rudi nyuma Yaliyomo endelea

Kwa hayo mimi nikamwuliza Imam a.s.,

“Ewe Maula ! Je yakitokea hayo katika zama za uhai wangu mimi nifanyeje?”

Kwa hayo Imam a.s akamjibu,

“Kwa hakika kile ulichonacho wewe uwasaidie hao watu kwa hali na mali na kwa hata cheo chako ulicho nacho na kwa wadhifa wako ulio nao uwasaidie ipasavyo.”

744.  Abu Basir anasema kuwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliitolea

maelezo Ayah ya Qur'an Tukufu Surah Al Baqara, 2, ayah ya 267       isemayo:

Enyi mlio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa.

amesema Kuwa:

“Zama kabla ya Islam watu walikuwa wamejilimbikizia mali iliyopatikana kwa njia zisizo halali (kwa njia zilizo haramu) na baada ya wao kusilimu, walikuwa wakidhani kuwa kwa kutoa mali iliyo patikana kwa njia haramu, watakuwa wametakasisha mali yao iliyo halali, kwa hivyo Allah swt alitoa amri kuwa sadaka  itolewe kutoka mali iliyo halali tu.”

745.  Kwa kuzungumzia ayah hiyo ya juu Shahab amenakili riwaya kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Ambamo amesema kulikuwa na kaumu moja ambayo walikuwa na mali nyingi iliyo chafu  (iliyopatikana kwa njia za haramu ). Wakati wao walipoukubalia Islam walianza kuchukizwa na malimbikizo yao hayo machafu na wakataka kutoa kwa njia za sadaka. Allah swt aliwaonya kwa kuwaambia kuwa sadaka  hutolewa kutokea mali iliyo halali tu.”

746.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Iwapo watu watachuma au watajipatia mali kwa mujibu wa hukumu za Allah swt na wakaitumia kinyume na hukumu za Allah swt au iwapo watachuma kwa njia zilizo kinyume na hukumu za Allah swt na wakazitumia kwa mujibu wa hukumu za Allah swt; katika hali zote mbili Allah swt hazikubalii.

Katika kutaka kukubaliwa sharti ni kwamba mapato hayo yawe yamepatikana kwa njia zilizo halali na zitumiwe katika njia zilizo halali vile vile.”

747.  Halabi anasema kuwa mtu mmoja alimwuliza Al Imam Ja'afer

as-Sadiq a.s. kuhusiana na ayah hii katika Qur'an Tukufu Surah Al Baqarah, 2, ayah ya 267:

Enyi mlio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa.

Na hapoAl Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akasema:

“Wapo baadhi ya watu ambao baada ya kuingia katika Uislam bado wameendelea kubakia na mali iliyopatikana kwa njia zisizo halali. Na humo kulikuwa na mmoja ambaye kwa makusudi alianza kutoa sadaka kutoa mali hiyo isiyo halali. Na Allah swt alimzuia kufanya hivyo yaani sadaka  haiwezi kutolewa isipokuwa kutokea mali iliyotokana kwa njia halali.”

748.  Katika Ma’anil Akhbar Al Imam Hassan al-'Askari a.s. kwa

kupitia sanad amenakili riwaya moja kutoka Al Imam Ja'afer

as-Sadiq a.s. kuwa amesema:

“Wale ambao wanajiona utukufu na wakubwa na ambao wanatenda matendo kwa mujibu wa nafsi zao, mfano wake ni wa yule mtu ambaye mimi nilisikia watu wakimsifu sana na kumheshimu sana, na hivyo mimi nikawa na shauku ya kutaka kuonana na mtu huyo lakini katika hali ambayo yeye hataweza kunitambua. Siku moja mimi nilimwona alikuwa amezingirwa na watu. Baada ya muda mchache kupita mimi nikamwona yeye ametoka humo na akawa anaondoka, basi mimi nilimfuata nyuma yake.

Tulipita katika duka la muuza mikate, huyo mtu kwa kuficha macho yake na kificho ficho akaiba mikate miwili. Kwa hakika mimi nilistaajabishwa mno, na nikadhani kuwa labda wao wana maelewano fulani kabla ya tukio hilo.

Tukaendelea mbele yeye akamghafilisha mfanya biashara huyo na akaiba makomamanga mawili humo. Na hapa pia nikafikiria kwa labda wao watakuwa na maelewano kama hayo kabla ya kutokea tukio hili, nikiwa hapo nikaingiwa na wazo kuwa je iwapo watakuwa na maelewano kama hayo basi kwa nini achomoe vitu kimafichoficho?

Basi mimi niliendelea kumfuata nyuma yake, tukafika njiani akamwona mtu mmoja mgonjwa basi huyo akasimama kwa mgonjwa huyo na akatoa ile mikate miwili na hayo makomamanga mawili, akampa huyo mgonjwa.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwuliza huyo mtu kulikuwa na dharura gani kwa kufanya hivyo. Mtu huyo kwa kuniona mimi akasema je wewe ni Ja’afar bin Muhammad ? Nami nikamjibu naam, basi yeye hapo akaanza kusema nasikitika sana kwa kutokujitambulisha kwako hapo kuja kukufikishia faida (kwa sababu Imam a.s. alikuwa hakujionyesha kuwa yeye ni Imam bali alikuwa amejiweka kama yeye ni mtu wa kawaida)

Imam a.s. akamwambia kwa hakika matendo yako hayo yana aibisha.

Basi yeye akasema kuwa Allah swt anasema katika Qur'an Tukufu Surah An A’Am, 6, Ayah 160:

Afanyae wema atalipwa mfano wake mara kumi. Na afanyae ubaya hatalipwa ila sawa nao tu. Na wao hawatadhulumiwa.

Ama kwa mujibu wa ayah ya Qur'an Tukufu mimi nimeiba mikate miwili hivyo nimetenda madhambi mawili na nimeiba makomamanga mawili hivyo nimetenda madhambi wawili na kwa ujumla nimetenda madhambi manne.

Na pale mimi nilipompa mgonjwa sadaka  mimi kwa kila wema nimepata malipo kumi ya thawabu hivyo jumla nimepata malipo ya thawabu arobaini. Na kutoka arobaini ukitoa nne ninayo mema thelathini na sita bado.”

Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu:

“Mama yako akae kwenye kilio chako! Wewe kwa hakika umeitoa maana isivyo ya Ayah za Qur'an Tukufu. Je wewe huelewi ayah ya Qur'an Tukufu isemayo Surah Al Ma’ida, 5, Ayah ya 30:

Basi nafsi yake ikampelekea kumuuwa nduguye, akamuuwa na akawa miongoni mwa wenye kukhasirika.

Kwa mujibu wa ayah hiyo wewe umeiba mikate miwili umetenda madhambi mawili na kwa kuiba makomamanga mawili umetenda madhambi mawili mengine na hivyo jumla umetenda madhambi manne, na pale ulipotoa hiyo mali yaani mikate na makomamanga, kama sadaka  bila idhini ya mwenye mali basi umetenda madhambi mengine manne. Kwa hivyo umetenda madhambi nane kwa pamoja. Sasa wewe unafikiria mema hayo arobaini yametoka wapi?”

Kwa hakika mtu huyo aliduwaa, akimwangalia Imam a.s. na akajiondokea zake.

Baada ya hapo Imam a.s. akasema kwa kujitolea maana potofu ya ayah za Qur'an Tukufu vile isivyo sahihi ndio matokeo yake haya na vile vile kuwapotosha watu wengine pia.”

749.  Katika tafsiri Ayyashi Al Imam Muhammad al-Baquir a.s.

amenakiliwa akitoa tafsiri ya ayah Surah Al Baqara, 2,  ayah ya 267:

Enyi mlio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa.

Imam a.s. akaelezea:

“Miongoni mwa watu kulikuwa kumelimbikwa mali iliyopatikana kwa riba na njia zingine zisizo za halali, basi wao walinuia kutoa sadaka  humo, na ndipo Allah swt alipowakataza kufanya hivyo (kutoa sadaka  kutoka mali iliyopatikana kwa njia za haramu hairuhusiwa).”

750.  Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. ameripoti riwaya kutoka kwaAl Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa amesema:

“Katika vitu vya kuleta uokovu mojawapo ni kuwalisha chakula wale wenye kuwa na shida na dhiki, na pili mtu awe ni mwanzilishi awe ni mwanzo wa kutoa salamu na vile vile wakati watu wamelala usingizi mtu anaamka kwa ajili ya kusali na kufanya ‘ibada.”

751.  Muhammad  Yakub amenakili kutoka ‘Ali bin Ibrahim ambaye

naye amenakili kutoka Muhammad bin ‘Isa bin ‘Ubaid ambaye naye amenakili kutoka Ahmad bin Muhammad naye amenakili kutoka ibn Fazzal Ma’aruf naye kutokea Tha’alaba bin Maymun ambaye naye pia amenakili riwaya hiyo kutoka kwa Zararah, kuwa

752.  Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:

“Allah swt hupendezewa mno kulishwa chakula wale wenye dhiki na shida na njaa, na vile vile hupendezewa kutolewa kwa dhabihu (qurbani).”

753.     Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amesema:

“Yeyote yule ambaye hakubahatika kutufanyia sisi wema basi ni wajibu wake kuwafanyia mema na kuwatimizia mahitaji ya marafiki zetu.  Na yeyote yule ambaye hakubahatika kudhuru makaburi yetu basi adhuru makaburi ya wafuasi na marafiki zetu.”

754.      Muhammad bin Ali bin Hussein Jamil amenakili riwaya moja kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Miongoni mwenu mtu aliye bora kabisa ni yule mwenye moyo mkarimu yaani mwenye moyo wa kutoa na mtu mwovu kabisa ni yule ambaye ni bahili. Na usafi wa imani dalili yake ni kwamba huwawia kwa wema muumin wenzake na kuwatimizia dharura na mahitajio yao. Bila shaka yeyote yule anayewafanyia hisani ndugu zake katika imani basi ndiye mpenzi wa Allah swt kwa sababu katika kufanya wema huko kuna mambo mengi yanayomzuia mtu asiingie katika mitego ya Sheitani na vile vile asiingie Jahannam, na kwa matokeo yake ndiye mtu anayeingia Jannat.”

Baada ya hapo Imam a.s. alimwambia Jamil, “Ewe Jamil! Habari hizi uwafikishie wenzako.

Kwa hayo mimi nikasema, “Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Niwe fidia juu yako. Je ni watu gani hao?”

Imam a.s. akasema: “Hao ni wale ambao wanawafanyia wema ndugu zao katika imani wakati wa shida huwa pamoja nao na vile vile wakati wa furaha pia huwa nao.”

755.     Sheikh Sadduq a.s. amenakili riwaya kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye amesema kuwa:

“Yeyote yule ambaye hakupata fursa kufanya wema nasi, basi awafanyie wema wapenzi na wafuasi wetu basi atapata thawabu za kutufanyia wema sisi. Na vile vile ambaye hakubahatika kutuzuru sisi katika uhai wetu na uhai wake basi awazuru wapenzi na wafuasi wetu, basi atapata thawabu kama za kutuzuru sisi.”

756.     Safwan Al-Jammal anasema kuwa siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimwambia Mu’alla bin Hunais:

“Ewe Mu’alla! Uwe wa Allah swt, ili Allah swt aweze kukutunza na kukuhifadhi.

Kwa hayo Mu’alla alianza kusema:

“Je hivyo inawezekanaje?”

Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu, uwe na hofu ya Allah swt, uwe daima ukimwona yeye katika mawazo yako, kwa hiyo yeye atakifanaya kila kitu kiwe kikikuogopa wewe, na vile vile kitakuwa kikikuwazia wewe na kukujali wewe. Ewe Mu’alla ili kujipatia mapenzi ya Allah swt lazima uwatendee watu matendo mema, na utambue wazi wazi kuwa Allah swt anapendezewa sana na moyo wa ukarimu na huchukizwa sana na ubahili na huwa na uadui nao.

Angalia !  Wewe kama utaniomba chochote na mwisho wake wewe ukaaza kufanya mapenzi nami, na badala yake mimi nitafurahishwa sana iwapo wewe hautaniomba chochote na hautapata chochote kutoka kwangu na baada ya hayo wewe bado ukawa na mapenzi nami.

Na kwa hakika ukiniuliza mema yote naweza kuyafanya kwa ajili yako basi ukweli ni kwamba sifa zote ni za Allah swt kwa sababu yeye amekupitishia neema yake kwa mikono yangu mimi nimekuwa ni kipitishio tu kwa ajili yako kwa hiyo yeye ndiye anayestahiki sifa zote.”

“Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimwambia, “Nyamaza!”

Wale mafukara ambao wanawajali ndugu na jamaa zao na kuwawia wema wenzao, Allah swt huwapa ujira mzuri sana, kwa sababu Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu: Surah Sabaa, 34,

ayah 37:

Na si mali yenu wala watoto wenu watakao kukaribisheni kwetu muwe karibu, isipo kuwa aliye amini na akatenda mema. Hao basi watapata malipo maradufu kwa walio yafanya. Nao watakuwa salama katika maghorofa.

757.     Sheikh Quleyni amenakili riwaya kutoka kwa Ahmad bin ‘Isa kuwa Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:

Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake  na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea

758.  Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.amesema kuwa kwa neno ‘Innama’ inamaanisha kuwa katika kazi zenu au shughuli zenu zote, mwenye kuwa na haki zaidi kuliko yeyote juu ya nafsi zenu na mali zenu ni Allah swt, baada yake ni Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na baada yake ni, Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. na hadi kufikia Qiyama Maimamu a.s. kutokea kizazi chake.

Vile vile Allah swt ameelezea fadhila zao kwa kusema

Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:

Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake  na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea

Kisa katika ayah hii ni kwamba Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa akisali sala ya Dhuhuri, alipomalizia raka’a ya pili tu akatokezea mwombaji. Siku hiyo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa amevaa  Khullah yenye thamani ya Dirham elfu moja ambayo alikuwa amepewa zawadi na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.  Na Imam a.s. alipokuwa katika hali ya Ruku’u, kulitokezea maskini mmoja ambaye akasema, “Ewe Walii wa Allah swt na muumin halisi, iwe salamu juu yako, naomba unipe mimi maskini sadaka yoyote. Kwa hayo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. aliinamisha chini Hulla na kwa ishara akamwambia huyo maskini aichukue.”

Kwa tukio hili ndipo Allah swt alipoteremsha ayah hii kwa ajili yake na kwa ajili ya kizazi chake na kuonyesha fadhila na kufuzu kwao. Fadhila zao kuwa wanagawa sadaka  hata kama watakuwa katika hali ya Rukuu.

Kwa hakika imekuja kujulikana kuwa yule maskini aliyekuja kuomba alikuwa si mtu bali alikuwa ni Malaika ambaye alikuja kuomba, na vile vile katika kizazi kizima cha Maimam a.s. pia tumeona mara nyingi sana Malaika huwa wanakuja kuomba katika sura ya maskini.

759.     Katika kitabu kiitwacho Ihtijaj humo Tabarasi amenakili riwaya kutoka Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ameelezea kuhusu ayah hiyo kuwa:

 “Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. katika hali ya sala akiwa katika Ruku’u alitimiza wajibu wake na akatoa Zaka na Allah swt ndipo alipoiteremsha hiyo ayah na makusudio yake yalikuwa ni kupata ridhaa ya Allah swt.”

760.     Ali bin Ibrahim katika kitabu chake Tafsir ananakili riwaya kutoka kwa baba yake Ma’arifat Safwan kuwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:

“Siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipokuwa amekaa pamoja na ‘Abdullah bin Salam kulikuwa na kikundi cha Mayahudi pia. Na wakati huo ikateremshwa ayah ya Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:

Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake  na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea

Baada ya hapo mara Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akatoka nje haraka na akaelekea msikitini na huko njiani alikutana na mwombaji mmoja na hivyo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza:

“Je kuna mtu aliyeweza kukusaidia?”

Basi huyo mwombaji akasema,

“Naam, kuna mtu anayesali msikitini humo ndiye aliyenisaidia.”

Na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alivyoukaribia msikiti akamwona huyo mtu si mwingine bali ni Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.

Na riwaya hii vile vile imenakiliwa na Abu Hamza ambaye ameandika katika Tafsir Ayyashi.

761.      Muhammad bin Ali bin Hussein katika kitabu cha Amali amenakili riwaya kutoka Abul Ja’rud Ma’rifat kuwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amenakiliwa riwaya kuwa amezungumzia kuhusu ayah Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:

Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake  na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea

kama ifuatavyo:

“Katika Mayahudi ambaye mnafiki mmoja alipoukubalia Uislam akaanza kuiga:

“Ewe Mtume wa Allah swt! Je ni nani Wasii na Khalifa wako? Na nani huyo atakaye kuwa Walii baada yako?”

Ndipo hapo ayah hiyo ilipoteremshwa na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akawaambia inukeni, basi hao wote wakainuka na wakaanza kuelekea msikitini. Walipofika msikitini wakakutana na maskini mmoja akitoka nje na hivyo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwuuliza, “Je kuna mtu yeyote aliyekupa chochote ?” Huyo akasema “Kwa nini isiwe hivyo pete hii je niliyoipata?” Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema,”Je ni nani aliyekupa?”

Huyo mwombaji akasema “Huyo mtu ambaye bado anasali.”

Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema

“Je alipokupa hiyo pete alikuwa katika hali gani?”

Huyo mwombaji akasema alikuwa katika hali ya Ruku’u. Na hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipopaaza sauti ya Takbira yaani Allahu Akbar na wale wote waliokuwepo pamoja naye nao pia walitoa Takbira kwa nguvu na sauti na hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ndipo alipowaambia wote:

“Mtambue wazi kuwa baada yangu Walii ni huyu Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. na wa si mwingine”

Karta anasema kuwa

“Kwa mujibu wa riwaya zilizopatikana kuwa katika sala moja aliitoa Hullah, na katika sala ya pili alitoa pete basi inadhihirika kuwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. anatoa sadaka katika hali ya sala zaidi ya mara moja ndivyo inavyothibitika kwa mujibu wa riwaya zinazopatikana.”

762.     Ayyashi katika Tafsir yake ananakili riwaya moja kutokea kwa mwana wa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kwa Ammar Yasir amesema:

“Siku moja Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alipokuwa akisali sala ya Sunnah aliahirisha tendo moja kiasi kwamba mpaka akavua pete yake kwa ajili ya kumpa aliyekuja kuomba. Na pale Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipokuja basi alimwelezea hivyo. Na wakati huwo iliteremshwaayah yake hadi kufikia :

Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:

Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake  na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea

Basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alitusomea ayah hiyo na akasema,

“Yeyote yule ambaye mimi ni Mawla wake basi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ni Mawla wake. Ewe Allah swt! Uwe na mapenzi na yule ambaye anawapenda wao, na uwe na uadui na yule ambaye anafanya uadui pamoja nao.”

763.     Halabi anasema kuwa yeye alipomwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. basi Imam a.s. akamjibu:

“Naam kabisa! Al Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. aligawa nusu ya mali yake katika njia ya Allah swt – hadi kwamba nguo kwa nguo, Dinar kwa Dinar, alivigawa vyote katika njia ya Allah swt, na alikwenda Hija ishirini kwa kutembea na miguu.”

764.            Mtume Muhammad  s.a.w.w. Amesema, Wasa'il ush-Shi'ah,

J. 6, Uk. 13:

“Umma wangu utaendelea kuishi kwa heri pale watapokuwa waaminifu miongoni mwao,

watakapokuwa wakirejesha amana watakazokuwa wakiachiana, na

watakapokuwa wakitoa sadaka kutoka mali zao;

Lakini, Iwapo wao hawatatimiza wajibu hizo, basi watakumbwa na ukame na baa la njaa.”

765.        Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., Nahjul Balagha, uk.512, Msemo 254 :

“Enyi wana wa Adam ! Muwe wawakilishi wenu wenyewe katika mali yenu na mfanye kile chochote kile mnachotaka kufanyiwa nyie baada ya kifo chenu.”

Tanbih

 Iwapo mtu atataka baada ya kifo chake sehemu fulani ya mali utajir wake utumike katika kutoa sadaka au misaada, basi asisubiri mpaka afe bali aitumie popote pale atakapo katika uhai wake kwa sababu inawezekana kuwa baada ya kifo chake warithi wake wasiweze kutekeleza kwa mujibu wa vile alivyotaka au usia wake na labda inawezekana asipate wakati wa kuandika usia hivyo akakosa fursa hiyo.”

766.            Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Amesema, Kanz-ul-

'Ummal, J. 6, Uk. 371:

“Toeni sadaka na muwatibu wagonjwa wenu kwa hayo, kwa sababu sadaka [59] kwa hakika inatoa balaa na magonjwa; na inaongezea umri wenu ukawa mrefu na kuongezeka kwa thawabu zenu.”

767.            Imenakiliwa kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.

akisema, Al-Ithna-'Asheriyyah, Uk. 85:

“Nilipokuwa nimekwenda mbinguni, mimi niliona mistari mitatu imeandikwa juu ya mlango wa Jannat:

Mstari wa kwanza ulikuwa umeandikwa Bismillah Rahman Rahim; Mimi ni Allah swt na hakuna Allah swt mwingine isipokuwa mimi na Rehema zangu zinazidi adhabu zangu.

Mstari wa pili ulikuwa umeandikwa Bismillah Rahman Rahim; Sadaka inalipwa kwa mara kumi (10) na mkopo unalipwa mara kumi na nane (18), na kuwajali maJama’a na ndugu kunalipwa mara thelathini (30).

Mstari wa tatu ulisomwa yeyote yule anayeelewa wadhifa Wangu na Ukuu wangu basi kamwe asinishutumu mimi katika maswala ya maisha.”

768.     Taus-ibn-il-Yamani anasema kuwa yeye alimsikia Al Imam

Zaynul 'Abediin a.s. akisema sifa za muumin ni tano na pale alipoombwa kuzitaja alijibu, Khisal-i-Sadduq, Uk. 127:

“Ucha Allah swt katika hali ya upweke,

 kutoa sadaka wakati unaohitajika,

Subira anapopatwa na matatizo au anapokuwa na shida,

uvumilivu wakati wa ghadhabu,

 ukweli ponapokuwa na hofu.”

KUTOA SADAKA NA UBAHILI:

769. Mali ya mchoyo huliwa na warithi wake au hupeperuka bila

        kujulikana.

770. Hakuna mtu mwenye upweke vile alivyo bahili.

771. Mchoyo ni mweka/mtunzi hazina wa warithi wake.

772. Ubahili na uchoyo huangamiza upendo wa urafiki wa kweli.

773. Ubahilifu ni kujipatia ubadhirifu.

774. Kuwa mchoyo kwa kile ulichonacho ni kutomwamini Allah swt.

775. Sifa ya upole na wema huangamizwa kwa ubahili.

776. Fedha haimnufaishi mwenye kuwa nayo hadi hapo atenganapo nayo.

777. Maovu hufichwa kwa ukarimu.

778. Bora wa watu ni yule afaaye watu

779. Hakutakuwa kuwafadhili watu kwa mifuko mitupu.

780. Fadhila huuliwa kwa matumizi fidhuli.

781. Uachie ngome ya Sadaqa iilinde ufanisi wako.

782. Kutoa baada ya kughairi ni bora zaidi kuliko kughairi baada ya kutoa.

783. Uso ulio mcheshi ni mojawapo ya ne’ema mbili.

784. Usimuudhi mtu yeyote yule pale akutakiapo kila la kheri.

785. Fadhila na ukarimu hupatiwa sifa.

786. Fadhila ya kweli (kwa moyo safi) huondoa dhiki zote

787. Makosa ya mwenye kutoa fadhila ni afadhali kuliko dharau ya mchoyo.

788. Fadhila isiongozwe kwa uoga wala kuwa na matumainio ya kupata chochote (tamaa).

KUWAJALI NDUGU NA MAJAMA’A.

789.            Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Amesema, Bihar

al-Anwaar, J. 74, Uk. 89:

“Yeyote yule anayetaka kuongezewa riziki na baraka na siku yake ya mauti icheleweshwa, basi inambidi awajali ndugu na maJama’a zake.”

790.            Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s., Bihar al-Anwaar, J. 73,

Uk. 138:

“Mali haiwezi kulimbikana kupita kiasi isipokuwa kwa njia tano:

Ubahili kupita kiasi,

matarajio makubwa sana,

 uroho kupita kiasi,

 kuvunja uhusiano pamoja na ndugu na maJama’a za mtu mwenyewe, na

 kuijali na kuipenda dunia hii kuliko Akhera.”

791.     Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. Amesema, Al-Usul-i- Kafi , J. 2, Uk. 150:

“Kuwajali Jama’a na ndugu kunaleta faida tano:

Kutakasika na kukubalika kwa matendo ya mtu

Kuongezeka katika utajiri na mali

Kuondoa balaa na shida mbalimbali

Kurahisisha maswala yake katika Akhera

Umri kuwa mrefu.”

792.            Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Amesema, Al-Khisal

Uk. 179:

“Kuna makundi matatu ya watu ambao hawataruhusiwa kuingia Jannat:

Wanywaji wa pombe,

Wachawi [60], na

wale wanaokana Jama’a na ndugu zao.

KUWAHURUMIA WAZAZI.

793.            Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., Mustadrak

Al-Wasa'il-ush-Shiah, J. 15, Uk. 176:

“Furaha ya Allah swt ipo katika furaha ya wazazi wa mtu (kama ndio hivyo ni kweli, basi adhabu na ghadhabu zake pia zipo katika ghadhabu za wazazi wa mtu).”

794.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Bihar al-Anwaar,

 J. 74, Uk. 85:

“Bora ya matendo ni:

Kusali kwa wakati wake,

kuwa mwema na mwenye huruma na mwenye mapenzi kwa wazazi wake, na

kuchangia katika vita vitakatifu vya Jihad (dhidi ya Mapagani) katika njia ya Allah swt.”

795.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Safinat-ul-Bihar,

J. 2, Uk. 553:

“Iwapo mtu anataka Allah swt ampunguzie makali ya mauti, basi lazima awajali Jama’a na ndugu zake, na awawie wema wazazi wake. Na pale mtu anapofanya hivyo, basi Allah swt atampunguzia makali ya mauti na kamwe hatapata umaskini katika maisha yake.”

796.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Al-Usul-i- Kafi,

J. 2, Uk. 349:

“Yeyote yule anayewatazama wazazi wake kwa macho ya ghadhabu, hata kama wao hawakuwa waadilifu kwake, basi Allah swt hatazikubalia ibada za mtu huyo (hadi hapo atakapofanya Tawba).”

797.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Al-Kafi J. 5, Uk. 554:

“Watendee wazazi wako kwa huruma ili na watoto wako waje wakutendee vivyo hivyo; na uwe mcha Allah swt kwa wake wa watu wengine ili wake zako wabakie wacha Allah swt.”

798.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Al-Kafi J. 2, Uk. 162:

“Safari moja mtu alimwijia Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na kumwuliza namna ya kuwashughulikia wazazi. Hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimjibu

uwe mwenye huruma kwa mama yako:

uwe mwenye huruma kwa mama yako na

uwe mwenye huruma kwa mama yako;

 Uwe mwenye huruma kwa baba yako

uwe mwenye huruma kwa baba yako; na

 uwe mwenye huruma kwa baba yako lakini huruma hiyo uianzie kwa mama yako kabla ya baba yako.”

HAKI ZA WATOTO.

799.            Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwambia Al Imam

'Ali ibn Abi Talib a.s., Wasa'il ush-Shi'ah, J. 31, Uk. 290:

“Ewe Ali ! Allah swt huwalaani wazazi wale wanao wafanya watoto wao wasiwe watiifu kwao kwa sababu ya kuwalaani kwao.”

800.     Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alimwambia mmoja ya wafuasi

wake, Nahjul Balagha Uk. 536, Msemo, No. 352:

“Usiupitishe wakati wakati wako mwingi pamoja na mke wako na watoto wako waliokuwa wakubwa, kwa sababu kama mke wako na watoto wako ni wampendao Allah swt, basi Allah swt hatawaacha wapenzi wake bila ya kuwajali, iwapo watakuwa ni maadui wa Allah swt, basi kwa nini wewe uwe na wasiwasi na ujiweke mashughuli kwa ajili ya maadui wa Allah swt.

Na mambo mawili yanayoweza kuchukuliwa katika wanaume katika kuhusiana na kuwapatiapo familia zao.  Moja ni kutokutimiza wajibu wake kwao,  na pili kinachotajwa hapa ni kulimbikiza kupita kiasi kwa mali kwa ajili yao.”

801.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Al-Kafi J. 6, Uk. 47:

“Chukueni hatua za kuwafundisha watoto wenu riwaya na ahadith za Ahlul Bayt a.s. kabla watoto wenu hawajaharibika na hawajachafuliwa akili zao.”

802.            Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., Man la Yahdharul

Faqih, J. 3, Uk. 483:

“Heri ya mtu kwa mtoto wake ni kule kwa mtoto wake kuwa heri kwa wazazi wake.”

803.            Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., Nahjul Balagha,

Msemo 399:

“Haki ya mtoto kwa wazazi wake ni kwamba apewe jina[61] zuri kabisa, afundishwe adabu njema na afundishwe Qur'an kwa kanuni zake.”

804.            Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., Al-Kafi J. 6,

 Uk. 47:

“Wafundisheni watoto wenu kuogelea na kulenga shabaha.”

805.            Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., Kanz-ul-

'Ummal, J. 16, No. 45, 330:

“Watoto wenu wanapokua kufikia umri wa miaka saba, wafundisheni sala, wanapokuwa na umri wa miaka kumi, muwalazimishe kusimamisha sala; na mutenganishe vitanda vyao vya kulalia.”

806.            Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin a.s. : Man la Yahdharul

 Faqih, J. 2, Uk. 622:

“Haki ya mtoto wako ni kwamba wewe utambue wazi kuwa yeye amekuja humu duniani kwa kukupitia wewe, kwa hiyo yaliyo sahihi na yaliyo mabaya yanatokana na wewe. Wewe unawajibika kumpa mafunzo na elimu bora, kumwelekeza kwa Allah swt, na kumsaidia katika kumtii Allah swt. Kwa hivyo iwapo utamsaidia utamfanyia hisani mtoto wako, basi utaweza kufikia malengo hayo; na kama wewe utamwia kiovu, basi hayo yatakurejea wewe mwenyewe.”

807.            Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Amesema, Bihar al-

Anwaar, J. 104, Uk. 95:

“Muwaheshimu watoto wenu na muwafundishe kuwa wema, mtasamehewa na Allah swt.”

KUNYOYESHA MAZIWA

808.            Amesema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., Man la

Yahdharul Faqih, J. 3, Uk. 561:

“Naam malipo ya mwanamke wakati wa mimba yake hadi kuzaa mtoto, na wakati pale anapolea mtoto ni sawa na kuwekwa askari katika kituo cha kulinda mipaka ya Waislam dhidi ya hujuma za makafiri, kwa ajli ya Allah swt.  Kwa hivyo iwapo atakufa katika kipindi hiki, basi mwanamke huyo atakuwa katika daraja la mashahidi.”

809.            Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., Wasa'il ush-Shi'ah,

J. 21, Uk. 452:

“Hakuna maziwa yenye faida zaidi kwa mtoto isipokuwa maziwa anayonyonya kutoka kwa mama yake.”

rudi nyuma Yaliyomo endelea