rudi nyuma | Yaliyomo | endelea |
Mtume Mtukufu s.a.w.w. akasema: "Ndiyo, naapa kwa Aliyonayo roho yangu mkononi mwake."
"Ewe Salman,
6. wakati huo watawala watakuwa wadhalimu
7. Mawaziri watakuwa waasi,
8. na wadhamini (wale waliopewa amana kwa kuaminiwa) watafanya hiana,
9. hakika wakati huo maovu yatakuwa mema na mema yatakuwa maovu,
10. wale wafanyao hiana wataaminiwa na waaminifu watafikiriwa kuwa si waaminifu;na mwongo atasadikiwa,na msema kweli atahesabiwa mwongo.
11. Wakati huo kutakuwapo na utawala wa wanawake XE "wanawake" ,
12. Masuria watashauriwa,
13. na watoto watakaa juu ya mimbar XE "mimbar" ,
14. udanganyifu utahesabiwa kuwa ni uerevu
15. na Zaka itakuwa ni kama kutozwa faini;na mateka ya vita (yaani mali ya ummah XE "ummah" ) yatakuwa kama ni mali ya mtu binafsi;na mtu atakuwa mjeuri kwa wazazi wake na atakuwa mwema kwa marafiki zake,
16. na wakati huo kutatokea na nyota XE "nyota" zenye mikia (comets)."
Salman akasema: "Haya yatatokea,ewe Mtume wa Allah swt?"
Mtume Mtukufu s.a.w.w. akasema: "Ndiyo,naapa kwa Aliyonayo roho yangu mkononi mwake."
"Ewe Salman!
17. wakati huo mwanamke XE "wanawake:mwanamke" atakuwa mshiriki wa mumewe katika biashara,
18. na mvua XE "mvua" itakuwa moto XE "moto" sana
19. na watu wema watabaki katika huzuni;na masikini hawata heshimiwa;na wakati huo masoko yatakaribiana,
20. Tena huyu atasema,"Mimi sikuuza chochote,na yule atasema, "Mimi sikupata faida yoyote." Kwa hivyo hutamkuta mtu yeyote asiyemlalamikia Allah swt.
"Ewe Salman!
21. tena itatokea iwapo watu watawazungumzia watawala wao, watawaua, na ikiwa watanyamaza kimya, watanyang'anywa mali yao, watanyimwa heshima zao,watamwaga damu XE "damu" yao na mioyo ya watu itajaa woga;kisha hutamwona mtu yeyote ila atakuwa mwoga,mwenye khofu,ametishika na ameshstushwa”
"Ewe Salman!
22. Bila shaka wakati huo mambo fulani yataletwa kutoka Mashariki
23. na mambo fulani yataletwa kutoka Magharibi,
24. Basi ole kwa watu walio dhaifu (wa imani) katika Ummah XE "Ummah" wangu kutokana na hayo; Ole ya Allah swt iwe kwa hayo. Wao hawatakuwa na huruma juu ya wadogo wao,wala hawatamsamehe yeyote aliyefanya kosa.Miili yao itakuwa ya wanadamu,lakini mioyo yao itakuwa ya mashetani."
"Ewe Salman!
25. Wakati huo wanaume XE "wanaume" watawaashiki wanaume,
26. na wanawake XE "wanawake" watawaashiki wanawake;
27. na watoto wa kiume watapambwa kama wanawake;
28. na wanaume watajifanya kama wanawake
29. na wanawake wataonekana kama wanaume;
30. na wanawake watapanda mipando
31. Hapo tena patakuwepo laana ya Allah swt juu ya wanawake wa Ummah XE "Ummah" wangu."
"Ewe Salman!
32. Bila shaka wakati huo Misikiti XE "Misikiti" itapambwa (kwa dhahabu n.k.) kama inavyofanywa katika masinagogi na makanIssa,
33. na Qur’an XE "Quran" zitapambwa (kwa nakshi na rangi za kupendeza n.k.)
34. na minara (ya misikiti) itakuwa mirefu;na safu za watu wanaosimama katika sala XE "sala" zitazidi,lakini nyoyo zao zitachukiana na maneno yao yatatofautiana."
"Ewe Salman!
35. Wakati huo wanaume XE "wanaume" watatumia mapambo ya dhahabu;kisha watavaa hariri,na watatumia ngozi za chui."
"Ewe Salman!
36. Wakati huo riba XE "riba" itakuwako,
37. na watu wata- fanyia biashara kwa kusemana na rushwa
38. na dini itawekwa chini,na dunia itanyanyuliwa juu."
"Ewe Salman!
39. Wakati huo talaqa XE "talaqa" zitazidi
40. na mipaka ya Allah swt hayatasimamishwa
41. Lakini hayo hayatamdhuru Allah swt."
"Ewe Salman!
42. Wakati huo watatokea wanawake XE "wanawake" waimbaji,
43. na ala za muziki
44. na wabaya kabisa watawatawala Ummah XE "Ummah" wangu."
"Ewe Salman!
45. Wakati huo matajiri katika Ummah XE "Ummah" wangu watakwenda Kuhiji kwa matembezi,na walio wastani kwa biashara,na masikini kwa kujionyesha.
46. Hivyo basi wakati huo watakuwapo watu ambao watajifundisha Qur’an XE "Quran" si kwa ajili ya Allah swt na wataifanya Qur’an XE "Quran" kama ala ya muziki.
47. Na watakuwapo watu ambao watasoma dini si kwa ajili ya Allah swt
48. na idadi ya wanaharamu itazidi
49. watu wataiimba Qur’an XE "Quran" ,
50. na watu watavamiana kwa uroho wa kidunia."
"Ewe Salman!
51. Haya yatatokea wakati heshima zitakapo- ondoka,na madhambi yatatendwa
52. na watu waovu watakuwa na uwezo juu ya watu wema,
53. na uongo utaenea na mabishano (matusi XE "matusi" ) yatatokea
54. na umasikini utaenea,
55. na watu watajiona kwa mavazi yao
56. na itakuwepo mvua XE "mvua" wakati si wake
57. na watu watacheza dama, kamari na Ala za muziki,
58. na hawatapenda kuhimizana mema wala kukatazana maovu
59. na kwa ajili hali itakavyokuwa hata itafikia wakati huo kuwa Muumin atakuwa na heshima ndogo kuliko hata mjakazi
60. na wanaosoma na wanaotumia wakati wao katika kumwabudu Allah swt watalaumiana.
61. Hao ndio watu watakaoitwa wachafu na wanajisi katika Ufalme wa mbinguni."
"Ewe Salman!
62. Wakati huo matajiri hawataogopa chochote isipokuwa mtu masikini; hadi kwamba masikini wataendelea kuomba kati ya ijumaa mbili,na hawatamwona mtu yeyote wa kutia chochote mikononi mwao."
"Ewe Salman!
63. Wakati huo itazungumzwa Ruwaibidhah."
Salman akauliza:"Ni nini Ruwaibidhah ? Ewe Mtume wa Allah swt, baba na mama yangu wawe fidia kwako."
Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akajibu:
64. "Watu fulani watazungumza kuhusu mambo ya watu ambayo hayakuwahi kuzungumzwa namna hii zamani.
65. Tena baada ya muda mchache machafuko yatatokea duniani,na kila nchi itafikiri kuwa machafuko yapo katika nchi yao tu."
66. "Watabaki katika hali hiyo kwa muda ambao Allah swt atapenda wabaki;
67. kisha ardhi itatapika vipande vya moyo wake dhahabu, fedha na madini mengineyo; (Hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.) alinyosha kidole chake penye nguzo, na akasema: "Kama hizi (kwa ukubwa), lakini siku hiyo dhahabu wala fedha hazitamsaidia mtu yeyote. Na hii ndiyo maana ya maneno ya Allah swt 'Hakika dalili Zake zimekuja.'[100]
Imam a.s. alisema:
1 "Haki itakuwa imetokomezwa na watu walio katika haki XE "haki" hawatapatikana.
5. Dhulma na uonevu utaenea katika miji yote.
6. Kufuata Qur’an XE "Quran" kimatendo itajulikana kama tabia ya kizamani.
7. Zitatolewa maana ya Aya za Qur’an XE "Quran" kwa mujibu wa matakwa ya watu,hivyo mafhum ya Qur’an itakuwa imebadilishwa na kupotoshwa.
8. Wadhalimu watakuwa wakiwa kandamiza wale walio katika haki.
9. Uchokozi na uchochezi utatokea kutoka kila pande na pembe.
10. Matendo maovu na kukosa aibu vitaenea na kuzagaa kila mahala.
11. Ulawiti XE "Ulawiti" utakuwa ni jambo la kawaida.
12. Muumin atakuwa akionekana kama mtu dhalili ilhali waovu watakuwa wakiheshimiwa
13. Vijana hawatakuwa wakiwaheshimu wakubwa wao.
14. Huruma itakuwa imepotea kabisa.
15. Waovu watakuwa wakitukuzwa kwa udhalimu wao na hakutakuwapo na mtu yeyote wa kuwapinga.
16. Wanaume watafurahishwa mno kwa kuingiliana na wanaume XE "wanaume" wenzao.
17. Wanawake watawaoa wanawake XE "wanawake" wenzao.
18. Mapesa yatatumika kwa ajili ya matumizi yale yaliyo haramishwa na Allah swt.
19. Starehe, anasa na zinaa XE "zinaa" zitashamiri.
20. Zinaa XE "Zinaa" itajulikana kama maadili yaliyopitwa na muda.
21. Muumin atatengwa kwa sababu ya kufanya ibada za Allah swt.
22. Jirani mmoja atafurahi mno kwa kumuudhi na kumbughudhi jirani mwenzake.
23. Wazushi (kama Salman Rushdie wa Uingereza) watatukuzwa na kusifiwa katika kueneza fitina na yale wanayozusha.
24. Ushauri mzuri utakanwa.
25. Milango ya wema yatafungwa wakati milango ya maovu yatafunguliwa.
26. Al-Kaaba XE "Kaaba" haitatumika au haitafikika kwa sababu ya vikwazo na ugumu utakaowekewa mahujaji.
27. Watu watalazimishwa kuacha kwenda Makkah XE "Makkah" kuhiji.
28. Watu hawatakuwa wakitimiza ahadi zao watakazokuwa wakizitoa.
29. Wanaume watakuwa wakitumia dawa za kuamsha tamaa za kiume kwa ajili kulawiti na wanawake XE "wanawake" watakuwa wakitumia vyakula vya mafuta ili kujitayarisha kwayo.
30. Baadhi ya wanaume watakuwa wakiishi kwa kujipatia mapesa kwa kuuza mikundu yao.
31. Na wanawake watakuwa wakijipatia mapesa kwa kufanyisha biashara kuma zao.
32. Wanawake wataunda vilabu vyao,mashirika na umoja wao.
33. Wanaume atajigeuza kama wanawake na watavutia na wanawake.
34. Wanaume watajirembesha kama wanawake.
35. Ulawiti utachukuliwa kama ndiyo ustaarabu na starehe ya kweli. Na Banu Abbas watalipia ulawiti.
36. Wanawake wataona fakhari kwa kuwa na waume nje ya mume mmoja wa ndoa na vivyo hivyo wanaume XE "wanaume" watakuwa hivyo hivyo.
37. Heshima itakuwa ikitolewa kwa utajiri wa mtu na wala si ucha Mungu.
38. Riba XE "riba" ndiyo itakayokuwa biashara ya kila siku.
39. Ushahidi wa uongo utakuwa ukIssadikiwa mno.
40. Kile alichokiharamisha Allah swt kitachukuliwa ni halali na chochote kile alichokihalalisha Allah swt kitachukuliwa ni haramu.
41. Maamrisho ya Dini yatageuzwa kwa mujibu wa matakwa yao.
42. Wachokozi na waovu watatenda maovu kwa udhahiri bila ya khofu yoyote ile na Muumin hawataweza kuwazuia vyovyote vile.
43. Watawala watawapenda mno Makafiri kuliko Muumiin.
44. Rushwa XE "Rushwa" ndiyo itakuwa njia ya kujitimizia kazi kutoka maofIssa wanaohusika.
45. Wanaume wata walawiti wake zao.
46. Watu watakuwa wakiuawa kwa visingizio vidogo vidogo na magomvi madogo madogo.
47. Wanawake watawafanyia wanaume dhihaka, nao watashawishiwa kufanya uhusiano na wanawake XE "wanawake" .
48. Wanaume wataishi kwa mapato ya wake zao zitakazopatikana kwa zinaa XE "zinaa" .
49. Wanawake watakuwa wakiendesha hukumu majumbani huku wanaume wakiwatii wake zao kwa sababu wanawake hao ndio watakuwa wenye mapato.
50. Wanawake watatumiwa katika kupatikana huduma mbalimbali.
51. Kula kiapo kwa jina la Allah swt litakuwa ni jambo lililowekwa ulimini.
52. Pombe XE "Pombe" na kamari vitapatikana kila mahala na vitakuwa vimezagaa.
53. Wanawake XE "wanawake" wa Kiislamu wataingiliana na Makafiri,ambapo Waislamu hawataweza kuwazuia na wala hawatakuwa na uwezo kama huo.
54. Maadui wetu watasaidiwa na watawala na marafiki zetu watadhalilishwa kiasi kwamba hata kiapo chao hakitakubaliwa.
55. Udanganyifu na hila ndizo zitakuwa desturi miongoni mwa watu.
56. Usomaji na usikilizaji wa Qur’an XE "Quran" utakuwa ni bughudha kwa watu.
57. Kusikiliza mambo fidhuli ndiyo itakuwa ikipendelewa na watu.
58. Jirani hatamstahi jirani mwenzake illa kwa khofu ya ulimi mkali na mchafu.
59. Sheria na kanuni za Allah swt hazitatambuliwa na waovu hawataadhibiwa kwa maamrisho hayo.
60. Ghiba na kulaghaiana ndivyo vitakuwa vitu vya kawaida.
61. Madhumuni ya Hajj na Jihad yatakuwa mbali na yale ya Kiislamu.
62. Misikiti XE "Misikiti" itarembeshwa kwa dhahabu.
63. Watawala watawataka ushauri kwa nia ya Makafiri.
64. Litakuwa ni jambo la kawaida kuibia katika uzani na vipimo vya biashara.
65. Kumwaga damu XE "damu" ya watu wegine litakuwa ni jambo la kawaida.
66. Watu watajigamba kwa ndimi zao chafu zenye matusi XE "matusi" mabaya ili kuwatishia watu wengine.Imam a.s. aliendelea kusema:
67. "Watu watakuwa wakipuuzia sala XE "sala" na kutojali.
68. Watu hawatakuwa wakilipa zaka XE "zaka" ingawaje watakuwa na utajiri mkubwa.
69. Sanda za maiti zitakuwa zikiibiwa na kuuzwa tena.
70. Mauaji yatakithiri mno kiasi kwamba hata wanyama pia wataanza kuuana wenyewe kwa wenyewe.
71. Watu watakuwa wakIssali katika mavazi ya kiajabu.
72. Macho na mioyo itapoteza nuru zao za heshima na huruma.
73. Watu watakuwa wamejishughulisha na maswala ya kutafuta mali na mapesa tu.
74. Watu watasali kwa kuonyesha tu.
75. Watu watatafuta ilimu ya Dini kwa ajili ya kujipatia mali ya dunia.
76. Ushirika katika makundi yatakuwa ndiyo mambo ya maisha.
77. Wale watakaojipatia riziki kwa njia ya halali,watasifiwa kwa midomo tu.
78. Matendo maovu na machafu yataenea hata Makkah XE "Makkah" na Madina XE "Madina" .
79. Watu waliokufa watafanyiwa mizaha na vichekesho.
80. Mwaka hadi mwaka hali itakuwa ikiendelea kuharibika kuwa mbaya zaidi.
81. Matajiri wataigwa.
82. Masikini, mafukara watafanyiwa dhihaka na kufedheheshwa.
83. Matukio ya kudura kama yale ya mitetemeko,maporomoko n.k. yatakuwapo lakini watu watakuwa hawaviogopi.
84. Matendo maovu yatakuwa yakitendwa kiwaziwazi.
85. Wazazi watatupa watoto wao na watoto watawatusi wazazi wao na daima watakuwa wakitaka mali na utajiri wa wazazi wao.
86. Wanawake hawatawatii na kuwafuata waume XE "wanaume" wao.
87. Siku itakayopita bila ya mtu kutenda madhambi,basi itachukuliwa ni siku yenye nuksi.
88. Watu wenye uwezo wataficha mali muhimu na kuviuza kwa bei ya ulanguzi.
89. Waombaji na walaghai watajumuika katika kucheza kamari na kulewa.
90. Pombe XE "Pombe" itatumika kama ni kitu chenye kuponya i.e.dawa.
91. Makafiri watatukuzwa juu ya watu wengine na Muumin watadhalilishwa na kupuuzwa.
92. Kutafanywa malipo kwa ajili ya kutoa Adhan na sala XE "sala" .
93. Misikiti XE "Misikiti" itajaa kwa watu wasiokuwa na khofu ya Allah swt.
94. Watu wenye fahamu na akili kasoro ndio watakaokuwa wakiongoza sala XE "sala" za jamaa' na watu kama hao kamwe hawatashutumiwa au kusutwa na badili yake wataheshimiwa."
Kwa nyekundu kunamaanisha damu XE "damu" yaani kumwagika kwa damu nyingi mno kwa sababu za vita na mauaji ya aina mbalimbali.
Na kifo cheupe kinamaanisha kuzuka kwa maafa XE "maafa" ya magonjwa ambayo yatakuwa daima yakienea na kuzuka kila mahala."
Tanbihi: Kwa vifo XE "vifo" vyekundu hapo juu tunaelewa kuwa kutakuwapo na vita vya kutisha mno ambapo damu XE "damu" itakuwa ikimwagika kutoka kila pembe ya dunia.Tunasikia kila siku katika maredio na televisheni vile dunia yetu hii ilivyokumbwa na mauaji kila pande. Na ama kuhusiana na kifo cheupe, tunasikia vile magonjwa mbalimbali ya saratani, ukimwi n.k. yanavyoua watu kwa mamilioni.
1686. Imam Ali ibn Abi Talib a.s. alianza kuelezea: "Kumbukeni kuwa kabla ya kuja kwake,
UDONDOZI WA UBASHIRI
1687. Kutoka dalili na mabashiri ya kudhihiri kwa Imam Mahdi XE "Mahdi" a.s. hapa kuna madondoo machache ambayo yamechambuliwa:
1. Uasi wa Sufiani XE "Sufiani" ,
1689. Hadith hii ifuatayo inatuonyesha dhahiri kuwa kuna haja ya kuwapo kwa Imam wa zama na kumtii yeye ni faradhi kwetu sisi,kama vile wanavyoinakili Maimamu wa Kishiah na vile vile Wanazuoni wa Ahli Sunna pia wananakili vivyo hivyo katika vitabu vyao. Hadithi mashuhuri ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. inayopokelewa na madhehbu yote ni kama ifuatavyo:
rudi nyuma | Yaliyomo | endelea |