rudi maktaba >Fiqh >Yaliyomo >

 

MAJIBU YETU

  • Riwaya hiyo ni ya Said bin Jubeir, ambae alikuwa akifanya Mut'a Makka na Ibnu Abbas pamoja na wafuasi wake walikuwa wakiiona Mut'a kuwani halali.
  • TAZAMA: Al'Musannaf J. 7 uk. 496

    Tafsirul Qurtubi J.5 uk. 133

    Al'Mughuniya Ibnu Quddama J. 7 uk. 571

  • Riwaya hiyo ni nyonge sana.
  • TAZAMA:

    Tahdhibut Tahdhibi J. 2 uk. 198.

  • Riwaya hiyo ndani yake mna Hajjaji bin Artat:-
  • "Amesema Ibnu Abdil Hakami, nimemsikia Shafii akisema:

    Amesema: Hajjaji bin Artat, Hautimii muruwa wa mtu (heshima) mpaka awache sala ya jamaa nikamwambia, Mwenyeezi Mngu na auondoe murua huu." Amesema Al'Asmai:- Mtu wa kwanza kupokea rushwa Basra katika ukadhini Hajjaji bin Artat."

    TAZAMA:

    Mizanul Itidali J. 1 uk. 459

    Sasa, tuache hadithi zilizothibiti, tushike ya mtu, Ambae anaona ni murua kuacha sala ya jamaa? Mtu ambae ndiye kadhi wa kwanza kula rushwa Basra? Hadithi hiyo haina mashiko tupa nje. La ajabu zaidi hapa ni kwamba, japo baadhi ya Masheikh wao wanaharamisha ndoa ya Mut'a, lakini wanaruhusu kujipuli!! Na baadhi ya masheikh wao wamejawizisha Hadaa, kumuowa mwanamke ukinuia utamwacha baada ya muda fulani kufika bila ya yeye kujua!! Fat'wa hii ni ya lbnu Taymiyya.

    TAZAMA:

    Majmu'u Fatawa Ibnu Taymiyya J.32/147.

    Fat'wa ya kujipuli, angalia vitabu:- Alhalalu Walharamu uk. 161

    Sublus Sallami J. 3 uk. 974.

    Na vingine vingi katika wanazuoni wa Kihanafi na Hanbali waweza kuyapata hayo ya kujawizisha Ponyeto (Kujipuli)