MWAKA MPYA WA KIISLAAM

Inasemwa kuwa, katika mwaka wa kumi na sita Hijra, masahaba walikutana kujadili juu ya tarehe ya Kiislaamu itakayojulisha mwanzo wa mwaka.

Imam Ali (a.s.) Alisema kuwa: "Ifanywe kuwa ni mwanzo wa mwaka mpya, ile siku Aliyohama Mtume (s.a.w) akaacha ardhi ya shirki"

Taz: Fat'hul Bari J. 7 Uk. 209

Tarikhut Tabari J. 2 Uk. 112

Tarikh Ibn Athir J. 2 Uk.526

Alkhutat wal'athar J. 1. Uk. 284

Kwakuwa maafikiano yamepita kuwa mwanzo wa mwaka wa Kiislaamu uanze kwa kufuata tukio la Hijra, na kwamba Hijra imetokea mfungo sita, basi mfungo tano ni mwezi wa kumi na mbili na mfungo sita ni mwezi wa kwanza wa mwaka mpya wa Kiislaamu.