HISTORI  FUPI YA IMAM  JAAFAR  SWAADIQ (A.S)

JINA LAKE NA NSABU YAKE  (A.S).

Jina lake ni Jaafar bin Mohammad bin Ally bin Husein bin Ally bin abi twalib  (a.s).

MAMA  YAKE  (A.S).

Mama  yake ni Ummu Far’wa binti  Qaasim bin  Mohammad bin abii Bakar.

KUNIA  YAKE  (A.S).

1-  Abu  abdillah. 2-  Abu ismaail.

MAJINA YAKE  MASHUHURI  (A.S).

1-  Aswaadiq.  2-  Aswabir. 3-  Al faadhil.  4-  Atwaahir.   5-  Al kaamil.  6-  Al munjiy, na mengineyo.

TAREHE  YA KUZALIWA KWAKE (A.S).

Alizawa tarehe 17 mwezi wa Rabiul awwal mwaka 83 hijiria, na kuna kauli nyingine tofauti na hiyo.

SEHEMU  ALIPO ZALIWA  (A.S).

Alizaliwa  katika mji wa Madinatul munawwarah.

WAKEZE  (A.S).

1- Fatima binti wa  Hussein bin Ally bin Hussein (a.s), na wakeze wengine  walikuwa ni vijakazi.

WATOTO  WAKE (A.S).

1- Ismaail.  2-  Abdallah.  3-  Mussa. 4-  Is’haaq. 5-  Mohammad.  6-  Abbas.  7- Ally.   8-  Ummu Far’wa.  9-  As’maa. 10-  Fatima.

NEMBO YA PETE YAKE (A.S).

Pete yake ilikuwa na Nembo ifuatayo: (Allahu waliyyii wa ismatii min khalqihi), na kuna kauli nyingine tofauti na hiyo.

UMRI  WAKE (A.S).

Ali ishi kwa muda wa miaka 65.

MUDA WA  UIMAMU WAKE (A.S).

Uimamu wake  ulidumu kwa muda wa miaka 34.

WATAWALA WA  ZAMA  ZAKE  (A.S).

Ali ishi katika zama za  watawala wa aina mbili,  1-  Watawala wa banii  umayyah, 2-  watawala wa bani Abbas. 

Watawala wa banii Umayyah: 1- Haashim bin Abdul milk.  2-  Ibrahiim bin Waliid.  3-  Mar’wan Al himaar.     Ama watawala wa bani Abbas: 1- Abul Abbas Assaffah.  2-  Abuu jaafar  Al mansuur  Dawaaniqiy.

TAREHE YA KUFA KWAKE  SHAHIDI  (A.S).

Alikufa shahidi tarehe 25 mwezi wa shawwal mwaka 148 hijiria, na zimetajwa tarahe nyingine tofauti na hizi.

SEHEMU ALIPO FIA (A.S).

Ali  kufa shahidi  katika  mji wa madinatul  munawwarah.

SABABU YA KUFA KWAKE  SHAHIDI (A.S).

Aliuwawa  (a.s) kwa kulishwa sumu  katika zama za khalifa wa bani Abbas aitwae  Mansuur  Dawaaniqiy.

SEHEMU ALIPO ZIKIWA  (A.S).

Alizikwa  katika makaburi ya  Baqii yaliyoko katika mji  wa madinatul munawwrah.