JANNAT na
JAHANNAM
( Peponi na Motoni )
Kitabu hiki kimekusanywa na kutarjumiwa na:
Amiraly
M.
H.
Datoo
Bukoba –
www.al-islam.org and ebooked by www.ShiaLibrary.com and www.islamkutuphanesi.com . May Allah be pleased with all. |
( Peponi )
Sunday, February 03, 2002
Ingawaje Qur’an
Tukufu inatujulisha vya kutosha kuhusu
Jannat
(Pepo ) na
Jahannam ( Motoni ), vile vile tunapata
habari zaidi kutoka
Ahadith Qudsi
zilizoletwa na Malaika Jibraili a.s. kwa Mtume Muhammad s.a.w.w. ambaye
ananakiliwa na Imam Ali a.s. na Maimamu Kumi na moja a.s. waliobakia. Mtume
s.a.w.w. wakati wa Me’raj aliweza kuona na kutembea Peponi, kula matunda ndani
mwake na kuangalia yale yaliyokuwamo. Vile vile alitembelea jahannam au Motoni
ambamo aliweza kujionea vile wahalifu walivyokuwa wakiadhibiwa kwa madhambi
Al Tirmidhi na
Abu Daud wananakili
Ahadith Qudsi
ifuatayo kutokea Mtume Muhammad s.a.w.w.:
Allah swt
alipoumba Jannat na Jahannam, alimtuma Malaika Jibraili a.s. kwenda Jannat,
akisema, “Angalia ndani mwake kile nilichokiwatengenezea wakazi wa humo.”
Malaika Jibraili a.s. alikwenda akaangalia vizuri na kwa makini, na aliporudi
kwa Allah swt alisema, “Kwa utukufu wako naapa kuwa hakuna atakayeisikia illa
atatamani kuingia humo.” Kwa hayo Allah swt alizungushia vizuizi na magumu
mbalimbali, na alimwamrisha Malaika Jibraili akaangalie vizuizi na magumu
yaliyozungushiwa. Malaika Jibraili a.s. aliporudi baada ya kuyaangalia kwa
makini, alimwambia Allah swt, “Kwa Utukufu wako, Naapa na kuhofu kuwa hakuna
hata mtu mmoja ambaye ataweza kuingia ndani mwake.”
Allah swt alimwambia, “Sasa nenda kaangalie
Jahannam na yale niliyowaandalia wakazi
wake.” Malaika Jibraili a.s. alikwenda na kuona tabaka moja baada ya nyingine.
Aliporejea akasema,”Kwa utukufu wako, hakuna hata mtu mmoja atakayetamani
kuingia ndani humo atakapoisikia.” Hapo Allah swt aliamrisha kuzungushiwa
vivutio na vipotoshavyo, na kumwamuru Jibraili a.s. kurudi kuangalia tena.
Aliporudi Jibraili a.s. alisema, “Kwa kiapo cha Utukufu Wako! Hakika ninahofu
kuwa hakuna mtu atakayeweza kujiepusha kuingia ndani humo.”
Sasa tujaribu
kuchunguza na kuelewa zaidi kuhusu sehemu hizi mbili :
Jannat
na
Jahannam
1). Maelezo juu ya Jannat ( Peponi )
Jannat ni mahala ambapo kunatofautiana hali ya
starehe, pema na furaha za kila aina. Si kama Jahannam ambapo ni shimo refu mno
la moto mkali, Jannat ni eneo ( tambarare au imeinuka kidogo), kiasi kwamba
hata mito yake haivunji kuta zake bali inabubujika vyema. Kuna Jannat
au Bustani zaidi ya moja. Ayah ya Qur’an ya
Surah Al-Rahman (Sura 55 ) inatujulisha neno moja
Mudhamutan ambayo inaelezea Bustani mbili zilizo za rangi zilizoiva
za kijani, ambapo Ayah ya 62 ya Sura hiyo hiyo inatuambia “mbali na Bustani
hizi mbili zipo Bustani zingine mbili,” zikijumlisha kuwapo kwa Bustani nne kwa
ujumla katika Akhera. Bora ya Jannat ni
Bustani ya Eden,
orjanat ‘adan.
Katika kitabu
Lisan al-‘Arab, j.13, Uk. 99, sisi twaambiwa kuwa
Jannat
inamaanisha : Bustani ya miche ya matunda
mbalimbali.
Jannat ‘Adan imeelezwa katika :
AYAH |
SURAH |
|
AYAH |
SURAH |
72 |
Al-Tawbah , 9 |
|
31 |
Al-Kahf, 18 |
23 |
Al-Ra’d,
13 |
|
61 |
Al-Maryam, 19 |
31 |
An-Nahl, 16 |
|
76 |
Ta-Ha , 20 |
33 |
Al-Fatir, 35 |
|
50 |
As-Sad, 38 |
8 |
Al-Ghafir, 40 |
|
12 |
Al-Saff,
61 |
8 |
Al-Bayyinah,
98 |
|
|
|
Katika ukurasa
wa 279, juzuu 13 ya kitabu
Lisan al-‘Arab,
twaambiwa kuwa
Jannat ‘Adan
inamaanisha kuwa “Mahala pa milele”, Bustani ya Kati (al-awsat).”
Kitabu
hichohicho kinatutambulisha katika uk.427, juzuu ya 7 kuwa
al-awsat inaweza kumaanisha kuwa : iliyo Bora.
Hakuna shaka kuwa tutaweza kuona na kupata
maelezo na mafafanuzi zaidi juu ya
Jannat
‘adan
kuliko kusema tu
al-firdows, Jannat au Peponi, katika
Qur’an Tukufu. Hali hii inatuacha sisi kwa kudadisi kuwa mahala bora kabisa, na
iliyokuu, inayolengwa katika Jannat zote ni
Jannat
‘Adan.
Peponi, au
al-Firdows kama vile inavyoitwa katika
Kiarabu, ni neno la kuazimwa. Waarabu aliowatokezea Mtume Muhammad s.a.w.w.
walikuwa hawana itikadi ya maisha baada ya kufa, na
Jannat na
Jahannam. Na
kwa hakika swala hili lilikua gumu kwake Mtume s.a.w.w. alipoanza kuhubiri.
Sura-i-Yasin,36, Ayah ya 78 inatuelezea
‘Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa
kwake – akasema: “Nani atakaihuisha mifupa na hali imesagika ?”
Vile vile Qur’an
inatuambia katika, Sura
Ya-Sin, 36; Ayah
79:
Sema: “Ataihuisha yule aliyeiumba mara
ya kwanza, naye ni Mjuzi wa kila (namna ya ) kuumba”
Hata mwandishi
wa kazi nzuri kabisa za Kiarabu,
Lisan
Al-‘Arab, hanauhakika iwapo neno hili
Majumba yao
yaliyokuwa yamejengwa kwa udongo uliochomwa au uliokaushwa kwa jua, walikuwa
wakiishi kwa kujumuika katika mashamba yao kama ilivyo katika swala
Swala hili
linaweza kujitosheleza kuandika kitabu kikubwa sana ambapo si makusudio yetu hapa,
hivyo kwa mukhtasari sana tuangalie milango yake ya kuingilia kama ilivyoonwa
na Mtume Muhammad s.a.w.w. ambaye ananakiliwa katika
Bihar al-Anwar j. 8, uk. 144, akielezea kama ilivyofikishwa na
Abdullah ibn Mas’ud kama ifuatavyo :
“Wakati Allah
swt aliponiruhusu kwenda
Jannat,
Jibrail
a.s. aliniambia, “Mimi nimeamrishwa kukutembeza na kukuonyesha yote yaliyomo
ndani mwa
Jannat na Jahannam.”
Hivyo mimi niliiona
Jannat na baraka na mema yote yaliyokuwamo na vile vile nimeiona
Jahannam pamoja na mateso yote yaliyomo.
Jannat
inayo milango minane, kila mlango inayo misemo
minne, ambayo kila mojawapo ni bora kuliko ulimwengu mzima na kile ambacho kipo
ndani mwake ni kwa ajili ya wale wanaotafakari na kufuatilia kwa kutenda
kimatendo.
Na
Jahannam inayo milango saba, na kila mlango inayo misemo mitatu,
ambapo kila msemo ni afadhali kuliko dunia yetu hii na kilichomo ndani mwa kila
msemo ni kwa ajili ya kutafakari na kuyatendea kazi. Malaika Jibraili a.s.
aliniambia,
“Ewe Muhammad ! Soma
yaliyoandikwa katika milango hizi !” Na hivyo mimi niliyasoma yote.
Katika
mlango wa kwanza wa
Jannat
kumeandikwa : Hakuna mungu
mwingine isipokuwa Allah swt tu; Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Wake;
Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ni mja
(Walii) Wake halisi; zipo njia mbalimbali
za kujipatia kila kitu, na njia za kujipatia riziki ni nnne : kutosheleka,
kutumia katika njia sahihi, kukana kisasi na kufanya uhusiano pamoja na watu
waliookoka yaani katika njia nyoofu.
Katika
mlango wa pili wa
Jannat
kumeandikwa : Hakuna mungu mwingine isipokuwa Allah swt tu;
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Wake; Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.
ni mja
(Walii) Wake halisi; zipo njia mbalimbali za kujipatia kila kitu, na
na njia za kujipatia furaha katika maisha ya Aakhera ni nnne : Kuonyesha huruma
kwa mayatima, kuwawia wema wajane, kuwasaidia wacha-mungu katika kufanikisha
malengo yao na kuwaangalia na na kuwasaidia masikini na wasiojiweza.
Katika
mlango wa tatu wa
Jannat
kumeandikwa : Hakuna mungu mwingine isipokuwa Allah swt tu;
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Wake; Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.
ni mja
(Walii) Wake halisi; zipo njia mbalimbali za kujipatia kila kitu, na
na njia za kujipatia siha njema katika maisha haya mafupi ni nne : Kuongea kwa
uchache, kulala kidogo, kutembea kidogo na kula kidogo.
Katika
mlango wa nne wa
Jannat
kumeandikwa : Hakuna mungu mwingine isipokuwa Allah swt tu;
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Wake; Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.
ni mja
(Walii) Wake halisi; Yeyote yule amwaminiaye Allah swt na siku ya
Qiyamah basi lazime awe mkarimu kwa wageni wake; Yeyote yule amwaminiaye Allah
swt na siku ya Qiyamah basi lazime awe mkarimu kwa jirani zake; Yeyote yule
amwaminiaye Allah swt na siku ya Qiyamah basi lazime awe mkarimu kwa wazazi
wake; Yeyote yule amwaminiaye Allah swt na siku ya Qiyamah basi lazime awe ni
mwenye kusema mema au anyamaze kimya.
Katika
mlango wa tano wa
Jannat
kumeandikwa : Hakuna mungu mwingine isipokuwa Allah swt tu;
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Wake; Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.
ni mja
(Walii) Wake halisi; Yeyote yule ambaye hataki kunyanyaswa siku ya
Qiyamah, basi naye asimnyanyase mtu yeyote; Yeyote yule ambaye hataki
kusengenywa siku ya Qiyamah, basi naye asimsengenye mtu yeyote; Yeyote yule
ambaye hataki kudhalilishwa siku ya Qiyamah, basi naye asimdhalilishe mtu
yeyote; Mtu yeyote yule ambaye anataka kujishikiza kwa umadhubuti katika maisha
haya mafupi na yale ya Aakhera, basi lazima atoe shahada kuwa : Hakuna mungu mwingine
isipokuwa Allah swt tu; Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Wake; Al-Imam
'Ali ibn Abi Talib a.s. ni mja
(Walii) Wake halisi.
Katika
mlango wa sita wa
Jannat
kumeandikwa : Hakuna mungu mwingine isipokuwa Allah swt tu;
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Wake; Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.
ni mja
(Walii) Wake halisi; Yeyote yule anayetaka kaburi lake liwe pana na
lenye nafasi ya kutosha (kutombana) basi ajenge Misikiti; Yeyote yule anayetaka
wadudu na minyoo ya ardhini wasimle, aifanye Misikiti iwe nyumba yake ( yaani
awe akiizuru kwa mara nyingi kama kwamba anaishi humo ); Yeyote yule anayetaka
kubakia freshi, (yaani asipate shida na taabu za kiu katika maisha haya na ya
Aakhera ambapo kila mtu atakuwa akitafuta hata tone moja la maji ) basi awe
akifagia Misikiti; na yeyote yule amabye anataka kuiona nafasi yake hapo
Jannat
basi atengeneze sakafu na kuweka
mazulia au mikeka katika Misikiti.
Katika
mlango wa saba wa
Jannat
kumeandikwa : Hakuna mungu mwingine isipokuwa Allah swt tu;
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Wake; Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.
ni mja
(Walii) Wake halisi.
Moyo
halisi unapatikana kwa mema manne : Kuwatembelea wagonjwa, kutembea nyuma ya
jeneza, kununua sanda kwa ajili ya maiti na kulipa madeni.
Katika
mlango wa nane wa
Jannat
kumeandikwa : Hakuna mungu mwingine isipokuwa Allah swt tu;
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Wake; Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.
ni mja
(Walii) Wake halisi; Yeyote yule anayetaka kuingia katika milango
hii basi lazima awe na sifa nne zifuatazo : Ukarimu, adabu njema, moyo wa
kujitolea na kujiepusha katika kuwadhuru waja wa mungu.
Al-Majlisi,
katika uk. 131, j. 8, ya kitabu chake kiitwacho
Bihar al-Anwar,
ananakili uk. 39, j. 2, ya
AI-Kaisal,ambapo Ubayy anamnakili Sa’d anayemnakili al-Barqi
akimnakili babake akimnakili na kuthibitisha kuwa ibn al-Nasr akimnakili ‘Amr
ibn Shemr akimnakili Jabir ibn Abdullah al-Ansari akimnakili Imam Ja"fer
al-Sadiq a.s. akisema, "Fikirieni kuhusu Allah swt kwa bora ya mawazo
yenu, na mjue kuwa
Jannat
inayo milango nane na upana wa kila mlango ni
upana wa miaka arobaini.
Katika hotuba
mbalimbali katika
Nahjul Balagha,
Al-Imam
'Ali ibn Abi Talib a.s. anazielezea kwa undani na mapana sana kuhusu
Jannat
na
Jahannam;
hapa ninawadondosheeni machache vile anavyoelezea
Jannat
:
“Kipeo cha
furaha na mustarehe na pongezi au hongera inatofautiana sana baina ya mtu mmoja
na mwingine au mahala moja na nyingine; starehe zake kamwe haziishi; wale
waliobahatika kuingia na kuishi humo kamwe hawafukuzwi au kuhamishwa, na kamwe
hawapatwi na uzee, na kamwe hakuna anayeambukizwa ugonjwa wa ubakhili
(Hotuba nambari 85). Wao hawajivuni wala
kujigamba wala kamwe hawazaliani watoto. (Hotuba nambari 161).
Hakuna
anayeingia
Jannat
isipokuwa wale
ambao wanaouelewano mwema (na kufuata nyayo zao) pamoja na Ma-Imamu a.s.
kutokea kizazi cha Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.
na ambao ndio waliothibitishwa ndivyo katika
Siku ya Qiyamah
(Hotuba nambari 152).
Iwapo utaingiwa
na imani kwa
kile utakachoelezewa kuhusu
Jannat, basi nafsi yako itajitoa
mbali na mavutio ya macho na mapotoshi ya duniani humu (ambayo yanafurahisha
macho tu ) utashangazwa kuona vile miti ilivyopangwa katika mistari na mizizi
yao ikiwaimefukiwa katika marundo ya
maski
(mishki) katika mwambao wake. Matunda yao yanaweza kuchumwa kwa urahisi. Wakazi
wake wanakarimiwa kila wakati kwa vinywaji vya asali halisi na mivinyo
mbalimbali, ambayo haileweshi ulevi, wakazi wa humo watakuwa wakistarehe katika
majumba yao ya fakhari. Itakuwa imeezekwa kwa
‘Arsh-i-Ilahi (mbingu ya Allah swt ); starehe zake ndizo nuru, na
wakazi ndani ya
Jannat
huwa mara kwa
mara wakitembelewa na Malaika wa Allah swt.
Raha na furaha
kubwa kwa ajili ya wakazi wa
Jannat
itakuwa ni kule kuwa karibu na Allah swt na
watakuwa na mawasiliano naye kwa ukaribu zaidi. Allah swt atakuwa akiongea nao
kama vile mwenyeji anapokuwa akizungumza na wageni wake.
Katika uk. 114,
j. 8, ya kitabu chake
Sahib,
al-Bukhari
anamnakili Ma’ath ibn Asad akimnakili Abdullah akimnakili Malik ibn Anas
akimnakili Zayd ibn Aslam akimnakili ‘Ata ibn Yasar akimnakili Abu Sa’eed
al-Khudri, Allah swt awe radhi nae, akimnakili Mtume wa Allah swt akisema kuwa
Allah swt atawahutubia wakazi wa
Jannat
kwa kusema : “Enyi watu wa
Jannat
! nao watamjibu Allah swt kwa
kusema, “Labbayk
Mola wetu! Kwa
furaha Yako!”
Na hapo ndipo
atakapowauliza, “Je mmetosheka na kuridhika ?” Nao watamjibu, “Je kweli
itawezekanaje sisi tusitosheke na kuridhika wakati ambapo ulichotupatia sisi
haujawapatia viumbe vyako vingine ?”
Hapo atasema, “Mimi nitawapatieni mema zaidi ya hayo,” nao watasema,
“Ewe Mola wetu ! Je ni jambo gani lililobora zaidi ya hayo ?”
Allah swt atasema, “Mimi nitawateremshieni
rehema na baraka zangu ziwe juu yenu, na kamwe sitawaghadhabikieni.”
Mwandishi huyu
huyu, katika Sura juu ya
Tawhid,
anamnakili Muhammad ibn Sinan akimnakili Fulayh akimnakili Hilal akimnakili
‘Ata ibn Yasar akisema kuwa siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa
akisema
hadith na katika kikao icho
alikuwapo bedui mmoja alikuwapo hapo. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alisema
kuwa Bedui mmoja miongoni mwa wakazi a
Jannat
alimwomba ruhusa Allah swt kwa ajili
ya kutaka kulima ardhi, ambapo Allah swt alimwuliza, “je haukupata chochote
kile ulichokihitaji (kutokea miti na mimea ya humu
Jannat
?). ”
Mbedui huyo
alijibu, “Naam (nimepata kila kitu nilichokuwa nimekihitaji, lakini bado
ninapendelea kulima ardhi.”
Kwa hayo
allah swt alimruhusu kufanya hivyo; basi alipanda mbegu ardhini na katika
sekundi chache tu zikaota katika miti na kukomaa na kutoa matunda mengi mno
kama milima.
Kwa hayo ndipo Allah swt
alipomwambia, “Chukua, Ewe mwana wa Adam, kwani hakuna kinachoweza kukuridhisha
wewe!”
Kwa kusikia hayo, yule Mbedui
aliyekuwa ameketi anayasikia hayo, akainuka na kusema, “Ewe Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. ! Mtu huyo bila shaka alikuwa akitoka Quraish au kutokea
Ansar, kwani wao ndio wakulima ambapo sisi Mabedui si wakulima.”
Kwa kuyasikia hayo, Mtume Muhammad Mustafa
s.a.w.w. alionyesha tabasamu.
Tabia na shauku
ya kukusanya na kulimbikiza ipo katika mishipa ya wanadamu, al-Tirmithi, katika
uk. 89-90, J. 2, ya kitabu chake
Jami’,
anainakili
hadith ya Mtume Muhammad Mustafa
s.a.w.w. ambapo anawajulisha
Ma-Sahaba
kuwa wakazi wa
Jannat
watakuwa wakijumuika kila mara humo katika
karamu mbalimbali kama ukumbusho wao walivyokuwa wakizipitisha Ijumaa wakati
wakiwa humu duniani, nao watakuwa wakienda
bazaar
(masoko au gulio) ambapo watakuwa wakijichagulia nguo, vito vya thamani au
chochote kile watakachokuwa wakikitaka na kuvichukua katika makazi yao.
“Bustani ya
Eden,” yaani
Jannat ‘Adan, imetajwa
katika Qur’an katika mahala pengi zaidi ya moja.
Kwa mujibu wa Ibn Mas’ud, ni sehemu ambayo
iliyopo katikati ya
Jannat
. Kwa mujibu wa al-Dhahhak, ni mji
uliopo ndani ya mji, ambamo wakazi wake ni Mitume a.s., Mashahidi, na ma-Imamu
a.s. watakuwa wakiishi huku wamezungukwa na wengine. Majengo yake yamejengwa
kwa jawhari, Lulu, na vito vyenye thamani, dhahabu, almasi,fedha na kuvikwa kwa
muski, na, kwa mujibu wa Muqatil na
al-Kalbi, hewa nzuri na baridi itakuwa ikipepea kutokea
‘Arsh ikiitumbukiza katika (kama ukungu wa )
mushk nyeupe. Hata Ibilisi, shaytani, aliwaonea wivu wanaadamu kwa
sababu ya
Bustani ya ‘Eden.
Katika ukurasa
wa
115 wa kitabu
Al-Mahasin,
Muhammad ibn Qays anamnakili Imam Abu Ja’fer al-Baqir
a.s. akisema kuwa, “Siku moja Shaitani alimwona Mtume Nuh a.s.akisali, basi
Shaitani alimwonea wivu Mtume Nuh a.s. na hakuweza kujizuia, akasema. “Ewe Nuh
! Allah swt aliyetukuka, Mkuu, amejenga mwenyewe
Bustani ya Eden , akapanda miti na kutiririsha mito ndani mwake. Na
kisha akaangalia mandhari hayo na kusema, “Kwa hakika waumini na waongofu ndio
washindi ! La, Kwa Utukufu wangu ! Mtu mwenye utovu wa adabu (mwenye madhambi)
kamwe hataingia kuishi humu.’”
Aina za vyakula
na vinywaji vinazungumziwa na kutajwa katika Qur’an na Sunnah, na vile vile
hur al-‘ayn wanawake wenye macho makubwa
ndio watakaokuwa wake wa wale waliobahatika, lakini hapa mtu anaweza kujiuliza
swala bila ya kujizuia : Je ni kitu gani kile kitakachowafurahisha mno wakazi
wa
Jannat
?
Je yatakuwa ni vinywaji, vyakula, sauti kama
za muziki zitokanazo na matawi na majani ya miti ya
Jannat
, au nyimbo zitakazokuwa zikiimbwa na hawa
hur al-‘Ayn ama mmoja mmoja au
kimakundi, zitakazokuwa zikimsifu Allah swt na kumtukuza ?
Katika Tafsiri ya
Tafsir,
al-’Ayyashi,
kama ilivyoandikwa katika uk. 139, J. 8, ya
Bihar
al-Anwar,
anamnakili Abu Baseer akimnakili Abu Abdullah Imam Ja’fer
al-Sadiq a.s. akisema, ‘Wakazi wa
Jannat
watastarehe
vyakula na vinywaji zaidi kuliko masuala ya kujamiiana.”
Katika ukurasa
wa 438-439 ya kitabu cha Ali ibn Ibrahim
Tafsir,
kama ilivyonakiliwa katika uk. 120-121, J. 8, ya al-Majlisi
Bihar al-Anwar,
imeelezwa kuwa Ibn Abu
‘Umayr anamnakili Abu Busayr kuwa yeye alimwuliza mara moja Abu Abdullah Imam
Ja’fer al-Sadiq a.s. kuchochea hisia zake za matamanio kuhusu
Jannat
, Imam a.s. alimjibu, “Ewe Abu
Muhammad ! Je kunaweza kuhisiwa manukato mazuri kabisa ya
Jannat
hata kutokea mwendo
wa maelfu ya miaka, na makazi patakatifu katika
Jannat
ni yale ambapo
Majini
na wanadamu watakwenda; humo watahudumiwa
vyakula na vinywaji vya kila aina bila ya kupungua au kuisha kwa kitu chochote
kile.
Bora miongoni mwa wakazi za
Jannat
ni yule ambaye, atakapoingia katika mabustani
yake, ataona mabustani matatu ( na wala si bustani moja ) iliyojaa wanawake,
wajakazi, mito na matunda ya kila aina ambayo yatafurahisha macho na moyo wake
kwa furaha isiyoelezeka. Mtu huyo atakapokamilisha kumshukuru na kumtukuza
Allah swt, yeye ataambiwa kukiinua kichwa chake kwa ajili ya kuiangalia Bustani
ya pili, kwani kutakuwamo yale yasiyokuwamo katika Bustani ya kwanza. Kwayo,
atamsifu na kumtukuza Allah swt na kumwomba, “Ewe Mola wangu ! Ninakuomba unipe
Bustani hii (badala ya ile ya kwanza)!
Kwa hayo Allah swt atamwambia, Iwapo nitakupa Bustani hii, basi wewe
utaanza kunitaka nikupatie nyingine badala ya hii !
Basi huyo mtu atasema, “Kwa hakika hii tu
ndiyo ninayoihitaji, Ewe Mola wangu!”
Na
wakati atakapoingia humo ndani, furaha zake zitaongezeka zisizo na kifani, na
atamshukuru na kumsifu na kumtukuza Allah swt, na hapo ndipo milango
itakapoamrishwa kufunguliwa na ataambiwa kuinua kichwa chake.
Pale Bustani ya
milele itakapokuwa wazi mbele yake, yeye ataangalia mara kwa mara kama
alivyokuwa ametaza hapo awali. Wakati furaha zake zitakapokuwa zimezidi kifani,
atasema, “Usifiwe Ewe Mola wangu ! Kwa hakika sifa hazina kiwango cha kukusifu
kwa yale yote uliyonijaalia : Bustani na kuniepusha na
Jahannam
( Motoni ).”
Hapo,
Abu Busayr hakuweza kujizuia kwa kuangua kilio, na alijikaza na akamwomba Imam
a.s. amwelezee zaidi.
Al-Imam Muhammad
al-Baqir a.s. akaendelea kumwambia, “Ewe Abu Muhammad! Katika kingo za mito ya
Jannat
kuna wanawake wanaowasubiri waume
zao kama vile zilvyo miti iliyoota katika mstari. Pale atakapomchukua mmoja,
basi mwingine atakuwa ameshawekwa kuziba pengo hilo.”
Abu Busayr
akasema, “Niwe fidia kwako! Tafadhali sana naomba uniambie zaidi!”
Al-Imam Muhammad
al-Baqir a.s. aliendelea kumwambia, “Mumin
ataozeshwa kwa bikira mia nane, elfu nne
tayyibs
(ni wanawake waliokua ama hawakuolewa ambao ni wajane wacha-mungu wema au
waliochiwa na waume zao) na
hur al-‘Ayn
wawili.”
“Bikira mia nane ?!” Abu Busayr
alimwuliza Al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. kwa mshangao mkubwa sana. “Naam. Yeye
atawaona hivyo hivyo pale atakapojamiiana nao.”
“Maisha yangu yaweyametolewa kwa ajili yasko,” alisema Abu Busayr, “ Je
hur al-‘Ayn
wameumbwa kwa kitu gani ?”
Al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. alimjibu kuwa wameumbwa kwa mada ya
Jannat
iliyoumbwa, na kuongezea, “miguu
yao itakuwa ikionekana hata kama kutavishwa mavazi sabini.”
Abu Busayr
alimwuliza Al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. ,”Maisha yangu yawe fidia kwako, je
wanazungumza chochote huko ?”
Al-Imam
Muhammad al-Baqir a.s. alimjibu, “Wao wanazungumza yale ambayo hakuna mwanadamu
aliyewahi kuyasikia.”
Abu busayr
aliuliza, “Je ni nini hayo ?”
Al-Imam
Muhammad al-Baqir a.s. alimjibu, “ Sisi tutaishi milele na kamwe hatutakufa!
Sisi ni wale waliobarikiwa, hivyo kamwe hatutahangaika na kutaabika ! Sisi ni
wale tuishio na kamwe hatutatengana ! Sisi ni wale wenye furaha na kutosheka,
hivyo kamwe hatuna mashitaka ! Habari njema kwa wale waliokuwa wameumbwa kwa
ajili yetu, na habari njema kwa ajili ya wale tuliokuwa tumeumbiwa! Sisi ni
wale ambao kama tungening’inia angani, basi nuru yetu ingeling’arisha kila
sehemu .’”
Ibn Qawlawayh,
na vile vile al-Majlisi ambaye katika uk. 143, J. 8, ya kazi yake
Bihar al-Anwar,
anamnakili Sa’d
akimnakili Ibn ‘Eisa akimnakili Sa’ eed ibn Janah akimnakili Abdullah ibn
Muhammad akimnakili Jabir ibn Yazid akimnakili Imam Abu Ja’fer al-Baqir (as)
akiwanakili Mababu zake a.s. ( yaani ma-Imamu a.s.) wakisema kuwa Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. alisema, “Mitume yote imekatazwa kuingia
Jannat
kabla yangu, na mataifa yote
yamekatazwa kuingia humo kabla ya waumini watufuatao sisi, sisi Ahlul Bayt
a.s., kuingia ndani mwake.” Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amenakiliwa
akisema, uk.139, J.8 ya
Bihar al-Anwar,
akisema, “Jannat
inayo milango
sabini na moja ya kuingilia : Ahlul Bayt a.s. yangu na wafuasi wao wataingilia
milango sabini, wakati ambapo watu wengine wataingilia mlango uliobakia.”
Furaha nyingine
ya
Jannat
ni kwamba kule hakuna
kuzeeka kwa wakazi wa
Jannat
, na
kamwe hawatapatwa na maumivu ya aina yoyote yale, na kamwe hawatataka
kujisaidia kwa choo ndogo au kubwa; na badala yake kile wakilacho kitatoka
mwilini kama jasho lenye manukato mazuri mno. Hawatakuwa na ukiritimba wa aina
yoyote ile na kamwe hawatanyimwa kitu chochote kile. Matamanio yao yatatimizwa,
na furaha zao kamwe hazitaisha na kamwe hawatajisikia wanyonge wasio na raha. Tunamwomba
Alah swt atuingize
Jannat
bila ya kujali mema kiasi gani tufanyayo,
kwani Yeye ndiye pekee wakutuhurumia na kutufanyia hisani. Yeye ndiye
anayetujaalia moyoni mwetu moyo wa kufanya mema: Ni yeye pekee anayetuwezesha
sisi kufanya mema, na ni Yeye pekee ambaye anakubalia mema yetu na kutulipa
thawabu zake, kwani ni dhahiri kuwa sisi
tusingaliweza kujifanyia mema kwa uwezo wetu wenyewe. Allah swt ndiye pekee
chanzo cha wema na ndiye wema pekee.
Mwishoni, kila
mtu anajawa na shauku ya kujiuliza vile
Jannat
itakavyokuwa kwa ujumla. Kwa mujibu
wa habari tulizozisoma hapo juu, kuhusu
Jannat
‘Adnan
inaelezwa kuwa itakuwa ni
mzunguko na Bustani ya Eden itakuwa katikati ikizungukwa na Bustani zinginezo
za wale waliokuwa wafuasi na wapenzi wa ahlul Bayt a.s. ya wananyumba ya Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. na kuyafuata matendo yake,wakizungukwa na wale
waliokuwa waaminifu kwao kwa maneno na vitendo, n.k. Iwapo utaendelea kutoka
hoja hiyo, iwapo upeo wa matendo na malipo yako yatakavyokuwa kidogo, ndivyo atakapokuwa
katika
Jannat
na furaha zake. Ukiwa na daraja la juu basi
utafaidika zaidi, na ikiwa daraja lako ni chini kidogo basi, na starehe za huko
pia zitakuwa zimepungua kidogo. Uduara unamaanisha kudumu kwa milele. Bustani
hiyo inadhaniwa kuwa ni duara, lakini Allah swt ndiye ajuaye zaidi.
Sababu zimfanyazo mtu kuingia Jannat
Kwa hakika Imani na matendo
mema ndiyo masuala bora kabisa na ambayo yanamletea furaha mtu na inasadikiwa
kuwa ndiyo ufunguo wa
Jannat
na baada yake sababu zote zitakazoendelea
kuelezwa basi mutaona kuwa zote hizo ni matawi ya hoja hili na Allah swt pia
anasema kuhusu Imani na Matendo mema kuwa mtu yeyote atakayetekeleza hayo humu
duniani basi Allah swt lazima atamjaalia
Jannat. Allah swt
anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura
al-Baqarah ,2 , Ayah 82
Na wale walioamini na wakatenda mema,
hao ndio watu wa Jannat , humo watadumu.
Taqwa inamaanisha
kujiepusha yaani yale yote yaliyosemwa na Ahlul Bayt a.s. ya Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. kuwa ni halali basi ndiyo halali na yale yote yaliyosemwa ni
haramu basi yawe ni haramu. Allah swt ametoa ahadi kuwa atakayeishi kwa Taqwa
basi mahala pake patakuwa ni
Jannat. Na hivyo ndivyo maana anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura
al-Maryam ,19 ,
Ayah 63 :
Hiyo ndiyo Jannat tutayowarithisha katika waja wetu
walio kuwa wachamungu
Vile vile
twaambiwa katika Qur’ani Tukufu , Sura
al-Hujurat ,49, Ayah 13 :
Enyi watu ! Hakika Sisitumekuumbeni kutokana na
mwanamume na mwanamke. Na tumekujaalieni kuwa na mataifa na makabila ili
mjuane. Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu kwa
Allah swt ni
huyo aliye mchamungu zaidi katika nyinyi….
Yaani kuwafanyia
watu mambo mema na matendo yetu yawe mema kwa ujumla na kwa hakika haya ndiyo
mambo mema na bora kabisa na ndiyo sababu za kuingia
Jannat. Allah swt anatuambia
katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Maidah,5, Ayah 85 :
Basi Allah swt atawalipa, kwa yale waliyoyasema,
Bustani zipitazo mito katika yake; humo watadumu. Na haya ndiyo malipo ya wafanyao
wema.
Allah swt
anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al- Tawbah, 9, Ayah 111
Hakika Allah swt amenunua kwa Waumini nafsi zao na
mali zao kwa kuwa wao watapata Jannat. Wanapigana katika Njia ya Allah swt –
wanauwa na wanauwawa. Hii ni ahadi aliyojilazimisha kwa Haki katika Taurati na
Injili na
Qur'an. Na nani atimizae ahadi
kuliko Allah swt ? Basi furahini kwa biashara yenu mliy fanya naye. Na huko
ndiko kufuzu kukubwa.
Yaani mtu hafuati
matamanio ya nafsi yake na badala yake anaikhilafu. Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Naziat, 79, Ayah 40 – 41 :
Na ama yule anayeogopa kusimamishwa mbele ya Allah
swt Mlezi, na akijizuilia nafsi yake na matamanio,
Basi huyo, Jannat itakuwa ndiyo makaazi yake !
Allah swt
atuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al- Waqia, 56, Ayah 10 – 13 :
Na wa mbele watakuwa mbele.
Hao ndio watakao karibishwa
Katika Bustani zenye neema.
Tumeshaona kuwa
Jihadi imeshatajwa hapo mwanzoni (
Jihadi na kuwa Shahidi, nam. 4 ) hapa Jihadi imekuja lakini pamoja na Hijrah.
Yaani Hijra ni Jihadi mojawapo kwa ajili ya Mumin. Tumeona kuwa Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. aliiacha Makkah na kwenda Madina, hii ilikuwa ndiyo Jihadi
mojawapo ambayo ndiyo kwa ajili ya Allah swt na Dini.
Allah swt
anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al- Tawbah, 9, Ayah 20-22 :
Wale walioamini na wakahama, na wakapigana Jihadi
katika
njia ya Allah swt kwa mali yao na
nafsi zao, hao wana cheo kikubwa zaidi mbele ya Allah swt . Na hao ndio wenye
kufuz.
Mola wao Mlezi anawabashiria rehema zitokazo kwake,
na radhi, na Bustani ambazo humo watapata neema za kudumu.
Watadumu humo milele. Hakika kwa Allah swt yapo
malipo makubwa.
Kufanya Subira na
Ustahimilivu wakati mtu anapopatwa na shida na matatizo mbalimbali ama
yakupoteza mali, kufiwa, kuugua n.k
Katika vitabu tunapata habari kuwa Mitume a.s na Maimamu a.s. pia
wamepitia shida kali kali ambazo wao wamezifanyia subira na ustahimilivu kwa
ajili ya furaha ya Allah swt . Qur’ani Tukufu , Sura al-Dahar, 76, Ayah 12 :
Na atawajaza Bustani za Jannat na maguo ya hariri
kwa vile walivyo subiri
Vile vile Allah
swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Ra’d, 13, Ayah 24 :
Hao ndio watu wa Jannat, watadumu humo, kuwa ni
malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.(Wakiwaambia) Assalamu ‘Alaikum ! amani iwe
juu yenu, kwa sababu ya mlivyo subiri! Basi ni mema mno
malipo ya Nyumba ya Akhera.
Inambidi mtu awe
madhubuti katika Dini kama ukuta wa Shaba yaani awe na uwezo wa kukabiliana na
kila sura itakayojitokeza mbele yake kiasi kwamba kamwe hataweza kulega lega
katika dini na kamwe hataweza kurudi nyuma katika msimamo wake wa Dini. Allah
swt anasema katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Ahqaf, 46,
Ayah 13 – 14 :
Hakika waliosema:Mola wetu Mlezi ni Allah swt ;
kisha wakatengenea, hawatajuwa na khofu, wala hawatahuzunika.
Inatubidi sisi
kumtii Allah swt pamoja na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ili kuwa mustahiki
wa
Jannat
. Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa, 4, Ayah 13 :
…. Na anayemtii Allah swt na Mtume wake, Yeye
atamtia katika Jannat zipitazo mito kati yake, wadumu humo. Na huko ndiko
kufuzu kukubwa.
Iwapo kama
hakutakuwapo na uhalisi katika kila jambo basi hakutakuwa na usahihi wa kitu au
jambo hilo. Uhalisi lazima uwepo katika Imani, matendo na akili na fahamu zetu
na kwa hakika huu ndio ufunguo wa kuingia
Jannat
na
ndivyo maana Allah swt ameweka sharti hili la kumwezesha mtu kuingia
Jannat
na Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu
, Sura al-Safaat, 37, Ayah 39 – 43 :
Wala hamlipwi ila hayo hayo mliyokuwa mkiyafanya.
Isipokuwa waja wa Allah swt
walio khitariwa.
Haom ndio watakaopata riziki maalumu,
Matunda, nao watahishimiwa.
Kwa hakika sharti
hili ni la umuhimu wa aina yake kwani kila jambo tulifanyalo linahitaji ukweli
na kama hakuna ukweli basi kila kitu kitaharibikiwa. Allah swt anatuambia
katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Maidah,5, Ayah 119 :
Allah swt atasema: Hii ndiyo Siku ambayo wasemao
kweli utawafaa ukweli wao. Wao watapata Bustani zipitazo mito kati yake. Humo
watadumu milele. Allah swt amewawia radhi, nao awe radhi naye. Huku ndiko
kufuzu kukubwa.
Inambidi kila mtu
atulie na kujitakasisha nafsi yake mwenyewe kwa kila jambo na hivyo alete
mapinduzi ndani mwake. Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura Ta-Ha,
20, Ayah 75– 76 :
Na atakayemjia naye ni Muumini aliye tenda mema,
basi hao ndio wenye vyeo vya juu.
Bustani za milele zipitazo mito kati yake,wadumu
humo. Na hayo ni malipo ya mwenye kujitakasa.
Allah swt anatutaka
sisi tule na tuwalishe wengine pia tuwe wakarimu na kamwe tusiwe mabakhili na
tuombe Tawba kwa ajili ya madhambi yetu. Allah swt anatuambia katika Qur’ani
Tukufu , Sura Ali Imran, 3,
Ayah
133-136 :
Na yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi, na Jannat
ambayo upana wake ni mbingu na ardhi, iliyowekwa tayari kwa wachamungu,
Ambao hutoa wanapokuwa na wasaa na wanapokuwa na
dhiki, na wanajizuia ghadhabu, na wasamehevu kwa watu; na Allah swt huwapenda
wafanyao wema;
Na ambao pindiwafanyapo uchafu au wakjidhulumu nafsi
zao humkumbuka Allah swt na wakamwomba msamaha kwa dhambi zao – na nai
anayefuta dhambi isipokuwa Allah swt ? – na wla hawapendelei na waliyo yafanya
na hali wanajua.
Hao malipo yao ni msamaha kwa Mola wao Mlezi, na
Bustani zipitazo mto kati yake. Humo watadumu, na mwema mno ujira wa watendao.
Kuna msemo kwamba
Mwogopeni yule mtu ambaye hamwogopi Allah
swt ! Na wala musimwogope yule mtu ambaye anamwogopa Allah swt !
Kwa sababu yule mtu ambaye anamwogopa Allah
swt kamwe hatakudhuru nyuma yako na atakuwa akijua kuwa Allah swt
hatafurahishwa na hatua yoyote ile ya kukuletea madhara. Ndiyo maana tunaambiwa
kuwa tusiwaogope Waumini, tuongee nao waziwazi bila ya kuwa na hofu ya aina
yoyote, lakini bila ya kuwatuhumu.
Lakini yule asiye na hofu ya Allah swt atatafuta kila hila na mbinu za
kukudhuru wewe kwa sababu hana hofu ya Allah swt. Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Rahman, 55,
Ayah 46 :
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Allah swt
atapata Jannat (Bustani) mbili
Vile vile
nitapenda kuwaleteeni Hadith ya Al-Imam Ja’afar as-Sadiq a.s. amesema katika
Majma’ul Bayan :
“Mtu yeyote ambaye anajua na kutambua wazi kuwa mimi
nifanyapo jema au baya, basi Allah swt yupo anashuhudia matendo yangu haya,
basi mtu kama huyu daima atakachokuwa akikifanya basi atakuwa mwangalifu mno
katika matendo yake na atajiambia kuwa lau nitafanya kazi hii njema basi Allah
swt atalipa mema kadha na kadha na lau nitafanya maasi na madhambi, basi Allah
swt ataniandikia adhabu kadha wa kadha. Kwa hivyo watu kama hawa wamewekewa
Bustani mbili katika
Jannat.”
Ama kuhusu mtu
atakaye fuata masuala haya mawili basi Allah swt atamjaalia
Jannat
na uthibitisho wake ni kwa mujibu wa Qur’ani
Tukufu , Sura al-Mujadilah, 58, Ayah 21 :
Allah swt ameandika : Hapana shaka Mimi na Mtume
wang tutashinda. Hakika Allah swt ni Mwenye nguvu, mwenye kushinda.
Tawalla maana yake ni kuwa rafiki wa Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. na Ahl al-Bayt a.s. na
Tabarra
inamaana ya kujiepusha na kujiweka mbali na kutokuwa na uhusiano wowote pamoja
na wale maadui wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. pamoja Ahl al-Bayt a.s.
Katika maana yake
ni kwamba inambidi kila Mwislamu awe akisali sala zote zilizofaradhishwa juu
yake kwa kuzingatia umuhimu na nyakati zake. Zipo Sala nyingi ambazo
tumefaradhishiwa katika Islam kwa mfano Sala tano za siku, Sala za matukio kama
mitetemeko, kupatwa kwa jua au mwezi, n.k. (rejea vitabu vya
fiq-hi). Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Ma’arij, 70,
Ayah 22 -34 :
Isipokuwa wanaosali,
Ambao wanadumisha Sala zao,
Na ambaokatika mali yao iko haki maalumu
Kwa mwenye kuomba na anayejizuilia kuomba;
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao
Mlezi.
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo
Na ambao anahifadhi tupu zao.
Isipokuwa kwa wake zao, au iliyowamiliki mikono yao
ya kuume, basi hao hawalaumiwi –
Lakini wanaotaka kinyume ya haya, basi hao ndio
wanaoruka mipaka.
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
Na ambao wanazihifadhi sala zao.
Hao ndio watakao hishimiwa Jannat.
( Motoni )
Maelezo juu ya Jahannam ( Motoni )
Waislamu
wanatimiza nguzo ya Sumu kwa sababu waweze kuepukana na adhabu za
Jahannam
.
Je
Jahannam
ni mahala pa
namna gani na humo kuna adhabu za aina gani
?
Kumeandikwa
vitabu vingi vikizungumzia swala hili. Qur’an Tukufu inayomaelezo ya kutosha
yanayozungumzia mateso na adhabu za kiakili na kimwili kwa ajili ya wale
watakaoingizwa humo kwa kutokana kwao kutoishi vile alivyotaka Allah swt, kwa
sababu wao hawakutimiza ahadi yao pamoja na Allah swt alivyokuwa amewapa, ambao
hawakutimiza makusudi ya kuumbwa kao yaani kumwabudu Allah swt na si mwingine.
Adhabu kama hizo
zinaweza kuangaliwa na kurejewa katika Surah zifuatazo :
al-Baqarah,Aali-’Imran,
alMaaida, al-An" am, al-A’raf, al-Anfal, Younus, Hud, al-Ra’d, al-Hijr,
al-NahI, Maryam, Taha, al-Hajj, al-Muminoon, al-Noor, al-Furqan, al‘Ankabut,
Luqman, al-Sajdah, al-Ahzab, Saba, al-Zumar, Ohafir, al-Tur, al-Hashr,
al-Ma’arij, al-furuj, al-Fajr, al-Nisaa., Katika Surah nyingi, kwa hakika
Qur’an imeteremka kuwaonya wanaadamu dhidi ya moto wa
Jahannam
na kuwaelekeza
katika furaha ya kudumu milele : Ufalme usiokwisha kamwe.
Je
Jahannam
ina umbo gani la kuonekana ?
Tupitie Ayah ya Qur’an Tukufu Surah ya
Al-Balad, 90, Ayah ya 19-20 zisemazo :
Lakini waliokanusha Aya Zetu, hao ndio
watu wa upande wa shari. Moto uliofungiwa (kila upande) utakuwa juu yao.
“Kufungiwa
inamaanisha kufunikwa;
Jahannam
inaweza kulinganishwa kama mtungi, wenye
kifuniko, juu ya jiko, kwamba chungu kinachomwa ndani na nje.
Maana itakuwa wazi zaidi tusamapo Ayah
zifuatazo za Qur’ani Tukufu
Surah
al-Humazah, 104, Ayah 5 – 9 :
Hasha! Bila shaka atavurumizwa katika
(Moto unaoitwa)
Hutama.
Na ni jambo gani litakalokujulisha (hata
ukajua) ni nini ( Huo Moto unaoitwa ) Hutama ? Ni Moto wa Allah swt uliowashwa
(kwa ukali barabara ). Ambao unapanda nyoyoni. Hakika huo (Moto) watafungiwa
(wewemo ndani yake ). Kwa magogo marefu marefu
“Kufunikwa
juu yao” inamaanisha sawa na vile ilivyo katika Ayah ya 90 : 20 hapo juu. Na
mistari yake inaweza kumaanisha kwenda undani zaidi, na mistari hiyo
‘inaongezeka,’ kiurefu, na kwa hakika Allah
swt ndiye ajuaye zaidi.
Je miale ya moto wa
Jahannam
iko yenye ukubwa
kiasi gani ? Jibu lake tunapewa na Muumba wetu na
Jahannam
Qur’ani Tukufu
Surah al-Mursalat, 77: Ayah ya 32:
"Hakika (Moto huo) hutoa macheche yaliyo kama majumba."
Katika
mlango wa kwanza wa
Jahannam
kumeandikwa sentenso tatu:
Yeyote yule atakayekuwa na matumaini katika Allah swt basi daima atakuwa mtu
mwenye furaha na mafanikio; Yeyote anayekuwa na khofu ya Allah swt basi
anajaaliwa usalama; mtu mwovu na aliyepotoka na mstahiki wa adhabu za Allah swt
ni yule ambaye hana matumaini yoyote kwa Allah swt na wala hana khofu ya aina
yoyote ile ya Allah swt.
Katika
mlango wa pili wa
Jahannam
kumeandikwa yafuatayo: Yeyote yule asiyetaka kufanywa uchi
Siku ya Qiyama, basi awavalishe nguo wale walio uchi humu duniani, Yeyote yule
asiyetaka kupatwa na kiu Siku ya Qiyamah, basi awanywishe wale wenye kiu humu
duniani, Yeyote yule asiyetaka kupatwa na njaa Siku ya Qiyamah, basi awalishe
wale wenye njaa humu duniani.
Katika
mlango wa tatu wa
Jahannam
kumeandikwa : Allah swt huwalaani wale wasemao uongo,
Allah swt huwalaani wale walio mabakhili,
Allah swt huwalaani wale wanaowanyanyasa na kuwakandamiza wanyong.
Katika
mlango wa nne wa
Jahannam
kumeandikwa sentenso tatu: Allah swt humdhalilisha yule
ambaye anaidharau Dini ya Islam,
Allah
swt humdhalilisha yule anayewakashifu Ahl al-Bayt a.s. ya wananyumba ya Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. ; Allah swt humdhalilisha yule ambaye anawasaidia
wadhalimu katika kuwadhulumu watu.
Katika
mlango wa tano wa
Jahannam
kumeandikwa sentenso : Msiendekeze matamanio yenu, kwani
matamanio yanapingana na tendo la kusadikisha;Musiyaongelee zaidi yale yasiyowahusu
kwani mtaondoka katika Baraka za Allah swt; na kamwe msiwe wasaidizi wa
madhalimu.
Katika
mlango wa sita wa
Jahannam
kumeandikwa sentenso: Mimi nimeharamishiwa kukubalia
Mujtahid (hawa ni wale ambao wamefikia
upeo wa
Ijtihad, uwezo wa kutoa
fatwa. Rejea vitabu vya
Fiqh ndipo utakapoweza kupata ilimu
zaidi katika somo hili). Mimi nimeharamishiwa kukubalia wale wanaofunga saumu.
Katika
mlango wa saba wa
Jahannam
kumeandikwa sentenso tatu: Ujihisabie mwenyewe matendo
yako kabla hujafanyiwa hisabu ya matendo yako; ikaripie nafsi yako kabla wewe
hujakaripiwa; na mwabudu, Allah swt aliye Mkuu na aliyetukuka, kabla ya wewe
hujafika mbele yake na ambapo hautaweza tena kumwabudu na kumtukuza.
Kwa kuwa marejeo
kuhusu
Jahannam
yapo yanapatikana kwa wingi kutoka Qur’ani
Tukufu, sisi sasa tutajaribu kurejea mapokezi na maelezo kuhusu
Jahannam
kutokea
Ahadith za
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na Ma-Imamu a.s. kuhusu
adhabu,vitisho vya
Jahannam
, mahala
palipojaa joto la hali ya juu yenye kuumiza, mahala ambapo moto wake unawekewa
vipande vya kiberiti au mrututu ambayo kila moja ni kubwa kama milima mikubwa
kabisa ulimwenguni. Zipo sehemu kubwa kabisa kama hizo ambapo wale waliokwisha
adhibiwa hupelekwa kupoozwa na kugandishwa kama barafu. Kwa maneno mengine,
wanatolewa kutoka hali moja ya mto mkali
kabisa na kupelekwa katika hali nyingine ya bariki kabisa. Katika sayari yetu
kuna milima yenye theluji na milima yenye kutoa volkeno ambayo hutoa miyeyuko
ya mawe kama lava; na hivyo ndivyo ilivyo hali ya
Jahannam
: kuna hali zote mbili za joto kali na baridi kali.
Katika uk.309 ya
kitabu cha al-Selek,
The Divine
Traditions, mkusanyiko wa
Ahadith
al-Qudsi, Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amenakiliwa akisema kuwa siku
moja
Jahannam
ilimlalamikia Allah swt kwa kusema, : “Ewe
Mola! Hata sehemu zangu zinateketezana!” na kwa hayo Allah swt aliiruhusu
kupumua mara mbili, mara moja katika majira ya baridi na mara nyingine katika
majira ya joto kali. Kwa sababu ya kupumua kwake huku ndiko kumetokezea misimu
hii miwili yenye joto kali na baridi kali. Iwapo Allah swt angalikuwa ameruhusu
zaidi ya mara mbili basi kusingalikuwapo na maisha ulimwenguni humu.
Chakula
cha watu wa Jahannam
na Jannat
Wakati wakazi wa
Jannat
watakuwa wakila kila aina ya matunda mazuri na
yenye ladha tamu, wakazi wa
Jahannam
watakuwa
wakila chakula kama miiba ambayo itakuwa ikiwasakhama katika koo zao, kamwe
haitawafikia tumboni mwao, na wala hawataweza kutapika.
Na hii ndiyo chakula mojawapo ya watu wa
Jahannam
. Aina nyingine ya chakula
kinachotayarishwa kwa ajili ya wakazi wa
Jahannam
ni usaha wa majeraha ya wale
wanaopata mateso katika
Jahannam
, na
kuchemshwa katika joto la kupasua matumbo yao.
Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. amenakiliwa katika uk.145, J.1 ya al-Zamakhshari’s
Rabee’ al-Abrar akiwa amemwuliza Malaika
Jibrail a.s., “Je ni kwa nini mimi kamwe sijamwona Malaika Mikaili a.s.
akicheka au kutabasamu?” Malaika Jibraili a.s. alimjibu: “Mikaili kamwe
hakucheka wala kutabasamu kuanzia pale
Jahannam
ilipoumbwa. ”
Anas, Allah swt airehemu rohoyake,
amenakiliwa na al-Zamakhshari akisema kuwa mfano wa kiwango kidogo kabisa cha
adhabu ya
Jahannam
ni kama kwamba mtu anatengenezewa pea ya viatu
ambavyo anapovaa bongo inachemka na kutokota. Habari zaidi kuhusu sehemu hii ya
kutisha zinapatikana katika al-Zamakhshari, ambazo ni kama zifuatazo :
Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. amesema, “Katika safari yangu ya usiku wa (‘Israa), mimi
nilisikia sauti kubwa mno, hivyo nilimwuliza Malaika Jibrail a.s., ‘Je sauti
hii kubwa ni ya nini, Ewe Jibraili ?’
Naye alinijibu, ‘Ni jiwe lililotupwa kutokea juu kuangukia ndani mwa
Jahannam
, na imekuwa ikianguka kwa muda
wa vipindi sabini vya baridi, na sasa ndipo ilipofika chini.”
Abu ‘Asim ‘Ubayd
ibn ‘Umayr ibn Qatadah al-Laythi, Hakimu wa Makkah (d.
Abu Sa’eed
al-Khudri amenakiliwa akisema, “iwapo milima itapigwa kwa rungu mara moja
inayotumiwa na Malaika wa
Jahannam
,
basi itavunjika vipande vipande na kuwa vumbi.”
Tawoos ibn
Keesan al-Khawlani amenakiliwa akisema, “Wakati
Jahannam
ilipoumbwa, Malaika walishtushwa mno, na wakati nyie
wanaadamu mulipoumbwa, basi walitulia.”
Al-Hasan ibn
Yasar al-Basir amesema, “Kwa kiapo cha Allah swt! Hakuna hata mja mmoja wa
Allah swt anayeweza kustahimili joto
Hisham ibn
al-Hassan al-Dastoo’i alikuwa hazimi taa wakati wa usiku, na wakati wananyumba
yake walipompinga kwa kumwambia, “Sisi hatuwezi kutofautisha baina ya usiku na
mchana !” Yeye aliwajibu, “Kwa kiapo cha Allah swt ! Mimi ninapozima taa wakati
wa usiku, hukumbuka kiza kikali cha kaburini, na hivyo sipati usingizi.”
Adhabu katika
Jahannam
itakuwa kwa mujibu wa aina za madhambi
zilizofanywa wakati wa maisha ya mtu humu duniani. Kwa mfano, Wale ambao
walilimbikiza mapesa humu duniani bila ya kutoa
Zaka na kodi zinginiezo za kidini, basi hao watachomwa kwenye paji
la uso kwa yale waliyoyalimbikiza, pembeni mwao, na migongoni mwao. Kwa maneno
mengine, sehemu zote za mwili wao.
Abu Zar
al-Ghaffari, Allah swt amwie radhi, alikuwa akisema, “Waambieni wale ambao
hupenda kulimbikiza utajiri wao kuwa watachomwa nayo juu ya paji la uso wao,
pembeni mwao, na migongoni mwao hadi watakapokuwa wamejaa kwa mioto.”
Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. amesema, kama vile tuambiwavyo katika uk.243, J.8, ya
Bihar al-Anwar, “Hakuna Mja wa Mwenyezi
Mungu mwenye utajiri au mali na hataki kulipa
Zaka isipokuwa kwamba atachomwa kwa vipande hivyo vya mapesa
vitakavyokuwa vimepashwa moto katika moto wa
Jahannam
na kwamba
watatumbukizwa katika adhabu hizo kuanzia juu ya vipaji vyao vya nyuso zao na
migongo yao hadi pale Allah swt atakapokuwa amemaliza kupokea mahisabu na
adhabu za waja wake Siku ya Qiyamah, muda ambao ni wa maelfu ya miaka kwa
mujibu wa mahisabu yetu. Hapo ndipo watakapotumwa ama kuingia
Jannat
au
Jahannam
.”
Abu Umamah
anamnakili Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akielezea aina na vinywaji
watakaopewa wakazi wa
Jahannam
. Anasema, “Italetwa mbele yake, naye
atachukizwa nayo; na itakapoletwa karibu yake, itauchoma uso wake na kifuvu
kitadondoka. Iwapo ataweza kunywa hata kidogo kutokamo, basi matumbo yake
yatakatika vipandevipande na kutokezea sehemu za nyuma ya kutokezea choo.”
Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. ameripotiwa akisema, “Sala za mtu anayekunywa pombe hazikubali
kwa siku arobaini; na iwapo atakufa huku pombe ikawamo tumboni mwake, basi
Allah swt atamlazimisha anywe
sadiid,
maji yatokayo kwenye sehemu za uchi wa malaya ambayo yatakusanywa katika birika
huko
Jahannam
na kupewa watu hawa, na kwayo matumbo na ngozi
zao zitachomwa.”
Riwaya hii
imeelezwa na Shu’ayb ibn Waqid ambaye anamnakili al-Husain ibn Zayd ambaye
anamnakili Imam Ja’fer al-Sadiq a.s. kama ilivyoelezwa katika uk. 244, J. 8,
ya
Bihar
al-Anwar, “Wale wenye madhambi mbali na zinaa au mauaji, watapewa vinywaji
vya risasi na shaba iliyoyeyushwa”, kama vile Ibn Mas’ud anavyonakiliwa katika
Bihar al-Anwar akisema.
Mujahid anasema
kuwa hayo yatakuwa ni usaha na damu za wale walioadhibiwa, ambapo Ibn Jubayr
anasema ni ‘maji meusi; kwani
Jahannam
ni nyeusi, miti yake ni meusi, na nyuso na
miili ya wakazi wake pia inakuwa imegeuka kuwa nyeusi.
Hoja hii inachukuliwa
na al-Dhahhak. Adhabu za ziada zitakazokuwa zikitolewa
Jahannam
zitakuwa za nyoka
na nge ambao makucha yao yatakuwa, kwa mujibu wa Ibn ‘Abbas na wengineo
wanaripoti hivyo, makubwa na marefu kama minazi.
Nyoka watakuwa wanene kama tembo, na nge
watakuwa wakubwa kama punda weusi. Na mara kwa mara wakazi wa
Jahannam
watakuwa wakipigwa vipigo kwa makonde yao kama
marungu: Iwapo wao watakuwa katika tabaka za juu za
Jahannam
, basi vipigo hivyo
vitawaangusha katika tabaka zinginezo, na kila tabaka litakuwa na joto na
mateso makali kuliko tabaka lililotangulia, kwa muda wa miaka sabini. Mara
watakapofikia tabaka la chini, miale mikali ya moto itawatupa tena, na vivyo
hivyo itakavyokuwa ikiendelea. Hakutakuwa na muda wa kuomba msamaha kwa ajili
yao.
Je ni mahala gani palipo pabaya zaidi katika
Jahannam
?
Ibn Mas’ud na
Ibn ‘Abbas wamenakiliwa katika uk.241 – 242, J.8, ya al-Majlisi
Bihar al-Anwar anasema kuwa wanafiki
watawekwa katika tabaka la chini kabisa
Kwa sasa turejee
Nahjul Balagha na tuangalie vile
Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. anavyotupatia picha ya
Jahannam
, tumwombe Allah
swt asitutumbukize humo :
‘Janga kubwa kwa
mtu ni kule kutumbukia katika
Jahannam
;
yeye atajihisi kuwa anachemshwa mzimamzima, na ataona mateso yake yasiyona
mwisho, na kiumbe fulani kinakoroma na kupumua, viumbe vyote vilivyo humo
hukosa raha na kamwe hawapati fursa ya kupumzika, na kamwe hawatapata kupumzika
kutokana na adhabu zake au mauti ya uhakika. Yeye hasinzii hata kidogo wala
hakutakuwa na mapumziko katiko mateso yake : Kutakuwa na maumivu yakudumu kiasi
ambacho tunamwomba Allah swt atunusuru na kutusaidia .’
( Hotiba
83 ).
‘Kwa hakika ni
mahala pabaya kabisa kuliko sehemu yoyote ile, mahala ambapo mikono ya wakazi
wake yanakuwa yamefungwa shingoni mwaio, na vichwa vyao vimefungwa na miguu yao
kwa minyororo na mavazi yao yametengenezwa kwa
lami. Mashati yao yametengenezwa kwa moto wakati ambapo adhabu zao za
moto usiozimika kamwe hazitakwisha kwamwe mahala ambapo mlango wake utakuwa
umejazwa watu, katika moto mkali kabisa kiasi kwamba sauti zao zinasikitisha na
kutisha, na miale ya moto ikipaa na kufikia kila sehemu na wala hakuna kujitoa
kutoka humo na wala hakuna muda utakaokwisha,na wala haina mwisho wake kwa wale
wanaotekeezwa na kuchomwa humo.’
(
Hotuba 109 ).
‘Joto lake ni
kali mno, kufikia chini kwake ni mbali mno, sakafu yake ni chuma, vinywaji
vyake ni usaha.’
(Hotuba 120 )
‘Siku ya Qiyamah,
madhalimu wote wataletwa bila ya kuwapo na mtu yoyote wa kuwasaidia au
kuwatetea, na hivyo watatumbukizwa katika moto wa
Jahannam
na humo atasagwasagwa kama vile machine za kusaga
zifanyavyo, hadi hapo atakapojigonga kichwa katika sakafu ya chini kabisa.’ (
Hotuba 164 )
‘Iwapo Malik
(msimamizi wa
Jahannam) atakuwa
mkali, husababisha sehemu yake moja kuminyana na sehemu zingine, anapogombeza,
milango yake huruka juu na chini (hutema kama volkano). (Hotuba 183 )
Mazungumzo juu
ya
Jahannam
yanatudhihirishia wazi
kuwa umbali, mahala na nafasi ni vitu vya uhakika katika maisha yajayo kama
vile yalivyo katika maisha yetu haya. Ushahidi wa kusema kuwa
Jahannam
itasogezwa au kupelekwa sehemu moja kutokea
sehemu nyingine, unapatikana katika Ayah ya 23 ya Surah al-Fajr (Surah namba 89
) na katika Ayah zinginezo pia :
Basi Siku hiyo italetwa Jahannam. Siku
hiyo mwanadamu atakumbuka, lakini kukumbuka huko kutamfaa nini ?
Kwa hakika wale
watakaokuwa wakiihamisha
Jahannam
kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa
Amri ya Allah swt, hawatakuwa wenfgine isipokuwa ni Malaika ambao sisi
hatuwaoni duniani humu lakini punde tutakapo kufa, tutaanza kuwaona, naomba
mazungumzo haya juu ya Malaika tuyaachilie hapa kwani yatahitaji kutungiwa
kitabu kingine, na kwa sasa hivi somo hili litatuchukua mbali, Insha-Allah,
tutaweza kuwatungieni kitabu kingine juu ya Malaika.
Lazima ikumbukwe
kuwa picha yote iliyotolewa kuhusu
Jahannam
hatujaelezea kuhusu mateso na adhabu
yanayotokana kuwa pamoja na Mashetani, Pepo mbaya na Majini waliolaaniwa ambao
wote hao watakuwa pamoja na wanaadamu waliolaaniwa. Tukiangalia mateso
wanayopewa viumbe hivi, makelele yao, sehemu zao zikivutwa na kunyofolewa, na
wakichunwa ngozi kutoka miili yao … yanatisha mno kama
Jahannam
yenyewe. Kumbuka
vile Allah swt alivyomwelezea mwanadamu kuwa ameumbwa kwa ubora wote. Wanaadamu
watakaotumbukizwa katika
Jahannam
wataelewa
vyema zaidi kuliko wengine, wakati ambapo wale watakaokuwa wameongoka watakuwa
wamepona uhakika wa kuteswa.
Wale ambao
wamesoma masimulizi ya
Saint Joan of Arc
(1412 – 1431 ), Mfaransa mashuhuri, mbali na umri wake wa kati, aliwaongoza
Wafaransa katika ushindi dhidi ya majeshi ya Waingereza huko Orleans, kumbuka
kuwa yeye alikuwa ni Pepo mbaya, na anapendelea kutembea juu ya miti iwakayo
moto kutokea ncha moja ya dunia hadi nyingine kuliko kuangalia tu. Sasa hebu
fikiria kuwa nao katika Pepo za milele. (Yeye haoni ajabu kutembea juu ya moto,
je na wewe unaomsimamo kama huo…?)
Kwa kifupi hivyo
ndivyo ilivyo
Jahannam
na adhabu na
mateso yake. Kama tungaliweza kuangalia hata mara moja au kuwaangalia wakazi
wake, basi kwa hakika tusingalijali kufunga saumu kila siku ya maisha yetu, na
wala si katika mwezi wa Ramadhani tu, Mwezi wa Allah swt, mwezi
wa msamaha na baraka, lakini maisha yetu
yote.
Sababu zimfanyazo mtu
kuingia
Jahannam
Hoja hii ipo ya
kwanza katika mfululizo wa sababu za kumfanya mtu aingie
Jahannam
na sababu zote zifuatazo
ndizo matawi ya
Kufr na Nifaq na
Allah swt amewafanyia makhususi
Jahannam
watu wenye sifa hizi mbili. Allah swt
anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa, 4,
Ayah 140 :
Naye amekwisha kuteremshieni katika Kitabu hiki ya
kwamba mnapo sikia Aya za Allah swt zinakanushwa na zinafanyiwa kejeli, basi
msikae pamoja nao, mpaka waingie katika mazungumzo mengine. Hivyo mtakuwa nanyi
mfano waohao. Hakika Allah swt atawakusanya wanafiki na makafiri wote pamoja
katika Jahannam.
Vile vile Allah swt
anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa, 4 ,
Ayah 145 :
Hakika wabnafiki watakuwa katika tabaka ya chini
kabisa Jahannam , wala hutompata yeyote wa kuwanusuru.
2. Kuwazuia wale wanaotenda kazi katika njia ya
Allah swt
Kuna watu wengi
ambao wanatabia ya kuzua uzushi na kuwazuia kwa njia mbali mbali wale
wanaofanya tabia na kutenda matendo mema kwa mujibu wa Sunnah na tabia ya Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. na Ahl al-Bayt a.s. kwa hivyo watu kama hawa ndio
waliowekwa katika sababu ya kwanza ya kuingizwa
Jahannam
. Allah swt anatuambia
katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa, 4
,
Ayah 55 :
Basi wapo miongoni mwao walioamini, na wapo
walioyakataa. Na Jahannam yatosha kuwa ni moto wa kuwateketeza.
Leo kila mzazi
anataka watoto wake wamfuate na kumtii vile atakavyo yeye mwenyewe akiwa kama
mzazi na vile vile kila atengenezacho mtu hutegemea kuwa kitu hicho kitamfaa na
kumfanyia kazi kwa makusudio ya kukitengeneza na ndivyo vivyo hivyo Allah swt
ametuumba sisi pamoja viumbe vingine vyenye uhai na visivyo na uhai kwa sababu
na makusudio maalumu, nayo ni utiifu kwa Amri Zake na kumfuata Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. pamoja na Ahl al-Bayt a.s.
Hivyo kwa
kutomtii Allah swt na
Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. pamoja na Ahl al-Bayt a.s. ni dhambi kuu na ndicho
kitakachotutumbukiza
Jahannam
moja kwa moja. Allah swt anatuambia
katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Jinn, 72 , Ayah 23 :
….. Na wenye kumuasi Allah swt na Mtume wake, basi
hakika hao watapata Moto wa Jahannam wadumu humo milele.
Vile vile twaambiwa na Allah
swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa, 4 , Ayah 115 :
Na anayempinga Mtume baada ya kudhihirikia uwongofu,
na akafuata njia isiyokuwa ya Waumini, tutamuelekeza aliko elekea, na
tutamwingiza katika Jahannam. Na hayo ni marejeo maovu.
4.
Kudhihaki
Ayah za Allah swt
Kuna baadhi yetu
tunayo tabia ya kuzifanyia dhihaka Ayah, amri na hukumu za Allah swt ambapvyo
ni tabia ovu kabisa na hatimaye humtumbukiza
Jahannam
bila ya yeye kutambua
athari mbaya ya tabia yake hiyo. Upeo wetu wa ilimu na maarifa ni mdogo sana
kiasi cha kutufanya sisi tukajivunia na kufanya ufakhari mbele ya Allah
swt
na tukajifanya hodari mbele ya
maamrisho yake. Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Kahaf, 18,
Ayah 106 :
Hiyo Jahannam ni malipo yao kwa walivyokufuru na
wakafanyia kejeli Ishara zangu na Mitume wangu.
5.
Kutotumia
viungo vya mwili dhidi ya Allah swt
Tunaonywa kuwa
tusivitumie viungo vyetu vya mwili kama macho, mdomo, masikio, miguu na mikono,
n.k. dhidi ya Allah swt katika kutenda maasi na madhambi. Tunaelewa vyema
kabisa kuwa Siku ya Qiyamah viungo vyote hivi vitatoa ushahadi wa kipekee kwa
kila kilichotenda humu duniani na Allah swt amesema wazi waqzi katika Sura
al-Ya-Sin kuwa Siku hiyo ya Qiyamah hakuna
nafsi
yoyote ile itakayolipwa mema au kuadhibiwa isipokuwa kwa yale waliyoyatenda tu.
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-‘A’raf,
7,
Ayah 179 :
Na tumeiumbia Jahannam majini wengi na watu. Wana
nyoyo, lakini hawafahamu kwazo. Na wana macho, lakini hawaoni kwayo. Na wana
masikio, lakini hawasikii kwayo. Hao ni nyama howa, bali wao ni wapotofu zaidi.
Hao ndio walio ghafilika.
6. Kumtii na kumfuata Shaitani
Humu duniani watu
wengi mno tumekuwa wafuasi na mashabeki wakubwa wa Shaitani kiasi kwamba hata
Allah swt tumemsahau kama yupo na anayajua yale yote tuyafanyayo. Sisi tunayakimbilia
kila yaliyo maovu bila hata ya kuyafikiria matokeo yao kama yatatunufaisha au
kutudhuru. Na kwa hakika mambo mengi mno tuyafanyayo sisi kimatokeo ni
kutudhuru tu. Kila aina za tabia mbaya sisi tunaongoza kama kunywa pombe,
bangi, madawa ya kulevya, zinaa na uasherati wa kil aina, wizi, uongo,
kudhulumiana na kufanyiana khiana, n.k. na hata wengi wetu kuthubutu kusema
kuwa sala, saumu havina umuhimu wowote katika Islam na maisha ya mwanadamu. Kwa
hakika tunakuwa tumejawa na kasumba za Kishetani ambazo zinatuangamizi moja kwa
moja. Allah swt anasema katika
Ayat
ul-Kursi kuwa wale wanaokufuru na wanaomfanya Shaitani kuwa kiongozi wao,
basi Allah swt huwatoa katika
Nuru na
kuwatumbukiza katika
Kiza.
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-‘A’raf, 7, Ayah 18 :
Akasema : Toka humo, nawe umekwisha fedheheka,
umekwisha fukuzwa. Hapana shaka atakaye kufuata miongoni mwao, basi nitaijaza
Jahannam kwa nyinyi nyote.
Kwa hakika hii ni
tabia mbaya kabisa katika maisha ya mwanadamu kwani anajiona yeye yu bora na
afadhali kuliko watu wengine wote ama kwa kujivunia ilimu aliyoipata, uzuri,
watoto, mali, siha, n.k. lakini yote yaho si ya kujivunia kwani vyote ni vitu
vyenye kuangamia na kuisha pasi na sekundi hata moja. Mfano mtu kama huyo anaweza
akaugua ugonjwa kwa muda mfupi atawehuka au akapoteza fahamu zake, hivyo
akasahau yote aliyokuwa akiyajua. Vile vile mtu anayejivunia afya na mwili wake
anaweza kupatwa na ugonjwa wa moyo, na akapooza mwili kiasi kwamba hata chakula
analishwa akiwa amelala na anajisadia choo kidogo na kikubwa akiwa kitandani,
hoi hawezi hata kujipangusa mwenyewe. Je majivuno yamekwenda wapi ? Na huu ni
uatamaduni wa Shaitani ambao kwetu sisi ndio tunaouona kama ndio desturi nzuri.
Mtu masikini akiketi karibu nawe, je utakuwa masikini au utajiri wako
utamwendea huyo masikini ?
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura az-Zumar, 39,
Ayah
32 :
BASI NI NANI dhalimu mkubwa kuliko yule
aliyemsingizia uwongo Allah swt na kuikausha kweli imfikiapo ?
Je! Siyo katika Jahannam makazi ya hao
makafiri?
Na vile vile
Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu ,
Sura al-A’raf, 7, Ayah 36 :
Na wale watakaokanusha Ishara zetu na wakazifanyia
kiburi, hao ni atu wa Motoni; humo watadumu.
Kwa kutaka
misaada kutoka wadhalimu kunatupeleka katika
Jahannam
bila kipingamizi kwani tunaelewa wazi kabisa
kuwa mdhalimu (jina linajitosheleza kwa kujieleza ) ni mtu ambaye anamdhulumu
mtu au watu hivyo hakuna kheri kwao kwani watataka kila mtu adhulumiwe tu kwa
njia moja au nyingine. Na kwa kumwomba yeye msaada atajenga chuki na uhasama
baina ya watu ili yeye aweze kunufaika. Allah swt anatuambia katika Qur’ani
Tukufu , Sura al-Hud, 11,
Ayah 113 :
Wala msiwategemee wanao dhulumu, usije ukakuguseni
Moto. Wala nyinyi hamna walinzi badala ya Allah swt , wala tena hamtasaidiwa.
Vile vile Allah swt
anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Maidah,5,
Ayah 2 :
…. Na saidianeni katika wema na uchamungu. Wala
msisaidiane katika dhambi na uadui….
Kwa hakika sisi
binadamu tunajitumbukiza katika maasi na madhambi basi tunasahau kuwa Allah swt
yupo anatuangalia na kuyajua matendo yetu yote. Na katika hali hii sisi huwa
tunasahau kuwa baada ya maisha ya humu duniani na kufa kwetu, kuna Aakhera. Na
kuisahau huku ndiko kunakotutumbukiza
Jahannam
.
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Jathiyah, 45,
Ayah
24 :
Na walisema:Hapana ila huu uhai wetu a duniani –
twafa na twaishi, na hapana kinacho tuhiliki isipokuwa
dahar. Laini wao hawana ilimu ya hayo, ila wao wanadahani tu.
Sisi tumepotea
kiasi kwamba dunia hii tumeichukulia kama kwamba ndipo tutakapoishi milele
wakati tunawaona watu wanakufa usiku na mchana, wote hawa wanaiacha dunia kwa
mikono mitupu. Wapo humo wanaobahatika sanda au kuzikwa na wengine humo wapo
ambao hata sanda hawabahatiki na badala ya kuzikwa wanaliwa na wanyama na kuoza
kama vile kufa maji, kuchomwa moto n.k. Lakini haya yote tunayaona kama mzaha
bila kuyatilia maanani kuwa nasi pia tuko njiani kwenda huko na tutayaacha yote
humu humu duniani isipokuwa matendo yetu mema ndiyo yatakayotufaa katika safari
yetu ya Aakhera. Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. anasema
Safari ndefu lakini matayarisho ya safari ni madogo. Tukiwa watumwa
wa dunia basi tutatumbukia
Jahannam
.
Hapa Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema katika
Mizanul
Hikmah kuwa “Mapenzi ya dunia ndiyo chanzo chote cha kila aina ya
madhambi.” Na vile vile Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-
‘Asra’, 17, Ayah 18 :
Anayetaka yapitayo upesiupesi, tutafanya haraka
kumletea hapa hapa tunayoyataka kwa tumtakaye. Kisha tumemwekea Jahannam ;
ataingia humo hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa na kufurushwa.
Sisi wanaadamu
tunayo tabia ya kulimbikiza utajiri yaani kulimbikiza mali na mapesa bila ya
kujali haki zilizowekwa na Dini yetu Tukufu kama vile kutoa Zaka, Khums,
Sadaqa, kuwasaidia jamaa na mayatima, wajane na wale wenye shida n.k. Kwa
hakika Qur’ani Tukufu
inatuambia
waziwazi kuwa sisi tunapenda kujiongezea tu hadi hapo tutakapofika makaburini,
kamwe hatukinai wala kutosheka, na tufikapo makaburini ndipo tutakapoamka na
kuzindukana na usingizi wetu huo wa upotofu.
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Tawbah, 9,
Ayah
34 – 35 :
Enyi mlioamini! Hakika wengi katika makuhani na
wamonaki wanakula mali za watu kwa batili na wanazuiliz Njia za Allah swt. Na
wanaokusanya dhahabu na fedha, wala hawazitumii katika Njia ya Allah swt.
Wabashirie khabari ya adhabu iliyochungu.
Siku (mali yao) yatakapotiwa moto katika moto wa
Jahannam , na kwa hayo vikachomwa vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo
yao, “Haya ndiyo (yale mali) mliojilimbikia nafsi zenu, basi onjeni (adhabu ya
) yale mliyokuwa mkikusanya.”
(Imeelezwa katika riwaya kuwa neno
lililotumika katika Ayah hii
kanz
inamaanisha mali yoyote ile
ambamo
zaka haijatolewa).
Hapa neno hili
Katika uwanja wa
vita badala ya kuwasaidia Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na Maimamu a.s. mtu
anaweza kuacha wao vitani
na yeye
akatoroka. Basi mtu kama huyu ataingizwa
Jahannam
na Allah swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu
, Sura al-Anfal, 8,
Ayah
15 – 16 :
Enyi Mlioamini! Mkikutana na waliokufuru vitani
msiwageuzie mgongo.
Na atakayewageuzia mgongo wake siku hiyo – isipokuwa
kwa mbinu za vita au kuungana na kikosi – basi atakuwa amestahiki ghadhabu ya
Allah swt . Na pahala pake ni Jahannam, na huo ni mwisho muovu.
Kwa kumwaga damu
ya mtu asiye na hatia kutatufikisha katika
Jahannam
kwani hii itakuwa ni dhuluma na ndiyo maana
kuna mahakama na vyombo vya sheria vya kufuatilia masuala ya watu anapokumbwa
na matatizo na watu wengine. Haifai kwa mtu kujichukulia sheria mikononi kwani
inawezekana mtu mmoja akamwua mtu mwingine kwa kudhania tu pasi na ushahidi wa
kutosha au bila kufikiria vyema kwani wakati huo mtu huyoanakuwa katika hasira
na jazba. Katika Islam kuna uongozi sahihi umewekwa kwa ajili ya kufuatilia
kila jambo na swala. Kwa kufuatilia maswala kwa uchunguzi na kufikia jibu au
muafaka kunadumisha upendo na amani katika jamii zetu na kwa hakika haya ndiyo
yanayomfurahisha Allah swt na ndipo hapo tunapojaaliwa baraka na rehema na
neema Zake. Allah swt hataki mwenye nguvu na uwezo kuwadhulumu wanyonge na
dhaifu. Haki ifuatwe ipasavyo.
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Maida, 5,
Ayah
32 :
Kwa sababu ya hayo tuliwaandikia Wana wa Israili ya
kwamba aliye muuwa mtu bila ya yeye kuuwa, au kufanya uchafuzi katika nchi,
basi ni kama amewauwa watu wote. Na mwenye kumuokoa mtu na mauti ni kama
amewaokoa watu wote. Na hakika wakiwajia Mitume wetu na hoja zilizo wazi. Kisha
wengi katika wao baada ya haya wakawa waharibifu katika nchi.
Vile vile Allah swt
anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa,4,
Ayah 93 :
Na mwenye kumuuwa Mumiin kwa kukusudia, basi malipo
yake ni Jahannam humo atadumu, na Allah swt amemkasirikia, na amemlaani, na
amemuandalia adhabu kubwa.
Kwa hakika kwa
mtu anayemwaga damu ya mtu asiye na hatia, huadhibiwa adhabu nne na huko
Jahannam
atawekwa peke yake, daima ghadhabu za Allah
swt zitakuwa juu yake, laana za Allah swt zitakuwa juu yake na adhabu kubwa
kabisa itamwangukia. Habari hizi pia ziko katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Ali
Imran, 3, Ayah 21 :
Hakika wanaozikataa Ishara za Allah swt , na
wakawauwa Manabii pasipo haki, na wakawauwa watu waamrishao Haki wabashirie
adhabu kali.
Watu wa
Jannat
watawauliza watu wa
Jahannam
kile kilichowaingiza
Jahannam.
Nao watawajibu kuwa wao hawakuwa miongoni mwa waliokuwa wakisali. Allah swt
anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Muddathir, 74,
Ayah 39 – 46 :
Isipokuwa watu wa kuliani.
Hao watakuwa katika mabustani, wawe wanaulizana
Khabari za wakosefu:
Ni nini kilichokupelekeni Motoni (Saqar) ?
Waseme : Hatukuwa miongoni waliokuwa wakisali.
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
Na tulikuwa tukizama pamoja na waliozama katika
maovu.
Na tulikuwa tukiikanusha Siku ya malipo.
Katika maisha
yetu Dini yetu imetuwekea masharti ya kutozwa kodi mbalimbali ambazo zimeelezwa
vyema na kwa uwazi katika vitabu vya
fiq-hi
kwa ajili ya kutakasisha mali zetu.
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Fussilat,41,
Ayah 7 :
Ambao hawatoi Zaka na wanaikataa akhera.
Duniani humu
hakuna mtu ambaye anaomba watoto wake wawe mayatima na kutaabika kwa mateso
yaliyopo humu duniani. Lakini kunapotokea hali ya watu wengine kuwadhulumu
mayatima, basi hao hujishughulisha kwa kila hila na mbinu katika kufanikisha
azma yao hiyo ya kuwadhulumu mayatima. Badala ya kuwa waangalizi wa mayatima,
wao ndio wanawadhulumu na kuwafanyia maisha yao yakawa magumu kwani watoto hao
watashindwa kusoma mashuleni, hawataweza kuvaa mavazi mazuri, hawataweza kuishi
maisha mazuri na vile vile hawataweza kupatiwa matibabu mazuri kwa ajili ya
hayo. Sasa jee haya ndiyo yanayomfurahisha Allah swt
au tunamghadhabisha na hatimaye atuadhibu ?
Halafu tutasema kuwa Allah swt anatuonea.
Kwa kifupi sisi
tunatakiwa tuwe walezi wa mayatima. Ipo Hadith tukufu kuwa Yatima anapotoa
pumzi moja ya kusikitika, basi ;Arshi Ilahi inatetemeka na Malaika huangua
kilio.
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa,4,
Ayah
10 :
Hakika wanaokula mali ya mayatima kwa dhuluma,
hapana shaka yoyote wanakula matumoni mwao moto, na watingia Motoni.
Allah swt
ameharamisha kutoza na kupokea riba kwa sababu riba inawadumaza watu kiuchumi
na hatimaye hata kufilisika. Tunasikia kila mahala kunakuwapo na kilio kikubwa
cha watu hata mashirika na hata nchi mbalimbali ikiwemo yetu, wote wakilia
kilio cha kunyonywa kwa kutozwa riba ambayo inawawia ngumu kuilipa na hatimaye
kutumbukia katika madeni makubwa makubwa ambayo kuyalipa tena ni vigumu mno.
Watu wengi wamewahi kuchukua
riba lakini wameshindwa kurejesha
Unachukua mfuko
mtupu na kuurudisha ukiwa mnono au unamchukua ng’ombe aliyekonda na kumrudisha
akiwa amenona sana!
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al- Baqarah, 2, Ayah 275 :
Wale walao riba riba hawasimami ila kama
anavyosimama aliyezugwa na Shaitani kwa kumgusa. Hayo ni kwa kuwa wamesema:
Biashara ni kama riba. Lakini Allah swt ameihalalisha biashara na ameiharamisha
riba. Basi aliyefikiwa na mawaidha kutoka kwa Mola wake Mlezi,, kisha
akajizuia, basi yake ni yaliyokwisha pita, na mambo yake yako kwa Allah swt. Na
wenye kurudia basi ao ndio watu wa Motoni, humo watadumu.
Allah swt huiondolea baraka riba, na huzibariki
sadaka…
Sisi wanaadamu
tunayo tabia na desturi ya kutoa shukurani kwa jema lolote tunalofanyiwa na
watu wenzetu. Lakini ni ujeuri wetu sisi kwamba hatutoi shukurani ipasavyo kwa
Allah swt amabye ametujaalia kila aina ya neema kama macho, miguu, mikono,siha,
mali, watoto,
n.k. kwa hakika hatuwezi
kuzihesabu neema za Allah swt (rejea Sura ar-Rahmaan ) hata tukizikalia pamoja
na makompyuta zetu.
Allah swt pia
anatarajia kuwa mja wake atakuwa ni mtu mwenye kumshukuru na kumnyenyekea kwa
neeza zote anazomjaalia, lakini sisi badala ya kufanya hivyo, ndivyo
tunavyozidi kuleta ufisadi na uchafuzi humu duniani kwa neema hizo hizo
anazotujaalia Allah swt
kwa ajili ya
mambo mema. Tunafanya kiburi na majivuno mbele ya Allah swt lakini tunasahau
kuwa hatumpunguzii chochote Allah swt
na
badala yake iwapo tutamshukuru basi Allah swt atatuzudushia katika maslahi
yetu.
Hebu zingatia
kuwa kuna masikini mwombaji mmoja akiwa mlangoni mwako, utampa chochote kile
ili mradi umempa. Lakini kuna mwingine anakuja mlangoni mwako na kuanza
kukusifu na kukutukuza na kukuombea dua nzuri nzuri, basi bila shaka huyu
utampa mambo mazuri zaidi ya yule wa kwanza. Jaribu kusoma maana ya Ayah za
Sura al-Fatiha (al-Hamdu ) utaona kuwa kunaanza kumsifu na kumtukuza Allah swt
kwa mpangilio maalum na hapo katikati ndiko kunaanza sisi kujiombea maslahi
yetu. Sasa katika hali kama hii Allah swt kamwe hawezi kutunyima kile
tumwombacho.
Tujaribu kujifunza kutoka
watoto wadogo hususan wanapoomba kitu utaona wanavyobembeleza.
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Ibrahim, 14,
Ayah 28 – 29 :
Hebu hukuwaona wale waliobadilisha neema ya Allah
swt kwa kukufuru, na wakawafikisha watu wao kwenye nyumba ya maangamizo ?
Nayo ni Jahannam ! Wataingia. Maovu yaliyoje makazi
hayo !
Mwanadamu
hujipatia malimbikizo ya mali kwa ilimu aliyonayo. Wengine wanapenda kufanya
kwa uhalali wakati wengine wanafanya kwa kuibia katika mizani yaani wanapouza
huuza kwa kupunguza, au huuza kitu kisicho sahihi au huiba katika vipimo vya
uzito na urefu na upana, au huchanganya mali ili kufikisha ujazo kwa mfano
kuongezea changarawe katika nafaka, maji katika maziwa, mafuta tofauti huongezwa
katika mafuta ya aina nyingine au kumbandika mtu mali hafifu kwa kupokea malipo
ya kifaa imara, n.k. Hivyo Qur’ani Tukufu inatukanya vikali mno pamoja na
Ahadith za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na Ma-Imamu a.s.
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Mutaffifiin, 83, Ayah 1 – 10 :
Ole wao hao wapunjao!
Ambao wanapojipimia kwa watu hudai watimiziwe.
Na wao wanapowapimia watu kwa kipimo au mizani
hupunguza.
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
Katika Siku iliyo kuu,
Siku watapomsimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu
wote ?
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka
yamo katika Sijjin.
Unajua nini Sijjin ?
Kitabu kilichoandikwa.
Watu wanapokuwa
hawana kazi au shughuli za kufanya, basi utawaona wengine kazi zao ni
kuzitafuta aibu za wengine na kuanzisha mgumzo ya kuwasengenya watu. Kwa hakika
tutambue wazi kuwa anayemsema mwinge vibaya mbele yetu basi atatusema sisi
vibaya mbele ya wengine, hivyo inabidi kujiepusha na watu kama hawa. Je ni nani
aliye humu duniani ambaye hana kasoro ? Basi huyo si mwanadamu bali ni Malaika
! Huyo anayezitafuta aibu za wengine, mwenyewe anazijua aibu zake, hivyo
inambidi ajichungulie vyema unani mwake kabla ya kuwasema wengine.
Vile vile tutambue wazi kuwa Allah swt
hatatusamehe madhambi yetu ya kumsema mtu vibaya hadi hapo huyo mtu atusamehe
yeye mwenyewe kwa furaha yake.[2]
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Humaza, 104,
Ayah 1 - 5
Ole wake kila safihi, msengenyaji !
Aliyekusanya mali na kuyahisabu.
Anadhanim kuwa mali yake yatambakisha milele !
Hasha! Atavurumishwa katika
Hutama
Na nani atakujuvya ni nini Hutama ?
Moto wa Allah swt uliowashwa.
Ambao unapanda nyoyoni.
Hakika huo utafungiwa nao
Kwenye nguzo zilionyooshwa.
Kwa hakika mtu
anapopata neema za Allah swt inambidi amshukuru kwa kila alichopewa lakini
utaona watu kila wanapozidishiwa neema basi na ukafiri ndivyo unavyozidi
kumwingia. Kwa kuwa sasa anao utajiri basi ataanza uasherati wa kila aina hata
kuanzisha majumba ya kunywia pombe na kuchezea kamari na kuwaweka malaya ati ni
kwa ajili ya starehe zake na marafiki zake. Kwa hakika hayo yote ni ufujaji wa
Neema za Allah swt kwani utamwona mtu hatosheki kwa kidogo wala hakinai kwa
kingi. Tusifuje neema za Allah swt na badala yake tuzitumie itupasavyo ili
tuweze kujenga Aakhera yetu kwa Neema hiyo hiyo kama kutoa misaada kwa wenye
kuhitaji, kuwasaidia mayatima na wajane na walemavu, kusaidia mahospitali,
kuwachimbia watu visima kwa wenye shida
ya maji, kuwalipia karo wale wanaohitaji ili waweze kusoma na kuilimika,
n.k.
Allah swt
anatuambia katika Qur’ani Tukufu, Sura al-Mumin,23, Ayah 43 :
Hapana umma uwezao kutanguliza ajali yake wala
kuikawiza.
Vile vile Allah
swt anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Asra’,17,
Ayah 27 :
Kahika wabadhirifu ni ndugu wa Masheitani. Na
Shaitani ni mwenye kumkufuru Mola wake Mlezi.
Sisi
tunaponeemeka basi tunaona kuwa kuna vipingamizi vingi mno kupita kiasi katika
maisha na starehe zetu, hivyo ndio mwanzo wetu wa kuanza kujifanyia vile
tutakavyo, na kwa kufanya hivyo ndipo tunaanza kufanya makosa na madhambi moja
baada ya nyingine. Tunafikia kiwango cha kusema kuwa bila madhambi maisha
hayana raha. Allah swt atuepushe na hali kama hiyo, nyoyo zitakuwa zimekufa!
Allah swt anatuambia katika
Qur’ani Tukufu , Sura al-Zukhruf, 43,
Ayah 74 :
Kwa hakika wakosefu watakaa katika adhabu ya
Jahannam
Hawatapumzishwa nayo na humo watakata tamaa.
Kila
Mwislamu inambidi afuate na kutekeleza kila
amri ya Allah swt bila ya kuvunja hiki wala kile na kutokufuata itakavyo nafsi
yake. Allah swt ametuwekea mipaka ya kila jambo.
Allah swt
anatuambia katika Qur’ani Tukufu , Sura al-Nisaa, 4,
Ayah 14 :
Na anayemuasi Allah swt na Mtume wake, na
akaipindkia mipaka yake, (Allah swt ) atamtia Motoni adumu humo, na atapata
adhabu ya kudhalilisha.
MADHAMBI YAMFANYAYO MTU KUINGIA JAHANNAM
Makala
haya yametarjumiwa na kushereheshwa na:
Amiraly
M.H.Datoo
P.O.Box
838 Bukoba – Tanzania
(8/7/2000)
Hadithi
hii ilisomwa na : Sheikh Akmal
Hussein Taheri – Bukoba
Mwanadamu yupo daima anatenda madhambi kutokana na nafsi yake mwenyewe. Malaika walipomwabia Allah swt kuwa mjumbe wake huyu atakuwa mtenda madhambi. Naye Allah swt akawaabia kuwa yeye ayajua zaidi kuliko wao.
Mtu yule ambaye atakusanya
fedha na kuziweka mahala pamoja bila ya kufaidika yeye wala kuwasaidia wengineo
ambapo wapo ndugu zake Waislamu wenye shida ambapo maisha yao yamewawia magumu.
Mtume s.a.w.w. amesema kuwa “ufukara ni
mbaya zaidi ya ukafiri”.
Vile vile
Imam Ali a.s. amesema
Daima muchunge kuwa mwenye “shida masikini
asikuijie bali ni wajibu wako wewe uwafikie”
Wakati mwingine mwanadamu
hufikia wakati wa kukufuru ama kwa kukusudia au bila kukusudia. Siku moja mtu
mmoja alikuwa akisafiri kwenda mji mwingine kwa ndege. Ndugu yake ambaye
alikuwa akimsindikiza uwanjani hapo alimwuliza “Ewe ndugu yangu ! Je hautakuwa
na shida ya fedha wakati ukiwa safarini ?”
Ndugu yake ambaye alikuwa akisafiri alimjibu “Naam Ndugu yangu ! Mimi sitakuwa muhtaji wa Allah swt kwa muda wa juma
moja hivi.”
Ndege iliruka na katika
muda wa nusu saa hivi kulipatikana habari kuwa ndege hiyo imeanguka na wasafiri
wote wameuawa.
Hapa siwezi kusema kuwa watu
wote hao wamekufa kwa sababu ya kuadhibiwa mtu mmoja aliyetoa maneno ya kashfa
dhidi ya Allah swt. Na kwa maani hii ndipo tunapoambiwa kuwa sisi tusijihusishe
na mahala ambapo panapotendeka maasi na madhambi kwa sababu inawezekana adhabu
za Allah swt zikateremshwa hapo na wewe ukakumbwa pamoja humo.
Kisa cha kijana mwenye
madhambi.
Ma'adh anasema:
"Siku moja nilikuwa nkijiandaa kwenda
kwa Mtume s.a.w.w. , na mara nikamwona kijana mmoja akilia mno, basi hapo
nilimwuliza sababu ya kilio chake hicho.
Huyo kijana alinibu kuwa yeye ni mwenye dhambi kubwa mno.
Basi hapo nilimwambia aje pamoja nami kwa
Mtume s.a.w.w. ili amwombee msamaha kwa Allah swt.
Hapo huyo kijana alisema kuwa alikuwa akiona
aibu kuja mbele ya Mtume s.a.w.w. kwa sababu ya dhambi zake."
Hapo Ma'adh aliendelea na safari yake hadi
kwa Mtume s.a.w.w. na kumwelezea yale yaliyotokea.
Basi Mtume s.a.w.w.alimwambia akamlete yule
kijana.
Alipofikambele ya Mtume
s.a.w.w. aliulizw,
'Je umekuwaje, walia
kwa nini?
Hapo huyo kijana akasema,
"Ewe Mtume wa Allah swt! Dhambi langu ni
kubwa mno!"
Hapo Mtume
s.a.w.w.aliendelea kumwuliza,
"Je
kosa lako kubwa au mbingu? "
Akajibu, 'Kosa langu!'
'Je kubwa
au dunia nzima?
Akajibu, kosa
langu!
Je kosa lako kubwa au msamaha
wake Allah swt?
Hapo huyo kijana akasita
na hatimaye kukubali kuwa 'Msamaha wa Allah swt ni mkubwa!
Bassi hapo Mtume s.a.w.w. alimwuliza, sasa
niambie kosa lako.
Huyo kijana akaanza
kusema:
"Ewe Mtume wa Allah
swt!
Palitokea kufariki kwa binti mmoja
mzuri mno wa kabila la ansaar, na mimi nilikwenda usiku ule kulifukua kaburi
ili kutaka kuiba sanda aliyokuwa amevishwa huyo maiti, shetani alinighalibu na
kunifanya nikatenda tendo la kinyama kwa maiti huyo, binti aliyekuwa uchi mbele
yangu.
Hapo ndipo maiti hiyo ilipota
sauti ya masikitiko na kunilaani kwa kuniambia kuwa Allah sw ataniingiza motoni
na kuniunguza humo kuteketea.
Ewe mtume
wa allah swt kwahakika, baada ya matamshi hayo ya maiti huyo, mimi nimekosa
furaha ya kila aina na nimeingiwa na woga na nadhani nitaweza kuangamia katika
hali kama hii iwapo itaendelea kunisumbua.
Hapo mtume s.a.w.w. alimwambia huyo kijana:
"Ondoka haraka mbele yangu kwani
inawezekana moto wa Jahannam ukanikumba nami pia."
Je kwa nini Mtume s.a.w.w. alisema
hivyo?
kwa sababu dhambi lilikuwa kubwa
mno!
Kwa mujibu wa riwaya, kijana
huyo baada ya kuambiwa hivyo, aliondika akiwa amesikitika mno na kuelekea
katika milima ya mji wa madina, huko alikaa kwa muda wa siku arobaini akiwa
akilia na kuomba Toba kwa Allah swt. Baada ya siku arobaini kupita,
alisema:
"Ewe Allah swt!
Iwapo umeshakwisha kuikubalia Toba yangu,
basi naomba unijulishe kwa kumpitia Mtume wako.
Na iwapo bado haujaikubali Toba yangu, basi naomba uniteremshie miale ya
moto kutoka mbinguni ili inichome na kuniunguza ili niteketee kabisa!"
Basi hapo iliteremka Aya ya
134 - 135 ya sura Ali Imraan (3):
"Na
wale ambao, wanapofanya tendo la kuaibisha au kudhulumu nafsi zao, wakamkumbuka
Mwenyezi Mungu na kuomba msamaha wa madhambi yao, na ni nani awasamehee
madhambi isipokuwa Mwenyezi Mungu?
Na
ambao hawabakii (kwa kukusudia) katika yale waliyoyafanya maovu hali walikuwa
wakiyajua hayo,"
Sisi sote tunatambua kuwa
kuwa kutakuwa na adhabu katika makaburi kwa ajili ya kila mmoja ikiwa ni
Mwislamu au asiye Mwislamu. Lakini kunatofauti katika adhabu hizo baina ya
makundi hayo mawili ya watu kwani makafiri, wanafiki na wasio wasio Waislamu
itakuwa zaidi kuliko Waislamu. Lakini kuna baadhi ya Waislamu ambao wao wenyewe
humu duniani wanapuuzia baadhi ya mambo na hivyo katika kituo cha kwanza cha
safari ya Aakhera na ambacho ndicho baada ya dunia, watakumbana na magumu na
mazito.
1. Sababu za adhabu za Kaburini
Ninapenda kuwaleteeni
Hadith ya kwanza kutoka
Bihar al-Anwar, J.6, uk. 222
inayomnakili Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.
1
Kuchonganisha na kufitinisha
“Kwa hakika adhabu ya kaburi ni kali mno kwa yule
mtu ambaye ni mchonganishi(mambo na maneno ya hapa anayapeleka huko na ya kule
anayaleta huku na kufitinisha )
2.
Kutojiepusha na vilivyo Najis
Sisi tunapuuzia
mno na hatutilii muhimu
Najis iwe
katika katika hali yoyote ile kwa mafano mkojo, mavi ,damu na vitu vingi mno
vinajulikana.
3.
Kutowawia wema wananyumba yake
Mara nyingi
tunaona kuwa mtu anakuwa mchungu na mkali kwa familia yake na hata wengine
huwadhulumu wake na watoto wake na kuwaonea na kuwanyanyasa. Na hii ndiyo
sababu moja kubwa ya adhabu kali za kaburini. Hivyo inambidi mtu awe mwema na
mpole na mwenye mapenzi kwa mke na watoto wake na inambidi kuwalinda na
kuwatimizia mahitaji yao na kuwalinda.
Sa’ad ibn Ma’adh
alikuwa ni
Sahabah wa Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. na alikuwa mwzuri sana na kwamba sanda na mazishi yake
yalikuwa yamesimamiwa na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. mwenyewe na hata
kuteremka katika kaburi lake aliteremka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na vile
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa Malaika wengi mno walikuwa
wameshiriki katika mazishi yake.
Mama yake
alipopata habari hizo, alisema kuwa Allah swt amjaalie
Jannat na kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alijibu, “Bila
shaka ! Lakini atakuwa na adhabu kali mno kaburini !” Kwa kusikia hayo Masahaba
waliuliza, “Je itawezekanaje hivyo wakati bwana Sa’ad alikuwa ni mja na Sahaba
mwema ?”
Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa
s.a.w.w. aliwajibu, “Naam, alikuwa ni mtu mwema lakini alikuwa mkali kwa mke
wake, na hivyo atapata adhabu kali humo kaburini.”
Bihar al-Anwar, J.6, uk. 220
4.
Kuteketeza na kufuja Neema za Allah swt
Yaani kutokutumia
yema na ipasavyo neema za Allah swt alizomjaalia mwanadamu ziwe katika hali ya
siha yake, watoto au mali. Ama mali ni kule kutumia kupita kiasi
kinachohitajika au kutumia visivyo muhimu.
5.
Kunkatalia mume kujamiiiana
Kunawahi kutokea
mara nyingi miongoni mwa watu kuwa mume anapohitaji kujamiiana na mke wake, mke
humyima mume wake tendo hilo la kutimiza haja yake. Kwa hapa mwanamke kama huyu
ndiye anatishio kubwa la adhabu kali za kaburini.
Sisi tunatabia ya
kupuuzia na kuidharau Sala tano za siku na zinginenezo zilizofaradhishwa. Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. , “Yeyote yule anayeipuuzia Sala, si miongoni mwetu.”
Na vile vile amesema, “Mtu kama huyo hatapata nusura yetu Siku ya Qiyama.”
Vile vile Al-Imam
Musa al-Kadhim a.s. amesema kuwa baba yake mzazi Al-Imam Ja'afar as-Sadiq a.s.
amesema, “Wakati wake wa mwisho, alimwambia kuwa ‘mtu yeyote anayeipuuzia Sala
basi hatapata nusura zetu Siku ya Qiyama.’”
Mara nyingi
tunaona kuwa wadhalimu wanawadhulumu watu wengine na sisi katika hali kama hiyo
tukibakia kimya bila ya kujaribu kuwatetea hao wanaodhulumiwa, basi hivyo
ndivyo itakuwa ndivyo sababu yetu ya kuadhibiwa kaburini.
Siku hizi
tumekuwa na tabia moja ya kujiburudisha na yo ni kuandaa mabaraza ya kukaa na
kuwakejeli na kuwasengenya watu, kuchimbua aibu zao na kuongezea chumvi na
pilipili katika maneno yetu ili kunogesha hadithi zetu. Tunasahau kuwa kufanya
hivi sisi tunamharibia jina na sifa za mtu ambaye labda hakuyafanya hayo.
2. Sababu za kupunguzwa kwa adhabu za Kaburini
Kama vile
tulivyokwisha kuona kuwa zipo sababu zinazosababisha adhabu za kaburini basi
tusife moyo kuwa hakuna njia ya kupunguzwa au kuwa hafifu. La, si hivyo, daima
zipo sababu za kupunguziwa adhabu hizo za kaburini na vile vile hali yetu ikawa
njema zaidi humo kaburini.
1.
Sala za Tahajjudi au Salatil Layl
Inambidi mtu
asali sala raka’a nane za
salatil Layl
na raka’a mbili za
shufa’a na raka’a
moja ya
witri ambamo katika
qunuti
yake kunasomwa
Astagh firullah wa atubu Ilaihi mara
sabini. Basi zipo Ahadith zinazosadikiwa hususan kutokea kwa Al-Imam ‘Ali
ar-Ridha a.s. katika
Safinatul Bihar,J.2,
Uk.397 maudhui Kuhusu Kaburi
kwamba : “Iwapo mja anasali raka’a nane za
salatil
Layl na raka’a mbili za
shufa’a
na raka’a moja ya
witri ambamo katika
qunuti
yake kunasomwa
Astagh firullah wa atubu Ilaihi mara
sabini, basi hatakosa faida zake kama zifuatazo, atakuwa amepona
fishar-i-kabr na ataepukana na Moto
wa
Jahannam
, umri wake utakuwa mrefu, Allah swt ataongezea baraka katika riziqi
yake.”
2.
Kutekeleza
Rukuu na
Sujuda kwa
usahihi
katika
Sala
Kwa mtu ambaye
anasali sala zake vile ipasavyo, basi hatakuwa na sababu ya kujibiringita kama
kwamba anafanya mazoezi ya mwili, kumbe masikini anasali. Tunawaona wengi sana
wakisali lakini kwa mbio kama kwamba wanashindana na katika hali kama hii hata
usomaji na matamshi pia hayawezi kamwe kuwa sahihi. Tunasali ilimradi tu
tumesali, sasa sala hiyo inamaana yoyote mbele ya Allah swt ?
3.
Kusali Sala zilizo Sunnah na kutoa Sadaqah
Tunasisitizwa mno
kutimiza Sala zilizofaradhishwa na vile vile tupate muda wa kusali zilizo
Sunnah na vile vile kusoma
Dua kidogo na vyote hivyo kwa
unyenyekevu na kwa moyo uliotulia. Sambamba na hayo tutoe
sadaqah kuwasaidi masikini ambavyo kuna faida kwa pande zote mbili.
Anapokufa Mumiin
basi inatubidi kusali sala hiyo usiku wa kwanza kuzikwa kwake kwani inamsaidia
maiti huyo na vile vile iwapo tutawasalia wengine basi Allah swt atatujaalia
watu wa kutusalia pale tutakapokufa ili nasi tufaidike na thawabu hizo ambazo
zitatupunguzia adahabu zetu,
5.
Kwenda Makkah kwa ajili ya Kuhiji
Inatubidi sisi
katika maisha yetu kwa mara moja kwenda Kuhiji, lakini kwa kutimiza masharti ya
amri hiyo. Na tuwe na moyo kwa ajili ya hivyo. Wapo watu wengi ambao wanapuuzia
swala hili ambalo ni faradhi kwao.
6.
Kifo katika usiku wa kuamkia Ijumaa au siku
ya Ijumaa
Iwapo mtu
atabahatika kufa katika usiku wa kuamkia Ijumaa au siku yenyewe ya Ijumaa, basi
adhabu za kaburini zitapungua. Sisi hatutambui fadhila na Baraka za usiku huu
na siku ya Ijumaa katika maisha yetu. Lau mtu atafanya utafiti kujua zaidi basi
atashangaa kusikia au kusoma fadhila na baraka zake.
Wakati wa kumzika
maiti huwekewa matawi mawili yalio mabichi. Inasemekana kuwa mtu huyo hatakuwa
na adhabu za kaburi kwa kipidi cha kubakia ubichi ka matawi hayo.
8.
Kumwagia maji juu ya kaburi
Ipo riwaya kuwa
kwa kumwagia maji juu ya kaburi kutamfanya mtu huyo aliyezikwa humo asipate
adhabu za kaburini hadi hapo kutapokauka maji juu ya kaburi hilo.
9.
Kusomwa kwa Surah maalum za
Qur'an Tukufu
Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa , “Mtu yeyote atakayesoma
Surah Al-Hakumu Takathur… atapona adhabu za kaburi.” Na vile vile
Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema kuwa “Yeyote atakayeisoma
Surah al-Nisaa kila siku ya Ijumaa basi
huyo atapona adhabu za kaburi .”
Safinat
al-Bihar, J.2, Uk. 397
Na Al-Imam
Ja'afar as-Sadiq a.s. amesema kuwa ,”Mtu yeyote atakayesoma
Surah al- Qalam, hatapata adhabu za
kaburini.” Na vile vile
iwapo atasma
Sura Zukhruf au kusomwa kwa
Sura al-Ya-Sin (ambayo inajulikana kama
ndiyo moyo wa
Qur'an Tukufu ) ama wakati
wa magharibi au usiku kabla ya kulala, hatapata adhabu za kaburi.”
Vile vile kusomwa
kwa Ayah za mwisho katika
Surah
al-Baqarah, kutamwepusha na adhabu za kaburi, Ayah zenyewe ni :
Rabbana la tuakhidhna in nasina au akhta’ana.
Rabbana wala tuhamilna ‘alayna isran kama hamaltahu ‘alal ladhina min qablina
Rabbana wala tuhammilna ma la taqatalana bihi wa’afu ‘anna waghfirlana warhamna
anta Mawlana fansurna ‘alal qawmil kafiriin.
10.
Kuuawa katika njia ya Allah swt
Iwapo mtu
atafariki akiwa katika njia ya Allah swt kama katika vita , basi mtu huyo hana
adhabu ya kaburi. Na hivyo ndivyoamesema Allah swt katika Qur'an Tukufu, Surah
Ali-Imran , Ayah 169 – 170 yaani ni kwamba wale wanaouawa katika njia ya Allah
swt si watu waliokufa bali ni mashahidi na wapo hai.
11. Kumsalia Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. na Ahlul Bayt a.s.
Na kwa kumsalia
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. pamoja Ahl ul-Bayti a.s. kwa wingi kutamwepusha
mtu na adhabu za kaburini.
Vile vile ipo
katika riwaya kuwa mtu yeyote aanzaye dua yake kwa
Bismillahir Rahmanir Rahiim na
Salawati
(Allahumma Salli ‘ala Muhammadin wa Ale
(ahali) Muhammad )
na kumalizia kwa
Salawati, basi kamwe dua yake hiyo haitarudishwa kwani
salawati inakubaliwa na Allah swt. Sasa itawezekanaje mwanzo wa dua
na mwisho wa dua vikakubaliwa na vya katikati vikatupiliwa mbali ?
12.
Mapenzi ya Ahlul Bayt a.s.
Tunaelewa
waziwazi vile fadhila za Ahlul Bayt a.s. zilivyo na vile Allah swt pamoja Mtume
Muhammad Mustafa s.a.w.w. walivyokuwa wakiwasifu hao na kutufaradhishia mapenzi
yao juu yetu na hata kama
salaikisaliwa
bila ya kusomwa kwa
salawati
ndani
yake basi sala hiyo itakuwa batili.
Kuwapenda Ahlul
Bayt a.s. ni kuwapenda wafuasi na marafiki zao na kuwachukia na kuwalaani
maadui wao. Je itawezekanaje adui wa kiongozi na mpenzi wako akawa rafiki yako
?
13.
Mwanamke kufanyia subira umasikini na shida
za mume wake
Kwa hakika katika
maisha yetu haya ya duniani kuna mambo mengi mno ambayo yanajitokeza katika
maisha ya ndoa. Kuna wakati ambapo mume huwa ni masikini, hivyo inambidi
mwanamke aumke kufanya subira na kustahimili shida zinazojitokeza na kumpata
hima bwana wake ili sivunjike moyo bali aendelee na jitihada zake za kuondokana
na umasikini. Vile vile kunawezekana kwa mume kuwa mtu mwovu ambaye hana
matendo mema kama mlevi, mgomvi n.k.
Katika sura zote hizo na zinginezo, inambidi mwanamke afanye subira na
kujaribu kustahimili katika mazingira hayo, na wla si kuamua kumpa talaka mume
au kutoroka nyumbani. (Ingawaje talaka ni neema mojawapo ya Allah swt, hivyo
isitumie vibaya ).
14.
Kusoma Ziyarah ya Imam Hussein a.s.
Imesisitizwa
kuzuru kaburi
Iwapo mtu
atazikwa katika maeneo yanayozunguka kaburi
16.
Kuwasaidia masikini na wasiojiweza
Kwa kutoa misaada
kwa ajili ya kuwasaidia masikini na wasiojiweza na wale wanaohitaji misaada,
kwa hakika kutamwepusha mtu na adhabu za kaburi. Inawezekana mtu akatoa hivyo
katika uhai wake kwa ajili ya kupata thawabu yeye mwenyewe au akatoa kwa niaba
ya wale waliokwisha fariki dunia hii, basi thatwabu hizo zitawafikia hao
marehemu.
Siku moja alifariki mtu
mmoja katika zama za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambaye alikuwa tajiri mno.
Aliacha wusia kuwa mali zote zilizokuwa zimejaa mabohari yake zigawiwe sadaqah
kwa masikini, baada ya kifo chake. Kwa hivyo, kwa mujibu wa wusia wake, baada
ya kifo chake, mabohari yalianzwa kugawia vyakula kwa masikini. Mtume Muhammad
Mustafa s.a.w.w. alikuwepo hapo na mwishoni wakati wanapitisha ufagio,
waliokota kipande cha tende moja, na kwa kuiondoa hiyo, Mtume Muhammad Mustafa
s.a.w.w. alisema, “Lau huyu mtu angalikuwa ametoa angalau hata kama mbegu moja
kama hii ya tende katika uhai wake, basi mbegu moja ya tende ungali kuwa na
thawabu ya mlima wa Abu Qobays (mlima mkubwa mno).”
Makala mchanganyiko
1. SABABU ZINAZOFANYA NYOYO KUFA
Makala
haya yametarjumiwa na kushereheshwa na:
Amiraly
M.H.Datoo
P.O.Box
838 Bukoba – Tanzania
Hadithi
hii ilisomwa na : Sheikh Akmal
Hussein Taheri – Bukoba
Al – Imam Ja’afer as-Sadiq
a.s
amesema kuwa Mtume Muhammad s.a.w.w.
amesema kuwa
mambo manne husababisha nyoyo za watu kufa ambazo ni:
1.Kutenda dhambi baada ya
nyingine
Mwanadamu anapoanza kutenda
madhambi nafsi yake inamzuia na kumtolea lawama ili asitende maovu. Lakini
pindi anapoanza kukaribia madhambi, roho yake inaanza kuzoea na ile hali ya
kujilaumu inaanza kupungua nguvu na hivyo ndivyo anavyojizoeza na hatimaye
anahisi kuwa ni jambo la kawaida wakati wa kutenda dhambi. Kwa hivyo anatenda
ovu moja na kuendelea kuyatenda mengine mengi bila ya kuhisi kuwa na dhambi na
hata unafika wakati ambapo hajisikii vema hadi hapo anapokuwa ametenda
madahmbi. Kwa kutoa mifano, ipo mifano mingi mno mbele yetu zilizo bayana. Mtu
mmoja anapokaribia kunywa pombe, atakataa kata kata, lakini utaona
akibembelezwa na kushurutishwa na marafiki zake walio waovu wenye kuwa ajaribu
kidogo, na akishajaribu kidogo watamlazimisha anywe zaidi na zaidi. Na hali hii
itakapoendelea bele hivi hivi, utaona mtu huyo ndiye wa kwanza kuagiza pombe na
vile vile atakuwa akijiwekea nyumbani mwake. Heshima zote atakuwa amezipoteza
na maovu yote yatakuwa yametundikwa shingomi mwake kwani atapoteza fedha,
ataharibu siha yake, atawatukana wazazi, kaka, ndugu, majamaa na hata kuthubutu
kuwapiga mke na watoto wake. Kwa kifupi familia nzima itakuwa imetumbukizwa
katika janga kubwa.
Huyu pamoja na pombe
ataongezea dhambi lingine la kuwatafuta malaya na kuvuta bangi na madawa ya
kulevya. Haya ndiyo maangamizo makubwa kabisa.
Allah swt amewaamrisha
Malaika kuwa:
Mtu anaponuia kutenda jambo
jema wamwamdikie thawabu. Na anapoanza kutembea katika kulifanya tendo jema
basi hapo pia anaongezewa thawabu nyingi na pale anapolianza kutenda tendo jema
basi huongezewa zaidi ya hayo na anapomaliza kulitenda tendo jema basi hapo
analipwa thawabu nyingi mno zisizo na
hisabu.
Lakini
mtu anaponuia kutenda dhambi basi hapo haandikiwi adhabu, na anajitoa kwenda
kutenda dhambi napo pia haandikiwi kwa sababu inawezekana akarudia njiani na
anapolianza tendo ovu pia kuna uwezekano wa kutolikamilisha na kwa masikitiko
makubwa, anapolikamilisha basi kwa huruma zake Allah swt, huandikiwa dhambi
moja tu.
2. Kuongea zaidi pamoja na
wanawake
Islam haitukatazi kuongea na
wanawake wasio wake zetu lakini kinachokatazwa ni ile hali ya watu kuongea
mambo ambayo yanapita mipaka na huku ndiko kunapoanza kuteketea maadili.
Utawasikia watu wakizungumza pamoja na wanawake mambo ambayo hayana heshima na
kufanyiana dhihaka na hatimaye wanapozoeana katika tabia hii utakuta
wanaanza
maneno ya kudalilisha kuwa
wanapendana na wanahamu ya kuingiliana, na haya ndiyo yanayo tokea. Bwana Daud
alimwusia mwanae kuwa ajiepushe na mazungumzo pamoja na wanawake kwani mwanamme
anapokutana na mwanamke, katikati yao huwa yupo Sheitani kwa ajili ya kuleta
madhambi.
Uislamu unamtaka mwanamke
abakie katika hadhi na heshima aliyopewa na Allah swt. Hivyo mwanamke
anapoongea na mwanamme inambidi asitoe sauti nyororo yenye kuvutia bali
inambidi atoe sauti ambayo haitamfurahisha mwanamme na hivyo asitamani kuongea
tena na mwanamke huyo. Na kwa misingi hii, mwanamme hatakiwi kumtolea salaam
mwanamke ili asije akaisikia sauti yake. Lakini dunia hii imebadilika, leo
katika maredio na televisheni utawaona wanawake hata wanasoma Qur’an kwa sauti
za kuvutia.
Vile vile tusisahau kuwa
kuwadokozea macho wanawake pia ni dhambi. Zipo zinaa za macho na midomo.
3. Kuzozana pamoja na mwehu
Yeye atasema na wewe
utasema
bila ya kufikia maelewano baina
yenu. Mutazozana kwa muda mrefu wakati ambapo watu watakaokuwa wakiwaona
hawatajua tofauti baina yenu. Mwishoni hamtafikia jambo la kheri.
Hao ni watu ambao hawaongei
katika mipaka ya ilimu, dini na adabu.
4. Kukaa pamoja na watu
waliokufa
Kwa kukaa na kufanya mazoea
ya urafiki pamoja na watu waliopotoka, kutatufanya na sisi pia tupotee na
kutumbukia katika ujeuri, majivuno na takaburi mambo ambayo Allah swt hayapendi
na anyachukia na kuyaadhibu. Qur’an inatuambia kuwa nyoyo zao zina magonjwa na
Allah swt anawaongezea magonjwa baada ya magonjwa kwa kutokana na maovu yao
yanavyoongezeka.
Kwa hayo Waislamu
walimwulizaa Mtume s.a.w.w.
Je ni
wakina nani waliokufa?
Mtume s.a.w.w. aliwajibu
Kwa waliokufa wanamaanishwa wale matajiri
wenye takabburi na majivuno. Urafiki pamoja na watu kama hawa
utakufanya wewe uwe na tamaa ya dunia na kujipatia mali ufahari na majivuno.
Hao wanachokithamini ni kile kinachowaletea faida wao tu. Dharau majivuno ndiyo
mavazi yao.
Hapa kuna aina nne ya watu:
(1). Wale wanaokula na kuwalisha wengine
(2) Wale wanaokula na kuwanyima wengine
(3)
Wale hawali wenyewe na wala
hawawapi wengine wale
(4) Wale
wanaowanyan’ganya wengine ili wale peke yao.
Nasiha: Inatubidi sisi tujiepushe na mambo yote ambayo
Allah swt hapendezewi na tufuate Hadithi na Sunna za Mtume s.a.w.w. pamoja na
Maimamu
25th
June 2000
Makala haya yamekusanywa na
kutarjumiwa na
Amiraly
M.H.Datoo
-
Bukoba
Tanzania
Masomo ya
akhlaq-
maadili katika Islam ni mojawapo ya bora ya sayansi na inamwelekeza
asomaye hadi katika
elimu ya kujielewa nafsi yake mwenyewe
ambayo Islam inaamini kuwa ni fardhi. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)
amesema: “Yeyote yule aliyeitambua nafsi
yake (mwenyewe) basi hakika ametambua Allah.”
Hivyo hivyo kuna mapokezi
mengi ya habari kuhusu umuhimu wa somo hili hata Mtume Mtukufu (s.a.w.w)
amebainisha kuwa: “Mimi nimetumwa kuja kukamilisha maadili.
Tuanze kuzichambua aina za
nafsi alizonazo mwanadamu vile alivyo:
Hapana shaka kuwa mwanadamu
hana zaidi ya moja, lakini hii nafsi au roho inayo masharti fulani fulani. Kwa
hiyo, hali ya kuonyesha kama ‘nafsi ya kujilaumu’ ‘au nafsi ya kuamrisha’
‘nafsi inayotosheka’ (kama vile vielezwavyo katika Qu’rani), na hivyo
haidhihirishi idadi ya nafsi. Upande mwingine, yote haya ni miongoni mwa ngazi
za sifa ambazo zinaleta kwa ukamilifu na ustawi wa hali ya nafsi, pamoja na
yale yanayoozesha nafsi na kuleta maovu.
NAFSI SAFI AU THABITI (nafsi
au thabiti.)
Katika Qur’rani Tukufu, aina mbili hizo za masharti za nafsi zinaelezwa:-“Isipokuwa mwenye kuja kwa Mwenyezi Mungu na moyo safi” (26:89)
Uhalisi huu ni
aina ya moyo, na moyo halisi (safi) ni ule ambao haufungamani na upande wa
kuhangaika wala upande ule wa wapotofu.
Imenakiliwa
kutoka kwa Imamu Sadique (a.s) kuwa: “Moyo ulio msafi- halisi ni ule
ambamo hakuna chochote kile ila Allhah
(s.w.t) tu”
Katika hali hii,
Nafsi imetunukiwa hatua mojawapo ya umuhimu kuwa kamilifu. Hivyo inamaanisha
kuwa hakutakuwa na mapenzi mbali na ile ya Allhah tu.
Kuna habari
nyigine iliyonakiliwa kutoka kwa Mtume Mtumfu (s.a.w.w.) ambamo twaambiwa:
“Imani ya mtu haitokamilika hadi hapo mimi niwe mpenzi wake kuliko hata baba
yake, mama yake, watoto wake mali yake na hata kuliko maisha yake.”
Ndivyo hivyo,
nafsi safi ni nafsi ambamo hakuna mapendo mengine yoyote yale isipokuwa Allah
(s.w.t.) na wale wapendwao kwa ajili ya Allah (Mtume na Ahali yake)
NAFSI YENYE
KUTUBU (al-Nafs al- Muniib).
Sharti lingine la
moyo au Nafsi ni ‘kutubu’ na hivyo huitwa moyo wenye kutubu au nafsi yenye
kutubu. Hivyo huwa daima inarudi kwa Mwenyezi Mungu.
“.. Na anayemuogopa ( Mwenyezi Mungu
Mwingi wa kurehemu, na hali ya kuwa humuoni na akaja kwa m oyo ulioelekea ( kwa
Mwenyezi Mungu).” (50:33)
Kuwa na khofu ya
Mwenyezi Mungu pale mtu awapo peke yake ni mojawapo ya masharti bora ya nafsi,
na hii ina maanisha kuwa nafsi imemtambua Allah (s.w.t) kiasi kile kuwa
hakutakuwa na tofauti yoyote itakapokuwa pekee yake au katika kundi la watu.
Hata kama hakutakuwa na mtu yeyote karibu nayo, basi ile khofu ya Allah
(s.w.t.) imo ndani yake thabiti. Hii haipo katika kundi la zile nafsi zilizo
ghafilika katika maasi na matendo maovu wakiwa katika kundi la watu au wakati
wengine watakapokuja julishwa, na hawatajizuia nayo na hata kama iwapo
watakapopewa habari zilizo bainika. Hii ni ile aina ya nafsi ambayo haielewi
kuwa Mwenyezi Mungu yupo anaangalia yote na Aliye dhahiri popote pale na kwa
hakika aina hii ya nafsi haipo pamoja na Allah na wala haitorudi kamwe kwa
Allah.
NAFSI MWONGOZI (al- Nafs al-
Muhtadi).
Sharti lingine la
nafsi ni ile iongozwayo. Qur’rani inatuambia: (64:11).
“..Anayemuamini
Mwenyezi Mungu huuongoza moyo wake”
Mtu ambaye moyo
wake ukiwa umeongozwa na kujitosa katika habari ya imani na sheria Tukufu za
Allah (subahana wa Tala), yeye anaielewa njia yake vyema kabisa. Zile imani
atakazokubalia na matendo yake yale yampasa kuyatenda huwa ni dhahiri kwake
kuelewa vyote hivyo kwa uadilifu.
NAFSI ILIYO
RIDHIKA (al-Nafs al- Mutmaina)
Sharti lingine lijulikanalo vyema la moyo au nafsi ni “kuridhika.
Qur’an:
“ Sikiliza: Kwa kumkumbuka
Mwenyezi Mungu nyoyo hutulia. “(13:28)
Na vile vile
mwishoni mwa sura al-Fajr twaabiwa (89:28)
“Ewe nafsi yenye
kutua”!
“Rudi kwa Mola
wako, hali ya utaridhika.”
Nafsi iliyo
ridhika ni ile iliyokwisha ridhika, ina maanisha kuwa mtu yupo anapigana vita
vikali na matakwa yake na kwa kuyatimiza yale yaliyo fardhi kwake katika dini
na kujiepusha na yale yaliyoharamishwa, na anajipa umuhimu kwa kuelimisha na
kuikamilisha nafsi yake hadi hapo yeye hapindukii kutii chochote kile isipokuwa
Allah (swt) tu. Ni marufuku kwake kuelekea pale penye madhambi na huwa ni mwenye
kupenda amani na utulivu na huwa ni mwenye kujiridhikia mwenyewe hadi hapo yeye
huwa thabiti kama jabali madhubuti. Hakuna madhambi, matakwa ya ubinafsi,
tamaa, mvutano wa dunia, mapenzi ya mali au cheo yatakayoweza kuja kumpotosha
yeye na kumwelekeze pengine na vile vile hakuna sheitani atakayeweza mghalimu
na kumpotosha yeye.
Hali ya juu
kabisa ya sharti hili kama ilivyokuwa katika Mtume mtukufu (s.a.w.w.) na ma -
Imamu (a.s.), waliokuwa halisi kuwa hata mawazo ya kutaka kutenda madhambi
hayakutokea kamwe.
AL-NAFS
AL-MUTTAQI
(nafsi ya
tahadhari ya uadilifu):
Sifa nyigine ya
nafsi inajulikana kama uangalifu wa uadilifu wa nafsi, (The virtuosly cautious
self) nafsi ambayo imejaa kwa khofu na tahadhari. Hali hiyo inatokana na
nyakati fulani kwa kupotoshwa na (kwa akili na roho) huzungukwa na uchafu na
ubovu ili nafsi iingie sharti sawa sawa na itahadharishwe na madhambi. Nafsi
ikiwa katika hali
hiyo huitwa nafsi ya
tahadhari ya uadilifu:-
“...Anayezihishimu
alama za (dini ya ) Mwenyezi Mungu, basi hili
ni jambo la katika utawala wa nyoyo. “(22:32)
Kwa mtu yule
ambaye imani yake inafikia kiwango hiki cha “Taqwa” kiwango cha tahadhari ya
uadilifu, huheshimu na kumthamini Allhah (s.w.t.) na yele yote yaliyotolewa
ishara nae kama Dini, Msikiti, sheriah, waumini wake Makka Ka’aba Tukufu n.k.
kwa ufupi. Chochote kile kinachohusika na Mungu huwa kina kuwa na umuhimu na ta
‘adhima kubwa kwa mtu kama huyu wa namna hii. Na hii ndiyo kwa hakika matokeo
ya
‘taqwa’
NAFSI NYENYEKEVU (al- Nafs al-
Mukhbit)
Hali nyingineyo
ya Nafsi ni unyenyekevu (uvumilivu), yaani humaanisha kuwa mtu mwenye nafsi
hali hii huwa mnyenyekevu mbele ya maamrisho ya Allah (swt)
Kwa mara nyingine
tena twaambiwa katika Surah al Halj: (22:54)
“..waiamini,
na ili zinyenyekee kwake nyoyo zao”
Kwa sababu nyoyo
hizi hujiimamisha chini mbele ya Mungu na maamrisho yake, na wale wenye kuwa na
nyoyo hizo hujiwakilisha kwa Allhah s.w.t
hawavunji kamwe maamrisho
ya
Mwenyezi Mungu na wala hazisaliti au kuzipinga.
NAFSI HALISI (al-Nafs
al-Zakiyyah):
Aina nyigine ya
nafsi ni ile nafsi au roho iliyo mtakatifu (the pure self). Katika Qur’ani
Tukufu, Mwenyezi Mungu anakula kiapo cha jua, mwezi mbingu, ardhi na vitu
vingine na baadaye akisemea nafsi, anatuambia:
“Bila shaka amefaulu aliyeyeitakasa (nafsi yake) na
bila shaka amejihasiri aliyeiviza (nafsi yake)” (91:9 & 10)
Ni dhahiri kuwa
inambidi mtu afanye jitihada ili kufikia hatua hii. Kabla ya yote yale
mengineyo, nafsi lazima iwe huru kutoka sifa zote zile zilizo ovu na hapo ndipo
uwanja utakuwa tayari kwakuzitambulisha sifa zilizo nzuri na bora kabisa na kwa
uanzishaji na uendelezaji. Mtu ambaye nafsi yake itatakasika, basi
amehakikishiwa msamaha (ukovu) na kufikia kipeo cha furaha ya milele. (The
person whose self become purified is assured of salvation and bliss!)
NAFSI YA
KUKARIPIA - LAUMU (al-Nafs al- Lawwama).
Inawezekana
wakati mwingine kuwa hivyo kwa vyovyote vile na kiasi chochote kile cha
madhambi ayafanyayo, mtu
hajisikii
chochote cha kutenda kosa, wala hasikitiki, wala hajilaumu mwenyewe. Nafsi kama
hiyo ni ile iliyoshindikana. Hata hivyo, ile nafsi baada ya kuanguka na kutenda
madhambi na itajikaripia yenyewe na kujishutumu yenyewe, kabla ya yeyote yule
kufanya hivyo, basi imeingia katika sharti tukufu mojawapo la nafsi itakiwavyo
kuwa. Qur’ani Tukufu inatuelezea:
“Naapa kwa siku ya Kiama. Tena naapa kwa nafsi
inayojilaumu; (kuwa mtafufuliwa na mtalipwa)”. (75:1-2).
Ni dhahiri kuwa
iwapo Mwenyezi Mungu akiapia kwa vitu, basi kuna utukufu wake humo. Nayo pia ni
wazi kuwa yeyote yule aifunzae nafsi yake vyema hadi ule wakati wa kutenda
madhambi, yenyewe (nafsi) hujaa masikitiko na kujilaumu, basi imefikia mojawapo
ya vina vya utakatifu.
NAFSI
ILIYOFUNGULIWA HERI (al-Nafs al-Mulham):
Sharti lingine la
nafsi ni kuongozwa na Mungu. Twaambiwa kaika Qur’ani:
“ Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake”
(91:8)
Maongozi haya ni
kutia moyo kwa nafsi wakati itapokuwa katika hali ya kutakasika- ‘Nafsi halisi
si’ ambayo tumeishaizumgumzia. Ni lazima iwapo nafsi itaelekezwa kwa mujibu wa
madhambi basi muongozo na kufunguliwa kwa heri kutoka kwa Allah (swt) yatafikia
kikomo chake.
Kwa kupingana na
sifa na masharti ya nafsi ambazo ni sababu ya furaha ya milele na utakatifu,
baadhi ambazo zimekwisha tajwa hapo awali, pia hapo hapo kuna sifa na masharti
yanayosababisha maovu ya nafsi, sasa tuziangalie.
NAFSI YENYE
MADHAMBI (al-Nafs al-Athima):
Iwapo roho au
nafsi ya mtu ikiwa na tabia ya kutenda madhambi, basi huitwa yeye madhambi.
Qur’ani inazungumzia kulipa kwa amana:
“Na atakaeficha
basi hakika moyo moyo wake ni wenye kuingia
dhambini.”(2:283)
Hii inathibitisha
kuwa nafsi ya yeyote yule ambaye ameshajizoelesha madhambi ni nzito na ni wazi
na tayari kwa kutenda madhambi wakati wowote ule.
NAFSI ILIYO
SINZIA (al-Nafsal-Ghafil)
Sababu mojawapo
ya kushidwa na kufifia kwa nafsi ni kulegea au kusinzia au kuwa zembe. Kwa
kutenda mambo maovu na kwa kuendelea kutenda madhambi ndiko kunakosababisha
nafsi kuelekea palipo paovu na kutomsikia Allah (swt). Anaelezea Mwenyezi Mungu
katika Qur’ani Tukufu
“Wala usiwatii wale ambao
tumezighafilisha nyoyo zao wakafuata
matamanio yao.” (18:28)
NAFSI ZILIZOTIWA
MUHURI (al-Nafs al- Matbu)
Hapa inamaanisha
kufungwa muhuri juu yake na hivyo ndivyo hatua ya mwisho
ya kungwa, inatuambia:
“Na watakaokuwa na uzani khafifu, basi hao ndio
waliozitia hasarani nafsi zao
kwasababu ya kuzifanyia ujeuri Aya zetu.”
Popote pale mtu
anapokuwa fidhuli au juvi kuelekea Allhah (swt) hadi kudharau na kutokubali
ujumbe wake na maamrisho ya Allah ambayo Mwenyezi Mungu ambazo amewekea mbele
yake, au , iwapo yeye atazikubalia, anazipa umuhimu kidogo na kuwa na kosa la
upinzani basi hapo moyo wake unaingia katika hatua ile ambayo ni sawa na kama
tahadhari, maamrisho Matukufu na yale yaliyo haramishwa hayatakuwa na athali
yoyote ile kwake yeye. Na hii ni hatua mojawapo ya kudidimiza kwa nafsi na
kushindwa kwake.
NAFSI ILIYO
POFUKA ( al-Nafs al- Amya):
Hali nyingine ya
Nafsi ni kupofuka. Qur’ani inatuambia kuwa:
“Kwa hakika macho hayapofuki, lakini nyonyo ambazo
zimo vifuani ndizo zinapofuka. (22:46)
Nyoyo hizi
zinaona vingine mbali na Allah (swt) na hazimwoni Mwenyezi Mungu. Nyoyo za aina
hizi huona yale tu yatakayo yenyewe bila ya kuyazingatia yale maamrisho ya
Allah (swt) na kwa hakika ndizo zilivyo kama vile vimepofuka tu.
NAFSI YENYE
MARADHI (al-Nafs al-Maridha):
“Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu
amewazidishia maradhi.”(2:10)
Ugonjwa wa aina
hii inawezekana kuonekana mioyoni mwetu kwa sababu ya yale madhambi tuyafanyayo
sisi siku hadi siku. Kama vile mtu mgojwa huwa hana hamu ya vyakula wala madawa
ambavyo ni vyenye manufaa kwake na vile vile vyakula vizuri havitakuwa na ladha
yoyote kwake, ndivyo vivyo hivyo kuhusu NAFSI iliyougua, kwani inapatikana
kuonywa ( na Mwenyezi Mungu) na kukaribia kwa upole kwa mapendo na matakwa yake
ya humu ulimwenguni na akhera kuwa yenye adhabu kali sana na yenye kutisha mno.
Kilicho zaidi ni kwamba mtu aliyeugua hivyo ni yule mwenye, kuipendelea kwa
ajili ya nafsi yake yale yote yaliyo mabaya na maovu, kwani huwa avutiwa navyo
kama kambwa ndivyo vyenye kumfaa yeye. Kwa hakika hii ndiyo ile nafsi ilikwisha
ugua; kama vile ilivyo kifo kwa mtu hatakayetibiwa magonjwa yake na hivyo
ndivyo vinaweza kutokea kwa ajili ya aina hii ya nafsi iwapo haitoweza kutibiwa
kabla ya ugonjwa kuenea pote na hatimaye mtu aweza kuangamia.
Popote pale mtu
aonapo kuwa yeye hatamani chochote kile atakiwacho kukifanya yaani kumkumbuka
Mwenyezi Mungu katika sala na kutii Sheria Tukufu za Dini ambazo hazimfai na
ambazo ni chungu kwake, kwa hivyo ni wazi kabisa kuwa atambua kuwa huo moyo
wake umeshaanza kuugua maradhi, na bila ya kisita inambidi afanye kila hila
awezayo ili ajielekeze kwa mujibu wa aya za Qur’rani Tukufu, kwa watawa na
walio waumini halisi na wale walio hodari katika elimu na ujuzi huu: waganga
waa moyo, i.e.., wanavyuoni waelewao na wafuatao mienendo ya Mtume Mtukufu
(s.a.w.w.), ili waweze kuitibu nafsi
ya
aina hiyo iliyopatwa na maradhi.
NAFSI INAYOKWENDA
UPANDE (al-Nafs al-Za’igha):
Moyo au Nafsi pia
inaweza kusemwa kuwa inakwenda upande au inapotoka. Aina hii ya Nafsi ni ile
ichaguayo upotofu wakati ipatiwapo chaguo katika hali mbili ya wema na uovu.
Kama mategemeo
yote ya maisha, katika sehemu zote za Imani, maadili na matendo, mambo yake
yote yaliyo dhahiri na yale yote yaliyo batili mwake, mwanadamu daima anakubwa
na mgawanyiko wa njia mbili mbele yake , mtu ambaye amefaulu na kufurahika ni
yule ambaye daima anachagua njia ile aitakayo Mwenyezi Mungu. I.e njia iliyo
nyooka (Sirat al-Mustaqeem) ya dini katika kila hali. Hata hivyo, mtu ambaye
moyo wake unampotosha, huwa daima ndiye achanguaye njia ya upotofu
Katika Qur’ani,
kuzungumzia mifano na mafumbo ya aya na kwa kuelezea wazi wazi, Mwenyezi
Mungu anatuambia:
“Wale ambao nyoyoni mwao mna upotofu wanafuata zile
zinazobabaisha kwa kutaka kuwaharibu watu kutaka na kujua hakika yake
vipi.”(3:7)
Hivi kwa kuchagua
mfano (mutashabih au allegorical) wa aya za Qur’ani ili kuitumia Qur’ani kwa
kuhakikisha matakwa ya mtu binafsi ni sampuli ya ile nafsi iliyopotoka.
NAFSI YA MOYO
MGUMU (al-Nafs al-Qasiya)
Sharti lingine la
nafsi kuwa hivyo ni kutokana na moyo mgumu na katili.
“..Na tukazifanye nyoyo zao kuwa ngumu”
(5:13)
“..Kwa hivi nyoyo zao zikiwa ngumu” (57:16)
Hali kama hii
inaelezewa katika aya zinginezo pia. Nyoyo kama hizi zina sifa kama zile za
jiwe na chuma, kuwa hakuna chochote kile kiwezacho kuathiri au kuacha alama
yoyote juu yake ila kwa mshindo mkali tu moto. Hadi kufikia hali ya moyo kuwa
mgumu kiasi hiki ni dhahiri ikionekana vile maovu yalivyo mteka huyo mtu hadi
akawa mtumwa wa matakwa na maovu yake. Kwa hakika imepotoka!
NAFSI WASIWASI (al-Nafs al-Murtaba):
Nafsi ya aina hii
imo katika hali hii ya wasiwasi kuhusu vile vitu iipasavyo kuvijua na
kuviamini. Shaka kuhusu mizizi ya dini ya Islam kama vile kushuka kuwapo kwa
Allah (swt), akhera, Unabuwa na vile vile Uimamu (a.s.), na kushuku matawi ya
Dini kama vile sala, saumu na mema na mengineyo mengi.
“Nyoyo zao zina shaka; kwahivyo wanasitasita kwa
ajili ya shaka yao.” (9:45)
Hii ni mojawapo
ya sababu ya upotofu wa Nafsi na ni fardhi kwa watu wale walio katika hali kama
hii kujielekeza hadi aya za Quarani na hadithi Tufuku za Mtume (s.a.w.w.) na ma
-Imam (a.s.) na kwa wanavyuoni wa dini ili kuweza kutokomeza hali hii kabla ya
kutanda juu ya Nafsi nzima undani mwake. Ama sivyo, iwapo hali kama hii
haitashughulikiwa na badala yake ikapuuzwa na kubakia Nafsini, basi
itamwelekeza mtu katika hali ya kukatiza na kukataliwa (kupuuzwa na
kudhoofika).
NAFSI ILIYOPATA
KUTU (al-Nafs-al-Ra’ina):
‘KUTU’ ni shida
nyingineyo ambayo nafsi inaweza kupatwa kwani ni sawa na ule mfano wa kioo cha
kujitazamia, iwapo ile poda itabanduka basi hutaweza kujitamazama kiooni. Basi
kioo cha moyo ambavyo ni sehemu ya umuhimu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu utukufu
wa ukamilifu wake, fadhila zake zitamorudishwa kwake, hazitoweza rudishwa iwepo
itashika kutu, na hatimaye itaweza kupoteza ile nguvu ya kupeleka ujumbe wako
kwa Mwenyezi Mungu.
Ingawaje
mwanadamu hawezi kumtazama Mwenyezi Mungu kwa macho yake, lakini anao uwezo wa
kumwona Mwenyezi Mungu, Utukufu wake na Ukuu wake kwa kupitia NURU iliyomo
katika Nafsi yake. Nafsi ile ambayo imeshakwisha shikwa na kutu ambamo sasa
hakuna uwezo wa kurudishia (reflect ) kutoka na kwa Mwenyezi Mungu, basi bila shaka
itatapatapa huko na huko ikimtafuta sheitani na hasa kwa mujibu wa matilaba
yake. Qurani ikiwa inatumbusha kuwa:
“Sivyo hivyo! Bali yametia juu ya nyoyo zao (maovu)
waliokuwa wakiyachuma.” (83:14)
Katika ‘aya hii
twaelezewa vyema kabisa kuwa chanzo cha kupatwa kwa kutu kwa Nafsi ni kule
kutenda madhambi. Kwa hivyo kila dhambi itatupia uzito (itatanda kiza juu ya
moyo; na ifikiapo hali kama hii, inambidi mtu afanye Tawba mara moja kwa
ajili ya kuyasafisha hayo matendo maovu na
atende matendo mema ili kuzuia kupotea kwa nuru iliyotunukiwa Nafsi yake. Vile
vile, twaambiwa katika hadithi Tukufu kuwa: “Mtu mwenye furaha kuu katika siku
ya Kiama ni yule atakaye yaona maneno aliyokuwa akiyatamka ‘naomba msamaha wa
Mwenyezi Mungu’ chini ya kila dhambi alilolitenda. Kwa Hivyo inambidi kila
Mwislam mmoja wetu apige msasa kila ovu alilolitenda ama sivyo, Mwenyezi Mungu
azitowazo onyo zake za upole zitabadilika na kuwa ghadhabu kubwa sana.
NAFSI AMURU (al-Nafs al- Ammara):
Nafsi isiyofunzwa
hasa wakati wa ujana wa mtu, huamuru kutendwa kwa matnedo ya madhambi bila
kiasi. Katika Qurani, kuhusu kisa cha Mtume Yussuf, Nafsi inasemwa:
“Nami sijitasi
Nafsi yangu; kwa hakika (kila) Nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu
(12:53)
Sentensi hiyo
inaonyesha kuwa ilitamkwa na Zuleikha aliyekuwa amependa Nabii Yussuf. Pale
alipotoa ushahidi, alithibitisha kuwa ndiye chanzo cha uovu huo. Kwani Yussuf
alikuwa hayupo wakati huo wa ushahid, lakini kwa kuwa Zuleikha alikuwa hana
hila yoyote ile zidi ya Yussuf. Pia kuna uwezekano kuwa hayo yametamkwa na
Yussuf au ni wote vyovyote vile, Qur’an inatuambia kuwa “Nafsi ni yenye
kuamrisha sana maovu. (12:53)
Nafsi yoyote ile
isiyokuwa imeongozwa kwa mujibu wa mfano ya Islam, huwa daima inavutwa popote
pale penye madhambi na
ma’asiyah kwani
yote hayo yako yamedhalilishwa kabisa. Mfano wa Nafsi hii ni sawa na mtoto
mchanga atakaye kila kitu kuchezea bila kutazama ubora wake, faida au hasara
zake, iliramdi yeye apate kuchezea tu, Nafsi ya yule aliye na utamaduni mzuri,
aliyekomaa na kubaleghe inavutika pale penye mema na hujiepusha na matilaba
yake; na ile nafsi elimishwa na inavutika pale penye maovu ya kila aina na
kwa hivyo lazima ifunzwe vyema, itasaidia
kutakasisha hiyo Nafsi.
HATIMAYE: Kile
kilichoelezwa hapo kinasema kuwa Nafsi inaweza kuwa bora kabisa ama mbovu
kabisa au vinazidiana katika vina na ngazi.
Kuna nafsi zifikiapo kuitwa ‘Nafsi halisi na
‘Nafsi ridhika’ n.k.
na vile vile
kuna zinapofifia hadi kufikia hali mbaya kabisa na matokeo yake ni majanga,
majonzi na maovu na kufikia ile sifa ya “kupigwa mihuri” au ‘zilizopofuka’ na
‘zenye maradhi’ zikiwa ni kama mifano.
Hali hii
inadhihiridha kuwa Nafsi zinapangwa na kila mtu anayo Nafsi moja tu.
JE
UMEJING’AMUA UNA NAFSI YA AINA GANI UNDANI MWAKO??
(JITAHADHARISHE)!
Makala
haya yametarjumiwa
na:
Amiraly
M.H.Datoo
P.O.Box
838 Bukoba – Tanzania
Amesema al-Imam Muhammad
al-Baquir a.s. :
Al-Kafi, j. 2, uk.330
“Zipo aina tatu
za dhuluma: “Aina ya
kwanza ni ile
ambayo Allah swt anatoa msamaha na ya
pili
ni ile ambayo haitolei msamaha na aina ya
tatu ni ile ambayo yeye haipuuzi.”
Ama dhuluma ambayo
anaisamehe ni ile ambayo mtu huitenda baina yake binafsi na Allah swt. Na
dhuluma ambayo Allah swt haisamehe ni kukufuru na dhuluma ambayo haipuuzii ni
ile ambayo inatendewa dhidi ya haki za watu.”
Ufafanuzi:
Aina ya tatu ya dhuluma ni
ile ambayo mtu hukiuka na kuvunja haki za watu. Njia saheli ya kutaka
kusamehewa ni kwanza kumridhisha yule ambaye haki zake zimekiukwa na kuvunjwa.
Iwapo mtu huyo atamsamehe yule aliyemvunjia haki zake, basi hapo dhuluma hiyo
itageuka kuwa dhuluma dhidi yake binafsi. Na hapo ndipo ataweza kuwa mstahiki
wa kuomba msamaha wa Allah swt.
Imenakiliwa kutoka Jaafer
ibn Muhammad naye kutokea Baba, naye kutokea kwa Babu yake naye kutokea kwa
Imam Ali ibn Abi Talib a.s. kwamba Mtume s.a.w.w. alisema katika
wasia
wake.
Alisema Mtume s.a.w.w. “ Ewe
Ali ! Kuna makundi manne ambamo watu wanapatikana wamegawanyika kwa mujibu wa
matendo yao humu duniani.[3]
A. Kupanda daraja
1.
Kutawadha wudhuu katika baridi
Kwa hakika ni jambo gumu mno kuamka na kujiweka
tayari kwa ajili ya ibada za Allah swt hasa kama utakuwapo kazita sehemu ambazo
kuna baridi kali ambapo hata kunakuwa na hatari ya watu wengine kuathirika kwa
baridi kali. Wakati huyo unakuwa ndio wakati mzuri wa kujipatia usingizi mnono
na nguvu za Shaitani zinakuwa zikitushawishi sisi tutoe visingizio mbalimbali
ili mradi tusiamke na kufanya ibada za sala hususan za Alfajiri.
2.
Kusubiri sala baada ya sala .
Mumin wa kweli kwa hakika anakuwa akiusubiri wakati
wa sala kuwadia kwa ajili ya kutaka kusali sala kwa mara nyingine. Fursa hii
anaisubiri kwa hamu kwa sababu anapata fursa kwa mara nyingine kumwabudu na
kumshukuru Allah swt na ni wakati mwema kwa ajili ya kuomba Tawba ya madhambi
yake na vile vile ni wakati mwingine wa kujipatia neema na baraka za Allah swt.
Kwa kifupi mumin huyoo amabye anausubiri wakati wa sala uwadie anakuwa na hamu
ya kujipatia bahati ya kuweza kujiweka mbele ya Allah swt.
Tukiangalia mfano wa kidunia, iwapo mimi nitaambiwa
kuwa nimepewa kibali cha kumzuru Raisi wa nchi yetu nyakati fulani fulani kwa
siku. Hivyo mimi baada ya kumzuru mara ya kwanza kwa siku, nitakuwa na hamu na
shauku ya kuwadia kwa muda wa mara pili na hivyo hivyo kwa mara zote. Kwa
hakika nitaiona saa ikienda pole pole mno.
Na hivyo ndivyo inavyokuwa hali ya Mumin kwa ajili
ya kutaka kuwa mbele ya Allah swt kwa nyakati angalau mara tano kwa siku.
3.
Kutembea usiku na mchana kwa miguu kuelekea
Jamaa’
Mumin kwa hakika daima hupenda kujumuika pamoja na
jama’a yake katika mambo yote ya jumuiya yake na sala za jama’a .
Mtume s.a.w.w.
amesema:
“Kwa hakika Allah swt hawakutanishi Ummah wangu
katika upotofu, na mkono Wake uko pamoja na Ummah huo, kwa hakika atakayejitoa
humo basi atambue kuwa amejitoa kwa ajili ya Jahannam….”
Mizan al - Hikmah.
1.
Kutoa na kupokea salaam kwa unyenyekevu.
Mumin huwa daima mwepesi wa kutoa salaam na kujibu
salaam anazotolewa. Kamwe hawi mtu mwenye dharau wala kutegea kutolewa salaam
au mwenye kiburi.
Allah swt anatuambia katika Quran kuwa tutolewapo
salaamu ni faradhi kuijibu ama kwa kurejea salaam hiyo hiyo au kuijibu kwa
ubora zaidi.
Mtume s.a.w.w. alikuwa akiviziwa na ma Sahaba wake
kwa kujificha kiasi kwamba wapate fursa ya kutangulia kutoa salaam kwa sababu
Mtume s.a.w.w. alikuwa ndiyo daima mtu wa kutoa salaa kwa mara ya kwanza. Sasa
sisi tunayo kiburi cha
nini ? Kwa hakika
Allah swt anatuambia kuwa Salaam ni kauli itokayo Kwake.
2.
Kuwalisha chakula wale wanaohitaji.
Mumin kwa hakika huwa na moyo wa huruma kiasi kwamba
hawezi kula peke yake huku watu wengine wakiwa katika hali ya kubakia katika
njaa. Na si hayo tu bali huwa na moyo wa kutaka kuwasaidia binadamu wenzake
katika kila hali awezayo yeye.
Yeye huwa karimu na kamwe hawi bakhili ambaye yeye
mwenyewe hula bila ya kuwapa wenzake.
3.
Kusali sala za Tahajjud ( salat al - Layl au usiku wa manane ).
Mumin huwa anasali sala za usiku wa manane (Tahajjud
) wakati ambapo watu wanapokuwa wamelala usingizi mnono. Na husali kwa kutaka
ridhaa ya Allah swt na wala si kwa kujionyesha kwa watu.
Kwa hakika sala hii huwa ikisaliwa na Mitume
a.s. na Ma-Imamu a.s. kila siku bila ya
kukosa. Hii ni ibada ambayo mtu huwa anamnyenyekea Allah swt wakati ambapo
anakuwa ametulia kiroho na kiakili. Huwa hana mawazo au mambo yanayomsumbua
huku na huko. Hivyo inamaanisha kuwa ibada hii inafanyika kwa roho khalisi na
mtu hukubaliwa ibada zake haraka zaidi katika sala hizi.
Imam Hussain a.s. siku ya Aashura alimwusia dada
yake Bi. Zainab binti Ali ibn Albi Talib a.s. kuwa : “Ewe dada yangu Zainab !
Naomba usinisahau katika sala zako za usiku i.e. Salat al-Layl.”
C. Waangamio
1.
Tabia mbovu
Wale watu wote wanaoingia katika kikundi hiki cha
wenye tabia mbovu kwa hakika mwisho hao hujikuta kuwa wameangamia na kupoteza
maisha yao. Yaani maji yameshakwisha mwagiga hayazoeleki tena. Tabia kama hizi
zinamwigiza katika upotofu na kiburi na kujiona kuwa wao ndio watu
waliostaarabika lakini kumbe ni kinyume na hali hiyo kwani Allah swt hawapendi
wale wanaojifakharisha na kutakabari.
2.
Kutii nafsi zao
Iwapo mtu ataitii nafsi yake katika kumpotosha basi
atakuwa kwa hakika amepotoka na kuangamia humu duniani na Aakhera kwa pamoja.
Amesema Mtume Mtukufu s.a.w.w.: “Yeyote yule
atakayeitambua nafsi yake (mwenyewe) basi hakika amemtambua Allah swt.”
Vile vile amesema kuwa : “ Kwa hakika hodari kabisa
ni yule ambaye ameighalibu nafsi yake.” Yaani nafsi yake haimpotoshi katika
mambo mengi mno kama vile ulafi, uchoyo, ubakhili, uasherati, ukafiri,
maasi
n.k.
Iwapo mtu atatawaliwa na nafsi yake basi atakuwa
mtumwa wa nafsi yake.
Msomaji
anaombwa kusoma makala niliyoyatoa katika Sauti ya Bilal , P.O.Box 20033 DSM
juu ya maudhui Maadili ya Kiislamu - sura izungumziayo juu ya sifa 18 za
nafsi,Juzuu XXXI, Na. 5, Rabiul Aakhar 1418, Septemba 1997. (Iliyochapwa katika
sehemu mbili.)
3.
Kujifakharisha
Kwa hakika mtu anapoambukizwa ugonjwa huu basi
atambue kuwa ameangamia humu duniani na Aakhera kwa pamoja. Mtu anapenda
kujionyesha kuwa yeye ndiye mtu bora zaidi kuliko
wengine kwa sababu ya kupata kwa mali zaidi
au ilimu au wadhifa. Vitu vyote hivi ambavyo sisi tunavijua kuwa ni vyote
vyeneye kuangamia na kupotea na tutaviacha humu humu duniani.
Mtu katika sura hizi anaanza kukufuru kwani anaanza
kuwasema na kuwaona watu wenzake kama wanyama na waovu kiasi cha kuthubutu
kusema ati wanamsumbua na kumpotezea wakati wake. Inambidi yeye kutambua kuwa
Allah swt amemwingiza katika mtihani hivyo inambidi afanye mema ili aweze
kufuzu.
D. Uokovu
1.
Hofu ya Allah swt katika hali ya dhahiri na batini
Iwapo mtu atataka kupata uokovu inambidi awe na
khofu ya Allah swt wakati akiwa peke yake na vile vile anapokuwa mbele ya watu.
Isiwe kwamba mtu anapokuwa peke yake anaruhusiwa kufanya madhambi na wakati
anapokuwa mbele ya watu kujionyesha kuwa ni mtu ambaye ana khofu ya Allah swt
kupita watu wengine.
Kutenda madhambi
katika hali yoyote yanayo adhabu kali.
2.
Kusudio madhubuti katika umasikini na utajiri
Mtu inambidi awe na makusudio yake madhubuti bila ya
kuyumbishwa katika hali ya umasikini na utajiri pia. Kwa sababu anapokuwa na
moyo wa kuwasaidia watu wenzake katika ufukara asiupoteze katika hali awapo
tajiri. Iwapo alikuwa msalihina awapo katika ufukara basi aendelee vile vile
kwani asije akatoa kisingizio cha kukosa wakati katika utajiri na biashara
zake.
Vile vile mtu anapokuwa katika umasikini inambidi
awe madhubuti katika imani yake ili asije akakufuru na kushuku uadilifu wa
Allah swt kwa shida azipatazo maishani mwake. Kila mtu anakumbana na misukosuko
mbalimbali humu duniani hivyo inambidi kuimarisha imani yake.Huo pia huwa ni
wakati wa mtihani kutoka kwa Allah swt, na inambidi ajaribu kufuzu.
3.
Uadilifu katika shida na raha
Inambidi mtu awe daima katika mizani ya kauli yake
asije akatamka maneno ambayo yatamkufurisha wakati anapokuwa katika shida au
raha. Anapokuwa katika shida asije akasema kuwa Allah swt amemtupa au hamjali
wala hazisikii duaa zake (Allah swt atuepushe na wakati huo) na pale anapokuwa
katika utajiri na starehe asije akakufuru kuwa yeye hana shida ya kitu chochote
au mtu yeyote kwani anacho kile anachokihitaji, hivyo kujifanya maghururi na
mwenye takabbur. Kwa hakika Allah swt hawapendi watu kama hawa.
Kwa wale walio matajiri inawabidi wafanye mambo mema
kwa kutoa misaada kwa misikiti,madrasa masikini na mahala pote pale penye
kupata ridhaa za Allah swt na wale walio masikini na mafukara inawabidi wakinai
kwa kile walichonacho na wamshukuru Allah swt kwa kile anachowajaalia.
Maneno yetu yawe yamepimwa vyema kabla ya kuyatamka
kwani isije tukasema mambo ambayo yatatufanya sisi tuwe mustahiki wa adhabu za
Allah swt. Na wala tusiwaseme watu vibaya kwani na hayo pia yatatufanya sisi
tuwe mustahiki wa Adhabu za Allah swt.
Hadith
hii imesomwa na Sheikh Akmal Hussain kutoka
Moshi, Tanzania.
Hadith hii imeshereshwa
na:
Amiraly M.H.Datoo
8th May 1998
Jannat
11:35, 3:112, 3:113, 10:15,
10:13, 3:111, 10:14, 9:354, 14:119, 15:205, 17:315, 18;375, 18:129, 19:9,
19:123,
19:124,
19:137,
20:218,
20:213,
20:399,
14:83,
14:83, 14:84, 4:18, 4:20, 8:117, 8:123
Maana
ya
Jahiim
j 5 uk. 256;
Jahannam
:
11:20, 1:294,
14:357, 15:204, 17:232, 12:178, 18:130, 18:383, 19:141, 20:7, 20:412, 20:438,
8:350,
8:351,
8:352,
8:113,
8:114,
8:115,
20:9
(Namba inayotangulia ni ya
Juzuu na inayofuata ni nambari za ukurasa.)
(Marejeo haya ni ya Al-Mizan fi tafsiril
Qur’an, zipo juzuu 20. Chapa ya Intesharat Bayan, Teheran, Nasir khosru,
Teheran. Jamhuri ya Kiislamu ya Iran)
Hotuba: 16; 27; 28; 64;
66; 79; 83; 157; 171; 167; 160; 75; 109; 106; 119; 120; 124; 128; 12; 144; 152;
156; 193; 176; 165; 183; 192; 191; 193; 199;
Msemo: 199;
Barua: 17; 27; 31; 28;
41; 76;
Wasia: 24
Misemo ya hekima: 31; 368; 228; 349; 387; 429; 456; 131; 42
(Marejeo haya ni ya Chapa ya
Sub-hi Salehe, Beirut. Libanon)
NDOTO YA Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.
Siku
moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliingia Msikitini na kuwaambia Ma-Sahaba,
“Je niwasimulieni ndoto niliyoiota ?”
Ayah
za
Qur'an Tukufu zizungumziazo Jannat
Makala
haya yemkusanywa na kutarjumiwa na
Amiraly
M.H.Datoo
- Bukoba Tanzania
Utaratibu ufuatao umetumika
kuandika Surah na Ayah za
Qur'an Tukufu
:
5 : 119
hii ikimaanisha kuwa katika
Surah ya 5 ya
Qur'an Tukufu Ayah ya 119.
No. |
Maudhui inayozungumzwa |
Sura namba na Ayah namba |
1 |
Afya bora katika
Jannat
|
19 : 62 |
2 |
Ahadi na
Jannat |
25 : 16 |
3 |
Allah swt na Wakazi wa
Jannat
|
35 : 34,
36 : 58 |
4 |
Amani ya Wakazi wa
Jannat |
52 : 20 |
5 |
Bahati za Wakazi wa Jannat
|
52 : 25 |
6 |
Baraka za
Jannat
|
2:25, 2:36, 10:10, 15:46, 16:31, 22:23, 22:24, 25:10, 43:71, 43:73,
47:12, 47:15, 52:17, 52:18, 52:19, 52:22, 55:48, 55:50, 56:23, 56:33, 56:37,
57:12, 69:23, 69:24, 76:20, 76:22, 77:43, 82:13, 85:11, 87:8 |
7 |
Batili katika
Jannat
|
19 : 62 |
8 |
Bi. Hawa katika
Jannat |
7:19, 7:20, 7:22 |
9 |
Bustani ya
Jannat
|
13:23, 15:45, 16:31,
47:15, 61:12, 65:11, 66:8, 76:14,
85:11,98:7 |
10 |
Chakula cha Wakazi wa
Jannat |
8 : 74 |
11 |
Chakula cha watu wa
Jannat
|
56:21 |
12 |
Chemichemi ya Tasnim katika
Jannat |
83:27, 83:28 |
13 |
Chemichemi za
Jannat
|
15:45, 44:52,55:50, 76:17,
88:12 |
14 |
Daraja za
Jannat
|
17:21, 46:19, 55:62 |
15 |
Familia ya Wakazi wa
Jannat
|
52 : 21 |
16 |
Furaha
ya Wakazi a
Jannat
|
7:43, 88:9, 101:1 |
17 |
Furaha katika
Jannat
|
37 : 58 |
18 |
Furaha za Wakazi wa
Jannat |
37 : 45 |
19 |
Habari njema za
Jannat
|
50 : 35 |
20 |
Hali za
Jannat
|
35:35, 76:29 |
21 |
Hariri iliyofumwa ya
Jannat |
76:21 |
22 |
Heshima katika
Jannat
|
37 ; 42,
39 : 73 |
23 |
Heshima ya Wakazi wa
Jannat
|
36 : 56 |
24 |
Hotuba za Wakazi wa
Jannat |
88 : 11 |
25 |
Hour al-‘Ayn katika
Jannat |
37 : 48 |
26 |
Huruma za Wakazi wa
Jannat
|
44:53, 56:16 |
27 |
Huzuni katika
Jannat |
35:34, 35:35, 36:48 |
28 |
Imani katika
Jannat
|
36:55 |
29 |
Jannat katika
maisha baada ya hapa ulimwenguni |
2 : 25 |
30 |
Jannat kwa ajili ya
wema |
35: 33 |
31 |
Jannat Mlezi |
37 : 42 |
32 |
Jannat na maisha ya
baada ya hapa ulimwenguni |
3 : 133 |
33 |
Jannat na
wacha-mungu |
50 : 31 |
34 |
Jannat ya wacha
mungu |
3 : 133 |
35 |
Jannat ya Wacha
mungu |
13:35 |
36 |
Jannat ya
Wacha-mungu |
38 : 49 |
37 |
Jinn katika
Jannat
|
55:46 |
38 |
Kauli njema za wakazi wa
Jannat
|
56 : 25 |
39 |
Kazi katika
Jannat |
36 : 55 |
40 |
Kinywaji cha Wakazi wa
Jannat |
37:45 |
41 |
Kitulizo cha Wakazi wa
Jannat
|
18 : 31 |
42 |
Kituo cha karibu katika
Jannat |
83:28 |
43 |
Kuchekeshana kwa Wakazi wa
Jannat
|
52:23
|
44 |
Kuelekea Jannat
|
5:119, 9:89 |
45 |
Kuingia katika
Jannat
|
2:214, 3:185, 4:13,15:45,
15:46, 18:31, 1963, 36:26, 40:8 |
46 |
Kuishi katika
Jannat
|
14:23, 15:47, 15:48, 76:16 |
47 |
Kuishi kifahari katika
Jannat
|
35:34 |
48 |
Kuisifu
Jannat |
25 : 76 |
49 |
Kujamiiana katika
Jannat
|
37 : 42 |
50 |
Kujamiiana kwa Wakazi wa
Jannat |
15 : 47 |
51 |
Kunyimwa kwa
Jannat
|
5:72, 7:40, 38:77, 70:39 |
52 |
Kuridhika katika
Jannat |
92 : 21 |
53 |
Kuwastarehesha Wakazi wa
Jannat
|
3 : 198 |
54 |
Lungilungi ( ua)
|
56 : 28 |
55 |
Maamkiano katika
Jannat
|
14:23, 19:62, 33:44, 36:58 |
56 |
Maamkizi ya Watu wa
Jannat
|
13:23, 13:24, 14:23,
15:46, 56:26 |
57 |
Mafundisho ya Wakazi wa
Jannat
|
7:43, 56:25, 78:35 |
58 |
Mahala ilipo
Jannat
|
53 : 15 |
59 |
Mahala pa kupumzikia kwa ajili ya Wakazi wa
Jannat |
25 : 24 |
60 |
Maisha ya Wakazi wa
Jannat
|
7 : 49 |
61 |
Majadiliano katika
Jannat
|
37 : 54 |
62 |
Majeruhi katika
Jannat
|
36 : 58 |
63 |
Makazi katika
Jannat |
9 : 72, 10 : 9 |
64 |
Makazi ya Jahannam na
Jannat
|
7 : 50 |
65 |
Makazi ya
Jannat na Jahannam
|
7 : 44, 7:54 |
66 |
Malaika wa
Jannat |
39 : 73 |
67 |
Malazi ya Wakazi wa
Jannat
|
55:54 |
68 |
Malezi katika
Jannat |
36:57, 37:42 |
69 |
Malezi ya Wakazi wa
Jannat |
19 : 62 |
70 |
Malipo ya
Jannat |
2:25, 9:89,
9:11 |
71 |
Maneno katika
Jannat |
22:24 |
72 |
Manukato ya
Jannat |
83:26 |
73 |
Mapambo ya Wakazi wa
Jannat
|
18 : 31 |
74 |
Mapenzi na usawa miongoni mwa Wakazi wa
Jannat |
10:23, 21:102, 21:103,
35:35, 50:34, 50:35, 52:23, 52:25, 55:54, 55:76, 56:12, 56:15, 56:20, 56:28,
56:31, 76:41, 88:15, 88:16 |
75 |
Mapokezi katika
Jannat |
25:75 |
76 |
Masharti ya
Jannat
|
25 : 16 |
77 |
Mashujaa wa Imani katika
Jannat |
9:21, 9:98, 61:12 |
78 |
Matembezi katika
Jannat |
39 : 73 |
79 |
Matunda ya
Jannat
|
44:55, 47:15, 55:52,
55:54, 55:68, 56:20, 56:28, 56:32, 69:23,
76:14 |
80 |
Mavazi ya
Jannat
|
76 : 21 |
81 |
Mavazi ya Wakazi wa
Jannat
|
18:31, 22:23, 44:53 |
82 |
Mazulia ya
Jannat
|
88 : 16 |
83 |
Mazungumzo na Wakazi wa
Jannat |
37 : 50 |
84 |
Mazungumzo ya kipuuzi katika
Jannat |
19 : 62 |
85 |
Mikusanyiko katika
Jannat
|
15 : 47 |
86 |
Miti ya
Jannat |
3:198, 4:57, 56:28, 56:29 |
87 |
Mito ya
Jannat
|
88 : 15 |
88 |
Mito ya
Jannat
|
2:25, 3:198, 4:57, 5:119,
7:43, 9:72, 9:89, 9:100,10:9, 58:22, 61:12, 65:11, 66:8, 98:7 |
89 |
Mtume Adam a.s. katika Jannat
|
2:35, 2:36, 7:19, 7:20, 7:22,
20:118 |
90 |
Mtume katika
Jannat |
9 : 89 |
91 |
Mwanamwali mzuri wa
Jannat kwa ajili
Wacha-mungu |
38 : 49 |
92 |
Mwito kuelekea
Jannat
|
2: 221 |
93 |
Neema za Wakazi wa
Jannat
|
52:22, 52:23, 77:43 |
94 |
Ombi katika
Jannat |
36:57, 41:31, 44:55 |
95 |
Sababu za
Jannat
|
19: 60, 57:21, 58:11,
58:22, 61:12, 66:8, 76:6, 76:12, 85:11 |
96 |
Shughuli za Wakazi wa Jannat |
26:55, 83:25 |
97 |
Shukurani za Wakazi wa
Jannat
|
7:43, 10:10, 35:35 |
98 |
Sifa kwa ajili ya
Jannat |
3:136, 3:142, 5:65, 14:23,
20:75, 25:15, 25:75 |
99 |
Starehe za Wakazi wa
Jannat
|
36:56, 36:57, 52:18, 87:8, 89:26 |
100 |
Starehe za Wakazi wa
Jannat
|
7:43, 15:47 |
101 |
Starehe za Wakazi wa
Jannat |
35:33, 36 :56, 37:58 |
102 |
Starehe zilizopo katika
Jannat
|
37:42, 27:45, 37:48, 39:32 |
103 |
Tafrija za Wakazi wa
Jannat
|
56 : 16 |
104 |
Uchovu katika
Jannat |
15:48, 35:35 |
105 |
Udugu wa Wakazi wa
Jannat
|
10 : 10 |
106 |
Ufalme wa
Jannat |
18:31, 52:20, 55:76,
56:15, 83:35, 88:13 |
107 |
Uhalisi wa Wakazi wa
Jannat |
7 : 43 |
108 |
Uhuru katika
Jannat
|
39:73 |
109 |
Uhuru wa Wakazi wa
Jannat
|
56:33 |
110 |
Ukaribisho kwa Wakazi wa
Jannat
|
50 : 34 |
111 |
Ukarimu wa Wakazi wa
Jannat |
37:42 |
112 |
Ukuu wa Wakazi wa
Jannat |
41 : 40 |
113 |
Ukweli katika
Jannat |
5 : 119 |
114 |
Ukweli wa
Jannat |
39 : 32 |
115 |
Ukweli wa Wakazi wa
Jannat |
15 : 47 |
116 |
Umilele katika
Jannat |
2:25, 2:82, 3:136, 3:198,
4:13, 4:57, 4:122, 5:85, 18:3, 19:61, 25:16, 25:76, 35:35, 37:58, 39:73 |
117 |
Umilele wa
Jannat
|
43:71, 4:73, 44:56, 47:15,
48:5, 50:34, 56:33, 57:12, 64:9, 65:11, 76:11, 76:19, 98:8 |
118 |
Urafiki wa Wakazi wa
Jannat
|
52:25 |
119 |
Uroho wa
Jannat
|
70 : 36 |
120 |
Usahihi wa Wakazi wa
Jannat |
15 : 46 |
121 |
Usalama wa Wakazi wa
Jannat |
50:34, 52:18 |
122 |
Usalama wa Wakazi wa
Jannat |
15:46 |
123 |
Ushindani kwa ajili ya
Jannat
|
3 : 133 |
124 |
Usumbufu katika
Jannat
|
35 : 35 |
125 |
Utajiri wa
Jannat |
55 : 64 |
126 |
Utayari wa
Jannat |
3 : 133 |
127 |
Uthamini wa
Jannat |
9:89, 9:100, 13:24, 20:76,
44:57, 57:21 |
128 |
Utofauti katika
Jannat
|
17:21 |
129 |
Uuwezo wa
Jannat
|
12 3 : 133 |
130 |
Uwastani wa
Jannat |
76:13 |
131 |
Uwingi wa
Jannat
|
55 : 62 |
132 |
Uzoefu wa Wakazi wa
Jannat
|
44:53, 56:16 |
133 |
Vijana wa Wakazi wa
Jannat |
56: 17 |
134 |
Vinywaji vya
Jannat
|
47:15, 56:18, 56:19,
76:16, 76:17, 83:26, 83:27, 88:14 |
135 |
Vito vya thamani katika
Jannat
|
22:23, 35:33, 76:21 |
136 |
Vitu vya fahari vya Wakazi wa
Jannat
|
7 : 50 |
137 |
Vyakula vya
Jannat
|
83 : 26 |
138 |
Vyakula vya
Jannat |
7:50, 43:71, 47:15 |
139 |
Wafanya ‘ibada katika
Jannat
|
3:136, 16:31, 19:85,
38:49, 39:73, 44:55, 44:55, 47:15, 50:35, 52:17, 52:18, 52:19, 52:20, 52:21,54:54,
54:55, 78:32, 78:37 |
140 |
Wahamiaji katika
Jannat
|
9:21, 9:22, 22:59 |
141 |
Wahudumu kwa ajili ya Wakazi wa
Jannat |
52:24, 76:15 |
142 |
Wahudumu wa
Jannat |
52:24, 56:17, 76:19 |
143 |
Wakazi wa
Jannat katika
Jannat
|
22 : 24 |
144 |
Wakazi wa
Jannat katika
Jannat |
22 : 24 |
145 |
Wakazi wa
Jannat na Hour
al-‘Ayn |
37 : 48 |
146 |
Wakazi wa
Jannat na marafiki
zao |
37 : 54 |
147 |
Wakazi wa
Jannat na Wake zao |
36 : 56 |
148 |
Walio okoka katika
Jannat |
76:6, 83:23, 88:10 |
149 |
Wanawake wa
Jannat |
56:36 |
150 |
Warithi
wa
Jannat
|
23 : 10 |
151 |
Washika Vikombe wa
Jannat |
76:15, 76:16, 83:23 |
152 |
Watenda mema katika
Jannat |
11:23 |
153 |
Watenda Usahihi katika
Jannat |
3:198, 10:9, 76:5, 77:44,
82:13, 83:23, 83:24 |
154 |
Watu wa
Jannat
|
7:40, 7:43, 7:49, 25:15 |
155 |
Watu wa Vitabu na
Jannat
|
2 : 111 |
156 |
Waumini katika
Jannat |
7:49, 9:22, 9:72, 9:100, 10:9, 11:23, 30:15, 40:81, 41:31, 43:70,48:5,
56:39, 57:12, 61:12, 64:9, 69:24, 70:35,76:22, 85:11, 98:8
|
157 |
Zawadi za Wakazi wa
Jannat |
18 : 3 |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
[1] Nipo ninakitayarisha kitabu juu ya maudhui haya.
[2] Iwapo utapenda kusoma habari zaidi juu ya maudhui
haya ya Tawbah, jipatie kitabu nilichokitafsiri cha Syed Dastaghib Sirazi
kinachozungumzia ka marefu na mapana kuhusu
somo hili.
[3]
Ninajaribu
kutoa maelezo machache ili kuwezesha kueleweka vizuri ili nawe msomaji uweze
kuchangia mawazo na kuweza kupanua ilimu yako. Hata hivyo itawabidi kufanya
utafiti zaidi ili kujua mafhum ya usia huu vizuri zaidi.