Imepokewa kwa Jaabir Bin Abdullah Al'Ansar amesema:-
"Sisi tulikuwa tukifanya Mut'a wakati wa Mtume S.A.W. na wakati wa Abubakar na nusu katika utawala wa Umar, kisha akaikataza Umar."
Fat'hul Bari J. 11 uk. 76
Umdatul Qary J. 8 uk. 310
Sharhu Sahihi Muslim J. 8 uk. 233
Musnadu Ahmad J. 3 uk. 380
Bidayatul Mujtahid J. 2 uk. 58
Zadul Maad J. 1 uk. 208 - 209.
Sheikh Muhammad Sharif yeye anasema "ILIKUWAKO" si sawa na "IKO MPAKA LEO" Basi jambo gani lililofanya Shia waamini iko mpaka leo? Ni sababu nne:
Tafsirul Kabir 3.3 uk. 200
Musnad Ahmad J.1 uk. 52
AI'Mughuniya ya Ibnu Quddama J. 7 uk. 572
Sheikh Muhammad Sharif anashangaa, vipi sahaba walimwogopa Umar, wakanyamaza wasimpinge?
Jawabu:- Hakuogopewa. Wako waliompinga kwa vitendo, wakaendelea kuoa na kuolewa Mut'a bila kujali maneno yake. Katika waliompinga Umar ni:-
Haya utayapata katika vitabu hivi:-
Kama ambavyo masunni wote wamempuuza Umar bunul Khattab, katika Tamattu'u ya Hija wanaendelea bila kujali kelele zake. Tazama vitabu vyao (Masunni) vya Fiq'h katika mlango:- AINA ZA KUHIRIMIA wamegawanya aina tatu:- QIRAN, TAMATU'U, (ambayo Umar bunul Khattab ameipiga marfuku) na IFRAD. Wanazuoni wote wa kisunni wamekubaliana waendelee nazo, licha ya kukataza Umar Tamattu'u ya Hija.
Na hata kama walinyamaza, ni aibu? Kwani hawakunyamaza?
Fiq'hus Sunna J. 2 uk. 231
Kwa hiyo katika zama za Mtume S.A.W. mtu akiacha talaka tatu mara moja huhesabiwa ni talaka moja tu, kwa mujibu wa hukumu ya Mtume S.A.W. Mwenyeezi Mngu anasema:- "Haiwi wa mwanamume aliyeamini wala mwanamke aliyeamini, Mwenyeezi Mngu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao." 33:36. Ulipofika utawala wa Umar bunul Khattab yeye akaamuru talaka tatu ni tatu kinyume na amri ya Mtume!!
Mtume hakuleta sala ya taraweh iia wala haikuwako katika zama za Abu Bakar. Katika sala za jamaa za sunna aIizofundisha Mtukufu Mtume S.A.W. taraweh haimo, bali huo ni uzushi wa Umar bunul Khattab.
At'Tabaqatul Kubra J. 3 uk. 281
AI'MiIaI Wannihal J. 1 uk. 78
Sheikh Muhammad Sharif anakataa kuwa Umar ndiye aliyekataza Mut'a yeye anasema:-
Ilivyo ni kwamba: Sayyidna Umar alipanda katika mimbari akasema:- "Kwa nini watu wanaowa hii Mut'a na hali Mtume amaeikataza; sikilizeni mimi sitaletewa yeyote aliyeowa ndoa hiyo isipokuwa nitampopoa mawe." Hivyo ndivyo anavyosema Sheikh Muhammad Sharif.
Jawabu:- Hilo halikubaliki, kwa sababu mategemeo ya hadithi hiyo ni mabovu kabisa.
Mizanul Itidali J. 4 uk. 184
Lisanul Mizani J. 6 uk. 95
Sasa, vipi utalinganisha hadithi hiyo na zile tulizokwisha zitaja?!!. Kwa hiyo riwaya hiyo haina mashiko tupa nje. Sasa, tuje kwa Ibnu Abbas:- Sheikh Muhammad amesema hivi:- Ibnu Abbas mwenyewe alipokwenda akaulizwa na masahaba kwamba: Ewe Ibnu Abbas Fat'wa yako imefika mbali, watu wametunga mashairi, akasema:- "LA ILAHA ILLALLAH, ASTAGH'FIRULLA INNAMA HIYA KAL'MAYTAT" Hivyo ndiyo alivyosema Sheikh Muhammad, na sisi tunamwambia kuwa maneno ya Ibnu Abbas yalikuwa hivi:- INNA LILLAHI WAINNA ILAYHI RAJIUN WALLAHI MA BIHADHA AFTAYTU WALA HADHA ARADTU WALA AH'LALTU MIN'HA ILLA MA AHALLALLAHU MINAL MAYTATI WADDAMI WALAHMIL KHINZIR".
Maana yake, "Sisi ni wa Mwenyeezi Mngu na sisi tutarejea kwake, Wallahi haya sikuyatolea fat'wa na wala sikuyataka. Na sikuihalalisha ila vile alivyohalalisha Mwenyeezi Mngu katika nyamafu na damu na nyama ya nguruwe."