rudi maktaba >Akida >Yaliyomo >

KAZI NA UJUMBE WA YESU

"Maana Mwana wa Mtu alikuja kuwaokoa wale waliopotea". (Mathayo18:11)

"Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo". (Mathayo 15:24)

Yesu pia aliweka wazi ni nini Mwenyezi Mungu alimtaka afanye:

"Mimi sikunena kwa mamlaka yangu mimi mwenyewe, ila Baba aliyenituma ndiye aliyeniamuru niseme nini na niongee nini". (Yoshua12:49)

"Msidhani ya kuwa nimekuja kutengua sheria ya Musa au mafundisho ya Manabii, sikuja kutengua bali kukamilisha". (Mathayo 5:17)

Uchunguzi makini wa maneno ya Yesu unaonyesha kwamba, kinyume na Wakristo wanavyo fikiri, Yesu hakuwa na nia ya kuanzisha dini mpya; alikuja tu kuukamilisha na kuusisitizia ujumbe ambao Mwenyezi Mungu aliwapa Mitume wote waliotangulia kabla yake: kuwa Mwanadamu alitakiwa atii sheria za Mwenyezi Mungu na amuabudu Mwenyezi Mungu tu.

Hakuna wakati wowote katika kazi na maisha yake ya utume ambapo Yesu alidai kuwa zaidi ya mwanaadamu, aliyepewa ufunuo na kuongozwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu. Bila chembe ya shaka yeye mwenyewe alijiita kuwa ni mwana wa mtu, na akaweka wazi, katika aya nyingi ndani ya injili, kwamba yeye hakuwa lolote isipokuwa ni Mjumbe na Mtume aliyetumwa na Mwenyezi Mungu.

"Yesu akamjibu, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mwenyezi Mungu peke yake". (Marko 10:18)

".. anayenipokea mimi, hanipokei mimi bali anampokea Yule aliyenituma". (Marko 9:37)

"Na uzima wa milele ndio huu, kukujua wewe uliye peke yako, Mungu wa kweli na kumjua Yesu kristo uliyemtuma". (Yohana 17:3)

"Mimi nimewaambieni ukweli niliousikia kwa Mungu, ninyi mwataka kuniua". (Yohana 8:40)

"Nakwenda juu kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu". (Yohana20 :17)

Licha ya juhudi zake zote - maneno ya ajabu pamoja na miujiza mingi - Yesu alikataliwa, hususan na watu wake.

Miaka mitatu baada ya kuanza kazi yake ya utume, alikamatwa na kuhukumiwa kwa shutuma kwamba anasambaza maneno ya chuki miongoni mwa watu dhidi ya watawala na maneno mabaya dhidi ya vitu vyao vitukufu vya kidini. Mafanikio yalikuwa yamemkwepa - katika mwisho wa maisha yake hapa duniani, alikuwa amepata wafuasi kidogo sana wasiozidi 500.

Hali hii ilibadilika baadaye baada ya kuja nabii mpya, aliyedai kuzungumza kwa jina la Yesu, miaka michache baadaye.