ZAMA ZITAKAZOFIKA...

Makala haya yametarjumiwa na kushereheshwa na:Amiraly M.H. Datoo

Hadithi hii ilisomwa na: Sheikh Akmal Hussein Taheri - Bukoba.

Amesema Mtume sa.w.w. kuwa: Utafika wakati katika Ummah wangu ambapo:

  1. Nyuso za watu zitakuwa za kibinadamu lakini nyoyo zao zitakuwa za kishetani na mfano wao utakuwa kama mnyama mwenye kudhuru na ambaye daima hutaka damu tu

  2. Kamwe hawazuii watu kutotenda maovu bali wao wenyewe watakuwa wakiyatenda hayo hayo

  3. Iwapo watu kama hao watafuatwa basi watawatumbukiza watu katika hali ya mashaka

  4. Iwapo utaongea nao, basi daima watakukadhibisha

  5. Na iwapo utajaribu kujitenga nao basi wataanza kukusengenya

  6. Kwao Sunnah ni bida'a na bida'a kwao ni Sunnah mifano ni mingi kama hii ya Mi'raji, uzawa wa Mtume sa.w.w. , n.k.

  7. Watu walio na heshima kwao ndio wanachukuliwa kuwa waovu

  8. Na wale walio waovu miongoni mwa watu ndio wanaoheshimiwa na kutukuzwa

  9. Waumini miongoni mwao ni watu waliokandamizwa

  10. Ambapo waovu ndio wanaotukuzwa kwao

  11. Watoto wao hawana heshima wala tabia njema

  12. Na wake zao watakuwa waovu kiasi kwamba waume zao watakuwa wamewachoka wake zao na watajaribu kujiepusha nao. (Wanawake kutovaa hijabu na mavazi ya heshima yenye kuwasitiri wao, kujipamba na kujirembesha kwa ajili ya wengine, kupeana mikono na wanaume wasio waume zao. Ama wanaume pia hawapo nyuma katika masuala kama haya kwani utayasikia kuwa wanaume wengine wanao wake wa pembeni hata bila ndoa, vile vile utawasikia wauza pombe kuwa biashara yao inaanguka katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ati wanywaji wa pombe wengi ni Waislamu

  13. Maulamaa wao hawawaongozi kwa mema na wala hawawakatazi dhidi ya maovu yaliyo miongoni mwa Waumini (ati kwa sababu za fedha na hofu ya maslahi yao kwamba yeye hujiinamisha mbele ya matajiri na kuwadhalilisha masikini

  14. Kuomba msaada wao ni kujidhalilisha

  15. Na kwa kuwaomba msaada wakati wa shida, basi huwadharau waombaji

  16. Na kuomba chochote kutoka kwa watu kama hawa ni umasikini na ufukara

  17. Na utakapofika wakati kama huo, basi Allah swt hatawanyeshea mvua hata kwa tone moja wakati utakapofika msimu wa mvua na badala yake kutakuwapo na mvua pasi na msimu wake. Sasa jee mvua zisizo za msimu zinasaidia vipi ? Jee hii si dalili ya adhabu na maafa ?

  18. Na watu watasalitiwa na wadhalimu waovu kabisa

  19. Ili watu hao watawapeleka watu kuelekea makali ya adhabu

  20. Nyakati hizo watu wataomba dua lakini hazitakubaliwa

  21. Nyuso za watu zitakuwa za kibinadamu lakini nyoyo zao zitakuwa za kishetani na mfano wao utakuwa kama mnyama mwenye kudhuru na ambaye daima hutaka damu tu

  22. Kamwe hawazuii watu kutotenda maovu bali wao wenyewe watakuwa wakiyatenda hayo hayo

  23. Iwapo watu kama hao watafuatwa basi watawatumbukiza watu katika hali ya mashaka

  24. Iwapo utaongea nao, basi daima watakukadhibisha

  25. Na iwapo utajaribu kujitenga nao basi wataanza kukusengenya

  26. Kwao Sunnah ni bida'a na bida'a kwao ni Sunnah mifano ni mingi kama hii ya Mi'raji, uzawa wa Mtume sa.w.w., n.k.

  27. Watu walio na heshima kwao ndio wanachukuliwa kuwa waovu

  28. Na wale walio waovu miongoni mwa watu ndio wanaoheshimiwa na kutukuzwa

  29. Waumini miongoni mwao ni watu waliokandamizwa

  30. Ambapo waovu ndio wanaotukuzwa kwao

  31. Watoto wao hawana heshima wala tabia njema

  32. Na wake zao watakuwa waovu kiasi kwamba waume zao watakuwa wamewachoka wake zao na watajaribu kujiepusha nao. (Wanawake kutovaa hijabu na mavazi ya heshima yenye kuwasitiri wao, kujipamba na kujirembesha kwa ajili ya wengine, kupeana mikono na wanaume wasio waume zao. Ama wanaume pia hawapo nyuma katika masuala kama haya kwani utayasikia kuwa wanaume wengine wanao wake wa pembeni hata bila ndoa, vile vile utawasikia wauza pombe kuwa biashara yao inaanguka katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ati wanywaji wa pombe wengi ni Waislamu

  33. Maulamaa wao hawawaongozi kwa mema na wala hawawakatazi dhidi ya maovu yaliyo miongoni mwa Waumini (ati kwa sababu za fedha na hofu ya maslahi yao kwamba yeye hujiinamisha mbele ya matajiri na kuwadhalilisha masikini

  34. Kuomba msaada wao ni kujidhalilisha

  35. Na kwa kuwaomba msaada wakati wa shida, basi huwadharau waombaji

  36. Na kuomba chochote kutoka kwa watu kama hawa ni umasikini na ufukara

  37. Na utakapofika wakati kama huo, basi Allah swt hatawanyeshea mvua hata kwa tone moja wakati utakapofika msimu wa mvua na badala yake kutakuwapo na mvua pasi na msimu wake. Sasa jee mvua zisizo za msimu zinasaidia vipi ? Jee hii si dalili ya adhabu na maafa ?

  38. Na watu watasalitiwa na wadhalimu waovu kabisa

  39. Ili watu hao watawapeleka watu kuelekea makali ya adhabu

  40. Nyakati hizo watu wataomba dua lakini hazitakubaliwa.