Hadith Ya Mufazzal

 

 

MAWAZO

 

 

 

 

 

The .HTML version of this book is taken from
www.al-islam.org and ebooked by www.ShiaLibrary.com and www.islamkutuphanesi.com . May Allah be pleased with all.

 

 

UTANGULIZI

 

 

KWA JINA LA ALLAH MWENYE REHEMA NA MWENYE KUREHEMU.

 

Sifa zote njema ni zake Yeye ambaye ameumba bila ya Yeye mwenyewe kuumbwa.

Nilfikiriya mwenyewe kuwa ni mwenye bahati sana kwa kupewa fursa hii ya kuchapisha na kupanga tena upya kitabu hiki.

Ningependa kuhakikisha pande zote kwamba hakuna kishawishi chochote cha pesa kwenye uchapishaji huu, na kwamba imefanywa tu kwa kutaka radhi za Allah (s.w.t.).

Namshukuru pia Akhiy Mohammed Kanju aliyegeusha kitabu hiki kwenye Kiswahili.

 

Mtumishi wa Allah

 

 

 

Bashir Alidina

 

 

 

 

 

 

 

Asili Ya Hadith

 

 

 

 

Muhammad Bin Sanah anasimulia kwamba Mufazzal Bin Umar alimsimulia hivi :

 

"Siku moja baada ya Sala ya Alasiri nilikaa baina ya Mimbari na Kuba la Mtukufu Mtume (s.a.w.) nikitafakari juu ya ukubwa wa vyeo vitukufu, ambavyo kwamba Allah (s.w.t.) amenijalia Maulana Bwana wetu Muhammad Mustafa (s.a.w.) ambavyo kwa ujumla Ummah ulikuwa hauna habari wala kwa ule ukubwa wa fadhila wala kwa sifa zake zilizo kamili wala kwa utukufu wake wa pekee.

Nikiwa nimezama katika kuwaza huko, mara alitokea Bin Abi Al Auja, kafiri mshirikina na akakaa umbali wa kuweza kumsikia. Sahiba wake alimfuata na akakaa kwa utulivu ili kusikiliza.

Bin Ali Auja alianza mazungumzo kwa kusema, "Mwenye Kuba hili amepata fadhila kubwa za pekee kwa ukamilifu wa heshima kuu katika yote aliyoyafanya." Sahaba wake aliongeza kwa kuthibitisha akasema: "Alikuwa filossofa na alifanya dai kubwa likiungwa mkono na miujiza ambayo kwamba ilishangaza akili za kawaida. Waliojifanya ni wenye hekima walizama kwa undani wa vina vya akili zao kupenya kwenye maajabu hayo (ili kuyajua) lakini bila mafanikio.

Ujumbe wake ulipokubaliwa na watu wastaarabu, wenye maarifa na wasomi watu kwa ujumla waliingia katika imani yake makundi kwa makundi. Sehemu za ibada na Misikiti ya sehemu zote ambako popote ulipofika wito wa utume wake ulianza kusikika kwa nguvu na kueleweka pamoja; na jina lake (kutajwa) sambamba na lile la Allah (s.w.t.) bila ya tofauti yoyote ya bahari na bara,  mlima na tambarare, bonde, siyo mara moja lakini mara tano kwa siku wakati wa Adhana na Iqamah.  Lilipata jina lake (limepata) kuambatanishwa na lile la Allah (s.w.t.) na maelezo yenye lengo la kuendeleza kumbukumbu yake na kuuweka ujumbe wake uwe ni wenye elimu ya kuendelea."

Bin Ali Auja akasema: "Weka kando habari za kumtaja Muhammad (s.a.w.) ambaye kuhusu yeye, akili yangu ina shangazwa vikubwa na mawazo yangu yamefadhaishwa.

Hebu tuongelee ukweli katika msingi wa watu kukubali imani ya Muhammad (s.a.w.) - Mwenye Rehema kwa ulimwengu. Je, kuna kiumbe wa namna hiyo au hapana?"

Kisha alirejea katika asili na uumbaji wa mpangilio mkubwa wa ulimwengu. Alifanya dai lisilosadikika kwamba hakuna aliyeviumba na hakuna Muumba, wala Msamii wala Mtengenezaji - Ulimwengu umejitokeza wenyewe. Katika kuwepo na ataendelea kuwepo na kwa hiyo hauna mwisho."

Nilijisikia vibaya umno kusikia hivi na nikamwambia : "Ewe usiye amini! Huwamini katika imani ya Allah (s.w.t.) kwa kukanusha moja kwa moja kuwepo kwake ambaye amekuumba wewe katika umbo zuri, akakugeuza kutoka hali moja kwenda hali nyingine, mpaka ukafikia katika umbo ulionalo sasa? Lau ungejifikiria wewe mwenyewe na lau akili zako nzuri zingekusaidia kiukweli, ungeweza kutambua katika nafsi yako mwenyewe hoja hizi za wazi za kuwepo kwa Allah Mtukufu Ishara ya vitu vyake vyote anavyoviruzuku na ushahidi wa Usanii wake usio na mipaka.

Alisema, "Tutajadili suala hili kama utapanga kwa utaratibu misingi ya kusadikisha hoja ambazo tutazikubali, vinginevyo huna haki ya kutia maneno yasiyo kuwemo bila ujuzi wa majadiliano. Kama wewe ni mfuasi wa Ja'far Bin Muhammad (a.s.) haikupasi wewe kuzungumza katika tabia ambayo unaifanya kwani yeye si mwenye mtindo wa kuzungumza hivi wala habishani na sisi katika hali ya utovu wa adabu namna hii. Amesikia zaidi maneno yetu kuliko ulivyofanya wewe, lakini kamwe hajatumia maneno yoyote yasiyo adabu, wala kamwe kujibu kwa ukali kuanzisha ugomvi. Ni mwenye kuvumilia sana, mwenye heshima, mwenye akili (za kuhoji) na mwanachuoni aliyepevuka. Yeye kamwe si mkali wala si mwenye hasira. Anayasikiliza maneno yetu kwa usikivu sana. Huvuta hoja zetu kiasi kwamba wakati tunapomaliza kabisa silaha zetu (hoja) na kufikiri kwamba tumemnyamazisha yeye kwa maneno machache huibuka tena, kuyavunja maoni yetu yote na kutufanya kuwa mabubu hivyo kwamba tukaachwa bila kuwa na uwezo wa kujibu hoja za Mtukufu Mstahiki. Kama wewe ni mfuasi wake, basi zungumza nasi katika tabia hiyo hiyo.

Kwa hili, nilitoka nje nikiwa na huzuni mno na mawazo tele kwasababu ya kutokuamini kwao katika Allah (s.w.t.) na matokeo ya huzuni na majonzi ya Uislamu na Wachaji wake, kwasababu ya kutokuamini kwao na usahifi usio na maana wa ulimwengu huu.

Nilikwenda mwenyewe kwa Bwana wangu, Imam Ja'afar Al Sadiq (a.s.). Aliponiona nimehuzunika, aliniuliza sababu ya kuwa hivyo. Nilimsimulia mazungumzo ya wale mushirikina na jinsi nilivyo jaribu kuoenyesha uongo wa hoja zao.

Aliniambia nije siku inayofuatiya (yaani kesho yake) wakati atakapo weka wazi kwangu ustadi mkubwa mno wa mwenye nguvu zote msanifu aliyedhihirika katika ulimwengu wote ulio na wanyama, na ndege, wadudu, vitu vyote vilivyo hai ama viwe ni wanyama au jamii ya mimea, miti izaayo matunda au dufu na ile isiyo na matunda, mboga zinazolika na zisizolika - maelezo ya kiustadi yatakayokuwa kama kifungua macho kwa wale ambao watakubali maelekezo; faraja kwa waumini na fadhaa kwa wazushi.

Niliposikia haya, nilirudi kutoka sehemu yake tukufu nikiwa katika hali ya furaha. Ujio wa usiku ule ulionekana kuwa mrefu kwasababu ya shauku yangu kubwa ya kujifunza kutoka kwa Mwanachuo mstahiki huyo, mambo aliyoahidi kuyaeleza kesho yake.

 

 

 

 

 

 

Baraza La Kwanza Mwanadamu

 

 

 

 

 

 

Mwanadamu

 

Asubuhi na mapema niliwasili mwenyewe na baada ya kukaribishwa vizuri, nikisimama kiheshima mbele ya sehemu yake tukufu, na kushukua nafasi yangu ya kukaa ambayo nimepewa. Kisha yeye (a.s.) alikwenda kwenye chumba cha faragha ambacho mara kwa mara huenda kujipekesha. Na mimi vile vile nilinyanyuka baada ya kuamrishwa, nilimfuata. Aliingia chumba kile cha faragha na miminilikaa chini mbele yake.

Akasema, "Mufazzal! Nahisi kwamba umekuwa na usiku mrefu kwa sababu ya shauku yako kwa ajili ya kesho. Nilithibitisha maneno yake kiheshima.

Alianza, "Allah (s.w.t.) alikuwepo kabla hakujakuwa na kitu chochote na utakuwepo kiroho kupindukia milele. Atukuzwe Yeye kwa vile Ameufanya ufunuo wake kwetu. Kwake Yeye Anastahiki shukurani zetu za dhati kwa sababu ya tunu yake kwetu. Ametupa sisi daraja kubwa pamoja na elimu bora na akatuanisha sisi pamoja na utukufu wa cheo (kwani kwa vile tu) kizazi cha Hadhrat Ali Ibne Abu Talib (a.s.) kupita viumbe vyote kwa elimu yake, ikiwa ni dhamana tukufu, pamoja nasi ya upambamizi wa (mambo) ya ulimwengu huu.

Niliomba ruhusa aweke picha kamili yale yote yaliyotoka mdomoni (kinywani) mwake, kwa vile nilikuwa na kila kitu muhimu kwa kuandikia, kitu ambacho alikubali kwa furaha.

Akasema, "Ewe Mufazzal! Wababaishaji wameshindwa kufahamu siri na sababu zilizo msingi wa asili ya viumbe, na akili zao zimebaki kutokuwa na habari ya ustadi usio na kosa uendeleao kuwepo chini ya uumbaji wa jamii mbali mbali (za viumbe) wa bahari na bara, tambarare na miinuko miinuko.

Wakawa makafiri, na kwa sababu ya kasoro ya elimu yao na ufinyu wa akili, wakaanza ulaghai ushindanao pamoja na ukweli, kiasi kwamba waliukataa uumbaji na kudai kwamba ulimwengu wote huu hauna maana yoyote ni bure tu, bila kuwa na ustadi wowote wa usanii juu ya uhusikaji na usanii au Muumba - bila kusudio usio na mwisho bila uwiyano au utulivu.

Allah (s.w.t) yu mbali mno na yale yote wanayomhusisha nayo. Na wapotelee mbali! Kulioje Kupotoka kwao! katika upofu wao wa kupotoka na bumbuazi, wako kama watu vipofu wapapasao kulia na kushoto katika nyumba iliyopambwa vizuri, iliyojengwa vizuri pamoja na mabusati mazuri, vitu vitamu vya chakula na vinywaji, aina mbalimbali za nguo na vitu vingine muhimu vya matumizi ya lazima, vyote vimewekwa kwa kutosheleza kwa kiasi kizuri na kuwekwa kwa ukamilifu makini na ustadi wa kusanii. Katika upofu wao wameshindwa kuliona jengo hilo na mapambo yake. Wanapita kutoka chumba kimoja kwenda kingine, wakiendelea mbele na kurudi nyuma. Kama kwa bahati yeyote mmoja kati yao atakuta kitu chochote katika mahali pake kinatoa hitaji, na asijue kusudio la kuwekwa pale na asijue (usitajwe) usitadi ulio chini yake, huenda akaanza kumlaumu Mjenzi wa (hilo) jengo kwa chuki zake na hasira, wakati ambapo, kusema kweli, makosa ni yake kwa kutokuwa na uwezo wa kuona.

Kutokulingana huku kwa tabia hushikilia vizuri katika kadhia ya tapo, ambalo hukataa nguvu iumbayo na hoja hiyo ipendeleayo usanii wa Kiungu. Hushindwa kutambua ubora wa riziki zao, ukamilifu wa uumbaji na uzuri wa Usanii, wanaanza kutangatanga katika mapana ya dunia, wakifadhaishwa kwa kutokuweza kwao kufahamu kwa akili zao sababu na misingi iliyo chini yake. Hutokea hivyo wakati mwingine kwamba mmoja miongoni mwao anayo habari ya kitu, lakini katika ujinga wake juu ya ukweli wake, kusudio na mtaji, huanza mara moja kulitafutia kosa akisema, "Ni kosa lisilothibitika."

Wafuasi wa Mani (Mtu aliyeanzisha Dhehebu la Zorasti wakati wa Mfalme Shapur mwana wa Urdisher, ambaye aliamini Utume wa Isa (a.s.) lakini akaukataa ule wa Musa (a.s.) na ambaye aliamini katika Uwili wa Uungu kama Waumbaji wa vizuri vyote na viovu katika ulimwengu huu - Nuru moja kama Muumba wa vitu vizuri, nyingine ya giza, kama ile ya wanyama wakali na viumbe vyenye madhara) ambao, kama valivyo washupavu katika kundi potovu la uovu, wameanza kutangaza waziwazi upotofu wao. Mbali na haya, baadhi ya watu wengine ambao waliopotoka nao pia wamepotea kutoka fadhila za Kiroho (Kiungu) kwa kutamka tu kama yakini halisi isiyothibitika au isiyowezekana.

Inampasa mtu ambaye Allah (s.w.t.) amemjaliya na elimu ya maajabu ya Kiroho ya ukweli na ambaye amemuongoza kwenye imani yake, na ambaye amepewa kuona na kutafakari juu ya ujuzi wa usanii ulio chine ya uumbaji, na ambaye ametunukiwa uelezaji wa sifa wa vitu hivyo, juu ya msingi wa akili isadikishayo na sifa nzuri. Inampasa mtu kama huyo kumtukuza Allah (s.w.t.) kwa ukamilifu kama Mola wake na fadhila za Kimbinguni, na kumuomba Yeye kwa kumzidishia elimu ya mambo ya Kiroho na msimamo imara ndani yake, na uwezo wa juu wa maelezo juu ya hayo.

Yeye (s.w.t.) asema, "Nitaongeza fadhila zangu, kama mtakuwa ni wenye kushukuru, na adhabu yangu ni kali kama hamtakuwa wenye kushukuru."

Muundo wa Ulimwengu huu ni mwongozo wa juu zaidi na hoja ya kuwepo Allah (s.w.t.) - jinsi sehemu zake (huo ulimwengu) zilivyounganishwa pamoja na kuwa na ufundi mzuri wa Usanii.

Hali ya kufaa kutafakari na akili kuangalia kuhusu sehemu moja moja hudhihirisha kwamba ulimwengu huu unalinganishwa na nyumba iliyopambwa na vitu vyote muhimu kwa ajili ya mwanadamu.

Mbingu hii ni kama chandalua; ardhi imetandazwa kama busati ambapo nyota zimewekwa katika safu juu ya safu zikijitokeza kama taa zilizowashwa katika sehemu zao. Vito vya thamani vimehifadhiwa kama kwamba ni nyumba yenye mkusanyo wa vitu vingi. Mbali na hivi kila kitu kiko tayari kupatikana kukidhi mahitaji ya mtu binafsi.

Mtu, katika Ulimwengu huu, ni kama bwana mmiliki mwenye nyumba, akiwa ni mwenye kumiliki kila kitu ndani yake.

Na siyo jamii tofauti za mimea zipatikanazo kukidhi mahitaji ya mtu binafsi - baadhi ni chakula cha wanyama, nyingine ni dawa kwa Wanadamu; baadhi ni kwa mapambo tu, baadhi ni kumpatia mtu manukato kwa burdani yake, baadhi ni dawa kwa wanyama, baadhi ni lishe kwa Mwanadamu, baadhi kwa ndege tu na nyingine kwa wanyama wa miguu miine peke yao na kuendelea. Jamii tofauti za wanyama zimepangiwa kazi kwa mahitaji na faida maalum.

 

 

 

 

KUUMBWA KWA MWANADAMU

 

Tunaanza sasa na maelezo ya kuumbwa Mwanadamu kabla hujajifundisha somo litokanalo humo. Hatua ya kwanza katika kuumbwa kwa Mwanadamu hurejea kwenye hali wakati Kijusu (Mimba) kinapowekwa kimpango katika tumbo la uzazi, ingawa imefungwa ndani ya aina tatu za sitiri zilizo wazi na aina tatu za viza. Ya kwanza ikiwa ni ile ya ukuta wa nje, ya pili ni ya tumbo la uzazi na ya tatu ni ya Kondo la nyuma. Huu ni wakati ambapo kijusu hakiwezi kujilisha wala kuondoa madhara yoyote yatokanayo nayo.

Mtiririko wa Heidh umeadilishwa ili kutoa lishe kwa ajili yake, kama vile maji yanavyochukua lishe kupeleka kwenye mimea. Hivyo mpango huu huendelea mpaka kufikia wakati ambao viungo vyake vimekamilishwa, ngozi juu ya mwili wake huwa imara kiasi chakustahimili hali ya hewa - hivyo kwamba haiwezi kupata madhara yoyote kutoka kwenye hewa na macho yake yanapata uwezo wa kustahimili mwanga. Wakati vyote hivi vinapokuwa vimekwisha fanyika, mama yake hupatauchungu wa uzazi, ambao kwa ukali humtikisa kumfikisha kwenye kuhangaika, kufikia upeo wa kuzaliwa mtoto.

Na kwa kuzaliwa mtoto, mtiririko wa heidhi uliokuwa ukipeleka lishe kwenye tumbo la uzazi unabadilishwa kwenda kwenye matiti ya mama.

Ladha yake inabadilishwa hivo hivo na rangi yake, na kuwa lishe aina ya pekee tofauti ambayo hufaa hasa kwa hali ya mtoto, kama na wakati ahitajiayo (hayo) hayo, kulinganishwa na mtiririko wa damu.

Wakati ule ule wa kuzaliwa kwake anaanza kutikisa na kulamba midomo yake kwa ulimi wake kuonyesha hamu yake ya (kunyonya) maziwa hukuta jozi ya matiti ya mama yake matamu mno yaliyohifadhiwa yakining'inia tayari kwa kumpatia lishe kwa ajili yake. Hupata lishe yake kutoka maziwa katika njia hii mpaka wakati huo, kwa vile mwili wake bado ni mororo, viungo vyake na matumbo yake ni laini na dhaifu.

 

 

MENO NA NDEVU

 

Kama aanzavyo kutembea na kuhitaji chakula kigumu kujenga mwili weneye nguvu, magego yake hutokeza kutafuna vyakula kurahisisha uyeyushaji wachakula tumboni. Huendelea na lishe hiyo mpaka anapofikia balehe.

Mwnaume anaota nywele katika uso kama alama ya uume kupata heshima kama mwanaume, hivyo kupita hatua ya utoto na kufanana na wanawake. Mwanamke huuweka uso wake safi, upendezao na bila nywele, kuuweka umaridadi wake na umbo zuri. Kama mvutio kwa wanaume katika huduma ya kulifanya Taifa liishi.

Je, unaweza ukafikiria hali ambayo mtu katika kupitia kwenye hatua zote hizi tofauti ameongozwa na kukamilishwa, zinaweza zikatoka bila ya kuwa na Msanii na Muumba? Je, unafikiri kama mtiririko wa heidhi usingegeuzwa kwake wakati ni kijusu katika tumbo la uzazi,je, asingeweza kukauka kama vile mimea ikaukavyo, ikinyimwa maji? Na je, kama isingekuwa ni kusukumwa kwa uchungu wa uzazi baada ya kukomaa kwa uzazi, je, asingezikwa katika tumbo la uzazi kama vile mtoto anaeishi anavyozikwa katika ardhi?

Na je, kama asingepatiwa aina nzuri ya maziwa, je, asingekufa kwa njaa? kama asingelishwa na lishe nzuri zenye kulingana na hali ya uwezo wake ya kuukamilisha mwili wake na kama meno yake yasingetoka katika wakati mahususi, je, isingekuwa matatizo kwake kula, kutafuna na kuyeyusha chakula chake? Na kama asingepitia kipindi cha utoto cha kunyonya, mwili wake usinge umia katika sulubu na kudhoofika kwa kazi yoyote kwa matokeo ya mabadiliko ya kudumu juu ya mama yake kwa kumfanya ashughulike na silika yake tu na kumlea, bila muda wa kutafuta mtoto wa pili?

Uso wake usingeota nywele katika wakati mahususi, je asingekuwa yu ngali katika hali yautoto na maumbile ya wanawake, bila ya murua wowote au sifa kama vile matoashi ambao wana sura mbaya kwa kukosekana ndevu?

Ni nani basi huyo, ambaye amemuumba mtu bure bure tu, ambaye amekuwa mjenzi wa thamani yake, ambaye daima ni mwenye hadhari kumpatia mahitaji yake wakati wote?

 

 

UPUUZI WA ULAHIDI

 

Kama kujitokeza kwa uumbaji bila Msanii maalum kuna weza kukubalika chini ya masharti ya kawaida hii, basi matilaba ya Kizazi na uwiano thabiti wa uumbaji unaweza kuwa chanzo cha kosa na fadhaa, kwa vile viwili hivi vinapingana na kujitokeza kwa uumbaji bila usanii maalum.

Maelezo kama hayo ni ya upuuzi wa hali ya juu kwamba mpango na kurekebisha kwa pasa kutokea hivi bila Muumba, na mpango mbaya na usio faa wa usanii na maumbile vingepaswa kuhusishwa na Muumba. Asemaye hivi ni juha kwa sababu kitu chochote kilicho tengenezwa bila usanii kamwe hakiwezi kuwa sawa na kulingana ambapo visivyo mpango na ukaidi haviwezi kuepo pamoja na usanii wa mpango. Allah (s.w.t.) yuko mbali na wanayo sema wapotofu.

Na kama mtoto angezaliwa na akili pevu, angepumbazishwa na ulimwengu huu jinsi ulivyo mgeni kwake, katika mazingira yasiyoeleweka yaliyo zunguukwa na wanyama na ndege wa kila aina pande zote, ambavyo vingeonekana katika macho yake kila muda wa siku.

Ifikirie katika hali ya mtu anayehamia nchi nyingine kutoka jela ya nchi nyingine, kama ana akili timamu, utamwona akiwa ametatazika na kufadhaika. Hawezi kujifundisha lugha ngeni kiasi cha kutosha kwa mara moja, wala kuupata mwenendo na tabia za mahali hapo. Kwa upande mwingine, yule ambaye anachukuliwa kama mfungwa kupelekwa nchi ngeni katika siku zake za mwanzo wakati akili yake ni changa, mara moja atajifundisha lugha hiyo, mwenendo na tabia za sehemu hiyo.

Hivyo hivyo, kama mtoto angezaliwa na akili pevu angeshangazwa katika kufumbua macho yake na kuona vitu mbali mbali vilivyopangwa kwa mpango namna hiyo, aina mbali mbali ya maumbile na mawazo yaliyo wazi ya umoja na faraka. Kwa muda mrefu, asingeelewa ni lini amekuja na ni wapi alipofikia na iwapo yale yote aliyokuwa akiyaona ni ndoto.

Kisha, kama angezaliwa na akili pevu angejisikia kinyaa na kushushwa hadhi, kujiona yeye mwenyewe ni mwenye kupakatwa huku na huku miknoni, akilishwa kwa maziwa, kufungwa ndani ya vitata (desturi ya Waarabu) na kulazwa katika susu - hatua zote hizi zikiwa za muhimu kwa mtoto wachanga kwasababu ya umororo na ulaini wa miili yao.

Yasingekuwepo haya, kama wangezaliwa na akili pevu, kudekezwa huku, wala kudekezwa kule, wala upole huu kwa watoto wachanga katika akili za watu wazima ambako kikawaida huonekana kutokana na huba kwa watoto ambao hawakufundishwa kwa sababu ya unyofu wao hujenga hadhari maalum kw ajili yao. kwa hivyo anazaliwa katika ulimwengu huu bila kuelewa kitu chochote, bila kuelewa kabisa ulimwengu na kila kilichomo humo. Anayaangalia mambo yote haya na akili yake changa na upungufu wa kuelewa, na hivyo hajiskii kutatazika.

Akili yake na kuelewa kidogo kidogo, polepole muda hadi muda, kukua kidogo kidogo, hivyo ili kumuingiza kwa taratibu kwenye vitu vilivyo mzunguuka na kuizoeza akili yake ipasavyo ili kumzoesha kwa hayo bila kuhitaji udadisi zaidi na maajabu, hivyo kumwezesha kutafuta riziki yake kwa utulivu pamoja na kuelewa na kupanga, kuweka juhudi zake humo, na kujifunza masomo ya utii, makosa na utovu na adabu.

Na tazama! Kuna sehemu nyingine za mambo. Kama mtoto mchanga angezaliwa na akili pevu pamoja na kuelewa kazi zake, kungelikuwa na nyakati chache za deko lihisiwalo katika kawaida ya mtoto mdogo, na mahitaji, ambayo kwamba wazazi wanajikuta nyakati zote tangu mwanzo wanajishughulisha kwa mambo ya vijana wao, yasingejitokeza. Pendo na huba, vihisiwavyo kwa watoto wa kawaida, kufuatia taabu walizopitia kwa ajili yao, isingekuwepo baina ya wazazi na vizazi vyao. Kwa sababu ya akili zao pevu, watoto wasingehitaji matunzo ya wazazi. Mtengano ungeanza punde tu baada ya kuzaliwa kwa mtoto mchanga kutoka kwa wazazi wake. Hata mama au dada wangekuwa wageni kwake na kwa hivyo (pia) katika mipaka ya ndoa.

Huoni kwamba kila kitu kikubwa au kidogo kimeumbwa katika mpango usio kombo bila dosari au kosa?

 

 

MACHOZI

 

Hebu tizama faida ya matokeo kwa watoto itokanayo na kulia. Kuna maji katika ubongo wa mtoto ambayo kama hayakutolewa, huweza kusababisha matatizo au maradhi, hata pengine jicho kupotea. Kutoka kwa maji kutoka katika ubongo wake huliacha kuwa na afya na macho kuwa na mng'aro zaidi, mtoto anafaidika kwa kulia, ambapo wazazi wake katika kutokojua kwao, hujaribu kuzuia kulia kwake kwa kumpatia matakwa yake, bila kujua faida ya huko kulia.

Ziko faida nyingine kama hizo ambazo walahidi wameshindwa kuzifahamu, na kama wangeweza kuzifahamu, wasingeweza kukanusha kuwepo kwa faida hizo katika hili. Watu wenye elimu ya kiroho wanaelewa ni nini kisichotambulikana kwa wakanushaji hawa. Hutokea hivyo wakati mwingine kwamba viumbe hawajui hekima iliyoko humo, ingawa iko katika elimu ya Muumba.

 

 

MATE

 

Udende utokao midomoni mwa watoto huweza kusababisha uharibifu mkubwa kama hautaruhusiwa kutiririka. Hii inaweza kuonekana kwa wale wenye mate mengi ambao huzama chini katika hali ya mabaradhuli, mapunguani na wapumbavu, na kuwa chambo cha magonjwa mengine kama kiharusi - (kupooza) mwili nzima na (kiharusi cha) uso.  Allah Azza Wa Jalla, ameamrisha kwamba maji haya yanapasa kutolewa kwa njia ya mdomo ili kumweka katika siha nzuri kwa uzuri wake wa baadae.

Majaaliwa yametoa fadhila hii, ya uzito ambao wao hawajui. Wanaruhusiwa nafasi hii kupata elimu ya hekima iliyomo ndani yake, ili kwamba wawe wenye elimu ya Kiroho na kama watu hawa wangeshukuru fadhila zote hizi, wasingebakia katika dhambi kwa muda mrefu hivi. Hivyo sifa zote na utukufu ni wake Yeye. Ukubwa ulioje wa rehema zake. Baraka zake ni kwa wote wawe wamestahiki au hawastahiki, Yuko mbali, ametukuka juu ya yale wanayosema watu hawa waliopotoka.

 

 

VIUNGO VYA JINSIA

 

Hebu fikiria viungo vya mwanaume na mwanamke vya ngono. Kiungo cha mwanaume kina uwezo wa kuamka (kwa ashiki) na kuongezeka ili kuweza kuutolea manii mfuko wa uzazi - hiyo ikiwa ndiyo kazi yake, ikiwa chenyewe hakina uwezo wa kukuza kilenga na kwa hivyo kuhitaji uhamisho wa manii kwenda mfuko wa uzazi wa mwanamke - mfuko ulio ndani ulinganao na kuhifadhi kiufanisi matone mawili ya mbegu za uzazi, kukuza kilenga kwa kutanuka kikadiri kwa kuongezeka ukubwa wake, kuzuia shinikizo lolote juu yake, kukihifadhi mpaka kinaimarishwa na kufanywa imara. Je, haikusanifiwa hivyo na msanii aonae kwa undani zaidi? Je, kazi zote hizi za ustadi, au kadiri hizi jamala (uzuri) zimejitokeza hivi hivi zenyewe? Allah Azza Wa Jalla Yu mbali, ametukuka juu ya upotofu wa Washirikina.

 

 

VIUNGO VYA JUMLA

 

Hebu fikiria viungo mbali mbali vya mwili, kazi zitakiwazo kwa kila kimoja kufanya na ukamilifu wa usanii uliomo ndani ya kila kiungo.

Mikono yote imekusudiwa kutumika kwa shughuli, miguu yote imekusudiwa kwa mwendo, macho kwa kuona kwayo, mdomo ni kuchukua chakula ndani, tumbo ni kukiyeyusha, ini ni kusindika lishe yake kwa kusambaza kwenye sehemu mbali mbali za mwili baada ya chakula hicho kufanyizwa kuwa damu, nyongo, maji ya tezi, belghamu, tundu za mwili zimekusudiwa kuondoa uchafu mwilini na utaona kwamba kila kiungo, kimelinganishwa barabara kufanya kazi zake maalum, kimefanyizwa kwa usanii kamili."

Nilisema, "Maulana! Baadhi ya watu huwamini kwamba yote haya ni matokeo ya kazi ya maumbile - kila kiungo hujitokeza na kuwepo kama na wakati kihitajiwapo na maumbile."

Yeye (a.s.) akasema, "Hebu waulize kama maumbile yanayofanya kazi katika mpango mzuri namna hiyo na uzuri wa taratibu za umbo vile vile huhitaji kuwa na elimu na uwezo au ni pasipo akili na sababu, bila uwezo na bila elimu?"

Kama wakikubali kwamba inahitaji kuwa na elimu na uwezo, kipi basi kinawazuia katika imani ya kuwepo muumba? Tunachosema ni kwamba vitu vyote vimeumbwa na mmoja ambaye ni Bwana wa Elimu na Uwezo. Wanasema kwamba hakuna Muumba na bado wanakubali kwamba Maumbile yamefanya hivi kwa ustadi na mpango. Kana kwamba maumbile hayo ndiyo sababu ya kuumbwa kwao, ambapo wanamkana Muumba. Kama watasema kwamba maumbile hufanya vitu kama hivi bila ya elimu na uwezo - bila kujua inachokifanya wala bila kuwa na uwezo wakukifanya katika uhusiano pamoja na aina na usanii na ustadi ule unaendelea kuwamo katika mambo yote, inashangaza kwamba kitu kinaweza kufanywa bila ulinganifu wa uwezo wa kukifanya na bila ya elimu ya kufanya hicho kitu. Kwa hivyo ni wazi kwamba kitendo huanzia kutoka kwa Muumba mwenye kujua yote, Ambaye amepanga kama njia ya pekee katika Uumbaji wake kutokana na Ujuzi wake, ambao watu hawa huita Maumbile. Kwa maneno mengine Allah (s.w.t.) Ameamuru njia ya kutengeneza kila kitu kutokana na sababu halisi na kanuni.

Kama kwa mfano, mbegu huhitaji maji kuchipua hakuna mvua hakuna nafaka; mtoto anazaliwa kwa muungano na Mume na Mke, na bila mpago huu wa muungano na kukutana kwa mbegu za uzazi; hakuna mtoto awezaye kuzaliwa; maji hugeuka hewa kusababisha wingu, wingu hilo husukumwa na upepo huku na huko na kuleta mvua; hakuwezi kuwepo na mvua bila taratibu hii.

Walahidi hawa huchukulia sababu hizi na maumbile kama ndiyo Muumba haswa, wakikanusha kuwepo kwa Muumba juu ya yote haya. Hili ni kosa la dhahiri, kwa kuwa maji hayana uhai, na mpaka yapatishwe uhai na mtoaji wa uhai, vipi yatatoa nafaka?

Na inawezekana vipi manii isyokuwa na akili, igeuke kuwa mtoto mchanga, ila itiwe nguvu na Mwenye Enzi zote Kuumba kichwa kutoka sehemu moja, mikono na miguu kutoka sehemu zingine, mifupa kutoka sehemu nyingine? Maumbo mengine ya uumbaji yanaweza kufikiriwa ipasavyo.

 

 

LISHE

 

Hebu fikiria lishe isambazwavyo katika mwili, na mpango wa kistadi uliomo ndani yake.

Hebu ona kwamba kifikapo tumboni, chakula kinaratibiwa kuwa mseto wa matibabu na mseto huo unahamishiwa kwenye ini na kapilari mororo zifanyazo kimia katika kiungo hicho.

Tumbo linageuzwa kuwa kama mrekebishaji kwa kuhamisha vitu kwenda kwenye ini katika hali iliyo safishwa sana, kuzuia madhara katika umbo hili laini.

Kisha ini huchukuwa mseto huo wa lishe ulioingizwa ndani yake, na kwa ustadi usiofahamika huubadili kuwa damu ili kusukumwa na moyo kwenda sehemu zote za mwili kwa kutumia mishipa ya damu, katika hali kama ya mifereji ya kunyweshea ionekanavyo katika mabustani na mashamba kusambaza maji kwenda sehemu yoyote ihitajikayo kunyweshwa.

Uchafu wote na sumu hutolewa na kupelekwa kwenye viungo vilviyokusudiwa kutoa nje uchafu na sumu hizo, kama kibofu cha nyongo, utumbo, tezi za jasho za makwapa na nyonga, na kadhalika. Jauhari ya nyongo huenda kwenye kibofu cha nyongo, baadhi ya jauhari huenda kwenye bandama na unyevunyevu huenda kwenye kibofu cha mkojo.

Hebu fikiria ustadi ambao umefanywa katika kuujenga mwili! Uzuri ulioje uliounganishwa kwa viungo hivi! Jinsi mishipa (ya damu na maji), utumbo na kibofu n.k. vimepangwa kukusanya uchafu wa mwili ili kwamba kuuzuia kutokana na kutawanyika mwili wote na kusababisha magonjwa na uchafu.

Basi utukufu ni wake yeye ambaye ameumba viungo hivi kutokana na mpango wneye sifa na ustadi. Sifa zote ni zake Yeye, Ambaye anastahiki kwayo."

 

 

MAENDELEO YA JUMLA YA MWILI WA MWANADAMU

 

Nilisema. "Kunradhi Maulana! Nieleze kukua kwa mwili kidogo kidogo, hatua kwa hatua mpaka kufikia ukamilifu wake."

Yeye (a.s.) akasema, "Hatua ya kwanza ya kukua huku ni kijusu ndani wa mfuko wa uzazi - isiyooenekana kwa jicho na isiyofikiwa kwa mkono. Kukua kwake hutokea kwa kasi, mpaka anakamilishwa katika mwili pamoja na viungo vyote na sehemu kukamilika kwa kila jambo, moyo, ini, utumbo na sehemu zote zifanyazo kazi, mifupa, misuli, nono, mishipa ya ubungo, mishipa ya damu, mifupa laini n.k. vyote vimekuzwa kikamilifu.

Anaingia ulimwengu huu, na unaona jinsi anvyoendelea kukua pamoja na viungo vyake katika uwiyano, wakati huo huo akihifadhi maumbo yake yote bila ongezeko lolote au upungufu wowote. Hakuna mtengano wowote wa sehemu, kuongezeka chochote katika nyama au kuondolewa chochote kilichozidi. Mwili huendelea kukua, huku ukihifadhi umbo lake lililoumbwa vema, mpaka kukomaa kwake, iwe muda wake wa uhai umerefushwa au kufupishwa mapema.

Je, si mpango wake wa maana sana na ustadi mzuri uliosanifiwa na Msanii mweny kujua yote?"

 

 

UBORA WA MTU JUU YA WANYAMA

 

Hebu fikiria ubora wa uumbwaji wa mtu juu ya wanyama. Anasimama wima na kukaa sawa sawa kumuwezesha kushika vitu mikononi mwake, kuvipata kwa viungo vyake, kufanya kazi kwa mpango.  Kama mtu angekunjwa kama wanyama, asingeweza kufanya kazi azifanyazo sasa.

 

 

HISIA TANO ZA FAHAMU

 

Hisia tano za fahamu ni bora zaidi, tofauti na zile za wanyama kwa maana ya hulka na ufanisi ili kwamba kumjaalia sifa maalum kwa sababu hii.

Macho yamewekwa katika kichwa kana kwamba ni taa iliyowekwa juu ya nguzo kumuwezesha kuona kila kitu. Hayakuwekwa katika sehemu za chini za miguu kuilinda salama dhidi ya majeraha na ajali wakati wa kazi au mwendo, ambao ungeweza kuyadhuru na kudhoofisha ufanisi wake.

Yangewekwa katikati ya sehemu ya mwili kama vile tumboni, mgongoni au kifuani, ingekuwa vigumu kuyazunguusha au kuona vitu kwa mgeuko wa haraka. Kichwa ni kivutio - sehemu bora kabisa kwa hisia hizi za fahamu, pakufaa kulinganisha na kiungo kingine chochote.

Hisia hizi za fahamu ziko tano kwa idadi kujibu aina zote za vichokoo na bila kukiacha kichokoo chochote kutogundulika.

Macho yamehulkiwa ili kutofautisha kati ya rangi. Rangi zingelikuwa hazina maana bila kuwa na welekevu huu wa macho, kwa vile rangi hizi zipo kwa njia ambayo kwamba vitu vyaweza kutofautishwa kutoka kimoja na kingine, au macho hayo yangepata burudani kwayo.

Masikio yamewekwa katika kichwa kutambua sauti, ambazo kwamba zisingekuwa na maana bila uwelekevu huu wa masikio. Kadhalika ni sawa na hali ya hisia nyingine za fahamu - bila welekevu wa hisia ya fahamu ya kuonja, vyakula vyote vitamu vingekuwa visivyokolea, bila hisia ya fahamu ya kugusa, hisia ya joto, baridi, ulaini, ugumu, ingekuwa sawasawa tu kana kwamba hazipo; na bila hisia ya kunusa, manukato yote yangekuwa kama kifu.

Na hivyo hivyo, kama kungekuwa hakuna rangi, macho yangekuwa hayana nguvu. Bila sauti, masikio pia yasingekuepo. Hivyo hebu fikiria jinsi ilivyoamrishwa kwamba kuna uafikiano wa dhahiri baina ya kiungo cha hisia ya fahamu na hisia - kichokoo kuingiliana - kiutendaji kazi zao kiuafikiano. Hatuwezi kusikia kwa macho yetu, wala kutofautisha rangi kwa masikio yetu, wala kunusa ila kwa pua zetu, na kadhalika.

Kisha kuna vijumbe (media) viunganishavyo vilivyowekwa kati ya kiungo cha hisia na kichokoo cha hisia, ambapo bila hivyo kiunganisho (baina ya viungo) kisingewekwa. Kama kwa mfano kutokuepo nuru kuinga'risha rangi, macho hushindwa kutambua rangi na bila hewa kufanya mawimbi ya sauti, masikio yasingekuwa na uwezo wa kutambua sauti yoyote.

Basi yaweza kufichika, kutoka kwa ambaye amejaliwa na akili nzuri na mtu ambaye hutumia akili yake sawa sawa, baada ya maelezo yote haya niliyotoa kuhusu mwingiliano wa viungo vya hisia, hisia-kichokoo na vijumbe (media) viunganishavyo kukamilisha hatima hii, kwamba kazi yote hii imepangwa na kutekelezwa na mjuzi wa yote mwenye nguvu zoto Allah (s.w.t.).

Yawezekana utratibu huu, ustadi huu utokee to wenyewe? Vipi maumbile yenyewe yataweza kufahamu namna gani jicho au sikio liumbwe, na kazi zipi kila kimoja izifanye na kijumbe (medium) gani kitakifaa kila kimoja kama njia kwa mfungano sahihi ili kukiumba kila kimoja?

Je, ni yenye kuwazika katika maumbile yasiyo na akili, isipokuwa Msanii Mwenye nguvu zote avipangilie juu ya Msingi wa ujuzi wa Mwenye kujua yote?

Hebu fikiria hali ya mtu ambaye amepofuka macho yake na hasara anayopata katika kazi zake za kila siku. Hawezi kufahamu pa kuweka mguu wake, iwapo miguu yake itaangukia katika bonde katika muinuko, wala hawezi kuona mbele, wala kutambua rangi, wala hawezi kufahamu uso wa furaha au wakuchukizwa. Hatakuwa na uwezo wa kujua penye shimo, wala kujua adui na upanga (mkononi) uliofutwa, wala hawezi kufanya kazi yoyote ya mikono kama kuandika, biashara au utengenezaji wa kipambo kidogo. Ubongo wake hudokeza njia fulani kumuwezesha kutembea huku na huku au kula chakula chake, ambapo bila hivyo angelikuwa sawa na jiwe lililotulia.

Kadhalika ni sawa nahali ya mtu mwenye kasoro katika kusikia. Hupata hasara juu ya mambo mgeni. Hana furaha ya kusema katika maongezi, wala fahamu ya kuhisi sauti ya kupendeza au mbaya. Watu wanapata tabu ya kuongeya naye, hujichukia mwenyewe. Ingawa yu hai, yuko kama aliyekufa kwa upande wa kuongea. Ingawa yupo, bado ni kama mtu aliye mbali sana asiye na habari za aina yoyote.

Mtu asiye na akili ni mwenye hali mbaya sana kuliko ng'ombe, kwani hata ng'ombe hutambua mambo mengi yasio na maana kwake. Je, huoni kwamba viungo hivi, mambo haya akili hizi na kila kitu kingine kihitajiwacho kwa marekebisho yake na ambapo bila hivyo yuko katika hasara kubwa katika hali ya ukamilifu wa kuumbwa kwake, amevipatiwa ipasavyo?

Je, vyote hivi vimetengenezwa bila uwiyano, owezo na elimu? Hakika sivyo! Kiumuhimu hivi ni matokeo ya Usanii halisi na mpango wa Msanii Mwenye nguvu zote."

Niliuliza, "Maulana! Vipi inakuwa kwamba baadhi ya watu wanapungukiwa katika viungo hivyo na mambo hayo na wanapatwa na hasara hizo ambazo umezieleza?"

Yeye (a.s.) akasema: "Ni kwa ajili ya ukumbusho kwa mtu aliyepungukiwa viungo na watu wengine hali kadhalika.

Mfalme anaamrisha raia zake katika njia za namna hii, amri kama hiyo haichukiwi, bali inafurahiwa kwa hila na kusifiwa.

Watu hao ambao wameumizwa hivyo watafidiwa baada ya kufariki, maadamu ni wenye shukurani kwa Allah (s.w.t.) na kugeukia kwake kiukarimu hivyo kwamba shida zote walizopata kutokana na upungufu wa viungo hivyo kuonekana duni katika ulinganifu (kwa fidia walizopata). Kiasi kwamba kama baada ya kufariki watapewa nafasi ya kurudi tena kwenye shida hizo, wangeikaribisha fursa hiyo ili kupata fidia kubwa zaidi.

 

 

MAUMBO KATIKA JOZI NA KIMOJA KIMOJA

 

Hebu fikiria ustadi na usanii uliooanishwa katika msingi wa Uumbaji wa viungo na maumbo katika jozi au kitu kimoja. Hebu fikiria kichwa ambacho kimeumbwa ni kitu kimoja na hii si kwasababu nyingine, bali kuweka kwa kusudi fulani tu, kisiwe kimeumbwa kwa zaidi ya kitu kimoja. Kichwa cha pili ingekuwa ni ongezeko la uzito tu, usio na umuhimu kabisa, kwa kuwa kichwa kimoja hukusanya hisia zote za fahamu zihitajiwazo kwa mtu. Vichwa viwili ingekuwa na maana ye sehemu mbili za watu. Hivyo kama angetumia kimoja kuzungumzia, kingine kingekuwa hakina kazi. Kutumia vyote kwa pamoja kwa mazungumzo hayo hayo kusingekuwa na maana yoyote kwani hakuna kusudi la zaidi lipatikanalo kwayo.

Mtu angekuwa amekwazishwa mno katika shughuli zake anazopaswa kufanya, kama angaliumbwa na mkono mmoja badala ya miwili.

Je, huoni kwamba fundi seremala au fundi mwashi angeshindwa kuendelea na kazi yake kama mmoja wa mikono yake umepooza?

Na hata kama angejaribu kufanya kazi yake kwa mkono mmoja hawezi kuifanya kiustadi na kiufanisi kama ambavyo angefanya kwa mikono miwili.

 

 

SAUTI

 

Hebu fikiria sauti ya mtu na mazungumzo, na kuumbwa kwa viungo vinavyohusika na hii sauti. Kongomeo, ambalo hutoa sauti ni kama mrija ambapo ulimi, midomo na meno hutengeneza sauti kuwa herufi na maneno.

Je, huoni kwamba kibogoyo hawezi kutoa sauti ya erufi ya 'S', ambaye midomo yake imekatwa hawezi kutamka 'F', ambapo ulimi mzito hauwezi kutoa sauti ya 'V'? Zumari hufanana mno nalo (hilo kongomeo). Kongomeo hufanana na Mfuko ambamo hewa hupulizwa humo, kulingana na mapafu yenye hewa.

Misuli inayowezesha mapafu kutoa sauti hufanana na vidole vinavyo bonyeza hewa ya mfuko kwenda kwenye bomba. Midomo na meno ambayo hutengeneza sauti kuwa herufi na maneno hulingana na vidole katika tundu zabomba na kutoa muziki na wimbo.

Kongomeo hapa linachukuliwa kuwa sambamba na zumari kwa njia ya maelezo, ambapo kwamba kiuhakika zumari ni ala (ya muziki) iliyotengenezwa katika mfano wa kiungo cha asili, kongomeo.

Viungo vya kunena vilivyo fafanuliwa hapa, yatosha kuwa mfano sahihi wa herufi. Iwayo yote, viungo hivi, matumizi mengine yamefanyizwa anwani na hivi. Kongomeo kwa mfano, limebuniwa hivyo kuingiza hewa safi kwenye mapafu kwa kusambaza kwenye damu na moyo, ambapo kama likishindwa hata kwa muda mdogo tu, ingeleta kifo.

 

 

ULIMI NA MDOMO

 

Ulimi umefanyizwa kutofautisha kati ya mionjo mbalimbali ya vyakula kimoja kutoka kingine, kitamu kutoka kichungu, kichungu halisi kutoka kitamu, kichungu cha chumvikutoka kitamu. Ulimi vile vile husaidia kuhisi uzuri wa maji na chakula. Meno hutafuna chakula kuwa laini vyakutosha kuyeyushwa. Vilevile huzuia midomo kubonyea ndani ya kinywa. Kibogoyo anaonekana kuwa na ndomo iliyolegea. Midomo husaidia kunyonya maji ndani, hivyo kuruhusu kiasi cha kufaa kuingia tumboni kama yahitajiwavyo, sio kuvimbiza kwa kulingana kwake na kuleta kusongwa roho katika koo, au kuacha uvimbe kwa baadhi ya vitu vya ndani kwa uwezo wa kutiririka kwake kwa nguvu. Zaidi ya hapa, midomo miwili inafanya kazi, kama mlango kuweka mdomo kufunga upendapo. Tumekueleza namna mbali mbali za matumizi yaliyofanywa na hiyo midomo na ulimi na matokeo ya faida (za kimaumbile) kutoka kwayo, kama vile chombo cha aina moja kiwezavyo kufanya miradi tofauti. Kwa mfano shoka ambayo fundi seremala anaweza kuitumia na ambayo yaweza kutumika kuchimba ardhi na kwa matumizi mengine.

 

 

MAUNGO YA KUHIFADHI

 

Kama ukiangalia kwenye ubongo, utaona umefunikwa katika ngozi nyembamba moja juu ya nyingine kuuhifadhi kutokana na madhara na mtikisiko. Fuvu la kichwa huuhifadhi kama kofia ya chuma dhidhi ya kuvunjwa vipande pande kwa kugonga au mshindo kwenye kichwa. Fuvu limefunikwa na nywele kama mfuniko wa manyoya ya kondoo kuulinda salama dhidhi ya joto na baridi.

Nani, basi, isipokuwa Allah Mwenye Nguvu zote ameujalia ubongo na usalama huo na kifuniko, na ambaye amekifanya ni asili ya hisia za fahamu, na ambaye amefanya mipango kwa hifadhi yake ya ajabu katika kulinganisha na sehemu nyingine zote za mwili kwa sababu ya kiwango cha umuhimu wake katika uwelekevu wa mwili?

Hebu fikiria ukope, jinsi ulivyoundwa kama pazia la jicho pamoja na kope zake kama kitani, kwa kunyanyulia na kuteremshia pazia. Hebu angalia mboni ilivyowekwa kwenye tundu ikifunikwa na kivuli cha pazia na nywele.

Nani ameustiri moyo ndani ya kifua na kuufunika na pazia ambalo mnaliita utando? Nani aliyepanga hifadhi yake kwa njia ya mbavu, misuli na nyama zilizosokotwa katika njia ambayo ni ya kuzuia kitu chochote kisiingie ndani yake na kusababisha mchubuko? Nani aliyezifanyiza tundu mbili katika koo, moja kwa utoaji wake wa sauti imewekwa kwa ukaribu na mapafu na niyingine inaitwa umio inaelekea kwenye tumbo kwa upitishaji wa chakula. Na ni nani aliyeyweka kilango, kimio, (kidaka tonge) juu ya tundu inayoelekea kwenye kongomeo, kuzuia chakula kuingia kwenye mapafu, ambacho kingesababisha kifo kama kama isinge dhibitiwa hivyo? Nani aliyefanya mapafu kupuliza hewa kwenye moyo pasipokuchoka bila kupumzika kuondoa sumu ambazo vinginevyo zingeuaribu?

Nani aliyetengeneza misokoto ya misuli, izuiyao mkojo na kinyesi kutoka nje, kama vigwe vya mfuko, kufunguliwa au kufungwa kwa kupenda sio kuchurizika wakati wote wenyewe, na kuwa matokeo ya udhia wa kudumu katika maisha?   Kadhalika kuna mambo ambayo kadiri ingekadiria, lakini mengine ambayo mtu hana elimu nayo, yako mbali na ukadiriaji. nani amejaalia kunepa huku kwa misuli ya tumbo ambalo limeamrishwa kuyeyusha chakula cha ukakasi? Na ni nani aliyeifanya ini laini na mororo kupokea lishe iliyochujwa na katika hali ya kusfishwa sana na kufanya kazi kwa uborazaidi kuliko tumbo? Yawezekana kazi zote hizi kufanywa na yoyote isipokuwa na Mwenye Enzi yote Mwenye Nguvu zote? Unaweza ukufikiria kwamba yote haya yaweza kufanywa na maumbile mfu? Hakika sivyo! Vyote hivi ni mpango wa Mwenye nguvu zote msanii Mwenye Enzi zote, ambaye ana elimu iliyojaa na ana ukamilifu wa Enzi zote kabla ya uumbaji. Yeye ni Allah, Mjuzi wa yote Mwenye nguvu zote.

Hebu fikiria kwa nini ute mororo wa mfupa ulivyowekwa kwa hifadhi ndani ya Mirija ya mfupa - kwa ajili tu ya kuuhifadhi dhidhi ya kuharibika kwa kuathiriwa na joto la jua ambalo linge uyeyusha, au kule (kuathirika) kwa baridi ambako kungeufanya ugande, ambapo maisha yangeangamia - ute wa mfupa ni kichanganyiko muhimu cha asili kitoleacho nishati kwa mahitaji ya mwili.

Na kwa nini huu mzunguko wa damu umewekwa katika mishipa ya damu, isipokuwa ni kwamba ifanye kazi ndani ya mwili na sio kutiririka nje? Kwa nini hizi kucha zimewekwa kwenye vidole isipokuwa ni kwamba ziweze kuvihifadhi dhidhi ya madhara, na kusaidia katika ufanisi mzuri, kwani bila kuwa nazo, kuwepo kwa nyama peke yake kusingemuwezesha mtu kuokota kitu kwa kufinya kutumia kalamu kwa kuandika au kuweka uzi kwenye sindano?

kwa nini sikio limewekwa sehemu nyingi kama nyumba ya jela, isipokuwa ni kwamba sauti zingechukuliwa kwenda kwenye utando (ngoma ya sikio) kwa utambuzi bila madhara kwalo kwa mshindo na mgongano wa hewa?

kwa nini nyama hizizisokotwe juu ya nyonga na matako ya mtu, isipokuwa ni kwamba, asipate kutaabika kwa ugumu wa sakafu katika kukaa kama ilivyo kwa mtu mwembamba na mwenye umbo lililodhoofika, mpaka kitu kiwekwe kati yake na sakafu kupunguza ugumu, kama mto au tandiko?

Nani aliyeumba taifa la kibinadamu kama mwanaume na mwanamke? Ni Yeye Ambaye ameamrisha taifa kustawi kwa njia ya muungano wa jinsia mbili au iwayo yote kudumisha wingi wa nguvu zake kwa njia wa utofautishaji wa jinsia hizo mbili.

Na ni nani aliyemfanya kuwa yeye ni Mzazi wa kizazi? Kwa hakika ni Yule Ambaye alitia tumaini ndani yake. Isingekuwa shauku hii kusuka suka kifua chake, kwa nini kuwe na chagiza (hamu ya ndani) ya wao kwa wao kuungana. Tizama uzazi wa vitu vinavyoishi kati yao ambavyo havikuwekwa ulazima (wa kuzaa) kwa muungano na kijinsia, lakini huletwa kwa hatua fulani ya kukua ya uke. Havina utofautishaji wa ume na uke kabisa. Je, yawezekana mtu yoyote, kwa mfano, kueleza kati ya ume na uke wa nyigu?

Nani aliyempa yeye (mtu) viungo kwa kufanya kazi? Hakika ni yule ambaye amemfanya (kuwa) mfanya kazi. Na ni nani aliyemfanya mfanyakazi? Hakika ni yule ambaye ameuumba kuwa mhitaji kwani mtu asingelifanya kazi kama hanahaja ya kukidhi. Kama asinge kuwa na haja kukidhi njaa yake, kwa nini ajitaabishe, kwa nini ajitie katika shighuli na utendaji. Angelikuwa hana haja ya kulinda nwili wake salama dhidhi ya joto na baridi, kwa nini impase kujifundisha kushona, kutengeneza sindano,kusokota nyuzi, kufuma, ukulima wa pamba na kadhalika. Na kutowepo kwa yote haya, ni matumizi gani yangelikuwa kwa viungo vya kufanya kazi na vidole? Na ni nani aliyemuumba yeye fukara? Hakika ni Yule Ambaye ameumba kwa ajili yake hali ya ufukara. Na ni nani aliyemuumba kwa ajili yake hali ya ufkara? Hakika ni Yule Ambaye amejichukulia juu yake mwenyewe jukumu la kumpatia mahitaji.

Nani amemjaalia yeye (mtu) kuwa na akili? hakika ni Yule Ambaye amefanya malipo na adhabu kama kanuni kwa ajili yake. Asingelihitaji akili kama asingelipasika kwa malipo na adhabu. Mwenye Nguvu zote Muumba amemjalia yeye kuwa na akili ili kutofautisha kati ya jema na ovu, Akiwa ameamua juu ya malipo na adhabu kama kanuni kwa ajili yake kupata malipo kwa wema na adhabu kwa uovu. Viumbe hai ambavyo havipasiki malipo na adhabu havina hisia ya jema na ovu, wala havijui kutofautisha baina ya haramu na halali, na aina ya matendo yaliyokatazwa na yaliyo ruusiwa. Walakini hutambua mambo yahitajiwayo nao kwa ajili ya kuishi kwa jamii yao au kiupweke. Kama kwa mfano, ndege anayo lazima ya kutambua kwamba (yeye) ndege ni mawindo ya tai, na hivyo kumuona kwake tu, humfanya aruke kwa kasi, au kulungu hujua vizuri kwamba simba angemchanilia mbali, hivyo kule kumuona kwake tu, hukimbia kuokoa maisha yake.

Nani aliye mjalia kuwa na maarifa na fahamu? Hakika ni Yule Ambae amembariki yeye kwa nishati. Na ni nani aliye mbariki yeye kwa nishati? Hakika ni Yule Ambaye ameamuru uthibitisho wa kuongoza juu yake. nani anamsaidia yeye katika shughuli zote hizi ambazo kwayo mipango yake hushindwa? hakika ni yule, ambaye anastahili shukurani zetu za juu mno.

hebu fikiria mambo niliyo kwisha kukuelezea. Je, yawezekana kuwepo na mpangilio na taratibu kama hizi bila ya kuwepo upangaji? Hakika sivyo! Allah Mwenye Nguvu zote yu mbali na ametukuka juu ya mambo wanayoyasema watu hawa.

Iwapo ungeona ubao mmoja wa mlango ukiwa na komeo lililokazwa juu yake. Je, unaweza kufikiria kwamba limefungwa hapo bila ya kusudio lolote? Hakika utatanabahi kwamba liko pale kuunganishwa kwenye ubao mwingine kwa faida ya dhahiri. Kadhalika utaona kiumbe wa kiume kama mmoja katika jozi kimeumbwa kwa ajili ya kiumbe mwanamke kwa muungano kuendeleza taifa.

Allah (s.w.t.) awaangamize wale ambao wanadai kuwa ni mafilosofa, lakini ni wadhaifu wa kuona katika kuyaendea maajabu haya ya uumbaji na hulka ambazo wamezikana katika uumbaji wa ulimwengu, usanii wa Msanii mwenye Nguvu zote na Kupenda kwa Bwana Mpangaji.

Hebu tizama kwa macho ya uheshima katika fadhila kubwa ya Allah Mwenye nguvu zote katika kutulia kwa taabu baada ya kula chakula na kinywaji. Je, huu siyo uzuri wa mpango katika ujenzi wa nyumba kwamba choo chapaswa kuwa sehemu iliyotengwa kwa hii nyumba?

Katika njia kama hiyo, Allah Mwenye Nguvu zote ametengeneza tundu kwa ajili ya uchafu utokao katika mwili wa mtu katika sehemu ya faragha. Siyo katika uwazi wala  haikujitokeza, bali imewekwa hivyo kwa kufichika kikamilifu kwa muunganiko wa nyonga na matako na nyama zao. Wakati mtu anataka kukidhi haja na akawa katika hali ya kuchutama, tundu huruhusu uchafu kutoka.

Hebu fikiria seti ya meno katika kinywa cha mtu, baadhi ni makali, ambayo huchanja na kupasua chakula. Mengine ni butu ambayo utafuna na kufunda. Kwa vile aina zote zinahitajika, amepatiwa ipasavyo.

 

 

NYWELE NA KUCHA

 

Hebu fikiria na tambua ustadi uliomo ndani kwa nini ni sahihi kunyolewa nywele na kucha kupunguzwa. Zinakua na kuongezeka na hivyo huhitaji kukatwa. Kwa ajili hiyo hazina hisia kuepusha maumivu kwa mtu. kama kukata hivyo kungesababisha maumivu, ima zingeachwa zikue bila mpangilio na kuwa mzigo wa kuudhi, au ingelitia maumivu katika kukatwa."

Niliuliza, "Maulana! Kwa nini zisirekebishwe bila ya kutononeka kufikia kwamba kukatwa kwao kuwe lazima?"

Yeye (a.s.) alisema, "naam, ziko baraka zisizo na idadi za Allah Mwenye Nguvu zote kwa Viumbe vyake zifahamikazo kwao, na ambazo kama wangelizijua, wangeshukuru kwayo.

Elewa kwamba matatizo na maradhi ya mwili yanatulizwa kwa njia ya nywele hizi zitokazo nje ya vinyweleo. Vidole hupata nafuu ya maradhi yao kupitia kwenye kucha. hiindiyo sababu ukataji wa kucha kwa juma, kunyoa kichwa na kuondoa nywele zilizozidi lazima kufanywe, ili kwamba kucha na nywele ziweze kukua haraka na kutuliza maradhi na matatizo, kama sivyo, maradhi hubaki yamezuiwa mwilini kufuatiwa na maumivu na magonjwa.

Hakuna ukuaji wa nywele uanoruhusiwa kwenye sehemu za mwili ambako zingeleta madhara kwamtu. Kama nywele zingeota ndani ya macho angepofuka. kama zingeota ndani ya kinywa, je, maji na chakula visingezuiwa? kama zingeota kwenye matumbo ya viganja vya mikono, je, zisingepunguza uwezo wa hisia ya kugusa na hali hiyo isingeingilia ufanyaji sahihi wa kazi nyingi na utambuzi wa ugusaji halisi?

Kuna ustadi mkubwa uliomo ndani kuweka sehemu makhsusi za mwili bila nywele. Je, maumbile yangeweza kuwa na utambuzi wa busara nzuri au mipango ya usanii huu mzuri ingeweza kuhusishwa na haya maumbile?

Msiba uwapate walahidi hawa na upumbavu wao. hii habari ya uumbaji, na tizama ilivyo kosa na madhara kwa hayawani na manyama wengine, ambao uzazi wao hutegemea ngono, wanafananishwa hivyo hivyo.

Unaona kwamba miili yao yote imefunikwa na nywele, isipokuwa sehemu maalum kwa sababu hizo hizo. hivyo fikiria habari hii ya uumbaji na tizama jinsi gani njia za makosa na madhara zilivyoepukwa ambapo maadili na faida vimewekwa salama.

Wakati wafuasi hawa wa mani na wale wa namna yao walipojaribu kukana imani hii katika uumbaji wa kimadhumuni, waliona kosa la uotaji wa nywele katika kinena na makwapa. Walishindwa kufahamu kwamba kuota huko kumetokea kwa sababu ya unyevunyevu unaochuruzika kwenye sehemu hizo. nywele hizo huota pale kama vile majani yaotavyo katika sehemu ambayo maji hujikusanya. Je, huoni namna gani sehemu zinavyotayarishwa kwa kukusanya uchafu na kuuzuia?

bado busara nyingine iliyomo ndani yake, ni kwamba, inaondoa udhia mmoja zaidi mtu engediriki, kuhusiana na mwili wake, na yeye ni, mbali na hayo, kwa vile ameshughulishwa na usafi wa mwili wake na uondaji wa nywele zake, kazuilika kufanya matendo ya uchoyo, ukatili, kiburi na ufedhuli, ambayo kwamba hangepata fursa ya kuyafanya.

Hebu fikiria mate katika kinywa na ona hekima iliyomo ndani yake. Yamefanyizwa hivyo ili kuhakikisha mchirizi wa kudumu kuweka unyevu katika koo na kaa la kinywa siyo kuruhusu ukavu kwayo ambao ungesababisha kifo. Bila hayo chakula kisingeweza kutafunika wala kisingemezeka. Yote haya ni wazi na kuthibitishwa kwa uchunguzi. Na elewa kwamba maji haya chimbuko lake nikutokana na chakula na yakifika ndani husaidia kazi ya nyongo.

 

 

KUFUNIKWA KWA TUMBO

 

Baadhi ya wabishanaji wajinga na wadai wenye akili pungufu katika filosofia, kwa sababu ya uelewaji wao wenye kasoro na elimu potofu, wamesema, "Ingelikuwa vizuri zaidi kama tumbo la mtu lingekuwa kama joho kumuwezesha daktari kulifngua apendapo, kuangalia vitu vyake vya ndani na kuingiza mkono wake ndani kwa ajili ya matibabu, na sio kama jinsi lilivyo (kuwa na ukuta wa nyama na ngozi), limefichwa ki-ajabu kwa kuonekana na macho na kufikiwa na mkono. Magonjwa ya ndani yanaweza tu sasa kupimwa kwa dalili za ugonjwa kwa uchunguzi wa mkojo, mapigo ya mishipa na kadhalika, ambapo haziko katika kosa na shaka kufikia kwamba kosa kama hilo katika uchunguzi wa mapigo ya mishipa na mkojo laweza kusababisha kifo.

Lau kama wangejua wadai hawa wajinga katika Filosofia na washindani, kwamba ingeondoa hofu yote ya ugonjwa na kifo.  Basi mtu angepumbazika na maisha yake ya umilele na ya siha nzuri, ambayo yangemfanya kuwa mkaidi na mwenye majivuno.  Tumbo lililo wazi lingeruhusu mchuruziko wa daima wa unyevunyevu, hivyo kuharibu kikao chake, kitanda na mavazi yake mazuri; kwa ufupi, maisha yake yote yangekuwa katika hali hizo.

Tumbo, ini na moyo hufanya kazi sawasawa kutokana na joto muhimu, ambalo lingeathiriwa na hewa ya nje ipitayo kwenye tumbo lifanyiwalo matibabu, lililowazi lionekanalo na jicho na kufikiwa na mkono.  Hii ingesababisha kifo.

Huoni kwamba udhanifu wote juu ya asili ya kweli ya uumbaji na muundo usio na maana ni wa upuuzu?

 

 

MATAMANIO

 

Hebu fikiria jambo la kulisha, kupumzika na ngono, ambavyo vimeumbwa kwa ajili yake na manufaa yaliyomo ndani yao.  Kila kimoja katika hivyo kinasukumiwa tamanio, ambalo husababisha hamu na msisimko kwayo.  Njaa huhitaji chakula ambacho huleta uhai na nishati katika mwili na uimara wake.  Usingizi huhitaji kupumzika kwa ajili ya afya ya mwili kuondoa uchovu.

Kama mtu angekula chakula kwa ajili tu ya mahitaji ya mwili wake bila tamanio kutoka ndani limlazimishalo kula, inawezekana kwamba angeupa mwanya ulegevu kwa sababu ya uchovu au shinikizo, mwili wake ungedhoofika na kusababisha kifo, kama vile mtu aachavyo kunywa dawa ambayo ndiyo pekee ahitajiayo kustawisha hali yake.  Na hii ingesababisha kifo chake.

Kadhalika angeacha usingizi kwa ulegevu na kwa hiyo kudhoofisha mwili wake, kama angekusudia tu kwa sababu hii ya kupumzika kwa ajili ya mwili wake na uondoshaji wa uchovu wa viungo vyake.  Kama kuzaa kungekuwa ndiyo lengo pekee la muungano kwa jinsia isingekuwa yamkini kwa upande wake kuzembea, na kutokea kupungua kwa idadi ya watu na mwisho wa kukoma kwao, kwani kuna watu hawana hamu ya kuwa na Kizazi (Watoto) wala haja yoyote kwayo.

Angalia, basi  kwamba tendo lile lile linalohusu siha ya mtu na ustawi limetiliwa nguvu kwa tamanio lishurutishalo lililowekwa ndani yake katika asili yake likimwongoza kwayo.

 

 

STADI ZA MAUMBO YA MWILI

 

Na elewa kwamba umbo la mwili lina Stadi nne :-

(1) Stadi ivutayo - Hii hupokea chakula na kukisukuma ndani ya tumbo.

(2) Stadi ya kuhifadhi - Hii  hukihifadhi chakula kwa ajili ya kufanyiwa taratibu za kawaida juu ya chakula hicho.

(3) Stadi ya kugeuza - Hii hufanya chakula kutoa mseto wake ili kuusambaza katika mwili.

(4) Stadi ya kuondosha - Hii huondoa uchafu baada ya Stadi ya kugeuza kukamilisha kazi yake.

Hebu fikiria mrekebisho huu uliofanywa mwilini baina ya Stadi hizi nne.  Hizi zimefanywa kutosheleza mahitaji ya mwili kama sehemu ya Usanii wa Mwenye Kujua Yote.

Bila Stadi ya kuvuta, angewezaje kukitumia chakula hicho ambacho ni muhimu kwa ujenzi na ustawi wa mwili wake?

Bila Stadi ya kuhifadhi, vipi chakula hicho kingehifadhiwa tumboni kwa kuyeyushwa?

Bila Stadi ya kugeuza, vipi chakula kingetengenezwa kupata mseto kwa kusambazwa mwilini bila usumbufu?

Na bila Stadi ya kuondosha, vipi uchafu, uliotolewa na tumbo ungeweza kuondoshwa kila wakati?

Je, huoni jinsi Mtukufu Mwenye Nguvu zote Allah Ameamuru  na  kuzipanga Stadi hizi kwa ajili ya kazi na sharti la kuleta Afya ya mwili kwa kutimiza Ufundi wake na Enzi Kuu ya Mamlaka?

Hebu ngoja tuonyeshe kwa mfano.  Hebu chukulia mwili kama Ikulu  ya Kifalme, pamoja na watumishi wake na jamaa wakaao humo.  Wako wafanya kazi wakihusika na uendeshaji wake.  Mmoja wao amepewa jukumu la kuleta vyakula kwa jamaa.  Wa pili amepewa jukumu la kukihifadhi ili kiweze kuwekwa kwa kubadilishwa kuwa lishe.  Wa Tatu ni mwenye kukitengeneza na kukisambaza.  Wa nne kufagia uchafu ulioachwa.

Mfalme wa Ikulu hiyo ni Mwenye Kujua Yote, Mwenye Nguvu zote, Mola wa Ulimwengu Wote.  Ikulu ni Mwili wa Mtu, jamaa ni viungo vya mwili, ambapo Stadi Nne zile ni Wafanyakazi.

Huenda, pengine, ukafikiria maelezo niliyoyatoa kuhusu Stadi hizi nne na kazi zao kama nyingi mno zisizo na umuhimu.  Bado maelezo yangu hayafuati mpango wa Vitabu uliotolewa na Madaktari, wala 0mahadhi ya mazungumzo yangu hayafuati ya kwao, Watu hao wamezitaja Stadi hizi nne katika msingi wa kwamba unahitajika katika fani ya uganga kwa ajili ya kuponyesha.  Tunautaja kutoka mtizamo wa hitaji lake la kuimarisha imani na matengenezo ya watu vichwa ngumu, kama yalivyo maelezo yangu machache yenye ufafanuzi mpana na mfano, kuonyesha Usanii wa Mwenye Kujua Yote.

 

 

STADI ZA SAIKOLOJIA

 

Fikiria juu ya Stadi zilizowekwa ndani ya nafsi ya mwanadamu na jinsi zilivyopangwa katika kuelewa, kuamua, kudhania, kuhoji, kukumbuka n.k.  Ingekuwa vipi hali ya mtu kama angenyimwa Stadi ya kumbukumbu, na kwa kiasi gani mambo yake ya maisha yangevurugika - mambo yake ya kiuchumi, na biashara yake.  Asingekumbuka anachowiwa na watu wengine na anachowia wengine.  Maafikiano ya bei aliyofanya, alichosikia na alichosema:-

Asingekumbuka aliyemfanyia tendo jema na aliyemtendea tendo ovu, na kipi kilichomnufaisha na kipi kilichomdhuru.  Asingekumbuka njia aliyopita mara nyingi. 

Asingekumbuka kitu chochote hata kama angeendelea kujifunza Sayansi maisha yake yote, wala asingeliweza kuamua juu ya itikadi au imani, wala kuweza kulinganisha kitu kimoja na kingine kwa muafaka.  Kwa kweli, angeliambuliwa nje ya utu moja kwa moja.  Hebu ona faida iliyoje ya Stadi hizi kwa mtu.  Ukiziacha nyingine, hebu fikiri juu ya moja na nafasi ichukuayo katika maisha yetu.

Hata fadhila kubwa zaidi ambayo kumbukumbu ni yenye usahaulifu, bila huo mtu hangepata faraja katika huzuni yoyote, wala  daima hangeondokana na maudhi, wala ansigeondokana na uovu.  Angeshindwa kupendezwa na chochote katika vitu vya ulimwengu huu, kwa sababu ya kumbukumbu za huzuni zenye nguvu, wala kamwe hangekubali tumaini lolote la kudhoofisha nadhari ya Mamlaka yake ya husuda ya wenye kuhusudu.

 Je, huoni jinsi Stadi zikinzanazo za kumbukumbu na usahaulifu zilivyoumbwa ndani ya mtu, kila moja imeamrishwa kwa lengo maalum?

Na watu wale, kwa mfano wafuasi wa Mani, ambao huamini katika Waumbaji wawili tofauti wa ulimwengu wote hawawezi kwa njia yoyote kutegemewa kufikiria vitu viwili tofauti kama waumbaji wa Stadi hizi mbili tofauti, kwani stadi hizi mbili zinazo faida ambazo unaziona kutokana nazo.

Hebu fikiria ubora ambao kwamba mtu peke yake amejaaliwa na hakuna kiumbe kingine ashirikianae nao (huo ubora) - Stara.  Bila hiyo (Stara), hakuna mtu ambaye angeonyesha ukarimu kwa mgeni, wala yoyote kuweza kutekeleza ahadi yake, wala haja ya mtu yoyote kuweza kutekelezwa, wala wema wowote kupatikana.  Kuna Wajibati nyingi zinafanywa tu kwa Stara.  Yule ambaye anaacha Stara, hakiri haki za wazazi  wake, wala wajibati za ndugu wa damu, wala kuheshimu dhamana yake, wala kuepuka ufedhuli. 

Je, huoni jinsi yote haya yalivyo jaalia katika mtu kiukamilifu hivyo ili kumnufaisha yeye na kukamilisha mambo yake?

 

 

UZUNGUMZAJI NA UANDISHI

 

Fikiria baraka ya uzungumzaji ambao kwamba amejaaliwa na Allah Azza wa Jallah, ambao ni chombo cha kuelezea wazo lake la ndani (moyoni) na hisia zake kunjufu zichipukazo kutokana na fikira yake na ambao kwa huo pia huelewa maana za ndani za wengine.  Bila Stadi hii angelikuwa kama wanyama wa miguu minne si wa kuweza kupeleka wazo lake mwenyewe la moyoni kwa wengine wala kuelewa maneno ya mzungumzaji.

Na hivyo ndivyo ilivyo katika fani ya uandishi ambayo ni njia ya kujua habari za watu waliopita na kwa kuwafikishia wale wote waliopo kwa vizazi vijavyo.  Kutokana na fani hiyo hiyo, mafanikio ya Sayansi na maandiko yanahifadhiwa katika vitabu kwa muda mrefu.  Kutokana na fani hiyo hiyo, huhifadhiwa mijadala na taarifa kati ya mtu mmoja na mwingine.  Bila fani hii, muda mmoja usingelijulikana  kabisa kutoka mwingine; wala zisingepatikana habari zozote kutoka kwa wale walio mbali na nchi zao.

Sayansi pia zingetoweka.  Taarifa juu ya uadilifu na uungwana zingelipotea na madhara makubwa katika mambo ya mwanadamu yangelitokea kama vile pia katika mafundisho ya dini na simulizi, ambayo watu huhitaji kujua na elimu hiyo ingekuwa isiyowezekana.

Pengine ungefikiria kwamba, hoja hii imetimizwa na mtu kwa msaada wa kubuni kwake mwenyewe na akili zake.  Hairithiwi katika maumbile ya mtu.  Na hali ni hiyo hiyo katika kuzungumza na lugha, kwani hili pia ni jambo la istilahi na azimio, huamuliwa na watu kufuatana na maafikiano yao ya kuelewana katika kuzungumza.  Hivyo ndiyo sababu makundi tofauti yana lugha tofauti na maandishi yao, kwa mfano, Kiarabu, Kishamo, Kiebrania, Kirumi n.k.; ambayo kila moja ni tofauti na nyingine, kila moja ikiwa imeamua juu ya istilahi zake yenyewe ya lugha na maneno.

Kwa ambaye anafanya dai kama hilo, jibu litakuwa kwamba ingawa katika mambo yote haya kupanga kwa mtu na kutenda kume changia katika lengo, bado njia ambazo kwayo kupanga kwake na kutenda kumefikiliza lengo, ni kipaji katika ukarimu wa Allah Azza Wajalla uliyomo kwayo.  Iwapo asingetunukiwa mahadhi ya kuzungumza, au akili isingeliwekwa juu yake kumwongoza katika harakati hizo, asingelikuwa na uwezo wa kuzungumza, na kama asingebarikiwa  kuwa na Kiganja na vidole, kamwe isingeliwezekana kwake kuandika.  Na huo ni msingi uliowekwa na Mwenye Nguvu zote Muumbaji na Asili ya Maumbile ya mtu kama fadhila maalum, kwa fadhila hiyo yoyote mwenye kushukuru kwayo atapata  malipo ya Mbinguni, ambayo yoyote atakaye ikanusha atapuuzwa, kwani Allah Azza Wa Jallah ni Mwenye Kujitegemea kwa ulimwengu wote.

 

 

MIPAKA YA ELIMU

 

Fikiria mambo ambayo kwamba elimu amejaaliwa nayo mtu na yale ambayo hakupewa elimu nayo.  Amejaaliwa na Elimu kwa mambo yote haya ambayo humpelekea kwenye mema yake kwa upande wa imani hali kadhalika na maisha yake hapa duniani.

Elimu ya Kiroho ya Allah Azza Wa Jallah Muumba inapatikana kwa njia za hoja na ushahidi upatikanao katika kuwepo kwa uumbaji.  Na pia elimu ya mambo ya wajibu juu yake, kwa mfano, haki kwa Wanadamu wote, upendo kwa wazazi, kutekeleza dhamana, huruma kwa wanao onewa na  kudhulumiwa n.k. elimu na ruhusa ambayo Mataifa yote wanayo kimaumbile  ni ukweli na mambo, ima kwa kupatana nasi au dhidi yetu.

Kadhalika amepewa elimu ya vitu vile ambavyo ni vya manufaa kwa maisha yake kidunia, kwa mfano ukulima, uendelezaji wa kilimo cha bustani, ufugaji, kutoa maji kutoka kwenye visima na chemchemi, utafiti wa miti shamba kwa ajili ya matumizi ya uganga, uchimbaji wa aina mbalimbali za mawe ya thamani, uzamiaji katika bahari, mipango aina mbalimbali ya kuwinda wanyama na ndege, uvivu, viwanda, kazi na mbinu za biashara na mambo mengine ambayo yanahitaji maelezo marefu, ambamo mna utekelezaji wa mambo ya maisha ya kidunia ya mtu, uboreshaji wa mambo ya dini yake na ya ulimwengu wake.  Elimu kama hiyo imefanywa  ipatikane kwake kama ilivyo bora kwa faida zake.

Mambo, ambayo elimu iko nje ya uwezo wake, wala hali yake haiihitaji, hayafanuliwi kwake, kwa mfano, elimu ya ghaibu, mambo ambayo yatatokea baadae au baadhi ya mambo yaliyotokea wakati uliopita, yale yanayo fungamana kwa yaliyo ndani ya bahari na katika eneo kubwa la ulimwengu, au yaliyo katika akili za watu yaliomo katika tumbo la uzazi n.k.  Watu waliodai kuwa na elimu ya hayo madai yao yalibatilishwa kufuatia matukio yao kuwa kinyume chake.

Hivyo hebu angalia, kwamba elimu ya vitu aliyopewa mtu ni ya muhimu kwa mambo yake ya Kilimwengu na ya Kidini.  Amezuiliwa kujua vitu visivyo vya lazima kumvuta katika ubora wake na kasoro yake katika yote haya mna uzuri wake.  Hebu fikiria kwa nini mtu hakupewa elimu ya muda wa maisha yake.

Kama angejua muda wa maisha yake duniani kuwa mfupi maisha yake yote yangechukiza, kwa kujua hivi angelingojea muda wake wa kufa.  Hali yake ingekuwa ya mtu ambaye mali yake yote imepotea au karibuni sana itapotea.  Na angehisi umasikini wake na uhitaji.  Jinsi gani angehofia katika kutazamia kuharibika kwa mali yake na ufukara wa mwisho, huzuni na uchungu ambao angeuona kwa tazamio la kifo ungekuwa mkubwa zaidi kuliko ule wa tazamio la kuharibika kwa mali yake, kwani mwenye kupoteza mali yake wakati wote hubakia na tumaini kwamba huenda atapata zaidi ya hiyo na hilo lingempatia faraja katika akili yake

Kinyume chake yule ambaye amesadikishiwa mwisho wa maisha yake atakuwa amevunjika moyo zaidi.  Kama angelikuwa na muda mrefu wa kuishi, tumaini hili katika kuishi kwake kungempa tumaini lisilofaa.  Angeweza kuelemezwa na anasa na ufisadi juu ya dhana kwamba angeomba toba katika siku za mwisho za maisha zilizobakia kwa anasa hizi za sasa zinazo mshughulisha.  Hili ni jambo ambalo Allah (s.w.t.) halitaki kutoka kwake wala halitaki kwa viumbe vyake.

Iwapo unaye mtumishi ambaye anaendelea kukukosea kwa mwaka mzima, na anatumaini husamehewa dhidi ya utumishi mzuri wa siku moja au mwezi mmoja.  Hakika usingeipenda na mtumishi huyu asingekuwa na sifa sawa na mtumishi mzuri ambaye daima  yuko tayari kutii amri yako.

Unaweza kuleta kinzano kwa hili kwa kusema kwamba haitokei kwamba mtu hupita njia ya upotofu, kisha akatubia na toba yake ikakubaliwa.  Jibu letu kwa hili ni kwamba hii hutokea tu wakati mtu ameshindwa na ashiki yake kufikia hali isiyoweza kuzuilika, lakini wakati wote hana uamuzi katika utii wake juu ya dhana kuonyesha toba baadae wakati anajiingiza katika hawaa kwa sasa Allah (s.w.t.) hamsamehi nje ya Rehema Zake zisizo na mwisho (yaani anasamehewa ndani ya Rehema za Allah (s.w.t.).

Lakini katika Suala la yule ambaye ameamua juu ya upotofu kiasi atakachopenda, akitegemea msamaha katia hatua ya baadae, anajaribu kwa sababu hii kumdanganya Yeye, ambaye hawezi kudanganywa, akifikiria kupata anasa zaidi za muda huu huku akitegemea kusamehewa kwa sababu ya toba yake ya baadae.  Pia, kwa hali hii ya jambo hili, kwamba kwa sababu ya aina fulani ya mfumo wa maisha wa kujiingiza katika anasa huenda usingemruhusu hata nafasi kwa ajili ya toba hususan katika uzee, wakati mwili umepita kiasi kikubwa cha udhaifu umzuiao kuyatekeleza mategemeo yake.

Na mwenye kutafuta visingizio katika kutoa toba yake, isingewezekana kwake katika kifo cha shambulio la ghafla na angeutoka ulimwengu bila kutubia.  Angekuwa kama mdaiwa ambaye ana bidii ya kulipa madeni yake lakini huahirisha mara kwa mara mpaka kifo kumfikia mali yake huharibika na madeni yake husimama dhidi yake, kwa hiyo ni katika usawa wa mambo kwamba elimu ya muda wa kuishi mtu ifanywe ni siri kwake ili kwamba ategemee kifo kumtokea wakati wowote na katika hofu hiyo, aepuke uasi na kuchagua kufanya tendo jema.

Unaweza kuleta Kinzano nyingine kwamba ikiwa muda wake wa kuishi ni siri kwake, na daima yuko kwenye wasiwasi kuhusu kifo chake, hufanya maovu na matendo ya haramu.  Majibu yetu kwa hili ni kwamba mpango uko katika kulingana na hali ijitokezayo.  Kama mbali na haya yote mtu hajizuii na uovu, ni dalili ya tabia yake kupoteka na ugumu wa moyo wake.  Hakuna kosa katika kupanga kama mgonjwa baada ya kujulishwa kikamilifu faida za dawa makhsusi na makosa ya mambo  maalum mabaya, haitamfaa kutumia taarifa kwa kuto heshimu maelekezo ya Daktari.  Daktari si wa kulaumiwa bali mgonjwa aliyekengeuka kufuata agizo la mganga.

Mbali na wasiwasi kuhusu kifo ambao anao kwa sababu ya kutokujua  kwake kuhusu muda wa maisha yake, haachi kufanya maasi.  Angekakamia katika fisadi na uovu sana wa dhambi zisizoelezeka, iwapo angeipata elimu kamilifu ya muda wa maisha yake na kuishi.  Kwa ajili hiyo wasiwasi kuhusu kifo kwa namna yoyote ni bora kwake kuliko tumaini lake la kuishi maisha marefu.  Kama kuna jamii ya watu ambao, mbali na wasiwasi wao kuhusu kifo, ni wazembefu na hawafaidiki kwa ushauri, kuna jamii nyingine hufaidika kwa ushauri, hujiepusha kutenda dhambi na badala yake kutenda mema.  Huwapa wenye kuhitaji na masikini kwa kutoa Sadaka ya vitu vyao vizuri.  Isingekuwa haki kuinyima jamii hii kutokana na kupata faida kwayo.

 

 

NDOTO

 

Hebu fikiria kdoto na ustadi wake uliomo ndani yake.  Kuna ndoto zinazotokea kuwa kweli na ndoto ambazo hazitokei kuwa kweli, zote zimechanganyika.

Kama ndoto zote ni za kweli watu wote wangelikuwa Mitume.  Kama ndoto zote zingekuwa za urongo zingalikuwa hazina faida bali huzidi na kutokuwa na maana.

Ndoto wakati mwingine ni za kweli ambazo humnufaisha katika shughuli zake za maisha chini ya mwongozo wao, au kuepusha, hasara ambayo amejulishwa kwayo.  Zaidi siyo za kweli isiwe watu wakazitegemea.

 

 

KUWAPATIA WANADAMU MAHITAJI

 

Hebu fikiria vile vitu ambavyo unaviona viko duniani vimewekwa kukidhi mahitaji ya mwanadamu.

Udongo kwa kujenga nyumba, Chuma kwa ajili ya Kiwanda, mbao kwa kujengea, mashine n.k. Jiwe kwa matumizi kama kijaa, shaba kwa ajili ya vyombo vya nyumbani, dhahabu na fedha kwa ajili ya shughuli za biashara, johori kwa ajili ya hazina, nafaka kwa ajili ya chakula, vitu vya manukato kwa ajili ya burdani, madawa kuponya ugonjwa, wanyama wa miguu minne kama wanyama wa kubeba mizigo, miti mikavu kama nishati, majivu kwa ajili ya dawa (kemikali) mchanga kwa manufaa ya ardhi na inawezekana mtu kuhesabu vitu vyote hivi ambavyo havina idadi?

Unafikiri kwamba kama mtu ataingia nyumba na kuiona imewekewa mahitaji yote ya mwanadamu; nyumba nzima imejaa hazina na kila kitu kimewekwa kwa madhumuni halisi, anaweza akafikiria vitu vyote hivyo vimejipanga vyenyewe bila ya yeyote kuupanga (mpango huo)?  Sasa vipi itawezekana mtu yeyote mwenye akili akadokeza kwamba ulimwengu huu na vitu vyote hviti vimejitokeza vyenyewe?

Jifunze somo kutokana na vitu ambavyo vimeumbwa kukidhi mahitaji ya mwanadamu na ustadi mkubwa uliomo ndani yao.  Nafaka zimezalishwa kwa ajili yake lakini amepewa jukumu la kazi ya kuzisaga, kuukanda unga na kupika.  Sufi imezalishwa kwa ajili yake ambayo lazima aichambue, kusokota nyuzi na kuzitengeneza nguo.  Mti umetengenezwa kwa ajili yake lakini lazima apande mbegu, ainyweshe na kuichunga.  Miti shamba imeumbwa kama madawa kwa ajili yake lakini lazima aitafute aichanganye na kuifanyiza dawa.

Kadhalika utaona vitu vyote vilivyotengenezwa na Muumba kukidhi mahitaji ya mwanadamu katika njia ambayo kwamba hakuna mpango wa mtu ungeweza kufanya kazi kwa kutoshelezea kazi yao na kutumia kwayo. Haja na hali kwa kazi hiyo imeachwa juu yake kwa faida yake.  Kama Allah (s.w.t.) angefanyiza vifaa vyote hivi na mtu hana la kufanya kwa njia ya mshughuliko wake, angeanza kuzunguuka juu ya ardhi katika pande zote nne na ardhi isingeweza kuvumilia udhia wake.  Mtu asingekuwa na maisha ya raha kama mahitaji yake yote yangetimizwa bila juhudi na, wala asinge furahia kitu kama hicho.

Huoni kwamba mgeni akaae kwa muda na mahitaji yake yote yakitekelezwa kama kawaida na mwenyeji, bila juhudi yoyote kwa upande wake kuhakikisha ulaji wake, kinywaji, malazi au kikao, anachoka kwa kukaa kwake bure na kutokushughulika.  Anahitaji baadhi ya shughuli, ingekuwa vipi hali yake kama kutokushughulika kwake kungekuwa ni kwa maisha yake yote?

Hii basi imeamriwa kwa mtu kuhodhi mipaka yake kufanya shughuli zake kwa faida zake, isiwe ulegevu na kutokushughulika kukamsababishia unyong'onyevu.

Zaidi ya hayo angezuiwa kutokana na kufanya kazi hizo kwa vile ziko nje ya uwezo wake, na ambazo hazina faida kwake hata kama zimekamilishwa.

Elewa kwamba haja ya msingi ya mtu ni chakula na maji.   Ona mpango ambao umo humo.

Mtu anahitaji zaidi maji kuliko mkate, kwa sababu anaweza kuvumilia njaa kwa muda mrefu kuliko kiu.  Anahitaji maji kwa kunywa, kutawadha, kufua nguo, kunywesha wanyama wa miguu minne, kunywesha mimea.  Kwa hiyo maji, yametolewa kwa wingi bila kuhitaji  kuya-nunua kumwokoa mtu kwa haja ya kuyatafuta.  Mkate lazima upatikane kwa juhudi na kupanga kumfanya mtu ashughulike na kazi yake na kumzuia kutokana na majivuno na kiburi na kazi zisizo na maana.

Huoni kwamba mtoto katika umri wake wa mwanzo anapelekwa kwa mwalimu kwa ajili ya maelekezo kumzuilia na michezo wakati wake wote, ambayo ingempelekea yeye au Mzazi wake kwenye matatizo.  Kadhalika kama mtu angewekwa bila shughuli angejitwalia majivuno na kiburi na angejiingiza katika matendo ambayo yangemdhuru vibaya sana.

Mtu aliyezaliwa na kulelewa katika malezi ya anasa chini ya masharti ya ukwasi na jamaa wake wengi, ni wazi atatumbukia kwenye tabia hizo, kufafanisha hali hiyo.

 

 

KUFAFANULIWA KWA MAUMBO

 

Elewa kwa nini mtu mmoja hafanani na mwingine kama walivyo ndege na wanyama n.k., wakiwa wamefanana mmoja na mwingine.  Unaona kundi la kulungu na kundi zima la kwale kila moja akifanana na mwingine bila tofauti kubwa kati yao, ambapo kwamba watu, kama unavyoona, wana maumbo yenye kupambanulika na hulka, kiasi kwamba hakuna watu wawili wanaofanana kwa mfumo ule ule.

Sababu ni haja ya kila mmoja inatakikana atambuliwe mwenyewe kwa umbo mahsusi na sura, kwa vile wataendesha biashara miongoni mwao ambayo haiwahusu wanyama.  Huoni kwamba mshahaba wa wao kwa wao miongoni mwa wanyama na ndege hakuwaletei madhara?  Sivyo ilivyo kwa mtu, kwani ikiwa kwa bahati jozi ya mapacha watafanana katika umbo, watu wanahisi kuchanganyikiwa kwa kiasi kikubwa katika kushughulika nao ambacho angepasa apewe huyu kinatolewa kwa mwingine kwa makosa.  Mmoja anashikiliwa pahala pa mwingine katika adhabu (au kisasi).

Hutokea hivyo katika mambo mengine hivyo hivyo kwa sababu ya mshabaha.  Mshabaha wa wanadamu unaweza kuwa na madhara zaidi. Nani basi, aliyetoa ufasaha huu na ukamilifu, ambao una pumbaza mawazo?  Hakika ni Yeye yule aliye umba yote haya, ambaye Rehema zake zimeenea kwa vitu vyote.

Je, utamwamini mtu asemae kwamba picha iliyoko ukutani, ambayo unaiona, imejitokeza yenyewe bila msaada wa msanii?  Hakika sivyo, utamcheka.  Vipi basi unaweza kuamini kwama mtu anayeishi akiwa na stadi za uzungumzaji na mwendo  anaweza kujitokeza na kuwepo mwenyewe, ambapo huko tayari kukubali imani hiyo kuhusu picha isiyo na uhai?

 

 

KADIRI YA UKUAJI

 

Kwa nini inatokea kwamba miili ya watu haikui kuupita mpaka mahsusi mbali na ukweli kwamba wanaendelea kuishi na kula?  Hii ni kwa sababu gani kama si kwa utambuzi wa ndani?

Mwenye Nguvu zote Allah Ameamuru hivyo kwamba kila jamii zote za viumbe vyenye uhai vyapaswa kuwa na ukomo maalum wa kukua si ukubwa zaidi wala udogo zaidi.  Vimeendelea kukua mpaka kufikia ukomo huo na kisha husimama kukua, ingawa, ulishaji unaendelea bila kusimama.  Kama isingeamuriwa hivyo vingeendelea kukua mpaka miili yao ingekuwa nje ya mipaka itambuliwayo.

 

 

UCHOVU NA MAUMIVU

 

Kwa nini katika suala hususan la wanadamu kwamba mwendo na shughuli huleta uchovu kwao na wanaepuka kazi laini kwa sababu tu mahitaji yake kama mavazi n.k., huhitaji juhudi zaidi?  Kama mtu hakupata shida na maumivu, vipi angeweza kuepuka matendo ya uovu, kusujudi mbele za Allah (s.w.t.) au kuwahurumia watu?

Huoni kwamba mara tu mtu anapopatwa na maumivu, basi hugeuka kumuelekea Allah (s.w.t.) kwa unyenyekevu kamili, akioma mbele ya Mola wake ili arejeshewe Afya yake na kufungua mikono yake katika ukarimu?  Kama mtu asingepata maumivu kwa kupigwa, vipi Serikali zingewarudi wakaidi?  Vipi atoto wangefundisha Sayansi na Sanaa?  Vipi watumwa wangejisalimisha kwa Mabwana zao kwa hiari?

Je, hakuna onyo katika yote haya kwa Ibn Abi Al Auja na Sahaba zake ambao wanakana madhumuni, na wafuasi wa Mani ambao wanakana Ustadi ulio ndani ya Kazi na maumivu?

Iwapo Viumbe vya Kiume tu au vya Kike tu vingeumbwa katika viumbe hai, je, Jamii yao isingetoweka? Hivi ndiyo sababu ya kuhifadhi jamii zao, kwamba mchanganyiko wa viumbe vya Kiume na vya Kike umeletwa kwa viumbe katika uwiano ulio sawa.

Kwa nini inakuwa kwamba wanaume na wanawake wanapofikia baleghe, ni Wanaume peke yao tu huota ndevu?  Je, haiko katika kawaida na amri ya Usanii?  Hii ni kwa sababu mwanaume ameumbwa kama Bwana ma Mwanamke kama Mtunzaji wa Nyumba.  Mwanambe huyo ndiye msimamizi wa maslahi ya Mume na msiri wake.  Mwanaume, kwa hivyo, amepewa ndevu kumpa sifa na kuonekana Bwana wa Heshima.  Mwanamke anaruhusiwa urembo na uzuri badala yake kama mvuto kwa muungano.

Je, huoni sifa hizi kamili kwamba uumbaji huu unapatikana kwa Usanii wa Mwenye Kguvu zote Allah?  Kila kitu kinapasika kwa kipimo halisi.  Hakuna kinachotolewa ambacho hakihitajiki.”

Sasa ilikuwa ni adhuhuri, Bwana wangu alinyanyuka kwa ajili ya Sala akaniambia nije kwake siku ifuatayo (kesho).  Insha Allah. Nikiwa nimejawa na furaha kwa maelezo niloyo yapata, nilirudi na moyo wa shukurani kwa Allah (s.w.t.) kwa ajili ya Baraka niliyopatiwa juu yangu.

Nilikuwa na usiku mzuri kwa ajili ya maelekezo yenye thamani yaliyowekwa juu yangu na Bwana wangu.

 

 

 

 

Baraza La Pili Ufalme Wa Wanyama

 

 

 

 

 

 

 

UFALME WA WANYAMA

 

Asubuhi na mapema niliwasili kwa Bwana wangu, na baada ya kupata ruhusa ya kuingia katika vyumba vyake niliketi kwa ruhusa yake.

Yeye (a.s.) alianza:  Sifa zote njema zamstahiki Yeye Ambaye ni Muumba wa mabadiliko ya nyakati Ambaye huleta hatua moja baada ya nyingine na hali moja baada ya nyingine ya miongo ya muda, kuwalipa wema na kuwaadhibu waovu, kwa sababu ni Mwenye Haki.  Majina yake yote yametukuzwa.  Baraka zake ni adhimu.  Hafanyi dhuluma hata ndogo kwa viumbe wake, walakini, mtu anajifanyia udhalimu mwenyewe!

Maneno ya Allah (s.w.t.) mwenyewe yanathibitisha ushuhuda kwa haya: "Basi atakayefanya kheri (jema) uzani wa mdudu chungu atauona.  Na atakayefanya uovu uzani wa mdudu chungu (pia) atauona" (Qur'an 99:7 - 8).

Kuna Aya nyingine katika Kitabu Kitukufu katika maana hii hii zikitoa kinaganaga maelezo ya mambo yote.  Uwongo hauwezi kuja mbele yake wala nyuma yake.  Ni kitabu kilichofunuliwa  na Mwenye Nguvu zote Mwenye Kustahiki Shukurani Allah.  Ni kwa maelezo haya kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema kwa jambo hili kwamba " Matendo yenu yatarudishwa kwenu."

Imam (a.s.) aliinamisha chini kichwa chake kwa muda na akasema: "Ewe Mufazzal! Mwanadamu amefadhaika na kupotea, ni kupofu, amepumbazika katika ukaidi wake, kufuatia mashetani yao na vioja.  Wana macho lakini hawaoni, wana ndimi lakini ni mabubu na hawaelewi.  Wana masikio lakini hawasikii. Ni wenye furaha katika ufisadi wao duni.  Wanadhania wameongozwa vema.  Wamepotoshwa kutoka sifa za viumbe vyenye akili.  Wanakula juu ya mboga zilizonajisiwa na uchafu wa watu wachafu. Wanadhani wenyewe wako salama kutokana na msiba wa kifo cha ghafla na adhabu ya matendo.  Ole! Ajali mbaya iliyoje iwapatao watu hawa!"

Hii ilinifanya mimi nitoe machozi, na Imam (a.s.) alinifariji kwa kusema kwamba nimeokolewa, kwa sababu ya kuikubali iman na elimu ya kiroho, na nimepatiwa wokovu.

 

 

ULIMWENGU WA WANYAMA

 

Yeye (a.s.) aliendelia:  Sasa napenda kukuelezea kuhusu ulimwengu wa Wanyama, ili kwamba upate maelezo zaidi kuhusu (Ulimwengu) huo kama ulivyopata kuhusu mengine.

Hebu fikiria umbile la mwili na mfumo wa muundo uliomo katika uumbaji wao.  Siyo wagumu kama mawe, kwani wangekuwa hivyo, wasingeweza kufanya shughuli, wala siyo laini kwani kwa hali hiyo wasingeweza kuzunguusha vichwa vyao au wenyewe kusimama wima bila mhimili.

Wamefanyizwa  na misuli hiyo ya kupinda kama kuinama na kujikunja.  Wametengenezwa kwa mifupa migumu ambayo imeshikwa kwa misuli na ambayo imefungwa pamoja kwa makano juu ya kila mfupa.  Ifunikayo mifupa hii na misuli hii ni ngozi yao ambayo huenea juu ya mwili vote.

Wanasesere wa miti na matambara yaliyo zunguushwa juu yao na kufungwa na vigwe na Sandarusi ya gundi ju ya umbo lote, itafafanisha jambo hili, ifanye mbao iwe kama mifupa, matambara kama misuli, vigwe kama makano no sandarusi kama ngozi.

Kama inawezekana katika hali ya viumbe vyenye uhai na mwendo kujitokeza kuwepo kwa vyenyewe, ingekuwa busara kutegemea kutokea maumbo haya yasio na uhai.  Na kama haiwezekani kwa wanasesere hawa, itakuwa ni upuuzi zaidi kwa wanyama.

Kisha angalia kwa uangalifu sana kwenye miili yao, imefanyizwa kwa misuli na mifupa kama ya wanadamu.  Wamejaaliwa macho na masikio, ili kwamba kumuwezesha mtu kupata huduma kutoka kwao, wasingaliweza kutekeleza lengo lake (huyo mtu) kama wangekuwa vipofu au viziwi.

Wamenyimwa Stadi za akili na hoja, ili kwamba wabakie ni wenye kutii kwa watu na wasije wakawa wasiotii hata kama akihusishwa na kazi nzito isiyovumilika na kuelemea.

Kinzano laweza kuletwa katika hali ya watumwa wanadamu, wenye akili na hoja, hutii mabwana zao kiunyonge japokuwa ni dhiki na kazi ngumu.

Jibu kwa hili ni kwamba watu wa aina hii ni wachache kiidadi.  Wengi wa watumwa ni wafanyaji kazi ngumu bila kupenda, ambapo wanyama ni watii hata katika kulemewa kuzito na wakati wa kuzunguusha kijaa n.k. hawawezi kuathirika kwa mfadhaiko kama kazi zao mahsusi zihusikavyo kwa mtu.

Kama mtu angefanya kazi ya ngamia mmoja au nyumbu, watu wengi wangehitajika, na kusababisha kizuizi katika shughuli nyingine.  Majukumu haya rahisi yangechukua wafanyakazi wote, bila kuacha watu wowote kando kwa ajili ya Sanaa na Taaluma.  Zaidi ya hayo watu wangepatwa na uchovu wa akili.

Hebu fikiria miundo ya aina tatu ya viumbe hai ifuatayo, na Sifa ambazo kwamba wamejaaliwa nazo.

(1) Mtu, akiwa ameamriwa kuwa na akili na hoja kufanya kazi hizo za ufundi kama useremala, uashi, uhunzi, kushona n.k. amejaaliwa kuwa na viganja vipana na vidole vinene kumwezesha kushika aina zote za ala zilizo muhimu kwa ajili ya taaluma hizi.

(2) Wanyama walao nyama, wakiwa wameamriwa kuishi kwa kula wanyama (nyama) wametunukiwa viganja laini na makucha yawezekanayo kufichika ndani.  Ni wazuri kwa kuwinda lakini hawafai kwa kazi za sanaa za kitaaluma.

(3) Wanyama walao majani, wakiwa wameamriwa si kwa sanaa za kitaaluma wala kwa uwindaji, wametunukiwa, baadhi na kwato zilizopasuliwa kuwasaidia kutokana na ugumu wa ardhi wakati wa kulisha ambapo wengine wana kwato imara kuwawezesha kusimama sawa sawa juu ya ardhi kwa ulinganifu mzuri kama wanyama wa mizigo.

Wanyama walao nyama katika mfumo wao wa kuumbwa wana meno makali, kucha ngumu, na vinywa vipana kuwasaidia katika lishe yao kwa chakula cha mnyama kama ilivyoamriwa kwao, na wameumbwa ilivyo.  Wamepewa silaha hizo na vyombo vya kazi kwa kuwafaa katika uwindaji.

Kwa ulinganifu wa sawa, utaona mdomo na kucha vikiwafaa kwa kazi zao mahsusi.  Kama kucha hizo wangepewa wanyama walao majani, zingekuwa mbaya zaidi kuliko manufaa kwani kamwe hawawindi wala kukamata kiwiliwili.  Na wanyama walao nyama wangepewa kwato badala ya kucha wangeshindwa kupata mahitaji yao katika kukosekana vifaa vya kufaa kwa mahitaji hayo.

Huoni kwamba aina zote hizi za wanyama wametunukiwa sawasawa na vitu vyenye kufaa (kwa kusudi la kila mmoja) kwa ulinganifu na haja zao, humo kwayo mna kuishi kwao.

Sasa watazame wanyama wa miguu minne na angalia jinsi wanavyowafuata Mama zao.  Kamwe hawahitaji kubebwa wala kulishwa kama ilivyo kwa watoto wa kibinadamu.  Hii ni kwasababu  kwamba mama wa watoto hao hawana nyenzo ambazo mama wa watoto wa Kibinadamu wanazo.  Wana Upendo, Huba na Elimu ya Sanaa ya Maumbile na Mikono maalum na Vidole vya kuwanyanyulia.  Wamefanyizwa hivyo ili kuwasaidia katika aina zote za kazi.

Utaona namna hiyo hiyo katika ndege, kwa mfano, Vifaranga vya Kuku, Kwale na jamii ya Kuku (k.v. Kanga) huanza kuokota nafaka na kwenda huku na huko  mara tu vinapoanguliwa kutoka kwenye mayai.  Ndege ambao vifaranga vyao ni dhaifu, bila nguvu ya kusimama, kwa mfano wale wa porini na njiwa wa nyumbani, wana mama wenye silika zaidi za kimama, ili kwamba wawaletee lishe kwenye vinywa vya vifaranga vyao waliyoiweka kwenye maumio yao.

Malisho aina hiyo huendelea mpaka vifaranga viweze kujikimu   vyenyewe.  Njiwa hana makinda wengi kama kuku, kuwezesha majike kuyalea kiutoshelezaji bila kuwaua kwa njaa.  Hivyo kila kimoja hupata mgao wa kutosha kutoka baraka za Mwenye Nguvu zote Mwenye Kujua yote Allah (s.w.t.)

Hebu tizama jinsi miguu ya wanyama ilivyoumbwa katika jozi kuwawezesha kutembea kwa urahisi, ambapo ingekuwa vigumu, kama ingeliumbwa katika idadi ya witir.  Mnyawa atembeaye hunyanyua  mguu mmoja ambapo mwingine anautuliza juu ya ardhi.  Wenye miguu miwili ananyanyua mmoja na kupata msaada juu ya mwingine.  Wa miguu minne hunyanyua jozi moja na kutulia juu ya pande tofauti.

Kama mnyama wa miguu minne angenyanyua jozi ya miguu katika upande mmoja, tutusa kwa jozi ya upande mwingine kungekuwa kugumu kama ambavyo ubao hauwezi kusimama juu ya miguu miwili.  Mguu wa mbele wa upande wa kulia na mguu wa nyuma wa upande wa kushoto inanyanyuliwa pamoja, na kinyume chake.  Kwa ajili ya mwendo thabiti.

Je, huoni kwamba punda anaendesha Kijaa kama kazi nyongeza ya ubebaji mizigo, kwa kuwa farasi anaruhusiwa pumziko na faraja kwa kulinganishwa na punda?  Na ngamia anafanya kazi zaidi, ambayo haiwezi kumalizwa na idadi ya watu.

Ingekuwa hali gani kama angekataa kutii amri?  Husalimu Amri hata kwa mtoto aliyepo hapo!  Vipi Maksai anasalimu amri kwa Bwana wake akilima Shamba na mhimili shingoni mwake?

Farasi wenye asili bora hukimbia kuelekea makali ya panga na mikuki kama wafanyavyo mabwana zao wakati wa mapigano.  Mtu mmoja anaweza akachunga kundi la kondoo.  Kama kondoo wangetawanyika kila mmoja akaenda njia yake, vipi mtu angeweza kuwatafuta?

Kadhalika, Jamii nyingine za wanyama ni zenye kufaa kwa mtu, kwa nini?  Hii ni kwa sababu hawana akili yoyote, wala uwezo wowote wa kuhoji mambo.  Kama wangelikua na akili, wangejitoa katika kutekeleza kazi nzuri ya mahitaji ya mtu.

Ngamia angekataa kusalimu amri, na fahali angeasi dhidi ya bwana wake, kondoo wangetawanyika na kadhalika.  Kama wanyama wa kuwindwa wangekuwa na akili na hoja wangeshindana kwa ajili ya vitu vya kula na watu.  Nani basi angeweza kushindana na ushauri wao wa pamoja dhidi ya watu?

Je, huoni jinsi walivyozuiwa kutokana na kufanya hivyo?  Wanaogopa makazi ya watu na kumkimbia mwanadamu, badala ya mwanadamu kuwaogopa wao (na kuwakimbia).  Hawatoki nje wakati wa mchana kutafuta chakula, bali wakati wa usiku.  Wanaogopa watu na utukufu wao wote utishao bila kupata dhara lolote au onyo kutoka kwao.  Kama hii isingeamriwa hivyo, wangekuja wakirukaruka kwenye makazi ya wanadamu na kufanya maisha yao kuwa ya mashaka.

Mbwa, (akiwa) miongoni mwa hayawani, amejaaliwa tabia maalum, utii kwa bwana wake, utumishi wake kwake na ulinzi wake kwake. Huweka ulinzi wakati wa usiku wa giza, hubweka huko na huko katika nyumba akilinda usalama dhidi ya wezi.  Yuko tayari kujitoa mhanga maisha yake ili kumwokoa mtu na watu wake.  Huo ndio utii wake kwa bwana wake.  Anaweza kujiweka na njaa na maumivu kwa ajili ya bwana wake.

Kwa nini, mbwa ameumbwa katika mfumo huu, isipokuwa tu amtumikie na kumlinda mtu, na meno yake imara, kucha madhubuti, ubwekaji wa kutisha, kwa nini?  Ni kwa kuwatisha wezi na kuwazuia kukaribia mali iliyo dhaminiwa kwa ulinzi wake.

Tizama katika nyuso za wanyama wa miguu minne na angalia vipi zilivyoumbwa.  Utaona kwamba macho yao yamewekwa mbele, wasije wakagonga ukuta au kutumbukia shimoni.  Utaona vinywa vyao vimepasuliwa chini ya pua.  Kama vingekuwa kama vile vya watu wasingeweza kuokota chochote kutoka ardhini.  Huoni kwamba mtu haokoti chakula chake kwa kinywa chake?  Hufanya hivyo kwa mikono yake.

Huu ni ubora wa pekee kwa mtu katika mlingano na walishi wengine.  Kwa kuwa wanyama wa miguu minne hawakupata mikono kama hiyo kuwawezesha kuokota majani, sehemu ya chini ya pua imepasuliwa humwezesha kuokota majani na kuyatafuna.  Anasaidiwa zaidi na midomo iliyo refushwa kufikia vitu vilivyoko mbali zaidi kama vile afikiavyo vilivyo karibu zaidi.

Fikiria mikia ya wanyama na faida zilizoamriwa kwayo.  Ni aina fulani ya mfuniko kwa viungo vyake vya siri vya kutolea uchafu.  Vilevile husaidia kufukuza inzi na mbu ambao hutua juu ya uchafu katika miili yao.  Mkia yao imefanyiwa mfano wa mapanga boi ambayo kwa hiyo hufukuzia inzi na mbu.  Vile vile hupata afueni kwa kupungia mikia yao daima.

Wanyama hawa husimama juu ya migu yote minne, hawana muda wa kuitembeza huku na huku, kwa hivyo, huhisi kufarijika kwa kupungia mikia yao.

Kuna faida nyingine hata hivyo ambazo mawazo ya mwanadamu si yenye kuweza kuzishika na ambazo zinajulikana tu inapotokea haja, miongoni mwa faida hizi, mkia ni silaha ya zaidi sana mkononi kwa kuunyongotoa kumtoa mnyama anasapo kwenye matope.  Mwengo wa mkia unaweza vile vile kutumiwa na watu kwa manufao kadhaa.

Kiwiliwili cha wanyama hawa kimefanywa bapa kwa kulala juu ya miguu yote minne kurahisisha ngono kwa sababu ya hali ya sehemu zao zinazohusiana.

 

 

TEMBO

 

Fikiria mkonga wa tembo na ustadi mkubwa uliopo katika muundo wake.  Unasaidia dhumuni la kuchukua chakula na maji kupeleka ndani tumboni, kama mkono wa mtu.  Bila huo tembo hawezi kunyanyua chochote kutoka ardhini, kwa kuwa shingo yake siyo ndefu vya kutosha, ambayo angeweza kuinyoosha mbele kama wanyama wa miguu minne.

Kwa kutokuwepo kwa shingo ndefu amepewa mahala pake mkonga mrefu ili kwamba aweze kuunyoosha na kukidhi haja yake.  Nani aliyempa kiungo hiki kufidia kwa kutokuwepo kwa kile kilicho kosekana?  Hakika, Yeye Ambaye ni Mwenye Huruma Sana juu ya Viumbe Vyake.  Na hii itawezekana vipi bila kupanga Usanii kama ilivyojitokeza kwa Wataalam wapotofu na walahidi?

Kwa kinzano kwamba kwa nini hakujaaliwa kuwa na shingo sawa kama ile ya wanyama wengine, jibu ni kwamba kichwa na masikio vya tembo vikiwa ni vizito sana vingeweza kusababisha mvuto mkubwa wa nguvu, hata pia kuvunjika, hivyo kichwa chake kimeungwa moja kwa moja na mwili kukikinga dhidi ya matokeo hayo na badala yake kwa ajili hiyo mkonga umefanyizwa kushughulikia madhumuni yote hayo inayohitaji, pamoja na yale ya kulisha.

 

 

TWIGA

 

Hebu fikiria umbo la twiga na asili mbalimbali ya viungo vyake vifananavyo na wanyama wengine mahsusi.  Kichwa chake hufanana na ile cha farasi, shingo kama ile ya ngamia, kupasuka kwato kama zile za ng'ombe, na ngozi yake kama ile ya chui.

Baadhi ya watu wajinga wamedhania kwamba haya ni matokeo kutokana na muungano wa aina mbalimbali za wanyama wajao sehemu za kunyweshea, jamii moja binafsi huingia katika muungano wa ngono na jamii nyingine binafsi, na kutokea uzao wa namna hii.   Na kwa hiyo unakuwa mfano wa umbo mbalimbali.

Kusema hivi ni kuudhihirisha ujinga, na ukosefu wa elimu ya kiroho ya Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.) utukufu uwe kwake.  Hakuna mnyama aingiaye kwenye muungano ufanyikao kati ya farasi na ngamia jike au ngamia na ng'ombe.  Muungano wa ngono unaweza kuwepo (au kutokea) tu kati ya wanyama wenye umbo linalofanana katika kuumbwa, kwa mfano farasi na punda jike hutokea (kuzaliwa) kwa nyumbu, au mbwa mwitu na mbweha hutokea (kuzaliwa) chotara.

Hata hivyo, kamwe haitokei kwamba uzao wa muungano wa namna hiyo unaweza kuchukua kiungo kimoja kutoka mmoja wa mwenzi mwingine.  Twiga ana kiungo kimoja kifananacho na kile cha farasi, mwingine na kile cha ngamia ukwato wa mwingine na  ule wa ng'ombe.  Lakini unaona kwamba nyumbu kichwa chake, masikio yake, mgongo wake, mkia na kwato zake vi katikati baina ya vile vya punda na vya farasi, na ndivyo ulivyo mlio wake u katikati baina ya mlio wa farasi na mlio wa punda.  Hoja hii yaonyesha kiutoshelezaji kwamba twiga si uzao wa muungano wa jamii inayojifanyia tu, bali ni ajabu moja ya uumbaji wa ajabu wa Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.) kuthibitisha Enzi yake Kuu.

Yapasa pia ifahamike kwamba Muumba wa jamii za Wanyama zisizo idadi Huumba viungo vyovyote vile Apendavyo ya hivyo vilivyo sawa kimoja na kingine na vile vingine ambavyo havifanani.  Anaongeza katika uumbaji chochote apendacho na hukataza humo namna Apendavyo.  Hii ni kwamba Enzi Yake Kuu iweze kuthibitishwa na hakuna kitu kinachoweza kumzuia katika lolote Apendalo.

Kwa nini shingo yake ni ndefu na faida gani zipatikanazo kwake kutokana nayo?  Faida ipo katika kumwezesha kufikia majani na matunda ya miti mirefu kwa lishe yake ambapo anaishi, anakaa, na amezaliwa na sehemu zake za kujilishia, ni misitu minene.

 

 

KIMA

 

Hebu fikiria uumbaji wa Kima na ufanano ambao upo kati ya viungo vyake na vile vya mtu, kichwa, mabega yote, kifua na viungo vya ndani.

Zaidi ya hayo, amepewa akili na utambuzi/uwelekevu kwa sababu ya hizo huelewa ishara na maelekezo ya bwana wake.  Kwa ujumla huiga matendo ya mtu kama anavyomwona.  Yuko karibu sana na mtu katika ubora wake, tabia na asili ya kuumbwa.

Inapasa iwe kama ni onyo kwa mtu kwamba azingatie akilini kwamba katika asili na umbo ni sawa na wanyama akifanana nao kwa ukaribu sana na kama asingepewa akili, ujuzi/utambuzi na uzungumzaji angekuwa sawa tu kama wanyama.

Kuna maongezeko kidogo katika muundo wa (kuumbwa) kima umtofautishao na mtu k.m. kinywa, mkia mrefu, nywele zifunikazo mwili mzima.  Tofauti hizi, hata hivyo, zisingemzuia kuwa mwanadamu, kama angelipewa stadi za hoja, akili na uzungumzaji kama mtu.  Tofauti yenyewe hasa ya mpaka baida yake na mtu, kwa hiyo, ni kwa ajili (ya kukosa) tu njia za hoja, akili na uzungumzaji.

 

 

NGOZI YA MNYAMA

 

Hebu fikiria Rehema za Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.)kwa wanyama hawa katika kuipa miili yao mfuniko wenye aina mbali mbali za nywele kuwalinda dhidi ya misukosuko/matatizo ya kipupwe.  Na wamepewa kwato, zilizopasuliwa na zisizopasuliwa, au miguu fumba kwa kuwahifadhi.  Si wenye mikono, wala viganja wala vidole kusokotea nyuzi na kufuma, na kwa hiyo mavazi yao yamefanywa ni pamoja na sehemu ya umbo la miili yao, kuwahifadhi maisha yote bila kutengeneza na kubadilisha.

Mtu, iwayo yote, ana mikono na ufundi wa kufuma nguo na kusokota nyuzi.  Hutengeneza nguo na mara kwa mara huibadilisha kwa faida nyingi upande wake.  Miongoni mwa hizo hujishughulisha na utengenezaji nguo zake na kwa hiyo akaepukana kutokana na shughuli (mbaya) zenye kudhuru na uvivu.  Huiacha kazi yake ya kushona wakati apendapo kuwa nyumbani.  Anaweza kutengeneza aina mbalimbali za mavazi kwa burdani apatayo katika kubadili kwa njia ya fahari na kadhalika.  Hutayarisha soksi na viatu kwa njia ya utendaji mzuri kuhifadhi miguu yake.  Vibarua, na wafanya biashara kwayo hupata riziki zao na riziki za jamaa zao.  Hizi aina tofauti za nywele huwasaidia wanyama kama mavazi ambapo kwato zao na miguu - fumba kama viatu.

 

 

KUZIKA MFU

 

Hebu fikiria tabia hii ya asili ya wanyama, nayo ni, ufichaji wa miili ya wafu wakati inaokufa kama vile watu wanavozika maiti wao.  Hakuna hata mwili mfu mmoja wa hayawani na wanyama unaoonekana.  Hawako mbali sana kiasi cha kutokuonekana.  Kwa ukweli idadi yao ni kubwa zaidi kuliko ile ya watu.

Yatazame makundi ya kulungu, nyati, punda wa porini, mbuzi mawe na paa na pia jamii mbali mbali za wanyama na hayawani kama vile simba, nyumbu, mbwa mwitu, chui n.k., na aina aina za wadudu waishio ndani ya matumbo ya ardhi na kutembea juu take, katika majangwa na milima, na kadhalika ndege warukao kama kunguru, kwale, bata, korongo, njiwa, na ndege wa mawindo.  Hakuna mizoga yao tunayoiona isipokuwa michache ambayo mwindaji huipata, kama mawindo au ile inayonyafuliwa na hayawani.  Likiwa ni jambo la ukweli, wakati wanyama hawa wanapopata hisia za kukaribia kifo (kufa), ujificha katika baadhi ya sehemu za siri na kufia humo.

Zitazame sanaa ambazo mtu (mwanadamu) amejifunza kutoka wanyama hawa - mfano wake wa kwanza.  Aliona kunguru wawili wakipigana.  Mmoja akamuua mwingine na kisha akauzika mwili wake mfu, hivyo Kabil akajifundisha kuchimba shimo na kuzika maiti ya ndugu yake Habil.  Hayo yalifanyika chini ya mwongozo wa Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.).  Wanyama hawa walipewa hisia hizi kumwokoa mwanadamu (mtu) kutokana na msiba wa matatizo hayo na milipuko ya magonjwa ambayo yangeweza kuja (kutokea).

 

 

SILIKA ZA WANYAMA

 

Fikiria silika ambazo kwazo (wanyama) kwa desturi wamepewa na Mwenye Kguvu zote Allah kwa Rehema zake zisizo na mwisho ili kwamba asiache kiumbe chochote kunyimwa Rehema zake ingawa hii haiko chini ya Stadi za kufikiria hali ya usawa.

Paa humeza nyoka lakini hanywi maji hata kama kiu yake itakavyokuwa kali namna gani, kwa kuchelea sumu inayosambaa ndani ya mwili wake ambayo kwa sababu ya maji ingemuua.  Huzunguukia mapipa ya maji.  Hupiga kelele kwa sababu ya ukali wa kiu lakini hagusi maji kwa kuchelea (kuogopa) kifo.  Unaona kujizuia kukubwa huku ambako wanyama hawa wanako bila kujali kiu kali kwa sababu ya hofu au dhara katika hali ambayo mtu mwenye akili na busara hawesi kustahimili.

Mbweha nae, asipopata chakula kwa njia yoyote ile hujifanyia "kifo cha hadaa na kulitanua tumbo lake kuwadanganya ndege waamini kuwa kafa.  Maru tuu ndege wakija kumzunguuka kwa kutaka kuunyofoa mwili  uonekanao kama mzoga, huwashambulia na kufanya mlo mzito wa nyama zao.

Sasa, sema, nani aliyetoa wlekevu huu kwa mbweha asiyezungumza na asiye na akili?  Hakika ni Yeye Yule Ambaye amechukua juu Yake Mwenyewe Jukumu la kumlisha.  Kwa vile mbweha hawezi kufanya shughuli zile ambazo hayawani wengine wanaweza, k.m.  shambulio la moja kwa moja juu ya mtesi, amepewa werevu na hadaa kama njia za kujipatia riziki (maisha).

Dolfin (Samaki kama nyangumi mdogo) huhitaji ndege kama watesi.  Humkamata samaki na kumuua na kumuweka ili kwamba aelee juu ya maji ambapo yeye mwenyewe akijificha chini yake akiyavuruga maji wakati wote kuufanya mwili wake ufichike.  Mara tuu ndege anapomrukia ghafla yule samaki, huruka kwa ghafla juu yake na kumshikilia yule ndege.  Kwa werevu huu humpata mtesi wake (riziki).”

 

 

CHATU NA WINGU

 

Kisha niliomba maelezo kuhusu chatu na wingu.

Imam (a.s.) akajibu kwamba: “Wingu ni mfano wa Malaika kumkamatia (kumshikilia) chatu wake popote atakapomwona, kama vile jiwe la sumaku linavyoshikilia chuma.  Hanyanyui kichwa chake kutoka ardhini kwa sababu ya kuchelea (kuogopa) wingu hilo, isipokuwa katika (majira ya) kiangazi wakati anga ni nyeupe bila dalili ya wingu na kisha litokeapo tu (hilo wingu) mara moja hutoweka.”

Niliuliza, “Kwa nini wingu limefanywa mtawala wa chatu kumshililia popote litakapomwona?”

Imam (a.s.) akajibu,"Kumwokoa mtu (mwanadamu) kutokana na madhara yake."

 

 

SIAFU

 

Nilisema, "Maulana! umetoa maelezo ya ulimwengu wa wanyama kwa ukamilifu kufanya kama kifungua macho kwa kila mtu.  Tafadhali hebu toa baadhi ya maelezo kuhusu Siafu na ndege".

Imam (a.s.) akasema,"Timaza katika taya za siafu huyu mdogo.  Je, unaona kasoro yoyote ndani yao inayoathiri faida yake?  Je, umetoka wapi ulinganifu huu na hadhari?  Hakika ni kutokana na ustadi uleule na usanii ambao umetomika katika ujenzi wa uumbaji wote, mkubwa au mdogo.

Hebu tizama siafu jinsi wanavyokusanyika pamoja kukusanya chakula kwa ajili yao.  Utaona kuwa wakati siafu wengi wakiazimia kuchukua nafaka kupeleka kwenye nymba zao wanafanana na watu wengi wanaojishughulisha na kupeleka nyumbani nafaka zao.  Siafu kwa kweli huonyesha juhudi na shughuli ambazo watu hawawezi kuzifanya.  Huoni jinsi wanavyosaidiana kila mmoja katika kuchukua nafaka kama watu?  Wanazivunja nafaka vipande vipande zisije zikachipua na kuwa zisizo na maana kwa dhumuni lao.  Kama zikipata unyevu nyevu, huzisambaza zipate kukauka.  Siafu hotoboa mashimo yao sehemu zilizonyanyuka, mbali kutokana na hatari ya mafuriko.

Shughuli zote hizi, iwayo yote, hazipo bila uamuzi wa hoja, wenye silika halisi, ambazo kwazo miundo yao imejaaliwa nazo, kwa ukarimu wa Mwenye Nguvu zote Allah.

 

 

BUIBUI

 

Hebu mtizame mdudu aitwae "Lais" (aina ya buibui) kwa kawaida huitwa simba wa inzi.  Ukubwa ulioje wa werevu na ustadi na upole aliojaaliwa mao kwa utafutaji wa riziki zake.  Uatona kwamba wakati ana hisia ya kufikiwa na inzi humpuuza kwa muda kujifanya kama kamba vile mwili wenyewe ni usio na uhai (umekufa).  Wakati akihisi kwamba inzi hayupo katika hofu yoyote ya kukamatwa na hana habari kabisa ya kuwepo kwake (buibui) huanza kunyemelea kuielekea katika mwendo wa kunyata pole pole hatua kwa hatua mpaka amfikie karibu kiasi cha kuweza kuikamata, akiwa yu ngali ameishikilia, huikumbatia na kuizingira kwa mwili wake wote kuzuia kuponyoka kwake.  Hushikilia hivyo mpaka ahisi kuwa inzi huyo ameishiwa nguvu na viungo vyake vimetulia, na hapo sasa huigeukia za kuila.  Hii ndiyo njia aitumiayo kwa kuishi.

Buibui wa kawaida hutanda utando wake na kuutimia kama mtego kwa kukamatia inzi.  Hukaa amejificha ndani yake.  Mara tu inzi anaponaswa humrukia kumkamata na kumkata  kata katika vipande.  Huendelea kuishi katika njia hii.  Na hali hii indivyo ilivyo kwa mbwa, simba muwinda na mtengo wa kunasia wakati wa kuwinda.  Hebu angalia mdudu huyu mnyonge jinsi alivyotunukiwa na silika (akili) ya kukamatia windo lake ambalo mtu hawezi kufanya bila kutumia matengo na ala (vyombo vya kazi).

Usitoe kasoro katika kitu chochote, kwani kila kitu kina funzo (Somo) la kufundisha kama vile siafu n.k.  Maana nzuri mara nyingi huelezewa kwa kitu kidogo bila kupunguza thamani yake kama vile dhahabu haipunguki thamani kama itapimwa dhidi ya (vipimo) vitu vitokanavyo  na chuma.

 

 

NDEGE

 

Hebu fikiria umbo la mwili wa ndege kama alivyoamriwa kwamba angeruka juu angani.  Ametunukiwa mwili mwepesi na kiulinganifu muundo imara.  Ana miguu miwili badala ya minne, vidole vinne badala ya vitano, tundu moja kwa kutolea uchafu badala ya mbili. 

Ametunukiwa kifua kilichochongoka (kumuwezesha) kuruka angani kama vile mashua ilivyojengwa kupasua majini.  Ana manyoya marefu magumu katika mbavu zake na mkia kumsaidia kuruka juu.  Mwili wote umefunikwa na manyoya kwa kujazwa hewa ya kurukia juu angani.

Kwa kuwa imeamriwa kwake kwamba lishe yake itakuwa ya nafaka na nyama ambazo atameza bila ya kutafuna, meno yamekosekana katika umbo lake na amepewa mdomo imara kwa kutafutia chakula ambao kwa huo anaweza kuokotea chakula.  Hauumizwi wakati aokotapo wala kuvunjika amegapo nyama. 

Kwa vile hana meno lakini hula nafaka na nyama mbichi, joto jingi hufanyizwa ndani ya tumbo lake ambalo hufanya kazi ya kupika chakula chake bila kuhitaji kutafuna.  Ni kama vile mfano wa mbegu za zabihu hutoka nje ya tumbo la mtu kama zilivyo ambapo zinapikika kabisa/kikamilifu katika tumbo la ndege.

Wameumbwa hivyo kwamba watage mayai badala ya kuzaa watoto ili kwamba wasije wakapata uzito wa aina yoyote wa kuvumilia wakati wa kuruka kwa sabubu ya kilengwa katika mfuko wa uzazi kikaacho humo ili kikuzwe kikamilifu.

Kila kitu katika muundo wake kimeumbwa hivyo ili kiwe cha kutosheleza kufaa kwa hali yake katika maisha.  Iliamriwa pia kwamba ndege ambao ni wenye kuruka juu angani wakae kwa juma moja au juma mbili au juma tatu wakilalia mayai, kwa kutotoa vifaranga vyao.  Kisha huvigeukia kwa hadhari yao yote. 

Analo gole kubwa la kutosha kuwaletea vifaranga vyake na chakula ambacho kwama kwa hicho pia anaweza kujilisha.

Nani aliyemuwekea majukumu kwanza ajaze gole lake kwa nafaka zilizochumwa shambani, na kisha aweke mavuno hayo katika umio la vifaranga? 

Kwa nini anachukua taabu yote hiyo ingawa hana stadi ya kuhoji wala hana mategemeo yoyote ambayo mtu hawazia kuhusu watoto wao - heshima, kuishi kwa jina, na urithi n.k.  Hii ni shughuli ambayo huonyesha kwamba ni fadhila maalum kwa vifaranga vyake chini ya mgawo maalum wa Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.) ambao udege mwenyewe hawezi kujua, wala kuhoji juu yake.  Na ni nini hicho?  Ni mpango kwa ajili ya kuishi kwa taifa.

 

 

KUKU

 

Hebu mtizame kuku na uone jinsi alivyo na wasiwasi wa kutaga mayai na kutotoa vifaranga ingawa hana kiota chochote mahsusi wala si mayai kutoka jamii hiyo hiyo.  Hupiga kidoko (mlio wa kuku mwenye vifaranga au anayetaka kutaga), hutimua manyoya yake, huacha lishe yake, isipoluwa ipewe mayai ya kulalia na kutotoa vifarange, kwa nini? 

Ni hivyo ili kuhifadhi taifa.  Isingeamriwa hivyo kiasili, nani ambaye angeifadhili kwa hifadhi ya taifa, ingawa haina stadi ya akili au ya kuhoji?

Hebu tizama kwenye umbo la yai na jauhari nyeupe na njano ndani yake.  Sehemu moja ni kwa ajili ya kufanyizwa kifaranga ambapo inyingine ni ya kukipatia lishe mpaka wakati huo kitakapolitoka yai. 

Hebu fikiria ustadi ulio ndani yake kwa vile umbo la kifaranga lilikuwa libebwe humo kiusalama ndani ya ganda (kaka) bila kuruhusu zahama yoyote ya nje, lishe yake imewekwa ndani yake ambayo ni ya kutosha mpaka kitoke nje. 

Mtu ambaye amefungwa (jela) kiusalama bila ya fikio lolote kwake huwa anapatiwa chakula cha kadiri kumtosha mpaka kuachiliwa kwake.

 

 

UMIO LA NDEGE

 

Hebu fikiria gole/umio la ndege na ustadi ulio ndani yake.  Tumbo limekaribiwa na mrija mwembamba kuruhusu lishe kufika ndani yake kwa kiasi kidogo kidogo.  Bila gole/umio nafaka ingalichukua muda kufika tumboni. 

Ndege katika ujuzi wake wa kuhisia hali ngumu ya baadae, hujaza gole/umio lake kwa haraka. Gole/umio lake limeumbwa katika muundo wa shanti (aina ya mkoba)  iliyoangikwa mbele yake, ili kwamba ijae kwa haraka kwa chochote kile ikipatacho, kisha pole pole hukihamishia tumboni.

Kuna faida nyingine katika gole/umio.  Baadhi ya ndege hushughulika na kuhamisha chakula kuwapelekea watoto wao.  Gole/umio huwasaidia kukihamisha kwa urahisi.

 

 

MANYOYA YA NDEGE

 

Baadhi ya watu wa mafundisho haya ya maumbo ya asili hudai kwamba rangi kuwa mbalimbali na maumbo tofauti ya ndege vimetokana tu na mchanganyiko wa vitu vya asili na tabia katika linganifu mbalimbali.  Havikutokea kuwa hivyo kutokana na Usanii wowote mahsusi.

Urembo huu unaouona kwenye tausi au kwale na uzuri halisi, kama kwamba msanii fulani mwenye brashi nzuri ameitimiza sanaa ya uzuri wa picha. 

Utaweza vipi mchanganyiko huu usio wa akili uulete uzuri huo wenye kuonekana bila kombo yoyote? 

Ikiwa vitu hivi vya sanaa vimejitokeza kuwa viumbe bila ya Msanii Mwenye Nguvu zote, ni vipi uzuri huu  na mfanano ungehifadhika?

Hebu tizama kwa makini katika manyoya ya ndege, utayaona kama nguo iliyofumwa na nyuzi nzuri.  Unywele mmoja umesokotwa na mwingine kama vile kipande kimoja cha uzi kinavyosokotwa na kingine. 

Tizama katika umbo lake.  Kama unalifungua, hufunguka bila kuchanika kuruhusu kewa kujazwa ndani na kuruhusu ndege kuruka wakati  apendao.  Ndani ya unyoya utaona ufito madhubuti uliofunikwa na kitu kama unywele ili kwamba, kwa sababu ya umadhubuti wake huyashikilia (manyoya haya).  Ufito u wazi ndani (kama mrija) ili kwamba usiwe mzigo kwa ndege huyo na kuzuia urukaji wake.

 

 

NDEGE WA MIGUU MIREFU

 

Je, umewahi kuona ndege wa miguu mirefu na ukadiriki kufikiria faida aliyonayo kwa miguu mirefu hiyo?

Mara nyingi (ndege huyo) huonekana kiulinganifu katika maji ya kina kifupi.  Utamwona kana kwamba yuko katika lindo mahali alipo akiwa amesimama juu ya miguu yake mirefu. 

Hufanya lindo kwa vipitavyo katika maji.  Akiona kitu chochote chenye kulika pole pole hukisogelea na hudaka na kumshikilia mtesi wake. Kama miguu yake ingekuwa mifupi zaidi, tumbo lake lingegusa maji katika nyendo zake za kumnyemelea mtesi wake na pengine lingevimba na kushindwa kumkamata mtesi wake.  Kwa hiyo ametunukiwa na mihimili (miguu) miwili mirefu kukidhi/kutimiza haja yake bila kikwazo.

 

 

UPATIWAJI RIZIKI

 

Hebu fikiria kazi nyingine za umahiri (ufundi) ambazo zimetumika katika kuumbwa kwa ndege.  Unaona kila ndege mwenye kinga ya miguu mirefu amepewa shingo ndefu vilevile kumuwezesha kuokota chakula chake kutoka ardhini.  Wakati mwingine hutokea kwamba mdomo mrefu unatengenezwa kufanya kazi ya shingo ndefu ikipelekea kwenye urahisi utakiwao.

Je, huoni kwamba uumbaji wowote unaofikiria utauona barabara na umejaa ustadi?

Tizama kwenye mimea ambayo ndege hawa wanaitafuta nyakati za mchana.  Haitokei kamwe kwamba haipatikani lakini hawaipati ikiwa  imekusanyika mahali pamoja.  Wanaipata kwa  kuitafuta na kwenda huku na huko.  Hali kama hii hujitokeza katika viumbe wengine

Utukufu ni wake Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.).  Ambaye amegawanya riziki na akapanga njia mbalimbali za namna ya kuisambaza.

Haikupangwa katika hali ya kwamba isifikiwe (isipatikane hiyo riziki) kwa viumbe ambavyo huihitaji wala haikupangwa, kwamba njia ya kuifikia iwe nyepesi na kwamba ipatikane bila juhudi zozote kufanyika kwani kuwa hivyo kungekuwa hakuna maana kama chakula kingelipatikana kwa wingi katika sehemu moja yoyote ile wanyama wangekuwa walafi, kamwe wasingeitoka sehemu hiyo, ingepelekea kutokuyeyushwa chakula tumboni na (kutokea) maangamizi.

Watu pia, kwa sababu ya uwingi (wa riziki) wangepatwa na hali ya kuwa na kiburi na majivuno na matokeo ya misiba na matendo maovu."

 

 

NDEGE WA USIKU

 

Imam (a.s.) aliniuliza, "Unajua kuhusi ndege kama vile bundi na popo ambao hutoka nje wakati wa usiku tu, na kuhusu vitu walavyo kama chakula chao?”

Nilijibu,"Sijui."

Yeye (a.s.) akasema, "Chakula cha hawa ni mchanganyiko wa aina mbalimbali za wadudu waliotawanyika katika anga, k.m. mbu, nondo, wadudu walio kama nzige na buibui n.k.  Siku zote wako kwenye anga, hakuna sehemu ilivyo huru bila wao kuwepo.  Kama ukiwasha taa usiku juu ya paa au sehemu yoyote ya eneo la nyumba, wengi wa aina mbalimbali za wadudu hao hujikusanya kuizunguuka taa (hiyo).

Wametokea wapi?  Hakika wametokea sehemu za karibu tu.  Kama mtu yoyote atasema kwamba wanatokea misituni na mashambani, atajibiwa kwa kuulizwa kwamba ni vipi wanafika upesi sana na vipi wanaweza kuiona taa iliyowashwa ndani ya nyumba iliyozunguukwa na nyumba nyingine nyingi, ambapo kusema kweli hawachukui muda mrefu kuja kuizunguuka hiyo taa.  Ni wazi kutokana na hili kwamba wote hawa wametawanyika kila mahali katika anga na ndege wale wanaotoka usiku kuwakamata na kujilisha kwa hao.

Tizama vipi lishe ilivyoandaliwa kwa ajili ya ndege ambao wanatoka usiku kwa njia ya wadudu hawa, waliotawanyika katika anga.

Jaribu kuelewa madhumuni ya uumbaji wa viumbe hivi vyenye uhai, isije ikawa mtu fulani akafikiria kwamba vimeumbwa bure bila faida yoyote.

Popo ni kiumbe wa ajabu, yu katikati baina ya ndege na mnyama wa miguu minne, kwa kweli amejamiika zaidi kwa mnyama wa miguu minne, na masikio mawili yatokezayo, meno na nywele nzuri.  Huzaa watoto wake, ambao huwalisha kwa maziwa yake.  Hukojoa na kunya.  Hutembea katika misimu yote minne.  Tabia hizi zote ni kinyume (tofauti) na zile za ndege.  Hujitokeza nje usiku tu na kujilisha kwa wadudu waliosambaa katika anga.

Baadhi (ya watu) husema hali chochote, bali huishi tu kwa hewa fufutende (vuguvugu) kama lishe.

Hii siyo sahihi kwa sababu mbili, kwani kukojoa na kunya, ni vithibitisho vya matumizi ya chakula kigumu.  Kisha ana meno, kama asingekuwa anakula, meno yangekuwa hayana maana, ambapo kwamba hakuna kitu katika uumbaji kisicho na maana.

Kiumbe huyu ana sifa zijulikanazo vizuri.  Kinyesi chake kimechanganyika na vitu vingine.  Umbile lake la kushangaza lenyewe ni la ajabu.  Huruka huku na huko kama apendavyo kwa faida yake mwenyewe - ishara ya Ujuzi Mkuu wa Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.).

Ndege afumae (kiota) hujenga kiota chake wakati mwingine katika miti.  Kama akiona nyoka mkubwa anaelekea kwenye Kiota chake, hupatwa na wasiwasi.  Hutafuta huku na huko njia za usalama Mara tuu anapopata mbegu yenye miba huichuma na kuitupa kutokea kwa juu kwenye mdomo uliowazi wa nyoka.  Nyoka huanza kugaragara kwa uchungu na humsukasuka mpaka kufikia kifo.

Kama nisingekuelezea hivi, je, ungeweza kudhania kwamba mbegu yenye miba ingeweza kuwa na faida kama hizi, au mtu yoyote  angeweza kufikiri kwamba ndege mkubwa au mdogo, angeweza kufanikisha mpango kama huo?

Jifunze somo kutokana na hili.  Yako mambo mengine mengi yenye faida zisizojulikana ambazo huhitaji maelezo ya matukio mapya au habari zitakiwazo kufahamika.

 

 

NYUKI

 

Hebu fikiria kuhusu nyuki na juhudi za pamoja za kuzalisha asali na kundi la nyuki la pande sita, na werevu mwingi wa silika uliowekwa ndani (yake).  Utaona ni wa kustaajabisha mno na wa kutatanisha, wakati ukifikiria kazi zake. Utaona uzalishaji wao (wa asali) ni mkubwa kabisa na ni tumizi zuri kwa wanadamu.

Na kama utamtizama fundi huyo (nyuki) utamuona hana akili, asingeweza kujitambua mwenyewe, nini la kusema kuhusi mengine.

Hivyo kuna hoja iliyo wazi katika hili kwamba usahihi katika ufundi na ustadi si vyenye kutokana na nyuki (mwenyewe) bali ni (Ufundi na Ustadi) Wake Yeye Mwenye Kuweza yote,     Ambaye amemuumba katika umbo hilo na akamtiisha kwa kuwahudumia wanadamu.

 

 

NZIGE

 

Hebu mtizame nzige alivyo mnyonge, lakini aliye imara.  Hakuna yoyote awezaye kujikinga dhidi ya kundi la nzige, kama litauvamia mji.

Je, hujui kwamba kama yeyote yule katika Wafalme wa ulimwengu mzima atoke na majeshi na jamaa zake kuwapiga nzige, asingeshinda?

Je, hii siyo hoja yenye kudhihirisha Uwezo Mkuu wa Mwenye Ngugu zote Allah (s.w.t.) kwamba (viumbe) vyenye nguvu nyingi kabisa katika uumbaji wake visingeweza kuhimili shambulio la viumbe vilivyo dhaifu kabisa katika Viumbe Vyake?  Watazame jinsi wanavyoifunika ardhi yote kama mafuriko, wakizagaa juu mlimani, jangwani, uwandani na mjini, wote kwa umoja, hivyo kwamba kundi lao huzuia hata mwanga wa jua.

Sasa kadiria ni miaka mingapi ingehitajika kutengeneza kundi hilo kwa mkono (wa mtu).

Mwenye Nguvu zote Allah ametoa hapa hoja nyingine ya uwezo Wake Mkuu ambao hakuna kiwezacho kuupunguza na kwa huo hakuna kiwezacho kuuongeza.

 

 

SAMAKI

 

Hebu fikiria samaki na hili  ambazo zipo chini ya mazingira iliyo amriwa kuendelea kupelekea maisha yake.  Haina miguu, kwa kuwa makazi yake ni katika maji na haihitaji kutimbea (na miguu).  Haina mapafu, kwa vile haiwezi kuvuta hewa.  Imewekwa (iishi) chini ya uso wa maji.

Badala ya miguu, imejaaliwa na mapezi madhubuti ambayo kwayo hupazua maji katika pande zote; kama vile baharia wa mashua akatavyo  maji katika pande zote kwa makasia yake.  Ina mfuniko wa magamba mazito yaliyounganishwa na kile lingine kama pete za koti la deraya kujilinda dhidi ya ajali.  Ina stadi kali ya kunusa, kama fidia kwa uoni dhaifu usababishwao hivyo na maji.  Hunusa kitu chake kutoka kwa mbali na (hapo) hukifuatia.  Ni kwa njia ipi nyingine ingeweza kutumia kufahamu asili na mahali kilipo chakula (chake)?  Na, elewa vilevile, kwamba inazo tundu sehemu zote kuanzia kinywani mpaka masikioni, ambazo kwazo maji hupita na kuipa stawisho la kuburudika sawasawa kama lile linalopatikana kwa wanyama wengine kwa kuvuta kewa halisi iliyopoa  ya upepo wa asubuhi.

Sasa, fikiria tabia zake za kiuzazi.  Idadi ya mayai ndani ya samaki ni zaidi ya kadiri.  Sababu ni kuongeza chakula kiwezekanacho kuwa kwa viumbe vingine hai kwa vile wengi zaidi katika wao wanaishi kwa kula samaki pembezoni mwa madimbwi ya maji, katikati ya mapori. Mara tu samaki apitapo, humrukia juu yake.  Kwa vile samaki ni mawindo ya hayawani, ndege, watu na hata samaki wengine, mambo yamepangwa kwa namna kuiweka idadi ya samaki kuwa juu.

Hebu fikiria aina za wanyama wenye rangi mbalimbali, ma-kaka (maganda), maisha ya majini na jamii mbalimbali za samaki, kupata fununu ya ustadi mkubwa mno wa Mwenye nguvu zote Allah kwa upande mmoja na silika (maumbile) dhaifu ya elimu hii imilikiwayo na viumbe.  Hawana mpaka katika idadi wala sifa zao hauziwezi hujulikana, isipokuwa kwamba asijue moja baada ya nyingine kwa fursa ziwezazo kutokea.

Kama kwa mfano "Cochineal" (vitu vyenye rangi angavu nyekundu iliyofanywa kutokana na miili iliyokauka ya aina fulani ya wadudu), rangi yake ilisomwa yote na watu, imeelezwa mbweha azururaye ufukweni mwa bahari, alimpata na kumla Halzuuni (mdudu mwenye rangi).  Mdomo wake ulipatwa na rangi.  Rangi hiyo iliwavutia watu ambao walianza kumtumia mdudu "Cochineal" kama rangi ya kuchovyea vitu.  Viko vitu vingine vingi ambavyo tabia zao huja kujulikana kwa watu mara kwa mara.”

Ilikuwa adhuhuri.  Bwana wangu aliamka kwa ajili ya Sala, akiniambia nije kwake (tena) mapema asubuhi ijayo.

Nilirejea nyumbani nikiwa nimefurahishwa maradufu kwa tunu ya maelekezo katika elimu niliyopata kutoka kwake.

Kwa shukurani nyingi kwa Mwenye Nguvu zote Allah niliupitisha usiku huo kwa kufurahia sana.

 

 

Baraza La Tatu Mazingira

 

 

 

 

 

 

 

MAZINGIRA

 

Niliwasili mapema asubuhi ya siku ya tatu, na kwa kuruhusiwa, niliingia, na nilipoombwa kukaa nilikaa.

Yeye (a.s.) alianza, “Ewe Mufazzal! nimekuelezea kwa kina na ukamilifu zaidi kuhusu uumbaji wa mwanadamu na usanii ustaajabishao wa Mwenye Nguvu zote Allah ambao umepelekea kwenye ukamilifu wake na masomo ya kujifunza kutokana na mabadiliko kidogo ya manzili zake.  Vilevile nimeshughulika na maelezo ya ulimwengu wa Wanyama.

Sasa natoa maelezo yenye kuhusu anga, jua, mwezi, nyota, mbingu, mchana na usiku, kiangazi na kipupwe, pepo, kanuni za misimu minne, mvua, miamba, milima, ulimwengu wa mimea, mitende na miti ya kawaida kuonyesha kwayo ishara na masomo ya kujifundisha humo.

 

 

MBINGU

 

Hebu itizame rangi ya mbingu na ona jinsi Usanii ufaavyo kwa makusudio (ya mambo).  Rangi hii mahsusi ni dawa ifaayo kuliko zote kwa kutia afya na nguvu ikilinganishwa na rangi nyingine zote. Hata madaktari humuelekeza mtu kuangalia kwenye rangi ya kijani au katika rangi nyingine iliyozidi katika kijani kibichi kwa ajili ya maradhi fulani ya jicho.

Madaktari walio wafanisi (hodari) humuelekeza mtu mwenye udhaifu wa kuona kuangalia kwenye beseni la rangi ya kijani lililojazwa maji.

Hebu  tizama jinsi Mwenye Nguvu zote Allah alivyoiumba mbingu kwa rangi ya kijani ikageuzwa kuonekana nyeusi ili isije ikasababisha upungufu fulani, kwa kule kurudia rudia kuangalia.

Hali hii hii ambayo watu wameigundua kitokana na kufikiri na kufanya majaribio ni hali halisi ili kwamba wale ambao wangejifunza somo kutoka humo, na wapotofu - Allah (s.w.t.) awaangamize, wanapotoka.

 

 

MAWIO NA MACHWEO (YA JUA)

 

Hebu fikiria kuchomoza na kuchwa kwa jua katika kuingia kwa mchana na usiku.  Bila kuchomoza jua, shughuli zote za ulimwengu zingesimama.  Ulimwengu ungezama katika giza bila kuwepo uwezekano wa kazi au maisha (riziki).  Kungekuwa hakuna raha (furaha) katika maisha bila ya athari nzuri ya mwanga wa jua.

Faida za mawio ya jua ziko wazi kabisa na hazihitaji simulizi nyingi.  Hebu fikiria kuchwa kwa jua.  Kama lisinge tua, watu wasingepata wasaa wala pumziko lolote.  Watu bila kukosa, huhitaji kupumzika na kupata faraja ili kuziponya stadi ya kuyeyusha na utumiaji mzuri wa chakula (mwilini) na kutuliza na kupumzisha mishipa ya fahamu ya mwili.

Tamaa yao, kwa kutaka kuendelea kufanya kazi (bila ya kupumzika), kungesababisha matatizo makubwa kimwili, kwani wengi wameazimia na kukakamia kwamba mpaka usiku uwafunike, hawatakuwa na faraja na pumziko, katika utafutaji wa maisha (riziki) na ulimbikizaji wa mali.

Kuendelea kuwaka kwa jua daima, nako kungeipasha ardhi kwa joto kali sana na (hivyo) kurudishwa nyuma kwa maisha ya wanyama na mimea.  Mwenye Nguvu zote Allah kwa ajili hiyo, ameamuru kwamba kutakuwa na vipindi vya kuwaka jua na vya giza, kama taa ambayo huwashwa na watu wa nyumbani pindi tu wanapoihitaji, na huzimishwa isipohitajika, ili kuwapa faraja na pumziko. 

Nuru na giza vinakinzana vyenyewe kwa vyenyewe na bado vyote vimefanywa kufaa kwa faida za uboreshaji wa ulimwengu na mtengenezo mzuri.

 

 

MISIMU MINNE YA MAJIRA YA MWAKA

 

Kisha hebu fikiria misimu minne ya majira ya mwaka, kwa matokeo ya upandaji juu wa jua na utelemkaji wake (kutua) na faida na mpango uliomo humo.

Miti na mimea hupata mchipuko (muinuko)wa uhai ndani ya vipindi viwili muhimu vya mwenendo wa jua.

Ugandaji wa mvuke katika anga husababisha kufanyika mawingu hatimae kuleta mvua.  Wanyama huimarika miili yao na kupata nguvu katika msimu huu. 

Kuna upatikanaji wa joto muhimu la uhai katika kiangazi na vile vile pia kukua kwa vitu ambavyo hukomaa katika kipupwe, mimea hupata maua na matunda katika msimu huu.  Wanyama hupata msisimko wa kufanya ngono.

Anga hupatishwa joto katika kiangazi ambalo hupelekea katika kuiva kwa matunda.  Taka za mwili hukazwa.  Ardhi hukauka na kufaa kwa ujenzi na shughuli nyingine.

Hewa husafika wakati wa kipupwe, maradhi  hupitishwa (huepushwa).  Miili hupata afya.  Usiku huwa mrefu zaidi na hivyo kusaidia katika kufanya majukumu fulani kwa sababu ya vipindi virefu.

Hewa katika msimu huu hufaa shughuli nyingi na vile vile, ambazo zitachukua muda mrefu kusimulia.

 

 

JUA

 

Sasa fikiria mwendo wa jua kupitia mafungu kumi na mbili ya Zodiac (Burji) kuukamilisha mwaka na ustadi uliomo ndani yake.  Hiki ni kipindi ambacho kina misimu hii minne ya majira - Kipupwe Kiangazi, Masika na Demani ("Spring") katika ukamilifu wao.  Nafaka na matunda huiva katika mwendo huu wa jua katika mwaka kukidhi haja za wanadamu.  Mafuatano ya nyakati hizi za mwaka ni muendelezo unaojirudia rudia

Je, hujui kwamba kupita kwa jua hili katika kanda za mbinguni, kutoka ukanda wa Samaki (pisces) na mpaka kuurudia tena, hufanya mwaka mmoja?  Miaka hii n.k. imeendelea kuwa kama vipimo vya kukadiria muda tangu mwanzo wa dunia katika nyakati zote zilizopita.  Watu wanakadiria kwayo vipindi vya muda wa maisha, mikopo, mikataba, na mambo mengine ya biashara.  Ni katika mwenendo wa jua hili kwamba mwaka hukamilika na ukadiriaji sahihi wa wakati ukaanzishwa.

Hebu tizama jinsi jua litoavyo mwanga wake katika ulimwengu na ustadi gani jua hili limeamriwa kwayo.  Kama lingeangaza daima kwenye sehemu moja ya "Zodiac", bila kubadilisha sehemu yake, faida za mionzi yake isingepenya katika pande zote kwa sababu ya kuwepo milima na kuta.

Kwa hiyo, limeumbwa hivyo kwamba linachomoza kutoka Mashariki katika wakati wa kabla ya adhuhuri, likitoa mwanga wake juu ya vitu vilivyoko upande wa Magharibi, huenda hivyo daima, likieneza mwanga wake kutoka upande huu kwenda upande huu mpaka kuelekea upande wa Magharibi kutoa na kutawanya mwanga wake juu ya vitu ambavyo vilishindwa kuupata wakati wa kabla ya adhuhuri, hivyo ili kutoruhusu pembe yoyote kubakia bila faida na dhumuni lililokusudia kufanya.

Kama kwa mwaka mzima au sehemu yake tu hali ingebadilika kuwa kinyume, unaweza ukafikiria msiba wa wanadamu.  Kwakweli  ni njia ipi wangeweza kuitumia kwa kuishi?

Je, mtu hachunguzi  mpango huu adhimu ambamo humo taratibu zake zingeshindwa kabisa?  Zinafanya kazi kwa kujiendesha zenyewe bila kuzembea, wala hazichelewi nyuma ya muda uliowekwa kwa uendeshaji wa utaratibu wa ulimwengu huu na ustawi (wake).

 

 

MWEZI

 

Kuna ishara iliyofunuliwa na Mwenye Nguvu zote Allah katika uumbaji wa mwezi -kielekezo kizuri.  Watu kwa ujumla wanakadiria miezi katika msingi wake, lakini mwaka haukuanzishwa kisawasawa nao.  Mwendo wake haukufanyizwa mabadiliko ya msimu wala nyakati za kuchanua maua na kuiva kwa nafaka.  Hii ndiyo maana hesabu ya miezi  na miaka ya miezi iwakaya hutofautiana kutoka hesabu ya miezi na miaka ya jua.  Mieze ya miezi iwakayo hubadilika, hivyo kwamba wakati mwingine mwizi ule ule una angukia katika majira ya Kiangazi na wakati mwingine katika kipupwe.  Na hivyo ndivyo ilivyo kwa miezi mingine.  Kwa mfano mwezi wa Muharram unaweza ukachukua kipindi ndani ya majira ya Kiangazi wakati mwingine, (na) ndani ya majira ya msimu wa mvua kwa nyakati nyingine na ndani ya majira ya Kipupwe katika wakati mwingine.  Hii huonyesha kwamba hesabu ya miezi kwa miezi iwakayo na hesabu ya miezi ya jua huendelea kubadilika na hailingani kwa kila mwingine.

Fikiria kwa nini mwezi huwaka usiku na ustadi uliomo ndani yake.  Viumbe hai huhitaji ubaridi kidogo upatikanao kutokana na giza ili kupata pumziko na faraja.  Kukosekana kabisa kwa mwanga na giza leusi kusingekuwa na ubora wowote, hata hivyo, bila ya uwezekano kwa kazi ya aina yoyote.  Watu huhitaji kufanya kazi kidogo kwa kutaka kupata burdani la kupumzika wakati wa mchana.  Inaweza ikawa kwamba kwa ajili ya ukomo (ukali) wa joto (la jua) anaweza akafanya kazi katika mwanga wa mwezi kwa mfano, kilimo,  ukamuaji wa maziwa, ukataji kuni n.k.  Mwanga wa Mwezi huwasaidia watu kufanya kazi kwa kutafuta maisha yao  (riziki) wakati wowote wanapopenda kufanya hivyo.  Wasafiri huuona ni mvutio katika safari zao.  Kuchomoza mwezi kumeamriwa kwa vipindi mbali mbali vya usiku ambao unafanywa kuwa na mwanga mdogo zaidi kuliko wa jua kwa wakati wa kipindi sawa, wasije watu wakaanza kufanya kazi katika taratibu ile ile kama wanavyofanya wakati wa mchana bila kupumzika hata kulazimisha kifo.

Katika awamu tofauti za mwezi, kutokea kwake kama mwezi mwandamo, kutoweka kwake wakati wa mausiku ya mwishoni mwishoni, kufifia kwake na kupungua na kupatwa kwake, kuna vielekezo mahsusi kwamba mabadiliko yote haya yameamriwa kwa faida ya ulimwengu na Mwenye Nguvu zote Muumba Allah (s.w.t.) ambavyo vinaweza vikasaidia kama mwongozo kwa mtu yoyote apendae kuufuata mwongozo huo.

 

 

NYOTA

 

Hebu fikiria kuhusu nyota na nyendo zao zenye kupambanulika.  Kuna baadhi miongoni mwao ambazo hazisogei kutoka maeneo yaliyokusudiwa kwa ajili yao.  Ziko nyingine ambazo husogea kutoka eneo mpaka eneo na zina nyendo zao zenye kupambanulika.  Kila moja katika hizo ina nyendo mbili moja kwa sababu ya taratibu ya mwendo wa ulimwengu mzima kwa muelekeo wa upande wa magharibi, na mwingine ni mwenndo wake yenyewe kwa muelekeo wa upande wa mashariki.

Hii hufananishwa kwa nyendo mbili za mdudu chungu akiwa upande wa juu wa Kipande cha Kijaa.  Kijaa huzunguuka kwa upande wa kulia na mdudu chungu huenda upande kinyume (kushoto).  Katika hali hii mdudu chungu atakuwa na nyendo mbili - moja ni ya mwendo wake mwenyewe, mwelekeo wa mbele na mwingine usiokusudiwa, pamoja na Kijaa.

Sasa hebu ulizia kutoka watu hawa ambao hudai kwamba nyota hizi zimejitokeza kuwepo zenyewe bila ya Usanii wa Msanii  Mwenye Nguvu zote, ya kwamba ni kitu gani kilichokuwa pingamizi kwa maumbo yao haya yote yawe ni yenye kusimama tu mahali pamoja au yote kuwa yenye kuzunguuka (kutembea)?

Uumbaji bila Muumba huthubutu mfumo mmoja, kwa nini kutokee nyendo aina mbili tofauti juu ya mfumo mahsusi na uliopendelewa?  Yote haya huonyesha wazi kabisa kwamba mwendo wa namna mbili za nyota kama unavyoendelea sasa, ni matokeo ya dhumuni halisi, Usanii na Ustadi, siyo kitu cha bure kisicho na maana kama wanavyodai  Walahidi hawa wapendao vitu vya kidunia tu.

Kama Kinzano litaletwe kwamba kwa nini baadhi ya nyota zimetulia ambapo nyingine zina sogea,  jibu letu litakua kwamba kama zote zingekuwa zimetulia, ishara pambanuzi ambazo zinaonyeshwa  sasa na nyendo zao kutoka eneo mpaka eneo (lingine) zisingekuwepo.  Siri nyingi hufahamika kwa matukio yaliyohusishwa na juu na nyota nyingine kwa sababu ya nyendo zao katika njia zao mahsusi.  Faida  ipatikanayo sasa katika suala la msimu wa nafaka na hata bashirio n.k. katika nyendo za nyota chache kwa sasa, isingeweza kufikiwa.

Kama zote zingekuwa na msogeo, kituo chao cha kufika kisingekuwa na doria za kuweza kutambuliwa.  Mwenendo wa Sayari zisogeazo katika maeneo yao yalizopangiwa, huwezesha kupatikana taarifa muhimu, kama kadiri ya mwendo wa msafiri inavyopimwa kwa kipimo cha umbali.  Kwa kutokuwepo vipimo vya maili, au hatua, kadirio la kiasi cha mwendo lingekuwa vigumu (kufanyika).

Kadhalika, kama nyota zote hizi zingekuwa na msogeo na misogeo ya matakwa tofauti wakati huo, kadirio la kiasi cha msogeo wao lisingewezekana, kwa sababu katika mahali pa kwanza zilikuwa hazina idadi kuwezekana kufanya hesabu kwa chombo chochote kile cha kufanyia hesabu au mnajimu, na pili kwa sababu ya mahali pao ziliopo - baadhi ziko upande wa mashariki, nyingine upande wa magharibi, bado nyingine ziko pande wa kasikazini na tena nyingine katikati au katika ncha (mbili za dunia) au hapa, pale na kila mahali.  Maeneo yao yangekuwa vigumu kwa kweli kupangika, na tatu kwa sababu ya ugumu utakanao na nyota zote kupitia katika safu kumi na mbili.  Kisha ingekuwa haiwezekani kufanya upambanuzi wa aina yoyote, na kwa sababu hii dhumuni lote la msogeo wao na kuwepo kungebatilishwa.

Kama zote zingesogea kwa kiasi cha mlingano mmoja wa usogeo, lengo lililomo lingefanywa kuonekana bila faida yoyote kwa mchanganyiko wa makundi yao (nyota).

Kinzano katika hali hiyo kutoka kwa fundi mtoa makosa lingepata nafasi kwa kusema kwamba ulinganifu wa mwendo (msogeo) juu ya mfumo mmoja huonyesha kutokuwepo kwa Msanii - Muumba, kama tulivyokwisha kubalisha kwa ushahidi wa maelezo kuwepo kwa uhai wa Mwenye Nguvu zote Alah (s.w.t.).  Ndiyo maana ni wazi kabisa kwamba nyendo zao tambuzi, mabadiliko  na mizunguuko yao ikiwa ni yenye malengo, ni kazi ya usanii na upambanuzi.

Hebu fikiria nyota ambazo hutokea vipindi fulani fulani katika mwaka na hupotea wakati wa vipindi vingine vya mwaka, kwa mfano, kilimia (Pleides), Mpini kata (Orion), jozi ya nyota za "Sirius" na "Canopus".  Kama zote zingetokea kwa pamoja, hakuna hata moja ingejitokeza kuwa kama alama maalum kwa watu kuipambanua, kuijua na kupata  mwongozo, kama watu wapatavyo maarifa kutokana na kupotea kwa "Orion" na "Taurus" (thaura).  Kutokea huku na kupotea kwa lika kimoja katika nyakati mahsusi kuliamriwa kwa faida ya wanadamu.

Kama vile nyota za kilimia ziliamriwa kutokea na kupotea katika nyakati tofauti kwa faida mahsusi za watu, kadhalika kundi la nyota la "Bear"  limeamriwa kwa mandhari isiokoma kamwe isipotee, kwa vile ina jukumu lingine la kufanya, ikiwa kama boya kwa ajili ya watu kutafuta njia zao katika vijia katikati ya msitu na bahari.

Kwa vile nyota za kundi hili (la falaki) daima ziko kwenye mandhari (zinaonekana), watu huzitizama mara tu wanapohitaji kujua kijia kwa upande wowote. Mambo yote haya mbalimbali hutekeleza faida za wanadamu.

Mbali na hayo, ndani yake mna mwelekezo wa wakati, kwa ajili ya kilimo, (jumla), kilimo cha bustani, usafiri katika nchi kavu na baharini.  Vilevile kuna udhahiri wa mambo mengine ambayo yana rejea kwenye nyakati tofauti, kwa mfano kunyesha mvua, kuvuma kwa pepo majira ya misimu ya Kiangazi na Kipupwe.

Zaidi ya hayo, watu hupata njia yao kwa msaada wao (nyota) ndani ya Safari (zao) katika nyanda zinazotisha na bahari zinazoogofya wakati wa masaa ya masiku ya giza.  Juu ya hayo, kuna masomo mengi makubwa ya kujifundisha kutoka nyota hizi ambazo sama huenda mbele, baadhi hurudi nyuma katika muelekeo wa upande wa Mashariki au wa Magharibi.

Mambo ya Kimbinguni, mwezi na jua husogea kwa haraka sana, na kama yangekuwa karibu zaidi nasi na mwendo wao ungekuwa ni wa kusikiwa kiusawasawa kama ilivyo je, hufikiri kwamba macho yangekuwa kiwi kwa mng'aro wao na miali kama vile yanavyokuwa kiwi kwa miali ya radi wakati inapoanza kutoa miali moja kwa moja, ikiiwasha anga iliyoko kati ya nchi na mbingu kama moto?

Mfano mwingine wa hili ni nyumba yenye dari lake lililofungwa na mishumaa mingi iwakayo ikikizunguuka kichwa kwa nyendo za kasi sana.  Maho yatalazimika kupofuka na mhusika kuanguka chini kifudifudi.  Hebu angalia jinsi ilivyoamriwa kwamba (jua na mwezi) vingetembea kwa kasi yao iliyopo sasa katika umbali mkubwa mno kutoka sisi ili kuuzuia uwezo wetu wa kuona dhidi ya uharibifu na ugonjwa, wakati bado zinakuwa na masafa yao ya ajabu kwa dhumuni  yatakayo yahudumia.

Nyota ni zenye kung'ara tu kutoshako kutoa mwanga wakati wa ukosekanaji wa mwezi na kutuwezesha sisi kutembea huku na huko katika vimulimuli vyao.  Mtu nyakati nyingine huhitaji kusafiri wakati wa usiku, na katika kukosekana kumetameta kwao, angeona ni vigumu kujisogeza katika njia yake.

Hebu fikiria upole na ustadi ulioamriwa katika uumbaji huu.  Giza nalo pia lilihitajika na kwa hiyo kipindi kimewekwa, na kuongezeka kwa vimuli muli, ili kutekeleza malengo tuliyokwisha yashughulikia.

 

 

ULIMWENGU

 

Hebu fikiria ulimwengu pamoja na jua lake, mwezi wake, nyota zake na "Zodiac"' ambazo daima zinazunguuka kwa kupasika na amri halisi na hukumu ili kuleta humo faida nyingi kwa wakazi wa ardhini, kwa mnyama wa rangirangi na falme za mimea katika mabadiliko ndani ya misimu minne ya majira, siku na mausiku, ambavyo (vyote hivi) vimeelezewa kwako.  Je, mtu yeyote mwenye akili timamu anaweza kufikiri kwamba mpango huu ulioratibishwa na usanii ambao hutegemea kanuni na utaratibu wa ulimwengu unaweza kujitokeza na kuwepo hivi hivi bila ya Msanii Mwenye Kujua Yote?

Kama mtu mmoja atasema kwamba ni bahati tu ndiyo iliyosababisha hivi (ulimwengu huu kujitokeza na kuwepo), ni kwa nini hasi hasemi jambo lile lililo sawa katika uhusiano kwa gurudumu la Kiajemi ambalo analiona likizunguuka, (na) likinyweshea shamba lililooteshwa kwa miti na mboga? Anaona vipuli vyake vyote vimetengenezwa kupasika na mpango halisi, kila kipuli kimeunganishwa kwa kupatana na kingine kwa mfumo wa kutekeleza mahitaji ya vifao vyake.

Na kama akitoa maelezo kama hayo kuhusu gurudumu la Kiajemi basi maoni gani kumhusu yeye watu watamuazia kwa kuyasikia maneno yake?  Hakika huyu ni asiye na akili mtu mpumbavu aliyepungukiwa na akili.  Je, haoni jinsi jauhari na asili ya gurudumu la Kiajemi, ambalo lenyewe ni kufu na lisilo na akili, lingeweza kujitokeza lenyewe likiwa pakoja na ukusudiaji kamili kwa mahitaji ya shamba?  Je, yawezekana kweli mtu yeyote mwenye akili timamu kulikubali hili?

Je, atalikataa hili katika suala la gurudumu la mbao la Kiajemi ukiwemo mpango na ustadi mdogo, kwamba siyo sehemu ya uhunzi iliyopangwa na kusaniwa, na bado ataweza kusema kwamba ulimwengu huu mkubwa mno na wa ajabu ambao umejaa miradi iliyo nje ya ufahamu wa mwanadamu, ukifanya kazi kwa uso wote wa dunia na vitu vyote vilivyomo ndani yake uwe umejitokeza kuwepo kwa bahati bila ya ujuzi na ustadi au kipimo? 

Je, mtu anazo njia au mbinu za kuonea usawa kama kitu chochote kile kinaiendea mrama mbingu, kama vile vipuli vya mbao vinapotoka nje ya taratibu (kuharibika).

 

 

MCHANA NA USIKU

 

Hebu fikiria uhusiano wa saa za mchana na usiku.  Zimerekebishwa kwa faida ya uumbaji.  Saa za mchana au za usiku hazizidi saa kumi na tano.

Je, unajua kwamba kama masaa ya mchana yangerefushwa kufikia masaa mia moja au mia mbili, uhai wa wanyama na mimea ungetoweka? 

Kipindi hicho kirefu bila pumziko na wasaa (faraja) kingewaua hayawani, ambapo wanyama wa miguu minne wangeendelea tu kujilisha. 

Watu, vilevile, wangeendelea kufanya kazi tu bila kusimama na kutokezea kuhatarika kwa maisha.  Uhai wa mimea ungeteketea  kabisa kwa kuathiriwa na kipindi kirefu cha joto la mchana.

Kadhalika, kama usiku ungerefushwa ukalingana kiusawa, jamii zote za viumbe hai vingezuilika kutembea huku na huko kutafuta lishe na matokeo ni  kufa njaa.  Mimea ingepoteza joto lao muhimu, kukawia na kutoweka, kama vile unavyoona ile mimea ambayo imewekwa hivyo kwa kupata mwanga mdogo tu wa jua.

 

 

JOTO NA BARIDI

 

Fikiria mzunguuko wa joto na baridi kuhusu ongezeko, punguko na usawa, na kutokea misimu minne ya majira ya mwaka ifuatanayo mmoja baada ya mwingine katika ulimwengu na ikishughulika kwa faida yetu.

Zaidi ya hayo, miili husitawi na kutiwa afya kwayo.  Hii hupelekea kwa afya zao na maisha marefu, kwani kukosekana kwa athari ya joto na baridi moja baada ya ingine kwa mawumbo yenye mwili wangeumia kwa uharibifu, mvunjiko na udhoofu.

Hizi mbili (joto na baridi), kimoja kuchukua nafasi ya kingine kidogo kidogo na pole pole.  Utaona kwamba mipunguko inatoa nafasi kidogo kidogo kwa mfuatio wa muongezeko wa mwingine.  Ikiwa mmoja ghafla umeingilia kati utaratibu wa mwingine.  Ungepelekea kwenye madhara makubwa, kwenye ugonjwa kwa viumbe vyenye mwili kama vile mtu awezavyo kupata dhara na ugonjwa, kama kwa ghafla atajitoa kutoka ndani ya bafu yenye maji moto na kujiingiza katika sehemu ya baridi.  Mwenye Nguvu Zote Allah (s.w.t.) ameamuru badiliko la joto na baridi kidogo kidogo kumzuia mtu kutokana na dhara la ghafla wa badiliko.

Kama yeyote yule atadai kwamba ukidogo kidogo huu na kawio, katika mjio wa matokeo ya joto na baridi hufanya mzunguuko wa jua na mwinamo wake ukivutia sana muda wa mchana, anaweza kuulizwa kama sababu ipi kuhusu msunguuko wa jua na mwinamo wake wa kidogo kidogo ukivutia sana kawio na ukidogo kidogo.  Kama atajibu kwamba ni kwa sababu ya anga za pande za Mashariki na Magharibi, anaweza kuulizwa kama kwa nini iwepo hivyo.  Maswali katika kusudio hili yataendelea kurudiwa rudiwa kuulizwa mpaka alazimike kukubali umuhimu wa kuwepo Mwenye Kujua yote, Mwenye Dhumuni na Msanii.

Bila joto, matunda mabichi, machachu yaliyo magumu yasingeweza kupevuka yakawa na utamu na maji mengi yatumikayo kwa kiungo au viungo, vibichi au vikavu.  Bila baridi, vikonyo visingechipua masikio ya punje kwa usaaji mwingi mno kwa utoshelezaji wa lishe na mbegu.

Je huzitambui faida za joto na baridi, pamoja na sifa zao zote ni chanzo cha matatizo kwa miili vile vile?  Mna fundisho kwa wale ambao wangetafakari juu ya hili na uthibitisho kwamba taratibu zote hizi ni kwa faida ya ulimwengu na, kila kimoja katika viumbe kuna faida kwayo kutokana na Usanii wa Mwenye Nguvu zote Mwenye kujua yote.

 

 

HEWA

 

Ngoja nikufahamishe kuhusu baraka za hewa.  Je, huoni wakati inapoacha kuvuma kuna udhia ukaribiao msongo wa roho?  Watu wenye afya kamili huanza kuugua wanaoumwa hudhoofika, matunda huharibika, mboga mboga huoza, maumbo ya mwili huambukizwa na nafaka huozeshwa?  Hii huonyesha kwamba kuvuma kwa hewa ni kwa faida ya uumbaji wa mpango wa Mwenye Nguvu zote Mwenye Kujua yote.

Tabia (sifa) nyingine ya hewa imeelezwa hapa.  Sauti hufanyizwa kwa mgongano wa vitu, kimoja juu ya kingine.  Inapeperushwa na hewa mpaka kuyafikia masikio.  Watu wote huendelea kuongea sehemu ya kipindi cha usiku au cha mchana kuhusiana na mahitaji ya shughuli za kila siku.  Kama hutuba hii ingeacha alama yake katika hewa kama ambavyo maandishi yaachavyo chapa kwenye karatasi, anga yote iizunguukayo dunia ingejazwa kwayo, na kufuatia mashaka na fadhaa.  Wangehitaji badiliko katika  anga - hewa.  Hoja kwa ajili hii ingekuwa kubwa zaidi kuliko ile ya badiliko la karatasi, kwa kiasi kwamba hutuba ya kuongea imependekezwa zaidi kuliko maelezo ya kuandikwa.

Mwenye Nguvu zote Muumba, Utukufu ni wake, ameumba njia hii ya ajabu, ambayo huhifadhi fikira (chapa) kwa muda utoshao tu kuhudumia mahitaji ya watu wa dunia na hufanya hali nzuri itengenezwe kwa fikira mpya kupatikana nayo, ambayo ungesababisha mgongano kwayo.

Kupata fundisho kutokana na baraka za upepo uliopoa uitwao hewa ni lenye kukutosha.  Hii hewa ni msingi wa uhai kwa maumbo yenye miili.  Husaidia kupata uhai wakati tunaivuta ndani kutoka  mahali pasipoeleweka na kuiruhusu na kuhusikana na roho ndani ya mwili.  Hewa hii hii ni njia au chombo kwa kupeleka mawasiliano katika mfumo wa mawimbi ya sauti kwenda sehemu za mbali.  Hewa hii hii huchukua harufu nzuri kutoka sehemu hadi sehemu.  Hebu angalia vipi hewa hupeperusha aina mbalimbali za manukato kwenye pua yako.  Na vilevile sauti.  Hewa hii hii ni chombo cha kuchukulia joto na baridi, ambavyo hupishana kimipango kwa faida ya ulimwengu.

Hewa inayovuma ni upepo ambao huondoa maradhi mengi ya mwili.  Huhamisha mawingu kutoka mahali fulani mpaka mahali pengine kwa faida ya jumla kwa njia ya kuganda mvuke na kuleta mvua.  Kisha huyakaza na yanatawanyika mbali.  Husababisha mimea kutoa maua na matunda.  Hufanya milo laini matunda kuwa na maji mengi.  Hupoza maji kuwa baridi.  (Hewa) Inawasha mioto na kukausha unyevunyevu.  Kwa ufupi, husaidia na kuhuisha vitu vyote vya ardhini.  Bila kuvuma huku kwa hewa (upepo) mboga mboga zingekauka, uhai wa wanyama ungetoweka na kila kitu kingepotea.

 

 

ARDHI

 

Fikiria vitu vinne vilivyopo vya asili vilivyoumbwa na Mwenye Nguvu zote Allah kukamilisha dhumuni la kuumbwa kwao kiutoshelezaji.  Miongoni mwao ni ardhi na eneo lake.  Je, ingetosheleza vipi kwa mahitaji ya mwanadamu kuhusu ujenzi wa nyumba, kilimo, mashamba ya majani, misitu, vichaka, miti shamba (kwa kutengenezewa dawa) na madini ya thamani, kama isingekua kubwa mno?

Mtu asingependezwa na angelaumu kuhusu nyanda zisizo na miti na sehemu zenye kutisha zisizokalika na kuhoji utumikaji wake.  Hizi ni sehemu za kuishi wanyama pori, (ni) makazi yao na mbuga za kujilishia.

Watu wana eneo kubwa mno la kuhamia kama wakihitajia kufanya hivyo.  Sehemu nyingi za uwanda zisizokalika zimegeuzwa kuwa bustani za matunda na majumba makubwa kwa kuyafanya makazi ya kudumu ya wanadamu.  Kama ardhi isingekuwa kubwa kno, watu wenweye wangejiona (wangejikuta), kama waliojengewa ukuta ndani kwa ngome nyembamba, kwani wasingeweza kutoka kwenye nyumba zao hata kama wangeshinikizwa na hali ngumu.

Tena, fikiria silika iliyopewa ardhi nayo ni kwamba imewekwa sawa vizuri mno ili kutolekeza kuwa makazi yenye kufaa kwa viumbe vyote.  Mtu amewezeshwa humo kutembea huku na huko, apate pumziko na wasaa (faraja) ajihusishe katika kilimo na biashara kwa uthabiti halisi.  Kama ingeelekezwa katika muinamo ingekuwa vigumu kusimamisha majengo na kufanya biashara na kazi n.k. chini ya hali hizi za matetemeko ya mara kwa mara, maisha yao yangekuwa mbali mno na yale ya kupendeza. 

Hebu yaelewe haya kutokana na matetemeko ya ardhi ambayo hudumu kwa muda tu na bado watu wanaopatwa nayo huyakimbia makazi yao.  Wangepataje basi pumziko na wasaa kama hali ya ardhi ingekuwa ya tetemeko wakati wote?

Kama mkinzani akiuliza kwamba ni kwa nini tetemeko la ardhi hutokea, atajibiwa kwamba tetemeko la ardhi na misiba mingine kama hiyo iko katika asili ya ilani na maonyo kwa watu kuchukua hadhari dhidi ya matendo maovu.  Kadhalika matatizo ya misiba ambayo huipata miili yao na mali zao yana dhumuni lilelile kimaoni, wawe tayari kufanya matengenezo yao na uboreshaji.  Kama wakiwa wema, malipo watakayopata akhera yatazidi thamani ya vitu vyote vya kidunia.  Hutokea wakati mwingine kwamba kuna malipo yapatikanayo hapa hapa katika ulimwengu huu, kama malipo hayo ni yenye faida katika ujumla wa watu.

Ardhi katika asili yake ni baridi na kavu, hayo ndivyo yalivyo mawe.  Je, unaweza kuona kwamba kama ardhi ingepewa asili ya ukavu zaidi kidogo kuwa ngumu kama jiwe ingeweza kuzalisha mimea yoyote ambayo kwama ni tegemeo la uhai wa wanyama? 

Je, kilimo cha aina yoyote kingewezekana au aina yoyote ya ujenzi kuwezekana? 

Je, huoni kwamba inakushikana shikana kidogo zaidi kuliko jiwe?  Mgeuko wa ulaini kutokana na asili yake ni kwa ajili ya kutegemewa.

Sura nyingine ya asili ya ardhi kama ilivyoamriwa na Mwenye Nguvu zote Allah; Utukufu ni Enzi Yake Kuu, ni mwinamo wake wa kidogo kidogo kutoka kaskazini kuelekea kusini.  Kwa nini Mwenye Nguvu zote Allah, Utukufu uwe kwake, ameiamuru hivyo?  Hakika ni kwa kuruhusu ziada ya maji baada ya kuinywesha nchi yatiririkie baharini, kama vile paa (la nyumba) limefanywa kuinama kutoka upande mmoja kuelekea mwingine kuzuia maji kujikusanya na kuruhusu upitaji wake kuwa rahisi.  Nchi imefanywa kuinama kwa sababu hiyo. 

Kama isingekuwa hivyo, ardhi yote ingejazwa na maji yaliyosimama na kutokea kuzuiwa katika biashara na mawasiliano ya  barabarani.

 

 

HEWA

 

Kadhalika, kama hewa isingepatikana kwa wingi mno, watu wangesongwa roho kwa sababu ya moshi na mvuke kuisongasonga.  Kama anga isingekuwa kubwa mno, isingefanya kazi kama kijumbe kwa ajili ya mwanga na mawingu mazito, ambayo sasa yanajikusanya kidogo kidogo kwa kufyonza maji.  Maelezo ya hii hewa yamekwisha tolewa ambayo yanapasa kutosha.

 

 

MOTO

 

Na hiyo ndiyo hali ya moto.  Ungekuwa mwingi kama maji na hewa, ungeteketeza kila kitu katika ulimwengu, bila kuacha njia yoyote ya kuanzisha kudhibitiwa kwa moto huo, kwani, ni wenye faida kwa mtu kama ilivyo kazi.

Kwa namna hiyo umetunzwa kwenye kuni.  Unaweza kutumika wakati inapotokea haja.  Umehifadhiwa kwa njia ya kuni.  Hauruhusiwi kuzimishwa wote kabisa bali baadhi yake unahifadhiwa.  Kwa namna hiyo huuhitajiki kuweka bila kikomo kwani kufanya hivyo kungeleta usumbufu sana.  Wala si wa kutawanyika sana kufanya uteketeze kila kitu katika ujirani wake.  Imeumbwa tu katika kipimo sawa huepusha upungufu.

Una sifa nyingine, kuridhia, umekusudiwa kwa faida ya wanadamu tu.  Wanyama hawana haja nao.  Uchumi wa wanadamu ungeridhika vikubwa katika kukosekana kwa moto.  Ama kwa wanyama wa miguu minne wao hawana matumizi nao.

Kama Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.) alivyoamuru matumizi yake (huo moto) yawe kwa ajili ya wanadamu peke yao mtu amejaaliwa kuwa na viganja na vidole ili kwamba aweze kuuwasha na atumie, wakati ambapo wanyama hawakutunukiwa na viungo hivyo.  Hana hivyo, wamewezeshwa kuvumilia kwa utulivu kutokana na usumbufu wa ushari wa tumbo na kuwaokoa kutokana na matatizo ambayo mtu atayapata kwa kukosekana moto.

Ngoja nikuambie sifa ndogo ya moto, ambayo ni bora sana na ya kufaa, kukuelewesha, ni taa hii ambayo watu huiwasha kupata mahitaji maalum ya usiku kama watakavyo.  Bila huo  maisha ya wanadamu, yangefananishwa na kuzikwa kaburini.  Angewezaje mtu kusoma, kuandika, kufuma, kushona kwa mashine au kushona kwa mkono katika giza la usiku?  Nini ingekua taabu ya mtu anayeumwa kutokana na maumivu ya ugonywa akihitajia kutaka kuweka dawa ya kusugua au kunyunyizia daw ya uvumbi kama uganga uponyao?

 

 

MAJI

 

Kama maji haya yasingekuwa mengi mno yakitiririka kutoka kwenye chemchem, mabonde na mifereji, yangesababisha udhia mkubwa mno kwa watu, ambao huyahitajia wenyewe, kunywesha wanyama wao wa miguu minne na hayawani, kwa kilimo chao, mimea yao na mashamba yao ya nafaka.  Na wakati huo huo wanyama wakali, ndege na hayawani au samaki na viumbe hai vyenye asili ya nchi kavu na majini vinavyoishi majini vingeumia kiasi kikubwa mno.

Mbali na hayo, yana faida nyingine ambazo una habari nazo, lakini thamani kubwa sana na sifa kwayo wewe huzijui.  Kisha hebu ona, mbali na faida za jumla na zenye thamani zilizomo kwayo, kukubali ukweli, uhai wote wa hayawani na mimea katika uso wote wa ardhi una asili katika maji, yanatumika katika taratibu nyingine za vinywaji kuvifanya mororo kwa ladha ya kupendeza.  Hutumika kuondoa uchafu mwilini hali kadhalika na kufulia nguo.  Udongo huloweshwa kwayo kuufanya ufae kwa kutengezea vyombo vya nyumbani n.k. yanatumika kuzimishia moto kama utawaka kusababisha madhara.  Mtu hupata kuburudika baada ya uchovu na utumishi.  Vili vile kuna vitu vingine vihudumiwavyo na maji, ubora mkubwa na thamani iliyomo humo huweza kujulikana tu wakati wa kuhitajika.

Pamoja na kuhusu haya yote, unatia shaka juu ya thamani ya wingi huu wa maji  yatiririkayo katika mito na bahari, basi elewa kwamba maji haya haya ni makazi ya uhai kwa jamii nyingi ya wanyama waishio majini na samaki.  Hii ni nyumba ya hazina ya lulu, rubi, mawe njano na vitu aina mbalimbali ya vito vya thamani ambavyo hutolewa kutoka katika mito na bahari. Sehemu zinazozunguuka hifadhi za maji hukutwa kukiwa na harufu nzuri za "aloes".  Miti pamoja na harufu nzuri ya vitu vya rangi rangi na miti shamba (itengenezwayo dawa).

Zaidi ya hayo, ni njia ya usafirishaji.  Ni njia itumikayo kwa kubadilishana biashara kati ya nchi za mbali kutoka kila nchi nyingine k.m. kutoka nchi ya Irak kwenda nchi ya Uchina na kinyume chake (toka Uchina kwenda Irak) na Irak yenyewe.  Biashara ingeharibika kwa kutokuwepo kwa njia hizi, mbali na hayo uchukuzi juu ya migongo ya wanyama na ya wanadamu na bidhaa za biashara vingebakia kwenye nchi zalishaji na pia kubakia katika mikono ya walaji wenyeji.  Usafirishaji wao ungegharimu zaidi kuliko gharama zao za uzalishaji.  Hakuna mtu ambaye angethubutu kudiriki kuyasafirisha.

Hii ingepelekea kwenye upungufu wa aina mbili.  Vitu vingi vya (matumizi ya) lazima visingepatikana.  Wazia kwamba yichanganyiko vya matumizi ya dawa kuhitaji "henna" au "aloes" au matunda kama zambarau au baadhi ya dawa ya tiba au dawa ya lishe kutoka miji ya Asia au Ulaya, kama vingekuwa visafirishwe juu ya migongo tu bila njia ya mashua kupitia kwa kujitia kati ya bahari, vipi zingefika  Uhindini (India) na vipi Wahindi wangefaidika nazo.  Na kwa upande wa pili watu ambao sasa wanaendesha maisha yao kwa faida zipatikanazo kutokana na safari zao (za kibiiashara), wangepoteza tegemeo lao la kiuchumi.

Faida nyinginezo ni katika kupikia, kupashia mwili joto, juzikia vitu vya umajimaji na kuyeyushia vitu    vigumu n.k. ni nyingi mno kiasi kwamba haziwezi kuhesabika.  Ziko wazi kiasi kwamba haziwezi kuelezeka.

 

 

MVUA

 

Fikiria anga wakati ni nyeupe na wakati mvua inyeshapo.  Hupishana kwa faida ya ulimwengu.  Endeleo la hali moja yoyote kungesababisha machafuko (na matatizo).  Huoni kwamba inapoanza kunyesha mfululizo, mboga mboga na mimea huanza kuoza.  Miili ya hayawani hupata misukosuko. Anga - hewa huzidiwa na baridi na kufuatia maradhi, barabara na njia huharibika.  Wakati anga inapokuwa nyeupe kwa muda mrefu,  ardhi hukaushwa, mimea hunyauka.  Hapo mtu hupatwa na madhara kwayo.  Hewa hupata UKAVU na kufuatia magonjwa.

Wakati (hali)  zikipishana hivi kiutaratibu, hali ya hewa huwa sawasawa.  Kila moja kwa zamu yake hufidia upungufu wa (hali) nyingine.  Kila kitu huenda sawa.

Mkimzani angeuliza kwa nini haikuamriwa kwamba kusiwe na athari za madhara.  Jibu likakuwa kwamba hii ni hivyo ili kwamba mtu mara kwa mara asumbuliwe ili kumuepusha na kutenda maovu.  Mtu mgonjwa, kwa mfano, anapewa dawa chungu na isiyopendeza ili kumponya.  Kadhalika wakati mtu mwenyewe hujichukulia katika makuu na kiburi huhitaji kupewa kitu ambacho kitamsumbua ili kumkinga kutokana na hasara na madhara yaletwayo makusudi na muhuweka juu ya ukarimu na utengeneko mzuri.  Kama mfalme atawafanyia ukarimu watu wake, je, ukarimu wake huu hautavuta akili zao kwa heshima yake na mshangao?  Wakati ambapo ukifikiria ni mfananisho gani walio nao yale mamilioni na mvua ambayo ni chanzo cha upatikanaji wa chakula na hali ya kustawi kwa sehemu zote za ulimwengu kwa unyweshaji wake wa mashamba ya nafaka.

Huoni, baraka kubwa iliyoje ya mvua hii ndogo kwa wanadamu?  Bado watu ni wenye kuzembea kwayo.  Mara nyingi wakati kiasi cha haja  ndogo ya mtu kikizuiliwa, huanza kunung'unika na kufanya ufadhuli.  Hupendelea zaidi haja yake ndogo kuliko zile faida kubwa zenye matokeo mazuri.  Hii ni kwasababu ameshindwa kuthamini kuikamilifu sifa za fadhila hii bora.  Fikiria ustadi uliomo ndani ya myua ilinyesha na kumwagikia chini kutoka juu (na) kunywesha kila mahali na uwanda wa juu pia.  Kama ingekuwa ije kutoka kwa pembeni, ingeziwacha nyanda za juu zimenywesheka, (lakini) bila kuwepo eneo la kilimo.  Nchi zenye unywesheaji wa mifereji (ambao siyo kwa njia za asili) ni pungufu kwa eneo.

Maji ya mvua huienea ardhi yote.  Mara nyingi kilimo kinaweza kikaendeshwa katika sehemu kubwa ya majangwa na maeneo ya milimani na kutokea kupatikana wingi wa nafaka.

Watu wanaepushiwa taabu ya kuchukua maji kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine.  Mashambulizi mengi ya kikabila huibuka kutokana na umilikaji wa sehemu zenye maji ukifanywa na Mfalme mmoja na kulinyima kundi dhaifu.  Matukio kama hayo vile vile huzuiliwa.

Basi kwa kuwa iliamriwa, imepangwa hivyo ili kufanya hazi kama marasha rasha juu ya ardhi kuifanya ilowane na kuinywesha.  Kama ingekuja na wepesi wa haraka kama mafuriko, isingenywea ndani.  Katika hali ya mfuriko (mafuriko) ingeng'oa nafaka zote zilizosimama.  Kwa hiyo, basi imeamriwa kunyesha katika manyunyu mepesi, ili kuziwezesha mbegu kuchipua, nchi iweze kunywesheka na mimea iliyosimama ipate kustawishwa.

Kuna baraka nyingine katika unyweshaji huu.  Hutuliza miili, huisafisha anga, kuiondolea uvundo uliosababishwa na usimamaji  wa maji.  Mimea ya bustani huponywa ugonjwa na njano na kadhalika.

Kama mkinzani atasema, iwapo mvua nyakati nyingine husababisha hasara kubwa kwa uwingi wake au katika hali ya mvua za mawe, husababisha nafaka kuteketea na anga kupata unyevunyevu mwingi usiofaa kwa afya na hatimae kutokea magonjwa na matatizo.

Jibu litakuwa kwamba hasara hii pia wakati mwingine inakusudiwa kwa kumboresha mtu (na) kumkinga (au kumzuilia) kutokana na kujitumbukiza katika kuvuka mipaka ya Allah (s.w.t.).

Faida ambayo atakuja ipata katika uboreshaji wa imani yake itapita hasara aliyoipata katika mali zake za kilimwengu (alizomiliki).

Tizama kwenye milima hii iliyofanyizwa kwa udongo na mawe, ambayo mtu asiyojua hufikiri kama isiyo na maana na isiyo na umuhimu wowote.  Hufanya umbo lenye manufaa yenye kuonekana.  Miongoni mwao ni theluji ambayo huanguka na kubakia juu ya vilele vyao.  Yeyote yule anaweza kunufaika nayo, wakati ikiyeyuka hufanya chanzo cha chemchem za kububujika maji na vijito vya ajabu.  Hutoa mitishamba (ya dawa) na mimea ambayo haiwezi kukua sehemu tambarare na katika nyanda za chini.  Ina matundu na mapango kwa ajili ya hayawani wanyama wakali wawindao.  Hutumika kwa jinsi zilivyo ngome za muundo wa hali ya juu kiujenzi kama vituo vya ulinzi.  Huweza kuchangwa na kufanywa makazi.  Inakatwa na kufanywa vijaa.  Ina madini ya mawe ya thamani ya rangi rangi namna mbalimbali.

Mbali na haya, ina sifa nyingine, ambazo Yeye Pekee Ambaye ameiumba katika vipimo halisi, hujua kwa Elimu Yake ya asili ya umilele wote.

Fikiria aina mbambali za madini ambazo huchimbwa kwenye migodi kwa mfano, chkaa, chokaa malighafi (lime) itengenezwayo Saruji na chokaa (mortar), jipsa (gypsum), sumu mrututu (sulphurate of carsenicum), risasi (lead oxide), zebaki (mercury), shaba (copper), bati (tin), fedha (silver), dhahabu (gold), kito cha kijani (beryl), kito cha kundu (ruby), kito nyekundu (garmet) na aina mbambali  za mawe na kadhalika vikitokezea kupatikana lami (tar), mafuta mgando (vaseline), mrututu (Sulphur), mafuta ya taa (kerosene) hutumiwa na watu.

Je, basi hili ni fumbo kwa kiumbe mwenye akili kwamba hazina zote hizi zimewekwa kwa matumizi ya mtu ambazo anaweza kuzichimbua kama na wakati akizihitaji?

Watu hata hivyo, ni wenye tamaa na wanataka vitu vyenye thamani ndogo kuwa dhahabu na fedha.  Wanafanya juhudi kubwa katika upande huo lakini zaidi sana bila mafanikio.  Mipango yao haitoi faida.  Kama watu hawa wangefanikiwa katika kutafuta kwao elimu, ingekuwa elimu ya kawaida.  Dhahabu na fedha zingechimbuliwa kwa wingi mno kwamba zingepoteza thamani yao mbele ya macho ya watu.  Manufao yaliyopatikana kutokana na shughuli za madini na biashara yangepotea na si wafalme wala mtu yeyote yule angeweka bohari za mali hizo.

Walakini, watu walipewa elimu ya (kuwawezesha) kuibadilisha shaba kuwa shaba bandia na kuwa kioo, bati kuwa fedha na fedha kuwa dhahabu, ambayo haifanyi madhara sana.  Hebu tizama uone kwamba elimu ilitolewa mahali ambapo ikitumika haileti madhara sana, ambapo kwamba ile ambayo ni ya kudhuru imezuiwa.

Na wakati mtu akiingia kwenye mgodi anaweza akakuta ndani yake vijito visivyotambulika vya maji yatiririkayo na mawe yenye rangi ya kifedha.

Fikiria Usanii uliomo katika hili la Mwenye Nguvu zote Mwenye  Kujua yote.  Yeye (s.w.t.) anataka kuwapa watu wazo la kujua uwingi wa hazina zake na ukubwa wa Enzi Yake Kuu ili waelewe kwamba kama Yeye (s.w.t.) Akipenda, Yeye (s.w.t.) anaweza kutupa susu fedha uwingi na ukubwa wa viwango sawa na milima.  Yeye (s.w.t.) anaweza kufanya hilo, hata hivyo, kungekuwa na kipato kidogo kwa sababu uwingi wa johari ungepunguza thamani yao, kama ilivyoelezwa kabla.  Wachache wangenufaika kwayo.

Kuielezea kwa mfano, fikiria mtu amegundua kitu kipya, kwa mfano, vyombo au vitu vingine vya matumizi.  Ni vyenye ubora, vikubwa na vyenye thamani maadamu tu vipatikane kwa uchache na adimu.  Na wakati vitu hivyo vitazidi hitajio na kufidia kila mfuko (kila mtu) hupunguka katika thamani na huwa visivyo na maana.  Kila kitu hufikiriwa kuwa kizuri pale tu kinapokuwa adimu.

 

 

MIMEA

 

Fikiria mimea na mahitaji mbalimbali inayotimiza.  Tunda hutumika katika lishe, majani makavu kama chakula kwa wanyama, kuti kama nishati, mbao hutumika kwa (kazi ya) useremala wa kila aina.  Kuna faida mbalimbali zipatikanazo kutokana na maganda yao, majani, mizizi mikubwa na midogo na gundi.

Fikiria matunda tunayotumia kwa lishe yetu.  Kama yangekuwa yanapatikana sehemu moja badala ya kuwa yamening'inizwa kwenye matawi ambayo huyazaa, mchafuko ulioje wa mpango ungesababishwa katika maisha yetu! 

Lishe ingepatikana bila shaka yoyote, lakini vipi kuhusu manufaa yenye thamani tuyapatayo kutoka mbao za miti, majani makavu na sehemu nyingine tulizozitaja.

Zaidi ya hayo, furaha ambayo huletwa na uzuri wa kimandhari na hewa safi ya mimea kiulinganifu ni bora zaidi kwa  anasa na furaha za ulimwengu wote.

 

 

NAFAKA

 

Hebu fikiria jinsi kilimo kilivyoamriwa kustawi.  Mia au zaidi ya nafaka zinatoka kwenye mbegu moja.  Nafaka moja kutoka kwenye mbegu moja kungekuwa na mantiki.  Kwa nini basi kuongezeka huku?  Hakika ni kuizidisha nafaka ili kwamba hiyo hiyo isaidie kwa chakula kufikia vuno lingine mbali na uwekaji wa nyingine kama mbegu kwa wakulima.

Fikiria Mfalme akusudiaye kuujaza mji na watu.  Hupanga kutoa kiasi kikubwa cha nafaka ambacho kitatoshelezea wakazi kuwasaidia kwa chakula mpaka mavuno yajayo mbali na kuweka nyingine kwa ajili ya mbegu.  Angalia jinsi mpango huu unavyosimamiwa katika taratibu za Mwenye Nguvu zote Allah Utukufu uwe kwake, kwamba kilimo kingepelekea kwenye ongezeko kubwa sana kama hili ili kuhudumia vyote viwili, hitajio la lishe na vile vile kwa lile la mbegu.

Ni sawasawa hali hiyo katika miti, mimea na mtende.  Huzaa matunda mengi mno.  Unaona kwamba kuna mzizi mmoja, lakini kuna machipukizi mengi.  Kwa nini? 

Hakika kwa ajili ya dhumuni la kuzalisha zaidi kizazi kutokana na mbegu, baada ya watu kuziweka kwa matumizi yao.  Kama kungekuwa na mzizi mmoja bila ya matawi kuchipua kwa wingi hivyo, isingeyamkinika kuchukua chochote kutoka kwenye mimea kwa kupanda au kwa shughuli yoyote nyingine.  Katika hali ya kutokea maafa ya ghafla mimea ya asili ingetoweka bila ya kuwepo  uwezekano wa mmea mwingine kuchukua nafasi yake.

Fikiria nafaka za kunde, choroko, dengu na maharage.  Zote hukua kwenye maganda kama hifadhi ya madhara, mpaka zinapokomaa kwenye ugumu, kama vile kondo la nyuma.  Nafaka za ngano na nafaka nyingine kama hizo zimepangwa tabaka kwa tabaka katika maganda magumu, zikiwa na ncha kali kwenye miishilizo yao kama mikuki kuwazuia ndege na kuongeza mazao kwa wakulima.

Kama mkinzani akiuliza iwapo ndege hawapati kitu katika nafaka za ngano n.k. jibu kwake litakuwa kwamba hapana shaka wanazipata nafaka na imeamriwa hivyo kwao, kwa kuwa ndege nao vilevile ni katika viumbe vya Mwenye Nguvu zote Allah.  Yeye (s.w.t.) Amewaamria sehemu ya mazao ya ardhi.  Nafaka hizi zimehifadhiwa katika mifuniko wasije wakapata kumiliki nafaka yote kupelekea kwenye hasara ya dhahiri kwa upotezaji ulio tukutu. 

Katika kukosekana kwa hifadhi kama hii ndege wangeruka juu ya nafaka na kufanya kazi nyepesi (na ndogo) ya wao wote.  Wangeumia kutokana na uyeyushaji dhaifu wa chakula katika tokea jingine, kwa dhahiri ya madhara yao, Wakulima vile vile, wangekuwa wenye hasara.  Mifuniko hii ya hifadhi kwa hiyo, imetokea kupewa ili kwamba ndege wapate kiasi chao cha kuwatosha tuu kwa chakula, wakiacha sehemu kubwa kwa matumizi ya wanadamu.  Wanayo haki kubwa zaidi kwayo kwa sababu ya kazi iliyofanywa na wao, na hitaji lao la nafaka ni kubwa kuliko lile la ndege.

 

 

UZAO WA MIMEA

 

FIkiria uzao wa mimea na jamii mbalimbali za miti.  Huhitaji lishe sawa kama wanyama.  Hata hivyo haina vinywa vya kujilishia, wala haiwezi kwenda huku na huko kutafuta chakula chao. Kwa hiyo, imetnikiwa mizizi chini ya ardhi, kupokea lishe yao kwa upelekaji kwenye matawi yao, majani na matunda. 

Ardhi huihudumia kama mama ambamo kutoka humo inanyonya lishe yao kupitia mizizi yao ambayo huitumikia (kikazi) kama vinywa kuipatia chakula chao.  Kama vile watoto wadogo wa wanyama hujilisha kwa maziwa kutoka matiti ya mama zao. Je, huoni hizi mambo zilivyohimilishwa wima bila hofu au kuanguka au kuinamisha mahema na kutiwa ngvu kwa njia ya kamba zilizfungwa imara? 

Kadhalika, utauona kila mmea umesimikwa katika ardhi kwa mizizi iliyosambaa kila upande kuupa nguvu. Vipi miti mikubwa ya mitende yote ingesimama imara dhidi ya dhoruba?

Angalia! Ustadi wa uumbaji ulivyo tangulia mbele umahiri wa utendaji kazi.  Umahiri uliotumika katika kusimamisha mahema na kutiwa nguvu na mafundi, ulitumika nyuma kabla katika usanifishaji wa mpango wa usimikaji miti ambao hutangulia uhitaji wa mahema kwa mambo na nguzo vyote vikiwa vimepatikana kutokana na miti. 

Ni wazi kwamba umahiri huu umeigizwa kutoka ustadi uliotumika katika kusimika miti.

 

 

MAJANI

 

Fikiria utokaji wa majani ya mimea kwa uangalifu na utaona yametanda katika misokoto yake kitu kifananacho na mfumo wa mizizi itambaayo sehemu zake zote za marefu na mapana.  Baadhi yao ina kapilari nyororo iliyounganishwa na iliyo minene, yote ina nguvu sana na mizuri.  Kama ingetayarishwa kwa mkono mtu asingeweza kuwa na uwezo wa kufanya kazi juu ya mti mmoja katika muda wa mwaka.  Angelihitaji ala (zana), nia, kielelezo na mafunzo katika kuifanya.

Katika siku chache za majira ya msimu wa demani majani mengi mno hujitokeza kiasi kwamba milima na maeneo ya mabonde ya ardhi hujazwa nayo bila ya neno kusemwa au kufanywa shughuli yoyote kama vile tu katika matokeo ya wangwa kuenea vitu vyote - ruhusa ya mgawo mmoja usiodhuru.

Elewa, tena, jambo la asili linalohusikana na kapilari nyororo.  Zimefumwa katika misokoto ya majani ili kuinyweshea kama vile kimia cha kapilari katika mwili kichukuavyo lishe kupeleka sehemu zote.  Kuna ustadi mwingine katika vena (chelewa) nene za majani.  Kwa sababu ya uwezo wao wa kujirudi haraka na nguvu, hushikilia kwa nguvu msokoto wa jani kuyakinga kutokana na kuchanika.  Majani haya ni sawa na majani bandia yanayo tengenezwa kutokana na nguo na ambayo yametengenezwa kwa marefu na mapana na kushikishwa kwa nguvu dhidi ya uchakavu.  Kwa hiyo majani bandia yafanywayo kwa mkono hufuata yale ya asili, ingawa kamwe hayawezi kuweka uhai wa kweli.

 

 

MBEGU

 

Fikiria kokwa ya mbegu iliyochimbiwa ndani ya tunda, ambayo itawezesha kuzalisha nyingine iwapo mti utapotea kwa ajili ya baadhi ya majangwa.  Ni zao zuri tu la matumizi ya kudumu, linahifadhiwa katika sehemu witri liweze kupatikana katika sehemu nyingine kama hii ikipata ajali katika sehemu moja.  Kisha kwa sababu ya kurudi upesi kwenye hali zao za kawaida (baada ya kunyofolewa) na ugumu huzuia tunda kuwa laini sana na utovu mwingi.  Bali bila kokwa hizi matunda yangepasuka na kuwezesha udhaifu.

Baadhi ya kokwa zinalika na mafuta hukamuliwa kutoka nyinginezo kwa matumizi katika kazi tofauti.  Na kwa kuwa umejifunza dhumuni lifanywalo na kokowa, yakupasa ufikirie nyama ya tunda iliyofungika ndani ya mbegu ya tende na ile inayozunguuka kokwa ya zabibu, ubora kwayo na sababu gani ya umbo lake, ambapo kwamba ilikuwa inawezekana kutoa/kuzalisha badala ambayo isingekuwa ya kulika kama vile miti ya "cypress" na miti (mingine) maarufu.  Hakika ni hivyo kwamba mtu akute lishe tamu, afurahi.

Fikiria sifa, nyingine za mimea.  Utaona kwamba inaathiriwa na majira ya msimu wa masika, hivyo kwamba joto lao muhimu huhifadhiwa katika vitawi vyao, na malighafi kwa uzalishaji wa tunda hutengenezwa.  Majira ya msimu wa demani huivalisha majani na kupata aina zote za matunda, kama vile unavyopanga aina mbalimbali za vyakula vitamu mbele yako ambavyo vimepikwa kwa zamu. 

Hebu ona vitawi vitoavyo matunda yao kwako kwa mikono yao.

Na unayatazama kwa furaha maua ambayo yanakuja mbele yako juu ya vikonyo vyao kama kwamba vinajiwakilisha vyeme kwako?  

Nani amepanga hivi?  Hakika ni Yeye Ambaye ni Mwenye kujua yote Mwenye Kuamuru. Na ni dhumuni gani linakusudiwa kwayo?

Hakika, ni kwamba mtu afurahie matunda na maua.  Ajabu ilioje, kwamba badala ya shukurani kwa baraka hizi, watu humkana Mtoaji moja kwa moja.

 

 

KOMAMANGA

 

Hebu fikiria Komamanga na umahiri na ustadi ambao umetumika katika uzalishaji wake.  Utaona, ndani yake lote ni duara na madoido ya nafaka zilizowekwa tabaka juu ya tabaka, kama vile zimepangwa kwa mkono.  Nafaka  hizi zimegawanywa kwenye sehemu tofauti na kila sehemu imefunikwa katika kitani, zimefanyizwa katika hali iliiyo bora sana ya kipekee.  Zote hizi zimezunguukwa na ganda la nje.

Ustadi wa Kisanii uliomo humo ni kwamba kwa kuwa nafaka haziwezi kusaidiana kila moja katika ukuaji wa nyama ya tunda, utando umewekwa ndani ya Komamanga ya kulisha katika huo, unaona zote nafaka na nyama ya tunda zimetiwa ndani sana na kukazwa imara. Tando hizi husaidia kuziweka mahali pamoja zisizosogezeka.  Juu ya yote haya, mfunika wenye nguvu umewekwa kuziweka salama kutokana na madhara ya nje.

Hizi ni nukta chache kuhusu Komamanga, ambalo yoyote ambaye hupenda maelezo zaidi (kwa urefu) anaweza kuongeza mengi zaidi.  Maelezo yaliyotolewa hapa ni, hata hivyo, yenye kutosha kwa dhumuni la hoja na funzo.

 

 

MIMEA ITAMBAAYO

 

Hebu ona mtambaazi huu mnyonge (dhaifu).  Mitambaazi hii hutoa nje (huzaa) mamung'unya makubwa mno, matango na mitikiti -maji.  Ustadi ulioje umeendelea katika Usanii wake! Kwa kuwa imeamriwa kwamba itazaa matunda makubwa mno, mmea huu umesanifiwa utambae juu ya ardhi.  Ingekuwa kama mimea mingine isimamayo wima, usingeweza kuhimili mavumo yakushangaza ungevunjika na kuanguka chini kabla (ya mazao yake) hayajawa.  Angalia jinsi unavyojitandaza (na kuenea) juu ya udongo kuweka uzito wa mazao yake juu ya ardhi.  Pengine ungeweza kuona kwamba mizizi ya mitambazi mmung'unya na tikiti-maji husambaa katika ardhi na mazao yake (matunda) yakilala juu ya ardhi pande zote, kama vile paka alalae chini akinyonyesha watoto wake (maziwa) - matunda.

Fikiria ukweli kwamba mitambaazi hii hukua tu katika majira maalum ya misimu iliyowekwa kuifaa (mimea hii) katika joto kali la Kiangazi, kwa mfano, wakati watu huikaribisha kwa furaha.  Kama ingestawi katika kipupwe, watu wasingevumilia kuonekana kwao.  Kwa nyongeza inaweza kusababisha maradhi wakati wa kipupwe.

Hutokea wakati mwingine kwamba matango yanazaliwa katika kipupwe.  Watu kwa ujumla huyaepuka, isipokuwa walafi  pamoja na hisia ya madhara na magonjwa.

 

 

MTENDE

 

Fikiria mitende.  Kuna miti ya Kike miongoni mwao.  Kwa uzazi wao miti ya kiume huzaliwa pia, ambayo huzalisha bila ya kupangwa kilimo cha bustani.  (Miti) dume, kama yale (madume) ya wanyama, huzalisha, lakini yenyewe ni gumba.

Fikiria kiuangalifu shina la mtende.  Utaona kwamba limefumwa kama utando, ingawa hakuna nyuzi ndefu.  Liko kama vile kipande cha nguo kimefumwa na mkono kulifanya kuwa na nguvu na kunyooka kuweza kustahamili pepo zenye nguvu na ubebaji wa vichala vikubwa vya matunda, katika kukomaa, na kisha mwishowe kutumika kwa kupauliwa na madaraja.  Utaona ndani yake nyuzi zimesokotwa kwa marefu na mapana. Liko imara vya kutosha kutumika katika utengenezaji wa ala (zana). 

Kama lingekuwa gumu kama jiwe, lisingetumika katika majengo kama mbao, kwa mfano, milango kazi ya kimia, mbao za miti na makasha n.k.

MBAO

 

Kuna sifa moja kubwa katika mbao.  Inaelea juu ya maji.  Kila mtu anaijua hii lakini hatambui thamani yake kwa ukamilifu. 

Kutokuwepo kwa tabia hii, vipi mashua zingetengenezwa, ambazo hubeba milima ya bidhaa za biashara kutoka mji kwenda mji kwa juhudi kubwa?  Shida zilioje ambazo zingekuwa zistahimiliwe katika kusafirisha bidhaa za biashara? 

Vitu vingi vya matumizi vingetoweka sokoni au vingepatikana kwa bei ya aghali sana.

 

 

MITI SHAMBA

 

Fikiria hii miti shamba na tabia ambazo kila mmoja amejaaliwa nazo kama madawa.  Hupenyeza chini kwenye viungio, huteketeza takataka na jauhari za sumu kutoka humo, kwa mfano, ugonjwa uitwao, Shahtra, baadhi ya mitie mingine hutuliza ulegevu wa moyo, kwa mfano mti wenye dawa iitwayo "ateemoon", baadhi ya mingine huondoa riahi, kwa mfano siki, baadhi ya mingine hutuliza uvimbe, kwa mfano zabibu pori na kadhalika kwa ufanisi wao.

Nani basi ameijaalia kuwa na sifa kama hizi?  Hakika Yeye Ambaye ameiumba na dhumuni. Nani amewapa watu elimu kwayo?  Hakika Yeye ambaye ameyajaalia madawa haya na hali kama hizi.  Vipi mambo haya yangefika kwenye fahamu za mwanadamu kwa bahati na yenyewe tu kama wale waaminio mambo ya bahati nasibu wanavyodai?

Haya, hebu natukubali kwama mtu amejifunza yote haya kutokana na akili yake na hoja, taamuli na majaribio ya kimaabara.  Lakini ni nani amewafundisha wanyama? 

Baadhi ya hayawani, wanapojeruhiwa (na kuumia), hutumia miti shamba kujiponyeshea, na baadhi ya ndege wakiumwa kutokana na kufunga choo hupata afueni kwa kuharisha kwa kutumia maji ya bahari na kadhalika?

Unaweza, pengine, kutia shaka manufao/faida ya uhai wa mimea au faida za nchi zilizoachwa (vihameni) na za tambarare ambako  hakuna uhai wa binadamu upatikanao na kuufikiria kuwa wote ni bure na hauna maana.  Sivyo hivyo vilivyo.  Wanyama pori hujilisha kwayo na nafaka yao inatumiwa na ndege kwa chakula.  Vitawi vyao na kuni hutumiwa na watu kama nishati.

Kuna nukta nyingine vile vile zenye faida kuzijua.  Ina tumika kwa madawa ya kutibu (kuponya).  Ngozi hudubaiwa kwayo.  Nguo hutiwa rangi na kadhalika.  Inazo sifa nyinginezo pia.

 

 

VITU VISIVYO THAMANI

 

Je, hujui kwamba mti wa chini kabisa kwa daraja na uliodharauliwa ni (ule uitwao) "Khairya Baradi?"  Pia hiyo ina sifa mbalimbali.   Karatasi hutengenezwa kwayo kwa matumizi ya Wafalme na watu wa kawaida.  Hutengenezwa kuwa mikeka/busati kwa matumizi ya wote na vyote.  Hutumika katika kutengeneza vifniko vya kufunikia vyombo vya nyumbani vilivyotengenezwa kwa kioo n.k. ambavyo hujazwa nayo kuzuia kuvunjika.  Ina sifa nyingi nyinginezo kwa nyongeza ya hizi.

Kisha jifunze somo kutoka namna nyingi na faida ambazo hupatikana kutokana na viumbe vidogo na vikubwa kama vile pia kutoka vitu vile ambavyo havina thamani na vile ambavyo vina thamani.  Isiyo na thamani zaidi ya yote haya ni kinyesi cha ng'ombe na uchafu utokao mwilini ambao ni taka zisizo na thamani, na fikiria faida ambazo hupatikana kutokana nazo kwa kilimo na mboga.  Zina faida hivi kiasi kwamba hazina kifani.  Hakuna mboga mboga inayeweza kuwa na thamani isipokuwa iwe imewekewa mboji ambayo ni ya kuchukiza kiasi kwamba mtu haikaribii kwa kuona kinyaa.

Elewa hili nalo, kwamba thamani ya bidhaa haitegemei juu ya thamani ya pesa peke yake.  Ina thamani mbili tofauti katika masoko mawili tofauti.  Hutokea wakati mwingine kwamba bidhaa haina thamani katika soko la uchumi na bado bidhaa hiyo hiyo ina thamani katika soko la elimu.

Inaweza kuwa kwamba unaweza kufikiria kitu kwamba hakina faida kwa sababu ya thamani yake yu chini kifedha.  Hebu angalia ni thamani kubwa kiasi gani ingekuwa kwa uchafu wa wanadamu (kinyesi na mkojo) kama hali/sifa zake zingefahamika kwa mkemia.  Ni ukweli kwamba majaribio mahsusi ya kemia hayawezi kufanywa bila uchafu wa wanadamu."

Ilikuwa sasa ni wakati wa Sala za adhuhuri, na Imam (a.s.) aliniambia kuja siku ifuatayo (yaani kesho), Insha - Allah!

Nilirudi mwenye furaha kwa sababu ya maelezo niliyopata kutoka kwa Imam (a.s.).

Nilimshukuru Allah (s.w.t.) kwa maelezo yenye thamani niliyopokea.

Nilipitisha usiku kwa amani halisi.

 

 

 

 

 

 

 

Baraza La Nne Maafa Ya Kawaida

 

 

 

MAAFA YA KAWAIDA

 

Baada ya Sala za kawaida na kumshukuru Mwenye Nguvu zote Allah, Imam (a.s.) alisema, "Ewe Mufazzal! Nimekupa maelezo kwa kinaga hoja kwa kufafanua zaidi na uchunguzi kuhusu mpango halisi na Usanii kuhusiana na wanadamu, wanyama na ufalme wa mimea.  Inapasa itoshe kwa njia ya mafunzo kwa wote ambao wanatamani mwongozo.

Sasa nakupa maelezo kamili ya majanga na machafuko ambayo hutokea kwa nyakati na ambayo hawa watu wajinga husimamia kama hoja kwa ukano wao wa uumbaji na Usanii wenye dhumuni wa Muumba.

Nitaelezea vilevile kwa undani zaidi hekima iliyomo kwa kuletwa matatizo na machungu ambao walahidi na wafuasi wa dhehebu la Manichean wanakana na vile vile nitatoa maelezo kuhusu kifo na maangamizi ambayo madhehebu hizi wameyaleta kwenye mjadala, na wachunguzi wa zamani wa viumbe walivyosema.

 

 

MISIBA YA ASILI

 

Watu hao wamesema ulimwengu huu umejitokeza na kuwepo kwa bahati tupu, hivyo basi maelezo haya yatakuwa ni yenye kutupilia mbali hoja zao.  Allah (s.w.t.) awaangamize - kulioje kupotezwa kwao.  Baadhi ya watu wajinga wanatafsiri matukio haya ambayo hutokea wakati kwa wakati, kwa mfano milipuko ya maradhi ya kuambukiza, kutokuwepo kwa "Chlorophyll" (Klorofil) ya miti, mvua za mawe, nzige, kama hoja ya ukano wa dhumuni la uumbaji wa Muumba.

Jibu kwa hili ni kwamba kama hakuna Msanii wa ulimwengu huu, kwa nini hakuna machafuko makali zaidi, kama kwa mfano mvurugiko kamili wa ulimwengu wote, kupasuka kwa ardhi, ukomo wa kuchomoza jua, ukaukaji wa maji katika makalio ya mito ivyo kutoacha hata tone la maji kuweza kulowesha midomo, hewa kusimama tuli na kupelekea kwenye mvurungiko wa mpangilio wa mambo, kusambaa kwa maji ya bahari kwenye ardhi na kuizamisha.  Nani analinda matukio yote haya? Ni nani mpangaji wa mandhari hizi?

Wakati usemapo kwamba kama kungekuwa na Msanii na Muumba, Kundi kama hili la nzige lisingetufikia kusababisha madhara makubwa hivi, milipuko ya magonjwa haya ya kuambukiza yasingechukua kiwango kikubwa cha mamilioni ya maisha ya watu, mvua za mawe zisingekuwa kubwa na uzito hivyo hata mpaka kuharibu mashamba yetu ya nafaka.  Ikiwa yote haya ni katika hakika ya mambo, kwa nini ulimwengu huu usipate kuvurugika katika taratibu za uumbaji na kupelekea kwenye uangamizi wa ulimwengu wote?  Kwa nini bahari isizamishe ardhi kwa maji yabubujikayo?  Kwa nini hewa isisimame na kutulia tulii na hivyo kusongeka kwa viumbe hai vyote?  Kwa nini yote haya yasitokee?

Hii huonyesha kwamba Msanii yupo, ambaye huzuia tukio kama hilo ili kwamba ulimwengu usije chafuka na kuharibika wala jamii kuja kutoweka wala uharibifu kabisa wa jumla usitokee.  Kinachotokea ni kwa njia ya kawaida ya matokeo kutokana na matendo ya mtu mwenyewe, ni onyo la kujizuia na maovu yafanyikayo mara kwa mara katika hali ya milipuko ya magonjwa ya kuambukiza, nzige, kuangamia kwa nafaka na mashamba, mvua za mawe n.k.  Huu ni ukano wa hoja dhidi ya uumbaji wa kidhumuni.  Nawauliza kwa nini hii milipuko ya magonjwa ya kuambukiza na makundi ya nzige hayaendelei moja kwa moja hivyo ili kuungamiza ulimwengu?  Hufika mara chache, na baada ya muda, huondoka.

Je, huoni kwamba huu ulimwengu umehifadhiwa dhidi ya misiba hii ya kutisha na machafuko?  Kama mojawapo lolote katika matukio haya lingetokea katika ulimwengu huu, ungeharibika kabisa moja kwa moja.  Majanga haya hutukia mara chache, katika hali ya ukali uliopunguzwa ili tu kuwaonya watu na kuzirekebisha tabia zao kuwa nzuri.

Hayadumishwi bali huondolewa kama na wakati mtu apatapo fadhaa kuhusiana na usalama wao.  Majanga haya hutukia kama onyo na kuondolewa kwa Rehema za Ki-Ungu.

 

 

MAISHA HURIA BILA MATATIZO

 

Kama vile waumini wa dhehebu la Manichean wametia shaka ustahiki wa majanga haya na matatizo ambayo huwapata watu, katika njia hiyo hiyo walahidi wameshindwa kuelewa ukweli wa asili yao na kuyaelezea kama yasio na maana.  Wote kwa pamoja wanasema kwamba kama ulimwengu ungeliachwa na Mwenye Huruma, Mpole na Muumba, Mwenye Rehema, Matokeo haya ya kuchukiza yasingelitokea.  Ambaye kwamba amesimamisha hoja hii anajaribu kutanabali kwamba ingelikuwa bora kama maisha ya mtu katika ulimwengu huu yangekuwa huria bila ya matatizo.

Ingekuwa hivyo, kiburi cha mtu na uchoyo vingempelekea kwenye tabia ambayo isingekuwa katika ulinganifu na dini au maisha yake ya dini.  Kama vile unavyoona watu wamelelewa katika anasa na wasaa (faraja) na ambao wengi wao kabisa wanasahau utu wao na hali yao ya kuwa wamelelewa na kukuzwa na mtu fulani.  Wanasahau kwamba wanaweza kupata maumivu fulani au huzuni au kwamba misiba fulani inaweza kuwapata.  Hata husahau iwapo kuna kuwahurumia watu wanyonge au kuwasikitikia watu wenye kuhitaji.  Hawako tayari kuongozwa kuhisi kusikitika kwa matatizo ya watu wengine au kuhisi kuhurumia juu ya wanyonge au kuonyesha upendo kwa nafsi zenye matatizo.

Wakati, hata hivyo, matatizo yanapowapata, huhisi uchungu wake na hapo akili hufunguka wanazindukana kwa kiwango kikubwa zaidi kuliko katika ukadiri ya ujinga wao na upumbavu.  Wanaanza kutenda katika njia ambayo iliwapasa juu yao wakati wote.  Kama matatizo haya yasingewapata, wangeendelea kujiona kama waungu (na) kuendesha maisha yao katika hali ya kiburi, kutokuwa na masikitiko au huruma na mtu yoyote yule.  Je, tabia kama hii ingekuwa ni yenye faida kwa dini yao na ulimwengu huu?  Hakika sivyo!  Pamoja na dini potofu wangepata madhara ya kilimwengu.  Watu wangewachukia na kuwalaani.  Watu wachoyo kama hawa wangesababisha mchafuko katika ulimwengu huu katika mambo yote, kazi biashara, elimu na tabia ya wao kwa wao n.k.

Watu wanaokana mambo haya, wakiyaona kama yasiyo na maana, ni kama wale watoto wadogo ambao wanalaumu dawa vhungu na isiyo pendeza na kuchukizwa na tahadhari dhidi ya vyakula vyenye madhara.  Hawataki kazi, na hupenda kucheza tu huria (bila kuzuiwa) hupenda kujiingiza katika mambo ya kipumbavu, kula na kunywa bila pingamizi au kizuizi.  Hawajui kwamba ruhusa kama hii na uvivu kutadumaza ukuaji wa akili zao, uadilifu wao na miili yao, kwamba vyakula hivi vya kumezeka lakini vyenye madhara vinaweza kupelekea kwenye mateso tofauti tofauti na magonjwa.  Uboreshaji wao umo katika upatikanaji wa elimu, na dawa zina faida nyingi kwao mbali na huko kutokumezeka kidogo.

Wanasema ni kwa nini watu hawakupewa tabia ya kutokufanya dhambi ili kwamba Mwenye Nguvu zote Allah hangehitajika na kuwatia adabu kwa uchungu wa matatizo.  Jibu kwao litakuwa kwamba katika hali hii mtu hangekuwa na thamani ya itibari (sifa) yoyote kwa uzuri wala kupasika na malipo kwayo.

Kama wataendelea kusema zaidi kwamba kuruhusiwa kila aina ya anasa na wasaa (faraja) lingekuwepo wapi dhara lolote humo kama hangepata itibara au malipo kwa wema wa uzuri wake?  Jibu litakuwa ni kulifikisha swali hili kwa mtu mwenye akili timamu na mwenye siha nzuri na kumwambia akae tu bila kufanya kazi, na kumhakikishia ukamilifu wa mahitaji yake yote bila juhudi zozote.  Kisha tazama kama akili yake itakubaliana na hilo.  Utamwona kuridhika zaidi na kutosheka kwa kidogo apatacho kwa juhudi yake kuliko kupata kikubwa na kingi ambacho huja kwake bila stahiki, pasipo kukifanyia juhudi.  Kadhalika baraka za Akhera (ulimwengu ujao) zitakuwa zenye tabia ya namna ile ile kwao ikiwa tu kama zimepatikana kwa juhudi.

Kwa hiyo mtu anaruhusiwa boma mbili za baraka.  Kwanza kabisa kupata ujira mkubwa kwa juhudi zake katika ulimwengu huu wa sasa (dunia).  Pili, ameonyeshwa njia za kuitafuta kwa juhudi zake ili kwamba apate ridhio la kiwango cha juu sana kwa fanikio hilo.  Ni kawaida kabisa kwa mtu kutokuruhusu kukipa thamani kitu chochote kilichopatikana bila juhudi au haki.  Kinyume chake, chochote apatacho kwa matokeo ya juhudi na haki, hukiwekea bohari kubwa.  Na kwa hali hiyo, baraka za Mwenye Nguvu zote Allah ambazo zitawekwa juu yake kwa wema wa kujizuia kwake ndani ya mipaka iliyoamriwa zitakuwa bora zaidi kithamani kwake kwa mlinganisho, na hali ya akili ambapo hakuwa ni mwenye kuzuia tamaa zake mbaya na kila kitu kilicho haramu kimekoma kuwa na mvuto kwa ajili yake.  Katika haki hii, baraka za Akhera zilizowekwa na Mwenye Nguvu zote Allah zisingekuwa na thamani hivyo kwake.  Malipo ambayo kwamba atapata kwa matokeo ya juhudi ya nguvu zake na chumo yatakuwa ya thamani kubwa sana kwake.

Kama sasa wanasema iwapo haitokei hivyo kwamba baadhi ya watu wamependezwa sana kupata baraka bila haki yoyote, kwa hiyo, hoja gani italetwa juu ya kadhiaa hizi kwa watu ambao watahisi kupendezwa kwa kupata baraka za akhera?

Jibu litakuwa kwamba hili ni somo kwamba watu watashawishika kwalo, kwamba watapata baraka za Akhera bila juhudi itapelekea kwenye namna zote za madhara yaliyoletwa  makusudi, hali ya kutenda dhambi, ushukaji wa uadilifu na uovu.  Nani basi angejizuia kutokana na uovu wa uadilifu au kufanya juhudi kuwa na tabia njema wakati kwamba ameshajijua mwenyewe kama mpokeaji mstahiki wa baraka za Akhera?  Nani angekuwa na hakika ya hatua ya maisha, heshima na mali yake mwenyewe na ya ahali wake kuhsu madhara ambayo watu wangefanya kama kungekuwa na hofu ya adhabu na kisasi?  Uharibifu kwayo ungesababishwa katika maisha haya ya sasa kwa watu kabla ya siku ya mwisho (ya ulimwengu huu).

Haki na ustadi vyote vingetupwa. Ingetiliwa shaka kama ukosekana taratibu huku na mchafuko kungeingia kwenye usanii.

Vile vile huzungumzia matatizo na usumbufu ambao wakati mwingine yana matumizi ya jumla yakiwaumiza na watu wema na kupelekea watu waovu bila kudhurika. Wanasema, itawezekana vipi kuwa Usanii wenye kufaa wa Mwenye kujua yote, hoja gani unaleta?

Jibu kwa hili itakuwa kwamba matatizo kama haya huwapata wote wema na waovu/wabaya na kuna faida kwa makundi yote zilizoamriwa na Mwenye Nguvu zote Allah.  Wema huteseka kwa matatizo na usumbufu mwingi na malipo ya baraka kwao husababisha shukurani na Wokovu ndani yao.

Na kwa watu waovu matatizo yao huanza kutokea kutokana na tabia ovu.  Iko faida ya uboreshaji kwa wale wote ambao wangeepushwa kutokana na kishindo cha matatizo haya.

Mbali na makundi mawili haya, kwa watu wema hali ya uzuri ni chanzo cha furaha na kishawishi zaidi na utambuzi wa uendeleaji wa tabia njema zaidi.  Kwa wafanya maovu pia hifadhi dhidi ya madhara ni fadhila maalumu kutoka kwa Mwenye Nguvu zote Rehema za Allah zinaonyeshwa kwao bila ya wao kujistahiki.  Hii huwavuta wawe wapole na kuwasamehe wale ambao hufanya ubaya kwao.

Mkinzani anaweza kusema kwamba matatizo kama haya huangukia mali zao, bado wakati mwingine miili yao huteseka hata kuangamia, kama vile kuunguzwa, kufa maji, kuchukuliwa na mafuriko au kuzikwa ungali hai.

Jawabu kwao litakuwa kwamba Mwenye Nguvu zote Allah ameamuru ndani yake uzuri wa makundi yote.  Kwa watu wema kwa sababu ya kuutoka ulimwengu huu na matatizo yake na mauchungu yake, na kwa watu waovu ni kwamba uwezo wao wa kufanya dhambi kwayo huondolewa.

Kwa muhtasari, Mwenye Nguvu zote Allah hugeuza matokeo ya matendo yote haya kwa kujua kwake yote na Mwenye Enzi Kuu na kuelekeza wenye uboreshaji, kama vile mti unapoangushwa chini na upepo, seremala mzuri huugeuza kwa matumizi yenye faida.

Kadhalika, Mwenye Nguvu zote Msanii hugeuza matokeo ya maafa haya ambayo huzipata mali zao na miili yao kwa faida zao na uboreshwaji wao.  Kama mtu atauliza kama ni kwa nini misiba hii iwapate watu, jibu litakuwa, wasije wakageukia kwenye hali ya kutenda kwa sababu ya kipindi kirefu cha Usalama, wasije watenda maovu wakajiingiza moja kwa moja katika hali ya kufanya madhambi ambapo watu wema wakawa ni wenye kuzembea katika kufanya mema.

Aina zote hizi za tabia huwazidi nguvu watu wakati wanapopewa muda mrefu wa starehe na faraja.  Matukio kama haya huwafanya kuonyeka na kuwaepusha kutokana na tabia hizi - na ndani yao muna uzuri kwao. 

Kama wangeondolewa matatizo moja kwa moja, wangevuka mipaka ya kufanya dhambi kama vile walivyofanya watu wa nyakati zilizopita hivyo kwamba ilibidi wateketezwa kwa dharika kuisafisha ardhi kutokana nao.

 

 

KIFO

 

Kuna nukta moja imefungwa kwenye akili za wakanushaji hawa wa Usanii na dhumuni, kuitaja ni, kifo na uharibifu.  Wanafikiri kwamba ingekuwa sawasawa kama mtu angepewa hai wa milele bila tatizo lolote au dhara.

Ni  muhimu kuchukua hoja hii na kuipeleka kwenye mwishilizio wa kihoja ili kuona kwamba inapelekea kwenye maokeo gani.  Hebu tazama kwamba kama watu wote, wangeishi maisha ya umilele, ardhi hii ingekuwa finyu sana kwao; wasingepata nafasi ya kutosha kwa makazi yao, kilimo chao na mahitaji ya riziki kwa kuendeshea maisha yao.  Ijapokuwa shoka la kudumu la kifo linafanya kazi wakati wote, wakati ambapo kuna migongano kuhusiana na makazi na mashamba ya nafaka, hata vita hupiganwa na damu kumwagwa juu ya suala hili.  Ingekuwa vipi hali yao kama asingekufa hata mtu mmoja wakati uzazi wa watu wapya unaendelea?  Sasa hivi hata ingawa vifo vinaendelea, tunayo matatizo haya.

Je, kungekuwa na hatari za namna gani kama daima asingekufa hata mtu mmoja?  Watu wangezidiwa nguvu kwa choyo, tamaa mbaya na ugumu wa nyoyo.  Kama wangehakikishiwa uhai wa umilele, hakuna ambaye angetosheka na anavyomiliki.  Hakuna ambaye angekubali kutoa chochote kwa wenye kuhitajia (mafukara na masikini), wala kusingekuwa na faraja baada ya msiba.  Wangechoshwa na maisha na mambo yote ya ulimwengu.  Mtu mwenye maisha marefu huchoshwa nayo, hutamani mno kutokewa na kifo na kupata afueni.

Wanasema kwamba ingepaswa iamriwe kwamba matatizo yote na maradhi yangeondolewa kutoka miongoni mwao, hivyo kwamba wasingependelea kukiomba kifo wala kuwa ni wenye kukitamani.  Jibu kwa hili ni kwamba wangetumbukia kwenye njia za uovu na utovu wa utii.

Kama wakisema kwamba kuondoa fadhaa na upungufu wa nyumba na hali (mbaya) za maisha, uzazi wao ungesimamishwa, jibu litakuwa kwamba katika hali hiyo idadi isiyoelezeka ya viumbe ingekoseshwa fursa ya kuingia katika ulimwengu huu na hivyo kukoseshwa baraka za Mwenye Nguvu zote Allah katika uhai wa ulimwengu huu na wa Akhera, ikiwa kizazi kimoja kingeruhusiwa kuingia bila uwezo wa uzazi zaidi.

Na kisha wangesema kwamba Yeye (s.w.t.) angeliumba watu wote,wale waliozaliwa na wale watakaozaliwa katika siku zijazo, katika mkupuo mmoja.

Jibu kwao litakuwa, kama lilivyokwisha elezwa tayari, kwamba matukio yatajitokeza kama vile upungufu wa nyumba na njia za Kilimo.  Wapi nafasi ya kutosha ingepatikana kwa kjengea nyumba, kuendeshea kilimo, kuanzishwa kwa mawasiliano.  Katika hali hiyo kutokuwepo kwa mahusiano ya kijinsia (kwa ngono), kusingekuwa na faida za kujamii (umma) niongoni mwa jamaa na ndugu, hakuna msaada wa wao kwa wao katika nyakati za shida na huzuni.  Wapi ingepatikana furaha ya mzazi katika kuwalea watoto?

Hii huonyesha kwamba upande woote mawazo yasogeavyo mbali kutoka Usanii wa kidhumuni, huhakikisha kuwa siyo wa kuthibitika ni upumbavu na upuuzi.

 

 

DHULUMA

 

Mkinzani anaweza, pengine, kuleta pingamizi kutoka nukta nyingine ya mtazamo na kusema kuwa vipi itaweza kujulikana kwamba  kuna Muumba na Msanii, wakati tunaona katika maisha mtu mwenye nguvu akijitwalia kila kitu, mwenye nguvu kumkandamiza mnyonge, wakati ambapo mnyonge anaonewa na anatukanwa.  Wema ni windo la taabu na matatizo wakati mwovu mno ni mwenye afya na tajiri.  Yule ambaye haheshimu kanuni na kawaida haadhibiwi kwa haraka.

Kwa hayo inamaliziwa kwa kusema kwamba kama kungekuwa na Usanii ueneao na kuujaza ulimwengu wote, shughuli zote zingeendeshwa sawasawa.  Watu wema wangelishwa vizuri na wabaya na waovu wangepata hasara.  Wenye nguvu wangezuiwa kuwakandamiza wanyonge.  Mwenye kutenda uovu angepata adhabu haraka.

Jibu kwa hili litakuwa kwamba katika hali hii wema, ubora maalum wa mtu ungepoteza thamani yake.  Vilivyobaki katika Uumbaji havina ubora wa ushawishi katika ahadi za malipo ya Mwenye Nguvu zote Allah na hivyo kutoa tamaa zao kwenye nidhamu ya tabia ya uzuri.  Wao, katika hali hiyo wangekuwa kama wanyama wa miguu minne, ambao wako chini ya udhibiti kwa fito (fimbo) na uhitajio wa tumbo.  Kwa wao daima ama huonyeshwa jambia, au hupewa ukoka kuwaweka katika mpango.  Hakuna hata mmoja ambaye angetenda katika upasiko pamoja na ushawishi wa kupata jaha ya Kiroho au Jahannamu.  Wangedhalilishwa na kushushwa daraja kutoka daraja ya ubinadamu kupewa ile ya unyama.  Hakuna ambaye angejali baraka za Kiroho.  Mtu angefanyia bidii shughuli za malipo ya mara moja ya wakati huo huo (papo hapo).  Mtu mwema angetenda kwa kujipatia chakula tu na kwa mali za kilimwengu, wakati mtu mwovu angejizuia kutokana na ukandamizaji na uonevu kwa sababu tu ya hofu ya adhabu ya ghafla ya wakati kuo huo hivyo kwamba matendo yote ya watu yangevutwa katika hali ya papo hapo ya wakati huo.  Kusingekuwepo na wazo hata la mbali sana kwa ajili ya malipo mema na adhabu zilizoamriwa na Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.) wala wasingepasika kwenye baraka za Kiroho za Akhera.  Yote haya, yangepelekea kwenye hali mbaya.

Ijapokuwa, na yote haya, umasikini na ukwasi uliotajwa na mkizani haviko moja kwa moja mbali na ilivyokusudiwa.  Ni ukweli kwamba kama watu wanavyofahamu watu wema pia hupata rasilimali za mali za ulimwengu huu, hivyo kwamba watu wasije wakadhania kwamba ni wasioamini tu (Makafiri) ndiyo waliopendelewa nayo, hali ya kwamba watu wema wamenyimwa starehe za maisha haya (ya dunia) wasije watu kwa ujumla wakajichukulia tabia ya ujeuri.  Unaona vile vile kwamba wajeuri wanaadhibiwa katika ulimwengu huu, wakati ujeuri wao unapovuka mipaka yote na watu wakadhurika mno kutokana na jeuri zao hizo, kama vile Firauni alikufa maji, Nebukadreza aliumbuliwa na Bilbis aliuwawa.

Kama katika maelezo ya baadhi ya Dhumuni la Maana sana, nje ya uwezo wa watu, baadhi ya waovu wanapewa raha kidogo au baadhi ya watu wema malipo yao yanaahirishwa mpaka siku ya baadaye, hakugeuzi kusudio na maana ya Usanii, kwani kadhia kama hizo hufanyika pia hata katika watawala wa ulimwengu.

Hii hata hivyo, haipunguzi nguvu ya sera.  Kwa ukweli Kadhia hizi, wakati zinachelewesha, zinaonekana kuwa zenye ulinganifu zaidi na sera za utawala na ni zenye kuona mbali.  Na kama ushahidi mzito wa kutosha wenye nguvu na mwishilizio kwayo yote haya yakalazimisha kwenye imani ya kwamba lazima kuwepo Muumba na Msanii wa vitu vyote vya ulimwengu huu, kitu gani kinaweza kumzuia Yeye (s.w.t.) kupanga uzuri kwa viumbe vyake?  Hakuna akili ya mwanadamu iwezayo kudhania kwamba Muumba atauwacha Uumbaji wake hivi hivi tu (huria), isipokuwa iwe kwamba kwa ukosefu wa nguvu na uwezo, kwa ujinga au umakusudi, yote haya ambayo ni mageni kwa Usanii wa Allah Mwenye Nguvu zote.  Allah (s.w.t.) Si Asiye na uwezo kwa uboreshaji wa Uumbaji Wake, wala Si Asiye na habari na hali zao, wala Allah (s.w.t.) aepushilie mbali, Yeye kimakusudi anapotoka.

Kushindwa kufanya vizuri kwa sababu ya kukosa nguvu na uwezo, ujinga na upunguani, kunaeleweka zaidi kama ilivyo kwamba asiye na nguvu na uwezo hana uwezo wa kuumba viumbe watakatifu hawa wa ajabu, mjinga hana utambuzi wa njia za maadili na ustadi wakati mkaidi hawezi kugeuka akawa kwenye Uumbaji Mtukufu huu wa kazi hii muhimu na ya ufundi mkuu.

Na mambo kuwa kama yalivyo, hueleweka kwamba Muumba wa ulimwengu atakuwa, kama jambo la kweli na sawa, aangalia kwenye uboreshaji wa Uumbaji wake ingawaje maana ya Usanii yaweza isitambulikane kwa watu kwa ujumla.  Hata mamlaka za kiulimwengu hazifahamiki, ambazo kwa kuchunguza zaweza kuonekana sahihi wakati zikiwekwa kwenye kipimo.

Ikiwa una mashaka na asili ya dawa au lishe, na baada ya majaribio mara mbili au tatu asili yake ikawa dhahiri kabisa, je, hutaiondolea mashaka yote kuhusu asili yake kwenye akili yako?

Kwa nini basi usilipasikie jambo hili na kipimo?  Kwa nini usitambue kwamba lolote linaloamriwa na Mwenye Nguvu zote Allah ni katika faida zilizo bora mno kuliko zote kwa viumbe vyake? Vipi basi kuhusu hawa watu wajinga, ambao mbele za ushahidi mzito huu, ambao hauwezi kukadiriwa hawawezi kuvutika na Muumba na Msanii wa ulimwengu?

Hata kama nusu ya ulimwengu na vilivyomo vingeonekana kuwa vimeharibika na visivyo na mpango, itakuwa hoja mbovu na elimu potofu.  Kuufikiria kama usio na Dhumuni na Usanii, kwa kuwa nusu nyingine iko katika hali ya ukamilifu na uzuri, ambao huondoa mara moja neno lisilothibitika.  Huwezekana vipi neno kama hili lisilothibitika likubaliwe kwa kuwa kila kitu katika ulimwengu kinaonekana kwa kuchunguzwa na uangalizi, kuwa vilivyopangwa na hali ya uzuri zaidi, kiasi hivyo kwamba hakuna kinachoweza kudhaniwa ambacho hakina mfano bora zaidi miongoni mwa Uumbaji wa Ki-Mungu.

Elewa kwamba ulimwengu unaitwa kwa jina la 'Cosmos', ambalo lina maana ya mapambo katika lugha ya Kiyunani, na Mafilosofa na wajifanyao wahenga.  Imeitwa hivyo kwa sababu ya ukamilifu wa mpangilio.  Kwa nini wasiuite Amri ya Ki-Mungu?  Jina la 'Cosmos' huonyesha kwamba mpango mzuri wa maongozi ya Mungu yako kwenye msingi wa utashi na umaridadi.

Nashangazwa na watu hawa ambao wanaachilia makosa katika elimu ya uganga, ambayo ni yenye hitilafu sana, lakini huleta hoja za kutaka kujua mpango wa ulimwengu, ambao ni kamili bila waa (kosa).

Nashangazwa na mwenendo wa wadai wa filosofia, ambao hawana elimu ya utukufu wa Uumbaj na bado wanahoji utukufu wa Mwenye Nguvu zote Allah.  Namshangaa hususan mtu huyu mwenye bahati mbaya na duni, Mani, ambaye anadai kuelewa maajabu ya elimu wakati  ni mjinga halisi wa hoja za ubora mno wa Uumbaji, na hivyo kujitia kwenye kuhoji Hekima Kuu ya Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.) katika Kadhia ya Uumbaji.

 

 

KUWEPO KWA MWENYEZI MUNGU

 

Juu ya wote hao, Walahidi ni wa kuhurumiwa, ambao wanataka kumwona kwa macho yao Yule Ambaye ni fumbo hara kwa akili, wameamua kukana kabisa kuwepo kwake.  Walidai kwa nini  Hawezi kuzunguukwa ndani ya akili?  Hushinda akili kama vile vitu vilivyo nje ya fani ya kuona, haviwezi kutambulika kwa macho.

Kama kwa mfano, unaona kipande cha jiwe kinapita juu angani (kimerushwa), mantiki ya maana utakayo chukuwa ni kwamba mtu fulani kalitupa juu.  Jicho linaweza likawa halikuliona (likitupwa) na bado akili hutambua hivyo kwa sababu ya uwezo wake wa utambuzi, ya kwamba kipande cha jiwe hakiwezi kujirusha chenyewe juu angani.  Unaona kwamba jicho limesimama katika hatua fulani na haliwezi kuendelea mbele.  Kadhalika akili husimama ghafla katika mpaka wake ilioruhusiwa katika kadhia ya kuwapo pote kiroho.  Haiwezi kuendelea mbele zaidi.

Tunasema, hata hivyo, kwamba akili ambayo hutambua kwamba mtu humiliki dhati na nafsi (roho), ijapokuwa ni ukweli kwamba hakuna aliyeiona dhati kwa macho ya umbo, akili hiyo hiyo yapasa kuwa na uwezo wa kufahamu na kukubali kuwepo kwa Muumba, bila kuwa na uwezo wa kutambua Nafzi Yake.

Na kama sasa wakiuliza kwa nini Ameweka wajibat (ulazima) juu ya mtu mdogo kupata utambuzi Wake kwa akili zake kwa kuwa hawezi kutambua Yeye kikamilifu, jibu litakuwa kwamba dai la kumtambua Yeye ni kwenye masharti kwa kiwango ambacho akili ya mwanadamu inaweza kufanya, kwa uwezo ilionao.  Ni kuamini kuwepo Kwake na Kutii amri na makatazo Yake.  Hawatakiwi kuzunguuka kuwepo Kwake Pote (kila mahali) na Sifa Zake.  Hakuna mtawala atakaye raia zake wajue hali ya miliki na ukamilifu wake, Yote yale atakiwayo ni uaminifu na utii kwa sheria za nchi.

Wazia kwamba mtu atausogelea moango wa Ikulu ya Kifalme na kumtaka Mtawala ajitokeze kwake ili amjue kikamilifu, tena zaidi angeweza akaacha kumtii, hujiweka Mwenyewe wazi katika hatia.  Kadhalika yeye ambaye hushurutia imani yake kwa Mwenye Nguvu zote Muumba kwa elimu kamili ya kuwepo Kwake Pote humchukiza Mwenye Nguvu zote Allah (s.w.t.).

Na kama watauliza kuwa ni kwa nini ni mpungufu, jibu litakuwa kwamba dhana haiwezi kuruka kina cha utukufu wake na bado ijaribu kupata kimo kile ambacho ni nje ye uwezo wake, kwa kweli hata utambuzi wa vitu vya hali ya chini viko nje ya mpaka wake.

Jua hutoa kielelezo Kwayo.  Unaliona hutoa mwanga kwenye ulimwengu wote na bado hakuna anayejua ukweli uliopo unaolihusu.  Mna idadi ya mambo yasiyothibitika (yanayokubaliwa kwa ajili ya hoja tu) kulihusu (hilo jua) kwa maelezo hayo na kwa kuwa maoni tofauti miongoni mwa wanachuoni yapo kuhusu hilo.

Baadhi wanazema ni umbo Kimbinguni lenye uwazi ndani uliojaa moto unaotoa miali kutoka tundu mahsusi.  Baadhi husema kwamba ni namna ya "nebula" (jamii ya nyota nyingi kama wingu).  Baadhi wanasema liko kama kioo katika kimaumbile, lenye uwezo wa kuhifadhi joto na kisha kutapanya nuru yake ulimwenguni.  Baadhi wanasema kwamba ni umbo nyororo kabisa lililotangamana na maji.  Wengine wanasema kwamba asili nyingi mbalimbali za moto zimeungana pamoja.

Bado wengine wanathibitisha kwa maneno ya hoja tu kwamba ni  ziada ya kitu cha asili kwa vile vingine vinne vya asili (ardhi, maji, hewa na moto).

Watu hawa wamehitilafiana (wametofautiana) miongoni mwao wenyewe kwa wenyewe kuhusu umbo lake (jua).  Wengine wanasema liko bapa kama ukurasa (wa kitabu), wengine hulifikiria kama mpira usunguukao.  Vile vile kuna tofauti kwenye ukubwa wake.  Baadhi hufikiria kuwa sawa kwa ukubwa kama ardhi.  Wengine wanafikiri ni dogo kwa ukubwa kuliko ardhi.  Baadhi wanasema ni kubwa kuliko kisiwa hiki kikubwa mno (dunia).  Watu wa elimu ya jometri (geometry) wanasema kwamba liko mara mia moja na sabini kwa ukubwa wa ardhi.

Inaonyeshwa na maelezo yanayokinzana ya watu hawa kwamba hawajui asili yake.  Akili imekuwa haina uwezo wa kuelewa asili ya jua ambalo macho yanaweza kuona na akili kutambua, yawezekana vipi basi Nafsi Yake iwe ifahamike Ambaye ni nje ya weupe wa akili na kufichika kutokana na mawazo?

Kama wao, basi wanasema kwa nini Amefichika kutokana na mawazo, jibu litakuwa kwamba hakujificha kwa kitu kilichotengenezwa kama mtu anavyoweza kuwa nyume ya milango na mapazia kutokana na kuonwa (kuonekana) na  watu wengine.  Wakati tunaposema kwamba Mwenye Nguvu zote Allah haonekani kwa macho tunamaanisha kwamba kuwapo Kwake Pote ku-laini mno kwa mawazo na akili za kiumbo kuweza kufahamu kuwapo Kwake Pote, kama vile nafsi (roho) ni laini mno, ingawa ipo pia ni moja miongoni mwa Uumbaji na bado ni nje ya duru ya mawazo.

Kama sasa watasema ni kwa nini Yulaini mno kuwepo juu ya kila kitu, swali hili litakuwa lisilothibitika, kwani zaidi sana sana Muumba wa kila kitu lazima awe juu ya kila kitu na dhahiri kwayo.

 

 

UTUKUFU UWE KWA MWENYE NGUVU ZOTE ALLAH!

 

Kama wanauliza kwamba kwa nini imejulikana kwamba Yeye ni juu ya kila kitu na dhahiri kwayo?  Jibu litakuwa kwamba kuna ilani nne za elimu katika  niaba hii:-

(1)  Kuona kama kuwapo kwa kitu ni thabiti.

(2)  Asili halisi na nafsi kwayo.

(3)  Ni sifa gani ilizonazo?

(4)  Kwa nini ni kwa vipi kuwapo Kwake.

Hakuna kiumbe anayeweza kutumia ilani hizi katika kuhusiana na Muumba, ila kujua tu kwamba Yupo.  Hakuna anayeweza kujua kuhusu nafsi yake.  Kuuliza kwa nini na kuwepo Kwake wapi kumhusu Yeye moja kwa moja (ni swali) lisilothibitika, kwa kuona kuwa Yeye ni Muumba wa kila kitu, na hakuna chochote kiwezacho kusimama kama chanzo au sababu ya kuwapo Kwake.

Kwa vile watu wamekwisha elewa kwamba Yeye yupo, siyo lazima kwamba wajue na Nafsi Yake pia, kame vile uelewaji wa roho hakufanyi kuwa na elimu ya asili.  Hali ni sawa hivyo hivyo kwa asili ya vitu vingine vya Kiroho. Kama wanasema kwamba unamzungumzia Yeye kama aliye mbali na kutambuliwa kwa vile Yeye ni Hai asiyejulikana, jibu litakuwa kwamba kwa upande mmoja kimaoni kwa kweli ni hivyo, kama akili inataka kupata elimu ya Nafsi/Asili yake.  Kwa upande mwingine wa maoni, hata hivyo, Yeye yuko karibu kuliko kila kitu, kwa kuwa ufanisi wa hoja umefanya kuthibitisha kuwapo Kwake.

Kwa hiyo, kutoka mtazamo wa upande mmoja, Yeye yuko dhahiri, na hakufichika kwa ye yote, kutoka mtazamo wa upande mwingine Yeye amefichika kwa kufikiwa na akili za hisia za mwili wa mwanadamu. Ni hivyo hivyo na akili.  Hujulikana kwa hoja na ushahidi lakini asili yake ni fumbo.

Wataalamu wa viumbe hai na mimea wanasema maumbile hayafanyi chochote bure wala kuacha chochote feleti (bila kufanyika) ambayo hupelekea kwenye ukamilifu wa kitu, hutoa ushuhude kwa hili.  Jibu Kwao litakuwa, nani aliyefundisha maumbile ustadi huu na elimu ya mipaka ya kila kitu, isiruke mipaka ya maana halisi na kwenda nje ya uwezo wote, wakati ambapo hili ni jambo ambalo akili haijifundishi hata baada ya majaribio ya uchunguzi wa mara kwa mara?

Kama wanasema kwamba maumbile yana hali ya kujua yote na kuweza yote, kwa hiyo wanakubali kile walichokikana, kwani hizi ni sifa za Muumba, kwamba Yeye ni Mwenye Kujua yote (Hekima Kuu) na ni Mwenye Kuweza yote (Enzi zote).  Wamempa Yeye jina la "maumbile", sisi tunamwita Yeye Allah, Mwenye Nguvu zote, Mwenye Kujua yote, Mwenye Kuweza yote n.k.  Kama wanakana hilo, basi Uumbaji wote huu wenye Ustadi unaita kwa nguvu kwamba ulimwengu huu sharti uwe ni kazi ya Muumba ambaye ana sifa hii kubwa mno - Mwenye kujua yote.

Miongoni mwa watu wa kale walikuwepo baadhi ambao walikana Dhumuni na Usanii.  Waliamini kwamba ulimwengu ulijitokeza na kuwepo wenyewe kwa bahati tu.

Hoja yao ilikuwa kwamba wakati mwingine watoto wachanga wanazaliwa tofauti na umbo la kawaida kama vile waweza kuwa wameharibika viungo kwa ongezeko la kidole au kwa ubaya wa sura usio wa kawaida.  Wamehoji kwamba ulimwengu umejitokeza kuwapo bila dhumuni na mpango.  Kwamba (watoto hao) wamejitokeza kuwa hai wenyewe na kwa bahati tu.

Mtaalam mmoja aitwae Aristotle alikania hoja yao.  Jibu lake lilikuwa kwamba kama kitu chochote, hutokea kwa kadiri ionekanavyo kwa bahati, hicho pia kina sababu mahsusi ambazo hukipotea kutoka shughuli zake za kawaida.  Bahati ile kamwe haiko kwenye daraja la shughuli za Kawaida ambazo huenda zikaendelea daima.

Unaona jamii tofauti za wanyama wafuatao mtindo wa kawaida na kupata maumbo dhahiri, kwa mfano mtoto mchanga wa kibinadamu wakati anazaliwa ana mikono miwili, miguu miwili na vidole vitano (vya mikono na miguu) kila mmoja kama inavyoonekana kikawaida miongoni mwa watu.  Hata hivyo, wakati mwingine, mambo huwa tofauti - kinyume kutokana na baadhi ya sababu zinazoathiri jauhari za uzazi ambazo hufanya kukua kwa kilengwa katika mfuko wa uzazi; kama vile inavyotokea hivyo kwa sababu ya baadhi ya khitilafu katika ala (zana za kazi), ambazo anafanyizia kitu maalum ambacho kinatengenezwa, hakiji sawa na usanii wa fundi. 

Kadhalika, sababu fulanihutambaa kwa mtoto wa wanyama ambazo hupelekea kuharibika viungo, kupungua au kuongezeka katika mipaka, lakini kijumla wako kikawaida mfumo sawa bila kombo.

Kama vile khitilafu itambaavyo, kwenye mambo fulani katika hali ya njia halisi bila kuwa kinyume na mpango na bila kutoa ushahidi kwamba siyo vyombo vya ufundi vya mafundi; kadhalika mambo fulani yanaathiwa na vikwazo fulani katika shughuli za kawaida za maumbile, hauwezi kufanya kuwa ni sababu katika pendeleo la kutokea hivi hivi na bahati.  Kwa hiyo yeyote, ambaye juu ya msingi wa kweli kinume na maumbile, husema kwamba kila kitu kimejitokeza kuwepo kwa bahati tu, anafanya kitu kisichothibitika na maelezo yasiyo na akili.

Kama wanasema ni kwa nini vitu fulani vina maumbo kamili ambapo vingine vina kasoro moja, jibu litakuwa kwamba ni kuonyesha kwamba vitu vya ulimwengu haviko kwa sababu ya ulazimisho wa maumbile wala si lazima kwamba kama ilikuwa kwa sababu ya maumbile, vyote vingepaswa kuwa na mfumo mmoja kama wakinzani hawa wanavyosema. Yote haya hutokea chini ya kupenda na Dhumuni la Mwenye Nguvu zote, Muumba kwamba, Yeye Ameweka mfumo fulani na kiutaratibu kwa vingi ambapo ameruhusu kasoro kwenye taratibu katika baadhi ya mambo kuonyesha kwamba maumbile pia yako chini ya udhibiti wa mpango bora na ustadi, kwamba yenyewe pia, yanategemea juu ya kupenda kwa Muumba kwa shughuli zake na ukamilifu.

 

UTUKUFU UWE KWA MWENYE NGUVU ZOTE ALLAH, MHIFADHI WA MALIMWENGU !

 

Elimu ambayo nimeiweka juu yako yapasa isomwe kwa moyo.  Yapasa uwe na shukurani kwa Mwenye Nguvu zote Allah na Mhimidi Yeye kwa baraka Zake.  Yapasa uwatii Wapenzi Wake.

Nimetoa kidogo jumla yote ya elimu na ushahidi wa Mpango mkamilifu na Dhumuni kama hoja kwa uumbaji wa ulimwengu huu.  Fikiri na tafakari juu ya hii na jifunze somo kwayo.”

Nilimuahidi Imam (a.s.) kupambanua siri ya maana ya yote haya.

Imam (a.s.) aliweka mkono juu ya kifua changu na akasema: "Kumbuka yote haya na hutayasahau".

Nilizirai.  Wakati nilipopata fahamu zangu, Imam (a.s.) akasema: "Ewe Mufazzal!  Unajisikiaje sasa?"

Nilijibu: "Kwa msaada wa Mola wangu, ninajitegemea kwa kurejea kwenye kitabu hiki ambacho nimekiandika.  Kila kitu kiko kwenye kumbukumbu yangu kama vile naweza kuonyesha yote kutoka viganja vya midono yangu.  Utukufu uwe kwa Mola wangu Mwenye Nguvu zote Allah, ambaye kwake zinastahiki Shukurani na Sifa njema kama zinavyopasika."

Imam (a.s.) akasema: “Ewe Mufazzal! Uwe mkamilifu kwenye utulivu katika akili yako, ubongo na hoja. Insha-Allah, nitakupa maelezo ya mbingu na ardhi na vitu vyote vilivyoumbwa na Mwenye Nguvu zote Allah kama maajabu yake ya Uumbaji na jamii mbalimbali na makundi ya malaika mpaka uu kabisa kwenye "zenith" na sifa zao pamoja na viumbe vyote kuchangnya majini na binadamu, mpaka kwenye nukta ya mwisho ya "nadir", ili uelewe kwamba uliyojifundisha kwa sasa ni sehemu ndogo tu ya yote. 

Unaweza kwenda sasa.  Unayo nafasi tukufu karibu yetu na heshima hii katika nyoyo za maumini kama inavyohisika hamu ya maji wakati mtu ana kiu.  Usiniulize kuhusu niliyokuahidi mpaka mimi mwenyewe nisikie kupenda kuzungumza na wewe kwayo.”

Nilirudi kutoka kwa Imam (a.s.) na tunu ambayo hakuna mtu yeyote amediriki kuipokea.

 

 

Mufazzal Ibn Umar