Waislamu kote ulimwenguni hufunga mwezi ambao ni mwema kuliko miezi yote, ulio na masiku bora kuliko masiku yote, wenye masaa ya baraka kuliko masaayote na amali zifanyikazo katika mwezi huo ni makbuli kuliko baki ya maombi. Nao ni mwezi wa Ramadhani.
Mwezi huu wa Ramadhani ambao ni mwezi wa tisa wa miezi wa Kiislamu, ni mwezi wa pekee wa aina yake kwa utukufu. Ni mwezi wa kusameheana, kuombeana heri na hata kufanya ibada kwa wingi na kwa usahali kabisa.
Mwezi huu una matukio mbali mbali ya kihistoria ambayo hayatasahaulika, na ambayo vile vile hupambanua wazi utukufu wake.
Imam Ja'far Assadiq alisema kutoka kwa Babuye, (Mtume s.a.w.) "Taurati ilishuka na kumfikia Nabii Musa (a.s.) tarehe 6 Ramadhani, nayo Injili iIiteremshiwa Nabii Isa (a.s.) tarehe 12 za Ramadhani, kadhalika Zaburi ya Nabii Daud (a.s.) iliteremshwa mnamo tarehe 18 za Ramadhani, vile vile Qur'ani Takatifu iliteremka katika usiku wa Lailatul Qadri ambao kwa kawaida huwa katika mwezi huu wa Ramadhani."
Bila shaka hiyo ni heshima kuu kabisa. Na umejionea mwenyewe, hakuna kitabu kati ya vitabu vitukufu vinne kutoka kwa Mungu kilicheshuka ila kilishuka mwezi huu wa Ramadhani, na hayo yote ni kuonyesha utukufu wa mwezi huu. Kwa hivyo lazima vitendo vyetu katika mwezi huu viwe vitukufu kama mwezi wenyewe ulivyo.
Na katika Historia, tunasimuliwa baadhi ya matulio ya mwezi huu huu wa Ramadhani, kwa mfano:
Alipigwa upanga msikitini huko Kufa, Iraq alipokuwa amekwenda kusali sala ya Alfajiri, na alifariki siku ya tatu yake, yaani tarehe 21 Ramadhani.
Sayyidna Ali, Simba wa Mungu alishirikiana sana na Mtume (s.a.w.) na kuhudhuria vita vyote pasina kukimbia na ndiye aliyebaki kitandani cha Mtume alipokuwa akihamia Madina.