Kimeandikwa na
www.al-islam.org and ebooked by www.ShiaLibrary.com and www.islamkutuphanesi.com . May Allah be pleased with all. |
Kimekusanywa na kutarjumiwa na
AMIRALY M. H.
DATOO
BUKOBA
–
Bismillahir
Rahmanir Rahiim
Natanguliza kumshukuru Allah swt pamoja na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na Ma-Imamu a.s. walionijaalia Tawfiqi ya kuweza kuwaleteeni mbele yeni kitabu hiki.
Mimi nimekitarujumu kitabu Dhambi Kuu la kutokulipa Zaka, Khums na Sadaka katika Kiswahili na wakati nikiwa nikiifanya kazi hiyo, niliona itakuwa afadhali iwapo Sadaka pia nitakitayarishia kitabu chake. Na hivyo ndicho hiki kipo mikononi mwenu.
Kwa hakika sisi tunakuwa daima tukitoa sadaka lakini hatujui habari zaidi kuhusu Sadaka na hivyo nimevutiwa na kazi aliyokuwa ameifanya Marehemu Mullah Asghar M.M.Ja’afer, aliyekuwa Mwenyekiti wa World Federation of Khoja Shi’a Ithna-Ashery Muslim Communities, na hivyo nimekitarjumu katika Kiswahili.
Kitabu hiki cha Sadaka ni sehemu ya Kitabu kiitwacho Wasa’il as-Shi’a mlango wa Kitabuz - Zakaat cha Sheikh Hurri ‘Aamili.
Vile vile kumeongezewa habari za Elimul Hadith na Majma’ul Hadith kutokea juhudi zilizofanywa na Maulama wa Kishi’a.
Ni matumaini yangu kuwa kitabu hiki kitatufaidisha sote na tutakuwa na moyo zaidi wa kutoa Sadaka.
Amiraly M.H.Datoo
BUKOBA- Tanzania
Katika sehemu hii, twategemea kuzungumzia kwa mukhtasari msimamo wa Shia kuhusu uandikaji wa Hadith kutokea mwanzoni. Itaonekana kuwa ni kinyume na msimamo wa wengine kuhusu swala hili. Msimamo wa Kishia ulisisitiza mno juu ya uandikaji wa Hadith zikisaidia uhifadhi wake wakati ambapo Maulamaa mashuhuri wa Kisunni, hata kufikia mwanzoni mwa karne ya 3A.H./9 A.D. walikuwa wakipinga uandikaji wa Hadith. Ni baada ya uandikaji wa Hadith ulipokuwa dhahiri hao wanaopinga walipoanza kwenda kinyume na Hadith walizokuwa wamezitoa wakipinga uandishi na uenezaji wake na hapo wakaanza kuziandika.
Alba ibn al-Ahmad ananakili kuwa mara moja Ali ibn Abi Talib a.s. wakati akitoa Hotuba juu ya mimbar, alibainisha: "Je, ni nani atakayeinunua elimu kwa Dirhamu moja?" Al-Harith ibn al-A' war alinunua karatasi yenye thamani ya Dirhamu moja na kumwijia Imam Ali ibn Abi Talib a.s. na kuandika kiasi cha kutosha cha elimu juu yake.[1] Riwaya hii inatuonyesha vile Imam a.s. alivyokuwa akisisitiza juu ya uandikaji.
Imam Hassan ibn Ali ibn Abi Talib a.s.
ameripotiwa akiwashauri watoto wake
"Nyinyi sasa ni watoto wa Ummah ambao
katika maisha ya mbeleni mtakuwa wakubwa wao.
Jielimisheni Elimu; na yeyote yule miongoni mwenu atakayeweza kuhifadhi
(kukariri) elimu (yaani Hadith), basi aiandike na kuiweka nyumbani mwake."[2]
Imeripotiwa kuwa Hujr ibn Adi, mmoja wa Sahaba wa Mtume s.a.w.w. na Imam Ali ibn Abi Talib a.s., aliziandika Hadith za Imam Ali ibn Abi Talib a.s. katika kitabu na kuzirejea pale alipohitaji msaada wa mwongozo katika masuala mbalimbali [3] Mifano hii inadhihirisha umuhimu aliokuwa ameuambatanisha Imam Ali ibn Abi Talib a.s., watoto wake na Sahaba wake katika uandikaji wa Hadith. Mifano miwili ifuatayo itaonyesha dhahiri vile Imam Ali ibn Abi Talib a.s. alivyokuwa akisisitiza umuhimu wa Hadith na kuzihifadhi.
Umar ibn Ali anaripoti kuwa mtu mmoja
alimwuliza Imam Ali ibn Abi Talib a.s. ni vipi kuwa yeye (i.e. Ali) aliweza
kunakili na kusimulia Hadith nyingi za Mtume s.a.w.w. kuliko Sahaba wengineo. Imam Ali ibn Abi Talib a.s. alijibu:
"Hii ni kwa sababu daima nilipokuwa nikimwuliza swali Mtume s.a.w.w.,
alikuwa akinijibu maswali yangu. Na pale
nilipokuwa nikiwa kimya, basi Mtume s.a.w.w. alianzisha mazungumzo
mwenyewe." [4]
Ali ibn Hawshab anaripoti kutoka Makhul,
mwanachuo kutokea
Na hapo alimwambia Imam Ali ibn Abi Talib a.s. "Mimi nimemwomba Allah swt kuwa masikio hayo yawe ni yako." Baadaye Imam Ali ibn Abi Talib a.s. alisema: "Mimi kamwe sikusahau Hadith yoyote au chochote kile kilichosikilizwa na sikio langu kikisemwa na Mtume s.a.w.w. [5]
Umar ibn al-Harith anasema:
"Wakati mmoja Ali a.s. aliuelekeza uso wake kuelekea mbinguni na kuurudisha chini akisema:"Mwenyezi Mungu na Mtume wake s.a.w.w. wamesema kweli." "Je, kilikuwa nini?" Kikundi cha watu kiliuliza. Imam Imam Ali ibn Abi Talib a.s. alisema: "Mimi ni mpiganaji wa vita na vita vinarithishia mtu ulaghai. Vivyo hivyo, ninaweza kukubali iwapo nitaporomoka kutokea mbinguni kwa ajili ya kunaswa na ndege kuliko kumsingizia uwongo Mtume wa Allah swt. Kwa hivyo fuateni chochote kile mukisikiacho kikitoka kwangu........" [6]
Kauli juu ya uandishi wa Hadith pia zimenakiliwa kutoka Maimamu wengine.
Al-Imam al-Sadiq a.s. alisema:
"Andikeni na kuieneza elimu yenu miongoni
mwa ndugu zenu, na iwapo mtafariki basi watoto wenu watarithi vitabu
vyenu. Itafika siku ambapo patatokea
machafuko na hapatakuwapo na mtu wa kumfanya rafiki na wala hapatakuwa na
chochote cha kuweza kutegemewa isipokuwa ni vitabu tu....[7]
Al-Imam al-Sadiq a.s. pia amenakiliwa kwa
kusema: "Hifadheni vitabu vyenu
kwani mutakuja kuvihitaji hivyo siku moja." Vile vile ameripotiwa akisema kuwa nguvu za
moyo na kuhifadhi akilini inategemea mno juu ya maandishi.[8]
Abu Basir anaripoti kuwa aliambiwa na Imam al-Sadiq a.s.: "Baadhi ya watu waliotoka Basrah walikuwa wakija na kuniuliza kuhusu Hadith na waliziandika. Je, kwa nini nawe hauziandiki?" Na aliongezea kusema, "Elewa wazi wazi kuwa wewe kamwe hautaweza kuhifadhi Hadith bila ya kuiandika."[9]
Idadi kubwa ya mapokezi yanaonyesha kuwa Maimamu a.s. walikuwa navyo vitabu na maandishi ambavyo walirithi kutoka vizazi vilivyowatangulia.[10]
Katika riwaya nyingine Imam Ali ibn Abi Talib a.s. ameripotiwa akiwa amesema: "Ikamateni elimu (kwa kuiandika)," ambavyo aliirejea mara mbili [11] Imeripotiwa kutoka Ja'bir kuwa Abu Hanifa alikuwa akimwita al-Imam al-Sadiq a.s. "Kutubi" (yaani mwenye vitabu) kwa sababu ya kutumia mno vitabu, na Imam a.s. alifurahishwa kwa jina kama hilo. [12]
Vile vile imeripotiwa kuwa al-Imam Muhammad ibn Ali al-Baqir a.s. ameziandika Hadith za Mtume s.a.w.w. ambazo zilikuwa zikinakiliwa na Jaabir ibn Abdullah Ansaari. [13]
(Ingawaje taarifa hii inaonyesha kuwa siyo ya ukweli kwani Jaabir alikuwa ameshakwisha kufariki wakati Imam a.s. alikuwa na umri wa miaka mitano tu, labda inawezekana kuwa Hadith ziliandikwa na mjumbe).
Kwa kuwa riwaya (desturi) ya uandishi wa Hadith ilikuwapo miongoni mwa Shia tangia mwanzoni, wao walikuwa wanaongoza katika uandishi wa Hadith na Fiqh. Dr. Shawqi Dayf anaandika:
"Mwelekeo na umuhimu wa Mashia katika
uandishi wa Fiqh umekuja daima ni madhubuti mno. Sababu nyuma yake ilikuwa ni
imani
Al-Allamah al-Sayyid Sharaf al-Din anaandika:
“Imam Imam Ali ibn Abi Talib a.s. na wafuasi
wake walitilia mkazo na kufuatilia swala la uandishi kuanzia mwanzo
kabisa. Jambo la kwanza kabisa
lililotiliwa mkazo na kufuatiwa na Imam Ali ibn Abi Talib a.s. ilikuwa ni
kuiandika Quran nzima, ambayo aliifanya baada ya kifo cha Mtume s.a.w.w. kwa
kuiandika kimpangilio wa ufunulio wa Aya za Qurani.Katika Qurani hiyo pia
alikuwa ameonyesha ni aya zipi zilizokuwa 'amm au khass, mutlaq au muqayyad,
muhkam au mutashabih. Baada ya kukamilisha hayo, aliendelea na kazi ya
ukusanyaji wa kitabu kwa ajili ya Fatimah, ambacho kilikuwa kikijulikana kwa
vizazi vyao
Marehemu Sayyid Hassan al-Sadr anaandika kuwa Abu Rafi, aliyekuwa mawla wa Mtume s.a.w.w. ndiye aliyekuwa wa kwanza miongoni mwa Mashia kwa kukikusanya kitabu. [16] al-Najashi katika Fihrist ameelezea kuwa Abu Rafi alikuwa ni mtunzi katika kizazi cha kwanza cha Mashia. Mfuasi wa Imam Ali ibn Abi Talib a.s. Abu Rafi alishiriki katika vita vya Imam Ali ibn Abi Talib a.s. na alikuwa ni mwangalizi wa hazina ya Serikali huko Kufah. Kitabu chake kilichokuwa kikiitwa Kitab al-Sunan wa al-ahkam wa al-qadhaya, ambacho kilikuwa kimeanza kwa sura izungumziayo Salat, kufuatiwa na sura juu ya Saumu, Hajj, Zakat, kutolewa kutoka kwa Imam Ali ibn Abi Talib a.s. katika Kufah, Kitabu hiki kilinakiliwa na Zayb ibn Muhammad ibn Ja'afer ibn al-Mubarak katika nyakati za al-Najashi.
Ali ibn Abi Rafi, mwana wa Abu Rafi, aliye
tabi't na Mshia khalisi ameweza vile vile kukusanya kitabu kilichokuwa na sura
mbali mbali juu ya mambo ya Sheria
Miongoni mwa mapokezi ambayo inatuonyesha
kuwa ma-Imam a.s. walikuwa navyo vitabu
"Mimi nilikuwa pamoja na al-Hakam ibn
Utaybah na tulimtembelea al-Imam al-Baquir a.s. Al-Hakam alimwuliza swali Imam
a.s. Abu Ja'afer a.s. alikuwa akimstahi
Katika riwaya nyingineyo ameripotiwa Imam al-Baquir a.s. akisema: "Katika kitabu cha Imam Ali ibn Abi Talib a.s. nimepaona ambapo Mtume s.a.w.w. akisema: 'Wakati zakat itakapokuwa hailipwi, basi baraka itapotea kutoka ardhi." [20]
Vile vile ipo imeripotiwa kuwa Imam al-Sadiq a.s. amesema:
Baba yangu alisema:
"Mimi nimesoma katika kitabu cha Imam Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa Mtume s.a.w.w. ameandika mkataba baina ya Muhajirun na Ansar na watu wengineo wa Yathrib ambao waliungana naye, ikisemwa humo hivi: "Jirani ni sawa na mtu mwenyewe; asitendewe visivyo haki au kutendewa madhambi. Utukufu wa jirani wa mtu ni sawa na ule utukufu wa mama yake." [21]
Katika riwaya nyingine al-Imam al-Sadiq a.s. amesema:
Imeelezwa katika kitabu cha Imam Ali ibn Abi Talib a.s.
"Mfano wa dunia ni sawa na mfano wa nyoka: ngozi yake nyororo mno, lakini ndani yake ni sumu kali mno. Mtu aliye mwenye busara hujiweka naye mbali, lakini jahili anafanya kila aina ya jitihada ya kutaka kuikaribia." [22]
Kwa mujibu wa
riwaya nyingineyo, habari ifuatayo imetoka katika kitab adab Amir al-Muminiin:
Mtu yeyote asijaribu
kurejea katika mithali katika masuala ya Din,
kwani amri ya Allah swt haiwezi kutambuliwa kwa mithali. Watatokezea watu ambao watakuwa wakirejea
katika mithali, na hao watakuwa na uadui pamoja na Din. [23]
Zurarah anaripoti:
Nilimwuliza al-Imam al-Baquir a.s. kuhusu hisa ya babu katika urithi. Imam a.s. alijibu: "Sijawahi kumwona mtu yeyote yule akilisemea swali hili bila ya kuongezea mawazo yake ya kibinafsi, isipokuwa Amir al-Muminiin Ali ibn Abi Talib a.s.." Mimi nilimwuliza: "Na jee alisema nini?" Imam a.s. alinijibu: "Njoo kesho, mimi nitakusomea kutoka kitabuni." Mimi nilisema, "Mimi niwe fidia juu yako, naomba uiseme katika mtungo wa Hadith kwani Hadith zako ni afadhali kwangu kuliko kukisoma kitabu." Imam a.s. alisema: "Tafadhali usikilize kile nilichokuambia. Njoo kesho na mimi nitakusomea kutoka kitabu hicho." Siku ya pili mimi nilimwendea Imam a.s. wakati wa adhuhuri. Jaafer ibn Muhammad mwanae Imam a.s. alinikaribia na Imam a.s. alimwambia kunisomea kitabu hicho........[24]
Katika riwaya nyingine, Imam al-Sadiq a.s. anasema:
"Ipo imeelezwa katika Kitabu cha Imam Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa mtu anywaye pombe na mwenye kumsaidia aliyelewa (muskir) basi wote wanastahili kuadhibiwa, ambavyo ni sawa katika sura zote mbili." [25]
Muhammad ibn Muslim, Sahaba wa Imam al-Baquir a.s. asema:
"Abu Jaafer alinisomea kitabu kitab
al-faraidh, ambacho yalikuwemo yaliyosemwa na mtume s.a.w.w. na kuandikwa na
Imam Ali ibn Abi Talib a.s.." [26]
Habari zote zilizotajwa hapo juu, ambazo ni
chache
Mambo yote hayo yanakuelekeza katika uimara
na uhakikisho wa usahihi wa Hadith zilizonakiliwa na Mashia. Hii ni kwa sababu pamoja na kuendelea na
maongozo ya Maimamu a.s. hadi kufikia katikati ya karne 3 A.H./9 A.D., Hadith
za Mashia zilitoa watunzi wengi mno na ambao maandishi yao kuanzia kipindi cha
al-Imam al-Sadiq a.s. yamekuwa kwa hakika ni katika idadi kubwa sana. Iwapo mtu ataweza kutupia macho Rijal
al-Najashi, basi huyo ataweza kuona kuwa wafuasi wa Imam a.s. wametupatia kazi
kubwa ambazo zimetumika
Ukweli ni kwamba, Mashia idadi yao ndogo kwa upande mmoja na maisha ya hatari waliyokuwa wakiishi kwa upande wa pili ambayo iliwazuia watu waovu na wenye kuvizia majukumu kuingia katika Ushia pamoja na umuhimu uliosisitizwa na Maimamu a.s. na wafuasi wao katika uandishi, ndivyo vilivyoleta matokeo ya utajiri na usahihi wa Fiqh ya Kishia. Haya ndiyo faida ambazo hazikupatikana kwa Ahl al-Sunnah kwani, kwanza, wingi wa idadi yao, pili, kwa kuwa madhehebu ya Sunni ndiyo iliyokuwa Dini ya utawala wa Dola, na tatu, kwa sababu ya ukosefu wa Hadith zilizoandikwa kwa Waislam kwa ujumla kuyafuatilia yale yanayotokana na ukweli wa misingi ya kihistoria.
Kazi zote zilizopo hadi leo zinazohusu Hadith zilikuwa zimekusanywa katika kipindi cha karne 2 A.H./8 A.D. au katika karne ya 3 A.H./9 A.D. Historia inatuonyesha kuwa katika kukaribia karne ya 2 A.H. kulitokezea idadi ndogo ya Muhaddithun ambao walianza kuziandika Hadith, ingawaje hazikuwa na mpangilio. Baadaye mkusanyiko huu mdogo ulikuwa kiini cha kazi zote kubwa. Hata hivyo wingi wa Hadith zilizopo sasa kwa kukusanywa, zilienezwa kwa desturi ya kutamkwa (kusemwa), na wakati zilipokuja kuandikwa vitabuni, zilikuwa hazikuwahi kuandikwa popote kabla yake.
Ucheleweshwaji katika kuandikwa kwa Hadith ni swala mojawapo muhimu katika historia ya Hadith. Umuhimu wake ni wa ukweli kwamba kucheleweshwa huu kuliathiri hasa kuhusu utunzi na idadi ya Hadith pamoja na uwepesi wao wa kuzushwa (zikaongezwa na kupunguzwa na hatimaye zikawa ni zile zilizo na uongo) na matatizo mengi mengineyo yanayohusiana.
Jambo la umuhimu huu katika swala hili
linawahusu wale ambao ndio waliokuwa wamesababisha ucheleweshwaji huo wa
kuandikwa kwa Hadith. Mwelekeo wao
ulikuja
Kila kinachoweza kukusanywa kwa shida
katika Historia ni kwamba baadhi ya Makhalifa walizuia uandikaji wa Hadith kwa
sababu fulani fulani. Baada
Wao walizihifadhi Hadith za Mtume s.a.w.w.
kwa kuzikariri tu (kwa kuzihifadhi akilini mwao tu).
Al-Zuhri anasema:
"Sisi tulikuwa tukichukia mno uandishi wa elimu, hadi hapo wakuu wetu walipotulazimisha kuyaandika hayo. Hapo baadaye tulikuja kugundua kuwa hapakuwapo na yeyote miongoni mwa Waislam waliopinga."
Al-Zuhri anaendelea kusema:
"Wafalme waliniambia kuandika elimu
('ilm, i.e. Hadith) kwa ajili
Ni dhahiri,
'Umar ibn Abd al-Aziz (101 A.H./719 A.D.) ndiye aliyekuwa Khalifa wa kwanza kuamrisha wanazuoni wa miji mbalimbali kuziandika Hadith na kumpelekea huyo Khalifa maandishi yote. [29] Imeripotiwa kuwa Khalifa alimwandikia Muraah ibn Kathir akimwomba amwandikie Hadith za Mtume s.a.w.w. [30] Vile vile yeye alimwandikia Abu Bakr ibn Muhammad Hazm: "Andika Hadith yoyote ile ya mtume s.a.w.w. uliyonayo na kunitumia na chochote kile kilichonakiliwa kutoka kwa Umar, kwa sababu ninayo hofu kuwa utafika wakati ambapo Hadith zitakuwa zimetoweka." [31] Yeye pia aliwaandikia watu wa Madinah akiwataka wamwandikie chochote kile kilichobakia cha Hadith za Mtume s.a.w.w. [32]
Ripoti hizi zinaonyesha wazi wazi kuwa uandikaji wa Hadith haukuwa jambo lenye umuhimu hadi wakati huo, hata hivyo, haimaanishi kuwa hapakuwepo na Hadith zilizokuwa zimeandikwa hadi wakati huo.
Pamoja na kifo cha Umar ibn Abd al-Aziz kazi hii haikufuatiliwa na Makhalifa waliofuata, na kwa mara nyingine tena uandikaji wa Hadith uliangukia katika kusahauliwa. Kukariri (kuhifadhi katika akili) ndiyo iliyokuwa njia iliyobakia.
Hadith za kusemwa mdomoni tu (bila ya maandiko) ndiyo iliyokuwa njia ya uenezaji wakati ambao Sunni walirithi kutoka vizazi vyao vilivyowatangulia, ilisababisha upinzani mkubwa mno katika kuziandika Hadith. Sisi twaweza kuelewa vyema hali hii wakati tutakapokuja kujua kuwa baadhi ya Muhaddithun walichukizwa mno na uandishi wa Hadith hadi kufikia mwishoni mwa karne ya 2 A.H./8 A.D. Kauli za wanahistoria kuhusiana na ukusanyaji wa Hadith hapo mwanzoni zinaelezea hayo hayo.
Abd al- Razzaq anaelezea kuwa mtu wa kwanza
kuzikusanya Hadith alikuwa Abd al-Malik ibn Jurayj, aliyejulikana
Al-Dhahabi anaandika kuwa, katika kipindi
hiki ndipo Wanazuoni wa Kiislamu
walianza kuandika Hadith, Fiqh na tafsiri katika mwaka 143 A.H./760 A.D. Wafuatao ndio waliokuwa wakiongoza katika
kazi hizo nao ni Ibn Jurayj katika mji wa Makkah, Malik (179 A.H./795 A.D.)
huko Madinah, al-Anzai katika
Mahali pengine yeye ni mbainifu zaidi
wakati asemapo: "Ibn Jurayj na Ibn Abi Urwah walikuwa ni miongoni mwa watu
wa kwanza katika ukusanyaji wa Hadith na Muammar ibn Rashid alikuwa ni wa
kwanza miongoni mwao huko
Ni dhahiri, ingawaje Hadith zilikuwa zikikusanywa kwa kiasi fulani katika siku hizo, kazi ya ukusanyaji ilianza kuzorota kwa sababu ya upingamizi uliofuatia kifo cha Umar ibn Abd al-Aziz, na vile anavyosema al-Dhahabi, kazi hiyo ya ukusanyaji wa Hadith uliahirishwa au kuachwa kwa kipindi cha nusu karne.
Ibn Hajar anasema:
“Kazi ya ukusanyaji na upangaji (tabwib) wa
Hadith ulianza katika miaka ya mwishoni mwa kipindi cha tabi'un, yaani ni
kwamba, wakati ambapo Wanazuoni wa Kiislam walipokuwa wameenea katika
miji. Wa kwanza katika ukusanyaji wa Hadith
walikuwa ni Rabi ibn Subayh na Sa'id ibn Abi Urwah......hadi wakuu miongoni mwa
Wanazuoni wa tabaka la tatu walipokusanya ahkam. [38]
Al-Dhahabi pia
anaelezea kitu
“Wakati Islam ilipoenea katika sehemu
mbalimbali, na miji ya Islam ilipopanuka, tabi'un walisambaa mote humo. Baada ya muda, mkuu wao alipofariki dunia na
hivyo ndivyo ilivyokuwa imekuja kuathiri ukusanyaji wa Hadith. Wanazuoni walianza kuhisi haja ya kuziandika
Hadith na kuzihifadhi kwa njia ya kuziandika.
Katika maisha yangu, lilikuwa ni jambo la maana la kuziandika Hadith,
kwa sababu kukariri tu kuna uwezekano mkubwa wa kuweza kuja kupoteza fahamu au
kuzipotoa. Baada
Kutokana na taarifa hizo, tunaweza
kumalizia kuwa, kotekote, kulikuwapo na vipindi vitatu katika mpitilio wa
Hadith za kutamkwa. Kipindi cha kwanza
kilichukua/kilidumu mwanzoni hadi mwishoni mwa karne ya 1 A.H. /7 A.D. katika
kipindi hiki uandishi wa Hadith haukuwapo wala haukujaribiwa isipokuwa tu
katika hali chache ambapo Sahaba walijaribu kuziandika kwa
kwenda kinyume na amri ya Makhalifa. Katika kipindi cha pili, kuanzia mwanzoni
mwa karne ya 2 A.H./8 A.D. hadi kwa kufikia katikati, kulitokezea uandishi na ukusanyaji wa Hadith katika hali isiyokuwa
kamilifu na pia mambo yaliyoandikwa yaliweza kukusanywa. Katika kipindi cha
tatu, kilichoanzia katikati ya karne ya 2 A.H./8 A.D., uangalifu mkubwa
ulielekezwa katika ukusanyaji na uandikaji wa Hadith ikiwa ni shughuli muhimu
kimsingi. Vitabu vichache mno
vilivyoandikwa katika kipindi hiki vinaweza kupatikana na baadhi ya mikusanyiko
ya zamani
Kwa mujibu wa ripoti ya al-Dhahab, musnad ya kwanza ilikusanywa na Nu'aym ibn Hammad. [41] Yahya al-Hamani [42] huko Kufah na al-Musd [43] huko Basrah nao ndio waliokuwa wa kwanza miongoni mwa Wanazuoni wa miji hii katika kukusanya musnad.
Inafahamika vyema kabisa kuwa Mtume s.a.w.w., kuanzia mwanzoni kabisa mwa Utume wake, aliupatia umuhimu zaidi kuhusu uandishi wa Qurani. Kimatokeo Qurani ikawa ipo mbali na makosa au mabadiliko (tahrif). Hata hivyo, katika hali ya Hadith kwa mujibu wa imani yetu mbali na ruhusa au amri ya Mtume s.a.w.w. kwa kuhusiana na uandishi wa Hadith na mbali na ukweli kwamba Hadith zilikuwa zimeandikwa katika zama za uhai wa Mtume s.a.w.w. , sio kwamba tu kuwa haukupewa umuhimu kwa kazi, pia iliweza hata kupingwa. Upingamizi huo ulisababisha matatizo mengi kuhusiana na Hadith, ambayo tutayaona hapo mbeleni.
Uchelewesho huo wa kuziandika Hadith na matokeo yenye hatari yalifanya kikundi kimoja kumtupia lawama na 'udhubillah Mtume s.a.w.w. Wao walitambua wazi kuwa upingamizi wa uandishi wa Hadith iwapo itatokea kwa Mtume s.a.w.w. , basi haitaweza kulaumiwa, kwani Mtume s.a.w.w. hawezi kulaumiwa; hata hivyo, iwapo wataielezea kwa wengine basi itatoboa udhaifu wao. Kwa hivyo, walimwelekezea Mtume s.a.w.w. kuwa ndiye aliyekataza kuandikwa kwa Hadith.
Mawaidha na Nasiha maneno aliyoyazungumza Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Hadith kwa kifupi, maneno yoyote yaliyotoka mdomoni kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. mbali na ayah za Qur'an Tukufu, ama yale aliyoyatenda kuonyesha, hayo yote ni Hadith. Vile vile maneno na matendo yote ya Ma’asumin a.s. pia ni Hadith yaani yataingizwa katika Hadith. Kutokana na Hadith sisi tunaweza tukajua na kufuatilia na kutekeleza mambo ambayo ni usuli – Furu’, Sunnah na faradhi.
Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kwa maisha yake yote alikuwa pamoja na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Hivyo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. popote pale alipokuwa akiwapa watu nasiha na mawaidha katika mambo mbalimbali na kuwaongoza katika masuala mbalimbali basi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. daima alikuwa akinufaika na hayo yaliyokuwa yakisemwa na kutendwa na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na ndivyo alivyosema “Sisi ndio dalili za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na vile vile ndio Sahaba wake halisi, na sisi ndio ufunguo wa hazina yake ya ilimu na mlango wa mji wake wa ilimu[44] alioutangaza Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na mtu yeyote hawezi kuingia katika nyumba au mji isipokuwa kwa kupitia mlango wake.”
Kwa kiapo cha Allah swt ! Mimi nina ilimu na ma’arifa ya Utume na maneno ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Sisi Ahlul Bayt a.s. ni milango ya hekima na kwa hakika sisi ndio tunayo nuru ya hukumu za Allah swt. (Nahjul Balagha).
Katika historia tunapata habari kuwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ndio aliyekuwa mtu ambaye amekusanya na kuwa na hazina kubwa ya Hadith za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Tumepata kuona kuwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. yeye daima alikuwa akiziandika Hadith za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na kuzielewa na kuzikariri vyema kabisa. Na kwa amri ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ndipo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alitayarisha kitabu kimoja ambamo kumeandikwa Hadith za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na Sunnah zake, na kitabu hicho kinaitwa Sahifat Jami’a na kitabu kingine kinaitwa Kitabul Faraidh, ambamo katika vitabu hivyo vyote viwili kumeandikwa Ahkam za Sharia. Vitabu hivyo vimenakiliwa katika vitabu vingine mfano Sahih Buhari amenakili kwenye kitabu chake ambao ni upande wa Masunni. Na upande wa Mashi’ah Ma’ulamaa wa Kishi’ah Sheikh Sadduq a.r. amenakili katika kitabu kinachoitwa Manla yahdharulfaqih na Sheikh Tusi a.r. kinachoitwa Tahdhib na Thiqqatul Islam Quleyni r.a amenakili katika Al Kafi.
Kwa hakika Mashiah wana mchango mkubwa
“Mwanzoni mwa Waislam kulikuwa na utata
katika uandishi wa Hadith, kwa sababu
baadhi
1. Mtumwa wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliyekuwa akiitwa Abu Rafi’, na ambaye alikuwa miongoni mwa wale Waislam wa mwanzoni kabisa.
Bwana ‘Abbas mjomba wake Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ndiye aliyekuwa amempa zawadi huyo, na wakati huyo mtumwa alipo mpa habari Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa mjomba wake huyo Bwana ‘Abbas ameukubalia Uislam, basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kwa kusikia hiyo habari njema alimfanya huru huyo mtumwa kwa sababu ya kuleta habari hizo njema. Katika fadhila zake tunaona kuwa yeye alifanya Hijra mara mbili, na amesali katika Qibla zote mbili na amefanya Bay’a ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. mara mbili.
Na vile vile ameshiriki katika vita vya Jihad vingi
2. Bwana Salman Muhammad (Al Farsi) ambaye baada ya kifo cha Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliandika habari za Jasliq kwa niaba ya Mfalme wa Roma
3. Asbagh bin
Nabata, aliandika usia wa Al Imam
'Ali ibn Abi Talib a.s. alioumfanyia Bwana Malik Ashtar, vile vile aliandika
Nasiha alizomfanyia mtoto wake Muhammad. Asbagh bin Nabata alikuwa ni mmoja wa Ma-Sahaba wa karibu
4. Suleim bin Kais
Al Hilali yeye ameandika kitabu chenye Ahadith
ambacho kinatumika mpaka sasa hivi na kwa mara ya mwisho kilikuwa kimechapwa
huko Najaf Al Ashraf, nchini
5. Mitham al-Tammaar yeye alikuwa mmoja wa Ma-Sahaba mashuhuri na mshupavu wa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. yeye naye ameandika kitabu ambacho Sheikh Sadduq amekitumia katika ‘Aamali na vile vile Tabari ametumia katika Basharatul Mustafa.
6. Zaid bin Wahab Aljahni
ambaye ametunga kitabu kimoja ambamo ameandika hotuba zote za Al Imam 'Ali ibn
Abi Talib a.s. alizokuwa akizitoa siku za Ijumaa na Idi, kwa hakika ameufanyia
‘umma huu ihsani kubwa
7. Mkusanyiko mkubwa
kabisa wa semi na Dua za Ma’sumin a.s. yanayojulikana
8. Jabir bin Yazid bin Al Harith Al Jaufi, yeye ameziandika yaani yeye katika nuru ya ahadith za Masumin a.s. ameandika Tafsiri, vita vya Jamal, Siffin, na Naherwaan, na vile vile ameandika kuuawa kwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. na Al Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. Yeye amefariki katika mwaka 128 Hijriyyah.
9. Bwana Abu Hamza Thumali (aliyefariki mwaka 150 Hijriyyah) alikuwa mmoja Sahabi mashuhuri mwaminifu kabisa wa Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. na Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. na ameweza kutunga kitabu kiitwacho Annawadir Wa-Dhuhud. Vile vile amefanya tafsiri ya Qur'an Tukufu pia.
10. Vile vile miongoni
ma Ma-Sahaba wa Al Imam Zaynul
'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. na Al Imam Muhammad al-Baquir
a.s. alikuwa akiitwa Muhammad bin Keis Al Bijalli ambaye ameandika kitabu
kiitwacho Qadhaya Al Imam ‘Ali ibn Abi
Talib a.s.
11. Aban bin Taghlib (aliyefariki mwaka 141 Hijriyyah) ni kwamba wote wanaafikiana kuwa yeye ameishi katika zama za Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s., Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., na Hadith zao alizozileta huyu Aban bin Taghlib zinasemwa kuwa ni Asili. Yaani inamaanisha kuwa Hadith zake hizo yeye alizoziandika zimetoka moja kwa moja kutoka kwa Maimamu a.s. na si kwa kupitia watu wengine walizozisikia inamaanisha kuwa ni yeye mwenye amezisikia hizo.
12. Takriban waliosomea ilimu ya Hadith ilifikia elfu nne au na zaidi kuanzia katika zama za Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. Siku moja Hassan bin Ali Alwashakhi yeye alikutana na wale watu waliokuwa wakizoea kuzisema Hadith si chini ya mia tisa katika Masji Al-Kufa, na wengi wa wale waliokuwa wakizisema hizo Hadith walikuwa wakisema tumeambiwa Hadith hii na Ja’afar bin Muhammad yaani zilikuwa ni Hadith asili ambazo huyo mtu amezisikia moja kwa moja kutoka kwa Maimamu a.s.
13. Ibn Nadhir katika
kitabu chake Fahrist amemwandikia yule Yunusu bin ‘Abdul Rahman na habari zake
kuwa ni mtu mmoja mwaminifu na mwenye kutegemewa kabisa ambaye miongoni mwa Ma-Sahaba wa Al Imam Musa al-Kadhim a.s.
na Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. Kwa hakika kitabu hiki ni chenye manufaa
14. Ibn Nadiim katika kitabu chake Fahrist amewaandika watoto wawili wa Sa’id bin Himad ambao ni Hussein na Hassan na vile vile ameandika habari zao pia, kuwa hawa watu walikuwa ni hodari kabisa katika ‘ilimu ya Hadith, Fiq-h na Manaqib. Hao wote walikuwa wana kitabu walichokitunga juu ya Hadith na walikuwa ni miongoni mwa Ma-Sahaba wa Al Imam Muhammad Taqi Al Jawad a.s. na Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s.
15. Fadhl Bin Shaazan Nishapouri (aliyefariki 260 Hijriyyah) yeye amewahi kuwa Sahaba wa Maimam watatu a.s. ambao ni, Al Imam Muhammad at-Taqi a.s., Al Imam 'Ali an-Naqi a.s. na Al Imam Hassan al-'Askari a.s. Naye ameandika vitabu vitatu:
· Cha kwanza Kitabul Faraidh Al Akbar,
· cha pili Kitabu Faraidh Al Awsat,
· cha tatu Kitabu Faraidh Al-Asghar ambacho ni mashuhuri.
16. Na baada ya hapo hii kazi ya ukusanyaji na uandishi wa Hadith ulikuwa umeendelezwa na Ma-Sahaba na wazee na wameweza kuleta kazi nne zilizo kubwa kabisa. Kazi hizo nne ambazo mpaka leo zinajulikana kwa jina la mashuhuri Kutub Al-‘Arbi’a yaani inajulikana kwa jina la vitabu vinne. Kitabu Cha kwanza kabisa ni Al Kafi, ambacho kimetayarishwa na kuandikwa na Thiqqatul Islam Al Quleyni a.r. (amefariki mwaka 329 Hijriyyah) katika kitabu hiki zipo Hadith takribani elfu kumi na sita. Vile vile kuna kitabu kingine kinachoitwa Man la haydharul faqih ambacho kimeandikwa na Bwana Abu Ja’afer As-Sadduq humo takribani Hadith elfu sita zinapatikana. Vile vile kulikuwa na kitabu chake kingine kijulikanacho kwa jina Madinatul ‘Ilm ambacho Shahid a.r. amekizungumzia.
Na kwa kutokana na fitina za zama hizi kitabu hiki hakipo yaani hakipatikani Na Sheikh Sadduq a.r. katika mwaka 381 Hijriyyah.
Vile vile
tunapata vitabu viwili mashuhuri na vyenye faida
Kwa hakika katika
zama zote hizi ilimu hii ya Hadith na
katika nuru ya Ayah za Qur'an Tukufu na Sunnah
ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ‘ummah umeweza kuwatambua na kuwafuata Ahlul
Bayt a.s. na kuweza kujipatia ma’arifa yao na Ma-Sahaba. Katika kila zama kazi
zilikuwa zikifanyika kwa kiwango fulani katika kuendeleza jitihada hizi za Hadith lakini katika mwaka wa 11 Hijriyyah kulifanywa kazi moja kwa kiasi
kikubwa
Kwa hakika Maulamaa wamefaidika sana na Hadith zilizo andikwa katika Bihar Al Anwar na vile vile inadhihirisha vile wanavyoonyesha kuisifu na kuiheshimu kazi hiyo na hapa nimejaribu kuwaletea baadhi ya majina yao ambao wamekuwa katika zama zake hizo na mmoja miongoni mwao kama Marhum ‘Allamah Majilisi alipewa ruhusa ya kunakili yaani ‘ijaza ya riwaya.
1. Muhammad bin Hassan Hurri ‘Aamili aliyefariki mwaka 1104 na mwandishi wa kitabu kinachoitwa Wasa’il as-Shi’ah, nacho kimechapwa si chini ya Juzuu ishirini.
2. Mullah Muhsin
Faiz Khashani aliyefariki 1091 na ambaye ni mwandishi wa Al-wafi Kitabu hiki kina
Juzuu kumi na nne kinazungumzia juu ya Usul,
Furu’, Sunan, na Ahkam.
3. Mulam ‘Abdullah bin Nurullah Bahrani mwandishi wa kitibu kiitwacho Al Awalim kitabu hiki kiko katika Juzuu mia moja.
4. Sheikh Muhammad Ridha bin Abdul Latif Tabrizi, aliyefariki mwaka 1158 na ni mwandishi wa kitabu kiitwacho As-Shifa’.
Kitabu hiki cha sadaqah ambacho kipo kwa mikononi mwenu, Hadith zake zimetolewa kutoka Wasa’il as-Shi’ah na tunaona vyema kuwaleteeni habari chache kuhusu kitabu na mtunzi wake.
Sheikh Hurri ‘Aamili baada ya jitihada zake
nyingine kwa muda wa miaka ishirini mfululizo amekigawa kitabu hicho katika
sehemu sita katika fani mbalimbali na kuzigawia Hadith kimpangilio mzuri kabisa kwa na hakika anastahili pongezi
kubwa
Mwandishi wa Al-Mizaan fi Tafsir al-Qur'an yaani As-Sayyid Muhammad Hussein Tabatabai kuhusu Wasa’il as-Shi’ah anaandika :
Kwa hakika kitendo hicho ni kipeo cha hali ya
juu kabisa katika maswala ya Fiq-h na Mafuqahaa na Mujtahidiin wanakitegemea
Sheikh Hurri Aamili alikuwa ni mwandishi
yaani ni mtu mwenye habari, na ni mmoja wa waandishi wa vitabu vinne vya
kutegemewa kabisa ambavyo vimeisha kwisha kuelezwa hapo nyuma. Kwa hakika katika zama zetu hizi kuna pengo
kubwa sana la ma’ulamaa kama hao ambalo haliwezi kuzibwa kwa hakika athari ya
mapengo hayo yanaonekana katika zama zetu na zile zitakazo kuja kwa sababu
mapango yamebakia wazi yanaongezeka na maulamaa wengi wametumia kazi ya Bwana
Hurri ‘Aamili kama vile Said Abul Qasim Al-Khui ametumia katika Mu’jamur Rijaal na kumtaja kuwa Bwana
Sheikh ‘Aamili alikuwa ni mtu wa maswala ya habari pia. Hivyo hivyo hali kadhalika Sheikh ‘Aamili
alizaliwa katika Jabal ‘Aamil kijiji kimoja kijulikanacho
Katika sehemu mwisho ya Wasa’il as-Shi’ah ‘Aamili anaandika kuhusu Alama Majlisi a.r. anaandika kuwa: Yeye ni mwisho katika wale waliokuwa wamenipa idhini, nami nilimpa idhini.
Mbali na kitabu cha Wasa’il as-Shi’ah, Sheikh ‘Aamili ameandika vitabu vingine ishirini
na sita ambavyo vingi vyake vina Juzuu mbalimbali. Kwa hakika mwanga wake huo
mkubwa alioutoa kwa ajili ya madhehebu ya Ahlul Bayt a.s. ni mkubwa
Tunaomba Allah swt awajaalie kila la heri Ma’ulamaa wakubwa waliojitolea mhanga kuinusuru dini hii tukufu ya Islam.
Kwa hakika kitabu hiki cha sadaka ni sehemu moja tu ndogo au tunaweza kusema ni
sura mojawapo katika Juzuu ishirini za Wasa’il
as-Shi’ah katika sura inayoitwa Kitabu
cha Zakah. Mkiangalia kazi yake yote hiyo kwa hakika hamtakuwa na la
kusema. Na surah hii inaitwa Kitabu cha Sadaka
ambacho kinazunguzia mambo juu ya sadaka na humo zipo surah hamsini na
nne sasa mfikirie
Kwa hiyo ndugu msomaji sababu ya kupenda kuchukua maudhui haya ni mambo mawili,
Kwa hakika ukiweza kuangalia utaona kuwa
ilimu ya Hadith imehifadhiwa na
kuendelezwa na hii Madrssah ya Ahlul Bayt a.s. ambapo kwa wengine jambo hili
halikupewa uzito wala tahadhari ya aina yoyote ile. Leo ukiangalia katika
ulimwengu wa Masunni utaona kuwa vitabu vyao vilivyopo wamshukuru ‘Umar ibn
‘Abdul Aziz na
Vile vile mtarjumu wa kitabu hiki ambaye yeye ametokea ‘Umma huu na amesomea, hivyo ameona afadhali kuwa kazi aifanye ili aweze kuleta mbele ya umma huu na kwa ajili ya manufaa ya wana-‘umma huo kwa hivyo itasaidia pia kumtaarufisha mwandishi wa kitabu hiki.
Sote kwa pamoja tunaomba kwa Allah swt nguvu zetu na jitihada zetu hizi azikubalie. Iwapo kumetokezea au kumebakia kasoro zozote katika kutarjumu basi tunamwomba Allah swt atusamehe na ninawaomba Wanazuoni na wenye Ilimu wajaribu kusaidia turekebishe kwa sababu katika kukitarjumu kitabu hiki hapakuwapo na matayarisho kamili kuanzia awali.
Na kazi hii imefanywa kwa nia njema kwa matarajio kuwa itatumika kwa nia njema na itafaa kutukupeleka mahala pema. Inshallah.
Naomba kazi yangu hii niiweke mbele kwa idhini ya Allah swt.
Na kuiweka mbele ya Al Imam Muhammad
Sahibuz-Zamaan a.s. iwe ni
KATIKA AHADITH: KUNIYYAT NA
ALQAAB
Mara nyingi tunaposoma vitabu vya riwaya tunapata majina mengine yaliyotofauti na majina ya asili. Hivyo tunaona katika Ahadith kuwa Ma’asumiin a.s. wanatambulishwa kwa majina yanayoitwa Kuniyyat au Iaqab, kwa mfano: Qala Abul Hasan ( yaani amesema Abul Hasan ) au Qala Abu ‘Abdillah (yaani amesema Abu ‘Abdillah) n.k. na hapo ndipo tunakuwa hatuelewi ni Ma’sum a.s. yupi ambaye amesema hayo.
Waarabu wanayo desturi ya kuwaita wazee wao
si kwa majina
Wakati wa kujaribu kufafanua juu ya Laqab au Kuniyyat kunatiliwa maanani kuhusu maneno na maana ya Hadith, zama za kusemwa na habari za wale wanaoziripoti, ndipo hapo panapoweza kutambuliwa kwa Alqaab au Kuniyyat katika Hadith hiyo kunatambulishwa Ma’sumiin a.s. yupi.
Hivyo kuelezea hayo na mengineyo, maelezo yafuatayo yatasaidia kutoa mwanga katika swala hili kwa ujumla:
1. ABUL QASIM Kuniyyat hii inatumika kwa ajili ya Mtume Muhammad
s.a.w.w. na Imam al-Mahdi a.s. Iwapo
kutaripotiwa riwaya kuwa Abul Qasim tu, basi
ijulikane kuwa ni Imam al-Mahdi a.f
2. ABU MUHAMMAD Zipo Hadith chache mno zinazojulikana kuwa Imam Hasan
a.s. Hata hivyo hiyo ndiyo Kuniyyat yake.
3. ABU ‘ABDILLAH
Kuniyyat
hii inatumika kwa ajili ya Imam Hussein a.s na vile vile inatumika kwa ajili ya
Imam Ja’afer as-Sadiq a.s.
4. ABUL HASAN
Kuniyyat hii inatumika kwa ajili ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. , Imam Musa ibn Ja’afer a.s., Imam Ali ibn Musa al-Ridha a.s. na Imam Ali an-Naqi a.s. Iwapo kutakuwapo na Abul Hasan tu katika riwaya, basi kutatambuliwa Imam Musa ibn Ja’afer a.s. Na iwapo kutaandikwa Abul Hasan Thani (Abul Hasn wa pili) basi kutakuwa kumefanywa ishara ka Imam Ali ar-Ridha a.s. na pale panapoandikwa Abul Hasan Thalith (Abul Hasan wa tatu) basi tujue kuwa kunamaanishwa Imam Ali an-Naqi a.s.
5. ABU MUHAMMAD
Kuniyyat hii inatumika kwa ajili ya Imam Hasan a.s., Imam Zaynul Aabediin a.s na Imam Hasan al-‘Askari a.s. lakini iwapo kutaandikwa riwaya kwa Abu Muhammad tu tutatambua kuwa riwaya hiyo ni kutoka Imam Hasan al-‘Askari kwa sababu riwaya za Imam Zaynul Aabediin a.s. zinatajwa kwa jina lake tu, bali zipo riwaya chache mno tu kwa Kuniyyat yake.
6. ABU IBRAHIM
Katika
Hadith Kuniyyat hii inatumika hasa kwa ajili ya Imam Musa ibn Ja’afer a.s.
7. ABU IS-HAQ Kuniyyat hii inatumika kwa kumtambulisha Imam Ja’afer
as-Sadiq a.s.
8. ABU JA’AFER
Kuniyyat hii inatumika kwa ajili ya Imam Muhammad al-Baquir a.s. na Imam Muhammad Taqi a.s
Lakini iwapo kutakuwapo na Abu Ja’afer tu au Abu Ja’afer Awwal, (Abu Ja'afer wa kwanza) basi ijulikane kunamaanishwa kwa Imam Muhhammad al-Baquir a.s.
Na iwapo kutaandikwa Abu Ja'afer Thani (Abu Ja'afer wa pili) basi kutambuliwe kuwa ni Imam Jawad a.s.
Kwa mara chache mno Abul Hasan inatumika kwa ajili ya Imam Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. lakini mahala pengi mno kunatumika Kuniyyat yake mahsusi ya Abul Hassanain.
Wakati pale utakapoona riwaya zinanakiliwa kutoka kwa ‘Aalim, Sheikh Faqih au ‘Abdi Salih, basi mutambue kuwa kunamaanishwa kwa
Al Imam Musa al-Kadhim a.s.
Vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anajulikana kwa alqaab zifuatazo: Sheikh , Abu ‘Abdillah, Faqih na ‘Aalim.
‘Allamah Majlisi a.r. anasema kuwa mahala pengi mno katika riwaya kunapotajwa Faqih basi kunamaanishwa kwa Imam ‘Ali an-Naqi a.s. na kwa mara chache mno kunatumika Jawallaij kwa ajili ya Imam Hasan al-‘Askari a.s na Al Imam Muhammad Sahibuz-Zamaan a.s.
Naqi, Mazii, Sahibul ‘Askar na Hajul kunamaanisha Imam Hasna al-‘Askari a.s.
Sahib na Sahibuddaar zinatumika makhsusi kwa ajili ya Imam al-Mahdi a.s. Lakini Sahibun Nahiyah inapokuja, basi kwa mara nyingine hutumika kwa ajili ya Imam ‘Ali an-Naqi a.s. au Imam Hasan al-‘Askari a.s. ‘Allamah Majlisi anasema kuwa mara nyingine katika Ahadith hutumika maneno Ghaib, ‘Alil au Gharim basi inatubidi kuelewa Imam al-Mahdi a.s.
Iwapo kutakuwapo bi ahadihima (kwa mojawapo) basi itatubidi tuelewe kuwa ni ishara kwa Imam Muammad al-Baquir a.s. au Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.
Na iwapo tutakuwa bi ‘Askariyyen, tuelewe kuwa ni Imam Ali an-Naqi a.s. na Imam Hasan al-‘Askari a.s.
Vile vile iwapo tutaona bi Kadhimain basi kunamaanishwa Imam Musa al-Kadhim a.s. na Imam Mahammad at-Taqi a.s.
Kwa mukhtasari, zipo alqaab nyingi ambazo zinajulikana kimakhsusi kwa ajili ya Ma’sumiin a.s. kama vile Amir al-Muuminiin, Mujtaba Shahid, Zaynul Aabediin, Baquir, Sadiq, Kadhim, Ridha, Jawad, Hadi, ‘Askari, na Sahib uz Zamaan (salaam ziwe juu yao wote).
Kwa hakika somo hili ni kubwa na lenye kwenda kwa undani zaidi, lakini kwa ajili ya wasomaji, tunawaleteeni habari hizi kwa kifupi ili kuwafaidisha.
Katika lugha ya Kiarabu, mtu anayeripoti riwaya huitwa Rawi na sifa zake zimeelezwa na kubainishwa na Ma’ulamaa walio mabingwa wa ilimu ya Ahadith:
1. Rawi lazima awe mtu mwenye akili na fahamu timamu. Riwaya zozote zitakazotolewa katika hali ya kuwehuka au kurukwa na fahamu, basi hazitathaminika au kukubalika.
2. Ni lazima Rawi awe amebaleghe na Mukallaf, yaani shariah za Dini ziwe zimeshakwisha kuwa faradhi juu yake. Hapa inawajumuisha vijana na watoto na wale wote ambao bado hawajabaleghe lakini wanaweza kutofautisha baina ya wema na ubaya. Aina hii ya vijana hao huitwa Mumayyiz na hivyo riwaya zao zinapotimika masharti mengineyo, huweza kukubalika na kusadikika.
3. Ni lazima Rawi awe Mwislamu. Riwaya za mtu asiye Mwislamu haziwezi kuaminiwa au kusadikiwa.
4. Rawi lazima awe ni Mwislamu mfuasi wa Madhehebu ya Sh’iah Ithna-Asheria. Lakini iwapo kutakuwa na riwaya kutokea Mwislamu mfuasi wa Madhehebu mengine, basi kwa uzito wa dalili zinginezo na kufanya uchunguzi iwapo huyo Rawi ni mtu aaminiwaye katika historia.
5. Uadilifu wa Rawi pia ni sharti mojawapo, yaani asiwe akifanya madhambi makuu (Kabair Dhamb)[46] na wala asiwe akirudiarudia madhambi madogo madogo (Dhamb-i-Saghirah).
Sheikh Tusi a.r. ametilia mkazo swala hili kwa kuelezea kuwa kuna tofauti katika uadilifu wa Rawi na mtoa ushahidi. Iwapo Rawi ni fasiki na iwapo itathibitika kuwa yeye katika riwaya yake na habari zake ni mkweli bila ya udanganyifu, basi riwaya yake inaweza kufuatwa.
6. Rawi asiwe msahaulivu, bali awe ni mtu mwenye kukumbuka vyema na
udhibiti wake, (yaani haimaanishi kuwa Rawi
asiwe akisahau
Sayyid Ibn Taus
a.r. (amefariki 673 Hijriyyah) na ‘Allamah
Hilli a.r. (amefariki 726 Hijriyyah)
kwa juhudi zao, wao wamefanikiwa kutuletea kanuni nne kuu zijulikanazo usul-i-‘arbi’ah
ambazo ni
Rawi wote lazima wawe waaminifu na Shia Ithna-Asheri na riwaya hizo ziwe zikifika hadi kwa Ma’sumiin a.s.
Riwaya ambazo Rawi wake ni Mashiah na ambapo hapakufanywa uchunguzi wowote juu ya uadilifu wao.
Hadith kama hizo
zinajulikana
Yaani Rawi wote wawe wakiaminiwa lakini miongoni mwao si wote ambao ni Mashiah.
Ni riwaya zile ambazo hazina sifa hata mojawapo za hapo juu.
Tanbih lipo jambo moja la kuzingatia, kuwa Ma’ulamaa wanakubaliana na Hadith zilizo Sahih, Hasan na Muwath-thiq. Ama kuhusu Hadith zilizo dhaif ni kwamba iwapo atayamkinika kuwa Rawi hao si watu wa kutegemewa lakini maelezo na maana yake ni sawa na maana ile ya Ma’sumiin a.s. na katika sura hii, itaweza kukubalika, na wakati Ma’ulamaa wanaozisimulia basi nia yao huwa juu ya Hadith, bali huwa ni kutoa ushahidi tu.
Kwa mujibu wa kanuni hizi nne, mmefahamu kuwa Hadith inapoangukia kuwa dhaifu haimaanishi kuwa ni Hadith ya uongo, yenye mfululizo dhaifu, na kwa dalili zinginezo na kwa nyenzo zinginezo inaweza kuthibitika kuwa Hadith hiyo inaweza kukubalika, Lakini inapokuwa imekosewa kabisa basi huitwa Kidhb (uongo) au Iftira’ (tuhuma). Yaani utaratibu uliotumiwa wa kuwanasibisha Ma’sumiin a.s. haupo wenye ukweli, bali tunaweza kusema kuwa ni tuhuma. Hadith hizo ni uzushi mtupu. Katika historia ya ilimu ya Hadith, utaratibu huu mmoja ni tatizo kubwa mno kuling’amua iwapo Hadith hii ni uzushi au la.
Sayyid Murtadha ‘Alamal Hudaa a.r. anasema:
“Zipo baadhi ya sehemu za Hadith katika Mashia
na Waislamu wote kwa ujumla ambazo zimejazwa makosa na uzushi ambazo
zinatufanya kuzichukulia kuwa ni Hadith za uongo. Katika Hadith hizo kuna mambo fulanifulani
ambazo kwa hakika si rahisi kukubalika kiakili na ni pingamizi mtupu. Kwa mfano imani juu ya jabr (ushurutisho)
yaani mwanadamu ameshurutishwa na Allah swt katika matendo ya madhambi na uasi,
au siku ya Qiyamah Allah swt ataonekana n.k. na hivyo inamaanisha kuwa
kunahitajika uchuguzi na utafiti mkubwa katika kuthibitisha ukweli wa usahihi
wa Hadith
Imam Ali a.s. amesema: “Mtume Muhammad s.a.w.w. alisema
“Enyi watu, kumekithiri mno kuninasibishia mambo ya uzushi, hivyo mutambue kuwa mtu yeyote kwa makusudi ataninasabisha na uongo au uzushi wowote, basi hakuna mahala pale pengine isipokuwa ni Jahannam tu.”
Katika zama hizi ni lazima kufahamu ‘Ilmul Hadith na Rijal yaani kujua habari za wale wenye kuleta riwaya. Kazi hii ni ya wale mabingwa katika fani hii na wala si ya wale wenye ilimu kidogo ambao wamejua Kiajemi na Kiarabu kidogo hivyo wakaanza kuwapotosha watu.
Sasa tuangalie ni kwa sababu gani kumetokezea haja ya kutaka kuzichuja Ahadith na tuwaangalie watu mbalimbali ambao wamefanya juhudi za kuingiza uongo na uzushi na tuhuma katika Ahadith.
(1). Baada ya kifo cha Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kulizuka mgogoro kuhusu ukhalifa ambapo kulitokezea makundi mawili. Kundi moja likidai kuwa Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. alikuwa amekwisha elezea ni nani atakaye kuwa Khalifa baada yake na kundi la pili
likaanza kuzua Hadith kuwa swala
(2). Wakati Uthman alipouawa, basi Ma’uwiya bin abi Sufiyan kwa hila zake alitupa tuhuma za mauaji yalilengwa kwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Hapo kuliibuka Hadith za kuzuliwa katika kuwatukuza Bani Umayyah, umadhulumu wa Uthman na hukumu juu ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. katika mauaji ya Uthman. Si hayo tu, bali Hadith zile zilizokuwa zikielezea fadhila za Imam Ali a.s. pia zilianza kubadilishwa na kupotoshwa. Mfano, ipo ayah ya Qur’an tukufu: ‘wa minanaasi manyashrii nafsahubtighaa mardhatillah’ Aya hii inatoa shuhuda ya tukio lililotokea katika usiku wa Hijrah ambapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alijitolea nafsi yake kwa ajili ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Kwa amri za Mu’awiyah, Hadith hii ikageuzwa kuwa imeteremka kwa ajili ya Ibn Muljim kwa sababu yeye alikuwa ameiweka nafsi yake hatarini katika kumwua Imam Ali a.s.
(3). Makhariji walizua Hadith chungumzima kuhusu akida zao na Waislamu kwa ujumla pia walizizua Hadith nyingi mno katika upinzani wao
(4). Ma’ulamaa wa Kiislamu walianza kuzua na kutumia hizo Ahadith katika kuzieleza na kuziendeleza fikra, nadhiri na akida zao. Mu’tazila, Tasawwuf, Gulat na Ash-Ari na wengineo wote wakaanza kuzua Hadith katika kueneza imani zao. Iwapo utabahatika kukisoma kitabu kiitwacho Ihyaul Ulumiddiin basi ndipo utakapokuja kujua hali halisi ya uovu huu wa kuzua Ahadith za kiuongo dhidi ya Ma’sumiin a.s. ambazo kwa hakika hazikubaliki kuwa zimesemwa nao. Kwa kutoa mfano, tunawaleteeni chache ili muweze kuziangalia:
(a). Ahmad bin Mansur anasema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Baina mikono miwili ya Allah swt kuna maandiko fulani ambamo kuna majina ya wale watu ambao wanaitikadi kuhusu kuwapo kwa uso na kuonekana kwa Allah swt siku ya Qiyama. Na Malaika wanaona fakhari kwa majina hayo!
(b). Mamun bin Ahmad Harwi anamnakili Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akisema:
“Kuna mtu mmoja katika ‘Ummah wangu ambaye ni
hatari hata kuliko Shaytani, na jina
Tanbii: Mwandishi wa Lisanul Mizaan anaandika kuwa sababu kubwa ya kuizua Hadith hii ni kwamba huko Khurasan, wafuasi wa Imam Shafi’I walikuwa wengi.
(c). Ahmad bin Nasr anasema kuwa siku moja alimwota Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika ndoto akimwambia;
“Itakuwa wema kwako kumtii Shafi’i kwani anatokana nami na Allah swt yu radhi naye”
(d). Kwa hakika jambo lakusikitisha mno ni kwamba hawa wataalamu wa kuzua (wazushi) ni watu ambao wameilimika vyema katika masomo ya Qur’an na Hadith. Mafunzo ya Qur’an hayakuwa yenye maana kwao bali wametilia mkazo masilahi na ulafi wa dunia hii.
Ayatullah al-Khui
r.a. anaandika katika kitabu chake Al-Bayan
fi tafsiril Qur’an,
Wakati mtu mmoja alipomwuliza Abu Ismah kuwa amezitoa wapi Hadith chungu mzima kutokea kwa Ikramah na Ibn ‘Abbas kuhusu fadhila za Sura moja moja za Qur’an tukufu ? Alianza kusema: “Mimi niliona kuwa watu wameanza kuipa mgongo hiyo Qur’an na badala yake wanajishughulisha mno na fiqhi ya Abu Hanifa, watu wamejishughulisha kuisoma Maghazi ya Muhammad bin Is-Haq, basi mimi nimezusha Hadith hizo juu ya Qur’an kwa kutaka furaha ya Allah swt ………….!
(e). Wakati kulikuwapo utawala wa Bani ‘Abbas, basi Ma’ulamaa wenye tamaa ya dunia walizizusha Ahadith nyingi mno katika kuelezea fadhila za watawala hao. Katika Tarikhul Khulafa anaandika as-Sayyuti:
“Mtume Muhammad s.a.w.w. amesema kuwa yeye alipoona kuwa Bani Marwan wanachezea Mimbar yangu, basi hapo mimi nilisikitishwa mno. Na hapo baadaye nikaona Bani ‘Abbas pia wanachezea, na kwa hayo mimi nilifurahishwa mno.”
Abu Hurairah ananakiliwa riwaya moja kuwa siku moja Mtume Muhammad s.a.w.w. alitoka nje, na hapo alikutana na Baba mkubwa ‘Abbas, na alimwambia: “Ewe Abul Fadhl ! Je nikupe habari njema ?
‘Abbas alisema:
“Naam, Ewe Mtume
wa Allah swt !” Ndipo Mtume Muhammad s.a.w.w. aliposema: “Allah swt
ameitengeneza swala hili (yaani Dini hii ya Islam) kwangu na kuishia kwa ‘Ummah
wangu.” Na akaendelea kusema: “Wakati kizazi chako kitakapoishi
Tanbihi: Ni jambo la
kushangaza mno kuwa huyu huyu as-Suyuti ameandika kitabu kimoja juu ya masuala
ya uzushi kiitwacho Al-Lulil mansukh
(Lulu bandia) na amewatahadharisha Waislamu kujitahadharisha na Hadith
(f). Baadhi ya makafiri na maadui wa Islamu wamekuwa wakiishi miongoni
mwa Waislamu na kujihusisha katka harakati za kueneza sumu hii miongoni mwa
Waislamu kwa hila na njama mbalimbali.
Wao ili kutaka kutimiza mikakati
(g). Katika kipindi cha mwanzo cha Islam, watu walikuwa na shauku kubwa
ya kusikiliza visa na masimulizi mbalimbali na katika hali hii kuliibuka
wasimulizi wengi wa masimulizi kama hayo na hivyo wao walikuwa wakifanya kila
jitihada za kukusanya habari na porojo za kila aina na walikuwa wakiongezea
chumvi na pilipili ili kwamba mazungumzo yao yalete ladha nzuri na kuwavutia
watu. Matokeo yakawa ni kwamba Mayahudi
walikuwa wamezusha visa na hadithi nyingi kuhusu mitume yao, hivyo mazushi hayo
yakapata soko kubwa miongoni mwa Waislamu, na rundo kubwa hili linajulikana kwa
jina la Israiliyyaat [47] Hadith
zilizozushwa juu ya Mitume a.s. inapatikana katika Tarikhul Ambiya’ na hususan katika tafisiri za Ayah ambazo zinazungumzia habari za Mitume a.s.
Ibn Jawzi anaandika
kuwa Imam Ahmad bin Hambal na Yahya bin Mu’in walikuwa wakisali Msikitini na
wasimuliaji wakaja wakatandika mikeka
Wasimulizi
wakiendelea na masimulizi
Kwa hakika watu walipoyasikia haya walianza kuyumba na kwa kutoa shukurani zao walianza kuwatupia mapesa hao wasimulizi, nao walibakia kimya kwa muda zaidi kidogo ili waendelee kupata zawadi zaidi, na hapo ndipo Yahya bin Mu’in alipojitokeza na kumwita aje mbele yake. Msimulizi alikuja mbio mbio hapo mbele kwa kutarajia kupata zawadi nono, ndipo Yahya alipomwuliza: “Je habari zote hizi zisizo na miguu umeyatoa wapi?” Akajibu: “Nimemsikia Yahya bin Mu’in na Ahmad bin Hambal.”
Yahya na Ahmad bin Hambal walishikwa na bumbuwazi na walibakia wakitazamana, na hapo ndipo Yahya kwa hasira alimgeukia msimulizi na kumwambia: “Je hauoni aibu? Wewe umethubutuje kuzusha uongo dhidi yetu ilhali tukiwa mbele yako ? Jina langu ni Yahya bin Mu’in na huyu ndiye Ahmad bin Hambal.”
Yule msimulizi alianza kusema: “Mimi daima nimekuwa nikisikia kuwa Yahya bin Mu’in ni mtu mpumbavu na mjinga kabisa, na kwa hakika nimepata uthibitisho huo leo hii, kwa hakika ni ajabu kubwa !. Je dunia hii nzima ina Yahya bin Mu’in na Ahmad bin Hambal nyie wawili tu na wala haina wengine? Kwa kusema ukweli mimi nimewanakili riwaya mbalimbali Yahya bin Mu’in sabini na Ahmad bin Hanbal sabini.” Kwa kusema hayo msimulizi alijiondokea zake.
(h). Kulizuliwa Ahadith nyingi
mno katika kutukuza makabila na Miji ya Kiislamu. Tazameni mfano mmoja. Imeripotiwa kuwa al-Imam ar-Ridha a.s.
amesema kuwa Mji mtukufu wa
(i). Katika zama za Makhalifa watu walikuwa wakijishughulisha mno katika kuzusha Hadith za uongo au kuzigeuza maana ili waweze kupata zawadi, hongo au kutukuzwa miongoni mwa watu. Katika zama za Mahdi ‘Abbasi ambaye alikuwa khalifa wa Bani ‘Abbas, aliijiwa na mtu mmoja aitwaye Ghiyas Bin Ibrahim ambaye aliwakuta njiwa wengi mno katika kasri ya khalifa, na kwa hayo alisema: “Ipo riwaya kutokea Mtume Muhammad s.a.w.w. kuwa imeruhusiwa mashindano matatu tu yaani ngamia, farasi na njiwa.”
Kwa hayo, khalifa alimpa zawadi na wakati alipokuwa akiondoka, khalifa alimwambia:
“Mimi nashuhudia kuwa huyu aliyetupa mgongo amemnasibishia Mtume Muhammad s.a.w.w. uongo.”
(1). Habari zilizoelezwa katika Hadith zisiwe zikipingana na Ayah za Qur’an tukufu, yaani zisipingane na maamrisho ya Allah swt. Angalieni kuwa mara nyingi ‘Aam, khaas, mutlaq, muqayyad – kwa kutokujua mambo haya watu wanafikia uamuzi wa kusema kuwa Hadith fulani inakwenda kinyume na Ahadith, kunaleta hatari kubwa ya kupotosha maana sahihi ya Hadith.
(2). Hadith kamwe isiwe kinyume na akili bali iwe kwa mujibu wa akili.
(3). Iwapo Hadith itakuwa
ni salama kwa Dini na Madhehebu,
basi ipokelewe.
(4). Kwa kuitambua Hadith mambo yafuatayo yanatosha:
(a). Ujue lugha ya Kiarabu na kanuni zake kwa ukamilifu,
(b). Zaidi ya hayo inabidi Lisan-i-Suduur yaani kujua maarifa na ubalagha wa lugha ya Ma’sumiin a.s.
(c).Inabidi kuwa mjuzi wa historia ya Kiislamu na sirah za Ma’sumiin a.s.
(d). Ni lazima ajue Madhehebu na mwanzo wao na kuzijua itikadi zao kwa vyema.
(e). Itabidi mtu huyo awe amejiepusha na ta’assub yaani chuki za aina yoyote ile kwani hapo ndipo hapo atakapoweza kushughulikia bila ya upendeleo au ushawishi wa aina yoyote ile.
Faida kuu mojawapo ya kutoa Zaka ni kuongezeka kwa neema na baraka ya mali yetu iwapo itatolewa kwa kuzingatia kanuni na ustaarabu wa kutoa hivyo, na ni kinyume na mawazo na mipango ya ki-Shaytani, kwani mabakhili hufikiria daima kuwa kwa kutoa mali yao kwa ajili ya misaada na Sadaka na Zaka, basi mali yao hupungua na hivyo wanaweza kuwa masikini na kwa hakika hayo ndiyo mawazo na upotofu wa Shaytani.
Amesema Allah swt katika Quran: Surah al –Baqarah, Ayah 28 : “Allah swt huongezea katika Sadaka” yaani huongezea baraka humu duniani na vile vile kutakuwapo na malipo mengine huko Aakhera
Na amesema Allah swt katika Quran: Surah al
–
‘Chochote kile mtakachokitoa (katika njia yake), basi Atawalipeni (humu humu duniani) malipo yake, Naye ni Mbora wa wanao ruzuku.’
Amesema Allah swt katika Quran: Surah al –Rum, 30, Ayah 39 :
‘Na mnachokitoa kwa riba ili kiongezeke katika mali ya watu, basi hakiongezeki mbele ya Allah swt . Lakini mnachokitoa kwa Zaka kwa kutaka radhi ya Allah swt, basi hao ndio watakaozidishiwa.’
Katika Ayah hizo, tumeona kuwa kuongezeka zaidi mno na vile vile Baraka pia itakuwamo, vyote kwa pamoja. Katika kusisitiza hayo, zipo riwayah nyingi mno.
Amesema Bi. Fatimah az-Zahra a.s. bintie
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika hotuba aliyoitoa kuzungumzia Fadak
katika
“Kwa ajili ya kujitakasa na dhambi la Shirk, Allah swt ametufaradhishia kuikamilisha imani yetu ( yaani mtu yeyote anayetaka kujitakasisha na unajisi basi inambidi kuleta imani kwa moyo wake kamilifu), na Sala inamwepusha na magonjwa ya kiburi na kujifakharisha, na Zaka inamwepusha mtu kwa magonjwa ya ubahili ili mwanadamu awe mkarimu na mpenda kutoa kwa ajili ya mema ili atakasike) na hii pia ndiyo sababu kuu katika kujiongezea riziki .”
Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ameripotiwa akisema katika Al-Kafi:
“Yeyote yule anayetumia kutoka mali yake katika njia ya kheri, basi Allah swt anamlipa mema humu duniani na kumwongezea katika malipo yake.”
Vile vile ameripotiwa akisema Al Imam 'Ali
ibn Abi Talib a.s. katika Wasa’il
as-Shiah : Mlango Sadaka, Hadith 19,
J.6,
“Tafuteni riziki yenu kwa kutoa Sadaka.”
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripotiwa katika Kitab ‘Uddatud-Da’i kuwa alimwuliza mtoto wake :”Je nyumbani kuna kiasi gani kwa ajili ya matumizi ?”
Naye alimjibu : “Zipo Dinar arobaini tu.”
Imam a.s. alimwambia “Dinar zote hizo zigawe Sadaka.”
Kwa hayo mtoto wake alimwambia Imam a.s. “Ewe Baba ! Mbali na Dinar hizi arobaini, hatutabakia na akiba yoyote.”
Imam a.s. alimwambia : “Nakuambia kuwa zitoe Dinar zote Sadaka kwani ni Allah swt tu ndiye atakayetuongezea kwa hayo. Je wewe hauelwei kuwa kila kitu kina ufunguo wake ? Na ufunguo wa riziki ni Sadaka ( kutolea mema ).”
Kwa hayo, mtoto wake aliyekuwa akiitwa Muhammad, alizitoa Sadaka Dinar hizo na hazikupita siku kumi, Imam a.s. alitumiwa Dinar elfu nne. Hapo Imam a.s. alimwambia mwanae : “Ewe Mwanangu ! Sisi tulitoa Dinar arobaini tu na Allah swt ametupa Dinar elfu nne badala yake.”
Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Nahjul Balagha kuwa :
“Mtu anapokuwa masikini au mwenye shida basi fanyeni biashara pamoja na Allah swt kwa kutoa Sadaka.”
Al Imam ‘Ali ar Ridha a.s. alimwambia mfanyakazi wake : “Je leo umeshagawa chochote katika njia ya Allah swt .” Mfanyakazi huyo, “La, bado sijagawa.” Kwa kuyasikia hayo Imam a.s. alimjibu, “ Sasa kama haukufanya hivyo, basi Allah swt atatulipa nini badala ya tendo letu ? Hivyo hatutapata baraka wala neema yoyote kutoka kwa Allah swt . Tukitoa chochote ndipo Allah swt atatulipa kwa wingi badala yake.”
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameelezea
Hadith katika Al-kafi, Kitab ad-Du’a,
J. 2, Uk.595 moja kwa kutokea Ayah Fahuwa Yukhlifuhu (yaani chochote kile
kinachotolewa katika njia ya Allah swt , basi hulipa malipo yake kwa haraka
“Je utadhaniaje kuwa Allah swt anakiuka ahadi aliyoitoa ?”
Basi mwandishi akajibu : “La ! Sivyo hivyo.”
Ndipo Imam a.s. alimwuliza : “Sasa je kwanini wewe haupati malipo yako kwa yale unayoyatoa na kugawa ?”
Naye akajibu, “ Kwa hakika mimi sijui sababu zake.”
Imam a.s. alimjibu, “Iwapo miongoni mwenu
yeyote atakayekuwa akiipata riziki yake kwa njia zilizo halali, na
Kuhusiana na swala hili zipo Ayah na riwayah nyingi mno, lakini tunatua hapa. Marehemu Nouri katika kitabu chake Kalimah at-Tayyibah amezungumzia mengi na kwa mapana na undani zaidi kuhusu kutoa Sadaka katika njia ya Allah swt na amedondoa hekaya takriban arobaini ambamo ‘Alim Rabbani Akhwand Mullah Fath ‘Ali amenakili kisa cha jamaa yake ategemewae ambaye amesema,
“Mwaka mmoja ambapo hali ya ughali ilikuwa
imekithiri, nilikuwa na kipande kimoja cha ardhi ambapo nilikuwa nimepanda
Shayiri na ikatokea kuwa shamba langu
Wakulima wadogowadogo wote walipovuna
mazao yao, nami nikavuna kutoka mashamba yangu mengineo na nikawaambia
wafanyakazi wangu waende katika shamba ambalo nilikuwa nimeligawa kuwasaidia
wenye shida wakati huo, wakaangalie
Kwa hakika hao walipokwenda shambani humo walikuta shamba zima limejaa Shayiri kupita kiasi na baada ya kuvuna na kusafisha nilikuta kuwa nimepata mavuno mara dufu kuliko mashamba yangu mengineyo. Ingawaje humo watu wote walikuwa wakivuna kwa ajili ya chakula chao na familia zao, ilitakiwa kuwa tupu kumbe Allah swt amerudishia mavuno tena mara dufu.
Vile vile sisi tulikuwa tukipanda mwaka
mmoja na kuipumzisha ardhi mwaka mmoja, lakini shamba
Mimi kwa hakika nilistaajabishwa mno kuona hayo na nikajiuliza isije hiki kipande cha ardhi kikawa ni kitu kingine na mavuno yanapokuwa tayari, hupata mavuno mengi kabisa kuliko mashamba mengine yangu na ya watu wengineo.
Mbali na hayo, Merehemu amenakiliwa kuwa :
‘Yeye alikuwa na shamba moja la mizabibu
kandoni mwa barabara na kwa mara ya kwanza kulipozaa zabibu katika matawi yake,
alimwammuru mtunza shamba wake kuwa zabibu zote zilizopo kando ya barabara
aziache kwa ajili wapitao njia. Hivyo kila mpita njia alichuma na kula zabibu
zilizokuwa hapo na wengine hata walichukua pamoja nao. Msimu ulipokwa ukiisha
aliwaamuru wafanyakazi wake waende kuangalia
Vile vile imenakiliwa kuwa :
‘Kila msimu alipokuwa akivuna ngano na
kuzisafisha, alikuwa akizileta nyumbani kwake na hapo ndipo alipokuwa akitoa
Zaka yake. Lakini safari moja alipovuna na kusafisha, akiwa akielekea nyumbani
kwake aliwaza kuwa inambidi alipe Zaka haraka iwezekanavyo, kwani si vyema
kuchelewesha ulipaji wa Zaka. Ni ukweli kwamba ngano ipo tayari na mafukaraa na
masikini pia wapo. Hivyo aliwajulisha mara moja mafukaraa na masikini waje
kuchukua ngano, na hivyo akapiga mahisabu yake na kuwagawia sehemu
Katika kitabu kilichotajwa, Alhaj Mahdi Sultan Abadi amenakili kuwa :
‘Mwaka mmoja mimi nilipovuna mavuno,
nilipima uzito wa ngano na nikatoa na kuigawa Zaka yake. Na nafaka hizo
zilibakia mahala hapo hapo kwa muda wa mwezi mmoja ambapo wanyama pamoja na
mapanya walikuwa wakila humo. Na nilipokuja kurudia kupima uzito wake nikakuta
kuwa uzito wa ngano ulikuwa vile vile
Wanaostahiki malipo ni mke ( wa ndoa ya kudumu ) mtiifu na watoto wake na watoto wa watoto wake na vile inavyoendelea kuteremka chini na ambao wanahitaji msaada, basi ni faradhi. Vile vile baba na mama na babu mzaa baba na mama mzaa mama na vile itakavyoendelea juu na iwapo wanahitaji msaada wake na watu wengineo basi na kwa kiasi cha uwezo wake kama anao na iwapo hatawapa basi atatazamwa miongoni mwa watu kama qata’ rahmi . Na jambo hili limezungumziwa katika makala mengine.
Zipo aina nyingi za malipo yaliyo Sunnah.
Katika Ayah na riwayah nyingi mno
kumesisitizwa mno kuwa Sadaka itolewe
hususan katika siku ya Ijumaa, Siku ya ‘Arafah, katika mwezi Mtukufu wa
Ramadhani itolewe kwa makhususi ya majirani, majamaa n.k. Vile vile Sadaka ni dawa ya ugonjwa, huondoa
balaa, huleta riziki, huzidisha mali na huepusha vifo vya kutisha kama kuungua
moto, kuzama maji na kuwazuia Majinni na kwamba huondoa balaa sabini.
Kila utakavyotoa Sadaka zaidi basi
matokeo yake pia yatakuwa ni mazuri zaidi. Wala haina kiwango kidogo, kiasi
chochote mtu atakachokitoa kitatosha walau hata
Ni kitu ambacho mtu mmoja anampa mtu mwingine kwa ajili ya kuongezea urafiki ama awe masikini au tajiri. Na iwapo hivyo itakuwa kwa nia ya kutaka furaha ya Allah swt, basi itakuwa ni ‘ibada bora kabisa.
Imeripotiwa kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi
Talib a.s. katika Al-Kafi J.5,
“Iwapo mimi nitapenda kumpatia kitu rafiki yangu basi mimi nitampa zawadi kwani ninaipenda zaidi kuliko Sadaka.”
Zipo riwayah nyingi mno kuhusu kuwakarimu wageni na kamba hiyo ndiyo tabia njema ya Mitume a.s. Ipo riwayah moja kuwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kwa muda wa siku saba hakupata mgeni nyumbani kwake basi alisema huku akilia :
“Nasikitika mno na ninakhofu kuwa isije Allah swt akaniondolea rehema na baraka zake.”
Inatubidi sisi tuwe tumepanga viwango
maalumu vya kila siku au kila wiki au kila mwezi katika
Amesema Allah swt katika Quran: Surah al- Ma’arij, 70 , Ayah 24 – 25 :
Na ambao katika
Na mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba…
Al Imam Musa bin Ja’afer a.s. amepokelewa riwayah kuwa :
“Katika ukoo wa Bani Israil kulikuwa na mtu mwema ambaye alikuwa na mke aliye mwema pia. Siku moja aliota ndoto ambamo aliambiwa kuwa Allah swt amempangia kiasi fulani cha umri wake ambapo nusu ya umri huo utapita katika raha na mustarehe wakati nusu ya umri uliobakia utapita katika shida na dhiki na umasikini.
Hivyo Allah swt amekupa fursa wewe kuchagua iwapo utapenda kupitisha umri wako wa nusu ya awali ya raha na mustarehe na baadaye dhiki na umasikini ? Hivyo chagua mojawapo. Kwa hayo mtu huyo alijibu kuwa : ‘Mimi ninaye mke wangu aliye mwema na hushirikiana naye katika maswala yote, hivyo nitapenda kupewa muda wa kuweza kuongea naye kabla sijatoa uamuzi wa chaguo langu.’
Mke wake alimshauri mumewe kuukubalia umri ule wenye neema uwe ndio wa kuanzia kwani: ‘Inawezekana Allah swt anataka kututeremshia neema na baraka zake hivyo tukaongoka.’
Hivyo usiku uliofuatia, bwana huyo aliulizwa jibu alilolifikia katika uamuzi wake. Naye akajibu : ‘Mimi ninataka kuupitisha nusu ya umri wangu katika neema, raha na mustarehe.’ Kwa hayo akajibiwa kuwa hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa mujibu wa chaguo lake.
Kuanzia hapo yeye alijaaliwa kila aina ya raha
na akawa tajiri mkubwa mwenye
Katika kutajirika huku, mke wake akamwambia, ‘Ewe Bwanangu! Usiwasahau kuwasaidia na kukidhi haja za majamaa zetu na mafukara na masikini na uwe na uhusiano mwema pamoja nao. Na uwazawadie watu fulani fulani wakiwemo majirani na marafiki, zawadi mbalimbali.’
Mtu huyo alizingatia na kutekeleza ushauri
uliokuwa umetolewa na mke wake. Na hivyo alifungua milango ya kugawa
Kuisha huku kwa nusu ya kwanza ya umri
wake, aliota ndoto tena ambamo aliambiwa kuwa : ‘Kwa kutokana na uwema wako wa
kuwasaidia wenye shida na dhiki imekuwa kipaumbele kwako, basi Allah swt
amekubadilishia sehemu hii ya pili kuwa katika raha na mustarehe
Wakati wa mavuno kwa kiwango kile ambacho
bado Zaka haijapigiwa hisabu, inagawiwa kwa kuchota mkono moja kwa wapita njia
Na Yeye ndiye aliye ziumba bustani zenye kutambaa juu ya chanja, na zisiyo tambaa, na mitende, na mimea yenye matunda mbali mbali, na mizaituni na mikomamanga inayo fanana. Kileni matunda yake inapo zaa, na toeni haki yake siku ya kuvunwa kwake. Wala msitumie kwa fujo. Hakika Yeye hawapendi watumiayo kwa fujo.
Katika aina za Sadaka, aina hizi mbili za Sadaka ni Sunnah kwani Ayah ya Qur'an Tukufu pamoja na riwayah nyingi zimezungumzia na kusisitiza na ndio maana zimezungumziwa mbalimbali.
Yaani kuwakopa Waislamu ambao wanashida ya
kukopa deni ili kukidhi masuala
“Katika mlango wa Jannat kumeandikwa ‘Yapo mema kumi kwa mtoa Sadaka na mema kumi na nane kwa mkopeshaji madeni.’”
Vile vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, katika Al-Wafi :
“Wakati Mumin mmoja anapomkopesha Mumin
mwenzake deni kwa ajili ya kutaka ridhaa ya Allah swt , basi Allah swt anamhisabia
deni
Kila mara mtu atakapokuwa akimpa muhula mdaiwa wake kulipa deni lake, basi Allah swt atakuwa akimwandikia kuwa ametoa Sadaka kiasi hicho kwani yeye alikuwa na haki kamili ya kufanya na kulazimisha malipo lakini hakutumia nguvu kudai na badala yake amemwongezea muda mdaiwa wake, hivyo inamaanisha kuwa amemkopa mara mbili katika mali hiyo. Hivyo mtu huyo anakuwa mustahiki wa kupata thawabu za kutoa Sadaka kwa mara ya pili.
Vile vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripotiwa akisema kuwa :
“Kwa kupuuzia ‘Ma’un’ (mambo ya nyumbani ) ambayo Allah swt ameahidi katika Qur'an Tukufu adhabu, basi si Zaka inayozungumziwa, bali ni kuwasaidia kwa kuwakopa wale wenye shida na wenye shida wanapokuja kuazima vitu vya nyumbani, basi inabidi kuwa azima vitu vya nyumbani.”
Abu Basir amemwambia Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa
“Majirani zetu wanapokuja kuazima vyombo au vitu vingine vya nyumbani, na tunapo waazima basi huvunja vunja na kuviharibu vitu vyetu na hivyo sisi tunalazimika kuwakatalia kwa misingi hiyo, sasa je kuwakatalia huku ni dhambi ?”
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimjibu :
“Iwapo watu hao wanatabia kama hiyo, basi si dhambi kuwanyima.”
Kuwakopa Waislamu ambao wanashida ya kukopa
deni ili kukidhi masuala
“Katika mlango wa Jannat kumeandikwa ‘Yapo mema kumi kwa mtoa Sadaka na mema kumi na nane kwa mkopeshaji madeni.’”
Inabidi kuwapa muda au kuwasamehe madeni wale ambao hawana uwezo wa kuyalipa madeni hayo. Na kuhusiana na swala hili Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema :
“Iwapo mtu anataka asidhalilishwe Siku
ambayo hakuna mwingine wa kuwaokoa isipokuwa Allah swt , basi inambidi awape
muda wa kulipa madeni wadaiwa wake au kuwasamehe madeni
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema :
“Yeyote yule atakayempa muda wa kulipa madeni ambaye hana uwezo wa kulipa ( basi kwa ajili yake ) thawabu zake mbele ya Allah swt ni sawa na thawabu za kutoa Sadaka kila siku kwa kiasi hicho hadi atakapolipwa.”
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliambiwa kuwa :
“’Abdur Rahmaan bin Sababah anamdai deni marehemu mmoja, nasi twamwambia yeye kuwa amsamehe lakini yeye anakataa kata kata kumsamehe deni lake.”
Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akasema :
“Ole wake, je haelewi kuwa iwapo
atamsamehe marehemu deni
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema, Al-Kafi, J.2,
“Mtu yeyote atakayemsaidia Mumin kwa mavazi wakati wa baridi au joto basi Allah swt atamjaalia mavazi ya Jannat (Peponi au Paradiso ) na atampunguzia shida kali wakati wa kutoa roho yake (wakati anapokufa ) na atampanulia kaburi lake na Siku ya Qiyamah atakapotoka nje ya kaburi lake atakuwa akitoka katika hali ya furaha kwa kuonana na Malaika.”
Vile vile Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema, Al-kafi, J.2, Uk.205 :
“Iwapo Mwislamu yeyote atamsaidia mtu
asiye na mavazi kwa mavazi au aliye na dhiki ya mali, akasaidiwa ( nyumba,
Kutumia mali kwa ajili ya mema ya kudumu na kwa faida ya watu, kwa mfano kujenga Misikiti au Madrassah, daraja, barabara, kupanda miti, vyoo, kuchimba mito, visima vya maji au kuchapisha vitabu vya dini n.k. ambavyo daima huwafaidisha watu kwa muda mrefu na hivyo mwenye kujitolea kufanya vitu hivi pia huendelea kupata thawabu zake milele.
Merehemu Haji Nouri (r.a.) katika Dar-us-Salaam anamnakili Sheikh mkongwe na ‘A’alam Rabbani Sheikh ‘Abdul Hussein Tehrani ( r.a. ) kuwa :
“Mirza Nabi Khan ambaye alikuwa ni mtu makhsusi katika zama za Muhammad Shah Qajar, hadi alipofariki alikuwa mashuhuri katika kutenda maovu.
Usiku mmoja mimi niliota kuwa nipo ninatembelea Bustani mojawapo na kuangalia majumba ya Jannat ( Peponi au Paradiso ) na ninaye mtu mmoja ambaye ananiongoza na kunionesha na kunielezea habari mbalimbali. Basi tulifika mahala ambapo mtu huyo aliniambia kuwa hapa kuna maskani ya Mirza Nabi Khan na iwapo utapenda kumtembelea, basi yeye yupo ameketi hapo, mtu huyo alikuwa akinitolea ishara pa mahala hapo.
Mimi nilipoangalia kwa makini nikaona kuwa ameketi peke yake na aliponiona akanifanyia ishara kuwa nipande juu na nilipomfikia na kumkaribia, aliinuka na kunisalimia na kunikaribisha na kunikalisha sebuleni naye aliketi vile alivyokuwa akiketi humu duniani kwa tabia zake zile zile. Mimi kwa hakika nilikuwa nimeshikwa na bumbuwazi kwa hali aliyokuwa nayo.
Yeye aliweza kung’amua yale niliyokuwa nikiyawazia, na hivyo akaanza kuniambia kuwa, ‘Ewe Sheikh ! Bila shaka umeshtushwa na kustaajabishwa kwa kuniona katika hali hii hapa Jannat (Peponi) kwani matendo yangu yalikuwa maovu na yaliyokuwa yakistahili adhabu wakati bado nikiwa duniani, kwa hakika hivyo ndivyo ilivyokuwa hapo awali huko katika mji wa Taliqan, nilikuwa na machimbo ya chumvi ambapo kodi yake nilikuwa nikiituma Najaf kila mwaka kwa ajili ya kuomboleza kifo cha Al-Imam Hussein ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s. pamoja na wanayumba ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Na kwa hakika Allah swt alipendezewa na tendo langu hili na kwa malipo yake amenipatia maskani pamoja bustani hizi.’
Sheikh Marehemu Haji Nouri anasema kuwa, ‘Mimi niliamka na kutoka katika ndoto hiyo ya kushangaza na kustaajabisha. Na ndoto yangu hiyo niliielezea kwa wanafunzi wangu darasani. Katika darasa hilo kulikuwapo na mwanafunzi mtoto wa Mullah Muti’i Taliqani, ambaye alithibitisha kuwa hayo yalikuwa maneno ya kweli kuwa huyo alikuwa na machimbo ya chumvi huko Taliqan na kodi yake ipatayo kiasi cha Tuman mia moja ( Sarafu ya jamhuri ya Kiislamu ya Iran ) na kiasi hicho alikuwa akikituma Najaf na mzazi wangu ndiye aliyekuwa akiichukua pesa hizo kwa ajili ya kuandaa maombolezo hayo ya kila mwaka ya Al-Imam Hussein ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s.
Marehemu Sheikh aliyekuwa mwalimu alikuwa hajui iwapo huyo alikuwa akihusiana na Taliqan na akifanyisha maombolezi kila mwaka huko Najaf.’
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema , katika Al-Wafi, al-Kafi na kunakiliwa pia katika Tahdhiib :
“Baada ya kufariki kwa mtu, huongoka kwa mambo matatu
Sadaka ambayo aliitoa humu duniani na
ambayo inaendelea baada yake,Sunnah ambayo aliitekeleza kwa mfano Adhan ambayo
baada ya kifo chake ingali ikiendelea, Kuacha mtoto mwenye tabia na mienendo
mizuri ambaye atakuwa akimwombea dua na usamehevu kwa ajili yake ( na akifanya
mema kwa niaba ya baba yake,
Hapa nitapenda kuzungumzia machache kuhusu Sadaka
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa :
“Sadaka inalipia madeni na inaongezea katika barakah.”
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa :
“ Sadaka inamwepusha mtu na ajali mbaya.”
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa:
“Mtu yeyote yule aliye mja wa Allah swt akiwa Mumin akatoa Sadaka, basi Allah swt baada ya kifo chake huyo mtu huwaweka vyema na kuwasaidia wananyumba yake katika hali njema.”
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akaendelea kusema :
“Faida ya kutoa Sadaka ni kwamba inamsaidia kulipia madeni na viile vile kuongezea katika baraka.”
4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.
“Kusaidia na kutoa sadaka vyote hivyo vinaondoa umasikini na hurefusha umri wa mtu. Na yule anayetoa huweza kuepukana na aina sabini za ajali mbaya.
5. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika kuelezea
tafsiri ya aya, ya Qur'an Tukufu, Sura Al-Layl,
92 , Ayah ya 5 na 6 :
Ama mwenye kutoa na akamcha Mungu,
Na akaliwafiki lilio jema.
ndipo amesema kuwa;
Allah swt ndivyo anavyo walipa wale
watendao mema, kwa mema
Na vile vile amesema kuwa: anayetoa katika njia ya Allah swt basi Allah swt humjaalia kila aina ya tawfiqi katika kazi hiyo ya khairi.”
6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amemnakili Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa
“Mtu yeyote yule ambaye anamwamimi Allah swt kuwa atamlipa na atamwongezea zaidi ya kile anacho kitoa basi huyo mtu kwa moyo mkunjufu na bila aina ya ubakhili wowote atatoa sadaka na misaada kwa wingi kabisa.”
7. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amemnakili Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa
“Siku ya Qiyama ardhi itakuwa imepata moto kupita kiasi na mumin watakuwa katika kivuli na kivuli hicho itakuwa ni kile alicho kuwa akitoa Sadaka.”
8. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akisema kuwa:
“Enyi watu! Toeni sadaka bila shaka sadaka inaongezea katika mali yenu, na hivyo mtoe sadaka na Allah swt atawarehemu.”
9. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripotiwa katika Kitab ‘Uddatud-Da’i kuwa alimwuliza mtoto wake :
“Je nyumbani kuna kiasi gani kwa ajili ya matumizi ?”
Naye alimjibu : “Zipo Dinar arobaini tu.”
Imam a.s. alimwambia “Dinar zote hizo zigawe Sadaka.”
Kwa hayo mtoto wake alimwambia Imam a.s.
“Ewe Baba ! Mbali na Dinar hizi arobaini, hatutabakia na akiba yoyote.”
Imam a.s. alimwambia :
“Nakuambia kuwa zitoe Dinar zote Sadaka kwani ni Allah swt tu ndiye atakayetuongezea kwa hayo. Je wewe hauelwei kuwa kila kitu kina ufunguo wake ? Na ufunguo wa riziki ni Sadaka ( kutolea mema ).”
Kwa hayo, mtoto wake aliyekuwa akiitwa Muhammad, alizitoa Sadaka Dinar hizo na hazikupita siku kumi, Imam a.s. alitumiwa Dinar elfu nne. Hapo Imam a.s. alimwambia mwanae :
“Ewe Mwanangu ! Sisi tulitoa Dinar arobaini tu na Allah swt ametupa Dinar elfu nne badala yake.”
10. Al Imam Musa al-Kadhim a.s. amesema kuwa:
“ Toeni sadaka mjipatie riziki.”
11. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“ Toeni sadaka mjiongezee riziki yenu.
Bila shaka anayeamini kuwa Allah swt hulipa mambo yote. Basi yeye huwapa sadaka
masikini kwa kupita kiasi. Allah swt humjaalia riziki kwa njia mbalimbali
kwa kile huyu mtu akitoacho katika
12. Al Imam Muhammad al-Baquir
a.s. amesema kuwa Al Imam ‘Ali ibn
Abi Talib a.s. siku moja alitoa Dinar
moja
“Ya Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.! Je unaelewa kuwa pale mtu anapotoa Sadaka kwa mkono wake mwenyewe basi hujiepusha na mitego ya mashetani sabini, na kila shetani husema, ‘Ewe fulani, usitoe sadaka kamwe.’”
Akaendelea kusema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.
Ya Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.! Kile utoacho Sadaka kabla hakijaingia katika mkono wa yule anayeomba, kwanza hupitia katika mkono wa Allah swt.
Na baada ya hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alisoma aya hii ifuatayo ambayo iko katika Qur'an, Surah Tawbah,9, Ayah 104.
Je hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali sadaqah , na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu?
13. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akisema kuwa :
“Kuwa na akida ya Tawhid ni nusu ya sehemu ya dini, enyi watu! Toeni Sadaka ili mpate riziki zaidi”.
14. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. ametoa riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa :
“Kuwa
15. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:
“Toeni Sadaka asubuhi na mapema ili balaa zisiwafikieni katika siku nzima.”
16. Al Imam Ja'afer as-Sadiq
a.s. amenakili riwayah kutoka Al
Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa:
“Sadaka ni kinga dhidi ya moto wa Jahannam .”
17. Al Imam Ja'afer as-Sadiq
a.s. amesema kuwa Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema:
“ Enyi watu muwatibu wagonjwa wenu kwa kutoa Sadaka.”
18. Al Imam 'Ali ibn Abi
Talib a.s. katika Nahjul Balagha amesema
kuwa:
“Mnapoona riziki yenu inapungua na kuwa finyo basi muwe mkitoa sadaka ndivyo mtakuwa mkifanya biashara na Allah swt.”
19. Al Imam Ja'afer as-Sadiq
a.s. amesema kuwa:
“ Imani ya muumini inakuwa na sifa nne za lazima,
1. Awe na tabia njema,
2. Awe mkarimu na mwepesi wa kutoa
3. Asizungumze zaidi ya yale yanayo takikana (hazungumzi mambo ovyo ovyo)
4. Hutumia kile kiasi kinacho takiwa ,siyo mfujaji ( anaotoa katika njia ya Allah swt ).
1. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa:
“Iwapo mimi nitakwenda Hijja moja basi
afadhali niwafanye huru watumwa kumi, lakini iwapo mimi nitajichukulia jukumu
la kuwalisha familia ya Waislamu ambao wanashida ya chakula na ambao wanaishi
kwa njaa nikawamalizia shida zao, nikawavalisha nguo wale ambao hawana nguo, na
nikawarudishia heshima
2. Al Imam Musa al-Kadhim a.s. aliijiwa na mtu mmoja na aliyeuliza,
“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Mimi ninazo pesa na utajiri je ni jambo gani afadhali nitoe sadaka au nimnunue mtumwa na kumfanya huru?”
Kwa hayo Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alimjibu kuwa:
“Kuwa
mimi ninaonelea kuwa kutoa Sadaka ni afadhali zaidi.”
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Siku
moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza Maimuna binti Harun, Je
Kijakazi wako amekuwaje? Akasema Maimuna kwa hayo alimjibu Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w., ‘Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Mimi nimemfanya huru.’
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwambia “Iwapo
kama wewe ungelichukua jukumu la kumlisha, kumtunza, kumsaidia na kumwonea
huruma basi ingekuwa afadhali zaidi.”
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Muwatibu wagonjwa wenu kwa Sadaka, na muzuie maafa kwa kuomba dua na kutoa sadaka muongezee riziki zenu zipanuke, na kwamba Sadaka inawaepusheni na mitego ya mashetani sabini.”
2. Siku moja walikuja wagonjwa
wakilalamikia magonjwa
“Nendeni mtoe Sadaka kwa ajili ya magonjwa yenu na mtapona, iwapo mtu atatoa Sadaka kwa kile akitumiacho kwa siku dharura wake, basi Allah swt huahirisha hata kifo chake na vile vile humwepusha na ajali mbaya.”
1. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. aliulizwa na Sahaba mmoja :
“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Mimi watoto wangu wawili wamefariki na amebakia mtoto wangu mdogo.”
Kwa hayo Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. kamwambia:
“Basi toa Sadaka kwa niaba ya mtoto wako huyo.”
Na siku moja Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. alipomtembelea huyo mtu akamwambia,
“Mwambie mtoto wako huyo atoe Sadaka kwa
mkono wake walau kiasi kidogo chochote kile au hata
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona !
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona !
Vile viel Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. alimwelezea kuwa:
“Allah
swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah Al-Balad,90,
Ayah11 - 16
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani ?
Kumkomboa mtumwa;
Au kumlisha siku ya njaa
Yatima aliye jamaa,
Au masikini aliye vumbini
“Hivyo
ewe Sahabi uelewe kuwa Allah swt
anaelewa wazi wazi kuwa si watu wote wenye uwezo wa kuwanunua na wenye kufanya
huru watumwa hivyo yeye ameweka thawabu hizo hizo kwa wale watakao toa Sadaka au
watakao walisha yatima na masikini.”
2. Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alijiwa mtu mmoja mbele yake na kuelezea habari za mtoto wake, na kwa hayo Al Imam akamjibu :
“ Toa
Sadaka kwa niaba yake.”
Na
mtu huyo akajibu kuwa
“Sasa mtoto wake amekuwa na umri yaani amekuwa kijana.”
Basi Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alimwambia kuwa
“Mtoto wako atoe Sadaka kwa mkono wake, hata kama itakuwa ni kipande cha mkate, na hapo ndipo Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alisema riwayah ya Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. kuwa:
“Katika Israil alikuwa mtu mmoja aliyekuwa akimpenda mno mtoto wake, na akaona katika ndoto yake anaanmbiwa kuwa, mtoto wako huyo umpendaye mno atakufa usiku wa ndoa yake. Kulipowadia usiku wa arusi baba mzazi wa mtoto huyo, usiku kucha akawa katika wasiwasi na hakupata usingizi na kamwe hakupata raha usiku huo.
Na kulipo pambazuka asubuhi na mtoto alipotoka chumbani mwake akiwa hai basi baba yeke alimwuliza
‘Ewe mwanangu! Je katika usiku huu wako wa kuamukia leo umefanya mema yoyote?’
Kwa hayo mtoto akajibu
“Ewe baba yangu! hakuna jambo la maana sana lililotendeka, bali alitokezea masikini mmoja akaja mlangoni kuomba chakula, alikuwa na njaa na kile chakula walichokuwa wameniwekea, mimi nikampa chakula chote huyo mtu aliyekuja kuomba.’
Kwa hayo baba yake akasema
“Kwa sababu hii tu ndiyo Allah swt amekuondoshea balaa kubwa iliyokuwa ikupate wewe usiku huo.”
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa:
“Kwa kutoa Sadaka kwa mkono wako mwenyewe basi unajiepusha na ajali mbaya, unajiepusha na balaa na maafa sabini na mitego ya mashetani sabini na ambamo kila shetani yuko anakwambia ‘ewe fulani! Usitoe Sadaka kamwe.”
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Mgonjwa atoe Sadaka kwa mkono wake mwenyewe na anayempa amwambie amwombee dua”.
3. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika hadith zake amesema kuwa:
“Mkono uliye juu yaani mtoaji ni afahali kuliko mkono ule ulio chini yake, yaani mpokeaji.”
4. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:
“Kuna aina tatu ya mikono wa
· kwanza ni mkono ule wa Allah swt ambao uko juu kabisa na kwa hakika neema zote ni za Allah swt,
· mkono wa pili ni ule mkono wa yule mtu anaye toa, ambaye anatoa katika njia ya Allah swt na
· mkono wa tatu ni wa yule anaye pokea ambao mkono uliochini wa yule anayetoa. Kwa hivyo enyi watu chochote kile kinachobakia miongoni mwenu mtoe katika njia ya Allah swt na musikalifishe nafisi zenu”.
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa amemfanyia usia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.; Ewe Ali! Ninakufanyia usia wa mambo mema machache na uyakumbuke vyema.
Ewe Allah swt umsaidie Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Baada ya hapo wakati akifanya usia, Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alisema: Ama kuhusiana na sadaka tafadhali usiwe na mnunguniko wowote. Utoe kiasi kwamba mpaka uhisi kwamba wewe umefuja mali yako, lakini utambue wazi kuwa hiyo sio ufujaji bali hiyo umetoa katika njia ya Allah swt.”
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa kuna riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa
“Toeni Sadaka, angalau hata kwa sa’ ya tende, na kama sa’ moja hiyo hamnayo basi mtoe tende kwa kiganja kimoja na hata kama hivyo haitawezekana basi mtoe tende kiasi chochote kile na kama hivyo haitawezekana basi mtoe angalau kokwa moja ya tende, na kama hivyo pia haitawezekana basi yule masikini aliyekuja kuwaomba mumwambie maneno mazuri na matamu na maneno matakatifu katika kumwelezea kuwa hakuna chochote, na hayo pia ni sadaka.
Kwa sababu isitokee Siku ya Qiyama kwamba Allah swt atakapo kuuliza hesabu ya neema alizokujaalia akakuambia
‘Ewe mja! Mimi nilikupa mambo chungu
nzima, sasa hebu angalia nafsini mwako je kwa kutumia neema hizo wewe
umejiandalia nini?’
Na hapo wewe
utaangalia sehemu zote nne za dunia na utajawa na masikitiko, na utakuta hakuna
jambo lolote lile litakalo kuokoa dhidi ya adhabu za Allah swt.”
2. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa:
“Mtoe tende kiasi fulani kwani itawaokoa na moto wa Jahannam , mpanue riziki zenu na mteremshiwe riziki nyingi kwa kutoa Sadaka na kupitia dua mziondoe balaa na shida zenu.”
Mkumbuke kuwa kwa kutoa Sadaka hamtapungukiwa
katika
3. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa:
“Kulikuwa na mja mmoja aliyekuwa akifanya ibada ya Allah swt kwa umri wake wa miaka themanini.
Siku moja alimwona mwanamuke mmoja mzuri aliyekuwa akipendeza naye akawa ameingia katika mtego wake. Yeye alitimiza matamanio yake visivyo halali na mara akatokezea Malakul mauti (malaika anayetoa roho). Ulimi wake ulifunga kuongea na jasho lilianza kumtoka na kutokwa kwa roho na mara hapo alipita masikini akiomba.
Basi mtu huyu ambaye alikuwa katika hali ya kukata roho alimwambia yule masikini kwa ishara kuwa mahala fulani kuna mkate hivyo auchukue hivyo aweze kula huyo masikini, na masikini huyo alivyoelekezwa akauchukua mkate akaondoka zake.
Kwa hiyo ikatokea kwamba Allah swt aliibatilisha ibada zake za miaka themanini kwa sababu ya kuzini na ikatokea kwamba Allah swt akamsamehe madhambi yake yote kwa sababu ya kutoa Sadaka kwa moyo mkunjufu.”
4. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amesema kuwa;
“ Katika zama za Bani Israil kuliwahi kutokea baa la njaa ambao uliendelea kwa muda wa miaka mingi.
Katika wakati huo ikatokezea kwamba bibi kizee mmoja akiwa amekabwa na njaa hali ya juu alikuwa ameketi akiwa na kipande kidogo cha mkate huku akitaka kukila kipande hicho, mara akasikia mlangoni sauti ikisema ya masikini aliyekuwa amekuja kuomba:
‘Ewe mja wa Allah swt! Mimi nakufa kwa njaa naomba unisaidie, bibi kizee huyo akajiambia kwa hakika Sadaka ndiyo wakati huu muafaka wa kutoa, na kile alichokuwa akila akakitoa haraka akampa huyo aliyekuwa akiomba.
Bibi kizee huyo alikuwa na mtoto mmoja aliyekuwa amekwenda porini na ghafla kule alishambuliwa na mnyama. Kwa kusikia sauti ya mtoto wake huyo bibi kizee ikimwita, alikimbia kumfukuza mnyama huyo na kwa muujiza wa Allah swt ni kwamba, Allah swt alimtuma Malaika Jibrail a.s kwenda kumwokoa mtoto huyo katika mdomo na mabano ya mnyama wa huyo muuwaji, na Malaika Jibraili a.s. akamwambia ‘Ewe bibi kizee ! Je umefurahi sasa? Kwa kile ulichokitoa sadaka basi Allah swt naye amekulipa mema yake.”
5. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:
“ Mfanye mema katika hali ya shida na ufakiri, na wema huo ni Sadaka.
Toeni Sadaka kama itakuwa ni kiasi gani kwa udogo wake. Mnaweza kutoa kiasi cha tende mkajiokoa na Jahannam. Kwa hakika udogo huo siyo hoja na Allah swt ataulea udogo huo kama kwamba nyie mnavyo walea watoto wadogo wanaonyonya maziwa, na siku ya Qiyama wakati mema yenu hayo ( mliyokuwa mkisema ni madogo) yatakapoletwa mbele yenu mtaona kuwa ni sawasawa na ukubwa wa milima mikubwa sana.”
6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameseama kuwa Allah swt anasema kuwa :
“Hakuna kitu kingine mbali na Sadaka
ambacho mtu anaweza kumpatia mtu mwingine kidhahiri, na kwa hakika mimi ndiye
wakili wake musitahiki, na mimi ninayepokea kwa mikono Sadaka hiyo halafu hata
ikiwa kama ni tende kidogo haidhuru mimi ndiye ninaitunza,
Siku ya Qiyama huyo mtoa Sadaka atastaajabishwa
mno kwa Sadaka zake ndogo alizokuwa akitoa zimekuwa kubwa kama milima ya Uhud,
milima mikubwa
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa:
“Toeni Sadaka asubuhi na mapema kwa sababu kunaondoa balaa kwa siku nzima.”
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Kwa kutoa Sadaka asubuhi na mapema basi mtoa Sadaka huepukana na kila aina ya matatizo na mabaya yote kwa siku nzima.”
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Toeni Sadaka asubuhi, na kwa mapenzi kabisa, mwenyewe kutoa Sadaka amebahatika. Basi humwomba Allah swt amani kutokana na balaa zote zilizoko ardhini na mbinguni, na kwa hakika Allah swt humjaalia hivyo kwa sababu ya kutoa Sadaka.”
4. Al
Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anaelezea kuwa Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwusia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa:
“Ewe Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.! Sadaka huondoa balaa ambazo lazima zitatokezea, na kwa kutenda mema pamoja na ndugu na majamaa kunarefusha umri.
Ya Ali! Iwapo jamaa na ndugu ni watu wenye shida, basi kuwapa Sadaka hao haitakuwa ni Sadaka.
Ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.! Kusema maneno bila vitendo ni ya bure hayana maana, na Sadaka bila kuwa na nia nayo haiwi Sadaka.”
5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa: Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza mtu mmoja
“Je leo umefunga Saumu?”
Mtu huyo alijibu
“La hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.”
Tena Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza:
“Je leo umeshawahi kumtembelea aliye mgonjwa?”
Naye akajibu:
“Hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.”
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliendelea kumwuliza naye aliendelea kumjibu hapana hakufanya hivyo.
Mwishoni Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.aliendelea kumwuliza:
“Je umemlisha masikini yeyote?”
Naye akajibu: “Hapana Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.!”
Na hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipomwambia huyo mtu :
“Nenda kwa wananyumba wako, nenda ukawatendee na uwe nao kwa mema na uwawie wema, basi hayo ndiyo yatakuwa Sadaka yako kwao.”
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambaye ameseama:
“kwa baraka za Sadaka Allah swt humwondolea mwenye kutoa Sadaka balaa sabini, ambamo kuna magonjwa, madhara yatokanayo na moto, kuzama maji, kufunikwa na majumba mpaka kufa na atamwepusha ili asiwehuke au asiwe mwehu.”
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa:
“
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anaelezea kuwa: Siku moja Myaudi mmoja likuwa akienda kukata miti porini na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwangalia na kuwaambia Ma-Sahaba wake :
“Myahudi
huyu leo ataumwa na nyoka na kifo chake kitasababishwa na sumu ya nyoka.
Myahudi huyo
Na tena Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.
alipomwona Myahudi huyo akamwambia ateremshe mzigo wa kuni huo na auweke chini.
Na Myahudi akafanya hivyo alivyoambiwa, na katika mzigo huo wa kuni wakaona
kuna nyoka mweusi mwenye sumu kali
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza Myahudi yule,’Je wewe leo umefanya jambo gani?’
Myaudi huyo akasema: Mimi nimekata kuni na kuzifunga tu, lakini wakati nilivyokuwa nikirudi nilibakiwa na vipande viwili vya mkate na kipande kimoja mimi nikala na kipande kimoja nikampa masikini Sadaka.
Hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema kwa kiapo cha Allah swt ni kwa sababu ya Sadaka ndiko balaa hii imekuondokea, kwa hakika Sadaka humwepusha mtu na ajali mbaya.”
4. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. siku moja alikuwa pamoja na Ma-sahaba wake katika Masjid Nabawi, na upande mmoja wa ukuta ukaanguka chini. Kulikuwa na mtu mmoja hapo ambaye aliponea chupu chupu tu, kulianguka kizingiti kizito karibu na muguu wake. Lakini yeye bahati nzuri hakupata udhuru wowote.
Hapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. aliwaambia Ma-sahaba wake, hebu mwulizeni huyu mtu leo amefanya matendo gani? Na wakati alipoulizwa huyo mtu akasema:
“Mimi nilipotoka
nyumbani mwangu leo nilikuwa na kokwa chache za
tende. Na
kukatokezea na masikini mmoja akaniomba basi mimi nikampa
Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. akajibu
“Basi kwa sababu hiyo tu leo, Allah swt amekuepusha na balaa hii ambayo ingekumaliza.”
5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. siku mmoja alimwambia Sahabi wake Mayassari kuwa:
“Ewe Mayassari je wajua kuwa wewe umeisha fikiwa na mauti mara nyingi, lakini Allah swt amekuongezea umri wako zaidi kwa sababu ya wewe kuwa mkarimu na kuwajali jamaa na ndugu zako umewawia wema ndio maanake umri wako umezidi.”
1. Al Imam Hasan al-'Askary a.s. anasema kuwa:
“ Wakati mmoja Al Imam Ja'afer as-Sadiq
a.s. akiwa pamoja na wenzake walikuwa safari na wenzake hao walikuwa na
Na kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akawajibu:
‘Mkabidhini mali yenu yule ambaye ataweza
kuifadhi mali yenu, na kwa kweli ataitunza sana na baada la kupungua hata
itazidi pia, sio hayo tu na pale mutakapokuingiwa na shida ya
Kwa kusikia hayo hao wenzake aliokuwa nao katika safari wakamwuliza :
“Je ni nani huyo?”
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akawajibu:
“Yeye ni miliki wa malimwengu zote Allah swt.”
Basi hao wenzake wakamwuliza je tunaweza
kumkabidhi vipi
“Wale waliokuwa naye pamoja safarini walinuia hivyo kama vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alivyowaambi,a na Imam a.s. akawaambia sasa nyie mko katika amani ya Allah swt, na wakiwa wanaendelea na safari majambazi hao walikumbana nao na kwa kudura za Allah swt wao wakawapita salama usalimini bila ya kudhurika na kusumbuliwa, hadi wakafika mwisho wa safari yao.
Waliopofika tu mwisho wa safari yao wao wakatoa sehemu moja walizokuwa wamenuia kama Sadaka na sehemu iliyo bakia walifanyia biashara yao, na Allah swt akawajaalia baraka kiasi kwamba wakapata faida hata zaidi ya mara kumi.”
1.
Siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alikuwa Mina pamoja na Ma-sahaba wake wakila
zabibu. Mara akatokezea mtu mmoja na akaomba. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq
a.s. kwa mkono wake akachukua fungu moja la zabibu akampa basi huyo akakataa
kupokea, akisema “mimi sitaki zabibu hizi
bali ninataka pesa tasilimu
Basi kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia “Allah swt atakuzidishia” na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. hakumpa chochote, baada ya muda si muda huyo mwombaji tena akarudi kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. na akamwambia Imam a.s. “Nipe zile zabibu ulizokuwa ukitaka kunipa.” Na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia Allah swt atakutafutia njia yake, pamoja na hayo Imam a.s. hakumpa chochote.
Wakati bado wakiwa wamekaa akatokezea mtu
mwingine kuja kuomba, na Imam a.s. alitoa mbegu tatu tu za zabibu akampa huyo
mwombaji. Mwombaji huyo alianza kumshukuru Allah swt kwa kumjaalia riziki hiyo
na akaonyesha shukurani kwa ujumla. Kwa kusikia hayo Imam a.s. alichota mikono
ya zabibu miwili akampa na hapo tena huyo mwombaji akaendelea kumshukuru Allah
swt zaidi na zaidi. Kwa kusikia hayo tena Imam a.s. akamwambia mtumwa wake
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“ Mimi nilinunua ardhi pamoja na mtu mmoja. Mtu huyo huyo alikuwa ni mnujumi, kwa hiyo yeye kila alipokuwa akipiga mahesabu yake na elimu ya nyota yake aliyokuwa nayo alikuwa akiangalia saa nzuri ndipo alipokuwa akienda shambani mwake, nami bila kujali kama saa mbaya nilikuwa nikienda shambani mwangu, na sisi tulipokuwa tayari basi ardhi au sehemu yangu ikawa na faida zaidi kuliko sehemu yake.
Kwa hivyo yeye bila kusita katika hali ya kustaajabisha aliniambia mimi
sijawahi kuona
Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu ngoja nikwambie hadithi moja ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliyesema kuwa:
‘Mtu yeyote anayetaka Allah swt amwepushe na maovu na mabaya ya siku nzima basi yeye aianze siku yake kwa kutoa Sadaka, na yeyote anayetaka ajiepushe na balaa na maovu ya usiku basi yeye usiku unapoingia atoe Sadaka na ujue kwamba mimi daima ninapotoka nyumbani mwangu huwa ninatoa Sadaka. Kwa hivyo kufanya biashara na Allah swt hivi afadhali zaidi kuliko elimu yako ya nyota na kupiga ramli.”
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema :
“Mtoe Sadaka usiku kwa sababu huiondoa ghadhabu ya Allah
swt, husamehe madhambi mazito, na hukusababishia hesabu zako siku ya Qiyamah zikaenda
vizuri. Kutoa Sadaka katika siku
kunaiongezea
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“ Kwa kutoa Sadaka yaani kunapokucha kunayeyusha madhambi
4. Ibn ‘Abbas amesema kuwa: Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu, Sura Al-Baqarah,2, Ayah 274
Wale wanao toa mali zao usiku na mchana, kwa siri na dhaahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika
“Aya hiyo imeteremshwa makhsusi kwa ajili ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kwa sababu yeye alikuwa anazo Dinar chache ambazo wakati wa usiku yaani baadhi ya Dinar hizo wakati wa usiku na baadhi wakati wa mchana na zinginezo katika hali ya siri na zinginezo zikiwa ni dhahiri alizokuwa akitoa Sadaka katika njia ya Allah swt.”
1. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema kuwa:
“Kwa kutoa Sadaka kifichoficho ghadhabu za Allah swt hupoa.”
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Sadaka inayotolewa kidhahiri basi kuliko hiyo Sadaka inayotolewa kifichoficho ni afadhali zaidi.”
3. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. siku moja alisema kuwa:
“Mambo yanayomfikisha mtu moja kwa moja
kwa Allah swt
4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Kwa kutoa Sadaka kidhahiri kunaondoa aina sabini za balaa lakini kwa kutoa Sadaka kifichoficho kunamfanya mtu anusurike na ghadhabu za Allah swt.”
5. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:
“Baba yake Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. kila siku usiku alikuwa akitoka nyumbani pamoja na kifurushi cha fedha mgongoni mwake na mara nyingine alikuwa akichukua kufurushi cha vyakula na alikuwa akiwaendea wale wenye shida na dhiki.
Wakati akiwapelekea misaada hii majumbani mwao Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa akiufunika uso wake ili wasiweze kumtambua ni nani huyu anayewafikishia misaada mpaka majumbani mwao.
Wakati Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alipofariki ndipo hapo ikajulikana hawa wanaosaidiwa wenye shida hawapati misaada waliyokuwa wakipata, ndipo hapo wakajua kuwa aliyekuwa anawasaidia mpaka milangoni mwao alikuwa si mtu mwingine bali ni Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s . vile vile wakati Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alipolazwa wakati wa kuoshwa baada ya kufariki kulionekana mabegani mwake na mgongoni mwake alama zilikuwa zikionyesha kuwa alikuwa akibeba mizigo mizito kwa muda mrefu.
Na katika kipindi kimoja cha baridi kali
Vile vile Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. alisema kuwa:
“Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn
'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa
akiwasaidia na kuwalisha na kuwatunza familia zaidi ya mia moja katika mji wa Madina.
Na alipokuwa akikaa kula mayatima, wazee, wagonjwa na masikini walikuwa wakikaa
kula naye pamoja na Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib
a.s., na vile vile alikuwa akiwafungia vyakula kwa ajili ya kuwachukulia wale
waliokuwa majumbani mwao au
Vile vile yeye yasemekana kuwa alikuwa hakai kula pamoja na mama yake juu ya meza moja ya chakula na watu walipomwambia ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. wewe ni kigezo cha tabia njema na mfano bora katika Waislamu! Je kwanini hukai pamoja na mama yako katika kula chakula?.
Al Imam Zaynul 'Aabediin a.s. aliwajibu kuwa
“Mimi sikai na mama yangu kwa sababu yawezekana mama yangu akiangalia chakula moja labda akataka kuchukua na wakati huo mkono wangu ukawa mrefu kwenda kuchukua chakula hiki itakuwa kweli hiyo ni kitovu cha nidhamu na ndivyo maana yake ninajiepusha kukosa nidhamu mbele ya mama yangu.”
6. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:
“Mtu anapotoa Sadaka ya chakula kwa ajili ya kuwapa masikini na mafakiri basi mujue kuwa aina hiyo ya Sadaka huondoa ufakiri na humwepusha mtu na kumuondolea ufakiri, na kuurefusha umri wake na humwepusha na aina sabini za vifo vya kutisha (ajali mbalimbali).”
7. Vile vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Siku ya Qiyamah wakati kutakuwa na jua kali lichomalo basi watu aina saba watakuwa wamepewa kivuli na Allah swt na mmoja wao ni yule anayetoa Sadaka ya vyakula kiasi kwamba mkono wa kushoto haupati habari kuwa mkono wa kulia umetoa Sadaka.”
8. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:
“Enyi Waislamu! Je niwaambieni mambo matano ambayo kwa hakika ni mema, maneno hayo yanawapelekeni hadi Jannat.?
Ma-Sahabah wakajibu
“Naam lazima tuambie ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Naomba utuongoze.”
Kwa hayo Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. akasema:
“Mnapopatwa na misiba basi lazima ufanye subira na mujaribu kuficha, mutoe Sadaka kiasi kwamba mkono wa kulia unapotoa mkono wa kushoto usipate habari, muwatende mema wazazi wenu, na kwa hakika katika mambo hayo ndiyo kuna furaha ya Allah swt na kila mara mwezavyo kusema semeni La Haula wala Quwwata illa billahil ‘Aliyil ‘Adhiim kwa hakika hiyo ni hazina moja kubwa katika hazina za Jannat, na vile vile katika nyoyo zenu muwe na mapenzi ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. pamoja na Ahlul Bayt a.s.
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. daima ilikuwa akitoka usiku katika kiza huku amejitwisha mafurushi ya mapesa na vyakula kwa ajili ya kwenda kugawa kwa masikini katika mji wa Madina, alikuwa akiwafikishia misaada waitaji walipokuwa. Na siku ambayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliaga dunia, watu wakaona misaada imesimama na watu hawakufikiwa na misaada hiyo ndipo walipokuja kujua kuwa misaada hiyo ilikuwa ikiletwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye daima alikuwa akificha uso wake ili watu wasijue kuwa ni yeye anayewafikishia misaada hiyo.
2. Mu’alla ibn Khuns anasema kuwa:
“Usiku mmoja kulikuwa kukinyesha manyunyu
ya mvua, nikamwona Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akielekea katika makazi ya Banu
Sai’d nami nikajaribu kumfuata nyuma kisirisiri na mara nikasikia katika
‘Ya Allah swt! Ninaomba vitu hivi nivipate tena.’
Na hapo mimi nikatokezea karibu ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., nikatoa salamu. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. baada ya kuitikia salamu akaniambea je wewe ni Mua’alla ?
Nami nikamjibu :
‘Ndiyo ewe Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ! Niwe fidia juu yako.
Hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akaniambia:
‘Naomba uniokotee vitu hapo chini unisaidie.”
Mu’alla anasema mimi katika giza kizito hicho nikaanza kupapasa aridhini na nikakuta kumbe ni vipande vya mikate na wakati ninamkabidhi Imam a.s mikate nilivyo viokota katika giza kali nilihisi kifurushi alichokuwa nacho migongoni mwake kilikuwa kizito mno na hivyo nilimwomba Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. Lakini hakukubali nimsaidie kubeba kifurushi hicho.”
Lakini Imam a.s alikataa akaniambia
“Ninapendelea kuubeba uzito huu mimi mwenyewe kwa sababu huu ndiyo utakao kuwa ufanisi wangu katika siku ya Qiyamah na bora kwangu na hivyo unaweza kuja nami katika safari hii.”
Tulipokaribia katika makazi ya Banu Sa’id, Imam a.s. alikwenda kwa kila mmoja ambaye ni mwenye shida akamwekea mikate miwili na akarudi. Na wakati huo akaniambia kwa kutoa Sadaka usiku kunatuliza ghadhabu za Allah swt, na Allah swt usamehe madhambi makubwa, na kusahilisha hesabu katika siku ya Qiyamah.”
3. Zuhri anasema kuwa:
“Siku moja wakati wa baridi kali mno na ukungu ulikuwa umejaa mwingi mno mimi nilimwona Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. akiwa amejitwisha kifurushi kikubwa cha chakula na mzigo mkubwa wa kuni.
Nami sikusita nikamwambia ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Je nini haya?’
Imam a.s akanijibu nina nia mpango wa safari, na hivyo ndivyo ninavyojitayarisha kwa ajili ya mahitaji yangu.
Zuhri akasema:
‘Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Mimi nakupa mfanyakazi wangu ambaye atakusaidia kukubebea mizigo yako hiyo mizito.”
Al Imam Zaynul 'Aabediin a.s. alimkatalia nami nikamwambia,
“Basi nipe mimi mwenyewe nikupunguzie kukusaidia kukupunguzia huu mizigo. Kwa hayo Imam a.s. akajibu, lakini kwa kufanya hivyo mimi sitakuwa nimetoka katika wajibu wa kufika mwisho wa safari yangu vile inipasavyo kufika, kwa hiyo naomba uendelea na shughuli zako uniache peke yangu.”
Zuhri anasema:
“Baada ya kufika siku chache mimi nilipomwona Imam a.s nikamwambia,
“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa
s.a.w.w.! Mimi sioni
Imam a.s akamjibu:
“Naam ! Vile uchukuliavyo sivyo. Muradi
wangu ulikuwa ni safari ya Aakhera. Mimi nilikuwa nikijitayarisha kwa ajili ya
safari ya Mauti. Kumbuka kwamba kujikumbusha na kujitayarisha kwa mauti basi mambo
mawili ni muhim, kwanza kujiepusha na yaliyo haramishwa na pili ni kutoa muhanga
wa
4. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. katika baadhi ya misemo yake anasema.:
· “Toeni Sadaka kwa basabu kunatuliza ghadhabu za Allah swt .
· Toeni Sadaka katika njia ya Allah swt mngejariwa kwa sababu ya riziki muliyojaaliwa na Allah swt kwa kufanya hivyo nyinyi mtahesabiwa katka wale wanaopigana katika njia ya Allah swt.
· Yeyote yule ambaye ana imani kamili kuwa Allah swt hulipiza kile kinachopendwa na Mumin basi huyo mtu lazima ataitia nafsi yake katika shida na kwa kufanya mema.
· Muwatibu wagonjwa wenu kwa Sadaka .
·
Muilinde na muihifadhi na kulinda
· Urekebishe matumizi na mahitaji ya maisha yenu ili mweze kupima vyema.
· Kuwaza na mawazo ni nusu ya uzee unaoletwa nawe.
· Mwenye matumizi yenye mahesabu yaani anayebana matumizi kamwe hawezi kuwa mwenye shida na dhiki.
· Kumsaidia yule ni mtu ambaye anaheshima na mkuu na kumsaidia yule ambaye ana madeni haya maneno mawili hayana kifani yoyote.
· Kila jambo lina mazao yake, kwa hiyo mazao ya mema na kuwa na nia katika kutumia mali au chochote katika njia ya Allah na kwa ajili ya Allah swt basi mazao yake ni kwamba kufanya haraka kutekeleza azma hiyo na kamwe usifanye kucheleweshwa.
· Muongezee na mupanue riziki yenu kwa kutoa Sadaka, kabla hamjaijiwa na balaa, mwombe dua na kwa hakika mtaweza kujiepusha nayo na kujiokoa nayo.
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Kutoa Sadaka siku ya Ijumaa kuna thawabu na fadhila kubwa
2. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:
“Msimkatalie masikini anayeomba siku ya ‘Arafah. Lazima mpeni chochote kile.”
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Mtu yeyote atakaye kuwa ametoa Sadaka katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, basi yeye atakuwa ameepukana na balaa za aina sabini.”
1. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa ameulizwa na mmoja wa Ma-Sahaba wake,
“Ewe Mtume wa Allah swt! Ni Sadaka ipo iliyo bora kabisa kuliko zote!”
Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alijibu,
“Sadaka iliyo bora ni ile ya wakati ule ambapo mtoa Sadaka yuko salama u salimini, mwenye afya kamili na anayeishi maisha mema bila wasiwasi, na ambaye anauogopa umasikini.
Na wala msicheleweshe kiasi kwamba mpaka
kwamba mwisho wa maisha yenu yameisha wafikia shingoni, na hapo ndiyo mnaanza
kutoa usia kuwa kiasi fulani mpe masikini fulani na fulani mpe kiasi fulani na
kadhalika.
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliombwa na mtu mmoja kuwa ampatie nasiha, na hivyo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia:
“Tayarisha matayarisho yako ya safari, na
matayarisho yako hayo yatume kabla wewe hujaenda safari. Jifanyie matendo yako
mwenyewe yaani
3. Kwa kuzungumzia swala
tulilozungumziwa hapo No. 2 hapo juu
siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa amekwenda katika ghala la mtu
mmoja ambaye alikuwa amefanya usia kuwa baada ya kifo chake maghala yake yote
yaliyokuwa yamejaa kwa tende yagawiwe Sadaka kwa masikini. Na baada ya kifo chache
ikatekelezwa usia wake na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipokwenda kule
baada ya kufagia akakuta kokwa moja ya tende imebakia mguuni mwake basi Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. akainama akalichukua kokwa
“
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka kwa mababu zake a.s. kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema:
“Pale anapokuja mtu yeyote usiku kugonga mlango kwa nia ya kuomba msaada, basi msimvunje moyo, msaidieni na hasa inapokuwa mwombaji aliyekuja ni mwanaume.”
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Allah swt kwa kila kazi amemweka mweka-hazina
ambaye anaweka mahesabu yake isipokuwa Sadaka, ambaye mahesabu yake na utunzaji
wake anaweka Allah swt mwenyewe. Baba yangu mzazi wakati alipokuwa akimpa chochote
mwombaji alikuwa akikichukua tena na alikuwa akiubusu mkono wa huyo mwombaji, na alikuwa akiunusa kwa hamu
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema:
“Allah swt amesema kuwa mimi nimewateua mawakili kwa kila jambo na ambao ndio wanaosimamia na kuweka ripoti zake isipokuwa Sadaka ambayo mimi mwenyewe ndiye ninayetunza habari zake.”
1. Mu’alla bin Khunais amesema kuwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alikwenda katika makazi ya Banu Sa’id na wale wote waliokuwa na shida aliwawekea mikate na kuondoka zake. Hapo mimi nilimwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.:
Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimjibu :
“La! Hawa kama wangekuwa marafiki na wapenzi wetu na wafuasi wetu basi ningewaongezea kiasi cha punje ya chumvi”. [50]
Hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliponielezea kwa uwazi zaidi kwamba siku moja Mtume ‘Isa bin Maryam a.s. alikuwa akipita ufuoni mwa bahari, na akatoa mkate kidogo kutoka kifurushi chake akatupa baharini. Baadhi ya wale aliokuwa nao wakamwuliza!
“Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Je umefanya nini bwana? Nini maana ya kutupa mikate baharini?
Mtume Isa a.s akawajibu:
“Katika bahari kuna viumbe vya Allah swt na iwapo kutatokezea na viumbe vyovyote vitakavyo kula humo kutokana na nilichowatupia basi kwa hakika katika ufalme wa Allah swt nitakuwa na thawabu nyingi mno.”
2. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema:
“Pozeni nyoyo zenu kwa sababu ya kiu kali
kwani Allah swt hupendezewa
3.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alikuwa akifunga
safari baina ya Makkah na Madina, akaona kuwa kulikuwa na mtu mmoja aliyejitupa
chini ya mti mmoja. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwamwambia mtu mmoja aliyekuwa
naye, aende akamwulize hali yake, inawezekana labda alikuwa na kiu kali. Mtu
huyo alipomwendea huyo mtu aliyekuwa amelala chini ya mti na kumwuliza hali
yake basi ikajulikana kuwa mtu huyo alikuwa na kiu ya maji. Basi Al Imam
Ja'afer as-Sadiq a.s. alimnywesha maji na akaondoka kuendelea na safari
“Ewe
mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Huyu mtu alikuwa ni Mnasara, watu
Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu
“Naam ! Katika mazingira
4. Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa pamoja na wafuasi wake nao katika safari, na waliketi kwa ajili ya kula chakula. Na akatokezea swala mmoja ambaye alikuwa akitafuta chakula, Imam a.s. akamwambia huyo
‘Swala njoo karibu, njoo ule nasi! Usiwe na wasiwasi utulie na ujue hapa kwetu hautakuwa na hofu yoyote, upo katika usalama.”
Kwa kusikia hayo Swala huyo alimsogelea Imam a.s. na alikula pamoja nao.
5. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa Siku moja baba yake alikuwa pamoja na wenzake katika bustani yake na walipoketi kula chakula na mara akatokezea Swala mmoja aliyekaribia.
Hapo Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. . ambaye ni baba yake na Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. akasema:
“Ewe Swala, jina langu mimi ni Al Imam Zaynul 'Aabediin bin Al Imam Hussein ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s. na mama yangu Bi Fatima az-Zahra a.s., njoo ushiriki nasi katika kula. Na Allah swt kiasi alichokuwa amemjaalia cha chakula huyo Swala alikula.”
6.
Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:
“Hakuna mtu yeyote mwingine isipokuwa ni
Mwislamu tu anayeweza kuchinja wanyama wenu wa dhabihu siku ya Iddi na Sadaka, na unapotoa Sadaka katika kutoa humo lazima wapewe Waislamu tu.
Na unapotoa Sadaka katika
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwayah moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa mtu mmoja alimwuliza Mutume s.a.w.w. :
“Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Je ni Sadaka ipi iliyo bora kabisa?”
Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alijibu:
“Sadaka ile ambayo watakayo pewa wale jamaa na ndugu
ambao hata
2. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Iwapo wewe unatoa kumi kwa ajili ya Sadaka , basi ili kuwasaidia Mumin toa kumi na nane na yule ambaye hawezi kabisa msaidie kwa ishiririni na kwa ajili ya kuwasaidia jamaaa na ndugu kwa wema utoe ishirini na nne.”
3. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema Riwayah kutokea kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa amesema:
“Mtu yeyote atakaye wasaidia jamaa na ndugu zake katika kwenda Kuhijji au ‘Umra, basi Mtume Allah swt atamjaalia thawbu za Hijja mbili na ‘Umra mbili, na yoyote yule atakayemsaidia ndugu yake Mumin basi Allah swt atamlipa kusiko na kifani.”
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameseama kuwa:
“Iwapo mtu atawasaidia jamaa au ndugu zake ambao wana shida ni muhtaji basi hiyo siyo Sadaka.”
5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah moja ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akisema:
“Kwa mtu yeyote yule ambaye atakwenda
mwenyewe kwenda kumsaidia jamaa au ndugu yake mwenye shida na kutoa kitu
chochote kwenye mali yake na kumsaidia
basi Allah swt atamjaalia ujira wa mashahidi mia moja na kwa kila hatua
atakayotembea atamwandikia mema elfu arobaini,
na kiasi hicho hicho cha maovu yake yatasamehewa. Na vile vile kiasi
hicho hicho ataongezewa daraja
6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., aliulizwa na mtu mmoja :
“Ewe Mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Je yeyote yule anayekuja kuomba mlangoni anastahili kupewa Sadaka au badala yake tuwape jamaa na ndugu zetu Sadaka hiyo?”
Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliwajibu :
“Kwa hakika kuwapelekea msaada Sadaka jamaa na ndugu wa mtu zina thawabu nyingi zaidi.”
7. Al Imam Muhammad Sahibuz-Zamaan a.s. aliandikiwa barua na mtu mmoja akimwuliza
“Iwapo mtu anaweza kunuia kuwa mimi katika mali yangu nitatoa sehemu fulani ya mali nitamsaidia mtu fulani na katika kipindi hicho iwapo atakuja kujua kuna mtu katika ndugu na jamaa zake ambaye ni kweli anashida na anahitaji msaada wake basi je huyo mtu anaweza kubadilisha nia yake ya kumsaidia jamaa yake badala ya kumpa mtu aliyekuwa amenuia hapo kabla?”
Al Imam Muhammad Sahibuz-Zamaan a.s. akamjibu kuwa:
“Utaangalia ukaribu wa watu hao na yule aliye karibu nawe katika madhehebu umpatie na lau kama wote wawili kama watakuwa wanatokana na dhehebu moja tu basi kwa mujibu wa kauli ya Al Imam Musa al-Kadhim a.s. kuwa kugawanywe kati kati yaani watu wote wawili wapewe nusu kwa nusu, kwa sababu iwapo kutakuwa na jamaa na ndugu ambao wana shida na taabu basi huwezi kutoa Sadaka na kuwapa wengine. Na kwa hakika kwa kufanya hivyo utakuwa umepata thawabu na fadhila za Sadaka.”
1. Al Imam Muhammad Sahibuz-Zamaan a.s. aliandikiwa barua na mtu mmoja akimwuliza kuwa:
“Je inawezekana mimi nikatoa Zaka au Sadaka
kutoka
Na kwa hayo Imam a.s. alimjibu:
“Usimpe Zaka au Sadaka mtu yeyote mwingine isipokuwa wenzako na majamaa zako.”
2. Al Imam Muhammad Sahibuz-Zamaan a.s. aliulizwa:
“Je inawezekana kumpa Sadaka Nasibi (maadui wa Ahlul Bayt a.s. )?”
Imam a.s akamjibu kuwa:
“Musiwape Sadaka wala Zaka maadui wa Ahlul Bayt a.s. na ikiwezekana hata maji pia msiwape.”
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliulizwa kuwa:
“Je inaruhusiwa kumlisha mtu
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akajibu kuwa :
“Mtu ambaye humwelewi na
4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliulizwa kuwa:
“Mara nyingi tunaona masikini wanaokuja
kuaomba, lakini sisi tunakuwa hatuwafahamu, Je watu
Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliwajibu
“Kama wewe moyoni mwako utaingiwa na
huruma kwa ajili ya mtu huyo basi
unaweza kumpa, ingawaje hata
5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Kidhahiri wapo waombaji wengi ambao (wengi wanatoka vijijini na maeneo karibu ya mji ) hivyo nyie muwape Sadaka watoto, wanawake, wagonjwa, wadhaifu na wazee.”
6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Mnapoijiwa na masikini kwa ajili ya kuomba ambao ni wazee kabisa na wanawake na watoto na wasichana wadogo basi muwasaidie Sadaka na vile vile muwasaidie Sadaka wale mnaoijiwa huruma mioyoni mwenu.”
7. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliulizwa kuwa:
“Mijini mwetu wanakuja waombaji wengi
Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alijibu :
“Naam ! Mnaweza kuwapa.”
8. Al Imam 'Ali an-Naqi a.s. aliandikiwa barua na humo akaulizwa:
“Je tunaweza kuwasaidia wale masikini waliopo mitaani ambao hatujui dini na wala Madhehebu zao?”
Kwa hayo Al Imam 'Ali an-Naqi a.s. aliwajibu:
“
9. Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alimwambia muhudumu wake:
“Yeyote yule anayekuja kuomba nyumbani kwake basi asimruhusu akaondoka hadi pale ahakikishe kuwa amemlisha chakula, hususan siku ya Ijumaa.”
Mwandishi anasema kuwa mimi nilimwambia Imam,
“Ewe mjukuu wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Kila mwombaji huwa si msitahiki.”
Kwa hayo Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alinijibu
“Ninaogopa kuwa inawezekana mwombaji akawa msitahiki lakini mimi nikamfukuza, isije tukapata matatizo na dhiki iliyo mpata Mtume Ya’aqub a.s na nyumba yake.”
1. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:
“Msimvunje moyo mwombaji hata
2. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:
“Iwapo mtoaji atakuwa anajua wema na fadhila za kutoa Sadaka basi kamwe hatamrudisha mtu yeyote bila ya kumpa kitu chochote.”
3. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Kamwe msiwarudishe mikono mitupu waombaji. Iwapo waombaji wengine wasingekuwa waongo na wadanganyifu basi kamwe wengine wasingerudipo.”
4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kamwe hakumrudisha masikini yeyote
aliyemwomba asaidiwe Sadaka. Na
5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Mtume Ibrahimu a.s. daima amekuwa akiwahudumia na kuwakarimu wageni, na pale alipokuwa hakuwapata wageni wowote wale, basi alikuwa akifunga mlango wake na akitoka kwenda kuwatafuta wageni.”
Na katika hadithi hiyo hiyo tunapata wakati mmoja Malaika Jibrail alimwijia Mtume Ibrahim a.s. na kumwambia :
“Allah swt amenituma safari hii kwa mja wake
mmoja ambaye ameweka marafiki Wake
Kwa hayo Mtume Ibrahim a.s. akaingiwa na shauku ya kutaka kumjua na akasema :
“Tafadhali sana naomba unitambulishe huyo umzungumzaye, nami nitapenda kwenda mbele yake.”
Jibrail a.s. akasema :
“Ewe Khalil (rafiki)! Ndiwe wewe tu !”
Basi Mtume Ibrahim a.s. akamwambia :
“Ewe Jibrail a.s. ! Je kwanini umenifanyia hivyo ?”
Hapo Malaika Jibrail a.s. akamjibu :
“Kwa sababu wewe kamwe haujamnyooshea mkono yeyote, na wewe daima haujawahi kumkatalia yeyote aliyekuja kukuomba.”
6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema sema kuwa Mtume Allah swt alikuwa akisema
“Kamwe msimrudishe mikono tupu mwombaji. Hata kama mtakuwa katika hali ya ugumu kiasi gani.
7. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa Mtume Musa a.s. wakati alipokuwa akimlilia Allah swt, Allah swt alimwambia :
“Ewe Musa hata kwa ukimpa kidogo mpe ili
utunze heshima ya mwombaji, na
8. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripotiwa riwaya kuwa siku moja mtu mmoja alikuja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuomba kwa hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliwaangalia Ma-Sahaba wake na kuwaambia,
“Enyi Ma-Sahaba wangu ! Msaidieni.”
Na mmoja katika Ma-Sahaba wake akamsaidia kifaa cha dhahabu. Aliyekuja kuomba akasema
“Je leo ni -- yako?”
Yule Sahaba wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akajibu :
Naam ndiyo maana yake”.
Yule mwombaji akasema:
Mimi nimekubalia hivyo. Mimi si Jini wala si binadamu; bali mimi ni Malaika niliyetumwa na Allah swt nije nikujaribu na kwa hakika nimekuona wewe miongoni mwa watu wenye kushukuru neema za Allah swt. Mungu akujaalie kila la heri.”
9. Sa’ad bin Musayyab anasema kuwa Siku moja wakati wa swala ya asubuhi yeye alikuwa pamoja na Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s., akatokezea mwombaji mmoja na wakati huo Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. akasema:
“Mpeni huyo mwombaji---- kumbukeni kuwa---kamwe msimwondoe mwombaji katika hali ya kuhuzunika yaani msimwondoe mwombaji bila kumpa chochote”.
10. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ananakili riwaya kutoka baba yake mzazi a.s. kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:
“Mruhusu mwombaji aondoke hata kwa kidogo na kwa mapenzi na kwa huruma pia. Kwa sababu mara nyingi anayekuja kuomba huwa si kutoka binadamu au Majini bali huwa ni njia moja kwa kuwajaribia nyie kwa ajili ya kuwaongezea neema.”
11. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Nahjul Balagha :
“Masikini anapokuja kwenu basi anakuwa ni mjumbe wa Allah swt na yeyote yule atakaye muudhi na atakayemhudhunisha basi atakuwa amemhudhunisha Allah swt na yeyote yule atakaye kuwa amempa chochote basi ajue kuwa amempa Allah swt”.
12. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anaripoti kutoka kwa wazazi wake a.s ambao wamesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Wakati ‘Ummah wangu utakapogeuza uso au
utakapo wageuzia uso wale wanao hitaji msaada wao na watakapoanza kutembea kwa
maringo basi wakati huo Allah swt atasema: kwa kiapo cha utukufu na ukuu wangu
hawa watu watakomeshana wao kwa wao na hivyo ndivyo nitakavyo waonjesha adhabu
1. Walid bin Sahib anasema kuwa:
“Siku moja mimi nilikuwa kwa Al Imam
Ja'afer as-Sadiq a.s. na hapo akatokezea mwombaji mmoja. Imam a.s alimpa
chochote huyo mwombaji na akatokezea mwombaji wa pili naye akapewa chochote.
Hivyo hivyo akatokezea mwombaji wa nne basi Al Imam a.s akamwambia Allah
atakusaidia upate zaidi njia yako atakupanulia. Na baada ya hapo Imam a.s
akasema iwapo mtu atakuwa na Dirham takriban elfu thelathini au arobaini, na
akanuia akawa na mpango wa kuzitumia zote ambazo kimatokeo hatabakiwa na
chochote basi mtu
Kwa hayo mimi nikasema
“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Je ni makundi gani ya watu hawa watatu?
Kwa hayo Imam a.s akajibu
“Mmoja wao ni yule ambaye ana mapesa na
2. Ali ibn Hamza anasema kuwa:
“Mimi nilimwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq
a.s. swali kuwa yeye amesikika akisema mwalishe watatu---- na
1. Walid bin Sabih daima alikuwa akisema kuwa:
“Mtu yeyote anayetoa Sadaka na iwapo Sadaka hiyo itakubaliwa au Sadaka hiyo itarudishwa basi yule mtoa Sadaka haruhusiwi kuila au kuitumia tena hiyo Sadaka kwa ajili yake. Na badala yake hana njia yoyote isipokuwa aigawe Sadaka kwa mtu mwingine. Hatakuwa na ruhusa kwa vyovyote vile vya kuitumia hiyo Sadaka isipokuwa Sadaka itatolewa tena Sadaka kwa mtu mwingine. Vile vile mfano wake inachukuliwa kuwa mtu anapomfanya huru mtumwa katika njia ya Allah swt na kwa ajili ya kutaka furaha ya Allah swt basi kamwe hawezi kumchukua tena yule mtuma(aliyefanywa huru) akamfanya mtumwa wake. Na baada ya kumfanya huru mtumwa na mtumwa atakapo rudi kwake basi hawezi kumweka vile alivyokuwa amemweka mwanzoni kabla ya kumfanya huru katika njia ya Allah swt. Na vivyo hivyo ndivyo swala hizi zinausiana na Sadaka pia.”
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq
a.s. amesema:
“Yeyote yule atakayekuwa ametoa Sadaka na iwapo Sadaka hiyo itamrejea yeye tena basi yeye mwenyewe hataweza kuitumia wala hataweza kuiuza, kwa sababu kitu hicho kilishatolewa katika njia ya Allah swt na kwa ajili ya ridhaa ya Allah swt na hivyo hakuna kitakachoweza kushirikishwa katika swala hilo, na mfano wake pia ni sawa na ule wa kumfanya huru mtumwa hivyo hataweza kurudishwa tena katika utumwa.”
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq
a.s. anasema
“Iwapo mtu atanuia kutoa Sadaka kwa ajili
ya mtu fulani anayeuhitaji msaada huo na wakati huo akapata kujua kuwa mtu huyo
ameshaondoka, basi hawezi kuirudisha na kuichanganya hiyo
4. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa: Kuna mtu alimwuliza iwapo mtu alimfanya huru mtumwa bado ambaye hajafikia umri wa kubalehe je sheria inasemaje?
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimjibu
“Hakuna tatizo lolote ndani yake lakini
sheria itakayotumika hapo ni
1.
Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amesema:
“Dua ya mtu msiidharau au kusema kuwa haifai chochote. Mara nyingi dua muliyoombewa na Mayahudi au Manasara hukubaliwa. Ingawaje inawezekana kwa dua aliyo jiombea yeye mwenyewe haiwezi kukubalika.”
2.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Wakati mnapo wasaidia waombaji, muwaombe
wawaombeeni dua hata
3.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakiliwa na Abu Basir riwaya moja kuwa Al Imam Zaynul 'Abediin
ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:
“Wakati mtu anapomsaidia fakiri mwenye shida sana asiye
na uwezo, na pale fakiri huyo anapomwombea dua, basi dua hiyo lazima
inakubaliwa na Allah swt.”
4. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:
“Wakati mnapowapa chochote waombaji; basi muwaombe wawaombeeni dua, kwa sababu inawezekana kwa sababu ya udanganyifu na ulaghai wake dua zake zenyewe kwa ajili yake zisikubaliwe lakini kwa ajili yenu dua zake zitakubaliwa.”
5. Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s.:
“Alikuwa akimwambia mfanyakazi wake, zuia kwa punde kidogo sadaka, ili mwombaji amalize kuomba dua.”
6. Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. Na vile vile amesema:
“Dua ya fakiri na mwombaji kamwe hairudishwi
au haitupiliwi mbali.”
7.
Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi
Talib a.s. amemwamrisha mfanyakazi wake kuwa:
“Wakati unapowapa chochote waombaji basi
muwaambie wawe wakituombea heri.”
8.
Al-Imam a.s. amesema:
“Wakati muwapapo
chochote masikini na waombaji basi muwe mukiwaomba wawaombeeni dua kwa sababu
wanapo waombeeni dua kwa ajili yenu dua zao hukubalika na inawezekana dua zao
kwa ajili
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Iwapo mtu atapewa msaada ikapitia mikono themanini hadi ikamfikia aliye
mustahiki basi kila mkono utapata haki sawa sawa ya malipo.”
2.
Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Bora ya sadaka zote ni ile ambayo binaadamu baada ya kujitimizia mahitaji yake kwa moyo mkunjufu anatoa sadaka.”
3.
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Yule atakaye fikisha msaada katika hali nzuri kwa mwenye kustahiki basi huyo mfikishaji wa sadaka atapata thawabu sawa kama za yule atakaye toa sadaka yake – hata kama katika kufikisha msaada huo kwa anayestahiki itachukua mikono elfu arobaini basi wote watapata malipo sawa kabisa kwani Allah swt hana upungufu wala kasoro ya aina yoyote ile, na wale watu wanaofanya Taqwa na kutenda mema basi laiti kama mungeweza kuelewa uhakika wa swala hili.”
4.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Watoaji ni wa aina tatu
· kwanza ni Allah swt mwenyewe ambaye anatoa kwa ajili ya malimwengu zote.
·
Pili ni yule mwenye
· tatu ni yule msaada unaopitishwa katika mikono yake au ni mtu ambaye anafikisha misaada hiyo.”
5. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amenakiliwa riwaya na Abu Basir kuwa amesema:
“Watoaji ni wa aina tatu wa
· kwanza kabisa ni Allah swt,
·
wa pili ni yule ambaye anatoa kutoka
·
tatu ni yule
anayefikisha
1.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Allah swt
amefaradhisha kwa waja wake kwa kusisitiza kuwa
·
kwanza uadilifu
na mapenzi yake pamoja na muumini mwenzake
·
pili awe ameweka
hisa fulani au kiasi fulani katika
· tatu kumukumbuka Allah swt katika kila hali na hapa haimaanishi kuwa kwa kumsifu Allah swt peke yake au kwa kutoa uradi (tasbihi) bali hapa kuna maanisho ya kuwa kufanywe kwa kimatendo kabisa yale yaliyoelezwa katika dini yakiwa ni sehemu ya imani ya mtu.”
4.
Aban ibn Taghlib anasema
kuwa Siku moja yeye alimwomba Al
Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amwelezee haki za muumini mmoja juu ya muumini
mwingine. Kwa hayo Imam a.s. alimjibu :
“Ewe Aban! Achana nayo, usini shurutishe kukujibu ulicho uliza.
Nami nikamwambia :
“Ewe Mola wangu niwe fidia kwako.”
Na baada ya hapo niliendelea kumsisitiza Imam a.s. anielezee na ndipo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alipoanza kuniambia :
“Haki ya muumini mwenzako juu yako ni
kwamba nusu ya
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akagundua kuwa rangi ya sura yangu imebadilika na akaniambia,
“Ewe Aban je huna habari kuwa Allah swt ameelezea habari za wale watu ambao wamezipenda nafsi za watu wengine kuliko hata nafsi zao?”
Nami nikamujibu
“Bila shaka, niwe fidia juu yako.”
Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akaendelea kujibu,
“Kwa hivyo nyie
toeni nusu ya
4.
Muhammad bin
Ajlan anasema kuwa yeye alikuwa pamoja na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. na mara
akatokezea mtu mbele
“Je ndugu uliowaacha huko nyuma hali zao ziko je?”
Basi huyo aliyekuja akawasifu na akatoa sifa zao na akaelezea kuhusu hali zao zilivyokuwa. Kwa hayo Imam a.s. akauliza :
“Je matajiri miongoni mwao wanawatunzaje wagonjwa wao?”
Basi huyo mtu akajibu :
“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Kidogo tu.”
Na Imam a.s. akamwuliza
“Je hao matajiri wanaonana mara ngapi na masikini?
Basi huyo mtu akajibu :
“Mara chache
tu.”
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwuliza
“Je hao matajiri wanawasaidia kwa mikono
Kwa hayo huyo mtu akasema
“Ewe Mawla
! Wewe unaniuliza mambo ambayo katika
utamaduni wetu upo mchache
Kwa hayo Imam a.s. alimujibu
“Je wao watajidhaniaje kuwa wao ni Mashi’a wetu?”
4.
Abu Ismail anasema kuwa:Yeye
alimwambia Al Imam Muhammad al-Baquir a.s.,
“Ewe Maula niwe fidia juu yako! Kwa sasa hivi huko kuna Mashia wengi.”
Kwa hayo Imam a.s. akajibu:
“Je wanawasaidia na kuwahurumia mafakiri na wenye shida? Je wale wanao watendea mabaya sasa watu hao wema waliofanyiwa mabaya wanawasamehe hao wabaya walio watendea mabaya? Je wanasaidiana miongoni mwao katika kamari ? [51]”
Kwa hayo yote mimi nikajibu :
“Hapana sivyo hivyo.”
Hapo Imam a.s. akasema :
“Kwa hakika hao sio Mashia wetu. Basi mjue
wazi kuwa Mashia wetu mienendo
15.
Al Imam
Muhammad al-Baquir a.s. siku moja alimwuliza Sa’id
bin Hassan,
“Je inawezekana miongoni mwenu kuwa muumini mmoja akatia mkono katika mfukoni mwa muumini wa pili na akajitolea kiasi cha fedha alizo na shida nazo bila ya kusita au kuogopa na muumini yule aliyetiliwa mkono mfukoni mwake asimzuie?”
Said bin Hassan akamjibu
“Ewe Mawla! Kwa hakika mimi sina habari na
jambo
Kwa hayo Imam a.s. akamwambia
“Kwa hakika hakuna chochote.”
Hapo mimi nikamwambia Imam a.s. :
“Je hii inamaanisha kuwa sisi tumeisha teketea na kuangamia?”
Imam a.s. kwa hayo akamujibu :
“Sivyo hivyo, miongoni mwenu udugu na
upendo bado haujaingia nafsini mwenu.”
Na katika maswala ya dua imesha zungumziwa hadithi moja ambamo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema zipo aina tatu za dua ambazo kwa kufika kwa Allah swt hakuna mtu anayeweza kuzizuia. Miongoni mwake moja ni
·
dua ya muumini
anayemwombea muumini mwenzake na ambaye ametoa msaada kutoka
· dua kwa ajili ya muumini mwenzake ambaye pamoja na uwezo wake anaomba hivyo na ambaye baada ya kujua shida na dhiki kali ya muumini mwenzake hakuipuuzia bali amemsaidia.”
1.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliulizwa na mtu mmoja :
“Ewe Mawla! Je ni mtu gani mwenzi wako aliyebora kabisa?”
Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alijibu,
“Ni wale ambao wanawawia na kuwafanyia mema ndugu zao katika imani katika hali ya raha,starehe na shida.”
Na aliendelea kueleza kuwa
“Ewe Jamil,
yeyote yule aliye nacho kingi basi kutenda kwake mema ni rahisi
Allah swt katika
Qur’an Tukufu, Surah Hashri, 59, Ayah 9,
Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala hawaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa (Wahajiri), bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.
2.
Jamil bin Darraj anasema kuwa:
“Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alitukusanyisha na kutuambia
“Miongoni mwenu bora kabisa ni yule ambaye ni mkarimu na mtenda mema kwa wenzake na mwovu kabisa ni yule ambaye ni bahili na anawawia wengine kwa hali hiyo na bora ya matendo ni kule kutendeana mema pamoja na ndugu zenu na vile vile kuwatimizia haja na mahitaji yao na kwa hakika matendo haya yanamuudhi na kumvunja nguvu Shaitan na kunamwepusha mtu asiingie Jahannam na badala yake aingizwe Jannat. Ewe Jamil! Naomba uwafikishie habari hizi muumin halisi.”
3. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimfanyia usia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kwa kumwambia:
“Ewe Ali! Nina ku-usia mambo matatu ambayo kwa hakika yanathibitisha imani.
4.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwaya moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambaye
amesema:
“Bora ya sadaka ni ile ambayo inatolewa bila ya kuwa na shida yoyote na inatolewa kwa furaha.”
Mwandishi anasema hadithi hii inawahusu wale ambao wana watoto, familia na ndugu na majamaa. Yeye anakuwa na majukumu ya kuwauliza na kuwatimizia haja hawa watu wanaomtegemea yeye na hivyo baada ya kumalizana nao anatoa sadaka kwa furaha.
5.
Sama’a anasema kuwa:
“Siku moja alimwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.,
“Iwapo mtu
atakuwa na chakula cha kumtosha siku moja, je anaweza kumsaidia yule mtu
mwingine ambaye hana chochote? Au tuseme
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu,
“Katika suala hili yapo mambo mawili, miongoni
mwenu kuna watu ambao wao wanawasaidia na kuwapenda wengine zaidi kuliko nafsi
zao na ambapo Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah A-Hashr, 59,
Ayah 9 :
Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala wahaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa , bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.
Na jambo la pili
ni kwamba yule ambaye ana kiasi kile tu ambacho kinamtosha yeye tu, basi mtu
Naam, mkono ulio juu uko afadhali kuliko mkono uliopo chini (yaani yule anayempa mtu mkono wa juu na yule anayepokea ni mkono wa chini)na daima wakati wa kutoa lazima aanzie na wale ambao kwa hakika wako chini ya utunzaji wake (anawajibika kuwatunza na kuwasaidia na kuwatimizia mahitaji yao).”
6.
Al Imam Musa al-Kadhim a.s. aliambiwa na ‘Ali bin Sued Assinani: “Ewe Mawla! Naomba unifanyie usia”.
Kwa hayo Imam a.s. alimwambia
“Fanya Taqwa. Na umwogope Allah swt”.
Na hapo Imam a.s. alinyamaza kimya, basi yeye akasema :
“Ewe Imam a.s.! Nina shida kubwa
Katika kumjibu Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alimujibu,
“Funga saumu na utoe sadaka.”
Naye kwa kunyenyekea alisema:
“Je nitoe katika yale ambayo mimi ninasaidiwa na watu? Na nitoe kiasi gani kutoka humo?”
Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alimjibu
“Chochote kile Allah swt anachokufikishia katika riziki yako toa humo sadaka, kwa kufanya hivyo acha nafsi yako ivumilie kidogo kwa ajili ya kuwatolea wengine walio na shida pia.”
7.
Abu basir
ananakili riwaya moja ama kutoka kwa Al
Imam Muhammad al-Baquir a.s. au Al
Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:
“Yeye aliuliza, bora ya sadaka zote ni ipi?”
Imam a.s. akamujibu,
“Sadaka bora ni kutoka ile
Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu,
Surah A-Hashr, 59, Ayah 9 :
Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala wahaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa , bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.
8.
Hakika
hadithi moja ndefu Masufi walileta dalili moja mbele ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:
“Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu,
Surah A-Hashr, 59, Ayah 9 :
Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala wahaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa , bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.
Imam a.s. aliwajibu
“Kwa ayah hiyo ni ufafanuzi ambavyo
watendaji walikuwa wakitenda
Na sababu ya kufanya hivyo ni kwamba Allah swt anamwonea huruma muumin ili huyo muumin asiweze kuwaletea shida na kuwadhuru nafsi za wananyumba katika familia yao watoto – dhaifu na watoto wadogo, wote walio dhaifu, na ambao hawawezi kustahimili njaa, wazee waume kwa wanawake.
Iwapo mimi nitakuwa na kipande kimoja cha mkate na nikagawa sadaka, basi wale wote wanaonitegemea mie wataangamia na kuteketea.
Ndyio maana Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema, iwapo mtu atakuwa na kokwa tano za tende au mikate mitano au Dinar tano au Dirham tano na yeye anataka kuzitumia zote, basi itakuwa ni vyema kabisa iwapo yeye azitumie kwa ajili ya wazazi wake, na baadaye kwa ajili yake mwenyewe na watoto wake na tabaka la tatu kwa ajili ya ndugu na jamaa zake ambao wana shida na wanahitaji msaada wake, na baada ya hapo awasaidie majirani ambao ni mafakiri, na mwishoni kabisa atumie kwa ajili ya kuwasaidia wengineo katika njia ya Allah swt.
Na baadaye akaendelea kusema kuwa siku moja ilitokea mtu mmoja kutokea Ansaar alifariki(kufa). Kwa mujibu wa usia wake yeye alikuwa na watumwa watano au sita ambao wote walifanywa (kwa mujibu wa usia huo) huru na wakaondoka zao na huko nyuma familia yake hakuwaachia chochote watoto wadogo wadogo na wana nyumba yake wote wakawa ni muhtaji, wakawa wao sasa wanategemea misaada kutoka wengine ilhali huyu bwana alikuwa na watumwa watano au sita.
Na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipojulishwa habari hizo alisikitika mno na akasema,
“Laiti kama nyie mngelikuwa mmenijulisheni kabla kuwa mtu huyo amewafanya watoto na wenye nyumba yake kuwa muhtaji (ni watu wenye kuhitaji misaada na sadaka) basi mimi kamwe nisingelikubali mtu huyu azikwe katika makaburi ya Waislam.’
Hlafu anaedelea kusema kuwa wazee wetu wamenakili riwaya kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa mtoaji sadaka inambidi kwanza awatimizie mahitaji ya wale wanao mtegemea yeye; na wale ndugu na jamaa walio wakaribu zaidi ndio awape kwanza (yaani wazazi, mke, watoto na ndugu zake na majamaa wanaofuatia wa karibu zaidi) na baada ya hapo majamaa na ndugu wenye uhusiano wenye ujamaa nao wa mbali ndio wapewe”.
1.
Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. Amenakiliwa hadithi yake moja isemayo kuwa:
“Wakati muwapapo sadaka masikini muwaombe wawaombeeni dua, na akaendelea kusema, baadaye kuubusu mkono wa yule uliyemsaidia (uliyempa sadaka) kwa sababu sadaka unayoitoa kwanza inakwenda katika mikono ya Allah swt ndipo inapoingia katika mikono ya mwombaji.
Kama vile Allah
swt anavyosema katika Qur’an Tukufu,
Surah Tawba, 9, Ayah 104
Je hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali sadaqah , na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu?
2.
Ahmad bin Fahad anaandika
katika kitabu chake kuwa:
“ Al Imam Zaynul 'Abediin bin Hussein bin 'Ali bin Abi Talib a.s. wakati wa kutoa sadaka alikuwa akiubusu mkono wake mwenyewe, na mtu mmoja alimwuuliza sababu ya kufanya hivyo na Al Imam Zaynul 'Abediin bin Hussein bin 'Ali bin Abi Talib a.s. alimjibu,
“Kwa sababu kufanya hivyo ni kwamba sadaka kwanza inakwenda katika mkono wa Allah swt ndipo baadaye huishia katika mkono wa mwombaji.”
3.
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Sadaka
inayotolewa na muumin kwa hakika inafika mikononi mwa Allah swt na baadaye ndio
anapewa aliye mwombaji. Na akaendelea kuelezea ayah ya Qur’an Tukufu, Surah Tawba, 9, Ayah 104.
Je hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali sadaqah , na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu?
4.
Jabir Al J’ufi
amenakili riwaya kutoka Al Imam Muhammad
al-Baquir a.s. kuwa Al Imam Amir al-Muuminiin ‘Ali bin Abi Talib
a.s. amesema kuwa:
“Siku moja nilitoa sadaka ya Dinar moja, hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akaniambia,
“Je unajua sadaka inapotolewa na mkono wa muumin kabla yake yeye anakuwa amejitoa nje ya mitego ya masheitani sabini? Na kabla ya yule mwombaji hajapokea hiyo sadaka inakwenda katika mikono ya Allah swt?
Allah swt
anatuambia katika Qur’an Tukufu, Surah Tawba,
9, Ayah 104.
Je hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali sadaqah , na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu?
5.
Mu’alla bin
Hunais ananakili riwaya moja kutoka Al
Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa amesema:
“Kila kitu Allah swt amekiwekea mtunza hesabu wake, isipokuwa sadaka tu, kwamba yeye ndyeo mwenyewe anayeishughulikia. Na baba yangu a.s. alipokuwa akimpa masikini au mwombaji sadaka yoyote, alikuwa akiichukua tena akawa akiinusa na kuibusu na tena alikuwa akimrudishia mwombaji mikononi mwake kwa heshima na adabu.
Kwa sababu sadaka anayopewa mwombaji kwanza inakuwa imepitia katika mikono ya Allah swt ndipo inapoishia katika mikono ya yule anayeomba. Kwa hiyo mimi pia nimependelea kukibusu kitu kile ambacho kimeshaingia katika mikono ya Allah swt ndipo kikaenda katika mkono wa mwombaji!”
6.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Kwa kila kitu isipokuwa sadaka tu Allah swt amemweka Malaika kutunza habari zake – na sadaka ameiweka katika usimamizi wake mwenyewe.”
7.
Muhammad bin
Muslim ameripoti riwaya moja ama kutokea
Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. au
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:
“Al Imam Zaynul 'Abediin bin Hussein bin 'Ali bin Abi Talib a.s. kila alipokuwa akimpatia sadaka mwombaji basi alikuwa akiibusu mikono ya mwombaji huyo. Na alitokezea mtu akauliza sababu ya kufanya hivyo naye akajibu kwa sababu inatoka kwenye mikono ya Allah swt na inaingia katika mikono ya mwanadamu huyo mwombaji.”
1. Siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliijiwa na mtu mmoja ambaye akasema:
“Je kuna yeyote yule atakayeweza kunisaidia kwa kunikopa? Mmoja katika
Ma-Ansaar akainuka na kusema :
‘Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Mimi nina uwezo wa kumkopesha”.
Basi kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia:
“Mpe mifuko minne ya tende huyu mwombaji. Kwa
kusikia hayo huyo Ansaar akampa mwombaji
Baada ya kupita muda ,huyo Ansaar alimwijia
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kwa kufanya madai ya mifuko minne ya tende
aliyokuwa amemkopesha Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambayo Mtume alimpa mtu
sadaka, basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia Inshaallah basi
nitakutimizia. Na ikafika mara tatu huyu mtu akawa anakuja kuomba alipwe deni
Mwishoni huyo mtu akashidwa kusubiri na katika hali hiyo akasema,
“Ewe Mtume wa Allah swt! Inshaallah, nimeisikia mara nyingi vya kutosha.!”
Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akacheka na kuwageukia na Ma-Sahaba na kuwauliza,
“Je kuna yeyote miongoni mwenu ambaye anaweza kunikopesha?”
Basi mtu mmoja akainuka na kusema,
“Ewe Mtume wa Allah swt! Naomba ukope kwangu”
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kwa hayo akamwambia
“Je una kiasi gani?”
Na huyu katika kumjibu akamwambia
“Kiasi chochote utakacho kihitaji wewe.”
Hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia
“Mpe mifuko minane huyu Ansaari.”
Huyo Ansaar akasema
“Ewe Mtume wa Allah swt! Mimi nilikukopa mifuko minne tu, sasa kwa nini unanirudishia mifuko minane?”
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamjibu
“Mifuko minne ninakulipa na mifuko minne zaidi ninakuongezea zawadi kwa ajili yako.”
2.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema :
“Kwa hakika sadaka inayotolewa kwa moyo mkunjufu inalipia deni, na inaleta mfululizo wa baraka.”
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Mtu yeyote atakayeomba chochote bila ya kuwa na dharura yake, basi Allah swt atamfanya awe muhtaji kwa maswala hayo kabla ya kufa kwake, na kwa sababu ya kuomba kwake huku kusikostahiki, yeye ataadhibiwa na kutupwa Jahannam [52].”
2. Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali
ibn Abi Talib a.s. amesema:
“Kwa Allah swt amekula kiapo kuwa mtu yeyote bila ya kuwa na shida au dharura kama atamwomba mtu amsaidie, basi kuomba kwake huko kutamfanya yeye lazima siku moja awe mwombaji.”
3. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa akisema:
“Enyi watu mfuate na kutekeleza nasiha za
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.,
“Iwapo mtu yeyote atajifungulia milango ya kuomba, basi Allah swt atamfungulia milango ya ufukara na umaskini.”
4. Muhammad ibn Muslim ananakili riwaya kutoka
kwa Al Imam Muhammad
al- Baquir a.s. kuwa amesema:
“Ewe Muhammad! Iwapo waombaji wangelielewa
mabaya katika kuomba, basi kamwe wasingeweka mikono
5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Mtu yeyote ambaye ana maslahi ya vyakula vya kujitosheleza kwa muda wa siku tatu na pamoja na hayo anaendelea kuomba basi mtu huyo siku ya Qiyama atakuja mbele ya Allah swt huku uso wake utakuwa hauna nyama.”
6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Bila ya kuwa na dhiki na shida mwenye kula kwa kuomba basi ni sawa na mtu anayekunywa pombe.”
7. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:
“Mimi kwa kiapo cha Allah swt ninasema kuwa ni ukweli kabisa kuwa yeyote atakayeilisha nafsi yake kwa kujifungulia milango ya kuomba, basi Allah swt lazima atamfungulia milango ya ufukara na umaskini”
8. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Mtu yeyote anayejifungulia mlango wa kuomba, wakati anao uwezo wa kujilisha mwenyewe basi Allah swt atamfungulia milango sabini ya ufukara na umaskini, kiasi kwamba hakuna yeyote atakayeweza kuufunga hata mlango wake mdogo kabisa.”
9. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Mtu yeyote ambaye ataunyoosha mkono wake kwa
kuomba huku ana chakujitosheleza kwa siku moja pia, basi huyo mtu atahesabiwa
miongoni mwa wafujaji.”
10. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Siku ya Qiyama Allah swt hatawaangalia watu
wa aina tatu na wala hatawatakasisha na watu
· Kwanza ni mwanaume yule ambaye anafanya ulawiti,
· mwanamke yule ambaye hakubakia na haya yoyote na
· tatu ambaye pamoja na kuwa na mali bado anaendelea kuomba kwa watu.”
1. Muhammad bin
Muslim ameripoti riwaya kutoka kwa Al
Imam Muhammad
al-Baquir a.s. kuwa amesema:
“Ewe Muhammad !
kuomba.”
2. Al
Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Ole
wenu ! Kamwe msiwanyooshee watu mikono yenu kwa ajili ya kuwaomba kwani
itawadhalilisheni duniani, na mtakuwa mkijitafutia dhiki na shida na siku ya Qiyama
mtasimamishwa katika mazingara magumu kujibu mahesabu yake.”
3. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Mikono iko aina tatu,
· kwanza ni mkono ulio juu kabisa ambao ni wa Allah swt.
· Mkono wa pili ni ule ambao ni wa mtoaji na
· wa tatu ni wa yule wa mpokeaji ambao ni wa chini kabisa.
Kila ikiwezekana mjaribu kujiepusha na kuomba, kwa sababu hiyo itakuwa ni vizuizi katika riziki yenu hapo mbeleni.
Iwapo mtu atapenda kuinusuru na kuihifadhi na kuilinda heshim na aibu yake basi anaweza kujichumia na kujitafutia riziki yake mwenyewe kwani kunakuwapo na pazia mbele ya riziki..
Kwa kiapo cha Allah swt ambaye roho yangu iko mikononi mwake, iwapo mtu akienda msituni ambapo akakata kuni na siku hiyo hiyo akaziuza au kubadilishana kwa tende na sehemu moja ya tende hizo akajiwekea yeye kumalizia shida zake na sehemu mbili akizigawa katika kuwasaidia wengine katika njia ya Allah swt, basi kwa hakika matendo yake haya ni bora na afadhali kabisa kuliko kunyoosha mikono yake mbele ya watu kwa ajili ya kuomba, kwani pengine wao watampa kidogo au chochote na wengine watamdanganya na kumdharau au na hata kumdhalilisha.”
4. Abu Basir ameripoti riwaya kutoka Al Imam
Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:
“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliijiwa na
baadhi ya watu kutoka makabila ya Ansaar ambao baada ya kutoa salamu waliketi,
na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliwajibu salamu
Wao wakasema ewe Mtume wa Allah swt sisi tuna ombi letu moja. Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akawaambia wamwambie. Nao wakasema ni haja yetu moja kubwa kabisa. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kwa kusikia hayo akasema nawaombeni mniambie ili niweze kujua. Wao wakaanza kusema, ombi letu ni kwamba tunakuomba wewe uchukue dhamana yetu ya ya kuingia Jannat (Peponi).
Kwa kusika hayo Mtume Muhammad Mustafa
s.a.w.w. alikiinamisha kichwa chake, na kutumia vidole vyake alianza
“Ninaweza kuwapa dhamana hiyo kwa masharti kwamba kamwe katika mazingira yoyote yale nyie hamtamwomba mtu yeyote kitu chochote.”
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa hao
watu hali
5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Allah swt anamrehemu yule mja wake ambaye amebakia katika heshima utoharifu na katika desturi zake njema, na ambaye amejiokoa na hakuomba kwa hakika kuomba kunaleta udhalilisho duniani, na uelewe wazi kuwa watu humu duniani kamwe hawataweza kummalizia shida zake zote. Na hapo baadaye Imam a.s. akaelezea kisa kimoja kwa kifupi cha Hatim:
Wakati nafsi za watu zinapo kata tamaa kwa watu basi hapo kwa hakika yanaingia katika shida na taabu kubwa, na kwa uhakika tamaa ndio ufakiri mkubwa na tamaa ndiyo ufukara mkubwa.”
6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kwa kupitia Ma-Imamu a.s. ameripoti riwaya kuwa:
“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwusia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.,
“Ewe Ali ! Ni rahisi kabisa kuutia mkono wako katika mdomo wa nyoka mkubwa kuliko kumyooshea mkono yule ambaye alikuwa hayupo duniani na akaja akazaliwa baadaye.”
Na akamwambia Abu Dhar:
“Ewe
7. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Msiwe miongoni mwa watu wasio wajali watu,
msiwe
8. Katika kitabu Thawabul
A’amal imeandikwa riwaya ya Al
Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye amesema:
“Allah swt anamrehemu yule mtu ambaye ameweka desturi na tabia zake kitakatifu na amejizuia kwa njia zote asiombe kwa watu. Kwa hakika kuomba ni kudhalilika na kujidhalilisha duniani na hakuna duniani wale watu watakaoweza kumtimizia haja yake.”
9. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amesema:
“Allah swt amemfanya Mtume Ibrahim a.s. kuwa Khalil wake (Rafiki wake) kwa sababu yeye kamwe hakulitupilia mbali jambo ambalo alimwomba yeye na yeye mwenyewe kamwe hakumnyooshea mtu yeyote mikono yake isipokuwa kwa Allah swt.”
10. Imeripotiwa riwaya
kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema
kuwa:
“Allah swt bila shaka anawachukia
11.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Msiwaombe ndugu zenu mahitaji yenu, isitokee kwamba wao wakakataa kukutimizia maombi yako, na nyie mkachukia na mkaingia katika kukufuru.”
12.
Bwana Salman Al-Farsi r.a. anasema kuwa :
“Mpenzi wangu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amefanya usia na kusisitiza kabisa kuwa, mimi nisipuuzie mambo saba.
· Ya kwanza yeyote yule aliye mkubwa kuliko mimi nisimtupie macho yangu, bali nimtupie macho yule ambaye yuko chini yangu;
· niwe na mapenzi na maskini na
· niwe karibu nao,
· niseme ukweli daima hata kama utakuwa mchungu,
· niwatendee mema na kuwahurumia ndugu na majamaa zangu, hata kama yule nimfanyiaye hayo atanigeuzia mgongo,
· kamwe nisiunyooshe mkono wangu mbele ya watu kuwaomba na vile vile ameniusia kuwa
· daima niwe nikisema La Haula Wala Quwwata Illa bilahil ‘Aliyyil ‘Adhiim kwani hiyo ni hazina mojawapo katika hazina za Jannat.”
13. Al
Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Nahaj-ul-Balagha anasema:
“Muwe mkiziachia matamanio na mahitajio yenu kuliko kuwaomba waovu na wasio stahiki. Na akaendelea kusema na utakatifu na utukufu ni sifa moja ya kupendeza ya mafakiri, na hakika urembo wa shida na dhiki ni kushukuru.”
14. Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. amesema:
“Ujue kuwa uso wako unaong’ara kwa heshima na adabu, na wewe wakati unapokwenda kuomba na ukarefusha mikono yako kwa ajili ya kuomba basi heshima na adabu hiyo inayeyuka na kuanza kudondoka kutoka usoni mwako. Sasa ni kuangalia uyeyukaji huo unamdondokea nani ndio wewe unatakiwa ujue uangalie na ujue.”
15.
Ibn Fahad
ameripoti riwaya kutoka Al Imam Ja'afer
as-Sadiq a.s. kuwa:
“Shi’a wetu
hata
16.
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Mtu yeyote anayenyoosha mkono wake na kufungua kiganja chake kwa ajili ya kuomba, basi ushahidi wake utupiliwe mbali.”
17.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Iwapo mwombaji
angelikuwa akijua yale majukumu na wajibu walio nao katika kufanya hivyo, basi
kamwe asingeomba chochote kwa mtu yeyote. Na vile vile na kutokumpa mwombaji
pia kuna majukumu na wajibu mkubwa
18.
Siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliwaambia
Ma-Sahaba wake:
“Ni kwa nini hamfanyi bay’a yangu (utiifu wangu)?”
Basi Ma-Sahaba wakamjibu:
“Ewe Mtume wa Allah swt! Sisi tumeshakwisha kufanya bay’a yako tangu mwanzoni. Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema, mfanye bay’a katika swala ambalo mle kiapo kuwa nyinyi kamwe hamtanyoosha mikono yenu kwa wengine kwa ajili ya kuomba. Na baada ya kula viapo hivyo ikaonekana mandhari tofauti kabisa miongoni mwa Ma-Sahaba kiasi kwamba hata mtu alipokuwa akidondosha mkongojo wake basi alikuwa akiteremka kutoka usafiri wake wa mnyama kama ngamia n.k. kuteremka chini na kujiokotea mkonojo wake, na kamwe alikuwa hamwambii mtu mwingine amwokotee na kumpa hiyo bakora yake iliyoanguka”
19.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Iwapo mtu
atakwenda mbio mbio msituni akakata kuni na mzigo huo akauchukua kuja nao kwa
hiyo atakuwa ametunza heshima na hadhi yake, basi jambo
20.
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Yeyote yule aliyetuomba sisi tunampa na yeyote yule aliyetoa na yeyote yule aliye shukuru basi Allah swt atamfanya awe tajiri.”
21.
Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:
“Kwa kuwaomba watu mahitajio yako ni kuteketeza na kuangamiza heshima yako ni sawa na kuteketeza na kuangamiza heshima yako, na vile vile ustahi wako pia unamalizika. Na kwa hakika kile walichonacho wao utajiri wao inambidi mtu akate tamaa asitegemee chochote yaani asiwe na tamaa ya aina yoyote na hakika hii ndio inayo hesabika kuwa ni heshima kubwa ya muumin. Kumbukeni kuwa tamaa ni ufakiri wa aina mojawapo.”
22.
Ja’bir
amenakili riwaya kutoka Al Imam Ja'afer
as-Sadiq a.s. kuwa amesema:
“Allah swt ameweka karaha kwa wale wanao omba kwa kung’angania na kwa kufuatilia.”
1.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Enyi watu! Msiombe wakati watu wanapokuwa katika makundi, isitokee kwamba kwa sababu ya ubahili wao ikawawia nyie machungu.”
1.
Mufadhdhal bin Kais bin Rumman anasema kuwa:
“Yeye siku moja alikuwa katika huduma ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., na mimi nikamdokezea kidogo kuhusu matatizo niliyokuwa nayo. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia kijakazi wake:
Naomba ule mfuko. Na akaniambia Abu Ja’afar (Manthur) amenitumia hizi Dinar mia nne kwa ajili ya msaada, hivyo chukua wewe. Na uende ukamalize shida na dhiki uliyo nayo.”
Nami nikamwambia:
“Hapana! Kwa kiapo cha Allah swt mimi niwe fidia juu yako – mimi sina nia hivyo – mimi nilikuwa natarajia kuwa wewe uniombee dua kwa Allah swt ili shida na dhiki niliyonayo isiniwie ngumu bali iwe nyepesi.”
Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akasema,
“Pamoja na mimi kukuombea dua, kamwe usiwaambie mbele ya umati wa watu shida zako kwani kwa kufanya hivyo wewe utapoteza heshima na hadhi yako.”
2.
Harith
Hamdani anasema kuwa yeye amesikia hadithi ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kutokea kwa Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. kuwa:
“Maombi ni amana za Allah swt katika vifua vya watu na yeyote yule atakayeficha siri hiyo basi atapata thawabu za ibada.”
3. Kulayni anasema kuwa Bwana Luqman alikuwa akimpa mafunzo mwanake kwa kumwambia:
“Ewe mwanangu, mimi nimeisha kunywa dawa na magamba yaliyo chungu kabisa, lakini mbele ya shida na dhiki hakuna kitu kinachozidi uchungu wake. Iwapo wewe utapitia katika hali kama hiyo, basi kamwe usiseme maombi yako mbele ya watu, kwa sababu wewe katika macho yao utaanguka heshima na taadhima yako, na watu hao hawawezi kukufaidisha chochote na badala yake nakuomba umwombe yule ambaye anakujaribu kwa mitihani ya aina hiyo, na bila shaka ni yeye tu anayeweza kukuondolea matatizo na dhiki iliyokukabili, hivyo umwombe yeye tu (Allah swt). Yeye ni nani duniani ambaye amemwomba Allah swt na akarudi mikono mitupu, na yupo ambaye aliweka matarajio na matumaini yake kwa Allah swt na akajikuta ametoka mtupu?”
4.
Imeripotiwa
kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa
amesema:
“Ewe 'Ali! Allah swt ameweka ni amana miongoni mwa waja wake katika hali ya shida na ufukara, na yeyote yule atakayeweza kuificha hiyo amana basi ajue kuwa yeye ni mtu ambaye amedumisha ‘ibada na anapata fadhila za wale walio dumisha ‘ibada na wanao funga saumu, lakini yeyote yule ambaye anaitoboa na kuitangaza hiyo amana ya Allah swt kwa kudhihirisha na kufanya bayana siri ya shida na ufukara wake kwa wengine, na hao watu baada ya kumsikiliza hawamsaidii basi mjue kuwa huyo mtu kwa hakika wamemuua. Mauaji haya sio kwa upanga au kwa mkuki bali ameuawa kimoyo.”
5.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwaya kutoka Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa amesema:
“Enyi wenye
shida na masikini! Tunzeni heshima zenu na mpeni Allah swt furaha ya mioyo zenu
ili kwamba Allah swt awalipe mema kwa ufukara na shida zinazo wakabili na
1.
Imenakiliwa
riwaya kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq
a.s. amesema kuwa:
“Itakapo tokea miongoni mwenu mtu akazingirwa kabisa kwa hali mbaya, basi inambidi awajulishe jamaa na ndugu zake na asiiweke nafsi yake katika shida.”
2.
Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. amesema katika Nahaj –ul – Balagha kuwa:
“Mtu yeyote atakayemwambia mahitaji yake dharura zake kwa muumin basi ajue kuwa ameweka habari zake hizo kwa Allah swt, na yeyote yule atakayeleta dharura na mahitajio yake kwa kafiri basi ajue kuwa amekwenda kinyume na maamrisho ya Allah swt.”
3.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Katika hali tatu tu ndipo kunapo ruhusiwa kuomba ama sivyo hairuhusiwi.
· Kwanza katika kujinusuru mtu mwenyewe,
· kujinusuru na hasara kubwa kabisa ya mali na
·
tatu iwapo kwa
kutokuomba kutakuja kumpatia udhalilisho wa hali ya juu
4.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa:
“Mtu mmoja alimwijia Al Imam Hassan ibn 'Ali bin Abi Talib a.s. na kuomba chochote: Kwa hayo Imam a.s. akamwambia haistahiki kuomba isipokuwepo hizo sura tatu.
· Kwanza ama kuzuia umwagikaji wa damu,
· ama mtu akiwa na shida ya hali ya juu kabisa au
·
kujizuia kuja
kudhalilika vibaya
Sasa hebu wewe niambie wewe upo katika sura ipi kati ya hizi tatu?
Yeye akasema ‘Ewe mwana wa Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w.! Katika sura tatu ulizozitaja ipo mojawapo. Basi bila kusita
kwa haraka
1.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Heshima ya muumin ni kule kuamka kwa ajili ya sala za usiku, na vile vile heshima yake ni kule kutokuwa mwombaji wa watu.”
2.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwaya kutoka kwa
Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. kuwa amesema:
“Wewe lazima uwe na moyo wa kuishi vyema na watu na kuwaheshimu na kutosheka nao. Na kuishi nao vyema ni kule kuongea nao kwa upole na utamu na uwe na uso wenye tabasamu na uishi nao vile kwamba kila wakuonapo uwe ukionyesha furaha usoni mwako na hivyo utakuwa umejiwekea heshima katika jamii.”
3.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema:
“Iwapo kutatokezea miongoni mwenu anayemtegemea Allah swt azikubalie kila dua zake anazoziomba basi awe akiishi na watu wote kwa wema na kamwe asimtegemee mtu yeyote isipokuwa Allah swt peke yake na atakapo jiona kuwa yeye kwa hakika anao moyo kama huo basi atambue wazi kuwa chochote kile atakachomwomba Allah swt atampatia na kumjaalia.”
4.
Al Imam Zaynul 'Abediin bin Hussein bin 'Ali ibn Abi
Talib a.s. anasema kuwa:
“Iwapo mtu atataka wema wote kwa ajili yake ni kwamba yeye ajiepushe mbali na tamaa za kila aina ya kutamani yale waliyonayo watu, na kama yeye ana matamanio yoyote au maombi yoyote basi asiwategemee hawa watu bali zote azielekeze kwa moyo mkunjufu na halisi kwa Allah swt na lazima Allah swt atazikubalia dua na maombi yake na atamtimizia.”
5.
Abul A’ala bin A’ayan anasema
kuwa mimi nimemusikia Al Imam Ja'afer
as-Sadiq a.s. akisema:
“Enyi watu nyie mtajidhuru pale mtakapo peleka maombi yenu na mahitaji yenu kwa watu, na kwa hakika inafukuzia mbali heshima na adabu. Mkae na watu katika hali ya kuridhika na kuwa na uhusiano nao mzuri na kwa hakika hiyo ndiyo kwa ajili ya usalama. Kwa hakika tamaa yenu ndiyo dalili ya ufakiri wenu.”
6.
Ahmad bin
Muhammad bin Abi Nassr anasema kuwa yeye siku moja alimwambia Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. :
“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Ninaomba uniandikie barua moja kwa Ismail bin Daud, ili kwamba niweze kupata chochote kutoka kwake. Kwa hayo Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. akamwambia iwapo mimi kitu unachokitaka au cha kukutosheleza wewe ningekuwa nimekukataa, ndipo ningekuandikia, ama sivyo uchukue kile nilicho nacho mimi kwangu na ukitegemee hicho.”
7.
Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:
“Kwa hakika yale waliyonayo watu katika uwezo wao na kuridhika nayo ndimo humo kuna heshima ya muumin ya imani yake, je nyie hamjaisikia kauli ya Hatim? Hatim alisema kuwa pale mtakapoona nafsi zenu zimevutiwa kwa mali za watu wengine basi muelewe kuwa shida na taabu ziko zinawakaribia, na kwa hakika tamaa ni ufakiri ulio dhahiri.”
8.
Abdullah Bin
Sinan anasema kuwa yeye amemsikia Al
Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akisema:
“Kwa ajili ya muumin mapendezi ya dunia na akhera yako katika mambo matatu.
· Kwanza ni sala katika sehemu ya mwisho wa usiku,
· kutokuvutiwa na kutokuwa na husuda na mali na miliki wanayomiliki watu wengine na
· kuwa mwaminifu na mtiifu kwa ukamilifu wa Ahlul Bayt a.s. na mapenzi yao.”
9.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Alikuwapo mtu mmoja mbele ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na akamwuliza, ‘Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! naomba unionyeshe unieleze jambo moja nilifanye jambo ambalo Allah swt atakuwa radhi pamoja nami. Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimujibu:
Udumishe amani na upendo katika utamaduni wa
dunia, jambo ambalo kimatokeo utapata mapenzi ya Allah swt na usiwe na kijicho
na wivu wala tamaa kwa
10.
Ja’bir bin
Yazid ananakili riwaya kutoka kwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. kuwa
amesema:
“Usiwe na wivu choyo wala tamaa kwa
1.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema:
“Allah swt amechukia hafurahishwi na sifa sita na vile vile mimi sizifurahii hizo sifa sita na ndio nimefanya usia kwa mawasii na waumini wote kuwa vitu hivyo sita wajiepushe navyo na mojawapo ni kule baada ya kutoa sadaka mtu akaanza kumsema na kuvisema.”
a. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Baada ya kutenda mema mtu atakapovizungumzia hayo basi atayateketeza mema yake yote.”
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwaya kutoka kwa
Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. kuwa:
“Allah swt hakupendezewa na mambo sita na mimi vile vile katika kizazi changu Maimam wote sikupenda kutokezee sifa hizo, na vile vile Maimam pia nimewahusia kuwa wasizipende sifa hizo ziwepo katika muumin. Hivyo kila muumin anabidi ajiepushe na sifa hizo. Katika sifa hizo sita mojawapo ni ile baada ya kumfanyia mtu wema mtu anaanza kuyazungumzia huku na pale.”
4.
Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. anasema kuwa Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Allah swt hapendi sifa sita na hizo sifa sita mimi sikupendezewa kwa ajili ya mawasii watakao nifuata na waumini wote watakaonifuatia.
· Kwanza kusali isivyo kwa makini,
· pili katika hali ya saumu kujamiiana na mwanamke,
· tatu baada ya kutoa sadaka kutangaza na kuonyesha.
· Nne kuingia msikitini katika hali ya Janaba,
· kuwa na shauku ya kutaka kujua mambo ya watu majumbani mwao kunatendeka na kunaendelea nini, na
· sita kucheka makaburini mtu anapokuwa baina ya makaburi mawili.”
5.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kwa mamlaka yake amenakili riwaya kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa:
“Mtu yeyote atakaye msaidia muumin ndugu yake
na baadaye akaja akamwambia kuhusu wema huo akausema basi Allah swt hulirudisha
tendo
Na Imam a.s. aliendelea kusema: “Kwa sababu Allah swt anasema kuwa yeye ameiharamisha Jannat kwa ajili ya yule anayesema baada ya kutenda tendo jema na bahili na mchonganishi.
Muelewa wazi kuwa yule mtoa sadaka, hata anayetoa kiasi cha Dirham moja, basi Allah swt humlipa zaidi ya ukubwa wa mlima wa Uhud kwa neema za Jannat na yeyote yule atakaye saidia kufikisha hiyo sadaka kwa yule ambaye anahitaji basi Allah swt atamlipa mema hayo hayo, na kamwe hakutakuwa na punguzo lolote katika neema za Allah swt kwa ajili ya wote hao.”
6.
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika hotuba yake alisema:
“Yeyote yule atakaye tenda wema na kuwawia
wema ndugu wenzake, na akaanza kutanganza mema aliyoyafanya basi matendo ya
watu
Allah swt amewaharamishia Jannat watu wafuatao:
· Kwanza ni wale wanao tangaza mema waliyowafanyia watu wenzao, na
· Wale wanaowapotosha watu wengine,
· wafitini,
· wanywaji wa pombe,
· wale wanao tafuta makosa ya watu na aibu za watu,
· wale wenye tabia mbaya,
· wale walio makatili kwa wenzao na vile vile
· wale watu wanao watuhumu watu wengine kwa tuhuma za kuwazushia maovu.”
7.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwaya kutoka kwa mababu zake kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Allah swt amewazuieni nyinyi kwa matendo maovu takriban ishirini na manne na mojawapo ni jambo lile ambalo baada ya kutoa sadaka mtoaji anamwambia maneno aliyempatia.”
8. Bwana Abu Zahar Al Ghafar amenakili
riwaya kutoka Mtume Muhammad Mustafa
s.a.w.w. kuwa:
“Kuna aina tatu ya watu ambao Allah swt kamwe hatazungumza nao siku ya Qiyama.
· Kwanza ni yule mtu ambaye hatoi kitu chochote bila ya kumsema au kumwambia yule anayempa, na
· pili ni yule ambaye hachukui jukumu wala haoni umuhimu wa kuficha zehemu zake za siri na wa
· tatu ni yule ambaye anauza mali yake na kutaka faida kupindukia kiasi.”
9.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Mtu yeyote baada ya kumsaidia muumin
atamuudhi kwa kumwambia au kwa kumsengenya kiasi kwamba roho yake ikaumia basi
Allah swt huibatilisha sadaka na wema
10.
Al Imam Ja'afer
as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Aina tatu ya watu kamwe hawataingia Jannat.
· Moja ni yule ambaye wazazi wake wamemfanya Aak, wa
· pili mnywaji wa pombe (daima anakunywa pombe) na
· tatu ni yule baada ya kufanya mema huanza kusema na kutangaza.”
1.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. siku moja alimtumia mifuko mitano za Tende za Baqi’ (Jannatul Baqi’, ipo Madina ). Mtu huyo alikuwa muhtaji mwenye shida na daima alikuwa akitegemea msaada kutoka kwa Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s., na kamwe alikuwa harefushi mikono yake kwa wengine kwa ajili ya kuomba kwa watu wengineo. Mtu mmoja alipo yaona hayo basi alimwambia Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s.:
“Kwa kiapo cha Allah swt, huyu mtu hajakuomba chochote wewe kwa hivyo badala ya kumpa mifuko mitano mfuko mmoja tu ulikuwa ukitosha, na kwa hayo Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. akamwambia:
“Allah swt asiongezee idadi ya muumin
Mtu ambaye hathamini hajali shida za muumini
wengineo itakuwaje ategemee Jannat wakati huku yeye mwenyewe anafanya ubahili
katika
Yule asemaye daima “Ewe Allah swt wasamehe madhambi yao yote waume kwa wanawake Waislam” kwa hakika mtu kama huyu huwa anategemea Jannat tu je ni uadilifu gani kwa kusema tu kwa mdomo kuwaombea mema watu ambapo wao hawawafai watu wengine wanapokuwa na shida na dhiki huku wakiwa wanafanya ubahili kwa mali zao?”
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Kwa hakika uwema ni ule ambao mtu anamsaidia mtu kabla hajaombwa, na kumpa baada ya kujua hali yake inamaanisha umempa baada ya kujua hivyo. Inawezekana maskini huyo mtu usiku kucha akawa anatapatapa iwapo atafanikiwa au hatafanikiwa, huku akiwa amejawa mawazo niende kwa nani nisiende kwa nani, na hatimaye moyo ukiwa unadunda mwili ukiwa unatetemeka na akiwa amejawa na aibu kubwa anatokezea mbele yako.”
2. Yas’ab bin Hamza anasema
kuwa:
“Mimi siku moja nilikuwa pamoja na Al Imam
Musa al-Kadhim a.s., watu walikuwa wamekaa huku wamemzunguka, yaani watu wengi
walikuwapo. Watu walikuwa wakiulizia masuala ya halali na haramu, na mara
tukaona akaingia mtu mmoja mrefu na akaanza kusema, “Iwe salamu juu yako ewe
mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Mimi ni mpenzi na mfuasi wako wewe
na baba na mababu zako, na hivi nimerudi kutoka Hijja Tukufu. Mimi nimeibiwa
Imam a.s. akamwambia:
“Naomba ukae kidogo upumzike, Allah swt akurehemu. Na Imam a.s. aliendelea na mazungumzo yake pamoja na umati uliokuwa pale katika kuulizana na kueleweshana kuhusu maswala mbalimbali. Hatimaye mimi Khaysama na Suleiman Al-Ja’afari ndio tuliokuwa tumebakia na hapo Imam a.s. kwa kuniangalia mimi akasema:
“Je unaniruhusu mimi niende chumbani kwangu?”
Suleiman akasema
“Allah swt aiendeleze amri yako”.
Hapo Imam a.s. aliinuka na kuelekea katika chumba chake a baada ya muda si muda akatoka nje akafunga mlango na mwenyewe akasimama nyuma ya mlango na akatoa mkono tu nje huku akisema, je huyo msafiri kutoka Khurasan yuko wapi?”
Hapo mimi nikamjibu:
“Ya Imam a.s.! Mimi niko hapa.”
Na kwa hayo Imam a.s. akamwambia”
“Nimekupa hizi Dinar mia mbili ambazo
zitakusaidia wewe katika gharama na matumizi ya safari yako na vile vile
napenda nikujulishe kuwa hakuna haja tena ya hizi pesa kuzitolea sadaka ufikapo nyumbani kwako,
Seleiman Al-Ja’afar akauliza:
“Niwe fidia juu yako ewe Mwana wa Mtume s.a.w.w.! Kwa hakika wewe umefanya wema na ihsani mkubwa sana wenye huruma, lakini pamoja na hayo kwa nini umejificha?”
Kwa hayo Imam a.s. akamjibu
“Hakuna sababu nyingine ila sikutaka kuona uso wa mwombaji ukiwa umeingiwa na aibu na unyonge sababu ya kuomba. Je wewe hujaisikia hadith ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambamo amesema, kwa yeyote yule anayeficha wema hulipwa thawabu za Hijja sabini na yeyote yule baada ya kutenda maasi na madhambi anatangaza basi daima hubakia dhalili. Na yeyote yule anayeficha madhambi na maovu basi Allah swt humsamehe.”
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Jambo jema kabisa linalonisaidia mimi katika
kufanya wema katika kuwasaidia ni mkono ambao unawafikishia na mkono mwingine
unashirikiana naye. Na kwa hakika hao wanaokuja kuomba wanakuja na maombi
Wakati unapokuijia mtihani kwako kwa heshima zako pia inabidi uombe,
Basi uende kwa mtu mmoja aliye mkuu na aliye Sharifu kwa ajili ya kuomba kwake.
Kwa hakika, huyo mtu Sharifu na mkuu atakapokusaidia basi humo ndani hakutakuwa na maonyesho wala masengenyo, na badala yake ndani kutakuwa na unyenyekevu na kuhuzunika pamoja nawe.
Kumbuka wakati utakapotaka kupima katika mzani uombaji na utoaji sadaka na mema basi utaona sahani ya mzani ya uombaji utakuwa daima ni mzito kuliko nyingine yote.”
2. Warram bin Abi Faras ameandika riwaya kutoka Al
Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:
“Wenye imani dalili zao ni nne,
· kwanza nyuso zao huwa zina bashasha,
· ndimi zao zinakuwa zenye ukarimu na mapenzi,
· nyoyo zao zinakuwa zimejaa huruma, na
· wanakuwa na mkono wenye kutoa mkono unaopendelea kutoa sadaka na misaada nk.”
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa Mtume Muhammad
Mustafa
s.a.w.w. alikuwa
akisema:
“Kila kila aina ya wema na huruma ni sadaka.”
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akizungumzia neno Ma’arufu katika Qur’an
Tukufu, Surah Nisah, 4, Ayah 114:
Hakuna heri katika mengi ya wanayo shauriana kwa siri, isipokuwa kwa yule anaye amrisha kutoa sadaqah, au kutenda mema, au kupatanisha baina ya watu. Na mwenye kufanya hayokwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, basi tutakuja mpa ujira mkubwa.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Kwa ma’arufu kuna maanisha kule mtu kutimiza wajibu wake aliofaradhishiwa.”
1. Siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliwasaidia waombaji watatu na wa nne
alipokuja hakumpa chochote. Na
hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akasema:
“Iwapo mtu atakuwa na Dirham elfu thelathini au arobaini na zote akazigawa kwa kusaidia au sadaka bila ya kubakiza chochote kwa ajili ya wana nyumba wake basi huyo mtu atakuwa mmoja miongoni mwa watu watatu ambao dua zao hazikubaliwi na Allah swt. Na katika watu hawa watatu: mmoja ni yule ambaye bila kutimiza wajibu wake anagawa mali yote kama sadaka au kusaidia, na baada ya hapo anakaa akiomba dua:
“Ewe Allah swt naomba unipe riziki.”
Basi hapo atajibiwa, “Je mimi nilikuwa sikukufanyia njia ya kujipatia riziki?”
2. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Bora ya sadaka zote ni ile kufanya wakati mtu anapofanya katika hali unapokuwa sawa.”
3. Hisham bin Al Muthanna anasema:
“Kuna mtu mmoja alimwuliza Al Imam Ja'afer
as-Sadiq a.s. kuhusu tafsiri ya ayah Surah An Am, 6, Ayah 141.
Na Yeye ndiye aliye ziumba bustani zenye kutambaa juu ya chanja, na zisio tambaa, na mitende, na mimea yenye matunda mbali mbali, na mizaituni na mikomamanga inayo fanana na isiyo fanana. Kuleni matunda yake inapo zaa, na toeni haki yake siku ya kuvunwa kwake. Wala msitumie kwa fujo. Hakika Yeye hawapendi watumiayo kwa fujo.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimjibu,
“Katika Ansaar alikuwako mtu mmoja (aliwapa
jina lao) ambaye alikuwa ana shamba. Pale mazao yake yalipokuwa yakiwa tayari
yeye alikuwa akigawa yote katika sadaka, na alikuwa hawapi chochote watoto na
wana nyumba yake; na kwa tendo
4. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Baada ya mtu kujitolea kile kiasi alicho na dharura nacho kwa mujibu wa mahitaji yake na baadaye katika kiasi kinachobaki akitoa sadaka basi hiyo sadaka ni bora kabisa.”
5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema:
“Mojawapo katika Nasiha na Mawaidha ya Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. ilikuwa ni kila aina ya wema ni sadaka mojawapo, na sadaka iliyo bora kabisa ni pale kutoa wakati mtu
ameshajitimizia wajibu wake na ametosheka, na mkumbuke kuwa muwape wale ambao
kwao nyie mnawajibika kuwatimizia mahitaji
Mkono wa mtoaji ni afadhali kuliko mkono wa
mpokeaji. Kwa hakika mtu ambaye anachuma kwa uwezo wake na kutumia kwa ajili
yake na kuwatimiza mahitaji
6. Mtu mmoja alimwijia Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na kumlalamikia
kuhusu njaa:
“Basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimtuma mmoja wa wake zake naye alipowaendea wakamwambia kuwa wao walikuwahawana chochote isipokuwa maji ya kunywa tu, na kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia, je kuna yeyote yule atakaye mchukua mtu huyu kuwa mgeni wake kwa usiku huo?”
Na kwa hayo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. akasema,
“Ewe Mtume wa Allah swt ! Mimi nakubali
kumchukua huyu
Kwa kusikia hayo Bi. Fatimah az-Zahra a.s. akasema, tuna chakula kiasi cha kuwalisha watoto wetu tu lakini na mgeni pia ana haki yake.”
Na hapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. akasema
“Wewe walaze watoto, na uizime taa.”
Asubuhi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alipokuja mbele ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwelezea kisa kilivyotokea na wakati bado akiwa anaelezea kisa hicho ayah ifuatayo iliteremshwa Surah Al Hashri, 59, ayah 9. :
Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala hawaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa (Wahajiri), bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.
1. Muhammad bin Yaqub Kuleiyni amenakili riwaya kutoka Abu Nasar kuwa yeye amesoma barua ambayo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alimwandikia
Abu Ja’afar (Mutawakili, mtawala wa Ki Abbasi). Humo kulikuwa kumeandikwa:
“Ewe Abu Ja’afar ! nimepata habari kuwa wewe unapotoka nje wakati umekaa juu ya usafiri wako basi wafanyakazi wako wanakutoa nje kwa kupitia mlango mdogo, ili kwamba yule ambaye ana shida na mwenye kuuhitaji msaada wako asiweze kufaidika hivyo.
Mimi kwa kiapo cha haki yangu ninakusihi kuwa
kutoka kwako na kuingia kwako uwe kupitia mlango mkubwa na uwe na wingi wa
dhahabu, fedha na
Na hii nakuambia kwa sababu iwapo wewe utafuata hivyo basi Allah swt atakuwia wema, hivyo utumie na usiwe na shaka katika ahadi na neema za Allah swt mmiliki wa malimwengu yote.”
1. Safwan anasema kuwa siku moja Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. alimwuliza mmoja wa wahudumu wake:
“Je leo mmetoa chochote katika njia ya Allah swt ?”
Naye alijibu hapana, leo sijatoa chochote bado.”
Kwa hayo Imam a.s. alisema
“Sasa usipotoa hivyo unategemea Allah swt
atupe baraka kwa misingi gani? Lazima utoe kwa njia ya Allah swt hata
1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Ayah ya Qur'an Surah Al-Hajj, 22 , Ayah 28:
“Allah swt katika ayah hii anamaanisha kuwalisha wale walio na shida na kuwasaidia, ambapo wao kwa heshima zao wenyewe hawajitokezi nje mbele ya watu kuomba.”
2. Isack bin Ammar
amenakili riwaya kutoka Al Imam Ja'afer
as-Sadiq a.s. kuwa:
“Utafika wakati mmoja ambapo waombaji
wanaorefusha mikono
Kwa hayo mimi nikamwuliza Imam a.s.,
“Ewe Maula ! Je yakitokea hayo katika zama za uhai wangu mimi nifanyeje?”
Kwa hayo Imam a.s akamjibu,
“Kwa hakika kile ulichonacho wewe uwasaidie
hao watu kwa hali na
1. Abu Basir anasema kuwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliitolea maelezo Ayah ya Qur'an Tukufu Surah Al Baqara, 2, ayah 267 isemayo
Enyi malio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa.
Amesema
kuwa:
“Zama kabla ya Islam watu walikuwa wamejilimbikizia mali iliyopatikana kwa njia zisizo halali (kwa njia zilizo haramu) na baada ya wao kusilimu, walikuwa wakidhani kuwa kwa kutoa mali iliyo patikana kwa njia haramu, watakuwa wametakasisha mali yao iliyo halali, kwa hivyo Allah swt alitoa amri kuwa sadaka itolewe kutoka mali iliyo halali tu.”
2. Kwa kuzungumzia
ayah hiyo ya juu Shahab amenakili riwaya kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:
“Ambamo amesema kulikuwa na kaumu moja ambayo
walikuwa na
3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Iwapo watu watachuma au watajipatia mali kwa mujibu wa hukumu za Allah swt na wakaitumia kinyume na hukumu za Allah swt au iwapo watachuma kwa njia zilizo kinyume na hukumu za Allah swt na wakazitumia kwa mujibu wa hukumu za Allah swt; katika hali zote mbili Allah swt hazikubalii.
Katika kutaka kukubaliwa sharti ni kwamba mapato hayo yawe yamepatikana kwa njia zilizo halali na zitumiwe katika njia zilizo halali vile vile.”
4. Halabi anasema
kuwa mtu mmoja alimwuliza Al Imam
Ja'afer as-Sadiq a.s. kuhusiana na ayah hii katika Qur'an Tukufu Surah Al Baqarah, 2, ayah 267:
Enyi malio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa.
Na hapo
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akasema:
“Wapo baadhi ya watu ambao baada ya kuingia
katika Uislam bado wameendelea kubakia na
5. Katika Ma’anil Akhbar Al Imam Hassan al-'Askari a.s. kwa kupitia sanad amenakili riwaya moja kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa amesema:
“Wale ambao wanajiona utukufu na wakubwa na ambao wanatenda matendo kwa mujibu wa nafsi zao, mfano wake ni wa yule mtu ambaye mimi nilisikia watu wakimsifu sana na kumheshimu sana, na hivyo mimi nikawa na shauku ya kutaka kuonana na mtu huyo lakini katika hali ambayo yeye hataweza kunitambua. Siku moja mimi nilimwona alikuwa amezingirwa na watu. Baada ya muda mchache kupita mimi nikamwona yeye ametoka humo na akawa anaondoka, basi mimi nilimfuata nyuma yake.
Tulipita katika duka la muuza mikate, huyo mtu
kwa kuficha macho yake na kificho ficho akaiba mikate miwili. Kwa hakika mimi
nilistaajabishwa mno, na nikadhani kuwa labda wao wana maelewano fulani kabla
ya tukio
Tukaendelea mbele yeye akamghafilisha mfanya
biashara huyo na akaiba makomamanga mawili humo. Na hapa pia nikafikiria kwa
labda wao watakuwa na maelewano kama hayo kabla ya kutokea tukio hili, nikiwa
hapo nikaingiwa na wazo kuwa je iwapo watakuwa na maelewano
Basi mimi niliendelea kumfuata nyuma yake, tukafika njiani akamwona mtu mmoja mgonjwa basi huyo akasimama kwa mgonjwa huyo na akatoa ile mikate miwili na hayo makomamanga mawili, akampa huyo mgonjwa.
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwuliza huyo
mtu kulikuwa na dharura gani kwa kufanya hivyo. Mtu huyo kwa kuniona mimi
akasema je wewe ni Ja’afar bin Muhammad ? Nami nikamjibu naam, basi yeye hapo
akaanza kusema nasikitika
Imam a.s. akamwambia kwa hakika matendo yako hayo yana aibisha.
Basi yeye akasema kuwa Allah swt anasema
katika Qur'an Tukufu Surah An A’Am, 6, Ayah 160:
Afanyae wema atalipwa mfano wake mara kumi. Na afanyae ubaya hatalipwa ila sawa nao tu. Na wao hawatadhulumiwa.
Ama kwa mujibu wa ayah ya Qur'an Tukufu mimi nimeiba mikate miwili hivyo nimetenda madhambi mawili na nimeiba makomamanga mawili hivyo nimetenda madhambi wawili na kwa ujumla nimetenda madhambi manne.
Na pale mimi nilipompa mgonjwa sadaka mimi kwa kila wema nimepata malipo kumi ya thawabu hivyo jumla nimepata malipo ya thawabu arobaini. Na kutoka arobaini ukitoa nne ninayo mema thelathini na sita bado.”
Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu:
“Mama yako akae kwenye kilio chako! Wewe kwa
hakika umeitoa maana isivyo ya Ayah za Qur'an Tukufu. Je wewe huelewi ayah ya
Qur'an Tukufu isemayo Surah Al Maida, 5, Ayah ya 30:
Basi nafsi yake ikampelekea kumuuwa nduguye, akamuuwa na akawa miongoni mwa wenye kukhasirika.
Kwa mujibu wa ayah hiyo wewe umeiba mikate miwili umetenda madhambi mawili na kwa kuiba makomamanga mawili umetenda madhambi mawili mengine na hivyo jumla umetenda madhambi manne, na pale ulipotoa hiyo mali yaani mikate na makomamanga, kama sadaka bila idhini ya mwenye mali basi umetenda madhambi mengine manne. Kwa hivyo umetenda madhambi nane kwa pamoja. Sasa wewe unafikiria mema hayo arobaini yametoka wapi?”
Kwa hakika mtu huyo aliduwaa, akimwangalia Imam a.s. na akajiondokea zake.
Baada ya hapo Imam a.s. akasema kwa kujitolea maana potofu ya ayah za Qur'an Tukufu vile isivyo sahihi ndio matokeo yake haya na vile vile kuwapotosha watu wengine pia.”
7. Katika tafsiri Ayyashi Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amenakiliwa akitoa tafsiri ya ayah Surah Al Baqarah, 2, ayah ya 267:
Enyi malio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa.
Imam
a.s. akaelezea:
“Miongoni mwa watu kulikuwa kumelimbikwa mali
iliyopatikana kwa riba na njia zingine zisizo za halali, basi wao walinuia
kutoa sadaka humo, na ndipo Allah swt
alipowakataza kufanya hivyo (kutoa sadaka kutoka
1. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. ameripoti riwaya kutoka kwa
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa
amesema:
“Katika vitu vya kuleta uokovu mojawapo ni kuwalisha chakula wale wenye kuwa na shida na dhiki, na pili mtu awe ni mwanzilishi awe ni mwanzo wa kutoa salamu na vile vile wakati watu wamelala usingizi mtu anaamka kwa ajili ya kusali na kufanya ‘ibada.”
2. Muhammad Yakub amenakili kutoka ‘Ali bin Ibrahim ambaye naye amenakili kutoka Muhammad bin ‘Isa bin ‘Ubaid ambaye naye amenakili kutoka Ahmad bin Muhammad naye amenakili kutoka ibn Fazzal Ma’aruf naye kutokea Tha’alaba bin Maymun ambaye naye pia amenakili riwaya hiyo kutoka kwa Zararah, kuwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:
“Allah swt hupendezewa mno kulishwa chakula wale wenye dhiki na shida na njaa, na vile vile hupendezewa kutolewa kwa dhabihu (qurbani).”
3. Hisham bin Hakam amenakili riwaya kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:
“Tendo lililo bora na la kipenzi mbele ya Allah swt ni kule kumlisha muumin mwenye njaa mpaka akashiba, ama kummalizia shida aliyonayo au kumlipia deni lake.”
4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Siku moja waliletwa wafungwa ambao walikwisha kutolewa hukumu ya kuuawa mbele ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Basi ikatokea kwamba mmoja wa wafungwa hao alipoletwa mbele ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Malaika Jibrail a.s. akaja akamwambia Mtume :”Ewe Mtume wa Allah swt ! Huyu mtu adhabu yake iahirishwe kwa leo. Na wengine waliendelea kuletwa na hukumu zikapitishwa na hatimaye wakauawa. Na mwisho yule mtu aliporudishwa mbele ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na tena Malaika Jibrail a.s. akatokezea akamwambia:
“Ewe Mtume wa Allah swt ! Allah swt anakusalimia na huyu mtu huwa anawalisha wale wenye kuwa na shida, na mkarimu kwa wageni, mwenye kusubiri wakati wa shida na dhiki, anayechukulia majukumu na wajibu wa watu wengine kwa kuwasaidia.”
Basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwambia huyo mtu kuwa Malaika Jibrail a.s. amekuja na kumwambia habari hizo, na hivyo yeye alikuwa akimfanya yeye awe huru.
Kwa kujibu huyo mtu akasema:
“Je Allah swt, mola wako amependezewa na matendo yangu hayo?”
Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia, “Naam! Na kwa hakika mtu huyo papo hapo aliisoma Kalimah ya Shahada na akaukubalia Uislam na akawa Mwislam papo hapo; na akasama:
“Kwa kiapo cha Allah swt ambaye amekutuma wewe
katika haki, mimi kamwe sijamrudisha mtu yeyote akiwa amehuzunika yaani bila
kusaidiwa kutoka
5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anamnakili baba yake Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. kuwa amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Kisu kinapita haraka
1. Al-Kuleyni anaandika riwaya kuwa Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. :
“Ilikuwa ni tabia yake kuwa alikuwa kila
alipokuwa akikaa kula alikuwa ana beseni moja ambamo alikuwa akiweka kila aina
chakula iliyokuwa mbele yake kidogo kidogo na alikuwa akitoa hukumu kuwa beseni
hiyo ipelekwe kugawiwa kwa wenye shida na muhitaji. Na hapo akasoma ayah ya Qur'an
Tukufu ifuatayo: Surah Al Balad, 90, ayah
11:
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
Na baadaye akasema Allah swt anaelewa wazi wazi kuwa katika uwezo wa kila mtu kumfanya huru mtumwa kwa hiyo na hivi ndivyo alivyofungua njia ya kumfikisha mtu hadi kuingia Jannat.”
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. katika Sadaka alizokuwa akitoa alikuwa akitoa sukari pia.
Kwa hivyo kulitokea mtu mmoja akamwuliza, Yabna Rasulallah! Kwa nini unatoa sukari? Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alijibu:
“Mimi ninapenda sana sukari, na ninapenda kuwa
niwe nikitoa Sadaka kwa kile kitu
ninachokipenda
1. Al-Kuleyni amemnakili Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye
naye amemnakili
Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. riwaya kuwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:
“Siku ya Qiyama tendo jema kabisa malipo yake watapewa wale watu ambao wamefanya wema katika kugawa maji.”
Riwaya hiyo hiyo Sheikh Sadduq a.s. ameielezea pia.
2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Sadaka iliyo bora kabisa ni ile ya kuutuliza moyo unaowaka kwa kiu cha maji.”
3. Ali ibn Ibrahim amenakili riwaya kutoka kwa baba yake kuwa
Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Pale panapokuwa na maji na mtu akatoa Sadaka ya kuwagawia watu maji basi Allah swt humjaalia thawabu za kumfanya huru mtumwa mmoja, na pale ambapo hakuna maji kabisa na mtu akatoa Sadaka ya kugawa maji basi Allah swt humhuisha mtu mmoja na kwa hakika mtu anayemhuisha mtu mmoja ni sawa sawa na kuhuisha ulimwengu mzima.”
Riwaya hii vile vile Sheikh as-Saduq ameinakili.
4. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:
“Siku moja alikuja Mwarabu mmoja kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na kumwambia:
“Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Naomba unionyeshe tendo ambalo litaniingiza mimi peponi. Kwa kusikia hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema: Chukua Mashk (chombo cha kujazia maji iliyokuwa ikitumika katika zama hizo na ilikuwa ikitengenezwa kwa ngozi) na uwapelekee maji hayo familia ambayo ipo inateseka kwa kukosa maji na kiu kinawasumbua sana kiasi kwamba watakapo pata maji hayo watayanywa kwa haraka sana. Basi uelewe kuwa wewe utaipata Jannat kabla hata maji hayo hayajaisha au Mashk yako hiyo haijatoboka.”
5. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:
“Bila shaka, Allah swt anafurahishwa mno kwa kuona mtu anawanywesha maji wanaadamu au wanyama ambao kwa joto au kiu kali kabisa kinacho wasumbua hao na Allah swt siku ya Qiyama atamjaalia kivuli. Na kwa hakika hakutakuwa na kivuli kingine chochote isipokuwa kile kilichotolewa na Allah swt tu.”
6. Ibn Abbas anasema kuwa mtu mmoja katika kutaka kumhurumia Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema:
“Ewe Mtume wa Allah swt! Je ni tendo gani lile nifanye mimi ili niweze kuwa mustahiki wa kuingia Jannat?”
Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia:
“Nunua Mashk moja mpya na uwe ukiwanywesha watu maji kutoka humo, hadi Mashk yako hiyo itakapofika hatua ya kuja kutoboka (yaani itakapo chakaa au kuzeeka). Basi kwa tendo hili kwa hakika ndilo litakalo kufikisha wewe Jannat.”
7. Abu Hamza Thumali amenakili riwaya kutoka kwa Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa amesema:
“Yeyote yule atakaye mlisha na kumshibisha muumin ambaye ana njaa basi Allah swt siku ya Qiyama atamlisha matunda ya Jannat, na yeyote yule atakaye tuliza kiu cha muumin ambaye ana kiu basi Allah swt siku ya Qiyama atamnywesha maji ambayo yamepigwa lakiri. Na yeyote yule atakaye mvalisha mavazi nguo muumin ambaye kwa hakika ana shida basi Allah swt siku ya Qiyama atamvalisha mavazi kijani ya Jannat.”
1. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amesema:
“Yeyote yule ambaye hakubahatika kutufanyia sisi wema basi ni wajibu wake kuwafanyia mema na kuwatimizia mahitaji ya marafiki zetu. Na yeyote yule ambaye hakubahatika kudhuru makaburi yetu basi adhuru makaburi ya wafuasi na marafiki zetu.”
2. Muhammad bin Ali bin Hussein Jamil amenakili riwaya moja kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:
“Miongoni mwenu mtu aliye bora kabisa ni yule
mwenye moyo mkarimu yaani mwenye moyo wa kutoa na mtu mwovu kabisa ni yule
ambaye ni bahili. Na usafi wa imani dalili yake ni kwamba huwawia kwa wema
muumin wenzake na kuwatimizia dharura na mahitajio
Baada ya hapo Imam a.s. alimwambia Jamil, “Ewe Jamil! Habari hizi uwafikishie wenzako.
Kwa hayo mimi nikasema, “Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Niwe fidia juu yako. Je ni watu gani hao?”
Imam a.s. akasema: “Hao ni wale ambao wanawafanyia wema ndugu zao katika imani wakati wa shida huwa pamoja nao na vile vile wakati wa furaha pia huwa nao.”
3. Sheikh Sadduq a.s. amenakili riwaya kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye amesema kuwa:
“Yeyote yule ambaye hakupata fursa kufanya
wema nasi, basi awafanyie wema wapenzi na wafuasi wetu basi atapata thawabu za
kutufanyia wema sisi. Na vile vile ambaye hakubahatika kutuzuru sisi katika
uhai wetu na uhai wake basi awazuru wapenzi na wafuasi wetu, basi atapata
thawabu
4. Safwan Al-Jammal anasema kuwa siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimwambia Mu’alla bin Hunais:
“Ewe Mu’alla! Uwe wa Allah swt, ili Allah swt aweze kukutunza na kukuhifadhi.
Kwa hayo Mu’alla alianza kusema:
“Je hivyo inawezekanaje?”
Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu, uwe na hofu ya Allah swt, uwe daima ukimwona yeye katika mawazo yako, kwa hiyo yeye atakifanaya kila kitu kiwe kikikuogopa wewe, na vile vile kitakuwa kikikuwazia wewe na kukujali wewe. Ewe Mu’alla ili kujipatia mapenzi ya Allah swt lazima uwatendee watu matendo mema, na utambue wazi wazi kuwa Allah swt anapendezewa sana na moyo wa ukarimu na huchukizwa sana na ubahili na huwa na uadui nao.
Angalia !
Wewe kama utaniomba chochote na mwisho wake wewe ukaaza kufanya mapenzi
nami, na badala yake mimi nitafurahishwa
Na kwa hakika ukiniuliza mema yote naweza kuyafanya kwa ajili yako basi ukweli ni kwamba sifa zote ni za Allah swt kwa sababu yeye amekupitishia neema yake kwa mikono yangu mimi nimekuwa ni kipitishio tu kwa ajili yako kwa hiyo yeye ndiye anayestahiki sifa zote.”
5. Ali ibn Ibrahim anaandika katika tafsiri yake kuwa mtu mmoja alitokezea katika kikao cha Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. na humo akaanza kuwazungumzia matajiri na mara akaanza kuwasema vibaya na kuwatukana.
Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimwambia, “Nyamaza!”
Wale mafukara ambao wanawajali ndugu na jamaa
zao na kuwawia wema wenzao, Allah swt huwapa ujira mzuri
Na si mali yenu wala watoto wenu watakao kukaribisheni kwetu muwe karibu, isipo kuwa aliye amini na akatenda mema. Hao basi watapata malipo maradufu kwa walio yafanya. Nao watakuwa salama katika maghorofa.
1. Sheikh Quleyni
amenakili riwaya kutoka kwa Ahmad bin ‘Isa kuwa Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:
Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.
“Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema
kuwa kwa neno ‘Innama’ inamaanisha kuwa katika kazi zenu au shughuli zenu zote,
mwenye kuwa na haki zaidi kuliko yeyote juu ya nafsi zenu na
Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:
Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.
Kisa katika ayah hii ni kwamba Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa akisali sala ya Dhuhuri, alipomalizia raka’a ya pili tu akatokezea mwombaji. Siku hiyo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa amevaa Khullah yenye thamani ya Dirham elfu moja ambayo alikuwa amepewa zawadi na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Na Imam a.s. alipokuwa katika hali ya Ruku’u, kulitokezea maskini mmoja ambaye akasema, “Ewe Walii wa Allah swt na muumin halisi, iwe salamu juu yako, naomba unipe mimi maskini sadaka yoyote. Kwa hayo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. aliinamisha chini Hulla na kwa ishara akamwambia huyo maskini aichukue.”
Kwa tukio hili ndipo Allah swt alipoteremsha
ayah hii kwa ajili yake na kwa ajili ya kizazi chake na kuonyesha fadhila na
kufuzu kwao. Fadhila zao kuwa wanagawa sadaka hata
Kwa hakika imekuja kujulikana kuwa yule
maskini aliyekuja kuomba alikuwa si mtu bali alikuwa ni Malaika ambaye alikuja
kuomba, na vile vile katika kizazi kizima cha Maimam a.s. pia tumeona mara
nyingi
2. Katika kitabu kiitwacho Ihtijaj humo Tabarasi amenakili riwaya kutoka Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ameelezea kuhusu ayah hiyo kuwa:
“Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. katika hali ya sala akiwa katika Ruku’u alitimiza wajibu wake na akatoa Zaka na Allah swt ndipo alipoiteremsha hiyo ayah na makusudio yake yalikuwa ni kupata ridhaa ya Allah swt.”
3. Ali bin Ibrahim katika kitabu chake Tafsir ananakili riwaya kutoka kwa baba yake Ma’arifat Safwan kuwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:
“Siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.
alipokuwa amekaa pamoja na ‘Abdullah bin Salam kulikuwa na kikundi cha Mayahudi
pia. Na wakati huo ikateremshwa ayah ya Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5,
Ayah 55:
Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.
Baada ya hapo mara Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akatoka nje haraka na akaelekea msikitini na huko njiani alikutana na mwombaji mmoja na hivyo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza:
“Je kuna mtu aliyeweza kukusaidia?”
Basi huyo mwombaji akasema,
“Naam, kuna mtu anayesali msikitini humo ndiye aliyenisaidia.”
Na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alivyoukaribia msikiti akamwona huyo mtu si mwingine bali ni Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.
Na riwaya hii vile vile imenakiliwa na Abu Hamza ambaye ameandika katika Tafsir Ayyashi.
4. Muhammad bin Ali bin Hussein katika kitabu cha Amali amenakili riwaya kutoka Abul Ja’rud Ma’rifat kuwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amenakiliwa riwaya kuwa amezungumzia kuhusu ayah
Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:
Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.
Kama ifuatavyo:
“Katika Mayahudi ambaye mnafiki mmoja alipoukubalia Uislam akaanza kuiga:
“Ewe Mtume wa Allah swt! Je ni nani Wasii na Khalifa wako? Na nani huyo atakaye kuwa Walii baada yako?”
Ndipo hapo ayah hiyo ilipoteremshwa na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akawaambia inukeni, basi hao wote wakainuka na wakaanza kuelekea msikitini. Walipofika msikitini wakakutana na maskini mmoja akitoka nje na hivyo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwuuliza, “Je kuna mtu yeyote aliyekupa chochote ?” Huyo akasema “Kwa nini isiwe hivyo pete hii je niliyoipata?” Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema,”Je ni nani aliyekupa?”
Huyo mwombaji akasema “Huyo mtu ambaye bado anasali.”
Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema
“Je alipokupa hiyo pete alikuwa katika hali gani?”
Huyo mwombaji akasema alikuwa katika hali ya Ruku’u. Na hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipopaaza sauti ya Takbira yaani Allahu Akbar na wale wote waliokuwepo pamoja naye nao pia walitoa Takbira kwa nguvu na sauti na hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ndipo alipowaambia wote:
“Mtambue wazi kuwa baada yangu Walii ni huyu Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. na wa si mwingine”
Karta anasema kuwa
“Kwa mujibu wa riwaya zilizopatikana kuwa katika sala moja aliitoa Hullah, na katika sala ya pili alitoa pete basi inadhihirika kuwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. anatoa sadaka katika hali ya sala zaidi ya mara moja ndivyo inavyothibitika kwa mujibu wa riwaya zinazopatikana.”
5. Ayyashi katika Tafsir yake ananakili riwaya moja kutokea kwa mwana wa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kwa Ammar Yasir amesema:
“Siku moja Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alipokuwa akisali sala ya Sunnah aliahirisha tendo moja kiasi kwamba mpaka akavua pete yake kwa ajili ya kumpa aliyekuja kuomba. Na pale Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipokuja basi alimwelezea hivyo. Na wakati huwo iliteremshwaayah yake hadi kufikia :
Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:
Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.
Basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alitusomea ayah hiyo na akasema,
“Yeyote yule ambaye mimi ni Mawla wake basi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ni Mawla wake. Ewe Allah swt! Uwe na mapenzi na yule ambaye anawapenda wao, na uwe na uadui na yule ambaye anafanya uadui pamoja nao.”
1. Halabi anasema kuwa yeye alipomwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. basi Imam a.s. akamjibu:
“Naam kabisa! Al Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi
Talib a.s. aligawa nusu ya
MWISHO.
Na |
MAUDHUI |
SURAH : AYAH |
1 |
‘Ibada
katika Sadaka |
2:261; 2:262; 2:265; 2:272; 9:99;
76:9; 90:6 |
2 |
‘Ibada
na Sadaka |
|
3 |
Asili
ya Sadaka |
4:78; 4:79 |
4 |
Athari
za Sadaka |
2:177; 2:261; 2:268; 2:271; 3:92;
3:180; 5:12; 32:16; 47:36; 51:19 57:7; 57:10; 57:11; 57:24; 68:17; 69:34;
70:35; 90:17; 92:21 |
5 |
Baraka
zitokanazo na Sadaka |
30:39 |
6 |
Biashara
na Sadaka |
34:39 |
7 |
Faida
za Sadaka |
9:103 |
8 |
Habari
watoao Sadaka |
|
9 |
Hishima
katika Sadaka |
2:148 |
10 |
Imani
baada ya Sadaka |
41:6 |
11 |
Imani
na Sadaka |
32:16 |
12 |
Kanuni
za Sadaka |
2:177; 6:141; 9:104 |
13 |
Kasoro
katika kutoa Sadaka |
|
14 |
Kuachwa
kwa Sadaka |
3:180; |
15 |
Kuepusha
Sadaka |
63:10 |
16 |
Kunyenyekea
katika Sadaka |
3:92 |
17 |
Kusikitika
kuhusu Sadaka |
90:4; 90:6 |
18 |
Kusita
katika Sadaka |
2:195; 2:254; 2:268; 9:67; 63:10 |
19 |
Kutumia
|
2:215; 2:245; 17:29; 23:57; 23:100;
24:33; 47:36; 47:37; 47:38; 57:11; 63:10; 68:19; |
20 |
Kuwa
na moyo kwa Sadaka |
2:177 |
21 |
Lipeni
Sadaka kutokea mbao |
|
22 |
Mabaya
katika Sadaka |
2:262; 2:264 |
23 |
Mabedui
na Sadaka |
9:98 |
24 |
Mafanikio
ya Sadaka |
90:10 |
25 |
Majamaa
wapewe Sadaka |
2:177; 2:215 |
6 |
Makatazo
kutoka Sadaka |
63:7 |
27 |
Malengo
ya Sadaka |
3:117 |
28 |
Malipo
ya Sadaka |
35:32 |
29 |
Malipo
ya Sadaka |
56:18 |
30 |
Mambo
mapya katika Sadaka |
57:10 |
31 |
Manufaa
ya Sadaka |
2:195; 2:272 |
32 |
Masharti
ya Sadaka |
76:9 |
33 |
Masikini
wapewe Sadaka |
2:215; 51:19 |
34 |
Masikitiko
juu ya Sadaka |
90:6 |
35 |
Matumizi
ya Sadaka |
2:273 |
36 |
Mumin
na Sadaka |
27:3 |
37 |
Mwelekeo
katika Sadaka |
2:148 |
38 |
Nia
katika Sadaka |
92:19 |
39 |
Njia
za Sadaka |
|
40 |
Nyayo
za Sadaka |
9:103; 51:19; 58:12 |
41 |
Ongezeko
kufuatia Sadaka |
30:39 |
42 |
Sadaka
bora kabisa |
2:273 |
43 |
Sadaka
itokanayo na urithi |
89:19 |
44 |
Sadaka
kwa kupiga magoti |
|
45 |
Sadaka
watoao makafiri |
6:136 |
46 |
Sadaka
watoao Wanafiki |
|
47 |
Sadaka
ya Allah swt |
2:195; 2:245; 3:17; 30:38; 42:38;
56:18; 63:7; 63:10; 64:16; 64:17; 65:7; 73:20; 92:18; |
48 |
Sadaka
za makafiri |
6:136 |
49 |
Swala
la Sadaka |
2:215 |
50 |
Taratibu
ya Sadaka |
2:215 |
51 |
Uchoyo
katika Sadaka |
47:37; 53:34; 57:10; 57:24; 68:17;
68:19; 68:28; 69:34; 89:17 |
52 |
Ufujaji
katika kutoa Sadaka |
|
53 |
Uhakika
wa Sadaka |
2:261; 2:265; |
54 |
Umuhimu
wa Sadaka |
2:196; 2:277; |
55 |
Umuhimu
wa Sadaka |
6:141 |
56 |
Unafiki
katika Sadaka |
2:264; 2:266; 2:270; |
57 |
Upotevu
au Sadaka ? |
34:39 |
58 |
Ushawishi
katika Sadaka |
2:245; 3:180; |
59 |
Utaratibu
wa Sadaka |
3:92 |
60 |
Uthamini
wa Sadaka |
9:104 |
61 |
Utumiaji
wa Sadaka |
2:273 |
62 |
Uwajibu
katika Sadaka |
2:262; 2:263; 2:264; 2:266; 90:6 |
63 |
Uwastani
katika Sadaka |
2:195; 25:67 |
64 |
Uwema
katika Sadaka |
2:177 |
65 |
Vipangimizi
katika Sadaka |
2:268 |
66 |
Vipimo
vya Sadaka |
2:219 |
67 |
Wakati
wa Sadaka |
2:274 |
68 |
Wanafiki
na Sadaka |
63:7 |
69 |
Wayahudi
na Sadaka |
|
70 |
Sadaka
za wana wa Israil |
2:83 |
71 |
Sadaka
za Mayahudi |
|
72 |
Utaratibu
wa Sadaka |
9:104 |
AMIRALY M. H.
DATOO -
BUKOBA
e-mail : datooam@hotmail.com
Na unaweza kuvipata katika Internet katika :
http://www.al-islam.org/kiswahili
1.
UHARAMISHO WA KAMARI
2.
UHARAMISHO WA RIBA
3.
UHARAMISHO WA ULEVI
4.
UHARAMISHO WA ULAWITI
5.
UHARAMISHO WA ZINAA
6.
7.
8.
USAMEHEVU KATIKA ISLAM
9.
TAJWID ILIYORAHISISHWA
10.
KITABU
CHA TAJWID
11.
KESI
YA FADAK
12.
TAWBA
13.
BWANA
ABU TALIB a.s.
14.
FADHAIL
ZA IMAM ALI IBN ABI TALIB a.s.
15.
TADHWIN
AL-HADITH
16.
TAFSIRI
YA JUZUU’ ‘AMMA
17.
HUKUMU
ZILIZOTOLEWA NA IMAM ALI IBN ABI TALIB a.s.
18.
MSAFARA
WA AL-IMAM HUSSEIN IBN ‘ALI IBN ABI TALIB A.S MADINA –
19.
DALILI
ZA QIYAMA NA KUDHIHIRI KWA IMAM MAHDI a.s.
20.
NDOA
KATIKA ISLAM
21.
MAKALA
MCHANGANYIKO No. 1
22.
MAKALA
MCHANGANYIKO No. 2
23.
UWAHHABI
– ASILI NA KUENEA KWAKE
24.
HEKAYA
ZA BAHLUL
25.
SHADA
LA
26.
HIARI
NA SHURUTISHO KATIKA ISLAM
27.
WAANDISHI
MASHIA KATIKA SAHIH NA SUNNAHN ZA AHL SUNNA
28.
USINGIZI
NA NDOTO
29.
MAJINA
KWA AJILI YA WATOTO WAISLAMU
30.
QURBAA
- MAPENZI YA WANANYUMBA YA MTUME S.A.W.W.
31.
TUSIUPOTEZE
WAKATI
32.
DHAMBI
KUU LA KUTOKULIPA ZAKA, KHUMS NA SADAKA
33.
JANNAT
NA JAHANNAM
34.
MASIMULIZI
YA HADITH KUTOKA QUR’AN
35.
SADAKA
36.
FAHISTI YA AYAH ZA QUR’AN TUKUFU KIMAUDHUI
[1] *Tabaqat al-Kubra , j. 6, uk.168,; Taqyid
al-'ilm , uk. 89,90; Kanz al-‘ummal, j. 10, uk. 156; Rabi’
al-Abrar, j.. 3 , uk. 294
[2] Bihar al- Anwar,
vol. 2 uk. 152; al- Taratib al - idariyyah vol. 2, uk. 246; Sunan al - Darimi,
vol 1, uk.
130; Ilal al - Hadith, vol. 2,
uk. 438; Taqiyyad al - Ilm, uk. 91; Jami’bayan al - ‘ilm, uk.99; Kanz
jumat al - Imam al - Hasan
min Tarikh Dimashq, uk. 167.
[3] Al - Tabaqat all-
Kubra, vol. 6 uk.220.
[4] Ansab al -
ashraf, vol. 2 uk.98; na Hadith no. 1980 kutokea
maisha ya Imam Ali (a.s.) katika
Tarikh
Dimashq Historia ya Damascus); Bihar al- Anwar, vol.2 uk. 230; al - Fadhail
ya Ibn Hanbal, Hadith
no. 222.
[5] Ansab al -
Ashraf, vol. 1, uk. 121; Tarikh Dameshq, vol. 38, uk. 202; Hilyat al - awliya,
vol. 1, uk. 67;
Shawahid al - tanzil, Hadith
no. 1009.
[6] Ansab al -
Ashraf, vol. 2, uk. 145.
[7] Bihar al - Anwar,
vol. 2 uk. 50 kutoke ashf al - Mahajjah.
[8] Bihar al - Anwar,
vol. 2, uk. 152.
[9] Bihar al - Anwar,
vol. 2, uk 153.
[10] Kwa ajili ya kutaka kuelezwa zaidi juu ya
Hadith zizungumziazo swala hili urejea Makatib al –
Rasul, vol. 1, uk. 71 na 89 iliyoandikwa na
Ali Ahmad Miyanji.
[11] Taqyid al - ilm,
uk. 89.
[12] Rawdhat al -
Jannat, vol. 8, uk. 169.
[13] Taqyid al - Ilm,
uk. 104.
[14] Tarikh al - adab
al - ‘ Arabi, “al -’ Asr al - Islami”, uk.
453, ambapo masimulizi kama hayo hayo
yametolewa na Mustafa Abd al - Razzaq; rejea
Tamhid li - tarikh al - falsafah al -
Islamiyyah,
uk.202,203.
[15] Al-Muraja’at ,
uk. 305,306, iliyochapishwa na
al-’Alami,Beirut.
[16] Ta’asis al-Shiah
li-ulum al-Islam, uk.280, iliyochapishwa
na al-Alami, Beiru.
[17] Rijal al-Najishi,
uk.3,4, iliyochapiswa Qum.
[18] Qamus al-Rijal, chini ya maisha ya Muhammad ibn Abd Allah
ibn al-Hassan;Rawdhat al Jannat
vol. 8,uk. 169.
[19] Rijal
al-Najashi,uk. 3,4, iliyochapishwa Qum.
[20] Fur’ al - Kafi,
vol.2, uk.666; kwa mifano mingine rejea Fur al-Kafi, vol.7 uk.77.
[21] Wasa’il al-Shiah,
sura juu ya Zakati; rejea Makatib al-Rasul vol. 1, uk.73.
[22] Was’il Shiah, sura juu ya Jihad (vita vitukufu); Makatib al-Rasul,
uk.176.
[23] Wasa’il al-Shiah, sura juu ya Qadha.
[24] Furu al-Kafi,
vol.7, uk 94.
[25] Was’il al-Shiah, sura juu ya al - Hudud.
[26] Furu al - Kafi,
Vol. 7. uk.98.
[27] Al-Tabaqat
all-kubra, vol 2. uk. 389; al-Musnaf ya Abd
al-Razzaq, vol. 1, uk. 285; Taqyid
al-Ilm. uk
107.
[28] Jami’bayan
al-Ilm, vol.1, uk.92.
[29] Al-Musannaf ya Abd-Razzaq, vol.7, uk.337.
[30] Al-Tabaqat
al-Kubra, vol.7, uk 447.
[31] Sunan al-Darimi,
vol.1,uk.126; Taqyid al-Ilm uk. 105,106.
[32] Sunan al Darimi,
vol.1. uk. 126; Akbhar Isbahan, vol
1, uk. 312; Tadhrib al-rawi, uk. 90 ya al-
Siyuti..
[33] Al-Jarh wa
al-ta’dil, vol. 1, uk.184.
[34] Tarik al-Khulafaa,
uk. 261 ya al-Suyuti.
[35] Tadhkirat
al-Huffadh, vol. 1, uk. 169,170,191,203.
[36] Jami’bayan
al-Ilm, vol. 1, uk.88,91.
[37] Jami’bayan
al-Ilm, vol. 1, uk.92.
[38] Muqaddamata Fath
al-Bari, uk.4,5.
[39] Tadhkirat
al-Huffadh, vol.1, uk.160.
[40] Kashf al -zunun,
vol. uk. 237.
[41] Tadhkirat
al-huffadh, vol. 1, uk.419.
[42] Ibid., vol.uk.
423 (kama hapo 44)
[43] Tadhkirat
al-huffadh, vol.1, uk.423; Tadrib al-rawi uk. 88,89.
[44] Ipo Hadith ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa “Mimi ni mji wa elimu na Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. ni mlango wake” na vile vile amesema “Mimi ni hazina ya elimu na Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. ni ufnguo wake.” Na zipo Hadith nyingi kama hizo.
[45] Nimetarjumu orodha ya Rawi 100 wa Kishi’ah wanaojuikana na walio ma’arufu katika vitabu vya Ahl as-Sunnah. Kwani wengi wa Masunni wanadai kuwa Mashi’ah ni Rafidhi (walio asi ) na wengine majaheli kuthubutu kusema kuwa Mashi’ah ni Makafiri. Hivyo itakuwa vyema iwapo utapata makala hayo ukayasoma.
[46] Mimi ninetarjumu baadhi ya vitabu ,kama inavyoonekana katika fahiristi hapo nyuma ya kitabu hiki, zinazozungumzia madhambi mbalimbali.
[47] Msomaji anaombwa kujaribu kusoma kitabu nilichokitarjumu katika lugha ya Kiswahili kwa jina la Tadhwin al-Hadith (Uchunguzi juu ya ukusanyaji na uandishi wa Hadith) ambamo swala hili limezungumzwa kwa marefu na mapana.
[48] Ndugu msomaji kitabu hiki kinazungumzia mambo ya sadaqah na kuna kitabu kimoja nimekitarjumu katika lugha ya kiswahili kinachozungumzia dhambi kuu, kutokulipa zaka na sadaqah. Kwa hiyo ili kutaka kusema habari zaidi kuhusu zaka naomba usome kitabu hicho hutapata kulipa mambo marefu na mapana juu ya zaka.
[49] Mara nyingi sisi hatufanyi mambo mema hatutoi Sadaka, hatusali
hatufungi saumu na tunafanya usia wakati wa kufa tunategemea tuache usia kwamba
kazi fulani nilikuwa nataka kuifanya mtoto wangu aifanye, Sadaka fulani
nilikuwa nataka kuitoa mtoto wangu aitoe, siku fulani sikusali mtoto wangu
anisalie, saumu sikufunga mtoto wangu anifungie saumu zangu nk. Kwa hakika
mambo
[50] Yaani Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alikuwa anamaanisha hapa kuwa angewaongezeapo kidogo.
[51] Nimekitarjumu kitabu juu ya kamari : Katika Islam Uharamisho wa Kamari. Na kimechapwa na Bilal Muslim Mission of Tanzania, DSM, Box 200333
[52] Nimekitarjumu kitabu juu ya Jannat (Peponi ) na Jahannam (Motoni)