Sala ya ayaat ina rakaa mbili, na kila rakaa ina rukuu tano, na namna yake ni kama ifuatavyo:
Kwanza utanuwia na kutoa takbira na kusoma suratul faatiha –yaani- al hamdu na sura nyingineyo kamili, kisha utarukuu na utakapo inuka kutoka kwenye rukuu utasoma suratul faatiha na sura nyingine kamili, kisha utarukuu na utainuka kutoka kwenye rukuu na utasoma tena al hamdu na sura nyingine na utafanya hivyo hadi zifike rukuu tano, na utakapo maliza rakaa ya tano na kuinuka, utasujudu mara mbili kama ufanyavyo katika sala za faradhi za kila siku, kisha utasimama kwa ajili ya rakaa ya pili.na utafanya kama ulivyo fanya katika rakaa ya kwanza, na ukimaliza utasoma tashahhudi kamaufanyavyo katika sala zingine.
Na inajuzu kusoma tu suratul faatiha mara moja na kusoma baada ya suratul fatiha aya kadhaa katika sura nyingine kwa sharti kwamba isiwe chini ya aya moja ikiwa si jumla iliyo kamili kwa kauli ya ahwat, kisha utarukuu naukiinuka kutoka kwenye rukuu utasoma kipande kingine cha sura hiyo kwa kuanzia sehemu ulipo ishia kisha utarukuu, na utafanya hivyo na kuikamilisha surahiyo katika rakaa ya nne kisha utarukuu, na utafanya hivyo hivyo katika rakaa ya pili.
Na inajuzu kutenganisha kwa kusali rakaa ya kwanza kwa utaratibu huu ulio tangulia, na katika rakaa ya pili kutumia utaratibu huu au kinyume chake, na kuna namna nyingine ya kuisali sala hii lakini hakuna haja ya kuielezea.
Mas’ala: Ni sunna kusoma kunuut katika sala ya ayaat kabla ya rukuu ya pili, rukuu ya nne, rukuu ya sita, rukuu ya nane na rukuu ya kumi, na inajuzu kutosheka kwa kunuut moja kabla ya rukuu ya kumi.
Mas’ala: kauli ya ahwat inasema kuwa haitoshelezi kusoma bismillahi baada ya al hamdu katika sala ya ayaat kama tulivyo eleza hapo kabla.
Mas’ala: Ina juzu kuisali sala ya ayaat kwa sura ya jamaa, kama ambavyo inajuzu kuisali mtu mmoja mmoja, lakini ikiwa hakuweza kumdiriki imam katika rukuu ya kwanza katika rakaa ya mwanzo au rakaa ya pili ataisali peke yake.
Mas’ala: Mambo yote tuliyo yataja katika sala za kila siku kama masharti ya sala na mambo yabatilishayo sala na hukumu za shaka na sahau hutumika katika sala ya ayaat.
Mas’ala: Ikiwa mtu atatia shaka kuhusiana na idadi ya rakaa katika sala ya ayaat na hakuweza kuipa uzito idadi fulani kati ya pande mbili hizo sala yake itabatilika, na ikiwa atatia shaka katika idadi ya rakaa, hata zitilia maanani ikiwa ni baada ya kuvuka sehemu hiyo ama ikiwa bado hajavuka sehemu hiyo atajengee katika idadi ndogo na ataitekeleza sehemu aliyo itilia shaka.
Mas’a’la: Ikiwa mtu atafahamu ya kuwa jua au mwezi vimepatwa, na hakusali sala ya ayaat kwa kuasi au kwa kusahau hadi kupatwa huko kuka ondoka, ni wajibu wake kulipa sala hiyo, na hakuna tofauti kati ya kupatwa jua lote au nusu yake, na kauli ya ahwat ya wajibu ni kuwa inabidi kuoga kabla ya kuilipa ikiwa lilipatwa lote, na ikiwa hakuisali kwa kuasi, na ikiwa hakufahamu ya kuwa jua au mwezi ulipatwa hadi kupatwa huko kukatoweka , ikiwa kupatwa huko kwa jua au kupatwa kwa mwezi ilikuwa ni lote kiasi kwamba jua lote au mwezi wote ulipatwa, hapo itawajibika kuilipa la sivyo haitakuwa wajibu, na kauli ya ahwatul awlaa inasema kuwa inabidi kuilipa sala ya ayaat hata katika matukio mengine tofauti na kupatwa kwa jua au mwezi na sawa awe amefahamu kutokea kwa tukio hilo wakati lilipo tokea au hakufahamu.
Mas’ala: Haijuzu kwa mwenye hedhi na mwenye nifasi kusali sala ya ayaat na kauli ya ahwatul awlaa ni kuwa atailipa baada ya kuwa twahara.
Mas’ala: Ikiwa mukallaf anajukumu la kusali sala ya ayaat na faradhi ya kila siku, anahiyari ya kuitanguliza yoyote ile aitakayo, ikiwa wakati utakuwa ni mpana wa kuweza kuzitekeleza sala hizo, ama ikiwa wakati uliopo unatosha kwa sala moja wapo na usitoshe kwa nyingine ataitanguliza ile ambayo wakati wake umekuwa finyu zaidi.
Kisha ataitekeleza ile ambayo wakati wake ni mpana, na ikiwa wakati wa sala zote mbili umekuwa finyu ataitanguliza sala ya kila siku, na ikiwa ataitakidi ya kuwa wakati wa sala ya ayaat ni mpana na akaanza kusali sala za kila siku, kisha ikabainika kuwa wakati was ala hiyo ni finyu, ataikata sala hiyo ya kila siku na atasali sala ya ayaat, ama ikiwa ataitakidi ya kuwa wakati wa sala ya kila siku ni mpana na akaanza kuisali sala ya ayaat kisha ikabainika ya kuwa wakati wa sala ya kila siku ni finyu, ataikata na kusali sala ya kila siku, na atarudi kuisali sala ya ayaat kwa kuanzia sehemu alipo ikatia ikiwa halikutokea tendo libatilishalo sala na ambalo haliitenganishi na sala ya kila siku.