rudi maktaba > Fiqh > Yaliyomo >

Mambo Yanayomhusu Maiti

Kimetungwa na : Sayyid Muhammad Mahdi al-Musawy al-Shushtari

DIBAJI

Namshukuru Mwenyezi Mungu. Ule waadi niliotoa katika gazeti letu la "Sauti Ya Bilal", la mwezi Sept. 1974, toleo Ia No. 5, nilisema, nitaandika kitabu kizima kuhusu mambo anayofanyiwa Maiti kwa kirefu Inshallah, Alhamdulillah Mwenyezi Mungu kwa baraka ya Muhammad na Aali zake watakatifu [s] kautimiza kwa kunipa tawfiki ya kuchapisha kitabu hiki.

Kwa kuwa wafuasi wa madhehebu ya Ahlul Bait [a] ambayo hujulikana kwa jina la "Shia Ithnaashariya", makao humu Afrika ya Mashariki (East Africa) ambao wanatumia zaidi Lugha ya Kiswahili, na mpaka hivi sasa kitabu chenye kueleza mambo anayofanyiwa Maiti kwa wajibu ya Madbehebu ya Shia Ithnaashariya hakikuwepo, imetubidi kutayarisha kitabu hicho ili Waislamu Shia waweze kufuata wakati wanapohitajia. Wabillahi At-tawfiq Wassalatu Wassalamu Alaa Muhammadin Wa Aa'lihi At-tahirin.

Al Ahqar Muhammad Mahdi Al -Muusawy
Mwezi mosi R. Awwal (mfungo sita, 1396)
3rd MARCH, 1976