwamba alikunywa sana elimu ya Mtume kwenye chanzo asili chenyewe. Hiki ni kitu ambacho hakuna mtu mwingine yeyote aliyekifanya isipokuwa yeye."

(Ten Companions of Muhammad, uk. 150, 157, na 162)

Wanazuoni wote katika taratibu za tassawuff (usufi wa Kiislamu) wanafuatilia misingi ya mafundisho yao kwenye falsafa ya Ali. Yeye ndiye mtawala mkuu anayetambulika katika nyanja ya usufi. Madhumuni ya falsafa yake ni mapenzi yenye nguvu juu ya Allah swt., na mapenzi juu ya viumbe Vyake vyote.

Waadhi za Ali, hotuba, barua, maagizo, semi za ucheshi na methali za busara kwa ufupisho makini kabisa zilikisanifu Nahjul-Balagha (Somo la Hekima Fasaha), kuunda chemchemi ya falsafa ya Kiislamu, na nyumba ya hazina ya elimu za Qur'an. Zinamuelimisha msoma-ji katika namna nyingi mbalimbali za masomo kama vile Upweke wa Allah, utambuzi na mapenzi juu ya Allah; uhai na kifo; mbingu na ardhi; uumbaji na maangamizo ya mwisho; uadilifu binafsi na wa jamii; hiari na majaaliwa; serikali na kazi zake; maadili, mantiki na falsafa ya Qur'an; ufafanuzi wa Qur'an; historia na mantiki yake; sheria na hukumu; uhu-siano wa mtu na Allah na jamii; uhusiano kati ya sheria tukufu na zile zinazotumika; jamii bora; hekima na busara; msingi wa maadili wa dola; asili ya sheria halisi na mamlaka; haki na wajibu; na ujumbe wa Muhammad kama Mtume wa Mwisho wa Allah kwa wanadamu,

654

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

sunnah na Hadith zake.

Ali aliandika na kuzungumza kwa uzuri na ufahamu ulio kamilifu, na aliweka mkazo maalum juu ya usahihi. Ujumbe mwingi wa kiitikadi ulikoleza kabisa matini na tamathali za semi za Nahjul-Balagha.

Tirmidhi na Tabrani, wakusanyaji wa Hadith, wamemnukuu Muhammad, Mtume wa Allah swt. kwamba alisema: "Mimi ni Jiji la Elimu, na Ali ni Lango lake."

Kama mfuasi wa kwanza wa Muhammad (s.a.w.w.), Ali alitoa michango adhimu sana kwenye nyanja ya fikra pamoja na michango adhimu sawa na hiyo kwenye uwanja wa vitendo.

Huduma za kijeshi za Ali kwa Uislamu zinaelekea kufunika mafanikio yake kitaaluma. Zinahodhi mazingatio ya mwanafunzi wa historia, na hivyo ile picha ya jumla inaelekea kutoka "nje ya mtazamo." Kwa kweli, yeye alikuwa ndiye mwanzilishi wa udhibiti wa taaluma na mamlaka ya kielimu ya Waislamu. Hakuna khalifa kamwe ambaye alitoa mpan-go wa mfululizo nyaraka, maagizo, barua, waadhi na hotuba; na hakuna khalifa ambaye alijishughulisha mwenyewe kwenye uwanja mpana wa masuala, kama alivyofanya yeye. Maandishi yake, maagizo na hotuba juu ya ufafanuzi wa Qur'an ndio mategemeo ya kitaaluma ya Uislamu. Yeye alikuwa ni mfano kamili wa vipaji vingi.

Jurji Zaydan, mwanahistoria Mlebanoni-Mmisri, anaandika katika kitabu chake Collected Works, juz. I, uk. 550 kwamba wakati Amr bin Al-Aas alipovamia Misri, gavana wa Misri alitumia barua ile barua ambayo Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah swt aliyokuwa amemuandikia yeye gavana, miaka michache ya nyuma, akimualika kwenye Uislamu. Amr aliipokea barua hiyo, na ilikuwa na muhuri wa Mtume (s.a.w.w.).

Mwanahistoria huyu anaendelea kusema:

"Yeye Amr aliutambua ule muhuri wa Mtume. Kisha akauangalia ule mwandiko, na ulikuwa ni mwandiko wa Imam Ali ibn Abi Talib. Ali alikuwa ndiye mtu wa kwanza ambaye alianzisha sanaa ya uandishi katika (uenezaji wa) Uislamu. Alikuwa ndiye mwandishi wa Mtume. Walikuwepo waandishi wengine pia, na Amr bin Al-Aas alikuwa mmoja wao. Pale aliporidhika kwamba ilikuwa ni barua ya Mtume, yeye ali-ibusu., akaiweka juu ya kichwa chake, na kisha akaisoma kama ifuatavyo .."

Ali alikuwa, kwa hiyo, ndiye mwasisi ambaye "alihamasisha" sanaa ya maandishi katika huduma ya Uislamu. Abbas Mahmud Al-Akkad wa Misri, anasema katika kitabu chake, Abqariyyat Al-Imam Ali (Cairo, 1970):

655

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Ilibakia juu yake Ali kutoa mwongozo katika mafundisho ya Tawhiid (Upweke wa Allah swt.), katika haki za Kiislamu, katika sheria, katika fasihi ya Kiarabu (nahau), na katika ustadi wa uandishi wa Kiarabu. Tutakuwa sahihi kama tukiita kazi yake kuwa ndio msingi wa elimu za Kiislamu za zama zote. Au, vizuri zaidi, kama tukimwita yeye Ensaiklopidia ya Elimu yote ya Kiislamu katika karne ya kwanza ya Uislamu."

Wakati wa ukhalifa wake mwenyewe, Ali alilazimika kushughulika na mlolongo wa maasi, lakini kila alipopata vipindi vya nadra vya amani, alitumia fursa bora kabisa ya hivyo kuelewesha maadili ya Kiislamu kwenye umma wa Muhammad Mustafa.

Makundi ya wanaotafuta elimu walikusanyika huko Kufa kusikiliza mawaidha ya Ali.

Baada ya kila waadhi, alikaribisha maswali kutoka kwao. Mara kwa mara alikuwa aki-

waambia:

"Enyi Waislamu! Niulizeni swali lolote kuhusu jambo lolote mtakalokuwa nalo vich-wani mwenu, na fanyeni hivyo sasa hivi. Kumbukeni kwamba sitakuwa nanyi milele."

Ali alihimiza uhuru wa maswali na mijadala ya wazi juu ya masuala yote ya kidini, kima-fundisho, kisheria, kisiasa, kisaikologia na kisAyansi, na aliwahimiza Waislamu kuufanya Msikiti kuwa "baraza" kwa ajili ya kutoa mawazo yao kwa uhuru. Ali alikuwa na imani nzito juu ya heshima na thamani ya mtu binafsi, na haki yake ya uhuru wa kuamua katika ushawishi wake wa kidini, na katika desturi zake za kisiasa, kiuchumi na kijamii. Alikuwa na imani katika uwezo na kipaji cha mtu kutimiza majaaliwa yake kama mwakilishi wa Allah swt. katika dunia hii. Akiwahutubia watu katika moja ya tenzi zake maalum, alise-ma:

"Mnafikiria kwamba ninyi ni mwili mdogo (binadamu); bado ile dunia kubwa

(ulimwengu) imefichwa ndani yenu."

Ali alikaribia kuwa "mtu wa enzi." Yeye alikuwa ni walii, mwanazuoni, mfanyakazi, mshairi, mpiganaji, mshindi, hakimu, mwanafalsafa, mhisani, faqihi, msemaji fasaha, mtawala na mwanasiasa mweledi lakini juu ya mambo yote, alikuwa ndio wazo kuu la uzuri na ubora, la wale wanaume na wanawake wanaompenda Allah swt. Kitovu cha tabia yake kilikuwa ni mapenzi juu ya Allah swt. Alikuwa "amepumbazwa" na mapenzi juu ya Allah swt. Waadhi zake na hotuba zimejaa msisimko wa mapenzi haya. Ndani ya mojawapo, yeye alisema:

"Furaha yangu kubwa inanijia wakati ninapokuwa na subira juu ya Muumba wangu. Furaha hii ni kubwa sana kiasi kwamba siwezi kufikiria malipo mengine yoyote ambayo yanaweza kupita haya. Hayo ndio malipo yake yenyewe makub-wa."

656

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Katika hotuba nyingine yeye alisema:

"Mimi simuabudu Allah swt. kwa kuchochewa na shauku yangu ya kuingia Peponi kwa sababu hiyo ni ibada ya yule mtu anayefanya kazi kwa ajili ya mshahara wake. Mimi simuabudu Allah swt. kwa kuchochewa na hofu yangu ya kutupwa ndani ya jahannam kwa sababu hiyo ni ibada ya mtumwa. Mimi ninamuabudu Allah kwa sababu ya mapenzi yangu juu Yake, na kwa utambuzi kwamba Yeye peke yake ndiye mwenye kustahiki ibada na utii ninaompa Yeye."

Katika barua ambayo Ali alimwandikia rafiki yake, alisema:

"Kama yale mapazia yote yanayomficha Allah ili tusimuone yangenyanyuliwa kutoka machoni mwetu, na kama ingekuwa nijikute mimi mwenyewe mbele Yake bila ya lolote kati ya mapazia hayo, imani yangu juu ya kuwepo Kwake ingebakia vilevile hasa, kama ilivyo sasa hivi."

Ali alikuwa akifahamu kwa ukunjuvu zaidi juu ya wema na neema za Alllah zisizokuwa na kikomo. Moja ya dua zake alizokuwa akizipendelea sana ilikuwa:

"Ninaomba hifadhi ya nguvu za Mwenyezi Mungu, na ninaomba mazingira ya neema na baraka Zake zisizo na mpaka, na ninakualikeni kuomba pamoja nami ili kwamba Yeye atupe sisi hiari na uwezo wa kusalimisha matakwa yetu kwenye matakwa Yake, na atuwezeshe sisi kutenda vyema kwa heshima mbele Yake, na mbele ya viumbe Vyake vyote."

Chanzo cha vifungu vilivyonukuliwa hapo juu, sio akili au ubunifu wa Ali bali ni mapenzi yake makunjufu kwa Allah swt!

657

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ali na mifano bora ya uhuru na fursa

Ikiwa kama katika umma wa Muhammad, Mtume wa Uislamu, Ali alikuwa ndiye mjumbe mkuu wa amani, alikwa, bila shaka, pia ndiye mlinzi mkuu ndani yake wa uhuru na fursa za mtu binafsi.

Katika uchaguzi wa kiongozi wa Waislamu, Ali alifunikwa mara tatu lakini kwa kinyume kikubwa sana, ilikuwa ni kwake ambako waliiona fursa, kwa mara ya kwanza na ya mwisho katika historia yao, ya kuchagua kwa uhuru kiongozi wao wenyewe, na wakam-chagua. Katika kumchagua Ali, walikuwa bila kujua wakimchagua mdhamini wa uhuru wao wenyewe.

Kama ilivyoelezwa kabla, pale Muhajirin na Ansari hapo Madina waliposisitiza kwamba Ali achukue mamlaka ya serikali, na alikubali kufanya hivyo, alitangaza kwamba hakuna mtu hata mmoja aliyekuwa chini ya pingamizi lolote au chini ya shinikizo lolote la kuchukua kiapo cha utii kwake. Kwa hiyo, wale watu wote waliochukua kiapo cha utii kwake, walifanya hivyo kwa hiari.

Lakini walikuwepo watu wengi hapo Madina ambao sio tu walizuia kiapo chao cha utii kwa Ali bali pia walianza kuondoka Madina. Ali hakufanya jaribio la kuwazuia. Alipofahamishwa kuhusu kuondoka kwao, yeye alisema; katika utawala wake, kila mtu alikuwa huru kuishi Madina au kuondoka, na kwamba yeye hatamlazimisha mtu yeyote kuishi au kuondoka. Maadui zake walitaka kuondoka Madina naye akawaruhusu kuondoka, na hakuwauliza maswali yoyote.

Wengi wa masahaba wa Mtume waliokuwepo Madina, walikuwa wametoa kiapo cha utii kwa Ali. Miongoni mwao alikuwa ni Talha na Zubeir. Walikuwa wametegemea kwamba Ali angewafanya kuwa magavana wa Kufa na Basra. Lakini Ali aliteua watu wengine kwa ajili ya nafasi hizo mbili na kwa sababu hiyo wao wakaondoka Madina na makusudio ya kuvunja kiapo chao cha utii. Ali aliwaachia waende zao.

Sera hii ya "kutoingilia mambo" inapingana vikali na sera ya Umar ibn al-Khattab, khalifa wa pili, ambaye aliwazuia wale masahaba wakuu wa Mtume, hususan Muhajirin, kuan-damana na majeshi yake kwenda Uajemi au Syria au Misri, na kwa huzuni yao kubwa, ali-waamuru wao kubakia Madina. Alifanya hivyo kwa kudhania, kwa sababu ya hofu yake kwamba watatumia umaarufu na hadhi zao walizokuwa nazo kama masahaba wa Mtume, kama wangeruhusiwa kuingia kwenye yale majimbo mapya yaliyotekwa. Masahaba hao, mpaka hapo, walikuwa hawajafanya kitu chochote kutumia umaarufu wao. Lakini Umar

658

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

alikisia kwamba wangefanya, na kwa misingi ya kukisia huku, akawazuia uhuru wao wa kutembea.

Ali hakumzuia Talha na Zubeir hapo Madina kwa misingi ya kukisia kwake kwamba walikuwa na uhaini mioyoni mwao dhidi ya dola hiyo, ambao wote walikuwa nao.

Miezi michache baadaye, Aisha, Talha na Zubeir, walisimama katika maasi dhidi ya Ali, na wakaenda Basra. Lakini Ali bado hakutumia mbinu yoyote ya "kutumia nguvu" kuwafanya wakubaliane. Ilimbidi akabiliane na changamoto yao lakini alipendelea kufanya hivyo bila ya kutumia madaraka yake ya dola.

Kwanza kabisa, Ali alikuwa hakumwandikisha jeshini mtu yoyote. Yeye alikwenda kwenye Msikiti Mkubwa wa Madina, na akawaeleza Waislamu juu ya uasi wa Aisha, Talha na Zubeir. Aliwasihi wamuunge mkono katika kudumisha amani katika Dar-ul-Islam, na katika kulinda umoja wa dola. Aliwakumbusha pia kwamba wao walimpa kiapo chao cha kumtii yeye katika amani na katika vita. Lakini hapakuwa na majibu. Alirudia kuwasihi kwake katika siku ya pili na tatu na ya nne.

Baada ya siku nyingi, ni watu mia saba tu walioitikia maombi ya Ali, na ilikuwa ni pamo-ja na jeshi hili dogo ambapo aliondoka Madina. Hakuna wakati ambapo alijaribu kumlaz-imisha mtu yeyote kwenye jeshi lake. Watu wote wale waliopigana upande wake, walikuwa wa kujitolea.

Pili, Ali alitoa msamaha kwa raia wa Basra ingawa walistahili adhabu kwa ajili ya uhaini. Yeye, kwa kweli, hakuwafanya angalau kuwa wafungwa pale waliposhindwa kwenye vita. Yeye kwa hiyo aliwaruhusu marafiki na maadui zake vile vile kufurahia neema za uhuru.

Kukataa kwa Ali kuwazuia pale Madina wale watu ambao hawakumpa kiapo chao cha utii, ruhusa yake kwa Talha na Zubeir kuondoka Madina, na msamaha wake kwa wale waasi wa Basra, ni ushahidi fasaha wa kukusudia kwake kutetea maadili bora ya uhuru na fursa.

Ali alithibitisha kwamba, katika Ufalme wa Mbinguni juu ya Ardhi, uhuru na fursa havikuwa ni maadili madogo na yasiyo na uhakika za kuthaminiwa na Waislamu bali vilikuwa haki yao, na kwamba hawakuwa waishi kama wafungwa kwa maana yoyote ya istilahi hiyo. Uhuru uliopunguzwa ni kinyume na heshima ya uraia wa Ufalme wa Mbinguni. Kila ambaye aliingizwa kwenye Ufalme wa Mbinguni, alikuwa amekombole-wa; alipata kuwa huru na alibakia kuwa huru.

Wakati Ali alipochukua mamlaka ya serikali, umma wa Waislamu ulikuwa katika hali isiyokuwa ya kawaida. Tabaka lake la watawala lilikuwa limefikia hali ya utajiri wa kupin-dukia na kiburi cha mwisho kabisa cha madaraka. Alitambua kwamba ile hali ya kijamii,

659

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kiuchumi na kisiasa ya dola ilihitaji uundwaji upya wa serikali na jamii. Lakini jaribio lake la kuunda upya serikali na jamii lilikasirikiwa na matajiri na wenye nguvu, na kukasirika kwao kulifumuka katika vita vya Basra na Siffin, kama ilivyoonyeshwa hapo kabla. Kundi la tatu lililotangaza upinzani kwenye sera ya marekebisho ya Ali, lilitokana na Khariji. Wao walitaka kufanikisha malengo yao kwa kupitia mapinduzi ya vurugu na mageuzi ya nguvu. Waliliweka wazi kwamba hawatamruhusu Ali kurudisha ufanisi, umoja na nguvu kwenye serikali kwa njia ya amani na utaratibu.

Makhariji hao waliutukana uhuru amabao Ali aliutoa kwa Waislamu. Hawakushutumu tu sera zake bali pia waliitilia shaka imani yake yenyewe. Lakini yeye hakujaribu kuwazuia. Alizivumilia shutuma zao zisizo na kiasi na zenye kuchoma sana alimuradi hazikuvuruga amani, na hazikuhatarisha usalama wa Waislamu wengine.

Ali aliacha kosa la maoni livumilike ikiwa akili iliachwa huru kupigana nalo. Lakini Makhariji waliitumia kila fursa ya uhuru wao, na wakaanza kueneza vurugu uvunjaji wa sheria na vitisho katika ardhi. Ilikuwa ni pale tu walipovuka vitisho vya kuwauwa raia wema, wenye kufuata sheria, na hasa wakawaua wengi wao, ambapo Ali akalazimika kwenda kinyume nao kuzuia uovu wao.

Mji wa Kufa, makao makuu ya Ali, ulikuwa wazi kwa Makhariji na maadui zake wengine. Walifaidi uhuru kiasi kile kile walichofaidi marafiki zake. Waliishi hapo Kufa, au waliin-gia na kutoka walivyotaka. Ali kamwe hakumuweka hata mmoja wao kwenye uchunguzi.

Raia wote wa Dola ya Kiislamu - wanaume, wanawake na watoto - walilipwa mishahara yao kutoka kwenye Hazina ya Umma. Makhariji walichukua mafungu yao kama raia wengine. Ali na maafisa wake kamwe hawakufanya kamwe jaribio la kuwafanya wawe wachangamfu, watiifu na wenye kushawishika kirahisi kwa kupitia shinikizo la kiuchumi. Walibakia kuwa maadui wagumu wa dola na jamii walioahidi kuangamiza vyote, dola na jamii. Hatimae mmoja wao akaumuua yeye.

Hata baada ya yote haya, hata katika nyakati za giza kabisa, Ali hakuruhusu kamwe utajiri wa kinyume ufutilie mbali maadili ya uhutru na fursa kutoka kwenye moyo wa umma wa Muhammad. Uhuru na fursa vilibakia kwake yeye ni vya kulindwa kwa madhara yoyote, visivyoweza kuharibika, thabiti, kama imani yake binafsi katika ushindi mkubwa na usiopingika wa Haki na Ukweli.

Labda hakuna kitu ambacho ni rahisi sana kama kutukuza sana sifa za uhuru na fursa lakini Ali ndiye mtawala mweledi pekee katika ulimwengu mzima ambaye alitoa heshima zake kwavyo (uhuru na fursa), sio katika ufasaha wa kutamka, bali katika vitendo vya dhahiri. Hakuna mtawala katika historia ya ulimwengu aliyewahi kutoa uhuru zaidi kwa raia zake - marafiki na maadui halikadhalika - kuliko Ali! Uhuru aliotoa kwa raia zake kwanza

660

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ulimgharimu ushindi katika vita vya Siffin, na kiksha ukamgharimu maisha yake mwenyewe. Lakini inaonekana kwamba katika maoni yake, uhuru wao ulikuwa ni kitu cha thamani sana, na hakuonea wivu ile bei aliyolazimika kulipa ili kuuhifadhi. Utawala wa Ali ulikuwa ni mfumo mpya wa kidini kwa jamii ya mwanadamu, na matu-maini mapya kwa wanadamu. Hakuna tena kamwe, katika historia, Waislamu na wasiokuwa Waislamu walipoweza kufaidi uhuru na fursa kama hiyo waliyofaidi wakati wa ukhalifa wa Ali ibn Abi Talib!

Ali na Urithi wake

Ali alikuwa na dharau juu ya utajiri na ufahari; yeye alikuwa na heshima juu ya mtu binaf-si; na allikuwa na imani katika uwezo wa hali ya juu wa akili kama ikiachwa huru bila ya vikwazo vya kiasili na upendeleo. Yeye alikuwa ni adui wa upendeleo, na alipigana dhidi yake maisha yake yote.

Kama mlezi wa kweli wa Uislamu, Ali alikazia macho kwenye maslahi ya Uislamu tu. Kama ilibidi atoe mhanga maisha yake ili kulinda maslahi ya Uislamu, alifanya hivyo kwa furaha kabisa. Katika usiku wa Hijira ya bwana wake, Muhammad (s.a.w.w.), kutoka Makka kwenda Madina, yeye alilala kwenye hatari. Tokea siku ile, maisha yake yaliteng-wa kwa huduma kwa Muhammad na ulinzi wa Uislamu.

Katika kumchunguza Ali na amali zake, sehemu tatu kuu zinaonekana wazi. Ya kwanza ni tabia yake, ambayo takriban inakubalika kilimwengu kwamba ndio bora zaidi. Kwa nafsi yake na katika wadhifa wake alisimama nyuma ya mifano bora na kanuni ambazo zimewekwa wazi ndani ya Qur'an. Rekodi ya ukhalifa wake inaonyesha kwamba mifano yake bora na kanuni zake ni changamoto kwa kila kizazi cha Waislamu: usawa kwa watu wote, uhuru, usiokiukwa hata katika nyakati za vita na hali ya tahadhari ya "kitaifa"; maen-deleo ya binadamu yenye amani, kupitia fursa binafsi na msaada wa taasisi za serikali. Yeye, kwa hiyo, aliwakilisha ushindi mkubwa kabisa wa tabia na itikadi.

Ya pili ni mafanikio ya Ali kama kiongozi wa kijeshi. Alikuwa ni jemadari mwenye kipa-ji ambaye utu wake ulimshangaza kila mmoja. Aliwaongoza Waislamu kwenye vita kwa umahiri mzuri sana, ujuzi, uvumilivu na utulivu. Yeye peke yake ndiye aliyefanikiwa, kati ya watawala wote, katika kuchanganya kanuni za maisha na falsafa ya Uislamu pamoja na mkakatiki na mbinu za kisiasa na vita.

Ya tatu ni kile kiasi ambacho athari za mwenendo na maadili ya Ali zimechangia katika ustawi na umaarufu wa Waislamu. Aliwafundisha kwamba njia za kufanikishia malengo zilikuwa ni tukufu sana kama malengo yenyewe, na kwamba njia hizo kama malengo yenyewe, zilikuwa zisiwe na mashaka yoyote. Yeye dhahiri kabisa alijishughulisha na mambo ya msingi kabisa.

661

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Jamii ya Kiislamu iliyokamilifu ni ile ambamo watu na watawala wao wanatii sheria ya Allah swt. Madhumuni ya Ali kwa hiyo, yalikuwa ni kuusimika umma katika safu za wale watu ambao wanaitii sheria hiyo. Kwa kufanya hivyo, alipanua upeo wa maadili ya jamii ya Kiislamu, na akaimarisha misingi yake.

Ali aliwasilisha kwa umma wa Waislamu mlingano uleule wa tabia kama bwana na kion-gozi wake, Muhammad, alivyokuwa amefanya kabla yake; na wote wawili walionyesha uwezo ule ule na moyo ule ule wa uvumilivu wa kuweza kukabilana kwa mafanikio na mitihani mikali sana na changamoto ambazo kwazo ushindi na maafa, kwa kulandana, vili-wakabili wao.

Moyo wa kutoa kafara kwa ajili ya wajibu na utaratibu, ni urithi wa manabii wote wa Allah swt. Moyo huo huo ndio "urithi" wa Ali ibn Abi Talib kwa umma wa Muhammad Mustafa. Rehma na amani ya Allah juu yao na familia zao.

662

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Orodha ya "watu wa kwanza" katika Uislamu

Mtu fulani katika Uislamu alikuwa mwanaume wa kwanza au mwanamke wa kwanza kufanya au kusema kitu, na hili lilimfanya kuwa mwanaume au mwanamke mtangulizi. Ifuatayo ni orodha ya baadhi ya matendo ambayo yaliwafanya watendaji wake kuwa "watangulizi." Orodha hiyo, bila shaka, kwa hali yoyote ile sio kamilifu.

(1). Hashim, babu-mkuu (babu yake baba) yake Muhammad ibn Abdallah na Ali ibn Abi Talib, alianzisha mfumo wa kibiashara wa Hijazi, ambao, kwa nyakati zile, ulikuwa ni mapinduzi katika maisha ya kiuchumi ya Arabia. Kwa kufanya hivyo, aliwabadili Makuraish kutoka wachungaji na kuwa wafanyabiashara matajiri.

Ibn Ishaq:

"Inadaiwa kwamba Hashim alikuwa mtu wa kwanza kuanzisha safari mbili za mis-afara ya Makuraish, ya kiangazi na ya kipupwe, na wa kwanza kutoa (kuandaa) tharid (mchuzi) hapo Makka."

(2). Khadija binti Khuwaykid, mke wa Muhammad Mustafa, alikuwa wa kwanza kusil-imu.

(3). Mwanaume wa kwanza aliyeshuhudia kwamba Mungu ni Mmoja, na Muhammad alikuwa ni Mtume Wake, alikuwa ni Ali ibn Abi Talib.

(4). Sehemu ya kwanza ya kukutania katika Uislamu ilikuwa ni katika nyumba ya Arqam bin Abil-Arqam hapo Makka.

Betty Kelen:

"Uislamu wa mwanzoni ulikuwa ni vuguvugu la vijana, ambalo awali lilifikiriwa kama chama kisichokuwa na madhara. Walikuwepo katika siku zile takriban wanachama 40, na walikuwa wakipenda kukutana katika nyumba kubwa katika kiun-ga cha mji iliyokuwa mali ya kijana mmoja tajiri aitwaye Arqam wa kabila la Makhzum. Nyumba hiyo ya Aqram inakumbukwa na Waislamu kama sehemu ya kwanza ya kukutania ya Uislamu."

(5). Akina Yasir walikuwa ndio "familia nzima" ya kwanza kusilimu (nje ya familia Mtume mwenyewe). Yasir, mke wake, Sumayya; na mwana wao Ammar; wote watatu walisilimu mara tu walipousikia mwito wa Mtume wa Allah swt. Watu

663

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wengine wamedai kwamba alikuwa ni Abu Bakr aliyekuwa mkuu wa "familia nzima" ya kwanza kusilimu. Madai haya yanakosa ushahidi. Mtoto wa Abu Bakr, Abdur Rahman, alikuwa ni mwabudu sanamu, na alikpigana dhidi ya Mtume wa Allah katika vita vya Badr. Baba yake Abu Bakr, Abu Qahafa, alikuwa pia ni muabudu masanamu ambaye alikuja kuwa Muislamu tu baada ya kutekwa Makka mnamo mwaka 630.

(6). Wapagani wa Makka walimtesa Yasir na mke wake Sumayya, na mtoto wao Ammar, siku baada ya siku, kwa kuukubali Uislamu. Wote watatu walikuwa ndio Waislamu wa kwanza ambao Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah swt. aliwabashira kwamba wataingia Peponi.

(7). Sumayya, mke wa Yasir, alikuwa Mu'min wa kwanza aliyekufa shahidi katika Uislamu. Mume wake, Yasir alikuwa shahidi wa pili katika imani. Wote waliteswa mpaka kufa na wapagani hao. Mtoto wao, Ammar, alikuwa amepangiwa kupata sha-hada ya kifo cha Kishujaa ingawa alifanya hivyo katika vita vya Siffin mwaka 657. Waligeuka, kwa namna hii, kuwa familia ya wote Mashujaa katika Uislamu - sifa ambayo hakuna yoyote aliyewahi kushirikiana nao. Allah swt. Mwenyewe aliwach-agua kwa ajili ya heshima hii kubwa.

(8). Mtu wa kwanza kusoma Qur'an kwa sauti ndani ya Al-Kaaba alikuwa ni Abdallah ibn Mas'ud, sahaba na rafiki wa Muhammad (s.a.w.w.).

Ibn Ishaq

"Yahya b. Urwa b. Zubeir aliniambia kutoka kwa baba yake kwamba mtu wa kwanza kusoma Qur'an kwa sauti hapo Makka baada ya Mtume alikuwa ni Abdallah ibn Mas'ud."

(9). Mtu wa kwanza kuuawa kwenye viwanja vya Al-Kaaba alikuwa ni Al-Harith ibn Abi Hala, mpwa na mtoto wa kutwaliwa wa Khadija, mke wa Mtume. Pale huyu alipotangaza Umoja wa Allah ndani ya Al-Kaaba mbele ya mkusanyiko wa waabudu masanamu, walimfanyia ukatili wa kimwili. Al-Harith ibn Abi Hala aliin-gia kwenye ugomvi wa kujitetea. Wakamchoma kwa marudio rudio, na akaanguka chini amekufa. Kwa hiyo yeye akawa Shujaa wa tatu katika Uislamu.

(10). Ammar ibn Yasir alikuwa mtu wa kwanza katika Uislamu kujenga Msikiti. Alijenga msikiti wake hapo Makka penyewe.

Ibn Ishaq:

664

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Sufyan ibn Uyayna alitaja kwa idhini ya Zakariya kutoka kwa al-Shabi kwamba mtu wa kwanza kujenga msikiti alikuwa ni Ammar ibn Yasir."

(11). Mas'ab ibn Umayr alikuwa ndio mtumishi wa kwanza katika Uislamu. Mnamo mwaka 621, kikundi cha raia kutoka Yathrib (Madina) kilikuja Makka. Walikutana na Mtume huko Aqaba; wakasilimu, na wao wakamuomba Mtume kuwapa kwenda naye Madina, mwalimu wa Uislamu na Qur'an. Mtume (s.a.w.w.) akamtuma Mas'ab ibn Umayr, binamu ya baba yake, kwenda pamoja nao. Hii ilikuwa ni mara ya kwanza kuchaguliwa mtumishi katika Uislamu. Mas'ab ibn Umayr alikuwa Mwakilishi wa Kwanza wa Muhammad Mustafa, Mtume wa Allah swt., katika wadhifa wowote ule.

(12). Abdallah, mtoto wa Abd al-As'ad, alikuwa mtu wa kwanza kuhama kutoka Makka kwenda (Yathrib) Madina mwaka 622.

(13). Bilal alikuwa ndio "muadhini " wa kwanza wa Uislamu. Sauti yake ilivuma hapo Madina kwa ukelele wa Allah-u-Akbar (Allah ni Mkubwa). Wakati Madina ilipokamilisha sifa zote za dola, ilijipatia hazina pia, na Muhammad (s.a.w.w.) akam-teua Bilal kuwa afisa-msimamizi wa hazina hiyo. Alikuwa msimamizi wa Bayt-ul-Mal ya dola ya Madina. Hii ikamfanya awe Mtunza Hazina wa Kwanza wa Uislamu. Alifanya mgao wa mali zote. Yeye alikuwa pia anahusika na kugawa mali kwa wajane, mayatima, wasafiri na watu wengine masikini ambao walikuwa hawana njia ya kujikimu wao wenyewe.

(14). Hamza ibn Abdul-Muttalib, ami yake Muhammad na Ali. Alikuwa kamanda wa kijeshi wa kwanza katika Uislamu. Mtume wa Allah swt. alikuwa amemtuma yeye akiongoza Muhajirin 30 kwenda kuingilia kati msafara wa Makuraish, ukiongozwa na Abu Jahl. Lakini hakukuwa na mapambano, na kikosi hicho kikarudi Madina.

(15). Gavana wa kwanza wa Madina alikuwa ni Saad ibn Ubada Ansari. Katika mwaka wa pili wa Hijiria, Mtume mwenyewe aliongoza kikosi kwenda Waddan. Wakati wa kutokuwepo kwake, Saad ibn Ubada alisimama kama mtawala wa Madina.

(16). Kamanda wa kijeshi wa kwanza ambaye watu wake walihusika katika umwagaji damu, alikuwa ni Abdallah ibn Jahash, binamu wa Mtume. Yeye aliongoza kikosi cha watu saba kwenda Nakhla.

(17). Vita vya Badr, vilivyopiganwa mwaka 624, vilikuwa ndio pambano la kwanza, katika uwanja wa vita, kati ya Uislamu na upagani. Bingwa wa kipagani, Walid bin Utba, aliwatia changamoto mashujaa wa Uislamu kwenye pambano la watu wawili wawili. Changamoto yake ilijibiwa, kwa upande wa Uislamu, na Ali ibn Abi Talib,

665

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

mwanaume wa kwanza kusilimu. Ali alimuua Walid bin Utba baada ya dakika chache za ufundi wa kutumia upanga. Huu ulikuwa ndio mwanzo wa pambano refu kati ya Uislamu na upagani.

Lilikuwa liishe kama lilivyoanza, kwa ushindi wa Uislamu juu ya upagani, na Ali alikuwa ndiye muasisi wa ushindi huo.

(18). Ubaidullah ibn al-Harith ibn Abdul-Muttalib, alikuwa Muislamu wa kwanza kuuawa katika vita. Yeye alikuwa ni binamu ya Muhammad na Ali, na alikuwa ndiye Shahidi wa kwanza wa vita vya Badr.

(19). Zayd ibn Haritha alikuwa ndiye Muislamu wa kwanza kuuawa kwenye ardhi ya kigeni. Mnamo Septemba 629, Mtume alimtuma yeye kama jemadari mkuu wa jeshi ambalo lilikuwa lishambulie Warumi huko Syria. Majeshi hayo mawili yalikutana katika vita vya Muutah, na Zayd aliuawa katika vita hivyo.

(20). Akib ibn Usaid alikuwa gavana wa kwanza wa Makka. Ilikuwa ndio ajira ya kudumu ya kwanza kufanywa katika Uislamu. Akib alichukua mamlaka ya wajibu wake kama gavana wa Makka mnamo Januari 630.

666

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

"Mgawanyo wa lazima" wa Uislamu

Miaka ya awali ya Uislamu ilikuwa ni wakati wa majaribu magumu na mitihani mizito kwa Waumini. Kila siku iliwaletea makabilano mapya na, na changamoto mpya kutoka kwa washirikina, na pambano lisilokwisha, likiwa kwenye mazingira ya kikatili tu. Kazi yote ya Muhammad kama Mtume wa Mwisho wa Allah kwenye dunia hii, ambayo ilidumu kwa miaka 23 ya mwisho ya maisha yake, ilivunikwa na pambano hili.

Lilikuwa ni pambano kubwa sana. Ni wanaume na wanawake wa imani isiyoshindika, ujasiri thabiti, na nguvu zisizochoka tu ambao wangeweza kuishi katika mfadhaiko na wasiwasi wake. Ili kukabiana nalo, kwa hiyo, Uislamu ulitoa "majitu maarufu" yake wenyewe. Hayo "majitu maarufu" ya Uislamu yalikuwa watu binafsi wawili na vikundi viwili. Watu binafsi hao wawili walikuwa ni Abu Talib ibn Abdul-Muttalib na mwanawe Ali; na vikundi viwili hivyo vilikuwa ni Banu Hashim huko Makka, na Ansar huko Madina.

"Kituo cha uendeshaji" cha Abu Talib na Banu Hashim kilikuwa Makka ambapo "jukwaa" la migogoro ambamo Ali na Ansari walivutwa lilikuwa Madina. Kwa pamoja, wao wali-unda kile kinachoweza kuitwa "Mgawanyo wa Lazima" wa Uislamu. Kila kimojawapo cha vijenzi hivyo vinne vya "mgawanyo" huu kilikuwa na lazima kwa uhai wa Uislamu, na kila kimojawapo kilijaaliwa kutimiza wajibu maalum katika historia yake.

Kijenzi cha kwanza cha mgawanyo huu kilikuwa ni Abu Talib. Allah swt. alimpa kazi ya kumlinda Muhammad na kuutetea Uislamu. Nyumba yake huko Makka ilikuwa ndio chim-buko la Uislamu. Muhammad, Mtume wa wakati ujao, alizaliwa katika nyumba yake. Baadae, nyumba hiyo hiyo ikawa, kwanza "chuo" cha Muhammad, na kisha "ngome" ya Uislamu.

Abu Talib alikuwa mtu wa heshima kubwa, werevu na mamlaka lakini matatizo aliyokum-bana nayo, kama mtetezi wa Uislamu, yalikuwa makubwa kiasi kwamba hakuweza kuyashinda yote yeye peke yake. Ilimbidi, kwa hiyo, apate msaada. Lakini ni nani hapo Makka ambaye angeweza kumsaidia yeye dhidi ya Makuraish isipokuwa watu wa ukoo wake mwenyewe - Banu Hashim? Aliwakusanya hao, na ilikuwa ni msaada wao wa pamoja uliohakikisha uwepo na uhai wa Uislamu hapo Makka.

Ukoo wa Banu Hashim ulikuwa na msimamo na mtazamo mmoja katika kumuunga mkono Muhammad na Uislamu. Watu wake walithubutu miaka mitatu ya hatari na ya kunyimwa kama wakimbizi katika bonde la mlima lakini hawakumtelekeza Muhammad. Hao

667

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

washirikina walikatishwa tamaa na kufadhaishwa na umoja na mkabala wa kijasiri ulioonyeshwa na Banu Hashim kwao wao, na kwa dunia yote.

Siku alipokufa Abu Talib, ilielekea kwa Muhammad kwamba ile ngao yenye nguvu ya Uislamu ilikuwa imebomoka. Kifo cha Abu Talib hakikukatisha hata hivyo, ule utaratibu wa kumlinda Muhammad na kuutetea Uislamu ambao alikuwa ameuanzisha; uliendelezwa na mwanawe Ali, ambaye alijaaliwa kujipatia sifa zaidi hata kuliko baba yake maarufu katika utumishi kwa Uislamu. Kipaji chake kilijitokeza hapo Madina. Aliuvunja kabisa mtazamo wa kipagani wa Arabia. Lakini kama vile tu msaada wa Banu Hashim ulivy-oonekana kuwa wa lazima kwa ajili ya Uislamu hapo Makka, msaada wa Ansari ulionekana kuwa wa lazima kwa ajili hiyo hapo Madina. Maansari walijikusanya nyuma ya Muhammad hapo Madina kama vile Banu Hashim walivyokuwa wamejikusanya nyuma yake huko Makka.

Abu Talib na Ali, na wanaume na wanawake wa Banu Hashim na Ansari walikuwa wa kipekee kwa viwango vya wakati wao na vile vile kwa wakati wetu wenyewe. Wao walik-abiliana na kila changamoto kwa Uislamu, na waliushinda kila mgogoro katika muda wake. Wao peke yao walilinda na kutetea kanuni, heshima na urithi wa Uislamu. Majina ya mashujaa wote hawa hayajulikani kwenye historia lakini kila mmoja wao alikuwa na lazima kwa Uislamu. Kila mmoja wao, mwanaume au mwanamke aliunda ule "mgawanyo wa lazima" wa Uislamu. Bali ya mchango katika utumishi wa kila mmoja wao, huo "mgawanyo" wa Uislamu usingeweza "kutengemaa" kabisa.

Walikuwepo Waislamu wengine pia - masahaba wa Mtume - ambao walichukua majukumu wao wenyewe kwa viwango tofauti vya umuhimu katika historia ya Uislamu. Wengine wao walifanya majukumu makubwa na wengine madogo lakini hakuna hata mmoja kati yao aliyefanya majukumu ambayo yalikuwa makubwa vya kutosha kuyafanya yawe ya lazima. Wengi wao walijipatia sifa wenyewe baada ya kifo cha Mtume lakini kama wangekufa wakati wa uhai wake, wasingesikika kabisa. Katika wakati wa uhai wake, walikuwa ni watu wanaofuatia na wa pembeni ambao waliupata ukweli binafsi na kujik-weza baada tu ya kifo cha bwana wao.

John Kenneth Galbraith, mchumi na mwanadiplomasia wa Kimarekani, wakati mmoja aliutenga ule ugonjwa wa kiuandishi wa habari aliouita "uundaji." Kiini cha uundaji huo, yeye alisema, ni kumbadili mtu wa sifa za kawaida na kuwa mfano wa kihistoria usiosa-haulika milele. Hili linaoneka kufanyika kuwahusu wengi wa Muhajirin. Sifa zisizo na kifani zimetolewa kwa wingi sana juu yao, na katika masuala mengi, sifa hiyo imehusish-wa kwa Mtume mwenyewe, na kwa hiyo ikapewa "hadhi" ya Hadith (sunnah ya Mtume). Kwa kweli, nyingi ya "Hadith" hizi au sunnah zisizo na idadi si chochote zaidi ya upigaji chuku wa ajabu wa mawazo bunifu yenye hamasa ya mpenzi au wapenzi fulani wa masahaba.

668

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mifano ya "Hadith" zinazowatukuza baadhi ya masahaba wa Mtume (s.a.w.w.) ni mingi lakini hapa inawezekana kunukuu mmoja tu kati ya hiyo. Moja ya "Hadith" maarufu sana ni ile inayoitwa Hadith Ashara Mubaashara "Hadith ya masahaba kumi waliobashiri-wa pepo." Mtukufu Mtume anadaiwa kutoa uhakikisho wake binafsi kwa masahaba wake wakuu kumi kwamba wote hao wataingia peponi. Hao walikuwa ni:

1. Abu Bakr

2. Umar

3. Uthman 4.Ali

5. Talha

6. Zubeir

7. Abdur Rahman bin Auf

8.  Saad bin Abi Waqqas

9. Abu Ubaidah Aamir bin al-Jarrah

10.  Said bin Zayd

Usahihi wa Hadith hii unatia mashaka kwa sababu zifuatazo:

(1). Masahaba wote hawa ni Muhajirin na hakuna hata mmoja ambaye ni Ansari -kutelekezwa kunakoshangaza kweli! Kama vile tu Ansari walivyokuwa hawana nafasi katika serikali ya Saqifah, sasa itaonekana kwamba hawakuwa na nafasi huko peponi pia. Ni ajabu kweli kwamba Mtume hakuweza kumpata hata Ansari mmoja aliyekuwa anastahili kuwa kwenye kundi hili la watu kumi. Na bado, hata hivyo, walikuwa ni Ansari ambao walikuwa wametoa hifadhi kwa Uislamu na kwa hao Muhajirin wenyewe.

Muhammad Mustafa (s.a.w.w.) hakuwa ama mtovu wa shukurani au msahaulifu. Asingeweza kusahau ukarimu ulioonyeshwa na Ansari kwake. Kwa kweli, alikuwa ameupokea ukarimu wa Ansari kwa furaha kubwa. Kwa upande mwingine, yeye alikuwa na mashaka mengi katika kukubali wajibu wo wote kutoka kwa Muhajirin yeyote, na kamwe hakukubali. Kama hakuwa mtovu wa shukurani, na hakuwa hivyo, basi hii "Hadith" haiwezi kuwa ya kweli.

(2). Baadhi ya hawa wakazi wa peponi, walipokuwa wanaishi kwenye dunia hii, walikuwa wakipigana mmoja dhidi ya mwingine, na walikuwa wakijaribu kuuana. Wawili wa hao - Talha na Zubeir - walikuwa wakiwachochea watu kumuua khalifa aliyekuwa madarakani - Uthman - ambaye pia alikuwa mmoja wa kundi hilo hilo. Baadaye, wote hao walivunja kiapo chao cha utii kwa khalifa mwingine aliyekuwa madarakani - Ali - na wakamwaga damu ya maelfu ya Waislamu waliokuwa hawana hatia. Kwa kweli, Ali alijaribu kuwaokoa Waislamu hao hao wasiuliwe. Na bado, kulingana na Hadith

669

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

hii, wauaji hawa waliofichika na waathirika waliofichika - wote wataingia peponi!

(3). Hata miongoni mwa Muhajirin, walikuwepo watu ambao walikuwa na sifa kubwa kuliko baadhi ya hawa watu kumi lakini Mtume hakuwahakikishia hata mmoja wao kwamba ataingia peponi. Mas'ab ibn Umayr, Abdallah ibn Mas'ud, Bilal ibn Ribah, Zayd ibn Haritha, na mwanawe Usamah, na Abdallah ibn Rawaha, walikuwa na sifa nyingi kabisa kuliko Uthman, Abdur Rahman ibn Auf, Ubaidullah bin Aamir al-Jarrah, na Said bin Zayd, na bado Mtume hakuwapa uhakikisho wowote kwamba wataingia peponi.

Ilikuwa haijulikani ni kipimo gani cha kuamulia ni nani atakayeingia peponi, na ni nani atakayenyimwa ruksa ya kuingia. Kama uchamungu ndio kigezo cha kuingilia peponi, basi miongoni mwa masahaba - Muhajirin na Ansari pia - walikuwemo wengine wengi ambao walikuwa wachamungu zaidi na watiifu zaidi kuliko baadhi ya hawa watu kumi. Watano kati yao hawa walikuwa ni makabaila wakubwa. Walikuwa ndio nguzo za mfumo wa kik-abaila wa Waislamu.

Hakuna ubaya katika kuwa kabaila kama hivyo; lakini ukabaila, hususan katika muundo wake mtupu, ulikuwa ndio mfano wa mfumo wa kiuchumi dhidi yake ambao, Muhammad, Mtume wa Allah swt. alikuwa akipigana nao maisha yake yote. Alipigana dhidi yake kwa sababu ulisimama katika msingi wa unyonyaji wa kikatili na mwingi kwa masikini. Aliukuta ukabaila wa uporaji ukitumiwa na kulindwa na muungano wa wakiritimba wa Makuraish wa Makka. Muungano huo wa wakiritimba ulikuwa madhubuti, imara na usioshindika lakini kupitia juhudi za muda mrefu na za mfululizo, hatimae aliweza kuubo-moa.

Muhammad kamwe hakujihusisha na hao walezi wa mfumo wa kikabaila. Kwa upande mwingine, yeye alijihusisha na masikini. Mara kwa mara alikuwa akisema: Alfaqru fakhri (Umasikini ndio fakhari yangu). Lakini baada ya kifo chake, ule mfumo wa kikabaila ulichimbuka na ukafufuliwa. Ile Kamati ya Uchaguzi ambayo Umar aliyokuwa ameiteuwa ili kuchagua khalifa mpya, ilikuwa ni muungano wa ukiritimba wa makabaila (wapya), ulioanzishwa upya katika nyakati za Kiislamu. Ni kweli kwamba alimfanya Ali kuwa mmoja wa wachaguzi lakini baadae hakuwa kwenye kundi hilo. Kwa kweli. Uhusiano wake na muungano huu wa wakiritimba ulikuwa sawa sawa na ule wa Muhammad kwa muungano wa wakiritimba wa Makuraish kule Makka.

Miungano yote hii ilikuwa ni maalum (kwa watu fulani tu). Ule muungano wa Makka uli-watenga wale wasiokuwa Makuraish na masikini kutoka kwenye uanachama wake; ule muungano wa Madina uliwatenga Ansari na masikini kutoka kwenye uanachama wake. Miungano yote iliendeshwa na Makuraish kwa manufaa pekee ya Makuraish.

670

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ukabaila huu mpya "ulitakaswa" kwa sababu ya uhusiano wake na masahaba mashuhuri wa Mtume, na haraka sana ukapanda kwenye mahali pa utawala katika Dar-ul-Islam kiasi kwamba haikuwezekana kuung'oa tena.

Pale Ali alipojaribu kuung'oa, walezi wake (wa mfumo huo) walimpinga yeye, na Dola ya Kiislamu ikalipuka kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Muda si mrefu Ali akauawa, na baada ya kuuawa kwake, ukabaila wa unyang'anyi uka-jikuta uko huru kutamba bila kuzuiwa na kwa jeuri juu ya mandhari ya Uislamu.

Waislamu wa Shi'ah wanaichukulia "Ashara Mubashara" kama ni Hadith ya uongo kwa sababu haikubaliani na akili, na chini zaidi, pamoja na maadili ya kijamii ya Kiislamu. Wanaichukulia kama ni matokeo ya ule ugonjwa unaoitwa "uundaji." Kiini chake, wao Shi'ah wanaamini, kilikuwa ni kuwabadili watu wa kawaida kuwa mfano hasa wa kihisto-ria usiosahaulika milele.

671

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mihanga ya Muhammad kwa ajili ya Uislamu

Malengo Makubwa, ili yafatimie, yanahitaji mihanga, na kufanikiwa katika kupata hali halisi kutokana nayo kunakuja kwa gharama kubwa. Lengo kubwa zaidi, gharama kubwa zaidi atakayolipia mtu kulifanikisha. Mapambano ya mwanadamu kujikomboa kutoka kwenye minyororo ya utumwa na udhalimu yana umri wa maelfu ya miaka, na yamechukua maisha ya watu yasiyo idadi. Mapambano yanaendelea leo hii kama yalivyokuwa huko nyuma, na Hadith yake haina mwisho kwa sababu mapambano yenyewe hayana mwisho.

Matatu kati ya matukio muhimu katika mapambano ya mwanadamu kwa ajili ya uhuru ni yale Mapinduzi ya ki-Faransa ya mwaka 1789, Mapinduzi ya ki-Russi ya mwaka 1917, na Mapinduzi ya ki-China ya mwaka 1949. Haya pia ni matatu kati matukio ya maana sana katika historia ya ulimwengu. Mikondo ya damu iliibuka kufuatia mapinduzi haya, na yalivyokuwa yakipungua, yaliibeba ile mifumo na mifano ya kizamani ya ukan-damizaji na unyonyaji pamoja nayo. Mapinduzi haya yalianzisha nguvu mpya ambazo hadi leo hii zinaisukasuka dunia yote. Yalikuwa ndio gharama mwanadamu alikuwa ailipe kununua uhuru wake wa kisiasa na kiuchumi.

(Mapinduzi ya Kirusi na Dola ya Sovieti yalianguka, katika hayo, baada ya miaka 73 -mnamo mwaka 1990. Yalithibitika kutowezekana.)

Karne nyingi baadaye, yaani, katika karne ya saba, mapinduzi mengine yalibadili mwelekeo wa historia. Yalikuwa ni moja ya mapinduzi makubwa ya nyakati zote lakini jambo la kipekee kuhusu mapinduzi haya ni kwamba yalikuwa ya amani. Hayakutengeneza mikondo yoyote ya damu, na kwa kweli, yanapaswa kuitwa mapinduzi "yasiyo na umwagaji damu." Yalikuwa ni ujumbe wa amani. Amani ilikuwa ndio beji yake, na amani au Uislamu lilikuwa ndio jina lake.

Ingawa Uislamu ulitetea amani katika ulimwengu, haukuwa umewezekana bila ya mapambano. Ulikuwa, kwa kweli, umefungwa, kwa miaka 23, katika mapambano ya kumwaga damu kwa ajili ya uhai wake, na kama vile tu mavuguvugu makubwa juu ya ukombozi, ulihitaji vilevile mihanga. Ni ajabu kwamba Muhammad - Mjumbe wa Allah swt. na Mtume wa Uislamu - hakuwaiga viongozi wengine ambao wanawasukuma wafuasi wao kwenye milipuko ya vita kwa jina la "muhanga" kwa ajili ya mfano bora. Yeye mwenyewe alikuwa ndiye mtu wa kwanza kutoa makafara kwa ajili ya Uislamu.

Ufafanuzi wa Webster wa muhanga ni kupata hasara kwa ajili ya kuweka mfano bora. Mtu kutoa mali yake anayoithamini sana kwa ajili ya mfano mwema kunafanya kafara.

672

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Wengi wa manabii na mitume waliishi maisha ya muhanga. Ibrahim alimtoa mwanawe, Ismail, kama kafara; na Yahya (Yohana) alijitolea maisha yake mwenyewe kama kafara. Ismail angeweza kuuawa lakini akabadilishwa wakati ule ule na mwana kondoo. Yahya hata hivyo, yeye aliuawa, na kichwa chake kikabidhiwa kwa mwanamke fasiki kutuliza kiburi chake. Yeye ni mmojawapo wa wahanga (shahiid) wakubwa wa nyakati zote.

Hii ni miwili kati ya mifano mingi ya kafara ambayo ilihitaji ujasiri mkubwa na imani kubwa. Lakini yote kwa mtazamo wa ubora na ukubwa, ile mihanga Muhammad aliy-otoa kwa ajili ya Uislamu, inabakia kutolinganishika katika historia.

Tofauti lazima ionyeshwe hapa kati ya makafara ya mali na makafara ya uhai. Muhammad (s.a.w.w.) alifanya yote. Alitoa muhanga hali njema zake binafsi zote, na mali zote alizokuwa akimiliki kwa ajili ya Uislamu. Hili, bila shaka kila mtu analijua. Ambacho labda hakijulikani sana, ni ule ukweli kwamba baadhi ya jamaa zake wa karibu na wapenzi wake walikuwa wameuawa katika ketetea Uislamu. Ndugu zake Muhammad waliofanya maisha yao dhabihu kwa ajili ya Uislamu, ni kama wafuatao:

1. Al-Harith ibn Abi Hala, mwana wa kulelewa, na mpwawe Khadija. Aliuawa huko Makka.

2.Ubaidullah ibn al-Harith ibn Abdul-Muttalib, binamu yake. Aliuawa katika vita vya Badr.

3. Hamza ibn Abdul-Muttalib, ami yake. Aliuawa katika vita vya Uhud.

4. Mas'ab ibn Umayr, ami yake. Aliuawa katika vita vya Uhud.

5. Abdallah ibn Jahash, binamu yake. Aliuawa huko Uhud.

6. Zayd ibn Haritha, mwana wa kulea na rafiki. Yeye aliuawa katika vita vya Muutah.

7. Jaafar Tayyar ibn Abi Talib, binamu yake. Yeye aliuawa katika vita vya Muutah.

8. Ayman ibn Ubayd, kaka wa kunyonya. Huyu aliuawa katika vita vya Hunayn.

Hii ni orodha ya baadhi ya majina yanayotambulika sana katika Uislamu wote, na inaju-muisha ami zake wawili, binamu watatu, watoto wa kutwaliwa wawili, na kaka wa kunyonya mmoja wa Muhammad (s.a.w.w.). Ilikuwa ni kwa kupitia mihanga hii ambapo ali-

673

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ufanya Uislamu kutodhurika na kutoharibika.

Muhammad (s.a.w.w.) kamwe hakufanya jaribio la kutaka kuwalinda wale aliwapenda yeye mwenyewe. Walikuwa, kwa kweli, ni wale wapenzi wake ambao ndio walikuwa wa mbele kabisa katika kukabiliana na changamoto ya adui. Hakuna aliyekuwa akimpenda kuliko Ali, na bado, nafasi ya hatari kubwa zaidi katika kila makabiliano na wapagani -ndani ya Makka au Madina - ilikuwa siku zote imewekewa yeye.

Makafara makubwa kabisa kwa ajili ya Uislamu yote yalitolewa na Muhammad na Ali. Kwa upande mwingine, Abu Bakr na Umar hawakufanya makafara yoyote. Kwa jinsi makafara kwa ajili ya Uislamu yanavyohusika, wao hawana chochote cha kuonyesha. Wakati wowote ilipotokea changamoto kutoka kwa wapagani, kama ilivyokuja wakati wa vita vya Badr, Uhud na Khandaq, wao (Abu Bakr na Umar) hawakuipokea; na hakuna mtu wa familia zao aliyeuawa katika utetezi wa Uislamu katika wakati wowote ule. Ndugu pekee ambaye Umar alimpoteza kamwe kwenye mapambano ya Uislamu na upa-gani alikuwa ni mjomba wake, Abu Jahl, ambaye aliuawa katika vita vya Badr.

Taji la shahada ndio heshima kubwa na sifa kubwa ambayo Uislamu unaweza kuitoa juu ya Muislamu katika dunia hii. Wapendwa wa Muhammad na Ali walipata shahada nane katika uhai wa Muhammad (s.a.w.w.), na walitakiwa kupata nyingine nyingi zaidi baada ya kifo chake. Allah swt. awarehemu wote hao.

674

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Kushindwa kukubwa kwa Abu Bakr na Umar

Tofauti kati ya mwanasiasa na kiongozi mweledi, imesemekana kuwa, ni kwamba mwanasiasa anafikiria juu ya uchaguzi ujao, na kiongozi mweledi anafikiria juu ya kizazi kijacho. Inachomaanisha ni kwamba athari za mwanasiasa juu ya umma ni za mpito ambapo zile za kiongozi mweledi ni za kudumu.

Kuhusu viongozi ambao wamekwisha kufariki, watu wanawakumbuka kulingana na kama vitendo na mawazo yao vilibadilisha mwelekeo wa historia, na kama kazi zao zimekuwa sehemu ya urithi wa taifa.

Abu Bakr na Umar walikuwa ni viongozi weledi wakubwa na vitendo vyao na mawazo yao vilibadilisha mwelekeo wa historia. Bila ya mashaka yoyote, walikuwa ni viongozi wakubwa, washindi (wa vita) na watawala.

Lakini licha ya umashuhuri wote wa Abu Bakr na Umar, kuna eneo moja ambamo uono wao kama viongozi weledi uliwaangusha, na uliwaangusha kabisa. Eneo lenyewe linahu-siana na uongozi wa Waislamu. Walishindwa kuunda chombo cha urithiano kwa ajili ya umma wa Waislamu. Walishindwa kuanzisha mfumo wa uhamishaji wa amani wa madaraka kutoka kwa kiongozi aliyepo kwenda kwa mwingine.

Kabla ya Abu Bakr na Umar, bwana wao Muhammad (s.a.w.w.), Mtume wa Allah swt., alikuwa amesanifu chombo kwa ajili ya uhamishaji wa madaraka wa mpangilio na amani. Lakini kwa bahati mbaya sana, wao (Abu Bakr na Umar) walikibomoa. Badala yake, wao wakaunda chombo chao wenyewe. Chombo chao kilikuwa kinaendesheka lakini kilikuwa na "dosari" nyingi ndani yake.

Katika tofautisho linganishi na ule mpango wenye kipaji wa Muhammad kwa ajili ya kurithiana, Abu Bakr na Umar walitwaa mfumo wao wenyewe wa muda ndani ya Saqifah. Mfumo wao ulikuwa na mafanikio kwa maana ya kwamba uliyaweka madaraka mikononi mwao; wa kwanza na kisha wa pili wao wakawa warithi wa Muhammad. Hata hivyo, hakuna chenye kufanikiwa kama kurithiana! Lakini kama matukio yalivyokuja kuonyesha baadae, mfumo wao ulikuwa hauendani na mkakati wenye kufungamana. Kushikamana, na sio kamati maalum ya dharura yenye undani, ndio kitovu cha mkakati wa kama kiongozi mwenye ustadi.

Wakati Muhammad, Mtume wa Allah swt. alipofariki, Abu Bakr na Umar wakaanzisha ile al-Khilafat ar-Rashida (Makhalifa Walioongoka), na Abu Bakr akawa "khalifa aliyeongoka" wa kwanza. Miaka miwili baadae, alipokuwa anafariki, yeye akamteua

675

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Umar kama mrithi wake ambaye basi akawa "khalifa aliyeongoka" wa pili.

Miaka kumi baadae, Umar alikuwa amelala akifariki, na yeye alikabiliwa kwa mara nyingine tena na tatizo la kukabidhi madaraka. Lakini kile alichokifanya tu, ni kuunda chombo duni cha kutafuta kiongozi kwa ajili ya umma wa Waislamu ingawa alikuwa amepata uzoefu wa muda mrefu wa serikali na siasa.

Ule ubomoaji wa Abu Bakr na Umar wa chombo cha kuhamishia madaraka ambacho Muhammad Mustafa alikuwa amewapa umma wake, kulidhihirika kuwa ni balaa kubwa ndani ya historia ya Uislamu. Maurice Latey, akiandika kuhusu wafalme wa Kirumi, kati-ka kitabu chake, Patterns of Tyranny, kilichochapishwa na Atheneum, New York (1969), anasema:

"Matendo yanapamba malengo: na kwa ustadi wote wa kiutawala wa Augustus, utaratibu ambao kwao alitwalia madaraka, uliacha ufa mbaya katika msingi wa falme yake ambao mara kwa mara ulilitingisha jengo na hatimae kuliangusha."

Kwa ustadi wote wa kiutawala wa Abu Bakr na Umar, utaratibu waliochukulia madaraka, uliacha ufa mbaya katika msingi wa al-Khilafa ar-Rashida, ambao mara kwa mara ulilitingisha jengo na hatimae kuliangusha kabisa.

Al-Khilafa ar-Rashida ilibomoka katikati ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, mauaji na ghasia, kama vile Umar mwenyewe alivyokuwa ametabiri. Mu'awiyah ibn Abu Sufyan, ambaye alikuwa akiisubiria fursa hiyo kwa miaka thelethini, ya kuukamata ukhalifa, ali-ingia kuziba pengo la madaraka, na alifanya hivyo bila kuonyesha sura ya uchamungu au hata angalau ya kujifanya mtakatifu.

Kama ilivyoelezwa kabla, Muhammad, Mtume wa Uislamu, alikuwa bado yuko hai pale wale wenye uwezekano wa kuwa wagombea wa madaraka, na wafuasi wao walipokuwa wamebuni mpango au mpango mkuu ambao ulikuwa umekusudiwa kuchukua nafasi ya mpango wake wa urithi. Kwa mujibu wa mpango wao, Abu Bakr alikuwa awe mrithi wa kwanza, na Umar na Uthman wawe warithi wa pili na wa tatu wa Muhammad (s.a.w.w.). Muhammad yeye alijua kile ambacho baadhi ya masahaba zake walichokuwa wakijaribu kukifanya, na ilikuwa ni kwa kufahamu huku kwamba aliwaweka chini ya amri ya Usamah bin Zayd bin Haritha, akawaagiza kuondoka Madina, na kwenda kwenye mapambano ya kijeshi kwenye mpaka wa Syria. Lakini walipuuza maagizo yake na hawakwenda.

Masahaba waliutupa mpango wa urithi wa Muhammad, na wakamuweka Abu Bakr kwenye kiti cha ukhalifa. Kabla ya kifo chake yeye mwenyewe, miaka miwili baadae, yeye alimteua Umar kuwa khalifa. Miaka kumi baadae, wakati Umar alipokuwa anafari-

676

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ki, yeye "aliongoza bila kujulikana" uchaguzi wa Uthman kama mrithi wake mwenyewe, kama ilivyoelezwa mapema, na ule "mpango mkuu" ukafanya kazi kwa usahihi kabisa.

Lakini hakuna njia ya kufahamu kile Abu Bakr na Umar walichofikiri kwamba kinge-tokea baada ya Uthman. Inaelekea kwamba Umar alijaribu kuangalia mbele zaidi ya Uthman. Alipofikiria nyakati za baada ya Uthman, yeye "alimpitisha" Mu'awiyah kama mtu wake wa kuhifadhi. Kama vile Muhammad alivyokuwa amemuandaa Ali kwa ajili ya kuutawala umma wa Waislamu baada yake mwenyewe, Umar alimuandaa Mu'awiyah kwa madhumuni hayo hayo.

Mu'awiyah alikuwa amemsikia Umar akiusuta mtindo wa uchaguzi wa Abu Bakr kwenye ukhalifa kama ni "jambo lisilofikiriwa kabla, " jambo litokanalo na "athari za uovu" ambazo Allah swt. alikuwa amewaokoa nazo Waislamu. Kwa hiyo, wakati alipokuwa khalifa, akauzika ule mtindo ambao kwao Abu Bakr alichaguliwa kuwa khalifa. Aliufuta ule mfumo wa uchaguzi hivyo kukomesha kisheria ile desturi ambayo ilikuwa imeny-imwa uwezo wake halisi na Abu Bakr mwenyewe pale alipomteua Umar kama mrithi wake badala ya kuacha uchaguzi wa kiongozi kwa umma wa Waislamu.

Mu'awiyah aliivunja ile nyumba iliyokuwa imejengwa na Abu Bakr na Umar katika kinyume cha itikadi. Kuibukia kwa Mu'awiyah kwenye madaraka kuliashiria kushindwa kwa kustaajabisha kwa demokrasia ya "Kiislamu" au hasa ile ya Saqifah.

Charles Yost:

"Demokrasia sio suala la hisia tu, bali ni la uwezo wa kuona mbele. Mfumo wowote ambao hautilii maanani muda mrefu, utajichoma wenyewe katika muda mfupi."

(The Age of Triumph and Frustration).

Demokrasia ya Saqifah haikutilia maanani suala la muda mrefu, na ikajichoma yenyewe katika muda mfupi, na kutoka kwenye majivu yake akachomoza Mu'awiyah mwana wa Hind kwenye unyota-bingwa! Kama vile ambavyo Abu Bakr alivyoanzisha al-Khulafat ar-Rashida, Mu'awiyah aliweka utawala, na akaanzisha ufalme wa kiukoo. Juu ya maba-ki ya al-Khulafat ar-Rashida, yeye alisimamisha jengo la miliki ya Bani Umayya. Falsafa yake ya kisiasa ilisimama juu ya mkakati wa masafa marefu, wa kufuatana kwa wakati na wa kufungamana.

Miaka tisini baadaye, himaya ya Mu'awiyah ikafungwa. Katika mabaki ya miliki yake, Bani Abbasi wakasimamisha jengo la ufalme wao. Bani Abbasi pia waliweka utawala wa kiukoo, na falsafa yao ya kisiasa pia ilisimama juu ya mkakati wa masafa marefu, kufuatana kwa wakati, na kufungamana, na ukawa mwanzo wa "Golden Age" - kipindi cha

677

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

upeo wa ustawi wa fasihi na sanaa - cha Waarabu. Kipindi cha upeo wa ustawi wa fasihi na sanaa cha taifa lolote lile kinaashiria amani na neema. Kipindi hicho cha Waarabu kingeweza kuleta neema kwa baadhi ya watu lakini hakikulazimika kuleta amani kwa Waislamu. Hata pale madaraka ya Bani Abbasi yalipokuwa kileleni, miliki yao haikuwa na amani yoyote ya kweli.

G.E. Von Grunebaum:

"Dini pia ilikuwa ni hamasa ya maasi ambayo mara kwa mara yalitingisha himaya ya Bani Abbasi. Hata chini ya kiongozi wa kwanza wa Bani Abbasi, ambaye alishikilia madaraka baraabara, haukupita mwaka bila ya maasi ya namna fulani, makubwa au madogo."

(Classical Islam - A History 600-1258, uk. 88, 1970).

Hali ya kivita ndani ya Dola ya Kiislamu ilikuwa ni desturi, na ilitarajiwa kwamba vita vingejitokeza. Kugombea madaraka kulichukuliwa kama ni kawaida na kusikokwepeka. Mapambano haya yalikuwa ni "urithi" wa Saqifah kwa Waislamu. Wengi wa Waislamu walikuwa wamegeuka kuwa "wazoefu" wa vita vya wenyewe kwa wenyewe. Lakini kama kulikuwa hakuna vita, ilichukuliwa kama ni tukio la ajabu kabisa kiasi kwamba lilipumbaza imani. Mpito wa madaraka bila ya umwagaji damu ulionekana kama ni "kioja."

G.E.Von Grunebaum:

"Abu Yaqub Yusuf, mtoto wa Abd al-Mumin (Al-muhadith), alichukua madaraka bila ya tukio. Alianguka kwenye vita takatifu nyuma ya Santarem (Hispania) mnamo mwaka 1184. Viongozi wengine watatu waliofuatia pia, maarufu sana kati yao alikuwa ni mjukuu wa Abd al-Mumin, Yaqub al-Mansur (1184-1199) alipanda kwenye kiti cha ufalme bila haja ya kuzima maasi yoyote, uthabiti wa utawala wa kiukoo takriban usiokuwa na mfano katika Dar ul-Islam. (mkazo ulioongezwa)

(Classical Islam - A History 600-1258, uk. 187, 1970).

Kiongozi mweledi amejaaliwa na uono ambao unaweza kupenya kwenye vizazi na hata karne nyingi. Takriban kila taifa limetoa viongozi kama hao. Wale watu wa karne ya 18 waliorasimu lile Azimio la Uhuru wa Marekani, Katiba ya Muungano wa Mataifa ya Marekani (U.S.A), na ile Sheria ya Haki za Binadamu, walikuwa ni viongozi weledi kama hao. Walikuwa wabashiri. Walibuni chombo kwa ajili ya utaratibu wa uhamishaji wa madaraka, na kwa kufanya hivyo, wao waliwaokoa watu wa Marekani kutokana na kiwewe cha vita na umwagaji wa damu. Waliweka kinga za "ndaini kwa ndani" katika Katiba ili kwamba kuanzia mwaka 1789, madaraka yamepita kutoka kiongozi mmoja au

678

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

kutoka chama kimoja kwenda kingine bila ya tukio lolote. Walifupisha katika maneno 52 Dibaji ambayo ni tamko lenye kuridhisha sana la lengo la serikali ambalo limewahi kuandikwa kamwe.

Robert B. Downs:

"Mwanahistoria (wa Kimarekani) wa karne ya kumi na tisa, George Bancroft, aliamini kwamba wale kina Baba Waasisi walifanya chini ya uongozi wa kimungu, kwamba walikuwa wameelekezwa na Mungu kwanza kufanya mapinduzi ya kidemokrasia, na kisha kuandika katiba ya kidemokrasia."

(Books that changed America, London, 1970)

Ukiangalia ule mpito mfupi wa al-Khulafat ar-Rashida, inaweza kuonekana kwamba ulikuwa hauna muongozo wowote wa kimungu au baraka za kimungu.

Mnamo Januari 20, mwaka 1981, Bw. Ronald Reagan, raisi wa arobaini wa Marekani, alisema katika hotuba yake ya uzinduzi kwamba:

"Utaratibu wa kukabidhiana madaraka kama ulivyotakiwa kwenye Katiba unatendeka kama ulivyokuwa kwa takriban karne mbili, na wachache wetu husita na kufikiri ni jinsi gani hasa tulivyo wa kipekee. Mbele ya macho ya wengi katika dunia hii, sherehe hii ya kila baada ya miaka minne tunay-oikubali kwamba ni ya kawaida, kwao si chochote zaidi ya muujiza."

Wale "Mababa Waasisi" wa Marekani walifanikisha muujiza huu katika karne ya 18. Karne kumi na mbili kabla yao, Muhammad, Mtume wa Allah swt., alikuwa amekwisha fanikisha muujiza huohuo huko Arabuni. Hapa mwanafunzi wa historia anaweza kuona miujiza miwili katika "utaratibu wa uhamishaji madaraka." Lakini ambapo ule muujiza wa Mababa Waasisi wa Marekani ulitokea kuwezekana kuwapo, ule muujiza wa yule Mtume wa Arabuni ulitokea "kunyamazishwa!"

Kwa nini? Kwa sababu nyepesi sana, yaani, lile taifa changa la Kimarekani lilitoa uun-gaji mkono mkubwa na kwa moyo mkunjufu kwenye kanuni zilizohifadhiwa ndani ya "muujiza" wa Kimarekani lakini wale watu mashuhuri katika umma wa Kiislamu wal-izuia kuunga mkono kanuni zile zilizohifadhiwa katika muujiza wa Kiislamu.

Kama ilivyoelezwa mapema, Muhammad alizuiwa na masahaba zake mwenyewe katika utekelezaji wa ubunifu wake wa kimajaaliwa kwa ajili ya uhamishaji wa madaraka katika Ufalme wa Mbinguni juu ya Ardhi. Hawa masahaba walikuwa na ubunifu wa kwao wenyewe, na walifanikiwa katika kuutumia wakati wa kifo chake. Lakini kwa "mafanikio" yao, wao pamoja na mawakala wao walifungulia "Pandora's Box" utarat-

679

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

ibu wenye matatizo magumu yasiyowezekana ya ukingamizaji, makabiliano na migogoro katika Dar-ul-Islam ambayo ilichukua vifo vingi kutoka kwenye umma wa Waislamu. Waislamu wasiokuwa na idadi waliuawa katika vita vyao visivyo na idadi ambazo vilip-iganwa tu kwa sababu hapakuwa na chombo cha uhamishaji madaraka wa amani kutoka kwa mtawala mmoja kwenda kwa mwingine.

Wanahistoria wa kisasa wengi wameonyesha na wametoa maoni juu ya ukweli unaopin-gana wa vita na umwagaji damu katika Dar-ul-Islam, yaani, "Nyumba ya Amani."

Sir John Glubb:

"Kisiasa, nchi za Kiislamu, kwenye karne zao ndefu za uongozi, daima zilivurugwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya wanaodai kutawala. Tunaziona kwa mara nyingine tena mara kwa mara zikiwa jukwaa la maasi na utwaaji wa kijeshi wa madaraka, kabisa kama zilivyokuwa miaka 800 iliyopita. Kwenye historia yote, majeshi ya Kiislamu yamekuwa yakitumiwa katika mapambano ya ndani mara nyin-

gi zaidi kuliko kwenye vita vya nje.."

(The Lost Centuries, 1967)

Mwanahistoria mwingine ametoa maoni juu ya kuanguka kwa kisiasa na kimaadili kwa himaya ya Waislamu ambamo vijana wa kiume walikufa wakipigana vita vya mfululizo vya watawala wao, wakati watawala wenyewe wakijichimbia kwenye makasiri ya dha-habu, vito vya thamani, na yenye matowashi.

Herbert J. Muller:

"Wao (Bani Umayya) walianzisha ufalme wa kiukoo, wakaweka baraza la kidunia, wakaingiza matowashi kwenye majumba yao ya harimu, na kwa jumla walitawala kama wafalme wa kimashariki, wasiohusiana tena na wenzao katika mwenendo wa machifu wa Kiarabu. Kanisa na dola, kinadharia vikiwa ni kitu kimoja, vikawa kwa kweli vimetengana. Uislamu uliweka utii wenye ukungu kwenye nadharia, lakini haukuwa na mafundisho halisi ya kisiasa.

Bani Abbasi walijenga makao makuu mapya huko Baghdad, mji mpana wenye uzoefu wa mambo ya kimataifa ambao ulikuja kuwa Kiwanja cha Alfu lela ulela (Arabian Nights), na ustaarabu wenye nguvu zaidi kuliko wa Kiarabu. Waliufikisha Uislamu kwenye kilele cha utajiri wake wa mali na madaraka na uta-maduni wake wa ubunifu, kuleta ishara ya utukufu wake katika kipindi cha utawala wa Harun al-Rashid (786-809). Hata hivyo, bado katika kipindi hiki ule uozo wa msingi wa utawala wa Bani Abbasi ulikuwa tayari upo dhahiri. Harun alikuwa amepanda madarakani kirahisi sana kwa sababu kaka yake alikuwa ameuawa katika nyumba ya harimu; ilimbidi apambane na maasi mengi katika

680

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

himaya yake; na kifo chake kilifuatiwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya watoto wake. Ulimwengu wa Kiislamu mara ukaanza kugawanyika, kwa vile Uajemi, Hispania, Misri na majimbo mengine yaligeuka kuwa falme hum. He himaya iliyokuwa imejengwa kwa jina la Muhammad na Allah swt. haikuwa na uhusiano wowote na mamlaka yaliyokuwepo ya himaya ya kidunia ya Warumi.

Kwa kweli haikuwa kamwe ni himaya halisi yenye serikali ya kulingana. Umoja wa kiroho wa Uislam ulishindwa kutia msukumo wa umoja wa kisiasa; watawala wake walionyesha akili ndogo ya kisiasa na udhanifu mdogo zaidi. Ambapo makhalifa wa Bani Abbas walijionyesha kama wachamungu wenye imani halisi, wengi wao walikuwa ni wenye kukufuru na tena wabadhilifu wazembe sana, wak-itapanya mali ya Uislam katika maisha ya anasa. Kwa umakini kabisa walijifanya wenyewe kupambika na taji la ufalme, wakawa wanazidisha udikteta na kujiweka mbali na raia wao, na wakalifanya jeshi kuwa mali yao binafsi, wakiliandikisha kutoka miongoni mwa watumwa wa kigeni. Uvumbuzi mwingine ulikuwa ni chakari ambaye wakati wote aliandamana nao. Muasisi wa ufalme huo wa kiukoo, Abul Abbas, alijitwalia jina la Mmwagaji-damu; warithi wake mara kwa mara damu yao wenyewe ilimwagwa, katika mauaji yatokanayo na ulaji njama wa baraza. Kufikia karne ya kumi wale makhalifa wa Baghdad walikuwa vibaraka wa jeshi lao la "kitumwa", wakiwa hawana mamlaka halisi ya kisiasa au ya kiroho juu ya miliki zao zenye kufifia. Kile kisingizio cha kusikitisha cha utawala wao kilikomeshwa mwaka wa 1031. Makhalifa wengi walichomoza kila mahali katika Uislam, kama vile huko Misri na Hispania, lakini nao pia walikuwa na mamlaka ya majina tu. Mataifa mengine ya kiislam yalirudia ile Hadith ya Baghdad ya utukufu wa kifalme, ulaji njama, na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Mshairi mmoja wa Kiarabu alieleza kwa kifupi fundisho kwa ajili ya raia wao: "Pata watoto wa kiume - kwa ajili ya kifo! Jenga sana - kwa ajili ya uangamiaji! Songa mbele - njia hii inaelekea kwenye maangamizo!"

(The Loom of History, uk. 286-287, 1958)

Kuamua kutokana na taswira hii, amani yenyewe lazima itakuwa imezuiwa ndani ya Nyumba ya Amani (Dar-ul-Islam) kwa vile vita na umwagaji damu vilikuwa ni mazoea ya kawaida ya raia zake. Umma wa kiislam kwa hakika umelipa gharama kubwa sana kwa kushindwa kwake kukubali mpango wa Muhammad, Mtume wa Allah swt. kwa ajili ya uhamishaji wa madaraka.

681

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ni nani aliyeandika Historia ya Uislam na Vipi?

Historia, imesemekana, ni propaganda (uenezaji habari) wa kundi la upande wa washindi. Hii ina maana kwamba katika kila mgogoro, yule mshindi anaweza kuichezea historia kiasi inavyomridhisha yeye, na hakuna chochote ambacho yule aliyeshindwa anaweza kuki-fanya juu ya hilo. Ule upande ulioshinda unaweza kuzua Hadith na kuitangaza kama ukweli mtupu bila ya hofu ya kupingwa na mtu yoyote. Hauna tu ule uwezo wa kuzua Hadith yake wenyewe; unayo pia nguvu ya kuipachika Hadith ya kundi linalowapinga.

M. Shibli, mkuu wa wanahistoria kiislamu wa Kisunni wa India, anaandika katika kitabu chake maarufu cha wasifu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.), Sira-tun-Nabi, Juz. I, chapa ya 4, kilichochapishwa na Maarif Printing Press, Azamgarh, U.P., India, mwaka 1976:

"Miongoni mwa zile nguvu zote za kutoka nje ambazo zinadhuru na kuathiri uan-dishi wa historia, hakuna ambayo ina uwezo zaidi kuliko ya serikali. Lakini itakuwa siku zote ni chanzo cha fahari kwa Waislam kwamba kalamu yao kamwe haikukandamizwa na upanga. Kazi juu ya utungaji na ukusanyaji wa Hadith ilianzishwa wakati wa enzi ya Bani Umayya. Kwa miaka 90 mizima, kutoka Sindi huko India (India-Pakistan) mpaka Asia Ndogo na Andalusia huko Hispania, Ali na watoto wa Fatima walikuwa wakilaaniwa kutoka kila mimbari ya Msikiti baada ya kila hotuba ya Ijumaa. Maelfu na maelfu ya Hadith zenye kumtukuza Mu'awiyah zilitengenezwa, na zikaingizwa kwenye mzunguko. Katika enzi ya Bani Abbasi, Hadith zilivumbuliwa zenye kutabiri kuzaliwa na ubora wa kila khalifa wa Bani Abbasi kwa jina lake. Lakini ni yapi yalikuwa matokeo ya juhudi hizi kubwa? Wasimulizi (wakusanyaji wa kauli za Mtume) walitangaza hadharani kwa wakati huo huo (katika kipindi cha ukhalifa wa Bani Umayya na Bani Abbasi) kwamba Hadith hizi zilikuwa za uongo, na wakazikataa. Leo hii, tunajivunia kuse-ma kwamba elimu ya Hadith imeepukana na matusi yote na uchafu wote ule."

Takriban, lakini sio kabisa!

Kwa upande wa Hadith zisizo na idadi, jaribio la kuondoa taarifa potofu kutoka kwenye maelezo ya Hadith, au kuisahihisha, halikuufikia kamwe ule uwongo wa asili.

Hata baada ya uondoaji wa maneno machafu, kama ulikuwepo, sehemu ile ya maelezo ya Hadith ambayo inahusiana na maisha binafsi ya Muhammad, Mtume wa Uislam aliye-barikiwa, inakuwa imejaa yale ya ajabu, ya kushangaza, ya ubunifu na ya uongo. Hizi ni Hadith nyingi ambazo zinamfanya aonekane kama ni mtu wa tamaa na ufisadi; mtu wa visasi na ukatili; mpenda maslahi na asiye mwaminifu; na msaliti na asiye muadilifu. Kisha

682

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

zipo simulizi nyingine ambazo zinaweza kuitwa tu zenye lugha chafu.

Lakini ushahidi wa historia unakwenda kinyume na maelezo hayo mafupi juu ya wasifu wa Muhammad. Angeweza kuwa na mambo yote haya lakini hakuwa hivyo. Ni muhimu kwa hiyo, kwa Waislam na wasio Waislam vilevile, kutenganisha upuuzi na takataka kutoka kwenye uhakika na ukweli katika kuichunguza historia ya Uislam.

Ni vipi "simulizi" kama hizi ziliishinda akili ya kuzaliwa na mantiki, na kujipenyeza kwa hila kwenye maandishi ya Hadith na vilikuwaje vile vitendo na kauli ambazo zinaweza kuitwa tu kwamba ni za kuchukiza, zikavumishwa kama tabia ya mtu ambaye maisha yake hasa yalikuwa ni mfano halisi wa utakatifu wote, ukweli, uaminifu na wepesi?

Shibli amefanya jaribio la kijuujuu hasa la kujibu swali hili katika kifungu cha maneno kilichonukuliwa hapo juu. Anasema kwamba "wakala" wa nje mwenye nguvu sana mwenye kuathiri uandishi wa historia katika zama za Bani Umayya na Bani Abbas (661-1258) alikuwa ni serikali. Serikali ya siku zile ilikuwa na uwezo wa kuifanya historia iandikwe kwa "vipimo" vyake yenyewe. Himaya zote zilihisi kwamba zilikuwa huru kubadilisha historia au kuizuia historia, na wakati wowote walipoona ni kwa maslahi yao kufanya hivyo - kubuni 'historia.' Wakati ambapo Hadith nyingi zilibuniwa kwa sababu za kisiasa, zilikuwepo pia zile Hadith ambazo zilibuniwa kwa sababu za kianasa tu. Wapenda anasa wa mabaraza ya Damascus na Baghdad walitafuta "hifadhi" kwa ajili ya starehe zao ndani ya Hadith hizi.

Hadith ina maana ya maelezo. Kama mtu alimuona Mtume akifanya kitu au kumsikia akisema maneno fulani, na akasimulia jambo hilo kwa watu wengine, itaitwa ni Hadith au sunnah. Masahaba waliona ni wajibu wao kuzihifadhi sunnah zote za Mtume (s.a.w.w.) kwa faida ya umma wa Waislam kwa nyakati zote.

Hadith pia inaweza kuwa ni maoni ya Mtume juu ya mtu fulani. Kama alitoa sifa kwa saha-ba wake yeyote, au kama alimkosoa mtu yeyote, maneno yake yalipata utangazwaji mpana sana miongoni mwa Waislam. Wakati wa ukhalifa wa Mu'awiyah, nyingi ya Hadith hizi zilikuwa katika usambazwaji. Alikuwa mwepesi kutambua umuhimu wake, na akaamua kuzifanya ni silaha ya kisiasa katika kampeni zake dhidi ya Ali ibn Abi Talib na Bani Hashim.

Mu'awiyah ambaye alikuwa ndiye muasisi wa ule ufalme wa kiukoo wa ki-Bani Umayya, alijishindia "nishani' nyingine. Aliasisi "kiwanda kidogo" cha kutengenezea Hadith. Warithi wake, na baada yao, wale makhalifa wa Bani Abbas, walikilea "kiwanda" hicho ambacho kwa muda mrefu kilikuwa kikishughulika na kutengeneza Hadith kwa wingi. Ingawa Shibli anadai kwamba Hadith ziliondolewa maneno machafu na wakaguzi wakosoaji, wang'amuzi na wachambuzi wa hali ya juu, yalikuwepo mengi ambayo yalik-

683

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

wepa kugunduliwa na hao, na yanakubalika, leo hii, na kundi kubwa la Waislam, kwamba ni sahihi.

Mu'awiyah aliteua timu ya watu kuunda maelezo yenye kufaa kwake yeye binafsi na kwa maadui wengine wa Ali, na kuyahusisha kwa Mtume kama Hadith zake mwenyewe. Wakati huo huo, alizuia au alijaribu kuzuia zile Hadith halali ambazo zilikuwa zinamsifu Ali, na akaiagizia timu yake kutengeneza Hadith za kushusha hadhi yake. Wajumbe wa timu yake wakatunga Hadith za uwongo za tofauti zote, na wakaziingiza kwenye mzun-guko.

Baada ya kifo cha Mu'awiyah, kampeni hii iliendelezwa na warithi wake. "Waandishi wanaowatungia," "maafisa uhusiano," na "wajenga-majina" wao, kwa ustadi kabisa wakachanganya Hadith za uongo na zile za halali, na historia ya usanisi (ya kuungaunga) pamoja na historia ya kweli, wakitumaini kwamba "mchanganyiko" huo "utadhihirika" kama sehemu ya elimu ya mapokezi matukufu ya Waislam.

Mu'awiyah alikuwa na sababu nyingine moja ya kuingia kwenye kazi ya "utengenezaji Hadith." Alijua kwamba vizazi vya wakati ujao vitamuona kila mtawala wa Waislam kinyume na yule kiongozi mkamilifu - Muhammad (s.a.w.w.). Alijua pia kwamba kama watafanya hivyo, watamkuta yeye anahitilafiana kabisa na Muhammad. Alikuwa akitam-bua pia kwamba hata angefanya nini, asingeweza kupanda kama Muhammad; alijua kwa kweli kwamba asingeweza kufikia hata vile viwango vilivyovikiwa na watumwa wa Muhammad. Lakini ilionekana kwake kwamba ingawa isingewezekana kwake yeye kufikia ule usawa ambao Muhammad akisimama juu yake, iliwezekana kwake yeye kumshusha Muhammad hadi kwenye usawa ambao yeye Mu'awiyah alisimama juu yake kwa ile njia nyepesi ya kufifisha nuru ya sifa zake Muhammad (s.a.w.w.), kiasi kwamba na yeye pia aonekane kama binadamu wengine wa kawaida.

Mu'wiyah alitegemea kwamba ukosoaji wa wanahistoria dhidi yake utakuwa hauna nguvu sana kama wangeonyeshwa kwamba hata yule mtu mkamilifu kabisa -Muhammad, Mtume wa Allah swt. Mwenyewe - hakuwa huru kabisa kutokana na dosari za mwenendo. Ni wazi kabisa, mengi ya yaliyomo kwenye maelezo ya Hadith yalikuwa ni njama kwa ajili ya mauaji ya tabia ya Muhammad, Mtume wa Allah swt.

Mu'awiyah na wale wawekezaji wengine wa "kiwanda kidogo" chake walikuwa "wame-fanikiwa" katika jaribio lao la uuaji wa tabia ya Muhammad. Waliyachanganya maelezo ya Hadith pamoja na simulizi, visa na "matukio" yasivyokuwa na idadi, makusudio ya yote hayo yakiwa ni kumfanya Muhammad aonekane, machoni mwa vizazi vijavyo, kuwa chini kuliko unabii.

684

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ufuatao ni mfano wa moja ya sunnah za "kuchapishika" ambayo imetufikia sisi. Imeandikwa na Hakim Muhammad Said katika makala iliyochapishwa na Hamdard Academy, Karachi, Pakistan, mnamo mwaka wa 1972, katika kitabu kinachoitwa

Tadhkira-i-Muhammad:

"Mara tu baada ya ndoa yao, Muhammad, Mtume wa Allah, alipendekeza kwa mwali wake mpya, Aisha, kwamba wakimbie wote kushindana. Aisha alikuwa amepungua na mwembamba, na alimshinda mbio mume wake kwa urahisi. Miaka kadhaa baadae, Mtume alimtaka Aisha kukimbia dhidi yake kwa mara nyingine tena. (Alikuwa ame-ongezeka uzito katika ile miaka ya tangu lile shindano la kwanza). Wote wakakimbia, na safari hii Mtume akamshinda mbio Aisha. Maoni yake yakawa: 'Safari iliyopita ulikuwa wewe ndiye mshindi, ewe Humayra (jina la utani la Aisha) lakini safari hii mimi nimeshinda, na sasa matokeo kati yetu yamelingana." (Huenda kule kushindwa katika lile shindano la kwanza kulikuwa kunakera katika akili ya Mtume miaka yote hii.)

Muhammad, Mtume wa Allah swt., alikuwa na umri wa miaka 54 wakati alipokimbia katika mashindano na msichana wa miaka 9 au 10, na alishindwa; na alikuwa na umri wa miaka 60 wakati alipokimbia dhidi yake kwa mara ya pili, na akashinda!

Waislam wanatetea hadhi ya Mtume wao. Hivi "sunnah" hii ambayo wengi wao wanaamini kwamba ni ya kweli, ni yenye taswira hasa ya hadhi hiyo?

Inaelekea kwamba wale "wasimamizi" na wale "mameneja uzalishaji" ambao Mu'awiyah amewaajiri katika "viwanda vyake vya Hadith," walikuwa na haja moja tu, nayo ilikuwa ni wingi. Walikuwa wamekibuni "kiwanda" hicho kwa ajili tu ya uzalishaji wa "sunnah" kwa wingi. Ni dhahiri kwamba hawakuwa na haja ya "udhibiti wa ubora" wa mazao yao. Walipandikiza uwongo kwenye vitabu vyao, na kila uwongo ukaacha baada yake, kama unavyofanya wakati wote, "tone la sumu," lililochafua akili ya vizazi vya Waislam. Baadhi ya mazao yao (ya Hadith) ni matovu ya adabu kweli kweli. Hayo, kwa kweli, hayachapishiki. Wakosoaji na maadui wa Mtume (s.a.w.w.), bila ya kukwepa, wameonyesha shauku kubwa katika kuzikubali kama ni sahihi, na wamezinukuu katika vitabu vyao.

Wakosoaji na maadui hawa wa Mtume, hata hivyo, hawakuzingatia yale mambo ambayo usahihi wake hauna shaka yoyote. Kwa mfano, wameliacha lile suala la kwamba, huko Makka, Makuraish walimuahidi yeye (Mtume) mwanamke au wanawake wazuri zaidi kama malipo ikiwa ataacha kutangaza Uislam. Walisahau vile vile ule ukweli kwamba Muhammad alikuwa mtawala wa Madina, na kwamba angeweza kuoa msichana yoyote yule. Machifu wa Waarabu wangejivunia kumpa yeye mabinti zao.

685

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Mtume (s.a.w.w.) alioa wanawake wengi hapo Madina lakini wengi wao walikuwa ni wajane, na wala hawakuwa wadogo sana pia. Isipokuwa Khadija tu, wanawake wengine wote waliingia nyumbani kwake wakati alipokuwa kwenye miaka ya katikati ama ya mwishoni mwa hamsini. Waliingia maishani mwake katika wakati ambapo kudunda na kuchangamka na mng'ao na nguvu za ujana wake zilikuwa zimetoka siku nyingi, na nafasi yao ilikuwa imechukuliwa na mizigo inayoendelea kuongezeka ya Dola inayoen-delea kukua, na matatizo mengine yenye utata na ukubwa wa hali ya juu zaidi, yakimwachia muda mdogo sana au mwelekeo wa upoteaji wa muda kama huo kama inavyosimuliwa katika nyingi ya "sunnah."

Kwa ukusanyaji wa Hadith, Mu'awiyah alikuwa ametoa maagizo yafuatayo:

1.  Hadith zote za Mtume zenye kumsifu Ali au zinazounga mkono ubora wake kwa namna yoyote ile, lazima zizuiwe.

2.  Mtu yeyote anayesimulia wema wa Ali au kunukuu Hadith ya Mtume kuhusu suala hili, atafanya hivyo kwa kujihatarisha mwenyewe. Msaada wake toka serikalini na ujira vitazuiliwa kwake. Nyumba yake na mali nyingine zitakamatwa. Ushahidi wake kama shahidi hautakubaliwa katika mabaraza, na atatenganishwa na Waislam wengine.

3.  Kwa upande mwingine, kila sifa zinazoweza kufikirika hazina budi kuhusishwa na Abu Bakr, Umar, Uthman, na bila shaka kwa Mu'awiyah mwenyewe. Watu wahimizwe kuteneneza "Hadith" za Mtume zenye kuwasifu hawa watu wanne na marafiki zao. Yeyote yule atakayebuni Hadith kama hiyo, atakuwa ni kipenzi kwenye baraza la kifalme, na atapata zawadi nono katika cheo au pesa taslim au mashamba na kadhalika.

Kwa kulingana na uundwaji wa "kiwanda kidogo"chake kwa ajili ya utengenezaji wa "Hadith" za Mtume, Mu'awiyah pia alianzisha "viosha akili" kwa ajili ya Waislam. Alianzisha desturi ya kuvuruga kumbukumbu za Ali na wanawe kutoka kwenye mimbari ya kila msikiti ndani ya himaya yake ili kwamba watoto wa Kiislamu wawe wamezaliwa, wamekua , na wamekufa wakisikia laana nyingi juu ya Ali, na wasijue yeye alikuwa ni nani. Vizazi vizima viliishi na kufariki katika ujinga. Uwongo uliingizwa kwenye mzun-guko na serikali kwa kiwango kikubwa sana kiasi kwamba ikawa ndio dhana ya maisha yao. Mu'awiyah na warithi wake waliviweka "viosha akili" vyao katika kushughulika kama vile tu kile "kiwanda kidogo" chao.

Mu'awiyah aliandaa kila njia ya kuendeleza vita vya propaganda dhidi ya Ali na Banu Hashim. Msukumo wa shambulio hilo aliloanzisha dhidi yao, umedumu hadi kufikia nyakati zetu sisi wenyewe. Alifanya vita vyake kuanzia misikitini. Viongozi wa swala ndani ya misikiti hiyo walilipwa ili kuweka tafsiri za kipekee na za ajabu juu ya Aya za Qur'an katika jaribio la kumuonyesha Ali kwenye upungufu. Walijaribu kuwashawishi

686

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Waislamu wa kawaida kwamba itakuwa ni kwa maslahi yao katika "dunia zote mbili" kama watamuunga mkono Mu'awiyah dhidi ya Ali na Bani Hashim.

Michael C. Hudson:

"Wenye madaraka wana fursa ya vyombo vya habari na mikono ya elimu ya dola, na wanawadhibiti kupitia ruzuku wale wenye mamlaka ya kidini wenyewe."

(Islam and Development, uk. 16, 1980)

Ni lazima sasa ieleweke kwa msomaji kwamba historia ya Uislamu iliandikwa kwa maelekezo ya lile kundi ambalo lilishikilia vyombo vyote vya madaraka mikononi mwake. Na ni lazima pia iwe dhahiri kwake kwamba mengi ya maelezo ya kihistoria "yalioshwa" kwenye vile "viosha akili" vilivyoanzishwa na Mu'awiyah kabla hayajain-gia mikononi mwake yeye msomaji. Mu'awiyah alikuwa ni bingwa mkamilishaji sana wa sanaa ya propaganda.

Sir John Glubb:

"Athari kamili za propaganda hiyo hazijawa dhahiri bado, hata hivyo, tayari ni dhahiri kwamba mataifa mazima yanaweza kutiwa kasumba ya maoni potofu na viwango vya maadili maovu. Ni akili chache, kama zipo, zenye nguvu ya kutosha kuweza kukataa mawazo yanayochomozwa kwao wakati wote."

(The Course of Empire - The Arabs and Their Successors, 1965)

Kama Hadith yoyote ya Mtume wa Uislamu ilikuwa yenye kusifu Ali, usimuliaji wake ulipigwa marufuku na Mu'awiyah. Marufuku haya hayakuondolewa wakati alipokufa mwaka wa 680. Hayakuondolewa hata pale ufalme wake, wa Bani Umayya, ulipoanguka mnamo mwaka wa 750, na hayakuondolewa hata katika karne ndefu za ukhalifa wa Bani Abbasi.

Bani Abbasi waliwaangamiza Bani Umayya lakini walichangia pamoja nao chuki yao dhidi ya Ali na kwa kizazi cha Muhammad (s.a.w.w.). Katika suala hili, malengo na maslahi ya serikali ya Saqifah, Bani Umayya na Bani Abbas walikutana; ulikuwepo upatanifu wa kiitikadi miongoni mwao wote.

Bani Umayya na Bani Abbas walifanya kila lililowezekana kuzima ukweli wa historia. Wengi wa makhalifa wao waliwakataza raia zao kusema au kuandika kitu chochote kuhusu Ali isipokuwa uwongo. Ukweli ulikuwa kizuizini na uwongo ukawa umeenea kwenye miliki zao. Na bado, Ukweli ukajithibitisha wenyewe.

687

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Ukweli umefika na uwongo umetoweka; hakika uwongo (kwa asili yake) ndio wenye kutoweka. (Sura ya 17; Aya ya 81)

Maelezo ya kweli yalijitolewa na vyanzo ambavyo, katika masuala mengi, vilikuwa na uhasama kwa Ali. Hata wale maadui zake wakali sana kama Bani Umayya na Khariji, walikiri usafi wa tabia yake. Kama ilivyoelezwa hapo kabla, M. Shibli, mwanahistoria wa Kihindi, alionyesha kwamba Waislamu wa ki-Shi'ah hawakuandika historia yoyote. Historia yoyote tuliyonayo, kwa hiyo, imetufikia sisi kutoka kwa wasiokuwa Shi'ah au kwenye vyanzo vyisivyokuwa vya ki-Shi'ah. Imetufikia kutoka kwenye hifadhi za nyara-ka za serikali za Saqifah, Bani Umayya na Bani Abbasi. Kisa cha vitendo vitukufu vya Ali ibn Abi Talib, kama ule mng'aro wa Ukweli wenyewe, umejichuja kutoka kwenye hifadhi hizo.

Lakini wanahistoria wa kisasa hawatishiwi na serikali yoyote kwa kuandika historia ya kweli wala hawashawishiwi na ahadi za zawadi nono kwa kuandika historia za uwongo. Wanapaswa kwa hiyo, kuchunga vishawishi vya kuzima au kupotosha ukweli. Kama watanywea hata leo hii kwenye vishawishi hivi, kama wengi wa watangulizi wao walivy-ofanya wakati uliopita, basi inawezakuwa na maana tu kwamba wanatoa uaminifu wao sio kwenye kanuni bali kwa watu; sio kwenye ukweli bali kwenye taasisi na serikali; na sio kwenye hadhi zao bali kwenye misimamo ya hisia zao.

Uaminifu ni sifa tukufu alimuradi hauwi wa upofu, na kama hauondoi ule uaminifu wa hali ya juu kwenye ukweli na kwenye heshima, basi wanapaswa kukomba vinundu na mabaki ya historia, na wanapaswa pia kukataa vishawishi vya kuzusha kitu kinachoitwa "Meyers' Law" (Sheria ya Meyer) katika vitabu vyao. "Meyers 'Law" inaweka masharti kwamba:

"Kama ukweli haulingani na nadharia, basi ukweli huo uache kabisa."

Mwanahistoria bila ya kukwepa atakutana na ukweli ambao unaweza kuwa haumpendezi lakini ni lazima asiuzime. Yeye lazima aeleze mambo yote kama anavyoyagundua ikiwa anataka kutetea ukweli.

Lakini mwanahistoria huyo, kama yeye ni Muislamu, hana uchaguzi katika suala hili. Hayuko huru kuandika historia ya "msukumo" au ya "maneno ambatani." Yote anayoweza kufanya, kama anaandika historia, ni kung'ang'ania kwa uthabiti kabisa kwenye ukweli. Kama anaandika "historia" ya uwongo kwa sababu yoyote ile, atastahili tu ghadhabu ya Allah swt. Hapa, kama mahali pengine popote, Qur'an Tukufu, Kitabu cha Allah swt. kiko wazi, chenye mkazo, na yenye kauli moja katika hukumu yake kama ifuatavyo:

688

Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

Usahihi-76.jpg

"Na wala msichanganye haki na batili, na mkaficha haki hali ya kuwa mnajua." (Sura ya 2. Aya ya 42)

Usahihi-77.jpg

"Hakika wale wanaoficha tuliyoyateremsha katika dalili zilizo wazi na muongozo, baada ya sisi kuzibainisha kwa watu Kitabuni - Hao hulaaniwa na Mwenyezi Mungu, na laana ya wenye kulaani (pia)."(Sura ya 2. Aya ya 159)

Kama wanahistoria wa Kiislamu watazifanya hizi Aya mbili za Qur'an Tukufu kuwa "nyota ya uongozi" yao, watalindwa na makosa, na watalindwa pia kutokana na kuwa ama mawakala ama waathirika wa propaganda hiyo, watambue au wasitambue.

Katika kujaribu kuchafua jina la Ali ibn Abi Talib; katika kujaribu kudunisha kwa makusudi utumishi wake kwa Uislamu; na kwa kujaribu sana kuficha matendo yake mema, nyuma ya pazia la propaganda, kwenye kizazi cha baadae, maadui zake walikuwa wakitupa mavumbi kwenye uso mng'aavu wa jua. Waliibua mawingu ya mavumbi katika muundo wa propaganda kali sana na iliyoendelezwa dhidi yake, na bado, jua hilo lil-iangaza zaidi na zaidi.

Usahihi-78.jpg

"Na Mwenyezi Mungu ataifuta batili na ataithibitisha Haki kwa maneno Yake. (Sura ya 42; Aya ya 24)

Allah swt. alilibariki jina la Ali kwa milele yote. Jina lake ni alama ya upendo wa Allah swt., na ni alama ya Haki na Ukweli. Jina lake litadumu kwa muda mrefu kama Mapenzi ya Allah swt, na Haki na Ukweli, vitadumu katika dunia hii.

689