Basi tunataraji nchi nyingine zitachukua mfano wa Morocco kwa kuimarisha ndoa ya Mut'a. Lakini jukumu hili zaidi linawakabili Waislamu wake kwa waume popote walipo kuisoma na kuitumia ndoa hii, kwa sababu ni Sharia ya Mwenyeezi Mngu na Mtume wake.
Mwenyeezi Mngu anasema:- Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyeezi Mngu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na khiyari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyeezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotovu uliowazi." 33:36.