Mas’ala: Ni sunna kutoa adhana na kukimu katika sala za faradhi za kila siku sawa iwe ni adaa au kadhaa.
Na kushuhudia kwa kusema ash’hadu anna aliyan waliyyu llah. Hiyo ni kukamilisha shahada ya mtume au ujumbe wa mtume,na kusema hivyo ni sunna hata kama si sehemu ya adhana au iqamah, na vile vile kumsalia mtume na ahli zake pindi litajwapo jina lake tukufu.
Mas’ala: Sunna hii ya kuadhini na kukimu husisitizwa sana hasa katika sala ya magharibi na sala ya alfajiri kati ya faradhi za kila siku, kama ambavyo imesisitizwa sana kwa wanaume na hasa iqamah, bali kauli ya ahwat ya sunna kwa wanaume ni kuwa haipaswi kuiacha, na adhana na iqama haikutiliwa mkazo na kusisitizwa kwa wanawake.
Mas’ala: Sunna ya adhana na Iqama huporomoka katika sehemu zifuatazo:
1- pindi akiingia katika sala ya jamaa amboyo kabla yake ilitolewa adhana na kukimiwa sawa awe alieingia kwenye sala hiyo ni imam au ma’amuum.
2- Pindi akiingia msikitini na safu za jamaa zikawa hazikutengana na kupatikana nafasi baada ya kumaliza sala, ikiwa atataka kusali peke yake wakati huo si lazima kwake kuadhini na kukimu- bali kauli ya ahwat ni kuwa asitoe adhana isipokuwa kwa siri au pole pole- na ikiwa atataka kusali sala nyingine ya jamaa hata anza kwa kuadhini na kukimu lakini kwa sharti kuwa sehemu iwe ni ile ile –yaani- isiwe sehemu nyingine tofauti na ilipo saliwa jamaa ya kwanza na sehemu ambayo imesihi kusalia jamaa ya kwanza na iwe katika jamaa ya mwanzo wali adhini na kukimu.
3- Pindi atakapo sikia adhana na iqama mtu mwingine kwa ajili ya sala adhana na iqama hiyo itatosheleza na haitakuwa na haja ya kuadhini na kukimu, lakini ikiwa hapakuwa na mwanya kati ya sala yake na kati ya adhana na iqama aliyo isikia, na hakuna tofauti kati ya kuwa alie adhini na kukimu ni imam au maamum au mtu mwingine mwenye kusali sala ya furada (pekee)
Mas’ala: Adhana huporomoka katika sala ya pili kati ya sala zenye kushirikiana katika wakati, ikiwa atakusanya kati ya sala hizo pale ambapo atatekeleza sunna ya kukusanya- kama ikiwa atakusanya kati ya sala ya adhuhuri na alasiri siku ya arafa katika wakati wa mwanzo na magharibi na isha usiku wa iddi katika sehemu ya muzdalifa katika sala ya pili- bali katika sehemu zote ambazo ni sunna kukusanya kwa kauli iliyo adh’har, wakati wowote atakapo kusanya kati ya sala mbili za faradhi adaa’an adhana ya pili huporomoka, vile vile ikiwa atakusanya kati ya sala mbili za kadhaa na kuzisali kwenye kikao kimoja wakati huo adhana ina anguka isipokuwa katika sala ya mwanzo, na ihtiyat inasema yawezekana kuiacha adhana katika sehemu zote kwa kuwa si sheria bali haipaswi kutoa adhana na iqama katika sehemu mbili za mwanzo moja kwa moja hata kama ni kwa kutaraji kuwa kufanya hivyo ni kujikaribisha kwa Allah.
Mas’ala: Huzingatiwa nia katika adhana na iqama, pia utaratibu na kufuatanisha na iwe ni katika wakati wa sala, na huzingatiwa katika iqama mtu awe na twahara na atoe iqama kwa kusimama, na ni makruhu kuzungumza baada ya kusema qad qaamatis salaa isipokuwa litakalo husika na sala tu.
الله اکبر
Allahu akbar X 4
اشهد ان لا اله الا الله
Ash-hadu an lla ilaaha illa llaah X 2
اشهد ان محمد رسول الله
Ash-hadu anna muhammada rrasuulullaah X 2
اشهد ان عليا ولی الله
Ash-hadu anna ALiyan waliyyu llaah X 2
حی علی الصلوة
Hayya-alaa salaah X 2
حی علی الفلاح
Hayya-alal falaah X 2
حی علی خير العمل
Hayya-alaa kheyril-amal X 2
الله اکبر
Allahu akbar X 2
لا اله الا الله
Laa-ilaaha illa llaah X 2
الله اکبر
Allahu akbar X 2
اشهد ان لا اله الا الله
Ash-hadu an lla ilaaha illa llaah X 2
اشهد ان محمد رسول الله
Ash-hadu anna muhammada rrasuulullaah X 2
اشهد ان عليا ولی الله
Ash-hadu anna ALiyan waliyyu llaah X 2
حی علی الصلوة
Hayya-alaa salaah X 2
حی علی الفلاح
Hayya-alal falaah X 2
حی علی خير العمل
Hayya-alaa kheyril-amal X 2
قد قامت الصلوة
Qad qaamatis salaa X 2
الله اکبر
allahu akbar X 2
لا اله الا الله
Laa ilaaha illa llaah X 1