TAHRIFUL QUR'AN

Takriban, kuna aina tano za Tahrif, nazo ni kama ifuatavyo:

  1. Kupungua, au kuzidi, harfu au haraka, wakatihuo huo Qur'an isipotee kitu chochote.

    Tahrif aina hii, inapatikana katika Qur'an, hili linashuhudiwa kama ifuatavyo:

    1. Katika Surat Hud Aya 78 inasomwa: "HUNNA AT'HAARU LAKUM" katika silabi ya RAA kumetiwa dhamma, na katika qiraa kingine, inasomwa: "HUNNA AT'HARA" kwa nasbu.
    2. Taz: Tafsirul Qurtubi J. 9 Uk. 76

    3. Katika Surat Sabai Aya 19 inasomwa: "RABBANAA BAAI'D BAYNA ASFARINA" na katika qiraa kingine, inasomwa:- "RABBANAA BAA'DA" kwa madhi.
    4. Taz: Tafsir Qurtubi J. 14 Uk. 290

    5. Katika Suratul Baqara Aya 259 inasomwa: "KAYFA NUNSHIZUHA" na katika qiraa kingine, inasomwa: "KAYFA NUNSHIRUHA" kwa silabi ya RAA badala ya ZAA.
    6. Katika Suratul Waqia'h Aya 29 inasomwa:"WATWAL'H'IN MANDHUD" na katika qiraa kingine inasomwa: "WATWAL'I'N MANDHUD" kwa A'YN badala ya H'AA.
    7. Katika Surat Saad Aya 23 inasomwa: "LAHU TIS'U'N WATIS'U'NA NAA'JAH" na katika qiraa kingine inasomwa: "LAHU TAS'U'N WATAS'U'NA".

    1. Kupungua, au kuzidi neno moja au zaidi. Pamoja na kuwa nafsi ya Qur'an itabaki salama bila ya kupungua au kuzidi kitu.
    2. Katika zama za masahaba hali hii imetokea, ambapo Uthman bin Affan aliiunguza moto misahafu mingi. Na akatoa agizo kwa wawakilishi wake wote popote walipokuwa, waichome moto misahafu yote isipokuwa ile aliyoikusanya yeye.

      Taz: Manahilul I'r fani J. 1 Uk. 253

    3. Kuzidi au kupungua katika Aya au sura. Pamoja na kuwepo ukamilifu wa Qur'an, na wakaafikiiana Waislamu wote kuwa: Mtume (s.a.w.) aliisoma. Hali hii ipo, na mfano halisi ni kama ifuatavyo: "BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIM" Waislamu wote wanakubaliana kuwa, Mtume (s.a.w.) alikuwa akiisoma kabla ya kila sura isipokuwa Suratut Tawba.
    4. Kwa ndugu zetu Masunni imetokea hitilafu kati yao kuwa: "Bismillahi" si katika Qur'an, wengine wakasema: Ni katika Qur'an.

      Taz: Tafsirul Alus J. 1 Uk 39

      Tafsir lbn Kathir J. 1 Uk. 17

      Tafsirul Khazin J. 1 Uk. 18

      Tafsirush Shawkan J. 1 Uk. 7

      Ama Shia Ithna Ashar, wao wanakubaliana kuwa "Bismillahi" ni sehemu ya kila sura isipokuwa Suratut Tawba.

    5. Kuzidi baadhi ya Aya au sura yasiyokuwa Maneno ya Mwenyeezi Mungu. Tahrif aina hii haikubaliwi na Waislamu wote.
    6. Kupungua, yaani, Msahafu huu uliopo mikononi mwa Waislamu haukukusanya Qur'an yote iliyoteremshwa na Mwenyeezi Mungu, na kwamba Qur'an nyingine imepotea, Tahrif ama hii ipo, wako wanaothibitisha hilo, na wengine wanakataa kuwa haiko.