MUHARRAM SI MWANZO WA MWAKA

Baada ya kujua mwaka wa Kiislaam unaanza tarehe gani ya mwezi gani, kisha umeingia utata juu ya jambo hili kuwa: Muharram ndiyo mwanzo wa mwaka wa Kiislaamu kwa maana ya Hijra! Ndiyo maana unaona kila uingiapo Muharram baadhi ya Waislam hufanya hafla kubwa kuadhimisha, wakidhani kuwa umeingia mwaka mpya!!! Ukisoma tarikh utaona kuwa:

Imam Ali (a.s.) alisema mwaka mpya uanze ile siku aliyofukuzwa Mtume (s.a.w.) Makka akaenda Madina.

Imam Ali aliwaandikia watu wa Najran akasema.... "Na aliandika Ubeidullah bin Abi Rafii tarehe kumi mfungo tisa mwaka wa thalathini na saba kutoka Mtume (s.a.w.) aingie Madina".

Taz: Alkharaj Uk. 81

Jamharatu Rasailil ar'b J. 1 Uk. 82.

Imam Malik bin Anas anasema: Mwanzo wa mwaka wa Kiislaamu ni mfungo sita, kwa sababu ni mwezi ambao Mtume (s.a.w.) amehama (kutoka Makka kwenda Madina).

Taz: Albidayatu Wannihaya J. 3 Uk. 207.

Assakhawy amepokea kwa Al'Asmai kuwa wao walikuwa wakiandika mfungo sita, ni mwezi aliohamia Madina Mtume (s.a.w.).

Taz: AI'i'lanu Uk. 78

Amesema Assahib bin U'bbad kuwa: Mtume (s.a.w.) aliingia Madina tarehe kumi na mbili mfungo sita, na tarehe ikaanzia hapo. Kisha baadae jambo hili liligeuzwa likarudishwa mwezi wa Muharram".

Taz: U'nwanul Maa'rif Uk. 11