GHUSLI(Kuoga)

MAMBO YAWAJIBISHAYO GHUSLI.

Mambo yamuwajibishayo mtu kuoga ni sita:

1-Janaba.

2- Hedhi. 

3- Nifasi.

4- Istihadha.

5- Kumgusa maiti.

6- Kifo.

GHUSLI YA JANABA. (Kuoga janaba)

Ina thibitika janaba kwa mambo mawili:  1- kutokwa na manii katika sehemu za siri kama ilivyo zoweleka, na sehemu nyingine yoyote ikiwa utokaji huo ni wa kawaida, ama ikiwa si utokaji wa kawaida kutakuwa na ish’kaali, na umaji maji utokao  katika sehemu hizo baada ya manii na kabla ya kufanya istibraa ya mkojo hukumu yake ni sawa na janaba.

2- kukutana kijinsia kati ya mwanamke na mwanaume, hata kama hawakutoa manii,  na maingiliano hayo yawe ni sehemu ya mbele au ya nyuma, na kufanya hivyo kunamfanya mtu awe na janaba awe mwanamke au mwanamume, na ihtiyaati  inasema kuwa  yeyote atakae ingiliwa hata kama si mwanamke  itakuwa ni juu ya  wote wawili  muingiliaji na muingiliwaji kuoga janaba.

Mas’ala:   Inawajibika  kuoga janaba kwa ajili ya mambo manne: 1- Wakati wa sala ya wajibu isipokuwa sala ya maiti ( kumsallia maiti). 2- Sehemu za sala zilizo sahaulika, vile vile sala ya ihtiyaat,  na katika sijda ya sahau, si lazima kuwa na twahara japokuwa ni ahwat kuwa na twahara. 3-  Twawafu ya wajibu  hata kama itakuwa ni sehemu ya hajji ya wajibu au umra ya sunna.  4-  funga, na ufafanuzi wake utafatia.

Mas’ala:  Ni haramu kwa mwenye janaba mambo yafuatayo:  1-  Kugusa jina   tukufu la Mwenyezi Mungu  na majina yake mengine matukufu, pia  sifa  zake maalum kwa kauli iliyo ahwat, na kauli ya ahwat ni kuwa majina ya maasumiin pia.  2- Kugusa maandishi ya Qur’ani.  3- kuingia msikitini hata kama ni kwa kuchukua kitu msikitini,  ndio,  si haramu kuvuka msikitini kwa kuingilia mlango mmoja na kutokea mlango mwingine na kadhalika.  

4- kukaa msikitini.  5- kuweka kitu msikitini  hata kama ni katika hali ya kukatiza msikitini au kukiweka kwa kutokea nje.  6-  kuingia katika msikiti mtukufu wa makka na msikiti wa mtume (s.a.w) hata kama ni katika hali ya kukatiza. 7-  Kusoma sura moja wapo kati ya sura nne za azaaim,  nazo ni aya  ambazo pindi zisomwapo huwajibika kusujudu sijda ya wajibu,  na kauli ya ahwatul awlaa ni kuwa haipaswi kusoma aya yoyote katika sura za azaaim ambazo  kuna  aya ya sajda ya wajibu nazo ni (alifu laam tanziil, Haamim sajda, Suratun najm, na suratul alaq)

Mas’ala:  Sehemu za makaburi ya maasumiin huambatanishwa na hukumu za misikiti kwa kauli ya ahwat na haiunganishwi na hukumu hiyo  arwaqatiha…….- ikiwa haija thibiti ya kuwa ni msikiti kama ilivyo thibiti kwa baadhi- kama ambavyo

 haviunganishwina hukumu hii viwanja vya sehemu hizo tukufu  japo kuwa kauli iliyo ahwat inasema ni vema kuziunganisha sehemu hizo na hukumu hizo.

     NAMNA YA KUFANYA GHUSLI.

Mas’ala:  kuna aina mbili za uogaji: 1- Uogaji wa kupiga mbizi. 2- Uopgaji wa utaratibu.

!- Uogaji wa kupiga mbizi nao una aina mbili: !- Kupiga mbiozi kwa mara moja  na  kupiga mbizi kwa taratibu.

Na aina ya kwanza ni kuuzamisha  mwili  wote kwenye  maji na kufunikwa sehemu zote,  na kitendo hicho hufanyika kwa mara moja na huzingatiwa kuwa kuzama ndani ya maji taratibu ni utangulizi wa ghusli hiyo.

Na aina ya pili ni kuuzamisha mwili katika maji kidogo kidogo pamoja  na kuhakikisha kuwa mwili wote unazama  kama kawaida,  kwa hivyo basi kuzamisha kiungo kimoja kimoja inakuwa ni sehemu ya ghusli na sio utangulizi wake kama ilivyo katika aina ya kwanza na kauli ya adh’har  ni kuwa aina ya pili ni sahihi kama ilivyo kuwa ya kwanza.

Na katika sehemu ya pili huzingatiwa  kuwa kila kiungo cha mwili  kiwe nje ya maji kabla ya kukizamisha kwenye maji kwa makusudio ya kuoga, na katika sehemu ya kwanza inatosha tu  mwili wote au baadhi kuwa nje ya maji kisha ukavizamisha ndani ya maji kwa makusudio ya kuviosha.

2- Uogaji wa utaratibu:  na kauli ya ahwat ya wajibu kuhusiana na namna yake  ni kuwa,  kwanza ataosha kichwa chote na shingo,  kisha sehemu ya mwili iliyo bakia,  kama ambavyo  ni ahwat   kuosha  nusu ya upande wa kulia  kwanza, kisha nusu ya upande wa kushoto, japo kuwa kauli iliyo adh;har  ni kuwa hakuna utaratibu katika kuosha pande hizi mbili kwani inajuzu kuziosha kwa pamoja au kwa aina yoyote ilie nyingineyo.

Ni wajibu katika kuosha kila upande au kiungo kuchukua sehemu kidogo ya upande au kiungo kingine, sehemu ambayo inaungana  nayo, ikiwa hutafahamu mpaka wa sehemu ya wajibu isipo kuwa kwa kufanya hivyo.

Mas’ala:  Kauli ya ahwat  ya wajibu ni kuwa  ghusli  ya taratibu haithibiti kwa kukitingisha kichwa au shingo  kisha pande mbili  kwa lengo la kufanya ghusli- ikiwa kiwili wili chote kimo ndani ya maji- vile vile kuvitikisa baadhi ya viungo vikiwa ndani ya maji kwa lengo la kufanya ghusli, na pia wamesema  kuwa ghusli ya kupiga mbizi itathibiti  mara moja kwa kukitikisa kiwili wili kikiwa ndani ya maji kwa lengo la kufanya ghusli.

 Lakini hukumu hii ina ish’kaali na kauli ya ahwat ni kuwa haita tosheleza kufanya hivyo , ndio ikiwa ata piga mbizi na maji yakawa haya kuenea sehemu zote za kiwili wili  chake na akanuwia  ghusli ya kupiga mbizi kwa sehemu iliyo bakia  ambapo  nia hiyo ikawa sambamba na kufika maji kwenye sehemu hizo au ikiwa aliweka nia na kukusudia  kufanya ghusli mwanzoni mwa kupiga mbizi hadi wakati wa kuenea maji sehemu yote ya mwili  wake, katika kusihi kwake kuna kauli.

     MASHARTI YA KUFANYA GHUSLI.

Huzingatiwa katika ghusli masharti yote yazingatiwayo  katika udhu, isipo kuwa ni kwamba  ghusli inatofautiana na udhu katika sehemu mbili:  1-katika ghusli haizingatiwi kuwa  kiwili wili  kioshwe kutokea juu kwenda chini na limeelezwa hilo katika udhu kwa upana.    2-  Kufuatanisha  hakuzingatiwi katika ghusli  bali huzingatiwa katika udhu.

Mas’ala: Ghusli ya janaba hutosheleza katika udhu, na kauli iliyo wazi ni kuwa  hukumu hiyo huzihusu hata ghusli zinginezo za wajibu  au zele zilizo thibiti kuwa ni sunna pia, isipo kuwa ghusli ya istihadha mutawassit (ya kati) kwani ni lazima kutawadha baada ya kuoga- kama tutakavyo eleza hapo baadae- na kauli ya ahwat na iliyo awlaa ni kuwa  ni bora kutawadha  katika ghusli zingine pia- tofauti na ghusli ya janaba- kwa kutawadha kabla yake.

Mas’ala: Ikiwa mukallaf  (anae takiwa kutekeleza hukumu za sheri) anazo ghusli za aina tofauti kama ghusli ya janaba,  ghusli ya siku ya ijumaa,  ghusli ya Hedhi, na mengineyo  itajuzu kwake kufanya ghusli moja  kwa lengo la ghusli zote na hiyo inatosheleza katika ghusli zilizo bakia, kama ambavyo ina juzu kunuwia  ghusli ya janaba tu,  na ghusli ya janaba inatosheleza katika ghusli zilizo bakia,  ama ikiwa atanuwia ghusli nyingine tofauti na ghusli ya janaba  hakuna shaka kuwa ghusli hiyo itatosheleza tu kwa  ghusli aliyo  inuwia, ama ghusli hiyo kutosheleza katika ghusli zingine  kuna ishkaali na kauli iliyo adh’har ni kuwa itatosheleza,  ndio  katika kutosheleza  ghusli yoyote kwa  ghusli ya siku ya ijuma kuna ishkaali, ikiwa hakukusudia ghusli hiyo lau kwa sura ya ujumla,.

 kisha yaliyo tajwa ya kuwa inatosheleza ghusli moja katika  ghusli kadhaa  hukumu hiyo itatumika katika ghusli zote za wajibu  na sunna- ghusli za sehemu fulani au wakati fulani au kwa ajili ya lengo lingine- lakini kutumika hukumu hiyo katika ghusli zingine zilizo amrishwa kwa sababu ya kufanya  vitendo kadhaa- kama kumgusa maiti baada ya kumuosha – pamoja na sababu  nyingi hapo kutakuwa na ish’kali.

Mas’ala: Ikiwa mtu  atatokwa na hadathi ndogo wakati akioga au katikati ya ghusli ya janaba itambidi kuikamilisha ghusli hiyo, na kauli ya ahwati ni kuwa itambidi  wakati huo kutawadha baada ya ghusli, na hapo anayo hiari ya kubadilisha kwa kutumia ghusli ya kupiga mbizi badala ya ghusli ya utaratibu au kinyume chake  na wakati huo hakuna haja ya kutawadha  bila ya ishkali yoyote.

Mas’ala: Ikiwa atatia shaka  ya kuwa ameoga ghusli ya janaba au hapana, atajengea ya kuwa hakuoga, na ikiwa atatia shaka ya kuwa ameoga au hapana baada ya kumaliza kusali haitamlazimu kuirudia sala hiyo-isipokuwa sala hiyo ikiwa ni ya wakati maalum na shaka hiyo  ikatokea katika wakati wa sala hiyo na kisha akatokwa na hadathi ndogo baada ya sala, kauli ya ahwat inasema ni vema kuirudia wakati huo- na ni wajibu juu yake kuoga kwa kila kitendo ambacho kukitenda kwake ni sharti kuwa na twahara katika kuswihi kwake, au kujuzu kwake ni lazima uwe na twahara ya hadathi kubwa, bila kutofautisha  kati ya sala au laa hata kama ni kugusa  maandishi ya Qur’an, na ghusli hili lina weza kufanyika kwa aina mbili:

     Kwanza awe na yakini ya kuwa  ameamrishwakufanya ghusli hiyo na amri hiyo ima ni ya wajibu au sunna- kama  vile akikusudia kuoga ghusli ya ijumaa ua ghusli ya janaba  kwa mara nyingine baada ya sala  na wakati huo ni juu yake kutosheka na ghusli hiyo katika kufanya kila kitendo kinacho hitaji twahara katika kutekelezwa kwake sawa awe ametokwa na hadathi ndogo au laa.

 Pili: Iwe kinyume na hivyo kwa mfano kufanya ghusli hiyo kutokane na ihtimali au kuwe na ihtimali ya kuwa huenda janaba ilibakia, janaba  ambayo ameitiliashaka ya kuwa ameoga janaba hiyo  kabla ya sala au laa, na wakati huo atatosheka na   ghusli hiyo katika kutekeleza kitendo ambacho kutekelezwa kwake ni sharti kuwa na twahara kutokana na hadathi kubwa tu, kama kujuzu kukaaa msikitini,  ama matendo ambayo ni sharti kuwa na twahara katika kuyatekeleza kwake hata kama ni kutokana na hadathi ndogo  haitatosha katika kitendo hicho kuoga tu  bali itawajibika  kutawadha pia  ikiwa  ghusli hiyo itatanguliwa na kutoka kwa hadathi  kinyume na ikiwa haikutoka kabla.