rudi maktaba > Fiqh > Yaliyomo >
SUNNA ZA KUMWOSHA MAITI
- Awekwe mahala palipo juu, kama kitanda, au baraza n.k. na mahala pa kuwekea kichwa chake painuke zaidi kuliko miguu.
- Alazwe chali, miguu na nyayo zielekee Qibla (kama tulivyotaja katika mambo ya hali ya 'IHTIDHARI'.
- Maiti avuliwe nguo zote kwa upande wa chini (miguuni) hata ikibidi itatuliwe (ichanwe) lakini kwa idhini ya warithi wa maiti.
- Aoshwe chini ya sakafu, au banda au hema asioshwe chini ya mbingu.
- Uchimbwe "UFUO" wa kuingia maji ya kuoshea.
- Mwili wake wote uwe wazi isipokuwa utupu wake.
- Ufunikwe utupu wake hata ikiwa mkoshaji au watu wanaomuosha ni miongoni mwa wale wanaoruhusiwa kumwangalia.
- Mkoshaji apitishe mkono wake juu ya tumbo la maiti kwa taratibu lakini ikiwa maiti mwenye mimba ambaye mtoto pia amekufa tumboni hairuhusiwi kufanya hivyo.
- Mkoshaji asimame upande wa kulia wa maiti.
- Aanze kuosha upande wa kulia wa kichwa cha maiti.
- Mkoshaji aoshe mikono yake mara tatu hadi begani kwa kila 'GHUSLI' tatu.
- Mwoshaji anapokuwa anaosha kiwiliwili cha maiti anatakiwa aseme hivi: "Ewe Mola! Hiki ni kiwiliwili cha mja wako mwenye imani (Mumin) na umetoa roho yake kutoka kiwiliwili chake, na umetenga kati yao, basi msamehe kwako." Hasa wakati anapomgeuza.
- Asitangaze mwoshaji aibu yoyote aliyoiona mwini mwa maiti.