HISTORIA  FUPI  YA IMAM  MOHAMMAD  BAAQIR(A.S)

JINA LAKE NA NASABU YAKE  (A.S)

Jina lake  tukufu ni  Mohammad bin Ally bin  Hussein  bin Ally bin Abi twalib  (a.s)

MAMA  YAKE  (A.S).

Fatima binti  wa Imam  Hassan (a.s).

KUNIA YAKE  (A.S).

Abu Jaafar, na nyinginezo.

MAJINA  YAKE MASHUHURI  (A.S).

1-  Baaqir. 2-  Baaqirul  uluum.  3-  Ash-shaakir.  4-  Al haadiy, na mengineyo.

TAREHE YA KUZALIWA KWAKE  (A.S).

Alizaliwa tarehe 1 mwezi wa Rajab mwaka  57 hijiria, na inasemekana kuwa  alizaliwa tarehe 3 mwezi wa safar  mwaka huohuo, na kunakauli zingine tofauti na hiyo.

SEHEMU  ALIPO ZALIWA  (A.S)

Amezaliwa katika mji wa madinatul munawwarah.

WAKEZE (A.S).

1-  Ummu  Farwah  binti Qaasim.  2-  Ummu Hakiim binti Usaid  Athaqafiyyah. 3-4- walikuwa ni vijakazi.

WATOTO  WAKE  (A.S).

1-  Imam  Swadiiq  (a.s). 2-  Abdallah.  3-  Ibrahiim.  4-  Ubaidullah.  5-  Ally.  6-  Zainab.  7-  ummu Salamah.

NEMBO YA PETE YAKE (A.S).

P ete yake ilikuwa na nembo ifuatayo: (Al- izzatu lillahi, na zinginezo.

 UMRI WAKE (A.S).

Ali ishi kwa muda wa miaka  57.

MUDA WA UIMAMU  WAKE (A.S).

Uimamu wake ulidumu kwa muda wa miaka 19.

WATAWALA  WA ZAMA ZAKE (A.S).

1- Waliid bin Abdil malik.  2- Sulaiman bin abdul malik. 3-  Omar bin Abdul aziiz. 4-  Yaziid bin Abdul malik.  5-  Haashim bin  Abdul malik.

TAREHE YA KUFA KWAKE  SHAHIDI (A.S)

Alikufa shahidi tarehe 7 mwezi wa dhul hajji mwaka  114 hijiria.

SEHEMU ALIPO FIA SHAHIDI  (A.S).

Alikufa shahidi  katika mji wa  Madinatul munawwarah.

SABABU  YA KUFA KWAKE SHAHIDI (A.S)

Aliuwawa (a.s) kwa kulishwa sumu kupitia kwa Bwana  ibrahiim bin Waliid bin Yaziid katika zama za khalifa wa bani umayya  Haashim bin Abdul malik.

SEHEMU ALIPO  ZIKIWA (A.S).

Alizikiwa  katika makaburi ya Baqii  katika mji wa Madinatul Munawwarh.