rudi maktaba > Fiqh > Yaliyomo >
JOHARI ZA HEKIMA
Mambo manna ni mema, lakini manne ni bora zaidi kuyashinda,
- Haya ni njema kwa waume lakini kwa wanawake ni bora zaidi;
- Uadilifu kwa kila mmojo ni mwema lakini kwa viongozi (watawala) ni bora zaidi;
- Mzee kutubu madhambi ni vyema lakini kwa kijana ni bora zaidi;
- Ukarimu kwa matajiri ni mwema lakini kwa maskini ni bora zaidi.
(AL HAKIIM)
Mambo manne ni maovu, lakini manne mabaya zaidi kuyashinda.
- Kutenda dhambi kwa kijana ni kuovu, lakini kwa mzee ni kubaya zaidi;
- Mjinga kujishughulisha na Dunia ni kuovu, lakini kwa mwanachuo ni kubaya zaidi;
- Watu kutojishughulisha na ibada na kuwa wavivu ni kuovu, lakini kwa waalim na wanafunzi wa dini ni kubaya zaidi;
- Tajiri kujigamba na kujinaki ni kubaya; na kwa maskini ni kubaya zaidi.
(AL HAKIIM)