JINA NA NASABA YAKE

Jina lake ni Ali, Kunya (jina la utoto) yake ni Abul Hasan, na jina lake la heshima ni Naqi (Mtakatifu). Kwa sababu Imamu Ali bin Abi Talib [a] na Imamu Ali Ridha [a] nao walikuwa na Kunya ya Abul Hasan, Imamu Ali Naqi [a] anaitwa Abul Hasan wa Tatu. Mama yake ni Bibi Samanah Khatuun.