HISTORIA  FUPI  YA IMAM  ALLY  BIN  HUSSEIN  ZAINUL AABIDIN (A.S)

  

JINA LAKE NA NASABU YAKE (A.S)

Jina lake ni Ally bin Hussei bin Ally bin Abii twalib (a.s).

MAM YAKE (A.S).

Mama yake ni Shah Zanaan binti Yazdjard  bin Shahriyaar bin Kisraa, na inasemekana  kuwa jina lake ni  ( Shahri banu).

KUNIA YAKE (A.S).

1- Abuu  Mohammad.  2- Abuul Hassan.  3- Abuul Hussin   4-  Abuul qaasim.

MAJINA YAKE MASHUHURI (A.S).

1-  Zainul aabidiin,  2-  Sayyidul  Aabidiin,  3-  Assajjaad,  4-Dhu thafanaat,  Imamul  Muuminiin,  5-  Al mutahajjid,  6-  Azzahid,  7-  Al amiin,  Azzakiiyyu,  na mengineyo.

TAREHE YA KUZALIWA KWAKE (A.S).

Alizaliwa tarehe  5 mwezi wa Shaaban mwaka 380 hijiria, na imepokelewa pia kuwa alizaliwa tarehe 15 mwezi wa Jamadal Aakhir mwaka huohuo, na kuna kauli zingine tofauti na hizo.

SEHEMU ALIPO ZALIWA (a.s).

Alizaliwa katika mji wa madinatul munawwarah.

WAKEZE (A.S).

Imepokelewa kuwa  alioa wanawake  7,  1-  Ummu Abdallah bintil Hussein (a.s)  ama wengine sita walio bakia  walikuwa ni vijakazi.

WATOTO WAKE (A.S).

1-  Imam Baaqir  (a.s) (Mohammad bin Ally),  2-  Abdallah,  3-  Al hassan,  4-  Al Hussein,  5-  Zaid,  6-  Omar,  7-  Al Hussein Assughraa,  8-  Abdur rahmaan,  9-  Sulaimaan,  10-  Ally,  11-  Mohammadul  Asghar,  12-  Khadija,  13-  Fatima,  14-  Aliyyah,  15-  Ummu kuluthuum, na wengineo.

NEMBO YA PETE YAKE (A.S).

Pete yake ilikuwa na  Nembo ifuatayo: (Wamaa tawfiiqiy illa billahi), na kuna riwaya zingine  zizungumziazo  nemboya pete yake tofauti na hii.

VITABU VYAKE (A.S).

1-  Swahifatu  Sajjadiyyah,   2-  Risaalatul  Huquuq.

UMRI WAKE  (A.S)

Ali ishi kwa muda wa miaka  57.

MUDA WA UIMAMU WAKE  (A.S).

Uimamu wake ulidumu kwa muda wa miaka 35.

WATAWALA WA ZAMA  ZAKE (A.S).

Aliishi katika zama  za utawala wa   1-  Muawia, 2-  Yazid bin Muawia,  3-  Muawia bin Yazid, 4-  Mar’waan binil Hakam, 5-  Abdul malik bin Mar’waan   6-  Waliidi bin Abdul malik.

TAREHE YA KUFA  KWAKE   SHAHIDI (A.S)

 Wana historia  wametofautiana  kuhusiana na tarehe ya kufa kwake, Baadhi wamesema ya kuwa lifariki tarehe 12 mwezi wa muharram, na wengine wamesema tarehe 18 muharram, na wengine wamesema tarehe 25 muharram mwaka 94 au 95 hijiria.

SEHEMU  ALIPO FIA SHAHIDI (A.S).

Alikufa shahidi katika mji wa  Madinatul munawwarah.

SABABU YA KUFA  KWAKE SHAHIDI (a.s).

Ali lishwa sumu katika zama za mtawala  wa kibani umayyah  Waliidi bin Abdul malik.

SEHEMU ALIPO ZIKIWA (A.S).

Alizikwa  katika makaburi ya Baqii  kwenye mji wa (Madinatul Munwwarah).

Kwa maelezo zaidi rejea kitabu Buharul an’waar, juzu ya 42 kwa wale wenye kufahamu lugha ya kiarabu.