HISTORIA  FUPI YA  AMIRUL  MUUMININ ALLY(A.S).

JINA LAKE NA  NASABU YAKE.

Jina lake ni Ally bin abi twalib bin abdul mutwalib bin  haashim bin abdul manafi.

MAM  YAKE.

Mama yake ni  Fatima binti asad bin haashim bin abdul manafi.

KUNIA YAKE.

Kunia yake ni  1- Abul Hasssan. 2-  Abul Hussein. 3- Abu sibtwain. 4- Abu rihanatayni. 5-  Abu turab. na mengineyo.

MAJINA  YAKE  MSHUHURI.

1- Amirul  muuminin. 2- Sayyidul muslimiin. 3- Imamul  muttaqiin. 4- Qaidul ghuril muhajjalin. 5- Sayyidul awswiyaa.  6- Sayyidul  arab.  7-  Al murtadhaa.  8-  yaasubud  diin. 9- Haydar.  10-  Al anzaul batwiin.  11-  Asadullah. Na mengineyo.

TAREH YA KUZALIWA KWAKE (A.S).

Alizaliwa  tarehe  13 mwezi wa  Rajab baada  ya  mwaka wa tembo  kwa miaka  30 baada ya kuzaliwa mtume (s.a.w)

SEHEMU ALIPO ZALIWA (A.S).

Alizaliwa  katika mji wa makka  (ndani ya kaaba tukufu).

VITA  ALIVYO PIGANA (A.S).

Alishiriki katika vita vyote vya Mtume  (s.a.w) isipokuwa  vita vya Tabuuk kwani Mtume  (s.a.w) alimuamuru kubakia katika mji wa madinatul munawwarh na alifanya hivyo kwa ajili ya  kusimamia mambo ya mji huo  Mtume akiwa hayupo, ama vita  ambavyo  alivyo viendesha  yeye menyewe katika zama za utawala wake ni kama vifuatavyo: 1- Vita vya  Jamal. 2- vita vya swiffin. 3-  vita  vya Nahrawaan.

WAKEZE  (A.S)

1-  Fatima Zahraa  (a.s) binti wa Mtume (s.a.w), 2-  Umamah binti Abil Aasi, 3-  Ummul baniin Al kilaabiyyah, 4-  Laylaa binti Mas’ood,  5-  Asmaa binti Umais, 6-  Aswahbaau binti Rabiiah (Umm Habiib)  7-  Khawlah binti Jaafar.  8-  Ummu Saad binti Ur’wah.  9-  Makhba’atu binti Imri’il Qaisi.

WATOTO  WAKE  (A.S)

Wana historia wame tofautiana kuhusu idadi ya  watoto wake  Imam (a.s) lakini riwaya  zimekuwa zikizungumzia  kati ya 25 na 33, na hapa tuta taja walio mashuhuri  kati yao.

1- Imam Hassan bin Ally (a.s).  2-  Imam Hussein bin Ally (a.s).  3-  Ummul maswaaib Zainabul Kubraa (a.s).  4-  Zainab Assughraa.  5-  Al abbas  (Abul fadhli)  6-  Mohammad  Al awsat.  7-  Jaafar.  8-  Abdallah.  9- Othumaan. 10-  Mohammad binil Hanafiyyah.  11-  Yahyaa. 12-  Ummu Haaniy.  13-  Maymuunah.  14-  Jumanah (Ummu Jaafar).  15-  Nafiisah.

NEMBO YA PETE YAKE (A.S)

Nembo ya pete yake ilikuwa  kama ifuatavyo: (Al mulku lillahil waahidul qahaar), na kuna kauli nyingine  tofauti na hiyo.

UMRI  WAKE  (A.S).

Ali ishi kwa muda  wa miaka  63.

MUDA  WA UIMAMU WAKE  (A.S).

Uimamu  wake ulidumu kwa muda wa miaka 30.

TAREHE  YA  KUFA  KWAKE  SHAHIDI (A.S).

Imam  Ally  alikufa shahidi  tarehe  21 mwezi wa Ramadhan  mwaka 40 hijiria.

SABABU YA KUFA  KWAKE  SHAHIDI  (A.S).

Alikufa shahidi  kutokana na dharuba alilo pigwa na mal uun Abdurrahmaan bin muljim Al muraadiy  kwa upanga  kichwani kwake (a.s) akiwa katika hali ya sijda kwenye mihraab  ya msikiti wa  Al kufa.

SEHEMU ALIPO ZIKIWA (A.S).

Alizikiwa  katika mji wa (Najaful ashraf ), katika sehemu iitwayo Al harraa.