HISTORIA  FUPI   YA IMAM HUSSEIN BIN ALLY (A.S)

JINA LAKE NA NASABU YAKE (A.S).

Jina lake ni  Hussein bin Ally bin abi twalib bin Abdul mutwalib.

MAMA  YAKE (A.S).

Mama  yake ni Fatima Zahraa (a.s) binti wa Mtume (s.a.w).

KUNIA YAKE (A.S).

Abu abdillah.

MAJINA YAKE MASHUHURI (A.S).

1- Arrashiid.  2- Atwayyib. 3- Assayyid  Zakii.  4- Al mubaarak.  5-  Attaabiu limardhatillah. 6-  Addaliil alaa dhati llah.  7-  Assibtwi.  8-  Sayyidu  shabaab ahlil jannah.  9-  Sayyidu shuhadaa. 10-  Abuu aimmah, na  mengineyo.

TAREHE YA KUZALIWA KWAKE (A.S)

Alizaliwa tarehe 3 mwezi wa shaaban  mwaka wa 4 hijiria, na kuna kauli nyingine isemayo kuwa alizaliwa tarehe 5 mwezi wa shaaban mwaka huohuo, na kuna kuli zingine tofauti na hizo.

VITA VYAKE (A.S).

Alishiriki pamoja na baba yake  Amirul muuminin Ally  (a.s) katika vita vya Jamal, na vita vya Swiffiin, na vita vya Nahrawaan. Na alikuwa ni jemedari wa jeshi la  Imani dhidi ya jeshi l ukafiri na upotevu katika vita vya  karbalaa (yaani tukio la Twaf).

WAKEZE (A.S).

1-  Shaah Zanaan binti kisraa. 2-  Laylaa binti murrah Athaqafii.  3-  Ummu Jaafar  Al qadhaaiyyah,  4-  Rabaab binti imri’il qaisi  Al kilabaiyyah,  5-  ummu Is’haaq binti Twalha Attamiimiyyah.

WATOTO WAKE (A.S)

1- Alliyul  Akbar, 2-  Alliyul  Asghar, 3-  Jaafar, 4-  Abdallah Arradhii’u,  5-  Sakiinah,  6-  Fatima  bintil Hussein, na wengineo.

NEMBO YA PETE YAKE (A.S).

Inasemekana  kuwa  nembo ya pete yake ilikuwa ni (Likulli  ajalun kitaab) na kuna riway isemayo tofauti na hivyo.

UMRI  WAKE (A.S).

Ali  ishi kwa muda wa miaka  57.

MUDA WA UIMAMU WAKE (A.S).

Uimamu wake ulidumu kwa muda wa miaka  11.

    WATAWALA WA ZANA  ZAKE (A.S)

Ali  ishi katika zama za utawal wa  Muawia na mwanae  Yazid.

TAREHE YA KUFA KWAKE SHAHIDI (A.S).

Alikufa shahidi tarhe (10) mwezi wa Muharram mwaka  61 hijiria.

SEHEMU ALIPO FIA SHAHIDI (A.S).

Alikufa  shahidi katika mji mtukufu wa Karbalaa huko iraq.

SABABU YA KUFA KWAKE SHAHIDI (A.S).

Ali uwawa shahidi kwa   kuipigania na kuitetea  Dini ya babu yake Mohammd (s.a.w) katika vita vya karbalaa, dhidi ya jeshi la fasiki Yazidi bin Muawia.

MAHALI  ALIPO ZIKIWA (A.S).

Alizikiwa  katika mji mtukufu wa Karbalaa.

Kwa malezo zaidi rejea  kitabu buharul an’waar  juzu ya  40- 41, kwa wenye kufahmu lugha ya kiarabu.