rudi maktaba > Fiqh > Yaliyomo >

HADHARI MUHIMU

Akiwa maiti ni mwanamke, basi katika Talkini pale mwanzo atasema, "IS MA-IY IF-HA-MIY YAA" jina la mwanamke (maiti) huyo na baba yake na kama halijui atasema, "YAA AMATAL-LAAH;" tena ataendelea na hiyo Talkini kwa kusema, "HAL AN-TI ALAL AH-DIL LADHIY FAA-RIQ- TINAA".

Tena ataendelea vivyo hivyo mpaka atakapofika sehemu ya pili baada ya kutaja jina la maiti na baba, au kusema, "YAA AMA-TAL-LAAH". Tena ataendelea kusema: "IDHAA ATAA-KIL MA- LA-KAA-NI AL-MUQAR RABAANI RASUU-LAY-NI MIN INDIL-LAAHI TABAA RAKA WATA-AA-LA, WA SA-A-LAAKI ANRAB BIKI WA ANABIY-YIKI WA AN DIYNI-KI WA AN KITAA-BIKI WA AN QIB LATI-KI WA AN AIM MATIKI FALAA TA-KHAA-FIY-WA QUU-LIY".

Baadaye utaendelea vivyo hivyo hadi kufika kwenye, neno la "THUM-MA" litafuata NA la "IE-LA-MIY YAA" (kutaja jina lake na la baba yake YAA AMATAL-LAAH, tena utaendelea hadi kufika kwenye neno la AFA-HIM-TI (Jina na baba) au YAA AMATAL LAAH; utasema "THAB-BATA-KIL LAA-HU BIL QAWLI-TH THAA BITI WA HADAAKIL-LAA-HU ILAA SIRAA-TIM-MUS- TAQIYM AR-RAFAL-LAA-HU BAY NAKI WA BAY-NA AW LI-YAAIKI"; endelea na baadaye sema, "AL LAA HUMMA JAA-FIL AR DHA AN JAN BAY-HAA, WAS AD BIRUUHI HAA, ILAYK WA LAQ-QIHAA MIN-KA BUR HAA-ALLAA HUMMA AF-WAKA AF-WAKA".