ZAMA ZITAKAZOFIKA...
Makala haya yametarjumiwa na kushereheshwa na:Amiraly M.H. Datoo
Hadithi hii ilisomwa na: Sheikh Akmal Hussein Taheri - Bukoba.
Amesema Mtume sa.w.w. kuwa: Utafika wakati katika Ummah wangu ambapo:
-
Nyuso za watu zitakuwa za kibinadamu lakini nyoyo zao zitakuwa za kishetani
na mfano wao utakuwa kama mnyama mwenye kudhuru na ambaye daima hutaka damu
tu
-
Kamwe hawazuii watu kutotenda maovu bali wao wenyewe watakuwa wakiyatenda
hayo hayo
-
Iwapo watu kama hao watafuatwa basi watawatumbukiza watu katika hali ya mashaka
-
Iwapo utaongea nao, basi daima watakukadhibisha
-
Na iwapo utajaribu kujitenga nao basi wataanza kukusengenya
-
Kwao Sunnah ni bida'a na bida'a kwao ni Sunnah mifano ni mingi kama hii ya
Mi'raji, uzawa wa Mtume sa.w.w. , n.k.
-
Watu walio na heshima kwao ndio wanachukuliwa kuwa waovu
-
Na wale walio waovu miongoni mwa watu ndio wanaoheshimiwa na kutukuzwa
-
Waumini miongoni mwao ni watu waliokandamizwa
-
Ambapo waovu ndio wanaotukuzwa kwao
-
Watoto wao hawana heshima wala tabia njema
-
Na wake zao watakuwa waovu kiasi kwamba waume zao watakuwa wamewachoka wake
zao na watajaribu kujiepusha nao. (Wanawake kutovaa hijabu na mavazi ya heshima
yenye kuwasitiri wao, kujipamba na kujirembesha kwa ajili ya wengine, kupeana
mikono na wanaume wasio waume zao. Ama wanaume pia hawapo nyuma katika masuala
kama haya kwani utayasikia kuwa wanaume wengine wanao wake wa pembeni hata
bila ndoa, vile vile utawasikia wauza pombe kuwa biashara yao inaanguka katika
mwezi mtukufu wa Ramadhani ati wanywaji wa pombe wengi ni Waislamu
-
Maulamaa wao hawawaongozi kwa mema na wala hawawakatazi dhidi ya maovu yaliyo
miongoni mwa Waumini (ati kwa sababu za fedha na hofu ya maslahi yao kwamba
yeye hujiinamisha mbele ya matajiri na kuwadhalilisha masikini
-
Kuomba msaada wao ni kujidhalilisha
-
Na kwa kuwaomba msaada wakati wa shida, basi huwadharau waombaji
-
Na kuomba chochote kutoka kwa watu kama hawa ni umasikini na ufukara
-
Na utakapofika wakati kama huo, basi Allah swt hatawanyeshea mvua hata kwa
tone moja wakati utakapofika msimu wa mvua na badala yake kutakuwapo na mvua
pasi na msimu wake. Sasa jee mvua zisizo za msimu zinasaidia vipi ? Jee hii
si dalili ya adhabu na maafa ?
-
Na watu watasalitiwa na wadhalimu waovu kabisa
-
Ili watu hao watawapeleka watu kuelekea makali ya adhabu
-
Nyakati hizo watu wataomba dua lakini hazitakubaliwa
-
Nyuso za watu zitakuwa za kibinadamu lakini nyoyo zao zitakuwa za kishetani
na mfano wao utakuwa kama mnyama mwenye kudhuru na ambaye daima hutaka damu
tu
-
Kamwe hawazuii watu kutotenda maovu bali wao wenyewe watakuwa wakiyatenda
hayo hayo
-
Iwapo watu kama hao watafuatwa basi watawatumbukiza watu katika hali ya mashaka
-
Iwapo utaongea nao, basi daima watakukadhibisha
-
Na iwapo utajaribu kujitenga nao basi wataanza kukusengenya
-
Kwao Sunnah ni bida'a na bida'a kwao ni Sunnah mifano ni mingi kama hii ya
Mi'raji, uzawa wa Mtume sa.w.w., n.k.
-
Watu walio na heshima kwao ndio wanachukuliwa kuwa waovu
-
Na wale walio waovu miongoni mwa watu ndio wanaoheshimiwa na kutukuzwa
-
Waumini miongoni mwao ni watu waliokandamizwa
-
Ambapo waovu ndio wanaotukuzwa kwao
-
Watoto wao hawana heshima wala tabia njema
-
Na wake zao watakuwa waovu kiasi kwamba waume zao watakuwa wamewachoka wake
zao na watajaribu kujiepusha nao. (Wanawake kutovaa hijabu na mavazi ya heshima
yenye kuwasitiri wao, kujipamba na kujirembesha kwa ajili ya wengine, kupeana
mikono na wanaume wasio waume zao. Ama wanaume pia hawapo nyuma katika masuala
kama haya kwani utayasikia kuwa wanaume wengine wanao wake wa pembeni hata
bila ndoa, vile vile utawasikia wauza pombe kuwa biashara yao inaanguka katika
mwezi mtukufu wa Ramadhani ati wanywaji wa pombe wengi ni Waislamu
-
Maulamaa wao hawawaongozi kwa mema na wala hawawakatazi dhidi ya maovu yaliyo
miongoni mwa Waumini (ati kwa sababu za fedha na hofu ya maslahi yao kwamba
yeye hujiinamisha mbele ya matajiri na kuwadhalilisha masikini
-
Kuomba msaada wao ni kujidhalilisha
-
Na kwa kuwaomba msaada wakati wa shida, basi huwadharau waombaji
-
Na kuomba chochote kutoka kwa watu kama hawa ni umasikini na ufukara
-
Na utakapofika wakati kama huo, basi Allah swt hatawanyeshea mvua hata kwa
tone moja wakati utakapofika msimu wa mvua na badala yake kutakuwapo na mvua
pasi na msimu wake. Sasa jee mvua zisizo za msimu zinasaidia vipi ? Jee hii
si dalili ya adhabu na maafa ?
-
Na watu watasalitiwa na wadhalimu waovu kabisa
-
Ili watu hao watawapeleka watu kuelekea makali ya adhabu
-
Nyakati hizo watu wataomba dua lakini hazitakubaliwa.