rudi maktaba >Fiqh >Yaliyomo >

MADONDOO JUU YA SADAKA

Hapa nitapenda kuzungumzia machache kuhusu Sadaka

Sadaka inalipia madeni na kuongezea neema kwetu,

Sadaka inatuepusha na mauti katika hali mbaya

Siku ya Qiyama kutakuwa na jua na joto kali mno, lakini Mumin atakuwa katika kivuli, nacho ni Sadaka aliyokuwa akiitoa.

Toeni Sadaka asubuhi na mapema, ili balaa na matatizo yasiwafikieni katika siku nzima.

Muwatibu wagonjwa wenu kwa kutoa Sadaka

Kutoa Sadaka ni afadhali kuliko kumnunua mtumwa na kumfanya huru

Mtu mmoja alifiwa na watoto wawili, alibakia mmoja. Akashauriwa kutoa Sadaka. Toeni Sadaka kwa mikono yenu wenyewe kwani hamtakufa kifo kibaya na balaa zaidi ya 70 zitaepukwa na kujiepusha na mitego 70 ya Shaitani, kwani Shaitani yupo anasema, “Usitoe Sadaka.” Je tutamwitikia Shaitani ?

Toeni Sadaka hata kama ni tonge moja ya tende na kama hiyo pia hamuwezi basi toeni punje moja ya tende.

Sadaka inatuepusha na balaa 70 ambamo kuna magonjwa, madhara ya moto, kuzama maji, kuangukiwa na kufunikwa na majumba yanayoporomoka na kubomoka na kutokuwa masikini,

Unapokuwa na hofu ya kuibiwa, kuungua moto n.k. bali toa Sadaka.

1. ISISITIZWE KUTOA SADAKA KWA WENYE SHIDA, MASIKINI NA MADENI

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa :

“Sadaka inalipia madeni na inaongezea katika barakah.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa :

“ Sadaka inamwepusha mtu na ajali mbaya.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa:

“Mtu yeyote yule aliye mja wa Allah swt akiwa Mumin akatoa Sadaka, basi Allah swt baada ya kifo chake huyo mtu huwaweka vyema na kuwasaidia wananyumba yake katika hali njema.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akaendelea kusema :

“Faida ya kutoa Sadaka ni kwamba inamsaidia kulipia madeni na viile vile kuongezea katika baraka.”

4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Kusaidia na kutoa sadaka vyote hivyo vinaondoa umasikini na hurefusha umri wa mtu. Na yule anayetoa huweza kuepukana na aina sabini za ajali mbaya.

5. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. katika kuelezea tafsiri ya aya, ya Qur'an Tukufu, Sura Al-Layl, 92 , Ayah ya 5 na 6 :

Ama mwenye kutoa na akamcha Mungu,

Na akaliwafiki lilio jema.

ndipo amesema kuwa;

Allah swt ndivyo anavyo walipa wale watendao mema, kwa mema yao mara kumi, au hata mara laki moja na hata zaidi ya hapo.

Na vile vile amesema kuwa: anayetoa katika njia ya Allah swt basi Allah swt humjaalia kila aina ya tawfiqi katika kazi hiyo ya khairi.”

6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amemnakili Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa

“Mtu yeyote yule ambaye anamwamimi Allah swt kuwa atamlipa na atamwongezea zaidi ya kile anacho kitoa basi huyo mtu kwa moyo mkunjufu na bila aina ya ubakhili wowote atatoa sadaka na misaada kwa wingi kabisa.”

7. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amemnakili Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa

“Siku ya Qiyama ardhi itakuwa imepata moto kupita kiasi na mumin watakuwa katika kivuli na kivuli hicho itakuwa ni kile alicho kuwa akitoa Sadaka.”

8. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akisema kuwa:

“Enyi watu! Toeni sadaka bila shaka sadaka inaongezea katika mali yenu, na hivyo mtoe sadaka na Allah swt atawarehemu.”

9. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripotiwa katika Kitab ‘Uddatud-Da’i kuwa alimwuliza mtoto wake :

“Je nyumbani kuna kiasi gani kwa ajili ya matumizi ?”

Naye alimjibu : “Zipo Dinar arobaini tu.”

Imam a.s. alimwambia “Dinar zote hizo zigawe Sadaka.”

Kwa hayo mtoto wake alimwambia Imam a.s.

“Ewe Baba ! Mbali na Dinar hizi arobaini, hatutabakia na akiba yoyote.”

Imam a.s. alimwambia :

“Nakuambia kuwa zitoe Dinar zote Sadaka kwani ni Allah swt tu ndiye atakayetuongezea kwa hayo. Je wewe hauelwei kuwa kila kitu kina ufunguo wake ? Na ufunguo wa riziki ni Sadaka ( kutolea mema ).”

Kwa hayo, mtoto wake aliyekuwa akiitwa Muhammad, alizitoa Sadaka Dinar hizo na hazikupita siku kumi, Imam a.s. alitumiwa Dinar elfu nne. Hapo Imam a.s. alimwambia mwanae :

“Ewe Mwanangu ! Sisi tulitoa Dinar arobaini tu na Allah swt ametupa Dinar elfu nne badala yake.”

10. Al Imam Musa al-Kadhim a.s. amesema kuwa:

“ Toeni sadaka mjipatie riziki.”

11. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“ Toeni sadaka mjiongezee riziki yenu. Bila shaka anayeamini kuwa Allah swt hulipa mambo yote. Basi yeye huwapa sadaka masikini kwa kupita kiasi. Allah swt humjaalia riziki kwa njia mbalimbali kwa kile huyu mtu akitoacho katika mali yake.”

12. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. siku moja alitoa Dinar moja kama Sadaka na hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwambia :

“Ya Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.! Je unaelewa kuwa pale mtu anapotoa Sadaka kwa mkono wake mwenyewe basi hujiepusha na mitego ya mashetani sabini, na kila shetani husema, ‘Ewe fulani, usitoe sadaka kamwe.’”

Akaendelea kusema Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.

Ya Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s.! Kile utoacho Sadaka kabla hakijaingia katika mkono wa yule anayeomba, kwanza hupitia katika mkono wa Allah swt.

Na baada ya hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alisoma aya hii ifuatayo ambayo iko katika Qur'an, Surah Tawbah,9, Ayah 104.

Je hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali sadaqah , na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu?

13. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akisema kuwa :

“Kuwa na akida ya Tawhid ni nusu ya sehemu ya dini, enyi watu! Toeni Sadaka ili mpate riziki zaidi”.

14. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. ametoa riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa :

“Kuwa mali halisi ya mtu ni ile ambayo yeye ametolea sadaka.”

15. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:

“Toeni Sadaka asubuhi na mapema ili balaa zisiwafikieni katika siku nzima.”

16. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa:

“Sadaka ni kinga dhidi ya moto wa Jahannam .”

17. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema:

“ Enyi watu muwatibu wagonjwa wenu kwa kutoa Sadaka.”

18. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. katika Nahjul Balagha amesema kuwa:

“Mnapoona riziki yenu inapungua na kuwa finyo basi muwe mkitoa sadaka ndivyo mtakuwa mkifanya biashara na Allah swt.”

19. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“ Imani ya muumini inakuwa na sifa nne za lazima,

Awe na tabia njema,

Awe mkarimu na mwepesi wa kutoa

Asizungumze zaidi ya yale yanayo takikana (hazungumzi mambo ovyo ovyo)

Hutumia kile kiasi kinacho takiwa ,siyo mfujaji ( anaotoa katika njia ya Allah swt ).

2. KUSAIDIA FAMILIA YA WAISLAMU WENYE SHIDA NI AFADHALI KULIKO KWENDA HIJJA ZILIZO SUNNAH NA KUWAFANYA HURU WATUMWA

1. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa:

“Iwapo mimi nitakwenda Hijja moja basi afadhali niwafanye huru watumwa kumi, lakini iwapo mimi nitajichukulia jukumu la kuwalisha familia ya Waislamu ambao wanashida ya chakula na ambao wanaishi kwa njaa nikawamalizia shida zao, nikawavalisha nguo wale ambao hawana nguo, na nikawarudishia heshima yao miongoni mwa watu, basi mimi ninaona jambo hili ni afadhali na bora zaidi kuliko hata kwenda kuhiji Hijja sabini.”

2. Al Imam Musa al-Kadhim a.s. aliijiwa na mtu mmoja na aliyeuliza,

“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Mimi ninazo pesa na utajiri je ni jambo gani afadhali nitoe sadaka au nimnunue mtumwa na kumfanya huru?”

Kwa hayo Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alimjibu kuwa:

“Kuwa mimi ninaonelea kuwa kutoa Sadaka ni afadhali zaidi.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza Maimuna binti Harun, Je Kijakazi wako amekuwaje? Akasema Maimuna kwa hayo alimjibu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., ‘Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Mimi nimemfanya huru.’

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwambia “Iwapo kama wewe ungelichukua jukumu la kumlisha, kumtunza, kumsaidia na kumwonea huruma basi ingekuwa afadhali zaidi.”

3. KUWATOLEA WAGONJWA SADAKA NI SUNNAH

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Muwatibu wagonjwa wenu kwa Sadaka, na muzuie maafa kwa kuomba dua na kutoa sadaka muongezee riziki zenu zipanuke, na kwamba Sadaka inawaepusheni na mitego ya mashetani sabini.”

2. Siku moja walikuja wagonjwa wakilalamikia magonjwa yao mbele ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., naye akawaambia;

“Nendeni mtoe Sadaka kwa ajili ya magonjwa yenu na mtapona, iwapo mtu atatoa Sadaka kwa kile akitumiacho kwa siku dharura wake, basi Allah swt huahirisha hata kifo chake na vile vile humwepusha na ajali mbaya.”

4. MTOE SADAKA KWA NIABA YA WATOTO WENU NA WATOTO WENU WATOE SADAKA KWA MIKONO YAO HATA KAMA ITAKUWA KIDOGO KIASI GANI.

1. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. aliulizwa na Sahaba mmoja :

“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Mimi watoto wangu wawili wamefariki na amebakia mtoto wangu mdogo.”

Kwa hayo Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. kamwambia:

“Basi toa Sadaka kwa niaba ya mtoto wako huyo.”

Na siku moja Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. alipomtembelea huyo mtu akamwambia,

“Mwambie mtoto wako huyo atoe Sadaka kwa mkono wake walau kiasi kidogo chochote kile au hata kama kitakuwa ni kipande kidogo tu. Utambue wazi kuwa kiasi chochote kile hata kikiwa kiasi gani kama kitatolewa kwa roho safi basi mbele ya Allah huwa ni kipenzi, kwani Allah swt ameelezea kuwa: Qur’an Tukufu, Surah Az-Zilzalah,99, Ayah7 - 8

Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona !

Na anaye tenda chembe ya uovu atauona !

Vile viel Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. alimwelezea kuwa:

“Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah Al-Balad,90, Ayah11 - 16

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani ?

Kumkomboa mtumwa;

Au kumlisha siku ya njaa

Yatima aliye jamaa,

Au masikini aliye vumbini

“Hivyo ewe Sahabi uelewe kuwa Allah swt anaelewa wazi wazi kuwa si watu wote wenye uwezo wa kuwanunua na wenye kufanya huru watumwa hivyo yeye ameweka thawabu hizo hizo kwa wale watakao toa Sadaka au watakao walisha yatima na masikini.”

2. Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alijiwa mtu mmoja mbele yake na kuelezea habari za mtoto wake, na kwa hayo Al Imam akamjibu :

“ Toa Sadaka kwa niaba yake.”

Na mtu huyo akajibu kuwa

“Sasa mtoto wake amekuwa na umri yaani amekuwa kijana.”

Basi Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alimwambia kuwa

“Mtoto wako atoe Sadaka kwa mkono wake, hata kama itakuwa ni kipande cha mkate, na hapo ndipo Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alisema riwayah ya Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. kuwa:

“Katika Israil alikuwa mtu mmoja aliyekuwa akimpenda mno mtoto wake, na akaona katika ndoto yake anaanmbiwa kuwa, mtoto wako huyo umpendaye mno atakufa usiku wa ndoa yake. Kulipowadia usiku wa arusi baba mzazi wa mtoto huyo, usiku kucha akawa katika wasiwasi na hakupata usingizi na kamwe hakupata raha usiku huo.

Na kulipo pambazuka asubuhi na mtoto alipotoka chumbani mwake akiwa hai basi baba yeke alimwuliza

‘Ewe mwanangu! Je katika usiku huu wako wa kuamukia leo umefanya mema yoyote?’

Kwa hayo mtoto akajibu

“Ewe baba yangu! hakuna jambo la maana sana lililotendeka, bali alitokezea masikini mmoja akaja mlangoni kuomba chakula, alikuwa na njaa na kile chakula walichokuwa wameniwekea, mimi nikampa chakula chote huyo mtu aliyekuja kuomba.’

Kwa hayo baba yake akasema

“Kwa sababu hii tu ndiyo Allah swt amekuondoshea balaa kubwa iliyokuwa ikupate wewe usiku huo.”

5. MTOE SADAKA KWA MIKONO YENU WENYEWE hUSUSANI WANANYUMBA WATOE SADAKA KWA MIKONO YAO NA WANAYEMPA WAMWOMBE AWAOMBEE DUA NJEMA.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa:

“Kwa kutoa Sadaka kwa mkono wako mwenyewe basi unajiepusha na ajali mbaya, unajiepusha na balaa na maafa sabini na mitego ya mashetani sabini na ambamo kila shetani yuko anakwambia ‘ewe fulani! Usitoe Sadaka kamwe.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Mgonjwa atoe Sadaka kwa mkono wake mwenyewe na anayempa amwambie amwombee dua”.

3. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika hadith zake amesema kuwa:

“Mkono uliye juu yaani mtoaji ni afahali kuliko mkono ule ulio chini yake, yaani mpokeaji.”

4. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:

“Kuna aina tatu ya mikono wa

kwanza ni mkono ule wa Allah swt ambao uko juu kabisa na kwa hakika neema zote ni za Allah swt,

mkono wa pili ni ule mkono wa yule mtu anaye toa, ambaye anatoa katika njia ya Allah swt na

mkono wa tatu ni wa yule anaye pokea ambao mkono uliochini wa yule anayetoa. Kwa hivyo enyi watu chochote kile kinachobakia miongoni mwenu mtoe katika njia ya Allah swt na musikalifishe nafisi zenu”.

6. KUTOA SADAKA KILA MARA NA KWA WINGI NI SUNNAH

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa amemfanyia usia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.; Ewe Ali! Ninakufanyia usia wa mambo mema machache na uyakumbuke vyema.

Ewe Allah swt umsaidie Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Baada ya hapo wakati akifanya usia, Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alisema: Ama kuhusiana na sadaka tafadhali usiwe na mnunguniko wowote. Utoe kiasi kwamba mpaka uhisi kwamba wewe umefuja mali yako, lakini utambue wazi kuwa hiyo sio ufujaji bali hiyo umetoa katika njia ya Allah swt.”

7. KATIKA KUTOA SADAKA HATA KIASI KIDOGO CHOCHOTE KILE NI SUNNAH

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa kuna riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa

“Toeni Sadaka, angalau hata kwa sa’ ya tende, na kama sa’ moja hiyo hamnayo basi mtoe tende kwa kiganja kimoja na hata kama hivyo haitawezekana basi mtoe tende kiasi chochote kile na kama hivyo haitawezekana basi mtoe angalau kokwa moja ya tende, na kama hivyo pia haitawezekana basi yule masikini aliyekuja kuwaomba mumwambie maneno mazuri na matamu na maneno matakatifu katika kumwelezea kuwa hakuna chochote, na hayo pia ni sadaka.

Kwa sababu isitokee Siku ya Qiyama kwamba Allah swt atakapo kuuliza hesabu ya neema alizokujaalia akakuambia

‘Ewe mja! Mimi nilikupa mambo chungu nzima, sasa hebu angalia nafsini mwako je kwa kutumia neema hizo wewe umejiandalia nini?’

Na hapo wewe utaangalia sehemu zote nne za dunia na utajawa na masikitiko, na utakuta hakuna jambo lolote lile litakalo kuokoa dhidi ya adhabu za Allah swt.”

2. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa:

“Mtoe tende kiasi fulani kwani itawaokoa na moto wa Jahannam , mpanue riziki zenu na mteremshiwe riziki nyingi kwa kutoa Sadaka na kupitia dua mziondoe balaa na shida zenu.”

Mkumbuke kuwa kwa kutoa Sadaka hamtapungukiwa katika mali yenu. Na miongoni mwa jamaa zenu wanapokuwa na shida muwasaidiapo hiyo siyo Sadaka bali hiyo ni wajibu wenu.”

3. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa:

“Kulikuwa na mja mmoja aliyekuwa akifanya ibada ya Allah swt kwa umri wake wa miaka themanini.

Siku moja alimwona mwanamuke mmoja mzuri aliyekuwa akipendeza naye akawa ameingia katika mtego wake. Yeye alitimiza matamanio yake visivyo halali na mara akatokezea Malakul mauti (malaika anayetoa roho). Ulimi wake ulifunga kuongea na jasho lilianza kumtoka na kutokwa kwa roho na mara hapo alipita masikini akiomba.

Basi mtu huyu ambaye alikuwa katika hali ya kukata roho alimwambia yule masikini kwa ishara kuwa mahala fulani kuna mkate hivyo auchukue hivyo aweze kula huyo masikini, na masikini huyo alivyoelekezwa akauchukua mkate akaondoka zake.

Kwa hiyo ikatokea kwamba Allah swt aliibatilisha ibada zake za miaka themanini kwa sababu ya kuzini na ikatokea kwamba Allah swt akamsamehe madhambi yake yote kwa sababu ya kutoa Sadaka kwa moyo mkunjufu.”

4. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amesema kuwa;

“ Katika zama za Bani Israil kuliwahi kutokea baa la njaa ambao uliendelea kwa muda wa miaka mingi.

Katika wakati huo ikatokezea kwamba bibi kizee mmoja akiwa amekabwa na njaa hali ya juu alikuwa ameketi akiwa na kipande kidogo cha mkate huku akitaka kukila kipande hicho, mara akasikia mlangoni sauti ikisema ya masikini aliyekuwa amekuja kuomba:

‘Ewe mja wa Allah swt! Mimi nakufa kwa njaa naomba unisaidie, bibi kizee huyo akajiambia kwa hakika Sadaka ndiyo wakati huu muafaka wa kutoa, na kile alichokuwa akila akakitoa haraka akampa huyo aliyekuwa akiomba.

Bibi kizee huyo alikuwa na mtoto mmoja aliyekuwa amekwenda porini na ghafla kule alishambuliwa na mnyama. Kwa kusikia sauti ya mtoto wake huyo bibi kizee ikimwita, alikimbia kumfukuza mnyama huyo na kwa muujiza wa Allah swt ni kwamba, Allah swt alimtuma Malaika Jibrail a.s kwenda kumwokoa mtoto huyo katika mdomo na mabano ya mnyama wa huyo muuwaji, na Malaika Jibraili a.s. akamwambia ‘Ewe bibi kizee ! Je umefurahi sasa? Kwa kile ulichokitoa sadaka basi Allah swt naye amekulipa mema yake.”

5. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:

“ Mfanye mema katika hali ya shida na ufakiri, na wema huo ni Sadaka.

Toeni Sadaka kama itakuwa ni kiasi gani kwa udogo wake. Mnaweza kutoa kiasi cha tende mkajiokoa na Jahannam. Kwa hakika udogo huo siyo hoja na Allah swt ataulea udogo huo kama kwamba nyie mnavyo walea watoto wadogo wanaonyonya maziwa, na siku ya Qiyama wakati mema yenu hayo ( mliyokuwa mkisema ni madogo) yatakapoletwa mbele yenu mtaona kuwa ni sawasawa na ukubwa wa milima mikubwa sana.”

6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameseama kuwa Allah swt anasema kuwa :

“Hakuna kitu kingine mbali na Sadaka ambacho mtu anaweza kumpatia mtu mwingine kidhahiri, na kwa hakika mimi ndiye wakili wake musitahiki, na mimi ninayepokea kwa mikono Sadaka hiyo halafu hata ikiwa kama ni tende kidogo haidhuru mimi ndiye ninaitunza, kama vile mwanadamu anavyowatunza watoto wake.

Siku ya Qiyama huyo mtoa Sadaka atastaajabishwa mno kwa Sadaka zake ndogo alizokuwa akitoa zimekuwa kubwa kama milima ya Uhud, milima mikubwa sana.”

8. KILA SIKU ASUBUHI MTOE SADAKA NA MNUIE

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa:

“Toeni Sadaka asubuhi na mapema kwa sababu kunaondoa balaa kwa siku nzima.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Kwa kutoa Sadaka asubuhi na mapema basi mtoa Sadaka huepukana na kila aina ya matatizo na mabaya yote kwa siku nzima.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Toeni Sadaka asubuhi, na kwa mapenzi kabisa, mwenyewe kutoa Sadaka amebahatika. Basi humwomba Allah swt amani kutokana na balaa zote zilizoko ardhini na mbinguni, na kwa hakika Allah swt humjaalia hivyo kwa sababu ya kutoa Sadaka.”

4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anaelezea kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwusia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa:

“Ewe Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.! Sadaka huondoa balaa ambazo lazima zitatokezea, na kwa kutenda mema pamoja na ndugu na majamaa kunarefusha umri.

Ya Ali! Iwapo jamaa na ndugu ni watu wenye shida, basi kuwapa Sadaka hao haitakuwa ni Sadaka.

Ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.! Kusema maneno bila vitendo ni ya bure hayana maana, na Sadaka bila kuwa na nia nayo haiwi Sadaka.”

5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa: Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza mtu mmoja

“Je leo umefunga Saumu?”

Mtu huyo alijibu

“La hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.”

Tena Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza:

“Je leo umeshawahi kumtembelea aliye mgonjwa?”

Naye akajibu:

“Hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliendelea kumwuliza naye aliendelea kumjibu hapana hakufanya hivyo.

Mwishoni Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.aliendelea kumwuliza:

“Je umemlisha masikini yeyote?”

Naye akajibu: “Hapana Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.!”

Na hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipomwambia huyo mtu :

“Nenda kwa wananyumba wako, nenda ukawatendee na uwe nao kwa mema na uwawie wema, basi hayo ndiyo yatakuwa Sadaka yako kwao.”

9. KAMA KUNA HOFU YA KUJA KWA BALAA AMA KWA KUTOKEZEA UBAYA WOWOTE AU KWA SABABU YA UGONJWA NA HOFU YOYOTE BASI TOENI SADAKA.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambaye ameseama:

“kwa baraka za Sadaka Allah swt humwondolea mwenye kutoa Sadaka balaa sabini, ambamo kuna magonjwa, madhara yatokanayo na moto, kuzama maji, kufunikwa na majumba mpaka kufa na atamwepusha ili asiwehuke au asiwe mwehu.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa:

“Ili kutaka kuepukana na shari za madhalimu basi toeni Sadaka.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anaelezea kuwa: Siku moja Myaudi mmoja likuwa akienda kukata miti porini na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwangalia na kuwaambia Ma-Sahaba wake :

“Myahudi huyu leo ataumwa na nyoka na kifo chake kitasababishwa na sumu ya nyoka. Myahudi huyo kama kawaida yake alikata kuni na alijitwisha kichwani mwake na akarud akiwa salama.

Na tena Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipomwona Myahudi huyo akamwambia ateremshe mzigo wa kuni huo na auweke chini. Na Myahudi akafanya hivyo alivyoambiwa, na katika mzigo huo wa kuni wakaona kuna nyoka mweusi mwenye sumu kali sana huku akiuma kuni.

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza Myahudi yule,’Je wewe leo umefanya jambo gani?’

Myaudi huyo akasema: Mimi nimekata kuni na kuzifunga tu, lakini wakati nilivyokuwa nikirudi nilibakiwa na vipande viwili vya mkate na kipande kimoja mimi nikala na kipande kimoja nikampa masikini Sadaka.

Hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema kwa kiapo cha Allah swt ni kwa sababu ya Sadaka ndiko balaa hii imekuondokea, kwa hakika Sadaka humwepusha mtu na ajali mbaya.”

4. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. siku moja alikuwa pamoja na Ma-sahaba wake katika Masjid Nabawi, na upande mmoja wa ukuta ukaanguka chini. Kulikuwa na mtu mmoja hapo ambaye aliponea chupu chupu tu, kulianguka kizingiti kizito karibu na muguu wake. Lakini yeye bahati nzuri hakupata udhuru wowote.

Hapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. aliwaambia Ma-sahaba wake, hebu mwulizeni huyu mtu leo amefanya matendo gani? Na wakati alipoulizwa huyo mtu akasema:

“Mimi nilipotoka nyumbani mwangu leo nilikuwa na kokwa chache za tende. Na kukatokezea na masikini mmoja akaniomba basi mimi nikampa kama Sadaka .

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. akajibu

“Basi kwa sababu hiyo tu leo, Allah swt amekuepusha na balaa hii ambayo ingekumaliza.”

5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. siku mmojaalimwambia Sahabi wake Mayassari kuwa:

“Ewe Mayassari je wajua kuwa wewe umeisha fikiwa na mauti mara nyingi, lakini Allah swt amekuongezea umri wako zaidi kwa sababu ya wewe kuwa mkarimu na kuwajali jamaa na ndugu zako umewawia wema ndio maanake umri wako umezidi.”

10. MNAPOKUWA NA HOFU YA KUPATA HATARI KATIKA MALI, BASI MTOE SADAKA NA KAMA HAMPATI YULE ALIYEMUSTAHIKI, BASI MFANYE NIA SEHEMU HIYO MUITENGE NA MALI YENU.

1. Al Imam Hasan al-'Askary a.s. anasema kuwa:

“ Wakati mmoja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akiwa pamoja na wenzake walikuwa safari na wenzake hao walikuwa na mali nyingi sana. Na njiani wakapata habari kuwa wako majambazi wanaowapora matajiri mali zao. Kwa kusikia hayo hao matajiri walianza kutetemeka na wakaingiwa na hofu na wakaanza kumwuuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. je tufanyeje sasa?

Na kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akawajibu:

‘Mkabidhini mali yenu yule ambaye ataweza kuifadhi mali yenu, na kwa kweli ataitunza sana na baada la kupungua hata itazidi pia, sio hayo tu na pale mutakapokuingiwa na shida ya mali yenu basi yeye kila siku atawarudishia pamoja na nyongeza yake. ‘

Kwa kusikia hayo hao wenzake aliokuwa nao katika safari wakamwuliza :

“Je ni nani huyo?”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akawajibu:

“Yeye ni miliki wa malimwengu zote Allah swt.”

Basi hao wenzake wakamwuliza je tunaweza kumkabidhi vipi mali zetu hizi? Hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akawaambia: Toeni Sadaka muwape wale wanaostahiki. Kwa kusikia hayo wakauliza ewe mjukuu wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Hapa tulipo tutawatoa wapi hawa masikini na mafakiri tutawatafuta wapi? Basi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. aliwajibu: munuie kuwa sehemu moja ya mali yenu mtatoa Sadaka basi na msiwe na wasiwasi Allah swt atailinda mali yenu yote.

“Wale waliokuwa naye pamoja safarini walinuia hivyo kama vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alivyowaambi,a na Imam a.s. akawaambia sasa nyie mko katika amani ya Allah swt, na wakiwa wanaendelea na safari majambazi hao walikumbana nao na kwa kudura za Allah swt wao wakawapita salama usalimini bila ya kudhurika na kusumbuliwa, hadi wakafika mwisho wa safari yao.

Waliopofika tu mwisho wa safari yao wao wakatoa sehemu moja walizokuwa wamenuia kama Sadaka na sehemu iliyo bakia walifanyia biashara yao, na Allah swt akawajaalia baraka kiasi kwamba wakapata faida hata zaidi ya mara kumi.”

11. WAOMBAJI WANATAKIWA WARIDHIKE KWA KILE WANACHOPATA NI SUNNAH, KUWAONGEZEA WALE WALIORIDHIKA NA KUTOWAJALI WALE WASIORIDHIKA.

1. Siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alikuwa Mina pamoja na Ma-sahaba wake wakila zabibu. Mara akatokezea mtu mmoja na akaomba. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kwa mkono wake akachukua fungu moja la zabibu akampa basi huyo akakataa kupokea, akisema “mimi sitaki zabibu hizi bali ninataka pesa tasilimu kama zipo ndio nichukue”.

Basi kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia “Allah swt atakuzidishia” na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. hakumpa chochote, baada ya muda si muda huyo mwombaji tena akarudi kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. na akamwambia Imam a.s. “Nipe zile zabibu ulizokuwa ukitaka kunipa.” Na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia Allah swt atakutafutia njia yake, pamoja na hayo Imam a.s. hakumpa chochote.

Wakati bado wakiwa wamekaa akatokezea mtu mwingine kuja kuomba, na Imam a.s. alitoa mbegu tatu tu za zabibu akampa huyo mwombaji. Mwombaji huyo alianza kumshukuru Allah swt kwa kumjaalia riziki hiyo na akaonyesha shukurani kwa ujumla. Kwa kusikia hayo Imam a.s. alichota mikono ya zabibu miwili akampa na hapo tena huyo mwombaji akaendelea kumshukuru Allah swt zaidi na zaidi. Kwa kusikia hayo tena Imam a.s. akamwambia mtumwa wake kama tuna pesa zozote zile tulizo nazo kwetu mpe huyo. Na huyo mfanyakazi wa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kwa amri yake alimpa Dirham Ishirini alizokuwa nazo. Mwombaji akiwa anachukua Dirham akasema: ‘Ewe Allah swt! Nakushukuru mno sana na hakuna mwingine wa kushirkishwa nawe. Kwa kusikia hayo Imam a.s. nguo aliyokuwa amejifunika akampa huyo mwombaji na huyo mwombaji baada ya kuivaa na kujifunika na hiyo nguo akamshukuru Allah swt ambaye amemjaalia nguo ya kujifunika. ‘Ewe Aba ‘Abdillah! Allah swt akulipe kila la heri. Na baada ya kusema hayo akaondoka zake. Kwa kuona haya Ma-sahaba wakamwambia Imam a.s. kuwa kila alivyoendelea yeye kumsifu Allah swt ndivyo wewe ulivyoendelea kumpa na kama asinge omba kwa kutaja jina la Al Imam a.s. lazima angeendelea kumpa chochote zaidi ya hayo.”

12. ASUBUHI NA MAPEMA NA USIKU UNAPOINGIA NA SAA ZINAZOKUWA MBAYA UANPOTOKA NJE BASI MTOE sadaqah.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“ Mimi nilinunua ardhi pamoja na mtu mmoja. Mtu huyo huyo alikuwa ni mnujumi, kwa hiyo yeye kila alipokuwa akipiga mahesabu yake na elimu ya nyota yake aliyokuwa nayo alikuwa akiangalia saa nzuri ndipo alipokuwa akienda shambani mwake, nami bila kujali kama saa mbaya nilikuwa nikienda shambani mwangu, na sisi tulipokuwa tayari basi ardhi au sehemu yangu ikawa na faida zaidi kuliko sehemu yake.

Kwa hivyo yeye bila kusita katika hali ya kustaajabisha aliniambia mimi sijawahi kuona kama hivi. Mimi kila saa zilizokuwa nzuri nilikuwa nikija shambani mwangu. Na wewe bila kujali saa nzuri au mbaya ulikuwa ukija kwenye shamba lako. Sasa itakuwaje mimi nipate hasara au kasoro?

Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu ngoja nikwambie hadithi moja ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliyesema kuwa:

‘Mtu yeyote anayetaka Allah swt amwepushe na maovu na mabaya ya siku nzima basi yeye aianze siku yake kwa kutoa Sadaka, na yeyote anayetaka ajiepushe na balaa na maovu ya usiku basi yeye usiku unapoingia atoe Sadaka na ujue kwamba mimi daima ninapotoka nyumbani mwangu huwa ninatoa Sadaka. Kwa hivyo kufanya biashara na Allah swt hivi afadhali zaidi kuliko elimu yako ya nyota na kupiga ramli.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema :

“Mtoe Sadaka usiku kwa sababu huiondoa ghadhabu ya Allah swt, husamehe madhambi mazito, na hukusababishia hesabu zako siku ya Qiyamah zikaenda vizuri. Kutoa Sadaka katika siku kunaiongezea mali yako na kuilinda na kunaufanya umri wako uwe mrefu.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“ Kwa kutoa Sadaka yaani kunapokucha kunayeyusha madhambi kama vile chumvi inavyoyeyuka katika maji. Na kunapotolewa Sadaka usiku basi kunaondoa ghadhabu za Allah swt.”

4. Ibn ‘Abbas amesema kuwa: Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu, Sura Al-Baqarah,2, Ayah 274

Wale wanao toa mali zao usiku na mchana, kwa siri na dhaahiri, wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika

“Aya hiyo imeteremshwa makhsusi kwa ajili ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kwa sababu yeye alikuwa anazo Dinar chache ambazo wakati wa usiku yaani baadhi ya Dinar hizo wakati wa usiku na baadhi wakati wa mchana na zinginezo katika hali ya siri na zinginezo zikiwa ni dhahiri alizokuwa akitoa Sadaka katika njia ya Allah swt.”

13. NI VYEMA KUTOA SADAKA KIFICHOFICHO KULIKO KIDHAHIRI.

1. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema kuwa:

“Kwa kutoa Sadaka kifichoficho ghadhabu za Allah swt hupoa.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Sadaka inayotolewa kidhahiri basi kuliko hiyo Sadaka inayotolewa kifichoficho ni afadhali zaidi.”

3. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. siku moja alisema kuwa:

“Mambo yanayomfikisha mtu moja kwa moja kwa Allah swt kama kipitio au (Wasila) ni imani. Na baada yake ni kuwatendea mema ndugu na majamaa zake mtu, ambaye inaongezea baraka katika mali yake na umri wake ukawa mrefu na Sadaka inayotolewa kifichoficho inamfanya huyo mtu asamehewe madhambi yake, na madhambi aliyokuwa yamemgadhabisha Allah swt kwa sababu ya kutomtii, yanabadilishwa kuwa mema na baadaye ni tabia njema na uwema, mambo ambayo yanaepusha ajali mbaya na inamfanya huru mtu katika makucha ya udhalilisho.”

4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Kwa kutoa Sadaka kidhahiri kunaondoa aina sabini za balaa lakini kwa kutoa Sadaka kifichoficho kunamfanya mtu anusurike na ghadhabu za Allah swt.”

5. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:

“Baba yake Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. kila siku usiku alikuwa akitoka nyumbani pamoja na kifurushi cha fedha mgongoni mwake na mara nyingine alikuwa akichukua kufurushi cha vyakula na alikuwa akiwaendea wale wenye shida na dhiki.

Wakati akiwapelekea misaada hii majumbani mwao Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa akiufunika uso wake ili wasiweze kumtambua ni nani huyu anayewafikishia misaada mpaka majumbani mwao.

Wakati Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alipofariki ndipo hapo ikajulikana hawa wanaosaidiwa wenye shida hawapati misaada waliyokuwa wakipata, ndipo hapo wakajua kuwa aliyekuwa anawasaidia mpaka milangoni mwao alikuwa si mtu mwingine bali ni Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s . vile vile wakati Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alipolazwa wakati wa kuoshwa baada ya kufariki kulionekana mabegani mwake na mgongoni mwake alama zilikuwa zikionyesha kuwa alikuwa akibeba mizigo mizito kwa muda mrefu.

Na katika kipindi kimoja cha baridi kali sana yeye alikuwa amejifunika nguo ambayo ilikuwa inamsaidia asiisikie makali ya baridi wakati alikuwa ametoka nje ya nyumba anakwenda mahala fulani. Njiani alikutana na mtu ambaye alimwomba nguo hiyo ili naye aweze kujistiri na kujizuia dhidi ya makali ya baridi iliyokuwapo. Kwa maombi hayo Al Imam Zaynul 'Aabediin a.s. alimpa hiyo nguo naye akabaki bila nguo ya kujifunika au kujuzuia na baridi. Vile vile Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa kila mwaka akijifunika nguo ya kujizuia baridi na kipindi kilipokwisha alikuwa akiiuza na fedha zake zote zilizokuwa zikipatikana alikuwa akitumia katika kuwasaidia wenye kuhitaji misaada.”

Vile vile Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. alisema kuwa:

“Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa akiwasaidia na kuwalisha na kuwatunza familia zaidi ya mia moja katika mji wa Madina. Na alipokuwa akikaa kula mayatima, wazee, wagonjwa na masikini walikuwa wakikaa kula naye pamoja na Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s., na vile vile alikuwa akiwafungia vyakula kwa ajili ya kuwachukulia wale waliokuwa majumbani mwao au kama baba ni mzee alikuja kula huko basi alifungiwa chakula awapelekee mke na watoto zake nyumbani.

Vile vile yeye yasemekana kuwa alikuwa hakai kula pamoja na mama yake juu ya meza moja ya chakula na watu walipomwambia ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. wewe ni kigezo cha tabia njema na mfano bora katika Waislamu! Je kwanini hukai pamoja na mama yako katika kula chakula?.

Al Imam Zaynul 'Aabediin a.s. aliwajibu kuwa

“Mimi sikai na mama yangu kwa sababu yawezekana mama yangu akiangalia chakula moja labda akataka kuchukua na wakati huo mkono wangu ukawa mrefu kwenda kuchukua chakula hiki itakuwa kweli hiyo ni kitovu cha nidhamu na ndivyo maana yake ninajiepusha kukosa nidhamu mbele ya mama yangu.”

6. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:

“Mtu anapotoa Sadaka ya chakula kwa ajili ya kuwapa masikini na mafakiri basi mujue kuwa aina hiyo ya Sadaka huondoa ufakiri na humwepusha mtu na kumuondolea ufakiri, na kuurefusha umri wake na humwepusha na aina sabini za vifo vya kutisha (ajali mbalimbali).”

7. Vile vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Siku ya Qiyamah wakati kutakuwa na jua kali lichomalo basi watu aina saba watakuwa wamepewa kivuli na Allah swt na mmoja wao ni yule anayetoa Sadaka ya vyakula kiasi kwamba mkono wa kushoto haupati habari kuwa mkono wa kulia umetoa Sadaka.”

8. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:

“Enyi Waislamu! Je niwaambieni mambo matano ambayo kwa hakika ni mema, maneno hayo yanawapelekeni hadi Jannat.?

Ma-Sahabah wakajibu

“Naam lazima tuambie ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Naomba utuongoze.”

Kwa hayo Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. akasema:

“Mnapopatwa na misiba basi lazima ufanye subira na mujaribu kuficha, mutoe Sadaka kiasi kwamba mkono wa kulia unapotoa mkono wa kushoto usipate habari, muwatende mema wazazi wenu, na kwa hakika katika mambo hayo ndiyo kuna furaha ya Allah swt na kila mara mwezavyo kusema semeni La Haula wala Quwwata illa billahil ‘Aliyil ‘Adhiim kwa hakika hiyo ni hazina moja kubwa katika hazina za Jannat, na vile vile katika nyoyo zenu muwe na mapenzi ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. pamoja na Ahlul Bayt a.s.

14. KUTOA SADAKA USIKU NI SUNNAH

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. daima ilikuwa akitoka usiku katika kiza huku amejitwisha mafurushi ya mapesa na vyakula kwa ajili ya kwenda kugawa kwa masikini katika mji wa Madina, alikuwa akiwafikishia misaada waitaji walipokuwa. Na siku ambayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliaga dunia, watu wakaona misaada imesimama na watu hawakufikiwa na misaada hiyo ndipo walipokuja kujua kuwa misaada hiyo ilikuwa ikiletwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye daima alikuwa akificha uso wake ili watu wasijue kuwa ni yeye anayewafikishia misaada hiyo.

2. Mu’alla ibn Khuns anasema kuwa:

“Usiku mmoja kulikuwa kukinyesha manyunyu ya mvua, nikamwona Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akielekea katika makazi ya Banu Sai’d nami nikajaribu kumfuata nyuma kisirisiri na mara nikasikia katika giza kizito hicho kama kitu kimedondoka na nikamsikia Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akisema:

‘Ya Allah swt! Ninaomba vitu hivi nivipate tena.’

Na hapo mimi nikatokezea karibu ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., nikatoa salamu. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. baada ya kuitikia salamu akaniambea je wewe ni Mua’alla ?

Nami nikamjibu :

‘Ndiyo ewe Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ! Niwe fidia juu yako.

Hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akaniambia:

‘Naomba uniokotee vitu hapo chini unisaidie.”

Mu’alla anasema mimi katika giza kizito hicho nikaanza kupapasa aridhini na nikakuta kumbe ni vipande vya mikate na wakati ninamkabidhi Imam a.s mikate nilivyo viokota katika giza kali nilihisi kifurushi alichokuwa nacho migongoni mwake kilikuwa kizito mno na hivyo nilimwomba Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. Lakini hakukubali nimsaidie kubeba kifurushi hicho.”

Lakini Imam a.s alikataa akaniambia

“Ninapendelea kuubeba uzito huu mimi mwenyewe kwa sababu huu ndiyo utakao kuwa ufanisi wangu katika siku ya Qiyamah na bora kwangu na hivyo unaweza kuja nami katika safari hii.”

Tulipokaribia katika makazi ya Banu Sa’id, Imam a.s. alikwenda kwa kila mmoja ambaye ni mwenye shida akamwekea mikate miwili na akarudi. Na wakati huo akaniambia kwa kutoa Sadaka usiku kunatuliza ghadhabu za Allah swt, na Allah swt usamehe madhambi makubwa, na kusahilisha hesabu katika siku ya Qiyamah.”

3. Zuhri anasema kuwa:

“Siku moja wakati wa baridi kali mno na ukungu ulikuwa umejaa mwingi mno mimi nilimwona Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. akiwa amejitwisha kifurushi kikubwa cha chakula na mzigo mkubwa wa kuni.

Nami sikusita nikamwambia ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Je nini haya?’

Imam a.s akanijibu nina nia mpango wa safari, na hivyo ndivyo ninavyojitayarisha kwa ajili ya mahitaji yangu.

Zuhri akasema:

‘Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Mimi nakupa mfanyakazi wangu ambaye atakusaidia kukubebea mizigo yako hiyo mizito.”

Al Imam Zaynul 'Aabediin a.s. alimkatalia nami nikamwambia,

“Basi nipe mimi mwenyewe nikupunguzie kukusaidia kukupunguzia huu mizigo. Kwa hayo Imam a.s. akajibu, lakini kwa kufanya hivyo mimi sitakuwa nimetoka katika wajibu wa kufika mwisho wa safari yangu vile inipasavyo kufika, kwa hiyo naomba uendelea na shughuli zako uniache peke yangu.”

Zuhri anasema:

“Baada ya kufika siku chache mimi nilipomwona Imam a.s nikamwambia,

“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Mimi sioni kama wewe ulikwenda safari yoyote ile.”

Imam a.s akamjibu:

“Naam ! Vile uchukuliavyo sivyo. Muradi wangu ulikuwa ni safari ya Aakhera. Mimi nilikuwa nikijitayarisha kwa ajili ya safari ya Mauti. Kumbuka kwamba kujikumbusha na kujitayarisha kwa mauti basi mambo mawili ni muhim, kwanza kujiepusha na yaliyo haramishwa na pili ni kutoa muhanga wa mali katika njia ya Allah swt.”

4. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. katika baadhi ya misemo yake anasema.:

“Toeni Sadaka kwa basabu kunatuliza ghadhabu za Allah swt .

Toeni Sadaka katika njia ya Allah swt mngejariwa kwa sababu ya riziki muliyojaaliwa na Allah swt kwa kufanya hivyo nyinyi mtahesabiwa katka wale wanaopigana katika njia ya Allah swt.

Yeyote yule ambaye ana imani kamili kuwa Allah swt hulipiza kile kinachopendwa na Mumin basi huyo mtu lazima ataitia nafsi yake katika shida na kwa kufanya mema.

Muwatibu wagonjwa wenu kwa Sadaka .

Muilinde na muihifadhi na kulinda mali yenu kwa kutao zaka.

Urekebishe matumizi na mahitaji ya maisha yenu ili mweze kupima vyema.

Kuwaza na mawazo ni nusu ya uzee unaoletwa nawe.

Mwenye matumizi yenye mahesabu yaani anayebana matumizi kamwe hawezi kuwa mwenye shida na dhiki.

Kumsaidia yule ni mtu ambaye anaheshima na mkuu na kumsaidia yule ambaye ana madeni haya maneno mawili hayana kifani yoyote.

Kila jambo lina mazao yake, kwa hiyo mazao ya mema na kuwa na nia katika kutumia mali au chochote katika njia ya Allah na kwa ajili ya Allah swt basi mazao yake ni kwamba kufanya haraka kutekeleza azma hiyo na kamwe usifanye kucheleweshwa.

Muongezee na mupanue riziki yenu kwa kutoa Sadaka, kabla hamjaijiwa na balaa, mwombe dua na kwa hakika mtaweza kujiepusha nayo na kujiokoa nayo.

15. MUJIPATIE FADHILA KWA KUTOA Sadaka KATIKA SIKU TUKUFU NA MWEZI WA RAMADHANI.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Kutoa Sadaka siku ya Ijumaa kuna thawabu na fadhila kubwa sana.”

2. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:

“Msimkatalie masikini anayeomba siku ya ‘Arafah. Lazima mpeni chochote kile.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Mtu yeyote atakaye kuwa ametoa Sadaka katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, basi yeye atakuwa ameepukana na balaa za aina sabini.”

16. JE SADAQAH ITOLEWE WAKATI GANI?

1. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa ameulizwa na mmoja wa Ma-Sahaba wake,

“Ewe Mtume wa Allah swt! Ni Sadaka ipo iliyo bora kabisa kuliko zote!”

Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alijibu,

“Sadaka iliyo bora ni ile ya wakati ule ambapo mtoa Sadaka yuko salama u salimini, mwenye afya kamili na anayeishi maisha mema bila wasiwasi, na ambaye anauogopa umasikini.

Na wala msicheleweshe kiasi kwamba mpaka kwamba mwisho wa maisha yenu yameisha wafikia shingoni, na hapo ndiyo mnaanza kutoa usia kuwa kiasi fulani mpe masikini fulani na fulani mpe kiasi fulani na kadhalika. Kama tunaelewa kuwa mtu fulani kweli ni mstahiki wa msaada au Sadaka sasa kwa nini tusubiri mapaka sisi tunataka kufa ndiyo basi tuseme msaidieni wakati shida alikuwa nayo tangu hapo zamani?”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliombwa na mtu mmoja kuwa ampatie nasiha, na hivyo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia:

“Tayarisha matayarisho yako ya safari, na matayarisho yako hayo yatume kabla wewe hujaenda safari. Jifanyie matendo yako mwenyewe yaani kama unataka kufanya mema uyatende mema kabisa katika uhai wako na mambo yoyote yale ambayo unayoona yanafaida kwako uyatende wewe mwenyewe na wala usiwatupie wengine kama unaweza kujitimizia wewe mwenyewe.

3. Kwa kuzungumzia swala tulilozungumziwa hapo No. 2 hapo juu siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa amekwenda katika ghala la mtu mmoja ambaye alikuwa amefanya usia kuwa baada ya kifo chake maghala yake yote yaliyokuwa yamejaa kwa tende yagawiwe Sadaka kwa masikini. Na baada ya kifo chache ikatekelezwa usia wake na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipokwenda kule baada ya kufagia akakuta kokwa moja ya tende imebakia mguuni mwake basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akainama akalichukua kokwa hilo la tende moja akasema:

“Kama mtu huyu katika uhai wake angelikuwa amegawa kokwa hii moja ya tende basi angepata thawabu zaidi kuliko hata mlima mkubwa kabisa wa Uhud.”

17. MSIMRUDISHE ANAYE KUJA KUOMBA USIKU

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka kwa mababu zake a.s. kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema:

“Pale anapokuja mtu yeyote usiku kugonga mlango kwa nia ya kuomba msaada, basi msimvunje moyo, msaidieni na hasa inapokuwa mwombaji aliyekuja ni mwanaume.”

18. KATIKA IBADA ZOTE ZA SUNNAH SADAKA INAONGOZA.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Allah swt kwa kila kazi amemweka mweka-hazina ambaye anaweka mahesabu yake isipokuwa Sadaka, ambaye mahesabu yake na utunzaji wake anaweka Allah swt mwenyewe. Baba yangu mzazi wakati alipokuwa akimpa chochote mwombaji alikuwa akikichukua tena na alikuwa akiubusu mkono wa huyo mwombaji, na alikuwa akiunusa kwa hamu sana, na ndipo baadaye alipokuwa akimrudishia na kumpa kitu hicho hicho.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema:

“Allah swt amesema kuwa mimi nimewateua mawakili kwa kila jambo na ambao ndio wanaosimamia na kuweka ripoti zake isipokuwa Sadaka ambayo mimi mwenyewe ndiye ninayetunza habari zake.”

19. AINA ZA SADAQAH.

1. Mu’alla bin Khunais amesema kuwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alikwenda katika makazi ya Banu Sa’id na wale wote waliokuwa na shida aliwawekea mikate na kuondoka zake. Hapo mimi nilimwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.:

Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimjibu :

“La! Hawa kama wangekuwa marafiki na wapenzi wetu na wafuasi wetu basi ningewaongezea kiasi cha punje ya chumvi”.

Hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliponielezea kwa uwazi zaidi kwamba siku moja Mtume ‘Isa bin Maryam a.s. alikuwa akipita ufuoni mwa bahari, na akatoa mkate kidogo kutoka kifurushi chake akatupa baharini. Baadhi ya wale aliokuwa nao wakamwuliza!

“Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Je umefanya nini bwana? Nini maana ya kutupa mikate baharini?

Mtume Isa a.s akawajibu:

“Katika bahari kuna viumbe vya Allah swt na iwapo kutatokezea na viumbe vyovyote vitakavyo kula humo kutokana na nilichowatupia basi kwa hakika katika ufalme wa Allah swt nitakuwa na thawabu nyingi mno.”

2. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema:

“Pozeni nyoyo zenu kwa sababu ya kiu kali kwani Allah swt hupendezewa sana na tendo hilo. Kwa hakika amebahatika yule mtu ambaye anawamalizia kiu wanyama kwani yeye siku ya Qiyamah atapata msaada mkubwa sana atakapokuwa katika hali ya kiu.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alikuwa akifunga safari baina ya Makkah na Madina, akaona kuwa kulikuwa na mtu mmoja aliyejitupa chini ya mti mmoja. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwamwambia mtu mmoja aliyekuwa naye, aende akamwulize hali yake, inawezekana labda alikuwa na kiu kali. Mtu huyo alipomwendea huyo mtu aliyekuwa amelala chini ya mti na kumwuliza hali yake basi ikajulikana kuwa mtu huyo alikuwa na kiu ya maji. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimnywesha maji na akaondoka kuendelea na safari yao. Yule aliyekuwa naye safarini akasema,

“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Huyu mtu alikuwa ni Mnasara, watu kama hawa pia tunaweza kuwasaidia na kuwapa Sadaka?”

Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu

“Naam ! Katika mazingira kama haya inawezekana.”

4. Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa pamoja na wafuasi wake nao katika safari, na waliketi kwa ajili ya kula chakula. Na akatokezea swala mmoja ambaye alikuwa akitafuta chakula, Imam a.s. akamwambia huyo

‘Swala njoo karibu, njoo ule nasi! Usiwe na wasiwasi utulie na ujue hapa kwetu hautakuwa na hofu yoyote, upo katika usalama.”

Kwa kusikia hayo Swala huyo alimsogelea Imam a.s. na alikula pamoja nao.

5. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa Siku moja baba yake alikuwa pamoja na wenzake katika bustani yake na walipoketi kula chakula na mara akatokezea Swala mmoja aliyekaribia.

Hapo Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. . ambaye ni baba yake na Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. akasema:

“Ewe Swala, jina langu mimi ni Al Imam Zaynul 'Aabediin bin Al Imam Hussein ibn ‘Ali ibn Abi Talib a.s. na mama yangu Bi Fatima az-Zahra a.s., njoo ushiriki nasi katika kula. Na Allah swt kiasi alichokuwa amemjaalia cha chakula huyo Swala alikula.”

6. Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“Hakuna mtu yeyote mwingine isipokuwa ni Mwislamu tu anayeweza kuchinja wanyama wenu wa dhabihu siku ya Iddi na Sadaka, na unapotoa Sadaka katika kutoa humo lazima wapewe Waislamu tu. Na unapotoa Sadaka katika mali zinginezo unaweza kuwapa Kafir Zimmi ambao wenye kuhitaji misaada hiyo.”

20. KUWASAIDIA MAJAMAA NA NDUGU KUNA THAWABU ZAIDI.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwayah moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa mtu mmoja alimwuliza Mutume s.a.w.w. :

“Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Je ni Sadaka ipi iliyo bora kabisa?”

Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alijibu:

“Sadaka ile ambayo watakayo pewa wale jamaa na ndugu ambao hata kama alikuwa amekorofishana nao au amegombana nao au hawana uhusiano nao kwa sababu ya magomvi.”

2. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Iwapo wewe unatoa kumi kwa ajili ya Sadaka , basi ili kuwasaidia Mumin toa kumi na nane na yule ambaye hawezi kabisa msaidie kwa ishiririni na kwa ajili ya kuwasaidia jamaaa na ndugu kwa wema utoe ishirini na nne.”

3. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema Riwayah kutokea kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa amesema:

“Mtu yeyote atakaye wasaidia jamaa na ndugu zake katika kwenda Kuhijji au ‘Umra, basi Mtume Allah swt atamjaalia thawbu za Hijja mbili na ‘Umra mbili, na yoyote yule atakayemsaidia ndugu yake Mumin basi Allah swt atamlipa kusiko na kifani.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameseama kuwa:

“Iwapo mtu atawasaidia jamaa au ndugu zake ambao wana shida ni muhtaji basi hiyo siyo Sadaka.”

5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah moja ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akisema:

“Kwa mtu yeyote yule ambaye atakwenda mwenyewe kwenda kumsaidia jamaa au ndugu yake mwenye shida na kutoa kitu chochote kwenye mali yake na kumsaidia basi Allah swt atamjaalia ujira wa mashahidi mia moja na kwa kila hatua atakayotembea atamwandikia mema elfu arobaini, na kiasi hicho hicho cha maovu yake yatasamehewa. Na vile vile kiasi hicho hicho ataongezewa daraja lake mbele ya Allah swt na atamwandikwa miongoni mwa wale waja wake halisi waliofanya ibada yao kwa uhalisi kwa muda wa miaka mia moja.”

6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., aliulizwa na mtu mmoja :

“Ewe Mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Je yeyote yule anayekuja kuomba mlangoni anastahili kupewa Sadaka au badala yake tuwape jamaa na ndugu zetu Sadaka hiyo?”

Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliwajibu :

“Kwa hakika kuwapelekea msaada Sadaka jamaa na ndugu wa mtu zina thawabu nyingi zaidi.”

7. Al Imam Muhammad Sahibuz-Zamaan a.s. aliandikiwa barua na mtu mmoja akimwuliza

“Iwapo mtu anaweza kunuia kuwa mimi katika mali yangu nitatoa sehemu fulani ya mali nitamsaidia mtu fulani na katika kipindi hicho iwapo atakuja kujua kuna mtu katika ndugu na jamaa zake ambaye ni kweli anashida na anahitaji msaada wake basi je huyo mtu anaweza kubadilisha nia yake ya kumsaidia jamaa yake badala ya kumpa mtu aliyekuwa amenuia hapo kabla?”

Al Imam Muhammad Sahibuz-Zamaan a.s. akamjibu kuwa:

“Utaangalia ukaribu wa watu hao na yule aliye karibu nawe katika madhehebu umpatie na lau kama wote wawili kama watakuwa wanatokana na dhehebu moja tu basi kwa mujibu wa kauli ya Al Imam Musa al-Kadhim a.s. kuwa kugawanywe kati kati yaani watu wote wawili wapewe nusu kwa nusu, kwa sababu iwapo kutakuwa na jamaa na ndugu ambao wana shida na taabu basi huwezi kutoa Sadaka na kuwapa wengine. Na kwa hakika kwa kufanya hivyo utakuwa umepata thawabu na fadhila za Sadaka.”

21. IWAPO MWOMBAJI HAUMJUI MPE Sadaka KIDOGO ILI AWEZE KUWA NA HURUMA NA MAADUI WA AHLUL BAYT a.s. WASIPEWE Sadaka

1. Al Imam Muhammad Sahibuz-Zamaan a.s. aliandikiwa barua na mtu mmoja akimwuliza kuwa:

“Je inawezekana mimi nikatoa Zaka au Sadaka kutoka mali yangu nikampa mtu ambaye si jamaa wala ndugu yangu?”

Na kwa hayo Imam a.s. alimjibu:

“Usimpe Zaka au Sadaka mtu yeyote mwingine isipokuwa wenzako na majamaa zako.”

2. Al Imam Muhammad Sahibuz-Zamaan a.s. aliulizwa:

“Je inawezekana kumpa Sadaka Nasibi (maadui wa Ahlul Bayt a.s. )?”

Imam a.s akamjibu kuwa:

“Musiwape Sadaka wala Zaka maadui wa Ahlul Bayt a.s. na ikiwezekana hata maji pia msiwape.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliulizwa kuwa:

“Je inaruhusiwa kumlisha mtu kama humwelewi kuwa ni Mwislamu au si Mwislamu?”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akajibu kuwa :

“Mtu ambaye humwelewi na kama huelewi chochote kuhusu urafiki au adui, basi yeye unaweza kumpa. Kwa sababu Allah swt anasema tuwatendee watu mema. Lakini yule aliye mpingamizi wa haki au ambaye anaelekea kuhusu upotofu na madhambi au anayewachukua watu kuelekea upotovu na madhambi, huyo msimpe.”

4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliulizwa kuwa:

“Mara nyingi tunaona masikini wanaokuja kuaomba, lakini sisi tunakuwa hatuwafahamu, Je watu kama hawa tunaweza kuwapa?”

Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliwajibu

“Kama wewe moyoni mwako utaingiwa na huruma kwa ajili ya mtu huyo basi unaweza kumpa, ingawaje hata kama si kamili lakini hata kidogo itafaa.”

5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Kidhahiri wapo waombaji wengi ambao (wengi wanatoka vijijini na maeneo karibu ya mji ) hivyo nyie muwape Sadaka watoto, wanawake, wagonjwa, wadhaifu na wazee.”

6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Mnapoijiwa na masikini kwa ajili ya kuomba ambao ni wazee kabisa na wanawake na watoto na wasichana wadogo basi muwasaidie Sadaka na vile vile muwasaidie Sadaka wale mnaoijiwa huruma mioyoni mwenu.”

7. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliulizwa kuwa:

“Mijini mwetu wanakuja waombaji wengi sana kutoka vijiji na vitongoji ambavyo viko karibu na mji ambamo humo wamechanganyikana Mayahudi,Manasara, Wakristo na hata Majusi (Wanaohabudu moto) sasa katika sura hii je tunaweza kuwasaidia Sadaka ?”

Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alijibu :

“Naam ! Mnaweza kuwapa.”

8. Al Imam 'Ali an-Naqi a.s. aliandikiwa barua na humo akaulizwa:

“Je tunaweza kuwasaidia wale masikini waliopo mitaani ambao hatujui dini na wala Madhehebu zao?”

Kwa hayo Al Imam 'Ali an-Naqi a.s. aliwajibu:

“Kama mtaweza kuwatambua wale maadui na wenye chuki na Ahlul Bayt a.s. na mukiwasaidia basi Allah swt hatakulipeni chochote ama wale ambao nyie hamuelewi Madhehebu yao basi hakuna matatizo yoyote katika kuwapa Sadaka. Na muwasaidie masikini wale wowote wanaoomba kama mtaingiwa na huruma mioyoni mwenu. Hata kama hamtaweza kuwaelewa dini na madhehebu zao… Insha-Allah hakuna tatizo lolote katika kutoa Sadaka katika sura kama hizi.”

9. Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alimwambia muhudumu wake:

“Yeyote yule anayekuja kuomba nyumbani kwake basi asimruhusu akaondoka hadi pale ahakikishe kuwa amemlisha chakula, hususan siku ya Ijumaa.”

Mwandishi anasema kuwa mimi nilimwambia Imam,

“Ewe mjukuu wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Kila mwombaji huwa si msitahiki.”

Kwa hayo Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alinijibu

“Ninaogopa kuwa inawezekana mwombaji akawa msitahiki lakini mimi nikamfukuza, isije tukapata matatizo na dhiki iliyo mpata Mtume Ya’aqub a.s na nyumba yake.”

22. KUMRUDISHA MASIKINI NI KARAHA HATA KAMA USTAHIKI WAKE UTAKUWA MASHAKANI, LAKINI LAZIMA APEWE CHOCHOTE, NA KAMA HAKUNA CHOCHOTE CHA KUMPA BASI UNAWEZA KUMWONDOA KWA MANENO MAZURI NA MATAMU.

1. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:

“Msimvunje moyo mwombaji hata kama atakuwa amekuja kuomba katika usafiri wa farasi.”

2. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:

“Iwapo mtoaji atakuwa anajua wema na fadhila za kutoa Sadaka basi kamwe hatamrudisha mtu yeyote bila ya kumpa kitu chochote.”

3. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Kamwe msiwarudishe mikono mitupu waombaji. Iwapo waombaji wengine wasingekuwa waongo na wadanganyifu basi kamwe wengine wasingerudipo.”

4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kamwe hakumrudisha masikini yeyote aliyemwomba asaidiwe Sadaka. Na kama Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa hana chochote cha kumpa basi alikuwa akimwambia kwa lugha tamu Allah swt atakujaalia Insha-Allah.”

5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Mtume Ibrahimu a.s. daima amekuwa akiwahudumia na kuwakarimu wageni, na pale alipokuwa hakuwapata wageni wowote wale, basi alikuwa akifunga mlango wake na akitoka kwenda kuwatafuta wageni.”

Na katika hadithi hiyo hiyo tunapata wakati mmoja Malaika Jibrail alimwijia Mtume Ibrahim a.s. na kumwambia :

“Allah swt amenituma safari hii kwa mja wake mmoja ambaye ameweka marafiki Wake kama ni Khalil Wake.”

Kwa hayo Mtume Ibrahim a.s. akaingiwa na shauku ya kutaka kumjua na akasema :

“Tafadhali sana naomba unitambulishe huyo umzungumzaye, nami nitapenda kwenda mbele yake.”

Jibrail a.s. akasema :

“Ewe Khalil (rafiki)! Ndiwe wewe tu !”

Basi Mtume Ibrahim a.s. akamwambia :

“Ewe Jibrail a.s. ! Je kwanini umenifanyia hivyo ?”

Hapo Malaika Jibrail a.s. akamjibu :

“Kwa sababu wewe kamwe haujamnyooshea mkono yeyote, na wewe daima haujawahi kumkatalia yeyote aliyekuja kukuomba.”

6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema sema kuwa Mtume Allah swt alikuwa akisema

“Kamwe msimrudishe mikono tupu mwombaji. Hata kama mtakuwa katika hali ya ugumu kiasi gani.

7. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa Mtume Musa a.s. wakati alipokuwa akimlilia Allah swt, Allah swt alimwambia :

“Ewe Musa hata kwa ukimpa kidogo mpe ili utunze heshima ya mwombaji, na kama hicho pia hauna basi kwa maneno matamu na kauli nzuri umwambie na kumwomba msamaha. Kwa sababu miongoni mwa waombaji mara nyingine si lazima atokane na binadamu au Majini bali anakuwa ni Malaika wa Rehema. Kwa hiyo Malaika huyo ndiye anaye wajaribu watu na kile nilicho kushauri ndiyo ujaribu kutegemea kupata jibu lake na huwa anawaombeamo kwa hivyo, ewe mwana wa Imran angalia vile tabia yako itakavyo kuwa”.

8. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripotiwa riwaya kuwa siku moja mtu mmoja alikuja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuomba kwa hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliwaangalia Ma-Sahaba wake na kuwaambia,

“Enyi Ma-Sahaba wangu ! Msaidieni.”

Na mmoja katika Ma-Sahaba wake akamsaidia kifaa cha dhahabu. Aliyekuja kuomba akasema

“Je leo ni -- yako?”

Yule Sahaba wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akajibu :

Naam ndiyo maana yake”.

Yule mwombaji akasema:

Mimi nimekubalia hivyo. Mimi si Jini wala si binadamu; bali mimi ni Malaika niliyetumwa na Allah swt nije nikujaribu na kwa hakika nimekuona wewe miongoni mwa watu wenye kushukuru neema za Allah swt. Mungu akujaalie kila la heri.”

9. Sa’ad bin Musayyab anasema kuwa Siku moja wakati wa swala ya asubuhi yeye alikuwa pamoja na Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s., akatokezea mwombaji mmoja na wakati huo Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. akasema:

“Mpeni huyo mwombaji---- kumbukeni kuwa---kamwe msimwondoe mwombaji katika hali ya kuhuzunika yaani msimwondoe mwombaji bila kumpa chochote”.

10. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ananakili riwaya kutoka baba yake mzazi a.s. kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:

“Mruhusu mwombaji aondoke hata kwa kidogo na kwa mapenzi na kwa huruma pia. Kwa sababu mara nyingi anayekuja kuomba huwa si kutoka binadamu au Majini bali huwa ni njia moja kwa kuwajaribia nyie kwa ajili ya kuwaongezea neema.”

11. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema katika Nahjul Balagha :

“Masikini anapokuja kwenu basi anakuwa ni mjumbe wa Allah swt na yeyote yule atakaye muudhi na atakayemhudhunisha basi atakuwa amemhudhunisha Allah swt na yeyote yule atakaye kuwa amempa chochote basi ajue kuwa amempa Allah swt”.

12. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anaripoti kutoka kwa wazazi wake a.s ambao wamesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Wakati ‘Ummah wangu utakapogeuza uso au utakapo wageuzia uso wale wanao hitaji msaada wao na watakapoanza kutembea kwa maringo basi wakati huo Allah swt atasema: kwa kiapo cha utukufu na ukuu wangu hawa watu watakomeshana wao kwa wao na hivyo ndivyo nitakavyo waonjesha adhabu yao.”

23. BAADA YA KUMSAIDIA MASIKINI MARA TATU UNAWEZA KUMWAMBIA AONDOKE.

1. Walid bin Sahib anasema kuwa:

“Siku moja mimi nilikuwa kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. na hapo akatokezea mwombaji mmoja. Imam a.s alimpa chochote huyo mwombaji na akatokezea mwombaji wa pili naye akapewa chochote. Hivyo hivyo akatokezea mwombaji wa nne basi Al Imam a.s akamwambia Allah atakusaidia upate zaidi njia yako atakupanulia. Na baada ya hapo Imam a.s akasema iwapo mtu atakuwa na Dirham takriban elfu thelathini au arobaini, na akanuia akawa na mpango wa kuzitumia zote ambazo kimatokeo hatabakiwa na chochote basi mtu kama huyo atawekwa miongoni kwa wale watu ambao Allah swt huzitupiliambali dua zao.”

Kwa hayo mimi nikasema

“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Je ni makundi gani ya watu hawa watatu?

Kwa hayo Imam a.s akajibu

“Mmoja wao ni yule ambaye ana mapesa na mali na baada ya kutumia vyote anaomba ‘ewe Mola wangu naomba unipe riziki’. Basi hapo Allah swt anamjibu ‘Je mimi sikukupanulia njia na kukuwekea sababu za wewe kujiwekea riziki yako?”

2. Ali ibn Hamza anasema kuwa:

“Mimi nilimwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. swali kuwa yeye amesikika akisema mwalishe watatu---- na kama mnataka kuwapa chochote zaidi muwape ama sivyo nyie mmeshatimiza haki ya siku yenu hiyo”.

24. HAWEZI KURUDISHA Sadaka NA BAADA YA KUMTOA MTUMWA KAMA Sadaka HUWEZI KUMCHUKUA TENA KATIKA MILIKI YAKO.

1. Walid bin Sabih daima alikuwa akisema kuwa:

“Mtu yeyote anayetoa Sadaka na iwapo Sadaka hiyo itakubaliwa au Sadaka hiyo itarudishwa basi yule mtoa Sadaka haruhusiwi kuila au kuitumia tena hiyo Sadaka kwa ajili yake. Na badala yake hana njia yoyote isipokuwa aigawe Sadaka kwa mtu mwingine. Hatakuwa na ruhusa kwa vyovyote vile vya kuitumia hiyo Sadaka isipokuwa Sadaka itatolewa tena Sadaka kwa mtu mwingine. Vile vile mfano wake inachukuliwa kuwa mtu anapomfanya huru mtumwa katika njia ya Allah swt na kwa ajili ya kutaka furaha ya Allah swt basi kamwe hawezi kumchukua tena yule mtuma(aliyefanywa huru) akamfanya mtumwa wake. Na baada ya kumfanya huru mtumwa na mtumwa atakapo rudi kwake basi hawezi kumweka vile alivyokuwa amemweka mwanzoni kabla ya kumfanya huru katika njia ya Allah swt. Na vivyo hivyo ndivyo swala hizi zinausiana na Sadaka pia.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Yeyote yule atakayekuwa ametoa Sadaka na iwapo Sadaka hiyo itamrejea yeye tena basi yeye mwenyewe hataweza kuitumia wala hataweza kuiuza, kwa sababu kitu hicho kilishatolewa katika njia ya Allah swt na kwa ajili ya ridhaa ya Allah swt na hivyo hakuna kitakachoweza kushirikishwa katika swala hilo, na mfano wake pia ni sawa na ule wa kumfanya huru mtumwa hivyo hataweza kurudishwa tena katika utumwa.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema

“Iwapo mtu atanuia kutoa Sadaka kwa ajili ya mtu fulani anayeuhitaji msaada huo na wakati huo akapata kujua kuwa mtu huyo ameshaondoka, basi hawezi kuirudisha na kuichanganya hiyo mali katika mali yake na badala yake itambidi amgawie mtu mwingine.”

4. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa: Kuna mtu alimwuliza iwapo mtu alimfanya huru mtumwa bado ambaye hajafikia umri wa kubalehe je sheria inasemaje?

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimjibu

“Hakuna tatizo lolote ndani yake lakini sheria itakayotumika hapo ni kama ile ya kutoa Sadaka (yaani baada ya kumfanya huru mara moja hauwezi kumrudisha katika utumwa tena).”

25. NI SUNNAH KUWAAMBIA WAOMBAJI WAWAOMBEENI DUA NA VILE VILE NI SUNNAH KWA MWOMBAJI PIA KUWAOMBEA DUA WANAO WASAIDIA.

Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amesema:

“Dua ya mtu msiidharau au kusema kuwa haifai chochote. Mara nyingi dua muliyoombewa na Mayahudi au Manasara hukubaliwa. Ingawaje inawezekana kwa dua aliyo jiombea yeye mwenyewe haiwezi kukubalika.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Wakati mnapo wasaidia waombaji, muwaombe wawaombeeni dua hata kama dua zao wenyewe hazikubaliki kwa ajili yao wenyewe, mradi kuna uwezekano mkubwa kwa dua zao kwa ajili yenu zikakubalika.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakiliwa na Abu Basir riwaya moja kuwa Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“Wakati mtu anapomsaidia fakiri mwenye shida sana asiye na uwezo, na pale fakiri huyo anapomwombea dua, basi dua hiyo lazima inakubaliwa na Allah swt.”

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“Wakati mnapowapa chochote waombaji; basi muwaombe wawaombeeni dua, kwa sababu inawezekana kwa sababu ya udanganyifu na ulaghai wake dua zake zenyewe kwa ajili yake zisikubaliwe lakini kwa ajili yenu dua zake zitakubaliwa.”

Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s.:

“Alikuwa akimwambia mfanyakazi wake, zuia kwa punde kidogo sadaka, ili mwombaji amalize kuomba dua.”

Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. Na vile vile amesema:

“Dua ya fakiri na mwombaji kamwe hairudishwi au haitupiliwi mbali.”

Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. amemwamrishamfanyakazi wake kuwa:

“Wakati unapowapa chochote waombaji basi muwaambie wawe wakituombea heri.”

Al-Imam a.s. amesema:

“Wakati muwapapo chochote masikini na waombaji basi muwe mukiwaomba wawaombeeni dua kwa sababu wanapo waombeeni dua kwa ajili yenu dua zao hukubalika na inawezekana dua zao kwa ajili yao wenyewe hazikubaliki.”

26. KUSAIDIA KUWAFIKISHIA SADAQAH WANAO HITAJI NI SUNNAH.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Iwapo mtu atapewa msaada ikapitia mikono themanini hadi ikamfikia aliye

mustahiki basi kila mkono utapata haki sawa sawa ya malipo.”

Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Bora ya sadaka zote ni ile ambayo binaadamu baada ya kujitimizia mahitaji yake kwa moyo mkunjufu anatoa sadaka.”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Yule atakaye fikisha msaada katika hali nzuri kwa mwenye kustahiki basi huyo mfikishaji wa sadaka atapata thawabu sawa kama za yule atakaye toa sadaka yake – hata kama katika kufikisha msaada huo kwa anayestahiki itachukua mikono elfu arobaini basi wote watapata malipo sawa kabisa kwani Allah swt hana upungufu wala kasoro ya aina yoyote ile, na wale watu wanaofanya Taqwa na kutenda mema basi laiti kama mungeweza kuelewa uhakika wa swala hili.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Watoaji ni wa aina tatu

kwanza ni Allah swt mwenyewe ambaye anatoa kwa ajili ya malimwengu zote.

Pili ni yule mwenye mali na

tatu ni yule msaada unaopitishwa katika mikono yake au ni mtu ambaye anafikisha misaada hiyo.”

Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amenakiliwa riwaya na Abu Basir kuwa amesema:

“Watoaji ni wa aina tatu wa

kwanza kabisa ni Allah swt,

wa pili ni yule ambaye anatoa kutoka mali yake na

tatu ni yule anayefikisha kama msaidizi katika kufikisha msaada huo kwa mustahiki.”

27. KUTOA KATIKA MALI YAKO KWA AJILI YA KUMSAIDIA MUUMIN NI SUNNAH.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Allah swt amefaradhisha kwa waja wake kwa kusisitiza kuwa kama yafuatavyo,

kwanza uadilifu na mapenzi yake pamoja na muumini mwenzake kama vile ajipendeavyo yeye kwa ajili yake ndivyo ampendee muumini mwenzake.

pili awe ameweka hisa fulani au kiasi fulani katika mali yake kwa ajili ya kutaka kumsaidia muumin ndugu mwenzake. Na

tatu kumukumbuka Allah swt katika kila hali na hapa haimaanishi kuwa kwa kumsifu Allah swt peke yake au kwa kutoa uradi (tasbihi) bali hapa kuna maanisho ya kuwa kufanywe kwa kimatendo kabisa yale yaliyoelezwa katika dini yakiwa ni sehemu ya imani ya mtu.”

Aban ibn Taghlib anasema kuwaSiku moja yeye alimwomba Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amwelezee haki za muumini mmoja juu ya muumini mwingine. Kwa hayo Imam a.s. alimjibu :

“Ewe Aban! Achana nayo, usini shurutishe kukujibu ulicho uliza.

Nami nikamwambia :

“Ewe Mola wangu niwe fidia kwako.”

Na baada ya hapo niliendelea kumsisitiza Imam a.s. anielezee na ndipo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alipoanza kuniambia :

“Haki ya muumini mwenzako juu yako ni kwamba nusu ya mali yako iwe ni mali yake.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akagundua kuwa rangi ya sura yangu imebadilika na akaniambia,

“Ewe Aban je huna habari kuwa Allah swt ameelezea habari za wale watu ambao wamezipenda nafsi za watu wengine kuliko hata nafsi zao?”

Nami nikamujibu

“Bila shaka, niwe fidia juu yako.”

Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akaendelea kujibu,

“Kwa hivyo nyie toeni nusu ya mali yenu muwape ndugu zenu muumini, na kwa hayo pia haitamaanisha kuwa nyie mmethibitisha mapenzi yenu kikamilifu, kwa sababu bado mko mnalingana. Kujitolea mhanga na kufikia kiwango hicho itathibitika pale ambapo hata katika nusu ya mali mliyobakia nayo mkatoa mkawagawia muumini ndugu zenu.”

Muhammad bin Ajlan anasema kuwayeye alikuwa pamoja na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. na mara akatokezea mtu mbele yao akatoa salamu, na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwuliza

“Je ndugu uliowaacha huko nyuma hali zao ziko je?”

Basi huyo aliyekuja akawasifu na akatoa sifa zao na akaelezea kuhusu hali zao zilivyokuwa. Kwa hayo Imam a.s. akauliza :

“Je matajiri miongoni mwao wanawatunzaje wagonjwa wao?”

Basi huyo mtu akajibu :

“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Kidogo tu.”

Na Imam a.s. akamwuliza

“Je hao matajiri wanaonana mara ngapi na masikini?

Basi huyo mtu akajibu :

“Mara chache tu.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwuliza

“Je hao matajiri wanawasaidia kwa mikono yao hao masikini?

Kwa hayo huyo mtu akasema

“Ewe Mawla ! Wewe unaniuliza mambo ambayo katika utamaduni wetu upo mchache sana.”

Kwa hayo Imam a.s. alimujibu

“Je wao watajidhaniaje kuwa wao ni Mashi’a wetu?”

Abu Ismail anasema kuwa:Yeye alimwambia Al Imam Muhammad al-Baquir a.s.,

“Ewe Maula niwe fidia juu yako! Kwa sasa hivi huko kuna Mashia wengi.”

Kwa hayo Imam a.s. akajibu:

“Je wanawasaidia na kuwahurumia mafakiri na wenye shida? Je wale wanao watendea mabaya sasa watu hao wema waliofanyiwa mabaya wanawasamehe hao wabaya walio watendea mabaya? Je wanasaidiana miongoni mwao katika kamari ? ”

Kwa hayo yote mimi nikajibu :

“Hapana sivyo hivyo.”

Hapo Imam a.s. akasema :

“Kwa hakika hao sio Mashia wetu. Basi mjue wazi kuwa Mashia wetu mienendo yao na desturi na utamaduni wao ni kama vile nilivyoelezea hapo.”

Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. siku moja alimwuliza Sa’id bin Hassan,

“Je inawezekana miongoni mwenu kuwa muumini mmoja akatia mkono katika mfukoni mwa muumini wa pili na akajitolea kiasi cha fedha alizo na shida nazo bila ya kusita au kuogopa na muumini yule aliyetiliwa mkono mfukoni mwake asimzuie?”

Said bin Hassan akamjibu

“Ewe Mawla! Kwa hakika mimi sina habari na jambo kama hili.”

Kwa hayo Imam a.s. akamwambia

“Kwa hakika hakuna chochote.”

Hapo mimi nikamwambia Imam a.s. :

“Je hii inamaanisha kuwa sisi tumeisha teketea na kuangamia?”

Imam a.s. kwa hayo akamujibu :

“Sivyo hivyo, miongoni mwenu udugu na upendo bado haujaingia nafsini mwenu.”

Na katika maswala ya dua imesha zungumziwa hadithi moja ambamo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema zipo aina tatu za dua ambazo kwa kufika kwa Allah swt hakuna mtu anayeweza kuzizuia. Miongoni mwake moja ni

dua ya muumini anayemwombea muumini mwenzake na ambaye ametoa msaada kutoka mali yake kwa ajili ya ridhaa ya Allah swt na Ma’asumiin a.s. Na pili ni

dua kwa ajili ya muumini mwenzake ambaye pamoja na uwezo wake anaomba hivyo na ambaye baada ya kujua shida na dhiki kali ya muumini mwenzake hakuipuuzia bali amemsaidia.”

28. MTU AMBAYE AMEISHA TIMIZA MAHITAJI YA WATOTO WAKE NA NDUGU NA JAMAA ZAKE BASI INAMBIDI AJITAABISHE NAFSI YAKE KWA KUWAHUDUMIA WANGINE, HATA KAMA HUDUMA HIYO ITAKUWA NI BURE LAKINI NI SUNNAH.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliulizwa na mtu mmoja :

“Ewe Mawla! Je ni mtu gani mwenzi wako aliyebora kabisa?”

Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alijibu,

“Ni wale ambao wanawawia na kuwafanyia mema ndugu zao katika imani katika hali ya raha,starehe na shida.”

Na aliendelea kueleza kuwa

“Ewe Jamil, yeyote yule aliye nacho kingi basi kutenda kwake mema ni rahisi sana. Kwani Allah swt amewasifu wale walio nacho kidogo na huku wanafanya mema.

Allah swt katika Qur’an Tukufu, Surah Hashri, 59, Ayah 9,

Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala hawaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa (Wahajiri), bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.

Jamil bin Darraj anasemakuwa:

“Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alitukusanyisha na kutuambia

“Miongoni mwenu bora kabisa ni yule ambaye ni mkarimu na mtenda mema kwa wenzake na mwovu kabisa ni yule ambaye ni bahili na anawawia wengine kwa hali hiyo na bora ya matendo ni kule kutendeana mema pamoja na ndugu zenu na vile vile kuwatimizia haja na mahitaji yao na kwa hakika matendo haya yanamuudhi na kumvunja nguvu Shaitan na kunamwepusha mtu asiingie Jahannam na badala yake aingizwe Jannat. Ewe Jamil! Naomba uwafikishie habari hizi muumin halisi.”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimfanyia usia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kwa kumwambia:

“Ewe Ali! Nina ku-usia mambo matatu ambayo kwa hakika yanathibitisha imani.

Moja ni kwamba wakati wa shida na dhiki kutoa mali au chochote na kuitumia katika njia ya Allah swt

pili kuwawia waadilifu watu

tatu ni kuwapa elimu wale wanao tafuta elimu kama wanataka kujifunza elimu.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwaya moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambaye amesema:

“Bora ya sadaka ni ile ambayo inatolewa bila ya kuwa na shida yoyote na inatolewa kwa furaha.”

Mwandishi anasema hadithi hii inawahusu wale ambao wana watoto, familia na ndugu na majamaa. Yeye anakuwa na majukumu ya kuwauliza na kuwatimizia haja hawa watu wanaomtegemea yeye na hivyo baada ya kumalizana nao anatoa sadaka kwa furaha.

Sama’a anasema kuwa:

“Siku moja alimwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s.,

“Iwapo mtu atakuwa na chakula cha kumtosha siku moja, je anaweza kumsaidia yule mtu mwingine ambaye hana chochote? Au tuseme kama mtu ana chakula cha kuweza kumsaidia mwezi mmoja anaweza kuwasaidia wengine ambao hawana kiasi hicho au yeye hana zaidi bali ana kiasi kile tu cha kumtosha yeye,na hivyo hawezi kumsaidia mwingine basi mtu kama huyo atakuwa amelaumiwa na kushutumiwa?”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu,

“Katika suala hili yapo mambo mawili, miongoni mwenu kuna watu ambao wao wanawasaidia na kuwapenda wengine zaidi kuliko nafsi zao na ambapo Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah A-Hashr, 59, Ayah 9 :

Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala wahaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa , bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.

Na jambo la pili ni kwamba yule ambaye ana kiasi kile tu ambacho kinamtosha yeye tu, basi mtu kama huyo hayuko katika lawama.

Naam, mkono ulio juu uko afadhali kuliko mkono uliopo chini (yaani yule anayempa mtu mkono wa juu na yule anayepokea ni mkono wa chini)na daima wakati wa kutoa lazima aanzie na wale ambao kwa hakika wako chini ya utunzaji wake (anawajibika kuwatunza na kuwasaidia na kuwatimizia mahitaji yao).”

Al Imam Musa al-Kadhim a.s. aliambiwa na ‘Ali bin Sued Assinani: “Ewe Mawla! Naomba unifanyie usia”.

Kwa hayo Imam a.s. alimwambia

“Fanya Taqwa. Na umwogope Allah swt”.

Na hapo Imam a.s. alinyamaza kimya, basi yeye akasema :

“Ewe Imam a.s.! Nina shida kubwa sana. Mimi nimeshindwa kabisa sina uwezo wowote, yaani fikiria kwamba sina nguo yoyote juu ya mwili wangu iwapo fulani ibn fulani asingenivulia nguo zake akanipa na kunivalisha mimi.”

Katika kumjibu Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alimujibu,

“Funga saumu na utoe sadaka.”

Naye kwa kunyenyekea alisema:

“Je nitoe katika yale ambayo mimi ninasaidiwa na watu? Na nitoe kiasi gani kutoka humo?”

Al Imam Musa al-Kadhim a.s. alimjibu

“Chochote kile Allah swt anachokufikishia katika riziki yako toa humo sadaka, kwa kufanya hivyo acha nafsi yako ivumilie kidogo kwa ajili ya kuwatolea wengine walio na shida pia.”

Abu basir ananakili riwaya moja ama kutoka kwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. au Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Yeye aliuliza, bora ya sadaka zote ni ipi?”

Imam a.s. akamujibu,

“Sadaka bora ni kutoka ile mali ambayo mtu hana nyingi (kitu ambacho unacho kidogo au cha kukutosheleza tu wewe, unatoa humo sadaka), je wewe huna habari

Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah A-Hashr, 59, Ayah 9 :

Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala wahaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa , bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.

Hakika hadithi moja ndefu Masufi walileta dalili moja mbele ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah A-Hashr, 59, Ayah 9 :

Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala wahaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa , bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.

Imam a.s. aliwajibu

“Kwa ayah hiyo ni ufafanuzi ambavyo watendaji walikuwa wakitenda kama Allah swt alikuwa ameruhusu. Hakuna aliye wazuia hao, na ujira wao pia upo kwa Allah swt, lakini hiyo ni amri ya Allah swt ambayo ni kinyume na matendo yao.

Na sababu ya kufanya hivyo ni kwamba Allah swt anamwonea huruma muumin ili huyo muumin asiweze kuwaletea shida na kuwadhuru nafsi za wananyumba katika familia yao watoto – dhaifu na watoto wadogo, wote walio dhaifu, na ambao hawawezi kustahimili njaa, wazee waume kwa wanawake.

Iwapo mimi nitakuwa na kipande kimoja cha mkate na nikagawa sadaka, basi wale wote wanaonitegemea mie wataangamia na kuteketea.

Ndyio maana Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema, iwapo mtu atakuwa na kokwa tano za tende au mikate mitano au Dinar tano au Dirham tano na yeye anataka kuzitumia zote, basi itakuwa ni vyema kabisa iwapo yeye azitumie kwa ajili ya wazazi wake, na baadaye kwa ajili yake mwenyewe na watoto wake na tabaka la tatu kwa ajili ya ndugu na jamaa zake ambao wana shida na wanahitaji msaada wake, na baada ya hapo awasaidie majirani ambao ni mafakiri, na mwishoni kabisa atumie kwa ajili ya kuwasaidia wengineo katika njia ya Allah swt.

Na baadaye akaendelea kusema kuwa siku moja ilitokea mtu mmoja kutokea Ansaar alifariki(kufa). Kwa mujibu wa usia wake yeye alikuwa na watumwa watano au sita ambao wote walifanywa (kwa mujibu wa usia huo) huru na wakaondoka zao na huko nyuma familia yake hakuwaachia chochote watoto wadogo wadogo na wana nyumba yake wote wakawa ni muhtaji, wakawa wao sasa wanategemea misaada kutoka wengine ilhali huyu bwana alikuwa na watumwa watano au sita.

Na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipojulishwa habari hizo alisikitika mno na akasema,

“Laiti kama nyie mngelikuwa mmenijulisheni kabla kuwa mtu huyo amewafanya watoto na wenye nyumba yake kuwa muhtaji (ni watu wenye kuhitaji misaada na sadaka) basi mimi kamwe nisingelikubali mtu huyu azikwe katika makaburi ya Waislam.’

Hlafu anaedelea kusema kuwa wazee wetu wamenakili riwaya kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa mtoaji sadaka inambidi kwanza awatimizie mahitaji ya wale wanao mtegemea yeye; na wale ndugu na jamaa walio wakaribu zaidi ndio awape kwanza (yaani wazazi, mke, watoto na ndugu zake na majamaa wanaofuatia wa karibu zaidi) na baada ya hapo majamaa na ndugu wenye uhusiano wenye ujamaa nao wa mbali ndio wapewe”.

29. NI SUNNAH KUUBUSU MKONO WAKO MWENYEWE BAADA YA KUTOA SADAQAH NA KUKINUSA KITU NA KUKIBUSU KITU AMBACHO UNAKITOLEA SADAQAH.

Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. Amenakiliwa hadithi yake moja isemayo kuwa:

“Wakati muwapapo sadaka masikini muwaombe wawaombeeni dua, na akaendelea kusema, baadaye kuubusu mkono wa yule uliyemsaidia (uliyempa sadaka) kwa sababu sadaka unayoitoa kwanza inakwenda katika mikono ya Allah swt ndipo inapoingia katika mikono ya mwombaji.

Kama vile Allah swt anavyosema katika Qur’an Tukufu, Surah Tawba, 9, Ayah 104

Je hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali sadaqah , na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu?

Ahmad bin Fahad anaandika katika kitabu chake kuwa:

“ Al Imam Zaynul 'Abediin bin Hussein bin 'Ali bin Abi Talib a.s. wakati wa kutoa sadaka alikuwa akiubusu mkono wake mwenyewe, na mtu mmoja alimwuuliza sababu ya kufanya hivyo na Al Imam Zaynul 'Abediin bin Hussein bin 'Ali bin Abi Talib a.s. alimjibu,

“Kwa sababu kufanya hivyo ni kwamba sadaka kwanza inakwenda katika mkono wa Allah swt ndipo baadaye huishia katika mkono wa mwombaji.”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Sadaka inayotolewa na muumin kwa hakika inafika mikononi mwa Allah swt na baadaye ndio anapewa aliye mwombaji. Na akaendelea kuelezea ayah ya Qur’an Tukufu, Surah Tawba, 9, Ayah 104.

Je hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali sadaqah , na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu?

Jabir Al J’ufi amenakili riwaya kutoka Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. kuwa Al Imam Amir al-Muuminiin ‘Ali bin Abi Talib a.s. amesema kuwa:

“Siku moja nilitoa sadaka ya Dinar moja, hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akaniambia,

“Je unajua sadaka inapotolewa na mkono wa muumin kabla yake yeye anakuwa amejitoa nje ya mitego ya masheitani sabini? Na kabla ya yule mwombaji hajapokea hiyo sadaka inakwenda katika mikono ya Allah swt?

Allah swt anatuambia katika Qur’an Tukufu, Surah Tawba, 9, Ayah 104.

Je hawajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anapokea toba ya waja wake, na anazikubali sadaqah , na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba na Mwenye kurehemu?

Mu’alla bin Hunais ananakili riwaya moja kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa amesema:

“Kila kitu Allah swt amekiwekea mtunza hesabu wake, isipokuwa sadaka tu, kwamba yeye ndyeo mwenyewe anayeishughulikia. Na baba yangu a.s. alipokuwa akimpa masikini au mwombaji sadaka yoyote, alikuwa akiichukua tena akawa akiinusa na kuibusu na tena alikuwa akimrudishia mwombaji mikononi mwake kwa heshima na adabu.

Kwa sababu sadaka anayopewa mwombaji kwanza inakuwa imepitia katika mikono ya Allah swt ndipo inapoishia katika mikono ya yule anayeomba. Kwa hiyo mimi pia nimependelea kukibusu kitu kile ambacho kimeshaingia katika mikono ya Allah swt ndipo kikaenda katika mkono wa mwombaji!”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Kwa kila kitu isipokuwa sadaka tu Allah swt amemweka Malaika kutunza habari zake – na sadaka ameiweka katika usimamizi wake mwenyewe.”

Muhammad bin Muslim ameripoti riwaya moja ama kutokea Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. au Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Al Imam Zaynul 'Abediin bin Hussein bin 'Ali bin Abi Talib a.s. kila alipokuwa akimpatia sadaka mwombaji basi alikuwa akiibusu mikono ya mwombaji huyo. Na alitokezea mtu akauliza sababu ya kufanya hivyo naye akajibu kwa sababu inatoka kwenye mikono ya Allah swt na inaingia katika mikono ya mwanadamu huyo mwombaji.”

30. KATIKA KUTOA SADAQAH NI SUNNAH KUKOPA NA KUMLIPA MARADUFU ALIYEKUKOPA WAKATI WA KUTOA SADAQAH.

Siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliijiwa na mtu mmoja ambaye akasema:

“Je kuna yeyote yule atakayeweza kunisaidia kwa kunikopa? Mmoja katika

Ma-Ansaar akainuka na kusema :

‘Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Mimi nina uwezo wa kumkopesha”.

Basi kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia:

“Mpe mifuko minne ya tende huyu mwombaji. Kwa kusikia hayo huyo Ansaar akampa mwombaji kama vile Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alivyomwagiza”.

Baada ya kupita muda ,huyo Ansaar alimwijia Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kwa kufanya madai ya mifuko minne ya tende aliyokuwa amemkopesha Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambayo Mtume alimpa mtu sadaka, basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia Inshaallah basi nitakutimizia. Na ikafika mara tatu huyu mtu akawa anakuja kuomba alipwe deni lake na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kila mara alikuwa akimwambia Inshaallah nitafanikishia tu.

Mwishoni huyo mtu akashidwa kusubiri na katika hali hiyo akasema,

“Ewe Mtume wa Allah swt! Inshaallah, nimeisikia mara nyingi vya kutosha.!”

Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akacheka na kuwageukia na Ma-Sahaba na kuwauliza,

“Je kuna yeyote miongoni mwenu ambaye anaweza kunikopesha?”

Basi mtu mmoja akainuka na kusema,

“Ewe Mtume wa Allah swt! Naomba ukope kwangu”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kwa hayo akamwambia

“Je una kiasi gani?”

Na huyu katika kumjibu akamwambia

“Kiasi chochote utakacho kihitaji wewe.”

Hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia

“Mpe mifuko minane huyu Ansaari.”

Huyo Ansaar akasema

“Ewe Mtume wa Allah swt! Mimi nilikukopa mifuko minne tu, sasa kwa nini unanirudishia mifuko minane?”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamjibu

“Mifuko minne ninakulipa na mifuko minne zaidi ninakuongezea zawadi kwa ajili yako.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema :

“Kwa hakika sadaka inayotolewa kwa moyo mkunjufu inalipia deni, na inaleta mfululizo wa baraka.”

31. NI HARAMU KUOMBA KAMA HAKUNA HAJA.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Mtu yeyote atakayeomba chochote bila ya kuwa na dharura yake, basi Allah swt atamfanya awe muhtaji kwa maswala hayo kabla ya kufa kwake, na kwa sababu ya kuomba kwake huku kusikostahiki, yeye ataadhibiwa na kutupwa Jahannam .”

2. Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“Kwa Allah swt amekula kiapo kuwa mtu yeyote bila ya kuwa na shida au dharura kama atamwomba mtu amsaidie, basi kuomba kwake huko kutamfanya yeye lazima siku moja awe mwombaji.”

3. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa akisema:

“Enyi watu mfuate na kutekeleza nasiha za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., kama alivyosema:

“Iwapo mtu yeyote atajifungulia milango ya kuomba, basi Allah swt atamfungulia milango ya ufukara na umaskini.”

4. Muhammad ibn Muslim ananakili riwaya kutoka kwa Al Imam Muhammad

al- Baquir a.s. kuwa amesema:

“Ewe Muhammad! Iwapo waombaji wangelielewa mabaya katika kuomba, basi kamwe wasingeweka mikono yao mbele ya wengine; na iwapo mtoaji angezijuafaida na mema basi kamwe asingeuzuia mkono wake katika kutoa sadaka na misaada. Na vile vile Imam a.s.akaendelea kusema, bila shaka yule ambaye ana mali na uwezo na huku anaendelea kuwa mwombaji basi siku ya Qiyama atafika mbele ya Allah swt huku uso wake ukiwa umejeruhiwa.”

5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Mtu yeyote ambaye ana maslahi ya vyakula vya kujitosheleza kwa muda wa siku tatu na pamoja na hayo anaendelea kuomba basi mtu huyo siku ya Qiyama atakuja mbele ya Allah swt huku uso wake utakuwa hauna nyama.”

6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Bila ya kuwa na dhiki na shida mwenye kula kwa kuomba basi ni sawa na mtu anayekunywa pombe.”

7. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:

“Mimi kwa kiapo cha Allah swt ninasema kuwa ni ukweli kabisa kuwa yeyote atakayeilisha nafsi yake kwa kujifungulia milango ya kuomba, basi Allah swt lazima atamfungulia milango ya ufukara na umaskini”

8. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Mtu yeyote anayejifungulia mlango wa kuomba, wakati anao uwezo wa kujilisha mwenyewe basi Allah swt atamfungulia milango sabini ya ufukara na umaskini, kiasi kwamba hakuna yeyote atakayeweza kuufunga hata mlango wake mdogo kabisa.”

9. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Mtu yeyote ambaye ataunyoosha mkono wake kwa kuomba huku ana chakujitosheleza kwa siku moja pia, basi huyo mtu atahesabiwa miongoni mwa wafujaji.”

10. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Siku ya Qiyama Allah swt hatawaangalia watu wa aina tatu na wala hatawatakasisha na watu kama hawa watapewa adhabu kali kabisa.

Kwanza ni mwanaume yule ambaye anafanya ulawiti,

mwanamke yule ambaye hakubakia na haya yoyote na

tatu ambaye pamoja na kuwa na mali bado anaendelea kuomba kwa watu.”

32. MAOVU YA KUOMBA HATA KAMA ITAKUWA NI KIJITI AU MAJI.

1. Muhammad bin Muslim ameripoti riwaya kutoka kwa Al Imam Muhammad

al-Baquir a.s. kuwa amesema:

“Ewe Muhammad ! Kama mwombaji (laiti) angelijua kuwa katika kuomba maovu mangapi yamejificha ndani yake, basi kamwe asingenyoosha mikono yake katika

kuomba.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Ole wenu ! Kamwe msiwanyooshee watu mikono yenu kwa ajili ya kuwaomba kwani itawadhalilisheni duniani, na mtakuwa mkijitafutia dhiki na shida na siku ya Qiyama mtasimamishwa katika mazingara magumu kujibu mahesabu yake.”

3. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Mikono iko aina tatu,

kwanza ni mkono ulio juu kabisa ambao ni wa Allah swt.

Mkono wa pili ni ule ambao ni wa mtoaji na

wa tatu ni wa yule wa mpokeaji ambao ni wa chini kabisa.

Kila ikiwezekana mjaribu kujiepusha na kuomba, kwa sababu hiyo itakuwa ni vizuizi katika riziki yenu hapo mbeleni.

Iwapo mtu atapenda kuinusuru na kuihifadhi na kuilinda heshim na aibu yake basi anaweza kujichumia na kujitafutia riziki yake mwenyewe kwani kunakuwapo na pazia mbele ya riziki..

Kwa kiapo cha Allah swt ambaye roho yangu iko mikononi mwake, iwapo mtu akienda msituni ambapo akakata kuni na siku hiyo hiyo akaziuza au kubadilishana kwa tende na sehemu moja ya tende hizo akajiwekea yeye kumalizia shida zake na sehemu mbili akizigawa katika kuwasaidia wengine katika njia ya Allah swt, basi kwa hakika matendo yake haya ni bora na afadhali kabisa kuliko kunyoosha mikono yake mbele ya watu kwa ajili ya kuomba, kwani pengine wao watampa kidogo au chochote na wengine watamdanganya na kumdharau au na hata kumdhalilisha.”

4. Abu Basir ameripoti riwaya kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliijiwa na baadhi ya watu kutoka makabila ya Ansaar ambao baada ya kutoa salamu waliketi, na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliwajibu salamu yao.

Wao wakasema ewe Mtume wa Allah swt sisi tuna ombi letu moja. Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akawaambia wamwambie. Nao wakasema ni haja yetu moja kubwa kabisa. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kwa kusikia hayo akasema nawaombeni mniambie ili niweze kujua. Wao wakaanza kusema, ombi letu ni kwamba tunakuomba wewe uchukue dhamana yetu ya ya kuingia Jannat (Peponi).

Kwa kusika hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikiinamisha kichwa chake, na kutumia vidole vyake alianza kama kuchimba ardhini kwa vidole vyake. Muda si muda akainua kichwa chake juu na kusema

“Ninaweza kuwapa dhamana hiyo kwa masharti kwamba kamwe katika mazingira yoyote yale nyie hamtamwomba mtu yeyote kitu chochote.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa hao watu hali yao ilikuwa mbaya kabisa kiasi kwamba katika safari hata kama fimbo yao ilikuwa ikidondoka basi wao walikuwa hawamwombi mtu yeyote msaada na hivyo walikuwa wakiteremka chini kutoka wanyama wao na wakijiinulia fimbo zao na walipokuwa wakikaa juu ya meza kwa chakula, wao walikuwa hawawaombi wenzao maji. Bali walikuwa wakienda wenyewe pale penye maji na walikuwa wakiyanywa.”

5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Allah swt anamrehemu yule mja wake ambaye amebakia katika heshima utoharifu na katika desturi zake njema, na ambaye amejiokoa na hakuomba kwa hakika kuomba kunaleta udhalilisho duniani, na uelewe wazi kuwa watu humu duniani kamwe hawataweza kummalizia shida zake zote. Na hapo baadaye Imam a.s. akaelezea kisa kimoja kwa kifupi cha Hatim:

Wakati nafsi za watu zinapo kata tamaa kwa watu basi hapo kwa hakika yanaingia katika shida na taabu kubwa, na kwa uhakika tamaa ndio ufakiri mkubwa na tamaa ndiyo ufukara mkubwa.”

6. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kwa kupitia Ma-Imamu a.s. ameripoti riwaya kuwa:

“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwusia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.,

“Ewe Ali ! Ni rahisi kabisa kuutia mkono wako katika mdomo wa nyoka mkubwa kuliko kumyooshea mkono yule ambaye alikuwa hayupo duniani na akaja akazaliwa baadaye.”

Na akamwambia Abu Dhar:

“Ewe Aba Dhar! Ole wako kamwe usiombe kwa sababu ni udhalilisho na unakaribisha shida na taabu. Na vile vile siku ya Qiyama utatakiwa utoe mahesabu yake makubwa na marefu. Na akaendelea kusema “Ewe Aba Dhar! Kamwe usifungue kiganja chako kwa ajili ya kuomba. Naam, unyooshe mikono yako kwa Allah swt kwa kumshukuru kwa ile riziki aliyokupa.”

7. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Msiwe miongoni mwa watu wasio wajali watu, msiwe kama watu wenye kuwa na dhiki na shida kama maji mnayoyatema baada ya kupiga mswaki mnavyo sukutua.”

8. Katika kitabu Thawabul A’amal imeandikwa riwaya ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye amesema:

“Allah swt anamrehemu yule mtu ambaye ameweka desturi na tabia zake kitakatifu na amejizuia kwa njia zote asiombe kwa watu. Kwa hakika kuomba ni kudhalilika na kujidhalilisha duniani na hakuna duniani wale watu watakaoweza kumtimizia haja yake.”

9. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amesema:

“Allah swt amemfanya Mtume Ibrahim a.s. kuwa Khalil wake (Rafiki wake) kwa sababu yeye kamwe hakulitupilia mbali jambo ambalo alimwomba yeye na yeye mwenyewe kamwe hakumnyooshea mtu yeyote mikono yake isipokuwa kwa Allah swt.”

10. Imeripotiwa riwaya kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:

“Allah swt bila shaka anawachukia sana wale watu ambao hawana aibu ni mchafu (mwili na kiroho), na vile vile mtu yule ambaye amejigundisha kwa watu kwa tabia zake za kuomba omba.”

11. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Msiwaombe ndugu zenu mahitaji yenu, isitokee kwamba wao wakakataa kukutimizia maombi yako, na nyie mkachukia na mkaingia katika kukufuru.”

12. Bwana Salman Al-Farsi r.a. anasema kuwa :

“Mpenzi wangu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amefanya usia na kusisitiza kabisa kuwa, mimi nisipuuzie mambo saba.

Ya kwanza yeyote yule aliye mkubwa kuliko mimi nisimtupie macho yangu, bali nimtupie macho yule ambaye yuko chini yangu;

niwe na mapenzi na maskini na

niwe karibu nao,

niseme ukweli daima hata kama utakuwa mchungu,

niwatendee mema na kuwahurumia ndugu na majamaa zangu, hata kama yule nimfanyiaye hayo atanigeuzia mgongo,

kamwe nisiunyooshe mkono wangu mbele ya watu kuwaomba na vile vile ameniusia kuwa

daima niwe nikisema La Haula Wala Quwwata Illa bilahil ‘Aliyyil ‘Adhiim kwani hiyo ni hazina mojawapo katika hazina za Jannat.”

13. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. Nahaj-ul-Balaghaanasema:

“Muwe mkiziachia matamanio na mahitajio yenu kuliko kuwaomba waovu na wasio stahiki. Na akaendelea kusema na utakatifu na utukufu ni sifa moja ya kupendeza ya mafakiri, na hakika urembo wa shida na dhiki ni kushukuru.”

14. Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. amesema:

“Ujue kuwa uso wako unaong’ara kwa heshima na adabu, na wewe wakati unapokwenda kuomba na ukarefusha mikono yako kwa ajili ya kuomba basi heshima na adabu hiyo inayeyuka na kuanza kudondoka kutoka usoni mwako. Sasa ni kuangalia uyeyukaji huo unamdondokea nani ndio wewe unatakiwa ujue uangalie na ujue.”

Ibn Fahad ameripoti riwaya kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Shi’a wetu hata kama watakuwa wakifa kwa njaa basi kamwe wakati wowote ule hawatainyoosha mikono yao kwa mbele ya watu kwa ajili ya kuomba.”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Mtu yeyote anayenyoosha mkono wake na kufungua kiganja chake kwa ajili ya kuomba, basi ushahidi wake utupiliwe mbali.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Iwapo mwombaji angelikuwa akijua yale majukumu na wajibu walio nao katika kufanya hivyo, basi kamwe asingeomba chochote kwa mtu yeyote. Na vile vile na kutokumpa mwombaji pia kuna majukumu na wajibu mkubwa sana iwapo watu wangelijua basi kamwe wasingeli wakatalia kuwasaidia watu.”

Siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliwaambia Ma-Sahaba wake:

“Ni kwa nini hamfanyi bay’a yangu (utiifu wangu)?”

Basi Ma-Sahaba wakamjibu:

“Ewe Mtume wa Allah swt! Sisi tumeshakwisha kufanya bay’a yako tangu mwanzoni. Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema, mfanye bay’a katika swala ambalo mle kiapo kuwa nyinyi kamwe hamtanyoosha mikono yenu kwa wengine kwa ajili ya kuomba. Na baada ya kula viapo hivyo ikaonekana mandhari tofauti kabisa miongoni mwa Ma-Sahaba kiasi kwamba hata mtu alipokuwa akidondosha mkongojo wake basi alikuwa akiteremka kutoka usafiri wake wa mnyama kama ngamia n.k. kuteremka chini na kujiokotea mkonojo wake, na kamwe alikuwa hamwambii mtu mwingine amwokotee na kumpa hiyo bakora yake iliyoanguka”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Iwapo mtu atakwenda mbio mbio msituni akakata kuni na mzigo huo akauchukua kuja nao kwa hiyo atakuwa ametunza heshima na hadhi yake, basi jambo hilo ni afadhali kuliko udhalilisho wa kuomba.”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Yeyote yule aliyetuomba sisi tunampa na yeyote yule aliyetoa na yeyote yule aliye shukuru basi Allah swt atamfanya awe tajiri.”

Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:

“Kwa kuwaomba watu mahitajio yako ni kuteketeza na kuangamiza heshima yako ni sawa na kuteketeza na kuangamiza heshima yako, na vile vile ustahi wako pia unamalizika. Na kwa hakika kile walichonacho wao utajiri wao inambidi mtu akate tamaa asitegemee chochote yaani asiwe na tamaa ya aina yoyote na hakika hii ndio inayo hesabika kuwa ni heshima kubwa ya muumin. Kumbukeni kuwa tamaa ni ufakiri wa aina mojawapo.”

Ja’bir amenakili riwaya kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa amesema:

“Allah swt ameweka karaha kwa wale wanao omba kwa kung’angania na kwa kufuatilia.”

33. KUOMBA KATIKATI YA UMATI WA WATU SI VYEMA KABISA.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Enyi watu! Msiombe wakati watu wanapokuwa katika makundi, isitokee kwamba kwa sababu ya ubahili wao ikawawia nyie machungu.”

34. NI KARAHA (MAKRUH) KUDHIHIRISHA SHIDA NA UOMBAJI.

Mufadhdhal bin Kais bin Rumman anasema kuwa:

“Yeye siku moja alikuwa katika huduma ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., na mimi nikamdokezea kidogo kuhusu matatizo niliyokuwa nayo. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia kijakazi wake:

Naomba ule mfuko. Na akaniambia Abu Ja’afar (Manthur) amenitumia hizi Dinar mia nne kwa ajili ya msaada, hivyo chukua wewe. Na uende ukamalize shida na dhiki uliyo nayo.”

Nami nikamwambia:

“Hapana! Kwa kiapo cha Allah swt mimi niwe fidia juu yako – mimi sina nia hivyo – mimi nilikuwa natarajia kuwa wewe uniombee dua kwa Allah swt ili shida na dhiki niliyonayo isiniwie ngumu bali iwe nyepesi.”

Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akasema,

“Pamoja na mimi kukuombea dua, kamwe usiwaambie mbele ya umati wa watu shida zako kwani kwa kufanya hivyo wewe utapoteza heshima na hadhi yako.”

Harith Hamdani anasema kuwa yeye amesikia hadithi ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kutokea kwa Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. kuwa:

“Maombi ni amana za Allah swt katika vifua vya watu na yeyote yule atakayeficha siri hiyo basi atapata thawabu za ibada.”

Kulayni anasema kuwa Bwana Luqman alikuwa akimpa mafunzo mwanake kwa kumwambia:

“Ewe mwanangu, mimi nimeisha kunywa dawa na magamba yaliyo chungu kabisa, lakini mbele ya shida na dhiki hakuna kitu kinachozidi uchungu wake. Iwapo wewe utapitia katika hali kama hiyo, basi kamwe usiseme maombi yako mbele ya watu, kwa sababu wewe katika macho yao utaanguka heshima na taadhima yako, na watu hao hawawezi kukufaidisha chochote na badala yake nakuomba umwombe yule ambaye anakujaribu kwa mitihani ya aina hiyo, na bila shaka ni yeye tu anayeweza kukuondolea matatizo na dhiki iliyokukabili, hivyo umwombe yeye tu (Allah swt). Yeye ni nani duniani ambaye amemwomba Allah swt na akarudi mikono mitupu, na yupo ambaye aliweka matarajio na matumaini yake kwa Allah swt na akajikuta ametoka mtupu?”

Imeripotiwa kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa amesema:

“Ewe 'Ali! Allah swt ameweka ni amana miongoni mwa waja wake katika hali ya shida na ufukara, na yeyote yule atakayeweza kuificha hiyo amana basi ajue kuwa yeye ni mtu ambaye amedumisha ‘ibada na anapata fadhila za wale walio dumisha ‘ibada na wanao funga saumu, lakini yeyote yule ambaye anaitoboa na kuitangaza hiyo amana ya Allah swt kwa kudhihirisha na kufanya bayana siri ya shida na ufukara wake kwa wengine, na hao watu baada ya kumsikiliza hawamsaidii basi mjue kuwa huyo mtu kwa hakika wamemuua. Mauaji haya sio kwa upanga au kwa mkuki bali ameuawa kimoyo.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwaya kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa amesema:

“Enyi wenye shida na masikini! Tunzeni heshima zenu na mpeni Allah swt furaha ya mioyo zenu ili kwamba Allah swt awalipe mema kwa ufukara na shida zinazo wakabili na kama nyie hamtafanya (isije mkakufuru na kuvuka mipaka kwa sababu ya kukosa subira na hikima) hivyo basi mtambue kuwa mtapata adhabu na gadhabu za Allah swt.”

35. KURUHUSIWA KUMWAMBIA SHIDA ZAKO MUUMIN NA NDUGU PALE INAPOTOKEA.

Imenakiliwa riwaya kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Itakapo tokea miongoni mwenu mtu akazingirwa kabisa kwa hali mbaya, basi inambidi awajulishe jamaa na ndugu zake na asiiweke nafsi yake katika shida.”

Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. amesema katikaNahaj –ul – Balaghakuwa:

“Mtu yeyote atakayemwambia mahitaji yake dharura zake kwa muumin basi ajue kuwa ameweka habari zake hizo kwa Allah swt, na yeyote yule atakayeleta dharura na mahitajio yake kwa kafiri basi ajue kuwa amekwenda kinyume na maamrisho ya Allah swt.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Katika hali tatu tu ndipo kunapo ruhusiwa kuomba ama sivyo hairuhusiwi.

Kwanza katika kujinusuru mtu mwenyewe,

kujinusuru na hasara kubwa kabisa ya mali na

tatu iwapo kwa kutokuomba kutakuja kumpatia udhalilisho wa hali ya juu sana. Yaani mtu katika vitu hivyo vitatu kujiokoa na hali hizo tatu mtu anaweza kuomba msaada kwa wengine.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa:

“Mtu mmoja alimwijia Al Imam Hassan ibn 'Ali bin Abi Talib a.s. na kuomba chochote: Kwa hayo Imam a.s. akamwambia haistahiki kuomba isipokuwepo hizo sura tatu.

Kwanza ama kuzuia umwagikaji wa damu,

ama mtu akiwa na shida ya hali ya juu kabisa au

kujizuia kuja kudhalilika vibaya sana.

Sasa hebu wewe niambie wewe upo katika sura ipi kati ya hizi tatu?

Yeye akasema ‘Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Katika sura tatu ulizozitaja ipo mojawapo. Basi bila kusita kwa haraka sana Al Imam Hassan ibn 'Ali bin Abi Talib a.s. akamtolea dinar elfu hamsini na kumpa, na Al Imam Hussein ibn 'Ali bin Abi Talib a.s. akampa dinar elfu arobaini na tisa na ‘Abdulah bin Ja’afar akampa dinar elfu arobaini na nane.”

36. KUISHI NA WATU KWA WEMA NI SUNNAH NA KUTOKUWA NA TABIA YA KUWAOMBA OMBA WALA KUWA NA TAMAA KWA YALE WALIYO NAYO.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Heshima ya muumin ni kule kuamka kwa ajili ya sala za usiku, na vile vile heshima yake ni kule kutokuwa mwombaji wa watu.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwaya kutoka kwa Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. kuwa amesema:

“Wewe lazima uwe na moyo wa kuishi vyema na watu na kuwaheshimu na kutosheka nao. Na kuishi nao vyema ni kule kuongea nao kwa upole na utamu na uwe na uso wenye tabasamu na uishi nao vile kwamba kila wakuonapo uwe ukionyesha furaha usoni mwako na hivyo utakuwa umejiwekea heshima katika jamii.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema:

“Iwapo kutatokezea miongoni mwenu anayemtegemea Allah swt azikubalie kila dua zake anazoziomba basi awe akiishi na watu wote kwa wema na kamwe asimtegemee mtu yeyote isipokuwa Allah swt peke yake na atakapo jiona kuwa yeye kwa hakika anao moyo kama huo basi atambue wazi kuwa chochote kile atakachomwomba Allah swt atampatia na kumjaalia.”

Al Imam Zaynul 'Abediin bin Hussein bin 'Ali ibn Abi Talib a.s. anasema kuwa:

“Iwapo mtu atataka wema wote kwa ajili yake ni kwamba yeye ajiepushe mbali na tamaa za kila aina ya kutamani yale waliyonayo watu, na kama yeye ana matamanio yoyote au maombi yoyote basi asiwategemee hawa watu bali zote azielekeze kwa moyo mkunjufu na halisi kwa Allah swt na lazima Allah swt atazikubalia dua na maombi yake na atamtimizia.”

Abul A’ala bin A’ayan anasema kuwa mimi nimemusikia Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akisema:

“Enyi watu nyie mtajidhuru pale mtakapo peleka maombi yenu na mahitaji yenu kwa watu, na kwa hakika inafukuzia mbali heshima na adabu. Mkae na watu katika hali ya kuridhika na kuwa na uhusiano nao mzuri na kwa hakika hiyo ndiyo kwa ajili ya usalama. Kwa hakika tamaa yenu ndiyo dalili ya ufakiri wenu.”

Ahmad bin Muhammad bin Abi Nassr anasema kuwa yeye siku moja alimwambia Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. :

“Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Ninaomba uniandikie barua moja kwa Ismail bin Daud, ili kwamba niweze kupata chochote kutoka kwake. Kwa hayo Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. akamwambia iwapo mimi kitu unachokitaka au cha kukutosheleza wewe ningekuwa nimekukataa, ndipo ningekuandikia, ama sivyo uchukue kile nilicho nacho mimi kwangu na ukitegemee hicho.”

Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:

“Kwa hakika yale waliyonayo watu katika uwezo wao na kuridhika nayo ndimo humo kuna heshima ya muumin ya imani yake, je nyie hamjaisikia kauli ya Hatim? Hatim alisema kuwa pale mtakapoona nafsi zenu zimevutiwa kwa mali za watu wengine basi muelewe kuwa shida na taabu ziko zinawakaribia, na kwa hakika tamaa ni ufakiri ulio dhahiri.”

Abdullah Bin Sinan anasema kuwa yeye amemsikia Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akisema:

“Kwa ajili ya muumin mapendezi ya dunia na akhera yako katika mambo matatu.

Kwanza ni sala katika sehemu ya mwisho wa usiku,

kutokuvutiwa na kutokuwa na husuda na mali na miliki wanayomiliki watu wengine na

kuwa mwaminifu na mtiifu kwa ukamilifu wa Ahlul Bayt a.s. na mapenzi yao.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Alikuwapo mtu mmoja mbele ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na akamwuliza, ‘Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! naomba unionyeshe unieleze jambo moja nilifanye jambo ambalo Allah swt atakuwa radhi pamoja nami. Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimujibu:

Udumishe amani na upendo katika utamaduni wa dunia, jambo ambalo kimatokeo utapata mapenzi ya Allah swt na usiwe na kijicho na wivu wala tamaa kwa mali na miliki za watu jambo ambalo litahifadhi heshima yako machoni na mioyoni mwao.”

Ja’bir bin Yazid ananakili riwaya kutoka kwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. kuwa amesema:

“Usiwe na wivu choyo wala tamaa kwa mali za watu kwa hakika ni jambo jema kabisa kwa kuitakasisha nafsi yako kuliko hata kutoa mhanga wa mali. Vile vile wakati wa shida na dhiki fanya subira. Kuhifadhi heshima yako na utakatifu wako, mambo haya ni afadhali hata kuliko kugawa mali kwa watu. Kwa hakika kuwa na imani kamili juu ya Allah swt na kutotaka kutovutiwa kutokuwa na wivu au kijicho au tamaa kwa mali waliyonayo watu wengine ndio hayo mambo yaliyo bora kabisa katika maisha ya mwanadamu.”

37. SI VYEMA KUMSEMA MTU BAADA YA KUMSAIDIA AU KUMSEMA YULE ULIYEMPA SADAQAH.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema:

“Allah swt amechukia hafurahishwi na sifa sita na vile vile mimi sizifurahii hizo sifa sita na ndio nimefanya usia kwa mawasii na waumini wote kuwa vitu hivyo sita wajiepushe navyo na mojawapo ni kule baada ya kutoa sadaka mtu akaanza kumsema na kuvisema.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Baada ya kutenda mema mtu atakapovizungumzia hayo basi atayateketeza mema yake yote.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwaya kutoka kwa Mtume Muhammad

Mustafa s.a.w.w. kuwa:

“Allah swt hakupendezewa na mambo sita na mimi vile vile katika kizazi changu Maimam wote sikupenda kutokezee sifa hizo, na vile vile Maimam pia nimewahusia kuwa wasizipende sifa hizo ziwepo katika muumin. Hivyo kila muumin anabidi ajiepushe na sifa hizo. Katika sifa hizo sita mojawapo ni ile baada ya kumfanyia mtu wema mtu anaanza kuyazungumzia huku na pale.”

Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. anasema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Allah swt hapendi sifa sita na hizo sifa sita mimi sikupendezewa kwa ajili ya mawasii watakao nifuata na waumini wote watakaonifuatia.

Kwanza kusali isivyo kwa makini,

pili katika hali ya saumu kujamiiana na mwanamke,

tatu baada ya kutoa sadaka kutangaza na kuonyesha.

Nne kuingia msikitini katika hali ya Janaba,

kuwa na shauku ya kutaka kujua mambo ya watu majumbani mwao kunatendeka na kunaendelea nini, na

sita kucheka makaburini mtu anapokuwa baina ya makaburi mawili.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kwa mamlaka yake amenakili riwaya kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa:

“Mtu yeyote atakaye msaidia muumin ndugu yake na baadaye akaja akamwambia kuhusu wema huo akausema basi Allah swt hulirudisha tendo hilo halikubalii. Basi mtoaji atabakia na uzito juu yake na kwa lile jema alilolitenda hana malipo yoyote kutoka kwa Allah swt.”

Na Imam a.s. aliendelea kusema: “Kwa sababu Allah swt anasema kuwa yeye ameiharamisha Jannat kwa ajili ya yule anayesema baada ya kutenda tendo jema na bahili na mchonganishi.

Muelewa wazi kuwa yule mtoa sadaka, hata anayetoa kiasi cha Dirham moja, basi Allah swt humlipa zaidi ya ukubwa wa mlima wa Uhud kwa neema za Jannat na yeyote yule atakaye saidia kufikisha hiyo sadaka kwa yule ambaye anahitaji basi Allah swt atamlipa mema hayo hayo, na kamwe hakutakuwa na punguzo lolote katika neema za Allah swt kwa ajili ya wote hao.”

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika hotuba yake alisema:

“Yeyote yule atakaye tenda wema na kuwawia wema ndugu wenzake, na akaanza kutanganza mema aliyoyafanya basi matendo ya watu kama hawa yatatupiliwa mbali na hayatakuwa na maana yeyote.

Allah swt amewaharamishia Jannat watu wafuatao:

Kwanza ni wale wanao tangaza mema waliyowafanyia watu wenzao, na

Wale wanaowapotosha watu wengine,

wafitini,

wanywaji wa pombe,

wale wanao tafuta makosa ya watu na aibu za watu,

wale wenye tabia mbaya,

wale walio makatili kwa wenzao na vile vile

wale watu wanao watuhumu watu wengine kwa tuhuma za kuwazushia maovu.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwaya kutoka kwa mababu zake kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Allah swt amewazuieni nyinyi kwa matendo maovu takriban ishirini na manne na mojawapo ni jambo lile ambalo baada ya kutoa sadaka mtoaji anamwambia maneno aliyempatia.”

8. Bwana Abu Zahar Al Ghafaramenakili riwaya kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa:

“Kuna aina tatu ya watu ambao Allah swt kamwe hatazungumza nao siku ya Qiyama.

Kwanza ni yule mtu ambaye hatoi kitu chochote bila ya kumsema au kumwambia yule anayempa, na

pili ni yule ambaye hachukui jukumu wala haoni umuhimu wa kuficha zehemu zake za siri na wa

tatu ni yule ambaye anauza mali yake na kutaka faida kupindukia kiasi.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Mtu yeyote baada ya kumsaidia muumin atamuudhi kwa kumwambia au kwa kumsengenya kiasi kwamba roho yake ikaumia basi Allah swt huibatilisha sadaka na wema kama huo.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Aina tatu ya watu kamwe hawataingia Jannat.

Moja ni yule ambaye wazazi wake wamemfanya Aak, wa

pili mnywaji wa pombe (daima anakunywa pombe) na

tatu ni yule baada ya kufanya mema huanza kusema na kutangaza.”

38. MTU ANAPOTOA KITU KUSAIDIA BASI HAIRUHUSIWI KUMWAMBIA KUWA UMETOA ZAIDI KUPITA KIASI.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. siku moja alimtumia mifuko mitano za Tende za Baqi’ (Jannatul Baqi’, ipo Madina ). Mtu huyo alikuwa muhtaji mwenye shida na daima alikuwa akitegemea msaada kutoka kwa Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s., na kamwe alikuwa harefushi mikono yake kwa wengine kwa ajili ya kuomba kwa watu wengineo. Mtu mmoja alipo yaona hayo basi alimwambia Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s.:

“Kwa kiapo cha Allah swt, huyu mtu hajakuomba chochote wewe kwa hivyo badala ya kumpa mifuko mitano mfuko mmoja tu ulikuwa ukitosha, na kwa hayo Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. akamwambia:

“Allah swt asiongezee idadi ya muumin kama wewe humu duniani! Wewe mtu wa ajabu sana, mimi ndiye ninayempa lakini ubahili unaufanya wewe! Kumbuka kuwa mtu mwenye shida na anaye kutegemea wewe hakuombi, Je ni haki kuwa mwenye shida asipoomba basi asisaidiwe mpaka lazima aombe? Basi hapa inaonyesha heshima yake. Uso ule ambao unawekwa juu ya udongo kwa ajili ya ibada ya Allah swt katika hali ya sujuda itakuwa basi mimi nimeubadilisha ule sura badala ya kumwangukia Allah swt utakuwa umeniangukia mimi ! Na jambo ambalo silitaki mimi na wala silifanyi hivyo.”

Mtu ambaye hathamini hajali shida za muumini wengineo itakuwaje ategemee Jannat wakati huku yeye mwenyewe anafanya ubahili katika mali yake? !

Yule asemaye daima “Ewe Allah swt wasamehe madhambi yao yote waume kwa wanawake Waislam” kwa hakika mtu kama huyu huwa anategemea Jannat tu je ni uadilifu gani kwa kusema tu kwa mdomo kuwaombea mema watu ambapo wao hawawafai watu wengine wanapokuwa na shida na dhiki huku wakiwa wanafanya ubahili kwa mali zao?”

39. KUMSAIDIA MTU KABLA HAJAOMBA NA KUMSAIDIA KATIKA HALI YA KUTOKUJULIKANA NI NANI ANAYESAIDIA NI SUNNAH.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Kwa hakika uwema ni ule ambao mtu anamsaidia mtu kabla hajaombwa, na kumpa baada ya kujua hali yake inamaanisha umempa baada ya kujua hivyo. Inawezekana maskini huyo mtu usiku kucha akawa anatapatapa iwapo atafanikiwa au hatafanikiwa, huku akiwa amejawa mawazo niende kwa nani nisiende kwa nani, na hatimaye moyo ukiwa unadunda mwili ukiwa unatetemeka na akiwa amejawa na aibu kubwa anatokezea mbele yako.”

2. Yas’ab bin Hamza anasema kuwa:

“Mimi siku moja nilikuwa pamoja na Al Imam Musa al-Kadhim a.s., watu walikuwa wamekaa huku wamemzunguka, yaani watu wengi walikuwapo. Watu walikuwa wakiulizia masuala ya halali na haramu, na mara tukaona akaingia mtu mmoja mrefu na akaanza kusema, “Iwe salamu juu yako ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Mimi ni mpenzi na mfuasi wako wewe na baba na mababu zako, na hivi nimerudi kutoka Hijja Tukufu. Mimi nimeibiwa mali yangu yote na hivyo sitaweza kufika nchini kwangu (yaani nyumbani). Mimi naomba nisaidiwe sadaka kiasi kwamba niweze kufika nyumbani kwangu, na mimi nitakapo rudi katika mji wangu kiasi hicho cha fedha nitakitoa nigawe katika kuwasaidia wengine kama sadaka.

Imam a.s. akamwambia:

“Naomba ukae kidogo upumzike, Allah swt akurehemu. Na Imam a.s. aliendelea na mazungumzo yake pamoja na umati uliokuwa pale katika kuulizana na kueleweshana kuhusu maswala mbalimbali. Hatimaye mimi Khaysama na Suleiman Al-Ja’afari ndio tuliokuwa tumebakia na hapo Imam a.s. kwa kuniangalia mimi akasema:

“Je unaniruhusu mimi niende chumbani kwangu?”

Suleiman akasema

“Allah swt aiendeleze amri yako”.

Hapo Imam a.s. aliinuka na kuelekea katika chumba chake a baada ya muda si muda akatoka nje akafunga mlango na mwenyewe akasimama nyuma ya mlango na akatoa mkono tu nje huku akisema, je huyo msafiri kutoka Khurasan yuko wapi?”

Hapo mimi nikamjibu:

“Ya Imam a.s.! Mimi niko hapa.”

Na kwa hayo Imam a.s. akamwambia”

“Nimekupa hizi Dinar mia mbili ambazo zitakusaidia wewe katika gharama na matumizi ya safari yako na vile vile napenda nikujulishe kuwa hakuna haja tena ya hizi pesa kuzitolea sadaka ufikapo nyumbani kwako, asante na unaweza kuendelea na safari yako na itakuwa vyema tusitazamane nyuso. Msafiri huyo akachukua hizo pesa na kuondoka zake.”

Seleiman Al-Ja’afar akauliza:

“Niwe fidia juu yako ewe Mwana wa Mtume s.a.w.w.! Kwa hakika wewe umefanya wema na ihsani mkubwa sana wenye huruma, lakini pamoja na hayo kwa nini umejificha?”

Kwa hayo Imam a.s. akamjibu

“Hakuna sababu nyingine ila sikutaka kuona uso wa mwombaji ukiwa umeingiwa na aibu na unyonge sababu ya kuomba. Je wewe hujaisikia hadith ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambamo amesema, kwa yeyote yule anayeficha wema hulipwa thawabu za Hijja sabini na yeyote yule baada ya kutenda maasi na madhambi anatangaza basi daima hubakia dhalili. Na yeyote yule anayeficha madhambi na maovu basi Allah swt humsamehe.”

40. NI SUNNAH KUENDELEZA NA KUTUNZA MSAADA NA UKARIMU NA KUENDELEAZA MOYO WA KUTOA.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Jambo jema kabisa linalonisaidia mimi katika kufanya wema katika kuwasaidia ni mkono ambao unawafikishia na mkono mwingine unashirikiana naye. Na kwa hakika hao wanaokuja kuomba wanakuja na maombi yao ndipo wanapokuwa karibu nami zaidi. Kwa hakika nimeona kuwa wale wanao sahau waliyoyatenda mema kabla na baada ya kuurudisha mkono wao nyuma huonekana kuwa wao wanaanza kuyasahau mema yote. Kwa hakika moyo wangu kamwe haukuniruhusu kuwafukuza na kuwakatalia waombaji. Na baada ya hapo Imam a.s. alisoma mashairi ifuatayo:

Wakati unapokuijia mtihani kwako kwa heshima zako pia inabidi uombe,

Basi uende kwa mtu mmoja aliye mkuu na aliye Sharifu kwa ajili ya kuomba kwake.

Kwa hakika, huyo mtu Sharifu na mkuu atakapokusaidia basi humo ndani hakutakuwa na maonyesho wala masengenyo, na badala yake ndani kutakuwa na unyenyekevu na kuhuzunika pamoja nawe.

Kumbuka wakati utakapotaka kupima katika mzani uombaji na utoaji sadaka na mema basi utaona sahani ya mzani ya uombaji utakuwa daima ni mzito kuliko nyingine yote.”

2. Warram bin Abi Faras ameandika riwaya kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Wenye imani dalili zao ni nne,

kwanza nyuso zao huwa zina bashasha,

ndimi zao zinakuwa zenye ukarimu na mapenzi,

nyoyo zao zinakuwa zimejaa huruma, na

wanakuwa na mkono wenye kutoa mkono unaopendelea kutoa sadaka na misaada nk.”

41. KUHURUMIA NA KUSAIDIA NI SUNNAH NA HUKUMU ZINAZOHUSIANA NAZO.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa Mtume Muhammad Mustafa

s.a.w.w. alikuwa akisema:

“Kila kila aina ya wema na huruma ni sadaka.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akizungumzia neno Ma’arufu katika Qur’an

Tukufu, Surah Nisah, 4, Ayah 114:

Hakuna heri katika mengi ya wanayo shauriana kwa siri, isipokuwa kwa yule anaye amrisha kutoa sadaqah, au kutenda mema, au kupatanisha baina ya watu. Na mwenye kufanya hayokwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, basi tutakuja mpa ujira mkubwa.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Kwa ma’arufu kuna maanisha kule mtu kutimiza wajibu wake aliofaradhishiwa.”

42. NI SUNNAH KUWAWIA WANA NYUMBA WAKO KWA WEMA KABLA YA KUTOA SADAQAH KWA WATU WA NJE.

1. Siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliwasaidia waombaji watatu na wa nne

alipokuja hakumpa chochote. Na hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akasema:

“Iwapo mtu atakuwa na Dirham elfu thelathini au arobaini na zote akazigawa kwa kusaidia au sadaka bila ya kubakiza chochote kwa ajili ya wana nyumba wake basi huyo mtu atakuwa mmoja miongoni mwa watu watatu ambao dua zao hazikubaliwi na Allah swt. Na katika watu hawa watatu: mmoja ni yule ambaye bila kutimiza wajibu wake anagawa mali yote kama sadaka au kusaidia, na baada ya hapo anakaa akiomba dua:

“Ewe Allah swt naomba unipe riziki.”

Basi hapo atajibiwa, “Je mimi nilikuwa sikukufanyia njia ya kujipatia riziki?”

2. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Bora ya sadaka zote ni ile kufanya wakati mtu anapofanya katika hali unapokuwa sawa.”

3. Hisham bin Al Muthanna anasema:

“Kuna mtu mmoja alimwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuhusu tafsiri ya ayah Surah An Am, 6, Ayah 141.

Na Yeye ndiye aliye ziumba bustani zenye kutambaa juu ya chanja, na zisio tambaa, na mitende, na mimea yenye matunda mbali mbali, na mizaituni na mikomamanga inayo fanana na isiyo fanana. Kuleni matunda yake inapo zaa, na toeni haki yake siku ya kuvunwa kwake. Wala msitumie kwa fujo. Hakika Yeye hawapendi watumiayo kwa fujo.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimjibu,

“Katika Ansaar alikuwako mtu mmoja (aliwapa jina lao) ambaye alikuwa ana shamba. Pale mazao yake yalipokuwa yakiwa tayari yeye alikuwa akigawa yote katika sadaka, na alikuwa hawapi chochote watoto na wana nyumba yake; na kwa tendo lake hili Allah swt alikuwa akimhesabia yeye kama ni mfujaji na mbadhirifu.”

4. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Baada ya mtu kujitolea kile kiasi alicho na dharura nacho kwa mujibu wa mahitaji yake na baadaye katika kiasi kinachobaki akitoa sadaka basi hiyo sadaka ni bora kabisa.”

5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema:

“Mojawapo katika Nasiha na Mawaidha ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ilikuwa ni kila aina ya wema ni sadaka mojawapo, na sadaka iliyo bora kabisa ni pale kutoa wakati mtu ameshajitimizia wajibu wake na ametosheka, na mkumbuke kuwa muwape wale ambao kwao nyie mnawajibika kuwatimizia mahitaji yao.

Mkono wa mtoaji ni afadhali kuliko mkono wa mpokeaji. Kwa hakika mtu ambaye anachuma kwa uwezo wake na kutumia kwa ajili yake na kuwatimiza mahitaji yao basi Allah swt kamwe hatamlaumu.”

6. Mtu mmoja alimwijia Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na kumlalamikia

kuhusu njaa:

“Basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimtuma mmoja wa wake zake naye alipowaendea wakamwambia kuwa wao walikuwahawana chochote isipokuwa maji ya kunywa tu, na kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia, je kuna yeyote yule atakaye mchukua mtu huyu kuwa mgeni wake kwa usiku huo?”

Na kwa hayo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. akasema,

“Ewe Mtume wa Allah swt ! Mimi nakubali kumchukua huyu kama mgeni wangu kwa usiku wa leo.” Na walipofika nyumbani kwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. , Imam a.s. alimwuliza Bi. Fatimah az-Zahra a.s. “Je nyumbani kuna chakula chochote?”

Kwa kusikia hayo Bi. Fatimah az-Zahra a.s. akasema, tuna chakula kiasi cha kuwalisha watoto wetu tu lakini na mgeni pia ana haki yake.”

Na hapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. akasema

“Wewe walaze watoto, na uizime taa.”

Asubuhi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alipokuja mbele ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwelezea kisa kilivyotokea na wakati bado akiwa anaelezea kisa hicho ayah ifuatayo iliteremshwa Surah Al Hashri, 59, ayah 9. :

Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala hawaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa (Wahajiri), bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.

43. NI KARAHA KUKWEPA NJIA WANAYOPITA MASKINI. NI SUNNAH KUTOKEZEA MBELE YA WAOMBAJI NA KUWASAIDIA KITOSHELEVU KWA KUTOA SADAQAH.

1. Muhammad bin Yaqub Kuleiyni amenakili riwaya kutoka Abu Nasar kuwa yeye amesoma barua ambayo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alimwandikia Abu Ja’afar(Mutawakili, mtawala wa Ki Abbasi). Humo kulikuwa kumeandikwa:

“Ewe Abu Ja’afar ! nimepata habari kuwa wewe unapotoka nje wakati umekaa juu ya usafiri wako basi wafanyakazi wako wanakutoa nje kwa kupitia mlango mdogo, ili kwamba yule ambaye ana shida na mwenye kuuhitaji msaada wako asiweze kufaidika hivyo.

Mimi kwa kiapo cha haki yangu ninakusihi kuwa kutoka kwako na kuingia kwako uwe kupitia mlango mkubwa na uwe na wingi wa dhahabu, fedha na mali ili atakapo tokezea mbele yako mwombaji mwenye shida uweze kumsaidia. Wajomba zako wanapokuomba uwape Dinar hamsini na wake zao wanapokuomba uwape Dinar ishirini na tano na usiwape chini ya hapo kama utawapa zaidi basi hilo ni shauri lako.

Na hii nakuambia kwa sababu iwapo wewe utafuata hivyo basi Allah swt atakuwia wema, hivyo utumie na usiwe na shaka katika ahadi na neema za Allah swt mmiliki wa malimwengu yote.”

44. NI SUNNAH KUTOA KITU CHOCHOTE KILA SIKU KATIKA NJIA YA ALLAH SWT.

1. Safwan anasema kuwa siku moja Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. alimwuliza mmoja wa wahudumu wake:

“Je leo mmetoa chochote katika njia ya Allah swt ?”

Naye alijibu hapana, leo sijatoa chochote bado.”

Kwa hayo Imam a.s. alisema

“Sasa usipotoa hivyo unategemea Allah swt atupe baraka kwa misingi gani? Lazima utoe kwa njia ya Allah swt hata kama itakuwa ni Dirham moja.”

45. KUTOA SADAQAH NI SUNNAH LAKINI KUSAIDIA KUTOA MSAADA KWA KUTEGEMEANA NA WADHIFA WA MTU NI FARADHI.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Ayah ya Qur'an Surah Al-Hajj, 22 , Ayah 28:

Ili washuhudie manufaa yao na walitaje juna la Mwenyezi Mungu katika siku maalumu juu ya nyama haoa alio waruzuku. Basi kuleni katika hao na mlisheni mwenye shida aliye fakiri.

“Allah swt katika ayah hii anamaanisha kuwalisha wale walio na shida na kuwasaidia, ambapo wao kwa heshima zao wenyewe hawajitokezi nje mbele ya watu kuomba.”

2. Isack bin Ammar amenakili riwaya kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Utafika wakati mmoja ambapo waombaji wanaorefusha mikono yao kwa watu watakuwa wakiishi kwa starehe na wale watakao kaa kimya kwa kutunza heshima zao watakuwa wakifa kwa shida zitakazo kuwa zikiwakabili.

Kwa hayo mimi nikamwuliza Imam a.s.,

“Ewe Maula ! Je yakitokea hayo katika zama za uhai wangu mimi nifanyeje?”

Kwa hayo Imam a.s akamjibu,

“Kwa hakika kile ulichonacho wewe uwasaidie hao watu kwa hali na mali na kwa hata cheo chako ulicho nacho na kwa wadhifa wako ulio nao uwasaidie ipasavyo.”

46. SADAQAH KUTOLEWA KUTOKA MALI ILIYO HALALI NA HAIRUHUSIWI KUTOA SADAQAH KUTOKA MALI ILIYO HARAMU.

1. Abu Basir anasema kuwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliitolea maelezo Ayah ya Qur'an Tukufu Surah Al Baqara, 2, ayah 267 isemayo

Enyi malio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa.

Amesema kuwa:

“Zama kabla ya Islam watu walikuwa wamejilimbikizia mali iliyopatikana kwa njia zisizo halali (kwa njia zilizo haramu) na baada ya wao kusilimu, walikuwa wakidhani kuwa kwa kutoa mali iliyo patikana kwa njia haramu, watakuwa wametakasisha mali yao iliyo halali, kwa hivyo Allah swt alitoa amri kuwa sadaka itolewe kutoka mali iliyo halali tu.”

2. Kwa kuzungumzia ayah hiyo ya juu Shahab amenakili riwaya kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Ambamo amesema kulikuwa na kaumu moja ambayo walikuwa na mali nyingi iliyo chafu (iliyopatikana kwa njia za haramu ). Wakati wao walipoukubalia Islam walianza kuchukizwa na malimbikizo yao hayo machafu na wakataka kutoa kwa njia za sadaka. Allah swt aliwaonya kwa kuwaambia kuwa sadaka hutolewa kutokea mali iliyo halali tu.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Iwapo watu watachuma au watajipatia mali kwa mujibu wa hukumu za Allah swt na wakaitumia kinyume na hukumu za Allah swt au iwapo watachuma kwa njia zilizo kinyume na hukumu za Allah swt na wakazitumia kwa mujibu wa hukumu za Allah swt; katika hali zote mbili Allah swt hazikubalii.

Katika kutaka kukubaliwa sharti ni kwamba mapato hayo yawe yamepatikana kwa njia zilizo halali na zitumiwe katika njia zilizo halali vile vile.”

4. Halabi anasema kuwa mtu mmoja alimwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuhusiana na ayah hii katika Qur'an Tukufu Surah Al Baqarah, 2, ayah 267:

Enyi malio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa.

Na hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akasema:

“Wapo baadhi ya watu ambao baada ya kuingia katika Uislam bado wameendelea kubakia na mali iliyopatikana kwa njia zisizo halali. Na humo kulikuwa na mmoja ambaye kwa makusudi alianza kutoa sadaka kutoa mali hiyo isiyo halali. Na Allah swt alimzuia kufanya hivyo yaani sadaka haiwezi kutolewa isipokuwa kutokea mali iliyotokana kwa njia halali.”

5. Katika Ma’anil Akhbar Al Imam Hassan al-'Askari a.s. kwa kupitia sanad amenakili riwaya moja kutoka Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa amesema:

“Wale ambao wanajiona utukufu na wakubwa na ambao wanatenda matendo kwa mujibu wa nafsi zao, mfano wake ni wa yule mtu ambaye mimi nilisikia watu wakimsifu sana na kumheshimu sana, na hivyo mimi nikawa na shauku ya kutaka kuonana na mtu huyo lakini katika hali ambayo yeye hataweza kunitambua. Siku moja mimi nilimwona alikuwa amezingirwa na watu. Baada ya muda mchache kupita mimi nikamwona yeye ametoka humo na akawa anaondoka, basi mimi nilimfuata nyuma yake.

Tulipita katika duka la muuza mikate, huyo mtu kwa kuficha macho yake na kificho ficho akaiba mikate miwili. Kwa hakika mimi nilistaajabishwa mno, na nikadhani kuwa labda wao wana maelewano fulani kabla ya tukio hilo.

Tukaendelea mbele yeye akamghafilisha mfanya biashara huyo na akaiba makomamanga mawili humo. Na hapa pia nikafikiria kwa labda wao watakuwa na maelewano kama hayo kabla ya kutokea tukio hili, nikiwa hapo nikaingiwa na wazo kuwa je iwapo watakuwa na maelewano kama hayo basi kwa nini achomoe vitu kimafichoficho?

Basi mimi niliendelea kumfuata nyuma yake, tukafika njiani akamwona mtu mmoja mgonjwa basi huyo akasimama kwa mgonjwa huyo na akatoa ile mikate miwili na hayo makomamanga mawili, akampa huyo mgonjwa.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwuliza huyo mtu kulikuwa na dharura gani kwa kufanya hivyo. Mtu huyo kwa kuniona mimi akasema je wewe ni Ja’afar bin Muhammad ? Nami nikamjibu naam, basi yeye hapo akaanza kusema nasikitika sana kwa kutokujitambulisha kwako hapo kuja kukufikishia faida (kwa sababu Imam a.s. alikuwa hakujionyesha kuwa yeye ni Imam bali alikuwa amejiweka kama yeye ni mtu wa kawaida)

Imam a.s. akamwambia kwa hakika matendo yako hayo yana aibisha.

Basi yeye akasema kuwa Allah swt anasema katika Qur'an Tukufu Surah An A’Am, 6, Ayah 160:

Afanyae wema atalipwa mfano wake mara kumi. Na afanyae ubaya hatalipwa ila sawa nao tu. Na wao hawatadhulumiwa.

Ama kwa mujibu wa ayah ya Qur'an Tukufu mimi nimeiba mikate miwili hivyo nimetenda madhambi mawili na nimeiba makomamanga mawili hivyo nimetenda madhambi wawili na kwa ujumla nimetenda madhambi manne.

Na pale mimi nilipompa mgonjwa sadaka mimi kwa kila wema nimepata malipo kumi ya thawabu hivyo jumla nimepata malipo ya thawabu arobaini. Na kutoka arobaini ukitoa nne ninayo mema thelathini na sita bado.”

Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu:

“Mama yako akae kwenye kilio chako! Wewe kwa hakika umeitoa maana isivyo ya Ayah za Qur'an Tukufu. Je wewe huelewi ayah ya Qur'an Tukufu isemayo Surah Al Maida, 5, Ayah ya 30:

Basi nafsi yake ikampelekea kumuuwa nduguye, akamuuwa na akawa miongoni mwa wenye kukhasirika.

Kwa mujibu wa ayah hiyo wewe umeiba mikate miwili umetenda madhambi mawili na kwa kuiba makomamanga mawili umetenda madhambi mawili mengine na hivyo jumla umetenda madhambi manne, na pale ulipotoa hiyo mali yaani mikate na makomamanga, kama sadaka bila idhini ya mwenye mali basi umetenda madhambi mengine manne. Kwa hivyo umetenda madhambi nane kwa pamoja. Sasa wewe unafikiria mema hayo arobaini yametoka wapi?”

Kwa hakika mtu huyo aliduwaa, akimwangalia Imam a.s. na akajiondokea zake.

Baada ya hapo Imam a.s. akasema kwa kujitolea maana potofu ya ayah za Qur'an Tukufu vile isivyo sahihi ndio matokeo yake haya na vile vile kuwapotosha watu wengine pia.”

7. Katika tafsiri Ayyashi Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amenakiliwa akitoa tafsiri ya ayah Surah Al Baqarah, 2, ayah ya 267:

Enyi malio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa.

Imam a.s. akaelezea:

“Miongoni mwa watu kulikuwa kumelimbikwa mali iliyopatikana kwa riba na njia zingine zisizo za halali, basi wao walinuia kutoa sadaka humo, na ndipo Allah swt alipowakataza kufanya hivyo (kutoa sadaka kutoka mali iliyopatikana kwa njia za haramu hairuhusiwa).”

47. KULISHA CHAKULA NI SUNNAH.

1. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. ameripoti riwaya kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa amesema:

“Katika vitu vya kuleta uokovu mojawapo ni kuwalisha chakula wale wenye kuwa na shida na dhiki, na pili mtu awe ni mwanzilishi awe ni mwanzo wa kutoa salamu na vile vile wakati watu wamelala usingizi mtu anaamka kwa ajili ya kusali na kufanya ‘ibada.”

2. Muhammad Yakub amenakili kutoka ‘Ali bin Ibrahim ambaye naye amenakili kutoka Muhammad bin ‘Isa bin ‘Ubaid ambaye naye amenakili kutoka Ahmad bin Muhammad naye amenakili kutoka ibn Fazzal Ma’aruf naye kutokea Tha’alaba bin Maymun ambaye naye pia amenakili riwaya hiyo kutoka kwa Zararah, kuwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:

“Allah swt hupendezewa mno kulishwa chakula wale wenye dhiki na shida na njaa, na vile vile hupendezewa kutolewa kwa dhabihu (qurbani).”

3. Hisham bin Hakam amenakili riwaya kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Tendo lililo bora na la kipenzi mbele ya Allah swt ni kule kumlisha muumin mwenye njaa mpaka akashiba, ama kummalizia shida aliyonayo au kumlipia deni lake.”

4. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Siku moja waliletwa wafungwa ambao walikwisha kutolewa hukumu ya kuuawa mbele ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Basi ikatokea kwamba mmoja wa wafungwa hao alipoletwa mbele ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Malaika Jibrail a.s. akaja akamwambia Mtume :”Ewe Mtume wa Allah swt ! Huyu mtu adhabu yake iahirishwe kwa leo. Na wengine waliendelea kuletwa na hukumu zikapitishwa na hatimaye wakauawa. Na mwisho yule mtu aliporudishwa mbele ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na tena Malaika Jibrail a.s. akatokezea akamwambia:

“Ewe Mtume wa Allah swt ! Allah swt anakusalimia na huyu mtu huwa anawalisha wale wenye kuwa na shida, na mkarimu kwa wageni, mwenye kusubiri wakati wa shida na dhiki, anayechukulia majukumu na wajibu wa watu wengine kwa kuwasaidia.”

Basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwambia huyo mtu kuwa Malaika Jibrail a.s. amekuja na kumwambia habari hizo, na hivyo yeye alikuwa akimfanya yeye awe huru.

Kwa kujibu huyo mtu akasema:

“Je Allah swt, mola wako amependezewa na matendo yangu hayo?”

Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia, “Naam! Na kwa hakika mtu huyo papo hapo aliisoma Kalimah ya Shahada na akaukubalia Uislam na akawa Mwislam papo hapo; na akasama:

“Kwa kiapo cha Allah swt ambaye amekutuma wewe katika haki, mimi kamwe sijamrudisha mtu yeyote akiwa amehuzunika yaani bila kusaidiwa kutoka mali na miliki yangu.”

5. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anamnakili baba yake Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. kuwa amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:

“Kisu kinapita haraka sana katika shingo ya mnyama lakini kwa kasi zaidi ya kisu ni kile chakula anacholishwa yule mwenye kuhitaji na dhiki.(hivyo malipo yake ni kasi zaidi kwa Allah swt )”

48. MTOE SADAQAH KUTOKA VILE VITU MNAVYOVIPENDA SANA.

1. Al-Kuleyni anaandika riwaya kuwa Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. :

“Ilikuwa ni tabia yake kuwa alikuwa kila alipokuwa akikaa kula alikuwa ana beseni moja ambamo alikuwa akiweka kila aina chakula iliyokuwa mbele yake kidogo kidogo na alikuwa akitoa hukumu kuwa beseni hiyo ipelekwe kugawiwa kwa wenye shida na muhitaji. Na hapo akasoma ayah ya Qur'an Tukufu ifuatayo: Surah Al Balad, 90, ayah 11:

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

Na baadaye akasema Allah swt anaelewa wazi wazi kuwa katika uwezo wa kila mtu kumfanya huru mtumwa kwa hiyo na hivi ndivyo alivyofungua njia ya kumfikisha mtu hadi kuingia Jannat.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. katika Sadaka alizokuwa akitoa alikuwa akitoa sukari pia.

Kwa hivyo kulitokea mtu mmoja akamwuliza, Yabna Rasulallah! Kwa nini unatoa sukari? Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alijibu:

“Mimi ninapenda sana sukari, na ninapenda kuwa niwe nikitoa Sadaka kwa kile kitu ninachokipenda sana katika njia ya Allah swt.”

49. IMESISITIZWA MNO KUWANYWESHA MAJI WANAADAMU NA WANYAMA HATA KAMA HAPO KUTAKUWA NA MAJI MENGI MNO.

1. Al-Kuleyni amemnakili Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye naye amemnakili

Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. riwaya kuwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:

“Siku ya Qiyama tendo jema kabisa malipo yake watapewa wale watu ambao wamefanya wema katika kugawa maji.”

Riwaya hiyo hiyo Sheikh Sadduq a.s. ameielezea pia.

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Sadaka iliyo bora kabisa ni ile ya kuutuliza moyo unaowaka kwa kiu cha maji.”

3. Ali ibn Ibrahim amenakili riwaya kutoka kwa baba yake kuwa

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Pale panapokuwa na maji na mtu akatoa Sadaka ya kuwagawia watu maji basi Allah swt humjaalia thawabu za kumfanya huru mtumwa mmoja, na pale ambapo hakuna maji kabisa na mtu akatoa Sadaka ya kugawa maji basi Allah swt humhuisha mtu mmoja na kwa hakika mtu anayemhuisha mtu mmoja ni sawa sawa na kuhuisha ulimwengu mzima.”

Riwaya hii vile vile Sheikh as-Saduq ameinakili.

4. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema kuwa:

“Siku moja alikuja Mwarabu mmoja kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na kumwambia:

“Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.! Naomba unionyeshe tendo ambalo litaniingiza mimi peponi. Kwa kusikia hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema: Chukua Mashk (chombo cha kujazia maji iliyokuwa ikitumika katika zama hizo na ilikuwa ikitengenezwa kwa ngozi) na uwapelekee maji hayo familia ambayo ipo inateseka kwa kukosa maji na kiu kinawasumbua sana kiasi kwamba watakapo pata maji hayo watayanywa kwa haraka sana. Basi uelewe kuwa wewe utaipata Jannat kabla hata maji hayo hayajaisha au Mashk yako hiyo haijatoboka.”

5. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:

“Bila shaka, Allah swt anafurahishwa mno kwa kuona mtu anawanywesha maji wanaadamu au wanyama ambao kwa joto au kiu kali kabisa kinacho wasumbua hao na Allah swt siku ya Qiyama atamjaalia kivuli. Na kwa hakika hakutakuwa na kivuli kingine chochote isipokuwa kile kilichotolewa na Allah swt tu.”

6. Ibn Abbas anasema kuwa mtu mmoja katika kutaka kumhurumia Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema:

“Ewe Mtume wa Allah swt! Je ni tendo gani lile nifanye mimi ili niweze kuwa mustahiki wa kuingia Jannat?”

Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwambia:

“Nunua Mashk moja mpya na uwe ukiwanywesha watu maji kutoka humo, hadi Mashk yako hiyo itakapofika hatua ya kuja kutoboka (yaani itakapo chakaa au kuzeeka). Basi kwa tendo hili kwa hakika ndilo litakalo kufikisha wewe Jannat.”

7. Abu Hamza Thumali amenakili riwaya kutoka kwa Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. kuwa amesema:

“Yeyote yule atakaye mlisha na kumshibisha muumin ambaye ana njaa basi Allah swt siku ya Qiyama atamlisha matunda ya Jannat, na yeyote yule atakaye tuliza kiu cha muumin ambaye ana kiu basi Allah swt siku ya Qiyama atamnywesha maji ambayo yamepigwa lakiri. Na yeyote yule atakaye mvalisha mavazi nguo muumin ambaye kwa hakika ana shida basi Allah swt siku ya Qiyama atamvalisha mavazi kijani ya Jannat.”

50. NI SUNNAH KUWATENDEA MEMA WAUMIN NA KUWATIMIZIA MAHITAJI YAO KWA UWEZO ALIONAO MTU NA KUWA NA UHUSIANO MWEMA PAMOJA NA MASHIAH WENZAKE.

1. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amesema:

“Yeyote yule ambaye hakubahatika kutufanyia sisi wema basi ni wajibu wake kuwafanyia mema na kuwatimizia mahitaji ya marafiki zetu. Na yeyote yule ambaye hakubahatika kudhuru makaburi yetu basi adhuru makaburi ya wafuasi na marafiki zetu.”

2. Muhammad bin Ali bin Hussein Jamil amenakili riwaya moja kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa:

“Miongoni mwenu mtu aliye bora kabisa ni yule mwenye moyo mkarimu yaani mwenye moyo wa kutoa na mtu mwovu kabisa ni yule ambaye ni bahili. Na usafi wa imani dalili yake ni kwamba huwawia kwa wema muumin wenzake na kuwatimizia dharura na mahitajio yao. Bila shaka yeyote yule anayewafanyia hisani ndugu zake katika imani basi ndiye mpenzi wa Allah swt kwa sababu katika kufanya wema huko kuna mambo mengi yanayomzuia mtu asiingie katika mitego ya Sheitani na vile vile asiingie Jahannam, na kwa matokeo yake ndiye mtu anayeingia Jannat.”

Baada ya hapo Imam a.s. alimwambia Jamil, “Ewe Jamil! Habari hizi uwafikishie wenzako.

Kwa hayo mimi nikasema, “Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ! Niwe fidia juu yako. Je ni watu gani hao?”

Imam a.s. akasema: “Hao ni wale ambao wanawafanyia wema ndugu zao katika imani wakati wa shida huwa pamoja nao na vile vile wakati wa furaha pia huwa nao.”

3. Sheikh Sadduq a.s. amenakili riwaya kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye amesema kuwa:

“Yeyote yule ambaye hakupata fursa kufanya wema nasi, basi awafanyie wema wapenzi na wafuasi wetu basi atapata thawabu za kutufanyia wema sisi. Na vile vile ambaye hakubahatika kutuzuru sisi katika uhai wetu na uhai wake basi awazuru wapenzi na wafuasi wetu, basi atapata thawabu kama za kutuzuru sisi.”

4. Safwan Al-Jammal anasema kuwa siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimwambia Mu’alla bin Hunais:

“Ewe Mu’alla! Uwe wa Allah swt, ili Allah swt aweze kukutunza na kukuhifadhi.

Kwa hayo Mu’alla alianza kusema:

“Je hivyo inawezekanaje?”

Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamjibu, uwe na hofu ya Allah swt, uwe daima ukimwona yeye katika mawazo yako, kwa hiyo yeye atakifanaya kila kitu kiwe kikikuogopa wewe, na vile vile kitakuwa kikikuwazia wewe na kukujali wewe. Ewe Mu’alla ili kujipatia mapenzi ya Allah swt lazima uwatendee watu matendo mema, na utambue wazi wazi kuwa Allah swt anapendezewa sana na moyo wa ukarimu na huchukizwa sana na ubahili na huwa na uadui nao.

Angalia ! Wewe kama utaniomba chochote na mwisho wake wewe ukaaza kufanya mapenzi nami, na badala yake mimi nitafurahishwa sana iwapo wewe hautaniomba chochote na hautapata chochote kutoka kwangu na baada ya hayo wewe bado ukawa na mapenzi nami.

Na kwa hakika ukiniuliza mema yote naweza kuyafanya kwa ajili yako basi ukweli ni kwamba sifa zote ni za Allah swt kwa sababu yeye amekupitishia neema yake kwa mikono yangu mimi nimekuwa ni kipitishio tu kwa ajili yako kwa hiyo yeye ndiye anayestahiki sifa zote.”

5. Ali ibn Ibrahim anaandika katika tafsiri yake kuwa mtu mmoja alitokezea katika kikao cha Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. na humo akaanza kuwazungumzia matajiri na mara akaanza kuwasema vibaya na kuwatukana.

Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alimwambia, “Nyamaza!”

Wale mafukara ambao wanawajali ndugu na jamaa zao na kuwawia wema wenzao, Allah swt huwapa ujira mzuri sana, kwa sababu Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu: Surah Sabaa, 34, ayah 37:

Na si mali yenu wala watoto wenu watakao kukaribisheni kwetu muwe karibu, isipo kuwa aliye amini na akatenda mema. Hao basi watapata malipo maradufu kwa walio yafanya. Nao watakuwa salama katika maghorofa.

51. INARUHUSIWA KUTOA SADAQAH KATIKA HALI YA rUKU’U, BALI NI SUNNAH.

1. Sheikh Quleyni amenakili riwaya kutoka kwa Ahmad bin ‘Isa kuwa Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:

Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.

“Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa kwa neno ‘Innama’ inamaanisha kuwa katika kazi zenu au shughuli zenu zote, mwenye kuwa na haki zaidi kuliko yeyote juu ya nafsi zenu na mali zenu ni Allah swt, baada yake ni Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na baada yake ni, Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. na hadi kufikia Qiyama Maimamu a.s. kutokea kizazi chake.

Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:

Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.

Kisa katika ayah hii ni kwamba Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa akisali sala ya Dhuhuri, alipomalizia raka’a ya pili tu akatokezea mwombaji. Siku hiyo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa amevaa Khullah yenye thamani ya Dirham elfu moja ambayo alikuwa amepewa zawadi na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. Na Imam a.s. alipokuwa katika hali ya Ruku’u, kulitokezea maskini mmoja ambaye akasema, “Ewe Walii wa Allah swt na muumin halisi, iwe salamu juu yako, naomba unipe mimi maskini sadaka yoyote. Kwa hayo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. aliinamisha chini Hulla na kwa ishara akamwambia huyo maskini aichukue.”

Kwa tukio hili ndipo Allah swt alipoteremsha ayah hii kwa ajili yake na kwa ajili ya kizazi chake na kuonyesha fadhila na kufuzu kwao. Fadhila zao kuwa wanagawa sadaka hata kama watakuwa katika hali ya Rukuu.

Kwa hakika imekuja kujulikana kuwa yule maskini aliyekuja kuomba alikuwa si mtu bali alikuwa ni Malaika ambaye alikuja kuomba, na vile vile katika kizazi kizima cha Maimam a.s. pia tumeona mara nyingi sana Malaika huwa wanakuja kuomba katika sura ya maskini.

2. Katika kitabu kiitwacho Ihtijaj humo Tabarasi amenakili riwaya kutoka Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ameelezea kuhusu ayah hiyo kuwa:

“Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. katika hali ya sala akiwa katika Ruku’u alitimiza wajibu wake na akatoa Zaka na Allah swt ndipo alipoiteremsha hiyo ayah na makusudio yake yalikuwa ni kupata ridhaa ya Allah swt.”

3. Ali bin Ibrahim katika kitabu chake Tafsir ananakili riwaya kutoka kwa baba yake Ma’arifat Safwan kuwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amesema:

“Siku moja Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipokuwa amekaa pamoja na ‘Abdullah bin Salam kulikuwa na kikundi cha Mayahudi pia. Na wakati huo ikateremshwa ayah ya Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:

Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.

Baada ya hapo mara Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akatoka nje haraka na akaelekea msikitini na huko njiani alikutana na mwombaji mmoja na hivyo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alimwuliza:

“Je kuna mtu aliyeweza kukusaidia?”

Basi huyo mwombaji akasema,

“Naam, kuna mtu anayesali msikitini humo ndiye aliyenisaidia.”

Na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alivyoukaribia msikiti akamwona huyo mtu si mwingine bali ni Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.

Na riwaya hii vile vile imenakiliwa na Abu Hamza ambaye ameandika katika Tafsir Ayyashi.

4. Muhammad bin Ali bin Hussein katika kitabu cha Amali amenakili riwaya kutoka Abul Ja’rud Ma’rifat kuwa Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. amenakiliwa riwaya kuwa amezungumzia kuhusu ayah

Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:

Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.

Kama ifuatavyo:

“Katika Mayahudi ambaye mnafiki mmoja alipoukubalia Uislam akaanza kuiga:

“Ewe Mtume wa Allah swt! Je ni nani Wasii na Khalifa wako? Na nani huyo atakaye kuwa Walii baada yako?”

Ndipo hapo ayah hiyo ilipoteremshwa na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akawaambia inukeni, basi hao wote wakainuka na wakaanza kuelekea msikitini. Walipofika msikitini wakakutana na maskini mmoja akitoka nje na hivyo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akamwuuliza, “Je kuna mtu yeyote aliyekupa chochote ?” Huyo akasema “Kwa nini isiwe hivyo pete hii je niliyoipata?” Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema,”Je ni nani aliyekupa?”

Huyo mwombaji akasema “Huyo mtu ambaye bado anasali.”

Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. akasema

“Je alipokupa hiyo pete alikuwa katika hali gani?”

Huyo mwombaji akasema alikuwa katika hali ya Ruku’u. Na hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipopaaza sauti ya Takbira yaani Allahu Akbar na wale wote waliokuwepo pamoja naye nao pia walitoa Takbira kwa nguvu na sauti na hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ndipo alipowaambia wote:

“Mtambue wazi kuwa baada yangu Walii ni huyu Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. na wa si mwingine”

Karta anasema kuwa

“Kwa mujibu wa riwaya zilizopatikana kuwa katika sala moja aliitoa Hullah, na katika sala ya pili alitoa pete basi inadhihirika kuwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. anatoa sadaka katika hali ya sala zaidi ya mara moja ndivyo inavyothibitika kwa mujibu wa riwaya zinazopatikana.”

5. Ayyashi katika Tafsir yake ananakili riwaya moja kutokea kwa mwana wa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. kwa Ammar Yasir amesema:

“Siku moja Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alipokuwa akisali sala ya Sunnah aliahirisha tendo moja kiasi kwamba mpaka akavua pete yake kwa ajili ya kumpa aliyekuja kuomba. Na pale Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipokuja basi alimwelezea hivyo. Na wakati huwo iliteremshwaayah yake hadi kufikia :

Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:

Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.

Basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alitusomea ayah hiyo na akasema,

“Yeyote yule ambaye mimi ni Mawla wake basi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ni Mawla wake. Ewe Allah swt! Uwe na mapenzi na yule ambaye anawapenda wao, na uwe na uadui na yule ambaye anafanya uadui pamoja nao.”

52. KUGAWA NUSU YA MALI KATIKA SADAQAH NI SUNNAH.

1. Halabi anasema kuwa yeye alipomwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. basi Imam a.s. akamjibu:

“Naam kabisa! Al Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. aligawa nusu ya mali yake katika njia ya Allah swt – hadi kwamba nguo kwa nguo, Dinar kwa Dinar, alivigawa vyote katika njia ya Allah swt, na alikwenda Hija ishirini kwa kutembea na miguu.”

MWISHO.