AL-KASHIF

SWAHILI - JUZUU YA NNE - Vol-4
Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya


Yaliyomo

AL- IMRAN- (Sura ya tatu)

Aya 92:             Mali ndio sababu ya ugomvi...2

Aya 93-95:         Wana wa Israil na Chakula ..4

Aya 96-97:         Nyumba ya Kwanza..6

Aya 98-99:         Kukanusha dalili za ishara za Mwenyezi Mungu.9

Aya 100-103:     Kuwatii Makafiri...11

Aya 104:            Kuamrisha Mema..14

Aya 105-109:     Kuhitalifiana baada ya Mtume.18

 

 

Aya 110-111:     Umma wa Muhammad (s.a.w.w)..20Aya 112:            Wamepigwa chapa ya Udhalili..23

Aya 113-115:     Wote si Sawa.26

Hukumu ya Mwenye kuacha Uislamu.27

Aya 116-117:    Ukafiri haufai kitu.31

Aya 118-120:     Wasiri waovu..33

Aya 121:            Vita vya Uhud.36

Aya 122:           Makundi mawili...38

Aya 123-127:     Vita vya Badr..39

Aya 128-129:    Huna Lako Jambo..42

Aya 130-133: Msile Riba... 43

Aya 134-136: Sifa za wanamchao Mwenyezi Mungu.. 46

Aya 137-138: Zimepita Desturi.. 47

Ushenzi wa 5 June. 48

Aya 139-141: Msidhoofike.. 50

Aya 142-143: Thamani ya Pepo... 53

Nembo za Kidini..53

Mabadiliko ya Hulka na Fikra.54

Aya 144-147: Hakuwa Muhammad ila ni Mtume ...56

Ajali haina kinga..58

Kila Mtu ana alilolinuia...59

Aya 149-151: Mkiwatii ambao wamekufuru..62

Aya 152:            Mwenyezi Mungu amewatimizia .63

Aya 153-155: Mkawalipa majonzi kwa majonzi ..67

Siri ya kushindwa.69

Aya 156-158: Msiwe kama wale waliokufuru..71

Aya 159-160: Kama ungekuwa Mkali .73

Siri ya utukufu wa Muhammad..75

Kunyonyeshwa kwake na Malezi yake.75

Wasifu...75

Mtume wa ufukara..76

Utaratibu wa mwito wake..76

Siri ya utukufu wake.77

Aya 161-164: Mtume hafanyi hiyana..79

Uislamu unafanya maajabu..80

Aya 165-168: Ulipowafika Msiba.. 83

Aya 169-171: Wako hai mbele ya mola wao wakiruzukiwa..86

Aya 172-175: Waliomwitikia Mwenyezi Mungu.88

Shetani ni ombaomba na ni hodari. 90

Aya 176-178: Wanaokimbilia ukafiri.. 92

Kafiri na amali njema... 93

Aya 179:           Kupambanua wema na uovu. 96

Aya 180-182: Urithi wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu.98

Matajiri ni mawakala sio wenyewe..99

Aya 183-184: Kafara na Moto.102

Aya 185-186: Kila nafsi itaonja mauti..104

Aya 187:           Kazi ya wanavyuoni..106

Aya 188-89: Kusifiwa kwa wasiyoyafanya.107

Aya 190-195: Mwenyezi Mungu na wenye akili.110

Aya 196-198: Waliokufuru na wenye Taqwa..114

Aya 199-200: Waumini katika watu wa kitabu.116

Taqwa..116

 

 

AN-NISAA (Sura ya Nne)
Aya 1:                Amewaumba kutokana na nafsi moja.118
Aya 2:                Mali ya Mayatima..122

Aya 3-4:             Mkihofia kutofanya uadilifu basi ni mmoja..123

Ndoa ya mitala (Wake wengi)...125

Aya 5-6:             Msiwape wapumbavu malizenu.127

Kumwamini Mwenyezi Mungu na tatizo la maisha.128

Aya 7-10:           Wanaume wana fungu..133

Aya 11-12: Fungu la Mwanamume ni sawa na mara mbili ya Mwanamke..136

Aya 13-14: Mipaka ya Mwenyezi Mungu.143

Aya 15-16: Wafanya machafu...144

Aya 17-18: Wafanyao uovu kwa ujinga..146

Toba na Maumbile.148

Aya 19-21 Tangamaneni nao kwa wema..153

Mtaka yote, Hukosa yote..154

Ndoa ni kubadilishana Roho kwa Roho. 156

Aya 22-23 Walio haramu kuwaoa. 157

 

 


The .HTML version of this book is taken from
www.al-shia.com  and ebooked by
www.ShiaLibrary.com   and www.islamkutuphanesi.com  .
May Allah be pleased with all.

 

Haki ya kunakili imehifadhiwa na: AL-ITRAH FOUNDATION

ISBN: 9987 665 26 8

Kimeandikwa na:

Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya

Kimetafsiriwa na: Sheikh Hasan Mwalupa

P.O. Box 1017, Dar es Salaam/Tanzania. Email:mwalupa@hotmail.com

Kimehaririwa na: Dr.M.S. Kanju.

S.L.P 1017, Dar es Salaam. Email: drmkanju@yahoo.com Website: www.dartabligh.org

kupangwa katika kompyuta na: Ukhti Pili Rajabu.

Toleo la kwanza: Februari 2004 Nakala:5000

Kimetolewa na kuchapishwa na: Alitrah Foundation P.O. Box 1017 Dar es Salaam, Tanzania Simu:+255 22 2110640 Fax: +255 22 2126757 Email: alitrah@daiichicorp.com Website: www.alitrah.org

Kaashif4-2.jpg

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu walio-jitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Kama lilivyo jina la Tafsiri yenyewe ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo.

Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyo-viandika katika maudhui mbali mbalimbali na hivyo kujipatia wasomaji wengi sana.

Msomi huyu, mwenye fikra huru na anayetetea kile anachokiamini, ni mtu mwenye mawa-zo mapana na kuyaangalia mambo kwa undani sana, kipaumbele chake ni katika maslahi ya umma huu na amejaribu sana kwenda na wakati.

Sifa kubwa pekee ya mwanachuoni huyu ni kuwa yeye hakujihusisha sana na kung'ang'a-nia madhehebu fulani tu, labda hii yatokana na wadhifa wake wa ukadhi aliokuwa nao katika nchi ya Lebanon ambayo ina madhehebu mengi, ambapo sula la madhehebu ni nyeti nchini humo, hata hivyo yeye aliweza kuamua matatizo ya watu kwenye ofisi yake kulingana na madhehebu yao pale walipomwendea, hiyo ilimsaidia sana hata kuweza kutoa kitabu kitwacho 'Al-Fiqh a'laa madhaahabil-khamsah' (Fikhi ya madhehebu matano) yaani ya Hanafi, Maaliki, Shafi, Hambali na Shia (ambacho twataraji kitatoka hivi karibuni Inshaallah).

Jambo lililotupa msukumo wa kukifasiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ni zile faida nyin-gi atakazozipata msomaji na kujua mambo mengi na ya ajabu yaliyo mapya kwake ambayo si rahisi kuyapata kwa wafasiri wengine.

Msomaji atapata faida katika fani za Sayansi, Siasa, Historia, Mashairi, visa vizuri, na Saikolojia miongoni mwa mengine; ndiyo maana msomaji atashangaa kidogo anapoisoma Tafsiri hii atakapoona mwandishi amewataja na kuwanukuu watu kama kina Mfalme Edward, wanasyansi kama kina Enstein, Charlie Champlin (Mchekeshaji maarufu), na wengineo, hali inayoifanya tafsiri hii kuwa ni ya kipekee kabisa.

Mtindo alioutumia mwandishi ni sahali uliokusudiwa watu wa tabaka mbalimbali, wanavyuoni na watu wa kawaida.

i

Kaashif4-3.jpgKaashif4-4.jpg

Nia yetu ni kukigawanya kitabu hiki bure lakini tumelazimika kukiuza kwa bei nafuu ili kurud-isha gharama za uchapishaji.

Mwisho: Shukrani kubwa iwaendee bila ya kuwataja watu waliojitolea usiku na mchana, jopo la wafasiri, wahariri, wachapaji, waliotupa moyo na kutoa maoni yao na walioisimamia ili kuhakikisha kwamba kitabu kimemfikia msomaji.

Masahihisho

Katika Juzuu ya pili:

Uk. 23- Aya ya 177 badala ya soma

Uk. 23-25 Aya ya 177 tarjuma ya Kiswahili, mwisho kabisa wa Aya, badala "Hao ndio waliothubutu ( katika Imani) soma: "Hao ndio wasemao."

Uk. 29- Aya 184, Msitari wa tano- tarjuma ya Kiswahili " Na wale wasioweza, " Soma: "Wanaoweza kwa shida."

Uk. 35- Aya ya 192- badala ya               Ac.

soma

ii

Kaashif4-5.jpgKaashif4-6.jpgKaashif4-7.jpgKaashif4-8.jpg

Makosa ya Chapa.

Sikumbuki kama nimewahi kusoma kitabu kilichotoka kupigwa chapa, cha zamani au cha sasa, bila ya kukuta makosa ya chapa. Nafikiri sitasoma kitabu kisichokuwa hivyo. Nimejaribu sana kuliepuka hilo katika tungo zangu, lakini sikufanikiwa.

Nilikuwa sifikirii kama ninaweza kuona makosa haya katika maandishi ya msahafu mtuku-fu, kama yale yaliyo katika baadhi ya chapa; kwa mfano neno yabswatu kwa swad, badala ya yabsutu kwa sin, na katika chapa ya Tafsir Arrazi ya Misr ya mwaka 1935, Sura ya (2:146). Imeandikwa La Ya'alamuun, (hawajui) badala ya Ya'alamuun (wanajua). Mfano wa makosa haya hausameheki.

Katika Tafsir Al-Manar, chapa ya Pili, sura (5:212), imeandikwa "Fawqahum ila yawmil qiya-ma badala ya Fawqahum yawamal qiyama". Hatuwezi kusema kosa hili ni kubwa zaidi kuliko lile.

Lakini mkosaji atatuletea udhuru kwa msemo mashuhuri huko kwetu jabal amail 'Makosa ya chapa.'

Katika Tafsiri Majmau chapa ya Urfan, Sura (46:15), imeandikwa: " Hatta idaha balagha arbai' na sanah badala ya: Hattaidaha balagha ashuddahu arbai ' na sanah"

Kusema hivi sio kama ninajitetea kutokana na makosa ya chapa atakayoyakuta msomaji katika kitabu hiki, ijapokuwa naomba msamaha kama litatokea hili, lakini makusudio yangu hasa ni kumwambia yule atakayefungua macho yake kwenye makosa ya matamko ya kuu-fungia macho uzuri wa maana. Vilevile ninamwambia yule ambaye siku moja aliniambia: "Vitabu vyako vimejaa makosa ya chapa, kama kwamba hakuna kitu chochote katika vitabu hivyo isipokuwa makosa ya chapa tu. Wote hao ninawaambia: Mungu awasamehe na aniongoze mimi na nyinyi.

Vyovyote iwavyo, mimi ninaomba msamaha kutokana na makosa ya kifikra na ya chapa. Anasema Amirul Muminiin (a.s): "Watu wote ni wapungufu wenye kuchanganyikiwa, isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mwenyezi Mungu." Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye jukumu la kunikubalia yale niliyoyapatia na kunisamehe niliyakosea, kwa jaha ya Mtume na kizazi chake, ziwashukie rehema na amani (Amin).

MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYAH

iii

iv

Kaashif4-9.jpg

m

Kaashif4-10.jpgKaashif4-11.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

92.Hamtapata wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda; na chochote mnachokitoa, basi haki-ka Mwenyezi Mungu anakijua.

MALI NDIO SABABU YA UGOMVI Aya 92

Hamtapata wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda, na chochote mnachokitoa, basi Mwenyezi Mungu anakijua.

Makusudio ya wema hapa, ni utukuzo wa Mwenyezi Mungu na fadhila kwa mja wake.

Zimetangulia tafsir za Aya kadha kuhusu kutoa. Lakini Aya hii imetofautiana kabisa na Aya zingine zinazoelezea maudhui haya. Kwa sababu, haitosheki na kuamrisha kutoa tu, kama Aya nyinginezo, bali imeunganisha baina ya kupata mtu daraja ya juu mbele za Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwa kujitolea anavyovipenda. Kwa hiyo ibada isiyokuwa ya kujitolea, haikurubishi kwa Mwenyezi Mungu - kwa mujibu wa Aya hii - isipokuwa ikiambatana na kujitolea katika njia ya Mwenyezi Mungu.

Kwa hivyo basi, kauli yake Mwenyezi Mungu; "Hamtaufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda," ni tafsiri na ubainufu wa kila Aya na Riwaya inay-ohimiza kufanya amali kwa ajili ya kupata radhi ya Mwenyezi Mungu na kujikuru-bisha kwake hali ya kuwa ni ufafanuzi kwamba, kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu hakupatikani wala hakutapatikana ila kwa kujitolea mtu nafsi yake na mali yake anayoipenda. Ni kama kwamba Imam Ali (a.s.) alichukua kutokana na Aya hii, kauli yake: "Hapana haja ya Mungu kwa ambaye katika nafsi yake na mali yake hakuna fungu la Mungu."

Kutoa ni kugumu na hasa mali ambayo ndiyo mgomvi anayeipambanua imani ya asili. Mali ilikuwa na inaendelea kuwa ni yenye kuabudiwa na mamilioni ya watu. Watu wengi wanawazishwa na shetani kwamba wao wanamwabudu Mwenyezi Mungu (s.w.t.), kumbe kwa hakika wanaabudu pesa, lakini wenyewe hawatambui.

Kuna kisa kimoja kwamba Iblis, kabla ya kuanzishwa mfumo wa pesa, alikuwa na shughuli kubwa sana ya kuwapoteza watu na kuwaepusha na ibada ya Mwenyezi Mungu wawe waabudu sanamu. Kwa hiyo ikawa hana raha usiku na mchana. Baada ya kupita masiku, ukaja mfumo wa pesa ndipo Ibilisi akapumua, akafurahi sana, akaandaa hafla ya taarabu, akawa anacheza huku ameweka Dirham kwenye jicho moja na Dinar kwenye jicho jengine. Akasema: ( kuziambia pesa

2

2

Kaashif4-12.jpgKaashif4-13.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

hizo) "mmenipumzisha sasa, sitojali kama watu wanawaabudu nyinyi au wataabudu masanamu."

Kisa hiki kiwe ni cha kweli au uongo au hata kama ni katika vigano, lakini ni picha ya kweli. Kwa sababu hakuna tofauti kati ya kuabudu mali na kuabudu masanamu, kila moja inamwepusha mtu na Mungu na haki.

Bali kuabudu mali kuna athari mbaya zaidi, na kuna madhara zaidi. Kwa sababu, mara nyingi sana mali ndio kiini cha matamanio na ni chimbuko la ufisadi. Wale waliozihaini nchi zao wamefanya hivyo kwa sababu ya pesa. Na wale waliowapi-ga vita Mitume na watu wema na kuibadilisha dini na sharia ya Bwana wa Mitume, walifanya hivyo baada ya kupata chochote.

Kadiri nitakavyotia shaka, lakini siwezi kutia shaka kuwa walahidi na waabudu masanamu ambao hawakuzifanyia hiyana nchi zao wala kuwafanyia njama watu wema, kuwa ni bora mara elfu, kuliko mwenye kufunga, kuswali, kuhiji na kutoa zaka lakini anapanga njama pamoja na maadui kuuza nchi na riziki za waja.

Kwa hiyo hapana ajabu kwa mtu kupata daraja mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwa kujitolea kwa mali, ambapo kutokana na kutoa huku kunaonyesha haki kuwa juu ya batili na akhera juu ya ulimwengu.

Unaweza kuuliza kuwa, mbona kauli yake Mwenyezi Mungu "Hamtapata wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda." Kwa dhahiri inafahamisha kuwa pepo haipati ila yule aliye nazo atakayejitolea vizuri katika mali, ambapo watu wengi hawamiliki chochote.

Jibu: Msemo katika Aya tukufu unamhusu mwenye nacho. Ama asiyekuwa nacho, yeye ndio anapasa achukue sio kutoa, bali yeye ni sehemu mojawapo ya kutolea hiyo mali.

Zaidi ya hayo ni kwamba, ambao wanapigana jihadi kwa nafsi zao, wana cheo zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko wale ambao wanapigana jihadi kwa mali zao. Kwa sababu, kuitoa nafsi ni ukomo wa kutoa.

Kama ambavyo Aya imefahamisha, kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu kumed-haminiwa na kutoa na kujitolea. Basi vile vile imefahamisha kwamba, mali ni chimbuko la kheri na ni njia ya kumtii Mwenyezi Mungu; kama ambavyo pia ni kiini cha matamanio na ni ya kumridhisha shetani. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) anasema: "Mwenye kuitafuta dunia kwa ajili ya kujilimbikizia na kujifaharisha atakutana na Mwenyezi Mungu akiwa amekasirika. Na mwenye kuitafuta kwa kujistahi na kuichunga nafsi yake, atakuja siku ya Kiyama uso wake ukiwa kama mbalamwezi." Imam Ali (a.s.) anasema: "Hakupewa yeyote kitu katika dunia ila hupungua fungu lake katika akhera." Mmoja wa waliokuwepo akasema: 'Sasa sisi tunaitafuta dunia (Itakuaje?)' Imam akasaili: "Mnaifanyia nini?" Akajibu: 'Kujikimu mimi, wanangu na kutoa sadaka na kuhiji.' Imam akasema: "huku si kutafuta dunia, bali ni kutafuta Akhera."

3

3

Kaashif4-14.jpgKaashif4-15.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

93.Kila chakula kilikuwa halali kwa wana wa Israil ila alichojiharamishia Israil mwenyewe kabla ya kuteremshwa Tawrat. Sema: Leteni Tawrat muisome mkiwa ni wakweli.

94.Basi wenye kumzulia uongo Mwenyezi Mungu baada ya hayo, basi hao ndio madhalimu.

Kaashif4-16.jpg

95.Sema: Amesema kweli Mwenyezi Mungu. Basi fuateni mila ya Ibrahim aliyeshikamana na haki; wala hakuwa katika washirikina

Aya 93 - 95 WANA WA ISRAIL NA CHAKULA

MAANA

Kila chakula kilikuwa halali kwa wana wa Israel.

Aya hii kwa ufupi inasimulia kwamba, Aya nyingi zinaonyesha wazi kuwa Muhammad (s.a.w) na walio pamoja naye wako kwenye mila ya Ibrahim; wanamwamini Mwenyezi Mungu na aliyoteremshiwa Ibrahim, Ismail, Is-haq,Yakub na kizazi chake. Vile vile Musa, Isa na Mitume wengineo.

Maana yake kwa dhahiri ni kwamba, kila lililokuwa haramu katika dini ya Mitume hiyo basi ni haramu katika dini ya Kiislamu. Mayahudi walikuwa wakiitakidi kuwa nyama ya ngamia na maziwa yake ni haramu katika dini ya Mitume iliyotajwa. Wakamwona Muhammad anaihalalisha na kwamba, uhalalishaji huo unapingana na kauli yake kuwa yeye yuko kwenye mila ya Ibrahim, na kwamba yeye anaami-

4

4

Kaashif4-17.jpgKaashif4-18.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

ni alichoteremshiwa Ibrahim na Mitume walio baada yake.

Kwa kutegemea madai haya, wakatangaza na kueneza habari kwa makusudio ya kutia ila na kuleta shaka katika Uislamu kwamba Muhammad anajipinga mwenyewe. Anahalalisha chakula kilichokuwa haramu katika mila ya Ibrahim, na wakati huo huo anadai kwamba yuko katika mila ya Ibrahim. Ndipo Mwenyezi Mungu akawajibu kwa kusema: "Kila chakula kilikuwa halali kwa wana wa Israel." Yaani Ibrahim na waliomfuata, hawakuharamisha nyama ya ngamia na maziwa yake, bali kila chakula kilikuwa halali kwao. Na mayahudi ni wakadhibishaji na ni wazushi katika kuwanasibishia Mitume kuwa ndio wenye kuharamisha.

Ila alichojiharamishia Israil mwenyewe.

Israel ni Yakub bin Is-haq bin Ibrahim. Alikuwa hatumii baadhi ya vyakula kwa sababu zake zinazomhusu yeye tu, si kwa sababu ya kuharamishiwa na Mwenyezi Mungu. Ni kama mtu akiamua kutovuta sigara kwa sababu za kiafya n.k. Lakini alipojizuia ikawa ni desturi ya Wana wa Israil kumfuata baba yao katika yale aliyo-jizuilia mwenyewe na hilo lilikuwa kabla ya kuteremshwa Tawrat.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ametaja hivyo, kwa sababu aliwaharamishia vitu vingi baada ya Tawrat kutoka na dhambi walizozifanya; kama asemavyo Mwenyezi Mungu: "Basi kwa dhuluma ya Mayahudi tuliwaharamishia vitu vizuri walivyohalal-ishiwa, na kwa sababu ya kuzuilia kwao njia ya Mwenyezi Mungu kwa wingi" (4:160).

Ama aina ya vitu walivyoharamishiwa baada ya kuteremshwa Tawrat vimetajwa na Aya hii: "Na kwa wale walio mayahudi tuliharamisha kila(mnyama) mwenye kucha, na katika ng'ombe na kondoo tukawaharamishia mafuta yao isipokuwa yale iliyobeba migongo yao au matumbo au ile iliyogandamana na mifupa. Tuliwalipa hivyo kwa uasi wao. "Na hakika sisi ndio wa kweli."(6:146) Ufafanuzi zaidi utaku-ja mahali pake.

Kwa ujumla ni kuwa Waislamu wameafikiana kwa kauli moja kwamba asili ya kila kitu ni halali mpaka ithibiti kinyume chake.

Sema: Leteni Tawrat muisome mkiwa ni wenyewe kusema kweli.

Hii ni kujadiliana na mayahudi kwamba walete Tawrat ambayo ndiyo wanay-oitegemea waisome kadamnasi, wakiwa wanasema kweli katika madai yao ya uharamu wa ngamia au wengineo. Lakini wao baada ya pambano hili waliingia gizani na hawakuwa na ushujaa wa kuileta Tawrat, kwa sababu wao walikuwa wana yakini kabisa na ukweli wa Mtume (s.a.w) na uongo wao.

Mwenye kumzulia uongo Mwenyezi Mungu baada ya hayo.

Yaani baada ya kudhihiri hoja na kusimama dalili ya haki.

5

5

Kaashif4-19.jpgKaashif4-20.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Basi hao ndio madhalimu.

Kwa sababu wamepotea na kuwapoteza wengine kwa kuing'ang'ania na kuipinga haki.

Sema: amesema kweli Mwenyezi Mungu. Kwamba kila chakula kilikuwa halali kwa wana wa Israil na kwamba Muhammad ni Mtume wa haki.

Basi fuateni mila ya Ibrahim aliyeshikamana na haki.

Hapana budi kuashiria kwamba Muhammad (s.a.w) alikuwa katika mila ya Ibrahim na mila ya Mitume yote katika itikadi na misingi. Ama katika sharia alikuwa ni tofauti, ingawaje sharia zote zinasimamia masilahi, lakini masilahi yanatofautiana kulingana na hali ya mazingira na mnasaba. Kuafikiana sharia katika kuhalalisha chakula, hakuwezi kukulazimisha kuwa sharia moja katika pande zote.

Vyovyote iwavyo, ni kwamba makusudio ya Aya tulizozifafanua ni kuwakadhibisha mayahudi yale waliyowasingizia Mitume katika kuharamisha baadhi ya vyakula.

96.Hakika nyumba ya kwanza waliy-owekewa watu ni ile iliyoko Makka yenye kubarikiwa na mwongozo kwa viumbe.

97.Mna humo ishara zilizo wazi: Mahali aliposimama Ibrahim. Na mwenye kuingia humo huwa katika amani; Na ni haki ya Mwenyezi Mungu juu ya watu kuhiji nyumba hiyo kwa mwenye kuweza njia ya kuiendea. Na atakayekufuru, basi Mwenyezi Mungu si muhitaji wa viumbe.

NYUMBA YA KWANZA Aya 96 - 97 LUGHA

Neno 'Awwal' (Mwanzo) ni jina la kitu ambacho kimepatikana kwanza, ni sawa kipatikane kingine baadaye au la. Husemwa 'Ni mara yangu ya kwanza kuja hapa,

Kaashif4-21.jpg

6

6

Kaashif4-22.jpgKaashif4-23.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

na hii ndiyo mali yangu ya kwanza kuipata'.

Neno Bakka lina maana ya Makka mara nyingi herufi 'Ba', huja mahali pa Miim. Na Maana ya neno Bakka ni msongamano: watu huko Makka hupigana vikumbo kwa sababu ya wingi wao.

Arrazi katika Tafsir yake amenakili Riwaya kwamba Imam Baqir (a.s.) alikuwa akiswali Al -Kaaba. Mwanamke mmoja alipita mbele yake. Mtu mmoja akataka kumzuwia. Imam akamwambia : Mwache, hapa Makka panaitwa Bakka (msongamano) kwa sababu watu wanasongamana. Mtu anapita mbele ya mwanamke akiwa anaswali na Mwanamke naye anapita mbele ya mwananamume. Hilo hali-na ubaya kwa hapa.

MAANA

Hakika nyumba ya kwanza waliyowekewa watu ni ile iliyoko Makka.

Yameshatangulia maelezo kwa ufafanuzi zaidi - katika kufasiri Aya ya 142 na zina-zofuatilia katika Sura ya Pili (Baqara) - kuhusu waliyosema Mayahudi juu ya kugeuza Qibla kutoka Baytul-Muqaddas na kuwa Al-Kaaba.

Aya hii tuliyonayo inafugamana na Aya hizo za Sura ya (Baqara), hasa kauli ya wapumbavu: "Nini kilichowageuza kutoka Qibla chao walichokuwa wakikielekea ?" (2:142)

Kauli yake Mwenyezi Mungu "Hakika nyumba ya kwanza waliyowekewa watu," haina maana kwamba hiyo ndiyo nyumba ya kwanza duniani. Bali kwa dhahiri ni nyumba ya kwanza ya ibada. Kwa sababu watu wote wanashirikiana ndani yake. Kimsingi ni kwamba watu wote hawashirikiani katika nyumba moja, isipokuwa masuala ya kiujumla; kama vile ibada na twaa.

Baadhi ya wafasiri wamechafua kurasa katika kupekua na kunukuu kauli kuhusu Al-Kaaba, kwamba je, ndiyo nyumba ya kwanza kujengwa duniani au sio. Kwa hakika, hakuna faida yoyote ya utafiti huu. Kwa sababu hayaungani na msingi wa dini au matawi yake. Wala hakutakiwi kuitakidi ndio au hapana.

Yenye kubarikiwa,na mwongozo kwa viumbe.

Makusudio ya baraka hapa ni kuzidishiwa thawabu. Mtume (s.a.w) amesema: "Fadhila za Masjidul-haram, juu ya Msikiti wangu ni kama fadhila za msikiti wangu juu ya misikiti mingine." "Swala ya Msikiti wangu huu ni bora kuliko swala elfu za misikiti mwingine." "Mwenye kuhiji na asifanye uchafu au ufasiki, atatakasika kutokana na dhambi zake kama siku aliyozaliwa na mama yake." "Hijja safi haina malipo ila pepo." Na mengineyo mengi.

Ama kwamba ni uongofu kwa viumbe ni kwamba inakumbusha Mwenyezi Mungu na inaleta unyeyekevu.

7

7

Kaashif4-24.jpgKaashif4-25.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Mna humo ishara zilizo wazi: Mahali aliposimama Ibrahim.

Ni kama vile muulizaji ameuliza ni ipi dalili ya kwamba Al-Kaaba ni ya zamani, na kwamba ndiyo nyumba ya kwanza ya ibada na wala sio Baitul-Muqadas?

Aya hii inafaa kuwa ni jibu la swali hili, kwa sababu Ibrahim ni wa zamani naye ndiye aliyejenga Al-Kaaba. Kwa hiyo itakuwa ndiyo ya kale iliyotangulia kutokana na ukale wa mjenzi wake. Ama Baitul-Muqadas, ilijengwa na Nabii Suleiman nayo inaitwa mahali pa kuabudia pa Suleiman' mpaka sasa. Na kati ya Suleiman na Ibrahim kulipita karne nyingi. Mwenye tafsir Al-Manar amenukuu kutoka vitabu vya Mayahudi kwamba Suleiman alijenga Baitul-Muqadas miaka 1005 B.C. (Kabla ya kuzaliwa Isa)

Dalili ya kwamba Ibrahim ndiye aliyeijenga Al-Kaaba, ni athari za waziwazi zilizoko mpaka sasa; kama vile Maqam Ibrahim (Mahali aliposimama Ibrahim). Waarabu bado wananukuu kwa njia Mutawatir kutoka vizazi na vizazi kwamba sehemu hii maalum ya Msikiti ni sehemu aliyokuwa akisimama Ibrahim kuswali na kufanya ibada.

Kwa hivyo, kama linavyofahamisha jina la Msikiti wa Suleiman kwamba aliyeijenga Baitul Muqadas ni Suleiman, vile vile jina la Maqam Ibrahim, linafahamisha kuwa yeye ndiye aliyeijenga Al-Kaaba; na kwamba hiyo Al-Kaaba ndiyo iliyotangulia, kwa kuwa Ibrahim ametangulia.

Na mwenye kuingia humo huwa katika amani.

Imekwishapita tafsir yake katika (2:125) Na hayo ni fadhila ya dua ya Ibrahim.

Na ni haki ya Mwenyezi Mungu juu ya watu kuhiji nyumba hiyo kwa mwenye kuweza njia ya kuiendea.

Uwezo uko namna mbili: Kiakili, ambao ni uwezekano wa kufika Makka. Hilo sio sharti. Na wa Kisheria, ambao ni uwezo wa kiafya, usalama wa nafsi, mali na uwezekano. Hayo yakikamilika, Hijja inakuwa ni lazima. Ufafanuzi uko katika vitabu vya Fiqhi.

Na atakayekufuru, basi Mwenyezi Mungu si muhitaji wa viumbe.

Makusudio ya neno 'Kufru' hapa ni kukanusha kama tukilirudisha kwenye Al-Kaaba kwamba ndiyo nyumba ya kwanza ya ibada, au kwenye kutoitakidi wajibu wa Hijja. Na yatakuwa makusudio yake ni ufasiki kama tukilirudisha kwenye kuacha Hijja kwa kupuuza.

Kaashif4-26.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Kaashif4-27.jpg

98.Sema: Enyi watu wa Kitabu! Kwa nini mnazikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na hali Mwenyezi Mungu ni shahidi juu ya muyatendayo!

99.Sema: Enyi watu wa Kitabu! Kwa nini mnawazuilia njia ya Mwenyezi Mungu walioamini? Mkaitafutia kosa na nyinyi mnashuhudia. Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na muyatendayo

 

Aya 98 - 99KUKANUSHA DALILI NA ISHARA ZA MWENYEZI MUNGU

MAANA

Qur'an imejishughulisha sana na watu wa Kitabu, ikawateremeshia Aya kadha wa kadha zinazowakumbusha Tawrat na Injil na kuwaaibisha, kwa sababu ya kuzigeuza; ikawajadili kwa namna nzuri na kuwaelezea makosa yao mengi na dhambi zao.

Miongoni mwa Aya hizo, ni Aya hizi mbili:

Ya kwanza ni: "Sema: Enyi watu wa Kitabu! Kwa nini mnazikanusha ishara za Mwenyezi Mungu ambazo zimefahamisha Utume wa Muhammad (s.a.w); na kwamba Al-Kaaba ndiyo nyumba ya kwanza kuwekewa watu kwa ibada, pamoja na kuwa ishara hizo na hoja hizo ziko wazi kama jua, na hawezi kuzikanusha isipokuwa mwenye kiburi."

Ya pili ni "sema: Enyi watu wa Kitabu! Kwa nini mnawazuilia njia ya Mwenyezi

Mungu walioamini? Mkaitafutia kosa." Hawakutosheka na kufanya ufisadi hao

wenyewe, mpaka wakajishughulisha kuwaharibu wengine na kuwapoteza. Kwa

hiyo wamechanganya upotevu na kupoteza, na ufisadi na kuwafanya wengine

wawe wafisadi. Kila mfisadi anatamani na kufanya kadiri ya uwezo wake ili kuwe

na mafisadi wengi kwa kutumia misingi ya Iblis aliposema:

"Kwa kunihukumu kupotea, basi nitawapambia katika ardhi na nitawapoteza wote."

(15:39)

Tusisahau ishara ya aina hii ya upole wa kuwaambia watu wa Kitabu, na

kuwakumbusha vizuri kuwa wao ni watu wa dini na Kitabu, ili angalau waweze

kusikia mawaidha na kuongoka.

9

9

Kaashif4-28.jpgKaashif4-29.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

100.Enyi mlioamini! Mtakapotii kikundi katika watu wa Kitabu watawarudisha kuwa makafiri baada ya kuamini kwenu.

101.Na vipi mnakufuru na nyinyi mnasomewa Aya za Mwenyezi Mungu na Mtume wake mnaye? Na mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu basi ameon-gozwa katika njia iliyonyooka.

102.Enyi mlioamini mcheni Mwenyezi Mungu ipasavyo kum-cha; wala msife isipokuwa mmekuwa waislamu.

103.Na Shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msifarikiane; na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu juu yenu mlipokuwa maadui naye akaziunganisha nyoyo zenu; hivyo kwa neema yake mkawa ndugu; na mlikuwa ukingoni mwa shina la moto naye akawaokoa nalo. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyozibain-isha Aya Zake ili mpate kuongo-ka.

Kaashif4-30.jpg

10

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

..

Aya 100 - 103kUWATII MÂKAFIRİ.

MAANA

Enyi mlioamini! Mtakapotii kikundi katika watu wa Kitabu, watawarudisha kuwa makafiri baada ya kuamini kwenu.

Katika Aya mbili zilizotangulia, Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewahadharisha watu wa Kitabu kuipinga haki pamoja na kuwazuia waumini na njia Yake Mwenyezi Mungu.

Katika Aya hii, Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anawahadharisha waumini wasiwasikilize makafiri katika watu wa Kitabu wanaojaribu kuwapoteza waumini na kuwafitini na dini yao.

Imepokewa Riwaya kwamba, sababu za kushuka Aya hii ni kuwa baadhi ya mayahudi walikusudia kuirudisha tena fitna iliyokuwepo baina ya kabila la Ansar na Khazraj wasiwe na umoja baada ya Mwenyezi Mungu kuwaweka pamoja kwenye Uislamu. Kwa hiyo, makafiri wakawa wanawakumbusha uadui na mapigano waliyokuwa nayo wakati wa ujahiliya. Hasa siku ya vita ya Bughat ambayo Aus na Khazraj waliuana, na ushindi ukawa wa Aus. Mori ukawapanda wakawa karibu wapigane kama si kuwahi Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w).

Aya inafungamana na tukio hili, kama ambavyo inafungamana na jaribio la wahu-biri wa Kikristo wakati huu; na majaribio yote ambayo baadhi ya watu wa Kitabu na wengineo katika kutawanya umoja wa waislamu na kuwaepusha na dini yao, uza-lendo wao, na uhuru wao na kuwa windo la kila mnyang'anyi.

Haya ndiyo wayafanyao wakoloni wa Kimagharibi kwa waarabu. Na kazi hiyo hawaifanyi peke yao, bali wanashirikiana na vibaraka duni ambao wanawatii na kuwafuata; na waliokufuru dini yao baada ya kuamini na kuiuza nchi yao. Kwa hivyo basi, Aya inafungamana na vibaraka hawa na pia inafungamana na wanaohubiri fitina na ufisadi na wakapendelea ukafiri na upotevu. Ni sawa wawe ni katika watu wa Kitabu au wengineo; wa Mashariki na Magharibi. Vile vile, Aya hii inafungamana na wanawake wetu wanavyoiga wanawake wa kimagharibi katika kujiremba na kujipodoa, na vijana wetu katika kudharau dini na mwendo wa dini. Vile vile desturi zote za madhara na haramu tulizoziiga kutoka kwa wageni.

Aya kwa dhahiri inakataza kuwatii makafiri katika kufuru na kurtadi. Lakini, linalos-ababisha hilo linaenea katika kila uigaji unaomkasirisha Mwenyezi Mungu na Mtume.

Na vipi mnakufuru na nyinyi mnaosomewa Aya za Mwenyezi Mungu na

Kaashif4-31.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Mtume Wake mnaye.?

Yaani, haitakikani kwa Mwislamu kuathirika na kuwa katika upotevu wa wapoteza-ji, na kuwafuata makafiri katika desturi zao na hulka zao wakati ambapo yeye mwislamu anasoma Qur'an Tukufu na kumsikiliza Mtume Mtukufu, anayembain-ishia haki na kumuondolea kila shubha.

Anasema Nidhamuddin Al-Hasan Muhammad Annaisaburi katika Tafsir, Gharaibul-Qur'an: "Ama Kitabu kitabaki milele. Na Mtume (s.a.w) ingawaje amekwenda kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu, lakini nuru yake imebaki. Kwa sababu, kizazi na warithi wake wanakaimu nafasi yake. Kwa sababu hii ndipo Mtume akasema: "Mimi ninawaachia vizito viwili ambavyo kama mkishikamana navyo hamtapotea: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu."

Na mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu, basi ameongozwa katika njia iliyonyooka.

Kushikamana na Mwenyezi Mungu ni kushikamana na dini; dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni uislamu, nayo ndiyo hasa njia iliyonyooka. Makusudio ni kuwa mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu kwa haki kabisa, hawezi wala hataweza kuuwacha uislamu kwa namna yoyote ya majaribio na hadaa zitakavyokuwa.

Unaweza kuuliza: Imekuja Aya isemayo "Hakika Mola wangu yuko juu ya njia iliyonyooka." (11:56) Na wewe unafasiri kuwa njia iliyonyooka ni uislamu. Kwa hiyo itakuwa Mwenyezi Mungu yuko kwenye dini ya kiislamu.

Jibu: Hakika njia iliyoonyooka ikinasibishwa kwa mja, inakusudiwa uislamu. Ama ikinasibishwa kwa Mwenyezi Mungu inakusudiwa uadilifu na hekima; yaani yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu anapanga mambo kwa uadilifu na hekima Yake.

Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu ipasavyo kumcha; wala msife isipokuwa mmekuwa waislamu.

Kila mwenye kufanya ya wajibu na kujiepusha na mambo ya haramu, basi ndio amemcha Mwenyezi Mungu ipasavyo kumcha. Haya ndiyo maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu: "Mcheni Mwenyezi Mungu muwezavyo" (64:16)

Kwa sababu, lisilowezekana halikalifiwi na sharia. Na kila lisilowezekana kukalifi-wa, basi liko nje ya kumcha Mwenyezi Mungu. Ama kauli yake Mwenyezi Mungu "Msife isipokuwa mmekuwa waislamu;" ni kukataza kuacha uislamu na kuamrisha kuwa imara nao mpaka siku ya kifo.

Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msifarikiane.

Kamba ni maarufu; na makusudio yake hapa ni uislamu. Maana ya Aya nzima, ni

12

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

kuwa maadam waislamu ni wafuasi wa dini moja, Mtume mmoja na Kitabu kimo-ja, basi ni juu yao wote kuuchunga mfungamano huu wa kidini ambao ndio wenye nguvu zaidi kuliko mfungamano wa nasaba, na kuwa na hima nao; wala wasi-gawanyike vikundi.

Unaweza kuuliza: Je, mwito huu wa muungano wa kidini si aina ya ubaguzi wa dini?

Jibu: Hapana, mwito huu wa mshikamano wa wafuasi wa dini moja ni sawa na mwito wa mshikamano wa wanachama wa chama kimoja, au wa wafamilia moja. Mshikamano huu haulazimishi kuwabagua wengine. Bali ni kinyume na hivyo kati-ka uislamuu, ambapo unatoa mwito wa kuwapenda na kuwahurumia watu wengine bila ya kuangalia dini zao, fikra zao au kabila zao. Kwa hivyo basi undugu wa Kiislamu ni nguzo ya udugu wa kibinadamu.

Kwa ujumla ni kwamba kundi ambalo ni wajibu kusaidiana nalo, ni lile lililojiku-sanya na kusaidiana katika jambo lililo na radhi ya Mwenyezi Mungu na masilahi ya watu. Ama kukutana kusikokuwa na faida yoyote ya kuridhisha hakutakikani.

Imam Ali (a.s.) anasema: "Utengano ni kwa watu wa batili hata wakiwa wengi. Na kuungana ni kwa watu wa haki hata wakiwa wachahe." Na hiyo ndiyo tafsir ya Hadith mashuhuri: "Msaada wa Mwenyezi Mungu uko pamoja na wengi." Yaani kuwahusu wanaojumuika na kusaidiana kwa jambo la haki. Ama ikiwa ni kwa jambo la batili; basi hawatakuwa na yeyote zaidi ya shetani.

Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu juu yenu mlipokuwa maadui naye akaziunganisha nyoyo zenu; hivyo kwa neema yake mkawa ndugu.

Mwenyezi Mungu anawakumbusha waislamu wa kwanza vile walivyokuwa na misukusuko ya vita, bughudha na vita vya kuendelea, kama vile vita vya Aus na Khazraj vilivyodumu kwa muda wa miaka mia moja na ishirini, kama ilivyoelezwa kwenye Tafsir Tabari. Basi Mwenyezi Mungu akaziunganisha nyoyo zao kwa bara-ka ya uislamu mpaka wakawa ni ndugu wanaohurumiana na kunasihiana.

Jafar bin Abu Talib katika mazungumzo yake na Najjash alimwambia: "Tulikuwa watu wa ujahilia (ujinga) tukiabudu masanamu, tukila mizoga, tukifanya maovu, kuvunja undugu, kumfanyia uovu jirani na mwenye nguvu akimuonea mny-onge. Tulikuwa hivyo mpaka Mwenyezi Mungu akatuletea Mtume atokanaye na sisi; tunayemjua nasaba yake, ukweli wake, uaminifu na usafi wake. Akatulingania kwa Mwenyezi Mungu ili tumwabudu yeye peke yake na tuachane na kuabudu wasiokuwa Yeye - mawe na masanamu. Akatuamrisha kusema kweli, kutekeleza amana, kuunga undugu, kumfanyia wema jirani na kujizuia na haki za watu na damu (zao). Akatukataza kufanya maovu, kusema uongo, uzushi, kula mali ya yatima na kuwavunjia heshima wanawake wanaojistahi. Akatuamrisha tumwabudu Mwenyezi Mungu na kutomshirikisha na chochote. Pia akatuamrisha

13

3. Sura Al-Imran

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

kuswali, kutoa Zaka na kufunga."

Na mlikuwa ukingoni mwa shimo la moto naye akawaokoa nalo.

Yaani mlikuwa karibu na moto wa Jahannam, kwa ukafiri wenu, Mwenyezi Mungu akawaokoa nao kwa baraka ya Muhammad (s.a.w).

Kaashif4-32.jpg

104.Na liwepo miongoni mwenu kundi lenye kulingania kwenye heri, na kuamrisha mema na kukataza maovu. Na hao ndio wenye kufaulu

KUAMRISHA MEMA Aya 104

Makusuido ya heri hapa ni uislamu, na mema ni kumtii Mwenyezi Mungu, na maovu ni kumwasi. Maana yanayopatikana ni kwamba hapana budi kupatikane kundi la watu litakalowalingania wasiokuwa waislamu kwenye uislamu; kwenye lile linalomridhisha Mwenyezi Mungu, analolilipa thawabu na kuacha lile linalomkasirisha analoliletea adhabu.

Tamko kutokana na nyinyi katika Aya hii inafahamisha wajibu wa kuamrisha mema kwa njia ya kutosheana (kifaya). Yaani, wakilisimamia hilo baadhi, utakuwa wajibu umewaondokea wengine. Wala si lazima kuwa mwenye kutekeleza umuhimu huu, awe mwadilifu. Hapana, si hivyo, kwa sababu mbili:

Kwanza, kwamba sharti ya hukumu ni sawa na hukumu yenyewe, haithibiti ila kwa dalili wala hakuna dalili ya sharti ya uadilifu hapa; si kutoka katika Qur'an, Hadith au kutoka katika akili.

Pili, hukumu ya kuamrisha mema haitegemei maasi au utiifu wa mwengine katika hukumu.

Mafakihi wengi wameshartisha wajibu wa kuamrisha mema kuwa mwenye kuamrisha awe atakuwa salama, kiasi ambacho hatapata madhara yoyote kwa kuamrisha mema na kukataza maovu.

Lakini sharti hili haliingi sehemu zote, kwani, kupigana na anayetupiga kwa ajili ya dini yetu na nchi yetu ni wajibu, ingawaje tunafahamu kwamba, kwa kawaida kupigana huleta madhara.

14

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Inafaa kwa kila mtu kuyatoa mhanga maisha yake, akiwa na yakini kwamba kuji-toa mhanga huku kuna maslahi ya umma. Faida ya watu na nchi ni muhimu na adhimu zaidi kuliko maisha yake, bali hilo linashukuriwa mbele ya Mwenyezi Mungu na kwa watu. Kuna Hadith isemayo: "Jihadi bora zaidi ni tamko la haki mbele za Sultan dhalimu."

Kwa ufupi ni wajibu kukinga madhara yakiwa hayatakuwa na faida yoyote. Vyenginevyo, itajuzu kuyavumilia; kama inavyojuzu kwa mtu kukata kiungo kibovu katika viungo vyake kwa kupigania uhai wake na kuhofia kumalizika.

Zaidi ya hayo, mifumo ina athari zake. Baadhi ya mifumo inaifukuza haki na kumsababishia mtu matatizo. Na mingine inalazimisha fikra kwa msikilizaji bila ya kujitambua. Mwenye akili na hekima anafanya kulingana na hali ilivyo ya taratibu au ya nguvu.

Firaun alikuwa na ukomo wa Usultani na kupetuka mipaka; Musa na Harun hawakuwa hata na msaidizi, lakini pamoja na hayo waliamrishwa kumlingania kwenye haki. Lakini kwa njia ya upole. Hata Muumba wa ulimwengu, (ambaye limetukuka neno lake) mara nyingine amewaambia waja wake kwa vitisho na kusema: "Hakika nyinyi hamtanusuriwa nasi." (23:65) Mara nyingine hutumia upole na kusema:

"Je, hampendi Mwenyezi Mungu awasamehe na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe Mwenye kurehemu." (24:22)

Kwa ujumla kutangaza mwito wa uislamu kwa watu, na waislamu kuamrishana mema na kukatazana mabaya, ni katika nguzo za uislamu. Kwa hiyo kunawa-jibisha kuwapo kwa kikundi kitakachosimamia umuhimu huu, sawa na kulazimika kuwapo uongozi utakaosimamia amani na nidhamu, wafanya kazi wa viwandani, wakulima na wengineo ambao wanachangia maisha.

Huu ni msingi wa kila dini, kila dhehebu na kila fikra. Kwa sababu, hiyo ndiyo njia nzuri ya kueneza mwito, kupata ushindi na kuwazuia maadui. Angalia jinsi watu wa siasa na uchumi wanavyotilia umuhimu vyombo vya habari, kuvikuza na kuvi-tolea mamilioni ya mapesa na kufanya mizinga na habari kuwa bega kwa bega.

Hawakufanya hivyo ila ni kwamba wametambua, kutokana na uzowefu wao, kwamba habari ni silaha yenye nguvu kuliko mizinga na mabomu. Mmoja wa wakuu wa mapatano alisema baada ya kufaulu kwao katika vita vya ulimwengu: "Tumeshinda katika vita kwa mabomu ya karatasi." Yaani magazeti

Unaweza kuuliza, kwamba unawezaje kuziunganisha Aya hizi mbili:

"Na wawepo katika nyinyi watu wanaolingania kwenye heri na wanaoamrisha

mema na kukataza maovu." Na Aya isemayo:

"Enyi mlioamini! Jiangalieni nafsi zenu hatawadhuru aliyepotea ikiwa mmeongo-

ka." (5:105) Ambapo ya kwanza imefahamisha wajibu wa kuamrisha mema na ya

pili imefahamisha kutokuwepo wajibu huo kutokana na neno "Jiangalieni nafsi

zenu."

15

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Jibu: Makusudio ya Aya ya pili, ni kwamba mwenye kutekeleza wajibu wa kuamr-isha mema na kukataza mabaya, hatadhuriwa na upotevu wa aliyepotea wala upinzani wa mpinzani, maadamu yeye anaetekeleza wajibu wake tu, "Hakika ni juu yako kufikisha tu, na juu yetu ni kuhisabu." (13:40)

Swali la pili: kuna Hadith mashuhuri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) ise-mayo: "Mwenye kuona katika nyinyi uovu, na auondoe kwa mkono wake, akishindwa, basi (auondoa) kwa ulimi wake, akishindwa basi ni kwa moyo wake na hilo ni katika udhaifu zaidi wa imani."

Mpangilio huu unapingana na ilivyo desturi ya sharia, kiakili na kimazoweya; kwamba kuondoa uovu kunaanzia kwa ulimi halafu ndio vita. Sasa kuna wajihi gani wa kauli hii ya Mtume?

Jibu: Kuna tofauti kubwa sana baina ya kuondoa uovu na kukataza uovu, kwani kukataza uovu aghlabu ni kabla ya kutokea uovu wenyewe; ni kama vile kukinga, kama kuona kuwa mtu fulani anafikiria kuiba, ukamkataza kufanya wizi huo.

Ama kuondoa uovu, kunakuwa baada ya kutokea uovu wenyewe. Kwa mfano umejua kuwa mtu fulani ameiba mfuko wa mtu mwengine, hapo ukiwa unaweza kumnyang'anya na kumrudushia mwenyewe, basi ni wajibu kwako kulifanya hilo wewe mwenyewe, ikiwa kuna uwezekano wa kumyang'anya mwizi; na wewe usi-weze kupata madhara. Kama hukuweza ni wajibu kwako kumwamrisha mwizi aurudishe kwa mwenyewe na kumkataza kuuzuwia. Kama utashindwa na vishin-do vya mwizi, basi usikiridhie kitendo chake - baina yako na Mola wako. Kwa hivyo maudhui ya Hadith ni kugeuza uovu, si kukataza uovu.

1.Imeelezwa katika Tafsir Al-Manar kwamba Sheikh Muhammad Abduh alipokuwa akifasiri Aya hii katika darsa, miongoni mwa aliyoyasema ni: "Ni juu ya kila mtu kuamrisha mema kiasi cha uwezo wake."Akatoa mfano wa shia kuwa wao wanashikamana na msingi huu, wala hawaiachi fursa yoyote inapopatikana. Akatoa ushahidi wa hilo kuwa alipokuwa Beirut alihitajia mnyonyeshaji kwa ajili ya mtoto wake wa kike. Akaletewa mwanamke wa Kishia. Huyu mwanamke akawa anawalingania wake wa Sheikh kwenye madhehebu yake.

16

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

105.Wala msiwe kama wale walio-farakana wakahitalifiana baada ya kuwajia wao dalili zilizo wazi; na hao ndio wenye adhabu kubwa.

106.Siku ambayo nyuso zitang'aa na nyuso (nyingine) zitasawijika. Na ama ambao nyuso zao zitasawijika, (wataambiwa): Je mlikufuru baada ya kuamini kwenu? Basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakanusha.

107.Na ama ambao nyuso zao zitang'aa, watakuwa katika rehe-ma ya Mwenyezi Mungu. Wao humo watadumu.

108.Hizo ni Aya za Mwenyezi Mungu, tunakusomea wewe kwa haki; na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu viumbe.

109.Ni vya Mwenyezi Mungu vilivy-omo ardhini na vilivyomo mbin-guni; na kwa Mwenyezi Mungu hurejezwa mambo yote.

Kaashif4-33.jpg

17

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

KUHITALIFIANA BAADA YAMTUME Aya 105 109

MAANA

Wala msiwe kama wale waliofarakana wakahitalifiana baada ya kuwajia wao dalili zilizo wazi/

Aya hii inamalizia kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote ."

Makusudio ya wale waliofarakana ni watu wa Kitabu. Ambapo mayahudi walichangukana vikundi sabini na moja baada ya Mtume wao Musa. wakristo wakawa vikundi sabini na mbili baada ya Mtume wao Isa. Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu. "Baada ya kuwajia hoja iliyo wazi," inafahamisha kwamba mtu haadhibiwi kwa kuiacha haki na kufuata batili, ila baada ya kubainishiwa hoja.

Ama siri ya mkazo huu na kuupa kipaumbele muungano wa umma, ni kuwa utengano ndio kiini cha ufisadi na kwamba umma uliotengana hauwezi kuwa na maisha mazuri, wachilia mbali kuuita umma mwingine kwenye kheri.

Pamoja na kuwapo Riwaya nyingi, na Hadith zinazohimiza muungano wa waisla-mu, lakini bado wamefarakana na kuwa vikundi mbali mbali, wamewazidi mayahudi kwa vikundi viwili zaidi na wakristo kikundi kimoja; kama ilivyoelezwa katika Hadith mashuhuri.

Kuna Hadithi nyingine isemayo: "Mtakuwa na desturi ile ile ya waliokuwa nayo kabla yenu."

Akaulizwa: "Unakusudia mayahudi na manaswara ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?" Akasema: "Kumbe ninawakusudia kina nani? Utachanguka uthabiti wa waislamu."

Katika kitabu Al-Jam'u Bainas-Sahihayni cha Hamid, kwenye Hadith Na. 131, anasema: Katika yaliyoafikianwa kutoka Musnad ya Anas bin Malik, amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w): "Watanijia watu miongoni mwa sahaba zangu kwenye hodhi, nitakapowaona na watakapokuwa wanaletwa kwangu watazuiwa ili wasinifikie. Hapo nitasema: 'Ewe Mola! Sahaba zangu, sahaba zangu!' Nami nitaambiwa: 'Wewe hujui walizua nini baada yako.'"

Katika kitabu hicho hicho Hadith Na. 267 anasema: "Katika yaliyaofikianwa kutoka Musnad ya Abu Huraira kutoka katika njia mbali mbali, ni kwamba Mtume amesema: "Wakati nikiwa nimesimama - siku ya Kiyama - litatokea kundi la watu mpaka nitakapowatambua, atatokea mtu baina yangu na yao na awambie: 'Haya twen-deni.' Mimi nitauliza: Mpaka wapi? Naye aseme: 'Mpaka motoni.' Nami niulize wana nini? Naye ajibu: 'Hakika wao walirtadi baada yako.'"

18

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Siku ambayo nyuso zitang'aa na nyuso (nyingine) zitasawijika.

Makusudio ya Siku, ni Siku ya Kiyama. Kung'aa uso, ni fumbo la kuonyesha fura-ha ya mumin kufurahia radhi za Mwenyezi Mungu na fadhila Zake. Kusawijika uso ni huzuni ya kafiri na fasiki kwa ghadhabu na adhabu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu

Na ama ambao nyuso zao zitasawijika, (wataambiwa) "je, mlikufuru baada ya kuamini kwenu?"

Arrazi, Tabari na wafasiri wengine wengi wamenukuu kutoka kwa baadhi ya walio-pita, kwamba makusudio ya watakaoambiwa hivyo ni Khawariji. Kwa sababu Mtume alisema kuwahusu: "Hakika wao watachomoka kutoka katika dini, kama unavyochomoka mshale kutoka katika uta (upinde)." Lakini dhahiri ya Aya inamku-sanya kila mwenye kukufuru baada ya imani, wakiwemo Khawariji, watu wa bid'a na wenye maoni potofu. Kwa vile adhabu haihusiki tu na aliyekufuru baada ya imani bali inamuhusu kafiri yeyote, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: Onjeni adhabu, kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakanusha.

Na ama ambao nyuso zao zitang'aa, watakuwa katika rehema ya Mwenyezi Mungu, wao humo watadumu.

Rehma ya Mwenyezi Mungu ni Pepo. Kwa ufupi ni kwamba wale ambao wameshikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu, na kufanya mambo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na wakasaidiana kwenye mambo ya kheri na ya masilahi ya umma, basi watafufuliwa kesho wakiwa watukufu, wenye furaha na wenye kurid-hia.

Ama wale ambao wamehitalifiana kwa kuipupia dunia, wasiojishughulisha na dini wala umma au nchi, na ambao hawajishughulishi na lolote isipokuwa masilahi yao na ya watoto wao tu, basi wao watafufuliwa Siku ya Kiyama wakiwa madhalili, wenye hasara na makazi yao ni Jahanam, nayo ni marejeo mabaya kabisa.

Ajabu ya maajabu ni kwamba baadhi ya wenye nyuso zilizosawijika wanadai kuwa wanamzungumzia Mungu na kutumia Jina lake, lakini mtu akiwaambia "Muogopeni Mungu" wao husema: "Umemkufuru Mwenyezi Mungu." Aliyewatangulia katika hilo ni Abdul Malik bin Marwan aliposema pale alipochukua Ukhalifa: "Kuanzia leo atakayeniambia muogope Mwenyezi Mungu nitamkata kichwa chake."

Hizo ni Aya za Mwenyezi Mungu, tunakusomea wewe kwa haki.

Hizi, ni ishara ya Aya zinazoelekezea kuneemeshwa watu wema na kuadhibiwa makafiri. Msemo unamwelekea Muhammad (s.a.w),

muulizaji anaweza kuuliza: "Kuna faida gani katika habari hii, ikiwa Muhammad anajua kwa yakini kwamba Aya hizi ni haki na ni kweli?"

Jibu: Ni kawaida ya Qur'an kulikariri hilo katika Aya kadhaa. Na makusudio sio

19

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

kwa Muhammad hasa, bali ni kwa yule anayetia shaka na kudhani kwamba Aya hizi na mfano wake zinatoka kwa Muhammad, si kwa Mwenyezi Mungu.

"Na hukuwa mwenye kusoma kitabu chochote kabla ya hiki wala hukukiandika kwa mkono wako wa kuume, ingekuwa hivyo wangefanya shaka wabatilifu." (29:48)

Na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu viumbe.

Kwa sababu dhuluma ni mbaya na Mwenyezi Mungu ameepukana nayo. Aya hii ni dalili ya mkato kwamba Mwenyezi Mungu hakalifishi mja asiloliweza.

110.Mmekuwa ni umma bora mliotolewa kwa watu, mnaamr-isha mema na kukataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu. Na lau watu wa Kitabu wangeliamini ingekuwa heri kwao. Katika wao kuna wanaoamini na wengi wao ni wafasiki.

Kaashif4-34.jpg

111.Hawatawadhuru isipokuwa kuwaudhi tu, na wakipigana nanyi watawakimbia, kisha hawatasaidiwa.

UMMA WA MUHAMMAD Aya 110 - 111

 MAANA

Mmekuwa ni umma bora mliotolewa kwa watu, mnaaamrisha mema na kukataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu

Kuna njia kadhaa kuhusu Aya hii, kama ifuatavyo:

1) Katika makusudio ya umma, hakuna mwenye shaka kuwa makusudio ya umma

20

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

hapa ni Umma wa Muhammad (s.a.w), kwa dalili ya mfumo wenyewe wa maneno ulivyo na mtiririko wa misemo inayoelekezwa kwa waumini; kama vile; "Enyi ambao mmeamini mcheni Mwenyezi Mungu. Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu kwenu ." Mpaka kufikia kauli yake Mwenyezi Mungu: "Mmekuwa ni umma bora."

2). Je, makusudio ni waislamu wote katika wakati wote, au ni kuwahusu wale walio kuwa katika siku za kwanza za uislamu kama vile Masahaba na waliofuatia (tabiina)?

Jibu: Kuainisha makusudio ya umma hapa, kunahitaji kujua makusudio ya herufi kana (kuwa) ambayo ilivyo ni kuwa inahitaji isimu na habari yake. Pia hiyo kana inafahamisha kufanyika kitendo wakati uliopita, lakini haielezi ni wakati gani kime-fanyika hicho kitendo wala kuwa kinaendelea au la.

Isipokuwa hilo linaweza kufahamika kutokana na vitu vingine vilivyo pamoja nayo kimaneno au hali ilivyo. Kwa mfano kusema, Zaid alikuwa ni mwenye kusimama. Hapo inachukuliwa kutendeka tendo la kusimama na kuisha bila kuendelea. Yaani Zaid, hakuwa ni mwenye kusimama, basi akasimama kipindi fulani bila ya kuendelea kusimama maisha. Lililofahamisha hilo ni neno mwenye kusimama, yaani hawezi kusimama maisha. Lakini kama tukisema Mwenyezi Mungu amekuwa ni Mwingi wa maghufira Mwenye kurehemu, hapo hali inafahamisha kudumu kwa tendo lenyewe, kwa sababu rehema na maghufira haviepukani na dhati yake Mwenyezi Mungu, na dhati yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ni ya milele na milele. Kwa kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameufungamanisha ubora wa umma na kumwamini kwake, na kuamrisha mema na kukataza maovu, basi maana ya Aya yanakuwa ni: Enyi waislamu! Msiseme tu sisi ni umma bora mpaka muamrishe na kukataza maovu; na kwamba sifa hii ya ubora itawaondokea mara tu mnapopuuza hilo.

Kwa hivyo basi kana hapa inakuwa ni kamilifu, sio pungufu; yaani haihitaji khabar. Kwa maana hayo makusudio ni waislamu wote.2

3).Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu 'mliotolewa kwa Watu' inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemleta Muhammad na umma wake (s.a.w) ushinde umma zote za mwanzo ukiwa umechukua Kitabu cha Mwenyezi Mungu mkono mmoja na Hadith za Mtume kwenye mkono mwingine, huku ukiwalingania vizazi vishikamane na vitu viwili hivyo na kuvitegemea kwa itikadi, sharia na maadili. Kwa sababu ndio marejeo pekee yanayoweza kuhakikisha ufanisi wa mambo yote, kudhamini maisha ya kila mtu na kufungua uwanja wa wenye uwezo wa kufanya ijitihadi kwa misingi ya usawa, amani na uhuru wa watu wote. 3

2.Maelezo haya yanafahamika zaidi kwa wajuao Nahau- Mtarjumu,

3.Wajuzi wametunga vitabu kadhaa kuhusu maudhui haya. Baadhi ya watungaji ni watu wa nje, vingi katika hivyo vinatekeleza lengo; chenye faida zaidi - kwa maoni yangu - ni kijitabu cha Dkt Abdul-Wahid Wafi kiitwacho Al-musaawat fil-Islam. Ingawaje ni kidogo lakini kina mada nyingi na dalili nzito.

Aya hii katika madhumuni yake inaafikiana na Aya isemayo:

21

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

"Tumewafanya ni umma wa wastani, ili muwe mashahidi juu ya watu na Mtume awe shahidi juu yenu." (2:143)

Ikiwa waislamu hawatafanya harakati zozote za kulingania kwenye kheri au kuamrisha mema na kukataza mabaya, basi sifa za uongozi zitawaondokea na watakuwa na haja ya kiongozi atakayewaamrisha mema na kuwakataza maovu.

Ulikuwepo wakati ambapo waislamu walikuwa na harakati hizi. Wakati huo walikuwa wakistahili kuwa viongozi wa umma zingine; kisha wakapuuza; wakaen-delea hivyo mpaka wakawa wanakataza mema na kuamrisha maovu; kama tuon-avyo sasa. Leo vijana wamekuwa wanajivua kabisa na dini na hulka njema. Wakimwona mtu anaswali au kufunga husema kwa dharau: "Bado kuna Swala na Saumu katika karne ya ishirini?"

Mwenye Tafsir Al-Manar, katika kufasiri Aya hii, anasema: "Kwa kweli hasa ninasema, haukuzimika ubora wa umma uliotolewa kwa watu, mpaka pale ulipoacha kuamrisha mema na kukataza mabaya. Na haukuacha hivyo kwa kupenda au kupuuza amri ya Mwenyezi Mungu, bali ni kwa kulazimishwa na ufed-huli wa Wafalme wa bani Umayya na waliofuata nyayo zao."

Kwa msingi vitu hutajwa kwa kinyume chake; kama ambavyo hutajwa kwa kifani chake, basi tutaleta Hadith tukufu aliyoitaja Hafidh Muhibbudin Attabari, amesema: "Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) 'Mfano wa Ahlu bait wangu, ni kama safina ya Nuh mwenye kuipanda ataokoka, na mwenye kushikamana nayo ataokoka, na mwenye kuachana nayo ataghariki'".

Ama Hadith ya "Mimi nawaachia vizito viwili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Kizazi changu - Ahlul bait wangu," imepokewa na wapokezi 35 katika Masahaba.

Na lau wangeliamini watu wa Kitabu, ingelikuwa heri kwao.

Yaani lau watu waliopewa Tawrat na Injil, wangelimwamini Muhammad (s.a.w) ingelikuwa imani yao hiyo ni heri yao katika muda wa sasa na ujao.

Katika wao kuna wanaoamini na wengi wao ni wafasiki.

Yaani katika watu wa Kitabu kuna waliomwamini Muhammad (s.a.w); kama vile Abdullah bin Salam na watu wake, na wengineo katika wanaswara, na wengi wao walibaki katika ukafiri.

Neno Fasiq na Kafir yanapokezana maana, hutumiwa Fasiq kwa maana ya Kafiri na Kafir kwa maana ya Fasiq. Na Fasiq hapa ina maana ya kafiri.

Hawatawadhuru, isipokuwa kuwaudhi tu, na wakipigana nanyi watawakimbia

Madhara yako aina mbili: Kwanza, ni kiasi cha huzuni na kusikia uchungu tu, ambako kadiri siku zinavyokwenda nayo yanafutika; kama vile inavyotokea katika nafsi kwa kusikia habari mbaya.

22

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Pili, ni yale yanayogusa maisha na kuyumbisha; kama vile madhara yaletwayo na dola ya Israil ndani ya nchi ya Waarabu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewabashiria maswahaba wa Mtume (s.a.w) kwamba watu wa Kitabu: Hawatawadhuru isipokuwa kwa maneno tu, kama vile uzushi na mabezo. Ama katika uwanja wa vita, nyinyi ndio washindi. Amesema kweli Mwenyezi Mungu katika kiaga chake. Aliwapa ushindi waislamu wa mwanzo kwa wakristo na wengineo.

112.Wamepigwa na udhalili popote wanapokutanikana, isipokuwa ni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu. Na wames-tahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na wamepigwa na unyonge na udhalili. Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kuwaua Manabii pasi na haki, hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupetuka mipaka.

 Aya 112 WAMEPIGWA CHAPA YA UDHALILI

MAANA

Wamepigwa na udhalili popote wanapokutanikana isipokuwa ni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu. Na wamestahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na wamepigwa na unyonge na udhalili.

Wafasiri wameafikiana kuwa, Aya hii imeshuka kwa ajili ya mayahudi; kama ambavyo wameafikiana kuwa makusudio yake ni kuwa Mwenyezi Mungu ame-wanyima utukufu na takrima, na akawaandikia udhalili tangu ulipoanza uislamu hadi siku ya mwisho. Kwa sababu wao katika ufisadi na kupetuka mipaka wame-fikilia hatua ambayo hakuifikia na hataifikia yeyote.

Baada ya wafasiri kuafikiana juu ya hilo, wametofautiana kuhusu aina ya udhalili na unyonge walio nao (Mayahudi ambayo iko kwa kila kizazi). Tofauti hiyo hasa inatokana na tofauti ya hali ya mayahudi wakati wa kufasiri, ambapo walikuwa

Kaashif4-35.jpg

23

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

wakitoa kodi kwa waislamu, yaani kauli ya mfasiri imekuja kuakisi na walivyokuwa wayahudi. Hiyo si ajabu maadam mtu anaathirikia kwa anachokisikia na kukiona. Na tafsiri yangu ya Aya hii inafuata desturi hii.

Vyovyote iwavyo, ninavyofahamu ni kwamba udhalili wa mayahudi uliokusudiwa na Aya ni huku kutawanyika kwao duniani, Mashariki na Magharibi, wakiwa wako kwenye nchi mbali mbali. Wao daima ni wafuasi na wala sio wanaofuatwa na kuhukumiwa katika dola yao. Wako peke yao katika mambo yao.

Ama Israeli iliyoko Tel Aviv ni Dola ya jina tu, ilivyo hasa ni kambi tu ya kikoloni na ni kituo cha jeshi cha uchokozi. Hakika hii imedhihiri wazi wazi baada uchokozi wa Israel katika ardhi za Waarabu mnamo tarehe 5 Juni 1967. Ni uchokozi ambao wanaufanya waisrail ili kutekeleza mahitaji yao. Lau watauacha siku moja tu watanyang'anywa na waarabu.

Huo ndio udhalili hasa, kwa sababu mwenye heshima zake hutegemea nguvu zake mwenyewe na kujihami kwa mikono yake sio mikono ya wengine.

Kwa hali hii, inatubainikia kuwa makusudio ya kamba ya watu, ni msaada wa kihali na mali utolewao na mataifa ya kikoloni kwa ajili ya kambi ya kikoloni ya Israel.

Kwa hivyo basi tunaamini bila ya tashwish yoyote kwamba Dola ya Israil itaondo-ka tu kwa kuondoka ukoloni. Na ukoloni uko njiani kuisha iwe ni sasa au baadae. Wala maneno hayo sio ndoto, isipokuwa ni natija hasa itakayotokea, kama ilivy-oeleza Hadith ya Mtume:"Hakitasimama Kiyama mpaka muwapige vita mayahudi na kwamba jiwe litasema: Ewe Mwislamu! Huyu hapa Yahudi nyuma yangu muue." 4

Ama Kamba ya Mwenyezi Mungu ni fumbo la matakwa yake Mwenyezi Mungu

Mtukufu: yaani kwamba mayahudi wataendelea kuwa na udhalili mpaka

atakapotaka Mwenyezi Mungu: ni sawa na kauli yake Mwenyezi Mungu pia ise-

mayo:

"Moto ndio makazi yenu mtadumu humo milele ila apende Mwenyezi Mungu"

(6:128)

Kisha baada ya hapo, Mwenyezi Mungu amebainisha sababu iliyowajibisha udhalili wao na ghadhabu yake kwao, kwa kusema:

Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kuwaua Manabii pasi na haki; hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupetu-ka mipaka.

4.Hiyo imepokewa na Bukhar katika Juzuu ya 4 mlango Qitalul Yahud na Muslim katika Juzuu ya 2 mlango: la Taqumu ssaa

24

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Umetangulia mfano wa Aya hii katika Sura ya Baqara Aya 61. Unaweza kuuliza: Kuna wasiokuwa Mayahudi katika mataifa mengine waliokanusha dalili za Mwenyezi Mungu, kuwaua watu wema, kuasi na kupetuka mipaka; pamoja na hayo Mwenyezi Mungu hakuwapiga chapa ya udhalili na uduni. Je, kuna siri gani katika kuwahusisha Mayahudi?

Jibu: Mtu anaweza kupetuka mpaka kwa msukumo fulani unaotokana na masilahi yake na manufaa yake. Ama kupetuka mpaka si kwa lolote isipokuwa kwa kupen-delea tu kufanya dhambi, hakujatokea kwa yeyote isipokuwa mayahudi tu, na pupa hii ya kupenda dhuluma na uovu iko ndani ya dini ya mayahudi. Wao wanaitakidi kwamba Mwenyezi Mungu yuko na wao tu, sio wengineo; bali pia yuko dhidi ya maadui zao; na kwamba watu wote wameumbwa kwa ajili yao tu ili wawafanye vile watakavyo, sawa na mtu amfanyiavyo mnyama.

Jambo linalofahamisha zaidi sera yao hiyo, zamani na sasa, ni fedheha yao katika Palestina, hasa waliyo yafanya huko Dayr Yasin, kuwachinja wanawake na watoto.

Mwanzo walikuwa wakiwaua Mitume wakati dunia ilipokuwa na Mitume. Ama leo, ambapo hakuna Mitume wanawaua wasuluhishaji; kama vile Bernadotte,5 na wanawake na watoto. Kwa sababu, la muhimu katika itikadi yao na maumbile yao ni kuwaua watu wasiokuwa na hatia; wawe Mitume au wasuluhishi au watoto. Tawrat yao imeandika uhalali wa kumwaga damu ya wanawake na watoto, na imelihimiza hilo. Kwa ujumla ni kwamba kuzikanusha dalili za Mwenyezi Mungu, kuwaua wasuluhishi na watu wema wasio na hatia, na kufanya dhuluma na uchokozi, yote hayo ni dini na itikadi ya Mayahudi. Myahudi akimfanyia kosa mwengine asiyekuwa Myahudi basi anafanya kwa kujiburudisha tu, sio kwa haja fulani. Na kama akiacha kufanya hivyo, basi anaacha kwa kuogopa sio kwa kujis-tahi.

Hii ndiyo tofauti kati ya mayahudi na wasiokuwa mayahudi. Kwa hiyo hakuna ajabu kwa Mwenyezi Mungu kuwawekea udhalili popote walipo. Ama serikali habithi ya Israel ya sasa itaondoka tu, hakuna budi. Ushahidi mkub-wa wa kwisha kwake ni kwamba imefungamana na ukoloni, ukoloni ukiondoka nayo inaondoka. Na ukoloni lazima uondoke tu, hata kama ni baada ya miaka. Maadam maumbile ya kibinadamu yanaukataa ukoloni na kuupinga kwa damu yake, basi utaondoka tu.

Yote haya tuliyoayataja yanakamilisha kifungu cha 'Mayahudi hawana mfano' katika tafsiri ya Sura Baqara (2) Aya63 na 66.

5.Ni mjumbe wa amani, Msweden, aliyetumwa na Umoja wa mataifa mnamo mwaka 1948, kusimamia azimio la amani la umoja wa mataifa kuhusu Palestina, lakini Mayahudi wakamuua baada ya miezi mitatu.

25

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

113.Wote si sawa Katika watu wa Kitabu wamo walio na msimamo, wakasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku huku wakinyenyekea.

114.Wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na wanaamr-isha mema na wanakataza mabaya na wanaharakia mambo mema na hao ndio miongoni mwa watu wema.

115.Heri yoyote watakayoifaya-haitakataliwa. Na Mwenyezi Mungu anawajua wamchao.

WOTE SI SAWA Aya 113 -115

LUGHA

Mwenye Majmaul-bayan anasema: Tofauti kati ya neno Sura' na A'jala ni kwamba Sura' ni kufanya haraka linalojuzu kufanywa. Nako kunasifiwa. Na A'jala ni kufanya haraka jambo lisilofaa kufanywa, nako kunashutumiwa.

MAANA

Aya hizi tatu ziko wazi hazihitaji tafsir. Maana yake kwa ujumla ni kwamba watu wa Kitabu hawako sawa kwamba wote wamepotea, bali wako watu wema miongoni mwao. Wafasiri wengi wamechukulia sifa hii kwa aliyesilimu miongoni mwa watu wa Kitabu, na uzuri wa uislamu wake kimatendo na kiitikadi.

Kaashif4-36.jpg

26

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

HUKUMU YA MWENYE kuACHAUISLAMU

Mwito wa kumwamini Muhammad kama Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa

watu wa ulimwenguni bado upo mpaka Siku ya Mwisho. Nao unaelekezwa kwa

watu wote, wa Mashariki na Magharibi. Mwenyezi Mungu anasema:

"Sema : Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyote ."

(7:158).

Dalili ya ukweli wake ni mantiki ya kiakili, kuthibiti muujiza na kufaa dini kwa maisha. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) anasema: "Msingi wa dini yangu ni akili."

Na Mwenyezi Mungu anasema katika Kitabu chake Kitukufu: "Enyi ambao mmeamini muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume (wake) anapowaitia katika yale yatakayowapa maisha" (8:24)

Lengo letu sio kutoa dalili za Utume wa Muhammad (s.a.w),6 isipokuwa lengo ni kubainisha kuwa je, asiyeamini Utume wa Muhammad anastahili adhabu: au hapana budi ya ufafanuzi?

Kabla ya kumtofautisha mjuzi na asiye mjuzi na asiyemudu na mzembe, tutaonye-sha msingi na vipimo vya kwanza vya kustahili adhabu au kutostahili; kutokana na hivyo, uhakika utafumbuka na kuwapambanua watu.

Wote wameafikiana kwamba mtu, vyovyote awavyo, dini yoyote aliyo nayo, has-tahili adhabu ila baada ya kusimamishiwa hoja. Na hoja haisimami ila baada ya kuweza yeye kufikia kwenye dalili ya haki na kuweza kwake kuitumia. Hapo aki-acha hatakuwa na kisingizio.

Ikiwa hakupata dalili ya haki yenye msingi au aliipata akashindwa kuifikia au ali-ifikia na akatekeleza mtazamo wake wa haki mpaka akafikia mwisho, lakini pamo-ja na hayo haki haikumdhihirikia, basi yeye atakuwa na udhuru, kwa sababu ya kutokamilika hoja juu yake. Kwa sababu, asiyethibitikiwa na haki haadhibiwi kwa kuiacha, ila ikiwa amezembea katika utafiti.

Vile vile miongoni mwa kawaida za msingi ambazo zinaambatana na utafiti huu ni ile ya "Adhabu kuepukwa na mambo yenye kutatiza."

Kwa hiyo haijuzu kumhukumu mwenye kuiacha haki kuwa ni mwenye makosa anayestahili adhabu, maadamu tunaona kuwa kuna uwezekano kuwa anao udhuru katika kuacha kwake. Na kawaida hii inafungamana na watu wote, sio waisla-mu tu. Pia inakusanya aina zote za mipaka.

6Tumeonyesha dalili hizo tulipofasiri Sura Baqara Aya23 - 25. Vile vile tutataja sehemu ya hulka za Mtume (s.a.w) katika kufasiri Aya160 ya Sura hii tuliyonayo (Al-Imran).

27

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Mfano kawaida ya 'Mwenye kukosea katika ijtihadi, basi kosa lake linasamehewa'. Kawaida hii ni ya kiakili, haiwezekani kuihusisha na dini fulani tu, madhehebu, shina au tawi. Baada ya maelezo hayo hebu tuangalie hali hizi zifuatazo:

1)  Kuishi binadamu mji ulio mbali na uislamu na waislamu; wala hakufikiliwa na mwito au hata kusikia jina la Muhammad (s.a.w) katika maisha yake yote. Pia awe hajawaza kwa karibu au mbali kwamba duniani kuna dini yenye jina la kiis-lamu na Mtume aitwaye Muhammad (s.a.w). Hapana mwenye shaka kwamba huyu atasamehewa kwa kuwa hastahili adhabu. Maana akili ina hukumu ubaya wa adhabu bila ya ubainifu na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

"Na sisi si wenye kuadhibu mpaka tupeleke Mitume." (17:15) Bila shaka akili ni Mtume wa ndani kwa ndani, ila tu yenyewe ni dalili ya kupatikana Mwenyezi Mungu tu. Ama dalili ya kuthibiti Utume wa Mtume, hapana budi kuwako na muujiza na udhihirishwe na yeye mwenyewe pamoja na akili kuhuku-mu kutowezekana kudhihiri kwa wasiokuwa Mitume.

2)  Kuusikia mtu uislamu na Muhammad, lakini akawa hawezi kupambanua haki na batili, kwa sababu ya kushindwa kwake na kutoweza kufahamu dalili za haki na maarifa yake. Huyu pia anasamehewa. Kwa sababu yeye ni sawa na mtoto au mwenda wazimu. Mfano ni akitomwamini Muhammad (s.a.w) tangu udogo kwa kuwafuata wazazi wake na akajisahau alipokuwa mkubwa, akaendelea na itika-di yake bila ya kuitilia shaka yoyote, huyu atasamehewa. Kwa sababu kumkali-fisha aliyejisahau asiye na uwezo ni sawa na kumkalifisha aliyelala. Amesema Muhaqqiq Al-Qummi: "Kujikomboa kutokana na kuiga wazazi ni jambo lisilofikiriwa na wengi, bali hata linakuwa zito aghlabu kwa wanavyuoni walioto-sheka ambao wanadhani kuwa wamejivua kutokana na kuiga huko." Amesema tena: "Asiyeweza kung'amua wajibu wa kujua misingi, ni sawa na mnyama na mwedawazimu ambao hawana taklifa yoyote."

Sheikh Tusi anasema: "Mwenye kushindwa kupata uthibitisho yuko katika daraja ya mnyama."

Hata hivyo, ikiwa aliyejisahau atakumbushwa wajibu wa maarifa, au kuambiwa na mtu: "Wewe uko au hauko sawa katika itikadi yako", lakini pamoja na hayo akang'ang'ania na wala asifanye utafiti na kuuliza, basi huyo atakuwa ni mwenye dhambi, kwa sababu atakuwa ni mzembe, na kutojua kwa mzembe si kisingizio.

3)  Kutomwamini Muhammad (s.a.w) pamoja na kuwa anao uwezo wa kutosha wa kufahamu haki, lakini yeye alipuuza wala asijali kabisa: au alifanya utafiti pun-gufu na akauacha bila ya kuangalia mwisho wake; kama wafanyavyo wengi, hasa vijana wa kisasa. Basi huyu hatasameheka kwa sababu amekosea bila ya kujitahidi na alikuwa na uwezo wa kujua haki, lakini akapuuza. Ni wazi kuwa pia ataadhibiwa ambaye amefanya utafiti na akakinai, lakini pamoja na hayo akakataa kumwamini Muhammad (s.a.w) kwa ubaguzi na mali.

28

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

4).Kuangalia dalili na kuwa na mwelekeo wa kufuata haki kwa ikhlasi, lakini pamo-ja na hayo akakosa kuelekea kwenye njia ambayo itamwajibishia kumwamini Muhammad (s.a.w) ama kwa kushikamana kwake na mambo yenye kutatiza ya ubatilifu bila ya kuangalia ubatilifu wake, au kuchanganyikiwa na mengineyo ambayo yanazuia kuona haki. Huyu ataangaliwa hali yake, ikiwa atakanusha Utume wa Muhammad (s.a.w) kwa kauli ya mkato, basi yeye ataadhibiwa na kustahili adhabu. Kwa sababu yule ambaye imefichika kwake haki, haifai kwake kukataa moja kwa moja kukanusha haki. Inawezekana kuwa haki ipo lakini akazuiliwa, kuifika, na aghlabu huwa hivyo, kwa sababu mambo ya ulimwengu-ni yapo lakini tuyajuayo ni machache tu. Hali ni hivyo hivyo kuhusu kuwajua Mitume na wasuluhishi. Ni nani awezaye kujua kila kitu?

Watu wa mantiki wamelielezea hilo kwa ibara mbali mbali, miongoni mwazo ni: Kutokujua hakumaanishi kutokuwepo, kutopatikana hakumaanishi kuacha kupatikana, kuthibitisha na kukanusha kunahitaji dalili.

Tumewaona wanavyuoni wengi wakiungana na hakika hii. Wanazituhumu rai zao na kujichunga katika kauli zao; wala hawajifanyi kuwa wao ndio kipimo cha ukweli. Hawawezi kusema: "Rai hii ni takatifu isiyo na shaka, na nyinginezo si chochote." Bali wao huipa mtazamo wa kujiuliza kila rai. Dalili kubwa zaidi ya kuwa mtu hana elimu, ni kule kujidanganya mwenyewe, kuiona safi elimu yake, na kudharau rai na itikadi za wengine.

Zaidi ya hayo kuacha kukinai mtu mmoja miongoni mwa watu kuhusu Utume wa Muhammad (s.a.w) hakumruhusu kukanusha Utume wa Mtume Mtukufu (s.a.w) moja kwa moja. Na kama akifanya hivyo, basi atakuwa na jukumu. Hasa baada ya kuona idadi ya mabingwa ambao hawakuathiriwa na kurithi au mazingira, wakimwamini Muhammad na risala yake; si kwa lolote isipokuwa kuiheshimu haki na kuikubali hali halisi ilivyo. *7

Hayo ni ikiwa atapinga. Ama akiangalia dalili wala asikinai na pia asipinge; wakati huo huo akawa amenuia kwa moyo safi kuiamini haki wakati wowote itakapomd-hihirikia; kama vile mwanafiqh mwadilifu ambaye hufutu jambo kwa nia ya kubadil-isha mara tu ikimbainikia kuwa amekosea, basi huyu hatakuwa na jukumu, kwa sababu mwenye kukosea katika ijtihadi yake bila ya kufanya uzembe, hataadhibi-wa kwa kukosea kwake; kama inavyohukumu akili na maandishi pia. Imepokewa kutoka kwa Imam Jafar Sadiq (a.s.), amesema: "Lau kama watu wasipofahamu (jambo) wakasimama na wala wasipinge, basi hawakukufuru ." Katika Riwaya nyingine: "Hakika anakufuru tu akipinga ."

7.Miongoni mwao ni Leopold Fais Mu-Austria ambaye alijiita Muhammad Asad, na akatunga kitabu Al-Islam ala muftariq turuq. Mwengine ni Vaglire mwenye kitab Difa anil-Islam, na wengineo ambao maji-na yao siyajui. Nimesikia kuwa kuna Mwirani mmoja ameandika kitabu maalum cha majina ya watu wa ki-magharibi waliosilimu nao ni wengi.

29

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Sheikh Ansari katika kitabu chake maarufu Arrasil mlango wa Dhana katika Usul, anasema: "Hadith nyingi zimefahamisha kuthibiti ukati na kati baina ya kufuru na imani." Ya kwamba mpingaji ni kafiri, mwenye kuitakidi ni Mumin, na mwenye shaka si kafiri wala Mumin.

Katika Hadith zinazowezekana kuzitolea dalili ya kutoadhibiwa mwenye kufanya ijitihadi bila ya uzembe kama akikosea katika mambo ya itikadi, ni Hadith hii mashuhuri kwa sunni na shia:

"Akijitahidi hakimu na akapata basi atalipwa mara mbili. Na akijitahidi akakosea, basi atalipwa mara moja."

Kama mtu akisema kuwa Hadith hii inahusu mwenye kujitahidi katika matawi si katika masuala ya itikadi, kama walivyodai baadhi ya wanavyuoni, basi tutamjibu hivi: Linalomlinda, mwenye kujitahidi katika hukumu, asiadhibiwe ni kule kujichun-ga kwake na kutofanya uzembe katika utafiti. Na kinga hii inapatikana hasa katika masuala ya kiitikadi.

Zaidi ya hayo Mafaqihi wote wameafikiana kwa kauli moja kwamba mwenye kushindwa kuifikia itikadi ya kweli, anasamehewa. Miongoni mwao ni wale walio-husisha Hadith hii na matawi. Nasi hatuoni tofauti yoyote kati yake na yule mwenye kujitahidi, aliyetoa juhudi zake. Kwa sababu, wote wawili wameshindwa kujua maadam hawakuufikia uhakika.

Kwa ufupi ni kwamba mwenye kuipinga, haki yoyote, basi ataadhibiwa, ni sawa awe amejitahidi au la, isipokuwa kama hana maarifa, kama mnyama. Kama akibakia kwenye msimamo wa kutopinga wala kuthibiti sawa, kujitahidi na kuan-galia dalili au alifanya ijtihadi pungufu, basi ataadhibiwa. Ikiwa ameangalia dalili akajitahidi mpaka akafikia mwisho wake, basi yeye atasamehewa kwa sharti ya kubakia na mwelekeo wa haki kwa kuazimia kubadili msimamo wake wakati wowote itakapomdhihirikia haki.

Unaweza kuuliza: Umesema kuwa mwenye kushindwa kujua itikadi ya kweli -kama vile Utume wa Muhammad - atasamehewa. Vile vile mwenye kujitahidi ambaye hakuzembea katika jitihadi. Je, maana yake ni kuwa inajuzu kwetu kufanya naye muamala wa kiislamu, kama kuoa, kurithi n.k.

Jibu: Msamaha tunaoukusudia hapa ni kutostahiki adhabu akhera; ama kuoa na kurithi hapa duniani ni jambo jengine. Na kila asiyeamini utume wa Mtume Muhammad (s.a.w) kwa hali yoyote atakayokuwa, haifai kuwa na muamala naye wa kiislam k.v. ndoa, urithi n.k. Ni sawa awe kesho atapona au ataangamia; kama ambavyo mwenye kusema "Laila ilaha ilia Hah Muhammad Rasulullah" anastahiki ya waislamu, ni juu yake yaliyo juu yao, hata kama alikuwa ni fasiki, bali hata mnafiki vile vile.

30

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

116.Hakika wale ambao wamekufu-ru, haitafaa kitu mali yao wala watoto wao kwa Mwenyezi Mungu, na wao ndio watu wa motoni, wao humo watadumu.

3. Sura Al-Imran

Kaashif4-37.jpg

117.Mfano wa wanavyovitoa katika maisha haya ya dunia ni kama mfano wa upepo wenye baridi kali uliofikilia shamba la watu waliodhulumu nafsi zao, ukaliangamiza. Na Mwenyezi Mungu hakuwadhulumu, lakini wanajidhulumu wenyewe.

UKAFIRI HAUFAI KITU Aya 116 - 117

 MAANA

Hakika wale ambao wamekufuru, haitafaa kitu mali yao wala watoto wao kwa Mwenyezi Mungu.

Amesema Razi na mwenye Tafsir Al-Manar: "Wametofautiana wafasiri katika makusudio ya ambao wamekufuru. Kundi moja likasema kuwa ni baadhi ya makafiri. Wengine wakasema ni makafiri wote."

Ama tuonavyo sisi ni kwamba, makusudio ni kila mwenye kukhalifu haki na kuipin-ga kwa masilahi yake na ya watoto wake, na kuhofia mali yake na utajiri - vyovy-ote atakavyokuwa, Mwislamu au kafiri. Ni kweli kuwa tamko la Aya linawahusu makafiri lakini sababu inayowajibisha ambayo ni kutofaa kitu, inaenea kwa wote wanoikhalifu haki kwa msukumo wa hawaa zao; nao ndio wale aliowataja Mwenyezi Mungu (s.w.t.) katika Aya kadhaa kuwa wameiuza haki kwa thamani duni.

Mfano wa wanavyovitoa katika maisha haya ya dunia, ni kama mfano wa upepo wenye baridi kali uliofikilia shamba la watu waliodhulumu nafsi zao, ukaliangamiza.

31

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Yaani wale ambao wanachanganya utajiri wa halali na haramu na kuihalifu haki kwa ajili ya utajiri na kuutumia kwa ajili ya jaha, na starehe zao bila ya kujali dini au maadili, hakika matumizi ya hawa yameangamiza akili zao na kuharibu maadili yao, sawa na upepo wenye baridi kali unavyoangamiza shamba lililotayarishwa kuwa na mazao.

Kama watapata faida siku chache kwa kustarehe na kutosheleza uchu wao, basi watakuwa wamejipatia hasara na kuziuza nafsi zao kwa shetani; na wao watapata adhabu ya milele huko akhera.

Na Mwenyezi Mungu hakuwadhulumu, lakini wanajidhulumu wenyewe,

sababu wamejiiingiza kwenye matamanio wao wenyewe kwa hiyari yao.

kwa

Imam Ali (a.s.) anasema: "Watu duniani ni aina mbili: Mtu aliyeiuza nafsi yake ikamwangamiza (yaani ameiuza nafsi yake kwenye matamanio na hawaa zake), na mtu aliyeinunua nafsi yake akaiacha huru. (Yaani aliyeinunua nafsi yake na kuisafisha na matamanio.)"

118.Enyi ambao mmeamini Msiwafanye wasiri wasiokuwa katika nyinyi. Hawazembei kuwaharibia. Wanapendelea yanayowapa                 mashaka.

Imedhihiri chuki katika vinywa vyao, na wayafichayo vifuani mwao            ni            makubwa.

Tumewabainishia ishara ikiwa nyinyi ni wenye akili.

119.Hivyo basi! Nyinyi ndio hao muwapendao hali wao hawawapendi, nanyi mwaviami-ni vitabu vyote. Na wakikutana nanyi husema: Tumeamini, na wanapokuwa faraghani huwau-mia vidole kwa hasira. Sema: Kufeni na hasira zenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa yaliyo vifuani.

Kaashif4-38.jpgKaashif4-39.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Kaashif4-40.jpg

120.Ukiwagusa wema unawa-

sononesha, na kama likiwapata

baya wanalifurahia. Na kama

mkisubiri na mkaogopa, basi

hila zao hazitawadhuru kitu.

Hakika Mwenyezi Mungu ni

mwenye kuyazunguka wayaten-

dayo.

WASIRI WAOVU Aya 118 - 120

 MAANA

Katika Aya zilizotangulia, Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amezungumzia kuhusu watu wa Kitabu, washirikina na wenye kurtadi ambao walikufuru baada ya kuamini kwao. Wote hao amewapa kiaga na akawapa hoja, kisha akaamrisha waislamu wamche Mwenyezi Mungu, washikamane na kamba yake na waamrishe mema.

Baada ya yote hayo, sasa anawahadharisha waislamu wajiepushe na makafiri -ambao wanawadhamiria uovu waislamu na kuwatakia maangamizi - kwa kusema: Enyi ambao mmeamini! Msiwafanye wasiri wasiokuwa katika nyinyi. Hili kwa dhahiri ni katazo kwa waislamu kwa kila asiyekuwa katika dini yao bila ya kumvua yeyote. Hapo basi litakuja Swali hili:

Ni maarufu kuwa viongozi wa dini katika mataifa yote wanaeneza kwa wafuasi wao roho ya uadui na ubaguzi, dhidi ya dini nyingine. Na hii Qur'an nayo inakwenda njia hiyo hiyo, ambapo inawaamrisha waumini kujitenga na wengine na kutoa tahadhari ya kuwafanya marafiki. Sasa kuko wapi kuvumiliana katika Uislamu? Je, kuna tofauti gani baina ya waislamu na mayahudi walioambiana: "Wala msimwamini ila mwenye kufuata dini yenu?"3:73

Jibu: Aya haikuwatahadharisha Waislamu kujiepusha na wasiokuwa wao kwa kuwa si wafuasi; isipokuwa imewahadharisha na wale wanaowafanyia vitimbi. Hayo ndiyo maana wazi ya kauli yake Mwenyezi Mungu: Hawazembei kuwa-haribia; yaani wanajitahidi bila ya kufanya uzembe katika kuwadhuru na kuharibu mambo yenu. Na katika kauli yake: Wanapendelea yanayowapa mashaka.

Pia kauli yake Mwenyezi Mungu: Imedhihiri Yaani kuitia ila dini yenu, Mtume wenu na Qur'an yenu.

Na wayafichayo vifuani mwao ni makubwa kuliko yale yamiminikayo kwenye ndimi zao.

33

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Vile vile miongoni mwa sifa za wale aliowahadharisha Mwenyezi Mungu ni: wanapokuwa faragha huwaumia vidole kwa hasira. Na ukiwagusa wema unawasononesha na kama likiwapata baya wanalifurahia.

Sifa zote hizi, ndio sababu ziwajibishayo kuwakataza kuwafanya wasiri wenu. Kwa hiyo basi, kila mwenye sifa hizi ni wajibu kujitenga naye wala haijuzu kumfanya msiri; ni sawa awe ni mwislamu au si mwislamu.

Hivi sasa tuko katika mwaka 1967. Mnamo tarehe 5 Juni mwaka huu, ukoloni umeileta Israel kufanya uadui katika ardhi za Waarabu baada ya kufagiliwa njia na makombamwiko waovu wanaonasibika na dini ya waislamu na kabila ya Waarabu. Na waovu hawa mbele ya Mwenyezi Mungu wana hatia kubwa kuliko walahidi na washirikina ambao hawawaudhi wengine.

Kwa hiyo suala hapa ni la ushari na hiyana, sio suala la ukafiri na kukosa imani. Unaweza kuuliza: Ingawa mambo ni hivyo, kwa nini Mwenyezi Mungu amesema, 'wasiokuwa katika nyinyi,' badala ya kusema katika wahaini walio wafisadi?

Jibu: Aya ilishuka kwa sababu ya baadhi ya waislamu waliokuwa wakiungana na mayahudi kama walivyosema wafasiri. Kimsingi cha kuzingatia ni sababu iliyowa-jibisha sharia ya hukumu; sio sababu ya kushuka kwake. Kwa maneno mengine, ni kwamba hukumu itafuata dhahiri ya tamko, ikiwa hatujui sababu ya kushuka kwake. Ama tukiwa na yakini ya sababu yake basi hukumu itafuatia sababu, sio dhahiri ya tamko.

Tumewabainishia ishara ikiwa nyinyi ni wenye akili.

Makusudio ya neno ishara ni alama zinazo pambanua baina ya anayefaa kufany-wa msiri, na habithi ambaye ni wajibu kujitenga naye.

Hivyo basi! Nyinyi ndio hao muwapendao hali wao hawawapendi.

Dhahiri ya msemo ni kuwa unaelekezwa kwa kikundi kinachojinasibisha na uislam, wala hauswihi kuelekezwa kwa waislamu wote, si katika wakati wa mwanzo wala mwengineo. Kwani haikutokea hata siku moja kwamba waislamu waafikiane kuwapenda makafiri.

Sheikh wa wafasiri Tabari amesema na akafuatwa na wengi, kwamba waislamu kuwapenda wanaowachukia katika makafiri ni dalili kwamba uislam ni dini ya upendo na kuvumiliana.

Huku ni kusahau kwa Tabari na akafuatwa na wengi, kwamba uislamu kabisa hau-vumilii ufisadi na uhaini.

Tuonavyo sisi ni kwamba suala sio la kuvumiliana, isipokuwa ni suala la hiyana na unafiki kutoka kwa baadhi ya wanaojinasibisha na uislamu, na wakati huo huo wakifanya ujasusi kwa waislamu kwa ajili ya maadui wa nchi na dini. Kama

34

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

wafanyavyo leo vibaraka wa ukoloni wanaojulikana kwa jina la kikosi cha tano8 askari wa kukodiwa n.k. Kwa sababu, wanauza dini yao na nchi yao kwa kila anayewapa pesa tu.

Nanyi mwaviamini vitabu vyote.

Herufi Alif na lam hapa ni ya jinsi; yaani mwamini kila kitabu kilichoteremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu, ni sawa kiwe kimeteremshwa kwao au la. Nyinyi si kama wao wanaamini baadhi na kukanusha baadhi nyingine.

Na wakikutana nanyi husema tumeamini kwa ria na unafiki.

Haifai kwa mumin kufanya urafiki na mnafiki na mwenye ria (kujionyesha).

Na wanapokuwa faraghani huwaumia vidole kwa hasira.

Kuwaumia vidole ni fumbo la chuki zao na ukorofi wao kwenu. Hakuna kitu kina-chomkasirisha adui kuliko fadhila na hulka njema, vile vile umoja na kupatana kwa undugu. Tangu zamani hadi sasa adui anajaribu kuwatawanya waislamu na umoja wao.

Sema: Kufeni na hasira zenu.

Huu ni msemo wa kiarabu kwa mtu wanayamuombea abaki hivyo: Kama kusema; 'Kufa na ugonjwa wako.' Yaani Mwenyezi Mungu akubakishe na ugonjwa wako.

Kimsingi ni kwamba maneno haya huambiwa adui akiwa msemaji ana nguvu. Na hakuna nguvu kama umoja na kuungana.

Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa yaliyo vifuani kila yanayompitia mtu na anayowazia moyoni mwake katika misukumo ya kheri na shari. Yaani Mwenyezi Mungu anajua chuki na ukorofi wao.

Ukiwagusa wema unawasononesha na kama likiwapata baya wanalifurahia.

Hiyo ni kawaida ya kila adui. Wafasiri wanasema, kumetajwa kugusa katika wema kwa kutambulisha kuwa kheri ndogo tu aipatayo Mwislamu, humsononesha adui. Na kumetajwa kupata katika uovu, kufahamisha kuwa kukiwa na baya kwa waislamu, basi maadui huzidi furaha. Huu ni ufasaha wa kuelezea uadui ulivyo mkub-wa.

Na mkisubiri kwa twaa ya Mwenyezi Mungu na maudhi ya adui zake na mkao-gopa yaliyoharamishwa, na maasi, basi hila zao hazitawadhuru kitu.

o

.Franco aliposhambulia Madrid 1936 - 1939 alikuwa na vikosi vinne cha tano kilikuwa kiko ndani ya

nchi kikiwasiliana nao. Kwa hivyo ikiwa kila genge linalomtumikia adui ndani ya nchi linaitwa jina hilo.(Fifth column)

35

Kaashif4-41.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Anayekuwa na Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu huwa naye, na anayem-cha Mwenyezi Mungu humpatia njia.

121.Na uliporauka asubuhi kutoka kwa ahli zako kwenda kuwaan-dalia waumini mahali pa kupi-gana. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye kusikia, mjuzi

VITAVYAUHUD. Aya 121

Aya hii na nyingine kadhaa zinazofuatia zilishuka kuhusu tukio la vita vya Uhud ambalo kwa ufupi ni kama ifuatavyo:

Uhud ni jina la mlima ulioko Madina. Vita vya Uhud vilikuwa mnamo mwezi wa Shawwal (Mfungo mosi) mwaka wa tatu wa Hijra.

Baada ya kuuawa magwiji wa Kikuraish katika vita vya Badr, Abu Sufian alipata nafasi na akawa ndiye Rais wa Makuraish. Akawa anampangia njama Mtume (s.a.w.) pamoja na washirikina, akaweza kukusanya jeshi la wapiganaji elfu tatu. Akaenda nalo hadi karibu na mlima Uhud. Na alikuwa yuko pamoja na mkewe Hind bint Utba (mamie Muawiya).

Mtume (s.a.w) naye akatoka na wapiganaji elfu moja, lakini Abdallah bin Ubayya, kiongozi wa wanafiki alitaka kuwavunja nguvu watu kwa kujitoa, wakamwitikia watu mia tatu; Mtume akabaki na mia saba. Abdallah bin Amr (baba wa Jabir Al-ansari) alijaribu kumzuia bin ubayya na azma yake hiyo, lakini hakufaulu. Na koo mbili za Ansari zikajaribu kumfuata bin Ubayya, lakini Mwenyezi Mungu akawahi-fadhi na wakathibiti pamoja na Mtume (s.a.w). Wao walikuwa Bani Salama katika Khazraj na Bani Haritha katika Aus.

"Mtume (s.a.w) akapanga mbinu ya mapigano. Akaweka wapiga mishale hamsini kwenye mlima nyuma ya jeshi la waislamu waliokuwa wakiongozwa na Abdallah bin Jubair, akawaambia, "nyinyi mtatuhami kwa upande wa nyuma, wala msion-doke hapo mlipo tukishinda au tukishindwa."

Vita vilipochacha, Hind akawaongoza wanawake kupiga ngoma nyuma ya wanaume ili kuwachochea huku akiimba:

Mkikabili tutawakumbatia na mazulia kuwatandikia,

Na mkigeuka tutawakimbia mapenzi hatutawapatia Mtume (s.a.w.w) alipomsikia akasema:

4& 36

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Ewe Mwenyezi Mungu kwako nategemea na kwa ajili yako ninapigana. Tosha yangu ni Mwenyezi Mungu na bora ya mwenye kutegemewa ni Yeye

Bendera ya Makuraish ilibebwa na Twalha bin Abu Twalha Al-Abdi kutoka ukoo wa Abdu Ddar, Imam Ali akamuua, bendera ikachukuliwa na Said bin Abu Twalha, akauawa na bendera ikaanguka, akaichukua Musafi bin Abu Twalha naye akauawa na Imam, mpaka wakauawa watu tisa katika ukoo wa Abdu Ddar. Wakavunjiliwa mbali washirikina na kushindwa. Waislamu wakawa wanaokota ngawira.

Wapiga mishale walipoona kushindwa kwa washirikina na ndugu zao waislamu wanakusanya ngawira, waliondoka pale walipowekwa na Mtume (s.a.w). Kiongozi wao Abdallah bin Jubair akawaambia: "Bakini sehemu zenu, mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake." Lakini walikataa na wakaenda kunyakua ngawira. Jubair akabaki na watu kumi tu.

Khalid bin Al-Walid kuona hivyo aliwafuatia na kikosi cha washirikina. Wakawamaliza baada ya kupigana nao kiume.

Makuraish walipoona alivyofanya Khalid waliwazingira Waislamu na kuwasham-bulia mpaka wakamfikia Mtume (s.a.w). Akapigwa jiwe na washirikina likamjeruhi jicho, uso wake ukarowa damu, akajeruhiwa mdomoni na vishikio viwili vya kofia ya chuma vikamwingia usoni.

Hapo waislamu wakaanza kukimbia baada ya mtu mmoja kupiga kelele kuwa Muhammad ameuawa. Hakuna aliyebakia isipokuwa watu wachache wakion-gozwa na Ali bin Abu Talib, Abu Dujana na Suheli bin Hanif wakipigana kiume kumkinga Mtume.

Hind akumuhadaa Wahshi amuue Muhammad au Ali au Hamza. Akamuua Hamza kwa mkuki wake. Hind akalipasua tumbo la Hamza akamtoa ini lake akalila. Tangu siku hiyo alibandikwa jina la 'Mla maini.'

Katika vita hivyo waliuawa washirikina 22 na Waislamu 70 walikufa shahid. MAANA

Na uliporauka kutoka kwa ahli zako kwenda kuwaandalia waumini mahali pa kupigana.

Yaani, kumbuka ewe Mtume uliporauka kutoka nyumbani kwako kwenda kupanga sehemu watakayokaa wapiga mishale, wapanda farasi na waumini wengine uliokuwa nao.

37

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Kaashif4-42.jpg

122.(Kumbuka) makundi mawili miongoni mwenu yalipod-hamiria kufanya woga na Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kuwanusuru, na kwa Mwenyezi Mungu na wategemee waumini.

MAKUNDI MAWILI Aya 122

MAANA

Makundi mawili ni Bani Salama kutoka kabila la Khazraj na Bani Haritha kutoka Aus. Walikurubia kuathirika na harakati za Abdallah bin Ubayya, lau si kuwahiwa na nusura ya Mwenyezi Mungu. Na kauli yake Mwenyezi Mungu: Na Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kuwanusuru. Ni dalili ya mkato kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) huwapa tawfiki yake baadhi ya watu kinyume cha watu wengine. Kwa sababu Yeye hakuyaacha makundi hayo mawili yaogope na kukimbia. Mwenyezi Mungu ndiye Mjuzi zaidi wa anapopasaidia, kama ambavyo ni Mjuzi zaidi anapoweka utume Wake.

123.Hakika Mwenyezi Mungu ali-wanusuru katika vita vya Badr hali nyinyi ni madhalili. Basi mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kushukuru.

124.Ulipowaambia waumini: Je, hai-watoshi Mola wenu kuwasaidia kwa malaika elfu tatu wenye kuteremshwa.

125.Ndio! Kama mkisubiri na mkam-cha Mungu na wakawajilia katika wakati wao huu, atawasaidia Mola wenu na malaika elfu tano walio na alama.

Kaashif4-43.jpgKaashif4-44.jpg

3. Sura Al-Imran

Kaashif4-45.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

126.Na Mwenyezi Mungu hakuya-jaalia ila ni bishara kwenu ili mioyo yenu ipate kutulia. Na hapana nusra ila itokayo kwa M/Mungu Mtukufu, Mwenye hekima

127.Ili apate kuliangamiza kundi kati-ka waliokufuru au awadhalil-ishe,warejee hali ya kuwa ni wenye kuambulia patupu.

VITA VYA BADR Aya 123 - 127

Mwenyezi Mungu katika Aya hizi, anawakumbusha waislamu vita vya Badr ambavyo vilimalizika kwa ushindi wa Waislamu. Badr ni kisima kilichoko baina ya Makka na Madina. Kilikuwa ni cha mtu aitwaye Badr, ndio kikaitwa jina lake.

Msafara wa kibiashara wa Makuraish ulikuwa ukipitia hapo. Waislamu wakaamua kuukatiza msafara kwa kuushambulia. Msafara huo uliongozwa na Abu Sufyan, wakatoka wapiganaji washirikina kiasi cha elfu moja, wakiwa wamejiandaa tayari kuuhami msafara huu. Hapo vita vikaumana na waislamu walikuwa 313.

Waislamu walipata ushindi mkubwa sana katika vita hivi na hasara kubwa kwa washirikina, vita hivi vilisikika Uarabuni kote.

Tutarudia maelezo ya vita vya Badr Inshaallah tutakapofasiri Sura Anfal (8:7) MAANA

Hakika Mwenyezi Mungu aliwanusuru katika Badr hali nyinyi ni madhalili. Basi mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kushukuru.

Hii ni kuwakumbusha waislamu siku ya Badr kwa ajili ya taqwa ya nyoyo zao, wakati huo walikuwa wachache tena bila ya maandalizi ya nguvu. Ambapo idadi ya waislamu ilikuwa ni watu 313, wakiwa na farasi mmoja tu. washirikina walikuwa elfu moja na farasi mia moja, hata hivyo washirikina 70 waliuwawa na kutekwa 70. Waliobaki wakashindwa. Kusudio la kukumbushwa kwao haya ni kuwabainishia kwamba ushindi katika vita hauhisabiwi kuwa ndio ushindi wa mwisho, wala kushindwa katika vita hakuhisabiwi kuwa ndiko kushindwa kabisa, isipokuwa

39

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

ushindi wa mwisho ni wa wenye uthabiti na wanaomcha Mwenyezi Mungu, wenye ikhlasi. Yamefahamisha uhakika wa hilo, matukio na vita vya zamani na vya sasa; hasa vita vya pili vya dunia ambavyo vilianza mwaka 1939 na kumalizika 1945.

Ulipowaambia waumini hii ni kauli kutoka kwa Mtume (s.a.w) siku ya Badr: Je, haiwatoshi Mola wenu kuwasaidia kwa malaika elfu tatu wenye kuteremshwa.

Yaani wenye kuteremshwa kutoka mbinguni.

Ndiyo! Kama mkisubiri na kumcha Mwenyezi Mungu, na wakawajilia katika wakati wao huu, atawasaidia Mola wenu na Malaika elfu tano walio na alama.

Dhamiri ya wakawajilia inarudia washirikina. Yaani wakiwajia tena hao washiriki-na, Mwenyezi Mungu atawaletea malaika. Neno Musawimina linatokana na Simau (alama). Yaani wana alama inayofahamisha.

Hakika kauli hii ya Mwenyezi Mungu imefahamisha ufahamisho usiokubali Taawili yoyote kwamba Mwenyezi Mungu, uliotukuka uwezo wake, aliwasaidia waislamu kwa Malaika katika baadhi ya vita vyao. Hadith nyingi zimefahamisha hilo. Wameafikiana waislamu kwamba Mwenyezi Mungu aliwateremsha Malaika siku ya Badr kuwanusuru waumini, wakatofautiana kuhusu kuteremshwa kwao siku ya Uhud.

Hakuna mwenye shaka kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) aliwateremsha Malaika siku ya Badr kwa ajili ya kuwasaidia waumini, lakini hatujui kama ulikuwa ni msaa-da wa kuonekana kama vile kupigana, au ni msaada usionekana kama vile kuwa-hofisha washirikina, na kuwapa utulivu waumini. Mwenyezi Mungu ndiye mjuzi zaidi wala hatuna wajibu wowote wa kufanya utafiti na kulichunguza hilo, kwamba hata tukifanya utafiti hatuwezi kufikia kwenye yakini.

Hata hivyo ziko dalili zifahamishazo kwamba malaika huwa na sura za kibi-nadamu. Baadhi ya dalili hizo ni kama hizi zifuatazo:

(i) Aliyoyaelezea Mwenyezi Mungu kuhusu ugeni wa Ibrahim (a.s.); "Na wape habari kuhusu wageni wa Ibrahim . Hakika sisi tumetumwa kwa watu wenye makosa." (15:51 - 58)

(ii) Wageni wa Lut walioelezwa katika Sura 11:77

(iii) Kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema: "Akajifananisha kwake kwa (Sura ya) binadamu aliye kamili." (19:17)

(iv) Jibril alikuwa akimjia Mtume kwa Sura ya binadamu.

Lakini malaika kuwa na sura ya binadamu hakulazimishi kwamba wao walipigana kwa ajili ya Waislamu, bali inawezekana kuwasaidia kwa njia nyengine isiyokuwa kupigana.

Unaweza kuuliza: Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amesema: "Kwa hakika mimi nitawasaidia kwa malaika elfu moja watakaofuatana mfululizo." (8:9)

4& 40

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Kisha katika Aya hizi tunazozifasiri, ametaja elfu tatu; Aya inayofuatia hiyo akataja elfu tano moja kwa moja. Je, Mwenyezi Mungu aliwasaidia kwa elfu moja kwanza kisha elfu tatu, baadae tano na hivyo kuwa tisa?

Miongoni mwa yaliyojibiwa ni kwamba Mwenyezi Mungu aliwasaidia kwanza kwa elfu moja, kisha akaongeza elfu mbili, wakawa elfu tatu; tena akaongeza elfu mbili ikawa kwa ujumla ni elfu tano.

Mwengine amesema: Mwenyezi Mungu aliwasaidia waislamu siku ya Badr kwa malaika elfu moja. Kisha waislamu wakapata habari kwamba baadhi ya washirik-ina wanataka kuwasaidia Makuraish kwa idadi kubwa ya wapiganaji. Waislamu wakawa na hofu, na kuona taabu kwa sababu ya uchache wao. Ndipo Mwenyezi Mungu akawaahidi malaika elfu tano, ikiwa msaada utawajia Makuraish. Lakini kama ilivyosema Aya:

". kama mkisubiri na mkamcha mungu na wakawajia katika wakati wao huu ." lakini msaada haukuwajia Makuraish. Kwa hiyo wakatosheka Waislamu na msaada wa elfu moja tu.

Na Mwenyezi Mungu hakuyajaalia ila ni bishara kwenu na ili mioyo yenu ipate kutulia.

Yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewasaidia kwa malaika au aliwaahidi msaada, ili nyoyo zenu zipate utulivu kutokana na wingi wa idadi ya adui zenu na wala msikate tamaa kwa uchache wa idadi yenu.

Ili apate kuliangamiza kundi katika wale waliokufuru au awadhalilishe, ware-jee hali ya kuwa ni wenye kuambulia patupu.

Yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t.) aliwasaidia kwa malaika kuua na kuteka nyara, au awafedheheshe kwa kushindwa na waambulie patupu bila ya kuwa na tumaini la ushindi.

128.Huna lako jambo, au awataka-balie toba yao au awaadhibu, kwa sababu wao ni madhalimu.

129.Na ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo mbinguni na vilivy-omo ardhini. Humsamehe amtakaye na humwadhibu amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe mwenye kurehemu.

Kaashif4-46.jpgKaashif4-47.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

.

Aya 128 - 129HUNA LAKÖ JAMBO.

MAANA

Huna lako jambo.

Huenda waislamu kwa sababu ya kumtukuza Mtume wa Mwenyezi Mungu, wakadhani kwamba ametia mkono katika yaliyotokea Badr au wangeshindwa. Ndipo Mwenyezi Mungu akayaondoa mawazo haya kwamba mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu peke Yake. Hakika Qur'an imesisitiza sana katika Aya kadhaa kwamba Muhammad (s.a.w) ni mtoa bishara na muonyaji tu; ni mfikishaji wa hukmu za Mwenyezi Mungu kwa waja Wake.

Sio mbali kuwa hekima ya kukaririka huku na kutilia mkazo ni kwamba waislamu wasiingie ndani sana kuhusu Mtume wao kama walivyofanya wakristo kumhusu Bwana Masih (a.s.).

Au awatakabalie toba yao au awaadhibu, kwa sababu wao ni madhalimu.

Kauli hii inaungana na ile iliyosema au awadhalishe, yaani amri yote ni ya Mwenyezi Mungu; ama awatakabalie toba watakaposilimu au awaadhibu wak-ing'ang'ania ukafiri, kwa sababu wao wanastahili adhabu kwa dhuluma yao; yaani ukafiri wao.

Na ni vya Mwenyezi Mungu viliyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Ambaye ana ufalme wa mbingu na ardhi ni hakika kuwa na amri zote wala hakuna chochote anachoshirikiana na mwengine.

Humsamehe amtakaye na humwadhibu amtakaye.

Mara nyingi tumetaja kwamba akili inahukumu kuwa kafiri anastahili adhabu, laki-ni sio kuwa analazimika nayo; bali Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anaweza kumsame-he. Kwa ajili ya hekima fulani hata kama anastahili adhabu; sawa na unavy-omsamehe anayekufanyia uovu au kumsamehe unayemdai. Na rehema na usamehevu kutokana na Mwenyezi Mungu ndio zaidi kutokana na fadhila Yake na ukarimu Wake.

130.Enyi ambao mmeamini msile riba ziada juu ya ziada. Na mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kufaulu.

Kaashif4-48.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Kaashif4-49.jpg

131.Na uogopeni moto ambao ume-andaliwa makafiri.

132.Na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume ili mpate kurehemiwa.

133.Na harakisheni kuomba msama-ha kwa Mola wenu na pepo ambayo upana wake ni mbingu na ardhi imeandaliwa wamchao.

Aya 130 - 133 MSILE RIBA

 MAANA

Enyi ambao mmeamini! Msile riba ziada juu ya ziada. Na mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kufaulu

Wafasiri wametaja njia nyingi za kuiunganisha Aya hii na iliyo kabla yake. Nasi tumeshawahi kueleza mara nyingi kwamba miongoni mwa desturi ya Qur'an ni kuchanganya baadhi ya hukumu na hukumu nyingine. Zaidi ya hayo ni kwamba Aya zake zimeteremshwa kwa vipindi na kwa matukio mbali mbali.

Wametoa dalili baadhi kwa Aya hii kwamba riba iliyo haramu ni riba iliyo maradu-fu. Ama isiyokuwa maradufu, basi si haramu; kutokana na neno ziada juu ya ziada.

Ilivyo hasa ni kwamba riba ni haramu kwa mafungu yake yote na daraja zake zote. Umaradufu si sharti la ukatazo, isipokuwa ni kuonyesha vile walivyokuwa waki-fanya riba wakati wa ujahiliya. Zaidi ya hayo, ni kuweko Hadith na kuweko 'ijma', kwamba riba chache ni haramu kama ilivyo nyingi. Chochote ambacho wingi wake ni haramu, basi uchache wake pia ni haramu; iwe ni riba au si riba.

Mwenye Tafsir Al-Manar amerefusha ufafanuzi alipofasiri Aya hii. Mwisho aka-

malizia kuwa riba iko mafungu mawili:

Fungu la kwanza, ni riba ya muda; kwa mfano kushindwa mtu kulipa deni lake kati-

43

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

ka muda wa deni, wakaafikiana mdai na mdaiwa kuwa aongeze muda wa kulipa na aongeze mali. Yaani kila unapozidi muda ndipo mali ya kulipa inavyozidi. Akaendelea kusema mwenye Al-Manar: "Aina hii ya riba ni haramu hiyo yenyewe".

Fungu la pili, ni riba ya ziada kwa mfano kutoa mtu shillingi 100 kwa kutaka kulip-wa shillingi 110. Anasema mwenye Al-Manar kuwa riba hii, yenyewe sio haramu, isipokuwa ni haramu kwa sababu ya kufikia haramu; yaani kwa kuhofia kuwa riba ya muda ambayo ni haramu. Kwa maneno mengine ni kuwa riba ya muda ni haramu, kama lengo na riba ya ziada ni haramu kama njia ya kufikia lengo.

Kisha akaendelea kusema: "Riba ya ziada ni halali kwa dharura, bali hata kwa kuwa na haja; kama alivyosema Ibn Al-qayyim."

Hebu tuangalie maelezo yafuatayo:

(i) Imethibiti katika Qur'an na Hadith kwamba aina zote za riba ni haramu bila ya kutofautisha kuwa ni muda au la.

(ii) Kusema : "Bali kwa haja pia," ni katika kuteleza kwa kalamu. Kwani, ni dharura tu ndiyo ihalalishayo haramu. Ama haja hapana. Kuna tofauti kati ya haja na dharura, ni kwamba haja mtu anaweza asihitaji, japokuwa kwa kuivumilia. Ama dharura ni lazima kutekelezwa tu.

(iii) Dharura hapa haiwezi kupatikana kabisa. Si kwa mpokeaji wala kwa mtoaji. Mpokeaji riba, hana dharura yoyote. Kwa sababu anacho kitu cha kujisaidia japokuwa kwa siku moja (ndio maana akakopesha), ama yule mtoaji riba, ikiwa dharura imemfanya akope, basi haiwezi kumfanya atoe (yeye mwenyewe hana ndio maana akakopa). Na hilo si halali hata kama ataweka sharti, kwa sababu, sharti limebatilika. Na kama akichukua kwa nguvu, basi si halali kwa mchukuaji. Kwa sababu huko ni kula mali kwa batili.

(iv) Hebu tuseme, dharura inawezekana kwa anayepokea riba; itakuwa imeondoa hukmu tu, lakini maudhi hayajaondoka. Kwa mfano mwenye njaa ya kushiki-ka akiiba mkate bila shaka atakuwa ameondokewa na hukmu ya kupata dhambi lakini maudhui ya kurudisha thamani ya mkate bado yapo. Yaani analo jukumu la kumlipa mwenye mkate atakapokuwa na uwezo. Na mwenye kuhalalisha kuchukua riba kwa dharura hawezi kuwajibisha kuirudisha kwa mwenyewe ikiondoka shida.

Tumezungumza kwa ufafanuzi kuhusu riba katika Aya ya 275 Sura ya Baqara

Na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume ili mpate kurehemiwa.

Hapa kuna ufahamisho wa mambo mawili: Kwanza, kula riba ni kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume. Pili: mtu hapati rehema ya Mwenyezi Mungu kwa hali yoyote.

44

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Na harakisheni kuomba msamaha kwa Mola wenu na pepo ambayo upana wake ni mbingu na ardhi; imeandaliwa wamchao Mungu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kukataza kula riba, kuhadharisha na moto na kutoa mwito wa taqwa na kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume; baada ya yote haya ameamrisha kufanya haraka mambo ya kheri ambayo yanawajibisha radhi ya Mwenyezi Mungu na pepo yake. Heri na mambo mema zaidi ni kuhurumiana, kusaidiana na kutoa mali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu; kama itakavy-oeleza Aya ifuatayo: Ama kauli Yake: Upana wake ni mbingu na ardhi; ni fumbo la ukubwa.

134.Ambao hutoa katika raha na shida na wazuiao ghadhabu na wenye kusamehe watu na Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao hisani

135.Na ambao wakifanya jambo ovu au wakidhulumu nafsi zao humkumbuka Mwenyezi Mungu na kuomba msamaha wa dham-bi zao, na nani anayesamehe dhambi isipokuwa Mwenyezi Mungu, na hawaendelei na waliyoyafanya hali wanajua.

136.Hao malipo yao ni msamaha utokao kwa Mola wao, na mabustani yenye kupita mito chini yake. Ni wenye kudumu humo na ni malipo mema ya wenye kutenda.

Kaashif4-50.jpg

45

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

SIFA ZA WAMCHAO MWENYEZI MUNGU Aya 134 - 136

 MAANA

Mwenyezi Mungu amewasifu wanaomcha Yeye kwa sifa ambazo ni njema na ni bora hata kwa asiyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, sifa hizo ni kama hizi zifuatavyo:

i. Ambao hutoa katika raha na shida

Utajiri hauwafanyi kuwa na pupa na tamaa ya mali na kufanya ubahili. Wala ufakiri hauwakatishi tamaa wakajiona kuwa wao wanastahiki kuchukua zaidi kuliko kutoa. Bali katika hali zote mbili kwao ni sawa wanatoa kiasi wanavyoweza. Hadith inasema: "Toeni sadaka japokuwa ni upande wa tende."

ii. Na wazuiao ghadhabu

Hakuna kitu kifahamishacho zaidi nguvu ya imani na akili kubwa kuliko mtu kuim-iliki nafsi yake na kuzuia ghadhabu. Ikiwa kumeza ghadhabu kuna uchungu na mashaka ya nafsi, lakini ni kinga ya masaibu mengi na matatizo. Imam Ali (a.s.) katika kumuusia mwanawe, Imam Hasan (a.s.), anasema: "Meza ghadhabu, kwani mimi sikuona kinywa chenye utamu wa matokeo na ladha ya athari kuliko hicho."

iii. Na wenye kusamehe watu

Kumsamehe aliyekufanyia uovu kunashinda sana kuzuia ghadhabu. Kwa sababu mtu mara nyingi anaidhiki nafsi yake na kuzuia ghadhabu yake kwa msukumo fulani wa masilahi yake kama kujiepusha kujiingiza katika matatizo, ama kusamehe makosa ya watu huko ndiko kufanya hisani kuliko safi kabisa. Imam Ali (a.s.) anasema: "Ikiwa unamuweza adui yako, ujaalie msamaha wako ndio shukurani ya kuwa na uwezo huo."

iv. Na Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao hisani

Hisani inapatikana katika kila lenye manufaa ya kimaada au kimaana, iwe nyingi au chache, hata kama ni kusema: "Njia ni hii."

Sheikh Al-Maraghi, katika kufasiri Aya hii, anasema: "Ametaja Baihaqi kwamba, mjakazi wa Ali bin Husein (a.s.) alikuwa akimtilia maji ili atawadhe kwa ajili ya Swala. Birika ikamtoka mkononi na ikavunjika. Ali akainua kichwa chake; yule mjakazi akasoma Aya: "Na wazuiao ghadhabu." Akasema: "Nimezuia ghadhabu yangu."Akasoma tena mjakazi: "Na wenye kusamehe watu." Akasema: "Mungu akusamehe."

Mjakazi akaongeza : "Na Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao hisani." Akasema: "Nimekuacha huru kwa ajili ya Mwenyezi Mungu."

46

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

v. Na ambao wakifanya jambo ovu au wakidhulumu nafsi zao humkubuka Mwenyezi Mungu na kuomba msamaha wa dhambi zao

Uovu ni kama kuingilia haki za wengine, nako ni kuovu zaidi na kukubwa.

Kujidhulumu nafsi yake mtu, sio kuingilia haki za wengine, lakini kunaweza kuwa ni kuovu; kama vile ukafiri. Kwa hiyo kukutaja baada ya kutaja uovu ni katika hali ya kutaja ujumla baada ya kutaja mahsusi.

Kwa vyovyote iwavyo, ni kwamba Mwenyezi Mungu husamehe madhambi yote na hughufiria kila dhambi; iwe kubwa au ndogo. Kwa sharti yakutaka msamaha; yaani toba ya kweli. Yaani hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t.) humsamehe mwenye kutubu na akajing'oa kutoka kwenye dhambi. Ama mwenye kung'angania kufanya dhambi naye akiwa anajua kuwa ni dhambi, hawezi kughufiriwa na Mwenyezi Mungu. Maana yake ni kwamba mwenye kufanya uovu kwa kutojua ubaya wake, basi ni mwenye kusamehewa.

Hao malipo yao ni Msamaha.

Mfano wa Aya hii umeshapita katika Sura ya Baqara Aya 25 na 266.

137.Hakika zimepita desturi nyingi kabla yenu, basi tembeeni katika nchi na muone ulikuwaje mwisho wa wale waliokad-hibisha.

Kaashif4-51.jpg

138.Huu ni ubainifu kwa watu na mwongozo na mawaidha kwa wamchao.

Aya 137 - 138 ZIMEPITA DESTURI

MAANA

Hakika zimepita desturi nyingi kabla yenu.

Yametangulia maelezo kuhusu vita vya Uhud na walioshinda vita walikuwa ni washirikina. Kwa sababu wale waliokuwa wakilinda njia ya kupita adui waliiacha,

47

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

adui akawazungukia kwa nyuma.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anawaambia katika Aya hii Masahaba wa Mtume Muhammad (s.a.w): Wajue habari za watu waliopita na yaliyowapata wale walioacha msimamo, ili wapate fundisho kwa hilo, na wasirudie tena waliyoy-afanya katika Uhud ya kumwasi Mtume, kwa kuicha tupu njia ambayo waliamrish-wa wabakie hapo vyovyote itakavyokuwa. Kwa hiyo, walipokhalifu, yaliwapata yalowapata umma uliotangulia ambao uliwakhalifu Mitume yao.

Basi tembeeni katika nchi na muangalie ulikuwaje mwisho wa wale waliokadhibisha.

Makusudio sio kutembea hasa, bali ni kujua hali ya waliopita kwa njia yoyote ile. Hakuna mwenye shaka kwamba ni jambo la faida kwa mwenye akili kufanya utafi-ti wa hali za watu na kuchunguza sababu zilizowadhoofisha ili apate funzo na kuongoka kwenye lile lenye masilahi. Kwa ajili hii, ndio akasema Mtukufu wa ayasemayo:

Huu ni ubainifu kwa watu na mwongozo na mawaidha kwa wamchao.

Hii ni ishara ya kutaja desturi nzuri, ambazo mwenye kuzifuata hufaulu na mwenye kuziacha hupata hasara. Hapana budi ubainifu uwe kwa watu wote, ili iwe ni hoja kwa aliyeasi, na mwongozo na mawaidha kwa mwenye kumcha Mungu. Kwani hiyo ndiyo njia pekee inayopambanua baina ya mwasi na mtiifu. Lau si ubainifu kusingelikuweko na utiifu wala uasi.

USHENZI WA5 JUNI

Mnamo mwaka 1387 A. H. watu wa Bahrain waliniita ili nikatoe mihadhara ya kidi-ni kwa mnasaba wa mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Nilikaa kwao karibu siku 25 ambapo nilitoa mihadhara 20; na vijana walikuwa wakinitupia maswali mbali mbali. Siku moja nikajiwa na ujumbe wakasema: Tuzungumzie sababu za tukio la 5 Juni, bila ya mtazamo wa kidini.

Nami ni kasema:

Hakuna tofauti baina ya elimu na dini katika mtazamo wa kanuni na desturi inay-otawala maisha. Kwani matakwa ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) katika viumbe vyake na waja wake yanakwenda kwenye desturi za kielimu zilizonyooka na sababu za kawaida; bila ya kutofautisha baina ya waumini au makafiri. Kwa mfano anayejua kuogelea, ataogelea mpaka ufukweni kwa amani hata kama ni kafiri, na asiyejua atazama hata kama ni Mumin, vile vile mwenye kujiandaa vizuri na adui yake atamshinda, ikiwa adui yake hayuko katika hadhari na maandalizi hata kama ni mlahidi.

Na mwenye kufanya uzembe akapuuza, basi hupata hasara hata kama ni katika mawalii na wakweli. Mwenyezi Mungu anasema kuwaambia Masahaba wa Mtume (s.a.w): ". Wala msizozane msije mkavunjika moyo na kupotea nguvu

48

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

zenu ." (8:46)..

Imam Ali (a.s.) anasema: "Hakika hao - akikusudia watu wa Muawiya - wameshin-da kwa umoja wao kwenye batili. Na nyinyi - akiwakusudia watu wake -mmeshindwa kwa sababu ya kugawanyika kwenu kwenye haki yenu."

Kwa hivyo, haki haishindi kwa kuwa ni haki tu; na wala batili haishindwi kwa kuwa ni batili tu, bali kuna desturi katika maisha haya inayoendesha na kutawala jamii. Na Mwenyezi Mungu (s.w.t.) haiondoi au kubadilisha mwendo wake; sawa na ilivyo katika desturi ya maumbile.

Kwa hali hiyo basi, hakuna ajabu kwa wazayuni kuteka sehemu ya ardhi yetu, wakisaidiwa na wakoloni, maadamu sisi tumeghafilika, tukiwa tumegawanyika katika vijinchi ambavyo havina umoja wowote zaidi ya neno 'Uarabu.'

Hata hivyo, zamu ya kwanza inaweza kuwa kwa upande wa batili, lakini mwisho inakuwa kwa mwenye kusubiri na kumcha Mungu. Kwa sababu namna yoyote itakavyokuwa batili itakosa nguvu na sifa zitazoiwezesha kuendelea. Wakati wowote ule haki itakapopata wa kuipigania ambao wanaiamini na kujitolea mhanga kwa ajili yake, basi batili itatokomea tu.

Jambo lenye matumaini ni kwamba waarabu hawakusalimu amri, bali misukosuko na kushindwa kumewakomaza. Wakoloni walifikiri kwamba urefu wa njia utawad-hoofisha waarabu na kwamba kuzikalia kimabavu ardhi zao kutawafanya wanyenyekee. Lakini imeonekana kuwa wamekosea, na hakuna kitu kwa waarabu ila subira na bidii, iwe njia ni ndefu au fupi, nyepesi au nzito.

Unaweza kuuliza: Umesema kuwa matakwa ya Mwenyezi Mungu yanapita kwenye desturi iliyozoelekea; lakini mbona Mwenyezi Mungu (s.w.t) ali-waangamiza watu wa Nuh kwa tufani, watu wa Hud kwa upepo usiozuilika, watu wenye ndovu aliwamwagia mawe ya udongo mkavu, na Madain ya Lut ikaigeuza chini juu, yote hayo ni kwa sababu ya kuasi tu na kuihalifu haki; kama ilivyoelezwa katika Kitabu chake Kitukufu.

Jibu: Hekima ya Mwenyezi Mungu imepitisha matukio hayo ni maalum kupitia kwa Mitume waliotangulia tu na wala haikuendelea na kuenea kwa makafiri wote, kwa hiyo kutumia kipimo kwenye hilo ni nadra.

Swali la pili: Kwa nini haki isishinde katika hali zote, maadamu Mwenyezi Mungu anaitaka na anawataka watu wa haki, akichukia batili na wafuasi wake?

Jibu: Lau haki ingelishinda katika hali zote, watu wote wangelifuata kwa kupenda ushindi na kuchukia batili na ingelikuwa uzito kupambanua baina ya habithi ambaye anafuta haki kwa kukusudia manufaa na biashara, na mwema ambaye anafuata haki kwa njia ya haki na anayevumilia shida na matatizo. Zaidi ya hayo ni kwamba sababu hazijulikani ila baada ya kushindwa.

49

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Pili, lau matatizo angeyapeleka kwa wabatilifu daima na milele na kuwaepushia wenye haki, basi taklifa, thawabu na dhambi zingelibatilika vile vile. Kwa sababu kufuata haki katika hali hii kungelikuwa ni kwa nguvu na kushindwa, si kwa matak-wa na hiyari.

Kwa ufupi ni kwamba ni juu ya mwislamu kuizingatia vizuri maana ya Aya za Qur'an na kuzifanya ni kipimo cha itikadi yake, picha yake ya kushindwa na kushin-da, na nguvu na udhaifu, na kwamba kila kimoja katika mawili hayo yana njia yake mahsusi.

Kaashif4-52.jpg

139.Wala msidhoofike wala msi-huzunike kwani nyinyi ndio mlio juu ikiwa nyinyi ni waumini.

140.Kama mmepata jeraha, basi kuna kaumu wamekwishapata jeraha kama hilo, na siku za namna hii tunawaletea watu kwa zamu. Na ili apate kuwajua Mwenyezi Mungu ambao wameamini katika nyinyi na afanye miongoni mwenu mashahidi. Na Mwenyezi Mungu hawapendi madhalimu.

141 .Na ili awatakase Mwenyezi Mungu ambao wameamini na awaangamize makafiri.

Aya 139 - 141 MSIDHOOFIKE

MAANA

Wala msidhoofike wala msihuzunike.

Katika mambo anayoyapa kimaumbile kiongozi mwenye hekima ni kuwepo kwa moyo shupavu katika jeshi lake, na kutokuwa na udhaifu au hofu katika nafsi zao. Kwa sababu kushinda hakutegemei nguvu tu, isipokuwa kabla ya lolote kwanza ni

50

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

uthabiti na nguvu ya maazimio. Kwa hakika adui yako anaogopa zaidi kumpinga kuliko kumkabili kwako na silaha. Kwa sababu silaha hazina faida ikiwa hakuna uthabiti katika upinzani.

Tumeyaona magazeti na kusikia Idhaa za kikoloni zinavyotawanya matangazo kwa ajili ya ukoloni na uzayuni kwa njia ya kupiga vita nafsi na kuuharibu uthabiti wa waarabu.

Kujikomboa kimawazo, ndio nguzo ya kwanza ya kujitawala na kujikomboa. Qur'an imetuongoza kwenye hakika hii kwa kusema: "Wala msidhoofike wala msi-huzunike."

Ama kusema: kwani nyinyi ndio mlio juu ikiwa nyinyi ni waumini, ni kuonye-sha kuwa Uislamu uko juu na wala hakuna kinachokuwa juu yake, ambaye uisla-mu umemakinika katika moyo wake, hawezi kulegea wala kufazaika hasa katika njia ya uislamu na kuinua haki isipokuwa anaweza kulegeza kamba katika haki zake zinazomhusu yeye, sio zinazohusu dini yake na itikadi yake.

Kama mmepata jeraha, basi kuna kaumu wamekwishapata jeraha kama hilo.

Yaani yaliyowapata siku ya Uhud kutoka kwa adui naye yalimpata siku ya Badr, lakini hakudhoofika bali alijiandaa na akaurudisha mpira kwenu.

Na siku za namna hii tunawaletea watu kwa zamu.

Makusudio ya siku hapa ni nguvu; kwamba mara zinakuwa kwa hawa mara kwa wale. Kulikuwa na wakati nguvu zilikuwa kwa mali na watu tu. Lakini leo nguvu ni elimu na kukua viwanda. Kwa hiyo nchi isiyokuwa na elimu ni dhaifu, hata kama ina dhahabu nyeusi (petroli) au dhahabu ya njano. Na nchi yenye elimu ndiyo yenye nguvu hata kama ardhi yake ni tupu isiyokuwa na madini yoyote.

Mnyonge inabidi amnyenyekee mwenye nguvu atake asitake. Zamani elimu ilikuwa Mashariki kwenye nchi za waislamu, kisha ikahamia Magharibi. Inawezekana kuwa waislamu wakawa juu kielimu na kiviwanda miaka ijayo. Nani ajuae? Mwenyezi Mungu ndiye mjuzi zaidi.

Na ili apate kuwajua Mwenyezi Mungu ambao wameamini katika nyinyi.

Jumla hii inaungana na jumla inayokadiriwa hivi. Na siku za namna hii tunawaletea watu kwa zamu kwa hekima iliyopitisha zamu hii. Wala sio makusudio kwamba Mwenyezi Mungu hakuwa akiwajua waumini. Hakika Mwenyezi Mungu anajua siri na yaliyofichika, isipokuwa makusudio ni kuidhihirisha elimu yake kwa waumini ili watu wajulikane na wapambanuke na wengineo.

Mwenye Majmaul-Bayan anasema: "Hakika mmoja wetu akijua kuwa kesho itafi-ka atakuwa ameijua na ikifika pia atakuwa amekwishaijua. Kwa hiyo mabadiliko na matukio yanapatikana katika kile kinachojuliwa ambacho ni kesho sio yule

51

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

anayejua. Hivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Yeye anamjua mumin na kafir kabla ya kudhihirika kwa watu. Wakijitokeza wanakuwa wameju-likana mbele za watu."

Na afanye miongoni mwenu mashahidi

Shahidi ni yule anayejitolea kufa kwa kuihami itikadi yake, kwa sababu yeye anayaona mauti ni furaha na kuishi na madhalimu ni majonzi, kama alivyosema bwana wa mashahidi, Hussein bin Ali (a.s.). Na Qur'an imejaa utukuzo wa mashahidi; kama vile kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ".Basi hao wako pamoja na wale aliowaneemesha Mwenyezi Mungu miongoni mwa manabii na walio wakweli sana na mashahidi."(4:69)

Na Mwenyezi Mungu hawapendi madhalimu

Kwa hiyo hawezi kumchagua yeyote katika wao kwa kufa shahidi

Na ili awatakase Mwenyezi Mungu ambao wameamini

Lengo la kuweko zamu ya siku ni kuwa mtu afaidike na majaribio na atakase nafsi yake na machafu. Imesemekana kuwa neno Mahhisa ni mitihani na majaribio ambayo yanadhihirisha hakika ya mtu.

Na awaangamize makafiri. Arrazi anasema: "Maana iliyo karibu zaidi ni kuwa makusudio ya makafiri hapa ni kikundi maalum katika wao, nao ni wale ambao wamepigana vita na Mtume (s.a.w) siku ya Uhud. Tumesema hivyo kwa kujua kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu hakuwaangamiza makafiri wote, bali wengi katika wao walibakia kwenye ukafiri wao."

Maelezo haya ni sahihi ikiwa makusdio ya maangamizi ni adhabu ya duniani sio ya akhera.

142.Je, mwadhani mtaingia peponi na hali Mwenyezi Mungu haja wajua wale waliofanya jihadi miongoni mwenu na kuwajua wale waliofanya subira?

143.Kwa hakika mlikuwa mkiyata-mani mauti kabla ya kuyakuta; basi mmekwishayaona nanyi mwatizama.

Kaashif4-53.jpgKaashif4-54.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne 3. Sura Al-Imran ..

Aya 142 - 143THAMÂNİYÂ PEPO

 MAANA

Je, mwadhani mtaingia peponi na hali Mwenyezi Mungu hajawajua wale waliofanya jihadi miongoni mwenu na kuwajua wale waliofanya subira?

Aya hii imefahamisha wazi wazi kwamba uislamu una mfungamano mkubwa na amali njema hapa duniani na kwamba sharti ya kwanza ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu na kufuzu kwa radhi Zake na thawabu Zake ni jihadi, kujitolea, ukweli, ikhlasi, subira na uthabiti. Ama kujenga misikiti, sehemu za ibada, kufun-ga, kuswali na kusoma Qur'an na nyuradi, yote hayo na mengineyo sichochote ila ikiwa, ni nyenzo ya kazi itakayoleta manufaa kwa watu au itakayowakinga na mad-hara.

Aya hii tuliyonayo ambayo imefungamanisha kuingia peponi na jihadi na kuvumil-

ia taabu zake, iko katika maana pamoja na Aya hizi zifuatazo:

"Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kwa waumini nafsi zao na mali zao kwamba

wapate pepo, wanapigana katika njia ya Mwenyezi Mungu, kwa hiyo wanaua na

wanauwa. Ni ahadi iliyothibiti juu yake katika Tawrat na Injil na Qur'an ." (9:111)

Na Aya nyingine ni:

"Na aliye kipofu katika (dunia) hii basi katika akhera atakuwa kipofu na aliyepotea

zaidi njia." (17:72)

Inatosha kuwa ni dalili ya mkato ya hayo kauli yake Mwenyezi Mungu: "Na kwamba mtu hatapata ila yale aliyoyafanya. Na kwamba amali yake itaonekana. Kisha atalipwa malipo yaliyo kamili." (53: 39 - 41)

Miongoni mwa kauli za Imam Ali (a.s.) ni: "Pepo imezungukwa na machukivu na moto umezungukwa na anasa . Nafsi zenu hazina thamani zaidi ya pepo, kwa hivyo msiziuzie (kitu kingine) ila hiyo tu."

Yameshatangulia maelezo katika tafsir ya Aya 155 katika Sura ya Baqara, kifungu 'Thamani ya pepo.'

NEMBO ZA KIDINI

Nembo za kidini, ni kama sehemu za ibada na za kuswali zilizo takatifu, hilo hali-na shaka, bali ni dharura ya kidini, hapana budi kuwepo. Hakuna nchi yoyote au kikundi chochote ambacho kina msingi mmoja ila kitakuwa na nembo inayokionye-sha kikundi hicho au nchi hiyo, na inayowaweka pamoja wafuasi wake.

Lakini nembo peke yake si chochote, bali nembo ni lazima ifuatiliwe na vitendo na athari. Kwa hiyo Swala si kurukuu na kusujudu tu, bali Swala ni ile inayoiweka nafsi ya mwenye kuswali kujitakasa na maovu, wala muungano sio kuungana

53

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

kusoma tahlili na takbira, bali ni kusaidiana tukiwa na ikhlasi ya lile ambalo lina kheri ya wote.

Hivi sasa wengi wetu wamezifanya nembo za kidini ni vyombo vya kupoteza, na maficho ya miradi ya wakoloni na malengo ya uzayuni. Kwa sababu vyama vingi ambavyo vina majina ya kidini au ya kizalendo ni mashirika ya kijasusi ya nje. Na gharama zake zinatokana na faida itokayo katika mashirika ya mafuta. Lakini jambo la kutia moyo ni kuwa hayo yamefichuka kwa wote. Wenye ikhlasi hawavi-amini wala hawashirikiani navyo isipokuwa wahaini wanaouza dini yao na nchi yao kwa shetani.

Kwa hakika mlikuwa mkiyatamani mauti kabla ya kuyakuta; basi mmekwisha yaona nanyi mwatizama.

Msemo unaelekezwa kwa baadhi ya Sahaba wa Mtume (s.a.w), ambao kabla ya vita vya Uhud, walikuwa wakitamani kufuzu kwa kufa shahid, lakini mambo yalipowazidia, waliogopa, wakamwachia Mtume (s.a.w) adui yake na adui yao. Baadhi ya Riwaya zinasema kuwa miongoni mwa Masahaba walikuwako waliokuwa wakisema: vikija vita tukiwa na Mtume (s.a.w) tutapigana tu, walipotahiniwa na hilo hawakutekeleza ahadi. Ndipo Mwenyezi Mungu akawa-teremshia Aya hii. Makusudio ya kuona mauti ni kuona sababu zake kutoka kwenye mapambano ya mashujaa. Mwenyezi Mungu amewatahayarisha kwa Aya hii kutokana na vitendo vyao kuhalifu kauli zao.

MABADILIKO YA HULKA NA FIKRA

Kila mtu ana hali zake na mazingira yake yanayomuhusu. Hali hizi - aghlab - ndizo zinazotawala hulka na fikra zake. Kwa mfano mtu mnyonge anaiona mbaya zaidi dhulma kuliko mwenye nguvu. Na mwenye kukulia katika mazingira ya kuabudu masanamu hawezi kuona ubaya kuyatukuza, ila akiwa si mtu wa kawaida; kama vile Muhammad bin Abdullah. Kwani yeye kimaumbile yake tu alikuwa akichukia kila desturi mbaya ya watu wake.

Mara nyingine hali ya mtu inaweza kubadilika na kuwa tajiri baada ya kuwa mask-ini, au kinyume chake. Basi hapo hulka zake na fikra zake zinabadilika kufuatana na mabadiliko hayo. Kwa hiyo dhati ya mtu inabakia na sifa yake ikiwa hali yake ya kijamii haikubadilika.

Aghlabu hali ikibadilika na sifa za dhati nazo hubadilika. Tumewaona watu waliokuwa wakiwalaumu matajiri na maraisi, wakati wao ni mafukara wanaoon-gozwa, lakini mara tu walipopata mali na cheo wakavunja ahadi na kuwa wabaya zaidi ya waliokuwa wakiwalaumu jana.

Qur'an Tukufu imetilia mkazo nadharia hii kwa Aya hii tuliyo nayo, na pia Aya

nyingine isemayo:

"Na miongoni mwao wako waliomwahidi Mwenyezi Mungu: akitupa katika fadhila

54

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

zake, hakika tutatoa sadaka na tutakuwa miongoni mwa watu wema. Lakini alipowapa katika fadhila zake walizifanyia ubakhili na wakageuka na huku wakipu-uza."(9: 75 - 76)

Mwenye akili na uzoevu huituhumu nafsi yake wala halitilii mkazo kwa mawazo kila linalomtokea, kwa kuhofia kuwa bendera inayofuata upepo; kama ambavyo mumin wa kweli anabaki kuwa thabiti katika tabu na raha; maneno yake hufuatana na vitendo vyake katika hali zote na yote huyaelekeza kwa Mwenyezi Mungu peke yake.

Yamekuja maelezo katika tafsir ya Aya isemayo: "Na yeye ndiye ambaye ame-waumba katika nafsi moja kuna (iliyo) mahali pa milele na mahali pa muda." (6:98) kuwa, mahali pa milele ni imani iliyo thabiti, na mahali pa muda ni imani ya kuazi-ma, na hakuna kitu kinachofahamisha imani potofu kuliko kugongana kauli na vitendo. Ndio maana zikawa kauli za Mitume na Maimamu watakatifu ndio vitendo vyao hasa. Na vitendo vya wanafiki viko mbali na kauli zao.

144.Hakuwa Muhammad ila ni Mtume; wamekwisha pita Mitume kabla yake. Je, akifa au akiuliwa mtarudi nyuma? Na atakayerudi nyuma hatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu atawalipa wenye kushukuru.

145.Na nafsi haiwezi kufa ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu kama ilivyoandikwa ajali yake. Na anayetaka malipo ya dunia tutampa humo na anayetaka malipo ya akhera tutampa huko; na tutawalipa wenye kushukuru.

Kaashif4-55.jpg

55

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

146.Ni manabii wangapi waliopigana pamoja nao waumin wengi, nao hawakulegea kwa yale yaliyowa-sibu katika njia ya Mwenyezi Mungu, wala hawakudhoofika, wala hawakudhalilika. Na Mwenyezi Mungu anawapenda wanaosubiri.

3. Sura Al-Imran

Kaashif4-56.jpg

147.Halikuwa neno lao, ila ni kuse-ma: Ewe Mola wetu! Tughufirie dhambi zetu na kupita kwetu kiasi katika mambo yetu na uimarishe miguu yetu na utunusuru juu ya watu makafiri.

148.Mwenyezi Mungu akawapa malipo ya duniani na malipo ya akhera na Mwenyezi Mungu anawapenda watendao mema.

  aya 144 147 HAKUWA MUHAMMAD ILA NI MTUME MAANA.

Hakuwa Muhammad ila ni Mtume wamekwishapita Mitume kabla yake. Je, akifa au akiuliwa mtarudi nyuma?

Aya hii inaashiria tukio maalum ambalo ni vita vya Uhud; limekwishaelezwa. Kwa ufupi ni kuwa Mtume (s.a.w) aliwaamrisha wapiga mishale wasiondoke kwenye mlima kwa hali yoyote ile, ni sawa wawe waislamu wameshinda au wameshindwa. Lakini kundi kubwa la wapiga mishale walipoona kushindwa kwa washirikina katika muhula wa kwanza, waliziacha sehemu za nyuma za waislamu bila ya ulinzi na kuharakia nyara. Kwa hiyo washirikina wakawarudia waislamu: wengi wao wakauwawa na Mtume kujeruhiwa vibaya. Mnadi akanadi kuwa Muhammad

Kaashif4-57.jpg

56

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

ameuawa, watu wakamkimbia Mtume na akabakiwa na wachache tu, akiwemo Ali bin Abi Talib na Abu Dajana Al-ansari. Masahaba wengine wakasema: "Hatupati mtu wa kututakia amani kwa Abu Sufian?" wengine wakasema: "Lau Muhammad angelikuwa Mtume asingeuawa, rudieni dini yenu ya kwanza."

Qur'an imewakaripa walioshindwa, wenye shaka shaka ikiwaambia kuwa Muhammad ni Mtume aliye binadamu tu, anayefikisha risala ya Mola wake kwa waja wake, na anapofikisha, basi umuhimu wake umekoma. Na ujumbe wake haufungamani na utu wake wala haufi kwa kufa kwake, bali utabaki kwa kubakia Mwenyezi Mungu asiyekufa; sawa na Mitume wengine ambao walikufa au kuuwawa na ujumbe wao na mafunzo yao kubakia. Kwa maneno mengine, mwito haufi kwa kufa anayeutoa mwito huo; na misingi haiondoki kwa kuondoka watu.

Mfano mzuri wa hakika hii ni yale yaliyoelezwa katika Tafsir Tabari kwamba mtu mmoja katika Mujahirina alimpitia mtu mwengine katika Ansari akiwa ametapakaa damu. yule Muhajir akasema: "Je, wajua kuwa Muhammad ameuawa?" Ansari akasema: "Ikiwa ameuwawa tayari amekwisha fikisha ujumbe, basi ipi-ganieni dini yenu."

Katika hiyo hiyo Tabari na vinginevyo imeelezwa kuwa Anas bin Annadhr alimpitia Umar bin Khattab na Talha bin Ubaidullah na watu wengine katika Muhajir na Ansar wakiwa wamesalimu amri. Anas akawaambia: "Mbona mmekaa? wakasema: Muhammad ameuawa. Akasema: Ikiwa Muhammad ameuawa, lakini Mola wa "Muhammad hakuuawa, na mtayafanyia nini maisha baada ya Muhammad. Basi piganieni lile alilopigania na kufeni kwenye lile alilolifia." Kisha akaendelea kusema: "Ewe Mola wangu! Hakika mimi nakuomba msamaha na waliyoyasema hawa na ninajitenga na waliyokuja nayo." Kisha akaukamata barabara upanga wake akapigana mpaka akauawa. (radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie)

Ibn Al-Qayyim Al-Jawziy katika juzuu ya pili ya Zadul-Ma'ad uk. 253 anasema: Tukio la Uhud lilikuwa ni utangulizi na lawama kuhusu mauti ya Muhammad (s.a.w). Mwenyezi Mungu anawazindua na kuwakaripia kwa kurudi nyuma kwao, iwapo Mtume wa Mwenyezi Mungu atakufa au kuuwawa. Mwenye Tafsir Al-Manar akimnukuu mwalimu wake Sheikh Muhammad Abduh anasema: Neno 'mtarudi nyuma' linaenea katika kurtadi kwa kuacha dini na kuacha kuipa nguvu haki." Kisha akaongezea mwenye Al-Manar kwa kusema: hivi ndivyo ilivyo.

Kwa hiyo basi, kurudi nyuma kulikokusudiwa katika Aya hii hakuishii kwenye Tawhid peke yake, bali kunaenea kuacha kazi ya haki aliyoiusia Mtume (s.a.w). Haya yanatiliwa nguvu na yaliyoelezwa katika Sahihi Bukhari Jz 9 kitabul-Fitan kwamba Mtume atasema siku ya kiyama: "Ewe Mola wangu! (Hao) ni sahaba zangu." Naye ataambiwa "Wewe hujui walizuwa nini baada yako."

Hadith nyingine katika Hadith za Bukhari inasema: ".wewe hujui walibadilisha nini baada yako?" "Hapo nitasema: Basi kuangamia ni kwa mwenye kuibadilisha

4& 57

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

(dini yake) baada yangu." Hakuna mwenye shaka kwamba makusudio ya kubadil-isha hapa ni kuiacha sunna yake na kuhalifu kauli zake na sharia yake.

Na atakayerudi nyuma hatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu bali atajidhuru mwenyewe kwa kujiingiza katika machukivu na adhabu ya Mwenyezi Mungu.

Na mwenyezi Mungu atawalipa wenye kushukuru

Ibnul-Qayyim katika Zadul-Ma'ad uk. 254 anasema: "Na wenye kushukuru ni wale waliojua thamani ya neema wakathibiti nayo mpaka wakafa au kuuawa. Ilidhihiri athari ya lawama hii na yakahukumu maneno hayo siku alipokufa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w), akartadi mwenye kurtadi kwa kurudi nyuma.

AJALI HAINA KINGA

Na nafsi haiwezi kufa ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu - kama ilivyoandik-wa ajali yake. Aya hii iko katika maana ya Aya isemayo: ".Utakapofika muda wao hawatakawia hata saa moja wala hawatatangulia." (7:34)

Maana ni kuwa uhai na kifo viko mikononi mwa Mwenyezi Mungu na kwamba ajali imepangwa katika muda maalum anaoujua yeye; haiharakishwi wala haikawizwi. Ni sawa iwe sababu yake ni upanga, maradhi, uzee au mengineyo.

Imam Ali (a.s.) anasema: "Ajali inatosha kuwa ni mlinzi."Akasema tena: "Ajali ni ngome imara."

Katika Aya hii kuna mahimizo ya Jihadi, kwa sababu ajali ipo tu. Na wala hakuna yeyote atakayekufa kabla ya kufikilia ajali yake. Hata akijipeleka kwenye maangamizi.

Unaweza kuuliza: tunavyoshuhudia ni kuwa mauti yana sababu maalum: kama vile kuuliwa, kufa maji, majanga na mengineyo. Je hili si linakanusha kuwa ajali imepangwa kwa ujuzi wake Mwenyezi Mungu?

Hilo amelijibu Sheikh Muhammad Abduh - kama ilivyo katika Al-Manar- kwamba hakuna sababu za mauti zaidi ya ajali iliyokadiriwa na Mwenyezi Mungu. Kwani janga linaweza kuenea, lakini akafa kijana mwenye nguvu na akabaki mkongwe dhaifu. Ni majanga mangapi yaliyomwacha huyu ya kamuua yule. Na kama inge-likuwa sababu hizi zinawaenea wote, basi ingelithibiti athari yake kwa wote, bila ya kubakisha hata mmoja.

Swali la pili: Kama ni hivyo basi inatakikana muuaji asiwe na majukumu mbele ya Mwenyezi Mungu. Lakini Mwenyezi Mungu anasema:

"Na Mwenye kumua Muumin kwa kukusudia, basi malipo yake ni Jahannam, humo atadumu na Mwenyezi Mungu amemghadhibikia na amemlaani na amemwandalia adhabu kubwa (4:93).

Jibu: Mwenye kuuawa amekufa kwa muda wake, na mwenye kuuwa anastahili

4& 58

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

adhabu, kwa sababu amefanya lililokatazwa na Mwenyezi Mungu hali alikuwa anaweza kujiepusha nalo na kumwacha aliyemuua, afe na sababu nyingine. Kwa maneno mengine ni kuwa hapa kuna mambo mawili:

Kwanza: Kila mwenye kufanya jambo la haramu kwa makusudi, ana jukumu.

Pili: Mwenye kufanyiwa makosa ana muda wake maalum. Kwa hiyo hapo yamekuja mambo mawili katika maudhui moja, lakini kila moja lina hukumu yake na athari yake.

Na anayetaka malipo ya dunia tutampa humo na anayetaka malipo ya akhera tutampa huko: na tutawalipa wenye kushukuru.

Tamko la Aya linaenea kwa mambo yote na mfumo wa maneno unahusu jihadi. Maana yake ni kuwa mwenye kupigana kwa kutafuta faida na ngawira, si kwa kuta-ka thawabu za Mwenyezi Mungu na akauliwa, basi atakuwa amepata hasara ya dunia na akhera. Na kama akisalimika na jeshi likapata ngawira, atapata fungu lake na hatapata chochote katika thawabu za Mwenyezi Mungu, kama akipigana kwa kuinusuru haki na kuinyanyua dini atachukua fungu lake la ngawira na atas-tahiki malipo na thawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Vilevile hata akikusudia mambo mawili pamoja, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: ".Na kuna miongoni mwa watu asemaye: Mola wetu! Tupe katika dunia, na katika akhera hana sehemu yoyote. Na miongoni mwao yuko anayesema: Mola wetu! Tupe mema duniani na katika akhera (utupe) mema na utukinge na adhabu ya moto. Hao ndio wenye fungu katika waliyoyachuma na Mwenyezi Mungu ni mwepesi wa kuhisabu." (2: 200-202)

Jihadi inaweza kuchukuliwa na makusudio mawili pamoja: dunia na akhera kinyume na Saumu, Swala, Hijja na Zaka. Kwa sababu hayo yote ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu pekee yake ambayo yanaharibiwa hata na mchanganyiko mdogo.

KILA MTU ANA ALILOLINUIA

Mwenye kufuatilia Aya za Mwenyezi Mungu (s.w.t.) na Hadith za Mtume Wake (s.a.w) ataona kuwa nia ina athari kubwa katika kuhukumu kauli na vitendo vya watu. Mwenyezi Mungu anasema: "Anayetaka malipo ya duniani tutampa."

Akasema tena: "Anayetaka (dunia) ipitayo upesi, tutamharakisha humo tunayoy-ataka. na anayetaka akhera na akizifanyia juhudi amali zake na hali ya kuwa ni mu'min, basi hao juhudi yao ni yenye kushukuriwa." (17: 18-19).

Vilevile amesema: "Siku ambayo haitafaa mali wala watoto, isipokuwa mwenye kuja na moyo safi." (26: 88-89).

Katika Hadith tukufu imesemwa hivi: "kila mtu ana alilonuia.watu watafufuliwa kulingana na nia zao.. hakika amali (zote huzingatiwa) kwa nia. Nia ya mtu ni

59

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

bora kuliko vitendo vyake."

Wala hapana ajabu, kwani moyo ndio msingi. Mapigo yake ndiyo yanayopeleka uhai wa mtu na kuzimika kwake ndiko kuzimika uhai, ndipo mahali pa imani na ukanushaji, hofu na matarajio, mapenzi na chuki, ushujaa na woga, ikhlas na unafiki, kukinai na tamaa na mengineyo katika mambo mazuri na mabaya.

Hadith Qudsi inasema: "Haikunikunjua ardhi yangu wala mbingu yangu lakini moyo wa mja wangu mumin umenikunjua." Yaani umetambua ukubwa wa Mwenyezi Mungu.

Vitendo vyote hutendwa na kutengenezwa na moyo, kwa sababu ndio asili yake.

Kwa hivyo basi mtu anaweza kujichagulia njia yake yeye mwenyewe kwa kuch-agua malengo yake, kheri na shari anayachagua kuanzia mwanzo hadi mwisho, kama ambavyo sisi tunaweza kumhukumu kwa malengo anayojichaguliya mwenyewe.

Watu wa nadharia (ya upatikanao) wanasema: haiwezekani kumhukumu mtu ila baada ya kupita hatua ya mwisho katika hatua za maisha yake.. maana yake ni kuwa wanalazimisha kutopitisha hukmu ila kwa waliokufa tu. Ama walio hai hawahukumiwi au kulaumiwa. Ingawaje hawa wanaodai hivyo akiwemo kiongozi wao Sartre, wanawahukumu walio hai.

Unaweza kuuliza: Mara nyingi umeeleza - katika sehemu mbali mbali - kwamba vinavyozingatiwa ni vitendo na kwamba hakuna imani ila kwa takua na amali njema. Na haya si yanapigana na kauli yako ya hapa kwamba inayozingatiwa ni nia na malengo?

Jibu: Nia, tunayoikusudia hapa ni nguvu ya msukumo na azimio linalotia mkazo ambalo haliepukani na kitendo. Hilo limeelezwa na Aya isemayo: ". Na anayeita-ka akhera na akazifanyia juhudi amali zake." (17:19).

Na nia hii iko katika hukmu ya kitendo, bali ni kitendo hasa, kama alivyosema Imam Jafar as-Sadiq (a.s.). kwa sababu ndiyo asili ya kitendo na ni chimbuko lake. Na asiyekusudia hatendi. Kwa hivyo basi thawabu za nia hii ni thawabu za kitendo. Ama nia ya uovu, yaani kuazimia kufanya uovu, ni haramu bila ya shaka yoyote. Na mwenye kuazimia hayo anastahiki adhabu, lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t.) aweza kumuondoshea adhabu hiyo - kwa hisani yake - ikiwa hatofanya alilolinuiya, hata kama alilazimika kuliacha kwa nguvu. Hivyo, katika mtazamo wa Kiislamu, nia ya kheri ni kheri hata bila ya vitendo na nia ya shari si shari bila ya kitendo.

Ni Manabii wangapi waliopigana, pamoja nao waumini wengi. Nao hawakulegea kwa yale yaliyowasibu katika njia ya Mwenyezi Mungu, wala hawakudhoofika, wala hawakudhalilika. Na Mwenyezi Mungu anawapenda wafanyao subira.

60

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwapa ushindi Waislamu katika vita vya Badr, waki-wa ni wachache na wanyonge, waliona kwamba kila vita watashinda maadamu wako na Muhammad (s.a.w), hivyo kushindwa kwa siku ya Uhud kukawa ni jambo wasilolitazamia. Wakawa na yale tuliyokwisha yaeleza.

Katika Aya hii Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawapigia mifano wale waliolegea, wakadhoofika na kudhalilika na kutokuwa na subira siku ya Uhud, anawapigia mfano na wafuasi wa Mitume waliotangulia, ambao walikuwa na subira katika Jihadi, kuuliwa , kutekwa na kujeruhiwa, nao hawakukimbia, kama mlivyofanya nyinyi wafuasi wa Muhammad (s.a.w). Na ilikuwa ni laiki yenu muwaigize, muwe na mazingatio kwa hali zao; jambo ambalo linatakikana kwa waumini wanaopiga-nia dini yao na itikadi yao kwa nyoyo zao.

Halikuwa neno lao, yaani wafuasi wa Mitume waliotangulia,ila ni kusema:

"Ewe Mola wetu! Tughufurie dhambi zetu na kupita kwetu kiasi katika mambo yetu na uimarishe miguu yetu na utusaidie juu ya watu makafiri.

Hawakutia shaka kabisa katika dini yao na Mtume wao kama yale waliyoyafanya maswahaba wa Muhammad (s.a.w) siku ya Uhud. Hivi ndivyo anavyokuwa mu'min wa kweli, akijituhumu mwenyewe na kuona kuwa balaa zilizompata ni kwa ajili ya uzembe wake na kupetuka kwake mpaka katika amri za Mwenyezi Mungu, humuomba Mwenyezi Mungu msamaha na uongofu. Ama mu'min aliye kom-bokombo anamsukumizia Mungu na kusema: Mola wangu amenitweza.

Mwenyezi Mungu akawapa malipo ya duniani na malipo mema ya akhera, na Mwenyezi Mungu anawapenda wanaotenda wema. Malipo ya Mwenyezi Mungu na pendo lake linatosha kuwa ni fahari na ni akiba ya akhera. Aya hii inafahamisha kwamba kunyenyekea na kujituhumu kunakurubisha kwa Mwenyezi Mungu na humwinua mwenye kunyenyekea na kumweka kwenye daraja ya juu.

149.Enyi ambao mmeamini! Mkiwatii ambao wamekufuru watawarud-isha nyuma mtageuka kuwa ni wenye kuhasirika.

150.Bali Mwenyezi Mungu ndiye mlinzi wenu naye ndiye bora wa wasaidizi.

Kaashif4-58.jpgKaashif4-59.jpgKaashif4-60.jpg

r l-Kashif: Juzuu ya Nne                                                                  3. Sura Al-Imran

151.Tutatia hofu katika nyoyo za ambao wamekufuru kwa sababu ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kitu ambacho hakukiteremshia hoja; na makazi yao ni motoni nayo ndiyo makazi mabaya ya wad-halimu.

Aya 149-151 MKIWATII AMBAO WAMEKUFURU

LUGHA

Makusudio ya neno sultan ni hoja, limetumika neno hilo kwa vile hoja ina nguvu za kuikinga batili.

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Mkiwatii ambao wamekufuru watawarudisha nyuma.

Sheikh Maraghi katika kufasiri Aya hii anasema: "Makusudio ya 'ambao wamekufuru' ni Abu Sufyan, kwa sababu yeye ndiye mzizi wa fitina."

Kila mtu, awe na haki au batili, anataka watu wote wawe upande wake. Tofauti ni kwamba twaa ya mbatilifu ni hasara na madhara. Na twaa ya mwenye haki ni faida na manufaa, kwa ajili hii ndipo Mwenyezi Mungu akawahadharisha waumini na makafiri.

Bali Mwenyezi Mungu ndiye mlinzi wenu naye ndiye bora wa wasaidizi.

Mu'min hafikirii kumtii kafiri na kumpenda wala hababaishwi na hadaa zake au kumfanya ni mlinzi, isipokuwa Mungu tu peke yake ndiye anayemnusuru na maadui. Na ambaye Mwenyezi Mungu ndiye msaidizi wake, hatahitajia rafiki wala msaidizi mwingine.

Tutatia hofu katika nyoyo za ambao wamekufuru kwa sababu ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kitu ambacho hakukiteremshia hoja.

Yaani, enyi waislamu! Msiwaogope washirikina kwa sababu ya wao kuwashinda katika vita vya Uhud, kwani Mwenyezi Mungu atatia hofu katika nyoyo zao kutokana na nyinyi, kwa sababu wao wamemfanya Mwenyezi Mungu kuwa ana washirika bila ya dalili yenye mwelekeo, isipokuwa ni kwa kufuata tu.

62

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

2. Sura Al-Imran

Inasemekana kuwa Abu Sufian na washirikina wenzake walipoondoka Uhud kuelekea Makka, walisema: "Tumefanya vibaya sisi; tumewaua mpaka wakabakia wanyonge halafu tukawaacha, tuwarudieni! Tuwamalize" Walipoazimia hivyo Mwenyezi Mungu akawatia hofu, mpaka wakaacha yale waliyoyakusudia." Ni sawa sababu hii iwe ndiyo ya kushuka Aya au la, lakini tamko la Aya halikatai hayo.

152.Na hakika Mwenyezi Mungu aliwatimizia miadi yake mlipokuwa mkiwaua kwa idhini yake, mpaka mlipolegea na kuzozana katika amri na mkaasi. Baada ya kuwaonyesha mliyoyapenda. Kuna katika nyinyi wanaotaka ulimwengu na kuna katika nyinyi wanaotaka akhera. Kisha akawaepusha nao ili awafanyie mtihani na amekwisha wasame-he, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye hisani kwa waumini.

Aya 152 MWENYEZI MUNGU AMEWATIMIZIA

MAANA

Na hakika Mwenyezi Mungu aliwatimizia miadi yake mlipokuwa mkiwaua kwa idhini yake.

Bado maneno yanaelekezwa kwa Masahaba wa Mtume waliokuwa katika Uhud. Mtume alikuwa amekwisha waahidi kuwa ushindi ni wao siku hiyo kama wakifua-ta amri. Na Mwenyezi Mungu ametekeleza ahadi ya aliyoyasema kupitia kwa Mtume wake. Hilo ni kuwa Mtume (s.a.w) aliwaweka wapiga mishale kwenye mlima kuwalinda waislamu kwa nyuma, akawausia kutoondoka hata kama wakim-wona adui anadonwa na ndege. Na akawaahidi ushindi kwa sharti hili. Wapiga mishale walikuwa hamsini.

Kaashif4-61.jpg

63

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Vita vilipoanza wapiga mishale wa mstari wa mbele waliwadunga washirikina na Masahaba wengine wakawa wanawapiga kwa panga zao na kuwauwa haraka haraka mpaka washirikina wakashindwa. Na hii ndio maana ya 'mlipokuwa mki-waua kwa idhini yake.' Yaani mnawaua kwa amri ya Mwenyezi Mungu. Katika Tafsir ya Ibn Jarir Tabari na Maraghi na wengineo imetajwa kwamba, Talha bin Uthman mshika bendera ya washirikina aliye maarufu kwa kamanda, alisimama akasema: "Enyi watu wa Muhammad! Nyinyi mnadai kuwa Mwenyezi Mungu atatuharakisha motoni kwa panga zenu na zetu. Je nani aliye tayari nimharakishe peponi kwa upanga wangu au aniharakishe motoni kwa upanga wake?

Akajitokeza Ali bin Abu Talib (a.s.) akampiga na kumkata mguu, akaanguka na kuwa uchi. Talha akamwambia Ali, "Muone Mungu ewe binamu.!" Ali akamwacha; na Mtume akapiga takbira. Masahaba wakamwuliza Ali, "Kitu gani kilichokufanya usimmalize?"

Akajibu: "Amenilalamikia kwa jina la Mwenyezi Mungu." Hii ndiyo hulka ya Ali, moyo wake una upole hata kwa adui yake ambaye alikuwa tayari kumuua .

Mpaka mlipolegea na kuzozana katika amri na mkaasi baada ya kuwaonye-sha mliyoyapenda.

Baada ya washirikina kuanza kukimbia - ambapo walikuwa elfu tatu - bonde lilikuwa limejaa ngawira na huku wenzao wakiziokota, walinzi waliingiwa na tamaa na wakazozana, baadhi yao wakasema: "Twangoja nini hapa?" wakajipurukusha na wasia wa Mtume na alivyowatilia mkazo kubaki. Kiongozi wao Abdallah bin Jubairakawaambia. "Bakini wala msikhalifu amri ya Mtume (s.a.w)." lakini wengi wao wakaondoka kwenda kuokota ngawira na kumwacha kiongozi wao akiwa na watu wasiozidi kumi.

Kwenye uasi huu na mzozano Mwenyezi Mungu ndio anaashiria kwa kusema: "Mpaka mlipozozana katika amri na mkaasi" Ama kusema kwake: baada ya kuwaonyesha mliyoyapenda, ni ishara ya kushindwa washirikina na ngawira zao.

Khalid bi Al-Walid (aliyekuwa akipigana dhidi ya Mtume) akiwa pamoja na Abu Sufiyan, alipoona ngome iko tupu alichukua nafasi hiyo pamoja na kikosi cha washirikina kwenda kuwashambulia wapiga mishale waliobaki. Hawa walipigana kishujaa mpaka wote wakauwa shahidi na ngome ya nyuma wa waislamu ikawa tupu. Washirikina wakarudi uwanjani na kuwazingira waislamu kutoka mbele na nyuma, wengi wakauawa na kujeruhiwa. Mpira ukawageukia. Hii ndiyo natija hasa ya ugomvi na mizozano.

Kuna katika nyinyi watakao ulimwengu.

Hao ni wapiga mishale ambao waliacha sehemu zao kwa tamaa ya ngawira.

Na kuna katika nyinyi watakao akhera.

Hao ni wale waliobakia sehemu zao pamoja na kiongozi wao Abadallah bin Jubair

64

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

mpaka wakafa mashahid.

Kisha akawaepusha nao.

Yaani kuwarudishia makafiri baada ya kuwa nyinyi mmewashinda, kwa sababu ya kuzozana kwenu na kuasi kwenu.

Ili awafanyie Mtihani

Yaani, amewafanyia mtihani ili aonekane mwenye uthabiti katika imani na uvu-milivu na ampambanue mwenye ikhlasi na mnafiki.

Na amekwisha wasamehe; na Mwenyezi Mungu ni mwenye hisani kwa wau-mini.

Ni mara nyingi mtu hukosea kwa kuchanganyikiwa, kisha akarudia uongofu wake. Kwa hiyo Mwenyezi Mungu humsamehe kwa yale yaliyopita. Lakini mwenye kuru-dia ataadhibiwa na Mwenyezi Mungu.

153.(kumbukeni) mlipotoka mbio wala hamumtizami yeyote na hali Mtume anawaita nyuma yenu. Akawalipa majonzi kwa majonzi ili msihuzunike kwa mliyoyakosa wala kwa yaliyowa-sibu. Na Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyatenda.

Kaashif4-62.jpg

65

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3 Sura Al-Imran

154.Kisha baada ya majonzi akawateremshia utulivu, usin-gizi uliofunika kundi katika nyinyi, na kundi jingine limeshughulishwa na nafsi zao, wakimdhania Mwenyezi Mungu dhana ya kijinga isiyo ya haki. Wakisema: je, tuna chochote katika jambo hili? Waambie mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu. Huficha katika nafsi zao ambalo hawakudhihirishii wewe. Husema: lau ingelikuwa tuna lolote katika jambo hili tusin-geliuawa hapa. Waambie: lau mgelikuwa majumbani mwenu, wangetoka ambao wame-andikiwa kuuawa wakaenda katika maangamivu yao na ili Mwenyezi Mungu ayajaribu yaliyomo vifuani mwenu na ayasafishe yaliyomo nyoyoni mwenu. Na Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo vifuani.

155.Hakika wale waliogeuka siku yalipokutana makundi mawili, shetani ndiye aliyewateleze-sha kwa baadhi ya waliyoy-afanya, na Mwenyezi Mungu amekwisha wasamehe. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa Maghufira, mpole.

Kaashif4-63.jpg

66

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

MKAWALIPA MAJONZI KWA MAJONZI Aya 153-155

MAANA

(Kumbukeni) mlipotoka mbio wala hamumtizami yeyote na hali Mtume anawaita nyuma yenu.

Msemo unaelekezwa kwa wale walioshindwa siku ya Uhud naye anawakumbusha walivyowaogopa washirikina na kukimbia kwao bila ya kumwangalia yeyote, na bila ya kuitikia mwito wa Mtume (s.a.w) wakati alipokuwa anawaita, akiwa amesi-mama nyuma yao huku akisema: "Njooni enyi waja wa Mwenyezi Mungu. Mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Atakayerudi Pepo ni yake. "Alifanya hivyo Mtume ili awatulize kuwa yeye yuko hai, baada ya mtu mmoja kupiga kelele kwam-ba Muhammad ameuawa, na nyoyo za waislamu kutaharuki.

Akawalipa majonzi kwa majonzi.

Mtume aliwaamrisha wapiga mishale wasiondoke kwenye jabali kwa hali yoyote, wakaasi na kukhalifu amri yake. Mtume (s.a.w) akapata majonzi kwa hilo. Kwa hiyo Mwenyezi Mungu akawalipa wao majonzi ya kushindwa badala ya majonzi ya Mtume. Majonzi ya kwanza ni yale waliyoyapata Masahaba walioshindwa, na majonzi ya pili ni yale aliyoyapata Mtume.

Inasemekana kuwa majonzi yote mawili waliyapata Masahaba, na kwamba majonzi yalikuwa mengi; kama vile kuuawa ndugu zao, kushindwa na washirikina na majuto ya kuasi kwao.

Ili msihuzunike kwa mliyoyakosa,

Ambayo ni manufaa na ngawira.

Wala kwa yaliyowasibu,

Ambayo ni majeraha na kushindwa.

Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu amewaonyesha uchungu wa kuuliwa na kushindwa ili mjizoeze muweze kuvumilia shida na mashaka, na kuwa na subira juu ya twa'a ya Mwenyezi Mungu kwa hali yoyote itakavyokuwa natija, wala msihuzunike kutokana na kukosa ngawira au masaibu yaliyowapata.

Yametangulia maelezo kwamba wapiga mishale waliacha sehemu zao kwa tamaa ya ngawira, jambo ambalo lilisababisha kushindwa kwa waislamu. Kwa hiyo, Mwenyezi Mungu anatanabahisha kuwa wachukue funzo kutokana na kushindwa huku na wala wasimkhalifu tena Mtume.

Na Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyatenda,

Maana yako wazi, na makusudio ni kuhimiza twa'a na kukaripia maasi.

67

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Kisha baada ya majonzi akawateremshia utulivu, usingizi.

Waliokuwa pamoja na Mtume siku ya Uhud wamegawanyika sehemu mbili, kuna wale waliokuwa waumini wa kweli walioona uhakika kuwa uislamu utashinda tu, na kuwa Mwenyezi Mungu ataudhihirisha kuliko dini zote, kwa vile Mtume ame-waelezea hilo. Ama kushindwa katika vita moja au zaidi hakuwatoi katika uislamu. Ambao walikuwa wakiitakidi hivi ndio wanaoambiwa: 'kisha baada ya majonzi akawateremshia utulivu' - usingizi. Kulala wakati wa misukosuko ni neema kubwa inayosahihisha masaibu mengi.

Uliofunika kundi katika nyinyi.

Ni kundi hili hili tulilolitaja ambalo watu wake walikuwa na busara katika imani.

Kundi la pili, katika waliokimbia siku ya Uhud, ni wanafiki ambao Mwenyezi Mungu amewataja kwa sifa hizi zifuatazo.

1). Na kundi jingine limeshughulishwa na nafsi zao.

Kundi hili halifunikwi na usingizi ili wapate mfazaiko. Wafasiri wamesema watu hao ni Abdullah bin Ubayya, Mut'ib bin Qushairy na wafuasi wao. Aya hii inafa-hamisha kwamba imani kamili inahitaji mtu kujishughulisha na mambo ya waisla-mu, asipofanya hivyo huyo ni mpungufu wa imani. Kuna Hadith isemayo: "Asiyejishughulisha na mambo ya waislamu basi si mwislamu."

2). Wakimdhania Mwenyezi Mungu dhana ya kijinga isiyo ya haki.

Kila anayekata tamaa kwa rehma ya Mwenyezi Mungu au akamdhania Mwenyezi Mungu kwamba amefanya yasiyotakikana kuyafanya ameleta dhana ya kijinga. Miongoni mwao ni wale waliosema siku ya Uhud, kwamba Muhammad angelikuwa Mtume, asingeshindwa na washirikina, hawajui au wanajitia kutojua kuwa vita ni kushinda na kushindwa na kwamba mambo huangaliwa mwisho wake.

3). Wakisema: Je, tuna chochote katika jambo hili?

Yaani hatuna chochote, na Mwenyezi Mungu akamwamrisha Mtume wake kuwa-jibu kuwa hamna chochote kwa ajili yenu wala kwa mwengine, isipokuwa ni kwa Mwenyezi Mungu peke yake:

"Waambie mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu ."

Sisi letu ni kusikiliza na kutii tu. Aya hii iko katika mfano wa Aya ya 128 ya Sura hii.

Huficha katika nafsi zao uongo na unafiki ambalo hawakudhihirishii wewe kama vile kuwa wao husema, lau ingelikuwa tunalolote katika jambo hili tusin-geliuliwa hapa. Yaani, lau tungelikuwa na kitu katika jambo hili tusingelitoka kwen-da kupigana, na kama tungelitoka tungelipigana vizuri bila ya kuuliwa yeyote hapa; yaani, katika Uhud.

4& 68

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Kauli ya wanafiki kusema: 'Je tuna chochote katika jambo hili?' Kisha kusema: 'Lau tungelikuwa na kitu katika jambo hili.' Inafanana na mtu anayesema: 'Sina pesa, lau ningelikuwa nazo ningelifanya hivi na hivi.'

Waambie lau mngelikuwa nyumbani mwenu wangetoka ambao wameandiki-wa kuuawa wakaenda katika maangamivu yao.

Hili ni jibu la aliyesema: 'Lau tungelikuwa na kitu tusingeliuawa.' Njia ya majibu ni kwamba, hadhari haiondoi kadari na kwamba mpangilio hauzuwii makadirio, ni sawa jambo la vita liwe lenu au lisiwe.

Umekwisha tangulia ufafanuzi katika kufasiri Aya ya 145 ya Sura hii, kifungu 'Ajali imeandikwa.'

Na ili Mwenyezi Mungu ayajaribu yaliyomo vifuani mwenu na ayasafishe yaliyomo nyoyoni mwenu. Na Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo vifuani.

. Hekima ya janga la siku ya Uhud ni upambanuzi wa kutambua mumin na mnafi-ki na kudhihirisha hakika yao kwa watubiao kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa yaliyo katika nyoyo.

Kwa hivyo, mu'min anazidi imani kwa misukosuko na vile vile kwa malipo na thawabu. Na mnafiki anafichuka.

SIRI YA KUSHINDWA

Zaidi ya hayo yote ni kwamba lau mtu angeliishi maisha yake yote bila ya matata-tizo na shida yoyote, ingelikuwa ni jambo la kushangaza katika akili za watu. Matatizo ndiyo yasafishayo nafsi na kuzikomaza, na kuvumilia shida kunamfikisha mtu kwenye malengo yake.

Uzoefu umeonyesha kuwa hakuna mpinganaji yoyote au mwanasiasa, mfanya biashara, mwanachuoni, mwana fasihi, mfanyi kazi, au mkulima, aliyefanikiwa katika malengo yake, isipokuwa kwa uthabiti na kuvumilia shida.

Lau tutafanya utafiti ili tujue siri ya kutofaulu katika maisha, tutaona kuwa ni udhai-fu, kuhofia urefu wa njia na kutovumilia tabu na matatizo.

Nayasema haya nikiwa mimi mwenyewe nimefanya majaribio kutokana na uvu-milivu nimefikia ambayo sikuwa hata nikiyaota Al-hamdulillah. Nimejaribu nikawa na yakini kuwa subira inafanya miujiza na kwamba werevu bila ya subira na uvu-milivu haufai chochote.

Hakika wale waliogeuka siku yalipokutana makundi mawili, shetani ndiye aliyewatelezesha kwa sababu ya baadhi ya waliyoyafanya. Na Mwenyezi Mungu amekwishawasamehe; hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghu-fira, mpole .

69

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Wengi wamesema kuwa Aya hii inawahusu wapiga mishale walioamrishwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) wabakie sehemu zao ili kuwakinga waumini kwa upande wa nyuma, kisha wakaondoka wakidhania kuwa washirikina wameshindwa. Lakini Aya haikuwataja wapiga mishale na wengineo walioshind-wa siku ya Uhud.

Hata hivyo kuenea kwake kunahusu waumini na wala si kwa wanafiki, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu, amekwisha wasamehe kwa sababu Mwenyezi Mungu hawasamehi wanafiki wananong'ania unafiki wao ambao ni mbaya zaidi kuliko ushirikina wa waziwazi.

Kwa ufupi ni kwamba aliyeshindwa siku ya Uhud hana shaka na Mwenyezi Mungu na Mtume wake, isipokuwa alikimbia ama kwa tamaa au kutokua na subira na mshikamano, na mengineyo ambayo hawezi kujiepusha nayo asiyekuwa Masum, na ambayo hayana mfungamano na unafiki au shaka yoyote. Haya aliyasamehe Mwenyezi Mungu, hata kama ndiyo yaliyoleta yaliyotokea.

Imesemekana kwamba kauli ya Mwenyezi Mungu: Shetani ndiye aliyewateleze-sha, kwa baadhi ya waliyoyafanya; ni kwamba Shetani aliweza kuwatelezesha kwa sababu ya dhambi walizozifanya kabla ya Uhud. Lakini haya ni kiasi cha kud-hani tu. Lililo karibu zaidi ni kwamba kufanya, hapa ni ishara ya pupa yao na kutokuwa na subira. Shetani alipoona hivi akaitumia nafasi na kuwahadaa kuwa wameshinda na kuwapofua kuwa mambo ni salama.

Na wafasiri wote, watu wa sera na historia wameafikiana kuwa Imam Ali bin Abu Talib (a.s.) alikuwa ni mmoja wa waliobaki bila ya kukimbia.

156.Enyi mlioamini msiwe kama wale waliokufuru na wakawase-ma ndugu zao, waliposafiri kati-ka nchi au walipokuwa vitani: lau wangelikuwa kwetu wasingekufa na wasingeliuawa; ili Mwenyezi Mungu ayafanye hayo kuwa majuto katika nyoyo zao. Na Mwenyezi Mungu anahuisha na kufisha na Mwenyezi Mungu anaona mnay-oyatenda.

Kaashif4-64.jpgKaashif4-65.jpgKaashif4-66.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

157.Na kama mkiuawa katika njia ya Mwenyezi Mungu au mkifa, basi maghufira na rehma kutoka kwa Mwenyezi Mungu ni bora kuliko yale wanayoyakusanya.

158.Na kama mkifa au mkiuawa, nyote mtakusanywa kwa Mwenyezi Mungu.

Aya 156-158 MSIWE KAMA WALE WALIOKUFURU

MAANA

Enyi mlioamini msiwe kama wale waliokufuru.

Tamko la ambao wamekufuru, ni la kiujumla, linamkusanya kila kafiri; awe mnafiki au kafiri wa wazi wazi, bali wafasiri wengi wamesema; makusudio hasa ni wanafi-ki.

Na wakawasema ndugu zao.

Yaani: walisema waliyoyasema kwa ajili ya ndugu zao waliokufa.

Waliposafiri katika nchi au walipokuwa vitani; lau wangelikuwa kwetu wasin-gelikufa na wasingeliuawa.

Wanafiki walikuwa wakiyategemeza mauti ya msafiri kwenye safari na yule mwenye kuuawa vitani kwenye vita hivyo, sio kwa kuwa yameandikwa na Mwenyezi Mungu.

Mwenyezi Mungu amewakataza waumini kusema mfano wa maneno haya. Kwa sababu ndani yake mna kuitikia mwito wa hadaa za wanafiki na matamanio yao. Ikiwa hawatayasema hayo na kuyategemeza mauti ya anayekufa safarini au vitani kwa Mwenyezi Mungu, basi watakuwa wamevipinga vitimbi vya wanafiki kwao wenyewe na kuwapatisha hasara.

Makusudio ya udugu hapa ni kiujumla, yaani ndugu wa nasaba au kushabihiana katika itikadi na tabia.

Ili Mwenyezi Mungu ayafanye hayo kuwa majuto katika nyoyo zao.

Yaani, Mwenyezi Mungu amewakataza waumini kujifananisha na wanafiki kwa kauli na vitendo. Kwa sababu kujifananisha huku kunawafurahisha na

4& 71

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

kunathibitisha makusudio yao. Na kukosa kufanya hivyo kunawasumbua na kuwakasirisha.

Na Mwenyezi Mungu anahuisha na kufisha.

Ajali zote ziko kwenye uwezo wake, wala si kwa sababu ya vita au safari. Kwani anaweza kusalimika na yule aliyekaa mjini akafa. Hili ndilo jibu la kauli ya wanafi-ki, kuwa safari na vita vinasababisha mauti.

Na Mwenyezi Mungu anayaona mnayoyatenda.

Hili ni himizo la kumtii Mwenyezi Mungu na ni tishio la anayewaiga makafiri na wanafiki kwa kauli na vitendo.

Na kama mkiuliwa katika njia ya Mwenyezi Mungu au mkifa basi maghufira na rehema kutoka kwa Mwenyezi Mungu ni bora kuliko yale wanayoyaku-sanya.

Kila mwenye kuipigania haki au nafsi yake kwa upanga wake au kalamu yake au ulimi wake na akauawa, basi ameuawa katika njia ya Mwenyezi Mungu. Vilevile kupigania maisha na elimu au chochote kinachowafaa watu na akafa, basi amek-ufa katika njia ya Mwenyezi Mungu. Na kila mwenye kufa au kuuawa, katika njia ya Mwenyezi Mungu amewajibikiwa kusamehewa dhambi na kupanda daraja katika dunia na akhera.

Kauli yake Mwenyezi Mungu ni bora kuliko yale wanayoyakusanya ni kwamba lililo bora kwa mumini ni kuathirika na linalodumu kuliko linaloisha ambalo ni stare-he na anasa.

Na kama mkifa au mkiuawa, nyote mtakusanywa kwa Mwenyezi Mungu.

Huu ndio mwisho wa binadamu awe amefariki dunia kwa kuuawa au kwa sababu yoyote ile. Hapo ndipo penye malipo ya (matendo) yaliyopita, ikiwa kheri basi ni kheri na ikiwa ni shari basi ni shari. Mwenye akili anajiandaa na siku hii wala hawezi kufanya mchezo.

159.Kwa sababu ya rehma itokayo kwa Mwenyezi Mungu, umekuwa mpole kwao, lau ungelikuwa mkali mwenye moyo mgumu bila shaka wangelikukimbia. Basi wasamehe na uwaombee maghfi-ra na ushauriane nao katika mambo. Utakapoazimia, basi mtegemee Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu anawapenda wamtegemeao.

Kaashif4-67.jpgKaashif4-68.jpgKaashif4-69.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

160.Akiwasaidia Mwenyezi Mungu hapana wa kuwashinda. Na kama akiwaacha basi ni nani atakayewasaidia baada yake? Na wategemee kwa Mwenyezi Mungu waumini.

Aya 159-160 KAMA UNGEKUWA MKALI

MAANA

Kwa sababu ya rehma itokayo kwa Mwenyezi Mungu, umekuwa mpole kwao.

Katika Aya zilizotangulia Mwenyezi Mungu alikuwa akiwambia Masahaba wa Mtume (s.a.w); katika Aya hizi, Mwenyezi Mungu anamwambia Mtume wake mtukufu (s.a.w).

Yametangulia maelezo kwamba Waislamu walikwenda kinyume na amri ya Mtume (s.a.w) siku ya vita vya Uhud, na natija ilikuwa ni kushindwa wakamwacha Mtume kwenye shida, ambapo vita iliuma mchanga mpaka Mtume akajeruhiwa na maadui, akavunjwa meno ya mbele, ukachanika uso wake na ukawa unachuruzi-ka damu. Wakati huo akiwa bado na uthabiti pamoja na watu wachache, akaita wale wanaokimbia lakini wasimwitike.

Baada ya kwisha vita waislamu walirudi kwa Mtume (s.a.w), lakini Mtume hakuwalaumu ingawaje walikuwa wakistahili hivyo. Bali aliyapuuza, akawapokea na akazungumza nao kwa upole. Haukuwa upole huu ila ni rehma kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Ikiwa Mwenyezi Mungu amemsifu Mtume wake kuwa ni mvunja ghadhabu kwa watu wake pamoja na ubaya wao, basi itakuwa yeye mwenyewe Mwenyezi Mungu ni zaidi. Imam Ali anasema, katika kumsifu Mwenyezi Mungu: "Ghadhabu haimshughulishi kuwacha rehma yake." Na katika dua zilizopokewa imesemwa: "Ewe ambaye rehma yake imetangulia ghadhabu yake."

Kisha Mwenyezi Mungu anabainisha hikma ya upole kwa Mtume wake mtukufu kwa kusema: Lau ungelikuwa mkali mwenye moyo mgumu bila shaka wan-gelikukimbia, na maadui wangelikucheka na ujumbe kwako usingelitimu na kue-nea.

Kwa hakika makusudio ya kutumwa Mtume ni, kuongoza viumbe kwenye haki, nao viumbe hawawezi kumsikiliza isipokuwa yule mwenye upendo ambaye nafsi zao

73

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

zinamtegemea, na nafsi haitegemei isipokuwa kwa aliye na moyo rahim; kama moyo wa Muhammad (s.a.w.w) ambao ulikunjuka kwa watu wote hata kwa wanyama. Alisema kuhusu wanyama: "mnapochinja chinjeni vizuri, anoe mmoja wenu kisu chake na ampe raha anayemchinja" Akasema tena: "Kuna malipo kati-ka kumhudumia kila mwenye ini la joto." Hakika Mwenyezi Mungu alimsamehe Mumis kwa sababu alimwokoa mbwa asife na kiu."

Basi wasamehe katika mambo yanayokuhusu wewe ambapo walikuacha wakati wa dhiki na shida mpaka ukajeruhiwa. Na uwaombee maghufira katika haki inay-omhusu Mungu Mtukufu pale walipomwasi na kuacha vita. Kauli yake hii Mwenyezi Mungu inafahamisha kimaana kuwa Yeye amekwisha wasamehe na kuwaghufuria, vyenginevyo asingemwamrisha Mtume wake hilo.

Na ushauriane nao katika mambo.

Arrazi anasema: Maulama wengi wamesema kuwa alif na lam hapa sio ya kijum-la bali ni mahsusi tu, na kilichohusishwa katika Aya hii ni vita na kupambana na maadui. Kwa hivyo ushauri unahusika na vitu tu." wengine wakasema kuwa inaku-sanya mambo yote ya kidunia.

Kisha Razi akimnukuu Shafi anasema; kuwa mshawara hapa ni mapendekezo, sio wajibu, na kwamba hekima ya ushauri ni kuzituliza nyoyo zao tu. Kauli hii iko karibu na uzingatio. Kwa sababu, Maasum hawezi kutaka mwongozo kwa asiyekuwa Maasum.

Vyovyote itakavyokuwa ni kwamba dini kwa itikadi yake na sharia yake ni wahyi bila ya kuweko rai ya yeyote, hata Mtume mwenyewe ni mfikishaji tu na wala sio mtunga sharia. Na Mwenyezi Mungu amemwambia Mtume wake: "Huna lako jambo.." (3: 128) "Wewe ni muonyaji tu." (79:45)

Utakapoazimia, basi mtegemee Mwenyezi Mungu.

Yaani ukiazimia kufanya jambo kutokana na ushauri au usiokuwa ushauri, basi litekeleze kwa kufanya maandalizi kwa kutegemea msaada wa Mwenyezi Mungu katika kufaulu na kushinda.

Akiwasaidia Mwenyezi Mungu, hapana wa kuwashinda.

Msaada wake Mwenyezi Mungu Mtukufu unakuwa pamoja na kutekeleza sababu alizozijaalia Mwenyezi Mungu kuwa ni njia ya kufikia ushindi, ambazo pamoja na kumtegemea Mwenyezi Mungu, ni kukamilika maandalizi ambako Mwenyezi Mungu amekudokeza pale aliposema: "Na waandalieni nguvu muwezavyo" (8:60)

Na kama akiwaacha ni nani tena atakayewasaidia baada yake?

Mwenyezi Mungu huwaacha wale ambao hawana mjumuiko wa kheri. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: "Wala msizozane, msije mkalegea na kupoteza nguvu

74

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

zenu/' (8:46)..

Kwa ufupi ni kwamba kukamilisha maandalizi bila ya ikhlas hakuna faida yoyote, kama ilivyokuwa kwa Waislamu siku ya vita vya Hunain: "Na siku ya Hunain, ulipowapandisha kichwa wingi wenu, lakini haukuwafaa kitu, na ardhi ikawa finyu juu yenu ingawaje ni pana, kisha mkageuka mkarudi nyuma." (9:25)

Kama ambavyo ikhlas nayo bila ya maandalizi haifai kitu. Mwenye kutekeleza yote mawili (maandalizi na kumtegemea Mwenyezi Mungu), basi hana wa kumshinda. Kwa sababu Mwenyezi Mungu yuko pamoja naye; "panga na utawakali."

SIRI YA UTUKUFU WA MUHAMMAD

Abdullah, baba yake Mtume, alisafiri kwenda Sham (Syria ya sasa) kibiashara wakati mama yake akiwa na mimba yake. Katika safari ya kurudi, Abdullah ali-wapitia wajomba zake wa ukoo wa Najjar waliokuwa Madina, akaugua huko na kufariki. Kwa hivyo akafariki akiwa fakiri bila ya kumwachia mwanawe kitu cho-chote zaidi ya ngamia watano, kondoo wachache na mjakazi wa kihabeshi aliyekuwa akiitwa Ummu Ayman ambaye alikuwa ni mmoja kati ya walezi wake.

Mtume (s.a.w) alizaliwa Makka mwezi wa Rabi-ul-Awwal (mfungo sita), mwaka wa ndovu, sawa na mwezi wa Agosti 570A.D. kama ilivyotajwa.

KUNYONYESHWA KWAKE NA MALEZI YAKE

Mtume alinyoyeshwa na Thuwayba kisha akanyonyweshwa na Halima Saadiya. Mama yake alifariki akiwa na miaka 6 na babu yake alifariki akiwa na miaka 8. Kisha akalelewa na ami yake, Abu Talib na akamkinga hadi pumzi yake ya mwisho. Aliishi naye miaka 42. Mtume aliishi miaka 63 ambayo 53 aliimalizia Makka na 10 Madina.

WASIFU

Kiumbo alikuwa si mrefu si mfupi, alikuwa na kichwa kipana. Uso wa duara na mpana. Nyusi zake zilikuwa ziko karibu kuungana, katikati yake palijitokeza mshipa, ambao anapokasirika hufura na kuwa mwekundu.

Vilevile alikuwa na macho meusi na kope ndefu. Pua iliyochongoka, mwenye meno mazuri, ndevu nyingi na kifua kipana. Pia alikuwa na mikono mirefu, na alikuwa na weupe uliochanganyika na wekundu, na alikuwa na mwili mkakamavu.

Akasirikapo, uso wake huiva na anapohuzunika mara nyingi hushika ndevu zake. Alipokuwa akizungumza huashiria kwa kiganja chake chote na anapostaajabu hukigeuza. Anapozama katika mazungumzo hupiga dole lake gumba la kushoto kwenye kiganja chake cha kulia.

75

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Akiona jambo linalomchukiza alikuwa akigeuza uso wake na anapochemua (kupi-ga chafya) hujifunika. Alikuwa akicheka mpaka yakaonekana magego yake na alikuwa mwingi wa tabasamu.

Alikuwa hakatai chakula kinachopatikana wala hakalifishi kinachokosekana. Na kama hapati chakula, huvumilia mpaka kufikia hatua ya kufunga jiwe tumboni mwake kwa sababu ya njaa. Alikuwa anaweza kukaa mwezi mzima bila ya kupa-ta mkate. Siku moja alimtuma mtu kwenda kumkopea kwa myahudi mmoja, yule myahudi akakataa na akasema: "Muhammad hana shamba wala mifugo, ni nani atakayelipa?"

Vilevile Mtume hakuwa na kanzu, juba au shuka zaidi ya moja kwa wakati mmoja. Pia hakuwa na viatu zaidi ya jozi moja. Alikuwa na mkeka anaoulalia usiku na kuukalia mchana, mpaka akafanya alama mbavuni. Na alikuwa na mto wa ngozi uliojazwa ndifu. Wakati wa kulala alikuwa akiweka mkono wake chini ya shavu lake na hulalia upande wake wa kulia. Alikuwa akijishonea viatu na kanzu yake inapopasuka, na alikuwa akipanda punda.

Ingawaje utajiri wa Bara-arabu ulikuwa kwenye madaraka yake lakini alikuwa aki-toa kila kinachomfikia akiwa ni mtu asiyeogopa ufukara, kama alivyosifiwa na bedui mmoja.

MTUME NA UFUKARA

Lakini yote hayo hayana maana kwamba yeye alikuwa akiupenda ufukara na kuuridhia. Hapana! Bali alikuwa akiomba kuhifadhiwa nao na akisema: "Ewe Mwenyezi Mungu! Ninataka hifadhi kwako kutokana na ufukara, uchache wa mali na udhalili. Na ninataka hifadhi kwako na kushindwa na uvivu. Na ninataka hifadhi na kudhulumu au kudhulumiwa."

Mtume hakuwa akiupenda ufukara na kuuridhia, lakini maadamu alikuwa akiishi katika jamii fakiri, basi njia bora ni kuishi upande wa ufakiri na kuwa sawa nao kati-ka ulaji, mavazi na mahali pa kuishi. Wala hakuna kosa kubwa na dhulma kuliko kuwa kiongozi ameshiba na raia wake mmoja ana njaa.

Amirul-Muminiin Ali anasema: "Hakika Mwenyezi Mungu amewafaradhishia Maimamu waadilifu kujipima kwa kuwa sawa na watu ili maumivu ya ufukara yasimwathiri yakammaliza."

Amesema tena: "Je, nitosheke kuitwa Amirul-Mu'miniin (Kiongozi wa Waumini) na wala sishirikiani nao katika hali ngumu ya maisha."

UTARATIBU WA MWITO WAKE

Kwanza aliwaonya jamaa zake walio karibu. Hapo ni wakati iliposhuka Aya: "Na waonye jamaa zako walio karibu." (26:214)

76

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Basi akawafanyia chakula na akawaalika. Miongoni mwa maneno aliyowaambia ni, "Ni nani atakayekuwa msaidizi wangu katika jambo hili, awe ndugu yangu, wasii wangu na khalifa wangu kwenu?" wote wakanyamaa isipokuwa Ali bin Abu Talib aliyesema: "Mimi, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu." Basi akamshika shin-goni kwake akasema:

"Huyu ni ndugu yangu, wasii wangu na khalifa wangu kwenu, kwa hiyo msikilizeni na mumtii."

Watu wakanyanyuka huku wakicheka na kumwambia Abu Talib: "Umeamrishwa umsikilize na umtii mwanao mwenyewe!" Kisha Mtume akawalingania watu wake - Waarabu, kisha akamlingania kila mtu wa mwanzo hadi wa mwisho. Mwenyezi Mungu anasema; "Na hatukukutuma ila kwa watu wote." (34: 28)

Ama Mitume wengine walipelekwa kwa watu wao tu au watu wa zama zao tu. Ndio maana Nuh, Ibrahim, Hud, Swaleh, Musa na wengineo, walikuwa waki-waambia watu wanaowalingania kwenye imani kwa kutumia neno: "Enyi watu wangu."

Ama Muhammad (s.a.w) aliwaambia watu wote wa kila zama na kila miji, wa aina tofauti na lugha tofauti, kwa kusema: "Enyi watu! Mimi ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu kwenu nyote." (7: 158)

Pia Mtume aliwaandikia barua wafalme wa duniani, akiwemo Kisra na Kaizari na akawatumia ujumbe wake akiwalingania kwenye imani kuhusu risala yake.

SIRI YA UTUKUFU WAKE

Muhammad (s.a.w) alikuwa ni mwanaadamu; yeyote atakayemsifu kwa sifa ya muumbaji, mwenye kuruzuku, basi atakuwa amemkufuru Mwenyezi Mungu. Lakini watu wote kuanzia Adam mpaka mtoto wake wa mwisho, sio kama Muhammad, mtukufu zaidi katika wao, ni yule atakayethibitishwa utukufu na ubora wake na Muhammad. Ni sawa awe amethibitishiwa kwa nukuu na kuelezwa jina au kwa sifa ya kijumla, kama kusema: mbora wa watu ni yule anayewanufaisha zaidi watu.

Ama siri ya utukufu wa Muhammad ni kwamba yeye alikuwa akibeba matatizo ya watu wote. Alikuwa pamoja na mayatima na wajane na kuwatekelezea mahitaji yao. Hakuna yeyote awe rafiki au adui ila atamshughulikia na kumhurumia, kumpa usaidizi.

Maneno yangu haya hayatokani na ushabiki au malezi na mazingira la! Bali yana-tokana na kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema: "Na hatukukutuma wewe ila ni rehma kwa viumbe." (21:107)

Maana yake ni kuwa huruma zake, na kushughulikia kwake watu hakuko kwa jamaa zake, au marafiki zake tu bali kumeenea kwa watu wote, maadui na marafi-

77

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

ki, kama maji na hewa. Watu walimvunja meno, wakamjeruhi uso, lakini alisema: "Ewe Mwenyezi Mungu waongoze watu wangu hakika wao hawajui." Hakutosheka kuwaombea uongofu lakini aliwatakia udhuru kwa ujinga wao na kutofahamu.

Hakuna ajabu ikiwa Muhammad hakukasirika kwa ajili ya nafsi yake au kuzuia nafsi yake na anasa za dunia, isipokuwa ajabu ni kufanya kinyume na hivyo. Tabia hiyo ni lazima kwa yule aliyepelekwa kwa ajili ya kutimiza tabia tukufu na kuwalingania watu wote kumsadikisha na kuamini risala yake. Wala hakuna maana ya kusadikisha isipokuwa kusadikisha uadilifu na wema, wala kumwamini yeye isipokuwa kuamini haki na utu, sio yeye mwenyewe.

Siku moja mtu mmoja alimwita hivi: "Ewe bwana wetu, mtoto wa bwana wetu. Mbora wetu na mtoto wa mbora wetu!" Mtume akasema: "Asiwachezee shetani, mimi ni Muhammad mja wa Mwenyezi Mungu, na Mtume wake. Wallahi sipendi wanitukuze zaidi ya cheo changu."

Masahaba zake walikuwa wanapomuona hawamsimamii ingawaje ni kipenzi chao, kwa sababu walikuwa wanajua kuwa hapendi kusimamiwa. Pia alikuwa akichukia kutembea na mtu akiwa nyuma yake, hivyo humshika mkono na kumvuta ubavu-ni mwake ili watembee pamoja.

Hii ndiyo hulka ya Muhammad (s.a.w.). Ndio ni kweli kuwa watu wote si kama yeye, lakini hulka zake ndio kioo cha hakika ya uislamu. Yeyote mwenye kulinga-nia uislamu na asifuate mwendo wa Mtume wake, basi ni mdanganyifu, ni sawa atambue hivyo au asitambue au hata akijiona, na watu wakimwona yeye ni mtuku-fu zaidi.

161.Na Mtume hawezi kufanya hiyana. Na mwenye kufanya hiyana, atayaleta yale aliyoy-afanyia hiyana siku ya kiyama, kisha italipwa kila nafsi iliyoy-achuma, wala hawatadhulumi-wa.

162.Je, aliyefuata ya kumridhisha Mwenyezi Mungu ni kama aliyestahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na makazi yake ni jahannam. Hapo ni mahali pabaya pa kurejea.

Kaashif4-70.jpgKaashif4-71.jpg

3. Sura Al-Imran

Kaashif4-72.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

163.Wao wana daraja mbele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mwenye kuyaona yale wanayoyafanya

164.Hakika Mwenyezi Mungu ame-waneemesha waumini kwa kuwaletea Mtume miongoni mwao, anayewasomea Aya zake na anayewatakasa na kuwa-fundisha Kitabu na hekima. Na hakika kabla ya hapo walikuwa katika upotofu wa dhahiri.

 

Aya 161-164 MTUME HAFANYI HIYANA

MAANA

Na Mtume hawezi kufanya hiyana.

Imesomwa herufi 'ya' kwa fataha kwa mweko wa fai'l (mtendaji) kwa maana ya kuwa Mtume hafanyi hiyana katika ghanima na vinginevyo kama wanavyodhani wajinga.

Pia imesomwa kwa dhumma, kwa mweko wa mafu'l (mtendwa), kwa maana ya kuwa haifai kwa yeyote kumhini Mtume katika ghanima.

Katika tafsir nyingi, imeelezwa kuwa lililowafanya watu wa kikosi cha mishale kuondoka sehemu yao kuiacha tupu ngome ya nyuma ya waislamu siku ya vita vya Uhud, ni kuwa wao walihofia kuwa Mtume hatawagawia ghanima, wakifikiria kuwa anayechukuwa kitu basi ni chake. Mtume akawaambia: "Hivi mwadhani kuwa sisi twafanya hiyana? Ndipo ikashuka Aya. Tamko la Aya halikatai maana haya, hata mfumo wa Aya pia unakubali, kwa sababu bado ni katika tukio la Uhud.

Vyovyote iwavyo, lile ambalo tunalifahamu kwa ujumla, bila ya kuangalia sababu za kushuka, ni kwamba Ma'asum hawezi kufanya hiyana, kwa sababu ni mkweli, kwa kuwa yeye ni mkweli, hawezi kusema uongo, isipokuwa kama sio mkweli, na tamu ni tamu tu, haiwezi kuwa chungu isipokuwa kama utaviita vitu kwa kinyume, jambo ambalo linabatilisha upimaji wa mambo.

Na mwenye kufanya hiyana, atayaleta yale aliyoyafanyia hiyana siku ya kiya-

79

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

ma, kisha italipwa kila nafsi iliyoyachuma.

Yaani, mwenye kufanya hiyana na kuiba kitu kesho (siku ya kiyama) atakuja na dhambi ya alivyovifanyia hiyana na atapata aliyoyachuma bila ya kupungua cho-chote na atafedheheka mbele ya watu wote. Imesemekana pia kuwa atakuja na kitu chenyewe kilichoibwa. Kwa mfano mwenye kuiba ngamia, siku ya kiyama atakuja amebeba ngamia shingoni mwake. Hayo yamesemwa kwa kutegemezwa kwenye Hadith ndefu ya Mtume (s.a.w.)

Kama Hadith itakuwa sahih, basi itakuwa ni fumbo la kubeba madhambi ya maasi, sio kuchukua kitu chenyewe hasa. Na Aya hii iko katika mwelekeo wa Aya ise-mayo: "Mwenye kutenda uovu atalipwa kwa uovu huo, wala hatapata asiyekuwa Mwenyezi Mungu wa kumlinda wala wa kumsaidia." (4:123)

UISLAMU UNAFANYA MAAJABU.

Mwenye kufuatilia historia ya uislamu, ataona kwamba mafunzo ya Qur'an na Hadith yamefanya kazi yake na kuathiri katika nafsi za waislamu wengi, mpaka yakatokea makundi yanayoendelea na hulka njema, ambazo Mtume ametumwa kuzitimiza. Mwanajeshi wa kiislamu wa kawaida anaweza kupata nyara yenye thamani kubwa kutoka kwa adui na akaileta kwenye hazina ya waislamu bila ya kuhisi chochote rohoni mwake.

Ibn Athir katika Tarikh anasema: Waislamu walipoteka Madain, kamanda wa jeshi alikuwa Saad bin Abi Waqqas. Yeye alimweka Saad bin Umar bin Muqrin kuku-sanya nyara na ngawira akawa yeye ndiye anayekabidhiwa. Mwanajeshi mmoja akamjia na sanamu mbili ili azichanganye kwenye ngawira. Moja ilikuwa ni farasi wa dhahabu aliyepambwa kwa zumaridi na yakuti na juu yake kuna mtu aliyevish-wa taji la johari. Sanamu ya pili ilikuwa ni ya ngamia wa fedha aliyepambwa kwa yakuti akiwa na lijamu ya dhahabu iliyozungushwa johari. Hizi zilikuwa sanamu za Kisra alizokuwa akiziweka kwenye taji lake.

Yule anayekusanya mali alipoziona, alishikwa na mshangao akasema: "Hatujaona kitu kama hiki, mali yote tuliyonayo haifikii hii hata haikaribii pia." Kisha aka-muuliza yule askari: "Wewe ni nani?" akasema: "Sikwambii wala simwambii yey-ote asije akanisifu, lakini mimi namsifu Mwenyezi Mungu peke yake, nataraji thawabu zake na wala sitaki kitu kingine zaidi yake." Kisha akajiondokea. Yule mkabidhiwa akamfuatafuata na kumuuliza kwa watu mpaka akamjua kuwa ni Amir bin Abdu Qays.

Masimulizi haya unaweza kuyaona kama ngano tu, lakini Uislamu ukipata moyo mwema, basi hufanya maajabu sawa na ilivyo mbegu bora ya rutuba katika ardhi. Ama ardhi isiyo na rutuba haileti mazao bora, hata kama mbegu bora na mvua ikawa nyingi, Mwenyezi Mungu anasema: "Na nchi nzuri hutoa mimea yake kwa idhini ya Mola wake na nchi mbaya haitoi ila kwa taabu."(7:58)

Je, aliyefuata ya kumridhisha Mwenyezi Mungu ni kama aliyestahili ghad-habu ya Mwenyezi Mungu na makazi yake ni Jahannam. Hapo ni mahali pa

80

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

baya pa kurejea.

Aya hii inafanana na ile isemayo: "Je, tuwajaalie wale walioamini na wakatenda amali njema kuwa sawa na wafanyao uharibifu katika ardhi"? (38:28)

Amirul Mu'minin Ali (as) anasema: "Kuna tofauti kubwa kati ya amali mbili, amali ambayo inaondoka na kubaki taabu yake, na amali ambayo taabu yake inaondo-ka na kubaki malipo yake." Anaendelea kusema: "Haki ni nzito lakini ni nzuri na batili ni hafifu lakini ni balaa. Ni mwisho gani mbaya kuliko ghadhabu za Mwenyezi Mungu na adhabu ya moto."

Wao wana daraja mbele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mwenye kuyaona yale wanayoyafanya.

Dhamir ya wao inawarudia wenye kufuata ya kumridhisha Mungu. Maana yake ni kuwa watiifu wanatofautiana katika twa'a kati ya wale, wanaopigana jihadi wao wenyewe na wale waliokaa wasiokuwa na madhara. Vilevile waasi wanatofautiana katika maasi na katika makosa. Kwa hivyo ikawajibika hawa kutofautiana adhabu na wale katika thawabu.

Hakika Mwenyezi Mungu amewaneemesha waumin kwa kuwaletea Mtume miongoni mwao anayewasomea Aya zake na anayewatakasa na kuwa-fundisha Kitabu na hekima. Na hakika kabla ya hapo walikuwa katika upoto-fu wa dhahiri.

Umepita mfano wa Aya hii katika Sura ya Baqara Aya 129.

Kwa hali yoyote ile ni kwamba Aya hii imekusanya mambo yafuatayo:

1)          Mtume ni hisani kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa viumbe. Kwa sababu Mtume huwatoa ujingani kuwapeleka kwenye ujuzi, kutoka kwenye udhalili kwenda kwenye utukufu na kutoka kwenye maasi na adhabu kwenda kwenye twa'a na thawabu.

2)          Hisani hii imezidi kwa Waarabu hasa kwa sababu Muhammad (s.a.w.) anatokana nao, wanajifaharisha naye kwa umma zote.

3)          Yeye amewatakasa na uchafu wa shirk, masanamu, vigano, uzushi, kuiga kunakodhuru na ada mbaya.

4)          Anawafundisha Kitabu, yaani Qur'an ambayo imewapa umoja, kuhifadhi lugha yao na kuwahimiza elimu, na tabia njema. Vilevile Mtume amewa-fundisha hekima, ambayo ni kuweka mambo mahali pake. Inasemekana kuwa makusudio ya hekima ni Fiqh.

5)          Tafsir bora ya Aya hii ni yale maneno aliyoyasema Jafer bin Abu Talib kumwambia Najash wa Uhabesh. "Ewe mfalme, sisi tulikuwa ni watu wajinga, tukiabudu masanamu, tukila nyamafu na kufanya mambo mabaya. Vilevile tulikuwa wavunja undugu, kumfanyia ubaya jirani, na mwenye nguvu alikuwa akimwonea mnyonge. Tulikuwa hali hiyo mpaka Mwenyezi Mungu akatuletea Mtume atokanaye na sisi. Tunayemjua

81

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

nasaba yake, ukweli wake, uaminifu wake na usafi wake. Akatulingania

kwa Mungu mmoja peke Yake.

Tukavua yale tuliyokuwa tukiyaabudu sisi na baba zetu, miongoni mwa

mawe na masanamu. Akatuamrisha kusema kweli, kutekeleza amana,

kuunga udugu, kumfanyia wema jirani na kujizuiliya na mambo ya haramu

na kumwaga damu.

Vilevile alitukataza mambo maovu, kuzulia, kula mali ya yatima na kuwa-

tusi wanawake wanaojistahi. Na akatuamrisha kumwabudu Mwenyezi

Mungu na kutomshirikisha na chochote. Pia akatuamrisha kuswali, kutoa

zaka na kufunga."

Kwa ufupi Muhammad (s.a.w.) ndiye aliyeleta maendeleo kwa waarabu ya kiutu na ya kimataifa, lau si yeye waarabu wasingekuwa na historia yoyote wala jambo lolote la kutambuliwa.

165.Hivi mlipopata msiba - na nyinyi mmekwisha watia mara mbili yake - mnasema: imekuaje? Waambie hayo yanatokana na nyinyi wenyewe.           Hakika

Mwenyezi Mungu ni muweza wa kila kitu.

166.Na yaliyowasibu siku ya kuku-tana makundi mawili ni kwa idhi-ni ya Mwenyezi Mungu na ili wajue waumini.

167.Na ili awajue wale ambao wali-fanya unafiki, na wakaambiwa njooni mpigane katika njia ya Mwenyezi Mungu au mjikinge. Wakasema: Lau tungelijuwa ni vita tungeliwafuata. wao siku ile walikuwa karibu na ukafiri kuliko imani. Wanasema kwa midomo yao yale yasiyokuwa nyoyoni mwao. Na Mwenyezi Mungu anayajua vizuri wanayoyaficha.

Kaashif4-73.jpgKaashif4-74.jpgKaashif4-75.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

168.Wale waliosema kuhusu ndugu zao na wao wakiwa wamebaki nyuma: Lau wangelitutii wasingeuawa. Sema jizuilie na mauti (msife) ikiwa mnasema kweli.

ULIPOWAFIKA MSIBA Aya 165-168

 MAANA

Hivi mlipopata msiba - na nyinyi mmekwisha watia mara mbili yake - mnasema: imekuaje?

Yaani, ulipowapata msiba siku ya vita vya Uhud na nyinyi mlikwisha watia msiba zaidi ya huo siku ya Badr, mnasema imekuaje, na sisi tunapigana katika njia ya Mwenyezi Mungu?

Kwa ufafanuzi zaidi, ni kwamba vita vya Badr vilikuwa mwaka wa tatu. Katika Badr, waislamu walipata ushindi kwa kuwaua washirikina sabini na kuwateka sabi-ni. Vilevile waislamu walipata ushindi katika sehemu ya kwanza ya vita vya Uhud, na wakapata hasara sehemu ya pili, kwa sababu wapiga mishale walikhalifu amri ya Mtume (s.a.w.), hapo waislamu sabini wakauawa.

Tukilinganisha ushindi wa Waislamu siku ya Badr na ushindi wa washirikina siku ya Uhud, tunapata kuwa Waislamu ni mara mbili zaidi, kwa sababu maiti sabini kwa sabini. Waislamu wanabaki na mateka sabini Sasa kwa nini wanafiki na baadhi ya waislamu washikwe na mshangao kiasi hiki? Tena pamoja na kuuliza wameshindwaje na washirikina, na wao ni maadui wa Mwenyezi Mungu. Kwa nini basi wanafiki wanasahau ushindi wa Badr ambao ulikuwa zaidi?

Waambie: hayo yanatokana na nyinyi wenyewe.

Hili ni jawabu la kauli yao: 'Imekuaje'? maana yake nyinyi ndio sababu ya yaliy-owapata. Mtume alionelea kuwa watu wabaki Madina wasitoke, lakini mkakataa. Na mlipotoka, akawalazimisha mbakie sehemu alizowapangia, mkaondoka kwa sababu ya tamaa. Kwa ufupi ni kuwa kauli yake Mwenyezi Mungu: "Hayo yanatokana na nyinyi wenyewe." Ni sawa na kauli yake. "Hayo ni kwa sababu ya yaliy-otangulizwa na mikono yenu na kwamba Mwenyezi Mungu si mwenye kuwadhu-lumu waja." (3:182)

83

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Na yaliyowasibu siku ya kukutana makundi mawili, ni kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.

Makusudio ya 'siku' ni 'siku ya Uhud,' 'makundi mawili', ni waislamu na washiriki-na, na makusudio ya neno 'idhini' ya Mwenyezi Mungu, ni kujua kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu, kama alivyolitumia Mwenyezi Mungu neno hilo kwa maana ya kujua katika (2:179) wala haijuzu kuwa makusudio ya idhini iwe kuhalalisha kwa sababu Mwenyezi Mungu hawahalalishii makafiri kuwaua waislamu.

Na ili Mwenyezi Mungu awajue waumini na ili awajue wanafiki.

Yaani, masaibu ya Uhud yalikuwa na faida, kama vile kudhihirisha elimu yake Mwenyezi Mungu, kuwa watu watambue imani ya waumini na unafiki wa wanafiki. Wanafiki kabla ya tukio la Uhud hawakuwa wakijulikana wala kutofautiana na waumini. Kwenye tukio hilo walijulikana, kwa hiyo makusudio ya elimu ya Mwenyezi Mungu hapa ni kudhihirisha elimu yake ijulikane kwa wengine. Sio kwamba yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu alipata kujua baada ya tukio la Uhud. Kwa sababu yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anajua mambo kabla ya kutukia kwake. Maelezo ya Aya yameshatangulia katika kufasiri Aya ya 141 ya Sura hii.

Wakaambiwa njooni mpigane katika njia ya Mwenyezi Mungu au mjitetee.

Mwenyezi Mungu hubainisha nani aliyeyasema hayo kwa wanafiki. Kwa sababu yeye ameleta kauli kwa tamko la mbali na si kwa majina. Lakini wafasiri wengi wamesema kuwa Abdullah bin Ubayya alitoka pamoja na Mtume (s.a.w.) siku ya Uhud akiwa na wapiganaji 300. Walipofika katikati ya njia Abdallah alirudi na genge lake akakataa kupigana. Alifanya hivyo kwa ajili ya kuwavunja nguvu wengine wasipigane vita. Abdullah (babake Jabir Ansari) akawauliza: "Kwa nini mnarudi nyuma? Mkiwa na dini basi piganieni dini yenu. Haya ndiyo maana ya; 'mpigane katika njia ya Mwenyezi Mungu.' Na kama hamna dini, basi mzitetee nafsi zenu, watu wenu na mali zenu. Haya ndiyo maana ya 'au mjitee.' Watu wa historia pia wametaja kujitoa huku kwa bin Ubayya na watu wake na kauli ya Abdullah. Na tamko la Aya linafungumana na kitendo chao. Lakini haiku-taja majina ya waliofanya wala jina la msemaji.

Kwa vyovyote itakavyokuwa lakini wanafiki walijibu kauli ya mumini na wakasema: "Lau tungelijua ni vita bila shaka tungeliwafuata."

Yaani, kwamba Waislamu na washirikina hawatapigana, lau tungelihakikisha kuwa watapigana, basi tungelipigana pamoja na nyinyi.

Wengine wanasema kwamba makusudio ya jibu hilo la wanafiki ni kwamba kuka-biliana na washirikina sio kupigana, bali ni kujipeleka machinjioni kwa sababu ya idadi kubwa ya maadui.

Tamko la Aya linakubali maana zote mbili, lakini maana ya kwanza iko karibu zaidi na tamko la Aya.

84

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Wao siku ile walikuwa karibu zaidi na kufuru kuliko imani. Yaani, wanafiki waliposema lau tungelijua ni vita tungeliwafuata, walikusudia kuficha unafiki wao na kujiepusha na tuhuma. Lakini kauli yao ndiyo inayofahamisha zaidi unafiki wao, na ni kauli ya kuwasaidia washirikina; kwa sababu inafuata maslahi yao kutokana na inavyowavunja nguvu waliokuwa pamoja na Mtume (s.a.w.).

Wanasema kwa midomo yao lau tungelijua ni vita tungeliwafuata yale yasiyokuwa nyoyoni mwao bali ni uongo na unafiki. Na Mwenyezi Mungu ana-jua vizuri wanayoyaficha ambayo ni kumkufuru Mwenyezi Mungu na kumkanusha Mtume wake. Imam Ali (a.s.) anasema "Ulimi wa Mu'min uko nyuma ya moyo wake na moyo wa mnafiki uko nyuma ya ulimi wake," Yaani, kauli ya Mu'min ni kioo cha yaliyo moyoni mwake, kwa sababu yeye husema kile ana-chokiamini. Ama mnafiki ulimi wake uko mbali na moyo wake na ulimi wake una-fuata maslahi yake tu, na kutengeneza maneno vile yanavyotaka maslahi yake.

Wale waliosema kuhusu ndugu zao na wao wakiwa wamebaki nyuma, "Lau: wangelitutii wasingeuawa." Yaani, wanafiki walisema lau wale waliouawa siku ya Uhud wangelitufuata sisi wakabaki, asingeliuawa yeyote, kama vile ambavyo sisi tumebaki. Yameshatangulia maelezo yake katika tafsir ya Aya ya 156 ya Sura hii.

Sema: Jizuilieni na mauti (msife) ikiwa mnasema kweli.

Hapana! Hakuna anayeweza kuyakimbia mauti wala hayamwachi yanayemtaka. Imam Ali (a.s.) amesema: "Mauti yanafuata, hayamkosi aliyekaa wala hayamshin-di mwenye kuyakimbia, mauti ya utukufu ni kuuliwa. Naapa kwa ambaye nafsi ya mwana wa Abu Talib iko mikononi mwake, mapigo elfu kwangu si chochote kuliko kufa kitandani."

169.Na usiwadhanie kabisa wale waliouawa katika njia ya Mwenyezi Mungu kuwa wameku-fa, bali wako hai mbele ya Mola wao wanaruzukiwa.

170.Wanafurahia aliyowapa Mwenyezi Mungu katika fadhila zake, na wanawashangilia wale ambao hawajajiunga nao, walio nyuma yao, ya kwamba haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.

Kaashif4-76.jpgKaashif4-77.jpgKaashif4-78.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

171.Wanashangilia neema na fadhila za Mwenyezi Mungu na kwamba Mwenyezi Mungu hapotezi ujira wa waumini.

Aya 169-171 WAKO HAI MBELE YA MOLA WAO WAKIRUZUKIWA

MAANA

Na usiwadhanie kabisa wale waliouawa katika njia ya Mwenyezi Mungu kuwa wamekufa, bali wako hai mbele ya Mola wao wanaruzukiwa.

Anayeambiwa 'usiwadhanie' ni kila mwenye akili. Makusudio ya waliouwawa wako katika njia ya Mwenyezi Mungu, ni kila aliyeuawa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu; ni sawa awe amekuwa shahidi mbele za Mtume, kabla yake, au baada yake.

Dhahiri ya Aya ni kwamba mashahidi wako hai hivi sasa, na wala sio kuwa watakuwa hai pamoja na wengine siku ya ufufuo. Na wao wako hai kihakika, sio kimajazi, kama kutajwa vizuri n.k.

Hii ndio dhahiri ya Aya, na yapasa kuitegemea. Kwa sababu hakuna la kuwajibisha kutafuta maana nyingine, maadam uhai uko mikononi Mwenyezi Mungu Mtukufu anampa amtakaye wakati wowote autakao.

Wala hatujui dini au Umma uliotukuza mashahidi katika njia ya haki na uadilifu kama uislamu. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) anasema: "Kuchwewa na jua na kupambaukiwa ukiwa katika njia ya Mwenyezi Mungu ni bora kuliko dunia na vilivyo ndani yake." Na akasema, "Pepo iko kwenye ncha za mikuki." Ambayo ita-maliza dhulma, shari na batili.

Ama wale wanaokufa shahidi katika njia ya haki, wao na haki ni sawa katika mtazamo wa kiislamu, kwa sababu mwenye kuutoa uhai wake kwa ajili ya haki, utakatifu wake ni utakatifu wa haki yenyewe.

Wanafurahia aliyowapa Mwenyezi Mungu katika fadhila zake. Furaha yao ya fadhila hizi iko mara mbili.

Kwanza: Kwa kuwa wao wanastarehe kwa fadhila hiyo.

Pili:            Kwamba hili linafahamisha radhi ya Mwenyezi Mungu kwa wale walio-

jitolea uhai wao kwa ajili yake, sawa na zawadi ya mpenzi inayofa-hamisha upendo wake.

Na wanawashangilia wale ambao hawajajiunga nao, walio nyuma yao, ya kwamba haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.

86

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                          2. Sura Al-Imran

Kila Mumin anampendelea ndugu yake katika imani lile analolipendelea nafsi yake, lakini kwa sababu ya matatizo na kwa sababu fulani huenda mtu asifikie makusudio. Lakini wale waliokufa shahid katika njia ya Mwenyezi Mungu, wanao ndugu katika imani wanaowajua kwa majina wakiwa na iman na ikhlas kama wao, nao wamewaacha bado wako hai. Basi mashahidi watakapoona fadhila za Mwenyezi Mungu kwao, watafurahi na watashangilia kutokana na waliyoyapata, vilevile kwa ajili ndugu zao wanafuata njia yao katika iman, ikhlas na jihadi. Mashahidi Watashangilia kwa sababu, ndugu zao walio hai watapata kama waliyoyapata wao miongoni mwa fadhila na karama.

Aya hii ni dalili ya wazi kwamba mashahidi wako hai kabla ya siku ya kiama kwa sababu kushangilia kwao ndugu zao walio hai kumekwishapatikana, na wala sio kuwa kutapatikana kesho.

Wanashangilia fadhila na neema za Mwenyezi Mungu na kwamba Mwenyezi Mungu hapotezi ujira wa waumini. Unaweza kuuliza: kwa nini limerudiwa neno kushangilia na fadhila?

Jibu: Mashahidi wana furaha tatu.

Furaha ya kwanza: ni kwa yale waliyoyapata wao, kulikoelezwa na kauli yake Mwenyezi Mungu. Wanafurahia aliyowapa Mwenyezi Mungu kutokana na fadhila zake.

Furaha ya pili: ni kwa ajili ya ndugu zao wanaowajua ambao watajiunga nao, kama linavyoonyeshwa hilo na kauli yake Mwenyezi Mungu. "Na wanawashangilia wale ambao hawajajiunga nao."

Furaha ya tatu: ni kwa ajili ya kila Mumini wanayemjua na wasiyemjua shahidi na asiye shahidi. Hilo linaelezwa na kauli yake Mwenyezi Mungu: "Wanashangilia neema za fadhila za Mwenyezi Mungu." Linalotilia nguvu kuwa furaha hii ni kwa ajili ya waumini wote, ni kauli yake Mwenyezi Mungu: "Na Mwenyezi Mungu hapotezi ujira wa waumini."

Swali la pili. Mwenyezi Mungu ameunganisha fadhila na neema: na kuunganisha kunamaanisha tofauti. Tunavyoona sisi ni kwamba hakuna tofauti, sasa tofauti ni ipi hiyo?

Razi amejibu kuwa, neema ni thawabu na ujira anaostahiki mtenda amali kuwa ni malipo ya amali yake. Na fadhila ni ziada (Bahashishi) anayoitoa Mwenyezi Mungu kwa ukarimu sio kwa kustahiki.

Jibu hili la Razi halifungamani na chochote, isipokuwa kupendelea tu kuwepo tofauti. Tunavyoona sisi ni kwamba hakuna tofauti yoyote kati ya kusema: "Amenineemesha" na kusema: "Amenifadhili." Ilivyo hasa ni kwamba misamiati inaungana na kutofautiana tamko tu, kunatosha. Kuungana huku kunaitwa 'muungano wa tafsir' (Atfu Tafsir)

87

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

172.Wale waliomwitikia Mwenyezi

Mungu na Mtume baada ya

majeraha yaliyowapata; kwa

waliofanya wema na kumcha

Mwenyezi Mungu wana ujira

mkubwa.

173.Wale ambao waliambiwa na watu: Hakika watu wamewaku-sanyikia kwa hivyo waogopeni. Lakini yakawazidishia imani, wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosha na bora ya mwenye kutegemewa ni Yeye.

174.Basi wakarudi na neema za Mwenyezi Mungu na fadhila haukuwagusa ubaya na wakafu-ata radhi ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kubwa.

175.Hakika huyo ni shetani, anawatia hofu marafiki zake, basi msiwao-gope na niogopeni Mimi, ikiwa nyinyi ni waumini.

Aya 172-175 WALIOMWITIKIA MWENYEZI MUNGU

MAANA

Wale waliomwitikia Mwenyezi Mungu na Mtume baada ya majeraha yaliyowapata, kwa waliofanya wema na kumcha Mwenyezi Mungu wana ujira mkubwa.

Kaashif4-79.jpgKaashif4-80.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Inaelezwa katika vitabu vya Sera na Tafsir kuwa washirikina walipomaliza vita vya Uhud, walipokuwa wakirudi Makka, njiani walirudia kufikiria, wakajuta na kulaumi-ana. Wakaambiana: "Hatukuwamaliza Waislamu, kwa hiyo wataungana tena na watarudia mara nyingine tena." Hapo wakaazimia kumrudia Muhammad (s.a.w.), ili kumpiga vita, Mtume aliposikia hilo, alirudia kuwapanga watu wake haraka.

Mpigaji mbiu akanadi, "Asitoke na sisi yeyote isipokuwa yule tuliyokuwa naye jana!" Hapo wakakusanyika waislamu wakiwamo waliojeruhiwa, wakaenda kupi-ga kambi sehemu ya Hamraul Asad, kiasi cha maili nane kutoka Madina, wakimn-goja Abu Sufian na wenzake.

Mkusanyiko huo ulifaulu, kwa sababu washirikina walipojua kuwa waislamu wame-jikusanya upya, waliogopa na wakarudi Makka haraka sana. waislamu wakarudi Madina wakiwa na nguvu kwa upande fulani.

Wale ambao waliambiwa na watu: Hakika watu wamewakusanyikia, kwa hivyo waogopeni. Lakini yakawazidishia imani, wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosha na bora ya mwenye kutegemewa ni yeye.

Makusudio ya neno 'watu' la kwanza ni wale waliorudi wasiende vitani pamoja na Mtume (s.a.w.) hao ndio waliowambia waumini waliotakiwa na Mtume (s.a.w.) kupambana na washirikina kwa mara ya pili "Watu wamekusanyika, kwa hivyo waogopeni." Na makusudio ya neno 'watu' la pili ni washirikina waliojaribu kuwarudia waislamu.

Maana ni kuwa waumini pamoja na majeraha yao mabichi, lakini waliitika wito wa Mtume (s.a.w.) wa kukabiliana na Abu Sufian na jeshi lake bila ya kuwasikiliza wale waliowatia woga, Waliowaambia kuwa msitoke na Muhammad kwa sababu adui ana nguvu zaidi yenu. Badala yake kauli hii iliwazidishia imani kwa Mwenyezi Mungu na kuwa na imani na miadi yake, wakaendelea kumtii Mtume (s.a.w.) na kutaka kupigana na adui potelea mbali itakavyokuwa, kwa kusema: "Mwenyezi Mungu anatutosha na bora ya mwenye kutegemewa ni yeye."

Hivi ndivyo unavyokuwa msimamo na mshikamano wa mumini pamoja na imani yake. Haogopi kifo, kutekwa nyara au kuadhibiwa. Mtu mmoja wa ukoo wa Abdul-ash-hal anasema: "Mimi na ndugu yangu tulikuwa katika vita vya Uhud na kujeruhiwa. Mwito wa Mtume (s.a.w.) wa kutoka ulipotolewa, tulitoka pamoja na Mtume. Jeraha langu lilikuwa nafuu kuliko la ndugu yangu kwa hiyo akibaki nyuma nilikuwa nikimbeba."

Basi wakarudi na neema za Mwenyezi Mungu na fadhila, haukuwagusa ubaya na wakafuata radhi ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kubwa.

Waumini walitoka pamoja na Mtume hadi Hamral-Asad, kama walivyoamriwa lakini hawakupata lolote kutoka kwa adui. Hiyo ndiyo maana ya kusema: "Haukuwagusa na ubaya." Kwa sababu adui alipojua kuwa wamejikusanya tena, aliogopa na kurudi.

4& 89

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Baada ya adui kurudi, Waislamu wakarudi kwao na neema nyingi za Mwenyezi Mungu zikiwa ni salama, twa'a ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kumtisha adui. Kuna neema gani inayolingana na kutukuzwa na Mwenyezi Mungu na kusajiliwa fahari hii katika Lawh Mahfudh na katika Kitabu chake ambacho wanaki-soma watu duniani hadi siku ya ufufuo?

Hakika huyo ni shetani anawatia hofu marafiki zake, basi msiwaogope na niogopeni Mimi, ikiwa nyinyi ni waumini.

Kila anayemtii Mwenyezi Mungu, basi ni katika vipenzi vya Mwenyezi Mungu, na kila anayemwitikia shetani, basi ni katika marafiki zake. Mwenyezi Mungu anawaamrisha na anawakataza shari na kuwahadharisha nayo. Ama shetani yeye ni kinyume. Anawaamrisha nayo na anawakataza mema na kuwahofisha nayo, mfasiri Muhammad bin Ahmad Al-Kalabiy anasema katika Tafsir Tashil, makusudio ya shetani hapa ni Abu Sufian au aliyetumwa na Abu Sufian au Iblis.

Kauli ya aliyewaambia waumini "Hakika watu wamekusanyikia." Inatokana na mawazo ya shetani na kuhofisha kwake. Hakuna anayemsikiza isipokuwa rafiki zake wanaomtii. Ama wapenzi wa Mwingi wa rehema, kauli hii huwazidishia imani kwa kupigana jihadi na kujitolea mhanga kwa ajili ya uislamu na Mtume wa Uislamu.

Hayo ndiyo maana ya 'shetani anawatia hofu marafiki zake.' Ama marafiki wa Mwenyezi Mungu hawamwogopi shetani akiwahofisha. Na maana ya msiwaogope, ni msiwaogope washirikina kwa sababu wao ni marafiki wa shetani wenye kuogopewa kwa kuwapa sifa ya nguvu, ili wapate nafasi ya kueneza ufisadi duniani. Na Mu'min hamuogopi yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu.

SHETANI NI OMBAOMBA NA NI HODARI

Shetani ana majina mengi, kama: mlaaniwa, mwenye kuwekwa mbali na rehma, mpotevu na mpotezaji. Unaweza kumwita ombaomba, kwa sababu yeye husima-ma kwenye mlango wa moyo kwa kutia huruma na kubisha pole pole akitaka idhi-ni ya kuingia, ukichelewa kumfungulia, hukuomba kwa unyenyekevu na maneno matamu ya kukufanya umfungulie japo kidogo. Ukifanya hivyo tu huingia na kuan-za kukutolea hadaa na upotevu kutoka mfukoni mwake. Hapo ataanza kuufinika uhakika na kukubabaisha, na kuupamba uovu na kuufanya uonekane mzuri. Vilevile ataleta sura ya kazi njema kuwa mbaya, kupigania kuondoa batili kuwa kufuru, maovu kuyafanya mema na mema kuyafanya maovu. Pia atamvisha mhai-ni nguo ya mwema na mwenye ikhlas atamvisha nguo ya mfisadi, na mengineyo yenye hila na upotevu.

Njia kubwa anayoitumia kufikia malengo yake ni kutengeneza hofu kwa kuleta nguvu za marafiki zake ambao ndio watekelezaji wa miradi yake. Shetani ni fundi aliye hodari. Ama nguvu zake za utekelezaji ni wafuasi wake ambao wanaeneza ufisadi duniani.

Kwa ajili hii anawakuza na kuwatengenezea njia ya utekelezaji na kuwavisha

4& 90

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

kivazi cha utukufu na cheo, ili wasiwe na sauti au fikra yoyote ya kujitoa, usije ukadhoofika utawala wake na kukatika matarajio yake, shari na ufisadi wake kwa kuondoka athari yao.

Kwa ufupi ni kwamba kila anayewaogopa watu wa ufisadi na wapotevu lakini aka-patana na mmoja wao, basi atakuwa amepatana na upotevu wenyewe na atakuwa amesaini mkatataba wa mapenzi na udugu kati yake na shetani. Hiki ni kipimo kisichokosea kabisa katika kumpambanua mwenye kulingania kumwamini Mwenyezi Mungu na kumwogopa Yeye tu, na yule mwenye kumtawalisha shetani na kuathirika na twa'a yake, wala hakuna kitu kinachofahamisha uhakika huu kuliko kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.), 'msiwaogope na niogopeni Mimi,' ikiwa nyinyi ni waumini. Kwani maana yake ni kwamba mwenye kuacha kuwapiga jiha-di wafisadi na wapotevu kwa kuwaogopa, basi yeye ni katika marafiki wa shetani na wala hana chochote kwao. Aya hii iko karibu na kauli ya Mtume Mtukufu (s.a.w.) "Mwenye kuinyamazia haki ni shetani bubu."

176.Wala wasikuhuzunishe wale wanaokimbilia ukafiri. Hakika wao hawatamdhuru            kitu

Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu anataka asiwawekee fungu lolote huko akhera. Nao wana adhabu kubwa.

177.Hakika wale walionunua ukafiri kwa imani, hawatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu na wana adhabu iumizayo.

178.Wala wasidhanie kabisa wale waliokufuru kwamba muda tunaowapa ni heri kwa nafsi zao. Hakika tunawapa muda na wanazidi tu katika dhambi na wana adhabu idhalilishayo.

91

Kaashif4-81.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

WÂNÂÖkİMBİLÎÂ "UKAFİRİ Aya 176-178

MAANA

Wala wasikuhuzunishe wale wanaokimbilia ukafiri, hakika hao hawatamdhu-ru kitu Mwenyezi Mungu.

Yametangulia maelezo kuwa washirikina walikusanya makundi, wakaandaa jeshi la kumpiga vita Mtume (s.a.w.) na wanafiki walikuwa wakiwasaidia na wakiwapan-gia njama waislamu.

Katika Aya hii Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewataja wanafiki na washirikina kuwa ni waasi na wanafanya bidii kuipinga haki na kuipiga vita. Na Mtume (s.aw.) alikuwa akihuzunika na kuona uchungu kutokana na vitendo vyao hivi. Ndipo Mwenyezi Mungu Mtukufu akamwambia: Usihuzunike, wao hawatakudhuru na chochote wewe, wala Waislamu na dini ya Mwenyezi Mungu, na kwamba njama zao hizo zitapotea tu. Ama dini itakuwa na utukufu. Na kweli hazikupita siku nyin-gi Mwenyezi Mungu akaumakinisha uislamu Mashariki na Magharibi kwa watu ambao jana walikuwa wakikimbilia kuupiga vita.

Mwenyezi Mungu anataka asiwawekee fungu lolote huko akhera. Nao wana adhabu kubwa.

Huu ndio ukweli wa kila mwenye kuendelea na upotevu mpaka akafa. Unaweza kuuliza, kuwa dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa shari inatokana na Mwenyezi Mungu, kwa sababu , adhabu ya Jahannam ni shari, na Mwenyezi Mungu ame-watakia hiyo adhabu, itakuwaje?

Jibu: ni kweli kuwa Mwenyezi Mungu amewatakia adhabu, lakini ni baada ya kus-tahili, kwa sababu yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t.) aliwaamrisha kuamini na akawakataza kukufuru na akawaachia hiyari. Hivyo wakachagua ukafiri badala ya imani. Maana yake ni kwamba washirikina na wanafiki ndio waliosababisha adhabu. Baada ya wao kusababisha kwa hiyari yao, ndipo Mwenyezi Mungu akawatakia adhabu sawa na hakimu anayemtakia kifungo mwenye hatia baada ya kufanya makosa.

Hakika wale walionunua ukafiri kwa imani, hawatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu.

Neno 'walionunua' linafahamisha hiyari. Kwa sababu mnunuzi anachagua bid-haa na kuridhia anachokichukua badala ya thamani. Na kafiri ameridhia ukafiri badala ya imani, ndipo akastahili adhabu kali.

Unaweza kuuliza: kwa nini Mwenyezi Mungu amelikariri neno 'hawatamdhuru Mwenyezi Mungu kitu' katika Aya mbili, kuna siri gani?

92

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Jibu: makusudio ya Aya ya kwanza ni makafiri wa kiquraishi walioandaa jeshi la kumpiga Mtume (s.a.w.) na wale wanafiki waliokuwa wakiwasaidia. Aya ya pili, makusudio yake ni kila kafiri kuanzia wa mwanzo hadi wa mwisho, awe mpiga vita au la.

Kwa hiyo Aya ya kwanza inakuwa ni mahsusi, na ya pili ni kutaja kiujumla. Mara nyingi inakuwa hivi katika maneno ya watu ambao husema "Fulani amecheza kamari akajimaliza na kila mwenye kufanya hivyo ataangamia."

Wala wasidhanie kabisa wale waliokufuru kwamba muda tunaowapa, ni heri kwa nafsi zao. Hakika tunawapa muda na wanazidi tu katika (kufanya) dham-bi na wana wao adhabu idhalilishayo.

Umri wa mtu ni kama mali yake, akiitumia vizuri yeye, kwa watu wake na pia kwa watu wengine au jamaa zake wanaohitaji, basi atarudiwa na heri na wema. Kila mali yake inapozidi ndiyo kunavyozidi kutoa kwake na ndipo wema wake unavy-ozidi. Na kama akiitumia vibaya na kuitoa katika maasi, basi humrudia mabaya, na kila inavyozidi na kukuwa ndivyo anavyozidi uasi na ufisadi.

Umri nao ni hivyo hivyo. Mtu hufikilia wema kama akifanya amali nzuri na unakuwa ni sababu ya uovu wake, kama akifanya uovu. Hiyo ndiyo desturi ya Mungu kwa kijamii. Kila desturi iliyozoeleka inayojulikana kimaumbile au kijamii, basi ni desturi ya Mwenyezi Mungu katika viumbe vyake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amepitisha desturi yake kwa makafiri na watu wote. Amewapa muda kwa kurefusha umri ili mtu ajichagulie mwenyewe, kheri au shari. Lakini kafiri akaghurika kwa kupewa muda na akajiachia katika upotevu. Kwa hiyo ikawa natija ya kupewa kwake muda, ni uovu wake na adhabu yake. Kinyume na Mumini, Mwenyezi Mungu akichelewesha ajali yake kheri yake huzidi na wema huwa mwingi. Bali mwenye kufanya wema katika sehemu iliyobakia katika umri wake, hataadhibiwa kwa dhambi zake zilizopita, kama ilivyoelezwa katika Hadith tukufu.

Kwa hali hiyo basi, inatubainikia kuwa herufi Lam katika neno liyazdaadu ni ya mwishilio, sio ya sababu, yaani wanazidi tu na sio 'ili' wazidi.

KAFIRI NA AMALI NJEMA

Unaweza kuuliza: baadhi ya makafiri hufanya kheri kwa ajili ya kheri, na kila umri wao unavyozidi ndivyo wanavyozidi kuwanufaisha watu kwa elimu zao na juhudi zao zilizo nzuri kabisa. Je, hii haipingani na kauli yake Mwenyezi Mungu, na wanazidi tu, katika dhambi?

Jibu: mfumo wa Aya unakusudia dhambi tu, na kuwa wao kwa upande huu wanazidi ukafiri, na wala sio katika hali zote, kwani huenda wakawa ni wema katika baadhi ya matendo yao.

93

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Swali la pili: Je kafiri akifanya wema na kuwanufaisha watu, atapata thawabu, au wema wake huo ni sawa na kutofanya chochote?

Jibu: mtu kwa mtazamo wa imani na matendo (amali), atakuwa katika mojawapo

ya hali nne zifuatazo: -

1.Kuamini na kutenda amali njema, hali hii inafuatana na kauli ya Mwenyezi Mungu: "Hakika wale wanaosema mola wetu ni Mwenyezi Mungu, kisha wakawa na msimamo, wao huteremkiwa na Malaika (na kuwaambia): msiogope wala msihuzunike na furahieni pepo mliyokuwa mkiahidiwa." (41:30)

2.Kutomuamini Mwenyezi Mungu na kutofanya amali njema, hawa ni katika wale ambao: "Shetani amewatawala, kwa hivyo akawasahaulisha kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Hao ndio kundi la shetani ni lenye kupata hasara." (58:19)

3.Kuamini bila ya kufanya amali njema, hawa ni katika wanachama wa shetani kama wale waliotangulia. Lau angelikuwa ni mumin wa kweli, basi zin-geonekana alama za imani. Mtume (s.a.w.) anasema: "Hakuna inayookoa isipokuwa amali. Lau ningeasi ningeliangamia." Ama ikiwa amali yake njema imechanganyika na mbaya na akatubia, basi atakuwa katika Aya isemayo: "Na wako wengine waliokiri dhambi zao, wakachanganya vitendo vizuri na vingine vibaya. Huenda Mwenyezi Mungu akapokea toba zao. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kusamehe mwenye kurehemu." (9:102)

4.Kufanya amali njema bila ya kuamini, kama kafiri amlishaye mwenye njaa au amvishaye aliye uchi, atengenezaye barabara, kujenga nyumba za mayatima, au hospitali, kwa njia ya kheri ya kibinadamu. Imesemekana amali yake hii, kuwepo kwake na kutokuwepo ni sawa tu. Kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu: "Hakika Mwenyezi Mungu anawakubali wamchaye tu." (5:28)

Hapa Tunajibu hivi:

Kwanza: Makusudio ya kauli ya Mwenyezi Mungu: "Hakika Mwenyezi Mungu huwakubalia wamchaye tu," sio kuwa mtu akimwasi Mwenyezi Mungu katika jambo fulani, basi hamkubalii akimtii katika jambo jingine. Kama ni hivyo basi wasingekubaliwa isipokuwa waliohifadhiwa kutotenda dhambi (Maasum) tu, jambo ambalo linapingana na uadilifu wake na hekima yake. Isipokuwa makusudio ya Aya kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakubali isipokuwa amali safi isiyokuwa na uchafu wowote wa kidunia na kwamba mwenye kufanya tendo lolote kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu na kwa kheri basi atatosheka na aliyemfanyia.

Hakuna mwenye shaka kwamba mwenye kufanya kheri kwa ajili ya kheri na ubi-nadamu, basi amefanya kheri hiyo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ni sawa awe amekusudia hivyo au la. Na mwenye kufanya amali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, basi malipo yake yako kwa Mwenyezi Mungu.

Ama makusudio ya 'hapana dhambi zaidi ya ukafiri' ni kuwa ukafiri ni dhambi kubwa na kwamba dhambi yoyote kadiri itakavyokuwa kubwa haishindi ukafiri.

94

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Lakini hili - la kuwa ukafiri ni dhambi kubwa - ni jambo jingine, na malipo ya wema ni jambo jingine.

Pili: Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni mwadilifu, katika jumla ya uadilifu wake ni kwam-ba mwema na muovu hawako sawa bali mwema ana malipo yake na mwovu ana malipo yake. Wala sio lazima malipo ya mtenda mema asiyekuwa mu'min yawe akhera. Inawezekana yakawa duniani kwa kuondolewa madhara na balaa, kama asemavyo Mtume (s.a.w.): "Kufanya wema ni kinga ya mambo maovu."

Na pia sio kuwa malipo ya akhera ni pepo tu, inawezekana kuwa ni kwa kupun-guziwa adhabu, au kutokuwa na adhabu wala malipo kama ilivyo hali ya A'raf.

Kwa ufupi ni kuwa mtu atalipwa kwa vitendo vyake, vikiwa ni kheri basi atalipwa kheri na vikiwa ni shari atalipwa shari. Kafiri anastahili adhabu kutokana na ukafiri wake, na huenda akafanya kheri kwa ajili ya kheri akastahiki malipo mema. Kila tendo lina hisabu.

Ndio, ni kweli sisi hatujui aina ya malipo atakayolipwa mtenda wema asiyekuwa mu'min. Pia hatujui ni lini na wapi, duniani au akhera. Haya yanategemezewa kwenye ujuzi wa Mwenyezi Mungu na hekima Yake. Na kuyapanga hayo ni kama kushirikiana na Mwenyezi Mungu katika elimu yake. Basi na amwogope Mwenyezi Mungu mwenye kumwamini.

Kwa mnasaba huu tutataja maneno ya Sayyid Kadhim mwenye kitab U'rwathul-Wuthqa mlango wa waqf, maswala ya sharti ya niya ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Ninamnuku:

"Inawezekana kusema kwamba, thawabu zinathibiti kwa matendo mema, hata kama hayakusudiwa kwa ajili ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Kwa sababu anayeyatenda anastahiki kusifiwa kwa wenye akili, hata kama hakukusudia kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Basi ikiwa hivyo, sio mbali kustahiki fadhila kuto-ka kwa Mwenyezi Mungu mtukufu."

Kwa hiyo mwanachuoni huyu mkubwa anasema wazi kwamba inawezekana mtu kulipwa malipo mema kwa vitendo vizuri hata kama hakukusudia radhi ya Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo kutakuwa na uwezekano mkubwa zaidi kupewa malipo mema anayekusudia njia ya kheri na ubinadamu. Imekwishaelezwa mara nyingi kwamba akili haikatai kuwa yawezekana mwenye dhambi aneemeshwe kwa fadhila za Mwenyezi Mungu, isipokuwa linalokataliwa na akili ni kuadhibiwa na Mwenyezi Mungu yule asiyestahili adhabu.

95

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

179.Mwenyezi Mungu hakuwa mwenye kutaka kuwaacha waumini juu ya hali mliyo nayo mpaka awa-pambanue wabaya na wazuri. Na hakuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwafunulia mambo ya ghaibu, lakini Mwenyezi Mungu humchagua amtakaye katika Mitume yake. Basi mwaminini Mwenyezi Mungu na Mitume Yake. Na kama mtaamini na kuogopa basi mtakuwa na ujira mkubwa.

Kaashif4-82.jpg

Aya 179 KUPAMBANUA WEMA NA UOVU

MAANA

Mwenyezi Mungu hakuwa mwenye kuwaacha waumini juu ya hali mliyonayo mpaka awapambanue wabaya na wazuri.

Maadui wa Mtume (s.a.w.) walikuwa aina mbili: Kwanza ni washirikina, nao ni wale walioukataa uislamu kwa ndani na nje, wakatangaza vita tangu mwanzo wakaishia kuunda vikundi,wakajiandaa kwa nguvu wanazoziweza. Wakawa ni maadui wanaojulikana wazi wakitofautika na waislamu.

Aina ya pili ni wanafiki, nao ni wale walioficha ukafiri na uadui kwa Mtume na sahaba zake, wakadhihirisha mapenzi. Kazi yao ilikuwa ni njama dhidi ya Mtume (s.a.w.) ndani ya safu za waislamu mara wanawababaisha watu kwa uongo, mara nyingine wanawavuta waislamu kwenye maasi, au kuwavunja nguvu za kupam-bana na adui na kuwatia hofu. Na katika baadhi ya vita walikuwa pamoja na jeshi la waislamu, kisha wakajitoa njiani.

Wanafiki walimsumbua sana Mtume kuliko alivyosumbuliwa na washirikina. Kwa sababu, washirikina walikuwa maadui wanaoonekana wazi, lakini wanafiki walikuwa wakifanya vitimbi kwa kujificha na kuleta madhara kichinichini. Na hivyo ndivyo walivyo kwa yeyote anayelingania kheri, wakati wowote na mahali popote. Wanajaribu kuchafua katika safu za watu wazuri. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ame-wataja katika Aya nyingi, kama vile Aya ya 173 ya Sura hii, na katika Aya hii tuliy-

96

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

onayo na pia katika Aya isemayo: "Na namna hii tumefanyia kila Nabii adui, mashetani katika watu wa majini. Baadhi yao wanawafunulia wengine maneno ya kuwapamba pamba kwa kuwahadaa." (6:112)

Mtume aliamrishwa kuwafanyia hao wanafiki na kila aliyetamka shahada muamala wa kiislamu. Kuhifadhia damu zao na mali zao, kushirikiana nao katika vita na hata katika ngawira. Kwa sababu uislamu ulikuwa bado ni mchanga, lau atawaua au kuwafukuza wangelisema wakuzaji mambo kwamba Muhammad hampendi anayemwamini na asiyemwamini. Na washirikina wangelifanya hilo ni njia ya kuu-tangazia vibaya uislamu na Mtume wake.

Kwa sababu hiyo Mtume akawa hana la kufanya. Akiwakubali wataharibu na kuwaweka mbali waislamu na jihad, na akiwakataa alihofia mlinganio wake usipungukiwe na wasaidizi na wafuasi. Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii: "Mwenyezi Mungu hakuwa mwenye kuwaacha waumini." Yaani sio hekima ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwaacha katika hali hiyo, wanafiki wajifiche kwenye pazia la kudai Uislamu. La sivyo hivyo, bali anawafichua ili wajulikane na wafed-heheshwe mbele ya watu na wasibakiwe na pa kutolea vitimbi na ufisadi. Na jambo la kuwafedhehesha sio kutamka shahada, kurukuu na kusujudu, na mambo mengine ambayo ni mepesi kuyafanya. La! Bali ni jambo zito ambalo litawafichua wanafiki na wasibakie na nafasi yoyote ya ria na hadaa au vitimbi na kutia sumu.

Kwa mtihani huu mzito na amri ya kuwa na subira na kuwa na uthabiti katika vita vya Uhud, mtajua enyi waumini neema ya Mwenyezi Mungu kwenu na kwamba Yeye hakuwaacha katika hali mliyokua nayo, ya kuchanganyikana na maadui ambao mlitosheka nao hapo mwanzo kwa jina la uislamu. Makusudio ya wazuri ni waumini na wabaya ni wanafiki.

Na hakuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwafunulia mambo ya ghaibu.

Yaani si katika hekima yake Mwenyezi Mungu Mtukufu wala si katika desturi Yake kuwafahamisha watu elimu Yake na awaambie hili ni zuri na hili ni baya; bali ni juu yenu kuyafahamu hayo kupitia majaribio ya shida na misukosuko, kama ilivy-otokea Uhud wakati Mtume (s.a.w.) alipowaita maswahaba warudi kwa adui mara ya pili katika Hamraul Asad. Yaani Mwenyezi Mungu hamfahamishi yeyote yaliyo katika nyoyo za watu kuwa ni imani au unafiki, isipokuwa kuwaamrisha kujitoa mhanga kwa hali na mali, na kwenye utekelezaji ndipo anajulikana mwenye kujiti-atia na mwenyewe hasa.

Ndio, Mwenyezi Mungu anawafichulia baadhi ya Mitume yake juu ya unafiki wa huyu na imani ya yule, kwa hekima ambayo yeye mwenyewe Mungu anaijua zaidi. Haya ndiyo maana ya kauli yake. Lakini Mwenyezi Mungu huchagua katika Mitume yake amtakaye.

Kauli hiyo inafanana na kauli yake Mwenyezi Mungu isemayo: "Mjuzi wa ghaibu, wala hamdhihirishi ghaibu Yake yeyote isipokuwa Mtume aliyemridhia." (72: 26-27)

97

3. Sura Al-Imran

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

180.Na wasidhanie kabisa wale ambao wanafanyia ubakhili vile alivyowapa Mwenyezi Mungu katika fadhila zake kuwa ni bora kwao, bali ni shari kwao. Watatiwa mandakozi ya hivyo walivyofanyia ubakhili siku ya kiyama; na urithi wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ana habari ya mnayoyatenda.

181.Hakika Mwenyezi Mungu amek-wishasikia kauli ya wale waliosema: Hakika Mwenyezi Mungu ni fukara na sisi ni mata-jiri. Tutaandika yale waliyoyase-ma; na kuua kwao Mitume; na tutawaambia: onjeni adhabu ya kuungua.

182.Hayo ni kwa sababu ya yale yaliyotangulizwa na mikono yenu na kwamba Mwenyezi Mungu si dhalimu kwa waja.

Aya 180-182 URITHI WA MBINGU NA ARDHI NI WA MWENYEZI MUNGU

MAANA

Na wasidhanie kabisa wale ambao wanafanyia ubakhili vile alivyowapa Mwenyezi Mungu katika fadhila zake kuwa ni bora kwao, bali ni shari kwao.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuhimiza kujitolea mhanga kwa nafsi, amefuatishia kuhimiza kujitolea kwa mali. Makusudio ya Aya hii ni wale wanaojizuia kutoa Zaka na Khumsi ambazo ni wajibu, na wala sio kutoa sadaka ya sunna. Kwa sababu

Kaashif4-83.jpg

98

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

kiaga kikali ambacho kinaelezwa na Aya kinaonyesha kuacha wajibu, sio kuacha sunna.

Imesemekana pia kuwa makusudio ni mwenye kuficha jina la Muhammad (s.aw.) na sifa zake zilizokuja katika Taurat na Injil. Vilevile imesemekana ni kufanya ubakhili wa elimu kwa anayeihitajia. Lakini linalokuja haraka kwenye fahamu, ni kufanya ubakhili kwenye mali. Hilo linaonyeshwa na kauli yake Mwenyezi Mungu. Watatiwa mandakozi ya hivyo walivyovifanya ubakhili siku ya kiyama. Hii ni tafsiri ya; 'na ni shari kwao.'

Kutiwa mandakozi, hapa ni fumbo la adhabu kali, kama vile Mwenyezi Mungu alivyosema.

Siku (mali) itakapotiwa moto katika moto wa Jahannam na vichomwe vipaji vyao vya nyuso na mbavu zao na migongo.yao kwa mali hiyo." (9:35)

MATAJIRI NI MAWAKALA SIO WENYEWE

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amehimiza kutoa mali katika Aya kadhaa, nyingi katika hizo ameonyesha kuwa mali zote sio miliki ya aliyenazo, isipokuwa ni miliki ya Mwenyezi Mungu peke Yake na kwamba mtu amewekewa amana tu kuruhusiwa kuitumia kwa mipaka maalum bila ya kuikiuka kama alivyo wakala, hufuata matakwa ya mwenye mali katika matumizi yote.

Miongoni mwa Aya nyingine zilizotaja hayo ni: "Na tafuta - kwa yale aliyokupa Mwenyezi Mungu - makazi mazuri ya akhera." (28:77). "Toeni katika yale aliy-owapa Mwenyezi Mungu." (36:47) Aya iliyo wazi zaidi ni ile isemayo. "Na toeni katika yale ambayo (Mwenyezi Mungu) amewafanya kuwa makhalifa kwenye hayo" (57:7) maana ya kuwa khalifa ni kuwa kaimu.

Katika Hadith Qudsi anasema: "Mali (zote) ni zangu, na matajiri ni mawakala wangu, mafukara ni watu wangu (wanaonitegemea) basi mwenye kuwafanyia ubakhili watu wangu, nitamwingiza motoni bila ya kujali."

Kwa hivyo, Aya na Hadith zinafahamisha kuwa Uislamu haukubali miliki ya mtu kwa aina yoyote ile, ni sawa iwe ni miliki ya mtu binafsi kabisa, kama ulivyo mfumo wa kibepari, au milki ya kiwango maalum, kama ulivyo mfumo wa kijamaa, au hata miliki ya umma, kama ulivyo mfumo wa kikomunist.

Aina zote hizi zinakanushwa na uislamu na kubakia milki ya kihakika ya Mwenyezi Mungu peke Yake, lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amehalalishia mtu kutumia mali kwa ajii yake na watu wake kwa uzuri, na pia kuitumia katika njia ya kheri kwa sharti ya kuipata kwa njia ya halili siyo ya haramu; kama vile kughushi, kuhadaa, kunyang'anya, rushwa, riba, ulanguzi na kufanya biashara ya ulevi. Kwa hivyo ruhusa ya kuitawala mali na kutumia ni kwa kiwango maalum.

Unaweza kuuliza, baadhi ya Aya zinafahamisha kuwa mali ni milki ya mtu,kama "Piganeni jihadi kwa mali yenu" "Wapeni mayatima mali zao." Katika Hadith

4& 99

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

imeelezwa. "Damu zenu na mali zenu ni haramu (kwa mwengine)." Na "watu ni wenye mamlaka juu ya mali zao." Na bei na urithi ni katika mambo ya lazima ya dini na sheria ya kiislamu. Kwa hivyo basi, si haifai kusema kuwa uislamu hau-tambui milki ya mtu kwa aina zote?

Jibu: kutegemeza mtu kitu kunafaa kwa mnasaba ulio karibu. Kwa mfano kumwambia mgeni sahani yako au kumwambia mpotea njia, "hii ndiyo njia yako." Hapa inajulikana wazi kwamba mgeni hana sahani, isipokuwa makusudio ni mgeni ale kwa kutumia sahani hiyo 'na mpotea njia, hana njia isipokuwa ni kufuata hiyo njia. Kwa hiyo mali inaegemezwa kwa mtu kwa kutumia kwa njia ya halali na kwa ruhusa sio kwa njia ya milki; kama kauli yake Mwenyezi Mungu. "Na Mwenyezi Mungu amewafanyia wake katika jinsi yenu." (16:72)

Na kauli ya Mtume (s.a.w.) "Wewe na mali yako ni ya babako." Kwa dhahiri ni kwamba mke siye milki ya mume kabisa wala mtoto si milki ya kihakika ya mzazi.

Ama mauzo na mirathi ni utambulisho wa haki; yaani uislamu umemjaalia mwenye mali kuitambulisha itumiwe na mwengine, wakati huo huo umehalalisha haki maalumu kwenda kwa mrithi na mnunuzi. Na tofauti kati ya milki ya utambulisho na milki ya hakika ni kubwa.

Kwa ufupi ni kwamba uislamu umehalalishia mtu kuhodhi mali kwa sharti maalumu na kuitoa kwa sharti mahsusi, ukasisitiza sana juu ya masharti haya na kuharamisha kuyakiuka. Hii peke yake inatosha na ni dalili wazi kwamba mwanadamu ni wakala wa mali na si mwenye mali, kama si hivyo, basi ingelijuzu kwake kutumia bila ya masharti yoyote.

Ni vizuri tumalizie mlango huu kwa kauli ya Imam Jafar as-Sadiq (a.s.): "Mali ni ya Mwenyezi Mungu, nayo ni amana kwa waja wake. Amewaruhusu kula bila ya kui-fuja, kuvaa bila ya kuifuja, kuoa bila ya kuifuja na kupanda (k.v. farasi) bila ya kui-fuja. Itakayozidi hapo itarudi kwa mafukara waumini kurekebisha hali yao. Atakayefanya hivyo, basi anachokila ni halali, anachokinywa ni halali, ana-chokipanda ni halali na aliyemuoa ni halali, zaidi ya hivyo ni haram."

Hakika Mwenyezi Mungu amekwisha sikia kauli ya wale waliosema: Hakika Mwenyezi Mungu ni fukara na sisi ni matajiri.

Aya haikutaja majina ya waliotamka kufuru hii, lakini wafasiri wamenakili kuwa Mtume alipoteremshiwa Aya hii. "Ni nani atakayemkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mzuri." (2:245). Wayahudi wa Madina waliwokuwako wakati wa Mtume, walisema "Fukara tu, ndiye anayetaka mkopo kwa tajiri. Kwa hivyo Mwenyezi Mungu ni fukara na sisi ni matajiri." Hili sio la kushangaza kwa Mayahudi hasa wale matajiri. Kwa sababu misingi yao na kazi zao zinafahamisha wazi uovu huu na kutojali misimamo ya kibinadamu. Na mwenye kufuatilia historia ataona kuwa hakuna sehemu yoyote duniani isipokuwa imeathiriwa na ufisadi wao na malengo yao maovu.

Kaashif4-84.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Hakuna ufasaha unaofahamisha taswira ya hakika ya ukweli wa Uyahudi kuliko kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu. "Na utawaona wengi wao wanakimbilia kwenye dhambi na uadui na ulaji wao haramu. Hakika ni mabaya kabisa wayafanyayo. Mbona watawa wao na wanavyuoni wao hawakatazi maneno yao ya dhambi na ulaji wao haramu. Hakika ni mabaya kabisa wayafanyao. Na Mayahudi walisema: mkono wa Mwenyezi Mungu umefumba. Mikono yao ndiyo iliyofumba, na wamelaaniwa kwa yale waliyoyasema." (5: 62-64)

Sina shaka kabisa kwamba kila mwenye kuingilia hekima ya Mwenyezi Mungu na akasema kwa ulimi wake maneno, kwa mfano, 'Ilikuwa haifai kwa Mwenyezi Mungu kufanya hivi, isipokuwa angefanya hivi' sina shaka kuwa anayesema hivyo atakuwa pamoja na waliosema. Mkono wa Mwenyezi Mungu umefumba; atake asitake.

Tutaandika yale waliyoyasema. Hili ni kemeo la kiaga cha wale waliosema. "Hakika Mwenyezi Mungu ni fukara na sisi ni matajiri." Kwa sababu kuandika dhambi kunapelekea adhabu.

Na kuuwa kwao Mitume. Pia tutaandika wa kale wao walivyowaua Mitume. Kumenasibishwa kuua kwao, ingawaje walioua ni wa kale wao. Hayo yamek-wishaelezwa katika tafsir ya Aya 21 ya Sura hii.

Hayo ni kwa sababu ya yaliyotangulizwa na mikono yenu; na kwamba Mwenyezi Mungu si dhalimu sana kwa waja.

Vipi atadhulumu na Yeye amekataza dhulma na kuifanya kuwa ni kubwa ya mad-hambi makubwa na katika Aya nyingi akiita kuwa ni kufuru?

Zaidi ya hayo dhalimu anadhulumu kwa sababu tu anahitajia hicho anachokifanyia dhulma. Na Mwenyezi Mungu amejitosheleza na kila kitu. Kwa msingi huu wa kuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kujitosha na hahitajii kitu, kunathibitisha uadil-ifu wake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) vilevile kunathibitisha kwamba yeye hana mwili, kwa sababu mwili unahitaji vitu.

Kwa hivyo, inatubainika kubatilikia kwa madhehebu ya wanaosema kuwa shari inatokana na Mwenyezi Mungu, na kwamba yeye anamtengenezea maasi mja, kisha amwadhibu. Pengine watafute njia ya kuhepa kauli hii ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Hakika Mwenyezi Mungu si dhalimu wa waja. Kwa vile ametumia neno Dhallam lenye maana kudhulumu sana iwe anaweza kudhulumu kidogo, lakini sio sana! Mwenyezi Mungu ametakasika kabisa na wayasemayo madhalimu.

101

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Kaashif4-85.jpg

183.Wale ambao wamesema: Hakika Mwenyezi Mungu ametuahidi kuwa tusimwamini Mtume yey-ote, mpaka atuletee kafara itakayoliwa na moto. Sema: Hakika waliwajia Mitume kabla yangu kwa hoja zilizo waziwazi na kwa hayo mliyosema basi mbona mliwaua kama mu wa kweli?

184.Kama wakikukadhibisha, basi hakika           wamekadhibishwa

Mitume kabla yako waliokuja na hoja waziwazi na vitabu vya waadhi na kitabu chenye mwan-ga.

KAFARA NA MOTO Aya 183-184

 MAANA

Wale ambao wamesema: Hakika Mwenyezi Mungu ametuahidi kuwa tusimwamini Mtume yeyote, mpaka atuletee kafara itakayoliwa na moto.

Kila mwongo anadai kuwa ni mkweli, na anaupamba uongo wake kwa uzushi na tuhuma, hata wale wanaotajirika kwa vita na kuvichochea ili viwanda vyao vifanye kazi, wanadai kuwa wanawaua watu wasio na makosa, watoto na wanawake ili kuleta amani. Haya ndiyo mantiki ya kila mpinga haki na uadilifu kwa kuhofia chumo lake na manufaa yake.

Kwa hiyo hakuna geni kwa Mayahudi kumzulia Mwenyezi Mungu na kumwambia Muhammad (s.a.w.) kuwa hatukuamini, kwa sababu Mwenyezi Mungu ametuamr-isha kutomsadiki anayedai Utume mpaka atuonyeshe muujiza wa kutoa kafara yetu na iteketezwe na moto utokao mbinguni. Na Mayahudi waliomwambia Muhammad kauli hii, ndio hao hao waliosema kufuru ya kuwa Mwenyezi Mungu ni fukara na wao ni matajiri.

Sema: Hakika waliwajia Mitume kabla yangu kwa hoja waziwazi na kwa hayo mliyosema basi mbona mliwaua kama mu wa kweli?

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anamwamrisha Mtume wake Mtukufu kuwakatalia maneno yao na kuwajibu kwa matukio ya kihistoria kwa kuwaambia, wakale wenu

102 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

waliwataka Mitume waliotangulia muujiza huu muutakao nyinyi, wa kushuka moto kutoka mbinguni, akaudhihirisha Mwenyezi Mungu, lakini pamoja na hayo hawakuwaamini, bali waliwaua. Na nyinyi mko radhi na vitendo vya wa kale wenu. Walivyokuwa wao ndiyo mlivyo nyinyi kwa inadi. Lau mngelikuwa mwatafuta ukweli, mngelimwamini Muhammad (s.a.w.) baada ya kuwaletea hoja ya Utume wake.

Kama wakikukadhibisha, basi hakika wamekadhibishwa Mitume kabla yako waliokuja na hoja zilizo wazi wazi na vitabu vya waadhi na kitabu chenye mwanga.

Msemo unaelekezwa kwa Mtume Mtukufu (s.a.w.), lengo lake ni kumpa moyo kwa masaibu yaliyowapata wenzake waliotangulia. Sera yao ilikuwa ni kukabiliana na kupingwa na wenye inadi katika watu waovu, kama wana wa Israil na wanao-fanana nao, hata ingawaje walionyesha hoja kwa kila mkadhibishaji na mpinga haki.

Makusudio ya hoja zilizo waziwazi ni miujiza iliyo wazi inayofahamisha ukweli wa waadhi; mawaidha ya Mtume na hekima zao, na kitabu chenye mwanga ni Tawrat, kwa yanayomuhusu Muhammad na sifa zake. Na kwa kuwa Aya zilikuwa zikibain-isha mambo yao. basi hao ndio waliosema: Mwenyezi mungu ni fukara na kwam-ba Mwenyezi Mungu amewaahidi wasimwamini Mtume mpaka awajie na kafara

185.Kila nafsi itaonja mauti. Na bila shaka mtatekelezewa malipo yenu siku ya Kiyama. Mwenye kuepushwa na moto akatiwa peponi, basi huyo amefuzu. Na hayakuwa maisha ya dunia ila ni starehe idanganyayo.

186.Kwa hakika mtapata misuko suko katika mali zenu na nafsi zenu na mtasikia udhia mwingi kutoka kwa wale waliopewa Kitabu kabla yenu na kwa washirikina. Na mkisubiri na mkamcha mungu basi hayo ni miongoni maazimio.

Kaashif4-86.jpgKaashif4-87.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

KILA NAFSI ITAONJA MAUTI Aya 185-186

Kila nafsi itaonja mauti. Ni glasi inayozunguka kwa kila mtu, awe mwema au muovu. mfalme au kabwela. Haiwezekani wala hakuna njia yoyote ya kuyakim-bia mauti. Lile wanalofikiria madaktari ni kujaribu kurefusha maisha ya mtu tu, sio kukinga mauti. Jaribio la mwisho walilifanya madaktari la kurefusha maisha mwaka 1967, ni kupachika moyo mwengine wa mtu anayekaribia kufa, anatolewa moyo na kuwekwa kwa mwenye moyo mgonjwa baada ya kutolewa. Lakini jaribio hili halikufanikiwa, ingawaje lilifanyika mara kwa mara. Kukawa na mzozo kwa madaktari wakubwa wakasema hilo ni kosa lisilosameheka. Kwa sababu haiwezekani kuhakikisha kuwa yule anayetolewa moyo kweli angekufa baada ya muda mfupi? Kwani kifo hutokea kwa namna tofauti; kama vile kuzimia muda mrefu na kukosa kuvuta pumzi, wala hakuna njia ya kujua hali hii baina ya kifo na uhai. Mara ngapi madaktari wamethibitisha kifo, kisha wagonjwa wakarudiwa na uhai.

Jana nimesoma katika gazeti moja kwamba kikongwe mmoja Mmisri alizimia, watoto wake wakaita madaktari, wakathibitisha bila ya wasiwasi kwamba ameku-fa, baada ya kutangaza kifo, kutoa matangazo ya tanzia, kuchimba kaburi na watu kuhudhuria mazishi, alifungua macho yake na akawaambia watu waliokuja: "Nendeni kwenye shughuli zenu Mungu awalipe."

Ikiwa madaktari wameshindwa kuurefusha umri wa mtu na hata kumjua kama amekufa au ni mzima, basi kumkinga na mauti ndio hawawezi kabisa.

Bila shaka mtatekelezewa malipo yenu siku ya kiyama.

Hakuna malipo duniani kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) isipokuwa mtu atal-ipwa malipo kamili siku ya kiyama.

Wafasiri wengi wamesema kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) humpa mtu sehemu ya malipo ya amali yake baada ya mauti kabla ya Kiyama, kisha humalizia malipo yake Siku ya Kiyama. Kwa hivyo hapo ndipo unatimia utekelezaji kwa ukamilifu. Na wamedai kuwa neno Tuwaffauna linafahamisha hilo.

Ama sisi hatufahamu neno hilo zaidi ya lilivyoelezwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu. "Na hakika sisi tutawatekelezea fungu lao bila ya kupunguzwa." (11:109). Kauli hii haifahamishi kugawanywa, si kwa mbali wala karibu. Ndio, iko Hadith isemayo: "Hakika kaburi ni bustani katika mabustani ya pepo au ni shimo katika mashimo ya moto." Lakini hili ni jambo jengine na kufahamisha kugawanywa malipo ni jambo jengine.

Mwenye kuepushwa na moto akatiwa peponi basi huyo amefuzu.

Bali hata mwenye kuepushwa na moto na asitiwe peponi pia atakuwa amefuzu. Wanafalsafa wengi wamepanga kuwa 'kutokuwa na maumivu ni raha' na

104

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

'kutokuwa na uovu ni wema'

Na hayakuwa maisha ya dunia ila ni starehe idanganyayo.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amesifu kuwa ni starehe inayohadaa, kwa vile mtu ana-hadaika nayo, au kwa sababu mtu akimiliki kitu basi inatokea kujidanganya. Imam Ali (as) anasema: "Dunia inadhuru, inadanganya na inapita."

Kwa hakika mtapata misuko suko katika mali zenu na nafsi zenu, na mtasikia udhia mwingi kutoka kwa wale waliopewa Kitabu kabla yenu na kwa washirikina.

Hii ndiyo thamani ya haki na pepo. Ni mapambano machungu pamoja na wabatil-ifu, ni subira kutokana na tuhuma zao na uzushi wao, na kujitolea mhanga kwa nafsi na mali. Kadiri mtu anavyokuwa na nguvu katika dini yake ndivyo mitihani yake inavyozidi na kuwa mikubwa. Hilo ni kwa kwa sababu umuhimu wa watu wa haki unaleta machukivu kwa wabatilifu, kwani hakuna kupatana wala kupakana mafuta baina ya haki na batili. Watu wa batili walikuwa na bado ni wengi na wenye nguvu. Nao hawawezi kuwanyamazia maadui zao katika itikadi na misingi. Ni nani ajuaye kuwa unambughudhi na kumchukia, kisha akukubalie na kukunya-mazia? isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mola wako?

Kwa sababu hiyo ndipo ikawa historia ya Mitume na viongozi wazuri ni ya vita na jihadi pamoja na washirikina na wafisadi. Ama mitihani ya nafsi na mali na mengi-neo ni natija ya kila vita.

Makusudio ya wale waliopewa Kitabu kabla yenu ni mayahudi na manasara. Na waliofanya ushirikina ni Warabu waliotangaza vita na Mtume

Na mkisubiri kutokana na jihadi ya wabatilifu na misukosuko inayowapata na mkiogopa Mwenyezi Mungu katika yanayopasa kumwogopa, basi hayo ya kuwa na subira kutokana na misukosuko na kuogopa yaliyoharamishwa, ni miongoni mwa mambo ya kuazimia.

187.Na Mwenyezi Mungu alipochukua ahadi na wale waliopewa Kitabu, lazima mtakibainisha kwa watu wala hamtakificha. Wakakitupa nyuma ya migongo yao na wakakiuza kwa thamani ndogo. Basi ni mabaya waliyoyauza.

Kaashif4-88.jpgKaashif4-89.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

KAZI YA WANAVYUONI Aya 187

 MAANA

Na Mwenyezi Mungu alipochukua ahadi na wale waliopewa Kitab, lazima mtakibainisha kwa watu wala hamtakificha.

Serikali huanzisha vituo na kumpangia kila mtu kazi yake na pia huchukua ahadi kwa kila mfanya kazi kwamba ataitekeleza kwa uaminifu na kuwa ataadhibiwa yule atakayevunja miiko.

Mwenyezi Mungu ameumba binadamu, akamwamrisha lile lililo na kheri naye na akamkataza lile lililo baya kwake na linalomdhuru. Na amewachagua Mitume ili wafikishe hukumu zake kwa waja wake, akawaamuru wachukue ahadi ya Mwenyezi Mungu na kila wanayemfikishia hukumu hizi kwamba nao wazifikishe kwa watu.

Kwa hivyo, mwanachuoni wa dini ni mfanyikazi wa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) wa kubainisha yaliyoteremshiwa Mitume. Yeyote atakayeficha kitu, basi yeye atakuwa na jukumu la kuulizwa mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, sawa na mfanyikazi wa serikali anavyoulizwa kama hakutekeleza wajibu wake.

Hayo yameelezwa katika Aya kadhaa walizozitaja wanavyuoni katika mlango wa kuamrisha mema na kukataza mabaya. Kama vile:

Hakika wale wanaoficha tuliyoyateremsha, katika hoja na uwongofu; baada ya Sisi kuyabainisha kwa watu Kitabuni, hao anawalaani Mwenyezi Mungu na wanawalaani wanaolaani ( 2:159)

Na Mtume (s.a.w.) amesema: "Mwenye kuinyamazia haki ni shetani bubu." Sikwambii mwenye kuisaidia batili. Vilevile aliulizwa kuhusu jihadi ipendezayo zaidi kwa Mwenyezi Mungu, akasema: "Neno la kumpa ukweli kiongozi dhalimu." Imam Ali (a.s.) naye akasema: "Mwenyezi Mungu hatawaadhibu wajinga kwa kutojifundisha mpaka awaadhibu wenye elimu kwa kutoelimisha."

Haya yanaenea kwa wote, sio kwa wenye elimu tu, au watu wa dini au wasio na dini, au kwa mashinani au matawii, la! Ni kazi ya kila mtu.

Kauli ya Mwenyezi Mungu: "Na Mwenyezi Mungu alipochukua ahadi." inaenea kwa wote. Kwa sababu waliopewa Kitabu wanaingia mayahudi,manasara na waislamu. Bali Qur'an ndicho Kitabu Kitukufu, kama ambavyo wajibu wa kubainisha na uharamu wa kuficha unaingia katika Utume wa Muhammad (s.a.w.). na mengineyo katika misingi ya dini na matawi yake. Wengine wakasema inawaku-sanya mayahudi na manasara tu, kwa sababu wao walificha dalili za Utume wa Muhammad (s.a.w.) zilizo katika Tawrat na Injil. Lakini ilivyo ni kuwa inaonyesha

106

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

kuenea kwa kukosekana dalili ya kuhusika. Wakaitupa nyuma ya migongo yao.

Kutupa kitu nyuma ya mgongo ni fumbo la kuacha kukitilia manani, kama ambavyo kukikodolea macho ni fumbo la kukitilia maanani.

Na wakakiuza kwa thamani ndogo basi ni mabaya waliyoyauza.

Kila anayeificha haki kwa kuathirika na mambo ya kidunia bila ya kuangalia ya akhera, basi atakuwa amemuuzia shetani dini yake kwa thamani ndogo. Wengine hawatosheki na kuificha haki tu, bali wanakigeuza kitabu na Hadith kwa tamaa ya ukubwa na utajiri, na hawa ndio wanaolaaniwa na Mwenyezi Mungu na pia wenye kulaani.

188..Usiwadhanie kabisa wale ambao wanafurahia mambo waliyoyafanya na wakapenda kusifiwa kwa wasiyoyafanya -usiwadhanie kabisa kuwa wataokoka na adhabu, na wana wao adhabu iumizayo.

189.Na ufalme wa mbinguni na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mwenye uwezo juu ya kila kitu.

Aya 188-189 KUSIFIWA KWA WASIYOYAFANYA

MAANA

Furaha si haramu. Ni nani asiyefurahi akipata jambo la kheri au kuokoka na shari? Bali kufurahi kwa ajili ya kheri ya watu inaonyesha ukweli wa nia na furaha njema.

Mtume (s.a.w.) alifurahi kwa sababu ya kuwasili binamu yake Jafer bin Abu Talib

kutoka Uhabeshi, akambusu na akasema: "Sijui ni jambo gani kati ya mawili

litakalomshinda mwenzake kwa furaha, ni kwa kuwasili Jafar au kwa kuiteka

Khaibar?!"

Furaha isiyotakikana ni ile iliyo na msukumo wa mifundo, kufurahia matatizo ya

Kaashif4-90.jpg

107

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

wengine na majivuno, au kufurahi mtu kwa sababu amenyang'anya, akaua au kufanya ufisadi bila ya kuadhibiwa au kulaumiwa, au kufurahi kwa sababu ya kufanya hila na hadaa ili asifiwe na sifa asizokuwa nazo, na mengineyo ambayo tunayashuhudia huku na huko.

Baada ya utangulizi huu tunaelezea kwa ufupi kauli zinazohusu Aya hii: Usiwadhanie kabisa wale ambao wanafurahia mambo waliyoyafanya na wakapenda kusifiwa kwa wasiyoyafanya, usiwadhanie kabisa kuwa wataoko-ka na adhabu, na wana wao adhabu iumizayo. Yasemekana kuwa Aya hii ilishuka kwa wanavyuoni wa Kiyahudi ambao walificha jina la Muhammad na sifa zake zinazopatikana katika Tawrat, na wakati huo huo wanapenda wasifiwe kuwa ni wa kweli, na kwamba wao wako kwenye mila ya Ibrahim (a.s.)

Na ikasemekana kuwa ilishuka kwa ajili ya wanafiki, waliokuwa wakihepa kuun-gana na Mtume (s.a.w.) katika vita kwa kutoa sababu za uongo na Mtume alikuwa akionyesha kuwakubalia. Hilo liliwafurahisha sana na kupenda kusifiwa kwa wasiyoamini.

Kauli yenye nguvu ni kuwa baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuwataja wale waliochukua ahadi kuwa wasifiche haki, na wakaitupa ahadi, ndipo akawataja katika Aya hii kwamba wao wamefurahi kwa tendo lao hilo wakapenda kusifiwa kuwa ni wa kweli na wenye haki, na hali wao wako mbali nayo kabisa.

Kadiri watakavyoendelea katika upotevu wao hawatatoka katika mamlaka ya Mwenyezi Mungu na uwezo wake, wala hawataokoka na adhabu yake. Vipi isiwe hivyo. "Na ufalme wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mwenye uweza juu ya kila kitu." Kwa tafsir hii wanaingia katika Aya hii Mayahudi na Manasara walioficha yanayomhusu Muhammad (s.a.w.) na wanafiki katika Waislamu walioficha ukafiri na kudhihirisha imani.

Unaweza kuuliza, kwa nini Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema, 'usiwadhanie' baada ya kwisha kusema usiwadhanie ambao.'

Jibu: imekaririka hapa kwa sababu ya kuondoa mikanganyo baada ya maneno marefu. Matumizi haya yameenea siku hizi katika maandishi na idhaa.

Swali la pili: Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amesema: "Usiwadhanie kuwa wataokoka na adhabu." Na kisha akasema: "Na wana wao adhabu iumizayo." Pamoja na kuwa jumla ya kwanza inaitoshelezea ya pili.

Jibu: hapa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anatofautisha kati ya jumla mbili, kwa sababu ya kwanza imefahamisha kwamba wao si wenye kuokoka na adhabu bila ya kubainisha adhabu yenyewe kama ni hafifu au ni kali, ndipo akabainisha katika jumla ya pili kuwa ni katika aina ya adhabu iumizayo. Kama vile kusema: "Nakupenda tena nakupenda sana.'

108

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

190.Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kutofautiana usiku na mchana, ziko ishara kwa wenye akili.

3. Sura Al-Imran

191.Ambao humtaja Mwenyezi Mungu katika hali ya kusimama, na kukaa na kulala, na wanafikiria umbo la mbingu na ardhi. Mola wetu hukuviumba hivi bure. Utukufu ni wako, basi utuepushe na adhabu ya moto."

192.Mola wetu! Hakika wewe ambaye utamwingiza motoni utakuwa umemfedhehesha na hawatakuwepo wasaidizi kwa ajili ya madhalimu.

193.Mola wetu! Hakika sisi tumem-sikia mwenye kulingania anayelingania kwenye imani kwamba: mwaminini Mola wenu nasi tukaamini. Mola wetu! Tusamehe madhambi yetu na na utufutie makosa yetu na utu-fishe pamoja na watu wema."

194.Mola wetu! Na utupe uliyotuahi-di kwa Mitume yako, wala usitufedheheshe siku ya kiyama. Hakika wewe huvunji ahadi."

Kaashif4-91.jpgKaashif4-92.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Kaashif4-93.jpg

195.Akawakubalia Mola wao kwam-ba mimi sitapoteza amali ya mfanya amali miongoni mwenu, akiwa mwanamume au mwanamke, ni nyinyi kwa nyinyi. Basi wale waliohama na wakafukuzwa katika majumba yao na wakaudhiwa katika njia Yangu na wakapigana na wakauawa, bila shaka nitawafu-tia makosa yao na nitawaingiza katika mabustani ambayo hupita mito chini yake. Ndiyo malipo yanayotoka kwa Mwenyezi Mungu na kwa Mwenyezi Mungu kuna malipo mema.

MWENYEZI MUNGU NA WENYE AKILI Aya 190-195

Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kutofautiana usiku na mchana, ziko ishara kwa wenye akili.

Tulionyesha dalili za kutosha za kiakili juu ya kuweko Mwenyezi Mungu (s.w.t.) wakati wa kutafsiri Aya ya 22 na 164 ya Sura Baqara. Nayo iko katika maana ya Aya hii tuliyo nayo. Kwa vile hapa ni mahali pake, tutarudia kuyaeleza maudhui hayo kwa ufupi na kwa namna nyingine.

Njia nzuri ya kumjua Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni njia ambayo anaitolea dalili Yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu kuhusu kuweko kwake. Kwa ufupi ni kuangalia mwenye akili kwenye ulimwengu na kufikiria kwa undani maajabu Yake na siri iliy-omo ya mipangilio na maajabu kadhaa. Utaona kuwa kila kilichopo kinafahamisha makusudio na malengo, kwa kuwekwa mahali panaponasibiana na kuwa katika mpangilio wa ulimwengu na mwendo wa maisha.

Kutokana na misingi hii miwili (hisia na akili), inapelekea kabisa kujua sababu ya kwanza inayosifika na uhai, elimu, uweza na hekima ya hali ya juu. Nimewasikia watu wengi wakisema kuwa watu wote, hata walahidi, wanakubali kuwa iko sababu ya kwanza, isipokuwa waumini huiita Mwenyezi Mungu na wengine huiita maada au nguvu asili, kwa hiyo tofauti iko katika majina tu.

Kaashif4-94.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Lakini hilo ni kosa kubwa na ni kuleta shubha. Kwa sababu waumini wanaamini kuweko sababu hiyo, inayothibitishwa na akili sio kwa hisia, na kwamba sababu hiyo inasifika kwa sifa ya ujuzi, uweza, hekima na uadilifu. Ama wengine wanase-ma kuwa inaonekana kwa macho na kuguswa kwa mkono na kwamba hiyo ni kipo-fu na kiziwi. Kwa hiyo tofauti ya kauli mbili hizo ni mbali zaidi ya mbingu na ardhi.

Ambao humtaja Mwenyezi Mungu katika hali ya kusimama na kukaa na kulala na wanafikiria umbo la mbingu na ardhi. Mola wetu hukuviumba hivi bure, utukufu ni wako; basi utuepushe na adhabu ya moto.

Makusudio ya kusimama, kukaa na kulala kwa ubavu ni kwamba wao wako katika twa'a ya Mwenyezi Mungu wakati wowote. Makusudio ya kufikiria umbo la mbingu na ardhi ni kuwa wanamkubali Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Ama kumyenyekea Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kutaka kinga na adhabu ya moto, ni dalili ya ucha-ji Mungu na imani.

Arrazi anasema: "Aina za kuabudu ni tatu: Kusadikisha kwa moyo, kuthibitisha kwa ulimi na kutenda kwa viungo." Kwa hiyo kauli yake Mwenyezi Mungu 'wanam-taja Mwenyezi Mungu' inaonyesha ibada ya ulimi, 'katika hali ya kusimama kukaa na kulala kwa ubavu' inaonyesha ibada ya viungo, na kauli yake, na 'hufikiria umbo la mbingu na ardhi;' inaonyesha ibada ya moyo na fikra na roho.

Na mtu ni mkusanyiko wa hivi vitu vitatu. Kama ulimi utazama kabisa katika dhikri (utajo), viungo vikawa vinatenda na akili ikazama katika kufikiria, basi hapo ndipo atakuwa ameingia katika ibada kwa mwili wake wote."

Hakuna mwenye shaka kwamba kumtaja Mwenyezi Mungu, kumwamini na kumwabudu ni vizuri, lakini vizuri zaidi ya kumtaja kwa ulimi, kusimama usiku, kuswali na kufunga mchana, ni kufanya kazi kwa ajili ya watu na kujitolea katika maslahi ya umma. Na kila atakayetaka matukufu kutoka kwa Mwenyezi Mungu bila ya kujitoa mhanga huku, pamoja na kuwa na uwezo, basi atakuwa anatafuta kuthaminiwa bila ya thamani.

Kwa mnasaba wa kauli yake Mwenyezi Mungu. 'Mola wetu hukuviumba hivi bure' tutaonyesha kauli za Sunni wanaosema kuwa haifai kuleta sababu ya vitendo vya Mwenyezi Mungu kwa kuwa na makusudio au lengo. Kwa sababu Mwenyezi Mungu hapaswi na jambo lolote wala hakuna ubaya kwake wa kitu chochote. (Al-MawafiqJ. 8 uk. 202)

Sheikh Abu Zuhra katika kitab Madhahibul Islamiyya, anasema; "Wamesema Ashaira. Yaani sunni, kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameumba vitu si kwa sababu yoyote."

Shia wanasema kuwa vitendo vyote vya Mwenyezi Mungu Mtukufu vina sababu ya maslahi ya watu au ya utaratibu wa ulimwengu, kwa kuwa yeye ni mjuzi mwenye hekima. Wakatoa dalili ya Aya hii. "Mola wetu hukuviumba hivi bure."

Kaashif4-95.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

Pia inawezekana kuwajibu Sunni kwa kauli yao na vitendo vyao wala sio kwa Aya au riwaya. Kwamba wao wanafanya makisio na kuchukulia uzuri na maslahi yanayosababisha upole wa Mwenyezi Mungu katika kuwaangalia viumbe na kutengeneza vizuri hali zao, katika maisha yao ya duniani na akhera. Pia wanachukua asili ya hukumu za kisharia ya Mwenyezi Mungu kwa kukisia na kuonelea kuwa ni vizuri.

Vilevile wametunga vitabu mahsusi katika kubainisha hekima ya Mwenyezi Mungu katika maamrisho yake na makatazo yake. Maana ya hayo yote ni kuwa Yeye Mwenyezi Mungu haamrishi wala hakatazi isipokuwa kwa lengo sahihi na sababu yenye hekima.

Mola wetu! Hakika Wewe ambaye utamwingiza motoni, basi utakuwa umemfedhehesha.

Na sisi tunakutii kwa kutaka radhi Zako na kuepuka fedheha hii. Hivi ndivyo anavyokuwa mumini, anaweka mbele thawabu za Mwenyezi Mungu na adhabu yake. Kwa hiyo anatii kwa kuogopa adhabu na kutumaini thawabu. Imamu Ali (a.s) amesema: akiwasifu Waumini: "Wao na pepo ni kama walioiona wakiwa humo wanastarehe. Na wao na moto ni kama waliuona wakiwa ndani yake wanaadhibiwa."

Ama anayemwabudu Mwenyezi Mungu kwa dhati yake tu, sio kwa kutumaini pepo Yake au kuogopa moto wake, huyo ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na mwanafun-zi wake Imam Ali."

Na hawatakuwepo wasaidizi kwa ajili ya madhalimu.

Kila msaidizi wa batili katika dunia hii na ambaye ana haki za watu, basi yeye ni dhalimu, na itakapofika Siku ya haki na uadilifu hatakuwa na msaidizi. Mawaidha fasaha kabisa katika maudhui haya ni khutba ya Mtume alipohisi kukaribia mauti alisema: "Enyi watu ambaye nimemchapa mgongoni mwake, huu hapa mgongo wangu, na ambaye nimemchukulia mali yake hii hapa mali yangu, na achukue wala asiogope kumwekea nongwa. Kwani hiyo siyo hulka yangu. Isipokuwa nawataka mchukue haki zenu tu kama ziko kwangu, au kisasi ili nikutane na Mola wangu nikiwa na nafsi njema." Maelezo zaidi yako katika tafsir ya Aya 160 ya Sura hii kifungu cha 'Muhammad na hulka njema.'

Mola wetu hakika sisi tumesikia mwenye kulingania anayelingania kwenye imani kwamba muaminini Mola wenu, nasi tukaamini.

Hii ndio hali ya kila mwenye kuitafuta haki kwa njia ya haki anaufungua moyo wake kwa mwito wa haki na anaikubali mara tu anapoisikia kutoka kwa yoyote; sik-wambii akiwa ni bwana na Mitume na mwisho wa Mitume.

Akawakubalia Mola wao kwamba mimi sitapoteza amali ya mfanya amali miongoni mwenu, akiwa mwanamume au mwanamke.

112

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                          2. Sura Al-Imran

Yanayozingatiwa ni matendo, sio nasaba ya mtendaji au kabila yake, wala si kwa jinsia yake, awe mwanamume au mwanamke. Wote ni sawa katika uislamu. Huu ni uthibitisho wa haki ya mwanamke na utukufu wake. Ni nyinyi kwa nyinyi mwanamume ni baba wa mwanamke na mwanamke ni mama wa mwanamume, na kila mmoja ni kaka wa mwengine na mume wa mwengine; wote wanatokana na asili moja; wote mnatokana na Adam na Adam anatokana na mchanga. Kuna Hadith isemayo: "Wanawake ni ndugu baba mmoja mama mmoja wa wanaume." Yamekwishatangulia maelezo zaidi katika tafsir ya (2:228).

Basi wale waliohama na wakafukuzwa katika majumba yao na wakaudhiwa katika njia yangu na wakapigana na wakauawa, bila shaka nitawafutia makosa yao na nitawaingiza katika mabustani ambayo hupita mito chini yake. Ndiyo malipo yanayotoka kwa Mwenyezi Mungu na kwake Mwenyezi Mungu kuna malipo mema.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuyafungamanisha malipo na matendo mema na wala sio kwa jinsia, amebainisha kuwa matendo ambayo yatapata nyongeza ya thawabu ni kama haya yafuatayo.

1 .Kutoka mumini kwa hiyari yake katika mji wake ambao hawezi kusimamisha dini kwenda mji mwengine anaoweza kufanya hivyo. Kwa sababu ya Aya hii na Aya isemayo "Hakika Malaika watawaambia wale ambao wamewafisha hali ya kuwa wamezidhulumu nafsi zao: Mlikuwa katika hali gani? Watasema: "Tulikuwa wanyonge katika ardhi." Watawaambia: Kwani ardhi ya Mwenyezi Mungu haikuwa pana mkaweza kugura humo. Hao makazi yao ni jahannam, nayo ni marejeo mabaya kabisa." (4:97)

Kwa sababu ya Aya mbili hizo, mafakihi wametoa fatwa ya kuharamisha kukaa mtu mnyonge katika mji wa kikafiri ambao hawezi kutekeleza faradhi na nembo za Kiislamu, wakawajibisha kwake kuhamia mji wa waislamu ili kuweza kutekeleza yale yaliyo wajibu kwake isipokuwa kama atashindwa kuhama.

Jambo la kusikitisha siku hizi ni kuhusu vijana wetu wa Kiislamu wenye uwezo, wanakazania kwenda Amerika na Ulaya, si kwa jengine ila kwa kufuata ufuska, zinaa na ulevi.

2.Kutolewa waumini kwa nguvu majumbani mwao, kama washirikina wa Kiquraish walivyowafanyia wale waliomwamini Muhammad (s.a.w.) na kama walivyofanya waisrail kwa wapalestina.

3.Kuudhiwa katika njia ya haki. Hakuna yeyote anayeifuata ila ataudhiwa. Imeelezwa katika Hadith kwamba mtu hujaribiwa kwa kiasi cha dini yake. Ikiwa katika dini yake ni nzito basi huzidi mitihani na ikiwa ni nyepesi basi pia ata-jaribiwa kwa kiasi chake. Wala hakuna kitu kikubwa zaidi kwa malipo mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko kuvumilia maudhi kwa ajili ya dini ya Mwenyezi Mungu na kuwa na subira. "Ewe Mwenyezi Mungu tujaalie katika wenye kuvumilia.

4.Kujitoa mhanga katika njia ya haki. Wote hawa Mwenyezi Mungu atawafutia

113

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

maovu yao na zaidi ya hayo atawapa thawabu itakayofanana na utukufu wake na cheo chake.

Kukaririka neno malipo na utukufu ni kuonyesha kuwa malipo yake hayana mfano, kama ambavyo utukufu wake hauna mfano.

196.Kusikuhadae kabisa     kuzun-

gukazunguka, kwa     wale

ambao wamekufuru    katika miji.

197.Ni starehe ndogo. Kisha makazi yao ni Jahannam ni mahali pabaya pa kushukia.

198.Lakini wale waliomcha Mola wao watapata mabustani ambayo hupita mito chini yake. Watakaa humo milele.                Ndiyo

makaribisho yatokayo kwa Mwenyezi Mungu, na vilivyoko kwa Mwenyezi Mungu ni bora kwa watu wema.

Kaashif4-96.jpg

Aya 196-198 WALIOKUFURU NA WENYE TAQWA

MAANA

Maana ya matamshi ya Aya zote tatu yako wazi. La muhimu ni kubainisha makusudio kwa ujumla.

Wafasiri wengi wamesema kuwa kafiri anaishi maisha ya hapa duniani kwa raha, lakini mwisho wake huko akhera ni balaa na mashaka. Na mu'min anaishi kwa mashaka na dhiki, na mwisho wake ni mzuri. Na kwamba "Dunia ni jela ya mu'min na ni pepo ya kafiri."

Kaashif4-97.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

3. Sura Al-Imran

Tulivyofahamu sisi kutokana na Aya hizi ni kwamba zimeeleza tofauti baina ya wale walioathirika na dunia yao kuliko dini yao, na wala wasifanye kazi yoyote isipokuwa kwa maslahi yao ya kibinafsi, kama vile mayahudi na wanaofanana nao, na wale ambao wameitanguliza dini yao kuliko dunia yao kwa hali yoyote itakayokuwa.

Kundi la kwanza Mwenyezi Mungu ameliita makafiri kwa sababu wao wanaikufu-ru haki wala hawaipi uzito wowote. La pili ameliita wanaomcha Mwenyezi Mungu, kwa sababu linajiepusha na machukivu yake na maasia yake. Hakuna mwenye shaka kwamba mtu anayefanya tendo lolote kwa ajili ya dunia, akaipa kipaumbile na akahalalisha ya haramu kwa ajili ya dunia, basi takataka zote zitamwangukia, kama tunavyoshuhudia. Kinyume na mwenye kufanya zuhudi katika haramu na akathirika na njaa na kujinyima.

Makusudio ya kuzunguka zunguka katika miji ni kupata kwao neema za dunia. Huenda wakadhani kwamba dhahiri ya neema na starehe za wabatilifu ni kheri kwao, na kwamba dhahiri ya kujinyima kwa watu wa haki ni shari. Ndipo Mwenyezi Mungu akaiondoa dhana hii, kwamba ni kinyume cha hivyo. Kwa sababu neema ya wabatilifu ni starehe chache, kisha waingie katika Jahannam ambayo ni marejeo mabaya. Na kwamba shida ya wenye haki itaondoka, kisha itakuja neema ya milele na raha ya daima.

199.Na hakika miongoni mwa watu wa Kitabu wako wanaomwamini Mwenyezi Mungu na yaliy-oteremshwa kwenu na yaliy-oteremshwa kwao, kwa kum-nyenyekea Mwenyezi Mungu. Hawaziuzi Aya za Mwenyezi Mungu kwa thamani ndogo. Hao wana ujira wao kwa Mola wao. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwepesi wa kuhisabu.

200.Enyi ambao mmeamini! Fanyeni subira na mvumilie na muwe imara na mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kufaulu.

Kaashif4-98.jpgKaashif4-99.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

WAUMINI KATIKA WATUWA KItAbU Aya 199-200

 LUGHA

Imesemekana kuwa neno Isbiruu na Saabiruu yana maana moja. Pia imese-mekana kuwa Isbiruu lina maana ya kuvumilia adha ambayo haikusababishwa na mtu; kama maradhi, na Saabiruu ni kuvumilia adha inayotokana na mwengine.

MAANA

Na hakika miongoni mwa watu wa Kitabu wako wanaomwamini Mwenyezi Mungu na yaliyoteremshwa kwenu na yaliyoteremshwa kwao, kwa kum-nyenyekea Mwenyezi Mungu. Hawaziuzi Aya za Mwenyezi Mungu kwa thamani ndogo. Hao wana ujira wao kwa Mola wao.

Makusudio ya yaliyoteremshwa kwenu ni Qur'an na yaliyoteremshwa kwao ni Tawrat na Injil.

Aya inamhusu kila aliyemwamini na atakayemwamini Muhammad (s.a.w.) katika waliopewa kitabu, na wala haimhusu Najjash au Abdallah bin Salam tu, kama ilivyosemekana, kwa sababu tamko linawanea wote, wala hakuna dalili ya kuwa ni mahsusi. Ikiwa Mwenyezi Mungu anaweza kumkubalia anayemwamini Muhammad katika watu waliokuwa hawamwamini Mwenyezi Mungu wala Kitabu, basi uwezekano wa kumkubalia mtu wa Tawrat na wa Injil ni zaidi. Hasa kwa kuzingatia kuwa mtu anaacha dini yake, jambo ambalo ni gumu sana kwa mtu kuweza kuacha dini aliyoizoea na kuirithi.

Enyi ambao mmeamini! Fanyeni subira na mvumilie na muwe imara na mcheni Mwenyezi Mungu, ili mpate kufaulu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anamalizia Sura ya Al-Imran kwa Aya hii ambayo imeku-sanya taqwa ya Mwenyezi Mungu na amri ya kuwapiga jihadi maadui zake. Yamekwishatangulia maelezo kwa ufafanuzi kuhusu subira wakati wa kufasiri Aya ya 155 ya sura ya Baqara katika kifungu cha subira na kifungu cha aina ya malipo ya subira.

TAQWA

Nasi tunaihitimisha Sura hii tukufu kwa muhtasari kuhusu taqwa. Aliulizwa Imam Jafar As-Sadiq (a.s.) kuhusu Taqwa. Akasema" Ni asikose kukuona Mwenyezi Mungu pale alipokuamrisha na usiweko katika yale aliyokukataza." Kwa hiyo hapana budi katika taqwa kujua hukumu za Mwenyezi Mungu na kuzitumia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Kwa sababu ilimu bila ya matendo ni hoja kwa mtu, na matendo bila ya ilimu ni kama kutembea bila ya kutumia njia. Kwa msingi huu, taqwa inakuwa ndiyo dini, ndiyo hulka na ndiyo msingi wa mambo. Mtume (s.a.w.)

Kaashif4-100.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

anasema: "Msiseme Muhammad ni wetu, Wallahi! Marafiki zangu sio nyinyi wala si wengine isipokuwa wale wamchao Mwenyezi Mungu." Amesema tena: "Asiyekuwa Mwislamu, wakisalimika watu na mkono wake na ulimi wake, yuko karibu zaidi na Muhammad (s.a.w.) kuliko yule anayenasibika na uislamu, lakini asijizuie na kuwaudhi watu."

Zimekuja Aya kadhaa katika Qur'an kwamba kufuzu na kuokoka kesho ni kwa wanaomcha Mwenyezi Mungu peke yao. Katika ngano za watu wa kale kuna hekaya inayoishiria ukweli huu: Hapo zamani za kale paliondokea mtu mmoja aliyekuwa akipenda sana kusema: sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe vyote na mwisho ni wa wamchao Mwenyezi Mungu. Iblis alikasirika sana na hali hii. Hivyo akamtumia mmoja wa mashetani zake.

Akaenda na kumwambia: Sema, mwisho ni wa matajiri. Yule mtu akasema: Hapana , mwisho ni wa wamchao Mwenyezi Mungu. Walipozidi kubishana wali-afikiana waamuliwe na mtu watakayemuona kwanza, na atakayeshindwa akatwe mkono. Mara wakakutana na mtu mmoja wakamweleza, akasema: Mwisho ni wa matajiri, sio wa wamchao Mwenyezi Mungu." Yule mtu akakatwa mkono.

Yule mtu akaendelea kuyakariri maneno yake, sifa njema ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe vyote na mwisho ni wa wamchao. Shetani akamjia mara ya pili na kumwambia: Hukupata funzo? Je unataka tuamuliwe tena? yule mtu akajibu: Ndio akatokeza mtu mwengine akahukumu kuwa mwisho ni wa matajiri sio wa wamchao Mwenyezi Mungu. Yule mtu akakatwa mkono wa pili.

Licha ya hayo, yeye aliendelea kuyakariri yale maneno kuliko mara ya kwanza. Shetani akarudi tena akasema: Hivi sasa atakayeshindwa atakatwa kichwa. Yule mtu akakubali akasema: Naam. Mara wakakutana na mpanda farasi mmoja wakataka waamuliwe, naye baada ya kuelezwa kisa yule mpanda farasi akachukua upanga na kumdengua kichwa shetani huku akisema huu ndio mwisho wa wafisadi. Kisha Mwenyezi Mungu akamrudishia yule mtu mikono yake kama ilivyokuwa; yakathibiti aliyokuwa akiyasema. Lakini hii ni baada ya subira na uvu-milivu na kukatwa mkono wa kuume na kushoto. Ni muhali kwa mtu kufikilia malengo bila ya kuwa na subira na kuvumilia taabu na mashaka.

Kaashif4-101.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

4. Sura An-Nisaa

Kaashif4-102.jpg

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu

1.Enyi watu! Mcheni Mola wenu ambaye amewaumba kutokana na nafsi moja. Na akamuumba mkewe katika nafsi hiyo, na akaeneza kutokana na hao wawili wanaume wengi na wanawake. Na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye kwaye mnaombana na ndugu wa damu. Hakika Mwenyezi Mungu anawachunga.

4. SURA AN-NISAA

Sura hii imeshuka madina, ina Aya 176; ilishuka baada ya Sura Mumtahina (60). Mwenye Majmaul-bayan amenukuu kuwa katika Sura hii mna Aya mbili ambazo zimeshuka Makka nazo ni: 58 na 127

Imeitwa Sura ya wanawake, kwa sababu, imeanza kwa kuwataja wanawake na pia ina hukumu nyingi zinazofungamana nao.

aya 1 AMEWAUMBA KUTOKANA NA NAFSI MOJA

LUGHA

Neno Zawj lina maana ya aliye na mwengine wa jinsi yake (j°zi). Kwa hiyo mwanamke aliyeolewa ni jozi na mume aliyeoa ni jozi.

MAANA

Katika Aya hii kuna mambo yafuatayo:

1. Enyi watu! Mcheni Mola wenu.

Imesemekana kuwa msemo unawahusu watu wa Makka tu. Lakini ilivyo hasa ni kuwa unawaenea wote wanaokalifiwa na sharia. Kwa sababu dhahiri ya neno inawakusanya wote, wala hakuna dalili yoyote ya kuhusisha. Bali amri ya kumcha Mwenyezi Mungu inatilia mkazo kuwa inawaenea wote. Kwa sababu, wajibu wa

Kaashif4-103.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

kujiepusha na maasi, hauhusiki na watu fulani.

2. Ambaye amewaumba kutokana na nafsi moja.

Mwenye Tafsir Al-manar amemnukuu Sheikh wake Muhammad Abduh akisema: "Mwenyezi Mungu ameficha kuhusu nafsi aliyomuumbia mtu na ameileta kwa tamko Nakira (linaloenea). Kwa hiyo nasi tunaiacha kama ilivyofichwa. Pia Aya nyingine zinazomwambia mtu: "Ewe mwana Adam" haziondoi uficho huu. Wala hakuna kauli ya mkato kuwa watu wote ni watoto wa Adam. Inatosha kusihi kuwa msemo uliwahusu watu miongoni mwao wana wa Adam waliokuwa wakati wa kuteremshwa msemo huo."

Yametangulia maelezo katika kufasiri kisa cha Adam mwanzo mwanzo mwa Sura ya Baqara, akisema kwamba katika ardhi kulikuweko na aina ya watu waliokuwa katika jinsi hii wakafanya ufisadi na wakamwaga damu."

Kwa ufupi makusudio ya Sheikh Abduh ni kwamba Qur'an haithibitishi wala haikanushi kuwa Adamu ni baba wa watu wote; bali inawezekana kuweko na mababa kadhaa kwa watu, Adam akiwa mmoja wao. Na kwamba kauli ya Mwenyezi Mungu "Enyi wana Adamu."Inafahamisha kuwa wale waliokuweko wakati wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) walikuwa ni watoto wa Adam na wala haifahamishi kila aliyekuwako na atakayekuwako ni kizazi cha Adam.

Sisi tunamjibu, kwanza:

Maamrisho na makatazo yaliyokuja katika Qur'an na Hadithi hayahusiki na aliyekuwepo wakati wa kutolewa, bali yanamkusanya kila aliyekuwepo na atakayekuwepo mpaka siku ya mwisho. Kwa sababu kadhia la kisharia lina-muhusu aliyepo na asiyekuwepo bila ya tofauti yoyote sawa na mfano wa kusema: "Atakayetimiza miaka ishirini basi ni lazima afanye jambo fulani. Mwenyezi Mungu anasema: "Je sikuwaagiza enyi wanaadamu kuwa msimwabudu shetani? Hakika yeye ni adui aliye wazi kwenu." (36:60)

Kauli hii inawaenea watu wote bila ya kumtoa hata mmoja, ni sawa wawepo wakati iliposemwa au la.

Pili: Maamrisho na makatazo katika Qur'an na Hadith ambayo wameelezwa wanadamu, ikiwa yanawahusu waliokuwa wakati wa Mtume (s.a.w.w.), sisi tusin-gelazimika nayo, na wala isingefaa sisi kuzitolea dalili juu ya hukumu yoyote miongoni mwa hukumu za Mwenyezi Mungu. Waislamu wote akiwemo Sheikh Abduh wanatoa hoja kwa Qur'an na Hadith za Mtume (s.a.w.w.) bali ndio msingi wa kwanza wa kurejelea wa itikadi na sharia ya kiislam kwa dharura ya dini.

Ikiwa taklifa inawahusu watu wote, basi watu wote watakuwa ni kizazi cha Adam. Kwa hiyo basi Sura ya 36 na Aya hii "Enyi wanadamu asiwafitini shetani kama alivyowatoa wazazi wenu katika pepo." (7:27). na Aya: "Na (kumbuka) Mola wake alipoleta katika wanadamu kizazi chao kutoka migongoni mwao." (7:172). Na vile

Kaashif4-104.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                                4. Sura An-Nisaa

vile Aya isemayo: "Na hakika tumewatukuza wanadamu." (17:70), zote hizi zinakuwa ni ubainifu na tafsiri ya nafsi moja; na kwamba makusudio ya nafsi ni baba yetu Adam bila ya shaka yoyote.

Ama kauli ya Sheikh Muhammad Abduh kuwa kulikuweko na watu wengine kabla ya Adam iko mbali na tunayoyaeleza. Kwa sababu maneno yako katika jinsi ya viumbe iliyobaki sio jinsi iliyokwishapotea.

Zaidi ya hayo, Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ametuambia kwa kauli yake: "Enyi watu" na "Hakika tumewaumba kwa udongo." (22:5).

Vilevile Aya: "Hakika mfano wa Isa kwa Mwenyezi Mungu, ni kama mfano wa Adam; alimwumba kutokana na udongo," (3:59).

Aya hizi tukiziunganisha, natija itakuwa "Nyote mmetokana na Adam na Adam anatokana na udongo" kama inavyosema Hadith tukufu.

Tatu: Imethibiti kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w..) kwamba yeye amesema: "Mimi ni bwana mkubwa wa kizazi cha Adam." Je yuko mwislamu yey-ote anayedhani tu au kufikiria kuwa Mtume alikuwa anakusudia aina maalum ya watu na sio watu wote? Swali hili hasa limwelekee Sheikh Muhammad Abduh.

3. Na akamuumba mkewe katika nafsi hiyo.

Inassemekana kuwa herufi Min (katika) ni ya kuonyesha baadhi; na makusudio ni mkewe Hawa na kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu alimuumba kutokana na ubavu wa Adam. Pia imesemekana kuwa alimuumba kutokana na ziada ya udongo wa Adam, kama zielezavyo riwaya nyengine.

Ilivyo ni kuwa hakuna dalili ya kuonyesha baadhi, bali inawezekana kuwa ni ya kubainisha; mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na katika ishara zake ni kuwa amewaumbia wake zenu katika jinsi yenu. (30:21)" Maana yake ni kuwa kila nafsi na mkewe wameumbwa katika asili moja ambayo ni mchanga kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: " Na katika ishara zake ni kuwa amewaumba kwa udongo kisha mmekuwa watu wanaoenea." (30:20)

Ama kauli ya kuwa makusudio ya mke wake ni Hawa, haina dalili yoyote kutoka kwa Qur'an ambapo haikutajwa kabisa.

4 Na akaeneza kutokana na hao wawili wanaume wengi na wanawake.

Yaani na wanawake wengi pia. Haikutajwa sifa ya wengi kwa vile ile ya kwanza imefahamisha hii ya pili. Ajabu ni kauli ya Razi kwamba kwa kusifiwa wanaume kwa wingi, ni umashuhuri na kuonekana; kinyume na hali ya wanawake ambayo inakuwa ni kutokuwa mashuhuri na kufichika.

Kauli hii ya Razi inafahamisha tu kuwa amehukumia tabia ya mwanamke kulin-gana na desturi za jamii anayoishi. Kimsingi ni kuwa desturi hizi hugeuka na

120

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

kubadilika kutokana na wakati ulivyo. Kwa hiyo ni makosa kuchukua kipimo cha jumla kutokana na desturi maalum.

Vyovyote itakavyokuwa maana yake iko wazi, ni kwamba mtu anazaliwa kutokana na mke na mume; na kutokana na wawili wao (mke na mume) ndio mamilioni yanaenea kizazi baada ya kizazi. Inasemekana kuwa ulimwenguni hivi sasa kuna watu zaidi ya Billioni tatu*9 .

5. Na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye kwaye mnaombana na ndugu wa damu.

Hii ni ishara ya yale wayasemayo baadhi yetu kwa mfano 'haki ya Mungu au haki ya mama. (Kuomba mtu afanye kwa haki ya mungu au ya ndugu (kizazi))

Makusudio ya amri ya kumcha Mwenyezi Mungu na udugu wa damu ni kutekeleza haki zetu kwao. Aya iko katika mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu."Ya kwamba unishukuru mimi na wazazi wako." (31:14).

Kwa ufupi ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametuamrisha katika Aya hii kuogopa ghadhabu na adhabu yake, kuwafanyia mema ndugu wa damu, tusifanyiane kibri na tusidhulumiane. Kwa sababu wote ni wa asili moja. Amemalizia Mwenyezi Mungu kwa kusema: Hakika Mwenyezi Mungu anawachunga. Haya ni make-meo na ni kiaga kwa yule anayeasi na kung'ang'ania uasi.

*9Hapa ni wakati wa kuandikwa kitabu, ambapo hivi sasa wakati wa kufasiri mwaka 2004, inakisiwa kuwa duniani kuna watu zaidi ya Billioni tano.

121

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

4. Sura An-Nisaa

Kaashif4-105.jpg

2.Na wapeni mayatima mali zao wala msibadilishe kibaya kwa kizuri. Wala msile mali zao kwa mali zenu; hakika hiyo ni dhambi kubwa.

MALI YA MAYATIMA

Na wapeni mayatima mali zao.

Hapana budi yatima awe na mtu mwenye akili na mwaminifu atakayemlea na kuangalia mali yake kwa masilahi yake mpaka aweze kujitegemea na kujua baya na zuri. Aya hii inafungamana na mali za mayatima; inawaamrisha mawasii waichunge hiyo mali na wasiifuje; waitumie vizuri kwa ajili ya kuwalisha na wawape wenyewe watakapokuwa wakubwa.

Wala msibadilishe kibaya kwa kizuri.

Makusudio ya kibaya hapo ni mali ya haramu na kizuri ni mali ya halali. Maana yake msile na kustarehe kwa mali ya yatima na mali zenu mkazibania. Ikiwa mtafanya hivyo, basi mtakuwa mmebadilisha lile ambalo ameliharamisha Mwenyezi Mungu (mali ya yatima) kwa zuri, lile alilolihalalisha (mali yenu). Aya hii iko katika mwelekeo wa Aya isemayo: "Je, mnabadili vilivyo duni kwa vile vilivyo bora?"(2:61)

Wala msile mali zao kwa mali zenu; hakika hilo ni dhambi kubwa.

Makusudio ya msile hapo ni msitumie maana yake, msinufaike na mali za yatima kama mnavyofanya kwa mali zenu. Kwa sababu umuhimu wenu ni kuzichunga tu, na kuzitumia kwa masilahi ya mayatima. Na mkiligeuka hilo basi mtakuwa wakosaji wenye dhambi.

3.Na kama mkihofia kutowafanyia uadilifu mayatima, basi oeni mnaowapenda katika wanawake, wawili wawili na watatu watatu na wanne wane. Na mkihofia kuwa hamuwezi kufanya uadilifu, basi ni mmoja au wale ambao mikono yenu ya kuume imewamiliki. Hilo ni karibu zaidi na kutofanya dhuluma.

Kaashif4-106.jpgKaashif4-107.jpgKaashif4-108.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

4. Na wapeni wanawake mahari yao hali yakuwa ni zawadi. Kama waki-watunukia kitu katika hayo mahari, basi kuleni kwa raha na kunufaika.

MKIHOFIA KUTOFANYA UADILIFU BASI NI MMOJA. Aya ya 3-4

3.  Na kama mkihofia kutowafanyia uadilifu mayatima, basi oeni mnaowapen-da katika wanawake, wawili wawili na watatu watatu na wanne wanne. Na mkihofia kuwa hamuwezi kufanya uadilifu, basi ni mmoja au wale ambao mikono yenu ya kuume imewamiliki. Hilo ni karibu zaidi na kutofanya dhu-luma.

4.  Na wapeni wanawake mahari yao hali yakuwa ni zawadi. Kama waki-watunukia kitu katika hayo mahari, basi kuleni kwa raha na kunufaika.

NAHAU

Makusudio ya herufi Ma hapa ni wanawake. Wafasiri wamekanganywa kuhusu maana yake. Wengine wamefasiri kwa jinsi ya wanawake; wengine, kwa sifa na kuna wengine waliofasiri kwa kitu. Siri ya kubabaika kwao ni kauli ya watu wa Nahau kwamba herufi Ma ni ya kisichokuwa na akili na Man ndiyo ya mwenye akili. Lakini kimsingi ni kuwa Qur'an ni hoja juu ya watu wa Nahau, na wala watu wa Nahau si hoja juu ya Qur'an. Qur'an imetumia herufi Ma kwa mwenye akili katika Aya nyingi. Kama vile: "Na (kwa) mbingu na aliyeziweka." (91:5). Nyingine: "Wala nyinyi hamuabudu yule ninayemuabudu" Au kama ilivyotumia Man, kwa kisicho na akili. "Na wengine huenda kwa matumbo yao" (24:45)

Ndio ni kweli kwamba aghlabu ni kutumiwa Ma kwa kisicho na akili na Man kwa mwenye akili, lakini kuwa aghlabu ni kitu kingine na kutowezekana ni kitu kingine.

Maunganisho ya wawili wawili na watatu watatu na wanne wanne, yamekuja kwa 'na' na wala sio 'au'. Kwa sababu kila mtu aweza kuwa na hiyari ya idadi anayota-ka katika hii iliyotajwa. Lau ingeliunganishwa kwa au ingelikuwa maana yake atakayechagua wawili ndio hao hao, hawezi kuongeza, na mwengine aweze kuch-agua watatu tu na pia mwengine achague wane.

MAANA

Na kama mkihofia kutowafanyia usawa mayatima, basi oeni mnaowapenda katika wanawake, wawili wawili na watatu watatu na wanne wanne.

Msingi wa kuoa wake zaidi ya mmoja hadi kufikia wane umethibitishwa kisheria

123 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

kwa hukumu ya Qur'an na Hadith na ijmai kwa kauli na vitendo. Bali msingi huu unajulikana kuwa ni katika dharura za dini. Lakini haukuhalalishwa moja kwa moja, bali umewekewa masharti ya kuuhalalisha kwa dharura ya dini vilevile.

Hapa kuna swali linalojitokeza; kwamba maana yaliyo wazi katika Aya hii ni kwam-ba mwenye kuogopa kutofanya uadilifu katika mayatima basi aoe wake wawili, watatu na wane, na kwamba akifanya hivyo hakutobakia dhuluma yoyote. Bila shaka, kama maana yangekuwa haya, ingekuwa sawa na maneno ya kubobokwa, kwani hakuna mfungamano wote kati yake, na Qur'an zimepamban-uliwa Aya zake kutoka kwa Mwenye Hekima aliye Mjuzi?!

Jibu la swali hili liko wazi na ni jepesi, isipokuwa kutofautiana majibu ya wafasiri na kugongana kwao, kumemwacha msomaji gizani.

Kwa ufupi ni kuwa maneno tangu mwanzo yanahusiana na waliousiwa (mawasii) mayatima, ambao ndio waliokusudiwa katika kauli ya "na wapeni mayatima mali zao wala msibadilishe kibaya kwa kizuri wala msile mali zao." Baada ya kuambi-wa haya wenye kufungamana na mali ya yatima, ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akawaambia mawasii jambo jengine litakalofungamana na ndoa ya mayatima ambalo ni "Kama mkihofia kutofanya usawa katika mayatima: .Yaani katika ndoa ya mayatima. Neno 'ndoa' limefahamika kutokana na neno basi 'oeni' Huo ni mlango wa kuondoa cha kwanza kinachofahamishwa na cha pili; kama wase-mavyo watu wa Nahau.

Kukadiria kwake ni: Ama mambo yanayohusu kuoa wanawake katika mayatima, basi ni juu yenu enyi mawasii, kama mkiwaoa msiwanyime haki zao. Na kama mkihofia kutowafanyia haki kwa kuangalia kuwa wao wako peke yao, hakuna yeyote atakayewatetea, basi waacheni na muoe wengine, Mwenyezi Mungu amewapa nafasi kwa mayatima kama vile alivyowahalalishia wengineo kuoa mmoja, wawili, watatu au wane. Lakini vilevile kwa misingi ya usawa na kama mkihofia kutofanya usawa kwa zaidi ya mmoja, basi oeni mmoja.

Kwa maelezo hayo ndio maneno ya Aya yatakuwa yanaungana vizuri, sawa na kumwambia mwenzako. "Ikiwa huli aina hii, kwa sababu unakula sana na kuogopa kuvimbiwa, basi kula aina nyingine, lakini pia usile sana na utajitia kwenye mad-hara." Kila tamko tutakalo likadiria kwa maana hayo tuliyoyataja, basi yanakubali-ka nayo.

Imezoeleka kuwa Qur'an inafupisha maneno sana, na kuacha kutaja kila ambacho msomaji anaweza kukifahamu kwa ishara tu. Ikiwa yaonekana wafasiri watakuwa wanababaika, basi hiyo inafahamisha kuwa Aya hii ni ya mkato sana .(hivyo, inababaisha zaidi).

Mkihofia kutofanya uadilifu basi ni mmoja.

Makusudio ya usawa ni uadilifu (usawa) katika mavazi, mahali pa kuishi na mengineyo katika mambo ambayo yako ndani ya uwezo wa mtu. Ama yale ambayo yako nje ya uwezo wake; kama vile moyo kumpenda mmoja zaidi, basi

124

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                          2. Sura Al-Imran

hayalazimishwi usawa.

Kwa hivyo basi, ndio tunapata tofauti kati ya Aya hii na ile isemayo: "na hamtaweza

kufanya uadilifu baina ya wake (wenu) hata mkijitahidi vipi."(4:129)

Makusudio ya uadilifu katika Aya kwanza ni uadilifu katika kukidhi mahitaji yake, na katika ya pili ni uadilifu wa mapenzi ya moyo.

Unaweza kuuliza: Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewajibisha kutosheka na mke mmoja tu, ikiwa kunahofiwa dhuluma katika zaidi ya mmoja. Na kwa dhahiri ni kwamba hofu ya kinafsi mara nyingi hukosea kuliko kupata.

Na tumewashuhudia wanaume wengi wanashindwa na matamanio na kuongeza wake halafu wanakabiliwa na matatizo. Kwa hiyo sharti hili si sawa.

Jibu: Mushkeli huu hauepukiki, kama tutakusudia kuhofia hali ya nafsi. Ama ikiwa ni kuhofia hali ya nafasi ya mtu na afya yake, kwamba yeye anaweza zaidi ya mmoja, basi swali halitokuwa na haja.Vitu vya kimaada vya kidhahiri inawezekana kuvidhibiti kwa wepesi; wala katika sheria ya kiislamu hakuna kukadiria hali mah-susi ya mtu anayetaka kuoa wake wengi; kama ilivyo hivi sasa katika baadhi ya miji ya kiislamu.

Hilo ni karibu zaidi na kutofanya dhuluma.

Yaani kuwa na mke mmoja ni karibu zaidi na uadilifu na ni mbali zaidi na kufanya dhuluma. Hii ni ishara ya kuonyesha kuwa, ni juu ya mume kutosheka na mke mmoja, kwa sababu kuwa na zaidi ya mmoja kunaleta matatizo.

Katika Tafsir Al-Bayadhawi amesema kuwa baadhi ya wafasiri wamefasiri neno la tau'uluu kutoka neno I'yal ulezi mwingi; kwa maana ya kuwa ni bora mume asioe wake wengi ili asipate tabu na mashaka kwa ajili ya hao wake na watoto. Mwenye Tafsir Al-Manar amesema kauli hii ndiyo yenye nguvu zaidi. Na amesema Imam Ali: "Ulezi mchache ni moja ya nafuu".

Wapeni wanawake mahari yao hali ya kuwa ni zawadi.

Makusudio ya zawadi hapa ni ile ambayo Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameilazimisha kwa mume. Maana yake ni wapeni wanawake mahari yao, kwa sababu Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameyalazimisha kuwa ni zawadi sio kununua starehe. Kwa sababu wote wawili wanastarehe.

Kama wakiwatunukia kitu katika hayo mahari yao, basi kuleni kwa raha na kunufaika.

Mahari ni mali ya mke, anaweza kuitumia vile anavyotaka, wala haifai mume au mtu mwengine yeyote kumwingilia kwenye mahari; kama asemavyo Mwenyezi Mungu: ".Na mkawa mmempa mmoja wao chungu ya mali, basi msichukue kitu katika hiyo (mali)." Ila ikiwa atatoa ruhusa na kwa radhi yake sawa na mali nyingine.

NDOA YA MITALA (WAKE WENGI)

Kaashif4-109.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Uislamu umeweka sharia ya kuoa wake wengi kwa sharti. Hilo halina shaka, wala silo la kufanyiwa utafiti na Ijtihadi. Lakini mlango wa Ijthadi ulio wazi katika kufasiri sharti ya mwenye kutaka kuoa wake wengi, Mujtahid anaweza kusema: Makusudio ya kuhofia ni vile tu mume kufikiria kufanya dhuluma na kutofanya usawa kwa wake wengi. Kwa hiyo, kwa mujibu wa Mujtahdii huyu itakuwa hai-wezekani kuoa wake wengi isipokuwa kwa nadra. Kwa sababu mafikirio haya yako kwa wengi, na yanatiliwa mkazo na ufisadi tunauona katika majumba mengi yaliyo na mke zaidi ya mmoja.

Qur'an pia imekwishalidokeza hilo kwa kusema "Hilo ni karibu zaidi na kutofanya dhuluma." Yaani kutosheka na mmoja ni karibu na uadilifu na ni mbali na kufanya dhuluma. Kwa hiyo kufungamanisha kujuzu kuoa zaidi ya mke mmoja, na kusiwe na uonevu na ufisadi ni sawa na kufungamanisha na muhali (jambo lisilo wezekana) kulingana na inavyotokea mara kwa mara.

Jambo la kushangaza ni kwamba wale ambao wana uwezekano wa kuwafanyia uadilifu wake wengi na hali ya afya na mali zinawaruhusu, hawapendelei kuoa mke zaidi ya mmoja na wanaogopa hata kama wanatamani kufanya hivyo. Lakini wale ambao hawatarajiwi kufanya uadilifu kwa namna yoyote ile na kuharibu jamii na kizazi chao kwa kuoa wake wengi, hawa wanajipiga moyo konde kwa kuoa mke zaidi ya mmoja. Na jambo la kusikitisha zaidi ni kwamba wanavyuoni wa kidini wanapitisha ndoa za watu hawa, bila ya kusita na hata kuuliza na kupata jawabu, kama kwamba kuoa mke zaidi ya mmoja kumehalalishwa hivi hivi tu, bila ya sharti lolote.

Zaidi ya hayo, kuoa mke zaidi ya mmoja si katika wajibu wala sunna katika sharia ya kiislam, isipokuwa uislam umeruhusu kwa mambo maalum na masilahi mah-susi. Lakini maadui wa dini wamewachukulia wale vinukamito (wapendao kuoa sana) ambao hawajali masharti yoyote kuwa ni njia ya kutia ila na kuufedhehi uislam; kama ilivyo kawaida yao kutoa hoja kwa vitendo vya watu kuwa ndio vitendo vya dini na itikadi. Lau kama wangekuwa ni watu wa usawa basi wangelifanya kinyume, na kuitolea hoja dini juu ya watu wafanyao makosa na siyo dini.

Wakati uislam unashartiza mume asioe zaidi ya mke mmoja ila baada ya kuhakik-isha kuwa hakutakuweko ufisadi na dhuluma, huko kwenye miji ya Ulaya na Marekani kuna baadhi ya miji wanawake mara nyingi wanatembea na waume wa nje wanaowataka bila ya sharti lolote tena pengine mumewe akiwa anajua. Zaidi ya hayo, bunge la Uingereza mwaka uliopita lilipitisha sheria ya kulawiti na ikaungwa mkono na baadhi ya wakuu wa dini; mji wote ukajaa furaha kwa kuwa wamewahi wao kuendelea na kuwa na mwamko wa kisasa.

Miongoni mwa maajabu ni kwamba Kusini mwa India na sehemu za mpaka wa Kaskazini wanaruhusu mke kuwa kwenye ndoa na zaidi ya mume mmoja; na utaratibu huu bado unaendelea hadi leo.10

10.Kumbuka 'leo' hii 'mwaka jana' ni wa mwaka 1967 kilipoandikwa kitabu hiki -mfasiri

Kaashif4-110.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

5.Wala msiwape wapumbavu mali zenu ambazo Mwenyezi Mungu amewajaalia            kuwaendeshea

maisha. Na muwakimu katika mali hiyo na muwavishe, na muwaam-bie maneno mazuri.

6.Na wajaribuni mayatima mpaka wafikilie umri wa kuoa. Mkiwaona wana uwekevu, basi wapeni mali zao. Wala msizile kwa kuzifuja na kwa haraka kwa kuwa watakuwa wakubwa. Na aliye tajiri, basi na ajizuie; na atakayekuwa fukara, basi na ale kwa kiasi cha kawaida. Na mtakapowapa mali zao, basi washuhudizieni; na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mhasibu.

MSIWAPE WAPUMBAVU MALI ZENU Aya 5-6

LUGHA

Makusudio ya wapumbavu hapa ni wale wabadhirifu wanaotumia ovyo mali.

MAANA.

Wala msiwape wapumbavu mali zenu .

Imesemekana kwamba msemo unaelekezwa kwa kila mwenye mali na kwamba anaamrishwa kutompa ambaye ataitumia pasipo mahali pake; ni sawa mbadhiri-fu awe ni mtoto au mke wa mwenye mali. Vilevile wasii wake au mtu wa kando.

Pia imesemekana kuwa msemo unaelekezwa kwa mababa tu, kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewakataza kuwakabidhi watoto wao waasi mali waliyofadhiliwa na Mwenyezi Mungu na wanapozeeka wanaijutia.

Kaashif4-111.jpg

127

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Ilivyo hasa ni kwamba msemo unaelekezwa kwa wasimamizi, kwa maana ya kuwa enyi wasimamizi msiwape wabadhirifu mnaowasimamia mali zao. Hilo linafa-hamika kutokana na Mwenyezi Mungu anavyoendelea kusema, 'Na muwakimu na muwavishe katika mali hiyo.' Kwa sababu huu ni msemo unaelekezwa kwa wasimamizi. Zaidi ya hayo Aya zilizotangulia zinawahusu wasimamizi kwa hiyo inakuwa vizuri kufungamana na hizo.

Mbadhirifu, ni yule anayetumia ovyo mali yake; huyu hawezi kutumia mali yake isipokuwa kwa idhini ya msimamizi (walii) wake. Lakini anaweza kutumia vitu visivyoambatana na mali. Tumezungumzia kwa urefu kuhusu hukumu za mbadhirifu katika kitab Fiqhul-Imam Jafer As-sadiq, mlango wa Hajr.

Unaweza kuuliza: Kama msemo ungekuwa unawahusu wasimamizi wa mali za wabadhirifu, ingelazimika kusema, 'mali zao' na wala sio 'mali zenu', Sasa imekua-je?

Jibu; Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ametegemeza mali za wabadhirifu kwa wasimamizi wao kwa kuangalia kuwa ziko chini ya usimamizi wao. Na inajulikana kwamba kutegemezea kitu kunafaa hata kwa sababu ndogo tu.

KUMWAMINI MWENYEZI MUNGU NA TATIZO LA MAISHA

 Mali zenu ambazo amewajaalia kuwaendeshea maisha.

Razi anasema: "Maana yake ni kuwa maisha hayapatikani ila kwa mali. Ilipokuwa mali ndiyo sababu ya kuendesha maisha, ndipo Mwenyezi Mungu akaiita kuwa ni ya kuendeshea maisha kwa kutumia jina la chenye kusababishwa kwa sababu. Sababu anayomaanisha ni mali, na chenye kusababishiwa ni maisha."

Mwenye kufuatilia Aya za Qur'an na Hadith za Mtume, ataona kuwa uislam umeipa kipaumbele mali katika maisha, mpaka kufikia hatua ya kulinganisha sawa na nafsi katika Aya kadhaa; kama vile Aya hii: "Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kuto-ka kwa waumin nafsi zao na mali zao ili wapate pepo. (9:111)

Hapo Mwenyezi Mungu ameuza pepo yake kwa mali itolewayo kwa ajili yake; sawa na mfanyi biashara anavyouza bidhaa yake kwa ajili ya mali inayotolewa kwa ajili ya maslahi yake.

Aya nyingine ni ile isemayo; "Amewafadhilisha Mwenyezi Mungu wanaopigana jihadi kwa mali zao na nafsi zao." (4:95)

Kwa sababu hiyo ndipo mafakih wakasema: "Asili katika kila kitu ni halali mpaka uthibitike uharamu isipokuwa damu tupu na mali, hizo asili yake ni haramu (mpaka uthibitike uhalali)."

Qur'an imetumia neno 'kheri' kwa maana ya mali katika Aya nyingi mfano: "Na hakika yeye kwa sababu ya kupenda mali ni bakhili." (100:8) Hapo mali imetafsiri-

128

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

wa kutoka neon kheri.

Hata baadhi ya wafasiri wamesema kuwa neno kheri limetumika kwa maana ya mali tu katika Qur'an, lakini sisi hatuafikiani na rai hii, ingawaje twajua kuwa Aya nyingi zimeamrisha amali njema, kusaidiana kwa kheri na kujiandaa kwa kujikinga na maadui wa dini na wa nchi , na kwamba haiwezekani kutekelezeka yote isipokuwa kwa mali.

Mwenyezi Mungu amekataza kurundika mali na amewakemea wanaozirundika kwa adhabu kali; kama ambavyo amekataza kufanya israfu na ubadhirifu, na kuwachukulia wabadhirifu kuwa ni ndugu za mashetani, kwa sababu ubakhili na ubadhirifu unakwamisha maendeleo na uzaliishaji unaowafaa watu. Mtume (s.a.w.) amesema: "Mwenyezi Mungu akiitakia nyumba kheri, basi huwaruzuku watu wake wepesi katika maisha na tabia nzuri."

Na Imam Ali (a.s.) amesema: "Mtu hawezi kuonja hakika ya imani, mpaka awe na mambo matatu; Fiqh katika dini, subira katika masaibu na ukadiriaji mzuri katika maisha." Imam ameunganisha imani na utatuzi wa maisha katika dunia hii, kwa sababu ukadiriaji mzuri wa maisha, maana yake ni kufanya kazi vizuri na kutumia mazao ya kazi katika njia yake inayonufaisha.

Hii ni dalili wazi kuwa dini haitengani na maisha; na kwamba imewekwa kwa ajili ya maisha bila ya shaka. Yeyote atakayetenganisha dini na maisha na kuona kuwa ni kiasi cha kuwa ni nembo, ibada na kujinyima starehe tu, basi ama atakuwa ni mjinga aliyechukua dini kutoka kwa wanaoifanyia istihzai, au atakuwa ni mpin-zani wa haki.

Tulipofasiri Aya ya 182 ya sura iliyotangulia (Al-Imran) katika kifungu cha 'matajiri ni mawakala' tulitaja kuwa mali yote ni ya Mwenyezi Mungu na kwamba mtu anaruhusiwa kuitumia mali kwa mipaka maalum, ambayo kama ataikiuka, basi atakuwa amenyang'anya. Hebu rudia kidogo sehemu hiyo, kwani inaambatana na maudhui haya.

Tunaweza kuyarudia kama ikija Aya itakayofungamana nayo na tutafafanua tuliy-oyataja huko na hapa. Kwa sababu fikra haiwezi kukienea kitu kwa pande zake zote isipokuwa inaelekea yote kwenye upande ule unaogusiwa na Aya, mapokezi au tukio lolote.

Na muwakimu katika mali hiyo na muwavishe.

Msemo unaelekezwa kwa wasimamizi wa wabadhirifu. Makusudio ni kuwa wasi-mamizi wawatimizie mahitaji yao ya chakula, nguo, makazi masomo, kuoa n.k.

Unaweza kuuliza: Kwa nini amesema 'katika mali hiyo' na wala hakusema kutoka katika mali hiyo?

129

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Jibu: Lau angesema kutoka katika mali hiyo, basi ingelikuwa maana yake ni kuwa atumie asili ya hiyo mali (mtaji). Kwa hiyo ingelipungua au ingelikwisha yote. Ama kusema: 'Katika mali hiyo' ni kuwa mali iwe ni mtaji wa kutafutia riziki, kwamba msimamzi aizalishe mali hiyo na matumizi ya mbadhirifu yatokane na faida sio mtaji wenyewe.

Swali la pili: Kwa nini amehusisha kivazi; na inajulikana kuwa kivazi ni katika jumla ya kukimu?

Jibu: Amehusisha kivazi kwa kukipa umuhimu. Kwani huenda msimamizi akakipa umuhimu chakula na kughafilika na mavazi. Ndipo Mwenyezi Mungu akaikinga dhana hii kwa kutaja kivazi waziwazi.

Msimamizi wa mbadhirifu ambaye ubadhirifu wake umeanzia utotoni mpaka akakua nao, ni baba, na babu. Ama ikiwa ubadhirifu aliuanzia ukubwani (baada ya kubaleghe), basi msimamizi atakuwa ni kadhi.

Na muwaambie maneno mazuri

Baadhi ya wasimamizi huenda wakaona kuwa ni lazima wale wanaowasimamia wawasikilize na kuwatii, kama mzazi na mtoto wake. Ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akazindusha kwa kauli yake hii, ili kila msimamizi amchukulie upole anayemsimamia na kumfanyia mambo yamridhishayo na yanayomtuliza roho yake.

Na wajaribuni mayatima mpaka wafikilie umri wa kuoa. Mkiwaona wana uwekevu, basi wapeni mali zao.

Aya hii inafahamisha kuwa mtoto hapewi mali mpaka awe na sifa mbili: Kubaleghe na kuwa mwekevu. Yamekongamana madhehebu yote ya Kiislam kuwa kutoa manii kunafahamisha kubaleghe; kwa mwanamume na mwanamke, katika umri wowote na hali yoyote; iwe ni usingizini au akiwa macho. Wametoa dalili kwa Aya hii na Aya nyingine isemayo:

"Na watoto miongoni mwenu watakapobaleghe, basi na wapige hodi." (24:59), ambapo limetumika neno 'hulum' lenye maana ya kukomaa mwili kijinsia.

Na imethibiti Hadith kutoka kwa Mtume (s.a.w.) kuwa yeye amesema; "Imeondolewa kalamu (ya kuandika amali) kwa watu watatu: Mtoto mdogo mpaka atoke manii, mwenda wazimu mpaka apone na aliyelala mpaka aamke."

Ama uwekevu unathibiti kwa kupewa yatima mali yake kidogo aitumie. Ikiwa atai-tumia vizuri, basi atakuwa ni mwekevu na atapewa mali yake, vyenginevyo atazuiliwa, hata kama atafikisha miaka mia. Abu Hanifa anasema: "Mbadhirifu atapewa mali yake akiwa na miaka 25 (hata kama si mwekevu), "Hashia ibni Abidin J. 5 mlango wa Hajr.

130

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Wala msizile kwa kuzifuja.

Yaani enyi wasimamizi! Msipetuke mipaka mnayoruhusiwa katika kula mali mna-zozisimamia. Kwa sababu msimamizi anaweza kula mali ya anayemsimamia kwa sharti ya kuwa awe fukara; kama itakavyoelezwa.

Na kwa haraka kwa kuwa watakuwa wakubwa.

Msimamizi anaweza kufanya haraka kuitumia mali ya yatima kwa kuhofia asiwe mkubwa akachukua mali yake. Ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akakataza matu-mizi hayo ambayo faida yake inamwendea msimamizi, na akazindua kuhusu hatari ya uharamu wake.

Na aliyetajiri, basi na ajizuie; na atakayekuwa fukara, basi ale kwa kiasi cha kawaida.

Msimamizi ama atakuwa mwenye kujitosheleza au fukara. Kwa hiyo mwenye kuji-tosheleza ni lazima ajiepushe kula mali ya yatima na kukinai na riziki ya kutosha aliyopewa na Mwenyezi Mungu. Lakini kama ni fukara, basi inafaa kwake kutumia kiasi cha haja yake ya dharura bila ya kuzidisha.

Kuna Hadith isemayo kuwa Mtume (s.a.w.) aliulizwa na bwana mmoja kuhusu yatima akiwa hawezi kutumia mali yake kuwa atakula mali yake? Akamwambia: "Kula kwa njia ya kawaida," Na imesemekana atakula kwa njia ya mkopo. Lakini dhahiri ya Hadith inaibatilisha kauli hii.

Na mtakapowapa mali zao basi washuhudizeni: na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mhasibu.

Shia na Hanafi wanasema kuwa si wajibu kwa msimamizi kushuhudiza utoaji wa mali ya anayemsimamia akiwa mwekevu au baleghe. Na amri ya kushuhudiza katika Aya hii, wameichukulia kuwa ni sunna kwa ajili ya kuondosha tuhuma na kujiepusha na uhasama.

Shafii na Malik wamesema kuwa ni wajibu na wala sio sunna kwa kuchukulia dhahiri ya Aya hii.

131

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

4. Sura An-Nisaa

7.Wanaume wana fungu katika wali-choacha wazazi wawili na akraba, na wanawake (pia) wana fungu katika walichoacha wazazi wawili na akraba, kikiwa kidogo au kingi -fungu lililofaradhiwa.

8.Na wakati wa kugawanya watakapo-hudhuria wenye ukuruba na maya-tima na maskini, basi wapeni nao kitu katika hiyo na waambieni maneno mazuri.

9.Na wachelee wale ambao lau nao kama wangeacha nyuma yao wato-to wanyonge, wangehofia. Basi na wamche Mwenyezi Mungu na waseme kauli iliyo sawa.

10.Hakika wale ambao wanakula mali ya yatima kwa dhulma, haki-ka wanakula moto matumboni mwao; na wataungua katika moto uwakao.

Kaashif4-112.jpg

132

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

WANAUME WANA FUNGU Aya 7 - 10

MAANA

Aya nne hizi, kila moja ina mtazamo wake kama ifuatavyo:

1. Wanaume wana fungu katika walichoacha wazazi wawili na akraba, na wanawake (pia) wana fungu katika walichoacha wazazi wawili na akraba, kikiwa kidogo au kingi - fungu lililofaradhiwa.

Wazazi wawili wanafahamika; na akraba ni ndugu wa karibu wa kwa baba au mama; wakiwemo watoto, wajukuu na kuendelea chini, mababa, mababu na kuen-delea juu, kaka, dada na watoto wao, ami na shangazi na wajomba, mama wado-go na watoto wao. Wake kwa waume, wakubwa kwa wadogo; iwe ni shilingi moja au mamilioni.

Kurithi wote hao ni lazima katika sharia ya kiislam, haijuzu kuikhalifu kwa namna yoyote ile kwa dalili ya kauli ya Mwenyezi Mungu: "Fungu lililofaradhiwa." Hiyo inabatilisha yale yaliyokuwako wakati wa ujahilia, ya kuwazuwiya wanawake na wavulana wadogo wasirithi si kwa chochote isipokuwa tu, hawapandi farasi wala hawamzuwii adui. Ndipo uislam ukathibitisha haki ya mtu kurithi kwa kuan-galia umbile lake la kiutu na wala sio kwa misingi ya kuwa aweza kupigana kwa upanga na kufuma mshale.

Shia wametolea dalili Aya hii katika kubatilisha Asaba waliyoithibitisha Sunni -tutafafanua punde - ambayo ni kuwarithisha wanaume na kuacha wanawake kwa sababu fulani; kama vile ikiwa marehemu ameacha binti na mtoto wa kiume wa kaka na binti wa kaka. Hapo Sunni wanampa nusu bint, na nusu nyingine wanam-pa mtoto wa kiume wa kaka, lakini yule dadake hana chake ingawaje daraja ni sawa na huyu wa kiume. Au ikiwa maiti amemwacha dada, ami na shangazi . Qur'an inawarithisha wake kwa waume, na wao wanawarithisha wanaume tu.

Ama Mashia wao wanampa binti mali yote katika sura ya kwanza na ya pili. Kwa sababu yeye ndiye aliye karibu zaidi na marehemu kuliko kaka wa marehemu au mtoto wa kaka wa marehemu na zaidi kuliko ami yake.

2.  Na wakati wa kugawanya watakapohudhuria wenye ukuruba na mayatima na maskini, basi wapeni nao kitu katika hiyo na waambieni maneno mazuri.

Makusudio ya wenye ukuruba ni jamaa wa karibu wa marehemu ambao wamezui-lika kupata mirathi kutokana na kuweko walio karibu zaidi kama ndugu na mtoto au ami na ndugu n.k. Msemo katika 'wapeni' unaelekezwa kwa waritihi au man-aibu wao. Ni wazi kwamba waritihi huwapa sadaka hao wakiwa mafukara. Ama mayatima na masikini waliokusudiwa hapa, ni wale ambao hawana undugu na

133 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

aliyekufa. Na amri ya kutoa hapa ni ya sunna na wala sio ya wajibu. Kama vile kusema: "Toeni sadaka japokuwa ubale wa tende." Hapa kutoa sadaka sio wajibu, lakini ni sunna inayotiliwa mkazo.

3. Na wachelee (waogope) wale ambao lau nao kama wangeacha nyuma yao watoto wanyonge wangewahofia. Basi na wamche Mwenyenzi Mungu na waseme kauli iliyo sawa.

Neno 'Na wachelee', ni amri inayoelekezwa kwa wasimamizi wa mayatima maana yake ni kwamba, ni juu ya msimamizi kuifanyia mali ya yatima, kama vile ambavyo angependa yeye wafanyiwe watoto wake lau kama angekuwa amekufa, "Mtenda hutendewa"

Imepokewa kutoka kwa Imam Musa bin Jafer (a.s.) Kwamba "Mwenyezi Mungu amemwandalia anayetumia vibaya mali ya yatima, mateso mara mbili. Kwanza hapa duniani, kuwa mali ya watoto wake nayo itatumiwa vibaya, Pili ni akhera, ambayo ni moto,"

Imam Ali (a.s.) anasema: "Yafanyieni vizuri yaliyo baada ya wenzenu, watu watayafanyia vizuri yatakayokuwa baada yenu."

4.Hakika wale ambao wanakula mali ya mayatima kwa dhuluma hakika wanakula moto matumboni mwao; na wataungua katika moto uwakao.

Makusudio ya kula moto ni kula yale yawajibishayo adhabu ya moto. Hiyo ni katika kutumia kinachosababishwa ambacho ni moto kwa maana ya sababu ambayo ni kula haramu. Imeelezwa katika Hadith kwamba mwenye adhabu kubwa zaidi kati ya watu ni kiongozi dhalimu; mwenye kula mali ya yatima na mwenye kushuhudia uongo.

134

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

4. Sura An-Nisaa

11.Mwenyezi Mungu anawausia kwa watoto wenu; fungu la mwana-mume ni kama fungu la wanawake wawili. Wakiwa ni wanawake zaidi ya wawili, basi watapata theluthi mbili za ali-chokiacha (marehemu) na akiwa ni mmoja, basi atapata nusu. Na wazazi wake wawili kila mmoja atapata sudusi ya alichokiacha akiwa ana mtoto. Akiwa hana mtoto, na akarithiwa na wazazi wake wawili, basi mama yake atapata theluthi. Akiwa anao ndugu, basi mama yake atapata sudusi. Baada ya kutoa alivyousia au kuli-pa deni. Baba zenu na watoto wenu hamjui ni yupi katika wao aliye karibu zaidi kwa manufaa. Ni faradhi itokayo kwa Mwenyezi Mungu; hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi, mwenye hekima.

Kaashif4-113.jpg

135

4. Sura An-Nisaa

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nns 12.Nanyi mtapata nusu ya walichoki-

acha wake zenu ikiwa hawana

watoto. Ikiwa wana watoto; basi

mtapata robo ya walichokiacha

baada ya kutoa walivyousia au

kulipa deni. Na wao watapata

robo ya mlichokiacha ikiwa

hamna mtoto. Ikiwa mna mtoto,

basi watapata thumni ya mlichokiacha, baada ya kutoa mlivyousia

au kulipa deni. Ikiwa mwana-

mume au mwanamke anayerithi-

wa ni mkiwa naye ana ndugu wa

kike au wa kiume, basi kila mmoja

katika wao atapata sudusi.

Wakiwa wengi zaidi ya hivyo, basi

watashirikiana katika theluthi,

baada ya kutoa yaliyousiwa au

kulipa deni, pasi na kuleta dhara.

Ni wasia utokao kwa Mwenyezi

Mungu na Mwenyezi Mungu ni

Mjuzi, Mpole.

Aya 11 - 12 FUNGU LA MWANAMUME NI SAWA NA MARA MBILI YA MWANAMKE.

MAANA

Wakati wa ujahiliya, sababu za kurithi zilikuwa ni tatu;

Kwanza: Nasaba, lakini kwa wanaume tu, wanaoweza kushika silaha na kupi-gana. Ama wanawake na wanaume dhaifu hawakuwa na urithi. Lakini uislam ukaeneza urithi kwa wote.

Kaashif4-114.jpg

136

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Pili: Mtoto wa kupanga; yaani mtu kumfanya mtoto wa mwengine kuwa mwanawe hasa katika urithi na mengineyo. Uislam umelikataa hilo kwa kauli yake Mwenyezi Mungu:

"Wala hakuwafanya watoto wenu wa kupanga kuwa wana wenu hasa ." (33:4)

Tatu: Kuliana yaamini; yaani mtu kumwambia mwenzake: "Damu yangu ni yako, utanirithi na nitakurithi."

Huu ulikubaliwa na uislam kwa ufafanuzi huu ufuatao: Mwanzo ilikuwa aliyehama (Muhajiri) pamoja na Mtume (s.a.w.) kutoka Makka kwenda Madina akimrithi mwenzake aliyehama (Muhajir) ikiwa wana urafiki wa pamoja; na ilikuwa Muhajir anarithiwa na Muhajir tu, na si mwengine hata kama yuko karibu. Vile vile baada ya Mtume kuwafungisha undugu Sahaba zake walikuwa kama ndugu wawili wanaorithiana. Lakini baadaye uislam uliyafuta haya mawili (kuhama na kufungishwa undugu) Kwa Aya isemayo;

". Na ndugu wa tumbo wana haki zaidi wao kwa wao katika kitabu cha Mwenyezi Mungu." (8:75) Vile vile katika (33:6)

Kwa hiyo wajibu wa kurithi katika uislam, umethibiti juu ya mambo mawili: Nasaba na sababu . Na sababu ni mambo mawili Ndoa na usimamizi

Utakuja ubainifu kulingana na mpango wa Aya.

Ufuatao ni ufafanuzi wa matamko ya Aya mbili tulizonazo ambazo hizo pamoja na zinazofuatia zinazofungamana na urithi ni ufafanuzi wa aliyoyajumlisha Mwenyezi Mungu Mtukufu katika kauli yake iliiyotangulia: "Wanaume wana fungu."

1.Mwenyezi Mungu anawausia kwa watoto wenu; fungu la mwanamume ni kama fungu la wanawake wawili.

Akiwa marehemu ameacha watoto wa kiume na wa kike, wa kiume watapata sawa na sehemu ya wanawake wawili. Ikiwa wako wengine katika mirathi; kama vile mume au mke, baba au mama, au baba na mama. Kila mmoja atachukua fungu lake - kama tutakavyofafanua - na sehemu itakayobaki watapewa watoto wa kike na wa kiume; ambapo wa kike watachukua nusu ya watakayopata wa kiume. Hiyo ni kwa kuafikiana madhehebu zote za kiislam.

Vilevile yameafikiana madhehebu yote kwamba, marehemu akiacha mtoto wa kiume na wajukuu, basi mtoto wa kiume atawazuia wajukuu kurithi; ni sawa wajukuu wawe wa kike au wa kiume.

Yametofautia madhehebu ikiwa ataacha mtoto wa kike mmoja, wawili au zaidi bila ya kuacha mtoto wa kiume. Madhehebu mane yamesema kuwa mtoto wa kike mmoja atachukua nusu tu; wawili au zaidi watachukua theluthi mbili tu; kitaka-chobaki watapewa wengine.

137

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Shia Imamia wamesema kuwa mali yote ni ya mtoto wa kike akiwa mmoja au zaidi, wengineo hawana chao. Kwa Ufafanuzi zaidi rejea kitabu chetu Ahwalush-shakhsiya Alal-madhahibil Khamsa.

2.Na wakiwa ni wanawake zaidi ya wawili, basi watapata theluthi mbili za ali-chokiacha (marehemu). Na akiwa ni mmoja, basi atapata nusu.

Mwenye Majmaul-bayan amesema:

"Dhahiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kwamba watoto wa kike wawili hawastahiki theluthi mbili, isipokuwa zaidi ya wawili lakini Umma umesema kwa pamoja kuwa hukumu ya wawili ni sawa na ya zaidi ya wawili."

Na hivi ndivyo sahihi hasa, na kila sababu au taawili zozote zinazoelezwa kuhusu zaidi ya wawili ni za kukisia tu.

Hata hivyo hilo si muhimu, la muhimu zaidi ni kubainisha tofauti za madhehebu ya kiislam kuhusu mirathi ya watoto wa kike ikiwa marehemu hakuacha wa kiume. Kwa kauli moja mafakihi wameafikiana kuwa marehemu akiwa ameacha mtoto wa kike mmoja, atapata nusu kuwa ni fungu lake. Wakiwa ni wawili na zaidi wat-achukua theluthi mbili. Lakini wamehitalifiana kuhusu nusu itakayobaki baada ya kupewa binti mmoja na theluthi itakayobaki baada ya kupewa mabinti wawili, ipewe nani?

Sunni wamesema, itapewa kaka wa marehemu kwa kutegemea riwaya ya Taus kutoka kwa Ibn Abbas naye kutoka kwa Mtume (s.a.w.) kwamba yeye amesema: "Yaambatanisheni mafungu na watu wake na kinachobakia ni cha asaba waume." Shia wameikanusha Hadith ya Taus; kwa sababu yeye ni mwongo mno 11 . Na wamesema kuwa nusu ya pili itarudishwa kwa binti kwa hiyo atachukua mali yote. Kwa maana ya kuwa atachukua nusu kama fungu lake na nusu ya pili kwa kurud-ishiwa. Vile vile wakiwa wawili na zaidi watachukua theluthi iliyobaki.

Dalili yao Shia ni kuwa Qur'an imefaradhisha theluthi mbili kwa wawili, na zaidi ya nusu kwa bint mmoja. Kwa hiyo hapana budi kuweko na mtu atakayechukua sehemu iliyobaki; na Qur'an haikumweleza mtu huyo. Ndio maana kukazuka kut-ofautiana. Kwa hivyo basi ikawa hakuna kilichosalia isipokuwa Aya hii: Na ndugu wa tumbo wanahaki zaidi wao kwa wao. (8:75) na (33:6) Ambapo inafahamisha kuwa aliye karibu zaidi ndiye anayestahiki kuliko mwengine. Hakuna mwenye shaka kwamba binti yuko karibu zaidi ya kaka.

11.Sayyid Mohsin Amin anasema katika kitabu Naqdhul washia mlango wa 'Taasib': "Hata Taus mwenyewe amekanusha kuwa amepokea Hadith hii na akasema - huyo Taus - kwamba shetani ndiye aliyeiweka kauli hii kwenye ulimi wa aliyeninasibishia mimi." Sayyid amelipokea hilo kwa wapokezi wa kisunni.

138

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Zaidi ya hayo sio Shia peke yao waliosema kuwa mali yote ni ya binti mmoja au zaidi, bali Hanafi na Hambal pia wamesema kuwa marehemu akiacha binti mmoja au zaidi na asipatikane yeyote mwenye fungu au asaba basi mali yote ni ya binti, inagawaje Aya inasema:". basi watapata theluthi mbili za (mali) aliyoiacha, laki-ni akiwa ni mmoja basi atapata nusu."

Ikiwa Aya hii haimzuwii mtoto wa kike kuchukua mali yote katika namna waliy-oielezea Hanafi na Hambal, basi vile vile haiwezi kumzuia kwa namna nyingine. Kwa sababu dalili ya Aya ni moja haiwezi kugawanyika kwa namna yoyote ile.

Vile vile Hanafi na Hambal wamesema: Ikiwa marehemu ataacha mama bila ya mwengine yeyote mwenye fungu na asaba, basi mama atachukua mali yote. Thelutuhi ikiwa ni fungu lake na theluthi mbili kurudishiwa yeye, ingawaje Aya inasema: ". basi mama yake atachukua theluthi ." Ikiwa inawezekana kwa mama kuchukua mali yote ingawaje fungu lake ni theluthi, basi hata mtoto wa kike pia atachukua yote inagawaje fungu lake ni nusu au theluthi mbili.

Haya tumeyaeleza kwa ufafanuzi zaidi katika kitabu Ahwalush-shakhsiyya Ala madhahibil-khamsa, Na pia katika Juzuu ya sita ya Fiqh Imam Jafar As-Sadiq (as). Na Baraza kuu la waislam la Misr limetoa kitabu kikubwa kiitwacho Daw'atu-taqrib ambacho ndani yake mna utafiti kamili wa suala hili. Yale tuliyoyanakili ya Hanafi na Hambali yametoka katika kitabu Mughni cha Ibn Quddam na Mizani Shi'rani katika mlango wa Faraidh.

3. Na wazazi wake wawili kila mmoja wao atapata sudusi ya alichokiacha akiwa anaye mtoto.

Neno Walad (mtoto) linatumika kwa mtoto wa kike na kiume. Kwa sababu neno hilo linaotakana na Wilada (kuzaa), ambako kunaweza kuwa kwa wa kike na wa kiume. Na Qur'an imelitumia neno hilo kwa maana hayo pale iliposema: "Mwenyezi Mungu anausia kwa watoto wenu; mwanamume ni kama fungu la wanawake wawili." Au pale iliposema: "Haiwi kwa Mwenyezi Mungu kuwa na mtoto ."(19:35)

Makusudio ya wazazi wawili hapa ni baba na mama tu, haingii babu na bibi (nyanya). Ikiwa marehemu ameacha wazazi wawili na watoto, itaangaliwa: Ikiwa katika watoto yuko wa kiume wazazi watachukua sudusi 12 kila mmoja, kina-chobaki ni cha watoto hata ikiwa mtoto wa kiume ni mmoja tu. Ikiwa hakuna wa kiume, na wa kike wakawa zaidi ya mmoja, basi wazazi watachukua theluthi, na theluthi mbili zitakuwa ni za watoto wa kike. Hilo wameafikiana waislam wote.

12 Sehemu ya sita (1\6)

139

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Ikiwa mtoto wa kike ni mmoja tu pamoja na wazazi wawili, basi wazazi wawili kila mmoja atachukua sudusi na mtoto fungu lake ni nusu. Hapo itabaki sudusi ambayo Sunni wanasema itarudishwa kwa baba tu. Ama Shia wanasema itarud-ishwa kwa baba, mama na mtoto ikiwa mama hana kizuizi (kwa kuwepo ndugu wa marehemu); waitagawa mali mafungu matano moja la baba, moja la mama na matatu ya binti. Ikiwa mama atazuilika kwa kuwepo ndugu, basi ziada itarudishwa kwa baba na binti kwa mafungu manne, yaani ziada itagawanywa mafungu manne moja la baba na matatu ya binti.

4.Akiwa hana mtoto na akarithiwa na wazazi wake wawili; basi mama yake atapata theluthi. Akiwa anao ndugu, basi mama yake atapata sudusi.

Ikiwa marehemu hana mtoto wala mjukuu ikawa mirathi yake inakwenda kwa babake na mamake tu, basi mama atachukua theluthi ikiwa marehemu hana ndugu watakaomzuia mama kilichozidi sudusi. Ikiwa wapo hao ndugu, basi mama atachukua sudusi tu, kinachobaki katika hali zote mbili ni cha baba.

Madhehebu yametofautiana kuhusu idadi ya ndugu ambao watamzuia mama. Maliki wamesema, uchache wake ni kaka wawili na si kina dada. Hanafi Shafii na Hambali wamesema ni kaka wawili au dada wawili. Shia wanasema ni kaka wawili au mmoja na dada wawili; au dada wanne kwa sharti ya kuwa wawe ni ndugu wa marehemu baba mmoja mama mmoja au baba mmoja, na wawe wamekwisha zaliwa wakati wa kufa mrithiwa, sio kwenye mimba na pia baba awe hai. Hawa ndio ndugu wanaomzuwiya mama kurithi theluthi, lakini wao wenyewe hawarithi kitu wakati huo.

5. Baada ya kutoa alivyousia au kulipa deni.

Marehemu akiacha mali, kwanza itatumiwa katika mazishi yake (sanda na mahali pa kuzikwa). Kisha yatalipwa madeni yake ikiwemo Hijja, Zaka, Khums na nadhiri, kisha utatekelezwa wasia wake usiozidi theluthi ya mali. Baada ya hapo ndipo utaangaliwa urathi ambao ni kama kutoa kilichozidi haja.

Unaweza kuuliza: Ikiwa deni limetangulia wasia, mbona halikutangulia kutajwa katika Aya hii?

Jibu: Kutangalia huko kutajwa hakumaanishi kutangulia katika hukumu na utekelezaji. Kwa sababu kuunganisha kwa 'au' hakumaanishi kufuata mpango -kama ilivyo kinahau - isipokuwa kunamaanisha usawa katika hukmu. Ni kama vile kusema lianze lipi baada ya mazishi? Jibu litatokana na kupatikana dalili nyingine. Imethibiti kutoka kwa Mtume (s.a.w.) na Ijmai kwamba hakuna wasia wala mirathi isipokuwa baada ya kulipwa deni; na pia kuna Hadith nyingi zinazofahamisha kuwa marehemu ni rehani wa madeni yake.

6.Baba zenu na wa watoto wenu, hamjui ni yupi katika wao aliye karibu zaidi kwa manufaa. Ni faradhi itokayo kwa Mwenyezi Mungu; hakika Mwenyezi

140

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Mungu ni mjuzi mwenye hekima.

Hii ni jumla iliyoingia kati inayoonyesha kuwa siri ya makadirio ya mirathi haiwezi kufahamika kiakili isipokuwa anayeijua ni yule aliyemuumba mwanadamu; Yeye peke yake ndiye ajuaye linalomdhuru mtu na kumnufaisha.

Aya hii inafaa kuwa ni dalili kwamba hukumu za Mwenyezi Mungu zimewekwa kwa masilahi ya mtu na utengeneo wake. Kwa hivyo basi tunapata dalili ya imani ya mtu kwa matendo yake mema na tunapata dalili ya uovu wake kwa matendo yake maovu.

Ni faradhi itokayo kwa Mwenyezi Mungu sio kutoka kwa mtu ambaye anatawaliwa na matamanio. Tumeona tume nyingi za kutunga sheria na mabunge yakiweka sheria na kanuni kwa ajili ya masilahi ya wenye nguvu na kuwaonea wanyonge.

7.  Nanyi mtapata nusu ya walichokiacha wake zenu, ikiwa hawana watoto. Ikiwa wana watoto basi mtapata robo ya walichokiacha baada ya kutoa walivyousia au kulipa deni.

Waislam wote wameafikiana kuwa mke na mume wanashiriki katika mirathi na warithi wote. Mume atapata nusu ikiwa mke hana mtoto aliyezaa naye au aliyezaa na mume mwengine. Na mke atapata robo ikiwa ana mtoto aliyezaa naye au aliyezaa na mke mwengine.

8.  Na wao watapata robo ya mlichokiacha ikiwa hamna mtoto. Ikiwa mna mtoto, basi watapata thumni*13 ya mlichokiacha baada ya kutoa mliyou-sia au kulipa deni.

Mke atapata robo ya mali ya mumewe ikiwa hana mtoto aliyezaa naye au aliyezaa na mke mwengine, na atapata thumuni ikiwa ana mtoto aliyezaa naye au aliyezaa na mwengine.

Madhehebu mane yameafikiana kuwa makusudio ya mtoto (Walad) hapa ni mtoto wa marehemu na mjukuu aliyezaliwa na mtoto wa kiume tu, awe mume au mke. Ama mjukuu aliyezaliwa na mtoto wa kike hawezi kumzuia mke au mume kupata fungu lake kubwa. Bali Shafi na Maliki wamesema kuwa mjukuu wa mtoto wa kike harithi wala hamzuwii mwengine, kwa sababu yeye ni upande wa kukeni (fungu la rihami).

Shia Imamia wamesema kuwa makusudio ya mtoto ni mtoto yeyote na mjukuu yeyote wa mtoto wa kike au wa mtoto wa kiume. Kwa hiyo mjukuu wa kike wa mtoto wa kike atawazuilia mke na mume kupata fungu kubwa na pia atarithi.

13.Sehemu ya nane (1\8)

141

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Wake wakiwa wengi watashirikiana katika robo au thumni kwa kugawana sawa sawa.

Madhehebu mane yamesema: "Ikiwa marehemu hana mrithi zaidi ya mumewe au mkewe, basi kinachobaki hakirudishwi kwa mume huyo wala mke - Taz. Kitabu Mughni cha Ibn Quddama, Shia Imamia wametofautiana katika hilo kwa kauli tatu: Kwanza: Kurudishwa kinachobaki kwa mume tu, sio kwa mke. Kauli hii ndiyo maarufu kwa mafaqihi wa siku hizi na ndivyo wanavyofanya.

Pili: Kurudishiwa mke au mume katika hali zote.

Tatu: Kurudishiwa mke au mume wakati wa kughibu Imam mwadilifu. Na sisi tuko kwenye rai hii ambayo pia ni rai ya Sheikh Saduq, Najibuddin bin Said, Allama Hilly na Shahidi wa kwanza. Tumetaja dalili za kuchagua rai hii katika kitab Fiqhul-Imam Jafar As-Sadiq (A.S.) .

9.  Ikiwa mwanamume au mwanamke anayerithiwa ni mkiwa naye ana ndugu wa kiume au wa kike, basi kila mmoja katika wao atapata sudusi. Wakiwa wengi zaidi ya hivyo, basi watashirikiana katika theluthi.

Neno Kalala (ukiwa, kutokuwa na baba wala mtoto) limekuja mara mbili katika Qur'an, moja ikiwa hapa na jengine mwisho wa Sura hii. Makusudio yake hapa ni ndugu wasiokuwa baba na mama au mtoto. Neno hilo anaitwa nalo marehemu anayerithiwa na ndugu wa kiume au wa kike walio hai kama ambavyo anaitwa nalo mrithi ndugu wa kiume au wa kike aliye hai. Maana zote mbili - kama uzionavyo -zinafuatana. Kwa hiyo yoyote utakayoichukua ni sawa.

Wafasiri wameafikiana kuwa makusudio ya ndugu wa kiume au wa kike katika Aya hii ni ndugu wa upande wa kwa mama tu; bali hata wengine wamesoma Qiraa cha minalummi (wa upande wa mama).

Ama mirathi ya ndugu wa kiume au wa kike kwa baba na mama au kwa baba tu, hukumu yake itakuja katika Aya iliyoko mwisho wa sura hii.

Madhehebu yameafikiana kwamba mmoja katika ndugu (mtoto wa mama) atapata sudusi awe mwanamume au mwanamke. Wakiwa ni zaidi,wawe wa kike au wa kiume au mchanganyiko watapata theluthi kwa kugawana sawa sawa, mwanamke sawa na mwanamume.

10.  Baada ya (kutoa) yaliyousiwa au kulipa deni pasi na kuleta dhara.

Yametangulia maelezo kuwa hakuna mirathi ila baada ya kulipwa deni na kutekelezwa wasia. Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekataza kuleta dhara katika deni na wasia. Dhara katika deni ni kukiri au kuusia deni lisilokuwepo kwa kukusu-dia kuwadhuru warithi. Na dhara katika wasia ni kuzidisha kiwango cha theluthi ya mali yake. Kama akifanya hivyo utekelezaji wake utategemea ruhusa ya warithi. Hadith inasema: "Kuwaacha warithi wako wakiwa wanaojitosheleza ni bora kuliko

142 <

4. Sura An-Nisaa

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

kuwaacha hali ya kuwa ni mafukara omba omba."

Ni wasia utokao kwa Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mjuzi mpole.

Kila anachousia Mwenyezi Mungu ni wajibu kitekelezwe.

13.Hiyo ni mipaka ya Mwenyezi Mungu. Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, atamtia katika pepo ipitayo mito chini yake ni wenye kudumu humo, na huko ndiko kufuzu kukubwa.

14.Na mwenye kumwasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake na akapetuka mipaka yake, atamtia katika moto; ni mwenye kudumu humo, na atapata adhabu idhalil-ishayo.

Aya 13 - 14 MIPAKA YA MWENYEZI MUNGU

:

MAANA

Maana yako wazi, kwa ufupi ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) baada ya kubainisha viwango vya urithi kulingana na ujuzi wake na hekima yake, akamwahidi thawabu yule mtiifu na mateso yule mwasi; kwa kuhimiza utiifu na tishio la maasi.

Ametumia tamko la wengi (ni wenye kudumu) kwa watu wa peponi kwa vile watu wa peponi watastarehe kwa pamoja. Na kwa watu wa motoni ametumia tamko la mmoja (ni mwenye kudumu) kwa vile kila mmoja atakuwa akiteseka kivyake.

Kuna Hadith kadhaa zimepokewa kuhusu ubora wa ilimu ya mirathi (Faraidh), kwa vile inaangalia masilahi ya jamii na kumweka kila mtu na daraja yake kwa mare-hemu, bila ya kumnyima mwanamke wala mtoto mdogo; inaigawa mirathi yote bila kutoa nafasi ya kuilimbikiza mikononi mwa wachache; kama zilivyo baadhi ya taratibu za Kimagharibi ambazo zinamkusanyia urithi mtoto mkubwa.

Kaashif4-115.jpg

143 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

4. Sura An-Nisaa

Mtume (s.a.w.) amesema: "Jifundisheni ilimu ya mirathi na wafundisheni wengine, kwani mimi ni mtu nitakayekufa na kwamba ilimu - yaani sharia ya Kiislam - itazui-wa, na idhihiri fitina, mpaka itokee wawili watofautiane katika fungu wasipate atakayewaamua. Jifundisheni mirathi kwani hiyo ni katika dini yenu na kwamba kuijua ni nusu ya ilimu na ndio kitu cha kwanza kitakachowatoka umati wangu." Kauli yake hii Mtume ya mwisho (kitu cha kwanza kitakacho watoka umati wangu), ni ishara ya hizi sheria za kutungwa ambazo zimechukua mahali pa sharia ya Kiislam.

15.Na ambao hufanya uchafu mion-goni mwa wanawake wenu, washuhudizieni watu wane katika nyinyi. watakaposhuhudia, basi wazuilieni majumbani mpaka wafikwe na mauti au Mwenyezi Mungu awafanyie njia nyingine.

Kaashif4-116.jpg

16.Na wawili ambao hufanya uchafu katika nyinyi waudhini. Na waki-tubia na wakatengenea, basi waacheni. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwingi wa kukubali toba mwenye kurehemu.

WAFANYAO UCHAFU Aya 15 - 16

LUGHA

Neno Fahisha (uchafu) linatumiwa kwa maana ya zina au ulawiti.

MAANA

" Na ambao hufanya uchafu miongoni mwa wanawake wenu, washuhudizeni watu wane katika nyinyi"

144

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Zina haithibiti isipokuwa akiri mwenye kuifanya (mke au mume) mara nne; au kwa kushuhudiwa na watu wane waadilifu walio waislam; kama linavyofahamisha tamko la Aya 'Katika nyinyi.' Hapana budi kila mmoja katika mashahidi wane awe ameshuhudia waziwazi kuingia uume kwenye uke; kama kinavyoingia kijiti kwenye kichupa cha wanja. Kama mashahidi wakipungua au ushahidi wao ukotafautiana basi kila mmoja wao (hao mashahidi) atapigwa viboko themanini.

Na atakayemsingizia zinaa mume au mke na asilete mashahidi wane waadilifu basi atapigwa viboko thamanini, kwa hivyo ni bora mtu asitafute aibu za watu, kwani hilo huharibu jamii na kuzisambaratisha familia.

Watakaposhuhudia, basi wazuilieni majumbani mpaka wafikwe na mauti.

Yaani ikithibitika kuwa mwanamke amezini, basi atafungiwa nyumbani kwake mpaka afe, kama adhabu yake.

Au Mwenyezi Mungu awafanyie njia nyengine.

Inaonyesha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakuifanya adhabu hii kuwa ni ya daima, bali aliifanya kwa muda maalum, kisha alete sheria nyengine ya mwisho. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa, ambapo hukumu ya Aya hii iliondolewa na kufanywa adhabu ya kupigwa mawe mpaka kufa, akiwa mzinifu ameoa ua kuolewa; na kupigwa viboko mia akiwa mzinifu ni mseja. Ufafunuzi zaidi utakuja katka Sura ya Nur, Inshallah.

Na wawili ambao hufanya uchafu katika nyinyi waudhini.

Wametofautiana wafasiri katika neno Alladhani (wawili ambao), Wengi wamesema ni wazinifu mke na mume. Lakini ilivyo ni kwamba kauli hiyo iko kinyume na dhahiri. Kwa sababu neno Alladhani ni la waume wawili na kwamba hukumu ya mzinifu mwanamke imekwishatangulia wala hakuna wajibu wowote wa kukaririka bila ya kuweko utenganishao.

Ilivyo hasa makusudio ni wanaume wawili mfanyaji na mfanywa. Kwa sababu ya dhahiri ya neno Minkum yaani katika nyinyi wanaume.

Adhabu ya kulawiti ni kufanyiwa maudhi; kama vile kutahayariza, lakini adhabu hii iliondolewa - kama ile ya mzinifu wa kike ya kifungo cha maisha - na ikawa adhabu ya waume hao wawili ni kupigwa upanga mpaka kufa au kuchomwa moto, au kutupwa kutoka mlimani baada ya kufungwa mikono na miguu, au kuangushiwa ukuta. Kwa sababu hilo ni kosa baya lenye athari ya uovu ambao unamuondolea mtu ubinadamu wake na hugeuza hakika ya utu kichwa chini miguu juu. Wakale walisema: "Lau simba angeliingiliwa kinyume na maumbile, angelidhalilika."

Na wakitubia na wakatengenea, basi waacheni

145 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

4. Sura An-Nisaa

Yaani msiache kumuudhi mkosaji huyu kwa kusema tu, nimetubu na Mungu anisamehe, madam haikuthibiti kwake toba ya kweli ya vitendo na kuwa na mwe-nendo mzuri.

17.Hakika toba ikubaliwayo kwa Mwenyezi Mungu ni ya wale tu wafanyao uovu kwa ujinga kisha wakatubia haraka. Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu huwatakabalia toba zao na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi na Mwenye hekima.

18.Na si toba ya wale ambao hufanya maovu mpaka mmoja wao akafiki-wa na mauti akasema: Sasa mimi nimetubia, wala ambao hufa waki-wa Makafiri. Hao tumewaandalia adhabu iumizayo.

Aya 17 - 18 WAFANYAO UOVU KWA UJINGA

MAANA

Hakika toba ikubaliwayo kwa Mwenyezi Mungu ni ya wale tu wafanyao uovu kwa ujinga kisha wakatubia haraka.

Ujinga hapa ni kwa maana ya upumbavu wa kuacha uongofu na kufuata upotevu. Makusudio ya kutubia haraka ni kutubia mkosaji kabla ya kukaribiwa na mauti, kwani mauti yatakuja tu bila ya shaka yoyote, na kila kijacho ki karibu.

Maana kwa ujumla ni kuwa mwenye kufanya uovu, kisha akajuta na kutubia, basi Mwenyezi Mungu humkubalia toba yake na kumsamehe akawa kama hakufanya dhambi yoyote. Bali Mwenyezi Mungu atampa thawabu.

Kaashif4-117.jpg

146

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Unaweza kuuliza: Mbona dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa ni wajibu kwa Mwenyezi Mungu kukubali toba ya wanaojuta na hali twajua kuwa Mwenyezi Mungu ndiye awajibishaye kwa mwengine lile alitakalo, lakini hakuna anayeweza kumwajibishia yeye kitu chochote. Kwa sababu hana wa kufanana naye?

Jibu: Makusudio sio kuwa mwenginewe anamwajibisha Mwenyezi Mungu kukubali toba; isipokuwa makusudio ni kwamba fadhila zake na utukufu wake vinawajibisha kukubali huku; kama vile unavyomwambia mtu mkarimu "Ukarimu wako unakulazimisha kutoa," Mwenyezi Mungu anasema: "Mola wenu amejilaz-imishia rehema ." (6:54)

Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu huwatakabalia toba zao.

Maadamu wanataka kweli kurudi kwenye safu za waumini bora.

Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa toba ya kweli na ya uongo,mwenye hekima, ya kukubali toba.

Na si toba ya wale ambao hufanya maovu mpaka mmoja wao akafikiwa na mauti akasema sasa mimi nimetubia.

Hakika Mwenyezi Mungu hukubali toba ya anayetubia kwa sharti ya kutubia kabla ya kudhihirikiwa na alama za mauti. Ama mwenye kutubia huku akiwa anachun-gulia kaburi, basi toba yake haitakubaliwa. Kwa sababu hiyo ni toba ya kuishiwa na kukata tamaa.

Unaweza kuuliza: Utasemaje kuhusu Hadith ya Mtume (s.a.w.) isemayo: 'Mwenye kutubia saa moja tu, kabla ya mauti yake, basi Mwenyezi Mungu hum-takabalia na kwamba hata saa ni nyingi; mwenye kutubia na roho yake imefika hapa - akionyesha koo lake - basi Mwenyezi Mungu humtakabalia toba."

Jibu: Inabidi kuangalia vizuri riwaya hii kwa mambo haya yafuatayo: Kwanza: Hadith hii inakhalifu Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Na imethibiti kutoka kwa Mtume (s.a.w.) kuwa amesema: "Kumekuwa kwingi kuzuliwa mambo katika uhai wangu na kutazidi baada ya kufa kwangu. Na atakayenizulia, basi na ajich-agulie makazi yake motoni. Ikiwajia Hadith kutoka kwangu, basi ilinganisheni na Kitabu cha Mwenyezi Mungu; yanayoafikiana na Kitabu cha Mwenyezi Mungu yachukueni na yanachohalifiana na Kitabu cha Mwenyezi Mungu basi msiy-achukue."

Kwa ajili hiyo basi hatuikubali Hadith ya kukubaliwa toba wakati roho ikitolewa. Si ajabu kuwa baadhi ya viongozi wa Kibani Umayya na Bani Abbas waliwaambia wafuasi wao wakuu wawawekee Hadith hii, ili iwe ni hoja kwa wanaotawaliwa kwamba wao wanayo nafasi kwa Mwenyezi Mungu hata wakifanya dhuluma na ufisadi kiasi gani. Wao walikuwa na jopo la mafakihi waovu wa kuboresha viten-do vyao na kuifanya dini kulingana na matakwa ya ushetani.

147

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Pili: Fikra ya kukubaliwa toba wakati wa kufa ni hadaa ya kufanya madhambi na hii ni kazi ya shetani sio ya Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema.

Tatu: Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anakubali amali ya aliyeifanya kutokana na matakwa yake na uhuru wake kamili tu. Kwa dhahiri ni kwamba mtu anakuwa huru tu, ikiwa atafanya amali akiwa na uwezo wa kufanya na kuacha. Ama ikiwa anaweza kufanya tu, lakini hana uwezo wa kuacha; au anaweza kuacha tu bila ya kuwa na uwezo wa kufanya, basi atakuwa ni mwenye kuendeshwa bila ya hiyari. Hivi ndivyo ilivyo kwa kutubia wakati wa mauti kwani ilivyo ni kwamba mtubiaji katika hali hii ya mauti, huwa hawezi kufanya dhambi na maasi, sawa na atakavyoshindwa kesho yule atakayesema:

Mola wetu! Tuondolee adhabu hii hakika sisi ni wenye kuamini ." (44:12)

Ikiwa Mwenyezi Mungu atamkubalia toba anayechungulia kaburi, basi itatakikana

pia amkubalie anayeadhibiwa motoni.

Kwa hivyo ndipo Mwenyezi Mungu akawafanya sawa na kuwaunganisha pamoja pale aliposema: "Wala wale ambao hufa wakiwa makafiri."

Yaani pia Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakubali toba ya wale wanaokufa wakiwa makafiri, na wala hawajuti mpaka waone adhabu Siku ya Kiyama, bali pia hawakubaliwi wakiwa njiani kuendea Siku hii ya Kiyama; kama isemavyo Qur'an: "Hata yanapomfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu! Unirudishe ili nifanye mema katika yale niliyoyaacha. Hapana! Hakika hilo ni neno tu analolisema; na nyuma yao kuna kizuizi mpaka siku watakapofufuliwa." (23: 99-100)

Ni kweli kuwa kimtazamo wa kiakili inawezekana kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu awasamehe wenye dhambi hata kama hawakutubia kwa ukarimu wake tu. Lakini hilo ni jambo jengine na kukubaliwa toba wakati wa kufa ni jambo jengine.

TOBA NA MAUMBILE

Toba ni tawi litokanalo na kuwepo dhambi. Kwa sababu ni kutaka kusamehewa hizo dhambi. Na mtu haepukani na dhambi iwe ndogo au kubwa, isipokuwa aliye-hifadhiwa na Mwenyezi Mungu (Maasum). Imenasibishwa kwa Mtume (s.a.w.) kauli hii: "Ukighufiri unaghufiri dhambi zote, kwa mja wako mja yeyote."

Mwenyezi Mungu amewajibisha toba kwa mwenye dhambi, kama vile alivyowa-

jibisha Saumu na Swala. Miongoni mwa Aya zinazofahamisha wajibu ni Aya hii

tunayoifasiri. Na pia Aya hizi zifuatazo:

"Enyi mlioamini tubuni kwa Mwenyezi Mungu toba ya kweli." (66:8)

"Na kwamba mwombeni msamaha Mola wenu na mtubie kwake." (11:3)

"Na wasiotubia, basi hao ndio madhalimu." (49:11)

Kwa hakika hasa wajibu wa kutubia hauhitaji dalili; kwa sababu ni katika maswala ambayo yanakuwa na dalili pamoja. Kila mtu kwa maumbile yake anatambua

148

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

kuwa mkosaji lazima aombe msamaha kwa kosa lake na pia kumtaka msamaha yule aliyemkosea. Na hilo limekuwa ni jambo la kawaida la kimataifa hata kama kitendo kimefanyika kimakosa na bila ya kukusudia. Ndege ikiingia anga ya nchi nyingine au mashua ikiingia bahari ya nchi nyingine bila ya ruhusa, basi ni lazima itangaze kuomba msamaha wake vingenevyo italaumiwa na kanuni.

Kwa hivyo basi, kila Aya au mapokezi yanayofahamisha wajibu wa toba, ni uthibitisho wa hukumu ya kimaumbile na wala sio sharia mpya.

Basi mwenye kufanya dhambi na asitubie atakuwa amefanya uovu mara mbili. Kwanza amefanya dhambi, Pili, kuacha kutubia. Hali mbaya zaidi ni kuacha toba na kuiharibu kwa kurudia dhambi baada ya kumwahidi Mwenyezi Mungu kutekeleza twaa na kufuata amri. Mwenyezi Mungu anasema: "Mwenyezi Mungu amekwishayafuta yaliyopita; lakini atakayefanya tena Mwenyezi Mungu atampa adhabu," (5:95)

Hadith inasema: "Mwenye kuendelea na dhambi na huku anataka msamaha basi ni kama mwenye kucheza shere."

"Mwenyezi Mungu atawalipa shere zao na kuwaacha katika upotofu wao wakitan-gatanga ovyo." (2:15)

Dhambi inathibiti kwa kuacha aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu au kutenda aliy-oyakataza kwa makusudi na kung'ang'ania.' Kwa dhahiri ni kwamba hukumu za kiakili ndizo hukumu za Mwenyezi Mungu Mtukufu. Kwa sababu anafikisha hukumu zake kwa njia mbili: Akili na kwa ulimi wa Mtume wake. Natija ya mwisho ni kwamba hakuna dhambi wala adhabu bila ya ubainifu kama wasemavyo mafakihi waislamu; au bila ya maandishi kama wasemavyo wanasheria.

Kutokana na maelezo hayo yaliyotangulia, inatubainikia kuwa mtu anakuwa ni mwenye dhambi na mwasi ikiwa ameyafanya aliyokatazwa na Mwenyezi Mungu au kuacha aliyoamrishwa na Mwenyezi Mungu kwa makusudi na kujua. Lakini kama atafanya au kuacha kwa kusahau, au kulazimishwa au kwa kutojua kusikokuwa kwa uzembe na kupuuza, basi hatahisabiwa kuwa ni mwenye dhambi; na hakutakuwa na sababu za kuwajibisha toba. Mwenyezi Mungu anasema: "Mwenye kutubia baada ya dhulma yake." (5:39)

Kwa sababu kila mwenye kufanya dhambi basi amejidhulumu mwenyewe kwa kujiingiza kwenye hisabu na adhabu.

Toba ni kujuta mwenye dhambi aliyoyafanya na kutaka msamaha na maghufira kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kutorudia dhambi mara ya pili. Akirudia basi toba imebatilika na atahitajia kuweka upya ahadi madhubuti zaidi na moyo mnyenyeke-vu.

Imam Zainul-abiddin (a.s.) anasema: "Ikiwa kujuta ni toba basi mimi ni wa mwan-zo wa wenye kutubia. Na ikiwa kuacha kukuasi ni kurejea kwako, basi mimi ni wa mwanzo wa wenye kurejea kwako. Na ikiwa kutaka maghufira ni kuondolewa dhambi, basi mimi ni wa mwanzo wa wenye kutaka maghufira."

149

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Makusudio ya kutaka maghufira ni kufanya kwa vitendo sio kwa maneno. Kabla ya chochote kwanza aanze kurudisha haki za watu alizozidhulumu. Ikiwa amem-nyang'anya mtu shilingi basi airudishe; na ikiwa amewambia maneno mabaya au kumfanyia vitendo vibaya, basi amwombe msamaha. Kisha alipe faradhi zilizom-pita; kama vile Hija, Saumu na Swala.

Siku moja Amirul-muminin Ali (a.s.) alimsikia mtu mmoja akisema: "Namtaka maghufira Mwenyezi Mungu."

Imam Akasema: "Unajua kutaka maghufira? Hiyo ni daraja ya juu, na inakuwa katika maana sita."

Basi Imam akayataja ikiwa ni pamoja na kuazimia kutorudia dhambi, kurudisha haki za viumbe na kulipa faradhi nk. Yakitekelezeka hayo kwa anayetubia basi atakuwa miongoni mwa aliowahusu Mwenyezi Mungu kwa kauli yake: "Na hakika mimi ni mwingi wa kumsamehe anayetubia na akaamini na akatenda mema, tena akaongoka ". (20:82)

Yaani kuendelea na uongofu ambao ni imani na amali njema.

Hadith inasema: "Mwenye kutubia ni kama asiyekuwa na dhambi," Bali anakuwa

katika watu wema: Mwenyezi Mungu anasema:

". Tubieni kwake atawastarehesha starehe njema." (11:3)

Na akasema tena: ". Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanaotubia ." (2:222)

Mtume (s.a.w.) amesema: "Mwenye kujiona kuwa ni muovu basi yeye ni mwema." Ama siri ya kuwa mwema mtubiaji na ukubwa wa utukufu wa daraja yake mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni kule kujitambua mwenyewe na kuihisabu nafsi yake na kila aibu na upungufu na kuipigania hiyo nafsi jihadi kwa ukamilifu na utiifu. Hii ndiyo jihadi kubwa aliyoieleza Mtume (s.a.w.). Walikwisha sema Mitume na wenye hekima: "Jitambue," Makusudio yao ni kuwa mtu azitambue aibu zake na ajisafishe.

Pengine mtu anaweza kusema kuwa mtu hupitia mikondo mingi; kama vile wazazi wake, shule, jamii yake mazingira na mengineyo yanayoathiri utu wake bila ya kuweza kuyaepuka. Kwa hiyo basi mtu hawezi kuambiwa kuwa ana dhambi au ni mwovu. Kwa sababu dhambi ni ya jamii na ya mazingira, Ikiwa hakuna dhambi basi maudhui ya kutubia yanafutika kabisa.

Jibu: Ni kweli kuwa mazingira ya mtu yanamwathiri, lakini vile vile ni kweli kuwa matakwa ya mtu yanaathiri mazingira. Kwa sababu mtu na mazingira ni uhakika unaonekana, na kila kitu chenye uhakika unaonekana hakina budi kuwa na athari, vyinginevyo kitakuwa si chochote. Kwa hivyo basi mtu anaweza kuyaathiri mazingira yake, bali anaweza kuyageuza akiwa ni jasiri.

Mazingira anayoishi binadamu huwa yanamsababishia mtu kupendelea kuona

150

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                           3. Sura Al-Imran

natija yake na matunda yake. Kwa hivyo basi ni juu ya mtu kuangalia na kuy-achunguza matunda haya na hayo mapendeleo. Ikiwa yana mwelekeo mzuri, basi apate msukumo, vinginenvyo itambidi aachane nayo. Na hili sio jambo gumu.

Lau binadamu angekuwa hana uwezo wa kuyakabili mazingira, asingeliambiwa kwamba ni mwema au ni mbaya; na pia kusingekuwapo na adhabu au thawabu,. Vile vile kusingekuwako na njia ya kuelezea kuweko dini, hulka njema, sharia au kanuni.

Swali la pili: Umesema kwamba toba ni tawi la dhambi, ambapo tunajua kuwa Mitume na Maimam walikuwa wakitubia kwa Mwenyezi Mungu wakati wao wako mbali na dhambi.

Jibu: Mitume na Maimam wametwahirishwa na uchafu na maasi, hilo halina shaka. Lakini wao kutokana na walivyomjua Mwenyezi Mungu na kumwogopa sana, walijiona kama wana dhambi. Kwa hivyo walitubia dhambi ya kuwazia tu, wala haiko.

Na hiyo ni athari katika athari za kuhifadhiwa kwao na utukufu wao. Kwa sababu, mtukufu hajioni kuwa ni mtukufu, bali hajioni ni chochote kwa Mwenyezi Mungu, daima anajituhumu kuwa si mkamilifu katika kumtii Mwenyezi Mungu na kumwabudu. Kwa ajili hiyo ndipo humuomba msamaha na kumtaka msaada kwa mwisho mzuri kinyume na "Wale ambao bidii yao imepotea bure katika maisha ya dunia na wao wanafikiri kwamba wanafanya vizuri." (18:104)

Bora zaidi ya niliyoyasoma kuhusu maudhui haya ni kipande cha dua ya uokofu (munajat) ya Imam Zainul-abidin (a.s.) akiwa anamtaka Mwenyezi Mungu ampelekee mja mwema anayetakabaliwa dua ili mja huyu amwone Imam akiwa na hali mbaya ya kumwogopa Mwenyezi Mungu; aweze kuathirika na kumhuru-mia Imam amwombee kwa Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu aitakabalie dua ya mja huyu mwema. Hapo Imam aweze kuokoka na hasira ya Mwenyezi Mungu na machukivu yake. Na afuzu kwa kupata radhi Yake na maghufira Yake.

Haya ndiyo aliyoyasema Imam, namnukuu: "Huenda mmoja wao kwa rehema yako akanihurumia kwa msimamo wangu mbaya, akanionea huruma kwa hali yangu mbaya akaniombea dua inayosikilizwa zaidi kwako kuliko dua yangu; au uombezi (shafaa) unaotegemewa zaidi kwako kuliko uombezi wangu ambao utakua ni sababu ya kuokoka kwangu na ghadhabu yako na kufuzu kwangu kwa radhi yako."

Imam Zainul-abidin aliyasema haya siku ambayo hakuweko yeyote duniani anayekurubia sifa moja katika sifa zake adhimu. Hapo ndipo inapokuwa siri ya utukufu.

Baada ya maelezo yote haya ni kwamba toba ina maelezo mengi ambayo yanaweza kupanuliwa katika kitabu mbali kinachohusu toba tu. Huenda tuka-yarudia tena katika mahali patakapo nasibu.

151

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

4. Sura An-Nisaa

19.Enyi ambao mmeamini! Si halali kwenu kuwarithi wanawake kwa nguvu; wala msiwataabishe kwa kutaka kuwanyang'anya baadhi ya mlivyowapa, ila watakapo-fanya uchafu ulio wazi. Na kaeni nao kwa wema; na kama mki-wachukia basi huenda mkachukia kitu na Mwenyezi Mungu ame-jaalia heri nyingi ndani yake

20.Na mtakapotaka kubadilisha mke mahali pa mke na mkawa mumempa mmoja wao rundo la mali, basi msichukue katika mlichowapa. Je, mnakichukua kwa dhulma na kwa makosa yaliyo wazi?

21.Mtachukuaje na hali mmeingiliana na hali wao wamechukua kwenu agano madhubuti?

Kaashif4-118.jpg

152 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Aya 19 - 21 TANGAMANENI NAO KWA WEMA

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Si halali kwenu kuwarithi wanawake kwa nguvu.

Dhahiri ya Aya inaonyesha kukataza kuwachukulia wanawake kama wanyama na kuwarithi, kama walivyokuwa wakifanya wakati wa ujahiliya. Walikuwa wakimuhis-abu mwanamke kuwa ni katika jumla ya mali ya mirathi aliyoacha marehemu.

Mtu akifa msimamzi wa mali zake huja kumtupia nguo mjane, na kumchukua kwa hiyo nguo kama anavyochukua mateka au nyara. Akipenda anamuoa au amwoze mume mwengine na yeye (msimamizi) achukue mahari; kama anayeuza bidhaa na kuchukua pesa. Au akipenda anaweze kumfunga nyumbani mpaka ajikomboe kwa kitu atakacho kikubali.

Imesemekana kuwa makusudio sio kama ilivyo dhahiri ya Aya na kwamba kuna maneno yaliyokadiriwa kuwa ni msirithi mali za wanawake kwa nguvu. Na mfano wa kurithi kwa nguvu ni kuwa mwanamke na msimamizi wake wa karibu kama kaka; mwanamke akawa na mali na kaka yake akamzuwia kuolewa kwa kuwa na tamaa ya kumrithi. Kwa sababu akiolewa atarithiwa na mumewe na wanawe. Ndipo uislam ukaamrisha kumpa mwanamke uhuru wa kuolewa na kukataza kumzuia kwa tamko la kumrithi kwa nguvu. Kwa sababu kurithi ndio makusuido na lengo; na kuzuwia kuolewa ni sababu tu.

Sisi hatuoni tatizo kwa atakayechagua tafisiri ya kwanza au ya pili, au zote pamo-ja, maadamu uislam unakataza kumchukulia mwanamke kama bidhaa, na unam-pa uhuru katika kuolewa na kuchagua mume.

Wala msiwataabishe kwa kutaka kuwanyang'anya baadhi ya mlivyowapa.

Kama ambavyo si halali kwa mwanamume kummiliki mwanamke kama mnyama au kumzuilia kuolewa, vile vile si halali kwa mume kumfanyia uovu mkewe kwa kukusudia kuwa atoe mali ili ajikomboe. Ikiwa mke atatoa katika hali hii na mume akachukua mali, basi atakuwa ni mwenye dhambi. Kwa sababu mali ya mtu hai-wezi kuwa halali (kwa mwengine) isipokuwa kwa kuridhika mwenyewe. Hata hivyo ikibainika kuwa amefanya zina itajuzu katika hali hii kumpa dhiki mpaka atoe kitakachomridhisha, kutokana na kauli yake:

"Ila watakapofanya uchafu ulio wazi." Makusudio ya uchafu hapa ni zina. Kundi dogo la wanavyuoni limesema kuwa uchafu unakusanya pia unashiza14Mwenye Bahrul-muhita amenakili kutoka kwa Malik kwamba inafaa kwa mume kumdhikisha mkewe aliye nashiza na kumchukulia kila anachomiliki, Sheikh Muhammad Abduh anasema:

14Kutoka mke kwenye twaa ya mume.

Kaashif4-119.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Uchafu ni pamoja na zina, unashiza, wizi na mengineyo katika mambo yaliy-oharamishwa.

Tuonavyo sisi ni kuwa si halali kumdhikisha mke kwa ajili ya mali ila akiwa amezi-ni. Na ni haramu kumfanyia hivyo katika isiyokuwa zina, vyovyote itakavyokuwa dhambi; kwa kuangalia maana ya yakini yaliyokusudiwa na Aya.

Zaidi ya hayo kufanyika dhambi hakuhalalishi kula mali za wanayofanya dhambi. Kama si hivyo utaratibu ungeharibika na mambo yangekuwa sambe jambe. Ni nani atakayekuwa na uhalali wa kula mali ya mwenye dhambi? Je, ni mwenye dhambi kama yeye au asiyefanya (mwenye kuhifadhiwa na) dhambi? Ikiwa ni mwenye dhambi kama yeye basi vipi atahalalisha mali ya mwengine; na kama atakayechukua ni maasum basi yuko wapi?

Kwa hakika ni kwamba haijuzu kwa Kadhi kuhukumu kufuta mahari ya mke aliyethibitikiwa na zina kwa sababu ruhusa ya kumdhikisha na kuchukua kitu ina-muhusu mume tu., ni kati yake yeye na Mola wake. Na kwa ibara ya mafakihi, Inajuzu kuchukua mahari katika mfano wa hali kwa ridhaa hii sio kwa kulipa.

MTAKAYOTE, HUKOSAYOTE

Na kama mkiwachukia, basi huenda mkachukia kitu na Mwenyezi Mungu amejaalia heri nyingi ndani yake.

Huenda mtu akachukia baadhi ya mambo ya mkewe, asivumilie, akamwacha na kuoa mke mwengine. Mara huyu mke mwengine anakuwa mbaya zaidi na mwenye vitendo viovu kuliko yule wa kwanza. Hapo hujuta tena, ambapo hakufai chochote. Kwenye kitabu Aghani anasema: Farazdaq alimwacha Nawal, kisha akaoa mwanamke mwengine aliyeachwa, akajuta. Ikawa anamsikia akipiga kite na kumlilia mumewe wa kwanza. Basi akatunga shairi hili;

Mumewe wa kwanza amlilia, nami wangu wa kwanza namlilia.

Nimewaona wengi ambao huwa hawana chochote, mtu hamiliki hata chakula chake anaishi kwa kuombaomba tu, Mara anapata kazi inayomsaidia maisha yake na kutekeleza haja zake kiasi cha kutomtegemea mwengine, kisha huikataa kazi hiyo kwa kutaka zaidi. Basi Mwenyezi Mungu humtia adabu kwa kupata hali mbaya zaidi. Hapo hujuta tena ambako hakumfai chochote. Kuna methali maaru-fu isemayo; 'Mtaka yote hukosa yote.'

Vile vile tumeona wengi wenye shahada za juu lakini wakakubali kazi ile wanay-opata wakawa makarani tu au chini ya karani; wakangoja fursa wakimtegemea Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Si baadae sana mara hupanda kidogo kidogo mpaka kufikia cheo cha juu. Kuna Hadith isemayo: 'Kukinai ni miliki isiyotoweka na ni hazina isiyokwisha .'

Maana yake ni kuwa mwenye kutosheka na apatacho na wala asidharau ali-

154

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

chonacho au kutaka asicho nacho, basi yeye daima ni sawa na aliyenacho (mwenye hazina isiyoisha daima).

Na mtakapotaka kubadilisha mke mahali pa mke, na mkawa mumempa mmoja wao rundo la mali, basi msichukue katika mlichowapa.

Maana yako wazi na yanafupilizwa na kauli yake Mwenyezi Mungu: "Muwaache muacho mzuri." (33:49)

Kuachana kuzuri ni kutoa talaka pamoja na kutekeleza haki zake zote.

Baadhi ya wafasiri wanasema, kuwa wanavyuoni wametofautiana kufikia kauli kumi katika kuweka kiwango maalum cha mrundo wa mali kwa usahihi ni kuwa hilo ni fumbo la wingi. Na kisa cha mwanamke aliyempinga Umar bin Al-khattab -wakati alipotaka kumwekea kiwango cha mahari - kwa Aya hii, ni mashuhuri haki-na haja ya kukitaja.

Je, mnakichukua kwa dhulma na kwa makosa yaliyo wazi?

Yaani mnanyang'anya kwa batili na dhuluma. Unaweza kuuliza: Kwa nini Mwenyezi Mungu amehusisha kukataza kunyang'anya mali ya mke katika hali ya kutaka kubadilisha ambapo tunajua kuwa kunyang'anya ni haram, ni sawa kuwe ni kwa kutaka kubadilisha au la.

Jibu: Hakuna mwenye shaka kuwa kunyang'anya kokote ni haramu huenda ikawa hekima ya kuhusisha kutaja kubadilisha ni kuwa mume anaweza akadhani kuwa anaruhusiwa kuchukua mahari ya mke ikiwa anataka kubadilisha mke mwengine, kwa vile mke mwengine anachukua nafasi ya yule wa kwanza na kuwa itakuwa uzito kwake kutoa mahari mara mbili,. Ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akaondoa dhana hii, kwa kutaja kutaka kubadilisha.

Mtakichukuaje na hali mmeingiliana.

Baadhi ya wafasiri wamesema makusudio ya kuingiliana hapa ni kujamiiana tu. Wengine wamesema pia na faragha. Kundi jingine la tatu limesema kwa kuya-pamba meneno: "Makusudio ya kuingiliana ni mapenzi, hisia, mawazo, siri, huzu-ni, majibizano, makumbusho na simanzi .." Na sifa nyinginezo zilizopangwa. Mungu awarehemu! Tafsiri nzuri ya maana ya kuingiliana ni ile aliyoisema Sheikh Muhammad Abduh aliposema: "Ni ishara ya kwamba kila mmoja kati ya mume na mke ni sehemu inayotimiza sehemu nyengine; ni kama kwamba ilikuwa sehemu moja imetenganishwa na sehemu nyingine halafu ikaunganishwa kwa mwingiliano huu na kuwa moja."

Lakini ni bora zaidi tufasiri maingiliano kwa maana ya kufanyiana hisani, kwa kufu-

ata kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Wala msisahau hisani baina yenu."

(2:237)

Yaani hisani ya kila mmoja kwa mwengine, mke na mume. Mwenyezi Mungu

155 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                                4. Sura An-Nisaa

anamkubusha mume yale yaliyokuwepo kati yake na mkewe.

NDOA NI KUBADILISHANA ROHO KWA ROHO

Na hali wao wamechukua kwenu agano madhubuti.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amekupangia kufunga ndoa kwa matamko aliyoyataja katika kitabu chake kitukufu na kuwajibisha kuyatumia hayo tu; sawa na matamko ya ibada, na akakuongezea huko kufunga ndoa, utukufu ambao hauko katika mapatano mengine; kama vile bei, ajira n.k. Kwa sababu bei ni kubadilishana mali kwa mali. Ama ndoa ni kubadilishana roho kwa roho na akayafanya ni mapatano ya rehema na mapenzi sio mapatano ya kumiliki mwili badala ya mali.

Mafakihi wamesema: "Kufunga ndoa ni karibu zaidi na ibada kuliko mapatano mengine; na ni kwa sababu hii, ndipo wakaitegemeza kwenye jina la Mwenyezi Mungu Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kwa sunna ya Mtume wa Mwenyezi Mungu."

Sheikh Muhammad Shaltut anasema: "Kama tukijua kuwa neno Mithaq' (agano) limekuja katika Qur'an kwenye ibara za mambo yaliyo baina ya Mwenyezi Mungu na waja wake katika wajibu wa Tawhid, na kulazimiana na hukumu, vile vile katika mambo hatari ya dola moja na nyengine tu, basi hapa tutajua cheo cha kutaja hilo neno katika kufunga ndoa. Vile vile kama tukijua kuwa kulisifu neno Mithaq kwa neno Ghalidh (madhubuti) hakuna katika Qur'an isipokuwa katika maudhui ya ndoa tu, basi utazidi utukufu wa jambo hili ambao umeletwa na Qur'an."

22.Wala msiwaoe walioolewa na baba zenu, ila waliokwisha pita. Hakika hilo ni ovu na chukizo na njia mbaya.

Kaashif4-120.jpg

156

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne

23.Mmeharamishiwa mama zenu, na binti zenu, na dada zenu na shangazi zenu na khalat zenu, na binti wa kaka na binti wa dada, na mama zenu waliowanyonyesha na dada zenu wa kunyoyonya, na mama wa wake zenu na binti zenu wa kambo walio katika ulinzi wenu, waliozaliwa na wake zenu mliowaingilia-hapana vibaya juu yenu ikiwa hamkuwaingilia-na wake wa watoto wenu waliotoka katika migongo yenu, na kuku-sanya kati ya dada wawili, ila waliokwisha pita.           Hakika

Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusameh Mwenye kurehemu.

4. Sura An-Nisaa

Kaashif4-121.jpg

Aya 22 - 23: WALIO HARAMU KUWAOA

IRABU

Yametangulia maelezo katika kufasiri Aya ya 3 ya sura hii kuwa herufi Ma pia hutu-miwa kwa mwenye akili kama katika Aya hii: (Waliowaoa, baba zenu) kama ambavyo pia Man hutumiwa kwa asiyekuwa na akili; kama katika kauli yake Mwenyezi Mungu: Na wengine hutembea kwa matumbo yao (24:45) hapo ame-tumia neno Man kwa wanaotembea kwa matumbo ambao ni wanyama, hawana akili.

Watu wa 'Nahau' ni lazima wafuate Qur'an na wala sio kinyume. Ajabu ni kuwa wafasiri wengi wanafanya taawil katika Qur'an kwa sababu ya kauli ya watu wa Nahau, lakini hawabatilishi kauli ya watu wa Nahau kwa Qur'an.

157

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne 4. Sura An-Nisaa MAANA..

Mwenyezi Mungu(s.w.t.) ameharamisha kuoa aina kadhaa za wanawake. Na uharamu wao uko mafungu mawili: Fungu la kwanza ni la uharamu wa milele, kwa maana ya kuwa hakuna mabadiliko; kama vile mtoto, dada, shangazi n.k. Fungu la pili ni lile la uharamu wa muda; kama vile mke wa mtu mwengine au dada wa mke n.k. Ufafanuzi ni kama ufuatavyo:

1.Wala msiwaoe waliowaoa baba zenu ila waliokwishapita.

Ilikuwa mtu anamuoa mke wa baba yake aliyekufa, ikiwa mke huyo si mama yake. Bali hata Umayya, babu wa Abu Sufiyan alimwacha mkewe, akamwoza mwanawe akiwa hai. Uislam umelikataza hilo kwa kulitilia mkazo na kulizingatia kuwa ni Uovu na chukizo na njia mbaya.

Mafakihi na wafasiri wameafikiana kuwa uharamu unaenea kwa wake wa mababu wa upande wa baba au mama; na kwamba uharamu huu unapatikana kwa kufungika ndoa tu, iwe kumepatikana kuingilia au la. Lakini wametofautiana kwa baba aliyezini na mwanamke, je utapatikana uharamu kwa mtoto wake? Shia Imamia, Hanafi na Hambal, wamesema ni haramu. Shafi akasema hakuna uharamu. Na Malik ana riwaya mbili.

2.Mmeharamishiwa mama zenu.

Yaani mumeharamishiwa kuwaoa mama zenu, wakiwemo nyanya zenu wa upande wa baba na mama

3.Na binti zenu na kuja chini; wajukuu na vitukuu, vilembwe na vinying'inya na kuendelea

4.Na dada zenu.

Dada na kaka hapa ni ndugu mdogo au mkubwa; ni sawa wawe ni baba mmoja au mama mmoja, atakuwa haramu. Lakini ni halali kuoa dada wa dada na dada wa kaka, akiwa siye dada. Mfano wa hayo ni kuwa wewe una mtoto aitwaye Rauf, uliyezaa na mke mwingine ukamuoa mwanamke ambaye tayari amezaa na mume mwingine mtoto anayeitwa Hind, na Rauf naye akamuoa Hind. Sasa wewe na mamake Hind mkizaa mtoto atakuwa ni kaka wa sehemu mbili, ni kaka wa Rauf kwa upande wa baba yake na kaka wa Hind kwa upande wa mama yake kwa hiyo Rauf atakaua ameoa dada wa dada yake na Hind ameolewa na kaka wa kaka yake.

5.Na shangazi zenu.

Shangazi ni kila mwanamke ambaye ni dada wa mtu ambaye nasaba yako inare-jea kwake moja kwa moja au kupitia ngazi. Kwa hiyo shangazi yako ni dada wa baba yako ambaye amekuzaa wewe moja kwa moja. Shangazi wa baba yako ni dada wa babu yako ambaye amekuzaa wewe kupitia ngazi moja (baba yako) na shangazi wa babu yako ni dada wa baba wa babu yako ambaye amekuzaa wewe kupitia ngazi mbili (babu na baba) na kuendelea wote hao ni haramu.

158

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

Vilevile ni haramu shangazi wa mama yako. Kwa sababu yeye ni dada wa baba wa mama yako ambaye amekuzaa wewe kupitia ngazi moja (mama) na kuende-lea.

Ni halali kumuoa binti wa shangazi na wa ammi Kwa sababu yeye siye dada wa aliyekuzaa wewe. Bali ni binti wa kaka yake au dada yake.

6.Na khalati zenu

yaani dada za mama zenu. Ni kila mwanamke ambaye ni dada wa mtu ambaye nasaba yake inarejea kwako moja kwa moja au kupitia ngazi. Kwa hiyo khalat wako ni dada wa mama yako ambaye amekuzaa wewe moja kwa moja.Vilevile khalat wa mama yako ni dada wa nyanya yako ambaye amekuzaa wewe kupitia ngazi moja (mama yako) vile vile khalat wa baba yako hakuna tofauti isipokuwa huyu ni dada wa babu na yule ni dada wa nyanya. Pia khalat wa nyanya yako ni dada wa mama wa nyanya yako ambaye amekuzaa wewe kupitia ngazi mbili (mama na nyanya) na kuendelea. Wote hao ni haramu

Hata hivyo ni halali binti wa Khalat na wa mjomba, kwa sababu yeye si dada wa aliyekuzaa bali ni binti wa kaka au dada yake.

7.Na binti wa kaka na binti wa dada

Na kuendelea chini

8.Na mama zenu waliowanyonyesha na dada zenu wa kunyonya.

Wameafikiana kwa kauli moja kuitumia Hadith hii: "Ni haramu kwa kunyonyesha yale yaliyo haramu kwa nasaba." Kwa hivyo kila mwanamke aliye haramu kumuoa kwa nasabu atakuwa haramu pia kwa kunyonya, awe ni mama, dada au binti. Vile vile shangazi, khalat, binti wa kaka au binti wa dada.

Wametofautiana katika idadi ya kunyonyesha inayowajibisha uharamu. Shia Imamia wamesema ni manyonyesho kumi na tano kamili, ambayo hayakuingiliwa kati na nyonyesho la mwanamke mwengine. Au kunyonya mtoto mchana mmoja na usiku wake kwa sharti ya kuwa lishe yake katika muda huu iwe ni maziwa ya huyo mwanamke tu.

Shafii na Hambal wamesema, hapana, yawe ni manyonyesho matano kwa uchache. Hanafi na Malik wamesema kuwa uharamu unapatikana kwa kunyonyesha tu, kuwe kwingi au kuchache.

Kuna masharti mengine ya kunyonyesha tumeyataja kwa ufafanuzi katika kitabu Ahwalush-Shakhsiyya Alal-madhahibil Khamsa.

9.Na mama wa wake zenu.

Wameafikiana kuwa mama wa mke (mama mkwe) na kuendelea juu, ni haram mara tu ukifunga ndoa na binti yake hata kama hukumwingilia. Amekua pekee

159

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Nne                                                          4. Sura An-Nisaa

yule aliyesema kuwa kufunga ndoa tu, hakuharamishi mama mkwe mpaka aingili-we binti na akatoa dalili kwa Aya hii pale alipolifanya neno ambao mmewaingilia kuwa ni sifa ya mama za wake na wana wa kambo. Lakini mafakihi wamempinga kwa kauli hii kuwa sifa inamrudia aliye karibu zaidi na kwa Hadith sahihi kutoka kwa Mtume Mtukufu (s.a.w.). Aina zote hizo zilizotajwa ni haramu milele.

10.Na binti zenu wa kambo walio katika ulinzi wenu, waliozaliwa na wake zenu mliowangilia, iwapo hamkuwaingilia hapana vibaya juu yenu.

Wameafikiana kuwa binti wa mke hawi haramu kwa kufunga ndoa tu na mama yake bila ya kumwingilia. Kwa hivyo inajuzu kwake kumtaliki mama kabla ya kumwingilia kisha kumuoa binti yake.

Walio katika ulinzi wenu, haina maana kuwa wasio katika ulinzi wenu ni halali. Kwani binti wa kambo ni haramu tu hata kama hayuko chini ya ulinzi wa baba wa kambo. Imetajwa ulinzi kwa kubainisha kuwa aghlabu inakuwa hivyo.

Hanafi na Malik wamesema kugusa na kutazama kwa matamanio kunawajibisha uharamu, sawa na kuingilia. Shia Imamiya, Shafi na Hambal wamesema hakuna uharamu ila kwa kuingilia wala kugusa na kutazama hakuna athari ya kusababisha uharamu hata ikiwa ni pamoja na matamanio.

Wameafikiana kuwa hukumu ya kumwingilia mwanamke kwa kutatizika ni kama hukumu ya kuingilia kwa ndoa sahih katika yaliyotajwa. Maana ya kuingilia kwa kutatizika ni kuingiliana mwanamke na mwanamume kwa kufikiria kuwa ni mke na mume washaria, halafu ikabainika kuwa ni watu kando.

11.Na wake wa watoto wenu waliotoka katika migongo yenu

Wameafikiana kuwa mke wa mtoto na wa mjukuu, na kuendelea chini, ni haramu kwa baba, babu na kuendelea juu, hata kwa kufunga ndoa tu bila ya kumwingilia. Neno "kutoka katika migongo yenu," ni mtoto wa kumzaa mwenyewe, si mtoto wa kupanga yaani asiwe wa kulea. Ama mtoto wa kunyonya hukumu yake ni kama hukumu ya mtoto wa kumzaa, kutokana na Hadith: Ni haram kwa kunyonya yaliyo haramu kwa nasaba.

12.Na kukusanya kati ya dada wawili isipokuwa wale waliokwishapita.

Wameafikiana katika uharamu wa kukusanya dada wawili. Lakini kama mume aki-farikiana na mkewe kwa kifo au talaka, basi inajuzu kumwoa dada yake.

Imamia na Shafii wanasema kuwa mtu akimwacha mkewe talaka rejea, basi hai-juzu kufunga ndoa na dada yake mpaka eda ishe. Ama ikiwa ni talaka isiyokuwa rejea, basi inajuzu kumwoa dada yake katikati ya eda. Kwa sababu ni talaka isiyo na uwezekano wa kurejeana.

Madhehebu mengine yamesema kuwa hnti wa mke hawi haramu kwa kufunga ndoa tu na mama yake bila ya kumwingilia. Kwa hivyo inajuzu kwake kumtaliki mama kabla ya kumwingilia kisha kumuoa binti yake.

Walio katika ulinzi wenu, haina maana kuwa wasio katika ulinzi wenu ni halali. Kwani binti wa kambo ni haramu tu hata kama hayuko chini ya ulinzi wa baba wa kambo. Imetajwa ulinzi kwa kubainisha kuwa aghlabu inakuwa hivyo.

Hanafi na Malik wamesema kugusa na kutazama kwa matamanio kunawajibisha uharamu, sawa na kuingilia. Shia Imamiya, Shafi na Hambal wamesema hakuna uharamu ila kwa kuingilia wala kugusa na kutazama hakuna athari ya kusababisha uharamu hata ikiwa ni pamoja na matamanio.

Wameafikiana kuwa hukumu ya kumwingilia mwanamke kwa kutatizika ni kama hukumu ya kuingilia kwa ndoa sahih katika yaliyotajwa. Maana ya kuingilia kwa kutatizika ni kuingiliana mwanamke na mwanamume kwa kufikiria kuwa ni mke na mume washaria, halafu ikabainika kuwa ni watu kando.

11.Na wake wa watoto wenu waliotoka katika migongo yenu

Wameafikiana kuwa mke wa mtoto na wa mjukuu, na kuendelea chini, ni haramu kwa baba, babu na kuendelea juu, hata kwa kufunga ndoa tu bila ya kumwingilia. Neno "kutoka katika migongo yenu," ni mtoto wa kumzaa mwenyewe, si mtoto wa kupanga yaani asiwe wa kulea. Ama mtoto wa kunyonya hukumu yake ni kama hukumu ya mtoto wa kumzaa, kutokana na Hadith: Ni haram kwa kunyonya yaliyo haramu kwa nasaba.

12.Na kukusanya kati ya dada wawili isipokuwa wale waliokwishapita.

Wameafikiana katika uharamu wa kukusanya dada wawili. Lakini kama mume aki-farikiana na mkewe kwa kifo au talaka, basi inajuzu kumwoa dada yake.

Imamia na Shafii wanasema kuwa mtu akimwacha mkewe talaka rejea, basi hai-juzu kufunga ndoa na dada yake mpaka eda ishe. Ama ikiwa ni talaka isiyokuwa rejea, basi inajuzu kumwoa dada yake katikati ya eda. Kwa sababu ni talaka isiyo na uwezekano wa kurejeana.

Madhehebu mengine yamesema kuwa haijuzu kufunga naye ndoa ila baada ya kwisha eda, bila ya kutofautisha talaka rejea na nyengineyo.

160