AL-KASHIF
Vol.3
Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya



YALIYOMO

Aya 253:            Kuwafadhilisha Mitume..2

Aya 254:            Kutoa.....4

Aya 255:            Aya ya Kursiy....6

Mwenyezi Mungu na Desturi ya Maumbile...7

Kitu bila ya kitu...9

Aya 256-257: Hakuna kulazimisha katika dini...10

Kudumu Motoni..12

Aya 258:            Aliyehojiana na Ibrahim.15

Aya 259:            Aliyepita karibu na Mji...17

Hisabu ya Kaburini..18

Aya 260:            Ili Moyo wangu utulie....20

Aya 261-263:     Punje moja inayotoa mashuke saba......21

Aya 264-265:     Musiharibu sadaka zenu....24

Aya 266:            Je, mmoja wenu anapenda...?...25

Aya 267-268:     Kutoa katika vizuri..27

Aya 269:            Hekima.....28

Aya 270-271: Chochote mtoacho..30

Aya 272-274: Si juu yako kuwaongoza....32

Watu wa Sufa (Upenuni)....34

Zaka....35

Aya 275-281: Mnasaba...38

Neno Riba.39

Uharamu...39

Sababu ya Haramu.40

Aya 282-283: Deni.....46

Mkopo na Deni...47

Kumshukuru Muumba na Muumbwa.....48

Usufi...54

Aya 284:            Kama mkidhihirisha yaliyomo katika nyoyo zenu...56

Aya 285-286: Mtume ameamini....57

3 Sura Al-Imran

Aya 1-6....61

Aya 7-9:....65

Aya 10-13: Hazitawafaa kitu mali zao na watoto wao..70

Wenye Mali....71

Aya 14:              Kupenda matamanio....73

Raha...73

Aya 15-17: Yaliyo bora....75

Matunda ya imani..76

Aya 18-20 Mwenyezi Mungu, Malaika na wenye elimu... 77

Dini ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu...77

Vikundi sabini na tatu....79

Aya 21-22: Wanaowaua Mitume....81

Kuamrisha mema na kukataza mabaya.....82

Aya 23-25: Mayahudi tena...83

Aya 26-27: Humpa Ufalme amtakaye..85

Aya 28-30: Urafiki na kafiri...88

Aina za urafiki na kafiri.88

Taqiya.89

 

Aya 31-32: Kumpenda Mwenyezi Mungu..92

Aya 33-37: Mama wa Maryam...95

Fatima na Maryam...97

Aya 38-41: Zakariya.....99

Aya 42-44: Ewe Maryam Mwenyezi Mungu amekuteua....101

Ubora wa Qur'an kwa Wakristo.....102

Nani Bibi Mkuu wa Wanawake wa ulimwenguni?.103

Aya 45-51: Maryam Mungu akubashiria...106

Lisilowezekana kiakili na kidesturi..106

Aya 52-54: Ni nani wasaidizi wangu...110

Haki na manufaa...

Mwenyezi Mungu ni mbora wa wafanya hila....111

Aya 55-58: Kuondoka Ulimwenguni....113

Kutofautiana kuhusu Isa..113

Aya 59-63 Mfano wa Isa ni kama wa Adam....117

Mitume na Maasi...117

Mubahala.118

Ahlul Bait.120

 

Aya 64-68: Njooni kwenye neno la usawa...121

Aya 69-71: Wanajipoteza wenyewe....125

Uislamu ni dini yenye nguvu...125

Aya 72-74: Kuamini asubuhi na kukufuru jioni.127

Aya 75-76: Kuna waaminifu na wahaini katika watu wa kitabu..130

Hakuna maisha ila kwa ukakamavu wa kutojali mauti.130

Aya 77:              Asiye na ahadi hana dini..131

Aya 78:              Wanapinda ndimi zao kwa kitabu..132

Aya 79-80: Kuweni watumishi wa Mungu...134

Aya 81-83: Mshikamano wa Mitume..136

Mtume na Mrekebishaji...136

Irabu.136

Aya 84-85: Tumeamini Mitume yote...139

Aya 86-89 Atawaongozaje makafiri...140

Aya 90-91: Kisha wakazidi kukufuru...142
 


The .HTML version of this book is taken from
www.al-shia.com  and ebooked by
www.ShiaLibrary.com   and www.islamkutuphanesi.com  .
May Allah be pleased with all.

Haki ya kunakili imehifadhiwa na: AL-ITRAH FOUNDATION
SWAHILI - JUZUU YA TATU

ISBN: 9987 665 33 0

Kimeandikwa na:Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya

Kimetafsiriwa na: Sheikh Hasan Mwalupa

P.O. Box 1017, Dar es Salaam/Tanzania. Email:mwalupa@hotmail.com

Kimehaririwa na: Dr.M.S. Kanju.

S.L.P 1017, Dar es Salaam. Email: drmkanju@yahoo.com Website: www.dartabligh.org

kupangwa katika kompyuta na: Ukhti Pili Rajabu.

Toleo la kwanza: Februari 2004 Nakala:5000

Kimetolewa na kuchapishwa na: Alitrah Foundation P.O. Box 1017 Dar es Salaam, Tanzania Simu:+255 22 2110640 Fax: +255 22 2126757 Email: alitrah@daiichicorp.com Website: www.alitrah.org

Kaashif3-2.jpg

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu walio-jitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Kama lilivyo jina la Tafsiri yenyewe ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo.

Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyo-viandika katika maudhui mbali mbalimbali na hivyo kujipatia wasomaji wengi sana.

Msomi huyu, mwenye fikra huru na anayetetea kile anachokiamini, ni mtu mwenye mawa-zo mapana na kuyaangalia mambo kwa undani sana, kipaumbele chake ni katika maslahi ya umma huu na amejaribu sana kwenda na wakati.

Sifa kubwa pekee ya mwanachuoni huyu ni kuwa yeye hakujihusisha sana na kung'ang'a-nia madhehebu fulani tu, labda hii yatokana na wadhifa wake wa ukadhi aliokuwa nao katika nchi ya Lebanon ambayo ina madhehebu mengi, ambapo sula la madhehebu ni nyeti nchini humo, hata hivyo yeye aliweza kuamua matatizo ya watu kwenye ofisi yake kulingana na madhehebu yao pale walipomwendea, hiyo ilimsaidia sana hata kuweza kutoa kitabu kitwacho 'Al-Fiqh a'laa madhaahabil-khamsah' (Fikhi ya madhehebu matano) yaani ya Hanafi, Maaliki, Shafi, Hambali na Shia (ambacho twataraji kitatoka hivi karibuni Inshaallah).

Jambo lililotupa msukumo wa kukifasiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ni zile faida nyin-gi atakazozipata msomaji na kujua mambo mengi na ya ajabu yaliyo mapya kwake ambayo si rahisi kuyapata kwa wafasiri wengine.

Msomaji atapata faida katika fani za Sayansi, Siasa, Historia, Mashairi, visa vizuri, na Saikolojia miongoni mwa mengine; ndiyo maana msomaji atashangaa kidogo anapoisoma Tafsiri hii atakapoona mwandishi amewataja na kuwanukuu watu kama kina Mfalme Edward, wanasyansi kama kina Enstein, Charlie Champlin (Mchekeshaji maarufu), na wengineo, hali inayoifanya tafsiri hii kuwa ni ya kipekee kabisa.

Mtindo alioutumia mwandishi ni sahali uliokusudiwa watu wa tabaka mbalimbali, wanavyuoni na watu wa kawaida.

i

Kaashif3-3.jpgKaashif3-4.jpg

Nia yetu ni kukigawanya kitabu hiki bure lakini tumelazimika kukiuza kwa bei nafuu ili kurud-isha gharama za uchapishaji.

Mwisho: Shukrani kubwa iwaendee bila ya kuwataja watu waliojitolea usiku na mchana, jopo la wafasiri, wahariri, wachapaji, waliotupa moyo na kutoa maoni yao na walioisimamia ili kuhakikisha kwamba kitabu kimemfikia msomaji.

Masahihisho:

Katika Juzuu ya kwanza kuna makosa ya uchapishaji baadhi yamegunduliwa na wasomaji wetu, na wakatujulisha- tunawashukuru sana.

1.            Ukurasa wa xiii ibara ya 2- badala ya (5:212) ni (2:212)

2.            Ukurasa wa 7 Aya 3 kuna maneno yaliyoongezwa ambayo ni 'na wanaotoa Zaka'

3.            Ukurasa wa 19 Aya 26 maneno: "na huwaongoza wengi" yamekosekana katika Aya hii pale inaposema: huwapoteza kwa mfano huu wengi na huwaongoza wengi.

4.            Ukura wa 41 Aya 69 maneno ya mwanzo kabisa ya Kiarabu yamekatika nayo ni:

Kaashif3-5.jpg

5.            Ukurasa wa 65 Aya ya 109 maneno ya mwisho kabisa kwenye tarjuma ni: " ni Muwezo juu ya kila kitu- na sio anayeona mnayoyafanya.

6.            Ukurasa 87 sio 80:36 ni 80:34.

Tunawaomba wasomaji wetu watuandikie kila wanapoona kosa, na sisi tutafanya masahihisho katika kila Juzuu inayofuatia.

Mchapishaji

ii

Kaashif3-6.jpgKaashif3-7.jpg

Makosa ya Chapa.

Sikumbuki kama nimewahi kusoma kitabu kilichotoka kupigwa chapa, cha zamani au cha sasa, bila ya kukuta makosa ya chapa. Nafikiri sitasoma kitabu kisichokuwa hivyo. Nimejaribu sana kuliepuka hilo katika tungo zangu, lakini sikufanikiwa.

Nilikuwa sifikirii kama ninaweza kuona makosa haya katika maandishi ya msahafu mtuku-fu, kama yale yaliyo katika baadhi ya chapa; kwa mfano neno yabswatu kwa swad, badala ya yabsutu kwa sin, na katika chapa ya Tafsir Arrazi ya Misr ya mwaka 1935, Sura ya (2:146). Imeandikwa La Ya'alamuun, (hawajui) badala ya Ya'alamuun (wanajua). Mfano wa makosa haya hausameheki.

Katika Tafsir Al-Manar, chapa ya Pili, sura (5:212), imeandikwa "Fawqahum ila yawmil qiya-ma badala ya Fawqahum yawamal qiyama". Hatuwezi kusema kosa hili ni kubwa zaidi kuliko lile.

Lakini mkosaji atatuletea udhuru kwa msemo mashuhuri huko kwetu jabal amail 'Makosa ya chapa.'

Katika Tafsiri Majmau chapa ya Urfan, Sura (46:15), imeandikwa: " Hatta idaha balagha arbai' na sanah badala ya: Hattaidaha balagha ashuddahu arbai ' na sanah"

Kusema hivi sio kama ninajitetea kutokana na makosa ya chapa atakayoyakuta msomaji katika kitabu hiki, ijapokuwa naomba msamaha kama litatokea hili, lakini makusudio yangu hasa ni kumwambia yule atakayefungua macho yake kwenye makosa ya matamko ya kuu-fungia macho uzuri wa maana. Vilevile ninamwambia yule ambaye siku moja aliniambia: "Vitabu vyako vimejaa makosa ya chapa, kama kwamba hakuna kitu chochote katika vitabu hivyo isipokuwa makosa ya chapa tu. Wote hao ninawaambia: Mungu awasamehe na aniongoze mimi na nyinyi.

Vyovyote iwavyo, mimi ninaomba msamaha kutokana na makosa ya kifikra na ya chapa. Anasema Amirul Muminiin (a.s): "Watu wote ni wapungufu wenye kuchanganyikiwa, isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mwenyezi Mungu." Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye jukumu la kunikubalia yale niliyoyapatia na kunisamehe niliyakosea, kwa jaha ya Mtume na kizazi chake, ziwashukie rehema na amani (Amin).

MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYAH

iii

iv

Kaashif3-8.jpgKaashif3-9.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

253. Mitume hao tumewafadhilisha baadhi yao zaidi kuliko wengine. Miongoni mwao yuko ambaye Mwenyezi Mungu alisema naye; na wengine akawapandisha vyeo, na tukampa Isa mwana wa Maryam dalili zilizo wazi na tukamtia nguvu kwa roho takatifu. Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka wasin-gelipigana wale waliokuwa baada yao, baada ya kuwafikia dalili zilizo wazi; lakini walihitilafiana kuna katika wao walioamini na wengine katika wao waliokufuru, lakini Mwenyezi Mungu hufanya anayoy-ataka.

Kaashif3-10.jpg

KUWAFADHILISHA MITUME Aya ya 253

MAANA

Mitume hao tumewafadhilisha baadhi yao zaidi kuliko wengine.

Mwenyezi Mungu alimwambia Mtume Wake Muhammad (s.a.w.) katika mwisho wa Aya iliy-otangulia; "Na hakika wewe ni miongoni mwa Mitume," Halafu akafuatisha moja kwa moja na kauli Yake hii: "Mitume hao ..." Kwa hivyo basi, makusudio yanakuwa ni mitume wote ambao miongoni mwao ni Muhammad, sio kundi maalum, kama walivyosema wafasiri wengi.

Mitume wote ni sawa katika asili ya utume kuchaguliwa kwao na katika kufikisha ujumbe, wa Mwenyezi Mungu na kuongoza viumbe Vyake, lakini wanatofautiana katika mambo fulani. Yaani baadhi ya mitume wamekuwa mashuhuri kwa baadhi ya mambo fulani waliy-ohusika nayo, ambayo wengine hawakuwa nayo, ambayo Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ame-wasifu nayo katika Kitabu chake. Kwa mfano Ibrahim alikuwa mashuhuri kwa kuitwa rafiki wa Mwenyezi Mungu (Khalilullah) kutokana na kauli Yake Mwenyezi Mungu:

"....Na Mwenyezi Mungu amemfanya Ibrahim kuwa ni rafiki," (4:125).

Musa naye akawa mashuhuri kwa jina la aliyesema na Mwenyezi Mungu (Kalimullah)

kutokana na kauli Yake Mwenyezi Mungu:

"... Na Mwenyezi Mungu akasema na Musa maneno." (4:164)

Isa naye akawa mashuhuri kwa, roho wa Mwenyezi Mungu (Ruhullah); kama alivyosema

Mwenyezi Mungu: "Hakika Masihi Isa bin Maryam ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na neno

lake alilompelekea Maryam. Na ni roho iliyotoka kwake ... " (4:171)

2

2

Kaashif3-11.jpgKaashif3-12.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Muhammad naye akawa mashuhuri kwa, mwisho wa Mitume (khatamun nabiyyina) kwa kauli Yake Mwenyezi Mungu: "Na Mtume wa Mwenyezi Mungu na mwisho wa Mitume ..." (33: 40)

Mwenyezi Mungu ametaja baadhi ya Mitume waliofadhilishwa au baadhi ya yanayohusika nao, kwa kauli Yake:

Miongoni mwao yuko ambaye Mwenyezi Mungu alisema naye. Huyu ni Musa bin Imran kama walivyoafikiana wafasiri

Na wengine akawapandisha vyeo .

Mwenye Tafsiri ya Al Manar amesema: "Wafasiri wamesema huyo ni Mtume wetu ..." Na amesema Razi: "Umekubaliana umma wote kwamba Muhammad ni bora ya Mitume," Ametoa dalili 19 juu ya hilo kwa dalili, Miongoni mwa dalili hizo ni kwamba Ali bin Abu Twalib siku moja alitokeza kwa mbali, Mtume akasema: "Huyu ni bwana wa Waarabu."Aisha akasema: "Siye wewe bwana wa Waarabu? "Mtume akasema: "Mimi ni bwana wa walimwengu na yeye ni bwana wa Waarabu." Dalili bora zaidi juu ya ubora wa Mtume kwa Mitume wote na watu wema wote ni sharia

yake ilivyo na ukunjufu katika utukufu wake na utu wake. 1*

Na tukampa Isa mwana wa Maryam dalili zilizo wazi na tukamtia nguvu kwa roho takatifu.

Dalili zilizowazi hapa ni dalili ambazo zinadhihirisha haki; kama kufufua wafu, kuponyesha wagonjwa, kuumba ndege, n.k. Makusudio ya roho takatifu ni roho njema yenye kutakaswa. Imekwishapita tafsiri ya roho katika Aya ya 87 ya Sura hii.

Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka wasingelipigana wale waliokuwa baada yao.

Yaani baada ya Mitume kuwajia na hoja zilizowazi na kuzifafanua haki kwa dalili, basi watu wao walihitalifiana baada yao.

Kuna katika wao walioamini na wengine katika wao waliokufuru.

Unaweza kuuliza: Kauli Yake Mwenyezi Mungu: "Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka wasingelipigana. Si inafahamisha kwamba binadamu ni mwenye kuendeshwa hana hiyari na kwamba kukaririka jumla hii ni kutilia mkazo kunasibika kupigana na matakwa ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.)?

Jibu: Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amempa uwezo mja na akambainishia heri na shari na kumkataza hili na kumwamrisha lile. Mwenyezi Mungu anasema: "Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msiachane..." (3:103) Mtu akifuata njia ya mshika-mano na kupendana, atakuwa yeye mwenyewe ndiye anayenasibika na huko kufuata, kwa sababu kumetokana na yeye na kwa hiyari yake iliyomfanya aone bora njia hiyo kuliko njia ya kutoelewana; wakati huo huo huko kufuata njia hiyo ya mshikamano kunafaa kunasi-bishwe kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu Mwenyezi Mungu ndiye aliyemwezesha kuifua-ta na ndiye aliyemwamrisha kuifuata.

*1Wamesema sana kuhusu sababu za kuzorota kwa Waislamu na udhaifu wao katika nafsi zao; wametunga vitabu vingi kuhusu hilo na wakatoa sababu nyingi sana. Sisi tunaona sababu ya kwanza na ya mwisho ni kupuuzwa sharia ya Kiislamu kwa kinad-haria na kimatendo. Na ukoloni ulitambua hakika hii, kwa hivyo kazi walioifanya tangu walipokanyaga miji ya Waislamu ni kuiondoa sharia ya Kiislamu kwenye mashule na mahakama, na badala yake wakaweka sharia za kutungwa. Kwa hiyo wakawaweka mbali Waislamu na dini yao. Qur'an yao na Sunna ya Mtume wao, tutalifafanua hilo kila itakapohitajika.

3

3

Kaashif3-13.jpgKaashif3-14.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

Ama akifuata njia ya chuki na uhasama, basi njia hiyo itanasibika na mtu pekee wala haina-sibiki na Mwenyezi Mungu, kwa sababu mtu ameifuata kwa radhi yake na akaiona ni bora kuliko njia ya maafikiano; wala haifai kuinasibisha kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu Mwenyezi Mungu amemkataza.

Unaweza kuuliza tena: Kwa nini Mwenyezi Mungu amemwezesha mtu kuifanya shari ambapo ilikuwa inatakikana ampe hima ya kuaacha na kufanya heri tu?

Jibu: Lau Mwenyezi Mungu angelifanya hivi, binadamu asingebakiwa na fadhila yoyote wala vitendo visingekuwa na sifa ya heri na shari au vizuri na vibaya. Kwa sababu sifa hizi zinafungamana na matakwa ya mtu na hiyari yake. Bali lau Mwenyezi Mungu ange-limfanya mtu kufanya kitu fulani tu, kusingelikuwako na tofauti ya mtu na mawe au tofauti na unyoya ulio katika mavumo ya pepo. Kwa ajili hii na kwa ajili ya kudumu mtu na utu wake, hakutaka Mwenyezi Mungu kuwalazimisha watu kwenye kitu fulani

"Na kama angelitaka wasingelipigana."

Kwa ufupi kupigana ambako kumepatikana kati ya watu sio kama kumekhalifu matakwa ya Mwenyezi Mungu yanayoitwa Kun fa yakun. Isipokuwa kumekhalifu matakwa ya Mwenyezi Mungu ya sharia yake, ambayo ni ubainifu na uongozi; na hekima yake imetaka kumpa mtu uwezo wa kutosha wa kufanya heri na shari, ili ajichagulie yeye mwenyewe uongozi na heri na awe ni mtu anayetofautiana na mawe na wanyama.

254. Enyi mlioamini! Toeni katika vile tulivyowapa. Kabla haijafika siku ambayo hapatakuwa na biashara wala urafiki wala uombezi. Na makafiri ndio madhalimu.

Kaashif3-15.jpg

KUTOA Ay a ya 254:

MAANA

Mwenyezi Mungu amehimiza kutoa mali kwa mifumo mbali mbali. Yameshatangulia maelezo katika tafsiri ya Aya 245; na unakuja tena mfano wake katika Aya hii:

Enyi mlioamini! Toeni katika vile tulivyowapa.

Mwenyezi Mungu anahimiza kutoa pamoja na kuashiria kwamba mali iliyo na watu ni

4

4

Kaashif3-16.jpgKaashif3-17.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

mali Yake aliyoitoa Yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t.); na kwamba kesho fursa itakosekana, kwa hivyo ni juu ya mumin mwenye akili kuchukua fursa kabla ya kupitwa na wakati.

Kabla haijafika siku ambayo hapatakuwa na biashara wala urafiki wala uombezi.

Makusudio ya biashara hapa ni kulipa fidia ili kujikomboa na moto kwa mali; urafiki ni urafiki wa kusameheana na uombezi na kuombewa na mtu mwingine kuepukana na moto.

Maana yake ni kwamba kesho mtu atakuja peke yake hana chochote isipokuwa amali njema . Aya hii ina maana sawa na Aya ya 48 ya Sura hii. Tumeuzungumzia uombezi katika Aya hiyo.

Na makafiri ndio madhalimu.

Wamejidhulumu wenyewe kwa kuacha amali njema ambayo inawaokoa na adhabu. Kwa

ujumla ni kuwa neno dhulma na ukafiri yanakuja katika matumizi ya maana mamoja.

Mara nyingine hutumiwa ukafiri katika dhulma, kama alivyosema Mwenyezi Mungu

(s.w.t.):

"... Hakika ushirikina ni dhulma kubwa." (31:13)

Na mara nyingine hutumiwa dhulma katika ukafiri, kama alivyosema Mwenyezi Mungu

(s.w.t.):

"...Lakini madhalimu wanakanusha ishara za Mwenyezi Mungu..." (6:33)

255. Mwenyezi Mungu hakuna mola ila Yeye Aliye hai msimamizi wa kila kitu. Hakumshiki kusinzia wala kulala. Ni Vyake vilivyomo ardhini na vilivyomo mbinguni. Na ni nani huyo awezaye kuombea mbele Yake bila ya idhini Yake. Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawalijui lolote lililo katika elimu Yake ila kwa alitakalo. Elimu Yake imeenea mbingu na ardhi. Wala hakumshindi kuzilinda. Na Yeye ndiye Mtukufu aliye Mkuu.

Kaashif3-18.jpg

5

5

Kaashif3-19.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

 

Ay a ya 255:AYA YA KURSIY

MAANA

Mwenyezi Mungu hakuna mola ila yeye aliye hai, Msimamizi wa kila kitu.

Mwanafalsafa mashuhuri wa elimu inayohusika na mambo ya Mungu, aitwaye Mulla Sadra anasema: Neno Allah (Mwenyezi Mungu) linafahamisha kupwekeka dhati Yake Mwenyezi Mungu na sifa Zake. Kufahamisha juu ya kupwekeka katika dhati, ni kwamba jina hili tuku-fu haliitiwi mtu mwingine kiuhakika wala majazi. Mwenyezi Mungu anasema: "... Basi mwabudu Yeye tu na udumu katika ibada Yake. Je, unamjua (mwingine) mwenye jina lake?" (19:65)

Ama kufahamisha kupwekeka Kwake katika sifa, ni kwamba jina hili linafahamisha juu ya dhati yenye kukusanya kila sifa za ukamilifu na utukufu, kinyume cha majina mengine kama; Mjuzi, Mweza na Muumbaji, ambayo umoja wake haufahamishi isipokuwa umoja wa maana katika elimu, au uweza au utendaji.

Unaweza kuuliza: Hakika sifa za ukamilifu na utukufu ni nyingi na zenye kubadilika kulin-gana na kueleweka kwake; vipi ifae kusema zimepwekeka na tunaziona zinahisabika na kubadilika?

Jibu: Ukisema huyu ni mtu mjuzi yataeleweka mambo mawili -

Sifa na Mwenye kusifiwa; na vyote ni vitu tofauti. Mtu sio ujuzi na ujuzi sio mtu. Hayo ni kwa upande wa kiumbe. Ama kwa upande wa Muumbaji hakuna jingine isipokuwa kuweko kiutukufu; na huko kuweko ndiko ujuzi ndiko uwezo, na ndiko hekima, n.k. Hakuna sifa na mwenye kusifiwa vyote ni vimoja tu; na huku hakukufanana na kitu kingine.

Hakuna mola ila Yeye

Inasemekana maana yake ni hakuna anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Yeye. Lakini kueleweka kwake ni hakuna yoyote mwenye kukusanya sifa za uungu isipokuwa Yeye. Vyovyote iwavyo, maana zote mbili ni zenye kulazimiana.

Aliye hai Msimamizi wa kila jambo

Ukiunasibisha uhai kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, maana yake yanakuwa ni kukua, kuhisi na utambuzi. Lakini ukiunasibisha kwa Mwenyezi Mungu unakuwa ni elimu na uweza.

Makusudio ya kusimamia kila kitu ni kukisimamia katika mambo yake na kukipangilia vizuri. Mwenyezi Mungu anasema: "Akasema: Mola wetu ni Yule aliyekipa kila kitu umbo lake kisha akaongoza." (20:50)

Na amesema tena: "....Na ameumba kila kitu akakikadiria kipimo (chake)." (25:2)

Mulla Sadra anasema: Kauli ya Aliye Hai inafahamisha kwamba Yeye ni Mjuzi na Muweza. Na kauli ya Msimamizi wa kila kitu inafahamisha kuwa Yeye ni Mwenye kujisimamia Mwenyewe na kumsimamia mwingine. Kwa hiyo sifa mbili hizi ni zenye kuafikiana katika maana na ni zenye kuingiliana."

Anakusudia kuwa usimamizi hauepukani na uhai; kama vile ambavyo uhai kwa maana ya uwezo na elimu hauepukani na usimamizi.

MWENYEZI MUNGU NA DESTURI YA MAUMBILE

6

6

Kaashif3-20.jpgKaashif3-21.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Unaweza kuuliza: Je maana ya kusimamia Mungu juu ya mipango ya vitu vyote, ni kwam-ba mambo yote ya dhahiri ya kimaumbile mpaka mafungu yake yanasimamiwa na Mwenyezi Mungu moja kwa moja Yeye Mwenyewe bila ya kuweko kati sababu yoyote ya kimaada; kama inavyodhihiri katika Aya isemayo:

"Kisha tukamfanya tone la manii, katika makao madhubuti . Kisha tukaliumba tone hilo kuwa pande la damu, na tukaliumba pande la damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa na mifupa tukaivika nyama, kisha tukalifanya umbo jengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu mbora wa waumbaji." (23:13-14)

Kwa sababu yenye kuja haraka fahamuni katika Aya hii, ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameingilia Yeye Mwenyewe moja kwa moja kwenye makuzi mbali mbali ya tone la manii; na tunajua kuwa nadharia ya kielimu inasema kuwa tone la manii linakuwa na kuzi-di kulingana na kanuni maalum?

Katika kujibu hayo, hapana budi kupambanua kati ya jambo lisilokuwa la kawaida, kama vile kufufua wafu na kupatisha kitu bila ya kitu kingine, na matukio yanayo kuwa kulingana na kanuni za kimaumbile, kama kupatwa jua mwezi, n.k. Hili la aina ya kwanza linategemezwa kwake Mwenyezi Mungu moja kwa moja. Na hili la aina ya pili linategemea desturi ya maumbile na linategemezwa kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu Yeye ndiye aliyeweka desturi ya maumbile pamoja na vilivyomo ndani yake vikiwa ni pamoja na nguvu na viasili. Viasili hivi kwa kupitia njia zake vinafanya dhahiri za maumbile zikiwa ni pamoja na tone la manii.

"...Na ameumba kila kitu akakikadiria kipimo (chake)."(25:2)

Yaani anakipitisha katika desturi na kanuni za kitabia. Lau angelikuwa Yeye Mwenyezi Mungu ndiye anayesimamia umbile moja kwa moja bila ya kuweko kati kitu kingine, kusin-gelikuweko na sababu na msababishaji.

Kwa hivyo basi, inatubainikia kuwa kila mwenye kuamini kwamba kila tukio la kimaumbile linategemea Mwenyezi Mungu moja kwa moja bila ya kuweko kati sababu yoyote yenye kuhisiwa ambayo imegunduliwa na utaalamu au inaweza kugunduliwa, mtu huyo atakuwa mjinga mwenye kukosea katika imani yake. Na lau ingelikuwa sahihi imani yake hii, kusin-gelikuweko na wajibu wa kitendo chochote na elimu isingelikuwa na faida yoyote; wala uvumbuzi na maendeleo ya mtu yasingekuwa na athari yoyote.

Vile vile amekosa yule mwenye kuitakidi kwamba maumbile ndio kila kitu, kuwa ndiyo sababu ya kwanza na ya mwisho, wala hakuna kitu nyuma yake. Hayo ni makosa. Kwani kama ni hivyo kusingelikuwa na nidhamu wala athari yake na kungelikuwa na migongano na natija ingelikuwa kutokuwepo elimu wala uhai.

Haya tumeyafafanua zaidi katika Aya ya 21 ya Sura hii, kifungu cha Tawhid. Hakumshiki kusinzia wala kulala.

Mwenyezi Mungu alipobainisha kwamba Yeye ni Hai Msimamizi wa kila jambo, ameende-lea kulitilia mkazo hilo kwamba Yeye ni Mwenye kutukuka, haumzuwii usingizi wala kusa-hau au kitu chochote, katika kupanga kuumba Kwake kwa njia ya ukamilifu. Kwa sababu hilo linapingana na ukubwa Wake na kujitosha Kwake na kila kitu. Imam Ali amesema akimwambia Mola wake: "Sisi hatujui kiasi cha ukubwa wako, isipokuwa tunajua kuwa Wewe ni Aliye Hai wa Milele, Msimamizi wa kila jambo, hakukushiki kusinzia wala kulala; hutazamwi; wala halikuoni jicho, lakini Wewe unaliona; umezithibiti amali na ukazishika

7

7

Kaashif3-22.jpgKaashif3-23.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

barabara."

Ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini

Makusudio ya vilivyomo ni ulimwengu wote na kila kilichomo ndani yake hakitoki nje ya ufalme Wake na mipangilio Yake. Imam Ali (a.s.) aliulizwa kuhusu: "Hapana hila wala nguvu isipokuwa kwa msaada wa Mwenyezi Mungu."

Akajibu: "Sisi hatumiliki chochote mbele ya Mwenyezi Mungu, wala hatumiliki isipokuwa kile tulichomilikishwa; na anapomilikisha kile ambacho amekimiliki zaidi kuliko sisi, basi ame-tukalifisha nacho; na anapokiondoa, huwa ametuondolea taklifa."

Na ni nani huyo awezaye kuombea mbele Yake bila ya idhini Yake.

Umekuja mfumo wa swali kwa maana ya kukanusha; yaani hataombea yeyeote mbele Yake isipokuwa kwa amri Yake na hayo ni jibu na kubatilisha kauli ya washirikina kwamba masanamu ndiyo yanayowakurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu anawasimulia hao kwa kusema: "... Na wanasema: hao ndio waombezi wetu mbele ya Mwenyezi Mungu! Sema: 'Je, mnamwambia Mwenyezi Mungu asiyoyajua katika mbingu wala katika ardhi? ..." (10: 18)

Tumekwisha zungumzia uombezi katika Aya ya 48. Baadhi ya ulama wamesema kwamba siku ya Kiyama kutakuwa na aina mbalimbali za watu. Kama ifuatavyo:- Waliotangulia ambao ni wenye kukurubishwa; watakaokuwa upande wa kuume ambao ni watu wema watakaookoka, watakaokuwa upande wa kushoto ambao ni waovu watakao adhibiwa, na watakaokuwa na msamaha ambao amali zao njema zimechanganyika na maovu. Na hawa watakubaliwa kuombewa; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

" Na wengine walikiri dhambi zao, wakachanganya vitendo vyema na vingine viovu, huen-da Mwenyezi Mungu akapokea toba yao. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kusamehe Mwenye kurehemu." (9:102)

Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao.

Maana yake ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.), anajua yaliyokuwa na yatakayokuwa katika waja wake, iwe heri au shari; na anamjua mwombezi na anayeombewa na anayestahiki msamaha na thawabu au adhabu na mateso. Ikiwa mambo yako hivyo, basi uombezi (shafaa) hauna nafasi yoyote isipokuwa kwa amri Yake Mwenyezi Mungu kwenye mipaka Yake anayoridhia.

Wala hawalijui lolote lililo katika elimu Yake ila kwa alitakalo.

Dhamiri katika hawalijui inawarudia waja wote wakiwemo Malaika na Mitume. Makusudio ya elimu ni linalojulikana. Maana yako wazi. Ukipenda kujua zaidi unaweza kuangalia Aya hizi:" Yeye ni mjuzi wa siri; wala hamdhihirishii yoyote siri Yake isipokuwa Mtume aliyem-ridhia ..." (72: 26-27) "... Utakatifu niwako! Hatuna elimu isipokuwa ile uliyotufundisha ..." ( 2: 32)

Elimu Yake imeenea mbingu na ardhi.

Kauli zimekuwa nyingi na zimegongana kuhusu maana ya neno Kursiy. Baadhi ya kauli hizo ni za kumzungumzia Mwenyezi Mungu bila ya elimu, lakini bora ya kauli ni mbili: Ya kwanza, ni fumbo la utukufu Wake Mwenyezi Mungu na cheo chake yaani enzi. Ya pili, ni elimu; yaani elimu Yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) imezunguka kila kitu. Mpangilio wa maneno unarudia maana haya.

Kaashif3-24.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Wala hakumshindi kuzilinda na Yeye Ndiye Mtukufu aliye Mkuu

Yaani hakumtii mashaka wala uzito wowote kuilinda mbingu na ardhi na kupangilia vizuri yaliyomo ndani yake. Vipi isiwe hivyo! Na hali kuumba nzi na kuumba ulimwengu Kwake ni sawa tu; maadamu Yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t.) "... Akitaka chochote ni kukiambia kuwa, kikawa." (36:82)

KITU BILA YA KITU

Kutengeneza vitu kuko aina mbili: kutegeneza kitu kutokana na maada na kutengeneza bila ya maada. Na kunatofautiana kwa njia nyingi.

1.            Anayetengeneza kwa maada anahitaji harakati na zana, lakini asiyetengeneza kwa maada hahitaji.

2.            Wa maada anachoka, lakini asiyetumia maada hachoki.

3.            Mwenye kutumia maada hawezi kupata kitu bila ya kitu kingine, lakini kwa asiyetumia, hilo sio jambo zito.

Kwa hivyo inabainika kwamba kumlinganisha Muumbaji na Mwenye kuumbwa ni kulingan-isha na kisicholingana.

Itawezekana vipi kumfananisha mwenye kujitosha na mwenye kuhitajia; atakuwaje sawa na mwenye kushindwa?

256.        Hakuna kulazimisha katika dini; uongofu umekwisha pambanu-ka na upotofu. Basi anayemkataa taghuti na akamwamini Mwenyezi Mungu, hakika yeye ameshika kishiko madhubuti kisichovunjika. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mjuzi.

257.    Mwenyezi Mungu ni mtawala wa wale walioamini; huwatoa gizani na kuwaingiza katika mwangaza, lakini walio kufuru watawala wao ni mataghuti. Huwatoa kwenye mwangaza, na kuwaingiza katika giza, hao ndio watu wa motoni, watadumu humo.

Kaashif3-25.jpgKaashif3-26.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Ay a ya 256 - 257: HAKUNA KULAZIMISHA KATIKA DINI

MAANA

Hakuna kulazimishwa katika dini

Lau tungeiangalia jumla hii peke yake, tungelifahamu kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakuweka hukumu yenye aina yoyote ya kulazimisha na kwamba anayolazimishwa mtu katika kauli au vitendo hayaambatani na kitu chochote katika mtazamo wa sharia, si katika dunia wala akhera.

Lakini kauli Yake Mwenyezi Mungu "Uongofu umekwisha pambanuka na upotofu", ambayo ndiyo sababu ya kuacha kulazimisha, inaonyesha kuwa neno katika, hapa lina maana ya juu ya; Yaani uislamu haumlazimishi yeyote kukubali isipokuwa unamlazimisha mpinzani kwa hoja na dalili tu; kama inavyosema Qur'an: "Na sema: (Huu) ni ukweli uliotoka kwa Mola wenu, basi anayetaka na aamini na anayetaka na akufuru ..." (18:29) "... Je, wewe utawashurutisha watu kwa nguvu wawe waumini? (10:99)

Unaweza kuuliza: Hakika dini haiwezekani kufungamana na kulazimishwa, kwa sababu dini ni katika mambo ya moyo yaliyo nje ya uwezo. Sawa na kuleta picha ya kitu akilini. Vinavyoweza kufungamana na kulazimishwa ni kauli na vitendo ambavyo inawezekana kutendeka bila ya matakwa ya msemaji na mtendaji. Kwa hivyo umepita njia gani mpaka ukasema habari ya kukataza kulazimishwa juu ya dini?

Jibu: Hakika kauli Yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.): "Hakuna kulazimishwa katika dini" Imekuja kwa tamko la kuelezea habari. Kama hivyo ndivyo, basi swali litakuwa halina msin-gi, kwa sababu maana yatakuwa dini ni itikadi na hilo ni jambo linalorudia kwenye kukubali ambako mtu halazimishwi kukubali. Ikiwa tamko limekuja kwa kukusudiwa kukataza, basi maana yatakuwa ni: Enyi Waislamu msimlazimishe yeyote kusema "Lailaha illa Llahu Muhamadurasuli Llahi." baada ya kuwako hoja na dalili juu ya Tawhid na Utume.

Lakini jibu hili linaweza kuzalisha swali jipya kwamba hayo hayataafikiana na kauli ya Mtume (s.a.w.): "Nimeamrishwa nipigane na watu mpaka waseme: 'Laillahailla Ilah'; wakisema hivyo, basi damu zao na mali zao zimehifadhika na mimi."

Jibu: uislamu unaruhusu kupigana kwa sababu mbali mbali. Miongoni mwa sababu hizo ni: Kujikinga - Mwenyezi Mungu anasema: "Na piganeni katika njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanaowapiga, wala msipituke mipaka." (2: 190). Kudhulumiwa - Mwenyezi Mungu anasema : "... Lipigeni (kundi) lile linaloonea (wenzao) mpaka lirudi katika amri ya Mwenyezi Mungu ..." (49:9)

Kupigana ili kuudhihirisha uislamu, ijapokuwa ni kwa ulimi. Hilo ni kwa ajili ya maslahi yanayowarudia wote, sio waislamu peke yao. Na maslahi haya anayakadiria aliye Masum au naibu wake; wala haifai kwa mwislamu yeyote, vyovyote alivyo, kupigana kwa ajili ya kutamkwa tamko la uislamu au kuueneza, isipokuwa kwa amri ya Masum au naibu wake,

ambaye ni mujtahid*2 mwadilifu.

2 Mujtahid aliye marjaa: yaani kiongozi anayefuatwa katika madhehebu ya Shi'a katika zama za kughibu kwa Imam Mahdi (a.s)

10

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Ni kwa njia hii peke yake ndio inachukuliwa Hadith "Nimeamrishwa nipigane na watu ..."; Yaani mimi nitapigana nao nitakapoona mimi au kaimu wangu kwamba maslahi ya kiutu yanalazimisha kupigana kwa ajili ya 'Lailaha ilia Hah'.

Hapo inaonyesha kuwa kupigana kwa kujikinga au kuikinga dini na haki, hakungojei idhini ya yeyote. Tumekwisha yaeleza hayo katika tafsiri ya Aya ya 193 kifungu cha 'Uislamu unapiga vita dhulma na ufisadi.'

Uongofu umekwisha pambanuka na upotofu.

Makusudio ya uongofu hapa ni imani na upotofu ni ukafiri.

Mwenyezi Mungu amekwisha ibainisha haki kwa uwazi zaidi, na ubainifu na dalili zenye nguvu, mpaka kafiri akaishiwa na hoja au udhuru wowote. Mwenye kuijua njia ya haki na ya uongofu atakuwa amekwisha ijua njia ya upotofu na ya batili. Kwani hakuna kitu kingine baada ya haki isipokuwa upotofu.

Mulla Sadra anasema: Maana ya uongofu umekwisha pambanuka na upotofu ni kuitambua haki kutokana na batili na imani kutokana na ukafiri kwa dalili na hoja pamoja na kuzifahamu na kuziangalia vizuri. Yeyote mwenye kuikubali haki kwa kufuata tu, hana tofauti na mnya-ma. Hata hivyo mwenye kuwafuata watu wema kwa nia njema na kwa dhamiri nzuri ataya-pata yale watakayoyapata wao kesho.

Basi anayemkataa taghuti na akamwamini Mwenyezi Mungu, hakika yeye ameshika kishiko madhubuti kisichovunjika.

Kauli zimekuwa nyingi kuhusu tafsiri ya taghuti, baadhi ya wafasiri wamefikisha kauli tisa. Miongoni mwa hizo ni kuwa makusudio yake ni shetani. Nyingine ni dunia iliyo twevu. Iiliyo karibu na ufahamu na yenye kufahamisha kutokana na tamko lenyewe, ni kauli ya Sheikh Muhammad Abduh kwamba taghut ni yule ambaye kwa kumwabudu na kumwamini yeye, ndiyo sababu ya kupetuka mpaka na kutoka katika haki.

Makusudio ya kishiko madhubuti, ni kwenda kwenye njia iliyonyooka ambayo hapotei mwenye kuifuata. Maana kwa ujumla ni kwamba kumwamini Mwenyezi Mungu ni kishiko cha kutegemewa hakikatiki milele na kwamba mwenye kushikamana nacho hapotei.

Katika Sahih Muslim anasema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: Hakika mimi ninaacha kwenu vitu ambavyo kama mkishikamana navyo hamtapotea baada yangu, kimo-jawapo ni kikubwa kuliko kingine, nacho ni kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba yenye kuvutwa kutoka mbinguni hadi ardhini na kizazi changu Ahlul Bait wangu, vitu viwili hivyo havitaachana mpaka vije kwangu kwenye birika." Hadith hiyo pia imepokewa na Tirmidhyi.

Lakini hivi sasa vitu vyote hivyo viwili vimeachwa. Ndio Imam Ali (a.s.) akasema: "Utakuja wakati Qur'an haitabaki isipokuwa maandishi yake na Uislamu utabaki jina lake tu."

Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mjuzi.

Anasikia tamko la Tawhid kutoka kwa waumini, na la kufuru kutoka kwa makafiri; na anajua yaliyo katika nyoyo za watu wawili na atamlipa kila mmoja kwa amali zake.

11

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Mwenyezi Mungu ni mtawala wa wale walioamini; huwatoa gizani na kuwaingiza kati-ka mwangaza.

Wafasiri wametofautiana sana katika Aya hii. Baadhi yao wakazalisha mushkeli wa kiitika-di; mpaka Mulla Sadra akasema: "Kuna mushkeli mkubwa ambao ni vigumu kuutatua kwa wenye fahamu." Sheikh Muhammad Abduh amesema: "Hakika baadhi ya tafsiri ni tafsiri za wafasiri wasiokuwa wataalamu ambao hawafahamu mifumo ya lugha ya hali ya juu, au ni tafsiri za wasiokuwa Waarabu ambao zaidi huwa hawafahamu."

Ama sababu ya kutofautiana wafasiri na kuzalisha matatizo ya kiitikadi ni kwamba wao wamefahamu Aya kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni mtawala na mwangalizi wa mambo ya waumini tu; na wala sio kwamba waumini wanamfanya Yeye tu kuwa ni mtawala na mwangalizi wa mambo yao. Hapo kuna tofauti kubwa kati ya maana hizi mbili. Kuanzia hapa ndipo umekuja mushkeli katika wanavyofahamu wafasiri, kwamba utawala wa Mwenyezi Mungu na msaada Wake unakuwa kwa viumbe vyote katika nidhamu moja; na wala sio kwa waumini tu.

Vyovyote itakavyokuwa, kauli za wafasiri au wengi wao hazioani na mfumo, na kwamba maana yaliyo salama, ambayo hayana matatizo yoyote na yanayoafikiana na kauli Yake Mwenyezi Mungu, Basi anayemkataa taghuti na akamwamini Mwenyezi Mungu, hakika yeye ameshika kishiko madhubuti kisichovunjika ni kuwa waumini hawamfanyi mtawala asiyekuwa Mwenyezi Mungu wala hawamfanyi yeyote kuwa mlinzi wao isipokuwa Mungu pekee Yake; Kwake wanakimbilia, na kwa Kitabu Chake na sunna ya Mtume Wake wanaongoka katika itikadi zao, kauli zao na vitendo vyao. Wala hawategemei watu wapote-vu na mataghuti, hata wawe vipi. Kinyume chake ni makafiri ambao wanawafanya mataghuti ndio watawala wao.

Hapana mwenye shaka kwamba mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu na akaendelea kumtii na kuongoka kwa Aya Zake na ubainifu Wake kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu na msaada Wake atasalimika kutokana na giza la bid'a na upotevu,

vilevile matamanio na ujinga. Na atapata mwanga kwa nuru ya maarifa ya kweli na imani sahihi. Hayo ndiyo maana ya Huwatoa gizani na kuwaingiza katika mwangaza.

Lakini waliokufuru, watawala wao ni mataghuti. Huwatoa kwenye mwangaza na kuwiangiza katika giza.

Maana kwa ujumla ni kuwa makafiri wanawafanya watu wapotevu na mataghuti kuwa watawala wao badala ya Mwenyezi Mungu; wanachukua amri zao na kuacha makatazo yao. Hawa wanakwenda katika njia ya kuhiliki na wanawatoa kwenye mwangaza wa akili na maumbile na kuwatia katika giza ukafiri na uzushi.

KUDUMU MOTONI 

Watadumu humo.

Mara nyingi sana Qur'an imetaja kuwa kuna aina ya waasi watakaodumu motoni; na ime-bainisha kuwa miongoni mwa aina hii ni: Mwenye kumkufuru na akakadhibisha Aya zake. Mwenyezi Mungu anasema: "Na wale ambao wamekufuru na kukadhibisha ishara zetu, hao ndio watakoakuwa watu wa motoni, humo watadumu." (2:39)

12

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Mwenye kumua mumini kwa makusudi, Mwenyezi Mungu anasema: "Na mwenye kumuua Muumin kwa kukusudia, basi malipo yake ni Jahannam, humo atadumu ..." (4:93)

Mwenye kumwasi Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na kuruka mipaka. Mwenyezi Mungu anasema: "Na anayemuasi Mwenyezi Mungu na Mtume, na kuiruka mipaka ya Mwenyezi Mungu, atamwingiza motoni, humo atadumu." (4:14)

Mwenye kuzungukwa na makosa yake; Mwenyezi Mungu anasema:

"Ndio wanaochuma ubaya na makosa yao yakawazunguka, hao ndio watu wa motoni,

humo watadumu." (2:81)

Hapana mwenye shaka kwamba kwa mujibu wa uadilifu Wake Mwenyezi Mungu, hamwad-hibu isipokuwa mwenye kustahili adhabu na adhabu yake inatofautiana kwa ukali na udhai-fu kulingana na makosa na maasi. Kosa la mwenye kuhangaika akieneza ufisadi duniani, akaangamiza mimea na viumbe, si sawa na kosa la mwenye kuiba shillingi moja au aliyem-sengenya anayeshindana naye katika kazi.

Pamoja na haya tunaweza kujiuliza. kudumu katika moto kusikokuwa na mwisho, kugong-wa kichwa kwa macheche yaliyo kama majumba, kuvurumishiwa marungu ya chuma mgongoni na kujazwa tumbo kwa maji ya usaha; kisha mtu asife akapumzika wala asipun-guziwe angalau akapumua; mtu huyu ambaye anaumizwa na chawa na kufa kwa kusong-wa koo na jasho humfanya anuke; kama alivosema Amirul Muminin Ali (a.s.). Tujiulize je machungu yote haya makubwa kwa mnyonge huyu mwenye kushindwa na chawa, yanaafikiana na dhati ya Mwenyezi Mungu ambaye ni heri tupu na rehema, ukarimu, neema, upole na hisani?" Je inaingilika akilini mtu huyu kuadhibiwa milele au kunyimwa kabisa neema ... Au huko kuwa milele na kila ngozi inapoiva kubadilishwa ngozi nyingine bila ya kupumzika, yote hayo ni ya kujiuliza.

Akisema msemaji: Hakuna adhabu ambayo itazidi ya mwenye kumuua Hussein bin Ali (a.s.) au aliyetupa bomu la Atomic au Haidrojeni kwa watu na akawamaliza wote, au mwenye kuanzisha mambo mabaya, yakadumu na uovu wake ukazidi?

Jibu: Ni kweli kuwa hazidi yeyote katika uliowataja, lakini sio kila asi ni Yazidi wala sio kila bomu ni Atomic na Hadrojeni; wala sio kila desturi inawatawanya watu. Lakini swali halikuwa juu ya hawa, bali swali ni juu ya kudumu walio na daraja nyingine.

Unaweza kusema: Maelezo ya Qur'an na Hadith za Mtume juu ya kudumu milele utazi-fanyaje?

Jibu: Hakuna katika hizo inayokataa Taawil.

Ukisema tena kuwa, kila kilicho elezwa ikiwa kukielewa kunawezekana kwa dhahiri, basi ni wajibu kudumu juu ya dhahiri yake, kwa hiyo kudumu wakosaji katika moto si muhali.

Jibu: Ndio, lakini lichukuliwe la kudumu muda mrefu badala ya milele, kwa kukusanya kati ya Qur'an na dalili za rehema ambako, hakukataliki wala hakupingwi na sharia na akili.

Utasema mara ya tatu: Hakika mafaqihi hawawezi kuridhika na jawabu hili, kwa sababu wao hawaruhusu kuchukulia kinyume cha dhahiri ya tamko isipokuwa kwa sababu tatu: Kuunganisha na kitu kingine kwa kidesturi, kama vile kuchukulia mahsus kutoka katika jumla; au kisheria, kama kauli wazi yenye kuthibiti kutoka kwa Masum; au kiakili

13

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

kusikokubali uwezekano wa kinyume, Na sisi hatuna chochote katika hivyo vitatu.

Jibu: Kwanza: Ninadhani kuwa mafaqihi waliozitambua dalili za rehema ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) wataafikiana nami, kwamba inawezekana kuziacha dhahiri za dalili za kudu-mu milele katika moto kwa baadhi ya wakosaji. Miongoni mwa dalili hizo ni Hadith Qudsi: "Rehema yangu imeshinda ghadhabu yangu." Vilevile Hadith tukufu inayosema: Hakika waombezi siku ya Kiyama ni wengi na mwisho wa waombezi ni mwenye kurehemu wenye kurehemu. Na kwamba rehema yake Mwenyezi Mungu itaenea siku ya Kiyama mpaka ibil-isi atakuwa na tamaa na kunyoosha shingo yake.

Katika baadhi ya riwaya ni kwamba Hassan al Basri alisema: "Si ajabu kwa aliyeangamia, kuwa vipi ameangamia. Lakini ajabu ni ya mwenye kuokoka vipi ameokoka." Imam Zainul Abidin (a.s.) akasema: "Ama mimi ninasema; sio ajabu kwa aliyeokoka kuwa ameokoka vipi; isipokuwa ajabu ni kwa aliyeangamia kuwa ameangamia vipi pamoja na ukubwa wa rehema ya Mwenyezi Mungu!"

Tukiiunganisha riwaya hii na Aya inayosema:

"Sema! Enyi waja wangu waliojidhulumu! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu;

hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote ..." (39:53).

Tunapata ulinganisho mkataa wa kuacha dhahiri ya dalili za kudumu milele motoni.

Pili: Sisi tunazungumza mambo ya kiitikadi mkataa, sio masuala ya matawi ya kudhania; na mafaqihi pamoja na kujichunga kwao na nguvu ya imani zao, wanakuwa ni wataalamu wa hukumu za Mwenyezi Mungu za kisharia sio mambo ya itikadi. Bali wengi katika wao wako katika daraja ya kufuata yale yanayorudia sifa za Mwenyezi Mungu na vitendo Vyake.

Ama yale yanayorudia kwenye dalili za kuweko Muumbaji (s.w.t.) ni dalili za mzunguuko na kuendelea. Hata hivyo ni lazima ieleweke kuwa sisi tunaamini kuswihi kufuata katika misingi ya itikadi ikiafikana na mambo yalivyo.

Tatu: Akili huona vibaya kukhalifu ahadi, lakini sio kiaga. Ukimwambia mtu mwingine nitak-ufanyia wema; kisha uvunje ahadi, basi utakuwa mwenye kulaumiwa mbele za wenye akili. Ama ukamwambia unayemdai haki: Nitachukua haki yangu tu kutoka kwako kisha umsamehe, basi wewe utakuwa mwenye kusifiwa mbele ya Mwenyezi Mungu na watu; hasa akiwa yule unayemdai ni fukara na wewe ni tajiri. Na Mwenyezi Mungu ni tajiri kwa viumbe na adhabu zao. Na wao wana haja sana ya rehema Yake na msamaha Wake.

Swali la nne na la mwisho: Kwa nini unaleta taawil ya Aya za kudumu motoni na ni maana gani unayoyachukulia?

Jibu: Inawezekana kuchukulia maana ya kudumu muda mrefu, lakini sio milele; au kudumu motoni bila ya adhabu; kama hema la Hatimtai *3 au kuwepo Ibrahim katika moto.

*3 Katika baadhi ya riwaya ni kwamba Hatimtai ataingia motoni kwa sababu ya kufuru yake, lakini atakuwa na hema la kumkinga joto kwa sababu ya ukarimu wake. Huyu alikuwa ni mtu aliyepigiwa mfano kwa ukarimu wake wa kupin-dukia.

14

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

Haya yanatiliwa nguvu na yaliyopokewa katika baadhi ya Hadith kwamba baadhi ya watu wa motoni watakuwa wanacheza na makaa ya moto kama mpira wakirushiana. Hapana mwenye shaka kwamba mchezo huu hauwezi kuwa pamoja na adhabu hata hafifu sik-wambii kali yake. Na Mungu si Mwenye kushindwa kuufanya moto baridi na salama kwa asiyekuwa Ibrahim kama alivyoufanya kwa Ibrahim (a.s.).

Muhhiddin Ibn al Arabi anasema katika al Futuhul Makkiyya J2 uk. 127: "Hatobaki motoni mwenye kumwamini Mungu mmoja katika waliopelekewa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.), kwa sababu moto utarudi kuwa baridi na salama kwa wanaompwekesha Mwenyezi Mungu kwa baraka za Ahlul Bait katika akhera. Ni utukufu ulioje wa baraka za Ahlul Bait!

258. Je, hukumjua aliyehojiana na Ibrahim juu ya Mola wake kwa sababu Mwenyezi Mungu alimpa ufalme ? Ibrahim aliposema: Mola wangu ni yule ambaye huhuisha na kufisha. Yeye akasema: Mimi pia na huhuisha na kufisha. Ibrahim akasema: Hakika Mwenyezi Mungu hulichomoza jua mashariki, basi wewe lichomoze magharibi. Akafedheheka yule aliyekufuru, na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.

Kaashif3-27.jpg

AYA YA 258 ALIYEHOJIANA NA IBRAHIM.

MAANA

Mwenyezi Mungu, katika Aya iliyotangulia, amebainisha kuwa mtawala wa waumini ni Mwenyezi Mungu, na kwamba wao wanatoka katika giza la shaka kuingia kwenye mwangaza wa uongofu na imani. Na makafiri watawala wao ni mataghuti wanaowatoa kwenye mwangaza wa kimaumbile na kuwaingiza katika giza la ukafiri na upotevu.

Baada ya hapo anatoa kisa, kwa Mtume wake mtukufu juu, ya Mumin aliyetoka kwenye giza la shaka na kuingia katika nuru ya imani, katika Aya ijayo. Na kisa cha kafiri aliyehojiana na Ibrahim juu ya Mola wake baada ya kutoka kwenye nuru ya kimaumbile kwenda kwenye giza la ukafiri, katika Aya hii.

Je, hukumjua yule aliyehojiana na Ibrahim juu ya Mola wake, kwa sababu Mwenyezi Mungu alimpa ufalme? Ibrahim aliposema: Mola wangu ni yule ambaye huhuyisha na kufisha. Yeye akasema: 'Mimi pia na huhuyisha na kufisha'

15

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Hii ni hoja anayoitaja Mwenyezi Mungu kwa Mtume na kwa watu wote katika mfumo wa kus-taajabu pamoja na kukanusha.

Ibrahim (a.s.) alitoa mwito wa kutupiliwa mbali masanamu na mataghuti na kuwa kwenye dini ya uadilifu na usawa, lakini akapingwa na watawala., sio kwa kuona mwito wake sio sawa, bali ni kwa kuhofia manufaa na chumo lao na kupupia wasishuke vyeo vyao. Kama kawaida walianza kujadiliana na Ibrahim kwa maneno; waliposhindwa wakawa hawana la kusema, ispokuwa walitangaza vita na wakajaribu kummaliza kwa kumchoma katika moto; sawa na wanavyofanya wakoloni hivi sasa - wanaeneza propaganda za upotevu kwa njia ya magazeti, radio na mashirika ya habari yaliyonunuliwa; wakishindwa wanaanza kampeni za mapinduzi, wakishindwa hutupa mabomu ya Napalm kwa watu wanyonge wasiokuwa na hatia yoyote.

Basi yule ambaye amepetuka mpaka kwa mali na jaha alimuuliza Ibrahim: "Ni nani Mola wako?" Ibrahim akajibu: "Mola wangu ni yule anayempa uhai anayemtaka kisha huuondoa na wala hana anayeshirikiana naye katika hilo." Yule Taghuti akasema: "Mimi pia ninaweza hivyo." Akawaleta watu wawili; akamwua mmoja wao na kumwacha mwingine. Ibrahim alipoona kujigamba kwa Taghuti kwa kutegemea, maneno na kujitia kutofahamu hoja na maana halisi yaliyokusudiwa, alileta mfano mwingine ambao hauwezi kuingizwa makosa wala madai yoyote, akasema:

Hakika Mwenyezi Mungu hulichomoza jua Mashariki, basi wewe lichomoze Magharibi. Akafedheheka yule aliyekufuru.

Kwa sababu alishindwa kubabaisha na kupotosha. Hivi ndivyo anavyojaribu kufanya kila mbatilifu - kujisifu na kufanya hila; hila zinaposhindwa hudangana akawa hana la kufanya.

Kundi la wafasiri wamesema kuwa ni jawabu la pili la Ibrahim; la kwanza ni 'Ambaye huhuisha na kufisha' na la pili ni 'Basi wewe lichomoze magharibi' ili akate mjadala upesi bila ya kurefusha.

Razi na Sheikh Muhmmad Abduh, wanasema kuwa hilo ni kuleta mfano mwingine ili kufafanua zaidi dalili; kwa maana yakuwa yule ambaye anatoa uhai ndiye ambaye anali-chomoza jua kutoka mashariki; na kama ukiweza kuwafunika watu wako kwa mfano wa kwanza basi utashindwa kuwafunika katika mfano huu.

Vyovyote itakavyokuwa, iwe ni majibu mawili au mifano miwili, lakini ni kwamba kafiri alishindwa na kuzibwa mdomo; na alishindwa kwa vile hana haki, naye hana haki, kwa vile ni kafiri.

Na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu. Ambao wamejidhulumu kwa kui-nusuru batili na kuipinga haki.

Aya haikutaja jina la Taghuti kwa sababu, muhimu ni kupata mazingatio ya kisa sio jina la mhusika. Imetangaa kwamba alikuwa ni Namrud bin Kan'an bin Sam bin Nuh. Inasemekana kwamba yeye ndiye wa mwanzo kuvaa taji kichwani; akatakabari na kudai uungu. Tutarudia kuelezea kisa cha Ibrahim na watu wake katika Sura ya Anbiya (Mitume) na sehemu nyinginezo.

16

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

259. Au kama yule aliyepita karibu na mji nao umeangukiana sakafu zake, akasema: Mwenyezi Mungu atauhuisha vipi (mji) huu baada ya kufa kwake? Mwenyezi Mungu akamfisha kwa miaka mia, kisha akamfufua, akamuuliza: Umekaa muda gani? Akasema: Nimekaa muda wa siku moja au sehemu ya siku. Akasema: Bali umekaa miaka mia, tazama chakula chako na kinywaji chako hakikuharibika. Na mtazame punda wako na ili tuk-ufanye uwe ni ishara kwa watu. Na itazame mifupa jinsi tunavy-oinyanyua, kisha tunaivisha nyama. Basi yalipombainikia alise-ma: Najua kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye uwezo juu ya kila kitu.

ALIYEPITA KARIBU NA MJI Aya ya 259

MAANA

Aya iliyotangulia ilikuwa ni mfano kwa kafiri ambaye amemfanya Taghuti kuwa ni mlinzi na mtawala wake, na kutoka katika mwangaza na kuingia katika giza; na Aya hii ni mfano wa Mumin aliyemfanya Mwenyezi Mungu kuwa mtawala wake; akatoka gizani na kuingia katika mwangaza.

Au kama yule aliyepita karibu na mji nao umeangukiana sakafu zake akasema: Mwenyezi Mungu ataufufua vipi (mji) huu baada ya kufa kwake?

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakufafanua jina la mji wala jina la aliyepitia. Hapo ndipo wakahi-talifiana wafasiri - kwamba je, mtu huyo alikuwa kafiri, je alikuwa Uzairi (Ezra), Armila (Nehemia) au Khidhr? Vile vile wametofautiana kuhusu mji, je ulikuwa Baitil Maqdis au mji mwingine?Hakuna dalili yoyote juu ya hayo isipokuwa Hadith za Kiisrail tu.

Maana ya mji ulioangukiana sakafu zake ni kuwa hauna watu na majumba yamevunjika umebaki magofu; na swali lilikuwa la kuuliza kufufuliwa watu wa mji sio mji wenyewe.

Kaashif3-28.jpg

17

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Yule anayedai kuwa aliyepita katika mji alikuwa kafiri kwa vile alitia shaka katika kudura ya Mwenyezi Mungu, tunamwambia kuwa, sio kila anayepitiwa na shaka akilini mwake na akataka ufafanuzi, ni kafiri; bali ni kinyume cha hivyo. Ibrahim alimtaka Mola wake amuonyeshe anavyohuisha waliokufa na hali yeye alikuwa akilingania imani na yakini. Zaidi ya hayo ni kwamba kutaka kujua zaidi kudura ya Mwenyezi Mungu ndio imani yenyewe. Kwa hivyo basi linabainika kosa la anayedai kuwa aliyepita mjini alikuwa kafiri sio kwa jengine ispokuwa tu, ati amesema: Mwenyezi Mungu ataufufua vipi (mji) huu baada ya kufa kwake?

Hapana! Huko sio kukanusha, isipokuwa kubomoka huko alikokuona kulimfanya apigwe na butwaa na kushindwa kujua njia ambayo itawarudishia uhai watu wa mji huo.

Mwenyezi Mungu akamfisha kwa miaka mia.

Hayo yalikuwa ni mauti ya hakika sio majazi. Hapo hapahitaji taawil. Kisha akamfufua.

Alimfufua kama alivyokuwa. Wala si zito hilo kwa ambaye anauambia ulimwengu na kilicho katika ulimwengu 'kuwa', kikawa. Hakuna kitu cha ajabu kabisa kama kumlinganisha Muumbaji na viumbe katika uwezo Wake.

HISABU YA KABURINI

 Akamuuliza: Umekaa muda gani?

Hili ni swali la kuthibitisha, sio la kutaka kufahamu.

Akasema: Nimekaa muda wa siku moja au sehemu ya siku.

Lau si Ijmai (kongamano la wanavyuoni) na hadithi ingeliwezekana kusema kuwa hakuna hisabu kaburini wala kuulizwa, isipokuwa siku ya ufufuo kwa kutegemea Aya hii na Aya nyingine inayosema:

"Na siku kitakaposimama kiyama wataapa wenye makosa kuwa hawakudumu isipokuwa saa moja tu ..." (30:55)

Wala hakuna sababu ya wakosaji kuapa na kughafilika na muda uliopita toka kufa kwao isipokuwa kwa kukosa uhai, kwa sababu kuhisi muda hakuwi isipokuwa mtu huyo awe na uhai.

Sheikh Mufid katika kitabu Awailul Maqalat anasema kwamba, watu baada ya kufa wako tabaka nne: Tabaka ya kwanza ni yule aliyeijua haki na akaitumia. Huyu atapewa uhai mzuri baada ya mauti kabla ya kufufuliwa. Tabaka ya pili ni yule aliyeijua haki na asiitumie kwa inadi. Huyu vile vile atakuwa hai lakini ataadhibiwa. Tabaka ya tatu ni yule aliyefanya madhambi na maasi kwa kupuuza, sio kwa inadi. Huyu uhai wake ni wenye kutiliwa shaka baada ya kufa na kabla ya kufufuliwa. Tabaka ya nne ni wenye kuzembea kufanya twaa bila ya inadi na walio wanyonge. Hawa hawatafufuliwa, bali watabaki katika ulimwengu wa mauti mpaka siku ya kufufuliwa.

4& 18

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Sheikh Mufid amechukua ugavi huu kutokana na riwaya za Ahlul bait (a.s.); miongoni mwa hizo ni: "Hataadhibiwa kila maiti, isipokuwa ataadhibiwa kwa ukafiri hasa na atapata neema kwa imani hasa; na wasiokuwa hawa wawili watapuuzwa na wala hawataulizwa mpaka siku ya ufufuo. "Haya tumeyazungumza kwa ufafanuzi katika kitabu Falsafatul Mabdai Wal Ma'ad mlango wa "Baina ya dunia na akhera" na mlango "Hisabu ya kaburi."

Akasema: Bali umekaa miaka mia, tazama chakula chako na kinywaji chako hakikuharibika.

Amesema hakikuharibika na hakusema havikuharibika, kwa maana ya kuwa chakula na kinywaji ni aina moja tu katika kuharibika haraka. Maana ya hakikuharibika ni kwamba havikubadilika, pamoja na kupita miaka, bali vimebakia katika hali yake. Huu ni muujiza wa Mungu, kwa sababu chakula na kinywaji huharibika haraka. Hapa nahofia yule anayejaribu kuiambatanisha Qur'an na sayansi asije akasema kuwa vilikuwa katika jokofu (friji).

Na mtazame punda wako

Jinsi alivyogeuka na kuoza, lakini chakula na kinywaji vimebakia katika hali yake. Huu ndio muujiza zaidi na kudhihirisha kudura inavyogeuza kawaida. Kwa sababu anga ndiyo inayoathiri, kinywaji kingeharibika kabla ya punda, kwa sababu ndiye mwenye nguvu kuliko chakula na kinywaji. Kwa hivyo kufa punda na kudumu chakula, ni dalili ya kuwa Mwenyezi Mungu hashindwi na kitu chochote.

Inasemekana kuwa punda alibakia hai miaka mia bila ya kinywaji wala chakula. Kwa hali zote mbili, ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) aliyafanya hayo ili aondoe kustaajabu kwa Uzayr na kuona kwake ajabu ya kufufuliwa kwa mji huo; na pia ili amfanye kuwa ni hoja ya kupatikana ufufuo kwa yule atakayejua hali yake katika watu wa wakati huo. Hayo ndiyo makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.): "Na ili tukufanye uwe ni ishara kwa watu."

Na itazame mifupa jinsi tunavyoinyanyua, kisha tunaivisha nyama.

Wamehitalifiana kuhusu mifupa hii: Je ilikuwa ya Uzair au mifupa ya punda wake? Msemaji mmoja alisema kwamba hiyo ni mifupa ya mwenye punda, na kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alifufua jicho lake kwanza ili aone sehemu iliyobakia ya mwili jinsi inavyokusanyika na kupata uhai. lakini huku ni kujisemea tu juu ya Mwenyezi Mungu bila ya elimu. Lenye nguvu zaidi ni kwamba hiyo ni mifupa ya punda kwa sababu mwenye punda alisema: "Nimekaa muda wa siku moja au sehemu ya siku." Kwani lau angeliiona mifupa yake ilivy-oharibika, angelitambua urefu wa muda aliokaa Mwenyezi Mungu aliivika nyama; sawa na alivyoanza kumuumba. Imam Ali (a.s.) anasema: "Kuisha dunia baada ya kuweko sio ajabu kuliko kuianzisha."

Basi yalipombainikia alisema: Najua kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye uweza juu ya kila kitu.

Aliyasema haya baada ya kupitiwa na majaribio binafsi yasiyo na shaka. Vipi atie shaka na yeye ameshuhudia kwa macho miujiza mitatu: Kurudishwa hai baada ya kufa, kufufuliwa punda wake na kudumu chakula chake miaka mia bila kuharibika.

19

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

Funzo tunalolipata kutokana na kisa hiki ni kwamba mwenye akili hatakikani kukanusha lile lisilotambuliwa na akili yake, au lisiloafikiana na aliyoyasoma katika kitabu au kusikia kuto-ka kwa mwalimu wake, bali inatakikana ajizuie hata lile analoona linatofautiana na kanuni za kimaumbile. Elimu imethibitisha kuwa hakuna kanuni ya maumbile kabisa.

260. Na Ibrahim aliposema: Mola wangu! Nionyeshe jinsi unavyofu-fua wafu. (Mwenyezi Mungu) akasema: Huamini? Akasema: Kwa nini! (naamini) Lakini upate kutulia moyo wangu. Akasema: Basi chukua ndege wanne na uwakusanye kisha (uwachinje) uweke juu ya kila jabali sehemu katika wao. Kisha waite, watakujia mbio. Na jua kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hekima.

ILI MOYO WANGU UTULIE Aya 260

MAANA

Maana ya Aya yako wazi, lakini wafasiri wanataka kupata sababu ya kusema kwa hali yoyote itakayokuwa. Kwa hiyo wakaulizana sababu iliyomfanya Ibrahim kuuliza hivi, pamoja na kujua kwamba yeye anaamini ufufuo kwa imani isiyo na shaka yoyote. Kisha wakahi-talifiana katika jawabu lake kwa kauli kumi na mbili alizozitaja Razi.

Utafiti wao hauna msingi wowote, kwa sababu kuamini ghaibu hakupingani na kutaka kushuhudia kwa macho. Kwani kila mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu na Malaika Wake na yaliyokuja katika vitabu vyake katika habari za ghaibu, anatamani kushuhudia kwa macho yale aliyoyaamini kwa njia ya ghaibu na wahyi, isipokuwa Ali bin Abu Twalib aliye-sema: "Lau nitaondolewa pazia siwezi kuzidisha yakini (yangu)."

Vyovyote iwavyo Khalilurrahman (rafiki wa Mwenyezi Mungu) (a.s.) aliamini ufufuo kwa imani ya ghaibu kwa njia ya wahyi, kama Mitume wengine; kisha akapenda kushuhudia tukio kwa macho yake baada ya kushuhudia kwa moyo wake na akili yake. Kwa hilo zita-timia kwake njia zote za maarifa - kwa moyo, akili na majaribio.

Mwenyezi Mungu alilikubali ombi lake, akamwamrisha kuchukua ndege wane, awaku-sanye pamoja kisha awakatekate aweke fungu juu ya kila jabali; kisha awaite, watamjia haraka kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.

Kaashif3-29.jpg

20

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

Tunalomalizia katika Aya hii ni kwamba kutaka kufunuliwa siri ya uumbaji au ufufuo mara nyingine kunatokana na kutia shaka kwenye jambo hilo. Huko ndiko kunakopingana na kuamini kudura ya Mwenyezi Mungu na kuwa na imani na wahyi Wake na Mitume Yake. Mara nyingine kunatokana na kupenda kujua mambo na kupata maarifa pamoja na kuamini kudura ya Muumbaji na kuwa na imani na Mitume; hata kama hakuona jinsi Mwenyezi Mungu anavyofufua watu; kama ilivyokuwa kwa Ibrahim. Ombi hili halidhuru imani, lakini ni vigumu kulipata, bali haiwezekani, isipokuwa kwa Mtume, kama Ibrahim ambaye imani yake haitingishiki kwa kitu chochote, hata kama Mwenyezi Mungu hangemwitikia maombi yake.

Kwa hivyo basi atakayeshartisha majaribio na kuona kuwa ndio sharti la kuamini kwake ufufuo, basi yeye ni kafiri kabisa. Lau angelikuwa ni mwenye kuamini kudura ya Mwenyezi Mungu kweli, asingelikuwa na haja ya sharti hili, kwa sababu kudura yake Mwenyezi Mungu haishindwi na kitu chochote mbinguni wala ardhini.

261. Mfano wa wale wanaotoa mali zao katika njia ya Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa punje moja iliy-ochipuza mashuke saba; katika kila shuke pana punje mia. Na Mwenyezi Mungu humzidishia amtakaye, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa, Mjuzi.

262. Wale wanaotoa mali zao katika njia ya Mwenyezi Mungu kisha wasifu-atishie kile walichotoa na masim-bulizi wala udhia, wao wana ujira wao kwa Mola wao, wala hawatakuwa na hofu, wala hawatahuzunika.

263. Kauli njema na kusamehe ni bora kuliko sadaka inayofuatishiwa na udhia na Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Mpole.

Aya 261 263: PUNJE MOJA INAYOTOA MASHUKE SABA.

 MAANA

Kaashif3-30.jpg

21

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Mwenye kufuatilia Aya za Qur'an na kuzingatia maana zake atazikuta kuwa zinatilia umuhimu misingi mitatu: Kueneza mwito wa Kiislamu, Jihadi na kutoa mali katika njia ya Mwenyezi Mungu. hiyo ni kwamba misingi hii mitatu ina athari kubwa katika kuupa nguvu uislamu na kuenea kwake. Kwa hivyo Qur'an imehimiza misingi hiyo kwa mifano mbalim-bali ya kupendekeza na kutisha.

Zimeshatangulia Aya kadhaa za kuhimiza Jihadi na kutoa mali, na zitakuja nyingine. Hivi sasa mbele yetu kuna zaidi ya Aya kumi zinazozungumzia kutoa mali; katika hizo kuna zina-zomwahidi mtoaji badali ya mia saba au zaidi; nyingine zinakataza kufuatishia sadaka kwa masimbulizi na udhia; pia kuna nyingine zinazoamrisha kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kwa nia safi, na zinazoelezea kuwa kutoa kuwe kumetokana na chumo halali na zuri, sio

chumo la haramu na baya n.k.*4

Mfano wa wale wanaotoa mali zao katika njia ya Mwenyezi Mungu, ni kama mfano wa punje moja iliyochipuza mashuke saba; katika kila shuke pana punje mia. Na -Mwenyezi Mungu humzidishia amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye wasaa Mjuzi.

Wameulizana wafasiri, vipi Mwenyezi Mungu amepigia mfano punje inayotoa mazao haya na inajulikana kuwa haiko? Baadhi yao wakajibu kwamba hilo ni fumbo la wingi, sio kitu hasa. Wengine wamesema kuwa hayo ni makadirio; kwamba mwenye akili akijua kuwa punje yake itamletea mia saba, basi atatoa bila ya kusita.

Hapana shaka kuwa wafasiri wameuweka mbali sana mfano huu, kwa vile wao wamelin-ganisha kilimo kilivyokuwa wakati wao; ambapo hakukuwa na zana zozote zaidi ya ng'ombe, punda na jembe la mkono. Lau wengelikuwa wakati huu wasingeona ajabu yoy-ote katika mifano ya Mwenyezi Mungu, baada ya elimu kuingia katika kila kitu na zana na pembejeo za kilimo zinazotumiwa.

Zaidi ya hayo kutoa kwa Mola hakupungui wala hakudhibitiki. Kwa hiyo ongezeko la mia saba sio kiwango cha mwisho cha fadhila zake na kutoa Kwake. Kwa ajili hiyo ndipo akase-ma: "Na Mwenyezi Mungu humzidishia amtakaye."

Kama ambavyo ongezeko la mia saba linaweza kuzidi, basi vile vile linaweza kupungua, kulingana na hali ya kutoa kwenyewe. Huenda shillingi moja anayoitoa mtu na huku anai-hitaji ikawa bora mbele za Mwenyezi Mungu kuliko shilingi elfu zinazotolewa na aliyetoshe-ka nazo. Vile vile shilingi moja inayotolewa kwa ajili ya kuinua haki, dini na maadili, au inay-otolewa katika manufaa ya watu na kuwatoa katika dhulma na ufukara, shilingi hiyo ambayo athari yake itabaki na manufaa yake kudumu muda mrefu, ni bora mara millioni kuliko mael-fu yanayotumiwa katika anasa na maarusi ya watoto.

Wale wanaotoa mali zao katika njia ya Mwenyezi Mungu, kisha wasifuatishie kile walichotoa na masimbulizi wala udhia, wana ujira wao kwa Mola wao.

Mwenye Majmaul Bayan amesema: "Kusimbulia ni kumwambia uliyempa: Je, sikukufanyia wema? Au je, sikukupa? Na adha ni kusema: "Mwenyezi Mungu anipumzishe kwa kunie-pusha nawe na aniondolee balaa kwa ajili yako."

Maana ni kuwa, kutoa kunakobadilishiwa ziada na Mwenyezi Mungu, ni kule ambako mwelekeo wake ni kwa Mwenyezi Mungu peke Yake, sio kwa kutaka umashuhuri na kujionyesha na kuaibisha, kwa sababu hilo linabatilisha thawabu.

4Baadhi ya wafasiri wapya wamesema kwamba Aya hizi zinaweka utaratibu wa uchumi. Lakini kwa hakika ziko mbali na hayo, kwa sababu utaratibu wa uchumi kwanza kabisa unaangalia nyenzo za uzalishaji na wazalishaji wenyewe; na Aya hizi hazikuelezea hilo, isipokuwa zimewahimiza matajiri kutoa mali zao katika njia ya Mungu.

22

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

Kauli njema na kusamehe ni bora kuliko sadaka inayofuatishiwa na udhia.

Kauli njema ni maneno yanayokubaliwa na nyoyo. Makusudio ya kusamehe hapa ni kum-samehe mwenye kuomba ikiwa anaomba kwa lazima, au kutoa ufedhuli ikiwa mtu hakupa-ta alichoomba; kama ilivyo kwa baadhi ya waombaji. Yaani kumkabili muombaji kwa maneno mazuri na kuwa na subira naye, ni bora mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko kutoa kwenye kukabiliana na maudhi. Mtume (s.a.w.) anasema: "Muombaji akiomba msimkate maneno mpaka amalize, kisha mjibuni kwa upole; ama iwe ni kumpa (jap°) kichache au kumwambia vizuri"

Na Mwenyezi Mungu ni Mkwasi. Wa sadaka zote na twaa, na sisi ni mafukara tunaohita-ji msaada wake, upole wake na thawabu zake.

Mpole.Hafanyi haraka kutoa adhabu katika maisha haya, isipokuwa anamwacha muasi mpaka siku isiyokuwa na shaka.

264. Enyi mlioamini! Msiharibu sadaka zenu kwa masimbulizi na udhia; kama yule anayetoa mali yake kwa kuwaonyesha watu; wala hamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho. Basi mfano wake ni kama mfano wa jabali ambalo juu yake pana udongo, kisha likafikiwa na mvua kubwa na ikali-acha tupu. Hawana uwezo wa cho-chote katika walivyovichuma; na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu makafiri.

265. Na mfano wa wale wanaotoa mali zao kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na uimara wa nafsi zao ni kama mfano wa bustani iliyo mahali pa juu, ikafikiwa na mvua kubwa ikatoa mazao yake maradu-fu; na isipofikiwa na mvua kubwa, basi manyunyu (huitoshea). Na Mwenyezi Mungu anayaona mnay-otenda.

Kaashif3-31.jpgKaashif3-32.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

MUSIHARIBU SADAKAZENU. Ay a 264 -265:

 MAANA

Enyi mlioamini! Msiharibu sadaka zenu kwa masimbulizi na udhia; kama yule anayetoa mali yake kwa kuwaonyesha watu.

Katika Aya zilizotangulia Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amebainisha kwamba kuacha kusimbu-lia na kuudhi ni sharti la kupatikana malipo na thawabu katika kutoa; na kukosa kutoa sadaka na kauli njema ni bora kuliko kusimbulia na kuudhi, vilevile kwamba mwenye kutoa bila ya masimbulizi na udhia, atapewa malipo na thawabu bila ya hisabu; Akapigia mfano hilo kwa punje moja inayomrudishia mkulima punje mia saba.

Baada ya kubainisha haya yote anampigia mfano, katika Aya hii mwenye masimbulizi na adha kuwa sawa na mnafiki anayejionyesha, ambaye anatoa mali yake kwa kutaka sifa kwa watu, sio kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na thawabu zake.

Wala hamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho.

Yaani kitendo cha ria (kujionyesha) ni sawa na cha kafiri, kwa sababu wote hao hawataki radhi ya Mweneyzi Mungu. Kwa ajili hiyo ndipo zikaja Hadith Mutawatir kwamba ria ni shirk iliyojificha.

Basi mfano wake ni kama mfano wa jabali ambalo juu yake pana udongo, kisha likafikiwa na mvua kubwa na ikaliacha tupu. Hawana uwezo wa chochote katika walivyovichuma.

Mwenyezi Mungu kwanza amemfananisha mwenye kusimbulia anayeudhi na mnafiki anayejionyesha; kisha akamfananisha na jabali ambalo juu yake pana udongo. Kwa dhahiri ni kwamba shabihi wa shabihi ni shabihi, kama vile rafiiki wa rafiki.

Kwa hiyo inakuwa, mwenye kusimbulia anayeudhi, mnafiki na mwenye kuudhi na mwenye kujionyesha ni sawa na udongo juu ya jabali, na adha na ria ni kama mvua ambayo inaon-dosha udongo huo.

Na kauli ya Mwenyezi Mungu: "Hawana uwezo wa chochote." Maana yake ni kuwa kama ambavyo hakuna yeyote katika viumbe anayeweza kurudisha udongo huo, vile vile hawawezi wenye kujionyesha na wenye kuudhi kurudisha sadaka zao. Makusudio ni kwamba wao hawatanufaika nayo katika dunia, kwa sababu imekwishawatoka mikononi mwao; wala hawatanufaika nayo katika akhera kwa kuharibiwa na adha na ria.

Na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu makafiri

Makusudio ya kuongoza hapa, ni thawabu ya akhera, kwa sababu maneno yanahusu thawabu ya Mwenyezi Mungu,. Na makusudio ya makafiri ni kila anayefanya amali kwa ajili ya mwingine asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuna Hadith tukufu inayosema; "Kitakapokuwa Kiyama, atanadi mnadi: 'wako wapi wale waliokuwa wakiwaabudu watu? Simameni mchukue malipo yenu kwa wale mliokuwa mkiwatumikia, kwa sababu mimi sikubali amali iliyochanganyika na kitu chochote katika dunia na watu wake.'"

Na mfano wa wale wanatoa mali zao kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na uimara wa nafsi zao, ni kama mfano wa bustani iliyo mahali pa juu, ikafikiwa na mvua kubwa ikatoa mazao yake maradufu, na kama isiponyeshewa na mvua kubwa, basi manyun-yu (huitoshea).

4& 24

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

Baada ya Mwenyezi Mungu kupiga mfano wa sadaka ya wenye kujionyesha na wenye kuudhi, amepiga mfano, katika Aya hii, sadaka ya mwenye kujitakasa ; kama iliyo kawaida ya Mwenyezi Mungu kuleta mkabali wa vitu viwili vilivyo kinyume.

Ikiwa sadaka ya hao ni kama jabali lililofunikwa na mchanga, basi sadaka ya hawa ni kama bustani iliyo katika sehemu za miinuko, iliyojaa udongo ambao hauhofiwi kumomonyoka na kuondoka; sio kama ilivyo hali ya mchanga kidogo kwenye jabali; bustani hii huzaa matun-da katika mwaka mara mbili zaidi ya inavyozaa bustani ya kawaida, wala haikauki kamwe kutokana na udongo wake ulivyo mzuri; inatosheka na mvua ndogo tu, kwa sababu ya rutu-ba yake na mazingira yake mazuri.

Ama kauli yake Mwenyezi Mungu: "Kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na uimara wa nafsi zao," ni kuonyesha mambo mawili:

Kwanza, waumini wanataka radhi ya Mwenyezi Mungu kutokana na kutoa.

Pili, kutoa huku kunatokana na msukumo wa nafsi zao wenyewe na wala sio msukumo unaotoka nje.

Inasemekana kwamba uimara wa nafsi zao ni kwa maana ya kwamba wao wanajitahidi kutii kwa kutoa. Maana haya yanaweza kuwa sawa ikiwa herufi Min hapa iko katika maana ya Lam; kama ilivyo katika kauli yake Mwenyezi Mungu: "Kwa ajili ya makosa yao waligharik-ishwa ..." (71:25)

Baada ya hayo yote, Aya mbili hizi ni katika muujiza wa fasihi ambao huwezi kuupata mahali pengine isipokuwa katika maneno yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Kwanza, sadaka ya adha na sadaka ya ria ameifananisha na udongo ulioko kwenye jabali ambao unaondolewa na upepo na mvua. Kisha katika mkabala wa sadaka ya hasara, amefananisha na sadaka ya faida - sadaka ya imani, nayo ni kama bustani yenye rutuba inayotoa mazao kila mwaka, iwe na mvua nyingi au kidogo.

266. Je, mmoja wenu anapenda kuwa na kitalu cha mitende na mizabibu ipitayo mito kati yake, naye humo hupata mazao ya kila namna, na uzee ukamfikia, kisha ana watoto walio dhaifu; mara kifikiwe na kimbunga chenye moto kiungue? Hivi ndivyo anavyowabainishia Mwenyezi Mungu ishara ili mpate kufikiri.

Aya ya 266: JE, MMOJA WENU ANAPENDA...?

MAANA

Aya hii inamwambia kila mwenye kufanya amali na akaifuatishia na jambo litakaloon-doa malipo yake na thawabu zake; kama vile masimbulizi, udhia, kujionyesha, ukafiri na shirk. Hali ya kila mmoja katika hawa ni sawa na mwenye shamba analopatia man-

Kaashif3-33.jpgKaashif3-34.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

ufaa yeye na watoto wake, likapatwa na janga kubwa, likaangamia wakati ambapo analihi-tajia sana kutokana na uzee wake na udhaifu wa watoto wake ambao hawajaweza kujitege-mea; na wala hana kitu kingine zaidi ya shamba hilo.

Mfano huo ni kwamba mwenye kufanya heri, akaiharibu, siku ya Kiyama atakuwa na haja sana ya thawabu za amali alizozifanya, lakini atakuta amali zake zimekwenda bure, kwa vile alipokuwa akizifanya, hakukusudia radhi ya Mwenyezi Mungu; na wakati huo hataweza kufanya lolote; sawa na mzee aliyeunguliwa shamba lake baada ya kuwa mzee, naye ana watoto wanyonge wanaolihitajia. Kwa mfano huu ndio tunapata tafsiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

Na uzee ukamfikia, kisha ana watoto walio dhaifu; mara kimbunga chenye moto kik-ifikie kiungue?

Wafasiri wanasema imehusisha kutajwa mitende na mizabibu, kwa sababu ndio matunda mazuri kwa manufaa ya kiafya, ladha na mandhari pia. Lakini jibu hilo lilikuja katika wakati walioishi ambapo hapakuwa na matofaha, Matunda damu wala Machungwa au miwa. Lau wangelikuwa wakati huu wangelisema kuwa zimetajwa kwa sababu ni matunda bora ya wakati huo. Kwa hali hiyo inatubainikia kwamba hukumu juu ya vitu vya mazingira inapasa iwe kwa kulingana na kufungamana na wakati na mahali.

Unaweza kuuliza: Je, maneno hayapingani kuhusu kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.): "kitalu cha mitende na mizabibu." na kauli yake: "Naye humo hupata mazao ya kila namna?" (sasa je ni mitende na mizabibu iliyomo au mazao mengine?)

Jibu: Inawezekana kuwa mitende na mizabibu ndiyo mingi zaidi katika kitalu; au inawezekana vilevile kuwa makusudio ya mazao ni manufaa, kwa maana ya kuwa mwenye shamba anapata manufaa yake yote na faida.

267. Enyi mlioamini! Toeni katika vizuri mlivyovichuma na katika vile tulivyowatolea ardhini; wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali             nyinyi             wenyewe

msingevipokea isipokuwa kwa kuvifumbia macho. Basi jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Mwenye kusifiwa.

268. Shetani anawatisha na ufukara na anawaamrisha ubakhili; na Mwenyezi Mungu anawaahidi msamaha utokao kwake na fadhila na Mwenyezi Mungu ni Mkunjufu, Mjuzi.

Kaashif3-35.jpgKaashif3-36.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Ay a ya 267 - 268: KUTOA KATIKA VIZURI

 MAANA

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuhimiza sadaka katika Aya iliyotangulia na kubainisha ambayo anapaswa kusifika nayo mwenye kutoa sadaka, ikiwa ni pamoja na kumtakasia Mwenyezi Mungu katika sadaka yake na kujiepusha na ria, masimbulizi na kuudhi, sasa anataja sifa za sadaka yenyewe - kwamba inatakiwa iwe inatokana na mali nzuri na sio chafu. Hapo ndipo itakuwa sadaka imekamilika kwa njia zake. Mwenyezi Mungu anase-ma:

Enyi mlioamini! Toeni katika vizuri mlivyovichuma na katika vile tulivyowatolea kuto-ka ardhini

Lau tukiangalia Aya hii kwa dhahiri bila ya kuangalia Hadith za Mtume zilizobainisha wajibu wa kimali na kuweka kiwango cha kiasi chake na matumizi yake na pia aina yake, tungeli-fahamu kwamba katika mali yote anayochuma mtu kuna haki ya Mwenyezi Mungu ambayo anapaswa kuitoa kwa ajili ya radhi yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.), kwa sharti ya kutoa kizuri katika anavyovimiliki sio vibaya. Aya iliyo wazi zaidi ya hii ni ile inayosema: "Hamtapata wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda ..." (3: 92)

Kutoa huku ni wajibu katika mali yote; ni sawa iwe imetokana na ufundi, biashara au kilimo. Vilevile urithi, madini au kitu kingine chochote. Haya ndiyo yanayofahamishwa na matamko ya Aya. Kwa sababu kutoa kumekuja kwa tamko la amri ambayo inafahamisha wajibu. Kauli yake Mwenyezi Mungu: "Katika vizuri mlivyovichuma" inakusanya uchumi wote; na kauli yake; Na katika vile tulivyowatolea kutoka ardhini" inakusanya mimea, madini na siku hizi petroli.

Lakini Hadith za Mtume - ambazo ni tafsiri na ubainifu wa Qur'an hasa Aya za hukumu za sheria - zimeweka kiwango cha mali ya Zaka au Khums, vile vile nadhiri au kafara. Zikabainisha kiasi cha kutoa na wanaopewa. Wanavyuoni wa kifiqh wamelieleza hilo kwa ufafanuzi katika mlango wa Zaka, Khums, kafara na nadhiri. Kwa hiyo Aya itakuwa ni ya kuleta sharia hiyo ya kutoa na kutilia mkazo; sawa na kauli yake Mwenyezi Mungu:"Na simamisheni Swala na toeni Zaka ..." (2:110)

Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya.

Inasemekana kuwa sababu ya kushuka Aya ni kwamba baadhi ya Waislamu walikuwa wak-itoa sadaka zile tende mbovu. Na jumla hii ni kutilia mkazo jumla ya kwanza ambayo ni "toeni katika vizuri." Kwa ujumla ni kuwa toeni vizuri na wala msitoe vibaya.

Mafaqihi wametoa fatwa kwamba mwenye kumiliki aina ya mali ambayo baadhi yake ni nzuri na baadhi ni mbaya, haijuzu kwake kutoa mbaya, bali atatoa ile yenye uzuri wa wastani. Kama akichagua ile ya hali ya juu, basi ni bora zaidi. Lakini kama mali yote ni mbaya inajuzu kutoa mali mbaya kwa sababu haki inafungamana na dhati ya kitu kina-chotolewa.

27

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

Hali nyinyi wenyewe msingevipokea isipokuwa kwa kuvifumbia macho.

Hii ni hoja fasaha kwa yule anayetoa sadaka mbaya, Imam Ali (a.s.) anasema: "Kama unavyofanya nawe utafanyiwa."

Shetani anawatisha na ufukara na anawaamrisha ubakhili.

Maana ya kuwatisha na ufukara ni kuwatia wasiwasi wa kuwa na pupa na kuhofia kutoa, kuwa kunaleta ufukura na hali mbaya. Maana ya kuamrisha ovu ni kuhadaa kwa kutia kwake wasiwasi kufanya maasi na kuacha utii; kama vile ubakhili.

Na Mwenyezi Mungu anawaahidi msamaha utokao kwake na fadhila.

Mwenye kutoa vizuri katika mali yake kwa kutafuta radhi ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.), Mwenyezi Mungu amemuahidi mambo mawili:

Kwanza, kusamehe makosa yake mengi kama alivyosema: "Chukua sadaka katika mali zao, uwatakase na uwasafishe kwazo..." (9:103)

Pili, kumlipa kheri zaidi mwenye kutoa kuliko alichokitoa - Mwenyezi Mungu anasema: "... Na chochote mtakachokitoa, basi Yeye atakilipa naye ni mbora wa wanaoruzuku." (34:39)

Miongoni mwa maneno ya hekima ya Imam Ali (a.s.) ni: "Sadaka ni dawa yenye kuokoa," "Takeni riziki kwa sadaka" na "Fanyeni biashara na Mwenyezi Mungu kwa sadaka."

Ilipokuwa roho ya dini inatawala kwenye nafsi na kwenye mwelekeo wa malezi na tabia za watu, ilikuwa baba anampa mtoto wake pesa na kumwamrisha kutoa sadaka kwa fukara kwa kuitakidi kwamba sadaka itamwandalia njia ya tawfik na kufaulu.

269. Humpa hekima amtakaye. Na aliyepewa hekima hakika amepe-wa heri nyingi na hawakumbuki ila wenye akili.

  aya ya 269 HEKIMA

MAANA

Neno Hekima hutumiwa kwa maana nyingi, kama vile maslahi; mfano: "Hekima ya kitu hiki ni jambo fulani." Maana nyingine ni mawaidha; mfano: Hekima ni kitu (anachotafuta) kili-chompotea "mumin," Pia lina maana ya elimu na fahamu; kama anavyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t.): " Na hakika tulimpa Lukmani hekima ..." (31:12) Maana nyingine ya neno hekima ni Utume, Mwenyezi Mungu anasema: ".... Na tukampa hekima na kukata huku-mu." (38:20)

Kaashif3-37.jpg

28

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Vilevile neno hili linatumiwa kwa maana ya elimu ya Falsafa. Msemaji mmoja amesema: "Hekima ni elimu ya Fiqh", mwengine amesema ni elimu zote za kidini, watatu akasema ni kumtii Mwenyezi Mungu tu.

Vyovyote ilivyosemwa au itakavyosemwa, ni kwamba neno hekima haliwezi kutoka kwenye maana ya usawa na kukiweka kitu mahali pake kwa kauli na vitendo. Kwa hivyo mwenye hekima ni yule anayekihukumu kitu na kukileta kwa mujibu wa akili na hali ilivyo, sio kwa mujibu wa mapendeleo na matakwa. Kitu hicho hawezi kukifanyia haraka kabla ya muda wake au kukizuilia na wakati wake au kukipeleka kombo na mipaka yake.

Kwa hali hiyo basi, hekima haihusiki na mitume na mawalii tu au na wanafalsafa na wataala-mu tu, bali kila mwenye kufanya vizuri amali yoyote na akaiweka sawa, basi huyo ni mwenye hekima katika amali hiyo; awe ni mkulima au mfanyakazi, mwajiri au mwajiriwa. Vilevile ni sawa awe ni muhuburi, malenga, hakimu au askari, n.k. Sharti la kwanza na la mwisho la hekima ni kuthibiti lengo la kitendo kiakili, kisharia, kidunia na kidini.

Hapana mwenye kutia shaka kwamba ambaye hekima ni mwongozi wake atakuwa mwema katika nyumba mbili (duniani na akhera). Imam Jaffar Sadiq (a.s.) anasema: "Hakumneemesha Mwenyezi Mungu mja neema kubwa na tukufu zaidi kuliko hekima. Mwenyezi Mungu anasema: "Na aliyepewa hekima hakika amepewa heri nyingi na hawakumbuki ila wenye akili." Yaani hajui yeyote siri ya hekima aliyoitoa Mwenyezi Mungu isipokuwa mwenye kumtakasia Mwenyezi Mungu nafsi yake. Hekima ni uongofu, ni uthabiti wa vianzio vya mambo na ni kituo cha mwisho wa mambo."

Hapa inaonyesha kuwa kuna tofauti kati ya elimu na hekima. Elimu ni kujua mambo na mfungamano uliopo wa mambo hayo; vile vile kujua athari yake ya kheri au ya shari. Ama hekima inaamrisha akili kufuata usalama, kufuata dini iliyo sawa na kukitumia kitu mahala pake, palipoumbwa kwa ajili yake. Mfano elimu inatengeza chembechembe za bomu na kutengeneza maroketi, lakini haiangalii lengo lake, la kheri au la shari; wala haikatazi hili na kuamrisha lile. Lakini hekima haijishughulishi na utafiti wa mabomu na uvumbuzi wa maroketi hayo isipokuwa inaangalia matumizi ya maroketi hayo na kumwelekeza binadamu

lile litakalo mfanya kupata kheri na ufanisi sio uovu. *5

*5Nimesoma kwamba katika mataifa makubwa kuna mabomu ambayo moja linaweza kuwa na mpasuko wa tani mil-ioni mia moja, na kwa muda mchache tu, linaweza kuua watu milioni mia na ishirini; na kwamba kuna mabomu yana shabaha ya hali ya juu. Hii inatufahamisha uongo wa propaganda za wagunduzi wa vyombo hivyo, kwamba eti lengo lake ni usalama na ufanisi wa binadamu na kumchukua binadamu hadi mwezini kustarehe.

29

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

270. Chochote mtoacho, au nadhiri mnazoweka, basi Mwenyezi Mungu anakijua. Na madhalimu hawana wasaidizi.

271. Mkizidhihirisha sadaka ni vizuri; Na kama mkitoa kwa siri na kuwa-pa mafukara, basi hivyo ni bora zaidi kwenu na yatawaondokea baadhi ya maovu yenu na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mnayoyatenda.

aya 270 271 CHOCHOTE MTOACHO

Kaashif3-38.jpg

MAANA

Tena amerudia Mwenyezi Mungu kutaja kutoa na kukutilia mkazo kwa kusema: Chochote mtoacho au nadhiri mnazoweka basi Mwenyezi Mungu anakijua

Neno kutoa linakusanya kila kinachotolewa; kiwe cha wajibu au suna, kingi au kichache cha utii au maasi na kisiri au kidhahiri.

Maana ya nadhiri kilugha ni ahadi; na kisharia ni kujilazimisha mtu kutenda jambo fulani au kuliacha kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.

Tamko lake ni kusema yule mwenye kuweka nadhiri: "Ni juu yangu kufanya jambo fulani kwa ajili ya Mwenyezi Mungu." Haitoshi kukusudia tu, bila ya kusema, wala kusema bila ya kumtaja Mwenyezi Mungu au kutaja mojawapo ya majina yake matukufu. Lau anasema : "Nimeweka nadhiri kufanya kitu fulani likiwa jambo fulani", hiyo haiwezi kuwa nadhiri kwa kutokuwa na jina la Mwenyezi Mungu.

Vilevile nadhiri haiwezi kuwa kabisa, ikiwa imefungamana na jambo la haramu au maku-ruhu. Wakati wa Mtume (s.a.w.w.) mtu mmoja aliweka nadhiri ya kusimama tu bila ya kukaa wala kuwa kivulini, akiwa amefunga na asizungumze na mtu; Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akasema: "Mwamuruni azungumze akae kivulini na aendelee na Saumu yake."

Maana ya "Mwenyezi Mungu anakijua" ni kuwa Mwenyezi Mungu anajua lengo lolote la

30

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

kutoa litakalokuwa na kulipatia malipo; ikiwa ni heri basi ni heri na kama ni shari basi ni shari tu.

Na madhalimu hawana wasaidizi.

Makusudio ya madhalimu ni wote bila ya kuvua, wakiwa ni pamoja na wale wasiotoa cho-chote au wanaotoa vibaya au kwa ria. Vilevile wale wanaotoa kwa masimbulizi na adha au kuweka pasipokuwa mahali pake. Wengine ni wale wanaovunja ahadi na wasiotekeleza nadhiri. Wote hawa na walio mfano wao hawatakuwa na wasaidizi wala waombezi watakaowazuiilia na mateso ya Mwenyezi Mungu.

Kama mkizidhihirisha sadaka ni vizuri.

Yaani hakuna umakuruhu katika kudhihirisha sadaka maadam makusudio yake ni kwa ajili ya kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.). Imam Jaffar Sadiq aliulizwa kuhusu mtu anayefanya jambo la kheri, watu wakamwona akafurahi. Imam akasema: "Hapana ubaya; kila mtu anapenda kuonekana na watu kwa kheri, ikiwa hakufanya hilo kwa ajili ya huko kuonekana."

Na kama mkitoa kwa siri na kuwapa mafukara, basi hivyo ni bora zaidi kwenu.

Hapana shaka kwamba kuficha sadaka ni bora kuliko kuidhihirisha, kwa sababu kunakuwa mbali na shubuha ya ria na kudhihirisha haja ya mafukara mbele ya watu. Huwa mara nyingine kudhihirisha sadaka kuna maslahi; kwa mfano ikiwa ni kwa kutaka kutoa mfano kwa wengine, hapo kudhihirisha kutakuwa bora zaidi.

Inasemekana kuwa kuificha sadaka ya sunna ni bora kuliko kuidhihirisha; na kinyume chake kwa sadaka ya wajibu.

Hatujui hoja ya ufafanuzi huu na Hadith ya "Sadaka ya siri inazima ghadhabu ya mola" inakusanya ya wajibu na suna; kama ambavyo Aya inakusanya fukara mwislamu na asiyekuwa mwislamu. Mafaqihi wametoa fatwa ya kutoa sadaka ya sunna kwa asiyekuwa mwislamu akiwa ni muhitaji kutokana na kauli ya Mtume wa Mwenyezi Mungu :"Kulinywesha kila ini la joto kuna malipo."

Na yatawaondokea baadhi ya maovu yenu.

Neno Min hapa ni baadhi, kwa sababu sadaka haifuti madhambi yote isipokuwa inafuta baadhi tu.

Na Mwenyezi Mungu anajua mnayoyatenda

Maadam Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anajua siri, sawa na anavyojua dhahiri, basi siri ni bora, kwa sababu hilo liko mbali na ria, isipokuwa kama katika kudhihirisha kuna maslahi; kama kuwaonyesha mfano wengine ili watende. Na wenye ikhlasi wengi wanaficha sadaka zao; wanajitolea kwenye mambo ya kheri kwa majina ya watu wengine wema.

31

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

272. Si juu yako kuwaongoza, lakini Mwenyezi Mungu humwongoza amtakaye. Na mali yoyote mnay-oitoa ni kwa kwa ajili ya nafsi zenu, wala hamtoi ila kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu. Na mali yoyote mnayoitoa mtalipwa kwa ukamilifu wala hamtadhulumiwa.

273. Ni kwa ajili ya mafukara waliozuili-wa katika njia ya Mwenyezi Mungu, wasioweza kwenda huku na huko katika ardhi. Asiyewajua hali zao anawadhania kuwa ni matajiri kwa sababu ya kujizuia.

Utawafahamu kwa alama zao; hawaombi watu wakang'anga' nia. Na mali yoyote mnayoitoa, kwa hakika Mwenyezi Mungu anaijua.

274. Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao; wala haitakuwa hofu juu yao wala wao hawatahuzunika.

Kaashif3-39.jpg

 aya ay 272-274 SI JUU YAKO KUWAONGOZA MAANA

Si juu yako kuwaongoza, lakini Mwenyezi Mungu humwongoza amtakaye.

Yametangulia maelezo katika Aya ya 26 ya Sura hii kwamba neno Huda (uongofu) linatu-

32

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

miwa kwa maana nyingi; miongoni mwayo ni ubainifu na (uongofu), hiyo ni kazi ya Mtume. Maana nyengine ni tawfiki kutoka kwa Mwenyezi Mungu ya kuandalia njia ya kufanya kheri; nyingine ni kuongoka, yaani kukubali nasaha na kuzitumia, huku kunategemezwa kwa mja. Pia neno hilo lina maana ya thawabu na mengineyo.

Maana ya uongofu katika "Si juu yako kuwaongoza" ni kuongoka na kukubali nasaha; yaani, kuitumia kwao haki si juu yako wewe, isipokuwa ni juu yako kufikisha haki tu.

"... Basi juu yako ni kufikisha na juu yetu ni hisabu." (13:40)

Maana ya uongofu katika ; "Lakini Mwenyezi Mungu humwongoza amtakaye" ni tawfiki katika njia ya kheri.

Inasemekana kuwa sababu ya kushuka "Si juu yako kuwoangoza" ni kwamba waislamu walikuwa hawatoi sadaka isipokuwa kwa watu wa dini yao, ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia Mtume Wake kwa Aya hii na akataka kuwabanishia waislamu wote kwamba kafiri haadhibiwi kwa sababu ya kufuru yake kwa kunyimwa riziki na kudhikishwa ili alaz-imike kuamini; na haifai kwa yeyote kufanya hivyo hata kama ni Mtume wa Mwenyezi Mungu . " ...Basi je wewe utawalazimisha ili wawe waumini?" (10:99).

Aya inafahamisha kwamba sadaka ya sunna au ya wajibu inajuzu kuwapa wasiokuwa waislamu, lakini kauli ya Mtume (s.a.w.): "Nimeamrishwa kuchukua sadaka kutoka kwa matajiri wenu na kuitoa kwa mafukara wenu", inahusu sadaka ya sunna tu sio ya wajibu.

Na mali yoyote mnayoitoa ni kwa ajili ya nafsi zenu.

Huenda mtu akadhania kuwa kutoa ni hasara kwake na ni kuwanyima watoto wake na ndugu zake. Ndipo Mwenyezi Mungu akaondosha dhana hii, kwamba mwenye kutoa inam-rudia yeye kheri na nafuu katika dunia na akhera. Katika akhera atapata malipo na thawabu. Ama katika dunia, Sheikh Muhammad Abduh anasema: "Kutoa kunazuia mafukara kuwafanyia ubaya matajiri, kwa sababu mafukara wakiwa na dhiki, watakwenda kuwaibia matajiri, kuwaudhi na kuwanyang'anya. Kisha uovu wao huu unawaendea wengine; mara nyingine ufisadi huo huenea kwa ujumla na kuondoa raha na amani."

Sijui kama Sheikh Muhammad Abduh ameitoa fikra yake hii kutoka vyama vya wafanyakazi ambavyo vimewaletea matatizo matajiri na kuwalazimisha kukubali haki nyingi za wafanyakazi.

Wala hamtoi ila kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu.

Yaani, maadamu mnakusudia radhi ya Mwenyezi Mungu katika kutoa kwenu, basi Mwenyezi Mungu atakubali. Ni sawa muwe mumempa mwislamu au asiyekuwa mwislamu kwa sharti ya kuwa iwe ni mali nzuri sio mbaya. Pia kusiweko na masimbulizi na maudhi.

Inasemekana kuwa Aya ina maana ya kukataza kwa njia ya kutolea habari; yaani msitoe

isipokuwa kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu.

Na mali yoyote mnayoitoa mtalipwa kwa ukamilifu wala hamtadhulumiwa.

33

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Hata kutoa kukiwa kwa asiyekuwa mwislamu, lakini hamtapunguziwa chochote katika malipo, ikiwa mliyempa ni muhitaji.

WATU WA SUFA (UPENUNI)

Kuna jamaa waliohamia Madina, wakiacha miji yao mali zao na watu wao. Hapa Madina hawakuwa na maskani yoyote wala jamaa na hawakuwa na nyezo za kujichumia maisha, wala hawakuweza kusafiri kutafuta riziki. Idadi yao ilikuwa watu mia tatu, wengine wanase-ma ni mia nne. Wakawa wako msikitini tu, wakiabudu na kuzilinda nyumba za Mtume.

Pia walikuwa wakijifundisha Qur'an na kuihifadhi, jambo ambalo lilikuwa ni katika twaa bora zaidi, kwa sababu huko ni kuihifadhi dini. Wakati huo huo walikuwa wakitoka pamoja na Mtume katika kila vita. Walikuwa wakikaa upenuni mwa msikiti ndio maana wakaitwa watu wa upenuni (Ahlu Sufa).

Mtume (s.a.w.), alikuwa akiwahimiza na kuwaambia: "Furahini enyi watu wa Suffa; yeyote atakayekuwa na sifa mlizo nazo nyinyi katika umma wangu, basi yeye ni katika marafiki zangu."

Hao ndio wanaofaa zaidi kupewa sadaka. Kwa sababu wao ndio walioshukiwa na Aya hii:

Ni kwa ajili mafukara waliozuiwa katika njia ya Mwenyezi Mungu, wasioweza kwenda huku na huko katika ardhi. Asiyewajua hali zao anawadhania kuwa ni matajiri kwa sababu ya kujizuia. Utawafahamu kwa alama zao; hawaombi watu wakang'ang'ania.

Mwenyezi Mungu katika Aya hii amewataja watu wa Sufa kwa sifa tano:-

1.            Kujitolea kwa Jihadi na kutafuta elimu. Hiyo ndiyo maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu "waliozuiwa katika njia ya Mwenyezi Mungu", kwa sababu mvivu hawezi kuambiwa kuwa ameifunga nafsi yake katika njia ya Mwenyezi Mungu.

2.            Kushindwa kuchuma: ndiyo makusudio ya kusema kwake: "Wasioweza kwenda huku na huko."

3.            Kujizuia, Mwenyezi Mungu anasema: "Asiyewajua hali zao anawadhania kuwa ni matajiri kwa sababu ya kujizuia."

4.            Kuonekana kuwa ni mafukara kwa hali yao tu, sio kwa sababu ya kuombaomba: ndio maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu: "Utawafahamu kwa alama zao."

5.            Kuacha kuomba vilivyo mikononi mwa watu kwa kunga'ang'ania: Kwenye hilo Mwenyezi Mungu ameashiria kwa kusema "Hawaombi watu wakang'ang'ania".

Tumetaja katika tafsiri ya Aya ya 177 katika Sura hii, kwamba kuomba bila ya dharura ni haram.

Wale watowao mali zao usiku na mchana, kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao; wala haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.

Mwenyezi Mungu ametaja hukumu ya kutoa katika Aya kumi na nne mfululizo, ya mwisho ikiwa ni hii ambayo ni muhtasari wa yaliyotangulia na kutilia mkazo fadhila ya kutoa katika nyakati zote, iwe ni usiku au mchana, na kwa siri au kwa dhahiri.

34

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Razi ametaja kauli nyingi katika sababu za kushuka Aya hii, miongoni mwa hizo ni ile iliy-opokewa kutoka kwa Ibn Abbas, kwamba Ali bin Abu Twalib (a.s.) alikuwa na dirham nne tu, akatoa kwa siri na nyingine kwa dhahiri, ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii.

ZAKA

Zaka sio sadaka ya sunna, kwa sababu sadaka huitoa mwislamu kwa hiyari, wala haihitaji kufikia kiwango fulani na haina jengine zaidi ya kukusudia kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu peke Yake; na malipo yake yanaanzia maradufu ya kumi hadi maradufu ya mia saba na zaidi ya hapo, kiasi ambacho hakina mwisho kulingana na lengo la kutolewa kwake.

Ama Zaka, ni faradhi, ni haki ya lazima katika mali ya kiwango fulani na hutolewa kwa anayestahiki. Ni ya tatu katika nguzo tano za uislamu ambazo ni: Shahada mbili, Swala, Zaka, Saumu na Hijja. Baadhi ya wenye ghera na uislamu wanaona kuwa Zaka ni mpan-go wa uchumi au ni utaratibu fulani wa kiuchumi wa kiislamu. Wengine wanaichukulia kuwa ni kodi ya mali za matajiri.

Ukweli ni kwamba Zaka si kodi au mpango fulani wa kiuchumi. Kwa sababu sharti ya msin-gi ya kukubaliwa Zaka, ni nia ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu, bila hivyo haikubali-wi kabisa. Na kodi au utaratibu wa kiuchumi hauzingati sharti hii.

Zaidi ya hayo, utaratibu wa kiuchumi, kwa maana ya kisasa, kwanza unaangalia nyezo za uzalishaji; kama vile ardhi, madini na viwanda. Mfumo wa kibepari unazingatia kuwa ni milki ya mtu binafsi anayeimiliki. Ama mfumo wa kijamaa unazingatia kuwa ni milki ya umma inayoongozwa na serikali. Na Zaka haiangalii haya kabisa.

Ama kodi nayo inasimamiwa na kiongozi wa nchi katika kupatikana kwake na kuitoa; hai-wezekani kwa mtoaji kwa hali yeyote kuacha kuitoa kwa kiongozi, ambaye ndiye mwenye uwezo wa kuitumia.

Mafaqihi wote wanasema kuwa mwenye kumiliki mali anaweza kutoa Zaka bila ya idhini ya kiongozi, naye anaweza kuaminiwa, bila ya ushahidi wowote au kiapo, akisema kuwa amekwishatoa. Sasa Zaka na kodi ni wapi na wapi? Bali mafaqihi wamejuzisha kwa mkusanyaji Zaka kuitoa kwa mafukara yeye mwenyewe bila ya kuipeleka kwenye Baitul Mal (hazina ya Waislamu).

Imam Ali (a.s.) alimwambia mmoja wa wanaokusanya Zaka: "Tumia mali uliyonayo kwa wenye watoto wanaohitaji na wenye njaa." Kwa dhahiri ni kwamba kodi haina matumizi haya kabisa.

Mtu anaweza kusema: Faradhi ya zaka maana yake ni kukubali kwamba ufukara lazima uwepo, na kwamba uislamu unaukabili ufukara kwa sadaka, jambo ambalo natija yake ni kuweko tabaka ya utajiri na umasikini?

Jibu: Matumizi ya Zaka hayakufungika kwa fakiri na maskini tu, isipokuwa katika jumla ya matumizi yake ni maslahi ya umma, ambayo Mwenyezi Mungu ameyaeleza kwa ibara ya sabilillah (njia ya Mwenyezi Mungu) katika Aya nyingi. Kwa hiyo kama hakukupatikana fukara, basi Zaka hutumiwa katika njia hii. Kwa hali hiyo, Zaka hailazimishi kuweko fukara kwa namna yoyote, wala Zaka sio ikrari ya kusema ufukara ni chapa isiyoepukika. Pili: wajibu wa jamii ni kuwatunza masikini ili wasiwe ombaomba na wazururaji. Jambo hili

35

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

linapatikana hata katika miji ya kijamaa ambayo haikubali utabaka.

Tatu: Tutamfanyaje mgonjwa asiyeweza hata kununua dawa na mwenye njaa ambaye hana njia yoyote ya kupata chakula katika jamii inayoongozwa na ufisadi. Je tuache mpaka hali itakapokuwa nzuri na umasikini utakapoondoka? Au tuweke kanuni itakayodhamini maisha yao? Je, inawezekana kupatikana mabadiliko kwa msitari wa kalamu? bila ya kupi-tia vipindi vingi?

Hakika Uislamu unapiga vita aina zote za unyonge. Na Mtume (s.a.w.) aliutolea mawaid-ha. Baadhi ya riwaya zinasema: "Ufukara unakurubia kuwa kufuru". "Mwislamu mwenye nguvu ni bora kuliko mnyonge."

Ujumbe wa Mwenyezi Mungu una lengo la heshima ya mtu na utengeneo wake; na ufukara ni upungufu na madhila na ni mashaka na balaa. Kwa hivyo haiwezekani uislamu kuukubali. uislamu haukatai kuweko katika jamii tajiri na tajiri zaidi au mwenye nguvu na mwenye nguvu zaidi, isipokuwa unachokataa ni kuweko fukara na mnyonge.

Uislamu haukuweka Zaka kwa ajili ya masikini tu kama inavyodhaniwa bali ni kwa kutatua matatizo mengi, ukiwemo umasikini kama upo. Vilevile utumwa, ambapo unapatiwa uhuru na mali ya Zaka. Matatizo mengine ni kuhudumia askari wanaopigana Jihadi, na mengineyo katika maslahi ya umma; kama vile kujenga shule, hospitali, barabara na mira-di ya maji.

Tutaeleza ufafanuzi wa matumizi ya Zaka katika Sura ya (9:60) Inshallah.

Lau tunakadiria kuwa mtu ataweza kupitiwa na wakati ambao hauna masikini na mahitaji yote ya umma yametoshelezwa, kiasi ambacho matumizi ya Zaka hayatapatikana kabisa, basi bila shaka itaachwa. Na wakati huo utafika tu; kama ilivyokuja Hadith katika Sahih Bukhari Juzuu ya 9 mlango wa Fitan; anasema Mtume s.a.w.w: " Toweni sadaka, utakuja wakati mtu atatemebea na sadaka yake asipate wa kuikubali."

Zaidi ya hayo, uislamu umemwajibishia mtoaji Zaka wakati anapompatia muhitaji kuto-muudhi na kutomvunjia heshima yake na asikwaruze hisia zake. Kwamba huko kutoa ni wajibu wake na ni deni ambalo hapana budi kulitekeleza. Kwa kutilia mkazo maana haya Qur'an inasema:

"Na ambao katika mali yao iko haki maalum kwa ajili ya aombaye na anayezuilika kuom-ba." (70: 24 - 25)

Yamekwishatangulia maelezo katika tafsiir ya Sura hii Aya (262-263) kuhusu kuudhi.

Pamoja na kuwa Uislamu umezishinda sheria zote za dini zingine na za kufanywa na watu kwa kuweka sheria hii ya Zaka sheria hii ya kibinaadamu ambayo hawakuigundua waweka nidhamu ispokuwa baada ya Uislamu kwa mamia ya miaka na kuiita 'dhamana ya jamii', pamoja na yote hayo jambo bora zaidi kuwapa wahitaji katika mtazamo wa kiislamu, ni kuwaandalia kazi inayonasibiana na uwezo wao ili wahisi thamani ya uhai. Mwenyezi Mungu humpenda mja wake mumin anayejishughulisha na kazi.

Mwisho tunamaliza maelezo haya kwa kauli ya Imam Ja'far Asswadiq (a.s): "Kila kiungo

4& 36

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

katika viungo vyako kina Zaka ya Mwenyezi Mungu: Zaka ya jicho ni kuzingatia na kuli-fumba na mambo ya haramu, Zaka ya sikio ni kusikiliza elimu na hekima, Zaka ya ulimi ni kumshukuru Mwenyezi Mungu na kuwapa nasaha Waislamu, Zaka ya mkono ni kutoa na Zaka ya mguu ni kuhangaikia jihadi na kusuluhisha watu."

275. Ambao wanakula riba, hawainuki, ila kama ainukavyo ambaye amezugwa na shetani kwa wazimu. Hayo ni kwa sababu wanasema kuwa biashara ni kama riba. Mwenyezi Mungu amehalalisha biashara na ameharamisha riba. Na aliyefikiwa na mawaidha kutoka kwa Mola wake, akakoma, basi yake ni yaliyokwishapita na mambo yake yako kwa Mwenyezi Mungu. Lakini wanaorejea, basi hao ndio watu wa motoni; wao ni wenye kukaa humo milele.

276. Mwenyezi Mungu huipunguza riba na huizidisha sadaka. Na Mwenyezi Mungu hampendi kila kafiri afanyae dhambi.

277.Hakika wale walioamini wakafanya vitendo vizuri na wakasimamisha Swala na wakatoa Zaka, wao watap-ata ujira wao kwa Mola wao, wala haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.

Kaashif3-40.jpgKaashif3-41.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

278.Enyi mlioamini! Mcheni Mungu na acheni yaliyobaki katika riba, ikiwa mmeamini.

279.Na kama hamtafanya, basi jitangazieni vita na Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na mkiwa mme-tubu, basi haki yenu ni rasilimali zenu; msidhulumu wala msidhulu-miwe.

280.Na kama ana dhiki, basi angoje mpaka awe na uwezo. Na kama deni mkizifanya sadaka, basi ni bora kwenu ikiwa mnajua.

Kaashif3-42.jpg

281. Na iogopeni siku ambayo mtarud-ishwa kwa Mwenyezi Mungu, kisha kila nafsi ilipwe iliyoyachuma; nao hawatadhulumiwa.

Aya 275 - 281 MNASABA

Maudhui ya sadaka na riba yote ni mali, ingawa kuna tofauti ambayo ni: Sadaka hutolewa bila ya kutaka kurudishiwa; ni tohara, safi na dhamana. Ama riba ni kutoa kwa kutaka kurudishiwa mali pamoja na ziada; ni tamaa, uchoyo, uchafu, unyang'anyi na maangamizo. Kwa hiyo maudhui ni sawa, lakini hukumu na lengo ni kinyume kabisa. Ikiwa vitu hutajwa kwa mifano yake basi pia hutajwa kwa vinyume vyake. Ndio maana ikaja hukumu ya riba

38

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

mara tu baada ya hukumu ya sadaka (Zaka).

Kabla ya kuingilia kufasiri Aya, tutaanza kuonyesha riba inavyoeleweka katika sharia, dalili ya uharamu wake na yanayo sababisha uharamu.

NENO RIBA

Neno 'riba' katika lugha maana yake ni ziada; kama alivyolitumia Mwenyezi Mungu katika Sura (22:5).

Katika sharia, riba inagawanyika kwenye mafungu mawili: Riba ya kukopesha na riba ya kuzidishiana katika bei.

Maana ya riba ya kukopesha, ni mtu kumkopesha mwingine kitu chochote na kumlazimisha yule aliyemkopesha manufaa yoyote kwa sababu ya kumkopesha; kama vile kukopesha shillingi kumi kwa sharti ya kurudishiwa kumi na moja. Au kwa yasiyokuwa manufaa ya mali; kwa mfano mkopeshaji kumshurutisha aliyemkopesha amfanyie kazi fulani au amwaz-ime kitabu au kitu chochote. Mtume (s.a.w.) anasema "Kukopesha kokote kunakovutia manufa ni haramu." Hapo hakutofautisha aina ya manufaa. Hata hivyo kama mkopaji akili-pa deni pamoja na ziada ya ahsante, itafaa kwa mkopeshaji kuichukua. Mtume (s.a.w.) alikuwa akilipa deni pamoja na ziada, akisema: "Bora ya watu ni yule anayewakopesha watu vizuri."

Inatakikana tuzingatie kuwa riba inathibiti katika kukopesha kwa kushurutisha ziada na manufaa kwa namna yoyote ile ya ziada, ni sawa iwe ziada ya kipimo cha mizani ujazo, urefu au idadi. Vilevile ni sawa iwe ni katika namna ya mali iliyokopeshwa au namna nyingine. Kwa maneno mengine riba ya kukopesha haina tofauti katika dhati ya kitu kwa kitu au manufaa.

Ama riba ya bei ni kuzidishiana kitu kil kile, na masharti yake ni mawili:

Kwanza ni kupeana kwa ziada aina hiyo hiyo kwa jina lake la uhakika, kama kuuza ngano kwa ngano, au kuuza ngano nzima kwa unga wa ngano, kwa sababu unga umetokana na ngano nzima. Vilevile Wanga (nishaa) na unga, kwani vyote viwili vimetokana na asili moja ambayo ni ngano.

Dalili ya pili ni kuwa wanavyouziana viwe vinaweza kupimwa kwa ujazo au mizani tu. Kwa hiyo hakuna riba kwa vinavyouzwa kwa idadi; kama mayai. Inawezekana kuuzwa yai moja kwa mawili. Pia hakuna riba kwa kinachouzwa kwa kuonyeshana; kama nguo na wanya-ma.

Kwa ufupi ni kwamba riba ni haramu katika deni kwa namna yoyote ile, na katika bei ni haramu kwa vinavyopimwa kwa namna yoyote, kwa sharti ya kuwa vyote viwili viwe ni jinsi moja. Hayo tumeyafafanua zaidi katika kitabu chetu Fiqhul-Imam Jaffar Sadiq (a.s.) Mlango wa Riba.

UHARAMU

Riba ni haramu kwa nukuu ya Qur'an, Hadith mutawatir na kongamano la Waislamu wote,

39

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

tangu siku za Mtume (s.a.w.) mpaka leo. Bali uharamu wake hauhitaji dalili, kwa sababu ni katika mambo yaliyo wazi; kama vile wajibu wa Swala na uharamu wa zina. Kwa sababu hiyo ndipo mafaqihi wakahukumu kwamba mwenye kukanusha uharamu wa riba, basi ni kafiri, kwa vile amekanusha dharura ya dini iliyothibiti.

Kama ilivyo haramu kuchukua riba, pia ni haramu kuitoa. Hadith ya Mtume inasema: "Ameilaani Mwenyezi Mungu riba, mwenye kuila, mwenye kuuza, mwenye kununua, mwan-dishi wake na shahidi wake."

SABABU YA HARAMU

Mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu, kwamba Yeye ndiye mwenye kuweka sharia ya halali na haramu, basi hawezi kutaka mengi zaidi ya wahyi katika kuharamishwa riba.

Na kama ikitokea kuuliza sababu, basi haulizi kwa sababu ya kujikinaisha, isipokuwa ni kwa kutaka kufahamu tu; au kwa ajili ya kuwakinaisha wale walioelezewa na Aya hii:

"Na anapotajwa Mwenyezi Mungu pekee yake, mioyo ya wale wasioamini akhera huchafu-ka, na wanapotajwa wale asiyekuwa yeye wanafurahi." (39:45).

Vyovyote iwavyo ni kwamba wametaja sababu kadha za kuharimishwa riba. Miongoni mwa sababu hizo ni kama ifuatavyo:- Kupingana na misingi ya kibinadamu; kama vile kufanyiana wema, kusaidiana na kuoneana huruma. Kuwa hiyo riba maana yake ni kula mali ya batili. Kwa sababu mwenye kula riba anaichukua bila ya kufanya lolote.

Mtu anaweza kusema kuwa anayechukua riba hufanya kitu, kwa sababu mali yake anaitoa kwa aliyekopa ambaye anaitumia na kunufaika nayo. Kwa hivyo hali ya riba ni sawa na kukodisha ardhi, nyumba au mnyama.

Mtu akisema hivyo tutamjibu: Kuna tofauti kubwa kati ya kukodisha na riba, kwani mwenye kukodisha hana jukumu la kulipa kile alichokikodisha, kama kikifa au kikihariibika, isipokuwa kama yeye ndiye aliyesababisha. Lakini chenye kukopwa kikiharibika, basi mwenye kukopa atakilipa.

Kwamba mwenye kuchukua riba hupata faida daima na mwenye kukopa hupata hasara; matokeo yake, matunda yote yanaishia kwa mchukuaji riba Baadhi ya maprofesa wa mambo ya uchumi wa Ulaya wameijua aibu hii. Miongoni mwa hao wataalamu ambao wameinukia katika nidhamu za riba, ni Dkt. Schacht, Mjerumani, Meneja wa zamani wa Benki alisema katika mhadahara alioutoa Damascus mnamo mwaka 1953:

"Tukifanya mahesabu tutajua kuwa mali yote katika dunia inaishia kwenye idadi ndogo sana ya wanaokula riba. Hiyo ni kwa sababu anayekopesha kwa riba, daima hupata faida katika kila kitu, wakati ambapo mwenye kudaiwa kwa riba anatazamia kupata faida na hasara; hatimaye ndipo mali yote inaishia kwa yule mwenye uhakika wa faida. Nadharia hii iko njiani kuthibitika. Kwani wenye mali humiliki maelfu ya pesa. Ama wenye milki wote, na wenye viwanda ambao wanakopa kutoka katika mabenki, n.k. hawana lolote isipokuwa ni waajiriwa tu, wakiwatumikia wenye mapesa ambao wanachukua matunda ya jasho lao."

Kuna baadhi ya wataalamu wa kiuchumi waliothibitisha kwamba msingi na asili ya fikra ya riba unatokana na mayahudi, na watu wengine wamechukua fikra hiyo kutoka kwao, hayo

40

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

hayako mbali, kwani historia ya mayahudi wa kale na wa sasa inathibitisha kuwa Mungu wao, dini yao heshima ya siasa yao ni mali tu peke yake haina mshirika; na njia yoyote ya kuleta mali ni tukufu, hata kama ni umalaya, ukuwadi, uasi, wizi, unafiki au ria na uovu wowote ule.

MAANA.

Ambao wanakula riba, hawainuki, ila kama ainukavyo ambaye amezugwa na shetani kwa wazimu.

Shetani hamzugi yoyote, wala hana uwezo wowote wa kumfanya mtu kuwa mwenda wazimu. Isipokuwa hiyo ni tash'bihi na kuleta karibu ufahamu wa watu wanaosema kuhusu mtu aliiyepatwa na wazimu: "Amepagawa na Shetani."

Maana ya Aya ni kwamba hali ya wanaofanya riba, ni sawa na hali ya mwenda wazimu ambaye amezugwa, katika matendo yake, na kuwa shaghalabalaghala. Imepokewa Hadith kutoka kwa Ibn Abbas kuwa watu wa riba watafufuka kutoka makaburini mwao kama wenda wazimu, hiyo itakuwa ndio alama yao kwamba wao ni wala riba.

Hayo ni kwa sababu wamesema kuwa biashara ni kama riba.

Wamehalalisha riba kwa kuleta falfasa ya kuwa biashara na riba zinafanana kwa njia zote; basi kwa nini riba nayo isiwe halali? Si mtu anaweza kuuza kitu cha thamani ya shilling tano kwa shilingi sita na kwamba mtu anaweza kuuza kwa bei ya taslim shilingi moja tu na kwa mkopo shiling mbili? Kwa hiyo, eti inatakikana kuweko na ruhusa ya mtu kutoa shilingi kumi mpaka mwezi ujao kwa shilingi kumi na moja.

Mwenyezi Mungu anayajibu madai haya kwa kusema:

Mwenyezi Mungu amehalalisha biashara na ameharamisha riba.

Njia ya majibu hayo ni kuwa, kule kufanana kwa kidhahiri hakufanyi kuwa ndio kufanana kabisa. Kwani biashara ni kazi ya kibiashara yenye kutafuta manufaaa; mwuzaji anakuwa kati ya kupata faida na hasara, kwa hivyo faida yake ni mavuno ya taabu yake, na wala sio kula mali ya batil, ambapo riba ni faida tu na kuchukua ziada bila ya jasho, kwa hiyo inakuwa ni kula mali ya batili.

Kwa ajili hiyo ndio Mwenyezi Mungu akahalalisha biashara na akaharamisha riba. Basi kut-ofautiana kihukumu ni dalili ya kutofautiana kihali na kinyume chake.

Na aliyefikiwa na mawaidha kutoka kwa Mola wake, kisha akakoma, basi yake ni yaliyokwisha pita.

Yaani aliyekuwa amechukua riba, kabla ya kuteremshwa Aya ya kuiharamisha kisha akaacha baada ya kuharamishwa, Pia yule mwenye kusilimu sasa ikiwa amechukua riba kabla ya kusilimu kwake, si wajibu kurudisha baada ya kusilimu. Aya hii ni sawa na ile inayosema:

41

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

"Wala msiwaoe wake waliowaoa baba zenu, isipokuwa yale yaliyokwishapita ..." (4:22)

Kuacha kuchukulia mambo yaliyopita, kuko katika mambo mengi, hasa mambo ya mali. Wameeleza sababu kuwa ni kutoleta matatizo ya kiuchumi.

Na mambo yake yako kwa Mwenyezi Mungu

Wametaja njia nyingi katika kufasiri ibara hii, kiasi ambacho akili haiwezi kutosheka, amba-lo tumelifahamu sisi ni kuwa mwenye kuchukua riba bila ya kujua hukumu yake na akaacha baada ya kujua makatazo ya Mwenyezi Mungu kwa kumtii, basi Mwenyezi Mungu (s.w.t.) atamsaidia na kumtosheleza kwa halali yake. Kwa sababu ameacha haramu kwa kumtege-mea Mwenyezi Mungu; na mwenye kumtegemea Mwenyezi Mungu atamtoshea.

Lakini wanaorejea, basi hao ndio watu wa motoni; wao ni wenye kukaa humo milele.

Maana yake ni kuwa wale ambao hawafuati amri ya Mwenyezi Mungu wala kuacha makatazo yake na kuendelea kula riba kwa inadi na kupuuza, basi watawekwa milele motoni. Kwa sababu mfano wa inadi hii hauwi isipokuwa kutokana na kafiri mkanushaji.

Mwenyezi Mungu huipunguza riba na huizidisha sadaka. Na Mwenyezi Mungu ham-pendi kila kafiri afanyaye dhambi.

Yaani mwenye kula riba hutaka ziada katika mali yake, lakini riba kwa hakika ni kupungua mali na uchafu ulioharamishwa. Na haramu hutoa mali kutoka kwa aliye nayo na inafanya matumizi ya riba yawe kama matumizi ya mali ya kunyang'anya, zaidi ya hayo ni dhambi na adhabu.

Kimsingi ni kuwa kila linalokuwa ni sababu ya kumkasirisha Mwenyezi Mungu na adhabu, basi ni uchafu na upungufu na ni amali ya shetani.

Ama sadaka, inasafisha mali na kuitakasa na inaifanya thabiti miliki ya mwenye kutoa sadaka na Zaka. Vilevile inaleta radhi ya Mwenyezi Mungu na thawabu Yake. Huo ndio ukamil-ifu na ziada hasa. Kwa maneno mengine ni kwamba wingi, wa mali ya haramu ni uchache, na uchache wa mali ya halali ni wingi.Kafiri afanyae dhambi ni yule anayefanya inadi ya kula riba bila ya kushtuka na ni yule anayeendelea kufanya inadi ya kukataa kutoa Zaka, na kutoshtuka na vitendo vya Mwenyezi Mungu na kiaga chake.

Kwa kutegemea Aya hii, yafaa kusema kuwa waislamu wengi wakati huu ni makafiri wafanyao dhambi, kwa sababu ya kung'angania riba na kuacha kutoa Khums na Zaka.

Hakika wale walioamini wakafanya vitendo vizuri na wakasimamisha Swala na waka-toa Zaka, wao watapata ujira wao kwa Mola wao, wala haitakuwa hofu juu yao, wala hawatahuzunika.

Aya hii iko dhahiri katika maana, haihitaji tafsiri, zaidi ya hayo tafsiri yake imekwishapita katika Aya ya 25 na 82 ya Sura hii. Isipokuwa ameirudisha Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ahadi hii kwa kufuatisha ahadi baada ya kiaga na kinyume. Kwa hiyo alipoelezea kiaga cha wanaofanya riba amefuatishia ahadi kwa watu wema.

42

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Kwa ujumla Aya kwa dhahiri inafahamisha kuwa imani ya nadharia tu, bila ya vitendo si cho-chote.

Enyi mlioamini! Mcheni Mungu na acheni yaliyobaki katika riba, ikiwa mmeamini.

Kusema: Acheni yaliyobaki katika riba kunafahamisha kuwa uharamu sio katika yale yaliy-opita nyuma, kama tulivyoeleza.

Na kama hamtafanya, basi jitangazieni vita na Mwenyezi Mungu Na Mtume Wake.

Na hakuna jambo linalowajibisha kutangaza vita na Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Kwa anayeng'angania kula riba ila, ni kwa kuwa yeye ni kafiri au yuko katika hukumu ya kafiri; hata kama kula kwake riba ni kwa kupuuza tu, si inadi. Lakini riwaya zilizopokewa kutoka kwa Masum zimegawanya kula riba katika mafungu mawili.

Kwanza, ni yule anayekula kwa kuifanya halali. Huyo ni kafiri bila shaka yoyote, kwa sababu amekana dharura ya dini. Imam Jaffar Sadiq (a.s.) aliambiwa fulani anakula riba na anaita 'lubba" (kiini), akasema: "Nikimpata nitaikata shingo yake."

Pili, ni kula kwa kupuuza hukmu ya Mwenyezi Mungu pamoja na kuamini uharamu wake. Huyu atatakiwa kutubia mara ya kwanza na ya pili; kama akiendelea atauliwa. Imepokewa kutoka kwa Imam Sadiq (a.s.) kuwa mwenye kula riba atatiwa adabu baada ya kubainika, akirudia atatiwa adabu, akirudia atauliwa. Imesemekana kuwa atauliwa mara ya nne.

Na mkiwa mmetubu, basi haki yenu ni rasilmali zenu; msidhulumu wala msidhulu-miwe.

Yaani msimdhulumu mdaiwa kwa kumtaka zaidi ya rasilmali; wala msidhulumiwe kwa kupunguziwa rasilimali.

Na kama ana dhiki basi angoje mpaka awe na uwezo.

Kila mwenye kudaiwa riba, au isiyokuwa riba haijuzu kumdhiki ikiwa ana uzito; kama ambavyo pia haifai kwa mdaiwa kuchelewesha deni akiwa na uwezo. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) anasema: "Kama ambavyo si halali kwa mdeni wako kukucheleweshea deni akiwa na uwezo, vilevile si halali kwako nawe kumdhikisha akiwa na uzito."

Kiwango cha mwenye dhiki ni ambaye hamiliki chochote zaidi ya nyumba yake ya kukaa na vitu vyake vya dharura; kama nguo, vitabu na vyombo vya nyumbani vya lazima. Vilevile zana zake za kufanyia kazi zinazompatia chakula chake na cha familia yake na gharama yake ya siku moja. Vyote hivi si wajibu kuviuza kwa kulipa deni. Hayo tumeyataja kwa ufafanuzi katika kitabu 'Fiqhul-Imam Jaffar Sadiq' mlango wa Muflis.

Na kama (deni) mkizifanya sadaka, basi ni bora kwenu ikiwa mnajua.

Hapana shaka kwamba kumsamehe deni mwenye dhiki ni fadhila katika dini, bali ni katika utii mkubwa. Kwani hilo ni kumfanya apumue na kuweza kutekeleza haja zake vizuri. Imekuja Hadithi: "Mwenye kumvumilia mwenye uzito au kumsamehe, Mwenyezi Mungu atampa kivuli siku ambayo hakutakuwa na kivuli isipokuwa kivuli cha Mwenyezi Mungu."

43

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Mafaqihi wameafikiana kwa kauli moja kuwa mwenye kukopa katika dharura ya halali, kisha akashindwa kulipa, atalipiwa deni lake kutoka katika hazina ya waislamu (Baitul Maal). Imam Jaffar Sadiq (a.s.) anasema: "Mwenye kuchukua riziki hii kwa uhalali kwa ajili yake na ya watoto wake, ili airudishe baadae anakuwa kama mpigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu. Akishindwa kulipa na amkope Mwenyezi Mungu na Mtume wake."

Maana ya kumkopa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, ni kwamba deni lake litalipwa kutoka katika hazina ya waislamu. Na hilo ni kuitumia katika njia ya Mwenyezi Mungu.

Qur'an imelieleza hilo kwa kusema:

"Sadaka hupewa: mafukara na masikini na wanaozitumikia na wanaotiwa nguvu nyoyo zao na katika kuwakomboa watumwa na wenye madeni na katika njia ya Mwenyezi Mungu na wasafiri,. Ni faradhi inayotoka kwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye hekima." (9: 60)

Kauli yake Mwenyezi Mungu "Ikiwa mnajua" ni kutilia mkazo kufanya kitu kwa kujua; yaani maadamu mnajua kuwa kumsamehe deni mwenye dhiki ni heri, basi ni juu yenu kufanya kwa kujua kwenu hili.

Imesemekana kuwa makusudio ya kujua ni kufanya; yaani mkiwa ni wafanya heri, basi litoeni sadaka deni kwa mwenye dhiki. Maelezo haya hayako mbali, na kauli ya Imam Ali (a.s.) anasema: "Elimu iko na matendo, mwenye kujua hufanya, elimu hubaki kwa kuifanyia kazi, vinginevyo huondoka."

Wataalamu wengi wa kisasa hawaiti nadharia yoyote kuwa ni elimu mpaka wauone ukweli wake kwa kufuatishia na majaribio.

Na iogopeni siku ambayo mtarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, kisha kila nafsi ilipwe iliyoyachuma, nao hawatadhulumiwa.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kukataza riba kwa mkazo na kuamrisha kumfanyia subi-ra mdaiwa mwenye dhiki, au kumsamehe, katika Aya saba, kisha anafuatisha Aya anay-owahofisha waasi na siku ya hisabu na malipo na adhabu yake.

Katika Majmaul Bayan imeelezwa kuwa Aya hii ni ya mwisho kumshukia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) na kwamba yeye aliishi siku 21 tu baadaye.

44

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu
282. Enyi mlioamini! Mnapokopeshana deni kwa muda uliowekwa, basi liandikeni; na mwandishi aandike baina yenu kwa uadilifu. Wala mwandishi asikatae kuandika kama vile alivyomfunza Mwenyezi Mungu; basi na aandike. Na aandikishe yule ambaye iko juu yake haki; na amwogope Mwenyezi Mungu Mola wake; wala asipunguze chochote katika deni. Na kama yule ambayeuu yake iko haki ni mpum-bavu au mnyonge au yeye hawezi kutaja mwenyewe, basi na ataje msimamizi wake kwa uadilifu. Na muwashuhudishe mashahidi wawili katika watu wenu waume, kama hakuna wanaume wawili, basi ni mwanamume mmoja na wanawake wawili, katika wale mnaowaridhia kuwa mashahidi, ili kama mmoja wao akipotea, mmoja wao amkum-bushe mwingine. Na mashahidi wasikatae waitwapo. Wala msi-choke kuiandika ikiwa ndogo au kubwa, mpaka muda wake. Hayo ndiyo uadilifu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu na imara sana kwa ushahidi na ni karibu zaidi kut-ofanya shaka. Ila ikiwa ni biashara ya mkono kwa mkono mnayopeana baina yenu, basi si vibaya kwenu msipoandika. Na wekeni mashahidi mnapouziana, wala asitiwe tabu mwandishi wala shaidi. Na kama

2. Sura Al-Baqarah

Kaashif3-43.jpgKaashif3-44.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

mkifanya hivyo, basi hakika hilo ni ufasiki kwenu.          Na mcheni

Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu anawaelimisha; na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

2. Sura Al-Baqarah

283.Na kama mkiwa safarini na hamku-pata mwandishi, basi ni rahani itakayokabidhiwa. Na kama mmoja wenu akimwamini mwingine, basi aliyeaminiwa atekeleze uaminifu wake na amche Mungu, Mola wake. Wala msifiche ushahidi. Na atakayeuficha, basi hakika moyo wake ni wenye kuingia dhambini. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi kwa mnay-oyatenda.

 

Ay a 282 - 283 :DENI

MAANA

Mwisho mwisho wa Sura hii Mwenyezi Mungu ametaja hukumu za sharia zinazofungamana na Zaka, riba, deni, biashara na rahani. Masuala ya Zaka na riba yamekwisha tangulia. Hivi sasa tuko katika baadhi ya masuala ya deni, rahani na biashara.

Aya imetilia umuhimu sana kuandika deni na kuweko ushahidi; ambapo Mwenyezi Mungu ameamrisha kuandika kwa kuanza kusema: "Iandikeni" Pili, akasema: "Wala msichoke kuiandika" Na mara ya tatu, amebainisha hekima ya kuandika na kuweko ushahidi kwa kusema "Hayo ndiyo uadilifu zaidi na imara zaidi na karibu zaidi kutofanya shaka."

Pamoja na hayo mafaqihi wengi hawakuwajibisha kuandika deni na kuuza, wala kuweko ushahidi. Wameichukulia amri ya hilo kuwa ni sunna. Kauli yao hiyo ya suna inatiliwa

Kaashif3-45.jpg

46

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

nguvu na kuwa baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuamrisha kuandika na kuweko ushahi-di, amesema: "Kama mmeaminiana, basi aliyeaminiwa atekeleze amana";

Yaani kama mdai akimwamini mdaiwa bila ya kuandika wala ushahidi, basi ni juu ya mwenye kudaiwa kutekeleza. Hii ni ruhusa dhahiri ya kuacha kuandika na ushahidi. Itakuja tafsiri ya Aya hii Inshaallah.

Enyi mlioamini! Mnapokopeshana deni kwa muda uliowekwa, basi liandikeni.

Neno Tadayantum lina maana mbili: Kudaiana kwa mali na kulipiziana. Imam Ali (a.s.) anasema: "Kama utakavyomfanya (mwenzako) nawe utalipwa." Ilipokuwa neno tadayantum linachukua maana hizi mbili, ndio maana Mwenyezi Mungu akasema: "Tadaayan tum bidaynin. Ili kuondoa dhana ya kukusudia maana ya kulipa." Makusudio ya "Muda uliowekwa" ni muda wa kwisha deni uliotajwa iwe mwaka au mwezi, n.k.

Kusema Kwake Mwenyezi Mungu: "Basi liandikeni" ni amri ya kuandika deni, na amri inafa-hamisha wajibu, lakini imekuwa ni sera ya waislamu tangu zamani kutolazimika kuandika deni na kuweko ushahidi. Kwa hiyo amri ikachukuliwa kuwa ni suna na mwongozo.

MKOPO NA DENI

Mkopo unashirikiana na deni katika kuwa mtu ananufaika nao kwa kuutumia, na ni haki ya mtu katika dhima. Lakini mkopo unatofautiana na deni katika kuwa kitu chenye kukopwa kinalipwa cha aina hiyo hiyo katika jinsi yake na sifa; ukikopa pesa, basi dhima yako ni kulipa pesa, ni lazima urudishe mfano wake, sio kima.

Ama deni, *6dhima inathibiti kutokana na sababu fulani; kama kukopa, bei ya mkopo, kuoa kwa mahari ya kulipa baadaye jinai na mengineyo. Kwa hiyo deni ni kiujumla na linalipwa mfano wake likiwa na mfano; au kima ikiwa halina mfano

Na mwandishi aandike baina yenu kwa uadilifu.

Ilivyokuwa lengo la kuandika deni ni kudhamini haki ya mdai na mdaiwa na kuondoa ubishi kati yao, basi ni wajibu mwandishi awe mwaminifu mwenye kujua hukumu ya dini. Kwani kama akiwa mbumbumbu au mwenye upendeleo, basi lengo litakuwa limebatilika.

Unaweza kuuliza, kwa nini amesema aandike mwandishi kwa uadilifu na asiseme aandike mwandishi mwadilifu?

Jibu: Kwa sababu kuandika si sharti mwandishi awe mwadilifu; kama ilivyo kwa kadhi, mufti na imam wa jamaa katika Swala. Kwa sababu lengo la kuandika deni ni kudhamini na kuhi-fadhi haki; kama tulivyoeleza. Kwa hivyo inatosha mwandishi kuwa mwadilifu kwa upande huu tu; na wala sio katika kauli zake na vitendo vyake vyote. Kwa sababu hiyo inawezekana kusema kuwa Aya hii inafahamisha kuwa shahidi sio lazima awe na uadilifu wa kisheria, bali inatosha kutegemea kuwa ni mkweli na mwadilifu katika ushahidi wake, bila ya kumpendelea yeyote; na tutauchukulia uadilifu wa shahidi ulioelezwa katika hadithi kuwa ni uadilifu wa kiwango fulani na sio uadilifu kwa ujumla.

Kama ukisema kuwa kumpa shahidi hukumu ya mwandishi ni kutumia Qiyas na wewe si unasema Qiyas ni batili?

*6Tofauti ya maneno haya mawili ipo katika lugha ya kiarabu, kama ilivyoelezwa-mfasir

47

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Jibu: Mwandishi ni shahidi hata kama haitwi hivyo. Kwa maneno mengine, shahidi ni aina mbili - wa kutamka na kuandika; huyu anashuhudia kwa kuandika na yule anashuhudia kwa kutamka; na kuandika ni ndugu wa kutamka.

Wala mwandishi asikatae kuandika kama vile alivyomfunza Mwenyezi Mungu; basi na aandike.

Makusudio ya alivyomfunza ni alivyomwamrisha; na alivyoamrishwa, ni kuandika kwa uadil-ifu, bila ya kupendelea. Kusema kwake "basi na aandike" ni kutilia mkazo kauli Yake "asikatae." Siri ya mkazo huu, ni kwamba wale waliokuwa wanajua kuandika wakati ule walikuwa kidogo sana, endapo mwandishi atakataa huwa vigumu kumpata mwingine.

Unaweza kuuliza kuwa kauli Yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) "wala mwandishi asikatae" ni katazo, na katazo linafahamisha uharamu; kwa maana hiyo basi, ni wajibu kwa mwandishi kukubali kuandika deni; na tunajua kuwa kuandika huku ni suna sio faradhi. Sasa itakuwa-je tanzu izidi asili?

Jibu: Kama ambavyo kauli Yake Mwenyezi Mungu "basi iandikeni" tumeichukulia kuwa sunna, basi kauli Yake "Wala mwandishi asikatae" tunaichukulia kuwa ni makuruhu tu, wala sio haramu; isipokuwa ikiwa kuacha kuandika kutasababisha ufisadi na kusababisha wote wawili kuingia katika haramu, hapo ndio itakuwa kukataa ni haramu. Lakini hilo ni kwa upande wa kukinga ufisadi sio upande wa kuandika deni.

Na aandikishe yule ambaye iko juu yake haki; na amwogope Mwenyezi Mungu Mola wake; wala asipunguze chochote katika deni.

Ambaye haki iko juu yake ni mdaiwa. Maana ni kuwa ni wajibu kwa mdaiwa kutamka wazi-wazi mbele ya mwandishi, bila ya kupunguza, ili iwe ni ikrari yake kwa haki ya mwenyewe inayomlazimu yeye au warithi wake kulipa; haki inaweza kupotea kama hakuna uthibitisho wa madai.

Haya kwa uchache ndiyo yaliyo wajibu kwa mdaiwa juu ya aliyemkopa, ambaye amem-saidia kumaliza matatizo yake wakati wa dhiki.

Nimewaona watu wengi wakimnyeyekea mwenye mali kwa upole kabisa kwa kutaraji kukopeshwa ili kumaliza matatizo. Basi mara mtu anaposaidiwa, anageuka adui na kukataa deni, eti kwa vile tu mwenye mali anataka haki yake. Mbali ya kuwa wema kuulipia maovu ni haram kisheria, lakini hilo linaonyesha ukhabithi na ushenzi.

KUMSHUKURU MUUMBA NA MUUMBWA

Mwenyezi Mungu anasema:

"... kwamba unishukuru Mimi na wazazi wako ..." (31: 14)

Katika Hadith imesemwa: "Hamshukuru Mwenyezi Mungu asiyewashukuru watu". Hadith nyingine inasema: "Mwenye kutendewa wema na mtu, akamshukuru Muumba kwa kusema "Shukrani ni za Mwenyezi Mungu", na akamsahahu aliyemtendea wema, basi Mwenyezi Mungu (s.w.t.) haikubali shukrani mpaka amshukuru aliyemfanyia wema." Kwa

48

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

sababu hiyo ndio ukawa mashuhuri msemo:

"Asiyeshukuru kiumbe, hamshukuru Muumba."

Ulazima huu una siri nyingi:

1.Akili na sharia zinahukumu wajibu wa kumshukuru yeyote mwenye kutenda vizuri;

na mwenye kuacha shukrani hii, basi amemwasi Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni na

uasi kukanusha neema za Mwenyezi Mungu (s.w.t.). 2.Hadhi ya mtu ni hadhi ya Mwenyezi Mungu. Hadith imesema: "Mwenyezi Mungu

atamwambia mja katika waja wake: Kwa nini hukunitembelea nilipokuwa

mgonjwa?" Mja atasema: "Kutakata na maovu ni kwako, wewe ni mlezi wa waja,

huugui wala huumwi."

Mwenyezi Mungu atasema: "Alikuwa mgonjwa nduguyo mumin wala hukumtembelea.

Naapa kwa utukufu wangu, lau ungalimtembelea ungelinikuta mbele yake na ningelizian-

galia haja zako na kukutekelezea; na hayo ni kwa heshima ya mja wangu na Mimi ni

Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu."

3.Kumshukuru mwenye kukufanyia jambo zuri ni kutekeleza amana. Na kutekeleza amana ni dalili ya ukweli na amani, bali ndio asili ya fadhila. Kwani unapopatikana utekelezaji, ndipo hupatikana ukweli, ikhlasi, uaminifu na kujitolea. Na utekeleza ji haugawanyiki - mwenye kumtekelezea amana aliyemtenda wema, basi pia huwatekelezea watu wake, marafiki zake, nchi yake na watu wote kwa ujumla. Na asiyetekeleza amana kwa aliyemfanyia wema au kujitia hamnazo, basi hufanya hivyo hivyo kwa watu wake, marafiki zake, na nchi yake. Ndio maana kukasemwa:"Asiyetekeleza amana hana dini."

4.Inavyopendeza zaidi ni kutekeleza amana wakati wa shida. Kwa sababu kutekeleza wakati wa neema ni kutekeleza kwa ajili ya mali sio kwa ajili ya mwenye mali na ni kwa ajili ya dunia sio kwa ajili ya mwenye dunia.

Na kama yule ambaye juu yake iko haki ni mpumbavu au mnyonge au yeye hawezi kutaja mwenyewe, basi ataje msimamizi wake kwa uadilifu

Mpumbavu hapa ni yule mbadhirifu aisyeweza kutumia mali vizuri mnyonge ni mtoto mdogo, na asiyeweza kutaja ni mwenda wazimu, wote hawa hawafai kuandikisha au kufanya ikrari yoyote; isipokuwa ni lazima wasimamiwe mambo yao na wasimamizi (mawalii) wao wanaowaangalia.

Wasimamizi ni aina mbili: Msimamizi mahsusi ambaye ni baba na babu wa upande wa kwa baba; na msimamizi wa kiujumla ambaye ni hakimu wa sharia aliye mwadilifu au Mujtahid. Huyu hana usimamizi mpaka akosekane babu na baba. Ufafanuzi wa Swala hili uko kwenye kitabu Fiqh Imam Jaffar Sadiq.

Na muwashuhudishe mashahidi wawili katika watu wenu wanaume.

Hili ni jambo la pili katika mambo aliyoyazingatia Mwenyezi Mungu katika deni: La kwanza ni kuandika na pili ni ushahidi. Kanuni za kutungwa zimeweka sheria ya kupatikana mashahidi wawili katika mikataba rasmi; sawa na ilivyokuja katika Qur'an.

Shia Imamiya na Hanafi, wanasema sharti hilo ni, itakapokuwa mwenye kutolewa ushahidi

4& 49

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

ni mwislamu. Ama akiwa si mwislamu, basi ushahidi wa watu wa mila unakubaliwa kwa mila zao.

Malik na Shafi wamesema haukubaliwi ushahidi wa asiyekuwa Mwislamu hata kama anawashuhudia asiyekuwa mwislamu. Haya yanapatikana katika kitabu Mughni na Fathul Qadir mlango wa ushahidi.

Kama hakuna wanaume wawili, basi ni mwanamume mmoja na wanawake wawili katika wale mnaowaridhia kuwa mashahidi.

Haki za kimali zinathibiti kwa ushahidi wa wanaume wawili, au mwanamume mmoja na wanawake wawili au mwanamume mmoja na yamini, kwa maafikiano ya madhehebu yote; isipokuwa Abu Hanifa. Yeye anasema hautoshi ushahidi wa mtu mmoja na yamini.

Qur'an Tukufu imetaja ushahidi wa wanaume wawili na mwanamume mmoja na wanawake wawili tu. Ama kuthibiti haki ya kimali kwa shahidi mmoja na yamini kumefafanuliwa na Hadith.

Unaweza kuuliza: Je, inathibiti haki ya mali kwa ushahidi wa wanawake tu? Kisha je, inaweza kuthibiti kwa ushahidi wa wanawake wawili na yamini, kama ilivyo kwa mwanamume mmoja na yamini?

Jibu: Madhehebu yote yameafikiana kuwa haki za mali hazithibiti kwa ushahidi wa wanawake bila ya mwanamume na bila ya yamini, wametofautiana katika kuthibiti kwa ushahidi wa wanawake wawili na yamini. Malik na Imamiya wamesema inathibiti, wengine wamesema haithibiti.

Kauli Yake Mwenyezi Mungu "katika wale mnaowaridhia," inachukuliwa maana mbili: Kwanza ni kuwa makusudio ya kuridhia ni kuhusisha radhi kwa ushahidi wenyewe hasa, bila ya kuangalia hali ya shahidi. Kwa hiyo hakuna ulazima wa uadilifu wa shahidi, bali itatosha kwa Kadhi kutegemea kwamba ushahidi unaambatana na tukio; kama ulivyo ushahidi katika kanuni zilizotungwa, ambapo kadhi pekee ndiye anayekadiria ushahidi.

Maana ya pili ni kuridhia hali ya shahidi mwenyewe, kwa hivyo lazima shahidi awe mwadil-ifu., tamko la Aya linachukua maana zote mbili, lakini hadith na fatwa za Mafaqihi zinatilia nguvu matakwa ya uadilifu kwa shahidi mwenyewe, Imam Ali (a.s.) anasema: "Mshuhudieni ambaye mnaridhia dini yake, uadilifu wake utengeneo wake na kujiepusha kwake na dham-bi."

Kwa hivyo wakitoa ushahidi waadilifu wawili, basi ni juu ya Kadhi kuhukumu kwa mujibu wa ushahidi wao; ni sawa awe ameelewa kutokana na kauli yao au hakuelewa kwa kuchukulia Hadith. Ama akishuhudia asiyekuwa mwadilifu, hawezi kuhukumu kwa ushahidi wao isipokuwa kama amepata kuelewa kutokana na kauli yao, kiasi ambacho kujua ndio kutakuwa ni matokeo ya hukumu, sio ushahidi wa asiyekuwa mwadilifu.

Ili kama mmoja wao akipotea, mmoja wao amkumbushe mwingine.

Hapa pana maswali mawili:

Kwanza, kwa nini amesema: "Ili kama mmoja wao akipotea, mmoja wao amkumbushe

50

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

mwingine." Na wala asiseme: Amkumbushe mwingine tu.

Kuna haja gani ya kurudia nomino iliyo wazi katika jumla mbili ambazo hazikutengana kwa mbali wala karibu?

Hilo limejibiwa kwa njia nyingi, bora yao ni kuwa, ulipokuwa ushahidi wa wanawake wawili ni sawa na ushahidi wa mwanamume mmoja, basi ni wajibu kuukusanya ushahidi wa hao wanawake wawili, ili kwamba akisahau kitu, mwingine amkumbushe. Akimaliza, anaanza wa pili naye akisikilizwa na mwenzake wa kwanza, kama alivyofanya yeye. Kwa hiyo utakuwa ushahidi wa kila mmoja wao unatimiza ushahidi wa mwengine.

Maana hayo hayawezi kuja, isipokuwa kwa kurudi neno 'Mmoja wao' ili uweko mfungamano wa wawili, lau angelisema: amkumbushe mwengine tu, basi maana yangalikuwa: "Ili akisahau mmoja akumbushwe na wa pili. Kwa hiyo mmoja atakuwa anasema na mwingine ni mkumbushaji tu, na hayo siyo makusudio yake."

Kwa ujumla ni kuwa, si wajibu kuwakusanya pamoja mashahidi wakiwa wanaume; bali kuwatenganisha ni bora. Lakini kwa wanawake ni kinyume na hivyo.

Swali la pili: Kuna siri gani ya kuwa ushahidi wa wanawake wawili unalingana na ushahidi wa mwanamume mmoja?

Swali hili limejibiwa kwa njia nyingi. Miongoni mwazo ni kuwa mwanamke ana akili dhaifu. Kauli ya kushangaza ni kuwa kuna baadhi ya wafasiri wanaosema kuwa: Mwanamke ni mpole.

Kama kauli hii ingelikuwa sawa, basi ingelikuwa upole ni nusu ya ushahidi, hata kama ni mwanamume; na kila asiyekuwa mpole basi ni shahidi kamili, hata kama ni mwanamke!

Kauli yenye nguvu ni kuwa aghlab mwanamume anaweza kuzuwia hisia zake zaidi kuliko mwanamke. Na, jibu sahih zaidi ni kwamba ni juu yetu kuikubali amri hata kama hatujui hekima yake.

Kwa ujumla ni kwamba Kadhi mara nyingine anaweza kutegemea ushahidi wa mwanamke mmoja na kupata kujua kutokana na kauli yake zaidi, kuliko kutegemea ushahidi wa wanaume kumi wasiokuwa waadilifu. Na, inajuzu Kadhi kutoa hukumu kwa kujua kuliko-tokana na mwanamke, maadamu ni nyenzo ya kujua au kupata uhakika.

Na mashahidi wasikatae waitwapo.

Akikuita mdai, ili umtolee ushahidi juu ya haki au deni, basi ni wajib kifaya (wa kutosheana) juu yako kuitikia wito wake; yaani kama akitekeleza mwingine umuhimu huu, basi wajibu utakuwa umekuondokea; vinginevyo utakuwa na jukumu mbele ya Mwenyezi Mungu. Dalili ni Aya hii na Hadith Tukufu: "Atakapokuita mtu ili umshuhudilie juu ya haki au deni, basi usirudi nyuma."

Wala msichoke kuiandika ikiwa ni ndogo au kubwa, mpaka muda wake.

Makusudio ni kuhimiza kuandika deni bila ya kutofautisha uchache wake au wingi wake,

4& 51

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

maadamu lengo ni kuchunga kusitokee tofauti na mizozo.

Haya ndiyo uadilifu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu na imara sana kwa ushahidi na ni karibu zaidi kutofanya shaka.

Yaani kuandika deni na kulishuhudilia ndiyo bora na imara na ni karibu zaidi kuondoa shaka.

Unaweza kuuliza: Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameamrisha kuandika. Kwanza, kati-ka kauli yake: "Basi iandikieni"Pili. "Wala msichoke kuandika" Tatu, ameishiria hekima ya hilo, kwamba kuandika ndio bora na imara. Lakini pamoja na yote hayo mafaqihi wamefutu kuwa ni suna kuandika, sio wajibu. Wameendelea nalo hilo tangu zamani mpaka sasa. Nasi tuko pamoja nao kwa hilo, lakini kuna jambo jengine lisilokuwa kuandika deni na kul-ishuhudia, nalo ni kuwa mafaqihi wamewajibisha kadhi kuhukumu kwa mujibu wa ubainifu wenye uadilifu, hata kama hakupata kujua kitu kutokana na ubainifu huo. Na hilo si ni kufu-ata tamko tu? Jambo ambalo mafaqihi hawakulifuata, katika suala la kuandika, kuwa ni njia ya kuthibitisha, kama ubainifu, wakasema: "Haijuzu kuhukumu kwa maandishi mpaka akipata kujua kitu kutokana na maandishi na aridhike." Je, amri hii iliyokaririka haifahamishi kuwa kuandika ni njia ya kuthibisha haki.?

Jibu: Amri ya kuandika deni ili kuilinda haki kwenye kuthibiti, ni jambo moja, na kuzingatia ubainifu wenye uadilifu kuwa ni njia ya kuthibitisha haki, ni jambo jengine. Kwa hiyo ni wajibu kuhukumu kwa mujibu wa ubainifu, sawa awe mwenye kuhukumiwa amekiri au amekanusha.

Ama kuandika hapana budi kuulizwa mshtakiwa, akikiri, basi litakuwa ni suala la kukiri, na kama akikanusha, basi utahitajika uthibitisho kujaribu kupata uhakika kwa uchunguzi kwa kutumia njia nyingine; kama vile ushahidi, yamini au na kulinganisha hati ya mwandishi. Kwa hivyo basi maandishi peke yake hayatoshi, kuwa ni njia inayojitegemea.

Ila ikiwa ni biashara ya mkono kwa mkono mnayopeana baina yenu, basi si vibaya kwenu msipoiandika.

Hapa maneno yanahusu biashara ya mkono kwa mkono na ruhusa ya kuacha kuandika. Biashara ya mkono kwa mkono ni ile biashara ya kupeana muda huo huo. Maana ya mnay-oopeana baina yenu, ni kutoka mkono moja hadi mwengine, muuzaji anachukua thamani kutoka kwa mnunuzi na mnunuzi naye anachukua kile kilichotolewa mali kutoka kwa muuzaji.

Maana ya Aya kwa ujumla, ni kwamba si vibaya kuacha kuandika katika biashara ambayo thamani yake inatolewa muda huo huo. Ama siri ya kuacha kuandika, ni kwamba biashara hii hufanyika mara kwa mara kati ya watu; lau wangelikalifishwa kuandika kwa kila biashara, basi kungalikuwa na mashaka kwao hasa katika vitu vidogo.

Vyovyote itakavyokuwa ni kwamba sheria tukufu imewaachia watu mambo ya biashara kwa kiasi cha maslahi yao. Ikiwa maslahi yako kwenye kuandika, basi na waandike; kama ilivyo katika biashara ya viwanja, magari, n.k. Na, kama maslahi ni kuacha kuandika, kama biashara ya vyakula na mavazi, basi na waache.

52

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Mwenyezi Mungu alipoamrisha kuandika deni na biashara au kuruhusu kuacha ni amri ya kupendekeza na kuongoza kwenye mambo ambayo yatawaepushia tabu na matatizo. Hata hivyo Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anawakataza na kuharamisha hadaa, riba na kula mali kwa batili bila ya kutoa chochote.

Unaweza kuuliza; Kusema kuwa si vibaya kuacha kuandika biashara ya mkono kwa mkono inafahamisha kuwa ni vibaya kuacha kuandika deni. Kwa hivyo basi, kuandika deni ni wajibu kinyume na wanavyosema mafaqihi kuwa ni suna na wala si wajibu.

Jibu: Makusudio ya kauli Yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) "Basi si vibaya kwenu msipoiandi-ka," ni kukanusha ubaya na madhara ya kidunia, sio kukanusha dhambi na madhara ya kiakhera na kuwa kuandika ni wajibu.

Na wekeni mashahidi mnapouziana

Mafaqihi wote wameafikiana kuwa kushuhudia biashara ni sunna sio wajibu, isipokuwa watu wa madhehebu ya Dhahiri (Dhahiriya) wanasema ni faradhi sio sunna, kwa kuchuku-lia dhahiri ya tamko.

Wala asitiwe tabu mwandishi wala shahidi

Wanaouziana wakiafikiana kuandika na ushahidi basi ni juu ya mwandishi kuandika kwa uadilifu na shahidi kushuhudia kwa haki. Yamekwishatangulia maelezo kuhusu asitiwe tabu, katika kufasiri Aya ya 233.

Na kama mkifanya hivyo; basi hakika hilo ni ufasiki kwenu.

Ufasiki ni kutoka katika twaa ya Mwenyezi Mungu; na kila anayefanya kitu kilichokatazwa na Mwenyezi Mungu au kuacha kitu kilichoamrishwa na Mwenyezi Mungu, basi huyo ni fasiki aliyetoka katika twaa ya Mwenyezi Mungu mwenye kustahili ghadhabu na adhabu Yake.

Na Mcheni Mungu.

Kwa kutii amri Zake zote na makatazo yake yote.

Na Mwenyezi Mungu anawaelimsha; na Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu.

Anawaelimisha yale yaliyo na heri kwenu katika dini na dunia. Kimsingi ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hatufundishi Yeye moja kwa moja; wala haitii elimu katika akili zetu na nyoyo zetu; isipokuwa anatuelimisha kupitia wahyi anaouteremsha kwa Mitume Wake.

Wahyi huu unakusanya kila lile lililo na mwongozo na kutuongoza kwenye maslahi yanay-odhamini kudumu kwetu na utangamano wetu.

USUFI

53

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Masufi wote au baadhi wanasema hakuna njia ya maarifa na kumjua Mwenyezi Mungu na wahyi Wake na sharia na siri Zake isipokuwa kwa imani na takua (kumcha Mungu). Mwenye kumcha Mwenyezi Mungu, basi ndio amemjua na amejua sharia Yake na hukumu Zake; na ndio ameijua akhera na vituko vyake. Vilevile atakuwa ameifahamu Qur'an na Hadith bila ya darasa au taaluma yoyote. Hii wanaiita elimu ya ki-Mungu na wakatoa dalili kwa kauli Yake Mwenyezi Mungu:

Na mcheni Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu anawaelimisha.

Lakini tamko la Aya linakataa dalili hii. Kwa sababu lau ingelikuwa kama walivyosema basi, kinahw, tamko Yuallimukum lingejazimishwa kuwa ni jawabu la Ittaqu na lingeambatanish-wa na herufi Fai na wala sio kwa herufi Wau. Zaidi ya hayo maana katika fikra ya kauli hii ya kisufi, inafanana na kauli ya mtu aliyepagawa akisema: "Hakika nyumba haitimii kujeng-wa ila baada ya kukaliwa, na kwamba nguo haikamiliki kushonwa ila baada ya kuvaliwa."

Sijui Masufi wanadai vipi hali hii; na hali imekuja hadith mutawatir kutoka kwa Mtume (s.a.w.) inayosema: "Tafuteni elimu japokuwa China" na" Elimu ni kwa kujifundisha". Sisi hatuna shaka kabisa kwamba nadharia inadhihirika kwa kufuatilia na kutenda, na kwamba mtaalamu mwenye kufanya kazi, hufungukiwa na mambo mapya. Lakini hili ni jambo jengine na kuwa taqwa ni nyenzo ya maarifa ni jambo jengine.

Na kama mkiwa safarini na hamkupata mwandishi, basi ni itakayo kabidhiwa rahani

Baada ya Mwenyezi Mungu kuamrisha kuandika deni kwa ajili ya kulihifadhi, amejaalia rahani ndio tegemeo badala ya kuandika, kama kukiwa na udhuru.

Mafaqihi wameafikiana kwamba rahani haitimii bila kukabidhiana. Wametoa dalili kwa kauli hii: "Basi ni rahani itakayokabidhiwa" Ufafanuzi uko katika vitabu vya Fiqh; kama vile Fiqhul Imam Jaffar Sadiq Juzuu ya 4.

Unaweza kuuliza: Rahani inajuzu katika safari na nyumbani, na pamoja na kupatikana mwandishi au kukosekana; sasa nini makusudio hapa ya kuleta sharti la safari na kukosekana mwandishi?

Baadhi ya wafasiri wamelipuuza swali hili, ingawaje linaweza kumjia kila mwenye kujua hukumu za sheria. Wengine wamejibu kuwa Mwenyezi Mungu amepitisha kwa aghlabu, kwa kuwa wakati huo ilikuwa ni nadra kupatikana mwandishi safarini. Lakini iinavy-oonekana ni kwamba pia aghlabu ni kukosekana rahani katika safari. Kwani ni nani anayechukua vitu vinavyoweza kuwekwa rahani katika safari, isipokuwa kwa nadra tu?

Jibu: sahihi ni kwamba Aya kwa dhahiri inafahamisha kutojuzu rahani nyumbani, kwa kuchukulia kuwa sharti limefahamika; yaani kama hamko safarini basi hakuna rahani. Lakini dhahri hii haijuzu kuitegemea baada ya kuthibiti kwamba Mtume (s.a.w.) aliyeshuki-wa na wahyi, hakuitumia dhahiri hiyo.

Yeye aliwahi kuweka rahani deraya yake kwa myahudi alipokuwa nyumbani Madina. Wala hii sio Aya pekee ambayo tunaiacha dhahiri yake kwa Sunna ya Mtume. Na ni kwa sababu hii ndipo umma wa kiislam umesema, kwa kauli moja, kwamba haijuzu kuchukulia dhahiri ya Aya katika Aya za hukumu ya sharia, ila baada ya utafiti wa Hadith za Mtume zilizopokewa kutolea dalili Aya Tukufu.

54

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

Na kama mmoja wenu akimwamini mwengine,basi aliyeaminiwa atekeleze uaminifu wake, na amche Mungu, Mola wake

Yaani mdeni akiwa na dhana nzuri kwa mdaiwa, akampa bila ya cheti wala rahani au ushahidi wowote wa kutegemea, basi ni juu ya mdaiwa aiendeleze ile dhana nzuri na amrudishie mdai haki kamili.

Zaidi ya hayo hukumu hii ni ya ujumla haihusiki na deni tu, bali inachanganya amana zote. Mwenyezi Mungu amesema "Hakika Mwenyezi Mungu anawaamrisha kutekeleza (kuzirud-isha) amana kwa wenyewe..." (4:58)

Mtume naye anasema: "Msiangalie Swala ya mtu na Saumu yake, na wingi wa Hijja zake na umaarufu wake; na kuvuma kwake usiku, lakini angalieni ukweli wa mazungumzo yake na utekelezaji wake wa amana."

Imam Zainul Abidini (a.s.) anasema: "Lau kwamba aliyemuua baba yangu ananiwekea amana upanga aliomuulia baba yangu, basi nitamrudishia."

Wala msifiche ushahidi. Na atakayeuficha, basi hakika moyo wake ni wenye kuingia dhambini

Kuna tofauti kati ya kuchukua ushahidi na kuutekeleza. Maana ya kuuchukua ushahidi ni kuitwa ushuhudie haki au deni. Hapa kukubali ni wajib kifaya (wa kutosheana) na wala sio wajib ayni; kama tulivyyoeleza huko nyuma. Ama kuutekeleza ni kukuita mwenye haki baada ya wewe kuuchukua ushahidi, ili utoe katika mahakama; hapa huwezi kukataaa ikiwa haki haitaweza kuthibiti bila ya ushahidi wako, na kukawa hakuna madhara. Kama hutafanya basi utakuwa na dhambi kutokana na kauli Yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) "Wala msifiche ushahidi"

Na makusudio ya moyo wake kuingia dhambini, ni kwamba yeye ataadhibiwa adhabu ya kukusudia dhambi, kwa sababu kukusudia ni katika sifa za moyo.

284. Ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na kama mkidhihirisha lililo katika nafsi zenu, au mkilificha, Mwenyezi Mungu atawataka his-abu ya hilo; kisha amghufirie amtakaye, na amwadhibu amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.

Kaashif3-46.jpgKaashif3-47.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

Aya 284: KAMA MKIDHIHIRISHA YALIYOMO KATIKA NYOYO ZENU

MAANA

Ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na kama mkidhi-hirisha lililo katika nafsi zenu, au mkilificha, Mwenyezi Mungu atawataka hisabu ya hilo.

Mara nyingine katika moyo wa mtu hupita mawazo mabaya asiyowezea kuyazuia; kama vile kutamani kubomoka nyumba ya fulani au akanyagwe na gari. Katika mawazo kama haya hakuna hisabu wala adhabu, maadamu ni mawazo tu yasiyoonekana athari ya viten-do au maneno yake. Kwa sababu haya yako nje ya uwezo, kukalifishwa nayo ni kukali-fishwa yasiyowezekana.

Mara nyingine mtu huazimia maasi kabisa na kukusudia kuyafanya, mpaka anapokurubia kuyafanya, basi hurudi nyuma, ama kwa kumwogopa Mwenyezi Mungu au kuogopa watu. Basi ikiwa ni kwa kumwogopa Mwenyezi Mungu hupata thawabu, kwa sababu kunahisabi-wa ni kutubia. Na, kama ni kwa kuwaogopa watu, basi hakuna malipo yoyote, si thawabu wala adhabu, kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na ukarimu wake.

Kuna Hadith inayosema: "Mtu akikusudia wema na kisha asiufanye huandikiwa wema mmoja; na kama akiutenda, huandikiwa kumi. Na kama akikusudia uovu akaufanya, hundikiwa ovu moja, na kama hakuufanya, basi haandikiwi chochote."

Mara nyingine mtu huazimia kufanya maasi, na kuyafanya kwa vitendo. Maasi haya yako aina mbili: Kwanza ni kumwasi Mwenyezi Mungu waziwazi, bila ya kujali maneno ya watu na lawama zao. Hayo ndiyo makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu: "Na kama mkid-hihirisha yaliyomo katika nafsi zenu."

Aina nyingine ni ya kuficha maasi kwa unafiki na ria kufanya ufisadi kwa kujificha na kutangaza wema. Aina zote hizo anazijua Mwenyezi Mungu.

Kisha amghufirie amtakaye na amwadhibu amtakaye

Maadamu Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni mfalme wa mbingu na ardhi Muweza wa kila kitu, asi anao uweza wa kusamehe amtakaye katika uasi na kumwadhibu amtakaye kutokana na inavyohukimilia hekima Yake. Muhyiddin Ibn al Arabi anasema katika tafsiri yake kwamba Mwenyezi Mungu anamsamehe mwasi akiwa ana nguvu katika imani yake, lakini akawa amezukiwa tu kufanya maasi, sio kuwa yameota mizizi katika nafsi yake, na humwadhibu muasi aliye mdhaifu wa imani ambaye maasi yameota mizizi katika nafsi yake.

285. Mtume na Wa4umini, wote wameami-ni yaliyoteremshwa kwake kutoka kwa Mola wake, na wamemwamini Mwenyezi Mungu na Malaika Wake na Vitabu Vyake na Mitume Wake: Hatutofautishi baina ya yoyote katika Mitume wake. Na husema: Tumesikia na tumetii. Twaomba maghufira yako Mola wetu! Marejeo ni Kwako.

Kaashif3-48.jpgKaashif3-49.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

2. Sura Al-Baqarah

Kaashif3-50.jpg

286. Mwenyezi Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila uweza wake. Faida ya yale iliyoyachuma ni yake na hasara iliyochuma ni yake. Mola wetu! Usituadhibu tukisahau au tukikosa. Na usitutwike mzigo kama uliyowatwika wale waliokuwa kabla yetu. Mola wetu! Usitutwike tusiyoyaweza na utusamehe na utughufurie na uturehemu wewe ndio Mola wetu na utunusuru na watu makafiri.

MTUME AMEAMINI Aya ya 285 - 286

LUGHA

Makosa hutumiwa kwa maana tatu: Dhambi, kutokusudia, na kutofanya sawa. Maana hii ya mwisho, ndiyo iliyokusudiwa katika Aya.

MAANA

Mtume ameamini yaliyoteremshwa kwake.

Hapa kuna swali linalojitokeza - kwamba kila Mtume anaamini wahyi ulioteremshwa kwake, vinginevyo hatakuwa Mtume. Kwa hiyo kulielezea hili kunafanana na kuliweka wazi ambalo tayari liko wazi, na kujaribu kulipata ambalo lipo, jambo ambalo haliwezekani katika maneno ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwa hiyo hapana budi kuwe na lengo la kulielezea hilo. Ni lipi basi?

Jibu: Lengo sio tu kueleza kuwa Mtume (s.a.w.) amemuwamini Mwenyezi Mungu hapana! Kwani kila Mtume anazaliwa akiwa amemwamini Mwenyezi Mungu na Umoja wake, laki-ni sio kila Mtume anazaliwa akiwa Mtume, au kujua kuwa yeye ni Mtume isipokuwa Nabii Isa (a.s.) ambaye mara tu alipozaliwa alisema:

"Hakika mimi ni mja wa Mwenyezi Mungu, amenipa kitabu na amenifanya Nabii" (19:30)

Muhammad (s.a.w.) hakushukiwa na wahyi mpaka alipofika miaka arobaini katika umri wake mtukufu. Alipoambiwa na Jibril mara ya kwanza "Soma kwa jina la Mola wako ambaye ameumba" (96: 1)

57

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Alitia shaka na akahofia isije ikawa sauti ile ni wasiwasi na mawazo tu, mpaka akamwambia mkewe mpenzi, Khadija, aliyekwenda naye kwa Waraqa bin Naufal; kisha akampa maele-zo ya kutosha kwamba aliyemjia ni Malaika wala sio shetani.

Kwa hivyo basi inatubainikia kuwa lengo katika kauli yake Mwenyezi Mungu; "Mtume ameamini yaliyoteremshwa kwake" ni kwamba yaliyokuja katika Sura hii na mengineyo katika misingi ya imani na itikadi, maonyo, hukumu na kila aliyoyatolea habari Mtume, ni katika wahyi wa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Na wahyi huo hakuuamini Mtume ila baada ya kupitiwa na shaka, utafiti na kuchunguza vizuri; na baada ya kufunuliwa na uhakika kabisa. Kwa hiyo kila analolielezea Mtume, basi linatoka kwa Mwenyezi Mungu bila ya shaka yoy-ote.

MAELEZO:

Maulama wengi wa Kishia hawakubaliani na usahihi wa Kisa hiki, miongoni mwao ni Mwanachuoni Sayyid Muhammad Hussein Tabatabai katika Tafsir Al-Mizani anasema katika kufasiri sura ya Alaq (97:1), baada ya kutaja kisa cha Waraqa bin Naufal:

Kisa hiki hakiwezi kuepukana na shaka. Kinachodhoofisha usahihi wake ni shaka ya Mtume (s.a.w.w.) kwa Wahyi wa Mwenyezi Mungu na kusitasita kwake na kudhani eti amezugwa na shetani?!

Linalotia shaka zaidi ni kwamba yeye alipata uhakika wa Utume wake kutoka kwa Mkristo na hali Mwenyezi Mungu anasema katika Qur'ani "Sema mimi nina dalili ya wazi itokayo kwa Mola wangu" (6:57) sasa dalili ya wazi ni kauli ya Waraqa? Na Aya isemayo.

"Sema hii ndiyo njia yangu, ninailingania kwa Mwenyezi Mungu kwa ujuzi, mimi na wanaoni-fuata" (12:108) Je, ujuzi ndio huo alioupata kwa Waraqa? Na ujuzi wa wale wanaomfuata unatokana na kumfuata yeye asiyekuwa na uhakika? "Mwenyezi Mungu anasema tena "Hakika sisi tumekuletea Wahyi kama tulivyompelekea Wahyi, Nuh na Manabii baada yake." (4:163)

Je, hao Mitume wengine kupata kwao wahyi kulitegemea watu kama kina Waraqa?.

Ilivyo ni kuwa wahyi wa utume nilazima uwe na uhakika kutoka kwa Mtume mwenye kuwa unatoka kwa Mwenyezi Mungu.

Katika kufasiri Aya hii (Ameamini Mtume) mwenye Tafsir Al-Mizan anasema:

Ni kusadikisha imani ya Mtume na waumini. Amewekwa peke yake Mtume kisha akaun-ganishwa na waumini kwa kumtukuza.

Hii ni desturi ya Qur'an katika maelezo yanayohusiana na kumtukuza Mtume kumtaja yeye kwanza kisha kufuatishia wengine; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

"Basi hapo Mwenyezi Mungu aliteremsha utulivu wake juu ya Mtume wake na Waumini" (48:26)

"Siku ambayo Mwenyezi Mungu hatamfedhehesha Mtume na wale walioamini pamoja naye." (66:8)

Kwa ujumla sura ya Baqara imeanzia kwa kueleza sifa wanazostahiki kuwa nazo wachamungu .___________________________________________________________

58

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Kama vile kuamini ghaib, kuswali, kutoa, kuamini Mitume na akhera, kinyume na makafiri na wanafiki.

Kisha ikaelezea hali ya watu wa kitabu; hasa Mayahudi ambao Mwenyezi Mungu aliwa-neemesha kwa neema mbali mbali, lakini wakakufuru badala ya kushukuru. Hivyo Mwenyezi Mungu akawaadhibu kwa aina mbali mbali za adhabu; kama kujiua, kugeuzwa kuwa manyani , kushuka vimondo adhabu kutoka mbinguni n.k

Mwisho sura inaelezea wasifu wa Mtume na wafuasi wake kwamba wao ni kinyume na watu wa Kitab walivyoikabili neema ya Mwenyezi Mungu. Wamesikia na kutii, hali ya kumwamini Mwenyezi Mungu, Malaika wake, Vitabu Vyake na Mitume Yake bila ya kum-bagua yeyote katika Mitume.

Na waumini; wote wamemwamini Mwenyezi Mungu na Malaika wake na vitabu vyake na Mitume wake: Hatutofautishi baina ya yoyote katika Mitume wake

Maana kamili ya kumwamini Mwenyezi Mungu sio kuitakidi kwamba Yeye ni Muumbaji wa ulimwengu tu, hapana, mumin wa kweli ni yule anayemwamini Mwenyezi Mungu na Mitume na vitabu vilivyoteremshiwa wao pamoja na yaliyomo ndani yake, ikiwa ni pamoja na misingi, hukumu, Malaika na mengineyo katika mambo ya ghaibu, bila ya kuacha mengine. Mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu bila ya kuamini Vitabu Vyake na Mitume wake, au kuamini baadhi ya Vitabu Vyake na Mitume Wake, hukumu yake kesho mbele ya Mwenyezi Mungu ni hukumu ya asiyeamini kabisa.

Lau watu wa dini wangelichukua misingi ya kumwamini Mwenyezi Mungu na kila alilolileta, basi kusingekuwa na makundi na migogoro; lakini wao wameamini baadhi na wakakanusha baadhi, ndipo kukawa na uadui huu wa kuendelea.

Mwenyezi Mungu hakalifishi nafsi yoyote ila uweza wake.

Kwa sababu kukalifisha bila ya uwezo ni dhulma

"... Na kwamba Mwenyezi Mungu si dhalimu kwa waja." (3:182)

Lakini Ashaira wamejuzisha taklifa bila ya uwezo. Shia Imamiya na Muutazila

wamekanusha.

Faida ya yale iliyoyachuma ni yake; miongoni mwa kheri. Na hasara ya iliyochuma ni

yake.Miongoni mwa shari na maovu.

"Mwenye kufanya heri sawa na chembe ataiona. Na mwenye kufanya shari sawa na chem-be ataiona" (99: 7 -8)

Miongoni mwa rehema za Mwenyezi Mungu kwa waja wake ni kwamba mja akifanya wema humwandika hapo hapo, lakini akifanya uovu, humpa muda, akiomba msamaha na kujuta, hamwandikii kitu.

Baadhi ya wataalamu wanasema: Mtu hufanya wema kwa msukumo wa nafsi yake, kwa sababu ndio umbile lake; na hafanyi shari isipokuwa kwa vichocheo vya nje kama vile mazingira na malezi mabaya.

59

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                            2. Sura Al-Baqarah

Kwa hali hiyo ndio maana Mwenyezi Mungu akatumia neno Kasaba katika heri lenye maana ya kuchuma tu na akatumia neno Iktasaba katika shari lenye maana ya kuchuma zaidi.

Mola wetu! Usituadhibu tukisahau au tukikosa.

Hapa kuna mushkeli mashuhuri ambao umezungumzwa sana na umejaribiwa kujibiwa katika elimu ya Usul na Tawhid. Mushkeli wenyewe kwa ufupi ni kwamba kukosea na kusahau hakuko chini ya matakwa ya mtu na uwezo wake. Kwa hiyo kuadhibiwa hakuko; kwa mfano mwenye kusahau kuswali au akakosea katika kufahamu hukumu ya sharia, anahukumiwa kuwa na udhuru. Kwa hivyo basi hakuna maana wala haja ya kuomba kuon-dolewa adhabu.

La kustaajabisha ni jinsi alivyojibu Sheikyh Muhammad Abduh - kama alivyonakili mwenye Tafsiri ya al Manar - kwamba mwenye kusahau na mwenye kukosea inafaa kuadhibiwa kwa dalili ya sharia ya kiislamu na sharia zilizowekwa na binadamu, ambazo zimewajibisha kulipa mtu aliyeharibu mali ya mwingine kwa makosa, kama aliyeuwa kimakosa.

Kushangaza kwake ni kwamba, makusudio ya kuadhibiwa katika Aya ni adhabu na majuku-mu ya kitabia, sio gharama. Kwa hiyo anayemuua mtu kimakosa au kuharibu mali kwa makosa haadhibiwi wala haulizwi kitu upande wa kitabia; isipokuwa atahukumiwa kulipa gharama ya kimali tu, sawa na mtu anayedaiwa.

Jibu sahihi ni kwamba kukosea na kusahau mara nyingine humtokea mtu baada ya kujichunga. Aina hii ndiyo ambayo mtu husamehewa wala haifai kumwadhibu.. Hayo ndiyo makusudio ya Aya tukufu. Na pengine kosa na kusahau hutokea kwa sababu ya kuzembea na kuacha kujihifadhi, kwa namna lau angezindukana na kujilinda hayangemtokea. Aina hii huwa mtu hasamehewi na inafaa kumwadhibu. Hilo, katika dua, ndilo linaloombwa lion-dolewe. Kwa hiyo hapo hakuna mushkeli tena.

Mola wetu! Wala usitutwike mzigo kama uliyowatwika wale waliokuwa kabla yetu. Mola wetu! Usitutwike tusiyoyaweza.

Makusudio ya mzigo hapa ni taklifa na mashaka. Mwenyezi Mungu aliwatwika wana wa Israil, pale alipowaamrisha kuswali Swala hamsini mchana na usiku na katika taklifa za mashaka ambazo wamezitaja wafasiri walipofasiri: "Kama ulivyowatwika wale waliokuwa kabla yetu" Kwa hivyo maana yanakuwa usitukalifishe yaliyo mazito.

Unaweza kuuliza: Kauli ya Mwenyezi Mungu; "usitutwike tusiyoyaweza" ina maana sawa na "usitutwike mzigo" ambapo hapo ni kuunganisha jumla zenye maana sawa?

Jibu:Kama tukiangalia jumla ya"usitutwike tusiyoyaweza" kuwa ni jumla mbali iliyoepukana na mfumo wa maneno, basi itakuwa hivyo. Kwa sababu maana ya dhahiri ni usitutwike yaliyo na mashaka na sisi. Lakini tukiangalia kuwa iko pamoja na mfumo mzima wa maneno, itakuwa na maana ya: Usituadhibu adhabu tusiyoweza. Kwa hiyo ikafasiriwa adhabu kuwa ni lile linalopelekea adhabu tusiyoiweza na kuivumilia. Sheikh Murtadha al Ansari katika kitabu chake kinachoitwa al Rasail mlango wa Baraa anasema: "Sio mbali kuwa makusudio ya tusiyoyaweza katika Aya ni adhabu na mateso, kwa hiyo maana ya usitutwishe tusiyoyaweza ni usitupe adhabu tusiyoiweza."

Na utusamehe na utughufurie na uturehemu

Msamaha, maghufira na rehema ni matamko yenye kukurubiana, tofauti ni ndogo kwam-

60

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3 Sura Al-Imran

ba msamaha ni kutoadhibiwa tu; maghufira ni kutoadhibiwa na kusitiriwa dhambi, na rehe-ma ni kutaka kufadhiliwa na kuneemeshwa kwa thawabu.

Wewe ndiwe Mola wetu na utunusuru na makafiri.

Ambao wanaidharau dini ya Mwenyezi Mungu,na kumtukuza asiyekuwa Mwenyezi Mungu.

Katika Majmau imeelezwa kuwa imepokewa kutoka kwa Mtume (s.a.w.) kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) katika kila kifungu cha dua hii husema: "Nimefanya na nimeitikia (maombi)." Kwa hivyo basi ndipo ikawa sunna kusoma sana dua hii:

"Mola wetu! Usitutese kama tukisahau au tukikosea. Na usitutwike mzigo kama ulivy-owatwika wale waliokuwa kabla yetu. Mola wetu! Usitutwike tusiyoyaweza na utusamehe na utughufirie na uturehemu wewe ndiwe Mola wetu na utunusuru na watu makafiri."

AL -IMRAN

1.Alif laam miim

2.Mwenyezi Mungu hakuna mola isipokuwa yeye aliyehai msimamizi wa kila jambo .

3.Amekuteremshia kitabu kwa haki kina-chosadikisha yaliyokuwa kabla yake. Na aliteremsha Tawrat na Injil.

.Kabla yake ziwe ni uwongozi kwa watu na ameteremsha upambanuzi. Hakika wale waliokufuru Aya za Mwenyezi Mungu wana adhabu kali, na Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu Mwenye kutia adabu

5.Hakika MwenyeziMungu hakifichiki Kwake chochote kilichomo ardhini wala kilichomo mbingu.

Kaashif3-51.jpg

61

4

4

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

6.Yeye ndiye anayewatia sura matumboni jinsi anavyotaka. Hakuna Mola isipokuwa yeye mwenye nguvu Mwenye hekima.

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye kurehemu

Kaashif3-52.jpg

MAANA

Yamekwishapita maelezo kuhusu (Alif Laam Miim) katika mwanzo wa Sura Baqara. Vile vile maelezo ya hakuna Mola yameelezwa mwanzo wa Aya Kursiy (2: 255).

Amekuteremshia Kitabu kwa haki, kinachosadikisha yaliyokuwa kabla yake.

Makusudio ya Kitabu ni Qur'an; ambayo inasadikisha vitabu vilivyoteremshiwa Mitume waliotangulia.

Kimsingi ni kwamba kusadikishwa yaliyoteremshiwa Mitume waliotangulia, hakulazimishi kusadikisha vitabu vinavyonasibishwa kwao na baadhi ya makundi. Na sisi waislamu tumeamini kauli ya Mtume (s.a.w.), lakini pamoja na hivyo hatuamini kila kilicho katika vitabu vya Hadith zilizoelezwa kutokana naye. Ama yule anayeamini vitabu vilivyotangulia, basi ni juu yake kuamini Qur'an, vinginevyo atakuwa anajipinga yeye mwenyewe. Kwa sababu Qur'an inasadikisha vitabu hivyo. Kwa hiyo kuikadhibisha Qur'an ndio kuvikadhibisha vitabu vingine.

Na aliteremsha Tawrat na Injil kabla yake, ziwe ni uwongozi kwa watu.

Kuisifu Tawrat na Injil kuwa ni uongozi, kunalazimisha kuwa vimeteremshwa kwa haki; kama ambavyo kuisifu Qur'an kuwa ni uwongozi kunalazimisha kuwa imeteremshwa kwa haki. Kwa hivyo basi, kila kimoja katika vitabu vitatu hivyo ni cha haki na ni uwongozi.

Makusudio ya uwongozi hapa, ni ubainisho wa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) wa halali na hara-mu kupitia katika ulimi wa Mitume Yake. Na, ubainifu huu unamaanisha kujua hukumu za Mwenyezi Mungu. Ama kuzitumia hizo hukumu, kunahitaji aina nyingine ya uwongozi zaidi ya ubainifu. Mimi sikupata tamko jengine la kuelezea aina hiyo isipokuwa neno Tawfiq. Nayo inaashiriwa na neno lake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Kwa hakika wewe huwezi kum-wogoza umpendaye, lakini Mwenyezi Mungu humwongoza amtakaye." (28: 56)

Qur'an inalitumia Neno Tawrat kwa maana ya wahyi ulioteremshiwa nabii Musa (a.s.); na neno Injil kwa Wahyi ulioteremshiwa nabii Isa (a.s.). Lakini Qur'an imebainisha kuwa Tawrat na Injil inayozikubali sio zile zilizoko kwa mayahudi na wakristo hivi sasa.

Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: Miongoni mwa mayahudi wamo ambao huyabadilisha

maneno kuyatoa mahali pake. (4:46).

Na kwa wale waliosema: Sisi ni wanasara (Wakristo) tulichukua ahadi kwao, lakini

62

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

wakaacha sehemu ya yale waliyokumbushwa.

Enyi watu wa Kitabu! Amekwisha wafikia mtume wetu, anayewabainisha mengi mliyokuwa mkiyaficha katika kitabu. (5:14-15)

Wahubiri wa kimasihi wanayajua sana haya, lakini pamoja na hayo wanajisifu na kuwavun-ga watu kuwa Qur'an inakiri Tawrat na Injil iliyochezewa na mikono ya kugeuza.

Ilivyo, ni kuwa Qur'an yote ni moja na jumla moja; kwa hiyo haifai kuamini sehemu fulani na kukanusha sehemu nyingine.

Tawrat ni neno la Kiebrania lenye maana ya sharia; nayo imegawanywa kwenye vitabu vitano:

1.            Mwanzo, chenye maelezo ya kuanza kuumbwa ulimwengu na habari za Mitume.

2.            Kutoka, ndani yake mna historia ya wana wa Israil na kisa cha Musa.

3.            Kumbukumbu la Tawrat, humo mna hukumu za sharia ya Kiyahudi.

4.            Walawi, humo mna mambo ya ibada na ndege na wanyama walioharamishwa. Walawi ni kizazi cha mmojawapo wa watoto wa Yakub anayeitwa Lawi.

5.            Hesabu, ndani yake mna mkusanyiko wa koo za Wana wa Israil na majeshi yao.

Vitabu hivi vitano ni mkusanyiko wa vitabu vidogo vidogo vipatavyo thelathini na tisa, na wakristo wanaviita Agano la kale.

Ama Injil, asili yake ni neno la kiyunani; maana yake ni bishara (khabari njema). Na Injili kwa wakristo ni nne:

1.   Mathayo: Historia ya kutungwa kwake ina kiasi cha miaka 60 (A.D). Na iliandikwa katika lugha ya kiarmenia.

2.   Marko: iliyotungwa kwenye mwaka wa 63 au 65 (A.D) kwa lugha ya kiyunani.

3.   Luka: iliyotungwa pia kwa lugha ya kiyunani kwa tarehe ile ya Marko.

4.   Yohana: vile vile kwa lugha ya kiyunani kwenye mwaka 90 (A.D.)

Rai ya wakristo ilithibiti mwanzoni wa karne ya 5 A.D kwa kutegemea vitabu ishirini na saba katika vitabu vyao. Wakasema kwamba ni ufunuo (wahyi) kutoka kwa Mungu kwa kimaana sio kitamko. Na wakavipa jina la Agano jipya, likiwa ni mkabala wa lile la zamani wanalo-litegemea mayahudi.

Kwa hiyo Agano la zamani, ni agano la Musa; na lile jipya ni la Isa, umepita ufafanuzi unaombatana na hayo katika Sura ya pili, Aya ya tatu.

Na ameteremsha upambanuzi.

Yaani upambanuzi baina ya haki na batili. Wametofautiana sana kuhusu makusudio ya upambanuzi; je, ni akili, Zaburi, Qur'an au ni dalili inayopambanua baina ya haki na batili? Sheikh Muhammad Abduh amechagua akili. Mwenye Majmaul Bayan amechagua Qur'an. Tamko la Aya linachukua maana zote mbili.

Hakika wale waliozikufuru Aya za Mwenyezi Mungu wana adhabu kali, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mwenye kutia adabu.

63

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Wafasiri wanasema kwamba watu wapatao sitini katika wakristo wa Najran, Yemen, walim-fikia Mtume mnamo mwaka wa tisa Hijria; mwaka uliojulikana kama mwaka wa ugeni. Kwani wageni wengi walimfikia Mtume kutoka sehemu mbali mbali za Bara Arabu, wakielezea utii na mapenzi yao kwake, baada ya Mwenyezi Mungu kumpa ushindi kwa maadui.

Ugeni wa kinajran ulitoa hoja ya itikadi ya kikiristo ya utatu na uungu wa Isa. Kwa hoja ya kuwa Isa ni mtoto asiyekuwa na baba pamoja na miujiza aliyoifanya ambayo Qur'an imeielezea.

Vilevile wafasiri wanasema Sura ya Al-Imran kuanzia mwanzo wake hadi Aya thamanini ilishuka juu ya wakristo wa Najran na majibu yao: Mwenyezi Mungu akaanza kwa kutaja Tawhid (umoja) ili kukanusha utatu; kisha akataja Qur'an, Tawrat na Injil kwamba vitabu vitatu hivi vinamwepusha Mwenyezi Mungu na mtoto na kugawanyika. Vilevile vinakanusha uungu wa Isa. Kisha Mwenyezi Mungu akataja:

Hakika Mwenyezi Mungu hakifichiki kwake chochote kilichomo ardhini wala kili-chomo mbinguni.

Ikiwa ni majibu ya kauli ya wakristo kwamba Isa alikuwa akijua ghaibu.

Tena akaendelea Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kusema:

Yeye ndiye ambaye huwatia sura matumboni jinsi anavyotaka, hakuna Mola

isipokuwa Yeye Mwenye nguvu na Mwenye hekima.

Mwenyezi Mungu anayataja haya ili abatilishe kauli ya Wakristo kwamba Isa ni Mungu kwa sababu ya kutokuwa na baba; kwa maana ya kuwa Mungu haumbwi na kuwa tumboni mwa mama. Akipenda anaweza kumuumba kupitia baba na kama akipenda anaweza kumuum-ba bila ya baba, kwa kiasi kile hekima yake takatifu inavyotaka.

Kwa ufupi ni kuwa kutolea habari baadhi ya mambo ya ghaibu, kufufua baadhi ya wafu na kuzaliwa bila ya baba, hakumaanishi kuwa Isa (Yesu) ni Mungu. Kwa sababu Mungu ni yule anayejua mambo ya ghaibu, hakifichiki kwake chochote katika ardhi au mbinguni, Mwenye kufufua wafu wote sio baadhi, anayeweza kila kitu hata kuumba bila ya kitu kingine. Kwa dhahiri ni kwamba Isa hakuwa akijua ghaibu zote, wala hakuweza kufufua maiti wote na hakuumba yeyote tumboni mwa mama yake bila ya baba au na baba; bali kinyume chake ndio sahihi, kwani yeye ndiye aliyeumbwa ndani ya tumbo la uzazi

7.Yeye ndiye aliyekuteremshia Kitabu ndani yake zimo Aya zilizo waziwazi ambazo ndizo msingi wa Kitabu na nyingine zenye kufichikana. Wale ambao nyoyoni mwao mna upotofu wanafuata zile zinazotatiza kwa kutaka kuharibu na kutaka tafsiri yake. Na hajui tafsir yake isipokuwa

Kaashif3-53.jpg

64

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

Mwenyezi Mungu na waliozama katika elimu. Husema tumeziamini zote zimeto-ka kwa Mola wetu. Na hawakumbuki isipokuwa wenye akili.

3. Sura Al-Imran

8. Mola wetu! Usizipotoshe nyoyo zetu baada ya kutuongoza na utupe rehe-ma kutoka kwako. Wewe ndiwe mpaji mkuu.

Kaashif3-54.jpg

9.Mola wetu! Wewe ndiwe mwenye kuwakusanya watu katika siku isiyo na shaka ndani yake. Hakika Mwenyezi Mungu havunji miadi.

Aya 7 - 9

Yeye ndiye aliyekuteremshia Kitabu ndani yake zimo Aya zilizo waziwazi nazo ndizo msingi wa kitabu. Na nyingine zenye kufichikana.

Zilizo waziwazi ni Aya ambazo hazihitaji ufafanuzi na makusudio yake yanafahamika kwa njia ya mkato bila ya kuhitaji tafsiri, kuhusisha au kufutwa hukumu (Naskh). Wala haziwapi nafasi wale wenye maradhi ya kupoteza na kufikiri kwa taawili na kugeuza. Mfano: sema Yeye Mwenyezi Mungu ni mmoja ... Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kilajambo ... Wala had-hulumu (hata amali) sawa na chembe Hakika Mwenyezi Mungu haamrishi uovu ... Na kwamba Kiyama kitakuja hakuna shaka.

Na Aya nyenginezo ambazo anaweza kuzifahamu mwenye elimu na asiyekuwa na elimu.

Ama Aya zenye kufichikana ziko aina nyingi: Kuna zinazofahamika kiujumla bila ya upam-banuzi, mfano kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na tukampulizia katika roho yetu ... (21:91)

Kwa hakika kujua roho yenyewe hasa ni nini, hiyo ni siri ya Mungu haijui yeyote hata wataalamu pia. Na wala sio sharti anayeambiwa kitu kuwa lazima ajue anayoambiwa kwa

65

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

upambanuzi, bali inatosha tu kufahamu kiujumla.

Nyengine ni zile zinazofahamisha jambo linalokataliwa na akili mfano, kauli yake Mwenyezi Mungu: "Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema amestawi juu ya kiti cha enzi." (20:5)

Hapa akili inakataa kwamba Mwenyezi Mungu akae juu ya kiti, kwa sababu Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni zaidi ya wakati na mahali. Kwa hiyo hapo inabidi kuleta tafsiri kwa maana ya kutawala. Na hapana budi kuwa tafsiri (taawil) iwe ni dalili sahihi itakayotoa maana sahi-hi ya tamko; na hayo hawayajui isipokuwa watu maalum.

Aya nyingine iliyofichikana, ni kukubali tamko baina ya maana mbili na zaidi, mfano: Na wanawake walioachwa wangoje mpaka tohara tatu (2: 228). Hapo kuna 'Quruw' ambalo linakubali maana ya tohara na hedhi.

Nyengine ni kuwa tamko ni la kiujumla maana yake ya dhahiri yawaingiza wote ingawaje makusudio ni baadhi tu; mfano: "Na mwizi mwanamume na mwizi mwanamke, ikatwe mikono yao" (5:38)

Hapo wametajwa wezi wote pamoja na kujulikana kuwa kuna wezi wengine hawakatwi; kama ikiwa mwizi ni baba wa aliyeibiwa, au mwaka wa njaa, au kilichoibwa kikiwa hakikuhi-fadhiwa, au thamani ya kilichoibiwa ikiwa chini ya robo dinari.

Nyengine ni kufutwa hukumu na kuwekwa nyengine; kama vile kuswali kuelekea Baitul Maqdis, ambapo ilifahamika kuthibiti Kibla hiki na ikaendelea hukumu mwanzoni mwa uis-lam, kisha ikaja hukumu ya kufuta hilo na Kibla kikawa Al-kaaba.

Sio sharti kutotarajiwa kujulikana Aya za kufichikana kabisa. Kwani aina zote ukiondoa ile ya kwanza, inawezekana kwa wanavyuoni wa Usul - wanaojua njia za taawili, hukmu za kuhusisha na za kiujumla, kufuta na kufutwa na kutilia nguvu baina hukumu mbili zina-zopingana - kutoa hukmu za kuhusisha na za kiujumla, kupambanua baina ya kufuta na kufutwa, chenye nguvu na kisicho na nguvu na maana yanayoingilika akilini ambayo yame-fanyiwa taawili baada ya kutoingilika akilini.

Ndio! Kwa asiyekuwa na elimu, hizo Aya za kufichikana zinabaki kuwa hivyo hivyo, kwa kuwa haijuzu kufanya taawili au kuchukua dhahiri inayokubali kuhusisha au kufutwa. Kwa ufupi ni kuwa wanavyuoni wanajua maana ya Qur'an ambayo kwao ni fasihi iliyo wazi. Kwa sababu haiwezekani kuwa Mwenyezi Mungu ateremshe maneno yasiyokuwa na maana au yasiyofahamiwa na yeyote. Itakuwaje hivyo ikiwa yeye mwenyewe Mwenyezi Mungu anaamrisha kuizingatia vizuri Qur'an; na mazingatio hayaji ila kwa kinachoingilika akilini; na kisichofahamika hakiwezi kuzingatiwa.

Unaweza kuuliza kuwa Mwenyezi Mungu amekisifu Kitabu Chake kitukufu kwamba Aya zake zote ni Muhkam (zenye maana wazi) pale alipotumia neno Uhkimat(11:1) Tena akasi-fu kuwa Aya zake zote ni Mutashabihat (zenye kufichikana) kwa kutumia neno Mutashabihat (39: 29). Na katika Aya hii tunayofasiri amekisifu kuwa baadhi yake ni zenye kufichikana na nyengine ziko wazi wazi. Je, Kuna njia gani ya mkusanyiko wa Aya hizi?

Jibu: Makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu katika neno Uhkimat ni kuwekwa kwa mpango na kwamba yote ni fasaha iliyo na maana sahihi. Kwa hiyo tafsiri ni: "(Hiki) ni Kitabu ambacho Aya zake zimepangwa vizuri".

Makusudio ya Mutashabihat (kufichikana) ni kibalagha na kimwongozo. Kwa hiyo tafsiri ni: "Kitabu chenye kushabihiana."

66

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Na kuwa nyengine ni Muhkamat na nyengine ni Mutashabihat, ni kama tuliyvotangulia kuelezea kuwa ni baadhi ziko wazi na baadhi zinatatiza zinazohitaji tafsir na tafsir inahitaji maarifa na elimu.

Kwa hiyo hakuna mgongano baina ya Aya hizo tatu; ni kama mfano wa mwenye kusema: "Napenda safari, wala sipendi safari" lakini anakusudia kuwa anapenda safari katika nchi kavu lakini hapendi safari ya baharini. Sufi mmoja aliisema kumwambia Mola wake: Ee Mungu nimuonaye, hali yeye hanioni. Ee Mungu anionaye, wala mimi simuoni.

Anakusudia kwamba anamuona Mwenyezi Mungu akimfadhilisha lakini Mwenyezi Mungu hamuoni yeye akimtii, na Mwenyezi Mungu anamuona akimuasi wala yeye hamwoni akimwadhibu.

Swali la pili, nini makusudio ya msingi wa Kitabu? Jibu: Baada ya Mwenyezi Mungu kuelezea kwamba katika kitabu chake kuna Aya zenye kutatiza, ndipo akasema; lakini Aya za misingi ya itikadi - kama vile kumwamini Mwenyezi Mungu na kumwepusha na mshirika vilevile kuuamini utume wa Muhammad (s.a.w.) na siku ya mwisho - ziko wazi zenye kubainisha makusudio bila ya mikanganyo yoyote; wala hazina nafasi ya kufanyiwa taawili, kuhusishwa au kuwa imefutwa hukumu yake; anaweza kuzifahamu mjuzi na asiyekuwa mjuzi; wakati huo zikiwa ni msingi katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kwa sababu zinaeleza itikadi, na nyenginezo ni matawi.

Kwa hiyo hakuna udhuru wowote kwa ugeni wa Yemen na wengineo kutaka Aya za kutatiza; kama vile Aya inayomsifu Isa kuwa roho wa Mwenyezi Mungu na kuacha Aya zilizo wazi-wazi zinazokanusha uungu wa Isa. Hakuna lolote kwa mwenye kujitia kutojua Aya wazi-wazi na kutaka Aya zinazotatiza isipokuwa ni maradhi ya moyo na kukusudia ufisadi tu.

Swali la tatu: Kwa nini amesema: Msingi wa kitabu na asiseme Misingi ya kitabu.

Jibu: Amefanya umoja kwa kubainisha kwamba mkusanyiko wa Aya zote nyepesi kufa-hamika ni msingi wa Kitabu na wala sio Aya moja pekee kuwa ni msingi; mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu.

"Na tulimfanya mwana wa Maryam na mama yake ishara." (23:50). Ishara moja, wala hakusema ni ishara mbili, kwa sababu kila mmoja ni fungu la kutimiza ishara kwa hiyo mama hawezi kuwa ishara bila ya mwana, na mwana hawezi kuwa ishara bila ya mama.

Wale ambao nyoyoni mwao mna upotofu wanafuata zile zinazotatiza kwa kutaka kuharibu na kutaka tafsiri yake.

Makusudio ya upotofu hapa ni kuiacha haki, na kutaka kuharibu ni ishara ya kwamba wenye makusudio mabaya wanatafuta yale yenye kutatiza na kuyafasiri kwa tafsiri ya kuharibu nyoyo na kuharibu watu na dini ya haki, kwa mfano wanatoa ushahidi kwa kauli yake Mwenyezi Mungu: "Na tukampulizia roho yetu" kwamba Masih ni jinsi ya Mwenyezi Mungu kwa sababu kila mmoja ni roho, na wanajitia kutojua Aya zilizo waziwazi mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu:

"Hakika wamekufuru wale waliosema: Mwenyezi Mungu ni Masih mwana wa Maryam."

(5:17)

"Hakuwa Masih ila ni Mtume, na wamepita Mitume kabla yake, na mama yake ni mkweli."

(5:75)

"Hakika mfano wa Isa mbele za Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam; alimwumba

4& 67

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

kwa udongo kisha akamwambia kuwa akawa." (3:59) Zaidi ya hayo kuna Aya inayomuhusu Adam, isemayo: "Nikishamkamilisha na kumpuliza roho yangu ..." (15:29)

Kwa hiyo basi kutokana na madai yao, Adam pia atakuwa ni Mungu. Katika Majmaul-bayan imeelezwa kuwa mwanzo wa Sura Al-imran mpaka zaidi ya Aya the-manini, zimeshuka kwa ugeni wa Najran. Walikuwa watu sitini, wakafika Madina kwa Mtume. Ulipofika wakati wao wa kuswali walipiga kengele na wakaenda kuswali katika msikiti wa Mtume. Masahaba wakasema: "Mbona wanaswali msikitini kwako?" Mtume akasema: "Waacheni." Basi wakaswali wakielekea Mashariki.

Walipomaliza kuswali, Mtume alimwambia Seyyid na Aqib ambao walikuwa viongozi wa msafara na majibizano yakawa kama hivi ifuatavyo: Mtume : Silimuni wakristo: Wakristo: Tumekwisha silimu .

Mtume : Mmesema uongo, si waislamu kwa kudai kwenu kuwa Mwenyezi Mungu ana mtoto, kuabudu msalaba na kwa kula nyama ya nguruwe. Wakristo: Ikiwa Isa si mtoto wa Mwenyezi Mungu, basi baba yake ni nani? Mtume : Hamjui kwamba mtoto hufanana na baba yake?: "Hamjui kwamba Mwenyezi Mungu yuko hai, hafi? Na Isa alitoweka? Wakristo : "Ndio."

Mtume:                 Hamjui kwamba Mwenyezi Mungu ni msimamizi wa kila kitu?

Wakristo     :          Ndio

Mtume        :          Je, Isa anaweza hivyo?

Wakristo     :          La!

Mtume        :          Hivi hamjui kuwa Mwenyezi Mungu hali, hanywi wala haendi chooni?

Wakristo    :           Ndio

Mtume :           Hamjui kuwa Isa alichukuliwa mimba na mama yake, kama wanawake

wengine, akanyonyeshwa na akalishwa chakula na kwamba Isa anakula

ana kunywa na kwenda haja? Wakristo :              Ndio

Mtume :             Basi atakuwaje Mungu?

Wakristo :             Wakanyamaza wasiwe na la kusema. Ndipo Mwenyezi Mungu

akateremsha kuwahusu, mwanzoni mwa Sura Al-imran kiasi cha Aya

thamanini.

Na hajui tafsiri yake isipokuwa Mwenyezi Mungu na waliozama katika elimu.

Baadhi ya watu wanasema ni wajibu kuweka kituo kati ya neno Mwenyezi Mungu na waliozama; na kwamba waliozama ni maneno yanayoanza upya; kwa maana ya kuwa Mwenyezi Mungu peke yake ndiye anayejua Aya zenye kutatiza, na sio waliozama katika elimu.

Kitu cha kuangalia katika kauli hii ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ni Mwenye hekima, hawezi kuwaambia watu wasivyovijua na asivyotaka wajue; kama tulivyobainisha. Kwa hiyo sahihi ni kuwa neno 'waliozama katika elimu, linaugana na Mwenyezi Mungu; na kwamba maana yake ni anajua tafsiri yake Mwenyezi Mungu na waliozama katika elimu. Amirul-muminin Ali (a.s.) anasema: "Hiyo ni Qur'an iliyonyamaza na mimi ni Qur'an inayosema."

68

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Na Ibn Abbas alikuwa akisema: "Mimi ni miongoni mwa waliozama kaitka elimu; mimi nina-jua tafsiri yake ..."

Kwa ujumla ni kwamba mwenye elimu ya haki ni yule anayeepuka kusema bila ya ujuzi. Bali huko kuzama katika elimu ni kuepuka kusema bila ya ujuzi. Iko Hadith isemayo: "Kuepuka yenye kutatiza ni bora kuliko kujingiza katika maangamizi."

Unaweza kuuliza kwa nini Mwenyezi Muangu (s.w.t.) amefanya baadhi ya Aya za Qur'an ziwe wazi na nyengine zilizofichika? Kwa nini asizijalie kuwa waziwazi zote? Ili aweze kufa-hamu mjuzi na asiyekuwa mjuzi?

Swali hilo limejibiwa kwa majibu mengi, lenye nguvu zaidi ni kwamba mwito wa Qur'an unamwelekea mjuzi na asiye na ujuzi, mwerevu na mjinga; na kwamba katika maana yako yaliyo maarufu na yenye kuzoeleka na wote hawahitajii elimu na kujifunza katika kuyajua; yanaweza kueleweka kwa ibara iliyo wazi anayoifahamu kila anayeambiwa. Maana nyengine yako ndani yasiyoweza kufahamiwa ila baada ya darasa na elimu. Wala hai-wezekani kufahamika bila ya maandalizi hayo.

Hakika hii anaifahamu kila mtu. Basi hayo ndiyo yaliyofanya kuwa baadhi ya Aya ziwe dhahiri na nyengine za ndani; kuongezea kuwa mara nyengine hekima inataka kuweka maana ya ndani; kama kusema kwake Mwenyezi Mungu kupitia kwa Mtume wake.

Hakika sisi au nyinyi tuko kwenye uongofu au upotevu ulio wazi (34:24) Husema: "Tumeziamini, zote zimetoka kwa Mola wetu."

Hii ni jumla iliyoanza upya. Maana yake ni kuwa mjuzi wa haki husema kuwa Aya zilizo-fichikana na zile nyepesi zote ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Na mwenye kuziacha nyepesi na kujishughulisha na za kutatiza tu, kwa kutaka kuharibu basi huyo ni mfisadi mwenye maradhi ya moyo.

Na hawakumbuki isipokuwa wenye akili

Wale ambao wanajua hekima katika kupatikana za waziwazi na zisizowazi katika Qur'an wala hawazifanyi zile zilizo wazi kuwa ni njia ya kupoteza.

"Mola wetu! Usizipotoshe nyoyo zetu baada ya kutuongoza na utupe rehema kutoka kwako. Wewe ndiwe mpaji mkuu."

Hiyo ni dua anayoiomba kila mjuzi mwenye ikhlasi kwa kuhofia asiingie makosani na kufanya uzembe katika kutafuta yaliyo sawa.

10.Hakika wale ambao wamekufuru haz-itawafaa kitu mali zao na watoto wao kwa Mwenyezi Mungu; na hao ndio kuni za Moto.

Kaashif3-55.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

11.Kama desturi ya watu wa firauni na wale waliokuwa kabla yao. Walikadhibisha Aya zetu. Mwenyezi Mungu akawatia adabu kwa sababu ya dhambi zao; na Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.

12.Waambie wale waliokufuru: Mtashindwa na mtakusanywa mtiwe kwenye Jahannam; nako ni makao mabaya.

Kaashif3-56.jpg

13.Hakika ilikuwa ni ishara kwenu katika yale makundi mawili yalipokutana. Kundi moja likipigana katika njia ya Mwenyezi Mungu na jingine kafiri, likawaona mara mbili zaidi kuliko wao kwa kuona kwa macho hakika katika hayo kuna mazingatio kwa wenye busara.

Hazitawafaa kitu mali zao na watoto wao

Aya 10 -13

MAANA

Hakika wale ambao wamekufuru hazitawafaa kitu mali zao na watoto wao kwa Mwenyezi Mungu; na hao ndio kuni za moto.

Mwenye kufuatilia Aya za Qur'an, yenye hekima, kuhusu kuwazungumzia matajiri, ataziona kuwa zinawataja kwa sifa mbalimbali mbaya kama ifuatavyo:

-Ujeuri, Mwenyezi Mungu anasema.

Hakika binadamu hupetuka mipaka kwa kujiona amejitosha (96: 6-7)

-Kuhadaika, Mwenyezi Mungu anasema: "Na akaingia katika bustani yake na hali ya kuwa

anajidhulumu nafsi yake akasema: "Sidhani kabisa kuwa itaharibika. Wala sidhani kuwa

70

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

kiyama kitatokea ..." (18: 35-36)

-Tamaa Mwenyezi Mungu anasema: Na nikamjaalia awe na mali nyingi... Kisha anatumai nimzidishie .(74: 12-15)

-Kuwa na mawazo potofu kwamba mali itawakinga na adhabu ya Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu anasema: "Na wakasema: 'sisi tunazo mali nyingi na watoto wengi wala sisi hatutaadhibiwa." (34:35)

Mwenyezi Mungu ameziondoa dhana zote hizi kwa kusema kwamba mali na watoto hazi-toshelezi kitu, bali mali zitamfanya aliye nazo kuwa kuni kesho; kama vile miti. Wapotofu wanadhani kwamba mali zao na watoto wao wataweza kuwahami hapa duniani, lakini wanapokabiliana na wenye haki ana kwa ana katika uwanja wa vita hubainika unyonge wao. Kwa sababu Mungu huwapa nguvu wakweli kwa nusura yake na humdhalilisha yule mfisadi aliye mwongo sana.

WENYE MALI

Historia haijajua watu waovu na wadhalimu wakubwa zaidi wakati huu kuliko wenye mali na utajiri waliolundika. Wao ndio wanaoleta fitina, uharibifu na vita; wanapanga kila mbinu kujaribu kuzuia harakati zozote za ukombozi popote pale ulimwenguni. Wanaanzisha vyama vya vibaraka wao, vikosi vya umoja, wapelelezi na majasusi katika pembe zote za dunia ili waugeuze ulimwengu uwe ni kinyang'anyiro cha shirika la mamilionea.

Wao hawaamini Mungu wala utu au jambo lolote isipokuwa wanaamini hisa ambazo zitany-onya faida kutoka katika jasho la watu, damu yao na mustakbali wao. Dola zao zina-jishughulisha kueneza hofu, wasiswasi na ukandamizaji wa kichumi na kisiasa kwa wany-onge. Wanatumia kila mbinu kuwagawaya watu wasiwe na umoja, ili watu wote wawatu-mikie wao.

Kwa ajili hiyo, ndipo uislamu ukaharamisha ulanguzi na utajiri usiofuata sharia na kuwakan-damiza wanyonge. Na umewatisha wale wanaolimbikiza mali bila ya kuzitoa sabili na kuita wapetukaji mipaka.

Kama desturi ya watu wa firaun na wale waliokuwa kabla yao; walikadhibisha Aya zetu Mwenyezi Mungu akawatia adabu kwa sababu ya dhambi zao na Mwenyezi Mungu ni mkali wa adhabu.

Yaani wingi wa mali na watoto sio sababu ya kufuzu na kuokoka. Mara nyingi mafukara wameshinda matajiri na uchache ukashinda wingi. Historia imejaa ushahidi wa ukweli huu.

Firaun na watu wake walikuwa wengi wenye jaha, usultani, mali na vifaa, lakini pamoja na hayo Mwenyezi Mungu aliwafedhehesha na kumpa ushindi Musa asiyekuwa na mali wala wingi wa watu; kama ambavyo alimpa ushindi Nuh kwa watu wa zama zake, Ibrahim kwa Namrud, Hud kwa Ad na Saleh kwa Thamud. Kwa hiyo wingi na utajiri sio hoja. Na wanaomkadhibisha Mtume Muhammad (s.a.w.w) nao mwisho wao utakuwa hivyo hivyo.

Waambie wale waliokufuru: Mtashindwa na mtakusanywa mtiwe katika Jahannam, nako ni makao mabaya.

Imeelezwa katika Majamaul-bayan kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alipompa ushindi Mtume wake katika vita vya Badr,alipofika Madina Mtume aliwakusanya Mayahudi na

4& 71

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

kuwaambia: "Tahadharini yasije yakawapata yaliyowapata maquraish katika Badr."

Wakamwambia: "Usihadaike, wewe umekutana na watu wasiojua vita; lau ungelikutana na sisi ungelijua kwamba sisi ni watu;" ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii. Mwenyezi Mungu alitimiza miadi yake: Waislamu wakawaua Bani Quraydha wahaini na wakawafagia Bani Nadhir wanafiki, wakaichukua Khaybar na wakawatoza kodi wengine.

Hakika ilikuwa ni ishara kwenu katika yale makundi mawili yalipokutana na kundi moja lilipigana katika njia ya Mwenyezi Mungu na jingine kafiri, likiwaona mara mbili zaidi kuliko wao kwa kuona kwa macho

Mwenyezi Mungu katika Aya hii anawaonyaMayahudi, manaswara, waislamu na wenye busara wote kwa ujumla kuhusu vita vya Badr wakati kilipokutana kikosi cha Mtume ambacho ni Muhammad na sahaba zake na kikosi cha shetani ambacho kilikuwa zaidi ya watu elfu, wakiwa wamejisheheneza silaha za kutosha. Na kikosi cha Mtume kilikuwa ni theluthi tu ya idadi yao, wakiwa hawana zana zozote zaidi ya farasi wawili, deraya saba na panga nane, lakini pamoja na hayo Mungu aliwaandikia ushindi hao wachache; Mwenyezi Mungu akawaonyesha washirikina kuwa waislamu ni zaidi yao ingawaje ni wachache. Aya hii iko katika mwelekeo wa Aya inayosema:

"Na mlipokutana, akawaonyesha machoni mwenu kuwa wao ni wachache na akawafanya nyinyi ni wachache machoni mwao, ili Mwenyezi Mungu atimieze jambo lililokuwa liwe. Na mambo yote hurejezwa kwa Mwenyezi Mungu" (8 : 44)

Kwa mnasaba huu ni vizuri tutaje nasaha ya Imam Ali (a.s.) kwa khalifa wa pili alipomtaka ushauri katika vita vya Roma; Imam alisema:

" Yule aliyenusuru Waislamu wakiwa ni wachache bado yuko hai, hafi, wewe ukienda mwenyewe katika vita na ukakimbia basi waislamu hawatakuwa na ngome wala kimbilio. Wewe mpeleke mtu mwenye uzowefu na umwandalie watu wenye uzoefu na wenye ushauri. Ikiwa Mwenyezi Mungu atakudhihirisha ndivyo unavyotaka, vinginevyo utakuwa ni kimbilio la watu

14.Watu wamepambiwa kupenda mata-manio ya wanawake na watoto na mirundo ya dhahabu na fedha, na farasi wazuri, na mifugo na masham-ba. Hivyo ni vitu vya anasa katika maisha ya dunia; na kwa Mwenyezi Mungu ndiko kwenye marejeo mazuri.

Kaashif3-57.jpg

72

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

KUPENDA MATAMANIO Aya 14:

MAANA

Wametofautiana wafasiri kuwa ni nani anayewafanya watu kupenda matamanio. Baadhi wamesema ni Mwenyezi Mungu na wengine wakasema ni shetani. Lakini ukweli ulivyo, ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amempa mtu tabia ya kupendelea matamanio na shetani naye humtia wasiwasi mtu na kumfanyia nzuri amali mbaya; na ile mbaya anamfanyia aione nzuri. Hata hivyo kupenda wanawake, watoto na mali siko kubaya hasa; na wala Mwenyezi Mungu hakutuharamishia. Vipi isiwe hivyo na hali yeye Mwenyezi Mungu amesema: Waambie nimewahalalishia mema.

Na Mtume (s.a.w.) amesema: "Mimi ninapenda vitu vitatu katika dunia yenu: Manukato, wanawake, na kitulizo cha moyo wangu, Swala."

Makusudio ya matamanio hapa ni vitu anavyovipendelea mtu na kuhisi raha anapovipata.

Unaweza kuuliza neno matamanio linakusanya maana ya mapenzi; kama ambavyo mapen-zi yanakusanya maana ya matamanio. Kwa hivyo basi maana ya Aya yatakuwa kwamba watu wanapenda mapenzi na wanatamani matamanio. Na maneno ya Mwenyezi Mungu hayawezi kuwa katika hali hii ya kutonyooka.

Jibu: Kupenda kitu kuko namna mbili:

Kwanza: ni mtu kupenda kitu, lakini hapendi akipende, yaani nafsi yake inapenda kama ingewezekana asikipende kitu hicho. Kwa mfano mtu kupenda kuvuta sigara inayomdhu-ru. Mwenye pendo hili anataka limwondokee kila siku.

Pili: ni mtu kupenda kitu na yeye mwenyewe yuko radhi; kama mtu aliyezoweya kufanya amali za kheri. Mwenyezi Mungu anasema katika kumzungumzia Nabii Suleiman: Hakika mimi ninapenda pendo la kheri (38:32) Hili ni pendo la hali ya juu na mwenye pendo hilo hataki limwondokee.

Mrundo ni fumbo la wingi. Hadith inasema: "Lau mtu angekuwa na nyangwa mbili za dhahabu, basi angelitamani wa tatu; na wala hawezi kutosheka isipokuwa kwa mchanga."

Kupenda wanawake, watoto na mali, kunapatikana wakati wote bali hayo ni matamanio ya kila nafsi. Ama kupenda farasi, wanyama na mashamba, Mwenyezi Mungu amekuhusisha kukutaja kwa wakati huo kwa sababu ndio vitu vilivyopendelewa zaidi.

Wafasiri wengi kama vile Razi na mwenye Al-manar wamerefusha maneno katika kutaja kila moja katika aina hizi sita za ladha na starehe, lakini wametaja mambo ya dhahiri yanayoju-likana na kuhisiwa na wote. Kwa hiyo hatukujishughulisha nayo na tunaonelea ni vizuri tutaje raha katika kifungu kinachofuatia.

RAHA

Baadhi ya watungaji wanaona kuwa raha inaweza kukamilika kwa binadamu kama akiwa na nguzo hizi nane: Afya, mke anayeafikiana naye, mali ya kutekeleza haja na jaha itakay-ohifadhi utukufu. Nafikiri mwenye rai hii ameangalia raha kwa upande wake na haja yake,

73

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

sio kwa ilivyo hasa. Kama ni hivyo ataziweka wapi hisia za matatizo ya kilimwengu; kama vile hofu, mwisho mbaya na uongo, na matatizo mengineyo yanayousonga moyo.

Kwa kweli kabisa raha kamili bado haijapatikana kwa binadamu; na ninafikiri haitapatikana katika maisha haya, ispokuwa maisha mengine. Ama raha ya upande fulani na wakati fulani imeweza kumpitia mtu, ijapokuwa utotoni. Ni vizuri kufafanua raha ya upande fulani kama ifutavyo:

Kustarehe kuko kwa aina nyingi, kama kustarehe kwa kuangalia miti wakati wa maleleji na mito na maporomoko ya maji, au kusikiliza mashairi, au kustarehe kwa kusoma vitabu, na mengineyo katika mambo ya starehe za kiroho.

Katika starehe za kimaada ni wanawake, mali na watoto. Ama farasi wanyama na masham-ba hiyo ni katika jumla ya mali. Lakini starehe hizi zote hazimpi binadamu raha kamili, kwa sababu dunia haimnyookei yeyote kwa kila upande. Akiwa ana uwezo wa kuyamudu maisha, basi atakuwa na matatizo ya nyumbani au katika uzao wake.

Amirul Muumini Ali (a.s.) anasema: "Akipata raha mtu upande mmoja, atapata uchungu upande mwengine, Hawezi kupata mtu starehe ila atapata tabu"

Ama raha ya upande fulani tu yaani katika hali fulani hiyo anaipata mtu. Mfano mzuri ni ule niliousoma katika baadhi ya vitabu. Mtungaji anasema: Familia moja ilitoka kwenda kwenye matembezi; akiwemo mama, watoto, ami, mjomba, baba na babu. Walipofika wanapokwenda, mtoto alielekea kwenye nyasi, mwengine akachuma maua, mama naye akatengeneza sandwichi, ami akatafuna tofaha, mjomba akazungusha gramafoni (kinan-da), baba akajinyoosha mchangani akiwa anaangalia kondoo na babu naye akawa ana-jishughulisha na kuvuta buruma.

Basi ikawa kila mmoja anahisi raha kwa upande wake, lakini raha hiyo ni katika hali hiyo tu, sio katika hali zote. Hekima ya Mungu imepitisha kuwa raha kamili haiwezi kupatikana isipokuwa akhera. Kwa sababu hii ndipo akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu baada ya kutaja wanawake, watoto na mali kuwa kuna kilicho bora zaidi ya hivyo. Nimeona Riwaya kutoka kwa Imam Jaffar Sadiq (a.s.) akizingatiya kuwa tawfiki ya Mungu ni nguzo miongo-ni mwa nguzo za msingi wa raha. Na, hakika hii nimeijua kwa hisia na majaribio.

15.Sema: Je, niwambie yaliyo bora kuliko hayo kwa kwa wamchao Mungu? Kwa mola wao ziko bustani ambazo hupita chini yake mito; watakaa humo milele na wake walio-takaswa na wana radhi ya Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu anawaona waja.

Kaashif3-58.jpgKaashif3-59.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Kaashif3-60.jpg

16.Ambao wanasema: "Mola wetu! Hakika sisi tumeamini, basi tughufirie madhambi yetu. Na tuepushe na adhabu ya moto.

17.Wanaofanya subira na wanaosema kweli na watiifu na wanaotoa na wanaoomba maghufira kabla ya Alfajiri.

YALIYOBORA Aya 15-16

MAANA

Sema: Je, Niwaambie yaliyo bora kuliko haya kwa wamchao Mungu?

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwanza ametaja kupenda wanawake, mali na watoto; kisha vitu vyote hivi akaviita anasa za dunia, na dunia inaondoka; na akabainisha kwamba kwake ndiko kwenye marejeo mazuri, yaani kwamba mtu baada ya kurejea kwa Mola wake ataku-ta mambo mazuri zaidi kuliko wanawake, mali na watoto na kuliko dunia yote. Baada ya hapo ndipo anafafanua kwa Aya hii.

Kwa Mola wao ziko bustani ambazo huipita chini yake mito; watakaa humo milele na wake waliotakaswa na wana radhi ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu anawaona waja.

Haya matatu ni bora kuliko wanawake, mali na watoto, nayo ni marejeo mazuri. Kwanza ni, pepo ambayo haitakwisha sio kama shamba, farasi na mifugo. Pili ni wanawake waliotakaswa na hedhi, hadathi na uchafu wote. Vilevile wametakaswa na kila kinyaa. Tatu ni radhi ya Mwenyezi Mungu ambayo ni kubwa zaidi kuliko dunia na akhera kwa pamoja. Yote hayo Mwenyezi Mungu ameyafanya ni malipo ya mwenye kuogopa kusimama mbele za Mola wake na akaikataza nafsi (yake) na matamanio.

Wanaofanya subira, na wanaosema kweli na watiifu na wanaotoa na wanaoomba maghufira kabla ya Alfajiri.

Mwenye kusubiri ni yule anayekabiliana na mambo kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu; na kuridhia natija ya makabiliano yake. Msema kweli ni yule anayesema ukweli hata kama unamdhuru. Mtiifu ni yule mwenye kufanya ibada akiwa mtiifu. Mtoaji ni yule anayejitolea mali na kuwatolea watu wake katika njia ya Mwenyezi Mungu. Na, wakati wa kabla ya alfajiri; ni wakati bora kuliko wowote kwa ibada na dua; kama ilivyoelezwa katika Hadith. Kwa sababu wakati huo uko mbali kabisa na shub'ha ya ria; Na, ni wakati ambao usingizi ni mtamu sana; kwa hivyo inakuwa tabu kuamka. Na amali bora zaidi ni ile yenye mashaka na tabu, ingawaje kuhudumia mtu ni bora zaidi kuliko Swala na Saumu.

75

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

MATUNDAYAIMANI

Sifa zote hizi tano (subira, ukweli, utiifu, kutoa na msamaha) ni matunda ya misingi mitatu ya dini; yaani kumwamini Mwenyezi Mungu mmoja aliye pekee, kuamini utume wa Muhammad (s.a.w.w.) na kuamini siku ya mwisho.

Misingi hii siyo kuwa ni mambo tu ya dini, bali inayo matunda na hakika zinazokusanywa na umbile tukufu, na amali yenye kunufaisha katika uhai. Mwenyezi Mungu anasema: "Enyi mlioamini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume atakapowaita katika yale yatakayowapa maisha, (8:24)

Kila asili katika asili ya dini inasimama kwa misingi hii. Vilevile kila tawi katika matawi ya dini, ni misingi inayofungamanisha dini na matendo kwa ajili ya maisha.

Mwenyezi Mungu anasema: Basi naapa kwa Mola wako tutawauliza wote juu ya yale waliyokuwa wakiyatenda. (15: 92 - 93)

Je, mnadhani mtaingia peponi, bila ya Mwenyezi Mungu kuwapambanua wale waliopigana Jihadi miongoni mwenu na kuwapambanua waliofanya subira? (3:142)

Zimekuja Hadith kadhaa Mutawatir kwamba aina bora ya ibada na utiifu ni kufanya amali kwa ajili ya maisha mema na kwamba kubwa ya madhambi makubwa na maasi ni ufisadi na uadui kwa watu. Mtume anasema: "Karibu zaidi anapokuwa mja na Mola wake ni pale anapotia furaha katika moyo wa nduguye."

Amirul-Muminiin anasema: "Masurufu mabaya siku ya marejeo ni uadui kwa waja." Mjukuu wake, Imam Baqir, naye anasema: "Mwenyezi Mungu ana watu waliobarikiwa, watu wengine wanaishi katika hifadhi zao; nao ni kama tone. Na kuna watu ni vikwazo, wala watu wengine hawaishi katika hifadhi zao; nao ni kama nzige kila kitu wanakitaka."

18.Mwenyezi Mungu na Malaika na wenye elimu wameshuhudia ya kwamba hakuna Mola ila Yeye tu. Ndiye Mwenye kusimamia uadilifu. Hakuna mola isipokuwa Yeye, Mwenye nguvu Mwenye hekima.

19.Hakika dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu. Na hawakukhitali-fiana wale waliopewa Kitabu ila baada ya kuwajia ilimu. Kwa uhasidi uliokuwa baina yao. Na anayezikataa Aya za Mwenyezi Mungu basi Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.

Kaashif3-61.jpgKaashif3-62.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Kaashif3-63.jpg

20.Na kama wakikuhoji, basi sema: "Nimeusalimisha uso wangu kwa kumwelekea Mwenyezi Mungu, na walionifuata" Na waambie wale waliopewa Kitabu na wale wasiokuwa na kisomo na "Je,mmesilimu? Kama wakisilimu basi wameongoka; na kama wakikengeuka, basi juu yako ni kufikisha tu. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwaona waja

MWENYEZI MUNGU, MALAIKA NA WENYE ELIMU. Aya 18 - 20

Mwenyezi Mungu na Malaika na wenye elimu wameshuhudia ya kwamba hakuna Mola isipokuwa yeye; Ndiye mwenye kusimamisha uadilifu. Hakuna Mola isipokuwa Yeye, Mwenye nguvu Mwenye hekima.

Kujishuhudia Mwenyezi Mungu yeye mwenyewe kuwa ni mmoja ni kutokana na vitendo Vyake ambavyo haviwezi yeyote isipokuwa Yeye; Mwenyezi Mungu anasema: "Tutawaonyesha ishara zetu katika upeo wa mbali na katika nafsi zao mpaka iwabainikie kuwa haya ni haki. Je haikutoshi kwamba Mola wako ni shahidi wa kila kitu? (41:53)

Ama ushuhuda wa Malaika kwa umoja wa Mungu ni kwamba wao wana maumbile ya imani. Makusudio ya wenye elimu hapa ni Mitume na wanavyuoni wote wanaomjua Mungu ambao wamekuwa makaimu wa Mitume katika kumlingania Mwenyezi Mungu. Na ushahidi wa mwanachuoni unaambatana na hoja ya kumkinaisha anayetafuta uhakika.

Makusudio ya uadilifu hapa ni uadilifu katika dini na sharia na katika desturi ya maumbile na nidhamu yake, Mwenyezi Mungu anasema: Na hatukuumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yake kwa mchezo. (21:16)

Unaweza kuuliza nini makusudio ya kukaririka neno: 'Hakuna Mola isipokuwa yeye,' Katika Aya moja?

Jibu: Inajulikana kuwa katika njia ya Qur'an ni kukariri na kutilia mkazo misingi ya itikadi na misingi muhimu, hasa umoja. Hiyo ni kuondoa shaka. Tumefafanua kukaririka katika kifun-gu mbali, tulipofasiri Aya 48 Sura ya Baqara.

Imesemekana kuwa makusudio ya kauli ya kwanza ni kujulisha kuwa yeye pekee ndiye anayestahiki kuabudiwa. Na, ya pili ni kujulisha kuwa hakuna yeyote mwenye kusimamia uadilifu isipokuwa yeye.

DINI YA MWENYEZI MUNGU NI UISLAMU

Unaweza kuuliza: Dhahiri ya Aya, Hakika dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni uislam, inafa-hamisha kuwa dini zote za mitume - hata dini ya Ibrahim - si chochote isipokuwa dini ya

77

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Muhammad (s.a.w.w.) na Qur'an tu?

Jibu: Hapana, bali Aya hii inafahamisha kinyume kabisa na hivyo. Kwani dhahiri yake inatamka kwa lugha fasaha kwamba kila dini aliyokuja nayo Mtume miongoni mwa Mitume waliotangulia umbo lake linakuwa na mwito wa kiislamu ambao ameulingania Muhammad bin Abdullah (s.a.w.). Kwa ufafanuzi zaidi angalia hakika hizi zifuatazo:

1.Kabla ya jambo lolote kwanza, uislamu una mambo matatu; Kumwamini Mwenyezi Mungu na umoja wake, kuamini wahyi na Isma yake na kuamini ufufuo na malipo yake. Kila mmoja wetu anaamini kwa imani isiyokuwa na tashwish yoyote kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakupeleka Mtume yeyote isipokuwa kwa misingi mitatu hii. Kwa hali hiyo ndipo Mtume (s.a.w.) akasema: "Sisi Mitume dini yetu ni moja"Akaendelea kusema: "Mitume ni ndugu katika shughuli (zao) baba yao ni mmoja na mama zao ni mbali mbali".

2.Neno uislamu linatumiwa kwa maana nyingi; kama kunyeyekea, usafi na kusalimika na ila na uchafu. Hakuna mwenye shaka kwamba kila dini aliyokuja nayo Mtume katika Mitume wa Mwenyezi Mungu ni safi isiyokuwa na uchafu wowote. Kwa hiyo basi inafaa kulitumia neno uislam kwa dini zote za Mitume.

3.Rejea ya Qur'an ni moja, hakuna tofauti kati ya Aya zake, bali hiyo Qur'an inajifasiri yenyewe na kujitolea ushahidi hiyo yenyewe; kama alivyosema Imam Ali (a.s.): "Ikija Aya katika suala fulani au maudhui fulani, basi haifai kuiangalia peke yake, bali ni lazima kufu-atilia kila Aya zilizo na uhusiano na suala hilo na maudhui hayo na kuzikusanya katika jumla moja kwa kuunganisha na nyengine, kisha tutoe maana moja katika Aya zina-zooana."

Tunapoangalia Aya zinazoelezea uislamu katika uhakika huu, tunakuta kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewasifu Mitume wote kwa Uislamu katika Aya nyingi. Kwa hivyo tunajua kuwa neno la Mwenyezi Mungu, Hakika dini mbele za Mwenyezi Mungu ni Uislamu linaku-sanya dini zote za haki. Siri ya hilo ni hayo tuliyoyaeleza kwamba dini zote za Mitume zinadhamini mwito wa kiislamu katika uhakika wake na dhati yake.

Kwa kutilia mkazo imani ya Mwenyezi Mungu, wahyi na ufufuo. Ama tofauti inakuwa kait-ka matawi na hukumu, sio katika misingi ya itikadi na imani.

Hebu tuangalie Aya ambazo Mwenyezi Mungu amewasifu Mitume kwa uislamu, tangu zama za Nuh (a.s.) mpaka za Muhammad (s.a.w.w.), Amesema Mwenyezi Mungu kuhusu Nuh: Na wasomee habari za Nuh alipowaambia watu wake Enyi watu wangu! Nimeamrishwa niwe miongoni mwa waislamu. (10: 71-72).

Kuhusu Ibrahim na Yakub anasema: Na Ibrahim akawausia haya wanawe; na Yakub: "Enyi wanangu hakika Mwenyezi Mungu amewachagulia dini hii, basi msife ila mmekuwa waislamu. "(2:132).

Kuhusu Yusuf anasema: "Wewe ndiwe mlinzi wangu katika dunia na akhera, nifishe hali ya kuwa ni Mwislamu..." (12:101)

Kuhusu Musa anasema: "Na Musa akasema: Enyi watu wangu! Ikiwa nyinyi mme mwami-ni Mwenyezi Mungu, basi mtegemeeni yeye kama nyinyi ni waislamu" (10:84)

Kwa Umma wa Isa anasema: "Na nilipowafunulia wanafunzi (wako) kuwa niaminini mimi na Mtume wangu, wakasema: "Tumeamini na uwe shahidi kuwa sisi ni waislamu." (5:111)

78

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Aya iliyo wazi kuliko zote na inayomuenea wa kwanza na wa mwisho katika Mitume, wafuasi wao na wafuasi wa wafuasi, ni ile isemayo: "Na yeyote mwenye kutaka dini isiyokuwa ya Kiislamu, basi haitakubaliwa kwake, naye akhera atakuwa katika wenye khasara." (3:85)

Ikiwa Mwenyezi Mungu hatakubali isipokuwa Waislamu tu; na huku amekwisha wakubali Mitume kuanzia Adam, Nuh, Ibrahim, Musa, Isa na Mitume wote pamoja na wafuasi wao, basi natija itakuwa kwamba Mitume wote kuanzia Adam mpaka Muhammad (s.a.w.) na wanaowafuata, ni waislamu.

Imam Ali (a.s.) anasema: "Uislamu ni kujisalimisha, kujislaimisha ni yakini, yakini ni kusadikisha, kusadikisha ni kukiri, kukiri ni kutekeleza na kutekeleza ni matendo."

Na hawakuhitalifiana wale waliopewa Kitabu ila baada ya kuwajia elimu kwa uhasidi uliokuwa baina yao

Makusudio ya watu wa Kitabu hapa ni mayahudi. Inasemekana ni manasara. Na, inase-mekana ni wote, na hiyo ndio sahihi kwa sababu tamko ni la kiujumla na hakuna dalili ya umahsusi. Linalotilia nguvu kuwa tamko ni la kiujumla, ni kauli yake Mwenyezi Mungu:

"Na kwa wale waliosema: Sisi ni Wanaswara tulichukua ahadi yao, lakini wakaacha sehe-mu ya yale waliyokumbushwa, kwa hivyo tukaweka baina yao uadui na bughudha mpaka Siku ya Kiyama." (5:14)

Kuhusu tofauti ya Mayahudi anasema: "Na Mayahudi walisema: 'Mkono wa Mwenyezi Mungu umefumba'... "Na tumewatilia uadui na bughudha baina yao mpaka siku ya Kiyama." (5:64).

Katika mambo waliyohitalifiana Mayahudi ni uhai baada ya mauti. Baadhi yao wakasema, hakuna ufufuo kabisa, si katika maisha haya wala mengine na kwamba adhabu ya mwenye makosa na thawabu za mtu mwema zinapatikana katika maisha haya ya duniani. Kikundi kingine kinasema: "Watu wema watafufuliwa mara ya pili hapa duniani ili washiriki katika ufalme wa Masih ambaye atakuja zama za mwisho."

Ama itikadi ya Kikristo iligeukageuka, kabla ya kudumu kwenye utatu. Mwanzo ilikuwa inalingania kwenye ibada ya Mungu mmoja, kisha wakagawanyika makundi mawili: Kundi moja lilikuwa katika shirk na jengine likabakia kwenye Tawhid lakini likatofautiana kuwa je, Isa ana tabia mbili ya kiungu na nyengine ya kibinadamu; au ana tabia ya kiungu tu? Na mengine mengi yaliyoandikwa katika vitabu vya historia za dini. Tofauti hizo za kikristo zimeleta umwagikaji damu wa kufehedhesha kusikokuwa na mfano katika historia ya binadamu.

Tofauti ya mayahudi na manaswara (wakristo) hazikutokana na kutojua uhakika. mayahudi walijua kuwa kuna ufufuo; kama ambavyo wakristo walijua kuwa Isa ni mja miongoni mwa waja wa Mungu, lakini walihitalifiana kwa kutaka ukubwa katika dunia kwa uhasidi na ufisa-di.

VIKUNDI SABINI NATATU:

Imetangaa kwamba Mtume (s.a.w.) amesema: "Mayahudi wamegawanyika vikundi sabini na moja, Wakristo vikundi sabini na mbili na umma wangu utagawanyika vikundi sabini na tatu."

79

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Maneno yamekua mengi sana kuhusu Hadith hiyo: Kuna mwenye kusema kuwa ni dhaifu, mwengine anasema hiyo ni Hadith iliyopokewa na mtu mmoja ambayo sio hoja katika maudhui. Watatu naye anasema kuwa neno "Vikundi vyote vitaingia motoni" ni katika vitim-bi vya walahidi kwa kuwatia doa waislamu. Ama wanne amesema kwa tamko hili: "Vikundi vyote vitakuwa katika pepo isipokuwa wazandiki."

Sisi tuna mashaka na Hadith hii, kwa sababu asili ni kuacha kuchukua lolote linalonasi-bishiwa Mtume (s.a.w.) mpaka ithibiti kinyume (ukweli). Lakini kama tukihiyarishwa kati ya kukubali kwa "vyote vitakuwa motoni" na vyote vitakuwa peponi." Tutachagua peponi kutokana na sababu mbili:

Kwanza: Hiyo ndiyo iliyo karibu zaidi na rehema ya Mwenyezi Mungu. Pili: Kimsingi ni kwamba vikundi vya kiislamu vinavyotofautiana katika misingi (asili) havifi-ki sabini na tatu, kutofautiana katika matawi, hakupelekei kuingia motoni. Kwa sababu makosa kwenye matawi yanasamehewa yakiwa yametokea pamoja na kujichunga na baada ya kujitahidi.

Ni umbali ulioje kati ya Hadith hii inayonasibishwa kwa Mtume (s.a.w.w.) na kauli ya Ibn Arabi katika kitabu Futuhat: "Haadhibiwi yeyote katika umma wa Muhammad (s.a.w.) kwa baraka za Ahlu bait..."

"Na kama wakikuhoji, basi sema: Nimeusalimisha uso wangu kumwelekea Mwenyezi Mungu na walionifuata"

Mara nyingi mwanachuoni wa haki hupambana na mbishi mwenye batili. Wala hakuna dawa ya huyu isipokuwa kuachana naye. Na, yeyote mwenye kuhasimiana na mshari mwenye vurugu anakuwa mshirika wake katika dhambi.

Imam Ali (a.s.) anasema: "Mwenye kubisha sana hupata dhambi. "Kwa ajili hii, Mwenyezi Mungu amemwamrisha Mtume wake Mtukufu kuachana na wabatilifu, walio wapinzani, kwani hakuna ziada ya ubainifu na hoja.

"Hakika ni juu yako kufikisha tu, na ni juu yetu hisabu." (13:40)

Na waambie wale waliopewa kitabu yaani mayahudi na manaswara na wale wasio na

kisomo yaani washirikina katika waarabu . Mwenyezi Mungu amewanasibisha na neno wasio na kisomo kwa sababu wengi wao hawakujua kusoma na kuandika. Je mmesilimu? Baada ya kuwajia hoja. Kama wakisilimu basi wameongoka kwani hakuna kitu chochote zaidi ya uislamu, isipokuwa kufuru tu na upotevu. Na kama wakikengeuka basi juu yako ni kufikisha tu na kufikisha ndio mwisho wa kazi ya utume, kwani huko ndiko kunakotimiza hoja. Na Mwenyezi Mungu anawaona waja wote anawatendea wanayostahiki.

Faida tunazozipata kutokana na Aya hii ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemchagua Muhammad (s.a.w.) kuwa Mjumbe Wake na kwamba Yeye Mwenyezi Mungu amemwekea njia ya kuufikisha ujumbe huo ambao ni kutoa mwito kwa hoja na dalili; pamoja na kuidhibiti nafsi na kujiepusha na uhasama wa ubishani.

Kwa njia hii ya hekima hoja inatimia kwa mhalifu, mpinzani na asibakiwe na udhuru wowote au popote pa kukimbilia.

Wafuasi bora zaidi wa Mtume kwenye njia yake, ni watu wa elimu wanaojua dini yake na sharia yake; wenye kulingania kushika mafunzo yake na mwenendo wake.

80

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

21.Hakika wale ambao wanazikanusha Aya za Mwenyezi Mungu na wakawauwa manabii pasipo haki na wakawaua wanaoamrisha mambo ya haki, wabashirie adhabu iumizayo.

Kaashif3-64.jpg

22.Hao ndio ambao vitendo vyao vime-haribika katika dunia na akhera wala hawana wa kuwanusuru.

WANAOWAUA MITUME. Aya 21 - 22:

MAANA

Hakika wale ambao wanazikanusha Aya za Mwenyezi Mungu na wakawauwa manabii pasipo haki na wakawauwa wanaoamrisha mambo ya haki, wabashirie adhabu iumizayo.

Unaweza kuuliza sharia zote za Mwenyezi Mungu na za watu zinaharamisha kuua, bali watu wote wanamuona muuaji ni mkosa, hasa ikiwa aliyeuwawa ni katika watu wema. Kwa hiyo basi kuelezea kuwa muuaji ni mwenye makosa anayestahili adhabu, ni kama kufafan-ua kilichofafanuka, na hali tunajua kuwa maneno ya Mwenyezi Mungu yako katika mpangilio mzuri?

Jibu: Makusudio hapa ni mayahudi na wakristo waliokuwako wakati wa Mtume (s.a.w.) na wakakataa uislamu. Aya imeonyesha kuwa si jambo geni kwao kukataa na kuwa na inadi na uislamu. Kwa sababu mayahudi waliotangulia waliwaua manabii; kama vile Zakariya na manaswara waliotangulia waliwaua wale waliouonyesha wazi umoja wa Mungu na ubashiri wa Masih, kwa vile tu walikuwa wanaamrisha haki na uadilifu na kuutumia. Kwa hivyo Aya imo katika mfumo wa kukemea; kama ilivyo kuwa ni ya kuhofisha.

Swali la pili: Kuua hakukuwa kwa Ahlul-kitab waliokuwa wakati wa Muhammad (s.a.w.), sasa vipi wananasibishiwa wao pasipo haki?

Jibu: Tumekwishaeleza mara kadhaa kwamba waliokuja nyuma waliridhia yaliyofanywa na wa kale wao na mwenye kuridhia kitendo anakuwa mshirika. Mara nyingi anayoyafanya baba hutegemezewa mwana.

Swali la tatu: Kuwaua manabii hakukuwa haki kwa hali yoyote, sasa kuna faida gani katika msemo huu?

81

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Jibu: Ni kuonyesha kuwa fedheha ya kuwaua mitume si kwa sababu ya vyeo vyao na utukufu wao, bali ni fedheha isiyokuwa na udhuru wowote, na kwamba sio suala la watu au vikundi, bali ni suala zima la haki na ukosefu wa haki.

Hao ndio ambao vitendo vyao vimeharibika katika dunia na akhera

Kuharibika duniani ni kwamba wao wanalaaniwa na kila mtu, kutokana na athari zao mbaya walizoziacha. Ama huko akhera wanangojwa na adhabu.

KUAMRISHA MEMA NA KUKATAZA MABAYA

Mafakihi wametaja sharti za kuamrisha mema na kukataza mabaya, kama vile kutohofia mwamrishaji madhara ya nafsi yake, watu wake na mali yake. Lakini baadhi ya mafakihi wamelipinga sharti hili na kuwajibisha kuamrisha mema japo kutapelekea kifo; na wametoa dalili kwa Aya hii. Hoja yao ni kuwa mitume wameamrisha mema na kukataza mabaya, wakauliwa katika njia hii. Kwa ushahidi wa Qur'an tukufu.

Tunavyoona sisi ni kwamba mitume katika tabligh walikuwa wana jambo ambalo wanavyuoni hawana. Wao walikuwa wakiongozwa na wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.); kama wakiuwawa katika njia ya tabligh, watakuwa wameuwawa wakiwa wanatekeleza amri ya Mwenyezi Mungu. Ama wanavyuoni, wanategemea yale waliyoy-afahamu katika hukumu. Tunavyofahamu sisi kutokana na dalili hizi ni kwamba mtu yeyote inafaa kwake kunyamaza kwenye mambo mabaya ikiwa hakuna faida ya kidini na tena kuna madhara.

Ama ikiwa dhana yake imeelemea kuwa kutapatikana manufaa ya kidini kwa kuamrisha mema na kukataza mabaya, lakini kuna madhara, basi hapo itakuwa ni wajibu kuamrisha. Kwa hiyo lililopo ni kulinganisha kati ya kukinga nafsi na manufaa ya kuamrisha na kukataza. Ikiwa manufaa ya dini ndiyo muhimu; kama vile kuumaliza ukafiri, dhulma na ufisadi. Basi hapa itafaa kuyakubali madhara, na huenda ikawa wajibu. Na, ikiwa kujikinga na madhara ni muhimu zaidi kuliko kukataza mabaya; kama kukataza kula najisi, basi hapo itafaa kujikinga na huenda ikawa ni wajibu, kwa hivyo basi suala litakuwa linatofautiana kwa kutafautiana hali.

Na, inatubainikia kwamba kuwalinganisha wasiokuwa Manabii katika suala hili la Manabii ni kuwalinganisha na kitu kilicho tofauti. Tutalirudia suala hili pale litakaponasibika.

23.Je, huwaoni wale waliopewa sehemu ya Kitabu, wanaitwa kwenye Kitabu cha Mwenyezi Mungu ili kiwahukumu baina yao, kisha baadhi yao wanageu-ka wanakikataa.

Kaashif3-65.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

24.Hayo ni kwa sababu walisema: Hautatugusa moto isipokuwa kwa siku chache tu, na yakawadanganya katika dini yao yale waliyokuwa wakiyazua.

25.Basi itakuwaje tutakapowakusanya siku ambayo hapana shaka kuja kwake na itakapolipwa kila nafsi kwa ukamilifu kile ilichokichuma na wao h awataod h u l u m i wa.

MAYAHUDI TENA. Aya 23 - 25

Je huwaoni wale waliopewa sehemu ya Kitabu wanaitwa kwenye kitabu cha Mwenyezi Mungu ili kiwahukumu baina yao, kisha baadhi yao wanageuka wanakikataa.

Kaashif3-66.jpg

Wafasiri wanasema: di. Hapa Mwenyezi waliopewa Kitabu au mayahudi waliomhoji wamehifadhi Tawrat wengi. Au walihifadhi Muhammad Abduh.

Makusudio ya wale ambao wamepewa sehemu ya Kitabu ni mayahu-Mungu anasema waliopewa sehemu ya kitabu, na wala hakusema watu wa Kitabu; kama ilivyo katika sehemu nyingine, kwa sababu Mtume (s.a.w.) na akawaita kwenye Tawrat iwahukumie, hawakuwa yote, isipokuwa walihifadhi baadhi tu, kama walivyosema wafasiri matamko tu, bila ya kuzingatia maana yake; kama alivyosema Sheikh

Wengi wao ni wale ambao wanalingania kwenye kuamini vitabu vya Mwenyezi Mungu na msimamo wa kibinadamu, lakini wanasema tu, bila ya kutekeleza kwa vitendo. Na, waki-hojiwa, basi hubabaisha. Mifano ya hao ni mingi sana haina idadi. Kama vile watu walioanzisha vita na kuuwa mamilioni, wanadai kwamba wao ni watetezi wa amani. Miongoni mwazo ni zile dola ambazo zinawakandamiza watu huru na zinajigamba kuamini haki na uadilifu. Mfano mwengine ni mayahudi ambao Mtume (s.a.w.) aliwaita kwenye Kitabu chao Tawrat na kuwaambia nendeni kwenye kitabu hicho, kwani ndani yake mna sifa zangu, lakini walikipa mgongo na kufanya inadi, ndipo ikashuka Aya hii.

Kuna kundi la wafasiri waliosema kwamba Aya hii ilishuka kwa ajili ya yahudi mmoja aliyezi-ni na yahudi mwenzake, na mayahudi wakatofautiana katika suala hilo katika makundi mawili. Kundi moja likataka apigwe mawe mpaka afe na kundi jingine likataka ipunguzwe adhabu hiyo. Mzozo ulipozidi wakenda kwa Mtume kuamuliwa; Mtume akahukumu kuwa apigwe mawe, lakini lile kundi la pili likakataa, ndipo Mtume akawakumbusha Tawrat ambayo imeelezea pia habari ya kupiga mawe mzinifu, lakiniwakakataa.

83

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Kwa vyovyote itakavyokuwa sababu ya kushuka Aya hii, kwa hakika ina maana ya jumla na kumgusa yeyote mwenye kutangaza jambo, lakini yeye mwenyewe akajitia hamnazo na kulikataa. Kwa sababu linalozingatiwa ni matendo, sio alama na maneno matupu. Imam Ali (a.s.) anasema: "Hatafuzu kwa kheri ila mwenye kuifanya, wala hatalipwa mtu malipo ya shari isipokuwa mwenye kuifanya."

Hayo ni kwa sababu walisema: Hautatugusa moto isipokuwa kwa siku chache tu, na yakawadanganya katika dini yao yale waliyokuwa wakiyazua.

Mwenyezi Mungu ameeleza aina nyingi za uovu wa mayahudi katika kitabu chake kitukufu; kama vile kuua kwao mitume, kuabudu ndama, kusema kwao kuwa watakaoingia peponi ni mayahudi tu, kusema kuwa wao ni wana wa Mungu na wapenzi Wake na kudai kuwa moto utawagusa siku chache tu.

Mwenye Tafsir al-Manar amenakili kutoka kwa mwalimu wake Sheikh Muhammad Abduh kwamba yeye amesema: "Katika vitabu vya mayahudi walivyonavyo hamna kiaga chochote cha akhera."

Imenakiliwa kutoka kwa watu wanaochunguza na kufuatilia mambo kuwa Mayahudi hawaamini akhera, lakini kunukuu kunapingana na kauli ya Qur'an kwa mayahudi: "Hautatugusa moto isipokuwa kwa siku chache tu," na kule kusema kwao: "Hataingia peponi isipokuwa Yahud."

Si jambo la kushangaza kusema kuwa wahenga wa Kiyahudi walikuwa wakiamini akhera; kisha waliofuatia wakageuza na wakaondoa katika vitabu vyao kila linalofungamana na akhera. Katika Tafsir Al-manar akinukuliwa Sheikh Abduh, anasema: "Watafiti wa kiulaya wamethibtisha kuwa Tawrat imeandikwa baada ya nabii Musa (a.s.) kwa miaka nenda miaka rudi. La kushangaza zaidi kuliko yote hayo ni madai ya mayahudi, kwamba Mwenyezi Mungu anawapendelea wao na kwamba Mwenyezi Mungu amewaumba watu wengine kwa ajili ya kuwatumikia wao na kwa masilahi yao, sawa na wanyama. Kwa ajili ya fikra hii ndio wakajiita "Taifa la Mungu lilochaguliwa." Au "Taifa teule la Mungu"

Tukiachilia mbali muhali wa madai haya na kutoingilika akilini, pia tunavyoona ni ndoto na ni kumhukumia Mwenyezi Mungu, kwani hakuna jambo lolote la ghaibu linaloweza kuju-likana bila ya wahyi wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na, wahyi umekwisha walaani, kuwafedhehesha na kutaja adhabu yao.

Fedheha hiyo na adhabu itafichuka siku ambayo hawatakuwa na hila yoyote ya kuikinga, kwa hivyo ndipo Mwenyezi Mungu akasema:

Basi itakuwaje tutakapowakusanya siku ambayo hapana shaka kuja kwake na itakapolipwa kila nafsi kwa ukamilifu kile ilichokichuma na wao hawatadhulimiwa.

Thawabu za mtiifu hazitapunguzwa na huenda zikazidi, lakini adhabu haitazidishwa kabisa bali huenda ikapunguzwa na huenda Mwenyezi Mungu akasamehe kabisa.

Mimi nina yakini kabisa kwamba mwenye kumtarajia Mwenyezi Mungu katika dunia yake hii, na wala asimtarajie mwengine amtegemee Yeye tu katika matatizo yote kwa hali yoyote itakayokuwa, akiwa na imani kwamba asiyekuwa Mwenyezi Mungu si chochote isipokuwa ni njia na chombo tu; mwenye kuwa hivi nina yakini kuwa bila shaka atakuta yanayomrid-hisha kwa Mungu hata kama atakuwa ana maovu.

84

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

26.Sema Ewe Mola uliyemiliki ufalme wote humpa ufalme umtakaye na humwondolea ufalme umtakaye. Na humtukuza umtakaye na humdhalil-isha umtakaye. iko mikononi mwako kila kheri. Hakika wewe ni muweza wa kila kitu.

Kaashif3-67.jpg

27.Huingiza usiku katika mchana na huingiza mchana katika usiku na humtoa aliye hai kutoka aliye maiti na humtoa maiti kutoka aliye hai. Na humruzuku umtakaye bila ya ya his-abu.

HUMPA UFALME AMTAKAYE Aya 26 - 27

MAANA

Dhahiri ya Aya kwa ukamilifu inalingana na hali ya waislamu katika siku za mwanzo wa Uislamu: ambapo wakati huo hawakuwa na ufalme, nguvu wala usultani. uislamu ulianza katika hali ya ugeni, kama alivyosema Mtume (s.a.w.w.). ufalme ulikuwa wa wafursi na warumi. Lakini baada ya kuja ushindi wa Mwenyezi Mungu, mambo yaligeuka; aliye duni akawa mtukufu na mtukufu akawa duni. wafursi na warumi wakawa wanatawaliwa na waislamu baada ya kuwa wao ndio watawala.

Wasilamu wakawa watawala baada ya kuwa wanyonge wakiwaogopa watu, ndipo matak-wa ya Mwenyezi Mungu yakathibiti aliyoyabainisha kwa kauli yake: "Na tukataka kuwa-neemesha wale waliofanywa wanyonge katika ardhi na kuwafanya wawe viongozi na kuwafanya warithi." (28:5).

Sema: "Ewe Mola uliyemiliki ufalme wote"

Makusudio ya kumiliki ufalme, ni uweza wake juu ya kila kitu; ni kama kusema Mwenyezi Mungu amemiliki uwezo. Ameleta neno ufalme kwa sababu athari ya kumiliki kitu chochote ni uwezo wa mwenye kumiliki kukitumia wala hapana yeyote anayeweza au kumiliki kitu; isipokuwa kwa kumilikishwa na Mwenyezi Mungu na kupewa uwezo juu yake.

Humpa ufalme umtakaye

Aliwapa waislamu mwanzo pale walipoitikia mwito wa uislamu na kuutumia kwa vitendo.

85

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Na humuondolea ufalme umtakaye

Aliuvua kutoka kwa wafursi, na warumi na washirikina kwa sababu ya kuikufuru haki.

Na humtukuza umtakaye, nao ni waislamu. Na humdhalilisha umtakaye nao ni wafursi, warumi na washirikina wa kiarabu.

Iko mikononi mwako kila heri.

Makusudio ya kuwa mikononi ni kuwa na uwezo. Heri inakusanya kila lenye manufaa liwe la kimaana au kimaada. Na Mwenyezi Mungu amewapa heri nyingi waislamu kwa baraka za uislamu.

Hakika wewe ni muweza wa kila kitu.

Dalili ya uweza ni kuuvua ufalme kutoka kwa wenye nguvu na kuwapa wanyonge. Huingiza usiku katika mchana na huuingiza mchana katika usiku.

Ambapo sayari zinakuwa na harakati kwa uweza na msaada Wake; nyingine huzizunguu-ka nyingine, hapo hupatikana misimu ya mwaka; mara nyingine huchukua usiku katika mchana katika msimu fulani mpaka ukawa na masaa15 na mchana ukawa masaa 9. na mara nyuingine huuchuwa mchana katika usiku katika msimu mwingine mpaka ukawa na

masaa 15 na usiku ukawa masaa 9*7. Na humtoa aliye hai kutoka aliye maiti.

Kama vile kumtoa mumin kutoka kwa kafiri na mtukufu kutoka kwa aliye dhalili. Na humtoa maiti kutoka aliye hai.

Kama vile kumtoa kafiri kutoka kwa mumin na dhalili kutoka kwa mtukufu. Na humruzuku amtakaye bila hisabu,

Kama alivyowaruzuku waislamu wa kwanza, ufalme na utukufu kwa baraka za uislamu.

Na kama utauliza, kuwa je? ufalme wa mfalme dhalimu na usultani wake hutoka kwa Mungu na ni kwa utashi wake na matakwa yake?

Utalikuta jibu la swali lako hili katika tafsiri ya aya 246 Surah Al-Baqrah.

Zaidi ya hayo ni kwamba dhahiri ya Aya inatilia nguvu yale yaliyosemwa na kundi la wafasiri kuhusu sababu ya kushuka kwake. Kwa ufupi ni kwamba Mtume (s.a.w.) alipochukua hatua ya kuchimba handaki kwa ushauri wa Salman Farisi aliwakatia dhiraa arubaini kila sahaba kumi, na Salman alikuwa na nguvu, hivyo Ansar wakamtaka awe nao wakasema: "Salman ni wetu". Mtume akasema kauli yake iliyo mashuhuuri: "Salman ni katika sisi Ahlul-Bait.

Wakati Salman alipokuwa akichimba akakabiliwa na jiwe lililomshinda. Mtume alipoambiwa, alichukua sururu kutoka mikononi mwa Salman na kulivunja jiwe kwa mapigo matatu. Katika mapigo hayo Mtume (s.a.w.) aliona ikulu ya Fursi, Roma na Yemen; akawaambia sahaba zake: "Umati wangu utatawala ufalme wa Kisra na Kaizari". Basi wanafiki waliposikia waliy-achezea shere maelezo haya, ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii:

*7

Mwandishi amechukulia masaa ya Uarabuni ambako wako mbali na mstari wa Ikweta. Ama sisi tulio Afrika

Mashariki , tuko katika Mstari wa Ikweta ,usiku na Mchana katika vipindi vyote vya mwaka hautafautiani zaidi ya zaidi ya saa moja -Mtarjumu.

4& 86

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Sema: "Ewe Mola uliyemiliki ufalme wote! Humpa ufalme umtakaye na humwondolea ufalme umtakaye na humtukuza umtakaye na humdhalilisha umtakaye."

Ikiwa hii ndiyo sababu ya kushuka Aya hii au siyo, lakini dhahiri ya Aya haikatai, na matukio ya historia yanaunga mkono hilo.

28.Waumini wasiwafanye Makafiri kuwa ni marafiki badala ya waumini (wen-zao). Na mwenye kuyafanya hayo, basi hana kitu kwa Mwenyezi Mungu ila mtakapojilinda nao kwa kujihifadhi na anawatahadharisha Mwenyezi Mungu na Yeye mwenyewe marejeo ni kwa Mwenyezi Mungu.

29.Sema: Mkificha yaliyomo vifuani mwenu au mkiyadhihirisha Mwenyezi Mungu anayajua na anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.

30.Siku ambayo kila nafsi itakuta kheri iliyoitenda imehudhurishwa Na iliyoy-atenda katika uovu, itapenda lau kungekuwa na masafa marefu baina ya uovu huo na yeye. Na anatahad-harisha Mwenyezi Mungu na Yeye Mwenyewe, na Mwenyezi Mungu ni mpole kwa waja.

Kaashif3-68.jpgKaashif3-69.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

URAFIKI NA KAFIRI

Aya 28-30: LUGHA.

Neno Awliya lina maana ya wasimamizi, Makusudio yake hapa ni marafiki kwa maana ya wasaidizi

MAANA

Waumini wasiwafanye makafiri kuwa ni marafiki badala ya waumini (wenzao).

Mwenyezi Mungu hakutosheka na kukataza tu urafiki na makafiri kwa kusema ni haramu; kama vile uongo na kusengenya, bali amekuzingatia kuwa ni kufuru, kwa dalili ya neno lake:

Na mwenye kuyafanya hayo, basi hana kitu kwa Mwenyezi Mungu.

Kwani dhahiri ya kauli hiyo ni kuwa Mwenyezi Mungu yuko mbali na aliye na urafiki na makafiri; na aliye mbali na Mwenyezi Mungu, basi yeye ni Kafiri. Hili linatiliwa nguvu na Aya hizi:

"Na atakayefanya urafiki nao miongoni mwenu, basi huyo atakuwa pamoja nao." (5:51).

Huwapati watu wanaoamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho kuwa wanawapenda wale wanaompinga Mwenyezi Mungu na Mtume Wake; hata wakiwa ni baba zao au watoto wao au ndugu zao au jamaa zao."(58:22)

Dhahiri ya Aya hizi inafahamisha kuwa mwenye kumfanya kafiri kuwa rafiki basi naye ni kafiri. Hata hivyo kuna aina mbali mbali za kumfanya rafiki, nyingine zinawajibisha ukafiri na nyingine haziwajibishi. Ufafanuzi ni kama ufatavyo:

AINAZA URAFIKI NA KAFIRI

Kila aliyesema: Laillaha Illa Ilah Muhammadun rasulullah. Basi anakuwa na lile walilonalo waislamu wengine, na wao wako na lile alilo nalo, isipokuwa akiwafanya makafiri kuwa ni marafiki katika mojawapo ya hali zinazofuata:

1.Kuwa radhi na ukafiri wao, na hili ni muhali kwa mwislam kwa sababu kuridhia ukafiri ni

ukafiri.

2.Kujikurubisha kwa makafari kwa upande wa dini kwa kujaribu kufasiri Aya za Mwenyezi Mungu Mtukufu, na Hadith za Mtume Wake kwa yale yanayoafikiana na mapenzi ya makafiri, maadui wa Mwenyezi Mungu na Mtume, kiasi ambacho tafsiri hiyo itapingana na misingi ya kiislamu na kiitikadi. Ikiwa kwa makusudi na kujua. Huu vile vile ni ukafiri. Unaweza kuuliza: Mtu anayefanya hayo kwa ukaidi ni kafiri bila ya wasiwasi wowote, laki-ni mwenye kuyafanya kwa kupuuza tu, inafaa awe fasiki tu, sio kafiri; sawa na mwenye kuacha Swala akiwa anaamini kuwa ni wajibu na akanywa pombe akiwa anaamini kabisa kuwa ni haramu?

Jibu: Kutofautisha kati ya mkaidi na mpuuzaji kunakuja kwenye Fur'uu (matawi); kama vile Swala, kunywa pombe n.k. Ama kwenye mambo yanayorudia kwenye Usul (Misingi) ya dini na itikadi; kama vile umoja wa Mungu, utume wa Muhammad n.k. Basi kutamka tu

Kaashif3-70.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

kitu kinachokanusha kunawajibisha ukafiri. Ni sawa mtamkaji awe ametamka kwa ukaidi au kwa kupuuza.

3.Kuwa kachero au jasusi wa makafiri dhidi ya waislamu, Huyu ataangaliwa. Ikiwa ame-fanya hivyo kwa tamaa ya mali au jaha basi atakuwa mwenye makosa aliye fasiki, ama akifanya kwa sababu ya kuwapenda makafiri kwa kuwa wao ni makafiri na kwa kuwachukia waislamu kwa kuwa ni waislamu, basi huyo ni kafiri bila ya shaka yoyote.

4.Kuwapenda makafiri na huku akiwa anajua kabisa kwamba wao wanawapiga vita Waislamu wakiwa wanataka kuwadhalilisha na kuwatumia, basi huyu atakuwa ni mwenye dhambi na mshirika wa dhalimu katika udhalimu wake, hata kama huyo dhalimu ni mwis-lamu.

5.Kuwataka msaada makafiri wenye amani dhidi ya makafiri wasiokuwa na amani. Msaada huu unafaa kwa maafikiano ya Ijmai (kongamano). Watu wa historia na wafasiri wamenukuu kwamba Mtume (s.a.w.w.) aliwekeana mkataba wa kusaidiana na Bani Khuzaa inagawaje walikuwa washirikina. Pia alimtaka msaada Safwan bin Umayya -kabla hajasilimu - kwenye vita ya Hawazan. Vilevile aliwataka msaada Mayahudi wa Bani Qaynuqa na akawagawanyia mali.

Bali yamekuja maelezo kutoka kwa Allama Hili kwamba kundi la mafakihi wamejuzisha kutaka msaada kutoka kwa makafiri katika kuwapiga vita waislamu walio madhalimu. Kwa sababu kuwataka msaada kunaambatana na haki, si kwa ajili ya kuibatilisha batili.

6.Kufanya urafiki kwa sababu za mambo ya kawaida yaliyozoeleka, kama kushirikiana katika kazi au biashara na mengineyo mengi ambao hayahusu dini. Urafiki huu pia unafaa kwa kongamano la maulamaa. Kwa sababu kumpenda kafiri kutakuwa haramu kama kutapelekea kufanyika jambo la haramu, ama kukiwa sio wasila wa kufanya maasi, basi si haramu; bali huenda kukawa kunapendekezwa kama kuna manufaa na heri kwa nchi au watu. Na, Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameamrisha upendano, kuzoweyana na kusaidiana kwa watu wote bila ya kuangalia dini au mila zao. Mwenyezi Mungu Mtukufu anase-ma:

"Mwenyezi Mungu hawakatazi kuwafanyia wema na uadilifu wale ambao hawakupigana

nanyi kwa ajili ya dini wala hawakuwafukuza katika miji yenu. Hakika Mwenyezi Mungu

anawapenda wafanyao uadilifu."(60:8).

Sisi hatuna shaka kwamba katika makafiri kuna walio na hulka nzuri na tabia njema - ya ukweli, uaminifu na utekelezaji - kuliko wale tunaowaita na kujiita waislamu. Na kwamba kufanya urafiki nao ni bora zaidi - kibinadamu na kimaslahi ya umma - kuliko wale vibaraka wahaini wanaojionyesha kwa dini ya kiislamu. Maelefu ya rehema na amani yamwendee yule aliyesema: "Aliye karibu ni yule aliye karibu kwa tabia. Huenda aliye karibu akawa mbali zaidi ya aliye mbali na aliye mbali akawa karibu zaidi ya aliye karibu." Hakika hii huitambua mtu kimaumbile tu bila ya hisia zozote.

TAQIYA

Ila mtakapojilinda nao kwa kujihifadhi.

Historia ya Taqiya inaanzia na historia ya uislamu siku ulipokua dhaifu, na shujaa wa kwan-za alikuwa Ammar bin Yasir, pale aliposilimu yeye, baba yake na mama yake; wakaadhibi-wa na makafiri kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, wakavumilia adhabu na adha bila ya kulalami-ka. Mtume akawapitia wakiwa wanaadhibiwa: Hakuzidisha chochote Yasir zaidi ya kuse-ma: "Hali ndio hii ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu." Mtume naye akasema: "Vumilieni enyi

89

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

familia ya Yasir hakika ahadi yenu ni pepo." Akawa Yasir na mkewe Sumaiya ndio mashahi-di wa kwanza katika uislam.

Washirikina wakamlazimisha Ammar kusema maneno kuhusu Mtume wa Mwenyezi Mungu, akasema kwa ajili ya kujikinga na madhara kwa ajili ya nafsi yake. Hapa baadhi ya Maswahaba wakasema kuwa Ammar amekufuru; Mtume akasema: "Hapana hakika Ammar imani imemtanda kuanzia utosini hadi nyayoni..."

Ammar akaja kwa Mtume akiwa analia na kujuta. Mtume akampangusa machozi na kuuwaambia: "Usilie, hata kama watarudia, basi wewe rudia uliyoyasema." Hapo ikashuka Aya kumhusu Ammar: "Mwenye kumkufuru Mwenyezi Mungu baada ya kumwamini (ana adhabu kubwa) isipokuwa yule aliyelazimishwa hali ya kuwa moyo wake umetulia kwenye imani." (16:106)

Hakuna waliohitalifiana kuwa Aya hii, ilishuka kwa mnasaba huo wa Ammar. Kimsingi linalozingatiwa ni kuenea tamko, sio sababu za kushuka Aya. Na tamko hapa linamwenea kila mwenye kulazimishwa hali ya kuwa moyo wake umetulia kwenye imani.

Kisha ndipo ikashuka Aya hii tunayoifasiri kutilia mkazo Aya hiyo ya kuhusu Ammar, kama zilivyo Aya nyingine zifuatazo:

Na akasema mtu mmoja Mumin katika watu wa firaun afichaye imani yake ...(40:28) "... Isipokuwa vile mnavyolazimishwa" (6:119)

Ruhusa ya Taqiya haikuja kwenye kitabu cha Mwenyezi Mungu tu, bali katika Hadith vilevile. Ar-Razi katika Tafsir Kabir, na Sayyid Rashid Ridha katika Tafsir Al-Manar, na wengine wanasema: "Musailama Al-Kadhab aliwashika watu wawili katika swahaba wa Mtume, mmoja akamwambia: "Je, washuhudia kuwa mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu?"

Yule mtu akasema: "Ndio," basi akamwacha. Yule wa pili alipomwambia hivyo hivyo, alikataa, basi akamuua. Mtume alipopata habari hizo alisema: "Yule aliyeuawa amekufa na yakini yake na ukweli wake pongezi ni zake. Ama yule mwengine ameruhusiwa, (kufanya hivyo) hana neno."

Kuna Hadith katika Tafsir Al-Manar kwamba Bukhari katika Sahih yake akimnukuu Aisha anasema: "Mtu mmoja alibisha hodi kwa Mtume, Mtume akajisemea: "Mtu mbaya huyo", kisha akamruhusu kuingia na akazungumza naye vizuri."

Yule mtu alipoondoka Aisha akamwambia Mtume: "Si umesema uliyoyasema kuhusu mtu huyu, kisha umezungumza naye vizuri? Mtume akasema; "Hakika mwovu zaidi wa watu ni yule anayeachwa na watu kwa kujikinga na shari yake."

Na katika Bukhari tena kuna Hadith ya Abu Dardai inayosema: "Sisi tunatabasamu kwenye nyuso za watu na nyoyo zetu zinawalaani."

Zaidi ya hayo kuna Hadith nyingine zinafahamisha kujuzu Taqiya (kujikinga) kama vile Hadith: "Hapana dhara wala kudhuriana." Na "Umati wangu umesamehewa yale wanay-olazimika nayo." Hadith zote hizi mbili ni Mutawatir kwa upande wa Sunni na Shia.

Kwa kutegemea kitabu cha Mwenyezi Mungu na Hadith Mutawatiri za Mtume zilizo sahihi basi Sunni na Shia wamekongamana kwa kauli moja kuwa Taqiya inafaa. Anasema Al-Jasas mmoja wa Maimam wa Kihanafi katika juzuu ya pili ya kitabu Ahkamul Qur'an Uk. 10 chapa ya 1347 A.H. Ninamnukuu: "Ila kwa kujilinda nao" Yaani ni kuhofia kuangamia nafsi au baadhi ya viungo kwa hiyo kujilinda nao kwa kudhihirisha ukafiri bila ya kuutaikidi ... Na hilo limeafikiwa na watu wa elimu."

90

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Ar-Razi katika tafsiri yake amemnukuu Hassan Al-Basri akisema: "Taqiya inajuzu mpaka siku ya Kiyama". Vilevile amemnukuu Shafi kwamba yeye amejuzisha Taqiya kwa waisla-mu wote, ikiwa anamhofia mwislam mwenziwe katika tofauti zinazorudia masuala ya dini.

Mwenye Tafsir Al-Manar naye anasema kuhusu Aya hii: "Mwenye kutamka neno la kufru akiwa anajikinga na kuangamia kwa kulazimishwa sio kwa kuukubali ukafiri au kwa sababu ya kupenda dunia kuliko akhera, basi si kafiri na unakubaliwa udhuru wake kama alivyokubaliwa Ammar bin Yasir

Na amesema Sheikh Mustafa Azurqaa katika Kitabu Fiq-hul-Islam Fi Thawbihil Jadidi mada ya 600, anasema: "Kutishwa mtu kuuliwa kwa kulazimishwa ukafiri, kunamhalalishia kudhi-hirisha ukafiri ikiwa moyo umetulizana na imani."

Zaidi ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu, Hadith za Mtume na kongamano la Waislamu wa kisunni na kishia, pia akili inakubali Taqiya kwa sababu akili pia inaiona ni nzuri kutokana na desturi isemayo "Dharura inahalalisha yaliyokatazwa."

Kwa hiyo basi inatubainikia kuwa Taqiya ni kanuni ya sharia wanayoitegemea Mujtahid wa Kisunni na kishia katika kutoa hukumu. Na kwamba dalili yake ni Qur'an, Hadith, kongamano na akili. Kwa ajili hiyo Taqiya inakuwa ni funzo la kiislamu kwa waislamu wote na kuaminiwa na madhehebu zote; na wala sio ya madhehebu maalum kama wanavyodhania Khawarij.

Hapa kuna swali linalojitokeza; nalo ni ikiwa Taqiya inafaa kwa Qur'an, Hadith, akili na kongamano kutoka kwa Shia na Sunni, kwa nini wanasibishiwe Shia tu, kiasi kwamba Masheikh wengi wa kisunni wameinasibisha kwa Shia na kuwakebehi nayo?

Jibu: Kunasibishiwa au kuwa mashahuri zaidi kwa Shia, huenda ikawa ni kwa sababu ya kuwa wao walilazimika kuitumia zaidi ya watu wengine kwa kuangalia vikwazo vingi walivy-

ovipata wakati wa utawala wa Bani Umayya, Bani Abbas na waliowafuatia*8 . Kwa sababu ya kulazimika Shia kuwa na Taqiya mara nyingi au zaidi kuliko wengine, ndio maana waka-jishughulisha nayo na kuitaja katika vitabu vya fikh tena wakaifafanua kwa kubainisha mipa-ka yake na wakati wake wa kufaa kuifanya na kutofaa. Muhtasari wa waliyoyasema ni: Inafaa kwa ajili ya kuondoa madhara ya nafsi, na haifai kwa ajili ya kuleta manufaa au kuin-giza madhara kwa mwengine.

Ama yule anayeihusisha Taqiya na Mashia tu, ama atakuwa ni mjinga au atakuwa mwenye chuki. Hata hivyo hivi sasa Taqiya haitumiki (sana) baada ya kupita wakati wa hofu na vikwanzo.

Na anawatahadharisha Mwenyezi Mungu naye.

Yaani na dhati Yake ambayo inajua kila kitu, yenye uweza juu ya kila kitu na kumlipa kila mtu kwa amali yake.

Na marejeo ni kwa Mwenyezi Mungu.

Ambako italipwa kila nafsi ilichofanya.

8Angalia kitabu chetu Ashia wal-hakimun na mwanzo wa juzu ya tatu ya sharh Nahajul-Balagha ya Ibn Abdul-Hadid, uone aina za adhabu na ukandamizaji usio na mfano.

91

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Sema mkificha yaliyomo vifuani mwenu au mkiyadhihirisha Mwenyezi Mungu anaya-jua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kujuzisha Taqiya na kuiruhusu kwa mwenye kulazimika, anasema: linaloangaliwa mbele ya Mwenyezi Mungu ni lile lililo moyoni: na yeye anayajua ya moyoni mkifanya siri au kuyadhihirisha. Siku ambayo kila nafsi itakuta kheri iliyoitenda imehudhurishwa.

Lilivyokuwa Mwenyezi Mungu anajua kila kitu, muweza wa kila jambo; mkusanyaji wa watu siku isiyo na shaka. na mwadilifu asiyedhulumu, hayo yote yanamhakikishia mtu kukuta malipo ya amali yake.

Baadhi wanasema, mtu atakuta amali yake kesho ikiwa kama umbo zuri la kupendeza kama ni ya kheri; au kama ni mbaya basi itakuwa na umbo la kutisha. Lakini inavyojulikana ni kwamba amali ni mambo ambayo hayabaki wala haiwezekani kuyarudisha na kuyaona. Kwa hiyo makusudio ni kuwa mtu siku ya kiyama ataona malipo ya amali yake sio hiyo amali yenyewe.

Na iliyoyatenda katika uovu, itapenda lau kama kungekuwa na masafa marefu baina ya uovu huo na yeye.

Herufi Wau hapa ni kuanza maneno; yaani mwenye kumwasi Mwenyezi Mungu, hapo kesho atatamani kuweko na masafa kati yake na siku hiyo sawa na umbali wa Mashariki na Magharibi. Na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja.

Hata waasi pia, kwa sababu amewalazimisha wanayoyaweza na amewahadharisha na mwisho mbaya wa maasi. Pia amefungua mlango wa toba kwa yule ambaye nafsi yake imefanya maovu. Kwa hiyo mwasi habaki na udhuru.

31.Sema: Ikiwa mnampenda Mwenyezi Mungu, basi nifuateni Mwenyezi Mungu atawapenda na atawaghufiria madhambi yenu: na Mwenyezi Mungu ni mwenye kusamehe Mwenye kure-hemu.

32.Sema: Mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume, kama wakikataa, basi hakika Mwenyezi Mungu hawapendi makafiri.

KUMPENDA MWENYEZI MUNGU

Aya 31 - 32

MAANA

Sema: Ikiwa mnampenda Mwenyezi Mungu, basi nifuateni.

Yeyote anayempenda Mwenyezi Mungu, analazimika kumpenda Mtume wa Mweneyezi Mungu na Ahlu Bait wake, kwa sababu Mtume anawapenda. Na yeyote anayempenda

Kaashif3-71.jpg

92

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Mtume, analazimika kumpenda Mwenyezi Mungu, Mapenzi hayo mawili hayaachani. Mwenyezi Mungu anasema:

Mwenye kumtii Mtume basi ndio amemtii Mwenyezi Mungu (4:80)

Kwa sababu Mtume ndiye anayemsemea Mwenyezi Mungu na ndio ubainifu wake; vinginevyo mtu atakuwa ni adui. Yaani mwenye kufanya uadui na Mtume na Aali zake, basi ndio amejiwekea uadui na Mwenyezi Mungu, atake asitake. Kwa hivyo watu wa dini nyingine ambao wanalingania imani ya Mungu kisha wanamfanyia uadui Muhammad (s.a.w.) basi wao ndio maadui zaidi katika maadui wa Mwenyezi Mungu.

Kama mtu atasema kuwa kutojua kwao utume wa Muhammad ni udhuru; basi jibu ni kuwa hakuna udhuru kabisa kwa yule anayefuata mapenzi yake na akawa anawafuta tu mababu zake, isipokuwa baada ya kuthibitisha na kuangalia dalili zote juu ya utume wa Muhammad. Na, yeyote atakayeangalia dalili hizi kwa mtazamo wa uadilifu na kuchunga haki, ataamini na kunyeyekea.

Hakuna maana ya pendo la mdogo kwa mkubwa na mtumishi kwa bwana wake, isipokuwa ni utii na kufuata.

Na, kila anayependa yale anayoyachukia Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na akachukia yale anayoyapenda Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, basi yeye ni adui wa Mungu na Mtume wake; hata kama atafikiriwa kuwa ni katika wapenzi. Kwa sababu yale yanayod-haniwa kwake kuwa yeye ni mpenzi bila ya kuwako na athari yoyote, haya yatakuwa njozi tu.

Sema: Mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume, na wakikataa, basi hakika Mwenyezi Mungu hawapendi makafiri.

Dhahiri ya Aya hii inaonyesha kuwa hakika ya dini ni kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume, na kwamba kuuacha utiifu huo kunalazimisha ukafiri, bali ni ukafiri hasa kwa dhati yake, kutokana na kauli yake hiyo: "Na wakikataa, basi hakika Mwenyezi Mungu hawapendi Makafiri." Na wala hakusema hakika Mwenyezi Mungu hawapendi waasi au atawaadhibu, kwa maana kuwa Mungu ameuzingatia uasi kuwa ni ukafiri, sio sababu ya ghadhabu na adhabu tu.

Jambo hili lina hatari na kuhofisha sana, kiasi ambacho hawatabakia kwenye dini na kwenye uislamu isipokuwa wachache kabisa, ila ikiwa makusudio ya ukafiri hapa ni uasi; kama ilivyo katika Aya hii:

Na ni haki ya Mwenyezi Mungu juu ya watu kuhiji Nyumba hiyo kwa mwenye kuweza njia ya kuendea na anayekufuru basi Mwenyezi Mungu si mhitaji kwa walimwengu (3:97)

Kwa hali yoyote iwayo, sisi tunaamrishwa kidini na kisharia kumtendea kiislamu kila mwenye kutamka shahada mbili, kama vile urithi, ndoa, utwahara, na kulinda mali na damu yake. Yasiyokuwa hayo ataachiwa mwenyewe Mwenyezi Mungu (s.w.t.) sisi hatuna majukumu nayo.

93

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

33.Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adam na Nuh na watoto wa Ibrahim na watoto wa Imran juu ya wal-imwengu wote.

34.Kizazi cha wao kwa wao na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.

35.Aliposema mke wa Imran: Mola wangu! Nimeweka nadhiri kwako aliyemo tumboni mwangu kuwa wakfu. basi nikubalie hakika wewe ndiwe usikiaye uliye mjuzi.

36.Alipomzaa alisema: Mola wangu! Nimemzaa mwanamke - Na Mwenyezi Mungu anajua sana aliyemzaa - Na Mwanamume si kama mwanamke na nimemwita Maryam. Na mimi namkinga kwako, yeye na kizazi chake (uwalinde) na shetani aliye-fukuzwa.

Kaashif3-72.jpg

94

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

37.Basi Mola wake akamkubalia kwa kabuli njema na akamkuza makuzi mema. Na akamlea Zakariya. Kila mara Zakariya alipoingia Mihrab hukuta vyakula. Akasema: Ewe Maryam unatoa wapi hivi. Akasema: Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu hum-ruzuku amtakaye bila hesabu.

Kaashif3-73.jpg

MAMA WA MARYAM Aya 33 - 37

Neno Maryam katika lugha ya Kiibrania lina maana ya mtumishi wa Bwana (Mola). Na Mihrabu kwa Waislamu ni pale anaposimama Imam, na kwa Wakristo ni pale wanapopaita madhabahu

MAANA

Hakika Mwenyezi Mungu alimteua Adam na Nuh na watoto wa Imran na watoto wa Ibrahim juu ya walimwengu wote.

Muhammad bin Yusuf aliye mashuhuri kwa jina la Abu Hayan Al-Andalusi, katika Tafsir yake kubwa inayoitwa Al-bahrul Muhit anasema: Amesoma Abdullah; "Na kizazi cha Muhammad juu ya viumbe wote."

(Qiraa) hiki kikiwa sawa au si sawa lakini Aya ya Tat-hir inasema: Hakika Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu watu wa nyumba (ya Mtume) na kuwatakasa kabisa kabisa." (33:33),

Inatosha kuwa Aya hii ni dalili ya kuwa Mwenyezi Mungu amekiteua kizazi cha Muhammad (s.a.w.) na cheo chao na utukufu wao,yeye ni bora wa mitume wote basi kizazi chake pia ni bora ya vizazi vyote: bali ni kwamba wanachuoni wa umati wake ni kama mitume wa Bani Israil au ni bora kuliko mitume wa Bani Israil - sikumbuki tamko la Hadith yenyewe - hasa wakiwa wanavyuoni wenyewe ni kutokana na kizazi chake kitakatifu.

Vyovyote itakavyokuwa, Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameanza kwa kutaja Adam kwa sababu yeye ndiye baba wa kwanza wa watu kisha akamtaja Nuh ambaye ni baba wa pili wa watu kwa sababu wakazi wote wa duniani wanatokana na kizazi chake cha watoto wake watatu; Sam, Ham na Yafith, baada ya tufani iliyomaliza watu wote.

Mwenyezi Mungu aliwateua Adam na Nuh wao wenyewe tu, ndio maana hakutaja kizazi. Ama Ibrahim na Imran aliwateua pamoja na vizazi. Ibrahim naye ni baba wa mitume wote

95

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

baada ya Nuh, kwani tangu wakati wa Ibrahim hakukuwa na Mtume ila atakuwa ame-tokana na kizazi chake.

Kwa dhahiri ni kwamba makusudio ya Imran ni baba wa Maryam babu wa Isa, sio baba yake Musa. Kwa sababu jina hili limekuja tena mara ya pili, aliposema; "Aliposema mke wa Imran" Mfano huu uko katika mfano wa jina linalokuja katika jumla mbili kwa muundo mmoja; kama vile kusema; Mtukuze Zedi, hakika Zedi ni mtu mwema. Kwa hiyo basi makusudio ya kizazi cha Imran ni Bwana Masih na mama yake Maryam.

Inasemekana kwamba Imran (baba yake Musa) alikuwa na bint aitwaye Maryam aliyekuwa mkubwa wa Musa; na kwamba baina ya Imran huyu na Imran babu wa Isa kuna miaka 1800.

Makusudio ya viumbe wote ni kwamba kila mmoja wa waliotajwa alichaguliwa katika watu wa wakati wake tu sio kila wakati.

Kizazi cha wao kwa wao

Hakuna mwenye shaka kwamba Nuh anatokana na Adam na kwamba Ibrahim na kizazi chake wanatokana na Nuh; na Imran anatokana na Ibrahim. Kwa hiyo kulielezea hilo ni sawa na kufafanua kilichofafanuliwa, na maneno ya Mwenyezi Mungu, ni wajibu kuy-achukulia kwa mfumo mzuri. Sasa nini makusudio ya habari hii?

Jibu: Makusudio sio kutoa habari kwamba wa mbele anatokana na wa nyuma, la! Isipokuwa makusudio - kama ilivyo dhahiri ya mfumo wa maneno - ni kuwasifu; na kwamba wao wanafanana katika utakatifu na ubora.

Baada ya utangulizi huu, twende kwenye kisa cha mke wa Imran, mama yake Maryam na nyanya yake Isa (a.s.). Kwa ufupi ni kwamba Qufadh bin Qubail Mwisrail, alikuwa na binti wawili mmoja akiitwa Hana aliyeolewa na Imran- ambaye ni Mwisrail vilevile - aliyemzaa Maryam. Na wa pili ni Isha aliyeolewa na Zakariya na kumzaa Yahya. Kwa hiyo Yahya bin Zakaria na Mariam mamie Isa, mama zao ni ndugu na wala sio Isa na Yahya; kama watu walivyozoea. Hivi ndivyo ilivyo katika Majmal-Bayan.

Imran akafa huku Hanna akiwa na mimba, akaweka nadhiri kuwa aliyemo tumboni awe mtumishi wa Baitul-Maqdis. Akajidhalilisha kwa kumfanyia ikhlas Mwenyezi Mungu ili aikubali nadhiri yake. Hii ilikuwa inajuzu katika dini yao wala haijuzu katika dini ya kiislamu. Yeye alikuwa akitazamia kuzaa mtoto wa kiume, kwa sababu nadhiri ya mahekalu ilikuwa maarufu kwa watoto wa kiume tu. Alipomzaa mtoto wa kike alimwelekea Mwenyezi Mungu na kusema:"Nimezaa mwanamke... "Na mwanamume si sawa na mwanamke na nimemwita Maryam."

Mwenyezi Mungu akaikubali nadhiri ingawaje alikuwa mtoto mke. Waisrail wakabishana, kila mmoja akitaka kumlea Maryam. Ubishi ulipozidi waliafikiana wapige kura. Mshindi akawa Zakariya mume wa mamake mdogo. Wakati huo Zakariya alikuwa ndiye mkuu wa hekalu la kiyahudi. Akamshughulikia sana. Ikawa kila Zakariya anapokwenda kumtazama Maryam anakuta chakula, na walikubaliana kuwa asiendewe na yeyote, akamuuliza kwa mshangao:

Unatoa wapi hivi?

Akasema: Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. - Yaani moja kwa moja kutoka kwa Mungu bila ya kupitia kwa yeyote.

96

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Hakika Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hisabu.

Hakuna mwenye kutia shaka kwamba karama hii ni ya Maryam (a.s.). Ama kukanusha karama hii kuwa ati chakula alichokuwa akikiona Zakariya kwa Maryam kilitoka kwa wafad-hili wa kike waumini, ni kinyume na dhahiri ya Aya. Kwani karama hii ina ukubwa gani zaidi ya kumzaa Isa bila ya baba. Ikiwa karama hiyo ya chakula inatiliwa shaka, basi hii ya kuzaa itatiliwa shaka zaidi.

Maana ya "Akamkuza makuzi mema" ni kwamba yeye alikulia na tabia njema, kumtii Mwenyezi Mungu na kumwabudu. Imepokewa Hadith kutoka kwa Ibn Abbas kwamba Mariam alipofikia umri wa miaka tisa alikuwa akifunga mchana na kuswali usiku, mpaka akawashinda watawa. Inasemekana kwamba hakuwahi kufanya kosa lolote.

FATIMANA MARYAM

Alitokewa na mfano wa karama hii bibi wa wanawake Fatima bint wa Mtume wa Mwenyezi Mungu. Katika Tafsir Ruhul-Bayan ya Sheikh Ismail Haqi wakati wa kufasiri kisa cha Maryam kuhusu chakula anasema:

"Mtume alishikwa na njaa katika wakati wa kahati (ukame). Fatima akamletea mikate miwili na nyama, mara alipoona sahani imeshehenezwa mkate na nyama, alisema "umevipata wapi hivi? Akajibu: "Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hisabu." Mtume akasema: "Sifa njema ni za ambaye amekushabihisha na bibi wa Bani Isriali.' Kisha Mtume akamwita Ali, Hassan, Hussein na watu wa nyumbani kwake; wakala, wakashiba na chakula kikabaki kama kilivyo, Fatima akakigawanya kwa majirani zake."

Katika kitabu Dhakhairul-Uqaba cha Muhibbudin Attabari imeandikwa kuwa, siku moja Ali alikopa Dinar ili akawanunulie chakula watu wake. Akakutana na Mikdad bin As-wad, akiwa katika hali ya mfazaiko alipomuuliza, alisema: "Nimeacha familia yangu wanalia kwa njaa." Basi Ali akampa ile dinar, akaenda zake kuswali nyuma ya Mtume. Baada ya Swala Mtume alimuuliza Ali, "Je una chochote kwako tukale?" Kama kwamba Mtume alipewa wahyi wa kwenda kula kwa Ali. Basi Ali akawa amechanganyikiwa hana la kujibu. Mtume akamshi-ka mkono Ali wakaenda kwa Fatima, walipofika tu wakakuta chakula. Ali akasaili: "Umekipata wapi hiki?" Mtume akasema: "Hiyo ni thawabu za Dinar; inatoka kwa Mwenyezi Mungu naye humruzuku amtakaye bila ya hisabu. Sifa njema ni za Mwenyezi Mungu aliyekufanya kama Zakariya na akamfanya Fatima mfano wa Maryam. Kila mara Zakariya alipoingia Mihrab hukuta riziki."

Kisha Muhibuddin akaongeza kusema: "Ameitoa Hadith hii Al-Hafidh Dimeshqi katika Arbaina Twiwal.

Katika Sahih Muslim mlango wa fadhila za binti wa Mtume imeelezwa kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu alimwambia binti yake Fatima. "Hivi huridhii kuwa wewe ni bibi mkubwa wa waumini au bibi mkubwa wa umma huu." Anasema Seyyid Muhsin Al-Amin katika kitabu A'yanushia Juz. 2 sera ya Zahra, akimnukuu Bukhari katika Sahih yake; kwamba Mtume alisema: "Fatima ni bibi mkubwa wa wanawake wa peponi."

Vilevile Ibn Sibagh Al-Malik katika Fausulul-muhimma amemnukuu Ahmad katika Musnad akipokea kutoka kwa Mtume kwamba amesema: "Fatima ni bibi mkubwa wa wanawake wa ulimwengu."

Katika kitabu Dhakhairul-uqaba cha Muhibbuddin Attabari amesema: Siku moja Mtume alikwenda kumwangalia Fatima alipokuwa mgonjwa, akamuuliza "Waonaje ewe mwanan-gu?" Akajibu: "Naumwa sana na njaa yanizidisha ugonjwa." Mtume akasema: "Ewe

97

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

mwanangu huridhii kwamba wewe ni bibi mkubwa wa wanawake wa ulimwengu wote?

Akasema: "Maryam bint Imran atakuwa nani basi?"

Mtume akajibu: "Yule ni bibi mkubwa wa wanawake wa wakati wake, na wewe ni bibi

mkubwa wa wanawake katika dunia na akhera."

Kisha Tabari akasema kuwa Hadith hii imetolewa na Abu Umar na Al-Hafidh Abul-Kassim

Dimeshqi. Ufafanuzi uliobakia utakuwa katika tafsir ya Aya 42.

38.Pale pale Zakariya akamwomba Mola wake, akasema: Mola wangu nipe kutoka kwako mtoto mwema hakika wewe ndiwe usikiaye maombi.

39.Mara Malaika wakamlingania hali amesimama akiswali kwenye Mihrab kwamba           Mwenyezi           Mungu

anakubashiria (kupata mtoto) Yahya atakayekuwa mwenye kusadikisha neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu na Bwana na mtawa na Nabii anayetokana na watu wema.

40.Akasema: Mola wangu! Nitapataje mtoto na hali ukongwe umenifikia na mke wangu ni tasa! Akasema: Ndivyo hivyo Mwenyezi Mungu hufanya apendalo.

41 .Akasema: Mola wangu niwekee alama akasema             alama yako ni

kutozungumza na watu siku tatu isipokuwa kwa ishara tu. Na umtaje Mola wako sana na mtakase wakati wa jioni na asubuhi.

Kaashif3-74.jpgKaashif3-75.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

ZAKARIYA

Aya 38 - 41 MAANA

Pale pale Zakariya akamwomba Mola wake, akasema: Mola wangu nipe kutoka kwako mtoto mwema.

Tumekwishaeleza kuwa Zakariya alikuwa mume wa mama mdogo wa Maryam na kwamba yeye ndiye aliyemlea. Zakariya hakuwa na mtoto; na alipoona utengeneo wa Maryam na karama alizokuwa nazo, basi aliingiwa na mapenzi ya baba na kupenda kuzaa, Akamwomba Mwenyezi Mungu kwa unyenyekevu; na Mwenyezi Mungu akamwitikia maombi yake.

Mara Malaika wakamlingania, hali amesimama akiswali kwenye Mihrabu kwamba Mwenyezi Mungu anakubashiria (kupata mwana) Yahya.

Yahya ni jina alilopewa na Mwenyezi Mungu kabla ya kuzaliwa, na hakupewa jina hilo yoy-ote kabla yake kama ilivyoeleza Aya ya 7 katika Sura Maryam. Kwa hiyo basi hakuna haja ya kufanya utafiiti kwamba je, jina hili ni la Kiibrania au la kiarabu, kama ilivyo katika baad-hi ya tafsir. Hata hivyo, linaingia katika lugha, kwa maana ya uhai na linanasibika jina lake pamoja na kuuhuisha Mwenyezi Mungu (s.w.t.) utasa wa mama yake.

Mwenye kusadikisha neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu

Inasemekana kuwa neno la Mwenyezi Mungu ni ishara ya Isa ambaye Mwenyezi Mungu amemuumba kwa neno 'Kuwa' bila ya baba. Lakini kwa ujumla neno linachukuliwa kuwa ni Aya zake zote na hukumu zake.

Mwenye Majmaul-bayan anasema kuwa Yahya ni mkubwa kuliko Isa kwa miezi sita, yeye ndiye wa kwanza kumsadiki na kushuhudia kuwa kuzaliwa kwake ni muujiza kutoka kwa Mwenyezi Mungu; na hilo lilikuwa ni nguvu ya hoja kuhusu Isa. Kwa sababu watu walikuwa wakimwamini Yahya na kumkubalia anayoyasema.

Na atakayekuwa bwana kielimu, dini na tabia njema.

Na mtawa, yaani anayejizuwia na kufanya madhambi. Inasemekana ni kujizuwia na

wan awake.

Na Nabii atokanaye na watu wema.

Manabii wote ni wema, bali ni Maasum; na Maasum ni zaidi ya uadilifu na wema. Kwa hiyo makusudio ya watu wema ni kuwa Zakariya anatoka katika kizazi kitakatifu.

Haya yanaaafikiana na kauli ya Shia kuwa wazazi wote wa mitume ni wajibu wawe wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho.

La kushangaza ni kauli ya badhi ya wafsiri - kama katika Tafsiri ya Razi - Kwamba makusudio ya neno Mina-swalihin ni kuwa hakuna nabii isipokuwa amefanya maasi au kudhamiria kuasi isipokuwa Yahya, hakuasi wala kudhamiria kuasi. Mbali ya kuwa kauli hii inatia dosari cheo cha Mtume Muhammad (s.a.w.), pia inapingana na akili. Kwa sababu Mtume amelet-wa kuondoa maasi; kama akiasi watu watatoa hoja kuwa yeye pia anafanya. Ametakata Mwenyezi Mungu na wayasemayo wasiojua.

99

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Akasema: Mola wangu nitapataje mtoto na hali ukongwe umenifikia na mke wangu ni tasa! Akasema: Ndivyo hivyo hivyo; Mwenyezi Mungu hufanya apendalo.

Wanasema kuwa Zakariya aliposema haya, alikuwa na miaka 120 na mkewe miaka 98. Hapa kuna swali linalojitokeza, kuwa Zakariya aliomba Mwenyezi Mungu apewe mtoto mwema ikimaanisha kuwa yeye aliomba kitu kina-chowezekana katika itikadi yake, sasa vipi tena arudi kuona ajabu alipopewa habari na Malaika?

Jibu: Hiyo haikuwa ni kutia shaka au kushangazwa, isipokuwa ni kuutukuza uwezo wa Mwenyezi Mungu ambao umepetuka mipaka na kawaida; kama vile mtu anavyomwambia mtu aliyetoa sana vitu vya thamani. "Vipi umefanya jambo asilo-lifanya yeyote isipokuwa wewe?" Vilevile kuadhimisha huko na kustaajabu kunakusanya shukrani kwa Mwenyezi Mungu juu ya neema hii tukufu ambayo hata hakuifikiria. Vilevile tunapata faida kutokana na muujiza huu kwamba mtu asiyalinganishe matakwa ya Mwenyezi Mungu na lile ambalo yeye analiona linawezekana au la.

Akasema: Mola wangu! Niwekee alama: Kwa kuwa kutunga mimba ni jambo lisilojulikana upesi, alipenda Zakariya kujua itakapotungwa mimba, ili aanze kushukuru tangu mwanzo. Kwa hiyo ndio akamwomba Mola wake amjaalie alama itakayomfahamisha kutungwa mimba. Ndipo Mwenyezi Mungu akasema: Alama yako ni kutozungumza na watu siku tatu isipokuwa kwa ishara tu na umtaje Mola wako sana na mtakase wakati wa jioni na asubuhi.

Yaani alama ya kutungwa mimba ni kuwa ulimi wako utafungika na utashindwa kuzungumza na watu isipokuwa utaelewana nao kwa ishara utakuwa kama bubu, lakini ulimi wako utafunguka kiasi unachotaka wakati unapofanya ibada. Na huu ni muujiza wa pili baada ya mimba ya tasa.

Mwenye Tafsiri Al-Manar, akimnukuu Ustadh wake Sheikh Muhammad Abduh, anasema kuwa Mwenyezi Mungu alimwamrisha Zakariya ajishughulishe na dhikr na tasbih tu muda wa siku tatu bila ya kuzungumza na watu, basi atatoa ishara, baada ya siku tatu ndio atam-pa. Tafsir ya kwanza ndiyo iliyo wazi na mashuhuri zaidi.

42.Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteua na akakutakasa na akaku-teuwa juu ya wanawake wa ulimwen-guni.

Kaashif3-76.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Kaashif3-77.jpg

43.Ewe Maryam! Mnyenyekee Mola wako na usujudu na urukuu pamoja na wanaorukuu.

44.Hizi ni habari za ghaibu tunazokupa wahyi; nawe hukuwa nao walipotupa kalamu zao nani katika wao atamlea Maryam na hukuwa nao walipokuwa wakishindana.

EWE MARYAM MWENYEZI MUNGU AMEKUTEUA Aya 42 - 44

MAANA

Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake wa ulimwenguni.

Kwanza Mwenyezi Mungu amemtaja mama yake Maryam, mimba na nadhiri yake; kisha akamtaja Zakariya mlezi wa Maryam; akamtaja tena Maryam na kuruzukiwa kwake na Mwenyezi Mungu bila ya hisabu. Kisha akamtaja Zakariya, maombi yake na kukubaliwa kwake maombi. Hivi sasa anarudia tena kwa Maryam kama ilivyo kawaida ya Qur'an, kuingilia suala jengine ambalo linafungamana na suala la kwanza, kisha tena kulirudia suala la pili.

Makusudio ya kuteuliwa kwa kwanza, ni kukubaliwa kuwa waqfu wa kuitumikia nyumba ya Mwenyezi Mungu, kwa sababu hilo lilikuwa likihusika na wanaume, na kwa pili, ni kuzaa Mtume bila ya kuguswa na mtu yeyote. Inasemekana kuwa kuteuliwa kwa pili ni kutilia mkazo kuteuliwa kwa kwanza.

Kuhusu kutakaswa, mwenye Tafsir Al-manar anasema: "Kumefasiriwa kutakasika kwa maana ya kukosekana hedhi. Na imepokewa kuwa bibi Fatima Zahra hakutoka hedhi, na ndio maana akaitwa Zahra."

Tunaloliona kuwa lina nguvu ni kwamba kutakasika ni usafi wa Maryam, wa kutakasika na kila shubha kuhusu kuzaa kwake.

Kongamano la wanavyuoni limeafikiana kuwa Maryam hakuwa Mtume; na wala hakuna Mtume mwanamke. Mwenyezi Mungu anasema: Na hatukutuma kabla yako isipokuwa wanaume tuliowapa wahyi." (12:109).Na utume umekoma kwa Muhammad s.a.w.w

101

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Ama kule kuzungumza na Malaika, hakumaanishi kuwa yeye ni Mtume; hata mama yake Musa pia alizungumza na Malaika; kama Aya hii isemavyo: "Na tukampa wahyi mama yake Musa ya kwamba mnyonyeshe ... (28:7).

Tutafafanua zaidi kuhusu kuteuliwa Maryam Inshaallah.

UBORA WA QUR'AN KWA WAKRISTO

Yametangulia maelezo kwamba ujumbe wa Kinasara kutoka Najran ulikwenda Madina kumhoji Mtume wa Mwenyezi Mungu kuhusu utume wake, huku ukilingania uungu wa Isa, Mtume akawasomea: Ewe Maryam hakika Mwenyezi Mungu amekuteua na kukutakasa."

Kusoma kwa Mtume Aya hii kwa ujumbe wa kikristo wa Najran, ambao umekuja kuhojiana naye, ni dalili ya mkato juu ya utukufu wa uislam na ukweli wa Mtume Mtukufu. mayahudi hawakuichunga haki kwa kusema uongo na kumzulia Maryam pamoja na kuleta tuhuma kuhusu kuzaliwa kwake, lakini Mwenyezi Mungu amewakadhibisha na akaandika katika kitabu chake (Qur'an) usafi wake, na akakata njia zote za uzushi. Lau kama Muhammad hakuwa mkweli katika ujumbe wake na kutojiamini, basi angelificha hilo (la Maryam) kwa wakristo kwa namna ambayo mayahudi walimtukana Maryam na kumfanya mwongo.

Uislam kwa Aya hii umewatendea wema wakristo, wema mkubwa mno; lau si hivyo yange-lisikika mengi kutoka kwa baadhi ya waislam wakati wa kugombana, kama yale yaliyosiki-ka kwa mayahudi kuhusu Maryam mtakatifu. Lakini mwislamu anajua kuwa utakatifu wa bibi Maryam ni sehemu ya uti wa mgongo wa itikadi yake; na kwamba kumtusi ni kufru na ni kutoka katika uislam. Yatakuja maelezo zaidi katika kufasiri Aya (5:82) Inshaallah.

Ewe Maryam! Mnyenyekee Mola wako na usujudu na urukuu pamoja na wanaorukuu.

Alimwamrisha ibada kwa kujiandaa na jambo kubwa ambalo ni kumzaa Isa (a.s.). Jambo lolote kuu ni lazima liwe na maandalizi. Pia Mwenyezi Mungu alimwamrisha kuswali na kutoa Zaka madamu yuko hai.

Hizi ni habari za ghaibu tunazokupa wahyi.

Msemo unaelekezwa kwa Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu; maana yake ni kuwa unay-owaambia watu kwa ujumla na yale unayowahusisha wakristo na ujumbe wa Najran, kama vile kisa cha Maryam na mama yake, mke wa Imran na kisa cha Zakariya na Yahya, yote hayo na mengineyo hukuyasoma katika kitabu wala hukuyasikia kutoka kwa wasimulizi, kwa sababu wewe husomi na huandiki. Yote hayo ni ujuzi wa ghaibu na ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Na, hii ni hoja kwa wahasimu wako, na ni dalili ya ukweli wako. Wasimulizi kamwe hawakunukuliwa kusema kuwa ujumbe wa Najran uliweza kujibu au kupinga hoja hii.

Nawe hukuwa nao walipotupa kalamu zao nani kati yao atamlea Maryam na hukuwa nao walipokuwa wakishindana.

Kalamu ni kitu maarufu, ni ile ambayo inaandikiwa; na makusudio yake hapa ni mishale waliyokuwa wakipigia kura. Maana kwa ujumla ni kuwa kuwafahamisha kwako habari hii na undani huu kuhusu Maryam na Zakaria, kwamba hukusoma wala kusikia, basi imebakia kuwa umeona tu, lakini inajulikana kuwa kuna mamia ya miaka kati yako na kisa hicho (hivyo hukuona). Kwa hivyo basi kujua kwako habari hizo ni kwa wahyi tu.

Kwa ufupi kisa hicho cha kutupa 'kalamu' kwa kupiga kura, ni kwamba, Hanna, mke wa Imran alipomzaa Maryam alikuwa ameweka nadhiri kuwa atumikie Baitul-Maqdis. Na

102 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

alimzaa baada ya kufa baba yake (Imran). Basi makuhani na makasisi wa Israil wakashin-dana kuhusu atakayemlea. Hatimaye wakapiga kura ambayo ilimwangukia Zakariya, mume wa mamake mdogo. Akawa ndiye mlezi na msimamizi wake.

NANI BIBI MKUU WA WANAWAKE WA ULIMWENGUNI?

Imekwishaelezwa kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alimwambia Maryam:

"Na akakuteua juu ya wanawake wa ulimwengu."

Aya hii imeleta kutofautiana kati ya wanavyuoni wa Kiislamu; kwamba je, Maryam binti

Imran ndiye bora zaidi au Fatima binti Muhammad?

Kundi katika wanavyuoni wamesema kuwa wanawake bora ni wane Maryam binti Imran, Asiya binti Muzahim (mke wa Firaun), Khadija bint Khuwaylid na Fatima bint Muhammad. Hadith hii imetajwa katika Sahih sita; pia nimeiona katika Tafsir tabari, Razi, Bahrul-muhit, Ruheil-bayan, Maraghi na Al-Manar.

Wengine wamesema Maryam ndiye bora kutokana na Aya hii. Mashia na baadhi ya Masheikh wa Kisunni wamesema kwamba Fatima ni bora zaidi. Mwenye Tafsir Bahrul-muhit, wakati alipofasiri Aya hii: Alisema:

"Baadhi ya Masheikh wetu wamesema: Yale ambayo wameyasema wanavyuoni waki-wanukuu masheikh wao ni kwamba Fatima ni bora wa wanawake waliotangulia na watakao-fuatia; kwa sababu yeye ni sehemu ya Mtume."

Wale wanaosema Fatima ni bora, wametolea dalili hilo kutokana na Hadith Mutawatir zili-zopokewa kutoka kwa baba yake akisema: "Fatima ni sehemu yangu, atakayemkasirisha ndio amenikasirisha mimi." Ama kauli yake Mwenyezi Mungu kuhusu Maryam: "Na akakuteua juu ya wanawake wa ulimwenguni," makusudio yake ni wanawake wa ulimwenguni wa wakati wake si wakati wote. Ibara hii ni maarufu na imezoeleka; kama kusema: "Fulani ndiye mshairi hodari zaidi ya watu wote." Hapo anakusudiwa kuwa ni mshairi zaidi kwa wakati alioko au kwa watu wake tu. Mifano ya hilo katika Qur'an ni mingi, kama vile kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema kuhusu wana wa Israil:

"Na tukawafadhilisha juu ya walimwengu." (45:16)

Hakuna hata mmoja aliyehitalifiana na wenzake kuwa makusudio ya Aya hii ni walimwengu

wa wakati wao. Au kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

"Na Ismail na Al-Yasan na Yunus na Lut na wote tumewafadhilisha juu ya walimwengu."

(6:86)

Hakuna yeyote anayesema kuwa Lut ni bora kuliko Isa au kwamba ni sawa, au kuwa Ismail ni bora kuliko babake. Aya nyingine ni ile isemayo:

"Hakika mimi nimekuta mwanamke anawatawala; naye amepewa kila kitu..." (27:23) Yaani kila kitu kwa wakati wake.

Turudie kwenye wanawake wane ambao imepokewa Hadith kwamba wao ni wanawake bora. Tukiwaangalia bila ya kutilia maanani Hadith na Aya tutaona kwamba kila mmoja katika wao ana ubora wake kwa upande wake kuliko wengine.

Asiya mke wa Firauni alimwamini Mungu kwa Ikhlas akimtegemea Yeye peke Yake kuwa ndiye muhifadhi wake, wakati huo akiwa katika nyumba ya mtu mwovu zaidi kuliko yeyote, aliye kiongozi wa ukafiri na ulahidi. Akadhihirisha imani yake, hali ya kuupinga ukafiri na ufisadi wa Firaun na kupinga dhulma na utaghuti wake.

103 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Firaun akamlaza ardhini kwa kumpigilia vigingi mpaka akafa akiwa shahidi wa haki na imani. Karama hii hawakuwa nayo wanawake wengine watatu.

Bibi Maryam karama yake ni kumzaa Bwana Masih bila ya baba. Karama hii hakuwa nayo mwanamke yeyote duniani.

Bibi Khadija yeye ni wa kwanza kumwamini na kumsadiki Mtume wa Mwenyezi Mungu; akaswali yeye na Ali pamoja na Mtume (s.a.w.) - Swala ya kwanza katika uislam. Ndiye yeye aliyejitolea mali yake kwa ajili ya kuinusuru dini hii. Hivyo kwa mali yake na himaya ya Abu Twalib uislamu ulisimama na kuimarika. Karama hii nayo hakuwa nayo mwanamke yeyote ulimwenguni.

Ama Fatima yeye ni sehemu ya Mtume, vilevile ni nafsi yake kwa umbo, tabia na taqwa; linamridhisha Mtume lile analoliridhia yeye na linamuudhi lile linalomuudhi yeye. Yeye ni mama wa Hassan na Hussein mabwana wa vijana wa peponi. Na, ni mke wa bwana wa mbingu na ardhi baada ya Mtume. Karama hii nayo hakuwa nayo Khadija (mamake) wala Asiya au Maryam.

Ama kutofautisha ubora katika karama hizi, ni kama kujaribu kutofautisha ubora kati ya waridi na asmini au kati ya mahurulain wawili. Lakini inatosha kwa Fatima awe na jambo moja tu kutokana na baba yake, ambaye ni bora ya Mitume. Katika Sahih Bukhari Juz.5 mlango wa sifa za ukoo wa Mtume, kuna Hadith ya Mtume isemayo: "Fatima ni bibi (mkuu) wa watu wa peponi."

Ikiwa Fatima ni sehemu ya Mtume, basi mumewe Ali ni nafsi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Nafsi zetu" (3:61).

MAELEZO.

Utafiti huu unaungana na utafiti uliotangulia katika Tafsir ya Aya 36 ya Sura hii kifungu "Fatima na Maryam."

45.Waliposema Malaika: Ewe Maryam! Hakika            Mwenyezi            Mungu

anakubashiria neno litokalo kwake; jina lake ni Masih mwana wa Maryam; mwenye heshima duniani na akhera na ni miongoni mwa waliokurubish-wa.

46.Na atasema na watu katika uchanga na katika utu uzima na atakuwa miongoni mwa watu wema.

Kaashif3-78.jpgKaashif3-79.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

47.Akasema: "Mola wangu! Nitakuwaje na mtoto na hali hajanigusa mtu yey-ote?" Akasema: Ndivyo hivyo, Mwenyezi Mungu huumba anavyota-ka anapohukumu jambo, huliambi-a'kuwa'likawa.

48.Na atamfundisha kuandika na hekima na Tawrat na Injili.

49.Na Mtume kwa wana wa Israil. Mimi nimewajia na Ishara kutoka kwa Mola wenu, hakika mimi nitawafanyia kama namna ya ndege katika udongo; kisha nimpulizie awe ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na niwaponye vipo-fu na wenye mbalanga. Niwafufue wafu kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na niwaambie mnavyovila na mtakavyoweka akiba. Hakika katika haya ipo ishara kwenu mkiwa ni wenye kuamini.

Kaashif3-80.jpg

105 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

50.Na msadikishaji wa yale yaliyokuwa kabla yangu katika Tawrat, na ili niwa-halalishie baadhi ya mliyoharamishi-wana nimewajia na ishara kutoka kwa Mola wenu, kwa hiyo mcheni Mwenyezi Mungu na mtiini.

Kaashif3-81.jpg

51.Hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na ni Mola wenu basi mwabuduni. Hii ndiyo njia iliyony-ooka

MARYAM MUNGU AKUBASHIRIA Aya 45 - 51.

LUGHA.

Mwenye Tafsir Bahrul-muhit amenukuu kauli saba kuhusu sababu za kuitwa Masih (mpaka-ji au mpangusaji): Kupaka baraka, kupaka dini wakati wa kuzaliwa, kutwaharika na dhambi na kupanguswa na mbawa za Jibril.

Vile vile kupakwa uzuri, kupangusa uchafu kwa sababu mama yake alikuwa hatoki hedhi wala hakuchafuka na damu ya nifasi.

LISILOWEZEKANA KIAKILI NA KIDESTURI

Jambo lisilowezekana ni lile ambalo halikufanyika wala haiwezekani kufanyika siku za baadae. Nalo liko namna mbili: Kwanza ni kutowezekana kufanyika hilo lenyewe kidhati na kiakili, kwamba akili haikubali kuwezekana kutokea kwa namna yoyote; kama kuwa pamoja mambo mawili yaliyo kinyume: Mfano kuwa mtu ni mumin na wakati huo huo ni kafiri; au kipofu awe anaona na wakati huo huo awe kipofu, au bubu na msemaji wakati huo huo. Kwa hiyo jambo hilo litakuwa haliwezekani kiakili na kikawaida.

Namna ya pili: Ni kutozuilika kuwepo kwake kidhati na akili, bali inawezekana kwa namna fulani, lakini kwa kawaida halitokei. Mifano yake ni mingi sana, Qur'an tukufu imetaja matukio mengi sana; kama vile kukaa Ibrahim katika moto bila ya madhara yoyote kugeu-ka nyoka fimbo ya Musa, kusimama maji ya bahari kama milima, kuyeyuka chuma kama mshumaa kwa ajili ya Daud, nabii Suleiman kujua matamshi ya ndege na kufufuliwa Uzair baada ya miaka mia.

Mfano mwengine ni wa Isa kuzaliwa bila ya baba, kuzungumza wakati wa kuzaliwa, kufu-fua wafu, kuwaponya vipofu na wenye mbalanga bila ya tiba yoyote na kuwaambia watu vile walivyokula na walivyoviweka akiba katika majumba yao bila ya kuviona; au kumwambia mtu matukio yote haya. Na yote haya na mengineyo ambayo yanawezekana kutokea, laki-

106

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

ni sio kikawaida. Lau kama ingekuwa muhali kutokea, basi yasingewezekana kutokea kwa Mitume na wasiokuwa Mitume. Kwa hiyo ikiwa matukio haya yanawezekana kutokea na tena wahyi ukayatolea habari kutokea kwake waziwazi, basi ni wajibu kwa kila mumin kuyakubali bila ya kusita.

Kundi la wanafalsafa na wafasiri wametaja njia nyengine za kuumbwa Isa bila ya tone la manii ya baba, lakini waliyoyasema hayana msingi wowote. Ilivyo hasa ni kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ni muweza wa kila kitu, anafanya kitu kiweko kwa neno 'Kun' (kuwa) kutokana na kitu ambacho hakikuwepo. Na hekima yake ilipitisha ililotaka, basi limekuwa alilolitaka.

Sisi hatuna ulazima wa kujua kiini cha matukio aliyoyaleta Mwenyezi Mungu yasiyo ya kawaida; wala kujua vipi yametokea. Huenda akili zetu zikawa zinashindwa kujua kama zilivyoshindwa kujua hakika ya roho ambayo ni katika amri ya Mola.

Ndio! Tunaloweza kufahamu ni athari zake na natija zake, lakini sio kiini chake na hakika yake. Kwa hiyo Aya zinazomhusu Masih (a.s.) na zinazofanana nazo zinazohusu mambo mengine, tutazifasiri kwa misingi hii.

MAANA

Waliposema Malaika: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria neno litokalo kwake; jina lake ni Masih Isa mwana wa Maryam.

Makusudio ya Malaika hapa ni Jibril kutokana na kauli Yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: Na tukampelekea Roho wetu, akajifananisha kwake sawa na mtu (19:17) Ambapo makusudio ya Roho hapo ni Jibril. Amemtaja kwa tamko la wengi kwa sababu yeye ndiye kiongozi wa Malaika. Neno litokalo Kwake ni kusema Kwake "Kun fayakun" (kuwa ikawa)

Mwenye heshima duniani na akhera na ni miongoni mwa waliokurubishwa.

Heshima yake duniani, ni kufanywa mtakatifu na kuadhimishwa na watu mpaka siku ya ufu-fuo. Ama heshima yake huko akhera, ni utukufu wa daraja yake kesho kwa Mungu.

Na atasema na watu katika uchanga na katika utu uzima na atakuwa miongoni mwa watu wema.

Kusema katika uchanga ni kwa ajili ya kumtakasa mama yake na walivyomsingizia mayahu-di kuwa alitembea na Yusuf Seremala; Mungu awalaani! manaswara wamedai kuwa hakusema uchangani.

Ibn Abbas anasema: "Maneno ya Isa yalikuwa muda mchache na sio zaidi ya yaliyoelezwa katika Qur'an; kisha hakusema mpaka alipofikia makamo ya kusema, kama walivyo watoto wengine. Kauli hii inasaidiwa na mazingatio . Kwa sababu lengo la kuzungumza kwake ni kumwepusha mama yake na tuhuma na wasiwasi wa watu; na lengo likapatikana kwa aliy-oyasema.

Na katika utu-uzima.Yaani atawazungumzia watu Wahyi akiwa ni mtu mzima Huu ni muujiza mwengine wa kufahamisha Utume wake. Kwa sababu, hilo ni kulitolea habari jambo la ghaibu kwamba yeye ataishi mpaka marika ya utu-uzima. Inasemekana kuwa aliishi duniani miaka thelathini. Na, inasemekana kwamba aliletewa wahyi akiwa na umri wa miaka thelathini. Na akaishi miaka mitatu baadaye.

Akasena: "Mola wangu! Nitakuwaje na mtoto na hali hajanigusa mtu yeyote?"

107

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Swali hili ni la kutukuza uwezo wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Kwa sababu ni jambo lisilo la kawaida, hakuna wajihi wowote wa waliyoyaeleza baadhi ya wafasiri kwamba yeye ali-uliza kuwa je, atazaa kwa ndoa? Hakuna wajihi wa swali hili kwa sababu jibu lake Mwenyezi Mungu Mtukufu: Akasema: "Ndivyo hivyo; Mwenyezi Mungu huumba anavyotaka, anapohukumu jambo, huliambia 'kuwa' likawa." Linafahamisha kuwa yeye Maryam alikuwa akijua kwamba yeye atazaa bila ya kuingiliwa.

Na atamfundisha kuandika na hekima na Tawrat na Injili

Maana ya neno 'kitab' (katika lugha ya kiarabu) ni masdar ya kuandika, lakini mara nyingi linatumiwa kwa maana ya kitabu. Makusudio yake hapa, ni maana yake halisi (kuandika), kwa sababu kutajwa Tawrat na injil baada yake, kunatilia nguvu kuchukulia maana ya kuandika: Wengine wamesema maana yake ni kitabu na kwamba kutajwa Tawrat na Injil baada yake ni kutilia umuhimu tu; kama ilivyo katika kauli Yake Mwenyezi Mungu: Angalieni sana Swala na ile Swala ya katikati (2:238)

Hekima, ni kuliweka jambo mahali pake. Na Tawrat na Injil, Aya hii ni dalili mkataa kuwa Tawrat ndio nguzo ya kwanza ya dini ya kinaswara na kwamba Injil ni endelezo la Tawrat na baadhi ya marekebisho; kama vile kuhalalisha baadhi ya yaliyoelezwa kuwa ni haram, kunakoelezwa na kauli yake Mwenyezi Mungu: "Na ili niwahalalishie baadhi ya yale mliy-oharamishiwa."

Na Mtume kwa wana wa Israil

Mwenyezi Mungu alimtuma Muhammad (s.a.w.w.) kwa watu wote kama inavyosema Aya: "Na hatukukutuma ila kwa watu wote mtoaji bishara na muonyaji. Lakini watu wengi hawa-jui." (34:28)

Ama Isa akiwa Mwisrail, yeye alitumwa kwa watu wake, kutokana na muktadha wa dhahiri ya Aya hii, kuufanya ujumbe wake kuwa ni kwa watu wote, kunahitaji dalili.

Hakika mimi nimewajia na ishara kutoka kwa Mola wenu.

Msemo huu unatoka kwa Isa kuwaambia watu wake Waisrail akiwatolea hoja ya ukweli wa utume wake, kwamba yeye anayo miujiza inayofahamisha kuwa ametumwa na Mwenyezi Mungu; kama anavyotaja miujiza yenyewe kwa kusema:

"... Hakika mimi nitawafanyia kama namna ya ndege katika udongo, kisha nimpulizie, awe ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na niwaponyeshe vipofu na wenye mbalanga na niwafufue wafu kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na niwaambie mnavy-ovila na mtakavyoweka akiba majumbani mwenu. Hakika katika haya ipo ishara kwenu mkiwa ni wenye kuamini."

Hii ni miujiza minne:

Wa kwanza: Ni kuleta uhai katika udongo na kufanya ndege.

Pili: Kuponya aliyezaliwa kipofu na mwenye mbalanga.

Inasemekana elimu ya tiba likuwa imeendelea sana katika wakati wa Isa (a.s), lakini pamo-

ja na kuendelea kwao, Madaktari mabingwa walishindwa na magonjwa haya mawili (upofu

na mbalanga) ndipo Mwenyezi Mungu akayapoza kupitia mkono wa Isa bila ya tiba yoyote,

ukiwa ni muujiza unaofahamisha utume wake.

Tatu: kumrudishia uhai maiti.

Nne: kuelezea mambo ya ghaibu kutokana na wanavyokula na wanavyoweka akiba.

108

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Si kazi yetu kufanya utafiti wa kujua siri ya miujiza hii, au vipi ameleta uhai na kuponya maradhi yasiyotibika bila ya dawa; na kama tuking'ang'ania kufanya utafiti wa hayo, basi tutaishia kwenye shub'ha na giza. Linalobaki kwetu ni kusalimu amri na kuitambua hekima ya Mwenyezi Mungu na amri Yake ambayo Bwana Masih (a.s.) ameieleza wazi wazi na kwa kuikariri, kuwa yeye ameifanya kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, ili aufunge mlango wa wanaofikiri umungu wa Isa.

Tumetangulia kueleza katika Tafsir ya 2:225 kwamba Mwenyezi Mungu anaupitisha utarat-ibu wa maumbile kwenye desturi ya kawaida ya kimaumbile; isipokuwa kama hekima Yake ikitaka kufanya vingine kwa matakwa Yake ya kuumba ambayo ni ibara ya 'kuwa'. Hapo tena hakuna nafasi ya desturi wala kawaida.

Ama Isa kuelezea mambo ya ghaibu, kulikuwa ni kwa kupitia wahyi, na wala hakuhusika nako yeye pekee, bali mitume wote walielezea mambo ya ghaibu. Nuh alitengeneza safina kabla ya tufani, Shuaib alitolea habari mwisho wa maisha ya watu wake, Muhammad (s.a.w.) alitoa habari ya kuwa warumi wata washinda wafursi na ushindi wa watu wake dhidi ya dola zote hizo mbili na Imam Ali naye alitolea habari mapinduzi ya Zenj na mengineyo, mpaka akaambiwa: "Amirul-mumin! Hakika umepewa elimu ya ghaibu." Akasema: "Siyo ilimu ya ghaibu, bali ni mafundisho kutoka kwa mwenye elimu." Akimaanisha Mtume (s.a.w.) ambaye naye ameichukua kutokana na Wahyi.

52.Alipohisi Isa ukafiri wao alisema: "Nani watakuwa wasaidizi wangu kwa Mwenyezi Mungu?" Wanafunzi wakasema: "Sisi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu. Tumemwamini Mwenyezi Mungu nawe shuhudia kuwa sisi ni Waislamu.

53."Mola wetu! Tumeyaamini uliyoy-ateremsha, na tumemfuata Mtume, basi tuandike pamoja na washuhu-diao."

54.Na wakapanga hila; na Mwenyezi Mungu akapanga hila; na Mwenyezi Mungu ndiye mbora wa kupanga hila.

Kaashif3-82.jpgKaashif3-83.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

NI NANI WASAIDIZI WANGU.

Aya 52 - 54.

HAKI NA MANUFAA.

Hakuna yeyote mwenye akili timamu anayeweza kuipinga haki na kuitanguliza batili, isipokuwa kwa tamaa ya nafsi, au kutatizika katika fahamu yake, au kutojua dalili, au dosari katika utoaji dalili.

Ni wazi kwamba dalili za manabii zimetosheleza kabisa kuthibitisha unabii wao katika pande zote, mpaka kufikia kuondoa makosa ya fikra na mikanganyo, kiasi ambacho hazibakishi dalili zao hoja yoyote ya kuipinga haki, isipokuwa inadi na kiburi.

Yeyote mwenye kutafuta sababu iliyowafanya wapinzani kuwafanyia vitimbi mitume na kupinga ujumbe wao - baada ya kuona dalili na miujiza- ataona ni sababu ya manufaa ya kibinafsi na kupupia mali na jaha. Ushahidi wa hakika hii kutoka katika vitabu vya Mwenyezi Mungu na Hadith za Mtume, hauna idadi. Miongoni mwa mifano hiyo ni: Mataghuti wapen-da anasa katika watu wa Nabii Hud, walipinga, si kwa lolote isipokuwa tu, aliwaambia:

Je, manajenga juu ya kila mwinuko ukumbusho wa upuuzi? Na mnajijengea majengo ya fahari ili mkae milele? Na mnaposhambulia, mnashambulia kwa jeuri (28:127-130)

Matajiri katika watu wa Nabii Shuaib walimtisha na kumwambia:

"Ewe Shuaib hivi Swala zako zinakuamrisha tuyaache waliyokuwa wakiyaabudu baba zetu au tuache kufanya tupendavyo katika mali zetu ... Lau si jamaa zako tungelikupiga mawe." (11: 87, 91)

Kosa lake tu, ni kuwa aliwaambia:

"Na enyi watu wangu! Timizeni kipimo na mizani kwa uadilifu wala msiwapunguzie watu vitu

vyao; wala msiwe waovu katika nchi mkafanya uharibifu" (11:85)

Qarun alikuwa tajiri sana katika watu wa Musa na ni mtu aliye karibu zaidi naye kiudugu, lakini pamoja na hayo alimfanyia uadui alipompa waadhi huu "Na ufanye wema kama alivyokufanyia wema Mwenyezi Mungu wala usitafute kufanya ufisadi katika nchi; hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wafisadi."                                (28:77)

Abdalla bin Ubayya alikuwa ni katika viongozi na matajiri wa Madina. Mtume alipohamia huko, alipatwa na wivu; akamwambia Mtume maneno ya kutokubaliana naye. Sa'ad bin Ubada akamwambia Mtume: "Usiyatilie maanani maneno yake; kwani sisi tulikuwa tunata-

ka kumpa Ufalme, naye anaona kuwa wewe umemnyang'anya."*9

Yatosha kuwa ni dalili ya hakika hii, kauli yake Mwenyezi Mungu:

"Kila alipowajia Mtume na lile ambalo nafsi zao halilipendi, wengine waliwakadhibisha na

wengine wakawaua." (5:70)

Walimkadhibisha Bwana Masih (Yesu) na kujaribu kumuua, kwa sababu yeye aliwapa mwito wa mapenzi, uadilifu, usawa na kutolimbikiza dhahabu na huku wengine wana njaa na mahitaji. Miongoni mwa mafunzo yake ni: "Msilimbikize mali ardhini. Tajiri kuingia mlan-go wa mbinguni ni kama kamba nene kuingia kwenye tundu ya sindano."

*9Katika kufasiri Aya 61 ya Sura hii, tutaeleza vile ujumbe wa Najran ulivyoamini utume wa Muhammad, lakini wakakataa kukiri kwa sababu ya malipo wanayoyapata kutoka kwa mfalme.

Kaashif3-84.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

MAANA

Isa alipohisi ukafiri wao.

Kabla ya kuzaliwa nabii Isa, mayahudi walikuwa wakiamini Masih atakayekuja. Alipowajia na hoja na miujiza, walitofautiana; wakamwamini maskini na wanyonge ambao hawakuhofia kupoteza mali wala jaha, lakini matajiri na wenye jaha walimkanusha kwa kuhofia vyeo vyao na chumo lao; kama ilivyo kwa yeyote anayekuja kutengeza; awe mtume au si mtume, hata kama watamjua kuwa ni mkweli mwenye haki.

Baadhi ya wafasiri wamekosea waliposema kuwa Mayahudi walimkataa Muhammad kwa vile ni Mwarabu wa kizazi cha Ismail, na kwamba kama angekuwa ni myahudi wa kizazi cha Is-haq (a.s.) basi wangelimkubali! Mbona Isa alikuwa myahudi, lakini pamoja na hayo walimpiga vita na kujaribu kumuua na kutaka kumsulubu. Vilevile Muhammad waliompiga vita ni Mamwinyi wa Kiquraish. Siri ya hapa na huko ni moja tu, kupigania dunia na manu-faa na wala sio ubaguzi wa kikabila.

Vyovyote, itakavyokuwa, ni kwamba Isa alihisi watu wake waking'ang'ania ukafiri kwa inadi, na akapata tabu kutoka kwao; kama alivyopata tabu Muhammad (s.a.w.w.) kutoka kwa watu wake; ndipo Isa aliposema:

"Ni nani watakuwa wasaidizi wangu kwa Mwenyezi Mungu", yaani ni kina nani hao na wako wapi waumini wa kuinusuru na kuihami dini ya Mwenyezi Mungu, na ambao wataen-deleza tabligh baada yangu? Kwani kila mwenye ujumbe hana budi kuwa na wasaidizi watakaomwamini na kumwakilisha kwa watu.

Wanafunzi wakasema: "Sisi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu, tumemwamini Mwenyezi Mungu nawe shuhudia kuwa sisi ni Waislamu. Mola wetu! Tumeamini uliy-oyateremsha na tumemfuata Mtume, basi tuandike pamoja na wanaoshuhudia."

Kusema sisi ni waislamu ni dalili kwamba dini ya Mwenyezi Mungu ni moja tu tangu mwan-zo hadi mwisho wa kikomo. Dini yenyewe ni uislamu ndiyo waliyokuja nayo mitume wote. Tofauti iko kwenye baadhi ya hukumu na sura ya ibada tu. Kwa hivyo basi, kila anayemwamini Mwenyezi Mungu, Vitabu Vyake na Mitume Yake, basi huyo ni mwislam, hata kama atajiita mkristo au yahudi. Ufafanuzi wa hilo umetangulia katika kufasiri Aya 19 ya Sura hii.

Kauli ya wanafunzi: "Tuandike pamoja na wanaoshuhudia." Ni dua yao kumwomba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) awajaalie katika fungu la waumini walioshuhudia umoja wa Mungu na kuwa na uaminifu, ili wafuzu yale waliyofuzu wenye ikhlasi wenye kuridhiwa; na wapate karama kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.).

Katika tafsir nyingi imeelezwa kuwa wanafunzi walikuwa kumi na wawili. Baadhi ya wafasiri wametaja majina yao na kazi zao. Lakin sisi tunanyamaza kutokana na Hadith isemayo. "Nyamazeni aliyoyanyamazia Mwenyezi Mungu."

MWENYEZI MUNGU NI MBORA WA WAFANYA HILA

Na wakapanga hila; na Mwenyezi Mungu akapanga hila; na Mwenyezi Mungu ni mbora wa wapanga hila.

Kuna Aya nyingi nyingine zinazofanana na Aya hii, kama zifuatazo:

Na wanapanga hila; na Mwenyezi Mungu anapanga hila; na Mwenyezi Mungu ni mbora wa wapanga hila. (8:30.).

111

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Na wakapanga hila na sisi tukapanga hila, na hali hawatambui . (27:50).

Sema: Mwenyezi Mungu ni mwepesi zaidi wa kupanga hila, hakika wajumbe wetu wanaandika hila mnazozipanga (10:21).

Makusudio ya hila kwa makafiri na wanafiki, ni vitimbi, hadaa, hiyana na kupanga njama. Ama hila ya Mwenyezi Mungu, makusudio yake ni kuzitangua hila na njama za wenye hila; kama ilivyosema Aya:

"Na hila mbaya hazimpati ila yule aliyezifanya." (35:43).

Katika Qur'an kuna sifa nyingi sana alizosifiwa Mwenyezi Mungu ambazo kwa dhahiri

zinaonekana kuwa hafai kusifiwa nazo mfano:

Mwenye shukrani, Mumin, Mwingi wa toba na Mwenye kiburi. Lakini ukiyafikiri vizuri maana

yake, utayaona yako mahali pake.

Maana ya Mwenye shukrani ni kwamba yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anawalipa thawabu wenye kushukuru na watiifu. Mumin maana yake yeye ndio chimbuko la amani na salama. Mwingi wa toba, ni kwamba yeye anakubali toba za wenye kutubia. Na mwenye kiburi ni kwamba kila kilichomo ulimwenguni ni duni kwake yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Kwa maana hayo, inatubainikia kuwa hila ni haramu ikiwa itakusudiwa kumdhuru mwengine; na itakuwa halali ikiwa itakusudiwa kujikinga na madhara ya mtu binafsi au mwengine.

Hebu tutaje mifano miwili ya kubatilisha hila za Makfiri na vitimbi vyao:

. Mayahudi walipanga hila ya kumuua Isa (as), lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akaipan-gua njama yao, pale alipomfananisha Yahudha na Isa, yule myahudi aliyehimiza kuuliwa Isa, na akampaza Isa mbinguni.

. Maquraish kwa pamoja walipanga kummaliza Muhammad, kwa kumchagua kijana kuto-ka kila ukoo, wampige kwa panga zao akiwa amelala na damu yake iwe kwa wote. Lakini Mwenyezi Mungu akapangua hila zao, pale alipomwamuru kutoka Makka na Ali alale kitandani pake ili watu wafikirie kuwa Muhammad hajasafiri, walipovamia nyumba wakamkuta Ali ndiye aliyelalala kitandani .

55.Aliposema Mwenyezi Mungu: "Ewe Isa! Mimi nitakufisha. Na nikuinue kwangu, na nitakutakasa na wale waliokufuru, na nitawaweka wale waliokufuata, juu ya wale waliokufuru, mpaka siku ya kiyama. Kisha marejeo yenu yatakuwa kwangu, nitahukumu baina yenu katika yale mliyokuwa mkihitalifania.

Kaashif3-85.jpgKaashif3-86.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

56.Ama wale waliokufuru, nitawaadhibu adhabu kali katika dunia na Akhera, na hawana wa kuwanusuru.

57.Na wale walioamini na wakatenda matendo mema, atawalipa ujira wao. Na Mwenyezi Mungu hawapendi wenye kudhulumu.

Kaashif3-87.jpg

58.Haya tunayokusomea ni katika Ishara na mawaidha yenye hekima.

KUONDOKA ULIMWENGUNI

Aya 55 - 58

KUTOFAUTIANA KUHUSU ISA

Watu wametofautiana sana kuhusu nabii Isa. Wametofautiana kuhusu kupatikana kwake, tabia yake na hata kufa kwake; Kuna wanaosema kuwa hakuweko kamwe, na kwamba habari zake ni vigano tu, kauli hii ilijitokeza mnamo karne ya kumi na tisa (19) huko Ujerumani, Ufaransa na Uingereza. Ni kauli ya kipumbavu kabisa; kwani ni sawa na kuse-ma kuwa hakuna ukristo wala uislamu unaomwamini Isa. Wengine wamesema ni Mungu, wengine wakasema ni binadamu. mayahudi nao wakasema kuhusu Isa na mama yake mambo ambayo yanaweza kuitingisha hata Arsh.

Ama waislamu wametofautiana kama ifuatavyo: Wengi wamesema hakufa na kwamba yeye yuko hai kimwili na kiroho mbinguni au mahali pengine popote; na atatoka duniani wakati wa mwisho mwisho wa dunia. Kisha hapo ndipo Mwenyezi Mungu atamuua maua-ji ya kihakika. Waislamu wengine wamesema kuwa yeye amekwisha kufa mauti ya kiuhaki-ka na kwamba iliyopazwa ni roho yake tu, sio mwili.

Tofauti hii ya Waislamu imetokana na kutofautiana dhahiri ya Aya; kama ifuatavyo:

"... Na hawakumuuwa wala hawakumsulubu, lakini alifananishwa kwao. Na kwa hakika wale waliohitilafiana katika hayo wamo katika shaka nayo, hawana ujuzi nayo isipokuwa

113

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

kufuata dhana tu; na hawakumuuwa kwa yakini. Bali Mwenyezi Mungu alimnyanyua kwake na Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu na mwenye hekima." (4: 157 - 158).

Dhahiri Aya hii kwa kuongezea Hadith za Mtume, zinayonyesha kuwa nabii Isa yuko hai. Lakini Aya nyengine inayosema:

Uliponifisha wewe ukawa mchungaji juu yao ..." (5:117) pamoja na Aya hii tuliyonayo.

Maana yanayokuja haraka ni mauti. Na, maana ya dhahiri ni kuwa mimi nitakufisha na kukujaalia mahali patukufu kama ilivyo kuhusu Idris:

"Na tulimwinua daraja ya juu kabisa." (19:57).

Au kama ilivyo kuhusu mashahidi: Wala usidhani wale waliouliwa katika njia ya Mwenyezi Mungu kuwa ni wafu, bali wao wahai, wanaruzukiwa kwa Mola wao" (3:169)

Wale wanaosema kuwa Isa yuko hai kiroho na kimwili, wameleta taawili kuwa neno tawaf-faytani na Mutawaffika (kufisha) kwa njia nyingi zenye nguvu zaidi ni ile inayosema makusu-dio ni kufananishwa na mauti, si mauti ya kihakika. Kwa sababu anapopaazwa mbinguni anakuwa hana mfungamano tena na dunia; kwa hiyo anakuwa kama maiti.

Ama wale waliosema kuwa amekufa kiuhakika wameleta taawili ya neno Hawakumuua kwamba mayahudi hawakuua msingi wa Isa na mafundisho yake kwa sababu ya kumuua na kumsulubu. Lakini waliletewa mawazo tu, ya kuwa wameyamaliza mafunzo yake lakini bado yamesimama tu na yatabakia mpaka siku ya ufufuo.

Sisi tuko pamoja na kauli ya kwanza; kwamba Isa yuko hai, Mwenyezi Mungu alimwinua kwake baada ya kumkamilishia maisha yake duniani kwa namna isiyokuwa ya mauti. Tuko kwenye rai hii kwa kuangalia dhahiri ya Aya na yaliyopokewa kutoka kwa Sunni na Shia kwamba yeye bado yuko hai.

Lakini pamoja na hayo yote, sisi hatuoni faida yoyote ya kuhakikisha na kuangalia kwa undani kuhusu maudhui haya. Kwa sababu kuamini namna ya kubainika uhai wake hapa duniani, na kuinuliwa kwake si misingi ya dini wala misingi ya madhehebu. Pia si katika matawi yake, isipokuwa ni maudhui ya nje yasiyofungamana na maisha yetu si kwa karibu wala mbali. Mwenyezi Mungu kesho kamwe hatauliza watu kwamba Isa alikufa vipi, au vipi alivyoinuliwa. Tunachopaswa kuamini ni kuwa Isa ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, naye ameumbwa kwa neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu, na kwamba mama yake ni mtakatifu.

Zaidi ya hayo utafiti wa maudhui haya hauishii kwenye yakini ya kujua aina ya kwisha maisha ya Isa au kuinuliwa kwake. Kwa hiyo lililo bora ni kumwachia Mwenyezi Mungu (s.w.t.)."*10

Aliposema Mwenyezi Mungu: Ewe Isa! Mimi nitakufisha na nikuinue kwangu.

Baada ya mayahudi kung'ang'ania kutaka kumwua Isa na kupanga njama. Mwenyezi Mungu alimpa bishara ya kumwokoa na kuvunjilia mbali vitimbi vyao na kwamba atamkamil-isha muda wake kwa njia ya kawaida; atamgurisha kwenye ulimwengu mwengine ambako hatapata adha ya mtu yeyote na wala hakuna utawala wa yeyote ispokuwa Mwenyezi Mungu, hayo ndiyo maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

Tutaelezea zaidi katika tafsir ya 4:158.

Kaashif3-88.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Nitakutakasa na wale waliokufuru.

Yaani nitakuweka mbali na uchafu wao na utangamano wao mchafu na shari wanayoku-

takia.

Na nitawaweka wale waliokufuata juu ya wale waliokufuru mpaka siku ya kiyama.

Makusudio ya kuwa juu hapa ni kwa kinafsi na kiukamilifu na wala sio kifalme na kimali. Hapana mwenye kutia shaka kwamba wale waliomwamini Isa ni bora kuliko waliomkad-hibisha.

Kisha marejeo yenu ni kwangu niwahukumu katika yale mliyokuwa mkihitalifiana.

Hapa hapahitaji tafsir, kwani maana yaliyo dhahiri ndiyo yaliyokusudiwa. Zaidi ya hayo ni kwamba dhamir inaenea kwa wote waliohitalifiana kuhusu Bwana Masih katika sifa zake kila mahali na kila wakati.

Ama wale waliokufuru, nitawaadhibu adhabu kali katika dunia na akhera na hawana wa kuwanusuru.

Adhabu ya akhera inajulikana. Ama adhabu ya duniani ni kwamba yeye (kafiri) ni tofauti na mwislam katika vipengele vingi vya sharia, kama vile kufaa kumsengenya kafiri, au kuwa kafiri anauliwa akimuua mwislam, lakini mwislam hauliwi kwa kumuua kafiri, bali hana hata fidia - kama walivyosema mafakihi wengi - isipokuwa akiwa dhimii; lakini fidia ya dhimii

inatofautiana na ya mwislam kwa tofauti kubwa*11.

Na ama wale walioamini na wakatenda matendo mema, atawalipa ujira wao; Na Mwenyezi Mungu hawapendi wenye kudhulumu,

Katika Hadith imeelezwa kuwa dhalimu na mwenye kuridhia dhulma ni sawa. Imam Baqir (a.s.) anasema: "Dhulma ni aina tatu: dhulma anayoisamehe Mwenyezi Mungu, dhulma asiyoisamehe Mwenyezi Mungu, na dhulma asiyoiacha Mwenyezi Mungu. Ama dhulma anayoisamehe ni ile ya kujidhulumu mtu mwenyewe kati yake na Mola wake. Dhulma asiyoisamehe ni ile ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu, Ama dhulma asiyoiacha ni kuwadhulu-mu waja." Imam Ali (a.s.) anasema: "Kumdhulumu mnyonge ndio dhulma mbaya kabisa."

Haya tunayokusomea ni katika ishara na mawaidha yenye hekima.

Haya ni ishara ya yale ambayo Mwenyezi Mungu amemwelezea Mtume wake kuhusu habari za mamake Maryam, Maryam mwenyewe na Zakariya. Vilevile Yahya, Isa, wana-funzi, wayahudi na wapinzani.

Maana yake ni kuwa tumekusomea ewe Muhammad habari hii ili iwe hoja na dalili kwa yule unayejadiliana naye kuhusu Isa n.k. Ama kuwa habari hizi ni hoja ya Muhammad, ni kwamba yeye hajui kusoma wala hakuna mtu anayemwambia hayo. Kwa hiyo inabaki kuwa kujua kwake habari hizi ni kwa njia ya wahyi tu kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Makusudio ya mawaidha yenye hekima ni Qur'an.

*11Dhimmi ni kafiri anayeishi kwa amani na Waislam.

115

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

59.Hakika mfano wa Isa kwa Mwenyezi Mungu, ni kama mfano wa Adam; alimuumba kutokana na udongo, kisha akamwambia kuwa akawa.

60.Ni haki kutoka kwa Mola wako, basi usiwe miongoni mwa wenye shaka.

61.Na watakao kuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wana wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.

62.Hakika haya ni maelezo ya kweli, na hapana mola isipokuwa Mwenyezi Mungu Na hakika Mwenyezi Mungu ndiye mwenye nguvu mwenye heki-ma.

63.Na wakikataa, basi hakika Mwenyezi Mungu anawajua waharibifu.

Kaashif3-89.jpgKaashif3-90.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

MFANO WA ISA NI KAMA WA ADAM Aya 59 - 63.

MAANA

Hakika mfano wa Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam; alimuumba kutokana na udongo, kisha akamwambia kuwa akawa.

Wafasiri wanasema kuwa ujumbe wa Najran (Yemeni) ulimwambia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.w.t.): "Kwa nini unamshtumu sahibu wetu ?" (yaani Isa)

Akasema: "Vipi?"

Wakasema: "Wewe unasema kuwa yeye ni mja."

Akasema: "Ndiyo yeye ni mja wa Mwenyezi Mungu, na ni Mtume wake na ni tamko lake alilompelekea bikira Maryam."

Wakamuuliza: "Je, umekwishaona mtu asiyekuwa na baba?"

Ndipo ikashuka Aya: "Hakika mfano wa Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam"

Ikiwa riwaya hii ni sahih au si sahihi, lakini haya ndiyo maudhui ya Aya hii hasa. Kwa sababu wakristo walikuwa, na bado, wanaendelea kutoa hoja ya itikadi yao kuwa Isa ni Mungu, kwa vile amezaliwa bila ya baba. Lakini Mwenyezi Mungu ameivunja hoja yao hii kwa Adam; Ikiwa Isa ni mungu au mwana wa Mungu, kwa sababu ya kuzaliwa bila ya baba, basi Adam ndiye anayefaa zaidi kuwa Mungu, kwa sababu yeye amezaliwa bila baba wala mama. Hawakuijibu hoja hii, na wala hawatajibu mpaka siku ya mwisho.

Unaweza kuuliza kuwa inavyoonyesha kauli Yake Mwenyezi Mungu Mtukufu alimuumba kwa udongo ni kwamba Mwenyezi Mungu alimtengeneza Adam kwa ukamilifu; kwa maana ya kuwa kuumba kulitangulia kauli ya "Kun fayakun", kwa hiyo kulikuwa hakuna haja tena ya kauli hii kwa sababu maana yake ni kuumba kilichoumbwa; na maneno ya Mwenyezi Mungu hayafai kuwa hivyo.

Jibu: Mungu alimuumba Adam kwa vipindi; miongoni mwa vipindi hivyo ni kwamba yeye alimuumba kwa udongo, kisha akatia roho. Kwa hiyo maana yanakuwa: "Ewe udongo! Kuwa mtu aliye na nyama, damu, hisia na utambuzi."

MITUME NA MAASI

Ni haki kutoka kwa Mola wako ...

Yaani haya tuliyokuteremshia na kukufahamisha kuhusu Isa ni haki kutoka kwa Mola wako.

Basi usiwe miongoni mwa wenye shaka.

Unaweza kuuliza kuwa ni muhali Mtume kutilia shaka aliyoyatolea habari Mwenyezi Mungu. Kwa sababu shaka inapingana na imani, sikwambii isma. Sasa makatazo haya ni ya nini?

Wafasiri wamelijibu swali hili kwa majibu mawili: Kwanza: kwamba dhahiri inonyesha kuwa msemo unaelekezwa kwa Mtume, lakini makusudio ni wengine.

Pili: makusudio ni kuendelea Mtume na yakini.

Kaashif3-91.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Njia zote mbili inabidi kuziangalia vizuri kwa sababu zinamaanisha kuwa haifai kwa Mwenyezi Mungu kuwakataza maasi mitume Yake. Ilivyo hasa ni kwamba Mwenyezi Mungu anaweza kuwakataza mitume maasi kwa vile kwanza hiyo ni amri ya mkubwa kwa mdogo.

Pili: Isma si maumbile na tabia ya mitume mpaka iwe ni muhali kuweko uwezekano wa kufanya maasi. Kama ni hivyo basi wasingekuwa na ubora wowote. Wao wanaweza kufanya maasi, lakini hawafanyi maasi.

Kwa hiyo basi inafaa kwa Mwenyezi Mungu kuwapa makatazo, lakini makatazo yawe yana-toka Kwake Mwenyezi Mungu tu, sio kwa mtu mwengine. Kwa sababu hakuna aliye zaidi ya Mtume isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu tu.

Makatazo mengi yaliyokuja katika Qur'an yanachukuliwa kwa njia hii. Mfano kauli Yake Mwenyezi Mungu kumwambia kipenzi Chake Muhammad (s.a.w.w): "Wala usiwatii makafiri." (33:48).

Hatujui pengine wenyewe Mitume, walikuwa wakipenda makatazo haya kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.), bali pengine walikuwa wakiyataka hasa; kama vile Mumin mwema anavyotaka kupata mawaidha na kukumbushwa Mungu kutoka kwa mjuzi.

MUBAHALA

Na watakaokuhoji baada ya kukufikilia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake wetu na wanawake wenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.

Hii ndiyo Aya inayojulikana kwa jina la Aya ya Mubahala (maapizano), nayo ni miongoni mwa Aya zilizo msingi wa kitabu.

Kusudio la kwanza la Aya hii Tukufu ni kuimarisha dini na kuuthibitisha ujumbe wa Muhammad kwa njia ambayo elimu na wanavyuoni hawakuizoweya, na ambayo haiwezi yeyote isipokuwa Muumbaji wa ardhi na mbingu. Lakini ni njia ambayo inafahamika kiwepesi kwa mtu yeyote, awe mjuzi au si mjuzi. Kisa chenyewe kwa ufupi ni kama ifu-atavyo:

Aya hii inafungamana na mwaka wa tisa tangu Mtume kuhamia Madina. Mwaka huo uliju-likana kwa jina la mwaka wa ugeni. Kwa sababu Mtume alipata wageni kutoka sehemu mbali mbali za Bara arabu kuja kutangaza utii wao kwake, baada ya Mwenyezi Mungu kuli-inua neno la kiislamu na kuwapa ushindi waislam dhidi ya maadui zao.

Miongoni mwa ugeni alioupata Mtume, ulikuwa ni ujumbe wa watu sitini, wakristo kutoka Najran, Yemen. Inasemekana mlikuwa na wakubwa wao kumi na nne; akiwemo mkubwa wao na kiongozi wao, Abdul-Masih, mshauri wao, Ahyab akiwa na lakabu ya Sayyid na Askofu ambaye alitukuzwa sana na mfalme wa Roma, alimjengea kanisa na chuo na kumpatia mali na mshahara.

Mtume akawapokea kwa takrima. Ulipofika wakati wao wa kuswali, waligonga kengele na wakaswali katika Msikiti wa Mtume kuelekea Mashariki. Masahaba walipotaka kuwazuiya Mtume aliwakataza kwa kusema: "Waacheni."

Baada ya kutulia wageni hao, wakaanza kujadiliana na Mtume wa Mwenyezi Mungu kuhusu Isa wakidai kuwa yeye ni Mungu mara nyingine yeye ni mtoto wa Mungu na mara yeye ni watatu katika watatu. Wakaleta dalili ambazo tumekwisha zitaja na jinsi zilivyobatilishwa.

Kaashif3-92.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Aliyezibatilisha dalili za wakristo ni Mwenyezi Mungu mwenyewe, lakini kupitia kwenye ulimi wa Mtume (s.a.w.). Na, katika ugeni huo mlikuwa na maulama ambao ukweli hauwezi kuji-ficha kwao; kama vile Abu Haritha ambaye alikuwa kiongozi wa dini wa msafara. Yeye alikuwa na ndugu anayeitwa Kurzi. Abu Haritha baada ya kusikia aliyoyasikia kutokana na hoja za Mwenyezi Mungu zilizo wazi, alimwambia ndugu yake kwa siri kwamba Muhammad ndiye yule Mtume tuliyekuwa tukimngojea Nduguye akamwambia: "Sasa wangoja nini nawe una yakini na ukweli wake?"

Akamwambia: "Unajua, wafalme wametupa mali nyingi na wametutukuza sana, lau tukimwamini Muhammad watatuyang'anya kila kitu. Likamwingia moyoni hilo na akalificha; kisha akasilimu na kulisimulia ."

Ukweli wa riwaya hii hauhitaji dalili, kwa sababu hiyo yenyewe inafahamisha ukweli wake, na kiasi chake kinachukuliwa pamoja na riwaya hii; kama wanavyosema watu wa mantiki.

Watu wengi waliokanusha haki na kuipinga, walifanya hivyo kwa sababu ya masilahi yao ya kibinafsi kama tulivyoelezea kwa ufafanuzi katika Aya ya 54 ya Sura hii.

Mtume aliujadili ujumbe wa Najran kuhusu Isa, na akajadiliana nao kwa hoja yenye kubatil-isha uwongo na mantiki ya kisawasawa yasiyokubali kuongezewa chochote. Walipong'ang'ania upinzani, Mtume aliukata mjadala na kuwataka kufanya jambo jengine lisilofanana na mjadala, lakini litakalomaliza ugomvi mara moja na kumaliza ubishi wote. Aliwataka neno moja tu, ambalo hawezi kulikataa ila yule anayejijua kuwa ni mwongo. Tamko lenyewe ni 'Laana ya Mwenyezi Mungu iwe kwa waongo." Lakini tamko lenyewe litaambatana na muujiza ambapo utapanda ukelele kwenye kichwa cha mwongo na aone dunia yote ni moto.

Zimekuja Hadith Mutawatir katika vitabu vya Hadith na Tafsir, kama vile Sahih Muslim na Tirmidhi, Tafsir Tabari, Razi, Bahrul-Muhit, Gharaibul-Qur'an, Rawhul-Bayan, Al-Manar, Maraghib na nyenginezo nyingi. Hadith hizo zinaeleza kuwa, Mtume alitoka akiwa amem-beba Husein na kumshika mkono Hasan; Fatima na Ali wakimfuata nyuma akiwaambia nitakapoomba nyinyi itikieni amin.

Kiongozi wa kidini wa msafara akawaambia wenzake: "Enyi Manasara! Mimi ninaona nyuso ambazo, lau zitaomba jabali liondoke lilipo basi linaweza kuondoka. Kwa hiyo msiapizane nao msije mkaangamia" Kisha akasema: "Ewe Abul-Kassim tumeonelea tusiapizane na wewe." Akawaambia: "Basi silimuni," wakakataa; kisha wakasuluhishana watoe kodi.

Msafara ukarudi mikono mitupu, ukiwa umeshindwa na kufedheheka. Baada ya tukio hili, walisilimu wengi na kuwazidishia waumini imani na uthabiti.

Muhammad (s.a.w.w.) aliwaleta vipenzi vyake kwenye Mubahala akiwa na hakika ya ushin-di, kama kwamba uko mikononi mwake. Hakuna kitu kilichofahamisha uwazi na ukweli juu ya hoja ya utume wake kuliko tendo hili. Ni dalili iliyo wazi zaidi kuliko dalili ya mwangaza wa jua kuwa jua lipo. Sijui kama muujiza huu alikuwa nao Mtume mwengine yeyote. Ingawaje walikuwa wakiwaombea makafiri na kuitikiwa maombi yao.

Unaweza kuuliza: Mtume aliwataka baadhi ya makafiri waamini; waliposema: "Ewe Mwenyezi Mungu! Kama haya ni haki itokayo kwako, basi tupige kwa mvua ya mawe kuto-ka mbinguni au tuletee adhabu yoyote iumizayo."(8:32).

Lakini pamoja na hayo haikuwatukia adhabu hiyo.

Jibu: Mazungumzo tuliyo nayo yanahusu maapizano, ambayo yanathibiti kwenye maho-jiano na madai tu; vilevile hayajuzu ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu au mjumbe wake

Kaashif3-93.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

kuhofia kutojitokeza ukweli wa mkweli. Ama kauli ya makafiri (Tupige mvua ya mawe kuto-ka mbinguni) hayo ya mvua ya mawe si katika maapizano. Kwa hivyo, Mwenyezi Mungu ameahirisha adhabu yao mpaka siku ya kufufuliwa.

AHLUL BAIT

Katika aliyoyasema Razi kuhusu tafsir ya Aya ya Mubahala ni: "Imepokewa kuwa Muhammad (s.a.w.) alipotoka akiwa katika kitambaa cheusi, alikuja Hassan (r.a) akamwingiza, akaja Hussein (r.a.) akamwingiza, kisha Fatima, kisha Ali (r.a..). Mtume akasema: "Hakika Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu Ahlul bait watu wa nyumba ya Mtume na kuwatakasa kabisa kabisa." (33:33)

Anaendelea kusema Razi

Jua kwamba riwaya hii - kama wailivyoafikiana usahihi wake watu wa tafsir na Hadith -

inafahamisha kuwa Hassan na Hussein walikuwa watoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu,

kwa sababu aliahidi kuwaita watoto akawaita, Hassan na Hussein (a.s), kwa hivyo hilo lime-

wajibisha kuwa ni watoto wake.

Linalotilia mkazo hili ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

"Na katika kizazi chake Daud na Suleiman... na Zakariya na Yahya na Isa....." (6: 84-85)

Inavyojulikana ni kwamba Isa ananasibishwa kwa Ibrahim kwa upande wa mama, sio wa baba.

Nimefanya utafiti mrefu wa maudhui haya katika kitab Fadhail Imam Ali (fadhila za Imam Ali) na nikaweka mlango maalum wa 'watoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu.'

Hakika haya ni maelezo ya kweli, na hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu; na hakika Mwenyezi Mungu ndiye mwenye nguvu mwenye hekima. Na wakikataa, basi hakika Mwenyezi Mungu anawajua waharibifu.

maneno haya ni ishara ya yaliyotangulia kuhusu Isa na kwamba yeye ni Mtume, wala si mtoto wa zina (wa haramu) kama wanavyodai mayahudi; wala pia siyo Mungu au mwana wa Mungu, kama wanavyodai wakristo. Asiyeamini uhakika huu basi achana naye ewe Muhammad, kwa sababu Mwenyezi Mungu anajua mfisadi na mpotevu na ana uwezo wa kumwadhibu.

64.Sema: "Enyi watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno la usawa baina yetu na baina yenu. Kwamba tusimwabudu yo yote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala baadhi yetu wasiwafanye baadhi kuwa waungu zaidi ya Mwenyezi Mungu Wakikataa, semeni: "Shuhudieni ya kuwa sisi ni waisla-mu,

Kaashif3-94.jpgKaashif3-95.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

65.Enyi watu wa Kitabu! kwanini mnabishana juu ya Ibrahimu, na hali Tawrati na Injili havikuteremshwa ila baada yake? Basi, hamfahamu?

66.Je, nyinyi ni wale mnaojadiliana katika lile mlilolijua. Mbona (sasa) mnabishana katika lile msilolijua? Na Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye, nyinyi hamjui (kitu).

67.Ibrahimu hakuwa myahudi wala mnaswara (mkristo), lakini alikuwa mwenye kuachana na dini potofu, na kushikamana na haki; wala hakuwa katika washirikina.

68.Hakika watu wanaomkurubia zaidi Ibrahimu ni wale waliomfuata, na Mtume huyu na walioamini pamoja naye Na Mwenyezi Mungu ndiye Mlinzi wa waumini.

NJOONI KWENYE NENO LA USAWA Aya 64 - 68

MAANA

"Sema enyi watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno la usawa baina yetu na baina yenu. Kwamba tusimwabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu wala tusimshirikishe na cho-chote, wala baadhi yetu wasiwafanye baadhi kuwa ni miungu, zaidi ya Mwenyezi Mungu."

Kaashif3-96.jpg

121

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Mayahudi, wanaamini Tawrat, Wakristo wanaamini Tawrat na Injil, na waislam wanaamini Tawrat, Injil na Qur'an. Vitabu vyote hivi vitatu kwa pamoja vinakubali kuwa kuna mwenye kuutengeneza ulimwengu mwenye hekima, lakini wakristo wameingia ndani sana, wakam-fanya Mungu kuwa na washirika, wakamnasibishia mtoto na wakawafanya maaskofu wao ni miungu wanaowahalalishia na kuwaaharamishia. Imepokewa Riwaya kuwa Adiy bin Hatim alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu: "Hakika Mwenyezi Mungu anasema katika kitabu chake kitukufu:

"Wamewafanya makasisi wao na watawa wao kuwa ni waungu badala ya Mwenyezi Mungu." (9:31). Lakini wakristo hawawaabudu wanavyuoni na watawa." Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: "Kwani si walikuwa wakiwahalalishia na kuwa-haramishia, na nyinyi munakubali maneno yao?"

"Ndiyo." Adiyo akajibu.

Mtume akaongeza: "Basi ndio hivyo."

Bado tukiwa katika karne ya ishirini tunasoma magazetini kwamba fulani amekutana na Baba (Mtakatifu) na akambariki. Vilevile makadinali na maaskofu wakuu, hutoa baraka. Ama Waislamu, wao wanaitakidi kwamba baraka haiwezi wala haitakuwa ila kutoka kwa Mwenyezi Mungu: Rehema ya Mwenyezi Mungu na baraka zake ziko juu yenu." (11:73)

Ama Mayahudi, walimkana Isa (a.s.) na wakajaribu kumsulubu, wakamkana Muhammad

(s.a.w.w.) wakiwa wanajua ukweli wake.

Mwenyezi Mungu anasema:

"Lakini yalipowajia yale waliyokuwa wakiyajua waliyakanusha. Basi laana ya Mwenyezi

Mungu iko juu ya makafiri" (2:89)

Mtume alijadiliana na watu wa Kitabu kwa mjadala mzuri, na akawapa aina kadhaa za dalili zilizowanyamazisha, lakini bado waling'ang'ania ukafiri. Kisha akawaita kwenye maapizano, lakini wao wakaona bora watoe kodi kwa unyonge, kuliko kuikubali haki. Pamoja na yote hayo alijitahidi ili waamini; kama ilivyo kawaida yake na kila mpinzani mpaka Mwenyezi Mungu akamwambia: "Na wengi katika watu hawatakuwa wenye kuamini hata ukijitahidi vipi." (12:103)

"Hata ukiwa na jitihada ya kuwaongoza, lakini Mwenyezi Mungu hamuongozi yule anayepoteza." (16:37)

Kwa kutilia mkazo hoja kwa wapinzani na kuwadhihirishia hakika mbele ya Mtume na watu wote, ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia kuwa aachane na kujadiliana nao na kuapizana nao,na afuatane nao na njia hii ambayo anaishuhudia kila mwenye akili kuwa ni haki na uadilifu, bali ni njia ya wazi.

Njia yenyewe ni kuwaita kwenye lile linalokubaliwa na akili na vitabu vya dini kuwa nyote mlingane sawa katika kumwabudu Mwenyezi Mungu pekee asiye na mshirika; na wala wengine wasiwaabudu wengine. Pia baadhi ya watu wasiwe juu ya wengine. Na hili ndilo neno la uadilifu.

Wakikataa semeni: "Shuhudieni kuwa sisi ni Waislamu."

Yaani kama hawakukubali hata dhahiri hii na kuwa na inadi ya ushirikina, basi achana nao, na wewe pamoja na wale waliokuamini waambieni, sisi ni Waislamu.

Kuwashuhudisha makafiri kuhusu uislamu wa waislam, kuna faida mbili:

Kwanza: Kuwatambulisha makafiri kwamba wao hawawajali na ukafiri wao na kwamba

Muhammad na walio pamoja naye wanaiamini haki na kuitumia hata kama watakufuru watu

122 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

wa Mashariki na Magharibi.

Pili: Kuonyesha kuwa waislamu wanatofautiana na wengine kwa kumwabudu Mwenyezi Mungu mmoja pekee, wala hawafanyi baadhi kuwa waungu kinyume na Mwenyezi Mungu, au kuweko na yeyote mwenye mamlaka ya kuhalalisha, kuharamisha na kufuta madhambi; kama ilivyo kwa wasiokuwa waislamu.

Enyi watu wa Kitab! Kwa nini mnabishana juu ya Ibrahim, na hali Tawrat na Injil havikuteremshwa ila baada yake? Basi hamfahamu?

Qur'an imewajadili watu wa Kitabu kwa akili na mantiki, kwenye maapizano na kwenye neno la usawa - ambalo ni kumwamini Mungu peke yake. Kisha ikarudia tena mjadala na watu wa Kitabu; kama kawaida yake kulieleza jambo, halafu kueleza jengine hatimaye kulirudia lile la kwanza. Imerudia kuelezea kauli za watu wa Kitab na ubatilifu wake. Imetaja kauli ya mayahudi kwamba Ibrahim alikuwa myahudi na kauli ya manaswara kwamba Ibrahimu alikuwa mnaswara.

Qur'an Imejibu madai haya waziwazi, kuwa uyahudi ulitokea baada ya Musa, na baina ya Musa na Ibrahim kulikuwa na miaka elfu mbili. Unaswara nao ulizuka baada ya Isa na baina ya Isa na Ibrahim kuna miaka elfu; kama ilivyoelezwa katika Tafsir Rawhul bayan basi itakuwaje aliyetangulia awe katika dini ya aliyekuja nyuma? Basi hamfahamu?

Kauli ya wayahudi na wanaswara inatukumbusha kichekesho kimoja wanachokisimulia walebanon : Kwamba watu wawili walikuwa wakisafiri pamoja. Walipokuwa wakizungumza mmoja akamuuliza mwenzake:

."Umewahi kuhiji Makka Tukufu?"

."Ndio, nimetekeleza Al-hamdulillah"

." Umeona Zamzam huko?"

."Ndio, ni msichana mzuri sana!"

." Vipi wewe, si msichana! Ni kisima cha maji bwana!

." Ah! Basi wamekichimba baada ya kuhiji mimi."

Hekaya za madhehebu na vikundi vilivyozuka baada ya Mtume Mtukufu (s.a.w.w.) zinafanana kidogo na hoja za mtu huyo. Kila anayechukua dini yake kutoka kwa mtu yeye huwa ni aina hii isipokua kama itamthibitikia nukuu kutoka kwa Mtume Mtukufu (s.a.w.w.) kama vile kuthibiti Hadith Thaqalayni ambayo imewajibisha kufanya ibada kwa kitabu cha Mwenyezi Mungu na Ahlul Bait wa Mtume. Na ikavifanya sawa viwili hivyo . Tumeyafafanua hayo katika tafsir ya (2:39).

Je, nyinyi ni wale mliojadiliana katika lile ambalo mnalolijua. Mbona (sasa) mnabishana katika lile msilolijua na Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye na nyinyi hamjui ( kitu).

Mtu anaweza akahusika kujua jambo fulani au maudhui fulani. Hapo anaweza kujadiliana na kubishana; na wala sio lazima awe yuko sawa katika maneno yake na mjadala wake wote, isipokuwa la muhimu ni kuwa awe anajua japo kwa ujumla. Ama kujadiliana na kubishana katika jambo asilolijua kabisa, basi ni ujinga na upumbavu.

Watu wa Kitab wana dini yao wanayoitakidi; kwa hiyo kuna uwezekano wa kufanya mjadala unaohusiana na dini zao ijapokuwa kwa dhahiri lakini kufanya mjadala kuhusu dini ya Ibrahim hakuna njia yoyote hata kwa dhahiri, kwa sababu wao hawajui chochote.

123 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

-Ibrahim hakuwa myahudi wala mnaswara (mkristo) lakini alikuwa mwenye kuachana na dini potofu, na kushikamana haki, mwislamu wala hakuwa katika washirikina.

Hakuwa myahudi kwa sababu, baina yake na Musa kulikuwa miaka elfu, wala itikadi yake haiambatani na dini ya kiyahudi, kwa sababu imegeuzwa sio ile aliyokuja nayo Musa (a.s.). Wala hakuwa mkristo, kwa sababu baina yake na Isa ilipita miaka elfu mbili wala itikadi yake haiambatani na itikadi ya dini ya kimasihi, kwa sababu imegeuzwa, siyo aliyokuja nayo Isa (a.s.).

Ikiwa Ibrahim hakuwa mwislamu kwa maana iliyozoeleka, lakini alivyo yeye alikuwa mwislamu na imani yake inaambatana na imani ya uislamu. Kwa sababu, alikuwa akimwamini Mwenyezi Mungu na kumtakasa na shirk na kufananisha. Na huu ndiyo msingi wa asili ya dini ya Kiislam. Kwa hiyo, linabainika jibu la swali la atakayeuliza: Kwa nini Ibrahim ni mwislamu na Qur'an imeteremshwa baada yake? Umetangulia ufafanuzi kwamba Mitume wote walikuwa waislamu katika tafsir ya Aya ya 19 ya Sura hii.

Ama kauli yake Mwenyezi Mungu Hakuwa katika washirikina, ni kuwapinga wanaswara waliosema kuwa Masih ni mtoto wa Mungu wayahudi waliosema na Uzair ni mtoto wa Mungu na waarabu waliokuwa wakiabudu masanamu, vikundi vyote hivi vitatu vilijihusisha na Ibrahim.

Hakika watu wanaomkurubia zaidi Ibrahim ni wale waliomfuata Mtume huyu na walioamini pamoja naye.

Yaani wenye haki ya kujinasibisha na dini ya Ibrahim ni wale walioitikia mwito wake au wale ambao itikadi yao inaambatana na yake; kama Muhammad na walio pamoja naye. Imamu Ali anasema: "Hakika watu walio karibu zaidi na manabii ni wale wanaojua zaidi waliyoku-ja nayo, kisha akasoma Aya hii akaendelea kusema: "Hakika mpenzi wa Muhamamd ni yule anayemtii hata kama yuko mbali naye kiudugu; na hakika adui wa Muhammad ni yule anayemwasi Mwenyezi Mungu, hata kama akiwa karibu naye Muhammad kiudugu."

Na Mwenyezi Mungu ni Mlinzi wa waumini, wale wanaomwamini Yeye bila ya kuwa na mshirika; na wala hawamtegemei yeyote kwa kuondolewa madhara na kutaka manu-faa.

Hakuna kitu kinachofahamisha utukufu wa Imam Ali (a.s), ikhlasi yake, na kuepukana kwake na malengo ya kidunia, kuliko kauli hii na kuacha kujiambatanisha na udugu ingawa-je anajua kuwa yeye ndiye mtu wa karibu zaidi na Mtume kwa udugu. Yeye anategemea utukufu kutokana na nafsi yake na amali yake tu, na wala sio kutafuta asili na udugu au kwa kufunika mambo.

69.Kikundi katika watu wa Kitabu wanapenda kuwapoteza; wala hawapotezi ila nafsi zao, na hali hawatambui.

Kaashif3-97.jpg

124

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Kaashif3-98.jpg

70.Enyi watu wa Kitabu! Mbona mnazikataa Ishara za Mwenyezi Mungu na, hali nyinyi mnashuhudia?

71.Enyi watu wa Kitabu! Mbona mnaichanganya haki na batili, na mnaficha haki na hali mnajua?

WANAJIPOTEZA WENYEWE Aya ya 69 - 71

UISLAMU NI DINI YENYE NGUVU.

Kikundi katika watu wa Kitabu wanapenda kuwapoteza, wala hawapotezi ila nafsi zao na hali hawatambui.

Makusudio ya kikundi katika watu wa Kitab ni viongozi wa dini zao. Aya hii inaam-batana kabisa na wahubiri wa kikiristo. Wao wanafanya kadiri wawezavyo wawaingize waislamu kwenye ukristo. Wakishindwa basi wanajaribu kuwapoteza na kuwatia shaka kubwa katika uislamu, ili wabakie bila dini. Kwa kufanya hivyo wanajifanyia ubaya wao wenyewe bila ya kutambua. Kwa sababu kuudhoofisha uislamu,. kama dini inayoelekeza kuweko Mwenyezi Mungu mpangaji mwenye hekima, kunamaanisha kushindwa dini zote na viongozi wake walio na fikra hiyo waki-wemo wakristo. Hii ndiyo tafsir ya hawapotezi ila nafsi zo na hali hawatambui.

Sijui ni kwa nini wafasiri hawayazingatii maana haya pamoja na uwazi wake, ambapo wamesema kuwa makusudio ya watu wa Kitab kujipoteza wao wenyewe, ni adhabu yao kesho kwa sababu ya kujaribu kuwapoteza waislam. Ama Sheik Muhammad Abdu na Razi, wamefasiri kujipoteza wao kuwa ni jaribu lao la kuwapoteza waislam bila kufanikiwa, kwamba hakuna mwislamu yeyote aliyekubali au kudanganyika na upotofu wao. Lakini usahihi hasa ni tulioueleza. Kudhoofisha uislamu ni kudhoofisha dini zote na watu wake.

Vyovyote ilivyo uislamu pamoja na misingi yake una nguvu kiasi ambacho si rahisi kutingishwa na ukristo au na dini nyingine. Waabudu masanamu , milima na watu wa Kitabu wameingia kwa makundi katika uislamu kwa radhi yao na kukinai, wakiwemo wanavyuoni wao wakubwa. Sijui kama kuna Mwislamu wa kikweli kweli aliyeujua uislamu kiuhakika, ambaye ameuacha Uislamu.

Mwandishi wa kifaransa Henry Descarte anasema katika kitabu chake" Al-Islam sawani wa khawatwir," kifungu cha Uislamu Algeria anasema, ninamnukuu: "Tumeshuhudia Uislam ukionyesha nguvu zake na uhai wake kwa kupata waabudu mizimu wengi katika Afrika na

125 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

kuwafanya ni jeshi moja chini ya bendera ya Qur'an na hakuna katika watu Waislamu anayeweza kwenda kwenye dini nyingine."

Kwa mnasaba wa haya tunaleta kisa hiki kizuri cha kuvutia: Katika kumi la atatu la karne ya 20 kundi la wahubiri wa kikristo lilikwenda mji wa Amara ulioko Iraq ambao wakazi wake wote ni waislamu Shia. Jamaa hao walikwenda kwa lengo la kuwageuza wawe wakristo. Wakaanzisha mashule, na Zahanati, wakafanya matangazo na kuweka hafla wakamwaga mapesa. Mhubiri wao kila alipopanda jukwaani na kuelezea miujiza ya Yesu, Waislamu walikuwa wakipaza sauti" Salawatullah ala Muhammad wa Ali bayt Muhammad" (Rehema za Mwenyezi Mungu zimshukie Muhammad na watu wa nyumba ya Muhammad). Lilipokaririka hilo, walikata tama. Mapesa, shule, zahanati hazikulea manufaa yoyote kwao, wakarudi mikono mitupu.

Enyi watu wa Kitabu! Mbona mnazikataa ishara za Mwenyezi Mungu na hali nyinyi mnashuhudia?

Makusudio ya Ishara za Mwenyezi Mungu hapa ni dalili za utume wa Muhammad s.a.w.w ukweli wa Qur'an na utukufu wa mafunzo ya kiislamu.

Enyi watu wa Kitab Mbona mnachanganya haki na batili na mnaficha haki na hali mnajua.

Makusudio ya haki hapa ni yale yaliyowabainikia watu wa Kitabu kuhusu ukweli wa uislamu na nabii wake. baadhi ya watu wa kitabu walikuwa na bado wako wanaojaribu kuupaka matope uislamu na waislamu, wakimnasibisha Mtume pamoja na Qur'an uwongo na uzushi, kwa mfano wanadai kuwa Muhamamd anawalingania watu wamwabudu yeye kwa sanamu ya dhahabu, kwamba Muhammad alikuwa akipiga ngoma na nzumari na kwamba

yeye ana ugonjwa wa kupagawa n.k. Yote ni chuki na kutojiamini. *12

Dkt Zakiy Najib anasema katika kitabu chake Ayam fi Amrika kwamba yeye alipokuwa Amerika alihudhuria tamthilia iliyojaa dharau na kebehi kwa Quran na Uislam. Hiyo ndiyo nchi iliyoendelea ambayo inadai kuwa inabeba nembo ya dini na huku inatupa makombo-ra kwa wanyonge kwa madai ya kupiga vita ulahidi.

*12Upuuzi huu na mwingine uko katika utangulizi wa Kitab cha Decastre akiunukuu kutoka kwa watunzi wengi wa Magharib waliouweka kwa njia ya kupaka matope Uislamu; kisha akaupinga na kuujibu kwa nguvu za hoja. Amesema kweli Mwenyezi Mungu. "Na katika watu wa kitabu yuko ambaye ukimwamini na mrundo wa mali atakurudisha na yuko ambaye ukimpa amana ya dinar moja hakurudishii"

126

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

72.Kikundi katika watu wa kitabu kilise-ma: Yaami nini yale waliyoteremshi-wa wale walioamini mwanzo wa mchana na yakataeni mwisho wake, huenda wakarudi nyuma.

73.Wala msimwamini ila yule anayefuata dini yenu. Sema hakika uongozi hasa ni uongozi wa Mwenyezi Mungu. Kuwa atapewa yeyote mfano wa mliy-opewa nyinyi au wawahoji mbele ya Mola wenu. Sema hakika fadhila iko mikononi mwa Mwenyezi Mungu, humpa amtakaye na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa, Mjuzi.

Kaashif3-99.jpg

74.Humhusisha husisha na rehema yake amtakaye.Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye fadhila kubwa.

KUAMINI ASUBUHI NA KUKUFURU JIONI

Aya 72-74. MAANA

Kikundi katika watu wa Kitabu kilisema: Yaaminini yale waliyoteremshiwa wale walioamini, mwanzo wa mchana na yakataeni mwisho wake, huenda wakarudi nyuma.

Yaani warudi nyuma Waislamu. Aya inaonesha hadaa na njama walizokuwa wakizifanya viongozi wa watu wa Kitabu. Wakidhihirisha uislamu Asubuhi na kurtadi jioni, ili angalau waweze kuzitia shaka baadhi ya nafsi dhaifu za waislamu, ziseme kuwa lau si kuwa wame-ona Muhammad si mkweli wasingelitoka katika uislamu baada ya kusilimu.

127

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Unaweza kuuliza; je, waliwahi kufanya hila zao hizi walizozipanga, au ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alimpa habari Mtume wake na kuwafedhehesha kabla ya kuzitekeleza?

Jibu: Inavyofahamisha Aya ni kwamba wao walisema. Ama kuwa walifanya baada ya kuse-ma au hawakufanya; hayo yamenyamaziwa na Aya. Na, sisi vilevile tunayanyamazia yale aliyoyanyamazia Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo basi hakuna wajihi wowote wa waliyoy-aeleza baadhi ya wafasiri kwamba wao waliswali Swala ya asubuhi pamoja na Mtume kisha wakarejea jioni na kuswali sala yao ili watu waone kuwa wao wameona upotevu, isipokuwa kama ni riwaya sahihi.

Wala msimwamini ila yule anayefuata dini yenu.

Baadhi wameifahamu vibaya Aya hii na kuitolea ushahidi kuwa ni katika maneno ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) na kwamba eti sio maneno ya mayahudi, bali hata nimemsikia mtu zaidi ya mmoja akisema Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alikusudia kwa Aya hii kuwa tusimwamini yeyote isipokuwa aliye kwenye dini yetu.

Ilivyo hasa ni kwamba Aya hii ni sehemu ya maneno ya wapinzani wenye vitimbi katika watu wa Kitabu. Mwenyezi Mungu ameyanukuu kwa kuwasimulia wao; yaani baadhi ya watu wa Kitabu waliwaambia wengine: "Silimuni mchana na mkufuru jioni." Vilevile wakasema: "Wala msimwamini ila yule anayefuata dini yenu."

Sema hakika uongozi hasa ni uongozi wa Mwenyezi Mungu.

Jumla hii imeingia kati, aliyoambiwa Mtume na Mwenyezi Mungu kabla ya kumalizika masimulizi. Makusudio yake ni kujibu jaribio la watu wa Kitab na hadaa yao ya kudhihirisha uislam, kisha kurtadi, ili kuzitia shaka baadhi ya nafsi dhaifu za wafuasi wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.). Kwamba hadaa hii haina lolote. Kwa sababu uislam hauwezi kuondolewa au kuyumbishwa na vitimbi na hadaa. Mwenyezi Mungu anasema: "Na ambaye ameongozwa na Mwenyezi Mungu hana wa kumpoteza" (39:37)

Kuwa atapewa yeyote mfano wa mliyopewa nyinyi au wawahoji mbele ya Mola wenu.

Huu ndio mwisho wa masimulizi ya watu wa Kitabu hapa. Kwa ufupi ni kuwa viongozi wa watu wa Kitabu walikuwa wakiitakidi kwamba inawezekana Mwenyezi Mungu kumpeleka Mtume asiyekuwa mwisrail; na kwamba haukusimama kwao tu. Lakini baada ya kuja Muhammad (s.a.w.) walidhihirisha hasadi na wivu, ati vitabu vyao na dini yao inawajibisha Mtume awe ni katika Bani Israil tu.

Walidhihirisha hayo wakiwa wanajua kuwa wao ni waongo tena wataaadhibiwa na kuhoji-wa kesho mbele ya Mwenyezi Mungu. Wakaogopa haya yasiwafikie waislamu wasije waka-pata nguvu. Kwa hiyo baadhi yao wakawaambia wengine: Tahadharini kusema mbele za waislam kwamba sisi watu wa Kitab tunaitakidi kuwa inawezekana kuletwa Mtume asiyekuwa mwisrail. Au kusema mbele ya waislam kuwa sisi tutahojiwa na kushindwa kesho kwa sababu ya kuficha kwetu haki na kuipinga.

Kwa maneno mengine ni kwamba watu wa Kitabu hasa mayahudi walijua kabisa kuwa wao wako katika upotevu kwa sababu ya kumkadhibisha kwao Muhammad (s.a.w.w.) na wakaogopa kuwafahamisha waislam hakika hii. Ndipo wakausiana kuficha upotevu wao na kuonyesha kuwa Mtume hawi na hatakuwa mwarabu.

Hii ndiyo tabia ya mayahudi tangu walipopatikana hadi leo na mpaka siku ya mwisho. Wanasema uongo huku wakijua kuwa wao ni waongo, wakijificha kwa kuleta mikanganyo. Lakini mara moja wanafedheheka. Wala Qur'an sio kitabu pekee kilichosajili makosa na

128

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

uchafu wao, bali vitabu vyote vya kidini hasa Injil, vitabu vya historia, magazeti na idhaa; zote hizo zimekariri historia yao mbaya. Hii ndiyo siri ya kuwekewa vikwazo na kuteswa na uma mbali mbali; kuanzia Fira'un hadi Hitler. Hakuna taifa lolote duniani kuanzia zamani hadi sasa lililoungana nao isipokuwa Amerika tu, "Kwa sababu kufanana na kitu kunavu-tiana".

Sema hakika fadhila iko mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Humpa amtakaye na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa, Mjuzi.

Wafasiri wanasema makusudio ya fadhila hapa ni kuhusishwa utume; na kwamba kuko mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Humchagua kumpa utume yule anayefaa, awe mwisrail au mwarabu; na kwamba Yeye Mwenyezi Mungu amekwishawajibu mayahudi waliotangaza kwamba Mungu hapeleki mtume isipokuwa kutokana na wao.

Haya ndiyo waliyoyasema wafasiri na wakatoa dalili kwamba mfumo wa Aya unafahamisha hilo. Kwa sababu uko katika mazungumzo ya watu wa Kitabu, madai yao ya uongo na hila zao.

Lakini tunavyoona sisi ni kuwa neno fadhila katika Aya linabaki katika ujumla wake; na kwamba linakusanya utume, hekima, uongofu, uislam na mengineyo. Linathibiti katika kujibu mayahudi; kama vile linavyothibiti kiujumla. Kwa sababu utume ni katika jumla ya mafungu ya fadhla.

75.Na katika watu wa Kitabu yuko ambaye ukimwamini na mrundo wa mali atakurudishia. Na katika wao yuko ambaye ukimpa amana ya dinari moja hakurudishii, isipokuwa ukimsi-mamia hayo ni kwa kuwa walisema: "Hatuna lawama kwa wasiojua kuso-ma" Na wanamzulia uwongo Mwenyezi Mungu, na hali wanajua.

76.Sivyo hivyo, bali anayetimiza ahadi na akamcha Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu huwapenda wacha Mungu

Kaashif3-100.jpgKaashif3-101.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

KUNA WAAMINIFU NA WAHAIN I KATIKA WATU WA KITABU. Aya 75 - 76

MAANA.

Na katika watu wa Kitabu yuko ambaye ukimwamini na mrundo wa mali atakurud-ishia katika wao. Na yuko ambaye ukimpa amana ya dinar moja hakurudishii.

Makusudio ni kwamba katika watu wa Kitabu kuna ambao wako katika upeo wa uaminifu, hata ukiwaamini na mali nyingi, basi watatekeleza amana. Na pia wako walio katika upeo wa hiyana hawaaminiki hata kwa dinar moja tu. Umetajwa uaminifu wa mali, kwa sababu ndiyo mtihani sahihi wa kujua ubovu na uzima wa moyo wa mtu.

HAKUNA MAISHA ILA KWA UKAKAMAVU WA KUTOJALI MAUTI Isipokuwa ukimsimamia.

Mwenye hiyana hutaka zaidi ya haki yake wala hatekelezi haki ya watu, kwa sababu ni maiti wa dhamiri. Wala hakuna njia ya kuipata haki kutoka kwake isipokuwa kwa kumsimamia, kama alivyosema mwenye hekima kubwa. Maana ya kumsimamia mwenye hiyana mnyang'anyi ni kumsonga na kugombana naye kwa silaha yoyote uliyo nayo. Walikwishasema wahenga: "Uhuru huchukuliwa, wala hautolewi."

Kumsonga mhaini ni faradhi ya lazima; vinginevyo ufisadi ungelienea duniani. Kosa la kun-yamaza mdhulumiwa, ni sawa na kosa la dhalimu. Kwa sababu wote wawili wanaandaa kueneza dhulma na ufisadi. Lau dhalimu angelijua kuwa mdhulumiwa ana hisia za kutojali kufa kugombea haki yake, basi asingelidhulumu.

Majaribio yametufahamisha kuwa hakuna haki katika Umoja wa mataifa wala Baraza la usalama isipokuwa kwa kutumia nguvu; na kwamba hakuna maisha katika karne ya ishirini hasa Mashariki ya kati na hasa hasa waarabu, isipokuwa kwa ukakamavu wa kutojali mauti.

Hayo ni kwa kuwa walisema: Hatuna lawama kwa wasiojua kusoma.

Maana yake ni kuwa watu wa Kitabu walijihalalisha mali za waarabu, kwa sababu wao wal-idai kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hatawaadhibu kwa unyang'anyi huo.*13

Ndipo Mwenyezi Mungu akawajibu uzushi wao, kwa kusema: Na wanamzulia Mwenyezi Mungu uwongo na hali wanajua. Hakuna mwenye shaka kwamba mwenye kumzulia Mwenyezi Mungu kwa kukusudia, hiyana yake ni kubwa na kosa lake ni ovu zaidi.

Unaweza kuuliza: Mataifa yote na watu wa dini zote, bali hata walahidi pia, kuna waamini-fu na wenye hiyana; wakweli na waongo. Kuna walahidi kadhaa walio wakweli na kutekeleza amana kuliko wanaofunga na kuswali. Sasa kuna wajihi gani wa kuwahusisha watu wa Kitabu na kifungu hiki?

*13 Sijui haya mataifa ya Ulaya yanayopora mali ya mataifa ya kiarabu yanatokana na kizazi kilichosema hivyo! Dinari aina ya pesa itumikayo Bara Arabu.

130

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Jibu: Kwanza, katika Aya Mwenyezi Mungu amesema kuwa baadhi ya watu wa Kitab wanataka kuwapoteza, akasema tena wanataka kuamini asubuhi na kukufuru jioni. Na katika aya hizi anabainisha kuwa kuna waaminifu na wahaini. Na hii haimaanishi hakuna wengine wasiokuwa hivyo.

Pili: Inawezekana tuadhanie watu wa Kitabu wote wana hiyana; ndipo Mwenyezi Mungu akaondoa tuhuma hii, kwamba wao ni kama vikundi vingine na watu wa dini nyingine.

Si hivyo, bali anayetimiza ahadi yake na akamcha Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu huwapenda wacha mungu.

Ni kuthibitisha yale waliyoyakana watu wa Kitabu waliposema: Hatuna lawama kwa wasio-jua kusoma na kwamba wao ni waongo katika madai haya.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuthibitisha njia ya mwenye kujihalalishia mali za watu, anaeleza kuwa mwenye kutekeleza ahadi na akaogopa yaliyoharamishwa, basi yeye ni mwenye kupendeza mbele ya Mwenyezi Mungu. Imepokewa Hadith, Mtume amesema: "Hakuna kitu kilichokuwa wakati wa ujahiliya isipokuwa kiko chini ya wayo wangu, isipokuwa amana; kwani hiyo inatekelezewa mwema na muovu".

Imam Zainul-abidin (a.s.) anasema: "Lau aliyemuua baba yangu Hussein ataniwekea amana upanga aliomuulia baba yangu, basi nitamtekelezea amana yake." Imam Jaffer Assadiq (a.s.) anasema: "Mambo matatu hayana udhuru kwa yeyote: Kutekeleza amana kwa mwema au muovu, kuwatendea wema wazazi wawili wema au waovu na kutekeleza ahadi na mwema au muovu." Kwa sababu hiyo ndipo mafakihi wa Shia Imamia wakaafikiana kuwa Kafiri akitangaza vita na waislam, ni halali damu yake lakini haijuzu kum-fanyia hiyana. Kwa mfano lau alikuwa ametoa mali yake kwa mwislam, ni lazima arudishe amana pamoja na kujua kuwa inajuzu kumuua na kuchukua mali yake, lakini sio ile aliyoi-weka amana.

77.Hakika wale wanaouza ahadi ya Mwenyezi Mungu na viapo vyao kwa thamani ndogo. Hao hawatakuwa na sehemu yoyote akhera, wala Mwenyezi Mungu hatasema nao wala hatawatazama siku ya Kiyama, wala hatawatakasa, nao watapata adhabu iumizayo.

ASIYE NA AHADI HANA DINI

Aya 77

MAANA

Arrazi anasema katika kufasiri Aya hii: "Yanaingia katika Aya hii yote aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu, yale aliyoyatolea hoja, yaliyochukuliwa kutoka upande wa Mtume na

Kaashif3-102.jpg

131

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

yanaingia yale yanayomlazimu mtu mwenyewe. Kwa sababu yote hayo ni katika ahadi ya Mwenyezi Mungu ambayo ni lazima kuitekeleza."

Katika Hadith imeelezwa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) hakuhutubia hotuba yoyote isipokuwa alisema: "Asiye kuwa na uaminifu hana imani na asiyekuwa na ahadi hana dini."

Aya hii na Hadith hii na nyinginezo zinatufahamishia kuwa Uislam unafungamana na tabia na maadili; ndipo ukawajibisha kutekeleza mambo yote ya lazima ya kuamiliana na wengine; na ukakuzingatia kuwa ni kuamiliana na Mwenyezi Mungu, hata kama ni kuamiliana na mlahidi kwa sharti ya kuwa muamala wenyewe usipingane na misingi ya kimaadili; vinginevyo kutakuwa ni batili hakufai.

Vilevile kwa upande wa hukumu, ambapo uislam umemwajibishia kadhi kusikiliza sauti ya dhamiri na hoja ya kitabia kabla ya kusikiliza kauli ya wanaogombana.

Nadharia ya tabia; ndio mkazo wa kwanza wa sharia za kiislamu kwa kawaida zake zote na hukmu zake. Kwa ajili hii Mwenyezi Mungu amewatishia wale wanaovunja ahadi na wasiokuwa na uaminifu kwa kitisho ambacho hakumtisha yeyote katika wafanyao mad-hambi makubwa; pale aliposema:

Hao hawatakuwa na sehemu yoyote akhera, wala Mwenyezi Mungu hatasema nao wala hatawatazama siku ya kiyama wala hatawatakasa, nao watapata adhabu iumiza-yo.

Ama siri ya kuhimiza huku na kutoa tisho kwa wasiotekeleza ahadi ni kuchunga maslahi ya watu, kuweko kutegemeana kati ya watu na kuchunga haki, mambo ambayo ndio msingi wa amani na nidhamu.

78.Na hakika miongoni mwao kuna kundi linalopinda ndimi zao kwa Kitabu ili mpate kuyadhani hayo kuwa ni ya Kitabu wala si ya Kitabu. Na wanase-ma: Haya yametoka kwa Mwenyezi Mungu, na hali hayakutoka kwa Mwenyezi Mungu; na wanasema uwongo juu ya Mwenyezi Mungu na hali wanajua

WANAPINDA NDIMI ZAO KWA KITABU Aya 78

Aya hii ni mwendelezo wa Aya 75. Makusudio ya kupinda ni kugeuza. Kuna Aya nyingi zina-zoelezea kugeuza kwao maneno ya Mwenyezi Mungu, "Miongoni mwa hizo ni: Mmekifanya kurasa mlizoonyesha baadhi na kuficha nyingi."(6:91)

"Baadhi yao walikuwa wakisikia maneno kisha wakiyabadili baada ya kuwa wameyafa-hamu." (2:75)

Mtu atakayeiona Tawrat yao, atakubali kuwa wamezua, ambapo Mwenyezi Mungu amena-

Kaashif3-103.jpg

132

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

sibishiwa kula na kupigana hata miereka; kama ambavyo mitume wamenasibishiwa ulevi, na kuzini na mabinti zao.

Kugeuza kunathibiti kwa kuongeza au kupunguza; kama kuzidisha katika maandishi au kupunguza. Vilevile kunathibiti kwa kugeuza irabu, kama kumfanya mtendaji kuwa ndiye mtendwa. Pia kugeuza kunaweza kuthibiti kwa tafsir; kwa kufasiri kiuhakika badala ya kimajazi; mfano mkono wa Mwenyezi Mungu badala ya uwezo wa Mwenyezi Mungu.

Wafasiri wametofautiana kuhusu aina ya mageuzi iliyokusudiwa katika Aya hii.Sheikh Muhammad Abduh amesema kuwa makusudio ya kugeuza hapa ni kugeuza tafsir na kuli-pa tamko maana yasiyokusudiwa; akatoa mfano wa hilo kwa neno liliosemwa na Masih (Baba yetu aliye mbinguni) akiwa na makusudio ya huruma na upole wa Mwenyezi Mungu kwa waja wake, lakini baadhi ya wakubwa wa kikristo wamefasiri kuwa Mwenyezi Mungu ni baba wa Isa (Yesu) kiuhakika.

Tunavyoona sisi katika tafsir ya Aya hii ni kwamba kikundi hicho cha watu wa kitabu kilikuwa kikipindua tamko lenyewe na kuzusha fikra nyingine na kuwafanya watu wafikirie kuwa ni kitabu cha Mwenyezi Mungu ili wawe na itikadi ya batili. Kwa hiyo, tamko la kwanza la Kitabu katika Aya ni kinachodaiwa kuwa ni kitabu; na tamko la pili na la tatu ni sifa ambayo. Kukadiri kwake ni wanapinda ndimi zao kwa kinachodaiwa kuwa ni Kitabu ambacho kimegeuzwa, ili nyinyi watu, mkifikirie kuwa kinatokana na Kitabu cha hakika cha asili, na wala sio Kitabu kamwe.

Ama kauli Yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: Na wanasema hayo yanatoka kwa Mwenyezi Mungu na wala hayatoki kwa Mwenyezi Mungu, ni kutilia mkazo kauli yake: na wala hay-atokani na kitabu. Imesemekana kuwa hayo ni kutilia mkazo upande wa kuunganisha ujum-la juu ya umahusus. Kwa sababu kitabu kinahusika na wahyi ulioteremshiwa Mtume. Ama yale yanayotoka kwa Mungu yanakuwa ni Hadith za Mtume na hukumu ya kiakili.

79.Haiwezekani kwa mtu aliyepewa na Mwenyezi Mungu Kitabu na hekima na Unabii, kisha awaambie watu: Kuweni wa kuniabudu mimi badala ya Mwenyezi Mungu. "Kuweni watumishi wa Mwenyeezi Mungu. Kwa kuwa mnafundisha Kitabu na kwa sababu mnakisoma.

80. Wal a hatawaamrisha kuwafanya Malaika na manabii kuwa waungu. Je, atawaamrisha ukafiri baada ya kuwa nyinyi waislamu?

Kaashif3-104.jpgKaashif3-105.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

KUWENI WATUMISHI WA MUNGU

Aya 79 - 80 MAANA

Haiwezekani kwa mtu aliyepewa na Mwenyezi Mungu Kitabu na hekima na Unabii kisha awaambie watu: Kuweni wa kuniabudu mimi badala ya Mwenyezi Mungu.

Hapana mwenye shaka kwamba haiwezekani kwa mtu kupewa kitabu, hukumu na utume kuwaambia watu wamwabudu, kwa sababu hiyo ni kufuru na Mwenyezi Mungu hawachagui makafiri. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: "Na hakika tumewachagua kwa ujuzi juu ya walimwengu wote" (44:32)

Aya hii Tukufu ni jibu la wale wanaowawekea mitume na mawali baadhi ya sifa za Mungu. . Vilevile ni ushahidi kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwatakasa Mitume. Kwamba Mtume ana yakini kuwa yeye ni mja miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu na kwamba Mwenyezi Mungu pekee ndiye mwenye kuabudiwa. Sasa itawezekanaje yeye awatake waja wamwabudu yeye au waaabudu Malaika. Yeye anawaamrisha wawe waalimu na watumishi wa Mwenyezi Mungu kwa vitendo.

Imeelezwa katika Hadith kwamba mtu mmoja alimwambia Mtume: "Tukusujudie?" Mtume akajibu: "La, haitakikani kusujudiwa yeyote zaidi ya Mwenyezi Mungu." Mwengine naye alisema: "Je unataka tukuabudu na tukufanye Mungu." Akasema Mtume: "Mwenyezi Mungu anihifadhi na hilo! Sikuamrishwa hivyo wala sisemi hivyo."

Ama kisa cha Imam Ali kuwachoma moto wale waliomnasibisha uungu ni mashuhuri kiasi cha kutohitajiwa kutajwa. Kila mwenye kuwataka watu wamwabudu, basi ni kafiri; na kila mwenye kuwataka wamtukuze kwa makusudio ya kujitukuza na kujiweka juu, basi ni fasiki.

Unaweza kuuliza: "Aya imekusanya matamko matatu: Kitabu, hekima na unabii: na kila tamko maana yake yako wazi hayahitaji tafsir kama yakiwa peke yake. Lakini yakiwa pamo-ja katika jumla moja na yakaunganishwa, basi yanahitaji tafsir. Kwa sababu, maana yake yanaingiliana; hasa kupewa kitab na unabii. Na tunajua kuwa kuungana maneno kuna-maanisha tofauti na kubadilika. Sasa kuna njia gani ya kutofautisha matamko hayo matatu?

Jibu: Makusudio ya Kitabu ni Kitabu kilichoteremshwa na Mwenyezi Mungu kama Tawrat, Zabur, Injil na Qur'an. Makusudio ya hekima ni elimu na sunna za utume. Mwenyezi Mungu anasema Kuhusu Yahya: "Na tulimpa hekima akiwa mtoto (19:12)

Ama unabii maana yake ni maarufu; nao ingawaje unalazimisha kujua Kitabu na Sunna, lakini kuyajua hayo mawili hakulazimishi unabii. Kila nabii anajua Kitabu na Sunna, lakini sio kila anayejua Kitabu na Sunna ni nabii. Aya hii iko katika mfano wa Aya isemayo:"Hao ndio ambao tumewapa Kitabu na hekima na unabii". (6:89).

Lakini kuweni watumishi wa Mwenyezi Mungu kwa kuwa mnafundisha kitabu na kwa kuwa mnakisoma.

Yaani Mtume anawaambia watu kuweni wajuzi wa Kitabu cha Mwenyezi Mungu, wenye kukitumia na wenye kuwafundisha wengine, Sheikh Muhammad Abduh anasema: "Aya inafahamisha kuwa mtu atakuwa mtumishi wa Mwenyezi Mungu kwa kukijua Kitabu, kuki-fundisha kwa watu na kukitangaza. Na ni uthibitisho kuwa kujikurubisha kwa Mwenyezi

134

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Mungu hakuwi kwa elimu pekee, bali ni lazima kuwa pamoja na vitendo." Wala hatawaamrisha kuwafanya Malaika na manabii kuwa waungu.

Yaani Mtume haamrishi wala hatamwamrisha yeyote kuwafanya wengine kuabudiwa badala ya Mwenyezi Mungu.

Je, atawaamrisha ukafiri baada ya kuwa nyinyi Waislamu?

Wao ni Waislamu kwa sababu wao wamemwamini nabii na wakachukua kauli yake. Mwenye kumwamini nabii yeyote wakati wowote yeye ni mwislamu kwa mujibu wa istilahi ya Qur'an. Ufafanuzi wa hilo umetangulia katika kufasiri Aya ya 19 ya Surah hii.

Mwenye kufuatilia Aya za Qur'an na Hadith za Mtume wa Mungu, ataona kuwa miongoni mwa mambo ya asili yanayojitokeza zaidi, ambayo uislam unatofautiana na dini nyengine, ni kusisitiza kuwa haifai kwa hali yoyote kuinasibisha sifa ya Mungu kwa kiumbe, awe mtume, mfalme au walii.

Siri ya kulitilia mkazo hilo ni kwamba umbile la mtu linapondokea sana kwenye kutopea kama tunavyoshuhudia hilo kwa baadhi ya watu wa dini.

Pamoja na sisitizo hilo, lakini utawakuta waislam waliotopea (Ghulat) na kwamba Waislam leo - tukiwa katika karne ya ishirini - wanawanasibishia wafu mambo ambayo hayafai kuyanasibisha isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu peke yake, asiyekuwa na mshirika.

81.Na Mwenyezi Mungu alipochukua ahadi kwa manabii. Nikiwapa kitabu na hekima; kisha akawajia mtume msadikishaji wa yale yaliyo pamoja nanyi, ni juu yenu kumwamini na kumsaidia. Akasema: Je, mmekubali na mmechukua ahadi yangu kwa hayo? Wakasema: Tumekubali. Akasema: basi shuhudieni, na mimi ni pamoja nanyi katika mashahidi.

82.Na atakayegeuka baada ya hayo, basi hao ndio mafasiki.

Kaashif3-106.jpgKaashif3-107.jpgKaashif3-108.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

83.Je, wanataka dini isiyokuwa ya Mwenyezi Mungu na hali waliomo mbinguni na ardhini wanamtii yeye wapende wasipende. Na kwake yeye watarejeshwa.

MSHIKAMANO WA MITUME Aya 81 - 83

MTUME NA MREKEBISHAJI

Hakuna tofauti kati ya mtume na mrekebishaji katika ukweli wa nia na ikhlasi katika amali. Lakini wanatofautiana kwa kuwa mtume hakosei. Kwa vile yeye anasema na kutenda kwa wahyi utokao kwa Mwenyezi Mungu. Ama mrekebishaji, hufanya kwa kutegemea mtazamo wake na jitihadi yake. Na mwenye kujitahidi hukosea na kusibu. Kwa hivyo upo uwezekano wa kutofautiana katika jitihadi na mtazamo. Na imesihi kumwondokea jukumu akikosea.

Ama kutofautiana mitume kabisa, hilo haliwezekani. Kwa sababu wote wanategemea chim-buko moja - wahyi unaowaelekea wote. Kwa hivyo mitume ni sawa na wafanyikazi wa serikali katika kufikisha amri kwa wananchi.

Haya yanafungamana na kuwa Mwenyezi Mungu anapopeleka manabii wawili kwenye umma mmoja, wakati mmoja, basi watakuwa ni wenye kuafikiana katika kila kitu; kama ilivy-otokea kwa Musa na Harun (a.s.). Na kama watakuwa katika nyakati mbalimbali, watakuwa wanaafikiana wote katika fikra na misingi; kama vile kumwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho. Ikiwa kutakuwa na tofauti, basi ni tofauti katika picha yake na katika hukumu za matendo ambazo zinakwenda na wakati. Hata hiyo nayo wanaikubali Manabii wote kuwa ni ukweli na haki na ni dharura. Kwa hivyo basi hakuna tofauti kabisa kati ya manabii wote na ni kwa ajili hiyo ndipo kila mtume alisadikisha nabii mwenzake aliyemtangulia.

Unaweza kuuliza kuwa inawezekana nabii kumsadikisha nabii mwenzake aliyemtangulia. Bali ndivyo ilivyo hasa: sisi tunaamini utume wa Isa na Muhammad; Ibrahim naye akaami-ni aliyokuja nayo Nuh; Musa akaamini waliyo kuja nayo wote wawili; Isa akaamini waliyoku-ja nayo wote watatu na Muhammad (s.a.w.w.) akaamini waliyokuja nayo wote. Hili linaingi-lika akilini sana. Lakini litaingilikaje akili kuwa nabii aliyetangulia amwamini atakayekuja baadae, ambaye bado hajapatikana?

Jibu: Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anaampa wahyi Mtume aliyetangulia kwamba Yeye atamtuma Mtume baada yake na kubainisha jina lake na sifa zake. Na ni juu ya yule aliyetangulia kuwatangazia watu wa kizazi alicho yeye katika uma wake ili nao wawatangazie watakaofuatia. Kwa hivyo akija anayefuatia anakuta njia ya kusadikisha imani yake na ujumbe wake imeandaliwa.

Tumeyaeleza haya kuwa ni utangulizi na kurahisisha ufahamu Aya hizi zifuatazo.

IRABU

Inawezekana kusoma Lima kwa kuifanya herufi Lam ni ya Jarri. Kwa maana ya kuwa

Kaashif3-109.jpg

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Mwenyezi Mungu alipochukuwa ahadi kwa manabii kwa kwa ajili kuwapa Kitabu na hikima. Na inawezekana kusoma Lama, kwa fat-ha kuifanya lamu ni ya kuanzia (Mubtada). kwa maana ya, Mwenyezi Mungu alipochukua ahadi kwa manabii: Nikiwapa Kitabu na hekima.

MAANA

Na Mwenyezi Mungu alipochukua ahadi kwa Manabii: Nikiwapa kitabu na hekima; kisha akawajia mtume msadikishaji wa yale yaliyo pamoja nanyi, ni juu yenu kumwamini na kumsaidia.

Kutokana na mfumo wa maneno ulivyo inafahamika kuwa makusudio ya manabii hapa ni manabi na wafuasi wao na wala si manabii peke yao. Na makusudio ya mtume ni mtume Muhammad (s.a.w.w.); kama ilivyo Aya nyengine isemayo: "Na walipojiwa na mtume kuto-ka kwa Mwenyezi Mungu mwenye kusadikisha yale yaliyo pamoja nao kundi moja miongo-ni mwa wale waliopewa Kitabu lilitupa Kitabu cha Mwenyezi Mungu nyuma ya migongo yao kama kwamba hawajui." (2:101).

Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) baada ya kuwabainishia mitume na umma unaowafuata, katika misingi na matawi, alichukua ahadi kwao wote kwamba wamwamini Muhammad (s.a.w.) na wamsaidie; kama ambavyo naye Muhammad anawasadikisha waliomtangulia na vitabu walivyoviacha, kama vile Tawrat na Injil.

Kuchukua ahadi kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwa mitume ni kwa njia ya wahyi. Ama kwa wafuasi wa mitume ni kwa kupitia mitume. Yaani kila mtume anachukua ahadi kwa ulama wa umma wake kumwamini Muhammad na kumsaidia. Kwa maelezo ya ndani zaidi ni kwamba kuchukua ahadi kwa anayefuatwa ni lazima kuwe kwa mfuasi. Ikiwa ni wajibu kwa nabii kumwamini Muhammad basi imekuwa wajibu kwa wanaomfuata nabii huyo.

Maana ya umma kumwamini Muhammad na kumsaidia, ni kuitakidi kwamba yeye atakuja baada yao na walibashirie hilo. Mwenyezi Mungu anasema: "Na Isa aliposema: "Enyi wana wa Israil mimi ni mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu; nisadikishaye yaliyokuwa kabla yangu katika Tawrat na kutoa bishara ya mtume atakayekuja baada yangu jina lake ni Ahmad (61:6)"

Imam Ali (a.s.) anasema: "Mwenyezi Mungu hakupeleka Mtume yeyote ila huchukua ahadi naye kuhusu Muhammad (s.a.w.w.) na kumwamrisha kuchukua ahadi na watu kuwa watamwamini na kumsaidia, kama watazikuta zama zake"

Maana ya Umma kumwamini Muhammad (s.a.w.) na kumsaidia ni kumsadikisha wanavyuoni wao na viongozi wa dini zao na kuwatangazia wale wanaowategemea kwamba Muhammad bin Abdullah ndiye Mtume aliyebashiriwa na mitume, na kwamba jina lake liko katika Vitabu vya dini zao kama asemavyo Mwenyezi Mungu Mtukufu. "Ambao hum-fuata mtume ummi ambaye humkuta ameandikwa kwao katika Tawrat na Injil ...(7:157)

Na wala wasiyapindue maneno ya Mwenyezi Mungu kwa kufuru na inadi, kama alivy-owaelezea Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

Hali ya kuwa baadhi yao walikuwa wanasikia maneno ya Mwenyezi Mungu kisha wanayabadili baada ya kuwa wanayafahamu; na hali wanajua. (2:75)

Akasema: Je, mmekubali na mmechukua ahadi yangu kwa hayo? Wakasema: Tumekubali.

137

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Swali hapa ni la kuthibitisha na kutilia mkazo. Maana yake ni Mwenyezi Mungu aliziambia Umma kwa ndimi za mitume yao: Je, mmemkubali Muhammad na mmekubali ahadi? Umma ukasema: Ndio tumekubali wajibu wa kumwamini kumsaidia. Tumelikubali hilo na tumelazimiana nalo. Makusudio ya umma ni viongozi wa dini na wanavyuoni wao wanao-jua vitabu vya dini.

Akasema: Shuhudieni; yaani akasema Mwenyezi Mungu kwa ndimi za mitume Yake kwa umma shuhudizaneni kwamba mmekubali utume wa Muhammad (s.a.w.w.) na wajibu wa kumsaidia. Mimi ni pamoja nanyi katika mashahidi. Mwenyezi Mungu na Malaika wake na mitume Yake wanashuhudia kuchukuliwa kwa ahadi ya wanavyuoni wa kidini, na kumkubali kwao Muhammad (s.a.w.w.), lakini pamoja na hayo wanavyuoni wa kiyahudi na wa Kinaswara walikana ahadi hii; wakamkadhibisha Muhammad na kumfanyia vitimbi na kiburi kama zilivyofafanua Aya zilizotangulia.

Na atakayegeuka baada ya hayo.

Yaani atakayegeuza kumwamini Muhammad baada ya kuchukua ahadi ya kumkubali na kumsaidia.

Basi hao ndio mafasiki.

Makusudio ya mafasiki hapa ni makafiri. Kwa sababu kila mwenye kugeuza Aya kutoka katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu na akakanusha utume miongoni mwa mitume ya Mwenyezi Mungu huku akijua utume wake basi yeye ni kafiri,

Je, wanataka dini isiyokuwa ya Mwenyezi Mungu na hali waliomo mbinguni na ardhi-ni wanamtii yeye wapende wasipende.

Watu wote wanamwamini Mwenyezi Mungu bila ya kutofautiana mwema na muovu, isipokuwa kwamba mwema humwamini Mwenyezi Mungu kwa hiyari katika maisha haya. Na muovu atamwamini kwa nguvu siku ya kiyama itakapoondoka pazia, na kila mkanusha-ji ataona adhabu kinaga ubaga. Mwenyezi Mungu anasema: "Walipoiona adhabu yetu wakasema: Tunamwamini Mwenyezi Mungu pekee na tunawakataa tuliokuwa tukiwashirik-isha naye." (40:84).

Haya ndiyo maana ya 'wapende wasipende' tulivyofasiri ambayo si mazito kufahamiwa na yeyote vyovyote alivyo. Lakini Razi amefasiri kwa tafsiri ya kifalsafa. Aliyoyasema yako karibu, lakini ni kwa watu maalum watakaoelewa sio wote. Na hapa tunayanakili kwa ajili yao sio kwa ajili ya hawa:

"Kila kisichokuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kinawezekana kwa dhati yake; na kila chenye kuwezekana kwa dhati yake hakipatikani ila kwa kukipatisha yeye na hakikosekani ila kwa kukikosesha yeye. Kwa hiyo, kila kisichokuwa Mwenyezi Mungu ni chenye kumnyeyekea Mwenyezi Mungu Mtukufu katika njia zote mbili za kupatikana kwake na kukosekana kwake, Na, huo ndio ukomo wa kunyenyekea."

138

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

84.Sema tumemwamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyoteremshiwa na yale aliyoteremshiwa Ibrahim na Ismail na Is-haq na Yaqub na wajukuu zao na alichopewa Musa na Isa na manabii kutoka kwa Mola wao; hatut-ofautishi baina yao hata mmoja na sisi ni wenye kusilimu kwake.

85.Na mwenye kutaka dini isiyokuwa uis-lam haitakubaliwa kwake, naye katika akhera ni miongoni mwa wenye kupata hasara.

Kaashif3-110.jpg

TUMEAMINI MITUME YOTE Aya 84 - 85

MAANA

Aya hii ya 85 imekwishapita pamoja na tafsiri yake katika Sura ya Baqara Aya 136. Kwa ufupi ni kwamba mayahudi na manaswara wanaamini baadhi ya manabii na wanawakanusha baadhi yao. Ama waislam, wao wanaamini wote. Kwa sababu, mwito wa manabii ni mmoja na lengo lao pia ni moja. Kwa hiyo, kujaribu kuwatofautisha ni sawa na kusema ndiyo na hapana kwa jambo moja tofuati ya kuamini unabii wao ni sawa na kitu kimoja, kwamba sawa ni hapana kwa pamoja.

Na mwenye kutaka dini isiyokuwa Uislamu haitakubaliwa kwake.

Makusudio ya Aya hii yatajulikana kwa kurudia tafsiri ya Aya ya 19 ya Sura hii.

Nimewaona baadhi ya watu wakitoa dalili kuwa hakuna tofauti baina ya mwislam, myahudi na mkristo maadam wote wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, kwa Aya ise-mayo: "Hakika wale ambao wameamini na mayahudi na manaswara na wasabai, yeyote atayemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na akatenda mema, basi watapata malipo yao kwa Mola wao, wala haitakuwa hofu juu yao, wala hawatahuzunika." (2:62)

Hilo ni kosa kwa njia mbili: Kwanza kwamba makusudio ya waliotajwa katika Aya ni kila aliyekufa akiwa na imani na amali njema katika watu wa dini zilizomtangulia Muhammad (s.a.w.w.). Tumeyafafanua hayo wakati wa kufasiri Aya hiyo.

139

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

3. Sura Al-Imran

Pili: Hata kama dhahiri ya tamko la Aya inaonyesha kuwa inaenea wakati wote, lakini kauli yake Mwenyezi Mungu: Na mwenye kutaka dini isiyokuwa uislam hatakubaliwa," inaihu-sisha Aya hiyo na wale waliokuwa kabla ya wakati wa Muhammad tu. Ama mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, na asimwamini Muhammad baada ya kupewa kwake utume na ukawa mwito wake umemfikia, basi imani yake si chochote na yeye huko akhera atakuwa katika wenye kupata hasara.

86.Atawaongozaje Mwenyezi Mungu watu waliokufuru baada kuamini kwao, na wakashuhudia kwamba mtume ni wa haki na zikawafikia hoja zilizo wazi. Na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.

87.Hao malipo yao ni kushukiwa na laana ya Mwenyezi Mungu na ya Malaika, na ya watu wote.

88.Ni wenye kudumu humo. Hawatapunguziwa adhabu wala hawat-apewa nafasi.

89.Isipokuwa wale ambao wametubia baada ya hayo, na wakasahihisha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe mwenye kurehemu.

ATAWAONGOZAJE MAKAFIRI Aya 86 - 89

MAANA

Atawaongozaje Mwenyezi Mungu watu waliokufuru baada ya kuamini kwao, na

wakashuhudia kwamba mtume ni wa haki na zikawafikia hoja zilizo wazi wazi.

Kaashif3-111.jpg

140

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Makusudio ya Mtume ni Muhammad (s.a.w.); na watu, ni wanavyuoni wa kiyahudi na wa kinaswara kwa sababu Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewataja kuwa ni watu walioamini na wakashuhudia utume wake, lakini baada ya kuletwa na kuwajia wao ubainifu na dalili wazi juu ya utume wake, walimkanusha na wakakataa kumfuata. Sifa hizi zinalingana kabisa na wanavyuoni wa kiyahudi na wa kinaswara, kwa sababu, wao walikuta jina la Muhammad limeandikwa katika Tawrat na Injil, kwa hivyo wakawa wamemwamini kabla ya kuja kwake isipokuwa tu alipoletwa na kuwajia wao dalili walikufuru kwa chuki na hasadi na wakaifuta kila Aya inayofahamisha kwa uwazi au kwa umbali.

Unaweza kuuliza kuwa dhahiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu; Atawaongozaje Mwenyezi Mungu watu waliokufuru baada ya kuamin kwao, inaonyesha kuwa Mwenyezi Mungu hata-ki warudie tena kwenye uislamu hata kama watajaribu kutubia; jambo ambalo litawafanya wasistahili adhabu wala kuwa na lawama yoyote.

Jibu: Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anamsimamishia mja dalili za haki, akiamini, basi atakuwa katika wenye kuongoka; na uongofu wake utatokana na Mwenyezi Mungu. Kwa sababu, Mwenyezi Mungu ndiye aliyemsimamishia dalili za haki. Vile vile uongofu utakuwa ume-tokana na mja mwenyewe. Kwa sababu yeye ameongoka kwa hiyari yake. Akirtadi baada ya uongofu kwa kiburi na inadi, basi Mwenyezi Mungu atamwachilia mbali katika maisha haya, na wala hatamwekea dalili mpya.

Vilevile hawezi kumlazimishia uongofu kwa sababu hakuna taklifu ikiwa kuna kulazimisha.

Hao malipo yao ni kushukiwa na laana ya Mwenyezi Mungu na ya Malaika, na ya watu wote.

Yaani wanastahili hilo. Laana ya Mwenyezi Mungu ni kuelezea ghadhabu yake na machukivu yake. Na laana ya watu wote na Malaika ni dua yao ya kumtaka Mwenyezi Mungu awaadhibu na kuwaweka mbali na rehema yake.

Katika Nahjul-balagha imeelezwa kwamba Ali (a.s.) alikuwa akihutubu katika mimbari Kufa. Ash'ath akamkatiza na kumwambia "Laana ikushukie." Amirul-Muminini akasema: "Wajuaje laana itanipata au la, Mungu akulaani wewe na wakulani wanaolaani." Sheikh Muhammad Abduh katika kulifafanua hilo anasema: "Ash'ath katika masahaba wa Ali alikuwa kama Abdullah bin Ubayy katika masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) wote walikua viongozi wa wanafiki.

Ni wenye kudumu humo, hawatapunguziwa adhabu wala hawatapewa nafasi.

Dhamiri ya humo ni ndani ya Jahannam. Hawatapewa nafasi, yaani hawatapewa muda, bali wataadhibiwa haraka sana.

Isipokuwa wale ambao wametubia baada ya hayo, na wakasahihisha. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwingi wa kusamehe, mwenye kurehemu. Imekuja Hadith ise-mayo: "Mwenye kutubia ni kama asiyekuwa na dhambi." Imam Ali anasema: Mungu ham-fungulii mja mlango wa toba, akamfungia wa msamaha."

Unaweza kuuliza: Mtu akisilimu, kisha akartadi, kisha akarudi kwenye Uislamu lakini aka-puuza hukumu sio misingi; kama vile kuacha Swala na Saumu kwa uvivu na kupuuza. Je, toba yake itakubaliwa?

Jibu: Ndio, atakubaliwa. Kwa sababu, toba ilikuwa ya kukufuru, sio ya Swala au Saumu. Ama kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na wakasahihisha, ni kuzitengeneza dhamiri zao na kuthibiti kwenye uislam na kutortadi mara ya pili.

141

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu

90.Hakika wale ambao wamekufuru baada ya kuamini kwao, kisha wakazi-di kukufuru, haitatakabliwa toba yao; na hao ndio waliopotea.

3. Sura Al-Imran

Kaashif3-112.jpg

91.Hakika wale ambao wamekufuru na wakafa hali ya kuwa wao ni makafiri, basi haitakubaliwa kwa yeyote katika wao hata fidia ya dhahabu kwa kujaza ardhi yote lau angeliitoa. Hao watap-ata adhabu iumizayo wala hawatakuwa na msaidizi.

KISHA WAKAZIDI KUKUFURU Aya 90 - 91

Hakika wale ambao wamekufuru baada ya kuamini kwao, kisha wakazidi kukufuru, haitatakabliwa toba yao.

Maana ya kukufuru baada ya kuamini yako wazi. Ama kuzidisha kukufuru, kunakuwa kwa dhambi anazozifanya mwenye dhambi hasa kueneza ukafiri na kuwapiga vita waumini kwa kuwa tu ni waumini.

Unaweza kuuliza; Hakika Mwenyezi Mungu amehukumu - katika Aya iliyotangulia - kum-takabalia toba mwenye kukufuru baada ya imani; na katika Aya hii amehukumu kutomtaka-balia. Kuna wajihi gani wa kuungana haya?

Wafasiri wamejibu kwa majibu mengi. Yenye nguvu zaidi ni kwamba kukufuru baada ya kuamini kuko mafungu matatu. Kwanza: Kutubia toba ya kweli ambayo Mwenyezi Mungu ameitaja kwa kusema: Isipokuwa wale waliotubia.

Pili: Toba isiyo ya kweli ambayo Mwenyezi Mungu ametaja kwa kusema: Haitotakabaliwa toba yao."

Tatu: Ni kufa juu ya ukafiri kulikotajwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hakika wale ambao wamekufuru na wakafa hali ya kuwa wao ni makafiri.

Jibu tunaloliona sisi, ni kwamba mtu anaweza akahisi usahihi wa jambo au kutokuwa sahihi. Kisha akachangayikiwa na kuwaza kuwa hisia zake zimebadilika na kuwa si sahihi au kuwa ni sahihi baada ya kutokuwa sahihi; ingawaje hisia zake hasa hazijabadilika; ambapo kuitakidi kwake kuwa zimebadilika ni kwa mawazo tu.

142 <

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu                                                                 3. Sura Al-Imran

Vilevile mapenzi na chuki, mfano, mtoto wako anaweza kukufanyia ubaya na ukachukulia kuwa yeye ni mtu anayemchukia zaidi kuliko watu wote, na kwamba unataka aangamie, lakini huruma za ubaba bado ziko kwenye nafsi yako bila ya kutambua, mara ngapi tunashuhudia mtu akifanya jambo au kuliacha kwa kufuata desturi, kuiga au kwa kwa kuhu-rumia huku mwenyewe kiitakidi kuwa ni kwa njia ya dini.

Pia inaonyesha watubiaji wengi wa dhambi zao kuwa ni wa kweli, lakini kwa ndani bado wamebakia nayo waliyokuwa nayo. Watubiaji hawa ndio walielezwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hawatatakabaliwa toba yao. Ama wale walioelezwa na Aya iliyotangulia (Isipokuwa wale waliotubia), ni wale watubiaji wa kweli na wa haki.

Hakika wale ambao wamekufuru na wakafa hali ya kuwa wao ni makafiri, basi haitakubaliwa kwa yeyote katika wao hata fidiya ya dhahabu kwa kujaza ardhi yote.

Hakuna mwenye shaka kwamba mwenye kuishiliza maisha yake kwa ukafiri atahisabiwa hisabu ya makafiri.

Unaweza kuuliza; kuwa hakuna dhahabu siku ya kiyama wala hakuna njia yoyote ya kuweza kuimiliki wala kuitoa. Sasa kuna faida gani ya kuitaja.

Jibu: Makusudio ni kwamba hakuna njia ya kujikomboa kwa namna yoyote ile. Kimsingi ni kuwa kukadiri muhali si muhali. Katika aliyoyasoma Imam Ali, kuisifu Jahannam ni: "Haondoki mkazi wake wala hakombolewi mateka wake."

143 <